101 - Al-Qaari-'ah

 

  الْقَارِعَة

 

101-Al-Qaari’ah

 

101-Al-Qaari’ah: Utangulizi Wa Suwrah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

الْقَارِعَةُ ﴿١﴾

1. Al-Qaari’ah (janga kuu linalogonga).

 

 

مَا الْقَارِعَةُ ﴿٢﴾

2. Ni nini hiyo Al-Qaari’ah?

 

 

وَمَا أَدْرَاكَ مَا الْقَارِعَةُ ﴿٣﴾

3. Na nini kitakachokujulisha ni nini hiyo Al-Qaari’ah?

 

 

يَوْمَ يَكُونُ النَّاسُ كَالْفَرَاشِ الْمَبْثُوثِ ﴿٤﴾

4. Siku watakapokuwa watu kama vipepeo vilivyotawanyika.

 

 

 

وَتَكُونُ الْجِبَالُ كَالْعِهْنِ الْمَنفُوشِ ﴿٥﴾

5. Na majabali yatakuwa kama sufi iliyochambuliwa.

 

 

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ ﴿٦﴾

6. Basi yule itakayekuwa mizani yake nzito.

 

 

 

فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ ﴿٧﴾

7.  Basi huyo atakuwa katika maisha ya kuridhisha.

 

 

وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ ﴿٨﴾

8. Na yule itakayekuwa mizani yake khafifu. 

 

 

فَأُمُّهُ هَاوِيَةٌ ﴿٩﴾

9. Basi makazi yake ni Haawiyah.

 

 

وَمَا أَدْرَاكَ مَا هِيَهْ ﴿١٠﴾

10. Na nini kitakachokujulisha ni nini hiyo Haawiyah?

 

 

نَارٌ حَامِيَةٌ ﴿١١﴾

11. Ni moto uwakao vikali mno!

 

 

 

 

Share