Hiswnul-Muslim: Du’aa Na Adhkaar Kusoma Na Kwa Kusikiliza (Toleo Lilohaririwa)

 

  

Share

Hiwsnul-Muslim: Utangulizi Wa Alhidaaya

Hiwsnul Muslim (Toleo Lilohaririwa)

Utangulizi Wa Alhidaaya

www.alhidaaya.com

 

 

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمن الرَّحيم

 

Himdi Anastahiki Allaah (سبحانه وتعالى ) Rabb  wa walimwengu, Rahmah na amani zimshukie kipenzi chetu Nabiy Muhammad (صلى الله عليه  وآله وسلم ) na ahli zake, na Swahaba zake (رضي الله عنهم)  na wote waliotangulia kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Tunamshukuru Allaah (سبحانه وتعالى) kutuwezesha kukifanyia kazi upya kitabu cha Hiswnul-Muslim ili kizidi kuleta manufaa kwa jamii yetu. Tumeonelea kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kukifanyia kazi upya kwa kufanya yafuatayo:

 

 

1.  Kuweka Aayah na Suwrah zote kamilifu ili  imtosheleze msomaji  kutimiza nyiradi zake zote. Mfano Suwrah ya Aliyf Miym As-Sajdah, Al-Mulk, Al-Ikhlaasw, Al-Mu’awwidhataan n.k., ambazo anatakiwa Muislamu azisome kabla ya kulala.

 

 

2.  Kutaja Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وسلم) kwa ukamilifu katika baadhi ya nyiradi au du’aa yenyewe na pia katika marejeo chini ya ukurasa pamoja na kuweka tarjama yake.

 

 

3.  Kuweka marejeo bayana ya Hadiyth; Raawiy (msimulizi) na Muhaddithuwna (wakusanyaji wa Hadiyth) kwa kunukuu marejeo yao. Tumebainisha marejeo ya mjalada na ukurasa katika mabano ya (   ) na tumebainisha nambari ya Hadiyth katika mabano ya [   ]. Baadhi ya sehemu tumeweza kuongezea marejeo zaidi ya yale yaliyotajwa katika kitabu cha asili.

 

 

4.   Kuweka sauti za Adhkaar na Du’aa hizo pamoja na matamshi yake ili msomaji aliye na udhaifu wa kusoma Kiarabu aweze kusikiliza na kuweza kufuatilia kutamka vizuri Adhkaar na Du’aa hizo.

 

 

5.  Kubainisha Ahaadiyth na Adhkaar ambazo baadhi ya ‘Ulamaa wameona kuwa hazijathibiti hivyo ni dhaifu, na badala yake kutaja ambazo zilizo Swahiyh.

 

 

6.   Kubainisha nyiradi au du’aa ambazo si za Nabiy (صلى الله عليه وسلم) bali ni Athar (za Salafus-Swaalih).   

 

 

7.  Kuzitaja Adhkaar au Du’aa  (khasa zile ambazo aghlabu hutumika kusomwa), kwa kubadilisha sarufi mfano; inapokuwa ni mwanamke au hali ya wingi, mfano Du’aa ya maiti, au Du’aa Ukiwa Na Wahka Na Huzuni  (namba 120), ambayo mwanamke anapaswa aseme:

 

أللَّهُمَّ إنِّي أَمَتُك، بِنْتُ عَبْدِك، بنتُ أَمَتِك

Allaahumma inniy amatuka, bintu ’abdika, bintu amatika ... 

 

Ee Allaah, hakika mimi mja Wako mwanamke, binti wa mja wako, binti wa mja Wako mwanamke...

 

Pia mfano wa du’aa namba (79) ya Sayyidul-Istighfaar iliyopo katika Nyiradi za Asubuhi Na Jioni ambayo inataja kwa kumkusudia mwanamume, hivyo mwanamke aseme:

 

اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا أَمَتُكَ

Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illaa Anta Khalaqtaniy wa ana amatuka...

 

Ee Allaah, Wewe ni Rabb wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja Wako mwanamke...

 

Na kadhaalika .

 

 

8. Kumwekea msomaji asiyefahamu lugha ya Kiarabu kwa kutaja du’aa au nyiradi kamilifu kutokana na kubadilika wakati mfano du’aa namba  (80) katika  Nyiradi za Asubuhi Na Jioni pale inapotakiwa kubadilisha neno la

أَصْبَحْنا

Aswbahnaa (Tumeingia asubuhi)

 

Liwe badala yake:     

أَمْسَيْنا

Amsaynaa (Tumeingia jioni)

 

 

9. Kuipa maana sahihi baadhi ya misamiati khasa ambazo zinahusiana na mas-ala ya ‘Aqiydah.

 

 

10. Kufanya ulinganifu wa misamiati na kufafanua zaidi baadhi ya maana.

 

 

11.  Kutanabahisha makosa yanayotendwa na baadhi ya watu katika kutamka yasiyopasa ilhali yapasayo kutamkwa yamo katika kitabu hiki. Pia, kuongezea faida na fafanuzi ya baadhi ya maneno na kuweka tanbihi kadhaa.

           

 

Kwa ujumla tumejaribu kadiri Alivyotuwezesha Allaah (سبحانه وتعالى) kukifanyia kazi upya kwa kukiboresha ili kitoe faida kwa wingi kwa kila upande. 

 

 

Marekebisho yetu hayo, hatumaanishi kwamba tutakuwa kamilifu katika kukiweka sawa kitabu hiki, kwani ukamilifu pekee ni wa Allaah (سبحانه وتعالى).  Mwandishi wa Kitabu hiki amechukua juhudi kubwa kabisa kuaandaa kitabu kama hiki. Tunamuombea Allaah (سبحانه وتعالى) Amlipe malipo mazito kabisa katika Miyzaan yake ya hasanaat. Tunaomba vilevile thawabu ziwafikie pia kila atakayekifanyia kazi na kila atakayekitumia kitabu hiki.

 

 

Tunawaomba wasomaji pindi watakapoona kosa lolote lile watujulishe kupitia webmaster@alhidaaya.com

 

 

Tunamuomba Allaah (سبحانه وتعالى) Atusamehe makosa yetu na Atutaqabalie hii kazi iwe kwa ajili ya kupata Radhi Zake Pekee na Atulipe malipo mema kwayo.

 

وبِالله التَّوْفيق  وَصَلَّى اللهُ وَسَلَّمَ وَبَارَكَ عَلى نَبِيِّنَا مُحَمَّدٍ وَعَلى آلِهِ وَأَصْحَابِهِ أَجْمَعِينَ

 

Alhidaaya

 

 

 

Share

Hiwsnul-Muslim: Utangulizi Wa Mwandishi

Hiwsnul Muslim

Utangulizi Wa Mwandishi

www.alhidaaya.com

 

 

 

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمن الرَّحيم

 

Hakika Himdi ni za Allaah, tunamsifu, tunamuomba msaada na tunamuomba maghfirah, tunajikinga kwa Allaah kutokana na shari za nafsi zetu, na maovu ya matendo yetu. Anayemhidi Allaah hapana wa kumpoteza, na Anayempoteza, hapana wa kumhidi. Nashuhudia kwamba, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali ya kuwa Peke Yake, Hana mshirika, na nashuhudia kwamba Muhammad ni mja Wake na ni Rasuli Wake. Rahmah na amani zimfikie pamoja na ahli zake na Maswahaba zake na wanaowafuata hao kwa wema mpaka Siku ya malipo na Amsalimishe kwa amani nyingi.

 

 

Baada ya yaliyotangulia huu ni mukhtasari wa kitabu changu kiitwacho Hiswnul-Muslim min Adhkaaril-Kitaabi was-Sunnah.

 

Ninamuomba Allaah عزَّوجلَّ kwa Majina Yake mazuri, na Sifa Zake zilizotukuka, Ajaaliye kazi hii yenye ikhlaasw kwa ajili ya Radhi Zake, na Aninufaishe kwa hayo katika uhai wangu huu, na baada ya kufa, na Amnufaishe atakayekisoma, kukichapisha, au aliyekuwa ni sababu ya kukisambaza, hakika Yeye Allaah سبحانه Ndiye  Mlinzi na Muweza.

 

Rahmah na amani zimfikie Nabiy wetu  Muhammad na ahli zake na Maswahaba wake na wanaowafuata hao, kwa wema mpaka siku ya malipo.

 

 

 

Share

Hiswnul-Muslim: Fadhila Za Kumdhukuru Allaah

Hiswnul-Muslim

Fadhila Za Kumdhukuru Allaah

www.alhidaaya.com

 

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

فَاذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ وَاشْكُرُوا لِي وَلَا تَكْفُرُونِ ﴿١٥٢﴾

((Basi nidhukuruni na Mimi Nitakukumbukeni; na nishukuruni wala msinikufuru.))[1]  

 

 

 

 Na Anasema:

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾ وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

((Enyi mlioamini! Mdhukuruni Allaah kwa dhikri ya wingi. Na Msabbihini asubuhi na jioni))[2]   

 

 

Na Anasema:

   وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

((na Wanaume wanaomdhukuru Allaah kwa wingi na Wanawake wanaomdhukuru Allaah (kwa wingi); Allaah Amewaandalia maghfirah na ujira adhimu))[3]  

 

 

Na Anasema:

 

 وَاذْكُررَّبَّكَ فِي نَفْسِكَ تَضَرُّعًا وَخِيفَةً وَدُونَ الْجَهْرِمِنَ الْقَوْلِ بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ الْغَافِلِينَ ﴿٢٠٥﴾  

((Na mdhukuru Rabb wako katika nafsi yako kwa unyenyekevu na kwa khofu na si kwa jahara (kunyanyua sauti) katika kauli asubuhi na jioni; na wala usiwe miongoni mwa walioghafilika.))[4] 

 

 

 وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَثَـــلُ الـــذي يَـــذكُرُ ربَّـــهُ وَالـــذي لا يـــذكُرُهُ، مَثَـــل الحـــيِّ والمَيِّــتِ))

Na amesema  (صلى الله عليه وسلم): ((Mfano wa anayemdhukuru Rabb wake na asiyemdhukuru ni mfano wa aliye hai na maiti))[5]

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((أَلَا أُنَبِّئُكُمْ بِخَيْرِ أَعْمَالِكُمْ وَأَزْكَاهَا عِنْدَ مَلِيكِكُمْ وَأَرْفَعِهَا فِي دَرَجَاتِكُمْ وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ إِنْفَاقِ الذَّهَبِ وَالْوَرِقِ وَخَيْرٌ لَكُمْ مِنْ أَنْ تَلْقَوْا عَدُوَّكُمْ فَتَضْرِبُوا أَعْنَاقَهُمْ وَيَضْرِبُوا أَعْنَاقَكُمْ؟)) قَالُوا: بَلَى. قَالَ: ((ذِكْرُ اللَّهِ تَعَالَى))

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Hivi niwaambieni khabari ya matendo yenu bora, na ambayo ni masafi mno, mbele ya Rabb wenu, na ambayo ni ya juu mno katika daraja zenu, na ambayo ni bora kwenu kuliko kutoa dhahabu na fedha, na ambayo ni bora kuliko kukutana na adui zenu, mkawapiga shingo zao, nao wakakupigeni shingo zenu?)) Wakasema: [Maswahaba]: Ndio. Akasema: ((Ni kumdhukuru Allaah Ta’aalaa))[6]      

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((يَقُولُ اللَّهُ تَعَالَى أَنَا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي وَأَنَا مَعَهُ إِذَا ذَكَرَنِي فَإِنْ ذَكَرَنِي فِي نَفْسِهِ ذَكَرْتُهُ فِي نَفْسِي وَإِنْ ذَكَرَنِي فِي مَلَإٍ ذَكَرْتُهُ فِي مَلَإٍ خَيْرٍ مِنْهُمْ وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ بِشِبْرٍ تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ ذِرَاعًا وَإِنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ ذِرَاعًا تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ بَاعًا وَإِنْ أَتَانِي يَمْشِي أَتَيْتُهُ هَرْوَلَةً)) البخاري، مسلم، الترمذي و ابن ماجه

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Allaah Ta’aalaa Anasema: Mimi ni vile mja Wangu anavyonidhania. Niko pamoja naye anaponikumbuka. Anaponikumbuka katika nafsi yake, Nitamkumbuka katika nafsi Yangu, anapokumbuka katika hadhara, Nitamkumbuka katika hadhara bora zaidi. Na anaponikaribia shibiri Ninamkaribia dhiraa; anaponikaribia dhiraa, Ninamkaribia pima, anaponijia kwa mwendo (wa kawaida) ninamwendea mbio))[7] 

 

 

وعن عبد الله بن بسرٍ رضي الله عنهُ أنّ رجُلًا قال: يَا رَسُولَ اللهِ، إِنَّ شَرَائِعَ الإِسْلَامِ قَدْ كَثُرَتْ عَلَيَّ، فَأَخْبِرْنِي بِشَيْءٍ أَتَشَبَّثُ بِهِ. قَالَ: ((لَا يَزَالُ لِسَانُكَ رَطْبًا مِنْ ذِكْرِ الله))  

Imepokewa kutoka kwa kwa ‘Abdullaah Bin Busr  (رضي الله عنه)kwamba mtu mmoja alisema: Ee Rasuli wa Allaah! ‘Ibaadah za Dini zimekuwa nyingi kwangu, basi nieleze kitu ambacho nitaweza kudumu nacho. Akasema: ((Ulimi wako utaendelea kuwa laini kwa kumdhukuru Allaah))[8] 

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَرَأَ حَرْفًا مِنْ كِتَابِ اللَّهِ فَلَهُ بِهِ حَسَنَةٌ وَالْحَسَنَةُ بِعَشْرِ أَمْثَالِهَا لَا أَقُولُ الم حَرْفٌ وَلَكِنْ أَلِفٌ حَرْفٌ وَلَامٌ حَرْفٌ وَمِيمٌ حَرْفٌ))

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Anayesoma herufi moja katika kitabu cha Allaah basi anapata thawabu za jema moja na jema ni kwa mema kumi, sisemi kuwa ‘Alif Laam Miym’ ni herufi moja lakini ni kwamba ‘Alif’ peke yake ni herufi moja, na ‘Laam’ ni herufi, na ‘Miym’ ni herufi))[9]

 

 

وَعَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ قَالَ خَرَجَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَنَحْنُ فِي الصُّفَّةِ فَقَالَ: ((أَيُّكُمْ يُحِبُّ أَنْ يَغْدُوَ كُلَّ يَوْمٍ إِلَى بُطْحَانَ أَوْ إِلَى الْعَقِيقِ فَيَأْتِيَ مِنْهُ بِنَاقَتَيْنِ كَوْمَاوَيْنِ فِي غَيْرِ إِثْمٍ وَلَا قَطْعِ رَحِمٍ؟)) فَقُلْنَا يَا رَسُولَ اللَّهِ نُحِبُّ ذَلِكَ قَالَ: ((أَفَلَا يَغْدُو أَحَدُكُمْ إِلَى الْمَسْجِدِ فَيَعْلَمُ أَوْ يَقْرَأُ آيَتَيْنِ مِنْ كِتَابِ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ خَيْرٌ لَهُ مِنْ نَاقَتَيْنِ وَثَلَاثٌ خَيْرٌ لَهُ مِنْ ثَلَاثٍ وَأَرْبَعٌ خَيْرٌ لَهُ مِنْ أَرْبَعٍ وَمِنْ أَعْدَادِهِنَّ مِنْ الْإِبِلِ))

Na imepokewa kutoka kwa 'Uqbah bin 'Aamir(رضي الله عنه)   ambaye amesema, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alitujia tukiwa katika Swuffah akauliza: ((Kuna yeyote miongoni mwenu anayetaka kwenda  soko la Butw-haan au Al-'Aqiyq na akapata humo ngamia wawili (wa thamani kabisa wa kike) bila ya kutenda dhambi au kukata undugu?)) Tukajibu kwamba sote tunapenda kufanya na kupata hivyo. Kisha akasema: ((Basi aende mmoja wenu Msikitini akajifunze au asome Aayah mbili katika kitabu cha Allaah عزوجل basi akifanya hivyo ni bora kuliko ngamia (wa thamani kabisa wa kike).  Na Aayah tatu ni bora kuliko ngamia watatu, na Aayah nne ni bora kuliko ngamia wanne, na mfano wa hivyo hivyo wa Aayah kwa ngamia))[10]

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَعَدَ مَقْعَدًا لَمْ يَذْكُرِ اللَّهَ فِيهِ، كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللَّهِ تِرَةٌ, وَمَنِ اضْطَجَعَ مَضْجَعًا لَمْ يَذْكُرِ اللَّهَ فِيهِ ، كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللَّهِ تِرَةٌ))

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Anayekaa kikao chochote kile asimdhukuru Allaah katika kikao hicho basi ana dhambi kutoka kwa Allaah, na anayelala sehemu yeyote ile kisha asimdhukuru Allaah wakati wakuinuka sehemu hiyo basi ana dhambi kwa Allaah))[11] 

 

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَا جَلَسَ قَوْمٌ مَجْلِسًا لَمْ يَذْكُرُوا اللَّهَ فِيهِ وَلَمْ يُصَلُّوا عَلَى نَبِيِّهِمْ إِلَّا كَانَ عَلَيْهِمْ تِرَةً فَإِنْ شَاءَ عَذَّبَهُمْ وَإِنْ شَاءَ غَفَرَ لَهُمْ))  

Na amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Hapana watu wowote wale, wanaokaa kikao kisha wasimdhukuru Allaah humo, wala wasimswalie Nabiy wao ila watakuwa wana dhambi. Akipenda Atawaadhibu na Akipenda Atawaghufuria))[12]  

 

وقال صلى الله عليه وسلم: ((مَا مِنْ قَوْمٍ يَقُومُونَ مِنْ مَجْلِسٍ لَا يَذْكُرُونَ اللَّهَ فِيهِ إِلَّا قَامُوا عَنْ مِثْلِ جِيفَةِ حِمَارٍ وَكَانَ لَهُمْ حَسْرَةً))

Na amesema  (صلى الله عليه وسلم): ((Hapana watu wowote wale wanaosimama katika kikao walichokaa, kisha wasimdhukuru Allaah ila watakuwa wanasimama kama mzoga wa punda, na watakuja juta [kwa kutokumdhukuru Allaah]))[13]

 

 

 

 

[1] Al-Baqarah (2:152).

[2] Al-Ahzaab (33:41-42).

[3] Al-Ahzaab (33:35).

[4] Al-A’raaf (7:205).

[5] Hadiyth ya Abu Muwsaa Al-Ash’ariyy(رضي الله عنه -Al-Bukhaariy  pamoja Al-Fat-h (11/208) au namba [6407] na Muslim kwa tamshi kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:  

 

((مَثَلُ البَيْتِ الذي يُذكَرُ اللهُ فيه، والبيت الذي لا يذكرُ الله فيه مَثَلُ الحيِّ والميِّت))

((Mfano wa nyumba ambayo Allaah Anatajwa na ambayo hatajwi humo ni kama aliye hai na maiti)) (1-539) [779].

[6] Hadiyth ya ‘Abu Dardaa ‘Uwaymir bin ‘Aamir (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/459) [3377], Ibn Maajah (2/1246) [3790], na angalia Swahiyh Ibn Maajah (2/316) na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/139).

[7] Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه - Al-Bukhaariy (8/171) [7405], Muslim (4/2061) [2675] na tamshi la Al-Bukhaariy.

[8] At-Tirmidhiy (5/458) [3375], Ibn Maajah (2/1246) [3793], na taz. Swahiyh At-Tirmidhiy (3/139) na Swahiyh Ibn Maajah (2/317).

[9] Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd - (رضي الله عنه)  - At-Tirmidhiy (5/175) [2910] na taz. Swahiyh At-Tirmidhiy (3/9) na Swahiyh Al-Jaami’ Asw-Swaghiyr (5/340) [6469].

[10] Muslim (1/553) [803].

[11] Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه - Abu Daawuwd (4/264) [4856] na wengineo na taz. Swahiyh Al-Jaami’ (5/342) [6477].

[12] Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه - At-Tirmidhiy [3380] na taz. Swahiyh At-Tirmidhiy (3/140).

[13] Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه - Abu Daawuwd (4/264) [4855], Ahmad (2/389) na taz Swahiyh Al-Jaami’ (5/176) [5750].

Share

001-Hiswnul-Muslim: Kuamka Kutoka Usingizini

 

Hiswnul-Muslim

001-Kuamka Kutoka Usingizini

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[1]

الحَمْـدُ لِلّهِ الّذي أَحْـيانا بَعْـدَ ما أَماتَـنا وَإليه النُّـشور

 

AlhamduliLLaahil-LLadhiy Ahyaanaa ba’da maa amaatana wa Ilayhin-nushuwr

 

Himdi Anastahiki Allaah Ambaye Ametupa uhai baada ya kutufisha na ni Kwake tu kufufuliwa[1]

 

 

 

[2]

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحْـدَهُ لا شَـريكَ له، لهُ المُلـكُ ولهُ الحَمـد، وهوَ على كلّ شيءٍ قدير، سُـبْحانَ اللهِ، والحمْـدُ لله، ولا إلهَ إلاّ اللهُ واللهُ أكبَر، وَلا حَولَ وَلا قوّة إلاّ باللّهِ العليّ العظيم، رَبِّ اغْفرْ لي

 

Laa ilaaha illaAllaahu Wahdahu laa shariyka Lah, Lahul Mulku walahul Hamdu, wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr. Subhaana-Allaah, wal Hamdu liLLaah, walaa ilaaha illaAllaahu waAllaahu Akbar, walaa hawla walaa quwwata illa biLLaahil ‘Aliyyul ‘Adhwiym. Rabbighfir-liy

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na hali ya kuwa Peke Yake Hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza), Ametakasika Allaah na Himdi ni Zake, na hapana mwabudiwa wa haki  ila ni Allaah, na Allaah ni Mkubwa, na hapana uwezo wala nguvu, isipokuwa vyote vinatokana na Allaah Aliye juu, Aliye Mtukufu, Ee Rabb [Allaah] nighufurie[2]

 

 

[3]

الحمدُ للهِ الذي عافاني في جَسَدي وَرَدّ عَليّ روحي وَأَذِنَ لي بِذِكْرِه

 

AlhamduliLLaahil lladhiy ’Afaaniy fiy jasadiy waradda ’alayya ruwhiy waadhina liy bidhikrih

 

Himdi ni Zake Allaah Ambaye Amenipa uzima wa mwili wangu, na Akanirudishia roho yangu, na Akaniwezesha kumdhukuru[3]

 

 

[4]

 

Soma Aayah katika Suwratul-’Imraan (3: 190-200)

أَعُوذُ بِاللّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ  

 إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠ الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٩١ رَبَّنَا إِنَّكَ مَن تُدْخِلِ النَّارَ فَقَدْ أَخْزَيْتَهُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ ﴿١٩٢رَّبَّنَا إِنَّنَا سَمِعْنَا مُنَادِيًا يُنَادِي لِلْإِيمَانِ أَنْ آمِنُوا بِرَبِّكُمْ فَآمَنَّا ۚ رَبَّنَا فَاغْفِرْ لَنَا ذُنُوبَنَا وَكَفِّرْ عَنَّا سَيِّئَاتِنَا وَتَوَفَّنَا مَعَ الْأَبْرَارِ ﴿١٩٣رَبَّنَا وَآتِنَا مَا وَعَدتَّنَا عَلَىٰ رُسُلِكَ وَلَا تُخْزِنَا يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۗ إِنَّكَ لَا تُخْلِفُ الْمِيعَادَ ﴿١٩٤فَاسْتَجَابَ لَهُمْ رَبُّهُمْ أَنِّي لَا أُضِيعُ عَمَلَ عَامِلٍ مِّنكُم مِّن ذَكَرٍ أَوْ أُنثَىٰ ۖ بَعْضُكُم مِّن بَعْضٍ ۖ فَالَّذِينَ هَاجَرُوا وَأُخْرِجُوا مِن دِيَارِهِمْ وَأُوذُوا فِي سَبِيلِي وَقَاتَلُوا وَقُتِلُوا لَأُكَفِّرَنَّ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ وَلَأُدْخِلَنَّهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ثَوَابًا مِّنْ عِندِ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ عِندَهُ حُسْنُ الثَّوَابِ ﴿١٩٥ لَا يَغُرَّنَّكَ تَقَلُّبُ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي الْبِلَادِ ﴿١٩٦ مَتَاعٌ قَلِيلٌ ثُمَّ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۚ وَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴿١٩٧ لَـٰكِنِ الَّذِينَ اتَّقَوْا رَبَّهُمْ لَهُمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا نُزُلًا مِّنْ عِندِ اللَّـهِ ۗ وَمَا عِندَ اللَّـهِ خَيْرٌ لِّلْأَبْرَارِ ﴿١٩٨وَإِنَّ مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ لَمَن يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْكُمْ وَمَا أُنزِلَ إِلَيْهِمْ خَاشِعِينَ لِلَّـهِ لَا يَشْتَرُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ ثَمَنًا قَلِيلًا ۗ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ أَجْرُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴿١٩٩ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اصْبِرُوا وَصَابِرُوا وَرَابِطُوا وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٢٠٠[4]

 

 

[1]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan na Al-Baraa bin ‘Aazib (رضي الله عنهما)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/113), Muslim (4/2083)

 

[2]Hadiyth ya ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit (رضي الله عنه). Na pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

((مَنْ قَال ذلِكَ غُفِرَ لَهُ فَإنْ دَعَا اسْتجِيبَ لَه فَإنْ قَامَ فَتَوَضَّأ ثُمَّ صَلّى قُبِلَتْ صَلاَتهُ))

((Atakayesema Atasamehewa, na akiomba du’aa ataitikiwa, na akisimama akitawadha kisha akaswali, atakakubaliwa Swalaah yake)) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/39) na wengineo na tamshi la ibn Maajah na angali Swahiyh ibn Maajah (2/335)

 

[3]Hadiyth ya Abu Hurayrah(رضي الله عنه)  - At-Tirmidhiy (5/473) na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/144)

 

[4]Imetajwa katika Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) katika Al-Bukhaariy na Al-Fat-h (8/237) na Muslim (1/530).  Suwrat Aal-‘Imraan (3:190-200)

 

 

 

Share

002-Hiswnul-Muslim: Du'aa Ya Kuvaa Nguo

Hiswnul-Muslim

002-Du’aa Ya Kuvaa Nguo

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 [5]

الحمدُ للهِ الّذي كَساني هذا (الثّوب) وَرَزَقَنيه مِنْ غَـيـْرِ حَولٍ مِنّي وَلا قـوّة

 

AlhamduliLLaahil lladhiyy kasaaniy haadha (ath-thawb) warazaqaniyhi min ghayri hawlin minniy walaa quwwah

 

Himdi Anastahiki Allaah Ambaye Amenivisha nguo hii, na kuniruzuku pasina uwezo kutoka kwangu wala nguvu [1]

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya Mu’aadh bin Anas Al-Answaariyy (رضي الله عنه) - Ahlu-Sunnan isipokuwa An-Nasaaiy. Angalia: Irwaaa Al-ghaliyl (7/47)

 

 

 

Share

003-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuvaa Nguo Mpya

Hiswnul-Muslim

003-Du’aa Ya Kuvaa Nguo Mpya

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

[6] 

 

اللّهُـمَّ لَـكَ الحَـمْـدُ أنْـتَ كَسَـوْتَنيهِ، أَسْأَلُـكَ مِـنْ خَـيرِهِ وَخَـيْرِ مَا صُنِعَ لَـه، وَأَعوذُ بِكَ مِـنْ شَـرِّهِ وَشَـرِّ مـا صُنِعَ لَـهُ.

 

Allaahumma Lakal Hamdu Anta Kaswtaniyhi. As-aluka min khayrihi wa khayri maa swuni’a lahu, wa a’uwdhu bika min sharrihi wa sharri maa swuni’a lahu

 

Ee Allaah, Himdi ni Zako, Wewe Ndiye Uliyenivisha, nakuomba kheri ya nguo hii, na kheri ya kila ambacho nguo hii imetengenezewa, na najikinga Kwako kutokana na shari yake, na shari ambayo nguo hii imetengenezewa[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy, Sa’ad bin Maalik (رضي الله عنهما) - Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy na Al-Baghaawiy na angalia: Mukhtaswar Shamaail At-Tirmidhiy ya Al-Albaaniy (رحمه الله) (Uk. 47).

 

 

Share

004-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unayomuombea Aliyevaa Nguo Mpya

Hiswnul-Muslim

004-Du’aa Unayomuombea Aliyevaa Nguo Mpya

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[7]

تُبْـلي وَيُـخْلِفُ اللهُ تَعَالى

Tubliy wa YukhlifuAllaahu Ta’aalaa

 

Itakwisha [kwa kuzeeka na kupasuka] na Allaah Atakupa nyingine[1]

 

 

 

[8]

اِلبَـس جَديـداً وَعِـشْ حَمـيداً وَمُـتْ شهيداً

Ilbas jadiydan wa ’ish hamiydan wamut shahiydaa

 

Vaa nguo mpya, na ishi hali ya kuwa ni mwenye kushukuru, na kufa hali ya kuwa ni shahidi [2]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (4/41), na angalia: Swahiyh Abi Daawuwd (2/760)

 

[2] Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar bin al-Khatwaab (رضي الله عنهما) - Ibn Maajah (2/1178), Al-Baghaawiy (12/14) na taz Swahiyh Ibn Maajah (2/275)

 

 

 

Share

005-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuvua Nguo

Hiswnul-Muslim

005-Du’aa Ya Kuvua Nguo

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

[9]

بِسْمِ الله

BismiLLaah

 

Kwa jina la Allaah[1] (ninavua).

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abiy Twaalib na Anas bin Maalik  (رضي الله عنهما) - At-Tirmidhiy (2/505) na wengineo na taz Al-irwaa Namba [50] na Swahiyh Al-Jaami’ (3/203)

 

 

 

Share

006-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuingia Chooni

Hiswnul-Muslim

006-Du’aa Ya Kuingia Chooni

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

[10]

(بِسْمِ الله) اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِـكَ مِـنَ الْخُـبْثِ وَالْخَبائِث

 

(BismilLLaah) Allaahumma inniy a’uwdhu Bika minal khubthi wal khabaaith

 

 

(Kwa jina la Allaah) Ee Allaah najikinga kwako kutokana na mashaytwaan ya kiume na ya kike [1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy, (1/45), Muslim (1/283) na ziada: ((BismiLLaahi fiy awwalihi)) Imetoka kwa Sa’iyd bin Manswur. Taz Fat-h Al-Baariy (1/244)

 

 

 

Share

007-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kutoka Chooni

Hiswnul-Muslim

007-Du’aa Ya Kutoka Chooni

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[11]

غُفْـرانَك

Ghufraanak

 

Nakuomba maghfira[1] (Ee Allaah).

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Aaishah bint Abi Bakr As-Swiddiyq (رضي الله عنهما) - Aswhaab As-Sunan isipokuwa an-Nasaaiy ameitoa katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah. Taz takhriyj Zaad al-Ma’aad (2/386).

 

 

 

Share

008-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kabla Kutawadha

Hiswnul-Muslim

008-Du’aa Ya Kabla Kutawadha

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[12]

 

بِسْمِ الله

BismiLLaah

 

Kwa jina la Allaah[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah na wengineo (رضي الله عنهم) Hadiyth kikamilifu ni:

((لا صَلاةَ لِمَنْ لا وُضُوءَ لَهُ، وَلا وُضُوءَ لِمَنْ لَمْ يَذْكُرِ اسْمَ اللَّهِ عَلَيْهِ))

((Hakuna Swalaah kwa asiyekuwa na wudhuu, na hakuna wudhuu kwa asiyeutajia  jina la Allaah)) - Abu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad, na taz Irwaa Al-Ghaliyl (1/122)

 

 

 

 

Share

009-Hiswnul-Muslim: Du’aa Baada Ya Kutawadha

Hiswnul-Muslim

009-Du’aa Baada Ya Kutawadha

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

[13]  

 أَشْهَدُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ وَأَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ  

 

Ash-hadu an laa ilaaha illaAllaah, Wahdahu laa shariyka Lahu wa ash-hadu anna Muhammadan ‘Abduhu wa Rasuwluhu

 

Nashuhudia (kwa kuamini moyoni na kukiri) kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah, Peke Yake, wala Hana mshirika, na ni nashuhudia (kwa kuamini moyoni na kukiri) kwamba Muhammad ni mja wake na ni Rasuli Wake[1]

 

 

 

[14]

 اللَّهُمَّ اجْعَلْنِي مِنْ التَّوَّابِينَ وَاجْعَلْنِي مِنْ الْمُتَطَهِّرِينَ

 

Allaahummaj-’alniy minat-ttawaabiyna waj-’alniy minal mutatwahhariyn

 

Ee Allaah, nijaaliye niwe miongoni mwa wenye kutubu na nijaalie miongoni mwa wenye kujitoharisha[2]

 

 

 

[15]

 

سُبْحـانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْك

 

SubhaanakaAllaahumma wabihamdika, ash-hadu an laa ilaaha illa Anta astaghfiruka wa atuwbu Ilayka

 

Kutakasika ni Kwako ee Allaah,  na Himdi ni Zako, nashuhudia (kwa kuamini moyoni na kukiri) kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, nakuomba unighufurie na natubia Kwako[3]

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Uqbah bin ‘Aamir Al-Juhniy(رضي الله عنه)    Hadiyth imetaja atakayesema hivyo na imemalizikia Hadiyth kauli ya Rasuli (صلى الله عليه وسلم) :

((إلاَّ فُتِحَتْ لَهُ أَبْواب الْجَنَّة الثَّمَانِيَة يَدْخُلُ مِنْ أيُّها شآء))

((...basi itafunguliwa milango ya Jannah minane kwa ajili yake aingie wowote atakao))

- Muslim (1/209)

 

[2]Hadiyth ya ‘Umar bin Khatwwab (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (1/78)  na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (1/18)

 

[3]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy(رضي الله عنه)  -An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah’ (Uk. 173), [81] na taz  Irwaa al-Ghaliyl (1/135),  (3/94), 

 

 

Share

010-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kutoka Nyumbani

Hiswnul-Muslim

010-Du’aa Ya Kutoka Nyumbani

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [16]

 

     بِسْمِ اللهِ، تَوَكَّلْـتُ عَلى اللهِ وَلا حَوْلَ وَلا قُـوَّةَ إِلاّ بِالله

BismiLLaah, tawakkaltu ‘alaAllaah walaa hawla walaa quwwata illa biLLaah.

 

Kwa jina la Allaah (ninatoka) nimetawakali kwa Allaah, na hapana uwezo wala nguvu ila vyote vinatokana na Allaah[1] 

 

 

[17]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ أَنْ أَضِـلَّ أَوْ أُضَـلَّ، أَوْ أَزِلَّ أَوْ أُزَلَّ ، أَوْ أَظْلِـمَ أَوْ أَظْلَـمَ، أَوْ أَجْهَلَ أَوْ يُـجْهَلَ عَلَـيَّ .

 

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika an udhwilla aw udhwalla aw azilla aw uzalla aw adhwlim aw udhwlam aw ajhal aw yujhal ’alayya

 

Ee Allaah najikinga Kwako kutokana na kupotea au kupoteza, au kuteleza, au kumtelezesha mtu, au kudhulumu au kudhulumiwa, au kuwa mjinga au kufanywa mjinga[2]

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه)  Hadiyth kikamilifu:

 

((إمَنْ قَال إِذَا خَرَجَ مِنْ بَيْتِهِ: بِسْمِ اللَّهِ تَوَكَّلْتُ عَلَى اللَّهِ، لَا حَوْلَ وَلَا قُوَّةَ إِلَّا بِاللَّهِ، قَالَ: يُقَالُ لَهُ حِينَئِذٍ: كُفِيتَ، وَوُقِيتَ، وَهُدِيتَ، وَتُنَجَّى عَنْهُ الشَّيَاطِينُ، فَيَقُولُ لشَيْطان آخَرُ: كَيْفَ لَكَ بِرَجُلٍ قَدْ هُدِيَ وَكُفِيَ وَوُقِيَ))

 

((Atakayesema pindi akitoka nyumbani kwake: Tawakkaltu ‘alaa Allaah, laa hawla wa laa quwwata illa biLLaah....husemwa hapo: “Umelindwa, umekingwa na umeongozwa”, na huepushwa na shaytwaan, kisha shaytwaan mwengine husema: “Utawezaje (kumuandama) mtu aliyeongoka akalindwa na aliyekingwa?)) - Abu Daawud (4/325), At-Tirmidhiy (5/490) na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/151)

 

[2]Umm Salamah, Hind Bint Abiy Umayyah Al-Khazuwmiyyah - Ahlus-Sunan na taz Swhaiyh At-Tirmidhiy (3/152) na Swahiyh Ibn Maajah (2/336)

 

 

 

Share

011-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuingia Nyumbani

Hiswnul-Muslim

011-Du’aa Ya Kuingia Nyumbani

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

[18]

    بِسْـمِ اللهِ وَلَجْنـا، وَبِسْـمِ اللهِ خَـرَجْنـاَ، وَعَلـى رَبِّنـا تَوَكّلْـناَ

 

BismiLLaahi walajnaa, wa BismiLLaahi kharajnaa, wa ’alaa Rabbinaa tawakkalnaa

 

Kwa jina la Allaah tunaingia, na kwa jina la Allaah tunatoka, na Rabb wetu tumetawakali[1]

 

Kisha asalimie watu walio ndani kwa maamkizi ya Kiislamu:

 

السَّلامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ وَبَرَكَاتُهُ

”Assalamu ‘alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh”.

 

 

 


[1]Abu Maalik Al-Ash’ariyy (wametofautiana jina lake; wengine wamesema: ‘Ubayd au ‘Abdullaah, au ‘Amruw, au Ka’ab bin Ka’ab au ‘Aamir bin Al-Haarith (رضي الله عنه)   - Abu Daawud (4/325), na Isnaad yake imepewa daraja ya Hasan na Ibn Baaz katika Tuhfat Al-Akhyaar (Uk. 28), na Majmuw’ Fataawaa Ibn Baaz (26/35).

 

 

Tanbihi: Imaam Al-Albaaniy ameidhoofisha Du'aa ifuatayo ambayo inaanza kwa tamshi la ziyada:

 

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَ الْمَوْلَجِ ، وَخَيْرَ الْمَخْرَجِ ، بِسْمِ اللَّهِ وَلَجْنَا، وَبِسْمِ اللَّهِ خَرَجْنَا، وَعَلَى اللَّهِ رَبِّنَا تَوَكَّلْنَا، ثُمَّ لِيُسَلِّمْ عَلَى أَهْلِهِ

 

Imaam An-Nawawiy amesema katika Al-Adkhaar (23): “Inapendekezeka mtu anapoingia katika nyumba aseme: 

بسم الله

Na akithirishe kumdhukuru Allaah (عزّ وجلّ), kutokana na kauli ya Allaah (عزّ وجلّ):

 

(( فإذَا دَخَلْتُمْ بُيُوتاً فَسَلِّمُوا على أنْفُسِكُمُ تَحِيَّةً مِنْ عِنْدِ اللَّهِ مُبَارَكَةً طَيِّبَة))  

[An-Nuwr: 61].”

 

Na pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:  

إِذَا دَخَلَ الرَّجُلُ بَيْتَهُ فَذَكَرَ اللَّهَ عِنْدَ دُخُولِهِ وَعِنْدَ طَعَامِهِ  قَالَ الشَّيْطَانُ : لا مَبِيتَ لَكُمْ وَلا عَشَاءَ))

((Atakapoingia mtu nyumbani kwake akamdhukuru Allaah wakati wa kuingia na katika chakula, shaytwaan husema: Hakuna malazi wala chakula cha usiku)) [Muslim] [2018]

 

 

 

Share

012-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kwenda Msikitini

Hiswnul-Muslim

  012-Du’aa Ya Kwenda Msikitini

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 [19]

 

 اللَّهُمَّ اجْعَلْ فِي قَلْبِي نُورًا، وَفِي لِسَانِي نُورًا، وَفِي سَمْعِي نُورًا، وَفِي بَصَرِي نُورًا، وَمِنْ فَوْقِي نُورًا،  وَمِنْ تَحْتِي نُورًا، وَعَنْ يَمِينِي نُورًا، وَعَنْ شِمَالِي نُورًا، وَمِنْ أَمَامِي نُورًا، وَ مِنْ خَلْفِي نُورًا، وَاجْعَلْ فِي نَفْسِي نُورًا، وَأَعْظِمْ لِي نُورًا، وَعَظِّمْ لِي نُورًا، وَاجْعَلْ لِي نُورًا، وَاجْعَلْنِي نُورًا، اللَّهُمَّ أَعْطِنِي نُورًا، وَاجْعَلْ فِي عَصَبِي نُوراً، وَفِي لَحْمِي نُوراً،  وَفِي دَمِي نُوراً، وَفِي شَعْرَي نُوراً، وَفِي بَشَرِي نُوراً، اللَّهُمَّ اجْعَلْ لِي نوُراً فِي قَبْرِي، وَنُوراً فِي عِظَامِي، وَزِدْنِي نُوراً، وَزِدْنِي نُوراً، وَزِدْنِي نُوراً، وَهَبْ لِي نُوراً عَلَى نُورٍ.

 

Allaahummaj’al fiy qalbiy nuwran, wafiy lisaaniy nuwran,  wafiy sam-’iy nuwran, wafiy baswariy nuwran, wamin fawqiy nuwran,  wamin tahtiy nuwran, wa ’an yamiyniy nuwran, wa ‘an shimaaliy nuwran, wa a-’dhwimliy nuwran, wa ‘adhwimliy nuwran, waj-’alliy nuwran, waj-’alniy nuwran, Allaahumma a-’twiniy nuwran, waj-'al fiy ‘aswabiy nuwran, wafiy lahmiy nuwran, wafiy damiy nuwran, wafiy sha-’riy nuwran, wafiy bashariy nuwran. Allaahummaj-’alliy nuwran fiy qabriy, wanuwrna fiy ‘idhwaamiy, wazidniy nuwran, wazidniy nuwran, wazidniy nuwran, wahabliy nuwran ‘alaa nuwr

 

Ee Allaah, Weka katika moyo wangu nuru, na katika ulimi wangu nuru, na katika masikio yangu nuru, na katika macho yangu nuru, na juu yangu nuru, na chini yangu nuru, na kuliani kwangu nuru, na kushotoni kwangu nuru, na mbele yangu nuru, na nyuma yangu nuru, na Weka katika nafsi yangu nuru, na Nifanyie kubwa nuru, na Nifanyie nyingi nuru, na Uniwekee mimi nuru, na Unifanyie mimi nuru, Ee Allaah, Nipe nuru, na Uweke  katika  mishipa yangu nuru, na katika  nyama  yangu nuru, na katika damu yangu nuru, na katika nywele zangu nuru, na katika ngozi yangu nuru. Ee Allaah, Niwekee nuru katika kaburi langu, na nuru katika mifupa yangu, na Unizidishie nuru, na Unizidishie nuru, na Nizidishie nuru, na Nipe nuru juu ya nuru[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Kauli zote zimepatikana katika Al-Bukhaariy (11/116) kwa namba [6316], Muslim (1/526, 529, 530) kwa namba [763]  

 

 

 

 

Share

013-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuingia Msikitini

Hiswnul-Muslim

013-Du’aa Ya Kuingia Msikitini

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[20]

أَعُوذُ بِاللَّهِ الْعَظِيمِ، وَبِوَجْهِهِ الْكَرِيمِ، وَسُلْطَانِهِ الْقَدِيمِ، مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ.

 

A’uwdhu biLLaahil ‘Adhwiym wabi Wajhihil Kariym wa Sultwaanihil qadiym minash-shaytwaanir-rajiym

 

Najikinga na Allaah Aliye Mtukufu na kwa Wajihi Wake Karimu na kwa utawala Wake wa kale kutokana na shaytwaan aliyeepushwa na Rehma za Allaah[1]

 

 

بِسْـمِ الله، وَالصَّلاةُ وَالسَّلامُ عَلى رَسولِ الله، اللّهُـمَّ افْتَـحْ لي أَبْوابَ رَحْمَتـِك

BismiLLaah was-swalaatu was-salaamu ‘alaa Rasuwuli-LLaah. Allaahummaftah-liy abwaaba Rahmatika

 

 

Kwa jina la Allaa na Rehma[2] na amani zimfikie Rasuli wa Allaah[3]. Ee Allaah nifungulie milango ya Rehma Yako[4]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah ‘Amruw bin Al-Aasw (رضي الله عنهما)  imemalizikia Hadiyth:

 فَإذا قَالَ ذلك، قَالَ الشَّيْطانُ: حُفِظَ مِنِّي سائر الْيَوْم

 …atakaposema hivyo, shaytwaan husema: “Amehifadhiwa dhidi yangu siku nzima. -  Abu Daawuwd. Angalia: Swahiyh Al-Jaami’ [4591]

 

[2]Ibn As-Sunniy namba [88] na ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy (رحمه الله)

 

[3]Abu Daawuwd (1/126) na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (1/528)

 

[4]Muslim (1/494)، na katika Sunan ibn Maajah، Hadiyth ya Faatwimah (رضي الله عنها)، Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي ذُنُوبِي وَافْتَحْ لِي أَبْوَابَ رَحْمَتِك

((Allaahumma-ghfir-liy dhunuwbiy waf-tah liy abwaaba Rahmatika – Ee Allaah Nighufurie madhambi yangu na nifungulie milango ya Rehma Zako)) na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy (رحمه الله) na ina ushahidii wa Hadiyth nyingine. Angalia: Swahiyh Ibn Maajah (1/128-129)

 

 

 

 

Share

014-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kutoka Msikitini

Hiswnul-Muslim

014-Du’aa Ya Kutoka Msikitini

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[21]

 

بِسمِ الله وَالصّلاةُ وَالسّلامُ عَلَى رَسولِ الله، اللّهُـمَّ إِنّـي أَسْأَلُكَ مِـنْ فَضْـلِك، اللّهُـمَّ اَعْصِمْنـي مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجـيم

 

BismiLLahi wasw-swalaatu was-salaamu ’alaa RasuwliLLaah Allaahumma inniy as-aluka min fadhwlika Allaahumma a-’swimniy minash-shaytwaanir-rajiym

 

Kwa Jina la Allaah na Rehma na amani zimfikie Rasuli wa Allaah. Ee Allaah hakika mimi nakuomba katika fadhila Zako. Ee Allaah nitenge mbali na   shaytwaan aliyeepushwa na Rehma Zako [aliyelaaniwa] [1].

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) . Angalia matoleo ya wasimulizi wa Hadiyth zilizopita namba (20) na ziada:

اللّهُـمَّ اَعْصِمْنـي مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجـيم

((Allaahumma a-’swimniy minash-shaytwaanir-rajiym – Ee Allaah Nitenge mbali na shaytwaan aliyeepushwa na Rehma Zako)) ya Ibn Maajah. Angalia: Swahiyh Ibn Maajah (1/129)

 

 

 

 

Share

015-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Adhaana

Hiswnul-Muslim

015-Du’aa Za Adhaana

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[22]

 

Mtu akisikia Muadhini anaadhini anatakiwa asema kama anavyosema Muadhini, ila atakapo sema:

حَـيَّ عَلـى الصَّلاة

 

Hayya ’alasw-Swalaah

 

Njooni kwenye Swalaah

 

 حَـيَّ عَلـى الْفَـلاح

 

Hayya ’alal falaah

 

Njoni kwenye mafanikio

 

Yeye hatomuigiza bali anatakiwa aseme:

لا حَـوْلَ وَلا قُـوَّةَ إِلاّ بِالله

 

Laa Hawla walaa quwwata Illaa biLLaah[1]

 

Hapana uwezo wala nguvu ila za Allaah.

 

 

[23]

 

Muadhini akisema:

أَشْـهَدُ أَنْ لا إِلـهَ إِلاّ اللهُ أَشْـهَدُ انَّ مُحَمدا رَسُول الله

 

 Ash-hadu anlaa Ilaaha illa Allaah, ash-hadu anna Muhammada Rasuwlu Allaah.

 

Anatakiwa mtu aseme:

 

وَأَنا أَشْـهَدُ أَنْ لا إِلـهَ إِلاّ اللهُ وَحْـدَهُ لا شَـريكَ لَـه وَأَنَّ محَمّـداً عَبْـدُهُ وَرَسـولُه رَضيـتُ بِاللهِ رَبَّاً، وَبِمُحَمَّـدٍ رَسـولاً،  وَبِالإِسْلامِ دينَـاً .

Wa anaa ash-hadu an laa ilaaha illaAllaah Wahdau laa shariyka Lah, wa anna Muhammadan ’Abduhu wa Rasuwluhu, Radhwiytu biLLaahi Rabban wabi Muhammadin Rasuwlan wabil Islaami Diynaa.

Na mimi pia nashuhudia (kwa kuamini moyoni na kukiri) kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Mmoja Peke Yake, Hana mshirika na kwamba Muhammad ni mja Wake, na Rasuli Wake. Nimeridhika kuwa Allaah Ndiye  Rabb wangu, na kuwa Muhammad ni Rasuli wangu, na kuwa Uislamu ndio Dini yangu[2].

 

Sema hivyo baada ya tashahhad ya Muadhini[3]

 

 

 [24] 

 

Kisha baada ya kumjibu Muadhini mswalie Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وسلم)[4]  

Kisha sema:

 

اللّهُـمَّ رَبَّ هَذِهِ الدّعْـوَةِ التّـامَّة وَالصّلاةِ القَـائِمَة آتِ محَـمَّداً الوَسيـلةَ وَالْفَضـيلَة وَابْعَـثْه مَقـامـاً مَحْـمُوداً الَّذي وَعَـدْتَه [5]

Allaahumma Rabba haadhihidda’watit ttaammah, wasw-swalaatil qaaimah, aati Muhammadanil wasiylata walfadhwiylah, wab-‘ath-hu maqaaman mahmuwdani lladhiy wa’adtah. (Innaka laa Tukhliful-Miy’aad.. Haikuthibiti)

 

Ee Rabb wa wito huu uliotimu, na Swalaah ya kudumu! Mpe Muhammad Wasiylah na daraja ya juu zaidi, na Mfufue Umpe Maqaam ya kuhimidiwa Uliyomwahidi[6]

 

[26]

 

Ajiombee mtu baina ya Adhaana na Iqaamah kwani du’aa wakati huo hairudishwi[7]

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (1/125), Muslim (1/288)

 

[2]Hadiyth ya Sa’ad bin Abi Waqqaasw (رضي الله عنه)  Muslim (1/290)

 

[3]Ibn Khuzaymah (1/220)

 

[4]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw (رضي الله عنهما)  kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akisema:

 

إذَا سَمِعْتُمْ الْمُؤَذِّنَ فَقُولُوامِثْلَ مَا يَقُولُ ، ثُمَّ صَلُّوا عَلَيَّ ، فَإِنَّهُ مَنْ صَلَّى عَلَيَّ صَلاةً صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ بِهَا عَشْرًا . ثُمَّ سلُوا اللَّه لي الْوسِيلَةَ ، فَإِنَّهَا مَنزِلَةٌ في الجنَّةِ لا تَنْبَغِي إِلاَّ لعَبْدٍ منْ عِباد اللَّه وَأَرْجُو أَنْ أَكُونَ أَنَا هُو ، فَمنْ سَأَل ليَ الْوسِيلَة حَلَّتْ لَهُ الشَّفاعَةُ

 

((Mtakapomsikia muadhini basi semeni kama anavyosema, kisha niswalieni, kwani mwenye kuniswalia mara moja Allaah Atamswalia mara kumi, na kisha niombeeni (kupata) ‘wasiylah’ ambayo ni manzila (heshima maalum) huko Jannah. Haitomstahikia isipokua mja mmoja katika waja wa Allaah, nami ninatarajia kuwa mja huyo, na mwenye kuniombea “wasiylah” atapata uombezi (wangu Siku ya Qiyaamah)) - Muslim (1/288)

 

[5] Tanbihi: Kauli ya ziyada ni Dhwa’iyf:

انك لا تخلف الميعاد

Innaka Laa Tukhliful-Miy’aad 

 

‘Ulamaa wamesema kuwa haikuthibiti kama alivyorekodi Imaam Al-Albaaniy katika As-Silsilah Adhwa’iyfah [6714]

 

[6]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنهما)  - Al-Bukhaariy, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah na Ahmad kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ قالها حَلَّتْ لَهُ شَفَاعَتِي يَوْمَ الْقِيَامَةِ))

((Mwenye kusema hivo, atapata uombezi wangu siku ya Qiyaamah))

 

 

[7]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه)  - At-Tirmidhiy, Abu Daawuwd, Ahmad na taz Irwaa Al-Ghaliyl  (1/262)

 

 

 

 

Share

016-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Kufungulia Swalaah

Hiswnul-Muslim

016-Du’aa Za Kufungulia Swalaah

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[27] 

 

اللّهُـمَّ باعِـدْ بَيـني وَبَيْنَ خَطـايايَ كَما باعَدْتَ بَيْنَ المَشْرِقِ وَالمَغْرِبْ، اللّهُـمَّ نَقِّنـي مِنْ خَطايايَ كَمـا يُـنَقَّى الثَّـوْبُ الأَبْيَضُ مِنَ الدَّنَسْ، اللّهُـمَّ اغْسِلْنـي مِنْ خَطايـايَ بِالثَّلـجِ وَالمـاءِ وَالْبَرَدْ

 

Allaahumma baa’id bayniy wa bayna khatwaayaaya kamaa baa’adta baynal-Mashriqi wal-Maghrib. Allaahumma naqqiniy min khatwaayaaya kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danasi. Allaahumma-ghsiliniy min khatwaayaaya bith-thalji walmaai walbarad.

 

Ee Allaah niweke mbali na makosa  yangu kama Ulivyoweka mbali baina ya Mashariki na Magharibi, Ee Allaah nitakase na makosa yangu kama vile inavyoitakaswa nguo nyeupe na uchafu, Ee Allaah nisafishe na makosa yangu kwa theluji na kwa maji na kwa barafu[1].

 

 

 

[28]

سُبْـحانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمْـدِكَ وَتَبارَكَ اسْمُـكَ وَتَعـالى جَـدُّكَ وَلا إِلهَ غَيْرُك

 

Subhaanaka-LLaahumma wabihamdika watabaarakas-Smuka wa Ta’aalaaa Jadduka walaa ilaaha Ghayruka

 

Utakasifu ni Wako Ee Allaah, na Himdi ni Zako, na Limebarikika Jina Lako, na Umetukuka Ujalai Wako, na hapana mwabudiwa wa haki, ghairi Yako[2].

 

 

 

[29]

 

وَجَّهـتُ وَجْهِـيَ لِلَّذي فَطَرَ السَّمـواتِ وَالأَرْضَ حَنـيفَاً وَمـا أَنا مِنَ المشْرِكين، إِنَّ صَلاتـي، وَنُسُكي، وَمَحْـيايَ، وَمَماتـي للهِ رَبِّ العالَمين، لا شَريـكَ لَهُ وَبِذلكَ أُمِرْتُ وَأَنا مِنَ المسْلِـمين. اللّهُـمَّ أَنْتَ المَلِكُ لا إِلهَ إِلاّ أَنْت، أَنْتَ رَبِّـي وَأَنـا عَبْـدُك، ظَلَمْـتُ نَفْسـي وَاعْـتَرَفْتُ بِذَنْبـي فَاغْفِرْ لي ذُنوبي جَميعاً إِنَّـه لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إلاّ أَنْت، وَاهْدِنـي لأَحْسَنِ الأَخْلاقِ لا يَهْـدي لأَحْسَـنِها إِلاّ أَنْـت، وَاصْـرِف عَـنّْي سَيِّئَهـا، لا يَصْرِفُ عَـنّْي سَيِّئَهـا إِلاّ أَنْـت، لَبَّـيْكَ وَسَعْـدَيْك، وَالخَـيْرُ كُلُّـهُ بِيَـدَيْـك، وَالشَّرُّ لَيْـسَ إِلَـيْك، أَنا بِكَ وَإِلَيْـك، تَبـارَكْتَ وَتَعـالَيتَ، أَسْتَغْـفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيك

 

Wajjahtu wajhiya liLLadhiy fatwaras-samaawaati wal ardhwa haniyfan wamaa ana minal mushrikiyn. Inna swalaatiy, wanusuky, wamahyaaya wamamaatiy liLLaahi Rabbil ‘aalamiyn. Laa shariyka Lahu wabidhaalika umirtu wa anaa minal Muslimiyn. Allaahumma Antal-Maliku laa ilaaha illa Anta. Anta Rabbiy wa ana ‘abduka, dhwalamtu nafsiy wa’taraftu bidhambiy faghfirly dhunuwbiy jamiy’an innahu laa yaghfirudh-dhunuwba illa Anta. Wahdiniy liahsanil-akhlaaqi laa yahdiy liahsanihaa illa Anta, waswrif ‘annyi sayyiahaa laa yaswrif ‘anniy sayyiahaa illa Anta. Labbayka wasa’dayka walkhayru kulluhu biyadika, wash-sharru laysa Ilayka, ana bika wa Ilayka, Tabaarakta wa Ta’aalayta, astaghfiruka wa atuwbu Ilayka

 

Nimeuelekeza uso wangu kwa yule Ambaye Ameanzisha mbingu na ardhi hali ya kuelemea katika haki, na sikuwa mimi ni katika washirikina, hakika Swalaah yangu na kuchinja kwangu na uhai wangu, na kufa kwangu ni kwa Allaah Rabb walimwengu, Hana mshirika, na kwa hilo nimeamrishwa nami ni katika Waislamu. Ee Allaah, Wewe Ndiye Mfalme, hapana  mwabudiwa wa haki ila Wewe, Wewe Ndiye Rabb wangu na mimi ni mja Wako. Nimedhulumu nafsi yangu, na nimekiri madhambi yangu kwa hivyo nighufurie madhambi yangu yote, hakika haghufurii madhambi, ila Wewe. Na niongoze kwenye tabia nzuri kwani haongozi kwenye tabia nzuri ila Wewe. Niepushe na tabia mbaya, kwani hakuna mwenye uwezo wa kuniepusha na tabia mbaya ila Wewe.  Naitikia mwito Wako, na nina furaha kukutumikia, na kheri zote ziko mikononi Mwako, na shari haitoki Kwako, mimi nimepatikana kwa ajili Yako, na nitarudi Kwako, Umebarikika na Umetukuka, nakuomba maghfira na narudi Kwako kutubia[3] 

 

 

[30]

 

اللّهُـمَّ رَبَّ جِـبْرائيل، وَميكـائيل، وَإِسْـرافيل، فاطِـرَ السَّمواتِ وَالأَرْض، عالـِمَ الغَيْـبِ وَالشَّهـادَةِ أَنْـتَ تَحْـكمُ بَيْـنَ عِبـادِكَ فيـما كانوا فيهِ يَخْتَلِفـون. اهدِنـي لِمـا اخْتُـلِفَ فيـهِ مِنَ الْحَـقِّ بِإِذْنِك، إِنَّـكَ تَهْـدي مَنْ تَشـاءُ إِلى صِراطٍ مُسْتَقـيم

 

Allaahumma Rabba Jibraaiyla wa Mikaaiyla wa Israafiyla, faatwiras-samaawaati wal ardhw, ’Aalimal ghaybi wash-shahaadah, Anta Tahkmu bayna ’ibaadika fiymaa kaanuw fiyhi yakhtalifuwn. Ihdiniy limakhtulifa fiyhi minal haqqi biidhnika Innaka Tahdiy man Tashaau ilaa swiraatwil-mustaqiym

 

Ee Allaah Rabb wa Jibiriyl na Mikaaiyl na Israafiyl, Mwanzishi wa mbingu na ardhi, Mjuzi wa mambo ya ghaibu na yaliyo wazi, Wewe Unahukumu baina ya waja Wako katika mambo ambayo walikuwa wakitofautiana.  Niongoze mimi kwenye haki katika yale ambayo (watu) wametofautiana kwa idhini Yako.  Hakika Wewe unamuongoza Umtakae kwenye njia ilionyoka[4].

 

 

 

[31]

 

اللهُ أَكْبَـرُ كَبـيرا، اللهُ أَكْبَـرُ كَبـيرا، اللهُ أَكْبَـرُ كَبـيرا، وَالْحَـمْدُ للهِ كَثـيرا، وَالْحَـمْدُ للهِ كَثـيرا، وَالْحَـمْدُ للهِ كَثـيرا، وَسُبْـحانَ اللهِ بكْـرَةً وَأَصيـلا، أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّـيْطانِ مِنْ نَفْخِـهِ وَنَفْـثِهِ وَهَمْـزِه

 

Allaahu Akbar Kabiyraa, Allaahu Akbar Kabiyraa, Allaahu Akbar Kabiyrah, wal hamduliLLaahi kathiyraa, wal hamduliLLaahi kathiyraa, wal hamduliLLahi kathiyraa, wasubhaana-Allaahi bukratan wa aswiylaah, wasubhaana-Allaahi bukratan wa aswiylaah, wasubhaana-Allaahi bukratan wa aswiylaah. A’uwdhu biLLaahi minash-shaytwaani min nafkhihi wa nafthihi wa hamzihi

 

Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Himdi Anastahiki Allaah kwa wingi, Himdi Anastahiki Allaah kwa wingi, Himdi Anastahiki Allaah kwa wingi, Ametakasika Allaah asubuhi na jioni. Najikinga na Allaah kutokana na shaytwaan, na kibri yake, na kupulizia kwake na kutia kwake wasiwasi (katika nyoyo za binaadamu)[5]

 

 

[32]

 

اللّهُـمَّ لَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ  نـورُ السَّمـواتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فيـهِنَّ، وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ قَـيِّمُ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ  وَمَنْ فيـهِنَّ، (وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ رَبُّ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ  وَمَنْ فيـهِنَّ) (وَلَكَ الْحَمْدُ لَكَ مُلْـكُ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ  وَمَنْ فيـهِنَّ) (وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ مَلِـكُ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ) (وَلَكَ الْحَمْدُ) (أَنْتَ الْحَـقُّ،  وَوَعْـدُكَ الْحَـقُّ ، وَقَوْلُـكَ الْحَـقُّ، وَلِقـاؤُكَ الْحَـقُّ،  وَالْجَـنَّةُ حَـقُّ، وَالنّـارُ حَقُّ، وَالنَّبِـيّونَ حَـقُّ، وَمـحَمَّدٌ صلى الله عليه وسلم حقُّ ، والسَّاعَةُ حَـقُّ)  (اللّهُـمَّ لَكَ أَسْلَمتُ، وَعَلَـيْكَ تَوَكَّلْـت، وَبِكَ آمَنْـت، وَإِلَـيْكَ أَنَبْـتُ، وَبِـكَ خاصَمْتُ، وَإِلَـيْكَ حاكَمْـتُ، فاغْفِـرْ لي مـا قَدَّمْتُ، وَما أَخَّـرْتُ، وَما أَسْـرَرْتُ، وَما أَعْلَـنْتُ) (أَنْتَ المُقَـدِّمُ وَأَنْتَ المُـؤَخِّر، لاَ إلَهَ إِلاّ أَنْـت) (أَنْـتَ إِلـهي لا  إلَهَ  إِلاّ أَنْـت)

 

Allaahumma Lakal-Hamdu Anta Nuwrus-samaawati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Anta Qayyimus-samaawaati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Anta Rabbus-samawaati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hhamdu Laka Mulkus-samaawaati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Antal-Haqqu, wawa’dukal-haqqu, waqawlukal-haqqu, waliqaaukal-haqqu, wal-Jannata haqqun, wannaaru haqqun, wannabiyyuwna haqqun, wa Muhammadun  SwallaAllaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam haqqun, was-saa’atu haqqun. Allaahumma Laka aslamtu, wa ’Alayka tawakkaltu, wabika aamantu, wa Ilayka anabtu, wabika khaaswamtu, wa Ilayka haakamtu, faghfir liy maa qaddamtu wamaa akh-khartu, wamaa asrartu, wamaa a’lantu, Antal-Muqaddimu wa Antal-Muakh-khiru laa ilaaha illa Anta. Anta Ilaahiy laa ilaaha illa Anta

 

Ee Allaah, Himdi ni Zako, Wewe Ndiye Nuru ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na Himdi ni Zako, Wewe Ndiye sababu ya kusimama kwa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na Himdi ni Zako, Wewe Ndiye  Rabb wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake; na Himdi ni Zako, Wewe Ndiye  Mfalme wa mbingu na ardhi, na Himdi ni Zako, Wewe ni haki [kweli] na ahadi Yako ni ya kweli, na neno Lako ni la kweli, na kukutana na Wewe ni kweli, na Jannah ni kweli, na Moto ni kweli, na Manabii ni kweli, na Muhammad SwallaAllaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam ni kweli, na Qiyaamah ni kweli. Ee Allaah, Kwako nimejisalimisha, na kwako nimetawakali, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimerejea kutubia.

Na kwa ajili Yako (au kwa hoja na dalili Zako) nimetetea (maadui Wako). Na nimeelekea Kwako kukufanya Wewe ni Hakimu Wangu (kuhukumu baina yetu). Basi nighufurie niliyoyatanguliza na niliyoyachelewesha, na niliyoyaficha na niliyoyatangaza; Wewe Ndiye Al-Muqaddimu (Mwenye kutanguliza) na Al-Muakh-khiru (Mwenye kuchelewesha), hapana  mwabudiwa wa haki ila Wewe; Wewe Ndiye Mwabudiwa wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe.[6]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Huraryah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (1/181), Muslim (1/4190)

 

[2]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) - Aswhaab As-Sunan wanne na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (1/77) na Swahiyh Ibn Maajah (1/135)

 

[3]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib  (رضي الله عنه) - Muslim (1/534)

 

[4]Hadiyth ya ‘Aishah (رضي الله عنها)  -  Muslim (1/534)

 

[5]Hadiyth ya Jubayr bin Mutw-‘im (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/203), Ibn Maajah (1/265), Ahmad (4/85), na Muslim kutoka kwa ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) kama hivyo na mna kisa humo (1/420)

 

[6]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abaas (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/3), (11/116), (13/371, 423, 465), na Muslim kwa ufupi kama hivyo (1/532)

 

 

 

 

 

Share

017-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Wakati Wa Kurukuu

Hiswnul-Muslim

017-Du’aa Za Wakati Wa Kurukuu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[33]

سُبْـحانَ رَبِّـيَ الْعَظـيم

 

Subhaana Rabbiyal ’Adhwiym

 

Ametakasika Rabb wangu aliye Mtukufu[1]  (mara 3)

 

 

[34]

سُبْـحانَكَ اللّهُـمَّ رَبَّـنا وَبِحَـمْدِك، اللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي

 

Subhaanaka Allaahumma Rabbanaa wabihamdika, Allaahummaghfir liy

 

Utakasifu ni Wako Ee Allaah Rabb wetu na Himdi ni Zako Ee Allaah, nighufurie[2]

 

 

[35]

سُبـّوحٌ قُـدّْوس، رَبُّ الملائِكَـةِ وَالـرُّوح

 

Subbuwhun Qudduwsun  Rabbul-Malaaikati war-Ruwh

 

Mwingi wa kutakaswa, Mtakatifu, Rabb wa Malaika na Jibiriyl[3].

 

 

[36]

اللّهُـمَّ لَكَ رَكَـعْتُ، وَبِكَ آمَـنْت، ولَكَ أَسْلَـمْت، خَشَـعَ لَكَ سَمْـعي، وَبَصَـري، وَمُخِّـي، وَعَظْمـي، وَعَصَـبي، وَما استَقَـلَّ بِهِ قَدَمي

 

Allaahumma Laka raka’-tu, wabika aamantu, walaka aslamtu. Khasha’a Laka sam-’iy, wabaswariy, wamukh-khiy, wa ’adhwmiy, wa ‘aswabiy, wamas-taqalla bihi qadamiy

 

Ee Allaah Kwako nimerukuu, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimejisalimisha, umenyenyekea Kwako usikizi wangu, na uwoni wangu, na ubongo wangu, na mfupa wangu, na hisia zangu, na ambacho kimesimama juu ya miguu yangu[4].

 

 

[37]

سُبْـحانَ ذي الْجَبَـروت، والمَلَـكوت، وَالكِبْـرِياء، وَالْعَظَـمَه

 

Subhaana dhil-Jabaruwti wal-malakuwti, wal-kibriyaai, wal-‘adhwamah

 

Ametakasika Mwenye Ujabari (Utawala, Utukufu), na Ufalme, na Ukubwa, na Uadhama [5].

 

 

 

[1]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan (رضي الله عنه) - Ahlus-Sunan: Abu Daawuwd [871], At-Tirmidhiy [262], An-Nasaaiy (1/190), ibn Maajah [888], Ahmad (394, 382/5) na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/83)

 

[2]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)   - Al-Bukhaariy (1/99), Muslim (1/350)

 

[3]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)   - Muslim (1/353), Abu Daawuwd (1/230)

 

[4]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه)  - Muslim (1/534) na Maimamu wane wa Hadiyth isipokuwa ibn Maajah. Isipokuwa kauli ya Wamastaqalla bihi qadamiy haikupokelewa na Muslim wala Maimamu wanne, bali ametamka Ibn Hibbaan. Angalia: Swahiyh ibn Hibbaan [1901] na Swahiyh Ibn Khuzaymah [607]

 

[5]Hadiyth ya ‘Awf bin Maalik Al-Ashja’iyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/230), An-Nasaaiy (2/191), Ahmad (6/24) na isnadi yake ni Hasan.

 

 

 

Share

018-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuinuka Kutoka Kenye Rukuu

Hiswnul-Muslim

018-Du’aa Ya Kuinuka Kutoka Kenye Rukuu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 [38]

سَمِـعَ اللهُ لِمَـنْ حَمِـدَه

 

Sami’a Allaahu liman hamidah

 

Allaah Amemsikia mwenye kumsifu[1]

 

 

 

[39]

رَبَّنـا وَلَكَ الحَمْـدُ حَمْـداً كَثـيراً طَيِّـباً مُـبارَكاً فيه

 

Rabbanaa walakal-hamdu, hamdan kathiyran twayyiban mubaarakan fiyhi

 

Ee Rabb wetu, ni Zako Himdi, Himdi nyingi, nzuri, zenye Baraka[2]

 

 

 

[40]

 

مِلْءَ السَّمـواتِ وَمِلْءَ الأَرْض، وَما بَيْـنَهُمـا، وَمِلْءَ ما شِئْـتَ مِنْ شَيءٍ بَعْـدْ، أَهـلَ الثَّـناءِ وَالمَجـدْ، أَحَـقُّ ما قالَ العَبْـد، وَكُلُّـنا لَكَ عَـبدٌ، اللّهُـمَّ لا مانِعَ لِما أَعْطَـيْت، وَلا مُعْطِـيَ لِما مَنَـعْت، وَلا يَنْفَـعُ ذا الجَـدِّ مِنْـكَ الجَـد

 

Mil-as-samawaatil wamil-al-ardhwi wamaa baynahumaa, wamil-a maa Shi-ita min shay-in ba’du. Ahlath-thanaa-i walmajdi. Ahaqqu maa qaalal-‘abdu, wakullunaa Laka ‘abdun. Allaahumma laa maani’a limaa A’-twayta, walaa mu’-twiya limaa mana’-ta, walaa yanfa’u dhal-jaddi Minkal-jaddu

 

Zimejaa mbingu na zimejaa ardhi na vilivyomo ndani yake (Himdi Zako), na zimejaa (Himdi Zako) kwa Ulichokitaka baada yake, Wewe ni Mstahiki wa Sifa na Utukufu, ni kweli aliyoyasema mja (Wako), na sote (sisi) ni waja Wako, Ee Allaah, hakuna mwenye kukizuia Ulichokitoa, wala mwenye kutoa Ulichokizuia, na wala utajiri wa mtu haumnufaishi mwenye utajiri mbele Yako.[3].

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (2/282)

 

[2]Hadiyth ya Rifaa’ah bin Raafi’ Az-Zurqiyy (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (2/284)

 

[3]Hadiyth ya Abu Sa’iy Al-Khudriyy (رضي الله عنه) - Muslim (1/346)

 

 

 

Share

019-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Wakati Wa Kusujudu

Hiswnul-Muslim

019-Du’aa Za Wakati Wa Kusujudu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[41]

سُبْـحانَ رَبِّـيَ الأَعْلـى  

 

Subhaana Rabbiyal a’-laa

 

Ametakasika Rabb wangu Aliye juu[1]     (mara 3)

  

 

 

[42]

سُبْـحانَكَ اللّهُـمَّ رَبَّـنا وَبِحَـمْدِكَ، اللّهُـمَّ اغْفِرْ لي

 

Subhaanaka Allaahumma Rabbanaa wabihamdika, Allaahummagh-firliy

 

Utakasifu ni Wako Ee Allaah, Rabb wetu, na Himdi ni Zako, Ee Allaah nighufurie [2]

 

 

[43]

سُبـّوحٌ قُـدّْوس، رَبُّ الملائِكَـةِ وَالـرُّوح

 

Subbuwhun Qudduwsun, Rabbul-Malaaikati war-Ruwh

 

Mwingi wa kutakaswa, Mtakatifu, Rabb wa Malaika na Roho[3]         

 

 

[44]

 

اللّهُـمَّ لَكَ سَـجَدْتُ وَبِـكَ آمَنْـتُ، وَلَكَ أَسْلَـمْتُ، سَجَـدَ وَجْهِـيُ لِلَّـذي خَلَقَـهُ وَصَـوَّرَهُ وَشَقَّ سَمْـعَـهُ وَبَصَـرَهُ، تَبـارَكَ اللهُ أَحْسـنُ الخـالِقيـن

Allaahumma Laka sajjadtu, wabika aamantu, walaka aslamtu. Sajada wajhiya liLLadhiy khalaqahu, wa swaw-warahu, wa shaqqa sam-’ahu wa baswarahu, Tabaaraka-Allaahu Ahsanul-Khaaliqiyn

 

Ee Allaah Kwako nimesujudu, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimesilimu, umesujudu uso wangu kumsujudia Aliyeuumba na Akautia sura na Akaupasua usikizi wake na uwoni wake, Amebarikika Allaah Mbora wa waumbaji [4]

 

 

 

[45]

سُبْـحانَ ذي الْجَبَـروت، والمَلَـكوت، وَالكِبْـرِياء، وَالْعَظَـمَه

 

Subhaana dhil-Jabaruwti wal-malakuwti, wal-kibriyaai, wal-‘adhwamah

 

Ametakasika Mwenye Ujabari (Utawala, Utukufu), na Ufalme, na Ukubwa, na Uadhama [5].

 

 

 [46]

اللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي ذَنْـبي كُلَّـه، دِقَّـهُ وَجِلَّـه، وَأَوَّلَـهُ وَآخِـرَه وَعَلانِيَتَـهُ وَسِـرَّه

 

Allaahummagh-firliy dhambiy kullahu diqqahu wajillahu wa awwalahu wa aakhirahu wa ’alaaniyatahu, wasirrahu

 

Ee Allaah nighufurie dhambi zangu zote, ndogo na kubwa, za mwanzo na za mwisho, za dhahiri na za siri[6]

 

 

 

[47]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِرِضـاكَ مِنْ سَخَطِـك، وَبِمعـافاتِـكَ مِنْ عُقوبَـتِك، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْـك، لا أُحْصـي ثَنـاءً عَلَـيْك، أَنْـتَ كَمـا أَثْنَـيْتَ عَلـى نَفْسـِك

 

Allaahumma inniy a’uwdhu biridhwaaka min sakhatwika, wabimu’aafaatika min ’uquwbatika, wa a’uwdhu Bika Minka, laa uhswiy thanaa-an ’Alayka, Anta kamaa athnayta ’alaa Nafsika

 

Ee Allaah hakika mimi najikinga kwa radhi Zako kutokana na hasira Zako, na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako, na najikinga Kwako unihifadhi na Wewe, mimi siwezi kuzidhibiti sifa Zako, Wewe ni kama ulivyojisifu Mwenyewe[7].

 

 

 

[1]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan (رضي الله عنه) - Ahlus-Sunan: Abu Daawuwd [871], At-Tirmdhiy [262], An-Nasaaiy (1/190) Ibn Maajah [888], Ahmad [394, 382] na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/83)

 

[2]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) imetangulia namba 34 juu - Al-Bukhaariy (1/99), Muslim (1/350).

 

[3]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)  imetangulia juu namba 35 -Muslim (1/353), Abu Daawud (1/230)

 

[4]Hadiyth ya ‘Aliy bin Twaalib (رضي الله عنه) - Muslim (1/534) na wengineo.

 

[5]Hadiyth ya ‘Awf bin Maalik Al-Ashja’iyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/230), An-Nasaaiy (2/191), Ahmad (6/24) na isnadi yake ni Hasan.

Abu Daawuwd (1/230), Ahmad (6/24), An-Nasaaiy (2/191) na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/166)  (Pia imetangulia katika Du’aa Namba 37)  

 

[6]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Muslim (1/350)

 

[7]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)  - Muslim (1/352)

 

 

 

 

Share

020-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Kikao Kati Ya Sijdah Mbili

Hiswnul-Muslim

020-Du’aa Za Kikao Kati Ya Sijdah Mbili

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[48]

رَبِّ اغْفِـرْ لي، رَبِّ اغْفِـرْ لي

 

Rabbighfir-liy, Rabbighfir-liy

 

Rabb nighufurie, Rabb nighufurie[1]

 

 

 

[49]

اللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي، وَارْحَمْـني، وَاهْدِنـي، وَاجْبُرْنـي، وَعافِنـي وَارْزُقْنـي وَارْفَعْـني

 

Allaahummaghfir-liy, warhamniy, wahdiniy, wajburniy, wa ’aafiniy, warzuqniy, warfa’-niy

 

Ee Allaah nighufurie, na unirehemu, na uniongoze, na uniungie, na unipe afya, na uniruzuku na uniinue[2]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan (رضي الله عنه) Abu Daawuwd (1/231) na angalia: Swahiyh Ibn Maajah (1/148)

 

[2]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  - Aswhaab As-Sunan isipokuwa An-Nasaaiy; Abu Daawuwd [850], At-Tirmdihiy [284], Ibn Maajah [898],  na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/90) na Swahiyh ibn Maajah (1/148)

 

 

 

 

Share

021-Hiswnul-Muslim:Du’aa Za Sijdah Ya Kisomo

Hiswnul-Muslim

021-Du’aa Za Sijdah Ya Kisomo

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[50]

سَجَـدَ وَجْهـي للَّـذي خَلَقَـهُ وَصَـوَّرَهُ وَشَقَّ سَمْـعَـهُ وَبَصَـرَهُ بِحَـوْلِـهِ وَقُـوَّتِهِ فَتَبَارَكَ اللَّـهُ أَحْسَنُ الْخَالِقِينَ

 

Sajada wajhiya liLLadhiy khalaqahu, wa swaw-warahu, wa shaqqa sam-’ahu wa baswarahu bihawlihi wa quwwatihi, fa-Tabaaraka-Allaahu Ahsanul-Khaaliqiyn

 

Umesujudu uso wangu kumsujudia Ambaye Ameuumba na Akapasuwa masikio yake, na macho yake, kwa uwezo Wake na nguvu Zake,  ((Amebarikika Allaah Mbora wa waumbaji))[1]

 

 

 

[51]

 

اللّهُـمَّ اكْتُـبْ لي بِهـا عِنْـدَكَ أَجْـراً، وَضَـعْ عَنِّـي بِهـا وِزْراً، وَاجْعَـلها لي عِنْـدَكَ ذُخْـراً، وَتَقَبَّـلها مِنِّـي كَمـا تَقَبَّلْتَـها مِنْ عَبْـدِكَ دَاوُد

 

Allaahummak-tubliy bihaa ’Indaka ajran, wa dhwa’  ’anniy bihaa wizran, waj-’alhaa liy ’Indaka dhukhran, wa taqabbalhaa minniy kamaa taqabbaltahaa min ’abdika Daawuwd

 

Ee Allaah Niandikie Kwako kwa sijdah hii malipo, na Nifutie kwayo madhambi, na Ijaalie kwangu mbele Yako ni akiba, na Nikubalie kama Ulivyomkubalia mja wako Daawuwd.[2].

 

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) - At-Tirmidhiy (2/474), Ahmad (6/30), na Al-Haakim na Adh-Dhahabiy ameisahihisha(1/220) kwa ziada yake na Aayah ni namba (14) ya Suwratul-Muu-minuwn.   

[2]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  At-Tirmidhiy (2/473), Al-Haakim na Adh-Dhahabiy ameisahihisha (1/219).

 

 

Share

022-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Tashahhud

Hiswnul-Muslim

022-Du’aa Ya Tashahhud

www.alhidaaya.com

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[52]

 

التَّحِيّـاتُ للهِ وَالصَّلَـواتُ والطَّيِّـبات، السَّلامُ عَلَيـكَ أَيُّهـا النَّبِـيُّ وَرَحْمَـةُ اللهِ وَبَرَكـاتُه، السَّلامُ عَلَيْـنا وَعَلـى عِبـادِكَ الصَّـالِحـين، أَشْـهَدُ أَنْ لا إِلـهَ إِلاّ الله، وَأَشْـهَدُ أَنَّ مُحَمّـداً عَبْـدُهُ وَرَسـولُه

 

At-tahiyyaatu liLLaahi, was-swalawaatu, wat-twayyibaatu, Assalaamu ‘alayka ayyuhan-Nnabiyyu warahmatu-Allaahi wa Barakaatuh, Assalaamu ‘alaynaa wa ’alaa ‘IbaadiLLaahis-swaalihiyn. Ash-hadu an-laa ilaaha illa-Allaah wa ash-hadu anna Muhammadan ‘Abduhu wa Rasuwluhu

 

Maamkuzi mema na Rehma na mazuri yote (ni kwa Allaah), amani ziwe juu yako ee Nabiy na Rehma za Allaah na Baraka Zake,  amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Allaah walio wema. Nashuhudia kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na nashuhudia kwamba Muhammad ni mja Wake na ni Rasuli Wake[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رضي الله عنه)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (2/311), Muslim (1/301).

 

 

Share

023-Hiswnul-Muslim :Kumswalia Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) Baada Ya Tashahhud

Hiswnul-Muslim

023-Kumswalia Nabiy Muhammad  (صلى الله عليه وآله وسلم) Baada Ya Tashahhud

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[53] 

 

اللّهُـمَّ صَلِّ عَلـى مُحمَّـد وَعَلـى آلِ مُحمَّد كَمـا صَلَّيـتَ عَلـى إبْراهـيمَ وَعَلـى آلِ إبْراهـيم إِنَّكَ حَمـيدٌ مَجـيد، اللّهُـمَّ بارِكْ عَلـى مُحمَّـد وَعَلـى آلِ مُحمَّـد كَمـا بارِكْتَ عَلـى إبْراهـيمَ وَعَلـى آلِ إبْراهيم إِنَّكَ حَمـيدٌ مَجـيد .

 

Allaahumma Swalli ‘alaa Muhammad wa ‘alaa aali Muhammad, kamaa Swallayta ‘alaa Ibraahiyma wa ‘alaa aali Ibraahiyma, Innaka Hamiydun Majiyd. Allaahumma Baarik ‘alaa Muhammad, wa ‘alaa aali Muhammad, kamaa Baarakta ‘alaa  Ibraahiyma wa ‘alaa  aali Ibraahiyma, Innaka Hamiydun Majiyd.

 

Ee Allaah! Mswalie Muhammad, na ahli wa Muhammad, kama Ulivyomswalia Ibraahiym na juu ya ahli zake Ibraahiym, hakika Wewe ni Mwenye Kusifika Mtukufu. Ee Allaah! Mbariki Muhammad na ahli zake Muhammad kama Ulivyombariki Ibraahiym na juu ya ahli zake Ibraahiym, hakika Wewe ni Mwenye Kusifika Mtukufu[1]

 

 

[54]

 

اللّهُـمَّ صَلِّ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى أَزْواجِـهِ وَذُرِّيَّـتِه كَمـا صَلَّيْـتَ عَلـى آلِ إبْراهـيم، وَبارِكْ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى أَزْواجِـهِ وَذُرِّيَّـتِه كَمـا بارِكْتَ عَلـى آلِ إبْراهـيم إِنَّكَ حَمـيدٌ مَجـيد

 

Allaahumma Swalli ‘alaa Muhammad, wa ‘alaa azwaajihi wa dhurriyaatihi, kamaa Swallayta ‘alaa aali Ibraahiyma, wa Baarik ‘alaa Muhammad, wa ’alaa azwaajihi wa dhurriyaatihi, kamaa Baarakta ‘alaa aali Ibraahiyma, Innaka Hamiydun Majiyd

 

 

Ee Allaah! Mswalie Muhammad na wake zake na kizazi chake, kama Ulivyowaswalia ahli zake Ibraahiym, na Mbariki Muhammad na wake zake na kizazi chake kama Ulivyowabariki ahli zake Ibraahiym, hakika Wewe ni Mwenye Kusifika Mtukufu[2].

 

 

[1]Hadiyth ya Ka’ab bin ‘Ujrah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/408)

[2]Hadiyth ya Abu Humayd As-Saa’adiy Al-Mundhir (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/407), Muslim (1/306) na tamashi lake.

 

 

Share

024-Hiswnul-Muslim: Du’aa Baada Ya Tashahhud Kabla Ya Salaam

Hiswnul-Muslim

024-Du’aa Baada Ya Tashahhud Kabla Ya Salaam

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[55]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِـنْ عَذابِ القَـبْر، وَمِـنْ عَذابِ جَهَـنَّم، وَمِـنْ فِتْـنَةِ المَحْـيا وَالمَمـات، وَمِـنْ شَـرِّ فِتْـنَةِ المَسيحِ الدَّجّال

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika min ‘adhaabil qabri, wa min ‘adhaabi jahannam, wamin fitnatil mahyaa wal mamaati, wamin sharri fitnatil-Masiyhid-dajjaal

 

Ee Allaah hakika mimi najikinga Kwako na adhabu za kaburi, na adhabu ya Jahannam, na fitna ya uhai, na (fitna) ya kufa, na shari ya fitna ya Masihi-dajjaal[1].

 

 

 

[56]

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِـنْ عَذابِ القَـبْر، وَأَعـوذُ بِكَ مِـنْ فِتْـنَةِ المْسيحِ الدَّجّـال، وَأَعـوذُ بِكَ مِـنْ فِتْـنَةِ المْحْـيا وَالمْمـات. اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِنَ المْأْثَـمِ وَالمْغْـرَم

 

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika min ‘adhaabil qabri, wa a’uwdhu bika min fitnatil Masiyhid-dajaal wa a’uwdhu bika min fitnatil mahyaa wal mamaat, Allaahumma inniy a’uwdhu bika minal ma-athami wal maghrami

 

Ee Allaah!  Hakika mimi najikinga Kwako na adhabu ya kaburi, na najikinga Kwako na fitna ya Masihid-dajjaal, na najikinda Kwako na fitna ya uhai na (fitna) ya mauti, Ee Allaah, hakika mimi najikinda Kwako kutokana na dhambi na deni[2]

 

 

 

 [57]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي ظَلَـمْتُ نَفْسـي ظُلْمـاً كَثـيراً وَلا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْت، فَاغْـفِر لي مَغْـفِرَةً مِنْ عِنْـدِك وَارْحَمْـني إِنَّكَ أَنْتَ الغَـفورُ الرَّحـيم

Allaahumma inniy dhwalamtu nafsiy dhwulman kathiyraa, walaa  yaghfirudh-dhunuwba illa Anta, faghfir liy maghfiratan min ’Indika warhamniy, Innaka Antal-Ghafuwrur-Rahiym

 

Ee Allaah hakika mimi nimejidhulumu nafsi yangu dhulma nyingi, na haghufurii (yeyote) madhambi ila Wewe, basi nighufurie maghfira kutoka Kwako, na Unirehemu, hakika Wewe ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu[3].

 

 

[58]

 

اللّهُـمَّ اغْـفِرْ لي ما قَدَّمْـتُ وَما أَخَّرْت، وَما أَسْـرَرْتُ وَما أَعْلَـنْت، وَما أَسْـرَفْت، وَما أَنْتَ أَعْـلَمُ بِهِ مِنِّي أَنْتَ المُقَـدِّمُ، وَأَنْتَ المُـؤَخِّـرُ لا إِلهَ إِلاّ أَنْـت

 

Allaahuumaghfir liy maa qaddamtu wamaa akh-khartu, wamaa asrartu, wamaa a’-lantu, wamaa asraftu, wamaa Anta A’-lamu bihi minniy Antal-Muqaddimu wa  Antal-Muakh-khiru laa ilaaha illaa Anta

 

Ee Allaah nighufurie niliyoyatanguliza, na niliyoyachelewesha, na niliyoyafanya kwa siri, na niliyoyafanya kwa dhahiri na niliyoruka mipaka, na ambayo Wewe Unayajua zaidi kuliko mimi, Wewe Ndiye mwenye kutanguliza na Wewe Ndiye mwenye kuchelewesha, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe[4]

 

 

[59]

اللّهُـمَّ أَعِـنِّي عَلـى ذِكْـرِكَ وَشُكْـرِك وَحُسْـنِ عِبـادَتِـك

 

Allaahumma A’inniy ’alaa dhikrika washukrika wahusni ’Ibaadatika

 

Ee Allaah nisaidie kukudhukuru, na kukushukuru, na uzuri wa kukuabudu[5].

 

 

 

[60]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعوذُ بِكَ مِنَ البُخْـل، وَأَعوذُ بِكَ مِنَ الجُـبْن، وَأَعوذُ بِكَ مِنْ أَنْ أُرَدَّ إِلى أَرْذَلِ الـعُمُر، وَأَعوذُ بِكَ مِنْ فِتْنَـةِ الدُّنْـيا وَعَـذابِ القَـبْر.

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika minal-bukhli, wa a’uwdhu Bika minal-jubni, wa a’uwudhu Bika min an uradda ilaa ardhalil-’umri, wa a’uwudhu Bika min fitnatid-duniyaa wa ’adhaabil-qabr

 

Ee Allaah najikinga Kwako kutokana na ubakhili, na najikinga Kwako kutokana na uwoga, na najikinga Kwako kutokana na kurudishwa kwenye umri duni, na najikinga Kwako kutokana na fitna ya dunia na adhabu ya kaburi[6].

 

 

 

[61]

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ الجَـنَّةَ وأَعوذُ بِـكَ مِـنَ الـنّار

 

Allaahumma inniy as-alukal-Jannah wa a’uwdhu Bika minan-naar

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba Jannah na najikinga Kwako kutokana na Moto[7]

 

 

 

[62]

 

اللّهُـمَّ بِعِلْـمِكَ الغَـيْبِ وَقُـدْرَتِـكَ عَلـى الْخَلقِ, أَحْـيِني ما عَلِـمْتَ الحـياةَ خَـيْراً لـي، وَتَوَفَّـني إِذا عَلِـمْتَ الوَفـاةَ  خَـيْراً  لـي، اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْـأَلُـكَ خَشْيَتَـكَ في الغَـيْبِ وَالشَّهـادَةِ، وَأَسْـأَلُـكَ كَلِمَـةَ الحَـقِّ في الرِّضـا وَالغَضَـب، وَأَسْـأَلُـكَ القَصْدَ في الغِنـى وَالفَقْـر، وَأَسْـأَلُـكَ  نَعـيماً لا يَنْفَـد، وَأَسْـأَلُـكَ قُـرَّةَ عَيْـنٍ لا تَنْـقَطِعْ  وَأَسْـأَلُـكَ الرِّضـا بَعْـدَ القَضـاء، وَأَسْـأَلُـكَ بًـرْدَ الْعَـيْشِ بَعْـدَ الْمَـوْت، وَأَسْـأَلُـكَ لَـذَّةَ النَّظَـرِ إِلـى وَجْـهِكَ وَالشَّـوْقَ إِلـى لِقـائِـك، في غَـيرِ ضَـرّاءَ مُضِـرَّة، وَلا فِتْـنَةٍ مُضـلَّة، اللّهُـمَّ  زَيِّـنّا بِزينَـةِ الإيـمان، وَاجْـعَلنا هُـداةً مُهْـتَدين

 

Allaahumma bi ‘ilmikal-ghaybi wa Qudratika ‘alalkhalqi, Ahyiniy maa ‘alimtal-hayaata khayralliy, wa Tawaffaniy idhaa ‘alimtal-wafaata khayralliy. Allaahumma inniy as-aluka khashyataka filghaybi wash-shahaadati, wa as-aluka kalimatal-haqqi fir-ridhwaa walghadhwabi, wa as-alukal qaswda fil-ghinaa walfaqri, wa as-aluka na’iyman laa yanfadu, wa as-aluka qurrata ‘aynin laa tanqatwi’u, wa as-alukar-ridhwaa ba’dal-qadhwaai, wa as-aluka bardal-‘ayshi ba’dal-mawti, wa as-aluka laddhatan-nadhwari ilaa Wajhika, wash-shawqa ilaa liqaaika fiy ghayri dhawarraa mudhwirratin walaa fitnatin mudhwillatin. Allaahumma zayyinaa biziynatil-iymaani waj-’alnaa hudaatan muhtadiyna

 

Ee Allaah naomba kwa ujuzi Wako wa ghaibu na uwezo Wako juu Ulivyooumba, nihuishe ikiwa Unajua kwamba uhai ni bora kwangu, na nifishe ikiwa Unajua kuwa mauti ni bora kwangu. Ee Allaah, nakuomba kukuhofu Kwako kwa siri na dhahiri, na nakuomba neno la haki wakati wa furaha na ghadahbu, na nakuomba unifanye wastani (usawa) wakati wa utajiri na umasikini, na nakuomba neema isiyokoma, na kitulizo cha macho kisichokatika, na nakuomba niridhike kwa Uliyonikidhia (majaaliwa), na nakuomba maisha ya kuburudika baada ya mauti, na nakuomba ladha ya kukutazama Wajihi Wako na shauku ya kukutana Nawe, pasi na madhara yanayodhuru au fitna itakayoleta upotofu. Ee Allaah, tupambie kwa kipambo cha imani na tujaalie tuwe waongozi wenye kuongoka[8]

 

 

 

[63]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ يا اللهُ بِأَنَّـكَ الواحِـدُ الأَحَـد، الصَّـمَدُ الَّـذي لَـمْ يَلِـدْ وَلَمْ يولَدْ، وَلَمْ يَكـنْ لَهُ كُـفُواً أَحَـد، أَنْ تَغْـفِرْ لي ذُنـوبي إِنَّـكَ أَنْـتَ الغَفـورُ الرَّحِّـيم

 

Allaahumma inniy as-aluka yaa Allaahu biannakal-Waahidu Al-Ahadu, Asw-Swamadu Alladhiy lam yalid walam yuwlad walam yakun lahu kufuwan ahad, an Taghfiraliy dhunuwbiy Innaka Antal-Ghafuwrur-Rahiym

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba, Ee Allaah kwa vile Wewe ni Mmoja Uliye Pekee, Mwenye kutegemewa kwa haja zote, Ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa, na wala hakuna mfano wake na kitu chochote, nakuomba unighufurie madhambi yangu hakika Wewe ni Mwingi wa kughufuria Mwenye kurehemu[9].

 

 

 

 [64]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ بِأَنَّ لَكَ الْحَـمْدُ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْـتَ وَحْـدَكَ لا شَـريكَ لَـكَ المَنّـانُ يا بَديـعَ السَّمواتِ وَالأَرْضِ يا ذا الجَلالِ وَالإِكْـرام، يا حَـيُّ يا قَـيّومُ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ الجَـنَّةَ وَأَعـوذُ بِـكَ مِنَ الـنّار

 

Allaahumma inniy as-aluka bianna Lakal-Hamdu laa ilaaha illaa Anta Wahdaka laa shariyka Laka Al-Mannaanu yaa Badiy’as-samaawaati wal-ardhwi, yaadhal-Jalaali wal Ikiraami, yaa Hayyu yaa Qayyuwmu, inniy as-alukal-Jannata wa a’uwdhu bika minan-naari

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba, kwa vile Himdi ni Zako, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, hali ya kuwa Peke Yako huna mshirika, Mwingi wa Kuneemesha. Ee Mwanzishi wa mbingu na ardhi, Ee Mwenye Utukufu na Ukarimu, Ee Uliyehai daima, Msimamizi wa kila kitu, hakika mimi nakuomba Jannah, na najikinga Kwako kutokana na Moto[10]

 

 

 

[65]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ بِأَنَّـي أَشْـهَدُ أَنَّـكَ أنْـتَ اللهُ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْـت، الأَحَـدُ الصَّـمَدُ الَّـذي لَـمْ يَلِـدْ وَلَمْ يولَـدْ، وَلَمْ يَكـنْ لَهُ كُـفُواً أَحَـد.

Allaahumma inniy as-aluka bianniy ash-hadu Annaka Anta-Allaahu laa ilaaha illaa Anta Al-Ahadu Asw-Swamadu Alladhiyy lam yalid walam yuwlad walam yakun lahu kufuwan ahad

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba kwa vile nashuhudia  kwamba hakika Wewe ni Allaah hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, hali ya kuwa Pekee, Mwenye Kutegemewa kwa haja zote, Ambaye hakuzaa wala hakuzaliwa, na wala hakuna mfano wake na kitu chochote[11]

 

 

 


[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (2/102), Muslim (1/412), na tamshi la Muslim

[2]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) - Al-Bukhaariy (1/202), Muslim (1/412) na tamshi lake.

[3]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy (8/168),  Muslim (4/2078) 

[4]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه) - Muslim (1/534)

[5]Hadiyth ya Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (2/86), An-Nasaaiy (3/53) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/284)

[6]Hadiyth ya Sa’iyd bin Abi Waqqaasw (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/35) [2822]

[7]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd [792] na ibn Maajah na angalia: Swahiyh ibn Maajah (2/328)

[8]Hadiyth ya ‘Ammaar bin Yaasir (رضي الله عنه) - An-Nasaaiy (4/54-55), Ahmad  (4/364) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh An-Nasaaiy (1/280/281)

[9]Hadiyth ya Mahijan bin Al-Arda’ (رضي الله عنه) - An-Nasaaiy kwa tamshi lake (3/52), Ahmad (4/238) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh An-Nasaaiy (1/280)

[10]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) Imetaja mwisho wa Hadiyth:

((لَقَدْ دَعَا اللَّهَ بِاسْمِهِ الْأَعْظَمِ الَّذِي إِذَا دُعِيَ بِهِ أَجَابَ وَإِذَا سُئِلَ بِهِ أَعْطَى))

((kwa yakini amemuomba Allaah kwa Jina Lake Tukufu ambalo Anapoombwa kwalo Anaitikia na Anapotakwa kwalo jambo hutoa)) - Ahlus-Sunan; Abu Daawuwd [1495], An-Nasaaiy (3/52), ibn Maajah [3858] na taz Swahiyh ibn Maajah (2/329)

[11]Hadiyth ya Buraydah bin Al-Huswayb Al-Aslamiyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (2/62) [1493], At-Tirmidhiy (5/515) [3475], Ibn Maajah (2/1267) [3857], Ahmad (5/360), na angalia: Swahiyh ibn Maajah (2/329) na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/163)

 

 

Share

025-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Baada Ya Kutoa Salaam Ya Kumaliza Swalaah

Hiswnul-Muslim

025-Nyiradi Baada Ya Kutoa Salaam Ya Kumaliza Swalaah

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[66]

أَسْـتَغْفِرُ الله، أَسْـتَغْفِرُ الله، أَسْـتَغْفِرُ الله، اللّهُـمَّ أَنْـتَ السَّلامُ، وَمِـنْكَ السَّلام، تَبارَكْتَ يا ذا الجَـلالِ وَالإِكْـرام

 

Astaghfiru-Allaah, Astaghfiru-Allaah, Astaghfiru-Allaah. Allaahumma Antas-Salaam, wa Minkas-salaam, Tabaarakta yaa dhal-Jalaali wal-Ikraam

 

 

Namuomba Allaah maghfirah, Namuomba Allaah maghfirah,  Namuomba Allaah maghfirah. Ee Allaah Wewe Ndiye As-Salaam na Kwako ndiko kutokako amani, Umebarikika Ee Mwenye Ujalali na Ukarimu [1].

 

 

 

[67]

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْد، وهوَ على كلّ شَيءٍ قَدير، اللّهُـمَّ لا مانِعَ لِما أَعْطَـيْت، وَلا مُعْطِـيَ لِما مَنَـعْت، وَلا يَنْفَـعُ ذا الجَـدِّ مِنْـكَ الجَـد

 

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr. Allaahumma laa maani’a limaa A’-twayta, walaa mu’-twiya limaa mana’-ta, walaa yanfa’u dhal-jaddi Minkal-jaddu

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah hali ya kuwa Peke Yake Hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi, na Yeye ni Muweza wa kila kitu.  Ee Allaah, hakuna mwenye kukizuia Ulichokitoa, wala mwenye kutoa Ulichokizuia, na wala utajiri wa mtu haumnufaishi mwenye utajiri mbele Yako[2].

 

 

 

[68]

 

لا إلهَ إلاّ اللّه وحدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ الملكُ ولهُ الحَمد، وهوَ على كلّ شيءٍ قدير، لا حَـوْلَ وَلا قـوَّةَ إِلاّ بِاللهِ، لا إلهَ إلاّ اللّـه، وَلا نَعْـبُـدُ إِلاّ إيّـاه، لَهُ النِّعْـمَةُ وَلَهُ الفَضْل وَلَهُ الثَّـناءُ الحَـسَن، لا إلهَ إلاّ اللّهُ مخْلِصـينَ لَـهُ الدِّينَ وَلَوْ كَـرِهَ الكـافِرون

 

 

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr. Laa hawla walaa quwwata illaa biLLaah. Laa ilaaha illa-Allaah. Walaa na’-budu illaa Iyyaahu. Lahun-Ni’-matu walahul-fadhwlu walahuth-thanaaul-hasan. Laa ilaaha illa-Allaah Mukhliswiyna Lahud-diyna walaw karihal-kaafiruwn

 

”Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah hali ya kuwa Peke Yake Hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi, na Yeye ni Muweza wa kila kitu, hapana uwezo wala nguvu ila kutoka kwa Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, wala hatumwabudu ila Yeye, ni Zake neema, na ni Wake ubora, na ni Zake Sifa nzuri zote, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali ya kumtakasia Dini Yake, ijapokuwa wanachukia makafiri [3].

 

 

[69]

 سُـبْحانَ الله (ثلاثاً وثلاثين)

 

Subhaana-Allaah (mara 33)

 

Utakasifu ni wa Allaah  

الحَمْـدُ لله (ثلاثاً وثلاثين)    

 

 AlhamduliLlaah (mara 33)

 

 Himdi Anastahiki Allaah 

واللهُ أكْـبَر (ثلاثاً وثلاثين)

 

Allaahu Akbar (mara 33)

 

Allaah ni Mkubwa  

 

 

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحْـدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ الملكُ ولهُ الحَمْد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَـدير

 

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu wa-Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah, hali ya kuwa Peke Yake Hana mshirika. Wake ni Ufalme na ni Zake Himdi na Yeye ni Muweza wa kila kitu[4].

 

 

 بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيم. قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾ اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ﴿٣﴾ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ ﴿٤﴾

 

 

  بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ .قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾ مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ﴿٢﴾ وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ ﴿٣﴾ وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ ﴿٤﴾ وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ ﴿٥﴾

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ .قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ﴿١﴾ مَلِكِ النَّاسِ ﴿٢﴾ إِلَـٰهِ النَّاسِ ﴿٣﴾ مِن شَرِّ الْوَسْوَاسِ الْخَنَّاسِ ﴿٤﴾ الَّذِي يُوَسْوِسُ فِي صُدُورِ النَّاسِ ﴿٥﴾ مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ ﴿٦﴾

 

 

 (Kila baada ya Swalaah)[5]  

 

 

 

[71]

 

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ ۚ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۖ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا ۚ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٢٥٥

 

(Kila baada ya Swalaah) [6]

 

 

 

[72]

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ المُلكُ ولهُ الحَمْد، يُحيـي وَيُمـيتُ وهُوَ على كُلّ شيءٍ قدير. 

 

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu, Yuhyi wa Yumiytu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali ya kuwa Peke Yake, Hana mshirika. Ni wake Ufalme, na ni Zake Himdi, Anahuisha, Anafisha, na Yeye ni Muweza wa kila kitu.

(Mara 10 kila baada ya Swalaah ya Alfajiri na Magharibi)[7]  

 

 

 

[73]

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ عِلْمـاً نافِعـاً، وَرِزْقـاً طَيِّـباً، وَعَمَـلاً مُتَقَـبَّلاً

 

Allaahumma inniy as-aluka ’ilman-naafi’an, warizqan-twayyiban, wa ’ilman mutaqabbalaa

 

Ee Allaah,  nakuomba elimu yenye kunufaisha, na riziki iliyo nzuri, na ’amali zenye kutakabaliwa.   

(Baada ya kutoa salamu ya Swalaah ya Alfajiri) [8]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Thawbaan Al-Haashimiy (رضي الله عنه) - Muslim (1/414) [591]

[2]Hadiyth ya Al-Mughiyrah bin Shu’bah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (1/255) [844], Muslim (1/414) [593]. Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah ibn Zubayr amesema:  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akitamka Tahliyl (laa ilaaha illa Allaah) kila baada ya Swalaah:

 

[3]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Zubayr (رضي الله عنه) - Muslim (1/415) [594]

[4]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:    

 

((من سبح دبر كل صلاة ثلاثا وثلاثين وكبر ثلاثا وثلاثين وحمد ثلاثا وثلاثين وختم المائة بلا إله إلا الله وحده لا شريك له له الملك وله الحمد وهو على كل شيء قدير غفرت ذنوبه ولو كانت مثل زبد البحر))

((Atakaye sabbih kila baada ya Swalaah mara thelathini na tatu, akaleta takbiyr mara thelathini na tatu, akaleta tahmiyd mara thelathini na tatu akamalizia kwa Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah, Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu wa-Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr - ataghufuriwa makosa yake japokuwa ni mfano wa povu la bahari)) - Muslim (1/418) [597]

[5]Hadiyth ya ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) Suwrah mbili hizo [113 na 114) zinajulikana kama: “al-Maw’idhatayn” (zenye kukinga) na pia imetajwa kusomwa pia Suwrah Al-Ikhlaasw (112). Abu Daawuwd (2/86) [1523], An-Nasaaiy (3/68), na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (2/8) Na angalia: Fat-hul Baariy (9/62). 

 

[6]Hadiyth ya Abu Amaamah Al-Baahiliyy Swudayyu bin ‘Ajlaan (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 ((مَنْ قَرَأَ آيَةَ الْكُرْسِيِّ دُبُرَ كُلِّ صَلاةٍ مَكْتُوبَةٍ لَمْ يَمْنَعْهُ مِنْ دُخُولِ الْجَنَّةِ، إِلا الْمَوْتُ))

 ((Atakayeisoma kila baada ya Swalaah hakuna kitakachomzuia kuingia Jannah isipokuwa mauti) An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-yawm wal-laylah [1000] na ibn As-Sunniy [121], na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Al-Jaami’ (5/339) [6464], na Silsilat Al-Ahaadiyth As-Swahiyhah (2/697) [972].

[7]Hadiyth ya Abu Dhar Al-Ghafaariy Jundub bin Junaadah na wengineo (رضي الله عنهم)  Imekuja kauli yake (صلى الله عليه وسلم):

 ((مَنْ قالَ فِي دُبُرِ صَلاةِ الصُّبْحِ وَهُوَ ثانٍ رِجْلَيهِ قَبْلَ أنْ يَتَكَلَّمَ: لا إِلهَ إِلاَّ اللَّهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ يُحْيي وَيُمِيتُ وَهُوَ على كُلّ شَيْءٍ قَدِيرٌ عَشْرَ مرَّاتٍ كُتِبَ لَهُ عَشْرُ حَسَناتٍ، ومُحِيَ عَنْهُ عَشْرُ سَيِّئاتٍ، وَرُفِعَ لَهُ عَشْرُ دَرَجاتٍ، وكانَ يَوْمَهُ ذلكَ فِي حِرْزٍ مِنْ كُلّ مَكْرُوهٍ وَحُرِسَ مِنَ الشَّيْطانِ ولَمْ يَنْبَغِ لِذَنْبٍ أنْ يُدْرِكَهُ في ذلكَ اليَوْمِ إِلاَّ الشِّرْكَ باللَّهِ تَعالى))

((Atakayesema kila baada ya Swalaah ya Alfajiri kabla hajasogea kuondoka, na kabla ya kuongea na mtu ………. mara kumi, ataandikiwa mazuri kumi, na atafutiwa maovu kumi, na atapandishwa daraja kumi [za thawabu], na atalindwa siku hiyo na kila maovu na atakingwa na shaytwaan na hakuna dhambi itakayomkumba siku hiyo [ikamharibia amali zake] isipokuwa kumshirikisha Allaah Ta’aalaa)) -   At-Tirmidhiy (5/515) [3474], Ahmad (4/227) na angalia mapokezi yake  katika ‘Zaad Al-Ma’aad’ (1/300)

[8]Hadiyth ya Ummu Salamah (رضي الله عنها)    Ibn Maajah [925] na wengineo. Na angalia: Swahiyh Ibn Maajah (1/152) na Majma’ Az-Zawaaid (10/111).

 

 

Share

026-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Swalaatul-Istikhaarah

Hiswnul-Muslim

026-Du’aa Ya Swalaatul-Istikhaarah[1]

 

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[74]

 

عَنْ جَابِرٍ رضي الله عنه قَالَ : كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يُعَلِّمُنَا الاسْتِخَارَةَ  فِي الأُمُورِ كُلِّهَا كَمَا يُعَلِّمُنَا السُّورَةَ مِنْ الْقُرْآنِ يَقُولُ : إذَا هَمَّ أَحَدُكُمْ بِالأَمْرِ فَلْيَرْكَعْ رَكْعَتَيْنِ مِنْ غَيْرِ الْفَرِيضَةِ ثُمَّ لِيَقُلْ

 

Jaabir Bin ’Abdillaah  (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah  (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akitufundisha Swalaah ya Istikhaarah kama vile anavyotufunza Suwrah ya Qur-aan, akisema: ((Akikusudia mmoja wenu kufanya jambo, aswali rakaa mbili zisizo za faradhi, kisha aseme:

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْتَخيـرُكَ بِعِلْمِك، وَأسْتَقْـدِرُكَ بِقُـدْرَتِـك، وَأَسْـألُـكَ مِنْ فَضْـلِكَ العَظـيم، فَإِنَّـكَ تَقْـدِرُ وَلا أَقْـدِر، وَتَـعْلَـمُ وَلا أَعْلَـم، وَأَنْـتَ عَلاّمُ الغُـيوب، اللّهُـمَّ إِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ  (وَيُسَـمِّي  حاجته)  خَـيْرٌ لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري،  عَاجِلِهِ و آجِلِه , فَاقْـدُرْهُ لي وَيَسِّـرْهُ لي ثـمَّ بارِكْ لي فيـه، وَإِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ شَـرٌ  لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري،  عَاجِلِهِ و آجِلِه  فَاصْرِفْـهُ عَنّيِ  وَاصْرِفْني عَنْـهُ وَاقْـدُرْ ليَ الخَـيْرَ  حَيْـثُ كانَ ثُـمَّ أَرْضِـني بِـه.

 

Allaahumma inniy Astakhiruka bi ‘Ilmika, wa Astaqdiruka bi Qudratika, wa As-aluka min Fadhwlikal-‘Adhwiym, Fainnaka Taqdiru walaa aqdir, wa-Ta’-lam walaa a’-lam, wa-Anta ‘Allaamul-ghuyuwb. Allaahumma in Kunta Ta’-lamu anna haadhal-amra (ataje mtu hapa jambo lake) khayrul-liy fiy Diyniy wama’aashiy wa ’aaqibati  amriy ‘aajilihi wa aajilihi, Faqdurhu liy wa-Yassirhu liy thumma Baarik liy fiyh. Wain Kunta Ta’-lam anna haadhal-amra sharru liy fiy Diyniy wama’aashiy wa ’aaqibati  amriy ‘aajilihi wa aajilihi, Faswrifhu ‘annyi wa-Swrifniy ‘anhu waqdurliyal-khayra haythu kaana thumma Ardhwiniy bih

 

Ee Allaah hakika mimi nakutaka (muongozo) unichagulie kwa ujuzi Wako, na nakuomba Uniwezeshe kwa uwezo Wako, na nakuomba fadhila Zako kubwa, hakika Wewe Unaweza, nami siwezi, Nawe unajua nami sijui, Nawe ni Mjuzi wa ya ghayb. Ee Allaah, iwapo jambo hili kutokana na ujuzi Wako (utalitaja jambo lako) lina kheri na mimi katika Dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu,

katika Dunia yangu na Aakhirah yangu, basi nakuomba Uniwezeshe nilipate, na Unifanyie wepesi, kisha Unibariki. Na iwapo Unajua kwamba jambo hili ni shari kwangu katika Dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu katika Dunia yangu na Aakhirah yangu, basi liepushe na mimi nami niepushe nalo, na nipangie jambo jengine lenye kheri nami popote lilipo, kisha niridhishe kwalo[2].

 

Na hajuti mwenye kumtaka Itsikhaara Allaah na akawashauri waja waumini na akajidhatiti jambo lake. Anasema Allaah (سبحانه وتعالى)

وَشَاوِرْهُمْ فِي الْأَمْرِ ۖ فَإِذَا عَزَمْتَ فَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ

 ((na washauri katika mambo. Na unapoazimia basi tawakali kwa Allaah)[3]

 

 

 


[1] Istikhaarah ni kuomba chaguo. Na Swalaah hii inakusudiwa mtu anapotaka kufanya jambo fulani lenye kukubalika katika Shariy’ah kama mfano kuoa, kusafiri, kuchagua kazi, kuchagua masomo ya kidunia n.k basi unamwachia Allaah (سبحانه وتعالى) Akuchagulie. Kwa maana baada ya kuiswali Swalaah hii utakavyojaaliwa kupata mwongozo basi itakuwa umeshamkabili Allaah (سبحانه وتعالى) na umetwakali Kwake.

[2] Al-Bukhaariy (7/162) [1162]

[3] Aal-‘Imraan (3:159)

 

 

Share

027-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni

Hiswnul-Muslim

027-Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

 

Nyiradi za asubuhi na jioni.[1] Asubuhi ni baada ya Swalaah ya Alfajiri mpaka jua kuchomoza. Na jioni ni baada ya Swalaah ya Alasiri mpaka jua kuzama. Ila baadhi ya ‘Ulamaa wamesema kuwa baada ya jua kuzama na kuendelea. 

 

الْحَمْدُ لِلَّه وَحْدَهُ وَالصًّلاَةُ وَالسَّلاَمُ عَلَى مَنْ لاَ نَبَيِّ بَعْدَهُ

 

AlhamduliLlaahi Wahdahu was-Swalaatu was-salaamu ‘alaa man-laa Nabiyyi ba’dahu

 

Himdi ni za Allaah Pekee, Rehma na amani ziwe juu ya ambaye hakuna Nabiy baada yake.

 

 

[75]

 

أَعُوذُ بِاللّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ .

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ ۚ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۖ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا ۚ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٢٥٥[2]

 

 

 

 [76]

 

Soma Suwrah zifuatazo mara tatu kila moja[3]

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيم. قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾ اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ﴿٣﴾ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ ﴿٤﴾

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾ مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ﴿٢﴾ وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ ﴿٣﴾ وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ ﴿٤﴾وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ ﴿٥﴾

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ .قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ﴿١﴾ مَلِكِ النَّاسِ ﴿٢﴾ إِلَـٰهِ النَّاسِ ﴿٣﴾ مِن شَرِّ الْوَسْوَاسِ الْخَنَّاسِ ﴿٤﴾ الَّذِي يُوَسْوِسُ فِي صُدُورِ النَّاسِ ﴿٥﴾ مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ ﴿٦﴾

 

 

 

 [77]

أَصْـبَحْنا وَأَصْـبَحَ المـلكُ لله وَالحَمدُ لله، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحدَهُ لا شَريكَ لهُ، لهُ المُـلكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كلّ شَيءٍ قدير، رَبِّ أسْـأَلُـكَ خَـيرَ ما في هَذا الْيَوْمِ  وَخَـيرَ ما بَعْـدَهُ، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّ هَذا الْيَوْمِ  وَشَرِّ ما بَعْـدَهُ، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكَسَـلِ وَسـوءِ الْكِـبَر، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنْ عَـذابٍ في النّـارِ  وَعَـذابٍ في القَـبْر  

 

Aswbahnaa wa aswbahal-Mulku liLLaah wal-HamduliLlaah. Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu, wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr. Rabbi as-aluka khayra maa fiy haadhal yawmi wakhayra maa ba’-daahu, wa a’uwdhu bika minsharri haadhal yawmi washarri maa ba’-dahuu, Rabbi a’uwdhu bika minalkasli wasuw-il kibari, Rabbi a’uwdhu bika min ‘adhaabin finnaari wa ‘adhaabin filqabri

 

Tumeingia wakati wa asubuhi na umekuwa Ufalme ni wa Allaah,  na Himdi ni Zake Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali yakuwa Peke Yake, Hana mshirika. Ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza.  Rabb wangu, nakuomba kheri ya siku ya leo, na kheri ya baada ya siku hii, na ninajikinga Kwako kutokana na shari ya siku ya leo na shari ya baada ya siku hii.  Rabb wangu, najikinga Kwako kutokana na uvivu, na ubaya wa uzee ubaya. Rabb wangu, najikinga Kwako kutokana na adhabu ya Moto na adhabu ya kaburi[4] 

 

Na ikiingia jioni useme: 

 

 أَمْسَيْـنا وَأَمْسـى المـلكُ لله وَالحَمدُ لله، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحدَهُ لا شَريكَ لهُ، لهُ المُـلكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كلّ شَيءٍ قدير، رَبِّ أسْـأَلُـكَ خَـيرَ ما في هـذهِ اللَّـيْلَةِ وَخَـيرَ ما بَعْـدَهـا، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّ هـذهِ اللَّـيْلةِ وَشَرِّ ما بَعْـدَهـا، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكَسَـلِ وَسـوءِ الْكِـبَر، رَبِّ أَعـوذُبِكَ مِنْ عَـذابٍ في النّـارِ  وَعَـذابٍ في القَـبْر

Amsaynaa wa amsal-Mulku liLLaah wal-HamduliLLaahi. Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu, wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr. Rabbi as-aluka khayra maa fiy haadhihil-laylati wakhayra maa ba’dahaa, wa a’uwdhu bika minsharri haadhihil-laylati washarri maa ba’dahaa, Rabbi a’uwdhu bika minalkasli wasuw-il kibari, Rabbi a’uwdhu bika min ‘adhaabin finnaari wa ‘adhaabin filqabri

 

 

[78]

اللّهُـمَّ بِكَ أَصْـبَحْنا وَبِكَ أَمْسَـينا، وَبِكَ نَحْـيا وَبِكَ نَمـوتُ وَإِلَـيْكَ النِّـشور

 

Allaahumma bika aswbahnaa wabika amsaynaa, wabika nahyaa wabika namuwtu wailaykan-nushuwr

 

Ee Allaah, Kwako (kwa neema Zako) tumeingia katika asubuhi, na Kwako (kwa neema Zako) tumeingia jioni, na kwa ajili Yako ndio tumekuwa hai, na kwa ajili Yako tutakufa, na Kwako tutafuliwa[5].

 

Na jioni useme:

 

اللّهُـمَّ بِكَ أَمْسَـينا، وَبِكَ أَصْـبَحْنا، وَبِكَ نَحْـيا، وَبِكَ نَمـوتُ وَإِلَـيْكَ المَصـير

Allaahumma bika amsaynaa wabika aswbahnaa, wabika nahyaa wabika namuwtu wailaykal-maswiyr

 

Ee Allaah, Kwako (kwa neema Zako) tumefika jioni, na Kwako (kwa neema Zako) tumefika asubuhi, na kwa ajili Yako tuko hai na kwa ajili Yako tutakufa na ni Kwako tu marejeo.

 

 

 

[79]

 

اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا عَبْـدُك، وَأَنا عَلـى عَهْـدِكَ وَوَعْـدِكَ ما اسْتَـطَعْـت، أَعـوذُبِكَ مِنْ شَـرِّ ما صَنَـعْت، أَبـوءُ لَـكَ بِنِعْـمَتِـكَ عَلَـيَّ وَأَبـوءُ بِذَنْـبي فَاغْفـِرْ لي فَإِنَّـهُ لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْتَ .

 

Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illaa Anta Khalaqtaniy wa ana ‘abduka wa anaa ‘alaa ‘ah-dika wawa’-dika mastatwa’-tu, a’uwdhu bika minsharri maa swana’-tu, abuw-u Laka bini’-matika ‘alayya waabuw-u bidhambiy, faghfirliy fainnahu laa yaghfirudh dhunuwba illaa Anta

 

Ee Allaah, Wewe ni Rabb wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja Wako, nami niko juu ya  ahadi Yako, na agano Lako, kiasi cha uwezo wangu, najikinga Kwako kutokana na shari ya nilichokifanya, nakiri  Kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unighufurie  kwani hakuna wa kughufuria  madhambi ila Wewe[6]

 

Mwanamke aseme:

اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا أَمَتُكَ

Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illaa Anta Khalaqtaniy wa ana amatuka...

 

Ee Allaah, Wewe ni Rabb wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja Wako mwanamke...

 

 

 

[80]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَصْبَـحْتُ أَشْـهِدُك، وَأُشْـهِدُ حَمَلَـةَ عَـرْشِـك، وَمَلائِكَتِك، وَجَمـيعَ خَلْـقِك، أَنَّـكَ أَنْـتَ اللهُ لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ وَحْـدَكَ لا شَريكَ لَـك، وَأَنَّ ُ مُحَمّـداً عَبْـدُكَ وَرَسـولُـك [7]

 

Allaahumma inniy aswbahtu ush-hiduka wa ush-hidu hamalata ‘Arshika, wamalaaikatika wajamiy’a Khaliqika, Annaka Anta-Allaahu laa ilaaha illaa Anta Wahdaka laa shariyka Laka wa anna Muhammadan ‘Abduka wa Rasuwluka

 

Ee Allaah, hakika mimi nimefikia asubuhi nakushuhudia na nina washuhudia wabeba wa ‘Arshi yako na Malaika wako, na viumbe vyako vyote kwamba Wewe ndiye Allaah,  hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, hali ya kuwa Peke Yako Huna mshirika, na kwamba Muhammad ni mja Wako na ni Rasulli Wako.

 

(Useme mara 4 asubuhi na jioni)

 

 

Jioni useme:

 

 اللّهُـمَّ إِنِّـي أَمْسَيْتُ أَشْـهِدُك، وَأُشْـهِدُ حَمَلَـةَ عَـرْشِـك، وَمَلائِكَتِك، وَجَمـيعَ خَلْـقِك، أَنَّـكَ أَنْـتَ اللهُ لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ وَحْـدَكَ لا شَريكَ لَـك، وَأَنَّ ُ مُحَمّـداً عَبْـدُكَ وَرَسـولُـك  

Allaahumma inniy amsaytu ush-hiduka waush-hidu hamalata ‘Arshika, wamalaaikatika wajamiy’a khaliqika, Annaka Anta-Allaahu laa ilaaha illaa Anta Wahdaka laa shariyka Laka wa-anna Muhammadan ‘Abduka warasuwluka 

 

Ee Allaah, hakika mimi nimefikia jioni nakushuhudia na nina washuhudia wabeba wa ‘Arshi yako na Malaika wako, na viumbe vyako vyote kwamba Wewe ndiye Allaah,  hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, hali ya kuwa Peke Yako Huna mshirika, na kwamba Muhammad ni mja Wako na ni Rasuli Wako

 

 

 

 [81]

 

اللّهُـمَّ ما أَصْبَـَحَ بي مِـنْ نِعْـمَةٍ أَو بِأَحَـدٍ مِـنْ خَلْـقِك، فَمِـنْكَ وَحْـدَكَ لا شريكَ لَـك، فَلَـكَ الْحَمْـدُ وَلَـكَ الشُّكْـر[8] 

Allaahumma maa aswbaha biy min ni’-matiy aw biahadim min Khalqika faminka Wahdaka laa shariyka Laka, falakal-Hamdu walakash-shukru

 

Ee Allaah, sikuamka na neema yoyote au kati ya kiumbe Chako chochote, na neema ila inatoka Kwako hali ya kuwa peke Yako Huna mshirika, ni Zako  Himdi na ni Zako shukurani.

 

 

Jioni useme:

 

اللّهُـمَّ ما أَمْسَى بِي مِـنْ نِعْـمَةٍ أَو بِأَحَـدٍ مِـنْ خَلْـقِك، فَمِـنْكَ وَحْـدَكَ لا شريكَ لَـك، فَلَـكَ الْحَمْـدُ وَلَـكَ الشُّكْـر

Allaahumma maa amsaa biy min ni’-matiy aw biahadim min khalqika faminka Wahdaka laa shariyka Laka, falakal-Hamdu walakash-shukru

 

Ee Allaah, sikufikia jioni na neema yoyote au kati ya kiumbe Chako chochote, na neema ila inatoka Kwako hali ya kuwa peke Yako Huna mshirika, ni Zako  Himdi na ni Zako shukurani.  

 

[82]

 

اللّهُـمَّ عافِـني في بَدَنـي، اللّهُـمَّ عافِـني في سَمْـعي، اللّهُـمَّ عافِـني في بَصَـري، لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ. اللّهُـمَّ إِنّـي أَعـوذُبِكَ مِنَ الْكُـفر، وَالفَـقْر، وَأَعـوذُبِكَ مِنْ عَذابِ القَـبْر، لا إلهَ إلاّ أَنْـتَ. (ثلاثاً)

Allaahumma ‘aafiniy fiy badaniy, Allaahumma ‘aafiniy fiy sam-’iy, Allaahumma ‘aafiniy fiy baswariy, laa ilaaha illaa Anta. Allaahumma inniy a’uwdhu bika minalkufri walfaqri. Allaahumma inniy a’uwdhu bika min ‘adhaabil qabri laa ilaaha illaa Anta. (mara 3)

 

Ee Allaah,   nipe afya ya mwili wangu, Ee Allaah, nipe afya ya usikizi (masikio) wangu, Ee Allaah, nipe afya ya uoni (macho) wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe. Ee Allaah, hakika mimi najikinga Kwako kutokana na ukafiri, na ufakiri, na najikinga Kwako kutokana na adhabu ya kaburi, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe[9].  

 

 

[83]

حَسْبِـيَ اللّهُ لا إلهَ إلاّ هُوَ عَلَـيهِ تَوَكَّـلتُ وَهُوَ رَبُّ العَرْشِ العَظـيم

 

Hasbiya-Allaahu laa ilaaha illaa Huwa ‘Alayhi tawakkaltu wa Huwa Rabbul ’Arshil ‘Adhwiym   (mara 7 asubuhi na jioni)

 

Ananitosheleza Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake Yeye nimetawakali na Yeye ni Rabb wa Arshi Tukufu[10]

 

 

[84]

اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في الدُّنْـيا وَالآخِـرَة، اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في ديني وَدُنْـيايَ وَأهْـلي وَمالـي، اللّهُـمَّ اسْتُـرْ عـوْراتي وَآمِـنْ رَوْعاتـي، اللّهُـمَّ احْفَظْـني مِن بَـينِ يَدَيَّ وَمِن خَلْفـي وَعَن يَمـيني وَعَن شِمـالي، وَمِن فَوْقـي، وَأَعـوذُ بِعَظَمَـتِكَ أَن أُغْـتالَ مِن تَحْتـي

 

Allaahumma inniy as-alukal ‘aafiyah fid-dunyaa wal Aakhirah. Allaahumma inni as-alukal ‘afwa wal ‘aafiyata fiy Diyniy wa dunyaaya, wa ahliy, wa maaliy. Allaahumma-stur ‘awraatiy, wa-aamin raw’aatiy. Allaahumma-hfadhwniy min bayni yadayya, wamin khalfiy, wa ‘an yamiyniy, wa ‘an shimaaliy, wamin fawqiy, wa a’uwdhu bi’adhwmatika an ughtaala min tahtiy

 

Ee Allaah, hakika nakuomba msamaha na al’-aafiyah (afya, hifadhi, amani, salama) duniani na Aakhirah.  Ee Allaah, hakika nakuomba msamaha na al’-aafiyah katika Dini na dunia yangu, na ahli wangu, na mali yangu. Ee Allaah nisitiri aibu zangu na nitulize hofu yangu. Ee Allaah, nihifadhi mbele yangu, na nyuma yangu, na kulia kwangu, na kushoto kwangu, na juu yangu, na najikinga kwa Uadhimu Wako kwa kutekwa chini yangu [11]

 

 

[85]

 

اللّهُـمَّ عالِـمَ الغَـيْبِ وَالشّـهادَةِ فاطِـرَ السّماواتِ وَالأرْضِ رَبَّ كـلِّ شَـيءٍ وَمَليـكَه، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْت، أَعـوذُ بِكَ مِن شَـرِّ نَفْسـي وَمِن شَـرِّ الشَّيْـطانِ وَشِـرْكِه، وَأَنْ أَقْتَـرِفَ عَلـى  نَفْسـي سوءاً أَوْ أَجُـرَّهُ إِلـى مُسْـلِم .

 

Allaahumma ‘Aalimal-ghaybi wash-shahaadah, Faatwiras-samaawati wal-ardhwi, Rabba kulli shay-in wamaliykah. Ash-hadu an laa ilaaha illaa Anta. A’uwdhu Bika minsharri nafsiy, wamin sharri shaytwaani wa shirkihi, wa an aqtarifa ‘alaa nafsiy suuw-an aw ajurrahu ilaa Muslim

 

 (Soma tena nyiradi hiyo ila kwenye neno la: ‘wa shirkihi’ useme badala yake: “wa-sharakihi”)

 

 

Ee Allaah, Mjuzi wa ghayb na yaliyowazi, Mwanzishi wa mbingu na ardhi, Rabb wa kila kitu na Mfalme wake. Nashuhudia kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe. Najikinga Kwako kutokana na shari ya nafsi yangu na shari ya shaytwaan na shirki yake na kujichumia uovu kwa nafsi yangu au kumletea Muislamu[12]

 

 

 [86]

بِسـمِ اللهِ الذي لا يَضُـرُّ مَعَ اسمِـهِ شَيءٌ في الأرْضِ وَلا في السّمـاءِ وَهـوَ السّمـيعُ العَلـيم (ثلاثاً)

 

BismiLLaahiLLadhiy laa yadhwuru ma’-Smihi shay-un fil-ardhwi walaa fissamaai wa Huwas-Samiy’ul ‘Aliym (mara 3)

 

Kwa jina la Allaah Ambaye hakidhuru kwa jina Lake kitu chochote kile kilicho ardhini, wala mbinguni, Naye ni Mwenye Kusikia yote daima Mjuzi wa yote daima.[13]

 

 

[87]

رَضيـتُ بِاللهِ رَبَّـاً وَبِالإسْلامِ ديـناً وَبِمُحَـمَّدٍ صَلى الله عليه وسلم  نَبِيّـاً. (ثلاثاً)

 

Radhwiytu biLLaahi Rabban wabil Islaami Diynan wabi Muhammadin Swalla-Allaahu ‘alayhi wa sallam Nabiyyaa (mara 3)

 

Nimeridhika kuwa Allaah Ndiye Rabb wangu, na Uislamu ndio Dini yangu, na Muhammad (صلى الله عليه وسلم) kuwa ni Nabiy wangu[14]

 

 

[88]

يا حَـيُّ يا قَيّـومُ بِـرَحْمَـتِكِ أَسْتَـغـيث، أَصْلِـحْ لي شَـأْنـي كُلَّـه، وَلا تَكِلـني إِلى نَفْـسي طَـرْفَةَ عَـين

Yaa Hayyu Yaa Qayyuwm bi-Rahmatika astaghiythu, Aswlihliy sha-ani kullahu walaa takilniy ilaa nafsiy twarfata ‘aynin

 

Ee Uliye Uliyehai daima, Msimamizi wa kila kitu, kwa Rehma Zako ninakuomba uniokoe, nitengenezee mambo yangu  yote, wala usiniachie  nijitegemee mambo yangu mwenyewe (pasina kunisaidia) hata kwa muda (mdogo kama muda) wa kupepesa jicho[15]

 

 

 [89]

 

أَصْبَـحْـنا وَأَصْبَـحْ المُـلكُ للهِ رَبِّ العـالَمـين، اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ خَـيْرَ هـذا الـيَوْم، فَـتْحَهُ، وَنَصْـرَهُ، وَنـورَهُ وَبَـرَكَتَـهُ، وَهُـداهُ، وَأَعـوذُ بِـكَ مِـنْ شَـرِّ ما فـيهِ وَشَـرِّ ما بَعْـدَه.

Aswbahnaa wa aswbahal-Mulku liLLaahi Rabbil ‘Aalamiyn. Allaahumma inniy as-aluka khayra haadhal-yawmi fat-hahu, wanaswarahu, wanuwrahu, wabarakatahu, wahudaahu, wa a’uwdhu Bika minsharri maa fiyhi washarri maa ba’-dahu

 

Tumeingia asubuhi  na imefika asubuhi na Ufalme ni wa Allaah  Rabb wa walimwengu, Ee Allaah,  hakika mimi nakuomba kheri ya siku hii ya leo, ufunguzi wake na nusura yake, na nuru yake na baraka yake, na uongofu wake, na najikinga Kwako kutokana na shari ya kilicho ndani  ya siku hii, na shari ya baada ya siku hii[16]

 

Jioni useme:

 

أَمْسَيْـنا وَأَمْسـى المُـلكُ للهِ رَبِّ العـالَمـين، اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ خَـيْرَ هـذهِ اللَّـيْلَة، فَتْحَهـا، وَنَصْـرَهـا، وَنـورَهـا، وَبَـرَكَتَـهـا، وَهُـداهـا، وَأَعـوذُ بِـكَ مِـنْ شَـرِّ ما فـيهـاِ وَشَـرِّ ما بَعْـدَهـا

Amsaynaa wa amsal-Mulku liLLaah Rabbil ‘Aalamiyn. Allaahumma inniy as-aluka khayra haadhihil-laylati fat-hahaa, wanaswarahaa, wanuwrahaa, wabarakatahaa, wahudaahaa, wa a’uwudhu Bika minsharri maa fiyhaa washarri maa ba’dahaa

 

Tumeingia jioni na imefika jioni na Ufalme ni wa Allaah, Rabb walimwengu, Ee Allaah hakika mimi nakuomba kheri ya usiku huu, ufunguzi wake na nusura yake, na nuru yake na baraka yake, na uongofu wake, na najikinga kwako kutokana na shari ya kilicho ndani ya usiku huu, na shari ya baada ya usiku huu.

 

 

[90]

 

أَصْـبَحْنا علـى فِطْـرَةِ الإسْلام، وَعَلـى كَلِـمَةِ الإخْـلاص، وَعلـى دينِ نَبِـيِّنا مُحَـمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم وَعَاـى مِلَّـةِ أبينـا إِبْـراهيـمَ حَنيـفاً مُسْلِـماً وَمـا كـانَ مِنَ المُشـرِكيـن

 

Aswbahnaa ‘alaa fitwratil-Islaami, wa ‘alaa kalimatil-ikhlaasw, wa ‘alaa Diyni Nabiyyinaa Muhammadin Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam wa ‘alaa millati Abiynaa Ibraahiyma Haniyfan Musliman wamaa kaana minal-mushrikiyn

 

Tumeingia asubuhi na maumbile ya Kiislamu na neno la ikhlaasw na Dini ya Nabiy wetu Muhammad (صلى الله عليه وسلم), na milah (Dini) ya baba yetu Ibraahiym aliyejiengua na dini potofu akashika Dini ya haki na hali  ya kuwa  Musilamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Allaah.[17]

 

 

Jioni useme: 

 

 أَمْسَيْنا علـى فِطْـرَةِ الإسْلام، وَعَلـى كَلِـمَةِ الإخْـلاص، وَعلـى دينِ نَبِـيِّنا مُحَـمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم  وَعَاـى مِلَّـةِ أبينـا إِبْـراهيـمَ حَنيـفاً مُسْلِـماً وَمـا كـانَ مِنَ المُشـرِكيـن

Amsaynaa ‘alaa fitwratil-Islaami, wa ‘alaa kalimatil-ikhlaaswi, wa ‘alaa Diyni Nabiyyinaa Muhammadin Swalla-Allaahu ‘alayhi wasallam wa ‘alaa millati Abiynaa Ibraahiyma Haniyfan Musliman wamaa kaana minal-mushrikiyn

 

 

Tumeingia jioni na maumbile ya Kiislamu na neno la ikhlaasw na Dini ya Nabiywetu Muhammad (صلى الله عليه وسلم), na milah (Dini) ya baba yetu Ibraahiym aliyejiengua na Dini potofu akashika dini ya haki na hali  ya kuwa  Musilamu wala hakuwa ni mwenye kumshirikisha Allaah.

 

 

 

 [91]

سُبْحـانَ اللهِ وَبِحَمْـدِهِ

Subhaana-Allaahi wa Bihamdihi (mara mia moja)

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi ni Zake[18]

 

 

 [92]

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير

 

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr. (mara kumi)[19] (au mara moja ukisia uvivu)

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah  peke Yake, hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza[20]

 

 

[93]

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير

 

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr.   (mara mia atakapoamka)

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah  Peke Yake, Hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Mweza[21]

 

 

[94]

سُبْحـانَ اللهِ وَبِحَمْـدِهِ عَدَدَ خَلْـقِه، وَرِضـا نَفْسِـه، وَزِنَـةَ عَـرْشِـه، وَمِـدادَ كَلِمـاتِـه

 

Subhaana-Allaahi wa Bihamdihi, ’adada Khalqihi wa Ridhwaa Nafsihi, wa zinata ’Arshihi wamidaada Kalimaatih (mara 3 kila asubuhi na jioni)

 

Utakasifu ni wa Allaah  na Himdi ni Zake, kwa idadi ya viumbe Vyake, na radhi Yake, na uzito wa arshi Yake, na wino wa maneno Yake[22]

  

[95]

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ عِلْمـاً نافِعـاً وَرِزْقـاً طَيِّـباً، وَعَمَـلاً مُتَقَـبَّلاً

Allaahumma inniy as-aluka ‘ilman naafi’an warizqan twayyiban wa ‘amalam mutaqabbalan   (asubuhi)

 

Ee Allaah, hakika nakuomba elimu yenye kunufaisha na rizki njema na amali zenye kutakabaliwa[23]

 

 

[96]

أَسْتَغْفِرُ الَّلهَ وَ أَتُوبُ إِلَيْهِ

Astaghfiru-Allaahi wa atuwbu Ilayhi (mara mia kila siku)

 

Namuomba Allaah maghfirah na natubu (narejea) Kwake[24] 

 

 

[97]

أَعُوْذُ بِكَلِماتِ اللَّهِ التَّامَّتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ

A’uwdhu bikalimaatiLLaahit-ttaammati minsharri maa khalaq (mara 3 jioni na asubuhi)

 

Najikinga kwa maneno ya Allaah yaliyotimia kutokana na shari Aliyoiumba[25]

 

 

[98]

اللّهُـمَّ صَلِّ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى أَزْواجِـهِ وَذُرِّيَّـتِه، كَمـا صَلَّيْـتَ عَلـى آلِ إبْراهـيم. وَبارِكْ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى أَزْواجِـهِ وَذُرِّيَّـتِه، كَمـا بارِكْتَ عَلـى آلِ إبْراهـيم. إِنَّكَ حَمـيدٌ مَجـيد

Allaahumma Swalli ‘alaa Muhammadin wa ‘alaa azwaajihi wadhurriyatihi kamaa Swallayta ‘alaa aali Ibraahiym. Wabaarik ‘alaa Muhammadin wa ‘alaa azwaajihi wadhurriyatihi kamaa Baarakta ‘alaa aali Ibraahiym. Innaka Hamiydum-Majiyd

 

Ee Allaah Mswalie Muhammad, na wake zake, na kizazi chake, kama Ulivyowaswalia  ahli wa Ibraahiym.  Na mbariki  Muhammad, na wake zake, na kizazi chake, kama Ulivyowabariki ahli zake Ibraahiym, hakika Wewe Umesifika na Umetukuka[26]

 

 

[1]Imepokewa kutoka kwa Anas  (رضي الله عنه)amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 ((لَأَنْ أَقْعُدَ مَعَ قَوْمٍ يَذْكُرُونَ اللَّهَ تَعَالَى مِنْ صَلَاةِ الْغَدَاةِ حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ أَحَبُّ إِلَيَّ مِنْ أَنْ أَعْتِقَ أَرْبَعَةً مِنْ وَلَدِ إِسْمَاعِيل ، وَلَأَنْ أَقْعُدَ مَعَ قَوْمٍ يَذْكُرُونَ اللَّهَ مِنْ صَلَاةِ الْعَصْرِ إِلَى أَنْ تَغْرُبَ الشَّمْسُ أَحَبُّ إِلَيَّ مَنْ أَنْ أَعْتِقَ أَرْبَعَةً))

 ((Kukaa pamoja na watu wanaomtaja Allaah سبحانه وتعالى  kuanzia Swalaah ya Al-Fajiri mpaka kuchomoza jua kunapendeza zaidi kwangu mimi kuliko kuacha huru watu wanne miongoni mwa wana wa Ismaa’iyl. Na kukaa na watu wanaomtaja Allaah  سبحانه وتعالى kuanzia baada ya Swalaah ya Alasiri mpaka kuzama jua kunapendeza zaidi kwangu mimi kuliko kuwaacha huru watu wanne)) Abu Daawuwd [3667[ na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) Swahiyh Abi Daawuwd (2/698).

 

[2]Hadiyth ya Abi bin Ka’ab (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema kuhusu Aayatul-Kursiy:

  

((مَنْ قَالَهَا حِينَ يُصٍبح أجِير مِنَ الْجِنِّ  حَتَّى يُمْسي وَمَنْ  قَالَها حِينَ يُمسي أجِير مِنْهُمْ حَتَّى يُصْبح))   

((Atakayeisoma anapoamka asubuhi itamkinga na majini mpaka itakapofika jioni. Na atakayeisoma jioni atakingwa nao mpaka asubuhi)) (Aayatul-Kursiyy - Al-Baqarah 2:255) - Al-Haakim (1/562) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh At-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/273) [655]  

[3]Hadiyth ya ’Abdullaah bin Khubayb (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

((فمن قرأها ثلاث مرات حين يصبح وحين يمسي كفته من كل شي))

((Atakayezisoma mara tatu asubuhi na jioni  zitamtosheleza kwa kila kitu)) Abu Daawuwd (4/322) [5082], At-Tirmidhiy (5/567)[3575], na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/182)

 

[4]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas-‘wud (رضي الله عنه) - Muslim (4/2088) [2723]

 

[5] Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/466) [3391], na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/142)

 

[6]Hadiyth ya Shaddaad bin ‘Aws (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ قَالَهَا مِنْ النَّهَارِ مُوقِنًا بِهَا فَمَاتَ مِنْ يَوْمِهِ قَبْلَ أَنْ يُمْسِيَ فَهُوَ مِنْ أَهْلِ الْجَنَّةِ، وَمَنْ قَالَهَا مِنْ اللَّيْلِ وَهُوَ مُوقِنٌ بِهَا فَمَاتَ قَبْلَ أَنْ يُصْبِحَ فَهُوَ مِنْ أَهْلِ الْجَنَّةِ))

((Atakayesema mchana akiwa na yakini nayo, akafariki siku hiyo kabla kuingia jioni basi atakuwa mtu wa Jannah, na atakayesema usiku naye akiwa yakini nayo akafariki kabla hajafika asubuhi basi yeye ni mtu wa Jannah)) - Al-Bukhaariy (7/150) [2306]- Sayyid Al-Istighfaar:

 

[7] Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ قالها حين يصبح أو يمسي: أربع مرات أعتقه الله من النار))

((Atakaye yasema haya asubuhi au jioni mara nne Allaah Atamuepusha na Moto)) - Abu Daawuwd (4/317) [5069], Al-Bukhaariy katika ‘Adab Al-Mufrad [1201] An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [9] Ibn As-Sunniy [70], na ameipa daraja ya Hasan Shaykh Ibn Baaz katika Majmuw’ Al-Fataawa Isnaad ya An-Nasaaiy na Abu Daawuwd katika Nafhat Al-Akhyaar (Uk. 23). Na Ibnul-Qayyim pia ameipa daraja ya Hasan katika Zaad Al-Ma’aad.  

 

Tanbihi:  Ama baadhi ya ‘Ulamaa wamesema ni Dhwa’iyf kama Imaam Al-Albaaniy kama alivyorekodi katika Dhwa’iyf Al-Jaami Hadiyth namba [5371]. Lakini Imaam Al-Albaaniy amerekodi kwa tamshi tofauti kidogo kama ifuatavyo na akaipa daraja ya Swahiyh nayo ni Hadiyth ya Salmaan bin Farsiy (رضي الله عنه):

 

من قال : اللهمَّ إني أُشهدُك، وأُشهدُ ملائكتَك ، وحملةَ عرشِك ، وأُشهدُ من في السماواتِ ومن في الأرضِ أنك أنت اللهُ ، لا إلهَ إلا أنتَ وحدَك لا شريك لك ، و أشهدُ أنَّ محمدًا عبدُك و رسولُك ، من قالها مرةً أعتق اللهُ ثلثَه من النارِ ، و من قالها مرتيْنِ أعتق اللهُ ثلثيْهِ من النارِ ، و من قالها ثلاثًا أعتق اللهُ كلَّهُ من النارِ

 

[8]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Ghannaam (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

((مَنْ قَالَها حين يصبح فَقَدْ اَدَّى شُكر يَوْمِهِ وَمَنْ قَالَ مِثْل ذلِكَ حِينَ يُمْسي فَقَدْ أّدَّى شُكْر لَيْلَتِه))

((Atakayesema kila asubuhi atatekeleza shukurani ya siku nzima, atakayesema jioni atatekeleza shukurani ya usiku mzima)) - Abu Daawuwd (4/318) [5073], An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [7]. Ibn As-Sunniy [41], Ibn Hibbaan “Mawaarid” [2361] na isnaad yake ameipa daraja ya Hasan Ibn Baaz (رحمه الله) katika Tuhfat Al-Akhyaar (Uk. 24).

 

Tanbihi:  Imedhoofishwa na baadhi ya ‘Ulamaa na Shaykh Al-Albaaniy (رحمه الله) Angalia:  Al-Kalim At-Twayyib [26], Swahiyh Al-Jaami’ [5730],

 

[9]Hadiyth ya Abu Bakr (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (4/324) [5090], Ahmad (5/42), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [22], Ibn As-Sunniy [69], Al-Bukhaariy katika Adab Al-Mufrad na isnadi yake ameipa daraja ya Hasan Al-‘Allaamah Ibn Baaz (رحمه الله) katika Tuhfat Al-Akhyaaar (Uk. 26). Pia Swahiyh Abi Daawuwd (5090).

 

[10] Hadiyth ya Ummu Dardaa kutoka kwa Abuu Dardaa (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

((من قالها حين يصبح وحين يمسي سبع مرات كفاه الله ما أهمه من أمر الدنيا والآخرة))

((Atakayesema asubuhi na jioni itamtosheleza katika mambo yake yanayomtia hamu ya dunia na Aakhirah)).  Ibn As-Sunniy [71] Marfuw’aa na Abu Daawuwd Mawquwfaa (4/321), na isnadi yake ameisahihisha Shu’ayb na ‘Abdul-Qaadir Al-Arnaauwtw. Taz Zaad Al-Ma’aad (2/376) .

 

Tanbihi: Imaam Ibn Baaz (رحمه الله) amesema ni Dhwa’iyf katika Fataawa Ibn Baaz (9/294)  ila  akasema juu ya hivo ni maneno mazuri ya kutamkwa ila haikuthibiti Hadiyth hiyo.

 

[11]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd [5074], Ibn Maajah [3871]. Taz Swahiyh ibn Maajah (2/332), Taz Swahiyh Abi Daawuwd [5074]  

 

[12]Hadiyth ya Abu Hurayrah  (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy [3392], Abu Daawuwd [5067], na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/142)

 

[13]Hadiyth ya ‘Uthmaan bin ‘Afaan (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

((مَنْ قَالَها ثَلاثًا إذا أصْبَحَ وَثَلاثًا إذا أمْسَى لَمْ يَضُرُّهُ شَيْء))

((Atakayesema mara tatu asubuhi na jioni hatodhuriwa na chochote)) Abu Daawuwd (4/323) [5089, 5088]. At-Tirmidhiy (5/465) [3388], Ibn Maajah [3869], Ahmad (1/72), Taz Swahiyh Ibn Maajah (2/332), Swahiyh Abi Daawuwd (5088), Swahiyh Al-Jaami’ (5745), Majmuw’ Fataawa ibn Baaz (رحمه الله) (8/108) na isnadi yake imepewa daraja ya Hasan na Al-‘Allaamah Ibn Baaz (رحمه الله) katika Tuhfat Al-Akhyaar (Uk. 39)

 

[14]Hadiyth ya Thawbaan bin Bujdud (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ قَالَها ثَلاثًا حِينَ يُصْبحُ وَ ثَلاثًا حِينَ يُمسي كَانَ حَقًّا عَلى اللهِ أنْ يُرْضِيهِ يَوْم الْقِيَامَة))

((Atakayesema mara tatu atakapofika asubuhi na mara tatu atakapofika jioni imekuwa haki juu ya Allaah Aridhike naye Siku ya Qiyaamah)). Ahmad (4/337), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [4], Ibn As-Sunniy [68], Abu Daawuwd (4/318) [5072], At-Tirmidhiy (5/465) [3389]. Ibn Maajah. Taz Majma’ Az-Zawaaid (10/119) na ameipa daraja ya Hasan Ibn Baaz (رحمه الله) katika Tuhfat Al-Akhyaar (Uk. 39). Adh-Dhahabiy amesema Swahiyh. Imaam An-Nawawiy amesema Isnaad yake ni ya nguvu. Atw-Twabaraniy katika Kitaab Ad-Du’aa.

 

Tanbihi:  Imaam Al-Albaaniy ameidhoofisha katika As-Silsilah Adhw-Dhwa’iyfah [5020], Dhwa’iyf Al-Jaami’ [5735]. Ila kuna Hadiyth Swahiyh kama hiyo lakini bila ya kutajwa kuitamka mara tatu. Na pia imethibiti Hadiyth Swahiyh yenye tamshi kama hilo ambayo ni:

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( يَا أَبَا سَعِيدٍ مَنْ رَضِيَ بِاللَّهِ رَبًّا وَبِالإِسْلاَمِ دِينًا وَبِمُحَمَّدٍ نَبِيًّا وَجَبَتْ لَهُ الْجَنَّةُ))

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ee Abaa Sa’iyd! Atakayeridhia kwamba Allaah ni Rabb na Uislamu ni Dini na Muhammad ni Nabiy, atawajibika kupata Jannah)) [Muslim]

 

 

[15]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) Abu Daawuwd (4/3180), At-Tirmidhiy (5/465), Al-Haakim. Taz Swahiyh At-Targhiyb (1/273), Swahiyh Al-Jaami’ [5820] Katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [4] na Ibn As-Sunniy [68], na ameipa daraja ya Hasan bin Baaz (رحمه الله) katika Tuhfat Al-Akhyaar (Uk. 39)  

 

[16] Hadiyth ya Abu Maalik Al-Ash’ariyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (4/322) [5084], na isnadi yake ni Hasan kutoka kwa Shu’ayb na ‘Abdul-Qaadir Al-Arnaauwtw katika Tahqiyq Zaad Al-Ma’aad (2/273). Imaam Al-Albaaniy ameisahihisha katika Swahiyh Al-Jaami’[352].

 

 

[17]Hadiyth ya ‘Abdur-Rahmaan bin Abi Abzaa (رضي الله عنه) - Ahmad (3/406, 407) na Ibn As-Sunny katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [34]. Angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (4/209) [4674]. Taz  Majma’ Az-Zawaaid (10/119)

 

[18]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ قَال حِينَ يُصْبحُ وحِينَ يُمسي ... لَمْ يأْتِ أحَد يَوْم الْقِيامَةِ بِأفْضَلِ مِمَّا جَاءَ بِهِ، إلَّا أَحد قَال مِثْل ما قال، أوْ زادَ عَلَيْهِ))

((Atakayesema mara mia asubuhi na jioni  hatofika mtu siku ya Qiyaamah aliye bora kuliko aliyesema haya ila tu aliyesema kama haya au akazidisha)) Muslim (4/2071) [2733]

 

[19]Hadiyth ya Abu ‘Ayyaash (رضي الله عنه). Imesemekana jina lake ni Zayd bin Asw-Swwamit, au Zayd bin An-Nu’maan, au jina jengine - An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [24] Hadiyth ya Abu Ayyub Al-Answaariyy (رضي الله عنه) na tamshi lake: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ قالَ إذا أصْبَحَ : لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير كانَ لَهُ عَدْل رَقَبَة مِنْ وَلَدِ إسْماعِيل، وَكُتِبَ لَهُ عَشر حَسَناتِ وَحُطَّ عَنْهُ عَشر سَيِّئات، وَرُفِعَ لَهُ عَشر دَرَجات وَكانَ فَي حِرْزِ مِنَ الشَّيْطانِ حَتَّى يُمْسِي، وَإنْ قَالَها إذا أَمْسى كَانَ لَهُ مِثْل ذلِكَ حَتَّى يُصْبِحُ))

((((Atakayesema alfajiri: Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr  itakuwa ni kama kuacha huru mtumwa katika wana wa Ismaa’iyl, na Ataandikiwa mema kumi, na atafutiwa makosa kumi, atapandishwa daraja kumi, na atakuwa katika kinga ya shaytwaan mpaka afike jioni na akisema jioni atapata kama hivyo mpaka afike asubuhi)).  Hadiyth ya Abu ‘Ayyaash (رضي الله عنه) ametaja fadhila ya kusema mara moja pia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayesema atakapoamka asubuhi na atakapofika jioni, atapata thawabu sawa na kuacha huru mtumwa mmoja katika wana wa Ismaa’iy, ataandikiwa mema kumi, atafutiwa maovu kumi na atapandishwa vyeo kumi na itakuwa kinga kutokana na shaytwaan mpaka atakapofika jioni)) Na angalia: Swahiyh At-Targhiyb na At-Tarhiyb (1/272) [650], na Tuhfat Al-Akhyaar ya ibn Baaz (رحمه الله) (Uk. 55) 

 

[20] Abu Daawuwd (4/319) [5077], Ibn Maajah [3867]. Ahmad (4/60) na angalia: Swahiyh At-Targhiyb na At-Tarhiyb (1/270), Swahiyh Abi Daawuwd (3/957), Swahiyh Ibn Maajah (2/331), Zaad Al-Ma’aad (2/377)

 

[21] Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayesema   kwa siku mara mia, basi atapata sawa na thawabu za kuwaacha huru watumwa kumi na ataandikiwa mema mia moja na atafutiwa makosa mia moja, na atakuwa na kinga ya shaytwaan kwa siku hiyo yote hadi jioni na hatakuwa mtu yeyote mbora kumshinda ila yule aliyefanya zaidi yake)) Al-Bukhaariy  pamoja na Al-Fat-h, (4/95) [3293], Muslim (4/2071) [2691].

 

[22]Hadiyth ya Juwayriyyah bint Al-Haarith (رضي الله عنها)  mke wa Nabiy (صلى الله عليه وسلم) – Muslim (4/2090) [2726], Swahiyh Abi Daawuwd [1503]. Swahiyh At-Targhiyb [1574], Swahiyh Al-Jaami’ [5139], Swahiyh  Al-Adab Al-Mufrad [503].

 

[23]Hadiyth ya Ummu Salamah (رضي الله عنها) Ibn As-Sunniy katika ‘Amal Al-Yawam wal-Laylah [54], Ibn Maajah [925], Taz Swahiyh Ibn Maajah (1/152).  Majmu’a Fataawa ibn ‘Uthaymiyn (13/277), Ibn Hajar Al-Asqalaaniy katika Nataaij Al-Afkaar (2/329). Na isnadi yake ni Hasan kutoka kwa ‘Abdul-Qaadir na Shu’ayb Al-Arnaauwtw katika Tahqiyq Zaad Al-Ma’aad (2/375)

 

[24]Hadiyth ya Al-Agharr bin Yasaar Al-Muzaniy (رضي الله عنه)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/101) [6307], Muslim (4/2075) [2702], Ahmad Ad-Daarimiy. Taz Swahiyh Al-Jaami’ (944). Hadiyth imepokelewa kwa mapokezi mbali mbali na namna nyingine kama Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) katika Al-Bukhaariy kwa tamshi la Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم): ((Wa-Allaahi hakika mimi namuomba Allaah maghfirah na natubu Kwake zaidi ya mara sabiini kwa siku)) Na Allaah Anajua zaidi.

 

[25]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Ahmad (2/290), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [590], ibn As-Sunniy [68]. Angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/187), Swahiyh Ibn Maajah (92/266), Tuhfat Al-Akhyaar  (Uk. 45)  Na Taz  katika   Swahiyh Al-Jaami’ [6427] Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayesema mara tatu jioni hatodhuriwa na mdudu wa sumu usiku huo)

 

[26]Hadiyth ya Abu Dardaa (رضي الله عنه)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/4-7) [3369], Muslim (1/306) [407] na kwa tamshi lake. Na wengineo kwa mapokezi mbalimbali; Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayeniswalia  asubuhi mara kumi na jioni mara kumi, nitamuombea shifaa Siku ya Qiyaamah)). Riwaayah nyingine: ((Atakayeniswalia mara moja Allaah Atamswalia mara kumi)) Rejea Adhkaar [53, 54]

Share

028-Hiswnul-Muslim: Nyiradi Za Kulala

 

Hiswnul-Muslim

028-Nyiradi Za Kulala

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[99]

 

Unapokwenda kulala, kusanya viganja vyako uweke mdomoni, kisha usome Suwrah zifuatazo mara tatu kila moja, na upulize katika viganja, kisha upanguse kwavyo kiasi unachoweza katika mwili wako ukianza kichwani, usoni na mbele. Fanya hivyo mara tatu[1]

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيم. قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾ اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾ لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ﴿٣﴾ وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ ﴿٤﴾

 

  بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾ مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ﴿٢﴾ وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ ﴿٣﴾ وَمِن شَرِّ النَّفَّاثَاتِ فِي الْعُقَدِ ﴿٤﴾وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ ﴿٥﴾

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ .قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ﴿١﴾ مَلِكِ النَّاسِ ﴿٢﴾ إِلَـٰهِ النَّاسِ ﴿٣﴾ مِن شَرِّ الْوَسْوَاسِ الْخَنَّاسِ ﴿٤﴾ الَّذِي يُوَسْوِسُ فِي صُدُورِ النَّاسِ ﴿٥﴾ مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ ﴿٦﴾

 

 

 

 [100]

 

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ ۚ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۖ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا ۚ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٢٥٥[2]

 

[101]

 

Soma Aayah mbili za mwisho za Suwratul-Baqarah (2: 285-286):

 

 آمَنَ الرَّسُولُ بِمَا أُنزِلَ إِلَيْهِ مِن رَّبِّهِ وَالْمُؤْمِنُونَ ۚ كُلٌّ آمَنَ بِاللَّـهِ وَمَلَائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ لَا نُفَرِّقُ بَيْنَ أَحَدٍ مِّن رُّسُلِهِ ۚ وَقَالُوا سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا ۖ غُفْرَانَكَ رَبَّنَا وَإِلَيْكَ الْمَصِيرُ ﴿٢٨٥لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا ۚ لَهَا مَا كَسَبَتْ وَعَلَيْهَا مَا اكْتَسَبَتْ ۗ رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا ۚ رَبَّنَا وَلَا تَحْمِلْ عَلَيْنَا إِصْرًا كَمَا حَمَلْتَهُ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِنَا ۚ رَبَّنَا وَلَا تُحَمِّلْنَا مَا لَا طَاقَةَ لَنَا بِهِ ۖ وَاعْفُ عَنَّا وَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا ۚ أَنتَ مَوْلَانَا فَانصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ ﴿٢٨٦ [3] 

 

 

[102]

 

بِاسْمِكَ رَبِّـي وَضَعْـتُ جَنْـبي، وَبِكَ أَرْفَعُـه، فَإِن أَمْسَـكْتَ نَفْسـي فارْحَـمْها، وَإِنْ أَرْسَلْتَـها فاحْفَظْـها بِمـا تَحْفَـظُ بِه عِبـادَكَ الصّـالِحـين

 

Bismika Rabbiy wadhwa’-tu janbiy wabika arfa’uhu. Fain Amsakta nafsiy farhamhaa. Wain Arsaltahaa fahfadhw-haa bimaa Tahfadhwu bihi ’Ibaadakas-Swaalihiyn.

 

Kwa jina lako Rabb wangu, nimeweka ubavu wangu. Na kwa Msaada Wako nitaunyanyua, Ukiizuia (Ukiichukuwa) roho yangu basi Irehemu na Ukiirudisha basi Ihifadhi kwa kile Unachowahifadhi nacho Swaalihina (Waja wema) Wako.[4]

 

 

 

[103]

اللّهُـمَّ إِنَّـكَ خَلَـقْتَ نَفْسـي وَأَنْـتَ تَوَفّـاهـا لَكَ ممَـاتـها وَمَحْـياها، إِنْ أَحْيَيْـتَها فاحْفَظْـها، وَإِنْ أَمَتَّـها فَاغْفِـرْ لَـها. اللّهُـمَّ إِنَّـي أَسْـأَلُـكَ العـافِـيَة

 

Allaahumma Innaka Khalaqta nafsiy wa Anta Tawaffahaa. Laka mamaatuhaa wamahyaahaa. In-Ahyaytahaa fahfadhw-haa wain amattahaa faghfir lahaa. Allaahumma inniy as-alukal ‘aafiyah.

 

Ee Allaah, hakika Wewe Umeiumba nafsi yangu Nawe Utaifisha. Ni Wewe Unaumiliki umauti wake na uhai wake. Ukiipa uhai basi Ihifadhi, na Ukiifisha basi Ighufurie. Ee Allaah, hakika mimi nakuomba Al-‘Aafiyah.  [5]

 

Al-‘Aafiyah ni neno linalojumuisha  Allaah (عزّ وجلّ)  kumjaalia mja Wake salama na kumpa amani, na kumlinda na maradhi, balaa, majanga, madhara, misukosuko, na kila aina za shari za wanaadam na majini na kubakia salama katika Dini yake na Aakhirah yake.  

 

 

[104]

اللّهُـمَّ قِنـي عَذابَـكَ يَـوْمَ تَبْـعَثُ عِبـادَك

 

Allaahumma Qiniy ’Adhaabaka yawma Tab’athu ’Ibaadaka (mara 3)  

 

Ee Allaah Nikinge na adhabu Yako siku Utakayowafufua waja Wako[6]

 

 

 

 [105]

بِاسْـمِكَ اللّهُـمَّ أَمـوتُ وَأَحْـيا

 

Bismika-Allaahumma amuwtu wa ahyaa

 

Kwa jina lako Ee Allaah ninakufa na ninakuwa hai[7]

 

 

 

[106]

سُبْـحانَ الله.  أَلْحَمْدُ لِلَّه.  اللَّه أكْبَرُ

 

Subhaana-Allaah (mara 33)  AlhamduliLlaah (mara 33) Allaahu Akbar (mara 44)

 

Utakasifu ni wa Allaah. Himdi Anastahiki Allaah. Allaah ni Mkubwa[8]

 

 

 

[107]

 

اللّهُـمَّ رَبَّ السّمـواتِ السَّبْـعِ وَرَبَّ العَـرْشِ العَظـيم، رَبَّنـا وَرَبَّ كُـلِّ شَـيءٍ، فالِـقَ الحَـبِّ وَالنَّـوى، وَمُـنَزِّلَ التَّـوْراةِ وَالإنْجـيلِ والفُـرْقانِ. أَعُـوذُ بِـكَ مِن شَـرِّ كُـلِّ شَـيءٍ أَنْـتَ آخِـذٌ بِنـاصِـيَتِهِ. اللّهُـمَّ أَنْـتَ الأوَّلُ فَلَـيسَ قَبْـلَكَ شَيءٌ، وَأَنْـتَ الآخِـرُ فَلَـيسَ بَعْـدَكَ شَيءٌ، وَأَنْـتَ الظّـاهِـرُ فَلَـيْسَ فَـوْقَـكَ شَيءٌ، وَأَنْـتَ الْبـاطِـنُ فَلَـيْسَ دونَـكَ شَيءٌ، اقـْضِ عَنّـا الـدَّيْـنَ وَأَغْـنِنـا مِنَ الفَـقْرِ

 

Allaahumma Rabbas-samawaatis-sab’-i wa Rabbal-’Arshil-’Adhwiym. Rabbanaa wa Rabba kulli shay-in. Faaliqal-habbi wan-nnawaa, wa munzilat-Tawraati wal-Injiyli wal-Furqaan. A’uwdhu Bika minsharri kulli shay-in Anta Aakhidhun binaaswiyatihi. Allaahumma Antal-Awwalu falaysa Qablaka shay-un. Wa Antal-Aakhiru falaysa Ba’-daka shay-un. Wa Antadh-Dhwaahiru falaysa Fawqaka shay-un. Wa Antal-Baatwinu falaysa Duwnaka shay-un. Iqdhwi ‘annad-dayna waghninaa minal-faqri.

 

Ee Allaah Rabb wa mbingu saba na Rabb wa ’Arshi Tukufu. Rabb wetu na Rabb wa kila kitu. Mpasuaji wa mbegu na kokwa (zikawa miche) na Aliyeteremsha Tawraati na Injili  na Qur-aan. Najikinga Kwako kutokana na shari ya kila kitu. Wewe Ndiye Mwenye kukamata utosi wake. Ee Allaah Wewe Ndiye  wa Mwanzo hakuna kitu kabla Yako. Nawe Ndiye wa Mwisho  hakuna kitu chochote baada Yako. Nawe Ndiye Uliye juu hakuna kitu chochote juu Yako. Nawe Ndiye Uliye karibu hakuna kitu chochote kilicho karibu kuliko Wewe, Tulipie madeni yetu na Utuepushe na ufakiri[9]

 

 

[108]

الـحَمْدُ للهِ الَّذي أَطْـعَمَنا وَسَقـانا، وَكَفـانا، وَآوانا، فَكَـمْ مِمَّـنْ لا كـافِيَ لَـهُ وَلا مُؤْوِيَ

 

AlhamduliLlaahil-LLadhiy Atw’amaanaa wasaqaanaa, wakafaanaa, wa aawaanaa. Fakam mimman laa kaafiya lahu walaa muu-wiya

 

Himdi Anastahiki Allaah Ambaye Ametulisha na Ametunywesha na Akatutosheleza na Akatuhifadhi. Kwani wangapi ambao hawana wa kuwatosheleza wala wa kuwahifadhi[10]

 

 

 

[109]

 

اللّهُـمَّ عالِـمَ الغَـيبِ وَالشّـهادةِ فاطِـرَ السّماواتِ وَالأرْضِ رَبَّ كُـلِّ شَـيءٍ وَمَليـكَه، أَشْهـدُ أَنْ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْت، أَعـوذُ بِكَ مِن شَـرِّ نَفْسـي، وَمِن شَـرِّ الشَّيْـطانِ وَشِـرْكِه، وَأَنْ أَقْتَـرِفَ عَلـى نَفْسـي سوءاً أَوْ أَجُـرَّهُ إِلـى مُسْـلِم.

 

Allaahumma ‘Aalimal-ghaybi wash-shahaadah, Faatwiras-samaawati wal-ardhwi, Rabba kulli shay-in wamaliykah. Ash-hadu an-laa ilaaha illaa Anta. A’uwdhu Bika minsharri nafsiy, wamin sharri shaytwaani wa shirkihi, wa an aqtarifa ‘alaa nafsiy suuw-an aw ajurrahu ilaa Muslim

 

Ee Allaah, Mjuzi wa ghayb na yaliyowazi, Mwanzishi wa mbingu na ardhi, Rabb wa kila kitu na Mfalme wake. Nashuhudia kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe. Najikinga Kwako kutokana na shari ya nafsi yangu na shari ya shaytwaan na shirki yake na kujichumia uovu kwa nafsi yangu au kumletea Muislamu[11]

 

 

 

[110]

 

Soma Suwrah mbili zifuatazo: Aliyf Laam Miym Tanziyl (As-Sajdah) na Suwratul Mulk[12]

 

 

أَعُوذُ بِاللّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ. بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ

 

 الم ﴿١  تَنزِيلُ الْكِتَابِ لَا رَيْبَ فِيهِ مِن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٢ أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ ۚ بَلْ هُوَ الْحَقُّ مِن رَّبِّكَ لِتُنذِرَ قَوْمًا مَّا أَتَاهُم مِّن نَّذِيرٍ مِّن قَبْلِكَ لَعَلَّهُمْ يَهْتَدُونَ ﴿٣ اللَّـهُ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۖ مَا لَكُم مِّن دُونِهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا شَفِيعٍ ۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ ﴿٤ يُدَبِّرُ الْأَمْرَ مِنَ السَّمَاءِ إِلَى الْأَرْضِ ثُمَّ يَعْرُجُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ أَلْفَ سَنَةٍ مِّمَّا تَعُدُّونَ ﴿٥ ذَٰلِكَ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿٦ الَّذِي أَحْسَنَ كُلَّ شَيْءٍ خَلَقَهُ ۖ وَبَدَأَ خَلْقَ الْإِنسَانِ مِن طِينٍ ﴿٧ ثُمَّ جَعَلَ نَسْلَهُ مِن سُلَالَةٍ مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ ﴿٨ ثُمَّ سَوَّاهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِ ۖ وَجَعَلَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ ۚ قَلِيلًا مَّا تَشْكُرُونَ ﴿٩ وَقَالُوا أَإِذَا ضَلَلْنَا فِي الْأَرْضِ أَإِنَّا لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ ۚ بَلْ هُم بِلِقَاءِ رَبِّهِمْ كَافِرُونَ ﴿١٠ قُلْ يَتَوَفَّاكُم مَّلَكُ الْمَوْتِ الَّذِي وُكِّلَ بِكُمْ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمْ تُرْجَعُونَ ﴿١١ وَلَوْ تَرَىٰ إِذِ الْمُجْرِمُونَ نَاكِسُو رُءُوسِهِمْ عِندَ رَبِّهِمْ رَبَّنَا أَبْصَرْنَا وَسَمِعْنَا فَارْجِعْنَا نَعْمَلْ صَالِحًا إِنَّا مُوقِنُونَ ﴿١٢ وَلَوْ شِئْنَا لَآتَيْنَا كُلَّ نَفْسٍ هُدَاهَا وَلَـٰكِنْ حَقَّ الْقَوْلُ مِنِّي لَأَمْلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ ﴿١٣ فَذُوقُوا بِمَا نَسِيتُمْ لِقَاءَ يَوْمِكُمْ هَـٰذَا إِنَّا نَسِينَاكُمْ ۖ وَذُوقُوا عَذَابَ الْخُلْدِ بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿١٤ إِنَّمَا يُؤْمِنُ بِآيَاتِنَا الَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُوا بِهَا خَرُّوا سُجَّدًا وَسَبَّحُوا بِحَمْدِ رَبِّهِمْ وَهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ ۩ ﴿١٥ تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ خَوْفًا وَطَمَعًا وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ ﴿١٦ فَلَا تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٧ أَفَمَن كَانَ مُؤْمِنًا كَمَن كَانَ فَاسِقًا ۚ لَّا يَسْتَوُونَ ﴿١٨ أَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَلَهُمْ جَنَّاتُ الْمَأْوَىٰ نُزُلًا بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٩ وَأَمَّا الَّذِينَ فَسَقُوا فَمَأْوَاهُمُ النَّارُ ۖ كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا أُعِيدُوا فِيهَا وَقِيلَ لَهُمْ ذُوقُوا عَذَابَ النَّارِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ﴿٢٠ وَلَنُذِيقَنَّهُم مِّنَ الْعَذَابِ الْأَدْنَىٰ دُونَ الْعَذَابِ الْأَكْبَرِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ﴿٢١ وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن ذُكِّرَ بِآيَاتِ رَبِّهِ ثُمَّ أَعْرَضَ عَنْهَا ۚ إِنَّا مِنَ الْمُجْرِمِينَ مُنتَقِمُونَ ﴿٢٢ وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ فَلَا تَكُن فِي مِرْيَةٍ مِّن لِّقَائِهِ ۖ وَجَعَلْنَاهُ هُدًى لِّبَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿٢٣ وَجَعَلْنَا مِنْهُمْ أَئِمَّةً يَهْدُونَ بِأَمْرِنَا لَمَّا صَبَرُوا ۖ وَكَانُوا بِآيَاتِنَا يُوقِنُونَ ﴿٢٤ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَفْصِلُ بَيْنَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ﴿٢٥ أَوَلَمْ يَهْدِ لَهُمْ كَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَبْلِهِم مِّنَ الْقُرُونِ يَمْشُونَ فِي مَسَاكِنِهِمْ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ ۖ أَفَلَا يَسْمَعُونَ ﴿٢٦ أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا نَسُوقُ الْمَاءَ إِلَى الْأَرْضِ الْجُرُزِ فَنُخْرِجُ بِهِ زَرْعًا تَأْكُلُ مِنْهُ أَنْعَامُهُمْ وَأَنفُسُهُمْ ۖ أَفَلَا يُبْصِرُونَ ﴿٢٧ وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْفَتْحُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٢٨ قُلْ يَوْمَ الْفَتْحِ لَا يَنفَعُ الَّذِينَ كَفَرُوا إِيمَانُهُمْ وَلَا هُمْ يُنظَرُونَ ﴿٢٩ فَأَعْرِضْ عَنْهُمْ وَانتَظِرْ إِنَّهُم مُّنتَظِرُونَ ﴿٣٠

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١ الَّذِي خَلَقَ الْمَوْتَ وَالْحَيَاةَ لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلًا ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْغَفُورُ ﴿٢ الَّذِي خَلَقَ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا ۖ مَّا تَرَىٰ فِي خَلْقِ الرَّحْمَـٰنِ مِن تَفَاوُتٍ ۖ فَارْجِعِ الْبَصَرَ هَلْ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ ﴿٣ ثُمَّ ارْجِعِ الْبَصَرَ كَرَّتَيْنِ يَنقَلِبْ إِلَيْكَ الْبَصَرُ خَاسِئًا وَهُوَ حَسِيرٌ ﴿٤ وَلَقَدْ زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِمَصَابِيحَ وَجَعَلْنَاهَا رُجُومًا لِّلشَّيَاطِينِ ۖ وَأَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابَ السَّعِيرِ ﴿٥ وَلِلَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ عَذَابُ جَهَنَّمَ ۖ وَبِئْسَ الْمَصِيرُ ﴿٦ إِذَا أُلْقُوا فِيهَا سَمِعُوا لَهَا شَهِيقًا وَهِيَ تَفُورُ ﴿٧ تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ الْغَيْظِ ۖ كُلَّمَا أُلْقِيَ فِيهَا فَوْجٌ سَأَلَهُمْ خَزَنَتُهَا أَلَمْ يَأْتِكُمْ نَذِيرٌ ﴿٨ قَالُوا بَلَىٰ قَدْ جَاءَنَا نَذِيرٌ فَكَذَّبْنَا وَقُلْنَا مَا نَزَّلَ اللَّـهُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ كَبِيرٍ ﴿٩ وَقَالُوا لَوْ كُنَّا نَسْمَعُ أَوْ نَعْقِلُ مَا كُنَّا فِي أَصْحَابِ السَّعِيرِ ﴿١٠ فَاعْتَرَفُوا بِذَنبِهِمْ فَسُحْقًا لِّأَصْحَابِ السَّعِيرِ ﴿١١ إِنَّ الَّذِينَ يَخْشَوْنَ رَبَّهُم بِالْغَيْبِ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَأَجْرٌ كَبِيرٌ ﴿١٢ وَأَسِرُّوا قَوْلَكُمْ أَوِ اجْهَرُوا بِهِ ۖ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿١٣ أَلَا يَعْلَمُ مَنْ خَلَقَ وَهُوَ اللَّطِيفُ الْخَبِيرُ ﴿١٤ هُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ ذَلُولًا فَامْشُوا فِي مَنَاكِبِهَا وَكُلُوا مِن رِّزْقِهِ ۖ وَإِلَيْهِ النُّشُورُ ﴿١٥ أَأَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاءِ أَن يَخْسِفَ بِكُمُ الْأَرْضَ فَإِذَا هِيَ تَمُورُ ﴿١٦ أَمْ أَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاءِ أَن يُرْسِلَ عَلَيْكُمْ حَاصِبًا ۖ فَسَتَعْلَمُونَ كَيْفَ نَذِيرِ ﴿١٧ وَلَقَدْ كَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ فَكَيْفَ كَانَ نَكِيرِ ﴿١٨ أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الطَّيْرِ فَوْقَهُمْ صَافَّاتٍ وَيَقْبِضْنَ ۚ مَا يُمْسِكُهُنَّ إِلَّا الرَّحْمَـٰنُ ۚ إِنَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ بَصِيرٌ ﴿١٩ أَمَّنْ هَـٰذَا الَّذِي هُوَ جُندٌ لَّكُمْ يَنصُرُكُم مِّن دُونِ الرَّحْمَـٰنِ ۚ إِنِ الْكَافِرُونَ إِلَّا فِي غُرُورٍ ﴿٢٠ أَمَّنْ هَـٰذَا الَّذِي يَرْزُقُكُمْ إِنْ أَمْسَكَ رِزْقَهُ ۚ بَل لَّجُّوا فِي عُتُوٍّ وَنُفُورٍ ﴿٢١ أَفَمَن يَمْشِي مُكِبًّا عَلَىٰ وَجْهِهِ أَهْدَىٰ أَمَّن يَمْشِي سَوِيًّا عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿٢٢ قُلْ هُوَ الَّذِي أَنشَأَكُمْ وَجَعَلَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ ۖ قَلِيلًا مَّا تَشْكُرُونَ ﴿٢٣ قُلْ هُوَ الَّذِي ذَرَأَكُمْ فِي الْأَرْضِ وَإِلَيْهِ تُحْشَرُونَ ﴿٢٤ وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٢٥ قُلْ إِنَّمَا الْعِلْمُ عِندَ اللَّـهِ وَإِنَّمَا أَنَا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٢٦ فَلَمَّا رَأَوْهُ زُلْفَةً سِيئَتْ وُجُوهُ الَّذِينَ كَفَرُوا وَقِيلَ هَـٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَدَّعُونَ ﴿٢٧ قُلْ أَرَأَيْتُمْ إِنْ أَهْلَكَنِيَ اللَّـهُ وَمَن مَّعِيَ أَوْ رَحِمَنَا فَمَن يُجِيرُ الْكَافِرِينَ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ ﴿٢٨ قُلْ هُوَ الرَّحْمَـٰنُ آمَنَّا بِهِ وَعَلَيْهِ تَوَكَّلْنَا ۖ فَسَتَعْلَمُونَ مَنْ هُوَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٢٩ قُلْ أَرَأَيْتُمْ إِنْ أَصْبَحَ مَاؤُكُمْ غَوْرًا فَمَن يَأْتِيكُم بِمَاءٍ مَّعِينٍ ﴿٣٠

 

 

 

[111]

 

اللّهُـمَّ أَسْـلَمْتُ نَفْـسي إِلَـيْكَ، وَفَوَّضْـتُ أَمْـري إِلَـيْكَ، وَوَجَّـهْتُ وَجْـهي إِلَـيْكَ، وَأَلْـجَـاْتُ ظَهـري إِلَـيْكَ، رَغْبَـةً وَرَهْـبَةً إِلَـيْكَ، لا مَلْجَـأَ وَلا مَنْـجـا مِنْـكَ إِلاّ إِلَـيْكَ، آمَنْـتُ بِكِتـابِكَ الّـذي أَنْزَلْـتَ وَبِنَبِـيِّـكَ الّـذي أَرْسَلْـت

 

Allaahumma aslamtu nafsiy Ilayka, wa fawwadhwtu amriy Ilayka, wa wajjahtu waj-hiya Ilayka, wa alja-tu dhwahriy Ilayka, raghbatan warahbatan Ilayka. Laa malja-a walaa manjaa Minka illaa Ilayka. Aamantu Bikitaabikal-ladhiy Anzalta wabi Nabiyyikal-lladhiy Arsalta

 

Ee Allaah nimeisalimisha nafsi yangu Kwako, na nimekuachia mambo yangu Wewe na nimeuelekeza uso wangu Kwako na nimeutegemeza mgongo wangu Kwako, kwa matajarajio na kwa kukuogopa, hapana sehemu ya kukimbilia wala ya kujiokoa ila Kwako. Nimekiamini kitabu Chako Ulichokiteremsha na Nabiy Wako uliyemtuma[13]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (9/62) [5017], Muslim (4/1723) [2192]

[2] Suwratul-Baqarah (2: 255), Hadiyth ya Abu Huraryah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayeisoma atakapokuwa usiku kitandani atabakia katika hifadhi ya Allaah wala hatokaribiwa na shaytwaan mpaka aamke)) -  Al-Bukhaariy na Al-Fat-h (4/487) [2311]. Taz pia Adhkaar za Asubhi na Jioni [75]

[3]Hadiyth ya Abu Mas-‘uwd Al-Answaariyy ‘Uqbah bin ‘Amruw bin Tha’labah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayesoma usiku Aayah mbili za mwisho wa Suwratul-Baqarah zitamtosheleza)) Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (9/94) [4008], Muslim (1/554) [808].

[4]Hadiyth ya Abu Huraryrah (رضي الله عنه) Mwanzo wa Hadiyth ni kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم):  ((Akiamka mmoja wenu kutoka usingizini kisha akarudi basi akikungute kitanda kwa shuka yake mara tatu [aseme BismiLLaah] kwani hajui kilicho kuja baada yake, kisha akiweka ubavu wake [kitandani] aseme .....)) - Al-Bukhaariy (11/126) [6320], Muslim (4/2084) [2714].

[5]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar  (رضي الله عنهما) - Muslim (4/2083) [2712], na Ahmad kwa tamshi lake (2/79)

[6]Hadiyth ya Hafswah bint ‘Umar (رضي الله عنهما) mke wa Nabiy (صلى الله عليه وسلم) ametaja mwanzo wa Hadiyth kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akitaka kulala, akiweka mkono wake wa kulia chini ya shavu lake kisha anasema...)) - Abu Daawuwd kwa tamshi lake (4/311) [5045], na Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/143).

 

Tanbihi:  Imaam Al-Albaaniy amesema: “Bila ya kukariri mara tatu.”

[7]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na al-Fat-h (11/113) [6312], Muslim (4/2083) [2711] Hadiyth ya Al-Baraa-a (رضي الله عنه)

[8]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه) amesema: “Faatwimah alimwendea Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akimuomba mtumishi, akawa hakumkuta bali alimkuta ‘Aaishah (رضي الله عنهما) akamwachia maagizo ya haja yake. Akatujia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) wakati tumeshaingia kitandani akasema: ((Je nikujulisheni lilokuwa bora kwenu kuliko mtumishi? Mtakapopanda kitandani [kulala], semeni Subhaana-Allaah mara thelathini na tatu, na AlhamduliLLaah mara thelathini na tatu, na Allaahu Akbar mara thelathini na nne, kwani hivyo ni bora kwenu kuliko mtumishi)) -  Al-Bukhaariy  pamoja na Al-Fat-h (7/71) [3705], Muslim (4/2091) [2727].

[9]Hadiyth ya Abu Hurayrah  (رضي الله عنه)- Muslim (4/2084) [2713]

[10]Hadiyth ya Anas bin Maalik  (رضي الله عنه)- Muslim (4/2085) [2715]

[11]Hadiyth ya ‘Abdullaahh bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw  (رضي الله عنه)- Abu Daawuwd (4/317) [5083] na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/142)- Rejea juu [Du’aa namba 85] Nyiradi za Asubuhi na Jioni.

[12]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه) Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa  halali mpaka asome

 

ألم تَنْزِيلُ السَّجْدَةَ

Na,

تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ الْمُلْكُ 

At-Tirmidhiy [3404], An-Nasaaiy fiy ‘amal al-Yawm wal-Layl [707], na Taz Swahiyh Al-Jaami’ (4/255) [4873]

[13]Hadiyth ya Al-Baraaa bin ‘Aazib (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Ukitaka kulala tawadha udhu kama wa Swalaah kisha lalia ubavu wako wa kulia kisha sema ….)) – Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/113) [4788, 6315, 6313], Muslim (4/2081) [2710] na imekuja mwisho wa Hadiyth: ((Atakayesema hivyo akafariki usiku huo atafariki katika fitwrah [maumbile sahihi], na ifanyeni iwe ya [nyiradi] ya mwisho kuisoma)) Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/113) Muslim (4/2081)

 

 

Share

029-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unapojigeuzageuza Usingizini Usiku

Hiswnul-Muslim

029-Du’aa Unapojigeuzageuza Usingizini Usiku

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[112]

لا إِلـهَ إِلاّ اللهُ الـواحِدُ القَهّـار، رَبُّ السَّـمواتِ وَالأرْضِ وَما بَيْـنَهـما، العَزيـزُ الغَـفّار

 

Laa ilaaha illa-Allaahul-Waahidul-Qahhaar. Rabbus-samawaati wal ardhwi wamaa baynahumaal-’Aziyzul-Ghaffaar.

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah  Mmoja Pekee, Mshindi Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Rabb wa mbingu na ardhi na vilivyo kati yake, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika daima, Mwingi wa kughufuria.[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) Asome hivyo pale anapojigeuzageuza kuhangaika kupata usingizi) - Al-Haakim na ameisahihisha Adh-Dhahabiy (1/540), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [864] na ibn As-Sunniy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [757]. Na angalia: Swahiyh al-Jaami’ (4/213) [4693].

 

 

Share

030-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Wasiwasi Usingizini Au Kusikia Uoga Na Mfadhaiko

Hiswnul-Muslim

030-Du’aa Ya Wasiwasi Usingizini Au Kusikia Uoga Na Mfadhaiko

www.alhidaaya.com

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [113]

أَعـوذُ بِكَلِمـاتِ اللّهِ التّـامّـاتِ مِن غَضَـبِهِ وَعِـقابِهِ، وَشَـرِّ عِبـادِهِ وَمِنْ هَمَـزاتِ الشَّـياطينِ وَأَنْ يَحْضـرون.

 

A’uwdhu bikalimatiLLaahit-taammati min ghadhwabihi wa ’iqaabihi, washarri ’Ibaadihi, wamin hamazaatish-shayaatwini wa an yahdhwuruwn

 

Najikinga kwa maneno ya Allaah yaliotimia kutokana na ghadhabu Zake na adhabu Yake na shari ya waja Wake na vioja vya mashaytwaan na kunijia kwao[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aaasw (رضي الله عنه)  - Abu Daawud (4/12) [3893], na Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/171). Taz pia Sharh Al-‘Aqiydah Al-Waasitwiyyah ya Muhammad Khaliyl Al-Haraas uk (103], na ya Al-‘Uthaymiyn (Uk. 217).

 

 

Share

031-Hiswnul-Muslim: Ipasavyo Kufanya Na Kusema Mwenye Kuota Ndoto Njema Au Mbaya

Hiswnul-Muslim

031-Ipasavyo Kufanya Na Kusema Mwenye Kuota Ndoto Njema Au Mbaya

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[114]

 

Anayeota ndoto mbaya anatakiwa afanye yafuatayo:  

 

1- Atafili (ateme mate) kushotoni kwake mara tatu.

 

2-Aombe kinga kwa Allaah kutokana na shaytwaan kwa shari aliyoiota (aseme:

 

أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجيـم

A’uwdhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiym – mara tatu)

 

 

3-Asimuhadithie mtu yeyote[1]  

 

 

4-Agueuke upande mwengine (alioota ndoto mbaya)[2]    

 

 

[115]

 

5-Ainuke kuswali akitaka[3]   

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Qataadah bin Rib-’iyy;  imesemekana jina lake pia ni: Al-Haarith na pia imesemekana ni: ‘Amruw (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:  ((Ndoto nzuri inatoka kwa Allaah, na ndoto mbaya ni kutoka kwa shaytwaan. Atakapoota mmoja wenu kinachomchukiza, basi atakapozindukana, apulize kushotoni mwake mara tatu na aombe kinga kwa Allaah kutokana na shari yake, basi hakitamdhuru [kitu])). Na riwaayah nyingine: ((Atakayeota mmoja wenu atakachokipenda, asimhadithie yeyote isipokuwa yule anayempenda. Na atakapoota anachokichukia asimhadithie mtu, na atafili (ateme mate) kushotoni mwake mara tatu na aombe kinga kwa Allaah kutokana na shaytwaanir-rajiym kwa shari aliyoiota, basi haitamdhuru [kitu])) Kauli hizo ni kutoka Hadiyth katika Muslim (4/1772) [2261], Al-Bukhaariy [7044].   

[2]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنهما), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayeoota mmoja wenu ndoto anayoichukia, atafili (ateme mate) kushotoni mwake mara tatu, na aombe kinga kwa Allaah kutokana na shaytwaan mara tatu, na ageuke [kulala] upande mwengine)) - Muslim (4/1773) [2262].   

[3]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: “Muda utakapokuwa mfupi, njozi ya Muumini itakuwa haiongopi tena, na mwenye njozi ya kweli zaidi kati yenu ni yule aliye msema kweli zaidi, na njozi ya Muumini ni sehemu moja kati ya sehemu 46 za Unabii.  Na ndoto ni aina tatu: Njozi njema ambayo ni bishara toka kwa Allaah, na ndoto ya kuhuzunisha itokanayo na shaytwaan, na ndoto kutokana na mtu kuizungumzisha nafsi yake (mawazo yaliyotawala zaidi kwenye akili yake).” [Muslim (2263]4/1773)]

 

 

Share

032-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Qunuwt Ya Witr

Hiswnul-Muslim

032-Du’aa Ya Qunuwt Ya Witr

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[116]

 

اللّهُـمَّ اهْـدِنـي فـيمَنْ هَـدَيْـت، وَعـافِنـي فـيمَنْ عافَـيْت، وَتَوَلَّـني فـيمَنْ تَوَلَّـيْت، وَبارِكْ لـي فـيما أَعْطَـيْت، وَقِـني شَرَّ ما قَضَـيْت، فَإِنَّـكَ تَقْـضي وَلا يُقْـضى عَلَـيْك، إِنَّـهُ لا يَـذِلُّ مَنْ والَـيْت، (وَلا يَعِـزُّ مَن عـادَيْت) تَبـارَكْـتَ رَبَّـنا وَتَعـالَـيْت.

 

Allaahummah-diniy fiyman Hadayta, wa 'Aafiniy fiyman 'Aafayta, wa Tawallaniy fiyman Tawallayta, wa Baarik-liy fiymaa A'attawyta, wa Qiniy sharra maa Qadhwayta, fainnaka Taqdhwiy  walaa yuqdhwa 'Alayka. Innahu laa yadhillu man Waalayta, walaa ya'izzu man 'Aadayta, Tabaarakta Rabbanaa wa Ta'aalayta.

 

Ee Allaah! Niongoze pamoja na Uliowaongoza, na Unipe afya pamoja na Uliowapa afya njema, na Nifanye kuwa ni mpenzi Wako pamoja na Uliowafanya  wapenzi na Nibariki katika Ulichonipa na Nikinge na shari ya Ulilolihukumu kwani Wewe Unahukumu wala Huhukumiwi. Hakika hadhaliliki Uliyemfanya mpenzi (wala hana ’izzah (hadhi)  Uliyemfanya adui) Umebarikika Ee Rabb wetu na Umetukuka[1]

 

 

 

 [117]

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِرِضـاكَ مِنْ سَخَطِـك، وَبِمُعـافاتِـكَ مِنْ عُقوبَـتِك، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْـك، لا أُحْصـي ثَنـاءً عَلَـيْك، أَنْـتَ كَمـا أَثْنَـيْتَ عَلـى نَفْسـِك

 

Allaahumma inniy a'uwdhu bi Ridhwaaka min sakhatwika, wa bi mu'aafaatika min 'uquwbatika, wa a'uwudhu Bika Minka, laa ukhswiy Thanaa-an 'Alayka, Anta kamaa Athnayta 'Alaa Nafsika.

 

Ee Allaah! Hakika mimi najikinga kwa radhi Zako kutokana na hasira Zako na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako, na najikinga  Kwako kutokana na Wewe, mimi siwezi kuzidhibiti sifa Zako kwa kadiri ya idadi yake, Wewe ni kama Ulivyojisifu Mwenyewe[2]

 

 

 

 [118]

 

اللّهُـمَّ إِيّـاكَ نعْـبُدْ، وَلَـكَ نُصَلّـي وَنَسْـجُد، وَإِلَـيْكَ نَسْـعى وَنَحْـفِد، نَـرْجو رَحْمَـتَك، وَنَخْشـى عَـذابَك، إِنَّ عَـذابَكَ بالكـافرين ملْحَـق. اللّهُـمَّ إِنّا نَسْتَعـينُكَ وَنَسْتَـغْفِرُك، وَنُثْـنـي عَلَـيْك الخَـيْرَ، وَلا نَكْـفُرُك، وَنُـؤْمِنُ بِك، وَنَخْـضَعُ لَكَ وَنَخْـلَعُ مَنْ يَكْـفرُك

 

Allaahumma Iyyaaka na'-budu, walaka nuswwaliy wa nasjudu, wa Ilayka nas-'aa wa nahfidu, narjuw Rahmataka wa nakhshaa 'adhaabak, inna 'adhaabaka bilkaafiriyna mulhaqq. Allaahumma innaa nasta'iynuka wa nastaghfiruka, wa nuthniy 'Alaykal-khayra, wa laa nakfuruka, wa nu-uminu Bika, wa nakhdhwa'u Laka, wa nakhla'u man yakfuruka.

 

Ee Allaah! Wewe tu Ndiye tunayekuabudu, na Kwako tunaswali na tunasujudu, na Kwako tunakimbilia na tunakutumikia, tunataraji Rehma Yako na tunaogopa adhabu Yako, kwani adhabu Yako hakuna shaka kuwa makafiri itawafikia. Ee Allaah! Hakika sisi tunakutaka msaada na tunakuomba maghfirah na tunakusifu kwa kheri na wala hatukukufurishi na tunakuamini Wewe, na tunakunyenyekea na tunamuepuka anayekukufuru[3]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Al-Hasan bin ‘Aliy (رضي الله عنهما) - Aswhaabus-Sunan wane; Abu Daawuwd [1425], At-Tirmdhiy [464], An-Nasaaiy (1/252), Ibn Maajah [1178], Ahmad (1/200), Ad-Daarimiy (1/373), Al-Haakim (3/173), Al-Bayhaqiy (2/209) [497, 4987]. Taz pia Swahiyh At-Tirmidhiy (1/144) na Swahiyh Ibn Maajah (1/194), na Irwaa Al-Ghaliyl ya Al-Albaaniy (رحمه الله)  (2/172).

[2]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه), -Aswaabus-Sunan wane; Abu Daawuwd [ 1427], At-Tirmidhiy [3561], An-Nasaaiy (1/252), Ibn Maajah [1179], Ahmad (1/96, 118, 150), na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/180), Swahiyh Ibn Maajah (1/194) na Al-Irwaa (2/175)

[3]Hadyth ya ‘Umra bin Al-Khatwaab (رضي الله عنه) - Al-Bayhaqiy katika As-Sunan Al-Kubraa na ameisahihisha isnadi yake (2/211) na amesema Shaykh Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Arwaa Al-Ghaliyl na hii isnadi Swahiyh (2/170) nayo ni mawquwfun kwa ‘Umar (رضي الله عنه).

 

 

Share

033-Hiswnul-Muslim: Du’aa Baada Ya Salaam Katika Swalaah Ya Witr

Hiswnul-Muslim

033-Du’aa Baada Ya Salaam Katika Swalaah Ya Witr

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [119]

 

Mwisho kabisa baada ya kumaliza Swalaah yote na sio baada ya kila Rakaa mbili au nne. Mtu aseme:

 

سُـبْحانَ المَلِكِ القُدّوسِ

Subhaanal-Malikil-Qudduwsi (mara tatu).

 

Utakasifu ni wa Allaah Mfalme, Mtakatifu

 

Ya tatu yake aivute kwa sauti yake na huku akisema:

 

(ربِّ الملائكةِ والرّوح)

 Rabbil-Malaaikati war-Ruwh

 

Ee Rabb wa Malaika na wa Jibriyl[1]

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdur-Rahmaan bin Abzay (رضي الله عنه)- An-Nasaaiy (3/244), Ad-Daaraqutwniy na wengineo, na ilivyo katika mabano ni ziada ya Ad-Daaraqutwniy (2/31), na isnadi yake Swahiyh. Angalia: Zaad Al-Ma’aad kwa tahqiyq ya Shu’ayb Al-Arnaawutw, na ‘Abdul-Qaadir Al-Arnaawutw (1/337)

 

 

Share

034-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ukiwa Na Wahka Na Huzuni

Hiswnul-Muslim

034-Du’aa Ukiwa Na Wahka Na Huzuni

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

[120]

 

اللّهُـمَّ إِنِّي عَبْـدُكَ، ابْنُ عَبْـدِكَ، ابْنُ أَمَتِـكَ نَاصِيَتِي بِيَـدِكَ، مَاضٍ فِيَّ حُكْمُكَ، عَدْلٌ فِيَّ قَضَاؤكَ، أَسْأَلُـكَ بِكُلِّ اسْمٍ هُوَ لَكَ، سَمَّـيْتَ بِهِ نَفْسَكَ، أِوْ أَنْزَلْتَـهُ فِي كِتَابِكَ، أَوْ عَلَّمْـتَهُ أَحَداً مِنْ خَلْقِـكَ، أَوِ اسْتَـأْثَرْتَ بِهِ فِي عِلْمِ الغَيْـبِ عِنْـدَكَ، أَنْ تَجْـعَلَ القُرْآنَ رَبِيـعَ قَلْبِـي، وَنورَ صَـدْرِي، وجَلَاءَ حُـزْنِي، وذَهَابَ هَمِّـي 

Allaahumma inniy ‘abduka, ibnu-‘abdika, ibnu-amatika, naaswiyaatiy Biyadika, maadhwin fiyya hukmuka, ‘adlun fiyya qadhwaauka, as-aluka bikullismin huwa Laka, sammayta bihi Nafsaka aw Anzaltahu fiy Kitaabika, aw ‘Allamtahu ahadan min Khalqika, awis-staa-tharta bihi fiy ‘ilmil-ghaybi  ‘Indaka, an Taj-’alal-Qur-aana rabiy’a qalbiy, wanuwra swadriy, wajalaa huzniy, wadhahaaba hammiy.

 

Ee Allaah hakika mimi ni mja Wako, mwana wa mja Wako, mwana wa mja wako mwanamke, utosi wangu uko Mikononi Mwako, yaliyopita kwangu yako katika hukumu Yako, ni usawa kwangu kunihukumu Kwako, nakuomba kwa kila Jina ambalo ni Lako Ulilojiita Kwako Mwenyewe au Uliloliteremsha katika Kitabu Chako, au Ulilomfundisha yoyote yule kati ya viumbe Vyako, au Ulilolihifadhi Wewe mwenyewe (na kujihusisha kulijuwa) katika ilimu ya ghaibu Kwako, nakuomba Ujaalie Qur-aan kuwa ni rabiy' (uhuisho, raha, furaha na ustawisho) wa moyo wangu na nuru ya kifua changu, na ufumbuzi wa  huzuni yangu[1]

 

Mwanamke aseme:

 اللَّهُمَّ إنِّي أَمَتُك، بِنْتُ عَبْدِك، بنتُ أَمَتِك[2]

 

Allaahumma inniy amatuka, bintu ’abdika, bintu amatika ... 

 

Ee Allaah, hakika mimi mja Wako mwanamke, binti wa mja wako, binti wa mja Wako mwanamke...

 

 

 [121]

اللّهُـمَّ إِنِّي أَعْوذُ بِكَ مِنَ الهَـمِّ وَالْحُـزْنِ، والعًجْـزِ والكَسَلِ والبُخْـلِ والجُـبْنِ، وضَلْـعِ الـدَّيْنِ وغَلَبَـةِ الرِّجال.

 

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika minal hammi walhuzni, wal ‘ajzi walkasli, walbukhli, waljubni, wadhwal-‘id-dayni waghalabatir-rijaal

 

Ee Allaah hakika mimi najikinga Kwako kutokana na wahka na huzuni na kushindwa nguvu na  uvivu na ubakhili na uoga na uzito wa deni na kushindwa na watu[3]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin Mas-‘uwd (رضي الله عنه) - Ahmad (1/391) [452], Al-Haakim (1/509) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Al-Kalimi Atw-Twayyib [124].

 

[2] Majmuw’ Fataawaa Ibn Baaz (6/76) na Majmuw’ Fataawa Ibn Taymiyyah (2/177).  

 

[3]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) Al-Bukhaariy (7/158) [6363], Taz Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/173). At-Tirmidhiy “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akizidisha kuisoma du’aa hii”.

Share

035-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unapopatwa Janga Au Balaa

Hiswnul-Muslim

035-Du’aa Unapopatwa Janga Au Balaa

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [122]

 

لا إلَهَ إلاَّ اللَّهُ الْعَظـيمُ الْحَلِـيمْ، لا إلَهَ إلاَّ اللَّهُ رَبُّ العَـرْشِ العَظِيـمِ، لا إلَهَ إلاَّ اللَّهُ رَبُّ السَّمَـوّاتِ ورّبُّ الأَرْضِ ورَبُّ العَرْشِ الكَـريم

 

Laa ilaaha illa-Allaahul-‘Adhwiymul-Haliym. Laa ilaaha illa-Allaahu Rabbul-‘Arshil-‘Adhwiym. Laa ilaaha illa-Allaahu Rabbus-samawaati wa Rabbul-Ardhwi wa Rabbul-‘Arshil-Kariym.

 

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Aliye Mtukufu Mwenye kuvumilia (waja), hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Rabb wa ‘Arshi Tukufu, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Rabb wa mbingu na Rabb wa ardhi na Rabb wa ‘Arshi tukufu[1]

 

 

 

 [123]

 

اللّهُـمَّ رَحْمَتَـكَ أَرْجـو فَلا تَكِلـني إِلى نَفْـسي طَـرْفَةَ عَـيْن، وَأَصْلِـحْ لي شَأْنـي كُلَّـه لَا إِلَهَ إِلَّا أنْـت

 

Allaahumma Rahmatika arjuw falaa takilniy ilaa nafsiy twarfata ‘aynin, wa aswlih liy sha-aniy kullahu, laa ilaaha illaa Anta

 

Ee Allaah, Rehma Zako nataraji, usinitegemeze  kwenye nafsi yangu japo kwa muda wa upepesa jicho, na Unitengenezee mambo yangu yote, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe[2]

 

 

 

 [124]

لاَ إِلَهَ إِلَّا أنْـت سُـبْحانَكَ إِنِّي كُنْـتُ مِنَ الظّـالِميـن

 

Laa ilaaha illaa Anta Subhaanaka inniy kuntu minadhw-dhwaalimiyn

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, Utakasifu ni Wako,   Hakika mimi ni miongoni mwa waliojidhulumu[3] 

 

 

 

 [125]

اللهُ اللهُ رَبِّي لا أُشْـرِكُ بِهِ شَيْـئاً

 

Allaahu Allaahu Rabbiy laa ushriku Bihi shay-aa

 

Allaah Allaah Rabb wangu, simshirikishi na chochote[4]

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy (7/154) [6346], Muslim (4/2092) [2730] na Ahmad.

[2]Hadiyth ya Abu Bakr Nafiy’ bin Haarith Ath-Thaqafiyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (4/324) [5090], Ahmad (5/42),  ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (3/959) 

[3]Sa’ad bin Abi Waqqaasw (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/529) ]3505], Ahmad, Al-Haakim  na ameisahihisha na ameikubali Adh-Dhahaby (1/505) na Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/168) Du’aa ya Nabiy Yuwnus katika Suwratul-Anbiyaa (21:87) alipokuwa tumboni mwa samaki.

[4]Hadiyth ya Asmaa bint ‘Umays (رضي الله عنها)  - Abu Daawuwd (2/87) [1525] na Taz  Swahiyh Ibn Maajah (2/335).

 

 

Share

036-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Anaekutana Na Adui Au Mwenye Kutawala

Hiswnul-Muslim

036-Du’aa Ya Anaekutana Na Adui Au Mwenye Kutawala

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[126]

اللّهُـمَّ إِنا نَجْـعَلُكَ في نُحـورِهِـم، وَنَعـوذُ بِكَ مِنْ شُرورِهـمْ

 

Allaahumma innaa naj-’aluka fiy nuhuwrihim, wa na’uwdhu Bika min shuruwrihim

 

Ee Allaah,  hakika sisi tunakufanya Wewe Uwe katika vifua  vyao na tunajikinga Kwako kutokana na shari zao[1]

 

 

 

[127]

اللّهُـمَّ أَنْتَ عَضُـدي، وَأَنْتَ نَصـيري، بِكَ أَجـولُ وَبِكَ أَصـولُ وَبِك أُقـاتِل

 

Allaahumma Annta ’Adhwudiy, wa Anta Naswiyriy. Bika Ajuwlu wabika aswuulu wabika uqaatilu

 

Ee Allaah Wewe Msaidizi wangu Nawe Ndiye Mnusura wangu, Kwako ninazunguka na Kwako  ninavamia na Kwako ninapigana[2]

 

 

[128]

حَسْبُـنا اللهُ وَنِعْـمَ الوَكـيل

Hasbuna-Allaah wa Ni’-mal-Wakiyl

 

Allaah Anatutosheleza Naye ni Mbora wa kumtegemea [3]

 

 

 


[1]Hadiyth ya Abu Muwsaa Al-Ash’ariyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (2/89) [1037],   Taz Swahiyh Abi Daawuwd (1537). Ameisahihisha pia Al-Haakim na ameikubali Adh-Dhahaby (2/142).

[2]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (3/42) [2632], At-Tirmidhiy (5/572) [3584]na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/183).

[3]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما), “Ameisema Ibraahiym (عليه السلام) alipotupwa Motoni na ameisema Muhammad (صلى الله عليه وسلم) waliposema

 

إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ ﴿١٧٣﴾

 ((Hakika watu wamejumuika dhidi yenu, basi waogopeni” (Haya) Yakawazidishia iymaan; na wakasema: “Allaah Anatutosheleza Naye ni Mbora wa kumtegemea”)) (Suwrat Aal ’Imraan 3:173) - Al-Bukhaariy (5/172) [4563]. 

 

 

Share

037-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Mwenye Kuogopa Dhulma Ya Mwenye Kutawala

Hiswnul-Muslim

037-Du’aa Ya Mwenye Kuogopa Dhulma Ya Mwenye Kutawala

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[129]

 

أللَّهُمَّ رَبَّ السَّمواتِ السَّبْعِ وَرَبَّ الْعَرْشِ الْعَظِيم، كُنْ لِي جاَراً مِنْ (فُلانِ بْنِ فُلاَنٍ) وَأَحْزَابِهِ مِنْ خَلاَئِقِكَ أَنْ يَفْرُطَ عَلَيَّ أحَدٌ مِنْهُمْ أَوْ يَطْغَى، عَزَّ جاَرُكَ وَجَلَّ ثَناَؤُكَ، وَ لاَ إِلَهَ إلاَّ أَنْتَ

 

Allaahumma Rabbas-samaawatis-sab-’i wa Rabbal-‘Arshil-‘Adhwim, kun liy jaaran min (fulani bin fulani) wa ahzaabihi min Khalaaiqika an yafrutwa ‘alayya ahadun minhum aw yatw-ghaa. ‘Azza Jaaruka, wa Jalla Thanaauka, walaa ilaaha illaa Anta

 

Ee Allaah, Rabb wa mbingu saba, na Rabb wa ‘Arshi Tukufu, kuwa Mlinzi wangu kutokana na (fulani bin fulani [taja mtu unayemhofu])  na vikosi vyake miongoni mwa viumbe Vyako, kwa kunisaliti mmoja miongoni  mwao, au kunifanyia uadui. Imeimarika madhubuti hifadhi Yako, na zimetukuka sifa Zako na hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe[1]

 

 

 

 [130]

 

الله أكْبَر، الله أعَزُّ مِنْ خَلْقِهِ جَمِيْعاً، الله أعَزُّ مِمَّا أخَافُ وَأحْذَر، أعُوذُ بِاللهِ الَّذِي لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ، الْمُمْسِكِ السَّمَوَا تِ السَّبْعِ أَنْ يَقَعْنَ عَلَى الأَرْضِ ِإلاَّ بِإِذْنِهِ، مِنْ شَرِّ عَبْدِكَ (فلان) وَجُنُوْدِهِ وَأَتْبَاعِهِ وَأَشْيَاعِهِ، مِنَ اْلجِنِّ والإِنْسِ، اَلَّلهُمَّ كُنْ لِيْ جَاراً مِنْ شَرِّهِمْ، جَلَّ ثَنَاؤُكَ وَعَزَّ جَارُكَ، وَتَبَارَكَ اسْمُكَ، وَلاَ إلَهَ غَيْرُكَ

 

Allaahu Akbar, Allaahu A’azzu min Khalqihi jamiy’aa. Allaahu A’azzu mimmaa akhaafu wa ahdharu. A’uwdhu biLLaahi Alladhiy laa ilaaha illaa Huwa. Al-Mumsikis-samawaatis-sab-’i an yaqa’-na ‘alal-ardhwi illaa biidhnihi, min sharri ‘abdika (fulani - mtaje mtu unayemhofu) wa junuwdihi, wa atbaa’ihi, wa ash-yaa’ihii minal jinni wal insi. Allaahumma kunliy jaaran min sharrihim, Jalla Thanaauka, wa ‘Azza Jaaruka, wa Tabaarakas-Smuka walaa ilaaha Ghayruka [mara 3]

 

Allaah ni Mkubwa, Allaah, ni Mwenye nguvu na Mshindi kuliko viumbe Vyake vyote. Allaah ni Mwenye nguvu na Mshindi kuliko kila nikiogopacho na kujihadhari. Najikinga kwa Allaah Ambaye hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye tu Ambaye  Ameshikilia mbingu saba ili zisiangukie ardhi ila kwa idhini Yake, kutokana na shari ya mja  (fulani - mtaje mtu unayemhofu) na majeshi yake, na wanaomfuata, na wafuasi wake miongoni mwa majini na watu.  Ee Allaah, kuwa Mlinzi wangu kutokana na shari yao. Zimetukuka sifa Zako na Umehishimika ulinzi Wako na Limebarikika Jina Lako, na hapana mwabudiwa wa haki ghairi Yako[2]

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy fiy Al-Adab Al-Mufrad [707] na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Al-Adab Al-Mufrad [546]. 

[2]Du’aa ya ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy fiy Adabil-Mufrid [708] na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Al-Adab Al-Mufrad [546].

 

 

Share

038-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Adui

Hiswnul-Muslim

038-Du’aa Ya Kumuombea Adui

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[131]

اللَّهُمَّ مُنْزِلَ اْلِكتَابِ، سَرِيْعَ الْحِسَابِ، اِهْزِمِ الإْحْزَابَ، اللَّهُمَّ اِهْزِمْهُمْ وَزَلْزِلْهُمْ

 

Allaahumma Munzilal-Kitaab. Sariy’al-hisaabi. Ihzimil-Ahzaaba. Allaahumma Ihzim-hum wazalzil-hum

 

Ee Allaah, Mteremsha wa Kitabu, Mwepesi wa kuhisabu (waja Wako) Vishinde vikosi. Ee Allaah, washinde na watetemeshe[1]

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Abi Awfaa (رضي الله عنه) Muslim (3/1362) [1742].

 

 

Share

039-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unapoogopa Watu

Hiswnul-Muslim

039-Du’aa Unapoogopa Watu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[132]

اللَّهُمَّ اكْفِنِيهِمْ بِماَ شِئْتَ

Allaahummak-finiyhim bimaa Shi-ita

 

Ee Allaah, nitosheleze kutokana na wao kwa Unachotaka[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Swuhayb bin Sinaan, Abu Yahya Ar-Ruwmiy (رضي الله عنه) Muslim (4/2300) [3005].

 

Share

040-Hiswnul-Muslim: Du’aa Aliyepatwa Na Shaka Katika Iymani Yake

Hiswnul-Muslim

040-Du’aa Aliyepatwa Na Shaka Katika Iymani Yake

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

[132]

 

1-Aombe kinga kwa Allaah (aseme:)

أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجيـم

Au’wudhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiym

 

 

2-Aondoe moyoni kile kitu alichokifanyia shaka[1]

 

 

[134]

 

3-Kisha aseme:

آمَنْـتُ بِاللهِ وَرُسُـلِه

Aamantu BiLLaahi wa Rusulih

 

Nimemuamini Allaah na Rasuli Wake[2]

 

 

[135]

 

 

4-Kisha asome kauli ya Allaah Ta’aalaa:  

  هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣

 

3. Yeye Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yake, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na Aliye juu hakuna kitu juu Yake, na Aliye karibu, hakuna kitu kilichokaribu kuliko Yeye, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi. [3]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) – Kauli mbili hizo ni katika Hadiyth moja aliyoitoa Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/336) [3276], Muslim (1/120) [134], [214].

[2]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Muslim (1/119, 120) [134], [212].

[3]Ameisoma hivyo ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Abu Daawuwd (4/329) [5110] na ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (3/962). Aayah Suwratul Hadiyth (57:3). Na katika Muslim [2713] amepokea kuhusu Tafsiyr ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) Majina manne (ya Allaah) yaliyotajwa katika Aayah kwa du’aa yake (صلى الله عليه وسلم)

 

اللَّهُمَّ أَنْتَ الأَوَّلُ فَلَيْسَ قَبْلَكَ شَيْءٌ, وَأَنْتَ الآَخِرُ فَلَيْسَ بَعْدَكَ شَيْءٌ, وَأَنْتَ الظَّاهِرُ فَلَيْسَ فَوْقَكَ شَيْءٌ, وَأَنْتَ الْبَاطِنُ فَلَيْسَ دُونَكَ شَيْءٌ

((Ee Allaah, Wewe Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yako, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yako, na Uliye juu hakuna kitu juu Yako, na Uliye karibu, hakuna kitu kilichokaribu kuliko Wewe)).

 

 

Share

041-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kulipa Deni, Kinga Ya Wahka, Huzuni, Uvivu, Ubakhili n.k

Hiswnul-Muslim

041-Du’aa Ya Kulipa Deni, Kinga Ya Wahka, Huzuni, Uvivu, Ubakhili n.k

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[136]

 

اللّهُـمَّ اكْفِـني بِحَلالِـكَ عَنْ حَـرامِـك، وَأَغْنِـني بِفَضْـلِكِ عَمَّـنْ سِـواك

 

Allaahummakfiniy bihalaalika ’an haraamika, waghniniy bifadhwlika ’amman siwaak

 

Ee Allaah nitosheleze mimi na halali Yako kutokana na haraam, na Unitosheleze kwa fadhila Zako nisiwahitaji wengine ghairi Yako[1]

 

 

 

[137]

اللّهُـمَّ إِنِّي أَعْوذُ بِكَ مِنَ الهَـمِّ والْحَزَنِ، والعًجْـزِ والكَسَلِ والبُخْـلِ والجُـبْنِ، وضَلْـعِ الـدَّيْنِ وغَلَبَـةِ الرِّجال.

 

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika minal-hammi walhazani, wal-’ajzi walkasali, walbukhli, waljubni, wa dhwala’id-dayn, waghalabatir-rijaal

 

Ee Allaah hakika mimi najikinga Kwako kutokana na wahka na huzuni na kutoweza, na uvivu, na ubakhili, na uoga, na uzito wa deni na kushindwa na watu[2]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/560) [3563], na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/180)

[2]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (7/158) [6363] Imetajwa juu katika ‘Du’aa Ukiwa Na wahka na huzuni’ [121]

 

 

Share

042-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Aliyeingiwa Na Wasiwasi Katika Swalaah Yake Au Kisomo Chake

Hiswnul-Muslim

042-Du’aa Ya Aliyeingiwa Na Wasiwasi Katika Swalaah Yake Au Kisomo Chake

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[138]

أَعُوذُ بِاللَّهِ مِنَ الشَّيْطانِ الرَّجِيْمِ

Au’wudhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiym

 

Najikinga na Allaah kutokana na shaytwaan aliyelaaniwa. (Kisha utatema vijimate vichache upande wa kushoto mara tatu)[1] [yaani kama mwenye kupuliza].

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Uthmaan bin Abi Al-‘Aasw (رضي الله عنه) amesema: Nilimwambia Rasuli (صلى الله عليه وسلم): Ee Rasuli wa Allaah hakika Shaytwaan amenikalia kati yangu na kati ya Swalaah yangu na kisomo changu, ananitatiza.  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akasema: ((Huyo ni Shaytwaan aitwae Khanzab ukimuhisi amekujia basi muombe Allaah kinga kutokana na [wasiwasi] naye, na tema vijimate vichache kushotoni kwako mara tatu)) Akasema: ”Nikafanya hivyo Allaah akaniondoshea” - Muslim (4/1729) [2203].

 

 

 

Share

043-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Ambae Jambo Limekuwa Gumu Kwake

Hiswnul-Muslim

043-Du’aa Ya Ambae Jambo Limekuwa Gumu Kwake

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[139]

اللّهُـمَّ لا سَـهْلَ إِلاّ ما جَعَلـتَهُ سَهـلاً، وَأَنْتَ تَجْـعَلُ الْحَـزَنَ إِذا شِـئْتَ سَهـْلاً

 

Allaahumma laa sahla illaa maa Ja’altahu sahlan wa Anta Taj-’alul-hazna idhaa shi-ita sahlaa

 

Ee Allaah hakuna jepesi ila Ulilolifanya jepesi, Nawe Unalifanya (lilokuwa) gumu (liwe) jepesi Ukitaka[1]

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) - Ibn Hibbaan katika Swahiyh yake [2427] (Mawaarid) na ibn As-Sunniy [351] na Al-Haafidhw amesema: “Hii Hadiyth Swahiyh”. Na ameisahihisha ‘Abdul-Qaadir Al-Arnaawutw katika takhriyj Al-Adhkaar lin-Nawawy (Uk. 106).

 

 

Share

044-Hiswnul-Muslim: Analosema Na Kupaswa Kufanya Aliyefanya Dhambi

Hiswnul-Muslim

044-Analosema Na Kupaswa Kufanya  Aliyefanya Dhambi

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[140]

 

((Hakuna mja yeyote yule anayefanya dhambi kisha akatawadha vizuri na akaswali rakaa mbili, kisha akamtaka Allaah maghfirah ila Atamghufuria))[1] 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Bakr Asw-Swiddiyq (رضي الله عنه)  na mwisho wa Hadiyth kwamba Abu Bakr akasoma:

 

وَالَّذِينَ إِذَا فَعَلُوا فَاحِشَةً أَوْ ظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ ذَكَرُوا اللَّـهَ فَاسْتَغْفَرُوا لِذُنُوبِهِمْ وَمَن يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا اللَّـهُ وَلَمْ يُصِرُّوا عَلَىٰ مَا فَعَلُوا وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴿١٣٥ أُولَـٰئِكَ جَزَاؤُهُم مَّغْفِرَةٌ مِّن رَّبِّهِمْ وَجَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ وَنِعْمَ أَجْرُ الْعَامِلِينَ ﴿١٣٦

Na wale ambao wanapofanya uchafu (wa aina yoyote ule) au wakajidhulumu nafsi zao, humdhukuru Allaah wakaomba maghfirah kwa madhambi yao. Na nani anayeghufuria madhambi isipokuwa Allaah. Na hawaendelei katika waliyoyafanya na wao wanajua. Hao jazaa yao ni maghfirah kutoka kwa Rabb wao na Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo.  Uzuri ulioje ujira wa watendaji (wema) [Aal-‘Imraan 3: 135-136]- Abu Daawuwd (2/86) [1521], At-Tirmidhiy (2/257) [3006, 406], na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/283).

 

 

Share

045-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumfukuza Shaytwaan Na Wasiwasi Wake

Hiswnul-Muslim

045-Du’aa Ya Kumfukuza Shaytwaan Na Wasiwasi Wake

www.alhidaaya.com

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

Mambo yafuatayo yanatakiwa kufuatwa pindi anapotolewa shaytwaan:

 

 

[141]

 

1-Omba kinga kwa Allaah Akukinge naye[1]. (useme:

أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجيـم

 

Au’wudhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiym

 

 

 

[142]

 

2-Kuadhini  (yaani kutoa adhaana kama ya Swalaah)[2]

 

 

 

[43]

 

3-Kusoma nyiradi (zilizopokewa kutoka kwa Nabiy Muhammad صلى الله عليه وسلم)  na kusoma Qur-aan[3]

 

 

 


[1]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akisema anapofungua Swalaah:

أَعُوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ مِنْ هَمْزِهِ وَنَفْخِهِ وَنَفْثِهِ

((......A’uwdhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiymi min hamzihii wa nafkhihii wa nafathihi - Najilindia na Allaah kutokana na shaytwaan aliyefukuzwa, najilinda na (kutokana na) wazimu wake na kiburi chake, na ushairi [kutabana] wake)) - Abu Daawud (1/620) [771], At-Tirmidhiy (1/282) [242], Ahmad (15/81) [11472], na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/77). Na Allaah Anasema:

 

وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ ﴿٩٧ وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحْضُرُونِ ﴿٩٨

Na sema: “Rabb wangu! Najikinga Kwako kutokana na mnong’ono (uchochozi na wasiwasi) wa mashaytwaan,” “Na najikinga Kwako Rabb wasinihudhurie.” (Al-Mu-uminuwna 23:98-99)

 

[2]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Inapoadhiniwa kwa ajili ya Swalaah, shaytwaan hukimbia nyuma na kutoa mashuzi ili asisikie adhana. Adhana inapomalizika hugeuka. Inapokimiwa Swalaah hurudi nyuma. Inapomalizika hugeuka na kumshawishi mtu nafsi yake akisema: ”Kumbuka kadhaa! Kumbuka kadhaa” kuhusu jambo ambalo mtu hakuwa akilifikiria, mpaka hubakia mtu [amepotelewa] hajui kaswali [rakaa] ngapi)) - Al-Bukhaariy (1/151) [608], Muslim (1/291) [389],

 

[3]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Msifanye nyumba zenu makaburi. Hakika shaytwaan anakimbia nyumba inayosomwa humo Suwratul-Baqarah)) Muslim (1/539). Na mengineyo yanayomkimbiza shaytwaan ni: nyiradi za asubuhi na jioni, za kulala na kuamka, za kuingia nyumbani na kutoka, za kuingia Msikitini na kutoka humo na nyinginezo kati ya nyiradi zilizothibiti katika  Sunnah; mfano kusoma Aayatul-Kursiy wakati wa kulala, Aayah mbili za mwisho katika Suwratul-Baqarah. Na atakayesema:

 

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَـريكَ لهُ، لهُ المُـلْكُ ولهُ الحَمْـد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَدير

”Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr”  Mara mia itakuwa ni hifadhi kwake kutokana na shaytwaan siku yake nzima. Adhana pia inakimbiza shaytwaan kama ilivotangulia kutajwa.

 

 

Share

046-Hiswnul-Muslim: Du’aa Akitokewa Mtu Na Jambo Asiloridhika Au Akishindwa Kufanya Jambo

Hiswnul-Muslim

046-Du’aa Akitokewa Mtu Na Jambo Asiloridhika Au Akishindwa Kufanya Jambo

 www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [144]

قَدَّرَ اللهُ وَما شـاءَ فَعَـلَ

Qadara-Allaahu wamaa Shaa Fa’ala

 

Amepanga Allaah na Analolitaka Anafanya[1]

 

 


[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه),

 

قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((المُؤْمنُ القَوِيُّ خَيرٌ وَأَحَبُّ إِلَى اللهِ مِنَ المُؤْمِنِ الضَّعيفِ، وَفي كُلٍّ خَيرٌ. احْرِصْ عَلَى مَا يَنْفَعُكَ، واسْتَعِنْ بِاللهِ وَلا تَعْجَزْ. وَإنْ أَصَابَكَ شَيءٌ فَلا تَقُلْ لَوْ أنّي فَعَلْتُ كَانَ كَذَا وَكَذَا، وَلَكِنْ قُلْ: قَدرُ اللهِ، وَمَا شَاءَ فَعلَ؛ فإنَّ لَوْ تَفْتَحُ عَمَلَ الشَّيطَانِ)). رواه مسلم

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Muumini mwenye nguvu ni bora na anapendeza zaidi kwa Allaah kuliko Muumini dhaifu, na wote wana kheri. Fanya pupa kwa kile kitakachokunufaisha na taka msaada kwa Allaah wala usichoke na kikikupata kitu chochote kibaya basi usiseme: ”Lau kama ningefanya kadha na kadha yasingenitokea haya” lakini sema: 

قَدَّرَ اللهُ وَما شـاءَ فَعَـلَ

Qadara-Allaahu wamaa Shaa Fa’ala” kwani [neno la] ”Lau” linafungua amali za shaytwaan)) – Muslim (4/2052) [2664].

 

 

 

Share

047-Hiswnul-Muslim: Pongezi Ya Kupata Mtoto Na Jibu Lake

Hiswnul-Muslim

047-Pongezi Ya Kupata Mtoto Na Jibu Lake

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[145]

بَارَكَ اللَّهُ لَكَ فِي الْمَوْهُوبِ لَكَ وَشَكَرْتَ الْوَاهِبَ وَبَلَغَ أَشُدَّهُ وَرُزِقَتَ بِرَّهُ

 

Baaraka Allaahu laka fil mawhuwbi laka, wa shakartal-Waahiba, wa balagha ashuddahu, wa ruziqta birrahu.

 

Allaah Akubariki katika ulichopewa na umshukuru aliyekupa, na afike kuwa mkubwa na uruzukiwe wema wake.

 

Na aliyepongezwa atamuombea aliyempongeza kwa kumwambia:

 

باَرَكَ اللَّهُ لَكَ وَبارَكَ عَلَيْكَ وَجَزَاكَ اللّهُ خَيْراً وَرزَقَكَ اللَّهُ مِثْلُهُ وأَجْزَلَ َثَوابَكَ

Baaraka Allaahu laka wa Baaraka ’alayka, wa Jazaaka Allaahu khayraa, warazaqaka-Allaahu mithluhu, wa ajzala thawaabaka

 

Allaah Akubariki na Ateremshe Baraka juu yako, na Allaah Akujaze kheri, na Allaah Akuruzuku mfano wake na Afanye nyingi thawabu zako[1].

 

 

 

 

 

[1]Angalia: ‘Al-Adkhaar An-Nawawiy’ (Uk. 349) na Swahiyh Adhkaar An-Nawawiy ya Sulaym Al-Hilaaliy (2/713)

 

 

Share

048-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuwakinga Watoto

Hiswnul-Muslim

048-Du’aa Ya Kuwakinga Watoto

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 [146]

 

 كَانَ النَّبِيُّ صلَّى اللّه عَلَيْهِ وسَلَّم يَعُوذُ الْحَسَنْ وَالْحُسَيْن

 

Nabiy (صلى الله عليه وسلم) alikuwa  akiwakinga (wajukuu wake)  Al-Hasan na Al-Husayn akisema:

 

أُعيـذُكُمـا بِكَلِـماتِ اللهِ التّـامَّة، مِنْ كُلِّ شَيْـطانٍ وَهـامَّة، وَمِنْ كُـلِّ عَـيْنٍ لامَّـة

 

U’iydhukumaa bikalimaatiLLaahit-ttaammati min kulli shaytwaanin wa haammah, wa min kulli ’aynin laammah

 

Nawakinga kwa maneno ya Allaah yaliyotimia Awakinge kutokana na kila shaytwaan na uvamizi na kila jicho lenye kudhuru[1]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy (4/119) [3371].

 

 

Share

049-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumtembelea Mgonjwa

Hiswnul-Muslim

049-Du’aa Ya Kumtembelea Mgonjwa

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[147]

 

لا بأْسَ طَهـورٌ إِنْ شـاءَ الله

Laa ba-asa twahuwrun In Shaa Allaah

 

Hakuna neno, (ugonjwa) ni kusafishwa (na madhambi) Akipenda Allaah[1]

 

 

 

[148]

أَسْـأَلُ اللهَ العَـظيـم، رَبَّ العَـرْشِ العَـظيـم أَنْ يَشْفِـيَك

 

As-aluLLaaha Al-‘Adhwiyma Rabbal-‘Arshil-‘Adhwiymi an Yashfiyak (mara 7)

 

 Namuomba Allaah Mtukufu Rabb wa ‘Arshi Tukufu Akuponyeshe[2]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (10/118) [3616].

 

كَانَ النَّبِيّ صّلّى الله عليه وسلم إِذا دَخَلَ عَلى الْم إذا دخل على من يعوده قال: :لا بأس، طهور إن شاء الله

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa anapoingia kumzuru mgonjwa akimwambia:

لا بأْسَ طَهـورٌ إِنْ شـاءَ الله

 

[2]Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Hapana mja yeyote Muislamu anaemtembelea mgonjwa ambae wakati wake wa kufa bado haujafika na akamuombea mara saba, isipokuwa   Allaah Humponyesha mgonjwa huyo)) At-Tirmidhiy [2083], Abu Daawuwd [3106], Taz pia Swahiyh At-Tirmidhiy (2/210), Swahiyh Al-Jaami’ (5/180) [5766].

 

 

Share

050-Hiswnul-Muslim: Fadhila Za Kumtembelea Mgonjwa

Hiswnul-Muslim

050-Fadhila Za Kumtembelea Mgonjwa

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[149]

 

 

قَالَ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِذَا عَادَ الرَّجُلُ أَخَاهُ المُسْلِمَ مَشَى فِي خِرَافَةِ الجَنَّةِ حَتَّى يَجْلِسَ فَإِذَا جَلَسَ غَمَرَتْهُ الرَّحْمَةُ، فَإِنْ كَانَ غُدْوَةً صَلَّى عَلَيْهِ سَبْعُوْنَ أَلْفَ مَلَكٍ حَتَّى يُمْسِيَ، وَإِنْ كَانَ مَسَاءً صَلَّى عَلَيْهِ سَبْعُوْنَ أَلْفَ مَلَكٍ حَتَّى يُصْبِحَ)).

 

Amesema (صلى الله عليه وسلم): ((Mtu anapomtembelea ndugu yake Muislamu mgonjwa basi hutembelea katika bustani ya Jannah mpaka atakapoketi, na anapoketi hufunikwa na Rehma ikiwa ni asubuhi wanamtakia Rehma Malaika sabini elfu mpaka jioni. Na ikiwa ni jioni wanamtakia Rehma Malaika sabini elfu mpaka asubuhi))[1]

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه), At-Tirmidhiy [969] Ibn Maajah [1442], Ahmad (1/97). Na angalia: Swahiyh Ibn Maajah (1/244) na Swahiyh At-Tirmidhiy (1/286), na ameisahihisha pia Ahmad Shaakir.

 

 

Share

051-Hiswnul-Muslim: Du’aa Anayoomba Mgonjwa Aliyekata Tamaa Ya Kupona

Hiswnul-Muslim

051-Du’aa Anayoomba Mgonjwa Aliyekata Tamaa Ya Kupona

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[150]

أللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي وَارْحَمْـني وَأَلْحِقْـني بِالرَّفـيقِ الأّعْلـى

 

Allaahummagh-fir-liy war-hamniy wa alhiqniy birrafiyqil a’-laa

 

Ee Allaah, Nighufurie na Unirehemu na Unikutanishe na waja walio katika daraja za juu[1]

 

 

 

[151]

 

 

جَعَلَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عِنْدَ مَوْتِهِ يُدْخِلُ يَدَيْهِ فِي الْماءِ، فَيَمْسَحُ بِهِما وَجْهُهُ وَيُقُولُ:

 

لاَ إِلَهَ إِلاَّ الله، إِنَّ لِلْمَـوْتِ لَسَكَـراتٍ

 

Wakati Nabiy (صلى الله عليه وسلم) anakufa alikuwa akiingiza mikono yake ndani ya maji kisha akipangusa kwayo uso wake na akisema:

 

لاَ إِلَهَ إِلاَّ الله، إِنَّ لِلْمَـوْتِ لَسَكَـراتٍ

Laa ilaaha illa-Allaah, inna lilmawti sakaaraat

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah, hakika kifo bila shaka kina uchungu[2]

 

 

 

 [152]

 

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَاللّهُ أَكْبَـر، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شَريكَ لهُ، لا إلهَ إلاّ اللّهُ لهُ المُلكُ ولهُ الحَمْد، لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَلا حَـوْلَ وَلا قُـوَّةَ إِلاّ بِالله.

 

Laa ilaaha illa-Allaahu wa Allaahu Akbar, laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu, laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, laa ilaaha illa-Allahu Lahul-Mulku walahul-Hamdu, laa ilaaha illa-Allaahu walaa hawla walaa quwwata illaa biLLaahi

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na Allaah ni Mkubwa, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Peke Yake, hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah Mpweke Hana mshirika, hapana mwabudiwa iwa wa haki ni Allaah, ni Wake Ufalme na Himdi ni Zake, hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah na hapana uwezo wala nguvu isipokuwa kutoka kwa Allaah[3]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ’Aaisha (رضي الله عنها) - Al-Bukhaariy (7/10) [4440], Muslim (4/1893) [2444],  At-Tirmdihiy na  Ahmad.

[2]Hadiyth ya ’Aaisha (رضي الله عنها) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (8/144) [4440] na Hadiyth ya siwaak

[3]Abu Sa’iyd Al-Khudriyy na Abu Hurayrah (رضي الله عنهما), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

 مَنْ قَالَ لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ وَاللَّهُ أَكْبَرُ ، صَدَّقَهُ رَبُّهُ فَقَالَ : لا إِلَهَ إِلا أَنَا وَأَنَا أَكْبَرُ ، وَإِذَا قَالَ : لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ وَحْدَهُ ، قَالَ اللَّهُ : لا إِلَهَ إِلا أَنَا وَحْدِي ، وَإِذَا قَالَ : لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ ، قَالَ اللَّهُ : لا إِلَهَ إِلا أَنَا وَحْدِي لا شَرِيكَ لِي ، وَإِذَا قَالَ : لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ ، قَالَ اللَّهُ : لا إِلَهَ إِلا أَنَا لِيَ الْمُلْكُ وَلِيَ الْحَمْدُ ، وَإِذَا قَالَ : لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ وَلا حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلا بِاللَّهِ ، قَالَ : لا إِلَهَ إِلا أَنَا وَلا حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلا بِي ؛ وَكَانَ يَقُولُ : مَنْ قَالَهَا فِي مَرَضِهِ ثُمَّ مَاتَ لَمْ تَطْعَمْهُ النَّارُ

((Atakayesema:Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na Allaah ni Mkubwa”, Rabb wake amemsadiki, Husema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Mimi, Nami ni Mkubwa”. Na akisema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Peke Yake”. Allaah Husema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Mimi, Peke Yangu”. Na akisema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah Mpweke Hana mshirika”, Allaah Husema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Mimi Peke Yangu Sina mshirika”. Na akisema; “Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, ni Wake Ufalme na Himdi ni Zake”, Allaah Husema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Mimi, Ufalme ni Wangu na Himdi ni Zangu”. Na Akisema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah na hapana uwezo wala nguvu isipokuwa kutoka kwa Allaah”. Allaah Husema: “Hapana mwabudiwa wa haki ila Mimi na hapana uwezo wala nguvu isipokuwa Zangu”. Alikuwa (Nabiy (صلى الله عليه وسلم) akisema: Atakayesema hayo akiwa mgonjwa akafariki, moto hautamla)) -At-Tirmidhiy [3430], Ibn Maajah [3794], na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله). Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/152), Swahiyh Ibn Maajah (2/317), Swahiyh At-Targhiyb (3481)

 

Share

052-Hiswnul-Muslim: Kumlakinia Anaetokwa Na Roho

Hiswnul-Muslim

052-Kumlakinia Anaetokwa Na Roho

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[153]

 

  مَنْ كَانَ آخِرُ كَلامِهِ لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ دَخَلَ الْجَنَّةَ

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Mwenye kuwa neno lake la mwisho ni

 

لا إلهَ إلاّ اللّه

Laa ilaaha illa-Allaah

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah

 

ataingia Jannah))[1]

 

 

[1]Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (3/190) [3116] na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (5/432) [6479].

 

 

Share

053-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Aliyepatwa Na Msiba

Hiswnul-Muslim

053-Du’aa Ya Aliyepatwa Na Msiba

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[154]

إِنّا للهِ وَإِنَا إِلَـيْهِ رَاجِعُـونَ، اللهُـمِّ اْجُـرْني فِي مُصِـيبَتي، وَاخْلُـفْ لِي خَيْـراً مِنْـها.

 

Innaa liLLaahi wa innaa Ilayhi raaji’uwn, Allaahumma Ajirniy fiy muswiybatiy wa Akhlif liy khayran minhaa

 

Hakika sisi wa Allaah, na hakika sisi Kwake wenye kurejea, ee Allaah, Nilipe kwa msiba wangu na Nipe badala yake kilicho bora kuliko huo (msiba)[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Ummu Salamah -(رضي الله عنها) , “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Mja yeyote atakayepatwa na msiba akasema:

إِنّا للهِ وَإِنَا إِلَـيْهِ رَاجِعُـونَ، اللهُـمِّ اْجُـرْني فِي مُصِـيبَتي، وَاخْلُـفْ لِي خَيْـراً مِنْـها

Allaah Atampa thawabu na Atambadilishia kwa kilicho bora zaidi)). Akasema Ummu Salamah: ”Alipofariki Abu Salamah nilisema kama alivyoniamrisha Rasuli wa Allaah, na Allaah Akanibadilishia aliyebora kuliko yeye naye ni Rasuli wa Allaah” - Muslim  (2/632) [918].

 

 

Share

054-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumfunga Macho Maiti

Hiswnul-Muslim

054-Du’aa Ya Kumfunga Macho Maiti

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[155]

 

اللهُـمِّ اغْفِـرْ لِ (فُلاَنٍ - باسـمه) وَارْفَعْ دَرَجَتَـهُ فِي المَهْـدِيّيـنَ، وَاخْـلُفْـهُ في عَقِـبِهِ في الغَابِـرِينَ، وَاغْفِـرْ لَنَا وَلَـهُ يا رَبَّ العـالَمـين، وَافْسَـحْ لَهُ في قَبْـرِهِ وَنَـوِّرْ لَهُ  فِيهِ

 

Allaahummagh-fir-li (taja jina lake), warfa’ darajaatahu fil mahdiyyiyn, wakhluf-hu fiy ‘aqibihi fil ghaabiriyn. Waghfir lanaa walahu yaa Rabbal-‘Aalamiyn. Wafsah lahu fiy qabrihi wa nawwir lahu fiyhi.

 

Ee Allaah Mghufurie (jina la maiti) na Ipandishe daraja yake katika walioongoka, na weka badili yake kwa aliyowacha nyuma,  na Utughufurie sisi na yeye Ee Rabb wa walimwengu na Umkunjulie yeye katika kaburi lake na Umtilie nuru ndani yake[1] 

 

 

 

 

 

 

[1][1]Hadiyth ya Ummu Salamah -(رضي الله عنها)  Muslim (2/634) [920].

 

 

Share

055-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Maiti Wakati Anaposwaliwa

Hiswnul-Muslim

055-Du’aa Ya Kumuombea Maiti Wakati Anaposwaliwa

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[156]

 

(maiti mmoja mwanamume)

 

اللهُـمِّ اغْفِـرْ لَهُ وَارْحَمْـه، وَعافِهِ وَاعْفُ عَنْـه، وَأَكْـرِمْ نُزُلَـه، وَوَسِّـعْ مُدْخَـلَه، وَاغْسِلْـهُ بِالْمـاءِ وَالثَّـلْجِ وَالْبَـرَدْ، وَنَقِّـهِ مِنَ الْخطـايا كَما نَـقّيْتَ الـثَّوْبُ الأَبْيَـضُ مِنَ الدَّنَـسْ، وَأَبْـدِلْهُ داراً خَـيْراً مِنْ دارِه، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـه، وَزَوْجَـاً خَـيْراً مِنْ زَوْجِه، وَأَدْخِـلْهُ الْجَـنَّة، وَأَعِـذْهُ مِنْ عَذابِ القَـبْر وَعَذابِ النّـار

 

Allaahumma-ghfir lahu warham-hu, wa 'aafihi wa’-fu 'anhu, wa akrim nuzulahu, wa wassi' mudkhalahu, waghsilhu bilmaai wath-thalji walbaradi, wanaqqihi minal-khatwaayaa kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danas, wa abdilhu daaran khayran min daarihi, wa ahlan khayran min ahlihi, wa zawjan khayran min zawjihi, wa adkhilhul-Jannah, wa a’idh-hu min ‘adhaabil-qabri, wa ‘adhaabin-naar  

 

Eee Allaah, Mghufurie na Mrehemu, na Muafu na Msamehe na Mtukuze kushuka kwake (kaburini) na Mpanulie kuingia kwake, na Muoshe na maji na kwa theluji na barafu na mtakase na makosa kama inavyotakaswa nguo nyeupe kutokana na uchafu, na Mbadilishie nyumba bora kuliko nyumba  yake na jamaa bora kuliko jamaa zake, na mke bora kuliko mke wake, na Muingize Jannah na Mkinge na adhabu ya kaburi (na adhabu ya Moto)[1]

 

 

(maiti mmoja mwanamke)

 

 اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهَا وَارْحَمْهَا، وَعَافِهَا وَاعْفُ عَنْهَا، وَأَكْرِمْ نُزُلَهَا، وَوَسِّعْ مُدْخَلَهَا، وَاغْسِلْهَا بِالْمَاءِ وَالثَّلْجِ وَالْبَرَدِ، وَنَقِّهَا مِنْ الْخَطَايَا كَمَا نَقَّيْتَ الثَّوْبَ الأَبْيَضَ مِنْ الدَّنَسِ، وَأَبْدِلْهَا دَارًا خَيْرًا مِنْ دَارِههَا، وَأَهْلاً خَيْرًا مِنْ أَهْلِهَا، وَزَوْجًا خَيْرًا مِنْ زَوْجِهَا، وَأَدْخِلْهَا الْجَنَّةَ، وَأَعِذْهَا مِنْ عَذَابِ الْقَبْرِ وَعَذَابِ النَّارِ

 

Allaahumma-ghfir lahaa warham-haa, wa 'aafihaa wa’-fu 'anhaa, wa akrim nuzulahaa, wa wassi' mudkhalahaa, waghsilhaa bilmaai wath-thalji walbarad, wanaqqiha minal-khatwaayaa kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danas, wa abdilhaa daaran khayran min daarihaa, wa ahlan khayran min ahlihaa, wa zawjan khayran min zawjihaa, wa adkhilhal-Jannah, wa a’idh-haa min ‘adhaabil-qabri, wa ‘adhaabin-naar

 

(maiti zaidi ya mmoja)

 

 اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُمْ وَارْحَمْهُمْ، وَعَافِهِمْ وَاعْفُ عَنْهُمْ، وَأَكْرِمْ نُزُلَهُمْ، وَوَسِّعْ مُدْخَلَهُمْ، وَاغْسِلْهُمْ بِالْمَاءِ وَالثَّلْجِ وَالْبَرَدِ، وَنَقِّهِمْ مِنْ الْخَطَايَا كَمَا نَقَّيْتَ الثَّوْبَ الأَبْيَضَ مِنْ الدَّنَسِ، وَأَبْدِلْهُمْ دَارًا خَيْرًا مِنْ دَارِهِمْ، وَأَهْلاً خَيْرًا مِنْ أَهْلِهِمْ، وَزَوْجًا خَيْرًا مِنْ زَوْجِهِمْ، وَأَدْخِلْهُمْ الْجَنَّةَ، وَأَعِذْهُمْ مِنْ عَذَابِ الْقَبْرِ وَعَذَابِ النَّارِ

 

Allaahumma-ghfir lahum warham-hum, wa' aafihim wa’-fu 'anhum, wa akrim nuzulahum, wa wassi' mudkhalahum, waghsilhum bilmaai wath-thalji walbarad, wanaqqihim minal-khatwaayaa kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danas, wa abdilhum daaran khayran min daarihim, wa ahlan khayran min ahlihim, wa azwaajan khayran min azwaajihim, wa adkhilhumul-Jannah, wa a’idh-hum min ‘adhaabil-qabri, wa ‘adhaabin-naar

 

 

 

[157]

اللهُـمِّ اغْفِـرْ لِحَيِّـنا وَمَيِّتِـنا وَشـاهِدِنا، وَغائِبِـنا، وَصَغيـرِنا وَكَبيـرِنا، وَذَكَـرِنا وَأُنْثـانا. اللهُـمِّ مَنْ أَحْيَيْـتَهُ مِنّا فَأَحْيِـهِ عَلى الإِسْلام، وَمَنْ تَوَفَّـيْتَهُ مِنّا فَتَوَفَّـهُ عَلى الإِيـمان، اللهُـمِّ لا تَحْـرِمْنـا أَجْـرَهُ، وَلا تُضِـلَّنا بَعْـدَهُ

 

Allaahumma-ghfir li-hayyinaa wa mayyitinaa, wa shaahidinaa, wa ghaaibinaa, wa swaghiyrinaa, wa kabiyrinaa, wa dhakarinaa, wa unthaanaa. Allaahumma man ahyaytahu minnaa fa Ahyihi ‘alal-Islaami, waman tawaffaytahu minnaa fatawaffahu ‘alal-iymaan. Allaahumma laa tahrimnaa ajrahu, walaa tudhwillanaa ba’-dahu

 

Ee Allaah, Mghufurie aliyehai katika sisi na aliyekufa, aliyepo na asiyekuwepo, mdogo kati yetu na mkubwa, mwanamume kati yetu na mwanamke.  Ee Allaah,  Unayemweka hai kati yetu basi Muweke katika Uislamu, na Unayemfisha basi mfishe juu ya iymaan.  Ee Allaah,   Usitunyime thawabu zake wala usitupoteze baada yake[2]

 

 

 

[158]

 

الَّلهُـمِّ إِنَّ فُلانَ بْنَ فُلانٍ في ذِمَّـتِك، وَحَبْـلِ جِـوارِك، فَقِـهِ مِنْ فِتْـنَةِ الْقَـبْرِ وَعَذابِ النّـار، وَأَنْتَ أَهْلُ الْوَفـاءِ وَالْـحَقِّ، فَاغْفِـرْ لَهُ وَارْحَمْـهُ، إِنَّكَ أَنْتَ الغَـفورُ الـرَّحيم

 

Allaahumma inna (taja jina lake ’fulani bin fulani’) fiy dhimmatika, wahabli jiwaarik. Faqihi min fitnatil-qabri wa ’adhaabin-naar, wa Anta Ahlul-wafaai walhaqq. Faghfir-lahu warhamhu, Innaka Antal-Ghafuwrur-Rahiym.

 

Ee Allaah hakika (fulani bin fulani) yuko katika dhima Yako na kamba ya ujirani Wako, basi mkinge na fitina ya kaburi na dhabu ya Moto Nawe Ndiye Mstahiki wa utekelezaji na ukweli, basi Mghufurie na Mrehemu, hakika Wewe ni Al- Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu[3]

 

 

 

[159]

 

اللهُـمِّ عَبْـدُكَ وَابْنُ أَمَـتِك، احْتـاجَ إِلى رَحْمَـتِك، وَأَنْتَ غَنِـيٌّ عَنْ عَذابِـه، إِنْ كانَ مُحْـسِناً فَزِدْ في حَسَـناتِه، وَإِنْ كانَ مُسـيئاً فَتَـجاوَزْ عَنْـهُ

 

Allaahumma ’Abduka wabnu Amatika, Ihtaaja ilaa Rahmatika wa Anta Ghaniyyun ’an ’adhaabihi. In kaana muhsinan fazid fiy hasanaatih, wain kaana musiy-an fatajaawaz ’anhu

 

Ee Allaah, mja Wako na mtoto wa mja wako wa kike, ni muhitaji wa Rehma Yako, Nawe Huhitaji na kumuadhibu. Kwa hivyo akiwa ni mwema Mzidishie katika mema yake na akiwa ni muovu Yapite (Msamehe) madhambi yake[4]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Awf bin Maalik (رضي الله عنه) Muslim (2/663) [963], An-Nasaaiy na Musnad Ahmad

[2]Hadiyth ya Abu Hurayrah  (رضي الله عنه)  Ibn Maajah (1/480) [1498], Abu Daawuwd [3201], At-Tirmidhiy [1024], An-Nasaaiy [1988], Ahmad (2/368), Taz Swahiyh Abi Daawuwd [3201] Swahiyh Ibn Maajah (1/251) 

[3]Hadiyth ya Waathilah bin Al-Asqa’ (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (3/211), Ibn Maajah [1499]. Na angalia: Swahiyh Ibn Maajah (1/251) 

[4]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Al-Haakim na ameisahihisha na kuikubali Adh-Dhahabiy (1/359) na angalia: ‘Ahkaam Al-Janaaiz’ ya Al-Albaaniy (رحمه الله) (Uk.125)

 

 

Share

056-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Maiti Ya Mtoto Mdogo Wakati Wa Kumswalia

Hiswnul-Muslim

056-Du’aa Ya Maiti Ya Mtoto Mdogo Wakati Wa Kumswalia

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[160]

أللَّهُمَّ أَعِذْهُ مِنْ عَذابِ الْقَبْرِ

Allaahumma A’idh-hu min ’adhaabil-qabr

 

Ee Allaah mkinge na adhabu ya kaburi[1]

 

اللهُـمِّ اجْعَلْـهُ فَرَطـاً وَذُخْـراً لِوالِـدَيهِ، وَشَفـيعاً مُجَـاباً، اللهُـمِّ ثَـقِّلْ بِهِ مَوازيـنَهُما، وَأَعْـظِمْ بِهِ أُجُـورَهُـما، وَأَلْـحِقْـهُ بِصَالِـحِ الـمؤْمِنـين، وَاجْعَلْـهُ في كَفـَالَةِ إِبْـراهـيم، وَقِهِ بِرَحْمَـتِكَ عَذابَ الْجَـحِيمِ، وَأَبْـدِلْهُ داراً خَـيْراً مِنْ دارِه، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـه، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لإِسْلافِنَا، وَأَفْراطِنَا وَمَنْ سَبَقَنَاَ بِالإِيمَان

 

Allaahummaj-’alhu faratwan wa dhukhran li waalidayhi, wa shafiy’an mujaaba. Allaahumma thaqqil bihi mawaaziynahumaa wa A’-dhwim bihi ujuwrahumaa, wa alhiq-hu biswaalihil Mu-uminiyna, waj-’alhu fiy kafaalati Ibraahiyma, waqihi Birahmatika ’adhaabal-jahiym. Wa Abdilhu daaran khayran min daarihi, wa ahlan khayran min ahlihi. Allaahumma-Ghfir li-aslaafinaa, wa afraatwinaa, waman sabaqanaa bil iymaan.

 

Ee Allaah Mjaaliye kuwa ni kitangulizi na akiba kwa wazazi wake na ni kiombezi chenye kukubaliwa du’aa yake. Ee Allaah kwa ajili yake Zifanye nzito mizani za wazazi wake na Yafanye mengi malipo yao, na Mkutanishe na wema wa Waumini na Mjaalie awe katika dhamana ya Ibraahiym na Muepushe kwa Rehma Yako na adhabu ya Moto, na Mbadlishie nyumba bora kuliko nyumba yake, na jamaa bora kuliko jamaa zake. Ee Allaah, waghufurie waliotangulia na waliopita na waliotutangulia katika Iymaan (Uislamu)[2]

 

 

 

[161]

اللهُـمِّ اجْعَلْـهُ لَنا فَرَطـاً وَسَلَـفاً وَأَجْـراً

Allaahummaj-’alhu lanaa faratwan wa salafan wa ajraa.

 

Ee Allaah mfanye kwetu sisi ni kitangulizi cha malipo na dhamana na malipo[3]

 

 

 

[1]Du’aa ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Amesema Sa’iyd bin al-Musayyib: “Niliswali nyuma ya Abu Hurayrah aliyemswalia mtoto asiyetenda dhambi kamwe nikamsikia akisema (hivyo)”  Imepokewa na Maalik katika Al-Muwattwaa (1/288), Ibn Abi Shaybah katika Al-Muswannif (3/217), Al-Bayhaqiy (4/9), na isnadi yake ameisahihisha Al-Arnaawuutw katika utafiti wake ya ‘Sharh Sunnah lil-Baghawiy (5/357)

[2]Angalia: Al-Mughniy ya ibn Qudaamah (3/416) na Ad-Duruws Al-Muhimmah Li’aamatil-Ummah ya Shaykh ‘Abdil-Aziyz bin ‘Abdillaah bin Baaz (رحمه الله) (Uk 15).

[3]Du’aa ya Hasan Al-Baswry (رحمه الله), “Alikuwa Al-Hassan anamsomea mtoto mdogo Suwratul-Faatihah kisha anasema hivyo”. Al-Baghaawiy katika Sharh As-Sunnah (5/357) na ’Abdur-Razzaaq [6588] na Al-Bukhaariy ameihusisha katika Kitaab Al-Janaaiz [65] mlango wa ’Qiraat Al-Faatihaa ’Alal-Janaazah’ (2/113)

 

 

Share

057-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumtaazi (Kumhani) Aliyefiliwa

Hiswnul-Muslim

057-Du’aa Ya Kumtaazi (Kumhani) Aliyefiliwa

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[162]

إِنَّ للهِ ما أَخَذ، وَلَهُ ما أَعْـطـى، وَكُـلُّ شَيءٍ عِنْـدَهُ بِأَجَلٍ مُسَـمَّى، فَلْتَصْـبِر وَلْتَحْـتسِبْ

 

Inna liLLaahi maa Akhadha wamaa a’-twaa, wakullu shay-in ‘Indahu biajalin musammaa, faltaswbir waltahtasib

 

Kwa hakika ni Chake Allaah Alichokichukua na ni Chake Alichokitoa, na kila kitu Kwake kina muda maalum, basi vuta subira na taka malipo kwa Allaah[1]

 

 na akisema ifuatavyo  pia bora:

أَعْظَـمَ اللهُ أَجْـرَكَ، وَأَحْسَـنَ عَـزاءَ كَ، وَغَفَـرَ لِمَـيِّتِكَ

 

A’-dhwama-Allaahu ajrak, wa ahsana ’azaa-aka, wa ghafara limayyitika

 

Allaah Afanye malipo yako makubwa, na Akufanye kuzuri kutaaziwa (kuhaniwa) kwako na Amghufurie maiti wako[2]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Usaamah bin Zayd (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (2/80) [1284], Muslim (2/636) [933] na katika Musnad Ahmad

[2]Al-Adhkaar, lin-Nawawy (Uk. 126)

 

 

Share

058-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuingiza Maiti Ndani Ya Kaburi

Hiswnul-Muslim

058-Du’aa Ya Kumuingiza Maiti Ndani Ya Kaburi

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[163]

بِسْـمِ اللهِ وَعَلـى سُـنَّةِ رَسـولِ الله  

BismilLLaahi wa ’alaa Sunnati RasuwliLLaah

 

Kwa jina la Allaah, na kwa Sunnah ya Rasuli wa Allaah[1]

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Ummar (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (3/314) [3213] kwa isnadi Swahiyh na Ahmad (2/40) kwa lafdhw ya:

بِسْمِ اللّه وَعلى مِلَّة رَسول الله

((BismilLlaahi wa ‘alaa millati RasuwliLLaah)) na Isnaad yake ni Swahiyh

 

 

Share

059-Hiswnul-Muslim: Du’aa Baada Ya Kumzika Maiti Kaburini

Hiswnul-Muslim

059-Du’aa Baada Ya Kumzika Maiti Kaburini

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[164]

 

الَّلهُمَّ اغْفِرْ لَهُ الَّلهُمَّ ثَبِّتْهُ

Allaahumma-ghfir-lahu, Allaahumma Thabbit-hu

 

Ee Allaah Mghufurie, Ee Allaah Mthibitishe[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Uthmaan bin ‘Affaan (رضي الله عنه), “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akimaliza maiti kuzika anasimama mbele ya kaburi na kisha anasema:

 

 ((اسْتَغْفِرُوا لِأَخِيكُمْ وَاسْأَلُوا لَهُ التَّثْبِيتَ، فَإِنَّهُ الْآنَ يُسْأَلُ))

 

((Muombeeni maghfirah kwa Allaah ndugu yenu na muombeeni kuthibitishwa kwani hivi sasa anaulizwa)) - Abu Daawuwd (3/315) [3213], Al-Haakim na ameisahihisha na  Adh-Dhahaby ameikubali (1/370).

 

 

Share

060-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuzuru Makaburi

Hiswnul-Muslim

060-Du’aa Ya Kuzuru Makaburi

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

السَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ، (وَيَرْحَمُ اللَّهُ الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّا وَالْمُسْتَأْخِرِينَ) أَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ.

 

Assalaamu ’alaykum ahlad-diyaar minal Mu-uminiyna wal Muslimiyn, wainnaa In Shaa Allaahu bikum laahiquwn. (Wa yarhamu-Allaahu al-mustaqdimiyna minnaa wal musta-akhiriyna). As-alu-Allaaha lanaa walakumul-’aafiyah

 

Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za Waumini na Waislamu, nasi apendapo Allaah tutakutana nanyi (Na Allaah Awarehemu wa mwanzo na wa mwisho). Namuomba Allaah Atupe sisi nanyi Al-’Aafiyah[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Buraydah bin Al-Huswayb (رضي الله عنه) - Muslim (2/671) [975], Ibn Maajah na tamshi lake (1/494) [1547]kutoka kwa Buraydah  (رضي الله عنه). Yaliyo katika mabano ni Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) iliyopokelewa na Muslim (2/671) [974].

 

Al-‘Aafiyah: Ni neno linalojumuisha  Allaah (عزّ وجلّ)  kumjaalia mja Wake salama na kumpa amani, na kumlinda na maradhi, balaa, majanga, madhara, misukosuko, na kila aina za shari za wanaadam na majini na kubakia salama katika Dini yake na Aakhirah yake.  

 

 

Share

061-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Upepo Mkali

Hiswnul-Muslim

061-Du’aa Ya Upepo Mkali

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[166]

اللّهُـمَّ إِنَّـي أَسْـأَلُـكَ خَيْـرَها، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّها.

 

Allaahumma inniy as-aluka khayrahaa wa a’uwdhu Bika min sharrihaa

 

Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kheri ya upepo huu, na najikinga Kwako na shari yake[1]

 

 

 

[167]

اللّهُـمَّ إِنَّـي أَسْـأَلُـكَ خَيْـرَها، وَخَيْـرَ ما فيهـا، وَخَيْـرَ ما اُرْسِلَـتْ بِه، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّها، وَشَـرِّ ما فيهـا، وَشَـرِّ ما اُرْسِلَـتْ بِه.

 

Allaahumma inniy as-aluka khayrahaa wakhayra maa fiyhaa, wakhayra maa ursilat bihi. Wa a’uwdhu Bika min sharrihaa, washarri maa fiyhaa washarri maa ursilat bih

 

Ee Allaah nakuomba kheri yake na kheri ya kilicho ndani yake, na kheri ya iliyotumwa ndani yake. Na najikinga Kwako kutokana na shari yake na shari iliyoko ndani yake na shari iliyotumwa nao[2]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (4/326) [5097], Ibn Maajah (2/1228) [3727], na angalia: Swahiyh Ibn Maajah (2/305).

[2]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)  - Al-Bukhaariy (4/76) [3206], Muslim (2/616) [899].

 

Share

062-Hiswnul-Muslim: Du'aa Ya Radi

Hiswnul-Muslim

062-Du’aa Ya Radi

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[168]

سُبْـحانَ الّذي يُسَبِّـحُ الـرَّعْدُ بِحَمْـدِهِ، وَالملائِكـةُ مِنْ خيـفَته.

 

SubhaanaLLadhiy yusabbihur-ra’-du Bihamdihi wal Malaaikatu min khiyfaatih

 

Ametakasika Yule Ambaye radi zinamsabihi kwa Himdi Zake na Malaika pia (wanamsabihi) kwa kumkhofu[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Zubayr (رضي الله عنه) – “Abdullaah bin Zubayr (رضي الله عنه) alikuwa anaposikia radi basi huacha mazungumzo na badala yake husema hivyo” – Al-Muwattwa (2/992) na Amesema Al-Albaaniy (رحمه الله): Isnaad yake Swahiyh Mawquwfaa.

 

 

 

Share

063-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Istisqaa (Kuomba Mvua)

Hiswnul-Muslim

063-Du’aa Ya Istisqaa (Kuomba Mvua)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[169] 

اللّهُمَّ اَسْقِـنا غَيْـثاً مُغيـثاً، مَريئاً، مُريـعاً، نافِعـاً غَيْـرَ ضَّارٌ، عاجِـلاً غَـيْرَ آجِلٍ         

 

Allaahumma Asqinaa ghaythan mughiythaa, mariy-aa, muriy’aa, naafi’an ghayra dhwaarun, ’aajilan ghayra aajil

 

Ee Allaah Tunyesheleze mvua yenye kuokoa, nyingi yenye kustawisha, yenye manufaa isiyo dhuru, ya haraka isiyochelewa[1]

 

 

 

[170]

اللّهُمَّ أغِثْنـَا، اللّهُمَّ أغِثْنـَا، اللّهُمَّ أغِثْنـَا

 

Allaahumma Aghithnaa, Allaahumma Aghithnaa, Allaahumma Aghithnaa

 

Ee Allaah tunakuomba utuokowe kwa kututeremshia mvua, Ee Allaah tunakuomba utuokowe kwa kututeremshia mvua, Ee Allaah tunakuomba utuokowe kwa kututeremshia mvua[2]

 

 

 

 

[171]

اللّهُمَّ اسْقِ عِبادَكَ وَبَهـائِمَك، وَانْشُـرْ رَحْمَـتَكَ وَأَحْيِي بَلَـدَكَ المَيِّـت

 

Allaahummasqi ’ibaadaka, wa bahaaimaka, wanshur Rahmataka wa Ahyi baladakal-mayyit

 

Ee Allaah Wanyesheleze waja Wako, na wanyama Wako, na Eneza Rehma Zako na Fufua nchi Yako iliyokufa[3]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdullaah (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/303) [1169], ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/216).

[2]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (1/224)[ 1013], Muslim (2/613) [897].

[3]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما)  - Abu Dawwud (1/305) [1176], na Al-Albaaniy (رحمه الله) ameipa daraja ya Hasan katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/218)

 

 

Share

064-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Mvua Inaponyesha

Hiswnul-Muslim

064-Du’aa Ya Mvua Inaponyesha

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[172]

اللّهُمَّ صَيِّـباً نافِـعاً

Allaahumma swayyiban naafi’aa

 

Ee Allaah, Ijaaliye yenye kumiminika yenye kunufaisha[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (2/518) [1032]

 

Faida:  Mvua inaponyesha ni wakati wa kutakabaliwa du’aa.

 

 

 

Share

065-Hiswnul-Muslim: Du’aa Baada Ya Mvua

Hiswnul-Muslim

065-Du’aa Baada Ya Mvua

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikiliza

 

 

[173]

مُطِـرْنا بِفَضْـلِ اللهِ وَرَحْمَـتِهِ

Mutwirnaa bifadhwliLLaahi wa Rahmatih

 

 

Tumenyeshelewa kwa fadhila za Allaah na Rehma Zake[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Zayd bin Khaalid Al-Juhniy (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (1/205) [486], Muslim (1/83) [71].

 

 

Share

066-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kutaka Mvua Iondoke (Wakati Itakapoleta Madhara)

Hiswnul-Muslim

066-Du’aa Ya Kutaka Mvua Iondoke (Wakati Itakapoleta Madhara)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[174]

اللّهُمَّ حَوالَيْنا وَلا عَلَيْـنَا، اللّهُمَّ عَلى الآكَـامِ وَالظِّـرابِ، وَبُطُـونِ الأوْدِيةِ، وَمَنـابِتِ الشَّجَـرِ.

 

Allaahumma hawaalaynaa walaa ’alaynaa. Allaahumma ’alal aakaami wadh-dhwiraab, wa butwuunil awdiyah, wamanaabitish-shajar

 

Ee Allaah, Inyesheleze kwetu wala isiwe yenye kutuangamiza.  Ee Allaah Inyesheleze kwenye vichaka na milima na mabonde na kwenye mizizi ya miti[1].

 

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (1/224) [1013]. Muslim (2/614) [897].

 

 

Share

067-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuona Mwezi Unapoandama

Hiswnul-Muslim

067-Du’aa Ya Kuona Mwezi Unapoandama

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[175]
 

اللهُ أَكْـبَر، اللّهُمَّ أَهِلَّـهُ عَلَيْـنا بِالأمْـنِ وَالإيمـان، والسَّلامَـةِ والإسْلامِ، وَالتَّـوْفيـقِ لِما تُحِـبُّ وَتَـرْضَـى، رَبُّنـا وَرَبُّكَ اللهُ.

 

Allaahu Akbar, Allaahumma Ahillahu ‘alaynaa bil amni wal iymaani, wassalamaati wal Islaami, wattawfiyqi limaa Tuhibbu Rabbunaa watardhwaa Rabbuna wa Rabbuka-Allaah

 

Allaah ni Mkubwa, Ee Allaah, Uanzishe kwetu kwa amani na iymaan, na usalama na Uislamu, na taufiqi ya kile Unachokipenda Rabb wetu na kukiridhia, Rabb  wetu na Rabb wako ni Allaah[1]

 

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما)  - AT-Tirmidhiy (5/504) [3451], Sunan Ad-Daarimiy kwa tamshi lake (1/336), Ahmad kwa kauli tofauti kidogo, na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/157).

 

 

Share

068-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Wakati Wa Kufungua Swawm

Hiswnul-Muslim

068-Du’aa Ya Wakati Wa Kufungua Swawm

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[176]

 

 

ذَهَـبَ الظَّمَـأُ، وَابْتَلَّـتِ العُـروقُ، وَثَبَـتَ الأجْـرُ إِنْ شـاءَ اللهُ

 

Dhahabadh-dhwama-u wabtallatil ’uruwqu, wathabbatal ajru In Shaa Allaah

 

((Kiu kimeondoka, mishipa imelowana, na ujira umethibiti In Shaa Allaah)[1]

 

 

 

 

 [177]

اللّهُـمَّ إِنَّـي أَسْـأَلُـكَ بِرَحْمَـتِكَ الّتي وَسِـعَت كُلَّ شيء، أَنْ تَغْـفِرَ لِي

 

Allaahumma inniy as-aluka bi-Rahmatikallatiy wasi’at kulla shay-in an Taghfiraily

 

Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kwa Rehma Zako ambazo imeenea kila kitu, Unighufurie[2]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما)  - Abu Daawuwd (2/306) [2357] na wengineo. Taz Swahiyh Abi Daawuwd [2357], Swahiyh Al-Jaami’ (4/209) [4678]. 

 

Tanbihi:   Baadhi ya ’Ulamaa wameona ni Dhwa’iyf kama ibn ’Uthaymiyn katika Majmu’w Fataawa Ibn ’Uthaymiyn, na wengineo wamesema sababu katika wapokezi kuna Marwaan bin Saalim Al-Muqfayaa hajulikani.

[2]Du’aa ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما)  - Ibn Maajah (1/557) [1753], na ameipa daraja ya Hasan Al-Haafidhw katika ‘Takhriyj Al-Adhkaar’ . Angalia: ‘Sharh Al-Adhkaar’ (4/342). 

 

Tanbihi: Imaam Al-Albaaniy amerekodi kuwa ni Dhwa’iyf  katika: Dhwa’iyf Ibn Maajah [345], Dhwa’iyf At-Targhiyb [582], Al-Kalim Atw-Twayyib [164]

 

 

Share

069-Hiswnul-Muslim: Du’aa Kabla Ya Kula

Hiswnul-Muslim

069-Du’aa Kabla Ya Kula

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[178]

 

Atakapo kula mmoja wenu chakula basi aseme:

بِسْمِ الله

 

 

BismiLLaahi

 

Kwa Jina la Allaah

(إذا نسي فليقل) بِسْمِ اللَّهِ أَوَّلَهُ وَآخِرَهُ

 

 (Akisahau sema):  BismiLLaahi awwalahu wa aakhirahu

 

Kwa Jina la Allaah, mwanzoni na mwishoni[1]

 

 

 

[179]

 

Yeyote ambaye Allaah Amemruzuku chakula aseme:

 

اللّهُـمَّ بارِكْ لَنا فيهِ وَأَطْـعِمْنا خَـيْراً مِنْـهُ

Allaahumma Baarik lanaa fiyhi wa Atw-’imnaa khayran minhu

 

Ee Allaah Tubarikie [chakula hichi] na Tulishe bora kuliko hichi

 

 

Na yoyote ambaye Amemruzuku maziwa basi aseme:

اللّهُـمَّ بارِكْ لَنا فيهِ وَزِدْنا مِنْهُ

 

Allaahumma Baarik lanaa fiyhi wa Zidnaa minhu

 

Ee Allaah Tubarikie [kinywaji] hichi na Utuzidishie[2]

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عهما) , Kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم):

 

((إذا أكل أَحَدُكُمْ فَليَذْكُر اسْمَ اللَّه تعالى، فإنْ نسي أَنْ يَذْكُرَ اسْمَ اللَّه تَعَالَى في أَوَّلِهِ، فَليَقُلْ: بِسْمِ اللَّه أَوَّلَهُ وَآخِرَهُ))

 

((Atakapokula mmoja wenu, ataje Jina la Allaah Ta’aalaa, lakini akisahau kumtaja Allaah Ta’aalaa mwanzoni, basi aseme: ((Kwa Jina la Allaah, mwanzoni na mwishoni))  Abu Daawuwd (3/347),  At-Tirmidhiy  (4/288), Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (2/167)

 

[2]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  

 

 ((مَنْ أَطْعَمَهُ اللَّهُ الطَّعَامَ فَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِيهِ وَأَطْعِمْنَا خَيْرًا مِنْهُ وَمَنْ سَقَاهُ اللَّهُ لَبَنًا فَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ بَارِكْ لَنَا فِيهِ وَزِدْنَا مِنْهُ))

((Ambaye Allaah Amemruzuku chakula aseme: Ee Allaah Tubarikie [chakula hichi] na Tulishe bora kuliko hichi. Na ambaye Allaah Amemruzuku maziwa, aseme: Ee Allaah Tubarikie [kinywaji] hichi na Utuzidishie)) At-Tirmidhiy (5/506) [3455], na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/158).

 

 

Share

070-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Baada Ya Kula

Hiswnul-Muslim

070-Du’aa Ya Baada Ya Kula

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[180]
 

الْحَمْـدُ للهِ الَّذي أَطْعَمَنـي هـذا وَرَزَقَنـيهِ مِنْ غَـيْرِ حَوْلٍ مِنِّي وَلا قُوَّةٍ

 

AlhamduliLLaahil-lladhiy Atw-’amaniy haadhaa wa Razaqaniyhi min ghayri hawlin minniy walaa quwwah

 

Himdi Anastahiki Allaah Ambaye Amenilisha mimi (chakula) hichi na Akaniruzuku pasina uwezo wangu wala nguvu zangu[1]

 

 

 

 

 [181]

الْحَمْـدُ للهِ حَمْـداً كَثـيراً طَيِّـباً مُبـارَكاً فيه، (غَيْرَ مَكْفِيٍّ) وَلا مُوَدَّعٍ وَلا مُسْتَغْـنىً عَنْـهُ رَبُّـنا

 

AlhamduliLLaahi Hamdan kathiyran twayyiban mubaarakan fiyhi (ghayra makfiyyin) walaa muwadda’in walaa mustaghnaa ’anhu Rabbanaa

 

Himdi Anastahiki Allaah, Himdi nyingi nzuri, zenye Baraka ndani yake, (zisizotoshelezwa) wala kuagwa, wala kutoshwa nazo mtu. Ee Rabb wetu[2]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Mu’aadh bin Anas (رضي الله عنه) - Aswhaabus-Sunan isipokuwa An-Nasaaiy; Abu Daawuwd [4023], At-Tirmidhiy [3458], Ibn Maajah [3285]. Angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/159), Swahiyh Al-Jaami’ [6086] kwa daraja ya Hasan

 

[2]Hadiyth ya Abu Umaamah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (6/214) [5458], At-Tirmidhiy  kwa tamshi lake (5/507) [3456]

 

 

Share

071-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Mgeni Kumuombea Aliyemkaribisha Chakula

Hiswnul-Muslim

071-Du’aa Ya Mgeni Kumuombea Aliyemkaribisha Chakula

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 [182]

اللّهُـمَّ بارِكْ لَهُمْ فيما رَزَقْـتَهُم، وَاغْفِـرْ لَهُـمْ وَارْحَمْهُمْ

 

Allaahumma Baarik lahum fiymaa Razaqtahum waghfir lahum warhamhum

 

Ee Allaah, Wabariki katika Ulichowaruzuku na Waghufurie na Warehemu[1] 

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Busr (رضي الله عنه) - Muslim (3/1615) [2042], Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ahmad.

 

 

Share

072-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Aliyekupa Kinywaji Au Anayetaka Kukupa

Hiswnul-Muslim

072-Du’aa Ya Kumuombea Aliyekupa Kinywaji Au Anayetaka Kukupa

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[183]

اللّهُـمَّ أَطْعِمْ مَن أَطْعَمَني، وَاسْقِ مَن سَقانِي

 

Allaahumma Atw-’im man atw-’amaniy Wasqi man saqaaniy

 

Ee Allaah Mlishe aliyenilisha na Mnywishe aliyeninyweisha[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Al-Miqdaad bin Al-Aswad  (رضي الله عنه) - Muslim (3/126) [2055], Ahmad 

 

 

Share

073-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Uliye Futuru Kwake

Hiswnul-Muslim

073-Du’aa Ya Kumuombea Uliye Futuru Kwake

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[184]

أَفْطَـرَ عِنْدَكُم الصّـائِمونَ وَأَكَلَ طَعامَـكُمُ الأبْـرار، وَصَلَّـتْ عَلَـيْكُمُ الملائِكَـة

 

Aftwara ‘indakumu asw-swaaimuwna wa akala twa’aamakum al-abraar,  wa Swallat ‘alaykumul Malaaikah

 

Wafuturu kwenu waliofunga (Swawm) na wale chakula chenu watu wema, na wawaombee Rehma Malaika[1]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه)  - Sunan Abi Daawuwd (3/367) [3854], Ibn Maajah (1/556) [1747], An-Nasaaiy katika kitabu chake; ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah (296-298), na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (2/730).  Imetaja katika riwaayah: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akisema hivyo anapofuturu kwa watu wa nyumbani kwake”.  

 

 

Share

074-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Aliyealikwa Chakula Lakini Akawa Na Swawm

Hiswnul-Muslim

074-Du’aa Ya Aliyealikwa Chakula Lakini Akawa Na Swawm

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[185]

إِذَا دُعِيَ أَحَدَكُمْ فَلْيُجِبْ، فَإِنْ كَانَ صَائِماً فَلْيَصِلَ وَإِنْ كَانَ مُفْطِراً فَلْيَطْعَمْ.
(وَمَعَنَى فَليَصِلَ أَي فَلْيَدَعَ)
.

 

Akialikwa mmoja wenu aitike mwito, akiwa na Swawm basi aombe du’aa (kumuombea aliyemualika) na kama hana Swawm basi ale[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Huraryah (رضي الله عنه) - Muslim (2/1054) [1431].

 

 

Share

075-Hiswnul-Muslim: Anachosema Aliyetukanwa Hali Ya Kuwa Ana Swawm

Hiswnul-Muslim

075-Anachosema Aliyetukanwa Hali Ya Kuwa Ana Swawm

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[186]

إنِّي صَائِمٌ، إنِّي صَائِمٌ

Inniy Swaaim, Inniy Swaaim

Hakika mimi niko katika Swawm, hakika mimi niko katika Swawm[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Huraryah (رضي الله عنه)

 

((الصِّيَامُ جُنَّةٌ، فَلَا يَرْفُثْ وَلَا يَجْهَلْ، وَإِنْ امْرُؤٌ قَاتَلَهُ أَوْ شَاتَمَهُ فَلْيَقُلْ: إِنِّي صَائِمٌ مَرَّتَيْنِ- وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ، لَخُلُوفُ فَمِ الصَّائِمِ أَطْيَبُ عِنْدَ اللَّهِ تَعَالَى مِنْ رِيحِ الْمِسْكِ، يَتْرُكُ طَعَامَهُ وَشَرَابَهُ وَشَهْوَتَهُ مِنْ أَجْلِي، الصِّيَامُ لِي وَأَنَا أَجْزِي بِهِ، وَالْحَسَنَةُ بِعَشْرِ أَمْثَالِهَا))

 

((Swawm ni ngao. Kwa hiyo (atakayekuwa katika Swawm miongoni mwenu) asijimai (na mkewe) wala asifanye mambo ya upuuzi. Akitokea mtu kugombana naye au akamtukana, basi aseme mara mbili: “Hakika mimi niko katika Swawm! Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi mwake! Hakika harufu inayotoka kinywani mwa aliye na  Swawm ni nzuri mbele ya Allaah Ta’aalaa kuliko harufu ya misk. (Allaah Anasema kuhusu aliye na  Swawm): “Ameacha chakula chake na kinywaje chake na matamanio yake kwa ajili Yangu. Swawm ni Yangu, Nami Nitamlipa, na thawabu ya amali  nzuri ina malipo mara kumi”)) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (4/103) [1894], Muslim (2/806) [1151].

 

Share

076-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuomba Unapoona Matunda Yanachipua Kwenye Miti

Hiswnul-Muslim

076-Du’aa Ya Kuomba Unapoona Matunda Yanachipua Kwenye Miti

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

[187]

 

 

اللّهُـمَّ بارِكْ لَنا في ثَمَـرِنا، وَبارِكْ لَنا في مَدينَتِنـا، وَبارِكْ لَنا في صَاعِنـَا، وَبارِكْ لَنا فِي مُدِّنا

 

Allaahumma Baarik lanaa fiy thamarinaa, wa Baarik lanaa fiy madiynatinaa. Wabaarik lanaa fiy swaa’inaa, wa Baarik lanaa fiy muddinaa

 

Ee Allaah Tubarikie matunda yetu, na tubarikie Mji wetu, na Tubarikie pishi (swaa’a) yetu na tubarikie kibaba (mudd) chetu[1].

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Muslim (2/1000) [1373]

 

Swaa’a:  Ni pishi na ni sawa na taqriban Kilo 2 12 au 3 . 

 

 

Share

077-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kupiga Chafya (Kuchemua)

Hiswnul-Muslim

077-Du’aa Ya Kupiga Chafya (Kuchemua)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[188]       

 

Akichemua mmoja wenu aseme:

الْحَمْـدُ للهِ

 

AlhamduliLLaah

 

Himdi Anastahiki Allaah

 

Kisha mwenzake amwambie:

 

يَرْحَمُـكَ الله

Yarhamuka-Allaah

 

Allaah Akurehemu

 

Mwanamke aambiwe:

يَرْحَمُـكِ الله

 

YarhamukiLLaah

 

Kisha naye amjibu:

يَهْـديكُـمُ اللهُ وَيُصْـلِحُ بالَـكُم

Yahdiykumu-Allaahu wa Yuswlihu baalakum

 

Akuongoze Allaah na Akutengenezee mambo yako[1]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)   - Al-Bukhaariy (7/125) [6224]

 

Share

078-Hiswnul-Muslim: Anachoambiwa Kafiri Anapopiga Chafya (Kuchemua)

Hiswnul-Muslim

078-Anachoambiwa Kafiri Anapopiga Chafya (Kuchemua)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[189]

 

Anapopiga chafya Kafiri akamshukuru Allaah, aambiwe:

 

يَهْـديكُـمُ اللهُ وَيُصْـلِحُ بالَـكُم

 

Yahdiykumu-Allaahu wa Yuswlihu baalakum

 

Allaah Akuongoze na Akutengenezee mambo yako[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Muwsaa Al-‘Ash’ariyy (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy (5/82) [2739], Ahmad (4/400), Abu Daawuwd (4/308) [5038], na taz Swahiyh At-Tirmidhiy (2/354)

 

 

Share

079-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Aliyeowa

Hiswnul-Muslim

079-Du’aa Ya Kumuombea Aliyeowa

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[190]

بارَكَ اللّهُ لَك، وَبارَكَ عَلَـيْك، وَجَمَعَ بَيْـنَكُما في خَـيْر  

 

Baaraka-Allaahu laka, wa Baaraka ’alayka, wa jama’a baynakumaa fiy khayr

 

Allaah Akubariki na Abariki juu yako, na Awajumuishe katika kheri[1]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم)

 

كانَ إِذَا رَفّأَ الإنْسَانَ، إذَا تَزَوّجَ قالَ: ((بَارَكَ الله وبَارَكَ عَلَيْكَ. وَجَمَعَ بَيْنَكُمَا في الْخَيْرِ))

“Alikuwa mtu anapofunga ndoa husema: ((Allaah Akubariki na Abariki juu yako, na Awajumuishe katika kheri)) - Aswhaab As-Sunan isipokuwa An-Nasaaiy; Abu Daawuwd [2130], At-Tirmidhiy [1091], Ibn Maajah [1905] na taz Swahiyh Ibn Maajah (1/324) na Swahiyh At-Tirmidhiy (1/316)

 

 

 

Share

080-Hiswnul-Muslim: Du’aa Anayoomba Bwana Harusi Au Aliyenunuwa Kipando

Hiswnul-Muslim

080-Du’aa Anayoomba Bwana Harusi Au Aliyenunuwa Kipando

(Gari, Mnyama Na Kadhaalika)

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[191]

 

اللّهُـمَّ إِنَّـي أَسْـأَلُـكَ خَيْـرَها، وَخَيْـرَ ما جَبَلْـتَهَـا عَلَـيْه، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّها، وَشَـرِّ ما جَبَلْـتَهَـا عَلَـيْه

 

Allaahumma inniy as-aluka khayrahaa, wakhayra maa jabaltahaa ’alayhi. Wa a’uwdhu Bika min sharrihaa washarri maa jabaltahaa ’alayhi.

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba kheri ya (mke) huyu na kheri ya maumbile Uliyomuumba nayo. Na najikinga Kwako na shari yake, na shari ya maumbile Uliyomuumba nayo[1].

 

 

Na ukinunua mnyama mshike kichwa chake na kisha usome du’aa hiyo

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما) , kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم):

 

((إِذَا تَزَوَّجَ أَحَدُكُمُ امْرَأَةً أَوِ اشْتَرَى خَادِمًا، فَلْيَقُلْ : اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَيْرَهَا وَخَيْرَ مَا جَبَلْتَهَا عَلَيْهِ، وَأَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّهَا وَمِنْ شَرِّ مَا جَبَلْتَهَا عَلَيْهِ، وَإِذَا اشْتَرَى بَعِيرًا فَلْيَأْخُذْ بِذِرْوَةِ سَنَامِهِ وَلْيَقُلْ مِثْلَ ذَلِكَ))

((Atakapofunga ndoa mmoja wenu au akanunua khaadimaa aseme: Ee Allaah hakika mimi nakuomba kheri ya (mke) huyu na kheri ya maumbile Uliyomuumba nayo. Na najikinga Kwako na shari yake, na shari ya maumbile Uliyomuumba nayo. Na atakaponunua mnyama amshike kichwa chake na aseme hivyo)) - Abu Daawuwd (2/248) [2160, Ibn Maajah (1/617) [1918], na taz Swahiyh Ibn Maajah (1/324).

 

 

 

Share

081-Hiswnul-Muslim: Du’aa Kabla Kujimai (Kumuingilia Mke)

Hiswnul-Muslim

081-Du’aa Kabla Kujimai (Kumuingilia Mke)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[192]

بِسْمِ الله اللّهُـمَّ جَنِّبْنا الشَّيْـطانَ، وَجَنِّبِ الشَّـيْطانَ ما رَزَقْـتَنا

 

Bi Isimika-Allaah, Allaahumma Jannibnash-shaytwaana wa jannibish-shaytwaana maa Razaqtanaa

 

Kwa jina la Allaah, Ee Allaah, Tuepushe na shaytwaan na Muepushe shaytwaan na Ulichoturuzuku[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما) - Al-Bukhaariy (6/141) [32171] Muslim (2/1028) [1434], Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy.

 

 

Share

082-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Wakati Mtu Anapoghadhibika

Hiswnul-Muslim

082-Du’aa Ya Wakati Mtu Anapoghadhibika

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[193]

أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجيـم

 

A’uwdhu biLLaahi minash-shaytwaanir-rajiym

 

Najikinga kwa Allaah kutokana na shaytwaan aliyeepushwa na kuwekwa mbali na Rehma za Allaah[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Sulaymaan bin Swuradi -(رضي الله عنه)    - Al-Bukhaariy (7/99) [6048], Muslim (4/2015) [2610].

 

 

Share

083-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unapomuona Aliyepatwa Na Mtihani (Kilema, Maafa Na Kadhaalika)

Hiswnul-Muslim

083-Du’aa Unapomuona Aliyepatwa Na Mtihani

(Kilema, Maafa Na Kadhaalika)

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[194]

الْحَمْـدُ للهِ الّذي عافاني مِمّا ابْتَـلاكَ بِهِ، وَفَضَّلَـني عَلى كَثيـرٍ مِمَّنْ خَلَـقَ تَفْضـيلا.

 

AlhamduliLlaah Alladhiy ‘Aafaaniy mimmab-talakaa bihi wa fadhwalaniy ‘alaa kathiyrin mimman Khalaqa tafdhwiylaa

 

 

Himdi Anastahiki Allaah, Ambaye Ameniepusha na kile Alichokupa mtihani na Akanifanya mimi kuwa bora kuliko wengi miongoni mwa Aliowaumba[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) , Kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم)

 

((مَنْ راْ مُبْتَل فَقال: الْحَمْـدُ للهِ الّذي عافاني مِمّا ابْتَـلاكَ بِهِ، وَفَضَّلَـني عَلى كَثيـرٍ مِمَّنْ خَلَـقَ تَفْضـيلا، لَمْ يُصِبْهُ ذالك الْبَلاء))

 

((Atakayemuona aliyepatwa na mtihani akasema: Himdi ni za Allaah, Ambaye Ameniepusha na kile Alichokupa mtihani na Akanifanya mimi kuwa bora kuliko wengi miongoni mwa Aliowaumba, hatofikwa na mtihani huo)) - At-Tirmidhiy (5/493-4),  Ibn Maajah. Angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/153)

 

 

Share

084-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuomba Katika Kikao

Hiswnul-Muslim

084-Du’aa Ya Kuomba Katika Kikao

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[195]

 

 

عَنْ ابْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) قَالَ: كَانَ يُعَدُّ لِرَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فِي الْمَجْلِسِ الْوَاحِدِ مِائَةُ مَرَّةٍ مِنْ قَبْلِ أَنْ يَقُومَ:

 

Imepokewa kutoka kwa Ibn ’Umar (رضي الله عنهما)   ambaye amesema: ”Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa aksioma mara mia moja du’aa hii kabla hajasimama katika kikao chake  kimoja:

 

رَبِّ اغْفِـرْ لي، وَتُبْ عَلَـيَّ، إِنَّكَ أَنْـتَ التَّـوّابُ الغَـفُورُ

 

Rabbi-Ghfir liy wa tub ’alayya Innaka Antat-Tawwabul Ghafuwr

 

Allaah Nighufurie na Nikubalie toba yangu, hakika Wewe ni Mwingi wa  Kupokea tawbah, Mwingi wa kughufuria[1]

 

 

 

 

 

 

 

[1]At-Tirmidhiy [3432] na wengineo na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/153) na Swahiyh Ibn Maajah (2/321) na tamshi la At-Tirmidhiy.

 

 

Share

085-Hiswnul-Muslim: Kafara Ya Kikao

Hiswnul-Muslim

085-Kafara Ya Kikao

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[196]

سُبْحـانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْك

 

Subhaanaka-Allaahumma wabihamdika, ash-hadu an laa ilaaha illaa Anta astaghfiruka wa atuwbu Ilayka

 

Utakasifu ni Wako ee Allaah, na Himdi ni Zako. Nashuhudia kwamba hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe. Nakuomba Unigfhurie na ninarejea Kwako kutubia[1]

 

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah na wengineo   (رضي الله عنه), Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((مَنْ جَلَسَ فِي مَجْلِسٍ فَكَثُرَ فِيهِ لَغطُهُ فَقَالَ قَبْلَ أَنْ يَقُومَ: سُبْحَانَكَ اللَهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، أَشْهَدُ أَن لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ، أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتُوبُ إِلَيْكَ, إِلَّا غفَرَ لَهُ مَا كَانَ فِي مَجْلِسِهِ ذَلِكَ))

((Atakayekaa kikao akapiga porojo, kisha kabla ya kuondoka kikao hicho akasema:

 

سُبْحـانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْك

Subhaanaka-Allaahumma wabihamdika, ash-hadu an laa ilaaha illaa Anta astaghfiruka wa atuwbu Ilayka. Basi Allaah Atamghufuria yaliyojiri katika kikao hicho)) – Aswaabus-Sunan; Abu Daawuwd [4859], At-Tirmidhiy (5/494) [3433], An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah’ [397], Ibn Hibbaan (2/354) [594]. na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Al-Jaami’ [6192].

 

Na imethibiti kutoka kwa 'Aaishah (رضي الله عنها) amesema: “Hajapatapo kukaa Rasuli wa Allaah(صلى الله عليه وسلم)  kikao wala kusoma Qur-aan wala kuswali ila atamaliza na Du'aa hii’.  Akasema 'Aaishah (رضي الله عنها) nikamuuliza “Ee Rasuli wa Allaah, nakuona hukai kikao chochote wala husomi Qur-aan wala huswali Swalaah yoyote ile ila unaimalizia kwa kusoma maneno haya kwanini hasa?  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Ndio!  Aayesema kheri amalize kwa kheri na anayesema shari yanakuwa maneno haya ni kafara kwake)) Ameipokea An-Nasaaiy katika Amal al-Yawm wal-Laylah [308], Ahmad (6/77), na ameisahihisha Faaruwq Hamaadah katika tahqiqi yake ya ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah ya An-Nasaaiy (Uk. 273)

 

 

Share

086-Hiswnul-Muslim: Kumuombea Du’aa Anaekuombea Maghfirah Kwa Allaah

Hiswnul-Muslim

086-Kumuombea Du’aa Anaekuombea Maghfirah Kwa Allaah

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [197]

 

Akimuombea mtu maghfirah mwenzake akasema:

 

غَفَـرَ اللهُ لَكَ

Ghafara-Allaahu laka

 

Allaah Akughufurie

 

Amjibu:

وَلَكَ

 

Walaka

 

Nawe (Akughufurie)[1]

 

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah Bin Sarjis (رضي الله عنه)  amesema:

 

رَأَيْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَأَكَلْتُ مَعَهُ خُبْزًا وَلَحْمًا أَوْ قَالَ ثَرِيدًا. قَالَ: فَقُلْتُ لَهُ: ((أَسْتَغْفَرَ لَكَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)) قَالَ: ((نَعَمْ وَلَكَ)) ثُمَّ تَلَا هَذِهِ الْآيَةَ: ((وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ۗ))

 

”Nilimuona Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) nikala pamoja naye mkate na nyama [au thariydaa – mkate katika supu ya nyama] Nikamwambia: ”Allaah Akughufurie ee Nabiy. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) Akasema: ((Ndio, nawe pia  [Akufughufurie])). Kisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akasoma:

((وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ۗ))

((Na omba maghfirah kwa dhambi zako na (kwa dhambi za) Waumini wa kiume na Waumini wa kike))Muslim [2346]. Na riwaayah nyingine kwa tamshi tofuati kidogo katika Ahmad (5/82), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah (Uk. 218) [421] kwa tahqiyq ya Faaruwq Hamaadah. Aayah katika Suwrat Muhammad [19].

 

 

Share

087-Hiswnul-Muslim: -Du’aa Ya Kumuombea Aliyekufanyia Wema

Hiswnul-Muslim

087-Du’aa Ya Kumuombea Aliyekufanyia Wema

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[198]

جَزاكَ اللهُ خَـيْراً

 

 

 

Jazaaka-Allaahu khayraa (mwanamume mmoja)

 

Allaah Akujaze kheri[1]

 

جَزاكِ اللهُ خَـيْراً

 

 

Jazaaki-LLaahu khayraa (mwanamke mmoja)

 

جَزاكُمُ اللهُ خَـيْراً

 

Jazaakumu-Allaahu khayraa (wengi)

 

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Usaamah bin Zayd (رضي الله عنه)  -

 

((مَنْ صُنِعَ إِلَيْهِ مَعْرُوفٌ فَقَالَ لِصَاحِبِهِ: جَزَاكَ اللَّهُ خَيْرًا. فَقَدْ أَبْلَغَ فِي الثَّنَاءِ))

((Atakayetendewa jambo jema akamwambia aliyemtendea: ”Allaah Akujaze kheri” basi amefikia upeo wa kumsifu)) - At-Tirmidhiy [2035], na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ [6244] na Swahiyh At-Tirmidhiy (2/200).

 

 

Share

088-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kujikinga Na Dajjaal

Hiswnul-Muslim

088-Du’aa Ya Kujikinga Na Dajjaal

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[199]

((مَنْ حَفِظَ عَشْرَ آيَاتٍ مِنْ أَوَّلِ سُورَةِ الْكَهْفِ عُصِمَ مِنَ الدَّجَّال))

 

 ((Atakayehifadhi kwa moyo Aayah kumi za mwanzo wa Suwratul-Kahf atakuwa na kinga ya kujiepusha na Dajjaal))[1]

 

Pia kuomba kinga kwa Allaah kutokana na  fitna za Dajjaal baada ya tashahhud ya mwisho katika kila Swalaah[2]   

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Dardaa (رضي الله عنه)  - Muslim (1/555) [809] Na riwaayah nyingine ((Mwisho wa Suwratul-Kahf)) (1/556)

 

[2]Angalia: ‘Nyiradi baada ya Tashahhud kabla ya Salaam’. Namba [55, 56]  ambayo ni du’aa:

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِـنْ عَذابِ القَـبْر، وَمِـنْ عَذابِ جَهَـنَّم، وَمِـنْ فِتْـنَةِ المَحْـيا وَالمَمـات، وَمِـنْ شَـرِّ فِتْـنَةِ المَسيحِ الدَّجّال

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِـنْ عَذابِ القَـبْر، وَأَعـوذُ بِكَ مِـنْ فِتْـنَةِ المْسيحِ الدَّجّـال، وَأَعـوذُ بِكَ مِـنْ فِتْـنَةِ المْحْـيا وَالمْمـات. اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِنَ المْأْثَـمِ وَالمْغْـرَم

 

 

 

Share

089-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Anaekwambia Anakupenda Kwa Ajili Ya Allaah

Hiswnul-Muslim

089-Du’aa Ya Kumuombea Anaekwambia Anakupenda Kwa Ajili Ya Allaah

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[200]

 

  أَحَبَّـكَ الّذي أَحْبَبْـتَني لَه

Ahabbaka-lladhiy Ahbabtaniy Lah

 

Akupende Ambaye umenipenda mimi kwa ajili Yake[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) 

 

أَنَّ رَجُلًا كَانَ عِنْدَ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَمَرَّ بِهِ رَجُلٌ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ! إِنِّي لَأُحِبُّ هَذَا .فَقَالَ لَهُ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((أَعْلَمْتَهُ؟)) قَالَ: لَا. قَالَ: ((أَعْلِمْهُ)). قَالَ: فَلَحِقَهُ فَقَالَ: إِنِّي أُحِبُّكَ فِي اللَّهِ. فَقَالَ: أَحَبَّكَ الَّذِي أَحْبَبْتَنِي لَهُ

 

Mtu mmoja alikuwa (ameketi) pamoja na Nabiy (صلى الله عليه وسلم) akapita mtu mwengine akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nampenda huyu!” Nabiy (صلى الله عليه وسلم) akamuuliza: ((Je umemjulisha?)) akasema: “Hapana”. Nabiy (صلى الله عليه وسلم) akasema: ((Basi mjulishe)). Akainuka na kumwendea yule mtu akamwambia: “Hakika mimi nakupenda kwa ajili ya Allaah”. Yule mtu akajibu: “Akupende Ambaye umenipenda mimi kwa ajili Yake”. - Abu Daawuwd (4/333) [5125], ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Sunan Abi Daawuwd (3/965)

 

 

Share

090-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kumuombea Aliyekusaidia Kwa Mali

Hiswnul-Muslim

090-Du’aa Ya Kumuombea Aliyekusaidia Kwa Mali

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[201]

بارَكَ اللهُ لَكَ في أَهْلِكَ وَمالِكَ

Baaraka Allaahu laka fiy ahlika wa maalika 

 

Allaah Akubariki katika familia yako na mali yako[1]

 

 

 

 


[1]Kauli ya ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Awf (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (4/288) [2049].

 

 

Share

091-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unapolipa Deni

Hiswnul-Muslim

091-Du’aa Unapolipa Deni

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[202]

بارَكَ اللهُ لَكَ في أَهْلِكَ وَمالِك، إِنَّما جَـزاءُ السَّلَفِ الْحَمْدُ والأَداَءُ

 

Baaraka Allaahu laka fiy ahlika wa maalika. Innamaa jazaaus-salafi Alhamdu wal adaau

 

Allaah Akubariki katika familia yako na mali yako, hakika malipo ya deni ni kushukuru na kulipa[1]

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Abiy Rabiy’ah Al-Makhzumiyyu (رضي الله عنه),

 

استَقْرَضَ مِنِّي النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَرْبَعِينَ أَلْفًا فَجَاءَهُ مَالٌ فَدَفَعَهُ إِلَيَّ وَقَالَ: ((بَارَكَ اللَّهُ لَكَ فِي أَهْلِكَ وَمَالِكَ إِنَّمَا جَزَاءُ السَّلَفِ الْحَمْدُ وَالْأَدَاء))

 

 “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alinikopa elfu arubaini. Akapata mali akanilipa akasema:

 

بارَكَ اللهُ لَكَ في أَهْلِكَ وَمالِك، إِنَّما جَـزاءُ السَّلَفِ الْحَمْدُ والأَداَءُ

((Allaah Akubariki katika familia yako na mali yako, hakika malipo ya deni ni kushukuru na kulipa)) - An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah (Uk. 300) [372], na Ibn Maajah (2/809) [2424] na angalia: Swahiyh ibn Maajah (2/55)

 

 

Share

092-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuogopa Kuingia Katika Ushirikina

Hiswnul-Muslim

092-Du’aa Ya Kuogopa Kuingia Katika Ushirikina

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[203]

اللّهُـمَّ إِنّـي أَعـوذُبِكَ أَنْ أُشْـرِكَ بِكَ وَأَنا أَعْـلَمْ، وَأَسْتَـغْفِرُكَ لِما لا أَعْـلَم

 

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika an ushrika Bika waanaa a’-alamu wa astaghfiruka limaa laa a’-lam

 

Ee Allaah hakika mimi Najikinga Kwako kutokana na kukushirikisha hali ya kuwa najua na ninakuomba maghfirah na nisiyoyajua[1]

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya Abu Muwsaa Al-Ash’ariyy (رضي الله عنه), Kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم)

 

 خَطَبَنَا رَسُولُ اللَّهِ ‏ ‏صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ‏ ‏ذَاتَ يَوْمٍ فَقَالَ: ((أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا هَذَا الشِّرْكَ فَإِنَّهُ أَخْفَى مِنْ دَبِيبِ النَّمْلِ)) فَقَالَ لَهُ مَنْ شَاءَ اللَّهُ أَنْ يَقُولَ: "وَكَيْفَ ‏ ‏نَتَّقِيهِ وَهُوَ أَخْفَى مِنْ دَبِيبِ النَّمْلِ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟" قَالَقُولُوا: ((‏اللَّهُمَّ إِنَّا نَعُوذُ بِكَ مِنْ أَنْ نُشْرِكَ بِكَ شَيْئًا نَعْلَمُهُ وَنَسْتَغْفِرُكَ لِمَا لَا نَعْلَمُ))

“Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alituhutubia akasema: ((Enyi watu! Iogopeni shirki hii kwani imefichika zaidi kuliko kutambaa kwa sisimizi)) Akasema mmoja wa aliyejaaliwa na Allaah aseme: “Je vipi tujiokoe nayo na hali imefichika zaidi kuliko kutambaa kwa sisimizi ee Rasuli wa Allaah?”. Akasema: ((Semeni:

 اللَّهُمَّ إِنَّا نَعُوذُ بِكَ مِنْ أَنْ نُشْرِكَ بِكَ شَيْئًا نَعْلَمُهُ وَنَسْتَغْفِرُكَ لِمَا لَا نَعْلَمُ

Ee Allaah! Hakika sisi tunajikinga Kwako kutokana na kukushirikisha hali ya kuwa tunajua na tuinakuomba maghfirah kwa tusiyoyajua)) - Ahmad (4/403), na wengineo  na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (3/233) [3731] na Swahiyh At-Targhiyb wat-Tarhiyb ya Al-Albaaniy (رحمه الله) (1/122) [36].

 

Share

093-Hiswnul-Muslim: Du’aa Kwa Aliyekuombea Allaah Akubariki

Hiswnul-Muslim

093-Du’aa Kwa Aliyekuombea Allaah Akubariki

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[204]

 

Atakapokuombea mtu:

 

 

بارَكَ الله

 

Ujibu:

 

وَفيكَ بارَكَ الله                                            

Wa fiyka Baaraka-Allaahu

 

Na wewe Allaah Akubariki[1]

 

 

 


[1]Kauli ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)  - Ibn As-Sunniy (Uk.138) [278] na angalia: Al-Waabil Asw-Swayyib ya ibn Al-Qayyim (Uk. 304) tahqiyq Bashiyr Muhammad ‘Uyuwn.

 

 

Share

094-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kukhofia Mkosi Nuksi

Hiswnul-Muslim

094-Du’aa Ya Kukhofia Mkosi Nuksi

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[205]

اللّهُـمَّ لا طَيْـرَ إِلاّ طَيْـرُك، وَلا خَـيْرَ إِلاّ خَـيْرُك، وَلا إِلهَ غَيْـرُك

 

Allaahumma laa twayra illaa twayruka, walaa khayra illaa khayruka, walaa ilaaha Ghayruka

 

Ee Allaah hapana mkosi ila Ulioukadiria Wewe, na hapana kheri ila kheri Yako, na hapana mwabudiwa wa haki ghairi Yako.[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amruw (رضي الله عنه), Kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم):

 

((مَنْ رَدَّتْهُ الطِّيَرَةُ عَنْ حَاجَتِهِ فَقَدْ أَشْرَكَ)) قَالُوا: فَمَا كَفَّارَةُ ذَلِكَ؟ قَالَ: ((أَنْ يَقُولَ اللَّهُمَّ لاَ خَيْرَ إِلاَّ خَيْرُكَ وَلاَ طَيْرَ إِلاَّ طَيْرُكَ  وَلاَ إِلَهَ غَيْرُكَ))

 

((Atakayerudi nyuma pasina na kuitekeleza haja yake kwa sababu ya at-twiyarah [kuogopa mkosi] amefanya shirki)) Wakuliza: Basi nini kafara yake? Akajibu: ((Aseme:

 

اللَّهُمَّ لاَ خَيْرَ إِلاَّ خَيْرُكَ وَلاَ طَيْرَ إِلاَّ طَيْرُكَ وَلاَ إِلَهَ غَيْرُكَ

 Allaahumma laa khayra illa khayruka, wa laa twayra illa twayruka, wa laa ilaaha ghayruka – Ee Allaah, hakuna kheri ila Uiletayo Wewe, wala hakuna mkosi ila Ulioukadiria Wewe, na hapana mwabudiwa wa haki ghairi Yako))

 

Ahmad (2/220), Ibn As-Shunniy (292), na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Al-Ahaadiyth Asw-Swahiyhah (3/54) [1065]. Ama fali, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akipendezewa na kwa hivyo alisikia neno zuri kwa mtu akalipenda akasema: ((Tumechukua fali kutoka [mdomoni] kwako)) Abu Daawuwd [3917], Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Asw-Swahiyhah (2/363) kutoka kwa Abu Shaykh katika ‘Akhlaaq An-Nabiyy (صلى الله عليه وسلم)’ (Uk. 270).

 

At-Twayr, Atw-Twiyara  (Ndege): Itikadi za ushirikina kutabiri jambo kama lina nuksi, mkosi, ukorofi au kama lina kheri ili walitende. Hutumia ndege; humrusha basi anaporuka kuliani huitakidi kuwa ni kheri, na anaporuka upande wa kushoto huitakidi kuwa kuna shari. Hii ni shirki kubwa kwa sababu ni kubashiria mambo ya ghayb.

 

 

Share

095-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kupanda Mnyama Au Chombo Chochote Cha Kusafiria

Hiswnul-Muslim

095-Du’aa Ya Kupanda Mnyama Au Chombo Chochote Cha Kusafiria

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[206]

 

بِسْـمِ اللهِ وَالْحَمْـدُ لله، سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَـٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِينَ ﴿١٣ وَإِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ ﴿١٤  الحَمْـدُ لله، الحَمْـدُ لله، الحَمْـدُ لله، اللهُ أكْـبَر، اللهُ أكْـبَر، اللهُ أكْـبَر، سُـبْحانَكَ اللّهُـمَّ  إِنّي ظَلَـمْتُ نَفْسي فَاغْـفِرْ لي، فَإِنَّهُ لا يَغْفِـرُ الذُّنوبَ إِلاّ أَنْـت.

 

BisimiLLaah, wal HamduliLLaah, Subhaanalladhiy sakkhara lanaa haadhaa wamaa kunnaa Lahu muqriniyn, wainnaa ilaa Rabbina lamunqalibuwn. AlhamduliLLaah, AlhamduliLLah, AlhamduliLLaah, Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, Subhaanaka-Allaahumma inniy dhwalamtu nafsiy faghfirliy fainnahu laa yaghfirudh-dhunuwba illaa Anta

 

Kwa jina la Allaah, na Himdi Anastahiki Allaah, ((Utakasifu ni wa (Allaah) Ambaye Ametutiishia haya, na tusingeliweza wenyewe kumdhibiti. (huyu mnyama au chombo) “Na hakika kwa Rabb wetu, bila shaka tutarejea)) [Az-Zukhruf: 13-14]. Himdi Anastahiki Allaah, Himdi Anastahiki Allaah, Himdi Anastahiki Allaah, Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Utakasifu ni Wako Ee Allaah, hakika mimi nimejidhulumu nafsi yangu basi nighufurie, kwani hakuna mwenye kughufuria madhambi ila Wewe[1]

 

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abiy Twaalib (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (3/34) [2602], At-Tirmidhiy (5/501) [3446],  Ahmad,  na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/156)

 

 

Share

096-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Safari

Hiswnul-Muslim

096-Du’aa Ya Safari

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[207]

 

اللهُ أكبَر، اللهُ أكبَر، اللهُ أكبَر، سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَـٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِينَ ﴿١٣ وَإِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ ﴿١٤ اللّهُـمَّ إِنّا نَسْـأَلُكَ في سَفَـرِنا هذا البِـرَّ وَالتَّـقْوى، وَمِنَ الْعَمَـلِ ما تَـرْضى، اللّهُـمَّ هَوِّنْ عَلَـينا سَفَرَنا هذا وَاطْوِ عَنّا بُعْـدَه، اللّهُـمَّ أَنْـتَ الصّـاحِبُ في السَّـفَر، وَالْخَلـيفَةُ في الأهـلِ، اللّهُـمَّ  إِنّـي أَعـوذُبِكَ مِنْ وَعْـثاءِ السَّـفَر، وَكَآبَةِ الْمَنْـظَر، وَسوءِ الْمُنْـقَلَبِ في المـالِ وَالأَهْـل.

 

Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, Allaahu Akbar. Subhaanalladhiy sakkhara lanaa haadhaa wamaa kunnaa Lahu muqriniyn, wainnaa ilaa Rabbina lamunqalibuwn. Allaahumma innaa nas-aluka fiy safarina haadha al-birra wat-taqwaa, waminal ’amali maa Tardhwaa. Allaahumma hawwin ‘alaynaa safaranaa haadhaa, wa atwi ‘annaa bu’-dahu. Allaahumma Antasw-Swaahibu fis-safari, wal Khaliyfatu fil ahli. Allahumma inniy a’uwdhu Bika min wa’thaais-safari, wa kaabatil mandhwar, wa suw-il munqalabi filmaali wal ahli

 

Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, ((Utakasifu ni wa (Allaah) Ambaye Ametutiishia haya, na tusingeliweza wenyewe kumdhibiti. (huyu mnyama au chombo) “Na hakika kwa Rabb wetu, bila shaka tutarejea))  Ee Allaah,  hakika sisi tunakuomba katika safari yetu hii wema na taqwa, na katika matendo Unayoridhia, Ee Allaah, Ifanye nyepesi safari yetu hii, na Ifupishe umbali wake, Ee Allaah, Wewe Ndiye Unayesuhubiana nami katika safari na Mchungaji wa familia yangu.  Ee Allaah, hakika mimi najikinga Kwako kutokana na ugumu wa safari na ubaya  wa mtizamo na uovu wa kubadilikiwa katika mali na familia .

 

Wakati wa kurudi safari atayasema hayo yalioko juu na kisha atazidisha:

 

آيِبُـونَ تائِبُـونَ عابِـُدونَ لِرَبِّنا حـامِـدُونَ

 

Aayibuwna, taaibuwna, ‘aabiduwnaa, li Rabbinaa haamiduwna

 

 Tunarudi hali ya kuwa tunatubia, tunaabudu, na Rabb wetu tunamsifu[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما)  -  Muslim (2/998) [1342]

 

 

 

Share

097-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuingia Mjini Au Kijijini

Hiswnul-Muslim

097-Du’aa Ya Kuingia Mjini Au Kijijini

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[208]

 

أللّـهُمَّ رَبَّ السَّـمواتِ السّـبْعِ وَما أَظْلَلَـنَ، وَرَبَّ الأَراضيـنَ السّـبْعِ وَما أقْلَلْـنَ، وَرَبَّ الشَّيـاطينِ وَما أَضْلَلْـنَ، وَرَبَّ الرِّياحِ وَما ذَرَيْـنَ، أَسْـأَلُـكَ خَيْـرَ هذهِ الْقَـرْيَةِ وَخَيْـرَ أَهْلِـها، وَخَيْـرَ مَا فِيهَا، وَأَعـوذُ بِكَ مِنْ شَـرِّها وَشَـرِّ أَهْلِـها، وَشَـرِّ مَا فِيهَا

 

Allaahumma Rabbas-samaawaatis-sab’i wamaa adhw-lalna. Wa Rabbal-araadhwiynas-sab’i  wamaa aqlalna. Wa Rabbash-shayaatwiyni wamaa adhw-lalna. Wa Rabbar-riyaahi wamaa dharayna. As-aluka khayra haadhihil-qaryati wakhayra ahlihaa, wakhayra maa fiyhaa. Wa a’uwdhu Bika min sharrihaa, washarri ahlihaa, washarri maa fiyhaa

 

Ee Allaah Rabb wa mbingu saba na kila ambacho hizo mbingu zimekipa kivuli, na Rabb wa ardhi saba na kila ambacho zimebeba, na Rabb wa mashaytwaan na walichokipoteza, na Rabb wa upepo na ulichokibeba. Nakuomba kheri ya kijiji hichi na kheri ya watu wake na kheri ya vilivyo ndani yake, Najikinga Kwako na shari ya kijiji hichi na shari ya watu wake, na shari iliyomo ndani yake[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Swuhayb bin Sinaan Ar-Ruwmiy (رضي الله عنه) - Al-Haakim na ameisahihisha na ameikubali Adh-Dhahabiy  (2/100) na ibn As-Sunniy [524] na Al-Haafidhw ameipa daraja ya Hasan katika  Takhriyj Al-Adhkaar  (5/154). Ibn Baaz (رحمه الله) amesema: Na ameipokea An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah’ [547, 549] kwa Isnaad ya Hasan. angalia: Tuhfat Al-Akhyaar (Uk.370)

 

 

Share

098-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuingia Sokoni, Madukani

Hiswnul-Muslim

098- Du’aa Ya Kuingia Sokoni, Madukani

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[209]

 

لا إلهَ إلاّ اللّه وحدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ المُلْـكُ ولهُ الحَمْـد، يُحْيـي وَيُميـتُ  وَهُوَ حَيٌّ لا يَمُـوت، بِيَـدِهِ الْخَـيْرُ وَهوَ عَلىَ كلّ شيءٍ قَدِيرٌ.

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu, Yuhyiy wa Yumiytu wa Huwa Hayyun laa yamuwtu, Biyadihil-khayru wa Huwa  ‘alaa kulli shay-in Qadiyr

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah  hali ya kuwa Peke Yake, Hana mshirika, ni Wake Ufalme na ni Zake Himdi, Anahuisha na Anafisha, Naye ni Hai Asiyekufa, kheri iko mikononi Mwake, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza[1]

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Umar bin Khatwaab(رضي الله عنه)  Kauli ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم):

amesema: ((Atakayeingia sokoni akasema [hiyo du’aa] Allaah Atamuandikia mema milioni, Atamfutia maovu milioni, Atampandisha Daraja milioni)) na  ((atajengewa nyumba katika Jannah) At-Tirmidhiy (5/291) [3429], Al-Haakim (1/538), Ibn Maajah [2235] Ad-Daarimiy  na ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Ibn Maajah (2/21) na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/152). Na angalia: Swahiyh Al-Jaami’  (6231).

 

Tanbihi: ‘Ulamaa wamekhitilafiana kuhusu usahihi wake: Ibn Baaz  (رحمه الله) amesema: “Ni Dhwa’iyf, ila inapasa kumdhukuru Allaah (عزّ وجلّ) kwa wingi hata anapoingia sokoni kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها) kwamba: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akimdhukuru Allaah kila wakati.” Na pia Allaah (سبحانه وتعالى) Anatuamrisha:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾

Enyi walioamini!  Mdhukuruni Allaah kwa wingi wa kumdhukuru.

وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

Na Msabbihini asubuhi na jioni‏. [Al-Ahzaab: 41-42]

 

Share

099-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Wakati Mnyama Uliempanda Akileta Tabu

Hiswnul-Muslim

099-Du’aa Ya Wakati Mnyama Uliempanda Akileta Tabu

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[210]

بِسْـمِ اللهِ

BismiLLaah

 

Kwa jina la Allaah[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Usamah bin ‘Umayr (رضي الله عنه)  

 

كُنْتُ رديف النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَعَثَرَت  دابته، فَقُلْتُ: تَعِسَ الشَّيْطَانُ، فَقَالَ: ((لاَ تَقُلْ تَعِسَ الشَّيْطَانُ، فَإِنَّكَ إذا قُلْتَ ذلك تعاظم  حَتَّى يكون مِثل الْبَيْتِ، وَيَقُولُ: بِقُوَّتِي، وَلَكِنْ قُلْ: بِاسْمِ اللهِ، فَإِنَّكَ إذا قُلْتَ ذلك تصاغر يكون مِثْلَ الذُّبَاب)).

((Nilipanda mnyama nyuma ya Nabiy (صلى الله عليه وسلم) mnyama wake akajikwaa nikasema: “Aangamie shaytwaan”. Akasema: ((Usiseme hivyo kwani ukisema hivyo atavimba mpaka atakuwa kama nyumba, na kisha atasema: “Kwa nguvu zangu”. Bali sema: BismiLLaah, kwani ukisema hivyo atanyweya mpaka atakuwa kama nzi)) - Abu Daawuwd (4/296) [4982] na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (3/941)

 

 

 

Share

100-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Anaesafiri Kuwaombea Wakaazi

Hiswnul-Muslim

100-Du’aa Ya Anaesafiri Kuwaombea Wakaazi

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[211]   

  أَسْتَوْدِعُكُمُ اللَّهَ الَّذِي لاَ تَضِيعُ وَدَائِعُهُ

 

Astawdi’ukumu Allaha Alladhiy laa tadhwiy’u wadaai’uhu

 

Nawaacha katika amana ya Allaah Ambaye hakupotei amana Kwake[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  ((Anayeazimia kusafiri, amwambie aliyebakia:

 

  أَسْتَوْدِعُكُمُ اللَّهَ الَّذِي لاَ تَضِيعُ وَدَائِعُهُ

Ahmad (2/403), Ibn Maajah (2/943) [2825] na angalia: Swahiyh ibn Maajah (2/133)

 

 

Share

101-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Wakaazi Wanayomuombea Anaesafiri

Hiswnul-Muslim

101-Du’aa Ya Wakaazi Wanayomuombea Anaesafiri

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

 

 

[212]

أَسْتَـوْدِعُ اللَّهَ دِيـنَكَ وَأَمانَتَـكَ، وَخَـواتيـمَ عَمَـلِكَ

 

Astawdi’u Allaaha Diynaka, wa amaanataka, wa khawaatiyma ‘amalika

 

Naweka amana kwa Allaah Dini yako na uaminifu wako na mwisho wa matendo yako[1]

 

 

Mwanamke aambiwe:

أَسْتَـوْدِعُ اللَّهَ دِيـنَكِ وَأَمانَتَـكِ، وَخَـواتيـمَ عَمَـلِكِ

Astawdi’u Allaaha Diynaki, wa amaanataki, wa khawaatiyma ‘amaliki

 

 

[213]

زَوَّدَكَ اللَّهُ التقْوى، وَغَفَـرَذَنْـبَكَ، وَيَسَّـرَ لَكَ الخَـيْرَ حَيْـثُما كُنْـتَ

 

Zawwadaka -Allaahut-taqwa waghafara dhanbaka, wayassara lakal-khayra haythu maa kunta

 

Allaah Akuzidishie taqwa na Akughufurie madhambi yako, na Akufanyie wepesi katika kheri popote ulipo[2]

 

 

Mwanamke aambiwe:

زَوَّدَكِ اللَّهُ التقْوى، وَغَفَـرَذَنْـبَكِ، وَيَسَّـرَ لَكِ الخَـيْرَ حَيْـثُما كُنْـتِ

 

ZawwadakiLLaahut-taqwa waghafara dhanbaki, wayassara lakil-khayra haythu maa kunti

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما)

 

قال سالم بن عبدالله بن عمر، أنَّ عبدالله بن عمر رضي الله عنهما  كان يقول للرجلِ إذا أراد سفرًا: ادنُ مني أودِّعك كما كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يودعنا، فيقول….

 

Saalim bin ‘Abdullah bin ‘Umar amesema: Mtu alipotaka kusafiri, ‘Abdullaah bin Umar humwambia: Nikaribie nikuage kama alivyokuwa akituaga Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) husema:

أَسْتَـوْدِعُ اللَّهَ دِيـنَكَ وَأَمانَتَـكَ، وَخَـواتيـمَ عَمَـلِكَ

Ahmad (7/2), At-Tirmidhiy (5/499) [2443], Ibn Maajah na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (2/155), Swahiyh Ibn Maajah [2296] Silsilatus-Swahiyhah (14)

 

[2]Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه)  

 

قال: جاء رجلٌ إلى النبي -صلى الله عليه وسلم فقال: يا رسول الله، إني أريدُ سفرًا، فزوِّدني، فقال: ((زوَّدك اللهُ التقوى))، قال: زدني، قال: ((وغفر ذنبَك))، قال: زدني،قال: ((ويسَّر لك الخيرَ حيثما كُنْتَ))

Amesema: Alikuja mtu kwa Nabiy (صلى الله عليه وسلم) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah, mimi nataka kusafiri, basi nipatie (mahitajio ya safari; niombee du’aa ya Baraka). Akasema: ((Allaah Akuzidishie taqwa)) Akasema: Nizidishie: Akasema: ((na Akughufurie madhambi yako)) Akasema: Nizidishie: Akasema: ((Na Akufanyie wepesi katika kheri popote ulipo))  - At-Tirmidhiy [2444] Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/155)

 

 

Share

102-Hiswnul-Muslim:Kusema Allaahu Akbar, Subhaana Allaah Wakati Wa Kupanda Na Kushuka Mlima

Hiswnul-Muslim

102-Kusema Allaahu Akbar, Subhaana Allaah

Wakati Wa Kupanda Na Kushuka Mlima

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[214]

 

Imepokewakutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه) amesema: ‘Tulikuwa tukipanda mlima tunasema:

 

اللهُ أَكْـبَر

Allaahu Akbar

 

Allaah ni Mkubwa

 

 

Na tukishuka tunasema:

 

سُبْـحانَ الله  

 

Subhaana-Allaah

 

Utakasifu ni wa Allaah[1]

 

 

 

 

 

 

[1] Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/135) [2993]

 

 

Share

103-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Msafiri Unapoingia Usiku

Hiswnul-Muslim

103-Du’aa Ya Msafiri Unapoingia Usiku

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[215]   

سَمِـعَ سـامِعُ بِحَمْـدِ اللهِ وَحُسْـنِ بَلائِـهِ عَلَيْـنا. رَبَّنـا صـاحِبْـنا وَأَفْـضِل عَلَيْـنا عائِذاً باللهِ مِنَ النّـار

 

Sami’a (pia Samma’a) Saami’un BihamdiLLaah, wa husni balaaihi ‘alaynaa. Rabbanaa swaahibnaa, wa Afdhwil ‘alaynaa ‘aaidhan biLLaahi minan-naari

 

Amesikia msikilizaji kwa kumhimidi Allaah, na uzuri wa mitihani Yake juu yetu.  Rabb wetu kuwa nasi na Tufadhilishe hali ya kuwa tunajikinga na Allaah kutokana na Moto[1]

 

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah  (رضي الله عنه) - Muslim (4/2086) Na maana ya

سَمِـعَ سـامِعُ

Yaani: “Ameshuhudia shahidi juu ya kumhimidi kwetu Allaah Ta’aalaa kwa Neema Zake na uzuri wa mitihani Yake kwetu” Ama maana ya ‘Samma’a Saami’un ni: “Amefikisha msikilizaji kauli yangu hii kwa mwengine” Na amesema tanbihi kama hiyo katika Nyiradi za sihri na Du’aa.  Na kauli yake: 

رَبَّنـا صـاحِبْـنا وَأَفْـضِل عَلَيْـنا

Yaani: Tuhifadhi na Tufadhilishe kwa wingi wa neema Zako na Tuepushe na kila yanayochukiza”  Sharh An-Nawawy (17/39)

 

 

Share

104-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Msafiri Akishuka Sehemu Wakati Yuko Safarini Au Mahali Penginepo

Hiswnul-Muslim

104-Du’aa Ya Msafiri Akishuka Sehemu Wakati Yuko Safarini Au Mahali Penginepo

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [216]

أَعـوذُ بِكَلِـماتِ اللّهِ التّـامّاتِ مِنْ شَـرِّ ما خَلَـق

 

A’uwdhu Bikalimati-LLaahit-ttaammati min sharii maa Khalaq

 

Najikinga kwa maneno ya Allaah yaliyotimia na shari alichokiumba[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Khawlah bint Haakim (رضي الله عنهما)  

 

((مَنْ نَزلَ مَنزِلاً ثُمَّ قال : أَعُوذُ بِكَلِمات اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ ، لَمْ يضرَّه شَيْءٌ حتَّى يرْتَحِل مِنْ منزِلِهِ ذلكَ))

 

((Atakayeteremka katika kituo (au makazi) kisha akasema:

أَعـوذُ بِكَلِـماتِ اللّهِ التّـامّاتِ مِنْ شَـرِّ ما خَلَـق

Najilinda kwa maneno ya Allaah yaliyotimia na shari Alichokiumba - hakuna kitakachomdhuru hadi atakapoondoka katika kituo (au makazi) hicho)) - Muslim (4/2080) [2708].

 

Tanbihi:  Du’aa hii anaweza kuisoma mtu anapohamia sehemu mpya au nyumba mpya na si kufanya mambo ambayo yamezoeleka katika jamii kutendwa kama kuchinja na mialiko ya watu kukusanyika kusoma na mengineyo ambayo ni ya shirki na bid’ah.

 

 

 

Share

105-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Msafiri Akirudi Kutoka Safarini

Hiswnul-Muslim

105-Du’aa Ya Msafiri Akirudi Kutoka Safarini

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[217]

 

اللّهُ أَكْـبَر، اللّهُ أَكْـبَر، اللّهُ أَكْـبَر

Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, Allaahu Akbar

 

Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa.

 

Kisha sema:

 

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحْـدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ الملكُ ولهُ الحَمْد، وهُوَ على كُلّ شَيءٍ قَـدير، آيِبـونَ تائِبـونَ عابِـدونَ لِرَبِّـنا حـامِـدون، صَدَقَ اللهُ وَعْـدَه، وَنَصَـرَ عَبْـدَه، وَهَزَمَ الأَحْـزابَ وَحْـدَه.

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul-Mulku walahul-Hamd, wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr.  Aaibuwna, taaibuwna, ’aabiduwna li-Rabbinaa haamiduwna. Swadaqa-Allaahu Wa’dahu, wa Naswara ’Abdahu, wa Hazzamal-ahzaaba Wahdahu

 

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali ya kuwa Peke Yake, wala hana mshirika. Ufalme ni Wake, na Himdi ni Zake, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. Tunanarudi hali ya kuwa tunatubia, tunaabudu, na Rabb wetu tunamsifu. Amesadikisha Allaah ahadi Yake, na Amemnusuru mja Wake, na Amevishinda vikosi peke Yake[1]

 

 

 

[1] Imepokewa kutoka  kwa Ibn `Umar (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akirudi vitani au kutoka Hijjah katika kila akipanda mlima akisema hivyo. Al-Bukhaariy (7/163) [1797], Muslim (2/980) [1344].

 

 

 

Share

106-Hiswnul-Muslim: Anachopaswa Kusema Mtu Ikimfikia Khabari Ya Kufurahisha Au Ya Kusikitisha

Hiswnul-Muslim

106-Anachopaswa Kusema Mtu Ikimfikia Khabari Ya Kufurahisha Au Ya Kusikitisha

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[218]

 

Alikuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) ikimfikia khabari ya kufurahisha akisema:

 

الْحَمْـدُ للهِ الَّذي بِنِـعْمَتِهِ تَتِـمُّ الصّـالِحَات

 

AlhamduliLLaahiL-Ladhiy Bini’matihi tattimusw-swaalihaat

 

Himdi Anastahiki Allaah Ambaye kwa neema Yake yanatimia mambo mema.

 

Na ikimjia khabari ya kusikitisha kusema:

 

الْحَمْـدُ للهِ على كُـلِّ حاَلٍ

Alhamdu-liLLaahi ‘alaa kulli haal

 

Himdi Anastahiki Allaah kwa hali zote[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ’Aaishah (رضي الله عنها)   - Ibn As-Sunniy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [378], Al-Haakim akaisahihisha (1/499) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika  Swahiyh Al-Jaami’ (4/201) [4640]. Taz pia Swahiyh Ibn Maajah [3081].

 

 

Share

107-Hiswnul-Muslim: Fadhila Za Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وسلم)

Hiswnul-Muslim

107-Fadhila Za Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وسلم)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[219]

 

قال رَسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ صَلَّى عَلَيَّ صَلَاةً صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ بِهَا عَشْرًا))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayeniswalia mara moja basi Allaah Atamswalia mara kumi))[1]

 

 

 

[220]

قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((لا تجعلوا قبري عيدا، وصلوا علي فإن صلاتكم تبلغني حيث كنتم))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Msilifanye kaburi langu kuwa ni mahali pa kurejewa rejewa, na niswalieni kwani kuniswalia kwenu kunanifikia popote mlipo))[2]

 

 

[221]

وَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الْبَخِيلُ مَنْ ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَمْ يُصَلِّ عَلَيَّ))

Pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Bakhili ni yule ambaye nikitajwa haniswalii))[3]

 

 

[222]

وَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ لِلَّهِ مَلائِكَةً سَيَّاحِينَ فِي الأَرْضِ يُبَلِّغُونِي مِنْ أُمَّتِي السَّلام))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Hakika Allaah Ana Malaika wanamzunguka katika ardhi, wananiletea salaam kutoka kwa Ummah wangu))[4]

 

 

[223]

 

وَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم َ: ((مَا مِنْ أحَدٍ يُسَلِّمْ علَيَّ إلاَّ رَدَّ اللهُ رُوحِي حَتَّى أَرُدَّ عَلَيْهِ السَّلامَ))

Na pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Hakuna mtu yeyote anayeniswalia ila Allaah hunirudisha roho yangu ili nimrudishie salaam))[5]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Muslim (1/288) [408] Amesema Al-Bukhaariy katika Swahiyh yake: Abul Al-‘Aaaliyah amesema: “Swalah ya Allaah ni kumsifu kwake mbele ya Malaika na Swalah ya Malaika ni du’aa”

 

[2]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)   - Abu Daawuwd (2/218) [2042], Ahmad (2/367) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh  Abi Daawuwd (2/383)

 

[3]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه)   - At-Tirmidhiy (5/551) p3546], na wengineo na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (3/25) [2787] na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/177)

 

[4]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رضي الله عنه)  -  An-Nasaaiy (3/43), Al-Haakim (2/421) na ameisahihisha  katika Swahiyh An-Nasaaiy  (1/274)

 

[5]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Abu Daawuwd  (2041), na Al-Albaaniy (رحمه الله) ameipa daraja ya Hasan katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/283)

 

Tanbihi:  Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وسلم) ni kumswalia kama ilivyothibiti katika Sunnah navyo ni kama tunavyomswalia kwa Swalaatul-Ibraahimiyyah kwenye kikao cha Tashahhud kwenye Swalaah, au kumswalia kwa kifupi na kumswalia kila siku na kila mara anapotajwa na kukithirisha kumswalia siku ya Ijumaa. Lakini haijuzu mikusanyiko ya watu katika masiku wanayodai ni mawlid yake, akaswaliwa Nabiy (صلى الله عليه وسلم). 

 

 

 

Share

108-Hiswnul-Muslim: Fadhila Za Kueneza Na Kudhihirisha Maamkuzi Ya Kiislamu

Hiswnul-Muslim

108-Fadhila Za Kueneza Na Kudhihirisha Maamkuzi Ya Kiislamu

www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[224]

 

قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: لا تَدْخُـلُوا  الـجَنَّةَ حتـى  تُؤمِنُوا،  ولا تُؤمِنُوا  حتـى تَـحابُّوا  أوَلا أدُلُّكُمْ علـى شَيءٍ  إذا فَعَلْتُـمُوهُ تَـحَابَبْتُـمْ؟  افْشُوا السّلامَ  بَـيْنَكُمْ. 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Hamtoingia Jannah hadi muamini, na wala hamuwezi kuamini hadi mpendane. Je, nikujulisheni jambo ambalo mtakapolifanya mtapendana? Toleaneni Salaam baina yenu)) [1] 

 

 

 

[225]

 

Na amesema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم)

 

 ثَلاَثٌ مَنْ جَمَعَهُنَّ فَقَدْ جَمَعَ الإِيمَانَ: الإِنْصَافُ مِنْ نَفْسِكَ، وَبَذْلُ السَّلاَمِ لِلْعَالَمِ، وَالإِنْفَاقُ مِنَ الإِقْتَار

 

((Mambo matatu anaeyakusanya basi amekusanya imani; uadilifu wa nafsi yako na kutowa salaam kwa watu wote na kutoa swadaqah hali ya kuwa ni mchache wa mali))[2]

 

 

 

[226]

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ رَجُلًا سَأَلَ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: أَيُّ الْإِسْلَامِ خَيْرٌ؟ قَالَ:  تُطْعِمُ الطَّعَامَ وَتَقْرَأُ السَّلَامَ عَلَى مَنْ عَرَفْتَ وَمَنْ لَمْ تَعْرِفْ

 

Imepokewatoka  kwa ‘Abdullaah bin ’Amr  (رضي الله عنهما) kwamba mtu mmoja alimuuliza  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم): ”Ni Uislamu gani bora?”   Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akasema: ((Kulisha chakula, na kumsalimia unayemjua na usiyemjua))[3]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  Muslim (1/74) [54] na wengineo

 

[2]Hadiyth ya ‘Ammaar bin Yaasir  (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (1/82) - Mawquwfan Mu’allaqan (Ni Hadiyth iliyioshia kwa Swahaaba wa Nabiy (صلى الله عليه وسلم)  na kukatika sanad yake).

 

[3]  Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (1/55) [12], Muslim (1/65) [39]

 

 

Share

109-Hiswnul-Muslim: Namna Ya Kumrudishia Salaam Kafiri Anapokusalimia

Hiswnul-Muslim

109-Namna Ya Kumrudishia Salaam Kafiri Anapokusalimia

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[227]

 

إِذَا سَلَّم عَلَيْكُمْ أهْلُ الكِتَابِ؛ فَقُولُوا: وَعَلَيْكُمْ

 

Ahlul-Kitaab (Mayahudi na Manaswara) wakikuamkieni (maamkizi ya maangamizi) semeni:

وَعَلَيْكُمْ

Wa ’alaykum

 

Na juu yenu[1]

 

 

 

 


[1] Hadiyth ya Anas bin Maalik  (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/42) [6258], Muslim (4/1705) [2163].

 

Tanbihi:  Lakini wakikusalimieni kwa maamkizi mema yaliyo bayana na sahihi yaani wakisema:

 

السَّلامُ عَلَيْكُم

 

”Assalaamu ’alaykum”

 

Basi jibuni vizuri kama vile Alivyomrisha Allaah (سبحانه وتعالى) yaani mjibu:

وعليكم السلام

Wa ’alaykumussalaam

 

Imethibiti hivyo kutoka kwa ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  kuhusu Aayah:

 

وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا ۗ

Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo.  [An-Nisaa 4: 86] – Al-Bukhaariy katika Al-Adab Al-Mufrad [1107]

 

 

Ama wakikuamkieni kwa matamshi yasiyokuwa bayana kama vile ”assaam ’alaykum” bila ya kutamka herufi ya laam ambayo inapeleka kuleta maana ya: ”mauti yawe juu yenu”, basi ndio mjibu hivyo: ”Wa ’alaykum”

 

Hadiyth ya Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

((إِذَا سَلَّمَ عَلَيْكُمُ الْيَهُودُ فَإِنَّمَا يَقُولُ أَحَدُهُمُ السَّامُ عَلَيْكُمْ فَقُولوا: وَعَلَيْكَ))

 

((Akikusalimieni Myahudi, kawaida husema “Assaam ‘alaykum (mauti yakufikeni), basi semeni: “wa ‘alayka” (na kwako yakufikie)) Al-Bukhaariy [6257], Muslim [2164].

 

 

 

 

Share

110-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ukisikia Mlio wa Jogoo Au Wa Punda

Hiswnul-Muslim

110-Du’aa Ukisikia Mlio wa Jogoo Au Wa Punda

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[228]

 

قال رسول صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا سَمِعْتُمْ صِيَاحَ الدِّيَكَةِ فَاسْأَلُوا اللَّهَ مِنْ فَضْلِهِ؛ فَإِنَّهَا رَأَتْ مَلَكاً، وَإِذَا سَمِعْتُمْ نَهِيقَ الْحِمَارِ فَتَعَوَّذُوا بِاللَّهِ مِنَ الشَّيْطَانِ؛ فَإِنَّهُ رَأَى شَيْطَاناً))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Mkisikia mlio wa jogoo muombeni Allaah fadhila Zake kwani huwa amemuona Malaika. Na mkisikia mlio wa punda basi ombeni kinga kwa Allaah, kwani huwa amemuona shaytwaan))[1]

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/350) [3303], Muslim (4/2092) [2729].

 

 

Share

111-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unaposikia Mlio Wa Mbwa Usiku

Hiswnul-Muslim

111-Du’aa Unaposikia Mlio Wa Mbwa Usiku

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[229]

 

قال رسول اللّه صلى اللّه عليه وسلم‏:‏‏ ((‏إذَا سَمِعْتُمْ نُباحَ الكِلابِ وَنَهِيقَ الحَمِيرِ باللَّيْلِ فَتَعَوَّذُوا باللَّهِ، فإنَّهُنَّ يَرَيْنَ ما لا تَرَوْنَ))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Mkisikia mlio wa mbwa na wa punda usiku basi mtakeni kinga Allaah  kwani wao wanaona msiyoyaona))[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنهما) - Abu Daawuwd (4/327) [5103], Ahmad (3/306), na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Abi Daawuwd (3/961).

 

 

Share

112-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unayomuombea Uliyemtukana

Hiswnul-Muslim

112-Du’aa Unayomuombea Uliyemtukana

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[230]

 

 

قال رسول اللّه صلى اللّه عليه وسلم‏:‏‏ ((اللَّهُمَّ فَأَيُّمَا مُؤْمِنٍ سَبَبْتُهُ فَاجْعَلْ ذَلِكَ لَهُ قُرْبَةً إِلَيْكَ يَوْمَ الْقِيَامَة ))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

”Allaahumma faayyumaa Mu-uminin sababtuhu, Faj’-al dhaalika lahu qurbatan Ilayka Yawmal-Qiyaamah

 

Ee Allaah kwa Muislamu yoyote yule niliyemtukana basi fanya kwa hilo (liwe jambo) litakalomkurubisha Kwako (ni thawabu kwake) siku ya Qiyaamah[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Hurayrah  (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/171) [6361],  Muslim (4/2007) [2601] na tamshi lake ((Basi ijaalie kwake iwe utakaso na Rehma).

 

 

Share

113-Hiswnul-Muslim: Anachopaswa Kusema Muislamu Akimsifu Muislamu Mwenziwe

Hiswnul-Muslim

113-Anachopaswa Kusema Muislamu Akimsifu Muislamu Mwenziwe

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[231]

 

قال رسول اللّه صلى اللّه عليه وسلم‏:‏‏ ((إِذَا كَانَ أَحَدُكُمْ مَادِحًا صَاحِبَهُ لَا مَحَالَةَ فَلْيَقُلْ: أَحْسِبُ فُلَانًا وَاللَّهُ حَسِيبُهُ وَلَا أُزَكِّي عَلَى اللَّهِ أَحَدًا أَحْسِبُهُ إِنْ كَانَ يَعْلَمُ ذَاكَ كَذَا وَكَذَا))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Iwapo hakuna budi kwa mtu kumsifu mwenzake basi aseme: 

 

 أَحْسِبُ فُلَانًا وَاللَّهُ حَسِيبُهُ وَلَا أُزَكِّي عَلَى اللَّهِ أَحَدًا أَحْسِبُهُ ...

 

”Namdhania fulani (kwa kadhaa na kadhaa), na Allaah Ndiye Atakayemuhisabu wala simtakasi yeyote kwa Allaah.

 

Lakini namdhania (kadhaa wa kadhaa) ikiwa unajua hivyo (kwamba mtu huyo ana sifa nzuri))[1] 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Bakr (رضي الله عنه) Muslim (4/2296) [3000], Al-Bukhaariy [2662].

 

 

Share

114-Hiswnul-Muslim: Anayopaswa Kusema Muislamu Akisifiwa

Hiswnul-Muslim

114-Anayopaswa Kusema  Muislamu Akisifiwa

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[232]

اللَّهُمَّ لَا تُؤاَخِذْنِي ِبَما يَقُولُونُ، وَاغْفِرْ لِي مَالا يَعْلَمُونَ وَاجْعَلْنِي خَيْراً مِمَّا َيظُنُّونَ

 

Allaahumma laa Tuaakhidhniy bimaa yaquwluwn, waghfirliy maa laa ya’-lamuwn, waj-’alniy khayrn mimma yadhwunnuwn

 

Ee Allaah, Usinichukulie kwa yale wanayoyasema na Nighufurie kwa yale wasiyoyajua,  na Nijaalie bora kuliko wanavyonidhania[1]

 

 

 

[1]Kauli ya Swahaaba - Al-Bukhaariy katika Al-Adab Al-Mufrad (761), na ameisahihisha Isnaad yake Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Al-Adab Al-Mufrad [585]. Na yaliyo katika mabano ni ziada ya Al-Bayhaqiy katika Shu’b Al-Iymaan (4/228) kutoka njia nyingine.

 

 

Share

115-Hiswnul-Muslim: Vipi Alete Talbiyah Aliyehirimia Kwa Hajj Au 'Umrah

Hiswnul-Muslim

115-Vipi Alete Talbiyah Aliyehirimia Kwa Hajj Au 'Umrah

www.alhidaaya.com

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[233]   

لَبَّيْكَ اللَّهُمَّ لَبَّيْكَ، لَبَّيْكَ لا شَرِيكَ لَكَ لَبَّيْكَ، إنَّ الْحَمْدَ، وَالنِّعْمَةَ ،لَكَ وَالْمُلْكُ، لا شَرِيكَ لَكَ

 

Labbayka-Allaahumma Labbayk. Labbayka laa shariyka Laka Labbayk. Innal-Hamda, wan-ni’-matah, Laka wal-Mulk. Laa shariyka Lak.

 

Nimekuitikia (ee Allaah) nimekuitikia (ee Allaah), nimekuitikia (ee Allaah) Huna mshirika nimekuitikia (ee Allaah), hakika Kuhimidiwa na Neema na Ufalme ni Vyako Huna mshirika."[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما)   - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/408) [1549], Muslim (2/481) [1184].

 

 

Share

116-Hiswnul-Muslim: Takbiyrah Atakapofika Katika Hajarul-Aswad

Hiswnul-Muslim .

116-Takbiyrah Atakapofika Katika Hajarul-Aswad 

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[234]

 

 طَافَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم بِالْبَيْتِ عَلى بَعِيرٍ، كُلَّما أَتَى الرُّكْن أَشَارَ إِلَيْهِ بِشَيْءٍ عِنْدَهُ وَكَبَّرَ

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alitufu kuzunguka Al-Ka’bah juu ya ngamia. Kila alipofika katika rukn (Hajarul-Aswad) alikuwa anaashiria kwa kitu na kusema:

 

اللهُ أكْبَر

Allaahu Akbar

 

Allaah ni Mkubwa[1]

 

 

 

[1] Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/476), na ilokusudiwa ‘kitu’ ni fimbo yake. Angalia: Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/472).

 

Hajarul-Aswad: Jiwe jeusi lilioko pembe moja ya Al-Ka’bah

 

 

Share

117-Hiswnul-Muslim: Du’aa Baina Ya Nguzo Ya Al-Yamaaniy na Hajar Al-Aswad

Hiswnul-Muslim

117-Du’aa Baina Ya Nguzo Ya Al-Yamaaniy na Hajar Al-Aswad

 www.alhidaaya.com

 

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [235]

 

Alikuwa  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akisema baina yake:

 

 رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ

Rabb wetu Tupe katika dunia mazuri na katika Aakhirah (pia Tupe) mazuri na Tukinge na adhabu ya Moto[1]

 

 

 


[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin As-Saaib (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (2/179) [1892], Ahmad (3/411), Al-Baghaawiy katika Sharh As-Sunnah (7/128), na Al-Albaaniy (رحمه الله) ameipa daraja ya Hasan katika Swahiyh Abi Daawuwd (1/354). Aayah ni katika Suwrat Al-Baqarah (2:201)

  

 

 

Share

118-Hiswnul-Muslim: Du’aa Unaposimama Katika Mlima Wa Swafaa Na Wa Marwah

Hiswnul-Muslim

118-Du’aa  Unaposimama Katika Mlima Wa Swafaa Na Wa Marwah

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 [236]

Amesema Jaabir (رضي الله عنه)  katika Hadiyth ndefu aliyoielezea Hijah ya  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) kwamba alipokurubia Swafaa alisoma:

 

 إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ ۖ

Hakika Swafaa na Mar-wah ni katika alama za (Dini ya) Allaah[1] 

 

أَبْدَأُ بِمَا بَدَأَ اللهُ بِهِ

Abdau bimaa Badaa-Allaahu bih

 

Ninaanza kwa alichoanza Allaah

 

… Akaanza Swafaa akapanda mpaka akaiona Al-Ka’bah kisha akaielekea na kusema:

 

اللهُ أكْبَرُ، اللهُ أكْبَرُ، اللهُ أكْبَرُ

Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, Allaahu Akbar

 

Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa, Allaah ni Mkubwa.

 

… kisha atasema yafuatayo mara tatu akiomba du’aa (yoyote apendayo) baada ya kila mara:

 

لا إِلهَ إلاَّ  اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْدُ وهُوَ عَلى كُلِّ شَيءٍ قَديرٌ، لا إِلَهَ إلا اللهُ وَحْدَهُ أَنْجَزَ وَعْدَهُ، وَنَصَرَ عَبْدَهُ وَهَزَمَ الأَحْزَابَ وَحْدَهُ

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahu mulku walahul  Hamdu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr. Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu, Anjaza wa’dahu, Wa naswara ’abdahu,  wa hazzamal ahzaaba Wahdah

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, hali ya kuwa Peke Yake, wala hana mshirika. Ni wake ufalme na ni Zake Himdi, Naye juu ya kila kitu ni Muwezahapana mwabudiwa wa haki ila Allaah hali ya kuwa Peke Yake, Ametekeleza ahadi Yake, na Amemnusuru mja Wake, na Amevishinda vikosi Peke Yake.

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alisoma hivi mara tatu na baina yake akiomba du’aa, kisha akafanya alipokuwa Marwah kama alivyofanya alipokuwa Swafaa[2]

 

 

 

[1]Al-Baqarah (2: 158)

 

[2]Muslim (2/888) [1218].

 

 

Share

119-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Siku Ya ‘Arafah

Hiswnul-Muslim

119-Du’aa Ya Siku Ya ‘Arafah

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

[237]

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:

 

خَيْرُ الدُّعَاءِ دُعَاءُ يَوْمِ عَرَفَةَ، وَخَيْرُ مَا قُلْتُ أَنَا وَالنَّبِيُّونَ مِنْ قَبْلِي

Du’aa bora kabisa ni du’aa ya siku ya ’Arafah. Na bora ya niliyoyasema mimi na Manabii kabla yangu ni 

 

لا إِلَهَ إلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَريكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ ولَهُ الحَمْدُ وهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَديرٌ.

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul Mulku walahul Hamdu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr.

 

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah hali ya kuwa Peke Yake hana mshirika. Ni Wake Ufalme na ni Zake Himdi, Naye juu ya kila kitu ni Muweza.[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amru bin Al-‘Aasw (رضي الله عنهما)  - At-Tirmidhiy [3585] na Al-Albaaniy (رحمه الله) ameipa daraja ya Hasan katika Swahiyh At-Tirmidhiy (3/184) na katika Al-Ahaadiyth Asw-Swahiyhah (4/6)

 

 

Share

120-Hiswnul-Muslim: Adkhkaar Katika Mash’arul-Haraam (Muzdalifah)

 Hiswnul-Muslim

120-Adkhkaar Katika Mash’arul-Haraam (Muzdalifah)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[238]

 

حَدِيْث جَابِر بن عَبْدِ الله  (رضي الله عنهما): رَكِبَ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم الْقَصْوَاءَ حَتَّى أَتَى الْمَشْعَرَ الْحَرَامَ فَاسْتَقْبَلَ الْقِبْلَةَ (فَدَعاهُ  وَكَبَّرَهُ، وَهَلَّلَهُ، وَوَحَّدَهُ) فَلَمْ يَزَلْ وَاقِفاً حَتَّى أسْفَرَ جِداً فَدَفَعَ قَبْلَ اَنْ تَطْلُعَ الشَّمْسُ

 

Hadiyth ya Jaabir (رضي الله عنه)    kwamba: ”Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alimpanda Al-Qaswa (jina la ngamia wake) mpaka alipofika Mash’arul Haraam (Muzdalifah), kisha akaelekea Qiblah akamuomba Du’aa kwa Allaah, akaleta takbiyr  (akamtukuza - Allaahu Akbar), akaleta Tahliyl (akampwekesha – laa ilaaha illa Allaah) akamkanusha kuweko mwabudiwa mwengine na akampwekesha. Hakuacha kusimama mpaka kulipopambazuka ndipo alipoondoka kabla ya kutoka jua”[1]

 

 

 

[1]Muslim (2/891) [1218]

 

Faida:  Sehemu hiyo ya Muzdalifah Haajj anapaswa kumdhukuru Allaah (عزّ وجلّ) kwa kila aina ya Adhkaar, kuswali Jamaa’ah, na kuomba Du’aa, kuomba maghfirah, kumshukuru na kumsifu Allaah (عزّ وجلّ)  na kadhaalika.

 

 

Share

121-Hiswnul-Muslim: Takbiyr Katika Kurusha Kijiwe Kwenye Jamarah

Hiswnul-Muslim

121-Takbiyr Katika Kurusha Kijiwe Kwenye Jamarah

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[239]

 

يُكَبِّرُ كُلَّمَا رَمَى بِحَصَاةٍ عِنْدَ الْجِمار الثَّلاث، ثُمَّ يَتَقَدَّم، وَيَقِفُ يَدْعُو مُسْتَقْبِلَ الْقِبْلَةِ، رَافِعًا يَدَيْهِ بَعْدَ الْجَمرْةِ الأُولَى والثَّانِيَة، أمَّا جَمْرَةُ الْعَقَبَة فَيَرْمِيهَا وَيُكَبِّرُ عِنْدَ كُلِّ حَصَاةٍ وَيَنْصَرِفُ وَلا يَقِفُ عِنْدَهَا

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) Alikuwa  kila aliporusha kijiwe katika Jamarah (nguzo) tatu alisema:

 

أَللّهُ أَكْبَرُ

Allaahu Akbar

 

Allaah ni Mkubwa

 

...kisha akisogea na kusimama akielekea Qiblah akiomba du’aa huku akiinua mikono yake. Akifanya hivyo aliporusha vijiwe katika Jamarah ya kwanza na ya pili. Ama Jamarah ya tatu (Al-’Aqabah) alirusha na akamtukuza Allaah (Allaahu Akbar) kwa kila kijiwe kisha alikuwa hasimami bali akimaliza anaondoka”[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنهما)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/583-584), na taz tamshi yake huko. Na Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/581) na ameipokea Muslim pia [1296] Hadiyth ya ibn Mas-‘uwd (رضي الله عنه).

 

 

Share

122-Hiswnul-Muslim: Du’aa Wakati Wa Kustaajabu Na Wa Furaha

Hiswnul-Muslim

122-Du’aa Wakati Wa Kustaajabu Na Wa Furaha

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[240]

 

سُبْحَانَ اللهِ!

Subhaana Allaah!

 

Utakasifu ni wa Allaah[1]   

 

 

 

 [214] 

 

اللهُ أَكْبرُ!

Allaahu Akbar!

 

Allaah ni Mkubwa[2]

 

 

 

[1]Katika riwaaya kadhaa zenye maudhui kadhaa zimetajwa kauli hizo mbili; Subhaana Allaah! Allaahu Akbar! Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (1/210) [155], [390] [283], Muslim [371], [414], [314] na  (4/1857) [332]. Miongoni mwa riwaaya ni Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) :

 

أن النبي صلى الله عليه وسلم لقيه في بعض طريق المدينة وهو جنب فانخنس منه فذهب فاغتسل ثم جاء فقال: ((أين كنت يا أبا هريرة)) قال: كنت جنبا فكرهت أن أجالسك وأنا على غير طهارة. فقال: ((سبحان الله إن المسلم لا ينجس))

Nabiy alikutana naye katika mtaa mmojawapo wa Madiynah naye akiwa katika hali ya janaabah, akamkwepa akaenda kuoga kisha akarudi. Akamuuliza: ((Ulikuwa wapi ee Abaa Hurayrah?)) akajibu: “Nilikuwa katika hali ya janaabah hivyo nilichukia kukaa nawe na hali siko katika twahaarah”. Akasema: ((Subhaanah Allaah! Muislamu si najsi)) Al-Bukhaariy.

 

 

Tanbihi Kuhusu Kosa Lilozoeleka Katika Jamii: Sio kusema: ”Mtume!” kama ilivyozoeleka kwa wengi wanapopatwa na jambo kama kujikwaa au kusikia habari ya mshtuko na kadhaalika. Kumtaja Nabiy (صلى الله عليه وسلم) ni kumpandisha cheo cha Allaah, jambo ambalo yeye mwenyewe Nabiy (صلى الله عليه وسلم) amelikemea kulinganishwa Naye kwa sababu yeye ni kiumbe asiyeweza kumnufaisha mtu wala kumdhuru mtu. Tahadhari Muislamu kwani kumtaja Nabiy (صلى الله عليه وسلم) katika hali kama hizo kunapeleka kuwa ni shirki na ambayo ni dhambi kubwa!

 

 

[2]Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (8/441) [4741], na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (2/103) na (2/235), na Musnad ya Ahmad (5/218)

 

 

 

 

Share

123-Hiswnul-Muslim: Inavyopaswa Kufanya Mtu Akipata Khabari Ya Kufurahisha

Hiswnul-Muslim

123-Inavyopaswa Kufanya Mtu Akipata Khabari Ya Kufurahisha

(Kusujudu Sajdah Moja)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[242]

 

كانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم إذَا أَتَاهُ أَمْرٌ يَسُرُّهُ أَوْ يُسَرُّ بِهِ خَرَّ سَاجِداً شُكْراً للهِ تَبَارَكَ وَتَعَالَى

 

Pindi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) ilipokuwa ikimfikia khabari ya kufurahisha husujudu (Sajdah moja) kwa kumshukuru Allaah Tabaaraka Wa Ta’aalaa[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Bakr (رضي الله عنه)  - Ahlus-Sunan isipokuwa An-Nasaaiy; Abu Daawuwd [2774], At-Tirmidhiy [1578], ibn Maajah [1394], Taz Swahiyh Ibn Maajah (1/233) na Irwaa Al-ghaliyl (2/226)

 

 

 

Share

124-Hiswnul-Muslim: Jambo La Kufanya Na Kuomba Du’aa Anaposikia Maumivu

Hiswnul-Muslim

124-Jambo La Kufanya Na Kuomba Du’aa Anaposikia Maumivu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[243]

 Weka mkono wako juu ya sehemu inayokuuma na kisha useme:

بِسْمِ الله

BismiLLaah (mara 3)

 Kwa jina la Allaah    

Kisha useme mara saba:

  أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ

A’uwdhu biLLaahi wa Qudratihi min sharri maa ajidu wa uhaadhiru

 

Najikinga kwa Allaah na kwa uwezo Wake kutokana na shari ya ninachokisikia na ninachokitahadhari nacho[1]

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Uthmaan bin abi Al-‘Aasw (رضي الله عنه) - Muslim (4/1728) [2202],  Ibn Maajah na wengineo kwa usimulizi tofauti kidogo

Share

125-Hiswnul-Muslim: Du’aa Anayeogopa Kupatwa Na Kijicho

Hiswnul-Muslim

125-Du’aa Anayeogopa Kupatwa Na Kijicho

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[244]

 إِذَا رَأَى أَحَدُكُمْ مِنْ أَخِيهِ أَوْ مِنْ نَفْسِهِ أَوْ مِنْ مَالِهِ مَا يُعْجِبُهُ فَلْيُبَرِّكْهُ فَإِنَّ الْعَيْنَ حَقٌّ

Mmoja wenu akiona kwa ndugu yake au kwake, au mali yake kinachomfurahisha akiombee baraka kwani kijicho ni kweli[1] 

 

 

Useme:

اللّهُـمَّ بارِك عَلَـيه أو اللَّهُمَّ بَارِك عَلَيْكَ

Allaahumma Baarik ’alayh  (au) Allaahumma Baarik ‘alayka

 

Ee Allaah, Mbariki kwa hicho  au Allaah Akubariki kwacho

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Aamir bin Rabiy’ah na Sahl bin Hunayf (رضي الله عنهما)  - Ahmad (4/447), Ibn Maajah [3509], Maalik [1697, 1698] na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Swahiyh Al-Jaami’ (1/212) na angalia: Tahqiyq Zaad Al-Ma’aad ya Al-Arnaawuwtw (4/170)

 

 

Share

126-Hiswnul-Muslim: -Kinachopaswa Kusema Wakati Wa Mfazaiko

Hiswnul-Muslim

126-Kinachopaswa Kusema Wakati Wa Mfazaiko

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

لا إِلهَ إلاَّ اللهُ

Laa ilaaha illa-Allaah

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah[1]

 

 

 

 


[1]Hadiyth ya Zaynab bint Jahsh (رضي الله عنها)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/181) [3346], Muslim (4/2208) [2880] na imekuja kikamilifu:

 

أَنّ النَّبِيَّ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ دَخَلَ عَلَيْهَا فَزِعًا يَقُولُ: ((لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ ، وَيْلٌ لِلْعَرَبِ مِنْ شَرٍّ قَدِ اقْتَرَبَ ، فُتِحَ الْيَوْمَ مِنْ رَدْمِ يَأْجُوجَ وَمَأْجُوجَ مِثْلُ هَذِهِ)) وَحَلَّقَ بِإِصْبَعَيْهِ الإِبْهَامِ وَالَّتِي تَلِيهَا فَقُلْتُ : يَا رَسُولَ اللَّهِ أَنَهْلَكُ وَفِينَا الصَّالِحُونَ ؟ فَقَالَ: ((نَعَم ، إِذَا كَثُرَ الْخَبَثُ))

 

Nabiy alingia chumbani kwake akiwa katika hali ya kufazaika akasema:

لا إِلهَ إلاَّ اللهُ

((Laa ilaaha illa Allaah – hapana mwabudiwa wa hakiisipokuwa Allaah.  Ole kwa Waarabu kutokana na shari iliyokaribia. Leo limefunguka shimo katika boma la kizuzi cha Ya-ajuwj na Ma-ajuwj kama hivi!)) Akafanya kiduara kwa kufunga kidole chake cha gumba na cha shahada. Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah, hivi tutaangamia na hali tumo watu wema?”Akasema: ((Ndio pindi maovu yakizidi)).

 

 

 

 

Share

127-Hiswnul-Muslim: Inavyopaswa Kusema Wakati Wa Kuchinja

Hiswnul-Muslim

127-Inavyopaswa Kusema Wakati Wa Kuchinja

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[246]

 

بِسْمِ اللهِ واللهُ أَكْبَرُ (اللَّهُمَّ مِنْكَ ولَكَ) اللَّهُمَّ تَقَبَّلْ مِنِّي

 

BismiLLaah wa Allaahu Akbar. Allaahumma Minka walaka, Allaahumma Taqabbal minniy

 

Kwa jina la Allaah na Allaah ni Mkubwa (Ee Allaah huyu (mnyama) anatoka Kwako na ni Wako), Ee Allaah nitakabalie[1] 

 

 

 

[1]

 

بِسْمِ اللهِ واللهُ أَكْبَرُ

BismiLLaah Allaahu Akbar

 

ni Hadiyth ya Hadiyth ya Anas bin Maalik (رضي الله عنه) .

اللَّهُمَّ مِنْكَ ولَكَ

Allaahumma minka walaka

 

ni Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنهما)  Muslim (3/1557), Al-Bayhaqiy (9/287) na yaliyo katika mabano imeishia kwa Bayhaqiy (9/287) na wengineo na ibara ya mwisho kutoka katika riwaayah ya Muslim.

 

 

 

 

 

Share

128-Hiswnul-Muslim: Du’aa Ya Kuzuia Vitimbi Vya Mashaytwaan

Hiswnul-Muslim

128-Du’aa Ya Kuzuia Vitimbi Vya Mashaytwaan 

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

أَعُوذُ بكَلِمَاتِ اللهِ التَّامَّاتِ الَّتِي لَا يُجَاوِزُهُنَّ بَرٌّ ولَا فَاجرٌ مِن شّرِّ مَا خَلقَ، وبَرَأَ وذَرَأَ، ومِنْ شَرِّ مَا يَنْزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وِمنْ شَرِّ مَا يَعْرُجُ فيهَا، ومِن شَرِّ مَا ذَرَأَ في الأَرْضِ ومِنْ شَرِّ مَا يَخْرُجُ مِنْهَا، وِمنْ شَرِّ فِتَنِ اللَّيْلِ والنَّهارِ، ومِنْ شَرِّ كُلِّ طارِقٍ إِلَّا طَارِقاً يَطْرُقُ بخَيْرٍ يَا رَحْمَنُ.

 

A’uwdhu bikalimaati-LLaahit-taammaat, allatiy laa yujaawizuhunna barrun wa laa faajirun min sharri maa Khalaqa, wa baraa, wa dharaa, wa min sharri maa yanzilu minas-samaai, wa min sharri maa ya’-ruju fiyhaa, wa min sharri maa dharaa fil ardhwi, wa min sharri maa yakhruju minhaa, wa min sharri fitanil-layli wan-nahaari wamin sharri kulli twaariqin illaa twaariqan yatwruqu bikhayrin yaa Rahmaan

 

Nakinga kwa maneno ya Allaah yaliyokamilika ambayo hayapiti mwema wala muovu, na shari ya Alichokiumba, na Akakitengeneza na kukianzisha.  Na shari ya kinachoteremka kutoka mbinguni na shari ya kinachopanda huko, na shari ya kinachosambaa ardhini na shari ya inayotoka ndani yake, na shari ya fitna za usiku na za mchana na shari ya kila anayegonga usiku ila anayegonga kwa kheri Ee Rahmaan (Mwingi wa Rehma)[1]

 

 

 

 

[1]Hadiyth ya ‘Abdur-Rahmaan bin Khunays (رضي الله عنه) - Ahmad (3/419) kwa Isnaad Swahiyh na ibn As-Sunniy [637] na Isnaad yake ameisahihisha Al-Arnaawuwtw katika takhriyj yake ya At-Twahaawiyah (Uk.133) na angalia: Majmu’ Az-Zawaaid (10/127)

 

 

Share

129-Hiswnul-Muslim: Kuomba Maghfirah Na Kutubia

Hiswnul-Muslim

129-Kuomba Maghfirah Na Kutubia

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

[248]

 

 

قَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((وَاللَّهِ إِنِّي لأَسْتَغْفِرُ اللَّهَ وَأَتُوبُ إِلَيْهِ فِي الْيَوْمِ أَكْثَرَ مِنْ سَبْعِينَ مَرَّةً ))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Naapa kwa Allaa! Hakika mimi ninamuomba maghfirah Allaah na ninatubia Kwake katika kila siku zaidi ya mara sabini))[1]

 

 

 

[249]

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((يآيَّها النَّاسُ تُوبُوا إلى اللَّهِ، فَإنِّي أَتُوبُ إِلَيْهِ مائَةَ مَرَّةٍ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Enyi watu!  Tubieni kwa Allaah, kwani mimi ninatubia kwake kwa siku mara mia))[2]

 

 

[250]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ قَالَ أَسْتَغْفِرُ اللَّهَ الَّذِى لاَ إِلَهَ إِلاَّ هُوَ الْحَىُّ الْقَيُّومُ وَأَتُوبُ إِلَيْهِ؛ غُفِرَ لَهُ وَإِنْ كَانَ فَرَّ مِنَ الزَّحْفِ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayesema:

 

أَسْتَغْفِرُ اللهَ الْعَظِيمَ الَّذِي لَا إِلَهَ إلَّا هُوَ الحَيُّ القَيّوُمُ وأَتُوبُ إِلَيهِ

Astaghfiru-Allaahal-‘Adhwiyma Alladhiy laa ilaaha illaa Huwal-Hayyul-Qayyuwmu wa atuwbu Ilayhi

 

Namuomba maghfirah kwa Allaah Mtukufu Ambaye hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye, Aliyehai daima, Msimamizi wa kila kitu, na ninarejea kutubuia Kwake...

 

Allaah Atamghufuria kama ana makosa hata kama ya kukimbia vitani))[3]

 

 

 

[251]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((أَقْرَبَ مَا يَكُونُ الرَّبُّ مِنَ الْعَبْدِ فِي جَوْفَ اللَّيْلِ الآَخِرِ، فَإِنِ اسْتَطَعْتَ أَنْ تَكُونَ مِمَّنْ يَذْكُرُ اللَّهَ فِي تِلْكَ السَّاعَةِ، فَكُنْ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Wakati ambao mja anakuwa karibu na Rabb wake ni nusu ya mwisho wa usiku. Hivyo ukiweza kuwa miongoni mwa wanaomdhukuru Allaah kwa wakati huo basi kuwa))[4]

 

 

 

[252]

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((أقْرَبُ ما يَكُونُ الْعَبْدُ مِنْ رَبِّهِ وَهُوَ سَاجِدٌ فأكْثِرُوا الدًّعَاءَ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Sehemu ambayo anakuwa mja yuko karibu mno na Rabb wake ni wakati amesujudu, basi zidisheni du’aa wakati huo))[5]

 

 

[253]

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((‏إِنَّهُلَيُغَانُعَلَى قَلْبِي وَإِنِّي لَأَسْتَغْفِرُ اللَّهَ فِي الْيَوْمِ مِائَةَ مَرَّةٍ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Wakati mwingine hutanabahi kufunikwa moyo wangu (kughafilika kumdhukuru Allaah) huwa namuomba Allaah maghfirah mara mia moja kwa siku))[6]

 

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Huraryrah (رضي الله عنه)  - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/101) [6307].

 

[2] Muslim (4/2076)

 

[3]Hadiyth ya ibn Mas-‘uwd (رضي الله عنه)  - Abu Daawuwd (2/85) [1517], At-Tirmidhiy (5/569) [3577], Al-Haakim na ameisahihisha na ameikubali Adh-Dhahaby (1/511) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله). Angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/182), na Jaami’ Al-Uswuwl li-Ahaadiyth Ar-Rasuwl صلى الله عليه وسلم [4/389-390] kwa tahqiyq ya Al-Arnaawuwtw.

 

[4]Hadiyth ya Amruw bin ‘Abasah (رضي الله عنه) - At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy (1/279), Al-Haakim na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/183) na Jaami’ Al-Uswuwl kwa tahqiyq ya Al-Arnaawuwtw (4/144)

 

[5]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  - Muslim (1/350) [482].

 

[6]Hadiyth ya Al-Agharr Al-Muzaniy (رضي الله عنه) - Muslim (4/2075) [2702] Kadhalika angalia: Jaami’ Al-Uswuwl (4/386)

 

 

Share

130-Hiswnul-Muslim: Fadhila Za Tasbiyh, Tahmiyd, Tahliyl Na Takbiyr

Hiswnul-Muslim

130-Fadhila Za Tasbiyh, Tahmiyd, Tahliyl Na Takbiyr

www.alhidaaya.com

 

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

[254]

 

 َقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ قَالَ: سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ فِي يَوْمٍ مائَةَ مَرَّةٍ، حُطَّتْ خَطَاياهُ وَلَوْ كانَتْ مِثْلَ زَبَدِ الْبَحْرِ))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Mwenye kusema:

سُبْحَانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ

 

Subhaana-Allaahi wa Bihamdihi

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi ni Zake

 

mara mia kwa siku, atafutiwa madhambi yake hata kama yalikuwa mfano wa povu la bahari))[1]

 

 

 

[255]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((مَنْ قَال: لا إِلهَ إِلَّا اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْد، وهُوَ عَلى كُلِّ شَيءٍ قَديرٌ، عَشَرَ مَرَّاتْ كَانَ كَمَنْ أَعْتَقَ أَرْبَعَةَ أَنْفُسٍ مِنْ وَلَدِ إسْمَاعِيلَ))

 

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakayesema:

 

لا إِلهَ إِلَّا اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ المُلْكُ وَلَهُ الحَمْد، وهُوَ عَلى كُلِّ شَيءٍ قَديرٌ

 

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah  peke Yake, hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza.

 

… mara kumi, ni kama (thawabu za mtu) aliyewacha huru nafsi nne katika wana wa Ismaa’iyl))[2]

 

 

 

[256]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم:  كَلِمَتَانِ خَفِيفَتَانِ عَلى اللِّسَانِ، ثَقِيلَتَانِ فِي الْمِيزَانِ، حَبِيبَتانِ إلى الرَّحْمنِ  سُبْحانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ سُبْحَانَ اللهِ العَظِيمِ

 

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Maneno mawili ni mepesi mno juu ya ulimi, mazito mno katika mizani, yanapendeza mno mbele ya Rahmani (Mwingi wa Kurehemu) nayo ni:

سُبْحانَ اللهِ وَبِحَمْدِهِ سُبْحَانَ اللهِ العَظِيمِ

Subhaana Allaahi Wabihamdihi Subhaana Allaahil-’Adhwiym

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi ni Zake, Utakasifu ni wa Allaah Aliye Mtukufu[3]

 

 

 

[257]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((لأَنْ أَقُولَ: سُبْحَانَ اللهِ، والحَمْدُ للهِ، وَ لاَ إَلَهَ إلاَّ اللهُ، واللهُ أَكْبَرُ، أَحَبُّ إَلَيَّ مِمَّا طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Kusema kwangu:

 

سُبْحَانَ اللهِ، والحَمْدُ للهِ، وَ لاَ إِلَهَ إلاَّ اللهُ واللهُ أَكْبَرُ

Subhaana Allaah, WalhamduliLLaah, wa laa ilaaha illa Allaah, wa Allaahu Akbar

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi Anastahiki Allaah, na hapana mwabudiwa wa haki  ila ni Allaah, na Allaah ni Mkubwa.

 

… ni bora kwangu kuliko kila kilichoangaziwa na jua))[4]

 

 

 

[258]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((أَيَعْجِزُ أَحَدُكُمْ أَنْ يَكْسِبَ كُلَّ يَوْمٍ أَلْفَ حَسَنَةٍ؟)) فَسَأَلَهُ سَائِلٌ مِنْ جُلَسَائِهِ: "كَيْفَ يَكْسِبُ أَحَدُنَا أَلْفَ حَسَنَةٍ؟" قَالَ: ((يُسَبِّحُ مِائَةَ تَسْبِيحَةٍ فَيُكْتَبُ لَهُ أَلْفُ حَسَنَةٍ أَوْ يُحَطُّ عَنْهُ أَلْفُ خَطِيئَةٍ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Hivi anashindwa mmoja wenu kuchuma kila siku thawabu elfu?)) Mtu mmoja miongoni mwa waliokaa akamuuliza: ”Atachuma vipi mmoja wetu thawabu elfu?” Akamjibu: ((Aseme:

 

سُبْحَانَ اللهِ

Subhaana-Allaah

 

Utakasifu ni wa Allaah

 

… mara mia moja, basi ataandikiwa thawabu elfu moja, au atafutiwa madhambi elfu moja))[5]

 

 

 

[259]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((مَنْ قَال: سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ، غُرِسَتْ لَهُ نَخْلَةً فِي الْجَنَّةِ))

Na  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Atakaesema:

سُبْحَانَ اللهِ العَظِيمِ وبِحَمْدِهِ

 

Subhaana-Allaahil-’Adhwiym wa bihamdihi

 

Utakasifu ni wa Allaah Aliye Mtukufu na Himdi ni Zake.

 

 

… hupandiwa mtende katika Jannah))[6]

 

 

 

[260]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((يَا عَبْدَ اللَّهِ بْنَ قَيْسٍ، أَلا أَدُلُّكَ عَلَى كَلِمَةٍ مِنْ كَنْزِ الْجَنَّةِ؟)) قَالَ : قُلْتُ: "بَلَى يَا رَسُولُ اللهقَال: (( لا حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلا بِاللَّهِ ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Ee ’Abdallaahi bin Qays! Hivi nikujulishe hazina miongoni mwa hazina za Jannah?))  Nikamwambia: ”Ndio Ee Rasuli wa Allaah”. Akasema: ((Sema:

لاَ حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلاَّ باللهِ

Laa hawla walaa quwwata illaa BiLLaah

 

Hakuna uwezo wala nguvu ila za Allaah[7]

 

 

 

[261]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((أَحًبُّ الْكَلامِ إِلَى اللَّهِ أَرْبَعٌ: سُبْحَانَ اللَّهِ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ، وَلا إِلَهَ إِلا اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ، لا يَضُرُّكَ بِأَيِّهِنَّ بَدَأْتَ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Bora ya maneno kwa Allaah ni manne:

سُبْحَانَ اللهِ، والْحَمْدُ للهِ، وَلاَ إِلَهَ إَلاَّ اللهُ واللهُ أَكْبَرُ  

 

Subhaana-Allaah, walhamduliLLaah, wa laa ilaaha illa Allaah, wa Allaahu Akbar, 

 

Utakasifu ni waAllaah na Himdi Anastahiki Allaah, na hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na Allaah ni Mkubwa.

 

… si vibaya kuanza kwa lolote katika haya))[8]

 

 

 

[262]

 

 

جَاءَ أَعْرَابِيٌّ إِلَى رَسُولِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: "يَا رَسُولَ اللَّهِ عَلِّمْنِي كَلامًا أَقُولُهُ" فَقَالَ:  ((قُلْ: لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ كَبِيرًا، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ كَثِيرًا، وَسُبْحَانَ اللَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ، وَلا حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلا بِاللَّهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ)) قَالَ:" هَؤُلاءِ لِرَبِّي فَمَا لِي؟" قَالَ:   ((قُلِ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَارْزُقْنِي))

Alikuja mbedui mmoja kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akamwambia: ”Nifundishe maneno niyaseme: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akamwambia: ((Sema:

 

لاَ إِلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ، اللهُ أَكْبَرُ كَبيراَ والْحَمْدُ للهِ كَثيراً، سُبْحَانَ اللهِ رَبِّ العَالَمينَ، لاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ باللهِ العَزيزِ الْحَكِيمِ

Laa ilaaha illa Allaah Wahdau laa shariyka Lah. Allaahu Akbar Kabiyraa, WalhamduliLLaahi kathiyraa, Subhaana-Allaahi Rabbil ’aalamiyn. Laa hawla wa laa quwwata illaa biLLaahil ’Aziyzil-Hakiym

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah hali ya kuwa Peke Yake Hana mshirika. Allaah ni Mkubwa tena sana, na Himdi Anastahiki Allaah tena nyingi sana. Utakasiuf ni wa Allaah Rabb wa walimwengu. Hapana uwezo wala nguvu ila ni za Allaah, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika daima, Mwenye hikmah wa yote daima.

 

… yule mbedui kisha akasem: ”Haya ni ya Allaah ni yapi yangu?”  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akamwambia: ((Sema:

اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وارْحَمْنِي، واهْدِنِي، وارْزُقْنِي

Allaahummagh-fir-liy  warhamniy, wahdiniy, warzuqniy

 

Ee Allaah Nighufurie, na Nirehemu, na Niongoze, na Niruzuku[9]

 

 

 

[263]

 

كَانَ الرَّجُلُ إِذَا أَسْلَمَ، عَلَّمَهُ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الصَّلَاةَ، ثُمَّ أَمَرَهُ أَنْ يَدْعُوَ بِهَؤُلَاءِ الْكَلِمَاتِ:  ((اللهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَعَافِنِي وَارْزُقْنِي))

Pindi mtu anaposilimu, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) alikuwa akimfundisha kuswali kisha anamuamrisha kuomba kwa matamshi haya:

اللَّهُمَّ اغْفِرِ لِي، وارْحَمْنِي، واهْدِنِي، وعَافِنِي وارْزُقْنِي

Allaahummagh-fir-liy warhamniy, wahdiniy, wa ’aafiniy, warzuqniy

 

Ee Allaah Nighufurie, na Nirehemu, na Niongoze, na Nipe afya njema  na Niruzuku[10]

 

 

 

 [264]

 

وَقَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((إِنَّ أَفْضَلَ الدُّعَاءِ: الْحَمْدُ لِلَّه، وَأَفْضَلُ الذِّكْرِ: لاَ إلَهَ إِلاَّ الله))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema:  ((Bora ya du’aa ni mtu kusema:

الْحَمْدُ للهِ

AlhamduliLlaah

 

Himdi  ni za Allaah

 

na dhikri bora ni:

لاَ إِلَه إِلاَّ اللهُ

Laa ilaaha illa-Allaah

 

Hapana mwabudiwa wa haki ila ni Allaah[11]

 

 

 

[265]

 

 ((الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ: سُبْحَانَ الْلَّهِ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ، وَلَا إِلَهَ إِلَّا الْلَّهُ، وَالْلَّهُ أَكْبَرُ  وَ لاَ حَوٍلَ وَلا قُوَّةَ إِلاَّ باللهِ))

 

 Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Mema yanayobakia daima ni:

سُبْحَانَ اللهِ، والْحَمْدُ للهِ،لاَ إِلَهَ إَلاَّ اللهُ واللهُ أَكْبَرُ  وَلاَ حَوٍلَ وَلا قُوَّةَ إِلاَّ باللهِ)

 

Subhaana-Allaah, walhamduliLLaah, wa laa ilaaha illa-Allaah, wa Allaahu Akbar, walaa hawla walaa quwwata illa biLLaah, 

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi Anastahiki Allaah, na hapana mwabudiwa a wa haki ila Allaah, na Allaah ni Mkubwa, hapana uwezo wala nguvu isipokuwa ni za Allaah[12]

 

 

[1]Hadiyth ya Abu Huraryah (رضي الله عنه) - Al-Bukhaariy (7/168) [6405], Muslim (4/2071) [2691], na angalia: fadhila zake nyingine ((Atakayesema mara mia asubuhi na jioni…)) katika ‘Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni’ Du’aa Namba 91. 

  

[2]Hadiyth ya Abu Ayyuwb Al-Answaariyy (رضي الله عنه) -  Al-Bukhaariy (7/67), Muslim (4/2071) kwa tamshi yake na angalia fadhila zake  nyingine: “Atakayesema mara mia kwa siku, mara kumi, mara moja”  katika ‘Nyiradi Za Asubuhi Na Jioni’ Du’aa  [92, 93]   

 

 

[3]Hadiyth ya Abu Hurayrah  (رضي الله عنه)  - Al-Bukhaariy (7/168) [3462], Muslim (4/2072) [2694]

 

[4]Hadiyth ya Abu Hurayrah (رضي الله عنه) - Muslim (4/2072) [2695].

 

[5]Hadiyth ya Sa’iyd bin Abi Waqqaasw (رضي الله عنه) - Muslim (4/2073) [2140]

 

[6]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنهما)   At-Tirmidhiy (5/511) [3464, 3465], Al-Haakim (1/501), na ameisahihisha na ameikubali Adh-Dhahaby na angalia: Swahiyh Al-Jaami’ (5/531), na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/160)

 

[7]Hadiyth ya Abu Muwsaa Al-Ash’ariyy (رضي الله عنه)  (ambaye ndiye ‘Abdullaah bin Qays) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/213) [4205] , Muslim (4/2076) [2704].

 

[8]Hadiyth ya Samrah bin Jundub (رضي الله عنه) Muslim (3/1685) [[2137]

 

[9]Hadiyth ya Sa’ad bin Abi Waqqaasw (رضي الله عنه) Muslim (4/2072) [2696] na Abu Daawuwd amezidisha:  “Alipogeuka Mbedui, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) akasema:

((لَقَدْ مَلأ يَديهِ مِنَ الْخَيْر))

((Hakika mikono yake imejaa kheri)) (1/220) [832].

 

[10]Hadiyth ya Twaariq bin Ashiym Al-Ashja’iyy (رضي الله عنه) Muslim (4/2073) [2697], na katika riwaayah nyingine:

 

((فَإنَّ هَؤلآءِ تَجْمَعُ لَكَ دُنْيَاكَ وَآخِرَتك))

 ((Kwani hayo yanakukusanyia Dunia yako na Akhera yako))

 

[11]Hadiyth ya Jaabir bin ‘Abdillaah (رضي الله عنه) At-Tirmidhiy (5/462) [3383], ibn Maajah (2/1249) [3800], Al-Haakim (1/503) na ameisahihisha na ameiwafiki Adh-Dhahaby na angalia: Swahiyh Al-Jaami (1/362) [1104].

 

[12]Hadiyth ya Abu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) Ahmad (3/75) [513] kwa utaratibu wa Ahmad Shaakir na Isnaad yake ni Swahiyh. Na angalia: Majma’ Az-Zawaaid (1/297), na ibn Hajar ameipa nguvu katika Buluwgh Al-Maraam kutoka riwaayah ya Abu Sa’iyd kwa An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm Wal-Layl’ [484] na amesema:  Ameisahihisha Al-Haakim (1/512) na Ibn Hibbaan [840].

 

Tanbihi:  Imaam Al-Albaaniy amedhoofisha katika Dhwa’iyf Al-Jaami [828] kwa kuweko tamshi la:

 

لا حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلاَّ باللهِ

Akaisahihisha katika Swahiyh At-Targhiyb [366] yenye kutaja:

 

لا إلهَ إلَّا اللهُ ، و سُبحانَ اللهِ ، و اللهُ أكبرُ ، و لا حَولَ و لا قُوَّةَ إلَّا بالله

Na pia iliyothibiti nyengineyo ni Hadiyth ifuatayo:

 

((خُذُوا جُنَّتَكُمْ))  قُلْنَا يَا رَسُولَ اللهِ: مِنْ عَدُوٍّ قَدْ حَضَرَ؟ قَالَ: ((لاَ،جُنَّتَكُمْ مِنَ النَّارِ، قُولُوا : سُبْحَانَ اللهِ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ  وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ، فَإِنَّهَا يَأْتِينَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ مُنْجِيَاتٍ، وَمُقَدَّمَاتٍ ، وَهُنَّ الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jikingeni!)) Tukasema: Ee Rasuli wa Allaah; Je adui ameshatufikia? Akasema: ((Hapana bali kinga yenu kutokana na moto. Semeni:

 سُبْحَانَ اللهِ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ  وَلاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ

Subhaana-Allaah, wal-HamduliLLaah, wa laa ilaaha illa-Allaah, wa Allaahu Akbar

 

Utakasifu ni wa Allaah na Himdi Anastahiki Allaah, na  hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah, na Allaah ni Mkubwa.

 

Kwani yatakuja zitakuja hizo (Adhkaar) Siku ya Qiyaamah kama ni kinga na kitangulizi, nazo ni Mema yanayobakia daima)) [An-Nasaaiy fiy Sunan Al-Kubraa (10684), Atw-Twabaraniy fiy Al-Mu’jim Al-Awsatw (4027), na ameisahihisha Al-Abaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (3214), Swahiyh At-Targhiyb (1567), na kwa Riwaayah nyenginezo amesahihisha katika Swahiyh Al-Jaami’ (3264), (6/482)]  

 

 

Share

131-Hiswnul-Muslim: Vipi Alikuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Akimsabihi Allaah

Hiswnul-Muslim

131-Vipi Alikuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  Akimsabihi Allaah

www.alhidaaya.com

 

 

 Bonyeza Hapa Usikilize

 

[266]

 

عَنْ عَبْدُ اللَّه بِن عَمْرٍو (رضي الله عنهما) قَال: "رَأَيْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم يَعْقِدُ التَّسْبِيحَ بِيَمِينِه"

 

Imepokewatoka kwa ’Abdullaah Bin ’Amru (رضي الله عنهما)  amesema: ”Nimemuona Nabiy  (صلى الله عليه وسلم) anahesabu kumsabihi Allaah kwa mkono wake wa kulia[1]

 

 

 

 

 

 

[1]Abu Daawud kwa tamshi yake (2/81) [1502] , At-Tirmidhiy (5/521) [3486] na taz Swahiyhh Al-Jaami’ (4/271) [4865]

 

 

Share

132-Hiswnul-Muslim: Katika Mambo Ya Kheri Na Adabu Kwa Jumla (Na Kinga Ya Watoto Dhidi Ya Mashaytwaan)

Hiswnul-Muslim

132-Katika Mambo Ya Kheri Na Adabu Kwa Jumla

(Na Kinga Ya Watoto Dhidi Ya Mashaytwaan)

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

[267]

 

قَالَ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم: ((إِذَا كَانَ جُنْحُ اللَّيْلِ أَوْ أَمْسَيْتُمْ فَكُفُّوا صِبْيَانَكُمْ، فَإِنَّ الشّيَاطِيَ تَنْتَشِرُ يَنْتَشِرُ حِينَئِذٍ، فَإِذَا ذَهَبَ سَاعَةٌ مِنْ اللَّيْلِ فَخَلُّوهُمْ، وَأَغْلِقُوا الْأَبْوَابَ وَاذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ فَإِنَّ الشَّيْطَانَ لَا يَفْتَحُ بَابًا مُغْلَقًا، وَأَوْكُوا قِرَبَكُمْ وَاذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ، وَخَمِّرُوا آنِيَتَكُمْ وَاذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ وَلَوْ أَنْ تَعْرضُوا عَلَيْهَا شَيْئًا، وَأَطْفِئُوا مَصَابِيحَكُم))

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وسلم) amesema: ((Ikiingia jioni [yaani jua linapokuchwa wakati wa Magharibi] wazuieni watoto wenu kutoka toka nje kwani mashaytwaan wanatawanyika nyakati hizo. Ukishapita wakati waacheni.  Na fungeni milango yenu na mtajeni Allaah mnapoifunga [mseme: BismiLLaah], kwani shaytwaan hafungui mlango uliofungwa.  Na fungeni viriba vyenu vya maji, na mtajeni Allaah [mseme: BismiLLaah]. Na funikeni vyombo vyenu na mtajeni Allaah [semeni: BismiLLaah]  (funikeni) hata kama ni kwa kuwekea kitu ju.  Na zimeni taa zenu[1]

 

وَصَلَّى اللهَ وَسَلَّمَ وَبَارَكَ عَلى نَبِيِّنَا مُحَمَّدٍ وَعَلى آلِهِ وَأَصْحَابِهِ أَجْمَعِينَ

Wa swalla Allaahu aa sallama wa Baaraka ‘alaa Nabiyyinaa Muhammadi wa ‘alaa aalihi wa aswhaabihi ajma’iyna

 

 

 

 

 

[1]  Al-Bukhaariy pamoja na al-Fat-h (10/88), Muslim (3/1595)

 

 

Share