Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!- إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

 

 

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

Share

00-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! Utangulizi

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

 00-Utangulizi

 

Alhidaaya.com

 

 

بِسْمِ الله الرَّحْمنِ الرَّحِيم

 

الْحمْدُ لِلَّه وَالصَّلاةُ وَالسِّلامُ عَلى خَاتم الأنْبِيَاء وَالْمُرْسَلِين، الْمَبْعُوثُ رَحْمَةً لِلْعَالَمِين، مُحَمَّد وَعَلى آلِه وَأصْحابِه أجْمَعِين وَمَنْ تَبِعَهُمْ بِإِحْسَانٍ إِلَى يَوْمِ الدِّينِ.

Himdi Anastahiki Allaah, Swalaah na salaam zimfikie Nabiy na Rasuli wa mwisho, aliyetumwa awe rahmah kwa walimwengu, Muhammad, pamoja na ahli zake na Maswahaba zake wote, na wanaowafuata kwa ihsaan mpaka Siku ya Malipo.

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ ﴿١٣﴾

hakika shirki ni dhulma kubwa mno [Luqmaan: 13]

 

 

Kinyume ya shirki ni Tawhiyd ambayo ni kumpwekesha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika Rubuwbiyyah (Uola) Uluwhiyyah (‘ibaadah) Yake na katika Asmaa na Swifaat (Majina na Sifa nzuri) Zake.  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴿٦٥﴾

Kwa yakini umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: “Ukifanya shirki bila shaka zitaporomoka ‘amali zako na bila shaka utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.”

 

بَلِ اللَّـهَ فَاعْبُدْ وَكُن مِّنَ الشَّاكِرِينَ﴿٦٦﴾

Bali Allaah Pekee mwabudu, na uwe miongoni mwa wenye kushukuru. [Az-Zumar: 65-66]

 

 

Waislamu wengi wako katika hali ya kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa); wengine wakiwa wanatambua hatari zake, na wengine wakiwa hawatambui kuwa wanamshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), kwa sababu baadhi ya ‘amali zinazotendwa zinaonekana kuwa kama ni nzuri na hali zimeingia shirki ndani yake.

 

Imaam Muhammad bin ‘Abdil-Al-Wahhaab amesema katika Al-Qawaaid Al-Arba’: “Kwamba washirikina wa zama zetu ni waovu zaidi (shirki zao ni kubwa zaidi) kuliko washirikina wa awali, kwa sababu, wa awali walimshirikisha Allaah katika raha, lakini wakizitakasa ‘Ibaadah zao wakati wa shida. Ama washirikina wa sasa, shirki zao ni wakati wote, wakiwa katika raha au katika shida … na dalili ni kauli Yake Ta’aalaa:

 

فَإِذَا رَكِبُوا فِي الْفُلْكِ دَعَوُا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ فَلَمَّا نَجَّاهُمْ إِلَى الْبَرِّ إِذَا هُمْ يُشْرِكُونَ ﴿٦٥﴾

Wanapopanda merikebu humwomba Allaah wakiwa wenye kumtakasia Yeye Dini, lakini Anapowaokoa katika nchi kavu, tahamaki hao wanamshirikisha. [Al-‘Ankabuwt: 65]

 

Kwa hiyo, kuna umuhimu mkubwa wa Waislamu kujifunza somo hili ili kujitahadharisha na hatari zake ili waweze kufunga milango na njia zote kubwa na ndogo za shirki. Makala hizi In Shaa Allaah zitaweza kutambulisha na kubainisha matendo mengi yanayomshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na namna ya kuyaepuka, ili Muislamu abakie katika amri ya Muumba wake Ambaye Ameamrisha kuabudiwa Yeye Pekee bila ya kumshirikisha. Kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni katika dhambi kubwa mno kama alivyobainisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ سَأَلْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم: أَيُّ اَلذَّنْبِ أَعْظَمُ؟ قَالَ: ((أَنْ تَجْعَلَ لِلَّهِ نِدًّا, وَهُوَ خَلَقَكَ))‏  

Imepokelewa kutoka kwa ibn Mas-‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: “Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): Je, dhambi ipi kubwa mno?” Akasema: ((Kumfanyia Allaah mlinganishi (wa kumshirikisha) na hali Yeye Amekuumba)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Nukta chache zifuatazo ni mukhtasari wa hatari za kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

1. Shirki inaharibu ‘amali za mtu. Dhambi hii kubwa walitahadharishwa Rasuli wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa ukali mno pale Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaposema:

 

وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٨٨﴾

Na kama wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda. [Al-An’aam: 88]

 

 

2. Shirki ni dhambi pekee ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Haisamehe isipokuwa tu mtu akirudi kutubia Kwake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴿١١٦﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali. [An-Nisaa: 116]

 

 

3. Shirki inamtoa mtu nje ya Uislamu!

 

Imeelezwa shirki kuwa ni miongoni mwa matendo yanayomtoa mtu nje ya Uislamu, kama ilivyo katika Nawaaqidhw Al-Islaam cha Imaam Muhammad ibn Al-Wahhaab (Rahimahu-Allaah).

 

Na miongoni mwa mengi wanayotenda baadhi ya Waislamu ni kumwendea kahini anayetabiri mambo ya ghayb; elimu ambayo hakuna aijuae isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Hatari ya tendo hili ni kama alivyotahadharisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):   

 

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) عَنِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((مَنْ أَتَى كَاهِنًا، فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ

Imepokewa toka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayemkaribia kahini na kuamini anayoyasema basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم))  [Abu Daawuwd]

 

 

4-Mwenye kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni mwenye hatima mbaya mno ya makazi ya Moto. Ametahadharisha hilo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾

Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.” [Al-Maaidah: 72]

 

Tunataraji tawfiyq ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) makala hizi ziwazidishie elimu yenye manufaa Waislamu kuhusiana na somo hili na Atuepushe sote kumshirikisha Yeye Subhaanahu wa Ta’aalaa. 

 

 

 

Share

01-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Maana Ya Dhulma Na Shirki

   

 إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

01- Maana Ya Dhulma Na Shirki

 

Alhidaaya.com

 

Maana ya dhulma ni kuweka kitu mahali pasipo pake. Hivyo anayeabudu au kumwomba asiyekuwa Allaah atakuwa ameilekeza ‘ibaadah yake kwa asiyestahiki.

 

Maana ya shirki ni kumwekea Allaah mshirika katika Ar-Rubuwbiyyah (Uola) Wake au Uluwhiyyah (‘Ibaadah) Yake au Asmaa na Swifaat Zake.

 

عَنْ عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: لَمَّا نَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ، شَقَّ ذَلِكَ عَلَى النَّاس وَقَالُوا: أَيُّنَا لَمْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ؟! فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إنَّه لَيْسَ كَمَا تَعنُون! ألَمْ تَسْمَعوا ما قال الْعبْد الصَّالح؟  يَا بُنَيَّ لَا تُشْرِكْ بِاللَّـهِ ۖ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌإنَّما هُو الشِّرْك))

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Ilipoteremshwa Aayah hii: Wale walioamini na hawakuchanganya iymaan zao na dhulma; [An-An’aam: 82] Iliwatatiza watu  wakasema: “Nani katika sisi hajadhulumu nafsi yake?” Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Si kama vile mnavyomaanisha! Hamsikii pale mja mwema aliposema:  “Ee mwanangu! Usimshirikishe Allaah, hakika shirki ni dhulma kubwa mno!” [Luqmaan: 13] Hakika hiyo ni shirk.)) [Ahmad na riwaayah zinazofanana katika Al-Bukhaariy na wengineo]

 

 Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema: “Hakika kila Alichokikataza Allaah kinarejea katika dhulma na kila Alichokiamrisha kinarejea katika uadilifu, na ndio maana Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Anasema:

لَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلَنَا بِالْبَيِّنَاتِ وَأَنزَلْنَا مَعَهُمُ الْكِتَابَ وَالْمِيزَانَ لِيَقُومَ النَّاسُ بِالْقِسْطِ

Kwa yakini Tuliwapeleka Rusuli Wetu kwa hoja bayana, na Tukateremsha pamoja nao Kitabu na Miyzaan (shariy’ah) ili watu wasimamie kwa uadilifu. [Al-Hadiyd: 25]

 

Akajulisha kwamba Ametuma Rasuli na Ameteremsha Kitabu na shariy’ah kwa ajili ya watu wasimamie uadilifu”  [Majmuw’ Al-Fataawa li Ibn Taymiyyah (18/157)]

 

Kumshirikisha Allaah aghlabu ni katika Uluwhiyyah Yake kwa kumwomba asiyekuwa Allaah, au kuelekeza aina yoyote ya ‘ibaadah kwa asiyekuwa Allaah kama kuchinja, kuweka nadhiri, kuapa, kukhofu na kutaraji, kutawakkal, istighaathah (kuomba uokozi au kinga) au kujikurubisha na yeyote au chochote kile kisichokuwa Allaah.

 

Vile vile kumlinganisha Allaah na viumbe. Anasema Allaah:

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اعْبُدُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿٢١﴾

Enyi watu! Mwabuduni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni na wale wa kabla yenu mpate kuwa na taqwa.

 

الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ فِرَاشًا وَالسَّمَاءَ بِنَاءً وَأَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجَ بِهِ مِنَ الثَّمَرَاتِ رِزْقًا لَّكُمْ ۖ فَلَا تَجْعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿٢٢﴾

Ambaye Amewafanyieni ardhi kuwa ni tandiko na mbingu kuwa ni paa, na Akateremsha kutoka mbinguni maji, Akawatolea kwayo matunda kuwa ni riziki zenu. Basi msimfanyie Allaah waliolingana naye na hali ya kuwa nyinyi mnajua. [Al-Baqarah: 21-22]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 وَجَعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا لِّيُضِلُّوا عَن سَبِيلِهِ

Na wakamfanyia Allaah walinganishi ili wapoteze (watu) na njia Yake. [Ibraahiym: 30]

 

Na Anasema pia (سبحانه وتعالى):

قُلْ أَئِنَّكُمْ لَتَكْفُرُونَ بِالَّذِي خَلَقَ الْأَرْضَ فِي يَوْمَيْنِ وَتَجْعَلُونَ لَهُ أَندَادًا ۚ ذَٰلِكَ رَبُّ الْعَالَمِينَ﴿٩﴾

Sema: “Je, hivi nyinyi mnamkufuru Yule Aliyeumba ardhi kwa siku mbili, na mnamfanyia waliolingana Naye? Huyo Ndiye Rabb wa walimwengu.” [Fusw-Swilat: 9]

 

 

Share

02-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Shirki Ni Aina mbili Na Tofauti Zake

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

02- Shirki Ni Aina mbili Na Tofauti Zake

Alhidaaya.com

 

 

Shirki ni aina mbili; shirki kubwa na shirki ndogo.

 

1-Shirki Kubwa inamtoa mtu nje ya Uislamu, ‘amali zake zote zinaporomoka, mwenye kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa shirki kubwa huwa ni halali damu yake, na mali yake na ni mwenye kudumu Motoni ikiwa hatotubia kabla ya kufariki kwake. Na dhambi ya shirki kubwa ni dhambi pekee ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Hamsamehi mja atakapokufa bila kutubia. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ 

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. [An-Nisaa: 48]

 

Shirki kubwa ni kuelekeza ‘ibaadah na kuomba du’aa kwa asiyekuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Washirikina wao ndio kabisa hawamwabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) japokuwa huenda wengine wanaamini kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Muumba kama walivyoamini hivyo washirikina wa Makkah. Shirki yao imethibiti katika Uluwhiyyah (‘ibaadah) pale walipoabudu masanamu wakidai kuwa yanawakurubisha kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama ilivyotajwa katika Qur-aan:

 

وَالَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ

na wale waliojichukulia badala Yake walinzi (wakisema): “Hatuwaabudu isipokuwa ili wapate kutukurubisha kwa Allaah tumkaribie”  [Az-Zumar: 3]

 

Wengine ndio wamemshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na viumbe Vyake wakawafanya ni ilaah (waabudiwa) wao. Juu ya hayo, Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anamghufuria yeyote yule anayerudi kutubia Kwake baada ya kufuru na shirki kubwa kama hizo.  Dalili ni kauli zifuatazo katika Qur-aan:

 

لَقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ ۖ وَقَالَ الْمَسِيحُ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ اعْبُدُوا اللَّـهَ رَبِّي وَرَبَّكُمْ ۖ إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾

Kwa yakini wamekufuru wale waliosema: “Hakika Allaah ni Al-Masiyh mwana wa Maryam.” Na Al-Masiyh alisema: “Enyi wana wa Israaiyl! Mwabuduni Allaah, Rabb wangu na Rabb wenu. Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.”

 

لَّقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ ثَالِثُ ثَلَاثَةٍ ۘ وَمَا مِنْ إِلَـٰهٍ إِلَّا إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۚ وَإِن لَّمْ يَنتَهُوا عَمَّا يَقُولُونَ لَيَمَسَّنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٣﴾

Kwa yakini wamekufuru wale waliosema: “Hakika Allaah ni watatu wa utatu.” Na hali hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Ilaah Mmoja Pekee. Na wasipoacha yale wanayoyasema, bila ya shaka itawagusa wale waliokufuru miongoni mwao adhabu iumizayo.

 

أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى اللَّـهِ وَيَسْتَغْفِرُونَهُ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٧٤﴾

Je, hawatubii kwa Allaah na wakamwomba maghfirah? Na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Maaidah: 72-74]

 

2-Shirki Ndogo: Hii inajulikana kama riyaa, nayo ni kufanya ‘ibaadah au kutenda amali lakini kwa niyyah ya kujionyesh a kwa watu. Shirki hii haimtoi mtu nje ya Uislamu bali ‘amali zake huporomoka na, ni mwenye kuadhibiwa Motoni kwa kadiri ya madhambi yake.

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amewahofia Swahaabah aina hii ya shirki:

 

عن مَحْمُودِ بْنِ لَبِيدٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ إنَّ أخوَفَ ما أخافُ عليكم الشِّركُ الأصغرُ، قالوا: وما الشِّركُ الأصغر؟ قال: الرِّياءُ، يقولُ اللهُ عزَّ وجلَّ لأصحابِ ذلك يومَ القيامةِ إذا جازَى النَّاسَ اذهبوا إلى الَّذين كنتم تُرائون في الدُّنيا فانظُروا هل تجِدون عندهم جزاءً؟"  - صححه الألباني في السلسلة الصحيحة(951 )

Imepokelewa kutoka kwa Mahmuwd bin Labiyd ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Hakika ninachokihofia kwenu zaidi ni shirki ndogo. Wakasema: Ni ipi hiyo shirki ndogo? Akasema: Ar-Riyaa. Allaah ('Azza wa Jalla) Atawaambia watu wa Siku ya Qiyaamah pale watakapolipwa watu jazaa: Nendeni kwa wale mliokuwa mkijionyesha kwa ‘amali zenu duniani kisha tazameni je, mtakuta kwao jazaa? [Ahmad na ameisahihisha Shaykh Al-Albaaniy katika Silsilat Al-Hadiyth Asw-Swahiyhah (951)]

 

 

Share

03-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Shirki Ndogo - Riyaa (Kujionyesha)

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

03- Shirki Ndogo : Riyaa (Kujionyesha)

 

www.alhidaaya.com

 

 

‘Amali zote zinahitaji kutangulizwa na niyyah safi. Hadiyth mashuhuri ambayo ‘Ulamaa wamesema kuhusu Hadiyth hii kwamba ni nusu ya ya Dini kama alivyosema Imaam Abu Daawuwd, kwani Dini inakusanya vilivyo dhahiri kama vitendo na visivyo dhahiri kama niyyah. 

 إِنَّما الأَعْمَالُ بالنِّيَّاتِ وإنَّما لكُلِّ امْرِىءٍ ما نَوَى،    

Hakika ‘amali inategemea (malipo) kwa niyyah na kila mtu atapata kwa mujibu wa kila alichotilia niyyah. [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Imaam Ash-Shaafi’iy naye kasema Hadiyth hii ni nusu ya elimu. Naye Imaam Ahmad na Imaam Ash-Shaafi’iy wamesema Hadiyth hii inakusanya moja ya tatu ya elimu. Imaam Al-Bayhaqiy akafafanua maneno yao hayo kwa kusema, “Hayo ni kwa sababu, mtu huchuma thawabu kwa moyo wake, ulimi na mwili wake. Hivyo, niyyah inahusiana na moja ya viungo hivyo vitatu. [Ibn Hajr, Fat-h Al-Baariy, mj. 1, uk. 11]

 

Na sharti za kupokelewa ‘amali za mja ni ikhlaasw, niyyah safi ya ‘amali kwa kufuata amri ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Anavyoamrisha:

 

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ ﴿٥﴾

Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah wenye kumtakasia Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki na wasimamishe Swalaah na watoe Zakaah; na hiyo ndiyo Dini iliyosimama imara. [Al-Baayyinah: 5]

 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

Hivyo anayetaraji kukutana na Rabb wake, basi na atende ‘amali njema na wala asimshirikishe yeyote katika ‘ibaadah za Rabb wake.” [Al-Kahf: 110]

 

Yaani asifanye riyaa (kujionyesha) ‘amali zake kwa watu kama Swalaah, Hajj, Swawm, Zakaah, Swadaqah, kusoma Qur-aan, kufanyia watu wema na ihsaan kwa ajili ya kusifiwa, kujitukuza au kuonekana ni mwema na sifa kama hizo za riyaa.

 

Na Rasuli wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) aliwatahadharisha Swahaabah (Radhwiya Allaahu ‘anhum) kuhusu riyaa. Siku ya Qiyaamah pindi mtu atakapokuja na ‘amali zake itatambulikana kama zilikuwa za ikhlaasw au za riyaa kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema katika Hadiyth:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه وآله وسلم): ((إِنَّ اللَّهَ لاَ يَنْظُرُ إِلى أجْسمِكُمْ وَلاَ إِلَى صُوَرِكُمْ وَلَكِنْ يَنْظُرُ إِلَى قُلُوبِكُمْ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Hatazami viwiliwili vyenu wala sura zenu, lakini Anatazama nyoyo zenu)). [Muslim]

 

Nyoyo ndizo zitakazodhihirisha ikhlaasw ya mtu kwani humo ndipo kunapofichika shirki kama ilivyobainishwa katika Hadiyth ifauatayo:

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ، قَالَ: خَرَجَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَنَحْنُ نَتَذَاكَرُ الْمَسِيحَ الدَّجَّالَ، فَقَالَ: ((أَلا أُخْبِرُكُمْ بِمَا هُوَ أَخْوَفُ عَلَيْكُمْ عِنْدِي مِنَ الْمَسِيحِ الدَّجَّالِ؟)) قَالَ: قُلْنَا: بَلَى! فَقَالَ: ((الشِّرْكُ الْخَفِيُّ، أَنْ يَقُومَ الرَّجُلُ يُصَلِّي، فَيُزَيِّنُ صَلاتَهُ، لِمَا يَرَى مِنْ نَظَرِ رَجُلٍ)) سنن ابن ماجه (4204).

Imepokelewa kutoka kwa Abu Sa’iyd (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam) alikuja kwetu wakati tulikuwa tukijadiliana kuhusu Dajjaal, akasema: ((Je, niwajulisheni kile nikikhofiacho zaidi kwenu kuliko hata (hatari za) Dajjaal?)) Tukasema: Ndio. Akasema: ((Basi ni shirki iliyojificha. Mtu anasimama kuswali, anaipamba na kuiremba Swalaah yake kwa kujua kuwa kuna watu wanamtazama)) [Sunan Ibn Maajah (4204)]

 

Hiyo ni kama sifa ya wanafiki wanaomhadaa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Anavyosema:

 

 إِنَّ الْمُنَافِقِينَ يُخَادِعُونَ اللَّـهَ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا قَامُوا إِلَى الصَّلَاةِ قَامُوا كُسَالَىٰ يُرَاءُونَ النَّاسَ وَلَا يَذْكُرُونَ اللَّـهَ إِلَّا قَلِيلًا ﴿١٤٢﴾

Hakika wanafiki (wanadhani) wanamhadaa Allaah, na hali Yeye (Allaah) Ndiye Mwenye kuwahadaa. Na wanaposimama kuswali husimama kwa uvivu, wakijionyesha kwa watu na wala hawamdhukuru Allaah isipokuwa kidogo tu. [An-Nisaa: 142]

 

 

 

Share

04-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Shirki Inabatilisha ‘Amali

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno

 

04- Shirki Inabatilisha ‘Amali

 

Alhidaaya.com

 

 

‘Amali za Muislamu bila ya kuwa na niyyah safi kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) au ikhlaasw, huwa hazina thamani mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa dalili zifuatazo:

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

وَقَدِمْنَا إِلَىٰ مَا عَمِلُوا مِنْ عَمَلٍ فَجَعَلْنَاهُ هَبَاءً مَّنثُورًا ﴿٢٣﴾

Na Tutayaendea yale waliyoyatenda ya ‘amali yoyote ile, Tutayafanya   chembechembe za vumbi zinazoelea hewani zinazotawanyika. [Al-Furqaan: 23]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ﴿٦٥﴾

Kwa yakini umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: “Ukifanya shirki bila shaka zitaporomoka ‘amali zako na bila shaka utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.” [Az-Zumar: 65]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٨٨﴾

Na kama wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda. [Al-An’aam: 88]

 

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametaja katika Hadiyth Al-Qudsiy:

 

 

عنْ ابي هريرة رضي الله عنه أنَّه صلَّى الله عليه وسلَّم قال: ((قال الله تعالى: أنا أغْنى الشُّركاء عن الشِّرْك، فمَن عمل عملاً أشْرَك فيه معي غيري تركتُه وشِرْكه))    

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam amesema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: ‘‘‘‘Mimi Ni Mwenye kujitosheleza kabisa, Sihitaji msaada wala mshirika. Kwa hiyo, yule afanyaye amali kwa kunishirikisha na mtu, Nitaikanusha pamoja na mshirika wake.”  Yaani: hatopata ujira wowote kwa amali hiyo. [Muslim (2985), Ibn Maajah (4202)]

 

 

Mfano bayana wa kubatilika ‘amali za mtu kwa anayetoa swadaqah kwa riyaa ni kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ كَالَّذِي يُنفِقُ مَالَهُ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ فَمَثَلُهُ كَمَثَلِ صَفْوَانٍ عَلَيْهِ تُرَابٌ فَأَصَابَهُ وَابِلٌ فَتَرَكَهُ صَلْدًا ۖ لَّا يَقْدِرُونَ عَلَىٰ شَيْءٍ مِّمَّا كَسَبُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٢٦٤﴾

 Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia kama yule ambaye anatoa mali yake kwa kujionyesha kwa watu wala hamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama jabali juu yake pana udongo, kisha likapigwa na mvua kubwa ikaliacha tupu. Hawana uwezo juu ya lolote katika waliyoyachuma. Na Allaah Haongoi watu makafiri.  [Al-Baqarah: 264]

 

 

Share

05-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Hatima Ya Mwenye Riyaa (Kujionyesha)

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

05-Hatima Ya Mwenye Riyaa (Kujionyesha)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Juu ya kuwa ‘amali za mtu zinabatilika kwa sababu ya riyaa, vile vile hatima ya mwenye riyaa ni mbaya mno!

 

Mwenye kudhihirisha ‘amali zake kwa riyaa atafedheheshwa Siku ya Qiyaamah kwa dalili Hadiyth ifuatayo:

 

عَنْ جُنْدَبِ بْنِ عَبْدُ الله بْنِ سُفْيانَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ سَمَّعَ سَمَّعَ اللَّهُ بِهِ وَمَنْ رَاءَى رَاءَى اللَّهُ بِهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Jundab bin ‘Abdillaah bin Sufyaan (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: “Nabiy Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam amesema: ((Mwenye kudhihirisha ‘amali yake kwa riyaa, Allaah Atamfedhehesha Siku ya Qiyaamah, na mwenye kuwafanyia watu riyaa [kwa ‘amali njema ili aonekane ni mtukufu], Allaah Atazidhihirisha siri zake [Siku ya Qiyaamah])) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Mtu huyo mwenye riyaa hatosikia harufu ya Jannah:  

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  مَنْ تَعَلَّمَ عِلْمًا مِمَّا يُبْتَغَى بِهِ وَجْهُ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ لَا يَتَعلَّمُهُ إِلَّا لِيُصِيبَ بِهِ عَرَضًا مِنْ الدُّنْيَا لَمْ يَجِدْ عَرْفَ الْجَنَّةِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ  يَعْنِي رِيحَهَا.  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) amesema: ((Yeyote anayejifundisha elimu ambayo anapaswa kuitumia kwa ajili ya Allaah, (kisha akaitumia) kwa ya kupata manufaa ya kidunia hatonusa harufu ya Jannah Siku ya Qiyaamah)) [Abu Daawuwd (3656), Ibn Maajah (255) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (3664)]

 

 

Mwenye kuswali kwa riyaa   atapata maangamizi. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):  

 

فَوَيْلٌ لِّلْمُصَلِّينَ ﴿٤﴾

  Basi Ole kwa wanaoswali ...

 

 

الَّذِينَ هُمْ عَن صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ ﴿٥﴾

 Ambao wanapuuza Swalaah zao.

 

الَّذِينَ هُمْ يُرَاءُونَ ﴿٦﴾

Ambao wanajionyesha (riyaa). [Al-Maa’uwn: 4-6]

 

 

Watu watatu wa kwanza kuhesabiwa Siku ya Qiyaamah ni: aliyekufa Shahidi, ‘Aalim (aliyejifunza Dini na Qur-aan) aliyetoa mali yake katika njia ya Allaah. Lakini ambaye ameingiza riyaa katika ‘amali hizi basi ataingizwa Motoni:

 

عَنْ أبي هريرة رضي الله عنه قال: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهم عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ ((إِنَّ أَوَّلَ النَّاسِ يُقْضَى يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَلَيْهِ رَجُلٌ اسْتُشْهِدَ فَأُتِيَ بِهِ فَعَرَّفَهُ نِعَمَهُ فَعَرَفَهَا قَالَ: فَمَا عَمِلْتَ فِيهَا؟ قَالَ: قَاتَلْتُ فِيكَ حَتَّى اسْتُشْهِدْتُ، قَالَ: كَذَبْتَ وَلَكِنَّكَ قَاتَلْتَ لِأَنْ يُقَالَ جَرِيءٌ فَقَدْ قِيلَ ثُمَّ أُمِرَ بِهِ فَسُحِبَ عَلَى وَجْهِهِ حَتَّى أُلْقِيَ فِي النَّارِ، وَرَجُلٌ تَعَلَّمَ الْعِلْمَ وَعَلَّمَهُ وَقَرَأَ الْقُرْآنَ فَأُتِيَ بِهِ فَعَرَّفَهُ نِعَمَهُ فَعَرَفَهَا قَالَ: فَمَا عَمِلْتَ فِيهَا؟ قَالَ: تَعَلَّمْتُ الْعِلْمَ وَعَلَّمْتُهُ وَقَرَأْتُ فِيكَ الْقُرْآنَ، قَالَ: كَذَبْتَ وَلَكِنَّكَ تَعَلَّمْتَ الْعِلْمَ لِيُقَالَ عَالِمٌ وَقَرَأْتَ الْقُرْآنَ لِيُقَالَ هُوَ قَارِئٌ فَقَدْ قِيلَ ثُمَّ أُمِرَ بِهِ فَسُحِبَ عَلَى وَجْهِهِ حَتَّى أُلْقِيَ فِي النَّارِ، وَرَجُلٌ وَسَّعَ اللَّهُ عَلَيْهِ وَأَعْطَاهُ مِنْ أَصْنَافِ الْمَالِ كُلِّهِ فَأُتِيَ بِهِ فَعَرَّفَهُ نِعَمَهُ فَعَرَفَهَا قَالَ: فَمَا عَمِلْتَ فِيهَا؟ قَالَ: مَا تَرَكْتُ مِنْ سَبِيلٍ تُحِبُّ أَنْ يُنْفَقَ فِيهَا إِلَّا أَنْفَقْتُ فِيهَا لَكَ قَالَ كَذَبْتَ وَلَكِنَّكَ فَعَلْتَ لِيُقَالَ هُوَ جَوَادٌ فَقَدْ قِيلَ ثُمَّ أُمِرَ بِهِ فَـسُحِبَ عَـلَى وَجْهِهِ ثُمَّ أُلْقِيَ فِي النَّارِ ))

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi sallam) akisema: ((Wa mwanzo kuhesabiwa Siku ya Qiyaamah ni mtu aliyekufa shahidi katika vita, ataletwa na kujulishwa neema alizoneemeshwa na baada ya kuzijua ataulizwa (na Allaah): “Umezifanyia kazi gani neema hizi?” Atasema: “Nimepigana jihaad kwa ajili Yako mpaka nikafa shahidi.” Ataambiwa: “Umesema uongo, bali ulipigana ili isemwe kuwa wewe ni jasiri na imeshasemwa.” Kisha itaamrishwa abururwe kwa uso wake na kuingizwa Motoni. Na mtu (mwengine) 'Aalim aliyejifundisha Dini akaijua vizuri, akasoma na Qur-aan, ataletwa na kujulishwa neema alizoneemeshwa, kisha ataulizwa; “Umezifanyia kazi gani neema hizi?” Atasema: “Nimejifunza elimu nikafundisha na kwa ajili Yako nikasoma Qur-aan.” Ataambiwa: “Umesema uongo, bali ulijifunza elimu ili isemwe kuwa wewe ni ‘Aalim. Ukasoma Qur-aan ili isemwe kuwa wewe ni msomaji (mzuri), na imeshasemwa.” Kisha itaamrishwa abururwe kwa uso wake na kuingizwa Motoni. Na mtu (mwengine) Allaah Amempa wasaa, akampa kila aina ya mali, ataletwa na kujulishwa juu ya neema alizoneemeshwa, kisha ataulizwa: “Umezifanyia kazi gani neema hizi?” Atasema: “Sijaacha njia Unayopenda mtu atoe katika mali yake ila mimi nimetoa kwa ajili Yako.” Ataambiwa: “Umesema uongo, bali umetoa ili isemwe kuwa wewe ni mkarimu na imeshasemwa. Kisha itaamrishwa abururwe kwa uso wake na kuingizwa Motoni”. [Muslim]

 

 

Share

06-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Shirki Ni Miongoni Mwa Madhambi Makubwa

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

06- Shirki Ni Miongoni Mwa Al-Kabaair (Madhambi Makubwa)

 

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا ﴿٤٨﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amezua dhambi kuu. [An-Nisaa: 48]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا بَعِيدًا﴿١١٦﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amepotoka upotofu wa mbali.  [An-Nisaa: 116]

 

 

Na Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam):

 

 ((ألاَ أُنبِّئكم بأكبرِ الكبائر؟ الإشراك بالله)) متفق عليه.

((Je, hivi nikujulisheni madhambi makubwa kabisa? Ni kumshirikisha Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na pia Hadiyth:

 

عَنْ أبي أيوب الأنصاري رضي الله عنه انَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ جَاءَ يَعْبُدُ اللَّهَ وَلاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا وَيُقِيمُ الصَّلاَةَ وَيُؤْتِي الزَّكَاةَ وَيَجْتَنِبُ الْكَبَائِرَ كَانَ لَهُ الْجَنَّةُ)).‏ فَسَأَلُوهُ عَنِ الْكَبَائِرِ فَقَالَ‏: ((الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ وَقَتْلُ النَّفْسِ الْمُسْلِمَةِ وَالْفِرَارُ يَوْمَ الزَّحْفِ)).‏

Imepokelekewa kutoka kwa Abuu Ayyuwb Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayekuja akiwa anamwambudu Allaah wala hamshirikishi na chochote, na anasimamisha Swalaah, na anatoa Zakaah, na anajiepusha na Al-Kabaair (madhambi makubwa) atapata Al-Jannah)) Wakamuuliza kuhusu Al-Kabaair akasema: ((Kumshirkisha Allaah na kumuua Muislamu, na kukimbia (vita) siku ya mapambano (vita).)) [An-Nasaaiy (4009) na ameisahihisha Al-Albaaniy]

 

Na shirki ni katika mambo saba yanayoangamiza:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه (عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَمَا هُنَّ؟  قَالَ: ((الشِّرْكُ بِاللَّهِ وَالسِّحْرُ وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ وَأَكْلُ الرِّبَا وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ الْغَافلاَتِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akawaambia: ((Ni kumshirikisha Allaah, sihri [uchawi], kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa vita na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika.)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

Share

07-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Shirki Ni Kuharamishwa Kuingia Jannah Badala Yake Kuingizwa Motoni

 

  إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

07-Shirki Ni Kuharamishwa Kuingia Jannah Na Badala Yake Kuingizwa Motoni

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Mwenye kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) atakosa kuingia Jannah bali makazi yake yatakuwa ni ya kudumu Motoni kwa dalili zifuatazo:

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ﴿٧٢﴾

 Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. Na madhalimu hawatopata yeyote mwenye kunusuru.” [Al-Maaidah: 72]

 

 Na Hadiyth zifuatazo:

 

 عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: قال النبي صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ مَاتَ وَهُوَ يَدْعُو مِنْ دُونِ اللهِ نِدَّاً دَخَلَ النَّارَ )) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaahi bin Mas-‘uwd (Radhwiya Alaahu ‘anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayekufa akiwa katika hali ya kumuomba asiyekuwa Allaah kumfanyia mlinganishi (mshirika) ataingia Motoni)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na pia:

 

عن ابن مسعود رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ مَاتَ يُشْرِكُ بِاللَّهِ شَيْئًا دَخَلَ النَّارَ))  

Kutoka kwa Ibn Mas‘uwd pia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayefariki akiwa katika hali ya kumshirikisha Allaah kwa chochote ataingia Motoni)) [Al-Bukhaariy 1238, Muslim 92]

 

Pia:

 

  عن جابر رضي الله عنه: أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((مَنْ لَقِي اللهَ لاَ يُشْرِك بِهِ شَيْئاً دَخَلَ الْجَنَّة، وَمَنْ لَقِيَه يُشْرِك بِهِ شَيْئاً دَخَلَ النَّار)) 

Imetoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (Atakayekutana na Allaah akiwa hamshirikishi na chochote Ataingia Jannah, na atakayekutana Naye akiwa anamshirikisha na chochote ataingia Motoni)) [Muslim 94.]

 

Na pia:

 

عَن أَبي ذَرٍّ رضي الله عنه  عنِ النَّبيِّ صلَّى اللَّهُ عليهِ وسلَّمَ؛ أنَّهُ قالَ: ((أتاني جبريلُ عليهِ السَّلامُ  فبشَّرَني أنَّهُ من ماتَ من أمَّتِكَ لا يشرِكُ باللَّهِ شيئًا دخلَ الجنَّةَ))  قلتُ: وإن زنَى وإن سرقَ؟ قالَ: ((وإن زنَى وإن سرقَ))

Kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Amenijia Jibriyl ‘alayhis-salaam akanibashiria kwamba atakayefariki katika Ummah wangu akiwa hamshirikishi Allaah kwa chochote ataingia Jannah)). Nikasema: “Je hata akizini au akiiba?” Akasema: ((Hata akizini au akiiba)) [Al-Bukhaariy 1237, Muslim 94]

 

Na Hadiyth ya Abuu Huraryah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

  وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لاَ يَسْمَعُ بِي أَحَدٌ مِنْ هَذِهِ الأُمَّةِ يَهُودِيٌّ وَلاَ نَصْرَانِيٌّ ثُمَّ يَمُوتُ وَلَمْ يُؤْمِنْ بِالَّذِي أُرْسِلْتُ بِهِ إِلاَّ كَانَ مِنْ أَصْحَابِ النَّارِ

((Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, hasikii yeyote kuhusu mimi (kutumwa kwangu ujumbe) katika Ummah wa (Da’wah) Myahudi au Mnaswaara kisha afariki akiwa hayamini yale niliyotumwa nayo, isipokuwa atakuwa miongoni kwa watu wa Motoni)) [Muslim (1/80) Mlango wa Iymaan – Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu)]

 

Pia:

 

عَن عبدالله بن عمر جاءَ أعرابيٌّ إلى النَّبيِّ صلَّى اللَّهُ عليْهِ وسلَّمَ فقالَ: يا رسولَ اللَّهِ إنَّ أبي كانَ يصِلُ الرَّحمَ وَكانَ وَكانَ فأينَ هوَ؟ قالَ: ((في النَّارِ)) قالَ فَكأنَّهُ وجدَ من ذلِكَ فقالَ: يا رسولَ اللَّهِ فأينَ أبوكَ قالَ رسولُ اللَّهِ صلَّى اللَّهُ عليْهِ وسلَّمَ: ((حيثُما مررتَ بقبرِ مشرِكٍ فبشِّرْهُ بالنَّارِ)) قالَ: فأسلمَ الأعرابيُّ بعدُ وقالَ: لقد كلَّفني رسولُ اللَّهِ صلَّى اللَّهُ عليْهِ وسلَّمَ تعبًا ما مررتُ بقبرِ كافرٍ إلَّا بشَّرتُهُ بالنَّارِ

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Bedui mmoja alikuwa kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Baba yangu alikuwa akiunga undugu na alikuwa akifanya kadhaa wa kadhaa, je yuko wapi?” Akasema: (Motoni)). Ikawa kama kwamba lilikuwa jambo zito kwake. Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Je, baba yako yuko wapi?” Akasema: ((Utakapopita kaburi la Mushrik yeyote mbashirie Moto)). Bedui akasilimu baada ya hapo kisha akasema: “Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): amenitwika jukumu gumu kwamba kila nikipata kaburi la kafiri nimbashirie Moto.” [Swahiyh Ibn Maajah 1288]

 

Wala haifai kuwaombea wazazi makafiri wakafariki wakiwa katika hali ya ukafiri kwa kuwa imeshabainika kuwa ni watu wa Motoni, tena hata kama ni wazazi, ndugu au jamaa wa karibu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَن يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُوا أُولِي قُرْبَىٰ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمْ أَنَّهُمْ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ﴿١١٣﴾

Haimpasi Nabiy na wale walioamini kuwaombea maghfirah washirikina japokuwa ni jamaa zao wa karibu baada ya kuwabainikia kwamba wao ni watu wa moto uwakao vikali mno. [At-Tawbah: 113]

 

 

 

Share

08-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Sifa Mbaya Za Washirikina

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

08- Sifa Mbaya Za Washirikina

 

Alhidaaya.com

 

 

1-  Washirikina ni viumbe waovu kabisa kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَاۚ أُولَـٰئِكَ هُمْ شَرُّ الْبَرِيَّةِ ﴿٦﴾

Hakika wale waliokufuru miongoni mwa watu wa kitabu na washirikina watakuwa katika moto wa Jahannam, ni wenye kudumu humo; hao ndio waovu kabisa wa viumbe. [Al-Bayyinah: 6]

 

 

2-Washirikina ni wapotofu hawana akili kama vile wanyama walivyokuwa hawana akili, bali wapotofu zaidi kuliko wanyama!

 

Kwa sababu wana Aadam wamefadhilishwa kupewa akili kinyume na wanyama, lakini wana Aadam hao wanaomkufuru na kumshirkisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) ni wenye kufuata hawaa zao, hawatumii akili zao! Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 أَرَأَيْتَ مَنِ اتَّخَذَ إِلَـٰهَهُ هَوَاهُ أَفَأَنتَ تَكُونُ عَلَيْهِ وَكِيلًا ﴿٤٣﴾

Je, umemuona yule aliyefanya hawaa yake kuwa ndio mwabudiwa wake?  Je, basi utaweza wewe kuwa ni mdhamini wake?

 

 

أَمْ تَحْسَبُ أَنَّ أَكْثَرَهُمْ يَسْمَعُونَ أَوْ يَعْقِلُونَ ۚ إِنْ هُمْ إِلَّا كَالْأَنْعَامِ ۖ بَلْ هُمْ أَضَلُّ سَبِيلًا ﴿٤٤﴾

Je, unadhania kwamba wengi wao wanasikia au wanatia akilini? Wao si chochote isipokuwa kama wanyama, bali wao wamepotea zaidi njia. [Al-Furqaan: 43-44] 

 

 

3- Washirikina, kwa shirki na kufru zao, wamekuwa ni wenye kula na kustarehe kama wanyama. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَالَّذِينَ كَفَرُوا يَتَمَتَّعُونَ وَيَأْكُلُونَ كَمَا تَأْكُلُ الْأَنْعَامُ وَالنَّارُ مَثْوًى لَّهُمْ﴿١٢﴾

Na wale waliokufuru wanastarehe na wanakula kama walavyo wanyama wa mifugo na moto ndio makazi yao. [Muhammad: 12]

 

 

 

4- Washirikina ni vipofu, viziwi, mabubu, hawatumii akili!

 

Washirikina walipokuwa wakiitwa kufuata Uongofu wa Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kufuata Tawhiyd na kuacha kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) walikanusha, wakapigiwa mfano kama viziwi, mabubu, vipofu, hawana akili! Kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّبِعُوا مَا أَنزَلَ اللَّـهُ قَالُوا بَلْ نَتَّبِعُ مَا أَلْفَيْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا ۗ أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لَا يَعْقِلُونَ شَيْئًا وَلَا يَهْتَدُونَ﴿١٧٠﴾

Na wanapoambiwa: “Fuateni Aliyoyateremsha Allaah” Husema: “Bali tunafuata tuliyowakuta nayo baba zetu.” Je, japokuwa baba zao walikuwa hawaelewi kitu chochote na wala hawakuongoka?

 

 

 وَمَثَلُ الَّذِينَ كَفَرُوا كَمَثَلِ الَّذِي يَنْعِقُ بِمَا لَا يَسْمَعُ إِلَّا دُعَاءً وَنِدَاءً ۚ صُمٌّ بُكْمٌ عُمْيٌ فَهُمْ لَا يَعْقِلُونَ ﴿١٧١﴾

Na mfano wa wale waliokufuru ni kama mfano wa yule ambaye anapiga kelele kwa ambaye hasikii ila sauti na mwito. Viziwi, mabubu, vipofu kwa hiyo hawatii akilini. [Al-Baqarah: 170-171]

 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَقَدْ ذَرَأْنَا لِجَهَنَّمَ كَثِيرًا مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ ۖ لَهُمْ قُلُوبٌ لَّا يَفْقَهُونَ بِهَا وَلَهُمْ أَعْيُنٌ لَّا يُبْصِرُونَ بِهَا وَلَهُمْ آذَانٌ لَّا يَسْمَعُونَ بِهَا ۚ أُولَـٰئِكَ كَالْأَنْعَامِ بَلْ هُمْ أَضَلُّ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْغَافِلُونَ﴿١٧٩﴾

Kwa yakini Tumeumba Jahannam kwa ajili ya wengi katika majini na wana Adam. Wana nyoyo, lakini hawafahamu kwazo. Na wana macho, lakini hawaoni kwayo. Na wana masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama wanyama, bali wao ni wapotovu zaidi. Hao ndio walioghafilika. [Al-A’raaf: 179]

 

 

Na ndio maana wakawa viumbe waovu kabisa kwa kuwa hawakutaka kumtii Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipowalingania. Wakabakia katia shirki na kufru zao. Basi hawana kheri yoyote ile mbele ya Allaah. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ قَالُوا سَمِعْنَا وَهُمْ لَا يَسْمَعُونَ﴿٢١﴾

Na wala msiwe kama wale waliosema: “Tumesikia”; na hali wao hawasikii.

 

 

إِنَّ شَرَّ الدَّوَابِّ عِندَ اللَّـهِ الصُّمُّ الْبُكْمُ الَّذِينَ لَا يَعْقِلُونَ﴿٢٢﴾

Hakika viumbe viovu kabisa mbele ya Allaah ni viziwi, mabubu ambao hawatumii akili.

 

 

وَلَوْ عَلِمَ اللَّـهُ فِيهِمْ خَيْرًا لَّأَسْمَعَهُمْ ۖ وَلَوْ أَسْمَعَهُمْ لَتَوَلَّوا وَّهُم مُّعْرِضُونَ﴿٢٣﴾

Na kama Allaah Angelijua kuwa wana kheri yoyote ile, basi Angeliwasikilizisha; na kama Angeliwasikilizisha, wangeligeuka nao huku wakipuuza. [Al-Anfaal: 21-23]

 

 

 

5- Washirikina ni watu wa najisi!

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْمُشْرِكُونَ نَجَسٌ فَلَا يَقْرَبُوا الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ بَعْدَ عَامِهِمْ هَـٰذَا

Enyi walioamini!  Hakika washirikiana ni najisi, basi wasikaribie Al-Masjid Al-Haraam baada ya mwaka wao huu. [At-Tawbah: 28]

 

 

 

6-Imeharamishwa kufunga ndoa na washirikina! Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaamrisha:

 

وَلَا تَنكِحُوا الْمُشْرِكَاتِ حَتَّىٰ يُؤْمِنَّ ۚ وَلَأَمَةٌ مُّؤْمِنَةٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكَةٍ وَلَوْ أَعْجَبَتْكُمْ ۗ وَلَا تُنكِحُوا الْمُشْرِكِينَ حَتَّىٰ يُؤْمِنُوا ۚ وَلَعَبْدٌ مُّؤْمِنٌ خَيْرٌ مِّن مُّشْرِكٍ وَلَوْ أَعْجَبَكُمْ ۗ أُولَـٰئِكَ يَدْعُونَ إِلَى النَّارِ ۖ وَاللَّـهُ يَدْعُو إِلَى الْجَنَّةِ وَالْمَغْفِرَةِ بِإِذْنِهِ ۖوَيُبَيِّنُ آيَاتِهِ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٢١﴾

Na wala msiwaoe wanawake washirikina mpaka waamini. Na mjakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina japo akikupendezeni. Na wala msiwaozeshe (wanawake wa Kiislamu) wanaume washirikina mpaka waamini. Na mtumwa Muumini ni bora kuliko mshirikina japo akikupendezeni. Hao wanaitia katika moto na Allaah Anaitia katika Al-Jannah na maghfirah kwa idhini Yake. Na Anabainisha Aayaat (na shariy’ah) Zake ili wapate kukumbuka. [Al-Baqarah: 221]

 

 

 

 

 

Share

09-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kusujudu Na Kuinamia Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

09 Kusujudu Na Kuinamia Kwa Asiyekuwa Allaah

 

 

 

Washirikina wa kale walimshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa namna mbali mbali; kuna walioabudu masanamu wakiyasujudia na kurukuu mbele yao. Wengine walirukuu na kusujudia mwezi, nyota na jua, jambo ambalo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameliharamisha katika kauli Yake:

 

وَمِنْ آيَاتِهِ اللَّيْلُ وَالنَّهَارُ وَالشَّمْسُ وَالْقَمَرُ ۚ لَا تَسْجُدُوا لِلشَّمْسِ وَلَا لِلْقَمَرِ وَاسْجُدُوا لِلَّـهِ الَّذِي خَلَقَهُنَّ إِن كُنتُمْ إِيَّاهُ تَعْبُدُونَ﴿٣٧﴾

Na katika Aayaat (ishara, dalili) Zake, ni usiku na mchana, na jua na mwezi.  Msisujudie jua wala mwezi; bali msujudieni Allaah Ambaye Aliyeviumba ikiwa Yeye Pekee mnawambudu. [Fusw-swilat: 37]

 

 

Hali kama hii inatendwa na baadhi ya Waislamu kuinamia binaadamu wenzao katika maamkizi n.k. kwa kudhihirisha mapenzi, takrima na heshima.  Baadhi ya mila zinaamrisha watoto kuwainamia wazazi wao, au waalimu na watu wakubwa katika maamkizi. Kadhaalika, hata baadhi ya watu wa itikadi mbalimbali wenye vyeo wanapenda kusalimiwa kwa kuinamiwa! Kitendo hiki kinaingia katika kumshikirisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

 

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaahu) amesema: “Sujudu ni kwa ajili ya Allaah Pekee na shariy’ah ya Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni shariy’ah kamilifu kabisa, basi haijuzu kumsujudia yeyote asiyekuwa Allaah, ikiwa ni katika maamkizi wala katika ‘ibaadah. Ama katika shariy’ah zote, sujudu ya ‘ibaadah ndio haijuzu kabisa isipokuwa kwa Allaah. Isipokuwa ilikuwa zamani (kabla ya Uislamu) sujudu ilikuwa ikitumika kama maamkizi ya kudhihirisha heshima kama alivyofanya (Nabiy Ya’quwb) baba yake Nabiy Yuwsuf na ndugu zake na kama walivyofanya Malaika kumsujudia Aadam. Hii ni katika maamkizi ya takrima wala si kusudio la ‘ibaadah. Ama katika shariy’ah ya Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Allaah (‘Azza wa Jalla) Amekataza hivyo Akaifanya sujudu ni kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Pekee wala haijuzu kumsujudia yeyote; si Manabiy wala wengineo, hata Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza asisujudiwe na yeyote na akajulisha kwamba sujudu ni kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Pekee.” [Fataawaa Nuwr  ‘Alaa Ad-Darb (4/112-113)]

 

Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah amenukuu katazo kama hilo katika Majmuw’ Al-Fataawaa (1/377) .     

 

Na Al-Lajnah Ad-Daaimah lil-buhuwthil-‘ilmiyyah wal-Iftaa katika Fatwa namba (4400) wamefutu ifuatavyo:

 

“Yeyote aliyeamini Risala ya Nabiy wetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na yale yote aliyokuja nayo katika shariy’ah, kisha baada ya hapo akamsujudia yeyote asiyekuwa Allaah; ikiwa ni walii wake au mtu kaburini, au shekhe wa Twariyqah (Masufi)  basi yeye anahesabika kuwa ni kafiri aliyeritadi kutoka katika Uislamu, ni mshirikina akimshirikisha Allaah na wengineo katika ‘ibaadah hata kama atakuwa anatamka Shahada mbili wakati wa kusujudu kwake, kwa kuleta jambo lenye kupinga kauli yake kwa kumsujudia asiyekuwa Allaah.”

 

Katazo hilo limethibiti katika Qur-aan na Sunnah: 

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ أَبِي أَوْفَى، قَالَ: "لَمَّا قَدِمَ مُعَاذٌ مِنَ الشَّامِ سَجَدَ لِلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، قَالَ: ((مَا هَذَا يَا مُعَاذُ ؟)) قَالَ: أَتَيْتُ الشَّامَ فَوَافَقْتُهُمْ يَسْجُدُونَ لِأَسَاقِفَتِهِمْ وَبَطَارِقَتِهِمْ، فَوَدِدْتُ فِي نَفْسِي أَنْ نَفْعَلَ ذَلِكَ بِكَ، فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((فَلَا تَفْعَلُوا، فَإِنِّي لَوْ كُنْتُ آمِرًا أَحَدًا أَنْ يَسْجُدَ لِغَيْرِ اللَّهِ، لَأَمَرْتُ الْمَرْأَةَ أَنْ تَسْجدَ لِزَوْجِهَا، وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ، لَا تُؤَدِّي الْمَرْأَةُ حَقَّ رَبِّهَا حَتَّى تُؤَدِّيَ حَقَّ زَوْجِهَا، وَلَوْ سَأَلَهَا نَفْسَهَا وَهِيَ عَلَى قَتَبٍ لَمْ تَمْنَعْه))

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Abiy Awfaa (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Muaadh aliporudi kutoka Shaam alimsujudia Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Ee Mu’aadh! Nini hivyo?)) Akasema: “Nimekuja kutoka Shaam nikawakuta wanawasujudia Maaskofu na Mapadri wao nafsi yangu ikapenda nikufanyie hivyo.” Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Usifanye hivyo! Kwani hakika ingekuwa ni kumuamrisha mtu amsujudie asiyekuwa Allaah, basi ningeliamrisha mke amsujudie mumewe. Naapa kwa Ambaye nafsi ya Muhammad ipo Mikononi Mwake; Mke hatoweza kutimiza haki za Mola Wake mpaka atimize haki za mumewe, na hata kama atamtaka hali akiwa katika nundu la ngamia basi asimnyime)) [Riwaayah mbali mbali kama hiyo na hii ni lafdhw ya Ibn Maajah (1853) na ameisahihisha Al-Albaaniy]

 

Na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:

 

مَا كَانَ لِبَشَرٍ أَن يُؤْتِيَهُ اللَّـهُ الْكِتَابَ وَالْحُكْمَ وَالنُّبُوَّةَ ثُمَّ يَقُولَ لِلنَّاسِ كُونُوا عِبَادًا لِّي مِن دُونِ اللَّـهِ وَلَـٰكِن كُونُوا رَبَّانِيِّينَ بِمَا كُنتُمْ تُعَلِّمُونَ الْكِتَابَ وَبِمَا كُنتُمْ تَدْرُسُونَ ﴿٧٩﴾

Ni mustahili kwa mtu kwamba Allaah Amempa Kitabu na Al-Hukma na Unabii kisha awaambie watu: “Kuweni wenye kuniabudu mimi badala ya Allaah” Bali (atawaambia): “Kuweni Wanachuoni waswalihina kwa yale mliyokuwa mkiyafundisha ya Kitabu na kwa yale mliyokuwa mkiyasoma.” 

 

 

وَلَا يَأْمُرَكُمْ أَن تَتَّخِذُوا الْمَلَائِكَةَ وَالنَّبِيِّينَ أَرْبَابًا ۗ أَيَأْمُرُكُم بِالْكُفْرِ بَعْدَ إِذْ أَنتُم مُّسْلِمُونَ ﴿٨٠﴾ 

Na wala hakuamuruni kuwachukua Malaika na Manabii kuwafanya miola. Je, anakuamrisheni ukafiri baada ya nyinyi kuwa mmejisalimisha kwa Allaah? [Aal-‘Imraan: 79-80]

 

 

 

 

 

Share

10-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kumhusisha Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam Katika Kumshirikisha Allaah.

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

10-Kumhusisha Rasuli wa Allaah Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam

Katika Kumshirikisha Allaah. 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Baadhi ya Waislamu wanamhusisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa namna mbali mbali. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na Rasuli wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wamekemea mno kwa dalili kadhaa miongoni mwazo ni: 

 

Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba ilipoteremshwa kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

Na onya (ee Muhammad Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) jamaa zako wa karibu. [Ash-Shu’araa: 214]

 

 

Alisimama Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:

 

 ((يَا مَعْشَرَ قُرَيْشٍ!)) أَوْ كَلِمَةً نَحْوَهَا ((اشْتَرُوا أَنْفُسَكُمْ، لاَ أُغْنِي عَنْكُمْ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا، يَا بَنِي عَبْدِ مَنَافٍ لاَ أُغْنِي عَنْكُمْ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا، يَا عَبَّاسُ بْنَ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ لاَ أُغْنِي عَنْكَ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا، وَيَا صَفِيَّةُ عَمَّةَ رَسُولِ اللَّهِ لاَ أُغْنِي عَنْكِ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا ، وَيَا فَاطِمَةُ بِنْتَ مُحَمَّدٍ سَلِينِي مَا شِئْتِ مِنْ مَالِي لاَ أُغْنِي عَنْكِ مِنَ اللَّهِ شَيْئًا))

((Enyi maashara Quraysh!)) Au mfano wa maneno hayo ((Okoeni nafsi zenu, mimi sitowafaa kwa chochote mbele ya Allaah! Enyi Baniy ‘Abdi Manaaf! Mimi sitowafaa kwa chochote mbele ya Allaah!  Ee ‘Abbaas bin ‘Abdil-Mutwalib! Sitokufaa  kwa chochote mbele ya Allaah! Na ee Faatwimah bint Muhammad! Niombe utakacho katika mali, lakini sitokufaa kwa chochote mbele ya Allaah)) [Al-Bukhaariy (2753), Muslim (206)].

 

 

Amesema Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) katika Majmuw’ Fataawa wa Rasaail (9/285- 288):

 

“Ikiwa ujamaa wa karibu na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hautowafaa chochote jamaa zake, ni dalili hiyo kukatazwa tawassul kwa jaha ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kuwa jaha ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hainufaishi kwayo isipokuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na ndivyo ikawa kauli sahihi kabisa ya Wanachuoni ni uharamu wa tawassul kwa jaha ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).”

 

 

Na Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema katika Majmuw’ Fataawaa (3/98):

 

“Mwongozo na kipimo cha hakika ni kufuata yaliyokuja katika Qur-aan Al-Kariym na Sunnah Al-Mutwaharrah kwa kauli na na vitendo na kuitakidi. Ama unasaba, hakika hautofaa (mtu) wala hauna umuhimu kama alivyosema Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam:  

 

وَمَنْ بَطَّأَ بِهِ عَمَلُهُ لَمْ يُسْرِعْ بِهِ نَسَبُهُ

((…na ambaye kazorotesha ‘amali zake, haitomharakisha nasaba yake)). [Muslim]

 

Akasema: ((Enyi maashara Quraysh! Okoeni nafsi zenu, mimi sitowafaa kwa chochote mbele ya Allaah!)). Hivyo ndivyo alivyomwambia ‘Ammi yake na ‘Ammat (shangazi) yake, na binti yake Faatwimah. Basi ingekuwa unasaba utamfaa mtu, ungewafaa hao.”

 

 

Baadhi ya vitendo vinavyomhusisha    Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kama ifuatavyo:  

 

 

1-Kumtukuza mno Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka kumfikisha daraja ya Allaah!

 

Amekemea Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

لا تُطْرُونِي كَمَا أَطْرَتْ النَّصَارَى ابْنَ مَرْيَمَ فَإِنَّمَا أَنَا عَبْدُهُ فَقُولُوا عَبْدُ اللَّهِ وَرَسُولُهُ) رواه البخاري

Msinitukuze Kama Manaswara [Wakristo] walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi na mja kwa hiyo semeni, ‘mja wa Allaah na Mjumbe Wake’)). [Al-Bukhaariy na Muslim.]

 

Na pia Hadiyth:

 

 عَنْ أَنَسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ نَاسًا قَالُوا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! يَا خَيْرَنَا وَابْنَ خَيْرِنَا, وَسَيِّدَنَا وَابْنَ سَيِّدِنَا! فَقَالَ: ((يَا أَيُّهَا اَلنَّاسُ! قُولُوا بِقَوْلِكُمْ، وَلاَ يَسْتَهْوِيَنَّكُمْ اَلشَّيْطَانُ، أَنَا مُحَمَّدٌ عَبْدُ اَللَّهِ وَرَسُولُهُ، مَا أُحِبُّ أَنْ تَرْفَعُونِي فَوْقَ مَنْزِلَتِي اَلَّتِي أَنْزَلَنِي اَللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ)) رَوَاهُ النَّسَائِيُّ بِسَنَدٍ جَيِّدٍ

Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: kwamba watu walisema: “Ee Rasuli wa Allaah! Ee mbora wetu na mwana wa mbora wetu, na bwana wetu, na mwana wa bwana wetu!.” Akasema: ((Enyi watu! Semeni msemayo, asikupambieni shaytwaan hawaa zenu. Mimi ni Muhammad mja wa Allaah na Rasuli Wake. Sipendi mnipandishe cheo kuliko cheo changu ambacho Ameniteremshia Allaah Ázza wa Jalla)). [An-Nasaaiy kwa isnaad nzuri]

 

Na kutukuzwa kwengine ni vile kusifiwa mno kwa uzushi na pia kutajwa kwa sifa ambazo ni Sifa za Allaah Pekee. Mfano katika Mawlid mbalimbali kama Barzanjiy, Nuwn, Al-Hibshiy (Sumtud-Durar), Burdah n.k. Vilevile kwenye nyiradi mbalimbali miongoni mwa nyiradi za Kisufi kama, Swalaatun-Naariyah, Wasiylatush-Shaafi’, Dalaail Al-Khayraat, n.k.

 

i) Maneno ya shirki yaliyomo katika Swalaatun-Naariyah:

 

للهم صلي صلاةً كاملة وسلم سلاما تاما على سيدنا محمد الذي تنحل به العقد، وتتفرج به الكرب، وتقضى به الحوائج ، وتنال به الرغائب، وحسن الخواتيم ويستسقى الغمام بوجهه الكريم وعلى آله وصحبه في كل لمحة ونفس بعدد معلوم لك

 

 Ee Allaah, Mswalie  Swalaah iliyotimu bwana wetu Muhammad ambayo kwa fadhila zake, vizuizi vyote vinaondoka, mazonge (misukosuko) yanapoa, shida zote zinafarijika, na mahitaji yanakidhika, na inafikisha kwa yanayotamaniwa, na mwisho mwema wapatikana, na kwa fadhila zake yule mwenye uso mtukufu mawingu (mvua) huombwa kunyesha, na Swalah na Salaam ziwe juu ahli zake na Maswahaba wake kwa kila muda na kila pumzi kwa idadi ya kadiri ya Ujuzi Wako)

 

 

ii) Baadhi ya sifa za kumtukuza mno katika Mawlid ya Barzanjiy:

 

“Katika saa ya kuzaliwa Mtume alihudhuria Aasiyah na Maryam kutoka Mbinguni.”

 

“Wanyama walitamka kwa Kiarabu kuwa leo imechukuliwa mimba ya Mtume.”

 

“Wanyama wakapeana khabari ya kuchukuliwa mimba ya Mtume.”

 

“Majini wakatoa khabari kwa watu kuwa imechukuliwa mimba ya Mtume.”

 

“Katika saa ya kuzaliwa Mtume alihudhuria Aasiyah na Maryam kutoka Mbinguni.”

 

“Wanavyuoni wameona ni jambo zuri watu kusimama wakati inapotajwa kuzaliwa Mtume.”

 

“Akamwona Allaah kwa macho yake.”

 

 

iii) Baadhi ya maneno ya shirki kwenye Mawlid Ya Nuwn

 

“Lau kuwa si Mtume asingepatikana Aadam wala Ibraahiym….. na ufalme wa Nabii Sulaymaan…”

 

“Manabii wote ni manaibu wa Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakimwendeshea kazi yake.”

 

 

iv) Baadhi ya maneno ya shirki katika uradi wa Nabhaaniy: 

 

“Lau kuwa si Nabii Muhammad tusingekuja ulimwenguni wala tusingeishi!”

 

 

 

2-Kumuomba du’aa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) badala ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

Du’aa huelekezwa kwake kama kusema: “Ee Rasuli nisaidie”, “Ee Rasuli niondoshee dhiki, shida zangu”. Hakuna kiumbe yeyote mwenye uwezo wa hayo isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Angekuwa na uwezo huo basi yasingemfika madhara, mateso, maudhi mbali mbali yaliyomsibu kutoka kwa makafiri. Allaah Alimuamrisha awaambie washirikina:

 

قُل لَّا أَمْلِكُ لِنَفْسِي نَفْعًا وَلَا ضَرًّا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ ۚ وَلَوْ كُنتُ أَعْلَمُ الْغَيْبَ لَاسْتَكْثَرْتُ مِنَ الْخَيْرِ وَمَا مَسَّنِيَ السُّوءُ ۚ إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ وَبَشِيرٌ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ﴿١٨٨﴾

Sema: “Siimilikii nafsi yangu manufaa yoyote wala dhara yoyote isipokuwa Apendavyo Allaah. Na lau ningekuwa najua ya ghayb, bila shaka ningelijikithirishia ya kheri, na wala lisingelinigusa ovu. Mimi si chochote isipokuwa ni mwonyaji na mbashiriaji kwa watu wanaoamini.” [Al-A’raaf: 188]

 

 

Na Akamwambia tena aseme:

قُلْ إِنَّمَا أَدْعُو رَبِّي وَلَا أُشْرِكُ بِهِ أَحَدًا﴿٢٠﴾

Sema: (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi namuomba Rabb wangu na wala simshirikishi na yeyote.”

 

قُلْ إِنِّي لَا أَمْلِكُ لَكُمْ ضَرًّا وَلَا رَشَدًا﴿٢١﴾

Sema: “Hakika mimi sikumilikieni dhara na wala uongofu.”

 

قُلْ إِنِّي لَن يُجِيرَنِي مِنَ اللَّـهِ أَحَدٌ وَلَنْ أَجِدَ مِن دُونِهِ مُلْتَحَدًا﴿٢٢﴾

Sema: “Hakika hakuna yeyote awezaye kunilinda na Allaah na wala sitoweza kupata mahali pa kukimbilia. [Al-Jinn: 20-22]

 

 

Na pia Akamuamrisha Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) :

 

قُلْ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

 Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mtu kama nyinyi, nafunuliwa Wahy kwamba: Hakika Muabudiwa wa haki wenu ni Ilaah Mmoja Pekee. Hivyo anayetaraji kukutana na Rabb wake, basi na atende ‘amali njema na wala asimshirikishe yeyote katika ‘ibaadah za Rabb wake.” [Al-Kahf: 110]

 

 

3-Kumuomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mbele ya kaburi lake:

 

Kuna wanaoelekea kaburi lake wanapofika Masjid Nabawiy Madiynah na kumuomba. Inavyopasa ni kuelekea Qiblah. Allaah Anakataza wazi kumshirikisha Yeye ndani ya Misikiti na hata penginepo, pale Anaposema:

 

وَأَنَّ الْمَسَاجِدَ لِلَّـهِ فَلَا تَدْعُوا مَعَ اللَّـهِ أَحَدًا﴿١٨﴾

Na kwamba Misikiti ni kwa ajili ya Allaah, basi msiombe yeyote pamoja na Allaah. [Al-Jinn: 18]

 

Naye Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam amekataza:

((لا تجعلوا قبري عيدًا))

((Msifanye kaburi langu ni sehemu ya kurudiwa rudiwa [kuendewa kila mara])). [Musnad Ahmad, Muswannaf 'Abdur-Razzaaq]

 

Na akasema:

 

   لعنة الله على اليهود والنصارى اتخذوا قبور أنبيائهم مساجد

((Allaah Amewalaani Mayahudi na Manaswara, wamefanya makaburi ya Manabii wao kuwa misikiti)). [Al-Bukhaariy  (425) Muslim (531)]

 

 

4-Kutawassul (kujikurubisha) kwa du’aa kupitia kwake:

 

Mfano kusema: “Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kwa jaha ya Rasuli Wako Unikidhie haja zangu kadhaa, au Uniokoe na janga au balaa fulani, Unighufurie dhambi zangu n.k.”

 

Baada yakufariki Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) haipasi kutawassal kwake. Maswahaba waliacha kutawassal kwake bali walitawassal kwa ami yake ‘Abbaas kwa kuwa alikuwa hai wakati huo kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

 عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ  (رضي الله عنه)  أَنَّ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) كَانَ إِذَا قَحَطُوا اسْتَسْقَى بِالْعَبَّاسِ بْنِ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ فَقَالَ:  "اللَّهُمَّ إِنَّا كُنَّا نَتَوَسَّلُ إِلَيْكَ بِنَبِيِّنَا فَتَسْقِينَا وَإِنَّا نَتَوَسَّلُ إِلَيْكَ بِعَمِّ نَبِيِّنَا فَاسْقِنَا"  قَالَ" فَيُسْقَوْنَ

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba ‘Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) aliomba mvua kulipokuwa na ukame kwa kutawassal kwa ‘Abbaas bin ‘Abdil-Muttwalib akisema: “Ee Allaah, tulikuwa tunatawassal Kwako kupitia Nabiy wako, Ukatunyeshea mvua, na sasa tunatawassal Kwako kupitia ‘ami wa Nabiy Wako basi tunyweshee mvua”. Akasema: Wakanyweshewa mvua. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Share

11-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kutufu Makaburi Kuwaomba Waliomo Kaburini

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

11- Kutufu Makaburi Kuwaomba Waliomo Kaburini

Alhidaaya.com

 

 

Miongoni mwa shirki kubwa ni kutufu makaburini, kuwaomba au kutawassal kwa walio makaburini. Maiti hawasikii du’aa wala hawaitikii, bali hawana uwezo wa kumnufaisha mtu wala kumdhuru! Dalili ni kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) zifuatazo:  

 

 إِنَّ الَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ عِبَادٌ أَمْثَالُكُمْ ۖ فَادْعُوهُمْ فَلْيَسْتَجِيبُوا لَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴿١٩٤﴾

Hakika wale mnaowaomba badala ya Allaah ni waja kama nyinyi. Hebu waiteni wakuitikieni ikiwa nyinyi ni wakweli. [Al-A’raaf: 194] 

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَا تَدْعُ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُكَ وَلَا يَضُرُّكَ ۖ فَإِن فَعَلْتَ فَإِنَّكَ إِذًا مِّنَ الظَّالِمِينَ﴿١٠٦﴾

Na wala usiombe badala ya Allaah visivyokufaa wala visivyokudhuru. Na ukifanya, basi hakika utakuwa miongoni mwa madhalimu. [Yuwnus: 106] 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَالَّذِينَ يَدْعُونَ مِن دُونِهِ لَا يَسْتَجِيبُونَ لَهُم بِشَيْءٍ إِلَّا كَبَاسِطِ كَفَّيْهِ إِلَى الْمَاءِ لِيَبْلُغَ فَاهُ وَمَا هُوَ بِبَالِغِهِ ۚ وَمَا دُعَاءُ الْكَافِرِينَ إِلَّا فِي ضَلَالٍ ﴿١٤﴾

Na wale wanaowaomba badala Yake, hawawaitikii kwa chochote isipokuwa kama anayenyosha viganja vyake viwili vya mikono kwenye maji ili yafikie kinywani mwake, na wala hayafikii hata kidogo.  Na du’aa za makafiri hazipo ila katika upotofu.  [Ar-Ra’d: 14] 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ ۚ قُلْ أَفَاتَّخَذْتُم مِّن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ لَا يَمْلِكُونَ لِأَنفُسِهِمْ نَفْعًا وَلَا ضَرًّا ۚ قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الْأَعْمَىٰ وَالْبَصِيرُ أَمْ هَلْ تَسْتَوِي الظُّلُمَاتُ وَالنُّورُ ۗ أَمْ جَعَلُوا لِلَّـهِ شُرَكَاءَ خَلَقُوا كَخَلْقِهِ فَتَشَابَهَ الْخَلْقُ عَلَيْهِمْۚ قُلِ اللَّـهُ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ وَهُوَ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿١٦﴾

Sema: “Ni nani Rabb wa mbingu na ardhi?” Sema: “Ni Allaah.” Sema: “Je, mnawafanya wengineo badala Yake kuwa walinzi na hali hawamiliki kwa ajili ya nafsi zao manufaa wala dhara?”  Sema: “Je, kipofu analingana sawa na mwenye kuona, au je, viza vinalingana sawa na nuru?” Au wamemfanyia Allaah washirika walioumba kama uumbaji Wake, kisha yakafanana maumbile kwao?  Sema: “Allaah ni Muumbaji wa kila kitu, Naye ni Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Mshindi, Asiyepingika.” [Ar-Ra’d: 16] 

 

 

Nukuu kutoka Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah (1/206) inasema:

 “…wala haijuzu kuomba du’aa kwa Mawalii au wengineo baada ya kufa kwao, bali inajuzu kuwaomba waja wema wakuombee. Wala haijuzu kutufu makaburi, kwani kutufu ni makhsusi kwa Ka’bah tukufu pekee. Atakayetufu makaburini kwa ajili ya kujikurubisha na watu wake humo ni shirki kubwa, japokuwa akiwa anakusudia kujikurubisha kwa Allaah tu! Hivyo ni bid’ah inayochukiza kabisa kwani haipasi kutufu makaburi wala kuswali kuyaelekea hata kama itakuwa ni kwa makusudio ya kutaka radhi za Allaah.” 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa): 

وَالَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِهِ مَا يَمْلِكُونَ مِن قِطْمِيرٍ ﴿١٣﴾

Na wale mnaowaomba badala Yake hawamiliki hata kijiwavu cha kokwa ya tende.

 

 

إِن تَدْعُوهُمْ لَا يَسْمَعُوا دُعَاءَكُمْ وَلَوْ سَمِعُوا مَا اسْتَجَابُوا لَكُمْ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكْفُرُونَ بِشِرْكِكُمْ ۚ وَلَا يُنَبِّئُكَ مِثْلُ خَبِيرٍ ﴿١٤﴾

 Mkiwaomba, hawasikii maombi yenu, na hata wakisikia, hawatakuitikieni.  Na Siku ya Qiyaamah watakanusha ushirikina wenu, na wala hakuna atakayekujulisha vilivyo kamaMwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Faatwir: 13-14] 

 

 

Bali Siku ya Qiyaamah utadhihirika uadui baina yao na watawakanusha kabisa kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)! 

 

وَمَنْ أَضَلُّ مِمَّن يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَن لَّا يَسْتَجِيبُ لَهُ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَهُمْ عَن دُعَائِهِمْ غَافِلُونَ﴿٥﴾

 

“Na nani aliyepotoka zaidi kuliko ambaye anayeomba asiyekuwa Allaah ambaye hamuitikii mpaka Siku ya Qiyaamah; nao wala hawatambui  maombi yao.”

 

 

وَإِذَا حُشِرَ النَّاسُ كَانُوا لَهُمْ أَعْدَاءً وَكَانُوا بِعِبَادَتِهِمْ كَافِرِينَ﴿٦﴾

Na pale watakapokusanywa watu, (miungu ya uongo) watakuwa ni maadui wao, na watakuwa wenye kuzikanusha ‘ibaadah zao. [Al-Ahqaaf: 5- 6] 

 

 

 

Washirikina kabla ya Uislamu walikuwa wakiomba masanamu ya Al-Laata, ‘Al-‘Uzza na wengineo, na hawakuwa wakiitakidi kuwa wana uwezo wa kuumba au kuteremsha mvua bali walidai kuwa yanawakurubisha kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na kwamba masanamu hayo ni kama viombezi kwao. Kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa): 

 

وَالَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ إِنَّ اللَّـهَ يَحْكُمُ بَيْنَهُمْ فِي مَا هُمْ فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي مَنْ هُوَ كَاذِبٌ كَفَّارٌ ﴿٣﴾

na wale waliojichukulia badala Yake walinzi (wakisema): “Hatuwaabudu isipokuwa ili wapate kutukurubisha kwa Allaah tumkaribie” Hakika Allaah Atahukumu baina yao katika yale waliyokhitilafiana nayo. Hakika Allaah Hamwongoi aliye muongo, kafiri. [Az-Zumar: 3] 

 

Basi hakuna tofauti na wanaoomba wakaazi wa makaburi kwani sanamu, makaburi, matwaghuti… yote yana maana moja ya kuabudu au kuomba asiyekuwa Allaah; ikiwa ni maiti au hai, na sababu za kuomba ni kama hizo. Anakanusha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) hayo Anaposema:

 

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا ﴿٥٦﴾

Sema: “Iteni wale ambao mnadai (ni waabudiwa) pasi Naye, basi hawamiliki kukuondesheeni dhara na wala kuihamisha (kwa mwengine).” [Al-Israa: 56] 

 

 

Na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anamwambia Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) awajibu washirikina: 

 

 قُلْ أَفَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ إِنْ أَرَادَنِيَ اللَّـهُ بِضُرٍّ هَلْ هُنَّ كَاشِفَاتُ ضُرِّهِ أَوْ أَرَادَنِي بِرَحْمَةٍ هَلْ هُنَّ مُمْسِكَاتُ رَحْمَتِهِ ۚ قُلْ حَسْبِيَ اللَّـهُ ۖ عَلَيْهِ يَتَوَكَّلُ الْمُتَوَكِّلُونَ﴿٣٨﴾

Sema: “Je, mnaonaje wale mnaowaomba badala ya Allaah; ikiwa Allaah Atanikusudia dhara; je, wao wataweza kuondosha dhara Yake? Au Akinikusudia rahmah; je wao wataweza kuizuia rahmah Yake?” Sema: “Ananitosheleza Allaah”, Kwake watawakali wenye kutawakali. [Az-Zumar: 38] 

 

Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُل لَّا أَمْلِكُ لِنَفْسِي نَفْعًا وَلَا ضَرًّا إِلَّا مَا شَاءَ اللَّـهُ ۚ وَلَوْ كُنتُ أَعْلَمُ الْغَيْبَ لَاسْتَكْثَرْتُ مِنَ الْخَيْرِ وَمَا مَسَّنِيَ السُّوءُ ۚ إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ وَبَشِيرٌ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ﴿١٨٨﴾

Sema: “Siimilikii nafsi yangu manufaa yoyote wala dhara yoyote isipokuwa Apendavyo Allaah. Na lau ningekuwa najua ya ghayb, bila shaka ningelijikithirishia ya kheri, na wala lisingelinigusa ovu. Mimi si chochote isipokuwa ni mwonyaji na mbashiriaji kwa watu wanaoamini.” [Al-A’raaf: 188] 

 

Na pia Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَمَا لَهُمْ فِيهِمَا مِن شِرْكٍ وَمَا لَهُ مِنْهُم مِّن ظَهِيرٍ ﴿٢٢﴾

Sema: “Ombeni wale mnaodai kwa dhana (ni waabudiwa) badala ya Allaah, hawamiliki hata uzito wa sisimizi mbinguni wala ardhini, na wala hawana humo ushirika Naye, na wala Yeye (Allaah) Hana msaidizi miongoni mwao.” [Sabaa: 22] 

  

Tahadhari Muislamu kuingia katika shirki kubwa juu ya kuwa hao wanaoombwa hawawezi kukuitikia du’aa zako bali elekea kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ambaye Ndiye Mwenye uwezo wa kukunufaisha au kukuondoshea madhara kama Anavyosema: 

 

أَمَّن يُجِيبُ الْمُضْطَرَّ إِذَا دَعَاهُ وَيَكْشِفُ السُّوءَ وَيَجْعَلُكُمْ خُلَفَاءَ الْأَرْضِ ۗ أَإِلَـٰهٌ مَّعَ اللَّـهِ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ ﴿٦٢﴾

Au nani Anayemuitika mwenye dhiki mno anapomwomba, na Akamuondoshea ouvu na Akakufanyeni makhalifa wa ardhi? Je, yuko mwabudiwa pamoja na Allaah? Ni machache mno mnayokumbuka. [An-Naml: 62] 

 

 

Aayah hiyo aliisoma mtu alipofikwa na balaa la kukaribia kuuliwa, alipoisoma Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alimuokoa. [Tafsiyr Ibn Kathiyr] 

 

Tena Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Yuko karibu mno nawe na Mwenye kuitikia du’aa za kila anayemuomba, Anasema: 

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu (kwa ujuzi); Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186] 

 

 

Na fuata mafunzo Swahiyh kama alivyofundisha Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba unapozuru au kupitia makaburi usome du’aa: 

 

السَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ، (وَيَرْحَمُاللَّهُالْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّاوَالْمُسْتَأْخِرِينَ) أَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ. 

Assalaamu ’Alaykum ahlad-diyaar minal Mu-uminiyna wal Muslimiyn, wainnaa In Shaa Allaahu bikum laahiquwn. (Wa yarhamu-Allaahu al-mustaqdimiyna minnaa wal musta-akhiriyna). As-alu-Allaaha lanaa walakumul-’aafiyah.

 

Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za Waumini na Waislamu, nasi apendapo Allaahtutakutana nanyi (Na Allaah Awarehemu wa mwanzo na wa mwisho). Namuomba Allaah Atupe sisi nanyi afya njema. [Hadiyth ya Buraydah bin Al-Huswayb (Radhwiya Allaahu ‘anhu) - Muslim (2/671) [975], Ibn Maajah na tamshi lake (1/494) [1547] kutoka kwa Buraydah  (Radhwiya Allaahu ‘anhu). Yaliyo katika mabano ni Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) iliyopokelewa na Muslim (2/671) [974].] 

 

 

 

Share

12-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kuchinja Kwa Niyyah Ya Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

12 -Kuchinja Kwa Niyyah Ya  Asiyekuwa Allaah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaharamisha: 

 

 

حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ وَلَحْمُ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ لِغَيْرِ اللَّـهِ بِهِ وَالْمُنْخَنِقَةُ وَالْمَوْقُوذَةُ وَالْمُتَرَدِّيَةُ وَالنَّطِيحَةُ وَمَا أَكَلَ السَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى النُّصُبِ وَأَن تَسْتَقْسِمُوا بِالْأَزْلَامِ ۚ ذَٰلِكُمْ فِسْقٌ

 

Mmeharamishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na kilichotajiwa asiyekuwa Allaah katika kuchinjwa kwake, na aliyenyongwa au aliyepigwa akafa, au aliyeporomoka, au aliyepigwa pembe, na aliyeliwa na mnyama mwitu, isipokuwa mliyewahi kumchinja kihalali (kabla ya kufa); na waliochinjwa kwa ajili ya ‘ibaadah ya waabudiwa, na kupiga ramli kwa mishale. Hayo kwenu ni ufasiki. [Al-Maaidah: 3] 

 

 

Sababu kuchinja ni ‘ibaadah tukufu kabisa Ameamrisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ichinjwe kwa ajili Yake Pekee. 

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾

Basi swali kwa ajili ya Rabb wako na chinja kwa ajili Yake. [Al-Kawthar: 2] 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٢﴾

Sema: “Hakika Swalaah yangu, na kuchinja kafaara na ‘ibaadah zangu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah Pekee Rabb wa walimwengu.” [Al-An’aam: 162] 

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) amelaani mwenye kuchinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Hadiyth ya ‘Aliy bin Abiy Twaalib (Radhwiya Allaahu ‘anhu): 

 

عَنْ عَلِيِّ بن أبي طالب (رضي الله عنه) قَالَ: حَدَّثَنِي رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) بأرْبَعِ كَلِمَاتٍ: ((لَعَنَ اللَّهُ مَنْ ذَبَحَ لِغَيْرِ اللَّهِ, وَلَعَنَ اللَّهُ مَنْ لَعَنَ وَالِدَيْهِ, وَلَعَنَ اللَّهُ مَنْ آوَى مُحْدِثًا, وَلَعَنَ اللَّهُ مَنح مَنَارَ الأَرْضِ )) 

Imepokewa kutoka kwa ‘Aliy bin Abiy Twaalib (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alinihadithia maneno manne: ((Allaah Amemlaani anayechinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah, na Allaah Amemlaani anayewalaani wazazi wake, na Allaah Amelaani anayemkaribisha na kumhami mhalifu, na Allaah Amelaani anayemlaani mzazi wake, na Allaah Amelaani anayebadilisha mipaka ya ardhi [anayomiliki])) [Muslim] 

 

 

Pia: 

 

حديث ثَابِتُ بْنُ الضَّحَّاكِ قَالَ : نَذَرَ رَجُلٌ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنْ يَنْحَرَ إِبِلاً بِبُوَانَةَ فَأَتَى النَّبِىَّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: ‏إِنِّى نَذَرْتُ أَنْ أَنْحَرَ إِبِلاً بِبُوَانَةَ. فَقَالَ النَّبِىُّ -صلى الله عليه وسلم : ((هَلْ كَانَ فِيهَا ‏وَثَنٌ مِنْ أَوْثَانِ الْجَاهِلِيَّةِ يُعْبَدُ)) قَالُوا: لاَ. قَالَ: ((هَلْ كَانَ فِيهَا عِيدٌ مِنْ أَعْيَادِهِمْ )) ‏قَالُوا : لاَ. قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((أَوْفِ بِنَذْرِكَ فَإِنَّهُ لاَ وَفَاءَ لِنَذْرٍ ‏فِى مَعْصِيَةِ اللَّهِ وَلاَ فِيمَا لاَ يَمْلِكُ ابْنُ آدَمَ )). وصححه الألباني 

Imepokelewa kutoka kwa Thaabit ibn Adhw-Dhwahhaak (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba: “Mtu mmoja aliweka nadhiri kuchinja ngamia sehemu ya Buwaanah. Akaja kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Nimeweka nadhiri kuchinja ngamia Buwaanah”.  Akasema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Je kuliweko masanamu ya kijaahiliyyah (kabla Uislamu) yakiabudiwa?”. Wakasema:  “Hapana” Akasema: ((Je kuliweko sherehe za kijaahiliyyah zikifanywa hapo?)). Wakasema: “Hapana” Rasuli wa Allaahh (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Timiza nadhiri yako, kwani hakuna kutimiza nadhiri katika kumuasi Allaah, wala katika ambayo hayamiliki bin Aadam)). [Abuu Daawuwd na ameisahihisha Al-Albaaniy] 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah (1/226) wamefutu:  “Kuchinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah ni shirki na hukmu ya kichinjo ni hukmu ya nyamafu (mzoga) haijuzu kuliwa nyama yake hata kama imetajwa Jina la Allaah ikiwa imehakiki kuwa imechinjwa ghairi ya Allaah.” 

 

 

Na Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema katika Majmuw' Fataawa Ibn ‘Uthaymiyn (2/148):  “Kuchinja kwa ajili kwa ajili ya aisyekuwa Allaah ni shirki kubwa kwa sababu kuchinja ni ‘ibaadah, kwa hiyo anayechinja kwa ajili (niyyah) asiyekuwa Allaah ni mshirikina ambaye shirki yake inamtoa nje ya Uislamu – tunajikinga na Allaah – ikiwa amechinja kwa ajili ya Malaika au kwa ajili ya Nabiy yeyote au kwa ajili ya Khaliyfah yeyote au kwa ajili ya awliyaa (waja wema) au kwa ajili ya Mwanachuoni yeyote. Yote ni kumshirikisha Allaah (Subhanaahu wa Ta’aalaa) na inamtoa nje ya Uislamu. Na kuhusu kula nyama ya vichinjo hivyo ni haraam kwa sababu amechinjwa kwa ajili ya asiyekuwa Allaah na kila kinachochinjwa kwa ajili ya chochote ghairi ya Allaah au amechinjwa juu ya jiwe la madhabahu (mazimwi) ni haraam.”  

 

 

Hadiyth ifuatayo inadhihirisha kwamba hata ikiwa ni kiasi kidogo vipi kitu kinachokurubishwa pasi na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa kuchinja, huwa ni shirki na hatari yake humuingiza mtu Motoni:  

 

((دَخَلَ الْجَنَّةَ رَجُلٌ فِي ذُبَاب، وَدَخَلَ النَّار رَجُلٌ فِي ذُبَاب)): قَالُوا: وَكَيْفَ ذَلِكَ يَا رَسُولَ الله؟ قَالَ: ((مَرَّ رَجُلانِ علَى قَوْمٍ لَهُمْ صَنَمٌ لاَ يَجُوزُهُ أحَدٌ حَتَّى يُقَرِّبَ لَهُ شَيْئاً، فَقَالُوا لإَحَدِهِمَا: قَرِّبْ، قَالَ: لَيْسَ عِنْدِي شَيْءٌ أُقَرِّبَهُ، قَالُوا بِه: قَرِّبْ وَلَوْ ذُباَبًا، فَقَرَّبَ ذُبَاباً، فَخَلُّوا سَبِيْلَهُ، فَدَخَلَ النَّارَ، وَقَالُوا لِلآخر: قَرِّبْ، فَقَالَ: مَا كُنْتُ لأُقَرِّبَ لأحَدٍ شَيْئًا دُونَ الله عَزَّ وَجَلَّ. فَضَرَبُوا عُنقَهُ، فَدَخَلَ الْجَنَّةَ)) 

((Mtu mmoja ameingia Jannah kwa nzi, na ameingia Motoni mtu kwa ajili ya nzi)).  Wakasema: Vipi hivyo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Watu wawili walipitia mbele ya watu walikuwa na sanamu lao, hapiti mtu hadi ajikurubishe kwa kuchinja. Wakamwambia mmoja wao: Jikurubishe!  [Chinja!]  Akasema:  Sina kitu cha kujikurubisha. Wakasema: Jikurubishe japo kwa nzi.  Akajikurubisha kwa nzi.  Wakamwachia apite njia akaingia Motoni.  Wakawambia mwengine: Jikurubishe!  Akasema:  Sikuwa najikurubisha [nachinja] kwa yeyote pasi na Allaah ‘Azza wa Jalla. Wakampiga shingo [wakamuua] akaingia Jannah)). [Ahmad, Fataawaa Shaykh Ibn Baaz] 

 

 

Shaykh Fawzaan bin Fawzaan akifafanua Hadiyth hiyo anasema:  

“[Mtu wa kwanza] Ametoa udhuru kutokuwa na kitu. Hakusema “hakika kuchinja pasi na Allaah haijuzu au ni munkari” – Tunajikinga kwa Allaah.  Na hii inafahamika kwamba lau angelikuwa ana  mnyama wa kuchinja angelichinja. Wakamwambia: “Jikurubishe walau kwa nzi!” Akajikurubisha kwa nzi, yaani akafanya hivyo kwa ajili ya sanamu wakamwachia apite njia, akaingia Motoni kwa sababu ya shirki. Amejikurubisha pasi na Allaah, na 'ibra (zingatio) hapa ni niyyah na kusudio wala sio kuhusu kinachochinjwa.  Na kwamba hakuchukia jambo hili wala hakujiepusha nalo, bali ametoa udhuru kutokuwa na kitu na kwa hivyo amengia Motoni – Tunajikinga kwa Allaah. 

 

Na wakamwambia mwengine: “Jikurubishe!” Akasema:  “Sikuwa ni mwenye kuchinja chochote kwa ajili ya asiyekuwa Allaah ‘Azza wa Jalla.” Amejiepusha na amechukia shirki. Wakampiga shingo yake, kwa maana wamemuua akaingia Jannah kwa sababu ya Tawhiyd. 

 

Hivyo basi katika Hadiyth hii tukufu kuna mafunzo muhimu:  

 

 

Kwanza:  Hadiyth inaruhusu kuelezea habari za ummah zilizopita na kuelezea ilivyothibiti kwa ajili ya kuwaidhi na zingatio. 

 

 

Pili:  Katika Hadiyth kuna dalili ya kuharamishwa kujikurubisha kwa kuchinja pasi na Allaah, na mwenye kujikurubisha pasi na Allaah, atakuwa ametenda shirki kwa sababu mtu aliyeua nzi ameingia Motoni hata ikiwa ni kitu kichafu cha kutemwa (kidogo, duni mno). Na mtu wa pili amechukia shirki na amejiepusha japokuwa ilikuwa ni kitu cha kuchukizwa (duni) akaingia Jannah. 

 

 

Tatu: Kama alivyosema Shaykh (Rahimahu Allaah) kuhusu mas-alah ya niyyah ya 'amali za moyo, japokuwa ni kitu kichafu cha kutemwa (kidogo, duni mno) lakini itambulike kuwa niyyah ni 'amali ya moyo.  

 

 

Nne:  Kama alivyosema Shaykh (Rahimahu Allaah) kuhusu wepesi wa bin Aadam kukaribia Jannah na Moto ni kama alivyosema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ((Jannah iko karibu zaidi kwa mmoja wenu kuliko nyuzi za viatu vyake, na Moto kama hivyo)). [Al-Bukhaariy]  

 

Huyu amepigwa shingo yake (ameuliwa) akaingia Jannah. Na yule wamemwachia njia akaingia Motoni.   

 

Tano: Kwamba mtu aliyeua  nzi alikuwa Muumini, akaingia Motoni kwa sababu ya kujikurubisha kwake kwa nzi, kwa sababu angelikua kafiri, angeliingia Motoni kwa kufru yake si kwa kujikurubisha kwa nzi. Akadhihirisha kwamba alikuwa Muumini, na mas-alah haya ni khatari sana! 

 

Basi wako wapi wanaochinja kwa ajili ya makaburi, na majini, na mashaytwaan, na kwa ajili ya ardhi, na wachawi?

 

Akaonyesha kwamba shirki kubwa kabisa inamtoa mtu nje ya Dini japokuwa ikiwa ni kitu chepesi. Hivyo basi, suala la Tahwiyd na  ‘Aqiydah hayasamehe hayo.” [Sharh Kitaab At-Tawhiyd – Baab maa jaa-a fiy adhdhab-h li-ghayri-LLaah]  
 

     

 

 

Share

13-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kutundika Kitu Kwa Ajili Ya Kinga, Kumlinganisha Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

13- Kutundika Kitu Kwa Ajili Ya Kinga Na Kumlinganisha Allaah

Alhidaaya.com

 

 

Katika kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kutundika vitu ukatani au milangoni n.k. Itikadi ya kitendo hiki ni aina mbili;

 

Kwanza: kutundika kwa kuitakidi kwamba hicho kitu kilichotundikwa ni kinga ya jicho au husda n.k. Vinavyotundikwa huenda ikawa ni fremu za Aayah katika Qur-aan, au du’aa au Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Au wengine hutundika vitu kama pilipili na ndimu, aina ya vijiwe vya buluu vyenye jicho n.k.  Yote haya ni shirki kwa hiyo haijuzu abadani kwa sababu hakuna baya lolote la kumdhuru mtu isipokuwa kama Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amelikidhia kama Anavyosema:

 

مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۗ وَمَن يُؤْمِن بِاللَّـهِ يَهْدِ قَلْبَهُ ۚ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴿١١﴾

Hausibu msiba wowote isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na yeyote   anayemuamini Allaah, (Allaah) Huuongoza moyo wake. Na Allaah kwa kila kitu ni Mjuzi. [At-Taghaabun: 11]

 

Na kinyume chake ni kukosa kutawakali Kwake Subhaanahu wa Ta’aalaa na kukosa kufuata kinga iliyothibiti. Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Hukaym ifuatayo imethibitisha katazo hilo:  

 

((مَنْ تَعَلَّقَ شَيْئًا؛ وُكِّلَ إِلَيْهِ)) رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالتِّرْمِذِيُّ

((Atakayetundika kitu (kuitakidi ni kinga) basi amejiweka katika ulinzi wa hicho kitu alichokivaa)) [na kitamdhalilisha]. [Ahmad na At-Tirmidhiy. Hadiyth Marfu’w]

 

Tanbihi: Mifano ya vitu vinavyotundikwa kuitakidi kuwa kitamfaa au kumzuia shari ni: talasimu, hirizi, zindiko na vinginveyo kama ilivyobainishwa katika makala hizi.  

 

Haijuzu kabisa kutundikia kitu kuitakidi ni kinga, bali inatosha kabisa kutawakali kwa Allaah  kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema  :

 

وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ

Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza.  [Atw-Twalaaq: 3]

 

Na mafunzo Swahiyh ya kujikinga ni kama ilivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

 

عن خَوْلَةَ بِنْتَ حَكِيمٍ (رضي الله عنها) قالت: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ:  ((مَنْ نَزَلَ مَنْزلاَ ثُمَّ قَالَ: "أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ" لَمْ يَضُرَّهُ شَيْءٌ حَتَّى يَرْتَحِلَ مِنْ مَنْزِلِهِ ذَلِكَ)) رواه مسلم

Imepokelewa toka kwa Khawlat bint Hakiym (Radhiwa Allaahuu ‘anhaa) kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Atakayefikia mahali kisha akasema: 

أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ

 

A’uwdhu bikalimati-LLaahit-taammati min sharri maa Khalaq' (Najilinda kwa maneno ya Allaah yaliyotimia na shari ya Alichokiumba), hakuna kitakachomdhuru hadi atakapoondoka mahali pake hapo)). [Muslim]

 

 

Mafunzo mengine sahihi ni kusoma Adhkaar na nyiradi za asubuhi na jioni zilizothibiti.

 

Ama kuhusu kutundika Qur-aan, baadhi ya watu wanaona ni jambo la kupendeza lakini hakika haijuzu kwa sababu Qur-aan imeteremshwa kwa ajili ya Mwongozo, mawaidha, ukumbusho, na kusomwa na kufanyia kazi maamrisho yake na kuacha makatazo yake, na wala si kwa ajili ya kutundikwa. 

 

Ibnul-‘Arabiyy Al-Maalikiyy (Rahimahu Allaah) amesema:

“Kutundika Qur-aan si katika Sunnah, bali Sunnah ni kuisoma bila ya kuitundika.”

 

 

Aghlabu ya watu hutundika Aayatul-Kursiyy au Al-Maw’idhataan na Suwratul-Ikhlaasw ambazo ni nyepesi kabisa kuzihifadhi na kuzisoma na ndizo zilizothibiti katika mafunzo Swahiyh kwamba ni kinga ya Muislamu. Basi kwanini mtu atundike badala ya kuzisoma na kuzihifadhi?

 

Picha za baadhi ya vitu ambavyo baadhi ya watu wanavitundika wakiamini ni kinga:

 

                                       

 

 

     

                          

  

 

Pia kutundika vitu madukani au majumbani kama pilipili, ndimu n.k.

 

         

 

 

        

 

 

 

Pili: Kutundika Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ukutani mifano kama ifuatavyo:

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Haijuzu kutundika picha kama hizo, kwani haiwezekani kuwa Muumba na aliyeumbwa wawe katika daraja moja, hata kama niyyah ni kupamba nyumba au kudhihirisha mapenzi yao, kwa sababu wengi hudai kuwa hawakusudii kumlinganisha sawa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Basi kujiepusha na hilo ni bora hata kama mtu haitakidi hilo, kwani kukaa mbali na utata ndio njia ya salama katika Dini ya mtu.

 

Kadhaalika, Wanachuoni wamekemea jambo hili kama ifutavyo:

 

Fatwa ya 1 - Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah Wal-Iftaa imepitia yaliyofikishwa kwa Mufti Mkuu kutoka kwa muulizaji Humuwd ‘Abdul-Aziyz As-Saayigh kwa marejeo Nambari 6860 9/11/1421H.

 

Muulizaji ameuliza swali na haya hapa maelezo yake:

“Allaah Akuhifadhini, na kukhofia yanayojiri katika Dini hii na kutilia mkazo yanayofisidi ‘Aqiydah na ambayo yanaenea kwa Ummah huu kutoka kwa maadui wa Allaah na wa Dini Yake na wepesi wa watu kufuata mambo wanayodhania ni madogo mno lakini kumbe ni makubwa mno na ikawa kuondosha madhara yake ni vigumu. Kama ilivyokuwa hali katika watu wa Nuwh na masanamu yao; walivyoanza kuweka picha za waja wema wakaanza kuziabudu wakidhania ni jambo jema kumbe ni shirki iliyowasababisha watu waliofuata kuabudu masanamu.

 

Tunadhihirisha mbele yenu aina mbali mbali za picha zilizotayarishwa kuwekwa pande mbili; upande kuna Jina la Allaah (’Azza wa Jalla) na upande wa jina la Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Wala sijui lipi bado litakalojiri baada ya haya! Na baadhi ya ndugu wamewaandikia Baraza la Fatwa maombi haya ili kufuatilia maovu ya ‘Aqiydah wakitaraji mtoe maoni yenu ambayo huenda ikiwa ni sababu ya ufumbuzi na tiba ya kuondosha uovu huu, Allaah Awathibitishieni na Akulipeni kwa kuwanufaisha waja Wake Katika utiifu Wake.”

 

Jibu la Baraza la Fatwa:

 

Haijuzu kuandika Jina la Allaah Aliyetukuka [Allaah] pamoja na [Muhammad] jina la Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) sambaba katika karatasi au kwenye ubao [au vitambaa], au kutundika ukutani [kwa hali yoyote]. Huko ni kupindukia mipaka kwa haki yake Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na kumlinganisha yeye sawa na Allaah. Haya ni mas-alah miongoni mwa masuala ya shirki na hali yeye mwenyewe amekataza katika kauli yake, aliposema:

“Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi ni mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Rasuli Wake.”

 

Na hivyo ni wajibu kuondosha picha hizo au karatasi na kufutilia mbali maandishi kama hayo katika kuta au popote penye aina hizo za picha, ili tuilinde ‘Aqiydah na kufuata wasia wa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). 

Wa biLLaahi At-tawfiyq. Wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyinaa wa ‘alaa aalihi wa swahbihi wa sallam.

 

[Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah Lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah Wal-Iftaa]

 

 

Fatwa ya 2:  Fatwa ya Shaykh Ibn ‘Uthaymin (Rahimahu Allaah):  

Hakika kuandikwa Jina la Allaah (الله) upande mmoja na jina la (محمد) upande wa pili, yakiwa majina hayo yako sambamba na kama hivi:

 الله   ***  محمد     yanamfanya anayetazama kuona kwamba wako katika cheo kimoja na hali Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimjibu mtu mmoja aliyemwambia Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) “Atakavyotaka (au Akipenda) Allaah [In Shaa Allaah) na ukataka wewe.” Akamjibu: ((Je umenilinganisha mimi kuwa sawa Allaah? Bali sema: Akipenda Allaah [In Shaa Allaah] pekee)).

 

Na ikiwa maandishi kama hayo yamewekwa hivyo mbele ya wanaoswali, yatakuwa ni sababu ya kuwashughulisha watu na Swalaah zao. Pia ‘Ulamaa wakubwa wamechukizwa [na kukataza] kuandikwa kitu mbele ya Qiblah kwa sababu kitamshughulisha na kumshawishi mwenye kuswali. Hivyo, haipasi kuandikwa hivyo; namaanisha الله   ***  محمد    Na popote palipoandikwa hivyo panapaswa kufutiliwa mbali!

Na katika sharh yake ya Kitabu cha Buluwghul-Maraam, Kitabu cha Swalaah, Mlango wa Misikiti, Mkanda namba 16 upande wa pili, anasema Shaykh kuwa, kwa uchache maandishi kama haya ni shirk ndogo.”

Ameandika: Muhammad Bin Swaalih Al-‘Uthaymiyn 9/1/1420H.

 

 

Basi ndugu Waislamu tutahadhari kutundika vitu kama hivyo au chochote kile mfano wa hivyo kwa kuitakidi ni kinga au baraka.

 

 

 

 

Share

14-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kuvaa Kitu Kwa Ajili Ya Kinga

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

14 -Kuvaa Kitu Kwa Ajili Ya Kinga

Alhidaaya.com

 

 

Itikadi za watu kuvaa vitu au kujifunga navyo mwilini kwa kuepusha au kujikinga na kijicho, husda na madhara mengineyo. Jambo hili halijuzu kwa sababu hivyo vitu havina uwezo wa hayo wala hakuna atakayeweza kumuondoshea mtu madhara isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Anasema:

 

وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ وَإِن يَمْسَسْكَ بِخَيْرٍ فَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٧﴾

Na Allaah Akikugusisha kwa dhara, basi hakuna yeyote wa kukuondolea hiyo isipokuwa Yeye; na Akikugusisha khayr, basi Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. [Al-An’aam:  17]

 

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameharamisha hayo  katika Hadiyth mbali mbali:

 

 عَنْ قَيْسِ بْنِ السَّكَنِ الأَسَدِيِّ قَالَ: دَخَلَ عَبْدُ اللهِ بْنُ مَسْعُودٍ رضي الله عنه عَلَى امْرَأَةٍ، فَرَأَى عَلَيْهَا خَرَزًا مِنَ الحُمْرَةِ، فَقَطَعَهُ قَطْعًا عَنِيفًا، ثُمَّ قَالَ: إِنَّ آلَ عَبْدِ اللهِ عَنِ الشِّرْكِ أَغْنِيَاءُ، كَانَ مِمَّا حَفِظْنَا عَنِ النَّبِيِّ صلّى الله عليه وسلّم: ((إِنَّ الرُّقَى وَالتَّمَائِمَ وَالتِّوَلَةَ شِرْكٌ)) رواه الحاكم وقال: " صحيح الإسناد "، ووافقه الذّهبي والألبانيّ في "الصّحيحة" (برقم 331).

Imepokelewa kutoka kwa Qays bin As-Sakan Al-Asadiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Abdullaah bin Mas‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) aliingia kwa mwanamke ambaye alivaa shanga nyekundu, akazikatilia mbali kisha akasema: “Hakika ahli ya ‘Abdullaah hawahitaji shirki!”. Akasema pia: “Katika ambayo amehifadhi kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni: ((Hakika Ar-Ruqaa (zisizothibiti), At-Tamaaim, At-Tiwaalah ni shirki).)) [Al-Haakim amesema Isnaad Swahiyh na ameikubali Adh-Dhahabiy na Al-Albaaniy katika Asw-Swahiyhah (331)]

 

At-Tamaaim:  Wanachofungwa watoto (kama kitambaa cheusi au nyuzi n.k.) shingoni (au mkononi) kukinga jicho baya.

 

 

Ar-Ruqaa au Al-‘Azaaim: Ni tabano au azima inayosomwa. Imeruhusiwa tu inapokuwa haina shirki. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameiruhusu inapokuwa hali ya kudonelewa na mdudu sumu au anapopatwa mtu na jicho baya (au husda) au homa.

 

 

At-Tiwaalah (mvuto wa ndere): Kinachodaiwa kuwa kinasababisha mwanamke apendwe zaidi na mumeme au mume apendwe zaidi na mkewe.

 

 

Hadiyth nyenginezo zinazoharamisha kuvaa vitu kwa ajili ya kinga ni zifuatazo:

 

عَنْ أَبِي بَشِيرٍ الأَنْصَارِيِّ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) أَنَّهُ كَانَ مَعَ رَسُولِ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي بَعْضِ أَسْفَارِهِ، فَأَرْسَلَ رَسُولاً, أَنْ ((لاَ يَبْقَيَنَّ فِي رَقَبَةِ بَعِيرٍ قِلادَةٌ مِنْ وَتَرٍ أَوْ قِلادَةٌ إِلاَّ قُطِعَتْ)).

Imepokewa kutoka kwa Abu Bashiyr Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba alikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari mojawapo. Akamtuma mjumbe kuamrisha kwamba: ((Kusiachwe kidani cha uzi au kidani chochote katika shingo za ngamia isipokuwa kikatwe)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Pia:

 

 رَوَى أَحْمَدُ عَنْ رُوَيْفِعٍ قَالَ؛ قَالَ لِي رَسُولُ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((يَا رُوَيْفِعُ، لَعَلَّ الْحَيَاةَ سَتَطُولُ بِكَ؛ فَأَخْبِرِ النَّاسَ أَنَّ مَنْ عَقَدَ لِحْيَتَهُ، أَوْ تَقَلَّدَ وَتَرًا، أَوِ اسْتَنْجَى بِرَجِيعِ دَابَّةٍ أَوْ عَظْمٍ؛ فَإِنَّ مُحَمَّدًا بَرِيءٌ مِنْهُ))

Ahmad amepokea kutoka kwa Ruwayfi’ ambaye amesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameniambia: ((Ee Ruwayfi’! Huenda ukaishi zaidi baada yangu. Kwa hiyo wajulishe watu kwamba: Yeyote atakayefunga fundo ndevu zake, au akaweka nyuzi au mshipi shingoni mwake [kuwa ni talasimu] au akastanji na mkojo wa mnyama au mfupa, basi Muhammad amejitenga naye)). [Ahmad, Abuu Daawuwd]

 

 

Vitu ambavyo aghlabu hutumiwa na watu kuvivaa au kujifunga wakiamini vinawakinga:

 

 

a) Hirizi za vitambaa vyenye maandishi ndani ikiwa ya Quraan au mengineyo.

 

 

                   

 

   

 

 

 

 

 

b) Mtoto mchanga kupakwa masinzi au wanja usoni au kuandikwa Jina la Allaah!

 

 

c) Kuwapaka watoto wachanga wanja usoni na nakshi za nyota na mwezi, kwa kuamini ule wanja unazuia 'ayn (kijicho).  

 

 

d) Anapolazwa mtoto mchanga kukiwa chini ya mto wake vitu kama kisu, ndimu n.k.

 

 

e) Kuvalishwa vyuma mkononi.

 

f) Kuvalishwa mtoto mchanga au hata wakubwa, kidani chenye lakti ya Aayatul-Kursiy au Jina la Allaah! Ni jambo linalotendwa na wengi! Hakika ni kosa kubwa kwani ni kudhihirisha kutokumadhimisha Allaah kwa sababu kidani hicho anaingia nacho mtu chooni. Juu ya hivyo ni kuitakidi kuwa kinamkinga mtu na shari, uhasidi, jicho n.k. Imeshatangulia Hadiyth mbali mbali na Fataawa za ‘Ulamaa kukataza haya, na rejea mlango wa “Kutundika vitu”. 

 

g) Kuvalishwa kitambaa cheusi mkononi wengine wanatia mvuje ndani yake yenye harufu mbaya kuepusha majini.

 

h) Mapambo yenye kuandikwa Aayah za Qur-aan:

 

 

 

 

i) Mapambo ya vijiwe vya rangi ya buluu, vinginevyo vina jicho.

 

   

             

    

 

   

            

 

 

 

           

 

 

           

 

 

 

 

j) Kuvaa pete au mapambo yenye vito rangi kadhaa kwa kuitakidi rangi hizo zina maana ya wanachoita ‘bahati nzuri’ au kuleta hali fulani njema kutokana na tarehe au miezi ya kuzaliwa:

 

           

 

 

 

 

Share

15-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kuapa Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

15- Kuapa Kwa Asiyekuwa Allaah

Alhidaaya.com

 

 

 

Haijuzu Muislamu kuapa isipokuwa kwa Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa sababu kuapia kwa yeyote au chochote ni kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Inavyopasa kuapa ni ima kusema: “Wa-Allaahi”, au “BiLLaahi” au “Ta-Allaahi” kama ilivyothibiti katika Qur-aan. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kuapia chochote isipokuwa kwa Jina la Allaah akasema:

 

 مَنْ حَلَفَ بِغَيْرِ اللَّهِ فَقَدْ كَفَرَ أَوْ أَشْرَكَ

((Atakayeapa pasi na Allaah, atakuwa amekufuru na amemshirikisha Allaah) [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Hibbaan, Al-Haakim na wengineo na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee Ndiye Mwenye haki kuapia Atakacho kwani Yeye ni Muumba wa kila kitu. Ndio maana Anaapia katika Qur-aan vitu vingi; Wa-Tiyni waz-Zaytuni, Wal-‘Aswr, Wadh-Dhwuhaa, Wash-Shamsi, Wal-Layli, Wal-Fajr, Wal-‘Aadiyaat n.k.

 

Hata Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) haikumpasa kuapia chochote, na ndio maana tunaona anapotaka kuapa, mara nyingi husema:

 

وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ

Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake… [Akimkusudia Allaah]

 

 

Na akakataza katika Hadiyth mbali mbali zifuatazo kuapia kwa yeyote au kwa chochote isipokuwa kuapia kwa Allaah pekee:

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ رَضِي اللَّه عَنْهمَا أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَدْرَكَ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ وَهُوَ يَسِيرُ فِي رَكْبٍ يَحْلِفُ بِأَبِيهِ فَقَالَ : أَلَا إِنَّ اللَّهَ يَنْهَاكُمْ أَنْ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ مَنْ كَانَ حَالِفًا فَلْيَحْلِفْ بِاللَّهِ أَوْ لِيَصْمُتْ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaahi bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikutana na ‘Umar bin Al-Khattwaab akiwa katika msafara wa ngamia akawa ameapia kwa baba yake. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Tanabahi Allaah Anawakatezeni kuapia kwa baba zenu. Anayetaka kuapa basi aapie kwa Allaah au anyamaze kimya)) [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

Pia:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ - رضي الله عنه: لَا تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ, وَلَا بِأُمَّهَاتِكُمْ, وَلَا بِالْأَنْدَادِ, وَلَا تَحْلِفُوا إِلَّا بِاللَّهِ, وَلَا تَحْلِفُوا بِاللَّهِ إِلَّا وَأَنْتُمْ صَادِقُونَ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Msiapie kwa baba zenu wala mama zenu, wala kwa mnaowalinganisha na Allaah. Na wala msiape isipokuwa kwa Allaah, wala msiape kwa Allaah isipokuwa mnapokuwa mnasema ukweli)) [Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy]

 

Amekataza pia kuapia kwa uaminifu akasema Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam:

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ بُرَيْدَةَ عَنْ أَبِيهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: (لَيْسَ مِنَّا مَنْ حَلَفَ بِالأَمَانَةِ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Buraydah kutoka kwa baba yake kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Si miongoni mwetu anayeapia kwa amana)) [Ahmad (5/325) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika As-Silsilah Al-Hadiyth Asw-Swahiyhah (1/325)]

 

 

Na Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

مَن حلَف فقال في حَلِفه: باللات والعُزَّى، فليقل: لا إله إلا الله

((Yeyote atakayeapa akasema katika kiapo chake: “Naapa kwa Al-Laata, na Al-’Uzzaa” basi aseme: “Laa ilaaha illa-Allaah”)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na Ibn Mas-‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema:

 

لأَنْ أَحْلِفَ بِاللَّهِ كَاذِبًا أَحَبُّ إِلَيَّ مِنْ أَنْ أَحْلِفَ بِغَيْرِهِ صَادِقًا

“Ni bora kwangu kuapa kwa Jina la Allaah wakati naongopa kuliko kuapa kwa asiyekuwa Allaah kwa jambo la kweli.” [Majm’a Az-Zawaaid (4/180), na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Targhiyb (2953)]

 

 

 

Aina za viapo ni vitatu: 

 

 

1- Al-Yamiyn Al-Ghamuws (Kiapo cha uongo):

 

Ni kula kiapo huku kukusudia kuongopa, kama vile kusema: “Wa-Allaahi nimenunua kitu kadhaa kwa gharama ya fedha kadhaa”, na hali si kweli kuwa umenunua bei hiyo. Au kusema: “Wa-Allaahi nimefanya kadhaa”, na hali hakufanya. Kuapa hivi ni miongoni mwa madhambi makubwa kama alivyosema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو بْن الْعاص (رضي الله عنهما) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ َقَالَ: ((الْكَبَائِرُ الإِشْرَاكُ بِاللَّهِ وَعُقُوقُ الْوَالِدَيْنِ وَقَتْلُ النَّفْسِ وَالْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) البخاري

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amri bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa)  ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Al-Kabaair [Madhambi makubwa] ni kumshirikisha Allaah,  kuwaasi wazazi wawili, kuua nafsi na yamini [kiapo] ya uongo)) [Al-Bukhaariy]

 

Na katika riwaya nyingine:

 

أنَّ أَعْرَابِياً جَاءَ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّه,ِ مَا الْكَبَائِر؟ ُ قَالَ: ((الإشْرَاكُ بِاللَّهِ)) قَالَ: ثُمَّ مَاذَا؟ قَالَ: ((الْيَمِينُ الْغَمُوسُ)) قُلْتُ: وَمَا الْيَمِينُ الْغَمُوسُ؟  قَالَ: ((الَّذِي يَقْتَطِعُ مَالَ امْرِئٍ مُسْلِمٍ!)) يَعْنِ: بِيَمِينٍ هُوَ فِيهَا كَاذِبٌ

Alikuja Bedui mmoja kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Ni yepi Al-Kabaair [madhambi makubwa]?” Akasema: ((Kumshirikisha Allaah)) Akasema: Kisha yepi? Akasema: ((Yamini ya uongo)). Nikauliza: Ni ipi yamini ya uongo? Akasema: ((Ni ambayo mtu hujichukulia mali ya Muislamu!)) yaani akaapa kwa uongo. [Al-Bukhaariy]

 

Imeitwa Yamiyn Al-Ghamuws (kiapo cha uongo) kwa sababu yamzamisha mwenye yamini hiyo ndani ya dhambi na yamini hii ndiyo iliyokusudiwa katika kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

مَنْ حَلَفَ يَمينٍ صَبْرٍ لِيَقْتَطِعَ بِها مَالَ امْرِىءٍ مُسْلِمٍ، لَقِيَ اللهَ وَهُوَ عَلَيْهِ غَضْبانُ

((Atakayekula yamini hali yeye katika yamini hiyo anaongopa ili apate kwa yamini hiyo kumega mali ya mtu mwengine Muislamu basi mtu huyo atakutana na Allaah hali Amemghadhibikia)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hukmu yake:  Kuna kauli mbili,

 

i) Yamiyn Al-Ghamuws haina kafara bali mtu atubie tawbah ya kwelikweli. Ni rai ya Imaam Abiy Haniyfah, Imaam Maalik na Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahumu-Allaah). Pia Fatwa ya Al-Lajnatud-Daaimah (23/133) wamefutu: ”Al-Yamiyn Al-Ghamuws ni katika madhambi makubwa na haihitaji kafara kwa sababu ya ukubwa wa dhambi yake, bali inahitaji tawbah na kuomba maghfirah na ndio ilivyo sahihi kutokana na kauli za ‘Ulamaa.”

 

Na Shaykh Al-Islaamiy Ibn Taymiyyah amesema katika Majmuw’ Al-Fataawaa (34/139) baada ya kutaja ikhtilafu kuhusu kiapo cha Ghamuws….

“Wameafikiana kwamba dhambi haianguki kwa ajili ya kufanya kafara”. 

Amesema pia:

Ikiwa amemdhulumu mja mwenziwe basi amrudishie haki yake pamoja na kumuomba msamaha.

 

ii) Ama Imaam Ash-Shaafi’iy ameona inapasa kafara.  

 

 

2-Al-Yamiyn Al-Laghw (Kiapo cha upuuzi):

 

Hiki ni kile kiapo kipitacho katika ulimi wa Muislamu bila kukusudia, kama yule ambaye katika mazungumzo yake hujitokeza kwa wingi mno wa neno: “Wa-Allaahi hapana”. Hii ni kufuatia kauli ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa):

لغو اليمين كقول الرجل لا والله وبلى والله،

 “Upuuzi katika yamini ni maneno anayozungumza mtu, “Hapana Wa-Allaahi, Ndio Wa-Allaahi.” [Al-Bukhaariy]

 

Hukumu ya yamini aina hii ni kuwa haina dhambi wala kafara kwa mhusika, kwa kauli yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika Suwrah Al-Maaidah (5: 89):

 

لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ

Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi, [Al-Maaidah: 89]

 

 

 

3-Al-Yamiyn Al-Mun’aqidah (Kiapo cha kufungika):

 

Ni kukusudia jambo la baadae. Kama vile Muislamu kusema: “Wa-Allaahi nitalifanya jambo kadhaa” Au “Wa-Allaahi sitolifanya…” kisha akafanya kinyume chake.

 

Hukmu yake ni katika Suwrat Al-Maaidah (5: 89):

 

وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ

lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. [Al-Maaidah: 89]

 

ambayo inampasa afanye kafara:

 

فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚوَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٨٩﴾

Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini yamini zenu. Hivyo ndivyo Allaah Anavokubainishieni Aayaat (na hukmu) Zake ili mpate kushukuru.  [Al-Maaidah: 89]

 

 

Vinavyoapiwa kimakosa:

 

1- Kuapia vitu kadhaa:

 

Unapoapa kimakosa kwa kutumia vitu kuapia huhitaji kafara bali inakupasa urudi kutubia kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). ‘Ulamaa wamekubaliana hivyo kama alivyosema Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah katika Al-Fataawa Al-Kubraa (3/222): 

“Kuapia vitu viliyvoumbwa kama Al-Ka’bah, Malaika, mashekhe, wafalme, wazazi, makaburi ya wazazi n.k haihitajiki kafara kama ilivyokuwa ni rai ya Wanavyuoni. Bali imeharamishwa na Wanavyuoni na haramisho hili ni haraam kutokana na rai iliyo na nguvu kabisa”.

 

 

2- Kuapia kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

Baadhi ya watu huapa kwa tamshi la: “Wan-Nabiy!”, “Haki ya Mtume!” n.k.

 

 

3- Kuapia kwa Msahafu:

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) aliulizwa kuhusu hukmu ya kuapia Msahafu alijibu:

"Hairuhusiwi kuweka nadhiri au kuapa isipokuwa kwa Allaah au moja ya Sifa Zake. Ikiwa mtu ataapa kwa jina la Allaah, basi hakuna haja tena kuleta Msahafu kwa ajili ya kuapa kwa sababu kuapa kwa Msahafu haikufanyika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba. Hata baada ya Qur-aan kukusanywa katika Kitabu kimoja hawakuwa wakiapia Msahafu bali mtu alikuwa akiapa kwa Allaah bila ya kushika Msahafu."

[Fataawaa Nuwr 'Alaa Ad-Darb]

 

 

4- Kuapia kwa Al-Ka’bah:

 

Baadhi ya Waislamu hufikishana Makkah kuapizana kwa Al-Ka’bah jambo ambalo halijuzu bali ni kuvuka mipaka ya ‘Ibaadah, na kupoteza muda na mali ya kuwapeleka huko.

 

 

5- Kuapia wazazi, watoto:

 

Makatazo katika Hadiyth zilotanguliwa kutajwa juu.

 

 

6- Kuapia ‘amali njema kama Swiyaam (funga), Swadaqah n.k.

 

 

 

Share

16-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kuweka Nadhiri Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

16- Kuweka Nadhiri Kwa Asiyekuwa Allaah

 

Alhidaaya.com

 

 

Kuweka nadhiri ni mtu kuilazimisha nafsi yake kwa kitu ambacho hajalazimishwa na Shariy’ah.  Amesema Al-Isfhaan (Rahimahu Allaah) katika Mufradaat Alfaadhw Al-Qur-aan (uk. 797): “Nadhiri ni unapojishurutisha kutenda jambo lisilokuwa wajibu kwa sababu ya kutaka jambo fulani likutokee. Anasema Allaah:

 

إِنِّي نَذَرْتُ لِلرَّحْمَـٰنِ صَوْمًا 

Hakika mimi nimeweka nadhiri ya swawm kwa Ar-Rahmaan [Maryam: 26]

 

Baadhi ya ‘Ulamaa wameharamisha kwa dalili ya Hadiyth ifuatayo:

 

عن النبيَّ صلَّى اللهُ عليه وسلَّمَ ؛ أنه نهى عن النذر  وقال:  إنه لا يأتي بخير. وإنما يستخرج من البخيل

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza nadhiri akasema: ((Haileti khayr bali inatolewa kutoka kwa bakhili)) [Muslim (1639)]

 

Na katika riwaayah nyingine:

 

  نَهَى النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ عَنْ النَّذْرِ وَقَالَ:  إِنَّهُ لَا يَرُدُّ شَيْئًا وَلَكِنَّهُ يُسْتَخْرَجُ بِهِ مِنْ الْبَخِيلِ

Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza nadhiri akasema: ((Hakika hairudishi chochote, bali inatolewa kutoka kwa bakhili)) [Al-Bukhaariy (6693)]   

 

Na Hadiyth ya Mama wa Waumini ‘Aaishah  (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba  amesema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

 من نذر أن يُطِيعَ اللهَ فلْيُطِعْهُ ، ومن نذرَ أن يعصِيَه فلا يَعْصِه

((Aliyeweka nadhiri kumtii Allaah amtii, na aliyeweka nadhiri kumuasi Allaah, basi asimuasi))[Al-Bukhaariy (6696)]

 

 

Kutokana na Hadiyth hii, inadhihirisha kukubaliwa kwake nadhiri pindi mtu akiazimia, kwa dalili pia za Qur-aan:

وَمَا أَنفَقْتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوْ نَذَرْتُم مِّن نَّذْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُهُ

Na chochote mtoacho au mkiwekacho nadhiri, basi Allaah Anakijua. [Al-Baqarah: 270]

 

Na pia kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا﴿٧﴾

Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea kwa upana. [Al-Insaan: 7]

 

Na pia Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

ثُمَّ لْيَقْضُوا تَفَثَهُمْ وَلْيُوفُوا نُذُورَهُمْ

Kisha wamalize ‘ibaadah zao; wajisafishe taka zao na watimize nadhiri zao, [Al-Hajj: 29]  

 

 

Na kwa vile nadhiri ni aina ya ‘Ibaadah, haifai kuielekeza kwa asiyekuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) mfano kuifanya kwa ajili ya Nabiy, au Walii, au Shaykh, au kaburi na kadhaalika. Kufanya hivyo ni shirki kubwa inayomtoa mtu nje ya Uislamu.

 

Fataawa za ‘Ulaama kuhusu kuweka nadhiri kwa asiyekuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

Shaykh Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

Swali: 

 

Je, ikiwa mtu ameweka nadhiri mfano akasema: “Allaah Akinipa shifaa kwa magonjwa yangu, nitachinja kwa ajili ya Allaah katika kaburi la fulani ili kujikurubisha kwa Allaah. Je, inajuzu mfano wa ‘amali kama hii? Na je, kuna sehemu zilizoharamishwa kuchinja?

 

Jibu: 

 

Ikiwa ameweka nadhiri kuchinja kwa ajili ya Allaah katika kaburi, basi nadhiri hii ni ya maasi, haijuzu kuitimiza. Na kuchinja katika kaburi ikiwa imekusudiwa kujikurubisha kwa mwenye kaburi, hiyo ni shirki kubwa inayomtoa mtu katika Dini hata kama ataja Jina la Allaah wakati anachinja.

 

Na ikiwa kujikurubisha kwa Allaah basi hayo ni maasi makubwa na wasiylah (njia ya kujikurubisha) za shirki kwa sababu haijuzu kuswali kaburini wala kuomba wala kuchinja kaburini hata kama tunakusudia Allaah kwani hivyo ni kujifananisha na washirikina na wasiyla za shirki. 

 

Abuu Daawuwd amepokea kutoka kwa Thaabit bin Adhw-Dhwahaak (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba mtu mmoja aliweka nadhiri kuchinja ngamia katika Buwaanah. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: ((Je, kuliweko masanamu ya kijaahiliyyah (kabla Uislamu) yakiabudiwa?”

Wakasema: “Hapana” Akasema: ((Je, kuliweko sherehe za kijaahiliyyah zikifanywa hapo?)) Wakasema: “Hapana” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Timiza nadhiri yako, kwani hakuna kutimiza nadhiri katika kumuasi Allaah, wala katika ambayo hayamiliki bin Aadam)). [Abuu Daawuwd na ameisahihisha Al-Albaaniy]

 

 

 

Imaam bin Baaz (Rahimahu Allaah)

 

Swali:

 

Imenitokea mushkila nikaweka nadhiri kwa ajili ya mmojawapo wa ma-Imaam, kisha nikaja kutambua kuwa haifai kuweka nadhiri kwa asiyekuwa Allaah. Tambua kuwa sehemu aliyoko huyo Imaam iko mbali, je, inajuzu nilipize nadhiri hii kwa mafakiri au niifanyie kafara?

 

Jibu: 

 

Nadhiri hiyo ni baatwil, kwa sababu ni ‘ibaadah kwa asiyekuwa Allaah.  Inakupasa utubie kwa Allaah kwayo na urudi Kwake kwa kutubia na kuomba maghfirah na kujuta kwani nadhiri ni ‘ibaadah, Anasema Allaah Ta’aalaa:  

 

وَمَا أَنفَقْتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوْ نَذَرْتُم مِّن نَّذْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُهُ

Na chochote mtoacho au mkiwekacho nadhiri, basi Allaah Anakijua. [Al-Baqarah: 270]

 

Yaani: Atakulipeni kwayo. Na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

من نذر أن يُطِيعَ اللهَ فلْيُطِعْهُ، ومن نذرَ أن يعصِيَه فلا يَعْصِه

((Aliyeweka nadhiri kumtii Allaah amtii, na aliyeweka nadhiri kumuasi Allaah, basi asimuasi))  

 

Kwa hiyo nadhiri hiyo ni baatwil, na ni kumshirikisha Allaah (‘Azza wa Jalla) kama vile nadhiri kwa ajili ya ma-Imaam na waliokufa ni nadhiri baatwil na ni kumshirkisha Allaah, basi nadhiri haijuzu isipokuwa kwa ajili ya Allaah Pekee, kwa sababu ni ‘ibaadah kama vile Swalaah, na kuchinja na nadhiri, na kufunga Swiyaam na du’aa zote ni kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kama Anavyosema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ ﴿٥﴾

Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada. [Al-Faatihah: 5]

 

 

Na Anasema (Subhaanahu):

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ

Na Rabb wako Amehukumu kwamba: “Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee [Al-Israa: 23]

 

 

Na Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَادْعُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ وَلَوْ كَرِهَ الْكَافِرُونَ﴿١٤﴾

Basi mwombeni Allaah wenye kumtakasia Dini japokuwa wanachukia makafiri. [Ghaafir: 14]

 

 

 

Na Anasema (‘Azza wa Jalla):

وَأَنَّ الْمَسَاجِدَ لِلَّـهِ فَلَا تَدْعُوا مَعَ اللَّـهِ أَحَدًا﴿١٨﴾

Na kwamba Misikiti ni kwa ajili ya Allaah, basi msiombe yeyote pamoja na Allaah. [Al-Jinn: 18]

 

 

Basi ‘ibaadah ni haki ya Allaah, na nadhiri ni ‘ibaadah, na Swawmi ni ‘ibaadah, na Swalaah ni ‘ibaadah, na du’aa ni ‘ibaadah basi inawajibika kuisafisha kwa ajili ya Allaah Pekee. Kwa hiyo nadhiri hiyo ni baatwil, na haikupasi kufanya chochote, si kwa mafukara wala wengineo, bali inakupasa utubie tu na huna haja ya kuilipizia nadhiri hiyo kwa vile ni baatwil na ni shirki, ila tu utubie tawbah ya kikweli na kufanya matendo mema, Allaah Akuwafikie na Akuongoze katika yanayomridhisha na Akujalie ufanye tawbah ya kikweli.

 

 

 

 

Share

17-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kutabarruk (Kutafuta Kupata Baraka)

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

17 -Kutabarruk (Kutafuta Kupata Baraka)

Alhidaaya.com

 

 

 

Maana ya barakah ni wingi wa khayr na kuthibitika kwake. 

 

 

Tabarruk ni aina mbili; iliyothibiti ki-shariy’ah kwa kutajwa kitu fulani kina baraka kama Anavyosema Allaah (Subahaanahu wa Ta’aalaa) kuhusu Qur-aan:

 

كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٢٩﴾

Kitabu Tumekiteremsha kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) chenye Baraka, ili wapate kuzingatia kwa makini Aayaat zake, na ili wapate kukumbuka wenye akili. [Swaad: 29]

 

 

Mfano wa kutaka baraka za Kitabu hiki (Qur-aan) ni kama vile alivyosema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ الله عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ قَرَأَ حَرْفًا مِنْ كِتَابِ اللَّهِ فَلَهُ بِهِ حَسَنَةٌ وَالْحَسَنَةُ بِعَشْرِ أَمْثَالِهَا لَا أَقُولُ الم حَرْفٌ وَلَكِنْ أَلِفٌ حَرْفٌ وَلَامٌ حَرْفٌ وَمِيمٌ حَرْفٌ))

Imetoka kwa 'Abdullaahi bin Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema, ((Atakayesoma herufi moja katika Kitabu cha Allaah atapata hasanah (jema) moja, na kila hasanah moja ni sawa na thawabu kumi, wala sisemi 'Alif-Laam-Miym' ni herufi moja, bali Alif ni herufi moja na Laam ni herufi moja na Miymni herufi moja)) [At-Tirmidhiy (2910) na ameisahihisha Shaykh Al-Albaaniy katika As-Silsilah Asw-Swahiyhah (3327), Swahiyh Al-Jaami’ (6469)]

 

 

Tabarruk inagawanyika sehemu mbili:

 

 

1-Iliyothibiti katika Shariy’ah ambayo inatokana na Muislamu kufanya juhudi katika ‘amali fulani ili achume thawabu nyingi na apate khayr nyingi kabisa. Mifano ni michache ni:

 

i) Kusoma Qur-aan na kufuata hukumu na maamrisho yake kama ilivyothibiti katika Qur-aan na Sunnah (Aayah na Hadiyth zilizotangulia kutajwa juu). Na pia Anasema Allaah (Subhanaahu wa Ta’aalaa):

 

إنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّـهِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَّن تَبُورَ ﴿٢٩﴾

Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Allaah na wakasimamisha Swalaah, na wakatoa kutokana na yale Tuliyowaruzuku kwa siri na dhahiri wanataraji tijara isiyoteketea.

 

 

لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ ۚ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ ﴿٣٠﴾

Ili (Allaah) Awalipe ujira wao timilifu, na Awazidishie kutokana na fadhila Zake, hakika Yeye ni Mwingi wa kughufuria, Mwingi wa kupokea shukurani. [Faatwir: 29-30]

 

 

 

ii) Kuomba maghfirah kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ambayo matokeo yake ni kujipatia khayr nyingi kama ilivyo tajwa kuhusu kauli ya Nabiy Nuwh (عليه السلام) alipowalingania watu wake:

 

 

اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا﴿١٠﴾

Nikasema: “Ombeni maghfirah kwa Rabb wenu; hakika Yeye ni Mwingi mno wa kughufuria.

 

يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا﴿١١﴾

 “Atakutumieni mvua tele ya kuendelea.”

وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا﴿١٢﴾

 “Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakupeni mito.” [Nuwh: 10-12]

 

 

 

Na mifano michache miongoni mwa mingineyo katika Sunnah:

 

 

i) Kuswali katika Masjid Al-Haraam, Makkah ambayo Swalaah humo thawabu zake ni maradufu.   

 

عَنْ جَابِرٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((صَلَاةٌ فِي مَسْجِدِي  أَفْضَلُ مِنْ أَلْفِ صَلَاةٍ فِيمَا سِوَاهُ إِلَّا الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ، وَصَلَاةٌ فِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ أَفْضَلُ مِنْ مِائَةِ أَلْفِ صَلَاةٍ فِيمَا سِوَاهُ)) رواه أحمد وابن ماجه

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Swalaah katika Msikiti wangu ni bora kuliko Swalaah elfu kwengineko isipokuwa Al-Masjid Al-Haraam. Na Swalaah katika Al-Masjid Al-Haraam ni bora kuliko Swalaah elfu mia (laki moja) kwengineko)) [Ahmad, Ibn Maajah na imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy; Swahiyh Ibn Maajah (1163), Swahiyh Al-Jaami’ (3838)]

 

Pia:

 

 عن أبي هريرة رضي الله عنه ان رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((من قال : لا إلهَ إلَّا اللهُ وحدَه لا شريكَ له، له المُلْكُ وله الحمْدُ، وهو على كلِّ شيءٍ قديرٌ . في يومٍ مائةَ مرَّةٍ ، كانت له عِدلُ عشرِ رِقابٍ ، وكُتِبت له مائةُ حسنةٍ، ومُحِيَتْ عنه مائةُ سيِّئةٍ ، وكانت له حِرزًا من الشَّيطانِ يومَه ذلك حتَّى يُمسيَ ، ولم يأتِ أحدٌ بأفضلَ ممَّا جاء به إلَّا رجلٌ عمِل أكثرَ منه))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ’anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:  ((Atakayesema: Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku walahul-Hamdu wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr [Hapana muabudiwa wa haki ila ni Allaah  Peke Yake, hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza], mara mia kwa siku, basi atapata sawa na thawabu za kuwaacha huru watumwa kumi na ataandikiwa mema mia moja na atafutiwa makosa mia moja, na atakuwa na kinga ya shaytwaan kwa siku hiyo yote hadi jioni na hatakuwa mtu yeyote mbora kumshinda ila yule aliyefanya zaidi yake)) [Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h, (4/95) [3293], Muslim (4/2071) [2691].

  

Na pia:

 

عن عقبة بن عامر رضي الله عنه أن خرج رسولُ اللهِ صلَّى اللهُ عليهِ وسلَّمَ ونحنُ في الصُفَّةِ. فقال: ((أيكم يحبُّ أن يغدو كلَّ يومٍ إلى بطحانَ أو إلى العقيقِ فيأتي منهُ بناقتيْنِ كوماويْنِ، في غيرِ إثمٍ ولا قطعِ رحمٍ؟)) فقلنا: يا رسولَ اللهِ  نحبُّ ذلك. قال: ((أفلا يغدو أحدكم إلى المسجدِ فيُعَلِّمَ أو يقرأَ آيتيْنِ من كتابِ اللهِ عزَّ وجلَّ خيرٌ لهُ من ناقتيْنِ. وثلاثٌ خيرٌ لهُ من ثلاثٍ  وأربعٌ خيرٌ لهُ من أربعٍ. ومن أعدادهنَّ من الإبلِ))

 

Imetoka kwa 'Uqbah bin 'Aamir (Radhwiya Allahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alitujia wakati tulikuwa katika Swuffah akauliza, kuna yeyote miongoni mwenu anayependa kwenda soko la Butw-haan au Al-'Aqiyq na akapata humo ngamia wawili (wa thamani kabisa wa kike) bila ya kutenda dhambi au kukata undugu? Tukajibu: “Ee Rasuli wa Allaah! Tunapenda hivyo.” Akasema: ((Basi aende mmoja wenu Msikitini akajifunze au asome Aayah mbili katika Kitabu cha Allaah basi akifanya hivyo ni bora kuliko ngamia (wa thamani kabisa wa kike). Na Aayah tatu ni bora kuliko ngamia watatu, na Aayah nne ni bora kuliko ngamia wanne, na mfano wa hivyo hivyo wa Aayah kwa ngamia)) [Muslim]

 

 

2- Tabarruk iliyoharamishwa ambayo huwa shirki au bid’ah

 

Kuitakidi kwamba kiumbe fulani ana baraka na kumuomba kiumbe huyo khayr ambazo hana uwezo nazo isipokuwa Allaah, huwa ni shirki kwa sababu ni Allaah (Subhaanahu Ta’aalaa) Pekee Mwenye kutoka baraka kama alivyothibitisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عن جابر بن عبد الله رضي الله عنه: رأيْتُني مع النبيِّ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم وقدْ حَضَرَتِ العَصْرُ، وليس معَنا ماءٌ غيرَ فَضلَةٍ، فجُعِلَ في إناءٍ فأُتيَ النبيُّ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم بهِ، فأدْخَلَ يدَهُ فيه وفَرَّجَ أصابِعَهُ، ثم قال: ((حيَّ علَى أهلِ الوضوءِ، البَرَكَةُ مِن اللَّهِ)) فلقدْ رأيتُ الماءَ يَتَفَجَّرُ مِن بينِ أصابعِهِ، فتَوَضَّأ الناسُ وشَرِبوا، فجَعَلْتُ لا آلُو ما جَعَلتُ في بطْني منه، فعَلِمتُ أنَّه بَرَكَةٌ . قلتُ لجابرٍ :كَم كُنتُم يومَئِذٍ ؟ قال: ألْفًا وأربَعمِائةٍ

Imepokewa kutoka kwa Jaabir bin Abdillaah akisema: “Nilikuwa na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na muda wa kuswali Swalaah ya Al-‘Aswr ukafika. Tulikuwa hatuna maji isipokuwa maji kidogo tu ambayo yalikuwa ndani ya chombo ambayo yaliletwa kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Basi aliweka mkono wake ndani ya maji hayo na kutandaza vidole vyake na huku akisema: ((Njooni Haraka watu wote ambao wanataka kutawadha Hii ni baraka kutoka kwa Allaah)). Nikaona maji yakibubujika kutoka katika vidole vyake. Hivyo watu walitawadha na wengine wakawa wanakunywa maji hayo na mie nilitaka kunywa maji mengi kupita kiasi (kwa sababu nilijua kuwa ilikuwa ni baraka). Mpokeaji wa Hadiyth hii kutoka kwa Jaabir alisema kuwa nilimuuliza Jaabir Je, mlikuwa watu wangapi wakati huo? Akajibu, “Tulikuwa watu elfu moja na mia nne.” [Swahiyh Al-Bukhaariy(7/543) Swahiyh Muslim (4/779)]

 

 

Aghlabu shirki na bid’ah zinazotendwa katika kutabarruk:

 

 

i-Kufanya ‘ibaadah kadhaa kama kuomba du’aa na kuswali kuelekea kaburi la Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kuitakidi kuwa du’aa na Swalaah hiyo ni ya kutakabaliwa au inamridhisha Allaah (Subhanaahu wa Ta’aalaa):

 

Amesema Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah: “‘Ulamaa wengi wamewafikiana kwamba huu ni munkar uliozushwa na ni haraam, wala ma-Imaam wa Dini hawakutofautiana kwa hili.” [Ar-Radd ‘Alal-Bakriy, uk. 56]

 

Na akasema kuhusu du’aa mbele ya kaburi la Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Wala asisimame mtu kujiombea kwani hiyo ni bid’ah, wala hakutokea Swahaabah akisimama kaburini kujiombea bali walikuwa wakielekea Qiblah na wakiomba katika Masjid yake.” [Majmuw’ah Ar-Rasaail Al-Kubraa li Ibn Taymiyyah (2/408)], na Iqtidhwaa Swiraatw Al-Mustaqiym (2/681)]

 

 

ii- Kugusa kaburi na kuta za kaburi la Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) au Al-Ka’bah na kujipangusia mwilini, au kubusu kwa kutegemea kupata khayr na barakah.

Lililothibiti kubusiwa ni Al-Hajar Al-Aswad pekee lilioko katika Al-Ka’bah kwa dalili:

((إِنَّ مَسْحَ الْحَجَرِ الأَسْوَدِ ، والركنَ اليمانيِّ، يَحُطَّانِ الخطايا حطًّا))

((Kugusa Al-Hajar Al-As-wad na Ar-Rukn al-Yamaaniy ni kufutiwa madhambi))  [Hadiyth ya Ibn ‘Umar; Swahiyh Al-Jaami’ (2194)]

 

Na ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alipolibusu alisema:

 

 "إني أَعْلَمُ أَنَّكَ حَجَرٌ لا تَضُرُّ ولا تَنْفَعُ، وَلَوْلا أَنِّي رأيت النبي صلى الله عليه وسلم يُقَبِّلُكَ ما قَبَّلْتُكَ" - البخاري و مسلم

“Hakika mimi najua kwamba wewe ni jiwe usiloweza kudhuru wala kunufaisha, na ingelikuwa sikumuona Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anakubusu basi nami nisingelikubsu.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

iii-Kutabarruk sehemu sehemu ambazo zimetajwa katika Siyrah ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Imedhihirika watu wengi kukosea wanapofika Makkah au Madiynah kutekeleza ‘Umrah kupendelea kutembelea sehemu hizo wakiitakidi kuwa zina baraka na wengine hufika kujikalifisha kupanda majabali kama Jabal Ath-Thawr, Ghaar Hiraa, Jabali la ‘Arafah na sehemu nyinginezo.

Haikuthibiti kuwa Swahaabah (Radhwiya Allaahu ‘anhum) walitabarruk na chochote au popote alipopita au alipokaa kitako Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya kuwa wao walikuwa na mapenzi makubwa kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na wenye kutilia hima zaidi ya kutekeleza Sunnah.

 

Shaykh Al-Islaam amesema: “Kina Abu Bakr na ‘Umar na ‘Uthmaan na wengineo miongoni mwa Al-Muhaajiriyn na Answaar walikuwa wakisafiri kutoka Madiynah mpaka Makkah kutekeleza Hajj na ‘Umrah wala haikupokelewa kutoka kwao kuwa mmoja wao alikuwa akitafuta sehemu alizokuwa akiswali Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salalm). Basi ni dhahiri kwamba ingekuwa ni jambo la kupendekezwa wangekuwa wao ni wa kwanza kutangulia kufanya, kwani wao ni wajuzi zaidi wa Sunnah zake na wenye kufuata mno kuliko wengineo.” [Iqtidhwaa Swiraatw Al-Mustaqiym (2/748)]

 

Katika moja ya msafara wake kwenda vitani Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) pamoja na Swahaba zake walipitia sehemu wakataka kutafuta baraka kwa kuweka silaha zao katika mti, lakini aliwakataza. Na hii ni dalili pia haipasi kutabarruk kwa miti na vitu kama hivyo.

      

عن أَبِي وَاقٍد اللَّيْثِيِّ (رضي الله عنه) قَالَ: خَرَجْنَا مَعَ النَّبِيِّ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وآله وَسَلَّمَ) إِلَى حُنَيْنٍ وَنَحْنُ حُدَثَاءُ عَهْدٍ بِكُفْرٍ، وَلِلِمُشْرِكِينَ سِدْرَةٌ، يَعْكُفُونَ عِنْدَهَا وَيُنَوِّطُونَ بِهَا أَسْلِحَتَهُمْ، يُقَالَ لَهَا ذَاتُ أَنْوَاطٍ، فَمَرَرْنَا بِسِدْرَةٍ فَقُلْنَا: يَا رَسُولَ اللهِ اجْعَلْ لَنَا ذَاتَ أَنْوَاطٍ كَمَا لَهُمْ ذَاتُ أَنْوَاط. فَقَالَ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم):َ((الله أكبر! هَذَا كَمَا قَالَ قَوْمُ مُوسَى "اجْعَلْ لَنَا إِلَهًا كَمَا لَهُمْ آلِهَةٌ" وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَتَرْكَبُنَّ سُنَّةَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ))

Imepokewa kutoka kwa Abuu Waaqid Al-Laythiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Tulitoka pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwenda (vitani) Hunayn nasi ndio kwanza tumetoka katika ukafiri, na washirikina walikuwa na mkunazi wanaufanyia ‘ibaadah na walikuwa wakitundika silaha zao (kupata baraka). Wakiuita ‘Dhaatu Anwaatw’. Tukapita mbele ya mkunazi tukasema: “Ee Rasuli wa Allaah, tufanyie nasi Dhaata Anwaatw kama walivyokuwa nao (makafiri) Dhaatu Anwaatw.” Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Allaahu Akbar!  (Allaah ni Mkubwa!) Hivi ni kama walivyosema watu wa Muwsa “Tufanyie nasi muabudiwa kama walivyokuwa nao muabudiwa.” Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, mtafuata nyendo za walio kabla yenu [za ujahili na kufru].)) [At-Tirmidhiy; Swahiyh At-Tirmidhiy (2180)]

 

iv- Kutabarruk kwa Msahafu:

 

Shaykh Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amejibu Swali: “Kuweka Msahafu katika gari kwa ajili ya kujikinga na khatari au kujikinga na jicho ni bid’ah, kwani Swahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum) hawakuwa wakibeba Misahafu walipokuwa wakipanda ngamia wao kwa ajili ya kujikinga na khatari au jicho baya.” [Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb (2/4)]

 

 

v-Kutabarruk kwa watu kama mashekhe na wanaoitwa masharifu, kwa kuwagusa au kupangusa nguo zao au kuvaa nguzo zao au kunywa kinywaji walichoanza kunywa, au maji waliyoyatemea mate n.k. kwa kutegemea au kuitakidi vitu hivyo vina baraka.

 

Haikuthibiti kutoka kwa Swahaba kwamba walitabarruk kwa Swahaabah watukufu, kama Abu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) wala wengineo waliobashiriwa Jannah wala watu wa nyumba ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa hiyo kufanya hivyo si jambo lenye kukubalika katika Shariy’ah.

 

 

 

 

 

Share

18-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aanah (Kuomba Msaada) Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

18- Isti’aanah (Kuomba Msaada) Kwa Asiyekuwa Allaah

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Maana Ya Isti’aanah (kuomba msaada) na dalili zake:

 

Isti’aanah ni kuomba msaada. Na Isti’aanah kwa Allaah ni kuomba katika mambo ya Dini na ya dunia na inajumuisha mja kujidhalilisha kwa Mola wake na kuwa na yakini na kumtegemea Yeye (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Pekee kama Anavyosema:

فَاعْبُدْهُ وَتَوَكَّلْ عَلَيْهِ

basi mwabudu Yeye na tawakali Kwake. [Huwd: 123]

 

 

Na katika Suwratul-Faatihah ambayo inajumuisha aina zote za Tawhiyd, Muislamu anakariri katika Swalaah zake zote:

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ ﴿٥﴾

Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada. [Al-Faatihah: 5]

 

 

Kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِيَّاكَ نَعْبُدُ

Inathibitisha Tawhiyd ya Uluwhiyyah (kumpwekesha Allaah katika kumwabudu); yaani aina zote za ‘ibaadah zinahitaji kuelekezwa Kwake Pekee Subhaanahu wa Ta’aala.

 

Na

وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ 

Inathibitisha Tawhiyd ya Ar-Rubuwbiyyah (kumpwekesha Allaah katika Uola) kwa sababu ni kuomba msaada kwa Ar-Rabb (Mola) Ambaye ni Al-Khaaliq (Muumbaji), Ar-Raaziq (Mtoaji rizki), Al-Mudabbir (Mwendeshaji mambo), Al-Maalik (Mwenye kumiliki) Ambaye mambo yote yamo Mikononi Mwake. Kwa hiyo anapaswa Yeye kuombwa mahitaji yetu kama vile Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivyomuusia Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amehadithia:

 

كُنْتُ خَلْفَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم يًوْماً، فقال: ((يا غُلامُ، إنِّي أُعَلِّمُكَ كلِماتٍ: احْفَظِ اللهَ يَحْفَظْكَ، احْفَظِ اللهَ تَجِدْهُ تُجاهَك، إذا سأَلْتَ فاسْأَلِ اللهَ، وإذا اسْتَعنْتَ فاسْتَعِنْ باللهِ، واعْلَمْ أنَّ الأُمَّة  لَوِ اجْتَمَعَتْ على أَنْ يَنْفَعُـوكَ بِشَيءٍ لَمْ يَنْفَعُوكَ إلا بِشَيْءٍ قدْ كَتَبَهُ اللهُ لَكَ، وإن اجْتَمَعُوا على أن يَضُرَّوكَ بِشيءٍ لَمْ يَضُروكَ إلا بِشَيءٍ قَدْ كَتَبهُ اللهُ عَلَيْكَ، رُفِعَتِ الأقْلامُ وَجَفَّتِ الصُّحُفُ))

Siku moja nilikuwa nyuma ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: “Ee kijana! nitakufundisha maneno (ya kufaa); Mhifadhi Allaah (fuata maamrisho Yake na chunga mipaka Yake) Atakuhifadhi.  Muhifadhi Allaah utamkuta mbele yako. Ukiomba, muombe Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), ukitafuta msaada tafuta kwa Allaah. Tambua kwamba ikiwa ummah mzima utaungana kukunufaisha wewe kwa kitu, basi hutonufaika ila tu kwa kile Alichokwishakuandikia Allaah. Na wakikusanyika kukudhuru kwa chochote, hutodhurika ila tu kwa kile Allaah Alichokwishakukuandikia (kuwa kitakudhuru), kwani kalamu zimeshanyanyuliwa (kila kitu kishaandikwa) na swahifa zimeshakauka.” [At-Tirmidhiy, na amesema Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

Kumuomba bin-Aadam msaada wa jambo ambalo limo katika uwezo wake inafaa kwa dalili zifuatazo katika Qur-aan na Sunnah:

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ

Na shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na uadui. [Al-Maaidah: 2]

 

Na Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عن أبي هُرَيْرَة رضي اللهُ عنه، عن النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قال:  "مَنْ نَفَّسَ عَنْ مُؤمِنٍ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ الدُّنْيا نَفَّسَ اللهُ عَنْهُ كُرْبَةً من كُرَبِ يوْمِ القيامَةِ، ومَنْ يَسَّرَ على مُعْسِرٍ يَسَّرَ اللهُ عليه في الدنْيا والآخِرَةِ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِماً سَتَرَهُ الله في الدُّنْيا والآخِرَةِ  واللهُ في عَوْنِ الْعَبْدِ ما كانَ الْعَبْدُ في عَونِ أخيهِ"  

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Yeyote atakayemuondoshea shida ya kidunia Muislamu mwenzake, Allaah Atamuondoshea moja katika shida za Siku ya Qiyaamah. Na yeyote yule atakayemsaidia muhitaji (maskini) Allaah Atamsaidia haja zake hapa duniani na Aakhirah. Na yeyote yule atakayemsitiri Muislamu, Allaah Atamsitiri hapa duniani na Aakhirah. Allaah Humsaidia mja wake wakati wote madamu mja (huyo) yungali anamsaidia nduguye (Muislamu).” [Muslim]

 

Pia,   

 

عَنْ عَبْدِ الله بنِ عُمَرَ رَضِيَ الله عَنْهُما، أَنَّ النَّبِيَ صَلَّى الله عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: "أَحَبُّ النَّاسِ إِلَى الله أَنْفَعُهُمْ لِلّنَاسِ، وَأَحَبُّ الأَعْمَالِ إِلَى الله سُرُورٌ تُدْخِلُهُ عَلَى مُسْلِمٍ  أَوْ تَكْشِفُ عَنْهُ كُرْبَةً  أَوْ تَقْضِيَ عَنْهُ دَيْناً أَوْ تَطْرُدُ عَنْهُ جُوعاً، وَلأَنْ أَمْشِيَ مَعَ أَخِي المُسْلِمِ فِي حَاجَةٍ أَحَبُّ إِلَيَّ مِنْ أَنْ أَعْتَكِفَ فِى هَذَا المَسْجِدِ يعني مسجدَ المدينةِ شهرًا، وَمَنْ كَفَّ غَضَبَهُ سَتَرَ اللهُ عَوْرَتَه وَمَنْ كَظَمَ غَيْظَهُ وَلَوْ شَاءَ أَنْ يُمْضِيَه أَمْضَاهُ مَلأَ اللهُ قَلْبَهُ رَجاءً يَوْمَ القِيَامَةِ وَمَنْ مَشَى مَعَ أَخِيهِ المُسْلِمِ فِى حَاجَةٍ حَتَّى تَتَهَيَّأَ لَهُ أَثْبَتَ اللهُ قَدَمَهُ يَوْمَ تَزِلُّ الأَقْدَامُ وَإِنَّ سُوءَ الخُلُقِ لَيُفْسِدُ العَمَلَ كَمَا يُفْسِدُ الخلُّ العَسَلَ"

‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Mtu ambaye ni kipenzi kabisa kwa Allaah ni yule ambaye ni mbora kabisa katika kunufaisha wenziwe. Na ‘amali zilizokuwa kipenzi kabisa kwa Allaah ('Azza wa Jalla) ni furaha aingizayo kwa Muislamu, au kumuondoshea shida, au kumtimizia deni lake, au kumuondoshea njaa. Na hakika mimi kwenda kumtimizia ndugu yangu haja yake, ni kipenzi kwangu kuliko nikae I’tikaaf (kijifunga katika ‘ibaadah Msikitini) mwezi mzima katika Masjid hii (Masjid Nabawiy). Na atakayeacha ghadhabu zake, basi Allaah Atamsitiri aibu zake. Na atakayezuia ghaydhi (ghadhabu na huzuni moyoni) zake japokuwa haogopi kuzionyesha, lakini anazuia, Allaah Atamjaza moyo wake kwa matumaini Siku ya Qiyaamah. Na atakayetembea na nduguye katika kumtimizia haja mpaka akamsaidia kikamlifu basi Allaah Atamthibitisha miguuu yake Siku ambayo miguu haitothibitika. Hakika khulqu (tabia) mbaya inaharibu ‘amali kama vile siki inavyoharibu asali.” [As-Silsilah Asw-Swahiyhah (906)]

 

Mifano ya mtu kumuomba bin-Aadam mwenziwe;

 

“Ee fulani! Nakuomba unisaidie kunilipia deni langu!”

 

“Ee fulani! Nakuomba unisaidie kunilipia gharama za matibabu ili nitibiwe!”

 

Au kuomba msaada wa mtu kumsimamia kazi yake, kumpatia anachohitaji katika matumizi, au kuomba kushirikiana katika ‘amali za khayr, au kuomba kusaidia jambo lolote la khayr ambalo litampatia thawabu kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa kumfanyia wema mwenziwe kama ilivyothibiti katika Hadiyth zilizotangulia.

 

Ama kuomba jambo ambalo halimo katika uwezo wa ki-bin-Aadam hapo huwa ni shirki. Mfano mtu kumuomba mtu amsaidie kupata kizazi, au kumwendea mtabiri amsaidie kumtazamia mambo ya ghayb, au mchawi kumuomba amfanye awe tajiri, au kuwaomba msaada wa riziki walio kaburini au kuwaomba wawaondoshee maradhi n.k.

 

Hizo ni aina za ‘ibaadah zipasazo kuelekezwa kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee, kwa hiyo, 'Ibaadah kuielekeza kwa mwengine ni shirki kubwa kabisa kwa sababu ni kumshirikisha Allaah na viumbe Vyake katika mambo ambayo ni Allaah ('Azza wa Jalla) Pekee Mwenye uwezo nayo. Na shirki hii inamtoa mtu nje ya Uislamu kwa dalili kauli ya Allaah (Subahaanahu wa Ta’aalaa):

 

وَمَن يَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ لَا بُرْهَانَ لَهُ بِهِ فَإِنَّمَا حِسَابُهُ عِندَ رَبِّهِ ۚ إِنَّهُ لَا يُفْلِحُ الْكَافِرُونَ ﴿١١٧﴾

 

Na yeyote yule anayeomba du’aa (au kuabudu) pamoja na Allaah muabudiwa mwengine hana ushahidi wa wazi wa hilo; basi hakika hesabu yake iko kwa Rabb wake. Hakika hawafaulu makafiri. [Al-Muuminuwn: 117]

 

 

Ilhali Allaah ('Azza wa Jalla) Ametuamrisha tumuombe Yeye Pekee kama Anavyosema:

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu (kwa ujuzi); Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186]

 

 

Na Yeye Allaah ('Azza wa Jalla) Ndiye Mwenye kumuondoshea mtu dhiki zake Anapoombwa Yeye Pekee bila ya kumshirikisha, Anasema Allaah (Subahaanahu wa Ta’aalaa):

 

أَمَّن يُجِيبُ الْمُضْطَرَّ إِذَا دَعَاهُ وَيَكْشِفُ السُّوءَ وَيَجْعَلُكُمْ خُلَفَاءَ الْأَرْضِ ۗ أَإِلَـٰهٌ مَّعَ اللَّـهِ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ ﴿٦٢﴾

Au nani Anayemuitika mwenye dhiki mno anapomwomba, na Akamuondoshea ouvu na Akakufanyeni makhalifa wa ardhi? Je, yuko mwabudiwa pamoja na Allaah? Ni machache mno mnayokumbuka. [An-Naml: 62]

 

Na pia Akamuamrisha Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kumpwekesha na kutokumshirikisha na kwamba hata yeye Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hana uwezo wa kumnufaisha mtu wala kumdhuru wala kumjaalia hidaaya:

 

قُلْ إِنَّمَا أَدْعُو رَبِّي وَلَا أُشْرِكُ بِهِ أَحَدًا﴿٢٠﴾

Sema: (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi namuomba Rabb wangu na wala simshirikishi na yeyote.”

 

 

قُلْ إِنِّي لَا أَمْلِكُ لَكُمْ ضَرًّا وَلَا رَشَدًا﴿٢١﴾

Sema: “Hakika mimi sikumilikieni dhara na wala uongofu.” [Al-Jinn: 20-21]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَلَا تَدْعُ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُكَ وَلَا يَضُرُّكَ ۖ فَإِن فَعَلْتَ فَإِنَّكَ إِذًا مِّنَ الظَّالِمِينَ﴿١٠٦﴾

Na wala usiombe badala ya Allaah visivyokufaa wala visivyokudhuru. Na ukifanya, basi hakika utakuwa miongoni mwa madhalimu.

 

 

وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ وَإِن يُرِدْكَ بِخَيْرٍ فَلَا رَادَّ لِفَضْلِهِ ۚ يُصِيبُ بِهِ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۚوَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿١٠٧﴾

Na Allaah Akikugusisha dhara, basi hakuna wa kuiondosha isipokuwa Yeye. Na Akikutakia kheri, basi hakuna wa kurudisha fadhila Zake, Anasababisha kumfikia kwayo (fadhila Yake) Amtakaye katika waja Wake. Naye ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Yuwnus: 106-107]

 

 

Na maharamsho mengineyo mengi yanapatikana katika Qur-aan:

 

إِنَّ الَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ عِبَادٌ أَمْثَالُكُمْ ۖ فَادْعُوهُمْ فَلْيَسْتَجِيبُوا لَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ﴿١٩٤﴾

Hakika wale mnaowaomba badala ya Allaah ni waja kama nyinyi. Hebu waiteni wakuitikieni ikiwa nyinyi ni wakweli. [Al-A’raaf: 194]

 

 

Wale ambao wanaombwa, hawawezi kujiondoshea wenyewe madhara wala kujinufaisha Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا ﴿٥٦﴾

Sema: “Iteni wale ambao mnadai (ni waabudiwa) pasi Naye, basi hawamiliki kukuondesheeni dhara na wala kuihamisha (kwa mwengine).” [Al-Israa: 56]

 

 

Na Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَمَا لَهُمْ فِيهِمَا مِن شِرْكٍ وَمَا لَهُ مِنْهُم مِّن ظَهِيرٍ ﴿٢٢﴾

Sema: “Ombeni wale mnaodai kwa dhana (ni waabudiwa) badala ya Allaah, hawamiliki hata uzito wa sisimizi mbinguni wala ardhini, na wala hawana humo ushirika Naye, na wala Yeye (Allaah) Hana msaidizi miongoni mwao.” [Sabaa: 22]

 

 

Hakuna anachokipata yule ambaye anamshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) isipokuwa ni khasara duniani na Aakhirah na kujiweka katika upotofu:

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَعْبُدُ اللَّـهَ عَلَىٰ حَرْفٍ ۖ فَإِنْ أَصَابَهُ خَيْرٌ اطْمَأَنَّ بِهِ ۖ وَإِنْ أَصَابَتْهُ فِتْنَةٌ انقَلَبَ عَلَىٰ وَجْهِهِ خَسِرَ الدُّنْيَا وَالْآخِرَةَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْخُسْرَانُ الْمُبِينُ ﴿١١﴾

Na miongoni mwa watu yuko anayemwabudu Allaah ukingoni. Inapompata kheri, hutumainika kwayo; Na inapompata mtihani hugeuka nyuma juu ya uso wake (kurudia kufru). Amekhasirika duniani na Aakhirah. Hiyo ndiyo khasara bayana.

 

 

يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَضُرُّهُ وَمَا لَا يَنفَعُهُ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الضَّلَالُ الْبَعِيدُ ﴿١٢﴾

Humwomba badala ya Allaah ambavyo visivyomdhuru na wala visivyomnufaisha. Huo ndio upotofu wa mbali.

 

يَدْعُو لَمَن ضَرُّهُ أَقْرَبُ مِن نَّفْعِهِ ۚ لَبِئْسَ الْمَوْلَىٰ وَلَبِئْسَ الْعَشِيرُ ﴿١٣﴾

Humwomba yule ambaye dhara yake iko karibu kuliko manufaa yake. Bila shaka ni mlinzi muovu kabisa, na bila shaka ni rafiki muovu kabisa. [Al-Hajj: 11-13]

 

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَمَنْ أَضَلُّ مِمَّن يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَن لَّا يَسْتَجِيبُ لَهُ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَهُمْ عَن دُعَائِهِمْ غَافِلُونَ﴿٥﴾

 “Na nani aliyepotoka zaidi kuliko ambaye anayeomba asiyekuwa Allaah ambaye hamuitikii mpaka Siku ya Qiyaamah; nao wala hawatambui  maombi yao.” [Al-Ahqaaf: 5]

 

 

 

Pia, maharamisho kadhaa katika Sunnah za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yameshatangulizwa katika silsilah za maudhui hii ya “Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!”

 

 

 

Share

19-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Istighaathah Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

19 - Istighaathah (Kuomba Uokozi) Kwa Asiyekuwa Allaah

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

Maana Ya Istighaathah na dalili zake:

 

Istighaathah maana yake ni kuomba uokozi kwa ambaye ataweza kuokoa kutokana na hali ya shida, dhiki na kukaribia kudhurika au kuangamia. Na istighaathah kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) inajumuisha kujidhalilisha Kwake na kuitakidi kwamba hakuna mwengine atakayeweza kuokoa isipokuwa Yeye, kama vile hali ilivyokuwa katika vita vya Badr, Ibn Kathiyr amesema:

 

 

"Ilipokuwa siku ya Badr na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaona uchache wa Maswahaba wake na wingi wa adui zake, wakawa katika shida na khofu, akaelekea Qiblah na kuomba uokovu na akaendelea kumuomba Mola wake mpaka joho lake likamuanguka begani mwake, Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Akateremsha:

 

إِذْ تَسْتَغِيثُونَ رَبَّكُمْ فَاسْتَجَابَ لَكُمْ

Na pindi mlipomuomba uokovu Rabb wenu Naye Akakuitikieni  [Al-Anfaal: 9] [mpaka mwisho wa Aayah 13 Suwrat Al-Anfaal]

 

 

Kuomba uokovu kwa bin-Aadam kwa jambo ambalo limo katika uwezo wake inafaa kwa dalili kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuhusu kisa cha Nabiy Muwsaa (‘Alayhis-Salaam):

 

وَدَخَلَ الْمَدِينَةَ عَلَىٰ حِينِ غَفْلَةٍ مِّنْ أَهْلِهَا فَوَجَدَ فِيهَا رَجُلَيْنِ يَقْتَتِلَانِ هَـٰذَا مِن شِيعَتِهِ وَهَـٰذَا مِنْ عَدُوِّهِ ۖ فَاسْتَغَاثَهُ الَّذِي مِن شِيعَتِهِ عَلَى الَّذِي مِنْ عَدُوِّهِ

Na akaingia mjini wakati watu wake wako katika mighafiliko, akakuta humo watu wawili wanapigana; mmoja ni miongoni mwa kundi lake, na mwengine miongoni mwa adui wake. Akamsaidia kumuokoa yule ambaye katika kundi lake dhidi ya yule ambaye ni katika adui wake… [Al-Qaswasw: 15]

 

Pia, mtu anaweza kuomba uokovu kwa mwenziwe amuokoe kutokana na adui zake katika hali ya vita n.k. Au mfano mtu anapokuwa katika hali ya kukaribia kuzama baharini akaita: “Ee ndugu! Nazama niokoe!”

 

Ama kuomba uokovu kwa jambo ambalo halimo katika uwezo wa bin-Aadam, hapo huwa ni shirki. Mfano mtu kumuomba mwenziwe:

 

“Ee fulani! Nisaidie kuniokoa na Moto wa Jahannam na niingize Jannah!”

 

“Ee Fulani! Nisaidie kuniokoa katika upotofu unijaalie hidaaya!”

 

Au kuomba walio kaburini:

 

“Ee walii wangu, au shekhe wangu!

 

Au sharifu fulani! Nisaidie kuniokoka na adhabu za kaburi! Nisaidie kuniokoa katika maradhi niliyo nayo!”

 

Kadhaalika, kuomba uokovu kwa mazimwi, mashaytwaan n.k. kuitakidi kuwa wao wana uwezo wa kuokoa katika hali ambazo hakuna mwenye uwezo isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). 

 

Vilevile kuomba uokovu kwa kumchanganya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihu wa sallam) kwa mfano: kusema  "Ee Allaah  niokoe mie katika hizi dhiki kwa baraka Zako na baraka za Rasuli Wako."

 

Hivyo ni shirki kubwa na inamtoa mtu nje ya Uislamu.

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwamba hao wanaoombwa uokovu n.k. hawawezi wenyewe kujinusuru nafsi zao humo walimo makaburini wala Siku ya Qiyaamah hawatokuwa na uwezo wowote ule!

يَوْمَ لَا يُغْنِي مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ﴿٤١﴾

Siku ambayo jamaa wa karibu hatomfaa jamaa wa karibu chochote, na wala wao hawatonusuriwa. [Ad-Dukhaan: 41]

  

Hata Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwa na uwezo wa kumuokoa mtu kwa dalili kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema katika Aayah kadhaa kwamba yule Ambaye Ameshamhukumu kuwa ni mpotofu, basi hakuna wa kumhidi:

 

مَن يَهْدِ اللَّـهُ فَهُوَ الْمُهْتَدِ ۖ وَمَن يُضْلِلْ فَلَن تَجِدَ لَهُ وَلِيًّا مُّرْشِدًا ﴿١٧﴾

Ambaye Allaah Amemwongoza, basi yeye ndiye aliyehidika. Na Anayemwacha kupotoka basi hutompatia mlinzi wa kumuongoza. [Al-Kahf: 17]

 

Au ambaye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amemhukumu kuwa ni mtu wa Motoni, basi hakuna wa kumuokoka, Akamwambia Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

أَفَمَنْ حَقَّ عَلَيْهِ كَلِمَةُ الْعَذَابِ أَفَأَنتَ تُنقِذُ مَن فِي النَّارِ ﴿١٩﴾

Je, yule iliyemthibitikia neno la adhabu je, basi wewe utaweza kumuokoa aliyemo katika moto? [Az-Zumar: 19]

 

 

Alikuweko mnafiki mmoja akiwaudhi Waumini ikahadithiwa:

 

عن عُبَادَةَ بْنَ الصَّامِتِ (رضي الله عنه) قال: خَرَجَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ): قُومُوا نَسْتَغِيثُ بِرَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) مِنْ هَذَا الْمُنَافِقِ. فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ:  ((أنه لاَ يُسْتَغَاث بِي، وَإِنَّمَا يُسْتَغَاثُ باِلله))

Kutoka kwa ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitujia kisha Abu Bakr akasema: Simameni tutake msaada kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) atuokoe na mnafiki huyu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Hakika haipasi kuombwa uokovu kwangu, bali inapaswa kuombwa uokovu kwa Allaah)) [At-Twabaraaniy fiy Mu’jamil–Kabiyr]  

 

Pia Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba ilipoteremshwa kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

Na onya (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) jamaa zako wa karibu. [Ash-Shu’araa: 214]

 

 

دَعَا رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قُرَيْشًا فَاجْتَمَعُوا فَعَمَّ وَخَصَّ فَقَالَ: ((يَا بَنِي كَعْبِ بْنِ لُؤَيٍّ، أَنْقِذُوا أَنْفُسَكُمْ مِنْ النَّارِ، يَا بَنِي مُرَّةَ بنِ كَعْبٍ أَنْقِذُوا أَنْفُسَكُمْ مِنْ النَّارِ، يَا بَنِي عَبْدِ شَمْسٍ أَنْقِذُوا أَنْفُسَكُمْ مِنْ النَّارِ،يَا بَنِي عَبْدِ مَنَافٍ أَنْقِذُوا أَنْفُسَكُمْ مِنْ النَّارِ، يَا بَنِي هَاشِمٍ أَنْقِذُوا أَنْفُسَكُمْ مِنْ النَّارِ ، يَا بَنِي عَبْدِ الْمُطَّلِبِ أَنْقِذُوا أَنْفُسَكُمْ مِنْ النَّارِ، يَا فَاطِمَةُ أَنْقِذِي نَفْسَكِ مِنْ النَّارِ، فَإِنِّي لَا أَمْلِكُ لَكُمْ مِنْ اللَّهِ شَيْئًا غَيْرَ أَنَّ لَكُمْ رَحِمًا سَأَبُلُّهَا بِبَلَالِهَا))

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaita Maquraysh akawaonya kwa ujumla kisha makhsusi (kwa kabila fulani) akasema:  ((Ee Baniy Ka’ab bin Luayy, okoeni nafsi zenu kutokana na Moto!  Ee Baniy Murrah bin Ka’b, okoeni nafsi zenu kutokana na Moto! Ee Baniy ‘Abdi Shams, okoeni nafsi zenu kutokana na Moto. Ee Baniy ‘Abdi Manaaf, okoeni nafsi zenu kutokana na Moto.” Ee Baniy Haashim, okoeni nafsi zenu kutokana na Moto.” Ee Baniy ‘Abdil-Muttwalib, okoeni nafsi zenu kutokana na Moto.” Yaa Faatwimah, okoa nafsi yako kutokana na Moto! Kwani hakika mimi similiki uwezo wowote kwenu isipokuwa nitaendelea kuweka uhusiano wetu wa damu.)) [Muslim]

 

Anatahadharisha pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika kauli Zake mbali mbali:

 

وَالَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِهِ لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَكُمْ وَلَا أَنفُسَهُمْ يَنصُرُونَ﴿١٩٧﴾

Na wale mnaowaomba (na kuwaabudu) badala ya Allaah hawawezi kuwanusuru na wala hawawezi kujinusuru nafsi zao. [Al-A’raaf: 197]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 أَمْ لَهُمْ آلِهَةٌ تَمْنَعُهُم مِّن دُونِنَا ۚ لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَ أَنفُسِهِمْ وَلَا هُم مِّنَّا يُصْحَبُونَ ﴿٤٣﴾

Je, kwani wana waabudiwa wanaoweza kuwakinga Nasi?  Hawawezi kujinusuru nafsi zao na wala hawatolindwa Nasi. [Al-Anbiyaa: 43]

 

Na pia Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لَّعَلَّهُمْ يُنصَرُونَ ﴿٧٤﴾

Na wamejichukulia badala ya Allaah waabudiwa ili wakitumaini kuwa watawanusuru!

 

لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَهُمْ وَهُمْ لَهُمْ جُندٌ مُّحْضَرُونَ ﴿٧٥﴾

Hawawezi kuwanusuru, na watahudhurishwa (adhabuni) kama askari dhidi ya hao (waliowaabudu). [Yaasiyn: 74-75]

 

 

 

Share

20-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Isti’aadhah Kwa Asiyekuwa Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

20 - Isti’aadhah  (Kuomba Kinga) Kwa Asiyekuwa Allaah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

Isti’aadhah maana yake ni kuomba kujikinga kuepukana na shari. Na Isti’aadhah kwa Allaah ni kuomba kujikinga Kwake (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na kuitakidi kuwa unabakia katika hifdhi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na inapasa kujidhalilisha Kwake na kumtegemea Yeye Pekee kuwa Ndiye Atakayekukinga na shari zinazokusudiwa kujikinga nazo. 

 

Ibnul-Qayyim (Rahimahu Allaah) amesema:

“Tambua kwamba tamshi la عاذ na yanayohusiana katika Swarf (sarufi) inamaanisha kujihifadhi na kinga na kuokoka. Na hakika maana yake ni kukimbia kitu unachokiogopa kwa ambaye atakayekuepusha nacho. Na ndio maana ikaitwa Isti’aadhah kwake kama ilivyo maana ya kimbilio.” [Badaa’i Al-Fawaaid (2426)].

 

Isti’aadhah inaweza kuwa kwa kutaja Jina Lake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Anavyosema:

 

وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ الشَّيْطَانِ نَزْغٌ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ ۖ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ﴿٣٦﴾

Na utakapokuchochea uchochezi kutoka kwa shaytwaan, basi omba kinga kwa Allaah. Hakika Yeye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote. [Fusw-Swilat: 36]

 

 

Kujikinga na shaytwaan ni kwa sababu shaytwaan ni adui mkubwa kabisa kwa bin-Aadam, inahitajika kujikinga naye katika kila hali kwa sababu ya ahadi yake ya kuazimia kuwapotosha wanaadamu. Ndio maana Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaamrisha kujikinga naye pale anapoanza kuchochea.

 

Na katika hali ya kusoma Qur-aan pia inahitajika zaidi kujikinga naye. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameamrisha:

 

فَإِذَا قَرَأْتَ الْقُرْآنَ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ﴿٩٨﴾

Unaposoma kusoma Qur-aan basi (kwanza) omba kinga kwa Allaah dhidi ya shaytwaan aliyetokomezwa mbali na kulaaniwa. [An-Nahl: 98]

 

 

Na katika Swalaah inatakiwa kuomba kinga kutokana na shaytwaan kwa pindi anaposhawishi katika Swalaah kwa kusema:

أَعُوذُ بِاللَّه مِنْ شَرِّ خَنْزَبْ

A’uwudhu biLLaahi min sharri khanzab  

 

kama maelezo yalivyothibiti katika Hadiyth ifuatayo:

 

 عن عُثْمَانَ بْن أَبِي الْعَاصِ رضي الله عنه أنه أَتَى النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنَّ الشَّيْطَانَ قَدْ حَالَ بَيْنِي وَبَيْنَ صَلَاتِي وَقِرَاءَتِي يَلْبِسُهَا عَلَيَّ: فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((ذَاكَ شَيْطَانٌ يُقَالُ لَهُ خَنْزَبٌ، فَإِذَا أَحْسَسْتَهُ فَتَعَوَّذْ بِاللَّهِ مِنْهُ وَاتْفِلْ عَلَى يَسَارِكَ ثَلَاثًا)) قَالَ: فَفَعَلْتُ ذَلِكَ فَأَذْهَبَهُ اللَّهُ عَنِّي .

‘Uthmaan bin Abiy Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba alikwenda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika shaytwaan kanijia baina yangu na Swalaah yangu na kisomo changu akinivaa. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema ((Huyo ni shaytwaan anayeitwa Khanzab, basi ukimhisi jikinge naye kwa Allaah, na tema mate upande wa kushoto kwako  mara tatu)). Akasema: Nikafanya hivyo basi akaniondoka shaytwaan. [Muslim]

 

Isti’aadhah pia inawezekana kwa kutaja ‘Rabb’ kwa dalili ya Suwrah mbili katika Qur-aan zinajulikana kama ni Al-Mu‘awwidhataan (mbili za kujikinga)  

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾

Sema: “Najikinga na Rabb wa mapambazuko. [Al-Falaq: 1] mpaka mwisho wake na

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ﴿١﴾

Sema: “Najikinga na Rabb wa watu. [An-Naas: 1] mpaka mwisho wake.

 

Na isti’aadhah inafaa pia kwa kutumia Sifa Zake na Utukufu Wake. Ilipoteremka Aayah:

 

قُلْ هُوَ الْقَادِرُ عَلَىٰ أَن يَبْعَثَ عَلَيْكُمْ عَذَابًا مِّن فَوْقِكُمْ أَوْ مِن تَحْتِ أَرْجُلِكُمْ

Sema: “Yeye ni Muweza wa kukuleteeni adhabu kutoka juu yenu, au kutoka chini ya miguu yenu,  [Al-An’aam: 65]

 

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliomba kinga akasema:

 

أَعُوذُ بِوَجْهِكُ

Najikinga kwa Wajihi Wako [Hadiyth kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia Al-Bukhaariy]

 

Na pia kwa kuunganisha Jina Lake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) pamoja Sifa Zake kama ilivyothibiti katika kinga ya pale mtu anapopata maumivu akashika sehemu inayopatikana maumivu akasema:

 

أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ

A’uwdhu biLLaahi wa-Qudratihi min sharri maa ajidu wa uhaadhiru

 

Najikinga kwa Allaah na kwa Uwezo Wake kutokana na shari ya ninachokisikia na ninachokiogopa)) [Muslim, Ibn Maajah na wengineo kwa usimulizi tofauti kidogo]

 

Pia Isti’aadhah kwa kutumia Maneno Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa dalili:

 

 أَعُوْذُ بِكَلِماتِ اللَّهِ التَّامَّتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ

A’uwdhu bi-Kalimaati-LLaahit-ttaammati min sharri maa khalaq (mara 3 jioni na asubuhi)

 

Najikinga kwa Maneno ya Allaah yaliyotimia kutokana na shari Aliyoiumba [Hadiyth ya Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ameisimulia Ahmad (2/290), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [590], Ibn As-Sunniy [68]. Taz. Swahiyh At-Tirmidhiy (3/187), Swahiyh Ibn Maajah (92/266), Tuhfat Al-Akhyaar (Uk. 45)   katika Swahiyh Al-Jaami’ [6427] (Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayesema mara tatu jioni hatodhuriwa na mdudu wa sumu usiku huo”] 

 

Pia; Dalili nyingi zipo katika Sunnah kuhusu kuomba kinga za kila aina;

 

-Kuomba kinga kutokana na adhabu za Allaah za duniani na Aakhirah.

 

-Kuomba kinga kutokana na adhabu za kaburi, fitnah za Masiyh Ad-Dajjaal na fitna za uhai na fitnah za mauti.

 

-Kuomba kinga  kutokana na Moto wa Jahannam.

 

-Kuomba kinga kutokana na shari za mashaytwaan na majini.

 

-Kuomba kinga kutokana na shari za adui.

 

-Kuomba kinga kutokana na maradhi.

 

-Kuomba kinga kutokana na upotofu.

 

-Kuomba kinga kutokana na ufakiri na kufru,.

 

-Kuomba kinga kutokana na shari za viungo vya mwili, na vitu vinginevyo kadhaa.

 

-Pia kuomba kinga  kutokana na hali kadhaa wa kadhaa. [Rejea Du’aa za Sunnah ya Nabiy Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam]

 

Kujikinga kupitia kwa bin-Aadam inaruhusika pale inapokuwa jambo ambalo analoombwa kukinga ni katika uwezo wake kwa dalili:

 

 

عَنْ جَابِرٍ أَنَّ امْرَأَةً مِنْ بَنِي مَخْزُومٍ سَرَقَتْ فَأُتِيَ بِهَا النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَعَاذَتْ بِأُمِّ سَلَمَةَ زَوْجِ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((وَاللَّهِ لَوْ كَانَتْ فَاطِمَةُ لَقَطَعْتُ)) يَدَهَا فَقُطِعَتْ

Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba mwanamke mmoja katika Baniy Makhzuwm aliiba akaletwa kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akajikinga kwa Ummu Salamah ambaye ni mke wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Wa-Allaahi angekuwa ni Faatwimah (aliyeiba) ningelimkata mkono wake)) Ukakatwa mkono wake. [Muslim]

 

Pia kujikinga katika mahali kadhaa:

 

عَنْ أبي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((سَتَكُونُ فِتَنٌ الْقَاعِدُ فِيهَا خَيْرٌ مِنَ الْقَائِمِ، وَالْقَائِمُ خَيْرٌ مِنَ الْمَاشِي، وَالْمَاشِي فِيهَا خَيْرٌ مِنَ السَّاعِي، مَنْ تَشَرَّفَ لَهَا تَسْتَشْرِفْهُ، فَمَنْ وَجَدَ مَلْجَأً أَوْ مَعَاذًا فَلْيَعُذْ بِهِ))‏.‏

Abuu Huraryah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Kutatokea fitnah ambayo mtu aliyekaa kitako atakuwa bora kuliko yule aliyesimama, na aliyesimama atakuwa bora kuliko yule anayetembea, na anayetembea humo atakuwa bora kuliko anayekimbia. Atakayajitokeza kuingia katika fitnah hizi basi zitamuangamiza. Kwa hiyo yeyote atakayepata mahali pa kujikinga au kimbilio basi ajikinge kwayo)) [Al-Bukhaariy]

 

Na pia:

 

عَنْ عُبَيْدِ اللَّهِ ابْنِ الْقِبْطِيَّةِ، قَالَ دَخَلَ الْحَارِثُ بْنُ أَبِي رَبِيعَةَ وَعَبْدُ اللَّهِ بْنُ صَفْوَانَ وَأَنَا مَعَهُمَا، عَلَى أُمِّ سَلَمَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ فَسَأَلاَهَا عَنِ الْجَيْشِ الَّذِي يُخْسَفُ بِهِ وَكَانَ ذَلِكَ فِي أَيَّامِ ابْنِ الزُّبَيْرِ فَقَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((يَعُوذُ عَائِذٌ بِالْبَيْتِ فَيُبْعَثُ إِلَيْهِ بَعْثٌ فَإِذَا كَانُوا بِبَيْدَاءَ مِنَ الأَرْضِ خُسِفَ بِهِمْ))‏ ‏ فَقُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ فَكَيْفَ بِمَنْ كَانَ كَارِهًا؟  قَالَ: ((يُخْسَفُ بِهِ مَعَهُمْ وَلَكِنَّهُ يُبْعَثُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَلَى نِيَّتِهِ)) ‏ وَقَالَ أَبُو جَعْفَرٍ هِيَ بَيْدَاءُ الْمَدِينَةِ  

‘Ubaydu-Allaah bin Al-Qitwbiyyah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba: Haarith bin Abiy Rabiy’ah na ‘Abdullaah bin Abiy Swafwaan pamoja nami tulikwenda kwa Mama wa Waumini Ummu Salamah wakamuuliza kuhusu jeshi ambalo litadidimizwa ardhini, na hii ni pale wakati ambapo Ibn Zubayr  (alipokuwa gavana wa Makkah).  Akahadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: ((Atatafuta mtu kinga katika Nyumba Tukufu kisha jeshi litatumwa kwake (ili wamuue) basi litakapoingia ardhi kame iliyohamwa (jangwa) litadidimizwa)) Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Je itakuwaje kwa ambaye amelazimishwa hayo? Akasema: ((Atatadimizwa nao lakini atafufuliwa Siku ya Qiyaamah katika hali ya niyyah yake)) Abu Ja’far amesema: Ardhi kame ni Madiynah. [Muslim]  

 

Ama kujikinga kinyume na vile ilivyothibiti katika shariy’ah kwa kuomba kinga kwa mambo ambayo hakuna mwenye uwezo nayo isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) huwa ni shirki, kama vile walivyofanya washirikina walipokuwa wakijikinga kwa majini Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 وَأَنَّهُ كَانَ رِجَالٌ مِّنَ الْإِنسِ يَعُوذُونَ بِرِجَالٍ مِّنَ الْجِنِّ فَزَادُوهُمْ رَهَقًا﴿٦﴾

 “Na kwamba walikuwa wanaume miongoni mwa wana Aadam wanajikinga na wanaume miongoni mwa majini, basi wakawazidishia madhambi, uvukaji mipaka ya kuasi na khofu.” [Al-Jinn: 6]

 

 

Makosa yafanywayo na Waislamu wa sasa katika kujikinga kwa asiyekuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kufuata mila mfano;

 

-Baadhi ya watu  wanaojikinga katika kufunga ndoa kwa kumwaga damu ya mbuzi na kuikanyaga.

 

-Kuna wanaojikinga dhidi ya jicho baya au husda kwa kuvunja mayai kwenye hicho kitu alichonunua mtu kama vile gari mpya.

 

-Kuna wanaojikinga kwa mayatima kwa kuwafadhili kwa chakula kuitakidi kuwa du’aa yao inawatosheleza kujikinga.

 

-Kuna wanaojikinga na mashaytwaan wanapohamia nyumba mpya kwa kuchinja mbuzi au mialiko ya watu kusoma kisomo.

 

 

Kinga hizo zote hazijuzu bali mtu Muislamu anapaswa kutumia kinga zilizothibiti katika mafundisho Swahiyh  aliyokuja nayo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Mfano katika kuhamia nyumba mafunzo Swahiyh ni:

 

عن خَوْلَةَ بِنْت الحَكِيمِ قالت: سمعت رَسُولِ الله -صلى الله عليه وسلم -يقَولَ: ((مَنْ نَزَلَ مَنْزِلاً فقَالَ أَعُوذُ بِكلِمَاتِ الله التّامّاتِ مِن شَرّ مَا خَلَقَ لَمْ يَضُرّهُ شيءٌ حَتّى يَرْحَلَ مِنْ مَنْزِلِهِ ذَلِكَ))

Khawlat bint Hakiym amehadithia kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Atakayeteremka katika kituo (au makazi) kisha akasema: “A’uwdhu bi-Kalimaatil-LLaahit-taammati min sharri maa Khalaq - Najilinda kwa Maneno ya Allaah yaliyotimia na shari Alichokiumba” hakuna kitakachomdhuru hadi atakapoondoka katika kituo (au makazi) hicho)) [Muslim]

 

 

 

 

Share

21-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! - Kutabiria Ya Ghayb; Kheri, Shari, Nuksi, Unajimu

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

21-Kutabiria Ya Ghayb Ya Khayr Au Shari, Nuksi, Unajimu Na Kutazamia Kwa Mtabiri

Alhidaaya.com

 

 

 

Kubashiria mambo ya ghayb ni katika ujuzi wa ghayb ambayo hakuna mwenye ujuzi nayo isipokuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Anavyosema Mwenyewe (‘Azza wa Jalla):

 

 

قُل لَّا يَعْلَمُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ الْغَيْبَ إِلَّا اللَّـهُ ۚ وَمَا يَشْعُرُونَ أَيَّانَ يُبْعَثُونَ ﴿٦٥﴾

Sema: “Hakuna aliyoko katika mbingu na ardhi ajuaye ghayb isipokuwa Allaah. Na wala hawatambui lini watafufuliwa.” [An-Naml: 65]

 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَعِندَهُ مَفَاتِحُ الْغَيْبِ لَا يَعْلَمُهَا إِلَّا هُوَ

Na Kwake (Allaah) zipo funguo za ghayb; hakuna azijuaye ila Yeye tu [Al-An’aam: 59]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ اللَّـهَ عِندَهُ عِلْمُ السَّاعَةِ وَيُنَزِّلُ الْغَيْثَ وَيَعْلَمُ مَا فِي الْأَرْحَامِ ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤﴾

Hakika Allaah Ana elimu ya Saa (Qiyaamah), na Anateremsha mvua na Anajua yale yaliyomo katika tumbo la uzazi na nafsi yoyote haijui nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haijui itafia katika ardhi gani, hakika Allaah ni Mjuzi wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika [Luqmaan: 34]

 

 

Na kutabiria au kubashiria ya ghayb ni miongoni mwa shirki kubwa inayomtoa mtu nje ya Uislaam kwa dalili, kauli za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه،  عَنْ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ أَتَى كَاهِنًا، أَوْ عَرَّافًا، فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ، فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayemwendea kahini au mpigaji ramli akamuamini asemayo, basi atakuwa ameshakufuru yale aliyoteremshiwa nayo Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).” [Ahmad, na Aswhaabus-Sunan wanne, na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Targhiyb wat-Tarhiyb (3047)]

 

Na kwa dalili pia kuwa Swalaah hazikubalikiwi siku arubaini!

 

مَنْ أَتَى عَرَّافًا فَسَأَلَهُ عَنْ شَيْءٍ لَمْ تُقْبَلْ لَهُ صَلَاةٌ أَرْبَعِينَ لَيْلَةً

((Atakayekwenda kwa mtabiri akamuuliza kitu haitokubaliwa Swalaah yake siku arubaini)) [Muslim]

 

Basi jiulize ndugu Muislaam unayemshirikisha Allaah! Je, itakuwaje pindi akikufikia Malak-Al-Mawt (Malaika wa kufisha) akakutoa roho yako kipindi hicho wakati uko nje ya Uislaam?

 

Mifano ya njia zinazotabiriwa: 

 

1- Kwenda kwa mtabiri:

 

 

Mtabiri hutazamia kwa mikono na kumbashiria mtu mazuri yatakayomfika siku za mbele au mabaya yatakayomsibu mtu. Hutazamia ima kwa vikombe baada ya huyo mtu anayetazamiwa kunywa chai au kahawa ikabakishwa kidogo, basi huzungushwa kikombe chake cha chai au kahawa kisha hutabiriwa ya khayr au shari kumfikia. Au hutabiri kwa kuandika nambari katika vikaratasi, kwa nyota, au kutazamwa viganja vya mikono n.k.

 

2- Kutazamia kwa unajimu na kutangazwa kwenye magazeti na majarida (horoscope):

 

Pia, kuna wanaotabiri kwa njia ya unajimu (kutazamia nyota) kuhusiana na mwezi aliozaliwa mtu inayojulikana kama 'horoscope'.  Unajimu huu hutiwa magazetini na watu husoma kila mara kutabiri bahati zao au shari zitakazowasibu katika siku fulani. Wanadai kuwa sayari kama gemini, taurus, aries n.k. zinahusiana na mwezi wa mtu aliozaliwa na hivyo basi waliozaliwa katika sayari hizo siku hiyo kwao huwaathiri nafsi zao na kadhaa wa kadhaa.

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameharamisha unajimu:

 

 عن عبد الله بن عباس (رضي الله عنهما) عن النبي (صلى الله عليه وسلم): ((من اقتبس شعبةً من النجومِ فقد اقتبس شعبةً من السحرِ زاد ما زاد))

Amehadithia ‘Abdullaah bin ‘Abaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayejichumia tawi katika ujuzi wa unajimu, atakuwa amejichumia tawi katika sihri, na itaendelea kuzidi na kuzidi.” [Abuu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]

 

 

3- Kutabiri khayr au shari au nuksi kutokana na matukio fulani:

 

Ni mambo yanayotabiriwa na watu katika jamii za Kiislamu na kuyaitakidi kwamba ni mambo yatakayomtokea mtu. Mambo hayo huwa ima ya khayr au shari, au nuksi, mkosi, ukorofi n.k. Na hakika itikadi hizi miongoni mwa Waislaam zimekuwa kama ni jambo la kawaida  na ilhali ni jambo la khatari kabisa kwa kuwa ni miongoni mwa shirki kubwa ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Hamghufurii mtu asiporudi kutubia! Yanayotabiriwa yako mengi mno, ila haya yafuatayo ndio ambayo tumejaaliwa kuyajua na kuyanukuu:

 

a) Akitajwa mtu kisha hapo hapo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akajaalia huyo mtu atokee au asikike kwa simu n.k., basi hubashiriwa kuwa atakuwa na umri mrefu!

 

b) Jicho likimcheza mtu upande wa kushoto huamini kuwa itamfika shari na ikiwa upande wa kulia huamini kuwa itamfikia khayr! Na wengine husema: “Sharr ba’iyd na khayr qariyb”(shari iwe mbali na khayr iwe karibu).

 

c) Kusemwa: “Swallu ‘alan-Nabiy!” - inasemwa kwa ajili ya kuondosha jicho baya au husda! Na hutamkwa hivyo katika hali ya kuona jambo zuri, au katika sherehe za harusi kumkinga nayo bi harusi au wenye harusi. Pia kwa ajili ya kunyamazisha mzozano, au anapoona mtu jambo la ajabu n.k. Haya ni mambo ya bid’ah na inaingia katika shirki pia. Vile vile wanawake khaswa kusema kwao katika sherehe: “Aswalaatu was-salaamu ‘alaa habiybinaa Muhammad!” kisha hupigwa vigelegele! Haya pia ni katika bi’dah.

 

d) Pindi mtu akimuona paka mweusi basi inaitakidiwa kuwa siku hiyo itakuwa ni ya mkosi!

 

e) Mkono umkimuwasha mtu basi inabashiriwa kuwa kuna kupata pesa!

 

f) Akifagia mtu usiku basi inatabiriwa kuwa ni kuondosha baraka au kufukuza wageni!

 

g) Akipaliwa mtu hutabiriwa kuwa “anatajwa!”

 

h) Ukikata kucha zote pamoja (ya mikono na miguu) inatabiriwa kuwa shida zikija zitakuja zote pamoja!

 

i) Kushika mbao inaitakidiwa kuwa ni kuepusha hjicho baya na husda! Kwa hiyo unapotaja jambo zuri la kusifia jambo au mtu, itasemwa: “Shika mbao!”

 

j) Mtoto wa kike akivalishwa kofia ya mwanamume ni itikadi kuwa atakosa mahari! 

 

k) Mtu akipatwa na mtihani basi huambiwa akaoge na avue ile nguo kwani ile nguo ina mkosi na ikitokea kuirejea kuvaa ile nguo basi mtu huyo huwa na mashaka kupata tatizo tena. Hali hiyo hupelekea mtu kutoivaa tena ile nguo kwa kuamini akiivaa tu atapata tena mkosi!

 

l) Unapofagia ukapitishia ufagio kama kumsogezea taka binti basi ni itikadi kuwa hatoolewa! 

 

m) Mtoto akichetama na kujichungulia 'awrah (sehemu ya siri) yake, basi watu huamini kuwa mama yake atashika ujauzito!

 

Hizo ni baadhi ya itikadi potofu, za kishirikina na za kijaahiliyyah (zama za ujinga kabla ya Uislaam) kwa sababu washirikina walikuwa wanapotaka kufanya jambo kama vile kusafiri, walikuwa wanatabiria kwa Tatwayyur; (kubashiria mkosi kwa kumrusha ndege). Hurushwa ndege, basi pindi akiruka kuelekea upande wa kulia basi hubashiria kuwa ni khayr na pindi akiruka ndege huyo kuelekea kushoto, basi hubashiria ya shari na hivyo safari huvunjwa!

 

Ukaja Uislaam na kuharamisha shirki hiyo katika Qur-aan na Sunnah. Miongoni mwa Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):  

 

 عن عبد الله بن مسعود قال قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((الطِّيَرَةُ شِركٌ، الطِّيَرَةُ شِركٌ، الطِّيَرَةُ شِركٌ))

Ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atw-Twiyarah (kutabiri nuksi, mikosi n.k) ni shirki, Atw-Twiyarah ni shirki, Atw-Twiyarah ni shirki.” [Swahiyh At-Targhiyb (3098)]

 

Atw-Twiyarah: Maana yake ni kutabiria khayr au kinga ya shari na zaidi inatumika kutabiria nuksi.

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza katika Hadiyth nyengineyo:

 

 

عنْ عُرْوَةَ بْنِ عامِرِ (رضي الله عنه) قال: ذُكِرتِ الطَّيَرَةُ عِنْد رَسُولِ اللَّه صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فقَالَ: ((أحْسَنُهَا الْفَألُ، وَلا تَرُدُّ مُسْلِماً، فَإذا رأى أحَدُكُمْ ما يَكْرَه ، فَلْيقُلْ: اللَّهُمَّ لا يَأتى بالحَسَناتِ إلاَّ أنتَ، وَلا يَدْفَعُ السَّيِّئاتِ إلاَّ أنْتَ، وَلا حوْلَ وَلا قُوَّةَ إلاَّ بك))  

‘Urwah bin ‘Aamir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba: Ilitajwa habari ya kupiga fali mbaya (mkosi) mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Ilio bora zaidi ni kupiga fali nzuri, wala (kupiga fali mbaya) haimrudishi Muislaam (kutokutenda aliloazimia). Mmoja wenu atakapoona analolichukia, aseme: “Allaahumma laa yaa-tiy bil-hasanaat illa Anta, walaa yadfa’us-sayyiaat illa Anta, walaa hawla walaa quwwata illa Bika“ - Ee Allaah, hakuna anayeweza kuleta mambo mema isipokuwa ni Wewe, wala hakuna anayeweza kukinga mabaya isipokuwa ni Wewe. Hakuna uwezo (wa  kuepuka kutenda mabaya) wala nguvu (ya kutenda mema) isipokuwa ni Kwako.) [Hadiyth Swahiyh ameipokea Abu Daawuwd kwa isnaad Swahiyh]

 

Akasema pia: “Hakuna mkosi, na ni bora tegemea khayr (matumaini mema).” Wakauliza nini matumaini mema (matarajio ya kufanikiwa) Yaa Rasuwla-Allaah? Akasema: “Ni neno jema alisikialo mmoja wenu.” [Al-Bukhaariy]

 

Mas-alah haya ya kubashiria ghayb yanapasa kuzingatiwa kwa kina na kuazimiwa kuwafundisha watu khatari zake, kwa sababu watu wengi hawana ujuzi kuwa ni katika mambo ya kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wakidhania kuwa ni mambo ya kawaida. Kwa hiyo ni waajib wa kila Muislamu anayesoma makala hizi kufanya juhudi kuwafikisha Waislamu waepukane na shirki hizi.

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amebainisha jinsi mambo kama haya yanavyomwepesisha mtu kuingia katika kufru:

 

عَنْ زَيْدِ بْنِ خَالِدٍ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: صَلَّى لَنَا رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) صَلاةَ الصُّبْحِ بِالْحُدَيْبِيَةِ عَلَى إِثْرِ سَمَاءٍ كَانَتْ مِنَ اللَّيْلِ، فَلَمَّا انْصَرَفَ أَقَبْلَ عَلَى النَّاسِ، فَقَالَ ((هَلْ تَدْرُونَ مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ؟)) قَالُوا: اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمَ. قَالَ: ((قَالَ أَصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي وَكَافِرٌ، فَأَمَّا مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِفَضْلِ اللَّهِ وَرَحْمَتِهِ، فَذَلِكَ مُؤْمِنٌ بِي كَافِرٌ بِالْكَوْكَبِ، وَأَمَّا مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِنَوْءِ كَذَا وَكَذَا، فَذَلِكَ كَافِرٌ بِي مُؤْمِنٌ بِالْكَوْكَبِ))

Zayd bin Khaalid (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alituswalisha Swalaah ya asubuhi Hudaybiyah baada ya usiku wa mvua. Alipomaliza akawakabili watu akasema: “Je, mnajua Rabb wenu Amesema nini?” Wakajibu: Allaah na Rasuli Wake ndio wajuao. Akasema: ‘Allaah Amesema: Baadhi ya waja Wangu wameamka leo wakiwa wenye kuniamini, na wengine wamekufuru. Aliyesema kuwa mvua ni kutokana na fadhila na Rahmah za Allaah, basi huyo ni mwenye kuniamini wala haamini nyota. Ama aliyesema: Tumenyeshewa mvua kutokana na nyota fulani, yeye ni mwenye kunikufuru na mwenye kuamini nyota.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

22-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! Kumtii Kiumbe Katika Kumuasi Allaah

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

22 -Kumtii Kiumbe Katika Kumuasi Allaah

Alhidaaya.com

 

 

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza mtu kumtii kiumbe yeyote katika kumuasi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa dalili ya Hadiyth ifuatayo:

 

لاَ طَاعَةَ في مَعْصِيَةِ الله ، إِنَّمَا الطَّاعَةُ فِي المَعْرُوفِ

Hakuna kutii katika kumuasi Allaah, bali utiifu ni katika yanayokubalika ki-shariy’ah katika mema.[Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Muislamu anapaswa atii amri kwa anayepasa kumuamrisha hata kama ni jambo analolichukia madamu tu haliko katika kumuasi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama alivyoamrisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَلَى الْمَرْءِ الْمُسْلِمِ السَّمْعُ وَالطَّاعَةُ فِيمَا أَحَبَّ وَكَرِهَ إِلَّا أَنْ يُؤْمَرَ بِمَعْصِيَةٍ فَإِنْ أُمِرَ بِمَعْصِيَةٍ فَلَا سَمْعَ وَلَا طَاعَةَ

“Muislamu anapaswa kusikia na kutii kwa anayoyapenda na anayoyachukia, madhali hakuamrishwa kuasi. Na pindi akiamrishwa katika maasi, basi hakuna kusikia wala kutii.” [Al-Bukhaariy na Muslim

 

 

Mfano wa katika yasiyokubalika katika ki-shariy’ah ni kama usimulizi wa Hadiyth ifuatayo ambako kiongozi alitaka kuwaangamiza Waislamu katika moto:

 

عَنْ عَلِيٍّ، قَالَ: بَعَثَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سَرِيَّةً، وَاسْتَعْمَلَ عَلَيْهِمْ رَجُلًا مِنَ الْأَنْصَارِ وَأَمَرَهُمْ أَنْ يَسْمَعُوا لَهُ وَيُطِيعُوا، فَأَغْضَبُوهُ فِي شَيْءٍ، فَقَالَ: اجْمَعُوا لِي حَطَبًا، فَجَمَعُوا لَهُ، ثُمَّ قَالَ: أَوْقِدُوا نَارًا، فَأَوْقَدُوا، ثُمَّ قَالَ: أَلَمْ يَأْمُرْكُمْ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنْ تَسْمَعُوا لِي وَتُطِيعُوا؟ قَالُوا: بَلَى، قَالَ: فَادْخُلُوهَا، قَالَ: فَنَظَرَ بَعْضُهُمْ إِلَى بَعْضٍ، فَقَالُوا: إِنَّمَا فَرَرْنَا إِلَى رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مِنَ النَّارِ، فَكَانُوا كَذَلِكَ، وَسَكَنَ غَضَبُهُ، وَطُفِئَتِ النَّارُ، فَلَمَّا رَجَعُوا ذَكَرُوا ذَلِكَ لِلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَقَالَ: ((لَوْ دَخَلُوهَا مَا خَرَجُوا مِنْهَا، إِنَّمَا الطَّاعَةُ فِي الْمَعْرُوفِ))

Kutoka kwa ‘Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alituma jeshi chini ya uongozi wa mtu mmoja wa Answaar. Wakamkasirisha kwa sababu ya jambo fulani akawaambia: Kusanyeni kuni. Wakamkusanyia akasema: Niwashieni moto! Wakamuashia. Akasema: Kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakukuamrisheni mnitii? Wakasema: Ndio! Akasema. Basi uingieni!  Wakatazamana kisha wakasema: Hakika sisi tumekimbilia kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kujiepusha na moto. Wakawa hivyo hivyo. Kisha ghadhabu zake zikatulia na moto ukazimwa. Waliporudi kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakamwelezea yalivyojiri,  hapo yeye akasema: “Mngeliuingia, msingetoka kamwe humo. Hakika utiifu ni katika mema.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Katika ambayo hayapasi utiifu:

 

 

1. Kutii katika mambo ya haraam. Maswahaba walimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):  

 

 عَنْ عَدِيّ بْنِ حَاتِمٍ: أَنَّهُ سَمِعَ اَلنَّبِيَّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقْرَأُ هَذِهِ الآيَةَ: اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا إِلَـٰهًا وَاحِدًا ۖ لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۚسُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴿٣١﴾  فَقُلْتُ لَهُ: إِنَّا لَسْنَا نَعْبُدُهُمْ. قَالَ: ((أَلَيْسَ يُحَرِّمُونَ مَا أَحَلَّ اَللَّهُ فَتُحَرِّمُونَهُ وَيُحِلُّونَ مَا حَرَّمَ اَللَّهُ فَتُحِلُّونَهُ؟)) فَقُلْتُ بَلَى. قَالَ:((فَتِلْكَ عِبَادَتُهُم))رَوَاهُ أَحْمَدُ وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ

 

Imepokewa toka kwa ‘Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amemsikia  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisoma Aayah: Wamewafanya Wanachuoni Marabai wao wa dini na Wamonaki wao kuwa ni miola badala ya Allaah, na (pia) Al-Masiyh mwana wa Maryam na hali hawakuamrishwa isipokuwa kumwabudu Ilaah Mmoja Pekee. Hapana mwabudiwa wa haki ila Yeye. Utakasifu ni Wake kutokana na yale yote wanayomshirkisha nayo.   [At-Tawbah: 31] Nikasema: Hakika sisi hatuwaabudu. Akasema: "Je, kwani hawaharamishi Aliyoyahalalisha Allaah nanyi mkayaharamisha? Na wanahalalisha Aliyoyaharamisha Allaah nanyi mnayahalalisha?" Nikasema: Ndio. Akasema: "Basi hivyo ndivyo kuwaabudu." [Ahmad na At-Tirmidhiy na ameipa daraja ya Hasan]

 

 

2. Kuwatii wazazi katika maasi na kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

Mzazi anapaswa kupewa haki yake kumfanyia ihsaan na wema. Lakini pindi anapomuamrisha mwanawe katika kumshirkisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa njia yoyote ile, au kuamrisha kufuata bid’ah (uzushi) au maasi yoyote yale mengineyo ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wameyakataza, basi haipasi kabisa kumtii mzazi, hapo inapasa mtoto akatae kuwatii, na dalili ni kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا ۚ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٨﴾

Na Tumemuusia insani kuwafanyia wema wazazi wake wawili. Lakini wakikushikilia kuwa Unishirikishe na ambayo huna elimu nayo, basi usiwatii; Kwangu ni marejeo yenu, Nitakujulisheni yale mliyokuwa mkiyatenda. [Al-‘Ankabuwt: 8]

 

 

Na mifano mingi tunayo katika Siyrah za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu Maswahaba waliokataa kuwatii wazazi wao, mmojawapo ni Sa’d bin Abiy Waqqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye mama yake alichukia mno yeye kuingia katika Dini ya Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Akamwambia mwanae: “Naapa ima uachane na Dini yako hii mpya au nitajifungia kula na kunywa mpaka nife.” Sa’ad akamwambia: “Ee mama yangu nina mapenzi makubwa kwako kama mama yangu uliyenizaa, lakini mapenzi yangu kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na Rasuli Wake ni makubwa zaidi. Wa-Allaahi lau hata roho elfu moja na moja zitaondoka (kwa kunitaka nirudi dini yangu ya zamani) kamwe sitorudia dini yangu.”

 

3. Kumtii mume au mke katika maasi:

 

Mifano ya mke kumtii mumewe katika maasi ambayo yanajulikana katika jamii, ni mume kumtaka mke achonge nyusi zake na hali laana ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) inamfikia mwenye kunyofoa au kuchonga nyusi zake. 

 

Pia kumtii mume kutokujistiri kwa vazi la Hijaab.

 

Pia kumtii mume katika yaliyoharamishwa kama kumtaka jimai mchana wa Swawm ya Ramadhwaan, au kumtaka afanye naye tendo la ndoa wakati wa hedhi, au kumtaka amuingilie katika utupu wake wa nyuma... na mifano iko mingi.

 

Mfano mzuri tunao katika Qur-aan wa Aasiyah ambaye alikuwa mke wa Fir’awn muasi aliyejifanya kuwa mungu. Aasiyah alikataa kumtii mumewe katika maasi ya kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa sababu alimuamini Allaah. Fir’awn akamuadhibu adhabu kali na kumuua lakini yeye alibakia katika iymaan yake na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anampigia mfano wa wenye kuamini:

 

وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا لِّلَّذِينَ آمَنُوا امْرَأَتَ فِرْعَوْنَ إِذْ قَالَتْ رَبِّ ابْنِ لِي عِندَكَ بَيْتًا فِي الْجَنَّةِ وَنَجِّنِي مِن فِرْعَوْنَ وَعَمَلِهِ وَنَجِّنِي مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ﴿١١﴾

Na Allaah Amewapigia mfano wale walioamini; mke wa Fir’awn, aliposema: “Rabb wangu! Nijengee nyuma Kwako kwenye Jannah na niokoe na Fir’awn na vitendo vyake na niokoe na watu madhalimu.” [At-Tahriym: 11]

 

 

Siku ya Qiyaamah wanaofanyiana utiifu katika maasi hali itakuwa kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

يَوْمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمْ فِي النَّارِ يَقُولُونَ يَا لَيْتَنَا أَطَعْنَا اللَّـهَ وَأَطَعْنَا الرَّسُولَا ﴿٦٦﴾

Siku zitakapopinduliwa nyuso zao motoni, watasema: “Laiti tungelimtii Allaah, na tungelimtii Rasuli.”

 

 

وَقَالُوا رَبَّنَا إِنَّا أَطَعْنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَاءَنَا فَأَضَلُّونَا السَّبِيلَا ﴿٦٧﴾

Na watasema: “Rabb wetu! Hakika sisi tumewatii mabwana zetu, na wakuu wetu, basi wametupoteza njia.”

 

 

رَبَّنَا آتِهِمْ ضِعْفَيْنِ مِنَ الْعَذَابِ وَالْعَنْهُمْ لَعْنًا كَبِيرًا ﴿٦٨﴾

 “Rabb wetu! Wape adhabu maradufu, na walaani laana kubwa.” [Al-Ahzaab:  66-68]

 

 

4. Kumtii rafiki kuacha Swalaah na maasi mengineyo:

 

Kumtii rafiki anayemuamrisha mwenzie aache Swalaah ili wakimbilie katika michezo fulani, mechi za mpira n.k. Au kumtii rafiki katika kusililiza muziki na ngoma, kwenda sehemu zinazotendeka maasi n.k.

 

Siku ya Qiyaamah rafiki huyo atamkanusha mwenziwe kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَيَوْمَ يَعَضُّ الظَّالِمُ عَلَىٰ يَدَيْهِ يَقُولُ يَا لَيْتَنِي اتَّخَذْتُ مَعَ الرَّسُولِ سَبِيلًا ﴿٢٧﴾

Na siku dhalimu atakapotafuna mikono yake akisema: “Laiti ningeshika njia pamoja na Rasuli. 

 

يَا وَيْلَتَىٰ لَيْتَنِي لَمْ أَتَّخِذْ فُلَانًا خَلِيلًا ﴿٢٨﴾

 “Ee ole wangu! Laiti nisingelimfanya fulani kuwa rafiki mwandani.”

 

 

لَّقَدْ أَضَلَّنِي عَنِ الذِّكْرِ بَعْدَ إِذْ جَاءَنِي ۗ وَكَانَ الشَّيْطَانُ لِلْإِنسَانِ خَذُولًا ﴿٢٩﴾

 “Kwa yakini amenipoteza mbali na Ukumbusho baada ya kunijia.” Na shaytwaan kwa insani daima ni mwenye kutelekeza. [Al-Furqaan:  27- 29]

 

 

Ndugu Muislamu, inapokuwa ni amri ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya kujiepusha na maasi basi usimtii yeyote isipokuwa Yeye (‘Azza wa Jalla) na hapo ndipo itakapohakiki iymaan ya mtu kwa dalili ifuatayo ya Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 

 

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((ثَلاَثٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ وَجَدَ حَلاَوَةَ الإِيمَانِ: أَنْ يَكُونَ اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَحَبَّ إِلَيْهِ مِمَّا سِوَاهُمَا, وَأَنْ يُحِبَّ الْمَرْءَ لاَ يُحِبُّهُ إِلاَّ لِلَّهِ, وَأَنْ يَكْرَهَ أَنْ يَعُودَ فِي الْكُفْرِ كَمَا يَكْرَهُ أَنْ يُقْذَفَ فِي النَّارِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: "Mambo matatu atakayekuwa nayo, atapata utamu wa ‘iymaan: Allaah na Rasuli Wake wawe vipenzi zaidi kwake kuliko wengineo, ampende mtu na wala asimpende isipokuwa kwa ajili ya Allaah, na achukie kurudi katika ukafiri baada ya Allaah kumuokoa kutoka huko kama anavyochukia kuingizwa motoni." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hitimisho ni kwamba mtu anapochochewa kutenda maasi basi inamtosheleza kujibu kwa kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ifuatayo:

 

 إِنِّي أَخَافُ إِنْ عَصَيْتُ رَبِّي عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٣﴾

“Hakika nikimuasi Rabb wangu, nina khofu adhabu ya Siku adhimu.” [Az-Zumar: 13]

 

 

 

 

Share

23-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! Sihri (Uchawi) Na Michezo Ya Mazingaombwe

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

23- Sihri (Uchawi) Na Michezo Ya Mazingaombwe

 Alhidaaya.com

 

 

Neno “As-Sihr” (uchawi) maana yake ni kitendo cha kujikurubisha na shaytwaan na kwa msaada wake (shaytwaan) na uchawi ni kulibadilisha jambo mbali na uhakika wake, nako ni kuwadhihirishia watu jambo lisilo la kweli wakaliona kuwa ni la kweli.” [Lisaan Al-‘Arab]

 

 

Na Sihri ni tendo la kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kuwa linahusiana na shaytwaan 'aaswi mwenye kumkufuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Kauli Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

  

وَاتَّبَعُوا مَا تَتْلُو الشَّيَاطِينُ عَلَىٰ مُلْكِ سُلَيْمَانَ ۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيْمَانُ وَلَـٰكِنَّ الشَّيَاطِينَ كَفَرُوا يُعَلِّمُونَ النَّاسَ السِّحْرَ وَمَا أُنزِلَ عَلَى الْمَلَكَيْنِ بِبَابِلَ هَارُوتَ وَمَارُوتَ ۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنْ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَا إِنَّمَا نَحْنُ فِتْنَةٌ فَلَا تَكْفُرْ ۖفَيَتَعَلَّمُونَ مِنْهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِ بَيْنَ الْمَرْءِ وَزَوْجِهِ ۚ وَمَا هُم بِضَارِّينَ بِهِ مِنْ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْ ۚ وَلَقَدْ عَلِمُوا لَمَنِ اشْتَرَاهُ مَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ۚ وَلَبِئْسَ مَا شَرَوْا بِهِ أَنفُسَهُمْ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿١٠٢﴾

Na wakafuata yale waliyoyasoma mashaytwaan juu ya ufalme wa Sulaymaan; na Sulaymaan hakukufuru lakini mashaytwaan ndio waliokufuru; wanafundisha watu sihiri na yaliyoteremshwa kwa Malaika wawili katika (mji wa) Baabil; Haaruwt na Maaruwt. Nao wawili hawamfundishi yeyote mpaka waseme: “Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru.” Kisha wakajifunza kutoka kwa hao wawili yenye kupelekea kufarikisha kwayo baina ya mtu na mkewe. Na wao hawawezi kamwe kumdhuru yeyote kwayo isipokuwa kwa idhini ya Allaah; na wanajifunza yanayowadhuru na wala hayawanufaishi; na kwa yakini walijua kwamba atakayechuma haya hatopata katika Aakhirah fungu lolote, na ni ubaya ulioje walichojiuzia nafsi zao, lau wangelikuwa wanajua. [Al-Baqarah: 102]

 

 

Pia, sihri ni miongoni mwa Al-Kabaair (madhambi makubwa) na ni miongoni mwa ambayo yanamuangamiza mtu kwa dalili ya Hadiyth:

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَمَا هُنَّ؟  قَالَ: ((الشِّرْكُ بِاللَّهِ وَالسِّحْرُ وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ وَأَكْلُ الرِّبَا وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ الْغَافلاَتِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo yaa Rasuwla Allaah? Akawaambia: ((Ni kumshirikisha Allaah, sihri [uchawi], kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa kupambana na adui na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Na sihri ilikuwa ni miongoni mwa shirki za kaumu ya Fir’awn na ndio sababu mojawapo ya kutumwa Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam) kuwataka waache. Alipowaonesha miujiza ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wachawi wa Fir’awn hapo hapo walisujudu kwa kuwa walitambua kuwa sihri ni batili na ni shirki, wakakubali haki na wakajiepusha nayo kama ilivyokuja katika Qur-aan:

 

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ ﴿٤٣﴾

Muwsaa akawambia: “Tupeni vile mnavyotupa.”

 

 

فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ ﴿٤٤﴾

Wakatupa kamba zao na fimbo zao; na wakasema: “Kwa utukufu wa Fir’awn! Hakika sisi ni wenye kushinda.”

 

 

فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ ﴿٤٥﴾

Basi Muwsaa akatupa fimbo yake, tahamaki inameza vyote walivyovizua.

 

 

فَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ ﴿٤٦﴾

Basi wale wachawi wakaanguka wakisujudu.

 

قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٤٧﴾

Wakasema: “Tumemwamini Rabb wa walimwengu.

 

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ﴿٤٨﴾

 “Rabb wa Muwsaa na Haaruwn.” [Ash-Shu’araa: 43-48]

 

 

Na pia katika Suwrah nyengine baada ya wachawi kusujudu wakasilimu wakasema:

 

 إِنَّا آمَنَّا بِرَبِّنَا لِيَغْفِرَ لَنَا خَطَايَانَا وَمَا أَكْرَهْتَنَا عَلَيْهِ مِنَ السِّحْرِ ۗ وَاللَّـهُ خَيْرٌ وَأَبْقَىٰ ﴿٧٣﴾

“Hakika sisi tumemwamini Rabb wetu ili Atughufurie madhambi yetu, na yale uliyotushurutisha katika ya sihiri. Na Allaah ni Mbora Zaidi na Mwenye kudumu zaidi.” [Twaahaa: 73]

 

 

Fir’awn akatakabari na kukanusha haki akasema:

 

قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٤٩﴾

 (Fira’wn) Akasema: “Je, mmemwamini kabla sijakupeni idhini? Hakika bila shaka kubwa lenu ndiye amekufunzeni sihiri. Basi mtakuja kujua. Nitakukatenikateni mikono yenu na miguu yenu kinyume (kulia kwa kushoto), kisha nitakusulubuni nyote.” [Ash-Shu’araa: 49]

                   

 

Lakini wachawi baada ya kuamini wakasema:

 

قَالُوا لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ ﴿٥٠﴾

Wakasema: “Hakuna dhara yoyote! Hakika sisi tunarudi kwa Rabb wetu.

 

 

إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٥١﴾

“Hakika sisi tunatumai kwamba Rabb wetu Atatughufuria madhambi yetu kwa vile tumekuwa wa kwanza wenye kuamini.” [Ash-Shu’araa: 49-51]

 

 

Kuna aina mbili za uchawi: Kufanya sihri kwa ajili ya kumuathiri mtu na kufanya micheo ya sihri (mazingaombwe).

 

 

1- Kufanya sihri kwa ajili ya kumuathiri mtu:

 

 

Wachawi hutumia mashaytwaan kushirikiana nao. Hufanya sihiri kwa malengo mbali mbali; kumroga mtu apatwe na masaibu, maafa, au amuue, au afarikiane mke na mume kama ilivyotajwa juu katika Suwratul-Baqarah, au aelekeze mapenzi ya mtu kwa mtu fulani na mengi mengineyo. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameonya:

عن ابي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم: مَنْ عَقَدَ عُقْدَةً ثُمَّ نَفَثَ فِيهَا, فَقَدْ سَحَرَ, وَمَن ْسَحَرَ  فَقَدْ أَشْرَكَ, وَمَنْ تَعَلَّقَ شَيْئًا وُكِلَ إِلَيْهِ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayefunga fundo kisha akalipuliza amefanya uchawi. Na atakayefanya uchawi amefanya shirki, na atakayetundika kitu [talasimu, au kuvaa hirizi, zindiko] basi amejiweka katika ulinzi wa hicho kitu alichokivaa)) [na itamdhalilisha])) [An-Nasaaiy]

 

Na pia:

مَنْ أَتَى كَاهِنًا أَوْ سَاحِرًا فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ فَقَدْ كَفَر بِمَا أُنْزِلَ عَلى مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلّم

Atakayemwendea kahini au mchawi akasadiki yale anayoyasema basi amekufuru ambayo Ameteremshiwa nayo Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) [Tafsiyr Ibn Kathiyr; Hadiyth ina isnaad ya upokezi Swahiyh na kuna Hadiyth zinazokubaliana na hii].

 

 

Aghlabu ya njia wanazotumia wachawi na jinsi ya kumtambua mchawi: 

 

 

  • Huwakamata wale wenye ugonjwa wa ngozi (zeruzeru) na kuwaua na kutumia viungo vyao katika uchawi wao. Hii ni dhulma kubwa mno wanayowafanyia bin Aadamu wenzao! Allaah Awahifadhi bin Aadam hao waliosibiwa na maradhi hayo, jambo ambalo limekuwa ni mtihani kwao kudhulumiwa na wachawi!

 

  • Hutamka kauli au maneno ya kufru.

 

  • Huandika maneno katika vijikaratasi na kumtaka mtu avivae kama hirizi, au avifukize apate moshi wake, au kutundika vitu mahali fulani kama vile  katika miti, au kumtaka mtu atupe vitu baharini, au avifukie ardhini.

 

  • Humtaka mtu alete wanyama wenye sifa fulani, au wanyama wenye rangi fulani awachinje bila ya kutaja Jina la Allaah!

 

  • Husoma Qur-aan kinyumenyume, au kuikhini Qur-aan kwa kuiweka sehemu zisizopasa.

 

  • Huandika maneno ya Qur-aan na mengine ya kufru na kumtaka achemshe vikaratasi hivyo na kunywa maji yake, au hutia zaafarani au rangi kisha humfanyia kombe anywe kwa muda fulani.

 

  • Humuuliza mtu jina la mama yake.

 

  • Humtaka mtu nguo zake za ndani kwa ajili ya kupata jasho lake.

 

  • Humtaka mtu ajitenge na watu abakie katika chumba cha kiza na aepukane na jua kwa muda wa masiku.

 

  • Humtaka mtu asioge kwa masiku na aghalabu hutumia idadi ya arobaini (40).

 

  • Humpa mtu kinywaji kisha humtapisha kwa njia mbali mbali na kumzuga macho aone kuwa ametokwa na vidudu tumboni!

 

  •  Humzuga macho na mwili kwa njia zake na kumchoma visu mwilini bila ya mtu kuhisi maumivu.

 

  • Humpa mtu miiko asile vyakula fulani.

 

  • Aghlabu hutumia vitambaa vyekundu katika kazi zao za uchawi.

 

  •  Na mengine mengineyo.
  •  

Rejea Makala: Jini, Shaytwaan Na Mchawi

 

2- Kufanya Au Kuhudhuruia Michezo Ya Sihri (Mazingaombwe) 

 

 

Ama pia njia nyengine ya sihri ni watu kufanya michezo yake (mazingaombwe) na watu kugharamika kununua tiketi za kuingia michezoni kutazama uchawi. Hapo hufanya mazingaombwe ya kuwafanya watu watekwe akili zao na waone miujiza isiyokuwa ya kweli kama vile wachawi wa Fir’awn kabla ya kuamini kwao walipowahudhurisha halaiki ya watu uwandani wakayazuga macho yao:

 

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِمَّا أَن تُلْقِيَ وَإِمَّا أَن نَّكُونَ نَحْنُ الْمُلْقِينَ﴿١١٥﴾

 (Wachawi) Wakasema: “Ee Muwsaa, ima utupe wewe au tuwe sisi wa (kwanza) kutupa.” 

 

 

قَالَ أَلْقُوا ۖ فَلَمَّا أَلْقَوْا سَحَرُوا أَعْيُنَ النَّاسِ وَاسْتَرْهَبُوهُمْ وَجَاءُوا بِسِحْرٍ عَظِيمٍ﴿١١٦﴾

 (Muwsaa) Akasema: “Tupeni!” Basi walipotupa, waliyasihiri macho ya watu na wakawatia woga, na wakaja na sihiri kuu. [Al-A’raaf: 115-116]

 

 

Ee ndugu Muislamu! Jiepushe na sihri na wachawi ubakie salama katika maasi, kufru na shirki kubwa kama hii!  

 

Kwa aliyetendewa Sihri (uchawi) basi atafute Tiba ya Sunnah, maelezo yanapatikana katika kiungo kifuatacho:

 

10-Ruqya: Kutafuta Shifaa: Poza Ya Maradhi, Sihri (Uchawi) Katika Baadhi Ya Vyakula

 

 

 

 

Share

24-Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno! Vipi Kujiepusha Na Shirki

 

إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيم

 

Hakika Shirki Ni Dhulma Kubwa Mno!

 

24-Vipi  Kujiepusha Na Shirki

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Ndugu Muislamu! Hakika shirki ni dhulma kubwa mno! Kwa kumfanyia shirki Rabb wako Aliyekuumba, Ambaye unaishi katika ardhi Yake, Ambaye Anakuruzuku na Akakujaalia neema nyingi mno zisizohesabika, Ambaye Anakurehemu na Akakujaalia fadhila na neema za kila aina. 

 

 

Miongoni mwa neema Zake Allaah ('Azza wa Jalla) ni kukujaalia uhai mpaka hii leo uweze kutambua yanayomshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ili urudie kutubia Kwake kabla ya kufariki kwako. Basi hii ni fursa adhimu kwa kila aliyekuwa akimshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) atekeleze yafuatayo ambayo yatasaidia kumuepusha na shirki In Shaa Allaah:    

 

1. Tawbah ya kweli:

 

Rudi kwa Rabb wako kwa kutubia tawbah ya nasuha (kwelikweli) kama Anavyoamrisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللَّـهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا عَسَىٰ رَبُّكُمْ أَن يُكَفِّرَ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَيُدْخِلَكُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ يَوْمَ لَا يُخْزِي اللَّـهُ النَّبِيَّ وَالَّذِينَ آمَنُوا مَعَهُ ۖ نُورُهُمْ يَسْعَىٰ بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَبِأَيْمَانِهِمْ يَقُولُونَ رَبَّنَا أَتْمِمْ لَنَا نُورَنَا وَاغْفِرْ لَنَا ۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿٨﴾

Enyi walioamini! Tubieni kwa Allaah tawbah ya nasuha (kwelikweli); asaa Rabb   wenu Akakufutieni maovu yenu, na Akakuingizeni Jannaat zipitazo chini yake mito. Siku ambayo Allaah Hatomfedhehesha Nabiy (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na wale walioamini pamoja naye. Nuru yao itatembea mbele yao na kuliani mwao, watasema: “Rabb wetu! Tutimizie Nuru yetu, na Tughufurie, hakika Wewe juu ya kila kitu ni Muweza. [At-Tahriym: 8]

 

Twabah ya nasuha ina masharti yafuatayo:

 

a.     Kuomba maghfirah  

b.     Kuacha hayo maasi

c.     Kujuta

d.    Kuweka niyyah (azma) kuwa hatorudia tena

e.     Kama kaidhulumu haki ya mtu basi ni kuirudisha hiyo haki.  

 

Na kutubia shirki ni kujisalimisha katika Uislamu pekee kama alivyosema Imaam As-Sa’dy (Rahimahu Allaah) kuhusu Aayah:

 

قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوا إِن يَنتَهُوا يُغْفَرْ لَهُم مَّا قَدْ سَلَفَ وَإِن يَعُودُوا فَقَدْ مَضَتْ سُنَّتُ الْأَوَّلِينَ﴿٣٨﴾

Waambie waliokufuru kwamba wakikoma wataghufuriwa yaliyopita, lakini wakirudia, basi imekwishapita desturi ya watu wa awali. [Al-Anfaal: 38]

  

Akasema: “Wakikoma; inamaanisha kufru zao, nako ni kujisilimisha kwa Allaah Pekee bila ya kumshirikisha.”

 

Adhkaar mbalimbali zimethibiti katika Sunnah jinsi ya kuomba maghfirah, na Sayyidul-Istighfaar (du’aa kuu kabisa ya kuomba maghfirah) ni:

 

اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا عَبْـدُك، وَأَنا عَلـى عَهْـدِكَ وَوَعْـدِكَ ما اسْتَـطَعْـت، أَعـوذُبِكَ مِنْ شَـرِّ ما صَنَـعْت، أَبـوءُ لَـكَ بِنِعْـمَتِـكَ عَلَـيَّ وَأَبـوءُ بِذَنْـبي فَاغْفـِرْ لي فَإِنَّـهُ لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْتَ .

Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illaa Anta Khalaqtaniy wa ana ‘abduka wa anaa ‘alaa ‘ah-dika wawa’-dika mastatwa’-tu, a’uwdhu bika min sharri maa swana’-tu, abuw-u Laka bini’-matika ‘alayya wa abuw-u bidhanbiy, faghfirliy fainnahu laa yaghfirudh- dhunuwba illaa Anta.

 

Ee Allaah, Wewe ni Rabb wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja Wako, nami niko juu ya  ahadi Yako, na agano Lako, kiasi cha uwezo wangu, najikinga Kwako kutokana na shari ya nilichokifanya, nakiri  Kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unighufurie  kwani hakuna wa kughufuria madhambi ila Wewe. [Al-Bukhaariy (7/150) [2306] kutoka kwa  Shaddaad bin Aws Radhwiya Allaahu ’anhu]

 

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akistaghfiru mara 70 kila siku na katika riwaayah nyingine mara 100 kwa siku:

 

الْأَغَرِّ الْمُزَنِيِّ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: (إِنِّي لَأَسْتَغْفِرُ اللَّهَ فِي الْيَوْمِ مِائَةَ مَرَّةٍ) رواه مسلم   (2702

Al-Agharr Al-Muzaniyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba: ((Hakika mimi nastaghfiru kwa Allaah mara mia katika siku moja)). [Muslim (2702)]

 

Na vilevile: 

 

وقَالَ أَبُو هُرَيْرَةَ رضي الله عنه : سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ : ( وَاللَّهِ إِنِّي لاَسْتَغْفِرُ اللَّهَ وَأَتُوبُ إِلَيْهِ فِي الْيَوْمِ أَكْثَرَ مِنْ سَبْعِينَ مَرَّةً ) رواه البخاري (6307).

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ’anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Wa-Allaahi mimi nastaghfiru kwa Allaah na natubia Kwake zaidi ya mara sabini katika siku moja)). [Al-Bukhaariy (6307)]

 

Hivyo ni kusema: ”Astaghfiru Allaah wa atuwubu Ilayhi.”

 

Juu ya hayo, faida kadhaa za kuomba maghfirah zinamrudia bin-Aadam anayemuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) maghfirah.

 

 

2. Kuomba Isti’aanah (msaada) kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

Zidisha kuswali Swalaah za Sunnah na kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) humo Akuepushe na shirki. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَاسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلَّا عَلَى الْخَاشِعِينَ ﴿٤٥﴾

Na tafuteni msaada kupitia subira na Swalaah; na hakika hilo ni kubwa isipokuwa kwa wanyenyekevu. [Al-Baqarah: 45]

 

 

Pia, du’aa muhimu kabisa ya kujiepusha na shirki kama ilivyothibti katika Sunnah:  

 

اللّهُـمَّ إِنّـي أَعـوذُبِكَ أَنْ أُشْـرِكَ بِكَ وَأَنا أَعْـلَمْ، وَأَسْتَـغْفِرُكَ لِما لا أَعْـلَم

Allaahumma inniy a’uwdhu Bika an ushrika Bika wa anaa a’-alamu wa astaghfiruka limaa laa a’-lam

Ee Allaah hakika mimi Najikinga Kwako kutokana na kukushirikisha hali ya kuwa najua na ninakuomba maghfirah kwa nisiyoyajua. [Ahmad (4/403) na wengineo; Taz. Swahiyh Al-Jaami’(3/233) [3731] na Swahiyh At-Targhiyb wat-Tarhiyb ya Al-Albaaniy (1/122) [36]

 

 

 

3. Kumdhukuru Allaah Kwa Wingi: 

 

Mdhukuru mno Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) khaswa kwa kusoma Qur-aan kwa kuwa ni poza ya nyoyo kwa kila aina ya maradhi; kufru, shirki na kadhaalika. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَتْكُم مَّوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَشِفَاءٌ لِّمَا فِي الصُّدُورِ وَهُدًى وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ﴿٥٧﴾

Enyi watu! Kwa yakini yamekujieni mawaidha kutoka kwa Rabb wenu, na shifaa ya yale yaliyomo vifuani, na mwongozo na rahmah kwa Waumini. [Yuwnus: 57] 

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

اتْلُ مَا أُوحِيَ إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ وَأَقِمِ الصَّلَاةَ ۖ إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ۗ وَلَذِكْرُ اللَّـهِ أَكْبَرُ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا تَصْنَعُونَ ﴿٤٥﴾

Soma (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) uliyoletewa Wahy katika Kitabu na simamisha Swalaah, hakika Swalaah inazuia machafu na munkari. Na bila shaka kumdhukuru Allaah ni kubwa zaidi. Na Allaah Anajua yale mnayoyatenda. [Al-‘Ankabuwt: 45]

 

 

4. Kutafuta Na Kuongeza ‘Ilmu:

 

Mojawapo ya kinga ya shirki ni kuongeza ‘ilmu sahihi ya Dini hii tukufu ili kutambua yanayothibitisha Tawhiyd (Kumwpekesha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na yaliyo kinyume chake (yanayomshirikisha). Bila ya kuwa na ‘ilmu hutoweza kutambua. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ ۗ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٩﴾

Sema: “Je, wanalingana sawa wale wanaouja na wale wasiojua?” Hakika wanakumbuka wenye akili tu. [Az-Zumar: 9]

 

Na pia:

 

فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مُتَقَلَّبَكُمْ وَمَثْوَاكُمْ﴿١٩﴾

Basi jua kwamba laa ilaaha illa-Allaah, hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah na omba maghfirah kwa dhambi zako na kwa ajili ya Waumini wa kiume na Waumini wa kike. Na Allaah Anajua harakati zenu huku na kule na pahala penu pa kupumzikia. [Muhammad: 19] 

 

5. Kuwa Na Taqwa:

  

Kumcha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kila wakati, kila mahali. Jibriyl ('Alayhis-Salaam) alipomwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza maswali mojawapo lilikuwa kuhusu ihsaan akajibu:

  أنْ تَعْبُدَ الله كَأَنَّكَ تَرَاهُ فإنْ لَمْ تَكُنْ تَرَاهُ فإنَّهُ يَرَاك

((Umwabudu Allaah kama kwamba unamuona, na ikiwa humuoni, basi Yeye hakika Anakuona)) [Muslim]

 

 

6. Kuwaza Adhabu Za Allaah Duniani Na Aakhirah:

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

حُنَفَاءَ لِلَّـهِ غَيْرَ مُشْرِكِينَ بِهِ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَكَأَنَّمَا خَرَّ مِنَ السَّمَاءِ فَتَخْطَفُهُ الطَّيْرُ أَوْ تَهْوِي بِهِ الرِّيحُ فِي مَكَانٍ سَحِيقٍ ﴿٣١﴾

Muelemee haki kwa kumwabudu Allaah Pekee bila ya kumshirikisha. Na yeyote anayemshirikisha Allaah basi kama kwamba ameporomoka kutoka mbinguni, wakamnyakua ndege au upepo ukamtupa mahali mbali mno. [Al-Hajj: 31]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

لَّا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَقْعُدَ مَذْمُومًا مَّخْذُولًا ﴿٢٢﴾

Usifanye pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine, ukaja kushutumiwa na mwenye kutelekezwa mbali (motoni). [Al-Israa: 22]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتُلْقَىٰ فِي جَهَنَّمَ مَلُومًا مَّدْحُورًا ﴿٣٩﴾

Na wala usifanye pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine ukaja kutupwa katika Jahannam hali ya kuwa mwenye kulaumiwa na kufukuziliwa mbali.  [Al-Israa: 39]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuhusu sifa za ‘Ibaadur-Rahmaan (Waja wa Mwingi wa Rahmah):

 

وَالَّذِينَ لَا يَدْعُونَ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ وَلَا يَقْتُلُونَ النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَا يَزْنُونَ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ يَلْقَ أَثَامًا ﴿٦٨﴾

Na wale ambao hawaombi pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine na wala hawaui nafsi ambayo Allaah Ameiharamisha isipokuwa kwa haki, na wala hawazini. Na atakayefanya hivyo atakutana na adhabu.

يُضَاعَفْ لَهُ الْعَذَابُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَيَخْلُدْ فِيهِ مُهَانًا ﴿٦٩﴾

Ataongezewa adhabu maradufu Siku ya Qiyaamah, na mwenye kudumu humo akiwa amedhalilika.

 

إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ عَمَلًا صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يُبَدِّلُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِهِمْ حَسَنَاتٍ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٠﴾

Isipokuwa yule aliyetubu na akaamini na akatenda ‘amali njema; basi hao Allaah Atawabadilishia maovu yao kuwa mema.  Na Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.

 

وَمَن تَابَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَإِنَّهُ يَتُوبُ إِلَى اللَّـهِ مَتَابًا ﴿٧١﴾

Na atakayetubu na akatenda mema, basi hakika yeye anatubia kwa Allaah tawbah ya kweli. [Al-Furqaan:  68-71]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ وَالْمُشْرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَاۚ أُولَـٰئِكَ هُمْ شَرُّ الْبَرِيَّةِ ﴿٦﴾

Hakika wale waliokufuru miongoni mwa watu wa kitabu na washirikina watakuwa katika moto wa Jahannam, ni wenye kudumu humo; hao ndio waovu kabisa wa viumbe. [Al-Bayyinah: 6]

 

 

Na dalili nyingi nyenginezo zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah kuhusu adhabu za mwenye kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) zikiwemo ambazo zimetajwa katika milango iliyotangulia ya somo hili la ‘Hakika Shirki ni Dhulma Kubwa Mno’, basi rudia ee ndugu Muislamu upate kujikumbusha na kuwaidhika zaidi.

 

Wa biLLaahi At-Tawfiyq.

 

 

 

Share