Lu-ulu-un-Manthuwrun - لُؤْلُؤ مَّنثُور

 

 

 

 

 

Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake

 

Imekusanywa Na Kuandaliwa Na: Ummu Iyyaad

 

Imepitiwa Na 'Abdullaah Mu'aawiyah (Abu Baasim)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

 

Share

000-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Utangulizi

 

 

 

 

Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake

 

 

 

 

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمنِ الرَّحِيم

 

 

Utangulizi:

 

 

Himdi Anastahiki Allaah (سبحانه وتعالى) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimfikie Nabiy Muhammad (صلى الله عليه  وآله وسلم ) na jamaa zake, na Swahaba zake (رضي الله عنهم)  na wote waliotangulia kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Imekuwa ni waajib wa kila Muislamu kufikisha ujumbe kwa kuamrishana mema na kukatazana maovu kama Anavyoamrisha Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَلْتَكُن مِّنكُمْ أُمَّةٌ يَدْعُونَ إِلَى الْخَيْرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ ۚ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفلِحُونَ ﴿١٠٤﴾

Na watokeze kutoka kwenu umati wa watu unaolingania kheri na unaoamrisha mema na unaokataza munkari. Na hao ndio waliofaulu. [Aal-‘Imraan: 104]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ ۗ

Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu; mnaamrisha mema na mnakataza munkari na mnamwamini Allaah [Aal-‘Imraan 110]

 

 

Waajib huo wa kuamrishana mema na kukatazana maovu umetiliwa nguvu mno na jambo hili kuwa adhimu hadi kwamba baadhi ya 'Ulamaa wameona waongezee katika nguzo za kiislamu [Wujuwb Al-Amr Bil Ma’ruwf  Wan-Nahy ‘Anil-Munkari - Shaykh Swaalih Al-Fawzaan].  Wengineo wakanukuu dalili kadhaa, miongoni mwazo ni kauli za Allaah (سبحانه وتعالى) zilotangulia za Suwratul-‘Imraan.

 

Makemeo makali yametolewa na Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kutokukatazana maovu kama vile  Allaah (سبحانه وتعالى) Alivyowalaani waliopewa vitabu nyuma yetu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ ﴿٧٨﴾

Wamelaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israaiyl kwa lisani  ya Daawuwd na ‘Iysaa mwana wa Maryam. Hivyo ni kwa sababu ya kuasi kwao na walikuwa wakitaadi.

 

كَانُوا لَا يَتَنَاهَوْنَ عَن مُّنكَرٍ فَعَلُوهُ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ﴿٧٩﴾

Walikuwa hawakatazani munkari waliyofanya. Uovu ulioje waliyokuwa wakiyafanya. [Al-Maaidah: 78-79]

 

 

Bali kuna onyo kali la kuteremshiwa adhabu kwa kutokutekeleza amri hii na juu ya hivyo, ni sababu mojawapo ya kutokutakabaliwa du’aa zetu kama ilivyothibiti katika usimulizi ufuatao:

 

عن حُذيفةَ بنِ اليَمانِ عن النَّبيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلِيهِ وسَلَّم قال: ((والَّذي نَفْسي بيدهِ لتأمرُنَّ بالمعروفِ ولتَنهوُنَّ عن المنكرِ وليوشِكَنَّ اللهُ أنْ يبعثَ عليكُمْ عقاباً منهُ فتدعونَهُ فلا يَستجيبُ لكُمْ)) الترمذي وصححه الألباني

Imepokelewa toka kwa Hudhayfah bin al-Yamaani  (رضي الله عنه) kutoka kwa Nabiy kwamba amesema: ((Naapa kwa Yule nafsi yangu ipo mikononi mwake, mtaamrishana ma’ruwf [mema] na kukatazana munkari [maovu] ama Atawaunganishia kwa kuwapa mfano wake Allaah na kuwateremshia nyinyi adhabu itokayo Kwake, kisha mumuombe Yeye na Asiwajibu du’aa zenu)) [At-Tirmidhiy na akaisahihisha Al-Albaaniy]

 

 

Zimethibiti pia Hadiyth nyinginezo za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) zinazotoa maonyo zaidi ya hayo na zinazobashiria fadhila tukufu za kuamrishana mema na kukatazana maovu. Na hii ilikuwa ndio kazi ya Rusuli wote kuwalingania watu wao waachane na maovu na washikamane na yanayomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى). Na kutokana na umuhimu wake, Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ametuamrisha tufikishe ujumbe japo kwa Aayah moja kama alivyosema:

 

((بَلِّغُوا عَنِّي وَلَوْ آيَةً))

((Fikisheni kutoka kwangu [ujumbe] japo Aayah moja)) [Al-Bukhaariy]

 

 

Kitabu hiki kwa tawfiyq ya Allaah (سبحانه وتعالى), kitamsaidia yeyote anayetaka kufuata amri ya Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه  وآله وسلم ), kwani Hadiyth moja itamtosheleza kabisa mtu kulingania kutokana na maamrisho na makatazo yake.

 

 

Hadiyth zote (isipokuwa ya Hitimisho) nimezitoa katika kitabu cha Riyaadhus-Swaalihiyn kwa kuingia katika Milango yake na kutoa Hadiyth moja au zaidi yake ambazo nimehisi kuwa zina mafunzo muhimu kwa Muislamu na jamii kwa ujumla.

 

 

Nimejaribu kutoa ‘Mafunzo Na Mwongozo’ katika kila Hadiyth kwa kuweka nukta za maelezo mafupi.  Pia nimetaja Aayah za Qur-aan zinazohusiana na baadhi ya nukta nilizozitaja kwa kuona kuwa zitamsaidia mtu kuisherehi zaidi Hadiyth moja ikawa ni darsa kamili la kumtosheleza na kuwatosheleza anaowalingania. Kitabu hiki kinaweza pia kuwa ni mazoezi kwa mtu ikawa ni chanzo cha kutoa darsa kwa wenziwe.

 

Tanbihi: Baadhi ya nukta nimenukuu  kutoka :Nuzhatul-Muttaqiyn

 

 

Namshukuru Allaah (سبحانه وتعالى) Kuniwezesha kuandika Kitabu hiki cha Lu-ulu-um-Manthuwrun (Lulu Zilizotawanywa) kwani hakuna Awezeshaye ila Yeye tu:

 

 

وَمَا تَوْفِيقِي إِلَّا بِاللَّـهِ ۚ عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ وَإِلَيْهِ أُنِيبُ ﴿٨٨﴾

Na sipati tawfiyq (ya kuyawezesha haya) ila kwa Allaah. Kwake natawakali na Kwake narejea

 

 

Shukurani zangu za dhati kwa al-Akh Abu ‘Abdillaah Muhammad Baawaziyr, al-Akh Sa’iyd Baawaziyr, al-Akh Muhammad ‘Abdallah Al-Ma’awiy na al-Akh ‘Abdallah Mu’aawiyah kwa juhudi zao za kukipitia kitabu hiki, namuomba Allaah (سبحانه وتعالى) Awalipe malipo mema yawe mazito katika mizani zao za mambo mema Siku ya Qiyaamah. Aaamiyn.

 

 

Na namuomba Allaah (سبحانه وتعالى) Ajaalie kazi hii iwe kwa ajili ya kupata Radhi Zake Pekee na Ajaalie iwe yenye manufaa kwa ndugu zetu wa Kiislamu na namuomba Atughufurie na Atusamehe kwa makosa yoyote yatakayokuwemo. 

 

 

Wa-Swalla-Allaahu ‘alaa Muhammadin wa ‘alaa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

 

Ummu Iyyaad

14 Dhul-Qa’dah, 1432– 12 Oktoba 2011M

Kimehaririwa  Swafar 1439 H

 

 

 

 

Share

001-Lu-ulu-un-Manthuwrun :Allaah Hatazami Miili Wala Sura, Bali Anatazama Nyoyoni

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 1

Allaah Hatazami Miili Wala Sura, Bali Anatazama Nyoyoni

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ  (صلى الله عليه و آله وسلم): ((إِنَّ اللَّهَ لاَ يَنْظُرُ إِلى أجْسَامِكُمْ  وَلاَ إِلَى صُوَرِكُمْ وَلَكِنْ يَنْظُرُ إِلَى قُلُوبِكُمْ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika Allaah Hatazami viwiliwili vyenu wala sura zenu, lakini Anatazama nyoyo zenu)) [Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Umuhimu wa kuwa na niyyah safi na ikhlaasw katika kumuabudu Allaah (سبحانه وتعالى) kwani hivyo ndivyo tulivyoamrishwa:

 

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ

Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah wenye kumtakasia Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki na wasimamishe Swalaah na watoe Zakaah; na hiyo ndiyo Dini iliyosimama imara. [Al-Bayinah 98:5

 

 

2. Hima ya kutenda ‘amali njema baada ya kuwa na  niyyah safi.  

 

 

3. ‘Amali na ‘Ibaadah hazipokelewi isipokuwa niyyah ikiwa ni safi kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى). Kwa hiyo ‘amali zinazomshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) haizipokelewi. Aliwatahadharisha Rusuli na Manabii Wake Aliposema:

 

وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ ﴿٦٥﴾

  Kwa yakini umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako (kwamba): “Ukifanya shirki bila shaka zitabatilika ‘amali zako na bila shaka utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.” [Az-Zumar: 65]

 

 

Na pia:

وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٨٨﴾

Na kama wangemshirikisha bila shaka yangebatilika yale waliyokuwa wakitenda. [Al-An’aam: 88]

 

Na ‘amali zenye kumshirikisha hazina thamani yoyote mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zinazotawanyika. [Al-Furqaan: 23]

 

Pia rejea: Al-Kahf (18: 103-104, 110).    

 

 

 

4. Bin Aadam hawezi kuficha kitu kwa Allaah, Anatambua yaliyomo nyoyoni mwa waja Wake hataka kama ni khiyaana ndogo vipi basi Yeye Anaitambua. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

يَعْلَمُ خَائِنَةَ الْأَعْيُنِ وَمَا تُخْفِي الصُّدُورُ

(Allaah) Anajua khiyana za macho na yale yanayoficha vifua [Ghaafir : 19)

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ إِن تُخْفُوا مَا فِي صُدُورِكُمْ أَوْ تُبْدُوهُ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ  

Sema: “Mkificha yale yaliyomo katika vifua vyenu au mkiyafichua, Allaah Anayajua.  [Aal-‘Imraan (3:29)]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan  (3: 119, 154), Al-Mulk (67: 13), At-Taghaabun (64: 4), Huwd (11: 5),

 

Na na siri zote zitadhihirika Siku ya Qiyaamah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

يَوْمَ تُبْلَى السَّرَائِرُ ﴿٩﴾

Siku siri zitakapopekuliwa. [Atw-Twaariq (86: 9)]

 

 

Na Anasema pia:

وَحُصِّلَ مَا فِي الصُّدُورِ ﴿١٠﴾

Na yatapodhihirishwa yale yaliyomo vifuani? [Al-‘Aadiyaat (100: 10)]

 

 

Rejea pia: Al-An’aam (6: 60), Al-Jumu’ah (62: 8), Az-Zumar (39: 7), Luqmaan (31: 23).  

 

 

 

5. Siku ya Qiyaamah mali wala watoto hayatamfaa mtu isipokuwa atakayefika akiwa na moyo msafi uliosalimika na maovu kadhaa yakiwemo riyaa (kujionyesha). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

 “Siku hayatofaa mali wa watoto.

 

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

“Isipokuwa yule atakayemfikia Allaah na moyo uliosalimika. [Ash-Shu’araa (26: 88-89)]

 

 

 

6. Ni muhimu kwa Muislamu kuzitekeleza amri za Dini yake na si kwa mandhari pekee. Na mara nyingi watu huwa ni wenye kusema pindi anapotenda jambo ovu kuwa: “Lakini niyyah yangu ni nzuri”. Hapa Muislamu anatakiwa aizingatie Hadiyth nyengine inayosema: ((Hakika Allaah Hatazami viwiliwili vyenu wala sura zenu, lakini Anatazama nyoyo na ‘amali zenu)) [Muslim]

 

Hivyo,‘amali zinafaa ziende sambamba na Aliyoyateremsha Allaah na kuja nayo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

 

7. Usimhukumu mtu kwa mandhari yake, pindi ukimuona mtu shakili yake na hakuvaa mavazi ya Muumin ukadhania ni mtu muovu, huenda akawa ni mwema. Hali kadhalika, pindi ukimuona mtu shakili yake na mavazi yake ni ya ki-Muumin ukadhani kuwa ni mtu mwema kabisa, lakini huenda akawa ni mtu muovu. Wala usimdharau au kumkejeli mtu kwa mandhari yake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ  

Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao. [Al-Hujuraat (49: 11)]

 

 

8. Kuzingatia yanayomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى) daima.

 

 

9-Kukhofia riyaa kwani ni hatari mno huporomosha ‘amali zote: Hadiyth:

 

عنْ ابي هريرة رضي الله عنه أنَّه صلَّى الله عليه وسلَّم قال: ((قال الله تعالى: أنا أغْنى الشُّركاء عن الشِّرْك، فمَن عمل عملاً أشْرَك فيه معي غيري تركتُه وشِرْكه))    

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: "Mimi Ni Mwenye kujitosheleza kabisa, Sihitaji msaada wala mshirika. Kwa hiyo, yule afanyaye amali kwa kunishirikisha na mtu, Nitaikanusha pamoja na mshirika wake.”))  Yaani: hatopata ujira wowote kwa amali hiyo. [Muslim (2985), Ibn Maajah (4202)]

 

 

Pia:

 

 عَنْ أَبِي سَعِيدٍ مَرْفُوعًا: ((أَلا أُخْبِرُكُمْ مَا هُوَ أَخْوَفُ عَلَيْكُمْ عِنْدِي مِنَ الْمَسِيحِ الدَّجَّالِ؟)) قَالُوا بَلَى: قَالَ: ((الشِّرْكُ الْخَفِيُّ، يَقُومُ الرَّجُلُ فَيُصَلِّي فَيُزَيِّنُ صَلاتَهَ، لِمَا يَرَى مِنْ نَظَرِ رَجُلٍ إِلَيْه)) رَوَاهُ أَحْمَدُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd, Hadiyth Marfuw’: ((Je, niwajulisheni nikikhofiacho zaidi juu yenu kuliko hata Masiyh Ad-Dajjaal?)) Wakasema: Ndio. Akasema: ((Ni shirki iliyojfichikana kama vile mtu kuipamba Swalaah yake kwa kuwa anaangaliwa)) [Ahmad, Ibn Maajah]

 

 

Share

002-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Hupokea Tawbah Za Waja Usiku Na Mchana

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Alhidaaya.com 

 

Hadiyth Ya 2

Allaah Hupokea Tawbah Za Waja Usiku Na Mchana

 

 

عَنْ أَبِي مُوسَى عَبْدِ الله بنِ قَبَسٍ الأَشْعَرِيِّ  (رضي الله عنه) عن النَّبيّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قال: ((إِنَّ اللَّهَ تَعَالَى يَبْسُطُ يَدَهُ بِاللَّيْلِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ النَّهَارِ وَيَبْسُطُ يَدَهُ بِالنَّهَارِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ اللَّيْلِ حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ مِنْ مَغْرِبِهَا)) رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Muwsaa ‘Abdillaah bin Qays Al-Ash‘ariyy (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika Allaah Anakunjua Mkono Wake usiku ili Apokee tawbah ya mkoseaji mchana. Na Anakunjua Mkono Wake mchana ili Apokee tawbah ya mkoseaji usiku mpaka jua lichomoze Magharibi [mahali linapokuchwa])) [Muslim]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Umuhimu wa mja kukimbilia kutubu anapofanya maasi mchana au usiku. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَسَارِعُوا إِلَىٰ مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ

Na kimbilieni maghfirah kutoka kwa Rabb wenu na Jannah upana wake ni wa mbingu na ardhi imeandaliwa kwa wenye taqwa. [Aal-‘Imraan 3: 133]

 

Na pia rejea: At-Tahriym (66: 8), An-Nuwr (24: 31).

 

 

2. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa waja Wake kuwapa muda wa kutubia maasi, lau sivyo Angeliwaadhibu na kuwaangamiza hapo hapo wanapotenda maasi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَوْ يُؤَاخِذُ اللَّـهُ النَّاسَ بِمَا كَسَبُوا مَا تَرَكَ عَلَىٰ ظَهْرِهَا مِن دَابَّةٍ وَلَـٰكِن يُؤَخِّرُهُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ۖ فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِعِبَادِهِ بَصِيرًا ﴿٤٥﴾

Na lau Allaah Angeliwaadhibu watu kwa sababu ya waliyoyachuma, Asingeliacha juu ya ardhi kiumbe chochote kitembeacho, lakini Anawaakhirisha mpaka muda maalumu uliokadiriwa; utakapofika muda wao, basi hakika Allaah daima ni Mwenye kuona waja Wake. [Faatwir (35: 45)]

 

Rejeja pia:  An-Nahl (16: 61).

 

 

3. Rahma ya Allaah kwa waja Wake kutokutofautisha wakati wa tawbah japokuwa maasi mengine yanazidi mengineyo.

 

 

4. Tawbah inaendelea kupokelewa hadi milango ifungwe: Hadiyth: 

 

وعن أبي عبد الرحمن عبد الله بنِ عمَرَ بنِ الخطابِ رضيَ اللهُ عنهما عن النَّبي صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((إِنَّ الله عز وجل يَقْبَلُ تَوبَةَ العَبْدِ مَا لَمْ يُغَرْغِرْ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن)) 

Abuu ‘Abdir-Rahmaan, ‘Abdullaah bin ‘Umar bin Al-Khattwaab  (رضي الله عنهما)    amehadithia kwamba:  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)    amesema:  “Hakika Allaah  ‘Azza wa Jallaa Huikubali tawbah ya mja madamu roho yake haijafika kooni.” [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth hii ni Hasan, Ibn Maajah, Ahmad, na imepewa daraja ya Swahiyh na Al-Albaaniy]

 

Na pia:

 

عن أبي هُريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ تَابَ قَبْلَ أنْ تَطْلُعَ الشَّمْسُ مِنْ مَغْرِبِها تَابَ اللهُ عَلَيهِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mwenye kutubia kabla ya jua kuchomoza upande wa Magharibi, Allaah Atamkubalia tawbah yake.” [Muslim]

 

 

5. Hii inaonyesha mapenzi makubwa ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kuwapatia waja Wake fursa hii ya dhahabu ambayo haifai kupotezwa na waja wenyewe.

 

 

6. Hadiyth inatoa mafunzo kwa Muislamu kutokumhukumu mwenziwe kuwa hatoghufuriwa madhambi yake. Rejea Hadiyth namba (99).

 

 

7. Mja hata afanye madhambi makubwa vipi, asikate tamaa na Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى), kwani Yeye Hughufuria madhambi yote. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا ۚ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٥٣﴾

Sema: Enyi waja Wangu ambao wamepindukia mipaka juu ya nafsi zao: “Msikate tamaa na rahmah ya Allaah; hakika Allaah Anaghufuria dhambi zote; hakika Yeye Ndiye Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.” [Az-Zumar 39: 53]

 

 

8. Fadhila tele za tawbah zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah, miongoni mwazo ni.

 

Kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَتُوبُوا إِلَى اللَّـهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ

Na tubuni kwa Allaah nyote, enyi Waumini mpate kufaulu. [An-Nuwr: 31]

 

Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) aliamrishwa awaambie watu wake:

 

وَأَنِ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ يُمَتِّعْكُم مَّتَاعًا حَسَنًا إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى وَيُؤْتِ كُلَّ ذِي فَضْلٍ فَضْلَهُ ۖ وَإِن تَوَلَّوْا فَإِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ كَبِيرٍ﴿٣﴾

Na kwamba: “Mwombeni Rabb wenu maghfirah kisha tubuni Kwake, Atakustarehesheni starehe nzuri mpaka muda maalumu uliokadiriwa; na Atampa kila mwenye fadhila, fadhila Zake. Na mkikengeuka, basi hakika mimi nakukhofieni adhabu ya Siku kubwa.” [Huwd: 3]

 

Nabiy Nuwh  (عليه السلام) alipowalingania watu wake aliwaambia watubie kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na akawatajia fadhila tele:

 

فَقُلْتُ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا﴿١٠﴾

Nikasema: “Ombeni maghfirah kwa Rabb wenu; hakika Yeye ni Mwingi mno wa kughufuria.

 

يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا﴿١١﴾

“Atakutumieni mvua tele ya kuendelea.”

 

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا﴿١٢﴾

“Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakupeni mito.” [Nuwh: 10-12]

 

 

Na Nabiy Huwd (عليه السلام) aliwaambia watu wake:

 

وَيَا قَوْمِ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا وَيَزِدْكُمْ قُوَّةً إِلَىٰ قُوَّتِكُمْ وَلَا تَتَوَلَّوْامُجْرِمِينَ﴿٥٢﴾

“Na enyi kaumu yangu!  Mwombeni maghfirah Rabb wenu, kisha tubieni Kwake, Atakuleteeni mbingu zenye kunyesha mvua tele ya kumiminika na Atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu, na wala msikengeuke mkawa wahalifu.” [Huwd: 52]

 

وَأَنِ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ يُمَتِّعْكُم مَّتَاعًا حَسَنًا إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى وَيُؤْتِ كُلَّ ذِي فَضْلٍ فَضْلَهُ ۖ وَإِن تَوَلَّوْا فَإِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ كَبِيرٍ﴿٣﴾

Na kwamba: “Mwombeni Rabb wenu maghfirah kisha tubuni Kwake, Atakustarehesheni starehe nzuri mpaka muda maalumu uliokadiriwa; na Atampa kila mwenye fadhila, fadhila Zake. Na mkikengeuka, basi hakika mimi nakukhofieni adhabu ya Siku kubwa.” [Huwd: 3]

 

Na Hadiyth za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

 عن ابنِ عباسٍ رضي الله عنهما أنَّ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((لَوْ أنَّ لابنِ آدَمَ وَادِيًا مِنْ ذَهَبٍ أحَبَّ أنْ يكُونَ لَهُ وَادِيانِ، وَلَنْ يَمْلأَ فَاهُ إلا التُّرَابُ، وَيَتْوبُ اللهُ عَلَى مَنْ تَابَ)). مُتَّفَقٌ عليه

'Abdullaah bin ‘Abbaas na Anas bin Maalik (رضي الله عنهما) wamehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Lau mwana Aadam angalikuwa na bonde la dhahabu, angalipendelea awe na mabonde mawili, wala hakuna kitakachoweza kumtosheleza mdomo wake isipokuwa ni mchanga. Na Allaah Humkubalia tawbah ya yule mwenye kutubia.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na pia:

 

عن أَنَسُ بْنُ مَالِكٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((الَلَّهُ أَشَدُّ فَرَحًا بِتَوْبَةِ عَبْدِهِ حِينَ يَتُوبُ إِلَيْهِ مِنْ أَحَدِكُمْ كَانَ عَلَى رَاحِلَتِهِ بِأَرْضِ فَلاَةٍ فَانْفَلَتَتْ مِنْهُ وَعَلَيْهَا طَعَامُهُ وَشَرَابُهُ فَأَيِسَ مِنْهَا فَأَتَى شَجَرَةً فَاضْطَجَعَ فِي ظِلِّهَا قَدْ أَيِسَ مِنْ رَاحِلَتِهِ فَبَيْنَا هُوَ كَذَلِكَ إِذَا هُوَ بِهَا قَائِمَةً عِنْدَهُ فَأَخَذَ بِخِطَامِهَا ثُمَّ قَالَ مِنْ شِدَّةِ الْفَرَحِ: "اللَّهُمَّ أَنْتَ عَبْدِي وَأَنَا رَبُّكَ" ‏ أَخْطَأَ مِنْ شِدَّةِ الْفَرَحِ)) مسلم

 

Amesimulia Anas (رضي الله عنه): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: Allaah Hufurahikiwa mno na tawbah ya mja Wake wakati anapotubia Kwake kuliko furaha ya mmoja wenu aliyekuwa amempanda mnyama wake kwenye jangwa (la joto kali hakuna mtu), kisha mnyama huyo aliyebeba chakula chake na maji yake akampotea, na akakata tamaa kabisa ya kumpata tena. Akaenda kwenye mti, akalala chali ya kivuli chake huku akiwa amekata tamaa kabisa ya kumpata tena mnyama wake. Akiwa katika hali hiyo (ya kutojua nini la kufanya), mara anashtuka kumwona huyo amesimama mbele yake, akaikamata hatamu yake, na kwa ile furaha akasema:  "Ee Allaah, Wewe ni mja wangu na mimi ni Rabb wako.” Alikosea (kumshukuru Rabb wake) kwa wingi wa furaha aliyokuwa nayo.” [Muslim]

 

Na pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِيمَا يَحْكِي عَنْ رَبِّهِ عَزَّ وَجَلَّ قَالَ: ((أَذْنَبَ عَبْدٌ ذَنْبًا فَقَالَ: اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي ذَنْبِي،  فَقَالَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى:  أَذْنَبَ عَبْدِي ذَنْبًا فَعَلِمَ أَنَّ لَهُ رَبًّا يَغْفِرُ الذَّنْبَ وَيَأْخُذُ بِالذَّنْبِ ثُمَّ عَادَ فَأَذْنَبَ فَقَالَ:  أَيْ رَبِّ اغْفِرْ لِي ذَنْبِي،  فَقَالَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى: عَبْدِي أَذْنَبَ ذَنْبًا فَعَلِمَ أَنَّ لَهُ رَبًّا يَغْفِرُ الذَّنْبَ وَيَأْخُذُ بِالذَّنْبِ ثُمَّ عَادَ فَأَذْنَبَ فَقَالَ: أَيْ رَبِّ اغْفِرْ لِي ذَنْبِي،  فَقَالَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى: أَذْنَبَ عَبْدِي ذَنْبًا فَعَلِمَ أَنَّ لَهُ رَبًّا يَغْفِرُ الذَّنْبَ وَيَأْخُذُ بِالذَّنْبِ. اعْمَلْ مَا شِئْتَ فَقَدْ غَفَرْتُ لَكَ)) البخاري و مسلم

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kuhusu mambo aliyohadithia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  kutoka kwa Rabb Wake (‘Azza wa Jalla) kwamba ((Mja wa Allaah alifanya dhambi na akasema: Ee Rabb nighufurie dhambi zangu. Na yeye Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Akasema: Mja wangu kafanya dhambi kisha kajua kwamba anaye Rabb Ambaye Anaghufuria dhambi na Anayeadhibu kwa kufanya dhambi. Kisha akarudi tena kufanya dhambi akasema: Ee Rabb nighufurie dhambi zangu. Na yeye Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Akasema: Mja wangu kafanya dhambi kisha kajua kwamba anaye Rabb Ambaye Anaghufuria dhambi na Anayeadhibu kwa kufanya dhambi. Kisha akarudia tena dhambi na akasema: Ee Rabb nighufurie dhambi zangu. Na yeye Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Akasema: Mja wangu kafanya dhambi kisha kajua kwamba anaye Rabb Ambaye Anaghufuria dhambi na Anayeadhibu kwa kufanya dhambi. (Allaah Akasema): Fanya utakavyo, kwani Nimekughufuria)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

9. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akitubia mara 70 au mara 100 kwa siku, hivyo basi sisi tunapaswa kutubia zaidi ya hivyo:

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: سمعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((واللهِ إنِّي لأَسْتَغْفِرُ الله وأَتُوبُ إِلَيْه في اليَوْمِ أَكْثَرَ مِنْ سَبْعِينَ مَرَّةً)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)   akisema: “Wa-Allaahi mimi namuomba Allaah maghfirah na natubia Kwake zaidi ya mara sabini kwa siku.” [Al-Bukhaariy]

 

Na pia:

 

وعن الأَغَرِّ بنِ يسار المزنِيِّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا أَيُّهَا النَّاسُ، تُوبُوا إِلى اللهِ واسْتَغْفِرُوهُ، فإنِّي أتُوبُ في اليَومِ مائةَ مَرَّةٍ)). رواه مسلم.

Al-Agharri bin Yasaar Al-Muzaniyy (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)    amesema: “Enyi watu, tubieni kwa Allaah na mumuombe maghfirah. Hakika mimi natubia Kwake mara mia kwa siku.” [Muslim]

 

 

Share

003-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Akimtakia Khayr Mja Humpa Mtihani Duniani

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 3

Allaah Akimtakia Khayr Mja Humpa Mtihani Duniani

 

عَنْ أَنَسٍ (رضي الله عنه) قَال: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((إِذَا أَرَادَ اللَّهُ بِعَبْدِهِ الْخَيْرَا عَجَّلَ لَهُ الْعُقُوبَةَ فِي الدُّنْيَا وَإِذَا أَرَادَ اللَّهُ بِعَبْدِهِ الشَّرَّ أَمْسَكَ عَنْهُ بِذَنْبِهِ حَتَّى يُوَافِيَ بِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ)) وَ قال النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((إِنَّ عِظَمَ الْجَزَاءِ مَعَ عِظَمِ الْبلآءِ وَإِنَّ اللَّهَ إِذَا أَحَبَّ قَوْمًا ابْتَلاَهُمْ فَمَنْ رَضِيَ فَلَهُ الرِّضَا وَمَنْ سَخِطَ فَلَهُ السَّخَطُ)) رواه الترمذي وقال حديث حسن

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Anapompendelea mja Wake khayr, Humharakishia adhabu duniani. Na Allaah Anapomtakia mja Wake shari, Humzuilia dhambi zake mpaka Amlipe Siku ya Qiyaamah)). Na amesema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Hakika malipo makubwa kabisa yapo pamoja na mtihani mkubwa, na hakika Allaah Anapowapenda watu Huwapa mtihani. Basi atakayeridhika, atapata Radhi [za Allaah] na atakayechukia, atapata hasira. [za Allaah])) [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Allaah (سبحانه وتعالى) Huwa pamoja na anayesibiwa na mitihani akasubiri, na juu ya hivyo, ni alama ya mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

وَكَأَيِّن مِّن نَّبِيٍّ قَاتَلَ مَعَهُ رِبِّيُّونَ كَثِيرٌ فَمَا وَهَنُوا لِمَا أَصَابَهُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَمَا ضَعُفُوا وَمَا اسْتَكَانُوا ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الصَّابِرِينَ ﴿١٤٦﴾

Na wangapi katika Nabiy alipigana vita, na pamoja naye (walipigana) Wanachuoni waswalihina, basi hawakulegea kwa yaliyowasibu katika njia ya Allaah, wala hawakudhoofika na wala hawakunyong’onyea. Na Allaah Anapenda wanaosubiri.  [Aal-‘Imraan 3: 146]

 

Rejea: Al-Baqarah (2: 153), Al-Anfaal (8: 46).

 

 

2. Alama za kufutiwa dhambi Muislamu pindi anapokuwa na subra katika mitihani.

 

 

3. Watu hupewa mitihani kulingana na taqwa na Iymaan zao.

 

 

4. Mwenye kuwa na subra katika mitihani ndiye atakayepata khayr za Siku ya Qiyaamah na malipo mema kabisa, kinyume na atakayeshindwa kuwa na subra:  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا يُوَفَّى الصَّابِرُونَ أَجْرَهُم بِغَيْرِ حِسَابٍ

Hakika wanaosubiri watalipwa kikamilifu ujira wao bila ya hesabu. [Az-Zumar 39: 10]

 

 

5. Muumin inampasa awe radhi kwa mitihani inayomfikia wala asikate tamaa au kuchukia bali ashukuru, na hii ndio sifa mojawapo ya Muumini wa kweli kama ilivyotajwa katika Hadiyth:

 

عن أبي يحيى صهيب بن سنانٍ رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((عَجَبًا لأمْرِ المُؤمنِ إنَّ أمْرَهُ كُلَّهُ لَهُ خيرٌ ولَيسَ ذلِكَ لأَحَدٍ إلا للمُؤْمِن: إنْ أَصَابَتْهُ سَرَّاءُ شَكَرَ فَكانَ خَيرًا لَهُ، وإنْ أصَابَتْهُ ضرَاءُ صَبَرَ فَكانَ خَيْرًا لَهُ)). رواه مسلم

Kutoka kwa Abuu Yahyaa, Swuhayb bin Sinaan  (رضي الله عنه)    amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: “Ajabu kwa jambo la Muumin; hakika mambo yake ni khayr, wala hakuna anayepata hilo isipokuwa Muumin pekee; akipatwa na furaha hushukuru basi huwa ni khayr kwake, na akipatwa na madhara husubiri basi huwa khayr kwake.” [Muslim]

 

 

6. Jannah si wepesi kuipata ila baada ya kuwa na taqwa, kutenda ‘amali njema na kuwa na subira katika mitihani.

 

Rejea: Al-Baqarah (2: 214).

 

 

7. Kuipita mitihani ni thibitisho kuwa mtu huyo yuwapendwa na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

8. Fadhila tele za subira katika mitihani zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah, miongoni mwazo ni kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالصَّابِرِينَ فِي الْبَأْسَاءِ وَالضَّرَّاءِ وَحِينَ الْبَأْسِ ۗ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ صَدَقُوا ۖ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُتَّقُونَ ﴿١٧٧﴾  

na wanaosubiri katika dhiki za ufukara na maafa ya magonjwa na njaa na katika vita. Hao ndio waliosadikisha na hao ndio wenye taqwa. [Al-Baqarah: 177].

 

Na pia:

إِلَّا الَّذِينَ صَبَرُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ كَبِيرٌ﴿١١﴾

Isipokuwa wale waliosubiri na wakatenda mema hao watapata maghfirah na ujira mkubwa. [Huwd: 11]

 

Na pia:

 

جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا وَمَن صَلَحَ مِنْ آبَائِهِمْ وَأَزْوَاجِهِمْ وَذُرِّيَّاتِهِمْ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ يَدْخُلُونَ عَلَيْهِم مِّن كُلِّ بَابٍ﴿٢٣﴾

Jannaat za kudumu milele wataingia pamoja na waliotengenea miongoni mwa baba zao na wake zao na dhuria zao. Na Malaika wanawaingilia katika kila milango.

 

سَلَامٌ عَلَيْكُم بِمَا صَبَرْتُمْ ۚ فَنِعْمَ عُقْبَى الدَّارِ ﴿٢٤﴾

 “Salaamun ‘Alaykum! (Amani iwe juu yenu) kwa yale mliyosubiri.” Basi uzuri ulioje hatima njema ya makazi ya Aakhirah. [Ar-Ra’d: 23-24]

 

Na Hadiyth za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: (( مَا يَزَالُ الْبَلاَءُ بِالْمُؤْمِنِ وَالْمُؤْمِنَةِ فِي نَفْسِهِ وَوَلَدِهِ وَمَالِهِ حَتَّى يَلْقَى اللَّهَ وَمَا عَلَيْهِ خَطِيئَةٌ)) الترمذي وقال حديث حسن صحيح

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah  (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Mtihani utaendelea kumpata Muumini mwanamume na Muumini mwanamke katika nafsi yake na watoto wake, na mali yake mpaka akutane na Allaah akiwa hana dhambi)) [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

Na pia:

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنهما)  عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((مَا يُصِيبُ الْمُسْلِمَ مِنْ نَصَبٍ وَلاَ وَصَبٍ وَلاَ هَمٍّ وَلاَ حُزْنٍ وَلاَ أَذًى وىَ غَمٍّ حَتَّى الشَّوْكَةِ يُشَاكُهَا إِلاَّ كَفَّرَ اللَّهُ بِهَا مِنْ خَطَايَاهُ))

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy na Abuu Hurayrah  (رضي الله عنهما)    kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Muislamu hatopatwa na tabu, wala maradhi, wala hamu wala huzuni wala udhia wala ghamu [sononeko] hata mwiba unaodunga isipokuwa Allaah Humfutia madhambi yake kwa sababu ya hayo)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((مَثَلُ الْمُؤْمِنِ كَمَثَلِ الزَّرْعِ لاَ تَزَالُ الرِّيحُ تُمِيلُهُ وَلاَ يَزَالُ الْمُؤْمِنُ يُصِيبُهُ الْبَلاَءُ. وَمَثَلُ الْمُنَافِقِ كَمَثَلِ شَجَرَةِ االأرْزِ لاَ تَهْتَزُّ حَتَّى تَسْتَحْصِدَ)) متفق عليه

Kutoka kwa Abuu Hurayrah  (رضي الله عنه)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)    amesema: ((Mfano wa Muumini ni kama mti ulio na rutuba, upepo unaupiga huku na kule, na ataendelea Muumini kufikwa na mitihani. Na mfano wa mnafiki ni kama mti wa seda [aina ya mti wa mbao ya mkangazi], hautikisiki hadi ung’olewe wote mara moja)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Share

004-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Ukweli Unapelekea Jannah, Uongo Unapelekea Motoni

 

 

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 4

 

Ukweli Unapelekea Jannah, Uongo Unapelekea Motoni

 

 www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عَبْدُ الله إبنِ مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم قَالَ: ((إِنَّ الصِّدْقَ يَهْدِي إِلَى الْبِرِّ وَإِنَّ الْبِرَّ يَهْدِي إِلَى الْجَنَّةِ ، وَإِنَّ الرَّجُلَ لَيَصْدُقُ حَتَّى يَكُونَ صِدِّيقًا ، وَإِنَّ الْكَذِبَ يَهْدِي إِلَى الْفُجُورِ وَإِنَّ الْفُجُورَ يَهْدِي إِلَى النَّارِ ، وَإِنَّ الرَّجُلَ لَيَكْذِبُ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللَّهِ كَذَّابًا)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika ukweli unaongoza katika wema, na hakika wema unaongoza katika Jannah, na mtu ataendelea kusema ukweli mpaka aandikiwe mbele ya Allaah kuwa ni Swiddiyqaa (mkweli wa dhati). Na hakika uongo unaongoza katika uovu, na hakika uovu unapeleka motoni, na mtu ataendelea kusema uongo mpaka aandikiwe mbele ya Allaah kuwa ni muongo)).[Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Muislamu atangamane na wakweli ili naye apate tabia ya ukweli, nayo ni amri ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَكُونُوا مَعَ الصَّادِقِينَ﴿١١٩﴾

Enyi walioamini! Mcheni Allaah na kuweni pamoja na wakweli. [At-Tawbah 9: 119].

 

 

2. Umuhimu wa kuwa na sifa ya ‘ukweli’ na iwe sifa kuu ya Muumin.

 

Rejea: Al-Hujuraat (49: 150).

 

 

3. Kuhimizwa na pendekezo katika kusema ukweli, kwani ni sababu ya kutenda mema. Na tahadharisho la uongo kwani ni sababu ya kutenda maovu.

 

 

4. Hatari ya kufuata nyayo za shaytwaan za kuanza kusema uongo hadi unampeleka mtu motoni.

 

 

5. Mkweli atajulikana kwa kupewa sifa ya ‘mkweli’, na muongo atajulikana kwa kupewa sifa ya ‘muongo’.

 

 

 

6. Ukweli utamfaa mtu mwenyewe Aakhirah na matokeo na thawabu zake   ni kupata Jannah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ اللَّـهُ هَـٰذَا يَوْمُ يَنفَعُ الصَّادِقِينَ صِدْقُهُمْ ۚ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۚ رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ﴿١١٩﴾

Allaah Atasema: “Hii ndiyo Siku itakayowafaa Asw-Swaadiqiyna ukweli wao; watapata Jannaat zipitazo chini yake mito; ni wenye kudumu humo abadi.  Allaah Ameridhika nao, nao wameridhika Naye. Huko ni kufuzu adhimu.”  [Al-Maaidah 5: 119]

 

 

na matokeo na malipo ya muongo ni adhabu kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى). Rejea: Al-Ahzaab (33: 24).

 

 

7. Ukweli uwe kwa niyyah, kauli na ‘amali njema ili alipwe mtu malipo mema.

 

 

 

8. Allaah (سبحانه وتعالى) Amewasifu wakweli na Atawapa malipo mema kabisa.

 

Rejea: Al-Ahzaab (33: 35), Al-Hadiyd (57: 18).

 

 

 

9. Kusema uongo ni katika maovu ya ulimi, na ulimi usipochungwa unamuangamiza mtu.  

 

Rejea Hadiyth namba (37), (86), (87), (93), (94), (126).

 

 

 

10. Ikiwa huna hakika na jambo fulani ni bora kujiepusha kulisema ili ubakie salama na kusema uongo kwani ukweli ni utulivu na uongo ni mashaka. Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):
 

عن أبي محمد الحسن بنِ عليِّ بن أبي طالب رضي الله عنهما قَالَ: حَفظْتُ مِنْ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((دَعْ مَا يَرِيبُكَ إِلَى مَا لا يَرِيبُكَ؛ فإنَّ الصِّدقَ طُمَأنِينَةٌ، وَالكَذِبَ رِيبَةٌ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث صحيح))

Abuu Muhammad, Al-Hasan bin ‘Alliy bin Abiy Twaalib  (رضي الله عنهما)    amesema: Nimehifadhi kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  maneno haya: “Acha linalokutia shaka ufuate lisilokutia shaka; hakika ukweli ni utulivu na uongo ni mashaka.” [At-Tirmidhiy, na amesema Hadiyth  hii ni Hasan]

 

Share

005-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuvunjia Kiapo Kitendo Kiovu Kwa Kilicho Chema

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 5

 

Kuvunjia Kiapo Kitendo Kiovu Kwa Kilicho Chema

 Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أبي طريفٍ عَدِيَّ بْنَ حَاتِمٍ  الطَّائي (رضي الله عنه) قال: سَمِعْتُ رسول اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم) يَقُولُ: ((مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ ثُمَّ رَأَى أَتْقَى لِلَّهِ مِنْهَا فَلْيَأْتِ التَّقْوَى))  رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Twariyf ‘Adiyy bin Haatim (رضي الله عنه) amesema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Atakayeapa yamini [kufanya jambo] kisha akaona linalomridhisha zaidi Allaah kuliko aliloliapia, basi amche Allaah kwa kufanya linalomridhisha Allaah)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Aayah na Hadiyth nyingi zimesisitiza kuwajibika kuwa na taqwa na faida zake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا ﴿٧٠﴾

  Enyi walioamini! Mcheni Allaah na semeni kauli nyofu ya haki.

 

 

يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا ﴿٧١﴾

  Atakutengenezeeni ‘amali zenu, na Atakughufurieni madhambi yenu; na anayemtii Allaah na Rasuli Wake, basi kwa yakini amefanikiwa mafaniko adhimu. [Al-Ahzaab (33: 70-71)]

 

 

Rejea pia: At-Tawbah (9: 119), Al-Maidah 95: 35).

 

 

2. Mwenye kuazimia kufanya maasi asiyatende japokuwa ameyaapia kutenda.

 

 

3. Kuruhusika kuvunja kiapo na kafara zake kama ilivyotajwa katika kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٨٩﴾

Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini yamini zenu. Hivyo ndivyo Allaah Anavokubainishieni Aayaat (na hukmu) Zake ili mpate kushukuru. [Al-Maaidah (5: 89)]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (92), (102), (125).

 

 

4. Kujizua kuapa katika maasi kama kuapa katika kumvutia mteja biashara au katika kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  يَقُولُ:  ((الْحَلِفُ مَنْفَقَةٌ لِلسِّلْعَةِ مَمْحَقَةٌ لِلْكَسْبِ)) أَخْرَجَاهُ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kwa kuapa, [muuzaji] huenda akamshawishi  mnunuaji kununua bidhaa, lakini kunafuta Baraka za Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

وَعَنْ سَلْمَانَ: أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((ثَلاثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمْ اَللَّهُ وَلاَ يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ: أُشَيمِطٌ زَانٍ وَعَائِلٌ مُسْتَكْبِرٌ وَرَجُلٌ جَعَلَ اَللَّهَ بِضَاعَتَهُ لاَ يَشْتَرِي إِلاَّ بِيَمِينِهِ وَلاَ يَبِيعُ إِلاَّ بِيَمِينِه)) رَوَاهُ اَلطَّبَرَانِيُّ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ

Na Imepokelewa kutoka kwa Salmaan kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watu watatu ambao Allaah Hatowasemesha, wala Hatowatakasa, na watapata adhabu kali: Mzinifu mzee, maskini anayetakabari, na mtu aliyejaaliwa na bidhaa, lakini hanunui ila kwa kuapa [wa-Allaahi] na hauzi ila kwa kuapa [wa-Allaahi)) [At-Twabaraaniy kwa isnaad Swahiyh]

 

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mwenye kuapa akasema katika kiapo chake: Naapa kwa Laata na ‘Uzzaa (majina ya waabudiwa wa uongo) aseme: Laa ilaaha illa Allaah. Na atakayemwambia mwenzake: Njoo tuchezeshe kamari, basi atoe swadaqah.” [Al-Bukhaariy]

 

5. Umuhimu wa kupata radhi za Allaah (سبحانه وتعالى) kuliko jambo jengine lolote lile.

 

Share

006-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutawakali Kwa Allaah Na Kuwa Na Moyo Laini

 

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 6

Kutawakali Kwa Allah Na Kuwa Na Moyo Laini

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ: ((يَدْخُلُ الْجَنَّةَ أَقْوَامٌ أَفْئِدَتُهُمْ مِثْلُ أَفْئِدَةِ الطَّيْرِ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Wataingia Jannah watu ambao nyoyo zao ni mithali ya nyoyo za ndege)). [Muslim.] Kwa maana: Wenye kutawakali kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na nyoyo zao zikiwa laini.

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Waumini ni wenye nyoyo laini, kinyume na makafiri na wanafiki. Rejea: Al-Maaidah (5: 13).

 

 

2. Umuhimu wa kutawakali kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na kuwa na moyo mlaini (wenye yaqini), ni sababu ya kumuingiza Muislamu Jannah.

 

 

2. Muumin anapaswa asishughulishwe hadi kujiangamiza au kuingia katika chumo la haramu katika kutafuta maisha na rizki yake, kwani rizki inakutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى) Anayemruzuku ndege anayekutoka asubuhi bila ya kujua rizki yake, akarudi jioni akiwa amepata mahitajio yake.  

 

Rejea: Huwd (11: 6), Al-An’aam (6: 38).

 

Na kughushi ni miongoni mwa chumo la haramu. Rejea Hadiyth namba (101) kuhusu kughushi.

 

 

4. Kutawakali kwa Allaah (سبحانه وتعالى), kuwa na yakini na moyo laini ni miongoni mwa sifa kuu za Muumin. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٢﴾

Hakika Waumini ni wale ambao Anapotajwa Allaah, nyoyo zao zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali.

الَّذِينَ يُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ﴿٣﴾

Ambao wanasimamisha Swalaah na katika yale Tuliyowaruzuku hutoa.

 

أُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُؤْمِنُونَ حَقًّا ۚ لَّهُمْ دَرَجَاتٌ عِندَ رَبِّهِمْ وَمَغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ﴿٤﴾

Hao ndio Waumini wa kweli!  Wana daraja (za Jannah) kwa Rabb wao na maghfirah na riziki karimu.  [Al-Anfaal 8: 2-4]

 

Na Anasema pia Allaah (عزّ وجلّ):

 

فَمَا أُوتِيتُم مِّن شَيْءٍ فَمَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَمَا عِندَ اللَّـهِ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ لِلَّذِينَ آمَنُوا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٣٦﴾

Basi chochote mlichopewa katika kitu ni starehe ndogo za uhai wa dunia.  Na yale yaliyoko kwa Allaah ni bora zaidi na ni ya kudumu kwa wale walioamini na kwa Rabb wao wanatawakali.  [Ash-Shuwraa: 36]

 

Na rejea: Al-Ahzaab (33: 22), Aal-‘Imraan (3: 173-174).

 

5. Muumini anapaswa kutawakali kwa Allaah (سبحانه وتعالى) katika mambo yake yote kwani Allaah (سبحانه وتعالى) Anatosheleza kuwa mwenye kutegemewa kama Anavyosema:

 

وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ ۚ  

((Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza)) [Atw-Twalaaq (65: 3)]

 

6-Muumini anapofikwa na hali ya khofu au hatari, atawakali kwa Allaah (عزّ وجلّ) ili apate kulindwa na madhara na shari zote anazozikhofia. Hivi ndivyo kama alivyofanya Nabiy Ibraahiym (عليه السلام)  na Maswahaba  (رضي الله عنهم)  kama ilivyotajwa katika Hadiyth:

 

عن ابن عباس رضي الله عنهما أيضًا، قَالَ: حَسْبُنَا اللهُ وَنِعْمَ الوَكِيلُ، قَالَهَا إِبرَاهيمُ عليه السلام حِينَ أُلقِيَ في النَّارِ، وَقَالَها مُحَمَّدٌ صلى الله عليه وسلم حِينَ قَالُوا: إنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إيْمانًا وَقَالُوا: حَسْبُنَا الله ونعْمَ الوَكيلُ. رواه البخاري.

وفي رواية لَهُ عن ابن عَبَّاسٍ رضي الله عنهما، قَالَ: كَانَ آخر قَول إبْرَاهِيمَ صلى الله عليه وسلم حِينَ أُلْقِيَ في النَّارِ: حَسْبِي الله ونِعْمَ الوَكِيلُ

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنه)  amesema:

حَسْبُنَا اللهُ وَنِعْمَ الوَكِيلُ

“Allaah Anatutosheleza na Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.”

Amesema hivi Nabiy Ibraahiym (عليه السلام)    alipotumbukizwa motoni, na alisema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  pale watu (walipokodiwa na Maquraysh) walipowaambia (Waislaam): “Watu wamewakusanyikia, kwa hiyo waogopeni.” Lakini maneno hayo yaliwazidishia Iymaan (Waislamu) wakasema:

حَسْبُنَا اللهُ وَنِعْمَ الوَكِيلُ

“Allaah Anatutosheleza na Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.”  [Al-Bukhaariy]

Riwaayah nyingine; kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas  (رضي الله عنهما)  amesema: Kauli ya mwisho aliyotamka Nabiy Ibraahiym (عليه السلام)    wakati alipotumbukizwa kwenye moto ilikuwa ni kusema:

حَسْبِي الله ونِعْمَ الوَكِيلُ

“Allaah Ananitosheleza na Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.”

 

 

7. Kuomba du’aa ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu kutawakali:

 

عن ابن عباس رضي الله عنهما أيضًا: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يقول: ((اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمْتُ، وَبِكَ آمَنْتُ، وَعَليْك تَوَكَّلْتُ، وَإِلَيْكَ أنَبْتُ، وَبِكَ خَاصَمْتُ. اللَّهُمَّ إِنِّي أعُوذُ بعزَّتِكَ؛ لا إلهَ إلا أَنْتَ أنْ تُضلَّني، أَنْتَ الحَيُّ الَّذِي لا يَمُوتُ، وَالجِنُّ والإنْسُ يَمُوتُونَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ، وهذا لفظ مسلم واختصره البخاري

Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  amesimulia: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)   alikuwa akiomba: “Ee Allaah, kwa ajili Yako nimejisalimisha, Kwako tu nimeamini, na Kwako Pekee  natawakali, na Kwako tu nimerejea, kwa ajili Yako tu nakhasimiana. Ee Allaah, hakika mimi najilinda kwa utukufu Wako, hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Wewe, Usinipoteze. Wewe ni Hai Usiekufa, majini na wana-Aadam watakufa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 
 

Share

007-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kumwamini Allaah Na Kuwa Na Istiqaamah

 

 

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 7  

Kumwamini Allaah Na Kuwa Na Istiqaamah

 

www.alhidaaya.com

 

عَنْ أبي عَمْرَةَ سُفْيَانَ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ (رضي الله عنه)  قَالَ: قُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ قُلْ لِي فِي الإسْلاَمِ قَوْلاً لاَ أَسْأَلُ عَنْهُ أَحَدًا غَيْرَكَ)) قَالَ:  ((قُلْ آمَنْتُ بِاللَّهِ  ثُمَّ َاسْتَقِمْ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abu ‘Amrah Sufyaan bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه) amesema: Nilisema: “Ee Rasuli wa Allaah! Niambie neno katika Uislamu ambalo sitomuuliza yeyote badala yako”. Akasema: ((Sema: Nimemwamini Allaah kisha uwe na istiqaamah [msimamo])) [Muslim]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hadiyth hii ni miongoni mwa ‘Jawaami’ul-Kalim’ (Mjumuisho wa maana nyingi katika maneno machache) aliyopewa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم). Na thawabu za Istiqaamah (kuthibitika, msimamo katika Dini) zimetajwa katika kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ﴿٣٠﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara; Malaika huwateremkia: (kuwaambia): “Msikhofu, na wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo mlikuwa mkiahidiwa.”

 

نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَشْتَهِي أَنفُسُكُمْ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ﴿٣١﴾

 “Sisi ni rafiki zenu walinzi katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale mtakayoomba.

 

نُزُلًا مِّنْ غَفُورٍ رَّحِيمٍ﴿٣٢﴾

 “Ni mapokezi ya takrima kutoka kwa Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.”[Fusw-swilat 41: 30-32].

 

Na pia: 

 

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ﴿١٣﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara, basi hakutokuwa na khofu juu yao, na wala hawatohuzunika.

أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٤﴾

Hao ndio watu wa Jannah, ni wenye kudumu humo, jazaa kwa yale waliyokuwa wakitenda.  [Al-Ahqaaf 46: 13-14]

 

2. Umuhimu wa tawhiyd, kumpwekesha Allaah bila ya kumshirikisha.

 

Rejea: Al-An’aam (6: 102), Al-Baqarah (2: 163), Twaahaa (20: 14), Al-Qaswas (28: 88), Ghaafir (40: 65-66).

 

 

Na Hadiyth:

 

عَنْ عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: لَمَّا نَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُمْ بِظُلْمٍ، شَقَّ ذَلِكَ عَلَى النَّاس وَقَالُوا: أَيُّنَا لَمْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ؟! فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إنَّه لَيْسَ كَمَا تَعنُون! ألَمْ تَسْمَعوا ما قال الْعبْد الصَّالح؟  يَا بُنَيَّ لا تُشْرِكْ بِاللَّهِ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ - إنَّما هُو الشِّرْك))

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas‘uwd (رضي الله عنه)    ambaye amesema: Ilipoteremshwa Aayah hii: Wale walioamini na hawakuchanganya iymaan zao na dhulma [An-An’aam: 82] Iliwatatiza watu  wakasema: “Nani katika sisi hajadhulumu nafsi yake?” Akasema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ((Si kama vile mnavyomaanisha! Hamsikii pale mja mwema aliposema: “Ee mwanangu! Usimshirikishe Allaah, hakika shirki ni dhulma kuu!” [Luqmaan: 13] Hakika hiyo ni shirk.)) [Ahmad na riwaaya zinazofanana katika Al-Bukhaariy na wengineo]

 

Pia rejea Hadiyth namba (11), (12), (48), (125).

 

3. Kuwa na msimamo kunapeleka kufikia cheo cha juu na ukamilifu wa Iymaan.

 

Amesema ‘Umar bin al-Khattwaab (رضي الله عنه): “Istiqaamah ni kutekeleza amri na kuacha yaliyokatazwa, wala msimili na kugeuka geuka mgeuko wa fisi.”

 

 

4. Hii inaashiria kuwa Istiqaamah ina fadhila kubwa mpaka imekuja baada tu ya Iymaan. Na bila shaka Iymaan yenyewe haiwezi kusimama bila ya Istiqaamah.

 

Share

008-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kukimbilia Kutoa Swadaqah Kabla Ya Mauti

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 8  

Kukimbilia Kutoa Swadaqah  Kabla Ya Mauti

www.alhidaaya.com

 

 

عن أبي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ, أَيُّ الصَّدَقَةِ أَعْظَمُ أَجْرًا؟ قَالَ: ((أَنْ تَصَدَّقَ وَأَنْتَ صَحِيحٌ شَحِيحٌ تَخْشَى الْفَقْرَ وَتَأْمُلُ الْغِنَى وَلاَ تُمْهِلُ حَتَّى إِذَا بَلَغَتْ الْحُلْقُومَ قُلْتَ لِفُلاَنٍ كَذَا وَلِفلاَنٍ كَذَا وَقَدْ كَانَ لِفُلاَنٍ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: “Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Ni swadaqah ipi yenye ujira mkubwa zaidi?  Akasema: ((Ni utoe swadaqah nawe umzima, unataka mali bado, unakhofia ufukara na unatarajia utajiri. Wala usichelewe mpaka roho ikafika kwenye koo, ukaanza kusema: fulani ana haki kadhaa na fulani ana haki kadhaa na fulani alikuwa ana haki kadhaa)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Swadaqah ya aliye mzima ni bora kuliko ya mgonjwa kwa sababu aghlabu bin Aadam anakuwa mchoyo na bakhili anapokuwa katika afya kamili. Hivyo, atakapotoa wakati yu mzima itakuwa ni swadaqah ya niyyah safi na mapenzi ya kutoa kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

2. Kukimbilia kutenda mema wakati una umri na siha kabla ya kufikwa na mtihani wa magonjwa na ufukara. Rejea: Al-Baqarah (2: 148).

 

Na amrisho la kutoa swadaqah kabla ya kufika siku ambayo halitomfaa mtu lolote. Rejea: Al-Baqarah (2: 254).

 

 

3. Kukimbilia kutoa swadaqah kabla ya kufikwa na mauti kama Anavyoonya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ﴿١٠﴾

Na toeni katika yale Tuliyokuruzukuni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti akasema: “Rabb wangu! Lau Ungeliniakhirisha mpaka muda wa karibu hivi, basi ningetoa swadaqah na ningelikuwa miongoni mwa Swalihina.”

 

وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا ۚ وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١١﴾

Lakini Allaah Haiakhirishi kamwe nafsi yeyote inapokuja ajali yake na Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo. [ Al-Munaafiquwn (63: 10-11).]

 

 

4. Mali ya kudumu khasa ni ile anayoitoa Muislamu kabla ya kufariki kwake, ama baada ya hapo ni mali ya warithi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَا عِندَكُمْ يَنفَدُ ۖ وَمَا عِندَ اللَّـهِ بَاقٍ ۗ  

Mlivyo navyo nyinyi vinatoweka, na vilioko kwa Allaah ni vya kubakia. [An-Nahl (16: 96)]

 

 

Pia rejea Hadiyth namba (54), (62), (71), (77).  

 

Pia Hadiyth imepokelewa kutoka kwa Mutwarrif: ((Bin Aadam husema: Mali yangu, mali yangu!  Ee bin Aadam! Je, una mali yoyote isipokuwa uliyoimaliza, uliyoitumia, uliyoivaa kisha ikachafuka, au [bora mali] uliyoitolea swadaqah ikatangulizwa?)) [Muslim]

 

 

5. Kukumbuka mauti na kuyakhofia kila mara khasa unapotaka kufanya jambo jema au kutenda ovu.

 

 

6. Kutoa wakati unaaga dunia hakuruhusiwi ki-shariy’ah, na chochote utakachotoa wakati huo kuwapatia ahli yako na jamaa, hakitahesabiwa, kwani Allaah (سبحانه وتعالى) tayari Ashampatia kila mmoja haki yake kutoka kwa aliyefariki.

 

 

7. Inafaa mja atumie vyema neema ya afya, uzima na mali, kwani hivi ni vitu ambavyo havidumu. Na ikiwa hatoweza kuvitumia kwa maslahi yake na kujikurubisha kwa Allaah (سبحانه وتعالى), basi atakuwa amekhasirika. Rejea Hadiyth namba (9).

 

Share

009-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Neema Mbili Watu Wengi Wameghilibika Nazo; Siha Na Faragha

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 9

Neema Mbili Watu Wengi Wameghilibika Nazo; Siha Na Faragha

www.alhidaaya.com

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((نِعْمَتَانِ مَغْبُونٌ فِيهِمَا كَثِيرٌ مِنْ النَّاسِ: الصِّحَّةُ وَالْفَرَاغُ))  رواه  البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watu wengi wameghilibika katika neema mbili; siha na faragha [wasaa])).[Al-Bukhaariy.]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) hata wakati wa faragha kama Anavyosema:

 

 فَإِذَا فَرَغْتَ فَانصَبْ ﴿٧﴾

Basi utakapopata faragha fanya juhudi katika ‘ibaadah.

 

وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَارْغَب ﴿٨﴾

Na kwa Rabb wako elemea kwa raghba (kutakabaliwa).  [Ash-Sharh (94: 7-8)]

 

 

2. Siha na faragha yaani kuwa na wasaa (nafasi) ni raasilmali ya mtu, basi atakayetumia raasilmali yake vyema atapata faida, na atakayeipoteza atakhasirika na kujuta, na pindi yatakapomfika mauti  atatamani arudishwe duniani ili atumie vizuri neema hizi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩﴾

Mpaka itakapomfikia mmoja wao mauti, atasema: “Rabb wangu! Nirejeshe (duniani).”

 

 

لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ ۚ كَلَّا ۚ إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَائِلُهَا ۖ وَمِن وَرَائِهِم بَرْزَخٌ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ﴿١٠٠﴾

 “Ili nikatende mema katika yale niliyoyaacha.” (Ataambiwa) “Laa hasha!” Hakika hilo ni neno alisemaye yeye tu.  Na nyuma yao kuna barzakh mpaka Siku watakayofufuliwa.  [Al-Muuminuwn (23: 99-110)]

 

 

3. Umuhimu wa kunufaika kwa siha na faragha kabla ya kutoweka kwake, kwa kujikurubisha kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na kujitendea ‘amali njema. Hadiyth:

 

 

قال رسولُ اللهِ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم لرجلٍ وهو يَعِظُه: ((اغتنِمْ خمسًا قبل خمسٍ : شبابَك قبل هِرَمِك، وصِحَّتَك قبل سِقَمِك، وغناك قبل فقرِك، وفراغَك قبل شُغلِك، وحياتَك قبل موتِك))

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alimwambia mtu katika kumuwaidhi: ((Nufaika kwa mambo matano kabla ya matano; ujana wako kabla ya uzee wako, siha yako kabla ya maradhi yako, mali yako kabla ya ufukara wako, wakati wako wa faragha kabla ya kushughulishwa kwako, na uhai wako kabla ya mauti yako))  [Al-Haakim, Al-Bayhaqiy Ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (1077), Swahiyh At-Targhiyb (3355)]

 

Rejea Hadiyth namba (58).

 

 

4. Watu wengi hawathamini neema mbili hizi. Kuna ambao wanaopoteza muda wao kwa mambo yasiyowanufaisha katika Aakhirah, na wanaharibu miili yao na hali Uislamu umesisitiza kuchunga wakati na viwiliwili.

 

 

5. Muumin atumie wakati wake wote kwa kutenda mema na kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) ili ajiepushe na upuuzi na aweze kupata sifa miongoni mwa sifa za Waumini watakaopata Jannah ya Al-Firdaws.

 

Rejea: Al-Muuminuwn (23: 1-11).

 

 

 

6. Kutotumia neema alizopatiwa na Allaah (سبحانه وتعالى) ni kukhasirika kwa mja duniani na Aakhirah.

 

Rejea:  Al-‘Aswr (103: 1-2).

 

Rejea pia Hadiyth namba (7), (45), (54), (61).
 

7. Kutokutumia vizuri neema mbili hizo za Allaah (سبحانه وتعالى) na nyenginezo nyingi ni kukosa shukurani. Kinyume chake ni kumshukuru Allaah (عزّ وجلّ) na hapo faida inamrudia mtu mwenyewe kwa kuzidishiwa neema kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذْ تَأَذَّنَ رَبُّكُمْ لَئِن شَكَرْتُمْ لَأَزِيدَنَّكُمْ ۖ وَلَئِن كَفَرْتُمْ إِنَّ عَذَابِي لَشَدِيدٌ﴿٧﴾

Na pindi Alipotangaza Rabb wenu: “Ikiwa mtashukuru, bila shaka Nitakuzidishieni (neema Zangu); na mkikufuru, basi hakika adhabu Yangu ni kali. [Ibraahiym (14: 7)]

 

 

 

Share

010-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mja Atafufuliwa Kwa Kitendo Alichofariki Nacho

 

 

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 10

Mja Atafufuliwa Kwa Kitendo Alichofariki Nacho

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ جَابِرٍ (رضي الله عنه) قَال: قَالَ النَّبِيَّ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((يُبْعَثُ كُلُّ عَبْدٍ عَلَى مَا مَاتَ عَلَيْهِ)) رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه) ambaye amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kila mja atafufuliwa katika hali aliyofia)) [Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo

 

 

1. Hima ya kutenda mema na kubakia katika istiqaamah (kuthibitika katika Dini) ili kitendo cha mwisho kabla ya kufariki kiwe ni kitendo chema, na kiwe ni kiliwazo siku ya kufufuliwa. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ تَتَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ طَيِّبِينَ ۙ يَقُولُونَ سَلَامٌ عَلَيْكُمُ ادْخُلُوا الْجَنَّةَ بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٣٢﴾

Ambao Malaika huwafisha katika hali nzuri (Malaika) watasema: “Salaamun ‘Alaykum!” Amani iwe juu yenu ingieni Jannah kwa yale mliyokuwa mkitenda.”  [An-Nahl (16: 32).]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَنْ عَمِلَ صَالِحًا مِّن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَىٰ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَنُحْيِيَنَّهُ حَيَاةً طَيِّبَةً ۖ وَلَنَجْزِيَنَّهُمْ أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٩٧﴾

Mwenye kutenda mema miongoni mwa wanamume au wanawake naye ni Muumin, Tutamhuisha uhai mzuri, na bila shaka Tutawalipa ujira wao kwa mazuri zaidi ya yale waliyokuwa wakitenda.  [An-Nahl 16: 97].

 

Na pia rejea: Al-Hijr (15: 99), Al-‘Imraan (3: 102).

 

 

2. Umuhimu wa kupata husnul-khaatimah (mwisho mwema) kabla ya kuaga dunia na sio kuwa katika maasi, khasa pale mtu anapofikia katika umri mkubwa, kwa sababu kuna hatari ya mtu kugeuka kutoka katika twaa’ah (utiifu) na taqwa na kuingia katika maasi kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 

 

عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رضي الله عنه قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم -وَهُوَ الصَّادِقُ الْمَصْدُوقُ: ((إِنَّ أَحَدَكُمْ يُجْمَعُ خَلْقُهُ فِي بَطْنِ أُمِّهِ أَرْبَعِينَ يَوْمًا نُطْفَةً، ثُمَّ يَكُونُ عَلَقَةً مِثْلَ ذَلِكَ، ثُمَّ يَكُونُ مُضْغَةً مِثْلَ ذَلِكَ، ثُمَّ يُرْسَلُ إلَيْهِ الْمَلَكُ فَيَنْفُخُ فِيهِ الرُّوحَ، وَيُؤْمَرُ بِأَرْبَعِ كَلِمَاتٍ: بِكَتْبِ رِزْقِهِ، وَأَجَلِهِ، وَعَمَلِهِ، وَشَقِيٍّ أَمْ سَعِيدٍ؛ فَوَاَللَّهِ الَّذِي لَا إلَهَ غَيْرُهُ إنَّ أَحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ الْجَنَّةِ حَتَّى مَا يَكُونُ بَيْنَهُ وَبَيْنَهَا إلَّا ذِرَاعٌ فَيَسْبِقُ عَلَيْهِ الْكِتَابُ فَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ النَّارِ فَيَدْخُلُهَا. وَإِنَّ أَحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ النَّارِ حَتَّى مَا يَكُونُ بَيْنَهُ وَبَيْنَهَا إلَّا ذِرَاعٌ فَيَسْبِقُ عَلَيْهِ الْكِتَابُ فَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهْلِ الْجَنَّةِ فَيَدْخُلُهَا)) رواه البخاري ومسلم

Kutoka kwa Abuu 'Abdir-Rahmaan 'Abdillaah bin Mas-‘uwd  (رضي الله عنه)  ambaye amesema: “Ametusimulia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ambaye ni mkweli mwenye kuaminiwa: “Hakika kila mmoja wenu hukusanywa umbo lake katika tumbo la mama yake siku arubaini akiwa ni mkusanyiko wa mbegu (za uzazi za mama na baba), kisha arubaini zifuatazo huwa ni donge la damu, kisha arubaini zijazo huwa pande la nyama, kisha Allaah Humtuma Malaika kwake na kumpulizia roho (yake).  Na (Malaika huyo) anaamrishwa maneno manne; Kuandika rizki yake, ajali yake (umri atakaoishi duniani), amali zake, mtu muovu au mwema. Wa-Allaahi naapa kwa Yule Ambaye hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Yeye, hakika mmoja wenu huenda afanye ‘amali za watu wa Jannah hadi ikawa baina yake na Jannah ni dhiraa na kile kilichoandikwa kikathibiti akafanya ‘amali ya watu wa motoni akaingia motoni. Na mmoja wenu hufanya ‘amali za watu wa motoni hadi ikawa baina yake na moto ni dhiraa na hapo kile kilichoandikwa kikathibiti akafanya ‘amali ya watu wa Jannah akaingia Jannah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na katika riwaayah inayomalizikia: ((…’amali zinahesabika za mwisho)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 

3. Kutahadhari kubakia katika taqwa na twaa’ah (utiifu) wa Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) na kwa sababu Allaah (سبحانه وتعالى) Anawajua vyema waja Wake na yaliyomo moyoni Naye ni Mweza wa kugeuza nyoyo zao pindi wanapomuasi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ ۖ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَحُولُ بَيْنَ الْمَرْءِ وَقَلْبِهِ وَأَنَّهُ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ﴿٢٤﴾

Enyi walioamini! Muitikieni Allaah na Rasuli Anapokuiteni kwenye yale yenye kukuhuisheni na jueni kwamba Allaah Anaingilia kati baina ya mtu na moyo wake; na kwamba Kwake mtakusanywa. [Al-Anfaal (8: 24)].

 

 

4. Umuhimu wa kuomba du’aa ya kuthibitika katika Dini mpaka kufariki. Nayo ni du’aa ambayo alikuwa akiiomba sana Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

اللَّهُمَّ يَا مُقَلِّبَ الْقُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِك

((Allaahuuma Yaa Muqallibal-Quluub Thabbit Qalbiy 'Alaa Diynik – Ee Allaah, ee Mgeuza nyoyo, Thibitisha  moyo wangu katika Dini Yako)) [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan]

 

Na pia kuomba Du’aa ya Nabiy Yuwsuf (عليه السلام)

 

 (اللَّهُمَّ)  فَاطِرَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ أَنتَ وَلِيِّي فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۖ تَوَفَّنِي مُسْلِمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ ﴿١٠١﴾

(Ee Allaah) Muanzilishi wa mbingu na ardhi. Wewe ni Mlinzi, Msaidizi wangu duniani na Aakhirah. Nifishe hali ya kuwa Muislamu na Unikutanishe na Swalihina.” [Yuwsuf (12: 101)]

 

 

 

5. Hatari ya kutenda maasi yakaja kuwa ndio kitendo cha mwisho cha Muislamu, kwani mauti yanamfikia mtu bila ya taarifa, mfano kupatwa na ajali ukiwa katika kuendesha gari na huku unasikiliza muziki.   

 

 

 

6. Kilicho muhimu ni ‘amali za mwisho, basi atakayefanya ‘amali zake kuwa ni bora katika uhai wake wa mwisho atapata bishara njema na kheri Siku ya Qiyaamah, na atakayefanya maovu katika uhai wake wa mwisho atakutana na shari huko Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ تَتَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ ۖ فَأَلْقَوُا السَّلَمَ مَا كُنَّا نَعْمَلُ مِن سُوءٍ ۚ بَلَىٰ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٢٨﴾

Ambao Malaika huwafisha wakiwa wamejidhulumu nafsi zao, watasalimu amri (watasema): “Hatukuwa tukitenda uovu wowote.” (Wataambiwa): “Hapana! Hakika Allaah ni Mjuzi kwa yale mliyokuwa mkitenda.”

 

فَادْخُلُوا أَبْوَابَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا ۖ فَلَبِئْسَ مَثْوَى الْمُتَكَبِّرِينَ﴿٢٩﴾

 “Basi ingieni milango ya Jahannam ni wenye kudumu humo.” Ni uovu ulioje makazi ya wanaotakabari.

 

 

وَقِيلَ لِلَّذِينَ اتَّقَوْا مَاذَا أَنزَلَ رَبُّكُمْ ۚ قَالُوا خَيْرًا ۗ لِّلَّذِينَ أَحْسَنُوا فِي هَـٰذِهِ الدُّنْيَا حَسَنَةٌ ۚ وَلَدَارُ الْآخِرَةِ خَيْرٌ ۚ وَلَنِعْمَ دَارُ الْمُتَّقِينَ﴿٣٠﴾

Na wanapoambiwa wale waliokuwa na taqwa: “Nini Ameteremsha Rabb wenu?” Husema: “Kheri.” Kwa wale waliofanya ihsaan katika dunia hii watapata hasanah (mazuri). Na bila shaka nyumba ya Aakhirah ni bora zaidi. Na uzuri ulioje nyumba ya wenye taqwa.

 

 

جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۖ لَهُمْ فِيهَا مَا يَشَاءُونَ ۚ كَذَٰلِكَ يَجْزِي اللَّـهُ الْمُتَّقِينَ﴿٣١﴾

Jannaat za kudumu milele wataziingia humo, zipitazo chini yake mito. Watapata humo wayatakayo. Hivyo ndivyo Allaah Anavyowalipa wenye taqwa.

 

 

الَّذِينَ تَتَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ طَيِّبِينَ ۙ يَقُولُونَ سَلَامٌ عَلَيْكُمُ ادْخُلُوا الْجَنَّةَ بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٣٢﴾

Wale ambao Malaika huwafisha katika hali njema watasema: “Salaamun ‘Alaykum, (amani iwe juu yenu) ingieni Jannah kwa yale mliyokuwa mkitenda.” [An-Nahl (16: 28-32)]

 

 

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) Anasema:

 

إِنَّ الْعَبْدَ لَيَعْمَلُ عَمَلَ أَهْلِ النَّارِ، وَإِنَّهُ مِنْ أَهْلِ الْجَنَّةِ، وَيَعْمَلُ عَمَلَ أَهْلِ الْجَنَّةِ، وَإِنَّهُ مِنْ أَهْلِ النَّارِ، وَإِنَّمَا الأَعْمَالُ بِالْخَوَاتِيمِ ‏"‏‏.‏

((Hakika mja hutenda ‘amali za watu motoni lakini uhakika akaja kuwa ni mtu wa Jannah, na akaja kutenda ‘amali za watu wa Jannah lakini uhakika akaja kuwa mtu wa motoni. Hakika ‘amali zinahesabika za mwishoni)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 

7. Kutochoka wala kuzembea katika kufanya mema na kuacha kutenda maovu  kwa sababu hakuna anayejua wakati gani atatembelewa na Malakul-Mawt (Malaika wa kutoa roho). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمْ وَاخْشَوْا يَوْمًا لَّا يَجْزِي وَالِدٌ عَن وَلَدِهِ وَلَا مَوْلُودٌ هُوَ جَازٍ عَن وَالِدِهِ شَيْئًا ۚ إِنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ ۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِاللَّـهِ الْغَرُورُ ﴿٣٣﴾

Enyi watu! Mcheni Rabb wenu, na iogopeni Siku ambayo mzazi hatomfaa mwanawe na wala mwana hatomfaa mzazi wake chochote. Hakika ahadi ya Allaah ni haki; basi usikughururini uhai wa dunia, na wala (shaytwaan) mwenye kughuri asikughururini kuhusu Allaah.

 

 

إِنَّ اللَّـهَ عِندَهُ عِلْمُ السَّاعَةِ وَيُنَزِّلُ الْغَيْثَ وَيَعْلَمُ مَا فِي الْأَرْحَامِ ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤﴾

Hakika Allaah Ana elimu ya Saa (Qiyaamah), na Anateremsha mvua na Anajua yale yaliyomo katika tumbo la uzazi na nafsi yoyote haijui nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haijui itafia katika ardhi gani, hakika Allaah ni Mjuzi wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Luqmaan 31: 33-34)]

 

 

 

Share

011-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Daraja Za Iymaan Ni Sabini Na; Ya Juu Ni Tawhiyd Ya Chini Kuondosha Taka..

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 11

Daraja Za Iymaan Ni Sabini Na Kitu; Ya Juu Ni Tawhiyd,

Ya Chini Ni Kuondosha Taka Njiani

www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم):  ((الإيمَانُ بِضْعٌ وَسَبْعُونَ)) أَوْ ((بِضْعٌ وَسِتُّونَ شُعْبَةً، فَأَفْضَلُهَا قَوْلُ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ،  وَأَدْنَاهَا إِمَاطَةُ الأَذَى عَنْ الطَّرِيقِ، وَالْحَيَاءُ شُعْبَةٌ مِنْ الإِيمَانِ)) متفق عليه.

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Iymaan ni sabiini na kitu)) au alisema ((Tanzu sitiini na kitu. Ilio bora kabisa ni kauli ya ‘Laa ilaaha illa-Allaah’, na ya chini kabisa ni kuondosha taka njiani. Na kuona hayaa ni utanzu katika tanzu za Iymaan)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Faida:  Bidhw’ ni idadi baina ya tatu na tisa.

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Waumini wanatofautiana katika daraja za Iymaan zao.

 

 

2. Umuhimu na fadhila ya tawhiyd yaani kumpwekesha Allaah (سبحانه وتعالى) ambayo ni asili ya Iymaan.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُوَ الْحَيُّ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ فَادْعُوهُ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ ۗ الْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴿٦٥﴾

Yeye Ndiye Aliye hai daima hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye; basi muombeni Yeye wenye kumtakasia Dini. AlhamduliLLaah, Himidi Anastahiki Allaah Rabb wa walimwengu. [Ghaafir (40: 65)]

 

 

Rejea pia: Al-An’aam (6: 102), Al-Baqarah (2: 163), Twaahaa (20: 14).

 

Na pia Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

وَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ ۘ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۚ كُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ ۚ لَهُ الْحُكْمُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ

Na wala usiombe pamoja na Allaah mwabudiwa mwingine. Hakuna muabudiwa wa haki ila Yeye. Kila kitu ni chenye kuhiliki isipokuwa Wajihi Wake. Hukumu ni Yake Pekee na Kwake Pekee mtarejeshwa. [Al-Qaswasw (28: 88]

 

 

3. Iymaan na ‘amali vinakwenda sambamba, ni vitu viwili ambavyo haviwezi kutengana.

 

 

4. Kuona hayaa ni katika sifa za Waumini. Hayaa inahusiana na tabia njema kwa sababu inamzuia mtu kutenda maasi yote na inamweka kwenye hali ya utiifu wakati wote.

 

Rejea Hadiyth namba (68).

 

 

5. Kuwa na hayaa ni dalili ya ukweli wa Iymaan ya Muislamu.

 

 

6. Muumin asidharau kutenda jambo jema lolote hata dogo mno vipi kama kuondosha taka njiani kwani huenda hayo yakawa mazito katika miyzaan yake ya mambo mema Siku ya Qiyaamah.  

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ  

Na chochote kile cha kheri mnachokadimisha kwa ajili ya nafsi zenu, mtakikuta kwa Allaah. Ni bora, na ujira mkubwa zaidi.  [Al-Muzzammil (73: 23)]

 

Na rejea pia:  Al-Baqarah (2: 110)

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

Basi yule atakayetenda kheri uzito wa chembe (au sisimizi) ataiona. [Az-Zalzalah (99: 7)]

 

 

Rejea:  Al-Anbiyaa (21: 47).

  

Pia Hadiyth:

 

 عَنْ أَبِي ذَرٍّ، قَالَ: قَالَ لِيَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لَا تَحْقِرَنَّ مِنَ الْمَعْرُوفِ شَيْئًا، وَلَوْ أَنْ تَلْقَى أَخَاكَ بِوَجْهٍ طَلْقٍ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Dharr  (رضي الله عنه) amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Usidharau kufanya jambo jema lolote lile hata ikiwa kukutana na nduguyo kwa uso wa bashasha)) [Muslim]

 

 

7. Kukosekana haya ni kukosekana Iymaan, hivyo kunamfanya mja afanye lolote atakalo. Imepokewa kwa Abuu Mas-’uwd ‘Uqbah bin ‘Amr Al-Answaar Al-Badriy (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika katika maneno yaliyopatikana na watu kutokana na Manabii ni: Usipokuwa na hayaa, basi fanya utakalo)).[Al-Bukhaariy]

 

 

Share

012-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kufanya ‘Ibaadah Kwa Wastani Ili Kuweza Kuidumisha

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 12  

 

  Kufanya ‘Ibaadah Kwa Wastani Ili Kuweza Kuidumisha

 

 

 

عَنْ عَائِشَةَ (رضي الله عنها)  أَنَّ النَّبِيَّ (صلى الله عليه و آله وسلم ( دَخَلَ عَلَيْهَا وَعِنْدَهَا امْرَأَةٌ قَالَ: ((مَنْ هَذِهِ؟)) قَالَتْ:  هذِهِ فُلاَنَةُ تَذْكُرُ مِنْ صَلاَتِهَا. قَالَ: ((مَهْ عَلَيْكُمْ بِمَا تُطِيقُونَ ، فَوَاللَّهِ لاَ يَمَلُّ اللَّهُ حَتَّى تَمَلُّوا ، وَكَانَ أَحَبَّ الدِّينِ إِلَيْهِ مَادَامَ عَلَيْهِ صَاحِبُهُ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliingia kwake akamkuta mwanamke mmoja. Akauliza: ((Nani huyu?)) Akasema: Huyu ni fulani. Na akamuelezea kuhusu wingi wa Swalaah zake. Akasema: ((Acha! fanyeni yale muwezayo! Kwani Wa-Allaahi, Allaah Hachoki [kulipa thawabu] mpaka mchoke wenyewe. Na ‘Ibaadah Aipendayo zaidi ni ile inayodumishwa na mtendaji)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Uislamu haupendekezi wingi wa ‘Ibaadah wa kupita kiasi kwa khofu ya kuchoshwa nayo mtu akaiachilia mbali au kujikalifisha nayo.   Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

طه ﴿١﴾

Twaahaa

مَا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ لِتَشْقَىٰ ﴿٢﴾

Hatukukuteremshia Qur-aan ili upate mashaka. [Twaahaa (20: 1-2]

 

 

2. Ikiwa Allaah (سبحانه وتعالى) Hamkalifishi mtu, vipi mtu ajikalifishe nafsi yake? Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا

 

((Allaah Haikalifishi nafsi ila kwa wasaa [kadiri] iwezavyo)) [Al-Baqarah (2: 286)]

 

Na pia Anasema (سبحانه وتعالى):

لَا تُكَلَّفُ نَفْسٌ إِلَّا وُسْعَهَا

 

((Nafsi isijikalifishe ila kwa wasaa wake)) [Al-Baqarah (2: 233)]

 

 

3. Inapendekezwa kufanya wastani katika kufanya ‘Ibaadah ili mtu aweze kutimiza haki ya kila kitu.

 

Hadiyth: ((Na hakika Rabb wako Ana haki juu yako, na hakika mwili wako una haki juu yako, na hakika ahli wako ana haki juu yako…basi kipe kila kitu haki yake…)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

4. ‘Amali yenye thawabu zaidi ni ile inayodumishwa japokuwa ni kidogo.

 

 

5. Kufanya ‘Ibaadah kwa wastani kunapelekea zaidi kwenye utiifu wa ‘Ibaadah, umakini, ikhlaasw na kukubaliwa na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

6. Kidogo kinachoendelea kinazidi kingi kinachokatika.

 

 

7. Kuagiziwa hivyo ni kuwa ‘Ibaadah ni nyingi na uwezo wa mja una mipaka. Kwa hiyo, mja ajiweke katika mipaka hiyo ambayo itamuwezesha yeye kufanya mengi.

 

 

 

 

Share

013-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Atakayepitiwa Na Usingizi Bila Kusoma Nyiradi Zake Alipize Kabla Adhuhuri

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 13   

Atakayepitiwa Na Usingizi Bila Ya Kusoma Nyiradi Zake Alipize Kabla Ya Adhuhuri

 www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ (رضي الله عنه)  يَقُولُ:  قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((مَنْ نَامَ عَنْ حِزْبِهِ أَوْ عَنْ شَيْءٍ مِنْهُ فَقَرَأَهُ فِيمَا بَيْنَ صَلاَةِ الْفَجْرِ وَصَلاَةِ الظُّهْرِ كُتِبَ لَهُ كَأَنَّمَا قَرَأَهُ مِنْ اللَّيْلِ)) رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayelala na kupitiwa na hizbu yake [nyiradi zake] au chochote kutoka humo kisha akaisoma baina ya Swalaah ya Alfajiri na Swalaah ya Adhuhuri, ataandikiwa kama kwamba ameisoma usiku))  [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Umuhimu wa Muislamu kuhifadhi na kuendeleza nyiradi zake kila siku.

 

 

2. Anayepitwa na nyiradi zake, akimbilie kuzisoma nyakati zilotajwa katika Hadiyth ili apate fadhila zake kamilifu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى): 

 

 

وَهُوَ الَّذِي جَعَلَ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ خِلْفَةً لِّمَنْ أَرَادَ أَن يَذَّكَّرَ أَوْ أَرَادَ شُكُورًا ﴿٦٢﴾

Naye Ndiye Aliyejaalia usiku na mchana ufuatane kwa atakaye kukumbuka au atakaye kushukuru. [Al-Furqaan (26: 62)]

 

 

3. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa waja Wake kuwalipa thawabu wakati wanaposhindwa kupata wasaa au wanapokalifika na jambo kama ugonjwa n.k. Rejea: Al-Baqarah (2: 286)

 

Pia Hadiyth: Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:

 

 ((إِذَا ابْتَلَى اللَّهُ الْعَبْدَ الْمُسْلِمَ بِبَلَاءٍ فِي جَسَدِهِ قَالَ اللَّهُ لِلْمَلَكِ: اكْتُبْ لَهُ صَالِحَ عَمَلِهِ الَّذِي كَانَ يَعْمَلُ فَإِنْ شَفَاهُ غَسَلَهُ وَطَهَّرَهُ وَإِنْ قَبَضَهُ غَفَرَ لَهُ وَرَحِمَهُ))

 ((Allaah Akimjaribu mja Muislamu kwa kumpa mtihani katika mwili wake, Humwambia Malaika: “Mwandikie ‘amali zake njema alizokuwa akizitenda”. Akimpa shifaa [Akimponyesha] Humwosha na kumtakasa, na Akichukua roho yake, Humghufuria na Akamrehemu)) [Ahmad katika Musnad na amesema Al-Albaaniy: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

4. Rahmah ya Allaah (سبحانه وتعالى) na Uadilifu Wake kwamba Anatambua hali za waja Wake kushughulishwa na mambo kadhaa ya dunia yao na Aakhirah yao, Akawaamrisha wapunguze ‘ibaadah zao kama vile kusoma Qur-aan. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّ رَبَّكَ يَعْلَمُ أَنَّكَ تَقُومُ أَدْنَىٰ مِن ثُلُثَيِ اللَّيْلِ وَنِصْفَهُ وَثُلُثَهُ وَطَائِفَةٌ مِّنَ الَّذِينَ مَعَكَ ۚ وَاللَّـهُ يُقَدِّرُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ ۚ عَلِمَ أَن لَّن تُحْصُوهُ فَتَابَ عَلَيْكُمْ ۖ فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنَ الْقُرْآنِ ۚ عَلِمَ أَن سَيَكُونُ مِنكُم مَّرْضَىٰ ۙ وَآخَرُونَ يَضْرِبُونَ فِي الْأَرْضِ يَبْتَغُونَ مِن فَضْلِ اللَّـهِ ۙ وَآخَرُونَ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ۖ فَاقْرَءُوا مَا تَيَسَّرَ مِنْهُ ۚ وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَأَقْرِضُوا اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ وَاسْتَغْفِرُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿٢٠﴾

Hakika Rabb wako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Anajua kwamba unasimama (kuswali) karibu na thuluthi mbili za usiku au nusu yake, au thuluthi yake; na kundi miongoni mwa wale walio pamoja nawe. Na Allaah Anakadiria usiku na mchana. Anajua kwamba hamuwezi kuukadiria wakati wake na kusimama kuswali, basi Amepokea tawbah yenu. Basi someni kile kilicho chepesi katika Qur-aan. (Allaah) Anajua kwamba watakuweko miongoni mwenu wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wanatafuta fadhila za Allaah, na wengineo wanapigana katika njia ya Allaah. Basi someni kile kilicho chepesi humo. Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah, na mkopesheni Allaah karadhi nzuri. Na chochote kile cha kheri mnachokadimisha kwa ajili ya nafsi zenu, mtakikuta kwa Allaah. Ni bora, na ujira mkubwa zaidi. Na muombeni Allaah maghfirah, hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.  [Al-Muzzammil (73: 20)]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (12).

 

 

5. Asiitegemee mtu Hadiyth hii kwa kutokujihimiza kuamka usiku kufanya ‘Ibaadah, bali ajitahidi kila njia kujiwezesha kuamka kupata fadhila za Qiyaamul-Layl (Kisimamo cha usiku kwa ajili ya kuswali):  

 

Rejea: As-Sajdah (32: 16-17), Al-Israa (17: 79), Adh-Dhaariyaat (51: 15-18), Al-Muzzammil (73: 2-8).

 

 

6. Kuna fadhila tukufu za nyiradi na ‘amali za usiku, hivyo inatakiwa mja ajipinde katika kuzitekeleza.

 

 

7. Kuchuma fadhila za nyakati baina ya Alfajiri na Adhuhuri kwa kuleta nyiradi alizokosa mja yeyote yule.

 

 

Share

014-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuzishikilia Sunnah Kwa Magego Ili Kubakia Imara Na Kujiepusha Ikhtilaaf

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 14  

Kuzishikilia Sunnah Kwa Magego Ili Kubakia Imara Na Kujiepusha Na Ikhtilaaf

www.alhidaaya.com

 

عن أبي نَجِيح الْعِرْبَاضُ  بن سارية (رضي الله عنه) قال: وَعَظَنَا رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم) مَوْعِظَةً بَلِيغَةً وَجِلَتْ مِنْهَا الْقُلُوبُ  وَذَرَفَتْ مِنْهَا الْعُيُونُ. فَقُلْنَا:  يَا رَسُولَ اللَّهِ كَأَنَّها مَوْعِظَةُ مُوَدِّعٍ فأوْصِنا. فَقَالَ: ((أُوصِيكُمْ بِتَقْوَى اللَّهِ وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وَإِنْ تأَمَّرَ عَلَيْكُم عَبْدٌ حَبَشِيّ ، وَأَنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيَرَى اخْتِلاَفًا كَثِيرًا ، فَعَلَيْكُمْ بِسُنَّتِي وَسُنَّةِ الْخُلَفَاءِ الرَّاشِدِينَ الْمَهْدِيِّينَ ، عَضُّوا عَلَيْهَا بِالنَّوَاجِذِ وَإِيَّاكُمْ وَمُحْدَثَاتِ الأُمُورِ فَإِنَّ كُلَّ بِدْعَةٌ ضَلاَلَةٌ)) رواه أبو داوود والترمذي وقال حديث حسن صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Najiyh Al-‘Irbaadhw bin Saariyah (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alitupa mawaidha mazito (yenye maana kubwa), nyoyo zikaogopa na macho yakabubujikwa machozi. Tukasema: Ee Rasuli wa Allaah! Yanaonekana kama kwamba mawaidha ya kutuaga, basi tuusie.  Akasema: ((Nakuusieni kuwa na taqwa ya Allaah na kusikiliza na kutii japokuwa mtaongozwa na mtumwa Mhabashi. Hakika atakayeishi umri mrefu miongoni mwenu ataona ikhtilaaf nyingi. Kwa hiyo, shikamaneni na Sunnah zangu na mwenendo wa Makhalifa waongofu, yashikilieni kwa magego [mambo yao]. Na tahadharini na mambo yenye kuzushwa, kwani kila uzushi ni upotovu)) [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1.Wajibu wa kumcha Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kufuata maamrisho na makatazo Yake kama Anavyosema:

 

قُلْ أَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ ۖ فَإِن تَوَلَّوْا فَإِنَّمَا عَلَيْهِ مَا حُمِّلَ وَعَلَيْكُم مَّا حُمِّلْتُمْ ۖ وَإِن تُطِيعُوهُ تَهْتَدُوا ۚ وَمَا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿٥٤﴾

Sema: “Mtiini Allaah na mtiini Rasuli.” Mkigeukilia mbali, basi hakika jukumu lake ni lile alobebeshwa tu nanyi ni juu yenu yale mliyobebeshwa. Na mkimtii mtaongoka; na hapana juu ya Rasuli isipokuwa ubalighisho bayana.

 

 

وَعَدَ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَيَسْتَخْلِفَنَّهُمْ فِي الْأَرْضِ كَمَا اسْتَخْلَفَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ وَلَيُمَكِّنَنَّ لَهُمْ دِينَهُمُ الَّذِي ارْتَضَىٰ لَهُمْ وَلَيُبَدِّلَنَّهُم مِّن بَعْدِ خَوْفِهِمْ أَمْنًا ۚ يَعْبُدُونَنِي لَا يُشْرِكُونَ بِي شَيْئًا ۚ وَمَن كَفَرَ بَعْدَ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ ﴿٥٥﴾

Allaah Amewaahidi wale walioamini miongoni mwenu na wakatenda mema kwamba bila shaka Atawafanya makhalifa katika ardhi kama Alivyowafanya makhalifa wale waliokuwa kabla yao, na bila shaka Atawamakinishia Dini yao Aliyowaridhia, na bila shaka Atawabadilishia amani badala ya khofu yao; wawe wananiabudu Mimi wasinishirikishe na chochote; na yeyote yule atakayekufuru baada ya hapo, basi hao ndio mafasiki.

 

وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿٥٦﴾

Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah, na mtiini Rasuli ili mpate kurehemewa. [An-Nuwr 24: 54-56)]

 

 

Rejea pia:  Al-Anfaal (8: 46), Al-Ahzaab (33: 70), At-Tawbah (9: 119), Muhammad (47: 33).

 

Na jambo hilo limepatiwa kipaumbele kwa kutajwa mwanzo kwa kuwa umuhimu wake ni mkubwa sana.

 

 

2. Wajibu wa kumtii kiongozi anayeongoza kwa kufuata Shariy’ah japokuwa ni mtu anayeonekana kuwa duni, na inapotokea ikhtilaaf, arudie mtu katika Qur-aan na Sunnah.

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَأُولِي الْأَمْرِ مِنكُمْ ۖ فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۚ ذَٰلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلًا ﴿٥٩﴾

Enyi walioamini! Mtiini Allaah na mtiini Rasuli na wenye madaraka katika nyinyi. Mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allaah na Rasuli mkiwa mnamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Hivyo ni bora na matokeo mazuri zaidi. [An-Nisaa (4: 59)]

 

 

3. Hadiyth hii ni miongoni mwa miujiza ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kubashiria yatakayotokea, kwani zimeshadhihirika ikhtilaaf nyingi baina ya Waislamu.

 

 

4. Kufuata amri za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni dalili ya mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) na tahadharisho la kumkhalifu. Rejea: Aal-‘Imraan (3: 31), An-Nuwr (24: 63).

 

 

5. Umuhimu wa kufuata Sunnah za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na kuzishikilia bila ya kutoka nje ya mipaka na njia iliyonyooka ikapeleka kufarikiana Waislamu na kujitokeza makundi makundi. Rejea: Al-An’aam (6: 153).

 

Na kila kundi hufurahia watu wake wakijiona kuwa wako katika haki. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

مِنَ الَّذِينَ فَرَّقُوا دِينَهُمْ وَكَانُوا شِيَعًا ۖ كُلُّ حِزْبٍ بِمَا لَدَيْهِمْ فَرِحُونَ ﴿٣٢﴾

 (Wala msiwe) Miongoni mwa wale walioitenganisha dini yao wakawa makundi makundi. Kila kundi wananafurahia waliyonayo.  [Ar-Ruwm (30: 32)]

 

 

 

6. Kufuata Sunnah za Makhalifa Waongofu na kuamini kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Sunnah zao khaswa pale inapokuwa ni jambo walilolitenda wao bila ya kutendwa na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

7.  Kujiepusha kabisa na bid’ah (Uzushi), kwani hatari yake ni upotofu na motoni. [Hadiyth: ((Na kila upotofu unapeleka motoni)) [Muslim]

 

 

8. Vitendo vya bid’ah havina thamani wala havitapokelewa.

 

Rejea Hadiyth namba (15).

 

 

8. Kuonyesha usawa ulioletwa na Uislamu baina ya waja bila kujali tofauti ya ukoo, kabila, utaifa na mwengineo. Ndio tukaamrishwa kumfuata kiongozi mchaji Allaah hata kama ni mtumwa.

 

Rejea: Al-Hujuraat (49: 13)

 

 

9. Utiifu kwa Amiri ni wajibu, maadamu hajakuamrisha jambo la kumuasi Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

10. Fadhila za Maswahaba wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) waliopata hadhi ya kuwa Makhalifa baada ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

 

Share

015-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kitendo Cha Bid’ah Hakikubaliwi Katika Dini Yetu

 

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 15   

 

Kitendo Cha Bid’ah Hakikubaliwi Katika Dini Yetu

 

 

 

 

عَنْ عَائِشَة (رضي الله عنها)  قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم:  ((مَنْ أَحْدَثَ فِي أَمْرِنَا هَذَا مَا لَيْسَ مِنْهُ فَهُوَ رَدّ)) رواه  مسلم

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwenye kuzua katika hili jambo [Dini] letu lisilokuwemo humo, litakataliwa)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hadiyth hii ni asili ya Dini na nguzo kati ya nguzo kama alivyosema Imaam An-Nawawiy (رحمه الله). Hivyo basi, kuna umuhimu mkubwa wa kumtii Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), kwani hivyo ni kumtii Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّن يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللَّـهَ ۖ  

 Atakayemtii Rasuli basi kwa yakini amemtii Allaah [An-Nisaa 4: 80].

 

 

 

 

2. Dini ya Kiislamu ni Dini ya kufuata maamrisho na si ya kuongeza mambo na kuzusha. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا ۚوَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ﴿٧﴾

Na lolote analokupeni Rasuli (صلى الله عليه وآله وسلم) basi lichukueni, na analokukatazeni, basi acheni. Na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mkali wa kuakibu. [Al-Hashr 59: 7]

 

 

3. Jambo lolote linalotendwa kama ni ‘Ibaadah ya kujikurubisha kwa Allaah (سبحانه وتعالى) ambalo halimo katika Qur-aan na Sunnah ni bid’ah (uzushi) litakataliwa, na mzushi au mtendaji uzushi hatopata thawabu yoyote, hata ikiwa kwa niyyah safi, na itakuwa ni kupoteza juhudi zake na mali yake kwa jambo lisilo na thamani mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zinazotawanyika. [Al-Furqaan (25: 23)]

 

Rejea pia: Al-Kahf (18: 103-104).

 

 

4. Dini ya Kiislamu hairuhusu bid’ah yoyote bali inatilia nguvu kushikamana na Qur-aan na Sunnah, na hiyo ndio njia iliyonyooka ipasayo kufuatwa kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٥٣﴾

“Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kuwa na taqwa. [Al-An’aam (6: 153)]

 

Rejea pia: Yuwsuf (12: 108)

 

 

5. Hili ni onyo kwa Muislamu kutozua jambo lolote katika Dini kwani tayari Dini imekamilika kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ

Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni neema Yangu, na Nimekuridhieni Uislamu uwe Dini yenu.   [Al-Maa’idah (5: 3)]

 

 

Share

016-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Athari ya Kuelekeza Kwenye Hidaayah Na Upotofu

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 16  

 Athari ya Kuelekeza Kwenye Hidaayah Na Upotofu

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((مَنْ دَعَا إِلَى هُدًى كَانَ لَهُ مِنْ الأَجْرِ مِثْلُ أُجُورِ مَنْ تَبِعَهُ, لاَ يَنْقُصُ ذَلِكَ مِنْ أُجُورِهِمْ شَيْئًا, وَمَنْ دَعَا إِلَى ضَلاَلَةٍ كَانَ عَلَيْهِ مِنْ الإِثْمِ مِثْلُ آثَامِ مَنْ تَبِعَهُ لاَ يَنْقُصُ ذَلِكَ مِنْ آثَامِهِمْ شَيْئًا)) رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayelingania katika hidaayah, atapata ujira mfano wa aliyemfuata, bila ya kupunguziwa chochote katika ujira wao. Na atakayelingania katika upotofu, atapata dhambi mfano wa dhambi za waliomfuata bila ya kupunguziwa chochote katika dhambi zake)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 1. Fadhila za mlinganiyaji ni nyingi mno kwa kufuatwa anayoyalingania, na thawabu zake zinazidi hata baada ya kufariki kwake kwa kila atakayefuata. Rejea Hadiyth namba (54), (76), (77), (78), (80).

 

 

2. Ulinganiaji Dini ni katika mema yatakayoendelea baada ya kufariki kwake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الْمَالُ وَالْبَنُونَ زِينَةُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ خَيْرٌ عِندَ رَبِّكَ ثَوَابًا وَخَيْرٌ أَمَلًا ﴿٤٦﴾

  Mali na watoto ni pambo la uhai wa dunia. Na mema yanayobakia ni bora mbele ya Rabb wako, kwa thawabu na matumaini.   [Al-Kahf  (18: 46)]

 

 

Rejea pia: Maryam  (19: 76).

 

 

3. Fadhila za elimu na da’wah, nazo hazipatikani ila kwa kuwa na elimu ya Dini, na si kwa kufuata watu au matamanio. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ هَـٰذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّـهِ ۚ عَلَىٰ بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي ۖ وَسُبْحَانَ اللَّـهِ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ ﴿١٠٨﴾

  Sema: “Hii ndio njia yangu nalingania kwa Allaah, juu ya nuru za elimu na umaizi, mimi na anayenifuata.  [Yuwsuf (12: 108)]

 

 

 

4. Umuhimu wa kujifunza elimu sahihi, la sivyo kuna hatari nyingine, nayo ni kujitayarishia makazi ya motoni. Rejea Hadiyth namba (76).

 

 

5. Mlinganiyaji mema au maovu na mtendaji wake, watapata malipo sawasawa, mazuri au mabaya.

 

 

6. Mlinganiyaji atahadhari anayoyalingania, kwani akilinganiya maovu ataacha athari nyuma yake na atabeba dhambi zake na kila atakayemfuata. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ ۚ وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُّبِينٍ ﴿١٢﴾

Hakika Sisi Tunahuisha wafu, na Tunaandika yale waliyoyakadimisha na athari zao na kila kitu Tumekirekodi barabara katika daftari bayana. [Yaasiyn: 12]

 

 

 Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لِيَحْمِلُوا أَوْزَارَهُمْ كَامِلَةً يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۙ وَمِنْ أَوْزَارِ الَّذِينَ يُضِلُّونَهُم بِغَيْرِ عِلْمٍ ۗ أَلَا سَاءَ مَا يَزِرُونَ﴿٢٥﴾

Ili wabebe mizigo (ya madhambi) yao kamili Siku ya Qiyaamah, na mizigo ya wale waliowapoteza bila ya elimu. Tanabahi!  Uovu ulioje wanayoyabeba. [An-Nahl (16: 25).]

 

 

7. Muislamu atahadhari kufuata mafunzo ya ubatili na ajiepushe na wabatilifu wanaopotosha watu katika Dini.

 

 

8. Rusuli walipowalinganiya watu wao wasimshirikishe Allaah (سبحانه وتعالى) jibu la wengi wao lilikuwa kwamba wamewafuata mababa zao. Na hali imekuwa ni hivihivi kwa walio wakaidi katika jamii pindi mtu anaponasihiwa ache upotofu na uzushi. Rejea: Al-Baqarah (2: 170), Al-Maaidah (5: 104), As-Swaaffaat (37: 69-70), Az-Zukhruf (43: 22-23).

 

 

Share

017-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuondosha Munkari Kwa Mkono Au Ulimi Au Kuchukia Moyoni

 

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 17

 

Kuondosha Munkari Kwa Mkono Au Ulimi Au Kuchukia Moyoni

 

 

 

 

عن أبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيُّ (رضي الله عنه) قال: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم):  ((مَنْ رَأَى مِنْكُمْ مُنْكَرًا فَلْيُغَيِّرْهُ بِيَدِهِ فَإِنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَبِلِسَانِهِ فَإِنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَبِقَلْبِهِ وَذَلِكَ أَضْعَفُ الإيمَانِ)) رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) anasema: ((Atakayeona munkari [uovu] basi aubadilishe kwa mkono wake, na asipoweza basi kwa ulimi wake, na asipoweza basi kwa moyo wake [achukizwe] na huo ni udhaifu wa Iymaan)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Wajibu wa Muislamu kuamrisha mema na kukataza munkari kwa hali yoyote ile. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلْتَكُن مِّنكُمْ أُمَّةٌ يَدْعُونَ إِلَى الْخَيْرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفلِحُونَ ﴿١٠٤﴾

Na watokeze kutoka kwenu umati wa watu unaolingania kheri na unaoamrisha mema na unaokataza munkari. Na hao ndio waliofaulu. [Aal-‘Imraan (3: 104)]

 

Na pia Rejea: Aal-‘Imraan (3: 110), At-Tawbah (9: 71,  112), Al-Hajj (22: 41).

 

 

2. Kuamrisha mema na kukataza munkari ni jukumu la kila Muislamu na jamii, kwani ni fardhi kifaayah (ya kutosheleza). Walilaaniwa Ahlul-Kitaab wasiotimiza amri hii kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ ﴿٧٨﴾

Wamelaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israaiyl kwa lisani ya Daawuwd na ‘Iysaa mwana wa Maryam. Hivyo ni kwa sababu ya kuasi kwao na walikuwa wakitaadi.

كَانُوا لَا يَتَنَاهَوْنَ عَن مُّنكَرٍ فَعَلُوهُ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ﴿٧٩﴾

Walikuwa hawakatazani munkari waliyofanya. Uovu ulioje waliyokuwa wakiyafanya. [Al-Maaidah (5: 78-79)]

 

 

3. Imesemwa na ‘Ulaama kuwa Hadiyth hii ni thuluthi ya Dini. Na imesemwa pia kuwa Uislamu wote umo humo, kwani vitendo katika Shariy’ah ima ni vyema vinavyowajibika kutendwa au vitendo vya munkari vinavyowajibika kujiepusha navyo. Na baadhi ya ‘Ulamaa wameona kwamba lau ingelikuwa fardhi za Kiislamu zaidi ya sita, basi mojawapo ingelikuwa ni kuamrishana mema na kukatazana maovu. Na wengine wameongezea katika nguzo za Kiislamu.

 

 

 

4. Muislamu hatakiwi kuchangia katika maovu, bali kusaidia katika mema na uchaji Allaah. Rejea: Al-Maaidah (5: 2).

 

 

 

5. Waislamu wako tofauti katika uwezo wa kukataza maovu.

 

 

6. Iymaan ziko katika daraja tofauti. Inaongezeka katika kumtii Allaah (سبحانه وتعالى) na inapunguka katika kumuasi Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

7. Muumin ni yule anayekataza maovu na asipoweza achukie kwa moyo wake au sivyo atakuwa katika hatari ya kupotoka, kupata adhabu na kutokukubaliwa du’aa yake. Hadiyth: ((Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, hakika mtaamrishana ma’ruwf [wema] na mtakatazana munkari [maovu], au Allaah Atakuleteeni adhabu, kisha mtamuomba wala Hatokuitikieni)) [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan]

 

 

 

Share

018-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Alama Za Mnafiki Ni Tatu: Uongo, Kutokutimiza Ahadi, Kufanya Khiyana

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 18  

Alama Za Mnafiki Ni Tatu: Uongo, Kutokutimiza Ahadi, Kufanya Khiyana

www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((آيَةُ الْمُنَافِقِ ثلاَثٌ إِذَا حَدَّثَ كَذَبَ وَإِذَا وَعَدَ أَخْلَفَ وَإِذَا اؤْتُمِنَ خَانَ)) متفق عليه . وفي رواية: ((وَإِنْ صَامَ وَصَلَّى وَزَعَمَ أَنَّهُ مُسْلِمٌ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Alama za mnafiki ni tatu: anapozungumza husema uongo, anapotoa ahadi hukhalifu (hatimizi), na anapoaminiwa hufanya khiyana)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na katika riwaaya nyingine: ((Hata akifunga na akiswali na akidai kuwa yeye ni Muislamu)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Unafiki ni miongoni mwa maradhi ya moyo yanayokemewa sana katika Uislamu. Rejea: Al-Maaidah (5: 52), Al-Anfaal (8: 49).

 

 

2. Sifa tatu hizo ni sifa mashuhuri miongoni mwa sifa za wanafiki. Rejea: An-Nisaa (4: 143), Al-Baqarah (2: 8-15) Lakini hizo sio sifa pekee zinazowahusu wanafiki, bali wanazo sifa mbaya zaidi ya hizo.

 

 

3. Mwenye kuwa na sifa zote tatu hizo atahadhari mno kwani ni sifa mbaya mno asizopasa kuwa nazo Muislamu!

 

 

4. Kukimbilia kujirekebisha pindi Muislamu anapotambua kuwa ana sifa mojawapo kabla ya kumiliki sifa zote tatu.

 

 

5. Uislamu unafunza sifa njema za ukweli, kutimiza ahadi na uaminifu. Rejea: An-Nisaa (4: 58), An-Nahl (16: 91). Na sifa hizo njema ni miongoni mwa sifa za watakaopata Jannah ya Al-Firdaws Rejea: Al-Muuminuwn (23: 8). Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ﴿٣٢﴾

Na ambao amana zao na ahadi zao ni wenye kuchunga (na kuzitimiza). [Al-Ma’aarij (70: 32)]

 

 

6. Mtu anaweza kuwa na mandhari nzuri kwa mavazi na matendo ya uswalihina lakini  huenda akawa ana sifa za unafiki kama hizo. Na hii ni hatari kwake kwani Allaah ('Azza wa Jalla) Hatazami mandhari wala sura bali Anatazama yaliyo moyoni mwake.

 

 

Rejea Hadiyth namba (89), (125).

 

Share

019-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Dhulma Irudishwe Duniani Kabla Ya Malipo Ya Aakhirah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 19

 

Dhulma Irudishwe Duniani Kabla Ya Malipo Ya Aakhirah

www.alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ:  ((مَنْ كَانَتْ عِنْدَهُ مَظْلَمَةٌ مِنْ أَخِيهِ مِنْ عِرْضِهِ أَوْ  مِنْ شَيْءٍ  فَلْيَتَحَلَّلْهُ مِنْهُ الْيَوْمَ قَبْلَ أَنْ لاَ يَكُونُ دِينَارٌ وَلاَ دِرْهَمٌ ، إِنْ كَانَ لَهُ عَمَلٌ صَالِحٌ أُخِذَ مِنْهُ بِقَدْرِ مَظْلَمَتِهِ. وَإِنْ لَمْ يَكُنْ لَهُ أُخِذَ مِنْ سَيِّئَاتِ صَاحِبِهِ فَحُمِل عَلَيْهِ))  رواه البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Aliyekuwa na kitu cha dhulma cha nduguye kutokana na kumvunjia heshima au kitu chochote, basi amuombe amhalalishie leo kabla haijafika siku ambayo hakutakuwa na dinari wala dirham. Ikiwa ana ‘amali njema, basi zitachukuliwa kwa kadiri ya alichodhulumiwa. Na ikiwa hana, basi zitachukuliwa dhambi za aliyemdhulumu abebeshwe)). [Al-Bukhaariy.]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Tahadharisho la kumtendea mtu dhulma, kwani dhulma ni viza (giza) Siku ya Qiyaamah.

 

Hadiyth: ((Ogopeni dhuluma, kwani dhuluma ni viza Siku ya Qiyaamah)) [Muslim]

 

Na dhalimu ana adhabu kali Aakhirah. Rejea: Al-‘Araaf (7: 41), Maryam (19: 72),  Ghaafir (40: 52).

 

 

2. Allaah Ameharamisha dhulma na kutahadharisha kama ilivyo katika Hadiyth Al-Qudsiy:

 

عن أبي ذَرٍّ الْغِفاريِّ رضي الله عنه، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم فيما يَرْويهِ عن رَبِّهِ عَزَّ وجَلَّ أَنَّهُ قال:  (( يا عِبادي إنِّي حَرَّمْتُ الظُلْمَ على نَفْسِي وَ جعَلْتُهُ بَيْنَكُمْ مُحَرَّماً فلا تَظَالَمُوا))  رَوَاهُ مُسْلِمٌ     

Imepokelewa kutoka kwa Abu Dharr Al-Ghifaariyy (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  akisimulia yale aliyopokea kutoka kwa  Rabb wake (Aliyetukuka na Jalaali):  ((Enyi waja Wangu, Nimeikataza nafsi Yangu dhulma na Nimeiharamisha kwenu (hiyo dhulma), kwa hivyo msidhulumiane…[Muslim]

 

 

 

3. Kuwekeana heshima ni katika mambo makuu yanayohimizwa katika Uislamu.

 

 

4. Kutahadhari kuchuma ya haramu kwa kudhulumu watu kula mali zao bila ya haki. Rejea: An-Nisaa (4: 29, 161).

 

Na Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

 وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَكُم بَيْنَكُم بِالْبَاطِلِ وَتُدْلُوا بِهَا إِلَى الْحُكَّامِ لِتَأْكُلُوا فَرِيقًا مِّنْ أَمْوَالِ النَّاسِ بِالْإِثْمِ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٨﴾

Na wala msiliane mali zenu kwa ubatilifu na mkazipeleka (rushwa) kwa mahakimu ili mle sehemu katika mali ya watu kwa dhambi na hali mnajua. [Al-Baqarah (2: 188).]

 

 

5. Dhulma inaharibu ‘amali njema, kwani tajiri anayedhulumu atakuwa masikini Siku ya Qiyaamah, na masikini aliyedhulumiwa atakuwa tajiri Siku ya Qiyaamah. Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((أَتَدْرُونَ مَا الْمُفْلِسُ؟))‏ قَالُوا: الْمُفْلِسُ فِينَا مَنْ لاَ دِرْهَمَ لَهُ وَلاَ مَتَاعَ .‏ فَقَالَ: ((إِنَّ الْمُفْلِسَ مِنْ أُمَّتِي يَأْتِي يَوْمَ الْقِيَامَةِ بِصَلاَةٍ وَصِيَامٍ وَزَكَاةٍ وَيَأْتِي قَدْ شَتَمَ هَذَا وَقَذَفَ هَذَا وَأَكَلَ مَالَ هَذَا وَسَفَكَ دَمَ هَذَا وَضَرَبَ هَذَا فَيُعْطَى هَذَا مِنْ حَسَنَاتِهِ وَهَذَا مِنْ حَسَنَاتِهِ فَإِنْ فَنِيَتْ حَسَنَاتُهُ قَبْلَ أَنْ يُقْضَى مَا عَلَيْهِ أُخِذَ مِنْ خَطَايَاهُمْ فَطُرِحَتْ عَلَيْهِ ثُمَّ طُرِحَ فِي النَّارِ))  مسلم‏

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Je, Mnamjua muflis?)) Wakasema [watu]: “Muflis kwetu sisi ni yule miongoni mwetu asiyekuwa na dirhamu [pesa] wala vyenye kumnufaisha yeye hapa duniani”. Akasema (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Hakika muflis katika Ummah wangu ni yule atakayekuja Siku ya Qiyaamah na Swalaah, Swiyaam, na Zakaah, lakini amemtusi huyu, kumsingizia huyu mwingine kuwa amezini, amekula mali ya huyu, amemwaga damu ya mwingine na kumpiga mwengine. Thawabu zake zitapatiwa huyu na yule mpaka zimalizike. Na zinapokwisha basi madhambi ya hao [aliowadhulumu] atabandikwa nayo, hivyo kuingizwa Motoni))].  [Muslim]

 

 

6. Kuharakiza kulipa dhulma duniani wakati fursa bado ipo kabla ya kufikia mauti.

 

 

7-Hatari ya kumdhulumu mtu kwa sababu du’aa ya mwenye kudhulumiwa inatakabaliwa moja kwa moja:  Hadiyth:

عنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا) أَنَّ النَّبِيَّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) بَعَثَ مُعَاذًا إِلَى الْيَمَنِ فَقَالَ:  ((اتَّقِ دَعْوَةَ الْمَظْلُومِ فَإِنَّهَا لَيْسَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ اللَّهِ حِجَابٌ))

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas  (رضي الله عنهما)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alimpeleka Mu’aadh Yemen akasema: ((Iogope du’aa ya aliyedhulumiwa, kwani haina pazia baina yake na baina ya Allaah.)) [Al-Bukhaariy (2448), Swahiyh At-Tirmidhiy (2014), Swahiyh Al-Jaami’ (1037)]

 

Na pia Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنه):

   اتَّقوا دعوةَ المظلومِ، فإنها تَصعدُ إلى السماءِ كأنها شرارةٌ

((Ogopeni du’aa ya aliyedhulumiwa kwani inapanda mbinguni kama cheche za moto.)) [Al-Haakim katika Al-Mustadrak ameisahihisha Al-Albaaniy; Swahiyh Al-Jaami’ (118), Swahiyh At-Targhiyb (2228)]

 

8. Anayedhulumiwa ana Ahadi kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kwamba Atamnusuru na kumlipizia dhulma aliyotendewa kwa dalili Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ثَلاَثَةٌ لاَ تُرَدُّ دَعْوَتُهُمْ، الإِمَامُ الْعَادِلُ، وَالصَّائِمُ حَتَّى يُفْطِرَ، وَدَعْوَةُ الْمَظْلُومِ يَرْفَعُهَا اللَّهُ دُونَ الْغَمَامِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَتُفْتَحُ لَهَا أَبْوَابُ السَّمَاء، وَيَقُولُ بِعِزَّتِي لأَنْصُرَنَّكِ وَلَوْ بَعْدَ حِينٍ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah  (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: (([Watu] Watatu hazirudishwi du'aa zao; Imaam muadilifu, mwenye Swawm mpaka afuturu, na du'aa ya aliyedhulumiwa, Anainyanyua Allaah bila ya mawingu Siku ya Qiyaamah na inafunguliwa milango ya mbingu na Anasema: “Kwa Utukufu Wangu, Nitakunusuru japo baada ya muda”.)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (2526) Ibn Maajah, Ahmad]

 

 

 

9. Anayedhulumiwa avute subira kwa kutegemea kulipwa Aakhirah, thawabu za ‘amali njema kutoka kwa   aliyemdhulumu na pia madhambi yake kubebeshwa huyo mtu aliyemdhulumu.

 

 

10. Kwa jinsi dhulma ilivyokuwa inachukiwa na Allaah (سبحانه وتعالى), Ameiharamisha hata kuwatendea watu mafasiki wenye dhambi n ahata makafiri:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((دَعْوَةُ الْمَظْلُومِ مُسْتَجَابَةٌ وَإِنْ كَانَ فَاجِرًا فَفُجُورُهُ عَلَى نَفْسِهِ))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah Radhwiya ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Du’aa ya aliyedhulumiwa (dhidi ya aliyemdhulumu) ni yenye kuitikiwa japo akiwa ni mtendaji dhambi kwani dhambi zake ni dhidi ya nafsi yake.)) [Ahmad, Swahiyh At-Targhiyb (2229), Swahiyh Al-Jaami’ (3382)]

 

عَنْ أنس رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: اتَّقُوا دَعْوَةَ الْمَظْلُومِ وَإِنْ كَانَ كَافِرًا فَإِنَّهُ لَيْسَ دُونَهَا حِجَابٌ

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (رضي الله عنه)  kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Ogopeni du’aa ya aliyedhulumiwa hata akiwa ni kafiri, kwani haina baina yake kizuizi.)) [Ameisahihisha Al-Albaaniyn katika Swahiyh At-Targhiyb (2231)

 

Share

020-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Waumini Ni Kama Jengo Hutiliana Nguvu

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 20

 Waumini Ni Kama Jengo Hutiliana Nguvu

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي مُوسَى (رضي الله عنه) قال: قال رَسُولُ الله (صلى الله عليه و آله وسلم): ((الْمُؤْمِنَ لِلْمُؤْمِنِ كَالْبُنْيَانِ يَشُدُّ بَعْضُهُ بَعْضاً)) وَشَبَّكَ أَصَابِعَهُ - متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Muwsa (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin kwa Muumin mwenziwe ni kama jengo, baadhi yake hutilia nguvu baadhi nyingine)) Akaviumanisha vidole vyake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Waumini wa kweli ni wenye kuungana katika kila jambo lao. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ

Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki wandani wao kwa wao  [At-Tawbah (9: 71)]

 

 

2. Waumini ni ndugu, hivyo inawapasa kutilia nguvu umoja wao. Rejea: [Aal-‘Imraan (3: 200).

 

 

3. Umoja unatia nguvu kama jengo linavyokuwa imara, na hakuna faida kutengana, kwani jengo halitokuwa na faida pindi linapokosa kushikana. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى)

 

 إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الَّذِينَ يُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِهِ صَفًّا كَأَنَّهُم بُنْيَانٌ مَّرْصُوصٌ﴿٤﴾

Hakika Allaah Anapenda wale wanaopigana katika njia Yake safusafu kama kwamba wao ni jengo lililoshikamana barabara. [Asw-Swaff: 4]

 

 

 

4. Umoja unasababisha mapenzi baina ya Waislamu na kupendeleana kheri za kila aina.

 

Rejea Hadiyth namba (21), (22), (23, (42), (43).

 

 

Na kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم):

“Mfano wa Waumini katika kupendana na kurehemeana kwao na kuhurumiana kwao ni sawa na mwili mmoja, kikishtakia kiungo kimoja basi mwili mzima utakosa usingizi na kushikwa na homa” [Al-Bukhaariy].

 

 

5. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni mwalimu bora kabisa kwa kutoa mifano mizuri ya hikma na busara katika kuonyesha au kuelezea jambo.

 

Rejea: Al-Ahzaab (33: 21).

 

 

6. Ni mbinu nzuri ya Da‘wah au ufundishaji kwa Daa‘iyyah (mlinganiaji) au mwalimu kwa kuonyesha kitu kwa vitendo. Na kufanya hivyo kunamfanya msikilizaji kuelewa na kufahamu zaidi

 

Share

021-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kumpendelea Kheri Ndugu Yako Muislamu Kama Unavyojipendelea Nafsi Yako

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 21 

Kumpendelea Kheri Ndugu Yako Muislamu Kama Unavyojipendelea Nafsi Yako

www.alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَنَسٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ: ((لاَ يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى يُحِبَّ لإِخِيهِ مَا يُحِبُّ لِنَفْسِهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه)   kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hatoamini mmoja wenu mpaka ampendelee nduguye anayojipendelea nafsi yake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu unasisitiza Waumini kupendana na kuungana, na unapendelea ummah uwe mmoja wenye nguvu.

Rejea: Aal-‘Imraan (3: 200).

 

 

 

2. Iymaan zinatofautiana kwa daraja, Waumini wengineo iymaan zao ni kubwa kabisa kiasi cha kumpendelea mwenziwe anayojipendelea nafsi yake. Nayo si sifa nyepesi kuimiliki. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):   

 

 لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٩٢﴾

Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda. Na kitu chochote mnachotoa basi hakika Allaah kwacho ni Mjuzi. [Aal-’Imraan 92]

 

 

3. Waumini wapendeleane kheri daima, wakirimiane na waoneane huruma. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):  

 

مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّـهِ ۚ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ ۖ  

Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ni Rasuli wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi dhidi ya makafiri; wanahurumiana baina yao. [Muhammad: 29] 

 

 

 

4. Muumin daima awe ni mwenye kumnufaisha mwenziwe na jambo lao liwe moja katika kumtii Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Rejea: At-Tawbah (9: 71).

 

Rejea pia Hadiyth namba   (22), (23).

 

 

5. Muumin ayachukie maovu kumfikia mwenziwe kama anavyochukia kumfikia mwenyewe.

 

 

6. Muumin asiwe na sifa ya uchoyo, bali ajikhini nafsi yake kwa ajili ya nduguye. Kisa cha familia ya Abuu Twalha Al-Answaariy na mkewe Ummu Sulaym (رضي الله عنهما)  ambacho ni sababu ya kuteremshwa Aayah ya Suwrah Al-Hashr (59: 9).

 

  عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، ‏.‏ أَنَّ رَجُلاً، مِنَ الأَنْصَارِ بَاتَ بِهِ ضَيْفٌ فَلَمْ يَكُنْ عِنْدَهُ إِلاَّ قُوتُهُ وَقُوتُ صِبْيَانِهِ فَقَالَ لاِمْرَأَتِهِ نَوِّمِي الصِّبْيَةَ وَأَطْفِئِي السِّرَاجَ وَقَرِّبِي لِلضَّيْفِ مَا عِنْدَكِ - قَالَ - فَنَزَلَتْ هَذِهِ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba mtu alilala usiku kama mgeni kwa mtu mmoja katika Answaariy ambaye hakuwa na chakula isipokuwa chakula cha watoto wake akamwambia mkewe: “Laza watoto na zima taa karibisha wageni kwa (chakula) ulichonacho.” Ikateremka kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى): 

 

  وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ﴿٩﴾

 …na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji. Na yeyote anayeepushwa na ubakhili na tamaa ya uchu wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu. [Al-Hashr: 9]

 

 

7. Sifa ya kumpendelea mwenzio imesawazishwa na iymaan kwa maana kuwa ikiwa Muislamu hatompendelea nduguye anachokipendelea yeye, basi iymaan yake itakuwa na utata.

 

 

Share

022-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuhifadhi Undugu Wa Kiislamu, Haki, Heshima, Kutokufanyiana Uadui, Chuki Na Kudharauliana

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 22

 

Kuhifadhi Undugu Wa Kiislamu, Haki, Heshima,

Kutokufanyiana Uadui, Chuki Na Kudharauliana

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّه (صلى الله عليه و آله وسلم)  ((لاَ تَحَاسَدُوا وَلاَ تَنَاجَشُوا  وَلاَ تَبَاغَضُوا  وَلاَ تَدَابَرُوا  ولاَ يَبِعْ بَعْضُكُمْ عَلَى بَيْعِ بَعْضٍ، وَكُونُوا عِبَادَ اللَّهِ إِخْوَانًا. الْمُسْلِمُ أَخُو الْمُسْلِمِ لاَ يَظْلِمُهُ وَلاَ يَخْذُلُهُ وَلاَ يكذبه ولاَ يَحْقِرُهُ. التَّقْوَى هَاهُنَا)) وَيُشِيرُ إِلَى صَدْرِهِ ثَلاَثَ مَرَّاتٍ  ((بِحَسْبِ امْرِئٍ مِنْ الشَّرِّ أَنْ يَحْقِرَ أَخَاهُ الْمُسْلِمَ. كُلُّ الْمُسْلِمِ عَلَى الْمُسْلِمِ حَرَامٌ دَمُهُ وَمَالُهُ وَعِرْضُهُ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesema:  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msihusudiane, wala msipandishiane bei wala msibughudhiane, wala msikatane, wala msiingie katika biashara waliyokwishaingia wenzenu, nyote kuweni ni waja wa Allaah ndugu moja.  Muislamu ni ndugu wa Muislamu, hamdhulumu, wala haachi kumsaidia, wala hamdanganyi, wala hamdharau. Taqwa ipo hapa)) Akaashiria kifuani mwake mara tatu. ((Yatosha kuwa shari mtu kumdharau nduguye Muislamu. Kila Muislamu juu ya Muislamu mwenziwe ni haraam damu yake, mali yake, na heshima yake)).[Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu unasisitiza kuchunga haki na heshima baina ya watu, na unatahadharisha kudharauliana.

 

Rejea Hadiyth namba (87), (88), (89), (96) (97), (126).

 Na Allaah (سبحانه وتعالى) Anaonya:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿١١﴾

Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao. Na wala msifedheheshane kwa kutukanana na wala msiitane majina (mabaya) ya utani. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya iymaan. Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu. [Al-Hujuraat (49: 11)]

 

 

 

2. Uislamu unakataza kuudhiana.

 

Rejea: Al-Ahzaab (33: 58) na pia imeharamishwa kutendeana uadui bali imeamrishwa kushirikiana kwa wema. Rejea: Al-Maaidah (5: 2).

 

 

3. Waislamu wote ni ndugu Rejea: Al-Hujuraat: (49: 10).

 

 

4. Uhasidi, bughudha na chuki, ni miongoni mwa maradhi ya moyo yanayomhatarisha Muislamu siku ya Qiyaamah kufika mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) akiwa na moyo usiosalimika na ndio maana Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema katika Hadiyth hiyo ya maudhui: “Taqwa ipo hapa.” (akiashiria moyo mara tatu). Na Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 

 

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

 “Siku hayatofaa mali wa watoto.

 

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

 “Isipokuwa yule atakayemfikia Allaah na moyo uliosalimika. [Ash-Shu’araa (26: 88-89)]

 

 

 

5. Uislamu unasisitiza kuungana si kutengana au kukatana undugu.

Rejea:  Muhammad (47: 22-23).

 

 

6. Kuuana ni miongoni mwa madhambi makubwa, nayo yanahusiana na haki ya mtu. 

Rejea: An-Nisaa: (92-93).

 

 

7. Taqwa ipo moyoni, na inadhihirishwa kwa vitendo vyake, kukhofu kutenda uovu au kutenda mema.

 

 

8. Muislamu anafaa achunge sana asije kuingia katika haraam kwa kuvunja heshima ya nduguye, kumwaga damu yake au kula mali yake.

 

 

9. Hii ni Hadiyth ‘adhimu yenye kutufunza mahusiano mema na maingiliano mazuri baina ya Waislamu wao kwa wao na wana Aadam wote.

 

 

 

 

 

 

Share

023-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Atakayemtimizia Haja Nduguye Na Kumsitiri Atapata Faraja Na Sitara Siku Ya Qiyaama

 Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 23

 Atakayemtimizia Haja Nduguye Na Kumsitiri Atapata Faraja Na Sitara Siku Ya Qiyaama

 

www.alhidaaya.com

 

 عن ابْنَ عُمَرَ (رضي الله عنهما)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ: ((الْمُسْلِمُ أَخُو الْمُسْلِمِ لاَ يَظْلِمُهُ ولاَ يُسْلِمُهُ، وَمَنْ كَانَ فِي حَاجَةِ أَخِيهِ كَانَ اللَّهُ فِي حَاجَتِهِ، وَمَنْ فَرَّجَ عَنْ مُسْلِمٍ كُرْبَةً فَرَّجَ اللَّهُ عَنْهُ كُرْبَةً مِنْ كُرُبَاتِ يَوْمِ الْقِيَامَةِ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِمًا سَتَرَهُ اللَّهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)  kwamba Rasuli  wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muislamu ni ndugu wa Muislamu, hamdhulumu wala hamsalimishi [kwa adui]. Na atakayemtimizia haja nduguye, Allaah Atamtimizia haja yake. Na atakayemfariji [atakayemuondoshea] Muislamu dhiki yake, Allaah Atampa faraja ya dhiki zake Siku ya Qiyaamah. Na atakayemsitiri Muislamu mwenzake [aibu zake], Allaah Atamsitiri [aibu zake] Siku ya Qiyaamah)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Waislamu ni ndugu wanapasa kutendeana mema. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠﴾

Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa. [Al-Hujuraat: 10]

 

Pia rejea: Al-Maaidah (5: 2).

Rejea pia Hadiyth namba (20), (21).

 

 

 

2. Uislamu unakataza kufanyiana dhulma.

 

Rejea Hadiyth namba (19).

 

Pia Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema katika Hadiyth Qudsiy: ((Enyi waja Wangu! Mimi Nimejiharamishia dhuluma juu ya Nafsi Yangu na Nikaifanya ni haramu baina yenu basi msidhulumiane)). [Muslim]

 

 

3. Waislamu wanapasa kusaidiana dhidi ya adui.

 

 

4. Himizo la kusaidiana wakati wa dhiki na shida.

 

 

5. Himizo la kusitiriana aibu na onyo kali la kuieneza aibu, kashfa, uzushi n.k. kwa wengineo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿١٩﴾

Hakika wale wanaopenda uenee uchafu wa kashfa kwa wale walioamini; watapata adhabu iumizayo duniani na Aakhirah. Na Allaah Anajua nanyi hamjui [An-Nuwr (24: 19)]

         

 

6. Malipo ya Aakhirah ni makubwa zaidi kuliko ya duniani. Rejea An-Nahl (16: 41).

 

 

7. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuwalipa waja wanapotendeana wema.  

 

 

8. Muislamu akhiari kumwondoshea dhiki nduguye duniani apate kuondoshewa dhiki Siku ya Qiyaamah, kwani huko ndiko kwenye dhiki na shida kubwa zaidi.

 

Rejea: Al-Hajj (22: 1-2).

 

 

Share

024-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Uongo Unaruhusiwa Katika Kupatanisha Waliogombana Na Vitani

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 24:

Uongo Unaruhusiwa Katika Kupatanisha Waliogombana Na Vitani

www.alhidaaya.com

 

 عَنْ أُمَّ كُلْثُومٍ بِنْتَ عُقْبَةَ (رضي الله عنها) قَالَتْ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم) يَقُولُ: ((لَيْسَ الْكَذَّابُ الَّذِي يُصْلِحُ بَيْنَ النَّاسِ فَيَنْمِي خَيْرًا)) متفق عليه.

 وفي رواية مسلم زيادة  قَالَتْ: وَلَمْ أَسْمَعْهُ يُرَخِّصُ فِي شَيْءٍ مِمَّا يَقُولُ النَّاسُ إلاَّ فِي ثَلاَثٍ: تَعْنِي الْحَرْبَ، والإصْلاَحَ بَيْنَ النَّاس، وَحَدِيثَ الرَّجُلِ امْرَأَتَهُ وَحَدِيث الْمَرْأَةِ زَوْجَهَا

 

Imepokelewa kutoka kwa Ummu Kulthuum bint ‘Uqbah (رضي الله عنها) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Hajasema uongo yule mwenye kusuluhisha baina ya watu akawa anasambaza [habari ya] kheri, au anasema kheri)). [Al-Bukhaariy, Muslim]  

 

Na katika riwaayah ya Muslim kuna ziada inayosema: Akasema “Wala sikumsikia akiruhusu chochote katika uongo wanaosema watu isipokuwa katika mambo matatu.” Yaani katika vita, kusuluhisha baina ya watu, mwanamume kuzungumza na mkewe na mke kuzungumza na mumewe.”

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu umeharamisha kusema uongo isipokuwa katika hali tatu zilizotajwa.

 

Rejea Hadiyth namba (86).

 

 

2.  Umuhimu wa kuweko amani baina ya jamii ya Kiislamu kiasi kwamba kusema uongo ambao ni dhambi kubwa umehalalishwa kwayo.

Rejea Hadiyth namba (94).

 

 

3.  Fadhila za kusuluhisha waliokhasimikiana ni kubwa mno. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّا خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿١١٤﴾

Hakuna khayr katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha swadaqah, au mema, au kusuluhisha baina ya watu. Na atakayefanya hivyo kutaka radhi za Allaah, basi Tutampa ujira adhimu. [An-Nisaa (4: 114)]

 

 

4. Umuhimu wa mapatano na amani baina ya mke na mume na jamii kwa ujumla Rejea: An-Nisaa (4: 128), Al-Anfaal (8: 1) Al-Hujuraat (49: 10).

 

Rejea pia Hadiyth namba (29),

 

 

5. Uislamu ni Dini ya amani, na kuamkiana kwa maamkizi ya Kiislamu ni sababu mojawapo ya kuleta amani na kumwingiza Muislamu Peponi. Rejea Hadiyth namba (42), (72).

.

Share

025-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Wanyonge Na Masikini Watakuwa Jannah, Ama Wababe Wajeuri Na Wenye Kiburi Watakuwa Motoni

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 25

Wanyonge Na Masikini Watakuwa Jannah,

Ama Wababe Wajeuri Na Wenye Kiburi Watakuwa Motoni

www.alhidaaya.com

 

 

 

 

 

 

 عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((احْتَجَّتْ الْجَنَّةُ وَالنَّارُ فَقَالَتْ النَّارُ: فِيَّ الْجَبَّارُونَ وَالْمُتَكَبِّرُونَ.  وَقَالَتْ الْجَنَّةُ: فِيَّ ضُعَفَاءُ النَّاسِ وَمَسَاكِينُهُمْ: فَقَضَى الله بَيْنَهُمَا: إِنَّكِ الْجَنَّةُ رَحْمَتِي أَرْحَمُ بِكِ مَنْ أَشَاءُ.  وَإِنَّكِ النَّارُ عَذَابِي أُعَذِّبُ بِكِ مَنْ أَشَاءُ.  وَلِكِلَاكُمَا عَلَيَّ مِلْؤُهَا)) رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy(رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jannah na moto zilihojiana. Moto ukasema: Kwangu kunapatikana wababe wajeuri na wenye kiburi.  Jannah ikasema: Kwangu kunapatikana watu madhaifu na masikini wao.  Allaah Akahukumu baina yao (Akisema): Wewe Jannah ni Rahma Yangu, Nitamrehemu kwa sababu yako Nimtakaye. Na wewe moto ni adhabu Yangu, Nitamwadhibu Nimtakaye kwa sababu yako, na nyote Nitawajaza)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Allaah (سبحانه وتعالى) Anawaacha watu wawe huru kutenda wayatakayo baada ya kuwaonyesha njia ya haki na ya ubatilifu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴿٢﴾ إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا ﴿٣﴾

 

Hakika Sisi Tumemuumba bin-Aadam kutokana na tone la manii iliyochanganyika ili Tumjaribu; Tukamjaalia mwenye kusikia na kuona. Hakika Sisi Tumemuongoza njia; ima awe mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.   [Al-Insaan (67: 2-3)]

 

Rejea pia: Al-Balad (90: 8-10).

 

 

2. Hikma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuwajaalia baadhi ya watu kuwa ni masikini, wanyonge na wengineo kuwa ni matajiri wenye nguvu.

 

Rejea: An-Nahl (16: 71).  

 

Hata Manabii wamefadhilishwa wengine juu ya wengine kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

تِلْكَ الرُّسُلُ فَضَّلْنَا بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ ۘ مِّنْهُم مَّن كَلَّمَ اللَّـهُ ۖ وَرَفَعَ بَعْضَهُمْ دَرَجَاتٍ ۚ وَآتَيْنَا عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ الْبَيِّنَاتِ وَأَيَّدْنَاهُ بِرُوحِ الْقُدُسِ ۗ

Hao ni Rusuli, Tumewafadhilisha baadhi yao juu ya baadhi. Miongoni mwao kuna aliyesemeshwa na Allaah, na Akawapandisha baadhi yao vyeo. Na Tukampa ‘Iysaa mwana wa Maryam hoja bayana na Tukamtia nguvu kwa Ruwhil-Qudus (Jibriyl (عليه السلام.   [Al-Baqarah 2: 253].

 

 

 

3. Ujuzi wa Allaah (سبحانه وتعالى) kwamba baadhi ya waja Wake watakuwa ni wema japokuwa wao ni dhaifu, maskini na wanyonge, na hivyo hatima yao itakuwa ni kuingia Jannah. Na wengineo watakuwa wenye kutakabari na wababe wajeuri juu ya kuwa ni matajiri, hivyo hatima yao itakuwa ni kuingia motoni.   [Hadiyth: ((Wataingia Jannah Waislamu masikini kabla ya matajiri wao kwa nusu siku ambayo ni miaka 500)). [Swahiyh At-Tirmidhiy ya Al-Albaaniy]

 

 

4. Bishara njema ya Jannah kwa walio wanyonge duniani, na tisho la moto kwa wenye kutakabari na wababe wajeuri.

Rejea Hadiyth namba (55), (59), 60).

 

 

5. Hadiyth hii inatufunza kuwa kufaulu Aakhirah hakutegemei uwezo wa kifedha hapa duniani.

 

Share

026-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kulea Watoto Wa Kike Ni Kuwa Pamoja na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Peponi

 Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 26

Kulea Watoto Wa Kike Ni Kuwa Karibu Na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Peponi

www.alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ  (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((مَنْ عَالَ جَارِيَتَيْنِ حَتَّى تَبْلُغَا جَاءَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَنَا وَهُوَ كَهَاتَيْنِ)) وَضَمَّ أَصَابِعَهُ. رواه مسلم  

 

 Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayewasimamia kuwalea mabinti wawili mpaka wabaleghe, atakuja Siku ya Qiyaamah mimi na yeye ni kama hivi)), Akavishikanisha vidole vyake. [Muslim]

 

  

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila za kulea watoto wa kike ambao walikuwa wakidhalilishwa zama za ujaahiliyyah mpaka kufikia kuzikwa wangali hai. Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema kuwa wataulizwa kuhusu kuuliwa kwao:

 

 

وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ ﴿٨﴾

Na mtoto wa kike aliyezikwa hali akiwa yuhai atakapoulizwa.

 

بِأَيِّ ذَنبٍ قُتِلَتْ ﴿٩﴾

Kwa dhambi gani aliuliwa? [At-Takwir: 8-9]

 

 

2. Hoja kwa makafiri wanaozusha kwamba mwanamke wa Kiislamu hana haki wala hadhi. Bali Uislamu umemnyanyua mwanamke cheo chake na kumpatia hadhi kubwa. Hadiyth ifuatayo ni dalili mojawapo ya haya:

 

Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) na akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Ni nani miongoni mwa watu anayestahiki kwamba nimfanyie wema zaidi?” Akasema (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Mama yako.)) Yule mtu akasema: “Kisha nani?” Aksema: ((Mama yako.)) Akauliza tena yule mtu: “Kisha nani?” Akasema: ((Mama yako)). Yule mtu akauliza kwa mara nyingine: “Kisha nani?” Akasema: ((Baba yako) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Bali wanawake wamefadhilishwa mno kama ifuatavyo:

 

 

a) Allaah (سبحانه وتعالى) Ametanguliza kumtaja mwanamke kabla ya kumtaja mwanamume tokea akiwa tumboni kabla ya kuzaliwa kwao. Anasema:

 

لِّلَّـهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ ۚ يَهَبُ لِمَن يَشَاءُ إِنَاثًا وَيَهَبُ لِمَن يَشَاءُ الذُّكُورَ﴿٤٩﴾      

Ni wa Allaah Pekee ufalme wa mbingu na ardhi. Anaumba Atakavyo. Humtunukia Amtakaye wana wa kike, na Humtunukia Amtakaye wana wa kiume.

 

 

أَوْ يُزَوِّجُهُمْ ذُكْرَانًا وَإِنَاثًا ۖ وَيَجْعَلُ مَن يَشَاءُ عَقِيمًا ۚ إِنَّهُ عَلِيمٌ قَدِيرٌ﴿٥٠﴾

Au Huwachanganya wa  kiume na wa kike, na Humjaalia Amtakaye kuwa ni tasa, hakika Yeye ni Mjuzi wa yote, Muweza wa yote. [Ash-Shuwraa (42: 49-50)]

 

 

b) Haajar mama yake Nabiy Ismaa’iyl (عليه السلام) amefadhilishwa kuwa ni sababu ya Umati wa Kiislamu kutekeleza ‘ibaadah ya Sa’y – kutembea baina ya Swafaa na Marwah.

 

 

c) Aayah na Hadiyth kadhaa zimetaja haki za mwanamke. Rejea Hadiyth namba (29), (35), (40).

 

 

 

3. Kulea watoto wa kike malezi mema ya mafunzo ya Dini ni sababu ya mzazi kuingia Jannah. 

 

 

4. Sababu mojawapo ya kumjaalia mtu kuwa karibu na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) huko Jannah ni kuwalea mabinti malezi mazuri.

 

 

5. Ukarimu na upole wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa watoto na wazazi [At-Tawbah (9: 128)].

 

 

6. Muislamu anatakiwa awe mwadilifu kwa watoto wake katika malezi bila kubagua wavulana au wasichana.

 

 

7. Hii inaonyesha fadhila kubwa ya wasichana katika jamii ya Kiislamu. Ndio maana ikasemwa:  “Kumlea vyema msichana ni kutengeneza jamii.”

 

 

Share

027-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kila Mtu Ana Jukumu La Kuchunga Atakaloulizwa

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 27

Kila Mtu Ana Jukumu La Kuchunga Atakaloulizwa

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ ابْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ:  ((كُلُّكُمْ رَاعٍ وَكُلُّكُمْ مَسْئُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ،  وَالأمِيرُ رَاعٍ،  وَالرَّجُلُ رَاعٍ عَلَى أَهْلِ بَيْتِهِ، وَالْمَرْأَةُ رَاعِيَةٌ عَلَى بَيْتِ زَوْجِهَا وَوَلَدِهِ، فَكُلُّكُمْ رَاعٍ وَكُلُّكُمْ مَسْئُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ)) متفق  عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله  عنهما)   kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Nyote ni wachunga na kila mmoja wenu ataulizwa kuhusu alichokichunga. Kiongozi ni mchunga, na mume ni mchunga juu ya mkewe na mke ni mchunga juu ya nyumba ya mumewe na watoto wake. Kwa hivyo nyote ni wachunga na kila mmoja wenu ataulizwa kuhusu alichokichunga)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Kila Muislamu analo jukumu lake ambalo ni limekuwa ni amana kwake kuichunga. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّا عَرَضْنَا الْأَمَانَةَ عَلَى السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَالْجِبَالِ فَأَبَيْنَ أَن يَحْمِلْنَهَا وَأَشْفَقْنَ مِنْهَا وَحَمَلَهَا الْإِنسَانُ ۖ إِنَّهُ كَانَ ظَلُومًا جَهُولًا ﴿٧٢﴾

Hakika Sisi Tulihudhurisha amana kwa mbingu na ardhi na majabali vikakataa kuibeba na vikaiogopa; lakini insani akaibeba. Hakika yeye amekuwa dhalimu mno, jahili mno. [Al-Ahzaab (33: 72)]

 

 

 

2. Jukumu ni amana na kila Alitochuruzuku Allaah (سبحانه وتعالى) ni neema kwetu, ikiwa ni mali au mke, au mume, au watoto, au elimu, na kila mmoja ataulizwa kuhusu neema hizo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ ﴿٨﴾

Kisha bila shaka mtaulizwa Siku hiyo kuhusu kuhusu neema. [At-Takaathur: 8]

 

 

 

3. Kutimiza amana ni miongoni mwa sifa zitakazompatia Muislamu Jannah ya Firdaws kama zilivyotajwa katika Suwrah: Al-Muuminuwn (23: 1-11)  

 

 

4. Mume na mke washirikiane katika malezi ya watoto ili watoto wakuwe na kuinukia katika maadili mazuri ya Kiislamu.

 

 

5. Mwanamke wa Kiislamu ana cheo kikubwa kwa kuwa ana jukumu kubwa la ulezi wa nyumba yake, na ameahidiwa kupata Jannah.

 

Rejea Hadiyth namba (26).

 

 

6. Kutimizia amana au jukumu ni jambo mojawapo la kumwezesha mtu kuvuka As-Swiraatw Siku ya Qiyaamah

 

Hadiyth: ((...na zitatumwa amana na ar-rahm [fuko la uzazi; uungaji udugu], navyo vitasimama pembeni ya Swiraatw kuliani na kushotoni…..))].[Muslim]

 

 

 

 

Share

028-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuvumiliana Tabia Mbaya Katika Maisha Ya Ndoa Kwa Kukumbuka Tabia Zilizo Nzuri

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 28

Kuvumiliana Tabia Mbaya Katika Maisha Ya Ndoa Kwa Kukumbuka Tabia Zilizo Nzuri

www.alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ يَفْرَكْ مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَةً إِنْ كَرِهَ مِنْهَا خُلُقًا رَضِيَ مِنْهَا آخَرَ))  مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin [mume] asimchukie Muumin [mke]. Asipompendelea kwa tabia fulani ataridhika naye kwa tabia nyingine)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hakuna binaadamu aliyekamilika kwa tabia njema. Kila mmoja ana kasoro zake; huenda zikawa ni tabia zinazolingana; nzuri au mbaya. 

 

 

2. Kuishi pamoja kunadhihirisha tabia baina ya watu.

 

 

3. Inapasa kuvumiliana katika maisha ya ndoa, kwani kila mmoja ni mtihani kwa mwenziwe. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَجَعَلْنَا بَعْضَكُمْ لِبَعْضٍ فِتْنَةً أَتَصْبِرُونَ ۗ وَكَانَ رَبُّكَ بَصِيرًا ﴿٢٠﴾

Na Tumejaalia baadhi yenu nyinyi kwa nyinyi kuwa ni majaribio je mtasubiri? Na Rabb wako ni Mwenye kuona daima. [Al-Furqaan: 20]

 

 

4. Uislamu unamsisitiza mume kumfanyia wema mke.

 

Rejea: An-Nisaa (4: 19).

 

Rejea pia Hadiyth namba (29).

 

 

5. Hadiyth hii ni suluhisho mojawapo la kutatua matatizo baina ya mume na mkewe.

 

Rejea An-Nisaa (4: 128).

 

 

6. Inasisitizwa Muislamu kuchagua mke mwema, kwani ndio sababu ya furaha yake duniani na Aakhirah.

 

Rejea Hadiyth namba (35), (40).

 

 

7. Hii Hadiyth inamtaka mume awe makini wala asichukue hatua za haraka kama talaka ambayo huenda ikamletea majuto.

 

Share

029-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Aliyekamilika Iymaan Kwa Tabia Na Kumfanyia Wema Mke

 

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 29

 

Aliyekamilika Iymaan Kwa Tabia Na Kumfanyia Wema Mke

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((أَكْمَلُ الْمُؤْمِنِينَ إِيمَانًا أَحْسَنُهُمْ خُلُقًا  وَخِيَارُكُمْ خِيَارُكُمْ لِنِسَائِهِمْ خُلُقًا)) الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin aliyekamilika iymaan ni aliye na tabia njema kabisa, na wabora wenu ni walio bora kwa wake zao kwa tabia))  [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Swahiyh Hasan]

 

 

 

Mafunzo na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu unasisitiza kuwa na tabia njema kwa kila mtu.

 

 

 

2. Mume anasisitizwa kumfanyia wema mkewe katika maisha ya ndoa, si kumfanyia uovu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَلَا تَنسَوُا الْفَضْلَ بَيْنَكُمْ ۚ   

  Na wala msisahau fadhila baina yenu.  [Al-Baqarah (2: 237)]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

  وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ  

Na kaeni nao kwa wema. [An-Nisaa (4: 19)]

 

 

Pia rejea kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى): [Ar-Ruwm 30: 21]

 

 

3. Inapasa kuweko subira baina ya mume na mke katika mitihani inayowakabili ya maisha baina yao. [((Na mkisubiri ni kheri kwenu)) [An-Nisaa (4: 25)].

 

 

 

4. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni kigezo bora kabisa katika kuamiliana na wake [Al-Ahzaab (33: 21)].

 

Pia Hadiyth zifuatazo:

 

 

 ((Mbora wenu ni yule aliye mbora kwa mke wake, na mimi ni mbora kwa watu wangu wa nyumbani [ahli])) [Ibn Maajah na Ad-Daarimiy].

 

 

((Mwanamke ameumbwa kwa ubavu, na sehemu iliyopinda ya ubavu ni juu yake, ukijaribu kuunyoosha utauvunja, na lau utauacha utaendelea kupinda, nakuusieni [kuwafanyia wema]) wake zenu)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

((Allaah, Allaah, kwa wanawake,  hao ni wasaidizi wenu walio kwenye mikono yenu, mmewachukuwa kama ni amana kutoka kwa Allaah, na imekuwa halali tupu zao kwenu kwa neno lake Allaah  [iyjaab na qubuwl])) [Muslim, Abu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad]

 

Rejea pia Hadiyth namba (28), (35), (40).

 

 

Share

030-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mwanamke Asifunge Swawm Au Kumuingiza Mtu Kwenye Nyumba Bila Ya Idhini Ya Mumewe

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 30

Mwanamke Asifunge (Swawm)

Au Kumuingiza Mtu Kwenye Nyumba Bila Ya Idhini Ya Mumewe

 Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَحِلُّ لِلْمَرْأَةِ أَنْ تَصُومَ وَزَوْجُهَا شَاهِدٌ إلاَّ بِإِذْنِهِ. وَلاَ تَأْذَنَ فِي بَيْتِهِ إلاَّ بِإِذْنِهِ)) متفق عليه وهذا لفظ البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Si halali kwa mwanamke kufunga Swawm [ya Sunnah] ilhali mumewe yupo [hakusafiri] ila kwa idhini yake. Wala asimruhusu mtu kuingia nyumbani kwake ila kwa idhini yake)). [Al-Bukhaariy na Muslim kwa lafdhi ya Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo na Mwongozo:

 

 

 

1. Mwanamke hatakiwi kufunga Swawm ya Sunnah yoyote ila kwanza apate ruhusu ya mumewe, kwani huenda akawa anamhitajia kwa kitendo cha ndoa.

 

2. Mwanamke hapasi kumuingiza mtu yeyote nyumbani kwake bila ya ruhusa ya mumewe. Akumbuke kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ ۚ﴿٣٤﴾

Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi [An-Nisaa (4: 34)]

 

 

3. ‘Ibaadah za Sunnah zinashinda haki ya bin Aadam.

 

 

4. Mke kufuata Shariy’ah kama hii itamzuia mume kufanya zinaa.

 

 

5. Umuhimu wa kuhifadhi haki baina ya mke na mume. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَهُنَّ مِثْلُ الَّذِي عَلَيْهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ وَلِلرِّجَالِ عَلَيْهِنَّ دَرَجَةٌ ۗ

Nao wake wana haki kama ambayo (ya waume zao) iliyo juu yao kwa mujibu wa shariy’ah. Na wanaume wana daraja zaidi juu yao [Al-Baqarah (2: 228)]

 

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:

 

((لو كنتُ آمرًا أحدًا أن يسجدَ لغيرِ اللهِ ، لأمرتُ المرأةَ أن تسجدَ لزوجِها، و الذي نفسُ محمدٍ بيدِه ، لا تؤدِّي المرأةُ حقَّ ربِّها، حتى تؤدِّيَ حقَّ زوجِها كلَّه، حتى لو سألها نفسَها و هي على قَتَبٍ لم تمنَعْه))

 

((Ningeliweza kumuamrisha mtu amsujudie asiyekuwa Allaah,  ningelimuamrisha mke amsujudie mume wake. Naapa kwa Ambaye nafsi ya Muhummad imo Mikononi Mwake, mwanamke hatotimiza  haki za Rabb Wake mpaka atimize haki zote za mumewe. Akimtaka (kujamii naye) hata kama yuko katika kipando cha ngamia, basi asimkatalie)) [Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Abiy Awfaa - Sunan Ibn Maajah na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Ibn Maajah (1515), Swahiyh Al-Jaami’ (5295)

 

Rejea pia Hadiyth namba (29), (128),

 

 

6. Umuhimu wa kujilinda na maasi kwa jinsi ya kwamba hata ‘ibaadah ya Sunnah kama hiyo ya Swawm haitakiwi kutekelezwa juu ya kwamba ni ‘ibaadah yenye malipo makubwa kabisa ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) Amesema kuwa ‘ibaadah hii ni kwa ajili Yake na kwamba Yeye Ndiye Atakayemlipa mja kama ilivyotajwa katika Hadiyth:  ((Kila ‘amali njema ya mwana Aadam inalipwa mara kumi na inaongezewa thawabu kutoka kumi hadi mia saba, na Allaah Anasema isipokuwa Swawm, kwani hiyo ni kwa ajili Yangu na Mimi Ndiye Nitakayemlipa))]. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

7. Mke kufuata amri ya kutokumuingiza mtu yeyote yule nyumbani kwake. Na kufanya hivyo kutazuia fitna na hatari ya maasi ya zinaa.  

 

 

8. Utekelezaji wa Uislamu ni nidhamu kamili ya maisha hata katika mas-alah ya nyumba na unyumba. Nidhamu hii ikitofuatwa, basi kunatokea matatizo mengi katika utangamano baina ya mume na mke.

 

 

9. Kila Shariy’ah iliyoletwa na Uislamu ina hikma yake kubwa na hivyo Muislamu mwema na mzuri ni yule mwenye kuzifuata bila ya kuwa na uzito au kuchagua baadhi na kuacha baadhi yake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّـهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ ۗ وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا ﴿٣٦﴾

Na haiwi kwa Muumini mwanamme na wala kwa Muumini mwanamke, Anapohukumu Allaah na Rasuli Wake jambo lolote, iwe wana hiari katika jambo lao.  Na anayemuasi Allaah na Rasuli Wake, basi kwa yakini amepotoka upotofu bayana. [Al-Ahzaab (33: 36)]

 

 

 

Share

031-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Du’aa Ya Malaika Kila Siku Kwa Mtoaji Sadaka Na Mzuiaji

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 31

 

Du’aa Ya Malaika Kila Siku Kwa Mtoaji Sadaka Na Mzuiaji

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا مِنْ يَوْمٍ يُصْبِحُ الْعِبَادُ فِيهِ إلاَّ مَلَكَانِ يَنْزِلاَنِ فَيَقُولُ أَحَدُهُمَا: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُنْفِقًا خَلَفًا. وَيَقُولُ الأَخَرُ: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُمْسِكًا تَلَفًا)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kila siku inayowapambaukia watu kuna Malaika wawili wanateremka, mmoja wao akiomba: Ee Allaah! Mwenye kutoa [sadaka] mlipe zaidi. Na mwengine huomba: Ee Allaah! Mwenye kuzuia mpe hasara)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Inapendekezeka kutoa sadaka kila siku ili kupata du’aa ya Malaika na kukhofu kuombewa hasara. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾

Basi yule anayetoa (mali) na akamcha Allaah.

 

وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾

Na akasadikisha Al-Husnaa.

 

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧﴾

“Basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi”

 

وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾

Ama yule afanyaye ubakhili na akajiona amejitosheleza.  

 

وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾

Na akakadhibisha Al-Husnaa.

 

فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾

Na Tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu.

 

وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ ﴿١١﴾

Na itamsaidia nini mali yake atakapoporomoka kuangamia (motoni).  [Al-Layl (92: 5-11)]

 

 

 

2. Allaah (سبحانه وتعالى) Ametoa ahadi kumwongezea mwenye kutoa mali yake. Rejea: Al-Baqarah (2: 245, 261), Al-Hadiyd (57: 11), Sabaa (34: 39).

 

 

3. Inafaa kumuombea mtoaji sadaka, Allaah (سبحانه وتعالى) Amlipe zaidi kwa alichotoa, na du’aa kwa bakhili anayezuia kutoa katika Njia ya Allaah  (سبحانه وتعالى) hasara panapohitajika.

 

 

4. Sadaka ni katika ‘amali bora kabisa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى), kwani Ameitaja sana katika Qur-aan na hata kwamba Ameitanguliza kabla ya nafsi katika Aayah za Jihaad.

 

Rejea: An-Nisaa (4: 95), At-Tawbah (9: 20, 41, 81), Al-Hujuraat (49: 15), As-Swaff (61: 11).

 

 

5. Fadhila tele za kutoka sadaka katika Qur-aan na Sunnah. Rejea Hadiyth namba (32), (62).

Share

032-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutoa Sadaka Na Kukinai Badala Ya Kuombaomba

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 32

 

Kutoa Sadaka Na Kukinai Badala Ya Kuombaomba

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((الْيَدُ الْعُلْيَا خَيْرٌ مِنْ الْيَدِ السُّفْلَى وَابْدَأْ بِمَنْ تَعُولُ.  وَخَيْرُ الصَّدَقَةِ عَنْ ظَهْرِ غِنًى وَمَنْ يَسْتَعْفِفْ يُعِفَّهُ اللَّهُ وَمَنْ يَسْتَغْنِ يُغْنِهِ اللَّهُ)) البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini. Anza kwa unayemlisha. Sadaka bora ni inayotolewa baada ya kubakisha kitu. Anayejizuia [kutokuomba] Allaah Humtosheleza, na mwenye kukinai Allaah Humkinaisha)) [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu unapendekeza kutoa zaidi kuliko kuombaomba. Allaah (سبحانه وتعالى) Amewasifia aina ya watu kama hao, Anasema:

 

 لِلْفُقَرَاءِ الَّذِينَ أُحْصِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ لَا يَسْتَطِيعُونَ ضَرْبًا فِي الْأَرْضِ يَحْسَبُهُمُ الْجَاهِلُ أَغْنِيَاءَ مِنَ التَّعَفُّفِ تَعْرِفُهُم بِسِيمَاهُمْ لَا يَسْأَلُونَ النَّاسَ إِلْحَافًا ۗ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣﴾

(Swadaqah ni) Kwa ajili ya mafakiri waliozuilika katika njia ya Allaah hawawezi kwenda huku na kule katika ardhi (kutafuta rizki); asiyewajua huwadhania kuwa ni matajiri kutokana na staha ya kujizua kwao, unawatambua kwa alama zao, hawaombi watu kwa ung’ang’anizi. Na chochote mtoacho katika kheri basi Allaah kwacho ni Mjuzi. [Al-Baqarah (2: 273)]

 

 

2. Aina ya mkono na daraja zake katika mas-alah ya sadaka ni nne: (i) Wa juu kabisa ni mtoaji (ii) Unaojizuia kuchukua (iii) Unaochukua bila kuomba (iv) Unaoomba.

 

 

3. Anayejizuia kuomba kitu Allaah (سبحانه وتعالى) Humkidhia na Humuruzuku kukinai.

 

 

4. Kujizuia kuomba ni kutawakali kwa Allaah (سبحانه وتعالى) katika mas-alah ya rizki na ni miongoni mwa sifa za Muumin.

 

Rejea: Al-Anfaal (8: 2), An-Nahl (16: 42) Al-‘Ankabuwt (29: 59), Ash-Shuwraa (42: 36), At-Twalaaq (65: 2-3).

 

 

5. Sadaka bora ni ile anayoitoa mtu katika mali yake baada ya kujitosheleza mwenyewe na ahli zake.

 

 

6. Uislamu umesisitiza kutoa sadaka kwa kuanzia kwa ahli kama ilivyotajwa ((…anza kwa unayemlisha)).  

 

 

7. Fadhila za kutoa sadaka zimetajwa tele katika Qur-aan.

 

Rejea [Al-Baqarah (2: 245, 261), Al-Hadiyd (57: 11), Sabaa (34: 39)].

 

Rejea pia Hadiyth namba (31), (62),   

 

 

 

Share

033-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutaja Jina La Allaah Katika Chakula Na Kula Kilichoko Mbele Yako

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 33

 

Kutaja Jina La Allaah Katika Chakula Na Kula Kilichoko Mbele Yako

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عُمَرَ بْن أَبِي سَلَمَةَ عَبْدُ الله رَبيب رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَال:  كُنْتُ غُلاَمًا فِي حَجْرِ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَكَانَتْ يَدِي تَطِيشُ فِي الصَّحْفَةِ  فَقَالَ لِي رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يَا غُلاَمُ سَمِّ اللَّهَ تَعَالى، وَكُلْ بِيَمِينِكَ،  وَكُلْ مِمَّا يَلِيكَ)) فَمَا زَالَتْ تِلْكَ طِعْمَتِي بَعْدُ. متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Abi Salamah, ambaye ni mwanakambo wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: Nilikuwa kijana mdogo chini ya ulezi wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), na mkono wangu ulikuwa ukizungukazunguka katika sinia (ya chakula). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akaniambia: ((Ee ghulamu! Taja jina la Allaah (Ta’aalaa) na kula kwa mkono wako wa kulia, na ule kilicho mbele yako)). Basi huo ukawa ndio mtindo wangu wa kula baadaye.   [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Mafunzo na Mwongozo:

 

 

1. Kuwajibika kuwafunza watoto kila aina mojawapo wa tabia njema za Kiislamu na kuwatanabahisha makosa yao wanapoanza kuyatenda.

 

 

 

2. Miongoni mwa adabu za kuanza jambo lolote, kama kula chakula ni kuanza kwa ‘BismiLlaah’ (Naanza kwa Jina la Allaah), na kula kwa mkono wa kulia, na kula kilicho mbele ya sahani.

 

 

 3. Ruhusa ya kula pamoja au pekee. Lakini Hadiyth inaashiria kula katika sahani moja ni bora zaidi, na bila shaka inaleta baraka katika chakula. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّيْسَ عَلَى الْأَعْمَىٰ حَرَجٌ وَلَا عَلَى الْأَعْرَجِ حَرَجٌ وَلَا عَلَى الْمَرِيضِ حَرَجٌ وَلَا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَن تَأْكُلُوا مِن بُيُوتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ آبَائِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أُمَّهَاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ إِخْوَانِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَخَوَاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَعْمَامِكُمْ أَوْ بُيُوتِ عَمَّاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَخْوَالِكُمْ أَوْ بُيُوتِ خَالَاتِكُمْ أَوْ مَا مَلَكْتُم مَّفَاتِحَهُ أَوْ صَدِيقِكُمْ ۚ لَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَأْكُلُوا جَمِيعًا أَوْ أَشْتَاتًا ۚ فَإِذَا دَخَلْتُم بُيُوتًا فَسَلِّمُوا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ تَحِيَّةً مِّنْ عِندِ اللَّـهِ مُبَارَكَةً طَيِّبَةً ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمُ الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿٦١﴾

 Si vibaya kwa kipofu, na wala si vibaya kwa kilema, na wala si vibaya kwa mgonjwa, na wala nyinyi wenyewe kama mtakula majumbani mwenu, au majumbani mwa baba zenu, au majumbani mwa mama zenu, au majumbani mwa kaka zenu, au majumbani mwa dada zenu, au majumbani mwa ‘ammi zenu, au majumbani mwa shangazi zenu, au majumbani za wajomba wenu, au majumbani mwa makhalati zenu au za mliowashikia funguo zao, au rafiki yenu. Hakuna ubaya kama mkila pamoja au mbali mbali. Mtakapoingia majumbani toleaneni salaam; maamkizi kutoka kwa Allaah, yenye Baraka, mazuri. Hivyo ndivyo Anavyokubainishieni Allaah Aayaat ili mpate kutia akilini. [An-Nuwr (24: 61)]

 

 

4. Hima ya Maswahaba kufuata Sunnah, maamrisho na muongozo wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) tokea udogoni mwao.

 

 

5. Umuhimu wa kumfunza mtoto angali mdogo.

 

 

6. Kurekebisha kosa pale pale linapotokea kwa wakati wake munaasib na kwa upole.

 

 

7. Kutumia utaratibu na mfumo mzuri wa kumrekebisha mtu bila ya yeye kujihisi vibaya au kumfedhehesha. Hapa tunaona kuwa tatizo la mtoto lilikuwa ni mkono kuzungukazunguka katika sahani, lakini hilo lilitajwa mwisho na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

8. Kuwa makini katika kurekebisha jambo na kujali hisia za mtu japo za mtoto mdogo.

 

 

9. Maswahaba walikuwa makini katika kuyafikisha waliyopewa, kufundishwa na kunasihiwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), kwani walifahamu kuwa hayo hayakuwa yao pekee yao bali ni kwa Ummah wote.

 

 

10. Hadiyth inatupatia fundisho kujuzu kwa mwanamme kuwalea watoto wa mke wake aliyezaa na mume mwengine.

 

 

11. Mwanamme anayelea watoto wa kambo anatakiwa awalee kwa njia nzuri kama watoto wake wa uhusiano wa damu.   

 

Share

034-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuswali Wakati Wake, Kuwafanyia Wema Wazazi, na Kufanya Jihaad

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 34

Kuswali Wakati Wake, Kuwafanyia Wema Wazazi, na Kufanya Jihaad

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بن مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) قَالَ: سَأَلْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: أَيُّ الْعَمَلِ أَحَبُّ إِلَى اللَّهِ؟ قَالَ: ((الصَّلاَةُ عَلَى وَقْتِهَا)) قَالَ: ثُمَّ أَيٌّ؟ قَالَ: ((ثُمَّ بِرُّ الْوَالِدَيْنِ)) قَالَ: ثُمَّ أَيٌّ؟  قَالَ: ((الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Nilimuuliza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):  ‘amali gani inayopendeza zaidi kwa Allaah? Akasema: ((Swalaah kwa wakati wake)). Akasema: Kisha ipi? Akasema: ((Kisha kuwafanyia wema wazazi wawili)). Akasema: Kisha ipi? Akasema: ((Kufanya Jihaad katika Njia ya Allaah)).  [Al-Bukhaariy na Muslim.]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. ‘Amali zinatofuatiana kwa daraja, kwa maana kuwa nyinginezo zina thawabu zaidi ya nyingine.

 

 

2. Hima kubwa ya Maswahaba kupenda kujifunza mambo ya Dini yao, kwani walikuwa wakimuuliza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kila jambo wasilolijua.

 

 

3. Tabia njema ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na upole wake wa kuvumilia maswali kadhaa ya Maswahaba zake akiwajibu bila ya kuchoka.

 

 

4. Kuswali kwa wakati ni ‘amali bora kabisa kwa Allaah na ni amrisho katika Qur-aan.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا ﴿١٠٣﴾

Hakika Swalaah kwa Waumini ni fardhi iliyowekwa nyakati maalumu. An-Nisaa (4: 103).

 

Rejea pia Hadiyth namba (49), (79).

 

 

5. Uislamu unahimiza kuwafanyia wema wazazi wawili. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۚ إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣﴾

 

Na Rabb wako Amehukumu kwamba: “Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee na (Ameamrisha) kuwafanyia ihsaan wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee naye yuko pamoja nawe, au wote wawili basi usiwaambie, Uff! Na wala usiwakemee; na waambie maneno ya heshima.

 

 وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا

﴿٢٤﴾

Na wainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme: “Rabb wangu! Warehemu kama walivyonilea udogoni.” [Al-Israa (17: 22-23)]

 

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 83), An-Nisaa (4: 36), Al-An’aam (6: 151), Al-‘Ankabuwt (29: 8), Luqmaan (31: 14)].

 

Rejea pia Hadiyth namba (125).

 

 

6. Kuwafanyia wema wazazi ina thawabu zaidi kuliko kufanya Jihaad katika njia ya Allaah kwa dalili ya Hadiyth: Abdullaah bin ‘Amr Al-‘Aasw (رضي الله عنهما) alisimulia: Mtu mmoja alimkabili Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: Nitakubai juu ya Hijrah na kupigana jihaad katika njia ya Allaah nikitafuta ujira kutoka kwa Allaah. Akamuuliza: ((Je katika wazazi wako yuko aliye hai?)) Akajibu: Ndio, wote wako hai. Akamuuliza: ((Unatafuta ujira kutoka kwa Allaah?)) Akajibu: Ndio. Akamwamiba: ((Rudi kwa wazazi wako na uwafanyie wema)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

7. Kufanya jihaad katika njia ya Allaah ni mojawapo wa ‘amali kipenzi kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na Allaah (سبحانه وتعالى) Amewaahidi wafanyao jihaad kuwakinga na adhabu na kupata mema ya Jannah   Anasema:

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا هَلْ أَدُلُّكُمْ عَلَىٰ تِجَارَةٍ تُنجِيكُم مِّنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ﴿١٠﴾

Enyi walioamini! Nikujulisheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo?

 

 

 

تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَتُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ بِأَمْوَالِكُمْ وَأَنفُسِكُمْ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿١١﴾

Mumuamini Allaah na Rasuli Wake, na mfanye jihaad katika njia ya Allaah kwa mali zenu, na nafsi zenu. Hivyo ndiyo bora kwenu mkiwa mnajua.

 

 

يَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَيُدْخِلْكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ وَمَسَاكِنَ طَيِّبَةً فِي جَنَّاتِ عَدْنٍ ۚ ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ﴿١٢﴾

 (Allaah) Atakughufurieni madhambi yenu, na Atakuingizeni Jannaat zipitazo chini yake mito na masikani mazuri katika Jannaat za kudumu milele. Huko ndiko kufuzu adhimu.

 

وَأُخْرَىٰ تُحِبُّونَهَا ۖ نَصْرٌ مِّنَ اللَّـهِ وَفَتْحٌ قَرِيبٌ ۗ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ﴿١٣﴾

Na jengine mlipendalo; nusura kutoka kwa Allaah na ushindi wa karibu. Na wabashirie Waumini. [Asw-Swaff 61: 10-13]

 

Fadhia nyenginezo mbali mbali zimetajwa za kufanya jihaad. Rejea: Al-Maaidah (5: 35), Al-Anfaal (8: 74), Al-Baqarah (2: 218), An-Nisaa (4: 95), Al-‘Ankabuwt (29: 69), Al-Hujuraat (49: 15).

 

 

 

8. Mwanafunzi anatakiwa amuulize maswali mwalimu wake ambayo yatamsaidia katika dunia na Aakhirah yake.

 

 

9. Mwanafunzi anapaswa awe na adabu nzuri kwa mwalimu wake wala asitoke katika nidhamu hiyo ya adabu na haki za mwalimu na mwanafunzi kwa Mwalimu.

 

 

 

Share

035-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Starehe Bora Kabisa Ya Dunia Ni Mke Mwema

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 35

Starehe Bora Kabisa Ya Dunia Ni Mke Mwema

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو بْنِ الْعَاص (رضي الله عنهما)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((الدُّنْيَا مَتَاعٌ وَخَيْرُ مَتَاعِ الدُّنْيَا الْمَرْأَةُ الصَّالِحَة)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Dunia ni starehe, na bora ya starehe zake ni mke mwema)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo :

 

 

1. Umuhimu wa kuchagua mke mwema, mwenye taqwa.

 

Rejea: Hadiyth namba (40).

 

 

2. Sababu mojawapo ya furaha ya dunia na Aakhirah ni kuwa na mke mwema, mwenye taqwa.

 

 

3. Fadhila za mwanamke mwema mwenye taqwa kufananishwa na starehe na pambo la dunia. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ الشَّهَوَاتِ مِنَ النِّسَاءِ وَالْبَنِينَ وَالْقَنَاطِيرِ الْمُقَنطَرَةِ مِنَ الذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ وَالْخَيْلِ الْمُسَوَّمَةِ وَالْأَنْعَامِ وَالْحَرْثِ ۗ ذَٰلِكَ مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَاللَّـهُ عِندَهُ حُسْنُ الْمَآبِ   ﴿ ١٤﴾

Watu wamepambiwa huba ya matamanio miongoni mwa wanawake, na watoto, na mirundi ya mali iliyorundikwa ya dhahabu na fedha na farasi wenye chapa ya aina bora na wanyama wa mifugo na mashamba. Hayo ni starehe za uhai wa dunia, na Allaah Kwake kuna marejeo mazuri.  [Aal-‘Imraan (3: 14)]

 

 

4. Wema na taqwa ni miongoni mwa sifa njema anazopasa mwanamke wa Kiislamu kumiliki.

 

Rejea At-Tahriym (66: 11-12)

 

 

5. Mume anayeruzukiwa mke mwema ni neema kwake. Inampasa ailinde neema kwa kuishi naye vyema na kuwa na huruma naye na mapenzi ili apate kudiriki starehe za dunia na Aakhirah.

 

Rejea: Ar-Ruwm (30: 21), An-Nuwr (24: 26).

 

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ameusia waume kuwatendea wema wanawake zao katika Hadiyth kadhaa miongoni mwazo ni:

 

Kauli yake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

((Nakuusieni kuwafanyia wema wanawake))  [Al-Bukhaariy na Muslim

 

Na pia:

 

((واتَّقُوا اللهَ في النِّساءِ، فإنهن عندكم عَوَانٌ))

  ((Mcheni Allaah kuhusu wanawake kwani wao ni wasaidizi wenu…)   

 

Na pia amesema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

((Mbora wenu ni yule aliye mbora kwa familia yake na mimi ni mbora kabisa kwa familia yangu))  [At-Twabaraaniy]

 

Na amesema pia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

أن تطعمها إذا طعمت  وتكسوها إذا اكتسيت ولا تضرب الوجه ولا تقبّح   ولا تهجر إلاّ في البيت

((Kumlisha unapokula, na kumvisha unapovaa, wala usimpige usoni na kumharibu na usimtusi (kwa matendo yake na maneno yake) wala usimhame kwenda nyumba nyingine (umhame kitanda tu)) [Abuu Daawuwd, Ibn Maajah na Ahmad]

 

 Na amesema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

ارفق بالقوارير

((Wafanyieni wema vyombo vyenu (qawaariyra).” [Al-Bukhaariy]

 

Rejea pia Hadiyth namba (28), (29), (40).

 

 

 

Share

036-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Hana Iymaan Na Hatoingia Jannah Mwenye Kumtendea Jirani Shar

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 36

 

Hana Iymaan Na Hatoingia Jannah Mwenye Kumtendea Jirani Shari

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((وَاللَّهِ لاَ يُؤْمِنُ، وَاللَّهِ لاَ يُؤْمِنُ،  وَاللَّهِ لاَ يُؤْمِنُ!))  قِيلَ: مَنْ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟  قَالَ: الَّذِي لاَ يَأْمَنُ جَارُهُ بَوَائقَهُ)) متفق عليه

 وَفِي رِوَايَة: ((لاَ يَدْخُلُ الْجَنَّةَ مَنْ لاَ يَأْمَنُ جَارُهُ بَوَائِقَهُ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Wa-Allaahi hakuamini (hana Iymaan). Wa-Allaahi hakuamini, Wa-Allaahi hakuamini!)) Akaulizwa: Nani ee Rasuli wa Allaah?  Akasema: ((Ambaye jirani yake hasalimiki na shari zake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na katika riwaayah nyengine: ((Hatoingia Jannah ambaye jirani yake hasalimiki na shari zake)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu unasisitiza kumtendea wema jirani. Umuhimu wake hadi kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ameapa kwa Allaah! Na katika Hadiyth nyengine:

 

عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَا زَالَ جِبْرِيلُ يُوصِينِي بِالْجَارِ حَتَّى ظَنَنْتُ أَنَّهُ سَيُوَرِّثُهُ)). متفق عليه

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jibriyl hakuacha kuniusia jirani mpaka nikadhani kuwa atamrithisha [mali yangu])). [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

2. Mojawapo ya uthibitisho wa Iymaan ya Muumin ni kutomuudhi jirani.

 

 

3.Kumfanyia wema jirani ni sababu mojawapo ya kuingia Jannah, na kinyume chake ni kuingia motoni.

 

4. Muislamu anatakiwa ajiepushe na sifa mbaya ya kuudhi mtu na awe mwenye tabia njema na mwenye kulinda haki za watu.

 

 

5. Jirani ni aliye ubavuni, mtaani au hata aliye mbali. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَالْجَارِ الْجُنُبِ وَالصَّاحِبِ بِالْجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخْتَالًا فَخُورًا ﴿٣٦﴾

Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni ihsaan wazazi wawili na jamaa wa karibu, na mayatima, na masikini na jirani mwenye ujamaa na jirani asiye na ujamaa na rafiki wa karibu, na msafiri aliyeishiwa masurufu, na wale iliyowamiliki mikonoyenu ya kulia. Hakika Allaah Hapendi mwenye majivuno mwenye kujifakharisha.  [An-Nisaa (4: 36)]

 

 

6. Uislamu haukubagua kufanya wema hata kwa jirani asiye Muislamu anapaswa kutendewa wema.

Rejea: Al-Mumtahinah (60: 8-9).

 

 

7. Kumfanyia wema jirani na kutomuudhi ni katika uthibitisho wa Iymaan. Na Hadiyth: ((Mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho, basi asimuudhi jirani yake)) [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na at-Tirmidhiy]

 

 

Na pia Hadiyth: ((Mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho, amfanyie wema jirani yake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Share

037-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mwenye Iymaan Kweli Amkirimu Mgeni, Na Aseme Ya Kheri Au Anyamaze

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 37

 

Mwenye Iymaan Kweli Amkirimu Mgeni, Na Aseme Ya Kheri Au Anyamaze

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي شُرَيْحٍ الْخُزَاعِيِّ (رضي الله عنه) أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الأَخِرِ فَلْيُحْسِنْ إِلَى جَارِهِ،  وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الأَخِرِ فَلْيُكْرِمْ ضَيْفَهُ،  وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الأَخِرِ فَلْيَقُلْ خَيْرًا أَوْ لِيَسْكُتْ)) مسلم وروي البخاري بعضه

Imepokelewa kutoka kwa Abu Shurayh Al-Khuzaa’iyy( (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Anayemwamini Allaah na Siku ya Mwisho, basi amfanyie wema jirani yake, na anayemwamini Allaah na Siku ya Mwisho,  basi amkirimu mgeni wake, na anayemwamini Allaah na Siku ya Mwisho, basi azungumze kheri au anyamaze)) [Muslim na amepokea Al-Bukhaariy baadhi yake]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kumkirimu mgeni na kutokusema maovu ni mojawapo wa uthibitisho wa kumwamini Allaah (سبحانه وتعالى)  na Siku ya Mwisho. Rejea Hadiyth namba (36).

 

 

2. Ukarimu ni miongoni mwa tabia njema za Muumin na sababu ya kuingia Jannah.

 

3. Umuhimu wa kuchunga na kuzuia ulimi usiseme maneno ya upuuzi, kwani kila linalotamkwa linaandikwa na litaulizwa. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ قَعِيدٌ﴿١٧﴾

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni. 

 

 

مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾

Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 17-18]

 

Hadiyth: ((Kwa hakika mja atazungumza neno ambalo halizingatii [kuwa ni la kheri au la shari] ateleze nalo motoni umbali zaidi ya umbali ulioko baina ya Mashariki na Magharibi)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Rejea Hadiyth namba (86), (87), (93), (94),

 

4. Ulimi unaonena maovu unasababisha kila aina ya shari, kwa mgeni, jirani na jamii nzima kwa ujumla. Na Allaah (سبحانه وتعالى)  Anaamrisha kusema na watu yaliyo mema:

 

  وَقُولُوا لِلنَّاسِ حُسْنًا

Na semeni na watu kwa uzuri  [Al-Baqarah: (2: 83)]

 

 

5. Inapendekeza kukaa kimya panapokuwa hakuna faida ya kusema jambo na hiyo ni sifa mojawapo miongoni mwa sifa zitakazompatia Muislamu Jannah ya Al-Firdaws kwani hivyo ni kujiepusha na porojo na upuuzi. [Al-Muuminuwn: (23: 3]

 

Rejea pia Al-Furqaan (25: 72)

 

Share

038-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Anamuunga Anayeunga Kizazi Na Anamkata Anayekata Kizazi

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 38

 

Allaah Anamuunga Anayeunga Kizazi Na Anamkata Anayekata Kizazi

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ عَائِشَةَ (رضي الله عنها) قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الرَّحِمُ مُعَلَّقَةٌ بِالْعَرْشِ،  تَقُولُ مَنْ وَصَلَنِي وَصَلَهُ اللَّهُ وَمَنْ قَطَعَنِي قَطَعَهُ اللَّهُ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaisha (رضي الله عنها) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ((Uterasi [fuko la uzazi] limetundikwa katika ‘Arshi, linasema: Anayeniunga Allaah Atamuunga, na anayenikata Allaah Atamkata)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Jina la Allaah (سبحانه وتعالى) Ar-Rahmaan linahusiana na ‘rahm’ yenye maana ya: Uterasi (fuko la uzazi).

 

2. Allaah (سبحانه وتعالى) Amesisitiza sana kuunga kizazi kinachohusiana kwa damu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالَّذِينَ يَصِلُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيَخْشَوْنَ رَبَّهُمْ وَيَخَافُونَ سُوءَ الْحِسَابِ ﴿٢١﴾

Na ambao wanaunga yale Aliyoamrisha Allaah kuungwa na wanamkhofu Rabb wao, na wanakhofu hesabu mbaya.  [Ar-Ra’d (13: 21)]

 

 

3. Mwenye kutaka radhi za Allaah (سبحانه وتعالى)  basi aunge kizazi.

 

4. Hatari ya kukata kizazi; undugu na ujamaa wa uhusiano wa damu ni kukatwa na kulaaniwa na Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

فَهَلْ عَسَيْتُمْ إِن تَوَلَّيْتُمْ أَن تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ وَتُقَطِّعُوا أَرْحَامَكُمْ﴿٢٢﴾

Basi huenda nyinyi mkigeuka ndio mfanye ufisadi katika ardhi na kukata jamaa zenu wa uhusiano wa damu?

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ لَعَنَهُمُ اللَّـهُ فَأَصَمَّهُمْ وَأَعْمَىٰ أَبْصَارَهُمْ﴿٢٣﴾

Hao ndio ambao Allaah Amewalaani; Akawafanya viziwi na Akawapofua macho yao. [Muhammad: 22-23]

 

Rejea pia Al-Baqarah (2: 27).   

 

 

5. Kukata uzazi; undugu na ujamaa wa uhusiano wa damu, ni miongoni mwa dhambi kubwa kwa vile zinasababisha mtu kupata laana ya Allaah (سبحانه وتعالى).   

 

6. Mwenye kukata kizazi; undugu na ujamaa wa uhusiano wa damu, haingii Jannah kutokana na kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ((Haingii Jannah mwenye kukata udugu)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

6. Fadhila kadhaa kwa wenye kuunga undugu zimetajwa katika Hadiyth za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) mojawapo ni sababu ya kuongezewa umri mrefu na kuzidishiwa riziki na baraka:  ((Mwenye kupenda kutanuliwa rizki yake, na azidishiwe baraka katika umri wake aunge undugu wake)) [Al-Bukhaariy]  

 

Pia Hadiyth zifuatazo zimetaja fadhila nyinginezo: 

 

((Mwenye kumuamini Allaah na siku ya mwisho amkirimu mgeni wake, na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya mwisho aunge undugu wake)) [Al-Bukhaariy] 

 

Kutoka kwa Abuu Ayuwb Al-Answaariy (رضي الله عنه) kwamba mtu alisema: “Ee Rasuli wa Allaah! Nifahamishe tendo litakaloniingiza Jannah na litakaloniepusha na Moto.” Akasema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ((Umwabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, usimamishe Swalaah utoe Zakaah na uunge undugu)) [Al-Bukhaariy]

 

7. Kuunga undugu kunahitajia azimio la nguvu ambalo lina faida kwa mwenye kutekeleza. Hadiyth: Alikwenda mtu kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)   akasema: “Ee Rasuli wa Allaah, mimi nina ndugu nawaunga wananikata, nawafanyia wema na wao wananifanyia maovu, nawa mpole kwao wananifanya mjinga. Akasema: ((ikiwa uko kama unavyosema kanakwamba unawalisha majivu ya moto, na hutoacha kuwa unaungwa mkono na Allaah, ukidumu kwa hilo)) [Muslim]

 

 

 

Share

039-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Tofauti Ya Kuandamana Na Rafiki Mwema Na Muovu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake) 

Hadiyth Ya 39

Tofauti Ya Kuandamana Na Rafiki Mwema Na Muovu

Alhidaaya.com

 

عَنْ أَبِي مُوسَى الأَشْعَرِيِّ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((إِنَّمَا مَثَلُ الْجَلِيسِ الصَّالِحِ وَالسَّوْءِ كَحَامِلِ الْمِسْكِ وَنَافِخِ الْكِيرِ. فَحَامِلُ الْمِسْكِ إِمَّا أَنْ يُحْذِيَكَ، وَإِمَّا أَنْ تَبْتَاعَ مِنْهُ، وَإِمَّا أَنْ تَجِدَ مِنْهُ رِيحًا طَيِّبَةً. وَنَافِخُ الْكِيرِ إِمَّا أَنْ يُحْرِقَ ثِيَابَكَ، وَإِمَّا أَنْ تَجِدَ مِنْهُ  رِيحًا مُنْتِنَةً)) متفق عليه

 

Amesimulia Abuu Muwsaa Al-Ash-‘ariyyi (رضي الله عنه): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakika mfano wa mtu mwema anayekaa na watu, na mtu mwovu anayekaa na watu, ni kama mfano wa mbebaji miski na (mfua chuma) anayevuvia kipulizo. Mbebaji miski, ima atakupa, au utanunua kutoka kwake, au utapata harufu nzuri kwake. Ama anayevuvia kipulizo, ima atachoma nguo zako, au utapata harufu mbaya kutoka kwake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Umuhimu wa kuandamana na rafiki mwema, na tahadharisho la kuandamana na rafiki muovu.

 

 

2. Rafiki mwema ndiye mwenye kunufaisha ki-Dini na dunia, ama rafiki muovu ni mwenye kukhasirisha duniani na Aakhirah, na Siku ya Qiyaamah itakuwa ni majuto makubwa kuandama na rafiki muovu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَيَوْمَ يَعَضُّ الظَّالِمُ عَلَىٰ يَدَيْهِ يَقُولُ يَا لَيْتَنِي اتَّخَذْتُ مَعَ الرَّسُولِ سَبِيلًا ﴿٢٧﴾

 Na siku dhalimu atakapotafuna mikono yake akisema: “Laiti ningeshika njia pamoja na Rasuli. 

 

يَا وَيْلَتَىٰ لَيْتَنِي لَمْ أَتَّخِذْ فُلَانًا خَلِيلًا ﴿٢٨﴾

 “Ee ole wangu! Laiti nisingelimfanya fulani kuwa rafiki mwandani.”

 

لَّقَدْ أَضَلَّنِي عَنِ الذِّكْرِ بَعْدَ إِذْ جَاءَنِي ۗ وَكَانَ الشَّيْطَانُ لِلْإِنسَانِ خَذُولًا ﴿٢٩﴾

 “Kwa yakini amenipoteza mbali na Ukumbusho baada ya kunijia.” Na shaytwaan kwa insani daima ni mwenye kutelekeza. [Al-Furqaan (25: 27-29]

  

 

3. Rafiki mwema anamuathiri anayeandamana naye kwa tabia zake njema, na rafiki muovu pia anamuathiri anayeandamana naye kwa tabia zake mbovu.

 

 

4. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amefananisha harufu nzuri na mbaya kama tabia ambayo inamfikia haraka mtu puani kuisikia. Hivyo basi, haraka mno mtu anaweza kuathirika kwa tabia za mwenziwe zikiwa ni njema au tabia ovu. 

 

 

5. Hakuna atakayemfaa mwenziwe Siku ya Qiyaamah kwa lolote, hata  rafiki mwema hatoweza kumfaa mwenzake kila mmoja siku hiyo atakuwa analo la kumshughulisha mwenyewe.  Seuze basi iwe ni rafiki muovu? Rejea: Ghaafir (40: 18), Al-Haaqah (69: 35), Al-Ma’aarij (70 : 10).

 

 

Rejea Hadiyth Namba (47).

 

Pia Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عَنْ عائِشَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْها أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّمَ قالَ:  ((يُبْعَثُ النّاسُ يَوْمَ القِيامَةِ حُفاةً عُراةً غُرْلاً)) فَقالَتْ عائِشَةُ:  فَكَيْفَ بِالعَوْراتِ قالَ  (لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ)

Kutoka kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Watu watafufuliwa siku ya Qiyaamah bila ya viatu, uchi na bila ya kutahiriwa)) Akasema  ‘Aaishah: Vipi watakuwa uchi? Akasema: ((Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na hali ya kumtosheleza)) [Aayah Suwrah ‘Abasa (80: 37), Hadiyth katika An-Nasaaiy na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh An-Nasaaiy (2082)]

 

 

 

Share

040-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Sifa Nne Za Kuchagua Mke Mali, Nasaba, Uzuri Na Dini

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 40

Sifa Nne Za Kuchagua Mke Mali, Nasaba, Uzuri Na Dini

Alhidaaya.com

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((تُنْكَحُ الْمَرْأَةُ لأَرْبَعٍ: لِمَالِهَا  وَلِحَسَبِهَا   وَجَمَالِهَا  وَلِدِينِهَا. فَاظْفَرْ بِذَاتِ الدِّينِ تَرِبَتْ يَدَاكَ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah  (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Mwanamke huolewa kwa sababu nne; Kwa mali yake, nasaba yake [ukoo], uzuri wake na Dini yake. Tafuta mwenye Dini ubakie salama)). [Al-Bukhaariy na Muslim] (yaani usiharibikiwe katika maisha yako). 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu umetoa mwongozo katika kila jambo hata katika kutafuta mke mwema.

 

2. Kupata mke mwenye Dini ni sababu ya mume kupata utulivu katika maisha ya ndoa, kwani mke mwenye Dini atafuata shariy’ah za Dini yake na atajitahadharisha kutokutoka nje ya mipaka. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ ۚ  

Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi.  [An-Nisaa (4: 34)]

 

 3. Sifa njema nyenginezo za mke mwema mwenye Dini zimetajwa na Allaah (سبحانه وتعالى) katika kauli Yake:

 

 عَسَىٰ رَبُّهُ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبْدِلَهُ أَزْوَاجًا خَيْرًا مِّنكُنَّ مُسْلِمَاتٍ مُّؤْمِنَاتٍ قَانِتَاتٍ تَائِبَاتٍ عَابِدَاتٍ سَائِحَاتٍ ثَيِّبَاتٍ وَأَبْكَارًا﴿٥﴾

Akikutalikini, asaa Rabb Wake Akambadilishia wake bora kuliko nyinyi; Waislamu, Waumini, watiifu na wanyenyekevu, wanaotubia, wenye kufanya ‘ibaadah, wanaofunga Swiyaam au wanaohajiri kwa ajili ya Allaah, wajane, na walio bikra. [At-Tahriym: 5] 

 

 

4. Mke mwenye Dini ni mwenye kumnufaisha mumewe katika kushirikiana kwa kila upande wa maisha yao, ikiwa ni wakati wa furaha na shida, malezi ya watoto, kuhifadhi mali yake, siri yake, nayo ni furaha kamili kwa familia yote.

 

Hadiyth: ((Je, siwaambii hazina bora aliyonayo mwanamme? Ni mke mwema [mchaji Allaah]; ambapo anapomuangalia, anamfurahisha, na anapomuambia chochote, anamtii na anapokuwa hayupo nyumbani, anatizama [mke] maslahi ya mumewe)). [Abu Daawuwd]

 

 

6. Mke mwenye Dini ni sababu mojawapo ya kuidumisha ndoa.

 

 

7. Mke mwenye Dini bila shaka atakuwa ni mwenye taqwa na ni sababu mojawapo ya kupata mafanikio ya duniani na Aakhirah.

 

 

8. Katika uchaguzi wa mume au mke, Dini inatakiwa ipatiwe kipaumbele. 

 

 

Share

041-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Alama Tatu Za Kupata Utamu Wa Iymaan

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya   41

Alama Tatu Za Kupata Utamu Wa Iymaan

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((ثَلاَثٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ وَجَدَ حَلاَوَةَ الإِيمَانِ: أَنْ يَكُونَ اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَحَبَّ إِلَيْهِ مِمَّا سِوَاهُمَا، وَأَنْ يُحِبَّ الْمَرْءَ لاَ يُحِبُّهُ إِلاَّ لِلَّهِ, وَأَنْ يَكْرَهَ أَنْ يَعُودَ فِي الْكُفْرِ كَمَا يَكْرَهُ أَنْ يُقْذَفَ فِي النَّارِ)) متفق عليه

Amesimulia Anas bin Maalik (رضي الله عنه): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mambo matatu atakayekuwa nayo, atapata utamu wa imaan: Allaah na Rasuli Wake wawe vipenzi zaidi kwake kuliko wengineo, ampende mtu na wala asimpende isipokuwa kwa ajili ya Allaah, na achukie kurudi katika ukafiri baada ya Allaah kumwokoa kutoka huko kama anavyochukia kuingizwa motoni. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Muumin mwenye Iymaan ya kweli ni mwenye kumpenda Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) kuliko hata nafsi yake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

النَّبِيُّ أَوْلَىٰ بِالْمُؤْمِنِينَ مِنْ أَنفُسِهِمْ

Nabiy ana haki zaidi kwa Waumini kuliko nafsi zao [Al-Ahzaab (33: 6)]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ۖ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ

Na miongoni mwa watu wako wenye kuchukua asiyekuwa Allaah na kuwafanya kuwa ni wanaolingana (na Allaah) wanawapenda kama kumpenda Allaah. Na wale walioamini wana mapenzi zaidi kwa Allaah. [Al-Baqarah (2: 165)]

 

Na Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عَنْ أَنَسٍ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى أَكُونَ أَحَبَّ إِلَيْهِ مِنْ وَلَدِهِ وَوَالِدِهِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ)) أَخْرَجَاهُ

 

Imepokewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mmoja wenu hawi Muumini mpaka anipende mimi kuliko watoto wake na baba yake na watu wote)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 2. Allaah (سبحانه وتعالى) Ameonya kwamba Waumini wasipompenda au wasipofuata amri Zake au wakikengeuka, Atawaondoshelea mbali duniani, kisha Awalete waliobora zaidi yao na wampende Yeye zaidi.

 

[Rejea: Muhammad (47: 38), Al-Maaidah (5: 54)]

 

 

3. Utamu wa Iymaan unapatikana pale Muislamu atakapofuata amri za Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) na kuacha matamanio ya nafsi kando [Rejea: Aal-‘Imraan (3: 31)].

 

 

4. Utamu wa Iymaan unapatikana kutokana na kupenda kutekeleza ‘Ibaadah, Muumini anapozidisha ‘amali za Sunnah kama Swalaah, Swawm, sadaka hufikia daraja ya kupendwa na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

[Hadiyth Al-Qudsiy: ((Yeyote yule atakayefanya uadui kwa walii Wangu, Nitatangaza vita dhidi yake. Mja Wangu hanikaribii na kitu chochote Ninachokipenda kama ‘amali Nilizomfaridhishia, na mja Wangu huzidi kunikaribia kwa ‘amali njema za Sunnah ili Nimpende. Ninapompenda, huwa masikio yake yanayosikilizia, macho yake anayoonea, mikono yake anayopigania, miguu yake anayotembelea nayo, lau angeniomba kitu bila shaka Ningempa, lau angeniomba himaya bila shaka Ningelimkinga, na Sisiti juu ya kitu chochote kama Ninavyosita [kuichukua] roho ya mja Wangu Muumin: Anachukia mauti, Nami Nachukia kumdhuru)) [Al-Bukhaariy]

 

5. Inapasa kujenga mapenzi ya ikhlaasw pamoja na waja wema na kuandamana nao katika vikao vyao, kwani mapenzi yao ni kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى), na ndipo Muislamu atakapopata manufaa ya Dini yatakayomfikisha daraja ya Al-Walaa Wal-Baraa (Kupendana kwa ajili ya Dini ya Allaah na kuchukiana au kutengana kwa ajili yake) kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

((أَوْثقُ عُرَى الإِيمان: الموالاَةُ في الله والمعاداةُ في الله، والحب في الله، والبغضُ في اللَّه عز وجل))   

((Shikizo thabiti kabisa la iymaan ni kuwa na urafiki wa karibu kwa ajili ya Allaah na kujitenga kwa ajili ya Allaah, na kupenda kwa ajili ya Allaah, na kuchukia kwa ajili ya Allaah عزّ وجلّ)) [Hadiyth ya Ibn ‘Abaas (رضي الله عنهما) : Atw-Twabaraaniy katika Al-Kabiyr na ameisahihisha Al-Abaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (2539)]

 

 Na pia:

 

عَنْ أَبِي أُمَامَةَ ، قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ :  ((مَنْ أَحَبَّ فِي اللَّهِ وَأَبْغَضَ فِي اللَّهِ وَأَعْطَى لِلَّهِ وَمَنَعَ لِلَّهِ فَقَدِ اسْتَكْمَلَ الإِيمَانَ))  

Amesimulia Abuu Umaamah  (رضي الله عنه):  “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: “Atakayependa kwa ajili ya Allaah, akachukia kwa ajili ya Allaah, akatoa kwa ajili ya Allaah, na akazuia kwa ajili ya Allaah, basi atakuwa amekamilisha imaan.”  [Abuu Daawuwd na ameisahihisha Al-Albaaniy (4681)]

 

6. Kuchukia kufru na ufasiki na watu wake hata kama mtu ana uhusiano wa damu, kwani kafiri na fasiki huenda akamrudisha mtu katika kufru na ufasiki. [Rejea: Al-Mujaadalah (58: 22)].

 

 

 

 

 

 

Share

042-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haingii Jannah Mtu Ila Kwa Iymaan, Kupendana na Kutoleana Salaam

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  42

 

Haingii Jannah Mtu Ila Kwa Iymaan, Kupendana na Kutoleana Salaam

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لاَ تَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ حَتَّى تُؤْمِنُوا، وَلاَ تُؤْمِنُوا حَتَّى تَحَابُّوا، أَوَلاَ أَدُلُّكُمْ عَلَى شَيْءٍ إِذَا فَعَلْتُمُوهُ تَحَابَبْتُمْ؟  أَفْشُوا السَّلاَمَ بَيْنَكُمْ)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake! Hamtoingia Jannh mpaka muamini, wala hamtoamini mpaka mpendane. Je, niwajulishe jambo mtakapolifanya mtapendana? Enezeni Salaam baina yenu)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kutekeleza amri ya kuamkiana kwa maamkizi ya Kiislamu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا ﴿٨٦﴾

Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo. Hakika Allaah daima ni Mwenye kuhesabu kila kitu. [An-Nisaa: 86]

 

2. Maamkizi ya Kiislamu yana kheri na baraka, ndio maana Allaah (سبحانه وتعالى) Akaamrisha mtu anapoingia nyumbani kwake ayatamke, hata kama hakuna mtu ndani ya nyumba. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  ۚ فَإِذَا دَخَلْتُم بُيُوتًا فَسَلِّمُوا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ تَحِيَّةً مِّنْ عِندِ اللَّـهِ مُبَارَكَةً طَيِّبَةً ۚ  

Mtakapoingia majumbani toleaneni salaam; maamkizi kutoka kwa Allaah, yenye Baraka, mazuri.  [An-Nuwr (24: 61)]

 

3. Jannah haipatikani ila kuweko na Iymaan, na Iymaan haikamiliki ila Muislamu ampendelee nduguye anayoyapenda nafsi yake. [Rejea Hadiyth namba 21].

 

 

4. Iymaan haikamiliki ila kwa matendo na amri zake.

 

 

5. Maamkizi ya Kiislamu katika shariy’ah na inavyopasa kuamkiana ni “Assalaamu ‘Alaykum” Au: “Assalaamu ‘alaykum wa RahmatuLLaah” Au: “Assalaamu ‘alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh”  na si vinginevyo kutokana na Hadiyth:

 

عَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ  رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا  قَالَ: جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: "السَّلامُ عَلَيْكُمْ" فَرَدَّ عَلَيْهِ ثُمَّ جَلَسَ فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((عَشْرٌ))  ثُمَّ جَاءَ آخَرُ فَقَالَ: "السَّلامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ"  فَرَدَّ عَلَيْهِ فَجَلَسَ فَقَالَ: ((عِشْرُونَ)) ثُمَّ جَاءَ آخَرُ فَقَالَ: "السَّلامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ وَبَرَكَاتُهُ" فَرَدَّ عَلَيْهِ فَجَلَسَ فَقَالَ : ((ثَلاثُونَ)) رواه ابو داود والترمذي و قال حديث حسن

'Imraan bin Al-Huswayn (رضي الله عنهما) amesimulia: "Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: "Assalaamu 'Alaykum." Akamrudishia (Salaam) kisha yule mtu akaketi. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Kumi)) [Kwa maana amepata thawabu kumi]. Kisha akaja mtu mwengine, akasema: "Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaah." Naye akamrudishia, kisha yule mtu akaketi, Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ishirini)). Kisha akaja mtu mwingine akasema: "Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh." Naye akamrudishia kisha akasema ((Thelathini)) [Imesimuliwa na Abu Daawuwd na At-Trimidhiy na akasema Hadiyth Hasan na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (5195), Swahiyh At-Tirmidhiy (2869)]

 

 

Na haifai kuyafupisha katika maandishi kama ilivyozoeleka katika mitandao ya kijamii; baadhi ya watu kuandika: (AA) na vinginevyo. ‘Ulamaa wetu wamekemea jambo hili kwamba ni kinyume na maamrisho ya Qur-aan na Sunnah, na pia ni kujikosesha thawabu na fadhila zake.

 

 

5. Kutoleana Salaam ni sababu au chanzo cha kutambulisha na kujuana baina ya Waislamu, na kutoa Salaam kwa mtu mmoja kunaweza kuwafikia maelfu ya Waislamu na kupata fadhila, thawabu, na manufaa yake.

 

 

6. Maamkizi ya Kiislamu ni funguo za mapenzi baina ya Waislamu.

 

 

7. Maamkizi ya Kiislamu ndiyo yanayotofautisha baina ya Waislamu na makafiri.

 

 

8. Maamkizi ya Kiislamu yanalingana sawa na maana ya ‘Uislamu’ yaani amani.  

 

 

9. Fadhila ya Iymaan ni kumuingiza mtu Jannah.

 

 

 

 

Share

043-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Wanaopendana Kwa Ajili Ya Allaah Watakuwa Chini Ya Kivuli Chake

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya   43 

Wanaopendana Kwa Ajili Ya Allaah Watakuwa Chini Ya Kivuli Chake

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ اللَّهَ يَقُولُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ: أَيْنَ الْمُتَحَابُّونَ بِجَلاَلِي الْيَوْمَ أُظِلُّهُمْ فِي ظِلِّي يَوْمَ لاَ ظِلَّ إِلاَّ ظِلِّي)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika Allaah Atasema Siku ya Qiyaamah: Wako wapi wanaopendana kwa Utukufu Wangu? Leo Nitawaweka kivulini katika kivuli Changu, Siku ambayo hakuna kivuli isipokuwa kivuli Changu)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Bishara kwa Waumini wanaopendana kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwamba watapata fadhila ya kuwekwa kivulini Siku ambayo hakuna kivuli isipokuwa kivuli cha Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

2. Fadhila ya kujumuishwa pamoja katika Ardhw Al-Mahshar (ardhi ya mkusanyiko) Siku ya Qiyaamah, kabla ya kuingia Jannah.

 

 

3. Kupenda kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni jambo dogo mno kulingana na thawabu na fadhila zake.

 

 

4. Hadiyth hii ni tashjiy’ (himizo) kwa Waumini wanaopendana kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) wazidi kutenda mema, waambatane katika    kuamrishana mema na kukatazana maovu, na kufanyiana kila aina ya wema. Na fadhila yao ni Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) juu yao ya kivuli hicho, pamoja na mazuri waliyoandaliwa huko Jannah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ يَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَيُطِيعُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ ۚ أُولَـٰئِكَ سَيَرْحَمُهُمُ اللَّـهُ ۗ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ﴿٧١﴾

Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki wandani wao kwa wao, wanaamrisha mema na wanakataza munkari na wanasimamisha Swalaah na wanatoa Zakaah na wanamtii Allaah na Rasuli Wake. Hao Allaah Atawarehemu. Hakika Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [At-Tawbah (9: 71)]

 

 

Hivyo ndivyo hali ilivyokuwa ya Maswahaba wao kwa wao na kwa kipenzi chao Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kama Anavyosema Allaah. [Rejea Al-Fat-h (48: 29)].

 

 

5. Kuna haja kubwa ya kupendana kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) ili kupata kivuli Chake, kwani jua Siku hiyo litakuwa kali mno si kama jua la duniani, bali litakuwa karibu mno na utosi wa watu.

 

[Hadiyth: ((Watu saba Allaah  Atawafunika katika kivuli Chake, Siku ambayo hakutokuwa na kivuli ila kivuli Chake: Imaam muadilifu, kijana ambaye amekulia katika ‘Ibaadah ya Rabb wake, Mtu ambaye moyo wake umeambatana na Misikiti, watu wawili wanaopendana kwa ajili ya Allaah; wanakutana kwa ajili Yake na wanafarikiana kwa ajili Yake, mwanamme aliyetakwa na mwanamke mwenye hadhi na mrembo wa kuvutia akasema: "Mimi namkhofu Allaah!" Mtu aliyetoa Swadaqah yake akaificha hadi kwamba mkono wake wa kushoto usijue nini ulichotoa mkono wake wa kulia, na mtu aliyemdhukuru Allaah kwa siri macho yake yakatokwa machozi)) [Al-Bukhaariy, Muslim].

 

 

 

Share

044-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Akimpenda Mja Anamnadia Jibriyl Na Kumuamrisha Ampende Pamoja Na Wote

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  44

Allaah Akimpenda Mja Anamnadia Jibriyl Na Kumuamrisha Ampende Pamoja Na Wote

 

Alhidaaya.com

 

 

 

  عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِذَا أَحَبَّ اللَّهُ الْعَبْدَ نَادَى جِبْرِيلَ إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ فُلاَنًا فَأَحْبِبْهُ، فَيُحِبُّهُ جِبْرِيلُ، فَيُنَادِي جِبْرِيلُ فِي أَهْلِ السَّمَاءِ: إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ فلاَنًا فَأَحِبُّوهُ، فَيُحِبُّهُ أَهْلُ السَّمَاءِ ثُمَّ يُوضَعُ لَهُ الْقَبُولُ فِي الْأَرْضِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:((Allaah Anapompenda mja, Humnadia Jibriyl: Hakika Allaah Anampenda fulani, nawe mpende. Basi Jibrily humpenda. Naye Jibriyl anawanadia watu wa mbinguni [Malaika]: “Hakika Allaah Anampenda fulani, nanyi mpendeni. Basi nao walioko mbinguni humpenda, halafu huwekwa kabuli katika ardhi [watu wampende])). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila kubwa mno kupendwa na Allaah (سبحانه وتعالى) kama Alivyotubashiria kwamba watakuwa hawana khofu, wala huzuni wala baya au dhiki yoyote ile. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 أَلَا إِنَّ أَوْلِيَاءَ اللَّـهِ لَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ﴿٦٢﴾

Tanabahi!  Hakika vipenzi wa Allaah hawana khofu juu yao, na wala hawatohuzunika.

 

الَّذِينَ آمَنُوا وَكَانُوا يَتَّقُونَ﴿٦٣﴾

Ambao wameamini na wakawa wana taqwa.

   

لَهُمُ الْبُشْرَىٰ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۚ لَا تَبْدِيلَ لِكَلِمَاتِ اللَّـهِ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ﴿٦٤﴾

Watapata bishara katika uhai wa dunia na wa Aakhirah. Hakuna mabadiliko katika Maneno ya Allaah. Huko ndiko kufuzu adhimu. [Yuwnus (11: 62-64)]

 

 

2. Mapenzi yako baina wana Aadam kama baina ya mume na mke, familia, marafiki, mwalimu na mwanafunzi n.k, lakini mapenzi yaliyo muhimu zaidi ni mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

3. Apataye mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) atakuwa katika ulinzi wa Malaika, kwani wao wameamrishwa wampende na wamlinde mja huyo duniani na Aakhirah kuna ziada. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ﴿٣٠﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara; Malaika huwateremkia: (kuwaambia): “Msikhofu, na wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo mlikuwa mkiahidiwa.”

 

 

نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَشْتَهِي أَنفُسُكُمْ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ﴿٣١﴾

 “Sisi ni rafiki zenu walinzi katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale mtakayoomba.

 

نُزُلًا مِّنْ غَفُورٍ رَّحِيمٍ﴿٣٢﴾

 “Ni mapokezi ya takrima kutoka kwa Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.”  [Fusw-Swilat (41: 30-32)].

 

 

4. Waja wema wanapendeza machoni mwa watu baada ya kuwekewa na Allaah (سبحانه وتعالى) kabuli ardhini.

 

 

5. Hima ya kutenda mema yatakayosababisha kupata mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى). 

 

[Hadiyth Al-Qudsiy: ((Yeyote yule atakayefanya uadui kwa walii Wangu, basi Nitatangaza vita dhidi yake. Mja Wangu hanikaribii na kitu chochote Ninachokipenda kama ‘amali Nilizomfaridhishia, na mja Wangu huzidi kunikaribia kwa ‘amali njema za Sunnah ili Nimpende. Ninapompenda, Huwa masikio yake yanayosikilizia, macho yake anayoonea, mikono yake anayopigania, miguu yake anayotembelea nayo, lau angeniomba kitu, bila shaka Ningempa, lau angeniomba himaya bila shaka Ningelimkinga, na Sisiti juu ya kitu chochote kama Ninavyosita [kuichukua] roho ya mja Wangu Muumin, anachukia mauti, Nami Nachukia kumdhuru)). [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

 

Share

045-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mambo Manne Atakayoulizwa Mja Siku Ya Qiyaamah: Umri, Elimu, Mali na Mwili

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 45

Mambo Manne Atakayoulizwa Mja Siku Ya Qiyaamah:

Umri, Elimu, Mali na Mwili

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي بَرْزَةَ الأَسْلَمِيِّ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ تَزُولُ قَدَمَا عَبْدٍ يَوْمَ الْقِيَامَةِ حَتَّى يُسْأَلَ عَنْ عُمُرِهِ فِيمَا أَفْنَاهُ، وَعَنْ عِلْمِهِ فِيمَ فَعَلَ، وَعَنْ مَالِهِ مِنْ أَيْنَ اكْتَسَبَهُ وَفِيمَ أَنْفَقَهُ وَعَنْ جِسْمِهِ فِيمَ أَبْلاَهُ))  رواه الترمذي وقال: حديث حسن  صحيح

 

Kutoka kwa Abuu Barzah Al-Aslamiyy (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Nyayo za mja hazitoondoka [Siku ya Qiyaamah] mpaka aulizwe juu ya umri wake alivyoumaliza, elimu yake alivyoifanyia, mali yake ameichuma kutoka wapi na ameitumia kwa mambo gani, na mwili wake aliutumia kwa kazi gani)). [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hima ya Muislamu kutumia umri wake katika yale yanayomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

2. Mambo manne hayo ni miongoni mwa neema nyingi za Allaah (سبحانه وتعالى) kwa mja, anapaswa kushukuru kwa yakini, kauli na vitendo, na ataulizwa kuhusu neema hizo kama Anavyosema:

 

ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ ﴿٨﴾

Kisha bila shaka mtaulizwa Siku hiyo kuhusu kuhusu neema. [At-Takaathur: 8]

 

 

3. Himizo la kuchuma mali kutoka njia za halali na kuitumia katika yanayomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى) pamoja na kuitolea Zakaah na sadaka na tahadharisho la chumo la haramu. [Rejea: Al-Baqarah (2: 168), Twaahaa (20: 81].

 

 

4. Kuuhifadhi mwili usitende yaliyo haramu na kuutiisha pamoja na kuutumikia katika utiifu wa Allaah (سبحانه وتعالى), na kufanya ‘Ibaadah kwa wingi.

 

 

5. Kujifunza elimu iliyo na manufaa na aifanyie kazi kwa ikhlaasw anufaike nayo na anufaishe wengineo.

 

 

6. Tanabahisho kwa Muislamu kuwa na ikhlaasw katika ‘amali azitendazo.  Rejea: [Al-Kahf : 110].

 

 

7. Mambo manne hayo ni majukumu ya kila mtu Siku ya Qiyaamah. Hakuna atakayeondoka mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) bila kuulizwa.

 

 

8. Hadiyth hii ni tahadharisho la kujirekebisha, kwa mtu anayekwenda kinyume na yanayomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

9. Uhai na maisha ya dunia ni kama madrasa anayosoma mtu na kufanya juhudi, kisha mtihani wake na malipo ni Siku ya Qiyaamah. Atakayefanya kinyume chake, atapata khasara huko Aakhirah ambako kwenye maisha ya milele.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 مَّن كَانَ يُرِيدُ الْعَاجِلَةَ عَجَّلْنَا لَهُ فِيهَا مَا نَشَاءُ لِمَن نُّرِيدُ ثُمَّ جَعَلْنَا لَهُ جَهَنَّمَ يَصْلَاهَا مَذْمُومًا مَّدْحُورًا ﴿١٨﴾

Yeyote anayetaka (starehe za dunia) ipitayo upesi upesi Tunamharakizia humo Tuyatakayo, na kwa Tumtakaye. Kisha Tutamjaalia Jahannam aingie na kuungua hali ya kuwa mwenye kushutumiwa kufukuziliwa mbali (na rahmah ya Allaah).

 

 مَنْ أَرَادَ الْآخِرَةَ وَسَعَىٰ لَهَا سَعْيَهَا وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَأُولَـٰئِكَ كَانَ سَعْيُهُم مَّشْكُورًا ﴿١٩﴾

Na anayetaka Aakhirah na akaifanyia juhudi inayostahiki kufanyiwa, naye ni Muumin, basi hao juhudi zao ni za kushukuriwa. 

 

كُلًّا نُّمِدُّ هَـٰؤُلَاءِ وَهَـٰؤُلَاءِ مِنْ عَطَاءِ رَبِّكَ ۚ وَمَا كَانَ عَطَاءُ رَبِّكَ مَحْظُورًا ﴿٢٠﴾

Wote hao Tunawakunjulia; hawa na hao katika hiba za Rabb wako. Na hazikuwa hiba za Rabb wako zenye kuzuiliwa. [Al-Israa (17: 18-20)]

 

Na pia Rejea: [Ash-Shuwraa (42: 20)].

 

10. Umuhimu wa kufanya kazi, na mtu achunge sana kazi atakayofanya, kwa sababu chumo la haramu litampeleka mtu pabaya.

 

 

11. Muislamu anatakiwa katika  Shariy’ah achume chumo la halali na alitumie kwa njia za halali.

 

 

12. Katika riwaayah nyengine ya at-Tirmidhiy badala ya mwili inataja ujana umetumiwe vipi, kumaanisha kuwa kipindi hicho ni muhimu sana katika maisha ya mwana Adamu na ni wakati wa kuchuma mema mengi.

 

 

 

 

 

 

Share

046-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Ardhi Itashuhudia Matendo Ya Watu Siku Ya Qiyaamah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 46

Ardhi Itashuhudia Matendo Ya Watu Siku Ya Qiyaamah

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَرَأَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا)) قَالَ: ((أَتَدْرُونَ مَا أَخْبَارُهَا)) قَالُوا: اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ. قَالَ: ((فَإِنَّ أَخْبَارَهَا أَنْ تَشْهَدَ عَلَى كُلِّ عَبْدٍ أَوْ أَمَةٍ بِمَا عَمِلَ عَلَى ظَهْرِهَا، تَقُولُ عَمِلْتَ كَذَا وَكَذَا فِي يَوْمَ كَذَا وَكَذَا فَهَذِهِ أَخْبَارُهَا)) الترمذي  وقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alisoma: ((Siku hiyo itahadithia khabari zake.)). Akauliza: ((Mnajua nini khabari zake?)) Wakasema: Allaah na Rasuli Wake Wanajua zaidi. Akasema: ((Khabari zake ni kwamba itashuhudia juu ya kila mja mwanamme au mwanamke waliyoyatenda juu yake, itasema: Umefanya kadhaa na kadhaa, siku kadhaa na kadhaa. Basi hii ndio habari zake)). [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Himizo la kutenda mema na kujiepusha na maasi.

 

 

2. Uwezo wa Allaah (سبحانه وتعالى) kujaalia kila kitu kuzungumza Siku ya Qiyaamah; ardhi, viungo vya mwili wa mtu, ngozi n.k. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰ أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ ﴿٦٥﴾

Leo Tunatia vizibo juu ya vinywa vyao, na itatusemesha mikono yao, na itashuhudia miguu yao kwa yale waliyokuwa wakiyachuma. [Yaasiyn: 65]

 

Rejea pia: [An-Nuwr (24: 24), Ghaafir (40: 21-22)]

 

 

3. Tisho kubwa la mwenye kutenda maasi japokuwa mahali pa kutendwa maasi patakuwa ni mbali, kwani ardhi popote itamshuhudia matendo yake. [Rejea: Aal-‘Imraan (3: 30)].

 

 

4. Hakuna mtu atakayeweza kuficha maasi yake yoyote na Siku hiyo siri zote zitadhihirishwa. [Rejea: Al-Haaqah (69: 18), Atw-Twaariq (86: 9), Al-Qiyaamah (75: 13)].

 

5. Heshima ya Maswahaba kwa mwalimu wao, Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kusema hatujui jambo ambalo hawajui. Na si aibu kutojua jambo miongoni mwa mambo, bali ni sifa nzuri anayotakiwa kuwa nayo Muislamu.

 

 

 

Share

047-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kila Mmoja Atakuwa Analo La Kumshughulisha Siku Ya Qiyaamah

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 47

 

Kila Mmoja Atakuwa Analo La Kumshughulisha Siku Ya Qiyaamah

 

 

 

 

عَنْ عَائِشَةَ (رضي الله عنها)  قَالَتْ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((يُحْشَرُ النَّاسُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ حُفَاةً عُرَاةً غُرْلا)) قُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ، النِّسَاءُ وَالرِّجَالُ جَمِيعًا يَنْظُرُ بَعْضُهُمْ إِلَى بَعْضٍ؟  قَالَ: ((يَا عَائِشَةُ! الأَمْرُ أَشَدُّ مِنْ أَنْ  يُهِمَّهُم ذلِكَ))

 

وَفِي رِواية: ((ألأَمْرُ أَهَمُّ مِنْ أَنْ يَنْظُرَ بَعْضُهُمْ إِلَى بَعْضٍ)) متفق عليه

                                                                                                                                             Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها) ambaye amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Watu watafufuliwa Siku ya Qiyaamah ilhali hawana viatu, wako uchi, ni mazunga [hawakutahiriwa])). Nikamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Wanaume na wanawake wote watatazamana? Akasema: ((Ee ‘Aaishah! Hali itakuwa ngumu hata hawatoweza kushughulika na jambo hilo!))

 

Katika riwaayah nyingine imesema: ((Hali itakuwa ngumu mno kiasi kwamba hawatoweza kutazamana)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Hadiyth inaashiria kama taswira hali itakavyokuwa Siku ya Qiyaamah. [Rejeja Al-Infitwaar (82: 17-19), Al-Hajj (22: 1-2)].

 

 

2. Kila mmoja atakuwa na la kumshughulisha hata asijali aliyekuweko mbele yake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ ﴿٣٤﴾

Siku mtu atakapomkimbia ndugu yake.

 

وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ ﴿٣٥﴾

Na mama yake na baba yake.

 

وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ ﴿٣٦﴾

Na mkewe na wanawe.

 

لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ ﴿٣٧﴾

Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na hali ya kumtosheleza. [‘Abasa (80: 34-37)]

 

Rejea pia: [Al-Ma’aarij  (70: 10-14)].

 

3.  Watu watafufuliwa Siku ya Qiyaamah wakiwa pekee, watupu, hawana mtu wala chochote, kila walichomiliki wamekiacha duniani. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ جِئْتُمُونَا فُرَادَىٰ كَمَا خَلَقْنَاكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَتَرَكْتُم مَّا خَوَّلْنَاكُمْ وَرَاءَ ظُهُورِكُمْ ۖ  

  Na kwa yakini mmetujia mmoja mmoja kama Tulivyokuumbeni mara ya kwanza; na mmeyaacha nyuma yenu yote Tuliyokuruzukuni.  [Al-An’aam (6: 94]

 

Na rejea pia:  [Al-Kahf (18: 48),  Maryam (19: 93-95)].

 

 

4. Khofu ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها) kujisitiri hata Siku ya Qiyaamah.

 

 

5. Dalili ya sitara ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها) dhidi ya yale walivyomzulia wanafiki katika kisa cha Ifk [An-Nuwr (24: 11-26)] na yale wanayomzulia Mashia mpaka sasa.  

 

 

6. Kila mmoja atakuwa anaitizama na kuijali nafsi yake tu. [Hadiyth ndefu ya kuhusu Shafaa’ah (Uombezi) ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) pindi Nabiy Aadam, Nuwh, Muwsaa na Iysaa (عليهم السلام) watakapokataa kuwaombea watu Ash-Shafaa’ah watasema kila mmoja wao: “Nafsi yangu! Nafsi yangu! Nafsi yangu.” [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Share

048-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haki Ya Allaah Ni Kumwabudu Bila Kumshirikisha Na Kitu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  48

Haki Ya Allaah Ni Kumwabudu Bila Kumshirikisha Na Kitu

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ (رضي الله عنه)  قَالَ كُنْتُ رِدْفَ النَّبِيّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَلَى حِمَارٍ فَقَالَ:  ((يَا مُعَاذُ، تَدْرِي مَا حَقُّ اللَّهِ عَلَى عِبَادِهِ، وَمَا حَقُّ الْعِبَادِ عَلَى اللَّهِ؟)) قُلْتُ: اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ  قَالَ:  ((فَإِنَّ حَقَّ اللَّهِ عَلَى الْعِبَادِ أَنْ يَعْبُدُوهُ ولاَ يُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا، وَحَقُّ الْعِبَادِ عَلَى اللَّهِ أَنْ لاَ يُعَذِّبَ مَنْ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا)) قَقُلْتُ:  يَا رَسُولَ اللَّهِ،  أَفلاَ أُبَشِّرُ النَّاسَ؟  قَالَ: ((لاَ تُبَشِّرْهُمْ فَيَتَّكِلُوا)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه)  amesema: Nilikuwa nyuma ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) nimepanda punda, akasema: ((Ee Mu’aadh! Unajua nini haki ya Allaah juu wa waja Wake na haki ya waja juu ya Allaah?)) Nikajibu: Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi: Akasema:((Haki ya Allaah kwa waja Wake ni kwamba wamwabudu na wasimshirikishe na chochote. Na haki ya waja kwa Allaah ni kwamba Hatomwadhibu yeyote ambaye hamshirikishi na kitu)). Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nibashirie watu? Akasema: ((Usiwabashirie wasije kuitegemea)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Rahma za Allaah (سبحانه وتعالى) kwa waja kuwaghufuria na kutowaadhibu wanaporudi kutubu Kwake.

 

2. Haki ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kila mja ni kwamba wasimshirikishe na kitu chochote katika ‘Ibaadah zao. Allaah (سبحانه وتعالى) Amemuamrisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aseme:  

 

 

قُلْ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mtu kama nyinyi, nafunuliwa Wahy  kwamba: Hakika Mwabudiwa wa haki wenu ni Ilaah Mmoja Pekee. Hivyo anayetaraji kukutana na Rabb wake, basi na atende ‘amali njema na wala asishirikishe yeyote katika ‘ibaadah za Rabb wake” [Al-Kahf (18: 110)]

 

Rejea pia: [An-Nisaa (4: 36), Al-An’aam (6: 151)].

 

 

3.  Shirki ni miongoni mwa Al-Kabaair (Madhambi makubwa) kwa dalili kadhaa miongoni mwazo ni Hadiyth za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

(ألاَ أُنبِّئكم بأكبرِ الكبائر؟ الإشراك بالله)) متفق عليه.

((Je, hivi nikujulisheni madhambi makubwa kabisa? Ni kumshirikisha Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

عَنْ أبي أيوب الأنصاري رضي الله عنه انَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ جَاءَ يَعْبُدُ اللَّهَ وَلاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا وَيُقِيمُ الصَّلاَةَ وَيُؤْتِي الزَّكَاةَ وَيَجْتَنِبُ الْكَبَائِرَ كَانَ لَهُ الْجَنَّةُ)).‏ فَسَأَلُوهُ عَنِ الْكَبَائِرِ فَقَالَ‏: ((الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ وَقَتْلُ النَّفْسِ الْمُسْلِمَةِ وَالْفِرَارُ يَوْمَ الزَّحْفِ)).‏

Imepokelekewa kutoka kwa Abu Ayyuwb Al-Answaariyy (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Atakayekuja akiwa anamwambudu Allaah wala hamshirikishi na chochote, na anasimamisha Swalaah, na anatoa Zakaah, na anajiepusha na Al-Kabaair (madhambi makubwa) atapata Al-Jannah)) Wakamuuliza kuhusu Al-Kabaair akasema: ((Kumshirkisha Allaah na kumuua Muislamu, na kukimbia (vita) siku ya mapambano (vita).)) [An-Nasaaiy (4009) na ameisahihisha Al-Albaaniy]

 

[Rejea pia Hadiyth Namba 108] kuhusu madhambi makubwa yanayoangamiza.

 

 

4. Allaah (سبحانه وتعالى) Hamghufurii mja anayemshirikisha, lakini Anaghufuria  madhambi mengineyo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا ﴿٤٨﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amezua dhambi kuu. [An-Nisaa (4: 48)]

 

 

Rejea pia: [An-Nisaa (4: 116)]

 

 

5. Kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) kunamharamisha mtu na Jannah na makazi yake ni motoni. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ

Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni.  [Al-Maaidah (5: 72)].

 

 

6. Inafaa kubashiria habari njema ikiwa itasababisha mtu kutenda mema na kumweka mtu katika hali bora zaidi ya iymaan yake na taqwa.

 

 

7. Hikma ya njia aliyopendelea sana Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwafunza Maswahaba kwa kuwauliza maswali.

 

 

8. Dhihirisho la unyenyekevu wa Maswahaba ulikuwa kwamba hawajibu lolote wasilolijua ili kujionyesha uhodari wao wa kufahamu jambo, bali walimwachia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ajibu mwenyewe yale wasiyokuwa na ujuzi nayo. Hili ni funzo kwa mwanafunzi katika adabu za kutafuta elimu, na anapaswa mwanafunzi kuwa na unyenyekevu wa aina huu.

 

 

8. Matahadharisho mengi na makemeo na adhabu kali za kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) zimetajawa katika Qur-aan na Sunnah lakini watu wengi bado wanamshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى)!  

 

 

 

 

 

 

Share

049-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Swalaah Husafisha Madhambi Kama Anavyojisafisha Mtu Anapooga

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  49

Swalaah Husafisha Madhambi Kama Anavyojisafisha Mtu Anapooga

Alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ جَابِرٍ (رضي الله عنه) قَالَ:  قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((مَثَلُ الصَّلَوَاتِ الْخَمْسِ كَمَثَلِ نَهْرٍ جَارٍ غَمْرٍ عَلَى بَابِ أَحَدِكُمْ يَغْتَسِلُ مِنْهُ كُلَّ يَوْمٍ خَمْسَ مَرَّاتٍ)) مسلم  

 

 Kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mfano wa Swalaah tano ni kama mfano wa mto uliojaa maji mengi upitao mbele ya mlango wa mmoja wenu, anaoga mara tano kwa siku)). [Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Bainisho la umuhimu wa Swalaah za fardhi, na Aayah nyingi zimetaja maamrisho ya Swalaah.

 

 

 [Rejea: An-Nisaa (4: 103), Al-Baqarah (2: 43), An-Nuwr (24: 56), Ar-Ruwm (30: 31)].

 

 

2. Swalaah husafisha madhambi madogo madogo kama maji yanavyoondosha uchafu mwilini.

 

وَأَقِمِ الصَّلَاةَ طَرَفَيِ النَّهَارِ وَزُلَفًا مِّنَ اللَّيْلِ ۚ إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ۚ ذَٰلِكَ ذِكْرَىٰ لِلذَّاكِرِينَ﴿١١٤﴾

Na simamisha Swalaah katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku; hakika mema yanaondosha maovu. Hivyo ni ukumbusho kwa wanaokumbuka. [Huwd (11: 114)]

 

 

 3. Muumin anahifadhika kutenda maasi, kwani siku nzima kuna vipindi vya Swalaah vinavyomsubiri asimamishe Swalaah, kwa hiyo Swalaah ni kinga ya maasi. [Al-‘Ankabuwt (29: 45)].

 

 

4. Hadiyth inatoa mfano miongoni mwa  mifano ya kulingana, kubainisha, na kufahamisha jambo fulani.

 

 

5. Hikma ya maneno ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika kufunza Maswahaba zake kwa kupiga mifano mizuri iliyo sahali kufahamika kwao na kwetu sisi tunaposoma Hadiyth kama hizi. 

 

 

 

Share

050-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kafiri Analipwa Duniani Aakhirah Hatopata Kitu, Na Muumin Analipwa Duniani Na Aakhirah

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 50

Kafiri Analipwa Duniani Aakhirah Hatopata Kitu,

Na Muumin Analipwa Duniani Na Aakhirah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَنَسِ (رضي الله عنه) عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَال: ((إِنَّ الْكَافِرَ إِذَا عَمِلَ حَسَنَةً أُطْعِمَ بِهَا طُعْمَةً مِنْ الدُّنْيَا، وَأَمَّا الْمُؤْمِنُ فَإِنَّ اللَّهَ يَدَّخِرُ لَهُ حَسَنَاتِهِ فِي الأَخِرَةِ وَيُعْقِبُهُ رِزْقًا فِي الدُّنْيَا عَلَى طَاعَتِهِ)) 

وفي رواية: ((إِنَّ اللَّهَ لاَ يَظْلِمُ مُؤْمِنًا حَسَنَةً يُعْطَى بِهَا فِي الدُّنْيَا وَيُجْزَى بِهَا فِي الأَخِرَةِ.  وَأَمَّا الْكَافِرُ فَيُطْعَمُ بِحَسَنَاتِ مَا عَمِلَ بِهَا لِلَّهِ فِي الدُّنْيَا حَتَّى إِذَا أَفْضَى إِلَى الأَخِرَةِ لَمْ يَكُنْ لَهُ حَسَنَةٌ يُجْزَى بِهَا)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika kafiri anapotenda ‘amali nzuri hulipwa mwonjo duniani. Ama Muumin, Allaah Humwekea mema yake Aakhirah na Anamlipa rizki duniani kwa utiifu wake)).

 

Na katika riwaayah: ((Hakika Allaah Hamdhulumu Muumin kwa mema yake, hupewa duniani [kheri zaidi] na hulipwa Aakhirah. Ama kafiri, huonjeshwa duniani kwa mema yake aliyoyatenda kwa ajili ya Allaah mpaka akifika Aakhirah hatakuwa na jema la kulipwa)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Tofauti kubwa baina ya malipo ya kafiri na Muumin, na Waumini daima ndio watakaofaulu kwa kulipwa mema zaidi.

 

 

2. Vipimo vya Allaah (سبحانه وتعالى) katika kulipa ‘amali kutokana na niyyah na ‘Aqiydah ya mtu.

 

 

3. Kafiri hulipwa mema yake duniani; ima kwa ziada ya mali yake au kukingwa na shari, lakini Aakhirah hana sehemu yoyote. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 مَن كَانَ يُرِيدُ حَرْثَ الْآخِرَةِ نَزِدْ لَهُ فِي حَرْثِهِ ۖ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرْثَ الدُّنْيَا نُؤْتِهِ مِنْهَا وَمَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ﴿٢٠﴾

Yeyote yule aliyekuwa anataka mavuno ya Aakhirah Tunamzidishia katika mavuno yake; na yeyote yule aliyekuwa anataka mavuno ya dunia, Tutampa humo, lakini Aakhirah hatokuwa na fungu lolote. [Ash-Shuwraa (42: 20)]

 

 [Rejea pia:  Al-Muuminuwn (23: 55-56)].

 

 

 4. Kafiri hata akitenda ‘amali nzuri zenye uzito mno, juhudi zake ni za bure hazina thamani mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُم بِالْأَخْسَرِينَ أَعْمَالًا ﴿١٠٣﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Je, Tukujulisheni wenye kukhasirika mno kwa ‘amali?”

 

الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا ﴿١٠٤﴾

Ni wale ambao wamepoteza juhudi zao katika uhai wa dunia, na huku wao wakidhani kwamba wanapata mazuri kwa matendo yao.

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ وَلِقَائِهِ فَحَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَلَا نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَزْنًا ﴿١٠٥﴾

Hao ni wale waliozikanusha Aayaat za Rabb wao na kukutana Naye basi zimeporomoka ‘amali zao; hivyo Hatutowasimamishia Siku ya Qiyaamah uzito wowote. 

 

ذَٰلِكَ جَزَاؤُهُمْ جَهَنَّمُ بِمَا كَفَرُوا وَاتَّخَذُوا آيَاتِي وَرُسُلِي هُزُوًا ﴿١٠٦﴾

Hivyo ndio jazaa yao Jahannam kwa yale waliyoyakufuru na kuchukulia mzaha Aayaat Zangu na Rusuli Wangu. [Al-Kahf (18: 103-106)]

 

[Rejea pia: Al-Israa (17: 18)].

 

 

5. Muumin juhudi zake zinathaminiwa na anapata faida ya kulipwa duniani na Aakhirah malipo mema zaidi. [Rejea: Al-Israa (17: 19-20)].

 

 

6. Allaah (سبحانه وتعالى) Hamdhulumu mja ‘amali yake hata ndogo vipi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ ۖ وَإِن تَكُ حَسَنَةً يُضَاعِفْهَا وَيُؤْتِ مِن لَّدُنْهُ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿٤٠﴾

Hakika Allaah Hadhulumu hata uzito au chembe (au sisimizi). Na ikiwa ni ‘amali njema Huizidisha na Hutoa kutoka Kwake ujira adhimu.  [An-Nisaa (4: 40)]

 

[Rejea pia: Fusw-swilat (41: 46), Al-Zalzalah (99: 7), Yuwnus (10: 61), Al-Anbiyaa (21: 47)].

 

 

7. Allaah (سبحانه وتعالى) Anamlipa Muumin mara kumi zaidi kwa kitendo kimoja.

 

مَن جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا ۖ وَمَن جَاءَ بِالسَّيِّئَةِ فَلَا يُجْزَىٰ إِلَّا مِثْلَهَا وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ ﴿١٦٠﴾

Atakayekuja kwa ‘amali njema basi atapata (thawabu) kumi mfano wa hiyo. Na Atakayekuja kwa ovu basi hatolipwa ila mfano wake, nao hawatodhulumiwa. [Al-An’aam (: 160)]

 

 

 

Share

051-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Muumin Anahimiza Jeneza Lake, Kafiri Anakhofia Na Kupiga Mayoe!

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 51

Muumin Anahimiza Jeneza Lake, Kafiri Anakhofia Na Kupiga Mayowe!

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيَّ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِذَا وُضِعَتْ الْجِنَازَةُ وَاحْتَمَلَهَا النَّاسُ – أوِ الرِّجَالُ عَلَى أَعْنَاقِهِمْ، فَإِنْ كَانَتْ صَالِحَةً قَالَتْ: قَدِّمُونِي. وَإِنْ كَانَتْ غَيْرَ صَالِحَةٍ قَالَتْ: يَا وَيْلَهَا! أَيْنَ يَذْهَبُونَ بِهَا؟ يَسْمَعُ صَوْتَهَا كُلُّ شَيْءٍ إلاَّ الإِنْسَانَ وَلَوْ سَمِعَهُ صَعِقَ)) البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Linapowekwa jeneza na likabebwa na watu au wanaume shingoni mwao, basi anapokuwa [maiti] ni mwema husema: Nikadimisheni [nitangulizeni]. Lakini ikiwa si mtu mwema husema: Ole wake! Wanalipeleka wapi? Sauti yake inasikika na kila kitu isipokuwa binaadamu. Na lau angeisikia angelizimia)). [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Muumin anatamani ayafikie mema aliyoahidiwa na Allaah (سبحانه وتعالى) baada ya kufariki kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَعَدَ اللَّـهُ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَمَسَاكِنَ طَيِّبَةً فِي جَنَّاتِ عَدْنٍ ۚوَرِضْوَانٌ مِّنَ اللَّـهِ أَكْبَرُ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ﴿٧٢﴾

Allaah Amewaahidi Waumini wanaume na Waumini wanawake Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo na makazi mazuri katika Jannaat za kudumu milele. Na radhi kutoka kwa Allaah ndio kubwa zaidi. Huko ndiko kufuzu adhimu. [At-Tawbah (9: 72)]

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 122), Al-Maaidah (5: 9), At-Tawbah (9: 111), Luqmaan (31: 8-9), Az-Zumar (39: 20)

 

 

2. Kafiri au mtu muovu anakhofia adhabu aliyotishiwa nayo ambayo hakuiamini duniani.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَوْ تَرَىٰ إِذِ الظَّالِمُونَ فِي غَمَرَاتِ الْمَوْتِ وَالْمَلَائِكَةُ بَاسِطُو أَيْدِيهِمْ أَخْرِجُوا أَنفُسَكُمُ ۖ الْيَوْمَ تُجْزَوْنَ عَذَابَ الْهُونِ بِمَا كُنتُمْ تَقُولُونَ عَلَى اللَّـهِ غَيْرَ الْحَقِّ وَكُنتُمْ عَنْ آيَاتِهِ تَسْتَكْبِرُونَ ﴿٩٣﴾

Na lau ungeliona madhalimu pale wakiwa katika mateso makali ya mauti, na Malaika wamenyosha mikono yao (wakiwaambia): “Toeni nafsi zenu! Leo mnalipwa adhabu ya kudhalilisha kwa yale mliyokuwa mkiyasema juu ya Allaah pasi na haki, na mlikuwa mkitakabari kuhusu Aayaat Zake.” [Al-An’aam (6: 93)]

 

Na pia:

 

وَعَدَ اللَّـهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ هِيَ حَسْبُهُمْ ۚ وَلَعَنَهُمُ اللَّـهُ ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّقِيمٌ﴿٦٨﴾

Allaah Amewaahidi wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na makafiri moto wa Jahannam, ni wenye kudumu humo; unawatosheleza Na Allaah Amewalaani, na watapata adhabu ya kudumu.  [At-Tawbah (9: 68)]

 

Rejea pia:  Al-Jaathiyah (45: 28)

 

 

3. Ni Sunnah kuharakiza Jeneza.

 

 

4. Jeneza linabebwa na wanaume na si wanawake.

 

 

5. Baadhi ya sauti zinasikika kwa viumbe isipokuwa binaadamu na pia vitu vinginevyo visivyokuwahai. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِنَّكَ لَا تُسْمِعُ الْمَوْتَىٰ وَلَا تُسْمِعُ الصُّمَّ الدُّعَاءَ إِذَا وَلَّوْا مُدْبِرِينَ ﴿٥٢﴾

Basi hakika wewe huwezi kusikilizisha wafu, na wala huwezi kusikilizisha viziwi wito wanapokengeua wakigeuza migongo yao. [Ar-Ruwm (30: 52)]

 

Rejea pia: An-Naml (27: 80)

 

 

6. Dalili kwamba maiti anasikia ila hawezi kuongea.

 

 

7. Uthibitisho wa hali ya maisha ya Barzakh na matokeo ya adhabu za kaburi au neema zake.

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

052-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Muumin Angelijua Adhabu Za Allaah Asingelitarajia Jannah, Kafiri Angelijua Rahma Ya Allaah Asingelikata Tamaa Nayo

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 52

Muumin Angelijua Adhabu Za Allaah Asingelitarajia Jannah,

Kafiri Angelijua Rahma Ya Allaah Asingelikata Tamaa Nayo

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لَوْ يَعْلَمُ الْمُؤْمِنُ مَا عِنْدَ اللَّهِ مِنْ الْعُقُوبَةِ مَا طَمِعَ بِجَنَّتِهِ أَحَدٌ. وَلَوْ يَعْلَمُ الْكَافِرُ مَا عِنْدَ اللَّهِ مِنْ الرَّحْمَةِ مَا قَنَطَ مِنْ جَنَّتِهِ أَحَدٌ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Lau Muumin angalijua adhabu zilioko kwa Allaah, hakuna yeyote angelitarajia kuingia katika Jannah Yake. Na Lau kafiri angalijua Rahma zilioko kwa Allaah, hakuna yeyote angekata tamaa ya Jannah Yake)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kukhofia adhabu za Allaah (سبحانه وتعالى) na kutaraji Rahma Zake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

غَافِرِ الذَّنبِ وَقَابِلِ التَّوْبِ شَدِيدِ الْعِقَابِ ذِي الطَّوْلِ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ إِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Mwenye kughufuria dhambi, Anayepokea tawbah, Mkali wa kuakibu, Mwenye wingi wa Ukarimu, hakuna Mwabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake ndio mahali pa kuishia. [Ghaafir (40: 3)

 

Rejea pia: Al-Maaidah (5: 98), Az-Zumar (39: 53).

 

 

2. Muumin anapaswa kuwa katika hali ya khofu na matarajio hata anapotenda mema. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):  

 

وَالَّذِينَ يُؤْتُونَ مَا آتَوا وَّقُلُوبُهُمْ وَجِلَةٌ أَنَّهُمْ إِلَىٰ رَبِّهِمْ رَاجِعُونَ ﴿٦٠﴾

Na ambao wanatoa vile walivyopewa na huku nyoyo zao zinakhofu kwamba hakika watarejea kwa Rabb wao.

 

أُولَـٰئِكَ يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَهُمْ لَهَا سَابِقُونَ ﴿٦١﴾

Hao wanakimbilia katika mambo ya kheri; na wao ndio wenye kuyatanguliza.  [Al-Muuminuwn (23: 60-61)]

 

 

3. Muumin anatakiwa akimbilie kutenda mema apate Rahma na malipo mema ya Rabb wake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ يَرْجُونَ رَحْمَتَ اللَّـهِ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢١٨﴾

Hakika wale walioamini na wale waliohajiri na wakapigana jihaad katika njia ya Allaah, hao wanataraji rahmah ya Allaah, na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Baqarah (2: 218)]

 

 

4. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni pana mno, na adhabu Yake ni kali mno. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَالَ عَذَابِي أُصِيبُ بِهِ مَنْ أَشَاءُ ۖ وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ فَسَأَكْتُبُهَا لِلَّذِينَ يَتَّقُونَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَالَّذِينَ هُم بِآيَاتِنَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٥٦﴾

 (Allaah) Akasema: “Adhabu Yangu Nitamsibu nayo Nimtakaye. Na rahmah Yangu imeenea kila kitu. Basi Nitawaandikia wale wenye taqwa na wanaotoa Zakaah na ambao wao wanaziamini Aayaat (ishara, dalili) Zetu.” [Al-A’raaf (6: 156)]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل رَّبُّكُمْ ذُو رَحْمَةٍ وَاسِعَةٍ وَلَا يُرَدُّ بَأْسُهُ عَنِ الْقَوْمِ الْمُجْرِمِينَ ﴿١٤٧﴾

Wakikukadhibisha (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم); basi sema: “Rabb wenu ni Mwenye rahmah iliyoenea. Na wala haizuiliwi adhabu Yake kwa watu wahalifu.” [Al-An’aam (6: 147)]

 

 

Rejea pia: Al-A’raaf (7: 56).

 

 

5. Allaah (سبحانه وتعالى) Amewapa fursa makafiri wataraji Rahma na Jannah Yake, lakini ni chaguo lao kukubali haki au kubakia katika upotofu.

 

 

6. Jannah imejaa mazuri yasiyoweza kutambulikana katika akili ya binaadamu. Hadiyth: Al-Qudsiy: ((Nimewatayarishia waja Wangu wema kile ambacho jicho lolote halijapata kuona, na sikio lolote halijapata kusikia, na wala haijapata kupita katika moyo wa binaadamu)). [Al-Bukhaariy na Muslim]  Akasema Abuu Hurayrah: Kwa hivyo, soma ukitaka: ((Basi nafsi yoyote haijui  yaliyofichiwa katika yanayoburudisha macho)). [As-Sajdah (32: 17)]

 

 

7. Moto wa Jahannam na adhabu zake ni kali mno. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

فَالَّذِينَ كَفَرُوا قُطِّعَتْ لَهُمْ ثِيَابٌ مِّن نَّارٍ يُصَبُّ مِن فَوْقِ رُءُوسِهِمُ الْحَمِيمُ ﴿١٩﴾

Basi wale waliokufuru watakatiwa nguo za moto watamwagiwa juu ya vichwa vyao maji yachemkayo.

 

يُصْهَرُ بِهِ مَا فِي بُطُونِهِمْ وَالْجُلُودُ ﴿٢٠﴾

Yatayeyusha kwayo (maji hayo) yaliyomo matumboni mwao na ngozi zao.

 

وَلَهُم مَّقَامِعُ مِنْ حَدِيدٍ ﴿٢١﴾

Na watapata marungu ya vyuma.

 

كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا مِنْ غَمٍّ أُعِيدُوا فِيهَا وَذُوقُوا عَذَابَ الْحَرِيقِ ﴿٢٢﴾

Kila watakapotaka kutoka humo kwa dhiki, watarudishwa humo; na (wataambiwa): “Onjeni adhabu ya kuunguza.” [Al-Hajj (22: 19-22)]

 

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 560, Ibraahiym (14: 15-17), (49-50), Al-Muuminuwn (23: 103-108), Al-Furqaan (25:  65), Asw-Swaaffaat (37: 62-68), Ad-Dukhaan (44: 43-50)  

 

 

  

 

Share

053-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayelia Kwa Kumkhofu Allaah Hatoingia Motoni

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 53

Anayelia Kwa Kumkhofu Allaah Hatoingia Motoni

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ يَلِجُ النَّارَ رَجُلٌ بَكَى مِنْ خَشْيَةِ اللَّهِ حَتَّى يَعُودَ اللَّبَنُ فِي الضَّرْعِ. ولاَ يَجْتَمِعُ غُبَارٌ فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَدُخَانُ جَهَنَّمَ)) رواه الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hatoingia motoni mtu anayelia kwa sababu ya kumkhofu Allaah mpaka maziwa yarudi katika chuchu. Wala haliwezi kujumuika vumbi katika Njia ya Allaah na moshi wa Jahannam)). [At-Tirmdihiy na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Chozi la kumkhofu Allaah (سبحانه وتعالى) lina fadhila kubwa ya kuepushwa na moto.

 

 

2. Mifano anayopiga Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم ) ni ya aina ya pekee yenye mazingatio makubwa, sawa na mifano Anayopiga Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan kama Anavyosema:

 

وَلَقَدْ ضَرَبْنَا لِلنَّاسِ فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ مِن كُلِّ مَثَلٍ لَّعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٧﴾

Na kwa yakini Tumewapigia watu mifano ya kila aina katika hii Qur-aan ili wapate kukumbuka.

 

قُرْآنًا عَرَبِيًّا غَيْرَ ذِي عِوَجٍ لَّعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ ﴿٢٨﴾

Qur-aan ya Kiarabu isiyokuwa kombo ili wapate kuwa na taqwa. [Az-Zumar (39: 27-28)]

 

Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ صَرَّفْنَا لِلنَّاسِ فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ مِن كُلِّ مَثَلٍ فَأَبَىٰ أَكْثَرُ النَّاسِ إِلَّا كُفُورًا ﴿٨٩﴾

Na kwa yakini Tumesarifu namna kwa namna hii Qur-aan kwa watu, kwa kila mfano, lakini watu wengi wamekataa kabisa (haki; hawakukubali) isipokuwa kukufuru tu. [Al-Israa (17: 89)]

 

Na pia Anasema (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ صَرَّفْنَا فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ لِلنَّاسِ مِن كُلِّ مَثَلٍ ۚ وَكَانَ الْإِنسَانُ أَكْثَرَ شَيْءٍ جَدَلًا ﴿٥٤﴾

Na kwa yakini Tumesarifu namna kwa namna katika hii Qur-aan kwa watu, kwa kila mifano. Lakini binaadamu amezidi kuliko kila kitu kwa ubishi. [ Al-Kahf: 54]

 

Baadhi ya mifano hiyo Aliyoipiga Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan: Al-Baqarah (2: 261-266) Al-A’raaf (7: 40), (175-177), Yuwnus (10: 24), Ibraahiym (14: 24-27), An-Nahl (16: 75-76), Al-Hajj (22: 73), An-Nuwr (24: 35), (39-40), Az-Zumar (39: 29), Al-Hadiyd (57: 20), Al-‘Ankabuwt (29: 41), Huwd (11: 24), Al-Jumu’ah (62: 5)].

 

 

3. Umuhimu wa Muislamu kufahamu kauli za Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan, na anapoisoma awe anazingatia na kupata mafunzo pamoja na mawaidha, na imzidishie iymaan hata atokwe na machozi khasa pale anapopitia adhabu Zake aingiwe na khofu kwazo.

 

 

4. Fadhila za mtu kutoka ili kupigana katika Njia ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Share

054-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Maiti Anafuatiliwa Na Matatu: Ahli Zake, Mali Na Amali, Zinabaki Amali

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 54

Maiti Anafuatiliwa Na Matatu: Ahli Zake, Mali Na ‘Amali Zinabaki Naye Amali Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَنَسِ (رضي الله عنه) قَال: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((يَتْبَعُ الْمَيِّتَ ثَلاَثَةٌ: أَهْلُهُ وَمَالُهُ وَعَمَلُهُ. فَيَرْجِعُ اثْنَانِ وَيَبْقَى واحِدٌ: يَرِجِعُ أَهْلُهُ وَمَالُهُ وَيَبْقَى عَمَلُهُ)) متفق عليه

 

 Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Maiti hufuatwa na mambo matatu: ahli zake, mali yake, na ‘amali zake. Hurejea mawili na likabakia moja. Ahli zake na mali yake hurejea, na zikabakia ‘amali zake)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. ‘Amali njema anazozitanguliza mtu ni kheri yake kuliko anayoyaacha nyuma, na ‘amali hizi ndizo zitakazodumu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 مَا عِندَكُمْ يَنفَدُ ۖ وَمَا عِندَ اللَّـهِ بَاقٍ ۗ وَلَنَجْزِيَنَّ الَّذِينَ صَبَرُوا أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٩٦﴾

Mlivyo navyo nyinyi vinatoweka, na vilioko kwa Allaah ni vya kubakia. Na kwa yakini Tutawalipa wale waliosubiri ujira wao kwa mazuri zaidi ya yale waliyokuwa wakitenda. [An-Nahl 16: 96)]

 

 

2. Kila mmoja ataingia kaburini peke yake, ataacha kila kitu nyuma yake ila ‘amali zake ndizo zitakazomfaa zikiwa ni njema. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

وَلَقَدْ جِئْتُمُونَا فُرَادَىٰ كَمَا خَلَقْنَاكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَتَرَكْتُم مَّا خَوَّلْنَاكُمْ وَرَاءَ ظُهُورِكُمْ ۖ  

  Na kwa yakini mmetujia mmoja mmoja kama Tulivyokuumbeni mara ya kwanza; na mmeyaacha nyuma yenu yote Tuliyokuruzukuni.  [Al-An’aam (6: 94]

 

 

Rejea pia: Maryam (19: 95).

 

Na Rejea: Hadiyth namba (1).

 

 

3. Muumin anapasa akimbilie kutenda ‘amali njema nyingi zimfae Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَانِ إِلَّا مَا سَعَىٰ ﴿٣٩﴾

Na kwamba insani hatopata (jazaa) isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi.

 

وَأَنَّ سَعْيَهُ سَوْفَ يُرَىٰ ﴿٤٠﴾

Na kwamba juhudi yake itakuja kuonekana

 

ثُمَّ يُجْزَاهُ الْجَزَاءَ الْأَوْفَىٰ ﴿٤١﴾

Kisha atalipwa jazaa kamilifu. [An-Najm (53: 39-41)]

 

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 133), Al-Hadiyd (57: 21), Al-Hashr 59: 18), Al-Baqarah (2: 110), Al-Muddath-thir (74: 74).

 

 

4. Wanaobaki nyuma ya maiti iwe ni funzo kwao watambue kwamba nao bila shaka siku moja watapelekwa kaburini.

 

 

5. Rejea Hadiyth namba (8) (63) (72), (78). 

 

 

 

Share

055-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Matendo Ya Aliyeneemeshwa Na Aliye Na Shida Duniani Ndiyo Yenye Kuzingatiwa Aakhirah

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 55

Matendo Ya Aliyeneemeshwa Na Aliye Na Shida Duniani

Ndiyo Yenye Kuzingatiwa Aakhirah

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يُؤْتَى بِأَنْعَمِ أَهْلِ الدُّنْيَا مِنْ أَهْلِ النَّارِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ، فَيُصْبَغُ فِي النَّارِ صَبْغَةً ثُمَّ يُقَالُ: يَا ابْنَ آدَمَ! هَلْ رَأَيْتَ خَيْرًا قَطُّ؟ هَلْ مَرَّ بِكَ نَعِيمٌ قَطُّ؟ فَيَقُولُ لاَ وَاللَّهِ يَا رَبِّ! وَيُؤْتَى بِأَشَدِّ النَّاسِ بُؤْسًا فِي الدُّنْيَا مِنْ أَهْلِ الْجَنَّةِ، فَيُصْبَغُ صَبْغَةً فِي الْجَنَّةِ، فَيُقَالُ لَهُ: يَا ابْنَ آدَمَ! هَلْ رَأَيْتَ بُؤْسًا قَطُّ؟ هَلْ مَرَّ بِكَ شِدَّةٌ قَطُّ؟ فَيَقُولُ لاَ وَاللَّهِ يَا رَبِّ مَا مَرَّ بِي بُؤْسٌ قَطُّ ولاَ رَأَيْتُ شِدَّةً قَطُّ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Siku ya Qiyaamah ataletwa mtu wa motoni katika watu wa dunia aliyeneemeshwa neema nyingi mno, ataingizwa motoni kidogo kisha atatolewa: Ataulizwa: Ee mwana Aadam!  Je, umeona kheri yoyote? Ushawahi kuneemeka aslan? Atajibu: Hapana Wa-Allaahi Rabb wangu! Na ataletwa mtu aliyekuwa ana shida mno duniani katika watu wa Jannah. Ataingizwa Jannah kidogo kisha atatolewa. Ataulizwa: Ee mwana Aadam! Je, umeona shida yoyote? Ushawahi kutaabika aslan? Atajibu: Hapana Wa-Allaahi Rabb wangu! Haikunipitia shida yoyote abadan, wala sikuona taabu yoyote abadan)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Bishara kwa Muumin masikini kuhusu neema za Jannah yenye kudumu.

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ هُمْ خَيْرُ الْبَرِيَّةِ ﴿٧﴾

Hakika wale walioamini na wakatenda mema, hao ndio wema kabisa wa viumbe.

 

 

جَزَاؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًاۖ رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُۚ ذَٰلِكَ لِمَنْ خَشِيَ رَبَّهُ ﴿٨﴾

Jazaa yao iko kwa Rabb wao; Jannaat za kudumu milele zipitazo chini yake mito ni wenye kudumu humo abadi. Allaah Ataridhika nao, nao wataridhika Naye; hayo ni kwa yule anayemkhofu Rabb wake.  [Al-Bayyinah (98: 7-8)]

 

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (2: 14-15), At-Tawbah (9: 20-22) (72), Huwd (11: 108), Az-Zukhruf (43: 33-35).

 

 

2. Onyo kwa kafiri au muovu aliyetajiri kwamba Aakhirah kuna adhabu ya kudumu.

 

Rejea: An-Nahl (16: 117), Aal-‘Imraan (3: 197), Luqmaan (31: 23-24).

 

 

3. Aliye na shida, dhiki na taabu yoyote duniani, ni bishara kwake avute subira na atende mema apate starehe ya milele Aakhirah, kwani maisha ya dunia si lolote si chochote. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَمَا هَـٰذِهِ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَهْوٌ وَلَعِبٌ ۚ وَإِنَّ الدَّارَ الْآخِرَةَ لَهِيَ الْحَيَوَانُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿٦٤﴾

Na huu uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni pumbao na mchezo; na hakika Nyumba ya Aakhirah bila shaka hiyo ndiyo yenye uhai wa kweli hasa (wa milele), lau wangelikuwa wanajua! [Al-‘Ankabuwt (29: 64)].

 

 

 4. Funzo kwa mtu muovu aliye na mali, utajiri, na ukwasi kwamba starehe yake na mali haitamfaa kitu au kumuokoa na moto. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

 “Siku hayatofaa mali wa watoto.

 

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

 “Isipokuwa yule atakayemfikia Allaah na moyo uliosalimika. [Ash-Shu’araa (26: 88-89)].

 

 

Rejea pia: Aal-’Imraan (3: 91), Al-Maaidah (5: 36), Al-Kahf (18: 46).

 

 

5. Maisha ya dunia si lolote si chochote, bali ni starehe ya muda tu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اعْلَمُوا أَنَّمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا لَعِبٌ وَلَهْوٌ وَزِينَةٌ وَتَفَاخُرٌ بَيْنَكُمْ وَتَكَاثُرٌ فِي الْأَمْوَالِ وَالْأَوْلَادِ ۖ كَمَثَلِ غَيْثٍ أَعْجَبَ الْكُفَّارَ نَبَاتُهُ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَاهُ مُصْفَرًّا ثُمَّ يَكُونُ حُطَامًا ۖ وَفِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ شَدِيدٌ وَمَغْفِرَةٌ مِّنَ اللَّـهِ وَرِضْوَانٌ ۚ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿٢٠﴾

Jueni kwamba uhai wa dunia ni mchezo na pumbao na mapambo, na kufakharishana baina yenu na kushindana kukithiri katika mali na watoto; ni kama mfano wa mvua inayowafurahisha wakulima mimea yake, kisha yananyweya, basi utayaona yamepiga manjano, kisha yanakuwa mabua yaliyonyauka na kupondekapondeka.  Na Aakhirah kuna adhabu kali, na maghfirah kutoka kwa Allaah na radhi. Na uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni sterehe fupi za kughuri. [Al-Hadiyd (57: 20)]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 185), Ar-Ra’d (13: 26)].

 

 

6. Muumin ajitahidi kuchuma mema apate Jannah ya Neema na raha tupu.

 

 

7. Umasikini na utajiri duniani ni mtihani tu kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى), hivyo mwana Aadam asidanganyike na maisha yake.

 

 

Share

056-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Masikini Amtazame Aliye Chini Yake Wala Asitazame Aliye Juu Yake

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 56

Masikini Amtazame Aliye Chini Yake Wala Asitazame Aliye Juu Yake

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((انْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ أَسْفَلَ مِنْكُمْ وَلاَ تَنْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ فَوْقَكُمْ فَإِنَّهُ أَجْدَرُ أَنْ لاَ تَزْدَرُوا نِعْمَةَ اللَّهِ عَلَيْكُمْ)) متفق عليه وهذا لفظ مسلم.

 وفي رواية البخاري: ((إِذَا نَظَرَ أَحَدُكُمْ إِلَى مَنْ فُضِّلَ عَلَيْهِ فِي الْمَالِ وَالْخَلْقِ فَلْيَنْظُرْ إِلَى مَنْ هُوَ أَسْفَلَ مِنْهُ))

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mtazameni aliye chini yenu wala msimtazame aliye juu yenu, kwani [kufanya hivyo] ni haki zaidi msije  mkazidharau neema za Allaah juu yenu))[ Al-Bukhaariy na Muslim] Hii ni lafdhi ya Muslim.

 

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: ((Anapomtazama mmoja wenu aliyefadhilishwa zaidi kwa mali na umbo, basi amtazame aliye chini yake)).

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hikma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kujaaliwa baadhi ya watu matajiri, na baadhi yao masikini na kuwafadhalisha wengine juu ya wengineo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَنْ أَرَادَ الْآخِرَةَ وَسَعَىٰ لَهَا سَعْيَهَا وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَأُولَـٰئِكَ كَانَ سَعْيُهُم مَّشْكُورًا ﴿١٩﴾

Na anayetaka Aakhirah na akaifanyia juhudi inayostahiki kufanyiwa, naye ni Muumin, basi hao juhudi zao ni za kushukuriwa. 

كُلًّا نُّمِدُّ هَـٰؤُلَاءِ وَهَـٰؤُلَاءِ مِنْ عَطَاءِ رَبِّكَ ۚ وَمَا كَانَ عَطَاءُ رَبِّكَ مَحْظُورًا ﴿٢٠﴾

Wote hao Tunawakunjulia; hawa na hao katika hiba za Rabb wako. Na hazikuwa hiba za Rabb wako zenye kuzuiliwa.

انظُرْ كَيْفَ فَضَّلْنَا بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ ۚ وَلَلْآخِرَةُ أَكْبَرُ دَرَجَاتٍ وَأَكْبَرُ تَفْضِيلًا ﴿٢١﴾

Tazama vipi Tunavyowafadhilisha baadhi yao juu ya wengineo. Na bila shaka Aakhirah ni yenye daraja kubwa zaidi na fadhila kubwa zaidi. [Al-Israa 17: 19-21)]

 

 

2. Ni bora kumtazama aliye chini katika mambo ya mali duniani. Ama mas-alah ya Dini, ni jambo zuri kumtazama aliye juu ili Muislamu apate kujihimiza na kushindana kutenda ‘amali au kujifunza na amfikie nduguye huyo.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَيْسُوا سَوَاءً ۗ مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ أُمَّةٌ قَائِمَةٌ يَتْلُونَ آيَاتِ اللَّـهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَهُمْ يَسْجُدُونَ ﴿١١٣﴾

Hawako sawa sawa; miongoni mwa Ahlil-Kitaabi wako watu wenye kusimama (kwa utiifu) wanasoma Aayaat za Allaah nyakati za usiku na wao wanasujudu (katika Swalaah).

 

يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَيُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَأُولَـٰئِكَ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴿١١٤﴾

Wanamwamini Allaah na Siku ya Mwisho na wanaamrisha mema na wanakataza munkari na wanakimbilia katika mambo ya kheri, na hao ni miongoni mwa Swalihina.

 

وَمَا يَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَلَن يُكْفَرُوهُ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِالْمُتَّقِينَ ﴿١١٥﴾

Na kheri yoyote waifanyayo hawatokanushiwa (thawabu zake).  Na Allaah ni Mjuzi wa wenye taqwa.  [Aal-‘Imraan (3: 113-115)]

 

Rejea pia: Al-Muttwaffifiyn (83: 26), Al-Muuminuwn (23: 60-61).

 

 

3. Kumtazama aliye chini husaidia kukumbuka neema za Allaah (سبحانه وتعالى) na kushukuru kwa majaaliwa.

 

 

4. Haitakiwi kutamani kwa wivu na husda neema alizojaaliwa mwengine, bali ni kumshukuru na kumwomba Allaah (سبحانه وتعالى). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَلَا تَتَمَنَّوْا مَا فَضَّلَ اللَّـهُ بِهِ بَعْضَكُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ ۚ لِّلرِّجَالِ نَصِيبٌ مِّمَّا اكْتَسَبُوا ۖ وَلِلنِّسَاءِ نَصِيبٌ مِّمَّا اكْتَسَبْنَ ۚوَاسْأَلُوا اللَّـهَ مِن فَضْلِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴿٣٢﴾

Wala msitamani ambayo Allaah Amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine. Wanaume wanayo sehemu katika waliyoyachuma, na wanawake wana sehemu katika waliyoyachuma. Na muombeni Allaah fadhila Zake. Hakika Allaah daima ni Mjuzi wa kila kitu. [An-Nisaa (4: 32)]

 

Rejea pia: An-Nahl (16: 71).

 

 

5. Kumtazama aliye juu hupelekea kukufuru neema za Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

 

 

 

 

Share

057-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Dunia Ni Jela Kwa Muumin, Kafiri Kwake Ni Kama Jannah (Pepo)

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 57

Dunia Ni Jela Kwa Muumin, Kwa Kafiri Kwake Ni Kama Jannah (Pepo) 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الدُّنْيَا سِجْنُ الْمُؤْمِنِ وَجَنَّةُ الْكَافِرِ)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Dunia ni jela ya Muumin, na ni Pepo Ya Kafiri)) [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Muumin ameharamishwa asivuke mipaka kwa ajili ya matamanio yasiyo ya halali ya kidunia, bali astarehe kwa mazuri aliyohalalishiwa, hivyo huwa kama yuko jela. Ama kafiri, yeye yuko huru kufanya lolote linalomshawishi katika matamanio yake kwa vile anapendelea zaidi maisha ya dunia.

 

 

[Al-A’raaf: 32, Huwd: 15-16, Ar-Ra’d: 26, An-Nahl: 107-109].

 

 

2. Muumin huko Jannah atakuwa huru kutembea atakako. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَسِيقَ الَّذِينَ اتَّقَوْا رَبَّهُمْ إِلَى الْجَنَّةِ زُمَرًا ۖ حَتَّىٰ إِذَا جَاءُوهَا وَفُتِحَتْ أَبْوَابُهَا وَقَالَ لَهُمْ خَزَنَتُهَا سَلَامٌ عَلَيْكُمْ طِبْتُمْ فَادْخُلُوهَا خَالِدِينَ﴿٧٣﴾

Na wataendeshwa wale waliomcha Rabb wao kuelekea Jannah makundi-makundi, mpaka watakapoifikia na ikafunguliwa milango yake, na watasema walinzi wake: “Salaamun ‘Alaykum! Amani iwe juu yenu furahini na iingieni ni wenye kudumu.”

 

 

وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي صَدَقَنَا وَعْدَهُ وَأَوْرَثَنَا الْأَرْضَ نَتَبَوَّأُ مِنَ الْجَنَّةِ حَيْثُ نَشَاءُ ۖ فَنِعْمَ أَجْرُ الْعَامِلِينَ﴿٧٤﴾

Watasema: “AlhamduliLLaahi, Himidi Anastahiki Allaah Ambaye Ametuhakikishia kweli ahadi Yake, na Ameturithisha ardhi tunakaa popote katika Jannah tutakapo”. Basi uzuri ulioje ujira wa watendao. [Az-Zumar: 73-74]

 

 Rejea pia: Al-Kahf (18: 107-108).

 

Ama kafiri, yeye atakuwa jela yaani motoni, na hatoweza kutoka wala kubadilisha hali yake ya adhabu.

 

Rejea: Ghaafir (40: 47-50), Az-Zukhruf 43: 74-78), Al-Muuminuwn (23: 103-108), Ash-Shuwraa (42: 44).

 

 

 3. Dunia ni jela kwa Muumin kulingana na Jannah ya neema za kudumu Aliyoahidi Allaah (سبحانه وتعالى).

 

وَأَمَّا الَّذِينَ سُعِدُوا فَفِي الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ ۖ عَطَاءً غَيْرَ مَجْذُوذٍ﴿١٠٨﴾

Na ama wale walio furahani, basi watakuwa katika Jannah, ni wenye kudumu humo zitakavyodumu mbingu na ardhi isipokuwa Atakavyo Rabb wako. Ni hiba isiyokatizwa. [Huwd (11: 108)]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 14-15), At-Tawbah (9: 20-22) (72), Az-Zukhruf (43: (33-35), Al-Bayyinah (98: 7-8).

 

Lakini dunia ni Jannah kwa kafiri kulingana na adhabu ya kudumu Aliyoahidi Allaah (سبحانه وتعالى) Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَا يَغُرَّنَّكَ تَقَلُّبُ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي الْبِلَادِ ﴿١٩٦﴾

Isikudanganye kabisa kutangatanga kwa wale waliokufuru katika nchi.

 

مَتَاعٌ قَلِيلٌ ثُمَّ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۚ وَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴿١٩٧﴾ 

Ni starehe ndogo, kisha makazi yao ni Jahannam. Na ni mahala pabaya mno pa kupumzikia. [Aal-‘Imraan (3196-197)]

 

 

Rejea pia: An-Nahl (16: 117), Luqmaan: (31:23-24).

 

 

4. Muumin anatakiwa asiwe mwenye mapenzi makubwa ya dunia na starehe zake, bali awe na shauku ya kupenda nyumba ya kudumu ya Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا أُوتِيتُم مِّن شَيْءٍ فَمَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَزِينَتُهَا ۚ وَمَا عِندَ اللَّـهِ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ ۚ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿٦٠﴾

Na chochote mlichopewa katika vitu, basi ni starehe za uhai wa dunia na mapambo yake. Na yaliyoko kwa Allaah ni bora zaidi na yakubakia. Je, basi hamtii akilini? [Al-Qaswasw (28: 60)]

 

 

Rejea: Aal-‘Imraan (3: 14), Al-An’aam (6: 32), Al-Hadiyd (57: 20), Al-‘Ankabuwt (29: 64), Al-Kahf (18: 46), Ash-Shuwraa (42: 36), Ghaafir (40: 39), Az-Zukhruf (43: 33-35). 

 

 

Share

058-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Ishi Duniani Kama Mgeni Au Mpita Njia

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 58

Ishi Duniani Kama Mgeni Au Mpita Njia

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) قَالَ أَخَذَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ بِمَنْكِبِي فَقَالَ: ((كُنْ فِي الدُّنْيَا كَأَنَّكَ غَرِيبٌ أَوْ عَابِرُ سَبِيلٍ)). وَكَانَ ابْنُ عُمَرَ يَقُولُ: "إِذَا أَمْسَيْتَ فلاَ تَنْتَظِرْ الصَّبَاحَ وَإِذَا أَصْبَحْتَ فلاَ تَنْتَظِرْ الْمَسَاءَ وَخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِمَرَضِكَ وَمِنْ حَيَاتِكَ لِمَوْتِكَ"  البخاري

 

 Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alinikamata mabega yangu akasema: ((Kuwa duniani kama mgeni au mpita njia)). Na Ibn ‘Umar alikuwa akisema: “Utakapofika jioni usingojee asubuhi, na ukipambaukiwa usingojee jioni. Na chukua siha yako kabla ya maradhi yako, na uhai wako kabla ya kufa kwako.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kumkamata ‘Abdullaah bin ‘Umar mabegani ni dalili ya mapenzi yake kwa Maswahaba wake na pia inadhihirisha umuhimu wa jambo analotaka kumwarifu.

 

 

2. Kuishi duniani ni kama mgeni apitaye njia, kwani dunia si ya kudumu, bali Aakhirah ndio yenye maisha ya kudumu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا هَـٰذِهِ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَهْوٌ وَلَعِبٌ ۚ وَإِنَّ الدَّارَ الْآخِرَةَ لَهِيَ الْحَيَوَانُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿٦٤﴾

Na huu uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni pumbao na mchezo; na hakika Nyumba ya Aakhirah bila shaka hiyo ndiyo yenye uhai wa kweli hasa (wa milele), lau wangelikuwa wanajua! [Al-‘Ankabuwt (29: 64)].

 

Na Allaah (سبحانه وتعالى) Amepiga mfano mzuri wa maisha ya dunia Anaposema:

 

 

وَاضْرِبْ لَهُم مَّثَلَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا كَمَاءٍ أَنزَلْنَاهُ مِنَ السَّمَاءِ فَاخْتَلَطَ بِهِ نَبَاتُ الْأَرْضِ فَأَصْبَحَ هَشِيمًا تَذْرُوهُ الرِّيَاحُ ۗوَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقْتَدِرًا ﴿٤٥﴾

Na wapigie mfano wa uhai wa dunia kama maji Tuliyoyateremsha kutoka mbinguni, yakachanganyika kwayo mimea ya ardhi (ikasitawi), kisha yakawa makavu yaliyovurugika yanapeperushwa na pepo. Na Allaah daima juu ya kila kitu ni Mwenye Uwezo wa juu kabisa. [Al-Kahf (18: 45)]

 

 

3. Mgeni anayepita njia kuelekea aendako bila shaka amejitayarisha kubeba mahitajio yake, hali kadhalika mwana Aadam anahitaji kujibebea masurufu kuelekea safari ya Aakhirah, na masurufu bora kabisa ni taqwa.

 

Rejea: Al-Baqarah (2: 197).

 

 

4. Kukimbilia kufanya ‘amali njema na kutokufanyia usiri kwa kukhofia mauti yamfike mtu kabla ya kudiriki kutena hizo ‘amali. Mfano wa kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) na kutoa sadaka Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ﴿٩﴾

  Enyi walioamini! Zisikupurukusheni mali zenu na wala watoto wenu mkaacha kumdhukuru Allaah. Na yeyote atakayefanya hivyo basi hao ndio waliokhasirika.

 

 

وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ﴿١٠﴾

  Na toeni katika yale Tuliyokuruzukuni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti akasema: “Rabb wangu! Lau Ungeliniakhirisha mpaka muda wa karibu hivi, basi ningetoa swadaqah na ningelikuwa miongoni mwa Swalihina.”

 

وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا ۚ وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١١﴾

  Lakini Allaah Haiakhirishi kamwe nafsi yeyote inapokuja ajali yake na Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo. Al-Munaafiquwn  (63: 9-11)

 

 

Rejea pia: Ibraahiym (14: 31), Al-Baqarah (2: 254).

 

 

5. Siha na uhai ni neema mbili kwa Muumin apasazo kuzitumia kwa kutenda mema yatakayomfaa Aakhirah.

 

Rejea Hadiyth namba (9).

 

 

6. Hili ni fundisho kuwa tusikae duniani kama kwamba tutaishi milele.

 

 

7. Haifai kwa Muislamu kuifadhilisha dunia juu ya Aakhirah yake.

 

Rejea Hadiyth namba (57), (59), (60), (62).

 

 

8. Umuhimu wa kuutumia muda wako vyema hapa duniani.

 

 

 

Share

059-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuipa Mgongo Dunia Kutampatia Mtu Mapenzi Ya Allaah Pamoja Na Ya Watu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake) 

Hadiyth Ya 59

Kuipa Mgongo Dunia Kutampatia Mtu Mapenzi Ya Allaah Pamoja Na Ya Watu

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ السَّاعِدِيِّ (رضي الله عنه)  قَالَ: أَتَى النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ رَجُلٌ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، دُلَّنِي عَلَى عَمَلٍ إِذَا أَنَا عَمِلْتُهُ أَحَبَّنِي اللَّهُ وَأَحَبَّنِي النَّاسُ.  فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((ازْهَدْ فِي الدُّنْيَا يُحِبَّكَ اللَّهُ وَازْهَدْ فِيمَا فِي أَيْدِي النَّاسِ يُحِبُّوكَ)) إبن ماجه وغيره بأسانيد حسنة

 

Imepokelewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad As-Saa’idiyy (رضي الله عنه) amesema: “Alikuja mtu kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: “Ee Rasuli wa Allaah! Nijulishe ‘amali ambayo nikiifanya Allaah Atanipenda na watu pia watanipenda.” Akasema: ((Ipe mgongo dunia Allaah Atakupenda, na vipe mgongo vilivyomo kwa watu, watu watakupenda)). [Ibn Maajah na wengineo kwa isnaad Hasan]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kuipa mgongo dunia (zuhd) ni miongoni mwa sifa za Maswahaba na watu Wema waliopita mfano mmojawapo wa mwenye sifa hii ni Swahaba mtukufu Abu Dharr Al-Ghaffaariy (رضي الله عنه).

 

 

 2. Umuhimu wa kupata mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Rejea Hadiyth namba (44), (85).

 

 

Pia Hadiyth ya Al-Qudsiy Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema: ((Yeyote yule atakayefanya uadui kwa walii Wangu, Nitatangaza vita dhidi yake. Mja Wangu hanikaribii na kitu chochote Ninachokipenda kama ‘amali Nilizomfaradhishia, na mja Wangu huzidi kunikaribia kwa ‘amali njema za Sunnah ili  Nimpende. Ninapompenda, Huwa masikio yake yanayosikilizia, macho yake anayoonea, mikono yake anayopigania, miguu yake anayotembelea nayo, lau angeniomba kitu bila shaka Ningempa, lau angeniomba himaya bila shaka Ningelimkinga, na Sisiti juu ya kitu chochote kama Ninavyosita [kuichukua] roho ya mja Wangu Muumin: Anachukia mauti, Nami Nachukia kumdhuru)). [Al-Bukhaariy]

 

 

3. Kukinai na rizki ya halali aliyoruzukiwa mtu na kuridhika nayo baada ya kufanya juhudi ya kutafuta na kuifanyia kazi.

 

Rejea: Al-Maaidah (5: 88).

 

 

4. Mazuri yote yaliyomo duniani; mali, mapambo n.k. thamani yake iwe katika mkono wa mtu na si moyoni mwake. Wala asiathirike mtu na dunia bali aathirike na Aakhirah na  iwe ndio lengo lake, kwani huko ndiko kwenye maisha ya kudumu: Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 بَلْ تُؤْثِرُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا ﴿١٦﴾

Bali mnakhiari uhai wa dunia.

 

وَالْآخِرَةُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ ﴿١٧﴾

Na hali Aakhirah ni bora zaidi ya kudumu. [Al-A’laa (87: 16-17).

 

 

 

5. Kutosheka na kutokutafuta rizki ya haramu, na kuzuia nafsi matamanio yake, na kushukuru ya halali na kuitolea sadaka katika Njia ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Rejea: [Al-Baqarah (2: 172), An-Nahl (16: 114).

 

 

6. Kuipa dunia mgongo (zuhd) si kwa umasikini na kujidhalilisha kuwa daruweshi na mavazi mabovu na kutembea bila viatu na kubeba mitasbihi mikubwa na uvivu, bali ni kuikinaisha nafsi na kuizuia isitamani ya dunia bali itamani ya Aakhirah.

 

 

7. Kuridhia mja kwa alichopewa pasi na kutamani vya watu, kwani kutamani vya watu ni njia moja ya kupatikana kwa mizozo na ukhalifu duniani.

 

Rejea Hadiyth namba: (57), (58), (60) (62).  

 

 

 

 

 

Share

060-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Ingelikuwa Dunia Sawa Na Bawa La Mbu, Allaah Asingelimnywesha kafiri maji.

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 60

Ingelikuwa Dunia Sawa Na Bawa La Mbu, Allaah Asingelimnywesha Kafiri Maji

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لَوْ كَانَتْ الدُّنْيَا تَعْدِلُ عِنْدَ اللَّهِ جَنَاحَ بَعُوضَةٍ مَا سَقَى كَافِرًا مِنْهَا شَرْبَةَ مَاءٍ)) رواه الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ingelikuwa [thamani ya] dunia ni sawasawa na bawa la mbu mbele ya Allaah, Asingelimnywesha kafiri hata tama moja la maji)). [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Dunia haina thamani yoyote mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) hata kama imejaa mazuri vipi. Thamani yake ni kama bawa la mbu mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

اعْلَمُوا أَنَّمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا لَعِبٌ وَلَهْوٌ وَزِينَةٌ وَتَفَاخُرٌ بَيْنَكُمْ وَتَكَاثُرٌ فِي الْأَمْوَالِ وَالْأَوْلَادِ ۖ كَمَثَلِ غَيْثٍ أَعْجَبَ الْكُفَّارَ نَبَاتُهُ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَاهُ مُصْفَرًّا ثُمَّ يَكُونُ حُطَامًا ۖ وَفِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ شَدِيدٌ وَمَغْفِرَةٌ مِّنَ اللَّـهِ وَرِضْوَانٌ ۚ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿٢٠﴾

Jueni kwamba uhai wa dunia ni mchezo na pumbao na mapambo, na kufakharishana baina yenu na kushindana kukithiri katika mali na watoto; ni kama mfano wa mvua inayowafurahisha wakulima mimea yake, kisha yananyweya, basi utayaona yamepiga manjano, kisha yanakuwa mabua yaliyonyauka na kupondekapondeka.  Na Aakhirah kuna adhabu kali, na maghfirah kutoka kwa Allaah na radhi. Na uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni sterehe fupi za kughuri. [Al-Hadiyd (57: 20)]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 14-15).

 

 

2. Neema anazozichuma mtu duniani hazitomfaa isipokuwa anayezifanya kuwa ni za maisha yake ya kupita njia tu, na akapandikiza mema ili achume Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَن كَانَ يُرِيدُ حَرْثَ الْآخِرَةِ نَزِدْ لَهُ فِي حَرْثِهِ ۖ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرْثَ الدُّنْيَا نُؤْتِهِ مِنْهَا وَمَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ﴿٢٠﴾

Yeyote yule aliyekuwa anataka mavuno ya Aakhirah Tunamzidishia katika mavuno yake; na yeyote yule aliyekuwa anataka mavuno ya dunia, Tutampa humo, lakini Aakhirah hatokuwa na fungu lolote. [Ash-Shuwraa (42: 20)]

 

Rejea Hadiyth namba (58), (62).

 

 

3. Rizki zote hata maji zinakutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

4. Kudhalilishwa kwa kafiri.

 

 

5. Mbu ni kitu dhalili mno na kinachochukiza, na Allaah (سبحانه وتعالى) Amekipendelea kukipigia mfano kwa maadui wake.

 

 

6. Mwerevu ni yule anayetambua hakika ya jambo akaogopa kitu kinachochukiwa na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

 

Share

061-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Dunia Ni Kama Kivuli Anachokitumia Msafiri Kwa Muda Tu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake) 

Hadiyth Ya  61 

Dunia Ni Kama Kivuli Anachokitumia Msafiri Kwa Muda Tu

Alhidaaya.com

 

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ابن مسعود (رضي الله عنه)  قَال:  نَامَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَلَى حَصِيرٍ فَقَامَ وَقَدْ أَثَّرَ فِي جَنْبِهِ، فَقُلْنَا يَا رَسُولَ اللَّهِ! لَوْ اتَّخَذْنَا لَكَ وِطَاءً.  فَقَالَ:  ((مَا لِي وَمَا لِلدُّنْيَا؟ مَا أَنَا فِي الدُّنْيَا إِلاَّ كَرَاكِبٍ اسْتَظَلَّ تَحْتَ شَجَرَةٍ ثُمَّ رَاحَ وَتَرَكَهَا))  الترمذي وقال: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه)  amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alilala kwenye jamvi la mtende likamfanyia alama ubavuni mwake tukasema: Ee Rasuli wa Allaah! Tukufanyie godoro laini?  Akasema: ((Mimi na dunia wapi? Mfano wangu na dunia ni kama mpandaji [anayesafiri kwa mnyama] aliyepumzika kivulini chini ya mti, [muda mfupi tu] kisha akaondoka na kukiacha)). [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Dhihirisho la zuhd ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), yaani kuipa mgongo dunia.

 

 

2. Mapenzi na huruma za Maswahaba kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kama yeye vile anavyowapenda na kuwaonea huruma. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 لَقَدْ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِكُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِتُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُم بِالْمُؤْمِنِينَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ﴿١٢٨﴾

 

Kwa yakini amekujieni Rasuli anayetokana na nyinyi wenyewe, yanamtia mashaka (na huzuni) yanayokutaabisheni, anakujalini, mwenye huruma kwa Waumini ni mwenye huruma mno, mwenye rahmah. [At-Tawbah (9: 1280]

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّـهِ ۚ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ

 Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ni Rasuli wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi dhidi ya makafiri; wanahurumiana baina yao [Al-Fat-h (48: 29)]

 

 

3. Maisha ya dunia ni nyumba ya kupita, na maisha ya Aakhirah ndiyo ya milele. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا هَـٰذِهِ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَهْوٌ وَلَعِبٌ ۚ وَإِنَّ الدَّارَ الْآخِرَةَ لَهِيَ الْحَيَوَانُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿٦٤﴾

Na huu uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni pumbao na mchezo; na hakika Nyumba ya Aakhirah bila shaka hiyo ndiyo yenye uhai wa kweli hasa (wa milele), lau wangelikuwa wanajua! [Al-‘Ankabuwt (29: 64)]

 

 

Rejea pia: Al-An’aam (6: 32), Ghaafir (40: 39).

 

Rejea Hadiyth namba (58), (60).

 

 

4. Kujihimiza kujenga Aakhirah kwa ‘amali njema.

 

 

5. Mifano ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) yenye hikma, busara, mazingatio na mafunzo mazito.

 

 

6. Ni vizuri kutoa mifano ili kufahamisha jambo lieleweke kwa undani na kuzidisha iymaan ya mtu.

 

 

 

Share

062-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Sadaka Haipunguzi Mali, Msamaha Unazidisha Utukufu, Na Kunyenyekea Kunampandisha Mtu Daraja

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake) 

Hadiyth Ya 62

Sadaka Haipunguzi Mali, Msamaha Unazidisha Utukufu,

Na Kunyenyekea Kunampandisha Mtu Daraja

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا نَقَصَتْ صَدَقَةٌ مِنْ مَالٍ،  وَمَا زَادَ اللَّهُ عَبْدًا بِعَفْوٍ إلاَّ عِزًّا، وَمَا تَوَاضَعَ أَحَدٌ لِلَّهِ إِلاَّ رَفَعَهُ اللَّهُ عَزَّ وَ جَلَّ)) مسلم

                                                                                                

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kutoa sadaka hakupunguzi mali, Allaah Humzidishia mja ‘izzah (utukufu) kwa ajili ya kusamehe kwake.  Na   yeyote anayenyenyekea kwa ajili ya Allaah, Allaah Aliyetukuka Atampandisha Daraja [Atamtukuza].  [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kila anapotoa mtu sadaka, ndipo Allaah (سبحانه وتعالى) Anapomuongezea au Humlipa malipo mema Aakhirah, kwani Ameahidi hivyo kama Anavyosema:

 

مَّن ذَا الَّذِي يُقْرِضُ اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا فَيُضَاعِفَهُ لَهُ وَلَهُ أَجْرٌ كَرِيمٌ ﴿١١﴾

Nani ambaye atamkopesha Allaah karadha nzuri kisha (Allaah) Amuongezee maradufu na apate ujira mtukufu. [Al-Hadiyd (57: 11)]

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 245),  (261), Al-Anfaal (8: 60), At-Tawbah (9: 121), Sabaa (34: 39), At-Taghaabun (64: 17).

 

 

2. Kutoa katika Njia ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni miongoni mwa sifa za Muumin.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٢﴾

Hakika Waumini ni wale ambao Anapotajwa Allaah, nyoyo zao zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali.

 

الَّذِينَ يُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ﴿٣﴾

Ambao wanasimamisha Swalaah na katika yale Tuliyowaruzuku hutoa.

 

أُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُؤْمِنُونَ حَقًّا ۚ لَّهُمْ دَرَجَاتٌ عِندَ رَبِّهِمْ وَمَغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ﴿٤﴾

Hao ndio Waumini wa kweli!  Wana daraja (za Jannah) kwa Rabb wao na maghfirah na riziki karimu. [Al-Anfaal (8: 2-4)]

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 1-5), (265), (274), Aal-‘Imraan (3: 134),  At-Tawbah (9: 111), Al-Hajj (22: 35), As-Sajdah (32: 16), Ash-Shuwraa (42: 38), Adh-Dhaariyaat (51: 19), Al-Ma’aarij (70: 24).

 

 

 

3. Waliobashiriwa Jannah miongoni mwa Maswahaba; Abuu Bakr, ‘Umar, ‘Uthmaan bin ‘Affaan, ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Awf (رضي الله عنهم) walitoa mali zao kwa wingi na walizidi kupata kheri na Baraka.

 

4. Kusamehe ni miongoni mwa sifa za Muumin zinazomrejeshea faida mwenyewe. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي السَّرَّاءِ وَالضَّرَّاءِ وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾ 

Ambao wanatoa (kwa ajili ya Allaah) katika hali ya wasaa na katika hali ya shida, na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-‘Imraan (3: 134)]

 

Rejea pia: An-Nuwr 24: 22) (134).

 

5. Kunyenyekea ni sifa kuu miongoni mwa sifa za Muumin inayompandisha daraja mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

6. Kunyenyekea ni dalili ya kutokuwa na kiburi, na ni ufunguo wa Jannah.

 

Rejea Hadiyth namba (66).

 

 

Share

063-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Jiepushe Na Shaka, Kwani Halaal Na Haraam Imebainishwa, Moyo Ni Mfalme Wa Viungo

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 63

Jiepushe Na Shaka, Kwani Halaal Na Haraam Imebainishwa, Moyo Ni Mfalme Wa Viungo

Alhidaaya.com

 

 

           

عَن النُّعْمَانَ بْنَ بَشِيرٍ (رضي الله عنهما) قَال: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:  ((الْحَلاَلُ بَيِّنٌ وَالْحَرَامُ بَيِّنٌ، وَبَيْنَهُمَا مُتَشَابِهَاتٌ لاَ يَعْلَمُهَا كَثِيرٌ مِنَ النَّاسِ، فَمَنْ اتَّقَى الشُّبُهَاتِ اسْتَبْرَأَ  لِدِينِهِ وَعِرْضِهِ،  وَمَنْ وَقَعَ فِي الشُّبُهَاتِ وَقَعَ فِي الْحَرَامِ،  كَالرَّاعِي يَرْعَى حَوْلَ الْحِمَى َيُوشِكُ أَنْ يَرْتَعْ فِيهِ، أَلاَ وَإِنَّ لِكُلِّ مَلِكٍ حِمًى،  أَلاَ وَإِنَّ حِمَى اللَّهِ مَحَارِمُهُ، أَلاَ وَإِنَّ فِي الْجَسَدِ مُضْغَةً إِذَا صَلَحَتْ صَلَحَ الْجَسَدُ كُلُّه، وَإِذَا فَسَدَتْ فَسَدَ الْجَسَدُ كُلُّهُ أَلاَ وَهِيَ الْقَلْبُ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr  (رضي الله عنهما) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Hakika halaal iko wazi na haraam iko wazi. Baina ya mawili hayo mna yenye kutia shaka. Wengi miongoni mwa watu hawayajui. Basi atakayejiepusha yenye kutia shaka, atakuwa amejiepushia shaka katika Dini yake na heshima yake. Na Atakayetumbukia katika yenye kutia shaka, ataingia kwenye haraam. Kama mchunga anayechunga kando ya mipaka, ni haraka kulisha humo [mpaka mwingine wa watu]. Zindukeni!  Kila mfalme ana mipaka. Zindukeni! Kwa yakini mipaka ya Allaah ni haraam Alizoziharamisha. Zindukeni! Kwa yakini katika mwili mna kinofu [cha nyama], kinapokuwa sahihi, mwili wote unakuwa sahihi. Kinapoharibika, mwili wote unaharibika. Zindukeni! Kinofu hicho ni moyo)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Dini ya Kiislamu imefunza na kubainisha kila jambo na shariy’ah zake. Hakuna jambo lililoachwa. 

 

 

Rejea pia: An-Nahl (16: 89).

 

 

 

2. Himizo la kufuata yaliyo halaal na kujiepusha na yaliyo haraam.

 

 

3. Kutokufuata matamanio ya nafsi na kujiepusha na mambo yenye shaka kwani huenda yakampeleka mtu kuingia katika ya haraam. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 هُوَ الَّذِي أَنزَلَ عَلَيْكَ الْكِتَابَ مِنْهُ آيَاتٌ مُّحْكَمَاتٌ هُنَّ أُمُّ الْكِتَابِ وَأُخَرُ مُتَشَابِهَاتٌ ۖ فَأَمَّا الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِمْ زَيْغٌ فَيَتَّبِعُونَ مَا تَشَابَهَ مِنْهُ ابْتِغَاءَ الْفِتْنَةِ وَابْتِغَاءَ تَأْوِيلِهِ ۗ وَمَا يَعْلَمُ تَأْوِيلَهُ إِلَّا اللَّـهُ ۗ وَالرَّاسِخُونَ فِي الْعِلْمِ يَقُولُونَ آمَنَّا بِهِ كُلٌّ مِّنْ عِندِ رَبِّنَا ۗ وَمَا يَذَّكَّرُ إِلَّا أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٧

Yeye Ndiye Aliyeteremsha kwako Kitabu humo mna Aayaat zenye maana wazi, hizo ndio msingi wa Kitabu, na nyinginezo zisizokuwa wazi maana zake. Basi wale ambao katika nyoyo zao mna upotovu hufuata zile zisizokuwa wazi maana zake kutafuta fitnah (upotofu) na kutafuta maana zake zilofichika, na hakuna ajuae maana zake isipokuwa Allaah. Na wenye msingi madhubuti katika elimu husema: “Tumeziamini, zote ni kutoka kwa Rabb wetu.” Na hawakumbuki ila wenye akili. [Aal-‘Imraan (3: 7)]

 

 

4. Muumin afuate yaliyo na dalili na aache yasiyokuwa na dalili ili ajiepushe na uzushi.

 

 

5. Allaah (سبحانه وتعالى) Ameweka mipaka ya shariy’ah Zake katika kila kitu na Ametahadharisha anayevuka mipaka. Mifano yake ni katika: Al-Baqarah (2: 187), (229), (230), An-Nisaa (4: 13), Al-Mujaadalah (58: 4), At-Twalaaq (65: 1).

 

 

6. Wito wa kuisalimisha nafsi kwa undani nao ni moyo, uwe ni wenye iymaan, taqwa, amani na uliosalimika na kila ovu, kwani Allaah (سبحانه وتعالى) Atatazama katika nyoyo za watu. 

 

Rejea Hadiyth namba (1)

 

 

Rejea pia: Ash-Shu’araa (26: 88-89), Aal-‘Imraan (3: 91), Ghaafir (40: 19), At-Taghaabun (64: 4), Al-Mulk (67: 13).

 

 

7. Moyo ni mfalme wa viungo vyote, hivyo Muislamu anapaswa kuchunga moyo wake daima asifuate matamanio ili athibitike katika yanayomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى). Na hilo litaweza kupatikana tu lau tutayaendea ya ‘Ibaadah na kujiepusha ya haraam.

 

 

8. Kuna umuhimu mkubwa sana wa kuzitakasa nyoyo zetu.

 

 

 

Share

064-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Wema Ni Tabia Njema, Na Dhambi Ni Yenye Shaka Katika Nafsi Na Kuchukizwa Na Watu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 64

Wema Ni Tabia Njema, Na Dhambi Ni Yenye Shaka Katika Nafsi Na Kuchukizwa Na Watu

 

 Alhidaaya.com

 

 

 عَنْ النَّوَّاسِ بْنِ سِمْعَانَ (رضي الله عنه) عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قال: ((الْبِرُّ حُسْنُ الْخُلُقِ وَالإِثْمُ مَا حَاكَ فِي نَفْسِكَ وَكَرِهْتَ أَنْ يَطَّلِعَ عَلَيْهِ النَّاسُ)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa An-Nawwaas bin Sam’aan (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Wema ni tabia njema, na dhambi ni jambo lenye kutia shaka katika nafsi yako na ukachukia watu wasije wakalijua)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Maana ya Al-Birr ni aina zote za wema, hivyo asidharau mtu kufanya jambo lolote la kheri. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّيْسَ الْبِرَّ أَن تُوَلُّوا وُجُوهَكُمْ قِبَلَ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَلَـٰكِنَّ الْبِرَّ مَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالْكِتَابِ وَالنَّبِيِّينَ وَآتَى الْمَالَ عَلَىٰ حُبِّهِ ذَوِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ وَالسَّائِلِينَ وَفِي الرِّقَابِ وَأَقَامَ الصَّلَاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَالْمُوفُونَ بِعَهْدِهِمْ إِذَا عَاهَدُوا ۖ وَالصَّابِرِينَ فِي الْبَأْسَاءِ وَالضَّرَّاءِ وَحِينَ الْبَأْسِ ۗ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ صَدَقُوا ۖوَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُتَّقُونَ ﴿١٧٧﴾ 

Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa Mashariki na Magharibi lakini wema ni mwenye kuamini Allaah na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na akawapa mali juu ya kuipenda kwake jamaa wa karibu na mayatima na masikini na msafiri na waombao na katika kukomboa watumwa na akasimamisha Swalaah, na akatoa Zakaah na watimizao ahadi zao wanapoahidi, na wanaosubiri katika dhiki za ufukara na maafa ya magonjwa na njaa na katika vita. Hao ndio waliosadikisha na hao ndio wenye taqwa. [Al-Baqarah (2: 177)]

 

 

2. Muislamu amesisitizwa kuwa na tabia njema, kwani itampatia manufaa Aakhirah, mojawapo ni kuwa karibu na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) huko Jannah kama ilivyothibiti katika Hadiyth.

 

Rejea Hadiyth namba (66), (127).

 

 

3. Kutambua kitendo cha dhambi ni kwa ishara mbili: Kwanza ni kusitasita katika nafsi, inapasa haraka uepuke nacho kitendo hicho. Pili ni kuchukia au kukhofu watu wengine wasije kujua kuwa unatenda jambo ovu. 

 

 

4. Hadiyth hii ni dalili kwamba nafsi imeumbwa katika "fitwrah" yaani, maumbile ya asili ya Kiislamu; yaani asili ya roho kuwa katika kutakasika bila ya kumuasi Allaah (سبحانه وتعالى).  Anasema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

 ((Kila kinachozaliwa kinazaliwa katika Fitwrah…)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Rejea pia: Al-A’raaf (7: 172).

 

 

5. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwamba Hamhesabii mtu kitendo kiovu kikibakia katika nafsi bila ya kukitenda. Ama pale anapokitenda, ndipo atakapokuwa ameingia katika dhambi. Ni Rahma pia kwamba kila jambo la kheri analolitilia niyyah Muislamu, lina thawabu japo kama hakuwahi kulitenda. Na anapolitenda hupata thawabu mara kumi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَن جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا ۖ وَمَن جَاءَ بِالسَّيِّئَةِ فَلَا يُجْزَىٰ إِلَّا مِثْلَهَا وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ ﴿١٦٠﴾

Atakayekuja kwa ‘amali njema basi atapata (thawabu) kumi mfano wa hiyo. Na Atakayekuja kwa ovu basi hatolipwa ila mfano wake, nao hawatodhulumiwa. [Al-An’aam (6: 160)]

 

Na Hadiyth: ((Allaah Ameandika mema na mabaya. Kisha Akayabainisha. Basi atakayetia niyyah kutenda jema kisha asilifanye, ataandikiwa jema moja kamili. Atakapofanya hima na akalitenda, ataandikiwa mema kumi hadi kuzidi mia saba na ziada nyingi. Na atakayetia niyyah kufanya kitendo kibaya kisha asikifanye, ataandikiwa jema moja kamili. Atakapokifanya, ataandikiwa dhambi moja)).[Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

6. Hadiyth hii ni miongoni mwa zinazojulikana kuwa ni: ‘Jawaami’ul-Kalim’ (Mjumuisho wa maana nyingi katika maneno machache) aliyopewa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

 

Share

065-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Hatoingia Jannah Mwenye Chembe Ya Kiburi; Kukataa Haki Na Kudharau Watu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 65

Hatoingia Jannah Mwenye Chembe Ya Kiburi; Nayo Ni Kukataa Haki Na Kudharau Watu

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ  (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَدْخُلُ الْجَنَّةَ مَنْ كَانَ فِي قَلْبِهِ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ مِنْ كِبْر))  قَالَ رَجُلٌ: إِنَّ الرَّجُلَ يُحِبُّ أَنْ يَكُونَ ثَوْبُهُ حَسَنًا وَنَعْلُهُ حَسَنَةً.  قَالَ:  ((إِنَّ اللَّهَ جَمِيلٌ يُحِبُّ الْجَمَالَ،  الْكِبْرُ بَطَرُ الْحَقِّ وَغَمْطُ النَّاسِ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hatoingia Jannah ambaye moyoni mwake mna kiburi uzito wa chembe (au sisimizi)). Mtu mmoja akauliza: “Mtu hupenda nguo yake iwe nzuri na viatu vyake viwe vizuri [itakuwaje?]” Akasema: ((Hakika Allaah ni Mzuri Anapenda Uzuri. Kiburi ni kukataa haki na kudharau watu)).  [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uovu wa kuwa na kiburi ni sifa mbaya sana Anayoichukia Allaah (سبحانه وتعالى), kwani hata kama mtu ana chembe cha kiburi hatoingia Jannah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿١٨﴾

 “Na wala usiwageuzie watu uso wako kwa kiburi, na wala usitembee katika ardhi kwa maringo, hakika Allaah Hampendi kila mwenye majivuno mwenye kujifakharisha. [Luqmaan  (31: 18)]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿٢٣﴾

na Allaah Hapendi kila mwenye kujinata, anayejifakharisha. [Al-Hadiyd (57: 23)]

 

 

 

Rejea pia:  An-Nisaa (4: 36),  Ghaafir (40: 35).

 

 

 

2. Allaah Anatahadharisha mwenye kiburi kumuingiza Motoni. Hadiyth:

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ هَنَّادٌ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((قَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ الْكِبْرِيَاءُ رِدَائِي وَالْعَظَمَةُ إِزَارِي فَمَنْ نَازَعَنِي وَاحِدًا مِنْهُمَا قَذَفْتُهُ فِي النَّارِ)) أبو داود ، ابن ماجه و أحمد

Kutoka kwa Abu Hurayrah  (رضي الله عنه)    ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema:  ((Allaah Amesema: Kiburi ni joho Langu,  na utukufu ni kanzu Yangu, yule ashindanaye na Mimi katika kimoja katika hayo nitamvurumisha Motoni)) [Abu Daawuwd, Ibn Maajah na Ahmad]

 

 

 

3. Kibri ni maasi ya kwanza kutendwa pale Ibliys alivyofanya kiburi kutokumsujudia Aadam (عليه السلام) na kujiona yeye ni bora zaidi.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

إِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِّن طِينٍ ﴿٧١﴾

Pale Rabb wako Alipowaambia Malaika: “Hakika Mimi Namuumba mtu kutokana na udongo.

 

فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَ ﴿٧٢﴾

 “Basi Nitakapomsawazisha na Nikampuliza humo roho Niliyoiumba; basi mwangukieni kumsujudia.”

 

فَسَجَدَ الْمَلَائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ ﴿٧٣﴾

Wakamsujudia Malaika wote pamoja.

 

إِلَّا إِبْلِيسَ اسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ ﴿٧٤﴾

Isipokuwa Ibliys, alitakabari na akawa miongoni mwa makafiri.

 

 

قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسْجُدَ لِمَا خَلَقْتُ بِيَدَيَّ ۖ أَسْتَكْبَرْتَ أَمْ كُنتَ مِنَ الْعَالِينَ ﴿٧٥﴾

 (Allaah) Akasema: “Ee Ibliys! Nini kilichokuzuia usimsujudie Niliyemuumba kwa Mikono Yangu? Je, umetakabari, au umekuwa miongoni mwa waliojitukuza?”

 

قَالَ أَنَا خَيْرٌ مِّنْهُ ۖ خَلَقْتَنِي مِن نَّارٍ وَخَلَقْتَهُ مِن طِينٍ ﴿٧٦﴾

  (Ibliys) akasema: “Mimi ni bora kuliko yeye, Umeniumba kutokana na moto, naye Umemuumba kutokana na udongo.” [Swaad (38: 75-76)]

 

 

Rejea pia:  Al-Hijr (15: 32-33), Al-A’raaf (7: 12).

 

 

4. Kiburi kinaweza kuwa ni kukataa haki katika shariy’ah za Dini kama alivyokataa Ibliys amri ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

5. Kiburi kinaweza kuwa ni kudharau watu, kujiona, kujigamba, kujifakharisha kwa watu kwa ukabila, uzuri, mavazi, mali, elimu n.k. yote hayamfai mtu kitu Aakhirah akiwa ana chembe ya kiburi moyoni mwake.

 

Rejea Kisa cha Qaaruwn kilichotajwa katika Qur-aan: Al-Qaswasw (28: 76-83)].

 

 

6. Kujipamba na kuvaa mavazi mazuri masafi ni katika mambo mazuri katika Uislamu.

 

Rejea: Al-A’raaf (7: 31-32).

 

 

Share

066-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Nyumba Za Jannah Kwa Mwenye Tabia Njema, Anayeacha Mabishano Na Mjadala Hata Kama ni Mwenye haki, na Anayeacha Uongo

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 66

 

Nyumba Za Jannah Kwa Mwenye Tabia Njema, Anayeacha Mabishano Na Mjadala

Hata Kama ni Mwenye haki, na Anayeacha Uongo

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي أُمَامَةَ البَاهِلي (رضي الله عنه) قَال: قَال رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((أَنَا زَعِيم بَيْت فِي رَبَض الْجَنَّة لِمَنْ تَرَكَ الْمِرَاء وَإِنْ كَانَ مُحِقًّا، وَبِبَيْتٍ فِي وَسَط الْجَنَّة لِمَنْ تَرَكَ الْكَذِب وَإِنْ كَانَ مَازِحًا، وَبِبَيْتٍ فِي أَعْلَى الْجَنَّة لِمَنْ حَسُنَ خُلُقه)) حديث صحيح رواه أبو داود بإسناد صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Umaamah Al-Baahiliy (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:  ((Mimi ni mdhamini wa nyumba ya kando ya Jannah kwa anayeacha mabishano [wenye shaka] hata kama ni mwenye haki, na ni mdhamini wa nyumba iliyo katikati ya Jannah kwa anayeacha uongo japo ni kwa mzaha, na mdhamini wa nyumba iliyo mahala pa juu zaidi ya Jannah kwa ambaye tabia yake ni njema)). [Hadiyth Swahiyh ameipokea Abu Daawuwd isnaad yake ni Swahiyh]

           

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila ya subira pindi mtu anapodhulumiwa lakini akaacha mjadala usioleta manufaa ili kuepusha magomvi, na akasemehe juu ya kwamba ana haki ya kupigania kwa kulipiza kisasi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَجَزَاءُ سَيِّئَةٍ سَيِّئَةٌ مِّثْلُهَا ۖ فَمَنْ عَفَا وَأَصْلَحَ فَأَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ ۚ إِنَّهُ لَا يُحِبُّ الظَّالِمِينَ﴿٤٠﴾ وَلَمَنِ انتَصَرَ بَعْدَ ظُلْمِهِ فَأُولَـٰئِكَ مَا عَلَيْهِم مِّن سَبِيلٍ﴿٤١﴾ إِنَّمَا السَّبِيلُ عَلَى الَّذِينَ يَظْلِمُونَ النَّاسَ وَيَبْغُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ﴿٤٢﴾ وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾

Na jazaa ya uovu ni uovu mfano wake. Lakini atakayesamehe na akasuluhisha, basi ujira wake uko kwa Allaah, hakika Yeye Hapendi madhalimu. Na bila shaka anayelipiza kisasi baada ya kudhulumiwa, basi hao hawana sababu ya kulaumiwa. Hakika sababu ya kulaumiwa ni juu ya wale wanaodhulumu watu na wanakandamiza katika ardhi bila ya haki. Hao watapata adhabu iumizayo.Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa (42: 40-43)]

 

 

 2. Kuacha mzaha na maneno ya upuuzi ni sifa miongoni mwa sifa zitakazompatia Muumin Jannah ya Firdaws [Al-Muuminuwn (23: 1-11)].

 

 

3. Tabia njema ni mzizi wa kumuongoa Muislamu kwa kila upande na kumpatia fadhila za kila aina na malipo makuu kabisa ni ya mwenye tabia njema.

 

 

4. Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم) amesisitiza sana Muislamu kuwa na tabia njema katika Hadiyth kadhaa, na malipo yake si Jannah pekee bali pia ni kuwa karibu naye huko Jannah. Akasema pia katika Hadiyth ifuatayo kuwa yeye ametumwa kwa Ummah huu wa Kiislamu ili kutimiza tabia njema:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ الله عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ‏:‏ ((إِنَّمَا بُعِثْتُ لِأُتَمِّمَ صَالِحَ الأَخْلاقِ‏))

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Hakika nimetumwa ili nikamilishe khulqa (tabia) njema)) [Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy Swahiyh Al-Jaami’ (2349), Swahiyh Adab Al-Mufrad (207)]

 

 

Rejea pia: Hadiyth namba (65), (67), (127).

 

 

5. Fadhila za kuacha uongo ambao unamuingiza mtu katika unafiki na adhabu ya moto hata kama ni kwa mzaha tu.

 

 

6. Tusiwe ni wenye kupuuzia jambo hata tukiliona kuwa ni dogo sana kwa mizani zetu.

 

 

 

 

Share

067-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Sahilisheni, Msifanye Uzito, Wabashirieni Msiwakimbize Watu Katika Dini

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 67

Sahilisheni, Msifanye Uzito, Wabashirieni Msiwakimbize Watu Katika Dini

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَنَسِ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَسِّرُوا وَلاَ تُعَسِّرُوا وَبَشِّرُوا ولاَ تُنَفِّرُوا)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Sahilisheni wala msifanye uzito, wapendekezeni watu kheri na muwabashirie wala msiwakimbize)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Dini yetu ya Kiislamu ni nyepesi ila watu wenyewe wanaitilia uzito. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ ۚ  

Na Hakukufanyieni ugumu wowote ule katika Dini. [Al-Hajj (22: 78)].

 

 

2. Haipasi kuwafanyia Waislamu uzito katika Dini pale mtu anapowalingania (da’wah) ikasababisha kuwakimbiza.  Haipasi hata kwa makafiri pale anapowalingania waingie katika Uislamu, bali anapaswa atumie mawaidha mema na hikma kama Anavyoamrisha Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ وَجَادِلْهُم بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ ۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ ۖ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ﴿١٢٥﴾

Lingania katika njia ya Rabb wako kwa hikmah na mawaidha mazuri. Na jadiliana nao kwa ambayo ni mazuri zaidi. Hakika Rabb wako Yeye Anamjua zaidi aliyepotea njia Yake, Naye Anawajua zaidi waliohidika. [An-Nahl (16: 125)]

 

 

3. Muislamu anapaswa kumbashiria mwenziwe kila la kheri na kumpendelea mazuri.

 

Rejea Hadiyth namba  (21).

 

 

 

4. Hadiyth hii ni dalili ya kwamba Uislamu ni Dini nyepesi na sahali katika amri na fardhi zake na Shariy’ah ambazo hazimkalifishi mtu zaidi ya asiyoyaweza.

 

Rejea Al-Baqarah (2: 185) (286), Al-Maaidah (5: 6), An-Nuwr (24: 61), Al-Fat-h (48: 17), At-Tawbah (9: 91).

 

 

 

5. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) mwenyewe ametumwa kwetu kutusahilishia mambo yetu ya Kidini.

 

Rejea Al-A‘raaf (7: 157).

 

 

 

6. Mtu kujitakia mazito katika Dini ni sababu kuu ya watu kushindwa kutekeleza amri za Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم). Mazito hayo anayojitakia mtu ni kama vile kutenda ‘ibaadah ambazo hazimo katika Shariy’ah, mfano: Kuweka matanga ambayo yanamgharimu mtu kulisha watu. Hali kadhalika kualika watu katika kusherehekea mawlid, kukusanya watu kusoma du’aa pindi mtu kafikwa na jambo fulani, mkusanyiko wa khitma, mkusanyiko wa kumdhukuru Allaah, yote haya ni kujishughulisha katika matendo ambayo anayapotezea mali yake na muda wake. Mali hiyo na muda huo angeliweza kutumia katika yaliyoamrishwa katika Shariy’ah kwa kutoa katika njia ya Allaah, na muda kuutumia katika ‘ibaada zilizo sahihi.

 

 

 

 

 

 

 

Share

068-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuona Hayaa; Kusitahi Ni Katika Iymaan

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake) 

Hadiyth Ya 68

Kuona Hayaa; Kusitahi Ni Katika Iymaan

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ ابن عُمر (رضي الله عنهما)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَرَّ عَلَى رَجُلٍ مِنْ الأَنْصَارِ وَهُوَ يَعِظُ أَخَاهُ فِي الْحَيَاءِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((دَعْهُ فَإِنَّ الْحَيَاءَ مِنْ الإيمَانِ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Umar(رضي الله عنهما)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipita kwa mtu miongoni mwa Answaar akimnasihi nduguye kuhusu kuacha kuona hayaa. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Mwache, kwani hayaa ni katika iymaan)).  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Neno lenyewe la ‘hayaa’ asili yake ni ‘hayaat’ yaani uhai. Na uhai wa mwana Aadam ima ni uhai wa kutenda mazuri au maovu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَنْ عَمِلَ صَالِحًا مِّن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَىٰ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَنُحْيِيَنَّهُ حَيَاةً طَيِّبَةً ۖ وَلَنَجْزِيَنَّهُمْ أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٩٧﴾

Mwenye kutenda mema miongoni mwa wanamume au wanawake naye ni Muumin, Tutamhuisha uhai mzuri, na bila shaka Tutawalipa ujira wao kwa mazuri zaidi ya yale waliyokuwa wakitenda.  [Al-Nahl (16: 97)]

 

 

2. Hayaa imeambatanishwa na iymaan, palipo na hayaa pana iymaan, na palipo na iymaan pana hayaa.

 

 

3. Kila mtu anapokuwa na hayaa zaidi, ndipo iymaan yake inapozidi, kwani anapotaka kufanya kitendo kiovu hukumbuka kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Anamuona japo Yeye hamuoni, na hivyo huona hayaa na huomba maghfirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَالَّذِينَ إِذَا فَعَلُوا فَاحِشَةً أَوْ ظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ ذَكَرُوا اللَّـهَ فَاسْتَغْفَرُوا لِذُنُوبِهِمْ وَمَن يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا اللَّـهُ وَلَمْ يُصِرُّوا عَلَىٰ مَا فَعَلُوا وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴿١٣٥﴾

Na wale ambao wanapofanya machafu au wakajidhulumu nafsi zao (kwa maasi), humdhukuru Allaah wakaomba maghfirah kwa madhambi yao. Na nani anayeghufuria madhambi isipokuwa Allaah. Na hawaendelei katika waliyoyafanya na wao wanajua. [Aal-‘Imraan (3: 135)]

 

Hivyo basi, kutamzidishia mtu taqwa ya hali ya juu na kufikia daraja ya ihsaan.

 

Rejea Hadiyth namba 2 katika Aruba’iyn An-Nawawiy ya Jibriyl kuhusu Uislamu, Iymaan, Ihsaan].

 

4. Hayaa ni aina mbili: Inayohusu Dini na inayohusiana na watu, na baina yake kuna haya nzuri na mbaya.

 

Hayaa nzuri inayohusiana na Dini ni kuacha kutenda jambo linalochukiza mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) au limekatazwa na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

Hayaa mbaya inayohusiana na Dini, ni kuona aibu baada ya kufanya kitendo ambacho Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) wamekikataza.

 

Hayaa nzuri inayohusiana na watu ni kuacha kitendo kinachotia aibu kwa watu kama mke kutokumtolea ujeuri mumewe mbele za watu.

 

Na hayaa mbaya inayohusiana na watu ni kama vile mwanamke kuvaa mavazi yasiyositiri mwili wake na yasiyo ya heshima mbele ya watu.

 

5. Haya isiwe kisingizio cha kutokutenda mema.

 

 

 

 

 

Share

069-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Aliye Na Daraja Mbaya Mno Mbele Ya Allaah Siku ya Qiyaamah Ni Yule Anayeeneza Siri Ya Mkewe

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 69

Aliye Na Daraja Mbaya Mno Mbele Ya Allaah Siku ya Qiyaamah

Ni Yule Anayeeneza Siri Ya Mkewe

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أبي سَعِيدٍ الْخُدْرِيَّ (رضي الله عنه) قَال: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ مِنْ أَشَرِّ النَّاسِ عِنْدَ اللَّهِ مَنْزِلَةً يَوْمَ الْقِيَامَةِ الرَّجُلَ يُفْضِي إِلَى امْرَأَتِهِ وَتُفْضِي إِلَيْهِ ثُمَّ يَنْشُرُ سِرَّهَا)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika mwenye daraja mbaya mno mbele ya Allaah siku ya Qiyaamah, ni mwanamume anayejamiiana na mkewe kisha akaeneza siri yake)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kutoa siri ni miongoni mwa madhambi makubwa. Na Allaah (سبحانه وتعالى) Hamsamehe mwenye kufichua maasi yake ilhali Allaah (سبحانه وتعالى) Amemsitiri. Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عن ابي هُرَيْرَةَ، يَقُولُ سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: (( كُلُّ أُمَّتِي مُعَافًى إِلاَّ الْمُجَاهِرِينَ، وَإِنَّ مِنَ الْمَجَانَةِ أَنْ يَعْمَلَ الرَّجُلُ بِاللَّيْلِ عَمَلاً، ثُمَّ يُصْبِحَ وَقَدْ سَتَرَهُ اللَّهُ، فَيَقُولَ: يَا فُلاَنُ عَمِلْتُ الْبَارِحَةَ كَذَا وَكَذَا، وَقَدْ بَاتَ يَسْتُرُهُ رَبُّهُ وَيُصْبِحُ يَكْشِفُ سِتْرَ اللَّهِ عَنْهُ )) البخاري ‏

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kasema: Nimemisikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Dhambi za Ummah wangu zitasamehewa isipokuwa za Al-Mujaahiriyn [wanaotenda maasi waziwazi au wanaofichua maasi yao kwa watu].  Mfano wa kufichua huko siri ni mtu anayetenda kitendo usiku kisha akaamka hali ya kuwa Allaah Amemsitiri, lakini anasema: “Ee fulani, jana usiku nilitenda kadhaa wa kadhaa.” Ilhalia amekesha usiku akiwa katika sitara ya Rabb wake lakini yeye asubuhi anajifichulia sitara ya Allaah)) [Al-Bukhaariy]

 

 

2. Kuhifadhi haki za mke na mume. Hii inamhusu mke pia ambaye anatakiwa ajilinde yeye sitara yake, na ahifadhi mambo ya mumewe hasa anapokuwa mumewe hayupo naye, na kutokutoa siri zao. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ ۚ

Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi. [An-Nisaa (4: 34)]

 

 

3. Tahadharisho kali la kutangazia siri ya chumbani mwa wanandoa kwamba atapata daraja mbaya mno mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 4. Uislamu unahimiza kuhifadhiana siri baina ya mke na mume na watu kwa ujumla.

 

Rejea Hadiyth namba (23).

 

 

5. Vitendo vya ndoa baina ya mume na mke ni vitendo vya aibu vinavyopasa Muislamu awe na hayaa, na hivyo ni kuthibitisha iymaan yake.

 

Rejea Hadiyth namba (68).

 

 

6. Uovu wa kutoa siri baina ya wanandoa ni mkubwa. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema kuwa mfano wake ni kama wa shaytwaan mwanamme na mwanamke kukutana njiani na kufanya kitendo hicho mbele ya macho ya watu]. [Abuu Daawuwd Taz. Swahiyh Al-Jaami' (7037)]

 

 

 

 

 

Share

070-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Usiwe Mwenye Kuzoea Kufanya ‘Ibaadah Ya Sunnah, Naafilah, Kisha Ukaiacha

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

Hadiyth Ya 70

Usiwe Mwenye Kuzoea Kufanya ‘Ibaadah Ya Sunnah, Naafilah, Kisha Ukaiacha

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ (رضي الله عنهما)  قَالَ: قَالَ لِي رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يَا عَبْدَ اللَّهِ، لاَ تَكُنْ مِثْلَ فلاَنٍ كَانَ يَقُومُ اللَّيْلَ فَتَرَكَ قِيَامَ اللَّيْلِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amru bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما) amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliniambia: ((Ee ‘Abdullaah! Usiwe kama fulani, alikuwa akiamka usiku kuswali akaacha Qiyaamul-layl (kisimamo cha usiku kuswali)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila za kudumisha ‘amali njema japokuwa ni kidogo kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((‘Amali bora kabisa Azipendazo Allaah ni zenye kudumu japokuwa ni chache)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

2. Umuhimu wa kuwa na istiqaamah (msimamo) katika ‘Ibaadah kama Allaah (سبحانه وتعالى) Alivyomuamrisha Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

 وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ﴿٩٩﴾

Na mwabudu Rabb wako mpaka ikufikie yakini (mauti). [Al-Hijr (15: 99)] 

Rejea pia: Fusswilat (41: 30-32), Al-Ahqaaf (46: 13-14), Al-Ma’aarij (70: 23).

 

Rejea pia Hadiyth namba (7)

 

Na pia Hadiyth:

 

 

عن أبي عمر، وقيل: أبي عَمرة سفيان بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: قُلْتُ: يَا رَسُول الله، قُلْ لي في الإسْلامِ قَولًا لا أسْأَلُ عَنْهُ أَحَدًا غَيْرَكَ. قَالَ: ((قُلْ: آمَنْتُ بِاللهِ، ثُمَّ استَقِمْ)). رواه مسلم

Abuu 'Umar na pia imesemwa anajulikana kama: Abuu ‘Amrah Sufyaan bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه)  amesema: Nilimwambia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): Niambie neno katika Uislamu ambalo sitamuuliza yoyote zaidi yako. Akasema: ((Sema: Nimemuamini Allaah, kisha uthibitike imara)) [Muslim]

 

Kwa maana: Kuendelea kufanya ‘Ibaadah na kuwa na msimamo madhubuti katika Dini.

 

 

 

3. Kuacha ‘Ibaadah au ‘amali njema alizozizoea mtu, ni dalili ya kushughulishwa na dunia na kuwa mbali na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

4. Uislamu unapendelea wastani au ukatikati hata katika ‘Ibaadah, ili asijikalifishe mtu au kujichosha. Hadiyth kadhaa zimetajwa makatazo ya kujikalifisha au kufanya ‘ibaadah kwa wingi mno, miongoni mwazo ni:

 

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: دَخَلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم المَسْجِدَ فَإِذَا حَبْلٌ مَمْدُودٌ بَيْنَ السَّارِيَتَيْنِ، فَقَالَ: ((مَا هَذَا الحَبْلُ؟)) قالُوا: هَذَا حَبْلٌ لِزَيْنَبَ، فَإِذَا فَتَرَتْ تَعَلَّقَتْ بِهِ. فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((حُلُّوهُ، لِيُصلِّ أَحَدُكُمْ نَشَاطَهُ فَإِذَا فَتَرَ فَلْيَرْقُدْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

 

Na amepokea Anas (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliingia Masjid, akaona kamba imefungwa baina ya nguzo mbili. Akauliza: ((Kamba hii ni ya nini?)) Wakasema: Hii ni kamba ya Zaynab, anapochoka hujiegemeza kwayo. Basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ifungueni na kila mmoja wenu aswali kwa nguvu zake, atakapochoka alale)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na pia:

 

عن أنس رضي الله عنه قَالَ: جَاءَ ثَلاثَةُ رَهْطٍ إِلَى بُيُوتِ أزْوَاجِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، يَسْأَلُونَ عَنْ عِبَادَةِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا أُخْبِروا كَأَنَّهُمْ تَقَالُّوهَا وَقَالُوا: أَيْنَ نَحْنُ مِنَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم قدْ غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ وَمَا تَأخَّرَ. قَالَ أحدُهُم: أمَّا أنا فَأُصَلِّي اللَّيلَ أبدًا. وَقالَ الآخَرُ: وَأَنَا أصُومُ الدَّهْرَ وَلا أُفْطِرُ. وَقالَ الآخر: وَأَنا أعْتَزِلُ النِّسَاءَ فَلا أتَزَوَّجُ أبَدًا. فجاء رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إليهم، فَقَالَ: ((أنْتُمُ الَّذِينَ قُلْتُمْ كَذَا وَكَذَا؟ أَمَا واللهِ إنِّي لأخْشَاكُمْ للهِ، وَأَتْقَاكُمْ لَهُ، لَكِنِّي أصُومُ وَأُفْطِرُ، وأُصَلِّي وَأَرْقُدُ، وَأَتَزَوَّجُ النِّساءَ، فَمَنْ رَغِبَ عَنْ سُنَّتِي فَلَيْسَ مِنِّي)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Imepokelewa na Anas (رضي الله عنه) kwamba kundi la watu watatu lilikuja katika nyumba za wake wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  wakiuliza kuhusu ‘ibaadah za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).  Walipoelezwa waliziona kama ni kidogo, wakasema: Sisi hatuko sawa na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), yeye ameshaghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia na yatakayokuja. Mmoja wao akasema: Ama mimi, nitaswali daima usiku wote. Mwengine akasema: mimi nitafunga mwaka mzima. Mwengine akasema: Mimi nitawaepuka wanawake, sitaoa kamwe. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akawaendea na kuwauliza: ((Ninyi ndio mliosema kadhaa na kadhaa? Ama wa-Allaahi mimi ninamkhofu Allaah zaidi ya nina taqwa zaidi kulikoni ninyi; lakini mimi ninafunga na kufungua, ninaswali na ninalala, na pia ninaoa wake. Atakayekengeuka na Sunnah zangu basi si katika mimi)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba 12].

 

 

 

 

 

Share

071-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Jikinge Na Moto Japo Kwa Tende Au Neno Jema

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 71

 

Jikinge Na Moto Japo Kwa (Kutoa Swadaqa) Tende Au (Kutamka) Neno Jema

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ عَدِيِّ بْنِ حَاتِمٍ (رضي الله عنه) قَالَ: قَال رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((اتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ فَإِنْ لَمْ تَجِدْ فَبِكَلِمَةٍ طَيِّبَةٍ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Adiyy bin Haatim (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ogopeni moto japo kwa (kutoa swadaqah) nusu tende, na usipopata basi kwa (kutamka) neno jema)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kuogopa na kujikinga na moto kwa kila njia, ikiwa ni kutenda ‘amali kubwa au mno vipi kama mfano wa kutoa sadaka kokwa ya tende au neno jema, kwani moto wa Jahannam ni mkali mno! Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

  

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ عَلَيْهَا مَلَائِكَةٌ غِلَاظٌ شِدَادٌ لَّا يَعْصُونَ اللَّـهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ﴿٦﴾

Enyi walioamini! Jikingeni nafsi zenu na ahli zenu na moto ambao kuni zake ni watu na mawe; juu yake wako Malaika washupavu hawana huruma, shadidi, hawamuasi Allaah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa. [At-Tahriym (66: 6)]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ نَارُ جَهَنَّمَ أَشَدُّ حَرًّا ۚ لَّوْ كَانُوا يَفْقَهُونَ﴿٨١﴾

Sema: “Moto wa Jahannam ni mkali zaidi lau wangelifahamu.” [At-Tawbah (9: 81)]

 

 

 

2.  Yapendeza kutoa sadaka japokuwa kidogo mno na hakipotei chochote kinachotolewa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى), atakuja mja kukikuta katika hesabu yake Siku ya Qiyaamah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأَقْرِضُوا اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا ۚ وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ  

Na mkopesheni Allaah karadhi nzuri. Na chochote kile cha kheri mnachokadimisha kwa ajili ya nafsi zenu, mtakikuta kwa Allaah. Ni bora, na ujira mkubwa zaidi.  [Al-Muzzammil (73: 20)]

 

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 110), (273), Aal-‘Imraan (3: 30),    At-Tawbah (9: 121).

 

 

 

3.   Neno jema ni sadaka anaposhindwa mtu kumpa sadaka muombaji, basi asimkaripie wala asimsimbulie kumfanyia maudhi bali ampe maneno mema. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قَوْلٌ مَّعْرُوفٌ وَمَغْفِرَةٌ خَيْرٌ مِّن صَدَقَةٍ يَتْبَعُهَا أَذًى ۗ وَاللَّـهُ غَنِيٌّ حَلِيمٌ ﴿٢٦٣﴾

Kauli njema na msamaha ni bora kuliko swadaqah inayoifuata udhia. Na Allaah ni Mkwasi, Mvumilivu.

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ كَالَّذِي يُنفِقُ مَالَهُ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ صَفْوَانٍ عَلَيْهِ تُرَابٌ فَأَصَابَهُ وَابِلٌ فَتَرَكَهُ صَلْدًا ۖ لَّا يَقْدِرُونَ عَلَىٰ شَيْءٍ مِّمَّا كَسَبُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٢٦٤﴾

264. Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia kama yule ambaye anatoa mali yake kwa kujionyesha kwa watu wala hamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama jabali juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa ikaliacha tupu. Hawana uwezo juu ya lolote katika waliyoyachuma. Na Allaah Haongoi watu makafiri. [Al-Baqarah (2:263-264)]

 

Rejea pia: Adhw-Dhwuhaa (93: 10).

 

 

 

4.    Kutokudharau au kuacha kutenda jema lolote japo kama ni dogo mno vipi kwa sababu kila kitu kinaandikwa katika Daftari la matendo na mwana Aadam atakuja  kushuhudia kila jambo.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

Basi yule atakayetenda kheri uzito wa chembe (au sisimizi) ataiona.

 

وَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرًّا يَرَهُ ﴿٨﴾

Na yule atakayetenda shari uzito wa chembe (au sisimizi) ataiona. [Al-Zalzalah (99: 7-8)]

 

 

Rejea pia Maryam (19: 76).

 

Na rejea Hadiyth namba (11).

 

 

 

5.    Neno jema linaunganisha nyoyo za Waumini na kujenga mapenzi.

 

Rejea: Aal-‘Imraan (3: 159), na linaweza kumuingiza kafiri katika Uislamu.

 

 

 

6.  Muumin daima ni mtendaji mema, kubwa na dogo, na haachi wala hachoki. Mfano wake ni kama mti mzuri utoao matunda mazuri kila mara kila wakati. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا كَلِمَةً طَيِّبَةً كَشَجَرَةٍ طَيِّبَةٍ أَصْلُهَا ثَابِتٌ وَفَرْعُهَا فِي السَّمَاءِ ﴿٢٤﴾

Je, huoni vipi Allaah Amepiga mfano wa neno zuri kama mti mzuri mizizi yake imethibitika imara na matawi yake yanafika mbinguni? (marefu mno).

 

تُؤْتِي أُكُلَهَا كُلَّ حِينٍ بِإِذْنِ رَبِّهَا ۗ وَيَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٥﴾

Unatoa mazao yake kila wakati kwa idhini ya Rabb wake. Na Allaah Anapiga mifano kwa watu ili wapate kukumbuka.

 

وَمَثَلُ كَلِمَةٍ خَبِيثَةٍ كَشَجَرَةٍ خَبِيثَةٍ اجْتُثَّتْ مِن فَوْقِ الْأَرْضِ مَا لَهَا مِن قَرَارٍ ﴿٢٦﴾

Na mfano wa neno baya ni kama mti mbaya uliong’olewa juu ya ardhi hauna imara. [Ibraahiym (14: 24-26)]

 

Na rejea Hadiyth namba (140) ambayo ni hitimisho ya Hadiyth iliyotoa mfano wa mti mzuri kumlinganisha na Muumini mwenye maneno mema.    

 

 

 

7. Fadhila za kutoa sadaka zimetajwa kwa wingi katika Qur-aan na Sunnah.

 

Rejea Hadiyth namba (31), (62), (77),

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

072-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Enezeni Salaam, Lisheni Chakula, Ungeni Undugu, Swalini Tahajjud, Mtaingia Jannah Kwa Amani

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 72

Enezeni Salaam, Lisheni Chakula, Ungeni Undugu, Swalini Tahajjud,

Mtaingia Jannah Kwa Amani

 

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أبِي يُوسُفَ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ سَلاَمٍ (رضي الله عنه) قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  يَقُول: ((يَا أَيُّهَا النَّاسُ، أَفْشُوا السَّلاَمَ، وَأَطْعِمُوا الطَّعَامَ، وَصِلُوا الأَرْحَامَ، وَصَلُّوا وَالنَّاسُ نِيَامٌ،  تَدْخُلُوا الْجَنَّةَ بِسلاَمٍ)) رواه الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abu Yuwsuf ‘Abdullah bin Salaam  (رضي الله عنه) amesema: “Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Enyi watu! Enezeni [amkianeni kwa] Salaam! Na lisheni chakula, na ungeni undugu [na jamaa wa uhusiano wa damu], na swalini wakati watu wamelala, mtaingia Jannah kwa amani)). [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Maamkizi ya Kiislamu, kulisha watu, kuunga undugu na kuamka usiku kuswali, ni sababu mojawapo ya kumuingiza Muislamu Jannah, nayo ni mambo mepesi kabisa kuyatenda.

 

 

2. Amri, umuhimu na fadhila za kuamkiana kwa maamkizi ya Kiislamu.

 

Rejea:  An-Nisaa (4: 86), An-Nuwr (24: 27-28).

 

Na rejea pia Hadiyth namba (42).

 

Bonyeza Kiungo kifuatacho kwa faida ziyada:

 

Maamkizi Ya Kiislaam: Maamrisho Na Fadhila Zake

 

 

3. Sisitizo na himizo la kulisha maskini. Fadhila zake ni adhimu kama kuingizwa katika neema tele za Allaah (سبحانه وتعالى) huko Jannah.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا﴿٥﴾

Hakika Waumini watendao wema kwa wingi watakunywa katika vikombe vya mvinyo mchanganyiko wake ni (kutoka chemchemu iitawayo) kaafuwraa.

 

 

عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا عِبَادُ اللَّـهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفْجِيرًا﴿٦﴾

Chemchemu watakayokunywa humo waja wa Allaah, wataibubujua kwa wingi.

 

يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا﴿٧﴾

Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea kwa upana.

 

وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا﴿٨﴾

Na wanalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini na mayatima na mateka.

 

إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ اللَّـهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَاءً وَلَا شُكُورًا﴿٩﴾

“Hakika sisi tunakulisheni kwa ajili ya Wajihi wa Allaah, hatukusudii kwenu jazaa na wala shukurani. [Al-Insaan (76: 5-9)]

 

 

Neema hizo za Jannah zimeendelea kutajwa kwa wingi katika Suwrah hiyo tukufu ya Al-Insaan mpaka Aayah namba 22.  

 

Kinyume cha kutokulisha masikini ilhali mtu ana uwezo au kutokuhimiza kulisha maskini ni matahadharisho na adhabu zilizotajwa katika:

 

 

Rejea: Al-Haaqah (69: 34), Al-Fajr (89: 18), Al-Maa’uwn (107: 3).

 

 

 

4. Maamrisho ya kuunga udugu na fadhila zake na maonyo ya kukata undugu.

 

Rejea: Al-Baqarah (2: 27), Ar-Ra’d (13: 21 – 25), Muhammad (47: 22-23).

 

Rejea pia Hadiyth namba (38).

 

 

 

5. Umuhimu wa Qiyaamul-Layl (Kisimamo cha kuswali usiku) kama tarawiyh na kuamka usiku kuswali. Fadhila zake ni adhimu, Anasema Allaah (سبحانه وتعالى): 

 

تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ خَوْفًا وَطَمَعًا وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ ﴿١٦﴾

Mbavu zao zinatengana na vitanda, wanamuomba Rabb wao kwa khofu na matumaini, na katika yale Tuliyowaruzuku wanatoa.

 

فَلَا تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٧﴾

Basi nafsi yoyote haijui yaliyofichiwa katika yanayoburudisha macho. Ni jazaa kwa yale waliyokuwa wakiyatenda. [As-Sajdah (32: 16-17)]

 

Aayah hiyo inahusiana na Hadiyth ifuatayo ya Al-Qudsiy:

 

   

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ تَبَارَكَ وَتَعَالَى: أَعْدَدْتُ لِعِبَادِي الصَّالِحِينَ مَا لَا عَيْنٌ رَأَتْ وَلَا أُذُنٌ سَمِعَتْ وَلَا خَطَرَ عَلَى قَلْبِ بَشَرٍ)) قَالَ أَبُو هُرَيْرَةَ اقْرَءُوا إِنْ شِئْتُمْ: (( فَلَا تَعْلَمُ نَفْسٌ مَا أُخْفِيَ لَهُمْ مِنْ قُرَّةِ أَعْيُنٍ)) البخاري، مسلم، الترمذي وابن ماجه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Allaah تبارك وتعالى Amesema: Nimewatayarishia waja Wangu wema kile ambacho jicho lolote halijapata kuona na sikio lolote halijapata kusikia na wala haijapata kupita katika moyo wa binaadamu)) Akasema Abuu Hurayrah: Kwa hivyo, soma ukitaka: Basi nafsi yoyote haijui yaliyofichiwa katika yanayoburudisha macho. Ni jazaa kwa yale waliyokuwa wakiyatenda)) [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah]

 

Rejea pia: Adh-Dhaariyaat (51: 16-18).

 

 

6. Qiyaamul-Layl imetajwa kuwa ni Swalaah bora kabisa baada ya Swalaah fardhi kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

((أَفْضَلُ الصَّلاةِ بَعْدَ الْفَرِيضَةِ صَلاةُ اللَّيْلِ))  رواه مسلم.

((Swalaah iliyo bora kabisa baada ya fardhi ni Swalaah ya usiku)) [Muslim]

 

 

7. Kuamka kuswali usiku ni miongoni mwa sifa za Waja wa Ar-Rahmaan kama ilivyotajwa katika Al-Furqaan (25: 63-64).

 

 

 

8. Waamkao usiku kuswali hawako sawa na waja wengine. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَمَّنْ هُوَ قَانِتٌ آنَاءَ اللَّيْلِ سَاجِدًا وَقَائِمًا يَحْذَرُ الْآخِرَةَ وَيَرْجُو رَحْمَةَ رَبِّهِ ۗ قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ ۗ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٩﴾

Je, yule aliye mtiifu nyakati za usiku akisujudu, au akisimama (kuswali), anatahadhari na Aakhirah na anataraji rahmah ya Rabb wake (ni sawa na aliyekinyume chake?). Sema: “Je, wanalingana sawa wale wanaouja na wale wasiojua?” Hakika wanakumbuka wenye akili tu. [Az-Zumar (39: 9)]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 113)  

 

 

9. Kuamka kuswali usiku ni amri za Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) na kwetu pia.

 

 

Rejea: Qaaf (50: 39-40), Al-Insaan (76: 25-26), Al-Israa (17: 78-79), Al-Muzammil (73: 3-4).

 

 

 

 

Share

073-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutaja Jina Mlangoni Unapoulizwa “Nani Wewe”

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 73

Kutaja Jina Mlangoni Unapoulizwa “Nani Wewe”

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 عن جَابِرَ (رضي الله عنه) قَال: أَتَيْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  فَدَقَقْتُ الْبَابَ فَقَالَ:  ((مَنْ ذَا؟)) فَقُلْتُ: أَنَا. فَقَالَ: ((أَنَا أَنَا؟)) كَأَنَّهُ كَرِهَهَا. - متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه) ambaye amesema: “Nilimwendea Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم) nikagonga mlango akauliza: ((Nani huyu?)) Nikajibu: “Mimi”. Akasema: ((Mimi, mimi!?)) kama kwamba alikuwa amechukia.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Kubisha hodi mlangoni ni miongoni mwa Akhlaaq (tabia) njema na ni amri kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتًا غَيْرَ بُيُوتِكُمْ حَتَّىٰ تَسْتَأْنِسُوا وَتُسَلِّمُوا عَلَىٰ أَهْلِهَا ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ﴿٢٧﴾

Enyi walioamini! Msiingie nyumba zisizokuwa nyumba zenu mpaka muombe ruhusa na muwatolee salamu wenyewe. Hivyo ni bora kwenu ili mpate mkakumbuka. [An-Nuwr (24: 27)]

 

Rejea pia An-Nuwr (24: 59)]

 

 

2. Kubisha hodi ni mara tatu, na ikiwa mtu hakujibiwa, basi anapaswa asiingie bali arudi na kwenda zake kwani hivyo ndio heshima na itaepusha kufichuka siri za nyumba, na utakaso zaidi kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فِيهَا أَحَدًا فَلَا تَدْخُلُوهَا حَتَّىٰ يُؤْذَنَ لَكُمْ ۖ وَإِن قِيلَ لَكُمُ ارْجِعُوا فَارْجِعُوا ۖ هُوَ أَزْكَىٰ لَكُمْ ۚ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌ ﴿٢٨﴾

Na msipokuta humo yeyote; basi msiingie mpaka mruhusiwe. Na mkiambiwa: “Rejeeni!” Basi rejeeni. Huo ni utakaso zaidi kwenu. Na Allaah Mjuzi wa myatendayo. [An-Nuwr (24: 28)]

 

 

3. Ni Sunnah mtu kujitambulisha jina au umaarufu wake anapoulizwa jina lake baada ya kugonga mlango.

 

 

4. Inachukiza kujibu ‘mimi’ au vyovyote vinginevyo bila ya kutaja jina linalokutambulisha.

 

 

5. Kujitambulisha jina inatakiwa pia katika hali nyinginezo kama mtu anapokutana katika kiza cha njiani n.k akaulizwa jina lake.

 

 

6. Mafunzo haya ni sawa na mafunzo katika Hadiyth ya Israa Wal Mi’raaj pindi Jibriyl (عليه السلام) alipotaka idhini ya kuingia katika kila mbingu, alipoulizwa: “Nani?” Akajibu: “Jibriyl.” Akaulizwa: “Nani yuko na wewe?”  Akajibu: “Muhammad.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

7. Mafunzo pia kutoka kwa Maswahaba Abu Dharr na Ummu Haaniy (رضي الله عنهما) katika hali mbalimbali, walipomsalimia Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) akawauliza: ((Nani?)) wakajibu kwa majina yao. [Kila mmoja ametajwa katika Hadiyth ya pekee].

 

 

 

 

 

Share

074-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Yapendeza Kupiga Chafya Na Yachukiza Kupiga Miayo

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 74

 

Yapendeza Kupiga Chafya Na Yachukiza Kupiga Miayo

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أنَّ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِنَّ اللَّهَ يُحِبُّ الْعُطَاسَ وَيَكْرَهُ التَّثَاؤُبَ، فَإِذَا عَطَسَ أَحَدُكُمْ وَحَمِدَ اللَّهَ تَعَالى كَانَ حَقًّا عَلَى كُلِّ مُسْلِمٍ سَمِعَهُ أَنْ يَقُولَ لَهُ "يَرْحَمُكَ اللَّهُ" وَأَمَّا التَّثَاؤُبُ فَإِنَّمَا هُوَ مِنْ الشَّيْطَانِ فَإِذَا تَثَاءَبَ أَحَدُكُمْ فَلْيَرُدَّهُ مَا اسْتَطَاعَ، فَإِنَّ أَحَدَكُمْ إِذَا تَثَاءَبَ ضَحِكَ مِنْهُ الشَّيْطَانُ)) البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Hakika Allaah Anapenda chafya na Anachukia kupiga miayo. Anapopiga chafya mmoja wenu akamhimidi Allaah (تعالى) ni wajibu kwa kila Muislamu anayemsikia kumwambia: “Yarhamuka Allaah” (Allaah Akurehemu). Ama kupiga miayo, hakika hivyo ni kutoka kwa shaytwaan, basi anapopiga miayo mmoja wenu ajizuie kadiri awezavyo. Mtu anaposema: “Aaawh” shaytwaan humcheka)). [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Himizo la kufanya Anayoyapenda Allaah (سبحانه وتعالى) na kuacha Anayoyachukia.

 

 

2. Inapasa Kumuombea Rahma Muislamu anapopiga chafya baada ya kumhimidi Allaah (سبحانه وتعالى), kwani ni Sunnah na miongoni mwa haki baina ya Waislamu. Ameamrisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

 عن أبي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((حَقُّ الْمُسْلِمِ عَلَى الْمُسْلِمِ خَمْسٌ: رَدُّ السَّلَامِ وَعِيَادَةُ الْمَرِيضِ وَاتِّبَاعُ الْجَنَائِزِ وَإِجَابَةُ الدَّعْوَةِ وَتَشْمِيتُ الْعَاطِسِ)) البخاري ومسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba: Nimesikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Haki ya Muislamu kwa nduguye Muislamu ni tano: Kujibu Salaam, kumtembelea mgonjwa, kulisindikiza jeneza, kuitikia mwito na kumuombea mwenye kupiga chafya)) [Al-Bukhaariy Muslim]

 

 

3. Mafunzo kwa Waislamu kuombeana du’aa za Sunnah katika kupiga chafya; du’aa ya anayepiga chafya na anayemsikia mwenziwe kama ifuatavyo:

 

Anapopiga chafya mtu aseme:

الْحَمْـدُ للهِ

AlhamduliLLaah (Himdi Anastahiki Allaah)

Kisha mwenzake amwambie:

يَرْحَمُـكَ الله

Yarhamuka-Allaah (Allaah Akurehemu)

Kisha naye amjibu:

يَهْـديكُـمُ اللهُ وَيُصْـلِحُ بالَـكُم

Yahdiykumu-Allaahu wa Yuswlihu baalakum (Allaah Akuhidi na Akutengenezee mambo yako [Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)   katika Al-Bukhaariy (7/125)]

 

 

4. Kupiga chafya ni miongoni mwa neema za Allaah (سبحانه وتعالى) zisizohesabika, nayo ni inahusiana na afya ya mwana Aadam. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَآتَاكُم مِّن كُلِّ مَا سَأَلْتُمُوهُ ۚ وَإِن تَعُدُّوا نِعْمَتَ اللَّـهِ لَا تُحْصُوهَا ۗ إِنَّ الْإِنسَانَ لَظَلُومٌ كَفَّارٌ ﴿٣٤﴾

Na Akakupeni kila mnachomuomba. Na mkihesabu neema za Allaah hamtoweza kuziorodhesha hesabuni.  Hakika insani ni mwingi wa dhulma, mwingi wa kukufuru akosaye shukurani. [Ibraahiym (14: 34)]

 

 

5. Inafaa kujihamasisha mtu apige chafya kwa kufanya mazoezi ya mwili ili abakie katika afya. Ama kuzuia kwenda miayo, ni kutokula hadi mtu ashibe mno akavimbiwa na akawa mvivu mno hadi apige miayo.   

 

 

6. Masisitizo ya kuzuia mdomo mtu anapopiga miayo, nayo ina manufaa ya kiafya kwa bin Aadam kuzuia viini vya maradhi (vijidudu) kuingia mdomoni.

 

 

7. Uislamu unasisitiza afya na usalama bin Aadam.

 

 

8. Kujiepusha na kila jambo baya analopenda shaytwaan, na kuomba kujikinga naye. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ ﴿٩٧﴾

Na sema: “Rabb wangu! Najikinga Kwako kutokana na udokezi wa mashaytwaan,”

وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحْضُرُونِ ﴿٩٨﴾

“Na najikinga Kwako Rabb wasinihudhurie.” [Al-Muuminuwn (23: 97-98)]

 

Na pia kuomba kinga katika hali inayomkabili mtu inayopelekea wasiwasi na uchochezi wa shaytwaan, kama vile unapotaka kuanza kusoma Qur-aan au kuswali na kadhalika kama tulivofundishwa katika Qur-aan na Sunnah kwa kusema:

أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجيـم

A’uwdhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiym

 

Najikinga kwa Allaah kutokana na shaytwaan aliyeepushwa na kuwekwa mbali na Rehma za Allaah [Hadiyth ya Sulaymaan bin Swuradi -(رضي الله عنه)    - Al-Bukhaariy (7/99) [6048], Muslim (4/2015) [2610]

 

 

9. Maagizo yote yanayotolewa na Allaah (سبحانه وتعالى) na Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) ni kwa maslahi ya bin Aadam basi yasipuuzwe kabisa.

 

 

 

Share

075-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mwenye Kuakhirishia Au Kusamehe Deni, Atakuwa Katika Kivuli Cha Allaah Siku Ya Qiyaamah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 75

 

Mwenye Kuakhirishia Au Kusamehe Deni,

Atakuwa Katika Kivuli Cha Allaah Siku Ya Qiyaamah

 

Alhidaaya.com

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ أَنْظَرَ مُعْسِرًا أَوْ وَضَعَ لَهُ، أَظَلَّهُ اللَّهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ تَحْتَ ظِلِّ عَرْشِهِ يَوْمَ لاَ ظِلَّ إِلاَّ ظِلُّهُ)) رواه الترمذي وقَال حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Atakayemuakhirishia mwenye usiri [wa kulipa deni] au akamsamehe, Allaah Atamfunika kivuli Siku ya Qiyaamah chini ya kivuli cha ‘Arshi Yake, Siku ambayo hakutakuwa na kivuli isipokuwa kivuli Chake)). [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Uislamu unafunza kuoneana huruma katika hali ya dhiki kama kumsamehe mtu deni lake.

 

 

2.  Himizo la kusameheana deni, ima kuakhirisha wakati wake ulioahidiwa au kulisamehe lote. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 

وَإِن كَانَ ذُو عُسْرَةٍ فَنَظِرَةٌ إِلَىٰ مَيْسَرَةٍ ۚ وَأَن تَصَدَّقُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿٢٨٠﴾

Na ikiwa (mdaiwa) ni mwenye hali ngumu, basi (mdai) angoje mpaka afarijike. Na mkifanya deni kuwa ni swadaqah basi ni kheri kwenu mkiwa mnajua. [Al-Baqarah (2: 280)]

 

 

 

3. Fadhila kwa aliye na wasaa wa mali kusamehe deni kupata malipo mema Aakhirah na hiyo ni sifa ya Muhsin na kughufuriwa dhambi.

 Rejea: Aal ‘Imraan (3: 134), An-Nuwr (24: 22).

 

 

Pia Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:

 

عن حذيفة عن رسول الله صلى الله عليه وسلم  أنه قال: ((أُتِيَ اللهُ بِعَبْدٍ مِنْ عَبِيدِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ قَالَ: مَاذَا عَمِلْتَ لِي فِي الدُّنْيَا؟ فَقَالَ: مَا عَمِلْتُ لَكَ يَا رَبِّ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي الدُّنْيَا أَرْجُوكَ بِهَا،  قَالَهَا ثَلَاثَ مَرَّاتٍ، قَالَ الْعَبْدُ عِنْدَ آخِرِهَا: يَا رَبِّ إِنَّكَ كُنْتَ أَعْطَيْتَنِي فَضْلَ مَالٍ، وَكُنْتُ رَجُلًا أُبَايِعُ النَّاسَ، وَكَانَ مِنْ خُلُقِي الْجَوازُ، فَكُنْتُ أُيَسِّرُ عَلَى الْمُوسِرِ وَأُنْظِرُ الْمُعْسِرَ، قَالَ: فَيَقُولُ اللهُ عَزَّوَجَلَّ: أَنَا أَحَقُّ مَنْ يُيَسِّرُ، ادْخُلِ الْجَنَّة))

Hudhayfah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Siku ya Qiyaamah, mmoja wa waja wa Allaah ataitwa mbele Yake na Atamuuliza: Umefanya ‘amali gani kwa ajili yangu katika maisha yako? Atajibu: Ee Rabb wangu! Sikuwahi katika uhai wangu kufanya ‘amali kwa ajili Yako iliyo sawa na chembe ndogo! (Ataulizwa na atajibu) Mara tatu, kisha mara ya tatu atasema: Ee Rabb wangu! Ulinijaalia mali na nilikuwa nafanya biashara. Nilikuwa mpole, nikiwapa masharti mepesi wenye uwezo na nikiwapa muda wa kulipa wadaiwa. Allaah Atamwambia: Mimi Ndiye Mwenye haki zaidi ya kutoa masharti mepesi kwa hiyo, ingia Jannah!)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

4. Malipo yanalingana, kama ilivyo, kwamba mwenye deni anapomuondoshea dhiki mwenziwe duniani ya kulipa deni, naye pia Allaah (سبحانه وتعالى) Atamuondoshea dhiki Aakhirah.

 

Rejea Hadiyth namba (23).

 

 

5. Kuakhirisha au kusamehe deni ni mojawapo wa fadhila za kujipatia kivuli cha Allaah (سبحانه وتعالى) Siku ambayo jua litakuwa karibu mno na joto lake halitoweza kuvumilika.

 

Rejea Hadiyth namba (43). 

 

Na Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ   ((سَبْعَةٌ يُظِلُّهُمْ اللَّهُ فِي ظِلِّهِ يَوْمَ لا ظِلَّ إِلا ظِلُّهُ: الإِمَامُ الْعَادِلُ، وَشَابٌّ نَشَأ فِي عِبَادَةِ رَبِّهِ، وَرَجُلٌ قَلْبُهُ مُعَلَّقٌ فِي الْمَسَاجِدِ، وَرَجُلَانِ تَحَابَّا فِي اللَّهِ اجْتَمَعَا عَلَيْهِ وَتَفَرَّقَا عَلَيْهِ، وَرَجُلٌ طَلَبَتْهُ امْرَأَةٌ ذَاتُ مَنْصِبٍ وَجَمَالٍ فَقَالَ إِنِّي أَخَافُ اللَّهَ، وَرَجُلٌ تَصَدَّقَ بِصَدَقَةٍ فَأَخْفَاهَا حَتَّى لا تَعْلَمَ شِمَالُهُ مَا تُنْفِقُ يَمِينُهُ، وَرَجُلٌ ذَكَرَ اللَّهَ خَالِيًا فَفَاضَتْ عَيْنَاهُ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watu saba Allaah  Atawafunika katika kivuli Chake, Siku ambayo hakutokuwa na kivuli ila kivuli Chake: Imaam muadilifu, kijana ambaye amekulia katika ‘Ibaadah ya Rabb wake, Mtu ambaye moyo wake umeambatana na Misikiti, watu wawili wanaopendana kwa ajili ya Allaah; wanakutana kwa ajili Yake na wanafarikiana kwa ajili Yake, mwanamme aliyetakwa na mwanamke mwenye hadhi na mrembo wa kuvutia akasema: "Mimi namkhofu Allaah!" Mtu aliyetoa Swadaqah yake akaificha hadi kwamba mkono wake wa kushoto usijue nini ulichotoa mkono wake wa kulia, na mtu aliyemdhukuru Allaah kwa siri macho yake yakatokwa machozi)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

6. Muumin anapaswa ajiepushe na uchoyo, ubakhili wa nafsi na badala yake kuwapendelea wenziwe wapate anachokihitajia yeye, ili apate kuwa miongoni mwa watakaofaulu.

 

Rejea:  At-Taghaabun (64: 16).

 

Pia kisa cha Abuu Twalhah na Ummu Sulaym Rumayswaa’ bint Milhaan walipopata wageni wakawakirimu ilhali wao walikuwa wana njaa, Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha Aayah kama ilivyotajwa katika Hadiyth ifuatavyo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، ‏.‏ أَنَّ رَجُلاً، مِنَ الأَنْصَارِ بَاتَ بِهِ ضَيْفٌ فَلَمْ يَكُنْ عِنْدَهُ إِلاَّ قُوتُهُ وَقُوتُ صِبْيَانِهِ فَقَالَ لاِمْرَأَتِهِ نَوِّمِي الصِّبْيَةَ وَأَطْفِئِي السِّرَاجَ وَقَرِّبِي لِلضَّيْفِ مَا عِنْدَكِ - قَالَ - فَنَزَلَتْ هَذِهِ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba mtu alilala usiku kama mgeni kwa mtu mmoja katika Answaariy ambaye hakuwa na chakula isipokuwa chakula cha watoto wake akamwambia mkewe: “Laza watoto na zima taa karibisha wageni kwa (chakula) ulichonacho.” Ikateremka kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ﴿٩﴾

  

Na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji. Na yeyote anayeepushwa na ubakhili na tamaa ya uchu wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu. [Al-Hashr (59: 9)]

  

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

076-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Balighisheni Japo Kwa Aayah, Atakayemwongopea Nabiy Ajitayarishie Makazi Motoni

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 76

 

Balighisheni  Japo Kwa Aayah Moja, Atakayemwongopea Nabiy Ajitayarishie Makazi Yake Motoni

 

 

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو العَاص (رضي الله عنهما) أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((بَلِّغُوا عَنِّي وَلَوْ آيَةً،  وَحَدِّثُوا عَنْ بَنِي إِسْرَائِيلَ وَلاَ حَرَجَ، وَمَنْ كَذَبَ عَلَيَّ مُتَعَمِّدًا فَلْيَتَبَوَّأْ مَقْعَدَهُ مِنْ النَّارِ)) البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr Al-‘Aasw (رضي الله عنهما)   kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Balighisheni (fikisheni) kutoka kwangu japo Aayah moja. Na simulieni kuhusu habari za Wana wa Israaiyl wala hakuna dhambi [ubaya]. Na mwenye kunizulia uongo kwa makusudi, basi ajiandalie makazi yake motoni)). [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Umuhimu wa kubalighisha ujumbe, kuamrishana mema na kukatazana maovu japo kwa Aayah moja au Hadiyth moja.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ

Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu; mnaamrisha mema na mnakataza munkari na mnamwamini Allaah. [Aal-‘Imraan (3: 110)]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 104),   At-Tawbah (9: 71), (112), Al-Hajj (22: 41).

 

          

2. Umuhimu wa kutafuta na kujifunza elimu sahihi ili kutokubalighisha Hadiyth dhaifu au mambo ya uzushi.

 

 

 

3. Kuruhusiwa kusimulia habari za Wana wa Israaiyl ili kupata mafunzo na mazingatio, ila la muhimu ni kuhakikisha kama masimulizi yamethibiti usahihi wake.

 

 

 

4. Kuzusha yasiyo sahihi ni miongoni mwa madhambi makubwa kwa vile yanamfikisha mtu motoni, kwa hiyo inapasa kutahadhari mno! Hadiyth ifuatayo inataja hatari hizo ambazo zinampeleka mtu kwenye upotofu kwanza kisha motoni.

 

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ قَالَ: كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ فِي خُطْبَتِهِ يَحْمَدُ اللَّهَ، وَيُثْنِي عَلَيْهِ بِمَا هُوَ أَهْلُهُ، ثُمَّ يَقُولُ: مَنْ يَهْدِهِ اللَّهُ فَلَا مُضِلَّ لَهُ وَمَنْ يُضْلِلْهُ فَلَا هَادِيَ لَهُ إِنَّ أَصْدَقَ الْحَدِيثِ كِتَابُ اللَّهِ وَأَحْسَنَ الْهَدْيِ هَدْيُ مُحَمَّدٍ وَشَرُّ الْأُمُورِ مُحْدَثَاتُهَا وَكُلُّ مُحْدَثَةٍ بِدْعَةٌ وَكُلُّ بِدْعَةٍ ضَلَالَةٌ وَكُلُّ ضَلَالَةٍ فِي النَّارِ...)) مسلم، أبو داود، النسائي، ابن ماجه، أحمد، الدارمي

 

Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه)  ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  alikuwa akisema katika khutbah zake: ((Yule ambaye Allaah Amemhidi, hakuna wa kumpotoa, na yule ambaye Allaah Amempotoa hakuna wa kumhidi. Hakika maneno ya kweli kabisa ni Kitabu cha Allaah, na mwongozo mbora kabisa ni wa Muhammad, na jambo la shari kabisa ni uzushi, na kila jambo jipya (katika Dini) ni bid'ah (uzushi) na kila bid'ah ni upotofu, na kila upotofu ni motoni)) [Muslim, Abuu Daawuwd, An-Naasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad, Ad-Daarimiy]

 

 

 

5. Mwenye hadhari na khofu ya kuzusha mafunzo yasiyo sahihi na kumzulia uongo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), anadhihirisha wazi mapenzi yake kwa Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم), kwani hakuna apendaye kumzulia uongo kipenzi chake.

 

 

 

6. Dalili kadhaa kutoka katika Qur-aan na Sunnah zimetaja maamrisho na fadhila za kubalighisha kwa kuamrishana mema na kukatazana maovu na kulingania kwa ujumla (da’wah). Na kinyume chake ni kukemewa na kutahadharishwa na adhabu kwa anayepuuza.

 

 

عن حُذيفةَ بنِ اليَمانِ عن النَّبيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلِيهِ وسَلَّم قال: ((والَّذي نَفْسي بيدهِ لتأمرُنَّ بالمعروفِ ولتَنهوُنَّ عن المنكرِ وليوشِكَنَّ اللهُ أنْ يبعثَ عليكُمْ عقاباً منهُ فتدعونَهُ فلا يَستجيبُ لكُمْ)) الترمذي وصححه الألباني

Imepokelewa toka kwa Hudhayfah bin al-Yamaani  (رضي الله عنه) kutoka kwa Nabiy kwamba amesema: ((Naapa kwa Yule nafsi yangu ipo mikononi mwake, mtaamrishana ma’ruwf [mema] na kukatazana munkari [maovu] ama Atawaunganishia kwa kuwapa mfano wake Allaah na kuwateremshia nyinyi adhabu itokayo Kwake, kisha mumuombe Yeye na Asiwajibu du’aa zenu)) [At-Tirmidhiy na akaisahihisha Al-Albaaniy]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (16), (17),

 

Rejea pia utangulizi wa hizi Hadiyth.

 

 

Share

077-Lu-ulu-un-Manthuwrun: ‘Amali Zinakatika Isipokuwa Mambo Matatu: Swadaqah Inayoendelea, Elimu Inayonufaisha, Mwana Mwema

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 77

 

‘Amali Zinakatika Isipokuwa Mambo Matatu: Swadaqah Inayoendelea, Elimu Inayonufaisha, Mwana Mwema Anayemuombea Mzazi Wake

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِذَا مَاتَ ابْنُ آدَم انْقَطَعَ عَمَلُهُ إلاَّ مِنْ ثَلاَث: صَدَقَةٍ جَارِيَةٍ  أَوْ عِلْمٍ يُنْتَفَعُ بِهِ أَوْ وَلَدٍ صَالِحٍ يَدْعُو لَهُ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Bin Aadam akifa, ‘amali zake hukatika isipokuwa mambo matatu: Swadaqah inayoendelea, au elimu inayonufaisha, au mtoto mwema anayemuombea du’aa)). [Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Umuhimu wa kutenda mema yatakayomfaa mwana Aadam Aakhirah baada ya kufariki kwake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١٨﴾

Enyi walioamini! Mcheni Allaah, na nafsi itazame imetanguliza nini kwa ajili ya kesho, na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo. [Al-Hashr (59: 18)]

 

Rejea pia: Yaasiyn (36: 12).

 

 

2. Mifano ya kutoa swadaqah fiy SabiliLLaah (Katika njia ya Allaah) ni kama kujenga Msikiti, kuchimba kisima, kujenga hospitali au kuwahudumia wagonjwa, kuacha shamba linalotoa mazao wakanufaika nayo watu, n.k.

 

 

3. Fadhila za kutoa swadaqah zimetajwa tele katika Qur-aan na Sunnah. Rejea Hadiyth namba (8), (31), (62),

 

 

4. Umuhimu wa kujifunza elimu ya Dini na kuifunza ili ibakie kunufaisha watu.

 

 

5. Fadhila za elimu nyingi zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah. Mfano wa Hadiyth rejea Hadiyth namba (16), (78), (81).

 

 

6. Asiyekuwa na ‘ilmu anaweza kupata fadhila hizo kwa kujitolea mali yake kwa kujenga maraakiz za Sunnah na kuandaa madarasa, kusaidia katika da’wah kwa ujumla.

 

 

7. Umuhimu wa kulea watoto malezi mema ya Kiislamu ili watoke wana wema watakaomwombea mtu baada ya kufariki kwake.

 

Du’aa ya kuomba ili ajaaliwe mtu kuwa na kizazi chema mojawapo ni ambayo imetajwa katika sifa za ‘Ibaadur-Rahmaan (waja wa Mwingi wa Rahmah).

 

  رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا ﴿٧٤﴾

 “Rabb wetu! Tutunukie katika wake zetu na dhuria wetu viburudisho vya macho yetu, na Tujaalie kuwa waongozi kwa wenye taqwa.  [Al-Furqaan (25: 74)]  

 

Nabiy Zakariyaa (عليه السلام) naye aliomba pia aliposema:

 

  رَبِّ هَبْ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةً طَيِّبَةً ۖ إِنَّكَ سَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٨﴾

 “Rabb wangu Nitunukie kutoka Kwako kizazi chema hakika Wewe ni Mwenye kusikia du’aa yangu.” [Aal-‘Imraan (3: 38)]

 

 

 

8. Hakuna atakayeweza kumfaa mwenziwe Siku ya Qiyaamah ila ‘amali zake tu alizozitenda.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَانِ إِلَّا مَا سَعَىٰ ﴿٣٩﴾

Na kwamba insani hatopata (jazaa) isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi.

 

وَأَنَّ سَعْيَهُ سَوْفَ يُرَىٰ ﴿٤٠﴾

Na kwamba juhudi yake itakuja kuonekana

 

ثُمَّ يُجْزَاهُ الْجَزَاءَ الْأَوْفَىٰ ﴿٤١﴾

Kisha atalipwa jazaa kamilifu. [An-Najm (53: 39-41)]

 

 

 

Zaidi yake ni du’aa ya mwana mwema.

 

 

9. Kila mtu afanye juhudi ya kufanya ‘amali njema kabla ya kumfikia mauti kwa sababu hakuna kitakachomfaa katika safari yake ndefu ya maisha ya Al-Barzakh na Aakhirah isipokuwa kwa yale aliyoyatenda.

 

Rejea Hadiyth namba (54).

 

Share

078-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Viumbe Vyote Vinawaombea Wanaofunza Watu Kheri

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 78

 

Viumbe Vyote Vinawaombea Wanaofunza Watu Mambo Ya Kheri

 

 

 

 

عَنْ أَبِي أُمَامَةَ (رضي الله عنه) أنَّ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قال: ((فضْلُ الْعَالِمِ عَلَى الْعَابِدِ كَفَضْلِي عَلَى أَدْنَاكُم))  ثُمَّ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((إِنَّ اللَّهَ وَمَلاَئِكَتَهُ وَأَهْلَ السَّمَوَاتِ وَالأَرَض حَتَّى النَّمْلَةَ فِي جُحْرِهَا وَحَتَّى الْحُوتَ لَيُصَلُّونَ عَلَى مُعَلِّمِي النَّاسِ الْخَيْرَ)) رواه الترمذي  وقَالَ حَدِيثٌ حَسَنٌ.

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Umaamah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Ubora wa Mwanachuoni juu ya mfanya ‘Ibaadah, ni kama ubora wangu juu ya mwenye daraja ya chini miongoni mwenu)). Kisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema:((Hakika Allaah na Malaika Wake, na walio mbinguni, hata wadudu chungu waliomo katika mashimo yao, na hata samaki, wanawaombea maghfirah wanaowafundisha watu kheri)). [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila adhimu za mwenye elimu ya Dini kwamba viumbe vyote vinamuombea maghfirah.

 

 

2. Ukumbusho wa fadhila za mwenye elimu, mojawapo ya fadhila ni kwamba wamesifiwa ni waje wenye kumkhofu Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا يَخْشَى اللَّـهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ ۗ  

Hakika wanaomkhofu Allaah miongoni mwa waja Wake ni ‘Ulamaa. [Faatwir (35: 28)]

     

 

Na kwamba wao pamoja na Allaah (سبحانه وتعالى) na Malaika Wake wanashuhudia Tawhiyd ya Allaah (عزّ وجلّ) kama Anavyosema Mwenyewe Allaah (سبحانه وتعالى):

 

شَهِدَ اللَّـهُ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ وَالْمَلَائِكَةُ وَأُولُو الْعِلْمِ قَائِمًا بِالْقِسْطِ ۚ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١٨﴾

 

Allaah Ameshuhudia kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye; na (pia) Malaika na wenye elimu (kwamba Allaah) ni Mwenye kusimamisha (uumbaji Wake) kwa uadilifu. Hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Aal-‘Imraan (3: 18)]

 

Na pia wenye elimu ya Dini wanapandishwa daraja za juu na Allaah (سبحانه وتعالى):

   

 يَرْفَعِ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَالَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ دَرَجَاتٍ ۚ

Allaah Atawainua wale walioamini miongoni mwenu na waliopewa elimu daraja za juu.  [Al-Mujaadalah (58: 11)]

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 83), Al-‘Ankabuwt (29: 49), Az-Zumar (39: 9).

 

 

3. Himizo la kutenda linalomfaa mtu nafsi yake na wenginewe, jambo ambalo litamnufaisha hata baada ya kufariki kwake.

 

Rejea Hadiyth namba (77).

 

 

4. Kutafuta elimu ya kufikia cheo cha mwalimu au Mwanachuoni ni bora zaidi kuliko ‘Ibaadah za naafilah (Sunnah), kwani ‘Ibaadah inamnufaisha mtu pekee, lakini elimu haimnufaishi pekee, bali hata wengineo.

 

 

5. Dhihirisho la kuwapa heshima ‘Ulamaa wa Dini yetu na wanafunzi na kuwaombea maghfirah na du’aa nzuri.

 

 

6. Hadiyth hii inahimiza na kutilia nguvu mno suala la kutafuta elimu na kufunza watu hadi kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema katika Hadiyth ifuatayo kwamba dunia imelaaniwa isipokuwa kumdhukuru Allaah na Mwalimu na mwanafunzi anayejifunza Dini:

 

 

عن أبي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَال: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: (( أَلاَ إِنَّ الدُّنْيَا مَلْعُونَةٌ مَلْعُونٌ مَا فِيهَا إِلاَّ ذِكْرُ اللَّهِ ، وَمَا وَالاَهُ ، وَعَالِمٌ أَوْ مُتَعَلِّمٌ)) الترمذي وقال: حَدِيثٌ حَسَنٌ 

Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: “Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akisema: ((Zindukeni! Dunia imelaaniwa, kimelaaniwa kilichomo humo isipokuwa dhikru-Allaah (kumtaja Allaah) na jambo linalokaribiana na hilo (la kumtii Allaah), Mwanachuoni na anayejifunza [Dini])) [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan]

 

 

 

7. Fadhila tele za kutafuta elimu na kufundisha zimetajwa pia katika Hadiyth za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), miongoni mwazo ni zifuatazo:

 

 

عن أَبِي الدَّرْدَاءِ (رضي الله عنه) قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((مَنْ سَلَكَ طَرِيقًا يَبْتَغِي فِيهِ عِلْمًا، سَلَكَ اللَّهُ بِهِ طَرِيقًا إِلَى الْجَنَّةِ)) مسلم 

Imepokelewa toka kwa Abuu Ad-Dardaa (رضي الله عنه) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Anayetafuta njia ya kutaka elimu humo, Allaah Humpatia njia ya Jannah [Peponi])) [Muslim]

 

Pia:

 

عن سَهْل بنِ سَعد رَضيَ اللهُ عنهُ أنَّ النَّبيَّ صَلى اللهُ عليْه وسلم قال لعليٍ رضي اللهُ عنهُ: ((فواللهِ لأَنْ يَهْدِيَ اللهُ بِكَ رَجُلاً وَاحِداً خَيْرٌ لَكَ مِن حُمْرِ النَّعَم)) البخاري و مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Sahal bin Sa'ad (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema kumwambia ‘Aliy (رضي الله عنه): ((Wa-Allaahi, Allaah Akimhidi mtu mmoja kupitia kwako, ni kheri kwako kuliko ngamia mwekundu)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( مَنْ دَعَا إِلَى هُدًى كَانَ لَهُ مِنَ الأَجْرِ مِثْلُ أُجُورِ مَنْ تَبِعَهُ لاَ يَنْقُصُ ذَلِكَ مِنْ أُجُورِهِمْ شَيْئًا))  مسلم

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Yeyote anayelingania katika uongofu, atakuwa na ujira mfano ujira wa anayemfuata, hatapunguziwa kutokana ujira huo chochote)) [Muslim]

 

Pia:

 

 عن إبْنِ مَسْعُودٍ، قَالَ: سَمِعْتُ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: ((نَضَّرَ اللَّهُ امْرَأً سَمِعَ مِنَّا شَيْئًا فَبَلَّغَهُ كَمَا سَمِعَ فَرُبَّ مُبَلَّغٍ أَوْعَى مِنْ سَامِعٍ ‏)) الترمذي وصححه الألباني

 

Imepokelewa kutoka kwa bin Mas’uwd (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Nilimsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Allaah Amnawirishe mtu aliyesikia kitu kutoka Kwetu naye akakibalighisha kama alivyosikia. Huenda anayefikishiwa akawa ana fahamu zaidi kuliko aliyesikia)) [Imepokewa na At-Tirmidhiy na ameisahihisha Al-Albaaniy katka Swahiyh At-Tirmidhiy (2657), Swahiyh At-Targhiyb (89)]

 

 

Pia:

 

عن مُعَاوِيَةَ، قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ يُرِدِ اللَّهُ بِهِ خَيْرًا يُفَقِّهْهُ فِي الدِّينِ)) البخاري ومسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Mu'aawiyah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Akimtakia khayr (mja Wake) Humpa ufahamu (elimu) katika Dini)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Rejea pia Hadiyth namba (16), (80).

 

 

 

Share

079-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Fadhila Za Swalaah Ya Jamaa'ah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 79

 

Fadhila Za Swalaah Ya Jamaa’ah

 

 

 

 

عن ابنِ عمَر (رضي اللَّه عنهما) أَنَّ رسولَ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال: ((صَلاةُ الجَمَاعَةِ أَفضَلُ مِنْ صَلاةِ الفَذِّ بِسَبْعٍ وَعِشْرِينَ درَجَةً)) متفقٌ عليه

Imepokelewa kutoka kwa bin ‘Umar (رضي الله عنهما) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Swalaah ya Jamaa’ah ni bora kuliko Swalaah ya pekee kwa daraja ishirini na saba)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Umuhimu na amri ya kutekeleza amri ya kuswali Jamaa’ah kama vile Swalaah ya Ijumaa. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ وَذَرُوا الْبَيْعَ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya Swalaah siku ya Ijumaa, kimbilieni kumdhukuru Allaah na acheni kuuza na kununua. Hivyo ni kheri kwenu mkiwa mnajua. [Al-Jumu’ah (62: 9)]

 

 

 

2. Umuhimu wake hadi kwamba katika vita inawapasa Waislamu waswali Swalaah ya jamaa’ah.

 

Rejea: An-Nisaa (4: 102).

 

 

 

3. Muislamu ana fursa za kujichumia thawabu nyingi na kubwa kwa kuswali jamaa’ah kutokana na fadhila zake zilotajwa katika Hadiyth kadhaa miongoni mwazo ni:

 

عنْ عثمانَ بنِ عفانَ رضيَ اللَّه عنهُ قالَ : سمعتُ رسولَ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقولُ : ((مَنْ صَلَّى العِشَاءَ في جَـمَاعَةٍ، فَكَأَنَّما قامَ نِصْف اللَّيْل وَمَنْ صَلَّى الصبْح في جَمَاعَةٍ ، فَكَأَنَّما صَلَّى اللَّيْل كُلَّهُ)) رواه مسلم .

Kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (رضي الله عنه)  kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) anasema: ((Atakayeswali Swalaah ya Ishaa katika Jamaa’ah, atakuwa kama kwamba amesimama nusu ya usiku mzima. Na atakayeswali Asubuhi katika Jamaa’ah atakuwa kama kwamba ameswali usiku wote)) [Muslim]

 

Pia:

 

 

عنْ عثمانَ بنِ عفانَ رضي اللَّه عنهُ قال : قال رسولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : ((مَنْ شَهِدَ العِشَاءَ في جمَاعةٍ كان لهُ قِيامُ نِصْفِ لَيْلَة ، ومَنْ صَلَّى العِشَاءَ والْفَجْر في جمَاعَةٍ، كَانَ لَهُ كَقِيَامِ لَيْلَة)) قال التِّرمذي: حديثٌ حسن صحيحٌ .

Kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:  ((Atakayehudhuria Swalaah ya Ishaa katika Jamaa’ah atakuwa kama kwamba amesimama nusu usiku, na atakayeswali Ishaa na Alfajrii katika Jamaa’ah atakuwa kama kasimama usiku mzima)) [At-Tirmidhiy hadiyth hasan]

 

Pia,

 

عن أَبي هريرة رضيَ اللَّه عنهُ قال : قال رسولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : ((صَلاةُ الرَّجُلِ في جَماعةٍ تُضَعَّفُ عَلى صلاتِهِ في بَيْتِهِ وفي سُوقِهِ خمساً وَعِشْرينَ ضِعفًا، وذلكَ أَنَّهُ إِذا تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الْوُضُوءَ ثُمَّ خَرَجَ إِلى المَسْجِدِ، لا يُخْرِجُه إِلاَّ الصَّلاةُ، لَمْ يَخْطُ خَطْوةً إِلاَّ رُفِعَتْ لَه بهَا دَرَجَةٌ، وَحُطَّتْ عَنْه بهَا خَطِيئَةٌ، فَإِذا صَلى لَمْ تَزَلِ المَلائِكَة تُصَلِّي عَلَيْهِ مَا دَامَ في مُصَلاَّه، مَا لَمْ يُحْدِثْ، تَقُولُ: اللَّهُمَّ صَلِّ عَلَيْهِ، اللَّهُمَّ ارحَمْهُ. وَلا يَزَالُ في صَلاةٍ مَا انْتَظَرَ الصَّلاة))  متفقٌ عليه . وهذا لفظ البخاري

Kutoka kwa Abuu Huraryah (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Swalaah ya Jamaa’ah inazidi (thawabu) na Swalaah ya mtu nyumbani kwake au dukani kwake kwa mara ishirini na tano, kwa hivyo anapotawadha akafanya vizuri wudhuu wake, kisha akatoka kwenda Msikitini, hakuna lililomtoa ila Swalaah; basi hatembei hatua moja ila hupandishwa daraja (kwa hatua hiyo), na hufutiwa dhambi kwa hiyo hatua. Atakapokuwa anaswali, Malaika wanaendelea kumswalia madamu yumo kwenye Swalaah ikiwa hatozungumza. Husema (Malaika): “Ee Allah Mswalie na Mrehemu.” Na huendelea hivyo wakati anasubiri Swalaah nyingine)) [Al-Bukhaariy na Muslim] Na hili tamshi la Al-Bukhaariy.

 

 

 

4. Bainisho la fadhila nyingi za kuswali Jamaa’ah ziloashiriwa katika Hadiyth moja kwa kauli yake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Lau kama wangelijua yaliyomo humo (fadhila na faida) wangeliziendea (kuziswali) japo kwa kutambaa.”

 

Hadiyth:  

 

 

عن أَبي هُريرة رضيَ اللَّه عنهُ   قال : قال رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : ((لَيْسَ صَلاةٌ أَثْقَلَ عَلَى المُنَافِقينَ مِنْ صلاة الفَجْرِ وَالعِشاءِ وَلَوْ يَعْلَمُونَ ما فِيهما لأَتَوْهُما وَلَوْ حبْوًا)) متفق عليه .

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Hakuna Swalaah iliyo nzito kwa wanafiki kama Swalaah ya Alfajiri na ‘Ishaa. Lau kama wangelijua yaliyomo humo (fadhila na faida) wangeliziendea (kuziswali) japo kwa kutambaa)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

5. Umuhimu wake mwengine katika  Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، قَالَ سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: ((مَا مِنْ ثَلاَثَةٍ فِي قَرْيَةٍ وَلاَ بَدْوٍ لاَ تُقَامُ فِيهِمُ الصَّلاَةُ إِلاَّ قَدِ اسْتَحْوَذَ عَلَيْهِمُ الشَّيْطَانُ فَعَلَيْكَ بِالْجَمَاعَةِ فَإِنَّمَا يَأْكُلُ الذِّئْبُ الْقَاصِيَةَ)) قَالَ السَّائِبُ يَعْنِي بِالْجَمَاعَةِ الصَّلاَةَ فِي الْجَمَاعَةِ ‏.‏ابو داود بإسناد جيد وصححه الألباني

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Ad-Dardaai  amesema: Nimesikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Hakuna mahala penye watu watatu kitongojini au jangwani ambapo hakusimamishwi Swalaah miongoni mwao, isipokuwa shaytwaan huwaghilibu. Basi shikamaneni na Jamaa’ah hakika mbwa mwitu humla mbuzi alie mbali. [aliye peke yake])). As-Saaib amesema kuhusu maana ya Jamaa’ah ni kuswali pamoja (Jamaa’ah).  [Abuu Daawuwd, isnaad yake Jayyid. Taz Swahiyh Abiy Daawuwd (547)]  

 

 

 

6. Imetajwa umuhimu wake pia katika Hadiyth ya kipofu aliyemwendea Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kumtaka ruhusa asihudhurie Swalaah kwa vile hana wa kumuongoza, lakini Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alimwambia madamu anasikia Adhaan ajibu (mwito wa kwenda kuswali Jama’aah Msikitini).

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ: أَتَى النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ رَجُلٌ أَعْمَى فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنَّهُ لَيْسَ لِي قَائِدٌ يَقُودُنِي إِلَى الْمَسْجِدِ،  فَسَأَلَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنْ يُرَخِّصَ لَهُ فَيُصَلِّيَ فِي بَيْتِهِ، فَرَخَّصَ لَهُ فَلَمَّا وَلَّى دَعَاهُ فَقَالَ: ((هَلْ تَسْمَعُ النِّدَاءَ بِالصَّلَاةِ؟)) قَالَ: نَعَمْ، قَالَ: ((فَأَجِبْ)) رواه مسلم  

 

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba alikuja kipofu kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi sina mtu wa kuniongoza Msikitini. Akamuomba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amruhusu aswali nyumbani kwake. Akamruhusu. Alipogeuka, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwita na kumuuliza: ((Je, unasikia Adhaan?)) Akasema: Naam.  Akasema: ((Basi itikia)) yaani nenda kuswali. [Muslim]

 

 

7. Anayeacha kuswali Jamaa’ah amefananishwa kwa sifa za unafiki kama ilivyotangulia Hadiyth juu inayosema.

 

 

 ((Hakuna Swalaah iliyo nzito kwa wanafiki kama Swalaah ya Alfajiri na ‘Ishaa. Lau kama wangelijua yaliyomo humo [fadhila na faida] wangeliziendea [kuziswali] japo kwa kutambaa)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

8. Uislamu unasisitiza Waislamu kuungana kwa umoja kwa kila upande na kila hali.

 

 

Rejea: Aal-‘Imraan (3: 200), Asw-Swaff (61:4)

 

Rejea pia Hadiyth namba (20).

 

 

 

Share

080- Lu-ulu-un-Manthuwrun:Allaah Anamnawirisha Anayesikia Ujumbe Akabalighisha

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 80

 

Allaah Anamnawirisha Anayesikia Ujumbe Akabalighisha

 

 

 

 

 عن إبْنِ مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) ِقَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((نَضَّرَ اللَّهُ امْرَأً سَمِعَ مِنَّا شَيْئًا فَبَلَّغَهُ كَمَا سَمِعَه، فَرُبَّ مُبَلِّغٍ أَوْعَى مِنْ سَامِعٍ)) وراوه الترمذي وقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ  

 

Imepokelewa kutoka kwa bin Mas’uwd (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Allaah Amnawirishe mtu aliyesikia kitu kutoka kwetu naye akakibalighisha kama alivyosikia. Huenda anayefikishiwa akawa ana fahamu zaidi kuliko aliyesikia)). [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila na himizo la kutafuta elimu.

 

Rejea Hadiyth namba (16), (76) (78).

 

 

2. Umuhimu wa da’wah (kulingania Dini) japo kwa Aayah moja.

 

Rejea Hadiyth namba (77).

 

 

3. Tahadharisho na ukumbusho wa jukumu la kubalighisha elimu sahihi kwani ni amaana. Pindi mtu akibalighisha yasiyo sahihi akapotosha watu atabeba dhambi zao juu ya dhambi zake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لِيَحْمِلُوا أَوْزَارَهُمْ كَامِلَةً يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۙ وَمِنْ أَوْزَارِ الَّذِينَ يُضِلُّونَهُم بِغَيْرِ عِلْمٍ ۗ أَلَا سَاءَ مَا يَزِرُونَ﴿٢٥﴾

Ili wabebe mizigo (ya madhambi) yao kwa ukamilifu Siku ya Qiyaamah, na mizigo ya wale waliowapoteza bila ya kujua. Tanabahi!  Uovu ulioje wanayoyabeba. [An-Nahl (16: 25)]

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾

Na wala usifuatilie usiyo na elimu nayo. Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitaulizwa. [Al-Israa (17: 36)]

 

 

Rejea pia: Yaasiyn (36: 16), Al-‘Ankabuwt (29: 13)].

 

Rejea pia Hadiyth namba (16).

 

 

4. Umuhimu wa kuhifadhi Qur-aan na Hadiyth ili Muislamu aweze kubalighisha kwa Ummah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

بَلْ هُوَ آيَاتٌ بَيِّنَاتٌ فِي صُدُورِ الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ ۚ

 Bali hizo ni Aayaat bayana (zimehifadhika) katika vifua vya wale waliopewa elimu. [Al-‘Ankabuwt: 49]

        

 

 

5. Sikio ni kiungo muhimu kwa mwana Aadam kutokana na taathira yake ya kuingizwa iymaan baada ya kusikiliza Qur-aan na kauli za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), na ndio maana aghlabu katika Qur-aan utakuta Allaah (سبحانه وتعالى) Anatanguliza ‘kusikia’ kabla ya viungo vinginevyo. Mfano wa kauli Zake Allaah (سبحانه وتعالى) ni:

 

إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا﴿٢﴾

Hakika Sisi Tumemuumba insani kutokana na tone la manii iliyochanganyika ili Tumjaribu; Tukamjaalia mwenye kusikia na kuona.  [Al-Insaan (76: 2)]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَهُوَ الَّذِي أَنشَأَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ ۚ قَلِيلًا مَّا تَشْكُرُونَ ﴿٧٨﴾

Naye (Allaah) Ndiye Ambaye Aliyekuumbieni  kusikia na kuona na nyoyo. Ni machache mnayoshukuru. [Al-Muuminuwn: 23: 78)]

 

 

Na Anasema pia (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ مَكَّنَّاهُمْ فِيمَا إِن مَّكَّنَّاكُمْ فِيهِ وَجَعَلْنَا لَهُمْ سَمْعًا وَأَبْصَارًا وَأَفْئِدَةً فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُمْ سَمْعُهُمْ وَلَا أَبْصَارُهُمْ وَلَا أَفْئِدَتُهُم مِّن شَيْءٍ إِذْ كَانُوا يَجْحَدُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ﴿٢٦﴾

Na kwa yakini Tuliwamakinisha katika ambayo Hatukumakinisheni humo (nyinyi Maquraysh); na Tukawajaalia masikio na macho na nyoyo za kutafakari; lakini hayakuwafaa chochote masikio yao na wala macho yao na wala nyoyo zao za kutafakari walipokuwa wakikanusha kwa ujeuri Aayaat (hoja, ishara) za Allaah na yakawazunguka ambayo walikuwa wakiyafanyia istihzai. [Al-Ahqaaf (46: 26)]

 

Na pia Anasema (سبحانه وتعالى):

 

قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ أَمَّن يَمْلِكُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَمَن يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَيُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ الْأَمْرَ ۚ فَسَيَقُولُونَ اللَّـهُ ۚ فَقُلْ أَفَلَا تَتَّقُونَ﴿٣١﴾

Sema: “Nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini. Au nani anayemiliki kusikia na kuona; na nani anayemtoa aliye hai kutoka mfu, na anayemtoa mfu kutoka aliye uhai; na nani anayeendesha mambo (yote)?”  Watasema: “Ni Allaah”; basi sema: “Je basi hamuwi na taqwa?”   [Yuwnus (10: 31)]

 

Rejea pia:  An-Nahl (16: 78), Al-Mulk (67: 23), Huwd (11: 20), As-Sajdah (32: 9), Al-Israa (17: 36).

 

 

Na makafiri waliwakataza watu wasisikilize Qur-aan kwa sababu ilikuwa ikiwaathiri wengineo pindi wanapoisikiliza, na baadhi yao waliingia katika Uislamu kwa kusikia maneno ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَسْمَعُوا لِهَـٰذَا الْقُرْآنِ وَالْغَوْا فِيهِ لَعَلَّكُمْ تَغْلِبُونَ﴿٢٦﴾

Na wale waliokufuru wakasema: “Msiisikilize hii Qur-aan na ifanyieni rabsha huenda mkashinda.” [Fusw-Swilat 41: 26)]

 

 

Na ndio maana Allaah (سبحانه وتعالى) Akamuamrisha Rasuli Wake  (صلى الله عليه وآله وسلم) :

 

وَإِنْ أَحَدٌ مِّنَ الْمُشْرِكِينَ اسْتَجَارَكَ فَأَجِرْهُ حَتَّىٰ يَسْمَعَ كَلَامَ اللَّـهِ ثُمَّ أَبْلِغْهُ مَأْمَنَهُ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَوْمٌ لَّا يَعْلَمُونَ﴿٦﴾

Na ikiwa mmoja wa washirikina akikuomba umlinde, basi mlinde mpaka asikie Maneno ya Allaah (Qur-aan), kisha mfikishe mahali pake pa amani. Hivyo kwa kuwa wao ni watu wasiojua.  [At-Tawbah (9: 6)]

 

 

 

6. Athari ya sikio imewafanya Makafiri wajilaumu pale watakapoingizwa motoni kuwa laiti kama wangelisikiliza na kutia akilini. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلِلَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ﴿٦﴾

Na kwa wale waliomkufuru Rabb wao kuna adhabu ya Jahannam, na ubaya ulioje mahali pa kuishia. 

 

إِذَا أُلْقُوا فِيهَا سَمِعُوا لَهَا شَهِيقًا وَهِيَ تَفُورُ﴿٧﴾

Watakapotupwa humo, watausikia mkoromo wa pumzi wa kuchukiza nao unafoka.

 

تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ الْغَيْظِ ۖ كُلَّمَا أُلْقِيَ فِيهَا فَوْجٌ سَأَلَهُمْ خَزَنَتُهَا أَلَمْ يَأْتِكُمْ نَذِيرٌ﴿٨﴾

Unakaribia kupasuka kwa ghadhabu. Kila wanapotupwa humo kundi, walinzi wake watawauliza: “Je, hajakufikieni mwonyaji yeyote?” 

 

 

قَالُوا بَلَىٰ قَدْ جَاءَنَا نَذِيرٌ فَكَذَّبْنَا وَقُلْنَا مَا نَزَّلَ اللَّـهُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ كَبِيرٍ﴿٩﴾

Watasema: Ndio! Kwa yakini alitujia mwonyaji, lakini tulikadhibisha, na tukasema: “Allaah Hakuteremsha kitu chochote; nyinyi si chochote isipokuwa mumo katika upotofu mkubwa.”

 

وَقَالُوا لَوْ كُنَّا نَسْمَعُ أَوْ نَعْقِلُ مَا كُنَّا فِي أَصْحَابِ السَّعِيرِ﴿١٠﴾

Na watasema: “Lau tungelikuwa tunasikiliza au tunatia akilini, tusingelikuwa katika watu wa motoni.” 

 

فَاعْتَرَفُوا بِذَنبِهِمْ فَسُحْقًا لِّأَصْحَابِ السَّعِيرِ﴿١١﴾

Basi watakiri madhambi yao, na (wataambiwa): “Tokomeeni mbali watu wa motoni.”   [Al-Mulk 67: 6-11)]

 

 

 

7. Umuhimu wa kufikisha kwa wengine ambao hawakupata fursa ya kusikia kama vile Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipokhutubia Maswahaba katika Hijjatul-Widaa’i (Hajj ya kuaga) akawaambia:

 

(( أَلا فَلْيُبَلِّغِ الشَّاهِدُ مِنْكُمُ الْغَائِبَ))

((…basi abalighishe (afikishe ujumbe) aliyekuweko shahidi hapa miongoni mwenu kwa asiyekuweko)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 

8. Tofauti baina ya viumbe vya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa jinsi ambavyo mwenye kubalighishiwa huenda akawa na kipawa kizuri zaidi cha kufikisha kuliko aliyesikia mwanzoni akayafikisha kwa mwengine. Hata huenda mwanafunzi akaathirika zaidi na mafundisho baada ya kufikishiwa na mwalimu wake.

 

 

Share

081-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Adhabu Kali Kwa Anayeficha Elimu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 81

 

Adhabu Kali Kwa Anayeficha Elimu

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ سُئِلَ عَنْ عِلْمٍ فَكَتَمَهُ أَلْجَمَهُ اللَّهُ بِلِجَامٍ مِنْ نَارٍ يَوْمَ الْقِيَامَةِ)) رواه أبو داوود و الترمذي وقال: حديث حسن

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Anayeulizwa jambo katika elimu na akaficha, atafungwa lijamu ya moto Siku ya Qiyaamah)). [Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hatari ya kuficha elimu nayo inatokana na uchoyo wa elimu ambao watu wa kale walioneana wivu kwayo wakakhitilafiana. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَآتَيْنَاهُم بَيِّنَاتٍ مِّنَ الْأَمْرِ ۖ فَمَا اخْتَلَفُوا إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْعِلْمُ بَغْيًا بَيْنَهُمْ ۚ

 Na Tukawapa hoja bayana ya mambo (ya Dini). Basi hawakukhitilafiana isipokuwa baada ya kuwajia elimu kwa kufanyiana baghi na uhusuda baina yao [Al-Jaathiyah (45: 17)]

 

Reja pia: Al-Baqarah (2: 159), (174), Aal-‘Imraan (3: 19), Ash-Shuwraa (42: 14).

 

 

 

2. Kuficha elimu ni miongoni mwa dhambi kubwa kwa vile inastahiki adhabu kali kama ilivyotajwa katika Hadiyth na pia laana za Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ يَكْتُمُونَ مَا أَنزَلْنَا مِنَ الْبَيِّنَاتِ وَالْهُدَىٰ مِن بَعْدِ مَا بَيَّنَّاهُ لِلنَّاسِ فِي الْكِتَابِ ۙ أُولَـٰئِكَ يَلْعَنُهُمُ اللَّـهُ وَيَلْعَنُهُمُ اللَّاعِنُونَ ﴿١٥٩﴾

Hakika wale wanaoficha yale Tuliyoyateremsha katika hoja bayana na mwongozo baada ya kuwa Tumeyabainisha kwa watu katika Kitabu, hao Anawalaani Allaah na wanalaaniwa na kila mwenye kulaani.

 

إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا وَأَصْلَحُوا وَبَيَّنُوا فَأُولَـٰئِكَ أَتُوبُ عَلَيْهِمْ ۚ وَأَنَا التَّوَّابُ الرَّحِيمُ ﴿١٦٠﴾ 

Isipokuwa wale waliotubu na wakatengenea na wakabainisha (haki); basi hao Napokea tawbah zao, Na Mimi ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [Al-Baqarah (2: 159-160)].

 

 

 

3. Sababu mojawapo ya kumuingiza mtu motoni ni kuficha elimu, hivyo ni wajibu kutahadhari na jambo hili.

 

 

 

4. Ujinga wa kutokuelewa fadhila za kutoa elimu badala ya kuificha, kwani ndio itakayomfaa mtu baada ya kufariki kwake.

Rejea Hadiyth namba (16), (77), (78),  (80).

 

 

5. Kuifunza elimu ni kama kuitolea swadaqah, hivyo Allaah (سبحانه وتعالى) Humzidishia mtu kila anachokitoa kwa ajili Yake. Kinyume chake ni kama kuzuia mali bila ya kuitoa katika Njia ya Allaah.  Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((مَثَلُ الَّذي يَتعَلَّمُ العِلْمَ ثُمَّ لا يُحَدِّثُ بهِ، كمَثَلِ الَّذي يَكْنِزُ الكَنزَ فلا يُنْفِقُ منهُ)) أخرجه الطبراني في: المعجم الأوسط (689) وصححه الألباني في السلسة الصحيحة (3479)

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mfano wa ambaye anajifunza elimu kisha asiihadithie ni kama mfano wa ambaye anaweka hazina wala asiitoe [fiy sabiliLLaah])) [Atw-Twabaraaniy fiy Mu’jim Al-Awsatw (689), na ameisahihisha Al-Albaaniy katika As-Silsilah Asw-Swahiyhah (3479)]

 

 

6. Ni jambo la kufahamika kuwa kila unapotoa kitu kama elimu vile ndivyo inavyozidi kuongezeka kama vile Swadaqah. Na hivi ndivo shukurani kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kuwa ametoa mtu kile Alichomruzuku. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذْ تَأَذَّنَ رَبُّكُمْ لَئِن شَكَرْتُمْ لَأَزِيدَنَّكُمْ ۖ وَلَئِن كَفَرْتُمْ إِنَّ عَذَابِي لَشَدِيدٌ﴿٧﴾

 Na pindi Alipotangaza Rabb wenu: “Ikiwa mtashukuru, bila shaka Nitakuzidishieni (neema Zangu); na mkikufuru, basi hakika adhabu Yangu ni kali. [Ibraahiym 14: 7)]

 

 

  

Share

082-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Fadhila Za Siku Ya Ijumaa Na Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 82

 

Fadhila Za Siku Ya Ijumaa Na Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

 

 

 

عَنْ أَوْسِ بْنِ أَوْسٍ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ مِنْ أَفْضَلِ أَيَّامِكُمْ يَوْمَ الْجُمُعَةِ، فَأَكْثِرُوا عَلَيَّ مِنْ الصَّلاةِ فِيهِ، فَإِنَّ صَلاَتَكُمْ مَعْرُوضَةٌ عَلَيَّ)) قَالوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَكَيْفَ تُعْرَضُ صَلاتُنَا عَلَيْكَ وَقَدْ أَرَمْتَ؟  قَالَ: يَقُولُ:  بَلِيتَ  قَالَ: ((إِنَّ اللَّهَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى حَرَّمَ عَلَى الأَرْضِ أَجْسَادَ الأَنْبِيَاءِ)) رواه ابو داوُود بِاِسنادٍ صحيح

 

Imepokelewa kutoka kwa Aws bin Aws (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Hakika siku zenu zilizo bora mno ni siku ya Ijumaa, basi kithirisheni kuniswalia siku hiyo, hakika Swalaah zenu huwa naletewa)). Maswahaba wakauliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Vipi Swalaah zetu kuwa unaletewa na ilihali wakati huo utakuwa umeshaoza?” Akajibu: ((Hakika Allaah Ameiharamisha ardhi kula viwiliwili vya Manabii)).  [Abu Daawuwd kwa isnaad Swahiyh].

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Fadhila na utukufu wa Ijumaa kama zilivyotajwa katika miongoni mwa  Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( خَيْرُ يَوْمٍ طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ يَوْمُ الْجُمُعَةِ فِيهِ خُلِقَ آدَمُ وَفِيهِ أُدْخِلَ الْجَنَّةَ وَفِيهِ أُخْرِجَ مِنْهَا وَلاَ تَقُومُ السَّاعَةُ إِلاَّ فِي يَوْمِ الْجُمُعَةِ))

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Siku bora kabisa iliyochomoza jua ni siku ya Ijumaa, na hiyo ndio ameumbwa Aadam na hiyo ndio aliingizwa Jannah (Peponi) na akatolewa humo. Na Qiyaamah hakitosimamia siku yoyote isipokuwa siku ya Ijumaa)) [Muslim]

 

 Du’aa kutakabaliwa:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) ذَكَرَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ فَقَالَ:  ((فِيهِ سَاعَةٌ لاَ يُوَافِقُهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ وَهُوَ قَائِمٌ يُصَلِّي يَسْأَلُ اللَّهَ تَعَالَى شَيْئًا إلاَّ أَعْطَاهُ إِيَّاهُ)) وَأَشَارَ بِيَدِهِ يُقَلِّلُهَا

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ametaja Siku ya Ijumaa akasema: ((Humo mna saa haimwafikii mja Muislamu akiwa amesimama anaswali anamwomba Allaah تعالى kitu ila Anampa)). Akaashiria kuonyesha ukaribu wake [Al-Bukhaariy (935), Muslim (852) na wengineo]

 

Pia:

 

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ (رضي الله عنه) عَنْ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((يَوْمُ الْجُمُعَةِ اثْنَتَا عَشْرَةَ سَاعَةً ،لاَ يُوجَدُ فِيهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ يَسْأَلُ اللَّهَ شَيْئًا إلاَّ آتَاهُ إِيَّاهُ ، فَالْتَمِسُوهَا آخِرَ سَاعَةٍ بَعْدَ الْعَصْر))

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Siku ya Ijumaa kuna masaa kumi na mbili ambayo hapatikani mja Muislamu anayemwomba Allaah kitu ila Anampa, basi itafuteni baada ya Swalaah ya Alasiri))  [Swahiyh Abiy Daawuwd (1048), Swahiyh An-Nasaaiy (1388), Swahiyh Al-Jaami’ (8190)]

 

 

2.   Amri ya Allaah (سبحانه وتعالى) kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kama Anavyosema:

 

 

إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ ۚ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾

Hakika Allaah na Malaika Wake wanamswalia Nabiy. Enyi walioamini mswalieni na msalimieni kwa mamkizi ya amani na kwa tasliymaa. [Al-Ahzaab (33: 56)]

 

 

3. Fadhila za kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni nyingi na tukufu mno. Miongoni mwanzo ni Hadiyth:

 

 

عنْ عبد اللَّه بن عمرو بن العاص رضي اللَّه عنْهُمَا أنَّهُ سمِع رسُول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم يقُولُ: ((مَنْ صَلَّى عَلَيَّ صَلاَةً، صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ بِهَا عشْراً))  رواهُ مسلم

Imetoka kwa 'Abdullaah bin 'Amru bin Al'-Aasw (رضي الله عنهما)  kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Atakayeniswalia mara moja, Allaah Atamswalia mara kumi)) [Muslim]

 

Pia:

 

 عنْ أبي هُريْرةَ رضي اللَّه عنهُ أنَّ رسُولَ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال: ((ما مِنْ أحد يُسلِّمُ علَيَّ إلاَّ ردَّ اللَّه علَيَّ رُوحي حَتَّى أرُدَّ عَليهِ السَّلامَ)) رواهُ أبو داود بإسناد صحيحٍ

Imetoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Yeyote atakayeniswalia hurudishiwa roho yangu hadi nimrudishie salaam)) [Abuu Daawuwd kwa Isnaad ya Hasan]

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لاَ تَجْعَلُوا بُيُوتَكُمْ قُبُورًا، وَلاَ تَجْعَلُوا قَبْرِي عِيدًا، وَصَلُّوا عَلَيَّ فَإِنَّ صَلاتَكُمْ تَبْلُغُنِي حَيْثُ كُنْتُمْ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ وَرُوَاتُهُ ثِقَاتٌ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msifanye nyumba zenu makaburi, wala msilifanye kaburi langu kuwa ni mahali pa kurejewa rejewa na niswalieni, kwani kuniswalia kwenu kunanifikia popote mlipo)) [Abuu Daawuwd kwa isnaad Hasan ya wasimuliaji wanaotegemewa]

 

 

 

4. Kemeo la kutokumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عنْ أبي هُريْرةَ رضي اللَّه عنهُ قال: قال رسُولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم: ((رَغِم أنْفُ رجُلٍ ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَمْ يُصَلِّ علَيَّ))  رواهُ الترمذي وقالَ : حديثٌ حسنٌ .

 

Imetoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Amepata khasara mtu ambaye nimetajwa kwake na hakuniswalia)) [At-Tirmidhiy na kasema Hadiyth Hasan]

 

 

Pia:

 

 وعن علِيٍّ رضي اللَّه عنْهُ قال: قال رسُولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم: ((الْبخِيلُ من ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَم يُصَلِّ علَيَّ)) رواهُ الترمذي وقالَ : حديثٌ حسنٌ صحيحٌ .

Imetoka kwa 'Aliy (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Bakhili ni yule ambaye nimetajwa kwake na hakuniswalia)) [At-Tirmidhiy na kasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

 

5.   Himizo la kutenda mema na ‘ibaadah kwa wingi siku ya Ijumaa mfano: Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم ), kusoma Suwratul-Kahf, Swalaah ya Ijumaa na kumdhukuru mno  Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ وَذَرُوا الْبَيْعَ ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya Swalaah siku ya Ijumaa, kimbilieni kumdhukuru Allaah na acheni kuuza na kununua. Hivyo ni kheri kwenu mkiwa mnajua.

 

 

فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ وَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴿١٠﴾

Na inapomalizika Swalaah, tawanyikeni katika ardhi, na tafuteni katika fadhila za Allaah, na mdhukuruni Allaah sana ili mpate kufaulu.

 

 

وَإِذَا رَأَوْا تِجَارَةً أَوْ لَهْوًا انفَضُّوا إِلَيْهَا وَتَرَكُوكَ قَائِمًا ۚ قُلْ مَا عِندَ اللَّـهِ خَيْرٌ مِّنَ اللَّـهْوِ وَمِنَ التِّجَارَةِ ۚ وَاللَّـهُ خَيْرُ الرَّازِقِينَ﴿١١﴾

Na wanapoona tijara au pumbao wanaikimbilia, na wanakuacha umesimama. Sema: “Yaliyoko kwa Allaah ni bora zaidi kuliko pumbao na tijara, na Allaah ni Mbora wa wenye kuruzuku.   [Al-Jumu’ah (62: 9-11)]

 

 

6. Fadhila za Manabii kwamba miili yao haiozi.

 

 

7. Hima za Maswahaba kuuliza jambo wasilolifahamu na kupenda kujua zaidi.

 

 

Share

083-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Makatazo Ya Kujumuika Kaburini, Kumswalia Nabiy Kunamfikia

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 83

 

Makatazo Ya Kujumuika Kaburini, Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Popote Ulipo Kunamfikia

 

 

 

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ تَجْعَلُوا قَبْرِي عِيدًا، وَصَلُّوا عَلَيَّ فَإِنَّ صلاَتَكُمْ تَبْلُغُنِي حَيْثُ كُنْتُمْ)) رواه أبو داود بإسنادٍ صحيح

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msifanye [msijikusanye] kaburini mwangu kama mnavyojikusanya (wakati wa) sikukuu, niswalieni, hakika Swalaah yenu inanifikia popote mnapokuwa)). [Abuu Daawuwd kwa isnaad Swahiyh]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Makatazo ya vitendo visivyoruhusiwa wakati wa kuzuru kaburi la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kama kupandisha sauti, kugusa kuta na kujipangusa mwilini na usoni kutafuta baraka na mambo mengineyo ya uzushi ambayo mengineyo yanapelekea katika shirki. Baadhi ya Waislamu wanatenda haya katika kuzuru kaburi la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) huko Madiynah.  Hali kadhaalika katika kuzuru makaburi ya waja wema kuwaomba na hata kuwaabudu. Hivyo ni kupindukia mipaka ambayo imekatazwa katika Shariy’ah ya Dini yetu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى)

 

 يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَا تَغْلُوا فِي دِينِكُمْ

Enyi Ahlal-Kitaabi! Msipindukie mipaka katika dini yenu [An-Nisaa (4: 171)]

 

 

 

2. Pendekezo la kuzuru kaburi la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kufuata adabu zake katika Shariy’ah na si kinyume chake.

 

 

 

3. Amri ya kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ ۚ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾

Hakika Allaah na Malaika Wake wanamswalia Nabiy. Enyi walioamini mswalieni na msalimieni kwa mamkizi ya amani na kwa tasliymaa. [Al-Ahzaab (33: 56)]

 

 

Rejea Hadiyth namba (82).

 

 

4. Fadhila kwa Waislamu katika kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

Rejea Hadiyth namba (82)

 

 

 

Share

084-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mimi Ni Vile Mja Wangu Anavyonidhania. Niko Pamoja Naye Anaponitaja

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 84

 

Mimi Ni Vile Mja Wangu Anavyonidhania. Niko Pamoja Naye Anaponitaja

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يَقُولُ اللَّهُ تَعَالَى: أَنَا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي وَأَنَا مَعَهُ إِذَا ذَكَرَنِي، فَإِنْ ذَكَرَنِي فِي نَفْسِهِ ذَكَرْتُهُ فِي نَفْسِي، وَإِنْ ذَكَرَنِي فِي مَلَإٍ ذَكَرْتُهُ فِي مَلَإٍ خَيْرٍ مِنْهُمْ، وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ بِشِبْرٍ تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ ذِرَاعًا،

 وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ ذِرَاعًا تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ بَاعًا، وَإِنْ أَتَانِي يَمْشِي أَتَيْتُهُ هَرْوَلَةً)) متفق عليه

 

 Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ambaye amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alisema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: Mimi ni vile mja Wangu anavyonidhania. Niko pamoja naye anaponitaja. Anaponitaja katika nafsi yake, Ninamtaja katika nafsi Yangu, anaponitaja katika hadhara, Ninamtaja katika hadhara bora zaidi. Na anaponikaribia shibiri Ninamkaribia dhiraa, anaponikaribia dhiraa, Ninamkaribia pima, anaponijia kwa mwendo [wa kawaida] Ninamwendea mbio)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Wajibu wa kuwa na husnudhw-dhwann (dhana nzuri) kwa Allaah (سبحانه وتعالى) na kutokukata tamaa na Rahma Yake pindi mtu anapokuwa katika shida na dhiki au mtu anapotaka jambo fulani afanikiwe. Basi asichoke wala asikate tamaa kwani kukata tamaa ni kukufuru kama alivyosema Nabiy Ya’quwb (عليه السلام) kuwaambia wanawe katika kumtafuta Nabiy Yuwsuf (عليه السلام) :   

 

وَلَا تَيْأَسُوا مِن رَّوْحِ اللَّـهِ ۖ إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٧﴾

Wala msikate tamaa na faraja ya Allaah; hakika hawakati tamaa na faraja ya Allaah isipokuwa watu makafiri.”  [Yuwsuf (12: 87)]

 

 

Rejea pia Al-Baqarah (2: 249) pindi Muumini anapofikwa na hali ngumu kabisa ambayo anakaribiwa kushindwa nguvu.

 

 

 

2. Kuwa na husnudhw-dhwann (dhana nzuri) na Allaah (سبحانه وتعالى) katika kumuomba maghfirah na tawbah kwani Yeye Anapokea tawbah za waja Wake hata yawe ni madhambi makubwa vipi madam tu mja atarudi kuomba maghfirah na atatubia kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا ۚ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٥٣﴾

Sema: Enyi waja Wangu ambao wamepindukia mipaka juu ya nafsi zao: “Msikate tamaa na rahmah ya Allaah; hakika Allaah Anaghufuria dhambi zote; hakika Yeye Ndiye Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.” [Az-Zumar (39: 53)]

 

 

 

3. Kuwa na husnudhw-dhwann (dhana nzuri) na Allaah (سبحانه وتعالى) katika kumuomba du’aa pia ambayo ni mojawapo wa sababu ya kutakabaliwa du’aa kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ادْعُوا اللَّهَ وَأَنْتُمْ مُوقِنُونَ بِالإِجَابَةِ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّهَ لاَ يَسْتَجِيبُ دُعَاءً مِنْ قَلْبٍ غَافِلٍ لاَهٍ))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Muombeni Allaah huku mkiwa mna yakini kujibiwa, na jueni kwamba Allaah Hatakabali du’aa inayotoka katika moyo ulioghafilika au usiojali)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3479), Swahiyh Al-Jaami’ *245), Swahiyh At-Targhiyb (1653)]

 

 

 

 

4. Wasiya wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) siku tatu kabla ya kufariki kwake kwamba Muumini awe na husnudhw-dhwann (dhana nzuri) kwa Rabb Wake:   

 

 

عَنْ جَابِرٍ، قَالَ سَمِعْتُ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَبْلَ وَفَاتِهِ بِثَلاَثٍ يَقُولُ: ((لاَ يَمُوتَنَّ أَحَدُكُمْ إِلاَّ وَهُوَ يُحْسِنُ بِاللَّهِ الظَّنَّ)) مسلم

 Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه) ambaye amesema: Nimesikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Asife mtu isipokuwa awe ana husnudhw-dhwann (dhana nzuri) na Allaah)) [Muslim]

 

 

 

5. Miongoni mwa sifa za Waumini ni kuwa na husnudhw-dhwann (dhana nzuri) kwamba watakutana na Allaah (سبحانه وتعالى) huko Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَاقُو رَبِّهِمْ وَأَنَّهُمْ إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ﴿٤٦﴾

Ambao wana yakini kwamba hakika wao ni wenye kukutana na Rabb wao na hakika wao Kwake ni wenye kurejea. [Al-Baqarah (2; 46)]

 

 

 

 

6. Kinyume chake ni sifa za wanafiki na makafiri, na waovu wanaomdhania Allaah (سبحانه وتعالى) suw’udhw-dhwann (dhanna mbaya). Hao watapata adhabu za Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema (سبحانه وتعالى):

 

وَيُعَذِّبَ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْمُشْرِكِينَ وَالْمُشْرِكَاتِ الظَّانِّينَ بِاللَّـهِ ظَنَّ السَّوْءِ ۚ عَلَيْهِمْ دَائِرَةُ السَّوْءِ ۖ وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ وَلَعَنَهُمْ وَأَعَدَّ لَهُمْ جَهَنَّمَ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا﴿٦﴾

Na Awaadhibu wanafiki wa kiume na wanafiki wa kike na washirikina wa kiume na washirikina wa kike, wanaomdhania Allaah dhana ovu.  Utawafikia mgeuko mbaya; na Allaah Awaghadhibikie, na Awalaani, na Awaandalie  Jahannam, na paovu palioje mahali pa kuishia. [Al-Fat-h (48: 6)]

 

Ni sawa na wanafiki   katika vita vya Uhud wakimdhania Allaah (سبحانه وتعالى) dhana mbaya. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

  وَطَائِفَةٌ قَدْ أَهَمَّتْهُمْ أَنفُسُهُمْ يَظُنُّونَ بِاللَّـهِ غَيْرَ الْحَقِّ ظَنَّ الْجَاهِلِيَّةِ ۖ يَقُولُونَ هَل لَّنَا مِنَ الْأَمْرِ مِن شَيْءٍ ۗ قُلْ إِنَّ الْأَمْرَ كُلَّهُ لِلَّـهِ ۗ يُخْفُونَ فِي أَنفُسِهِم مَّا لَا يُبْدُونَ لَكَ ۖ يَقُولُونَ لَوْ كَانَ لَنَا مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ مَّا قُتِلْنَا هَاهُنَا ۗ  

Kundi likawashughulisha nafsi zao wakamdhania Allaah pasi na haki dhana ya kijahili; wanasema: “Je, tuna amri yoyote sisi katika jambo hili?” Sema: “Hakika amri yote ni ya Allaah.” Wanaficha katika nafsi zao yale wasiyokubainishia. Wanasema: “Lau tungelikuwa tuna amri yoyote katika jambo basi tusingeliuliwa hapa.”  [Aal-‘Imraan (3: 154)]

  

 

7. Fadhila za kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) ni nyingi mno na ‘ibaadah hii haina kikomo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾

Enyi walioamini!  Mdhukuruni Allaah kwa wingi wa kumdhukuru.

 

وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

Na Msabbihini asubuhi na jioni.

 

هُوَ الَّذِي يُصَلِّي عَلَيْكُمْ وَمَلَائِكَتُهُ لِيُخْرِجَكُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ ۚ وَكَانَ بِالْمُؤْمِنِينَ رَحِيمًا ﴿٤٣﴾

Yeye Ndiye Anakurehemuni, na Malaika Wake wanamuomba Akughufurieni na Akurehemuni ili Akutoeni kutoka katika viza kuingia katika Nuru. Naye daima ni Mwenye kurehemu Waumini.

 

تَحِيَّتُهُمْ يَوْمَ يَلْقَوْنَهُ سَلَامٌ ۚ وَأَعَدَّ لَهُمْ أَجْرًا كَرِيمًا ﴿٤٤﴾

Maamkizi yao Siku watakayokutana Naye; ni ‘Salaam’; na Amewaandalia ujira wa ukarimu. [Al-Ahzaab (33: 41-44)]

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 152), Aal-‘Imraan (3: 191-195), Ar-Ra’d (13: 28).

 

Rejea pia Hadiyth namba (85).

 

 

 

8. Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kwa dhahiri na siri, nyakati zote, katika kila hali ni ‘amali tukufu kabisa inayomkurubisha mja kwa Rabb wake kwani mja anapomdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى), Naye hukumbuka kama Anavyosema:

 

فَاذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ وَاشْكُرُوا لِي وَلَا تَكْفُرُونِ﴿١٥٢﴾

Basi nidhukuruni na Mimi Nitakukumbukeni; na nishukuruni wala msinikufuru. [Al-Baqarah (2: 152)] 

 

 

 

9. Anayetaka kukumbukwa na Allaah (سبحانه وتعالى) basi na amdhukuru na amshukuru apate malipo mema.  Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

Na wanaomdhukuru Allaah kwa wingi wanaume na wanawake; Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu. [Al-Ahzaab (33: 35)]

 

 

 

10. Hadiyth inadhihirisha mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa waja Wake wanaomdhukuru sana na wanaotenda ‘ibaadah ziada.

 

 

 

11. Dhihirisho la daraja ya vikao baina ya waja, Malaika, na Manabii. Wanavyuoni wamesema: “Hakika Manabii Wateule katika watu, ni bora kuliko Malaika Wateule kama Jibriyl. Na Malaika Wateule ni bora kuliko watu wa kawaida. Na watu wa kawaida nao ni wale wenye kutii, ni bora kuliko Malaika wa kawaida. Na Malaika wa kawaida ni bora kuliko watu wenye kufanya maasi.” [Nuzhat Al-Muttaqiyn (2: 217)]

 

 Rejea pia Hadiyth namba (98).

 

 

Share

085-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kumdhukuru Allaah Kunampandisha Cheo Mja Na Ni Miongoni Mwa ‘Amali Bora Kabisa

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 85

 

Kumdhukuru Allaah Kunampandisha Cheo Mja Na Ni Miongoni Mwa ‘Amali Bora Kabisa

 

 

 

 

عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((ألاَ أُنَبِّئُكُمْ بِخَيْرِ أَعْمَالِكُمْ، وَأَزْكَاهَا عِنْدَ مَلِيكِكُمْ، وَأَرْفَعِهَا فِي دَرَجَاتِكُمْ، وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ إِنْفَاقِ الذَّهَبِ وَالفِضَّةِ، وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ أَنْ تَلْقَوْا عَدُوَّكُمْ فَتَضْرِبُوا أَعْنَاقَهُمْ وَيَضْرِبُوا أَعْنَاقَكُمْ؟)) قَالُوا : بَلَى: قَالَ: ((ذِكْرُ اللَّهِ تَعَالَى)) رواه الترمذي. قَال الحاكم أبو عبد الله: إسناده صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abu Ad-Dardaa(رضي الله عنه)   ambaye amesema: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hivi niwaambieni khabari ya matendo yenu bora zaidi, na ambayo ni masafi mno mbele ya Rabb wenu, na ambayo ni ya juu mno katika daraja zenu, na ambayo ni bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na fedha, na ambayo ni bora kuliko kukutana na adui zenu mkawapiga shingo zao, nao wakakupigeni shingo zenu?))  Wakasema [Maswahaba]: Ndio. Akasema ((Ni kumdhukuru Allaah Ta’aalaa)). [At-Tirmidhiy na amesema Abu ‘Abdillaah: Isnaad yake ni Swahiyh]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Fadhila za kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) ni nyingi, na hii ni miongoni mwazo za kupewa ujira adhimu.   Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

 Na wanaomdhukuru Allaah kwa wingi wanaume na wanawake; Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu. [Al-Ahzaab (33: 35)]

 

 

 

2. Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kunasababisha utulivu wa moyo, furaha na amani. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

الَّذِينَ آمَنُوا وَتَطْمَئِنُّ قُلُوبُهُم بِذِكْرِ اللَّـهِ ۗ أَلَا بِذِكْرِ اللَّـهِ تَطْمَئِنُّ الْقُلُوبُ ﴿٢٨﴾

Wale walioamini na zikatua nyoyo zao kwa kumdhukuru Allaah. Tanabahi!  Kwa kumdhukuru Allaah nyoyo hutulia! [Ar-Ra’d (13: 28)]

 

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (2: 191-195), Al-Ahzaab (33: 41-44).

 

Rejea pia Hadiyth namba (84). 

 

 

 

3. Ukitaka Allaah (سبحانه وتعالى) Akukumbuke basi mdhukuru kwa wingi kama Anavyosema:

 

 اذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ وَاشْكُرُوا لِي وَلَا تَكْفُرُونِ﴿١٥٢﴾

Basi nidhukuruni na Mimi Nitakukumbukeni; na nishukuruni wala msinikufuru. [Al-Baqarah (2: 152)]

 

 

4. Kudumisha kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) wakati wote, kwani kuna faida na manufaa mengi kwa Muislamu; faida hizo zimetajwa katika Hadiyth hiyo tukufu kuwa ni kuwa na daraja bora kabisa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى), na kwamba kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kunashinda kutoa dhahabu na fedha katika njia ya Allaah na kwamba kuliko kupigana jihaad. 

 

 

 

5. Rahmah na fadhila za Allaah (سبحانه وتعالى) kuwapatia thawabu na kuwapandisha vyeo waja kwa kutenda ‘amali nyepesi kabisa inayohitaji ulimi pekee katika kumdhukuru.

 

 

 

6. Kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kila wakati kutamzuia mtu kunena yasiyopasa; kutokufanya ghiybah (kusengenya), namiymah (kufitinisha), na kumzuia mtu kila aina ya maovu yanayotokana na ulimi.

 

 

 

7. Ulimi ni kiungo muhimu kabisa katika mwili wa bin Aadam, unaweza kumfikisha mtu Jannah au motoni.

 

 

 

8. Umuhimu wa kudumisha du’aa ya kuwezesha kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) inayosomwa baada ya Swalaah ambayo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alimuusia Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه):

 

عَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَخَذَ بِيَدِهِ وَقَالَ: ((يَا مُعَاذُ وَاللَّهِ إِنِّي لأُحِبُّكَ وَاللَّهِ إِنِّي لأُحِبُّكَ))‏.‏ فَقَالَ: ((أُوصِيكَ يَا مُعَاذُ لاَ تَدَعَنَّ فِي دُبُرِ كُلِّ صَلاَةٍ تَقُولُ: اللَّهُمَّ أَعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ وَشُكْرِكَ وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ))‏ ‏.‏ وَأَوْصَى بِذَلِكَ مُعَاذٌ الصُّنَابِحِيَّ وَأَوْصَى بِهِ الصُّنَابِحِيُّ أَبَا عَبْدِ الرَّحْمَنِ ‏.‏

 

Imepokelewa kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alimshika mkono wake akasema: ((Ee Mu’aadh!  Wa-Allaahi mimi nakupenda! Wa-Allaahi mimi nakupenda!)) Akasema: ((Nakuusia ee Mu’aadh usiache kusema katika kila baada ya Swalaah:

 

 

اللّهُـمَّ أَعِـنِّي عَلـى ذِكْـرِكَ وَشُكْـرِك وَحُسْـنِ عِبـادَتِـك

Allaahumma A’inniy ’alaa dhikrika washukrika wahusni ’Ibaadatika

 

Ee Allaah nisaidie juu Kukudhukuru, na kukushukuru na kukuabudu kwa uzuri upasao. 

   [Hadiyth ya Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (2/86), An-Nasaaiy (3/53) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/284)].

 

 

 

9. Hima ya Maswahaba (رضي الله عنهم) kutaka kujua mambo kutoka kwa mwalimu wao mkuu; Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

10. Muislamu kutodharau kufanya jambo la kheri hata likionekana ni dogo katika nadharia ya mmoja wetu.

 

 

11. Rahmah ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa waja Wake kwa kuwapatia thawabu nyingi kwa jambo ambalo laonekana ni dogo sana.

 

 

 

 

Share

086-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Atakayedhamini Ulimi Na Utupu Atadhaminiwa Jannah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 86

 

Atakayedhamini Ulimi Na Utupu Atadhaminiwa Jannah

 

 

 

عَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ (رضي الله عنه) عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَنْ يَضْمَنْ لِي مَا بَيْنَ لَحْيَيْهِ وَمَا بَيْنَ رِجْلَيْهِ أَضْمَنْ لَهُ الْجَنَّةَ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Sahl bin Sa’d (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Atakayenidhaminia kilichomo baina ya taya zake (yaani ulimi) na kilichomo baina ya miguu yake (yaani utupu), nami nitamdhamini Jannah)).  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Hatari ya kutumia viungo viwili vya mwili katika maasi; ulimi na utupu ambavyo vinaweza kumpelekea mtu motoni.

 

Rejea Hadiyth namba (87), (88), (89), (93), (126).

 

 

2. Viungo viwili hivyo vinaweza kuwa ni sababu ya kufuzu au kuangamia mtu.

 

Rejea Al-Muuminuwn (23: 3) At-Twuur (52: 11-14).

 

 

3. Aayah kadhaa na Hadiyth kadhaa zimeonya kuhusu maovu ya ulimi kama vile kukufuru, kutukana, ghiybah, kuhamisha maneno, kufitinisha watu, ufedhuli n.k. Na adhabu zake ni duniani, kaburini na Aakhirah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَيْلٌ لِّكُلِّ هُمَزَةٍ لُّمَزَةٍ ﴿١﴾

Ole kwa kila mwenye kukebehi na kukashifu watu kwa ishara na vitendo na kwa kila mwenye kufedhehesha kwa ulimi. [Al-Humazah: 1]

 

Rejea pia Al-Hujuraat (49: 11-12), Al-Israa (17: 36)

 

 

 

4. Kila kiungo kitakuja kutamka maovu yaliyotendwa nacho hata ulimi pia utasema. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ وَأَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٢٤﴾

Siku zitakaposhuhudia dhidi yao ndimi zao, na mikono yao, na miguu yao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda.  [An-Nuwr (24: 24)]

 

 

 

5-Rejea kisa cha ifk katika Al-Bukhaariy kilichoelezewa kirefu na mwenyewe ‘Aaishah (رضي الله عنها), na kauli za Allaah (سبحانه وتعالى) katika An-Nuwr (24: 11-21), kisa ambacho ulimi ndio uliofanya kazi kumzulia Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها). Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِنَّ الَّذِينَ جَاءُوا بِالْإِفْكِ عُصْبَةٌ مِّنكُمْ ۚ لَا تَحْسَبُوهُ شَرًّا لَّكُم ۖ بَلْ هُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُم مَّا اكْتَسَبَ مِنَ الْإِثْمِ ۚ وَالَّذِي تَوَلَّىٰ كِبْرَهُ مِنْهُمْ لَهُ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿١١﴾

Hakika wale walioleta singizo la kashfa; (kumzulia ‘Aaishah  رضي الله عنها) ni kundi miongoni mwenu. Msiichukulie kuwa ni shari kwenu, bali ni kheri kwenu.  Kila mtu katika wao atapata yale aliyochuma katika dhambi. Na yule aliyejitwika sehemu yake kubwa miongoni mwao atapata adhabu kuu.

 

لَّوْلَا إِذْ سَمِعْتُمُوهُ ظَنَّ الْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بِأَنفُسِهِمْ خَيْرًا وَقَالُوا هَـٰذَا إِفْكٌ مُّبِينٌ ﴿١٢﴾

Kwa nini mlipoisikia (kashfa ya kusingiziwa), Waumini wanaume na Waumini wanawake wasiwadhanie wenzao kheri, na wakasema: “Hii ni kashfa ya kusingizwa iliyo dhahiri?”

 

 

لَّوْلَا جَاءُوا عَلَيْهِ بِأَرْبَعَةِ شُهَدَاءَ ۚ فَإِذْ لَمْ يَأْتُوا بِالشُّهَدَاءِ فَأُولَـٰئِكَ عِندَ اللَّـهِ هُمُ الْكَاذِبُونَ ﴿١٣﴾

Kwa nini hawakuleta mashahidi wanne? Na kwa vile hawakuleta mashahidi, basi hao mbele ya Allaah ndio waongo.

 

 

وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ لَمَسَّكُمْ فِي مَا أَفَضْتُمْ فِيهِ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿١٤﴾

Na lau si fadhila ya Allaah juu yenu na rahmah Yake duniani na Aakhirah, bila shaka ingekuguseni adhabu kuu kwa yale mliyojishughulisha nayo kuyaropoka,

 

 

إِذْ تَلَقَّوْنَهُ بِأَلْسِنَتِكُمْ وَتَقُولُونَ بِأَفْوَاهِكُم مَّا لَيْسَ لَكُم بِهِ عِلْمٌ وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥﴾

Mlipoipokea (kashfa ya uzushi) kwa ndimi zenu, na mkasema kwa midomo yenu, yale ambayo hamkuwa na elimu nayo; na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allaah ni kubwa mno.

 

وَلَوْلَا إِذْ سَمِعْتُمُوهُ قُلْتُم مَّا يَكُونُ لَنَا أَن نَّتَكَلَّمَ بِهَـٰذَا سُبْحَانَكَ هَـٰذَا بُهْتَانٌ عَظِيمٌ ﴿١٦﴾

Na kwa nini mlipoisikia (kashfa ya kusingiziwa) msiseme: “Haitupasi sisi tuzungumze haya; Subhaanak! Utakasifu ni Wako huu ni usingiziaji wa dhulma mkubwa mno!”

 

يَعِظُكُمُ اللَّـهُ أَن تَعُودُوا لِمِثْلِهِ أَبَدًا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٧﴾

Allaah Anakuwaidhini msirudie abadani mfano wa haya, mkiwa ni Waumini wa kweli.

 

وَيُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمُ الْآيَاتِ ۚ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ ﴿١٨﴾

Na Allaah Anakubainishieni Aayaat. Na Allaah Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

 

إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿١٩﴾

Hakika wale wanaopenda uenee uchafu wa kashfa kwa wale walioamini; watapata adhabu iumizayo duniani na Aakhirah. Na Allaah Anajua nanyi hamjui.

 

وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ وَأَنَّ اللَّـهَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٠﴾

Na lau si fadhila ya Allaah juu yenu na rahmah Yake, na kwamba Allaah ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu.

 

 

Na humo tunapata mafundisho kwamba pindi Muumini anaposikia usengenyaji au uzushi au usingiziaji wa kashfa anapaswa afanye yafuatayo:

 

  • Ajidhanie kheri na wema yeye mwenyewe kwanza, kwa hiyo asimdhanie nduguye maovu hayo.
  • Asiseme jambo au kudhania mpaka wapatikane mashahidi wanne.
  • Atambue kwamba ghiybah (kusengenya) na buhtaan (kusingizia uongo) si jambo dogo bali ni kubwa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى).  
  • Atambue kwamba usengenyeji na kumzulia mtu jambo ovu ni miongoni mwa dhulma ambayo itampatia khasara duniani na khasa Aakhirah.
  • Atanabahi kwamba haimpasi mtu kujisemea tu uzushi na usengenyaji, bali akimbilie kumtakasa  Allaah (سبحانه وتعالى) hapo hapo anaposikia kwa kusema “Subhaanak!”
  • Akhofu adhabu kali ya Allaah (سبحانه وتعالى) Aliyoahidi kuhusiana na maovu haya.
  • Atambue kwamba lau kama si fadhila za Allaah (سبحانه وتعالى) na Rahmah Zake basi ingewashika adhabu mapema zaidi na fedheha ya kusingizia jambo ambalo si la kweli, hivyo ingebalibakia kuwa ni majuto ya milele!

 

         

6. Hikma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuvificha viungo viwili hivyo katika mwili wa bin Aadam kwa kuvihifadhi, na bin Aadam anapaswa naye kuvihifadhi kwa kutovitumia kwa maovu.

 

 

7. Tahadharisho la kutumia ulimi katika maovu, kwani ulimi juu ya kuwa ni kiungo kidogo, lakini ni mfalme wa viungo kama ilivyotajwa katika Hadiyth:  

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ، رَفَعَهُ قَالَ: ((إِذَا أَصْبَحَ ابْنُ آدَمَ فَإِنَّ الأَعْضَاءَ كُلَّهَا تُكَفِّرُ اللِّسَانَ فَتَقُولُ اتَّقِ اللَّهَ فِينَا فَإِنَّمَا نَحْنُ بِكَ فَإِنِ اسْتَقَمْتَ اسْتَقَمْنَا وَإِنِ اعْوَجَجْتَ اعْوَجَجْنَا))

 

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:  ((Anapoamka binaadamu, viungo vyote vinakufurisha [vinaonya maovu ya] ulimi: Mche Allaah kwa ajili yetu, kwani sisi tuko chini yako, ukinyooka nasi tunanyooka, na ukienda pogo, nasi tunapinda)). [At-Tirmidhiy, ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (351), Swahiyh At-Tirmidhiy (2407)]

 

 

 

8. Muislamu akumbuke kwamba Malaika wawili wako tayari kuandika neno lolote linalotamkwa hata liwe dogo vipi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِ نَفْسُهُ ۖ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ الْوَرِيدِ﴿١٦﴾

Na kwa yakini Tumemuumba insani na Tunajua yale yanayowaza nafsi yake, na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa koo.

 

إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ قَعِيدٌ﴿١٧﴾

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni. 

 

مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾

Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf (50: 16-18)]

 

 

Rejea pia Al-Infitwaar (82: 10-12)].

 

 

9.  Neno moja tu litamkwalo likiwa zuri au ovu linaweza kuwa sababu ya kumridhisha au kumghadhibisha Allaah (سبحانه وتعالى) mpaka Siku ya Qiyaamah:

 

 

 عن أَبي عبد الرحمن بِلالِ بن الحارِثِ المُزَنِيِّ رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : ((إنَّ الرَّجُلَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ رِضْوَانِ اللهِ تَعَالَى مَا كَانَ يَظُنُّ أنْ تَبْلُغَ مَا بَلَغَتْ يَكْتُبُ اللهُ لَهُ بِهَا رِضْوَانَهُ إِلَى يَومِ يَلْقَاهُ ، وإنَّ الرَّجُلَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ سَخَطِ اللهِ مَا كَانَ يَظُنُّ أنْ تَبْلُغَ مَا بَلَغَتْ يَكْتُبُ الله لَهُ بِهَا سَخَطَهُ إِلَى يَوْمِ يَلْقَاهُ )). رواه مالك في المُوَطَّأ ، والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Abuu 'Abdir-Rahmaan Bilaal bin Al-Haarith Al-Muzniy (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Kwa hakika mja atazungumza neno linalomridhisha Allaah, wala asidhani kuwa litafikia lilipofikia, Allaah Amuandikie kwa neno hilo Radhi Zake hadi Siku ya Qiyaamah. Na Kwa hakika mja atazungumza neno linalomkasirisha Allaah, wala asidhani kuwa litafikia lilipofikia, Allaah Amuandikie kwa neno hilo hasira Zake hadi Siku ya Qiyaamah)) [Maalik katika Muwattwa na At-Tirmidhiy ambaye amesema Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

 

 

10. Allaah (سبحانه وتعالى) Ameonya kutokukaribia zinaa:

 

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

Na wala msiikaribie zinaa. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya kabisa.  [Al-Israa 17: 32)]

 

 

Rejea pia matahadharisho mengineyo ya kutokuzini na adhabu zake: An-Nuwr (24: 2), Al-Furqaan (25: 68).

 

 

11. Adhabu ya zinaa ni kali mno kwa jinsi kitendo hiki kilivyokuwa kiovu mno kwa sababu kinaathiri watendaje wake, na mtoto anayezaliwa kutokana na kitendo hicho cha zinaa, na huenda kikaathiri jamii nzima. Adhabu yake hiyo huenda ikastahiki kupigwa mawe mzinifu mpaka mauti yamfike kwa dalili ifuatayo:

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة وَزَيْد بْن خَالِد الْجُهَنِيّ فِي الْأَعْرَابِيَّيْنِ اللَّذَيْنِ أَتَيَا رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ أَحَدهمَا: يَا رَسُول اللَّه إِنَّ اِبْنِي هَذَا كَانَ عَسِيفًا - يَعْنِي أَجِيرًا - عَلَى هَذَا فَزَنَى بِامْرَأَتِهِ فَافْتَدَيْت اِبْنِي مِنْهُ بِمِائَةِ شَاة وَوَلِيدَة فَسَأَلْت أَهْل الْعِلْم فَأَخْبَرُونِي أَنَّ عَلَى اِبْنِي جَلْد مِائَة وَتَغْرِيب عَام وَأَنَّ عَلَى اِمْرَأَة هَذَا: الرَّجْم فَقَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((وَاَلَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَأَقْضِيَنَّ بَيْنكُمَا بِكِتَابِ اللَّه تَعَالَى الْوَلِيدَة وَالْغَنَم رَدّ عَلَيْك وَعَلَى اِبْنك مِائَة جَلْدَة وَتَغْرِيب عَام. وَاغْدُ يَا أُنَيْس - لِرَجُلٍ مِنْ أَسْلَم - إِلَى اِمْرَأَة هَذَا فَإِنْ اِعْتَرَفَتْ فَارْجُمْهَا))  فَغَدَا عَلَيْهَا فَاعْتَرَفَتْ فَرَجَمَهَا - البخاري  و مسلم

 

kutoka kwa Abuu Hurayrah na Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy (رضي الله عنهما)  katika kisa cha Mabedui wawili waliokuja kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم),  mmoja alisema: "Ee Rasuli wa  Allaah, mwanangu (wa kiume) aliajiriwa na bwana huyu kisha akafanya zinaa na mke wake. Nimemlipa fidia kwa ajili ya mwanangu kwa kumpa kondoo mia moja na mtumwa mwanamke. Lakini nilipowauliza watu wenye elimu, wamesema kwamba mwanangu apigwe mijeledi mia na ahamishwe mji kwa muda wa mwaka na mke wa huyu bwana apigwe mawe hadi afariki".  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, nitahukumu baina yenu wawili kutokana na kitabu cha Allaah. Rudisha mtumwa mwanamke na kondoo na mwanao apigwe bakora mia kisha mwanao ahamishwe mbali kwa muda wa mwaka. Nenda Ee Unays!)) Alimwambia mtu katika kabila la Aslam, ((Nenda kwa mke wa huyu bwana na akikiri makosa yake, basi mpige mawe hadi mauti [yamfike])) Unays akamuendea na akakiri makosa yake, kwa hiyo akampiga mawe hadi mauti. [Al-Bukhaariy na Muslim]

  

Share

087-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kusengenya Ni Kumtaja Mtu Kwa Asilolipenda Na Kuzua Ni Kutaja Jambo Asilokuwa Nalo

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 87

 

Kusengenya Ni Kumtaja Mtu Kwa Asilolipenda

Na Kuzua Ni Kutaja Jambo Asilokuwa Nalo

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((أَتَدْرُونَ مَا الْغِيبَةُ؟)) قَالُوا: اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ. قَالَ: ((ذِكْرُكَ أَخَاكَ بِمَا يَكْرَهُ)) قِيلَ: أَفَرَأَيْتَ إِنْ كَانَ فِي أَخِي مَا أَقُولُ؟  قَالَ: ((إنْ كَانَ فِيهِ مَا تَقُولُ فَقَدْ اغْتَبْتَهُ وَإِنْ لَمْ يَكُنْ فِيهِ فَقَدْ بَهَتَّهُ)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliuliza: ((Je mnajua maana ya Ghiybah [Kusengenya]?)) Wakasema: Allaah na Rasuli Wake wanajua. Akasema: ((Ni kumtaja ndugu yako kwa jambo analolichukia)). Akaulizwa: Hebu nieleze, iwapo ndugu yangu anayo yale niyasemayo? Akasema: ((Ikiwa analo hilo usemalo basi umeshamsengenya, na ikiwa hana hilo usemalo basi umeshamzushia uongo)).   [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Onyo la kutumia ulimi kwa maovu kama kupeana majina mabaya, kutukanana na ghiybah, Allaah (سبحانه وتعالى) Anaonya haya katika kauli Zake:

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿١١﴾

Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao. Na wala msifedheheshane kwa kutukanana na wala msiitane majina (mabaya) ya utani. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya iymaan. Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu.

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ﴿١٢﴾

Enyi walioamini!  Jieupusheni sana na dhana kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi, na wala wasisengenyane baadhi yenu wengineo. Je, anapenda mmoja wenu kwamba ale nyama ya nduguye aliyekufa? Basi mmelichukia hilo! Na mcheni Allaah! Hakika Allaah ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [Al-Hujuraat: 11-12]

 

Na adhabu zake kali zimetajawa katika Qur-aan na Sunnah. Rejea Al-Humazah (104: 1) Pia rejea Al-Israa (17: 36), An-Nuwr (24: 11-21).

 

Na rejea pia Hadiyth namba (86), (88), (93), (126).

 

 

2. Tofauti ya ghiybah na buhtaan ni kwamba ghiybah ni kumsengenya mtu kwa sifa aliyonayo. Ama buhtaan ni kumsingizia sifa ya uongo. Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى) katika kisa cha ifk alichozuliwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها)  kwa jambo ambalo hakulifanya:

 

وَلَوْلَا إِذْ سَمِعْتُمُوهُ قُلْتُم مَّا يَكُونُ لَنَا أَن نَّتَكَلَّمَ بِهَـٰذَا سُبْحَانَكَ هَـٰذَا بُهْتَانٌ عَظِيمٌ ﴿١٦﴾

Na kwa nini mlipoisikia (kashfa ya kusingiziwa) msiseme: “Haitupasi sisi tuzungumze haya; Subhaanak! (Utakasifu ni Wako) huu ni usingiziaji wa dhulma mkubwa mno!”  [An-Nuwr: 16]    

 

 

Na hivyo ni kuwaudhi Waumini jambo ambalo Allaah (سبحانه وتعالى) Amelikemea kama Anavyosema:

 

وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾

Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab (33: 58)]  

 

 

2. Kudhihirisha daraja ya maovu ya ulimi, ghiybah na kuzulia, kukashifu n.k.

 

Rejea kisa cha Ifk katika Al-Bukhaariy na Aayah zake katika Suwrah An-Nuwr (24: 11-20).

 

 

3. Kuwazulia Waumini maovu ni miongoni mwa madhambi saba makubwa yanayomuangamiza mtu yaliyotajwa katika Hadiyth namba (108).

 

Na adhabu yake pia ni kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿١٩﴾

Hakika wale wanaopenda uenee uchafu wa kashfa kwa wale walioamini; watapata adhabu iumizayo duniani na Aakhirah. Na Allaah Anajua nanyi hamjui.  [An-Nuwr 24: 19)]

 

 

 

4. Ghiybah, buhtaan, kukashifu, kufanya istihzai, kejeli, ni aina ya maradhi ya moyo muovu, nayo ni maradhi makuu katika jamii. Muumin wa kweli hujiweka mbali nayo ili afike Siku ya Qiyaamah akiwa na moyo uliosalimika. [Ash-Shu’araa: 88-89].

 

 

 

5. Ghiybah na buhtaan inakula ‘amali njema za mtu Siku ya Qiyaamah, kwani inahusiana na haki za bin Aadam ambazo hazisameheki ila mwenyewe asamehe. Dalili ni Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((أَتَدْرُونَ مَا الْمُفْلِسُ؟))‏ قَالُوا: الْمُفْلِسُ فِينَا مَنْ لاَ دِرْهَمَ لَهُ وَلاَ مَتَاعَ .‏ فَقَالَ: ((إِنَّ الْمُفْلِسَ مِنْ أُمَّتِي يَأْتِي يَوْمَ الْقِيَامَةِ بِصَلاَةٍ وَصِيَامٍ وَزَكَاةٍ وَيَأْتِي قَدْ شَتَمَ هَذَا وَقَذَفَ هَذَا وَأَكَلَ مَالَ هَذَا وَسَفَكَ دَمَ هَذَا وَضَرَبَ هَذَا فَيُعْطَى هَذَا مِنْ حَسَنَاتِهِ وَهَذَا مِنْ حَسَنَاتِهِ فَإِنْ فَنِيَتْ حَسَنَاتُهُ قَبْلَ أَنْ يُقْضَى مَا عَلَيْهِ أُخِذَ مِنْ خَطَايَاهُمْ فَطُرِحَتْ عَلَيْهِ ثُمَّ طُرِحَ فِي النَّارِ))  مسلم‏

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Je, Mnamjua muflis?)) Wakasema [watu]: “Muflis kwetu sisi ni yule miongoni mwetu asiyekuwa na dirhamu [pesa] wala vyenye kumnufaisha yeye hapa duniani”. Akasema (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Hakika muflis katika Ummah wangu ni yule atakayekuja Siku ya Qiyaamah na Swalaah, Swiyaam, na Zakaah, lakini amemtusi huyu, kumsingizia huyu mwingine kuwa amezini, amekula mali ya huyu, amemwaga damu ya mwingine na kumpiga mwengine. Thawabu zake zitapatiwa huyu na yule mpaka zimalizike. Na zinapokwisha basi madhambi ya hao [aliowadhulumu] atabandikwa nayo, hivyo kuingizwa Motoni))].  [Muslim]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (19).

 

Na Hadiyth ifuatayo:

 

عبد الله بن عمرو أنهم ذكروا عند رسول الله صلى الله عليه وسلم رجلاً فقالوا: لا يأكل حتى يُطعم، ولا يَرحل حتى يُرحل، فقال النبي صلى الله عليه وسلم: ((اغتبتموه)) فقالوا: يا رسول الله: إنما حدثنا بما فيه قال: ((حسبك إذا ذكرت أخاك بما فيه))  المحدث: الألباني -  المصدر : السلسلة الصحيحة

Kutoka kwa 'Abdullaah bin 'Amru (رضي الله عنه)  kwamba walimtaja mtu mmoja mbele ya Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakasema: "Hali hadi alishwe, wala haendi hadi apelekwe." Akasema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ((Mmemsengenya)).  Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah  wa Allaah, tumehadithia ya kweli aliyonayo." Akasema: ((Inakutosheleza kumsema ndugu yako kwa aliyonayo)) [Al-Albaaniy   katika Silsilatus-Swahiyhah]

 

 

 

6. Uislamu unafunza usalama kati ya jamii na kusisitiza kuheshimiana.  

 

Rejea Hadiyth namba (22), (23), (94), (126).

 

 

 

7. Hikma ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwafunza Maswahaba kwa kuwauliza jambo kwa swali, ambayo inamfanya mtu aelewe haraka jambo. Hii ni mojawapo ya njia nzuri sana ya ufundishaji ambayo inatumiwa leo na waalimu.

 

 

Share

088-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Miongoni Mwa Adhabu Za Kaburi: An-Namiymah, Asiyejisafisha Akimaliza Kukojoa

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  85

 

Miongoni Mwa Adhabu Za Kaburi: An-Namiymah (Kufitinisha), Na Asiyejisafisha Akimaliza Kukojoa

 

 

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) أنَّ َ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  مَرَّ بِقَبْرَيْنِ فَقَالَ: ((إِنَّهُمَا يُعَذَّبَانِ، وَمَا يُعَذَّبَانِ فِي كَبِير! بَلى إنَّه لكَبِيرٌ. أَمَّا أَحَدُهُمَا فَكَانَ يَمْشِي بِالنَّمِيمَةِ، وَأَمَّا الأَخَرُ فَكَانَ لاَ يَسْتَتِرُ مِنْ بَوْلِهِ)) متفق عليه وهذا لفظ إحدى روايات البخاري

Imepokelewa kutoka kwa bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم ) aliyapitia makaburi mawili akasema: ((Hakika hawa wanaadhibiwa. Wala hawaadhibiwi kwa sababu ya jambo kubwa. Bali la! Hakika ni jambo kubwa. Mmoja wao alikuwa akifitinisha, na mwengine alikuwa hajikingi na mkojo [anapokojoa])). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uharamisho wa kufitinisha baina ya watu jambo ambalo ni miongoni mwa madhambi makubwa yanayompatia mtu adhabu ya kaburi. Kwa sababu kufitinisha watu kunasababisha uadui baina ya ndugu wa Kiislamu. Allaah (سبحانه وتعالى) Anakataza hayo katika kauli Yake:

 

  وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٢﴾

 Na shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na uadui. Na Mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mkali wa kuakibu.  [Al-Maaidah (5: 2)].

 

 

 Na pia Allaah (سبحانه وتعالى) Anatahadharisha ufitinashaji kama Anavyosema:

 

وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ﴿١٠﴾

Na wala usimtii kila mwingi wa kuapa, dhalili.

هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ﴿١١﴾

Mwingi wa kukashifu, mpitaji huku na kule kwa kufitinisha. [Al-Qalam: 10-11]

 

 

 

2. Mfitinishaji haingii Jannah kwa dalili Hadiyth ifuatayo:

 

 عن حذيفة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((لا يَدْخُلُ الجَنَّةَ نَمَّامٌ))  رواه البخاري ومسلم

Kutoka kwa Hudhayfah (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Mchongezi (Mfitinishaji) hataingia Jannah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

3 Wajibu wa mtu kujitwaharisha vizuri anapomaliza kukojoa asiache athari yoyote ya mkojo, kwani Allaah (سبحانه وتعالى) Anapenda wanaojitwaharisha kama Anavyosema:

 

 فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُوا ۚ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُطَّهِّرِينَ﴿١٠٨﴾

Humo mna watu wanaopenda kujitwaharisha. Na Allaah Anapenda wanaojitwaharisha. [At-Tawbah (9: 108)]

 

Na Anasema pia:

 

 

وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْمَحِيضِ ۖ قُلْ هُوَ أَذًى فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي الْمَحِيضِ ۖ وَلَا تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطْهُرْنَ ۖ فَإِذَا تَطَهَّرْنَ فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللَّـهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ ﴿٢٢٢﴾ 

Na wanakuuliza kuhusu hedhi. Sema: “Hiyo ni dhara; basi waepukeni wanawake katika hedhi. Wala msiwakaribie kujimai nao mpaka watwaharike. Watakapotwaharika basi waendeeni kupitia pale Alipokuamrisheni Allaah.”  Hakika Allaah Anapenda wenye kutubia na Anapenda wenye kujitwaharisha.   [Al-Baqarah: 222].

 

 

4. Uislamu unafunza usafi wa kila aina khasa katika mwili  mwa bin Aadam.

 

 

5. Thibitisho la kuweko adhabu za kaburi na himizo la kujikinga nazo.

 

 

6. An-Namiymah ni miongoni mwa maradhi ya moyo yanayotokana na uhasidi, choyo, na kupendelea shari baina ya ndugu wanaopatana na kupendana. Hakuna kitakachomfaa mtu Siku ya Qiyaamah isipokuwa atakayefika akiwa na moyo uliosalimika na maovu mfano wa hayo ya uhasidi, chuki na kadhaalika. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

 “Siku hayatofaa mali wa watoto.

 

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

 “Isipokuwa yule atakayemfikia Allaah na moyo uliosalimika. [Ash-Shu’araa (26: 88-89)].

 

 

 

7. An-Namiymah ni aina ya ufisadi katika jamii jambo ambalo   Allaah (سبحانه وتعالى) Analiharamisha na Halipendi kabisa kama Anavyosema:

 

  وَلَا تَبْغِ الْفَسَادَ فِي الْأَرْضِ ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْمُفْسِدِينَ ﴿٧٧﴾

Na wala usitake ufisadi ardhini. Hakika Allaah Hapendi mafisadi.” [Al-Qaswasw (28: 77)].

 

 

 

8. Rejea pia Hadiyth namba (21), (22), (89), (94)

 

 

 

Share

089-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Watu Waovu Kabisa Ni Wenye Nyuso Mbili Za Unafiki

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  89

 

Watu Waovu Kabisa Ni Wenye Nyuso Mbili Za Unafiki

 

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَال: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((تَجِدُونَ النَّاسَ مَعَادِنَ، خِيَارُهُمْ فِي الْجَاهِلِيَّةِ خِيَارُهُمْ فِي الإِسْلامِ إِذَا فَقِهُوا، وَتَجِدُونَ خَيْرَ النَّاسِ فِي هَذَا الشَّأْنِ أَشَدَّهُمْ لَهُ كَرَاهِيَةً، وَتَجِدُونَ شَرَّ النَّاسِ ذَا الْوَجْهَيْنِ الَّذِي يَأْتِي هَؤُلاَءِ بِوَجْهٍ وَيَأْتِي هَؤُلاَءِ بِوَجْهٍ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mtawakuta watu wana asili wanaonasibika nazo; wabora wao katika ujaahiliya ndio wabora wao katika Uislamu watakapofahamu Dini [hukmu za Shariy’ah]. Na mtamkuta mbora wa watu katika jambo hili [la uongozi] ni mwenye kulichukia mno, na mtamkuta muovu wa watu ni mwenye nyuso mbili, ambaye anawaendea hawa kwa uso huu, na anawaendea wale kwa uso mwingine)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Mwenye nyuso mbili ni miongoni mwa sifa za wanafiki, nao ni watu waovu kabisa kama mfano wa wanafiki wa zama za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ambao walikuwa wakificha unafiki wao lakini Allaah (سبحانه وتعالى) Akawadhihirisha kwa kauli Zake kadhaa miongoni mwazo ni:

 

 

إِنَّ الْمُنَافِقِينَ يُخَادِعُونَ اللَّـهَ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا قَامُوا إِلَى الصَّلَاةِ قَامُوا كُسَالَىٰ يُرَاءُونَ النَّاسَ وَلَا يَذْكُرُونَ اللَّـهَ إِلَّا قَلِيلًا ﴿١٤٢﴾

Hakika wanafiki (wanadhani) wanamhadaa Allaah, na hali Yeye (Allaah) Ndiye Mwenye kuwahadaa. Na wanaposimama kuswali husimama kwa uvivu, wakijionyesha kwa watu na wala hawamdhukuru Allaah isipokuwa kidogo tu.

 

 

مُّذَبْذَبِينَ بَيْنَ ذَٰلِكَ لَا إِلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ وَلَا إِلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ ۚ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَلَن تَجِدَ لَهُ سَبِيلًا ﴿١٤٣﴾

 

Madhabidhabina baina ya hayo (iymaan na kufru), huku hawako wala huko hawako. Na ambaye Allaah Amempotoa huwezi kumpatia njia (ya kumwongoa). [An-Nisaa (4: 142-143)].

 

Kisha Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الْمُنَافِقِينَ فِي الدَّرْكِ الْأَسْفَلِ مِنَ النَّارِ وَلَن تَجِدَ لَهُمْ نَصِيرًا ﴿١٤٥﴾

Hakika wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika moto; na wala hutompata kwa ajili yao mwenye kunusuru. [An-Nisaa (4: 145)].

 

 

 

2. Wenye nyuso mbili huwa na hulka ya kusema ya mdomoni yasiyokuweko moyoni. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu wanafiki wa zama za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

 

 وَلِيَعْلَمَ الَّذِينَ نَافَقُوا ۚ وَقِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا قَاتِلُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أَوِ ادْفَعُوا ۖ قَالُوا لَوْ نَعْلَمُ قِتَالًا لَّاتَّبَعْنَاكُمْ ۗ هُمْ لِلْكُفْرِ يَوْمَئِذٍ أَقْرَبُ مِنْهُمْ لِلْإِيمَانِ ۚ يَقُولُونَ بِأَفْوَاهِهِم مَّا لَيْسَ فِي قُلُوبِهِمْ ۗ وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا يَكْتُمُونَ ﴿١٦٧﴾

Na ili Adhihirishe wale waliofanya unafiki na wakaambiwa: “Njooni mpigane katika njia ya Allaah au (angalau) lindeni.” Wakasema: “Lau tungelijua kuwa kuna kupigana bila shaka tungelikufuateni.” Wao siku hiyo walikuwa karibu zaidi ya ukafiri kuliko iymaan. Wanasema kwa midomo yao, yale yasiyokuwemo katika nyoyo zao. Na Allaah Anajua zaidi wanayoyaficha. [Aal-‘Imraan (3: 167)]

 

Rejea pia: At-Tawbah (9: 8), Al-Fat-h (48: 11).

 

 

 

3. Mwenye sifa hiyo mbaya ya kuwa na nyuso mbili anafananishwa na kinyonga anayejibadilisha rangi kwa hali anayojipendelea nafsi yake. Ni hatari zaidi kuliko mtu muovu anayejulikana wazi. Na mtu kama huyu ni mwenye kusababisha ufisadi baina ya ndugu na jamii.

 

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (21), (22), (88), (94) ambazo zimetaja matahadharisho ya maovu kama haya pamoja na mwongozo wa kuweka usalama baina ya ndugu katika jamii.  

 

 

 

4. Hapa tunafahamishwa ubora na umuhimu wa kufahamu mambo haswa ya Dini, kwani bila kufahamu tutapotea na kupoteza watu.

 

 

 

5. Walio bora katika nyakati za ujinga ni wale walioweza kufanya mambo mema na mazuri. Watu hao wanaposilimu ubora wao unaendelea, kwani Uislamu umehimiza sana kufanya mema. Waliotajwa hapa haswa ni Maswahaba na wale watakaokuja baada yao mpaka Siku ya Qiyaamah.

 

 

 

6. Muislamu haifai kupigania uongozi, akichanguliwa na Waislamu ni vyema. Na hapo atakuwa ni mwenye kusaidiwa na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

Share

090-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Adhabu Kwa Waongopao Ndoto, Kusikiliza Siri Za Watu, Wachoraji Picha Zenye Roho

 

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya   90

 

Adhabu Kwa Waongopao Ndoto, Kusikiliza Siri Za Watu, Wachoraji Picha Zenye Roho

 

 

 

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَنْ تَحَلَّمَ بِحُلْمٍ لَمْ يَرَهُ كُلِّفَ أَنْ يَعْقِدَ بَيْنَ شَعِيرَتَيْنِ وَلَنْ يَفْعَلَ، وَمَنْ اسْتَمَعَ إِلَى حَدِيثِ قَوْمٍ وَهُمْ لَهُ كَارِهُونَ أَوْ يَفِرُّونَ مِنْهُ صُبَّ فِي أُذُنِهِ الأنُكُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ، وَمَنْ صَوَّرَ صُورَةً عُذِّبَ وَكُلِّفَ أَنْ يَنْفُخَ فِيهَا وَلَيْسَ بِنَافِخٍ))   البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Anayedai kuwa ameona ndoto ambayo hakuiona, atalazimishwa apige fundo kati ya punje mbili za shayiri, wala hatoweza kufanya hivyo. Na anayesikiliza mazungumzo ya watu na ilhali wenyewe wanachukia, au wanamkimbia [mazungumzo yao asiyasikie], atamiminiwa risasi iliyoyeyuka Siku ya Qiyaamah. Na anayechora picha [ya chenye roho], ataadhibiwa na atalazimishwa aivuvie [aitie] roho wala hatoweza kuivuvia)). [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Tisho kali la mwenye kuongopea watu kuhusu ndoto, kwani hivyo ni kumzulia uongo Allaah (سبحانه وتعالى) na kuwazulia watu.

 

 

 

2. Adhabu kali kwa anayesikiliza siri za watu, nalo ni miongoni mwa madhambi makubwa.  

 

 

 

3. Kusikiliza siri za watu ni miongoni mwa maradhi ya moyo, nayo yanakutokana na kuchunguza mambo ya watu yaliyokatazwa. Allaah (سبحانه وتعالى) Anakataza katika kauli Yake:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا  

Enyi walioamini!  Jieupusheni sana na dhana kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi.   [Al-Hujuraat (49: 12)].

 

 

 

4. Kila kiungo cha mwana Aadam kinachotenda maovu, kitakuja kumchongea mtu Siku ya Qiyaamah,  yakiwemo masikio kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

حَتَّىٰ إِذَا مَا جَاءُوهَا شَهِدَ عَلَيْهِمْ سَمْعُهُمْ وَأَبْصَارُهُمْ وَجُلُودُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٢٠﴾

Mpaka watakapoufikia yatashuhudia dhidi yao, masikio yao, na macho yao, na ngozi zao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda.

 

 

وَقَالُوا لِجُلُودِهِمْ لِمَ شَهِدتُّمْ عَلَيْنَا ۖ قَالُوا أَنطَقَنَا اللَّـهُ الَّذِي أَنطَقَ كُلَّ شَيْءٍ وَهُوَ خَلَقَكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴿٢١﴾

Na wataziambia ngozi zao: “Mbona mnashuhudia dhidi yetu?” Zitasema: “Ametutamkisha Allaah Ambaye Ametamkisha kila kitu, Naye Ndiye Aliyekuumbeni mara ya kwanza na Kwake mtarejeshwa.

 

 

وَمَا كُنتُمْ تَسْتَتِرُونَ أَن يَشْهَدَ عَلَيْكُمْ سَمْعُكُمْ وَلَا أَبْصَارُكُمْ وَلَا جُلُودُكُمْ وَلَـٰكِن ظَنَنتُمْ أَنَّ اللَّـهَ لَا يَعْلَمُ كَثِيرًا مِّمَّا تَعْمَلُونَ﴿٢٢﴾

 “Na hamkuwa mkijisitiri hata yasishuhudie masikio yenu, na wala macho yenu, na wala ngozi zenu; lakini mlidhania kwamba Allaah Hajui mengi katika yale mnayoyatenda.

 

وَذَٰلِكُمْ ظَنُّكُمُ الَّذِي ظَنَنتُم بِرَبِّكُمْ أَرْدَاكُمْ فَأَصْبَحْتُم مِّنَ الْخَاسِرِينَ﴿٢٣﴾

 “Na hivyo dhana yenu mliyokuwa mkimdhania Rabb wenu, imekuangamizeni, mmekuwa miongoni mwa waliokhasirika.”  [Fusw-swilat (41: 20-23)].

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾

Na wala usifuatilie ambayo usiyokuwa nayo ujuzi. Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitakuwa vya kuulizwa (Siku ya Qiyaamah).  [Al-Israa (17: 36)]

 

 

 

5. Tisho kali kwa mwenye kuchora picha yenye roho, kwani wanamwiga Muumba kuhusu Uwezo Wake ambao hakuna Awezaye kuumba chochote isipokuwa Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) na kwamba ni watu watakaopata adhabu kali kabisa.

 

Hadiyth kadhaa zimetahadharisha adhabu zake, miongoni mwazo ni:

 

عَنْ عَائِشَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) قَال: ((أَشَدُّ النَّاسِ عَذَابًا يَوْمَ القِيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهِئُونَ بِخَلْقِ اللَّهِ))

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watakaokuwa na adhabu kali Siku ya Qiyaamah ni wanaomuiga Allaah katika uumbaji Wake)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na pia:

 

  عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) :  سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((كُلُّ مُصَوِّرٍ فِي النَّارِ يُجْعَلُ لَهُ بِكُلِّ صُورَةٍ صَوَّرَهَا نَفْسٌ يُعَذَّبُ بِهَا فِي جَهَنَّمَ))

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kila mchoraji picha atakuwa motoni. Kila picha aliyoichora, itatiwa roho nayo itamuadhibu katika Jahannam)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((قَالَ اللهُ تَعَالَى: وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنْ ذَهَبَ يَخْلُقُ كَخَلْقِي؛ فَلْيَخْلُقُوا ذَرَّةً، أَوْ لِيَخْلُقُوا حَبَّةً، أَوْ لِيَخْلُقُوا شَعِيْرَةً ))  أَخْرَجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Aliyetukuka Amesema: Nani dhalimu zaidi kuliko anayejaribu kuumba kama kuumba Kwangu? Basi na waumbe chembe moja au waumbe punje ya nafaka, au waumbe chembe ya shayiri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]  

 

 

 

6. Kila ‘amali ovu au nzuri ina malipo yake tofauti.

 

 

 

7. Mifano ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu kutisha jambo lisilowezekana kutendwa au kutendeka kama kupiga fundo kati ya punje mbili za shayiri, na Allaah (سبحانه وتعالى) Anatoa mifano kama hiyo katika kauli Zake:

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ ضُرِبَ مَثَلٌ فَاسْتَمِعُوا لَهُ ۚ إِنَّ الَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ لَن يَخْلُقُوا ذُبَابًا وَلَوِ اجْتَمَعُوا لَهُ ۖ وَإِن يَسْلُبْهُمُ الذُّبَابُ شَيْئًا لَّا يَسْتَنقِذُوهُ مِنْهُ ۚ ضَعُفَ الطَّالِبُ وَالْمَطْلُوبُ ﴿٧٣﴾

Enyi watu! Imepigwa mfano basi isikilizeni kwa makini! Hakika wale mnaowaomba badala ya Allaah hawawezi kuumba nzi japo wakijumuika kwa hilo. Na nzi akiwapokonya kitu chochote kile hawawezi kukiambua tena. Amedhoofika mwenye kutaka matilabu na mwenye kutakiwa. [Al-Hajj (22: 73)].

 

 

Na pia mfano wa ambaye anamkanusha Allaah (سبحانه وتعالى) na Aayat Zake:

 

إِنَّ الَّذِينَ كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا وَاسْتَكْبَرُوا عَنْهَا لَا تُفَتَّحُ لَهُمْ أَبْوَابُ السَّمَاءِ وَلَا يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ حَتَّىٰ يَلِجَ الْجَمَلُ فِي سَمِّ الْخِيَاطِ ۚ وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُجْرِمِينَ ﴿٤٠﴾

Hakika wale waliokadhibisha Aayaat Zetu na wakazifanyia kiburi, hawatofunguliwa milango ya mbingu na wala hawatoingia Jannah mpaka ngamia aingie katika tundu ya sindano. Na hivyo ndivyo Tunavyowalipa wakhalifu.  [Al-A’raaf (7: 40)].

 

 

 

 

 

Share

091-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Aliyehifadhi Qur-aan Anatukuzwa Duniani Na Aakhirah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 91

 

Aliyehifadhi Qur-aan Anatukuzwa Duniani Na Aakhirah

 

 

 

 

عن جابر (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ كَانَ  يَجْمَعُ بَيْنَ الرَّجُلَيْنِ مِنْ قَتْلَى أُحُدٍ  يَعْنِي  فِي الْقَبْرِ ثُمَّ َيَقُولُ: ((أَيُّهُمَا أَكْثَرُ أَخْذًا لِلْقُرْآنِ ))  فَإِذَا أُشِيرَ لَهُ إِلَى أَحَدِهِمَا قَدَّمَهُ فِى اللَّحْدِ – رواه البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akiwajumuisha kaburini watu wawiliwawili katika Mashahidi wa vita vya Uhud, kisha akiuliza: ((Ni yupi kati yao aliyebeba [aliyehifadhi] Qur-aan zaidi?)) Anapoashiriwa mmojawapo humtanguliza katika mwanandani.   [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Utukufu wa hali ya juu wa Qur-aan kwani ni maneno ya Rabb Mumba wa kila kitu.

 

 

 

2. Qur-aan humtoa mtu katika kiza cha upotofu na kumuingiza katika Nuru. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الر ۚ كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ لِتُخْرِجَ النَّاسَ مِنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ بِإِذْنِ رَبِّهِمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿١﴾

Alif Laam Raa. Kitabu Tumekiteremsha kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) ili uwatoe watu kutoka kwenye viza kuwaingiza katika nuru kwa idhini ya Rabb wao, waelekee katika njia ya Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Ibraahiym (14: 1)]

 

 

Rejea pia: Al-Maaidah (5: 160),  Al-Hadiyd (57: 9), Atw-Twalaaq (65: 11).

 

 

 

3. Fadhila tele kwa aliyehifadhi Qur-aan; huzipata duniani kabla ya Aakhirah. Miongoni mwa fadhila za duniani ni:

 

 

-Mwenye elimu ya Qur-aan hupewa uimamu katika Swalaah:

 

Kutoka kwa Abuu Mas’uwd Al-Answaariyy kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم) amesema: ((Awaswalishe watu yule mwenye kujua kusoma zaidi Kitabu cha Allaah na wakiwa katika kusoma wako sawa, basi mwenye ujuzi zaidi wa Sunnah, na wakiwa kwenye Sunnah wako sawa, basi aliyetangulia hijrah, na wakiwa katika hijrah wako sawa, basi mkubwa wao kwa umri, wala asiswalishe mtu katika nyumba yake wala katika mamlaka yake wala asikae kwa heshima yake  isipokuwa kwa ruhusa yake)).  [Al-Bukhaariy]  

 

 

-Mwenye elimu ya Qur-aan huwa ni mbora kabisa kati ya watu kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Hadiyth:

 

 

عن عثمانَ بن عفانَ رضي الله عنه أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلّم قالَ    ((خَيرُكُم مَنْ تعَلَّمَ القُرآنَ وعَلَّمَه))   صحيح البخاريِّ

Kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mbora wenu anayejifunza Qur-aan akaifunza)). [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abu Daawuwd, Ahmad] 

 

Rejea pia Hadiyth namba (80).

 

 

-Mwenye elimu ya Qur-aan hupewa uongozi katika vituo vya Dini, hufadhilishwa katika kuoa, hupendwa na watu:

 

قال عمر رضي الله عنه : أما إن نبيكم صلى الله عليه وسلم قد قال : (( إن الله يرفع بهذا الكتاب أقواماً ويضع  به آخرين ))  صحيح مسلم  

Kutoka kwa 'Umar (رضي الله عنه)  ambaye amesema, Nabiy wenu (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:    ((Allaah Atawanyanyua baadhi ya watu kwa kitabu hiki (Qur-aan) na Atawadhalilisha wengine kwa kitabu hiki))  [Muslim, Ibn Maajah, Ahmad] 

 

 

-Mwenye elimu ya Qur-aan ni miongoni mwa watu makhsusi wanaopendwa na Allaah (سبحانه وتعالى):

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: (( إِنَّ لِلَّهِ أَهْلِينَ مِنْ النَّاسِ)) قَالُوا يَا رَسُولَ اللَّهِ مَنْ هُمْ قَالَ:  ((هُمْ أَهْلُ الْقُرْآنِ أَهْلُ اللَّهِ وَخَاصَّتُهُ)) أحمد و إبن ماجه

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Anao watu wake kati ya wanaadam)). Wakamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah ni nani hao? Akasema: ((Hao ni watu wa Qur-aan na ni watu wa Allaah na wateule Wake))  [Ahmad, Ibn Maajah]

   

 

-Mwenye elimu ya Qur-aan atahifadhiwa na fitna za Masiyhud-Dajjaal kwa kuhifadhi Aayah za mwanzo za Suratul-Kahf.  [Muslim] 

 

 

 

4. Fadhila za Aakhirah ni nyingi zaidi ya kwanza iliyotajwa katika Hadiyth kwamba anaanza maisha yake ya Aakhirah kwa kufadhilishwa anapoingizwa kaburini. Fadhila nyinginezo ni kama zifuatazo:

 

-Qur-aan itamuombea shafaa’ah, atavalishwa taji na Malaika, na kuu zaidi atapata Radhi za Allaah (سبحانه وتعالى)

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَجِيءُ الْقُرْآنُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَيَقُولُ يَا رَبِّ حَلِّهِ ، فَيُلْبَسُ تَاجَ الْكَرَامَةِ ثُمَّ يَقُولُ: يَا رَبِّ زِدْهُ, فَيُلْبَسُ حُلَّةَ الْكَرَامَةِ ثُمَّ يَقُولُ: يَا رَبِّ ارْضَ عَنْهُ فَيَرْضَى عَنْهُ فَيُقَالُ لَهُ: اقْرَأْ وَارْقَ.  وَتُزَادُ بِكُلِّ آيَةٍ حَسَنَةً))  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Qur-aan itakuja siku ya Qiyaamah na itasema: “Ee Rabb, Mpambe” [Mwenye kuhifadhi Qur-aan]. Kisha atavalishwa taji. Kisha [Qur-aan] itasema: “Ee Rabb, muongezee”. Kisha huyo mtu atavishwa nguo ya heshima. Kisha itasema: “Ee Rabb Ridhika naye”. Allaah, Ataridhika naye. Kisha ataambiwa: “Soma na panda”. Atapokea thawabu zaidi ya mema kwa kila Aayah [atakayosoma])   [At-Tirmidhy na Al-Haakim]

 

 

-Hupandishwa Daraja Jannah:

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:  ((يُقَالُ لِصَاحِبِ الْقُرْآنِ اقْرَأْ وَارْتَقِ وَرَتِّلْ كَمَا كُنْتَ تُرَتِّلُ فِي الدُّنْيَا فَإِنَّ مَنْزِلَتَكَ عِنْدَ آخِرِ آيَةٍ تَقْرَأُ بِهَا))

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Huambiwa Aliyeiandama na Qur-aan: Soma na panda [juu katika daraja za Jannah] na uisome kwa 'Tartiyl' [kufuata hukmu zake] kama ulivyokuwa ukiisoma ulipokuwa duniani, kwani makazi yako ni pale utakapofika katika Aayah ya mwisho utakayoisoma)).  [At-Tirmidhiy, Abu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad] 

 

 

-Pia kwa kuhifadhi Suratul-Baqarah na Suratul-‘Imraan zitakuwa ni kivuli chake Siku ya Qiyaamah. [Muslim]

 

 

 

5. Kila mwana Aadam Muislamu au kafiri anaihitaji Qur-aan kwani ni poza ya vifua dhidi ya shirki, kufru, unafiki, uasi, uhasidi na kila aina ya maradhi ya moyo yaliyotajwa katika Qur-aan na Sunnah. Bali ni hazina bora ya kila kitu kuliko hazina zinazotafutwa na kupendwa na watu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَتْكُم مَّوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَشِفَاءٌ لِّمَا فِي الصُّدُورِ وَهُدًى وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ﴿٥٧﴾

Enyi watu! Kwa yakini yamekujieni mawaidha kutoka kwa Rabb wenu, na shifaa ya yale yaliyomo vifuani, na mwongozo na rahmah kwa Waumini.

 

قُلْ بِفَضْلِ اللَّـهِ وَبِرَحْمَتِهِ فَبِذَٰلِكَ فَلْيَفْرَحُوا هُوَ خَيْرٌ مِّمَّا يَجْمَعُونَ﴿٥٨﴾

Sema: “Kwa fadhila za Allaah na kwa rahmah Yake basi kwa hayo wafurahi.” Hayo ni kheri kuliko wanayoyakusanya. [Yuwnus (10: 57-58)]

 

 

 

6. Wahyi wa Qur-aan umeitwa Ruwh (roho) kama ilivyotajwa katika Qur-aan, ni kama kumpa mtu uhai wa moyo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ رُوحًا مِّنْ أَمْرِنَا ۚ مَا كُنتَ تَدْرِي مَا الْكِتَابُ وَلَا الْإِيمَانُ وَلَـٰكِن جَعَلْنَاهُ نُورًا نَّهْدِي بِهِ مَن نَّشَاءُ مِنْ عِبَادِنَا ۚ وَإِنَّكَ لَتَهْدِي إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ﴿٥٢﴾

 Na hivyo ndivyo Tulivyokuletea Ruwh (Qur-aan) kutoka amri Yetu. Hukuwa unajua nini Kitabu wala iymaan, lakini Tumeifanya ni Nuru, Tunaongoa kwayo Tumtakaye miongoni mwa waja Wetu. Na hakika wewe (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) bila shaka unaongoza kuelekea njia iliyonyooka. [Ash-Shuwraa (42: 52)].

  

 

Vile vile Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 أَوَمَن كَانَ مَيْتًا فَأَحْيَيْنَاهُ وَجَعَلْنَا لَهُ نُورًا يَمْشِي بِهِ فِي النَّاسِ كَمَن مَّثَلُهُ فِي الظُّلُمَاتِ لَيْسَ بِخَارِجٍ مِّنْهَا ۚ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلْكَافِرِينَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٢٢﴾

Je, aliyekuwa maiti kisha Tukamhuisha na Tukamjaalia nuru anatembea kwayo kati ya watu, ni sawa na yule ambaye yumo katika viza si mwenye kutoka humo? Hivyo ndivyo walivyopambiwa makafiri yale waliyokuwa wakiyatenda. [Al-An’aam: 122]

 

 

7. Qur-aan imejumuisha kila jambo, na ufumbuzi wa kila tatizo kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

  وَنَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ تِبْيَانًا لِّكُلِّ شَيْءٍ وَهُدًى وَرَحْمَةً وَبُشْرَىٰ لِلْمُسْلِمِينَ﴿٨٩﴾

 Na Tumekuteremshia Kitabu kikiwa ni kielezo bayana cha kila kitu na ni mwongozo na rahmah na bishara kwa Waislamu. [An-Nahl (16: 89)]

 

 

 

8. Jamii isisitize mafunzo ya Qur-aan kwa watoto na watu wazima, yakiwemo kuifundisha usomaji wake kwa Tajwiyd (hukmu zake), kuiihifadhi, kufundisha lugha ya Kiarabu ili kuifahamu tafsiyr yake. Mafunzo haya yapewe umuhimu sawa kuliko yanavyopewa umuhimu wa masomo ya kisekula, kwani haya ndiyo yatakayomfaa mtu duniani na Aakhirah.

 

 

 

Share

092-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Makatazo ya Kuapa Pasi Na Allaah, Kujiua, Kutekeleza Nadhiri Kwa kitu Asichokimiliki, Kumlaani Muumin

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 92

 

Makatazo ya Kuapa Pasi Na Allaah, Kujiua,

Kutekeleza Nadhiri Kwa kitu Asichokimiliki, Kumlaani Muumin

 

 

 

 

عن أَبِي زَيْد بْنِ ثَابِت بن الضَّحاك الأنْصاريِّ (رضي الله عنه) وَهُوَ مِنْ أَهْل بَيْعَةِ الرِّضْوَانِ، قَال: قَال رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ بِمِلَّةٍ غَيْرِ الإِسْلاَمِ كَاذِبًا مُتَعَمِّداً  فَهُوَ كَمَا قَالَ، وَمَنْ قَتَلَ نَفْسَهُ بِشَيْءٍ عُذِّبَ بِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلَيْسَ عَلَى رَجُلٍ نَذْرٌ فِي شَيْءٍ لاَ يَمْلِكُهُ، وَلَعْنُ الْمُؤْمِنِ كَقَتْلِهِ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Zayd bin Thaabit bin Adh-Dhwahaak Al-Answaariy (رضي الله عنه)  naye ni katika walioshuhudia Bay’atur Ridhwaan amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Atakayeapa yamini kwa mila isiyokuwa ya Uislamu kwa uongo na makusudi, basi atakuwa ni kama alivyoapa. Na anayejiua kwa kitu, ataadhibiwa nacho Siku ya Qiyaamah. Wala haimpasi mtu kutekeleza nadhiri ya kitu asichokimiliki. Na kumlaani [kumwapiza] Muumin ni sawa na kumuua)). [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Tahadhirisho la kuapa pasi na Allaah (سبحانه وتعالى), kwani ni shirki na kufru kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

عَنْ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) أَنّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَال: ((مَنْ حَلَفَ بِغَيْرِ اللَّهِ فَقَدْ كَفَرَ أَوْ أَشْرَك)) رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ وَصَحَّحَهُ الْحَاكِمُ

Na Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayeapa kwa asiye  Allaah, amekufuru au amefanya shirki)) [At-Tirmidhiy na ameikiri ni Hasan, na Al-Haakim ameikiri ni Swahiyh, na Abu Daawuwd, na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy]

 

Rejea pia Hadiyth namba (5).

 

 

2. Haramisho la kujiua na tahadharisho la adhabu yake kwamba afanyae hivyo, atakariri kujiua Siku ya Qiyaamah kwa njia ile ile aliyojiulia duniani:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ تَرَدَّى مِنْ جَبَلٍ فَقَتَلَ نَفْسَهُ، فَهْوَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ، يَتَرَدَّى فِيهِ خَالِدًا مُخَلَّدًا فِيهَا أَبَدًا، وَمَنْ تَحَسَّى سَمًّا فَقَتَلَ نَفْسَهُ، فَسَمُّهُ فِي يَدِهِ، يَتَحَسَّاهُ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدًا مُخَلَّدًا فِيهَا أَبَدًا، وَمَنْ قَتَلَ نَفْسَهُ بِحَدِيدَةٍ، فَحَدِيدَتُهُ فِي يَدِهِ، يَجَأُ بِهَا فِي بَطْنِهِ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدًا مُخَلَّدًا فِيهَا أَبَدًا)) البخاري ومسلم

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Yeyote atakayejitupa kutoka mlimani na kujiua, atatupwa ndani ya moto milele. Atakayekunywa sumu na kujiua, basi atatupwa motoni na huko atakuwa akiinywa hiyo sumu milele. Atakayejiua kwa kipande cha chuma, atatiwa motoni akiwa na kipande hicho cha chuma akijitwanga nacho tumboni kwake humo motoni milele))].  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

3. Kutekeleza nadhiri ya kitu asichomiliki mtu ni dhulma na kukhini haki ya mwenyewe.

 

 

 

4. Haramisho la kumlaani (kumwapiza) Muumin kitendo ambacho kimefananishwa na mauaji. Haya ni katika madhambi makubwa. Hii inadhihirisha kuwa Uislamu unampendelea mtu usalama na amani daima.

 

 

5. Kulaani kitu, au wakati au mnyama au mtu kwa ujumla kumekatazwa katika Hadiyth kadhaa, na kwamba laana humrudia mtu mwenyewe ikiwa haistahiki kulaani kitu. Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

  عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنِ النَّبِيِّ (صَلَى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ تَعَالَى: يُؤْذِينِي ابْنُ آدَمَ يَسُبُّ الدَّهْرَ، وَأَنَا الدَّهْرُ أُقَلِّبُ الْلَّيْلَ وَالنَّهَارَ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Ta’aalaa Amesema: Bin Aadam ananiudhi, kwani anatukana dahari [wakati au zama], na hali Mimi ni Ad-Dahr [Namiliki kila kitu na uwezo], Nageuza usiku na mchana)). [Al-Bukhaariy]

 

 

 

6. Allaah (سبحانه وتعالى) Amelaani watu kadhaa katika Qur-aan; wanaokata undugu, madhalimu na wengineo. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنِ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا ۚ أُولَـٰئِكَ يُعْرَضُونَ عَلَىٰ رَبِّهِمْ وَيَقُولُ الْأَشْهَادُ هَـٰؤُلَاءِ الَّذِينَ كَذَبُوا عَلَىٰ رَبِّهِمْ ۚ أَلَا لَعْنَةُ اللَّـهِ عَلَى الظَّالِمِينَ﴿١٨﴾

Na nani dhalimu zaidi kuliko yule anayemtungia uongo Allaah. Hao watahudhurishwa mbele ya Rabb wao, na mashahidi watasema: “Hawa ndio wale waliomzulia uongo Rabb wao!” Tanabahi! Laana ya Allaah iko juu ya waliodhulumu. [Huwd (11: 18)]

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 88, 159, 161),  Aal-‘Imraan (3: 87), Al-Ahzaab (33: 57), Muhammad (47: 23), An-Nisaa (4: 52).

 

 

 

7. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amelaani watu kadhaa katika Ahaadiyth, mfano ((Anayekula ribaa, anayeilipia na anayeiandika na anayeishuhudia)). [Muslim]

 

 

 

Share

093-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kumtukana Muislamu Ni Ufasiki Na Kupigana Naye Ni Ukafiri

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 93

 

Kumtukana Muislamu Ni Ufasiki Na Kupigana Naye Ni Ukafiri

 

 

 

 

عَنْ ابْن مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) قَال: قَالَ رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((سِبَابُ الْمُسْلِمِ فُسُوقٌ وَقِتَالُهُ كُفْرٌ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa bin Mas’uwd (رضي الله عنه)  ambaye amesema: “Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Kumtukana Muislamu ni ufasiki, na kupigana naye ni ukafiri)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kutukana, kwani ni kudharauliana, kuvunjiana heshima, hadhi na kusababisha ukhasama baina ya Waislamu. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ameonya:  ((…Kila Muislamu juu ya Muislamu mwenziwe ni haramu damu yake, mali yake na heshima yake)).  [Muslim]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (22), (87), (88), (89), (94), (126).

 

 

2. Uislamu unasisitiza masikilizano na amani baina ya watu, kwani kutukanana na kupigana ni kunyimana haki na kunasababisha ukosefu wa usalama na amani baina ya watu katika jamii.

 

 

3. Makatazo ya kupigana na Muislamu, kwani wote ni ndugu, na pindi wanapopigana huwa ni waajib kwa wengine kuwapatanisha kama Anavyoamrisha Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ ۚ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٩﴾

Na ikiwa makundi mawili ya Waumini yakipigana, basi suluhisheni baina yao. Lakini mojawapo likikandamiza jengine, basi piganeni na ambalo linakandamiza mpaka lielemee kwenye amri ya Allaah. Likishaelemea, basi suluhisheni baina yao kwa uadilifu, na timizeni haki haki. Hakika Allaah Anapenda wanaotimiza haki.

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠﴾

Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa. [Al-Hujuraat (49: 9-10)]

 

 

4. Kupigana na ndugu Muislamu kumefananishwa na ukafiri, hivyo ni onyo linalohusiana na iymaan ya mtu.

 

 

  

Share

094-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuweka Amani Baina Ya Watu Kwa Ulimi Na Kuacha Yaliyoharamishwa

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 94

 

Kuweka Amani Baina Ya Watu Kwa Ulimi Na Kuacha Yaliyoharamishwa

 

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو (رضي الله عنهما) قَال: قَال رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الْمُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ الْمُسْلِمُونَ مِنْ لِسَانِهِ وَيَدِهِ  وَالْمُهَاجِرُ مَنْ هَجَرَ مَا نَهَى اللَّهُ عَنْهُ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah in ‘Amr (رضي الله عنهما) ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muislamu ni yule anayeweka amani kwa watu [ambaye Waislamu wenziwe wanasalimika] kwa ulimi na mkono wake. Na mhamaji ni yule anayehama Aliyoyakataza Allaah)).  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uislamu asili yake ni ‘amani’ na hata maamkizi yetu ni ya amani. 

 

Rejea Hadiyth namba (72).

 

 

2. Himizo la kuepusha kila maudhi baina ya Waislamu kwa kila njia, kwa maneno maovu, kuumizana au kupigana.

 

Rejea Hadiyth namba (22), (87), (88), (89), (93), (126).

 

 

3. Aayah na Hadiyth nyingi zimetaja yanayohusiana na mambo yaliyoharamishwa na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Rejea Hadiyth namba (139).

 

Na baadhi ya mambo ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) Ameyaharamisha:

 

 

 قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۖ وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم مِّنْ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكُمْ وَإِيَّاهُمْ ۖ وَلَا تَقْرَبُوا الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ ۖ وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿١٥١﴾

Sema: “Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote, na muwafanyie ihsaan wazazi wawili, na wala msiwaue watoto wenu kutokana na umasikini. Sisi Tunakuruzukuni pamoja nao. Na wala msikaribie machafu yaliyo dhahiri na yaliyofichika. Na wala msiue nafsi ambayo Ameiharamisha Allaah (kuiua) isipokuwa kwa haki (ya shariy’ah). Hivyo ndivyo Alivyokuusieni kwayo mpate kutia akilini.” [Al-An’aam (6: 151)]

 

Baadhi ya maharamisho hayo yanaendelea kutajwa hadi Aayah namba 153.

 

 

4. Himizo la kuacha kila aina ya maasi.

 

 

5. Kuhama kumelinganishwa na kuacha maasi, kwa vile si jambo jepesi kulitenda, na maasi pia ni jambo gumu, kwani si wepesi kuacha matamanio yake mtu na si wepesi kumwepuka shaytwaan.

 

 

 

Share

095-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kuepushwa Moto Na Kuingizwa Jannah Ni Kumwamini Allaah Na Kuwatendea Watu Analopenda Kutendewa

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 95

 

Kuepushwa Moto Na Kuingizwa Jannah Ni Kumwamini Allaah

Na Kuwatendea Watu Analopenda Kutendewa

 

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو (رضي الله عنهما) قَال: قَال رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ أَحَبَّ أَنْ يُزَحْزَحَ عَنْ النَّارِ وَيَدْخُلَ الْجَنَّةَ فَلٍتَأْتِهِ مَنِيَّتُهُ وَهُوَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآَخِرِ، وَالْيَاْتِ إِلَى النَّاسِ مَا يُحِبُّ أَنْ يُؤْتَى إِلَيْه)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رضي الله عنهما) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Anayependa aepushwe na moto na aingizwe Jannah, basi afanye hima mauti yake yamfikie ilihali anamwamini Allaah na Siku ya Mwisho, na awatendee watu analopenda kutendewa)).  [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1.  Iymaan ni ufunguo wa kuingia Jannah. Basi Muislamu aamini nguzo zote sita za iymaan, ya kwanza kabisa ni kumwamini Allaah (سبحانه وتعالى).  Nguzo hizo zimetajwa katika Hadiyth ndefu ya Jibriyl kumjia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kumuuliza maswali kadhaa akajibu kuhusu iymaan:

 

 

(أنْ تُؤمِنَ باللهِ، وَمَلائِكَتِهِ، وَكُتُبهِ، وَرُسُلِهِ، وَاليَوْمِ الآخِر، وتُؤْمِنَ بالقَدَرِ خَيرِهِ وَشَرِّهِ)).   مسلم

((Ni kumwamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Rasuli Wake na siku ya Qiyaamah, na  kuamini Qadar  (majaaliwa ya Allaah) ya kheri zake na shari zake)) [Muslim]

 

 

2. Iymaan pia imeambatana na kupendeleana kheri yale ambayo mtu anapendelea nafsi yake kama  ilivyotajwa katika Hadiyth

 

عنْ أَنَسٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ: ((لاَ يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى يُحِبَّ لإِخِيهِ مَا يُحِبُّ لِنَفْسِهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hatoamini mmoja wenu mpaka ampendelee nduguye anayojipendelea nafsi yake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

Rejea Hadiyth namba (21).

 

 

3. Uislamu umefunza kila jambo la kumwepusha mtu moto na la kumwingiza Jannah. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema katika Hadiyth:

 

عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه غن النبي صلى الله عليه وسلم: ((مَا تَرَكْتُ مِن شَيءٍ يُقَرِّبُكُمْ إِلى الجَنَّةِ إِلاَّ أَمَرْتُكُمْ بِهِ، وَلاَ مِن شيءٍ يُبعدُكُمْ عَنِ النَّارِ إِلاَّ نَهَيْتُكُمْ عَنْهُ))

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Sijaacha jambo lolote litakalokukurubisheni na Jannah isipokuwa nimekuamrisheni. Na wala lolote litakalokuepusheni na moto isipokuwa nimekukatazeni)) [Al-Haakim (2/5), Al-Bayhaqiy fiy Shu’ab Al-Iymaan (7/299), ameisahihisha Al-Albaaniy: As-Silsilah Asw-Swahiyhah (2866)]

 

 

 

4. Hatima ya bin Aadam ni ima Jannah au moto, na anayefaulu ni yule mwenye kuingia Jannah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوْنَ أُجُورَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۖ فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ۗ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿١٨٥﴾

Kila nafsi itaonja mauti. Na hakika mtalipwa kikamilifu ujira wenu Siku ya Qiyaamah. Basi atakayewekwa mbali na moto na akaingizwa Jannah kwa yakini amefuzu. Na uhai wa dunia si lolote ila ni starehe ya udanganyifu. [Aal-‘Imraan (4: 185)]

 

Rejea pia Huwd (11: 105-108), Ash-Shuwraa (42: 7).

 

 

5. Himizo la kutenda ‘amali njema na kudumisha hadi yamfikie mauti na hivyo ni kudiriki husnul-khaatimah (mwisho mwema).

 

 

6. Thibitisho la kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم

 

عَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ : ((مَنْ كَانَ آخِرُ كَلامِهِ لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ دَخَلَ الْجَنَّةَ)) رواه أبو داود ( 3116 ) وحسَّنه الألباني في " إرواء الغليل ( 3 / 149 ) .

Kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayekuwa maneno yake ya mwisho ni Laa ilaaha illa Allaah ataingia Jannah)). [Abuu Daawuwd, Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Irwaa Al-Ghaliyl (3/149), Swahiyh Al-Jaami’ (6479), Swahiyh Abiy Daawuwd (3116)] 

 

 

7. Mapendekezo na himizo la kutendeana wema baina ya Waislamu na kupendeleana kila aina za kheri na kuepushana shari.

 

Rejea Hadiyth namba (20), (21), (22), (23)

 

 

 

8. Sababu za kujiepusha na moto na kuingia Jannah ni nyepesi kabisa mtu kuzidiriki akiazimia kama anavyosema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) . 

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ قَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏ ((الْجَنَّةُ أَقْرَبُ إِلَى أَحَدِكُمْ مِنْ شِرَاكِ نَعْلِهِ، وَالنَّارُ مِثْلُ ذَلِكَ)) البخاري

Kutoka kwa ‘Abdullaah (رضي الله عنه) amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jannah iko karibu zaidi kwa mmoja wenu kuliko nyuzi za viatu vyake, na moto kama hivyo)). [Al-Bukhaariy]

 

Share

096-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haifai Kubughudhiana, Kuhusudiana, Kuendeana Kinyume, Kukatana Na Kukhasimiana Kwa Zaidi Ya Siku Tatu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 96

 

Haifai Kubughudhiana, Kuhusudiana, Kuendeana Kinyume,

Kukatana Na Kukhasimiana Kwa Zaidi Ya Siku Tatu

 

 

عَنْ أَنَسُ (رضي الله عنه) أنّ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ تَبَاغَضُوا، وَلاَ تَحَاسَدُوا، وَلاَ تَدَابَرُوا، وَلاَ تَقَاطَعوا، وَكُونُوا عِبَادَ اللَّهِ إِخْوَانًا، وَلاَ يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أَنْ يَهْجُرَ أَخَاهُ فَوْقَ ثَلاَثَةِ أَيَّامٍ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msibughudhiane [msichukiane], wala msihusudiane, wala msipeane mgongo, wala msikatane, kuweni waja wa Allaah ni ndugu, wala haifai kwa Muislamu kumhama nduguye kwa zaidi ya siku tatu [asiseme naye])). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kubughudhiana, kuhusudiana, kuendeana kinyume, kukatana, kukhasimiana, yote ni maovu yanayohusu haki baina ya watu na ambayo yanaleta mtafaruku baina ya watu.

 

Rejea Hadiyth namba (22), (42), (72), (93), (94).

 

 

 

2.  Maovu hayo ni aina ya maradhi ya moyo. Ikiwa Muislamu anayo maradhi kama hayo basi ajitahidi kusoma du’aa ifuatayo iliyomo katika Aayah ya Qur-aan:

 

 رَبَّنَا اغْفِرْ لَنَا وَلِإِخْوَانِنَا الَّذِينَ سَبَقُونَا بِالْإِيمَانِ وَلَا تَجْعَلْ فِي قُلُوبِنَا غِلًّا لِّلَّذِينَ آمَنُوا رَبَّنَا إِنَّكَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ﴿١٠﴾

“Rabb wetu! Tughufurie na ndugu zetu ambao wametutangulia kwa iymaan na wala Usijaalie katika nyoyo zetu mafundo ya chuki kwa wale walioamini; Rabb wetu! Hakika Wewe ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu. [Al-Hashr (59: 10)]

 

 

 

3. Bin Aadam ni dhaifu, ana hisia za moyo anapoudhiwa, lakini ni Rahmah ya Allaah (سبحانه وتعالى) kumpa mja Wake muda wa siku tatu kuungulika na  kuvumilia. Kisha inampasa arudishe moyo wake katika kusamehe, kupuuzilia mbali na kujaribu kusahau.

 

Katika kisa cha Ifk, Abu Bakr (رضي الله عنه) aligoma kwanza kuendelea kumpa sadaka jamaa yake aliyehusika katika kumzulia Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها), lakini Allaah (سبحانه وتعالى) Alipoteremsha kauli Yake ifuatayo, Abu Bakr alikiri kuwa anataka kughufuriwa madhambi yake, na akaendelea kuitoa sadaka yake kwa jamaa huyo jamaa yake:

 

وَلَا يَأْتَلِ أُولُو الْفَضْلِ مِنكُمْ وَالسَّعَةِ أَن يُؤْتُوا أُولِي الْقُرْبَىٰ وَالْمَسَاكِينَ وَالْمُهَاجِرِينَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ۖ وَلْيَعْفُوا وَلْيَصْفَحُوا ۗ أَلَا تُحِبُّونَ أَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَكُمْ ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٢﴾

Na wala wasiape wale wenye fadhila miongoni mwenu na wenye wasaa wa mali kuwa hawatowapa (swadaqah) jamaa wa karibu, na masikini, na Muhaajiriyn katika njia ya Allaah. Na wasamehe na waachilie mbali. Je, hampendi Allaah Akughufurieni? Na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.  [An-Nuwr (24: 22)]

 

 

Na kusamehe watu pamoja na kuzuia ghadhabu kutokutamka maneno maovu ni katika sifa za ihsaan na Allaah (سبحانه وتعالى) Anampenda mtu huyo mwenye kusamehe watu kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

الَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي السَّرَّاءِ وَالضَّرَّاءِ وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾ 

Ambao wanatoa (kwa ajili ya Allaah) katika hali ya wasaa na katika hali ya shida, na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-‘Imraan (3: 134)]

 

Na atakayeanza kumsemesha mwenziwe ni mbora zaidi ya mwengine. Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): 

 

 عن أبي أيوب الأنصاري رضي الله عنه قال : قال النبي صلى الله عليه وسلم: ((لا يَحِلُّ لِمُسْلِمٍ أَنْ يَهْجُرَ أَخَاهُ فَوْقَ ثَلَاثِ لَيَالٍ، يَلْتَقِيَانِ فَيُعْرِضُ هَذَا وَيُعْرِضُ هَذَا، وَخَيْرُهُمَا الَّذِي يَبْدَأُ بِالسَّلام))  

((Haimpasi Muislamu amhame ndugu yake kwa zaidi ya siku tatu hata wanapokutana huyu anamgeuzia [uso] huyu na huyu anamgeuzia [uso] huyu. Na aliye mbora wao kati ya hao wawili ni yule anayeanza kutoa salaam)). [Al-Bukhaariy na Muslim] Pia:

 

Na katika Riwaayah nyengine:

 

((فَمَنْ هَجَرَ فَوْقَ ثَلاَثٍ فَمَاتَ دَخَلَ النَارَ ))  

((Atakayemhama [mwenzake] kwa zaidi ya siku tatu akafariki, basi ataingia motoni)). [Abuu Daawuwd]

 

Rejea pia Hadiyth namba (97).

 

 

 

4. Waislamu wote ni ndugu. Kwa hiyo, wanapasa kupendana, kuoneana huruma, kuheshimiana, kutokuudhiana na kuoneana choyo n.k.

 

Rejea Al-Hujuraat (49: 10), Al-Fat-h (48: 29).

 

 

 

5. Ni wajibu wa Waislamu kuwasuluhisha waliokhasimikiana, kwani fadhila zake ni kuu na zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّا خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿١١٤﴾

Hakuna khayr katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha swadaqah, au mema, au kusuluhisha baina ya watu. Na atakayefanya hivyo kutaka radhi za Allaah, basi Tutampa ujira adhimu. [An-Nisaa (4: 114)]

 

Rejea pia Al-Hujuraat (49: 10).

 

Na ni wajibu kwa waliokhasimikiana kusameheana, kwani kuna malipo mema.  

 

 

Share

097-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Wanakhasimiana Hawataingia Jannah Hadi Wapatane Na Hawatapokelewa ‘amali Zao

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 97

 

Wanaokhasimiana Hawataingia Jannah Hadi Wapatane Na Hawatapokelewa ‘Amali Zao

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((تُفْتَحُ أَبْوَابُ الْجَنَّةِ يَوْمَ الإثْنَيْنِ وَيَوْمَ الْخَمِيسِ، فَيُغْفَرُ لِكُلِّ عَبْدٍ لاَ يُشْرِكُ بِاللَّهِ شَيْئًا إِلاَّ رَجُلاً كَانَتْ بَيْنَهُ وَبَيْنَ أَخِيهِ شَحْنَاءُ، فَيُقَالُ: أَنْظِرُوا هَذَيْنِ حَتَّى يَصْطَلِحَا! أَنْظِرُوا هَذَيْنِ حَتَّى َصْطَلِحَا!)) مسلم  وَفي رواية: ((تُعْرَضُ الأَعْماَلُ فِي كُلِّ يَوْمِ خَمِيسٍ واثْنِيْن)) وَذَكَرَ نَحْوَهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Milango ya Jannah hufunguliwa kila siku ya Jumatatu na Alkhamiys, na ataghufuriwa kila mja asiyemshirikisha Allaah kwa chochote, isipokuwa mtu aliye na utesi baina yake na nduguye, hapo husemwa: “Waacheni hawa mpaka wapatane! Waacheni hawa mpaka wapatane!”)).  [Muslim] 

 

Katika Riwaayah nyingine: ((‘Amali hutandazwa kila siku ya Alkhamiys na Jumatatu)), na akataja kama hivyo. [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Jannah imeharamishwa kwa ndugu waliokhasimiana.

 

 

2. Kukhasimiana ni maovu yaliyofananishwa na kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

3. Muislamu anaweza kupoteza muda na nguvu zake kutenda ‘amali zisizopokelewa na Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zinazotawanyika. [Al-Furqaan (25: 23)].

 

 

4. Baadhi ya mas-alah watu wanayachukulia mepesi, lakini kumbe yana uzito mno mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى), kama vile hali ilivyokuwa katika kisa cha ‘Ifk’ – kusingiziwa kashfa Mama wa Waumini ‘Aaisha   (رضي الله عنها)  Aliposema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥﴾

na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allaah ni kubwa mno. [An-Nuwr: 15]

 

 

5. Wajibu wa Waislamu kusuluhisha waliokhasimiana ili wachume thawabu zake na wapate fadhila zake

 

 

Rejea An-Nisaa (4: 114), Al-Hujuraat (49: 10).

 

Rejea Hadiyth namba (24), (96). 

 

 

6. Uislamu unasisitiza mno undugu, amani, na mapenzi baina ya Waislamu.

 

Share

098-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Dhana Mbaya Ni Mazungumzo Ya Uongo Kabisa

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 98

 

Dhana Mbaya Ni Mazungumzo Ya Uongo Kabisa

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِيَّاكُمْ وَالظَّنَّ فَإِنَّ الظَّنَّ أَكْذَبُ الْحَدِيثِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Tahadharini na dhana mbaya, kwani hakika dhana ni mazungumzo ya uongo kabisa)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Tahadharisho la kuwa na dhana mbaya ambayo inampeleka mtu kufikia maovu mengine ya kujasusi na ghiybah kama Anavyotahadharisha Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ﴿١٢﴾

 

Enyi walioamini!  Jieupusheni sana na dhana kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi, na wala wasisengenyane baadhi yenu wengineo. Je, anapenda mmoja wenu kwamba ale nyama ya nduguye aliyekufa? Basi mmelichukia hilo! Na mcheni Allaah! Hakika Allaah ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [Al-Hujuraat (59: 12)]

 

 

2. Dhana mbaya zinaweza kumfikisha mtu kuchuma dhambi kubwa inayoangamiza ya kusingizia uovu watu.

 

Rejea Hadiyth namba (87) (88), (89), (104).

 

 

3. Dhana mbaya imefananishwa na uongo wa hali ya juu kabisa, nayo ni aina ya maradhi ya moyo ya kufuata matamanio ya nafsi. 

 

 

4. Shariy’ah za Kiislamu na adhabu zinahukumiwa kwa yakini na si kwa dhana tu. Na ndio maana wanatakiwa mashahidi wanne katika jambo la hadd (adhabu zilizowekwa katika Shariy’ah).

 

Rejea An-Nuwr (24: 4-9), An-Nisaa (4: 15).

 

 

5. Dhana mbaya inaleta vurugu na malumbano katika jamii, hivyo huchelewesha maendeleo.

 

 

6. Dhana mbaya pia huleta utesi baina ya watu.

 

 

 

Share

099-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kumhukumia Mtu Kuwa Hatoghufuriwa Dhambi Zake Ni Kuporomoka 'Amali Zake

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 99

 

Kumhukumia Mtu Kuwa Hatoghufuriwa Dhambi Zake Ni Kuporomoka ‘Amali

 

 

 

 

عَنْ جُنْدَبٍ بن عَبْدِ الله (رضي الله عنه) قَال: قَال رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((قَالَ رَجُلٌ:  وَاللَّهِ لاَ يَغْفِرُ اللَّهُ لِفُلاَنٍ. فَقَالَ اللهُ عَزَّ وّجّلَّ:  مَنْ ذَا الَّذِي يَتَأَلَّى عَلَيَّ أَنْ لاَ أَغْفِرَ لِفلاَنٍ؟  فَإِنِّي قَدْ غَفَرْتُ لِفلاَنٍ وَأَحْبَطْتُ عَمَلَكَ)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Jundab bin ‘Abdillaah  (رضي الله عنه) ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم ) amesema:  ((Mtu mmoja alisema: Wa-Allaahi! Allaah Hatomghufuria fulani! Allaah Aliyetukuka na Jalali Akasema: Ni nani huyo anayeniapia kuwa Sitomghufuria fulani? Mimi Nimeshamghufuria fulani na Nimeziporomosha ‘amali zako)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Tahadharisho la kuapa viapo visivyokuwa vya kheri. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

  وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ  

Na hifadhini yamini zenu.  [Al-Maaidah (5: 890]

 

 

 

2. Tisho la kuchukia Waislamu wengineo.

 

 

3. Bainisho la wasaa na Rahmah ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwamba Anamghufuria Amtakaye hata kama ana madhambi makubwa vipi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا ۚ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٥٣﴾

 Sema: Enyi waja Wangu ambao wamepindukia mipaka juu ya nafsi zao: “Msikate tamaa na rahmah ya Allaah; hakika Allaah Anaghufuria dhambi zote; hakika Yeye Ndiye Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.” [Az-Zumar: 53]

        

Rejea pia:  Al-Araaf (7: 56),   Al-An’aam (6: 147).

 

 

4. Hakuna ajuaye hatima yake wala ya mwenziwe, hivyo haipasi kumhukumia mtu kuwa ana madhambi na kwamba hatoghufuriwa au kumtakasa mtu na kumtukuzia malipo yake.

 

 

5. Katazo la kuingilia hukmu ya Allaah (سبحانه وتعالى) inayomhusu Yeye Pekee, nayo ni ukosefu wa adabu kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

6. Tahadharisho la kuporomoshwa ‘amali za mtu kwa kumhukumia mtu hatima yake.

 

 

7. Hakuna bin Aadam asiyekuwa na makosa kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

 ((كلُّ بني آدمَ خطَّاءٌ وخيرُ الخطَّائينَ التوَّابونَ))

((Kila bina Aadam ni mkosa,  lakini mbora kwa wale wenye kukosea ni wale wenye kutubia)) [Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Ibn Maajah (3447), Swahiyh Al-Jaami’ (4515)].

 

Na kumhukumia mtu maovu yake ni kujisahau mtu nafsi yake ni dalili ya mtu kujiona kuwa yeye ni mbora kuliko wenziwe.

 

 

 

Share

100-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayedhihirisha Furaha Kwa Msiba Wa Mwenziwe Huenda Akaonjeshwa Yeye Msiba

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 100 

 

Anayedhihirisha Furaha Kwa Msiba Wa Mwenziwe Huenda Akaonjeshwa Yeye Msiba

 

 

 

 

عَنْ وَاثِلَةَ بْنِ الأسْقَعِ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((لاَ تُظْهِرْ الشَّمَاتَةَ لإَخِيكَ فَيَرْحَمَهُ اللَّهُ وَيَبْتَلِيكَ)) رواه الترمذي وَقَالَ هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ

Imepokelewa kutoka kwa Waathilah bin Al-Asqa’i (رضي الله عنه) amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم ) amesema: ((Usidhihirishe furaha kwa msiba alioupata nduguyo, Asije Allaah Akamrehemu na Akakuonjesha wewe)). [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kufurahia msiba wa mwenzio, kwani Waislamu wote ni ndugu na inawapasa kuoneana huruma na kupendeleana kheri.

 

Rejea Al-Hujuraat (49: 10), Al-Fat-h (48: 29).

 

 

2. Muislamu aumie anapoumia nduguye na afurahi anapofurahi nduguye.

 

Rejea Hadiyth namba (20), (21).

 

Pia Hadiyth:  

عن النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَثَلُ الْمُؤْمِنِينَ فِي تَوَادِّهِمْ وَتَرَاحُمِهِمْ وَتَعَاطُفِهِمْ مَثَلُ الْجَسَدِ؛ إِذَا اشْتَكَى مِنْهُ عُضْوٌ تَدَاعَى لَهُ سَائِرُ الْجَسَدِ بِالسَّهَرِ وَالْحُمَّى))

Kutoka kwa Nu’maan bin Bashiyr kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mfano wa Waumini katika kupendana na kurehemeana kwao na kuhurumiana kwao ni sawa na mwili mmoja, kikishtakia kiungo kimoja, basi mwili mzima utakosa usingizi na kushikwa na homa)). [Al-Bukhaariy]

 

 

3. Hali ya furaha na misiba, shida na faraja, umaskini na utajiri n.k. huzunguka baina ya watu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِن يَمْسَسْكُمْ قَرْحٌ فَقَدْ مَسَّ الْقَوْمَ قَرْحٌ مِّثْلُهُ ۚ وَتِلْكَ الْأَيَّامُ نُدَاوِلُهَا بَيْنَ النَّاسِ

 Inapokuguseni majeraha basi yamekwisha wagusa watu majeraha kama hayo. Na hizo ni siku Tunazizungusha zamu (za mabadiliko ya hali) baina ya watu  [Aal-‘Imraan: 140] 

  

 

4. Tahadharisho katika Hadiyth hiyo kuwa Allaah (سبحانه وتعالى) kumjaalia anayefurahia msiba wa mwenziwe umfikie naye apate kuonja dhiki yake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَا تَهِنُوا فِي ابْتِغَاءِ الْقَوْمِ ۖ إِن تَكُونُوا تَأْلَمُونَ فَإِنَّهُمْ يَأْلَمُونَ كَمَا تَأْلَمُونَ ۖ وَتَرْجُونَ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا يَرْجُونَ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿١٠٤﴾

Wala msilegee kuwaandama watu (maadui). Mkiwa mnaumia basi nao pia wanaumia kama mnavyoumia. Na mnataraji kutoka kwa Allaah wasiyoyataraji wao. Na Allaah daima ni Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote. [An-Nisaa (4: 104)]

 

 

Share

101-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayeghushi Katika Biashara Amekanwa Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

 

Hadiyth Ya  101

 

Anayeghushi Katika Biashara Amekanwa Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَرَّ عَلَى صُبْرَةِ طَعَامٍ فَأَدْخَلَ يَدَهُ فِيهَا فَنَالَتْ أَصَابِعُهُ بَلَلاً فَقَالَ: ((مَا هَذَا يَا صَاحِبَ الطَّعَامِ؟)) قَالَ:  أَصَابَتْهُ السَّمَاءُ يَا رَسُولَ اللَّهِ. قَالَ: ((أَفَلاَ جَعَلْتَهُ فَوْقَ الطَّعَامِ كَيْ يَرَاهُ النَّاسُ، مَنْ غَشَّ فَلَيْسَ مِنِّي))  مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipitia katika mrundo wa chakula (nafaka), akaingiza mkono wake ndani. Vidole vyake vikagusa umajimaji. Akasema: ((Ee mwenye chakula, ni nini hii?)). Akajibu: “Ee Rasuli wa Allaah! Kimepatwa na manyunyu”. Akasema: ((Si ungeliweka juu ya chakula ili watu wakione! Anayeghushi si katika mimi)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kughushi katika kuuza, na muuzaji anapaswa adhihirishe bidhaa anayoiuza inapokuwa na kasoro au ila.  Allaah Anaonya Anaposema:

 وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

Ole kwa wanaopunja.

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ﴿٢﴾

Ambao wanapopokea kipimo kwa watu wanataka wapimiwe kamilifu.

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ﴿٣﴾

Na wanapowapimia (watu) kwa kipimo au wanawapimia kwa mizani wanapunja. [Al-Mutwaffifiyn: 1-3]

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 161), Huwd (11: 85), Ash-Shu’araa (26: 83),  Al-Israa (17: 35).

 

 

2. Kughushi ni kula mali za watu bila ya haki jambo ambalo Ameliharamisha Allaah (سبحانه وتعالى) Anaposema:

 

وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَكُم بَيْنَكُم بِالْبَاطِلِ وَتُدْلُوا بِهَا إِلَى الْحُكَّامِ لِتَأْكُلُوا فَرِيقًا مِّنْ أَمْوَالِ النَّاسِ بِالْإِثْمِ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٨﴾

Na wala msiliane mali zenu kwa ubatilifu na mkazipeleka (rushwa) kwa mahakimu ili mle sehemu katika mali ya watu kwa dhambi na hali mnajua. [Al-Baqarah (2: 1880]

 

Rejea pia An-Nisaa (4: 29, 161)

 

 

3. Kughushi kunasababisha ufisadi katika ardhi na uadui baina ya jamii.

 

 

4. Kughushi ni khiyana na dhulma, nako ni kuchukua haki ya mtu. Ni dhambi ambazo Allaah (سبحانه وتعالى) Hazisamehi. Aliyefanya hivyo atachukuliwa ‘amali zake njema Siku ya Qiyaamah apewe mdhulumiwa, kama hana, atabebeshwa maovu ya mdhulumiwa.

Rejea Hadiyth namba (19).

 

 

5. Kuingiza kwake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) mkono wake katika chakula kunatoa mafunzo kwa wenye majukumu ya masoko kuchunguza biashara na bidhaa zinazouzwa ili kuzuia dhulma.

 

 

 

 

Share

102-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Atakhasimiana na Anayevunja Ahadi Kwa Kiapo, Anayemdhulumu Mwajiriwa

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 102

 

Allaah Atakhasimiana na Anayevunja Ahadi Kwa Kiapo, Anayemdhulumu Mwajiriwa

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ تَعَالى: ثلاَثَةٌ أَنَا خَصْمُهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ: رَجُلٌ أَعْطَى بِي ثُمَّ غَدَرَ، وَرَجُلٌ بَاعَ حُرًّا فَأَكَلَ ثَمَنَهُ، وَرَجُلٌ اسْتَأْجَرَ أَجِيرًا فَاسْتَوْفَى مِنْهُ وَلَمْ يُعْطِ أَجْرَهُ)) البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema:((Allaah Aliyetukuka Amesema: Watu watatu Mimi  Nitakhasimiana nao Siku ya Qiyaamah: Mtu aliyempa nduguye ahadi kwa kutumia Jina Langu kisha akavunja ahadi hiyo. Mtu aliyemuuza muungwana na akala thamani yake. Na mtu aliyemwajiri mwajiriwa naye akammalizia kazi yake, wala asimpe ujira wake)). [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Maamrisho ya kutimiza ahadi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَأَوْفُوا بِالْعَهْدِ ۖ إِنَّ الْعَهْدَ كَانَ مَسْئُولًا ﴿٣٤﴾

Na timizeni ahadi; hakika ahadi itakuwa ni ya kuulizwa  [Al-Israa (17: 34)]

 

Rejea pia Al-Maaidah (5 :1)

  

Na asiyetimiza ahadi, atakuwa na sifa ya wanafiki ambao walikuwa hawaachi kuvunja ahadi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

إِنَّ شَرَّ الدَّوَابِّ عِندَ اللَّـهِ الَّذِينَ كَفَرُوا فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ﴿٥٥﴾

Hakika viumbe viovu kabisa mbele ya Allaah ni wale waliokufuru nao hawaamini.

 

الَّذِينَ عَاهَدتَّ مِنْهُمْ ثُمَّ يَنقُضُونَ عَهْدَهُمْ فِي كُلِّ مَرَّةٍ وَهُمْ لَا يَتَّقُونَ﴿٥٦﴾

Ambao umepeana nao ahadi, kisha wanavunja ahadi yao kila mara, na wala hawana taqwa. [Al-Anfaal (8: 55-56)]

 

Rejea pia: Al-Baqarah (2: 100), Ar-‘Rad (13: 25).

 

Rejea pia Hadiyth namba  (18).

 

 

 

2. Kutimiza ahadi ni miongoni mwa sifa za wenye taqwa kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّيْسَ الْبِرَّ أَن تُوَلُّوا وُجُوهَكُمْ قِبَلَ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَلَـٰكِنَّ الْبِرَّ مَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالْكِتَابِ وَالنَّبِيِّينَ وَآتَى الْمَالَ عَلَىٰ حُبِّهِ ذَوِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ وَالسَّائِلِينَ وَفِي الرِّقَابِ وَأَقَامَ الصَّلَاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَالْمُوفُونَ بِعَهْدِهِمْ إِذَا عَاهَدُوا ۖ وَالصَّابِرِينَ فِي الْبَأْسَاءِ وَالضَّرَّاءِ وَحِينَ الْبَأْسِ ۗ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ صَدَقُوا ۖ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُتَّقُونَ ﴿١٧٧﴾ 

Sio wema kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa Mashariki na Magharibi lakini wema ni mwenye kuamini Allaah na Siku ya Mwisho na Malaika na Kitabu na Manabii, na akawapa mali juu ya kuipenda kwake jamaa wa karibu na mayatima na masikini na msafiri na waombao na katika kukomboa watumwa na akasimamisha Swalaah, na akatoa Zakaah na watimizao ahadi zao wanapoahidi, na wanaosubiri katika dhiki za ufukara na maafa ya magonjwa na njaa na katika vita. Hao ndio waliosadikisha na hao ndio wenye taqwa. [Al-Baqarah (2: 177)]

 

Na pia kutimizia ahadi ni miongoni mwa sifa zitakazomfikisha Muumin katika Jannah ya Al-Firdaws. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):  

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

قَدْ أَفْلَحَ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١﴾

Kwa yakini wamefaulu Waumini.

الَّذِينَ هُمْ فِي صَلَاتِهِمْ خَاشِعُونَ ﴿٢﴾

Ambao katika Swalaah zao huwa wananyenyekea.

 

وَالَّذِينَ هُمْ عَنِ اللَّغْوِ مُعْرِضُونَ ﴿٣﴾

Na ambao wanajiepusha na mambo ya upuuzi.

 

وَالَّذِينَ هُمْ لِلزَّكَاةِ فَاعِلُونَ ﴿٤﴾

Na ambao wanatoa Zakaah.

 

وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ ﴿٥﴾

Na ambao wanazihifadhi tupu zao.

 

إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ ﴿٦﴾

 

Isipokuwa kwa wake zao, au kwa iliyowamiliki mikono yao ya kuume basi hao hawalaumiwi.

 

فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ ﴿٧﴾

Lakini atakayetaka kinyume ya hayo; basi hao ndio wapindukao mipaka.

 

وَالَّذِينَ هُمْ لِأَمَانَاتِهِمْ وَعَهْدِهِمْ رَاعُونَ ﴿٨﴾

Na ambao amana zao na ahadi zao wanazichunga.

 

وَالَّذِينَ هُمْ عَلَىٰ صَلَوَاتِهِمْ يُحَافِظُونَ ﴿٩﴾

Na ambao wanazihifadhi Swalaah zao.

 

أُولَـٰئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَ ﴿١٠﴾

Hao ndio warithi.

 

الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿١١﴾

Ambao watarithi (Jannah) ya Al-Firdaws, wao humo ni wenye kudumu. [Al-Muuminuwn (23: 1-11)]

 

 

 

Rejea pia: Ar-Ra’d (13: 20-24), Al-Ma’arij (70: 32). 

 

 

3. Inaruhusiwa kuvunja kiapo kwa kubadilisha jambo ovu kwa jambo jema.

 

Rejea Hadiyth namba (5).

 

 

4. Allaah (سبحانه وتعالى) Amemsifu Nabii Ismaa’iyl kwa sifa ya kutimizia ahadi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى)  

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِسْمَاعِيلَ ۚ إِنَّهُ كَانَ صَادِقَ الْوَعْدِ وَكَانَ رَسُولًا نَّبِيًّا ﴿٥٤﴾

 Na mtaje katika Kitabu Ismaa’iyl. Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Rasuli na Nabiy. [Maryam (19: 54)]

 

 

 

5. Uislamu unahimiza haki baina ya watu na uhuru wa bin Aadam.

 

 

6. Makatazo ya kumdhulumu mwajiriwa kwa kutokumlipa ujira wake, kwani kufanya hivyo ni khiana, nayo ni dhulma. Allaah (سبحانه وتعالى) Amekataza hilo Anaposema:

 

 وَمَا كَانَ لِنَبِيٍّ أَن يَغُلَّ ۚ وَمَن يَغْلُلْ يَأْتِ بِمَا غَلَّ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۚ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفْسٍ مَّا كَسَبَتْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ﴿١٦١﴾

Na haikuwa (ni tabia) kwa Nabiy yeyote kukhini (ngawira). Na yeyote atakayekhini atakuja na kile alichokikhini Siku ya Qiyaamah. Kisha italipwa kamilifu kila nafsi yale iliyoyachuma nao hawatodhulumiwa [Aal-‘Imraan (3: 161)]

 

 

7. Mtu anayekhasimiwa na Allaah (سبحانه وتعالى), tena Siku ya Qiyaamah, atakuwa katika adhabu kali. Hivyo, ni juu yetu tufanye  yatakayotupatia uhusiano mzuri na Muumbaji wetu, na mambo yote Aliyotukataza tuwe mbali nayo.

 

 

8. Aina nyingi za dhulma na adhabu zake zimetajwa mno katika Qur-aan na Sunnah. 

 

 

 

Share

103-Lu-ulu-un-Manthuwrun Allaah Hatowazungumzisha Wala Kuwatazama Wanaoburuza Nguo Zao, Msimbulizi, Na Mwapaji Uongo Kwa Ajili Ya Kuuza Bidhaa

 

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya  103

 

Allaah Hatowazungumzisha Wala Kuwatazama Wanaoburuza Nguo Zao, Msimbulizi,

Na Mwapaji Uongo Kwa Ajili Ya Kuuza Bidhaa

 

 

 

 

عَنْ أَبِي ذَرٍّ (رضي الله عنه)  عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((ثلاَثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمْ اللَّهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلاَ يَنْظُرُ إِلَيْهِمْ وَلاَ يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ)) قَالَ فَقَرَأَهَا رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ثلاَثَ مِرَارٍ. قَالَ أَبُو ذَرٍّ: خَابُوا وَخَسِرُوا، مَنْ هُمْ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: ((الْمُسْبِلُ، وَالْمَنَّانُ، وَالْمُنَفِّقُ سِلْعَتَهُ بِالْحَلِفِ الْكَاذِبِ)) مسلم و في رواية له: ((وَالْمُسْبِلُ إِزَارَهُ)) يَعْن الْمُسْبِلَ إزَارَهُ وَثوْبَهُ أسْفَلَ مِنَ الْكَعْبَيْنِ لِلْخُيَلاءِ

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Dharr (رضي الله عنه)  amesema: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم ) amesema: ((Watu watatu Allaah Hatowazungumzisha Siku  ya Qiyaamah, wala Hatowatazama, wala Hatowatakasa, na watapata adhabu inayoumiza)). Akayakariri maneno hayo mara tatu. Abuu Dharr akasema: “Wamepita patupu na wamekhasirika! Ni nani hao ee Rasuli wa Allaah?”  Akasema: ((Al-Musbil - mwenye kuburuza nguo yake, mwenye kutoa na kukizungumzia [kusimbulia] alichokitoa, na mwenye kuuza bidhaa zake kwa kutumia kiapo cha uongo)). [Muslim] Na pia: ((anayeburuza izari yake)). [Muslim] yaani nguo yake kuvuka chini ya mafundo ya miguu kwa kiburi.

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

1. Haramisho la mwanamme kuburuza nguo yake, kwani ni alama ya kiburi

 

Hadiyth: ((Ole wako na kuburuza nguo [kuvuka mafundo ya miguu], kwani kuburuza nguo ni alama ya kiburi)). [Fat-hul-Baariy Mj. (10), uk. (264)]

 

 

2. Haramisho la masimbulizi, kwani yanasababisha udhalilifu kwa yule anayepewa. Allaah (سبحانه وتعالى) Anataja makatazo yake na makemeo yake, na pia Anataja fadhila za asiyesimbulia kutoa mali yake katika Aayah zifuatazo: 

 

 الَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ثُمَّ لَا يُتْبِعُونَ مَا أَنفَقُوا مَنًّا وَلَا أَذًى ۙ لَّهُمْ أَجْرُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ وَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴿٢٦٢﴾

Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Allaah kisha hawafuatishii kwa waliyoyatoa masimbulizi wala udhia watapa ujira wao kwa Rabb wao, na wala hakuna khofu juu yao na wala hawatohuzunika.

 

قَوْلٌ مَّعْرُوفٌ وَمَغْفِرَةٌ خَيْرٌ مِّن صَدَقَةٍ يَتْبَعُهَا أَذًى ۗ وَاللَّـهُ غَنِيٌّ حَلِيمٌ ﴿٢٦٣﴾

Kauli njema na msamaha ni bora kuliko swadaqah inayoifuata udhia. Na Allaah ni Mkwasi, Mvumilivu.

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ كَالَّذِي يُنفِقُ مَالَهُ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ صَفْوَانٍ عَلَيْهِ تُرَابٌ فَأَصَابَهُ وَابِلٌ فَتَرَكَهُ صَلْدًا ۖ لَّا يَقْدِرُونَ عَلَىٰ شَيْءٍ مِّمَّا كَسَبُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٢٦٤﴾

Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia kama yule ambaye anatoa mali yake kwa kujionyesha kwa watu wala hamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama jabali juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa ikaliacha tupu. Hawana uwezo juu ya lolote katika waliyoyachuma. Na Allaah Haongoi watu makafiri. [Al-Baqarah (2: 262-264)]

 

 

3. Haramisho la kuapa uongo kwa ajili ya kuuza bidhaa, kwani hivyo ni ulaghai na khiyana.

 

Rejea Hadiyth namba (101).

 

 

4. Kuburuza nguo, masimbulizi, kuapa uongo kwa ajili ya kuuza bidhaa ni miongoni mwa madhambi makubwa, kwani yatamharamisha Muislamu kutazamwa na Allaah (سبحانه وتعالى) Siku ya Qiyaamah na watapata adhabu kali.

 

 

5. Haya ni makosa ambayo athari yake inaonekana katika jamii. Na jamii yoyote ambayo ina matatizo haya, basi maendeleo huwa hayapatikani kwani yanaleta bughudha, uadui, khusma na kudharauliana.

 

 

6. Amri ya kutokuburuza nguo kwa wanaume imekuwa ni jambo la kufanyiwa istihzai, kejeli na masikhara kwa wanaotimiza amri hii, kwa kuwa kanzu zao ziko juu ya mafunzo ya miguu yao. Huchekwa na kupewa majina kadhaa ya istihzai kama vile ‘watawa’, ‘kirongwe’, ‘njiwa’ n.k. Watambue Waislamu wanaowafanyia istihzai ndugu zao hao kwamba ni maovu watakayohesabiwa Siku ya Qiyaamah. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَوْ أَنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا مَا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا وَمِثْلَهُ مَعَهُ لَافْتَدَوْا بِهِ مِن سُوءِ الْعَذَابِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۚ وَبَدَا لَهُم مِّنَ اللَّـهِ مَا لَمْ يَكُونُوا يَحْتَسِبُونَ﴿٤٧﴾

Na kama wale waliodhulumu wangelikuwa na vile vyote vilivyomo ardhini na pamoja navyo mfano wake, bila shaka wangelifidia kwayo kutokana na adhabu mbaya ya Siku ya Qiyaamah. Na yatawafichukia kutoka kwa Allaah ambayo hawakuwa wanatarajia.  

 

وَبَدَا لَهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ﴿٤٨﴾

Na yatawafichukia maovu ya yale waliyoyachuma, na yatawazunguka yale waliyokuwa wakiyafanyia istihzai. [Az-Zumar (39: 47-48)]

 

Na Anasema pia (سبحانه وتعالى):

إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ ﴿٢٩﴾

Hakika wale waliofanya uhalifu walikuwa (duniani) wakiwacheka wale walioamini.

 

وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ ﴿٣٠﴾

Na wanapowapitia wanakonyezana.

 

وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ ﴿٣١﴾

Na wanaporudi kwa ahli zao, hurudi wenye kufurahika kwa dhihaka. …. [Al-Mutwwaffifiyn (83: 29-36)]

 

 

Rejea pia: Huwd (11: 8), An-Nahl (16: 34), At-Tawbah (9: 65).

 

 

 

 

Share

104-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kunong’ona Mbele Ya Wengineo Husababisha Maudhi Na Dhana Mbaya

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 104

 

Kunong’ona Mbele Ya Wengineo Husababisha Maudhi Na Dhana Mbaya

 

 

 

 

عَنْ ابْن مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) أنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَال: ((إِذَا كُنْتُمْ ثلاَثَةً فلاَ يَتَنَاجَى اثْنَانِ دُونَ الآخَرِ حَتَّى تَخْتَلِطُوا بِالنَّاسِ مِنْ أَجْلِ أَنْ يُحْزِنَهُ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mnapokuwa watatu, basi wawili wasinong’onezane bila kumshirikisha mwengine hadi wajiunge watu wengine [kumtoa katika upweke yule aliyeachwa katika mazungumzo] na watu, kwa sababu kufanya hivyo kutamhuzunisha [yule wa tatu])). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kunong’onezana wawili anapokuweko mtu wa tatu ili   asiudhike na kuhisi vibaya.

 

 

2. Kunong’onezana mbele ya wengineo huenda kukasababisha kutia shaka au dhana mbaya kwa ambaye hakushirikishwa katika mnong’ono.

 

 

3. Makatazo ya kunong’onezana pasi na kuwashirikisha wengineo hata ikiwa ni zaidi ya idadi iliyotajwa na hata kwa jambo la kheri haipasi. Na kwa jambo la shari Amekataza Allaah (سبحانه وتعالى).

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا تَنَاجَيْتُمْ فَلَا تَتَنَاجَوْا بِالْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ وَمَعْصِيَتِ الرَّسُولِ وَتَنَاجَوْا بِالْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Mnaponong’onezana, basi msinong’onezane kuhusu dhambi na uadui na kumuasi Rasuli, bali nong’onezaneni kuhusu wema na taqwa; na mcheni Allaah Ambaye Kwake Pekee mtakusanywa.

 

إِنَّمَا النَّجْوَىٰ مِنَ الشَّيْطَانِ لِيَحْزُنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَلَيْسَ بِضَارِّهِمْ شَيْئًا إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ﴿١٠﴾

Hakika mnong’ono unatokana na shaytwaan ili awahuzunishe wale walioamini, na wala hawezi kuwadhuru chochote isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na kwa Allaah watawakali Waumini. [Al-Mujaadalah: 9-10]

 Rejea pia: Al-Maaidah (5: 2)

 

 

4. Uislamu unapendelea amani baina ya ndugu na kufunza adabu njema na njia za kuepusha kila aina ya maudhi au maovu ya nafsi.

 

 

5. Kutokunong’onezana ni katika adabu za kikao baina ya Waislamu.

 

 

6. Athari ya hivyo ni mbaya, kwani dhana hiyo mbaya inaweza kuzaa uadui na chuki.

 

 

Share

105-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Atawatesa Watesao Watu Duniani

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 105

 

Allaah Atawatesa Watesao Watu Duniani

 

 

 

 

عَنْ هِشَامُ بْنُ حَكِيمِ بْنِ حِزَامٍ (رضي الله عنهما) أنّهُ  مَرَّ بِالشَّامِ عَلَى أُنَاسٍ وَقَدْ أُقِيمُوا فِي الشَّمْسِ وَصُبَّ عَلَى رُءُوسِهِمْ الزَّيْتُ فَقَالَ: مَا هَذَا؟ قِيلَ: يُعَذَّبُونَ فِي الْخَرَاجِ،  فَقَالَ: أَشْهَدُ لَسمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((إِنَّ اللَّهَ يُعَذِّبُ الَّذِينَ يُعَذِّبُونَ النَّاسَ  فِي الدُّنْيَا)) فَدَخَلَ على الأمِيرِ، فَحَدَّثَهُ فأمَرَ بِهِمْ فَخلوا – رواه مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Hishaam bin Hakiym bin Hizaam (رضي الله عنهما) kwamba aliwapitia watu Shaam waliosimamishwa juani na kumwagiwa mafuta vichwani mwao. Akasema: Nini hii? Ikasemwa: “Wanateswa sababu ya kutokulipa kodi”. Akasema: “Nashuhudia hakika nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Allaah Atawatesa wanaowatesa watu duniani)). Akaingia kwa Amiyr, akamwelezea, akawaamrisha, wakaacha. [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Kushindwa kulipa kodi au gharama zozote kusiwe ni sababu ya kuwatesa watu, bali inapasa mwenye wasaa afikirie hali ya Muislamu mwenzake na ashirikiane naye kwa kila njia kumsahilishia hali yake, kama kumpa muda wa kulipa deni lake au kumsamehe. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِن كَانَ ذُو عُسْرَةٍ فَنَظِرَةٌ إِلَىٰ مَيْسَرَةٍ ۚ وَأَن تَصَدَّقُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿٢٨٠﴾

Na ikiwa (mdaiwa) ni mwenye hali ngumu, basi (mdai) angoje mpaka afarijike. Na mkifanya deni kuwa ni swadaqah basi ni kheri kwenu mkiwa mnajua.  [Al-Baqarah (2: 280)].

 

Na Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴿٢

Na shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na uadui. Na Mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mkali wa kuakibu. [Al-Maaidah: 2]

 

 

2. Tisho la kuwaadhibu watu waliodhaifu, maskini bila ya haki.

 

 

3. Hima ya Maswahaba kuamrisha mema na kukataza maovu, na hiyo ni amri kwa Waumini wote.

 

Rejea: Aal-‘Imraan (3: 104, 110), At-Tawbah (9: 71, 112), Al-Hajj (22: 41).

Pia Hadiyth: Imepokewa kwa Jariyr bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه) kuwa alimbai Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kusimamisha Swalaah, kutoa Zakaah na kumnasihi kila Muislamu.. [Musim]

 

 

4. Waislamu wanapaswa kuoneana huruma pindi wanapoona ndugu zao wanateswa, na wafanye hima kuwaokoa katika mateso.

 

Rejea Al-Fat-h (48: 29).

 

 

5. Tahadharisho la madhalimu kutokana na dhulma.

 

Rejea Hadiyth namba (19), (93).  

 

 

 

Share

106-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Mwanamke Aliyeadhibiwa Kwa Ajili Ya Kumtesa Paka

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 106

 

Mwanamke Aliyeadhibiwa Kwa Ajili Ya Kumtesa Paka

 

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((عُذِّبَتْ امْرَأَةٌ فِي هِرَّةٍ حَبَسَتْهَا حَتَّى مَاتَتْ جُوعًا فَدَخَلَتْ فِيهَا النَّارَ، لاَ هِيَ أَطْعَمْتِهَا  وَسَقَيْتِهَا إِذْ هِيَ حَبَسْتِيهَا وَلاَهِيَ تَرَكَتْها تَأكُلُ مِنْ  خَشَاشِ الأرْضِ)) متفق

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwanamke fulani aliadhibiwa kwa sababu ya paka aliyemfungia mpaka akafa kwa njaa, akaingia motoni [kwa sababu] alipomfungia hakumpa chakula wala hakumnywesha maji wala hakumwacha aende akale vidudu ardhini)).  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Tisho kwa wanaotesa wanyama wanaowafuga kwa kuwafungia na kutokuwapa chakula au maji kwamba adhabu yao ni kuingizwa motoni.

 

 

2. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni pana mno hata kwa viumbe Vyake vyote, mpaka wanyama wadogo. Kila kiumbe kapatiwa rizki Yake, kama Anavyosema:

 

 وَمَا مِن دَابَّةٍ فِي الْأَرْضِ إِلَّا عَلَى اللَّـهِ رِزْقُهَا وَيَعْلَمُ مُسْتَقَرَّهَا وَمُسْتَوْدَعَهَا ۚ كُلٌّ فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ﴿٦﴾

 

Na hakuna kiumbe chochote kitembeacho katika ardhi isipokuwa riziki yake iko kwa Allaah; na (Allaah) Anajua mahali pake pa kustakiri na pa kuhifadhiwa kwake. Yote yamo katika Kitabu kinachobainisha. [Huwd (12: 6)]

 

 

3. Kwa hiyo haipasi bin Aadam kumzuilia mnyama chakula chake.

 

 

4. Funzo kwamba wanyama wanapaswa kupewa haki zao kama viumbe vinginevyo.

 

 

5. Bainisho la ruhusa ya kufuga baadhi ya wanyama nyumbani kama paka. 

 

 

6. Muislamu ni lazima awe kielelezo chema katika kuwatendea viumbe wote wema na kuwapatia haki zao kikamilifu.

 

 

 

Share

107-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayeirejelea Hiba Yake Ni Kama Mbwa Anayerudia Matapishi Yake

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 107  

 

Anayeirejelea Hiba Yake Ni Kama Mbwa Anayerudia Matapishi Yake

 

 

 

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما)  أَنَّ رَسُولَ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قال: ((الَّذِي يَعُودُ فِي هِبَتِهِ كَالْكَلْبِ يَرْجِعُ فِي قَيْئِهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Anayeirudia hiba yake ni kama mbwa anayerudia matapishi yake)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kukirudia (kukichukua tena) kitu alichokitoa mtu kama zawadi n.k.

 

 

2. Kupeana zawadi, hiba n.k. kunajenga mapenzi baina ya ndugu, hivyo anapoirudia au anapoidai hiba alioitoa, italeta madhara ya kubomoa mapenzi yaliyoko baina ya ndugu hao.

 

Hadiyth: ((Peaneni zawadi mtapendana)). [Imaam Maalik katika al-Muwattwaa’ na Atw-Twabaraaniy katika Al-Awsatw]

 

 

3. Uislamu unazuia kila aina za maudhi baina ya watu.

 

 

4. Mfano wa vilotajwa; mbwa na matapishi, vyote ni vitu vichafu. Hii ni dalili jinsi gani uovu wa kufanya jambo hilo, kwamba hiba imefananishwa na matapishi, na mbwa amefananishwa na mtu anayerudia hiba yake.

 

 

5. Kupeana zawadi ni miongoni mwa ‘amali njema atakazokuta malipo yake mtu Siku ya Qiyaamah, kwa hiyo asitamani kukirudia anachokitoa. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى): 

 

 وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ

Na chochote kile cha kheri mnachokadimisha kwa ajili ya nafsi zenu, mtakikuta kwa Allaah. Ni bora, na ujira mkubwa zaidi. [Al-Muzzammil: 20]

 

Na rejea pia:  Aal-‘Imraan (3: 92), Sabaa (34: 39)

 

Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى): 

 

وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿١١٠﴾

na lolote mnalolitanguliza kwa ajili ya nafsi zenu katika kheri mtalikuta kwa Allaah, hakika Allaah kwa yale myafanyao ni Mwenye kuona. [Al-Baqarah (2: 110)]

 

 

 

 

 

 

Share

108-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Madhambi Saba Yanayoangamiza

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 108

Madhambi Saba Yanayoangamiza

 

Alhidaaya.com

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه عن النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَمَا هُنَّ؟  قَالَ: ((الشِّرْكُ بِاللَّهِ وَالسِّحْرُ وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ وَأَكْلُ الرِّبَا وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ الْغَافلاَتِ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Ni kumshirikisha Allaah, sihri [uchawi], kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa kupambana na adui na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Imaam An-Nawawiy amesema: “Hadiyth hii ni dalili kwamba maasi na dhambi kubwa kabisa ni kumshirikisha Allaah.

 

 

2. Shirki ni dhambi isiyosamehewa ikiwa hatotubia mtu kabla ya kufariki kwake kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ 

 Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae [An-Nisaa (4: 48, 116)]

 

 

3. Na anayemshirikisha Allaah hatoingia Peponi kama Anavyoonya Allaah (سبحانه وتعالى):

  إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾

  Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru. [Al-Maaidah (5: 72)]

 

Bali kutomshirikisha ni ufunguo wa Jannah kutokana na Hadiyth: ((Atakayefariki akiwa hakumshirikisha kitu Allaah Ta’aalaa, Ataingia Peponi)). [Muslim]

 

Rejea pia Hadiyth namba (11), (48), (95).

 

 

4. Kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) ni dhulma kubwa kabisa, kwani Yeye ni Muumba wa kila kitu.

 

Rejea:  Luqmaan (31: 13), Al-An’aam (6: 82).

 

 

5. Aayah na Hadiyth nyingi zimetaja ubaya wa kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Rejea Hadiyth namba (119), (131), (136).

 

 

6. Haramisho la kuua mtu bila ya haki.

 

Rejea Al-An’aam (6: 151), An-Nisaa (4: 92-93), Al-Furqaan (25: 68), Al-Israa (17:33).

 

 

7. Haramisho la kula ribaa. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 الَّذِينَ يَأْكُلُونَ الرِّبَا لَا يَقُومُونَ إِلَّا كَمَا يَقُومُ الَّذِي يَتَخَبَّطُهُ الشَّيْطَانُ مِنَ الْمَسِّ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ قَالُوا إِنَّمَا الْبَيْعُ مِثْلُ الرِّبَا ۗ وَأَحَلَّ اللَّـهُ الْبَيْعَ وَحَرَّمَ الرِّبَا ۚ فَمَن جَاءَهُ مَوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّهِ فَانتَهَىٰ فَلَهُ مَا سَلَفَ وَأَمْرُهُ إِلَى اللَّـهِ ۖ وَمَنْ عَادَ فَأُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ ۖ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٢٧٥﴾

Wale wanaokula ribaa hawatosimama (Siku ya Qiyaamah) ila kama anavyosimama yule aliyezugwa na shaytwaan kwa kuguswa na kupatwa. Hivyo kwa sababu wao wamesema: “Hakika biashara ni kama ribaa.” Na Allaah Amehalalisha biashara na Ameharamisha ribaa. Basi atakayefikiwa na mawaidha kutoka kwa Rabb wake akakoma; basi ni yake yale yaliyopita, na hukumu yake iko kwa Allaah. Na atakayerudia basi hao ni watu wa motoni, wao humo ni wenye kudumu.

يَمْحَقُ اللَّـهُ الرِّبَا وَيُرْبِي الصَّدَقَاتِ ۗ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ ﴿٢٧٦﴾

Allaah Huifuta baraka (mali ya) ribaa na Huzibariki swadaqah. Na Allaah Hapendi kila kafiri apapiae madhambi. [Al-Baqarah: (275-276)]

 

 Na Aayah zinaendelea hadi namba (279).

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 130) na Hadiyth nyingi zimeharamisha ribaa.

 

Rejea pia Hadiyth namba (109).

   

 

 

8. Haramisho ya kula mali ya yatima. Rejea: Al-An’aam (6: 152), Al-Israa (17: 34), An-Nisaa (4: 2)]. Na pia Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

  إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ۖ وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا ﴿١٠﴾

Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao moto, na watauingia moto uliowashwa vikali mno.  [An-Nisaa (4: 10)]

 

 

9. Aayah nyingi na Hadiyth zimesisitiza kuhusu kuwatendea wema mayatima na fadhila za kulea.

 

Rejea: Al-Baqarah (2: 83,  177,  215, 220),  An-Nisaa (4: 6,  36), Al-Anfaal (8: 41), Al-Hashr (59: 7), Al-Fajr (89: 17), Adhw-Dhwuhaa (93: 9).

 

 

10. Haramisho la kukimbia vita. Rejea Al-Anfaal (8: 15-16).

 

 

11. Haramisho la kuwatuhumu wanawake wema na adhabu yake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى): 

 إِنَّ الَّذِينَ يَرْمُونَ الْمُحْصَنَاتِ الْغَافِلَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ لُعِنُوا فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَلَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿٢٣﴾

Hakika wale wanaowasingizia machafu wanawake watwaharifu, walioghafilika, Waumini; wamelaaniwa duniani na Aakhirah na watapata adhabu kuu.

يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ وَأَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٢٤﴾

Siku zitakaposhuhudia dhidi yao ndimi zao, na mikono yao, na miguu yao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda. [An-Nuwr (24: 23-24)]

 

Rejea pia An-Nuwr (24: 4, 19)  

 

 

12.  Uislamu umemdhihirishia bin Aadam mambo ya kheri na maovu yatakayomuangamiza.

 

 

13. Mambo haya mpaka katika mambo yanayoangamiza ni kuwa yanavunja mahusiano baina ya mja na Muumba Wake na baina ya waja wao kwa wao.

 

 

14. Uislamu umekuja kujenga uhusiano mwema baina ya wana Aadam ili watu wakae kwa kuheshimiana baina yao. Mambo haya (yaliyotajwa) yanapofanyika, yanaharibu uhusiano mwema na kuvunja jamii.

 

 

 

Share

109-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Amelaaniwa Mla Ribaa, Mwakilishi Shahidi, Na Mwandishi Wake

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 109  

 

Amelaaniwa Mla Ribaa, Mwakilishi Shahidi, Na Mwandishi Wake

 

 

 

 

عَنْ إبنِ مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) قَالَ: لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ آكِلَ الرِّبَا وَمُؤْكِلَهُ مسلم. زاد الترمذي وغيره:  وَشَاهِدَيْه وَكَاتِبَهُ  

Imepokelewa kutoka kwa bin Mas’uwd (رضي الله عنه) amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amemlaani mla ribaa na mwakilishi wake”. [Muslim, At-Tirmidhiy] Na At-Tirmidhiy na wengineo wameongeza: “… na mashahidi wake na mwandishi wake.”

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kula ribaa na tisho lake kuwa ni kupata laana ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

2. Haramisho la ribaa limekemewa kwa hali ya juu kabisa hadi kwamba imetangazwa vita pamoja na Allaah na Rasuli Wake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِن لَّمْ تَفْعَلُوا فَأْذَنُوا بِحَرْبٍ مِّنَ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ۖ وَإِن تُبْتُمْ فَلَكُمْ رُءُوسُ أَمْوَالِكُمْ لَا تَظْلِمُونَ وَلَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٩﴾

Na msipofanya basi tangazeni vita kutoka kwa Allaah na Rasuli Wake. Na mkitubu basi mtapata rasilimali zenu msidhulumu na wala msidhulumiwe. [Al-Baqarah (2: 279)]

 

Na hadi imekuwa Aayah hizo zinafuatia Aayah ya mwisho kuteremshwa kama walivyonukuu Ma’ulamaa wa Tafsiyr: 

 

 وَاتَّقُوا يَوْمًا تُرْجَعُونَ فِيهِ إِلَى اللَّـهِ ۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفْسٍ مَّا كَسَبَتْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ ﴿٢٨١﴾

Na iogopeni Siku mtakayorejeshwa ndani yake kwa Allaah, kisha kila nafsi italipwa kamilifu iliyoyachuma nao hawatodhulumiwa. [Al-Baqarah (2: 281)]

 

 

 

3. Kula ribaa ni miongoni mwa mambo saba yanayoangamiza.

 

Rejea Hadiyth namba (108).

 

 

4. Dhambi za ribaa zinamfikia sawasawa anayewakilisha, shahidi na mwandishi wake. Hii ni sawa na mwenye kutenda uzushi katika Dini kwamba akishirikiana na jambo la bid’ah, atapata dhambi sawa na aliyeanzisha. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ ۚ وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُّبِينٍ ﴿١٢﴾

 Hakika Sisi Tunahuisha wafu, na Tunaandika yale waliyoyakadimisha na athari zao na kila kitu Tumekirekodi barabara katika daftari bayana. [Yaasiyn (36: 12)]

 

 

Rejea pia An-Nahl (16: 25).  

 

Rejea pia Hadiyth namba (16).

 

 

5. Muumin ajiepushe na shubuhaat (mambo yenye shaka, utata, tuhuma) ili aepukane na maasi kama haya, kwani kuna hatari ya kufuata matamanio na baadhi ya watu wanaotoa Fatwa zisizokubalika ki-Shari’ah.

 

Rejea Aal-Imraan (3: 7).

 

Rejea pia Hadiyth namba (64). 

 

 

6. Uislamu unazuia hatua zote za kufikisha maovu kwa kumzuia kila anayeshiriki katika ovu hilo.

 

 

Share

110-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayejionyesha Kwa Watu (Riyaa) Allaah Atamfedhehesha Siku Ya Qiyaamah

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 110

 

Anayejionyesha Kwa Watu (Riyaa) Allaah Atamfedhehesha Siku Ya Qiyaamah

 

 

 

عَنْ جُنْدَبِ بْنِ عَبْدُ الله بْنِ سُفْيانَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ سَمَّعَ سَمَّعَ اللَّهُ بِهِ وَمَنْ رَاءَى رَاءَى اللَّهُ بِهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Jundab bin ‘Abdillaah bin Sufyaan (رضي الله عنه) amesema: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: 

Mwenye kuzungumza (au kusoma) ili watu wamsifu, Allaah Atamfedhehesha Siku ya Qiyaamah, na mwenye kuwafanyia watu riyaa (kwa amali njema ili aonekane ni mtukufu), Allaah Atazidhihirisha siri zake (Siku ya Qiyaamah).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Riyaa ni shirki ya kujificha.

 

 

2. Tahadharisho la riyaa na kujitukuza kwa jambo Alilolikataza Allaah (سبحانه وتعالى) [An-Najm: 32].

 

 

3. Makatazo ya kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) katika ‘amali. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

فَوَيْلٌ لِّلْمُصَلِّينَ ﴿٤﴾

Basi Ole kwa wanaoswali ...

الَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ ﴿٥﴾

Ambao wanapuuza Swalaah zao.

الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ ﴿٦﴾

Ambao wanajionyesha (riyaa). [Al-Maa’uwn: 4-6]

 

Reja pia: Al-Kahf (18: 110), Al-Baqarah (2: 264), An-Nisaa (4: 38, 142).

 

 

4. Riyaa inabatilisha ‘amali za Muislamu, huenda mtu akafanya juhudi na kupoteza muda, zikawa hazina thamani. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zinazotawanyika. [Al-Furqaan 25: 23)]

 

Rejea pia Al-Kahf (18: 103-104).

 

 

5. ‘Amali za kwanza kuhukumiwa Siku ya Qiyaamah ni zile ambazo zitamdhihirisha mtu ikhlaasw yake.

Hadiyth: “Watu watatu watakuwa wa mwanzo kuhukumiwa Siku ya Qiyaamah; Aliyekufa shahidi, aliyejifunza elimu na Qur-aan akaifunza, aliyetoa mali yake. Wote wataingizwa motoni kwa kuwa wametenda kwa ajili ya kuonyesha watu.” [Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy]

 

 

6. Hapana budi kuwa na ikhlaasw katika kila ‘amali anayoitenda Muislamu kwa ajili ya kuzitafuta radhi za Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee.

 

7. Muhimu kusoma Du’aa ya Sunnah ili kujikinga na riyaa: 

 

اللّهُـمَّ إِنّـي أَعـوذُبِكَ أَنْ أُشْـرِكَ بِكَ وَأَنا أَعْـلَمْ، وَأَسْتَـغْفِرُكَ لِما لا أَعْـلَم

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika an ushrika Bika waanaa a’-alamu wa astaghfiruka limaa laa a’-lam

Ee Allaah hakika mimi Najikinga Kwako kutokana na kukushirikisha hali ya kuwa najua na ninakuomba maghfira na nisiyoyajua

 

Ni Hadiyth ya Abuu Muwsaa Al-Ash’ariyy (رضي الله عنه), Kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم)

 

 خَطَبَنَا رَسُولُ اللَّهِ ‏ ‏صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ‏ ‏ذَاتَ يَوْمٍ فَقَالَ: ((أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا هَذَا الشِّرْكَ فَإِنَّهُ أَخْفَى مِنْ دَبِيبِ النَّمْلِ)) فَقَالَ لَهُ مَنْ شَاءَ اللَّهُ أَنْ يَقُولَ: "وَكَيْفَ ‏ ‏نَتَّقِيهِ وَهُوَ أَخْفَى مِنْ دَبِيبِ النَّمْلِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟" قَالَقُولُوا: ((‏اللَّهُمَّ إِنَّا نَعُوذُ بِكَ مِنْ أَنْ نُشْرِكَ بِكَ شَيْئًا نَعْلَمُهُ وَنَسْتَغْفِرُكَ لِمَا لَا نَعْلَمُ))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alituhutubia akasema: ((Enyi watu! Iogopeni shirki hii kwani imefichika zaidi kuliko kutambaa kwa sisimizi)) Akasema mmoja wa aliyejaaliwa na Allaah aseme: “Je vipi tujiokoe nayo na hali imefichika zaidi kuliko kutambaa kwa sisimizi ee Rasuli wa Allaah?”. Akasema: ((Semeni: Ee Allaah! Hakika sisi tunajikinga Kwako kutokana na kukushirikisha hali ya kuwa tunajua na tuinakuomba maghfira kwa tusiyoyajua)) - Ahmad (4/403), na wengineo  na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (3/233) [3731] na Swahiyh At-Targhiyb wat-Tarhiyb ya Al-Albaaniy (رحمه الله) (1/122) [36].

 

 

 

8. Muumin anayejitahidi kufanya ‘amali kwa ikhlaasw asimwache shaytwaan kumtia wasiwasi kuwa anafanya kwa riyaa akaogopa kutenda mema yake.

Hadiyth: Abuu Dharr (رضي الله عنه) alimuuliza Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم): ‘‘Ee Rasuli wa Allaah! Je, unaonaje kama mtu anafanya matendo mazuri, kisha watu wakamsifia kwa matendo yake? Akajibu: ((Hiyo ni sehemu ya baraka na radhi kwa Muumin [zitakazohifadhiwa kwake siku ya Qiyaamah])). [Muslim]

 

 

Share

111-Lu-ulu-un-Manthuwrun : Wanaume Na Wanawake Wasio Maharimu Wasitazamane Uchi Wala Wasilale Pamoja

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 111

 

Wanaume Na Wanawake Wasio Maharimu Wasitazamane Uchi Wala Wasilale Pamoja

 

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَنْظُرُ الرَّجُلُ إِلَى عَوْرَةِ الرَّجُلِ، وَلاَ الْمَرْأَةُ إِلَى عَوْرَةِ الْمَرْأَةِ، ولاَ يُفْضِي الرَّجُلُ إِلَى الرَّجُلِ فِي ثَوْبٍ وَاحِدٍ، وَلاَ تُفْضِي الْمَرْأَةُ إِلَى الْمَرْأَةِ فِي الثَّوْبِ الْوَاحِدِ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwanamme asitazame uchi wa mwanamme, wala mwanamke asitazame uchi wa mwanamke, wala mwanamme asilale na mwanamme mwenzie katika nguo moja, wala mwanamke asilale na mwanamke mwenzie katika nguo moja)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kutazamana uchi japokuwa ni kwa jinsi moja, seuze ikiwa ni baina ya mwanamme na mwanamke. Kwani hayo huenda yakapelekea katika maasi ya uliwati na usagaji.

 

Rejea An-Nuwr (24: 30, 31)]. 

 

 

2. Uislamu umehimiza kujisitiri na kusitiriana, na umefunga milango yote itakayopelekea kwenye zinaa na Allaah (سبحانه وتعالى) Akatahadharisha hilo Anaposema:

 

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

  Na wala msiikaribie zinaa. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya kabisa. [Al-Israa (17: 32)]

 

 

Na Allaah (سبحانه وتعالى) Amewaahidi Jannah ya Al-Firdaws wanaojisitiri sehemu zao za siri. Ametaja sifa hizo kadhaa zikiwemo: 

 

 وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ ﴿٥﴾

Na ambao wanazihifadhi tupu zao.

 

إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ ﴿٦﴾

Isipokuwa kwa wake zao, au kwa iliyowamiliki mikono yao ya kuume basi hao hawalaumiwi. [Al-Muuminuwn: 5-6]

 

 

 

3. Haramisho la kutazama uchi wa mwanamume kutoka kitovuni hadi magotini.

 

 

4. Haramisho la kutazama uchi wa mwanamke. Na ambaye si mahram wake, ni mwili wote isipokuwa uso na viganja.

 

Rejea An-Nuwr (24: 31).

 

 

5. Zinaa huweza kuwa ni ya uhakika kujamiiana kwa haramu, au kutazama uchi wa mtu na machafu, au kwa kusikiliza yanayohusiana nayo kama ilivyothibiti katika  Hadiyth  kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)   kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Ameandika kila sehemu ya zinaa ambayo humuingiza mtu katika shauku. Hakutokuwa na kuikwepa. Zinaa ya macho ni kutazama, ya masikio ni kusikiliza, ulimi ni kunena maneno, mkono ni kuunyoosha, mguu ni hatua zake, na moyo hupata matamanio, na tupu husadikisha [hutenda] au hukadhibisha [huacha])). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

6. Makatazo kwa  wanawake kuvaa nguo zinazodhihirisha sehemu nyingi za mwili katika shughuli za furaha kama harusini n.k. kwa kisingizio kuwa wako na wanawake wenziwao. Wanavuka mipaka na hali mwanamke wa Kiislamu anatakiwa avae mavazi ya kumfunika vizuri abakie katika sitara na heshima na si kama mavazi ya wanawake makafiri. Itambulike kuwa sitara ya mwanamke katika mavazi mbele ya wanawake wenzao ni sawasawa na inavyopasa wanapokuwa mbele ya mahaarim zao kwamba wasionyeshe isipokuwa uso, nywele, shingo, mikono na miguu (kuanzia kifundoni na nyayo na si juu yake).

 

Rejea Hadiyth namba (114).

 

 

7. Jambo lolote linaloompelekea mtu katika maasiya, limekatazwa katika Uislamu.

 

 

Share

112-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Ikhtilaatw - Wanawake Kuchanganyika Na Wasio Mahaarim

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 112

 

Ikhtilaatw – Wanawake Kuchanganyika Na Wasio Mahaarim

 

 

 

عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِيَّاكُمْ وَالدُّخُولَ عَلَى النِّسَاءِ)) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ الأَنْصَارِ: يَا رَسُولَ اللَّهِ أَفَرَأَيْتَ الْحَمْوَ؟ قَالَ:  ((الْحَمْوُ الْمَوْتُ))  متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Tahadharini na kuingia kwa wanawake!)) Mtu mmoja katika Answaariy akauliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Nieleze akiwa ni shemeji?” Akamwambia:  ((Shemeji ni mauti!)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Mahaarim au Mahram ni wanaume ambao hawaruhusiki ki-shariy’ah kuwaoa wanawake kama vile baba, ‘ammi, mjomba, kaka, watoto wa dada na watoto wa kaka.

 

 

2. Al-Hamw ni jamaa wa karibu wa mume kama kaka yake, mtoto wa kaka yake, mtoto wa ‘ami yake n.k.

 

 

3. Makatazo ya ikhtilaatw (kuchanganyikbaina ya wanaume na wanawake wasio mahaarim zao kama Alivyokataza Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu wake wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

 وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ۚ ذَٰلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ ۚ

Na mnapowauliza wake zake haja, waulizeni nyuma ya pazia. Hivyo ni utwaharifu zaidi kwa nyoyo zenu na nyoyo zao [Al-Ahzaab (33: 53)]

 

 

4. Makatazo ya jamaa za mume kuwa faragha na mke, kwani hilo ni jepesi kuchanganyika nao, kwa vile wako karibu na kutokea fitna ni wepesi kabisa.

Hadiyth: Kutoka kwa 'Umar (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hachanganyiki mwanamume na mwanamke ila shaytwaan huwa ni watatu wao)). [At-Tirmidhiy]

 

 

5. Uislamu umetahadharisha kila aina ya shari na kukaribia zinaa na umehimiza amani baina ya jamii. 

 

Rejea: Al-Israa (17: 32).

 

 

6. Kufananishwa Al-Hamw na mauti ni dalili jinsi uwezekano mwepesi wa kutokea fitna, kwani aghlabu shemeji huwa na huruma.

 

 

7. Tatizo kubwa lipo katika jamii kuchanganyika na mashemeji, na ndio maana fitna nyingi hutokea katika jamii.

 

 

8. Ni kawaida kwa watu kutochukua tahadhari kwa maingiliano kama hayo na madhara yake ni makubwa katika jamii.

Share

113-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Wamelaaniwa Wanaume Wanaojifananisha Na Wanawake Na Wanawake Wanaojifananisha Na Wanaume

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 113

 

Wamelaaniwa Wanaume Wanaojifananisha Na Wanawake

Na Wanawake Wanaojifananisha Na Wanaume

 

 

 

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) قَالَ: لَعَنَ رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الْمُخَنَّثِينَ مِنْ الرِّجَالِ وَالْمُتَرَجّلاتِ مِنْ النِّسَاءِ. وفي رواية: لَعَنَ رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الْمُتَشَبِّهِينَ مِنْ الرِّجَالِ بِالنِّسَاءِ وَالْمُتَشَبِّهَاتِ مِنْ النِّسَاءِ بِالرِّجَالِ. البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amewalaani wanaume wanaojifananisha na wanawake na wanawake wanaojifananisha na wanaume”. Na katika riwaya nyingine imesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amewalaani wanaume wanaojishabihisha na wanawake, na wanawake wanaojishabihisha na wanaume.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la wanaume na wanawake kujifananisha sawa kwa mavazi, sauti, mwendo, mapambo n.k. kwani hivyo ni upotofu wa shaytwaan aliyeahidi kuwapotoa. Na Allaah (سبحانه وتعالى) Amewatahadharisha kwa makazi ya moto kama Anavyosema:

 

 لَّعَنَهُ اللَّـهُ ۘ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿١١٨﴾

Allaah Amemlaani. Na (shaytwaan) akasema: “Kwa hakika nitashika katika waja Wako sehemu maalumu.”

وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا ﴿١١٩﴾

 “Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio ya kulaghai, na nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawatukuze), na nitawaamrisha watabadili maumbile ya Allaah.” Na atakayemfanya shaytwaan kuwa rafiki mwandani badala ya Allaah basi kwa yakini amekhasirika khasara bayana.

يَعِدُهُمْ وَيُمَنِّيهِمْ ۖ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلَّا غُرُورًا ﴿١٢٠﴾

Anawaahidi na anawashawishi matamanio ya uongo. Na shaytwaan hawaahidi isipokuwa ulaghai.

 

أُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَلَا يَجِدُونَ عَنْهَا مَحِيصًا ﴿١٢١﴾

Hao makaazi yao ni Jahannam, na wala hawatopata makimbilio ya kutoka humo. [An-Nisaa (4: 118-121)]

 

 

2. Inapotajwa laana katika Aayah au Hadiyth, basi ni uthibitisho kuwa jambo lililotajwa ni miongoni mwa madhambi makubwa, kwani laana ni kuwekwa mbali na Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

3. Wanaojifananisha na wengine, ni ukosefu wa adabu mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama kwamba kumkosoa kuwa umbo Alowaumba nalo la fitwrah (asili ya maumbile), limekosewa au halifai kwao, na hali Amemuumba mwana Aadam kwa kumtofautisha kiwiliwili, sura, rangi n.k. kwa hikmah Yake.

 

Rejea: Al-Muuminuwn (23: 12-14), At-Tiyn (95: 4), Ar-Ruwm (30: 22).

 

 

4. Allaah (سبحانه وتعالى) Ameweka Shariy’ah za kumtosheleza bin Aadam zenye maslahi naye zitakazozuia ufisadi katika jamii. Rejea Al-Maaidah (5: 48).

 

 

Na pia mwendo mzuri kabisa wa kuigiza wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللَّـهَ وَالْيَوْمَ الْآخِرَ وَذَكَرَ اللَّـهَ كَثِيرًا ﴿٢١﴾

Kwa yakini mna kigezo kizuri kwa Rasuli wa Allaah kwa mwenye kumtaraji Allaah na Siku ya Mwisho [Al-Ahzaab (33: 21)]

 

 

5. Ufisadi umeenea katika jamii; wanaume kuiga mavazi na mapambo ya kike, kama kuweka nywele ndefu, kuvaa herini, kuvaa nguo za kubana n.k. Na wanawake kuvaa masuruwali ya kubana, kukata nywele fupi n.k. yote ambayo yanamtoa mtu kutoka katika fitwrah (umbile la asili aloumbwa nalo).

 

 

 

 

Share

114-Lu-ulu-un-Manthuwrun :Wanawake Wanaovaa Nguo Lakini Wako Uchi Wenye Vichwa Vya Manundu Hawatoingia Jannah Wala Hawatasikia Harufu Yake

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 114  

 

Wanawake Wanaovaa Nguo Lakini Wako Uchi Wenye Vichwa Vya Manundu

Hawatoingia Jannah Wala Hawatasikia Harufu Yake

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((صِنْفَانِ مِنْ أَهْلِ النَّارِ لَمْ أَرَهُمَا: قَوْمٌ مَعَهُمْ سِيَاطٌ كَأَذْنَابِ الْبَقَرِ يَضْرِبُونَ بِهَا النَّاسَ، وَنِسَاءٌ كَاسِيَاتٌ عَارِيَاتٌ مُمِيلاَتٌ مَائِلاَتٌ رُءُوسُهُنَّ كَأَسْنِمَةِ الْبُخْتِ الْمَائِلَةِ، لاَ يَدْخُلْنَ الْجَنَّةَ وَلاَ يَجِدْنَ رِيحَهَا، وَإِنَّ رِيحَهَا لَيُوجَدُ مِنْ مَسِيرَةِ كَذَا وَكَذَا)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Aina mbili za watu wa motoni sijawaonapo [hawapo katika zama zangu]: Watu walio na mijeledi mfano wa mikia ya ng’ombe wanawapiga watu kwa mijeledi hiyo [kwa dhulma], na wanawake waliovaa nguo na ilhali wako uchi, wakitembea kwa maringo huku wakiyanyonga mabega yao na wakiwafunza wengineo kutenda kama hivyo, vichwa vyao ni kama nundu za ngamia-bukhti wanaodemadema. Hawatoingia Jannah wala hawataisikia harufu yake, na kwa hakika harufu yake husikika umbali kadha wa kadhaa)). [Muslim]

 

Ngamia bukhti – ni aina ya ngamia wenye shingo ndefu.

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kuwapiga watu kwa dhulma na tisho kwamba hawatoingia Jannah bali wala hawatasikia  harufu yake.

 

 

 

2. Haramisho kwa wanawake kutokuvaa vazi la Hijaab Aliloamrisha Allaah (سبحانه وتعالى) lenye sitara na heshima. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ ۖ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ ۚ

Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao na wahifadhi tupu zao, na wala wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa yale yanayodhihirika. Na waangushe khimaar (shungi) zao mpaka vifuani mwao, na wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa kwa waume zao, au baba zao, au baba za waume wao, au wana wao wa kiume, au wana wa kiume wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kiume wa kaka zao, au wana wa kiume wa dada zao, au wanawake wao (wa Kiislamu), au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, au wafuasi wanaume wasio na matamanio ya jimai miongoni mwa wanaume au watoto ambao hawatambui kitu kuhusu sehemu za siri za wanawake. Na wala wasipige miguu yao yakajulikana yale wanayoyaficha katika mapambo yao. [An-Nuwr (24: 31)]

 

 

Na rejea Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى) katika Al-Ahzaab (33: 59).

 

3. Hadiyth imetoa pia onyo kali la mwenye kuasi kutokuingia Jannah na kutoisikia harufu yake. 

 

 

4. Wanawake wengi hawatambui vazi khasa la Hijaab. Hujifunika kichwa na huku uso umejaa mapambo, na nguo za mikono mifupi, za kubana zinazodhirisha maumbile ya mwili wote na nyinginezo hata kuonekana mwili wake ndani, na zilizojazwa mapambo ya rangi na ming’aro. Mwanamke anapaswa ajifunze sharti la vazi la Hijaab kwamba;

 

(i) Avae Jilbaab lisitiri kiwiliwili chote cha mwanamke, (pamoja na khilafu iliyopo kati ya wanachuoni kuhusu suala la uwajibu wa kuufunika uso na kutoufunika);

 

(ii) Jilbaab la mwanamke lisiwe na mapambo;

 

(iii) Kitambaa cha Jilbaab kinatakiwa kiwe kizito (kisioneshe vazi la ndani);

 

(iv) Jilbaab linatakiwa liwe pana (lisibane);

 

(v) Jilbaab halitakiwi kutiwa manukato;

 

(vi) Jilbaab halitakiwi lifanane na mavazi ya kiume;

 

(vii) Jilbaab halitakiwi lifanane na mavazi ya makafiri;

 

(viii) Jilbaab halitakiwi liwe ni katika mavazi ya fakhari.

 

 

5. Mwili wa mwanamke ni thamani ambayo inapasa kuhifadhiwa na kufichwa ili isipotee thamani yake. Mfano wake ni kama lulu katika kombe ambayo imehifadhika humo.

 

 

6. Mwanamke ambaye havai vazi la Hijaab, anayejipamba na kudhihirisha mapambo yake mbele ya wasiokuwa mahram wake, anakusanya madhambi mengi kwa kuwatamanisha wanaume wenye nyoyo za matamanio. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى) kuhusu Wake wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Aayah hizi zinawahusu wanawake Waumini wengineo wote:

 

 

يَا نِسَاءَ النَّبِيِّ لَسْتُنَّ كَأَحَدٍ مِّنَ النِّسَاءِ ۚ إِنِ اتَّقَيْتُنَّ فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ مَرَضٌ وَقُلْنَ قَوْلًا مَّعْرُوفًا ﴿٣٢﴾

Enyi wake wa Nabiy!  Nyinyi si kama yeyote yule katika wanawake; mkiwa na taqwa, basi msilegeze kauli asije akaingiwa tamaa ambaye moyoni mwake mna maradhi na semeni kauli inayokubalika.

 

 

وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ ۖ وَأَقِمْنَ الصَّلَاةَ وَآتِينَ الزَّكَاةَ وَأَطِعْنَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ ۚ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ﴿٣٣﴾

Na bakieni majumbani mwenu, na wala msionyeshe mapambo na uzuri kwa ajinabi kujishaua kama zama za ujahili. Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah na mtiini Allaah na Rasuli Wake. Hakika Allaah Anataka Akuondosheeni maovu enyi ahli wa nyumba (ya Nabiy) na Akutakaseni mtakaso barabara.  [Al-Ahzaab (33: 32-33)]

 

 

7. Wenye majukumu juu ya wanawake; mume, baba, kaka n.k. wanapaswa kuwahimiza na kuhakikisha kuwa wanawake wao wanavaa vazi la Hijaab, kwani wasipofanya hivyo watakuja kuulizwa kuhusu jukumu na amana yao waliyopewa kuichunga.

 

Rejea Hadiyth namba  (27).

 

 

8. Wanawake wasiovaa Hijaab wanadhania kwamba wako katika maendeleo na kuwadharau wanaovaa Hijaab, na ilhali ni kinyume chake, kwamba wanaovaa vazi la Hijaab wana hadhi zaidi kuliko wasiovaa mbele ya watu na zaidi mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى). Je, yupi aliyekuwa na heshima zaidi? Anayevaa Hijaab au wale  wanaotumiliwa kwa picha za tupu zao katika biashara zao? 

 

 

9. Makatazo kwa wanawake wanaovaa nguo za wazi mno maharusini kwa kisingizio kuwa wako mbele ya wanawake wenziwao. Hivyo, wanafikia kuvaa nguo za kudhihirisha sehemu za mwili na hali mipaka yake ni kuonyesha sehemu ambazo huwa wazi wanapokuwa wakifanya kazi za nyumba majumbani mwao kama uso, nywele, shingo, mikono na miguu. Hivyo ni kwa sababu sehemu hizo pia ndio sehemu zinazovaliwa mapambo ya wanawake kama herini, vidani, bangili, vikufu vya miguu.    

 

Rejea Hadiyth namba (111).

 

 

 

 

Share

115-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Makatazo Ya Kunyoa Baadhi Ya Nywele Na Kuacha Baadhi

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 115

 

Makatazo Ya Kunyoa Baadhi Ya Nywele Na Kuacha Baadhi

 

 

 

 

عَنْ ابْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ رَأَى صَبِيًّا قَدْ حُلِقَ بَعْضُ شَعْرِهِ وَتُرِكَ بَعْضُهُ فَنَهَاهُمْ عَنْ ذَلِكَ وَقَالَ: ((احْلِقُوهُ كُلَّهُ أَوْ اتْرُكُوهُ كُلَّهُ)) أبوا داود بإسناد صحيح على شرط البخاري و مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم) alimuona mvulana zimenyolewa baadhi ya nywele kichwani mwake na nyingine zimeachwa. Akawakataza, na akasema: ((Mnyoweni zote au ziacheni zote)). [Abuu Daawuwd kwa isnaad Swahiyh ‘alaa shartw (kwa mujibu wa masharti ya) Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Katazo la kunyoa baadhi ya nywele na kuacha baadhi, ambao Kiislamu inaitwa Qaza‘, hivyo ni kujibadilisha umbile na pia kuiga makafiri wanaonyoa kila aina za staili ya nywele.

 

 

2. Uislamu umetoa kila aina ya mafunzo hata ya kumweka Muislamu katika mandhari nzuri kabisa ya fitwrah (maumbile ya asili) na heshima. Kujibadilisha maumbile hayo ya asili ni katika hila za shaytwaan aliyeahidi kuwapotoa watu:

 

 وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ 

 “Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio ya kulaghai, na nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawatukuze), na nitawaamrisha watabadili maumbile ya Allaah.”  [An-Nisaa (4: 119)]

    

Rejea Hadiyth namba 113.

 

 

3. Baadhi ya wazazi wanawaachia watoto wao kunyoa nywele staili za makafiri ‘panki’ na kuona kuwa ni maendeleo na fakhari kuiga makafiri na hali ni kumpotosha mtoto. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amekataza kuiga makafiri katika Hadiyth:

 

 عَنْ ابْنِ عُمَرَ قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ تَشَبَّهَ بِقَوْمٍ فَهُوَ مِنْهُمْ))

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayejifananisha na watu basi yeye ni miongoni mwao)) [Abuu Daawuwd na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (3401)]

 

 

4. Ruhusa ya ima kunyoa nywele zote au kuziacha zote, ila tu zisiachwe ndefu hadi kushabihiana na wanawake. Na pia zikiwa ndefu basi zisibakishwe matimtimu, bali zinatakiwa zitizamwe kwa kuchanwa na kupakwa mafuta.

 

 

 

 

Share

116-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Wamelaaniwa Wanaopiga Chale (Tattoo), Wanaochonga Nyusi Na Meno

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 116  

 

Wamelaaniwa Wanaopiga Chale (Tattoo), Wanaochonga Nyusi Na Meno

 

 

 

 

عَنْ عَبْد الله ابْن مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) قَالَ: لَعَنَ اللَّهُ الْوَاشِمَاتِ وَالْمُوتَشِمَاتِ وَالْمُتَنَمِّصَاتِ وَالْمُتَفَلِّجَاتِ لِلْحُسْنِ، الْمُغَيِّرَاتِ خَلْقَ اللَّهِ، فَقَالَتْ لَهُ امْرَأَةٌ فِي ذَلِكَ، فَقَالَ: "وَمَا لِي أَلْعَنُ مَنْ لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَهُوَ فِي كِتَابِ اللَّهِ؟ قَالَ الله تَعَالى: ((وَمَا آتَاكُمْ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانْتَهُوا)) متفق عليه

‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه) alisema: “Allaah Anawalaani wanaopiga chale na wanaotaka kupigwa chale, na wanaochonga nyusi na wanaochonga meno wakaacha mwanya kwa sababu ya uzuri, wanaobadilisha maumbile Aliyoyaumba Allaah.” Mwanamke mmoja akamlaumu juu ya jambo hilo (la kulaani). Akasema (‘Abdullaah): “Kwa nini nisimlaani aliyelaaniwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na ilhali iko ndani ya Kitabu cha Allaah? Allaah Aliyetukuka Anasema: ((Na lolote analokupeni Rasuli (صلى الله عليه وآله وسلم) basi lichukueni, na analokukatazeni, basi acheni. [Al-Hashr (59: 7)])). [Al-Bukhaariy na Muslim] Na katika riwaayah nyingine imetajwa: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amemlaani mwenye kuunga na mwenye kuungwa (nywele)…” [Al-Bukhaariy]

 

Kupiga chale ni kuikwangua ngozi itoke damu, kisha apake wanja au kitu kingine kisha inakuwa rangi ya kijani (tattoo).

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kujibadilisha chochote katika umbo la mtu kwa ajili ya kujipamba ikiwa ni kuzidisha au kupunguza, isipokuwa ikiwa kuna dharura ya matibabu.

 

 

2. Haramisho kwa wanawake kunyoa nyusi na kwamba wanaotoa na wanaotolewa watapata laana ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

3. Haramisho la kuunga nywele na kuvaa mabaruka (wigi), kwani ni kubadilisha maumbile ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 4. Kupiga chale, kuchonga nyusi na meno, yote hayo ni miongoni mwa madhambi makubwa, kwa vile yametajiwa laana ya Allaah (سبحانه وتعالى) ambayo ni kuwekwa mbali na Rahma Yake.

 

 

5. Makatazo hayo ni katika mila za makafiri ambazo haipasi Muislamu kuwaiga, kwani wao wanadhamiria mno Waislamu kuwaiga mila zao na wanapenda mno kuona Muislamu ameacha Dini yake. Allaah (سبحانه وتعالى) Anatahadharisha:

 

 وَلَن تَرْضَىٰ عَنكَ الْيَهُودُ وَلَا النَّصَارَىٰ حَتَّىٰ تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمْ ۗ

Na hawatoridhika nawe Mayahudi wala Manaswaara mpaka ufuate mila zao. [Al-Baqarah (2: 120)]

 

 

6. Kujibadilisha umbo ni hila za shaytwaan anayemtia mtu matamanio ya nafsi. [An-Nisaa (4: 117-121)].

 

Rejea Hadiyth namba (113).

 

 

Share

117-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kusema Analolijua Mtu Au Kukiri Kutokuwa Na Ujuzi Wa Jambo Na Kujikalifisha Nalo

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 117  

 

Kusema Analolijua Mtu Au Kukiri Kutokuwa Na Ujuzi Wa Jambo Na Kujikalifisha Nalo

 

 

 

 

عَنْ مَسْرُوقٍ (رضي الله عنه) قَالَ: دَخَلْنَا عَلَى عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ فَقَالَ: يَا أَيُّهَا النَّاسُ، مَنْ عَلِمَ شَيْئًا فَلْيَقُلْ بِهِ، وَمَنْ لَمْ يَعْلَمْ فَلْيَقُلْ اللَّهُ أَعْلَمُ فَإِنَّ مِنْ الْعِلْمِ أَنْ يَقُولَ لِمَا لاَ يَعْلَمُ: اللَّهُ أَعْلَمُ. قَالَ اللَّهُ تَعَالى لِنَبِيِّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ وَمَا أَنَا مِنْ الْمُتَكَلِّفِينَ)) البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Masruwq(رضي الله عنه)  amesema: “Tulikwenda kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (siku moja) akatuambia: “Enyi watu! Anayejua kitu aseme, na asiyejua aseme: “Allaah Anajua.” Hakika miongoni mwa elimu ni kusema katika usilolijua: “Allaah Anajua.” Allaah Alimwambia Rasuli Wake   (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Sikuombeni ujira wowote juu ya hili, na wala mimi si miongoni mwa wenye kujidai kuzusha chochote kisichohusu. [Swaad (38: 86)])).  [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kujikalifisha katika mas-alah ya elimu ya Dini. 

 

 

2. Kutokusema jambo la Dini bila ya kuwa na elimu sahihi yenye dalili wala kutoa Fatwa isipokuwa kwa mwenye elimu ya kutosha. Rejea: Yuwsuf (12: 108).

 

 

3. Allaah (سبحانه وتعالى) Ameonya kujiamulia mtu hukmu bila ya dalili, kwani hivyo ni kumzulia Yeye uongo. Anasema (سبحانه وتعالى):

 

 وَلَا تَقُولُوا لِمَا تَصِفُ أَلْسِنَتُكُمُ الْكَذِبَ هَـٰذَا حَلَالٌ وَهَـٰذَا حَرَامٌ لِّتَفْتَرُوا عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَفْتَرُونَ عَلَى اللَّـهِ الْكَذِبَ لَا يُفْلِحُونَ﴿١١٦﴾

Na wala msiseme zinayotetea ndimi zenu uongo; hii halaal na hii haraam ili mumtungie Allaah uongo. Hakika wale wanaomtungia Allaah uongo hawafaulu. [An-Nahl (16: 116)]

 

 

4. Elimu ya Mwanachuoni (‘Aalim) haipunguki kwa kutokujua jambo na kulikiri.

 

 

5. Funzo kutoka kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na himizo la kufuata kigezo chake.

 

 

6. Inapokuwa halijui jambo analoulizwa mtu la elimu ni vyema aseme: “Allaah Anajua”: na anapolijua aseme: “Na Allaah Anajua zaidi.”

 

 

7. Kukiri kutokujua jambo la elimu ni dalili ya unyenyekevu wa mtu na kinyume chake ni kujionyesha sifa ya upeo wa elimu asiyokuwa nayo hakika mtu, kwani kila mmoja ana upeo wa kiasi fulani tu cha elimu. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَفَوْقَ كُلِّ ذِي عِلْمٍ عَلِيمٌ ﴿٧٦﴾

Na juu ya kila mwenye elimu yuko mwenye elimu zaidi. [Yuwsuf (12: 76)].

 

Share

118-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutokuomboleza Kwa Kupiga Mashavu, Kupasua Mifuko Na Kuomba Maombi Ya Kijahilia

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 118  

 

Kutokuomboleza Kwa Kupiga Mashavu, Kupasua Mifuko Na Kuomba Maombi Ya Kijahilia

 

 

 

 

عَنْ عَبْد الله ابْن مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لَيْسَ مِنَّا مَنْ ضَرَبَ الْخُدُودَ وَشَقَّ الْجُيُوبَ وَدَعَا بِدَعْوَى الْجَاهِلِيَّةِ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه) amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Si miongoni mwetu anayejipiga mashavu, akapasua mifuko na akaomba maombi ya kijahilia)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kujipiga mashavu, kupasua mifuko au nguo, kuomboleza n.k.

 

 

2. Muislamu anapaswa aridhike na majaaliwa ya Rabb wake Anapomkidhia msiba, na si kuchukiwa, kwani huenda ikampeleka kukufuru. Aamini Qadhwaa na Qadar (Yaliyohukumiwa na Yaliyokadiriwa)  na Allaah (سبحانه وتعالى) Yameshaandikwa katika Lawhum-Mahfuudhw [Ubao Uliohifadhiwa mbingu ya saba]. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي أَنفُسِكُمْ إِلَّا فِي كِتَابٍ مِّن قَبْلِ أَن نَّبْرَأَهَا ۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ﴿٢٢﴾

Hausibu msiba wowote katika ardhi au katika nafsi zenu isipokuwa umo katika Kitabu kabla hatujautokezesha. Hakika hayo kwa Allaah ni mepesi.

 

لِّكَيْلَا تَأْسَوْا عَلَىٰ مَا فَاتَكُمْ وَلَا تَفْرَحُوا بِمَا آتَاكُمْ ۗ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿٢٣﴾

Ili msisononeke juu ya yale yaliyokuondokeeni na wala msifurahie kwa yale Aliyokupeni (Allaah); na Allaah Hapendi kila mwenye kujinata, anayejifakharisha. [Al-Hadiyd (57: 22-23)]

   

      

3. Kuomboleza kwa sauti na kujipiga au kuchana nguo kunamuadhibisha maiti kaburini

 

Hadiyth: ((Maiti anaadhibika kaburini mwake kwa anayoombolezewa)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

4. Anayeomboleza ataadhibiwa Siku ya Qiyaamah

 

Hadiyth: ((Mwombolezi asipotubia kabla ya kufa kwake, Siku ya Qiyaamah atavalishwa kanzu ya lami na deraya ya upele)). [Muslim]

 

 

5. Kuomboleza kwengine ni kunyoa kichwa kwa ajili ya msiba. Hii imekatazwa katika Hadiyth ifuatayo:   

 

Wakati fulani Abuu Muwsaa aliugua na kuhisi maumivu makubwa, kwa maumivu hayo akazimia ilhali kichwa chake kipo chini ya uangalizi wa mwanamke mmoja katika jamaa zake, mwanamke yule baada ya kuona hali ya Abuu Muwsaa akapiga kelele kwa nguvu lakini Abuu Muwsaa hakuweza kusema kitu kwa hali aliyokuwa nayo, baada ya kuzindukana akasema, ‘Mimi najikosha kwa yale aliyojikosha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  kwani Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alijikosha na haya yafuatayo (hakuyataka kabisa yatokee): Asw-Swaliqah; yaani mtu mwenye kunyanyua sauti yake kwa juu wakati wa msiba, na Al-Haaliqah; mwenye kunyoa nywele zake wakati wa msiba na Ash-Shaaqqah; anayerarua na kuchana nguo zake wakati wa kuomboleza.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

6. Muislamu afuate mafunzo ya Sunnah katika msiba. Kulia kunaruhusiwa bila ya kutoa sauti na kuomboleza.

 

 

 

 

 

Share

119-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayemwendea Mtazamaji Ramli Akamsadiki Hatokubaliwa Swalaah Siku Arubaini

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 119

 

Anayemwendea Mtazamaji Ramli Akamsadiki Hatokubaliwa Swalaah Siku Arubaini

 

 

 

عَنْ صَفِيَّةَ بِنْتِ أبِي عُبِيْدٍ عَنْ بَعْضِ أَزْوَاجِ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَ (رضي الله عنهم) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَنْ أَتَى عَرَّافًا فَسَأَلَهُ عَنْ شَيْءٍ لَمْ تُقْبَلْ لَهُ صَلاَةٌ أَرْبَعِينَ لَيْلَةً)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Swafiyyah bint Abiy ‘Ubayd kutoka kwa baadhi ya wakeze Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwenye kumwendea mtazamiaji [mpiga ramli] akamwuliza jambo na akamsadiki, hatokubaliwa Swalaah yake siku arubaini)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kuwaendea watabiri na makahini na kusadiki wayasemayo na kwamba Swalaah haitokubaliwa siku arubaini.

 

 

2. Kuna hatari kubwa ya kumsikiliza mtabiri au kahini na kumwamini, kwani kutamkosesha Muislamu thawabu za ‘amali njema kama Swalaah, kwani hiyo ni aina ya shirki kwa vile anaingilia elimu ya ghayb ya Allaah (سبحانه وتعالى) na hivyo humtoa mtu nje ya Uislamu kwa dalili ya Hadiyth zifuatazo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ : (( مَنْ أَتَى حَائِضًا أَوْ امْرَأَةً فِي دُبُرِهَا أَوْ كَاهِنًا فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ))

((Mwenye kumuingia mwenye hedhi, au mwanamke kwa nyuma, au kumwendea mchawi na kumuamini kwa anayosema, basi amekufuru aliyoteremshiwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)). [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na isnaad yake ni Swahiyh]

 

Na pia:

 

مَنْ أَتَى كَاهِنًا أَوْ سَاحِرًا فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ فَقَدْ كَفَر بِمَا أُنْزِلَ عَلى مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلّم

Atakayemwendea kahini au mchawi akasadiki yale anayoyasema basi amekufuru ambayo Ameteremshiwa nayo Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) [Tafsiyr Ibn Kathiyr; Hadiyth ina isnaad ya upokezi Swahiyh na kuna Hadiyth zinazokubaliana na hii].

 

 

3. Umuhimu wa kujifunza mas-alah ya hatari kama haya ambayo humtoa mtu katika Uislamu. Ni kwa kuwa, masuala haya ni dhambi Asizozisamehe Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Rejea: An-Nisaa (4: 48, 116),  na kwamba anayemshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) ataharamishwa na kuingia katika Jannah, bali pia makazi yake yatakuwa ni ya motoni! Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾

Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.” [Al-Maaidah (5: 72)]

 

Rejea pia Hadiyth namba (108), (136).

 

 

4. Wayasemayo watabiri yanayotokea kweli ni kwa kuwa wamepatiwa habari kutoka kwa majini wanaotega sikio, kisha kuyahamisha kwa wengine. Rejea: Al-Jinn (72: 6-10).

 

 

5. Ieleweke kuwa mbali na kutokubaliwa Swalaah siku arubaini, Muislamu aliyefanya kosa hilo ni lazima aswali. Kutoswali kwake ni dhambi nyingine kubwa.

 

 

Share

120-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Malaika Hawaingii Nyumba Yenye Mbwa Au Picha Za Viumbe

Lu-ulu-un-Manthuwrun:

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

 

Hadiyth Ya 120

 

Malaika Hawaingii Nyumba Yenye Mbwa Au Picha Za Viumbe

 

 

 

 

عَنْ أَبِي طَلْحَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ تَدْخُلُ الْملاَئِكَةُ بَيْتًا فِيهِ كَلْبٌ ولاَ صُورَةٌ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Twalhah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Malaika hawaingii nyumba ambayo yumo mbwa au picha [za viumbe vyenye roho])). [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

 Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Muislamu atahadhari kufuga mbwa bila ya sababu ya kufuga na kuweka picha, kwani kufanya hivyo anajikosesha kheri na baraka katika nyumba yake kwa kuwa Malaika hawatoingia.

 

 

2. Waislamu watahadhari kuzuia Malaika kutokuingia majumbani mwao kwa kuweka picha zenye viumbe, [Hadiyth: Imepokelewa kutoka kwa 'Aaishah (رضي الله عنها) amesema: "Nilifungua pazia la chumba cha hazina ambalo lilikuwa na picha (katika maelezo mengine: ambalo lilikuwa lina picha za farasi wenye mbawa). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipoliona, alilichanilia mbali na uso wake ukabadilika kuwa mwekundu kisha akasema: ((Ee 'Aaishah, watu watakaopewa adhabu kali kabisa mbele ya Allaah siku ya Qiyaamah ni wale wanaoigiza maumbile ya Allaah)).

 

Kkatika riwaayah nyengine:

 

 ((Hakika wanaochora picha hizi wataadhibiwa na wataambiwa: Tieni uhai vile mlivyoviumba!))

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akaendelea kusema: ((Hakika Malaika hawaingii nyumba ambayo ina picha)). ‘Aaishah akasema: Tukalikata pazia na tukalitumia kufanyia mto au mito miwili. Nimemuona akiegemea mto mmojawapo uliokuwa na picha (zilizokatwa na kuharibiwa).

 

 

3. Malaika waliokusudiwa ni Malaika wa rahmah, kwani Malaika wengine kama wanaoandika matendo ya mwana Aadam, hao hakuna budi waweko kwa ajili ya kazi yao. Nao ni Malaika waliopewa sifa ya: raqiyb (mchungaji, shahidi) na: ‘atiyd (asiyekukosa kuweko), yu tayari kuandika, kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِ نَفْسُهُ ۖ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ الْوَرِيدِ﴿١٦﴾

Na kwa yakini Tumemuumba insani na Tunajua yale yanayowaza nafsi yake, na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa koo.

 

إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ قَعِيدٌ﴿١٧﴾

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni. 

 

مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾

Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 16-18]

 

 

 

4. Picha zilokusudiwa ni za viumbe wa aina yoyote wenye roho. Pia chochote kilichochongwa kama vinyago vya watu, wanyama n.k.

 

 

 

5. Kufuga mbwa katika nyumba huwa ni kujikalifisha Muislamu na twahaara yake na mas-alah ya usafi kwa ujumla kama harufu mbaya, na kutosalimika vyombo, nguo, sehemu ya kuswalia na utwahara n.k.

 

 

6. Ni makosa katika jamii kwa wanaotundika picha zao ukumbini mwao wakiwa hawakuvaa mavazi ya hijaab. Mahali hapo huingia watu wasio mahaarim wa wanawake wa nyumba hiyo. Bali hata mtu akiwa na stara kamili, bado haijuzu kuweka picha kutokana na uharamu wake na pia kutoingia Malaika katika nyumba yenye picha.

 

 

7. Shariy’ah imekuja kuziba njia zote za kumpeleka mtu katika kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) katika uumbaji wake ambayo ni dhambi kubwa. Hivyo, Shariy’ah ikakataza kutundikwa picha zenye viumbe.

 

 

8. Shariy’ah imekuja kuondosha uzito na ugumu wa aina yoyote ile. Na kuweka mbwa ni njia moja inayompatia uzito mfugaji kwa kuiweka nyumba na yeye mwenyewe katika hali ya usafi na utwahaara.

 

 

 

Share

121-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Misikiti Si Ya Kuchafuliwa Bali Ni Ya Kumdhukuru Allaah

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 121  

 

Misikiti Si Ya Kuchafuliwa Bali Ni Ya Kumdhukuru Allaah

 

 

 

 

عَنْ أَنَس (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُول اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قال: ((إِنَّ هَذِهِ الْمَسَاجِدَ لاَ تَصْلُحُ لِشَيْءٍ مِنْ هَذَا الْبَوْلِ وَلاَ الْقَذَرِ، إِنَّمَا هِيَ لِذِكْرِ اللَّهِ تَعَالى وَقِرَاءَةِ الْقُرْآنِ)) أوْ كَماَ قَالَ رَسُولُ الله  صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ -    مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Hakika hii Misikiti, haifai kukojoa wala kutia uchafu. Hakika imejengwa kwa ajili ya kumtaja Allaah na kusoma Qur-aan)) au kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).  [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kukojoa Msikitini au kutupa uchafu wowote. Ikiwa ni wa najsi, basi haifai zaidi.

 

 

2. Ni wajibu kwa kila Muislamu kuhifadhi Misikiti, kwani ni sehemu inayofanywa ‘Ibaadah.

 

 

3. Kuhifadhi Misikiti kwa kila njia, usafi, amani na usalama baina ya watu n.k.

 

 

4. Haifai kupiga gumzo Msikitini wala kutenda lolote isipokuwa kuswali na kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kwa usomaji wa Qur-aan, kumsabbih, kumhimidi Allaah (سبحانه وتعالى), kumtukuza n.k.

 

 

 

5. Kulinda Misikiti na kila ovu ni alama ya mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) na kuvitukuza vitukufu Vyake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 ذَٰلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّـهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ

Ndio hivyo iwe na yeyote anayeadhimisha vitukufu vya Allaah basi hivyo ni kheri kwake mbele ya Rabb wake. [Al-Hajj (22: 30)]

 

Na pia Anasema (سبحانه وتعالى):

 

 ذَٰلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّـهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ ﴿٣٢﴾

 

Ndivyo hivyo, na yeyote anayeadhimisha Ishara za Allaah, basi hayo ni katika taqwa ya nyoyo. [Al-Hajj (22: 32)]

 

 

 

6. Kwa minajili hiyo, Muislamu anatakiwa awe ni mwenye kuondosha kohozi au uchafu wowote anaouona Msikitini pasi na kumngojea mtu maalumu kama mhudumu au msafishaji.

 

Hadiyth: Imepokewa kutoka kwa Abuu Dharr(رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم) amesema: ((Nilionyeshwa ‘amali za Ummah wangu, nzuri na mbaya. Nikapata katika ‘amali zao nzuri ni udhia unaoondoshwa njiani. Na nikapata katika ‘amali zao mbaya kohozi linaloachwa Msikitini pasi na kuzikwa)). [Muslim]

 

 

 

 

Share

122-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haifai Kupandisha Sauti Za Mazungumzo Misikitini

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 122  

 

Haifai Kupandisha Sauti Za Mazungumzo Misikitini

 

 

 

عَنْ السَّائِبِ بْنِ يَزِيدَ الصَّحابيِّ (رضي الله عنه) قَالَ: كُنْتُ قَائِمًا فِي الْمَسْجِدِ، فَحَصَبَنِي رَجُلٌ، فَنَظَرْتُ فَإِذَا عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ (رضي الله عنه)، فَقَالَ: اذْهَبْ فَأْتِنِي بِهَذَيْنِ،  فَجِئْتُهُ بِهِمَا، قَالَ: مِنْ أَيْنَ أَنْتُمَا؟ قَالاَ: مِنْ أَهْلِ الطَّائِفِ. قَالَ: لَوْ كُنْتُمَا مِنْ أَهْلِ الْبَلَدِ لأوْجَعْتُكُمَا، تَرْفَعَانِ أَصْوَاتَكُمَا فِي مَسْجِدِ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ! - البخاري

 

Imepokelewa kutoka kwa Swahaba, As-Saaib bin Yaziyd (رضي الله عنه)  amesimulia: Nilikuwa Msikitini. Mtu mmoja akanirushia kijiwe. Nilipomtazama alikuwa ni ‘Umar bin Al-Khattwaab(رضي الله عنه) . Akaniambia: “Nenda ukaniletee watu wale wawili”.  Nikaenda nikawaita.  ‘Umar akawauliza: “Nyinyi mmekuja kutoka wapi?” Wakamjibu: “Tunakutoka Twaaif” Akawaambia: “Lau mngelikuwa ni wenyeji wa mji huu, ningaliwapiga! Mnazinyanyua sauti zenu katika Msikiti wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)?” [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kupandisha sauti Msikitini hata ikiwa ni kwa kusoma Qur-aan au kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى). Na inakuwa haraam inapokuwa inaleta tashwishi au mabishano.

 

 

2. Muislamu anatakiwa aifanye sauti yake wastani katika ‘Ibaadah. Anaamrisha hivyo Allaah (سبحانه وتعالى):

 وَلَا تَجْهَرْ بِصَلَاتِكَ وَلَا تُخَافِتْ بِهَا وَابْتَغِ بَيْنَ ذَٰلِكَ سَبِيلًا ﴿١١٠﴾

 Na wala usisome kwa jahara Swalaah yako na wala usiifiche kimya kimya, bali shika njia (ya wastani) baina yake. [Al-Israa (17: 110)]

 

Na pia Rejea: Al-A’raaf (7: 55)

 

 

3. Inakuwa ni vizuri kumuashiria mtu Msikitini au kumtupia kitu kwa ajili ya kumtanabahisha jambo badala ya kutoa sauti.

 

 

4. Wajibu wa kutekeleza adabu za Msikitini zikiwemo kutokupandisha sauti, kutokuzozana, mijadala n.k.

 

 

5. Kuamrisha mema na kukataza maovu mahali popote khasa Msikitini ambako ni mahali patukufu kabisa wanapokusanyika Waislamu kwa ‘Ibaadah zao. 

 

 

6. Inaruhusiwa kiongozi kumuadhibu kwa kumpiga mtu anayekwenda kinyume na shariy’ah za Dini.

 

 

7. Jukumu la kiongozi kuzuia maovu yanayotendwa popote.

Rejea Hadiyth namba (27).    

 

 

8. Kutokuwaadhibu au kuwasamehe wageni wanaotenda maovu ambayo hayakuwekewa adhabu maalumu na shariy’ah katika mji usio wao bila ya kujua.

 

 

9. Nyumba za Allaah (سبحانه وتعالى) ni kwa ajili ya ‘Ibaadah na utiifu, hivyo inabidi kutekeleza humo yanayoamrishwa, kuepukana na yanayokatazwa kama yaliyotajwa juu, kufanya biashara n.k.

 

Rejea: An-Nuwr (24: 36-38).

 

 

10. Kutukuza vitukufu vya Allaah (سبحانه وتعالى) ni dalili ya taqwa na mapenzi ya Dini yetu hii ya Kiislamu tukufu.

 

Rejea: Al-Hajj (22: 30, 32).

 

 

 

 

 

Share

123-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayekwenda Kuswali Asile Kitunguu Au Kitunguu Thomu

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 123

 

Anayekwenda Kuswali Asile Kitunguu Au Kitunguu Thomu

 

 

 

عَنْ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ (رضي الله عنه) أنَّهُ خَطَبَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ فَقَالَ فِي خُطْبَتِهِ: ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا النَّاسُ تَأْكُلُونَ شَجَرَتَيْنِ مَا أَرَاهُمَا إلاَّ خَبِيثَتَيْنِ: الْبَصَلَ وَالثُّومَ! لَقَدْ رَأَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ إِذَا وَجَدَ رِيحَهُمَا مِنْ الرَّجُلِ فِي الْمَسْجِدِ أَمَرَ بِهِ فَأُخْرِجَ إِلَى الْبَقِيعِ، فَمَنْ أَكَلَهُمَا فَلْيُمِتْهُمَا طَبْخًا-    مسلم

Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه) kwamba alikhutubia Siku ya Ijumaa akasema katika khutbah yake: Kisha enyi watu! Mnakula miti miwili, siioni isipokuwa ni ya kukirihisha; kitunguu na kitunguu thomu; Hakika nimemuona Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم) anaposikia  harufu zake kwa mtu Msikitini, akiamrisha atolewe aende Al-Baqiy’. Atakayevila, basi aiue (harufu yake) kwa kuipika vyema.  [Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kula kitunguu na kitunguu thomu na chochote chenye harufu mbaya kwa anayekwenda Msikitini, ila ikiwa vimepikwa vizuri na harufu yake haipo tena.

 

 

2. Ni vizuri kwa Muislamu awe katika hali ya usafi kila mara na khasa anapochanganyika na wenziwe na mahali pa ‘Ibaadah ili asikirihishe watu kwa uchafu na harufu mbaya. 

 

 

3. Muislamu anapotaka kuswali au kwenda Msikitini, inampasa kubadilisha nguo zilokuwa chafu kwa mwenye kufanya kazi nje kwenye joto, au zinazonuka moshi wa sigara au aina yoyote ya harufu mbaya. Mwanamke pia anayekutoka jikoni baada ya kupika na kusafisha, inampasa aoge na avae nguo safi ndipo amkabili Allaah (سبحانه وتعالى) kwa ‘Ibaadah ya Swalaah, kwani hata Malaika wanachukizwa na harufu mbaya.

 

 

4. Uislamu umesisitiza usafi wa mtu binafsi na pia unajali kuweko amani baina ya watu na kutoudhiana au kukirihishana kwa jambo lolote litakalosababisha chuki au kufarikiana.

 

 

5. Viongozi wa Misikiti wahakikishe na wachunge usafi wa Msikiti na kukataza yote yanayotendwa ambayo ni kinyume na adabu za Msikitini.

 

 

6. Allaah (سبحانه وتعالى) Anastahiki zaidi kuvaliwa nguo nzuri zenye manukato mazuri anapokabiliwa kwa ajili ya ‘Ibaadah. Ameamrisha hivyo:

 

يَا بَنِي آدَمَ خُذُوا زِينَتَكُمْ عِندَ كُلِّ مَسْجِدٍ

Enyi wana wa Aadam! Chukueni mapambo yenu (ya mavazi ya sitara na twahara) katika kila mahala pa ‘Ibaadah. . [Al-A’raaf: 31]

 

Pia Hadiyth: 

إِنَّ اللَّهَ جَمِيلٌ يُحِبُّ الْجَمَالَ

((Hakika Allaah ni Mzuri Anapenda Uzuri)). [Muslim]

 

 

7. Usafi wa kila aina kwa ujumla utimizwe katika Swalaah; mwilini, nguo, mahali pa kuswalia n.k.

 

 

8. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ameamuru Waislamu wanapokwenda Msikitini kwa ajili ya Swalaah, wasiwe na harufu inayokutokana na kula vitu viwili ambavyo ni halaal kishariy’ah, seuze Muislamu kutumia vya haramu ambavyo vina harufu mbaya kama sigara, n.k.

 

 

 

Share

124-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Anayeapa Kwa Asiyekuwa Allaah Amekufuru

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 124  

 

Anayeapa Kwa Asiyekuwa Allaah Amekufuru

 

 

 

عَنْ عَبْد الله ابْنَ عُمَرَ (رضي الله عنهما) أّنَّهُ سَمِعَ رَجُلاً يَقُولُ: لاَ وَالْكَعْبَةِ. فَقَالَ ابْنُ عُمَرَ: لاَ يُحْلَفُ بِغَيْرِ اللَّهِ فَإِنِّي سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((مَنْ حَلَفَ بِغَيْرِ اللَّهِ فَقَدْ كَفَرَ أَوْ أَشْرَكَ)) رواه الترمذي وَقَالَ حَدِيثٌ حَسَنٌ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar  (رضي الله عنهما) kwamba amemsikia mtu akiapa: “Hapana! Naapa kwa Al-Kaabah!” Ibn ‘Umar akamwambia: Haifai kuapiwa chochote isipokuwa Allaah, kwani hakika mimi nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Allaah hakika ameshakufuru, au ameshafanya shirki)). [At-Tirmidhiy na amesema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Haramisho la kuapia kitu au chochote isipokuwa kwa Jina la Allaah (سبحانه وتعالى).

Rejea Hadiyth namba (92), (125).

 

 

2. Hatari ya kuapia kisichokuwa Allaah (سبحانه وتعالى) kinamtia mtu katika madhambi makubwa ya shirki. Na ikiwa amekusudia juu ya kwamba anajua haijuzu, basi kunamtoa mtu nje ya Uislamu.

 

 

3. Baadhi ya yanayotumika kimakosa katika jamii katika kuapia ni:

 

  • Kuapia Mswahafu.
  • Kuapia kwa mama mzazi au wazazi wawili.
  • Kuapia Al-Ka’bah
  • Kuapia kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).
  • Kuapia kwa vitukufu mbali mbali vya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

4. Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee Ndiye Mwenye Kustahiki kuapia chochote Atakacho, kwani Yeye Ni Muumba wa kila kitu. Na hivyo Ameapia vitu vingi katika Qur-aan. Suwrah nyingi katika Juzuu za 29 na 30 zimeanza na viapo vya Allaah (سبحانه وتعالى), mfano Allaah (سبحانه وتعالى) Ameapia kwa Tiyn na Zaytuwn, Ameapia kwa Siku ya Qiyaamah, Ameapia kwa jua, mwezi, nyota, nchi ya Makkah, mbingu, ardhi, usiku, mchana, Alfajiri, zama au Swalaah ya Alasiri, na vitu vingi vinginevyo.

 

 

5. Anapoapia jambo mtu, kisha akafanya kinyume chake, basi atimize kafara ya kiapo cha yamini kutokana na amri ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٨٩﴾

Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini yamini zenu. Hivyo ndivyo Allaah Anavokubainishieni Aayaat (na hukmu) Zake ili mpate kushukuru. [Al-Maaiidah (5:89)]

 

 

Hata hivyo, kiapo kisiapiwe kwa chochote isipokuwa kwa Jina la Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

6. Juu ya hivyo, Allaah (سبحانه وتعالى) Hamchukulii mtu kwa kiapo cha upuuzi ila kile kilokusudiwa kama Anavyosema:

 

 لَّا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا كَسَبَتْ قُلُوبُكُمْ ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿٢٢٥﴾

Allaah Hatokushikeni kwa viapo vyenu vya upuuzi lakini Atakuchukulieni kwa yaliyochuma nyoyo zenu. Na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mvumilivu [Al-Baqarah (2: 225)]

 

ila tu kiapo kisiapiwe kwa chochote isipokuwa kwa Jina la Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

7. Jambo la kuapa linachukuliwa wepesi na watu na hali linaweza kuwa ni la hatari mno, na Allaah (سبحانه وتعالى) Ametahadharisha kuhifadhi viapo vyetu kama ilivyotajwa katika Aayah ya juu hapo kwenye Al-Maaidah (5: 89).

 

 

 

 

 

Share

125-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Miongoni Mwa Madhambi Makubwa Ni Kumshirikisha Allaah, Kuwaasi Wazazi, Kuua Mtu, Kuapa Uongo

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 125

   

Miongoni Mwa Madhambi Makubwa Ni Kumshirikisha Allaah,

Kuwaasi Wazazi, Kuua Mtu, Kuapa Uongo

 

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو بْن الْعاص (رضي الله عنهما) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ َقَالَ: ((الْكَبَائِرُ الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ، وَعُقُوقُ الْوَالِدَيْنِ، وَقَتْلُ النَّفْسِ، وَالْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) البخاري وفي رواية لَهُ: أنَّ أَعْرَابِياً جَاءَ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّه، مَا الْكَبَائِر؟ ُ قَالَ: ((الإشْرَاكُ بِاللَّهِ))  قَالَ: ثُمَّ مَاذَا؟ قَالَ: ((الْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) قُلْتُ: وَمَا الْيَمِينُ الْغَمُوسُ؟  قَالَ: ((الَّذِي يَقْتَطِعُ مَالَ امْرِئٍ مُسْلِمٍ!)) يَعْنِ: بِيَمِينٍ هُوَ فِيهَا كَاذِب

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amri bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما)  amesema kuwa Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Madhambi makubwa ni kumshirikisha Allaah,  kuwaasi wazazi wawili, kuua nafsi na yamini [kiapo] ya uongo)).  [Al-Bukhaariy] Na katika riwaayah nyingine: “Alikuja Mbedui mmoja kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah? Ni yepi madhambi makubwa? Akasema: ((Kumshirikisha Allaah)) Akasema: Kisha yepi? Akasema: ((Yamini ya uongo)). Nikauliza: Ni ipi yamini ya uongo? Akasema: ((Ni ambayo mtu hujichukulia mali ya Muislamu!)) yaani akaapa kwa uongo. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Uharamisho wa kuapa uongo na zaidi inapokuwa ni kwa ajili ya kula mali za watu bila haki na kwa ubatilifu, ikiwa ni kwa ribaa au kwa dhulma ya aina yoyote. Allaah (سبحانه وتعالى) Anatahadharisha:

 

وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَكُم بَيْنَكُم بِالْبَاطِلِ وَتُدْلُوا بِهَا إِلَى الْحُكَّامِ لِتَأْكُلُوا فَرِيقًا مِّنْ أَمْوَالِ النَّاسِ بِالْإِثْمِ وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٨﴾

  Na wala msiliane mali zenu kwa ubatilifu na mkazipeleka (rushwa) kwa mahakimu ili mle sehemu katika mali ya watu kwa dhambi na hali mnajua. [Al-Baqarah (2: 188)]

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَأَخْذِهِمُ الرِّبَا وَقَدْ نُهُوا عَنْهُ وَأَكْلِهِمْ أَمْوَالَ النَّاسِ بِالْبَاطِلِ ۚ وَأَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ مِنْهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿١٦١﴾

Na kuchukua kwao ribaa na hali walikatazwa kuichukua; na kula kwao mali za watu kwa ubatilifu. Na Tumeandalia kwa makafiri miongoni mwao adhabu iumizayo. [An-Nisaa (4: 161).

 

Rejea pia An-Nisaa (4: 29).

 

 

 

2. Kiapo cha uongo ni miongoni mwa madhambi makubwa yanayostahiki adhabu kali kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

3. Kiapo cha uongo kimesawazishwa kuwa sawa na kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) na kuua mtu, na kuasi wazazi, kwani yote ni dhulma zinazohusiana na haki za watu.

 

Rejea Hadiyth namba (19). 

 

 

4. Aina ya viapo ni vitatu;

 

(i) Al-Yamiyn Al-Ghamuws (Kiapo cha uongo):

 

Ni kula kiapo huku anakusudia kuongopa, kama vile kusema: “Wa-Allaahi nimenunua kitu kadhaa kwa shilingi laki moja”, naye hakukinunua hivyo. Hukmu yake: Atimize kafara kama ilivyotajwa katika Al-Maaidah (5: 89). Lakini kafara pekee katika kiapo hiki haitotosha, bali pamoja na kafara, mhusika anatakiwa alete tawbah na kuomba maghfirah (msamaha), kwani kosa hili ni kubwa sana, na hasa ikiwa yamini hiyo itamfikisha kwenye kumega haki ya mtu mwengine kwa njia isiyo ya halaal. Hii ndio kauli ya jamhuri (Wanachuoni wengi).

 

(ii) Al-Yamiyn Al-Laghw (Kiapo cha upuuzi):

 

Ni kile kipitayo ulimini mwa Muislamu bila kuikusudia, kama yule ambaye katika mazungumzo yake hujitokeza kwa wingi mno wa neno: “Wa-Allaahi hapana”. Hukmu yake ni: ((Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi)) kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى) katika Al-Maaidah (5: 89). 

 

(iii) Al-Yamiyn Al-Mun’aqidah (Kiapo cha kufungika):

 

Ni kukusudia jambo la baadaye. Kama vile Muislamu kusema: “Wa-Allaahi nitalifanya jambo kadhaa” Au “Wa-Allaahi sitolifanya…” kisha akafanya kinyume chake. Hukmu yake:  ((….lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti)) kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى) katika Al-Maaidah (5: 89).

 

 

5. Haya ni tahadhari kwetu tusiingie katika madhambi hayo makubwa ambayo yanaangamiza kama yalivyotajwa hapa shirki, kuwaasi wazazi, kuua pasi na haki na pia yamini ya uongo.

 

 

 

6.  Haramisho la kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى). Rejea Hadiyth namba (48), (108), (119).

 

 

 

7.  Haramisho la kuwaasi wazazi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۚ إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣﴾

Na Rabb wako Amehukumu kwamba: “Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee na (Ameamrisha) kuwafanyia ihsaan wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee naye yuko pamoja nawe, au wote wawili basi usiwaambie, Uff! Na wala usiwakemee; na waambie maneno ya heshima.

 

وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

Na wainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme: “Rabb wangu! Warehemu kama walivyonilea udogoni.” [Al-Israa (17: 23-24)]

 

Na baadhi ya Hadiyth za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu kuwaasi wazazi:

 

عَنْ أَنَس وَغَيْره أَنَّ النَّبِيّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ لَمَّا صَعِدَ الْمِنْبَر ثُمَّ قَالَ  (( آمِينَ آمِينَ آمِينَ)) " قِيلَ يَا رَسُول اللَّه عَلَامَ مَا أَمَّنْت ؟ قَالَ (( أَتَانِي جِبْرِيل فَقَالَ يَا مُحَمَّد رَغِمَ أَنْف رَجُل ذُكِرْت عِنْده فَلَمْ يُصَلِّ عَلَيْك قُلْ آمِينَ فَقُلْت آمِينَ ثُمَّ قَالَ رَغِمَ أَنْف رَجُل دَخَلَ عَلَيْهِ شَهْر رَمَضَان ثُمَّ خَرَجَ فَلَمْ يُغْفَر لَهُ قُلْ آمِينَ فَقُلْت آمِينَ ثُمَّ قَالَ رَغِمَ أَنْف رَجُل أَدْرَكَ وَالِدَيْهِ أَوْ أَحَدهمَا فَلَمْ يُدْخِلَاهُ الْجَنَّة قُلْ آمِينَ فَقُلْت آمِين))  صحيح الترمذي و قال الشيخ الأباني حسن صحيح  

Imepokelewa kutoka kwa Anas na wengineo kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alipopanda juu ya minbar aliitikia ((Aamiyn, Aamiyn, Aamiyn)). Alipoulizwa kwa nini ameitikia hivyo akasema: ((Amenijia Jibriyl akasema: “Ee Muhammad, ole wake yule ambaye unapotajwa hakuswalii, hivyo sema Aamiyn”. Nikasema Aamiyn. Kisha akasema: “Ole wake yule ambaye umeingia mwezi wa Ramadhwaan kisha akatoka bila ya kughufuriwa, kwa hiyo sema Aamiyn”. Nikasema Aamiyn. Kisha akasema: “Ole wake yule ambaye amewakuta wazazi wake au mmoja wa wazazi wake lakini wasimuingize Jannah. Hivyo sema Aamiyn”. Nikasema Aamiyn)) [Swahiyh At-Tirmidhiy na kasema Shaykh Al-Albaaniy kuwa Hadiyth hiyo ina daraja ya Hasan Swahiyh]

 

Kuwatii wazazi na kutokuwaasi ni katika haki zao kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Hadiyth:

 

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: “Mtoto hawezi kumlipa babake (kwa yale aliyomfanyia) isipokuwa anapomkuta kuwa ni mtumwa, akamnunua kisha kumwacha huru.” [Muslim, Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy].

 

Rejea Hadiyth namba (34),

 

 

8. Haramisho la kuua mtu bila ya haki.  Allaah (سبحانه وتعالى) Ametaja katika Aayah kadhaa zikiwemo:

 

وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ أَن يَقْتُلَ مُؤْمِنًا إِلَّا خَطَأً ۚ وَمَن قَتَلَ مُؤْمِنًا خَطَأً فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ وَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ إِلَّا أَن يَصَّدَّقُوا ۚ فَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ عَدُوٍّ لَّكُمْ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ ۖ وَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُم مِّيثَاقٌ فَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ وَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ شَهْرَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ تَوْبَةً مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿٩٢﴾

Na haiwi kwa Muumin amuue Muumin ila kwa kukosea tu. Na atakayemuua Muumin kwa kukosea basi aachilie huru mtumwa Muumin na atoe diya kwa kuifikisha kwa ahli zake, isipokuwa watolee wenyewe swadaqah. Na ikiwa ni miongoni mwa watu wa maadui zenu naye ni Muumin, basi (aliyeua) aachilie huru mtumwa Muumin. Na ikiwa ni miongoni mwa watu ambao kuna mkataba baina yenu na baina yao; basi wapewe diya kuifikisha kwa ahli wake na aachiliwe huru mtumwa Muumin. Asiyepata, afunge Swiyaam miezi miwili mfululizo; kuwa ni tawbah kwa Allaah. Na Allaah daima ni Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote. 

 

وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ وَأَعَدَّ لَهُ عَذَابًا عَظِيمًا ﴿٩٣﴾

Na atakayemuua Muumini kwa kusudi, basi jazaa yake ni Jahannam, ni mwenye kudumu humo na Allaah Atamghadhibikia na Atamlaani na Atamuandalia adhabu kuu. [An-Nisaa (4: 92-93)]

 

 

Na Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ يَلْقَ أَثَامًا ﴿٦٨﴾

Na wale ambao hawaombi pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine na wala hawaui nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na wala hawazini. Na atakayefanya hivyo atakutana na adhabu. [Al-Furqaan  (25: 68)]

 

 

Rejea pia Hadiyth namba (108), (132).

 

 

Share

126-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Muumin Si Anayekashifu Watu, Au Kulaani, Kunena Machafu Au Mwenye Ufidhuli

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 126

 

Muumin Si Anayekashifu Watu, Au Kulaani, Kunena Machafu Au Mwenye Ufidhuli

 

 

 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ابْن مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((لَيْسَ الْمُؤْمِنُ بِالطَّعَّانِ ولاَ اللَّعَّانِ وَلاَ الْفَاحِشِ وَلاَ الْبَذِيءِ)) رواه الترمذي وَقَالَ حَدِيثٌ حَسَنٌ   

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaahi bin Mas’uwd (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin si yule anayekashifu watu, wala anayelaani sana, wala anayenena machafu, wala mfedhuli na mtovu wa adabu)). [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Hasan]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Ukamilisho na uthibitisho wa iymaan ya Muumin ni kutokuwa na sifa mbovu kama hizo za kukashifu, kulaani, kunena machafu na utovu wa adabu.

 

 

2. Uislamu unasisitiza tabia njema, kwani ni sababu kuu ya kuweko amani baina ya watu na inazuia ufisadi na mtafaruku.

 

 

 

3. Muumin anapaswa kuwa na tabia njema na kujiepusha na tabia ovu kama alivyotufunza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Hadiyth nyingi.

 

Rejea Hadiyth namba (21), (22), (23), (65), (67), (94), (95).

Naye ni kigezo bora kabisa kwetu kwa tabia na khulka zake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى) kumwambia Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم):

 

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤﴾

Na hakika wewe bila shaka una tabia adhimu. [Al-Qalam (68: 4)]

 

 

Rejea pia: Aal-‘Imraan (3: 159), At-Tawbah (9: 128).

 

Na inapaswa kumfuata. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللَّـهَ وَالْيَوْمَ الْآخِرَ وَذَكَرَ اللَّـهَ كَثِيرًا ﴿٢١﴾

Kwa yakini mna kigezo kizuri kwa Rasuli wa Allaah kwa mwenye kumtaraji Allaah na Siku ya Mwisho na akamdhukuru Allaah kwa wingi. [Al-Ahzaab (33: 21)]

 

 

 

4. Ulimi wa Muumin unapasa kutoa maneno mazuri daima na si maovu yanayompatia dhambi. Hadiyth kadhaa zimeonya kuhusu maovu ya ulimi.

 

Rejea Hadiyth namba (87), (88), (89), (93), (98).

 

 

 

5. Maneno maovu, kulaani, kukashifu n.k. ni miongoni mwa dhambi zinazohusiana na haki za watu, nazo Allaah (سبحانه وتعالى) Hazisamehi hadi aliyetendewa asamehe, au malipo ni Siku ya Hesabu kwa kuchukuliwa mema yake mtu na kutupiwa madhambi.

 

Rejea Hadiyth namba (19).

 

 

6. Maneno maovu na machafu ni ukosefu wa kuwa na haya jambo ambalo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amelilinganisha na iymaan.

 

Rejea Hadiyth namba (69).

 

 

 

Share

127-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Watakaokuwa Karibu Na Watakaokuwa Mbali Kabisa Na Nabiy Siku Ya Qiyaamah

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

 

Hadiyth Ya 127  

 

Watakaokuwa Karibu Na Watakaokuwa Mbali Kabisa

Na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  Siku Ya Qiyaamah

 

 

 

 

عَنْ جَابِرٍ ((رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِنَّ مِنْ أَحَبِّكُمْ إِلَيَّ وَأَقْرَبِكُمْ مِنِّي مَجْلِسًا يَوْمَ الْقِيَامَةِ، أَحَاسِنَكُمْ أَخْلاَقًا، وَإِنَّ أَبْغَضَكُمْ إِلَيَّ وَأَبْعَدَكُمْ مِنِّي مَجْلِسًا يَوْمَ الْقِيَامَةِ، الثَّرْثَارُونَ وَالْمُتَشَدِّقُونَ وَالْمُتَفَيْهِقُونَ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ قَدْ عَلِمْنَا الثَّرْثَارُونَ وَالْمُتَشَدِّقُونَ، فَمَا الْمُتَفَيْهِقُونَ؟ قَالَ: ((الْمُتَكَبِّرُونَ)) رواه الترمذي وَقَالَ حَدِيثٌ حَسَنٌ

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir((رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika wanaopendeza mno kwangu na watakaoketi karibu mno nami Siku ya Qiyaamah, ni wale wenye tabia njema. Na hakika wanaochukiza mno kwangu na watakaokuwa mbali nami Siku ya Qiyaamah, ni wale wenye porojo, wanaojigamba na "mutafayhiquwn")). Wakauliza (Maswahaba): Ee Rasuli wa Allaah! Tumewajua wenye porojo na wanaojigamba. Je, al-mutafayhiquwn ni wepi? Akajibu: ((Ni wenye kiburi)). [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Himizo la kuwa na tabia njema ambayo itamjaalia Muislamu kuwa karibu na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Siku ya Qiyaamah. Na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amefunza mengi kuhusu tabia njema, kwa kauli na vitendo. Allaah (سبحانه وتعالى) Amemsifu Aliposema:

 وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤﴾

Na hakika wewe bila shaka una tabia adhimu. [Al-Qalam (68: 4)]

 

Na Hadiyth ifuatayo inathibitisha:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ الله عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ‏:‏ ((إِنَّمَا بُعِثْتُ لِأُتَمِّمَ صَالِحَ الأَخْلاقِ‏))

 

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Hakika nimetumwa ili nikamilishe khulqa (tabia) njema)) [Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy Swahiyh Al-Jaami’ (2349), Swahiyh Adab Al-Mufrad (207)]

 

Rejea pia Hadiyth namba (66).

 

 

2. Makatazo ya kutoa porojo, kwani humpeleka mtu kusema yasiyopasa na yatakayomghadhibisha Allaah (سبحانه وتعالى), au kuudhi watu kwa kila aina za uovu wa ulimi; ghiybah, namiymah, kejeli, istihzai, kuvunja heshima n.k.

 

 

3. Kuzuia ulimi usinene ila yaliyo mema. Allaah (سبحانه وتعالى) Anaonya hayo katika Aayah kadhaa miongoni mwazo ni:

 

مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾

Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf (50: 18)]

 

 

Pia Hadiyth kadhaa zimeonya kuhusu ulimi na madhara yake.  

 

Rejea Hadiyth namba (86), (87), (88).

 

Rejea pia Al-Israa (17: 36), Al-Hujuraat (49: 11-12), An-Nuwr (24: 15).

 

 

4. Allaah (سبحانه وتعالى) Anatahadharisha kukaa na watu wanaotoa porojo ambao huzifanyia mpaka Aayaat za Allaah (سبحانه وتعالى) porojo.  Anasema  (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذَا رَأَيْتَ الَّذِينَ يَخُوضُونَ فِي آيَاتِنَا فَأَعْرِضْ عَنْهُمْ حَتَّىٰ يَخُوضُوا فِي حَدِيثٍ غَيْرِهِ ۚ وَإِمَّا يُنسِيَنَّكَ الشَّيْطَانُ فَلَا تَقْعُدْ بَعْدَ الذِّكْرَىٰ مَعَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٦٨﴾

  Na unapowaona wale wanaoshughulika kupiga porojo katika Aayaat Zetu; basi jitenge nao mpaka watumbukie kwenye mazungumzo mengineyo. Na kama shaytwaan akikusahaulisha, basi baada ya kukumbuka, usikae pamoja na watu madhalimu.  [Al-An’aam (6: 68)]

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 140), At-Tawbah (9: 64-66).

 

 

5. Desturi  ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwafunza Maswahaba msimiati isiyozoeleka baina yao katika kuzungumza lugha ya Kiarabu. Lakini hii isifahamike vibaya kwa kuwa Muislamu hapaswi kuzungumza maneno magumu yasiyofahamika khasa ikiwa anaozungumza nao si wenye ujuzi wa lugha anayoizungumza, bali adhihirishe kauli yake ieleweke kwa kutumia maneno ya kawaida. Katazo hili liepushwe katika uandishi pia.

 

 

6 Makatazo ya kujigamba na kuwa na majivuno na kiburi. Allaah (سبحانه وتعالى) Anatahadharisha na Anawachukia wenye kiburi. Anasema:

 

وَلَا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿١٨﴾

  “Na wala usiwageuzie watu uso wako kwa kiburi, na wala usitembee katika ardhi kwa maringo, hakika Allaah Hampendi kila mwenye majivuno mwenye kujifakharisha. [Luqmaan (31: 18)]

 

Na pia:

لِّكَيْلَا تَأْسَوْا عَلَىٰ مَا فَاتَكُمْ وَلَا تَفْرَحُوا بِمَا آتَاكُمْ ۗ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿٢٣﴾

Ili msisononeke juu ya yale yaliyokuondokeeni na wala msifurahie kwa yale Aliyokupeni (Allaah); na Allaah Hapendi kila mwenye kujinata, anayejifakharisha. [Al-Hadiyd (57: 23)]

 

Rejea pia Hadiyth namba (25), (65).

Share

128-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Amelaaniwa Mke Anayemkatalia Mumewe Kujimai Bila Ya Sababu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 128

 

Amelaaniwa Mke Anayemkatalia Mumewe Kujimai Bila Ya Sababu

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِذَا دَعَا الرَّجُلُ امْرَأَتَهُ إِلَى فِرَاشِهِ فَأَبَتْ فَبَاتَ غَضْبَانَ عَلَيْهَا لَعَنَتْهَا الْمَلآئِكَةُ حَتَّى تُصْبِحَ)) متفق عليه وَفي رواية: ((حَتَّى تَرْجِعَ))

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Mwanamume atakapomwita mkewe kitandani [ili ajimae naye] akakataa, akalala [mume huyo] akiwa amemkasirikia [mkewe], Malaika watamlaani [mke huyo] mpaka apambaukiwe)). [Al-Bukhaariy na Muslim].   Na katika riwaayah: ((Mpaka arejee).

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Mke anapaswa kutimiza haki ya mume kwa kumuitikia anapomhitaji kitandani. Isipokuwa tu anapokuwa katika hali ya hedhi, kwani hilo limekatazwa na Allaah (سبحانه وتعالى) kama Anavyosema:

 

وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْمَحِيضِ ۖ قُلْ هُوَ أَذًى فَاعْتَزِلُوا النِّسَاءَ فِي الْمَحِيضِ ۖ وَلَا تَقْرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطْهُرْنَ ۖ فَإِذَا تَطَهَّرْنَ فَأْتُوهُنَّ مِنْ حَيْثُ أَمَرَكُمُ اللَّـهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ ﴿٢٢٢﴾ 

Na wanakuuliza kuhusu hedhi. Sema: “Hiyo ni dhara; basi waepukeni wanawake katika hedhi. Wala msiwakaribie kujimai nao mpaka watwaharike. Watakapotwaharika basi waendeeni kupitia pale Alipokuamrisheni Allaah.”  Hakika Allaah Anapenda wenye kutubia na Anapenda wenye kujitwaharisha [Al-Baqarah (2: 222)]

 

Na Hadiyth kadhaa zimekataza mume kujimai na mke mwenye hedhi; miongoni mwazo ni:

 

“Mwenye kumuingia mwenye hedhi au mwanamke kwenye dubur (uchi wa nyuma) au kumwendea mtabiri na kumuamini kwa anayosema basi amekufuru kwa aliyoteremshiwa Muhammad.” [Swahiyh At-Tirmidhiy (135), Swahiyh Ibn Maajah (528), As-Silsilah Asw-Swahiyhah (7/1130)].

 

Lakini mume anaruhusika kustarehe na mkewe isipokuwa kujimai kwa dalili ya Hadiyth:

 

عن  أنس رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ الْيَهُودَ كَانُوا إِذَا حَاضَتِ الْمَرْأَةُ؛ لَمْ يُؤَاكِلُوهَا. فَقَالَ النَّبِيُّ -صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((اصْنَعُوا كُلَّ شَيْءٍ إِلاَّ النِّكَاحَ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mayahudi walikuwa hawali na mwanamke anapokuwa katika hedhi. Lakini Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Fanyeni naye kila jambo isipokuwa kujimai)) [Muslim]

 

 

Ama katika hali ya ugonjwa au machofu makali, mume anapaswa kumvumilia mkewe katika hali hiyo. Na mke anapokuwa katika Swawm ya Ramadhwaan, hapasi kumtii mumewe kumkubalia kujimai naye.

 

 

2. Mwanamke asipomkidhia mumewe haja yake ya kitendo cha ndoa, anastahiki adhabu ya kulaaniwa na Malaika mpaka akiamka asubuhi. Hii inadhihirisha jinsi gani umuhimu wa jambo hili, kwani litaweza kumzuia mume asitoke nje kutenda maasi ya zinaa.

 

 

3. Mwanamume kawaida ni mwenye matamanio zaidi ya kitendo cha ndoa kuliko mwanamke, na ni hikma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuwaumba kila mmoja kwa kutofautiana mwili, matamanio n.k. Na ndio maana akakatazwa mwanamke kufunga Swawm za Sunnah bila ya ruhusa ya mumewe.

 

Rejea Hadiyth namba (30).

 

 

4. Tahadharisho hili la mke kumkatalia mume kujimai naye bila ya sababu inayoruhusika ki-shariy’ah njia kubwa kwa Uislamu kufunga mlango wa shari, kwani kiubinaadamu, mtu akiwa ana hasira anaweza kutoa talaka na hivyo nyumba kuvunjika. Au pia ikiwa shauku ya mwanamme ni kubwa, anaweza kuzini, na hivyo kuvunja mahusiano mema na mkewe na hata pengine kumletea ugonjwa mbaya unaotokana na kuzini nje.

 

 

 

Share

129-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haifai Kutia Chokaa Makaburi Au Kujengea Au Kukalia

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 129  

 

Haifai Kutia Chokaa Makaburi Au Kujengea Au Kukalia

 

 

 

عَنْ جَابِرٍ (رضي الله عنه) قَالَ: نَهَى رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنْ يُجَصَّصَ الْقَبْرُ وَأَنْ يُقْعَدَ عَلَيْهِ وَأَنْ يُبْنَى عَلَيْهِ. مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه)  amesema:  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم) amekataza kaburi kutiwa chokaa (liwe imara), kuketiwa juu yake na kujengewa. [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kupaka kaburi chokaa au kutia alama yoyote ile. Na kuzidisha inapovuka mipaka ya kulipamba huwa ni haraam.

 

 

2. Uharamisho wa kuketi juu ya kaburi, kwani hivyo ni utovu wa adabu juu ya maiti kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم((Msiswali juu ya makaburi wala msiketi juu yake)). [Muslim]

 

Rejea Hadiyth namba (83), (137).

 

 

3. Kuyajengea makaburi hatimaye kutapelekea watu kuyatukuza na kufanya mahali pa ‘Ibaadah, jambo liloharamishwa.  Ni kama vile Aswhabul-Kahf (watu wa pangoni) walivyofanyiwa na watu baada ya kufariki kwao:

 

وَكَذَٰلِكَ أَعْثَرْنَا عَلَيْهِمْ لِيَعْلَمُوا أَنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ وَأَنَّ السَّاعَةَ لَا رَيْبَ فِيهَا إِذْ يَتَنَازَعُونَ بَيْنَهُمْ أَمْرَهُمْ ۖ فَقَالُوا ابْنُوا عَلَيْهِم بُنْيَانًا ۖ رَّبُّهُمْ أَعْلَمُ بِهِمْ ۚ قَالَ الَّذِينَ غَلَبُوا عَلَىٰ أَمْرِهِمْ لَنَتَّخِذَنَّ عَلَيْهِم مَّسْجِدًا ﴿٢١﴾

  Na hivyo ndivyo Tulivyowatambulisha kwa watu ili wajue kwamba ahadi ya Allaah ni haki. Na kwamba Saa haina shaka yoyote humo. Pale walipozozana baina yao kuhusu jambo lao. Wakasema: “Jengeni jengo juu yao; Rabb wao Anawajua vyema.” Wakasema wale walioshinda katika shauri lao: “Bila shaka tutajenga msikiti juu yao.” [Al-Kahf 18: 21)]

 

Makatazo ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) pia katika Hadiyth kadhaa zikiwemo:

 ((Hakika watu waovu kabisa watakaokutana na alama za Qiyaamah ni wale wanaofanya makaburi kuwa ni Misikiti [mahali pa ‘Ibaadah])). [Ahmad na amesimulia Abu Haatim katika Swahiyh yake]

 

Na pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Awalaani Mayahudi na Manasara, kwani wamefanya makaburi ya Manabii wao kuwa ni sehemu za ‘ibaadah.)) [Imesimuliwa na Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

4. Makatazo ya kujengea kaburi kwa vile ni mila za kikafiri na upotezaji wa mali kwa jambo lisilopasa. Na kujengewa pia kutasababisha watu wengine kutopata nafasi ya kuzikwa makaburini.

 

 

5. Muislamu anapaswa kupewa heshima yake hata baada ya kufariki kwake na kutomfanyia mambo yanayokatazwa katika Shariy’ah.

 

 

Share

130-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Analaaniwa Anayefanya Haja Njia Wapitazo Watu Au Kivulini

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 130

 

Analaaniwa Anayefanya Haja Njia Wapitazo Watu Au Kivulini

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اتَّقُوا اللَّعَّانَيْنِ)) قَالُوا: وَمَا اللَّعَّانَانِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: ((الَّذِي يَتَخَلَّى فِي طَرِيقِ النَّاسِ أَوْ فِي ظِلِّهِمْ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jilindeni [jiepusheni] na sehemu mbili zinazopelekea mtu kulaaniwa)). [Maswahaba] Wakauliza: Ni sehemu zipi hizo zinazopelekea mtu kulaaniwa? Akasema: ((Ni mtu kufanya haja katika njia wanazopita watu au katika vivuli wanavyoketi)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Makatazo ya kufanya haja njiani kwani kufanya kunaleta maudhi kwa watu na pia upo uwezekano wa kusambaza ugonjwa.

 

2. Anaposhikwa mtu na haja akawa hana mahali basi aingie sehemu isiyopitwa na watu au kichakani kufanya haja.

 

 

3. Uislamu umehimiza usafi wa bin Aadam kwa kila upande; kiwiliwili, nguo hata njiani ili ajilinde na uchafu unaosababisha maradhi na abakie salama katika siha.

 

 

4. Usafi na tawahara ni jambo linalopendeza na Allaah (سبحانه وتعالى)  Anapenda wanaojiweka katika hali hiyo kama Anavyosema:

 إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ ﴿٢٢٢﴾

Hakika Allaah Anapenda wenye kutubia na Anapenda wenye kujitwaharisha. [Al-Baqarah (2: 222)]

 

 

5. Uislamu unapendelea na kuhimiza heshima na sitara ya mtu. Kufanya haja njiani bila ya kuwa na udhuru ni kukosa hayaa, nako ni ukosefu wa Iymaan.

 

Rejea Hadiyth namba (68).

 

 

6. Makatazo ya kufanya haja njiani ni miongoni mwa madhambi makubwa kwa vile yanahusiana na laana ya Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

 7. Pia kukatazwa kwenda haja vivulini mwa watu ni kuwaudhi watu na kuwakosesha sehemu ya kupumzika.  Na tufahamu kuwa tumekatazwa kuwaudhi watu.

 

 

8. Pia tabia ya baadhi ya watu kutupa taka njiani, au wale walioko ndani ya magari kutupa vikopo vya soda, juisi na kadhalika, ni katika mambo yasiyokubalika kutendwa katika Uislamu. 

Share

131-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Allaah Ameridhia Kuabudiwa, Kutokumshirikisha, Kuungana Na Anachukia Uvumi, Udadisi Na Kupoteza Mali

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 131

 

Allaah Ameridhia Kuabudiwa, Kutokumshirikisha, Kuungana

Na Anachukia Uvumi, Udadisi Na Kupoteza Mali

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ اللَّهَ يَرْضَى لَكُمْ ثلاَثًا وَيَكْرَهُ لَكُمْ ثلاَثًا: فَيَرْضَى لَكُمْ أَنْ تَعْبُدُوهُ ولاَ تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا، وَأَنْ تَعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّهِ جَمِيعًا ولاَتَفَرَّقُوا،

 وَيَكْرَهُ لَكُمْ قِيلَ وَقَالَ، وَكَثْرَةَ السُّؤَالِ، وَإِضَاعَةِ الْمَالِ )) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:  ((Hakika Allaah Anawaridhia mambo matatu na Anachukia kwenu mambo matatu; Anawaridhia mumwabudu Yeye, wala msimshirikishe kwa chochote, na mshikamane nyote na kamba ya Allaah wala msifarikiane. Na anachukia kwenu uvumi, kuuliza sana na   kupoteza mali)). [Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Maana ya Tawhiyd ni kumwambudu Allaah (سبحانه وتعالى) bila ya kumshirikisha na chochote.

 

 

 

2. Himizo na amri ya kumwabudu Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 يَا أَيُّهَا النَّاسُ اعْبُدُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿٢١﴾

Enyi watu! Mwabuduni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni na wale wa kabla yenu mpate kuwa na taqwa. [Al-Baqarah (2: 21)]

 

Rejea pia: Yuwnus (10: 3), Al-An’aam (6: 102).

 

 

 

3. Haramisho la kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) na chochote. Aayah na Hadiyth nyingi zimekataza. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ و

Sema: “Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote. [Al-An’aam (6: 151)]

 

Rejea pia: An-Nisaa (4: 36), Al-A’raaf (7: 33).

 

 

 

4. Kumwabudu Allaah (سبحانه وتعالى) bila ya kumshirikisha na chochote ni ujumbe walioulingania Rusuli wote kwa kaumu zao. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ ﴿٢٥﴾

Na Hatukutuma kabla yako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Rasuli yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana Muabudiwa wa haki ila Mimi; basi Niabuduni.” [Al-Anbiyaa (21: 25)]

 

Rejea pia: An-Nahl (16: 36), Al-‘Araaf (7: 59), (65), (73), (85), Al-‘Ankabuwt (29: 16), Al-Maaidah (5: 72).

 

 

 

5. Himizo na amri ya Waislamu kushikamana pamoja bila ya kufarikiana.

 

Rejea: Aal-‘Imraan (3: 103).

 

 

 

6. Chukizo na makatazo ya kuzungumza habari za uvumi, porojo n.k. Haya yanakutokana na uovu wa ulimi unaompelekea mtu katika ghiybah (kusengenya), namiymah (kufitinisha), n.k. Imesisitizwa kuuhifadhi ulimi mtu asitamke neno ila la kheri.

 

Rejea Hadiyth namba (37).

 

 

 

7. Makatazo ya kuuliza sana maswali au jambo ikiwa halina maana au halihitajiki, kuepusha mjadala na kupoteza muda wa Mwalimu.

 

 

 

8. Makatazo ya kupoteza mali katika njia zisizokubalika kishariy’ah na zisizomridhisha Allaah (سبحانه وتعالى), kama kufuja katika sherehe za harusi za kifakhari, ambazo watu kushindana na kujionyesha. Huu ni ubadhirifu Alioukataza Allaah (سبحانه وتعالى) na kusema kwamba wabadhirifu ni ndugu wa shaytwaan. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَآتِ ذَا الْقُرْبَىٰ حَقَّهُ وَالْمِسْكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ وَلَا تُبَذِّرْ تَبْذِيرًا ﴿٢٦﴾

 

Na mpe jamaa wa karibu haki yake, na masikini, na msafiri (aliyeharibikiwa); na wala usifanye ubadhirifu wa ufujaji mkubwa. 

 

إِنَّ الْمُبَذِّرِينَ كَانُوا إِخْوَانَ الشَّيَاطِينِ ۖ وَكَانَ الشَّيْطَانُ لِرَبِّهِ كَفُورًا ﴿٢٧﴾

 

Hakika wabadhirifu wamekuwa ni ndugu wa mashaytwaan, na shaytwaan amekuwa kwa Rabb wake ni mwingi wa kukufuru. [Al-Israa (17: 26-27)]

 

Rejea pia Al-Furqaan (25: 67).

 

 

 

9. Kutumia mali katika shughuli za bid’ah kama mawlid, matanga, khitmah n.k. ni kupoteza mali yake Muislamu na muda wake bure kwa ‘amali isiyokubaliwa.  

 

 

 

10. Muislamu anafaa afahamu kuwa mali ni amana kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى), hivyo basi asiitumie ovyo kwa sababu atasimama mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuulizwa vipi ameipata na vipi ameitumia:   

 

 

Hadiyth: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:

 

لا تزولُ قدَما عبدٍ يومَ القيامةِ حتَّى يُسألَ عن أربعٍ: ((عن عُمرِهِ فيمَ أفناهُ؟ وعن علمِهِ ماذا عمِلَ بهِ؟ وعن مالِهِ مِن أينَ اكتسبَهُ، وفيمَ أنفقَهُ؟ وعن جسمِهِ فيمَ أبلاهُ؟))

((Mguu wa mmoja wenu hautoweza kunyanyuka Siku ya Qiyaamah mpaka aulizwe mambo manne: Umri wake ameupitisha vipi; na elimu yake ameifanyia kazi vipi, mali yake ameipata na kuitumia vipi, na mwili wake ameutumia na kuuchakaa vipi))]. [At-Tirmidhiy kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) ameisahihisha Al-Albaaniy katika: Swahiyh At-Targhiyb (3592)]

 

 

 

Share

132-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Amelaaniwa Anayemwelekeza Nduguye Silaha

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 132

 

Amelaaniwa Anayemwelekeza Nduguye Silaha

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يُشِيرُ أَحَدُكُمْ عَلَى أَخِيهِ بِالسِّلاَحِ فَإِنَّهُ لاَ يَدْرِي لَعَلَّ الشَّيْطَانَ يَنْزِعُ فِي يَدِهِ فَيَقَعُ فِي حُفْرَةٍ مِنْ النَّارِ)) متفق عليه – وفي رواية لمسلم قال: قَالَ أبو الْقاَسِم (صلى الله عليه و آله وسلم): ((مَنْ أَشَارَ إِلَى أَخِيهِ بِحَدِيدَةٍ فَإِنَّ الْمَلآئِكَةَ  تَلْعَنُهُ حَتَّى يَدَعَهُ وَإِنْ كَانَ أَخَاهُ لإبِيهِ وَأُمِّهِ(( 

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mmoja wenu asimwelekezee silaha nduguye, kwani hajui pengine shaytwaan huenda akamshopoa katika mkono wake ikawa ndio sababu ya kuingia katika shimo la moto)). [Al-Bukhaariy na Muslim] Na katika riwaya nyingine: “Amesema Abul-Qaasim (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Atakayemwelekezea nduguye chuma [silaha], basi hakika Malaika wanamlaani mpaka aiondoshe, hata kama ni kaka yake kwa baba na mama)).  [Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kumwelekezea mtu silaha, kwani hivyo ni kumtishia mtu na kumkosesha amani na utulivu wa nafsi.

 

Rejea Hadiyth namba (94).

 

 

2. Makatazo haya hayapasi hata kwa asiyekuwa Muislamu ikiwa hana hatia yoyote, kwani huenda akamuua bila ya haki jambo lililoharamishwa.

 

Rejea Al-Mumtahinah (60: 8-9).

 

Bali kumuua mtu ataingizwa motoni, na atapata ghadhabu za Allaah, laana Yake, na adhabu kubwa kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى):

 وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ وَأَعَدَّ لَهُ عَذَابًا عَظِيمًا ﴿٩٣﴾

Na atakayemuua Muumini kwa kusudi, basi jazaa yake ni Jahannam, ni mwenye kudumu humo na Allaah Atamghadhibikia na Atamlaani na Atamuandalia adhabu kuu. [An-Nisaa (4: 93)]

 

 

3. Makatazo haya ni miongoni mwa madhambi makubwa kwa vile yanahusiana na laana za Malaika.

 

 

4. Mzaha katika kuleta madhara na kuhatarisha maisha ya mtu haukubaliki katika Shariy’ah ya Kiislamu.

 

 

5. Haipasi kubeba silaha bila ya kuwa na mahitaji nayo, kama upanga, kisu, kiwembe n.k.

 

 

6. Tahadharisho la vitimbi vya shaytwaan ambaye yuko tayari kumpotosha mtu aingie motoni kwa kila njia

 

Rejea Al-Hijr (15: 39), Al-A’raaf (7: 16-18).

 

 

7. Uislamu unalinda usalama na amani ya bin Aadam.

 

Rejea Hadiyth namba (93).

Share

133-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Makatazo Ya Kuvaa Hariri, Diybaaj (Hariri Iliyotariziwa) Na Kunywa Katika Vyombo Vya Dhahabu Na Fedha

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 133 

 

Makatazo Ya Kuvaa Hariri, Diybaaj (Hariri Iliyotariziwa)

Na Kunywa Katika Vyombo Vya Dhahabu Na Fedha

 

 

 

عَنْ حُذَيْفَة (رضي الله عنه) أنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ نَهَانَا عَنْ الْحَرِيرِ وَالدِّيبَاجِ وَالشُّرْبِ فِي آنِيَةِ الذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ, وَقَالَ: ((هُنَّ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا وَهِيَ لَكُمْ فِي الآَخِرَةِ)) متفق عليه. وفي رواية في الصحيحن عَنْ حُذَيْفَةُ  (رضي الله عنه) قَال: سَمِعْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((لاَ تَلْبَسُوا الْحَرِيرَ وَلاَ الدِّيبَاجَ ولاَ تَشْرَبُوا فِي آنِيَةِ الذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ وَلاَ تَأْكُلُوا فِي صِحَافِهَا((

 

Imepokelewa kutoka kwa Hudhayfah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم ) amekataza (kuvaa nguo za) Hariri, na diybaaj (hariri ya kimashariki iliyotariziwa) na kunywa katika vyombo vya dhahabu na fedha, akasema: ((Hivyo ni vyao [makafiri] duniani, navyo ni vyenu Aakhirah)). [Al-Bukhaariy na Muslim] Na katika riwaayah nyingine iliyopokelewa kutoka kwa Hudhayfah (رضي الله عنه) amesema: Nimemsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Msivae hariri wala diybaaj (hariri iliyotariziwa), wala msinywe katika vyombo vya dhahabu na fedha, wala msile katika sinia zake)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Diybaaj: ni aina ya hariri nzito iliyotariziwa kama makhmeli.

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la wanaume kuvaa hariri, kwa vile ni dalili ya kiburi, ufakhari na kujifananisha na makafiri. Ama wanawake wameruhusika kama walivyonukuu Ma’ulamaa.

 

 

2. Haramisho la kutumia vyombo vya kulia vya dhahabu na fedha, kwa vile ni dalili ya kiburi, na pia israfu ya mali.

 

Na Hadiyth pia imethibitisha haramisho hilo kwa onyo kali la moto wa Jahannam:

 

وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ الْلَّهُ عَنْهَا، قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ الْلَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏:(( الَّذِي يَشْرَبُ فِي إِنَاءِ الْفِضَّةِ إِنَّمَا يُجَرْجِرُ فِي بَطْنِهِ نَارَ جَهَنَّمَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ 

Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika anayekunywa katika vyombo vya fedha anameza moto wa Jahannam tumboni mwake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

3. Haramisho la wanaume kuvaa dhahabu ila pete ya fedha wanaruhusiwa. Ama wanawake, wao wameruhusiwa kuvaa dhahabu za kiasi na wachunge kuzilipia Zakaah.

 

 

4. Makatazo ya kuvaa hariri na kutumia dhahabu na fedha ni miongoni mwa madhambi makubwa kwa vile yameahidiwa adhabu kali ya moto Hadiyth: ((Anayekunywa katika chombo cha fedha, hakika anagogomoa [anasukutua mpaka kooni] tumboni mwake moto wa Jahannam))]. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

5. Muislamu anapaswa atamani starehe za Aakhirah zilizoahidiwa Aakhirah kuliko starehe za duniani ambazo ni za wakati tu.  

Rejea Hadiyth namba (57), (58), (60), (61).

 

Kutamani starehe za Aakhirah na kuipa mgongo dunia ni katika sifa ya ‘zuhd’ apasayo kuwa nayo Muumin.

 

Rejea Hadiyth namba (59).

 

 

6. Aayah nyingi zimetaja starehe za watu wa Jannah kwamba huko watakuwa wanatumia vyombo vyao vya dhahabu, fedha na mapambo ya hariri, lulu n.k. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا عِبَادِ لَا خَوْفٌ عَلَيْكُمُ الْيَوْمَ وَلَا أَنتُمْ تَحْزَنُونَ﴿٦٨﴾

 “Enyi waja Wangu! Hakuna khofu juu yenu leo, na wala nyinyi hamtohuzunika.”

 

الَّذِينَ آمَنُوا بِآيَاتِنَا وَكَانُوا مُسْلِمِينَ﴿٦٩﴾

“Ambao wameamini Aayaat Zetu na wakawa Waislamu.”

 

ادْخُلُوا الْجَنَّةَ أَنتُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ تُحْبَرُونَ﴿٧٠﴾

Ingieni Jannah nyinyi na wake zenu mfurahishwe.

 

 

يُطَافُ عَلَيْهِم بِصِحَافٍ مِّن ذَهَبٍ وَأَكْوَابٍ ۖ وَفِيهَا مَا تَشْتَهِيهِ الْأَنفُسُ وَتَلَذُّ الْأَعْيُنُ ۖ وَأَنتُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴿٧١﴾

Watapitishiwa sahani za dhahabu na bilauri, na humo mna yale yanayotamani nafsi na ya kuburidisha macho, nanyi humo ni wenye kudumu.

 

وَتِلْكَ الْجَنَّةُ الَّتِي أُورِثْتُمُوهَا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٧٢﴾

Na hiyo ni Jannah ambayo mmerithishwa kwa yale mliyokuwa mkitenda.

 

لَكُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ كَثِيرَةٌ مِّنْهَا تَأْكُلُونَ﴿٧٣﴾

Mtapata humo matunda mengi mtakayokuwa mnakula. [Az-Zukhruf: 68-73]

 

Rejea pia: Al-Kahf (18: 30-31), Al-Hajj (22: 22-23), Asw-Swaaffaat (37: 40-49), Ad-Dukhaan (44: 51-57), Muhammad (47: 15), Atw-Twuwr (52: 17-24), Ar-Rahmaan (55: 46-77), Al-Waaqi’ah (56: 14-40), Al-Insaan (76: 11-22),  An-Nabaa (78: 31-37), Al-Ghaashiyah (88: 8-16).

 

 

 

7. Muislamu anapasa kujiepusha na kila jambo linalotendwa na makafiri kama Anavyotahadharisha Allaah (سبحانه وتعالى) Rejea Al-Baqarah (2: 120).

 

 

Na inampasa Muislamu kushikamana na mila na desturi za Kiislamu

 

Share

134-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Makatazo Ya Kujishabihisha Na Makafiri

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 134

 

Makatazo Ya Kujishabihisha Na Makafiri

 

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أنَّ رَسُول اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قال: ((إنَّ اليَهُودَ وَالنَّصَارى لاَ يَصْبغُونَ، فَخَالِفُوهُمْ))  متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika Mayahudi na Manaswara hawapaki rangi, wakhalifuni)).  [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

Maana yake: Ni kupaka rangi mvi za ndevu na mvi za nywele kichwani kwa rangi manjano au nyekundu. Ama kupaka rangi nyeusi, imekatazwa kama ilivyothibiti dalili yake katika Hadiyth iliyopokelewa na Muslim

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Pendekezo la kupaka rangi ili kuficha mvi kwa rangi ya manjano au nyekundu. Kutumia hinna ni bora zaidi, kwani ni Sunnah ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم). Juu ya hivyo, ni mada asili na kawaida na haileti madhara.

 

 

2. Makatazo ya kupaka rangi nyeusi ni kwa wanaume na wanawake, kwani hiyo inakuwa ni ghushi.

 

 

 

3. Kujiepusha kujifananisha na makafiri katika matendo yao kama mavazi yao, na kujipamba kwao.

 

Rejea Hadiyth namba (113), (115), (116).

 

 

4. Makatazo ya kujifananisha na makafiri katika kila jambo, na hivyo pia ni kutokufuata mila zao ambazo zimekuwa ni kigezo kwa Waislamu wengi wasiojua uovu wake au ambao bado hawataki kuacha maovu hayo. Mfano kusherehekea au kukubali mialiko ya sikukuu zao kama Krismasi, Mwaka mpya wa Kikristo na wa Hijri (wa Kiislamu), Pasaka, kusherehekea Siku ya Wajinga (April Fool), Siku ya mama (Mother’s day), Siku ya wapendanao (Valentine), Siku ya kuzaliwa (Birthday), n.k.

 

 

5. Kujifananisha na makafiri katika sherehe zao ni miongoni mwa madhambi makubwa, kwani humo wanamshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى). Na Allaah (سبحانه وتعالى) Ameonya kufuata au kutaka mila yaani Dini zao. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَن تَرْضَىٰ عَنكَ الْيَهُودُ وَلَا النَّصَارَىٰ حَتَّىٰ تَتَّبِعَ مِلَّتَهُمْ ۗ  

Na hawatoridhika nawe Mayahudi wala Manaswara mpaka ufuate mila zao.  [Al-Baqarah (2: 120)]

 

 

Na pia rejea: Aal-'Imraan (3: 85).

 

 

6. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) pia ameonya kuwafuata na kujifananisha na makafiri. Hadiyth: ((Kuweni kinyume na Washirikina, punguzeni masharubu na fugeni ndevu)). [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

Pia amesema (صلى الله عليه وآله وسلم) ((Mtafuata nyendo za wale waliokuja kabla yenu hatua kwa hatua mpaka itafika wakiingia katika shimo la kenge, na nyinyi mtaingia pia)) Wakasema (Maswahaba): Ee Rasuli wa Allaah! Je, unamaanisha Mayahudi na Manaswara?  Akasema: ((Hivyo nani basi mwengine?)). [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

Na pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Anayejishabihisha na watu, basi naye ni miongoni mwao)). [Ahmad na Abu Daawuwd]

 

 

7. Shakhsiya ya Muislamu ni makhsusi katika kufuata maamrisho ya Dini yake, mavazi yake, adabu zake, kuandamana kwake na marafiki, na anapaswa kufuata Sunnah za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) wala haipasi kuwafuata wasio Waumini katika ada na mila zao.

 

 

 

Share

135-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Makatazo Ya Kustanji Na Kugusa Uchi Kwa Mkono Wa Kulia

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 135  

 

Makatazo Ya Kustanji Na Kugusa Uchi Kwa Mkono Wa Kulia

 

 

 

عَنْ أَبِي قَتَادة (رضي الله عنه) عن النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قال: ((إذا بَالَ أَحَدُكُمْ فَلا يَأْخُذَنَّ ذَكَرَهُ بِيَمِينِهِ وَلاَ يَسْتَنْجِ بِيَمِينِهِ وَلاَ يَتَنَفَّسْ فِي الإِنَاءِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abu Qataadah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Anapokojoa mmoja wenu, asiishike kabisa dhakari yake [uchi wake] kwa mkono wake wa kulia, wala asistanji kwa mkono wake wa kulia, wala asipumue katika chombo)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Chukizo la kutumia mkono wa kulia wakati wa kustanji, kwani mkono huo wa kulia unatumika kwa kulia chakula. Amekataza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Hadiyth nyengineyo:

 

عن سَلْمَانَ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: لَقَدْ نَهَانَا رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏ "أَنْ نَسْتَقْبِلَ اَلْقِبْلَةَ بِغَائِطٍ أَوْ بَوْلٍ، أَوْ أَنْ نَسْتَنْجِيَ بِالْيَمِينِ، أَوْ أَنْ نَسْتَنْجِيَ بِأَقَلَّ مِنْ ثَلَاثَةِ أَحْجَارٍ، أَوْ أَنْ نَسْتَنْجِيَ بِرَجِيعٍ أَوْ عَظْمٍ" رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Salmaan (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alitukataza kuelekea Qiblah wakati wa kwenda haja kubwa au ndogo, wala tusijisafishe kwa mkono wa kulia, au kujisafisha kwa mawe yasiyotimia matatu, au kujisafisha kwa kinyesi cha wanyama au mfupa.” [Imetolewa na Muslim]

Makatazo hayo yanawahusu wanaume na wanawake sawasawa.

 

Rejea Hadiyth namba (33).

 

 

2. Inaruhusiwa kustanji kwa mkono wa kulia kwa dharura. Mfano anapokuwa mtu ameumia mkono wa kushoto, au amekatazwa kutumia maji kutokana na madhara fulani ya kiafya au ugonjwa au kidonda.

 

 

3. Makatazo ya kupumua katika chombo anachonywea maji mtu. Hii imethibitika katika sayansi madhara yake kwamba viini vya maradhi huingia katika chombo vikamsababishia mtu magonjwa.

 

 

4. Uislamu umetahadharisha kila jambo linalopelekea katika uovu na maasi, na umefunza na kuhimiza siha na afya ya mtu kwa ujumla.

 

 

5. Uislamu umefunza tabia na maadili mema kabisa ya kutumia mkono wa kulia kwa ajili ya mambo mazuri na yenye utukufu kama kula, kunywa, kuandika, kuamkiana, kuvaa nguo, viatu, kutoka msalani (chooni), kumdhukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kwa tasbiyh baada ya Swalaah, kulala pia iwe kwa ubavu wa kulia n.k. Ama mkono na mguu wa kushoto utumike kwa mambo ya kinyume chake, kama kuingia chooni, kujisafisha tupu, kuokota uchafu, kuubeba n.k.

 

 

 

 

Share

136-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kutabiri Ya Ghayb Kwa Kupiga Fali (Rajua Mbaya) Kutokana Na Tukio Fulani Ni Shirki

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 136

 

Kutabiri Ya Ghayb Kwa Kupiga Fali (Rajua Mbaya)

Kutokana Na Tukio Fulani Ni Shirki

 

 

 

 

عنْ عُرْوَةَ بْنِ عامِرِ (رضي الله عنه) قال: ذُكِرتِ الطَّيَرَةُ عِنْد رَسُولِ اللَّه صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فقَالَ: ((أحْسَنُهَا الْفَألُ، وَلا تَرُدُّ مُسْلِماً، فَإذا رأى أحَدُكُمْ ما يَكْرَه، فَلْيقُلْ: اللَّهُمَّ لا يَأتى بالحَسَناتِ إلاَّ أنتَ، وَلا يَدْفَعُ السَّيِّئاتِ إلاَّ أنْتَ، وَلا حوْلَ وَلا قُوَّةَ إلاَّ بك)) حديثٌ صَحيحٌ رَوَاهُ أبو داودُ بإسنادٍ صَحيحٍ

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Urwah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) amesema: Ilitajwa habari ya kupiga fali mbaya (mkosi) mbele ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ilio bora zaidi ni kupiga fali nzuri, wala [kupiga fali mbaya] haimrudishi Muislamu [kutokutenda aliloazimia]. Mmoja wenu atakapoona analochukia, aseme: “Allaahumma laa yaa-tiy bil-hasanaat illaa Anta, walaa yadfa’us-sayyiaat illa Anta, walaa hawla walaa quwwata illaa Bika - Ee Allaah, hakuna anayeweza kuleta mambo mema isipokuwa ni Wewe, wala hakuna anayeweza kukinga mabaya isipokuwa ni Wewe. Hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kutoka Kwako)) [Hadiyth Swahiyh ameipokea Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Maana ya twayr (ndege) ni  kupiga fali.

 

 

Wakati wa ujahiliya, Waarabu walikuwa wakichukua ndege (طير) na humtumilia kuonyesha ishara nzuri au mbaya. Mfano wanapotaka kusafiri humrusha ndege yule, akiruka upande wa kulia, basi wanaamini kuwa ni safari ya salama, na kama akiruka upande wa kushoto, basi huwa hawasafiri. Uislamu umekuja na kuondoa shirki kama hiyo kama alivyotukataza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Hadiyth kadhaa, miongoni mwa hizo ni:   

 

 

عَنْ أَنَسٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لَا عَدْوَى وَلَا طِيَرَةَ وَيُعْجِبُنِي الْفَأْلُ))  قَالُوا:  وَمَا الْفَأْلُ؟ قَالَ: ((الْكَلِمَةُ الطَّيِّبَةُ))

Kutoka kwa Anas (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakuna ‘adwaa wala hakuna twiyarah [itikadi ya kutabiri mkosi, nuksi] na inanipendekeza Al-Fa-l)) Wakauliza: Nini Al-Fa-lu? Akajibu: ((Neno zuri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na pia:

 

عن ابْنِ مَسْعُودٍ مَرْفُوعًا: ((الطِّيَرَةُ شِرْكٌ، الطِّيَرَةُ شِرْكٌ، وَمَا مِنَّا إِلاَّ وَلَكِنَّ اللَّهَ يُذْهِبُهُ بِالتَّوَكُّلِ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَالتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ. وَجَعَلَ آخِرَهُ مِنْ قَوْلِ ابْنِ مَسْعُودٍ

Na kutoka kwa Ibn Mas’uwd ni Hadiyth Marfuw’: ((Atw-Twiyarah [itikadi ya kutabiri nuksi, mikosi n.k] ni shirki, Atw-Twiyarah ni shirki. Na hakuna yeyote miongoni mwetu asiyehisi jambo moyoni [Kuhusu Atw-Twiyarah] lakini Allaah Huiondoa kwa kutawakali Kwake)) [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth hii Hasan Swahiyh] Na imetajwa kwamba kauli ya mwisho ni ya Ibn Mas’uwd.

 

Pia Hadiyth: 

 

((Hakuna mkosi, na ni bora tegemea khayr [matumaini mema])). Wakauliza nini matumaini mema (matarajio ya kufanikiwa) ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Ni neno jema alisikialo mmoja wenu)) [Al-Bukhaariy]

 

 

2. Kubashiria jambo la ghayb ni miongoni mwa madhambi makubwa, kwani ni kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qadhwaa na Qadar Yake. (Yaliyohukumiwa na Yaliyokadiriwa).

 

 

3 Muislamu awe na iymaan ya kutambua kwamba hakuna yeyote au lolote litakaloweza kumdhuru isipokuwa lile lililokwishaandikwa.

 

Rejea Hadiyth namba (6).

 

Pia

 

 

عن ابنِ عباسٍ رضي الله عنهما، قَالَ: كنت خلف النَّبيّ صلى الله عليه وسلم يومًا، فَقَالَ: ((يَا غُلامُ، إنِّي أعلّمُكَ كَلِمَاتٍ: احْفَظِ اللهَ يَحْفَظْكَ، احْفَظِ اللهَ تَجِدْهُ تُجَاهَكَ، إِذَا سَألْتَ فَاسأَلِ الله، وإِذَا اسْتَعَنْتَ فَاسْتَعِنْ باللهِ. وَاعْلَمْ: أنَّ الأُمَّةَ لَوْ اجْتَمَعَتْ عَلَى أنْ يَنْفَعُوكَ بِشَيءٍ لَمْ يَنْفَعُوكَ إلا بِشَيءٍ قَدْ كَتَبهُ اللهُ لَكَ، وَإِن اجتَمَعُوا عَلَى أنْ يَضُرُّوكَ بِشَيءٍ لَمْ يَضُرُّوكَ إلا بِشَيءٍ قَدْ كَتَبَهُ اللهُ عَلَيْكَ، رُفِعَتِ الأَقْلاَمُ وَجَفَّتِ الصُّحفُ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن صحيح)).

 

Imepokelewa kutoka kwa ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema: “Siku moja nilikuwa nyuma ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akaniambia: ((Ee Ghulamu! [Kijana] nitakufundisha maneno [ya kufaa]; Mhifadhi Allaah [fuata maamrisho Yake na chunga Mipaka Yake] Atakuhifadhi.  Muhifadhi Allaah na utamkuta mbele yako. Ukiomba, muombe Allaah, ukitafuta msaada, tafuta kwa Allaah. [Lazima] ujue kuwa ikiwa taifa zima litaungana kukunufaisha wewe kwa kitu, basi hutonufaika ila tu kwa kile Alichokwisha kukuandikia Allaah. Na wakikusanyika kukudhuru kwa chochote, hutodhurika ila tu kwa kile Allaah Alichokwisha kukuandikia [kuwa kitakudhuru], kwani kalamu zimeshanyanyuliwa [kila kitu kishaandikwa] na sahifa zimeshakauka [Hakuna kupangwa tena wala kupanguliwa]) [Ahmad na at-Tirmidhiy]

 

 

 

4. Hata Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuwa na uwezo wa kujikinga na dhara au kujua ya ghayb. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُل لَّا أَمْلِكُ لِنَفْسِي نَفْعًا وَلَا ضَرًّا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ ۚ وَلَوْ كُنتُ أَعْلَمُ الْغَيْبَ لَاسْتَكْثَرْتُ مِنَ الْخَيْرِ وَمَا مَسَّنِيَ السُّوءُ ۚ إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ وَبَشِيرٌ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ﴿١٨٨﴾

Sema: “Siimilikii nafsi yangu manufaa yoyote wala dhara yoyote isipokuwa Apendavyo Allaah. Na lau ningekuwa najua ya ghayb, bila shaka ningelijikithirishia ya kheri, na wala lisingelinigusa ovu. Mimi si chochote isipokuwa ni mwonyaji na mbashiriaji kwa watu wanaoamini.” [Al-A’raaf (7: 188)]

 

Rejea pia:  Al-An’aam (6: 50), (59), An-Naml (27: 65).

 

 

5. Baada ya Uislamu, shirki ya aina hii pia hutendeka ingawa si ya kutumia ndege, bali kubashiria ya ghayb kutokana na tendo fulani na kulihusisha na mkosi au nuksi. Mifano ifuatayo inayojulikana:

 

 

(a) Jicho likimpiga mtu upande wa kushoto husema ni shari hiyo inakuja.

 

 

(b) Akimuona mtu paka mweusi, basi siku hiyo itakuwa ni ya ukorofi.

 

(c) Mkono ukimuwasha mtu anasema pesa.

 

(d) Akifagia usiku anaondoa baraka.

 

(e) Akipaliwa mtu, husema kuwa mtu anamtaja.

 

(f) Akikata kucha zote pamoja (ya mikono na miguu) ina maana kwamba shida zikija zitakuja zote pamoja n.k!

 

Hivyo Muislamu anapaswa kuacha itikadi za kidhana kama hizi, kwani khatari yake zinapelekea kwenye kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) na mafikio yake ni makazi ya moto.

 

 

6.Kubashiria ya ghayb ni sawa na mtabiri, na pindi Muislamu akiamuamini anayoyatabiri, basi hukutoka nje ya Uislamu.

 

Rejea Hadiyth namba (119).

 

 

Share

137-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Viumbe Waovu Kabisa Wajengao Misikiti Katika Makaburi Ya Waja Wema Wakachora Picha Zao

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 137

  

Viumbe Waovu Kabisa Wajengao Misikiti Katika

Makaburi Ya Waja Wema Wakachora Picha Zao

 

 

 

عَنْ عَائِشَةَ (رضي الله عنها) قَالَتْ:  لَمَّا اشتَكَى النَبي صلى الله عليه وسلم  ذَكَرَ بعْضُ نِسَائِهِ كَنِيسَة رَأتْهَا بأرض الحَبَشةِ يُقَالُ لَهَا "مَارِيَةُ"  وَكَانَتْ أُمُّ سَلَمَةَ وَأمُّ حَبيبَةَ أتتا أرْضَ الحَبَشَةَ،  فَذَكَرَتَا من حُسْنِهَا وَتَصَاوير فِيهَا، فَرَفَعَ رَأسَهُ صلى الله عليه وسلم وَقالَ: ((أولئِكَ إِذَا مَاتَ فِيهِم الرَّجُلُ الصالح  بَنَوْا عَلَى قَبْرِهِ مَسْجِداً ثُمَّ صَورُوا فِيهِ تِلْكَ الصُّورَ، أولئِكَ شِرَارُ الْخَلْقِ عِنْدَ الله)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها)   amesema: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipougua, mmoja katika wakeze alitaja kanisa aliloliona katika nchi ya Uhabashi liitwalo ‘Maariyah’. Ummu Salamah na Ummu Habiybah walikuwa wamewahi kwenda nchi ya Uhabashi. Wakataja uzuri wake na picha zilizokuwa humo. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akakiinua kichwa chake akasema: ((Hao, anapokufa mwema miongoni mwao, hujenga Msikiti juu ya kaburi lake. Kisha wakazichora ndani yake picha hizo. Hao ni viumbe waovu mbele ya Allaah)). [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Haramisho la kujenga Misikiti katika makaburi, kwani ni kushabihiana na makafiri na hivyo ni shirki kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) katika Hadiyth: Imepokelewa kutoka kwa Jundub bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه)  amesema: “Nilimsikia Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) kabla hajaondoka duniani kwa siku tano akisema: ((Fahamuni! Hakika waliokuwa kabla yenu walikuwa wakiyafanya makaburi ya Manabii wao ni Misikiti. Fahamuni! Msiyafanye makaburi ni Misikiti, hakika mimi nawakataza jambo hilo)). [Muslim]

 

 

2. Kutembelea makaburi ya waja wema kwa kutufu kaburini mwake au kuligusa na kujipangusa, na kuwaomba ni bid’ah (uzushi) na miongoni mwa shirki kubwa, kwani ni kuitakidi kuwa waja wema hao wana uwezo wa kuwanufaisha na kuwadhuru na hali hakuna awezaye hayo isipokuwa Allaah (سبحانه وتعالى). Anasema (سبحانه وتعالى):   

 

 يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَضُرُّهُ وَمَا لَا يَنفَعُهُ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الضَّلَالُ الْبَعِيدُ ﴿١٢﴾

Humwomba badala ya Allaah ambavyo visivyomdhuru na wala visivyomnufaisha. Huo ndio upotofu wa mbali.

 

يَدْعُو لَمَن ضَرُّهُ أَقْرَبُ مِن نَّفْعِهِ ۚ لَبِئْسَ الْمَوْلَىٰ وَلَبِئْسَ الْعَشِيرُ ﴿١٣﴾

Humwomba yule ambaye dhara yake iko karibu kuliko manufaa yake. Bila shaka ni mlinzi muovu kabisa, na bila shaka ni rafiki muovu kabisa. [Al-Hajj (22: 12-13)]

 

 

Rejea pia: Al-A’raaf (7: 194, 197), Al-Israa (17: 56),  Sabaa (34: 22), Yuwnus (10: 18, 106-107), Al-‘Ankabuwt (29: 17).  

 

 

3. Kuwatukuza wafu katika makaburi yao na kuwafanyia ‘ibaadah ni katika ujahili unaofanana na washirikina wa Makkah waliokuwa wakitoa hoja zao kuwa hawakuwa wakiwaabudu bali ni kujikurubisha kwa Allaah: Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):  

  وَالَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ

Na wale waliojichukulia badala Yake walinzi (wakisema): “Hatuwaabudu isipokuwa ili wapate kutukurubisha kwa Allaah tumkaribie. [Az-Zumar (39: 3)]

 

 

 

4. Swalaah mbele ya kaburi ni haraam, ikiwa ni katika Msikiti au mbali na Msikiti.

 

 

5. Wanaodai kuwa kaburi la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) liko katika Msikiti ni kutokufahamu hali halisi ilivyokuwa ya kwamba:

 

(i) inajulikana kuwa Msikiti wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ulijengwa kabla ya kufariki kwake, kwa hiyo haukujengwa katika kaburi lake.

 

(ii) Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuzikwa katika Msikiti wake, bali alizikiwa nyumbani kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها) nyumba ambayo ilitengana na Msikiti. Ila kosa lilitokea wakati Msikiti ulipopanuliwa mwisho wa karne ya kwanza, ulipobomolewa na kujengwa upya na kupanuliwa ndipo vyumba vya wake zake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) vilipoingia katika eneo la Msikiti na ndani ya moja ya vyumba ndipo lilipo kaburi la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  na kwa sababu pia haifai kuvunjwa kaburi lake au kufukuliwa na kuhamishwa.

Rejea Hadiyth namba (83), (129).

 

 

6. Haramisho la kuchora picha za viumbe wenye roho.

 

Rejea Hadiyth namba (120).

 

 

7. Mwenye kutenda mambo hayo mawili; kujenga Misikiti kaburini na kuchora picha ni kiumbe mwovu kabisa mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) kutokana na sababu zake zilizotajwa na kukatazwa.

 

 

8. Hima kubwa ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwafunza Waumini yasiyopasa kutendwa kama shirki ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) haisamehi ikiwa mtu hakurudi kutubia. Hakuweza kuvumilia kusikia maovu, na akatoa nasiha hapohapo juu ya kuwa alikuwa anaugua.

 

 

9. Nasiha hizo za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ni miongoni mwa nasiha za mwisho katika uhai wake.

 

Share

138-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Haramisho La Kuomboleza Zaidi Ya Siku Tatu

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 138

 

Haramisho La Kuomboleza Zaidi Ya Siku Tatu

 

 

 

عَنْ زَيْنَبَ بِنْتِ أَبِي سَلَمَةَ  (رضي الله عنهما) قَالَتْ: دَخَلْتُ عَلَى أُمِّ حَبِيبَةَ (رضي الله عنها) زَوْجِ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ حِينَ تُوُفِّيَ أَبُوهَا أَبُو سُفْيَانَ بْنُ حَرْبٍ، فَدَعَتْ بِطِيبٍ فِيهِ صُفْرَةُ خَلُوقٍ، أَوْ غَيْرِهِ،  فَدَهَنَتْ مِنْهُ جَارِيَةً، ثُمَّ مَسَّتْ بِعَارِضَيْهَا . ثُمَّ قَالَتْ: وَاللَّهِ مَا لِي بِالطِّيبِ مِنْ حَاجَةٍ غَيْرَ أَنِّي سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، يَقُولُ عَلَى الْمِنْبَرِ: ((لا يَحِلُّ لامْرَأَةٍ تُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ أَنْ تُحِدَّ عَلَى مَيِّتٍ فَوْقَ ثَلاثِ لَيَالٍ، إِلا عَلَى زَوْجٍ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا)) قَالَتْ زَيْنَبُ: فَدَخَلْتُ عَلَى زَيْنَبَ بِنْتِ جَحْشٍ (رضي الله عنها) حِينَ تُوُفِّيَ أَخُوهَا، فَدَعَتْ بِطِيبٍ فَمَسَّتْ مِنْهُ ثُمَّ قَالَتْ: أَمَا وَاللَّهِ مَا لِي بِالطِّيبِ مِنْ حَاجَةٍ غَيْرَ أَنِّي سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ عَلَى الْمِنْبَرِ: ((لا يَحِلُّ لامْرَأَةٍ تُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ أَنْ تُحِدَّ عَلَى مَيِّتٍ فَوْقَ ثَلاثِ لَيَالٍ إِلاَّ عَلَى زَوْجٍ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Zaynab bin Abiy Salamah (رضي الله عنهما) amesema: “Niliingia kwa Ummu Habiybah (رضي الله عنها) mkewe Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipofiliwa na baba yake Abuu Sufyaan bin Harb. Akaitisha manukato manjano au manukato ya aina nyingine. Akampaka mjakazi wake na akajipaka mashavuni. Kisha akasema: “Wa-Allaahi sikuwa na haja ya kujipaka manukato isipokuwa nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema juu ya mimbari: ((Si halali kwa mwanamke anayemwamini Allaah na Siku ya Mwisho kumuombolezea maiti zaidi ya siku tatu, isipokuwa amkalie mumewe (eda) miezi minne na siku kumi)). Zaynab akasema: Kisha nikamwendea Zaynab bint Jahshi (رضي الله عنها) alipofiliwa na ndugu yake. Akaitisha manukato, akajipaka kisha akasema: “Wa-Allaahi sikuwa na haja ya manukato, isipokuwa nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Si halali kwa mwanamke anayemwamini Allaah na Siku ya mwisho kumuombolezea maiti zaidi ya siku tatu, isipokuwa amkalie mumewe (eda) miezi minne na siku kumi)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

 

1. Makatazo ya kuomboleza aliyefiwa zaidi ya siku tatu, kwani hivyo ni kinyume na Shariy’ah ya Dini yetu.

 

 

 

2. Ukamilifu wa iymaan kutokana na kauli ((…anayemwamini Allaah na Siku ya mwisho…)) ni kufuata amri hiyo ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kutokuomboleza zaidi ya siku tatu.  

 

 

 

3. Muda wa msiba katika Uislamu usizidi siku tatu, na mtu anaweza kujizuia na kustahamili hata siku moja inatosha kuomboleza, na hali hiyo inathibitisha iymaan ya hali ya juu ya kukubali Qadhwaa na Qadar (Yaliyohukumiwa Na Yaliyokadiriwa).

 

 

 

4. Hakuna katika mapokezi kunakoashiria kuwa wanaume wanaomboleza au wanakaa masiku kufanya maombolezi, hayo ni mambo ya wanawake kwa sababu ya maumbile yao na udhaifu wao wa kuhimili, hivyo Shariy’ah ikawaruhusu wanawake waomboleze lakini isizidi siku tatu. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alifiliwa na wanawe na ‘ami zake na jamaa zake wengine lakini hakuwahi kufanya maombolezi au kutenga masiku ya kuomboleza.

 

 

5. Ilivyo katika Sunnah, ni kumtayarishia chakula mfiwa ili awe katika mapumziko wakati wa huzuni. Hivyo ndivyo alivyoamrisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipofariki Ja’far (رضي الله عنه) katika vita vya Tabuwk, akasema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Watengenezeeni familia ya Ja'far chakula, kwani wamefikwa na jambo lenye kuwashughulisha))  [Abuu Daawuwd na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Abaaniy katika Ahkaam Al-Janaaiz.

 

 

 

6. Shariy’ah ya eda ya mwanamke aliyefiwa na mumewe ni miezi minne na siku kumi. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 وَالَّذِينَ يُتَوَفَّوْنَ مِنكُمْ وَيَذَرُونَ أَزْوَاجًا يَتَرَبَّصْنَ بِأَنفُسِهِنَّ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا ۖ فَإِذَا بَلَغْنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا فَعَلْنَ فِي أَنفُسِهِنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۗ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٢٣٤﴾

Na wale wanaofishwa miongoni mwenu na wakaacha wake, hao wake wangojee peke yao (eda) miezi minne na siku kumi. Watakapofikia muda wao, si dhambi kwao katika yale waliyoyafanya katika nafsi zao kwa ada ya shariy’ah. Na Allaah kwa yale myatendayo ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-Baqarah (2: 234)]

 

 

7. Kumkalia aliyefiwa matanga ni kumkalifisha kwa kila upande; wasaa wake wa kupumzika, faragha yake, kuwahudumia na kutumia mali yake kwa mambo yasiyopasa. Imekuwa ada ovu katika jamii kumkalia matanga mfiwa, kisha husababisha kutendwa mambo ya bid'ah kama kusoma Khitmah au nyiradi kwa pamoja, mazungumzo ya siasa, mipira, upuuzi wa kidunia, kusengenyana na kucheza karata, dumna, na wengine kula mirungi, kuvuta sigara na mengineo ya haraam.

 

 

8. Anayefiwa anatakiwa awe na iymaan ya mafunzo ya Dini yake na awe na msimamo. Asijali kuambiwa kuwa hamthamini mtu wake aliyefariki kwa kutokuweka matanga kama ilivyokuwa ni itikadi ya baadhi ya watu.

 

 

 

Share

139-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Kujiepusha Na Aliyoyaharamisha Allaah

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 139

 

Kujiepusha Na Aliyoyaharamisha Allaah

 

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّهُ قَالَ: ((إِنَّ اللَّهَ يَغَارُ وَغَيْرَةُ اللَّهِ أَنْ يَأْتِيَ الْمُؤْمِنُ مَا حَرَّمَ اللَّه)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Hakika Allaah Ana hisia ya  ghera, na ghera  ya  Allaah [inachomoza] pale mtu anapofanya [maasi] Aliyoyaharamisha Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Amesema Shaykh Muhammad bin Swaalih bin ‘Uthaymiyn (رحمه الله): “Ghera ni sifa ya hakika ya Allaah (سبحانه وتعالى) lakini si ghera kama ghera yetu, bali Yake ni kubwa na tukufu zaidi. Na Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Hikma Yake, Amewajibisha kwa waja Wake mambo fulani na Ameharamisha mengine. Aliyowajibisha ni khayr kwao kwa ajili ya Dini yao na dunia yao, kwa   ukaribu wao na mustakbali wao. Na Aliyowaharamishia ni shari kwao kwa ajili ya Dini yao na dunia yao, kwa ukaribu na mustakbali wao. Hivyo basi, Anapoharamisha jambo, Allaah (سبحانه وتعالى) Huwa na ghera pale mtu anapoenda kutenda maharamisho Yake. Na vipi mja ayaendee Aliyoyaharamisha Allaah (سبحانه وتعالى) na hali Ameyaharamisha kwa ajili ya maslahi ya mja? Pamoja na kuwa hakuna madhara kwa Allaah (سبحانه وتعالى) pale mwana Aadam anapomuasi, lakini Allaah Ana ghera, kwa kuwa vipi mwana Aadam anajua kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) ni Al-Hakiym (Mwenye Hikma), na Ar-Rahiym (Mwenye Kurehemu), na wala Haharamishi jambo kwa sababu tu ya kumkosesha asilipate, bali kwa ajili ya maslahi yake, kisha anakuja  mja  akamuasi   Allaah (سبحانه وتعالى) kwa maasi? Seuze basi aje kutenda zinaa? Tunamuomba Allaah (سبحانه وتعالى) Al-‘Aafiyah, kwani Rasuli (صلى الله عليه وآله وسلم) amethibitisha kwa kusema: ((Hakuna mwenye ghera zaidi ya Allaah wakati anapozini mja wake au ummah Wake uzini)) [Al-Bukhaariy]

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Ameharamisha kwa waja Wake zinaa na Amekusanya hilo katika kauli Yake:

 

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

Na wala msiikaribie zinaa. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya kabisa.  [Al-Israa (17: 32)]  

 

 

Kwa hiyo mja anapozini, Allaah (سبحانه وتعالى) Huwa na ghera kali na tukufu kuliko ghera ya mja. Hali kadhalika kuyaendea maasi kama liwati ya kaumu Luutw.

 

Rejea: Al-A’raaf (7: 80).

 

Pia kuiba, kunywa pombe, kula haraam na kadhalika. Yote Allaah (سبحانه وتعالى) Huwa na ghera nayo…” [Sharhu Riyaadhwis-Swaalihiyn ya Ibn ‘Uthaymiyn]

 

 

 

2. Hadiyth hii ni miongoni mwa ‘Jawaami’ul-Kalim’ (Mjumuisho wa maana nyingi katika maneno machache) aliyopewa  Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), kwani imekusanya maharamisho yote yanayojulikana katika Shariy’ah ya Kiislamu. Na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى) imethibitisha:

 

وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ﴿٧﴾

Na lolote analokupeni Rasuli ((صلى الله عليه وآله وسلم basi lichukueni, na analokukatazeni, basi acheni. Na mcheni Allaah. Hakika Allaah ni Mkali wa kuakibu.  [Al-Hashr (59: 7)]

 

 

 

3. Hadiyth hii inathibitishia kuwa ghera ni miongoni mwa Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى), na itikadi ya Ahlus-Sunnah wal-Jamaa’ah kwamba Sifa Zake zinazomuelekea Yeye Pekee kwa Dhati Yake na si kama sifa za bin Aadam kama Anavyosema Mwenyewe Allaah (سبحانه وتعالى):

 

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ﴿١١﴾

Hakuna chochote kinachofanana Naye, Naye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ash-Shuwraa (42: 11)]

 

 

 

4. Muislamu anapaswa kujiepusha na maharamisho yote ya Allaah (سبحانه وتعالى) na yaliyokuja katika Sunnah za Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) khasa maasi makubwa kama kumshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kila njia, kuzini, liwati, kuua bila ya haki, kuiba, kula ribaa, kutoa shahada ya uongo n.k. Allaah (سبحانه وتعالى) Anayataja baadhi ya hayo katika kauli Zake:

 

وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ يَلْقَ أَثَامًا ﴿٦٨﴾

Na wale ambao hawaombi pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine na wala hawaui nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na wala hawazini. Na atakayefanya hivyo atakutana na adhabu.

 

يُضَاعَفْ لَهُ الْعَذَابُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَيَخْلُدْ فِيهِ مُهَانًا ﴿٦٩﴾

Ataongezewa adhabu maradufu Siku ya Qiyaamah, na mwenye kudumu humo akiwa amedhalilika.

 

 

إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يُبَدِّلُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٠﴾

Isipokuwa yule aliyetubu na akaamini na akatenda ‘amali njema; basi hao Allaah Atawabadilishia maovu yao kuwa mema.  Na Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.

 

وَمَن تَابَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَإِنَّهُ يَتُوبُ إِلَى اللَّـهِ مَتَابًا ﴿٧١﴾

Na atakayetubu na akatenda mema, basi hakika yeye anatubia kwa Allaah tawbah ya kweli.

 

وَالَّذِينَ لَا يَشْهَدُونَ الزُّورَ وَإِذَا مَرُّوا بِاللَّغْوِ مَرُّوا كِرَامًا ﴿٧٢﴾

Na wale ambao hawashuhudii uongo, na wanapopita kwenye upuuzi hupita kwa heshima.

 

وَالَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ لَمْ يَخِرُّوا عَلَيْهَا صُمًّا وَعُمْيَانًا ﴿٧٣﴾

Na wale ambao wanapokumbushwa Aayaat za Rabb wao, hawapinduki kuzifanyia uziwi na upofu. [Al-Furqaan (25: 68-73)]

 

 

Na Aayah nyingi nyinginezo zimetaja maharamisho kama hayo.

 

Rejea pia Hadiyth namba, (15), (19), (36), (38), (66), (82), (87), (88), (89), (90), (92), (93), (94), (97), (101), (102), (103), (108), (109), (113), (114), (116), (119), (120), (124), (125), (126), (128), (130), (131), (132).

 

Kinyume chake, Muislamu anapaswa kwa ujumla kumtii Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) kama Anavyoamrisha katika Aayah nyingi miongoni mwazo ni:

 

 قُلْ أَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ ۖ فَإِن تَوَلَّوْا فَإِنَّمَا عَلَيْهِ مَا حُمِّلَ وَعَلَيْكُم مَّا حُمِّلْتُمْ ۖ وَإِن تُطِيعُوهُ تَهْتَدُوا ۚ وَمَا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿٥٤﴾

 

Sema: “Mtiini Allaah na mtiini Rasuli.” Mkigeukilia mbali, basi hakika jukumu lake ni lile alobebeshwa tu nanyi ni juu yenu yale mliyobebeshwa. Na mkimtii mtaongoka; na hapana juu ya Rasuli isipokuwa ubalighisho bayana. [An-Nuwr (24: 54)]

 

 

 

 

 

Share

140-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Hitimisho: Mfano Wa Mti Mzuri (Mtende) Na Muumin

 

Lu-ulu-un-Manthuwrun

 

(Mkusanyiko Wa Hadiyth Mbali Mbali Na Mafunzo Yake)

 

Hadiyth Ya 140

 

Hitimisho - Mfano Wa Mti Mzuri (Mtende) Na Muumin

 

 

 

Kuhitimisha mkusanyiko wa Hadiyth hizi, Hadiyth ifuatayo na maelezo yanayofuatia, kunapatikana sifa za kila aina zinazolingana na sifa za Muumin: 

 

 

عَنْ ابْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) قَال: كُنَّا عِنْد رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: ((أَخْبِرُونِي عَنْ شَجَرَة تُشْبِه - أَوْ - كَالرَّجُلِ الْمُسْلِم لاَ يَتَحَاتّ وَرَقهَا صَيْفًا وَلاَ شِتَاء وَتُؤْتِي أُكُلَهَا كُلّ حِين بِإِذْنِ رَبّهَا)) قَالَ اِبْن عُمَر: فَوَقَعَ فِي نَفْسِي أَنَّهَا النَّخْلَة وَرَأَيْت أَبَا بَكْر وَعُمَر لاَ يَتَكَلَّمَانِ فَكَرِهْت أَنْ أَتَكَلَّمَ فَلَمَّا لَمْ يَقُولُوا شَيْئًا. قَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وآله وَسَلَّمَ: ((هِيَ النَّخْلَة)). فَلَمَّا قُمْنَا قُلْت لِعُمَرَ: يَا أَبَتَاهُ وَاَللَّه لَقَدْ كَانَ وَقَعَ فِي نَفْسِي أَنَّهَا النَّخْلَة. قَالَ: مَا مَنَعَك أَنْ تَتَكَلَّم؟ قُلْت: لَمْ أَرَكُمْ تَتَكَلَّمُونَ فَكَرِهْت أَنْ أَتَكَلَّم أَوْ أَقُول شَيْئًا.  قَالَ عُمَر: لَأَنْ تَكُون قُلْتهَا أَحَبُّ إِلَيَّ مِنْ كَذَا وَكَذَا - البخاري

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)  ambaye amesema: "Tulikuwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akauliza: ((Niambieni kuhusu mti unaofanana na (au) ulio kama Muislamu, ambao majani yake hayaanguki wakati wa majira ya joto, wala wakati wa majira ya baridi, na hutoa matunda yake kila mara kwa idhini ya Rabb wake)). Ibn ‘Umar akasema: “Niliufikiria kuwa ni mtende, lakini niliona vibaya kujibu nilipoona Abuu Bakr na ‘Umar hawakujibu”. Akasema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Ni mtende)). Tulipoondoka, nilimwambia ‘Umar: “Ee baba yangu! Wa-Allaahi nilihisi kuwa ni mtende”. Akasema: “Kwa nini basi hukutaja?” Nikasema: “Nilikuoneni kimya, nikaona vibaya kusema kitu”. Akasema ‘Umar: "Ungelisema, ingelikuwa bora kwangu kuliko kadhaa na kadhaa” (Yaani ningelikuwa na fakhari zaidi kuwa wewe mwanangu ndiye uliyeweza kujibu pekee). [Al-Bukhaariy]

 

 

Mafunzo Na Mwongozo:

 

 

1. Njia nzuri ya kumfunza mtu kwa kuuliza swali kama alivyokuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwauliza Maswahaba mara nyingi katika mas-alah ya Dini, mfano Hadiyth namba (88) ((Je, mnajua maana ya Ghiybah? [Kusengenya])) Wakasema: Allaah na Rasuli Wake wanajua. Akasema: ((Ni kumtaja ndugu yako kwa jambo analolichukia)). [Muslim].

 

Na hii ni njia iliyokuwa ikitumiwa mara nyingi na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Na ni mbinu ya ufundishaji ambayo inatumiwa leo katika maraakiz mbalimbali.

 

 

 

2. Hikma ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kupiga mifano mizuri.

 

Rejea mifano ya Hadiyth namba (20), (49), (57), (60), (107).

 

 

 

3. Dhihirisho la adabu na khulka ya Swahaba Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) kutokujibu mbele ya hadhara ya mzazi wake na kuwaachia wakubwa wake wajibu. Hii inadhihirisha pia unyenyekevu wake.

 

 

 

4. Elimu ina upeo wake kwa kila mtu, mdogo anaweza kuwa na ujuzi zaidi kuliko mkubwa. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَفَوْقَ كُلِّ ذِي عِلْمٍ عَلِيمٌ ﴿٧٦﴾

Na juu ya kila mwenye elimu yuko mwenye elimu zaidi. [Yuwsuf (12: 76)]

 

Na ndio maana hata katika Swalaah, mwenye elimu zaidi ya Qur-aan hata kama ni mdogo anaongoza Swalaah.

 

 

5. Hadiyth nzima imeufananisha mtende na Muumin ambaye sifa zake zote ni nzuri, mwenye khayr na aliyepewa baraka, na mwenye kupendelea usalama na amani kama ifuatavyo:

 

 

1-Mtende:

Umethibiti ardhini kwa mizizi yake

 

Muumini:

Anathibiti iymaan yake daima na huwa na iymaan ya hali ya juu.

 

 

 

2-Mtende:

Tunda lake ni zuri na tamu.

 

Muumini:

Mazungumzo na vitendo vyake ni vizuri na vya kupendeza, na si mwenye maneno maovu yanayoudhi, kudharau, kukashifu, kusengenya, kufitinisha n.k.

 

 

 

 

3-Mtende:

Umepambika vizuri na kufunikika.

 

Muumini:

Mavazi yake ni mazuri ya heshima.

 

 

 

4-Mtende:

Ni wepesi kula tunda lake.

 

Muumini:

Ni wepesi kujadiliana na watu kwa hoja, dalili na kwa busara.

 

 

 

5-Mtende:

Una faida kwa anayekula, kwani matunda yake yana siha mwilini na huwa ni  kinga ya maradhi, uchawi, na kila aina ya maovu kwa kula (aina ya) tende saba  (za aina ya 'ajwah) asubuhi kabla kula chochote.

 

Rejea Hadiyth kuhusu kula tende saba (za aina ya 'ajwah) asubuhi katika Al-Bukhaariy na Muslim.

 

 

Muumini:

EIimu yake anayotoa ina faida kubwa ya kuwaongoza Waislamu na wasio Waislamu kutoka katika upotofu kuingia katika hidaaya na hivyo ni kuutakasa moyo  katika usalama wa shirki na maovu mengineyo, kinyume na moyo wenye maradhi ya shirki, unafiki n.k.

 

 

 

6-Mtende:

Ni mti madhubuti sana wenye kustahmili upepo mkali.

 

Muumini:

Iymaan yake imethibiti vizuri hata anapopata misukosuko na mitihani, huwa na moyo mkubwa wa kustahmili kama ilivyothibiti katika Hadiyth:  

 

((عَجَبًا لإَمْرِ الْمُؤْمِنِ إِنَّ أَمْرَهُ كُلَّهُ خَيْرٌ، وَلَيْسَ ذَاكَ لإَحَدٍ إلاَّ لِلْمُؤْمِنِ. إِنْ أَصَابَتْهُ سَرَّاءُ شَكَرَ فَكَانَ خَيْرًا لَهُ،  وَإِنْ أَصَابَتْهُ ضَرَّاءُ صَبَرَ فَكَانَ خَيْرًا لَهُ)) مسلم

 

((Ajabu ya jambo la Muumin kwamba kila jambo lakeni kheri. Na halipatikani hili isipokuwa kwa Muumin. Anapofikwa na jambo zuri hushukuru nayo ni kheri kwake na anapofikwa na jambo lenye madhara husubiri nayo ni kheri kwake)) [Muslim]

 

 

 

7-Mtende:

Kila unapokuwa mkubwa unazidi kutoa matunda na faida nyinginezo.

 

Muumini:

Kila anapozidi umri huongezeka elimu, busara na huzidi kunufaisha watu kwa khayr zake.

 

 

Na Allaah (سبحانه وتعالى) Anajua zaidi.

 

 

Huo ndio mfano wa mti mzuri unaofanana na Muumini. Na ni sawa Allaah (سبحانه وتعالى) Anavyofananisha neno zuri na mti mzuri katika kauli Yake: 

 

 أَلَمْ تَرَ كَيْفَ ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا كَلِمَةً طَيِّبَةً كَشَجَرَةٍ طَيِّبَةٍ أَصْلُهَا ثَابِتٌ وَفَرْعُهَا فِي السَّمَاءِ ﴿٢٤﴾

Je, huoni vipi Allaah Amepiga mfano wa neno zuri kama mti mzuri mizizi yake imethibitika imara na matawi yake yanafika mbinguni? (marefu mno).

 

تُؤْتِي أُكُلَهَا كُلَّ حِينٍ بِإِذْنِ رَبِّهَا ۗ وَيَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٥﴾

Unatoa mazao yake kila wakati kwa idhini ya Rabb wake. Na Allaah Anapiga mifano kwa watu ili wapate kukumbuka. [Ibraahiym (14: 24-25)]

 

 

Ama mfano wa neno ovu na mti muovu Anaendelea Allaah (سبحانه وتعالى) kusema:

 وَمَثَلُ كَلِمَةٍ خَبِيثَةٍ كَشَجَرَةٍ خَبِيثَةٍ اجْتُثَّتْ مِن فَوْقِ الْأَرْضِ مَا لَهَا مِن قَرَارٍ ﴿٢٦﴾

Na mfano wa neno baya ni kama mti mbaya uliong’olewa juu ya ardhi hauna imara. [Ibraahiym (14: 26)]

 

 

Mfano huo wa neno baya ni neno la kufru la kafiri kwa kutokuamini kwake. Amesema Imaam As-Sa’diy (رحمه الله): “Ni mti mbaya kama mti wa “handhwal” na aina yake. Mti huu hauthibitiki wala hautoi matunda mazuri, na hata kama utatoa, basi ni matunda mabaya. Hivyo ndivyo neno la kufru na maasi, halithibitiki kwa manufaa moyoni, wala halitoi ila maneno maovu na vitendo viovu vinavyomdhuru mtu huyo na wala havimnufaishi wala ‘amali zake njema hazipandi kwa Allaah kutakabaliwa, wala ‘amali zake hazimfai nafis yake wala haziwafai wenigneo.”

 

Mti wa handhwal: Ni mti unapatikana jangawani au kichakani, matunda yake yana mibamiba na machungu kama vile mchongoma.

 

 

Kisha Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema kuwa Humthibitisha mwenye kuamini katika maisha ya dunia na pia maisha ya Aakhirah kwa neno hilo lililothibiti kama mti, yaani: “Laa ilaaha illa-Allaah.”

 

 

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَيُضِلُّ اللَّـهُ الظَّالِمِينَ ۚ وَيَفْعَلُ اللَّـهُ مَا يَشَاءُ﴿٢٧﴾

Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika uhai wa dunia na Aakhirah. Na Allaah Huwaacha kupotoka madhalimu. Na Allaah Anafanya Atakavyo. [Ibraahiym (14: 27)]

 

 

Duniani huthibiti kumuamini Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kuendesha maisha yake yote yakiwa katika mipaka ya Rabb wake (عزّ وجلّ) na kutenda mema na kupandishwa ‘amali zake na kutakabaliwa na Allaah (سبحانه وتعالى). Na baada ya kufariki kwake huthibitika kwa kuweza kujibu maswali atakayoulizwa na Malaika wawili kaburini ambao ni Munkar na Nakiyr kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 

 

عَنْ الْبَرَاء بْن عَازِب رَضِيَ اللَّه عَنْهُ أَنَّ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ ((الْمُسْلِم إِذَا سُئِلَ فِي الْقَبْر شَهِدَ أَنْ لاَ إِلَه إِلاَّ اللَّه وَأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُول اللَّه فَذَلِكَ قَوْله (يُثَبِّتُ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ)) البخاري  وَرَوَاهُ مُسْلِم أَيْضًا وَبَقِيَّة الْجَمَاعَة

Imepokelewa kutoka kwa Al-Baraa bin ‘Aazib (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم) amesema: ((Muislamu akiulizwa katika kaburi, atashuhudia kwamba: "Laa ilaaha Illa-Allaah wa anna Muhammadar-Rasuwlu-Allaah" (Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na Muhammad ni Rasuli wa Allaah), basi hiyo ndiyo maana ya kauli ya Allaah: ”Allaah Huwatia imara wenye kuamini kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na Aakhirah”)) [Al-Bukhaariy na Muslim na wengineo]

 

 

Hadiyth nyingine imeelezea:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة قَالَ : قَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يُثَبِّتُ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاة الدُّنْيَا وَفِي الآخِرَة)) قَال: ((ذَلِكَ إِذَا قِيلَ لَهُ فِي الْقَبْر مَنْ رَبّك وَمَا دِينك وَمَنْ نَبِيّك؟ فَيَقُول رَبِّي اللَّه وَدِينِيّ الإسْلاَم, وَنَبِيِّي مُحَمَّد, جَاءَنَا بِالْبَيِّنَاتِ مِنْ عِنْد اللَّه فَآمَنْت بِهِ, وَصَدَّقْت. فَيُقَال لَهُ: صَدَقْت عَلَى هَذَا عِشْت وَعَلَيْهِ مُتّ وَعَلَيْهِ تُبْعَث))  

 

Imekutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم ) amesema: ((Allaah Huwatia imara wenye kuamini kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na Aakhirah)). Akasema: ((Hivyo atakapoulizwa kaburini; Nani Rabb wako, nini Dini yako, nani Rasuli wako? Atasema: Rabb wangu ni Allaah, Dini yangu ni Islaam na Rasuli wangu ni Muhammad, ametuletea dalili za wazi kutoka kwa Allaah, nikamuamini na nikamsadikisha. Ataambiwa: Umesema ukweli, umeishi kwa hayo, umefia kwa hayo na utafufuliwa kwa hayo)). [Atw-Twabariy (16: 596)] 

 

 

 

 

 

 

Share