Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam

 

 

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam

 

 

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

Share

01-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An’aam: Kutokumshirikisha Allaah

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An’aam

 

01-Kutokumshirikisha Allaah

 

 

 

 

 

 Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۖ وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم مِّنْ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكُمْ وَإِيَّاهُمْ ۖ وَلَا تَقْرَبُوا الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ ۖ وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿١٥١﴾

Sema: “Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote, na muwafanyie ihsaan wazazi wawili, na wala msiwaue watoto wenu kutokana na umasikini. Sisi Tunakuruzukuni pamoja nao. Na wala msikaribie machafu yaliyo dhahiri na yaliyofichika. Na wala msiue nafsi ambayo Ameiharamisha Allaah (kuiua) isipokuwa kwa haki (ya shariy’ah). Hivyo ndivyo Alivyokuusieni  kwayo mpate kutia akilini.”

 

 

وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ حَتَّىٰ يَبْلُغَ أَشُدَّهُ ۖ وَأَوْفُوا الْكَيْلَ وَالْمِيزَانَ بِالْقِسْطِ ۖ لَا نُكَلِّفُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا ۖ وَإِذَا قُلْتُمْ فَاعْدِلُوا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۖ وَبِعَهْدِ اللَّـهِ أَوْفُوا ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ﴿١٥٢﴾

 “Na wala msiikaribie mali ya yatima isipokuwa kwa njia ya ihsaan mpaka afikie umri wa kupevuka. Na timizeni kipimo na mizani kwa uadilifu. Hatukalifishi nafsi isipokuwa kadiri ya uwezo wake. Na mnaposema basi fanyeni uadilifu japokuwa ni jamaa wa karibu. Na timizeni ahadi ya Allaah. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kukumbuka.”

 

 

وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ﴿١٥٣﴾

 “Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kuwa na taqwa.” [Al-An’aam: 151-153].

 

 

Wasiya uliokusudiwa katika Aayah hizo ni miongoni mwa maamrisho ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Hizi ni amri kumi zilokusanyika pamoja katika Suwrah hiyo tukufu ya Al-An’aam, lakini maamrisho kama hayo na mengineyo yametajwa pia katika Suwrah nyenginezo mbali mbali na katika Aayah mbali mbali kwenye Qur-aan.

 

Maamrisho kama hayo  yanafanana na maamrisho ya Allaah ('Azza wa Jalla) kwa  Ahlul-Kitaab (Mayahudi na Manaswara) kwani wao pia wameamrishwa mema na kuharamishwa maovu.   Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُلْ يَا أَهْلَ الْكِتَابِ تَعَالَوْا إِلَىٰ كَلِمَةٍ سَوَاءٍ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ أَلَّا نَعْبُدَ إِلَّا اللَّـهَ وَلَا نُشْرِكَ بِهِ شَيْئًا وَلَا يَتَّخِذَ بَعْضُنَا بَعْضًا أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ ۚ فَإِن تَوَلَّوْا فَقُولُوا اشْهَدُوا بِأَنَّا مُسْلِمُونَ ﴿٦٤﴾

Sema: “Enyi Ahlal-Kitaabi! Njooni katika neno lililo sawa baina yetu na baina yenu, kwamba tusiabudu isipokuwa Allaah Pekee, na wala tusimshirikishe na chochote, na wala wasichukue baadhi yetu wengine kuwa miola badala ya Allaah.” Wakikengeuka; basi semeni: “Shuhudieni kwamba sisi ni Waislamu.” [Aal-‘Imraan: 64]

 

 

Wasiya Wa Kwanza: Kutokumshirikisha Allaah ('Azza wa Jalla):

 

Anasema Allaah:

 

قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا

Sema: “Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote, [Al-An’aam: 151]

 

 

Shirki ni dhambi pekee ambayo Allaah ('Azza wa Jalla) Hamsamehe mtu ikiwa hakutubia kama Anavyosema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا ﴿٤٨﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amezua dhambi kuu. [An-Nisaa: 48]

 

Na kauli Yake Allaah ('Azza wa Jalla) nyengineyo kama hiyo:

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴿١١٦﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali.  [An-Nisaa: 116]

 

 

Shirki ni katika dhambi kubwa mno na  inamuangamiza mtu:

 

Amesema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

((ألاَ أُنبِّئكم بأكبرِ الكبائر؟ الإشراك بالله)) متفق عليه.

((Je, hivi nikujulisheni madhambi makubwa kabisa? Ni kumshirikisha Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه (عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَمَا هُنَّ؟  قَالَ: ((الشِّرْكُ بِاللَّهِ وَالسِّحْرُ وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ وَأَكْلُ الرِّبَا وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ الْغَافلاَتِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akawaambia: ((Ni kumshirikisha Allaah, sihri [uchawi], kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa vita na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika.)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Mwenye kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) hatoingia Jannah bali makazi yake yatakuwa ni motoni. Kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾

 Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.” [Al-Maaidah: 72]

 

Na Hadiyth kadhaa zimethibitisha, chache miongoni mwazo ni zifuatazo:

 

 

أَبِي ذَرّ رَضِيَ اللَّه عَنْهُ قَالَ : قَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  ((أَتَانِي جِبْرِيل فَبَشَّرَنِي أَنَّهُ مَنْ مَاتَ لَا يُشْرِك بِاَللَّهِ شَيْئًا مِنْ أُمَّتك دَخَلَ الْجَنَّة قُلْت وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ ؟ قَالَ وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ قُلْت وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ ؟ قَالَ وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ قُلْت وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ ؟ قَالَ وَإِنْ زَنَى وَإِنْ سَرَقَ وَإِنْ شَرِبَ الْخَمْر))متفق عقيه

 

Kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Amenijia Jibriyl akanibashiria kwamba yeyote katika Ummah wangu atakayefariki akiwa hakumshirikisha Allaah na chochote, ataingia Peponi. Nikasema: Hata ikiwa amezini na ikiwa ameiba? Akasema: Hata kama ikiwa amezini na ameiba. Nikasema: Hata ikiwa amezini na ikiwa ameiba? Akasema: Hata ikiwa amezini na ikiwa ameiba. Nikasema: Hata ikiwa amezini na ikiwa ameiba?  Akasema: Hata ikiwa amezini na ikiwa ameiba na ikiwa amekunywa pombe)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Pia:

 

 عن جابر رضي الله عنه: أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((مَنْ لَقِي اللهَ لاَ يُشْرِك بِهِ شَيْئاً دَخَلَ الْجَنَّة، وَمَنْ لَقِيَه يُشْرِك بِهِ شَيْئاً دَخَلَ النَّار)) 

Imetoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (Atakayekutana na Allaah akiwa hamshirikishi na chochote Ataingia Jannah, na atakayekutana Naye akiwa anamshirikisha na chochote ataingia Motoni)) [Muslim 94.]

 

 

Na:

 

عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: قال النبي صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ مَاتَ وَهُوَ يَدْعُو مِنْ دُونِ اللهِ نِدَّاً دَخَلَ النَّارَ )) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaahi bin Mas-‘uwd (Radhwiya Alaahu ‘anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayekufa akiwa katika hali ya kumuomba asiyekuwa Allaah kumfanyia mlinganishi (mshirika) ataingia Motoni)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

عن ابن مسعود رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ مَاتَ يُشْرِكُ بِاللَّهِ شَيْئًا دَخَلَ النَّارَ))  

Kutoka kwa Ibn Mas‘uwd pia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayefariki akiwa katika hali ya kumshirikisha Allaah kwa chochote ataingia Motoni)) [Al-Bukhaariy 1238, Muslim 92]

 

Tafadhali bonyeza kiungo kifuatacho upate faida ziyada na bayana kabisa kuhusiana na shirki:

 

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ --- Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

 

 

  

 

Share

02-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An’aam: Kuwafanyia Wema Wazazi

 

Wasiya Kumi Wa Allaah

 

02-Kuwafanyia Wema Wazazi

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا

na muwafanyie ihsaan wazazi wawili [Al-An’aam: 151]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake   (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wmesisitiza sana kuwafanyia wazazi wema. Baadhi ya dalili zake ni:

 

 

Kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kutaja ihsaan kwa wazazi wawili baada ya kutaja kumwabudu Yeye, jambo ambalo linadhihirisha umuhimu wa kuwatendea wema wazazi wawili:

 

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۚ إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣﴾

Na Rabb wako Amehukumu kwamba: “Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee na (Ameamrisha) kuwafanyia ihsaan wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee naye yuko pamoja nawe, au wote wawili basi usiwaambie, Uff! Na wala usiwakemee; na waambie maneno ya heshima.

 

وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

Na wainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme: “Rabb wangu! Warehemu kama walivyonilea udogoni.” [Al-Israa: 23-24]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَإِذْ أَخَذْنَا مِيثَاقَ بَنِي إِسْرَائِيلَ لَا تَعْبُدُونَ إِلَّا اللَّـهَ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا

Na pindi Tulipochukua fungamano ya wana wa Israaiyl (Tukawaambia): “Msiabudu isipokuwa Allaah; na muwafanyie ihsaan wazazi wawili, [Al-Baqarah: 83]

 

Hadiyth za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

 عَنْ اِبْن مَسْعُود رَضِيَ اللَّه عَنْهُ أَنَّهُ قَالَ : سَأَلْت رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَيّ الْعَمَل أَفْضَل ؟ قَالَ الصَّلَاة عَلَى وَقْتهَا قُلْت ثُمَّ أَيّ ؟ قُلْ بِرّ الْوَالِدَيْنِ قُلْت ثُمَّ أَيّ ؟ قَالَ الْجِهَاد فِي سَبِيل اللَّه)) البخاري و مسلم

Kutoka kwa Ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): Kitendo gani bora kabisa? Akasema: ((Swalaah kwa wakati wake)) Kisha nikasema: Kisha kipi? Akasema: ((Kuwafanyia wema wazazi wawili)): Kisha nikasema: Kisha kipi? Akasema: ((Jihadi katika njia ya Allaah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hata wazazi wasiokuwa Waislamu wanapaswa kutendewa wema madamu tu hawataamrisha kumshirikisha Allaah ('Azza wa Jalla) kama Anavyosema:

 

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا ۚ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٨﴾

Na Tumemuusia insani kuwafanyia wema wazazi wake wawili. Lakini wakikushikilia kuwa Unishirikishe na ambayo huna elimu nayo, basi usiwatii; Kwangu ni marejeo yenu, Nitakujulisheni yale mliyokuwa mkiyatenda. [Al-‘Ankabuwt: 8]

 

Wazazi wanapaswa kutendewa wema hata baada ya kufariki kwao kwa kuwatendea ‘amali kadhaa ambazo zinawafikia thawabu zake kwao. Bonyeza kiungo kifuatacho kwa faida zaidi:  

 

‘Amali Za Kuwatendea Wazazi Waliofariki Waendelee Kupokea Thawabu

 

 

 

 

 

Share

03-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An’aam: Kutokuua Watoto

 

  Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

03- Kutokuua Watoto

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم مِّنْ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكُمْ وَإِيَّاهُمْ ۖ

na wala msiwaue watoto wenu kutokana na umasikini. Sisi Tunakuruzukuni pamoja nao. [Al-An’aam: 151]

 

 

Makafiri walikuwa wakiwaua watoto wao ima kwa khofu ya kuwa hawatoweza kuwapatia chakula au kuwaua wasichana kwa sababu ya kuwadhalilisha. Siku ya Qiyaamah wataulizwa kuhusu dhulma hii, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ ﴿٨﴾

Na mtoto wa kike aliyezikwa hali akiwa yuhai atakapoulizwa.

 

 

بِأَيِّ ذَنبٍ قُتِلَتْ ﴿٩﴾

Kwa dhambi gani aliuliwa? [At-Takwiyr: 8-9]

 

 

Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَبْد اللَّه بْن مَسْعُود رَضِيَ اللَّه عَنْهُ أَنَّهُ سَأَلَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَآله وَسَلَّمَ ((أَيّ الذَّنْب أَعْظَم ؟)) قَالَ ((أَنْ تَجْعَل لِلَّهِ نِدًّا وَهُوَ خَلَقَك)) قُلْت ثُمَّ أَيّ  قَالَ ((أَنْ تَقْتُل وَلَدَك خَشْيَة أَنْ يُطْعَم مَعَك)) قُلْت ثُمَّ أَيّ ؟ قَالَ ((أَنْ تُزَانِي حَلِيلَة جَارك))  ثُمَّ تَلَا رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ   ((وَاَلَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّه إِلَهًا آخَر وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْس الَّتِي حَرَّمَ اللَّه إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ)) البخاري و مسلم

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba alimuuliza Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): Dhambi gani kubwa? Akasema: ((Kumfanyia Allaah mshirika na hali Yeye Amekuumba)) Nikasema: Kisha ipi? Akasema: ((Kumuua mtoto wako kwa khofu ya kutoweza kumpatia chakula chake)) Nikasema kisha ipi? Akasema: ((Kuzini na mke wa jirani yako)) Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasoma:

 

وَاَلَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّه إِلَهًا آخَر وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْس الَّتِي حَرَّمَ اللَّه إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ

Na wale ambao hawaombi pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine na wala hawaui nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki [Al-Furqaan: 68]  [al-Bukhaariy na Muslim]

 

Ibn ‘Abbaas, Qataadah na As-Suddi na wengineo wamesema kuhusu: 

مِّنْ إِمْلَاقٍ

kutokana na umasikini

 

“Sio kuwaua kwa sababu nyinyi ni masikini. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema katika Suwratul-Israa:

 

وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُمْ خَشْيَةَ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُهُمْ وَإِيَّاكُمْ ۚ إِنَّ قَتْلَهُمْ كَانَ خِطْئًا كَبِيرًا ﴿٣١﴾

Na wala msiue auladi wenu kwa kukhofia ufukara. Sisi Tunawaruzuku wao na nyinyi. Hakika kuwaua imekuwa ni hatia kubwa. [Al-Israa: 31]

 

Kutajwa wao kwanza kuwa Allaah Anawaruzuku kuna maana kwamba msikhofu umasikini kwa sababu ya kuwalisha watoto wenu, kwani hakika rizki yao inatoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).”

 

 

Share

04- Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kutokukaribia Machafu

 

  Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

04- Kutokukaribia Machafu

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

وَلَا تَقْرَبُوا الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ

Na wala msikaribie machafu yaliyo dhahiri na yaliyofichika. [Al-An’aam: 151]

 

 

Maana ya الْفَوَاحِشَ

 

Kila tabia na kitendo kibaya ikiwa ni cha kutendwa au cha kutamkwa ambacho kinatoka nje ya fitwrah (maumbile asili) ya mwana Aadam. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameharamisha katika kauli Zake zifuatazo:

 

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚ يَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ﴿٩٠﴾

Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini ili huenda mkapata kukumbuka. [An-Nahl: 90]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ اللَّـهَ لَا يَأْمُرُ بِالْفَحْشَاءِ

“Hakika Allaah Haamrishi machafu. [Al-A’raaf: 28]

 

 

Na pia Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa)

 

 

 اتْلُ مَا أُوحِيَ إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ وَأَقِمِ الصَّلَاةَ ۖ إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ

Soma (ee Muhammad Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) uliyoletewa Wahy katika Kitabu na simamisha Swalaah, hakika Swalaah inazuia machafu na munkari [Al-'Ankabuwt: 45]

 

Mara nyingine katika Qur-aan fahshaa (kwa matamshi ya ujumla) inakusudiwa ni zinaa au liwati ambayo yamekatazwa kuyakaribia kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

Na wala msiikaribie zinaa. Hakika huo ni uchafu umekuwa na ni njia mbaya kabisa. [Al-Israa: 32]

 

Na Anasema pia Allaah ('Azza wa Jalla):

 

وَلُوطًا إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَتَأْتُونَ الْفَاحِشَةَ مَا سَبَقَكُم بِهَا مِنْ أَحَدٍ مِّنَ الْعَالَمِينَ ﴿٨٠﴾

Na (Tulimtuma) Luutw, alipowaambia kaumu yake: “Je, mnafanya uchafu (wa liwati) ambao hajakutangulieni nao yeyote katika walimwengu?” [Al-A’raaf: 80]

 

 

Na katika Sunnah:

 

عَنْ اِبْن مَسْعُود رَضِيَ اللَّه عَنْهُ قَالَ : قَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ((لَا أَحَد أَغْيَر مِنْ اللَّه مِنْ أَجْل ذَلِكَ حَرَّمَ الْفَوَاحِش مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ)) متفق عليه

Kutoka kwa Ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema:  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakuna mtu mwenye wivu zaidi ya Allaah. Ndio maana Akaharamisha vitendo vichafu vinavyotendwa kwa dhahiri na kwa siri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na pia:

 

 

عن سَعْد بْن عُبَادَة قال: لَوْ رَأَيْت مَعَ اِمْرَأَتِي رَجُلًا لَضَرَبْته بِالسَّيْفِ غَيْر مُصَفَّح فَبَلَغَ ذَلِكَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ ((أَتَعْجَبُونَ مِنْ غَيْرَة سَعْد ؟ فَوَاَللَّهِ لَأَنَا أَغْيَر مِنْ سَعْد وَاَللَّه أَغْيَر مِنِّي مِنْ أَجْل ذَلِكَ حَرَّمَ الْفَوَاحِش مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ)) متفق عليه

Kutoka kwa Sa’ad bin ‘Ubaadah ambaye amesema: “Nikimuona mtu na mke wangu [wakifanya zinaa] nitamuua kwa upanga!” Ilipomfikia Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) habari hii alisema: ((Je, mnastaajabu wivu wa Sa’ad? Naapa kwa Allaah, mimi nina wivu zaidi kuliko Sa’ad, na Allaah Ana wivu zaidi yangu. Ndio maana Akaharamisha madhambi machafu yanayotendwa kwa dhahiri na kwa siri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]   

 

 

Na pia al-fuhsh (machafu) imetajwa kwa ujumla katika kauli Zake Allaah ('Azza wa Jalla):

 

الَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَائِرَ الْإِثْمِ وَالْفَوَاحِشَ إِلَّا اللَّمَمَ

 

Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. [An-Najm: 32]

 

وَالَّذِينَ يَجْتَنِبُونَ كَبَائِرَ الْإِثْمِ وَالْفَوَاحِشَ وَإِذَا مَا غَضِبُوا هُمْ يَغْفِرُونَ﴿٣٧﴾

Na wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu na wanapoghadhibika wao wanasamehe. [Ash-Shuwra: 37]

 

 

Dalili kuwa fuhsh (machafu) ina maana ya machafu mengineyo kama kutukana, kulaani, ghiybah (kusengenya) n.k ni kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

  

 إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿١٩﴾

Hakika wale wanaopenda uenee uchafu wa kashfa kwa wale walioamini; watapata adhabu iumizayo duniani na Aakhirah. Na Allaah Anajua nanyi hamjui. [An-Nuwr: 19]

 

 

Na Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عبد الله بن مسعود  رضي الله عنه  أن رسول الله  صلى الله عليه وسلم  قال: ((ليس المؤمن بالطعان ولا اللعان ولا الفاحش ولا البذيء))  رواه أحمد و إسناده صحيح

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muumini siye mwenye kutukana, wala kulaani, wala al-faahish [mwenye kufanya machafu] wala mwenye ujeuri)) [Imesimuliwa na Imaam Ahmad kwa isnaad Swahiyh]

 

 

Na pia,

 

عَنْ عَائِشَة قَالَتْ دَخَلَ عَلَى رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَهُود فَقَالُوا: السَّام عَلَيْك يَا أَبَا الْقَاسِم" فَقَالَتْ عَائِشَة : وَعَلَيْكُمْ السَّام قَالَتْ : فَقَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ " ((يَا عَائِشَة إِنَّ اللَّه لَا يُحِبّ الْفُحْش وَلَا التَّفَحُّش)) قُلْت أَلَا تَسْمَعهُمْ يَقُولُونَ السَّام عَلَيْك" ؟ فَقَالَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  (( أَوَمَا سَمِعْت أَقُول وَعَلَيْكُمْ)) البخاري

 

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) ambaye amesema: Baadhi ya Mayahudi walikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakamuamkia kwa kumwambia: “As-saam ‘alayka yaa Abal Qaasim” [kwa maana mauti yakufikie Ee baba wa Qaasim]. Basi nikasema: “Wa ‘alaykumus-saam” [kwa maana na mauti yakufikieni]. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Ee ‘Aaishah, hakika Allaah, Hapendi al-fuhsh wala at-tafahhush [uchafu na kutoa maneno machafu)). Nikasema: Je, hukuwasikia walivyosema “As-saam ‘alayka?” Akasema: ((Je, hukusikia nimewajibu “Wa ‘alaykum” [Na juu yenu])) [Al-Bukhaariy] 

 

 

Hadiyth hii inatufunza kwamba mtu anapokutukana ni bora kunyamaza au kumjibu lakini bila ya kurudia maneno machafu aliyotamka yeye, lakini sio kutamka maneno machafu.

 

Pia Hadiyth nyengine Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametahadharisha:

 

وعن أبي هريرة أن رسول الله صلى الله عليه و سلم قال  ((إياكم و الفحش؛ فإن الله لا يحب الفاحش و المتفحش)) رواه أبو داود و أحمد و إسناده صحيح.

 

((Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Tahadharini na uchafu, kwani Allaah Hapendi mwenye kufanya uchafu na mwenye kutamka machafu)) [Abu Daawuwd, Ahmad kwa isnaad Swahiyh]

 

 

Na pia mara nyengine al-fuhsh (machafu) ina maana ya ubakhili kama katika kauli za Allaah ('Azza wa Jalla):

 

الشَّيْطَانُ يَعِدُكُمُ الْفَقْرَ وَيَأْمُرُكُم بِالْفَحْشَاءِ

Shaytwaan anakutishieni ufukara na anakuamrisheni machafu, (ubakhili), [Al-Baqarah: 268]

 

Na pia:

 

  يَا أَيُّهَا النَّاسُ كُلُوا مِمَّا فِي الْأَرْضِ حَلَالًا طَيِّبًا وَلَا تَتَّبِعُوا خُطُوَاتِ الشَّيْطَانِ ۚ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ ﴿١٦٨﴾

Enyi watu! Kuleni katika vilivyomo ardhini vya halali, vizuri; na wala msifuate hatua za shaytwaan. Hakika yeye kwenu ni adui wa wazi.

 

 

إِنَّمَا يَأْمُرُكُم بِالسُّوءِ وَالْفَحْشَاءِ وَأَن تَقُولُوا عَلَى اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿١٦٩﴾ 

Hakika hakuna isipokuwa anakuamrisheni maovu na machafu (na ubakhili) na mseme dhidi ya Allaah msiyoyajua.  [Al-Baqarah: 168-169]. 

 

 

Baadhi ya madhara ya al-fuhsh (machafu)

 

 

1-Kujitenga mbali na Allaah ('Azza wa Jalla) kwa sababu Yeye (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Hapendi wenye kutenda uovu huu kutokana na makatazo Yake.

 

 

2-Machafu ya zinaa na liwati 

 

Uislamu umeharamisha starehe za haraam, umeharamisha zinaa, ushoga, na kumuendea mke kinyume na maumbile. Taathira zake ni nyingi zikiwemo maradhi mabaya, kashfa na aibu, mtoto atakayezaliwa katika zinaa ataleta taathira kubwa mbaya katika jamii nzima.

 

 

3-Kujitenga mbali na watu kwani husababisha magomvi, chuki na uadui, mfarakano na kukhasimikiana.

 

 

4-Kujipatia malipo mabaya duniani na Akhera.

 

 

 

 

 

 

 

Share

05-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kutokuua Nafsi Aliyoharamisha Allaah Ila Kwa Haki

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

05-Kutokuua Nafsi Aliyoharamisha Allaah, Ila Kwa Haki

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ

Na wala msiue nafsi ambayo Ameiharamisha Allaah (kuiua) isipokuwa kwa haki (ya shariy’ah). [Al-An’aam: 151] 

 

Adhabu kali mno zifuatazo Amezitahadharisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa atakayemuua Muislamu bila ya haki:

 

 

1-Kuingizwa motoni na kudumu milele.

 

2-Kughadhibiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

 

3-Kulaaniwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)

 

4-Kuandaliwa adhabu kubwa.

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ وَأَعَدَّ لَهُ عَذَابًا عَظِيمًا ﴿٩٣﴾

Na atakayemuua Muumini kwa kusudi, basi jazaa yake ni Jahannam, ni mwenye kudumu humo na Allaah Atamghadhibikia na Atamlaani na Atamuandalia adhabu kuu. [An-Nisaa: 93]

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuonya pia katika Hadiyth:

 

عن ابْنِ مَسْعُودٍ رضي اللهُ عنه قالَ: قالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((لاَ يَحِلُّ دَمُ امْرِئٍ مُسْلِمٍ  إلاّ بإحْدَى ثَلاَثٍ: الثَّيِّبُ الزَّاني، وَالنَّفْسُ بالنّفْسِ، وَالتَّارِكُ لِدِيِنِهِ الْمُفَارِقُ لِلْجَماعَةِ)).  رَوَاهُ الْبُخَارِيّ وَمُسْلِمٌ    

Kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye alisema: Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Damu ya Muislamu haipasi kumwagwa isipokuwa katika hali tatu: Mzinzi muolewa (Mtu  mzima aliyeoa au aliyeolewa), uhai kwa uhai (nafsi kwa nafsi) na kwa yule anayeacha Dini  na akajifarikisha na  jama’ah   (amejitenga na watu wa Dini yake)) [Imesimuliwa na Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hata kuua wasio Waislamu pasi na haki pia imeharamsihwa. Mwenye kufanya hivyo hataisikia harufu ya Pepo kwa dalili:

 

 عَنْ عَبْد اللَّه بْن عُمَر عَنْ النَّبِيّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَرْفُوعًا ((مَنْ قَتْل مُعَاهَدًا لَمْ يُرَحْ رَائِحَة الْجَنَّة وَإِنَّ رِيحهَا لَيُوجَد مِنْ مَسِيرَة أَرْبَعِينَ عَامًا))

 

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar ambaye amesema: ((Yeyote aliyeua mtu ambaye alikuwa katika ahadi na kuhifadhiwa na Waislamu, hatasikia harufu ya Jannah japokuwa harufu yake inasikika umbali wa miaka arubaini)) [Al-Bukhaariy]

 

Na pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة عَنْ النَّبِيّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَنْ قَتَلَ مُعَاهَدًا لَهُ ذِمَّة اللَّه وَذِمَّة رَسُوله فَقَدْ أَخْفَرَ بِذِمَّةِ اللَّه فَلَا يُرَحْ رَائِحَة الْجَنَّة وَإِنَّ رِيحهَا لَيُوجَد مِنْ مَسِيرَة سَبْعِينَ خَرِيفًا))

 

Na kutoka wa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Yeyote aliyeua mtu akiwa katika ahadi yya kuhifadhiwa na Waislamu, na ambaye ananufaika na dhamana ya Allaah na Rasuli Wake, atakuwa ameharibu dhamana ya Allaah, (kwake). Hatasikia harufu ya Jannah japokuwa harufu yake inasikika kutoka umbali wa miaka sabini)) [al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Share

06-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kutokuikaribia Mali ya Yatima Ila Kwa Kukusudia Ihsaan

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

06-Kutokuikaribia (Kutumia) Mali ya Yatima Ila Kwa Kukusudia Ihsaan

 

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

 وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ حَتَّىٰ يَبْلُغَ أَشُدَّهُ

 

“Na wala msiikaribie mali ya yatima isipokuwa kwa njia ya ihsaan mpaka afikie umri wa kupevuka. [Al-An’aam: 152]

  

 

Mwenye kula mali ya yatima bila ya haki ni kama kula moto tumboni mwake na juu ya hivyo atapata adhabu ya moto. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ۖ وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا ﴿١٠﴾

Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao moto, na watauingia moto uliowashwa vikali mno. [an-Nisaa: 10]

 

 

Hali kadhalika haifai kuikaribia mali ya yatima kwa ubadhirifu, na kuwabadlishia vizuri vyao kwa vilivyo vibaya. Anaonya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa): 

 

وَآتُوا الْيَتَامَىٰ أَمْوَالَهُمْ ۖ وَلَا تَتَبَدَّلُوا الْخَبِيثَ بِالطَّيِّبِ ۖ وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَهُمْ إِلَىٰ أَمْوَالِكُمْ ۚ إِنَّهُ كَانَ حُوبًا كَبِيرًا ﴿٢﴾ 

Na wapeni mayatima mali zao, na wala msibadilishe kibaya (chenu) kwa kizuri (chao). Na wala msile mali zao pamoja na mali zenu. Hakika hilo limekuwa ni dhambi kubwa. [An-Nisaa: 2]

 

Anayelea Yatima amekuwa na jukumu kubwa mbele ya Allaah, kwa hivyo inampasa mlezi huyo atahadhari mno na ajiepushe kuwadhulumu kwa hali yoyote ile.

 

Zilipoteremshwa Aayah hizo kuhusu mayatima pamoja na Aayah ya 10 Suwratun-Nisaa tuliyoinukuu juu hapo, Maswahaba waliokuwa wakilea mayatima, walikhofu hata kuchanganyika kula nao. Khofu yao iliwafanya hadi kwamba waogope kula chakula chao kilichokuwa kikibakia, wakawa wanakiweka na kurudia tena kuwapa au kukiwacha kiharibikeHali hii ilikuwa ngumu kwao ndipo walipomkabili Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuuliza. Maelezo ni kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، قَالَ لَمَّا نَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ ((‏وَلاَ تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلاَّ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ))‏ وَ‏((‏إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَى ظُلْمًا‏))‏ قَالَ: اجْتَنَبَ النَّاسُ مَالَ الْيَتِيمِ وَطَعَامَهُ فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَى الْمُسْلِمِينَ فَشَكَوْا ذَلِكَ إِلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَأَنْزَلَ اللَّهُ: ((‏وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْيَتَامَى قُلْ إِصْلاَحٌ لَهُمْ خَيْرٌ‏)) ‏ إِلَى قَوْلِهِ ‏((‏لأَعْنَتَكُمْ‏)).

 

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba pale Aayah hizi zilipoteremshwa: 

 

 ‏وَلاَ تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلاَّ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ

 

 “Na wala msiikaribie mali ya yatima isipokuwa kwa njia ya ihsaan…”

 

إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَى ظُلْمًا‏)

 

 “Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma…”   akasema: Watu walijiepusha na mali ya yatima pamoja na chakula chake, ikawa ni mashaka kwa Waislamu wakashitaki kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)     hapo ikataremka:

 

 ‏وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْيَتَامَى قُلْ إِصْلاَحٌ لَهُمْ خَيْرٌ

“Na wanakuuliza kuhusu mayatima. Sema: “Kuwatengeneza ni kheri…” mpaka kauli Yake:

 

لأَعْنَتَكُمْ‏

“Angelikutieni katika shida.” [Sunan An-Nasaaiy katika Kitaab Al-Wiswaayaa, Baab maa lil-waswiyyi min maal al-yatiym idhaa qaama ‘alayhi].

 

 

 Aayah kamili ni kama ifuatavyo:

 

 وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْيَتَامَىٰ ۖ قُلْ إِصْلَاحٌ لَّهُمْ خَيْرٌ ۖ وَإِن تُخَالِطُوهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ الْمُفْسِدَ مِنَ الْمُصْلِحِ ۚ وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَأَعْنَتَكُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴿٢٢٠﴾

Na wanakuuliza kuhusu mayatima. Sema: “Kuwatengeneza ni kheri.  Na mkichanganya mambo yenu na yao basi hao ni ndugu zenu.   Na Allaah Anamjua fisadi na mtengenezaji. Na lau Angetaka Allaah Angelikutieni katika shida.” Hakika Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Baqarah: 2:220]

 

 

 

 

 

Share

07-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kutimiza Vipimo Na Mizani Kwa Uadilifu

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

07- Kutimiza Vipimo Na Mizani Kwa Uadilifu

 

 

 

 

 Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):  

 

وَأَوْفُوا الْكَيْلَ وَالْمِيزَانَ بِالْقِسْطِ

 

Na timizeni kipimo na mizani kwa uadilifu [Al-An'aam: 152]

 

 

Ni amri ya kutekeleza haki wakati wa kutoa na kupokea, kununua na kuuza kama Anavyoonya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

Ole kwa wanaopunja.

 

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ﴿٢﴾

Ambao wanapopokea kipimo kwa watu wanataka wapimiwe kamilifu.

 

 

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ﴿٣﴾

Na wanapowapimia (watu) kwa kipimo au wanawapimia kwa mizani wanapunja.

 

 

أَلَا يَظُنُّ أُولَـٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ ﴿٤﴾

Je, hawadhanii kwamba wao watafufuliwa?

 

 

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿٥﴾

Kwenye Siku adhimu.

 

 

يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٦﴾

Siku watakayosimama watu kwa Rabb wa walimwengu. [Al-Mutwaffifiyn: 1-6]

 

 

Kutokupima kwa uadilifu ni kumdhulumu mtu haki yake ambayo ni dhulma isiyosameheka hadi dhalimu amrudishie aliyemdhulumu hapa hapa duniani, laa sivyo Akhera itasimama mizani ya haki na hapo dhulma zote zitadhihirika na kila aliyemdhulumu mwenziwe atamlipa kwa mema yake na kutupiwa yeye dhalimu madhambi ya aliyedhulumiwa, kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قَالَ:  ((مَنْ كَانَتْ عِنْدَهُ مَظْلَمَةٌ مِنْ أَخِيهِ مِنْ عِرْضِهِ أَوْ  مِنْ شَيْءٍ  فَلْيَتَحَلَّلْهُ مِنْهُ الْيَوْمَ قَبْلَ أَنْ لاَ يَكُونُ دِينَارٌ وَلاَ دِرْهَمٌ ، إِنْ كَانَ لَهُ عَمَلٌ صَالِحٌ أُخِذَ مِنْهُ بِقَدْرِ مَظْلَمَتِهِ. وَإِنْ لَمْ يَكُنْ لَهُ أُخِذَ مِنْ سَيِّئَاتِ صَاحِبِهِ فَحُمِل عَلَيْهِ))  رواه البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)    kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: ((Aliyekuwa na kitu cha dhulma cha nduguye kutokana na kumvunjia heshima au kitu chochote, basi amuombe amhalalishie leo kabla haijafika siku ambayo hakutakuwa na dinari wala dirham. Ikiwa ana ‘amali njema, basi zitachukuliwa kwa kadiri ya alichodhulumiwa. Na ikiwa hana, basi zitachukuliwa dhambi za aliyemdhulumu abebeshwe)). [Al-Bukhaariy.]

 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anahimiza kupima kwa haki katika Aayah nyinginezo kwa kauli Zake:

 

 

 وَأَوْفُوا الْكَيْلَ إِذَا كِلْتُمْ وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ ۚ ذَٰلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلًا ﴿٣٥﴾

Na timizeni kamilifu kipimo mnapopima, na pimeni kwa kipimo cha sawasawa. Hivyo ni kheri na bora zaidi matokeo yake. [Al-Israa: 35]

 

 

Na pia Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 أَلَّا تَطْغَوْا فِي الْمِيزَانِ ﴿٨﴾

Ili msivuke mipaka (kudhulumu) katika mizani.

 

 

وَأَقِيمُوا الْوَزْنَ بِالْقِسْطِ وَلَا تُخْسِرُوا الْمِيزَانَ ﴿٩﴾

Na simamisheni uzani kwa uadilifu, na wala msipunguze mizani. [Ar-Rahmaan: 8-9]

 

 

Makatazo haya yanawahusu zaidi wenye kufanya biashara. Mfanya biashara anapaswa kupima anachouza kwa haki bila ya kupunguza. Mfano ikiwa mnunuajia amelipia kitu cha kilo 2, basi muuzaji apime hivyo hivyo, isipungue ikawa kilo 1.9 au chini yake. Ama muuzaji akipenda mwenyewe kumzidishia mnunuaji, hivyo ni jambo zuri la wema lakini     kupunguza haifai kabisa.

 

 

Kipimo cha haki pia inakusudiwa kutokuuza kitu  kibaya au kughushi kwa aina yoyote ile katika uuzaji.     Yote hayo inakuwa ni dhulma katika kumuuzia mtu kitu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Ameharamisha katika Hadiyth:

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَرَّ عَلَى صُبْرَةِ طَعَامٍ فَأَدْخَلَ يَدَهُ فِيهَا فَنَالَتْ أَصَابِعُهُ بَلَلاً فَقَالَ: ((مَا هَذَا يَا صَاحِبَ الطَّعَامِ؟)) قَالَ:  أَصَابَتْهُ السَّمَاءُ يَا رَسُولَ اللَّهِ. قَالَ: ((أَفَلاَ جَعَلْتَهُ فَوْقَ الطَّعَامِ كَيْ يَرَاهُ النَّاسُ، مَنْ غَشَّ فَلَيْسَ مِنِّي))  مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alipitia katika mrundo wa chakula (nafaka), akaingiza mkono wake ndani. Vidole vyake vikagusa umajimaji. Akasema: ((Ee mwenye chakula, ni nini hii?)). Akajibu: “Ee Rasuli wa Allaah! Kimepatwa na manyunyu”. Akasema: ((Si ungeliweka juu ya chakula ili watu wakione! Anayeghushi si katika mimi)). [Muslim]

 

 

Wala haipasi kuapa kwa uongo katika biashara kwa dalili Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي ذَرٍّ (رضي الله عنه)  عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((ثلاَثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمْ اللَّهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلاَ يَنْظُرُ إِلَيْهِمْ وَلاَ يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ)) قَالَ فَقَرَأَهَا رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ثلاَثَ مِرَارٍ. قَالَ أَبُو ذَرٍّ: خَابُوا وَخَسِرُوا، مَنْ هُمْ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ قَالَ: ((الْمُسْبِلُ، وَالْمَنَّانُ، وَالْمُنَفِّقُ سِلْعَتَهُ بِالْحَلِفِ الْكَاذِبِ)) مسلم  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: “Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Watu watatu Allaah Hatowazungumzisha Siku  ya Qiyaamah, wala Hatowatazama, wala Hatowatakasa, na watapata adhabu inayoumiza)). Akayakariri maneno hayo mara tatu. Abuu Dharr akasema: “Wamepita patupu na wamekhasirika! Ni nani hao ee Rasuli wa Allaah?”  Akasema: ((Al-Musbil - mwenye kuburuza nguo yake, mwenye kutoa na kukizungumzia [kusimbulia] alichokitoa, na mwenye kuuza bidhaa zake kwa kutumia kiapo cha uongo)). [Muslim] 

 

 

 

Watu wa mji wa Madyan ambao walitumiwa Nabiy Shu’ayb ‘('Alayhis-Salaam) walikuwa wakitenda dhulma hiyo, imetajwa katika Qur-aan:   

 

كَذَّبَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٧٦﴾

Watu wa Al-Aykah wamemkadhibisha Rusuli.

 

 

إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٧٧﴾

Alipowaambia Shu’ayb: “Je hamtokuwa na taqwa?”

 

 

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٧٨﴾

 “Hakika mimi kwenu ni Rasuli mwaminifu.

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٧٩﴾

 “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٨٠﴾

 “Na wala sikuombeni ujira wowote juu yake.  Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Rabb wa walimwengu.”

 

 

أَوْفُوا الْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا مِنَ الْمُخْسِرِينَ ﴿١٨١﴾

 “Timizeni kipimo na wala msiwe miongoni mwa wenye kupunja.

 

 

وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ ﴿١٨٢﴾

 “Na pimeni mizani kwa uadilifu iliyosawa.

 

 

وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ ﴿١٨٣﴾

 “Na wala msiwapunje watu vitu vyao, na wala msieneze uovu katika ardhi hali ya kuwa ni wenye kufanya ufisadi. [As-Shu’araa: 176-183]

 

 

Kisa chao kimetajwa pia katika kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَإِلَىٰ مَدْيَنَ أَخَاهُمْ شُعَيْبًا ۗ قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ ۖ قَدْ جَاءَتْكُم بَيِّنَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ ۖ فَأَوْفُوا الْكَيْلَ وَالْمِيزَانَ وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ بَعْدَ إِصْلَاحِهَا ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ﴿٨٥﴾

Na kwa (watu wa) Madyan (Tuliwapelekea) kaka yao Shu’ayb.  Akasema: “Enyi kaumu yangu! Mwabuduni Allaah, hamna Mwabudiwa wa haki ghairi Yake.  Kwa yakini imekujieni hoja bayana kutoka kwa Rabb wenu. Basi timizeni kipimo na mizani wala msipunje watu vitu vyao wala msifanye ufisadi ardhini baada ya kutengenea kwake. Hivyo ni bora kwenu ikiwa mmeamini.” [Al-A’raaf: 85]

 

 

 

 

 

Share

08-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kushuhudia Na Kufanya Uadilifu Japokuwa Dhidi Ya Jamaa Wa Karibu

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

08- Kushuhudia Na Kufanya Uadilifu Japokuwa Dhidi Ya Jamaa Wa Karibu

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa):

 

وَإِذَا قُلْتُمْ فَاعْدِلُوا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ

Na mnaposema basi fanyeni uadilifu japokuwa ni jamaa wa karibu. [Al-An’aam: 152]

 

Ni kusema ukweli na kuweka uadilifu katika kushuhudia jambo dhidi ya mtu binafsi au watu walio na uhusiano wa karibu.   Uadilifu huu unaweza kuwa katika kutoa hukmu, au kushuhudia jambo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika kauli Yake nyengine:  

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ شُهَدَاءَ لِلَّـهِ وَلَوْ عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَوِ الْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ ۚ إِن يَكُنْ غَنِيًّا أَوْ فَقِيرًا فَاللَّـهُ أَوْلَىٰ بِهِمَا ۖ فَلَا تَتَّبِعُوا الْهَوَىٰ أَن تَعْدِلُوا ۚ وَإِن تَلْوُوا أَوْ تُعْرِضُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا ﴿١٣٥﴾

  Enyi walioamini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu mtoapo ushahidi kwa ajili ya Allaah japokuwa ni dhidi ya nafsi zenu au wazazi wawili, au jamaa wa karibu. Akiwa tajiri au maskini Allaah Anawastahikia zaidi. Basi msifuate hawaa mkaacha kufanya uadilifu. Na mkiupotoa au mkikanusha basi hakika Allaah daima kwa yale myatendayo ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [An-Nisaa: 135]

 

 

 Na pia Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

Kusema yaliyo haki na kufanya uadilifu inapaswa hata kwa mtu ambaye una chuki na uadui naye, madamu tu yuko katika haki basi lazima useme ukweli.   Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ لِلَّـهِ شُهَدَاءَ بِالْقِسْطِ ۖ وَلَا يَجْرِمَنَّكُمْ شَنَآنُ قَوْمٍ عَلَىٰ أَلَّا تَعْدِلُوا ۚ اعْدِلُوا هُوَ أَقْرَبُ لِلتَّقْوَىٰ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿٨﴾

Enyi walioamini!  Kuweni wasimamizi madhubuti kwa ajili ya Allaah mkitoa ushahidi kwa uadilifu. Na wala chuki ya watu isikuchocheeni kutokufanya uadilifu. Fanyeni uadilifu; hivyo ni karibu zaidi na taqwa. Na mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo.  [Al-Maaidah: 8]

 

Uadilifu unatakiwa pia hata katika kugawa vitu baina ya watu wenye haki navyo: 

 

عَنْ النُّعْمَان بْن بَشِير أَنَّهُ قَالَ : نَحَلَنِي أَبِي نُحْلًا فَقَالَتْ أُمِّي عَمْرَة بِنْتُ رَوَاحَةَ : لَا أَرْضَى حَتَّى تُشْهِد عَلَيْهِ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَجَاءَهُ لِيُشْهِدهُ عَلَى صَدَقَتِي فَقَالَ  ((أَكُلَّ وَلَدِك نَحَلْت مِثْلَهُ ؟))  قَالَ لَا قَالَ:  ((اِتَّقُوا اللَّه وَاعْدِلُوا فِي أَوْلَادكُمْ)) وَقَالَ – ((إِنِّي لَا أَشْهَد عَلَى جَوْر))  قَالَ فَرَجَعَ أَبِي فَرَدَّ تِلْكَ الصَّدَقَة" البخاري و مسلم

Kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr ambaye amesema: “Baba yangu alinipa zawadi lakini mama yangu ‘Amrah bint Rawaahah hakuridhikia hadi ashuhudie Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Baba yangu akamwendea, akamtaka ashuhudie kunipa kwake zawadi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: ((Je, umewapa hivyo hivyo kwa watoto wako wengine?)) Akajibu. Hapana. Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Mche Allaah, na adilisha [timiza haki] kwa watoto wako)) Akasema: ((Mimi sishuhudii dhidi ya dhulma)) Kisha baba yangu akarudisha zawadi yake: [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

09-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kutekeleza Ahadi Ya Allaah

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

09- Kutekeleza Ahadi Ya Allaah

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

وَبِعَهْدِ اللَّـهِ أَوْفُوا

 

Na timizeni ahadi ya Allaah. [Al-An’aam: 152]

 

Kutimiza ahadi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), ni kutimiza amri Zake Alizotuamrisha na kujiepusha na makatazo yote katika Qur-aan na Sunnah.

 

 

Mojawapo ya ahadi baina yetu na baina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni ile ahadi iliyopokelewa na wana Aadam wote kabla ya kuumbwa.   Tukashuhudia na kuchukua ahadi kwamba tutamtii Muumba wetu na hatutamshirikisha. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):  

 

 

 وَإِذْ أَخَذَ رَبُّكَ مِن بَنِي آدَمَ مِن ظُهُورِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَأَشْهَدَهُمْ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ أَلَسْتُ بِرَبِّكُمْ ۖ قَالُوا بَلَىٰ ۛ شَهِدْنَا ۛ أَن تَقُولُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّا كُنَّا عَنْ هَـٰذَا غَافِلِينَ﴿١٧٢﴾

  Na pindi Rabb wako Alipochukua katika wana wa Aadam kutoka migongoni mwao, kizazi chao, na Akawashuhudisha juu ya nafsi zao, “Je, Mimi siye Rabb wenu?” Wakasema: “Ndio bila shaka, tumeshuhudia!” (Allaah Akawaambia): “Msije kusema Siku ya Qiyaamah: hakika sisi tulikuwa tumeghafilika nayo haya." [Al-A'araf : 172]

 

 

 

Ahadi nyengineyo ni kuunga undugu. Allaah ('Azza wa Jalla) Anawaonya wanaovunja ahadi Zake kwamba watakuwa miongoni mwa waliokhasirika:

 

 الَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهْدَ اللَّـهِ مِن بَعْدِ مِيثَاقِهِ وَيَقْطَعُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٢٧﴾

Wale wanaovunja ahadi ya Allaah baada ya kuifunga Kwake na wanakata Aliyoyaamrisha Allaah kuungwa, na wanafanya ufisadi katika ardhi, hao ndio wenye khasara. [Al-Baqarah: 27]

 

 

Kutimiza nadhiri pia ni miongoni mwa kutimiza ahadi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Anavyosema:

 

 يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا﴿٧﴾

Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea kwa upana. [Al-Insaan: 7]

 

 

Vile vile kutimiza ahadi tunazoahidiana sisi waja Wake. Mfano ahadi baina ya wanandoa, ahadi katika deni, ahadi katika kuamiliana kwa aina yoyote, kwa sababu ahadi hizo ni jukumu lipasalo kutimizwa. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَأَوْفُوا بِالْعَهْدِ ۖ إِنَّ الْعَهْدَ كَانَ مَسْئُولًا ﴿٣٤﴾

Na timizeni ahadi; hakika ahadi itakuwa ni ya kuulizwa [Al-Israa: 34]

 

 

Ahadi pia ni kutimiza miadi ya kukutana mahali kwa muda fulani.   Swala hili ni tatizo sugu katika jamii kwa vile imekuwa ni kawaida watu kutokutimiza miadi mpaka imepewa msemo kuwa ‘miadi ya Kiswahili’ kwa sababu ya kuchelewa katika mahali na muda walioahidiana watu kwa masaa kadhaa!  Mpaka imekuwa wenye shughuli kutaja nyakati za uongo za mialiko kwa kukhofu watu kuchelewa. Na wale wachache wenye kutimiza ahadi wanapofika mapema kwenye shughuli iwe wamepoteza muda wao kuwasubiri wale wanaochelewa kufika.  Kisha watu huona kuwa miadi ya kweli ni miadi ya Kizungu na hali mafunzo haya tumepewa sisi Waislamu kabla ya hao Wazungu kuja kuyatimiza.  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuhusu Nabiy Ismaa’iyl ‘('Alayhis-Salaam):

 

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِسْمَاعِيلَ ۚ إِنَّهُ كَانَ صَادِقَ الْوَعْدِ وَكَانَ رَسُولًا نَّبِيًّا ﴿٥٤﴾

Na mtaje katika Kitabu Ismaa’iyl. Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Rasuli na Nabiy. [Maryam: 54]

 

 

Mfano wa kutokutimiza ahadi ni kuahidi kumpa mwenzio kitu fulani, au kumuahidi kumsaidia tatizo lake fulani, kisha unapofika wakati unamkimbia usitimize ahadi yako. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameonya kuwa hiyo ni miongoni mwa alama za unafiki:     

 

((آية المنافق ثلاث : إذا حدث كذب ، وإذا وعد أخلف ، وإذا اؤتمن خان)) رواه البخاري ومسلم.

((Alama za Mnafiki ni tatu; anapozungumza huongopa, anapotoa ahadi huenda kinyume [hatimizi], na anapoaminiwa hufanya khiyana)) [Al-Bukhaariy na Muslim]  

 

 

Share

10-Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam: Kufuata Njia Iliyonyooka Na Sio Njia Nyinginezo

 

Wasiya Kumi Katika Mwisho Wa Suwrah Al-An'aam  

 

10- Kufuata Njia Iliyonyooka Na Sio Njia Nyinginezo

 

 

 

 Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ﴿١٥٣﴾

 “Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kuwa na taqwa.”  [Al-An’aam:  153]

 

Wasiya huu wa kumi ni muhimu kabisa kutekelezwa kwa sababu ni njia ya  Muislamu kijiweka katika usalama wa Dini yake kwa kubakia katika Tawhiyd, Dini safi na kuthibitisha iymaan na taqwa yake na pia ujieupusha na shari za shaytwaan. Kubakia katika Njia iliyonyooka ni kubakia katika nyendo za Salafus-Swaalih (Wema waliopita).

 

Ufafanuzi wa Swiraatwul-Mustaqiym (Njia iliyonyooka) kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ جَابِر قَالَ : "كُنَّا جُلُوسًا عِنْد النَّبِيّ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَخَطَّ خَطًّا هَكَذَا أَمَامه فَقَالَ ((هَذَا سَبِيل اللَّه)) وَخَطَّيْنِ عَنْ يَمِينه وَخَطَّيْنِ عَنْ شِمَاله وَقَالَ ((هَذِهِ سُبُل الشَّيْطَان)) ثُمَّ وَضَعَ يَده فِي الْخَطّ الْأَوْسَط ثُمَّ تَلَا هَذِهِ الْآيَة" ((وَأَنَّ هَذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُل فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَنْ سَبِيله ذَلِكُمْ وَصَّاكُمْ بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ)) وَرَوَاهُ أَحْمَد وَابْن مَاجَهْ  

Kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: “Tulikuwa tumekaa pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akachora mstari mbele yake, akasema: ((Hii ni njia ya Allaah)). Kisha akachora mistari miwili upande wa kulia (wa huo mstari mkuu) na miwili upande wa kushoto yake, kisha akasema: ((Hizi njia za shaytwaan)) Kisha akaweka mkono wake katika njia ya katikati akasoma:

 

وَأَنَّ هَذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُل فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَنْ سَبِيله ذَلِكُمْ وَصَّاكُمْ بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ

 

((Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kuwa na taqwa.”)) [Ahmad na Ibn Maajah]  

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametoa maonyo mengi na kutahadharisha tusitoke nje ya Swiraatwul-Mustaqiym (Njia iliyonyooka), akafafanua katika Hadiyth:

 

عَنْ النَّوَّاس بْن سَمْعَان عَنْ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ ((ضَرَبَ اللَّه مَثَلًا صِرَاطًا مُسْتَقِيمًا وَعَنْ جَنْبَيْ الصِّرَاط سُورَانِ فِيهِمَا أَبْوَاب مُفَتَّحَة وَعَلَى الْأَبْوَاب سُتُور مُرْخَاة وَعَلَى بَاب الصِّرَاط دَاعٍ يَقُول يَا أَيّهَا النَّاس اُدْخُلُوا الصِّرَاط الْمُسْتَقِيم جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا وَدَاع يَدْعُو مِنْ فَوْق الصِّرَاط فَإِذَا أَرَادَ الْإِنْسَان أَنْ يَفْتَح شَيْئًا مِنْ تِلْكَ الْأَبْوَاب قَالَ وَيْحك لَا تَفْتَحهُ فَإِنَّك إِنْ تَفْتَحهُ تَلِجهُ فَالصِّرَاط الْإِسْلَام وَالسُّورَانِ حُدُود اللَّه وَالْأَبْوَاب الْمُفَتَّحَة مَحَارِم اللَّه وَذَلِكَ الدَّاعِي عَلَى رَأْس الصِّرَاط كِتَاب اللَّه وَالدَّاعِي مِنْ فَوْق الصِّرَاط وَاعِظ اللَّه فِي قَلْب كُلّ مُسْلِم))  وَرَوَاهُ التِّرْمِذِيّ وَالنَّسَائِيّ

Kutoka kwa An-Nawwaas bin Sam’aan kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Ametoa mfano wa Swiratwul-Mustaqiym [njia iliyonyooka] na katika pande mbili za hii njia, kuna kuta mbili zilizokuwa na milango ya kutokea. Katika milango hiyo, kuna mapazia yaliyoteremshwa chini. Na katika mlango wa njia hii kuna muitaji “Enyi watu! Njooni muingie katika Njia Iliyonyooka pamoja msigawanyike”. Kisha kuna muitaji mwengine anayeita kutoka juu ya njia ambaye humwambia mtu anapotaka kuondosha pazia katika milango yoyote hii. “Ole wako! Usifungue mlango huu, kwani ukiufungua utakuja kuingia humo. Njia Iliyonyooka ni Uislamu. Kuta mbili ni mipaka ya Allaah. Milango iliyofunguliwa inaongoza katika maharimisho ya Allaah. Muitaji katika lango la njia ni kitabu cha Allaah (Qur-aan), na muitaji kutoka juu ya njia ni mawaidha ya Allaah katika moyo wa kila Muislamu)) [Ahmad]  

 

Na akasisitiza kubakia katika manhaj yake ili Muislamu abakie salama katika Dini yake. Miongoni mwa matahadharisho yake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na masisitizo hayo ni Hadiyth zifuatazo:

 

Amesema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

((افترقت اليهود على إحدى وسبعين فرقة، وافترقت النصارى على اثنتين وسبعين فرقة، وستفترق هذه الأمة على ثلاث وسبعين فرقة كلها في النار إلا واحدة)) فقال الصحابة: من هي يا رسول الله؟ قال: ((من كان على مثل ما أنا عليه وأصحابي)) الترمذي والحاكم

((Waligawanyika Mayahudi katika makundi sabini na moja, na waligawanyika Manaswara katika makundi sabini na mbili, na utagawanyika Umma wangu katika makundi sabini na tatu, yote yataingia motoni ila moja!)) Maswahaba wakasema: 'Ni kundi lipi hilo Ee Rasuli wa Allaah?  Akajibu: ((Ni lile ambalo litakuwa katika mwenendo wangu hii leo na Maswahaba zangu)) [Imepokewa na Maimaam At-Tirmidhiy na Al-Haakim]

 

 Na akasema pia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

 ((أُوصِيكُمْ بِتَقْوى اللَّه، وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وإِنْ تَأَمَّر عَلَيْكُمْ عَبْدٌ حبشيٌ، وَأَنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيرى اخْتِلافاً كثِيرا. فَعَلَيْكُمْ بسُنَّتي وَسُنَّةِ الْخُلُفَاءِ الرَّاشِدِينَ الْمَهْدِيِّينَ، عضُّوا عَلَيْهَا بالنَّواجِذِ، وإِيَّاكُمْ ومُحْدثَاتِ الأُمُورِ فَإِنَّ كُلَ بِدْعَةٍ ضلالَةٌ)) رواه أبو داود، والترمذِي وقال حديث حسن صحيح

((Nakuusieni kumcha Allaah, usikivu na twaa hata ikiwa kiongozi wenu (Au atakayekuamrishen) ni Mtumwa wa Habash. Mtakaoishi miongoni mwenu mtaona ikhtilafu nyingi. Kwa hiyo shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa waliongoka baada yangu.  Ziumeni kwa magego (zikamateni kwa nguvu wala msiziache). Na tahadharini na mambo ya uzushi kwani kila bid'ah ni upotofu)) [Abu Daawuwd, At-Trimidhiy kasema Hadiyth Hasan Swahiyh]   

 

Na akasema pia:

 

((تَرَكْتُ فِيكُمْ مَا اِنْ تَمَسَّكْتُمْ بِهِ لَنْ تَضِلُّوا بَعْدِي اَبَداً  كِتَابُ الله وَسُنَّتِي))

((Nakuachieni kile ambacho mkikishikilia hamtapotea abadan baada yangu nacho ni Kitabu cha Allaah   na Sunnah zangu)) [Hasan: Imesimuliwa na Maalik katika al-Muwattwa (2/899) na al-Haakim (1/93), kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa). Imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy katika as-Silsilah as-Swahiyhah (Namba 1871)]

 

Tahadhari na shaytwaan ambaye yumo katika jihadi kubwa ya kuwapotosha watu kwa kuwatoa nje ya Swiraatwul-Mustaqiym (Njia iliyonyooka); alisema kumwambia Allaah ('Azza wa Jalla):

 

 قَالَ فَبِمَا أَغْوَيْتَنِي لَأَقْعُدَنَّ لَهُمْ صِرَاطَكَ الْمُسْتَقِيمَ ﴿١٦﴾

  (Ibliys) Akasema: “Basi kwa kuwa Umenihukumia kupotoka, nitawakalia (waja Wako) katika njia Yako iliyonyooka.”

 

 

ثُمَّ لَآتِيَنَّهُم مِّن بَيْنِ أَيْدِيهِمْ وَمِنْ خَلْفِهِمْ وَعَنْ أَيْمَانِهِمْ وَعَن شَمَائِلِهِمْ ۖ وَلَا تَجِدُ أَكْثَرَهُمْ شَاكِرِينَ ﴿١٧﴾

 “Kisha nitawaendea mbele yao na nyuma na kuliani kwao na kushotoni kwao, na wala Hutopata wengi wao wenye kushukuru.” [Al-A’raaf: 16-17]

 

 

WabiLLaahi At-Tawfiyq

 

 

 

Share