Sifa Kumi Za Waumini Katika Suwrah Al-Ahzaab Na Fadhila Zake

 

 

 

Sifa Kumi Za Waumini Katika Suwrah Al-Ahzaab

Na Fadhila Zake

 

www.alhidaaya.com

 

 

Share

01-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Waislamu Wanaume Na Wanawake

 

 Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

01-Waislamu Wanaume Na Wanawake

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

 إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ وَالْحَافِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَالْحَافِظَاتِ وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao swadaqah wanaume na wanawake, na wafungao Swawm wanaume na wanawake, wanaojihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, na wanaomdhukuru Allaah kwa wingi wanaume na wanawake; Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu. [Al-Ahzaab: 35]

           

 

Kama tunavyoona katika hiyo Aayah tukufu kuwa hizo ni sifa kumi Alizozitaja Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ambazo pindi Muislamu akizimiliki atapata kughufuriwa madhambi yake na kupata ujira mkubwa kutoka kwa Allaah ('Azza wa Jalla). Hivyo kila mmoja wetu apime nafsi yake na kuhesabu kama yumo katika kumiliki sifa hizi zote kumi.

 

Ikiwa mtu anamiliki sifa mojawapo au zaidi yake, basi ajitahidi kuzifanyia kazi zote ili akamilishe kuwa na sifa hizo.

 

 

Sababu ya kuteremshwa Aayah hii:

 

 

 عن عبد الرحمن بن شيبة، سمعت أم سلمة زوج النبي صلى الله عليه وسلم تقول: قلت للنبي صلى الله عليه وسلم: ما لنا لا نُذْكَرُ في القرآن كما يذكر الرجال؟ قالت: فلم يَرعني منه ذات يوم إلا ونداؤه على المنبر، قالت، وأنا أسَرّح شعري، فلففت شعري، ثم خرجت إلى حُجْرة من حُجَر بيتي، فجعلت سمعي عند الجريد، فإذا هو يقول عند المنبر) يا أيها الناس، إن الله يقول:   إن المسلمين والمسلمات والمؤمنين والمؤمنات)) إلى آخر الآية  (الإمام أحمد)

 

Imetoka kwa 'Abdur-Rahmaan bin Shaybah kwamba: Nimemsikia Ummu Salamah    mke wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  akisema:  “Nilimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): Kwa nini sisi wanawake hatutajwi (sana) katika Qur-aan kama wanavyotajwa wanaume? Kisha siku moja bila ya mimi kutambua, alikuwa akiita katika Minbar nami nilikuwa nikichana nywele zangu, nikazifunga nywele zangu nyuma kisha nikaingia chumbani katika vyumba vya nyumba yangu, nikaanza kusikiliza, naye alikuwa akisema kutoka katika Minbar: ((Enyi watu! Allaah Anasema: “Hakika Waislamu wanaume na Waislamu wanawake na Waumini wanaume  na Waumini wanawake…)) mpaka mwisho wa Aayah. [Imaam Ahmad] 

 

 

Sifa ya kwanza:

 

 إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ

 Hakika Waislamu wanaume na wanawake 

 

 

Zinatambulika nguzo za Kiislamu kuwa ni tano. Muislamu anapaswa kuzitimiza zote ili ukamilike Uislamu wake. Nguzo hizo zimetajwa katika Hadiyth ifuatayo:

 

 عبدالله بن عمر  قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم (( بُنِـيَ  الإِسْلاَمُ علـى خَمْسٍ: شَهادَةِ أنْ لا إِلٰهَ إلا الله وأنَّ مُـحَمَّداً رَسُولُ الله وإِقامِ الصَّلاَةِ وإِيتاءِ الزَّكاةِ وَحَجِّ البَـيْتِ وَصَوْمِ رَمَضَانَ)) البخاري

 

Kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Uislamu umejengeka kwa matano; Kushuhudia kwamba hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah na kuswali [Swalaah tano], kutoa Zakaah, kuhiji katika Nyumba [Makkah] na Swawm ya Ramadhwaan)) [Al-Bukhaariy]

 

Maana Ya Islaam: 

 

Maana ya ‘Islaam’ ni kujisalimisha na kunyenyekea kwa Allaah, na pia inatokana na neno 'salaam' lenye maana ya  'amani'. Kwa hiyo tunapoamiliana na watu ikiwa ni Waislamu au wasio Waislamu inatupasa tuonyeshe sifa hii yenye maana asili ya Dini ya Allaah ('Azza wa Jalla), sifa ya usalama na amani kwa sababu Dini hii tukufu ni ya amani na usalama na sio kama inavyodhaniwa na baadhi ya makafiri.

 

Muislamu aweke usalama na amani kwa wasio Waislamu katika kutaamuli nao kwa kutokuwatendea maovu, kutimiza ahadi nao, kutaamuli nao vizuri katika biashara na kadhalika madamu wao hawakufanyia maudhi au kuwasababishia madhara Waislamu kwa lolote.  Dalili ni kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ لِلَّـهِ شُهَدَاءَ بِالْقِسْطِ ۖ وَلَا يَجْرِمَنَّكُمْ شَنَآنُ قَوْمٍ عَلَىٰ أَلَّا تَعْدِلُوا ۚ اعْدِلُوا هُوَ أَقْرَبُ لِلتَّقْوَىٰ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿٨﴾

Enyi walioamini!  Kuweni wasimamizi madhubuti kwa ajili ya Allaah mkitoa ushahidi kwa uadilifu. Na wala chuki ya watu isikuchocheeni kutokufanya uadilifu. Fanyeni uadilifu; hivyo ni karibu zaidi na taqwa. Na mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo.  [Al-Maaidah: 8]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

لَّا يَنْهَاكُمُ اللَّـهُ عَنِ الَّذِينَ لَمْ يُقَاتِلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَلَمْ يُخْرِجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ أَن تَبَرُّوهُمْ وَتُقْسِطُوا إِلَيْهِمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٨﴾

Allaah Hakukatazeni kuwafanyia wema na uadilifu wale wasiokupigeni vita katika Dini, na wala hawakukutoeni kutoka majumbani mwenu. Hakika Allaah Anapenda wafanyao uadilifu. [Al-Mumtahinah: 8]

 

 

Pindi Muislamu atakapotaamuli na asiye Muislamu kama tunavyomarishwa na Allaah ('Azza wa Jalla) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na tukafuata mifano na mwongozo wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyothibiti katika Siyrah yake, basi makafiri watapata kujua maana halisi ya Uislamu na kuupenda na ndio maana utasikia makafiri wengi wanaingia katika Dini ya Kiislamu baada ya kusoma Siyrah na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kutambua tabia zake na jinsi alivyotaamuli na makafiri ikawa ni sababu ya wengi kuingia katika Uislamu. 

 

Ama kwa Waislamu dalili tele zipo mojawapo ni Hadiyth tukufu ifuatayo inayotaja khasa kuhusu kuwekeana usalama na amani:

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو (رضي الله عنهما) قَال: قَال رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الْمُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ الْمُسْلِمُونَ مِنْ لِسَانِهِ وَيَدِهِ  وَالْمُهَاجِرُ مَنْ هَجَرَ مَا نَهَى اللَّهُ عَنْهُ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah in ‘Amr (رضي الله عنهما) ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muislamu ni yule anayeweka amani kwa watu [ambaye Waislamu wenziwe wanasalimika] kwa ulimi na mkono wake. Na mhamaji ni yule anayehama Aliyoyakataza Allaah)).  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

02-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Waumini Wanaume Na Wanawake

 

 Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

02 - Waumini Wanaume Na Wanawake

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

((إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ…..))

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Katika Aayah hiyo tukufu, Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametaja sifa ya pili ambayo ni Waumini baada ya kutaja Waislamu. Kwa hivyo kuna tofuati hapo baina ya Muislamu na Muumini, na dalili ya kutofuatiana inapatikana pia katika Hadiyth ifuatayo:

 

 

 عن عامر بن سعد عن أبيه قال: أعطى النبيّ صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّم رجالا ولم يعط رجلا منهم شيئا ، فقال سعد: يا رسول الله أعطيت فلانا وفلانا  ولم تعط فلانا شيئا وهو مؤمن ، فقال النبيّ صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّم: أو مُسْلِمٌ؟ حتى أعادها سعد ثلاثا ، والنبيّ صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّم يقول: أوْ مُسْلِمٌ ، ثم قال النبي صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّم إني أُعْطِي رِجالا وأَدَعُ مَنْ هُوَ أحَبُّ إليَّ مِنْهُمْ ، لا أُعْطِيه شَيْئا مَخافَةَ أنْ يُكَبُّوا فِي النَّارِ عَلى وُجُوهِهِمْ"  أحمد وأخرجاه في الصحيحين من حديث الزهري .

 

Imetoka kwa 'Aamir bin Sa'ad bin Abi Waqqaasw (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa baba yake ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitoa (baadhi ya vitu) na kuwapa baadhi ya watu na akaacha kuwapa baadhi yao. Sa'ad akasema: "Ee Rasuli wa Allah, umempa fulani na fulani na fulani na fulani, lakini hukumpa chochote fulani ingawa naye ni Muumini." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Au Muislamu)). Sa'ad akarudia kusema kauli hiyo mara tatu kila mara Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alijibu: ((Au Muislamu)). Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

akasema: ((Huenda nikawapa baadhi ya watu na nisiwape chochote wengine, ingawa wa mwisho ni kipenzi kwangu kuliko wa mwanzo. Siwapi vitu (hao) kwa khofu kwamba huenda wakatupwa katika moto)) [Ahmad na Al-Bukhaariy na Muslim wamesimulia kutoka kwa Az-Zuhriy]

 

 

Dalili nyengineyo ya kutofautisha baina ya Uislamu na Muumini ni katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Mabedui walipoingia Uislamu walimjia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia kuwa wao wameamini. Lakini Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anawajulisha kuwa kuna tofauti ya kusilimu na kuamini:

 

 قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا ۖ قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَـٰكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي قُلُوبِكُمْ ۖ وَإِن تُطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَا يَلِتْكُم مِّنْ أَعْمَالِكُمْ شَيْئًا ۚ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١٤﴾

Mabedui walisema: “Tumeamini!” Sema (ee Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)): “Hamkuamini, lakini semeni: “Tumesilimu.” Kwani iymaan haijaingia bado nyoyoni mwenu. Na mtakapomtii Allaah na Rasuli Wake, Hatokupunguzieni katika ‘amali zenu kitu chochote. Hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Hujuraat: 14]

 

Aayah hii inathibitisha kuwa daraja ya Muumini ni ya juu kuliko ya Muislamu, na hii ni rai ya ‘Ulamaa wa Ahlus-Sunnah wal-Jamaa'ah. Na Aayah hii imeonyesha kwamba kuamini ni kumtii Allaah ('Azza wa Jalla)  kufuata yale yote Aliyotuamrisha na kujiepusha na yale Aliyotuharamisha katika Qur-aan.

 

Na kumtii Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni kufuata amri zake na mafunzo yote aliyotuletea katika Sunnah zake, hapo ndipo Iymaan itakuwa imeingia moyoni mwa Muislamu.

 

Mfano kutofanya maasi yaliyotajwa katika Hadiyth ifuatayo ya Abuu    Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu):

 

((لا يزني الزاني حين يزني وهو مؤمن ، ولا يشرب الخمر حين يشربها وهو مؤمن ، ولا يسرق السارق حين يسرق وهو مؤمن)) البخاري

((Hazini mzinifu  anapozini  hali ya kuwa ni Muumini, wala hanywi pombe   anapokunywa hali ya kuwa ni  Muumini, wala haibi mwizi  anapoiba hali ya kuwa ni Muumini)) [Al-Bukhaariy]

 

 

Kisa cha Julaybiyb na Swahaabiyah aliyemtii Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

 

Swahaba aliyeitwa Julaybiyb alijulikana sana kuwa alikuwa ni mtu duni asiyemiliki mali na hakuwa ni mzuri kwa sura na umbo, na alikuwa ni mtu wa kuchekesha watu. Kwa hivyo hakuna aliyetaka kumuozesha binti yake. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alimuuliza Julaybib kama anataka kuoa, naye akamjibu: "Ee Rasuli wa Allaah, nani atakayekubali nimuoe mimi? Sina nyumba wala wala mali wala chochote katika mapambo ya dunia."

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamtuma mtu mmoja aende nyumba ya Answaariy fulani ambao walikuwa ni familia yenye kujulikana kwa kabila lao maarufu kubwa lenye kujulikana kwa heshima na wenye hali nzuri. Alipopiga hodi, alifungua mlango mama wa binti huyo. Swahaba akamjulisha kuwa ametumwa na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuleta posa kwa binti yake. Mama huyo alifurahi sana kudhania kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ndiye anayetaka kumposa binti yake.

Swahaba Alipomjulisha kuwa sio kwa ajili ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  bali ni kwa ajili ya Julaybiyb, mama huyo alisema: "Nani? Julaybib? Hapana! Hatumuozeshi yeye binti yetu!" Mara yule binti alisikia mazungumzo hayo akaja kuuliza vizuri: "Nani anayetaka kuniposa?" Mama mtu akamuelezea kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amemtuma mtu aje kumposa yeye kwa ajili ya Julaybiyb. Binti huyo alimwambia mama yake: "Vipi mama unakataa amri ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)? Fuata amri yake kwani hakuna kitakachonidhuru.” (Katika usemi mmoja ni kwamba hapo hapo Aayah ifuatayo iliteremshwa [Ibnu Kathiyr 7:692-694]) na katika usemi mwingine aliwaambia wazazi wake: "Hamkusikia kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّـهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ ۗ وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا ﴿٣٦﴾

Na haiwi kwa Muumini mwanamme na wala kwa Muumini mwanamke, Anapohukumu Allaah na Rasuli Wake jambo lolote, iwe wana hiari katika jambo lao.  Na anayemuasi Allaah na Rasuli Wake, basi kwa yakini amepotoka upotofu bayana. [Al-Ahzaab: 36]

 

Ikabidi wamuozeshe binti yao kwa Julaybiyb. Kisha katika vita fulani alitoka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba miongoni mwao ni Julaybiyb na baada ya ushindi wa vita hivyo, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  aliwauliza Maswahaba kabla ya kurudi:  ((Je, kuna mtu aliyekosekana?)) Wakataja baadhi ya Maswahaba waliokosekana kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akawauliza tena wakasema: "Hakuna mtu mwingine aliyekosekana.” Lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Lakini mimi naona kwamba Julaybiyb amekosekana)) yaani hayupo na sisi.  (Nendeni mkamtafute miongoni mwa waliouliwa)). Wakaenda Maswahaba kumtafuta wakamkuta ameuawa akiwa karibu yake makafiri saba ambao aliwahi kuwaua yeye Julaybiyb. Maswahaba wakamjulisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  ambaye alikwenda na kusimama karibu naye kisha akasema: ((Ameua saba kisha wakamuua. Yeye ni wangu na mimi ni wake)).

 

Alisema hivyo mara mbili au tatu, kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akambeba kwa mikono yake na kwenda kumzika. Na akamuombea Du'aa mke wake:

 

 

((الَّلهُمَّ، صَبَّ عَلَيْهَا [الخير] صَبَّا، وَلاَ تَجْعَل عَيْشَها كَدَّا))

((Ee Allah, Mjaze kheri (nyingi) zilizojaa na Usimjaaliye maisha yake kuwa ni ya shida [tabu na mashaka]))

 

Imesemekana kwamba hakuweko mjane aliyekuwa ana maisha mema kama maisha ya mke wa Julaybiy (Radhwiya Allaahu ‘anhaa).

 

[Kisa kimesimuliwa na Imaam Ahmad Muslim na An-Nasaaiy]

 

 

Baada ya Aayah hiyo katika Suratul-Hujuraat inayotujulisha kwamba kuamini ni kumtii Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kisha Anaendelea Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Kutujulisha nani hasa ni Waumini wa kweli waliosadiki:

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ لَمْ يَرْتَابُوا وَجَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ﴿١٥﴾

Hakika Waumini ni wale waliomwamini Allaah na Rasuli Wake, kisha wakawa si wenye shaka, na wakafanya jihaad kwa mali zao na nafsi zao katika njia ya Allaah. Hao ndio wakweli. [Al-Hujuraat: 15]

 

 

Mfano mwengine wa wale walioamini kweli katika kupigana Jihaad kwa nafsi zao katika kisa kifuatacho cha  Handhwalah Aliyeoshwa na Malaika:

 

Handhwala bin Abi 'Aamir ni Swahaba ambaye alifunga ndoa usiku ambao ulinadiwa vita vya Uhud. Aliwahi kulala na mke wake usiku huo mmoja lakini iliponadiwa sauti ya kutoka kwenda Jihaad hakuna chochote kilichomshughulisha wakati huo ila ni kutoka na kukimbilia vitani hata hakuwahi kukoga janaba.

 

Baada ya vita kumalizika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaambia Maswahaba kwamba Malaika wamemuosha Handhwalah. Akawatuma wakaulize nyumbani kwake alitoka vipi? Mkewe akawajulisha kuwa alitoka bila ya kuwahi kukoga janaba. Walipokwenda kumtazama Handhwalah walimuona akichirizikwa na maji kama kwamba katokwa kukoshwa. Tokea siku hiyo akajulikana na kuitwa "Aliyeoshwa na Malaika."

 

Hao ndio Maswahaba walioamini kweli wakajitolea nafsi zao bila ya kuona umuhimu wa jambo lolote jengine kuliko amri ya Allaah ('Azza wa Jalla) kuhusuu Jihaad katika Njia ya Allaah.

 

 

 

Share

03-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Watiifu Wanaume Na Wanawake

 

 Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

03 – Watiifu Wanaume Na Wanawake  

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) :

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Maana ya Qunuwt (kutii) kwa ujumla katika lugha ya  Qur-aan na katika tafsiyr ya Aayah zinazotaja neno hilo ni: Utiifu katika hali ya utulivu.

Kwa ufafanuzi zaidi ni; kukaa kimya na kuleta du'aa, tasbihi, Swalaah, unyenyekevu katika ‘ibaadah khasa kisimamo cha usiku cha Swalaah na kusoma Qur-aan. Ndio maana du'aa katika Swalaah ya mwisho ya usiku ikaitwa  du'aa ya Qunuwt Al-Witr na ambayo inasomwa katika hali ya kusimama. Na pia Hadiyth ifuatayo imethibitisha maana hiyo:

 

 

عبدالله بن عمرو عن النبي صلى الله عليه وسلم ((من قام بعشرِ آياتٍ لم يُكتبْ من الغافلينَ ، ومن قام بمئةِ آيةٍ كُتبَ من القانتينَ ومن قام بألفِ آيةٍ كُتبَ من المُقَنْطِرينَ)) صحيح أبي داود  

 

Amesimulia ‘Abdullaah bin ‘Amr (رضي الله عنه): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Atakayesimama usiku kuswali na akasoma Aayah kumi, hatoandikiwa kuwa miongoni mwa walioghafilika, na atakayesimama kuswali akasoma Aayah mia, ataandikiwa ni miongoni mwa watiifu, na atakayesimama kuswali akasoma Aayah elfu, ataandikwa miongoni mwa wenye mirundi (ya thawabu).’ [Abuu Daawuwd, Al-Albaaniy ameisahihisha: Swahiyh Abiy Daawuwd (1398), Swahiyh Al-Jaami’ (6439)]

 

 

Vile vile Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:

 

أَمَّنْ هُوَ قَانِتٌ آنَاءَ اللَّيْلِ سَاجِدًا وَقَائِمًا يَحْذَرُ الْآخِرَةَ وَيَرْجُو رَحْمَةَ رَبِّهِ

Je, yule aliye mtiifu nyakati za usiku akisujudu, au akisimama (kuswali), anatahadhari na Aakhirah na anataraji rahmah ya Rabb wake (ni sawa na aliyekinyume chake?). [Az-Zumar: 9]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

  وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ﴿٢٣٨﴾

na simameni mbele ya Allaah katika hali ya utiifu. [Al-BaqaraH; 238]

 

Maryam mama yake Nabiy ‘Iysaa ‘('Alayhis-Salaam) amepewa sifa hiyo ya kuwa miongoni mwa A-Qaanitiyn katika kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَمَرْيَمَ ابْنَتَ عِمْرَانَ الَّتِي أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا فَنَفَخْنَا فِيهِ مِن رُّوحِنَا وَصَدَّقَتْ بِكَلِمَاتِ رَبِّهَا وَكُتُبِهِ وَكَانَتْ مِنَ الْقَانِتِينَ﴿١٢﴾

Na Maryam binti wa ‘Imraan ambaye amehifadhi tupu yake, Tukampulizia humo (katika nguo yake) kupitia kwa Ruwh Wetu (Jibriyl), na akasadikisha Maneno ya Rabb wake, na Vitabu Vyake, na akawa miongoni mwa watiifu na wanyenyekevu. [At-Tahriym: 12]

 

 

Na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akamumrisha:

 

يَا مَرْيَمُ اقْنُتِي لِرَبِّكِ وَاسْجُدِي وَارْكَعِي مَعَ الرَّاكِعِينَ ﴿٤٣﴾

 “Ee Maryam!  Kuwa mtiifu kwa Rabb wako, na sujudu, na rukuu pamoja na wanaorukuu.” [Al'Imraan: 43]

 

 

Kisa Maryam mama wa Nabiy ‘Iysaa ‘('Alayhis-Salaam) kinachothibitisha sifa yake ya utiifu:

 

 

Hannah bint Faaquwdh alikuwa mke wa Bwana 'Imraan. Imesemekena kwamba alikuwa hakujaaliwa kupata watoto na kwamba siku moja aliona ndege akimlisha kinda chake. Alipoona hivyo akatamani sana kupata mtoto akaomba du'aa kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amjaalie kizazi. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akamtakabalia du'aa yake akashika mimba. Akaweka nadhiri kumfanya mwanawe awe mwenye kumakinika katika ‘ibaadah na kuihudumia Baytul-Maqdis (Msikiti wa Aqswaa). Hivyo alipotambua kuwa amekwishabeba mimba akaweka hiyo nadhiri. Kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِذْ قَالَتِ امْرَأَتُ عِمْرَانَ رَبِّ إِنِّي نَذَرْتُ لَكَ مَا فِي بَطْنِي مُحَرَّرًا فَتَقَبَّلْ مِنِّي ۖ إِنَّكَ أَنتَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٣٥﴾ 

Pale aliposema mke wa ‘Imraan: “Rabb wangu, hakika mimi nimeweka nadhiri Kwako kilichomo katika tumbo langu kuwa ni wakfu kukutumikia, basi nitakabalie. Hakika wewe ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote. [Al-'Imraan: 35]

 

Kwa maana: Wewe Unasikia du'aa yangu na Unatambua niyyah yangu. Mama yake Maryam hakujua kama atajaaliwa mtoto wa kiume au wa kike. Alipojifungua mtoto wa kike aliona kwamba mwanamke sio kama mwanamume kwa kukusudia katika kujifunga na ‘ibaadah Msikitini. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَلَمَّا وَضَعَتْهَا قَالَتْ رَبِّ إِنِّي وَضَعْتُهَا أُنثَىٰ وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا وَضَعَتْ وَلَيْسَ الذَّكَرُ كَالْأُنثَىٰ ۖ وَإِنِّي سَمَّيْتُهَا مَرْيَمَ وَإِنِّي أُعِيذُهَا بِكَ وَذُرِّيَّتَهَا مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ ﴿٣٦﴾

Basi alipomzaa akasema: “Rabb wangu, hakika mimi nimezaa mwanamke,” na Allaah Anajua zaidi alichokizaa. “Na mwanamme si kama mwanamke. Nami nimemwita Mayram nami namkinga Kwako na dhuria wake kutokana na shaytwaan aliyetokomezwa mbali na kulaaniwa. [Al-'Imraan: 36]

 

 

Maana ya Maryam ni 'Mtumishi wa Allaah'.

 

Aayah hiyo inathibitisha kuruhusiwa kumpa jina mtoto siku ile ile anayozaliwa (kama ambavyo imethibiti kumpa jina mtoto katika siku ya saba wakati wa kumfanyia 'Aqiyqah), na vile vile ni dhahiri katika Aayah hii kwamba hii ilikuwa pia ni shariy’ah ya watu waliokuwa kabla yetu.  Na pia iko katika Sunnah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliposema:

 ((وُلِدَ لِي اللَّيْلَةَ وَلَد سَمَّيْتُهُ بِاسْمِ أبِي إبْرَاهِيمَ))

((Usiku huu mtoto (wa kiume) amezaliwa kwangu na nimemwita jina la baba yangu Ibraahiym)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Kama Aayah ilivyomalizikia kwamba Bibi Hannah alimuomba  Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amkinge mwanawe na shaytwaan. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akamtakabalia du'aa yake na dalili ni Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu):

 

 ((مَا مِن مَوْلُودٍ يُولَدُ إلا مَسَّه الشَّيْطَانُ حِينَ يُولَدُ، فَيَسْتَهِلّ صَارخًا مِنْ مَسِّهِ إيَّاهُ، إلا مَرْيَم َوابْنَهَا)) ثم يقول أبو هريرة: اقرأوا إن شئتم: (( وَإِنِّي أُعِيذُهَا بِكَ وَذُرِّيَّتَهَا مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ ))

((Hakuna kizazi chochote kinachozaliwa ila shaytwaan anakigusa kinapozaliwa, na mtoto huanza kulia kwa sababu ya kuguswa huko, isipokuwa Maryam na mtoto wake [yaani 'Iysaa ('Alayhis-Salaam)]

 

Abuu Hurayrah kisha akasema someni mkipenda: ((nami namkinga Kwako na dhuria wake kutokana na shaytwaan aliyetokomezwa mbali na kulaaniwa.)) [Aal-‘Imraan: 36] [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Maryam akapelekwa Msikitini tokea utoto wake na akakulia huko na mama yake akamtoa kama ni zawadi ya Baytul-Maqdis.

 

Baada ya kufariki baba yake Maryam, wale waliokuwa na jukumu la kuihudumia Baytul-Maqdis waligombania kumlea Maryam.   Walisema kwamba kwa vile ni mtoto wa Bwana 'Imraan ambaye alikuwa ni Imaam wao basi ni jukumu lao kumlea. Zakariyyah ('Alayhis-Salaam)  naye akadai kumlea Maryam akasema: "Nipeni mimi kwani ndugu wa mama yake ni mke wangu." Wakasema: "Nyoyo zetu hazitopenda umlee wewe kwa sababu ni mtoto wa Imaam wetu." Ikabidi wafanye kura ya kutupa kalamu zao walizokuwa wakiandikia Tawrati katika mto wa Jordan. Yule ambaye kalamu yake itaelea katika mto ndiye atakayemlea Maryam.  Walipozitupa kalamu zao, zote zilizama isipokuwa ya Zakariyyah  ‘('Alayhis-Salaam) ambaye pia naye alikuwa ni bwana wao, Mwanachuoni wao na pia ni Rasuli wa Allaah. 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anakitaja kisa hiki katika Qur-aan kwa Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kisha Anawatanabahisha makafiri  kwamba hizi ni habari za ghaibu ambazo hakuzijua Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kabla, kwa maana, haya maelezo ya Qur-aan si maneno ya Rasuli wa Allaah  kama wanavyodai makafiri. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

ذَٰلِكَ مِنْ أَنبَاءِ الْغَيْبِ نُوحِيهِ إِلَيْكَ ۚ وَمَا كُنتَ لَدَيْهِمْ إِذْ يُلْقُونَ أَقْلَامَهُمْ أَيُّهُمْ يَكْفُلُ مَرْيَمَ وَمَا كُنتَ لَدَيْهِمْ إِذْ يَخْتَصِمُونَ ﴿٤٤﴾ 

Hizo ni khabari za ghayb Tunakufunulia Wahy (ee Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).  Na hukuwa pamoja nao walipotupa kalamu zao, ili nani kati yao amlee Maryam. Na hukuwapamoja nao walipokhasimiana. [Al-'Imraan: 44]

 

Basi alipozaliwa Maryam, Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Alikubali nadhiri ya mama yake Akamjaaliya kuwa na tabia njema na kupata elimu ya Dini yake kutoka kwa Nabiy Zakariyyah ‘('Alayhis-Salaam) hata akawa mtiifu mwenye taqwa ya hali ya juu na akapata sifa ya 'utiifu' kama alivyotajwa katika Aayah hizo za juu. Alikuwa akifanya ‘ibaadah kutwa kucha.    Ikawa kila mara Zakariyyah ‘('Alayhis-Salaam) anapoingia katika mihraab (sehemu yake aliyokuwa akiswalia) anamkuta ana matunda ya ajabu; yaani, pindi ukiwa ni msimu wa baridi anamkuta ana matunda ya msimu wa joto na pindi akiingia msimu wa joto anamkuta ana matunda ya msimu wa baridi, ndipo alipomuuliza kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَتَقَبَّلَهَا رَبُّهَا بِقَبُولٍ حَسَنٍ وَأَنبَتَهَا نَبَاتًا حَسَنًا وَكَفَّلَهَا زَكَرِيَّا ۖ كُلَّمَا دَخَلَ عَلَيْهَا زَكَرِيَّا الْمِحْرَابَ وَجَدَ عِندَهَا رِزْقًا ۖقَالَ يَا مَرْيَمُ أَنَّىٰ لَكِ هَـٰذَا ۖ قَالَتْ هُوَ مِنْ عِندِ اللَّـهِ ۖ إِنَّ اللَّـهَ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿٣٧﴾ 

Basi Rabb wake Akampokea kwa kabuli njema na Akamkuza mkuzo mzuri na Akamfanya Zakariyyaa kuwa mlezi wake. Kila Zakariyyaa alipoingia kwake katika chumba cha kuswalia alikuta kwake kuna riziki Akasema: “Ee Maryam! Umepata wapi hivi? ”Akasema: “Hivi ni kutoka kwa Allaah. Hakika Allaah Anamruzuku Amtakaye bila ya hesabu.” [Al-'Imraan: 37]

 

[Kisa kama kilivyonukuliwa katika tafsiyr ya Ibn Kathiyr]

 

Na Maryam mama yake Nabiy ‘Iysaa ‘('Alayhis-Salaam) ni miongoni mwa wanawake walio bora kabisa kama alivyotujulisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika Hadiyth:

 

عن أبي موسى الأشعري قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم  ((كَمُلَ مِنَ الرِّجَالِ كَثِيرٌ وَلَمْ يَكْمُلْ مِنَ النِّسَاءِ إِلا مَرْيَمُ بِنْتُ عِمْرَانَ وَآسِيَةُ امْرَأَةُ فِرْعَوْنَ"))

 

 وقد أخرجه الجماعة إلا أبا داود  ولفظ البخاري:

((كَمُلَ مِنَ الرِّجَالِ كَثِيرٌ وَلَمْ يَكْمُلْ مِنَ النِّسَاءِ إِلا آسِيَةُ امْرَأَةُ فِرْعَوْنَ، وَمَرْيَمُ بِنْتُ عِمْرَانَ ، وَإنَّ فَضْلَ عَائِشَةَ عَلَى النِّسَاءِ كَفَضْلِ الثَّرِيدِ عَلَى سَائِرِ الطَّعَامِ)).

Kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash'ariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)     amesema: ((Wanaume wamepata ukamilifu, na hawakukamilika wanawake ila  Maryam bint 'Imraan na Aasiyah mke wa Fir'awn)) [Imesimuliwa na wote isipokuwa Abu Daawuwd.

 

Na katika usemi wa Al-Bukhaariy]:

 

((Wanaume wengi wamefikia daraja ya ukamilifu lakini hakuna mwanamke aliyefikia daraja hiyo isipokuwa Aasiyah mke wa Fir'awn, na Maryam bint 'Imraan. Na ubora wa 'Aishah (mke wake) kwa wanawake wengine ni kama mfano wa ubora wa thariyd (chakula cha mchuzi wa nyama na mkate) kwa vyakula vingine))  

 

 

Share

04-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Wasemao Kweli Wanaume Na Wanawake

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

04- Wasemao Kweli Wanaume Na Wanawake  

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake [Al-Ahzaab: 35]

 

Sifa ya nne ni: Wasemao kweli.

 

 Inakusudiwa katika usemi wao, vitendo vyao, na niyyah zao kama baadhi ya wafasiri wa Qur-aan walivyonukuu.

 

Vile Vile Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametunasihi tuambatane na wanaosema kweli Anaposema:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَكُونُوا مَعَ الصَّادِقِينَ﴿١١٩﴾

Enyi walioamini! Mcheni Allaah na kuweni pamoja na wakweli. [At-Tawbah: 119]

 

 

Kusema kweli ni alama ya iymaan kama ambavyo kusema uongo ni alama ya unafiki kama anavyosema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam:

 

 

عَلَيْكُمْ بِالصِّدْقِ فَإِنَّ الصِّدْق يَهْدِي إِلَى الْبِرّ وَإِنَّ الْبِرّ يَهْدِي إِلَى الْجَنَّة وَإِيَّاكُمْ وَالْكَذِب فَإِنَّ الْكَذِب يَهْدِي إِلَى الْفُجُور وَإِنَّ الْفُجُور يَهْدِي إِلَى النَّار وَلَا يَزَال الرَّجُل يَصْدُق وَيَتَحَرَّى الصِّدْق حَتَّى يُكْتَب عِنْد اللَّه صِدِّيقًا وَلَا يَزَال الرَّجُل يَكْذِب وَيَتَحَرَّى الْكَذِب حَتَّى يُكْتَب عِنْد اللَّه كَذَّابًا)) مسلم

 ((Shikamaneni na ukweli, kwani ukweli unapeleka katika wema, na wema unapeleka Peponi. Na jihadharini na uongo, kwani uongo unapeleka kwenye uovu, na uovu hupeleka katika moto. Mtu huendelea kusema ukweli na kujitahidi kuendelea hivyo hadi itarekodiwa na Allaah kuwa ni mkweli. Na mtu huendelea kusema uongo na ataendelea kufanya hivyo hadi itarekodiwa na Allaah kuwa ni muongo)) [Muslim]

 

Baadhi ya Maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhu)  hawajapata kusema uongo maishani mwao tokea siku za Ujaahiliyyah (zama za ujinga yaani kabla ya Uislam) wala hawakuwahi kusema uongo katika Uislam. Na mmoja wao ni Abubakar (Radhwiya Allaahu ‘anhu)  ambaye alipewa sifa hiyo ya: Asw-Swiddiyq.

 

Abubakar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) na sababu za kupewa sifa ya Asw-Swiddiyq' (Msema kweli ).

 

 

Al-Imaam An-Nawawiy amesema: "Ummah umekubaliana kwa pamoja bila ya kupingana kwamba amepewa cheo cha 'Asw-Swiddiyq kutokana na kuitikia kwake haraka kumuamini Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)   bila ya kusita na kukubali maneno yake kwamba daima ni ya ukweli. Alibakia kuwa mkweli maishani mwake kote wala hajapata kusema uongo  hata mara moja."

 

Ibn Kathiyr amesema: "Kuhusu cheo chake cha   Asw-Swiddiyq inasemekana kwamba alipewa tokea zama za Ujaahiliyyah kutokana na ukweli uliojulikana kwamba alikuwa ni mkweli. Vile vile imesemekana kwamba amepewa cheo hicho kwa sababu alikuwa daima yuko tayari kumwamini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)   katika kila jambo alilosema."

 

Baadhi ya matukio yaliyodhihirisha ukweli wake Abu Bakr Asw-Swiddiyq na wepesi wake wa kuamini lolote alilosema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na sifa zake nyenginezo:

 

 

 1-Katika kisa cha Israa Wal-Mi'raaj alipobakia thabiti na kuwaambia makafiri kwamba ikiwa Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  mwenyewe ametamka maelezo hayo ya safari ya Israa wal Mi’raaj basi ni kweli!

 

Ibn Kathiyr amesema: "Al-Hasan Al-Baswriy na Qataadah wamesema: Alijulikana kwa mara ya kwanza kwa cheo hiki asubuhi ya siku ya tukio la Israa." Al-Haakim amesimulia kutoka kwa 'Aishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) ambaye amesema: “Washirikina walikuja kwa Abubakar wakamwambia:  Umemsikia rafiki yako anavyodai? Anadai kwamba amesafiri kwenda Baytul-Maqdis kwa usiku mmoja! Akauliza: Je, amesema mwenyewe hivyo?" Wakajibu: "Ndio." Akasema: "Basi amesema ukweli! Naamini ukweli wake katika mambo yaliyo ya ajabu zaidi kuliko hayo, kama habari kutoka mbinguni asubuhi na jioni.”  (yaani wahyi wa Qur-aan). Tokea hapo Abubakar akapewa cheo na sifa ya Asw-Swiddiyq.  [Ibn Kathiyr kasema Isnaad yake ni nzuri].

 

Al-Haakim amesimulia kutoka Nazaal ibn Swabrah ambaye amesema: "Tulimwambia 'Aliy: "Ee kamanda wa Waumini! Tuelezee kuhusu Abubakar.” Akasema: "Ni mtu aliyepewa jina la Asw-Swiddiyq na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa kauli ya Jibriyl  ('Alayhis-Salaam)   na kauli ya Muhammad  (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

 

Alikuwa ni Khalifa wa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Yeye Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliridhika naye katika Dini yetu na aliridhika naye katika mambo yetu ya kidunia." [Ibn Kathiyr kasema: Isnaad yake ni nzuri]

 

Na katika vita vya Uhud, Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  aliliambia (kwa kulipapasa) jabali  la Uhud lilipotikisika:

 

((أثبت أحد فإنما عليك نبي وصديق وشهيدان))

((Tulia kwani juu yako yumo Nabiy, Asw-Swiddiyq na Mashuhadaa wawili)) (yaani Umar na Uthmaan (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa)) [Al-Bukhaariy]

 

 

2-Kisa maarufu cha kuhama kwake (Hijrah) pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa ameacha familia yake ili abakie na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

Maswahaba wote waliruhusiwa na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhama (Hijrah kutoka Makkah kwenda Madiynah) isipokuwa Abubakar. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akimwambia abakie ili awe swahibu yake katika Hijrah na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akatimiza pendekezo la Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Katika msafara wa hijrah makafiri walimtafuta Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutaka kumuua wakakimbilia katika pango la At-Thawr. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameteremsha kauli Yake: 

 

إِلَّا تَنصُرُوهُ فَقَدْ نَصَرَهُ اللَّـهُ إِذْ أَخْرَجَهُ الَّذِينَ كَفَرُوا ثَانِيَ اثْنَيْنِ إِذْ هُمَا فِي الْغَارِ إِذْ يَقُولُ لِصَاحِبِهِ لَا تَحْزَنْ إِنَّ اللَّـهَ مَعَنَا ۖ فَأَنزَلَ اللَّـهُ سَكِينَتَهُ عَلَيْهِ وَأَيَّدَهُ بِجُنُودٍ لَّمْ تَرَوْهَا وَجَعَلَ كَلِمَةَ الَّذِينَ كَفَرُوا السُّفْلَىٰ ۗ وَكَلِمَةُ اللَّـهِ هِيَ الْعُلْيَا ۗوَاللَّـهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ﴿٤٠﴾

Msipomnusuru (Rasuli), basi Allaah Amekwishamnusuru, pale walipomtoa (Makkah) wale waliokufuru akiwa wa pili katika wawili; walipokuwa katika pango, alipomwambia swahibu yake: “Usihuzunike, hakika Allaah Yu Pamoja nasi.” Basi Allaah Akamteremshia utulivu Wake, na Akamsaidia kwa majeshi msiyoyaona, na Akajaalia neno la waliokufuru kuwa chini. Na Neno la Allaah kuwa ndilo lililo juu. Na Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [At-Tawbah: 40]

 

 

3- Alipolia wakati Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  alisema: ((Hakika kuna mja alipewa uchaguzi na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa)  baina ya Duniya na Aakhirah, mja akachagua Aakhirah)). Abubakar alijua kuwa huyo mja ni Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na alitambua kauli hiyo imemaanisha kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  ataaga duniya karibuni. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

4- Alipobakia kuwa thabiti katika kifo cha Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakati Maswahaba waliduwaa hawakujua la kufanya, akatoa khutbah ya kuwatuliza.

 

 

 

5- Kuthibitika kwake ingawa alikuwa pekee katika kupeleka jeshi na       kumfanya Usaamah bin Zayd awe mwenye kuongoza jeshi.

 

 

 

6- Kung'angania kwake katika kupigana na watu waliotoka nje ya Uislam baada ya kifo cha Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

 

 

7- Alipomchagua 'Umar ibnil-Khatwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuwa Khaliyfah wa      Waislam, jambo ambalo limeainishwa na ‘Ulamaa kuwa ni jambo muhimu la mafanikio.

 

 

 

Share

05-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Wanaosubiri Wanaume Na Wanawake

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

05 - Wanaosubiri Wanaume Na Wanawake  

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ 

 

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, [Ahzaab: 35]

 

 

Sifa ya tano ni wanaosubiri wanaume na wanawake.   Fadhila za subira zimetajwa tele katika Qur-aan na Sunnah.  

 

Aina za subira:

 

 

1. Subira katika utiifu.

 

‘Ibaadah zinahitaji subira; kama Swalaah inahitajia unyenyekevu ambao haupatikani bila ya kuwa na subira kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَاسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلَّا عَلَى الْخَاشِعِينَ ﴿٤٥﴾

Na tafuteni msaada kupitia subira na Swalaah; na hakika hilo ni kubwa isipokuwa kwa wanyenyekevu. [Al-Baqarah: 45]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الصَّابِرِينَ ﴿١٥٣﴾

Enyi walioamini! Tafuteni msaada kwa subira na Swalaah; hakika Allaah Yu pamoja na wanaosubiri. [Al-Baqarah: 153]   

 

 

Swawm pia inahitajia subira kukaa na njaa na kiu na kujizuia na matamanio ya nafsi.

 

Zakaah hali kadhalika inahitajia subira kwa sababu inahitaji azimio la nguvu mtu kuitoa mali yake.

 

Hajj nayo inahitajia subira kutokana na mashaka yanayotokana na safari hii na kutekeleza taratibu za Hajj.

 

 

 

2.Subira katika kujiepusha na maasi:

 

Nayo ni kufanya jihaad ya nafsi kuzuia matamanio maovu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:

 

..أيُّ الْهِجْرَةِ أَفْضَلُ، قَالَ: ((أَنْ تَهْجُرَ مَا كَرِهَ رَبُّكَ))

Hijrah gani iliyokuwa bora zaidi? Akasema: ((Ni kuhama yale Anayochukia Rabb wako)) [Swahiyh An-Nasaaiy 4176]

 

Mfano mwenye kupenda sana muziki, ambapo mara nyingi shaytwaan katika jambo hili humfanyia binaadamu liwe gumu kabisa kwake kuliepuka, kwani anaweza Muislamu kuacha maasi mengine makubwa lakini inapofika kutaka kuacha nyimbo (muziki) huwa ni jambo zito, kwa vile wengi wanafikiri kuwa nyimbo si maasi makubwa na hali Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amekataza katika Qur-aan Anaposema:

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْتَرِي لَهْوَ الْحَدِيثِ لِيُضِلَّ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَيَتَّخِذَهَا هُزُوًا ۚ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ﴿٦﴾

Na miongoni mwa watu yuko ambaye hununua maneno ya upuuzi ili apoteze (watu) njia ya Allaah bila elimu, na huichukulia mzaha. Hao watapata adhabu ya kudhalilisha. [Luqmaan: 6]

 

 

Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema kuhusu   Aayah hii: "Naapa kwa Allaah hii ina maana ni nyimbo" [At-Twabariy 20:127]

 

 

3. Subira katika da’wah (kulingania).

 

 

Hii ni kazi ngumu kabisa ambayo mitihani yake imewasibu Rusuli wa Allaah.

 

Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye pia alipata maudhi makubwa ya kutukanwa, kupigwa na kutengwa, na ndipo kila mara Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alikuwa akimkumbusha kuwa si pekee mwenye kupata misukosuko ya watu, bali Rusuli wenzake pia wamepitia maudhi na Akimsimulia visa vya Manabii na Rusuli katika Qur-aan.

 

Kazi ya da’wah (kulingania) inapasa pia itekelezwe na watu wa Ummah huu. Na pindi mtu akianza da’wah basi akaye tayari kupata maudhi na avute subra.  Luqmaan alimnasihi mwanawe:

 

يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلَاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ وَاصْبِرْ عَلَىٰ مَا أَصَابَكَ ۖ إِنَّ ذَٰلِكَ مِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ ﴿١٧﴾

 “Ee mwanangu! Simamisha Swalaah, na amrisha mema na kataza ya munkari, na subiri juu ya yale yatakayokusibu. Hakika hayo ni katika mambo ya kuazimiwa. [Luqmaan: 17]

 

 

 Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَالْعَصْرِ ﴿١﴾

Naapa kwa Al-‘Aswr (zama).

 

إِنَّ الْإِنسَانَ لَفِي خُسْرٍ ﴿٢﴾

Hakika mwana wa Aadam bila shaka yumo katika khasara.

 

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ ﴿٣﴾

Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema na wakausiana haki na wakausiana subira. [Al-'Aswr: 1-3]

 

 

 

4-Subira katika maafa, misiba na kadhalika:

 

Maafa, madhara, misiba mbali mbali inahitaji subira na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amewabashiria wenye kusubiri kupata fadhila zake Anaposema: 

 

 

وَلَنَبْلُوَنَّكُم بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفِ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ مِّنَ الْأَمْوَالِ وَالْأَنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ ۗ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ ﴿١٥٥﴾

Na bila shaka Tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri.

 

الَّذِينَ إِذَا أَصَابَتْهُم مُّصِيبَةٌ قَالُوا إِنَّا لِلَّـهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ﴿١٥٦﴾

Wale ambao unapowafika msiba husema: “Hakika sisi ni wa Allaah na hakika sisi Kwake ni wenye kurejea.”

 

أُولَـٰئِكَ عَلَيْهِمْ صَلَوَاتٌ مِّن رَّبِّهِمْ وَرَحْمَةٌ ۖ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُهْتَدُونَ ﴿١٥٧﴾

Hao zitakuwa juu yao Barakah kutoka kwa Rabb wao na rahmah, na hao ndio wenye kuongoka. [Al-Baqarah: 155-157]

  

 

Vile vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Huwapa waja Wake wema wenye kuvuta subira ujira mwingi usiohesabika kama Anavyosema: 

 

إِنَّمَا يُوَفَّى الصَّابِرُونَ أَجْرَهُم بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿١٠﴾

Hakika wanaosubiri watalipwa kikamilifu ujira wao bila ya hesabu. [Az-Zumar: 10]

 

 

Na Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuelezea fadhila za subira vile vile katika Hadiyth nyingi, chache ni kama zifuatazo:

 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قال : قال رسول اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ : ((مَنْ يَتَصَبَّرْ يُصَبِّرْهُ اللَّهُ، وَمَا أُعْطِيَ أَحَدٌ عَطَاءً خَيْرًا وَأَوْسَعَ مِنْ الصَّبْر))  البخاري ومسلم

    

Kutoka kwa Abuu Sa'iyd Al-Khudriyyih (Radhwiya Allaah 'anhu) kwamba, amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam: ((Atakayetaka kusubiri (kufanya subira) basi Allaah Atampa subira. Na hakupewa mtu jambo la kheri na pana kama subira)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 Pia:

 

عَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رضي الله عنها أَنَّهَا قَالَتْ : سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُول((مَا مِنْ مُسْلِمٍ تُصِيبُهُ مُصِيبَةٌ فَيَقُولُ مَا أَمَرَهُ اللَّهُ " إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ، اللَّهُمَّ أْجُرْنِي فِي مُصِيبَتِي وَأَخْلِفْ لِي خَيْرًا مِنْهَا " إِلا أَخْلَفَ اللَّهُ لَهُ خَيْرًا مِنْهَا)) روى مسلم

  

Imetoka kwa Ummu Salamah (Radhwiya Allahu 'anhaa) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Muislamu yeyote atakayepatwa na msiba akasema yale aliyoamrisha na Allaah:

إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ، اللَّهُمَّ أْجُرْنِي فِي مُصِيبَتِي وَأَخْلِفْ لِي خَيْرًا مِنْهَا

 

 Sisi ni wa Allah nasi Kwake tutarejea. Ee Allaah Nipe ujira katika msiba wangu na nibadilishie ulio bora kuliko huo."

Basi Allaah Atampa ulio na kheri kuliko huo [msiba])) [Muslim]

 

 

Katika waja wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) waliokuwa na subira ya ajabu ni Nabiy Ayyuwb ('Alayhis-salaam) pindi aliposibiwa na kupoteza mali, na kupatwa na maradhi na kufariki watoto wake wote akavuta subra miaka mingi mpaka Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akamfariji.

 

 

Kisa Cha Subira Ya Swahaabiyyah Al-Khansaa:  

 

Jina lake hasa ni Tamaadhwur Bint 'Amru bin Ash-Shariyd bin Rabaah As-Sulaymiyyah. Alijulikana kwa jina la Al-Khansaa  na vile vile  Umm Ash-Shuhadaa (mama wa Shuhadaa) kutokana na watoto wake waliofariki katika jihaad. Pia alijulikana kuwa ni mwanamke mwenye haiba nzuri iliyojaa fadhila, tabia njema njema, ushujaa na subira kubwa.

 

Alipokuwa katika ujaahiliyyah (kabla ya Uislaam), alikuwa akitunga mashairi ya beti mbili tatu hadi walipofariki kaka zake Mu'aawiyah na Swakhar bin 'Amru, alifikwa na huzuni kubwa sana hata akawatungia mashairi. Mashairi hayo yakawa maarufu, naye akawa mashuhuri. Inavyosemekana hakuweko mwanamke aliyekuwa hodari wa mashairi kama yeye.

 

Baada ya vifo vya kaka zake, alikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pamoja na watu wake wa Bani Sulaym akasilimu.

 

Ilipofika wakati wa vita vya Qaadisiyyah alidhihirisha subira yake kubwa alipokwenda vitani pamoja na watoto wake wanne wa kiume na akawausia kwa kuwaambia maneno yafuatayo:

 

"Enyi watoto wangu, naapa kwa Yule Ambaye hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, nyinyi ni watoto wa baba mmoja, sikumkhini baba yenu, mmesilimu kwa kutii, mmehajiri kwa khiari yenu…" hadi akasema "Mtakapoamka kesho In Sha-Allaah kwa salama, nendeni vitani kupigana na adui zenu, kwani mnajua Aliyowaandalia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ya thawabu nyingi kwa kupigana na makafiri. Tambueni kuwa nyumba ya milele (Jannah) ni bora kuliko nyumba ya kutoweka (Dunia), Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اصْبِرُوا وَصَابِرُوا وَرَابِطُوا وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٢٠٠﴾

Enyi walioamini! Subirini na zidini kuvuta subira na bakieni imara na mcheni Allaah ili mpate kufaulu. [Al-'Imraan: 200].

 

 

Wakaenda vitani na alipopata habari ya vifo vyao wote alisema: "AlhamduLLaah kwa Yule Aliyenipa heshima ya kuuliwa kwao (wanangu) na namuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Aniunganishe nao kwa Rahma Zake".

 

Al-Khansaa (Radhwiya Allaahu 'anhaa) alifariki katika Ukhalifa wa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu ‘anhu).

 

Share

06-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Wanyenyekevu Wanaume Na Wanawake

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

06 - Wanyenyekevu Wanaume Na Wanawake  

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Khushuw' ina maana nyingi, miongoni mwazo ni:

 

Utulivu, ushwari, udhalili kama Anvosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَخَشَعَتِ الْأَصْوَاتُ لِلرَّحْمَـٰنِ

na sauti zitafifia kwa Ar-Rahmaan [Twaahaa: 108] 

 

 

Pia khushuw’ ina maana ni khofu kwa dalili Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pindi alipowauliza Maswahaba:

 

((أَيُّكُمْ يُحِبُّ أَنْ يُعْرِضَ اللَّهُ عَنْهُ))‏ قَالَ:  فَخَشَعْنَا

((Nani miongoni mwenu anayependa Allaah Amgeuzie Uso Wake?)) akasema: “Tukakhofu.” [Muslim]

 

Na pia ni ulaini na kutahadhari, kuogopa; mfano pindi mtu anaposikia kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) nyoyo zikaingia khofu na unyenyekevu.  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ ﴿١٦﴾

Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumdhukuru Allaah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki.  [Al-Hadiyd: 16]

 

 

Na khushu’w mahali pake ni moyoni kisha inaathiri viungo vinginevyo:   Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٢﴾

Hakika Waumini ni wale ambao Anapotajwa Allaah, nyoyo zao zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali. [Al-Anfaa; 2]

 

 

Kinyume chake ni ugumu; yaani nyoyo kuwa ngumu na kutokuwa na khofu mtu anaposikia kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Aayah ya juu hapo ya Suwrah Al-Hadiyd ilivyomalizik:

 

وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ ﴿١٦﴾

wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki.  [Al-Hadiyd: 16]

 

 

Na pia kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

اللَّـهُ نَزَّلَ أَحْسَنَ الْحَدِيثِ كِتَابًا مُّتَشَابِهًا مَّثَانِيَ تَقْشَعِرُّ مِنْهُ جُلُودُ الَّذِينَ يَخْشَوْنَ رَبَّهُمْ ثُمَّ تَلِينُ جُلُودُهُمْ وَقُلُوبُهُمْ إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ ۚ ذَٰلِكَ هُدَى اللَّـهِ يَهْدِي بِهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَمَا لَهُ مِنْ هَادٍ ﴿٢٣﴾

Allaah Ameteremsha kauli nzuri kabisa, Kitabu; zinazoshabihiana ibara zake, zenye kukaririwa kila mara, zinasisimua kwazo ngozi za wale wanaomkhofu Rabb wao, kisha zinalainisha ngozi zao na nyoyo zao katika kumdhukuru Allaah. Huo ndio mwongozo wa Allaah Humwongoza kwao Amtakaye. Na ambaye Allaah Amempotoa basi hana wa kumuongoa. [Az-Zumar: 23]

 

 

Khushuw’ pia ina maana kuzungumza kwa utaratibu kwa uangalifu, hadhi, raghba, khofu na unyenyekevu kama hali za Manabii. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَوَهَبْنَا لَهُ يَحْيَىٰ وَأَصْلَحْنَا لَهُ زَوْجَهُ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَيَدْعُونَنَا رَغَبًا وَرَهَبًا ۖ وَكَانُوا لَنَا خَاشِعِينَ ﴿٩٠﴾

Basi Tukamuitikia na Tukamtunukia Yahyaa, na Tukamtengenezea mke wake. Hakika wao walikuwa wakikimbilia katika mambo ya kheri na wakituomba kwa raghba na khofu, na walikuwa wenye kutunyenyekea. [Al-Anbiyaa: 90]

 

 

Linalomtia mtu hamasa kuwa katika hali hiyo ni khofu ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na utambuzi kuwa Allaah ('Azza wa Jalla) Anaona yote tunayoyatenda kama ilivyothibiti katika Hadiyth ndefu alipokuja Jibriyl ('Alayhis-salaam) kwa Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kumuuliza maswali kadhaa:   

 

((...أنْ تَعْبُدَ الله كَأَنَّكَ تَرَاهُ فإنْ لَمْ تَكُنْ تَرَاهُ فإنَّهُ يَرَاك))

((….. na umuabudu Allah kama kwamba unamuona, na kama humuoni basi Yeye Anakuona))  

 

Khushuw' katika Swalaah:

 

Khushuu (unyenyekevu) ni jambo gumu na kubwa hakika hasa katika Swalaah kwani shaytwaan ndipo mahali anapopenda sana kumharibia mtu ‘amali yake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَاسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلَّا عَلَى الْخَاشِعِينَ ﴿٤٥﴾

Na tafuteni msaada kupitia subira na Swalaah; na hakika hilo ni kubwa isipokuwa kwa wanyenyekevu. [Al-Baqarah: 45]

 

 

Kwa hiyo kunahitajika du’aa na kinga ya kumwepuka shaytwaan katika Swalaah jambo ambalo pindi mja akiswali kwa khushuw’, atapata fadhila zake zikiwemo kupata Jannah ya Al-Firdaws kwa kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):  

 

 بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ ﴿١﴾

 

 

قَدْ أَفْلَحَ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١﴾

Kwa yakini wamefaulu Waumini.

 

الَّذِينَ هُمْ فِي صَلَاتِهِمْ خَاشِعُونَ ﴿٢﴾

Ambao katika Swalaah zao huwa wananyenyekea. [Al-Muuminuwn: 1]

 

Aayah zinaendelea mpaka kauli Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 أُولَـٰئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَ ﴿١٠﴾

Hao ndio warithi.

 

الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿١١﴾

Ambao watarithi (Jannah) ya Al-Firdaws, wao humo ni wenye kudumu.  [Al-Muuminuun: 10-11]

 

Vipi kupata khushuw’ katika Swalaah:

 

 

1-Kwenda msalani kukidhi haja kubwa na ndogo kabla ya Swalaah.

 

 

2-Kula kama una njaa kabla ya kuswali

 

 

3-Kutia vizuri wudhuu.  

 

 

4-Kuweka Sutrah (Kizuizi) mbele yako.

 

 

5-Kutokuvaa nguo za rangi au zenye maneno hasa kama unaswali Jamaa  ili isiwashughulishe wengineo. 

 

 

6-Kukumbuka mauti.  

 

 

7-Kwa wanawake wanaoswali nyumbani, kutokuswali mbele ya watu   wanaozungumza, watoto na kutokuweko sauti za televisheni, radio n.k.

 

 

8-Kuanza kwa du’aa za kufungulia Swalaah na kujikinga na shatywaan kama ilivyothibiti katika Sunnah.

 

 أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّـيْطانِ مِنْ نَفْخِـهِ وَنَفْـثِهِ وَهَمْـزِه

 

 Najikinga na Allaah kutokana na shaytwaan, na kibri yake, na kupulizia kwake na kutia kwake wasiwasi (katika nyoyo za binaadamu) [Hadiyth ya Jubayr bin Mutw-‘im (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/203), Ibn Maajah (1/265), Ahmad (4/85), na Muslim kutoka kwa ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) kama hivyo na mna kisa humo (1/420)]

 

 

9-Kujikinga na shaytwaan ndani ya Swalaah anapokupotezea khushuw’, nayo ni kutema mate kidogo kama kupuliza upande wa bega la kushoto mara tatu na kuomba kinga.  

 

 

10-Kuweka mkono wa kulia juu ya kushoto kwenye kifua vizuri.

 

 

11-Kutambua kwamba upo mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na unaposoma Al-Faatihah Anakujibu.

 

 

12-Kutazama sehemu ya kusujudu unaposimama.

 

 

13-Kuzingatia Quraan unapoisoma.

 

 

14-Kusoma Qur-aan kwa sauti nzuri katika katika Swalaah za jahriyyah (kisoma cha sauti).

 

 

15-Kunong'ona kwenye Swalaah za Sirriyah (Swalah za kimya) bila ya kutoa sauti sana au bila ya kuswali kimya sana.

 

 

16-Kuswali kwa twumaaninah: ni utulivu na kwa vituo na kutimiza kila kitendo bila ya kuharakisha kwa kupumzika kiasi hadi uhakikishe kila sehemu ya kiungo kimetulia mahala pake wakati wa kurukuu, kusimama baada rukuu, kusujudu, baina ya sijda mbili, ukitoka kusujudu kabla hujanyanyuka n.k.1-    

 

 

 

Share

07-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Watoao Sadaka Wanaume Na Wanawake

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

07- Watoao Sadaka Wanaume Na Wanawake

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao swadaqah wanaume na wanawake, [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Sadaka ni kufanya wema kwa watu wenye kuhitaji na ambao ni dhaifu na wasiokuwa na uwezo kuwatoshelezea mahitaji yao.

 

Kutoa sadaka ni ‘amali njema ya kumtii Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Aliyoyaamrisha katika Qur-aan na kutafuta radhi Zake:

 

 

وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَلِأَنفُسِكُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ اللَّـهِۚ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٢﴾

Na chochote cha kheri mtoacho basi ni kwa ajili ya nafsi zenu. Na hamtoi ila kutaka Wajhi wa Allaah. Na chochote mtoacho katika kheri mtalipwa kamilifu nanyi hamtodhulumiwa [Al-Baqarah: 272]

 

 

Al-Hasan Al-Basri amesema: "Kila Muumini anapotumia (sadaka) pamoja na matumizi yake mwenyewe hutafuta radhi za Allaah [Ibn Haatim 3:1115].

Abubakar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alijulikana kuwa na sifa hiyo ya ukarimu wa kutoa sadaka na ndio maana zilipoteremka Aayah:

وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾

Na ataepushwa nao mwenye taqwa kabisa.

 

 

الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾

Ambaye anatoa mali yake kujitakasa.

 

 

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾

Na hali hakuna mmoja yeyote aliyemfanyia fadhila yoyote hata amlipe.

 

 

إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠﴾

Isipokuwa kutaka Wajihi wa Rabb wake Aliyetukuka.

 

وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١﴾

Na bila shaka atakuja kuridhika. [Al-Layl: 17-21]

 

 

Wafasiri wa Qur-aan wametaja kuwa Aayah hizo zinamhusu Abuu Bakar As-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwa sababu   yeye ni mwenye kustahiki kupewa sifa hizo pamoja na sifa nyingine nyingi njema. Hakika yeye alikuwa ni mkweli, mwenye taqwa ya hali ya juu, mkarimu aliyekuwa akitoa daima mali yake kwa wanaohitajia na alimsaidia sana Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kutoa mali yake katika njia ya Allaah.

 

Muislam anapotoa sadaka kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), basi thawabu zake zitakuwa zimeshafika kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) hata kama sadaka yake imemfikia asiyestahiki akaja kutambua baadaye kwa dalili:

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رَسُول اللَّه - صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ (( قَالَ رَجُل "لَأَتَصَدَّقَنَّ اللَّيْلَة بِصَدَقَةٍ" فَخَرَجَ بِصَدَقَتِهِ فَوَضَعَهَا فِي يَد زَانِيَةٍ فَأَصْبَحَ النَّاس يَتَحَدَّثُونَ  "تُصُدِّقَ عَلَى زَانِيَة" فَقَالَ : "اللَّهُمَّ لَك الْحَمْد عَلَى زَانِيَة لَأَتَصَدَّقَنَّ اللَّيْلَة بِصَدَقَةٍ" فَوَضَعَهَا فِي يَد غَنِيّ فَأَصْبَحُوا يَتَحَدَّثُونَ "تُصُدِّقَ اللَّيْلَة عَلَى غَنِيّ" قَالَ : "اللَّهُمَّ لَك الْحَمْد عَلَى غَنِيّ لَأَتَصَدَّقَنَّ اللَّيْلَة بِصَدَقَةٍ" فَخَرَجَ فَوَضَعَهَا فِي يَد سَارِق فَأَصْبَحُوا يَتَحَدَّثُونَ "تُصُدِّقَ اللَّيْلَة عَلَى سَارِق" فَقَالَ : "اللَّهُمَّ لَك الْحَمْد عَلَى زَانِيَة وَعَلَى غَنِيّ وَعَلَى سَارِق" فَأُتِيَ فَقِيلَ لَهُ "أَمَّا صَدَقَتك فَقَدْ قُبِلَتْ وَأَمَّا الزَّانِيَة فَلَعَلَّهَا أَنْ تَسْتَعِفَّ بِهَا عَنْ زِنًا وَلَعَلَّ الْغَنِيّ يَعْتَبِر فَيُنْفِق مِمَّا أَعْطَاهُ اللَّه وَلَعَلَّ السَّارِق أَنْ يَسْتَعِفَّ بِهَا عَنْ سَرِقَته")). البخاري و مسلم

Imetoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mtu mmoja alisema: "Leo nitatoa sadaka." Akatoka na sadaka yake na (bila ya kujua) akampa mzinifu. Asubuhi ya pili watu wakasema: "Sadaka imetolewa kwa mzinifu." Yule mtu akasema: "Yaa Allaah! Himdi ni Zako (Nimetoa sadaka yangu) kwa mzinifu. Usiku wa leo nitatoa sadaka tena." Akatoka na sadaka yake na (bila ya kujua) akampa tajiri. Siku ya pili (watu) wakasema: "Usiku wa jana tajiri kapewa sadaka." Akasema: "Yaa Allaah! Himdi ni Zako. (Nimetoka sadaka) kwa tajiri. Usiku wa leo nitatoa sadaka tena." Akatoka na sadaka yake na (bila ya kujua) akampa mwizi. Asubuhi ya pili (watu) wakasema: "Usiku wa jana mwizi alipewa sadaka." Akasema: "Yaa Allaah! Himdi ni Zako (nimetoa sadaka) kwa mzinifu, tajiri na mwizi." Akaja mtu na kumwambia: "Sadaka uliyoitoa imekubaliwa. Kwani mzinifu, huenda sadaka ikamzuia kufanya uzinifu. Ama tajiri, huenda ikampa fundisho naye atoe (sadaka) mali yake aliyopewa na Allaah. Ama mwizi, huenda ikamzuia kuiba.")) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Aayah nyingi na Hadiyth zimetaja kuhusu fadhila za kutoa sadaka. Na Muislamu anapotoa sadaka Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Humlipa duniani marudufu na Akhera pia hupata ujira wake. Na jambo la kutia moyo katika kutoa sadaka ni kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametuhakikishia kuwa tunapotoa basi ni kama mkopo tunaomkopesha Yeye kama Anavyosema: 

 

مَّن ذَا الَّذِي يُقْرِضُ اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا فَيُضَاعِفَهُ لَهُ وَلَهُ أَجْرٌ كَرِيمٌ ﴿١١﴾

Nani ambaye atamkopesha Allaah karadha nzuri kisha (Allaah) Amuongezee maradufu na apate ujira mtukufu. [Al-Hadiyd: 11]

 

Na Muislamu asidharau kutoa japo iwe ni kitu kidogo mno kadiri ya tendo moja.

 

وعَن عَدِيِّ بنِ حاتم رضي اللَّه عنه أَن رسول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال :  (( اتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمَرةٍ)) متفقٌ عليه

Imetoka kwa 'Adiyyi bin Haatim (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jikingeni na moto hata kwa kipande cha tende)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Kisa Cha Aliyetoa  Sadaka Kutoka Katika Shamba Lake:

 

   

عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال  ((بيْنَما رَجُلٌ يَمشِي بِفَلاةٍ مِن الأَرض ، فَسَمِعَ صَوتاً في سَحَابَةٍ : اسقِ حَدِيقَةَ فُلانٍ ، فَتَنَحَّى ذلكَ السَّحَابُ فَأَفْرَغَ مَاءَهُ في حَرَّةٍ ، فإِذا شرجة من تِلْكَ الشِّراجِ قَدِ اسْتَوعَبَتْ ذلِكَ الماءَ كُلَّهُ فَتَتَبَّعَ الماءَ ، فإِذا رَجُلٌ قَائِمٌ في حَدِيقَتِهِ يُحَوِّلُ المَاءَ بمِسحَاتِهِ ، فقال له : يا عَبْدَ اللَّهِ ما اسْمُكَ قال : فُلانٌ، للاسْمِ الَّذِي سَمِعَ في السَّحَابَةِ ، فقال له : يَا عَبْدَ اللَّهِ لِمَ تَسْأَلُنِي عَنِ اسْمِي ؟ فَقَال : إني سَمِعْتُ صَوتاً في السَّحَابِ الذي هذَا مَاؤُهُ يقُولُ : اسقِ حَدِيقَةَ فُلانٍ لإسمِكَ ، فما تَصْنَعُ فِيها ؟ فقال : أَما إِذْ قُلْتَ هَذَا ، فَإني أَنْظُرُ إِلى ما يَخْرُجُ مِنها ، فَأَتَّصَدَّقُ بثُلُثِه ، وآكُلُ أَنا وعِيالي ثُلُثاً ، وأَردُّ فِيها ثُلثَهُ)) . رواه مسلم

 

Imetoka kwa Abuu Hurayra (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Wakati mtu mmoja alikuwa anatembea njiani katika ardhi ya ukame ambayo haina alama ya maji, alisikia  sauti inatoka kutoka katika mawingu ikisema: "Mwagia maji shamba la fulani!" Mawingu yakaelekea upande fulani na kuanza kumwaga maji juu ya miamba tambarare. Mchiriziko ukatiririka katika mfereji mkubwa. Mtu huyo akaufuata mfereji huo hadi ukafika katika shamba na akamuona mwenye kumiliki shamba amesimama katikati yake akiyatandaza maji kwa sepeto (huku anabadilisha njia ya maji yaelekee katika sehemu nyingine ya shamba lake). Akamuuliza: "Ee mja wa Allaah! Jina lako nani?" Akamwambia jina lake ambalo ni lile lile alilolisikia kutoka katika mawingu. Mwenye shamba akamuuliza: "Ee mja wa Allaah! Kwa nini umeniuliza jina langu?" Akamjibu: "Nimesikia sauti kutoka katika mawingu yaliyomwaga maji ikisema: "Mwagia maji shamba la fulani." Basi nataka kujua huwa unaifanyia jambo gani?" Akasema: "Kwa vile umeniuliza nitakuambia: Hupima mapato ya shamba na kugawa thuluthi moja katika sadaka, na thuluthi moja natumia mwenyewe na familia yangu, na thuluthi moja nairudisha katika (kuizalisha) shamba")) [Muslim]

 

Muumini anapotoa Sadaka basi ni ahadi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kumzidishia fadhila Zake mbali mbali. Ama asiyependa kutoa sadaka juu ya kuwa na uwezo basi ni tahadharisho kwake kuombewa du’aa na Malaika apate khasara katika mali yake kama ilivyothibiti katika Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا مِنْ يَوْمٍ يُصْبِحُ الْعِبَادُ فِيهِ إلاَّ مَلَكَانِ يَنْزِلاَنِ فَيَقُولُ أَحَدُهُمَا: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُنْفِقًا خَلَفًا. وَيَقُولُ الأَخَرُ: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُمْسِكًا تَلَفًا)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)   kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: ((Kila siku inayowapambaukia watu kuna Malaika wawili wanateremka, mmoja wao akiomba: Ee Allaah! Mwenye kutoa [sadaka] mlipe zaidi. Na mwengine huomba: Ee Allaah! Mwenye kuzuia mpe hasara)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na kisa katika Qur-aan kinachothibitisha khasara ya wanaozuia kutoka sadaka:

 

 

Alikuweko mtu mmoja ambaye alikuwa ana mashamba ambayo yakitoa mazao na matunda mbali mbali, na kila anapochuma mazao alikuwa akigawa sehemu tatu; sehemu moja akiirudisha katika kuzalisha tena mazao, sehemu ya pili akila yeye pamoja na watoto wake, na inayozidi alikuwa akitoa sadaka. Alipofariki na watoto wake waliporithi shamba hilo, hawakutaka kufanya kama alivyokuwa akifanya baba yao. Walisema: "Hakika baba yetu alikuwa mpumbavu kutoa mazao ya shamba kuwapa masikini. Tukizuia sisi tusiwape, basi tutakuwa na mazao mengi yetu wenyewe!" Usiku mmoja wakapanga mpango na wakaapa kuwa wakiamka asubuhi yake watakwenda kuchuma mazao yote ili masikini watakapokuja kuomba hawatotambua wamefanya hivyo. Na wala hawakusema "In Shaa Allaah!" Lakini Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Alitaka kuvunja kiapo chao na Akawapa mtihani kwa kuwaangamizia shamba lao usiku huo. Akalifanya shamba likauke kabisa na lipige weusi kama vile limeungua au kama mfano lilokwishavunwa kisha likawa kavu kabisa.

 

Walipoamka asubuhi, wakaitana ili waende shambani kuchuma mazao kama walivyopanga na kuapa. Wakaondoka huku wakinongo'nezana ili mtu yeyote asiwasikie.

 

Wakaenda, lakini walipofika walidhani kuwa wamepotea maana hawakulitambua shamba lao kabisa.  Hapo tena ndio wakatambua kuwa hakika shamba lao ni hilo ambalo limeangamia!  Wakakosa kila kitu, wakaanza kulaumiana wenyewe kwa wenyewe na majuto yakawa  makubwa!

 

 

Kisha tena wakakiri makosa yao na kujirudi nafsi zao wakaomba kwa Rabb wao  Awaghufurie na mwishowe wakawa watu wema.

 

 

Baadhi ya Salaf wamesema kuwa watu hao walikuwa ni watu kutoka Yemen.  Sa'iyd bin Jubayr amesema kuwa: "Ni watu kutoka katika kijiji kilichoitwa Darawaan ambacho kilikuwa ni maili sita kutoka Sanaa."

 

Imesemekena vile vile kuwa ni miongoni mwa Ahlul-Kitaab kutoka Ethiopia. Na Allaah Anajua zaidi [Tafsiyr ya Ibn Kathiyr] 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ameelezea kisa hichi katika Suwratul-Qalam kama ifuatavyo:

 

إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ﴿١٧﴾

Hakika sisi Tumewajaribu (Maquraysh) kama Tulivyowajaribu watu wa shamba, pale walipoapa kuwa bila shaka watayavuna (mazao yake) watakapopambaukiwa asubuhi.

 

وَلَا يَسْتَثْنُونَ﴿١٨﴾

Na wala hawakusema In-Shaa Allaah.  

 

فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ﴿١٩﴾

Basi (shamba lao) likazungukwa na chenye kuzunga (moto) kutoka kwa Rabb wako na hali wao wamelala.

 

 

فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ﴿٢٠﴾

Likawa kama lilovunwa ikabakishwa majivu meusi.

 

فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ﴿٢١﴾

Wakaitana, walipopambaukiwa asubuhi.

 

 

أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ﴿٢٢﴾

Kwamba nendeni asubuhi mapema shambani mwenu, mkiwa mnataka kuvuna.

 

 

فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ﴿٢٣﴾

Wakatoka na huku wanakwenda kimya kimya wakinong’onezana.

 

 

أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ﴿٢٤﴾

Kwamba: “Asikuingilieni humo kwa hali yoyote leo masikini.”

 

 

وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ﴿٢٥﴾

Wakatoka asubuhi mapema kwa kusudio la nguvu, wakidhani wana uwezo (wa kuwazuia maskini).

 

 

فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ﴿٢٦﴾

Basi walipoliona wakasema: “Hakika sisi bila shaka Tumepotea.”

 

 

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ﴿٢٧﴾

 (Walivyotanabahi!): “Bali sisi tumenyimwa!”

 

 

قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ﴿٢٨﴾

Mbora wao akasema: “Je, sikukuambieni kwanini hamumsabbih (Allaah?)”

 

 

قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ﴿٢٩﴾

Wakasema: “Ametakasika Rabb wetu! Hakika Sisi tulikuwa madhalimu.”

 

 

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ﴿٣٠﴾

Wakakabiliana wenyewe kwa wenyewe wakilaumiana.

 

 

قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ﴿٣١﴾

Wakasema: “Ole wetu! Hakika sisi tumekuwa warukao mipaka.”

 

 

عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ﴿٣٢﴾

 “Asaa Rabb wetu Akatubadilishia lililo bora kuliko hilo hakika sisi kwa Rabb wetu ni wenye raghba.”

 

 

كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ﴿٣٣﴾

Hivyo ndivyo adhabu, na bila shaka adhabu ya Aakhirah ni kubwa zaidi lau wangelikuwa wanajua. [Al-Qalam: 17-33]

 

 

Tunataraji kuwa mafunzo haya na visa hivyo vitakuwa ni mafunzo kwetu ambayo yatatukinaisha na kutuzidishia iymaan zetu tupende kutoa sadaka kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kuwapa masikini, ndugu, jamaa na wenye kuhitaji, mayatima, na kutoa katika njia ya Allaah.    

 

 

Share

08-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Wafungao Swawm Wanaume Na Wanawake

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

08-Wafungao Swawm Wanaume Na Wanawake

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ

 

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao swadaqah wanaume na wanawake, na wafungao Swawm wanaume na wanawake [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Maana Ya Swawm Kilugha:

 

 

Swawm ni kufunga na kujizuilia. Huenda ikawa ni kujizua kula chakula, kinywaji au kitu chochote kingine hata kujizua kuongea kwa dalili ya kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Alipomuamrisha Maryam mama yake Nabiy ‘Iysaa ‘('Alayhis-Salaam) afanye baada ya kumzaa mwanawe:

 

 

فَكُلِي وَاشْرَبِي وَقَرِّي عَيْنًا ۖ فَإِمَّا تَرَيِنَّ مِنَ الْبَشَرِ أَحَدًا فَقُولِي إِنِّي نَذَرْتُ لِلرَّحْمَـٰنِ صَوْمًا فَلَنْ أُكَلِّمَ الْيَوْمَ إِنسِيًّا ﴿٢٦﴾

 “Basi kula na kunywa na litue jicho lako. Na utakapokutana na mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri ya swawm kwa Ar-Rahmaan hivyo leo sitomsemesha mtu yeyote.”   [Maryam: 26]  

 

 

Maana ya Swawm ki-Shariy’ah:

 

 

Ni kuacha kula na kunywa pamoja na matamanio ya mwili na tumbo kuanzia kupambazuka kwa Alfajiri hadi linapozama jua yaani wakati wa Magharibi pamoja na niyyah ya kumwabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

 

  

Hukmu ya Swawm ilikwishawatangulia walio kabla yetu kwa kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa): 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾

Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyofaridhishwa kwa walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa. [Al-Baqarah: 183]

 

 

Swawm ni aina mbili:

 

 

Swawm ya wajib: Ni Swawm ya mwezi wa Ramadhwaan, Swawm ya kafara, fidia na Swawm ya kuondosha nadhiri.

 

Swawm za Sunnah: Ni kama Swawm ya siku ya ‘Arafah, Swawm ya ‘Ashuraa, Jumatatu na Alkhamiys, Ayaamul-Biydhw (siku tatu katika mwezi wa Hijri 13, 14 na 15), na pia Swawm nyinginezo kama katika mwezi wa Muharram n.k.

 

Kuna aina mbili za watu wanaofunga:

 

a) Wanaofunga kwa kujizuia kula, kunywa na matamanio ya mwili, lakini hawazuii ndimi zao, wala macho na masikio yao, wala viungo vyao vinginevyo  kuzuia yale yaliyoharamishwa. Pia aina ya wafungaji wenye kupoteza muda wao katika upuuzi bila ya kutekeleza ‘ibaadah zipasazo kutekelezwa mtu anapokuwa katika Swawm.

 

 

b) Wanaofunga kwa kutekeleza ipasavyo swawm zao kwa ‘ibaadah na kutenda mema kwa wingi na kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa wingi.   Ni wenye taqwa na iymaan ya kutaraji malipo ya Swawm zao na ni wenye kuthamini fadhila za Swawm. 

 

 

Swawm ni ‘ibaadah tukufu kabisa na fadhila zake ni nyingi sana, chache miongoni mwazo ni:

 

 

Fadhila Za Swawm Kwa Ujumla Na Swawm Za Ramadhwan:

 

1. Swawm ni ‘Ibaadah mahsusi ya Allaah ('Azza wa Jalla):

 

 

عن أبي هريرة  رضي الله عنه  قال: قال رسول اللَّه  صلى الله عليه وسلم: (( قالَ اللَّهُ:  كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ لَهُ إِلاَّ الصِّيَامَ، فَإِنَّهُ لِي، وَأَنَا أَجْزِي بِهِ‏.‏ وَالصِّيَامُ جُنَّةٌ، وَإِذَا كَانَ يَوْمُ صَوْمِ أَحَدِكُمْ، فَلاَ يَرْفُثْ وَلاَ يَصْخَبْ، فَإِنْ سَابَّهُ أَحَدٌ، أَوْ قَاتَلَهُ فَلْيَقُلْ إِنِّي امْرُؤٌ صَائِمٌ‏.‏ وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَخُلُوفُ فَمِ الصَّائِمِ أَطْيَبُ عِنْدَ اللَّهِ مِنْ رِيحِ الْمِسْكِ، لِلصَّائِمِ فَرْحَتَانِ يَفْرَحُهُمَا إِذَا أَفْطَرَ فَرِحَ، وَإِذَا لَقِيَ رَبَّهُ فَرِحَ بِصَوْمِهِ ‏)) رواه البخاري.

 

Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema:

((Allaah ‘Azza wa Jalla Amesema: “Kila ‘amali ya bin Aadam inamhusu yeye isipokuwa Swiyaam, kwani hakika hiyo inanihusu Mimi, Nami Ndiye Ninayeilipia.  Na Swawm ni ngao, na itakapokuwa siku ya Swawm ya mmoja wenu, basi asitamke maneno yasiyolaiki, wala asifanye maasia, wala asipayuke ovyo. Ikiwa mtu atamvuta watukanane au wapigane, basi aseme: “Hakika mimi nimefunga”. Naapa kwa Ambaye Nafsi ya Muhammad iko Mkononi Mwake, hakika kutaghayari harufu ya kinywa cha mwenye Swawm kunanukia mbele ya Allaah kuliko harufu ya miski. Mwenye Swawm ana furaha mbili anazozifurahikia; anapofungua hufurahika kwa Swawm yake, na atakapokutana na Mola wake atafurahi kwa Swawm yake)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 

2.  Mwenye Swawm anaghufuriwa madhambi yake:

 

قال صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ صَامَ رَمَضَانَ إِيمَانًا وَاحْتِسَابًا غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ))   أخرجه البخاري ومسلم

Amesema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Atakayefunga Ramadhwaan kwa iymaan na kutaraji malipo ataghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia)) [Al Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

3- Swawm ni ngao

 

عن عثمان بن عفان رضي الله عنه، قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول:  الصِّيامُ جُنَّةٌ من النَّارِ ، كَجُنَّةِ أحدِكمْ من القِتالِ))

Imepokelewa toka kwa ‘Uthmaan bin ‘Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu)  akisema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Swiyaam ni ngao dhidi ya moto, kama ngao ya mmoja wenu katika mapigano)) [Ibn Maajah, amiesahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Ibn Maajah (1336),  Swahiyh Al-Jaami’  (3879)]

 

 

 

4. Kufunga (Swawm) ni kuepushwa na moto masafa ya miaka sabini.

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رضي الله عنه قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: مَنْ صَامَ يَوْماً فِي سَبِيلِ اللَّهِ بَعَّدَ اللَّهُ وَجْهَهُ عَنْ النَّارِ سَبْعِينَ خَرِيفًا .

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayefunga  Swawm siku moja kwa ajili ya Allaah, Allaah Atamweka mbali uso wake na moto masafa ya miaka sabini)) [Muslim 2/208]

 

Na katika Hadiyth nyingine pia:

 

عن جابر رضِي الله عنه عن النبيِّ  صلى الله عليه وسلم  قال: ((الصِّيام جُنَّة يَستَجِنُّ بها العبدُ من النار))   

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swiyaam ni kinga itamuokoa mja kutokana na moto [wa Siku ya Qiyaamah])) [Ahmad 2/402, Swahiyh At-Targhiyb 1/411 na Swahiyh Al-Jaami’ 3880]

 

 

5. Mwenye kufunga (Swawm) atafunguliwa mlango wa Rayyaan huko Jannah.

 

عَنْ سَهْلٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِنَّ فِي الْجَنَّةِ بَابًا يُقَالُ لَهُ الرَّيَّانُ يَدْخُلُ مِنْهُ الصَّائِمُونَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ لَا يَدْخُلُ مِنْهُ أَحَدٌ غَيْرُهُمْ يُقَالُ أَيْنَ الصَّائِمُونَ فَيَقُومُونَ لَا يَدْخُلُ مِنْهُ أَحَدٌ غَيْرُهُمْ فَإِذَا دَخَلُوا أُغْلِقَ فَلَمْ يَدْخُلْ مِنْهُ أَحَدٌ ))

Imepokelewa kutoka kwa Sahl (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika katika Jannah kuna mlango unaitwa Rayyaan, wataingia humo siku ya Qiyaamah wenye kufunga (Swawm), hatoingia yeyote mwingine. Itasemwa: “Wako wapi waliokuwa wakifunga? Watasimama kuingia hatoingia yeyote mwengine, watakapoingia, utafungwa, basi hatoingia mwengine)) [Al-Bukhaariy 1763, Muslim 1947]

 

 

6. Swawm ni kwa ajili ya Allaah Pekee na mwenye Swawm hupata furaha mbili; anapofuturu na atakapokutana na Rabb Wake. Na harufu ya mdomo wake ni nzuri mbele ya Allaah kuliko harufu ya misk.

 

 

عنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ يُضَاعَفُ الْحَسَنَةُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا إِلَى سَبْعمِائَة ضِعْفٍ قَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ إِلَّا الصَّوْمَ فَإِنَّهُ لِي وَأَنَا أَجْزِي بِهِ يَدَعُ شَهْوَتَهُ وَطَعَامَهُ مِنْ أَجْلِي لِلصَّائِمِ فَرْحَتَانِ فَرْحَةٌ عِنْدَ فِطْرِهِ وَفَرْحَةٌ عِنْدَ لِقَاءِ رَبِّهِ وَلَخُلُوفُ فِيهِ أَطْيَبُ عِنْدَ اللَّهِ مِنْ رِيحِ الْمِسْكِ))

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu): ((Kila 'amali njema ya mwana Aadam inalipwa mara kumi na inaongezewa thawabu kutoka kumi hadi mia saba, na Allaah (‘Azza wa Jalla) Anasema: Isipokuwa Swawm, kwani hiyo ni kwa ajili Yangu na Mimi Ndiye Nitakayemlipa; ameacha matamanio yake na chakula chake kwa ajili Yangu. Kwa anayefunga atapata furaha mbili; furaha anapofuturu na furaha atakapoonana na Rabb wake, harufu inayotoka kinywani mwa aliye na Swawm ni nzuri mbele ya Allaah kuliko harufu ya misk)) [Muslim na Ahmad]

 

 

7. Du’aa ya mwenye Swawm inakubaliwa.

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ثَلاَثَةٌ لاَ تُرَدُّ دَعْوَتُهُمْ,  الإِمَامُ الْعَادِلُ, وَالصَّائِمُ حَتَّى يُفْطِرَ, وَدَعْوَةُ الْمَظْلُومِ ...))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (([Watu] Watatu hazirudishwi du'aa zao; Imaam muadilifu, mwenye Swawm mpaka afuturu, na du'aa ya aliyedhulumiwa…)) [Ahmad na Ibn Maajah. Pia Al-Bayhaqiy 3/345 na As-Silsilah Asw-Swahiyhah 1797]

 

 

8. Swawm itakuombea Shafaa-‘ah Siku ya Qiyaamah.

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رضي الله عنهما أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((الصِّيَامُ وَالْقُرْآنُ يَشْفَعَانِ لِلْعَبْدِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ، يَقُولُ الصِّيَامُ:  أَيْ رَبِّ مَنَعْتُهُ الطَّعَامَ وَالشَّهَوَاتِ بِالنَّهَارِ فَشَفِّعْنِي فِيهِ.  وَيَقُولُ الْقُرْآنُ: مَنَعْتُهُ النَّوْمَ بِاللَّيْلِ فَشَفِّعْنِي فِيهِ.  قَالَ : فَيُشَفَّعَانِ))

Imepokelewa kutoka  kwa 'Abdullaah bin ‘Amr  (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa)  kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swiyaam na Qur-aan zitamuombea shafaa’ah mja siku ya Qiyaamah. Swiyaam itasema: “Ee ee Rabb!  Nimemzuia chakula chake na matamanio wakati wa mchana, basi nnamuombea shafaa-‘ah.” Na Qur-aan itasema: “Nimemzuia usingizi wake wakati wa usiku basi nnamuombea shafaa-‘ah.” Akasema: ((Basi [viwili hivyo] vinaombea shafaa-‘ah na kukubaliwa]. [Ahmad (174/2) Al-Haakim (1/554), Al-Bayhaqiy (3/181) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jaamiy’ 7329]

 

 

9. Swawm hakuna mfano wake.

 

عَنْ أَبِي أُمَامَةَ  قَالَ: أَتَيْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَقُلْتُ: مُرْنِي بِأَمْرٍ آخُذُهُ عَنْكَ قَالَ: ((عَلَيْكَ بِالصَّوْمِ فَإِنَّهُ لَا مِثْلَ لَهُ))  

Kutoka kwa Abuu Umaamah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikasema: “Niamrishe jambo [litakalonifaa Aakhirah] nilichukue kwako.” Akasema: ((Shikilia Swawm kwani hakika hakuna mfano wake)) [An-Nasaaiy]

 

 

10. Ukifariki ukiwa katika Swawm utaingia Jannah nayo ni Husnul-Khaatimah.

 

عن حذيفة  رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قَال: ((مَن خُتِمَ له بصيام يومٍ دخل الجنة))

Imepokelewa kutoka kwa Hudhayfah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayekuwa 'amali yake ya mwisho kabla ya kufariki ni Swiyaam ataingia Jannah)) [Ahmad 5/391. Swahiyh At-Targhiyb 1/412, Swahiyh Al-Jaami’ 6224]

 

 

 

11. Swawm hufuta madhambi yatokanayo na mtu kufitinika na mkewe na mali yake:

 

سأل عمر رضي الله عنه قال: من يحفظ حديثًا عن النبي صلى الله عليه وسلم في الفتنة؟  قال حذيفة: أنا سمعته يقول: ((فِتْنَةُ الرَّجُلِ فِي أَهْلِهِ وَمَالِهِ وَجَارِهِ تُكَفِّرُهَا الصَّلَاةُ وَالصِّيَامُ وَالصَّدَقَةُ)).

‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu)  aliuliza: “Nani anahifadhi Hadiyth toka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu fitnah?” Hudhayfah akasema: Mimi nimemsikia akisema: ((Kufitinika mtu kutokana na mke wake, mali yake na jirani yake, (dhambi yake) hufutwa na Swalaah na Swawm na swadaqah..)) [Al-Bukhaariy]

 

 

12. Fadhila Za Swawm Jumatatu Na Alkhamiys:

 

عن أبي هريرة رضي الله عنه: تُعرَضُ الأعمالُ يومَ الاثنينِ والخميسِ فأحبُّ أن يُعرَضَ عملي وأنا صائمٌ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Amali zinapandishwa siku ya Jumatatu na Alkhamiys, basi napenda kwamba zipandishwe 'amali zangu nikiwa mimi nina Swawm.” [Swahiyh At-Tirmidhiy 747, Swahiyh At-Targhiyb 1041]

 

Na kuhusu Swiyaam ya Jumatatu:

 

عَنْ أَبِي قَتَادَةَ الْأَنْصَارِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سُئِلَ عَنْ صَوْمِ الِاثْنَيْنِ فَقَالَ: ((فِيهِ وُلِدْتُ وَفِيهِ أُنْزِلَ عَلَيَّ)).

Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu Swawm ya Jumatatu akasema: “Nimezaliwa siku hiyo na siku hiyo nimeteremshiwa (Qur-aan).” [Muslim]

 

 

13-Fadhila Za Swiyaam Ayyaam Al-Biydhw:

 

 

عَنْ أَبي ذَرٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيهِ وَسَلَّمَ (مَنْ صَامَ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَذَلِكَ صِيَامُ الدَّهْرِ)) فَأَنْزَلَ اللهُ تُصْدِيقَ ذَلِكَ في كِتَابِهِ الْكَرِيمِ: ((مَنْ جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا))، الْيَوْمُ بِعَشَرَةِ أَيّامٍ. أخرجه أحمد والترمذي وقال حديث حسن ، والنسائي وابن ماجه وابن خزيمة

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Yeyote atakayefunga (Swawm) kila mwezi siku tatu, ni sawa na Swawm ya milele)) Kisha Allaah Akateremsha Aayah ithibitishayo hayo: “Atakayekuja kwa ‘amali nzuri basi atapata (thawabu) kumi mfano wa hiyo.” Siku moja kwa malipo ya siku kumi. [Imepokewa na At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan, An Nasaaiy na Ibn Maajah, Ibn Khuzaymah na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Al-Irwaa (4/102)]. Aayah: Suwrat Al-An’aam (160)]

 

Maana Ya Al-Biydhw:  Masiku hayo yameitwa ‘Al-Biydhw’ (meupe) sababu usiku wa siku hizo hung’aa kutokana na mwanga wa mwezi. Ayyaam Al-Biydhw (Masiku Meupe) tarehe zake ni 13, 14 na 15 katika kila mwezi wa kalenda ya Kiislamu.

 

عَنْ جريرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَن النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((صِيَامُ ثَلاثَةِ أَيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ صِيَامُ الدَّهْرِ، أَيَّامُ الْبِيضِ صَبِيحَةَ ثَلاثَ عَشَرَةَ وَأَرْبَعَ عَشَرَةَ وَخَمْسَ عشَرَةَ))   

Imepokelewa kutoka kwa Jariyr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swiyaam siku tatu kila mwezi ni sawa na swiyaam ya milele; na masiku meupe ni tarehe kumi na tatu, kumi ay a na kumi na tano [13, 14, 15])) [An-Nasaaiy (2420) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Targhiyb (1040)]

 

عن أبي ذر رضي الله عنه: قال لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((يَا أَبَا ذَرٍّ، إِذَا صُمْتَ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَصُمْ ثَلاثَةَ عَشَرَ وَأَرْبَعَةَ عَشَرَ وَخَمْسَةَ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: ((Ee Abuu Dharr! Endapo utafunga (Swawm) siku tatu za kila mwezi, basi funga siku ya 13, ya 14, ay a 15)) [Imepokewa na At-Tirmidhiy na kasema Al-Albaaniy kuwa ni Swahiyh]

 

قال صلى الله عليه وسلم: ((أَلا أُخْبِرُكُمْ بِمَا يُذْهِبُ وَحَرَ الصَّدْرِ صَوْمُ ثَلاثَةِ أَيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْر))

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Je, nikujulisheni jambo litakaloondosha uovu wa moyo? Ni kufunga (Swawm) siku tatu kila mwezi)) [An-Nasaaiy (2/2386) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh An-Nasaaiy (2249)]

 

Asw-Suyuutwiy (Rahimahu Allaah) amesema katika An-Nihaayah: Uovu wa moyo ni; udanganyifu, wasiwasi, na imesemwa pia ni uhasidi, chuki, na imesemwa pia uadui na imesemwa ghadhabu”

 

 

14-Fadhila Za Swawm ya ‘Arafah

 

عَنْ أَبِي قَتَادَةَ رضي الله عنه أن النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ :  ((صِيَامُ يَوْمِ عَرَفَةَ أَحْتَسِبُ عَلَى اللَّهِ أَنْ يُكَفِّرَ السَّنَةَ الَّتِي قَبْلَهُ وَالسَّنَةَ الَّتِي بَعْدَهُ )) أخرجه مسلم

Abuu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swawm ya 'Arafah nataraji (kwa Allaah) kufuta madhambi ya mwaka uliopita na wa baada yake)) [Muslim]

 

 

15-Fadhila Za Swawm ya ‘Ashuraa na mwezi wa Muharaam:

 

عَنْ أَبِي قَتَادَةَ اَلْأَنْصَارِيِّ  رضى الله عنه {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ‏ صلى الله عليه وسلم ‏سُئِلَ عَنْ صَوْمِ يَوْمِ عَرَفَةَ.‏ قَالَ: " يُكَفِّرُ اَلسَّنَةَ اَلْمَاضِيَةَ وَالْبَاقِيَةَ "، وَسُئِلَ عَنْ صِيَامِ يَوْمِ عَاشُورَاءَ.‏ قَالَ: " يُكَفِّرُ اَلسَّنَةَ اَلْمَاضِيَةَ " وَسُئِلَ عَنْ صَوْمِ يَوْمِ اَلِاثْنَيْنِ، قَالَ: " ذَاكَ يَوْمٌ وُلِدْتُ فِيهِ، وَبُعِثْتُ فِيهِ، أَوْ أُنْزِلَ عَلَيَّ فِيهِ "} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Answaariy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliulizwa kuhusu Swawm ya siku ya ‘Arafah akasema: “Hufuta madhambi ya mwaka uliopita na unaobakia.” Akaulizwa kuhusu Swawm ya siku ya ‘Aashuwraa akasema: “Inafuta madhambi ya mwaka uliopita.”  Akaulizwa kuhusu Swawm ya siku za Jumatatu, akasema: “Hiyo ni siku niliyozaliwa na siku niliyopewa Unabiy na ni siku niliyoteremshiwa Qur-aan.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

16-Fadhila za Swawm Za Sitta Shawwaal:

 

وَعَنْ أَبِي أَيُّوبَ اَلْأَنْصَارِيِّ رضى الله عنه‏ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {مَنْ صَامَ رَمَضَانَ، ثُمَّ أَتْبَعَهُ سِتًّا مِنْ شَوَّالٍ كَانَ كَصِيَامِ اَلدَّهْرِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Ayyuwb Al-Answaariyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kufunga Ramadhwaan, kisha akafuatishia siku sita za mwezi Shawwaal. huwa kama Swiyaam ya  mwaka mzima.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

18-Fadhila Za Swawm ya Nabiy Daawuwd:

 

Amesema ‘Abdullaah bin ‘Amr bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: “Funga inayopendeza zaidi kwa Allaah ni funga ya Nabii Daawuwd … alikuwa anafunga siku moja na anakula siku moja” [Al-Bukhaariy, Muslim na an-Nasaaiy].

 

 

Swahaabiyaah aliyekuwa akipenda kufunga sana:  Hafswah bint ‘Umar ibnil-Khatwaab  (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa)

 

 

Ni mtoto wa ‘Umar ibnil-Khatwaab Khaliyfah wa pili wa Waislamu. Aliolewa na Khunis ibn Hudhaafa bin Qays As-Sahaamiy ambaye alikuwa katika kabila ya Quraysh. Mumewe alihajiri mara mbili; kwenda Abyssinia na kwenda Madiynah. Alipigana vita vya Badr kisha Uhud akariki akimuacha Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) akiwa na miaka kumi na nane.

 

‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alihuzunika kwa msiba ya binti yake. Kila alipokwenda nyumbani kwake akimtazama hali yake huwa anahuzunika. 

 

 

Baada ya muda akaamua kumtafutia mume binti yake akaanza kwa Abuu Bakar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye ni rafiki mpenzi wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Alipomuomba amuoe, Abuu Bakar hakumjibu kitu. ‘Umar akarudi akiwa amevunjika moyo na wala hakuamini Abuu Bakar kumkatalia ombi lake.

 

Kisha akaenda kwa ‘Uthmaan bin ‘Affaan (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye mkewe ni Ruqayyah mtoto wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).  Alipomuomba, alimjibu kuwa: “Sipendi kuoa kwa hivi sasa.”

 

Umar akazidi kusikitika. Akaenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kumlalamikia kuhusu Abuu Bakar na ‘Uthmaan, Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuambia: ((Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) ataolewa na mtu aliye bora kuliko ‘Uthmaan na ‘Uthmaan ataoa aliye bora kuliko Hafswah)) [Al-Bukhaariy]

 

‘Umar Alifurahi akawa anamuambia kila aliyemuona. Abuu Bakar alipomuona, alitambua furaha yake akampa hongera kisha akamuomba msamaha na kumuambia: “Usikasirike na mimi kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimtaja Hafswah (Radhwiya Allahu ‘anhaa) kabla na sikuweza kutaja siri yake. Ingelikuwa hakumtaja ningelimuoa”.

 

Watu wote Madiynah walifurahiwa na ndoa ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Hafswah bint ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) hivyo akaungana na mama waumini wengine kwa furaha.

 

Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa alikuwa rafiki mkubwa wa ‘Aishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) hivyo walipatana sana. Imesemekana kwamba Rasuli wa Allaah alimpa talaka Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) mara moja kutokana na makosa aliyoyafanya ya kutoa siri,  lakini alimrudia kutokana na amri kutoka kwa Jibryil (‘alayhis-salaam) alipomuambia: “Mrudie Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwani yeye anafunga (Swawm) na kuswali usiku kucha.”

 

Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) alitambua makosa yake akajirudi na kuwa mke mtiifu na mwema. 

 

Alipofariki Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Abuu Bakar alipokuwa Khaliyfah, Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) alichaguliwa kuwa msimamizi   wa nuskha ya kwanza ya Qur-aan. Aliendelea kumwabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa kufunga (Swawm) na kutunza Qur-aan. Kabla ya kuuawa baba yake, Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) aliachiwa kuwa msimamizi wa mirathi yake.

 

Hafswah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) alifariki katika uongozi wa Mu’aawiyah ibn Abu Sufyaan. Alimuamrisha kaka yake ‘Abdullah bin 'Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) yale aliyoamrishwa na baba yake.  

 

 

 

 

 

 

Share

09-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Wanaume Na Wanawake Wanojihifadhi Tupu Zao

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

09-Wanaume Na Wanawake Wanojihifadhi Tupu Zao

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ وَالْحَافِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَالْحَافِظَاتِ

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao swadaqah wanaume na wanawake, na wafungao Swawm wanaume na wanawake, wanaojihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Kuhifadhi tupu kujiepusha na yote Aliyoyaharamisha Allaah ('Azza wa Jalla) kama zinaa, liwaat (wanaume kwa wanaume) na pia wafanyao uchafu baina ya wanawake kwa wanawake.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametahadharisha kutokukaribia zinaa Anaposema:

 

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

Na wala msiikaribie zinaa. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya kabisa. [Al-Israa: 32]

 

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametahadharisha pia katika Hadiyth kadhaa zikiwemo:

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَنْظُرُ الرَّجُلُ إِلَى عَوْرَةِ الرَّجُلِ، وَلاَ الْمَرْأَةُ إِلَى عَوْرَةِ الْمَرْأَةِ، ولاَ يُفْضِي الرَّجُلُ إِلَى الرَّجُلِ فِي ثَوْبٍ وَاحِدٍ، وَلاَ تُفْضِي الْمَرْأَةُ إِلَى الْمَرْأَةِ فِي الثَّوْبِ الْوَاحِدِ)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwanamme asitazame uchi wa mwanamme, wala mwanamke asitazame uchi wa mwanamke, wala mwanamme asilale na mwanamme mwenzie katika nguo moja, wala mwanamke asilale na mwanamke mwenzie katika nguo moja)). [Muslim]

 

 

Na pia:

 

 

عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِيَّاكُمْ وَالدُّخُولَ عَلَى النِّسَاءِ)) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ الأَنْصَارِ: يَا رَسُولَ اللَّهِ أَفَرَأَيْتَ الْحَمْوَ؟ قَالَ:  ((الْحَمْوُ الْمَوْتُ))  متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Tahadharini na kuingia kwa wanawake!)) Mtu mmoja katika Answaariy akauliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Nieleze akiwa ni shemeji?” Akamwambia:  ((Shemeji ni mauti!)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na pia:

 

 

Kutoka kwa 'Umar  (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hachanganyiki mwanamume na mwanamke ila shaytwaan huwa ni watatu wao)). [At-Tirmidhiy]

 

Na pia:

 

Hadiyth  kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)   kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Ameandika kila sehemu ya zinaa ambayo humuingiza mtu katika shauku. Hakutokuwa na kuikwepa. Zinaa ya macho ni kutazama, ya masikio ni kusikiliza, ulimi ni kunena maneno, mkono ni kuunyoosha, mguu ni hatua zake, na moyo hupata matamanio, na tupu husadikisha [hutenda] au hukadhibisha [huacha])). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Waumini wenye kuhifadhi tupu zao ni wale ambao hawamkaribii yeyote isipokuwa wale waliohalalishwa nao na wale iliyomiliki mikono yao ya kuume kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ﴿٢٩﴾

Na ambao wanahifadhi tupu zao.

 

إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ﴿٣٠﴾

Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa.

 

فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ﴿٣١﴾

Basi yeyote yule atakayetaka kinyume ya hayo, basi hao ndio warukao mipaka. [Al-Ma'aarij: 29-31]

 

 

Sifa hii vile vile ni miongoni mwa sifa Alizozitaja Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuwa pindi Muislamu akizimiliki, ataingizwa Jannah ya Al-Firdaws kama ilivyotajwa katika Suwratul-Muuminuwn:

 

وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ ﴿٥﴾

Na ambao wanazihifadhi tupu zao.

 

إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ ﴿٦﴾

Isipokuwa kwa wake zao, au kwa iliyowamiliki mikono yao ya kuume basi hao hawalaumiwi.

 

 

فَمَنِ ابْتَغَىٰ وَرَاءَ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْعَادُونَ ﴿٧﴾

Lakini atakayetaka kinyume ya hayo; basi hao ndio wapindukao mipaka. [Al-Muuminuwn 5-8]

 

Zinaendelea Aayah mpaka kauli Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

أُولَـٰئِكَ هُمُ الْوَارِثُونَ ﴿١٠﴾

Hao ndio warithi.

 

الَّذِينَ يَرِثُونَ الْفِرْدَوْسَ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿١١﴾

Ambao watarithi (Jannah) ya Al-Firdaws, wao humo ni wenye kudumu. [Al-Muuminuwn: 1-11]

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pia ametubashiria Jannah kwa wenye kuhifadhi tupu zao aliposema:

 

((مَنْ يَكْفُل لِي مَا بَيْن لَحْيَيْهِ وَمَا بَيْن رِجْلَيْهِ أَكْفُل لَهُ الْجَنَّة)) البخاري

((Atakayenipa dhamana (ya kuhifadhi) baina  ya ndevu (ulimi) zake na miguu yake (tupu) basi atadhaminiwa Jannah)) [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Muislamu pindi akiinamisha macho yake na wanawake wakitii amri ya Allaah ('Azza wa Jalla) kuhusu kutimiza hukmu za hijaab, basi wataweza kujilinda na hayo yaliyotahadharishwa.  Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaamrisha:

 

قُل لِّلْمُؤْمِنِينَ يَغُضُّوا مِنْ أَبْصَارِهِمْ وَيَحْفَظُوا فُرُوجَهُمْ ۚ ذَٰلِكَ أَزْكَىٰ لَهُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ خَبِيرٌ بِمَا يَصْنَعُونَ ﴿٣٠﴾

Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao na wahifadhi tupu zao. Hivyo ni utakaso zaidi kwao. Hakika Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale wayatendayo. 

 

 

وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْيَضْرِبْنَ بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ ۖ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ لَمْ يَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ ۚ وَتُوبُوا إِلَى اللَّـهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٣١﴾

Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao na wahifadhi tupu zao, na wala wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa yale yanayodhihirika. Na waangushe khimaar (shungi) zao mpaka vifuani mwao, na wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa kwa waume zao, au baba zao, au baba za waume wao, au wana wao wa kiume, au wana wa kiume wa waume zao, au kaka zao, au wana wa kiume wa kaka zao, au wana wa kiume wa dada zao, au wanawake wao (wa Kiislamu), au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, au wafuasi wanaume wasio na matamanio ya jimai miongoni mwa wanaume au watoto ambao hawatambui kitu kuhusu sehemu za siri za wanawake. Na wala wasipige miguu yao yakajulikana yale wanayoyaficha katika mapambo yao. Na tubuni kwa Allaah nyote, enyi Waumini mpate kufaulu. [An-Nuwr: 30-31]

 

 

Wanawake wasiotimiza hijaab, wameharamishwa Jannah na hawatasikia hata harufu yake:

 

 

  عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((صِنْفَانِ مِنْ أَهْلِ النَّارِ لَمْ أَرَهُمَا: قَوْمٌ مَعَهُمْ سِيَاطٌ كَأَذْنَابِ الْبَقَرِ يَضْرِبُونَ بِهَا النَّاسَ، وَنِسَاءٌ كَاسِيَاتٌ عَارِيَاتٌ مُمِيلاَتٌ مَائِلاَتٌ رُءُوسُهُنَّ كَأَسْنِمَةِ الْبُخْتِ الْمَائِلَةِ، لاَ يَدْخُلْنَ الْجَنَّةَ وَلاَ يَجِدْنَ رِيحَهَا، وَإِنَّ رِيحَهَا لَيُوجَدُ مِنْ مَسِيرَةِ كَذَا وَكَذَا)) مسلم

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه  وآله وسلم ) amesema: ((Aina mbili za watu wa motoni sijawaonapo [hawapo katika zama zangu]: Watu walio na mijeledi mfano wa mikia ya ng’ombe wanawapiga watu kwa mijeledi hiyo [kwa dhulma], na wanawake waliovaa nguo na ilhali wako uchi, wakitembea kwa maringo huku wakiyanyonga mabega yao na wakiwafunza wengineo kutenda kama hivyo, vichwa vyao ni kama nundu za ngamia-bukhti wanaodemadema. Hawatoingia Jannah wala hawataisikia harufu yake, na kwa hakika harufu yake husikika umbali kadha wa kadhaa)). [Muslim]

 

  

Hadiyth hiyo ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inatudhihirikia uhakika wake kwani tunawaona baadhi ya dada zetu wanaovaa nguo wakidhani wamejisitiri kumbe wako uchi.  Utamuona mwanamke amejifunika kichwa tu akidhania ndio maana ya hijaab lakini mwili wake wote haukusitirika kwa sababu vazi lake halikutimiza masharti yake ya hijaab ambayo ni mwanamke kujigubika jilbaab limfunike mwili mzima (pamoja na khilafu iliyopo kati ya Wanachuoni kuhusu suala la uwajibu wa kuufunika uso na kutoufunika).  Jilbaab hilo lifuate masharti yafuatayo: 

 

 

1. Jilbaab liwe refu la kukufunika mwili mzima mpaka miguu, na kama halikufunika miguu basi mwanamke avae soksi.  

 

 

2.  Jilbaab liwe pana na sio lenye kuonyesha umbo, yaani lisiwe lenye kubana popote mwilini.  

 

 

3.  Jilbaab liwe zito na si jepesi la kuonyesha mwili.

 

 

4.  Jilbaab lisiwe na marembo yoyote yale ya kuvutia.

 

 

5. Jilbaab halitakiwi lifanane na mavazi ya makafiri.

 

 

6.  Jilbaab halitakiwi liwe ni katika mavazi ya fakhari.

 

 

7. Wanawake kutokuvaa nguo zinazofanana na nguo za kiume.

 

  

8.    Kutotia manukato.

 

 

Dada zetu wa Kiislamu watakapotimiza haya watakuwa wamekamilisha hijaab zao na watakuwa katika stara pamoja na kusitiri jamii na ndipo watakapokuwa wamejitahidi kujihifadhi waweze kuingia katika sifa hiyo ya kuhifadhi tupu zao.  

 

 

Kisa cha Zahrah na safari yake ya kuvaa hijaab. 

 

 

"Safari yangu ya hijaab au labda niseme "hijaab inayopasa ki-shariy’ah” ni ndefu na ya pole pole na sio ya tamthilia.   

 

Nilikuwa na umri wa miaka 14 nikienda shule pamoja na kaka yangu na dada zangu. Baba yangu alikuwa akitupeleka na kuturudisha shuleni. Kwa vile baba yangu alikuwa ana kazi nyingi sana na wakati wake ulikuwa wa dhiki, aliamua kutuwekea teksi kwa muda wa wiki mbili.  Dereva wa teksi alikuwa mtu mwema na mchangamfu. Alikuwa akitutolea visa na vichekesho wakati tunaelekea shuleni na kurudi. Tukaanza kumpenda na kumheshimu kama vile ni mjomba wetu. Hakuwa anajua Kiingereza, lakini siku moja alitupa tafsiyr ya Qur-aan ya Marmaduke Pickthall.

 

Siku moja wakati anaturudisha nyumbani, mara ghafla akasema: "Wasichana wa Kiislamu ni lazima wavae hijaab." Maneno yake yakawa yananigonga masikioni siku nzima! Sikupata kuvaa hijaab kabla, na karibu nisba ya 99% ya wasichana darasani mwangu hawakuwa wanavaa hijaab, wala sikupenda fikra hiyo ya kuvaa hijaab mwenyewe. Lakini sikuweza kupinga aliyoyasema dereva huyo ingawa sikuwa na pendekezo nalo jambo hili, na sikuweza kukanusha kwamba wanawake wa Kiislamu wanapaswa kuvaa hijaab.

 

Nikaanza kuvaa kitambaa cha kichwa siku ya pili na nakiri kwamba nilianza kuvaa kwa sababu ya heshima niliyo kuwa nayo ya dereva huyo bila ya kufikiri kwamba ni makosa kwani nilitakiwa nimkumbuke Mola wangu kwanza. Na sikuwa na sababu ya kunizua kuvaa hijaab. Wazazi wangu walifurahia uamuzi wangu.

 

 

Siku za mwanzo, nilianza kuvaa kitambaa cha kichwa kwa kujifunika nusu na huku baadhi ya nywele zikionekana! Nilitambua kuwa hivyo sivyo ilivyopasa kuvaliwa. Baada ya hapo nikatamuba unafiki wangu nikaanza kuivaa vizuri na kufunika nywele zote. Haikuwa wepesi ingawa nilikuwa naishi katika nchi ya Kiislamu na marafiki zangu walikuwa wakiniuliza: "Kwa nini unafanya hivyo? Unaonakana kama mzee!”

 

Kwao wao, jambo hilo lilikuwa ni kama tendo la watu wazima tu. Na sisi tulio vijana tukiwa bado shuleni tunatakiwa tuwe na uhuru wa mavazi. Lakini AlhamduliLLaah sikuwasikiliza maneno yao kwani hijaab ilinifanya nionekane mtu makini na heshima zaidi. Nikaamua kuivaa moja kwa moja. Nikaanza kuvaa nguo zilizofunika mikono yote, na zilizokuwa pana kila mahali nilikokwenda hadi ilipofika mwezi wa Septemba nikajifunza kwamba jilbaab ni lazima nikaanza kuvaa jilbaab.

 

Nikitazama nyuma nawaza kwamba hijaab imenisaidia sana kuniunda kama mwanamke hasa wa Kiislam. Nilipoanza kuivaa hata sikuwa nadumisha Swalaah zangu tano. Lakini  AlhamduliLLaah hatua baada ya hatua hijaab yangu imenisaidia kufunga milango yote ya shari na mambo yasiyopasa ya Kiislamu yaliyonizunguka katika mazingira yangu. Nimeunda picha fulani katika macho yangu na ya wengine, hivyo ikanibidi niishi katika kigezo hicho cha picha hiyo; picha ya staha.”

 

 

 

Share

10-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Wanaume Na Wanawake Wanaomdhukuru Mno Allaah

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

10- Wanaume Na Wanawake Wanaomdhukuru Mno Allaah

 

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ وَالْحَافِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَالْحَافِظَاتِ وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao swadaqah wanaume na wanawake, na wafungao Swawm wanaume na wanawake, wanaojihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, na wanaomdhukuru Allaah kwa wingi wanaume na wanawake; Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu. [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa wingi ni sifa ya mwisho kutajwa katika Aayah hiyo tukufu.  Na kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni ‘ibaada pekee ambayo haina mipaka ya kutekelezwa kwake kutokana na kauli ya Allaah ('Azza wa Jalla):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾

Enyi walioamini!  Mdhukuruni Allaah kwa wingi wa kumdhukuru. [Suratul-Ahzaab: 41]  

 

 

Na kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni ‘ibaadah nyepesi kabisa inayoweza kudumishwa:

 

4-Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni ‘ibaadah nyepesi inayowezwa kudumishwa:

 

عن عبد الله بن بسرٍ رضي الله عنهُ أن رجلاً قال : يا رسول الله إن شرائع الإسلام قد كثرت علي فأخبرني بشيءٍ أتشبث به. قال : (( لا يزال لسانك رطباً من ذكر الله)) ألترمذي إبن ماجه وصححه شيخ الألباني   

Imepokelewa kutoka kwa Abdullaah Bin Busr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba mtu mmoja alisema: “Ee Rasuli wa Allaah! ‘Ibaadah za Dini zimekuwa nyingi kwangu, basi nieleze kitu ambacho nitaweza kudumu nacho?” Akasema: ((Ulimi wako utaendelea kuwa rutuba (yaani sio ukavu) kwa kumdhukuru Allaah)) [At-Tirmidhiy na Ibn Maajah na imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy]

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametutajia jinsi ya kufikia daraja la kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa wingi katika Hadiyth zifuatazo:

 

قَالَ اِبْن أَبِي حَاتِم  عَنْ أَبِي سَعِيد الْخُدْرِيّ رَضِيَ اللَّه عَنْهُ قَالَ : إِنَّ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ ((إِذَا أَيْقَظَ الرَّجُل اِمْرَأَته مِنْ اللَّيْل فَصَلَّيَا رَكْعَتَيْنِ كَانَا تِلْكَ اللَّيْلَة مِنْ الذَّاكِرِينَ اللَّه كَثِيرًا وَالذَّاكِرَات))   أبو داود ،

Ibn Abiy Haatim amesesma kutoka kwa Abuu Sa'iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:  (Mume akimuamsha mkewe usiku wakaswali Rakaa mbili watakuwa usiku huo ni miongoni mwa wale wanaume na wanawake wanaomdhukuru Allaah sana))   [Abuu Daawuwd]

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَة رَضِيَ اللَّه عَنْهُ قَالَ : كَانَ رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَسِير فِي طَرِيق مَكَّة فَأَتَى عَلَى جُمْدَان فَقَالَ ((هَذَا جُمْدَان سِيرُوا فَقَدْ سَبَقَ الْمُفَرِّدُونَ)) قَالُوا وَمَا الْمُفَرِّدُونَ ؟ قَالَ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ((الذَّاكِرُونَ اللَّه كَثِيرًا وَالذَّاكِرَات)) ثُمَّ قَالَ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ((اللَّهُمَّ اِغْفِرْ لِلْمُحَلِّقِينَ)) قَالُوا وَالْمُقَصِّرِينَ قَالَ ((اللَّهُمَّ اِغْفِرْ لِلْمُحَلِّقِينَ)) قَالُوا وَالْمُقَصِّرِينَ قَالَ ((وَالْمُقَصِّرِينَ)) إمام أحمد تفرد به من هذا الوجه، ورواه مسلم دون آخره

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba:  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitembea katika njia ya Makkah na alipofika mlima wa Jumdaan akasema: ((Huu ni (mlima wa) Jumdaan, endeleeni kwani Mufarriduwn wametangulia mbele)). Wakasema: Ni nani Mufarraduun? Akasema: ((Wanaomdhukuru Allaah sana wanaume na wanawake)). Kisha akasema: ((Ee Allaah, Waghufurie walionyoa nywele zao)). Wakasema: "Na waliopunguza". Akasema: ((Ee Allah Waghufurie walionyoa nywele zao)). Wakasema: "Na waliopunguza". Akasema: ((Na waliopunguza)). [Imaam Ahmad kaipokea kwa masimulizi hayo, na Muslim bila ya maelezo ya mwisho]

 

 

Na pia kuomba du’aa:

 

 

عَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَخَذَ بِيَدِهِ وَقَالَ: ((يَا مُعَاذُ وَاللَّهِ إِنِّي لأُحِبُّكَ وَاللَّهِ إِنِّي لأُحِبُّكَ))‏.‏ فَقَالَ: ((أُوصِيكَ يَا مُعَاذُ لاَ تَدَعَنَّ فِي دُبُرِ كُلِّ صَلاَةٍ تَقُولُ: اللَّهُمَّ أَعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ وَشُكْرِكَ وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ))‏ ‏.‏ وَأَوْصَى بِذَلِكَ مُعَاذٌ الصُّنَابِحِيَّ وَأَوْصَى بِهِ الصُّنَابِحِيُّ أَبَا عَبْدِ الرَّحْمَنِ ‏.‏

 

Imepokelewa kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alimshika mkono wake akasema: ((Ee Mu’aadh!  Wa-Allaahi mimi nakupenda! Wa-Allaahi mimi nakupenda!)) Akasema: ((Nakuusia ee Mu’aadh usiache kusema katika kila baada ya Swalaah:

اللّهُـمَّ أَعِـنِّي عَلـى ذِكْـرِكَ وَشُكْـرِك وَحُسْـنِ عِبـادَتِـك

Allaahumma A’inniy ’alaa dhikrika washukrika wahusni ’Ibaadatika

 

Ee Allaah nisaidie juu Kukudhukuru, na kukushukuru na kukuabudu kwa uzuri utakikanao  

 

[Hadiyth ya Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (2/86), An-Nasaaiy (3/53) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/284)].

 

 

Fadhila za kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni nyingi mno, baadhi yake ni zifuatazo:

 

 

1-Ukimdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Naye Atakukumbuka kama Anavyosema:

 

فَاذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ وَاشْكُرُوا لِي وَلَا تَكْفُرُونِ﴿١٥٢﴾

Basi nidhukuruni na Mimi Nitakukumbukeni; na nishukuruni wala msinikufuru. [Al-Baqarah: 152]

 

 

 

2-Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni ‘ibaadah bora kabisa yenye daraja ya juu:

 

 

 عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((ألاَ أُنَبِّئُكُمْ بِخَيْرِ أَعْمَالِكُمْ، وَأَزْكَاهَا عِنْدَ مَلِيكِكُمْ، وَأَرْفَعِهَا فِي دَرَجَاتِكُمْ، وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ إِنْفَاقِ الذَّهَبِ وَالفِضَّةِ، وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ أَنْ تَلْقَوْا عَدُوَّكُمْ فَتَضْرِبُوا أَعْنَاقَهُمْ وَيَضْرِبُوا أَعْنَاقَكُمْ؟)) قَالُوا : بَلَى: قَالَ: ((ذِكْرُ اللَّهِ تَعَالَى)) رواه الترمذي. قَال الحاكم أبو عبد الله: إسناده صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abu Ad-Dardaa(رضي الله عنه)   ambaye amesema: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hivi niwaambieni khabari ya matendo yenu bora zaidi, na ambayo ni masafi mno mbele ya Rabb wenu, na ambayo ni ya juu mno katika daraja zenu, na ambayo ni bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na fedha, na ambayo ni bora kuliko kukutana na adui zenu mkawapiga shingo zao, nao wakakupigeni shingo zenu?))  Wakasema [Maswahaba]: Ndio. Akasema ((Ni kumdhukuru Allaah Ta’aalaa)). [At-Tirmidhiy na amesema Abu ‘Abdillaah: Isnaad yake ni Swahiyh]

 

 

3-Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni kuwa karibu Naye:

 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يَقُولُ اللَّهُ تَعَالَى: أَنَا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي وَأَنَا مَعَهُ إِذَا ذَكَرَنِي، فَإِنْ ذَكَرَنِي فِي نَفْسِهِ ذَكَرْتُهُ فِي نَفْسِي، وَإِنْ ذَكَرَنِي فِي مَلَإٍ ذَكَرْتُهُ فِي مَلَإٍ خَيْرٍ مِنْهُمْ، وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ بِشِبْرٍ تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ ذِرَاعًا،  وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ ذِرَاعًا تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ بَاعًا، وَإِنْ أَتَانِي يَمْشِي أَتَيْتُهُ هَرْوَلَةً)) متفق عليه

 Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ambaye amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alisema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: Mimi ni vile mja Wangu anavyonidhania. Niko pamoja naye anaponitaja. Anaponitaja katika nafsi yake, Ninamtaja katika nafsi Yangu, anaponitaja katika hadhara, Ninamtaja katika hadhara bora zaidi. Na anaponikaribia shibiri Ninamkaribia dhiraa, anaponikaribia dhiraa, Ninamkaribia pima, anaponijia kwa mwendo [wa kawaida] Ninamwendea mbio)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Madhara ya kutokumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla):

 

 

1-Kukaa katika kikao bila ya kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni kujichumia dhambi.

 

 

قال صلى الله عليه وسلم: ((مَا جَلَسَ قَوْمٌ مَجْلِسًا لَمْ يَذْكُرُوا اللَّهَ فِيهِ وَلَمْ يُصَلُّوا عَلَى نَبِيِّهِمْ إِلَّا كَانَ عَلَيْهِمْ تِرَةً فَإِنْ شَاءَ عَذَّبَهُمْ وَإِنْ شَاءَ غَفَرَ لَهُمْ))  

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Hapana watu wowote wale, wanaokaa kikao kisha wasimdhukuru Allaah humo, wala wasimswalie Nabiy wao ila watakuwa wana dhambi. Akipenda Atawaadhibu na Akipenda Atawaghufuria))  [Hadiyth ya Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)   - At-Tirmidhiy [3380] na taz. Swahiyh At-Tirmidhiy (3/140)] 

 

Na pia: 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَعَدَ مَقْعَدًا لَمْ يَذْكُرِ اللَّهَ فِيهِ، كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللَّهِ تِرَةٌ, وَمَنِ اضْطَجَعَ مَضْجَعًا لَمْ يَذْكُرِ اللَّهَ فِيهِ ، كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللَّهِ تِرَةٌ))

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Anayekaa kikao chochote kile asimdhukuru Allaah katika kikao hicho basi ana dhambi kutoka kwa Allaah, na anayelala sehemu yeyote ile kisha asimdhukuru Allaah wakati wakuinuka sehemu hiyo basi ana dhambi kwa Allaah)) [Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه)   - Abu Daawuwd (4/264) [4856] na wengineo na taz. Swahiyh Al-Jaami’ (5/342) [6477].

 

 

 

2-Kukaa katika kikao bila ya kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni kama mzoga wa punda na kuwa na majuto.

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَا مِنْ قَوْمٍ يَقُومُونَ مِنْ مَجْلِسٍ لَا يَذْكُرُونَ اللَّهَ فِيهِ إِلَّا قَامُوا عَنْ مِثْلِ جِيفَةِ حِمَارٍ وَكَانَ لَهُمْ حَسْرَةً))

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Hapana watu wowote wale wanaosimama katika kikao walichokaa, kisha wasimdhukuru  Allaah ila watakuwa wanasimama kama mzoga wa punda, na watakuja juta [kwa kutokumdhukuru Allaah])) [Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه)   - Abu Daawuwd (4/264) [4855], Ahmad (2/389) na taz Swahiyh Al-Jaami’ (5/176) [5750].

 

 

 

3-Asiyemdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) ni kama mtu aliyekufa.

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَثَـــلُ الـــذي يَـــذكُرُ ربَّـــهُ وَالـــذي لا يـــذكُرُهُ، مَثَـــل الحـــيِّ والمَيِّــتِ))

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Mfano wa anayemdhukuru  Mola wake na asiyemdhukuru ni mfano wa aliye hai na maiti)) [Hadiyth ya Abu Muwsaa Al-Ash’ariyy(رضي الله عنه)   -Al-Bukhaariy  pamoja Al-Fat-h (11/208) au namba [6407] 

 

 

 

Swahaba ‘Abdullaah Ibn ‘Amru Ibn Al-‘Aasw - Swahaba aliyekuwa akimdhukuru sana Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

Ni Swahaba ambaye aliingia katika Uislamu kabla ya baba yake tokea siku aliyochukua kiapo cha utiifu.   Alikuwa mwenye moyo uliojaa nuru ya twaa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

   

Alitumia wakati wote katika kusoma na kuifahamu Qur-aan ili utakapofika wakati wa kumalizika wahyi wote awe ameshaihifadhi yote. Na hakuisoma tu kwa ajili ya uwezo wa kuihifadhi, bali aliisoma na kufuata amri zake kama Maswahaba wengineo.

 

‘Abdullah ibn ‘Amru ibn Al-‘Aasw alikuwa mwenye taqwa ya hali ya juu na mtekelezaji ‘ibaadah kwa wingi.

 

Katika vita dhidi ya maadui wa Kiislamu alionekana katika mstari wa mbele kabisa akitamani kufariki kama shahidi. Na alikuwa akionekana daima Msikitini, na alikuwa mwenye kupenda kufunga swawm na kuswali Swalaah za usiku. Ulimi wake ulikuwa ni wa kila mara kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla). Alikuwa akikhitimisha Qur-aan kila siku moja.

 

Hali yake hii ilimfanya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amnasihi apunguze ‘ibaadah ili aweze kutekeleza mengineyo yenye haki naye.   

 

Hadiyth yake mashuhuri imerekodiwa na Maimaam sita wa Hadiyth. 

 

 

  "كنت أصوم الدهر، وأقرأ القرآن كل ليلة، قالفإما ذكرت لرسـول الله  صلى الله عليه وسلم ، وإما أرسل لي، فأتيته، فقال: "ألم أُخبر أنك تصوم الدهر وتقرأ القرآن كل لـيـلـة ؟" فقلت: بلى يا نبي الله؛ ولم أرد إلا الخـيـر، قال: "فـإن بحـسـبك أن تصوم من كل شهر ثلاثة أيام... ، ثم قال: "واقرأ القرآن في كل شهر"، قال: قلت: يا نبي الله: إني أطيق أفضل من ذلك، قال: "فاقرأه في سـبـع، ولا تـزد عـلــى ذلك، فإن لزوجك عليك حقاً، ولزورك عليك حقاً، ولجسدك عليك حقاً، قال: فشددت؛ فشدد علي، قال: وقال لي النبيصلى الله عليه وسلم: "لعلك يطول بك العـمــر"، فصرتُ إلى الذي قال لي النبيصلى الله عليه وسلم ، فلما كبرت وددت أني قبلت رخصة النبي صلى الله عليه وسلم.

“Nilikuwa nikifunga mwaka mzima, na nikisoma Qur-aan kila usiku. Alipojulishwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniita kwake nikaenda. Akasema: ((Nimesikia kwamba unafunga mwaka mzima na unasoma (unakhitimisha) Qur-aan kila usiku?)) Nikasema: Ndio ee Rasuli wa Allaah. Wala sitaki lolote ila kheri tu. Akasema: ((Inakutosheleza ukifunga katika kila mwezi siku tatu…)) Kisha akasema: ((Na usome Qur-aan (ukhitimishe) kila mwezi)). Akasema: Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah, mimi hakika naweza kufanya vizuri zaidi ya hivyo. Akasema: ((Basi soma katika siku saba na usizidishe juu ya hivyo, kwani mke wako ana haki na wewe, na wageni wako wana haki kwako, na mwili wako una haki kwako)). Akasema: Kila nikimkazania (nizidishe ‘ibaadah) alikuwa akinikazania (nipunguze). Akasema: Akaniambia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Huenda umri ukawa mrefu kwako)) Nikaendeleza (‘ibaadah) kama alivyoniambia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Nilipokuwa mkubwa kiumri nilipendelea kufuata rukhsa aliyonipa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

 

 

Share

11-Sifa Kumi Na Fadhila Zake: Maghfirah Na Ujira Adhimu Baada Ya Kuzichuma Sifa Kumi

 

Sifa Kumi Na Fadhila Zake

 

11-Maghfirah Na Ujira Adhimu Baada Ya Kuzichuma Sifa Kumi

 

 

 

Aayah kamili kuhusu sifa kumi ni: 

 

 

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ وَالْحَافِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَالْحَافِظَاتِ وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

Hakika Waislamu wanaume na wanawake, na Waumini wanaume na wanawake, na watiifu wanaume na wanawake, na wasemao kweli wanaume na wanawake, na wanaosubiri wanaume na wanawake, na wanyenyekevu wanaume na wanawake, na watoao swadaqah wanaume na wanawake, na wafungao Swawm wanaume na wanawake, wanaojihifadhi tupu zao wanaume na wanawake, na wanaomdhukuru Allaah kwa wingi wanaume na wanawake; Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu.  [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Baada ya kutajwa sifa kumi katika Aayah tukufu, na pindi zikitekelezwa, Allaah ('Azza wa Jalla) Ameahidi kuwaghufuria madhambi waja Wake na kuwalipa ujira mkubwa, mtukufu. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu. [Al-Ahzaab: 35]

 

 

Vile vile Anasema katika Aayah nyingine:

 

 

وَعَدَ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ۙ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ عَظِيمٌ ﴿٩﴾

Allaah Amewaahidi wale walioamini na wakatenda mema; watapata maghfirah na ujira adhimu. [Al-Maaidah: 9]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni mwingi wa kughufuria madhambi ya waja Wake, kama ilivyothibiti katika Qur-aan:

 

وَإِنِّي لَغَفَّارٌ لِّمَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا ثُمَّ اهْتَدَىٰ ﴿٨٢﴾

Na hakika Mimi bila shaka ni Mwingi mno wa kughufuria kwa anayetubia na akaamini na akatenda mema kisha akaendelea kuongoka.  [Twaaha: 82]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَهُوَ الَّذِي يَقْبَلُ التَّوْبَةَ عَنْ عِبَادِهِ وَيَعْفُو عَنِ السَّيِّئَاتِ

Naye Ndiye Ambaye Anapokea tawbah kutoka kwa waja Wake, na Anasamehe maovu [Ash-Shuwraa: 25]

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَمَن يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ يَسْتَغْفِرِ اللَّـهَ يَجِدِ اللَّـهَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١١٠﴾

Na atakayetenda ovu au akajidhulumu nafsi yake; kisha akamwomba Allaah maghfirah; atamkuta Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa: 110]

 

 

Na Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عن أَنَسُ بْنُ مَالِكٍ قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((قَالَ اللَّهُ تَبَارَكَ وَتَعَالَى يَا ابْنَ آدَمَ،  إِنَّكَ مَا دَعَوْتَنِي وَرَجَوْتَنِي غَفَرْتُ لَكَ عَلَى مَا كَانَ فِيكَ وَلَا أُبَالِي، يَا ابْنَ آدَمَ لَوْ بَلَغَتْ ذُنُوبُكَ عَنَانَ السَّمَاءِ ثُمَّ اسْتَغْفَرْتَنِي غَفَرْتُ لَكَ وَلَا أُبَالِي، يَا ابْنَ آدَمَ إِنَّكَ لَوْ أَتَيْتَنِي بِقُرَابِ الْأَرْضِ خَطَايَا ثُمَّ لَقِيتَنِي لَا تُشْرِكُ بِي شَيْئًا لَأَتَيْتُكَ بِقُرَابِهَا مَغْفِرَةً))  أخرجه الترمذي وحسنه الألباني في الصحيحة  

Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Allaah  Tabaaraka wa Ta’aalaa  Amesema: Ee bin-Aadam! Hakika ukiniomba na ukanitaraji (kwa malipo) Nitakughufuria yale yote uliyonayo na wala Sijali, Ee bin-Aadam! Lau zingefikia dhambi zako ukubwa wa mbingu, kisha ukaniomba maghfirah, Ningekughufuria bila ya kujali (kiasi cha madhambi uliyoyafanya). Ee bin-Aadam! Hakika ungenijia na madhambi yakaribiayo ukubwa wa ardhi, kisha ukakutana nami na hali hukunishirikisha chochote, basi Nami Nitakujia na maghfirah yanayolinga nayo.” [At-Tirmidhiy na Shaykh Al-Albaaniy kaipa daraja ya Hasan]

 

Vile vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameahidi kutuingiza katika Jannah  kwa Rahmah Yake pindi tukiifanyia kazi kwa kutenda mema.  Basi ni kujitahidi kuchuma sifa kama hizo kumi ambazo zinahitaji azimio dhubuti, jitihada na subira, na matarajio. Ndio maana Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُبَوِّئَنَّهُم مِّنَ الْجَنَّةِ غُرَفًا تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ نِعْمَ أَجْرُ الْعَامِلِينَ﴿٥٨﴾

Na wale walioamini na wakatenda mema, bila shaka Tutawawekea makazi ya ghorofa katika Jannah, yapitayo chini yake mito, ni wenye kudumu humo. Uzuri ulioje ujira wa watendao.

 

 

الَّذِينَ صَبَرُوا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ ﴿٥٩﴾

Ambao walisubiri na kwa Rabb wao wanatawakali. [Al-‘Ankabuwt: 58-59]

 

Neema za huko Peponi zimetajwa katika Aayah nyingi za Qur-aan na katika Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), miongoni mwazo ni:  

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ﴿٤١﴾

Hakika wenye taqwa wamo katika vivuli na chemchemu.

 

 

وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ﴿٤٢﴾

Na matunda katika yale wanayoyatamani.

 

 

كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ﴿٤٣﴾

(Wataambiwa): “Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda.”

 

 

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ﴿٤٤﴾

Hakika hivyo ndivyo Tunavyowalipa wafanyao ihsani. [Al-Mursalaat: 41-44]

 

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 أُولَـٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ ﴿٤١﴾

Hao watapata riziki maalumu.

 

 

فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ ﴿٤٢﴾

Matunda; nao ni wenye kukirimiwa

 

 

فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ﴿٤٣﴾

Katika Jannaat za neema.

 

 

عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ ﴿٤٤﴾

Juu ya makochi ya enzi wakikabiliana.

 

 

يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ ﴿٤٥﴾

Wanazungushiwa gilasi za mvinyo kutoka chemchemu.

 

 

بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ ﴿٤٦﴾

Nyeupe, ya ladha kwa wanywaji.

 

 

لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ ﴿٤٧﴾

Hamna humo madhara yoyote na wala wao kwayo hawataleweshwa.

 

 

وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ ﴿٤٨﴾

Na watakuwa nao wanawake wenye staha wanaoinamisha macho, wenye macho mapana mazuri ya kuvutia. 

 

 

كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ ﴿٤٩﴾

 (Wanyororo, watakasifu) kama kwamba mayai yaliyohifadhiwa. [Asw-Swaafaat: 41-49]

 

 

Hiyo ni ahadi ya Allaah ('Azza wa Jalla) ambayo hakika Yeye Haendi kinyume nayo kama Anavyosema:

 

 لَـٰكِنِ الَّذِينَ اتَّقَوْا رَبَّهُمْ لَهُمْ غُرَفٌ مِّن فَوْقِهَا غُرَفٌ مَّبْنِيَّةٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ۖ وَعْدَ اللَّـهِ ۖ لَا يُخْلِفُ اللَّـهُ الْمِيعَادَ﴿٢٠﴾

 Lakini wale waliomcha Rabb wao, watapata maghorofa yaliyojengwa juu yake maghorofa, yanapita chini yake mito.  Ni ahadi ya Allaah. Allaah Hakhalifu miadi. [Az-Zumar: 20]

 

 

Kisa Cha Swahaba 'Amru bin Al-Jamuw’ aliyetamani Jannah:

 

 

'Amru bin Al-Jamuw’ (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikuwa kilema. Alikuwa na watoto wa kiume wanne ambao walikuwa wakihudhuria vita mbali mbali.

Ulipofika wakati wa vita vya Uhud, 'Amru (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alitamani kupigana vita hivyo lakini watu walimzuia kwa vile ni kilema wakimwambia: "Wewe umeruhusiwa kutokupigana vita kutokana na hali yako, kwa hiyo huna haja ya kwenda vitani." Lakini yeye akawajibu: "Inasikitisha kuwa watoto wangu wapate Jannah nami nisiipate."

 

wake pia alitaka sana mumewe apate fadhila ya kufariki katika hali ya Shahidi,  hivyo akamshikilia aende hivyo hivyo japokuwa   ni kilema, akimwambia: "Sioni kama  udhuru huo wako utakuzuia kwenda kupigana vita, ila labda naona kama una khofu tu ya kwenda vitani!”

 

Aliposikia hivyo 'Amru (Radhwiya Allaahu 'anhu) alijitayarisha kwenda vitani akaelekea Qiblah na kuomba: "Ee Allah Usinirudishe kwa familia yangu tena!"

 

 

Imesemekana kwamba alikwenda vitani na alionekana akipigana na huku akisema kwa fakhari: "Naapa kwa Allaah, hakika mimi naitamani Jannah!”

Mtoto wake alikuwa akimfuatilia nyuma yake. Wakipigana hadi wote wakauliwa.

 

 

Mke wake aliposikia kuwa mumewe na mtoto wake wamefariki, alituma ngamia ili wachukuliwe miili yao. Imesemekana kwamba miili yao ilipopandishwa juu ya ngamia na kuondoka, ngamia huyo aligoma kusimama. Alipolazimisha kusimama aligoma kuelekea Madiynah bali alirudia kuelekea jabali la Uhud. Mkewe alipoulizwa kuhusu hilo, akasema kuwa 'Amru (Radhwiya Allaahu ‘anhu) aliomba du'aa kuwa asirudishwe kwao. Na ndio ikawa sababu ya kugoma ngamia kurudi Madiynah.

 

 

 

 

 

Share