Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika (آداب الزفاف في السنة المطهرة)

 Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika

 

آداب الزفاف في السنة المطهرة

 

تأليف: العلامة المحدث محمد ناصرالدين الألباني

 

Kimeandikwa Na: Shaykh Muhammad Naaswirud-Diyn Al-Albaaniy

 

Kimefasiriwa Na: Abuu 'Abdillaah   

 

 

بسم الله الرحمن الرحيم

Share

01-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Dibaji Ya Mfasiri

 

بسم الله الرحمن الرحيم

 

Kitabu hiki ni mfululizo wa vitabu vya Kiislamu vyenye lengo la kuwafahamisha Waislamu Dini yao katika mas-ala ya Ndoa; Ibada na sharia zote za halali na haramu zinazohusiana na maisha ya ndoa.

Nimekichagua kitabu hiki kukifasiri kwa sababu sijaona kitabu kingine kilichoelezea mas-ala ya Ndoa kwa kina na dalili nyingi kama kilivyochambuliwa na kitabu hiki.

 
Ama kwa nini nimeamua kufasiri kitabu kuhusu mas-ala haya; msukumo mkubwa ulionituma kufasiri kitabu katika mas-ala haya ni kuwa leo hii kumekuwa na uharibifu mkubwa katika kufanikisha mas-ala haya ya Ndoa kuanzia inapofungwa Nikaah, karamu, na sherehe zake hadi zinapomalizika Watu wameacha Uislamu na kuridhia mila za kimagharibi, kikabila na mila potofu zinazowatoa Waislamu kwenye Dini yao.

 

Ni maswali mengi yamekuwa yakiulizwa kuhusu mas-ala haya katika mtandao na haswa katika tovuti (website) ya Kiislamu kwa lugha ya kiswahili iitwayo www.alhidaaya.com ambayo yametoa msukumo huo, kadhalika katika kuiendea kazi hii ya mwandishi mwanachuoni wa karne Shaykh Muhammad Naaswirud-Diyn Al-Albaaniy.

 

Hii ni zawadi yangu ndogo kwa mke wangu, wana ndoa wote, wana darsa wangu na wahusika wa Alhidaaya kwa juhudi kubwa za kufanikisha kazi hii.

 
Namuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ajaaliye hiki kitabu kilete manufaa kwa jamii yetu katika mas-ala ya Ndoa na Atutaqabalie hizi juhudi kwa kutujazia katika Miyzaanul-Hasanaat yetu siku ya Qiyaamah.

Abuw 'Abdillaah (3 Rabiy'u Ath-Thaaniy 1428/20 April 2007))

 

Share

02-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Utangulizi Wa Mtungaji

Sifa zote zamstahiki Allaah سبحانه وتعالى Ambaye Amesema katika aayah iliyo wazi kwenye Kitabu Chake:

 

 

 

((وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً إِنَّ فِي ذَلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ))

 

 

((Na katika Ishara Zake ni kuwa Amekuumbieni wake zenu kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Naye Amejaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaofikiri)) (Ar-Ruum 30: 21)

 
Na Swalah na Salaam zimwendee kipenzi Chake Muhammad ambaye amesema katika Hadiyth Swahiyh:

 

 

((تَزَوَّجُوا الْوَدُودَ الْوَلُودَ فَإِني مُكَاثِرٌ بِكُمُ الأَنْبِيَاءَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ))

((Oeni wapenzi wazaao, kwani nitashindana na Mitume wengine kwa idadi ya wafuasi siku ya Qiyaamah)).[1]

Baada ya utangulizi huu:

 

Katika Uislamu kuna desturi na taratibu ambazo zatakikana kufuatwa na za mtu anayeoa au anayetaka kufunga ndoa. Waislamu wengi leo hata wale ambao wanajitahidi katika ibada mbali mbali, hawajui kabisa hizi desturi za Kiislamu. Kwa hiyo, nimeamua kuandika makala hii ndefu yenye faida kwa kuelezea wazi mambo haya katika mnasaba wa harusi ya mtu ambaye ni kipenzi changu. Natumai kuwa itamsaidia yeye na ndugu wengineo waumini katika kumfuata Bwana wa Mitume alivyotuamrisha kutokana na amri ya Mola Wa Ulimwengu.

 
Baada ya hapo nimetahadharisha kuhusu baadhi ya mas-ala muhimu kwa kila anayeoa, na ambayo yamekuwa ni mitihani kwa wake wengi.

 

Namuomba Allaah سبحانه وتعالى Ajaaliye kitabu hiki kiwe ni chenye manufaa na Ajaaliye kazi hii iwe ya ikhlaas yenye kumridhisha Yeye Pekee kwani Yeye Ndiye Mwema na Rahiym.

 

 

 

Ifahamike kwamba kuna desturi nyingi katika sherehe za ndoa, lakini yaliyonishughulisha zaidi katika uandishi huu wa haraka, ni yale mambo yaliyo Sahihi katika Sunnah za Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Muhammad ambayo hayawezi kukanushwa kutokana na msimamo maalumu wa mfululizo wa usimulizi (sanad) ambao hauna shaka katika muundo wake na maana yake. Hivyo yeyote atakayesoma na kufuata maelezo haya atakuwa katika msingi uliothibiti wa Dini yake na atakuwa katika hali ya matumaini ya uhalali wa vitendo vyake.

 
Namuomba Allaah سبحانه وتعالى Amkhitimishe kwa furaha na thawaab kwa kuanza maisha yake ya ndoa kwa kufuata Sunnah na Amjaaliye miongoni mwa waja Wake Aliyewaelezea katika kauli Yake:

 

 

((وَالَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا))

 

 

((Na wale wanaosema: Mola wetu! Tupe katika wake zetu na watoto wetu yaburudishayo macho, na Utujaalie tuwe waongozi kwa wachaji Allaah)) (Al-Furqaan 25: 74)

 

Na mwisho mwema ni wa waja wanaomcha Allaah kama Anavyosema Mola wa Ulimwengu:

 

 

 

((إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ ﴿41 وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ ﴿42 كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿43 إِنَّا كَذَلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنينَ))

 

 

((Hakika wachaji Allaah watakuwa katika vivuli na chemchem. Na matunda wanayoyapenda. Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.  Hakika ndio kama hivyo Tunavyowalipa watendao mema)) (Al-Mursalaat 77: 41-44)

 

 

 

Adabu na desturi hizo ni hizi zifutazo:

 

 

[1] Ahmad na At-Twabaraaniy kwa isnaad iliyo hasan, na Ibn Hibbaan amekiri kuwa ni Swahiyh kutoka kwa Anas

Share

03-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Huruma/Upole Kwa Mke Wako Unapotaka Kukutana Kinyumba

Inapendekezwa kuwa mtu anapotaka kufanya tendo la ndoa na mkewe katika siku ya kwanza ya ndoa, ambembeleze na amuonyeshe hali ya huruma na upole kama kumkaribisha kinywaji na kadhalika. Kama tunavyojifunza katika Hadiyth ya Asmaa bint Yaziyd ibn As-Sakaan ambaye alisema:

 

إني قَيَّنْتُ عائشة لرسول الله صلى الله عليه وسلّم، ثم جئته، فدعوته لجَلْوَتِهَا، فجاء فجلس إلى جنبها، فُاتي بعُسٍّ لينٍ، فشرب ثم ناوله النبي صلى الله عليه وسلّم فخفضت رأسها واستحيت، قالت أسماء: فانتهرتُها، وقلت لها: خذي من يد رسول الله صلى الله عليه وسلّم، قالت: فأخذت فشربت شيئاً، ثم قال لها النبي صلى الله عليه وسلّم: «أَعْطِي تِرْبَكِ» قالت أسماء: فقلت: يا رسول الله، بل خذه فاشرب منه، ثم ناولنيه من يدك، فأخذه فشرب منه ثم ناولنيه، قالت: فجلست ثم وضعته على ركبتي ثم طفقت أُديره وأُتبعه شَفَتِي لأصيب منه مَشْرَبَ النبي صلى الله عليه وسلّم، ثم قال لنسوة عندي: «نَاوِلِيْهِنَّ» فقلن: لا نشتهيه، فقال النبي صلى الله عليه وسلّم: «لا تَجْمَعْنَ جُوْعاً وكَذِباً»

"Nilimpamba ‘Aaishah kwa ajili ya Mjumbe wa Allaah, kisha nikamwita aje kumfunua na kumuangalia. Alikuja, akakaa pambizoni mwake, akaleta kikombe kikubwa cha maziwa ambayo alikunywa. Kisha akamkaribisha ‘Aaishah ambaye aliinamisha kichwa chake kwa kuona haya. Nikamgombeza na kumwambia: Pokea kutoka kwenye mikono ya Mtume Akachukua na kunywa kidogo. Kisha Mtume akamwambia: ((Wape mengine rafiki zako)) Hapo nilisema: Ee Mjumbe wa Allaah bora chukua mwenyewe na kunywa na kisha unipe mimi kwa mikono yako. Akachukua na kunywa kidogo kisha akanipa mimi. Nikakaa chini na kuyaweka katika magoti yangu. Kisha nikaanza kukizungusha na kukifuatia kwa mdomo wangu ili nifikie pale alipokunywa Mtume. Kisha Mtume akasema kuhusu wanawake waliokuwepo pamoja na mimi: ((Wape wanywe)) Lakini wakasema: Hatuyataki (Yaani hawana njaa). Mtume akasema, ((Msichanganye njaa na uongo))[1]

 

 

 


[1] Ahmad na Al-Humaidiy. Ahmad ameipokea kwa isnaad mbili, kila moja inathibiti nyingine

 

Share

04-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuweka Mkono Wako Juu Ya Kichwa Cha Mkeo Na Kumuombea

Inampasa mume, wakati wa kufunga ndoa na mkewe na kabla hajamuingilia, kuweka mkono wake juu ya kichwa chake (sehemu ya utosini), na kutaja jina la Allaah سبحانه وتعالى na kuomba Baraka za Allaah سبحانه وتعالى kama katika kauli ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم:

 

 ((إذَا تَزَوَّجَ أَحَدُكُمْ امْرَأَةً أَوْ اشْتَرَى خَادِماً ، [فليأخذ بناصيتها]  [وليسم الله عز وجل]،  فَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَهَا وَخَيْرَ ما جَبَلْتَهَا عَلَيْهِ، وأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا وَمِنْ شَرِّ مَا جَبَلْتَهَا عَلَيْهِ)) 

((Anapofunga ndoa mmoja wenu na mwanamke au anapomuajiri mfanyakazi basi amuekee mkono katika kipaji cha uso wake ataje jina la Allaah utosini mwake na kusema “Ee Allaah hakika mimi nakuomba kheri ya (mke) huyu na khayr uliyomuumbiya na najilinda Kwako na shari yake, na shari ya Uliyomuumbiya))[1]

 

 

[1] Al-Bukhaariy katika "Af'aalul-'ibaad", Abu Daawuud, Ibn Maajah, Al-Haakim, Al-Bayhaaqiy na Abuu Ya'alaa ikiwa ni isnaad hasan

Share

05-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuswali Mume Na Mke Pamoja

Inapendekezwa mume na mke kuswali Raka'ah mbili pamoja usiku wa ndoa yao. Hii imehadithiwa kutoka kizazi cha mwanzo cha Waislamu (Salafus Swaalih) kama katika masimulizi mawili yafuatayo:

Kwanza:

 

تزوجت وأنا مملوك، فدعوت نفراً من أصحاب النبي صلى الله عليه وسلم فيهم ابن مسعود وأبو ذر وحذيفة، قال: وأقيمت الصلاة، قال: فذهب أبو ذر ليتقدم، فقالوا: إليك! قال: أو كذلك؟ قالوا: نعم، قال: فتقدمت بهم وأنا عبد مملوك، وعلموني فقالوا:  إذا دخل عليك أهلك فصل ركعتين، ثم سل الله من خير ما دخل عليك، وتعوذ به من شره، ثم شأنك وشأن أهلك. 

 

Imetoka kwa Abu Sa'iyd Mawla Abu Asyad ambaye amesema: "Nilioa wakati nilipokuwa mtumwa. Nikaalika baadhi ya Maswahaba wa Mtume miongoni wao alikuwa Ibn Mas'uud, Abu Dharr na Hudhayfah. Adhaan ya Swalah iliponadiwa, Abu Dharr alianza kusogea mbele na wengine wakamwambia: Hapana! Akasema: 'Ni hivyo?' (Yaani nisiswalishe?) Wakasema: 'Ndio. Kisha nikasogea mbele na kuswalisha ingawa nilikuwa mtumwa niliyemilikiwa. Wakanifundisha kwa kusema: 'Atakapokujia mkeo, swali Raka'ah mbili kisha muombe kheri ya kile kilichokujia na jikinge kwake kutokana na shari yake. Kisha ni khiari yako na khiari ya mkeo"[1]

Pili:

 

 عن شقيق أنه قال:  جاء رجل يقال له: أبو حريز فقال: إني تزوجت جارية بكراً، وإني خشيت أن تَفْرَكَنِي، فقال عبد الله: أَلاَ إِنَّ إلالْفَ مِنَ الله وَإِن الفَرك مِنَ الشَّيْطان ليكره إليه ما أحل الله له، فإذا دخلت عليها، فمرها فلتصل خلفك ركعتين.( زاد في رواية أخرى عن ابن مسعود): اللهمَّ بَارِكْ لِي فِي أَهْلِي وَبَارِكْ لَهُمْ فِيَّ، اللَّهُمَّ ارزقهم مني وارزقني منهم، اللَّهم اجمعْ بيننا ما جمعت إلى خير، وفرِّق بيننا إذا فرقت إلى خير.

Imetoka kwa Shaqiyq ambaye amesema: "Mtu mmoja aliyeitwa Abu Hariyz alikuja na akasema: 'Nimeoa msichana mdogo na nakhofu kuwa atanibughudhi (atanitweza), 'Abdullaah Ibn Mas'uud akaniambia: 'Hakika upole (ukaribu) ni kutoka kwa Allaah سبحانه وتعالى na uhasama (chuki) ni kutoka kwa Shaytwaan ambaye anapenda kukuchukizeni (kuhizi) yale Aliyoyaruhusu Allaah سبحانه وتعالى. Kwa hiyo, mkeo atakapokuja kwako, mwambie aswali nyuma yako Raka'ah mbili'. (katika riwaaya nyingine ya masimulizi hayo hayo, 'Abdullaah aliendelea kusema) ((Ee Allaah, Nibarikie mke wangu, na Mbariki yeye kwangu. Ee Allaah Waruzuku kwangu na Niruzuku Kwao. Ee Allaah Tuunge pamoja madamu Utatuunga katika khayr na Tufarikishe (tuwe mbali mbali) Utakapotupeleka kwa yaliyo bora))[2]

 

 

 

[1] Ibn Abi Shaybah na 'Abdur-Razzaaq

[2] Ibn Abi Shaybah, At-Twabaraaniy na 'Abdur-Razzaaq: Swahiyh

Share

06-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: (Du'aa) Ya Kusema Wakati Wa Kumuingilia Mkeo

 

 

Mume anapotaka kumuingilia mkewe, inampasa daima aseme:

بِسْمِ الله اللّهُـمَّ جَنِّبْنا الشَّيْـطانَ، وَجَنِّبِ الشَّـيْطانَ ما رَزَقْـتَنا

Bismillahi, Allaahuuma Jannibnaa-sh-Shaytwaan, Wa Jannibish-Shaytwaana Maa Razaqtanaa

 

Kwa jina la Allaah, Ee Allaah Tuepushe na Shaytwaan, na Muepushe shaytwaan na Ulichoturuzuku (yaani kizazi).

 
Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema kuhusu hili:

 

((فإن قضى الله بينما ولداً؛ لم يضره الشيطان أبداً))  

 

((Baada ya hapo Allaah سبحانه وتعالى Akijaalia, watapata mtoto ambaye Shaytwaan hatoweza kumdhuru abadan))[1]

 

 

[1] Al-Bukhaariy

Share

07-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Vipi Mume Akutane Kinyumba Na Mkewe

Mume na mke, wanaruhusiwa kukutana kinyumba, kwa mtindo wowote wanaopenda, lakini tendo la ndoa liwe katika sehemu yake ya mbele tu ya maumbile. Kuhusu hili Allaah Anasema:

 

 

((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ))

 

((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo))  (Al-Baqarah 2: 223) yaani mpendavyo, kwa kupitia nyuma au kupitia mbele

Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-ala haya nitazitaja mbili:

Kwanza:

عن جابر رضي الله عنه قال:  قالتِ اليهودُ: إنَّمَا يكونُ الحَوَلُ إذَا أَتَى الرجُلُ امْرَأَتَهُ من خَلْفِهَا، فأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَكُمْ فَأْتُوا حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ)) مِنْ بَيْنِ يَدَيْهَا وَمِنْ خَلْفِهَا وَلاَ يَأْتِيْهَا إِلاَّ في المَأْتَى. 

Imetoka kwa Jaabir رضي الله عنه ambaye amesema Mayahudi walikuwa wakisema kwamba mtoto huwa kengeza ikiwa mwanamume atakutana na mkewe kinyumba kwa mtindo wa nyuma yake. Baada ya hapo Allaah Akateremsha aayah, ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo)) (Al-Baqarah 2: 223)   ((Ikiwa ni kwa mtindo wa kupitia mbele yake au kupitia kwa nyuma yake lakini sehemu ya maumbile ya kukutana iwe ni ya mbele))[1]

Pili:

 

عن ابنِ عَبَّاسٍ، قال: «إنَّ ابنَ عُمَرَ ـ وَالله يَغْفِرُ لَهُ ـ أوْهَماَ إِنَّمَا كَانَ هٰذَا الْحَيُّ مِنَ الأَنْصَارِ وَهُمْ أَهْلُ وَثَنٍ مَعَ هٰذَا الْحَيِّ مِنْ يَهُودَ وَهُمْ أَهْلُ كِتَابٍ وكَانُوا يَرَوْنَ لَهُمْ فَضْلاً عَلَيْهِمْ في الْعِلْمِ، فَكَانُوا يَقْتَدُونَ بِكَثِيرٍ مِنْ فِعْلِهِمْ، وكَانَ مِنْ أَمْرِ أهْلِ الْكِتَابِ أنْ لا يأْتُوا النِّساءَ إلاَّ عَلَى حَرْفٍ، وَذٰلِكَ أسْتَرُ ما تَكُونُ المَرْأةُ، فَكَانَ هٰذَا الْحَيُّ مِنَ الأَنْصَارِ قَدْ أخَذُوا بِذٰلِكَ مِنْ فِعْلِهِمْ، وَكَانَ هٰذَا الْحَيُّ مِنْ قُرَيْشٍ يَشْرَحُونَ النِّسَاءَ شَرْحاً مُنْكَراً، وَيَتَلَذِّذُونَ مِنْهُنَّ مُقْبِلاَتٍ ومُدْبِرَاتٍ وَمُسْتَلْقِيَاتٍ، فَلَمَّا قَدِمَ المُهَاجِرُونَ المَدِينَةَ تَزَوَّجَ رَجُلٌ مِنْهُمْ امْرَأَةً مِنَ الأَنْصَارِ، فَذَهَبَ يَصْنَعُ بِهَا ذٰلِكَ فَأَنْكَرَتْهُ عَلَيْهِ وَقَالَتْ إِنَّمَا كُنَّا نُؤْتَى عَلَى حَرْفٍ فَاصْنَعْ ذٰلِكَ، وَإِلاَّ فَاجْتَنِبْنِي حَتَّى شَرِيَ أَمْرُهُما، فَبَلَغَ ذٰلِكَ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم فَأَنْزَلَ الله عَزَّوَجَلَّ:  ((نِسَاؤُكُمْ حَرْثٌ لَكُمْ فَأْتُوا حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ)) أيْ مُقْبِلاَتٍ وَمُدْبِرَاتٍ وَمُسْتَلْقِيَاتٍ يَعْنِي بِذٰلِكَ مَوْضِعَ الْوَلَدِ
 

Imetoka kwa Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما ambaye amesema: "Kwamba Ibn 'Umar na Allaah Amghufurie au Awaghufurie. Maanswari ambao walikuwa wapagani wakiabudu miungu mingi. Waliishi na Mayahudi ambao ni Ahlul-Kitaab. Maanswari wakaona kwamba Mayahudi ni bora kuliko wao katika elimu na walikuwa wakifuata mifano yao katika mambo mengi. Watu wa vitabu walikuwa wakifanya mapenzi (kujimai) na wake zao kwa (kuwaingilia upande) hii ikiwa ni njia ya staha kabisa kwa mwanamke na Maanswari wakafuata mfano wao huo. Watu hawa kutoka Quraysh, upande mwingine walikuwa wakiwafichua wanawake wao katika njia isiyopendeza. Wakistarehe nao kwa mitindo ya kupitia mbele (mtindo wa kuelekeana uso kwa uso), kupitia kwa nyuma (au mtindo wa kuwainamisha), au wakiwalaza chali. Muhaajiruun walipohamia Madiynah, mmoja wao alimuoa mwanamke kutoka kwa Answaar. Akaanza kumfanyia hivyo (mitindo hiyo) lakini (mwanamke) akamkatalia na kumwambia: Sisi tulikuwa tunakutana kinyumba kutoka upande, kwa hiyo fanya hivyo au jitenge nami!" Mabishano yao yakamfikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kisha Allaah سبحانه وتعالى Akateremesha Aayah ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo)) Yaani kupitia mbele au nyuma, au kulazwa chali. Iliyokusudiwa ni sehemu inayotoa watoto.”[2]

 

 

 

[1] Al-Bukhaariy na Muslim

[2] Abu Daawuud, Al-Haakim na wengineo ikiwa isnaad yake ni hasan

 

Share

08-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuharamishwa Liwati

 

 

Imekatazwa mwanamume kumuingilia mkewe kwa nyuma. Hii inafahamika kutokana na Aayah iliyotajwa hapo juu (kwa vile 'konde zenu' inakusuduwa ni sehemu inayotoa mazao tu). Na kutokana na usimulizi ulioelezewa hapo juu. Vile vile kuna Hadiyth nyingine kuhusu maudhui kama zifuatazo:

 
Kwanza:

 

عن أم سلمة قالت: لما قدم المهاجرون المدينة على الأنصار تزوّجوا من نسائهم، وكان المهاجرون يجبون وكانت الأنصار لا تجبي، فأراد رجل من المهاجرين امرأته على ذلك، فأبت عليه حتى تسأل رسول الله صلى الله عليه وسلم، قالت: فأتته فاستحيت أن تسأله، فسألته أم سلمة فنزلت ((نساؤُكُمْ حَرْثٌ لَكُمْ فَأْتُوا حَرْثَكُمْ أَنّى شِئْتُم)) وقال: «لا إلاّ في صَمَّامٍ واحِدٍ»  

Imetoka kwa Ummu Salamah رضي الله عنها kwamba: Muhaajiriyn walipokuja Madiynah kwa Ma-Answaar waliwaoa wanawake wao. Wanawake wa Muhaajiriyn walikuwa wakilala kifudifudi (wakati wa kujimai na waume zao) na wanawake Ma-Answaar hawakuwa wakifanya hivyo. Mwanamume mmoja Muhaajir alitaka mkewe afanye hivyo akakataa. Akaenda kwa Mtume lakini aliona hayaa kumuuliza swali hilo, kwa hiyo Ummu Salamah alimuulizia kisha Aayah ikateremshwa inayosema: ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo)). Mtume akasema: ((Hapana! (Sio kila njia upendayo) bali isipokuwa ni pale penye tundu)) (la mbele) [1]

 
 

Pili:

عن ابن عباس رضي الله عنهما قال:  جاء عُمَر بن الخطاب إلىٰ رسول الله فقال: يا رسول الله، هلكتُ! قال: ((وما الذي أهلكك؟)) قال: حَوَّلْتُ رَحْلِي الليلة، فلم يردَّ عليه شيئاً، فأُوْحِيَ إلىٰ رسول الله هذه الآيةُ:  ((نساؤكم حرث لكم فأتوا حرثكم أنىٰ شئتم)) يقول: ((أَقْبِلْ، وأَدْبِرْ، واتقي: الدُّبر، والحَيضة))

Imetoka kwa Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما ambaye amesema: Alikuja 'Umar ibnul-Khatwtwaab kwa Mjumbe wa Allaah akasema: Ewe Mjumbe wa Allaah, Nimeangamia! Akasema: ((Nini kilichokuangamiza?)) Akasema: Nimepindua kipando changu usiku. Lakini (Mtume) hakumjibu kitu.

Akateremshiwa Aayah hii ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo)) Akasema: ((Kwa (mtindo) wa mbele, nyuma lakini chunga kumuingilia (sehemu ya maumbile ya nyuma) na akiwa katika hedhi))[2]

 
 

Tatu:

عن خُزَيْمَةَ بنِ ثابتٍ أَنَّ رجلاً سَأَلَ النبيَّ عن إتيانِ النساءِ في أَدْبَارِهِنَّ أو إتيانِ الرجلِ امْرَأَتَهُ في دُبُرِهَا، فقالَ النبيُّ: «حلالٌ»، فلمَّا وَلَّى الرجلُ دعاهُ أَوْ أَمَرَ بِهِ فدُعِيَ فقالَ: «كيفَ قلتَ، في أيِ الخُرْبَتَيْنِ أَوْ فِي أَيِّ الخُرْزَتَيْنِ أو في أيِّ الخُصْفَتَيْنِ أَمِنْ دُبُرهَا في قُبُلِهَا فَنَعَمْ، أَمَّا مِنْ دُبُرِهَا في دُبُرِهَا فَلاَ، إنَّ اللَّهَ لا يَسْتَحْيِي من الحقِّ، لا تَأْتُوا النساءَ في أَدْبَارِهِنَّ»

Imetoka kwa Khuzaymah ibn Thaabit رضي الله عنه "Mtu mmoja alimuuliza Mtume kuhusu kuwaingilia wanawake kwa nyuma au mwanamume kumuendea mkewe kwa nyuma yake. Akasema Mtume kuwa ni ((Halaal)). Alipoondoka Mtume alimwita au aliamrisha aitwe, akasema: ((Ulisema nini? Njia gani kati ya tundu mbili umemaanisha? Ikiwa ulimaanisha kutoka kwa nyuma na kumuingilia mbele (sehemu yake ya siri ya mbele) basi sawa. Lakini ikiwa umemaanisha nyuma katika sehemu yake ya siri ya nyuma basi hapana! Hakika Allaah Haoni hayaa katika haki. Msiwaingilie wake zenu katika njia zao za nyuma))[3]

 
Nne:

((لا يَنْظُرُ اللَّهُ إلى رَجُلٍ أَتَى امْرَأَةً في دُبُرِهَا))

((Allaah Hatomtazama mwanamume anayemuingilia mwanamke kwa nyuma))[4]

 
 

Tano:

 (( مَلْعُون مَنْ ياَتِي النِّسَاءَ فِي مَحَاشِهِنَّ)) ( يعني : أدبارهن)

 

((Amelaaniwa anayewaendea wanawake katika njia zao za nyuma))[5]
 

Sita:

((مَنْ أَتى حَائِضاً أَوِ امْرَأَةً فِي دُبُرِها أَوْ كَاهِناً فَصَدَقَهُ بِمَا يَقُولُ  فقدْ كَفَرَ بمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ))

((Atakayemuingilia mwenye hedhi au mwanamke kwa nyuma au atakayemuendea kahini (mtabiri) akamuamini anayomwambia atakuwa amekufuru yaliyoteremshwa kwa Muhammad))[6]

 

 

 

[1] Ahmad, At-Tirmidhiy na wengineo ikiwa ni Swahiyh

[2] An-Nasaaiy katika “‘Ishratun-Nisaa” ikiwa ni isnaad hasan, At- Tirmidhiy na wengineo

[3] Ash-Shaafi'iy, Al-Bayhaaqiy na wengineo ikiwa ni Swahiyh

[4] An-Nasaaiy ikiwa ni isnaad hasan, na imetiliwa nguvu katika "Al-Ishrah", At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan

[5] Abu Daawuud, Ahmad na wengineo ikiwa ni isnaad hasan na imetiliwa nguvu

[6] Abu Daawuud, At-Tirimidhiy na wengineo: Swahiyh

Share

09-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuchukua Wudhuu Baina Ya Vitendo Viwili Vya Ndoa

 

 

Mume anapofanya jimai na mkewe katika njia ya halali (ya haki) na akipenda kumrudia mara nyingine (kujimai), basi achukue wudhuu kwanza kutokana na kauli ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم:

 

 ((إِذَا أَتَى أَحَدُكُمْ أَهْلَهُ، ثُمَّ أَرادَ أَنْ يَعُودَ فَلْيَتَوَضَّأ  ْ(بينهما وضوءاً)  ( وفي رواية: وضوءه للصلاة )، فَإِنَّهُ أَنْشَطُ لِلْعَوْدِ))

((Mmoja wenu anapomjia mkewe kisha akipenda kumrudia mara nyingine, basi achukue wudhuu baina ya nyakati (vitendo) mbili (katika riwaaya nyingine wudhuu ule ule kama wa Swalah) kwani hakika itampa (nashati) uchangamfu kurudia kwake))[1]

 



[1] Muslim, Ibn Abi Shaybah na wengineo

Share

10-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuoga Ni Bora Zaidi

 

   

Kwa vyovyote, kukoga josho (ghuslu) kunapendeza zaidi kuliko kufanya wudhuu katika hali kama hizi.  Abu Raafi' amesimulia kwamba:

 

 

أنَّ النَّبي صلى الله عليه وسلم طاف ذَاتَ يَوْمٍ علَى نِسائِهِ يَغْتَسِلُ عِنْدَ هَذِهِ وَعِنْدَ هَذِهِ. قال فَقُلْتُ لَهُ: يا رسولَ الله ألاَ تجْعَلُهُ غُسْلاً وَاحِداً؟ قال: ((هَذَا أزْكَى وَأطْيَبُ وَأطْهَرُ))

 

 

"Mtume aliwazungukia (aliwaingilia) wake zake usiku mmoja, akikoga katika kila nyumba ya mmoja wao". Yeye (msimuliaji) alimuuliza Mtume, je, si ungeliweza kukoga mara moja tu?' (yaani mwishoni). Mtume akajibu: ((Hivi ni utakaso zaidi, usafi na bora))[1]

 





[1] Abu Daawuud, An-Nasaaiy: Hasan katika "Al-Ishraah" na wengineo

 

 

 

 

Share

11-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kukoga Pamoja Mume Na Mke

Inaruhusiwa kwa mume na mke kukoga pamoja katika sehemu moja hata kama mume ataona sehemu za siri za mke na mke ataona sehemu za siri za mumewe. Hii imethibitika katika Hadiyth Swahiyh mbali mbali, miongoni mwa hizo ni:

 

Kwanza:

 

عَنْ عَائِشَة ، قَالَتْ: كُنْتُ أَغْتَسِلُ أَنَا وَرَسُولُ اللّهِ مِنْ إِنَاءٍ. ـ بَيْنِي وَبَيْنَهُ ـ، وَاحِدٍ (تختلف أيدينا فيه). فَيُبَادِرُنِي حَتَّى أَقُولُ: دَعْ لِي، دَعْ لِي. قَالَتْ: وَهُمَا جُنُبَانِ

 

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye alisema: "Nilikuwa nakoga na Mtume kutoka chombo kimoja cha maji kilichowekwa baina yetu (kiasi kwamba mikono yetu ilikuwa ikipishana katika maji). Alikuwa akishindana na mimi hadi nikasema: Nibakishie (maji), nibakishie (maji)". Akaongeza: "Tulikuwa katika hali ya janaba" (yaani hali ya kutoka katika tendo la ndoa).[1]

Pili:

 

عن معاوية بن حدِّهِ ، قَالَ: قُلْتُ يَا نَبِيَّ الله عَوْرَاتُنَا مَا نَأْتِي مِنْهَا وَمَا نَذَرُ؟ قَالَ:  ((احْفَظْ عَوْرَتَكَ إِلاَّ مِنْ زَوْجَتِكَ أَوْ مَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ)). قُلْتُ: يَا رَسُولَ الله إذَا كَانَ الْقَوْمُ بَعْضُهُمْ في بَعْضٍ؟ قَالَ ((إِنِ اسْتَطَعْتَ أَنْ لاَ يَرَاهَا أَحَدٌ فَلاَ تُرِيَنَّهَا)) قَالَ قُلْتُ يَا نَبِيَّ الله إِذَا كَانَ أَحَدُنَا خَالِياً؟ قَالَ ((فَالله أَحَقُّ أَنْ يُسْتَحْيَى مِنْهُ مِنَ النَّاسِ))

 

Kutoka kwa Mu'aawiyah Ibn Haydah ambaye alisema: "Nilimwambia Ee Mjumbe Wa Allaah, sehemu gani ya tupu zetu zinaruhusiwa na zipi tujihadhari nazo?" Mtume akasema: "Chunga utupu wako isipokuwa kwa mkeo au wale iliyomiliki mikono yako ya kuume" Nikasema: "Ee Mjumbe wa Allaah, je, Vipi inapokuwa jamaa wanaishi pamoja?" Mtume akasema: "Ikiwa utahakikisha kuwa hakuna mtu atakayeona tupu zenu, basi fanya hivyo". Akasema: "Ee Mjumbe wa Allaah, je, vipi inapokuwa mmoja yuko pekee (amekaa uchi)?" Mtume akasema: "Allaah Anastahiki staha zaidi ya watu wengine”.[2]

 
Kwa hiyo inaruhusiwa wote mume na mke kutazamana na kugusa mwili wa mwenzake, mume au mke hata sehemu zao za siri.

 

 

 

[1] Al-Bukhaariy Na Muslim

[2] Ahmad, Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na wengineo: Swahiyh

Share

12-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kufanya Wudhuu Baada Ya Jimai Na Kabla Ya Kulala

Ni bora kabisa mume na mke wasilale baada ya kujimai mpaka wafanye wudhuu kwanza.  Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-alah haya kama zifuatazo:

 

Kwanza:

عن عائشةَ قالت: كان النبيُّ صلى الله عليه وسلم إِذا أرادَ أن [يأكل أو]  يَنامَ وهوَ جُنُبٌ غَسلَ فَرجَهُ وتَوضَّأَ وضوءه للصلاة  

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Kila alipotaka (kula) au kulala akiwa katika hali ya janaba, (yaani baada ya kujimai na kabla ya kukoga) Mtume alikuwa akiosha sehemu zake za siri na kufanya wudhuu kama wa Swalah"[1]

 

Pili:

عن أبن عمر  رضي الله عنهما أن عُمرُ  قال: يا رسول الله :  أَيَنامُ أحدُنا وهوَ جُنبٌ؟ قال: ((نَعمْ، إِذا تَوضَّأَ))  وفي رواية ((توَضَّأْ واغْسِلْ ذَكَرَكَ ثمَّ نَمْ))  وفي رواية ((نَعَمْ. لِيَتَوَضَّأْ ثُمَّ لْيَنَمْ، حَتَّى يَغْتَسِلَ إِذَا شَاءَ))  وفي أخرى: ((نَعَمْ، وَيَتَوَضَّأُ إِنْ شاءَ))

 

Imetoka kwa Ibn 'Umar رضي الله عنهما kwamba 'Umar رضي الله عنه alisema: "Ee Mjumbe wa Allaah, tunaweza kulala tukiwa katika hali ya janaba?" Mtume akajibu: "Ndio baada ya kufanya wudhuu"[2]

 

Katika riwaya nyingine "Fanya wudhuu na osha sehemu zako za siri kisha ndio ulale"[3]

 

Na katika riwaya nyingine "Ndio, unaweza kufanya wudhuu, kulala na kuoga unapopenda"[4]

 

Na katika riwaya nyingine pia: "Ndio na fanya wudhuu ukipenda"[5]

 
Riwaya ya mwisho inaonyesha kuwa wudhuu huu sio fardh.

 
 

Tatu:

عنْ عَمَّارِ بنِ يَاسِرٍ ، أنَّ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم قالَ: ((ثَلاَثَةٌ لاَ تَقْرَبُهُمْ المَلاَئِكَةٌ: جِيْفَةُ الْكَافِرِ، وَالمُتَضَمِّخُ بِالخُلُوقِ، وَالْجُنُبُ إلاَّ أنْ يَتَوَضَّأَ))

Imetoka kwa 'Ammaar ibn Yaasir kwamba "Mtume amesema: "Watu watatu Malaika hawawakaribii; maiti ya kafiri, mwanamume anayejitia manukato ya kike, na mwenye janaba (aliyefanya jimai) hadi afanye wudhuu"[6]

  
 

 

[1] Al-Bukhaariy na Muslim

[2] Al-Bukhaariy na Muslim

[3] Al-Bukhaariy na Muslim

[4] Muslim, Al-Bayhaaqiy na Abu Daawuud

[5] Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan: Swahiyh

[6] Abu Daawuud, Ahmad na wengineo: Hasan

Share

13-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Hukumu Ya Wudhuu Huu (Wa Baada Ya Kitendo Cha Ndoa Kabla Ya Kulala)

Wudhuu huu sio fardhi lakini unasisitizwa sana na umependekezwa kufanyika. Kuwa si fardhi ni kutokana na Hadiyth iliyosimuliwa na 'Umar رضي الله عنه:

عن عُمرُ أنه سَأل رسول الله صلى الله عليه وسلم:  أَيَنامُ أحدُنا وهوَ جُنبٌ؟ قال: ((نَعَمْ، وَيَتَوَضَّأُ إِنْ شاءَ)) 

 

Imetoka kwa 'Umar رضي الله عنه ambaye alimuuliza Mtume "Je, tunaweza kulala katika hali ya janaba?" Mtume alijibu "Ndio na ufanye wudhuu ukipenda"[1]

 
Hii pia inaungwa mkono na Hadiyth nyengine iliyosimuliwa na mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema,

كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَنَامُ وَهُوَ جُنُبٌ مِنْ غَيْرِ أنْ يَمَسَّ مَاء ً[حَتَّى يَقُوم بَعْد ذَلِكَ فَيَغْتَسِلْ] 

"Mtume alikuwa akilala katika hali ya janaba bila ya kuwa amegusa maji" [mpaka anapoamka baadaye na kukoga].[2]

 
Katika riwaya nyingine, mama wa waumini ‘Aaishahرضي الله عنها amesema:

 

كَانَ يَبِيتُ جُنُباً فَيَأتِيهِ بِلاَلْ، فَيُؤذِّنُه بالصَّلاة، فَيَقُومُ فَيَغْتَسِلْ، فَأَنْظُرْ إِلَى تحدر الْمَاءَ مِنْ رَأسِهِ، ثُمَّ يَخْرُجْ فَأَسْمَعْ صَوْتُهُ فِي صَلاة الْفَجْر، ثُمَّ يظِلُّ صَائِماً. قَال مُطَرِّفْ: فَقُلْت لِعُامِر: فِي رَمَضَانْ؟ قَال: نَعَمْ، سَوَاء رَمَضَان أَوْ غَيْره

"Alikuwa akipitisha usiku wake katika hali ya janaba mpaka Bilaal alipokuwa anakuja asubuhi kuadhini. Kisha alikuwa akiinuka na kukoga na huku nikiona maji yanavyomtiririka kutoka kichwani mwake, kisha akitoka na husikia sauti yake katika Swalah ya Alfajiri. Kisha hubakia amefunga". Mutwarrif akasema: 'Nikamuuliza 'Aamir: Katika mwezi wa Ramadhaan?' Akajibu: "Ndio, katika Ramadhaan na pia katika miezi mingine".[3]

 

 

 

[1] Ibn Hibbaan: Swahiyh

[2] Ibn Abi Shaybah, At-Tirmidhiy, Abu Daawuud na wengineo: Swahiyh

[3] Ibn Abi Shaybah, Ahmad na wengineo: Swahiyh

Share

14-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kutayamamu Badala Ya Wudhuu Katika Hali Ya Janaba

 

 

Vile vile inaruhusiwa kufanya Tayammum mara nyingine badala ya wudhuu kabla ya kulala. Hii ni kutokana na Hadiyth ya Bibi ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema:

 

كانَ رسولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلّم إذا أجنبَ فأرادَ أنْ  ينامَ توضأَ

 

"Mtume alipokuwa katika hali ya janaba na kila alipotaka kwenda kulala alikuwa akichukua wudhuu au akitayammum".[1]





 





[1] Al-Bayhaaqiy na Ibn Abi Shaybah: Hasan

Share

15-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kukoga Ni Bora Kabla Ya Kulala

 

 

Inapendeza kukoga kuliko uwezekano uliotajwa hapo juu (wa kutawadha baada ya janaba kabla ya kulala) kama ilivyo wazi katika Hadiyth ya 'Abdullah ibn Qays ambaye amesema,

 

سَأَلْتُ عَائِشَةَ كَيْفَ كَانَ كان صلى الله عليه وسلم  يَصْنَعُ فِي الْجَنَابَةِ؟ أَكَانَ يَغْتَسِلُ قَبْلَ أَنْ يَنَامَ أَمْ يَنَامُ قَبْلَ أَنْ يَغْتَسِلَ؟ قَالَتْ: كُلُّ ذٰلِكَ قَدْ كَانَ يَفْعَلُ، رُبَّمَا اغْتَسَلَ فَنَامَ، وَرُبَّمَا تَوَضَّأَ فَنَامَ. قُلْتُ: الْحَمْدُ لله الَّذِي جَعَلَ فِي الأَمْرِ سَعَةً

 

"Nilimuuliza mama wa waumini ‘Aaishah vipi Mtume alikuwa akifanya katika hali ya janaba? Je, alikoga kabla ya kulala au alilala kabla ya kukoga?" Alijibu: "Alifanya vyote hivyo, mara nyingine alikoga kisha akalala na mara nyingine alitawadha kisha akalala". "Nikasema: Sifa zote Anastahiki Allaah Aliyejaalia wepesi mkubwa katika jambo hili".[1]

 

 

 

 



[1] Muslim, Ahmad na Abu 'Awwaanah

Share

16-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Makatazo Ya Jimai (Kitendo Cha Ndoa) Wakati Wa Hedhi

Imekatazwa kwa mume kufanya jimai (kitendo cha ndoa) na mkewe wakati yuko kwenye hedhi. Hii ni dhahiri kutokana na Aayah ya Qur-aan:

 

((وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْمَحِيضِ قُلْ هُوَ أَذًى فَاعْتَزِلُواْ النِّسَاء فِي الْمَحِيضِ وَلاَ تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّىَ يَطْهُرْنَ فَإِذَا تَطَهَّرْنَ فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللّهُ إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ))

 

"Na wanakuuliza juu ya hedhi. Waambie, huo ni uchafu. Basi jitengeni na wanawake wakati wa hedhi. Wala msiwaingilie mpaka watwaharike. Wakishatoharika (na kujitoharisha) basi waendeeni Alivyokuamrisheni Allaah. Hakika Allaah Huwapenda wanaotubu na Huwapenda wanaojitakasa" (Al-Baqarah 2:222)

 
Vile vile kuna Hadiyth kuhusu mas-ala haya, miongoni mwa hizo ni:

Kwanza:

 

((مَنْ أَتَى حَائِضاً  أَوْ امْرَأَةً فِي دُبُرهَا، أَوْ كَاهِناً؛ فَصَدَقَهُ بِمَا يَقُول  فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أنْزلَ عَلىَ مُحَمَّد)) 

 

"Yeyote atakayejimai (kufanya kitendo cha ndoa) na mwanamke mwenye hedhi, au kwa kutumia njia ya nyuma, au kumwendea kahini (mtabiri) na kuamini aliyoambiwa, basi amekufuru yale aliyoteremshiwa Muhammad"[1]

 

Pili:

 

عن أنَسِ بنِ مَالِكٍ، قال: إنَّ الْيَهُودَ كَانَتْ إذَا حَاضَتْ مِنْهُم المَرْأةُ أخْرَجُوهَا مِنْ الْبَيْتِ وَلَمْ يُؤَاكِلُوهَا وَلَمْ يُشَارِبُوهَا وَلَمْ يُجَامِعُوهَا في الْبَيْتِ فَسُئِلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنْ ذَلِكَ، فأنْزَلَ الله تَعَالَى ذِكْرُهُ: ((وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ المَحِيضِ قُلْ هُوَ أذًى فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ في المَحِيضِ)) إلَى آخِرِ الآيَةِ. فقال رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((جَامِعُوهُنَّ في الْبُيُوتِ، وَاصْنَعُوا كُلَّ شَيْىءٍ غَيْرَ النِّكَاحِ)). فقالت الْيَهُودُ: مَا يُرِيدُ هَذَا الرَّجُلُ أنْ يَدَعَ شَيْئاً مِنْ أمْرِنَا إلاَّ خَالَفَنَا فِيهِ. فَجَاءَ أُسَيْدُ بنُ حُضَيْرٍ وَعَبَّاد بنُ بِشْرٍ إلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم فقالا: يارسولَ الله صلى الله عليه وسلم إنَّ اليَهُودَ تَقُولُ كَذَا وكَذَا، أفَلاَ نَنْكِحَهُنَّ في المَحِيضِ؟ فَتَمَعَّرَ وَجْهُ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم حَتَّى ظَنَنَّا أن قَدْ وُجِدَ عَلَيْهِمَا، فَخَرَجَا، فَاسْتَقْبَلَتْهُمَا هَدِيَّةٌ مِنْ لَبَنِ إلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَبَعَثَ في آثَارِهِمَا فَسَقاهُما، فَظَنَنَّا أنَّهُ لَمْ يَجِدْ عَلَيْهِمَا   

 

Kutoka kwa Anas ibn Maalik ambaye amesema: "Anapokuwa mmoja wa wanawake wao wako katika hedhi, Mayahudi walikuwa wakimuweka nje ya nyumba, na huwa hawali, hawanywi wala kulala naye katika nyumba. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipoulizwa jambo hili, Allaah سبحانه وتعالى Aliteremsha Aayah "Na wanakuuliza juu ya hedhi. Waambie, huo ni uchafu. Basi jitengeni na wanawake wakati wa hedhi" Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema:  "Kuweni nao katika nyumba na mfanye kila kitu nao isipokuwa jimai pekee". Mayahudi wakasema: 'Mtu huyu hataki kuacha lolote tulifanyalo ila alipinge'.  Akaja Usayd ibn Khudhwayr na 'Abbaad ibn Bishr wakasema: 'Ee Mjumbe wa Allaah, hakika Mayahudi wanasema kadha wa kadha, je, kwa nini tusifanye jimai wakati wa hedhi (ili tutofautiane na Mayahudi)?' Uso wa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ukabadilika hadi kwamba walifikiri amewakasirikia. Wakaondoka, na walipokuwa wanatoka, wakaona zawadi ya maziwa imeletwa kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamtuma mtu kuwafuata na kuwapa kinywaji cha maziwa, wakatambua kuwa hakuwakasirikia".[2]

 

 

[1] Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na wengineo: Swahiyh

[2] Muslim, Abu 'Awwaanah na Abu Daawuud

Share

17-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kafara (Malipo) Ya Mtu Anayejimai Katika Hedhi

 

 

Yeyote aliyeteleza, akafanya kosa la jimai na mke wake wakati yuko katika hedhi na kabla ya kuwa ametoharika, itampasa atoe thamani ya uzito wa dinari ya dhahabu au kiasi cha gramu 4.25 (kwa uhakika zaidi ni 4.2315) au nusu yake.

 
Hii ni kutokana na Hadiyth iliyopokelewa kutoka kwa 'Abdullaah bin 'Abbaas عنهما رضي الله kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم katika uhusiano wa mtu atakayemuingilia mkewe wakati yuko kwenye hedhi kama ifuatavyo:

 

عبد الله ابن عباسٍ رضي الله عنهما  فـي الَّذي يأتـي امرأَتَهُ وَهِيَ حَائِضٌ قال: ((يَتَصَدَّقُ بدينارٍ أو نصفِ دينارٍ))

"Mwache atoe dinari moja katika sadaka au nusu ya dinari"[1]
 

 


[1] At-Tirmidhiy, Abu Daawuud, At-Twabaraaniy na wengineo: Swahiyh

Share

18-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Yanayoruhusiwa Anapokuwa Katika Hedhi

Mume anaruhusiwa kustarehe na mkewe kwa njia yoyote isipokuwa sehemu zake za siri anapokuwa katika Hedhi. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu jambo hili:

Kwanza:

((...اصْنَعُوا كُلَّ شَيْءٍ إِلاَّ النِّكَاحَ))

"…fanyeni kila kitu isipokuwa jimai pekee"[1]

 
 

Pili:

عن عَائِشَةَ رضي الله عنها ، قَالَتْ:  كانَ رَسُولُ اللَّهِ، يَأْمُرُ إِحْدَانَا إِذا كَانَتْ حَائِضاً أَنْ تَتَّزِرََ ثُمَّ يُضَاجِعُهَا زَوْجُهَا وَقالَتْ مَرَّةً: يُبَاشِرُهَا.

Kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Tulipokuwa katika siku zetu (hedhi) Mtume alikuwa akituamrisha tuvae nguo kiunoni ili mume aweze kulala naye". Na akasema (mama wa waumini ‘Aaishah) pia …"Mumewe aweze kumkumbatia na kumpapasa".[2]

 

Tatu:

عن بَعْضِ أزْوَاجِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قالَتْ: إنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إذَا أرَادَ مِنَ الْحَائِضِ شَيْئاً ألْقَى عَلَى فَرْجِهَا ثَوْباً [ ثم صنع ما أراد]  

Kutoka kwa mmoja wa wake zake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipokuwa anataka kitu (kufurahi naye) kutoka kwa wake zake siku za hedhi, alikuwa anaweka nguo katika sehemu zake za siri kisha hufanya anavyotaka".[3]

 

 


[1] Muslim, Abu 'Awwaanah na Abu Daawuud

[2] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[3] Abu Daawuud: Swahiyh

Share

19-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Wakati Gani Unaruhusiwa Kurudia Jimai Baada Ya Hedhi?

Atakapokuwa ametwaharika kutokana na damu ya hedhi yote na kutoka kwake kumesimama kabisa, hapo anaruhusiwa kurudia kitendo cha jimai baada ya kuosha sehemu inayotoka damu, akafanya wudhuu au akakoga josho kamili (Ghuslu). Vyovyote kati ya haya matatu atakavyofanya itaruhusiwa kwao kurudia kitendo cha jimai kutokana na kauli ya Allaah سبحانه وتعالى katika Qur-aan:

  

َ ((فَإِذَا تَطَهَّرْنَ فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللّهُ إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ))

 
((Wakishatoharika basi waendeeni Alivyokuamrisheni Allaah. Hakika Allaah Huwapenda wanaotubu na Huwapenda wanaojitakasa))

(Al-Baqarah 2:222)
 

Huu ni msimamo wa Ibn Hazm, 'Atwaa, Qataadah, Al-Awzaa'iy na Daawuud Adh-Dhwaahiriy na Mujaahid kama alivyosema Ibn Hazm, "Zote tatu hizi ni Twahara, kwa hiyo yoyote mojawapo atakayefanya baada ya kusimama hedhi yake, basi atakuwa ni halali kwa mumewe."

Kauli hiyo hiyo inatumika kumaanisha kuwa ni kuosha sehemu ya siri katika Aayah iliyoteremshwa kuhusu watu wa Qubaa:

 

((فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُواْ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُطَّهِّرِينَ))

  

"…Humo wamo watu wanaopenda kujitakasa. Na Allaah Anawapenda wanaojitakasa" (At-Tawbah 9:108)

Hata hivyo, hakuna dalili yoyote katika Aayah au Sunnah inayoshurutisha Aayah "…Wakishatoharika basi waendeeni Alivyokuamrisheni Allaah…" (Al-Baqarah: 222) inayohusika katika maana tatu hizo, na kufanya hivyo kunahitaji dalili. (huu ni msimamo wa Ibn Hazm)

 

 

Share

20-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuhalalishwa ‘Azl (Kuchopoa Kabla Ya Kushusha)

Kwanza:

عن جابر رضي الله عنه قال:  كنّا نَعزلُ والقرآنُ يَنزِل.  وفي رواية:  كُنَّا نَعْزِلُ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم  :فَبَلَغَ ذلِكَ نَبِيَّ اللهِ صلى الله عليه وسلم فَلَمْ يَنْهَنَا عَنْهُ

Imetoka kwa Jaabir رضي الله عنه amesema: "Tulikuwa tunafanya 'azl wakati tunawaingilia wake zetu (hatumwagi ndani; tunachomoa utupu na kumwaga nje) na Qur-aan ilikuwa ikiteremshwa"[1]

 
Na katika riwaaya nyingine amesema: "Tulikuwa tukifanya tendo la ‘azl wakati wa maisha ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na hakutukataza kufanya hivyo".[2]

 
 

Pili:

 

عن أبي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ قال: جآء رَجُلٌ إِلى رَسُولِ الله صَّلى الله عليه وسلم فَقَال: إِنَّ لِي وَلِيدة وَأنا أعْزِلُ عَنْها  وَأَنَا أُرِيدُ ما يُرِيدُ الرِّجَالُ وَإنَّ الْيَهُودَ  زَعَمُوا أَنَّ الْمَوءُودَةُ الصُّغْرَى  الْعَزْلُ؟ فَقَالَ رَسُولُ الله: ((كَذَبَتْ يَهُودُ، لَوْ أَرَادَ اللَّهُ أَنْ يَخْلُقَهُ لَمْ تَسْتَطِعْ أَنْ تَصْرِفَهُ))

 

Imetoka kwa Abu Sa'iydil-Khudriy amesema: "Alikuja mtu kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: 'Ninaye  kijakazi (unaomiliki mkono wa kulia) na nilikuwa nikifanya ‘azl kwake, na mimi ninataka yale watakayo wanaume, na Mayahudi wanadai kuwa, 'Azl ni aina ndogo ya uuaji'. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Mayahudi wameongopa, Mayahudi wameongopa. Allaah Angelitaka kuumba mtoto usingeliweza kuzuia))[3]

 

Tatu:

 

عَنْ جَابِرٍ أَنَّ رَجُلاً أَتَى رَسُولَ اللّهِ فَقَالَ: "إِنَّ لِي جَارِيَةً هِيَ خَادِمُنَا وَسَانِيَتُنَا، وَأَنَا أَطُوفُ عَلَيْهَا وَأَنَا أَكْرَهُ أَنْ تَحْمِلَ". فَقَالَ: ((اعْزِلْ عَنْهَا إِنْ شِئْتَ. فَإِنَّهُ سَيأْتِيَهَا مَا قُدِّرَ لَهَا)) فَلَبِثَ الرَّجُلُ. ثُمَّ أَتَاهُ فَقَالَ: "إِنَّ الْجَارِيَةَ قَدْ حَبِلَتْ". فَقَالَ ((قَدْ أَخْبَرْتُكَ أَنَّهُ سَيَأْتِيهَا مَا قُدِّرَ لَهَا))

Imetoka kwa Jaabir kwamba alikuja mtu kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: 'Ninaye kijakazi ambaye anatuhudumia na kumwagia maji mitende yetu. Wakati mwingine humuendea (humuingilia) lakini sikupenda ashike mimba yangu. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Fanya ‘azl kwake, lakini kilichokadiriwa kwake huwezi kukizuia, kitakuwa)). Baada ya muda yule mtu akaja kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na akasema: 'Ameshika mimba!' Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamuambia, ((Nilikuambia kuwa vyovyote ilivyokadiriwa itakuwa))[4]
 

 

[1] Al-Bukhaariy na Muslim

[2] Muslim, An-Nasaaiy na At-Tirmidhiy

[3] An-Nasaaiy katika "Al-Ishraah", Abu Daawuud na wengineo: Swahiyh

[4] Muslim, Abu Daawuud na wengineo

Share

21-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kutofanya ‘Azl Ni Bora Zaidi

Kutokufanyika hiyo ‘azl kunapendekezwa kutokana na sababu mbalimbali:

Kwanza:

Ina madhara kwa mwanamke kwa vile inampunguzia starehe ya tendo lile kwani anayefanya hiyo ‘azl huwa anamkatisha kufika kileleni. Na hata ikiwa amekubali mwenyewe, bado kutakuwa kuna upungufu ufuatao:

 

Pili:

Tendo hilo linakanusha mojawapo ya kusudio la ndoa ambalo ni kukuza Ummah Wa Kiislamu kutokana na kizazi kama alivyosema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم:

 

((تَزَوَّجُوا الْوَدُودَ الْوَلُودَ فَإِني مُكَاثِرٌ بِكُمُ الأَنْبِيَاءَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ))

((Oeni wapenzi wazaao, kwani nitashindana na Mitume wengine kwa idadi ya wafuasi siku ya Qiyaamah))[1]

Na hii ndio maana Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alifananisha kama ni 'uuaji mdogo wa watoto wadogo' (ingawa si kama imeharamishwa kama 'uuaji wa watoto wadogo ilivyoharamishwa). Alipoulizwa alisema:

 

((ذََلِكَ الْوأد الْخَفِيِّ )).

 

((Huu ni uuaji wa siri wa watoto wadogo))[2]

Kwa sababu hii pia, yeye Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alionyesha kwamba kutokufanya ni bora zaidi katika Hadiyth iliyosimuliwa na Abu Sa'iydil-Khudriy رضي الله عنه akisema "’azl ilitajwa akiweko Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na akasema:

 

((ولم يَفْعَلْ ذَلِكَ أَحَدكُمْ؟!)) ( وَلَمْ يَقُلْ: فَلاَ يَفْعَلْ ذَلِكَ أَحَدكُمْ)  (( فَإَنَّهُ لَيْسَتْ نَفْس مَخْلُوقَةٌ إِلاَّ الله خَالِقُهَا))  وفي رواية ، فقال: ((وَإِنَّكُمْ لَتَفْعََلُونَ، وَإِنَّكُمْ لَتَفْعََلُونَ، وَإِنَّكُمْ لَتَفْعََلُونَ  مَا مِنْ نِسْمَةُ كاَئِنَة إِلى يَوْمِ اْلقِيَامَة إِلاَّ هِيَ كَائِنَة))  

((Kwa nini anafanya mmoja wenu?)) (tanbihi kwamba hakusema "asifanye mmoja wenu") ((Allaah Ndiye Muumba wa kila nafsi)) [3]

 
Katika riwaaya nyingine amesema: ((Mtafanya, mtafanya, mtafanya. Hakuna idadi ya watu iliyopo hadi siku Ya Qiyaamah ila itabaki)) (itakuwepo) (Maana: Hakuna mtu atakayeweza kupangua mipangilio aliyopanga Allaah, yaani kama hata mtu akitaka kuzuia kiumbe kisije kwa kufanya 'azl', basi kitakuja tu maadam Allaah Keshapanga iwe hivyo. Wa Allaahu A'alam)

 


[1] Abu Daawuud, An-Nasaaiy na wengineo: Swahiyh

[2] Muslim, Ahmad na Al-Bayhaaqiy

[3] Muslim

Share

22-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Nia Zinazopaswa Kuwekwa Na Wanandoa

Wote wawili, mume na mke waingie katika ndoa kwa kuwa na nia zifuatazo:

Kujiweka huru katika kutimiza matamanio ya jimai na kuhifadhi nafsi zao kutumbukia katika yale Aliyoyakataza Allaah سبحانه وتعالى (yaani uzinifu). Juu ya hivyo wanaandikiwa thawabu kama thawabu ya sadaka kila mara wanapojimai. Hii ni kutokana na Hadiyth ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ifuatayo iliyotoka kwa Abu Dharr:

 

أَنَّ نَاساً مِنْ أَصْحَابِ النَّبِيِّ قَالُوا لِلنَّبِيِّ : يَا رَسُولَ اللّهِ ذَهَبَ أَهْلُ الدُّثُورِ بِالأُجُورِ. يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي. وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ. وَيَتَصَدَّقُونَ بِفُضُولِ أَمْوَالِهِمْ. قَالَ: ((أَوَ لَيْسَ قَدْ جَعَلَ اللّهِ لَكُمْ مَا تَصَّدَّقُونَ؟ إِنَّ بِكُلِّ تَسْبِيحَةٍ صَدَقَةً. وَكُلُّ تَكْبِيرَةٍ صَدَقَةٌ. وَكُلُّ تَحْمِيدَةٍ صَدَقَةٌ. وَكُلُّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةٌ. وَأَمْرٌ بِالْمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ. وَنَهْيٌ عَنْ مُنْكَرٍ صَدَقَةٌ. وَفِي بُضْعِ أَحَدِكُمْ صَدَقَةٌ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللّهِ، أَيَأْتِي أَحَدُنَا شَهْوَتَهُ وَيَكُونُ لَهُ فِيهَا أَجْرٌ؟ قَالَ: ((أَرَأَيْتُمْ لَوْ وَضَعَهَا فِي حَرَامٍ أَكَانَ عَلَيْهِ فِيهَا وِزْرٌ؟ فَكَذٰلِكَ إِذَا وَضَعَهَا فِي الْحَلاَلِ كَانَ لَهُ أَجْرٌ))

Baadhi ya Maswahaba wa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم walimwambia: 'Ee mjumbe wa Allaah, wakwasi miongoni mwetu wamechukua thawabu (za Aakhirah). Wanaswali kama tunavyoswali, wanafunga kama tunavyofunga na wanatoa Sadaka kutoka ziada ya mali zao'. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Kwani Allaah Hakukujaalieni na nyinyi kuweza kutoa Sadaka? Hakika kila mara mkisema  'Subhaana-Allaah' (Ametakasika Allaah) ni Sadaka, na kila mkisema 'Allaahu Akbar' (Allaah ni Mkubwa Zaidi) ni sadaka, na kila mara mkisema 'AlhamduliLlaah' (Sifa zote ni za Allaah) ni Sadaka, na kila mkisema 'Laa Ilaaha Illa Allaah' ni Sadaka, na kuamrisha mema ni Sadaka, na kukataza maovu ni Sadaka na katika uhusiano wenu wa kujimai ni Sadaka)). Maswahaba wakasema:  'Ee Mjumbe wa Allaah, je, kuna thawabu ikiwa mmoja wetu atajitosheleza matamanio yake ya kujimai?' Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Je, hamuoni kwamba ikiwa atajitosheleza kwa yaliyo haramu si ingelikuwa ni dhambi juu yake?  Basi, vile vile atakapojitosheleza (kujimai) kwa njia ya halali atapata thawabu))[1]

 

 


[1] Muslim, An-Nasaaiy katika "Al-Ishraah" na Ahmad

Share

23-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Afanye Nini Siku Ya Pili Baada Ya Ndoa

Inapendekezeka kwa mume kwenda kwa jamaa zake ambao walikuja kumtembelea nyumbani kwake, siku ya pili kuwaamkia na kuwaombea. Wao pia inapendekezeka kumfanyia hivyo hivyo, kama ilivyo katika Hadiyth ifuatayo iliyosimuliwa na Anas رضي الله عنه:

 

أَوْلَم رَسُولُ الله إذ بنى بِزَيْنَبْ فَأَشْبَعَ الْمُسْلِمِينَ خُبْزاً وَلَحْماً ثُمَّ خَرَجَ إِلَى أُمَّهَاتِ الْمُؤْمِنِينَ فَسَلَّمَ عَلَيْهِنَّ وَدَعَا لَهُنَّ وَسَلَّمْنَّ عَلَيْه وَدعونَ لَهُ فَكَانَ يَفْعَلْ ذَلِكَ صَبِيحَة بنائه

"Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alialika karamu asubuhi ya usiku wa harusi yake na mama wa waumini Zaynab, ambayo aliwalisha Waislamu mikate na nyama mpaka wakashiba. Kisha akaenda kwa Mama za Waumini (wake zake wengine) akawasalimia na kuwaombea, nao wakarudisha (maamkizi na Du'aa) kwa upole. Hivi ndivyo alivyokuwa akifanya asubuhi baada ya usiku wa ndoa"[1]

 

 

[1] Ibn Sa'ad na An-Nasaaiy: Swahiyh

Share

24-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Nyumba Lazima Iwe Na Sehemu Ya Kuogea

Wanaofunga ndoa lazima wawe na sehemu ya kuogea nyumbani mwao. Na mume asimruhusu mkewe kwenda kuoga katika vyoo vya nje.  Hii imekatazwa na kuna Hadiyth mbali mbali zinazokataza jambo hili miongoni mwa hizo ni:

 
Kwanza:

 

عن جابر أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: ((مَنْ كانَ يُؤْمِنُ بالله واليومِ الآخِرِ فلا يُدْخِلْ حَلِيلَتَهُ الحَمَّامَ  وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بالله وَاليَوْمِ الآخِرِ فلا يُدْخِلْ الحَمَّامَ إلا بِمئزَرٍ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بالله وَاليَوْمِ الآخِرِ فلا يَقْعُدْ على مائِدَةٍ يُشْرَبُ عَلَيْها الخَمْرُ))

 
Imetoka kwa Jaabir ambaye amesema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alisema, ((Yeyote anayemuamini Allaah na siku ya mwisho, basi asimuache mke wake kwenda vyoo vya nje (vitumiwavyo na watu wote, Mwenye kuamini Allaah na Siku ya mwisho, asiende bafuni isipokuwa na (awe amevaa) nguo ya kiunoni. Na yeyote anayemuamini Allaah na siku ya mwisho asikae katika meza inayonywewa ulevi)) [1]

Pili:

Imetoka kwa Ummu Ad-Dardaa ambaye amesema:

 

خرجت من الحمام فلقيني رسول الله صلى الله عليه وسلم فقال: ((مِنْ أَيْنَ يا أُمَّ الدَّرْدَاءِ؟)) قالت: من الحمام، فقال: ((وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ مَا مِنْ امْرَأَةٍ تَضَعُ ثِيَابِها فِي غَيْرِ بَيْتِ أَحَدٍ مِنْ أُمَّهاتِها الإِ وَهِيَ هاتِكَةٌ كُلَّ سِتْرِ بَيْنَها وَبَيْنَ الرَّحْمٰنِ))

 

"Nilitoka kutoka vyoo vya nje nikakutana na Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم ambaye aliniambia: ((Umetoka wapi ewe Ummu Ad-Dardaa?)) Nikasema: Kutoka vyooni. Kisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake. Kila mwanamke anayevua nguo zake popote isipokuwa nyumba ya mmoja wa mama yake, atakuwa ameondosha stara yake mbele ya Ar-Rahmaan))[2]

 

Tatu:

Imetoka kwa Abu Al-Maliyh ambaye amesema:

 

دخل نسوة من أهل الشام على عائشة رضي الله عنها فقالت: لعلكن من الكورة التي تدخل نساؤها الحمام، سمعت رسول الله يقول: ((أَيُّما امْرَأَة وَضَعَتْ ثيابَها في غَيْرِ بَيْتِ زَوْجِها فَقَدْ هَتَكَتْ سِتْرَها فيما بَيْنَها وَبَيْنَ الله عَزَّ وَجَلَّ))

 

"Baadhi ya wanawake kutoka Ash-Shaam waliingia kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها na akasema: 'Mnatoka wapi?'  Wanawake wakajibu: 'Sisi ni watu wa Ash-Shaam' (ambayo sasa ni Syria). Bibi ‘Aaishah akasema: 'Labda nyinyi mnatoka katika wilaya (kitongoji) ambayo inawaruhusu wanawake kuingia katika vyoo vya nje?' Wakasema: 'Ndio'. Akasema: 'Ama mimi nimemsikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akisema: ((Mwanamke yeyote atakayevua nguo zake nje ya nyumba ya mumewe, amechana shela (ameondosha stara) ya hayaa baina yake na Allaah))[3]

 

[1] Al-Haakim, At-Tirmidhiy na wengineo: Swahiyh

[2] Ahmad: Swahiyh

[3] At-Tirmidhiy, Abu Daawuud na wengineo: Swahiyh

Share

25-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Makatazo Ya Kutangaza Siri Za Chumbani

Inakatazwa aidha mume au mke kueneza siri zao zozote za chumbani kwa mtu yeyote wa nje. Hadiyth zifuatazo zimekataza hivyo:

 

Kwanza:

 

((إِنَّ مِنْ أَشَرِّ النَّاسِ عِنْدَ اللّهِ مَنْزِلَةً يَوْمَ الْقِيَامَةِ، الرَّجُلَ يُفْضِي إِلَى امْرَأَتِهِ، وَتُفْضِي إِلَيْهِ، ثُمَّ يَنْشُرُ سِرَّهَا))

((Hakika miongoni mwa watu waovu kabisa siku ya Qiyaamah ni mwanamume anayemuingilia mkewe kwa jimai akamuitikia, kisha akaeneza siri zake))[1]

 

Pili:

 

عن أسماء بنت يزيد : أنها كانت عند رسول الله صلى الله عليه وسلّم ، والرجال والنساء قعود عنده . فقال: ((لَعَلَّ رَجُلاً يَقُولُ ما يَفْعَلُ اهْلِهِ، وَلَعَلَّ امْرَأَةً تُخْبِرُ بِمَا فَعَلَتْ مَعَ زَوْجِهَا؟)) ازَمَّ القَوْمُ، فَقلت: أي والله يا رسول الله، إنهم ليفعلون، وإنهنّ ليفعلن، قال: ((فَلا تَفْعَلُوا، فًّانَّمَا مَثَلُ ذَلِكَ مَثَلُ شَيْطانٍ لَقِيَ شَيْطَانَةً فَغَشِيَهَا وَالنَّاسُ يَنْظُرُونَ))

 

Imetoka kwa Asmaa bint Yaziyd ambaye amesema: "Alikuwa kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  na walikuweko wanaume na wanawake wamekaa. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Huenda mume akajadiliana anayoyafanya na mkewe au huenda mwanamke akamhadithia mtu aliyoyafanya na mumewe?)) Watu walikuwa kimya. Kisha nikasema: 'Ee Mjumbe wa Allaah, hakika wanaume na wanawake wote hunafanya hivyo'. Kisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Msifanye hivyo kwani ni kama mfano shaytwaan mwanamume amekutana na shaytwaan mwanamke njiani wakawa wanafanya jimai na huku watu wanawatazama))[2]

 

 

[1] Muslim, Ibn Abi Shaybah, Ahmad na wengineo

[2] Ahmad: Hasan au Swahiyh kutokana na kukubaliana (na masimulizi mengine)

Share

26-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Wajibu Wa Waliymah (Karamu)

Mume lazima afanye karamu baada ya kufunga ndoa.  Hii ni kutokana na amri ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliyompa 'Abdur-Rahmaan ibn 'Awf afanye na pia kutokana na Hadiyth iliyosimuliwa na Buraydah ibn Hasiyb ambaye amesema:

 

لَمَّا خَطَبَ عَلِي فَاطِمَةُ رَضِيَ الله عَنْهُ قال: قال رَسُولُ الله صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّمْ:  (( إِنَّهُ لاَ بُدَّ لِلْعرْس  مِنْ وَلِيمَة )) وَفِي رِوَايَة ((لِلْعَرُوس))

"'Aliy alipomposa Faatwimah alisema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: ((Hapana budi iwepo karamu, hapana budi bwana harusi afanye karamu)). Msimuliaji amesema: Sa’ad akasema, mimi nitaleta kondoo, na mwingine akajitokeza akasema, mimi nitaleta kadha wa kadha katika mahindi. Katika Riwaaya nyingine ma-Answaar walikusanya mahindi mengi[1]

 

 


[1] Ahmad na At-Twabaraaniy: Isnaad yake inakubalika kama alivyosema Al-Haafidhw Ibn Hajar katika Fathul-Baariy 9/188

Share

27-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Sunnah Ya Waliymah (Karamu)

Yafuatayo yanapaswa kutekelezwa katika karamu ya ndoa:

Kwanza:

Ifanyike siku tatu baada ya usiku wa ndoa kwani hii ndio desturi ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم iliyotufikia.[1]

 

 

فَعَنْ أَنَسْ رَضِيَ الله عَنْهُ قال:  بَنَى رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم  بِاِمْرَأةٍ، فَأَرْسَلَنيِ فَدَعَوْتُ رِجَالاً عَلىَ الطَّعَام 

Imetoka kwa Anas ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipofunga ndoa aliniita ili nialike baadhi ya wanaume kuja kula chakula"[2]

 

 
Vile vile imetoka kwa Anas ambaye amesema:

 

تزوَّج رسولُ الله صلى الله عليه وسلّم صفيَّة، وجعل عَتْقَها صَدَاقَها، وجعل الوليمةَ ثلاثةَ أيَّامٍ، وبَسَط نِطعاً جاءت به أمُّ سُليم، وألقى عليه أَقِطاً وتَمراً، وأطعمَ النَّاسَ ثلاثةَ أيَّامٍ

 

"Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alimuoa Swafiyah na uhuru wake ndio ulikuwa mahari yake. Alifanya karamu kwa muda wa siku tatu"[3]

 

Pili:

Inapasa kuwaalika watu wema katika karamu yake ikiwa ni matajiri au maskini.

 

عن أَبي سَعِيدٍ، أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ الله يقولُ: ((لا تُصَاحِبْ إِلاَّ مُؤْمِناً وَلاَ يَأْكُلْ طَعَامَكَ إِلاَّ تَقِيٌ))

Kutoka kwa Sa'iyd kwamba amemsikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akisema: ((Msiwe marafiki wa wowote isipokuwa waumini na wale chakula chenu watu wema pekee))[4]

 

 

Tatu:

Ikiwa mtu ana uwezo, afanye karamu ya kondoo mmoja au zaidi kutokana na Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ أَنَسْ رضي الله عنه قال: إِنَّ عَبْدُ الرَّحْمن بِنْ عَوْف قَدِمَ الْمَدِينَةَ  فآخى  رسولُ اللَّهِ بَيْنَهُ وبَيْنَ سَعْدِ بنِ الرَّبيعِ الأَنْصََارِي [فَانْطَلَقَ بِِهِ سَعَدْ إِلَى مَنْزِلِهِ، فَدَعَا بِطَعَام فأَكلَا]، فقال له سعد: أي أخي! أنا أكثر أهل المدينة ( وفي رواية: أكثر الأنصار )مالاً، فانظر شطر مالي فخذه ( وفي رواية: هلم إلى حديقتي أشاطركها  (، وتحتي امرأتان [وأنت أخي في الله  لا امرأة لك]، فانظر أيهما أعجب إليك [فسمها لي] حتى أطلقها [لك] [فإذا انقضت عدتها فتزوجها]، فقال عبد الرحمن: [لا والله]، بارك الله لك في أهلك ومالك، دلوني على السوق، فدلوه على السوق، فذهب، فاشترى وباع، وربح، [ثم تابع الغدو] فجاء بشيء من أقِطٍ- لبن مجفف يابس مستجر يطبخ به- وسمن [قد أفضله] [فأتى به أهل منزله]، ثم لبث ما شاء الله أن يلبث، فجاء وعليه ردع زعفران ( وفي رواية: وضر من خلوق )، فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم :(( مهْيَم؟)) فقال: يا رسول الله! تزوجت امرأة [من الأنصار]، فقال ((ما أصدقتها؟)) قال: وزن نواة من ذهب، قال: ((فبارك الله لك )) أولم ولو بشاة، [فأجاز ذلك]. قال عبد الرحمن: فلقد رأيتني ولو رفعت حجراً لرجوت أن أصيب [تحته] [ذهباً أو فضة]، [قال أنس: لقد رأيته قُسِم لكل أمرأة من نسائه بعد موته مائة ألف دينار]  ))

Anas amesema: "'Abdur-Rahmaan bin ‘Awf alikuja Madiynah na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akajengea udugu pamoja na Sa'ad ibn Ar-Rabiy' Al-Answaariy. Sa'ad alimchukua nyumbani kwake, akaagiza chakula na wakala pamoja. Kisha Sa'ad akasema: 'Ee ndugu yangu, mimi ni tajiri mkubwa kabisa katika watu wa Madiynah (katika riwaaya nyingine: "Katika Answaar" basi tazama nusu ya mali yangu na uchukue (katika riwaaya nyingine: 'Na nitagawa bustani yangu nusu). Pia ninao wake wawili (ilhali ndugu yangu kwa Allaah huna mke) basi mtazame yupi katika hao wangu aliyekupendeza zaidi ili nimpe talaka kwa ajili yako. Kisha baada ya kumalizika wakati wake wa kusubiri wa sheria (eda ya talaka) unaweza kumuoa. 'Abdur-Rahmaan akasema: 'Hapana Wa-Allaahi, Allaah Akubariki katika ahli na mali yako. Nionyeshe lilipo soko'. Akaonyeshwa njia ya sokoni akaenda huko. Akanunua na kuuza na kupata faida. Ilipofika jioni, alirudi kwa watu wake wa nyumbani akiwa na maziwa makavu ya kupikia na samli. Baada ya hapo siku zikapita hata akatokea siku moja na alama za zaafarani katika nguo yake. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akauliza, ((Kitu gani hiki?)) Akasema: 'Ee Mjumbe wa Allaah, nimeoa mwanamke miongoni mwa wanawake wa ki-Answaar. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  akauliza: ((Umempa nini mahari yake?)) Akasema: 'Abdur-Rahmaan akajibu, 'Dhahabu ya uzito wa dirham tano'.  Kisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Allaah Akubariki. Fanya karamu japo ya kondoo mmoja)) 'Abdur-Rahman akasema: 'Nilijiona niko katika hali ya kwamba ningelinyanyua jiwe lolote, ningetegemea kupata dhahabu au fedha chini yake'. Anas anasema: "Niliona baada ya mauti yake kila mke wake alirithi Dinari laki moja"[5]

 

 

  عَنْ أَنَسَ بْنَ مَالِكٍ ، يَقُولُ:  مَا رَأَيْت رَسُولُ الله صَلى الله عليه وسلم أَوْلَمَ عَلَى امْرَأَةْ مِنْ نِسَائِهِ مَا أَوْلَمَ عَلىَ زَيْنَبْ، فَإنَّهُ ذَبَحَ شَاة، [قَالَ: أَطْعَمَهُمْ خُبْزاً وَلَحْماً حَتىَّ تَرَكُوه]  

Vile vile kutoka kwa Anas ambaye amesema: "Sijapata kumuona Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akifanya karamu kubwa kama karamu ya ndoa kama aliyofanya kwa Zaynab. Alichinja kondoo na kulisha watu wote nyama na mikate mpaka wakashiba"[6]

 

 

[1] Fat-hul Baariy 9/242-244

[2] Al-Bukhaariy na Al-Bayhaaqiy

[3] Abu Ya'laa na wengine: Hasan

[4] Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na wengineo: Swahiyh

[5] Al-Bukhaariy, An-Nasaaiy na wengineo

[6] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

Share

28-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Waliymah (Karamu) Ya Ndoa Inaweza Kuwa Chochote Bila Ya Nyama

 

 

Inaruhusiwa kufanya karamu ya ndoa kwa chakula chochote kinachopatikana na kwa uwezo hata kama sio pamoja na nyama. Hii ni kutokana na Hadiyth ifuatayo iliyosimuliwa na Anas:

 

أَقَامَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم بَيْنَ خَيْبَرْ وَالْمَدِينَة ثَلاثَ لَيَالٍ يبني عَلَيْهِ بِصَفِيَّة، فدَعوتُ المسلمينَ إلى وَلِيمَتِهِ، فَمَا كَانَ فِيهَا مِنْ خُبْزٍ وَلاَ لَحْمٍ وما كان فيها إلاّ أن أمرَ بلالاً بالأنطاع فبُسطَت،  (وفي رواية) : فَحصت الأَرْض أَفَاحِيص، وَجِيءَ بِالأنْطاَع فَوَضَعت فِيهَا ) ، فَألْقَي عَلَيْهَا التَّمر وَالأَقطْ والسَّمْن [فَشَبَعَ النَّاسُ] 

"Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikaa baina ya Khaybar na Al-Madiynah kwa muda wa siku tatu siku ambazo alimuingilia (alimuoa) Swafiyah. Kisha nikawaalika Waislamu katika karamu yake ya ndoa. Hakukuwa na nyama wala mikate katika karamu, bali matandiko ya ngozi yaliletwa na juu yake zikawekwa tende, maziwa makavu na samli iliyo safi. Watu walikula hadi wakashiba"[1]

 

 

 



[1] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

Share

29-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Matajiri Kuchangia Gharama Za Karamu

 

           

Inapendekezeka kwa matajiri kusaidia katika matayarisho ya karamu ya ndoa kutokana na Hadiyth iliyosimuliwa na Anas kuhusu ndoa ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kwa Swafiyah:

حتى إِذا كان بالطريقِ جَهَّزَتْها له أمُّ سُليمٍ فأهدَتْها له منَ الليل، فأصبحَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم عَروساً، فقال: ((مَن كان عندَه شيءٌ فليجىءْ به))  ( وفي رواية)  ((من كان عنده فضل زاد فليأتنا به)) قال:  وبَسطَ نِطعاً فجعلَ الرجلُ يجيءُ بالأقط، وجعلَ الرجلُ يجيءُ  بالتمرِ، وجعلَ الرجلُ يجيءُ بالسَّمنِ  فحاسوا حَيساً،  (فجعلوا يأكلون من ذلك الحيس ويشربون من حياض إلى جنبهم من ماء السماء)  فكانتْ وَليمةَ رَسولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم

"Kisha tulipokuwa njiani, Ummu Sulaym alimtayarisha (Swafiyah) kwa ajili yake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na akamletea usiku. Kwa hiyo Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliamka asubuhi na bibi harusi mpya. Kisha akasema: ((Yeyote mwenye kitu alete)). Katika riwaaya nyingine alisema, ((Yeyote mwenye riziki zaidi alete)). Anas anaendelea (kusema): Kwa hiyo matandiko ya ngozi yakatandikwa na mtu mmoja alileta maziwa makavu, mwingine tende, na mwingine samli safi, kwa hiyo wakafanya Hais (hais ni mchanganyiko wa vitu hivyo vitatu). Watu wakala hiyo hais na kunywa kutoka vidimbwi vya maji ya mvua vilivyokuwa karibu, na hiyo ndiyo ikawa karamu ya ndoa ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم.   [1]

 



[1] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

Share

30-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Makatazo Ya Kualika Matajiri Pekee

 

 

Hairuhusiwi kualika matajiri pekee na kuwatenga masikini kwani Mtume صلى الله عليه وآله وسلم   amesema:

 

 

((شَرُّ الطَّعَامِ طَعَامُ الْوَلِيمَةِ يُدْعَىٰ لَهَا الأَغْنِيَاءُ وَيُتْرَكُ الْمَسَاكِينُ، وَمَنْ لَمْ يَجِبْ الدَّعْوَةَ فَقَدْ عَصَىٰ اللَّهَ وَرَسُولَهُ)).

 

((Chakula kiovu kibaya kabisa ni chakula cha karamu ya harusi ambayo wamealikwa matajiri na kutengwa kando masikini. Yeyote atakayekataa mualiko atakuwa amemuasi Allaah na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Wake))[1]

 





[1] Muslim na Al-Bayhaaqiy

Share

31-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Ni Wajibu Kuitikia Mwaliko

 

 

Ni wajibu kwa anayealikwa karamu kuhudhuria. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu jambo hili, miongoni mwa hizo ni:

 


Kwanza:

  ((فُكُّوا الْعَانِيَ، وَأَجِيبُوا الدَّاعِيَ، وَعُودُوا الْمَرِيضَ))

((Acheni huru wafungwa, itikieni (kubalini) mwaliko na tembeleeni wagonjwa))[1]

 



Pili:

 

((إِذَا دُعِيَ أَحَدُكُمْ إِلَى الْوَلِيمَةِ فَلْيَأْتِهَا  عَرْساً كَان أَوْ نَحْوه  وَمَنْ لَمْ يُجِبِ الدَّعْوَةَ، فَقَدْ عَصَى اللّهَ وَرَسُولَهُ))




((Anapoalikwa mmoja wenu katika karamu, basi ahudhurie, ikiwa ni karamu ya harusi au nyingineyo. Na yeyote asiyeitikia (asiyekubali) mwaliko basi atakuwa amemuasi Allaah na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Wake))[2]

 



[1] Al-Bukhaariy

[2] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

Share

32-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kukubali Mwaliko Hata Kama Umefunga (Swawm)

 

 

Anatakiwa mtu aitikie mwaliko hata kama amefunga kutokana na kauli ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم:

 

((إذَا دُعِيَ أحَدُكُم فَلْيُجِبْ، فإنْ كَانَ مُفْطِراً فَلْيَطْعَمْ، وَإنْ كَانَ صَائماً فَليُصَلِّ))  ( وَالصَّلاَةُ الدُّعَاءُ)

((Anapoalikwa mmoja wenu chakula inampasa akubali. Ikiwa hakufunga basi na ale, na kama kafunga basi ashiriki katika Swalah (Du'aa) zake)) (Na Swalah ni Du’aa”)[1]

 

 

 

 



[1] Muslim, Ahmad na wengineo

Share

33-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kufungua Swawm Kwa Ajili Ya Mwenyeji (Aliyekualika)

 

 

Mtu (aliyefunga) anaweza kufungua Swawm ikiwa ni Swawm ya Sunnah, haswa ikiwa mwenyeji wake amemuomba kufanya hivyo. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-ala haya:

 


Kwanza:

((إِذَا دُعِيَ أَحَدُكُمْ إِلَى طَعَامٍ فَلْيُجِبْ فَإِنْ شَاءَ طَعِمَ، وَإِنْ شَاءَ تَرَكَ))

 

((Mmoja wenu anapoalikwa chakula, ahudhurie, kisha akitaka kula anaweza kula na kama sivyo anaweza kuacha))[1]

 


Pili:

((الصَّائِمُ المتطوِّعُ أَمِيرُ نَفْسِهِ إِنْ شَاءَ صَامَ، وَإِنْ شَاءَ أَفْطَرَ))

((Mwenye kufunga (Swawm za) Sunnah, ni mwenye kujitawala humo (katika Swawm) akipenda akamilishe Swawm yake au akipenda afungulie))[2]





Tatu:

عن عائشة رضي الله عنها  قالت : دَخَلَ عَليَّ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَوْماً فَقَالَ: ((هَلْ عِنْدَكُمْ شَيْءٌ؟)) فَقُلْتُ: لاَ قَالَ: ((فَإنِّي صَائِمٌ)) ثُمَّ مَرَّ بِـــــي بَعْدَ ذٰلِكَ الْيَوْمَ وَقَدْ أُهْدِيَ إلَى حَيْسٌ فَخَبَّأْتُ لَهُ مِنْهُ وَكَانَ يُحِبُّ الحَيْسَ قَالَتْ: يَا رَسُولَ اللَّهِ إنَّهُ أُهْدِيَ لَنَا خَيْسٌ فَخَبَّأْتُ لَكَ مِنْهُ قَالَ: ((أَدْنِيهِ أَمَا إِنِّي قَدْ أَصْبَحْتُ وَأَنَا صَائِمٌ)) فَأَكَلَ مِنْهُ ثُمَّ قَالَ: ((إنَّمَا مَثَلُ صَوْمِ الْمُتَطَوِّعِ مَثَلُ الرَّجُلِ يَخْرِجُ مِنْ مَالِهِ الصَّدَقَةَ فَإنْ شَاءَ أَمْضَاهَا وَإنْ شَاءَ حَبَسَهَا))  

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah الله عنها رضي ambaye amesema: "Mjumbe wa Allaah alinijia siku moja na akasema, ((Je kuna chochote? [chakula?])) Nikasema: Hapana. Akasema:  ((Nimefunga)). Kisha akaja kwangu siku nyingine na wakati huo nilikuwa nimeletewa Hais, kwa hiyo nikamuwekea kwani alikuwa akipenda Hais. Mama wa waumini ‘Aaishah akasema, "Ewe Mjumbe wa Allaah, nimegaiwa Hais na nimekuwekea baadhi". Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم Akasema: ((Ilete, nimeanza siku kwa kufunga)). Kwa hiyo akala baadhi yake na akasema: ((Swawm ya hiari (Ya Sunnah) ni mfano kama mtu anayetoa sadaka kutoka mali yake. Akipenda anatoa na asipopenda anazuia))[3]



[1] Muslim, Ahmad na wengineo

[2] An-Nasaaiy katika 'Al-Kubraa', Al-Bayhaaqiy na Haakim: Swahiyh

[3] An-Nasaaiy: Swahiyh

Share

34-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Haitakiwi Kulipa Swawm Ya Sunnah

 

 

Mtu akiamua kufungulia Swawm ya Sunnah, sio lazima kwake kuilipa siku hiyo. Kuna Hadiyth mbili kuhusu mas-ala haya:


Kwanza:

عن أبي سعيد الخُدْرِيِّ أنه قالَ: صَنَعْتُ لرسولِ الله صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّمَ طعاماً فَأَتَانِي هو وَأَصْحَابُهُ، فَلمَّا وُضِعَ الطعامُ قالَ رجلٌ من القومِ: إنَّي صائمٌ، فقالَ رسولُ الله صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((دَعَاكُمْ أَخُوكُمْ وَتَكَلَّفَ لكُمْ))، ثم قالَ لَهُ:  ((أَفْطِرْ وصُمْ مكَانَهُ يوماً إنْ شِئْتَ))

Kutoka kwa Abu Sa'iydil-Khudriy ambaye amesema, "Nilimtayarishia chakula Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye alikuja pamoja na Swahaba zake. Kilipowekwa chakula mmoja wao akasema: 'Nimefunga'. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Ndugu yako amekualika na ametayarisha chakula kwa ajili yako)). Kisha akasema ((Fungua Swawm yako kisha funga siku nyingine badala yake ukipenda))[1]


Pili:

عن أبي جحيفة أن رسول الله صلى الله عليه وسلم آخى رَسُولُ الله بَيْنَ سَلْمَانَ وَأَبي الدَّرْدَاءِ فَزَارَ سَلْمَانُ أَبَا الدَّرْدَاءِ فَرَأَى أُمَّ الدَّرْدَاءِ مُتَبَذِّلَةً. فقَالَ: مَا شَأْنُكِ مُتَبَذِّلَةً قَالَتْ: إِنَّ أَخَاكَ أَبَا الدَّرْدَاءِ يقوم الليل ويصوم النهار  لَيْسَ لَهُ حَاجَةٌ فِي الدُّنْيَا، قالت: فَلَمَّا جَاءَ أَبُو الدَّرْدَاءِ فرحب به، وقَرَّبَ إليه طَعَاماً فَقَالَ لَهُ سُلَيْمَان: كُلْ: قال: َإِنِّي صَائِمٌ. قالَ: أقسمت عليك لتفطرنه مَا أَنَا بآكلٍ حَتَّى تَأْكُلَ، قالَ فَأَكَلَ معه ثُمَّ بات عِنْدَهُ. فَلَمَّا كَانَ من الَّليْلُ  أراد أبو الدرداء أن يقوم، فمنعه سلمان وقال له: إِنَّ لِجَسَدِكَ عَلَيْكَ حَقّاً، ، وَلِرَبكَ عَلَيْكَ حَقّاً ، [ولضيفك عليك حقا]، وَلأَهْلِكَ عَلَيْكَ حَقّا  صُمْ، وَأفْطُرْ، وَصَلّ، وَائتِ أَهْلَك، وَأعْطِ كُلِّ ذِي حَق حَقَّهُ، فَلَمَّا كَانَ فِي وَجه الصُّبْح، قال: قُمْ الآَنْ إِنْ شِئْتَ، قال: فَقَاما فَتَوَضَّآ، ثُمَّ رَكَعا، ثُمَّ خَرَجا إِلَى الصَّلاةِ، فَدنا أبُو الدَّرْداَء لِيُخْبِرَ رسول الله صلى الله عليه وسلم بِالَّذي أَمَرَهُ سَلْمَان، فَقال لَهُ رسول الله صلى الله عليه وسلم  (( يَا أَبا الدَّرْداء! ِإنَّ لِجَسَدِكَ عَلَيْكَ حَقاً )) مِثْل مَا قاَل سَلْماَن ( وفي رواية): ((صَدَقَ سَلْمَانُ)) 
  

Imetoka kwa Abu Juhayfah رضي الله عنه, kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliwaunga Salmaan رضي الله عنه na Abu Ad-Dardaa رضي الله عنه katika udugu wa Kiislam. Abu Juhayfah alisema: "Salmaan alikuja kumtembelea Abu Ad-Dardaa, na akamuona Ummu Ad-Dardaa (mke wa rafiki yake) yuko katika hali isiyo nzuri na alikuwa amevaa nguo zilizo chakaa Akamuuliza: Vipi mbona uko katika hali hiyo Ummu Ad-Dardaa? Akasema: 'Ndugu yako Abu Ad-Dardaa anakesha usiku katika Swalah na mchana anafunga na hahitaji chochote katika mambo ya dunia". Kisha Abu Ad-Dardaa akaja, akamkaribisha ndugu yake na akampa chakula. Salmaan akamuambia: 'Kula'. Lakini Abu Ad-Dardaa akasema: 'Nimefunga'. Salmaan Akasema: 'Naapa ya kwamba ni lazima ufungue Swawm yako. Sitokula hadi ule'. Kwa hiyo akala pamoja naye. Salmaan akalala usiku nyumbani kwake, na Abu Ad-Dardaa alipoamka usiku kuswali, Salmaan akamzuia na akamuambia: 'Ewe Abu Ad-Dardaa, mwili wako una haki juu yako, Mola wako Ana haki juu yako, wageni wako wana haki juu yako, na mke wako ana haki juu yako. Funga lakini pia fungua, swali (usiku) lakini pia muendee mke wako, na kila mmoja mpe haki yake'. Ilipofika karibu na Alfajiri, Salmaan akamuambia: 'Inuka sasa ukipenda'. Kisha wote wawili wakafanya wudhuu, wakaswali, na wakaenda kuswali msikitini. Abu Ad-Dardaa alipomkaribia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kumuambia kuhusu amri ya Salmaan kwake, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamwambia, ((Ewe Abu Ad-Dardaa, hakika mwili wako una haki juu yako)) Kama alivyosema Salmaan. Katika riwaaya nyingine alisema, ((Salmaan amesema ukweli))[2]



[1] Al-Bayhaaqiy na At-Twabaraaniy: Hasan

[2] Al-Bukhaariy, At-Tirmidhiy na Al-Bayhaaqiy

Share

35-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kutokubali Mwaliko Katika Shughuli Zenye Maasi Ndani Yake

 

 

Hairuhusiwi kuhudhuria shughuli alizoalikwa mtu ambazo zina mambo ya kumuasi Allaah سبحانه وتعالى ila ikiwa mtu atakwenda kwa nia ya kuwaeleza watu ubaya huo na kujaribu kuuondosha. Akifaulu kuondosha au kuzuia basi anaweza kubakia, na kama akishindwa basi aondoke. Kuna Hadiyth kuhusu mas-ala haya, miongoni mwa hizo ni:

 

Kwanza:

عَنْ عَلِيَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: صَنَعْتُ طَعَامَاً فَدَعَوْتُ رَسُولَ اللَّهِ فَجَاءَ فَرَأَىٰ تَصَاوِيرَ، فَرَجَعَ قَال:  فَقُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ مَا رَجَعَكَ بِأَبِي أَنْتَ وَأُمي ؟ قَالَ: ((إِنَّ فِي الْبَيْتِ سِتْرَاً فِيهِ تَصَاوِيرُ، وَإِنَّ المَلاَئِكَةَ لاَ تَدْخُلُ بَيْتَاً فِيهِ تَصَاوِيرُ))

 
Imetoka kwa 'Aliy رضي الله عنه ambaye amesema: "Nilitayarisha chakula kisha nikamualika Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم Alipokuja na akaona picha katika nyumba akageuka kuondoka. Nikamuambia: Ewe Mjumbe wa Allaah, jambo gani lililokurudisha, baba yangu na mama yangu wawe fidia yako? Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Kuna pazia katika nyumba hii ambalo lina picha, na Malaika hawaingii katika nyumba yoyote yenye picha))[1]

 

Pili:

عن عائشة أَنَّهَا اشْتَرَتْ نُمْرُقَةً فِيهَا تَصَاوِيرُ. فَلَمَّا رَآهَا رَسُولُ اللّهِ قَامَ عَلَى الْبَابِ فَلَمْ يَدْخُلْ. فَعَرَفْتُ، أَوْ فَعُرِفَتْ، فِي وَجْهِهِ الْكَرَاهِيَةُ. فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اللّهِ أَتُوبُ إِلَى اللّهِ وَإِلَىٰ رَسُولِهِ. فَمَاذَا أَذْنَبْتُ؟ فَقَالَ رَسُولُ اللّهِ : ((مَا بَالُ هٰذِهِ النُّمْرُقَةِ؟)) فَقَالَتِ: اشْتَرَيْتُهَا لَكَ. تَقْعُدُ عَلَيْهَا وَتَوَسَّدُهَا. فَقَالَ رَسُولُ اللّهِ : ((إِنَّ أَصْحَابَ هٰذِهِ الصُّوَرِ (  وفي رواية: إن الذين يعملون هذه التصاوير) يُعَذَّبُونَ يَوم الْقِيَامة وَيُقَالُ لَهُمْ: أَحْيُوا مَا خَلَقْتُمْ)) ثُمَّ قَالَ: ((إِنَّ الْبَيْتَ الَّذِي فِيهِ الصُّوَرُ لاَ تَدْخُلُهُ الْمَلاَئِكَةُ)).

 

 

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye alisema kwamba alinunua mito ambayo ilikuwa ina picha. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipoiona alisimama mlangoni na hakuingia. Nikatambua kuchukizwa kwake sana usoni mwake. Nikasema: "Ewe Mjumbe wa Allaah, ninatubu kwa Allaah na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Wake, nimefanya nini?" Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akauliza, ((Mto gani huu?)) Nikasema: Nimekununulia wewe ili uukalie na uutumie kama mto. Akasema: ((Hakika watu picha hizi [katika riwaaya nyingine] ((wale wanaochora picha hizi) wataadhibiwa siku ya Qiyaamah na wataambiwa: Vipeni uhai katika vile mlivyoviumba!)) Kisha akasema:  ((Nyumba ambayo inayo picha kama hizi hawaingii Malaika)) ’Aaishah akasema: Hakuingia tena hadi nilivyoondosha mto".[2]

 

Tatu:

 

(( مَنْ كَانَ يُؤْمِن بالله وَالْيَوْمِ الآخِر؛ فَلاَ يَقْعُدَنَّ عَلَى مَائِدَةٍ يُدَار عَلَيْها بِالْخَمْر )).

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((Yeyote anayemuamini Allaah na Siku ya Mwisho, asikae katika meza inayozungushwa ulevi))[3]

Desturi ya vitendo vya Salaf (kizazi cha mwanzo cha Waislamu) ilikuwa ndivyo hivi ambavyo tumevieleza hapa. Kuna mifano mingi lakini tutataja mifano michache tu:

 

Kwanza:

 

 

عن أَسْلَـمَ مولـى عُمَرَ أَنَّ عُمَرَ بنَ الـخطابِ رضي الله عنه حينَ قَدِمَ الشأْمَ فَصَنَعَ لهُ رجلٌ من النَّصَارَى طعاماً، فقالَ لِعُمَرَ: إنِّـي أُحِبُّ أَنْ تَـجِيْئَنِـي وتُكْرِمَنِـي أَنْتَ وأصحابُكَ، وهو رجلٌ من عظماءِ الشأْمِ، فقالَ لهُ عُمَرُ رضي الله عنه: إنَّا لا نَدْخُـلُ كَنَائِسَكُمْ من أجلِ الصورِ الَّتِـي فِـيْهَا، يعنـي التـماثـيلَ

 

Kutoka kwa Aslam mkombolewa wa 'Umar  kwamba 'Umar ibnul Khatw-Twaab alikuja Ash-Shaam. Mtu mmoja katika Manaswara alitayarisha chakula na akamuambia 'Umar: 'Nitapenda uje kwangu ili unipe heshima [muwe wageni wangu wa heshima] pamoja na Swahaba zako'. (Huyo mtu alikuwa ni mkuu miongoni mwa watu wa Ash-Shaam). 'Umar akamuambia, 'Hatuingii makanisa yenu kwa sababu ya mapicha yaliyomo humo.'[4]

 

Pili:

 
 

عن أبـي مسعودٍ أَنَّ رجلاً صَنَعَ لهُ طعاماً فَدَعَاهُ، فقالَ: أَفِـي البـيتِ صورةٌ، قالَ: نَعَمْ، فأَبَى أَنْ يَدْخُـلَ حتَّـى كَسَرَ الصورةَ، ثم دَخَـلَ

Imetoka kwa Abu Mas'uud 'Uqba bin 'Aamir kwamba mtu mmoja alimtayarishia chakula kisha akamualika. Abu Mas'uud akamuuliza yule mtu: 'Je kuna picha katika nyumba?" Yule mtu alimjibu: 'Ndio'. Hivyo Abu Mas'uud alikataa kuingia hadi picha zilipovunjwa kisha akaingia.[5]

 
Tatu:

 

  قَالَ الإِمَام الأَوْزاعِي: لاَ نَدْخُل وَلِيمَةُ فِيهَا طبل وَلاَ معْزَاف   

 

Imaam Al-Awzaa'iy amesema: "Hautuingii katika karamu iliyo na ngoma au ala za muziki"[6]

 

 

 

 

 

[1] Ibn Maajah na Abu Ya'laa

[2] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[3] Ahmad na At-Tirmidhiy: Swahiyh

[4] Al-Bayhaaqiy: Swahiyh

[5] Al-Bayhaaqiy: Swahiyh

[6] 'Abdul-Hasan Al-Harbiy katika 'Al-Fawaaidul Muntaqaat (4/3/1/) ikiwa Isnaad Swahiyh kutoka kwake

 

 

Share

36-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Yanayopendezwa Kufanywa Na Waalikwa

 

 

Mambo mawili yanapendekezwa kwa wale wanaohudhuria shughuli waliyoalikwa:


Jambo La
Kwanza: Du’aa Kumuombea Mwenyeji


Inampasa amuombee Du'aa mwenyeji wake baada ya kumaliza kula, Du'aa ambazo zimenukuliwa kutoka kwa Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم nazo ziko aina mbali mbali:

 


Kwanza:

عَنْ عَبْدُالله بِنْ بسر ، يَحدثْ أَنَّ أبَاهُ صَنَعَ لِلنَّبِيِّ طَعَاماً، فَدَعَاهُ فأجَابَهُ، فَلَمَّا فَرَغَ قَال: ((اَللَّهُمَّ اْرَحَمْهُمْ وَاغْفِرْ لَهُمْ وَبَارِكْ لَهُمْ فِيمَا رَزَقْتَهُمْ)).

 

Imetoka kwa 'Abdullah ibn Bisr baba yake alitayarisha chakula kwa ajili ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kisha akamualika. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye aliitikia na akahudhuria. Alipomaliza kula, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alisema ((Ewe Allaah, Waghufurie, Warehemu na Wabarikie yale Uliyowaruzuku)) (Allaahumma-Ghfir-Lahum War-hamhum, wa Baarik-Lahum Fiy-Maa Razaqtahum)[1]


Pili:

عن المقداد بن الأسود ،قال: قدمت أنا وصاحبان لي على رسول الله صلى الله عليه وسلم فأصابنا جوع شديد، فتعرضنا للناس فلم يُضِفْنا أحد، فانطلق بنا رسول الله صلى الله عليه وسلم إلى منزله وعنده أربع أَعْنُزٍ فقال لي: ((يا مِقْدادُ جَزِّىءْ أَلْبانَها بَيْنَنَا أَرْباعاً)) فكنت أجزئه بيننا أرباعاً [فيشرب كل إنسان نصيبه، ونرفع لرسول الله صلى الله عليه وسلم نصيبه]  فاحتبس رسول الله صلى الله عليه وسلم ذات ليلة فحدثت  أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قد أتى بعض الأنصار، فأكل حتى شبع، وشرب حتى روي، فلو شربت نصيبه، فلم أزل كذلك حتى قمت إلى نصيبه فشربته، ثم غطيت القَدح، فلما فرغت أخذني ما قدم وما حدث، فقلت: يجيء رسول الله صلى الله عليه وسلم جائعاً ولا يجد شيئاً فتسجَّيتُ،  قال: وعلي شملة من صوف كلما رفعت على رأسي خرجت قدماي، وإذا أرسلت على قدمي خرج رأسي، قال:] [وجعل لا يجيئني النوم]   وَجعلت أحدث نفسي، [قال: وأما صاحباي فناما]،    فبينا أنا كذلك، إذ دخل رسول الله صلى الله عليه وسلم فسلم تسليمة، يُسْمِعُ اليقظان ولا يُوقظ النائم، [ثم أتى المسجد فصلى]،   ثم أتىٰ القدح فكشفه فلم ير شيئاً، فقال: ((اللهمَّ أَطْعِمْ مَنْ أَطْعَمَني واسْقِ مَنْ سَقاني)) واغتنمت الدعوة،   [فعمدت إلى الشملة فشددتها علي]  فقمت إلى الشفرة فأخذتها، ثم أتيت الأعنز فجعلت اجتسها أيها أسمن، فلا تمر يدي على ضرع واحدة إلا وجدتها حافلاً،  [فعمدت إلى إناء لآل محمد ما كانوا يطعمون أن يحلبوا فيه]،  فحلبت حتى ملأت القَدَح،  ثم أتيت [به]   رسول الله صلى الله عليه وسلم، [فقال: ((أما شربتم شرابكم الليلة يا مقداد؟)) قال:]    فقلت: اشرب يا رسول الله، فرفع رأسه إليّ فقال: ((بعضُ سَوْآتِكَ ـ يا مِقْدادَ ـ ما الخبر؟)) قلت: اشرب ثم الخبر، فشرب حتى روى، ثم ناولني فشربت،  فلما عرفت أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قد روي وأصابتني دعوته، ضحكت، حتى ألقيت إلى الأرض، فقال: ((ما الخَبَرْ؟)) فأخبرته فقال: ((هٰذِهِ بَرَكَةٌ نَزَلَتْ مِنَ السَّماءِ فَهَلاَّ أَعْلَمْتَني حَتَّى نَسْقِيَ صاحِبَيْنا)) فقلت: [والذي بعثك بالحق]،  إذاً أصابتني وإياك، البركة فما أبالي من أخطأت

 

Imetoka kwa Al-Miqdaad ibn Al-Aswad رضي الله عنه ambaye alisema: "Nilikwenda na rafiki zangu wawili kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم (Madiynah). Tulikuwa na njaa na tukaomba msaada kwa watu wengine, lakini hakuna aliyetupokea kuwa wageni wao. Kisha Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم alituchukua nyumbani kwake na huko kulikuwepo na mbuzi wanne. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliniambia, ((Ewe Miqdaad, gawa maziwa baina yetu mara nne)). Nikagawa maziwa katika sehemu nne. Kila mmoja akanywa kiasi chake, na tukampelekea Mtume صلى الله عليه وآله وسلم sehemu yake. Usiku mmoja, Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم alikawia nje, nikaanza kuwaza akilini mwangu kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amekwenda kwa ma-Answaar na amekula mpaka ameshiba na amekunywa mpaka amekata kiu chake, basi kwa nini nisinywe sehemu yake? (kiasi chake cha maziwa) Ikaendelea hivyo hadi mwisho nikainuka na kunywa sehemu yake. Kisha nikafunika gilasi yake. Nilipomaliza, nikaanza kutia wasiwasi nilivyofanya, nikiwaza katika nafsi yangu kuwa sasa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم atakuja akiwa ana njaa na atakuta hakuna kitu. Nikajifunika blanketi la sufi. Nilipolivuta blanketi juu ya kichwa changu miguu yangu ilijitokeza na nilipojifunika miguu yangu, kichwa kilikuwa wazi hakikufunikwa. Sikuweza kulala, nikawa nawaza mambo katika nafsi yangu. Ama marafiki zangu wawili, walikuwa wameshalala. Nilibakia katika hali hii alipoingia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akanisalimia kwa sauti ya kusikika na mtu aliyekuwa macho, lakini ambayo isingelimuamsha aliyelala. Baada ya hapo akaenda msikitini na kuswali. Kisha akaijia gilasi na kuifungua lakini hakuona kitu ndani yake na akasema: ((Ewe Allaah Mlishe aliyenilisha na Mpe kinywaji yule anayenipa kinywaji)) (Allaahuuma Atw-'im Man Atw'amaniy Wasqi man Saqaaniy). Nikaamua kuchukua fursa ya Du'aa hii ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Nikachukua blanketi langu na nikalivaa kiunoni, nikachukua kisu kikubwa, nikawaendea mbuzi. Nikaanza kuwakagua kwa mikono yangu kutazama aliyenona kabisa ili nipate kumchinja kwa ajili ya Mjumbe wa Allaah lakini kila mikono yangu ikipita katika kila chuchu iliona kwamba zimejaa maziwa. Nikachukua chombo kilichokuwa cha watu wake wa nyumbani kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambacho hawakuweza kufikiria kuwa kitajaa maziwa nikaanza kukamua maziwa ya mbuzi hadi kikajaa. Kisha nikamletea Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye aliniambia, ((Hukunywa maziwa yako usiku huu ewe Miqdaad?)) Nikasema: 'Kunywa Ewe Mjumbe wa Allaah' Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akanyanyua kichwa chake na akasema, ((Ni aibu kwako ewe Miqdaad yaliyotokea)). Nikasema: 'Kunywa kwanza, kisha ndio habari. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akanywa mpaka akakata kiu chake kisha akanipa gilasi na nikanywa pia.


Nilipojua kwamba Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم ameshakata kiu chake na kwamba Du'aa yake imeshanihusu kuitumia nikaanza kucheka hadi nikaanguka chini kwa kicheko.

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Kuna nini?)). Nikamuelezea kisa chote. Akasema, ((Hii (yaani maziwa yasiyotegemewa) ni baraka kutoka mbinguni. Kwa nini usiniambie ili tungeliwapa pia rafiki zako sehemu? (ya hayo maziwa))). Nikasema: 'Naapa kwa Yule Ambaye Amekuleta kwa haki, madamu baraka zimekujia wewe na mimi, haikunishughulisha sana na kufikiria waliokosa maziwa haya'.[2]


Tatu:

 

عن أَنَسٍ أَوْ غيرِهِ  أن رسول الله صلى الله عليه وسلم [ كان يزور الأنصار، فإذا جاء إلى دور الأنصار جاء صبيان الأنصار يدورون حوله، فيدعوا لهم، ويمسح رؤوسهم ويسلم عليهم، فأتى إلى باب سعد بن عبادة فـ]   اسْتَأْذَنَ علـى سعدِ بنِ عُبَادَةَ رضي الله عنه فقالَ: ((السلامُ عَلَـيْكَ ورَحْمَةُ الله)) قال سَعْدٌ: وعلـيكَ السلامُ ورَحْمَةُ الله، ولـم يُسْمِعِ النبـيَّ حتَّـى سَلَّـمَ ثلاثاً، ورَدَّ علـيهِ سعدٌ ثلاثاً ولـم يُسْمِعْهُ، [وكان النبي صلى الله عليه وسلم لا يزيد فوق ثلاث تسليمات، فإن أذن له، وإلا انصرف]، فَرَجَعَ النبـيُّ، فاتَّبَعَهُ سعدٌ فقالَ: يا رسولَ الله بأَبِـي أنتَ ما سَلَّـمْتَ تسلـيـمةً إلاَّ وَهِيَ بأُذُنِـي، ولَقَدْ رَدَدْتُ علـيكَ ولـم أُسْمِعْكَ أَحْبَبْتُ أَنْ أَسْتَكْثِرَ من سَلاَمِكَ ومن البَرَكَةِ،  ثم دَخَـلُوا البـيتَ، فَقَرَّبَ لهُ زَبِـيباً، فَأَكَلَ نبـيُّ الله، فلـمَّا فَرَغَ قالَ: ((أَكَلَ طَعَامَكُمُ الأبرارُ، وصَلَّتْ عَلَـيْكُمُ الـملائكةُ، وأَفْطَرَ عِنْدَكُمُ الصائمونَ»))

Imetoka kwa Anas عنه رضي الله na wengineo, kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa akiwatembelea ma-Answaar. Kila alipokwenda nyumbani mwao watoto wao walikuwa wakija kumzunguka Naye hucheza nao na kuwapapasa vichwa vyao na kuwasalimia. Siku moja, alikuja mlangoni mwa Sa'ad ibn 'Ubaadah na akaomba ruhusa kuingia akisema: ((Assalaamu 'Alaykum)). Sa'ad akajibu 'Wa 'alaykumus salaam', lakini kwa sauti ambayo Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakuisikia. Ikafanyika hivyo mara tatu. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakupata kuomba ruhusa kuingia zaidi ya mara tatu ikiwa hakupewa idhini ya kuingia, bali huondoka. Akaondoka Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Sa'ad akamfuata na akasema: 'Ewe Mjumbe wa Allaah, baba yangu na mama yangu wawe fidia yako, kila mara ulipotoa salaam, nilikupa idhini lakini sikutaka uisikie kwa sababu nilipenda kusikia salaam nyingine na baraka kutoka kwako. Kwa hiyo karibu Ewe Mjumbe wa Allaah. Kisha wakaingia nyumbani na kumkaribisha ale zabibu. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akala, alipomaliza alisema, ((Wale chakula chenu watu wema, na wawaombee Rehema Malaika na wafuturu kwenu waliofunga)) (Akala Twa'aamakumul-Abraar Wa Swallat 'Alaykumul-Malaaikatu Wa Aftwara 'Indakumus-Swaaimuun)[3]

 

Jambo La Pili: Du’aa Kuwaombea Bwana na Bibi Harusi


Jambo la pili linalopendekezeka kwa wale wanaohudhuria karamu ya harusi ni kuwaombea Du'aa bwana na bibi harusi wajaaliwe kheri na baraka. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-ala haya:


Kwanza:

 

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللّهِ عنهما قال:  هَلَكَ أَبِي وَتَرَكَ سَبْعَ  بَنَاتٍ (أَوْ قَالَ تِسْعَ ) فَتَزَوَّجْتُ امْرَأَةً ثَيِّباً. فَقَالَ لِي رَسُولُ اللّهِ ((يَا جَابِرُ! تَزَوَّجْتَ؟)) قَالَ قُلْتُ: نَعَمْ. قَالَ: ((فَبِكْرٌ أَمْ ثَيِّبٌ؟)) قَالَ قُلْتُ: بَلْ ثَيِّبٌ، يَا رَسُولَ اللّهِ! قَالَ: ((فَهَلاَّ جَارِيَةً تُلاَعِبُهَا وَتُلاَعِبُكَ)) و في رواية: ((وَتُضَاحِكُهَا وَتُضَاحِكُكَ؟)) قَالَ قُلْتُ لَهُ: إِنَّ عَبْدَ اللّهِ هَلَكَ وَتَرَكَ تِسْعَ بَنَاتٍ (أَوْ سَبْعَ) وَإِنِّي كَرِهْتُ أَنْ آتِيَهُنَّ أَوْ أَجِيئَهُنَّ بِمِثْلِهِنَّ، فَأَحْبَبْتُ أَنْ أَجِيءَ بِامْرَأَةٍ تَقُومُ عَلَيْهِنَّ وَتُصْلِحُهُنَّ. قَالَ: ((فَبَارَكَ الّلهُ لَكَ)) أَوْ قَالَ لِي خَيْراً.

 
Imetoka kwa Jaabir ibn 'Abdullaah رضي الله عنه ambaye amesema: "Baba yangu alifariki na aliacha wasichana saba (au tisa). Nilimuoa mwanamke aliyekuwa thayyib [mjane] na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akaniuliza, ((Umeshaoa ewe Jaabir?)). Nikajibu, 'Ndio'. Akauliza tena, ((Je, ni bikra au mjane?)). Nikajibu, "Ni mjane". Akauliza, ((Kwa nini usingeoa msichana mdogo ambaye angelicheza nawe nawe ungelicheza naye?)) Katika riwaaya nyingine, ((na ambaye angelikuchekesha na ungelimchekesha)). Nikasema,  "Abdullaah amefariki na ameacha wasichana tisa [au saba] na sikupenda kuwaletea mke aliye sawa na wao kwa hiyo nimeoa mwanamke ambaye atakuwa na mas-uliya nao na kuwapa mafunzo vizuri". Mtume صلى الله عليه وآله وسلم   akasema, ((BarakAllaahu Laka)) (Allaah Akubariki) [au alisema jambo jema kwangu][4]


Pili:

 

وعن بريدة قال: قال نفر من الأنصار لعلي ـ رضي الله عنه ـ: عندك فاطمة ، فأتى رسول الله صلى الله عليه وسلّم (فَسَلَّم عليه ) فقال:  ((مَا حَاجَةُ ابنُ أَبي طَالِبٍ))   فقال: يا رسول الله، ذكرت فاطمة بنت رسول الله صلى الله عليه وسلّم، فقال: ((مَرْحَباً وأَهْلاً)) لم يزد عليها. فخرج علي بن أبي طالب على أولئك الرهط من الأنصار ينتظرونه، فقالوا: ما وراءك؟ قال: ما أدري غير أنه قال لي: ((مَرْحَباً وأَهْلاً)) قالوا: يكفيك من رسول الله صلى الله عليه وسلّم إحداهما، أعطاك الأهل والمرحب. فلما كان بعدما زوجه قال: ((يا عَلِيُّ إِنَّه لا بُدَّ لِلْعَرُوسِ مِنْ وَلِيْمَةٍ)) قال سعد: عندي كبش، وجمعَ له من الأنصار أَصْوُعاً من ذرة، فلما كانت ليلة البناء قال: ((لا تُحْدِثْ شَيْئاً حَتَّيه تَلْقَانِي)) فدعا رسول الله صلى الله عليه وسلّم بماء فتوضأ منه، ثم أفرغه عليَّ فقال: ((اللهمَّ بَارِكْ فِيهِمَا وبَارِكْ لَهُمَا في بِنَائِهِمَا))

Imetoka kwa Buraydah رضي الله عنه ambaye amesema: "Baadhi ya ma-Answaar walimuambia 'Aliy: 'Unaye Faatwimah!' Kwa hiyo 'Aliy akaenda kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم 'Aliy alipomsalimia alisema, ((Unahitaji nini ewe mwana wa Abu Twaalib?)). 'Aliy Akasema: "Ewe Mjumbe wa Allaah, Faatwimah mtoto wa Mjumbe wa Allaah ametajwa". Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Marhaban [karibu] na Ahlan)) [umo miongoni mwa familia])) kisha hakusema kitu zaidi. 'Aliy alirudi kwa kundi la ma-Answaar waliokuwa wakimsubiri na wakamuuliza imekuwaje. 'Aliy akasema: "Sijui amesema Marhaban na Ahlan". Wakasema, "mojawapo (ya maneno hayo mawili) kutoka kwa Mjumbe wa Allaah yangelitosheleza! Amekukaribisha kuwa mmoja katika wana familia. Kisha baada ya 'Aliy kumuoa Faatwimah, Mtume صلىالله عليه وآله وسلم akamuambia, ((Ewe 'Aliy, kila bwana harusi lazima afanye karamu)). Sa'ad akasema: "Mimi nina kondoo". Na kundi la ma-Answaar wakakusanya mahindi. Ulipofika usiku wa kuingia (usiku wa Ndoa), Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم alimuambia, ((Usifanye lolote hadi ukutane na mimi)). Kisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akaomba aletewe maji, akayatumia kwa wudhuu na akamwagia 'Aliy (yaliyobakia) huku akiomba, ((Ewe Allaah Wabariki hawa wawili na Wabariki katika kuingiliana kwao [ndoa yao]))[5]

 


Tatu:

عَنْ عَائِشَةَ ، قَالَتْ: تَزَوَّجَنِي النبي صلى الله عليه وسلم   فأتتني أمي فأدخَلَتني الدار، فَإِذَا نِسْوَةٌ مِنَ الأَنْصَارِ في البيت فَقُلْنَ: عَلَى الْخَيْرِ وَالْبَرَكَةِ، وَعَلَى خَيْرِ طَائِرٍ

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliponioa, mama yangu alikuja kwangu na akaniweka katika nyumba. Kuliwemo wanawake wa Answaar ndani ambao walisema: "(Ndoa) ya kheri na baraka, yaani ndoa yenye hadhi na kheri nyingi" ('Alal-Khayri Wal-Barakati Wa 'Ala Khayri Twaairiyn))[6]

 


Nne:

 

عن أبي هريرةَ ، عنِ النبيّ صلى الله عليه وسلّم أنَّهُ كانَ إذا رَفّأَ الإنسانَ إذا تزوج   قالَ: ((بارَكَ اللَّهُ لكَ وباركَ عليكَ وجمعَ بينكُمَا في خيرٍ))

 

Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه: "Kila mtu alipoanza kuishi na mkewe baada ya kumuoa, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم   alikuwa akisema, "Allaah Akubariki na Abariki juu yako, na Awajumuishe katika kheri" (Baaraka Allaahu Laka Wa Baaraka Allaahu 'Alayka Wa Jama'a Baynakumaa Fiy Khayrin)[7]

 

 



 

[1] Ibn Abi Shaybah, Muslim na wengineo

[2] Muslim, Ahmad na wengineo

[3] Ahmad, Al-Bayhaaqiy na wengineo: Swahiyh

[4] Al-Bukhaariy na Muslim

[5] Ibn Sa' na At-Tirmidhiy: Hasan

[6] Al-Bukhaariy, Muslim na Al-Bayhaaqiy

[7] Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na wengineo: Swahihy

 

 

Share

37-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuwaombea Bwana Harusi Na Bibi Harusi Watoto Wengi (Wa Kiume) Ni Msemo Katika Ada Ya Ujahiliya (Kabla Ya Uislam)

 

 

Haipasi kusema "Ujaaliwe watoto wengi wa kiume" kama wanavyofanya wengi walio wajinga katika jamii nyingi, kwa sababu ni ada/mila ya watu wa kabla ya Uislamu katika zama za ujinga (Ujaahiliyyah) ambayo imeharamishwa katika Hadiyth zaidi ya moja.

عَنِ الْحَسَنِ  قَالَ: تَزَوَّجَ عَقِيلُ بْنُ أَبِي طَالِبٍ امْرَأَةً مِنْ بَنِي جَثمٍ  فدخل عليه القوم، فقالوا     "بِالرِّفَاءِ وَالْبَنِينِ"  فقَالَ: لا تفعلوا ذلك [فإن رسول الله صلى الله عليه وسلم نهى عن ذلك]، قَالُوا فَمَا نَقُول يآ أبا زَيْد؟ قَال:  قُولُوا( كَمَا قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم): ((بَارَكَ اللَّهُ فِيكُمْ وَبَارَكَ لَكُمْ)). ( إنا كذلك كنا نؤمر)

Imetoka kwa Al-Hasan رضي الله عنه kwamba 'Uqayl ibn Abi Twaalib alimuoa mwanamke kutoka kabila la Jathm. Watu walikuja nyumbani kwake na wakasema: "Ujaaliwe kupata watoto wengi wa kiume". 'Uqayl akawaambia: 'Msifanye hivyo, kwani Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم amekataza hivyo'. Wakasema: Sasa tuseme nini ewe Abu Zayd? Akasema: Semeni kama alivyosema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم   ((Allaah Akubariki na Ateremshe Baraka juu yenu)). (Hivyo ndivyo tulivyoamrishwa kusema)"[1]

 

 

 



[1] Ibn Abi Shaybah, An-Nasaaiy na wengineo – yenye kutiliwa nguvu

Share

38-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Bibi Harusi Anaweza Kuwahudumia Wanaume

 

 

Hakuna ubaya kwa bibi harusi kuwahudumia mwenyewe wageni madamu atakuwa amevaa mavazi ya Kiislamu na ikiwa hakuna mategemeo ya uovu.
Hii ni kutokana na Hadiyth iliyosimuliwa na Sahl ibn Sa'ad ambaye amesema:

 

لما عرَّسَ أبو أُسَيد الساعِدِيُّ دعا النبيَّ صلى الله عليه وسلم وأصحابَهُ فما صنَع لهم طعاماً ولا قدم إليهم إلا امرأتُهُ أمُّ أُسيد، بَلَّتْ   (وفي رواية: أنقعت)  تَمَراتٍ في تَوْر من حجارةٍ منَ الليل، فلما فَرَغَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم من الطعام أماثَتْه له فسقَتْهُ تتْحِفُه بذلك . (فَكَانَتِ امْرَأَتُهُ يَوْمَئِذٍ خَادِمَهُمْ. وَهْيَ الْعَرُوسُ)

 

"Abu Usayd As-Saa'idiy alipooa na siku ile alipomuingilia mkewe, alimualika Mtume صلى الله عليه وآله وسلم pamoja na Maswahaba zake. Hakuna aliyetayarisha chakula au kuwahudumia isipokuwa mkewe Ummu Asyad. Aliroweka tende katika bakuli la udongo usiku uliopita. Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم alipomaliza kula, alimpakulia na kumtunikia, hivyo mkewe akawa ndiye mwenye kuwahudumia wageni na alikuwa ndiye bi harusi"[1]

 


Mavazi ya Kiislamu ni yale yanayotakiwa kuvaliwa kisheria

 

Nayo ni lazima yatimize masharti manane yafuatayo:

 
1) Mwili wote ufunikwe isipokuwa uso na viganja vya mikono.

 
2) Nguo isiwe yenye mapambo;

 
3) Lazima iwe nzito kiasi isiwe yenye kuonyesha mwili;

 
4) Lazima iwe ya kupwaya na sio ya kubana hata ikaonyesha kiwiliwili chake;

 
5) Asijitie manukato;

 
6) Isishabihi vazi la kiume;

 
7) Isishabihi mavazi ya kikafiri;

 
8) Isiwe ya kujionyesha, maana kwamba isiwe kwa ajili ya kiburi kuwa ni vazi bora kuliko la mwingine.


Katika kitabu kingine cha Shaykh Al-Albaaniy "Hijaab Ya Mwanamke Wa Kiislamu Katika Qur-aan Na Sunnah" ametoa hoja na dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah kwa kila sharti hizo)

 

 

 



[1] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

Share

39-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kuimba Na Kupiga Duff (Matari)

 

 

Inaruhusiwa mume kuwapa ruhusa wanawake katika harusi yake watangaze harusi kwa kupiga duff na kwa nyimbo zinazoruhusiwa tu. Nyimbo ziwe ni zile ambazo hazina maelezo ya uzuri wa maumbile au hazina maneno ya uovu. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-ala haya:

 


Kwanza:

عن الرُّبيِّعُ بنتُ مُعّوِّذِ بن عفراء: جاء النبيُّ صلى الله عليه وسلم فدخُلُ حين بُنِيَ عليَّ فجلسَ على فِراشي كمجلِسكَ منّي، (الخطاب للراوي عنها ) فجعلتْ جُوَيْرِياتٌ لنا يَضربنَ بالدُفِّ ويَندُبنَ مَن قُتلَ من آبائي يومَ بدرٍ، إذ قالت إحداهنَّ: "وفينا نبيٌّ يَعلمُ ما في غَدِ"، فقال: ((دَعي هذِهِ وقولي بالذيِ كنتِ تقولين))

Imetoka kwa Ar-Rubayy'i ibn Mu'awwidh رضي الله عنها ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliingia nyumbani kwangu baada ya usiku wa harusi na akakaa katika busati, akiwa karibu kama ulivyokuwa umekaa karibu na mimi (akiwa anamuelezea aliyeisimulia Hadiyth kutokwa kwake). Kisha vijakazi vyetu vya kike vikaanza kupiga duff na kuimba kwa kuwasifu waliouawa katika vita vya Badr". Kisha mmoja wao akasema: "Na miongoni mwetu yupo Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye anajua yatakayotokea kesho. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Acheni haya na rudieni kuimba miliyokuwa mkisema kabla ya haya))[1]

 


Pili:

 

عن عائشةَ أنها زَفَّتِ امرأةً إلى رجُلٍ منَ الأنصار، فقال نبيُّ الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا عَائِشَةُ! أَمَا كَانَ مَعَكُمْ لَهْوٌ؟ فَإِنَّ الأَنْصَارَ يُعْجِبُهُمُ اللَّهْوُ))

وفي رواية بلفظ : فقال

((فَهَلْ بَعَثْتُمْ مَعَهَا جَارِيَةً تَضْرِبُ بالدُّفِّ وتُغَنِّي؟)) قالت: تقول ماذا؟ قال: ((تقُولُ:

((أَتَيْنَاكُمْ أَتَيْنَاكُمْ

فَحَيُّونَا نُحَيِّكُمْ

لَوْلاَ الذَّهَبُ أَلاحْمَـرُ

مَا حَلَّتْ بِوَادِيْكُمْ

لَوْلا الحِنْطَةُ السَّمْرَاءُ

مَا سَمِنَتْ عَذَارِيْكُمْ))

 

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah الله عنها رضي kwamba alimharakiza? Au Alimsindikiza mwanamke kwa mumewe, siku ya harusi ya mwanamke kwa mume wa ki-Answaar. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamuambia, ((Ewe ‘Aaishah, hukuwa na nyimbo zozote (ulipokuwa unamsindikiza) kwani ma-Answaar wanapenda burudani au viburudisho?))[2]



Na katika riwaaya nyingine ya Hadiyth hii, inasemekana kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alisema, ((Ulimpeleka kijakazi mwanamke pamoja naye kumpigia duff na kuimba?)) Nikamuuliza: Aseme nini (aimbe nini)? Akasema, ((Mwache aseme:


Tumekujieni, Tumekujieni


Kwa hiyo tuamkieni ili tukuamkieni

 
Ingelikuwa sio dhahabu nyekundu


Asingelitwaa katika bonde lenu

 
Na isingelikuwa kwa mtama wa dhahabu

Wasingelinenepa Wanawari wenu))[3]

 

Tatu:

عن عائشةَ رضي الله عنها أَنَّ النبـيَّ سمع ناساً يُغَنُّونَ فـي عُرْسٍ وهم يقولونَ :

وأَهْدَى لَهَا أَكْبُشا  ً يُبَحْبِحْنَ فِـي الـمِرْبَدِ

وحِبُّكِ فـي النَّادِي   ويَعْلَـمُ ما فِـي غَد

وفي رواية:

  وزَوْجُكِ فـي النَّادِي ويَعْلَـمُ مَا فِـي غَدِ، قالتْ: فقالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((لا يَعْلَـمُ مَا فِـي غَدٍ إلاَّ الله سُبْحَانَهُ))  

Imetoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliwasikia watu wakiimba katika sherehe ya harusi wakisema:

 

"Na nitampa kondoo wake akichachawa (akirukaruka katika majani kwa furaha) katika karamu – Na mapenzi yako yapo katika klabu, na anajua kesho italeta nini.


Au katika maelezo mengine:

 
Na mumeo yuko katika klabu – Na anajua kesho italeta nini.

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Hakuna anayejua kesho italeta nini (kutatokea nini) isipokuwa Allaah سبحانه وتعالى))

 


Nne:

عن عامرِ بنِ سعدٍ البَجَلِـيِّ قالَ: دَخَـلْتُ علـى قَرَظَةَ بنِ كعبٍ وأبـي مسعودٍ وذَكَرَ ثالثاً،   ذَهَبَ عَلَـيَّ، وَجَوَارِي يَضْرِبْنَ بالدُّفِّ يُغَنِّـينَ، فقلتُ: تُقِرُّونَ علـى هَذَا وأَنْتُـمْ أصحابُ مـحمدٍ قالُوا: إنَّهُ قَدْ رُخِّصَ لَنَا فـي العُرُسَاتِ والنـياحةِ عندَ الـمُصِيْبَة  .وفي رواية:   وَفِي الْبُكاءِ عَلى الْمَيِّت فِي غَيْرِ نِيَاحَة

Kutoka kwa 'Aamir ibn Sa'ad Al Bajaliy ambaye amesema: "Nilimtembelea Qaradhwah bint Ka'ab na Abu Mas'uud na (akamtaja mwingine ambaye kanitoka), na nikawaona wajakazi wakipiga dufu na kuimba. Nikasema:  Nyote nyinyi mmenyamaza na mnakubali mambo haya na hali nyinyi ni Maswahaba wa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم? Wakasema: 'Kwa kweli, alitupa rukhsa ya kufanya haya katika sherehe za harusi na katika wakati wa maombolezo ya msiba".

 

Na katika riwaya nyingine (Wakati wa kilio kwa maiti bila kuwa na maombolezo (yenye kutaja kuhusu maiti na makelele).[4]

 


Tano:

عن أبي بلج يحيى بن سليم قال: قلت لمحمد بن حاطب: تزوجت امرأتين ما كان في واحدة منهما صوت، يعني دفاً، فقال محمد رضي الله عنه: قال رسول الله: ((فَصْلٌ مَا بَيْنَ الحَلالِ والحَرَامِ الصَوْتُ بالدَّفِّ)).

Kutoka kwa Abu Balaj Yahya ibn Saliym ambaye amesema: "Nilimuambia Muhammad ibn Haatwib: Nimeoa wanawake wawili na hakukuwa na sauti (yaani dufu) katika harusi yoyote. Muhammad akasema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((Yanayobainisha baina ya halaal (yaani ndoa za dhahiri) na yaliyoharamishwa (ndoa za siri) ni sauti za dufu))[5]

 


Sita:

قال رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم  : ((أَعْلِنُوا النِّكَاحَ))

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((Tangazeni ndoa))[6]

 



 

 

 



 

[1] Al-Bukhaariy

[2] Al-Bukhaariy

[3] At-Twabaraaniy katika 'Al-Awsatw' Hasan

[4] Al-Haakim, Al-Bayhaaqiy, An-Nasaaiy na wengineo

[5] An-Nasaaiy, At-Tirmidhiy na wengineo: Hasan

[6] An-Nasaaiy, At-Tirmidhiy na wengineo: Hasan

Share

40-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Kukataa Kufanya Mambo Yanayopingana Na Shari'ah

 

   

Anapofanya mtu sherehe ya ndoa, inampasa akatae kuingiza jambo lolote ambalo linalopingana (liloharamishwa) na shari'ah. Hii ni muhimu zaidi kuzingatia khaswa kuhusu ada nyingi ambazo zimekuwa ni mazoea kutendwa na Waislamu katika sherehe za ndoa, na kwa vile Maulamaa wa Kiislamu wamenyamaza kimya hata zikadhaniwa na Waislamu kuwa ni mambo yanayoruhusiwa. Nitazitanabahisha hapa zilizo muhimu katika ada hizo:

 


Kutundika Picha


Imeharamishwa kutundika picha za binaadamu au wanyama katika ukuta. Hakuna tofauti ikiwa ni picha za kuchorwa au za kupigwa au sanamu za kuchongwa zenye kivuli na zisizo na kivuli. Zote hizo ni marufuku. Ni vizuri mtu
kama hawezi japo kuziteketeza basi angalau aziondoshe.
(Shaykh Al-Albaaniy baada ya kutaja kuharamishwa aina zote za picha, zilizochorwa kwa mkono, za kamera au za vinyago, kisha anataja zilizoruhusiwa
kama watoto wa sanamu kama ilivyo katika Hadiyth ya ‘Aaishah رضي الله عنها na vile vile amekubali zile ambazo zinabidi kwa manufaa ya Waislamu mfano; picha za matibabu, picha za majambazi wanaotafutwa na kadhalika).


Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-ala haya:

 
Kwanza:

  عن عائشة رضي الله عنها قالت: دَخَلَ عَلَيَّ رَسُولُ اللّهِ وَقَدْ سَتَرْتُ سَهْوَةً لِي بِقِرَامٍ فِيهِ تَمَاثِيلُ.  ( وفي رواية: فيه الخيل ذوات الأجنحة)  فَلَمَّا رَآهُ هَتَكَهُ وَتَلَوَّنَ وَجْهُهُ وَقَالَ :((يَا عَائِشَةُ! أَشَدُّ النَّاسِ عَذَاباً عِنْدَ اللّهِ، يَوْمَ الْقيَامَةِ، الَّذِينَ يُضَاهُونَ بِخَلْقِ اللّهِ)) ( وفي رواية)

((إنَّ أصحابَ هذه الصُّورَ يُعذَّبُون، ويقال لهم: أحْيُوا ما خَلقتم،))  وقال: ((إن البيت الذي فيه الصُّورَ لا تدخله الملائكة)).  قَالَتْ عَائِشَةُ: فَقَطَعْنَاهُ فَجَعَلْنَا مِنْهُ وِسَادَةً أَوْ وِسَادَتَيْنِ.  [فَقَدْ رَأَيْتَهُ مُتَّكِئاً عَلى إِحْداهُمَا وَفِيهضا صُورَة] 

Kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Nilifungua pazia la chumba cha hazina ambalo lilikuwa na picha" (katika maelezo mengine: "ambalo lilikuwa lina picha za farasi wenye mbawa"). Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipoliona, alilichana na uso wake ukabadilika kuwa mwekundu kisha akasema, ((Ewe ‘Aaishah, watu watakaopewa adhabu kali kabisa mbele ya Allaah siku ya Qiyaamah ni wale wanaoigiza maumbile ya Allaah)) (katika usemi mwingine) ((Hakika wanaochora picha hizi wataadhibiwa na wataambiwa: Tieni uhai vile mlivyoviumba!)) Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akaendelea kusema, ((Hakika Malaika hawaingii nyumba ambayo ina picha)). ‘Aaishah akasema: Tukalikata pazia na tukalitumia kufanyia mto au mito miwili. Nimemuona akiegemea mto mmojawapo uliokuwa na picha"[1]

 


Pili:

عن عائشة رضيَ الله عنها قالت:  حَشَوتُ للنبيِّ صلى الله عليه وسلم وسادةً فيها تماثيُل كأنها نمرُقة، فجاءَ فقام بينَ البابين وجَعلَ يَتغيَّرُ وَجهُهُ، فقلتُ: ما لنا يا رسولَ الله؟  [أَتُوبُ إِلَى الله مِمَّا أَذْنَبْتُ]،  قَال: ((مَا بال هَذهِ ؟)) قُلْت: وِسَادة جَعلتُها لكَ لَتضْطَجِع عليها. قال:(( أما عَلِمْتِ أنَّ الْملائِكَةُ لا تََدْخلُ بَيْتاً فِيهِ صُورَة ؟ وَأنَّ مَنْ صَنَعََ الصُّورَةَ يُعذَّب يومَ القيامةِ فيقال: أحْيُوا ما خلقتم)) وفي رواية :((إنَّ أصحابَ هذه الصُّورِ يُعذَّبونَ يومَ القيامةِ))  [قَالَتْ: فَمَا دَخَل حَتَّى أَخْرَجتْها]    

Kutoka kwa ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema: "Niliujaza mto (pamba au sufi) kama wa kuegemea kwa ajili Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambao ulikuwa na picha. Alisimama baina ya milango miwili na uso wake ukabadilika rangi kwa ghadhabu. Nikasema: Nimefanya nini Ewe Mjumbe Wa Allaah? Nimetubu kwa Allaah kwa dhambi zozote nilizofanya. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Mto huu una nini?)) Nikasema: Nimueutengeneza kwa ajili yako ili uegemee. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Hukujua kama Malaika hawaingii katika nyumba ambayo ina picha na kwamba anayetengeneza picha hizi ataadhibiwa siku ya Qiyaamah na ataambiwa, huisha ulivyoviumba?)) (Na katika riwaaya) ((Wenye (kuchora) picha hizi wataadhibiwa siku ya Qiyaamah)). Akasema: Hakuingia hadi nilivyouondosha"[2]

 


Tatu:

قالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم ((أتَانِي جِبْرَائِلُ فقالَ لِي أتَيْتُكَ الْبَارِحَةَ فَلَمْ يَمْنَعْنِي أنْ أكُونَ دَخَلْتُ إلاَّ أنَّهُ كانَ عَلَى الْبَابِ تَمَاثِيلُ وَكَانَ في الْبَيْتِ قِرَامُ سِتْرٍ فِيهِ تَمَاثِيلُ وَكَانَ في الْبَيْتِ كَلْبٌ، فَمُرْ بِرَأْسِ التَّمْثَالِ الَّذِي في الْبَيْتِ يُقْطَعُ فَيَصِيرُ كَهَيْئَةِ الشَّجَرَةِ وَمُرْ بالسِّتْرِ فَلْيُقْطَعْ فَلْيُجْعَلْ مِنْهُ وِسَادَتَيْنِ مَنْبُوذَتَيْنِ تُوطَآنِ ومُرْ بِالْكَلْبِ فَلْيَخْرُجْ،   فَإنَّا لاَ نَدْخُل بيتاً فِيهِ صُورِة وَلاَ كَلْب))  وَإذَا الْكَلْبُ  [جرو]  لِحَسَنٍ أوْ حُسَيْنٍ كانَ تَحْتَ نَضَدٍ لَهُمْ ( وفي رواية: تحت سريره ) فَقَال:  ((يَا عَائِشَةُ مَتَىٰ دَخَلَ هٰذَا الْكَلْبُ هٰهُنَا؟)) فَقَالَتْ: وَاللّهِ مَا دَرَيْتُ. فَأَمَرَ بِهِ فَأُخْرِجَ  (ثم أخذ بيده ماءً فنضح مكانه)

 

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((Jibriyl عليه السلام alinijia na akaniambia: Nilikujia jana usiku na kitu pekee kilichonizuia kuingia ndani ni picha (binaadamu, yaani vinyago) katika mlango na pazia na katika nyumba kulikuwa na picha na kulikuweko na mbwa. Kwa hiyo kata kichwa cha picha mpaka kiwe kama ni mti tu, liendee pazia na lifanye mito miwili ya kuikalia na amrisha mbwa aondoshwe. Hakika sisi hatuingii nyumba ambazo zina picha au mbwa)). Mbwa alikuwa ni wa Hasan na Husayn ambaye alijificha chini ya sehemu ya kutundikia nguo. (katika riwaya nyingine imesema chini ya kitanda cha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  .. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Ewe ‘Aaishah, wakati gani ameingia mbwa huyu?)) Akasema: WaLlaahi sijui. Akaamrisha atolewe kisha akarashia maji kwa mikono yake mahali alipokuweko mbwa"[3]

 


Kufunika Ukuta Kwa Zulia


Jambo la pili linalopaswa kujiepusha nalo katika sherehe za harusi ni kwamba kusiweko na kufunikwa kuta kwa zulia au vibusati hata
kama vimetengenezwa kwa isiyokuwa hariri. Hii ni gharama na israaf ambayo hairuhusiwi katika Sharia. Nayo ni kutokana na Hadiyth ifuatayo kutoka kwa ‘Aaishah رضي الله عنها:

كان رسول الله صلى الله عليه وسلم غائباً في غزاة غزاها ، فَلَمَّا تَحَيَّنت قُفُولَه، فأخذتُ نَمَطاً (فيه صورة)، كانت لي فسترتُه على المَعْرِضِ، فلما  دَخَلَ رَسوُل الله صلى الله عليه وسلم  تَلَقَّيْتُهُ  فِي الْحجرة، فقلتُ: السلامُ عليك ورحمةُ اللَّهِ، الحَمْدُ للَّهِ الذي أَعَزَّكَ ونَصَرَكَ  وَأقَرَّ عَيْنَيْك وأَكْرَمَكَ، قَالَتْ  فَلَمْ يَرُدَّ عليَّ شيئاً  وَعَرَفْتُ فِي وَجْهِه الْغَضَب، وَدَخَلَ الْبَيْتَ مُسْرِعاً  وَأخَذَ النَّمْط بِيَدِهِ، فجذبه حَتَّى هتكه،  ثُمَّ قالَ: ((أتسترين الجدار؟!))  ((بستر فيه تصاوير؟!))، ((إنَّ اللَّهَ لم يَأْمُرْنَا فِيمَا رَزَقَنَا أنْ نَكْسُوَ الحِجَارَةَ  والطِّيْنَ)) قالتْ: فقطعنا منه وسادتين، وحَشَوْتُهما لِيفاً، فلَمْ يَعِبْ ذٰلكَ عليَّ  ( فكان صلى الله عليه وسلم يرتفق عليهما)

"Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipokuwa amekwenda katika vita vimojawapo, na wakati nikimtarajia kurudi, nilichukua busati langu ambalo lilikuwa lina picha nikafunika upande mmoja wa ukuta. Alipoingia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم nilikutana naye katika chumba cha nje na kumuambia: Assalaam 'Alaykum Ewe Mjumbe wa Allaah, Rahma na Baraka zikushukie. Sifa Zote ni za Allaah Aliyekuadhimisha?? Na Akakunusuru na adui wako, Akakutuliza macho?? Au Akawa pendezo la macho yako na Akukirimu". ‘Aaishah akaendelea: "Lakini hakunisemesha na nikatambua ghadhabu usoni mwake! Kisha akaingia ndani kwa haraka na akalivuta pazia kwa nguvu hadi akaliangusha kisha akasema, ((Unafunika ukuta na kwa pazia ambalo lina picha? Hakika Allaah Hakutuamrisha tuvishe mawe au saruji)). ‘Aaishah anaendelea: "Kwa hiyo tukalikata pazia na kulifanya mito miwili tukajaza na usumba. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakulipinga hili na alikuwa akiegemea mito hiyo"[4]


Hii ndio sababu kwamba Salafus Swaalih (wema waliotangulia) walikuwa wakigoma kuingia katika nyumba ambazo kuta zao zimefunikwa. Salim ibn 'Abdallaah kasema: "Niliona wakati wa maisha ya baba yangu. Alitangaza sherehe kwa watu na miongoni mwa walioalikwa alikuwa Abu Ayyuub. Walifunika kuta za nyumba yangu kwa kitambaa cha kijani. Abu Ayyuub alikaribia na kuingia katika nyumba na akaniona nimesimama. Kisha akatazama na akaona kuta za nyumba zimefunikiwa na mazulia ya kijani. Akasema:  'Ewe 'Abdallaah, umefunika kuta?' Baba yangu akaona hayaa akasema: 'Wanawake wana njia zao Ewe Abu Ayyuub!' (za kulazimisha jambo) Akajibu: 'Kuna wengine niliokhofu kuwa watatawaliwa na wanawake (yaani kwa kufanya makosa) lakini sikuwa na khofu kama hii kwako nawe'. Kisha akaondoka. Allaah Amrehemu."[5]

 


Kunyoa Nyusi


Jambo la tatu ovu la maasi ambalo Wanawake wengi wa Kiislamu wanalifanya ni kunyoa nyusi zao hadi zionekane
kama upinde au mwezi mwembamba. Wanafanya hivi wakidhania kuwa ni kuleta uzuri (wa sura) wakati ni jambo ambalo Mjumbe wa Allaah ameliharamisha na Allaah Anawalaani wanawake wanaonyoa nyusi.


Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم   amesema:

((لَعَنَ اللّهُ الْوَاشِمَاتِ وَالْمُسْتَوْشِمَاتِ، وَالْوَاصِلاَتِ،  وَالنَّامِصَاتِ وَالْمُتَنَمِّصَاتِ، وَالْمُتَفَلِّجَاتِ لِلْحُسْنِ الْمُغَيِّرَاتِ خَلْقَ اللّهِ))

((Allaah Amemlaani mwanamke anayefanya tattoo (kuchorwa kwa kuchanjwa) Na mwenye kuomba kufanyiwa, na anayetoa nyusi na mwenye kuomba kutolewa na anayechonga meno kuweka nafasi (mwanya), kubadilisha maumbile ya Allaah kwa ajili ya kupata uzuri))[6]

 


Kupaka Rangi Kucha Na Kuzikuza Kuwa Refu

 
Hii ni mila/ada nyingine ya kuchukiza ambayo imepangwa na kutendwa na wanawake wengi wa Kiislamu kutokana na upotovu wa wanawake nchi za kimagharibi. Wanawake hao wanapaka kucha zao kwa rangi nyekundu ya vanishi (minicore) na huku wakiyaacha makucha kuwa marefu. Hata vijana wengine wa Kiislamu wanafuga makucha
yao. Hii sio tu aina moja ya kubadilisha maumbile ya Allaah ambayo inastahiki laana ya Allaah kama tulivyoona hapo juu, bali pia ni kujifananisha na makafiri iliyokatazwa katika Hadithi nyingi na hii ni dhidi ya Fitwrah (hali ya kimaumbile na desturi ya Mitume wote).


Kuhusu kujifananisha na makafiri Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم   amesema:

((...وَمَنْ تَشَبَّهَ بِقَوْمٍ فَهُوَ مِنْهُمْ))

 ((Atakayejifananisha na watu, basi yeye ni miongoni mwao))[7] hali hii inakhalifu Fitwrah.


Na kuhusu kukata kucha, Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم   amesema:

 

((الْفِطْرَةُ خَمْسٌ : الْخِتَانُ،  و حلق العانة   وَقَصُّ الشَّارِبِ  وَتَقْلِيمُ الأَظْفَارِ، وَنَتْفُ الإِبِطِ،))  وَقَالَ أَنَس  رضي الله عنه : وُقِّتَ لَنَا فِي قَصِّ الشَّارِبِ، وَتَقْلِيمِ الأَظْفَارِ، وَنَتْفِ الإِبِطِ، وَحَلْقِ الْعَانَةِ، أَنْ لاَ نَتْرُكَ أَكْثَرَ مِنْ أَرْبَعِينَ يَوْماً

 

((Fitwrah ni mambo matano; khitaan (kutahiri), kunyoa nywele sehemu za siri, kukata masharubu, kukata kucha, na kunyofoa nywele za kwapa)) [8]

 
Anas
رضي الله عنه alisema, "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alituwekea muda wa kukata masharubu, kukata kucha, kunyoa nywele za kwapa, na kunyoa nywele za sehemu za siri kuwa tusiziache zaidi ya siku arubaini".[9]

 


Kunyoa Ndevu


Mila nyingine ya kuchukiza kama hizo nyingine au hata kuchukiza zaidi ni kama zile za kuwaiga makafiri na kuitakidi kuwa kunyoa ndevu ndio usafi na ni ustaarabu kuwaiga wazungu makafiri, hata imefikia hadi kuwa mume hawezi kuingia kwa mke wake siku ya harusi kama hajanyoa ndevu. Hii ni kinyume kabisa na sheria na inavunja sheria kwa njia nyingi
kama zifuatazo:

 


A. Kubadilisha Maumbile Ya Allaah.

 

Allaah سبحانه وتعالى Amesema Kuhusu Shaytwaan

 

((وَلأُضِلَّنَّهُمْ وَلأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الأَنْعَامِ وَلآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللّهِ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللّهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا))

 

 

((Na hakika nitawapoteza na nitawatia matamanio, na nitawaamrisha, basi watakata masikio ya wanyama, na nitawaamrisha, basi watabadili Aliyoumba Allaah. Na mwenye kumfanya shaytwaan kuwa ni mlinzi wake badala ya Allaah, basi huyo amekhasiri khasara ya dhaahiri)) (An-Nisaa: 119)


Hii ni matini na dalili iliyo dhahiri inayosema kwamba kubadilisha maumbile ya Allaah bila ya ruhusa Yake ni kutii amri ya shaytwaan na ni kumuasi Mola Mtukufu Mwenye Huruma. Kwa hiyo hakuna shaka kwamba Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم kuwalaani wanawake wanaobadilisha maumbile ya Allaah kwa ajili ya kuleta uzuri uliyotajwa kabla inawahusu pia wale wanaonyoa ndevu zao wakifikiri pia kama hii ni aina ya kuleta uzuri. Kwa hiyo laana inawahusu wao pia, khaswa kwa vile mas-ala mawili haya yanashirikiana katika sababu na zote zinasababisha laana ya Allaah. Sababu ya kusema hivyo "bila ya ruhusa ya Allaah" hapo juu, ni kwa vile hakuna atakayefikiria kwamba kunyoa nywele za siri na mengineyo yaliyotajwa katika Fitwrah kuwa yanahusiana na kubadilisha maumbile ya Allaah. Bali mambo haya yameruhusiwa na hata kusisitizwa na sheria.




B. Kuasi Amri za Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم

 

Juu ya hivyo, ni kumuasi Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ambaye amesema:

((قُصُّوا الشَّوَارِبَ، واعْفُوا اللِّحى))

 

((Kateni masharubu na acheni ndevu)).[10] Kama inavyojulikana katika Misingi ya Sheria ya Kiislamu (Usuulul-Fiqh) kuwa amri ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni wajibu isipokuwa mpaka upatikane muunganisho wa kufananisha, ambao ni kufanana na Kafiri (Qariynah) ipatikane ambayo itathibitisha kuwa yale yaliyokusudiwa katika amri ni mapendekezo na si wajibu.

 
Kuhusu ndevu, Mtume
صلى الله عليه وآله وسلم hakupata kunyoa ndevu zake, hakumruhusu yeyote kunyoa ndevu na wala hakushuhudia mtu aliyenyoa na kisha akaruhusu au kwa kukaa kimya. Kwa kifupi, dalili zote katika mas-ala haya yanatia nguvu ufahamu wa mwanzo wa amri ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kwamba ni wajibu kuziacha ndevu kukua na imeharamishwa kuzinyoa. Zifuatazo ni dalili za nyinginezo:

 


C. Kujifananisha na makafiri.

 

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema:

 

((جُزُّوا الشَّوارِبَ وارْخُوا اللِّـحَى خالِفُوا الـمَـجُوسَ))

((Punguzeni masharubu na acheni ndevu zenu ziwe ndefu, kuweni tofauti na Majusi))[11]

 



D. Kujishabihisha na Wanawake.

لَعَنَ رسول الله  صلى الله عليه وسلم  الْمُتَشَبِّهِينَ مِنَ الرِّجَالِ بِالنِّسَاءِ  وَالْمُتَشَبِّهَاتِ مِنَ النِّسَاءِ بِالرِّجَالِ

((Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amewalaani wanaume wanaojishabihisha na wanawake na wanawake wanaojishabihisha na wanaume))[12]

 

Kwa hakika mwanamume kunyoa ndevu zake ni kujifananisha na wanawake. Natumai kwamba dalili hizo tulizo zinukuu zitatosha kuwakinaisha wale waliofikwa na msiba wa kuhalifu amri za dini Namuomba Allaah Atujaalie sisi na wao usalama na kila Asilolipenda na Asiloridhika nalo.

 


Pete Ya Uchumba


Sita:


Waislamu wengi wanafuata na kutekeleza mila na desturi za kuvalishana pete ambayo inaitwa 'pete ya uchumba' (engagement ring). Mbali ya kuwa ni kigezo cha mila za makafiri kwa vile chanzo chake ni kutoka kwa manaswara, bali pia ni kukhalifu wazi wazi makatazo yaliyokuja katika nasw (matini) zilizo Swahiyh ambazo zimeharamisha kuvaa pete za dhahabu kwa Waislamu wanaume na wanawake kama tutakavyoeleze katika nasw (matini) zifuatazo:


Kwanza:

 

Kukatazwa Kwa Pete Ya Dhahabu

 

  ((نَهَى صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَنْ خَاتم الذَّهَب )).

 

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ameharamisha pete za dhahabu. (Al-Bukhaariy na Muslim)[13]

 


Pili:

عَنْ إبْنِ عَبَّاسٍ أَنَّ رَسُولَ اللّهِ رَأَىٰ خَاتِماً مِنْ ذَهَبٍ فِي يَدِ رَجُلٍ  فَنَزَعَهُ فَطَرَحَهُ وَقَالَ: ((يَعْمِدُ أَحَدُكُمْ إِلَىٰ جَمْرَةٍ مِنْ نَارٍ فَيَجْعَلُهَا فِي يَدِهِ))  فَقِيلَ لِلرَّجُلِ، بَعْدَ مَا ذَهَبَ رَسُولُ اللّهِ : خُذْ خَاتَمَكَ انْتَفِعْ بِهِ. قَالَ: لاَ. وَاللّهِ لاَ آخُذُهُ أَبَداً. وَقَدْ طَرَحَهُ رَسُولُ اللّهِ .

Kutoka kwa Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliona pete ya dhahabu katika kidole cha mwanamume, akaitoa na kuitupilia mbali na akasema, ((Je, mnataka mmoja wenu achukue kaa la moto na ajiwekee mkononi mwake?)) Baada ya Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم kuondoka mtu yule aliambiwa na watu, "Chukua pete yako na faidika nayo" (kwa kuiuza). Mtu huyo alisema: "Hapana, WaLlaahi, sitoichukua baada ya kutupwa na Mjumbe wa Allaah"[14]


Tatu:

 

عَنْ أَبِي ثَعْلَبَةَ الْخُشَنِيِّ ،: أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم أَبْصَرَ فِي يَدِهِ خَاتَما مِنْ ذَهَبٍ فَجَعَلَ يَقْرَعُهُ بِقَضِيبٍ مَعَهُ فَلَمَّا غَفَلَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم أَلْقَاهُ (فنظر النبي صلى الله عليه وسلم فلم يره في يده)   قَالَ: ((مَا أُرَانَا إلاَّ قَدْ أَوْجَعْنَاكَ وَأَغْرَمْنَاكَ))

 

Kutoka kwa Abu Tha'alabah Al-Khushaniy رضي الله عنه ambaye amesema kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliona pete ya dhahabu katika kidole chake akawa anaipiga kwa kijiti alichokuwa nacho. Alipokuwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hamtazami aliitupilia mbali. Kisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliitazama na hakuiona tena akasema, ((Umeitupa baada ya kukuumiza na kukutia maumivu))[15]


Nne:

عن عبد الله بن عمرو أنَّ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم رَأَى عَلىَ بَعْض أَصْحَابه خَاتماً مِن ذَهَب، فَأَعْرَضَ عَنْهُ، فَألْقَاه وَاتَّخَذَ خَاتِماً مِنْ حَديد قال: فَقال هذا شرٌّ هذا حلية أَهْل النَّار. فألقَاه وَاتَّخَذ خاتماً مِنْ وَرَق، فَسَكت عنه

Kutoka kwa 'Abdullaah ibn 'Amr رضي الله عنه ambaye amesema kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alimuona Swahaba mmoja amevaa pete ya dhahabu, akamgeuzia uso. Swahaba akaitupilia mbali pete na akavaa pete ya chuma. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamwambia, ((Hii ni mbaya zaidi. Pambo la watu wa motoni)). Kwa hiyo Swahaba akaitupilia mbali akavaa pete ya fedha. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakusema kitu kuhusu hiyo"[16]

 


Tano:

((مَنْ كَانَ يُؤْمِن بالله وَالْيَوْم الآخِر فَلاَ يَلْبس حَرِيراً وَلاَ ذَهَباً))

 

((Yeyote anayemuamini Allaah na Siku Ya Qiyaamah, basi asivae pete ya dhahabu))[17]

 


Sita:

 

((مَنْ لَبِسَ الذَّهَبَ مِنْ أُمَّتِي، فمَاتَ وَهُوَ يَلْبَسُهُ، حَرَّمَ الله عَلَيْهِ ذَهَبَ الجَنَّةِ))

 

((Yeyote atakayevaa dhahabu katika Umma wangu, na akifa akiwa ameivaa, ataharamishiwa na Allaah dhahabu ya Peponi))[18]

 

 



[1]Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[2] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[3]Abu Daawuud, An-Nasaaiy, At-Tirmidhiy na wengineo : Swahiyh

[4] Muslim, Abu 'Awwaanah na wengineo

[5] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[6] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[7] Abu Daawuud na Ahmad: Hasan

[8] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[9] Muslim, Abu Daawuud na wengineo

[10] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[11] Muslim na Abu 'Awwaanah

[12] Al-Bukhaariy, At-Tirmidiy na wengineo

[13] Al-Bukhaariy na Muslim

[14] Muslim, Ibn Hibbaan na At-Twabaraaniy

[15] An-Nasaaiy, Ahmad na wengineo: Swahiyh

[16] Al-Bukhaariy, Ahmad

[17] Ahmad: Hasan

[18] Ahmad: Swahiyh

 

Share

41-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Wajibu Wa Kuishi Mume Na Mkewe Kwa Huruma

 

 

Ni waajib wa Mume kuishi na mkewe katika hali njema kabisa na kuwa mpole kwake kwa yote Aliyoyaruhusu Allaah سبحانه وتعالى khaswa ikiwa mke ni mdogo kwa umri. Kuna Hadiyth mbali mbali kuhusu mas-ala haya:

 


Kwanza:

  قالَ رسُولُ اللّه صلى الله عليه وسلم ِ: ((خَيْرُكُمْ خَيْرُكُمْ لأَهْلِهِ، وَأَنَا خَيْرُكُمْ لاِهلِي))

   

Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((Mbora wenu ni yule ambaye ni mbora kwa wake zake, na mimi ni mbora wenu kwa wake zangu))[1]

 


Pili:

 

  قوله صلى الله عليه وسلم في خطبة حجة الوداع:  (( ...ألاَ واسْتَوْصُوا بالنِّسَاءِ خَيراً، فإنهن عَوانٌ عِنْدَكمْ لَيْسَ تَمْلِكُونَ مِنْهُنَّ شَيْئاً غَيْرَ ذلِكَ، إلاَّ أَنَّ يَأْتِينَ بِفَاحِشَةٍ مُبَيِّنَةٍ فَإِنْ فَعَلْنَ فَاهجُرُوهُنَّ في المضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ ضَرْباً غَيْرَ مُبَرِّحٍ. فَإنْ أطَعْنكُمُ فَلاَ تَبْغُوا علَيْهِنَّ سَبِيلاً. أَلاَ إنّ لَكُمْ عَلَى نِسَائِكُم حَقّاً. ولِنسَائِكمْ عَلَيْكُمْ حَقاً. فَأَمَّا حَقكُّمْ عَلَى نِسَائِكُمْ فَلاَ يُوطِئنَ فُرُشكُمْ مَنْ تَكْرَهُونَ ولاَ يَأْذَنَّ في بُيُوتِكُمْ لِمَنْ تَكْرَهُونَ. ألاَ وحَقهُنَّ عَلَيْكُمْ أنْ تُحسِنُوا إِلَيْهِنَّ فِي كِسْوَتِهِنَّ وطَعَامِهِن))

 

Kauli ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم katika Hijjat Al-Wadaai, ((Sikilizeni! Wafanyieni wema wanawake kwani wao ni wasaidizi wenu na hamuwamiliki zaidi ya hivyo.[2] Hamumiliki chochote kwao isipokuwa wakifanya uchafu ulio wazi. Wakifanya hivyo basi muwahame katika malazi (msijamiane nao) wapigeni pigo lisiloumiza (yaani watieni adabu tu msiwaumize) Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika nyinyi mna haki kwao na wao wana haki kwenu. Ama haki yenu kwa wake zenu ni wasimruhusu mtu msiyempenda kukalia zulia lenu wala wasimruhusu mtu msiyempenda kuingia nyumbani mwenu. Naam, na haki zao kwenu ni kuwafanyia wema katika kuwapatia mavazi na chakula chao"[3]


Tatu:

 

 ((لا يفرك( أي لا يبغض ) مُؤْمِنٌ مُؤمِنَة، إِنْ كَرِهَ مِنْهَا خَلْقاً رَضِيَ مِنْهَا آخر)) 

((Muumini mwanamume asimchukie Muumini mwanamke, ingawa anaweza kuchukia tabia moja (lakini) atapendekezewa na nyingine))[4]

 


Nne:

  ((أَكْمَلِ المؤمنينَ إيماناً أحْسَنُهُمْ خُلُقاً  وَخِيَاركُمْ خِيَاركُمْ لِنِسَائِكُمْ))

((Waumini waliokamilika kwa imani ni wale wenye tabia njema kabisa, na walio bora kabisa ni wale wanaowafanyia wema kabisa wanawake wao))[5]

 


Tano:

 

عَنْ عائِشَة رضي الله عنها قالت:  دَعانِي رسول الله صلى الله عليه وسلم (وَالْحَبَشَة يَلْعَبُونَ بِحرابِهِمْ في الْمَسْجِد)، (في يوم عيد)، فقال لي: ((يَا حميراء أَتُحِبِّينَ أَنْ تَنْظُرِي إِلَيْهْم؟)) فَقُلْتُ: نَعَمْ  (فأقامني وراءه)، فطأطأ لي منكبيه لأنظر إليهم، (فوضعت ذقني على عاتقه، وأسندت وجهي إلى خده)، فنظرت من فوق منكبيه ( وفي رواية: من بين أذنه وعاتقه ) (وهو يقول: ((دونك يا بني أرفده)) فجعل يقول: ((يا عائشة! ما شبعت!)) فأقول: لا، لأنظر منزلتي عنده) حتى شبعت(قالت: ومن قولهم يومئذ: أبا القاسم طيباً) وفي رواية:  (حتى إذا مللت، قال: ((حسبك؟)) قلت نعم، قال: ((فاذهبي))، وفي أخرى: ((قلت: لا تعجل، فقام لي، ثم قال : ((حسبك؟)) قلت: لا تعجل، (ولقد رأيته يرواح بين قدميه)، قالت: ما بي حب النظر إليهم، ولكن أحببت أن يبلغَ النساء مقامُه لي، ومكاني منه (وأنا جارية)، (فاقدروا قدر الجارية [العربة] الحديثة السن، الحريصة على اللهو)، [قالت: فطلع عمر، فتفرق الناس عنها والصبيان، فقال النبي صلى الله عليه وسلم : ((رأيت شياطين الإنس والجن فروا من عمر))،  قالت عائشة: قال صلى الله عليه وسلم يومئذٍ: ((لتعلم يهود أن في ديننا فسحة )). البخاري ومسلم وغيرهم.

 

Kutoka kwa mama wa waumini 'Aaishah kuwa alisema, "Siku ya 'Iyd Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuja kwangu wakati wa Habeshi (Wa-Ethiopia) walipokuwa wakicheza kwa kutumia mishale yao msikitini na kuniambia, ((Ewe mdogo mwekundu, unapenda kuwatazama?)) Nikajibu, Ndio. Kisha akanisimamisha nyuma yake na kuyateremsha mabega yake ili nipate kuwaona. Nikaweka kidevu changu mabegani mwake uso wangu ukiwa baina ya shavu lake. Nikawatazama kupitia kwenye mabega yake… huku akiniuliza mara kwa mara, ((Je, umetosheka?))  (kuwatazama) Nami niliendelea kusema: Bado, ili nijaribu kuona penzi lake kwangu hadi nilipotosheka". ‘Aaishah akasema: "Jambo moja walilosema siku hiyo ilikuwa ni: "Abu Al-Qaasim ni mwenye tabia njema". (Na katika riwaaya nyingine ilipokelewa kuwa alisema) "Nilipochoshwa na maonyesho, aliniuliza, ((Je, umetosheka?)) Nikajibu, "Usiniharakize". Kwa hiyo akaendelea kunisimamia. Aliponiuliza mara ya pili kama nimetosheka, nikamwambia tena asiniharakize. Nikamuona akibadilisha miguu yake kwa ajili ya machofu" ‘Aaishah akasema: "Sikuwa na hamu ya kuwatazama, bali nilitaka habari ziwafikie wanawake kuhusu Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kunijali na kusimama kwa ajili yangu (ili wajue jinsi gani alivyokuwa akinijali) ingawa nilikuwa msichana, (Na hii ) ili wathamini hali ya msichana mdogo kwa umri mwenye kupenda burudani na mchezo". ‘Aaishah akasema: "Kisha 'Umar akaja na watu wakatawanyika mpaka watoto. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Nimewaona mashaytwaan wote wa kibinaadamu na majini wakimkimbia 'Umar)). ‘Aaishah akasema, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema siku hiyo, ((Kwa hiyo Mayahudi wajue kuwa katika Uislamu kuna wasaa na ni Dini isiyokataza burudani na michezo??))[6]

 


Sita:

عنْ عَائِشَةَ،قَالَتْ: قَدِمَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم مِنْ غَزْوَةِ تَبُوكَ أَوْ خَيْبَرَ وَفِي سَهْوَتِهَا سِتْرٌ فَهَبَّتِ الرِّيحُ فَكَشَفَتْ نَاحِيَةَ السَّتْرِ عنْ بَنَاتٍ لِعَائِشَةَ لُعَبٍ، فقَالَ: ((مَا هٰذَا يَا عَائِشَةُ؟)) قالَتْ بَنَاتِي، وَرَأَى بَيْنَهُنَّ فَرَسَا لَهُ جَنَاحَانِ مِنْ رِقَاعٍ، فقَالَ: ((مَا هٰذَا الَّذِي أَرَى وَسْطَهُنَّ؟)) قَالَتْ فَرَسٌ، قَالَ: ((وَمَا هٰذَا الَّذِي عَلَيْهِ؟)) قُلْتُ جَنَاحَانِ، قَالَ: ((فَرَسٌ لَهُ جَنَاحَانِ؟)) قَالَتْ أمَا سَمِعْتَ أَنَّ لِسُلَيْمانَ خَيْلاً لَهَا أَجْنِحَةٌ، قَالَتْ: فَضَحِكَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم حَتَّى رَأَيْتُ نَوَاجِذَهُ .

Kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها ambaye amesema "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alirudi kutoka vita vya Tabuuk au vya Khaybar. Kulikuwa na pazia chumbani kwake. Upepo ukapeperusha na ukainua pazia na kuonyesha sehemu ya chumba ambacho Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliona watoto wa sanamu aliokuwa akichezea ‘Aaishah. Akauliza, ((Nini hii ewe ‘Aaishah?)) Akajibu, "Watoto wangu wa kike".  (Waarabu walikuwa wakiwaita masanamu "watoto wa kike"). Aliona pamoja nao farasi mwenye mbawa mbili aliyetengenezwa kwa kitambaa.  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akamuuliza tena mama wa waumini 'Aaishah, ((Na hii nini katikati?)). Akajibu, "Ni farasi". Akauliza tena, ((Na nini hivyo vilivyo juu ya farasi?)). 'Aaishah akajibu, "Mbawa mbili". Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Farasi mwenye mbawa mbili?)) ‘Aaishah akasema, "Je, hukusikia kuwa Nabii Sulayman alikuwa na farasi wenye mbawa?"  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم (baada ya kusikia hayo) alicheka mpaka nikayaona magego yake"[7]

 


Saba:

 

عن عائشةُ رضي الله عنها أَنَّهَا كانتْ معَ النبيِّ في سَفَرٍ وهي جاريةٌ، (قالت: لم أحمل اللحم، ولم أبدن)، فقالَ لأَصْحَابِهِ: ((تَقَدَّمُوا))، (فَتَقَدَّمُوا)، ثم قالَ: ((تَعَالَيْ أُسَابِقْكِ))، فَسَابَقْتُهُ فَسَبَقْتُهُ على رِجْلَيَّ، فلمَّا كانَ بَعْدُ، خرجتُ أيضاً مَعَهُ في سفرٍ، فقالَ لأَصْحَابِهِ: ((تَقَدَّمُوا))، ثم قالَ: ((تَعَالَيْ أُسَابِقْكِ))، ونسيتُ الَّذِي كانَ وقد حَمَلْتُ اللحمَ،[وبدّنت]، فقلتُ: وكيفَ أُسَابِقُكَ يا رسولَ اللَّهِ وأَنَا على هذِهِ الحالِ، فقالَ: ((لَتَفْعَلِنَّ))، فَسَابَقْتُهُ فَسَبَقَنِي، (فـجعل يضحك،) و فقالَ: ((هذِهِ بِتِلْكَ السَّبْقَةِ))

 

  
Kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah
عنها رضي الله kwamba alikuwa pamoja na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم katika safari naye akiwa ni msichana mdogo. (mama wa waumini 'Aaishah akielezea safari hiyo alisema), "Sikuwa mnene na wala sikuwa na mwili mkubwa". Wakati huo Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم aliwaambia Maswahaba wake, ((Tangulieni)). Walipotangulia na wakawa mbele yetu, Mtumeصلى الله عليه وآله وسلم akaniambia, ((Njoo nishindane na wewe mbio)) Nikamshinda mbio za mguu. Baada ya muda kupita hivi, nikawa naye tena katika safari na akawaambia tena Maswahaba wake, ((Tangulieni)) Kisha akaniambia, ((Njoo nishindane na wewe mbio)). Nilisahau kabisa mashindano ya mbio ya mwanzo. Juu ya hivyo nilikuwa nimenenepa. Nikamuambia, "Nitakimbia vipi nami niko katika hali hii?" Akanijibu, ((Utashindana nami)). Nikakimbia naye akashinda mbio. Akaanza kucheka na kusema, ((Hii ni kulipiza ushindi wako wa mwanzo))[8]

 


Nane:

 

عن عَائِشَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا إن كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ليؤتىٰ بالإناء فَأَشْرَبُ مِنْهُ وَأَنَا حَائِضٌ ثُمَّ  ثُمَّ يَأْخُذْهُ فَيَضَع فاهُ عَلَى مَوْضِع فيّ وَإنْ كُنْت لآخذ الْعَرَق فآكُل مِنْه، ثُمَّ يَأخُذه فَيَضَع فَاهُ عَلى مَوْضِع فيّ

 
Kutoka kwa mama wa waumini ‘Aaishah
رضي الله عنها ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa akiletewa gilasi ya maziwa ambayo nilikuwa nikinywa kwanza na huku niko katika hedhi. Kisha akiichukua gilasi na akiiweka mdomo wake pale nilipoweka mimi mdomo wangu na kunywa. Mara nyingine nilikuwa nikichukua kipande cha nyama na kukila kisha naye akikichukua na kuweka mdomo wake pale nilipokula mimi kisha hukila"[9]

 


Tisa:

عن جابر بن عبد اللَّه وجابر بن عمير رضَي اللَّهُ عنهُ   قالا: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((كُلُّ شَيْءٍ لَيْسَ فِيهِ ذِكْرِ اللَّهِ فَهُوَ (لغوٌ) وَسَهْوٌ وَلَعِبٌ إِلاَّ أَرْبَعَ (خصال): مُلاَعَبَةُ الرَّجُلِ امْرَأَتَهُ، وَتَأْدِيبُ الرَّجُلِ فَرَسَهُ، وَمَشْيَهُ بَيْنَ الهَدَفَيْنِ، وَتَعْلِيمُ الرَّجُلِ السبَاحَة

Kutoka kwa Jaabir ibn 'Abdillaah رضي الله عنه pamoja na Jaabir ibn 'Umar رضي الله عنه ambao wote wawili wameripoti kuwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema, ((Vitu vyote pasi na kumtaja Allaah ni upuuzi, usahaulifu na mchezo isipokuwa vitu vinne; mtu kucheza na mkewe, kumfundisha farasi, kutembea baina ya lengo lililokusudiwa, na kumfundisha mtu kuogelea))[10]

 



[1] At-Twahaawiy: Swahiyh

[2] Tuhfatul-Ahwadhiy Sharh At-Tirmidhiy 4/326 na Sharh Ibn Maajah 1/567

[3] At-Tirmidhiy na Ibn Maajah: Swahiyh

[4] Muslim na wengineo

[5] At-Tirmidhiy na Ahmad: Hasan

[6] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[7] Abu Daawuud, An-Nasaaiy katika 'Al-Ishraah': Swahiyh)

[8] Al-Humaydiy, An-Nasaaiy katika 'Al-Ishraah', Abuu Daawuud na wengineo: Swahiyh

[9] Muslim, Ahmad na wengineo

[10] An-Nasaaiy katika 'Al-Ishraah' At-Twabaraaniy na wengineo

Share

42-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Nasaha Kwa Mume Na Mke

 

Kwa kumalizia, natoa Nasaha zifuatazo kwa mume na mke

 
Kwanza:

-  Wanasihiane katika kumtii Allaah

 
- Wafuate amri za Allaah zilizomo kwenye Qur-aan na Sunnah

- Wasitangulize desturi na mila zao au madhehebu yao juu ya hukumu za kisheria alizoweka Allaah

Allaah Anasema:

((وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا))

 

"Haiwi kwa Muumini mwanamume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika jambo, Allaah na Mtume Wake wanapokata shauri katika jambo lao. Na mwenye kumuasi Allaah na Mtume Wake basi hakika amepotea upotofu ulio wazi" (Al-Ahzaab: 36)

 

Pili:

 

Kila mmoja wao atimize mas-uliyya yake aliyowajibishwa na Allaah سبحانه وتعالى Amemuwajibishia. Kwa hiyo mke asidai haki sawa na za mume katika haki zake zote na mume asitumie cheo chake alichofadhilishiwa na Allaah cha uongozi na mamlaka kwa kumkandamiza na kumdhulumu mke, kumpiga au kumuonea bila ya haki yoyote ile.

 

Allaah سبحانه وتعالى Anasema:

 

((وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ وَاللّهُ عَزِيزٌ حَكُيمٌ))

  

((Nao wanawake wanayo haki kwa Sharia kama ile haki iliyo juu yao. Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao. Na Allaah ni Mwenye Nguvu na Mwenye Hikima)) [Al-Baqarah: 228]

 

Katika Aayah nyingine Allaah سبحانه وتعالى Anasema:

 

((الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاء بِمَا فَضَّلَ اللّهُ بَعْضَهُمْ عَلَى بَعْضٍ وَبِمَا أَنفَقُواْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللّهُ وَاللاَّتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَاهْجُرُوهُنَّ فِي الْمَضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ فَإِنْ أَطَعْنَكُمْ فَلاَ تَبْغُواْ عَلَيْهِنَّ سَبِيلاً إِنَّ اللّهَ كَانَ عَلِيًّا كَبِيرًا))

 

((Wanaume ni wasimamizi wa wanawake, kwa kufadhiliwa na Allaah baadhi yao juu ya baadhi, na kwa mali yao wanayoitoa. Basi wanawake wema ni wale wenye kutii na wanaojilinda hata katika siri kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajilinde. Na ambao mnachelea kutoka katika utiifu wanasihini, muwahame katika malazi na wapigeni. Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika Allaah Ndiye Aliye juu na Mkuu)) [An-Nisaa: 34]

 

 

  وقد قال مُعَاوِيَةَ بن حيدة رضي الله عنه: يَارَسُولَ الله مَا حَقُّ زَوْجَةِ أَحَدِنَا عَلَيْهِ؟ قال: ((أَنْ تُطْعِمَهَا إذَا طَعِمْتَ، وَتَكْسُوَهَا إذَا اكْتَسَيْتَ وَلا تُقَبِّحْ وَلاتَضْرِبِ الْوَجْهَ، ( وَلا تَهْجُرْ إلاَّ في الْبَيْتِ كَيْفَ وَقَدْ أَفْضَى بَعْضكُمْ إِلَى بَعْضٍ؛ إِلاَّ بِمَا حلَّ عَلَيْهِنَّ)

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم : ((الْمُقْسِطُونَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَلَى مَنَابِرَ مِنْ نُورٍ عَنْ يَمِينِ الرَّحْمٰنِ وَكِلْتَا يَدَيْهِ يَمِينٌ، الْمُقْسِطُونَ عَلَى أَهْلِيهِمْ وَأَوْلاَدِهِمْ وَمَا وَلُّوا))

 

Mu'aawiyyah bin Haydah رضي الله عنه amesema: "Ewe Mjumbe wa Allaah, haki gani wake zetu wanazo juu yetu?" Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Muwalishe kama mnavyojilisha wenyewe, muwavishe kama mnavyojivisha wenyewe, wala msiwaombee ubaya, (hii ni kutokana na mila ya Waarabu kabla ya Uislamu wakiwaombea wake zao wanapokuwa na ghadhabu, "Allaah akujaalieni sura mbaya", msiwapige usoni mwao, na katika kuhama malezi msitoke nje ya nyumba kulala. Vipi (mtafanya mambo hayo) na ilhali mmekwisha ingiliana nyinyi kwa nyinyi, kwa hiyo fanyeni yale yaliyoruhusiwa kuwafanyia)) (iwe kwa sababu inayokubalika na shariy'ah"[1]   (katika riwaaya nyingine) Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  amesema, ((Wafanyao uadilifu watakuwa katika minbar ya mwangaza upande wa kulia wa Allaah na Mikono yote ya Allaah ni ya kulia[2], wale waliokuwa na uadilifu katika familia zao na kwa yote waliyopewa mamlaka))[3]

 

Wote wawili watakapojua na kutekeleza haya, Allaah سبحانه وتعالى Atawajaalia maisha mema na wataendelea kuishi hivyo hivyo maadamu watakuwa pamoja katika furaha na raha mustarehe. 

 

Anasema Allaah سبحانه وتعالى:

 

((مَنْ عَمِلَ صَالِحًا مِّن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَى وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَنُحْيِيَنَّهُ حَيَاةً طَيِّبَةً وَلَنَجْزِيَنَّهُمْ أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ مَا كَانُواْ يَعْمَلُونَ))

 
((Wafanyaji mema, wanaume au wanawake, hali ya kuwa ni Muumini, Tutawahuisha maisha mema; na Tutawapa ujira wao mkubwa kabisa kwa sababu ya yale mema waliyokuwa wakiyatenda)) (An-Nahl: 97)

 
 

Tatu:

Mwanamke khaswa inampasa kuwa mtiifu kwa mumewe kwa kadiri ya uwezo wake. Na hii ndivyo Allaah Alivyowafadhilisha wanaume juu ya wanawake kama ilivyo katika aayah mbili zifuatazo:

 

ِ((وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ))

  

((Na wanaume wana daraja zaidi kuliko wao)) (Al-Baqarah: 228

 

((الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاء))

 

 ((Wanaume ni wasimamizi wa wanawake)) (An-Nisaa: 34)

Kuna Hadiyth nyingi Swahiyh ambazo zimesisitiza maana hii, nazo zimeelezea dhahiri haki za mwanamke akiwa ni mtiifu au sio mtiifu. Ni muhimu kuzitaja baadhi ya Hadiyth hizo kama ni ukumbusho kwa wanawake wetu wa siku hizi kwa vile Allaah سبحانه وتعالى Anasema:

 

 

 

 ((وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَى تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ))

 

((Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini)) (Ad-Dhaariyaat: 55)

 

 
Kwanza:

 

((لا يَحِلُّ للمرأةِ ان تصومَ ( وفي رواية) (لاَ تَصُمِ الْمَرْأَةُ) وَزَوْجُهَا شَاهِدٌ إلاَّ بِإذْنِهِ (غَيْرِ شَهْرِ رَمَضَانَ) ولا تأذَن في بيته إلا بإِذنِهِ))

 

((Haimpasi mwanamke kufunga na wakati mumewe yupo ila kwa ruhusa yake isipokuwa Ramadhaan na wala asimruhusu mtu yeyote kuingia nyumbani kwake ila kwa ruhusa yake))[4]

 

Pili:

 

((إِذَا دَعَا الرَّجُلُ امْرَأَتَهُ إِلَى فِرَاشِهِ، فَلَمْ تَأْتِهِ، فَبَاتَ غَضْبَانَ عَلَيْهَا، لَعَنَتْهَا الْمَلاَئِكَةُ حَتَّى تُصْبِحَ)) وفي رواية: ((أَوْحَتَّى ترجع))، وفي أخرى: ((حَتَّى يُرْضى عَنْهَا))

 

((Mume atakapomwita mkewe kitandani na akikataa mke, na mume akawa ameghadhibika, basi Malaika watakuwa wanamlaani huyo mke mpaka asubuhi)) (katika riwaaya nyingine) ((Mpaka arudi kwake)) (na riwaaya nyingine) ((Mpaka aridhike naye))[5]

 

Tatu:

 

((وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لاَ تُؤَدِّي الْمَرْأَةُ حَقَّ رَبِّهَا حَتَّى تُؤَدِّيَ حَقَّ زَوْجِهَا وَلَوْ سَأَلَهَا نَفْسَهَا، وَهِيَ عَلَى قَتَبٍ، لَمْ تَمْنَعْهُ))

 

((Naapa kwa Yule Ambaye Nafsi ya Muhammad imo Mikononi Mwake, mwanamke atakuwa hakutimiza haki ya Mola wake hadi atimize haki ya mumewe, hata kama akimtaka akiwa juu ya tandiko la farasi, (basi hatakiwi) kumkatalia ombi lake))[6]

 

Nne:

 

((لاَ تُؤْذِي امْرَأَةٌ زَوْجَهَا فِي الدُّنْيَا  إِلاَّ قَالَتْ زَوْجَتُهُ مِنَ الْحُورِ الْعِينِ: لاَ تُؤْذِيهِ. قَاتَلَكِ اللَّهُ فَإِنَّمَا هُوَ عِنْدَكِ دَخِيلٌ أَوْشَكَ أَنْ يُفَارِقَكِ إِلَيْنَا))

 

((Kila mara mke anapomuudhi mumewe duniani, mke wake katika Mahuurul-'Ayn (Wake wa Peponi) husema: Usimuudhi, Allaah Akuangamize! Kwani yeye kwako ni mgeni tu, na karibu ataachana na wewe atatujia sisi))[7]

Tano:

 

عن حُصَيْنٍ بنِ مِـحْصَنٍ قالَ حدثتنـي عَمَّتِـي قالتْ: أتـيتُ رسولَ الله فـي بعضِ الـحاجةِ قالَ: «إِيْ هذِهِ أَذَاتُ بَعْلٍ أَنْتِ»، قلتُ: نَعَمْ، قال: «فكيفَ أَنْتِ لَهُ»، قالتْ: (فَقُلْتُ:) ما آلوهُ إلاَّ مَا عَجَزْتُ عنهُ، قالَ: «فأَيْنَ أَنْتِ منهُ، فإنَّـمَا هو جَنَّتُكِ ونَارُكِ»

 

Kutoka kwa Huswayn bin Mihswan ambaye amesema: "Shangazi yangu alinisimulia (Hadiyth) akisema, 'Nilikwenda kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم nikiwa nimehitaji baadhi ya haja, akasema, ((Ewe fulani! Je, umeolewa?)) Nikasema, "Ndio". Akaniuliza, ((Uko vipi na mumeo?)) Nikajibu, "Sina upungufu wowote kwake isipokuwa yale nisiyoyaweza kufanya". Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Basi jiangalie hali yako katika uhusiano wako kwake, kwani yeye ni ufunguo wako wa Pepo na Moto))[8]

 
Sita:

((إذا صَلَّتِ المَرْأَةُ خَمْسَها، (وصَامَتْ شَهْرَها)، وحَصَّنَتْ فَرْجَهَا، وأطَاعَتْ بَعْلَهَا، دَخَلَتْ مِنْ أيِّ أبوابِ الجَنَّةِ شَاءَتْ))

 

((Mwanamke atakaposwali Swalah zake tano, akahifadhi sehemu zake za siri (asifanye uzinifu), akamtii mume wake, ataingia peponi kupitia mlango wowote autakao))[9]

 

 


[1] Ahmad: Swahiyh

[2] Allaah ana mikono miwili na mikono yote miwili ni ya kulia. Uzindushi: Ahlu Sunnah wal Jama’ah wote humsifu Allaah kama Alivyojisifu mwenyewe au kama alivyosifiwa na Mtume Wake bila ya kuzidisha au kupunguza au kubadilisha jina au sifa yoyote ile, na wakati huo huo hawamfananishi Allaah na chochote kati ya alivyoviumba (Rejea Surat Shuuraa ayah ya 11)

Nu’aym bin Hammaad Shaykh wa Imaam Al-Bukhaariy amesema, ‘Mwenye kumfananisha Allaah na viumbe Vyake amekufuru. Na anayezikanusha sifa alizojisifia nazo Allaah Mwenyewe kwa kuisifia Nafsi Yake amekufuru. Na hakuna katika sifa alizojisifia nazo Allaah wala kusifiwa na Mtume Wake upinzani (Mfasiri)

[3] Muslim

[4] Al-Bukhaariy na wengineo

[5] Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo

[6] Ibn Maajah, Ahmad na wengineo: Swahiyh

[7] At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na wengineo: Swahiyh

[8] At-Twabaraaniy katika 'Al-Awrat', Ibn Maajah na Ahmad: Swahiyh

[9] At-Twabaraaniy katika 'Al-Awrat', Ibn Hibbaan na wengineo: Hasan au Swahiyh

 

 

Share

43-Adabu Za Ndoa Katika Sunnah Iliyotakasika: Wajibu Wa Mwanamke Kumhudumia Mumewe

 

Ninasema: baadhi ya Hadiyth zilizotajwa zinaonyesha dhahiri wajibu wa mwanamke kumtii na kumhudumia mumewe madamu anao uwezo, na hakuna shaka kwamba jambo la kwanza linaloingia humu ni huduma za nyumba na yote yanayohusika humo kama kulea watoto na kadhalika. Maulamaa wamekhitilafiana katika mas-ala haya, kwa mfano Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema katika 'Al-Fataawa' (2/234-235),

 
"Maulamaa wamekhitilafiana katika mas-ala haya kama inampasa kumhudumia kama kushughulika na fenicha za nyumba na kutayarisha chakula na vinywaji, kusaga unga na kupika chakula kwa ajili ya watumwa wake na kuwalisha farasi na kadhalika. Kuna wengine wanaosema, Huduma hii sio lazima. Kauli hii ni dhaifu, kama ilivyo udhaifu wa kauli za wale wanaosema kuwa mume haimpasi kumtendea wema au kujimai naye. Kwa vile hii haitokuwa ni kumfanyia wema, kama ni rafiki katika safari…Ikiwa hatomsaidia maana yake ni kuwa hajamtendea wema.

Na inasemekana: Na hii ndio sawa, kwamba kumhudumia ni wajibu kwa vile mumewe ameitwa ni bwana wake katika kitabu cha Allaah سبحانه وتعالى katika Sunnah ya Mjumbe wa Allaah  na mtumwa na mateka wanapaswa kuhudumiwa na kwa sababu hivyo ndivyo inavyojulikana sana.
Kisha kuna waliosema, Huduma nyepesi ya kawaida ni wajibu na wapo waliosema, ni wajibu kufanya wema na hili haswa ndio la sawa sawa.

 
Hivyo basi ni juu yake ahudumie katika mema ya kawaida ya mfano wake, hali hii inatofautiana na anuai za shughuli, kwa mfano mwanamke wa kibedui anatofautiana na mwanamke wa kijijini kwa anuai za shughuli na huduma anayotoa, kadhalika mwanamke mwenye nguvu atatofautiana na mwanamke dhaifu.

Nasema na hii ni Swahiyh Insha-Allaah, na ni usemi wa Maalik na Asbigh kama ilivyo katika 'Al-Fat-h' (9/418) na Abuu Bakar ibn Abu Shaybah na wengineo kama Al-Atwazijaariy wa Hanbali kama ilivyo katika 'Ikhtiyaaraat' (Ukurasa 145) na kundi la Maulamaa wa zamani na wa sasa kama ilivyo katika 'Az-Zaad' (4/46) na hatuoni dalili yoyote ya kufaa inayosema kuwa jambo hili halina uwajibu.

Na wengine wanasema: Kufunga ndoa kunahitaji starehe kufaidiana na sio kuhudumika rai hii imetupwa kwa sababu suala la starehe ni la wote.

 

Kama tunavyojua kuwa Allaah سبحانه وتعالى Amemuwajibisha zaidi mwanamume katika kumpatia mahitaji yake mke kama nguo, maskani na kumtimizia mahitajio yake. Kwa hiyo vile vile yeye mke pia anayo yaliyozidi kuwa wajibu kwake na hakuna zaidi ila ni kumhudumia. Khaswa kwa vile mume ndiye mwenye mamlaka ya mke, kwa hiyo ikiwa hatomhudumia, itabidi yeye mume amhudumie mke katika nyumba na hii itamfanya mke awe na mamlaka badala yake, jambo ambalo ni kinyume na Aayah ya Qur-aan kama ilivyo wazi. Kwa hiyo ni wajibu wa mke amhudumie mume.

 

Vile vile kuhudumu kwa mume kutaleta hali mbili zenye kugongana kwamba mume atazuilika kutafuta rizki na mahitajio mengine ambayo alipaswa kufanya na mwanamke atabakia nyumbani bila ya kufanya lolote.

Uharibifu/ufisadi huu upo dhahiri kabisa katika sheria ya Kiislamu, sheria ambayo imeweka usawa baina ya mume na mke katika haki mbali mbali, si hivyo tu bali pia umemfadhilisha mwanamume katika daraja na ndio maana Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakusikiliza malalamiko ya bintiye Faatwimah. Tunasoma malalamiko hayo katika Hadiyth ifuatayo,

 
“Faatwimah alikwenda kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kushitakia ugumu wa kazi za mikono nyumbani kwake, ingawaje hakumkuta babake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم lakini alimuachia maagizo Ummul Muuminina ‘Aaishah. ‘Aliy anahadithia kuwa (baada ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kupata salamu zile) Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikwenda kwao na wakati huo walikuwa wameshapanda kitandani yeye na mkewe kulala, ‘Aliy anasema, ‘Tulitaka kusimama (baada ya kumuona Mtume صلى الله عليه وآله وسلم) lakini akatukataza na kutuambia, “Hapo hapo mlipo” Akakaa katikati yetu pale kitandani kiasi nikahisi ule ubaridi wa miguu yake tumboni mwangu. Akutuambia, “Je, nikujulisheni jambo zuri zaidi kuliko lile mliloomba?” Mnapoingia kitandani semeni "Subhaana-Llaah' mara thelathini na tatu, 'Alhamduli-Llaah' mara thelathini na tatu na 'Allaahu Akbar' mara thelathini na nne, kwani hiyo ni bora kuliko kuwa na mtumishi”[1]

Kwa hiyo mnaona kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakumwambia 'Aliy, kuwa hana haja ya kukuhudumia bali inambidi (Faatwimah) amhudumie mumewe. Na yeye Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hakupendelea watu fulani katika kutoa sheria kama alivyotaja Ibn Al-Qayyim. Na anayetaka kujua zaidi kuhusu mas-ala haya basi asome kitabu chake cha thamani "Zaadul-Ma'aad' (4/45-46).

Majukumu ya mke kwa mumewe hayakatazi au kuzuia mume kumsaidia mke wake katika kazi zake. Hakuna kitu cha kudai mapendeleo ya usaidizi wa mume kwa mkewe ikiwa atapata wakati, bali hiyo ni mojawapo wa kutendeana wema baina ya mke na mume, na ndiyo mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها alisema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa akihudumia familia yake na Swalah ilipowadia alikuwa anakwenda kuswali"[2]

 
Na imenukuliwa katika 'Ash-Shamaa'il' (2/185) kutoka isnaad nyingine kwa maneno: "Mwanamume alikuwa akishughulikia nguo zake mwenyewe, akikamua kondoo maziwa, na akijihudumia mwenyewe". Na usimulizi wake ni Swahiyh na nyinginezo kidogo ni dhaifu.  Lakini Ahmad na Abu Bakar Ash-Shaafi'y wamenukuu kwa isnaad iliyo na nguvu kama nilivyoonyesha katika 'Silsilatul-Ahaadiythis-Swahiyhah' (Namba 670) na kufuzu ni kutokana na tawfiki ya Allaah سبحانه وتعالى.

Huu ni mwisho wa yale Aliyoniwezesha Allaah سبحانه وتعالى kuandika kuhusu ‘Adabu za Ndoa na Sherehe za Harusi’ katika kitabu hiki.

 

 

 

سُبْحـانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْك
 

 

Subhaanaka Allaahuumma Wa Bihamdika, Ash-Hadu An Laa Ilaaha Illa Anta, Astaghfiruka Wa Atuubu Ilayka.

 


[1] 'Aliy amesema: "Sikuiacha tena baada ya hapo". Ilisemwa:  Hata usiku wa Siffiyn? Akasema: "Hata   usiku wa Siffiyn" (imehadithiwa na Al-Bukhaariy 9/417-418)

 

[2] Imehadithiwa na Al-Bukhaariy (2/129 na 9/418), At-Tirmidhiy (3/314) ambaye amekiri ni Swahiyh, Al-Mukhlis katika 'Al-Mukhlisiyaat' (1/66) na Ibn Sa'ad (1/366)

 

Share