00-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Kitabu Cha Utangulizi Wa Maudhui Mbalimbali - كِتابُ الْمُقَدِّمات

 

 

 

(Mabustani Ya Swalihina)

 

كِتابُ الْمُقَدِّمات

Kitabu Cha Utangulizi Wa Maudhui Mbalimbali

  

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

Share

001-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ikhlaasw Na Kutia Niyyah Katika ‘Amali, Maneno, Hali Zilizodhihirika Na Zilizofichika

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الإخلاص وإحضار النية في جميع الأعمال والأقوال البارزة والخفية­

  001-Mlango Wa Ikhlaasw Na Kutia Niyyah Katika ‘Amali Zote,

Maneno, Hali Zilizodhihirika Na Zilizofichika.

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ اللهُ تَعَالَى

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ

Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah wenye kumtakasia niyyah Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki na wasimamishe Swalaah na watoe Zakaah; na hiyo ndiyo Dini iliyosimama imara.[Al-Bayyinah: 5]

 

لَن يَنَالَ اللَّـهَ لُحُومُهَا وَلَا دِمَاؤُهَا وَلَـٰكِن يَنَالُهُ التَّقْوَىٰ مِنكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ سَخَّرَهَا لَكُمْ لِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ ۗ وَبَشِّرِ الْمُحْسِنِينَ

Haimfikii Allaah nyama zake wala damu yake, lakini inamfikia taqwa kutoka kwenu. Hivyo ndivyo Tulivyowatiisha (hao wanyama) kwenu ili mpate kumtukuza Allaah (kusema: Allaahu Akbar) kwa yale Aliyokuongozeni; na wabashirie wafanyao ihsaan. [Al-Hajj: 37]

 

 قُلْ إِن تُخْفُوا مَا فِي صُدُورِكُمْ أَوْ تُبْدُوهُ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ وَيَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ

Sema: “Mkificha yale yaliyomo katika vifua vyenu au mkiyafichua, Allaah Anayajua. Na Anajua yale yaliyomo katika mbingu na yale yaliyomo katika ardhi. Na Allaah juu ya kila kitu ni Muweza.”  [Aal-‘Imraan: 29]

 

 

Hadiyth - 1

وعن أمير المؤمِنين أبي حَفْصٍ عمرَ بنِ الخطابِ بنِ نُفَيْلِ بنِ عبدِ العُزّى بن رياحِ بنِ عبدِ اللهِ بن قُرْطِ بن رَزاحِ بنِ عدِي بنِ كعب بنِ لُؤَيِّ بنِ غالبٍ القُرشِيِّ العَدويِّ رضي الله عنه قالَ: سَمِعتُ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقُولُ: ((إنّمَا الأَعْمَالُ بالنِّيّاتِ، وَإِنَّمَا لِكُلِّ امرِئٍ مَا نَوَى، فَمَنْ كَانَتْ هجرته إلى الله ورسوله، فهجرته إلى الله ورسوله، ومن كانت هِجْرَتُهُ لِدُنْيَا يُصيبُهَا، أَوْ امْرَأَةٍ يَنْكَحُهَا، فَهِجْرَتُهُ إِلى مَا هَاجَرَ إِلَيْه)). مُتَّفَقٌ عَلَى صِحَّتِهِ. رَوَاهُ إمَامَا الْمُحَدّثِينَ، أبُو عَبْدِ الله مُحَمَّدُ بْنُ إسْمَاعيلَ بْن إبراهِيمَ بْن المُغيرَةِ بنِ بَرْدِزْبهْ الجُعْفِيُّ البُخَارِيُّ، وَأَبُو الحُسَيْنِ مُسْلمُ بْنُ الحَجَّاجِ بْنِ مُسْلمٍ الْقُشَيريُّ النَّيْسَابُورِيُّ رضي اللهُ عنهما فِي صحيحيهما اللَّذَيْنِ هما أَصَحُّ الكُتبِ المصنفةِ.

Kutoka kwa Amiri wa Waumini, Abu Hafsw ‘Umar bin Al-Khatwaab bin Nufayl bin ‘Abdil ‘Uzza bin Riyaah bin ‘Abdillaah bin Qurt bin Razaah bin ‘Adiyyi bin Ka’ab bin Lua-yyi bin Ghaalib Al-Qurashiyyi Al-‘Adawiyyi (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: “Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa   aalihi wa sallam) akisema: “Hakika kusihi kwa ‘amali huzingatiwa na niyyah. Na hakika kila mtu atalipwa kwa kile alichokinuia. Ambaye hijrah yake itakuwa ni kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake, basi hijrah yake itakuwa ni kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake. Na ambaye hijrah yake ni kuiendea dunia ili aihodhi, au kumuendea mwanamke ili amuoe; basi hijrah yake itakuwa ni kwa aliloliendea.”  [Hadiyth hii imepokelewa na Maimaam wawili ‘Ulamaa wa Hadiyth, Abuu ‘Abdillaah Muhammad bin Ismaa’iyl bin Ibraahiym bin Al-Mughiyrah bin Bar-dizbah Al-Ju’fiyy Al-Bukhaariy, na Abul-Husayn Muslim bin Al-Hajjaaj bin Muslim Al-Qushayriyy An-Naysaaburiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) Wameipokea katika vitabu vyao ambavyo ndio Swahiyh katika vitabu vya Hadiyth vilivyosanifiwa]

 

 

                                                                              Hadiyth - 2                  

وعن أمِّ المؤمِنينَ أمِّ عبدِ اللهِ عائشةَ رضي الله عنها قالت: قالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَغْزُو جَيْشٌ الْكَعْبَةَ فإِذَا كَانُوا بِبَيْدَاءَ مِنَ الأَرضِ يُخْسَفُ بِأَوَّلِهِمْ وآخِرِهِمْ)). قَالَتْ: قلتُ: يَا رَسُولَ اللهِ، كَيْفَ يُخْسَفُ بأوَّلِهِمْ وَآخِرِهِمْ وَفِيهمْ أسْوَاقُهُمْ وَمَنْ لَيْسَ مِنْهُمْ؟! قَالَ: ((يُخْسَفُ بِأَوَّلِهِمْ وَآخِرِهِمْ ثُمَّ يُبْعَثُونَ عَلَى نِيّاتِهمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ. هذَا لَفْظُ الْبُخَارِيِّ 

Mama wa Waumini, Ummu ‘Abdillaah, ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa), amesimulia: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna jeshi litakalotaka kuivamia Al-Ka’bah, litakapofika katika ardhi ya jangwa, wote watadidimizwa.” Nikauliza: Eee Rasuli wa Allaah, vipi wote wadidimizwe na miongoni mwao kuna raia wa kawaida na hawakuwa miongoni mwao? Akajibu: “Wote watadidimizwa kisha watafufuliwa kulingana na niyyah zao.” [Hadiyth hii ni lafdh ya Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائِشةَ رضيَ اللهُ عنها قَالَتْ: قَالَ النبي صلى الله عليه وسلم: ((لا هِجْرَةَ بَعْدَ الفَتْحِ، وَلَكِنْ جِهَادٌ وَنِيَّةٌ، وَإِذَا اسْتُنْفِرْتُمْ فانْفِرُوا)). مُتَّفَقٌ عَلَيْه

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakuna hijrah baada ya Fat-hi (ukombozi wa Makkah), lakini kuna jihaad na niyyah. Na mnapohimizwa kutoka katika jihaad basi nendeni haraka.”  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أبي عبدِ اللهِ جابر بن عبدِ اللهِ الأنصاريِّ رَضي اللهُ عنهما قَالَ: كُنَّا مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم في غَزَاةٍ، فَقالَ: ((إِنَّ بالمدِينَةِ لَرِجَالًا ما سِرْتُمْ مَسِيرًا، وَلا قَطَعْتُمْ وَادِيًا، إلا كَانُوا مَعَكمْ حَبَسَهُمُ الْمَرَضُ)). وَفي روَايَة: ((إلا شَرَكُوكُمْ في الأجْرِ)). رواهُ مسلمٌ.
ورواهُ البخاريُّ عن أنسٍ رضي الله عنه قَالَ: رَجَعْنَا مِنْ غَزْوَةِ تَبُوكَ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم فقال: ((إنَّ أقْوامًا خَلْفَنَا بالْمَدِينَةِ مَا سَلَكْنَا شِعْبًا وَلا وَاديًا، إلا وَهُمْ مَعَنَا؛ حَبَسَهُمُ العُذْرُ))

Abu ‘Abdillaah, Jaabir bin ‘Abdillaah Al-Answaary (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Tulikuwa pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika vita fulani. Akasema: “Hakika Madiynah kuna watu ambao nyinyi hamkwenda mwendo wowote wala hamkupita jangwa lolote isipokuwa wao walikuwa nanyi, wamezuiliwa na ugonjwa.” Na katika simulizi nyingine imesema: “Isipokuwa wameshirikiana nanyi katika ujira.” [Muslim].

 

 

Hadiyth – 5

وعن أبي يَزيدَ مَعْنِ بنِ يَزيدَ بنِ الأخنسِ رضي الله عنهم وهو وأبوه وَجَدُّه صحابيُّون قَالَ: كَانَ أبي يَزيدُ أخْرَجَ دَنَانِيرَ يَتَصَدَّقُ بِهَا، فَوَضعَهَا عِنْدَ رَجُلٍ في الْمَسْجِدِ، فَجِئْتُ فأَخذْتُها فَأَتَيْتُهُ بِهَا. فقالَ: واللهِ، مَا إيَّاكَ أرَدْتُ، فَخَاصَمْتُهُ إِلى رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: ((لكَ مَا نَوَيْتَ يَا يزيدُ، ولَكَ ما أخَذْتَ يَا مَعْنُ)). رواهُ البخاريُّ.

Abu Yaziyd Ma’ni bin Yaziyd bin Al-Akhnas (Radhwiya Allaahu ‘anhum), yeye na baba yake na babu yake wote ni Maswahaba, amesema: Baba yangu Yaziyd alikuwa amezitoa dinaar akizitolea swadaqah. Akaziweka kwa mtu Msikitini. Nikaja nikazichukua na nikaja nazo. Akaniambia: Wa-Allaahi sikuwa nimekukusudia wewe!  Nikashtakiana naye kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), akasema: “Ee Yaziyd, utapata ulilolinuia, na ee Ma’ni! Ulichokichukua ni chako”. [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أبي إسحاقَ سَعدِ بنِ أبي وَقَّاصٍ مالِكِ بنِ أُهَيْب بنِ عبدِ منافِ ابنِ زُهرَةَ بنِ كلابِ بنِ مُرَّةَ بنِ كعبِ بنِ لُؤيٍّ القُرشِيِّ الزُّهريِّ رضي الله عنه أَحَدِ العَشَرَةِ المشهودِ لهم بالجنةِ رضي الله عنهم قَالَ: جاءنِي رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَعُودُنِي عَامَ حَجَّةِ الوَدَاعِ مِنْ وَجَعٍ اشْتَدَّ بي، فقُلْتُ: يَا رَسُولَ اللهِ! إنِّي قَدْ بَلَغَ بي مِنَ الوَجَعِ مَا تَرَى، وَأَنَا ذُو مالٍ وَلا يَرِثُني إلا ابْنَةٌ لي، أفأَتَصَدَّقُ بِثُلُثَيْ مَالِي؟ قَالَ: ((لا))، قُلْتُ: فالشَّطْرُ يَا رَسُولَ اللهِ؟ فقَالَ: ((لا))، قُلْتُ: فالثُّلُثُ يَا رَسُولَ اللهِ؟ قَالَ: ((الثُّلُثُ، والثُّلُثُ كَثيرٌ- أَوْ كبيرٌ- إنَّكَ إنْ تَذَرْ وَرَثَتَكَ أغنِيَاءَ خيرٌ مِنْ أنْ تَذَرَهُمْ عَالَةً يتكفَّفُونَ النَّاسَ، وَإنَّكَ لَنْ تُنفِقَ نَفَقَةً تَبْتَغي بِهَا وَجهَ اللهِ إلا أُجِرْتَ عَلَيْهَا حَتَّى مَا تَجْعَلُ في فِيِّ امْرَأَتِكَ))، قَالَ: فَقُلتُ: يَا رسولَ اللهِ، أُخلَّفُ بعدَ أصْحَابي؟ قَالَ: ((إِنَّكَ لَنْ تُخَلَّفَ فَتَعملَ عَمَلًا تَبتَغي بِهِ وَجْهَ اللهِ إلا ازْدَدتَ بِهِ دَرَجةً ورِفعَةً، وَلَعلَّكَ أنْ تُخَلَّفَ حَتّى يَنتَفِعَ بِكَ أقْوَامٌ وَيُضَرَّ بِكَ آخرونَ. اللَّهُمَّ أَمْضِ لأصْحَابي هِجْرَتَهُمْ ولا تَرُدَّهُمْ عَلَى أعقَابهمْ، لكنِ البَائِسُ سَعدُ بْنُ خَوْلَةَ)). يَرْثي لَهُ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ ماتَ بمَكَّة. مُتَّفَقٌ عليهِ.

Abu Is-haaq Sa’d bin Abi Waqqaas Maalik bin Uhayb bin ‘Abdi-Manaaf bin Zuhrah bin Kilaab bin Murrah bin Ka’b bin Lu-ayyi Al-Qurashiyy Az-Zuhriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu), ambaye ni mmojawapo kati ya waliobashiriwa Jannah, amesimulia: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alinitembelea mwaka wa Hajjatul-Wadaa’i kutokana na ugonjwa ambao uliokuwa umenishitadi. Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, ugonjwa umenifikisha kama unionavyo, nami ni mwenye mali nyingi, wala hakuna atakayenirithi isipokuwa bint yangu (mmoja tu). Je, nizitoe swadaqah thuluthi mbili za mali yangu? Akasema: “Hapana.” Nikasema: Basi nitoe nusu yake ee Rasuli wa Allaah? Akasema: “Hapana”. Nikasema: Je, thuluthi (moja)? Akasema: “Thuluthi (unaweza kutoa). Na hiyo thuluthi ni nyingi – kwa hakika uwaache wenye kukurithi ni wenye kujiweza, ni bora kulikoni kuwaacha wawe mafukara wakiomba watu. Na hakika hutatoa gharama ya matumizi ukawa unataka radhi za Allaah kwa matumizi hayo, isipokuwa utapewa ujira kwayo; hata unachokitia katika kinywa cha mkeo.” Nikamwambia: Eee Rasuli wa Allaah, nitaachwa (niishi muda mrefu) baada ya wenzangu?” Akasema: “Hakika hutoachwa ukafanya 'amali kwa ajili ya kutafuta radhi ya Allaah kwa 'amali hiyo, ispokuwa utazidi daraja na utukufu kwa 'amali hiyo. Na (huenda) ukaachwa (uishi) mpaka watu wanufaike kwa sababu yako, na wengine wadhuriwe kwa sababu yako. Ee Rabb! Wakamilishie Maswahaba wangu hijrah yao, wala usiwarejeshe nyuma kwa visigino vyao. Lakini masikini ni Sa’d bin Khawlah!” Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamsikitikia kwa kuwa amekufa Makkah.  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعنْ أبي هريرةَ عبدِ الرحمنِ بنِ صخرٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ الله لا ينْظُرُ إِلَى أَجْسَامِكُمْ، ولا إِلى صُوَرِكمْ، وَلَكن ينْظُرُ إلى قُلُوبِكمْ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah, ‘Abdir-Rahmaan bin Swakhr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kwa hakika Allaah hatazami viwiliwili vyenu wala sura zenu, lakini Anatazama nyoyo zenu na matendo yenu.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أبي موسى عبدِ اللهِ بنِ قيسٍ الأشعريِّ رضي الله عنه قَالَ: سُئِلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الرَّجُلِ يُقاتلُ شَجَاعَةً، ويُقَاتِلُ حَمِيَّةً، ويُقَاتِلُ رِيَاءً، أَيُّ ذلِكَ في سبيلِ الله؟ فقال رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَاتَلَ لِتَكونَ كَلِمَةُ اللهِ هي العُلْيَا، فَهوَ في سبيلِ اللهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Muwsaa, Abdillaah bin Qays Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa mtu aliyepigana kwa ajili ya kuambiwa shujaa, na anayepigana kwa taasubi (ukabila), na anayepigana kwa riyaa (kujionesha), ni yupo katika hao yupo katika njia ya Allaah? Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akajibu: “Anayepigana ili Dini ya Allaah iwe juu, basi huyo yupo katika njia ya Allaah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

 

وعن أبي بَكرَةَ نُفيع بنِ الحارثِ الثقفيِّ رضي الله عنه أَنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا التَقَى المُسلِمَان بسَيْفَيهِمَا فالقَاتِلُ وَالمَقْتُولُ في النّارِ)). قُلتُ: يا رَسُولَ اللهِ، هذا القَاتِلُ فَمَا بَالُ المقْتُولِ؟ قَالَ: ((إنَّهُ كَانَ حَريصًا عَلَى قتلِ صَاحِبهِ)). مُتَّفَقٌ عليهِ

Abu Bakrah, Nufay’i bin Al-Haarith At-Thaqafiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia kuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema: “Waislamu wawili wakipigana kwa panga zao, basi muuaji na aliyeuliwa wataingia motoni.” Nikauliza: Ee Rasuli wa Allaah, huyu aliyeua (ni sawa kuingia motoni)! Je, aliyeuliwa? Akajibu: “Yeye aliyeuliwa alikuwa na hamu ya kumuua mwenzie.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

 

وعن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((صَلاةُ الرَّجلِ في جمَاعَةٍ تَزيدُ عَلَى صَلاتهِ في بيتهِ وصلاته فِي سُوقِهِ بضْعًا وعِشرِينَ دَرَجَةً، وَذَلِكَ أنَّ أَحدَهُمْ إِذَا تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الوُضوءَ، ثُمَّ أَتَى المَسْجِدَ، لا يَنْهَزُهُ إِلا الصَلاةُ، لا يُرِيدُ إلا الصَّلاةَ: لَمْ يَخْطُ خُطْوَةً إِلا رُفِعَ لَهُ بِهَا دَرجَةٌ، وَحُطَّ عَنْهُ بها خَطِيئَةٌ حَتَّى يَدْخُلَ المَسْجِدَ، فإِذا دَخَلَ المَسْجِدَ كَانَ في الصَّلاةِ مَا كَانَتِ الصَّلاةُ هِي تَحْبِسُهُ، وَالمَلائِكَةُ يُصَلُّونَ عَلَى أَحَدِكُمْ مَا دَامَ في مَجْلِسِهِ الَّذِي صَلَّى فِيهِ، يَقُولُونَ: اللَّهُمَّ ارْحَمْهُ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ، اللَّهُمَّ تُبْ عَلَيهِ، مَا لَم يُؤْذِ فيه، مَا لَمْ يُحْدِثْ فِيهِ)). مُتَّفَقٌ عليهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mtu kuswali kwa jamaa’ah (ujira wake) huzidi kuswali sokoni kwake na nyumbani kwake kwa daraja zaidi ya ishirini. Nako ni kuwa, mmoja wao anapotawadha vizuri kisha akaenda Msikitini, hakusudii isipokuwa Swalaah, hakuna lililomuinua isipokuwa ni Swalaah tu, basi (atakuwa) hakuinua hatua isipokuwa atainuliwa daraja kwa hatua hiyo na ataondolewa dhambi kwa hatua hiyo mpaka aingie Msikitini, atakuwa angali yupo katika Swalaah maadamu Swalaah ndiyo iliyomzuia. Na Malaika humuombea rahmah mmoja kati yenu maadamu yupo katika kikao chake alichoswalia, wanaomba: “Ee Rabb Mrehemu, Ee Rabb Mghufurie! Ee Rabb Mpokelee tawbah yake!” (Hali inaendelea namna hiyi) maadamu hajaudhi au kupatwa na hadathi.” [Al-Bukhaary na Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

 

وعن أبي العبَّاسِ عبدِ اللهِ بنِ عباسِ بنِ عبد المطلب رضِيَ اللهُ عنهما، عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فيما يروي عن ربهِ تباركَ وتعالى قَالَ: ((إنَّ اللهَ كَتَبَ الحَسَنَاتِ والسَّيِّئَاتِ ثُمَّ بَيَّنَ ذلِكَ، فَمَنْ هَمَّ بحَسَنَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا كَتَبَها اللهُ تَبَارَكَ وتَعَالى عِنْدَهُ حَسَنَةً كامِلَةً، وَإنْ هَمَّ بهَا فَعَمِلَهَا كَتَبَهَا اللهُ عَشْرَ حَسَناتٍ إِلى سَبْعمائةِ ضِعْفٍ إِلى ضعَافٍ كَثيرةٍ، وإنْ هَمَّ بِسَيِّئَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا كَتَبَهَا اللهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلةً، وَإنْ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا كَتَبَهَا اللهُ سَيِّئَةً وَاحِدَةً)). مُتَّفَقٌ عليهِ.

‘Abul-‘Abbaas, ‘Abdillaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika aliyopokea kutoka kwa Rabb wake Mtukufu. Amesema: “Kwa hakika Allaah Ameandika mema na mabaya, kisha akabainisha hayo: Atakayefanya hamu ya kutenda jema kisha asitende, Allaah Aliyetukuka Atamuandikia Kwake jema moja kamili. Na akilifanyia hamu na akalitenda, Allaah Atamuandikia mema kumi hadi nyongeza mia saba, hadi nyongeza nyingi zaidi (zaidi ya hizo). Na akifanya hamu ya kutenda jambo baya kisha asilitende, Allaah Atamuandikia Kwake jema kamili. Na akifanya hamu ya kulitenda na akalitenda, Allaah Atamuandikia baya moja.” [Al-Bukhaary na Muslim]

 

 

Hadiyth – 12

 وعن أبي عبد الرحمن عبدِ الله بنِ عمرَ بن الخطابِ رضيَ اللهُ عنهما، قَالَ: سمعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، يقول: ((انطَلَقَ ثَلاثَةُ نَفَرٍ مِمَّنْ كَانَ قَبْلَكُمْ حَتَّى آوَاهُمُ المَبيتُ إِلى غَارٍ فَدَخلُوهُ، فانْحَدرَتْ صَخْرَةٌ مِنَ الجَبَلِ فَسَدَّتْ عَلَيْهِمُ الغَارَ، فَقالُوا: إِنَّهُ لا يُنْجِيكُمْ مِنْ هذِهِ الصَّخْرَةِ إِلا أنْ تَدْعُوا اللهَ بصَالِحِ أعْمَالِكُمْ. قَالَ رجلٌ مِنْهُمْ: اللَّهُمَّ كَانَ لِي أَبَوانِ شَيْخَانِ كبيرانِ، وكُنْتُ لا أغْبِقُ قَبْلَهُمَا أهْلًا ولا مالًا، فَنَأَى بِي طَلَب الشَّجَرِ يَوْمًا فلم أَرِحْ عَلَيْهمَا حَتَّى نَامَا، فَحَلَبْتُ لَهُمَا غَبُوقَهُمَا فَوَجَدْتُهُما نَائِمَينِ، فَكَرِهْتُ أنْ أُوقِظَهُمَا وَأَنْ أغْبِقَ قَبْلَهُمَا أهْلًا أو مالًا، فَلَبَثْتُ- والْقَدَحُ عَلَى يَدِي- أنتَظِرُ اسْتِيقَاظَهُما حَتَّى بَرِقَ الفَجْرُ والصِّبْيَةُ يَتَضَاغَوْنَ عِنْدَ قَدَميَّ، فاسْتَيْقَظَا فَشَرِبا غَبُوقَهُما. اللَّهُمَّ إنْ كُنْتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابِتِغَاء وَجْهِكَ فَفَرِّجْ عَنّا مَا نَحْنُ فِيهِ مِنْ هذِهِ الصَّخْرَةِ، فانْفَرَجَتْ شَيْئًا لا يَسْتَطيعُونَ الخُروجَ مِنْهُ. 

قَالَ الآخر: اللَّهُمَّ إنَّهُ كانَتْ لِيَ ابْنَةُ عَمّ، كَانَتْ أَحَبَّ النّاسِ إليَّ- وفي رواية: كُنْتُ أُحِبُّها كأَشَدِّ مَا يُحِبُّ الرِّجَالُ النساءَ- فأَرَدْتُهَا عَلَى نَفْسِهَا فامْتَنَعَتْ منِّي حَتَّى أَلَمَّتْ بها سَنَةٌ مِنَ السِّنِينَ فَجَاءتْنِي فَأَعْطَيْتُهَا عِشْرِينَ وَمائةَ دينَارٍ عَلَى أنْ تُخَلِّيَ بَيْني وَبَيْنَ نَفْسِهَا فَفعَلَتْ، حَتَّى إِذَا قَدَرْتُ عَلَيْهَا- وفي رواية: فَلَمَّا قَعَدْتُ بَينَ رِجْلَيْهَا، قالتْ: اتَّقِ اللهَ وَلا تَفُضَّ الخَاتَمَ إلا بِحَقِّهِ، فَانصَرَفْتُ عَنْهَا وَهيَ أَحَبُّ النَّاسِ إليَّ وَتَرَكْتُ الذَّهَبَ الَّذِي أعْطَيتُها. اللَّهُمَّ إنْ كُنْتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابْتِغاءَ وَجْهِكَ فافْرُجْ عَنَّا مَا نَحْنُ فيهِ، فانْفَرَجَتِ الصَّخْرَةُ، غَيْرَ أَنَّهُمْ لا يَسْتَطِيعُونَ الخُرُوجَ مِنْهَا. 
وَقَالَ الثَّالِثُ: اللَّهُمَّ اسْتَأْجَرْتُ أُجَرَاءَ وأَعْطَيْتُهُمْ أجْرَهُمْ غيرَ رَجُل واحدٍ تَرَكَ الَّذِي لَهُ وَذَهبَ، فَثمَّرْتُ أجْرَهُ حَتَّى كَثُرَتْ مِنهُ الأمْوَالُ، فَجَاءنِي بَعدَ حِينٍ، فَقالَ: يَا عبدَ اللهِ، أَدِّ إِلَيَّ أجْرِي، فَقُلْتُ: كُلُّ مَا تَرَى مِنْ أجْرِكَ: مِنَ الإبلِ وَالبَقَرِ والْغَنَمِ والرَّقيقِ، فقالَ: يَا عبدَ اللهِ، لا تَسْتَهْزِئْ بي! فَقُلْتُ: لا أسْتَهْزِئ بِكَ، فَأَخَذَهُ كُلَّهُ فاسْتَاقَهُ فَلَمْ يتْرُكْ مِنهُ شَيئًا. الَّلهُمَّ إنْ كُنتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابِتِغَاءَ وَجْهِكَ فافْرُجْ عَنَّا مَا نَحنُ فِيهِ، فانْفَرَجَتِ الصَّخْرَةُ فَخَرَجُوا يَمْشُونَ)). مُتَّفَقٌ عليهِ.

Abu ‘Abdir-Rahmaan, ‘Abdillaah bin ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Waliondoka watu watatu, miongoni mwa watu waliokuwa kabla yenu waliosafiri hadi wakaingia pangoni ili walale. Likaviringika jiwe kutoka juu ya jabali likawafungia pango. Wakasemezana: Hakuna kitakachowaokoa kutokana na jiwe hili isipokuwa mumuombe Allaah kwa ‘amali zenu njema. Mmoja miongoni mwao akaanza kuomba: Ee Rabb, nilikuwa nina wazazi wawili wazee wakongwe, nilikuwa sitangulizi (kabla yao kunywa maziwa) familia wala watumwa. Siku moja haja ya kutafuta kuni ikanipeleka mbali, sikuweza kuwarudia (mapema) mpaka wakalala. Nikawakamulia maziwa yao, nikawakuta wameshalala. Nikachukia kuwaamsha na (nikachukia pia) kuwapa maziwa familia na watumwa kabla yao. Nikawa na (bilauri) imo mikononi mwangu mpaka waamke, hadi alfajiri ikatokeza huku watoto wakipiga kelele kwa njaa miguuni mwangu; wakaamka na wakanywa maziwa yao. Ee Rabb, ikiwa nilifanya hivyo kwa kutaka radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo ya jiwe hili. Kukafunguka kidogo kidogo kwa namna ambayo hawawezi kutoka. Mwengine akasema: Ee Rabb, nilikuwa nina bint wa ‘ammi yangu, nilikuwa nikimpenda mno, (Riwaayah nyingine imesema): Nilikuwa nikimpenda kama vile wanaume wanavyopenda mno wanawake. Nikamtaka (kuzini nae), akanikatalia. Mpaka alipokuja mwaka wa ukame, akanijia nikampa dinaar 120 ili niwe nae faragha. Akakubali. Nilipokuwa nimeshamuweza, (Riwaayah nyingine inasema): Nilipoketi baina ya miguu yake akanambia: Mche Allaah, usiivunje pete ila kwa haki yake. Nikamuondokea nikiwa nampenda mno (wala sikumfanya chochote), na nikamuachia dhahabu niliyompa. Ee Rabb, ikiwa nilifanya hivyo kwa ajili ya kupata radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo. Jiwe likafunguka, lakini walikuwa hawawezi kutoka. Mtu wa tatu akasema: Ee Rabb, mimi niliwaajiri wafanyakazi, nikawapa ujira wao isipokuwa mtu mmoja, aliuacha ujira wake na akaenda. Nikauzalisha ujira wake mpaka ukawa ni mali nyingi. Baada ya muda akanijia na kuniambia: Ee mja wa Allaah, nipe ujira wangu! Nikamwambia: Kila unachokiona katika ngamia, ng’ombe, mbuzi na watumwa ni ujira wako! Akaniambia: Ee mja wa Allaah, usinifanyie istihzai (usinikebehi)!  Nikamwambia: Sikufanyii istihzai. Akachukua mali yote na akayachunga na wala hakubakisha mali yoyote. Ee Rabb, ikiwa nilifanya hivyo kwa kutaka radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo. Jiwe likafunguka wakatoka zao.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

002-Riyaadhw Asw-Swalihiyn: Mlango Wa Tawbah

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب التوبة

002 - Mlango Wa Tawbah

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ العلماءُ: التَّوْبَةُ وَاجبَةٌ مِنْ كُلِّ ذَنْب، فإنْ كَانتِ المَعْصِيَةُ بَيْنَ العَبْدِ وبَيْنَ اللهِ تَعَالَى لا تَتَعلَّقُ بحقّ آدَمِيٍّ فَلَهَا ثَلاثَةُ شُرُوط:
أحَدُها: أنْ يُقلِعَ عَنِ المَعصِيَةِ.
والثَّانِي: أَنْ يَنْدَمَ عَلَى فِعْلِهَا.
والثَّالثُ: أنْ يَعْزِمَ أَنْ لا يعُودَ إِلَيْهَا أَبَدًا. فَإِنْ فُقِدَ أَحَدُ الثَّلاثَةِ لَمْ تَصِحَّ تَوبَتُهُ.
وإنْ كَانَتِ المَعْصِيةُ تَتَعَلقُ بآدَمِيٍّ فَشُرُوطُهَا أرْبَعَةٌ: هذِهِ الثَّلاثَةُ، وأنْ يَبْرَأ مِنْ حَقّ صَاحِبِها، فَإِنْ كَانَتْ مالًا أَوْ نَحْوَهُ رَدَّهُ إِلَيْه، وإنْ كَانَت حَدَّ قَذْفٍ ونَحْوَهُ مَكَّنَهُ مِنْهُ أَوْ طَلَبَ عَفْوَهُ، وإنْ كَانْت غِيبَةً استَحَلَّهُ مِنْهَا. ويجِبُ أنْ يَتُوبَ مِنْ جميعِ الذُّنُوبِ، فَإِنْ تَابَ مِنْ بَعْضِها صَحَّتْ تَوْبَتُهُ عِنْدَ أهْلِ الحَقِّ مِنْ ذلِكَ الذَّنْبِ وبَقِيَ عَلَيهِ البَاقي.
وَقَدْ تَظَاهَرَتْ دَلائِلُ الكتَابِ والسُّنَّةِ، وإجْمَاعِ الأُمَّةِ عَلَى وُجوبِ التَّوبةِ.
التوبة: الرجوع عن معصية الله تعالى إلى طاعته، وطلب الاستحلال مِنَ المقذوف ونحوه إن بلغه ذلك، وإلا كفى الاستغفار

 

‘Ulamaa wamesema: ni wajibu kutubia kwa kila dhambi anayoitenda mtu. Maasi yanapokuwa ni baina ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta’aalaa) na mja Wake yasiyofungamana na haki ya mwana Aadam, yana shuruti tatu:

1-      Aache maasi

2-      Ajute juu ya kuyatenda

3-      Aazimie kutoyarudia tena kabisa. Moja katika shuruti hizo ikikosekana, tawbah yake haitosihi.

4-      Maasi yanapofungamana na haki ya mwana Aadam, basi shuruti za tawbah ni nne: ni hizo tatu zilizotangulia na ya nne ni: aache haki ya mwenyewe; ikiwa ni mali na mfano wake amrejeshee, ikiwa ni haddi (adhabu) ya kutukana au mfano wake, atammakinisha au amuombe msamaha. Na ikiwa ni kusengenya basi atamuomba amhalalishie. Yapasa atubie dhambi zote. Akitubia baadhi yake, tawbah yake itasihi kutokana na dhambi ile kwa watu wa haki, na atabakiwa na dhambi nyinginezo. Dalili ya Qur-aan, Hadiyth na ijmaa’ ya ummah zipo nyingi katika kuthibitisha namna inavyotakiwa mtu kutubia.

قَالَ الله تَعَالَى:

وَتُوبُوا إِلَى اللَّـهِ جَمِيعًا أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ

Na tubuni kwa Allaah nyote, enyi Waumini mpate kufaulu. [An-Nuwr: 31]

وَأَنِ اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ

Na kwamba: “Mwombeni Rabb wenu maghfirah kisha tubuni Kwake.”  [Huwd: 3]

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللَّـهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا

Enyi walioamini! Tubieni kwa Allaah tawbah ya nasuha (kwelikweli). [At-Tahriym: 8]

 

 

Hadiyth – 1

 عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: سمعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((واللهِ إنِّي لأَسْتَغْفِرُ الله وأَتُوبُ إِلَيْه في اليَوْمِ أَكْثَرَ مِنْ سَبْعِينَ مَرَّةً)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Wa-Allaahi mimi namuomba Allaah maghfirah na natubia Kwake zaidi ya mara sabini kwa siku.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 2

 

وعن الأَغَرِّ بنِ يسار المزنِيِّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا أَيُّهَا النَّاسُ، تُوبُوا إِلى اللهِ واسْتَغْفِرُوهُ، فإنِّي أتُوبُ في اليَومِ مائةَ مَرَّةٍ)). رواه مسلم.

Al-Agharri bin Yasaar Al-Muzaniyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Enyi watu, tubieni kwa Allaah na mumuombe maghfirah. Hakika mimi natubia Kwake mara mia kwa siku.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

 

وعن أبي حمزةَ أنسِ بنِ مالكٍ الأنصاريِّ- خادِمِ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم رضي الله عنه- قَالَ: قَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((للهُ أفْرَحُ بِتَوْبَةِ عَبْدِهِ مِنْ أَحَدِكُمْ سَقَطَ عَلَى بَعِيرهِ وقد أضلَّهُ في أرضٍ فَلاةٍ)). مُتَّفَقٌ عليه. 

وفي رواية لمُسْلمٍ: ((للهُ أَشَدُّ فَرَحًا بِتَوبَةِ عَبْدِهِ حِينَ يتوبُ إِلَيْهِ مِنْ أَحَدِكُمْ كَانَ عَلَى رَاحِلَتهِ بأرضٍ فَلاةٍ، فَانْفَلَتَتْ مِنْهُ وَعَلَيْهَا طَعَامُهُ وَشَرَابهُ فأَيِسَ مِنْهَا، فَأَتى شَجَرَةً فاضطَجَعَ في ظِلِّهَا وقد أيِسَ مِنْ رَاحلَتهِ، فَبَينَما هُوَ كَذَلِكَ إِذْ هُوَ بِها قائِمَةً عِندَهُ، فَأَخَذَ بِخِطامِهَا، ثُمَّ قَالَ مِنْ شِدَّةِ الفَرَحِ: اللَّهُمَّ أنْتَ عَبدِي وأنا رَبُّكَ! أَخْطَأَ مِنْ شِدَّةِ الفَرَحِ))     

Abuu Hamzah, Anas bin Maalik Al-Answaariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) mtumishi wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Huifurahia mno tawbah ya mja Wake kuliko mmoja wenu aliyempata kwa ghafla ngamia wake baada ya kwisha kumpoteza katika ardhi ya jangwa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Muslim inasema: “Allaah Ana furaha mno kwa mja Wake wakati anapomuomba tawbah kuliko mmoja wenu aliyekuwa juu ya ngamia wake katika ardhi ya jangwa, akimkimbia naye amebeba chakula chake na maji yake, akakata tamaa kuwa atampata; akauendea mti na akalala kivulini mwake naye ameshakata tamaa ya kumpata ngamia wake. Alipokuwa yuko katika hali hiyo, ghafla akamuona amemsimamia mbele yake, akamshika hatamu yake, halafu akasema kutokana na furaha kubwa: Ee Rabb! Wewe ni mja wangu nami ni Rabb wako! Amekosea kutokana na furaha kubwa (aliyonayo).”

 

 

Hadiyth – 4

 

وعن أبي موسَى عبدِ اللهِ بنِ قَيسٍ الأشْعريِّ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((إنَّ الله تَعَالَى يَبْسُطُ يَدَهُ بالليلِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ النَّهَارِ، ويَبْسُطُ يَدَهُ بالنَّهَارِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ اللَّيلِ، حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ مِنْ مَغْرِبِها)). رواه مسلم

Abuu Muwsa, 'Abdullaah bin Qays Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Hunyoosha Mkono Wake usiku ili yule aliyekosea mchana apate kutubia, na Hunyoosha mkono Wake mchana ili yule aliyekosea usiku apate kutubia, (hali hiyo huendelea) mpaka jua lichomozapo upande wa magharibi”  [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

 

وعن أبي هُريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ تَابَ قَبْلَ أنْ تَطْلُعَ الشَّمْسُ مِنْ مَغْرِبِها تَابَ اللهُ عَلَيهِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwenye kutubia kabla ya jua kuchomoza upande wa magharibi, Allaah Atamkubalia tawbah yake.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

 

 وعن أبي عبد الرحمن عبد الله بنِ عمَرَ بنِ الخطابِ رضيَ اللهُ عنهما عن النَّبي صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((إِنَّ الله عز وجل يَقْبَلُ تَوبَةَ العَبْدِ مَا لَمْ يُغَرْغِرْ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن)) 

Abuu ‘Abdir-Rahmaan, ‘Abdullaah bin ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu anhumaa) amehadithia kwamba:  Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:  “Hakika Allaah  ‘Azza wa Jallaa Huikubali tawbah ya mja madamu roho yake haijafika kooni.” [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth hii ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 7

 

وعن زِرِّ بن حُبَيْشٍ، قَالَ: أَتَيْتُ صَفْوَانَ بْنَ عَسَّالٍ رضي الله عنه أسْألُهُ عَن الْمَسْحِ عَلَى الخُفَّيْنِ، فَقالَ: ما جاءَ بكَ يَا زِرُّ؟ فقُلْتُ: ابتِغَاء العِلْمِ، فقالَ: إنَّ المَلائكَةَ تَضَعُ أجْنِحَتَهَا لطَالبِ العِلْمِ رِضىً بِمَا يطْلُبُ. فقلتُ: إنَّهُ قَدْ حَكَّ في صَدْري المَسْحُ عَلَى الخُفَّينِ بَعْدَ الغَائِطِ والبَولِ، وكُنْتَ امْرَءًا مِنْ أَصْحَابِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم فَجئتُ أَسْأَلُكَ هَلْ سَمِعْتَهُ يَذكُرُ في ذلِكَ شَيئًا؟ قَالَ: نَعَمْ، كَانَ يَأْمُرُنا إِذَا كُنَّا سَفرًا- أَوْ مُسَافِرينَ- أنْ لا نَنْزعَ خِفَافَنَا ثَلاثَةَ أَيَّامٍ وَلَيالِيهنَّ إلا مِنْ جَنَابَةٍ، لكنْ مِنْ غَائطٍ وَبَولٍ ونَوْمٍ. فقُلْتُ: هَلْ سَمِعْتَهُ يَذْكرُ في الهَوَى شَيئًا؟ قَالَ: نَعَمْ، كُنّا مَعَ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم في سَفَرٍ، فبَيْنَا نَحْنُ عِندَهُ إِذْ نَادَاه أَعرابيٌّ بصَوْتٍ لَهُ جَهْوَرِيٍّ: يَا مُحَمَّدُ، فأجابهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم نَحْوًا مِنْ صَوْتِه: ((هَاؤُمْ)) فقُلْتُ لَهُ: وَيْحَكَ! اغْضُضْ مِنْ صَوتِكَ فَإِنَّكَ عِنْدَ النَّبي صلى الله عليه وسلم، وَقَدْ نُهِيتَ عَنْ هذَا! فقالَ: والله لا أغْضُضُ. قَالَ الأعرَابيُّ: المَرْءُ يُحبُّ القَوْمَ وَلَمَّا يلْحَقْ بِهِمْ؟ قَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((المَرْءُ مَعَ مَنْ أَحَبَّ يَومَ القِيَامَةِ)). فَمَا زَالَ يُحَدِّثُنَا حَتَّى ذَكَرَ بَابًا مِنَ المَغْرِبِ مَسيرَةُ عَرْضِهِ أَوْ يَسِيرُ الرَّاكبُ في عَرْضِهِ أرْبَعينَ أَوْ سَبعينَ عامًا- قَالَ سُفْيانُ أَحدُ الرُّواةِ: قِبَلَ الشَّامِ- خَلَقَهُ الله تَعَالَى يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاواتِ والأَرْضَ مَفْتوحًا للتَّوْبَةِ لا يُغْلَقُ حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ مِنْهُ. رواه الترمذي وغيره، وَقالَ: ((حديث حسن صحيح)).

Zirru bin Hubaysh amesema: “Nilimuendea Swafwaan bin ‘Assaal (Radhwiya Allaahu ‘anhu) nikimuuliza kuhusu kupangusa juu ya khuffu mbili. Akaniuliza: Ni jambo lipi limekuleta Ee Zirru? Akasema: “Hakika Malaika humuwekea mbawa zao mwenye kutafuta ‘Ilmu kwa kumridhia anachokitafuta. Nikamwambia: “Kwa hakika nimeingiwa na shaka moyoni mwangu na kupangusa juu ya khuffu baada hajja kubwa na ndogo, nami nilikuwa mmoja katika Swahaba wa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa hivyo nimekuja kukuuliza je, uliwahi kumsikia akisema chochote katika hilo?” Akajibu: “Ndio. Alikuwa akituamuru tunapokuwa safarini tusivue khuffu zetu michana mitatu na masiku yake, isipokuwa tu kutokana na janaba, lakini kutokana na haja kubwa, ndogo na kulala (tusivue).” Nikamuuliza: “Je, ulimsikia akisema chochote juu ya mapenzi?” Akajibu: “Ndio. Tulikuwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) safarini, tulipokuwa tupo kwake, kwa ghafla akaitwa na Bedui kwa sauti kubwa: “Ee Muhammad!” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuitikia kwa sauti kama yake: “Njoo.” Nikamwambia (Bedui): “Nakuhurumia, teremsha sauti yako kwani upo mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na umekatazwa jambo hili!” Akasema: “Wa-Allaahi siteremshi!” Yule Bedui akasema: “Unaonaje kuhusu mtu anapenda watu na bado hajakutana nao?” Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Mtu atakuwa pamoja na ampendae siku ya Qiyaamah.” Basi akaendelea kutuzungumzia mpaka akautaja mlango upande wa magharibi mwendo wa upana wake au atasafiri mpandaji kwa upana huu miaka miaka arobaini au sabini. Akasema Sufyaan mmoja wa wapokezi:  “Upande wa Shamu. Allaah Aliuumba tokea siku Aliyoumba mbingu na ardhi hali ya kuwa umefunguliwa kwa ajili ya tawbah, haufungwi mpaka jua lichomoze upande huo.” [At-Tirmidhiy na wengineo, na akasema: Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 8

 

وعن أبي سَعيد سَعْدِ بنِ مالكِ بنِ سِنَانٍ الخدريِّ رضي الله عنه أنّ نَبِيَّ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((كَانَ فِيمَنْ كَانَ قَبْلَكمْ رَجُلٌ قَتَلَ تِسْعَةً وتِسْعينَ نَفْسًا، فَسَأَلَ عَنْ أعْلَمِ أَهْلِ الأرضِ، فَدُلَّ عَلَى رَاهِبٍ، فَأَتَاهُ. فقال: إنَّهُ قَتَلَ تِسعَةً وتِسْعِينَ نَفْسًا فَهَلْ لَهُ مِنْ تَوبَةٍ؟ فقالَ: لا، فَقَتَلهُ فَكَمَّلَ بهِ مائَةً، ثُمَّ سَأَلَ عَنْ أَعْلَمِ أَهْلِ الأَرضِ، فَدُلَّ عَلَى رَجُلٍ عَالِمٍ. فقَالَ: إِنَّهُ قَتَلَ مِائَةَ نَفْسٍ فَهَلْ لَهُ مِنْ تَوْبَةٍ؟ فقالَ: نَعَمْ، ومَنْ يَحُولُ بَيْنَهُ وبَيْنَ التَّوْبَةِ؟ انْطَلِقْ إِلى أرضِ كَذَا وكَذَا فإِنَّ بِهَا أُناسًا يَعْبُدُونَ الله تَعَالَى فاعْبُدِ الله مَعَهُمْ، ولا تَرْجِعْ إِلى أَرْضِكَ فَإِنَّهَا أرضُ سُوءٍ، فانْطَلَقَ حَتَّى إِذَا نَصَفَ الطَّرِيقَ أَتَاهُ الْمَوْتُ، فاخْتَصَمَتْ فِيهِ مَلائِكَةُ الرَّحْمَةِ ومَلائِكَةُ العَذَابِ. فَقَالتْ مَلائِكَةُ الرَّحْمَةِ: جَاءَ تَائِبًا، مُقْبِلًا بِقَلبِهِ إِلى اللهِ تَعَالَى، وقالتْ مَلائِكَةُ العَذَابِ: إنَّهُ لمْ يَعْمَلْ خَيرًا قَطُّ، فَأَتَاهُمْ مَلَكٌ في صورَةِ آدَمِيٍّ فَجَعَلُوهُ بَيْنَهُمْ- أيْ حَكَمًا- فقالَ: قِيسُوا ما بينَ الأرضَينِ فَإلَى أيّتهما كَانَ أدنَى فَهُوَ لَهُ. فَقَاسُوا فَوَجَدُوهُ أدْنى إِلى الأرْضِ التي أرَادَ، فَقَبَضَتْهُ مَلائِكَةُ الرَّحمةِ)). مُتَّفَقٌ عليه

وفي رواية في الصحيح: ((فَكَانَ إلى القَريَةِ الصَّالِحَةِ أقْرَبَ بِشِبْرٍ فَجُعِلَ مِنْ أهلِهَا))

Abuu Sa’iyd bin Maalik bin Sinaan Al-Khudriyy (Radhiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kulikuwepo mtu kabla yenu aliua watu tisini na tisa (99) akaulizia aliye mjuzi zaidi katika watu katika nchi ile. Akajulishwa mtawa (miongoni mwa Bani Israaiyl). Akamwendea, akamuuliza: “Nimeua watu tisini na tisa, je, nina tawbah?” Akamjibu: “Hapana!” Akamuua, akawa mtu wa mia. Kisha akauuliza mjuzi zaidi katika watu katika nchi ile. Akafahamishwa kuhusu  Mwanachuoni. Akamuuliza: “Nimeua watu mia. Je, nina tawbah?” Akamjibu: “Ndio, ni nani atakayezuia baina yako na tawbah? Nenda katika nchi fulani, huko kuna watu wanaomuabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) basi nenda ukamuabudu Allaah pamoja nao wala usirejee katika nchi yako, kwani hiyo ni nchi ya maovu.” Akaenda, hata alipofika nusu ya njia, alifikwa na mauti. Malaika wa rahmah wakaanza kuvutana na Malaika wa adhabu. Malaika wa rahmah  wakasema: “Alikuja hali ya kutubia na ameelekea moyo wake kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).” Malaika wa adhabu wakasema: “Yeye hakutenda khayr katu!” Akaja Malaika (mwengine) katika sura ya mwana Aadam, wakamfanya ndiye hakimu baina yao. Akawaambia: “Pimeni baina ya nchi mbili, katika nchi yoyote iliyopo karibu naye, atakuwa ni wa huko.” Wakapima, wakamkuta kuwa yupo karibu zaidi na  nchi anayokusudia kwenda. Malaika wa rahmah wakamchukua.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Swahiyh Al-Bukhaariy, imesema: “Akawa katika kijiji cha watu wema yu karibu nacho kwa shubiri moja. Akajaaliwa ni wa huko.”

Riwaayah nyingine ya Swahiyh Al-Bukhaariy, imesema: Allaah Akakiambia kijiji alichotoka: “Kuwa mbali!” na kijiji anachoenda: “Kuwa karibu!” Na Akawaambia pimeni baina yake.” Wakampata kuwa yupo karibu zaidi ya kijiji anachokwenda kwa shubiri moja; akasamehewa.”

Riwaayah nyingine inasema: “Akakaribia kwa kifua chake upande ule.”

 

 

Hadiyth – 9

 

وعن عبدِ الله بن كعبِ بنِ مالكٍ، وكان قائِدَ كعبٍ رضي الله عنه مِنْ بَنِيهِ حِينَ عمِيَ، قَالَ: سَمِعتُ كَعْبَ بنَ مالكٍ رضي الله عنه يُحَدِّثُ بحَديثهِ حينَ تَخلَّفَ عن رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم في غَزْوَةِ تَبُوكَ. قَالَ كعبٌ: لَمْ أتَخَلَّفْ عَنْ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم في غَزْوَةٍ غزاها قط إلا في غزوة تَبُوكَ، غَيْرَ أنّي قَدْ تَخَلَّفْتُ في غَزْوَةِ بَدْرٍ، ولَمْ يُعَاتَبْ أَحَدٌ تَخَلَّفَ عَنْهُ؛ إِنَّمَا خَرَجَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم والمُسْلِمُونَ يُريدُونَ عِيرَ قُرَيْشٍ حَتَّى جَمَعَ الله تَعَالَى بَيْنَهُمْ وبَيْنَ عَدُوِّهمْ عَلَى غَيْر ميعادٍ. ولَقَدْ شَهِدْتُ مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم لَيلَةَ العَقَبَةِ حينَ تَوَاثَقْنَا عَلَى الإِسْلامِ، وما أُحِبُّ أنَّ لي بِهَا مَشْهَدَ بَدْرٍ، وإنْ كَانَتْ بدرٌ أذْكَرَ في النَّاسِ مِنْهَا. وكانَ مِنْ خَبَري حينَ تَخَلَّفْتُ عَنْ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم في غَزْوَةِ تَبُوكَ أنِّي لم أكُنْ قَطُّ أَقْوى ولا أَيْسَرَ مِنِّي حِينَ تَخَلَّفْتُ عنْهُ في تِلكَ الغَزْوَةِ، وَالله ما جَمَعْتُ قَبْلَهَا رَاحِلَتَيْنِ قَطُّ حَتَّى جَمَعْتُهُمَا في تِلْكَ الغَزْوَةِ وَلَمْ يَكُنْ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يُريدُ غَزْوَةً إلا وَرَّى بِغَيرِها حَتَّى كَانَتْ تلْكَ الغَزْوَةُ، فَغَزَاها رسولُ الله صلى الله عليه وسلم في حَرٍّ شَديدٍ، واسْتَقْبَلَ سَفَرًا بَعِيدًا وَمَفَازًا، وَاستَقْبَلَ عَدَدًا كَثِيرًا، فَجَلَّى للْمُسْلِمينَ أمْرَهُمْ ليتَأهَّبُوا أُهْبَةَ غَزْوِهمْ فأَخْبرَهُمْ بوَجْهِهِمُ الَّذِي يُريدُ، والمُسلِمونَ مَعَ رسولِ الله كثيرٌ وَلا يَجْمَعُهُمْ كِتَابٌ حَافِظٌ (يُريدُ بذلِكَ الدّيوَانَ) قَالَ كَعْبٌ: فَقَلَّ رَجُلٌ يُريدُ أنْ يَتَغَيَّبَ إلا ظَنَّ أنَّ ذلِكَ سيخْفَى بِهِ ما لَمْ يَنْزِلْ فِيهِ وَحْيٌ مِنَ الله، وَغَزا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم تِلْكَ الغَزوَةَ حِينَ طَابَت الثِّمَارُ وَالظِّلالُ، فَأنَا إلَيْهَا أصْعَرُ، فَتَجَهَّزَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم وَالمُسْلِمُونَ مَعَهُ وطَفِقْتُ أغْدُو لكَيْ أتَجَهَّزَ مَعَهُ، فأرْجِعُ وَلَمْ أقْضِ شَيْئًا، وأقُولُ في نفسي: أنَا قَادرٌ عَلَى ذلِكَ إِذَا أَرَدْتُ، فَلَمْ يَزَلْ يَتَمادى بي حَتَّى اسْتَمَرَّ بالنَّاسِ الْجِدُّ، فأصْبَحَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم غَاديًا والمُسْلِمُونَ مَعَهُ وَلَمْ أقْضِ مِنْ جِهَازي شَيْئًا، ثُمَّ غَدَوْتُ فَرَجَعْتُ وَلَمْ أقْضِ شَيئًا، فَلَمْ يَزَلْ يَتَمَادَى بي حَتَّى أسْرَعُوا وتَفَارَطَ الغَزْوُ، فَهَمَمْتُ أنْ أرْتَحِلَ فَأُدْرِكَهُمْ، فَيَا لَيْتَني فَعَلْتُ، ثُمَّ لم يُقَدَّرْ ذلِكَ لي، فَطَفِقْتُ إذَا خَرَجْتُ في النَّاسِ بَعْدَ خُرُوجِ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَحْزُنُنِي أنِّي لا أرَى لي أُسْوَةً، إلا رَجُلًا مَغْمُوصًا عَلَيْهِ في النِّفَاقِ، أوْ رَجُلًا مِمَّنْ عَذَرَ اللهُ تَعَالَى مِنَ الضُّعَفَاءِ، وَلَمْ يَذْكُرْنِي رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم حَتَّى بَلَغَ تَبُوكَ، فَقَالَ وَهُوَ جَالِسٌ في القَوْمِ بِتَبُوكَ: ((ما فَعَلَ كَعْبُ بْنُ مَالِكٍ؟)) فَقَالَ رَجُلٌ مِنْ بَنِي سَلِمَةَ: يا رَسُولَ اللهِ، حَبَسَهُ بُرْدَاهُ والنَّظَرُ في عِطْفَيْهِ. فَقَالَ لَهُ مُعَاذُ بْنُ جَبَلٍ رضي الله عنه: بِئْسَ مَا قُلْتَ! واللهِ يا رَسُولَ اللهِ مَا عَلِمْنَا عَلَيْهِ إلا خَيْرًا، فَسَكَتَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم. فَبَيْنَا هُوَ عَلى ذَلِكَ رَأى رَجُلًا مُبْيِضًا يَزُولُ بِهِ السَّرَابُ، فَقَالَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم: ((كُنْ أَبَا خَيْثَمَةَ))، فَإذَا هُوَ أبُو خَيْثَمَةَ الأنْصَارِيُّ وَهُوَ الَّذِي تَصَدَّقَ بِصَاعِ التَّمْرِ حِيْنَ لَمَزَهُ المُنَافِقُونَ.
قَالَ كَعْبٌ: فَلَمَّا بَلَغَنِي أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قَدْ تَوَجَّهَ قَافِلًا مِنْ تَبُوكَ حَضَرَنِي بَثِّي، فَطَفِقْتُ أتَذَكَّرُ الكَذِبَ وأقُولُ: بِمَ أخْرُجُ مِنْ سَخَطِهِ غَدًا؟ وأسْتَعِيْنُ عَلى ذَلِكَ بِكُلِّ ذِي رأْيٍ مِنْ أهْلِي، فَلَمَّا قِيْلَ: إنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قّدْ أظَلَّ قَادِمًا، زَاحَ عَنّي البَاطِلُ حَتَّى عَرَفْتُ أَنِّي لَنْ أَنْجُوَ مِنْهُ بِشَيءٍ أَبَدًا، فَأجْمَعْتُ صدْقَهُ وأَصْبَحَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم قَادِمًا، وَكَانَ إِذَا قَدِمَ مِنْ سَفَرٍ بَدَأَ بِالمَسْجِدِ فَرَكَعَ فِيهِ رَكْعَتَيْنِ ثُمَّ جَلَسَ لِلنَّاسِ، فَلَمَّا فَعَلَ ذلِكَ جَاءهُ المُخَلَّفُونَ يَعْتَذِرونَ إِلَيْه ويَحْلِفُونَ لَهُ، وَكَانُوا بِضْعًا وَثَمانينَ رَجُلًا، فَقَبِلَ مِنْهُمْ عَلانِيَتَهُمْ وَبَايَعَهُمْ واسْتَغْفَرَ لَهُمْ وَوَكَلَ سَرَائِرَهُمْ إِلى الله تَعَالَى، حَتَّى جِئْتُ، فَلَمَّا سَلَّمْتُ تَبَسَّمَ تَبَسُّمَ المُغْضَبِ. ثُمَّ قَالَ: ((تَعَالَ))، فَجِئْتُ أمْشي حَتَّى جَلَسْتُ بَيْنَ يَدَيْهِ، فقالَ لي: ((مَا خَلَّفَكَ؟ ألَمْ تَكُنْ قَدِ ابْتَعْتَ ظَهْرَكَ؟)) قَالَ: قُلْتُ: يَا رسولَ الله، إنّي والله لَوْ جَلَسْتُ عِنْدَ غَيْرِكَ مِنْ أهْلِ الدُّنْيَا لَرَأيتُ أنِّي سَأخْرُجُ مِنْ سَخَطِهِ بِعُذْرٍ؛ لقَدْ أُعْطِيتُ جَدَلًا، ولَكِنِّي والله لَقَدْ عَلِمْتُ لَئِنْ حَدَّثْتُكَ اليوم حَدِيثَ كَذبٍ تَرْضَى به عنِّي لَيُوشِكَنَّ الله أن يُسْخِطَكَ عَلَيَّ، وإنْ حَدَّثْتُكَ حَدِيثَ صِدقٍ تَجِدُ عَلَيَّ فِيهِ إنّي لأَرْجُو فِيهِ عُقْبَى الله- عز وجل، والله ما كَانَ لي مِنْ عُذْرٍ، واللهِ مَا كُنْتُ قَطُّ أَقْوَى وَلا أَيْسَرَ مِنِّي حِينَ تَخَلَّفْتُ عَنْكَ. قَالَ: فقالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((أمَّا هَذَا فقَدْ صَدَقَ، فَقُمْ حَتَّى يَقْضِيَ اللهُ فيكَ)). وَسَارَ رِجَالٌ مِنْ بَنِي سَلِمَة فاتَّبَعُوني فَقالُوا لِي: واللهِ مَا عَلِمْنَاكَ أذْنَبْتَ ذَنْبًا قَبْلَ هذَا لَقَدْ عَجَزْتَ في أنْ لا تَكونَ اعتَذَرْتَ إِلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بما اعْتَذَرَ إليهِ المُخَلَّفُونَ، فَقَدْ كَانَ كَافِيكَ ذَنْبَكَ اسْتِغْفَارُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم لَكَ. قَالَ: فَوالله ما زَالُوا يُؤَنِّبُونَنِي حَتَّى أَرَدْتُّ أَنْ أرْجعَ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم فأُكَذِّبَ نَفْسِي، ثُمَّ قُلْتُ لَهُمْ: هَلْ لَقِيَ هذَا مَعِيَ مِنْ أَحَدٍ؟ قَالُوا: نَعَمْ، لَقِيَهُ مَعَكَ رَجُلانِ قَالا مِثْلَ مَا قُلْتَ، وَقيلَ لَهُمَا مِثْلَ مَا قيلَ لَكَ، قَالَ: قُلْتُ: مَنْ هُما؟ قَالُوا: مُرَارَةُ بْنُ الرَّبيع الْعَمْرِيُّ، وهِلاَلُ ابنُ أُمَيَّةَ الوَاقِفِيُّ؟ قَالَ: فَذَكَرُوا لِي رَجُلَينِ صَالِحَينِ قَدْ شَهِدَا بَدْرًا فيهِما أُسْوَةٌ، قَالَ: فَمَضَيْتُ حِينَ ذَكَرُوهُما لِي. ونَهَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم عَنْ كَلامِنا أيُّهَا الثَّلاثَةُ مِنْ بَيْنِ مَنْ تَخَلَّفَ عَنْهُ، فاجْتَنَبَنَا النَّاسُ- أوْ قَالَ: تَغَيَّرُوا لَنَا- حَتَّى تَنَكَّرَتْ لي في نَفْسي الأَرْض، فَمَا هِيَ بالأرْضِ الَّتي أعْرِفُ، فَلَبِثْنَا عَلَى ذلِكَ خَمْسِينَ لَيْلَةً. فَأمّا صَاحِبَايَ فَاسْتَكَانا وقَعَدَا في بُيُوتِهِمَا يَبْكيَان. وأمَّا أنَا فَكُنْتُ أشَبَّ الْقَومِ وأجْلَدَهُمْ فَكُنْتُ أخْرُجُ فَأشْهَدُ الصَّلاَةَ مَعَ المُسْلِمِينَ، وأطُوفُ في الأَسْوَاقِ وَلا يُكَلِّمُنِي أَحَدٌ، وَآتِي رسولَ الله صلى الله عليه وسلم فأُسَلِّمُ عَلَيْهِ وَهُوَ في مَجْلِسِهِ بَعْدَ الصَّلاةِ، فَأَقُولُ في نَفسِي: هَلْ حَرَّكَ شَفَتَيْه برَدِّ السَّلام أَمْ لا؟ ثُمَّ أُصَلِّي قَريبًا مِنْهُ وَأُسَارِقُهُ النَّظَرَ، فَإِذَا أقْبَلْتُ عَلَى صَلاتِي نَظَرَ إلَيَّ وَإِذَا الْتَفَتُّ نَحْوَهُ أعْرَضَ عَنِّي، حَتَّى إِذَا طَال ذلِكَ عَلَيَّ مِنْ جَفْوَةِ المُسْلِمينَ مَشَيْتُ حَتَّى تَسَوَّرْتُ جِدارَ حائِط أبي قَتَادَةَ وَهُوَ ابْنُ عَمِّي وأَحَبُّ النَّاس إِلَيَّ، فَسَلَّمْتُ عَلَيهِ فَوَاللهِ مَا رَدَّ عَليَّ السَّلامَ، فَقُلْتُ لَهُ: يَا أَبَا قَتَادَةَ، أنْشُدُكَ بالله هَلْ تَعْلَمُنِي أُحِبُّ الله وَرَسُولَهُ صلى الله عليه وسلم؟ فَسَكَتَ، فَعُدْتُ فَنَاشَدْتُهُ فَسَكَتَ، فَعُدْتُ فَنَاشَدْتُهُ، فَقَالَ: اللهُ ورَسُولُهُ أَعْلَمُ. فَفَاضَتْ عَيْنَايَ، وَتَوَلَّيْتُ حَتَّى تَسَوَّرْتُ الجِدَارَ، فَبَيْنَا أَنَا أمْشِي في سُوقِ الْمَدِينة إِذَا نَبَطِيٌّ مِنْ نَبَطِ أهْلِ الشَّام مِمّنْ قَدِمَ بالطَّعَامِ يَبيعُهُ بِالمَدِينَةِ يَقُولُ: مَنْ يَدُلُّ عَلَى كَعْبِ بْنِ مَالِكٍ؟ فَطَفِقَ النَّاسُ يُشِيرُونَ لَهُ إلَيَّ حَتَّى جَاءنِي فَدَفَعَ إِلَيَّ كِتَابًا مِنْ مَلِكِ غَسَّانَ، وَكُنْتُ كَاتبًا. فَقَرَأْتُهُ فإِذَا فِيهِ: أَمَّا بَعْدُ، فإِنَّهُ قَدْ بَلَغَنا أنَّ صَاحِبَكَ قَدْ جَفَاكَ وَلَمْ يَجْعَلْكَ اللهُ بدَارِ هَوانٍ وَلا مَضْيَعَةٍ، فَالْحَقْ بنَا نُوَاسِكَ، فَقُلْتُ حِينَ قَرَأْتُهَا: وَهَذِهِ أَيضًا مِنَ البَلاءِ، فَتَيَمَّمْتُ بهَا التَّنُّورَ فَسَجَرْتُهَا، حَتَّى إِذَا مَضَتْ أَرْبَعُونَ مِنَ الْخَمْسينَ وَاسْتَلْبَثَ الْوَحْيُ إِذَا رسولُ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم يَأتِيني، فَقالَ: إنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يَأمُرُكَ أنْ تَعْتَزِلَ امْرَأتَكَ، فَقُلْتُ: أُطَلِّقُهَا أمْ مَاذَا أفْعَلُ؟ فَقالَ: لا، بَلِ اعْتَزِلْهَا فَلا تَقْرَبَنَّهَا، وَأَرْسَلَ إِلَى صَاحِبَيَّ بِمِثْلِ ذلِكَ. فَقُلْتُ لامْرَأتِي: الْحَقِي بِأهْلِكِ فَكُوني عِنْدَهُمْ حَتَّى يَقْضِيَ اللهُ في هَذَا الأمْرِ. فَجَاءتِ امْرَأةُ هِلاَلِ بْنِ أُمَيَّةَ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم فَقَالَتْ لَهُ: يَا رَسُولَ الله، إنَّ هِلاَلَ بْنَ أمَيَّةَ شَيْخٌ ضَائِعٌ لَيْسَ لَهُ خَادِمٌ، فَهَلْ تَكْرَهُ أنْ أخْدُمَهُ؟ قَالَ: ((لا، وَلَكِنْ لا يَقْرَبَنَّكِ)) فَقَالَتْ: إِنَّهُ واللهِ ما بِهِ مِنْ حَرَكَةٍ إِلَى شَيْءٍ، وَوَالله مَا زَالَ يَبْكِي مُنْذُ كَانَ مِنْ أمْرِهِ مَا كَانَ إِلَى يَومِهِ هَذَا. فَقَالَ لي بَعْضُ أهْلِي: لَو اسْتَأْذَنْتَ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم في امْرَأَتِكَ فَقَدْ أَذِن لاِمْرَأةِ هلاَل بْنِ أمَيَّةَ أنْ تَخْدُمَهُ؟ فَقُلْتُ: لا أسْتَأذِنُ فيها رسولَ الله صلى الله عليه وسلم وَمَا يُدْرِيني مَاذَا يقُول رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا اسْتَأْذَنْتُهُ، وَأَنَا رَجُلٌ شَابٌ! فَلَبِثْتُ بِذَلِكَ عَشْرَ لَيَالٍ فَكَمُلَ لَنا خَمْسُونَ لَيْلَةً مِنْ حِينَ نُهِيَ عَنْ كَلاَمِنا، ثُمَّ صَلَّيْتُ صَلاَةَ الْفَجْرِ صَبَاحَ خَمْسِينَ لَيْلَةً عَلَى ظَهْرِ بَيْتٍ مِنْ بُيُوتِنَا، فَبَيْنَا أَنَا جَالِسٌ عَلَى الْحالِ الَّتي ذَكَرَ الله تَعَالَى مِنَّا، قَدْ ضَاقَتْ عَلَيَّ نَفْسي وَضَاقَتْ عَلَيَّ الأرْضُ بِمَا رَحُبَتْ، سَمِعْتُ صَوْتَ صَارِخٍ أوفَى عَلَى سَلْعٍ يَقُولُ بِأعْلَى صَوتِهِ: يَا كَعْبَ بْنَ مَالِكٍ أبْشِرْ، فَخَرَرْتُ سَاجِدًا، وَعَرَفْتُ أنَّهُ قَدْ جَاءَ فَرَجٌ. فآذَنَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم النَّاسَ بِتَوْبَةِ الله عز وجل عَلَيْنَا حِينَ صَلَّى صَلاةَ الفَجْر فَذَهَبَ النَّاسُ يُبَشِّرُونَنَا، فَذَهَبَ قِبَلَ صَاحِبَيَّ مُبَشِّرونَ وَرَكَضَ رَجُلٌ إِلَيَّ فَرَسًا وَسَعَى سَاعٍ مِنْ أسْلَمَ قِبَلِي، وَأَوْفَى عَلَى الْجَبَلِ، فَكانَ الصَّوْتُ أسْرَعَ مِنَ الفَرَسِ، فَلَمَّا جَاءني الَّذِي سَمِعْتُ صَوْتَهُ يُبَشِّرُني نَزَعْتُ لَهُ ثَوْبَيَّ فَكَسَوْتُهُمَا إيَّاهُ بِبشارته، وَاللهِ مَا أمْلِكُ غَيْرَهُمَا يَوْمَئِذٍ، وَاسْتَعَرْتُ ثَوْبَيْنِ فَلَبسْتُهُما، وَانْطَلَقْتُ أتَأمَّمُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يَتَلَقَّاني النَّاسُ فَوْجًا فَوْجًا يُهنِّئونَني بالتَّوْبَةِ وَيَقُولُونَ لِي: لِتَهْنِكَ تَوْبَةُ الله عَلَيْكَ. حَتَّى دَخَلْتُ الْمَسْجِدَ فَإِذَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم جَالِسٌ حَوْلَه النَّاسُ، فَقَامَ طَلْحَةُ بْنُ عُبَيْدِ اللهِ رضي الله عنه يُهَرْوِلُ حَتَّى صَافَحَني وَهَنَّأَنِي، والله مَا قَامَ رَجُلٌ مِنَ المُهَاجِرينَ غَيرُهُ- فَكَانَ كَعْبٌ لا يَنْسَاهَا لِطَلْحَةَ.
قَالَ كَعْبٌ: فَلَمَّا سَلَّمْتُ عَلَى رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ وَهُوَ يَبْرُقُ وَجْهُهُ مِنَ السُّرُور: ((أبْشِرْ بِخَيْرِ يَومٍ مَرَّ عَلَيْكَ مُذْ وَلَدَتْكَ أُمُّكَ)) فَقُلْتُ: أمِنْ عِنْدِكَ يَا رَسُول الله أَمْ مِنْ عِندِ الله؟ قَالَ: ((لا، بَلْ مِنْ عِنْدِ الله- عز وجل))، وَكَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا سُرَّ اسْتَنَارَ وَجْهُهُ حَتَّى كَأَنَّ وَجْهَهُ قِطْعَةُ قَمَرٍ وَكُنَّا نَعْرِفُ ذلِكَ مِنْهُ، فَلَمَّا جَلَسْتُ بَيْنَ يَدَيْهِ قُلْتُ: يَا رسولَ الله، إنَّ مِنْ تَوْبَتِي أنْ أنْخَلِعَ مِنْ مَالِي صَدَقَةً إِلَى اللهِ وَإِلَى رَسُولهِ. فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((أَمْسِكَ عَلَيْكَ بَعْضَ مَالِكَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ)). فقلتُ: إِنِّي أُمْسِكُ سَهْمِي الَّذِي بِخَيبَر. وَقُلْتُ: يَا رسولَ الله، إنَّ الله تَعَالَى إِنَّمَا أنْجَانِي بالصِّدْقِ، وإنَّ مِنْ تَوْبَتِي أنْ لا أُحَدِّثَ إلا صِدْقًا مَا بَقِيتُ، فوَالله مَا عَلِمْتُ أَحَدًا مِنَ المُسْلِمينَ أبْلاهُ الله تَعَالَى في صِدْقِ الحَدِيثِ مُنْذُ ذَكَرْتُ ذلِكَ لِرسولِ الله صلى الله عليه وسلم أحْسَنَ مِمَّا أبْلانِي الله تَعَالَى، واللهِ مَا تَعَمَّدْتُ كِذْبَةً مُنْذُ قُلْتُ ذلِكَ لِرسولِ الله صلى الله عليه وسلم إِلَى يَومِيَ هَذَا، وإنِّي لأرْجُو أنْ يَحْفَظَنِي الله تَعَالَى فيما بَقِيَ، قَالَ: فأَنْزَلَ الله تَعَالَى: {لَقَدْ تَابَ اللهُ عَلَى النَّبِيِّ وَالْمُهَاجِرِينَ وَالأَنْصَارِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ فِي سَاعَةِ الْعُسْرَةِ} حَتَّى بَلَغَ: {إِنَّهُ بِهِمْ رَؤُوفٌ رَحِيم وَعَلَى الثَّلاثَةِ الَّذِينَ خُلِّفُوا حَتَّى إِذَا ضَاقَتْ عَلَيْهِمُ الأَرْضُ بِمَا رَحُبَتْ} حَتَّى بَلَغَ: {اتَّقُوا اللهَ وَكُونُوا مَعَ الصَّادِقِينَ} [التوبة: 117: 119] قَالَ كَعْبٌ: واللهِ ما أنْعَمَ الله عَليَّ مِنْ نعمةٍ قَطُّ بَعْدَ إذْ هَدَاني اللهُ للإِسْلامِ أَعْظَمَ في نَفْسِي مِنْ صِدقِي رسولَ الله صلى الله عليه وسلم أنْ لا أكونَ كَذَبْتُهُ، فَأَهْلِكَ كما هَلَكَ الَّذينَ كَذَبُوا؛ إنَّ الله تَعَالَى قَالَ للَّذِينَ كَذَبُوا حِينَ أنْزَلَ الوَحْيَ شَرَّ مَا قَالَ لأَحَدٍ، فقال الله تَعَالَى: {سَيَحْلِفُونَ بِاللهِ لَكُمْ إِذَا انْقَلَبْتُمْ إِلَيْهِمْ لِتُعْرِضُوا عَنْهُمْ فَأَعْرِضُوا عَنْهُمْ إِنَّهُمْ رِجْسٌ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ يَحْلِفُونَ لَكُمْ لِتَرْضَوْا عَنْهُمْ فَإِنْ تَرْضَوْا عَنْهُمْ فَإِنَّ اللهَ لا يَرْضَى عَنِ الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ} لتوبة: 95، 96]
قَالَ كَعْبٌ: كُنّا خُلّفْنَا أيُّهَا الثَّلاَثَةُ عَنْ أمْرِ أُولئكَ الذينَ قَبِلَ مِنْهُمْ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم حِينَ حَلَفُوا لَهُ فَبَايَعَهُمْ وَاسْتَغْفَرَ لَهُمْ وأرجَأَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أمْرَنَا حَتَّى قَضَى الله تَعَالَى فِيهِ بذِلكَ. قَالَ الله تَعَالَى: {وَعَلَى الثَّلاثَةِ الَّذِينَ خُلِّفُوا} وَليْسَ الَّذِي ذَكَرَ مِمَّا خُلِّفْنَا تَخلُّفُنَا عن الغَزْو، وإنَّمَا هُوَ تَخْلِيفُهُ إيّانا وإرْجَاؤُهُ أمْرَنَا عَمَّنْ حَلَفَ لَهُ واعْتَذَرَ إِلَيْهِ فقبِلَ مِنْهُ. مُتَّفَقٌ عليه
وفي رواية: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ في غَزْوَةِ تَبْوكَ يَومَ الخَميسِ وكانَ يُحِبُّ أنْ يخْرُجَ يومَ الخمِيس
وفي رواية: وكانَ لا يقْدمُ مِنْ سَفَرٍ إلا نَهَارًا في الضُّحَى، فإِذَا قَدِمَ بَدَأَ بالمَسْجِدِ فَصَلَّى فِيهِ رَكْعَتَيْنِ ثُمَّ جَلَسَ فِيهِ

 ​'Abdullaah bin Ka’b bin Maalik  alikuwa miongoni mwa watoto wake anamuongoza Ka’b (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alipokuwa kipofu; amesema: “Nilimsikia Ka’b bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akihadithia kisa chake alipobaki nyuma ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika vita vya Tabuwk;  Ka’b ameeleza: “Sijawahi kamwe kubaki nyuma ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika vita vovote alivyopigana ila katika vita vya Tabuwk.  Sikushiriki vita vya Badr. Hakulaumiwa yeyote yote aliyebaki nyuma. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitoka pamoja na Waislamu wakiukusudia msafara wa Maquraysh hadi Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Aliwakutanisha na adui zao bila ya maagano. Nilishuhudia pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) usiku wa ‘Aqabah wakati tulipoandikiana mkataba juu ya Uislamu. Sipendelei kulinganisha hayo na vita vya Badr japokuwa Badr vinatajwa zaidi kuliko ‘Aqabah. 

 

Ama khabari yangu kuhusu vita hivi vya Tabuwk  ni pale nilipobaki nyuma ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nami sijapatapo kuwa ni mwenye nguvu na pesa kama nilipobakia nyuma katika vita hivi.  Wa-Allaahi sijawahi kuwa na ngamia wawili katu kabla ya hapo isipokuwa wakati wa vita hivyo. Alipokuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anataka kupigana vita alikuwa anaficha niyyah yake kwa kutaja vita vingine mpaka ilipofikia vita hivyo ambavyo alipigana katika siku za joto kali na akaelekea kwenye safari ya mbali na bara refu lenye maji kidogo. Akawapokea watu wengi, akawabainishia wazi Waislamu jambo lao (sehemu wanayokwenda) ili wajiandae kwa maandalizi ya vita hivyo. Akawaeleza sehemu anayoikusudia. Wakati huo Waislamu walikuwa wengi pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wala hakuna kitabu kinachoweza kuwajumuisha (yaani kitabu cha majina yao). Yeyote anayetaka kutoroka angelidhani kuwa anaweza kufanya hivyo madamu Wahyi haujateremka kutoka kwa Allaah. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akapigana vita hivyo wakati matunda yalipokuwa tayari (msimu wa mavuno), nami nilikuwa nikiyapendelea (mazao). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akajiandaa pamoja na Maswahaba zake, na nikawa nimepambaukiwa ili kujitayarisha pamoja naye.

Nikarudi wala sikufanya chochote, nikajiambia: “Naweza kufanya hivyo.” Hivyo nikawa najichelewesha mpaka Waislamu wakawa tayari na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakaondoka nami sijajitayarisha chochote. Asubuhi baada ya kuwa wao wameondoka nilitoka ili kujitayarisha lakini nilirudi bila ya kufanya chochote.  Kisha pia asubuhi ya pili yake nilitoka na kurudi bila kufanya chochote.  Hivyo ndivyo hali yangu mpaka wakawa wametoka na nikakosa hivyo vita. Hata hivyo nilitia niyyah kuondoka na kuwapata njiani; natamani kuwa ningefanya hivyo! Nikawa kila ninapotoka nje kutembea kati ya watu waliobaki ilinihuzunisha kuwa sikumuona mtu isipokuwa aliyetuhumiwa kwa unafiki au mtu dhaifu aliyepewa udhuru na Allaah.

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakunikumbuka mpaka alipofika Tabuwk. Akasema akiwa amekaa na watu huko: “Ka’b bin Maalik amefikwa na nini?” Mtu mmoja katika kabila la Banu Salamah akasema: “Ee Rasuli wa Allaah,  amezuiliwa kutazama nguo zake (yaani: anajiona).” Mu’aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akamwambia: “Umesema jambo baya! Wa-Allaahi ee Rasuli wa Allaah, hatumjui ila kwa khayr tu.” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akanyamaza. Alipokuwa yupo katika hali hiyo, alimuona mtu aliyevaa nguo nyeupe akipeperushwa na sarabi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Kuwa Abuu Khaythamah.” Akawa ndiye Abuu Khaythamah Al-Answaariyy, naye ndiye aliyetoa swadaqah pishi la tende pale wanafiki walipombeza.

Nilipopata khabari kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameelekea kuanza kurudi kutoka Tabuwk, nilijiwa na huzuni, nikawa nawaza niseme uongo, nikasema: “Vipi kesho nitaweza kuepuka na ghadhabu Zake Allaah?” Nikawa nikiomba usaidizi kwa jambo hilo kwa kila mwenye maoni miongoni mwa jamaa zangu. Nilipoambiwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameshakaribia kufika, uongo uliniondokea hata nikawa najua siwezi kumuepuka kwa lolote kabisa. Nikaamua kumueleza ukweli.

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anaporejea safari yoyote, huanza kuteremkia Masjid kuswali rakaa mbili kisha huketi na watu. Alipofanya hivyo alijiwa na wale watu waliorudi nyuma wakimtolea nyudhuru na wakimuapia. Walikuwa ni watu zaidi ya themanini. Akawakubalia nyudhuru zao, akachukua bay'ah  (kiapo cha utiifu), akawaombea maghfirah na siri zao akamuachia Allaah (Subhaanhu wa Ta’aalaa).

Nikaja mimi, nikamtolea salaam akatabasamu, tabasamu ya mtu aliyekasirishwa, akaniambia: “Njoo.” Nikaenda mpaka nikakaa kitako mbele yake. Akaniuliza: “Ni jambo gani lililokubakisha nyuma? Hukuwa umenunua ngamia?”  Nikamwambia: “Ee Rasuli wa Allaah, Wa-Allaahi mimi lau ningalikuwa niko mbele ya mtu mwengine asiyekuwa wewe katika watu wa kidunia, ningaliona naweza kuepuka hasira zake kwa udhuru. Hakika nimepewa ufasaha na nguvu ya kusema, Lakini Wa-Allaahi najua kuwa iwapo nitakuzungumzia uongo leo utakaoniridhia, itakaribia Allaah Akutie hasira juu yangu. Na nikizungumza mazungumzo ya kweli, utanikasirikia. Mimi nataraji mwisho mwema wa Allaah ‘Azza wa Jallaa.  Wa-Allaahi sikuwa nina udhuru. Wa-Allaahi, nilikuwa nina nguvu na wepesi nilipobakia nyuma!” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Ama huyu amesema kweli. Nenda mpaka Allaah Atakapokuhukumu.”

 

Watu katika kabila la Banu Salamah wakanifuata, wakanambia: “Wa-Allaahi hatukujui kama umeshawahi kufanya kosa kabla ya hili. Umeshindwa kutoa udhuru kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama walivyotoa wale wengine waliokuwa wamebaki nyuma? Dhambi yako ingalifutwa na istighfaar na du’aa ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) “Basi Wa-Allaahi, hawakuacha kunilaumu mpaka nikataka kumrudia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ili nijikadhibishe. Kisha nikawauliza: “Kuna yeyote aliyemkabili na jambo kama langu?” Wakajibu: “Ndio, watu wawili walimkabili wakasema mithli ya ulivyosema, wakaambiwa kama ulivyoambiwa.” Nikauliza: “Ni nani hao?” Wakajibu: “Muraarah bin Rabiy’ Al-‘Amriy na Hilaal bin Umayyah Al-Waaqify.” Wakanitajia watu wawili wema waliohudhuria vita vya Badr wenye kiigizo. Waliponitajia hao, nikaenda zangu.

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawakataza watu kuzungumza nasi watu watatu pekee miongoni mwa watu waliobaki nyuma. Watu wakatuepuka, au wakatubadilikia mpaka ardhi nikaiona moyoni mwangu imebadilika, si ardhi niijuayo! Tukawa katika hali hiyo masiku khamsini. Ama wale wenzangu wawili, walikuwa wametulia kwa unyenyekevu majumbani mwao wakilia tu. Lakini mimi nilikuwa kijana na mwenye nguvu. Nikawa nikitoka nikihudhuria Swalaah (za jamaa’ah) pamoja na Waislamu wengine, nilitembea masokoni wala hakuna yoyote anayenizungumzisha. Nikamuendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikamtolea salaam naye yupo katika majlis yake baada ya kuswali; nikajiuliza moyoni mwangu: “Ameitikia midomo yake kwa kuirejesha salaam?” Kisha nikaswali karibu yake naye nikimtazama kwa kuibia, nikielekea katika Swalaah yangu naye hunitazama, nikielekea upande wake hugeuka.

Jambo hilo likarefuka kwangu kutokana na Waislamu kujitenga. Nikauparamia ukuta wa bustani ya Abuu Qataadah naye ni bin 'ammi yangu na ni kipenzi zaidi kwangu; nikamsalimia; basi wa-Allaahi hakunirejeshea salaam.  Nikamwambia: “Ee Abuu Qataadah, nakuomba kwa jina la Allaah, je, unajua kuwa mimi nampemda Allaah na Rasuli Wake?” Akanyamaza, nikarejea tena nikamuomba akanyamaza. Nikarejea tena nikamuomba, akasema: “Allaah na Rasuli Wake Wanajua Zaidi.” Macho yangu yakabubujika machozi, nikaenda na kuuparamia ukuta.

Nilipokuwa natembea katika soko la Madiynah, nikamuona mkulima kutoka Shaam aliyekuja kuuza nafaka Madiynah, akaniuliza: “Ni nani atakayenionesha Ka’b bin Maalik?” Watu wakawa wanamuelekeza kwangu, akanijia na kunipatia barua inayotoka kwa mfalme Ghassaan, nami nilikuwa nikijua kusoma na kuandika. Nikaisoma ilikuwa imeandikwa: “Ama baada ya haya. Tumepata habari kuwa mwenzako amekuepuka, wala Allaah hajakujaalia kuwa katika nchi ya unyonge wala haki yako kupotea. Njoo kwetu tutakunafisi.” Nilipomaliza kuisoma, nilisema: “ Hii ni balaa nyingine!” Nikaichukua barua nikaitia katika tanuri na nikaichoma.

Zikapita siku arubaini kati ya zile siku khamsini, wahyi ukachelewa. Mara kwa ghafla mjumbe wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akanijia, akaniambia: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anakuambia umuepuke mkeo.” Nikauliza: “Nimtaliki au nifanyeje?” Akaniambia: “Hapana, kuwa mbali naye wala usimkurubie kabisa.” Akawatumia wenzangu kama hivyo. Nikamwambia mke wangu: “Nenda kwa jamaa zako uwe huko mpaka Allaah Atakapotoa hukumu katika jambo hili.” Mke wa Hilaal bin Umayyah akamwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Ee Rasuli wa Allaah, hakika Hilaal bin Umayyah ni mzee dhaifu na hana mtumishi, je, utachukia nikimhudumia?” Akajibu: “Hapana, lakini asijaribu kukukurubia.” Akasema: “Wa-Allaahi hawezi kutaharaki kukaribia chochote, na wa-Allaahi bado analia tokea yalipomtokea hadi leo hii!” Baadhi ya jamaa zangu wakaniambia: “Lau ungalimuomba udhuru Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu mkeo; kwani mke wa Hilaal bin Umayyah ameruhusiwa amhudumie. Nikasema: “Siwezi kumuomba idhini (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya mke wangu, nitajua lipi atakaloniambia (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwani mimi ni kijana!

Nikakaa kitako katika hali hiyo masiku kumi. Yakakamilika masiku khamsini tangu watu walipokatazwa nasi. Asubuhi ya kupambaukiwa siku ya khamsini, Niliswali Swalaah ya Alfajiri juu ya nyumba miongoni mwa majumba yetu. Nilipokuwa nimekaa kitako katika hali Aliyoitaja Allaah kutuhusu, nafsi yangu ikadhikika kwangu na ardhi ikawa dhiki kwangu ingawa ardhi hiyo ni kunjufu, nikaisikia sauti ya ukelele kutoka katika jabali la Sal’i, mtu akisema kwa sauti ya juu kabisa: “Ee Ka’b bin Maalik! Pokea bishara njema!” Nikaanguka kifudifudi kwa kusujudu, nikajua kuwa faraja imekuja. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) baada ya kuswali Swalaah ya Alfajiri amewajulisha watu juu ya tawbah yetu kwa Allaah (‘Azza wa Jallaa). Watu wakawa wakitupa bishara njema, watoaji biashara wakawaendea wenzangu wawili. Mtu mmoja akapanda farasi akanijia mbio, na mwengine katika kabila la Aslam aliyepanda juu ya jabali sauti yake ikanifikia haraka zaidi kulikoni yule mpanda farasi. Na aliponijia yule niliyemsikia sauti akinibashiria. Nilimvulia nguo zangu mbili na nikamvisha kwa sababu ya ile bishara yake. Wa-Allaahi siku hiyo nilikuwa sikumiliki isipokuwa nguo hizo tu. Nikaazima nguo mbili nikazivaa. Nikaondoka nikimkusudia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Nilipokuwa njiani, watu walikuwa wakikutana na mimi makundi kwa makundi wakinipa pongezi ya tawbah na wakiniambia: “Hongera kwa kupokelewa Tawbah na Allaah.”

Nilipoingia Masjid, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawa amekaa kitako kando yake kuna watu. Twalhah bin ‘Ubaydillaah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akainuka mbio kunipa mkono na kunipa pongezi. Wa-Allaahi hakuna yoyote katika Muhaajiriyn aliyeinuka isipokuwa ni yeye tu. Nikawa simsahau Twalhah kwa jambo hilo. Nilipomsalimia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema huku sura yake ikimeremeta kwa furaha: “Pokea bishara ya khayr siku iliyo bora toka uzaliwe.” Nikauliza: “Ni kutoka kwako ee Rasuli wa Allaah?” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akipatwa na furaha basi sura yake hung’aa kama kipande cha mwezi, jambo hilo tulikuwa tukilijua kwake. Nilipokaa kitako mbele yake, nilimwambia: “Ee Rasuli wa Allaah, kwa sababu ya kukubaliwa tawbah yangu nitatoa mali yangu yote kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake.” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: “Zuia baadhi ya mali yako, kwani hiyo ni khayr kwako.” Nikamwambia: “Mimi naizuia sehemu yangu iliopo Khaybar.” Na nikamwambia: “Ee Rasuli wa Allaah, hakika Allaah Ameniokoa kwa sababu ya ukweli wangu. Hivyo naahidi kuwa katika uhai wangu wote sitosema isipokuwa ukweli.” 

Wa-Allaahi simjui yeyote kati ya Waislamu ambaye Allaah Alimsaidia kusema ukweli kuliko mimi. Wa-Allaahi sikusema uongo tangu nilipomwambia ukweli Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka siku yangu hii leo. Nami nataraji Allaah Atanihifadhi kusema uongo maisha yangu yote. Allaah Akateremsha:

لَّقَد تَّابَ اللَّـهُ عَلَى النَّبِيِّ وَالْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ فِي سَاعَةِ الْعُسْرَةِ مِن بَعْدِ مَا كَادَ يَزِيغُ قُلُوبُ فَرِيقٍ مِّنْهُمْ ثُمَّ تَابَ عَلَيْهِمْ ۚ إِنَّهُ بِهِمْ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ﴿١١٧﴾

Kwa yakini Allaah Amepokea tawbah ya Nabiy na Muhajirina na Answaar ambao wamemfuata (Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم) katika saa ya dhiki (vita vya Tabuwk) baada ya nyoyo za kundi miongoni mwao zilikaribia   kuelemea mbali na haki (Allaah) Akapokea tawbah yao. Hakika Yeye kwao ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu.

 

وَعَلَى الثَّلَاثَةِ الَّذِينَ خُلِّفُوا حَتَّىٰ إِذَا ضَاقَتْ عَلَيْهِمُ الْأَرْضُ بِمَا رَحُبَتْ وَضَاقَتْ عَلَيْهِمْ أَنفُسُهُمْ وَظَنُّوا أَن لَّا مَلْجَأَ مِنَ اللَّـهِ إِلَّا إِلَيْهِ ثُمَّ تَابَ عَلَيْهِمْ لِيَتُوبُوا ۚ إِنَّ اللَّـهَ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ﴿١١٨﴾

Na (pia Allaah Akapokea tawbah) ya wale watatu waliobaki nyuma (kutokwenda vita vya Tabuwk; wakajuta mno) mpaka ardhi ikadhikika kwao juu ya kuwa ni pana na zikadhikika nafsi zao, na wakatambua kwamba hakuna pa kumkimbia Allaah isipokuwa (kuelekea) Kwake; kisha (Allaah) Akapokea tawbah yao, ili watubie. Hakika Allaah Yeye Ndiye Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu.

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَكُونُوا مَعَ الصَّادِقِينَ﴿١١٩﴾

Enyi walioamini! Mcheni Allaah na kuweni pamoja na wakweli. [At-Tawbah: 117- 119]

Wa-Allaahi Hakunineemesha neema yoyote katu baada ya kuniongoza katika Uislamu, neema  iliyo kubwa moyoni mwangu kuliko kumwambia ukweli Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Lau ningesema uongo Angeniangamiza kama Alivyowaangamiza wale waliosema uongo. Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amewaonya vibaya zaidi wasemao uongo kuliko yeyote; Akasema:

سَيَحْلِفُونَ بِاللَّـهِ لَكُمْ إِذَا انقَلَبْتُمْ إِلَيْهِمْ لِتُعْرِضُوا عَنْهُمْ ۖ فَأَعْرِضُوا عَنْهُمْ ۖ إِنَّهُمْ رِجْسٌ ۖ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ﴿٩٥﴾

Watakuapieni kwa Allaah, mtakaporudi kwao ili muwapuuze. Basi wapuuzeni; hakika wao ni rijs (uchafu) na makazi yao ni (Moto wa) Jahannam. Ni jazaa kwa yale waliyokuwa wakiyachuma.

يَحْلِفُونَ لَكُمْ لِتَرْضَوْا عَنْهُمْ ۖ فَإِن تَرْضَوْا عَنْهُمْ فَإِنَّ اللَّـهَ لَا يَرْضَىٰ عَنِ الْقَوْمِ الْفَاسِقِينَ﴿٩٦﴾

Watakuapieni ili muwaridhie. Mkiwaridhia, basi hakika Allaah Haridhii watu mafasiki. [At-Tawbah 95-96]

Sisi watatu tulitofautiana na wale walioapa mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawakubalia nyudhuru zao, akachukua bay'ah yao na kuwaombea maghfirah. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliacha kadhia yetu ibakie mpaka Allaah  (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akahukumu. Allaah Anasema:

وَعَلَى الثَّلاثَةِ الَّذِينَ خُلِّفُوا

Na (pia Allaah Akapokea tawbah) ya wale watatu waliobaki nyuma (kutokwenda vita vya Tabuwk; wakajuta mno) [At-Tawbah; 118]

Hapa haizungumziwi kuhusu kubaki kwetu nyuma kutokwenda vitani. Bali muradi wake ni vile Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alivyoiakhirisha kadhia yetu  kinyume na  kadhia ya wale walitoa nyudhuru kwa kula viapo akawakubalia.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine inasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitoka katika vita vya Tabuwk siku ya Alkhamisi na alikuwa akipenda kusafiri siku ya Alkhamisi.

Riwaayah  nyingine pia inasema: “Na alikuwa harudi kutoka safari ila mchana katika wakati wa Dhwuhaa anapokuja huanza kuteremkia Masjid akiswali humo rakaa mbili kisha akikaa kitako.

 

 

Hadiyth – 10

 

وَعَنْ أبي نُجَيد- بضَمِّ النُّونِ وفتحِ الجيم- عِمْرَانَ بنِ الحُصَيْنِ الخُزَاعِيِّ رضي الله عنهما: أنَّ امْرَأةً مِنْ جُهَيْنَةَ أتَتْ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم وَهِيَ حُبْلَى مِنَ الزِّنَى، فقالتْ: يَا رسولَ الله، أصَبْتُ حَدًّا فَأَقِمْهُ عَلَيَّ، فَدَعَا نَبيُّ الله صلى الله عليه وسلم وَليَّها، فقالَ: ((أَحْسِنْ إِلَيْهَا، فإذا وَضَعَتْ فَأْتِني)) فَفَعَلَ فَأَمَرَ بهَا نبيُّ الله صلى الله عليه وسلم، فَشُدَّتْ عَلَيْهَا ثِيَابُهَا، ثُمَّ أَمَرَ بِهَا فَرُجِمَتْ، ثُمَّ صَلَّى عَلَيْهَا. فقالَ لَهُ عُمَرُ: تُصَلِّي عَلَيْهَا يَا رَسُول الله وَقَدْ زَنَتْ؟ قَالَ: ((لَقَدْ تَابَتْ تَوْبَةً لَوْ قُسِمَتْ بَيْنَ سَبْعِينَ مِنْ أهْلِ المَدِينَةِ لَوَسِعَتْهُمْ، وَهَلْ وَجَدْتَ أَفضَلَ مِنْ أنْ جَادَتْ بنفْسِها لله- عز وجل-؟!)). رواه مسلم

Abuu Nujayd, ‘Imraan bin Huswayn Al-Khuza'iy (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amehadithia kwamba: Mwanamke kutoka kabila la Juhaynah alimuendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) naye ana mimba ya zinaa, akamwambia: “Ee Rasuli wa Allaah, nimetenda dhambi inayopaswa haddi (adhabu), kwa hiyo nipitishie.” Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwita msimamizi wake, akamwambia: “Mfanyie ihsaan atakapojifungua mlete.” Yule msimamizi akafanya kama alivyoamrishwa, halafu akaja naye. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaamuru, akafungwe kwa nguo zake, halafu akaamuru arajimiwe, kisha akamswalia. ‘Umar akamwambia: “Ee Rasuli wa Allaah, unamswalia na hali alikuwa amezini?” Akamwambia: “Kwa yakini ametubia tawbah ambayo lau ingeligawanya kwa watu sabini miongoni mwa watu wa Madiynah, ingewatosha. Je, ushawahi kuona lililo bora kuliko yeye kujileta mwenyewe kwa Allaah (‘Azza wa Jalla)?” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

 

وعن ابنِ عباسٍ رضي الله عنهما أنَّ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((لَوْ أنَّ لابنِ آدَمَ وَادِيًا مِنْ ذَهَبٍ أحَبَّ أنْ يكُونَ لَهُ وَادِيانِ، وَلَنْ يَمْلأَ فَاهُ إلا التُّرَابُ، وَيَتْوبُ اللهُ عَلَى مَنْ تَابَ)). مُتَّفَقٌ عليه

'Abdullaah bin ‘Abbaas na Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) wamehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

“Lau mwana Aadam angalikuwa na bonde la dhahabu, angalipendelea awe na mabonde mawili, wala hakuna kitakachoweza kumtosheleza mdomo wake isipokuwa ni mchanga. Na Allaah Humkubalia tawbah ya yule mwenye kutubia.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 12

 

وعن أبي هريرة رضي الله عنه أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((يَضْحَكُ اللهُ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَى إِلَى رَجُلَيْنِ يقْتُلُ أَحَدهُمَا الآخَرَ يَدْخُلانِ الجَنَّةَ، يُقَاتِلُ هَذَا في سَبيلِ اللهِ فَيُقْتَلُ، ثُمَّ يتُوبُ اللهُ عَلَى القَاتلِ فَيُسْلِم فَيُسْتَشْهَدُ)). مُتَّفَقٌ عليه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Huwacheka watu wawili, mmoja anamuua mwengine, wote wakaingia Jannah. Huyu atapigana na huyu katika njia ya Allaah, atauliwa. Kisha Allaah Atamsamehe aliyeua kwa kusilimu naye akafa shahiyd.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

003-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Subira

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب الصبر

003 – Mlango Wa Subira

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اصْبِرُوا وَصَابِرُوا وَرَابِطُوا وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ

Enyi walioamini! Subirini na zidini kuvuta subira na bakieni imara na mcheni Allaah ili mpate kufaulu. [Al-Baqarah: 200]

 

وَلَنَبْلُوَنَّكُم بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفِ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ مِّنَ الْأَمْوَالِ وَالْأَنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ ۗ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ

Na bila shaka Tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri. [Al-Baqarah: 155]

 

قُلْ يَا عِبَادِ الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا رَبَّكُمْ ۚ لِلَّذِينَ أَحْسَنُوا فِي هَـٰذِهِ الدُّنْيَا حَسَنَةٌ ۗ وَأَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةٌ ۗ إِنَّمَا يُوَفَّى الصَّابِرُونَ أَجْرَهُم بِغَيْرِ حِسَابٍ

Sema: “Enyi waja Wangu ambao mmeamini, mcheni Rabb wenu. Kwa wale waliofanya mazuri katika dunia hii watapata mazuri. Na ardhi ya Allaah ni pana. Hakika wanaosubiri watalipwa kikamilifu ujira wao bila ya hesabu. [Az-Zumar: 10]

 

وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ

Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [As-Shuwra: 43]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الصَّابِرِينَ

Enyi walioamini! Tafuteni msaada kwa subira na Swalaah; hakika Allaah Yu pamoja na wanaosubiri. [Al-Baqarah: 153]

 

وَلَنَبْلُوَنَّكُمْ حَتَّىٰ نَعْلَمَ الْمُجَاهِدِينَ مِنكُمْ وَالصَّابِرِينَ وَنَبْلُوَ أَخْبَارَكُمْ

Na bila shaka Tutakujaribuni mpaka Tutambue wenye kufanya jihaad miongoni mwenu na wenye kuvuta subira na tutazitahini habari zenu. [Muhammad: 31]

 

Aayah zinazoamrisha subira na kubainisha fadhila zake ni nyingi na mashuhuri.

 

 

Hadiyth – 1

وعن أبي مالكٍ الحارث بن عاصم الأشعريِّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((الطُّهُورُ شَطْرُ الإِيمان، وَالحَمدُ لله تَمْلأُ الميزَانَ، وَسُبْحَانَ الله والحَمدُ لله تَملآن- أَوْ تَمْلأُ- مَا بَينَ السَّماوات وَالأَرْضِ، والصَّلاةُ نُورٌ، والصَّدقةُ بُرهَانٌ، والصَّبْرُ ضِياءٌ، والقُرْآنُ حُجةٌ لَكَ أَوْ عَلَيْكَ. كُلُّ النَّاسِ يَغْدُو فَبَائعٌ نَفسَهُ فَمُعْتِقُهَا أَوْ مُوبِقُها)). رواه مسلم

Abuu Maalik, Al-Haarith bin ‘Aaswim Al-Ash’ariy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Wudhuu ni nusu ya iymaan, (kusema:) AlhamduliLLaah hujaza miyzaan, Subhaana Allaah wal-HamduliLLaah hujaza baina ya mbingu na ardhi, Swalaah ni nuru, Swadaqah ni hojja (kwa mwenye iymaan na kuitoa), subira ni mwangaza na Qur-aan ni hojja ya kukuokoa au kukuangamiza. Kila mtu huifanyia ‘amali nafsi yake, kuna mwenye kujiuza, mwenye kujiacha huru au mwenye kujiangamiza.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أبي سَعيد سعدِ بن مالكِ بنِ سنانٍ الخدري رضي الله عنهما: أَنَّ نَاسًا مِنَ الأَنْصَارِ سَألوا رسولَ الله صلى الله عليه وسلم فَأعْطَاهُمْ، ثُمَّ سَألوهُ فَأعْطَاهُمْ، حَتَّى نَفِدَ مَا عِندَهُ، فَقَالَ لَهُمْ حِينَ أنْفْقَ كُلَّ شَيءٍ بِيَدِهِ: ((مَا يَكُنْ عِنْدي مِنْ خَيْر فَلَنْ أدَّخِرَهُ عَنْكُمْ، وَمَنْ يَسْتَعْفِفْ يُعِفهُ اللهُ، وَمَنْ يَسْتَغْنِ يُغْنِهِ اللهُ، وَمَنْ يَتَصَبَّرْ يُصَبِّرْهُ اللهُ. وَمَا أُعْطِيَ أَحَدٌ عَطَاءً خَيْرًا وَأوْسَعَ مِنَ الصَّبْر)). مُتَّفَقٌ عليه

Abuu Sa’iyd, Sa’d bin Maalik bin Sinaan Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: “Watu fulani miongoni mwa Answaar walimuomba Rasuli  wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), naye akawapa, kisha wakamuomba tena, naye akawapa mpaka akamaliza chote alichokuwa nacho. Akawaambia baada ya kuwa ameshatoa kila kitu: “Khayr yoyote niliyonayo siwezi kuwanyima, mwenye kujizuia kuomba Allaah Atamlipa kwa kutoomba, mwenye kutosheka basi na Allaah Atamtosheleza zaidi, na Atakae jisubirisha basi na Allaah Atamzidishia subira. Hakuna yoyote yule aliyepewa zawadi bora na iliyokunjufu zaidi kulikoni subira.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

 وعن أبي يحيى صهيب بن سنانٍ رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((عَجَبًا لأمْرِ المُؤمنِ إنَّ أمْرَهُ كُلَّهُ لَهُ خيرٌ ولَيسَ ذلِكَ لأَحَدٍ إلا للمُؤْمِن: إنْ أَصَابَتْهُ سَرَّاءُ شَكَرَ فَكانَ خَيرًا لَهُ، وإنْ أصَابَتْهُ ضرَاءُ صَبَرَ فَكانَ خَيْرًا لَهُ)). رواه مسلم

Abuu Yahyaa, Swuhayb bin Sinaan (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Ajabu kwa jambo la Muumin; hakika mambo yake ni khayr, wala hakuna anayepata hilo isipokuwa Muumin pekee; akipatwa na furaha hushukuru basi huwa ni khayr kwake, na akipatwa na madhara husubiri basi huwa khayr kwake.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنَسٍ رضي الله عنه قَالَ: لَمَّا ثَقُلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم جَعلَ يَتَغَشَّاهُ الكَرْبُ، فَقَالَتْ فَاطِمَةُ رضي الله عنها: وَاكَربَ أَبَتَاهُ. فقَالَ: ((لَيْسَ عَلَى أَبيكِ كَرْبٌ بَعْدَ اليَوْمِ)) فَلَمَّا مَاتَ، قَالَتْ: يَا أَبَتَاهُ، أَجَابَ رَبًّا دَعَاهُ! يَا أَبتَاهُ، جَنَّةُ الفِردَوسِ مَأْوَاهُ! يَا أَبَتَاهُ، إِلَى جبْريلَ نَنْعَاهُ! فَلَمَّا دُفِنَ قَالَتْ فَاطِمَةُ رَضي الله عنها: أَطَابَتْ أنْفُسُكُمْ أنْ تَحْثُوا عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم التُّرَابَ؟! رواه البخاري.

Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) mambo yalivyomzidia uzito, ukamjia uchungu wa mauti, Faatwimah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) akasema: “Ee uchungu gani unaomshika baba yangu.”  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Baba yako hatoteseka baada ya leo.” Alipofariki Faatwimah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) akasema: “Ee baba yangu ameitika wito wa Rabb wake! Ee baba yangu Jannah ya Al-Firdaws ndio mashukio yake. Ee baba yangu! Kwa Jibriyl tunamuombeleza!” Alipozikwa, Faatwimah alisema: “Nyoyo zenu zimeridhika kwa kumiminia mchanga Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)?” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أبي زَيدٍ أُسَامَةَ بنِ زيدِ بنِ حارثةَ مَوْلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم وحِبِّه وابنِ حبِّه رضي اللهُ عنهما، قَالَ: أرْسَلَتْ بنْتُ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم إنَّ ابْني قَد احْتُضِرَ فَاشْهَدنَا، فَأَرْسَلَ يُقْرئُ السَّلامَ، ويقُولُ: ((إنَّ لله مَا أخَذَ وَلَهُ مَا أعطَى وَكُلُّ شَيءٍ عِندَهُ بِأجَلٍ مُسَمًّى فَلتَصْبِرْ وَلْتَحْتَسِبْ)) فَأَرسَلَتْ إِلَيْهِ تُقْسِمُ عَلَيهِ لَيَأتِينَّهَا. فقامَ وَمَعَهُ سَعْدُ بْنُ عُبَادَةَ، وَمُعَاذُ بْنُ جَبَلٍ، وَأُبَيُّ بْنُ كَعْبٍ، وَزَيْدُ بْنُ ثَابتٍ، وَرجَالٌ رضي الله عنهم، فَرُفعَ إِلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم الصَّبيُّ، فَأقْعَدَهُ في حِجْرِهِ وَنَفْسُهُ تَقَعْقَعُ، فَفَاضَتْ عَينَاهُ فَقالَ سَعدٌ: يَا رسولَ الله، مَا هَذَا؟ فَقالَ: ((هذِهِ رَحمَةٌ جَعَلَها اللهُ تَعَالَى في قُلُوبِ عِبَادِهِ)) وفي رواية: ((فِي قُلُوبِ مَنْ شَاءَ مِنْ عِبَادِهِ، وَإِنَّما يَرْحَمُ اللهُ مِنْ عِبادِهِ الرُّحَماءَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Zayd, Usaamah bin Zayd bin Haarithah muachwa huru wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kipenzi chake na ni mwana wa kipenzi chake (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Binti mmoja wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimpelekea salaamu Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa “Mwana wangu amejiwa na umauti, basi njoo.” Naye akamtuma mtu akimpelekea salaamu na akamwambia: “Allaah Ana khiyari ya kuchukua Anachotaka na kutoa Anachotaka. Kila kitu Kwake kina muda maalumu, basi asubiri na taraji malipo kwa Allaah.” Akamtumia tena ujumbe akimuapia aende. Akasimama, pamoja naye alikuwepo Sa’d bin ‘Ubaadah, Mu’aadh bin Jabal, Ubayyi bin Ka’b, Zayd bin Thaabit na wengineo (Radhwiya Allaahu ‘anhum). Yule mtoto akapelekewa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), akamkalisha katika paja lake na nafsi ya yule mtoto ikiwa katika hali ya woga, macho ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) yakabubujikwa na machozi, Sa’d akauliza: “Una nini yaa Rasula-Allaah?” Akamwambia: “Hii ni rahmah, Allaah Amejaalia katika nyoyo za waja Wake.”

Riwaayah nyingine imesema: “Katika nyoyo za Anaowataka miongoni mwa waja Wake. Hakika Allaah Huwarehemu wenye huruma katika waja Wake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن صهيب رضي الله عنه: أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((كَانَ مَلِكٌ فيمَنْ كَانَ قَبلَكمْ وَكَانَ لَهُ سَاحِرٌ فَلَمَّا كَبِرَ قَالَ للمَلِكِ: إنِّي قَدْ كَبِرْتُ فَابْعَثْ إلَيَّ غُلامًا أُعَلِّمْهُ السِّحْرَ؛ فَبَعثَ إِلَيْهِ غُلامًا يُعَلِّمُهُ، وَكانَ في طرِيقِهِ إِذَا سَلَكَ رَاهِبٌ، فَقَعدَ إِلَيْه وسَمِعَ كَلامَهُ فَأعْجَبَهُ، وَكانَ إِذَا أتَى السَّاحِرَ، مَرَّ بالرَّاهبِ وَقَعَدَ إِلَيْه، فَإذَا أَتَى السَّاحِرَ ضَرَبَهُ، فَشَكَا ذلِكَ إِلَى الرَّاهِب، فَقَالَ: إِذَا خَشيتَ السَّاحِرَ، فَقُلْ: حَبَسَنِي أَهْلِي، وَإذَا خَشِيتَ أهلَكَ، فَقُلْ: حَبَسَنِي السَّاحِرُ.

فَبَيْنَما هُوَ عَلَى ذلِكَ إِذْ أَتَى عَلَى دَابَّةٍ عَظِيمَةٍ قَدْ حَبَسَتِ النَّاسَ فَقَالَ: اليَوْمَ أعْلَمُ السَّاحرُ أفْضَلُ أم الرَّاهبُ أفْضَلُ؟ فَأخَذَ حَجَرًا، فَقَالَ: اللَّهُمَّ إنْ كَانَ أمْرُ الرَّاهِبِ أَحَبَّ إِلَيْكَ مِنْ أمْرِ السَّاحِرِ فَاقْتُلْ هذِهِ الدّابَّةَ حَتَّى يَمضِي النَّاسُ، فَرَمَاهَا فَقَتَلَها ومَضَى النَّاسُ، فَأتَى الرَّاهبَ فَأَخبَرَهُ. فَقَالَ لَهُ الرَّاهبُ: أَيْ بُنَيَّ أَنْتَ اليَومَ أفْضَل منِّي قَدْ بَلَغَ مِنْ أَمْرِكَ مَا أَرَى، وَإنَّكَ سَتُبْتَلَى، فَإن ابْتُلِيتَ فَلا تَدُلَّ عَلَيَّ؛ وَكانَ الغُلامُ يُبْرىءُ الأكْمَهَ وَالأَبْرصَ، ويداوي النَّاسَ مِنْ سَائِرِ الأَدْوَاء. فَسَمِعَ جَليسٌ لِلملِكِ كَانَ قَدْ عَمِيَ، فأتاه بَهَدَايا كَثيرَةٍ، فَقَالَ: مَا هاهُنَا لَكَ أَجْمعُ إنْ أنتَ شَفَيتَنِي، فَقَالَ: إنّي لا أشْفِي أحَدًا إِنَّمَا يَشفِي اللهُ تَعَالَى، فَإنْ آمَنْتَ بالله تَعَالَى دَعَوتُ اللهَ فَشفَاكَ، فَآمَنَ بالله تَعَالَى فَشفَاهُ اللهُ تَعَالَى، فَأَتَى المَلِكَ فَجَلسَ إِلَيْهِ كَما كَانَ يَجلِسُ، فَقَالَ لَهُ المَلِكُ: مَنْ رَدّ عَلَيْكَ بَصَرَكَ؟ قَالَ: رَبِّي، قَالَ: وَلَكَ رَبٌّ غَيري؟ قَالَ: رَبِّي وَرَبُّكَ اللهُ، فَأَخَذَهُ فَلَمْ يَزَلْ يُعَذِّبُهُ حَتَّى دَلَّ عَلَى الغُلامِ، فَجيء بالغُلاَمِ، فَقَالَ لَهُ المَلِكُ: أيْ بُنَيَّ، قَدْ بَلَغَ مِنْ سِحْرِكَ مَا تُبْرئ الأَكْمَهَ وَالأَبْرَصَ وتَفْعَلُ وتَفْعَلُ! فَقَالَ: إنِّي لا أَشْفي أحَدًا، إِنَّمَا يَشفِي الله تَعَالَى. فَأَخَذَهُ فَلَمْ يَزَلْ يُعَذِّبُهُ حَتَّى دَلَّ عَلَى الرَّاهبِ؛ فَجِيء بالرَّاهبِ فَقيلَ لَهُ: ارجِعْ عَنْ دِينكَ، فَأَبَى، فَدَعَا بِالمِنْشَارِ فَوُضِعَ المِنْشَارُ في مَفْرق رَأسِهِ، فَشَقَّهُ حَتَّى وَقَعَ شِقَّاهُ، ثُمَّ جِيءَ بِجَليسِ المَلِكِ فقيل لَهُ: ارْجِعْ عَنْ دِينِكَ، فَأَبَى، فَوضِعَ المِنْشَارُ في مَفْرِق رَأسِهِ، فَشَقَّهُ بِهِ حَتَّى وَقَعَ شِقَّاهُ، ثُمَّ جِيءَ بالغُلاَمِ فقيلَ لَهُ: ارْجِعْ عَنْ دِينكَ، فَأَبَى، فَدَفَعَهُ إِلَى نَفَرٍ مِنْ أصْحَابهِ، فَقَالَ: اذْهَبُوا بِهِ إِلَى جَبَلِ كَذَا وَكَذَا فَاصْعَدُوا بِهِ الجَبَل، فَإِذَا بَلَغْتُمْ ذِرْوَتَهُ فَإِنْ رَجَعَ عَنْ دِينِهِ وَإلا فَاطْرَحُوهُ. فَذَهَبُوا بِهِ فَصَعِدُوا بِهِ الجَبَلَ، فَقَالَ: اللَّهُمَّ أكْفنيهمْ بِمَا شِئْتَ، فَرَجَفَ بهِمُ الجَبلُ فَسَقَطُوا، وَجاءَ يَمشي إِلَى المَلِكِ، فَقَالَ لَهُ المَلِكُ: مَا فَعَلَ أصْحَابُكَ؟ فَقَالَ: كَفَانِيهمُ الله تَعَالَى، فَدَفَعَهُ إِلَى نَفَرٍ مِنْ أَصْحَابِهِ فَقَالَ: اذْهَبُوا بِهِ فاحْمِلُوهُ في قُرْقُورٍ وتَوَسَّطُوا بِهِ البَحْرَ، فَإنْ رَجعَ عَنْ دِينِهِ وإِلا فَاقْذِفُوهُ. فَذَهَبُوا بِهِ، فَقَالَ: اللَّهُمَّ أكْفِنيهمْ بمَا شِئْتَ، فانْكَفَأَتْ بِهمُ السَّفينةُ فَغَرِقُوا، وَجَاء يَمْشي إِلَى المَلِكِ. فَقَالَ لَهُ المَلِكُ: مَا فعلَ أصْحَابُكَ؟ فَقَالَ: كَفَانيهمُ الله تَعَالَى. فَقَالَ لِلمَلِكِ: إنَّكَ لَسْتَ بقَاتلي حَتَّى تَفْعَلَ مَا آمُرُكَ بِهِ. قَالَ: مَا هُوَ؟ قَالَ: تَجْمَعُ النَّاسَ في صَعيدٍ وَاحدٍ وتَصْلُبُني عَلَى جِذْعٍ، ثُمَّ خُذْ سَهْمًا مِنْ كِنَانَتي، ثُمَّ ضَعِ السَّهْمَ في كَبدِ القَوْسِ ثُمَّ قُلْ: بسْم الله ربِّ الغُلاَمِ، ثُمَّ ارْمِني، فَإنَّكَ إِذَا فَعَلْتَ ذلِكَ قَتَلتَني، فَجَمَعَ النَّاسَ في صَعيد واحدٍ، وَصَلَبَهُ عَلَى جِذْعٍ، ثُمَّ أَخَذَ سَهْمًا مِنْ كِنَانَتِهِ، ثُمَّ وَضَعَ السَّهْمَ في كَبِدِ القَوْسِ، ثُمَّ قَالَ: بِسمِ اللهِ ربِّ الغُلامِ، ثُمَّ رَمَاهُ فَوقَعَ في صُدْغِهِ، فَوَضَعَ يَدَهُ في صُدْغِهِ فَمَاتَ، فَقَالَ النَّاسُ: آمَنَّا بِرَبِّ الغُلامِ، فَأُتِيَ المَلِكُ فقيلَ لَهُ: أَرَأَيْتَ مَا كُنْتَ تَحْذَرُ قَدْ والله نَزَلَ بكَ حَذَرُكَ. قَدْ آمَنَ النَّاسُ. فَأَمَرَ بِالأُخْدُودِ بأفْواهِ السِّكَكِ فَخُدَّتْ وأُضْرِمَ فيهَا النِّيرانُ وَقَالَ: مَنْ لَمْ يَرْجعْ عَنْ دِينهِ فَأقْحموهُ فيهَا، أَوْ قيلَ لَهُ: اقتَحِمْ فَفَعَلُوا حَتَّى جَاءت امْرَأةٌ وَمَعَهَا صَبيٌّ لَهَا، فَتَقَاعَسَتْ أنْ تَقَعَ فيهَا، فَقَالَ لَهَا الغُلامُ: يَا أُمهْ اصْبِري فَإِنَّكِ عَلَى الحَقِّ!)). رواه مسلم

Swuhayb (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Alikuwepo mfalme kabla ya zama zenu. Alikuwa anae mchawi, yule mchawi alipozeeka alimwambia mfalme: “Mimi nimezeeka, niletee kijana nitakaemfunza uchawi.” (mfalme) akampelekea kijana ili amfunze. Alikuwa (yule kijana) katika njia anayoelekea kuna Rahibu (mtawa mwanaume). Akakaa kumsikiliza, akapendezewa na maneno yake, na alikuwa akitaka kumuendea mchawi yule hupita kwa Rahibu yule na kukaa naye na kumsikiliza, anapomwendea mchawi, humpiga. Jambo hili akamshitakia yule mtawa. (Mtawa) akamwambia: “Utakapomuendea mchawi mwambie: ‘Nimezuiliwa na watu wangu,’ na unapowarudia watu wako, waambie: Nimezuiliwa na mchawi.” Alipokuwa akiendelea katika hali hiyo, kwa ghafla akaona mnyama mkubwa aliyezuia watu. Akasema: “Leo ndiyo nitajua kati ya mtawa na mchawi nani aliye bora.” Akachukua jiwe na akasema: “Ee Rabb, ikiwa jambo la yule Mtawa linapendeza Kwako kuliko jambo la yule mchawi, basi muuwe mnyama huyu ili watu waweze kupita.” Akamrushia (jiwe) na akamuua, watu wakapita. Akamuendea Mtawa na kumueleza habari ile. Yule Mtawa akamwambia: “Ee mwanangu leo hii wewe ni bora kulikoni mimi, jambo lako limefikia jinsi ninavyoliona, kwa yakini utapata mtihani; basi utakapopata mtihani, usimjulishe yoyote yule kwangu.” Yule kijana akaanza kuwaponya waliozaliwa vipofu, wenye ukoma na akiwatibu watu kila aina ya maradhi. Jalisi wa mfalme aliyekuwa amepofoka, akasikia habari hii. Akampelekea zawadi nyingi, akamwambia: “Mimi sina uwezo wa kumponya yoyote, hakika Anaeponya ni Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Ukimuamini Allaah nitamuomba Naye Atakuponya.” Akamuamini Allaah, Allaah Akamponya. Akaenda kwa mfalme na kukaa nae kama anavyokaa nae (kila siku). Mfalme akamuuliza: “Ni nani aliyekuponya macho yako?” Akajibu: “Ni Rabb wangu.” Akamuuliza: “Unae Rabb asiyekuwa mimi?” Akamjibu: “Rabb wangu na Rabb wako ni Allaah.” Akamchukua na akamuadhibu mpaka akamtaja yule kijana. Yule kijana akaletwa mbele ya mfalme, akamuuliza: “Ee kijana wangu, uchawi wako umefikia kiwango cha kuwaponya vipofu na wenye ukoma, na unafanya kadhaa na kadhaa?” Akamwambia: “Mimi sina uwezo wa kumponya yoyote yule, kwa yakini Anaeponya ni Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).” Akamchukua na kumuadhibu mpaka akamtaja yule Mtawa. Mtawa akaletwa, akaambiwa: “Acha dini yako.” Akakataa. Akaitisha msumeno akauweka utosini mwake, akampasua vipande viwili vikaanguka (akamgawanya pande mbili). Halafu akaletwa jalisi wa mfalme. Akaambiwa: “Acha dini yako.” Akakataa. Msumeno ukawekwa utosini mwake, akapasuliwa pande mbili zikaanguaka. Kisha akaletwa yule kijana. Akaambiwa: “Wacha dini yako.” Akakataa. Akamkabidhi kwa askari wake, akawaambia: “Nendeni naye katika jabali kadhaa wa kadhaa, mtakapofika katika kilele chake na akawa ameiwacha dini yake, basi muacheni, ikiwa hakuacha basi mtupeni chini.” Wakaenda nae na wakapanda nae juu ya jabali. Yule kijana akaomba: “Ee Rabb! Nitosheleze na shari yao namna Upendavyo.” Lile jabali likatikisika wakaanguka. Akarudi kwa mfalme huku akitembea. Mfalme akamuuliza: “Wamekuaje watu wako?” Akamwambia: Allaah Amenitosheleza.” Akamkabidhisha kwa kundi (lingine) la maaskari wake. Akawaambia: “Mpelekeni na mumpandishe jahazi ndogo hadi katikati ya bahari, akiwacha dini yake muacheni, akikataa basi mtoseni.” Wakaenda naye, akaomba: “Ee Rabb! Nitosheleze na shari yao namna Upendavyo.” Jahazi likapinduka wakazama. Akarudi kwa mfalme akitembea. Mfalme akamuuliza: “Wamekuaje watu wako?” Akamwambia: “Allaah Amenitosheleza.” Akamwambia mfalme: “Hakika huwezi kuniua mpaka ufanye nitakalokuamuru.” Akamuuliza: “Ni jambo gani hilo utakaloniamuru?” Akamwambia: “Wakusanye watu katika uwanja ulio wazi, halafu unisulubishe juu ya gogo, halafu uchukue mshale utakaokuwa katika ziaka yangu, kisha utauweka mshale katika upinde, halafu useme: “Kwa jina la Allaah, Rabb wa kijana huyu”. Kisha unirushie. Hakika ukifanya hivyo, utafanikiwa kuniua.” Yule mfalme akawakusanya watu katika uwanja mmoja, akamtundika juu ya gogo, halafu akachukua mshale kutoka katika ziaka yake, kisha akauweka mshale katikati ya upinde, halafu akasema: “Kwa jina la Allaah, Rabb wa kijana huyu,” kisha akamrushia ule mshale ukaingia katika panda lake uso, akauweka mkono wake katika panda lake na akafa. Watu wakasema: “Tumemuamini Rabb wa kijana huyu.” Mfalme akaendewa na kuambiwa: “Je, umeliona ulilokuwa ukilitahadhari? Wa-Allaahi limekuwa ulilolikataa, watu wamekuwa na iymaan.” Akaamuru kuchimbwe mahandaki barabarani, mioto ikawashwa humo. Akasema: “Ambae hatoacha dini yake mtupeni humo.” Au huambiwa: “Jitoseni wenyewe.” Wakafanya hivyo. Akaletwa mwanamke aliye na mtoto wake. Akasimama na akafanya uoga kuingia humo, yule mtoto wake akamwambia: “Ee mama yangu, subiri hakika wewe upo katika haki!” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: مَرَّ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم بامرأةٍ تَبكي عِنْدَ قَبْرٍ، فَقَالَ: ((اتّقِي الله واصْبِري)) فَقَالَتْ: إِليْكَ عَنِّي؛ فإِنَّكَ لم تُصَبْ بمُصِيبَتي وَلَمْ تَعرِفْهُ، فَقيلَ لَهَا: إنَّه النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم فَأَتَتْ بَابَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، فَلَمْ تَجِدْ عِنْدَهُ بَوَّابينَ، فقالتْ: لَمْ أعْرِفكَ، فَقَالَ: ((إنَّمَا الصَّبْرُ عِنْدَ الصَّدْمَةِ الأُولى)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية لمسلم: ((تبكي عَلَى صَبيٍّ لَهَا)).

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipita akamuona mwanamke akilia mbele ya kaburi. Akamwambia: “Mche Allaah na usubiri.” Yule mwanamke akasema: “Niondokee, kwani hujapatwa na msiba kama wangu!” Wala hakumjua. Akaambiwa: Huyo alikuwa ni Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), akaenda hadi kwenye mlango wa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na hakuwakuta walinzi, akamwambia: “Nilikuwa sijakujua kama ni wewe.” Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Hakika subira ni mwanzo wa kupatwa na msiba.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema: “Alikuwa akimlilia mwanawe.”

 

 

Hadiyth – 8

 وعن أبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((يَقُولُ اللهُ تَعَالَى: مَا لعَبدِي المُؤْمِنِ عِنْدِي جَزَاءٌ إِذَا قَبَضْتُ صَفِيَّهُ مِنْ أهْلِ الدُّنْيَا ثُمَّ احْتَسَبَهُ إلا الجَنَّةَ)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema: “Mja wangu Muumin ni mwenye malipo nitakapomchukua mpenzi wake katika watu wa dunia kisha akataraji thawabu isipokuwa jazaa yake ni Jannah.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 9

وعن عائشةَ رضيَ الله عنها: أَنَّهَا سَألَتْ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الطّاعُونِ، فَأَخْبَرَهَا أنَّهُ كَانَ عَذَابًا يَبْعَثُهُ اللهُ تَعَالَى عَلَى مَنْ يشَاءُ، فَجَعَلَهُ اللهُ تعالى رَحْمَةً للْمُؤْمِنينَ، فَلَيْسَ مِنْ عَبْدٍ يَقَعُ في الطَّاعُونِ فيمكثُ في بلدِهِ صَابرًا مُحْتَسِبًا يَعْلَمُ أنَّهُ لا يصيبُهُ إلا مَا كَتَبَ اللهُ لَهُ إلا كَانَ لَهُ مِثْلُ أجْرِ الشّهيدِ. رواه البخاري

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) alimuuliza Rasuli  wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu twaa’uwn (ugonjwa wa tauni), akamwambia kuwa: “Ilikuwa ni adhabu ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akimpelekea Anayemtaka; Allaah Akaijaalia kuwa ni rahmah kwa Waumini. Hakuna mja yoyote yule atakaepata twaa’uwn akakaa katika mji ule kwa kusubiri na kutaraji thawabu akijua kuwa hakuna kitakachompata ila alichoandikiwa na Allaah, isipokuwa na ujira mfano wa (aliyekufa) shaahid.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: سمعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((إنَّ الله- عز وجل، قَالَ: إِذَا ابْتَلَيْتُ عبدي بحَبيبتَيه فَصَبرَ عَوَّضتُهُ مِنْهُمَا الجَنَّةَ)) يريد عينيه، رواه البخاري

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Hakika Allaah (‘Azza wa Jalla) Amesema: “Nitakapomjaribu mja Wangu kwa kukosa vipenzi vyake (macho mawili) na akasubiri, Nitambadilishia Jannah badala yake.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 11

 وعن عطَاء بن أبي رَباحٍ قَالَ: قَالَ لي ابنُ عَباسٍ رضي اللهُ عنهما: ألا أُريكَ امْرَأةً مِنْ أَهْلِ الجَنَّة؟ فَقُلْتُ: بَلَى، قَالَ: هذِهِ المَرْأةُ السَّوداءُ أتتِ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، فَقَالَتْ: إنّي أُصْرَعُ، وإِنِّي أتَكَشَّفُ، فادْعُ الله تَعَالَى لي. قَالَ: ((إنْ شئْتِ صَبَرتِ وَلَكِ الجَنَّةُ، وَإنْ شئْتِ دَعَوتُ الله تَعَالَى أنْ يُعَافِيكِ)) فَقَالَتْ: أَصْبِرُ، فَقَالَتْ: إنِّي أتَكَشَّفُ فَادعُ الله أنْ لا أَتَكَشَّف، فَدَعَا لَهَا. مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Atwaa bin Abiy Rabaah amesema: “’Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) aliniambia: Je, nikuonyeshe mwanamke ambae ni katika watu wa Jannah?” Nikwambia: “Ni mwanamke huyu mweusi, alimuendea Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kamwambia: “Mimi nina kifafa na huwa nafichulika wazi (sehemu za siri kinaponijia), niombee kwa Allaah.” Akamwambia: “Ukitaka subiri na ukitaka nitamuomba Allaah Akuponye.” Akasema: “Nitasubiri lakini mimi nafichulika wazi basi niombee kwa Allaah nisifichulike wazi (nisitirike nguo isinifunuke).” Akamuombea. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyh -12

 

وعن أبي عبد الرحمنِ عبدِ الله بنِ مسعودٍ رضي الله عنه قَالَ: كَأَنِّي أنْظُرُ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم يَحْكِي نَبِيًّا مِنَ الأَنْبِياءِ، صَلَواتُ الله وَسَلامُهُ عَلَيْهمْ، ضَرَبه قَوْمُهُ فَأدْمَوهُ، وَهُوَ يَمْسَحُ الدَّمَ عَنْ وَجْهِهِ، يَقُولُ: ((اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِقَومي، فَإِنَّهُمْ لا يَعْلَمونَ)). مُتَّفَقٌ علَيه

Abuu ‘Abdir-Rahmaan, ‘Abdulaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Kana kwamba namuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akieleza kuhusu Nabiy fulani, (‘Alayhimus-Salaam). Watu wake walimpinga na kumtoa damu usoni mwake, akiomba: “Ee Rabb! Waghufurie kaumu yangu, kwani wao hawajui!” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 13

 

وعن أبي سعيدٍ وأبي هريرةَ رضيَ الله عنهما، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((مَا يُصيبُ المُسْلِمَ مِنْ نَصَبٍ، وَلا وَصَبٍ، وَلا هَمٍّ، وَلا حَزَنٍ، وَلا أذَىً، وَلا غَمٍّ، حَتَّى الشَّوكَةُ يُشَاكُهَا إلا كَفَّرَ اللهُ بِهَا مِنْ خَطَاياهُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Sa’iyd na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) wamepokea kutoka kwa Nabiy  (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa amesema: “Muislaam hatopatwa na tabu, wala maradhi, wala hamu, wala huzuni, wala udhia, wala ghamu (sononeko) hata akichomwa na mwiba, isipokuwa Allaah Humfutia madhambi yake kwa sababu ya (matatizo) hayo.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 14

وعن ابنِ مسعودٍ رضي الله عنه قَالَ: دخلتُ عَلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم وهو يُوعَكُ، فقلت: يَا رسُولَ الله، إنَّكَ تُوْعَكُ وَعْكًا شَدِيدًا، قَالَ: ((أجَلْ، إنِّي أوعَكُ كمَا يُوعَكُ رَجُلانِ مِنكُمْ)). قلْتُ: ذلِكَ أن لَكَ أجْرينِ؟ قَالَ: ((أَجَلْ، ذلِكَ كَذلِكَ، مَا مِنْ مُسْلِمٍ يُصيبُهُ أذىً، شَوْكَةٌ فَمَا فَوقَهَا إلا كَفَّرَ اللهُ بهَا سَيِّئَاتِهِ، وَحُطَّتْ عَنْهُ ذُنُوبُهُ كَمَا تَحُطُّ الشَّجَرَةُ وَرَقَهَا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Nilimuendea Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) naye akiwa na homa. Nikamwambia: Yaa Rasula-Allaah, hakika huwa ukishikwa na homa basi huwa kali mno.” Akasema: “Ndiyo, hakika mimi hushikwa na homa kama vile watu wawili wanavyoshikwa na homa kati yenu.” Nikamuuliza: “Ni kwa vile una ujira mara mbili?” Akasema: “Ndiyo, ni hivyo. Hakuna Muislaamu yoyote anasibiwa na udhia kuanzia mwiba na kuendelea, isipokuwa Allaah humsamehe mabaya yake kwa udhia huo, na dhambi zake hupuputishwa kama vile mti unavyopuputika majani yake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 15

 وعن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ يُرِدِ اللهُ بِهِ خَيْرًا يُصِبْ مِنْهُ)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Anayependelewa khayr na Allaah Humpa msiba.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 16

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((لا يَتَمَنَّيَنَّ أَحَدُكُمُ المَوتَ لضُرٍّ أَصَابَهُ، فَإِنْ كَانَ لابُدَّ فاعلًا، فَليَقُلْ: اللَّهُمَّ أحْيني مَا كَانَتِ الحَيَاةُ خَيرًا لِي، وَتَوفّنِي إِذَا كَانَتِ الوَفَاةُ خَيرًا لي)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Asitamani mauti mmoja wenu kwa sababu ya madhara yaliyompata, akiwa hana budi ila atamani, basi aombe: Ee Rabb, Nihuishe madamu kuishi kuna khayr kwangu, na Unifishe iwapo kufa kuna khayr kwangu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 17

وعن أبي عبد الله خَبَّاب بنِ الأَرتِّ رضي الله عنه قَالَ: شَكَوْنَا إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم وَهُوَ متَوَسِّدٌ بُرْدَةً لَهُ في ظلِّ الكَعْبَةِ، فقُلْنَا: أَلا تَسْتَنْصِرُ لَنَا ألا تَدْعُو لَنا؟ فَقَالَ: ((قَدْ كَانَ مَنْ قَبْلَكُمْ يُؤْخَذُ الرَّجُلُ فَيُحْفَرُ لَهُ في الأرضِ فَيُجْعَلُ فِيهَا، ثُمَّ يُؤْتَى بِالمِنْشَارِ فَيُوضَعُ عَلَى رَأسِهِ فَيُجْعَلُ نصفَينِ، وَيُمْشَطُ بأمْشَاطِ الحَديدِ مَا دُونَ لَحْمِه وَعَظْمِهِ، مَا يَصُدُّهُ ذلِكَ عَنْ دِينِهِ، وَاللهِ لَيُتِمَّنَّ الله هَذَا الأَمْر حَتَّى يَسيرَ الرَّاكبُ مِنْ صَنْعَاءَ إِلَى حَضْرَموتَ لا يَخَافُ إلا اللهَ والذِّئْب عَلَى غَنَمِهِ، ولكنكم تَسْتَعجِلُونَ)). رواه البخاري.

وفي رواية: ((وَهُوَ مُتَوَسِّدٌ بُرْدَةً وَقَدْ لَقِينا مِنَ المُشْرِكِينَ شدَّةً))

Abuu ‘Abdillaah, Khabbaab bin Al-Arrat (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Tulimlalamika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) naye alikuwa ameegemea shuka yake katika kivuli cha Al-Qa’bah. Tukamwambia: “Hutuombei nusra, hutuombei du’ah?” Akatuambia: “Walikuwa waliopita kabla yenu, mtu alikuwa akifukuliwa ardhi na akitiwa humo, halafu ukiletwa msumeno ukiwekwa juu ya kichwa chake, akigawanywa pande mbili, na (mwengine) akichanwa kwa chanuo la chuma akitolewa nyama na mifupa, jambo hilo haliwi kipingamizi katika dini yake. Wa-Allaahi, Allaah Atalikamilisha jambo hili hata msafiri atembee kutoka Sanaa hadi Hadhwramawt hana anachoogopa isipokuwa Allaah, na kumkhofia mbwa mwitu asije akala mbuzi wake; lakini ninyi mnaharaka. [Al-Bukhaariy]

Riwaayah nyingine imesema: “Nae alikuwa ameegemea shuka yake. Kwa hakika tulipata mateso makubwa kutoka kwa mushirikiynah.”

 

 

Hadiyth – 18

وعن ابن مسعودٍ رضي الله عنه قَالَ: لَمَّا كَانَ يَومُ حُنَينٍ آثَرَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم نَاسًا في القسْمَةِ، فَأعْطَى الأقْرَعَ بْنَ حَابسٍ مائَةً مِنَ الإِبِلِ، وَأَعْطَى عُيَيْنَة بْنَ حصن مِثْلَ ذلِكَ، وَأَعطَى نَاسًا مِنْ أشْرافِ العَرَبِ وآثَرَهُمْ يَوْمَئِذٍ في القسْمَةِ. فَقَالَ رَجُلٌ: واللهِ إنَّ هذِهِ قِسْمَةٌ مَا عُدِلَ فِيهَا، وَمَا أُريدَ فيهَا وَجْهُ اللهِ، فَقُلْتُ: وَاللهِ لأُخْبِرَنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، فَأَتَيْتُهُ فَأخْبَرتُهُ بمَا قَالَ، فَتَغَيَّرَ وَجْهُهُ حَتَّى كَانَ كالصِّرْفِ. ثُمَّ قَالَ: ((فَمَنْ يَعْدِلُ إِذَا لم يَعْدِلِ اللهُ وَرسولُهُ؟)) ثُمَّ قَالَ: ((يَرْحَمُ اللهُ مُوسَى قَدْ أُوذِيَ بأكْثَرَ مِنْ هَذَا فَصَبر)). فَقُلْتُ: لا جَرَمَ لا أرْفَعُ إِلَيْه بَعدَهَا حَدِيثًا. مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Siku ya vita vya Hunayn, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwafadhilisha baadhi ya watu katika mgao; akampa Al-Aqra’ bin Haabis ngamia mia moja, akampa Uyaynah bin Hiswn mfano wake, na akawapa watu watukufu wa Kiarabu na akawafadhilisha katika mgao siku hiyo. Mtu mmoja akasema: “Wa-Allaahi huu ni mgao usio na uadilifu! Wala haujakusudiwa radhi ya Allaah!” Nikasema: “Wa-Allaahi nitamueleza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam); nikaenda na kumueleza aliyosema. Uso wake Rasuli  wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ukabadilika hata ukawa mwekundu. Kisha akasema: “Ni nani atakaefanya uadilifu ikiwa Allaah na Rasuli wake Hawakufanya uadilifu?” Halafu akasema: “Allaah Amraham Muwsa, hakika aliudhiwa zaidi ya hivi na akasubiri!” Nikasema: “Kwa hakika sitomueleza tena (mazungumzo kama haya ya kumuudhi).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyh – 19

وعن أنسٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا أَرَادَ الله بعبدِهِ الخَيرَ عَجَّلَ لَهُ العُقُوبَةَ في الدُّنْيا، وَإِذَا أَرَادَ اللهُ بِعَبدِهِ الشَّرَّ أمْسَكَ عَنْهُ بذَنْبِهِ حَتَّى يُوَافِيَ بِهِ يومَ القِيَامَةِ)).

وَقالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ عِظَمَ الجَزَاءِ مَعَ عِظَمِ البَلاَءِ، وَإنَّ اللهَ تَعَالَى إِذَا أَحَبَّ قَوْمًا ابْتَلاَهُمْ، فَمَنْ رَضِيَ فَلَهُ الرِّضَا، وَمَنْ سَخِطَ فَلَهُ السُّخْطُ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن))

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Anapompendea khayr mja Wake, Humuharakishia adhabu duniani. Na anapomtakia shari mja Wake, Huzuia dhambi zake ili Amlipe siku ya Qiyaamah.” 

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Malipo makubwa yapo pamoja na mitihani kubwa. Hakika Allaah Anapowapenda watu, Huwapa mitihani; atakayeridhika, basi atapata Radhi (za Allaah), na atakayechukia, atapata Hasira (za Allaah).” [At-Tirmidhiy, na amesema hadiyth hii ni Hassan]

 

 

Hadiyth – 20

وعن أنسٍ رضي الله عنه قَالَ: كَانَ ابنٌ لأبي طَلْحَةَ رضي الله عنه يَشتَكِي، فَخَرَجَ أبُو طَلْحَةَ، فَقُبِضَ الصَّبيُّ، فَلَمَّا رَجَعَ أَبُو طَلْحَةَ، قَالَ: مَا فَعَلَ ابْنِي؟ قَالَتْ أمُّ سُلَيم وَهِيَ أمُّ الصَّبيِّ: هُوَ أَسْكَنُ مَا كَانَ، فَقَرَّبَتْ إليه العَشَاءَ فَتَعَشَّى، ثُمَّ أَصَابَ منْهَا، فَلَمَّا فَرَغَ، قَالَتْ: وَارُوا الصَّبيَّ فَلَمَّا أَصْبحَ أَبُو طَلْحَةَ أَتَى رسولَ الله صلى الله عليه وسلم فَأخْبَرَهُ، فَقَالَ: ((أعَرَّسْتُمُ اللَّيلَةَ؟)) قَالَ: نَعَمْ، قَالَ: ((اللَّهُمَّ بَارِكْ لَهُمَا))، فَوَلَدَتْ غُلامًا، فَقَالَ لي أَبُو طَلْحَةَ: احْمِلْهُ حَتَّى تَأْتِيَ بِهِ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، وَبَعَثَ مَعَهُ بِتَمَراتٍ، فَقَالَ: ((أَمَعَهُ شَيءٌ؟)) قَالَ: نَعَمْ، تَمَراتٌ، فَأخَذَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم فَمَضَغَهَا، ثُمَّ أَخَذَهَا مِنْ فِيهِ فَجَعَلَهَا في فِيِّ الصَّبيِّ، ثُمَّ حَنَّكَهُ وَسَمَّاهُ عَبدَ الله. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

وفي رواية للبُخَارِيِّ: قَالَ ابنُ عُيَيْنَةَ: فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ الأَنْصارِ: فَرَأيْتُ تِسعَةَ أوْلادٍ كُلُّهُمْ قَدْ قَرَؤُوا القُرْآنَ، يَعْنِي: مِنْ أوْلادِ عَبدِ الله المَولُودِ.

وَفي رواية لمسلمٍ: مَاتَ ابنٌ لأبي طَلْحَةَ مِنْ أمِّ سُلَيمٍ، فَقَالَتْ لأَهْلِهَا: لا تُحَدِّثُوا أَبَا طَلْحَةَ بابْنِهِ حَتَّى أَكُونَ أَنَا أُحَدِّثُهُ، فَجَاءَ فَقَرَّبَتْ إِلَيْه عَشَاءً فَأَكَلَ وَشَرِبَ، ثُمَّ تَصَنَّعَتْ لَهُ أَحْسَنَ مَا كَانَتْ تَصَنَّعُ قَبْلَ ذلِكَ، فَوَقَعَ بِهَا. فَلَمَّا أَنْ رَأَتْ أَنَّهُ قَدْ شَبِعَ وأَصَابَ مِنْهَا، قَالَتْ: يَا أَبَا طَلْحَةَ، أَرَأَيتَ لو أنَّ قَومًا أعارُوا عَارِيَتَهُمْ أَهْلَ بَيتٍ فَطَلَبُوا عَارِيَتَهُمْ، أَلَهُمْ أن يَمْنَعُوهُمْ؟ قَالَ: لا، فَقَالَتْ: فَاحْتَسِبْ ابْنَكَ، قَالَ: فَغَضِبَ، ثُمَّ قَالَ: تَرَكْتِني حَتَّى إِذَا تَلطَّخْتُ، ثُمَّ أخْبَرتني بِابْنِي؟! فانْطَلَقَ حَتَّى أَتَى رسولَ الله صلى الله عليه وسلم فَأخْبَرَهُ بِمَا كَانَ فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((بَارَكَ اللهُ في لَيْلَتِكُمَا))، قَالَ: فَحَمَلَتْ. قَالَ: وَكانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم في سَفَرٍ وَهيَ مَعَهُ، وَكَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا أَتَى المَدِينَةَ مِنْ سَفَرٍ لا يَطْرُقُهَا طُرُوقًا فَدَنَوا مِنَ المَدِينَة، فَضَرَبَهَا المَخَاضُ، فَاحْتَبَسَ عَلَيْهَا أَبُو طَلْحَةَ، وانْطَلَقَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم. قَالَ: يَقُولَ أَبُو طَلْحَةَ: إنَّكَ لَتَعْلَمُ يَا رَبِّ أَنَّهُ يُعْجِبُنِي أنْ أخْرُجَ مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا خَرَجَ وَأَدْخُلَ مَعَهُ إِذَا دَخَلَ وَقَدِ احْتَبَسْتُ بِمَا تَرَى، تَقُولُ أُمُّ سُلَيْمٍ: يَا أَبَا طَلْحَةَ، مَا أَجِدُ الَّذِي كُنْتُ أجدُ انْطَلِقْ، فَانْطَلَقْنَا وَضَرَبَهَا المَخَاضُ حِينَ قَدِمَا فَوَلدَت غُلامًا. فَقَالَتْ لِي أمِّي: يَا أنَسُ، لا يُرْضِعْهُ أحَدٌ حَتَّى تَغْدُو بِهِ عَلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَلَمَّا أصْبَحَ احْتَمَلْتُهُ فَانْطَلَقْتُ بِهِ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم. وَذَكَرَ تَمَامَ الحَدِيثِ.

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Alikuwa mtoto wa Abuu Twalhah akiugua. Abuu Twalahah akapata safari na kusafiri. Yule mtoto akafariki. Abuu Twalhah aliporudi”, aliuliza: “Vipi hali ya mwanangu?” Ummu Sulaym (mama wa mtoto) akamwambia: “Ametulia zaidi ya alivyokuwa.” Akampelekea chakula cha jioni akala, kisha akalala na mkewe (akamjamii). Alipomaliza, Ummu Sulaym akamwambi: “Kamzikeni mtoto.” Abuu Twalhah alipopambaukiwa, alikwenda moja kwa moja mpaka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamueleza yaliyotokea. Akamuuliza: “Usiku mlifanya tendo la ndoa?” Akajibu: “Ndiyo” Akaomba: “Ee Rabb, Wabarikie.” Akazaa mvulana. Abuu Twalhah akaniambia: “Mbebe na umepeleke kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akapeleka na tende kadhaa. Akauliza: “Ana kitu?” Akajibu: “Ndiyo, tende kadhaa.” Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akazichua na kuzitafuna, kisha akachukua zile tende zilizokuwa kinywani mwake akazitia kwenye kinywa cha mtoto, halafu akamsugua na kumpa jina la ’Abdullaah”. [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema: “Ibnu Uyaynah amesema: “Mtu mmoja katika Answaariy akasema: “Nikawaona watoto tisa, wote wamehifadhi Qur-aan.” Yaani watoto wa ‘Abdullaah huyu aliezaliwa.

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema: “Abuu Twalhah alifiwa na mtoto aliyezaa naye kwa Ummu Sulaym akawaambia jamaa zake: “Msimueleze Abuu Twalhah habari ya mwanawe mpaka mimi niwe ndiye nitakaemueleza.” Akaja, akampelekea chakula jioni, akala na akanywa, halafu akajipamba kulikoni alivyojipamba siku zote. Akamjamii. Ummu Sulaym alipoona kuwa Abuu Twalhah ameshiba na amemjamii, alimwambia: “Ee Abuu Twalhah niambie lau watu wameazima kitu kwa watu fulani kisha hao watu wakataka kitu cha kilichoazimwa, je, wao wanahaki ya kuwanyima?” Akajibu: “Hapana.” Akamwambia: Basi taraji thawabu kwa msiba wa mwanao.” Abuu Twalhah akakasirika, na akasema: “Umeniwacha mpaka nimejichafua (kwa tendo la ndoa) halafu unaniambia habari ya mwanangu?” Akaenda kwa Rasuli  wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamueleza mambo yalivyokuwa. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawaombea “Allaah Awabarikie katika usiku wenu.” Ummu Sulaym akabeba ujauzito. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa safarini pamoja na Ummu Sulaym. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapowasili Madiynah akitoka safari, alikuwa haingii usiku. Walipowasili Madiynah Ummu Sulaym alianza kuhisi uchungu wa uzazi, Abuu Twalhah alibaki nyuma, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaendelea na safari. Abuu Twalhah akasema: “Ee Rabb, hakika Unajua ya kuwa mimi hufurahishwa kusafiri pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anaposafiri, na hupenda kurudi pamoja nae anaporudi, na nimezuilika kama Uonavyo.” Ummu Sulaym akasema: “Ee Abuu Twalhah sisikii uchungu tena niliousikia, tuondoke.” Tukaondoka. Akapatwa na uchungu tena wa kuzaa tulipokuwa tumeshawasili Madiynah, akajifungua mtoto wa kiume. Mama yangu akaniambia: “Ee Anas, mtoto huyu asinyonyeshwe na yoyote mpaka uende nae kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).” Kulipopambauka, nilimbeba na kwenda nae kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ...” Akaendelea mpaka mwisho wa Hadiyth.

 

 

Hadiyth – 21

وعن أبي هريرةَ رضي الله عنه أنّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((لَيْسَ الشَّدِيدُ بالصُّرَعَةِ، إنَّمَا الشَدِيدُ الَّذِي يَملكُ نَفْسَهُ عِنْدَ الغَضَبِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwenye nguvu si yule awashindae watu kwa miereka, bali mwenye nguvu ni yule anayemiliki nafsi yake wakati wa hasira.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 22

وعن سُلَيْمَانَ بن صُرَدٍ رضي الله عنه قَالَ: كُنْتُ جالِسًا مَعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، وَرَجُلانِ يَسْتَبَّانِ، وَأَحَدُهُمَا قدِ احْمَرَّ وَجْهُهُ، وانْتَفَخَتْ أوْدَاجُهُ، فَقَالَ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم: ((إنِّي لأَعْلَمُ كَلِمَةً لَوْ قَالَهَا لَذَهَبَ عَنْهُ مَا يَجِدُ، لَوْ قَالَ: أعُوذ باللهِ منَ الشَّيطَانِ الرَّجِيمِ، ذَهَبَ عنْهُ مَا يَجِدُ)). فَقَالُوا لَهُ: إنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((تَعَوّذْ باللهِ مِنَ الشَّيطَانِ الرَّجِيمِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Sulaymaan bin Swurad (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Nilikuwa nimekaa pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na watu wanatukanana, mmoja kati yao uso wake ulikuwa umeiva na mishipa yake ya shingoni imevimba. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Mimi nalijua neno, lau utalisema basi utaondokewa na hasira:

 

أعُوذ باللهِ منَ الشَّيطَانِ الرَّجِيمِ

“Aa’uwdhu biLLaahi mina shaytwaani rajiym (najilinda kwa Allaah dhidi ya shaytwaan aliyelaaniwa), ataondokewa na hasira.” Wakaenda wakamwambia kuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekwambia ujikinge kwa Allaah kutokana na shaytwaan aliyelaaniwa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 23

وعن معاذِ بنِ أَنسٍ رضي الله عنه أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((مَنْ كَظَمَ غَيظًا، وَهُوَ قَادِرٌ عَلَى أنْ يُنْفِذَهُ، دَعَاهُ اللهُ سُبحَانَهُ وَتَعَالى عَلَى رُؤُوسِ الخَلائِقِ يَومَ القِيامَةِ حَتَّى يُخَيِّرَهُ مِنَ الحُورِ العِينِ مَا شَاءَ)). رواه أَبو داود والترمذي، وَقالَ: (حديث حسن)

Mu’aadh bin Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema kuwa: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakaezuia hasira na akawa anaweza kuitekeleza, Allaah Atamuita siku ya Qiyaamah mbele ya halaiki ili Amchagulishe Huwrul ‘ayn anayemtaka.” [Abuu Daawud na At-Tirmidhiy, na amesema hadiyth hii ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 24

وعن أبي هريرةَ رضي الله عنه: أنَّ رَجُلًا قَالَ للنبي صلى الله عليه وسلم: أوصِني. قَالَ: ((لا تَغْضَبْ)) فَرَدَّدَ مِرارًا، قَالَ: ((لاَ تَغْضَبْ)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema kuwa: “Mtu mmoja alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Niusie.” Akamwambia: “Usighadhibike.” Akarudia ombi lake mara nyingi, (Nabiy Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Usighadhibike.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 25

وعن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَا يَزَالُ البَلاَءُ بالمُؤمِنِ وَالمُؤْمِنَةِ في نفسِهِ ووَلَدِهِ وَمَالِهِ حَتَّى يَلْقَى الله تَعَالَى وَمَا عَلَيهِ خَطِيئَةٌ)). رواه الترمذي، وَقالَ: (حديث حسن صحيح)

Abuu Hurayrah (Rahwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli  wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) “Muumin hatowacha kupatwa na balaa katika nafsi yake, watoto wake na mali yake mpaka akutane na Allaah ilihali hana dhambi.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 26

وعن ابْنِ عباسٍ رضي الله عنهما قَالَ: قَدِمَ عُيَيْنَةُ بْنُ حِصْنٍ، فَنَزَلَ عَلَى ابْنِ أخِيهِ الحُرِّ بنِ قَيسٍ، وَكَانَ مِنَ النَّفَرِ الَّذِينَ يُدْنِيهِمْ عُمرُ رضي الله عنه، وَكَانَ القُرَّاءُ أصْحَابَ مَجْلِس عُمَرَ رضي الله عنه وَمُشاوَرَتِهِ كُهُولًا كانُوا أَوْ شُبَّانًا، فَقَالَ عُيَيْنَةُ لابْنِ أخيهِ: يَا ابْنَ أخِي، لَكَ وَجْهٌ عِنْدَ هَذَا الأمِيرِ فَاسْتَأذِنْ لِي عَلَيهِ، فاسْتَأذَن فَأذِنَ لَهُ عُمَرُ. فَلَمَّا دَخَلَ قَالَ: هِي يَا ابنَ الخَطَّابِ، فَواللهِ مَا تُعْطِينَا الْجَزْلَ وَلا تَحْكُمُ فِينَا بالعَدْلِ. فَغَضِبَ عُمَرُ رضي الله عنه حَتَّى هَمَّ أنْ يُوقِعَ بِهِ. فَقَالَ لَهُ الحُرُّ: يَا أميرَ المُؤْمِنينَ، إنَّ الله تَعَالَى قَالَ لِنَبيِّهِ صلى الله عليه وسلم: {خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ} [الأعراف: 199] وَإنَّ هَذَا مِنَ الجَاهِلِينَ، واللهِ مَا جَاوَزَهاَ عُمَرُ حِينَ تَلاَهَا، وكَانَ وَقَّافًا عِنْدَ كِتَابِ اللهِ تَعَالَى. رواه البخاري

‘Abdullaah ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: “’Uyaynah bin Hiswn alikuja kutoka safari, akashukia kwa mtoto wa dada yake Al-Hurri bin Qays, naye alikuwa ni katika watu ambao ‘Umar alikuwa akiwakurubisha karibu naye, wanavyuoni walikuwa ndio wa majilisi ya ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) na katika ushauri wake; wawe ni wazee au vijana. ‘Uyaynah akamwambia mtoto wa dada yake: “Ee mtoto wa dada yangu, wewe una nafasi kwa huyu Amiyr, basi niombee idhini (niingie kwake).” Akamuombea idhini, ‘Umar akamruhusu. Alipoingia alisema: “Hii! Ee mwana wa Khattwaab! Wa-Allaahi hutupatii vitu vingi, wala huhukumu kwa audilifu kati yetu.” ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akakasirika hata akataka kumuadhibu. Al-Hurru akamwambia: “Ee Amiyr wa Waumini, hakika Allaah Alimwambia Nabiy Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)

خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ

“Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili” [Al-A’raaf: 199]

Hakika huyu ni katika majahili. Basi wa-Allaahi ‘Umar hakumfanya kitu Al-Hurru alipoisoma Aayah hii. Alikuwa ‘Umar amesimama wima katika kitabu cha Allaah.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 26

وعن ابن مسعود رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّهَا سَتَكونُ بَعْدِي أثَرَةٌ وأُمُورٌ تُنْكِرُونَها!)) قَالُوا: يَا رَسُول الله، فَمَّا تَأْمُرُنا؟ قَالَ: ((تُؤَدُّونَ الْحَقَّ الَّذِي عَلَيْكُمْ، وَتَسأَلُونَ الله الَّذِي لَكُمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

 ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika baada yangu kutakuwepo ubinafsi na mambo ambayo hamtokubaliyana nayo.” Maswahaba wakauliza: “Yaa Rasula-Allaah, kwahiyo unatuamrisha tufanye nini?” Akawaambia: “Mutaitekeleza haki inayowapasa, na mumuombe Allaah ambacho ni chenu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 27

  وعن أبي يحيى أُسَيْد بن حُضَير رضي الله عنه: أنَّ رَجُلًا مِنَ الأنْصارِ قَالَ: يَا رسولَ الله، ألا تَسْتَعْمِلُني كَمَا اسْتَعْمَلْتَ فُلانًا؟ فَقَالَ: ((إنكُمْ سَتَلْقَونَ بَعْدِي أَثَرَةً فَاصْبِرُوا حَتَّى تَلْقَوني عَلَى الحَوْضِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Yahyaa, Usayd bin Hudhwayr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Mtu mmoja katika Answaari alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Yaa Rasula-Allaah, mbona hunifanyi kuwa hakimu kama ulivyomfanya fulani?” Akamwambia: “Hakika baada yangu mtaona ubinasfi, basi subirini mpaka mkutane nami katika hodhi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 28

 وعن أبي إبراهيم عبدِ الله بن أبي أوفى رضي الله عنهما: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم في بعْضِ أيامِهِ التي لَقِيَ فِيهَا العَدُوَّ، انْتَظَرَ حَتَّى إِذَا مالَتِ الشَّمْسُ قَامَ فيهمْ، فَقَالَ: ((يَا أيُّهَا النَّاسُ، لا تَتَمَنَّوا لِقَاءَ العَدُوِّ، وَاسْأَلُوا الله العَافِيَةَ، فَإِذَا لقيتُمُوهُمْ فَاصْبرُوا، وَاعْلَمُوا أنّ الجَنَّةَ تَحْتَ ظِلالِ السُّيوفِ)). ثُمَّ قَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((اللَّهُمَّ مُنْزِلَ الكِتَابِ، وَمُجْرِيَ السَّحَابِ، وَهَازِمَ الأحْزَابِ، اهْزِمْهُمْ وَانصُرْنَا عَلَيْهمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Ibraahiym ‘Abdillaah bin Abiy Awfa (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika baadhi ya siku alizokutana na adui, alingoja hadi jua lilipopinduka, akasimama na akawaeleza: “Enyi watu, msitamani kukutana na adui, muombeni Allaah al-‘afiyah (salama), na mtakapo kutana nao, subirini, na fahamuni kuwa Jannah ipo chini ya vivuli vya panga.” Halafu Nabiy  (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaomba: “Ee Rabb Mteremsha Kitabu, Mwenye kuendesha mawingu, Mwenye kuyashinda makundi, Washinde na Utunusuru.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

004-Riyaadhw Asw Swaalihiyn: Mlango Wa Ukweli

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الصدق

004 – Mlango Wa Ukweli

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَكُونُوا مَعَ الصَّادِقِينَ

Enyi walioamini! Mcheni Allaah na kuweni pamoja na wakweli. [At-Tawbah: 119]

 وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ

Na wanaume wakweli na wanawake wakweli. [Al-Ahzaab: 33]

فَلَوْ صَدَقُوا اللَّـهَ لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ

Basi kama wangekuwa wakweli kwa Allaah, bila shaka ingalikuwa kheri kwao. [Muhammad: 21]

 

Hadiyth – 1

 

عن ابن مسعود رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((إنَّ الصِّدقَ يَهْدِي إِلَى البرِّ، وإنَّ البِرَّ يَهدِي إِلَى الجَنَّةِ، وإنَّ الرَّجُلَ لَيَصدُقُ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللهِ صِدِّيقًا. وَإِنَّ الكَذِبَ يَهْدِي إِلَى الفُجُورِ، وَإِنَّ الفُجُورَ يَهدِي إِلَى النَّارِ، وَإِنَّ الرَّجُلَ لَيَكْذِبُ حَتَّى يُكتَبَ عِنْدَ الله كَذَّابًا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa amesema: “Hakika ukweli unaongoza katika wema, na hakika wema unaongoza Jannah na mtu ataendelea kusema ukweli mpaka aandikiwe mbele ya Allaah kuwa ni mkweli. Na hakika uongo unaongoza katika uovu, na hakika uovu unapeleka motoni, na mtu ataendelea kusema uongo mpaka aandikiwe mbele ya Allaah kuwa ni muongo,” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

 

عن أبي محمد الحسن بنِ عليِّ بن أبي طالب رضي الله عنهما قَالَ: حَفظْتُ مِنْ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((دَعْ مَا يَرِيبُكَ إِلَى مَا لا يَرِيبُكَ؛ فإنَّ الصِّدقَ طُمَأنِينَةٌ، وَالكَذِبَ رِيبَةٌ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث صحيح))

Abuu Muhammad, Al-Hasan bin ‘Alliy bin Abiy Twaalib (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nimehifadhi kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) maneno haya: “Acha linalokutia shaka ufuate lisilokutia shaka; hakika ukweli ni utulivu na uongo ni mashaka.” [At-Tirmidhiy, na amesema Hadiyth  hii ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 3

عن أبي سفيانَ صَخرِ بنِ حربٍ رضي الله عنه في حديثه الطويلِ في قصةِ هِرَقْلَ، قَالَ هِرقلُ: فَمَاذَا يَأَمُرُكُمْ؟ يعني: النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ أبو سفيانَ: قُلْتُ: يقولُ: ((اعْبُدُوا اللهَ وَحدَهُ لا تُشْرِكوُا بِهِ شَيئًا، وَاتْرُكُوا مَا يَقُولُ آبَاؤُكُمْ، ويَأْمُرُنَا بالصَلاةِ، وَالصِّدْقِ، والعَفَافِ، وَالصِّلَةِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Sufyaan, Swakhr bin Harb (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia katika Hadiyth yake ndefu katika kisa cha Hiraqli (Heraclius).  Hiraqli akauliza: Anawaamrisha nini? Yaani Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikasema: Anatuambia: “Muabuduni Allaah Mmoja Pekee wala msimshirikishe kwa chochote. Na muwache walivyokuwa wakiabudu baba zenu.” Na akituamuru kuswali, kusema kweli, kujiepusha na machafu na kuunga undugu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

عن أبي ثابت، وقيل: أبي سعيد، وقيل: أبي الوليد، سهل بن حُنَيْفٍ وَهُوَ بدريٌّ رضي الله عنه: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ سَأَلَ الله تَعَالَى الشَّهَادَةَ بِصِدْقٍ بَلَّغَهُ اللهُ مَنَازِلَ الشُّهَدَاءِ وَإِنْ مَاتَ عَلَى فِرَاشِهِ)). رواه مسلم

Abuu Thaabit, na inasemekana: Abiy Sa’iyd, na inasemekana: Abil Waliyd, Sahl bin Hunayf (Radhwiya Allaahu ‘anhu) naye ni mpiganaji wa vita vya Badr amesimulia kuwa: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayemuomba Allaah kufa kifo cha shaahid kwa ukweli, Allaah Atamfikisha daraja za Mashuhadaa hata akifa kitandani mwake.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((غَزَا نبيٌّ مِنَ الأنْبِياءِ صَلَوَاتُ اللهِ وَسَلاَمُهُ عَلَيْهمْ فَقَالَ لِقَومهِ: لاَ يَتْبَعَنِّي رَجُلٌ مَلَكَ بُضْعَ امْرَأةٍ وَهُوَ يُريدُ أنْ يَبْنِي بِهَا وَلَمَّا يَبْنِ بِهَا، وَلا أحَدٌ بَنَى بُيُوتًا لَمْ يَرْفَعْ سُقُوفَهَا، وَلا أحَدٌ اشْتَرَى غَنَمًا أَوْ خَلِفَاتٍ وَهُوَ يَنْتَظِرُ أَوْلادَها. فَغَزا فَدَنَا مِنَ القَرْيَةِ صَلاةَ العَصْرِ أَوْ قَريبًا مِنْ ذلِكَ، فَقَالَ لِلشَّمْسِ: إِنَّكِ مَأمُورَةٌ وَأنَا مَأمُورٌ، اللَّهُمَّ احْبِسْهَا عَلَيْنَا، فَحُبِسَتْ حَتَّى فَتَحَ اللهُ عَلَيهِ، فَجَمَعَ الغَنَائِمَ فَجَاءتْ- يعني النَّارَ- لِتَأكُلَهَا فَلَمْ تَطعَمْها، فَقَالَ: إنَّ فِيكُمْ غُلُولًا، فَلْيُبايعْنِي مِنْ كُلِّ قَبيلةٍ رَجُلٌ، فَلَزِقَتْ يد رجل بِيَدِهِ فَقَالَ: فِيكُمُ الغُلُولُ فلتبايعني قبيلتك، فلزقت يد رجلين أو ثلاثة بيده، فقال: فيكم الغلول، فَجَاؤُوا بِرَأْس مثل رأس بَقَرَةٍ مِنَ الذَّهَبِ، فَوَضَعَهَا فَجاءت النَّارُ فَأكَلَتْها. فَلَمْ تَحلَّ الغَنَائِمُ لأحَدٍ قَبْلَنَا، ثُمَّ أحَلَّ الله لَنَا الغَنَائِمَ لَمَّا رَأَى ضَعْفَنا وَعَجْزَنَا فَأحَلَّهَا لَنَا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna Nabiy mmoja alitaka kwenda kupigana jihaad, akawaambia qaumu yake: “Yeyote aliyeoa na hajamleta mkewe kwake  lakini ana niyyah ya kufanya hivyo au yule aliyejenga kuta za nyumba lakini hajati paa, au yule aliyenunua mbuzi au ngami wenye mimba anangojea wazae,  basi anifuate kwa kujiunga katika jihaad.”  Baada ya hapo akaanza kuelekea na mujaahidina wake katika mji aliokusudia. Alipofika hapo karibu na mji karibu na Swalaah ya Alasiri, aliliambia jua: “Hakika wewe unafuata amri za Allaah, name nimeamrishwa, Ee Rabb, lizuie kwa ajili yetu.” Likazuiliwa mpaka Allaah Alipompa ushindi. Akazikusanya ghanima, moto ukaja ili upate kuziteketeza, lakini haukuweza kuziteketeza. Akawaambia: “Hakika kati yenu kuna aliyefanya khiyana, kwa hiyo katika kila kabila anbai (afunge kiapo cha ahadi) mtu mmoja.” Mkono wa mtu mmoja ukanata katika mkono wake. Akawaambia: “Kwenu kuna khiyana, kwa hivyo kabila lako lote linibai” Mikono ya watu wawili au watatu ikanata kwenye mkono wake.” Akawaambia: “Kwenu kuna khiyana,” Wakaleta dhahabu mfano wa kichwa cha ng’ombe. Yule Nabiy akaiweka, moto ukaja na ukaiteketeza. Ghanima haikuhalalishwa kwa yoyote kabla yetu. Kisha Allaah Akatuhalalishia ghanima Alipoona udhaifu wetu na ajizi yetu (na kukosa hila), Akatuhalalishia.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyh – 6

عن أبي خالد حَكيمِ بنِ حزامٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((البَيِّعَانِ بالخِيَار مَا لَمْ يَتَفَرَّقَا، فَإنْ صَدَقا وَبيَّنَا بُوركَ لَهُمَا في بيعِهمَا، وإنْ كَذَبَا وَكَتَمَا مُحِقَتْ بركَةُ بَيعِهِما)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Khaalid, Hakiym bin Hizaam (Radhwiya ALlaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amasema: “Wenye kuuziana wapo katika khiyari kabla hawajaachana. Watakaposema kweli na wakabainisha (kasoro au upungufu wa bidhaa), watabarikiwa katika biashara yao. Na wakificha na wakasema uongo; basi itaondolewa baraka ya biashara yao.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

005-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuchunga (Kumukhofu Allaah Kwa Siri Na Dhahiri)

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب المراقبة

005 – Mlango Wa Kuchunga (Kukmhofu Allaah Kwa Siri Na Dhahiri)

 

Alhidaaya.com

 

 

  قَالَ الله تَعَالَى:

الَّذِي يَرَاكَ حِينَ تَقُومُ

Ambaye Anakuona wakati unaposimama. [Ash-Shu’araa: 218]

 

وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ

Naye Yu Pamoja nanyi (kwa ujuzi Wake) popote mlipo. [Al-Hadiyd: 4]

 

هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ

Je, hakuna katika hayo kiapo kwa mwenye welekevu (akawa na taqwa)? [Al-Fajr: 5]

 

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ

Hakika Rabb wako bila shaka Yu tayari Awavizia. [Al-Fajr: 14]

 

يَعْلَمُ خَائِنَةَ الْأَعْيُنِ وَمَا تُخْفِي الصُّدُورُ

 (Allaah) Anajua khiyana za macho na yale yanayoficha vifua. [Ghaafir: 19]

 

 

Hadiyth – 1

عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه قَالَ: بَيْنَما نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَومٍ، إذْ طَلَعَ عَلَينا رَجُلٌ شَديدُ بَياضِ الثِّيابِ، شَديدُ سَوَادِ الشَّعْرِ، لا يُرَى عَلَيهِ أثَرُ السَّفَرِ، وَلا يَعْرِفُهُ مِنَّا أحَدٌ، حَتَّى جَلَسَ إِلَى النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، فَأَسْنَدَ رُكْبَتَيهِ إِلَى رُكْبتَيهِ، وَوَضعَ كَفَّيهِ عَلَى فَخِذَيهِ.

وَقالَ: يَا مُحَمَّدُ، أخْبرني عَنِ الإسلامِ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((الإسلامُ: أنْ تَشْهدَ أنْ لاَّ إلهَ إلاَّ الله وَأنَّ مُحمَّدًا رسولُ الله، وتُقيمَ الصَّلاةَ، وَتُؤتِيَ الزَّكَاةَ، وَتَصومَ رَمَضَانَ، وَتَحُجَّ البَيتَ إن اسْتَطَعْتَ إِلَيْهِ سَبيلًا)). قَالَ: صَدَقْتَ. فَعَجِبْنَا لَهُ يَسْأَلُهُ وَيُصَدِّقهُ!

قَالَ: فَأَخْبرنِي عَنِ الإِيمَانِ. قَالَ: ((أنْ تُؤمِنَ باللهِ، وَمَلائِكَتِهِ، وَكُتُبهِ، وَرُسُلِهِ، وَاليَوْمِ الآخِر، وتُؤْمِنَ بالقَدَرِ خَيرِهِ وَشَرِّهِ)). قَالَ: صَدقت. قَالَ: فأَخْبرني عَنِ الإحْسَانِ. قَالَ: ((أنْ تَعْبُدَ اللهَ كَأنَّكَ تَرَاهُ فإنْ لَمْ تَكُنْ تَرَاهُ فإنَّهُ يَرَاكَ)).

قَالَ: فَأَخْبِرني عَنِ السَّاعَةِ. قَالَ: ((مَا المَسْؤُولُ عَنْهَا بأعْلَمَ مِنَ السَّائِلِ)). قَالَ: فأخبِرني عَنْ أمَاراتِهَا. قَالَ: ((أنْ تَلِدَ الأَمَةُ رَبَّتَهَا، وأنْ تَرَى الحُفَاةَ العُرَاةَ العَالَةَ رِعَاءَ الشَّاءِ يَتَطَاوَلُونَ في البُنْيَانِ)).

ثُمَّ انْطَلقَ فَلَبِثْتُ مَلِيًّا، ثُمَّ قَالَ: ((يَا عُمَرُ، أَتَدْري مَنِ السَّائِلُ؟)) قُلْتُ: اللهُ ورسُولُهُ أعْلَمُ. قَالَ: ((فإنَّهُ جِبْريلُ أَتَاكُمْ يعْلِّمُكُمْ دِينَكُمْ)). رواه مسلم

‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Siku moja tulikuwa tumekaa mbele ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kwa ghafla akatutokea mtu mmoja ambaye nguo zake zilikuwa nyeupe pepe na nywele zake zilikuwa nyeusi sana; hakuwa na alama ya machofu ya safari na wala hapakuwa na hata mmoja katika sisi aliyemtambua. Alienda akakaa karibu na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaweka magoti yake karibu na magoti yake (Rasuli) na akaweka viganja vyake juu ya mapaja yake kisha akasema; Ee Muhammad! Niambie kuhusu Uislaamu.  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:  “Uislamu ni kukiri kuwa hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa  Allaah, na Muhammad ni Rasuli wake, kusimamisha Swalaah, kutoa Zakaah, kufunga swawm Ramadhwaan na kwenda kuhiji (Makkah) ukiweza.” (Akasema yule mtu yaani Jibriyl): “Umesema kweli.” Tulipigwa na mshangao kwa kumuuliza  kwake Rasuli na kumsadikisha.  Na akasema tena: Niambie kuhusu Iymaan.  Akasema: “Ni kumwamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Rasuli Wake na siku ya Qiyaamah, na  kuamini Qadar  (majaaliwa ya Allaah) ya kheri zake na shari zake.” (Akasema Jibriyl): “Umesema kweli.”. Akasema: “Hebu nielezee kuhusu Ihsaan.”  Akasema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Ni kumuabudu Allaah kama vile unamuona na kama humuoni basi Yeye Anakuona.”  Akasema (Jibriyl): “Niambie    kuhusu Qiyaamah.”  Akajibu Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Muulizwaji si mjuzi kama asivyo vilevile Muulizaji.” Kisha akamwambia: “Nijulishe alama zake.”: Akajibu Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Kijakazi atazaa bibi yake, na utaona wachunga wenda miguu chini, wenda uchi (wasio na uwezo wa kumiliki hata mavazi), mafukara (wasiokuwa hata na sehemu ya kuishi kwa umaskini) wakishindana kujenga majumba ya fahari.” Kisha akaondoka (Jibriyl) na nilitulia kidogo (nikitafakari). Kisha akasema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): "Ee 'Umar! Je, unamjua ni nani yule aliyekuwa akiuliza? Nikasema: Allaah na Rasuli wake wanajua zaidi.  Akasema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Ni Jibriyl, alikuja kuwafundisha dini yenu.” [Muslim]

 

Hadiyth – 2

عن أبي ذر جُنْدُب بنِ جُنادَةَ وأبي عبدِ الرحمنِ معاذِ بنِ جبلٍ رضي الله عنهما عن رسولِ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((اتَّقِ الله حَيْثُمَا كُنْتَ وَأتْبعِ السَّيِّئَةَ الحَسَنَةَ تَمْحُهَا، وَخَالِقِ النَّاسَ بِخُلُقٍ حَسَنٍ)). رواه الترمذي، وَقالَ: (حديث حسن)

Abuu Dharr, Jundub bin Junaadah na Abuu ‘Abdir-Rahmaan Mu’aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) wamehadithia kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mche Allaah popote ulipo, ufuatishe tendo jema baada ya tendo baya ili lifute, na utangamane na watu kwa tabia njema.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan]

 

Hadiyth – 3

عن ابنِ عباسٍ رضي الله عنهما، قَالَ: كنت خلف النَّبيّ صلى الله عليه وسلم يومًا، فَقَالَ: ((يَا غُلامُ، إنِّي أعلّمُكَ كَلِمَاتٍ: احْفَظِ اللهَ يَحْفَظْكَ، احْفَظِ اللهَ تَجِدْهُ تُجَاهَكَ، إِذَا سَألْتَ فَاسأَلِ الله، وإِذَا اسْتَعَنْتَ فَاسْتَعِنْ باللهِ. وَاعْلَمْ: أنَّ الأُمَّةَ لَوْ اجْتَمَعَتْ عَلَى أنْ يَنْفَعُوكَ بِشَيءٍ لَمْ يَنْفَعُوكَ إلا بِشَيءٍ قَدْ كَتَبهُ اللهُ لَكَ، وَإِن اجتَمَعُوا عَلَى أنْ يَضُرُّوكَ بِشَيءٍ لَمْ يَضُرُّوكَ إلا بِشَيءٍ قَدْ كَتَبَهُ اللهُ عَلَيْكَ، رُفِعَتِ الأَقْلاَمُ وَجَفَّتِ الصُّحفُ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن صحيح)).

وفي رواية غيرِ الترمذي: ((احْفَظِ الله تَجِدْهُ أَمَامَكَ، تَعرَّفْ إِلَى اللهِ في الرَّخَاءِ يَعْرِفكَ في الشِّدَّةِ، وَاعْلَمْ: أنَّ مَا أَخْطَأكَ لَمْ يَكُنْ لِيُصِيبكَ، وَمَا أصَابَكَ لَمْ يَكُنْ لِيُخْطِئَكَ، وَاعْلَمْ: أنَّ النَّصْرَ مَعَ الصَّبْرِ، وَأَنَّ الفَرَجَ مَعَ الكَرْبِ، وَأَنَّ مَعَ العُسْرِ يُسْرًا))

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Siku moja nilikuwa nyuma ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) (juu ya mnyama). Akaniambia: “Ee kijana, mimi nitakufundisha maneno: Mhifadhi Allaah Naye Atakuhifadhi. Mhifadhi Allaah utamkuta yupo mbele yako. Unapoomba, muombe Allaah. Unapotaka msaada, mtake Allaah. Fahamu kuwa, lau ummah (wote) utajikusanya ili wakunufaishe kwa jambo, basi hawataweza kukunufaisha ila kwa jambo Alilokuandikia Allaah; na wakijumuika ili wakudhuru kwa jambo, hawataweza kukudhuru ila kwa jambo Alilokuandikia Allaah. Kalamu zimeshasimama na karatasi zimeshakauka.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

Riwaayah nyingine isiyokuwa ya At-Tirmidhiy imesema: “Mhifadhi Allaah utamkuta Yupo mbele yako. Mjue Allaah katika raha Naye Atakujua katika shida. Ujue kuwa, lililokukosa halikuwa ni lenye kukupata, na lililokusibu halikuwa ni lenye kukukosa. Ujue kuwa nusura ipo pamoja na subira, faraja ipo pamoja na dhiki, na kwenye uzito kuna wepesi.”

 

Hadiyth – 4

عن أنسٍ رضي الله عنه قَالَ: إِنَّكُمْ لَتعمَلُونَ أعْمَالًا هي أدَقُّ في أعيُنِكُمْ مِنَ الشَّعْرِ، كُنَّا نَعُدُّهَا عَلَى عَهْدِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم مِنَ المُوبِقاتِ. رواه البخاري

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Kwa hakika ninyi mnafanya matendo ambayo machoni mwenu (mnayaona kuwa) ni madogo kulikoni unywele. Kwa hakika matendo hayo tulikuwa tukiyahesabu wakati wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni matendo yanayoangamiza.” [Al-Bukhaariy]

 

Hadiyth – 5

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّ الله تَعَالَى يَغَارُ، وَغَيرَةُ الله تَعَالَى، أنْ يَأتِيَ المَرْءُ مَا حَرَّمَ الله عَلَيهِ)). متفق عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Hufanya ghera, na ghera ya Allaah ni mtu kutenda Aliyoharamisha Allaah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hadiyth – 6

 عن أبي هريرةَ رضي الله عنه: أنَّه سَمِعَ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، يقُولُ: ((إنَّ ثَلاثَةً مِنْ بَني إِسْرَائِيلَ: أبْرَصَ، وَأَقْرَعَ، وَأَعْمَى، أَرَادَ اللهُ أنْ يَبْتَليَهُمْ فَبَعَثَ إِليْهمْ مَلَكًا، فَأَتَى الأَبْرَصَ، فَقَالَ: أَيُّ شَيءٍ أَحَبُّ إلَيْكَ؟ قَالَ: لَوْنٌ حَسنٌ، وَجِلدٌ حَسَنٌ، وَيَذْهبُ عَنِّي الَّذِي قَدْ قَذِرَنِي النَّاسُ؛ فَمَسَحَهُ فَذَهَبَ عَنْهُ قَذَرُهُ وَأُعْطِيَ لَونًا حَسنًا وجِلْدًا حَسَنًا. فَقَالَ: فَأيُّ المَالِ أَحَبُّ إِليكَ؟ قَالَ: الإِبلُ- أَوْ قالَ: البَقَرُ شكَّ الرَّاوي- فَأُعطِيَ نَاقَةً عُشَرَاءَ، فَقَالَ: بَاركَ الله لَكَ فِيهَا. فَأَتَى الأَقْرَعَ، فَقَالَ: أَيُّ شَيءٍ أَحَبُّ إلَيْكَ؟ قَالَ: شَعْرٌ حَسَنٌ، وَيَذْهَبُ عَنِّي هَذَا الَّذِي قَذِرَني النَّاسُ؛ فَمَسَحَهُ فَذَهبَ عَنْهُ وأُعْطِيَ شَعرًا حَسَنًا. قالَ: فَأَيُّ المَالِ أَحَبُّ إِليْكَ؟ قَالَ: البَقَرُ، فَأُعْطِيَ بَقَرَةً حَامِلًا، وَقالَ: بَارَكَ الله لَكَ فِيهَا.

فَأَتَى الأَعْمَى، فَقَالَ: أَيُّ شَيءٍ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ: أَنْ يَرُدَّ الله إِلَيَّ بَصَرِي فَأُبْصِرُ بِهِ النَّاسَ؛ فَمَسَحَهُ فَرَدَّ اللهُ إِلَيْهِ بَصَرهُ. قَالَ: فَأَيُّ المَالِ أَحَبُّ إِليْكَ؟ قَالَ: الغَنَمُ، فَأُعْطِيَ شَاةً والدًا، فَأَنْتَجَ هذَانِ وَوَلَّدَ هَذَا، فَكانَ لِهذَا وَادٍ مِنَ الإِبلِ، وَلِهذَا وَادٍ مِنَ البَقَرِ، وَلِهَذَا وَادٍ مِنَ الغَنَمِ.

ثُمَّ إنَّهُ أَتَى الأَبْرَصَ في صُورَتِهِ وَهَيئَتِهِ، فَقَالَ: رَجلٌ مِسْكينٌ قَدِ انقَطَعَتْ بِيَ الحِبَالُ في سَفَري فَلا بَلاغَ لِيَ اليَومَ إلا باللهِ ثُمَّ بِكَ، أَسْأَلُكَ بِالَّذي أعْطَاكَ اللَّونَ الحَسَنَ، والجِلْدَ الحَسَنَ، وَالمَالَ، بَعِيرًا أَتَبَلَّغُ بِهِ في سَفَري، فَقَالَ: الحُقُوقُ كثِيرةٌ. فَقَالَ: كأنِّي اعْرِفُكَ، أَلَمْ تَكُنْ أَبْرَصَ يَقْذَرُكَ النَّاسُ فقيرًا فأعْطَاكَ اللهُ!؟ فَقَالَ: إِنَّمَا وَرِثْتُ هَذَا المالَ كَابِرًا عَنْ كَابِرٍ، فَقَالَ: إنْ كُنْتَ كَاذِبًا فَصَيَّرَكَ الله إِلَى مَا كُنْتَ.

وَأَتَى الأَقْرَعَ في صُورَتِهِ وَهَيْئَتِهِ، فَقَالَ لَهُ مِثْلَ مَا قَالَ لِهَذا، وَرَدَّ عَلَيهِ مِثْلَ مَا رَدَّ هَذَا، فَقَالَ: إنْ كُنْتَ كَاذِبًا فَصَيَّرَكَ اللهُ إِلَى مَا كُنْتَ.

وَأَتَى الأَعْمَى في صُورَتِهِ وَهَيْئَتِهِ، فَقَالَ: رَجُلٌ مِسْكينٌ وابنُ سَبيلٍ انْقَطَعتْ بِيَ الحِبَالُ في سَفَرِي، فَلا بَلاَغَ لِيَ اليَومَ إلا بِاللهِ ثُمَّ بِكَ، أَسأَلُكَ بالَّذِي رَدَّ عَلَيْكَ بَصَركَ شَاةً أَتَبَلَّغُ بِهَا في سَفري؟ فَقَالَ: قَدْ كُنْتُ أعمَى فَرَدَّ اللهُ إِلَيَّ بَصَرِي فَخُذْ مَا شِئْتَ وَدَعْ مَا شِئْتَ فَوَ اللهِ لا أجْهَدُكَ اليَومَ بِشَيءٍ أخَذْتَهُ للهِ- عز وجل-. فَقَالَ: أمْسِكْ مالَكَ فِإنَّمَا ابْتُلِيتُمْ. فَقَدْ رضي الله عنك، وَسَخِطَ عَلَى صَاحِبَيكَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amemsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Allaah Alitaka kuwapa mtihani watu watatu katika wana Israaiyl: Mwenye ukoma, mwenye kunyonyoka nywele (kipara) na kipofu. Akawapelekea Malaaika. Akamwendea mwenye ukoma. Akamuuliza: “Kitu gani unachokipenda zaidi?” Akamjibu: “Napenda niwe na rangi nzuri, ngozi nzuri na niondokewe na hali hii ambayo watu wananidharau.” Yule Malaaika akampangusa, ukoma ukamuondokea na akapewa rangi na ngozi nzuri. Akamuuliza: “Unapenda mali gani?”  Akajibu: “Ngamia.”. Au alisema: Ng’ombe, (mpokezi amekuwa na mashaka kama ni ng’ombe au ngamia). Akapewa ngamia mwenye mimba (karibu na kuzaa). Akamuombea: “Allaah Akubariki”.

Akamuendea mwenye upara. Akamuuliza: “Kitu gani unachokipenda zaidi?” Akamjibu: “Nywele nzuri, na niondokewe na hali hii ambayo watu wananidharau.” Akampangusa, akaondokewa na upara na akawa na nywele nzuri. Akamuuliza: “Unapenda mali gani?” Akamjibu: “Ng’ombe.” Akapewa ng’ombe mwenye mimba. Akamuombea: “Allaah Akubarikie.” Akamuendea kipofu akamuuliza: “Kitu gani unachonapenda zaidi?” Akamjibu: “Napenda Allaah Anirudishie macho yangu ili nione watu.” Akampangusa. Allaah Akamrudishia macho yake. Akamuuliza. “Unapenda mali gani?” Akamjibu: “Mbuzi.” Akapewa mbuzi mwenye mtoto. Wale wenye ngamia na ng’ombe wanyama wao wakazaa, na mwenye mbuzi nae akazalisha. Mmoja wao akawa na bonde lililojaa ngamia, na mwengine ana bonde lililojaa ng’ombe na huyu ana bonde lililojaa mbuzi. Kisha, akamuendea mwenye ukoma katika sura yake na umbile lake (kama siku ile aliyokutana nae kwanza). Akamwambia: “Mimi ni masikini, rizki imenikatikia safarini, sina njia leo, (sina matumaini) isipokuwa kwa Allaah kisha kwako. Nakuomba kwa Ambaye Amekupa rangi nzuri, ngozi nzuri na mali, unipe ngamia ili nimalize safari yangu.” Akamjibu: “Haki zipo nyingi (nina majukumu mengi, kwa hiyo siwezi kukusaidia). Akamwambia: “Kana kwamba nakujua, si ulikuwa na ukoma na watu wanakudharau na ulikuwa fukara, na Allaah Akakupa?” Akamwambia: “Mali hii nimerithi kutoka kwa mababu na mababu.” Akamwambia: “Ikiwa unasema uongo, Allaah Akurudishe kama ulivyokuwa.” Akamuendea mwenye upara katika sura yake na umbile lake (kama siku ile aliyokutana naye kwa mara ya kwanza). Akamwambia kama alivyomwambia wa mwanzo. Naye akamrudishia jibu kama alivyomrudishia wa mwanzo. Akamwambia: “Ikiwa unasema uongo, Allaah Akurudishe kama ulivyokuwa.” Akamuendea kipofu katika sura yake na umbile lake (kama siku ile aliyokutana naye kwa mara ya kwanza). Akamwambia: “Mimi ni masikini, rizki imenikatikia safarini, sina njia leo, (sina matumaini) isipokuwa kwa Allaah kisha kwako. Nakuomba kwa Ambaye Amekurudishia macho yako, unipe mbuzi ili nimalizie safari yangu.” Akamjibu: “Kwa hakika nilikuwa kipofu, Allaah Akanirudishia kuona kwangu. Chukua unachotaka, wacha unachotaka. Wa-Allaahi sikufanyia uzito kwa kitu ulichokichukua kwa Ajili ya Allaah.” Akamwambia “Zuia mali yako. Hakika mumepewa mtihani. Hakika Allaah Ameshakuridhia na Amewaghadhibikia wenzio wawili.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hadiyth – 7

عن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مِنْ حُسْنِ إسْلامِ المَرْءِ تَرْكُهُ مَا لا يَعْنِيهِ)). حديث حسن. رواه الترمذي وغيرُه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Katika uzuri wa Uislaamu wa mtu, ni kuacha lisilomuhusu.” [Hadiyth hii ni Hasan. At-Tirmidhiy na wengine]

 

Hadiyth – 8

عن عُمَرَ رضي الله عنه عَنِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((لا يُسْأَلُ الرَّجُلُ فِيمَ ضَرَبَ امْرَأَتَهُ)). رواه أبو داود وغيره

‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mtu haulizwi sababu ya kumpiga mkewe.” [Abuu Dawuud na wengineo]

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

006-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Taqwa – Kumkhofu Allaah

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 باب التقوى

006 – Mlango Wa Taqwa – Kumkhofu Allaah

 

Alhidaaya.com

 

 

يَقُولُ اللهُ تَعَالَى:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ

Enyi walioamini! Mcheni Allaah kama apasavyo kuogopwa na wala msife isipokuwa nyinyi (mmeshakuwa) ni Waislaam (wanaojisalimisha kwa Allaah). [Aal-‘Imraan: 102]

فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُم

Basi mcheni Allaah muwezavyo. [At-Taghaabun: 16]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا

Enyi walioamini! Mcheni Allaah na semeni kauli nyoofu ya haki. [Al-Ahzaab: 70]

 

وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا

Na yeyote anayemcha Allaah; Humjaalia njia ya kutoka (shidani).

وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ

Na Atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii. Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza. [At-Twalaaq: 2-3]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن تَتَّقُوا اللَّـهَ يَجْعَل لَّكُمْ فُرْقَانًا وَيُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ۗ وَاللَّـهُ ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ

Enyi walioamini! Mkimcha Allaah Atakupeni upambanuo wa haki na batili, na Atakufutieni maovu yenu, na Atakughufurieni. Na Allaah ni Mwenye fadhila adhimu. [Al-Anfaal: 29]

 

Hadiyth – 1

 

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قِيلَ: يَا رسولَ الله، مَنْ أكرمُ النَّاس؟ قَالَ: ((أَتْقَاهُمْ)). فقالوا: لَيْسَ عن هَذَا نسألُكَ، قَالَ: ((فَيُوسُفُ نَبِيُّ اللهِ ابنُ نَبِيِّ اللهِ ابنِ نَبيِّ اللهِ ابنِ خليلِ اللهِ)) قالوا: لَيْسَ عن هَذَا نسألُكَ، قَالَ: ((فَعَنْ مَعَادِنِ العَرَبِ تَسْأَلوني؟ خِيَارُهُمْ في الجَاهِليَّةِ خِيَارُهُمْ في الإِسْلامِ إِذَا فقُهُوا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa: Yaa Rasula-Allaah, ni nani bora katika watu? Akajibu: “Ni yule aliyewazidi kwa kumcha Allaah.” Wakamwambia: Hatukuulizi kuhusu hili. Akawaambia: “Basi ni Yuwusuf Nabiy wa Allaah, Ibn Nabiy wa Allaah, ibn Nabiy wa Allaah, Ibn Khaliyl wa Allaah.” Wakasema: Hatukuulizi kuhusu hili. Akasema: “Mwaniuliza kuhusu koo za Waarabu? Wabora wao katika ujahiliyyah ndio wabora wao katika Uislamu iwapo watafahamu Dini.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth -2

 

عن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّ الدُّنْيَا حُلْوَةٌ خَضِرةٌ، وإنَّ اللهَ مُسْتَخْلِفُكُمْ فِيهَا فَيَنْظُرَ كَيفَ تَعْمَلُونَ، فَاتَّقُوا الدُّنْيَا وَاتَّقُوا النِّسَاء؛ فإنَّ أَوَّلَ فِتْنَةِ بَنِي إسرائيلَ كَانَتْ في النِّسَاءِ)). رواه مسلم

Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika dunia ni tamu rangi ya kijani, Hakika Allaah Amewatawalisha humo ili Awatazame mtakayotenda. Basi ogopeni dunia na waogopeni wanawake; hakika fitnah (mtihani) ya mwanzo kwa wana wa Israiyl ilikuwa ni katika wanawake.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

عن ابن مسعودٍ رضي الله عنه: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يقول: ((اللَّهُمَّ إنِّي أَسألُكَ الهُدَى، وَالتُّقَى، وَالعَفَافَ، وَالغِنَى)). رواه مسلم

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba: “Ee Rabb, nakuomba uongofu na taqwa na kuepuka mabaya na ukwasi.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

عن أبي طريفٍ عدِيِّ بن حاتمٍ الطائيِّ رضي الله عنه، قَالَ: سمعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ ثُمَّ رَأَى أتْقَى للهِ مِنْهَا فَليَأتِ التَّقْوَى)). رواه مسلم

Abuu Twariyf ‘Adiyyi bin Haatim At-Twaaiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Atakayeapa yamini kisha akaona linalomridhisha zaidi Allaah kulikoni aliloliapia, basi afanye linalomridhisha Allaah.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

عن أبي أُمَامَةَ صُدَيّ بنِ عجلانَ الباهِلِيِّ رضي الله عنه قَالَ: سَمِعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يَخْطُبُ في حجةِ الوداعِ، فَقَالَ: ((اتَّقُوا الله وَصلُّوا خَمْسَكُمْ، وَصُومُوا شَهْرَكُمْ، وَأَدُّوا زَكاةَ أَمْوَالِكُمْ، وَأَطِيعُوا أُمَرَاءكُمْ تَدْخُلُوا جَنَّةَ رَبِّكُمْ)). رواه الترمذي، في آخر كتابِ الصلاةِ، وَقالَ: (حديث حسن صحيح)

Abuu Umaamah, Swudayy bin ‘Ajlaan Al-Baahiliyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akikhutubia katika Hajjatil-Widaa’i akasema: “Mcheni Allaaah, swalini Swalaah zenu tano, fungeni Swawm mwezi wenu, toeni Zakaah za mali yenu na watiini viongozi wenu, mtaingia Jannah ya Rabb wenu.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

 

 

Share

007-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Yakini Na Kutawakali Kwa Allaah

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب في اليقين والتوكل

007 - Mlango Wa Yakini Na Kutawakali Kwa Allaah

 

قَالَ اللهُ تَعَالَى:

وَلَمَّا رَأَى الْمُؤْمِنُونَ الْأَحْزَابَ قَالُوا هَـٰذَا مَا وَعَدَنَا اللَّـهُ وَرَسُولُهُ وَصَدَقَ اللَّـهُ وَرَسُولُهُ ۚ وَمَا زَادَهُمْ إِلَّا إِيمَانًا وَتَسْلِيمًا ﴿٢٢﴾

Basi Waumini walipoona makundi, walisema: “Haya ndio yale Aliyotuahidi Allaah na Rasuli Wake, na Amesema kweli Allaah na Rasuli Wake; na haikuwazidishia isipokuwa iymaan na kujisalimisha. [Al-Ahzaab: 22]

 

 

الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ﴿١٧٣﴾

Wale walioambiwa na watu: “Hakika watu wamejumuika dhidi yenu, basi waogopeni” (Haya) Yakawazidishia iymaan; na wakasema: “Allaah Anatutosheleza, Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.”

  

فَانقَلَبُوا بِنِعْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ وَفَضْلٍ لَّمْ يَمْسَسْهُمْ سُوءٌ وَاتَّبَعُوا رِضْوَانَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ ذُو فَضْلٍ عَظِيمٍ ﴿١٧٤﴾

Basi wakarudi na neema kutoka kwa Allaah na fadhila; halijawagusa ovu lolote; na wakafuatilia radhi za Allaah.  Na Allaah ni Mwenye fadhila adhimu.  [Aal-‘Imraan: 173-174]

 

قَالَتْ لَهُمْ رُسُلُهُمْ إِن نَّحْنُ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَمُنُّ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۖ وَمَا كَانَ لَنَا أَن نَّأْتِيَكُم بِسُلْطَانٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١١﴾

Rasuli wao wakawajibu: “Sisi si chochote isipokuwa ni watu kama nyinyi, lakini Allaah Anamfadhilisha Amtakaye miongoni mwa waja Wake. Na haikutupasa sisi kukujieni kwa ushahidi isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na kwa Allaah watawakali Waumini.  [Ibraahiym: 11]

 

فَبِمَا رَحْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ لِنتَ لَهُمْ ۖ وَلَوْ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ الْقَلْبِ لَانفَضُّوا مِنْ حَوْلِكَ ۖ فَاعْفُ عَنْهُمْ وَاسْتَغْفِرْ لَهُمْ وَشَاوِرْهُمْ فِي الْأَمْرِ ۖ فَإِذَا عَزَمْتَ فَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُتَوكِّلِينَ ﴿١٥٩﴾

Basi ni kwa rahmah kutoka kwa Allaah umekuwa mpole kwao (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).  Na lau ungelikuwa mjeuri mwenye moyo mgumu wangelitawanyika mbali nawe (wakakukimbia). Basi wasamehe na waombee maghfirah na washauri katika mambo. Na unapoazimia basi tawakali kwa Allaah. Hakika Allaah Anapenda wanaotawakali. [Aal-‘Imraan:159]

 

وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ بَالِغُ أَمْرِهِ ۚ قَدْ جَعَلَ اللَّـهُ لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا﴿٣﴾

Na Atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii. Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza. Hakika Allaah Anatimiza kusudio Lake. Allaah Amejaalia kwa kila kitu makadirio.  [Atw-Twalaaq: 3]

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٢﴾

Hakika Waumini ni wale ambao anapotajwa Allaah nyoyo zao, zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali. [Al-Anfaal: 2]

 

Hadiyth – 1

عن ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((عُرِضَتْ عَلَيَّ الأُمَمُ، فَرَأيْتُ النَّبيّ ومَعَهُ الرُّهَيطُ، والنبي وَمَعَهُ الرَّجُلُ وَالرَّجُلانِ، والنبيَّ ولَيْسَ مَعَهُ أَحَدٌ إِذْ رُفِعَ لي سَوَادٌ عَظيمٌ فَظَنَنْتُ أَنَّهُمْ أُمَّتِي فقيلَ لِي: هَذَا مُوسَى وَقَومُهُ، ولكنِ انْظُرْ إِلَى الأُفُقِ، فَنَظَرتُ فَإِذا سَوادٌ عَظِيمٌ، فقيلَ لي: انْظُرْ إِلَى الأفُقِ الآخَرِ، فَإِذَا سَوَادٌ عَظيمٌ، فقيلَ لِي: هذِهِ أُمَّتُكَ وَمَعَهُمْ سَبْعُونَ ألفًا يَدْخُلُونَ الجَنَّةَ بِغَيرِ حِسَابٍ ولا عَذَابٍ))، ثُمَّ نَهَضَ فَدخَلَ مَنْزِلَهُ فَخَاضَ النَّاسُ في أُولئكَ الَّذِينَ يَدْخُلُونَ الجَنَّةَ بِغَيْرِ حِسَابٍ ولا عَذَابٍ، فَقَالَ بَعْضُهُمْ: فَلَعَلَّهُمْ الَّذينَ صَحِبوا رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، وَقالَ بعْضُهُمْ: فَلَعَلَّهُمْ الَّذِينَ وُلِدُوا في الإِسْلامِ فَلَمْ يُشْرِكُوا بِالله شَيئًا- وذَكَرُوا أشيَاءَ- فَخَرجَ عَلَيْهِمْ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: ((مَا الَّذِي تَخُوضُونَ فِيهِ؟)) فَأَخْبَرُوهُ فقالَ: ((هُمُ الَّذِينَ لا يَرْقُونَ، وَلا يَسْتَرقُونَ، وَلا يَتَطَيَّرُونَ؛ وعَلَى رَبِّهِمْ يَتَوكَّلُون)) فقامَ عُكَّاشَةُ بنُ محصنٍ، فَقَالَ: ادْعُ الله أنْ يَجْعَلني مِنْهُمْ، فَقَالَ: ((أنْتَ مِنْهُمْ)). ثُمَّ قَامَ رَجُلٌ آخَرُ، فَقَالَ: ادْعُ اللهَ أنْ يَجْعَلنِي مِنْهُمْ، فَقَالَ: ((سَبَقَكَ بِهَا عُكَّاشَةُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Nilionyeshwa ummah mbali mbali. Nikamuona Nabiy ana kipote, Nabiy mwengine ana mtu mmoja na wawili, na Nabiy mwengine hana mfuasi. Mara kwa ghafla, nikaonyeshwa kundi kubwa, nikadhani kuwa ni ummah wangu. Nikaambiwa: Huyu ni Muwsaa na Qawmu yake, lakini tazama upande huu. Nikatazama, nikaona kundi kubwa. Nikaambiwa: Tazama upande mwengine. Nikaona kundi kubwa, nikaambiwa: Huu ni Ummah wako, pamoja nao kuna watu sabini elfu wataingia Jannah bila hisabu wala adhabu.” Halafu akainuka na kuingia nyumbani kwake. Watu wakaanza kuzungumza na kujadiliana kuhusu wale watakaoingia Jannah bila hisabu wala adhabu. Baadhi yao wakasema: Labda hao ni wale waliosuhubiana na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Wengine wakasema: Labda hao ni wale waliozaliwa katika Uislamu na wala hawakumshirikisha Allaah na chochote. Wakaongea mambo mengi. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawatokea, akawauliza: “Mlikuwa mnazungumza kuhusu nini?” Wakamueleza. Akawaambia: “Hao ni wale ambao hawazingui (hawafanyi Ruqyyah) wala hawataki kuzinguliwa kutoka kwa mwengine, wala hawapigi ramli na wameegemea kwa Rabb wao tu.” Akasimama ‘Ukaashah bin Mihswan akasema: Muombe Allaah Anijaalie katika wao. Akamwambia: “Wewe ni katika wao.” Kisha akasimama mtu mwengine, akamwambia: Muombe Allaah Anijaalie miongoni mwao. Akamwambia: “Amekutangulia ’Ukaashah (daraja hiyo).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

عن ابن عباس رضي الله عنهما أيضًا: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يقول: ((اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمْتُ، وَبِكَ آمَنْتُ، وَعَليْك تَوَكَّلْتُ، وَإِلَيْكَ أنَبْتُ، وَبِكَ خَاصَمْتُ. اللَّهُمَّ إِنِّي أعُوذُ بعزَّتِكَ؛ لا إلهَ إلا أَنْتَ أنْ تُضلَّني، أَنْتَ الحَيُّ الَّذِي لا يَمُوتُ، وَالجِنُّ والإنْسُ يَمُوتُونَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ، وهذا لفظ مسلم واختصره البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba: “Ee Allaah, kwa ajili Yako nimejisalimisha, Kwako tu nimeamini, Wewe pekee nimekutegemea, Kwako tu nimerejea, kwa ajili Yako tu nakhasimiana. Ee Allaah, hakika mimi najilinda kwa utukufu Wako, hakuna Muabudiwa wa haki isipokuwa Wewe, Usinipoteze. Wewe ni Hai Usiekufa, majini na wana-Aadam watakufa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

عن ابن عباس رضي الله عنهما أيضًا، قَالَ: حَسْبُنَا اللهُ وَنِعْمَ الوَكِيلُ، قَالَهَا إِبرَاهيمُ صلى الله عليه وسلم حِينَ أُلقِيَ في النَّارِ، وَقَالَها مُحَمَّدٌ صلى الله عليه وسلم حِينَ قَالُوا: إنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إيْمانًا وَقَالُوا: حَسْبُنَا الله ونعْمَ الوَكيلُ. رواه البخاري.

وفي رواية لَهُ عن ابن عَبَّاسٍ رضي الله عنهما، قَالَ: كَانَ آخر قَول إبْرَاهِيمَ صلى الله عليه وسلم حِينَ أُلْقِيَ في النَّارِ: حَسْبِي الله ونِعْمَ الوَكِيلُ

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Allaah Anatutosha. Naye ni Mdhamini  bora kabisa, neno hili alisema Nabiy Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) alipotumbukizwa motoni, na alisema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) pale watu (walipokodiwa na Maquraysh) walipowaambia (Waislaam): “Maquraysh wamewakusanyikia, kwa hiyo waogopeni. Lakini maneno hayo yaliwazidishia Iymaan (Waislamu) wakasema: Allaah Anatutosha Naye ni Mdhamini bora kabisa.” [Al-Bukhaariy]

Riwaayah nyingine; kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Neno la mwisho alilolitamka Nabiy Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) wakati alipotumbukizwa kwenye moto ilikuwa ni kusema: “Allaah Ananitosha, Naye ni Mdhamini bora kabisa.”

 

 

Hadiyth – 4

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((يَدْخُلُ الجَنَّةَ أَقْوامٌ أفْئِدَتُهُمْ مِثلُ أفْئِدَةِ الطَّيرِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna watu wataingia Jannah nyoyo zao ni mithili ya ndege (Kwa ule ulaini wanyoyo za ndege namna zilivyo).” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

عن جابر رضي الله عنه: أَنَّهُ غَزَا مَعَ النبي صلى الله عليه وسلم قِبلَ نَجْدٍ، فَلَمَّا قَفَلَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَفَلَ معَهُمْ، فَأَدْرَكَتْهُمُ القَائِلَةُ في وَادٍ كثير العِضَاه، فَنَزَلَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَتَفَرَّقَ النَّاسُ يَسْتَظِلُّونَ بالشَّجَرِ، وَنَزَلَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم تَحتَ سَمُرَة فَعَلَّقَ بِهَا سَيفَهُ وَنِمْنَا نَوْمَةً، فَإِذَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَدْعونَا وَإِذَا عِنْدَهُ أعْرَابِيٌّ، فَقَالَ: ((إنَّ هَذَا اخْتَرَطَ عَلَيَّ سَيفِي وَأنَا نَائمٌ فَاسْتَيقَظْتُ وَهُوَ في يَدِهِ صَلتًا، قَالَ: مَنْ يَمْنَعُكَ مِنِّي؟ قُلْتُ: الله- ثلاثًا-)) وَلَمْ يُعاقِبْهُ وَجَلَسَ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية قَالَ جَابرٌ: كُنَّا مَعَ رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم بذَاتِ الرِّقَاعِ، فَإِذَا أَتَيْنَا عَلَى شَجَرَةٍ ظَلِيلَةٍ تَرَكْنَاهَا لرسول الله صلى الله عليه وسلم، فجاء رَجُلٌ مِنَ المُشْركينَ وَسَيفُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم معَلَّقٌ بالشَّجَرَةِ فَاخْتَرطَهُ، فَقَالَ: تَخَافُنِي؟ قَالَ: ((لا)). فَقَالَ: فَمَنْ يَمْنَعُكَ مِنِّي؟ قَالَ: ((الله)).

وفي رواية أبي بكر الإسماعيلي في صحيحه، قَالَ: مَنْ يَمْنَعُكَ مِنِّي؟ قَالَ: ((اللهُ)). قَالَ: فَسَقَطَ السيفُ مِنْ يَدهِ، فَأخَذَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم السَّيْفَ، فَقَالَ: ((مَنْ يَمْنَعُكَ مني؟)). فَقَالَ: كُنْ خَيرَ آخِذٍ. فَقَالَ: ((تَشْهَدُ أنْ لا إلهَ إلا الله وَأَنِّي رَسُول الله؟)) قَالَ: لا، وَلَكنِّي أُعَاهِدُكَ أنْ لاَ أُقَاتِلَكَ، وَلا أَكُونَ مَعَ قَومٍ يُقَاتِلُونَكَ، فَخَلَّى سَبيلَهُ، فَأَتَى أصْحَابَهُ، فَقَالَ: جئتُكُمْ مِنْ عنْد خَيْرِ النَّاسِ.

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia kuwa yeye alikwenda kupigana Jihaad sehemu za Najd akiwa pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliporejea, alirejea pamoja nao. Ikawakuta katikati ya mchana katika bonde lenye miti mingi ya miba. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akashuka. Wa nao wakaenea (huku na kule) wakitafuta vivuli vya miti. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alishuka chini ya mti wa samura (aina ya mti wenye miba), akautundika upanga wake, tukalala kidogo. Mara ghafla Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akatuita, akawa yupo na mbedui, akatuambia: “Mtu huyo kauchomoa upanga wangu nami nimelala, nikaamka nao upo mkononi mwake, akaniuliza: Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu? Nikamjibu: “Allaah mara tatu.” Wala hakumuadhibu, akaketi. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Riwaayah nyingine inasema: “Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Tulikuwa pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) huko Dhaatir-Riqaa’, tunapofika kwenye mti wenye kivuli, humuachia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Akaja mtu katika mushrikiyn na upanga wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) umetundikwa kwenye mti. Akauchomoa, akamuuliza: Unaniogopa? Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamjibu: “Hapana” Akamuuliza: Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu? Akamwambia: “Allaah”.

 

Riwaayah nyingine ya; Abuu Bakr Al-Ismaa’iyl katika sahihi yake, imesema: Akamuuliza: Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu? Akamwambia: “Allaah” Upanga ukamuanguka kutoka mkononi mwake. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akauchukua upanga ule. Akamuuliza: “Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu?” Akamjibu: Mbora mwenye kuuchukua. Akamuuliza: “Unashuhudia kuwa hakuna Anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah na kuwa mimi ni Rasuli Wake?” Akajibu: Hapana. Lakini nakuahidi kuwa sitakupiga vita, wala sitokuwa pamoja na watu wanaopigana na wewe. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuacha aende zake. Akawaendea Maswahaba zake, akawaambia: “Nimewajia kutoka kwa mbora wa watu.”

 

 

Hadiyh – 6

عن عُمَر رضي الله عنه قَالَ: سمعتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((لَوْ أَنَّكُمْ تَتَوَكَّلُونَ عَلَى اللهِ حَقَّ تَوَكُّلِهِ لَرَزَقَكُمْ كَمَا يَرْزُقُ الطَّيْرَ، تَغْدُو خِمَاصًا وَتَرُوحُ بِطَانًا)). رواه الترمذي، وَقالَ: (حديث حسن)

‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Lau mngelikuwa mnamtegemea Allaah ukweli wa kumtegemea, Angewaruzuku kama Anavyowaruzuku ndege. Wanatoka asubuhi wakiwa wana njaa na wanarudi wakiwa wameshiba.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 7

عن أبي عُمَارة البراءِ بن عازب رضي الله عنهما، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا فُلانُ، إِذَا أَوَيْتَ إِلَى فراشِكَ، فَقُل: اللَّهُمَّ أسْلَمتُ نَفْسي إلَيْكَ، وَوَجَّهتُ وَجْهِي إلَيْكَ، وَفَوَّضتُ أَمْري إلَيْكَ، وَأَلجأْتُ ظَهري إلَيْكَ رَغبَةً وَرَهبَةً إلَيْكَ، لا مَلْجَأ وَلا مَنْجَا مِنْكَ إلا إلَيْكَ، آمنْتُ بِكِتَابِكَ الَّذِي أنْزَلْتَ؛ وَنَبِيِّكَ الَّذِي أَرْسَلْتَ. فَإِنَّ مِتَّ مِنْ لَيلَتِكَ مِتَّ عَلَى الفِطْرَةِ، وَإِنْ أصْبَحْتَ أَصَبْتَ خَيرًا)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية في الصحيحين، عن البراءِ، قَالَ: قَالَ لي رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا أَتَيْتَ مَضْجِعَكَ فَتَوَضَّأْ وُضُوءكَ للصَّلاةِ، ثُمَّ اضْطَجعْ عَلَى شِقِّكَ الأَيمَنِ، وَقُلْ... وذَكَرَ نَحْوَهُ ثُمَّ قَالَ: وَاجْعَلْهُنَّ آخِرَ مَا تَقُولُ))

Abuu ‘Umaarah Al-Baraa bin ‘Aazib (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia mtu: “Ee fulani utakapokiendea kitanda chako, sema: Ee Allaah, nimejisalimisha Kwako, uso wangu nimeuwelekeza Kwako, mambo yangu nimekuachia Wewe, nimekuegemeza Wewe kwa kutaraji thawabu Zako na kuogopa dhambi Zako, hakuna sehemu ya kuegemea wala kukuepuka ila ni Kwako. Nimekiamini Kitabu Chako Ulichokiteremsha na Rasuli Wako Uliyemtuma. Basi utakapofikwa na mauti usiku huo, utakuwa umekufa katika Uislamu, na ukipambaukiwa utapata khayr.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Riwaayah nyingine iliyomo katika Sahihi Al-Bukhaariy na Sahihi Muslim; kutoka kwa Al-Baraa imesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: “Unapokwenda sehemu yako ya kulala, tawadha wudhuu wa Swalaah, kisha ulale kwa upande wako wa kulia na usema: (Akajata mfano wake kama ilivyotangulia) “Maneno hayo ndiyo yawe ya mwisho utakayoyasema.”

 

 

Hadiyth – 8

عن أبي بكرٍ الصِّديق رضي الله عنه عبدِ اللهِ بنِ عثمان بنِ عامرِ بنِ عمر ابنِ كعب بنِ سعدِ بن تَيْم بنِ مرة بن كعبِ بن لُؤَيِّ بن غالب القرشي التيمي رضي الله عنه وَهُوَ وَأَبُوهُ وَأُمُّهُ صَحَابَةٌ رضي الله عنهم قَالَ: نَظَرتُ إِلَى أَقْدَامِ المُشْرِكينَ وَنَحنُ في الغَارِ وَهُمْ عَلَى رُؤُوسِنا، فقلتُ: يَا رسولَ الله، لَوْ أَنَّ أَحَدَهُمْ نَظَرَ تَحْتَ قَدَمَيهِ لأَبْصَرَنَا. فَقَالَ: ((مَا ظَنُّكَ يَا أَبا بَكرٍ باثنَيْنِ الله ثَالِثُهُمَا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Bakr As-Swidiyq, ‘Abdullaah ‘Uthmaan bin ‘Aamir bin ‘Umar bin Ka’b bin Sa’d bin Taym bin Murrah bin Ka’b bin Lu-ayy bin Ghaalib Al-Qurashiy At-Taymiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) yeye, baba yake na mama yake wote ni maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum) amesema: Niliitazama miguu ya mshirikina nasi tupo pangoni nao wapo juu yetu (wanatutafuta ili watuue). Nikamwambia: Yaa Rasula-Allaah, lau mmoja wao atautazama mguu wake atatuona! Akasema: “Ee Abuu Bakr, unadhaniaje watu wawili ambao watatu wao ni Allaah?” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

عن أم المُؤمنينَ أمِّ سَلَمَةَ وَاسمها هِنْدُ بنتُ أَبي أميةَ حذيفةَ المخزومية رضي الله عنها: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا خَرَجَ مِنْ بَيتِهِ، قَالَ: ((بِسْمِ اللهِ تَوَكَّلتُ عَلَى اللهِ، اللَّهُمَّ إِنِّي أعُوذُ بِكَ أنْ أضِلَّ أَوْ أُضَلَّ، أَوْ أَزِلَّ أَوْ أُزَلَّ، أَوْ أظْلِمَ أَوْ أُظْلَمَ، أَوْ أجْهَلَ أَوْ يُجْهَلَ عَلَيَّ)) حديثٌ صحيح، رواه أبو داود والترمذي وغيرهما بأسانيد صحيحةٍ. قَالَ الترمذي: (حديث حسن صحيح). وهذا لفظ أبي داود

Mama wa Waumini, Ummu Salamah, jina lake ni Hindu bint Abiy Umayyah Hudhayfah Al-Makhzumiyyah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapotoka nyumbani kwake husema: “Kwa jina la Allaah, Nimeegemea kwa Allaah. Ee Allaah, kwa hakika najilinda Kwako nisije nikapotea au kupotezwa, au nikateleza au nikatelezeshwa, au nikadhumu au nikadhulumiwa au nikafanya ujinga au nikafanyiwa ujinga.” [Hadiyth hii, ni Sahihi imepokelewa na Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na wengineo kwa isnaad Sahihi. At-Tirmidhiy amesema: Hadiyth hii ni Hasan Sahih]

 

 

Hadiyth – 10

عن أنس رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَالَ- يَعْني: إِذَا خَرَجَ مِنْ بَيتِهِ: بِسمِ اللهِ تَوَكَّلْتُ عَلَى اللهِ، وَلا حَولَ وَلا قُوَّةَ إلا باللهِ، يُقالُ لَهُ: هُدِيتَ وَكُفِيتَ وَوُقِيتَ، وَتَنَحَّى عَنْهُ الشَّيطَانُ)). رواه أبو داود والترمذي والنسائي وغيرهم. وَقالَ الترمذي: (حديث حسن)، زاد أبو داود: ((فيقول- يعني: الشيطان-- لِشيطان آخر: كَيفَ لَكَ بِرجلٍ قَدْ هُدِيَ وَكُفِيَ وَوُقِيَ؟))

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayesema anapotoka nyumbani kwake. Kwa jina la Allaah nimeegemea kwa Allaah, hakuna namna ya kuepuka maasi wala nguvu ya kufanya ‘Ibaadah ila kwa msaada wa Allaah. Ataambiwa: Umeshaongozwa, umeshatoshelezwa, na umeshakingwa, na shaytwaan hujitenga naye.” [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na wengineo. At-Tirmidhiy amesema: Hadiyth hii ni Hasan]

Abuu Daawuwd ameongezea: Shaytwaan humueleza shaytwaan mwenzie: Utamuwezaje mtu aliyeongozwa, akatoshelezwa na akakingwa?

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: كَانَ أَخَوانِ عَلَى عهد النَّبيّ صلى الله عليه وسلم وَكَانَ أحَدُهُمَا يَأتِي النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم وَالآخَرُ يَحْتَرِفُ، فَشَكَا المُحْتَرِفُ أخَاهُ للنبي صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: ((لَعَلَّكَ تُرْزَقُ بِهِ)). رواه الترمذي بإسناد صحيحٍ عَلَى شرطِ مسلم

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Kulikuwepo  ndugu wawili zama za Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), mmoja alikuwa akienda kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) (na kukaa naye), na mwengine anafanya kazi; yule anayefanya kazi akamshitakia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) dhidi ya ndugu yake, Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Pengine wewe unaruzukiwa kwa sababu yake.” [At-Tirmidhiy kwa isnaad Swahiyh]

 

 

 

Share

008-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Istiqaamah Kuthibitika Imara

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب الاستقامة

008 - Mlango Wa Istiqaamah - Kuthibitika Imara (Kuwa Na Msimamo)

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ اللهُ تَعَالَى:

فَاسْتَقِمْ كَمَا أُمِرْتَ

Basi thibitika imara kama ulivyoamrishwa. [Huwd: 112]

 

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿٣٠﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara; Malaika huwateremkia (wanapofishwa kuwaambia): “Msikhofu, na wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo mlikuwa mkiahidiwa.”

 

نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَشْتَهِي أَنفُسُكُمْ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ ﴿٣١﴾

“Sisi ni walinzi wenu katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale mtakayoomba. [Fusw-swilat: 30-31]

 

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴿١٣﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara, basi hakutokuwa na khofu juu yao, na wala hawatohuzunika.

 

أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٤﴾

Hao ndio watu wa Jannah, ni wenye kudumu humo, jazaa kwa yale waliyokuwa wakitenda. [Al-Ahqaaf: 13-14]

 

 

Hadiyth – 1

 

وعن أبي عمرو، وقيل: أبي عَمرة سفيان بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: قُلْتُ: يَا رَسُول الله، قُلْ لي في الإسْلامِ قَولًا لا أسْأَلُ عَنْهُ أَحَدًا غَيْرَكَ. قَالَ: ((قُلْ: آمَنْتُ بِاللهِ، ثُمَّ استَقِمْ)). رواه مسلم

Abuu ‘Amru, au Abuu 'Amrah Sufyaan bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimwambia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam); niambie neno katika Uislamu ambalo sitamuuliza yoyote zaidi yako. Akasema: “Sema: Nimemuamini Allaah, kisha uthibitike imara.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

 

وعن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((قَارِبُوا وَسَدِّدُوا، وَاعْلَمُوا أَنَّهُ لَنْ يَنْجُوَ أَحَدٌ مِنْكُمْ بعَمَلِهِ)) قالُوا: وَلا أَنْتَ يَا رَسُول الله؟ قَالَ: ((وَلا أنا إلا أنْ يَتَغَمَّدَني الله برَحمَةٍ مِنهُ وَفَضْلٍ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Alisema: “Fanyeni wastani (msivuke mipaka) na muwe na msimamo. Jueni kwamba  hakuna yeyote yule miongoni mwenu atakayeokoka na 'amali yake.” Maswahaba wakamuuliza: Hata wewe ee Rasuli wa Allaah? Akajibu: “Hata mimi, isipokuwa Allaah Anifunike kwa rahmah na fadhila Zake.” [Muslim]    

 

 

 

Share

009-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kutafakari Viumbe ‘Adhiym Vya Allaah Dunia Kutoweka ...

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب التفكر في عظيم مخلوقات الله تَعَالَى، وفناء الدنيا وأهوال الآخرة وسائر أمورهما وتقصير النفس، وتهذيبها وحملها عَلَى الاستقامة

 

009 – Mlango Wa Kutafakari Viumbe ‘Adhiym Vya Allaah, Dunia Kutoweka – Vitisho Vya Aakhirah Na Mambo Mengine Yanayohusiana Nayo Nafsi Kufanya Taqswiyr, Kuiadabisha Nafsi Na Kuifanya Iwe Na Msimamo

 

قَالَ اللهُ تَعَالَى:

قُلْ إِنَّمَا أَعِظُكُم بِوَاحِدَةٍ ۖ أَن تَقُومُوا لِلَّـهِ مَثْنَىٰ وَفُرَادَىٰ ثُمَّ تَتَفَكَّرُوا ۚ

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika nakuwaidhini kwa jambo moja tu!  Msimame kwa ajili ya Allaah wawili wawili, au mmoja mmoja kisha mtafakari.” [Sabaa: 46]

 

إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠﴾ 

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na mabadiliko (ya mfuatano) ya usiku na mchana; bila shaka ni Aayaat (ishara, dalili, zingatio n.k) kwa wenye akili.

 

الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٩١﴾ 

Ambao wanamdhukuru Allaah (kwa) kusimama, na (kwa) kukaa na (kwa) kulala ubavuni mwao na wanatafakari katika kuumbwa mbingu na ardhi (wakisema): “Rabb wetu, Hukuumba haya bure. Subhaanak! (Utakasifu ni Wako!) Tukinge na adhabu ya moto. [Aal-‘Imraan: 190-191]

 

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ ﴿١٧﴾

Je, hawamtazami ngamia namna walivyoumbwa?

 

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ ﴿١٨﴾

Na mbingu vipi zilivyonyanyuliwa?

 

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ ﴿١٩﴾

Na majabali vipi yamekongomewa imara.

 

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ ﴿٢٠﴾

Na ardhi vipi ilivyotandazwa?

 

فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ ﴿٢١﴾

Basi kumbusha (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم); hakika wewe ni mkumbushaji tu. [Al-Ghaashiyah: 17-21]

 

أَفَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ

Je, hawakutembea katika ardhi wakatazama vipi imekuwa hatima ya ambao wa kabla yao? [Muhammad: 10]

 

 

 

 

Share

010-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukimbilia Mambo ya Khayr...

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب المبادرة إلى الخيرات، وحثِّ من توجه لخير على الإقبال عليه بالجد من غير تردد

010 – Mlango Wa Kukimbilia Mambo ya Khayr Na Kumuhimiza Anayefanya Khayr Kuielekea Kwa Jitihada Bila Kusitasita

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ اللهُ تَعَالَى:

فَاسْتَبِقُوا الْخَيْرَاتِ ۚ

Basi shindaneni kwenye khayraat. [Al-Baqarah: 148]

 

وَسَارِعُوا إِلَىٰ مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ ﴿١٣٣﴾ 

Na kimbilieni maghfirah kutoka kwa Rabb wenu na Jannah upana wake ni wa mbingu na ardhi imeandaliwa kwa wenye taqwa. [Aal-‘Imraan: 133]

 

 

Hadiyth – 1

عن أبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((بَادِرُوا بِالأعْمَال فتنًا كقطَعِ اللَّيْلِ المُظْلِمِ، يُصْبحُ الرَّجُلُ مُؤْمِنًا وَيُمْسِي كَافِرًا، وَيُمْسِي مُؤمِنًا ويُصبحُ كَافِرًا، يَبيعُ دِينَهُ بعَرَضٍ مِنَ الدُّنيا)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Zikimbilieni ‘amali njema kwani zitakuja fitnah (nyingi) kama mfano wa usiku na kiza. Mtu atapambaukiwa akiwa Muumin na akifikiwa na jioni hali ya kuwa ni kafiri, au atafikiwa jioni akiwa Muumin na atapambaukiwa akiwa kafiri, anaiuza Dini yake kwa thamani ya dunia.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

عن أبي سِروْعَة- بكسر السين المهملة وفتحها- عُقبةَ بن الحارث رضي الله عنه قَالَ: صَلَّيتُ وَرَاءَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم بالمَدِينَةِ العَصْرَ، فَسَلَّمَ ثُمَّ قَامَ مُسْرِعًا، فَتَخَطَّى رِقَابَ النَّاسِ إِلَى بعْضِ حُجَرِ نِسَائِهِ، فَفَزِعَ النَّاسُ مِنْ سُرْعَتِهِ، فَخَرَجَ عَلَيهمْ، فَرأى أنَّهمْ قَدْ عَجبُوا مِنْ سُرعَتهِ، قَالَ: ((ذَكَرتُ شَيئًا مِنْ تِبرٍ عِندَنَا فَكَرِهتُ أنْ يَحْبِسَنِي فَأمَرتُ بِقِسْمَتِهِ)). رواه البخاري.

وفي رواية لَهُ: ((كُنتُ خَلَّفتُ في البَيْتِ تِبرًا مِنَ الصَّدَقةِ فَكَرِهتُ أنْ أُبَيِّتَهُ)). ((التِّبْرُ))

Abuu Sirw’ah, ‘Uqbah bin Al-Haarith (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Niliswali nyuma ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Swalaah ya Al-‘Aswr Madiynah. Akatoa salaam kisha akainuka kwa haraka, akawa anaziruka shingo za watu kuelekea katika chumba cha mkewe. Watu wakapata mshangao kwa ile haraka yake. Kisha akawatokezea na kuwaona wamemstajabu kwa ile haraka yake, akawaambia: “Nilikumbuka kitu katika kipande cha dhahabu kilichokuwa kwetu, nikakichukua kisije kikanizuia, nikaamuru kigawanywe.” [Al-Bukhaariy]

 

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema:

“Nilikuwa nimeacha nyumbani kipande cha dhahabu cha Swadaqah, nikachukia kisije kikapitiwa na usiku (nacho kipo nyumbani).”

 

 

Hadiyth – 3

عن جابر رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رجل للنبي صلى الله عليه وسلم يَومَ أُحُد: أَرَأيتَ إنْ قُتِلتُ فَأَيْنَ أَنَا؟ قَالَ: ((في الجنَّةِ)) فَأَلْقَى تَمَرَاتٍ كُنَّ في يَدِهِ، ثُمَّ قَاتَلَ حَتَّى قُتِلَ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: mtu mmoja alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) siku ya Vita vya Uhud: Niambie nikiuliwa nitakwenda wapi? Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamjibu: “Jannah.” Akazitupa tende chache alizokuwa nazo mkononi mwake, kisha akapigana mpaka akauliwa. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

عن أبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ: جاءَ رَجُلٌ إِلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: يَا رسولَ الله، أيُّ الصَّدَقَةِ أعْظَمُ أجْرًا؟ قَالَ: ((أنْ تَصَدَّقَ وَأنتَ صَحيحٌ شَحيحٌ، تَخشَى الفَقرَ وتَأمُلُ الغِنَى، وَلا تُمهِلْ حَتَّى إِذَا بَلَغتِ الحُلقُومَ قُلْتَ لِفُلان كذا ولِفُلانٍ كَذا، وقَدْ كَانَ لِفُلانٍ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: Yaa Rasula-Allaah, ni swadaqah ipi yenye ujira mkubwa zaidi? Akajibu: “Utoe swadaqah nawe ni mzima, unatamani mali na unakhofia ufakiri na unatarajia utajiri, wala usichelewe mpaka roho ikafika kwenye koo, ukaanza kusema: Fulani ana haki kadhaa na fulani ana haki kadhaa, na fulani alikuwa ana haki kadhaa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

عن أنس رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم أخذ سيفًا يَومَ أُحُدٍ، فَقَالَ: ((مَنْ يَأخُذُ منِّي هَذَا؟)) فَبَسطُوا أيدِيَهُمْ كُلُّ إنسَانٍ مِنْهُمْ يقُولُ: أَنَا أَنَا. قَالَ: ((فَمَنْ يَأخُذُهُ بحَقِّه؟)) فَأَحْجَمَ القَومُ فَقَالَ أَبُو دُجَانَةَ رضي الله عنه: أنا آخُذُهُ بِحَقِّهِ، فأخذه فَفَلقَ بِهِ هَامَ المُشْرِكِينَ. رواه مسلم

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) anaelezea kuwa: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alichukua upanga siku ya Vita vya Uhud. Akauliza: “Ni nani atakayeuchukua upanga huu kutoka kwangu?” Kila mmoja wao akanyoosha mkono akisema: Mimi, mimi. Akawauliza: “Ni nani atakayeuchukua kwa haki yake?” Watu wakasita. Abuu Dujaanah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: Mimi nitauchukua kwa haki yake. Akauchukua, akawa anakata vichwa vya washirikina (katika Jihaad). [Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

عن الزبير بن عدي، قَالَ: أتينا أنسَ بن مالك رضي الله عنه فشكونا إِلَيْه مَا نلقى مِنَ الحَجَّاجِ. فَقَالَ: ((اصْبرُوا؛ فَإنَّهُ لا يَأتي عَلَيْكُم زَمَانٌ إلا والَّذِي بَعدَهُ شَرٌّ مِنهُ حَتَّى تَلقَوا رَبَّكُمْ)) سَمِعتُهُ مِنْ نَبِيِّكُمْ صلى الله عليه وسلم. رواه البخاري

Az-Zubayr bin ‘Adiyy amesema: Tulimuendea Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) tukamlalamikia hali tuliyoipata kwa Al-Hajjaaj. Akatuambia: Subirini, hakika haiji zama ila zama zilizokuja baadaye ni shari kulikoni zilizopita mpaka mkutane na Rabb wenu. Maneno haya nimeyasikia kutoka kwa Nabiy wenu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 7

عن أبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((بادِرُوا بِالأَعْمَالِ سَبْعًا، هَلْ تَنْتَظِرُونَ إلا فَقرًا مُنسيًا، أَوْ غِنىً مُطغِيًا، أَوْ مَرَضًا مُفسِدًا، أَوْ هَرَمًا مُفْندًا، أَوْ مَوتًا مُجْهزًا، أَوْ الدَّجَّالَ فَشَرُّ غَائِبٍ يُنْتَظَرُ، أَوْ السَّاعَةَ فالسَّاعَةُ أدهَى وَأَمَرُّ)). رواه الترمذي، وَقالَ: (حديث حسن)

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Zikimbilieni ‘amali njema kabla haijawafikia mambo saba. Je, mnangoja mpaka mfikwe na ufukara wenye kusahaulisha, au utajiri unaopoteza, au maradhi yenye kufisidi, au uzee uletao udhaifu wa akili, au mauti ya ghafla, au Dajjaal ambaye ndio kiumbe muovu asiyepaswa kusubiriwa, au Qiyaamah, na Qiyaamah ndio chenye balaa kubwa na uchungu mwingi zaidi!” [A-Tirmidhiy, na amesema Hadiyth hii ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 8

 أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ يَومَ خيبر: ((لأُعْطِيَنَّ هذِهِ الرَّايَةَ رَجُلًا يُحِبُّ اللهَ وَرَسُولَهُ يَفتَحُ اللهُ عَلَى يَدَيهِ)). قَالَ عُمَرُ رضي الله عنه: مَا أحبَبْتُ الإِمَارَة إلا يَومَئِذٍ، فَتَسَاوَرتُ لَهَا رَجَاءَ أنْ أُدْعَى لَهَا، فَدَعا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عليّ بن أبي طالب رضي الله عنه فَأعْطَاهُ إيَّاهَا، وَقالَ: ((امْشِ وَلا تَلتَفِتْ حَتَّى يَفتَح اللهُ عَلَيكَ)). فَسَارَ عليٌّ شيئًا ثُمَّ وَقَفَ ولم يلتفت فصرخ: يَا رَسُول الله، عَلَى ماذا أُقَاتِلُ النّاسَ؟ قَالَ: ((قاتِلْهُمْ حَتَّى يَشْهَدُوا أنْ لا إله إلا اللهُ، وَأنَّ مُحَمدًا رسولُ الله، فَإِذَا فَعَلُوا ذلك فقَدْ مَنَعوا مِنْكَ دِمَاءهُمْ وَأَمْوَالَهُمْ إلا بحَقِّهَا، وحسَابُهُمْ عَلَى الله)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema siku ya Vita vya Khaybar: “Kwa hakika bendera hii nitampa mtu anayempenda Allaah na Rasuli Wake, Allaah Ataleta ushindi kwa sababu yake.” ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) anasema: Sikuwahi kuupenda uamiri jeshi isipokuwa siku hiyo. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuita ‘Aliy bin Abiy Twaalib, akampa bendera ile. Akamwambia: “Nenda wala usigeuke mpaka Allaah Akupe ushindi.” ‘Aliy akatembea kidogo. Kisha akasimama wala hakugeuka nyuma, akauliza kwa sauti ya juu: Yaa Rasula-Allaah, nipigane na watu juu ya nini? Akamwambia: “Pigana nao mpaka washuhudie kuwa hapana Muabudiwa wa haki ispokuwa Allaah, na Muhammad ni Rasuli wa Allaah. Wakifanya hivyo, wameshahifadhika kutokana na nawe katika damu zao na mali yao ila kwa haki yake, na hisabu yao ipo kwa Allaah.” [Muslim]

 

 

 

Share

011-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kufanya Juhudi

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب المجاهدة

011 – Mlango Wa Kufanya Juhudi

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

وَالَّذِينَ جَاهَدُوا فِينَا لَنَهْدِيَنَّهُمْ سُبُلَنَا ۚ وَإِنَّ اللَّـهَ لَمَعَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٦٩﴾

Na wale waliofanya juhudi kwa ajili Yetu, bila shaka Tutawaongoza njia Zetu. Na hakika Allaah Yu Pamoja na watendao ihsaan. [Al-‘Ankabuwt: 69]

 

وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ ﴿٩٩﴾

Na mwabudu Rabb wako mpaka ikufikie yakini (mauti). [Al-Hijr: 99]

 

وَاذْكُرِ اسْمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلْ إِلَيْهِ تَبْتِيلًا ﴿٨﴾

Na dhukuru Jina la Rabb wako, na jitolee Kwake kwa kujitolea (kikamilifu). [Al-Muzzammil: 8]

 

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

Basi yule atakayetenda kheri (hata kama) uzito wa chembe ya atomu (au mdudu chungu) ataiona. [Zalzalah: 7]

 

وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ وَاسْتَغْفِرُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٠﴾

Na chochote kile cha kheri mnachokadimisha kwa ajili ya nafsi zenu, mtakikuta kwa Allaah. Ni bora, na ujira mkubwa zaidi. Na muombeni Allaah maghfirah, hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu). [Al-Muzzammil: 20]

 

وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣﴾

Na chochote mtoacho katika khayr basi Allaah kwacho ni Mjuzi. [Al-Baqarah: 273]

 

 

Hadiyth – 1

عن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ الله تَعَالَى قَالَ: مَنْ عادى لي وَلِيًّا فَقَدْ آذَنْتُهُ بالحَرْبِ، وَمَا تَقَرَّبَ إِلَيَّ عَبْدي بشَيءٍ أَحَبَّ إلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُ عَلَيهِ، وَمَا يَزَالُ عَبْدِي يَتَقرَّبُ إلَيَّ بالنَّوافِلِ حَتَّى أحِبَّهُ، فَإذَا أَحبَبتُهُ كُنْتُ سَمعَهُ الَّذِي يَسْمَعُ بِهِ، وَبَصَرَهُ الَّذِي يُبْصِرُ بِهِ، ويَدَهُ الَّتي يَبْطِشُ بِهَا، وَرِجْلَهُ الَّتِي يَمْشي بِهَا، وَإنْ سَأَلَني لأُعْطِيَنَّهُ، وَلَئِنِ اسْتَعَاذَنِي لأُعِيذَنَّهُ)). رواه البخاري

Imetoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu ‘anhu) kwamba: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Allaah (Ta’aalaa) Anasema: “Mwenye kumfanyia uadui kipenzi Changu, basi Nimeshamtangazia vita. Mja Wangu hajikurubishi Kwangu ila kwa jambo linalonipendeza mno kulikoni kutenda fardhi nilizomfaradhishia; mja Wangu ataendelea kujikurubisha Kwangu kwa kujitolea mpaka Nimpende. Nitakapompenda, Nitakuwa ni masikilizio yake anayosikilizia, na ni macho yake anayoonea, na ni mkono wake anaoshikia, na ni mguu wake anaotembelea. Akiniomba Nitampa, na akiomba kinga Kwangu Nitamkinga.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 2

عن أنس رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فيما يرويه عن ربّه عز وجل قَالَ: ((إِذَا تَقَربَ العَبْدُ إلَيَّ شِبْرًا تَقَربْتُ إِلَيْه ذِرَاعًا، وَإِذَا تَقَرَّبَ إلَيَّ ذِرَاعًا تَقَربْتُ مِنهُ بَاعًا، وِإذَا أتَانِي يَمشي أتَيْتُهُ هَرْوَلَةً)). رواه البخاري

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Nabiy(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu aliyopokea kutoka kwa Rabb Wake (‘Azza wa Jalla) Anasema: “Mja Wangu atakaponikaribia kwa shubiri, Nitamkaribia kwa dhiraa. Akinikaribia kwa dhiraa, Nitamkaribia kwa pima, na akinijia kwa kutembea nami Nitamkimbilia.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 3

عن ابن عباس رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((نِعْمَتَانِ مَغبونٌ فيهما كَثيرٌ مِنَ النَّاسِ: الصِّحَّةُ، وَالفَرَاغُ)). رواه البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Watu wengi wamepoteza neema mbili: afya na faragha [wakati].” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 4

عن عائشة رَضي الله عنها: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يقُومُ مِنَ اللَّيلِ حَتَّى تَتَفَطَّرَ قَدَمَاهُ فَقُلْتُ لَهُ: لِمَ تَصنَعُ هَذَا يَا رسولَ الله، وَقدْ غَفَرَ الله لَكَ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ؟ قَالَ: ((أَفَلا أُحِبُّ أنْ أكُونَ عَبْدًا شَكُورًا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa): Kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisimama usiku (kuswali) mpaka miguu yake ikivimba. Nikamuuliza: mbona unafanya hivi yaa Rasula-Allaah na hali ya kuwa Allaah Ameshakughufuria dhambi zako zilizotangulia na zitakazokuja? Akajibu: “Kwani sipendelei niwe ni mja mwenye kushukuru?” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

عن عائشة رضي الله عنها، أنَّها قَالَتْ: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا دَخَلَ العَشْرُ أَحْيَا اللَّيلَ، وَأيْقَظَ أهْلَهُ، وَجَدَّ وَشَدَّ المِئْزَر. مُتَّفَقٌ عَلَيه

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa): Alikuwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inapoingia kumi la mwisho (katika mwezi wa Ramadhwaan) hukesha usiku, akiwaamsha watu wa nyumbani kwake akijipinda na kukaza kikoi chake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

عن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((المُؤْمِنُ القَوِيُّ خَيرٌ وَأَحَبُّ إِلَى اللهِ مِنَ المُؤْمِنِ الضَّعيفِ، وَفي كُلٍّ خَيرٌ. احْرِصْ عَلَى مَا يَنْفَعُكَ، واسْتَعِنْ بِاللهِ وَلا تَعْجَزْ. وَإنْ أَصَابَكَ شَيءٌ فَلا تَقُلْ لَوْ أنّي فَعَلْتُ كَانَ كَذَا وَكَذَا، وَلَكِنْ قُلْ: قَدرُ اللهِ، وَمَا شَاءَ فَعلَ؛ فإنَّ لَوْ تَفْتَحُ عَمَلَ الشَّيطَانِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Amesema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) “Muumin mwenye nguvu ni bora na anapendeza mno mbele ya Allaah kulikoni Muumin dhaifu, na katika wote (hao) kuna khayr, fanya bidii katika jambo linalokunufaisha, na uombe msaada kwa Allaah na wala usifanye uvivu. Utakaposibiwa na jambo usiseme; Lau ningalifanya kadhaa na kadhaa, lakini sema: "Qadaru Allaahi wa maa Shaa Fa'ala - Allaah Amejaaliya, na Atakalo Yeye huwa." Kwani kusema; lau, hufungua ‘amali ya shaytwaan.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

عن أبي هريرة رضي الله عنه أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((حُجِبَتِ النَّارُ بالشَّهَواتِ، وَحُجِبَتِ الجَنَّةُ بِالمَكَارِهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Moto umezunguka kwa matamanio, na Jannah imezungukwa kwa machukivu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

عن أبي عبد الله حُذَيفَةَ بنِ اليمانِ رضي الله عنهما، قَالَ: صَلَّيْتُ مَعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ لَيلَةٍ فَافْتَتَحَ البقَرَةَ، فَقُلْتُ: يَرْكَعُ عِنْدَ المائَةِ، ثُمَّ مَضَى. فَقُلْتُ: يُصَلِّي بِهَا في ركعَة فَمَضَى، فقُلْتُ: يَرْكَعُ بِهَا، ثُمَّ افْتَتَحَ النِّسَاءَ فَقَرَأَهَا، ثُمَّ افْتَتَحَ آلَ عِمْرَانَ فَقَرَأَهَا، يَقرَأُ مُتَرَسِّلًا: إِذَا مَرَّ بآية فِيهَا تَسبيحٌ سَبَّحَ، وَإذَا مَرَّ بسُؤَالٍ سَأَلَ، وَإذَا مَرَّ بتَعَوُّذٍ تَعَوَّذَ، ثُمَّ رَكَعَ، فَجَعَلَ يَقُولُ: ((سُبْحَانَ رَبِّيَ العَظِيمِ)) فَكَانَ رُكُوعُهُ نَحوًا مِنْ قِيَامِهِ، ثُمَّ قَالَ: ((سَمِعَ اللهُ لِمَنْ حَمِدَهُ ربَّنا ولك الحمد)) ثُمَّ قَامَ قِيامًا طَويلًا قَريبًا مِمَّا رَكَعَ، ثُمَّ سَجَدَ، فَقَالَ: ((سُبْحَانَ رَبِّيَ الأَعْلَى)) فَكَانَ سُجُودُهُ قَريبًا مِنْ قِيَامِهِ. رواه مسلم

Abuu ‘Abdillaah, Hudhayfah bin Al-Yamaani (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Usiku mmoja niliswali na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaanza kusoma Suwratu Al-Baqarah. Nikasema (moyoni) atarukuu katika Aayah ya mia. Lakini akaendelea, nikasema atamaliza Suwrah yote katika rakaah moja. Akaendelea. Nikasema: Atarukuu akimaliza Suwrah hii, halafu akaianza Suwratu An-Nisaa. Akaisoma yote, kisha akaianza Suwratu Aal-‘Imraan, akaisoma yote. Alikuwa akisoma taratibu, anapoisoma Aayah yenye kumsabih Allaah, yeye humsabbih, na anaposoma Aayah ya kuomba yeye huomba, na anaposoma Aayah ya kujikinga yeye hujikinda. Kisha akarukuu na akawa anasema: “Subhaana Rabbiyal-‘Adhwiym - Ametakasika Rabb wangu Adhimu.” Rukuu yake ikawa inafanana na kisimamo chake, kisha akasema: “Sami’a Allaahu liman Hamidah Rabbanaa walakal Hamd - Allaah Amemsikia mwenye kumuhimidi, Ee Rabb wetu, ni Zako Wewe tu sifa njema.” Kisha akasimama kisimamo kirefu kinachokaribiana na rukuu, kisha akasujudu, akasema: “Subhaana Rabbiyal-A’laa - Ametakasima Rabb Aliye juu.” Sijdah yake yake ikakaribiana na kisimamo chake. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

عن ابن مسعود رضي الله عنه قَالَ: صَلَّيْتُ مَعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم لَيلَةً، فَأَطَالَ القِيامَ حَتَّى هَمَمْتُ بأمْرِ سُوءٍ! قيل: وَمَا هَمَمْتَ بِهِ؟ قَالَ: هَمَمْتُ أنْ أجْلِسَ وَأَدَعَهُ. مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: “Usiku mmoja niliswali na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akarefusha kisimamo hata nikafikiria kutenda jambo baya. Akaulizwa: kwani ulifikiri kufanya nini? Akajibu: Nilifikiria nikae chini na nimuache Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

عن أنس رضي الله عنه عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((يَتْبَعُ المَيتَ ثَلاَثَةٌ: أهْلُهُ وَمَالُهُ وَعَملُهُ، فَيَرجِعُ اثنَانِ وَيَبْقَى وَاحِدٌ: يَرجِعُ أهْلُهُ وَمَالُهُ، وَيَبقَى عَملُهُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Mambo matatu humfuata maiti: Familia yake, mali yake na ‘amali zake. Mawili kati ya hayo hurejea nayo na kubakia na moja; familia na mali hurejea na ikabakia ‘amali yake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

 عن ابن مسعود رضي الله عنه قَالَ: قَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((الجَنَّةُ أَقْرَبُ إِلَى أَحَدِكُمْ مِنْ شِرَاكِ نَعْلِهِ، وَالنَّارُ مِثلُ ذلِكَ)). رواه البخاري

‘Abdullaa bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Jannah ipo karibu zaidi kwa mmoja wenu kulikoni mkanda wa kiatu chake, na moto ni hivyo hivyo.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 12

عن أبي فِراسٍ ربيعةَ بنِ كعبٍ الأسلميِّ خادِمِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، ومن أهلِ الصُّفَّةِ رضي الله عنه، قَالَ: كُنْتُ أبِيتُ مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم فآتِيهِ بِوَضُوئِهِ وَحَاجَتِهِ، فَقَالَ: ((سَلْنِي)) فقُلْتُ: اسْأَلُكَ مُرَافَقَتَكَ في الجَنَّةِ. فَقَالَ: ((أَوَ غَيرَ ذلِكَ؟)) قُلْتُ: هُوَ ذَاكَ، قَالَ: ((فأَعِنِّي عَلَى نَفْسِكَ بِكَثْرَةِ السُّجُودِ)). رواه مسلم

Abuu Firaas, Rabi’ bin Ka’b Al-Aslamiy mtumishi wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na ni katika watu wa suffah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilikuwa nikilala kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikimpelekea maji ya kutawadhia na mahitajio yake mengineo. Akaniambia: “Niombe.” Nikamwambia: Nakuomba kuwa na wewe Jannah. Akaniuliza: “Una lingine?” Nikamjibu: Ni hilo tu. Akaniambia: “Nisaidie juu nafsi yako kusujudu kwa wingi.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 13

عن أبي عبد الله، ويقال: أَبُو عبد الرحمن ثوبان - مولى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم رضي الله عنه، قَالَ: سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: ((عَلَيْكَ بِكَثْرَةِ السُّجُودِ؛ فَإِنَّكَ لَنْ تَسْجُدَ للهِ سَجْدَةً إلا رَفَعَكَ اللهُ بِهَا دَرجَةً، وَحَطَّ عَنكَ بِهَا خَطِيئةً)). رواه مسلم

Abuu ‘Abdillaah, pia huitwa Abuu ‘Abdir-Rahmaan, Thawbaan muachwa huru wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Kithirisha kusujudu kwa wingi, kwani wewe hutosujudu sijdah (moja) isipokuwa Allaah Atakupandisha daraja kwa sijdah hiyo, na Atakuondoshea dhambi kwa sijdah hiyo.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 14

عن أَبي صَفوان عبد الله بنِ بُسْرٍ الأسلمي رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((خَيرُ النَّاسِ مَنْ طَالَ عُمُرهُ، وَحَسُنَ عَمَلُهُ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن))

Abuu Swafwaan, ‘Abdullaah bin Busri Al-Aslamiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mbora katika watu ni yule ambaye umri wake umerefuka na ‘amali zake zikatangamaa.” [At-Tirmidhiy, na amsema: Hadiyth hii ni Hasan]

 

 

Hadiyth -15

عن أنس رضي الله عنه، قَالَ: غَابَ عَمِّي أَنَسُ بْنُ النَّضْرِ رضي الله عنه عن قِتالِ بدرٍ، فَقَالَ: يَا رسولَ الله، غِبْتُ عَنْ أوّل قِتال قَاتَلْتَ المُشْرِكِينَ، لَئِن اللهُ أشْهَدَنِي قِتَالَ المُشركِينَ لَيُرِيَنَّ اللهُ مَا أصْنَعُ.

فَلَمَّا كَانَ يَومُ أُحُدٍ انْكَشَفَ المُسْلِمونَ، فَقَالَ: اللَّهُمَّ أعْتَذِرُ إلَيْكَ مِمَّا صَنَعَ هؤُلاءِ- يعني: أصْحَابهُ- وأبْرَأُ إلَيْكَ مِمَّا صَنَعَ هؤُلاءِ- يَعني: المُشركِينَ- ثُمَّ تَقَدَّمَ فَاسْتَقْبَلهُ سَعدُ بْنُ مُعاذٍ، فَقَالَ: يَا سعدَ بنَ معاذٍ، الجَنَّةُ وربِّ الكعْبَةِ إنِّي أجِدُ ريحَهَا منْ دُونِ أُحُدٍ. قَالَ سعدٌ: فَمَا اسْتَطَعتُ يَا رسولَ الله مَا صَنَعَ!

قَالَ أنسٌ: فَوَجَدْنَا بِهِ بِضْعًا وَثَمانينَ ضَربَةً بالسَّيفِ، أَوْ طَعْنةً بِرمْحٍ، أَوْ رَمْيَةً بسَهْمٍ، وَوَجَدْنَاهُ قَدْ قُتِلَ وَمَثَّلَ بِهِ المُشْرِكونَ فما عَرَفهُ أَحَدٌ إلا أُخْتُهُ بِبَنَانِهِ.

قَالَ أنس: كُنَّا نَرَى أَوْ نَظُنُّ أن هذِهِ الآية نزلت فِيهِ وفي أشباهه: {مِنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللهَ عَلَيْهِ} [الأحزاب: 23] إِلَى آخِرها. مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Ammiy yangu Anas bin Nadhwr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) hakuwepo katika Vita vya Badr. Akasema: Yaa Rasula-Allaah, nilighibu katika vita vya kwanza ulivyopigana na washirikina. Wa-Allaahi! Allaah Akinijaalia kuhudhuria katika kupigana na washirikina, Atawadhihirishia (washirikina) kile nitakachofanya. Siku ya Vita vya Uhud, Waislamu walikimbia akaomba: Ee Rabb, nakuomba msamaha kwa yale waliyoyafanya hawa (watu wake), na najitenga kwa yale waliyoyafanya washirikina. Halafu akaenda mbele, akakabiliwa na Sa’d bin Mu’aadh, akamwambia: Ee Sa’d bin Mu’aadh, Jannah! Naapa kwa Rabb wa Al-Ka’bah, naisikia harufu yake chini ya jabali la Uhud. Sa’d akasema: Sina uwezo wa kukueleza namna alivyofanya Anas bin An-Nadhwr yaa Rasula-Allaah. Anas bin Maalik anaelezea: Tukamkuta amepigwa zaidi ya mapigo themanini ya mapanga, au kudungwa mkuki au kurushia mshale. Tulimkuta ameshauliwa na washirikina na wamemkata pua na masikio yake. Basi hakuna aliyeweza kumtambua isipokuwa dada yake, alimtambua kwa ncha ya vidole vyake. Anas bin Maalik anaeleza: Tulikuwa tukiona au tukidhani Aayah hii Suwratu Al-Ahzaab: 23. Ilikuwa imeshuka kwa sababu yake na mfano wake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّـهَ عَلَيْهِ ۖ

Miongoni mwa Waumini, wapo wanaume wamesadikisha yale waliyomuahidi Allaah. [Al-Ahzaab: 23]  

 

 

Hadiyth – 16

عن أبي مسعود عقبة بن عمرو الأنصاري البدري رضي الله عنه قَالَ: لَمَّا نَزَلَتْ آيةُ الصَّدَقَةِ كُنَّا نُحَامِلُ عَلَى ظُهُورِنَا، فَجَاءَ رَجُلٌ فَتَصَدَّقَ بِشَيءٍ كَثيرٍ، فقالوا: مُراءٍ، وَجَاءَ رَجُلٌ آخَرُ فَتَصَدَّقَ بِصَاعٍ، فقالُوا: إنَّ اللهَ لَغَنيٌّ عَنْ صَاعِ هَذَا! فَنَزَلَتْ: {الَّذِينَ يَلْمِزُونَ الْمُطَّوِّعِينَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ فِي الصَّدَقَاتِ وَالَّذِينَ لا يَجِدُونَ إِلا جُهْدَهُمْ} [التوبة: 79]. مُتَّفَقٌ عَلَي

Kutoka kwa Abuu Mas'uwd ‘Uqbah bin ‘Amruw bin Al-Answaariy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Ilipoteremka Aayah ya swadaqah tulikuwa tukibeba mizigo kwa migongo yetu (pato lake tukitolea swadaqah). Akaja mtu, akatoa swadaqah mali nyingi. Wanafiki wakasema: Anajionyesha. Akaja mtu mwingine akatoa swadaqah kiasi cha pishi. Wanafiki wakasema: Allaah hana haja ya pishi la huyu! Ikashuka Aayah hii katika Suwrat At-Tawbah: 79. [Al-Bukhaariy na Muslim]

الَّذِينَ يَلْمِزُونَ الْمُطَّوِّعِينَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ فِي الصَّدَقَاتِ وَالَّذِينَ لَا يَجِدُونَ إِلَّا جُهْدَهُمْ

Wale wanaowafedhehesha wenye kujitolea kwa hiari katika kutoa swadaqah miongoni mwa Waumini, na (pia) wale wasiopata (kitu cha kutoa) isipokuwa juhudi zao. [At-Tawbah: 79]

 

 

Hadiyth – 17

عن أبي ذر جندب بن جُنادة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فيما يروي عن اللهِ تَبَاركَ وتعالى، أنَّهُ قَالَ: ((يَا عِبَادي، إنِّي حَرَّمْتُ الظُلْمَ عَلَى نَفْسي وَجَعَلْتُهُ بيْنَكم مُحَرَّمًا فَلا تَظَالَمُوا.

يَا عِبَادي، كُلُّكُمْ ضَالّ إلا مَنْ هَدَيْتُهُ فَاستَهدُوني أهْدِكُمْ.

يَا عِبَادي، كُلُّكُمْ جَائِعٌ إلا مَنْ أطْعَمْتُهُ فَاستَطعِمُوني أُطْعِمْكُمْ.

يَا عِبَادي، كُلُّكُمْ عَارٍ إلا مَنْ كَسَوْتُهُ فاسْتَكْسُونِي أكْسُكُمْ.

يَا عِبَادي، إنَّكُمْ تُخْطِئُونَ باللَّيلِ وَالنَّهارِ وَأَنَا أغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا، فَاسْتَغْفِرُوني أغْفِرْ لَكُمْ.

يَا عِبَادي، إنَّكُمْ لَنْ تَبْلُغوا ضُرِّي فَتَضُرُّوني، وَلَنْ تَبْلُغُوا نَفعِي فَتَنْفَعُوني.

يَا عِبَادي، لَوْ أنَّ أوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجنَّكُمْ كَانُوا عَلَى أتْقَى قَلْبِ رَجُلٍ وَاحِدٍ مِنْكُمْ مَا زَادَ ذلِكَ في مُلكي شيئًا.

يَا عِبَادي، لَوْ أنَّ أوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجنَّكُمْ كَانُوا عَلَى أفْجَرِ قَلْبِ رَجُلٍ وَاحِدٍ مَا نَقَصَ ذلِكَ من مُلكي شيئًا.

يَا عِبَادي، لَوْ أنَّ أوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجنَّكُمْ قَامُوا في صَعِيدٍ وَاحِدٍ فَسَألُوني فَأعْطَيتُ كُلَّ إنْسَانٍ مَسْألَتَهُ مَا نَقَصَ ذلِكَ مِمَّا عِنْدِي إلا كما يَنْقصُ المِخْيَطُ إِذَا أُدْخِلَ البَحْرَ.

يَا عِبَادي، إِنَّمَا هِيَ أعْمَالُكُمْ أُحْصِيهَا لَكُمْ ثُمَّ أوَفِّيكُمْ إِيَّاهَا، فَمَنْ وَجَدَ خَيرًا فَلْيَحْمَدِ الله وَمَنْ وَجَدَ غَيْرَ ذلِكَ فَلا يَلُومَنَّ إلا نَفْسَهُ)).

قَالَ سعيد: كَانَ أَبُو إدريس إِذَا حَدَّثَ بهذا الحديث جَثا عَلَى رُكبتيه. رواه مسلم

Abuu Dharr, Jundub bin Junaadah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika aliyopokea kutoka kwa Rabb wake (Ta’aalaa) Anasema: “Enyi waja Wangu, hakika Nimeharamisha dhulma, na Nimeijaalia ni haramu miongoni mwenu; kwa hivyo msidhulumiane. Enyi waja Wangu, nyote mmepotea isipokuwa Niliyemuongoza, kwa hivyo Niombeni uongofu Nami Nitawaongoa. Enyi waja Wangu, nyote mna njaa isipokuwa niliyemlisha, kwa hivyo niombeni chakula Nami Nitawalisha. Enyi waja Wangu, nyote mpo uchi isipokuwa Niliyemvisha, kwa hivyo niombeni Niwavishe, Nami Nitawavisha. Enyi waja Wangu, nyinyi mnakosea usiku na mchana, Nami Naghufuria dhambi zote; kwa hivyo niombeni maghfirah Nami Nitawaghufuria. Enyi waja Wangu, nyinyi hamuwezi kunidhuru wala hamuwezi kuninufaisha. Enyi waja Wangu, lau wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, wana Aadam wenu na majini wenu wangalikuwa sawa na moyo wa mchaji Allaah mno miongoni mwenu, basi hilo lisingalipunguza chochote katika Ufalme Wangu. Enyi waja Wangu, lau wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, wana Aadam wenu na majini wenu wangalikuwa sawa na moyo wa mtu muovu mno miongoni mwenu, basi hilo lisingalipunguza chochote katika Ufalme Wangu. Enyi waja Wangu, lau wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, wana Aadam wenu na majini wenu wangesimama katika uwanja mmoja, wakaniomba; Nami Nikampa kila mmoja ombi lake, isingalipungua chochote katika Nilichowapa isipokuwa ni kama vile sindano iliyochovywa baharini inavyopunguza maji. Enyi waja Wangu, hakika Nimezidhibiti ‘amali zenu, kisha Nitawalipa; atakayekuta khayr amuhimidi Allaah, na atakayekuta kinyume chake basi asilaumu isipokuwa ailaumu nafsi yake.” Sa’d (ambaye ni mpokezi wa Hadiyth hii) amesema: Abuu Idriys alikuwa, anapohadithia Hadiyth hii, akikaa kwa kupiga magoti. [Muslim]

 

 

Share

012-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Mahimizo Ya Kuzidisha Kutenda Khayr Mwisho Wa Umri

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الحث عَلَى الازدياد من الخير في أواخر العمر

012 – Mlango Wa Mahimizo Ya Kuzidisha Kutenda Khayr Mwisho Wa Umri

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

أَوَلَمْ نُعَمِّرْكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن تَذَكَّرَ وَجَاءَكُمُ النَّذِيرُ ۖ

“Je, kwani Hatukukupeni umri wa kukumbuka mwenye kukumbuka humo? [Faatwir: 37]

 

قَالَ ابن عباس والمُحَقِّقُونَ: أَو لَمْ نُعَمِّرْكُمْ سِتِّينَ سَنَةً؟ وَيُؤَيِّدُهُ الحديث الَّذِي سنذْكُرُهُ إنْ شاء الله تَعَالَى، وقيل: معناه ثماني عَشْرَة سَنَةً، وقيل: أرْبَعينَ سَنَةً، قاله الحسن والكلبي ومسروق ونُقِلَ عن ابن عباس أيضًا. وَنَقَلُوا أنَّ أَهْلَ المدينَةِ كانوا إِذَا بَلَغَ أَحَدُهُمْ أربْعينَ سَنَةً تَفَرَّغَ للعِبادَةِ

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) na ‘Ulamaa wenye tahakiki wamesema: “Je, hatukuwapa umri wa miaka sitini?” Kauli hii inatiliwa nguvu na Hadiyth itakayokuja in shaa Allaah (Ta’aalaa). Na imesemekana kuwa, maana yake ni: Miaka kumi na nane, na pia imesemekana ni miaka arobaini. Kauli hii imesemwa na Al-Hasan, Al-Kalbiy na Masruwq. Vile vile imenukuliwa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas wakaeleza kuwa: Watu wa Madiynah ilikuwa mtu akitimiza umri wa miaka arobaini, hujihusisha na ‘Ibaadah pekee.

 

 

Hadiyth – 1

 

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((أعْذَرَ الله إِلَى امْرِئٍ أَخَّرَ أجَلَهُ حَتَّى بَلَغَ سِتِّينَ سَنَةً)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Hakumbakishia udhuru mtu Aliyemuakhirishia mauti yake hata akafikia umri wa miaka sitini.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 2

 

عن ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: كَانَ عمر رضي الله عنه يُدْخِلُنِي مَعَ أشْيَاخِ بَدرٍ فكأنَّ بَعْضَهُمْ وَجَدَ في نفسِهِ، فَقَالَ: لِمَ يَدْخُلُ هَذَا معنا ولَنَا أبْنَاءٌ مِثلُهُ؟! فَقَالَ عُمَرُ: إنَّهُ منْ حَيثُ عَلِمْتُمْ! فَدعانِي ذاتَ يَومٍ فَأدْخَلَنِي مَعَهُمْ فما رَأيتُ أَنَّهُ دعاني يَومَئذٍ إلا لِيُرِيَهُمْ، قَالَ: مَا تقُولُون في قولِ الله تعالى: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} [النصر: 1].

فَقَالَ بعضهم: أُمِرْنَا نَحْمَدُ اللهَ وَنَسْتَغْفِرُهُ إِذَا نَصَرنَا وَفَتحَ عَلَيْنَا، وَسَكتَ بَعْضُهُمْ فَلَمْ يَقُلْ شَيئًا. فَقَالَ لي: أَكَذلِكَ تقُول يَا ابنَ عباسٍ؟ فقلت: لا. قَالَ: فما تقول؟ قُلْتُ: هُوَ أجَلُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم أعلَمَهُ لَهُ، قَالَ: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} وذلك علامةُ أجَلِكَ {فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا} [النصر: 3].

فَقَالَ عمر رضي الله عنه: مَا أعلم مِنْهَا إلا مَا تقول. رواه البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikuwa akiniingiza katika mashauri pamoja na wazee waliopigana katika Vita vya Badr, basi kana kwamba mmoja wao alikasirika moyoni mwake, akauliza: Mbona huyu anaingia pamoja na sisi na wakati sisi tunao watoto kama yeye? ‘Umar akamwambia: Huyu ni kama mnavyomjua! Siku moja akaniita na kuniingiza pamoja nao. Sikuona siku hiyo kuwa ameniita ila ni kwa ajili ya kutaka kuwaonesha wao. Akawauliza: Mnasemaje kuhusu kauli ya Allaah “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi?” Baadhi yao walisema: Tumeamriwa tumuhimidi Allaah na tumuombe maghfirah Allaah Atakapotunusuru na Kutupa ushindi. Baadhi yao walinyamaza wala hawakusema kitu. Akaniuliza: Nawe unasema hivyo hivyo ee Ibn ‘Abbaas? Nikamjibu: Hapana. Akasema: Unasemaje? Nikamwambia: Hayo ni mauti ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Allaah Alimjulisha Akamwambia: “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi.” Hiyo ndiyo alama ya mauti yako, Basi sabbih kwa Himidi za Rabb wako na muombe maghfirah; hakika Yeye daima ni Tawwaabaa (Mwingi mno wa kupokea tawbah).” [An-Naswr]

‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: Hivyo ulivyosema ndivyo ninavyojua. [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 3

 

عن عائشة رضي الله عنها، قَالَتْ: مَا صلّى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم صلاةً بَعْدَ أنْ نَزَلتْ عَلَيهِ: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} إلا يقول فِيهَا: ((سُبحَانَكَ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

وفي رواية في الصحيحين عنها: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُكْثِرُ أنْ يقُولَ في ركُوعِه وسُجُودهِ: ((سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وبِحَمدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي)).

وفي رواية لمسلم: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُكثِرُ أنْ يَقُولَ قَبلَ أنْ يَمُوتَ: {إذا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} … إِلَى آخِرِ السورة.

وفي رواية لَهُ: كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يُكثِرُ مِنْ قَولِ: ((سبْحَانَ اللهِ وَبِحَمدِهِ أسْتَغفِرُ اللهَ وأتُوبُ إِلَيْهِ)). قَالَتْ: قُلْتُ: يَا رسولَ اللهِ، أَراكَ تُكثِرُ مِنْ قَولِ سُبحَانَ اللهِ وَبِحَمدهِ أسْتَغْفِرُ اللهَ وأتُوبُ إِلَيْه؟ فَقَالَ: ((أخبَرَني رَبِّي أنِّي سَأرَى عَلامَةً في أُمَّتي فإذا رَأيْتُها أكْثَرْتُ مِنْ قَولِ: سُبْحَانَ اللهِ وبِحَمدهِ أسْتَغْفرُ اللهَ وَأَتُوبُ إِلَيْه فَقَدْ رَأَيْتُهَا: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} فتح مكّة، {وَرَأَيْتَ النَّاسَ يَدْخُلُونَ فِي دِينِ اللهِ أَفْوَاجًا * فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا}))

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakuswali Swalaah yoyote baada ya kuteremka Suwrah hii “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi.” Isipokuwa alikuwa akisema: “Kutakasika ni Kwako Rabb wetu, Ee Rabb nisamehe.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Swahiyh Al-Bukhaariy na Swahiyh Muslim; Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema katika rukuu yake na sujuwd yake: “Kutakasika ni Kwako Rabb wetu, Ee Rabb nisamehe.”

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema kabla ya kuondoka kwake duniani. “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi.” Mpaka mwisho wa Aayah. [An-Naswr]

Riwaayah nyingine tena ya Muslim imesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema: “Kutakasika ni kwa Allaah na shukurani zote ni Zake, namuomba Allaah msamaha na ninatubia Kwake.” Nikamuuliza Ee Rasuli wa Allaah, nakuona unakithirisha kusema: Kutakasika ni kwa Allaah na shukurani zote ni Zake, namuomba Allaah msamaha na ninatubia Kwake. Akajibu: Rabb wangu Ameniambiwa kuwa mimi nitaona alama katika Ummah wangu, nitakapoiona nikithirishe kusema: “Kutakasika ni kwa Allaah na shukurani zote ni Zake, namuomba Allaah msamaha na ninatubia Kwake.” Nami nimeshaiona: “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi, na utawaona watu wanaingia katika Dini ya Allaah makundi makundi, basi sabbih kwa Himidi za Rabb (Mola) wako na muombe maghfirah; hakika Yeye daima ni Tawwaabaa (Mwingi mno wa kupokea tawbah).” [An-Naswr]

 

 

Hadiyth – 4

 

عن أنس رضي الله عنه قَالَ: إنَّ اللهَ عز وجل تَابَعَ الوَحيَ عَلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم قَبلَ وَفَاتهِ حَتَّى تُوُفِّيَ أكْثَرَ مَا كَانَ الوَحْيَ عَلَيِّه. مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Allaah Alimteremshia Wahyi Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa wingi kabla ya kufariki kwake, alipofariki Wahyi ulikuwa umeshateremka mwingi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

 

عن جابر رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((يُبْعَثُ كُلُّ عَبْدٍ عَلَى مَا مَاتَ عَلَيهِ)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila mja atafufuliwa katika hali aliyokufa nayo.” [Muslim]

 

 

 

 

 

Share

013-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ubainifu Wa Njia Nyingi Za Khayr

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب في بيان كثرة طرق الخير

13 – Mlango Wa Ubainifu Wa Njia Nyingi Za Khayr

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢١٥﴾

Na lolote mlifanyalo katika khayr basi hakika Allaah kwa hilo ni Mjuzi.[Al-Baqarah: 215]

 

وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ﴿١٩٧﴾

Na lolote mlifanyalo katika ya khayr Allaah Analijua. [Al-Baqarah: 197]

 

فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

Basi yule atakayetenda kheri uzito wa chembe ya atomu (au mdudu chungu) ataiona. [Az-Zalzalah: 7]

 

مَنْ عَمِلَ صَالِحًا فَلِنَفْسِهِ ۖ ﴿١٥﴾

Yeyote atendaye jema, basi ni kwa ajili ya nafsi yake. [Al-Jaathiyah: 15]

 

 

Hadiyh – 1

 

عن أبي ذر جُنْدبِ بنِ جُنَادَةَ رضي الله عنه قَالَ: قُلْتُ: يَا رسولَ الله، أيُّ الأعمالِ أفْضَلُ؟ قَالَ: ((الإيمانُ باللهِ وَالجِهادُ في سَبيلِهِ)). قُلْتُ: أيُّ الرِّقَابِ أفْضَلُ؟ قَالَ: ((أنْفَسُهَا عِنْدَ أهلِهَا وَأكثَرهَا ثَمَنًا)). قُلْتُ: فإنْ لَمْ أفْعَلْ؟ قَالَ: ((تُعِينُ صَانِعًا أَوْ تَصْنَعُ لأَخْرَقَ)). قُلْتُ: يَا رَسُول الله، أرأيْتَ إنْ ضَعُفْتُ عَنْ بَعْضِ العَمَلِ؟ قَالَ: ((تَكُفُّ شَرَّكَ عَنِ النَّاسِ؛ فإنَّهَا صَدَقَةٌ مِنْكَ عَلَى نَفْسِكَ)). مُتَّفَقٌ عليه

Abuu Dharr, Jundub bin Junaadah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimuuliza Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Ni ‘amali gani bora zaidi? Akajibu: “Ni kumuamini Allaah na kupigana Jihaad katika njia Yake.” Nikamuuliza: Ni kupi kuacha huru mtumwa kuliko bora zaidi? Akajibu: “Ni yule aliye mbora na mzuri kwa watu wake na mwenye thamani kubwa.” Nikamuuliza: Nisipoweza? Akajibu: “Umsaidie mwenye kuhitaji au umsaidie kazi yule ambaye hana ujuzi nayo.” Nikamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah, nieleze iwapo sitoweza kufanya baadhi ya ‘amali? Akajibu: “Utaizuia shari yako isiwafikie watu; kufanya hivyo ni swadaqah juu ya nafsi yako.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

 

عن أبي ذر أيضًا رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((يُصْبحُ عَلَى كُلِّ سُلامَى منْ أَحَدِكُمْ صَدَقةٌ: فَكُلُّ تَسبيحَةٍ صَدَقَةٌ، وَكُلُّ تَحمِيدةٍ صَدَقَة، وَكُلُّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةٌ، وَكُلُّ تَكبيرَةٍ صَدَقَةٌ، وَأمْرٌ بِالمعرُوفِ صَدَقةٌ، ونَهيٌ عَنِ المُنْكَرِ صَدَقةٌ، وَيُجزئُ مِنْ ذلِكَ رَكْعَتَانِ يَركَعُهُما مِنَ الضُّحَى)). رواه مسلم

Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hupambaukiwa kila kiungo cha mmoja wenu kulazimika kutoa swadaqah. Kila Tasbiyh (Subhaana Allaah) ni swadaqah, kila Tahmiyd (AlhamduliLLaah) ni swadaqah, kila Tahliyl (Laa ilaaha illa-Allaah) ni swadaqah, na kila Takbiyr (Allaahu Akbar) ni swadaqah. Kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza maovu ni swadaqah. Yote haya hutosheleza na rakaa mbili za Dhwuhaa mtu anapoziswali.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((عُرِضَتْ عَلَيَّ أعْمَالُ أُمَّتِي حَسَنُهَا وَسَيِّئُهَا فَوَجَدْتُ في مَحَاسِنِ أعْمَالِهَا الأذَى يُمَاطُ عَنِ الطَّريقِ، وَوَجَدْتُ في مَسَاوِئِ أعمَالِهَا النُّخَاعَةُ تَكُونُ في المَسْجِدِ لا تُدْفَنُ)). رواه مسلم

Abuu Dharr (RadhwiyaAllaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Nilionyeshwa ‘amali nzuri na mbaya za Ummah wangu. Nikaona katika jumla ya mema yao ni kuondoshwa takataka njiani, na nikaona katika jumla ya mabaya yao ni kutema mate Masjid na wala yasifunikwe.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

 

عَنْهُ: أنَّ ناسًا قالوا: يَا رَسُولَ الله، ذَهَبَ أهلُ الدُّثُور بالأُجُورِ، يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ، وَيَتَصَدَّقُونَ بِفُضُولِ أمْوَالِهِمْ، قَالَ: ((أَوَلَيسَ قَدْ جَعَلَ اللهُ لَكُمْ مَا تَصَدَّقُونَ بِهِ: إنَّ بِكُلِّ تَسْبِيحَةٍ صَدَقةً، وَكُلِّ تَكبيرَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَحمِيدَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةً، وَأمْرٌ بالمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ، وَنَهيٌ عَنِ المُنْكَرِ صَدَقَةٌ، وفي بُضْعِ أَحَدِكُمْ صَدَقَةٌ)) قالوا: يَا رسولَ اللهِ، أيَأتِي أَحَدُنَا شَهْوَتَهُ وَيَكُونُ لَهُ فِيهَا أجْرٌ؟ قَالَ: ((أرَأيتُمْ لَوْ وَضَعَهَا في حَرامٍ أَكَانَ عَلَيهِ فِيهَا وِزرٌ؟ فكذَلِكَ إِذَا وَضَعَهَا في الحَلالِ كَانَ لَهُ أَجْرٌ)). رواه مسلم

Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Baadhi ya watu walimuendea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, matajiri wamechukua thawabu zote. Wao wanaswali kama tunavyoswali, wanafunga kama tunavyofunga na wanatoa swadaqah katika mali yao iliyobaki. Akawaambia: “Nanyi pia Allaah Amewajaalia cha kutolea swadaqah; kila Tasbiyh (Subhaana Allaah) ni swadaqah, na kila Takbiyr (Allaahu Akbar) ni swadaqah, na kila Tahliyl (Laa ilaaha illa-Allaah) ni swadaqah, na kila Tahmiyd (AlhamduliLLaah) ni swadaqah. Kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza maovu ni swadaqah, na mmoja wenu kujimai na mke wake ni swadaqah.” Wakauliza: Ee Rasuli wa Allaah, mmoja wetu anaenda kufanya matamanio yake na awe amepata swadaqah? Akawaambia: “Nielezeni lau kitendo kile atakifanya kwa njia ya haraam, si atapata dhambi? Vile vile atakapokitenda kwa njia ya halaal atakuwa na ujira.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ لي النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((لاَ تَحْقِرنَّ مِنَ المَعرُوفِ شَيئًا وَلَوْ أنْ تَلقَى أخَاكَ بِوَجْهٍ طَليقٍ)). رواه مسلم

Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alinambia: “Usidharau chochote katika wema hata kama ni kumtazama ndugu yako (Muislamu) kwa uso wenye bashasha.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

 

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((كُلُّ سُلامَى مِنَ النَّاسِ عَلَيهِ صَدَقَةٌ، كُلَّ يَومٍ تَطلُعُ فِيهِ الشَّمْسُ: تَعْدِلُ بَينَ الاثْنَينِ صَدَقةٌ، وتُعِينُ الرَّجُلَ في دَابَّتِهِ، فَتَحْمِلُهُ عَلَيْهَا أَوْ تَرفَعُ لَهُ عَلَيْهَا مَتَاعَهُ صَدَقَةٌ، وَالكَلِمَةُ الطَيِّبَةُ صَدَقَةٌ، وبكلِّ خَطْوَةٍ تَمشيهَا إِلَى الصَّلاةِ صَدَقَةٌ، وتُميطُ الأذَى عَنِ الطَّريقِ صَدَقَةٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

ورواه مسلم أيضًا من رواية عائشة رَضي الله عنها، قَالَتْ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّهُ خُلِقَ كُلُّ إنْسان مِنْ بَنِي آدَمَ عَلَى سِتِّينَ وثلاثمائة مفْصَل، فَمَنْ كَبَّرَ اللهَ، وحَمِدَ الله، وَهَلَّلَ اللهَ، وَسَبَّحَ الله، وَاسْتَغْفَرَ الله، وَعَزَلَ حَجَرًا عَنْ طَريقِ النَّاسِ، أَوْ شَوْكَةً، أَوْ عَظمًا عَن طَريقِ النَّاسِ، أَوْ أمَرَ بمَعْرُوف، أَوْ نَهَى عَنْ منكَر، عَدَدَ السِّتِّينَ والثَّلاثِمائَة فَإنَّهُ يُمْسِي يَومَئِذٍ وقَدْ زَحْزَحَ نَفسَهُ عَنِ النَّارِ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Viungo vyote vya wana Aadam vinawajibia kutoa swadaqah kwa kila siku inapochomozewa na jua. Kusuluhisha kwa uadilifu baina ya watu wawili ni swadaqah. Kumsaidia mtu juu ya mnyama wake ukampandisha au ukamnyanyulia mzigo wake ni swadaqah, kuongea neno zuri ni swadaqah, kila hatua unayoipiga kwenda Masjid ni swadaqah na kuondoa takataka njani ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Vile vile Muslim ameipokea Hadiyth hii kutoka katika riwaayah ya; ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika kila mwana Aadam ameumbwa kwa viungo (vilivyotengana) mia tatu na sitini, atakayemtukuza Allaah (kwa Allaahu Akbar), akamhimidi Allaah (AlhamduliLLaah), akampwekesha Allaah (laa ilaaha illa-Allaah) akamsabih Allaah (Subhaana Allaah), akamuomba Allaah maghfirah (Astaghfiru-Allaah), akaondoa jiwe katika njia wanayopita watu, au akaamrisha mema na kukataza maovu kwa hiyo idadi ya mia tatu na sitini, hakika siku hiyo atafikwa na jioni haliyakuwa ameepushwa na moto.”

 

 

Hadiyth – 7

 

عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ غَدَا إِلَى المسْجِد أَوْ رَاحَ، أَعَدَّ اللهُ لَهُ في الجَنَّةِ نُزُلًا كُلَّمَا غَدَا أَوْ رَاحَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Anayekwenda Masjid asubuhi au jioni, Allaah Humuandalia takrima  (mapokelewo  bora) Jannah kila anapokwenda, (iwe ni) asubuhi au jioni.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا نِسَاءَ المُسْلِمَاتِ، لا تَحْقِرنَّ جَارَةٌ لِجَارَتِهَا وَلَوْ فِرْسِنَ شاةٍ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

 

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaambia wanawake: “Enyi wanawake wa Kiislamu, jirani asidharau kamwe kumpa zawadi jirani yake japo ni kwato ya mbuzi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

 

عَنْهُ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((الإيمانُ بِضْعٌ وَسَبعُونَ أَوْ بِضعٌ وسِتُونَ شُعْبَةً: فَأفْضَلُهَا قَولُ: لا إلهَ إلا اللهُ، وَأَدْنَاهَا إمَاطَةُ الأذَى عَنِ الطَّريقِ، والحياءُ شُعبَةٌ مِنَ الإيمان)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Iymaan ni tanzu (matawi) sabini na kitu” au alisema: “ni tanzu (matawi) sitini na kitu, iliyo bora zaidi ni kusema: Laa Ilaaha illa-Allaah. Na ya chini ni kuondoa takataka njiani; na hayaa ni tawi katika matawi ya iymaan.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

 

عَنْهُ: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((بَينَما رَجُلٌ يَمشي بِطَريقٍ اشْتَدَّ عَلَيهِ العَطَشُ، فَوَجَدَ بِئرًا فَنَزَلَ فِيهَا فَشربَ، ثُمَّ خَرَجَ فإذَا كَلْبٌ يَلْهَثُ يأكُلُ الثَّرَى مِنَ العَطَشِ، فَقَالَ الرَّجُلُ: لَقَدْ بَلَغَ هَذَا الكَلْبُ مِنَ العَطَشِ مِثلُ الَّذِي كَانَ قَدْ بَلَغَ مِنِّي فَنَزَلَ البِئْرَ فَمَلأَ خُفَّهُ مَاءً ثُمَّ أمْسَكَهُ بفيهِ حَتَّى رَقِيَ، فَسَقَى الكَلْبَ، فَشَكَرَ الله لَهُ، فَغَفَرَ لَهُ)) قالوا: يَا رَسُول اللهِ، إنَّ لَنَا في البَهَائِمِ أَجْرًا؟ فقَالَ: ((في كُلِّ كَبِدٍ رَطْبَةٍ أجْرٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية للبخاري: ((فَشَكَرَ اللهُ لَهُ، فَغَفَرَ لَهُ، فأدْخَلَهُ الجَنَّةَ))

وفي رواية لهما: ((بَيْنَما كَلْبٌ يُطِيفُ بِرَكِيَّةٍ قَدْ كَادَ يقتلُهُ العَطَشُ إِذْ رَأَتْهُ بَغِيٌّ مِنْ بَغَايَا بَنِي إسْرَائِيل، فَنَزَعَتْ مُوقَها فَاسْتَقَتْ لَهُ بِهِ فَسَقَتْهُ فَغُفِرَ لَهَا بِهِ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kulikuwa na mtu aliyekuwa akitembea njiani, akashikwa na kiu, akaona kisima. Akateremka ndani na akanywa maji, kisha akatoka, mara akamuona mbwa ana hema anakula mchanga kwa sababu ya kiu. Yule mtu akasema: Mbwa huyu amepatwa na kiu kama kile kilichonipata. Akateremka kisimani, akaijaza maji khuffu yake halafu akaizuia kwenye mdomo wake, akapanda hata akafika juu, akamnywesha mbwa yule. Allaah Akamlipa na Akamghufuria.” Maswahaba wakauliza: Kwani sisi tuna ujira katika Wanyama? Akawajibu: “Kunywesha kila kilicho hai ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema: “Allaah Akamlipa, Akamghufuria na Akamuingiza Jannah.”

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy na Muslim zimesema: “Mbwa aliokuwa akizunguka kando ya kisima, alikaribia kufa kwa kiu, ghafla akaonekana na mwanamke mmoja wa kikahaba katika wana wa Israiyl, akaivua khuffu yake, akachotea maji na akamnywesha, akaghufuriwa kwa kitendo hicho.”

 

 

Hadiyth – 11

 

عَنْهُ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((لَقدْ رَأيْتُ رَجُلًا يَتَقَلَّبُ في الجَنَّةِ في شَجَرَةٍ قَطَعَهَا مِنْ ظَهْرِ الطَرِيقِ كَانَتْ تُؤذِي المُسْلِمِينَ)). رواه مسلم.

وفي رواية: ((مَرَّ رَجُلٌ بِغُصْنِ شَجَرَةٍ عَلَى ظَهرِ طَرِيقٍ، فَقَالَ: وَاللهِ لأُنْحِيَنَّ هَذَا عَنِ المُسْلِمينَ لا يُؤذِيهِمْ، فَأُدخِلَ الجَنَّةَ)).

وفي رواية لهما: ((بَيْنَمَا رَجُلٌ يَمْشي بِطَريقٍ وَجَدَ غُصْنَ شَوكٍ عَلَى الطريقِ فأخَّرَه فَشَكَرَ اللهُ لَهُ، فَغَفَرَ لَهُ))

 

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kwa hakika nilimuona mtu akitembea Jannah kwa sababu ya mti alioukata katikati ya njia uliokuwa ukiwaudhi Waislaamu.” [Muslim]

Riwaayah nyingine inasema: “Mtu mmoja alipita katikati ya tawi la mti uliokuwa katikati ya njia, akasema: Wa-Allaahi nitaliondoa tawi hili lisiwaudhi Waislaamu. Akaingizwa Jannah.”

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy na Muslim imesema: “Mtu mmoja alipokuwa akitembea njiani, akakuta tawi la mtu wenye miba njiani, akaliweka nyuma. Allaah Akamjazi na Akamghufuria.”

 

 

Hadiyth – 12

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الوُضُوءَ، ثُمَّ أَتَى الجُمعَةَ فَاسْتَمَعَ وَأنْصَتَ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْن الجُمُعَةِ وَزِيادَةُ ثَلاثَةِ أيَّامٍ، وَمَنْ مَسَّ الحَصَا فَقَدْ لَغَا)). رواه مسلم

 

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayetawadha vizuri kisha akaenda katika Swalaah ya Ijumaa, akasikiliza Khutbah na akanyamaza; ataghufuriwa baina ya Ijumaa hiyo na Ijumaa nyingine na ziada ya siku tatu, na atakayepangusa kwa vijiwe ameshafanya upuuzi.” [Muslim]

 

 

Hadiyh – 13

 

عَنْهُ: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا تَوَضَّأ العَبْدُ المُسْلِمُ، أَو المُؤمِنُ فَغَسَلَ وَجْهَهُ خَرَجَ مِنْ وَجْهِهِ كُلُّ خَطِيئَةٍ نَظَرَ إِلَيْهَا بِعَينهِ مَعَ المَاءِ، أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ، فَإِذا غَسَلَ يَدَيْهِ خَرَجَ مِنْ يَدَيهِ كُلُّ خَطِيئَة كَانَ بَطَشَتْهَا يَدَاهُ مَعَ المَاءِ، أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ، فَإِذَا غَسَلَ رِجْلَيهِ خَرَجَتْ كُلُّ خَطِيئَةٍ مشتها رِجْلاَهُ مَعَ المَاء أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ حَتَّى يَخْرُجَ نَقِيًّا مِنَ الذُّنُوبِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mja Muislaam au Muumin anapotawadha akaosha uso wake, litatoka katika uso wake kila dhambi alilolitazama kwa jicho lake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji. Atakapoosha mikono yake, litatoka kila dhambi alilolishika kwa mikono yake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji. Atakapoiosha miguu yake, itatoka kila dhambi aliyoiendea kwa miguu yake pamoja na maji au tone la mwisho la maji, mpaka atoke hali ya kuwa ni msafi na hana dhambi.” [Muslim]

 

 

Hadiyth - 14

 

عَنْهُ، عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((الصَّلَوَاتُ الخَمْسُ، وَالجُمُعَةُ إِلَى الجُمُعَةِ، وَرَمَضَانُ إِلَى رَمَضَانَ مُكَفِّراتٌ لِمَا بَيْنَهُنَّ إِذَا اجْتُنِبَتِ الكَبَائِرُ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Swalaah tano. Ijumaa mpaka Ijumaa, na Ramadhwaan mpaka Ramadhwaan ni yenye kufuta (madhambi) yaliyo baina yake pindi yatakapoepukwa al-kabaair (madhambi makubwa).” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 15

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((ألا أَدُلُّكُمْ عَلَى مَا يَمْحُو اللهُ بِهِ الخَطَايَا وَيَرْفَعُ بِهِ الدَّرَجَاتِ؟)) قَالُوا: بَلَى، يَا رسولَ اللهِ، قَالَ: ((إِسْبَاغُ الوُضُوءِ عَلَى المَكَارِهِ، وَكَثْرَةُ الخُطَا إِلَى المَسَاجِدِ، وَانْتِظَارُ الصَّلاةِ بَعْدَ الصَّلاةِ فَذلِكُمُ الرِّبَاطُ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Jee, niwajulishe jambo ambalo Allaah Hufuta dhambi kwa sababu yake na Hupandisha daraja kwa sababu yake?” Wakasema: Tujulishe Ee Rasuli wa Allaah. Akawaambia: “Kutawadha vizuri wakati wa kuona karaha, kwenda hatua nyingi Masjid na kuingojea Swalaah baada ya Swalaah. Basi kufanya hayo ndio ar-ribaatwh (kujifunga katika njia ya Allaah).” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 16

 

عن أبي موسى الأشعرِيِّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ صَلَّى البَرْدَيْنِ دَخَلَ الجَنَّةَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Muwsaa Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayeswali al-bardayni (Swalaah ya Al-Fajr na Al-‘Aswr) ataingia Jannah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 17

 

عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا مَرِضَ العَبْدُ أَوْ سَافَرَ كُتِبَ لَهُ مِثْلُ مَا كَانَ يَعْمَلُ مُقِيمًا صَحِيحًا)). رواه البخاري

Abuu Muwsaa Al- Ash’ariy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mja atakapougua au akasafiri, ataandikiwa mfano wa aliyokuwa akiyatenda alipokuwa nyumbani na alipokuwa mzima.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 18

 

عن جَابرٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((كُلُّ مَعْرُوفٍ صَدَقَةٌ)) رواه البخاري، ورواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahhu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila kitendo chema ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 19

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَا مِنْ مُسْلِمٍ يَغْرِسُ غَرْسًا إلا كَانَ مَا أُكِلَ مِنْهُ لَهُ صَدَقَةً، وَمَا سُرِقَ مِنهُ لَهُ صَدَقَةً، وَلا يَرْزَؤُهُ أَحَدٌ إلا كَانَ لَهُ صَدَقَةً)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Muislamu yeyote atakayepandikiza mti basi chochote kitakacholiwa katika mti huo ni swadaqah yake, na kitakachoibiwa ni swadaqah yake, na chochote kitakachopunguza itakuwa ni swadaqah yake.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 20

 

عَنْهُ، قَالَ: أراد بنو سَلِمَةَ أَن يَنتقِلوا قرب المسجِدِ فبلغ ذلِكَ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ لهم: ((إنَّهُ قَدْ بَلَغَني أنَّكُمْ تُرِيدُونَ أنْ تَنتَقِلُوا قُربَ المَسجِد؟)) فقالُوا: نَعَمْ، يَا رَسُول اللهِ قَدْ أَرَدْنَا ذلِكَ. فَقَالَ: ((بَنِي سَلِمَةَ، دِيَارَكُمْ تُكْتَبْ آثَارُكُمْ، ديَارَكُمْ تُكْتَبْ آثَارُكُمْ)). رواه مسلم

وفي روايةٍ: ((إنَّ بِكُلِّ خَطوَةٍ دَرَجَةً)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Watu wa kabila la Banu Salamah walitaka kuhamia karibu na Masjid. Habari hiyo ilimfikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Akawauliza: “Nimesikia kuwa mnataka kuhamia karibu na Masjid.” Wakajibu: Ndio Ee Rasuli wa Allaah, tumetaka kufanya hivyo. Akawaambia: “Enyi Banu Salamah, kaeni huko huko majumbani mwenu (msihame), hatua zenu zinaandikwa, kaeni huko huko hatua zenu zinaandikwa.” [Muslim]

Riwaayah nyingine imesema: “Hakika katika kila hatua kuna daraja.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 21

 

عن أبي المنذِر أُبيِّ بنِ كَعْب رضي الله عنه، قَالَ: كَانَ رَجُلٌ لا أعْلَمُ رَجلًا أبْعَدَ مِنَ المَسْجِدِ مِنْهُ، وَكَانَ لا تُخْطِئُهُ صَلاةٌ، فَقيلَ لَهُ أَوْ فَقُلْتُ لَهُ: لَوِ اشْتَرَيْتَ حِمَارًا تَرْكَبُهُ في الظَلْمَاء وفي الرَّمْضَاء؟ فَقَالَ: مَا يَسُرُّنِي أنَّ مَنْزِلي إِلَى جَنْبِ المَسْجِدِ إنِّي أريدُ أنْ يُكْتَبَ لِي مَمشَايَ إِلَى المَسْجِدِ وَرُجُوعِي إِذَا رَجَعْتُ إِلَى أهْلِي فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((قَدْ جَمَعَ اللهُ لَكَ ذلِكَ كُلَّهُ)). رواه مسلم

وفي رواية: ((إنَّ لَكَ مَا احْتَسَبْتَ))

Abuu Al-Mundhir, Ubayy bin Ka’b (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Alikuwepo mtu mmoja, sijui kama kuna mwengine aliyekuwa anaishi mbali zaidi na Masjid kulikoni mtu huyo, alikuwa hapitwi na Swalaah yoyote. Akaulizwa au nikamuuliza: Waonaje lau ungalinunua punda wakati wa giza na wakati mchanga ukiwa umepata joto? Akajibu: Sipendelei nyumba yangu iwepo karibu na Masjid, mimi nataka niandikiwe hatua zangu za kwenda Masjid na kurejea kwangu kwa familia yangu.” Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Allaah Ameshakujumuishia yote.” [Muslim]

Riwaayah nyingine imesema: “Umeshapata ulilotarajia.”

 

 

Hadiyth – 22

 

عن أبي محمد عبدِ اللهِ بنِ عمرو بن العاصِ- رَضي الله عنهما، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((أرْبَعُونَ خَصْلَةً: أعْلاَهَا مَنيحَةُ العَنْزِ، مَا مِنْ عَامِلٍ يَعْمَلُ بِخَصْلَة مِنْهَا؛ رَجَاءَ ثَوَابِهَا وتَصْدِيقَ مَوْعُودِهَا، إلا أدْخَلَهُ اللهُ بِهَا الجَنَّةَ)). رواه البخاري

Abuu Muhammad, ‘Abdullaah bin ‘Amruw bin ‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna mambo arubaini ya wema, la juu kabisa ni mtu akopeshe mbuzi wake. Hakuna yeyote atakayetenda mojawapo katika hayo kwa kutarajia thawabu zake na kusadikisha miadi yake, isipokuwa Allaah Atamuingiza Jannah.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 23

 

عن عَدِي بنِ حَاتمٍ رضي الله عنه قَالَ: سمعت النَّبيّ صلى الله عليه وسلم يقول: ((اتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بشقِّ تَمْرَةٍ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

وفي رواية لهما عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَا مِنْكُمْ مِنْ أَحَدٍ إلا سَيُكَلِّمُهُ رَبُّهُ لَيْسَ بَينَهُ وَبَيْنَهُ تَرْجُمَانٌ، فَيَنْظُرُ أَيْمَنَ مِنْهُ فَلا يَرَى إلا مَا قَدَّمَ، وَيَنْظُرُ أَشْأَمَ مِنْهُ فَلا يَرى إلا مَا قَدَّمَ، وَيَنظُرُ بَيْنَ يَدَيهِ فَلا يَرَى إلا النَّار تِلقَاءَ وَجْهِهِ، فَاتَّقُوا النَّارَ وَلَو بِشِقِّ تَمْرَةٍ، فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَبِكَلِمَةٍ طَيِّبَةٍ))

Abuu ‘Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Jikingeni na moto japo kwa kutoa kipande cha tende.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwake (‘Adiyy) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila mmoja wenu atazungumza na Rabb wake wala hakuna mwenye kutarjam baina yake na Rabb wake. Atatazama kuliani mwake, hataona ila alichotenda, atatazama kushotoni mwake, hataona ila alichotenda, atatazama mbele yake, hataona ila moto mbele yake. Basi ogopeni moto japo kwa kutoa kipande cha tende. Asiepata, azungumze neno jema.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 24

 

عن أنس رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ اللهَ لَيَرْضَى عَنِ العَبْدِ أنْ يَأكُلَ الأَكْلَةَ، فَيَحمَدَهُ عَلَيْهَا، أَوْ يَشْرَبَ الشَّرْبَةَ، فَيَحْمَدَهُ عَلَيْهَا)). رواه مسلم

Anas (Radhwiya Allaahu ‘amhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Humridhia mja anapokula chakula kimoja, Humhimidi Allaah kwa kukila, au anapokunya funda moja la maji Humhimidi Allaah kwa kunywa hicho kinywaji.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 25

 

عن أَبي موسى رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((عَلَى كلّ مُسْلِمٍ صَدَقَةٌ)) قَالَ: أرأيتَ إنْ لَمْ يَجِدْ؟ قَالَ: ((يَعْمَلُ بِيَدَيْهِ فَيَنْفَعُ نَفْسَهُ وَيَتَصَدَّقُ)) قَالَ: أرأيتَ إن لَمْ يَسْتَطِعْ؟ قَالَ: ((يُعِينُ ذَا الحَاجَةِ المَلْهُوفَ)) قَالَ: أرأيتَ إنْ لَمْ يَسْتَطِعْ، قَالَ: ((يَأمُرُ بِالمعْرُوفِ أوِ الخَيْرِ)) قَالَ: أرَأيْتَ إنْ لَمْ يَفْعَلْ؟ قَالَ: ((يُمْسِكُ عَنِ الشَّرِّ، فَإِنَّهَا صَدَقَةٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Kila Muislamu inampasa kutoa swadaqah.” Maswahaba wakamuuliza: Je itakuwaje asipopata cha kutoa? Akajibu: “Afanye kazi kwa mikono yake ajinufaishe na atoe swadaqah.” Akauliza: Jee, asipoweza? Akamwambia: “Atamsaidia mwenye haja anayesononeka.” Akamuuliza: Jee, asipoweza? Akajibu: “Ataamrisha wema.” Akauliza: Jee, asipofanya? Akamjibu: “Atajizuia kutenda shari, kwani huko pia ni kutoa swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

014-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Iktisadi Katika Twaa-ah (‘Ibaadah)

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الاقتصاد في الطَّاعَة

14 - Mlango Wa Iktisadi Katika Twaa-ah (‘Ibaadah)

 

Alhidaaya.com

 

 قَالَ الله تَعَالَى:

 

مَا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ لِتَشْقَىٰ ﴿٢﴾

Hatukukuteremshia Qur-aan ili upate mashaka. [Twaahaa: 2]

 

يُرِيدُ اللَّـهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ ﴿١٨٥﴾

Allaah Anakutakieni mepesi na wala Hakutakieni magumu. [Al-Baqarah: 185]

 

 

Hadiyth – 1

عن عائشة رضي الله عنها: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم دخل عَلَيْهَا وعِندها امرأةٌ، قَالَ: ((مَنْ هذِهِ؟)) قَالَتْ: هذِهِ فُلاَنَةٌ تَذْكُرُ مِنْ صَلاتِهَا. قَالَ: ((مهْ، عَلَيْكُمْ بِمَا تُطِيقُونَ، فَواللهِ لا يَمَلُّ اللهُ حَتَّى تَمَلُّوا، وكَانَ أَحَبُّ الدِّينِ إِلَيْهِ مَا دَاوَمَ صَاحِبُهُ عَلَيهِ)) مُتَّفَقٌ عَلَيه

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliingia kwake wakati alikuweko mwanamke. Akauliza: “Ni nani huyu?” Akamwambia: Huyu ni mtu fulani anayetajwa kusifiwa kwa Swalaah zake. Akasema: “Wacheni hayo! Fanyeni mnayoweza, wa-Allaahi, Allaah Hachoki kuwaandikia thawabu zenu mpaka mtakapochoka nyinyi wenyewe (kufanya ‘ibaadah). Na ‘amali bora kabisa mbele ya Allaah ni ile anayodumu nayo mwenye kuifanya.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: جَاءَ ثَلاثَةُ رَهْطٍ إِلَى بُيُوتِ أزْوَاجِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، يَسْأَلُونَ عَنْ عِبَادَةِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا أُخْبِروا كَأَنَّهُمْ تَقَالُّوهَا وَقَالُوا: أَيْنَ نَحْنُ مِنَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم قدْ غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ وَمَا تَأخَّرَ. قَالَ أحدُهُم: أمَّا أنا فَأُصَلِّي اللَّيلَ أبدًا. وَقالَ الآخَرُ: وَأَنَا أصُومُ الدَّهْرَ وَلا أُفْطِرُ. وَقالَ الآخر: وَأَنا أعْتَزِلُ النِّسَاءَ فَلا أتَزَوَّجُ أبَدًا. فجاء رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إليهم، فَقَالَ: ((أنْتُمُ الَّذِينَ قُلْتُمْ كَذَا وَكَذَا؟ أَمَا واللهِ إنِّي لأخْشَاكُمْ للهِ، وَأَتْقَاكُمْ لَهُ، لَكِنِّي أصُومُ وَأُفْطِرُ، وأُصَلِّي وَأَرْقُدُ، وَأَتَزَوَّجُ النِّساءَ، فَمَنْ رَغِبَ عَنْ سُنَّتِي فَلَيْسَ مِنِّي)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Imepokelewa na Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba kundi la watu watatu lilikuja katika nyumba za wake wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakiuliza kuhusu ‘ibaadah za Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Walipoelezwa waliziona kama ni kidogo, wakasema: Sisi hatuko sawa na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), yeye ameshaghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia na yatakayokuja. Mmoja wao akasema: Ama mimi, nitaswali daima usiku wote. Mwengine akasema: mimi nitafunga Swawm mwaka mzima. Mwengine akasema: Mimi nitawaepuka wanawake, sitaoa kamwe. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawaendea na kuwauliza: “Ninyi ndio mliosema kadhaa na kadhaa? Ama wa-Allaahi mimi ninamkhofu Allaah zaidi ya nina taqwa zaidi kulikoni ninyi; lakini mimi ninafunga swawm na kufungua, ninaswali na ninalala, na pia ninaoa wake. Atakayekengeuka na Sunnah zangu basi si katika mimi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن مسعود رضي الله عنه: أنّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((هَلَكَ المُتَنَطِّعُونَ)). قالها ثَلاثًا. رواه مسلم

Imepokewa kutoka ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Wameangamia wenye kushadidia mambo.” Amesema hivyo mara tatu. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

 

عن أَبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّ الدِّينَ يُسْرٌ، وَلَنْ يُشَادَّ الدِّيْنُ إلا غَلَبَهُ، فَسَدِّدُوا وَقَارِبُوا وَأبْشِرُوا، وَاسْتَعِينُوا بِالغَدْوَةِ وَالرَّوْحَةِ وَشَيءٍ مِنَ الدُّلْجَةِ)). رواه البخاري

وفي رواية لَهُ: ((سَدِّدُوا وَقَارِبُوا، وَاغْدُوا وَرُوحُوا، وَشَيءٌ مِنَ الدُّلْجَةِ، القَصْدَ القَصْدَ تَبْلُغُوا))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika Dini ni nyepesi, wala hakuna atakayetia uzito katika Dini ispokuwa itamshinda, basi fanyeni kwa wastani, na karibieni  katika ukamilifu na toeni bishara njema na ombeni msaada katika nyakati za asubuhi na jioni na baadhi katika nyakati za usiku.” [Al-Bukhaariy]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema: “Karibieni katika ukamilifu, fanyeni wastani, na wahini  nyakati za asubuhi, jioni na baadhi ya nyakati za usiku kwa wastani wastani, mtafikia (malengo).” 

 

 

Hadiyth – 5

 

 وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: دَخَلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم المَسْجِدَ فَإِذَا حَبْلٌ مَمْدُودٌ بَيْنَ السَّارِيَتَيْنِ، فَقَالَ: ((مَا هَذَا الحَبْلُ؟)) قالُوا: هَذَا حَبْلٌ لِزَيْنَبَ، فَإِذَا فَتَرَتْ تَعَلَّقَتْ بِهِ. فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((حُلُّوهُ، لِيُصلِّ أَحَدُكُمْ نَشَاطَهُ فَإِذَا فَتَرَ فَلْيَرْقُدْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Na amepokea Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliingia Masjid, akaona kamba imefungwa baina ya nguzo mbili. Akauliza: “Kamba hii ni ya nini?” Wakasema: Hii ni kamba ya Zaynab, anapochoka hujiegemeza kwayo. Basi Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Ifungueni na kila mmoja wenu aswali kwa nguvu zake, atakapochoka alale.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

 

وعن عائشة رضي الله عنها: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا نَعَسَ أَحَدُكُمْ وَهُوَ يُصَلِّي فَلْيَرْقُدْ حَتَّى يَذْهَبَ عَنْهُ النَّومُ، فإِنَّ أحدكم إِذَا صَلَّى وَهُوَ نَاعِسٌ لا يَدْرِي لَعَلَّهُ يَذْهَبُ يَسْتَغْفِرُ فَيَسُبُّ نَفْسَهُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Na kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Anaposinzia mmoja wenu huku akiwa anaswali, basi alale mpaka usingizi utakapommalizikia kwani mmoja wenu atakaposwali na hali anasinzia, hatofahamu anayoyasema, hivyo huenda akawa anakusudia kuomba maghfirah kumbe anaitukana nafsi yake.” [Al-Bukhariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

 

وعن أَبي عبد الله جابر بن سمرة رضي الله عنهما، قَالَ: كُنْتُ أصَلِّي مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم الصَّلَوَاتِ، فَكَانتْ صَلاتُهُ قَصْدًا وَخُطْبَتُهُ قَصْدًا. رواه مسلم

Abuu ‘Abdillaah, Jaabir bin Samurah (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilikuwa nikiswali pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) baadhi ya Swalaah na ilikuwa Swalaah yake ni ya wastani na khutbah yake ilikuwa ni wastani.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

 

وعن أبي جُحَيْفَة وَهْب بنِ عبد اللهِ رضي الله عنه قَالَ: آخَى النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم بَيْنَ سَلْمَانَ وَأَبي الدَّرْداءِ، فَزارَ سَلْمَانُ أَبَا الدَّرداءِ فَرَأى أُمَّ الدَّرداءِ مُتَبَذِّلَةً، فَقَالَ: مَا شَأنُكِ؟ قَالَتْ: أخُوكَ أَبُو الدَّردَاءِ لَيْسَ لَهُ حَاجَةٌ في الدُّنْيَا، فَجاءَ أَبُو الدَّرْدَاءِ فَصَنَعَ لَهُ طَعَامًا، فَقَالَ لَهُ: كُلْ فَإِنِّي صَائِمٌ، قَالَ: مَا أنا بِآكِلٍ حَتَّى تَأكُلَ فأكل، فَلَمَّا كَانَ اللَّيلُ ذَهَبَ أَبُو الدَّردَاءِ يَقُومُ فَقَالَ لَهُ: نَمْ، فنام، ثُمَّ ذَهَبَ يَقُومُ فَقَالَ لَهُ: نَمْ. فَلَمَّا كَانَ من آخِر اللَّيلِ قَالَ سَلْمَانُ: قُم الآن، فَصَلَّيَا جَمِيعًا فَقَالَ لَهُ سَلْمَانُ: إنَّ لِرَبِّكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِنَفْسِكَ عَلَيكَ حَقًّا، وَلأَهْلِكَ عَلَيكَ حَقًّا، فَأعْطِ كُلَّ ذِي حَقٍّ حَقَّهُ، فَأَتَى النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم فَذَكَرَ ذلِكَ لَهُ فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((صَدَقَ سَلْمَانُ)). رواه البخاري

Abuu Juhayfah, Wahb bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifunga undugu baina ya Salmaan na Abuu Dardaa. Salmaan akaenda kumtembelea Abuu Dardaa, akamuona mama Dardaa amevaa nguo iliyochakaa. Akamuuliza: Mbona upo hivyo? Akasema: Nduguyo Abuu Dardaa hana haja ya dunia (hataki wanawake). Abuu Dardaa akaja, akamtengenezea chakula nduguye (Salmaan) kisha akamwambia: Kula mimi nimefunga swawm. Salmaan akamwambia: Sitokula mpaka uanze wewe kula. Akala. Ulipofika usiku Abuu Dardaa akataka kuanza kuswali (Swalaah ya usiku). Salmaan akamwambia: Lala. Akalala. Ulipofika mwisho wa usiku Salmaan akamwambia sasa amka (uswali). Wakaswali wote. Kisha Salmaan akamwambia: Hakika Rabb wako Ana haki juu yako, na nafsi yako ina haki juu yako, na mkeo na familia yako wana haki juu yako. Kwa hiyo kila mmoja mpe haki yake.  Abuu Dardaa akamuendea Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akatajiwa hayo, hapo Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Salmaan amepatia” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 9

 

وعن أَبي محمد عبدِ اللهِ بنِ عَمْرو بن العاصِ رضي الله عنهما، قَالَ: أُخْبرَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم أنِّي أقُولُ: وَاللهِ لأَصُومَنَّ النَّهَارَ، وَلأَقُومَنَّ اللَّيلَ مَا عِشْتُ. فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((أنتَ الَّذِي تَقُولُ ذلِكَ؟)) فَقُلْتُ لَهُ: قَدْ قُلْتُهُ بأبي أنْتَ وأمِّي يَا رسولَ الله. قَالَ: ((فَإِنَّكَ لا تَسْتَطِيعُ ذلِكَ فَصُمْ وَأَفْطِرْ، وَنَمْ وَقُمْ، وَصُمْ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثةَ أيَّامٍ، فإنَّ الحَسَنَةَ بِعَشْرِ أمْثَالِهَا وَذَلكَ مِثلُ صِيامِ الدَّهْرِ)) قُلْتُ: فَإِنِّي أُطيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذلِكَ، قَالَ: ((فَصُمْ يَومًا وَأَفْطِرْ يَوْمَيْنِ)) قُلْتُ: فَإنِّي أُطِيقُ أفضَلَ مِنْ ذلِكَ، قَالَ: ((فَصُمْ يَومًا وَأفْطِرْ يَومًا فَذلِكَ صِيَامُ دَاوُد صلى الله عليه وسلم، وَهُوَ أعْدَلُ الصيامِ))

  وفي رواية: ((هُوَ أفْضَلُ الصِّيامِ)) فَقُلْتُ: فَإِنِّي أُطيقُ أفْضَلَ مِنْ ذلِكَ، فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((لا أفضَلَ مِنْ ذلِكَ))، قال: وَلأنْ أكُونَ قَبِلْتُ الثَّلاثَةَ الأَيّامِ الَّتي قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم أحَبُّ إليَّ مِنْ أهْلي وَمَالي

وفي رواية: ((أَلَمْ أُخْبَرْ أنَّكَ تَصُومُ النَّهَارَ وتَقُومُ اللَّيلَ؟)) قُلْتُ: بَلَى، يَا رَسُول الله، قَالَ: ((فَلا تَفْعَلْ: صُمْ وَأَفْطِرْ، وَنَمْ وَقُمْ؛ فإنَّ لِجَسَدِكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِعَيْنَيكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِزَوْجِكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِزَوْرِكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإنَّ بِحَسْبِكَ أنْ تَصُومَ في كُلِّ شَهْرٍ ثَلاثَةَ أيَّامٍ، فإنَّ لَكَ بِكُلِّ حَسَنَةٍ عَشْرَ أمْثَالِهَا، فَإِنَّ ذلِكَ صِيَامُ الدَّهْر)) فَشَدَّدْتُ فَشُدِّدَ عَلَيَّ، قُلْتُ: يَا رَسُول الله، إنِّي أجِدُ قُوَّةً، قَالَ: ((صُمْ صِيَامَ نَبيِّ الله دَاوُد وَلا تَزد عَلَيهِ)) قُلْتُ: وَمَا كَانَ صِيَامُ دَاوُد؟ قَالَ: ((نِصْفُ الدَّهْرِ)) فَكَانَ عَبدُ الله يقول بَعدَمَا كَبِرَ: يَا لَيتَنِي قَبِلْتُ رُخْصَة رَسُول الله صلى الله عليه وسلم.

   وفي رواية: ((أَلَمْ أُخْبَرْ أَنَّكَ تَصُومُ الدَّهرَ، وَتَقْرَأُ القُرآنَ كُلَّ لَيْلَة؟)) فقلت: بَلَى، يَا رَسُول الله، وَلَمْ أُرِدْ بذلِكَ إلا الخَيرَ، قَالَ: ((فَصُمْ صَومَ نَبيِّ اللهِ دَاوُد، فَإنَّهُ كَانَ أعْبَدَ النَّاسِ، وَاقْرَأ القُرْآنَ في كُلِّ شَهْر)) قُلْتُ: يَا نَبيَّ اللهِ، إنِّي أُطِيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذلِكَ؟ قَالَ: ((فاقرأه في كل عشرين)) قُلْتُ: يَا نبي الله، إني أطيق أفضل من ذلِكَ؟ قَالَ: ((فَاقْرَأهُ في كُلِّ عَشْر)) قُلْتُ: يَا نبي اللهِ، إنِّي أُطيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذلِكَ؟ قَالَ: ((فاقْرَأهُ في كُلِّ سَبْعٍ وَلا تَزِدْ عَلَى ذلِكَ)) فشدَّدْتُ فَشُدِّدَ عَلَيَّ وَقالَ لي النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((إنَّكَ لا تَدرِي لَعَلَّكَ يَطُولُ بِكَ عُمُرٌ)) قَالَ: فَصِرْتُ إِلَى الَّذِي قَالَ لي النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم. فَلَمَّا كَبِرْتُ وَدِدْتُ أنِّي كُنْتُ قَبِلتُ رُخْصَةَ نَبيِّ الله صلى الله عليه وسلم.

وفي رواية: ((وَإِنَّ لِوَلَدِكَ عَلَيْكَ حَقًّا))

وفي رواية: ((لا صَامَ مَنْ صَامَ الأَبَدَ)) ثلاثً

وفي رواية: ((أَحَبُّ الصِيَامِ إِلَى اللهِ تَعَالَى صِيَامُ دَاوُد، وَأَحَبُّ الصَّلاةِ إِلَى اللهِ تَعَالَى صَلاةُ دَاوُدَ: كَانَ ينام نصف الليل، ويقوم ثلثه، وينام سدسه، وكان يصوم يومًا ويفطر يومًا، وَلا يَفِرُّ إِذَا لاقَى))

وفي رواية قال: أنْكَحَني أَبي امرَأةً ذَاتَ حَسَبٍ وَكَانَ يَتَعَاهَدُ كنَّتَهُ-- أي: امْرَأَةَ وَلَدِهِ- فَيَسْأَلُهَا عَنْ بَعْلِهَا. فَتقُولُ لَهُ: نِعْمَ الرَّجُلُ مِنْ رَجُلٍ لَمْ يَطَأْ لَنَا فِرَاشًا، وَلَمْ يُفَتِّشْ لَنَا كَنَفًا مُنْذُ أتَيْنَاهُ. فَلَمَّا طَالَ ذلِكَ عَلَيهِ ذَكَرَ ذلك للنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: ((القِنِي بِهِ)) فَلَقيتُهُ بَعد ذلك، فَقَالَ: ((كَيْفَ تَصُومُ؟)) قُلْتُ: كُلَّ يَومٍ، قَالَ: ((وَكَيْفَ تَخْتِمُ؟)) قُلْتُ: كُلَّ لَيْلَةٍ، وَذَكَرَ نَحْوَ مَا سَبَقَ، وَكَانَ يَقْرَأُ عَلَى بَعْضِ أهْلِهِ السُّبُعَ الَّذِي يَقْرَؤُهُ، يَعْرِضُهُ مِنَ النَّهَارِ ليَكُونَ أخفّ عَلَيهِ باللَّيلِ، وَإِذَا أَرَادَ أنْ يَتَقَوَّى أفْطَرَ أيَّامًا وَأحْصَى وَصَامَ مِثْلَهُنَّ كرَاهِيَةَ أنْ يَترُكَ شَيئًا فَارَقَ عَلَيهِ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم

 

Abuu Muhammad, ‘Abdillaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw  (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliaambiwa kuwa mimi nasema: Wa-Allaahi nitafunga swawm mchana na nitaswali usiku maisha yangu yote. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniuliza: “Wewe ndiye uliyesema hivyo?” Nikamjibu:  Ndiyo, hakika nimesema, nakutolee fidia baba yangu na mama yangu ee Rasuli wa Allaah. Akaniambia: “Wewe hutaweza kufanya hivyo, kwa hivyo funga swawm na ule, lala na uswali, na ufunge swawm siku tatu kila mwezi; kwani jema moja hulipwa kwa mema kumi mfano wake, na hiyo ni kama swiyaam ya dahari!” Nikamwambia: Mimi naweza kufanya zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Basi funga swawm siku moja na ule siku mbili.” Nikamwambia: Mimi naweza zaidi ya hivyo. Akanambia: “Basi funga swawm siku moja na ule siku moja, hivyo ni swiyaam ya  Nabiy Daawuwd (‘Alayhis Salaam) nayo ndio Swawm ya wastani zaidi.”

Riwaayah nyingine imesema: “Hiyo ndiyo Swawm bora zaidi.” Nikamwambia: Mimi naweza zaidi ya hivyo. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: “Hakuna bora zaidi ya hivyo.” Kwa kweli lau ningelikubali zile siku tatu alizonipa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ingelipendeza kwangu zaidi kulikoni familia yangu na mali yangu.

Riwaayah nyingine imesema: “Si niliambiwa kuwa wewe unafunga swawm mchana na usiku wote unaswali?” Nikamjibu: Ndiyo ee Rasuli wa Allaah. Akaniambia: “Usifanye hivyo, funga swawm na ule, lala na uswali, hakika mwili wako una haki juu yako, na macho yako yana haki juu yako, na mkeo ana haki juu yako na mgeni wako ana haki juu yako, na hakika inakutosha ufunge swawm siku tatu kila mwezi; kwani katika kila jambo jema moja unapata mema kumi mfano wake; huko ndiyo swiyaam ya dahari!” Nikamkazania, nami nikakaziwa. Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, nina nguvu zaidi. Akanambia: “Funga Swawm ya Nabiy Daawuwd wala usizidishe juu ya hapo.” Nikamuuliza: Swawm ya Nabiy Daawuwd ilikuwaje? Akaniambia: “Nusu ya dahari.”

‘Abdullaah alipozeeka alikuwa akisema: Laiti kama ningelikubali ruhusa ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

Riwaayah nyingine imesema: “Si niliambiwa kuwa unafunga swawm dahari na unasoma Qur-aan yote kila usiku?” Nikamjibu: Ndiyo ee Rasuli wa Allaah, wala sijakusudia kufanya hivyo ila ni khayr tu. Akaniambia: “Funga Swawm ya Nabiy Daawuwd; kwani yeye aliwashinda watu kwa ‘ibaadah, na soma (ukhitimishe) Qur-aan kila mwezi.” Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, mimi naweza zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Soma kwa siku ishirini.” Nikamwambia: Ee Nabiy wa Allaah, mimi naweza zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Soma kwa siku kumi.” Nikamwambia: Ee Nabiy wa Allaah, mimi naweza zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Soma umalize kila baada ya siku saba, wala usizidishe uchache wa hapo.” Nikatia mkazo nami nikakaziwa. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: “Huwezi kujua pengine unaweza kuwa na umri mrefu.” Na kweli nikawa kama alivyoniambia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

Riwaayah nyingine imesema: “Na hakika mwanao ana haki juu yako.”

Na Riwaayah nyengine: “Hana Swawm mwenye kufunga daima.” Alikariri mara tatu.

Riwaayah nyingine imesema: “Swawm ipendezayo zaidi kwa Allaah ni Swawm ya Nabiy Daawuwd. Na Swalaah ipendezayo zaidi kwa Allaah ni Swalaah ya Nabiy Daawuwd; alikuwa akilala nusu ya usiku, akiswali thuluthi yake, akilala sudusi yake, na alikuwa akifunga swawm siku moja na akila siku moja, wala hakimbii anapokutana na adaui (vitani).”

Riwaayah nyingine imesema: Baba yangu alinioza mke mwenye nasaba nzuri, na alikuwa akimjulia hali mkwewe, akamuuliza hali ya mumewe, naye akimwambia: Mtu mzuri miongoni mwa watu.  Kuanzia anioe, hakuja kulala na mimi wala kujamiiana nami. Hali hii ilipoendelea kwa muda mrefu, alitajiwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Akasema: “Nileteeni kwangu”. Nami nikamuendea. Akaniuliza: “Unafunga swawm vipi?”  Nikamjibu: Kila siku. Akaniuliza: “Unahitimisha vipi Qur-aan?” Nikamjibu: Kila usiku. Akataja Hadiyth ambayo imetangulia kuelezwa.  

‘Abdullaah alikuwa akisoma kwa baadhi ya familia yake subu’ anayoisoma (yaani alikuwa akihitimisha kwa siku saba), akiisoma mchana ili apate tahfifu wakati wa usiku. Na anapotaka tahfifu kwa kufunga swawm kila siku alikuwa anaacha kufunga swawm baadhi ya siku  na baadaye kuzilipa. Anafanya hivyo kwa kuchelea asije kuacha mazoea aliyokuwa nayo mpaka wakati Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anafariki. 

 

 

Hadiyth – 10

 

وعن أبي رِبعِي حنظلة بنِ الربيعِ الأُسَيِّدِيِّ الكاتب أحدِ كتّاب رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: لَقِيَنِي أَبُو بَكر رضي الله عنه فَقَالَ: كَيْفَ أنْتَ يَا حنْظَلَةُ؟ قُلْتُ: نَافَقَ حَنْظَلَةُ! قَالَ: سُبْحَانَ الله مَا تَقُولُ؟! قُلْتُ: نَكُونُ عِنْدَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُذَكِّرُنَا بالجَنَّةِ وَالنَّارِ كأنَّا رَأيَ عَيْنٍ فإِذَا خَرَجْنَا مِنْ عِنْدِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم عَافَسْنَا الأَزْواجَ وَالأَوْلاَدَ وَالضَّيْعَاتِ نَسينَا كَثِيرًا، قَالَ أَبُو بكر رضي الله عنه: فَوَالله إنَّا لَنَلْقَى مِثْلَ هَذَا، فانْطَلَقْتُ أَنَا وأبُو بَكْر حَتَّى دَخَلْنَا عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم. فقُلْتُ: نَافَقَ حَنْظَلَةُ يَا رَسُول اللهِ! فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((وَمَا ذَاكَ؟)) قُلْتُ: يَا رَسُول اللهِ، نَكُونُ عِنْدَكَ تُذَكِّرُنَا بِالنَّارِ والجَنَّةِ كأنَّا رَأيَ العَيْن فإِذَا خَرَجْنَا مِنْ عِنْدِكَ عَافَسْنَا الأَزْواجَ وَالأَوْلاَدَ وَالضَّيْعَاتِ نَسينَا كَثِيرًا. فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((وَالَّذِي نَفْسي بِيَدِهِ، لَوْ تَدُومُونَ عَلَى مَا تَكُونونَ عِنْدِي، وَفي الذِّكْر، لصَافَحَتْكُمُ الملائِكَةُ عَلَى فُرُشِكُمْ وَفي طُرُقِكُمْ، وَلَكِنْ يَا حَنْظَلَةُ سَاعَةً وسَاعَةً)) ثَلاَثَ مَرَات. رواه مسلم

Abuu Rabi’y, Handhwalah bin Ar-Rabiy’ Al-Usayyidiy ambaye ni mmoja katika waandishi wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesimulia: “Siku moja Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikutana nami, akaniuliza: Vipi hali ee Handhwalah? Nikamwambia: “Handhwalah anajikhofia unafiki! Akasema: Subhaana Allaah! Umesema nini? Nikamwambia: Sisi huwa tupo mbele ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akitukumbusha Jannah na moto kana kwamba huwa tukiziona. Lakini tunapoondoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hushughulika na wake zetu na watoto wetu na shughuli za kuendesha maisha yetu, hivyo hutufanya tusahau mengi. Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: Wa-Allaahi nasi pia hukutana na hali kama hii. Mimi na Abuu Bakr tukaenda kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikamwambia: Handhwalah anajikhofia unafiki ee Rasuli wa Allaah, tunapokuwa kwako unatukumbusha moto na Jannah kana kwamba tunaziona kwa macho, tunapoondoka kwako, hushughulika na wake zetu na watoto wetu na shughuli za kuendesha maisha yetu, hivyo hutufanya tusahau mengi. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Naapa kwa Ambaye nasfi yangu ipo mikononi Mwake, lau mnadumu katika hali mnayokuwa nayo kwangu na katika kumdhukuru Allaah, basi Malaika wangewasalimia nyinyi mnapokuwa vitandani mwenu na njiani. Lakini ee Handhwalah, kuna wakati wa kutekeleza ‘ibaadah na kuna wakati wa kuangalia mambo ya maisha.” Alikariri hivyo mara tatu. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

 

وعنِ ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: بينما النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يخطب إِذَا هُوَ برجلٍ قائم فسأل عَنْهُ، فقالوا: أَبُو إسْرَائيلَ نَذَرَ أنْ يَقُومَ في الشَّمْسِ وَلا يَقْعُدَ، وَلا يَسْتَظِل، وَلا يَتَكَلَّمَ، وَيَصُومَ، فَقَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((مُرُوهُ، فَلْيَتَكَلَّمْ، وَلْيَسْتَظِلَّ، وَلْيَقْعُدْ، وَلْيُتِمَّ صَوْمَهُ)). رواه البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa ana khutubia, mara akamuona mtu amesimama. Akauliza kuhusu mtu huyo. Akaambiwa kuwa huyo ni Abuu Israaiyl ambaye ameweka nadhiri atasimama katika jua wala hatoki, wala hatajikinga na kivuli, wala hatazungumza na atafunga swawm. Basi Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Mwambieni azungumze, akae kivulini, akae chini na atimize Swawm yake.” [Al-Bukhaariy]   

 

 

Share

015-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuhifadhi ‘Amali

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب المحافظة عَلَى الأعمال

15 - Mlango Wa Kuhifadhi ‘Amali

 

Alhidaaya.com

 

 قَالَ الله تَعَالَى:

 

أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ﴿١٦﴾

Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa ukumbusho wa Allaah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? [Al-Hadiyd: 16]

 

وَقَفَّيْنَا بِعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ وَجَعَلْنَا فِي قُلُوبِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ رَأْفَةً وَرَحْمَةً وَرَهْبَانِيَّةً ابْتَدَعُوهَا مَا كَتَبْنَاهَا عَلَيْهِمْ إِلَّا ابْتِغَاءَ رِضْوَانِ اللَّـهِ فَمَا رَعَوْهَا حَقَّ رِعَايَتِهَا ﴿٢٧﴾

Na Tukamfuatisha ‘Iysaa mwana wa Maryam, na Tukampa Injiyl. Na Tukaweka katika nyoyo za wale waliomfuata upole na rahmah na uruhubani (maisha ya utawa); wameyaanzisha wao wenyewe Hatukuwaandikia hayo juu yao isipokuwa ni kutafuta radhi za Allaah. Lakini hawakuuchunga ipasavyo kuchungwa. [Al-Hadiyd: 27]

 

وَلَا تَكُونُوا كَالَّتِي نَقَضَتْ غَزْلَهَا مِن بَعْدِ قُوَّةٍ أَنكَاثًا ﴿٩٢﴾

Na wala msiwe kama yule mwanamke aliyezongoa uzi wake vipande vipande baada ya (kuusokota na) kuwa mgumu. [An-Nahl: 92]

 

وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ ﴿٩٩﴾

Na mwabudu Rabb wako mpaka ikufikie yakini (mauti). [Al-Hajr: 99]

 

 

Hadiyth – 1

وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ نَامَ عَنْ حِزْبهِ مِنَ اللَّيلِ، أَوْ عَنْ شَيءٍ مِنْهُ، فَقَرَأَهُ مَا بَيْنَ صَلاةِ الفَجْرِ وَصَلاةِ الظُّهْرِ، كُتِبَ لَهُ كَأَنَّمَا قَرَأَهُ مِنَ اللَّيلِ)). رواه مسلم

‘Umar bin Khatwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayelala asisome hizbu (nyiradi) yake ya usiku au chochote katika hizbu yake ya usiku au chochote katika hizbu hiyo, halafu akaisoma baina ya Swalaah ya alfajiri na Swalaah ya adhuhuri, ataandikiwa kana kwamba ameisoma usiku.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن عَمْرو بن العاص رَضِيَ الله عنهما، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا عبدَ اللهِ، لا تَكُنْ مِثْلَ فُلان، كَانَ يَقُومُ اللَّيلَ فَتَرَكَ قِيَامَ اللَّيلِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

‘Abdullaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Aliniambia: “Ee ‘Abdullaah, usiwe kama fulani, alikuwa akiswali usiku na kuacha kuswali usiku.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها، قَالَتْ: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا فَاتَتْهُ الصَّلاةُ مِنَ اللَّيلِ مِنْ وَجَعٍ أَوْ غَيرِهِ، صَلَّى مِنَ النَّهارِ ثنْتَيْ عَشرَةَ رَكْعَةً. رواه مسلم

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapopitwa na Swalaah ya usiku kwa sababu ya maradhi au jambo lingine,  huswali wakati wa mchana, rakaa kumi na mbili.” [Muslim]

 

 

Share

016-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Maamrisho Wa Kuzihifadhi Sunnah Na Adabu Zake

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب في الأمر بالمحافظة عَلَى السنة وآدابها

016 – Mlango Wa Maarisho Wa Kuzihifadhi Sunnah Na Adabu Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا ﴿٧﴾

Na lolote analokupeni Rasuli (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) basi lichukueni, na analokukatazeni, basi acheni. [Al-Hashr: 7]

 

 

وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ﴿٣﴾

Na wala hatamki kwa hawaa.

إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ ﴿٤﴾

Hayo si chochote isipokuwa ni Wahy unaofunuliwa. [An-Najm: 3-4]

 

 

 قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ﴿٣١﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi, Atakupendeni Allaah na Atakughufurieni dhambi zenu. [Aal-‘Imraan: 31]

 

لَّقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اللَّـهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ لِّمَن كَانَ يَرْجُو اللَّـهَ وَالْيَوْمَ الْآخِرَ وَذَكَرَ اللَّـهَ كَثِيرًا ﴿٢١﴾

Kwa yakini mna kigezo kizuri kwa Rasuli wa Allaah kwa mwenye kumtaraji Allaah na Siku ya Mwisho na akamdhukuru Allaah kwa wingi. [Al-Ahzaab: 21]

 

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٦٥﴾

Basi Naapa kwa Rabb wako, hawatoamini mpaka wakufanye wewe ni mwamuzi katika yale wanayozozana baina yao, kisha wasipate katika nyoyo zao karaha katika yale uliyohukumu na wajisalimishe, kwa kujisalimisha (kikamilifu). [An-Nisaa: 65]

 

فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ ﴿٥٩﴾

Mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allaah na Rasuli. [An-Nisaa: 59]

 

مَّن يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللَّـهَ ﴿٨٠﴾

Atakayemtii Rasuli basi kwa yakini amemtii Allaah. [An-Nisaa: 80]

 

إِنَّكَ لَتَهْدِي إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿٥٢﴾

Na hakika wewe (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) bila shaka unaongoza kuelekea njia iliyonyooka.

صِرَاطِ اللَّـهِ ﴿٥٣﴾

Njia ya Allaah… [As-Shuwraa: 52-53]

 

فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٦٣﴾

Basi watahadhari wale wanaokhalifu amri yake, isije kuwasibu fitnah au ikawasibu adhabu iumizayo. [An-Nuwr: 63]

 

وَاذْكُرْنَ مَا يُتْلَىٰ فِي بُيُوتِكُنَّ مِنْ آيَاتِ اللَّـهِ وَالْحِكْمَةِ ﴿٣٤﴾

Na kumbukeni yale yanayosomwa majumbani mwenu katika Ayaat za Allaah na Hikmah (Sunnah). [Al-Ahzaab: 34]

 

 

Hadiyth – 1

 

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((دَعُونِي مَا تَرَكْتُكُمْ، إِنَّمَا أَهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ كَثْرَةُ سُؤالِهِمْ واخْتِلافُهُمْ عَلَى أنْبيَائِهِمْ، فَإِذَا نَهَيْتُكُمْ عَنْ شَيْء فَاجْتَنِبُوهُ، وَإِذَا أمَرْتُكُمْ بشيءٍ فَأْتُوا مِنْهُ مَا اسْتَطَعْتُمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Jiepusheni kwa mambo ambayo sijawatajia, kwani hakika waliangamia wale walio kabla yenu kwa sababu ya kuuliza kwao maswali mengi na kukhitalifiana na Rasuli wao. Basi ninapowakataza jambo liepukeni, na ninapowaamuru jambo, basi fanyeni kwa kadiri muwezavyo.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

 

عن أَبي نَجيحٍ العِرباضِ بنِ سَارية رضي الله عنه قَالَ: وَعَظَنَا رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم مَوعظةً بَليغَةً وَجِلَتْ مِنْهَا القُلُوبُ، وَذَرَفَتْ مِنْهَا العُيُونُ، فَقُلْنَا: يَا رسولَ اللهِ، كَأَنَّهَا مَوْعِظَةُ مُوَدِّعٍ فَأوْصِنَا، قَالَ: ((أُوصِيكُمْ بِتَقْوَى اللهِ، وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وَإنْ تَأمَّر عَلَيْكُمْ عَبْدٌ حَبَشِيٌّ، وَإِنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيَرَى اختِلافًا كَثيرًا، فَعَليْكُمْ بسُنَّتِي وسُنَّةِ الخُلَفاءِ الرَّاشِدِينَ المَهْدِيِيِّنَ عَضُّوا عَلَيْهَا بالنَّواجِذِ، وَإِيَّاكُمْ وَمُحْدَثَاتِ الأُمُورِ؛ فإنَّ كلَّ بدعة ضلالة)). رواه أَبُو داود والترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن صحيح))

Abuu Najiyh Al-‘Irbaadhw bin Saariyah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitupa mawaidha mazito (yenye maana pana), nyonyo zikaingia khofu na macho  yakabubujikwa na machozi. Tukamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, inaonekana kana kwamba haya mawaidha ni yakutuaga, basi tuusie. Akasema: “Nawausia taqwa ya Allaah, kusikiliza na kutii, hata kama mkiongozwa na mtumwa mhabeshi. Hakika atakayeishi umri mrefu miongoni mwenu ataona khitilafu nyingi. Kwa hivyo ninyi shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za  Khulafaa Ar-Rashidiyna (Makhalifah waongofu) wenye kuongoza. Ishikilieni (Sunnah) kwa magego. Na tahadharini mambo yenye kuzushwa, hakika kila bid’ah ni upotevu.” [Abuu Daawuud na At-Tirmidhy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 3

 

عَنْ أَبي هريرةَ رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((كُلُّ أُمَّتِي يَدخُلُونَ الجَنَّةَ إلا مَنْ أبَى)). قيلَ: وَمَنْ يَأبَى يَا رَسُول الله؟ قَالَ: ((مَنْ أَطَاعَنِي دَخَلَ الجَنَّةَ، وَمَنْ عَصَانِي فَقَدْ أبَى)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Ummah wangu wote wataingia Jannah isipokuwa atakayekataa.” Akaulizwa: “Ni yupi atakayekataa Ee Rasuli wa Allaah? Akajibu: “Atakayenitii mimi ataingia Jannah, na atakayeniasi basi amekataa.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 4

 

عن أَبي مسلم، وقيل: أَبي إياس سَلمة بنِ عمرو بنِ الأكوع رضي الله عنه أنَّ رَجُلًا أَكَلَ عِنْدَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بِشِمَالِهِ، فَقَالَ: ((كُلْ بِيَمِينكَ)) قَالَ: لا أسْتَطيعُ. قَالَ: ((لاَ استَطَعْتَ)). مَا مَنَعَهُ إلا الكِبْرُ، فمَا رَفَعَهَا إِلَى فِيهِ. رواه مسلم

Abuu Muslim, pia anaitwa Abuu Iyaas, Salamah bin ‘Amruw bin Al-Akwa’ (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Mtu mmoja alikula kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mkono wake wa kushoto. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Kula kwa mkono wako wa kulia.” Yule mtu akasema siwezi. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Hutaweza!” Hakuna kilichomzuia isipokwa ni kibri. Basi hakuweza tena kuinua mkono wake hadi kinywani mwake. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

 

عن أَبي عبدِ الله النعمان بن بشير رَضيَ الله عنهما، قَالَ: سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((لَتُسَوُّنَّ صُفُوفَكُمْ، أَوْ لَيُخَالِفَنَّ اللهُ بَيْنَ وُجُوهِكُمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

وفي رواية لمسلم: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُسَوِّي صُفُوفَنَا حتى كأنَّما يُسَوِّي بِهَا القِدَاحَ حَتَّى إِذَا رَأَى أَنَّا قَدْ عَقَلْنَا عَنْهُ. ثُمَّ خَرَجَ يَومًا فقامَ حَتَّى كَادَ أنْ يُكَبِّرَ فرأَى رَجلًا بَاديًا صَدْرُهُ، فَقَالَ: ((عِبَادَ الله، لَتُسَوُّنَّ صُفُوفَكُمْ أَوْ لَيُخَالِفَنَّ اللهُ بَيْنَ وُجُوهِكُمْ))

Abuu ‘Abdillaah, An-Nu’maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Wa-Allaahi mtazisawazisha safu zenu au Allaah Atazibadilisha nyuso zenu (ziwe kama wanyama au nyoyo zikhitilafiane).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema:

Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akizisawazisha safu kana kwamba alikuwa anasawazisha kwazo mshale, mpaka atuone kuwa tumefahamu juu ya umuhimu huo. Kisha siku moja akatoka, akasimama hata alipokaribia kupiga Takbiyr, akamuona mtu kifua chake kimetokeza, akasema: “Enyi waja wa Allaah, mtasawazisha safu zenu au Allaah Atazibadilisha nyuso zenu (ziwe kama wanyama au nyoyo zikhitilafiane).”

 

 

Hadiyth – 6

 

عن أَبي موسى رضي الله عنه قَالَ: احْتَرقَ بَيْتٌ بالمَدِينَةِ عَلَى أهْلِهِ مِنَ اللَّيلِ، فَلَمَّا حُدِّثَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم بشَأنِهِمْ، قَالَ: ((إنَّ هذِهِ النَّارَ عَدُوٌّ لَكُمْ، فَإِذَا نِمْتُمْ، فَأطْفِئُوهَا عَنْكُمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Muwsaa (Radhiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Siku moja nyumba iliteketea Madiynah wakati wa usiku na wenyewe wamo ndani. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipohadithhiwa habari hiyo, alisema: “Hakika huo moto ni adui yenu, mnapolala uzimeni.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

 

عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ مَثَلَ مَا بَعَثَنِي الله بِهِ مِنَ الهُدَى والعِلْم كَمَثَلِ غَيثٍ أَصَابَ أرْضًا فَكَانَتْ مِنْهَا طَائِفةٌ طَيِّبَةٌ، قَبِلَتِ المَاءَ فَأَنْبَتَتِ الكَلأَ والعُشْبَ الكَثِيرَ، وَكَانَ مِنْهَا أَجَادِبُ أمسَكَتِ المَاء فَنَفَعَ اللهُ بِهَا النَّاسَ فَشَربُوا مِنْهَا وَسَقُوا وَزَرَعُوا، وَأَصَابَ طَائفةً مِنْهَا أخْرَى إنَّمَا هِيَ قيعَانٌ لا تُمْسِكُ مَاءً وَلا تُنْبِتُ كَلأً، فَذَلِكَ مَثَلُ مَنْ فَقُهَ في دِينِ اللهِ وَنَفَعَهُ بمَا بَعَثَنِي الله بِهِ فَعَلِمَ وَعَلَّمَ، وَمَثَلُ مَنْ لَمْ يَرْفَعْ بِذَلِكَ رَأسًا وَلَمْ يَقْبَلْ هُدَى اللهِ الَّذِي أُرْسِلْتُ بِهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mfano wa Aliyonituma kwayo Allaah katika uongofu na elimu, ni mfano wa mvua nyingi iliyonyesha katika nchi, ikawa ina rutuba, ikakubali maji, ikaotesha nyasi na maji mengi. Na sehemu nyingine ikawa ni kavu na ngumu inayozuia maji, Allaah Akawanufaisha watu kwa mvua hiyo. Wakanywa, wakanywesha mifugo na kulimia kwayo. Na ikanyesha sehemu nyingine ambayo ni kavu haizuii maji, wala haioteshi nyasi. Basi mifano hiyo ni mfano wa mtu aliyekuwa na ufahamu mzuri katika Dini ya Allaah, yakamnufaisha yale Aliyonituma kwayo Allaah, akajifunza na akafundisha. Na mfano wa mwisho ni mfano wa mtu ambaye, hakuinua kichwa kwa jambo hilo na wala hakuukubali uongofu wa Allaah niliyotumwa nao.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

 

عن جابر رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَثَلِي وَمَثَلُكُمْ كَمَثَلِ رَجُلٍ أوْقَدَ نَارًا فَجَعَلَ الجَنَادِبُ والفَرَاشُ يَقَعْنَ فِيهَا وَهُوَ يَذُبُّهُنَّ عَنْهَا، وَأَنَا آخذٌ بحُجَزكُمْ عَنِ النَّارِ، وَأنْتُمْ تَفَلَّتونَ مِنْ يَدَيَّ)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mfano wangu na mfano wenu ni kama mtu aliyewasha moto, panzi na vipepeo wakawa wanaingia naye humo (mtu huyo) akawa anazuia wasiingie. Nami nimewashika viuno vyenu (sehemu ya kuifungia mkanda) kuwaokoa na moto, lakini mnaniponyoka mkononi mwangu (nashinda kuwazuia)!” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

 

عَنْهُ أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم أَمَرَ بِلَعْقِ الأَصَابِعِ وَالصَّحْفَةِ، وَقَالَ: ((إنَّكُمْ لا تَدْرونَ في أَيِّها البَرَكَةُ)). رواه مسلم.

وفي رواية لَهُ: ((إِذَا وَقَعَتْ لُقْمَةُ أَحَدِكُمْ فَلْيَأخُذْهَا، فَليُمِطْ مَا كَانَ بِهَا مِنْ أذىً، وَلْيَأكُلْهَا وَلا يَدَعْهَا لِلشَّيطَانِ، وَلا يَمْسَحْ يَدَهُ بالمنْدِيلِ حَتَّى يَلْعَقَ أصَابعَهُ فَإِنَّهُ لا يَدْرِي في أيِّ طَعَامِهِ البَرَكَةُ)).

وفي رواية لَهُ: ((إنَّ الشَّيطَانَ يَحْضُرُ أَحَدَكُمْ عِنْدَ كُلِّ شَيءٍ مِنْ شَأنِهِ، حَتَّى يَحْضُرَهُ عِنْدَ طَعَامِهِ، فَإذَ سَقَطَتْ مِنْ أَحَدِكُمْ اللُّقْمَةُ فَليُمِطْ مَا كَانَ بِهَا مِنْ أذَىً، فَلْيَأكُلْهَا وَلا يَدَعْهَا لِلشَّيطَانِ))

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha kulamba vidole na sahani, akasema: “Ninyi hamjui ni wapi penye baraka.” [Muslim] 

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema: 

 “Linapoanguka tonge la chakula la mmoja wenu, aliokote na aondoe taka iliyoingia na alile, wala asimuachie shaytwaan, wala asiupanguse mkono wake kwa kitambaa mpaka avilambe kidole vyake; kwani hajui ni katika chakula kipi kuna baraka.” 

Riwaayaha nyingine tena ya Muslim imesema:  

“Hakika shaytwaan anahudhuria katika kila jambo la mmoja wenu hata anahudhuria  kwenye chakula chake. Basi linapoanguka tonge la chakula la mmoja wenu, aondoe sehemu iliyoingia taka na alile, wala asimuachie shaytwaan.”

 

 

Hadiyth – 10

 

عن ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: قَامَ فِينَا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بِمَوعِظَةٍ، فَقَالَ: "يَا أيُّهَا النَّاسُ، إنَّكُمْ مَحْشُورونَ إِلَى الله تَعَالَى حُفَاةً عُرَاةً غُرْلًا" كَمَا بَدَأْنَا أَوَّلَ خَلْقٍ نُعِيدُهُ وَعْدًا عَلَيْنَا إِنَّا كُنَّا فَاعِلِينَ  

ألا وَإنَّ أَوَّلَ الخَلائِقِ يُكْسى يَومَ القِيَامَةِ إبراهيمُ صلى الله عليه وسلم، ألا وَإِنَّهُ سَيُجَاءُ بِرجالٍ مِنْ أُمَّتي فَيُؤخَذُ بِهِمْ ذَاتَ الشَّمالِ، فَأَقُولُ: يَا رَبِّ أصْحَابِي. فَيُقَالُ: إنَّكَ لا تَدْرِي مَا أحْدَثُوا بَعْدَكَ. فَأقُولُ كَما قَالَ العَبدُ الصَّالِحُ: {وَكُنْتُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا مَا دُمْتُ فِيهِمْ} إِلَى قولِهِ: {العَزِيزُ الحَكِيمُ} [المائدة: 117- 118] فَيُقَالُ لِي: "إنَّهُمْ لَمْ يَزَالُوا مُرْتَدِّينَ عَلَى أعْقَابِهِمْ مُنْذُ فَارَقْتَهُمْ" مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (رضي الله عنهما)   amesema: Siku moja Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  alisimama na kututolea mawaidha akasema: “Enyi watu, hakika mtafufuliwa na Allaah haliyakuwa hamna viatu, mpo uchi na bila kutahiriwa  (na magovi) Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

كَمَا بَدَأْنَا أَوَّلَ خَلْقٍ نُّعِيدُهُ

Kama Tulivyoanza umbo la awali Tutalirudisha tena [Al-Anbiyaa: 104]

 

Tanabahini! Hakika mtu wa kwanza atakayevishwa nguo ni Nabiy Ibraahiym (عليه السّلام). Tanabahini! Wataletwa watu katika Ummah wangu na watapelekwa upande wa kushoto (motoni), nami nitasema: “Ee Rabb wangu, Swahaba wangu!” Nitaambiwa: “Wewe hujui watu hawa walichokizua baada yako.” Hapo nitasema kama alivyosema mja mwema (Nabiy ‘Iysaa):

 

وَكُنتُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا مَّا دُمْتُ فِيهِمْ ۖ فَلَمَّا تَوَفَّيْتَنِي كُنتَ أَنتَ الرَّقِيبَ عَلَيْهِمْ ۚ وَأَنتَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ ﴿١١٧﴾

Na nilikuwa juu yao shahidi wakati nilipokuwa nao. Uliponikamilishia muda Ukanichukua juu, Ulikuwa Wewe Ndiye Mwangalizi juu yao. Na Wewe Ni Mwenye Kushuhudia kila kitu.

 

إِن تُعَذِّبْهُمْ فَإِنَّهُمْ عِبَادُكَ ۖ وَإِن تَغْفِرْ لَهُمْ فَإِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١١٨﴾

Ukiwaadhibu, basi bila shaka hao ni Waja Wako, na Ukiwaghufuria basi hakika Wewe Ndiye Mwenye Enzi na Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote. [Al-Maaidah (5:117-118]

 

Nitaambiwa: “Wao waliendelea kukengeuka na kugeuka nyuma kuondokelea mbali ulipowaacha.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

 

عن أَبي سعيد عبد الله بن مُغَفَّلٍ رضي الله عنه قَالَ: نَهَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الخَذْفِ، وقالَ: ((إنَّهُ لا يَقْتُلُ الصَّيْدَ، وَلا يَنْكَأُ العَدُوَّ، وإنَّهُ يَفْقَأُ العَيْنَ، وَيَكْسِرُ السِّنَّ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

وفي رواية: أنَّ قَريبًا لابْنِ مُغَفَّل خَذَفَ فَنَهَاهُ، وَقالَ: إنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم نَهَى عَن الخَذْفِ، وَقَالَ: ((إنَّهَا لا تَصِيدُ صَيدًا)) ثُمَّ عادَ، فَقَالَ: أُحَدِّثُكَ أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم نَهَى عَنْهُ، ثُمَّ عُدْتَ تَخذفُ!؟ لا أُكَلِّمُكَ أَبَدًا.

Abuu Sa’yd, ‘Abdullaah bin Mughaffal (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza al-khadhaf’ (kurusha vijiwe kwa kutumia kidole gumba na cha shahaadah) akasema: “Kwani hakiuwi windo wala hakimuuwi adui, bali hutoboa jicho na kuvunja jino tu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema:

“Jamaa mmoja wa karibu kwa Ibn Mughaffal alifanya khadhaf. Akamkataza na akamwambia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kitendo hiki (khadhaf), akasema: “Kwani hakiwindi windo” Kisha yule jamaa akarudia kitendo hicho. Akamwambia: Nimekuhadithia kuwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza jambo hilo kisha umerudia kitendo hicho cha khadhaf? Sitazungumza nawe kamwe!

 

 

Hadiyth – 12

 

 وعَن عابس بن رَبيعة، قَالَ: رَأيْتُ عُمَرَ بن الخطاب رضي الله عنه يُقَبِّلُ الحَجَرَ- يَعْنِي: الأسْوَدَ- وَيَقُولُ: إني أَعْلَمُ أنَّكَ حَجَرٌ مَا تَنْفَعُ وَلا تَضُرُّ، وَلَولا أنِّي رَأيْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يُقَبِّلُكَ مَا قَبَّلْتُكَ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

‘Aabis bin Rabiy’h amesema: Nilimuona ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akilibusu Hajarul Aswad (jiwe jeusi) na akasema: Hakika najua wewe ni jiwe, hunufaishi wala hudhuru, lau kama nisingelimuona Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akikubusu nisingelikubusu. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

017-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Wajibu Wa Kuifuata Hukumu Ya Allaah

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب وجوب الانقياد لحكم الله تعالى

وما يقوله من دُعِيَ إلى ذلك وأُمر بمعروف أو نُهي عن منكر

017–Wajibu Wa Kuifuata Hukumu Ya Allaah (Ta'aalaa)

Na Yale Anayotakiwa Mtu Kuyasema Pindi Anapoitwa Katika Hayo,

Akaamrishwa Mema Au Akakatazwa Munkari

 

Alhidaaya.com

 

 

قال الله تعالى:

 

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٦٥﴾

Basi Naapa kwa Rabb wako, hawatoamini mpaka wakufanye wewe ni mwamuzi katika yale wanayozozana baina yao, kisha wasipate katika nyoyo zao karaha katika yale uliyohukumu na wajisalimishe, kwa kujisalimisha (kikamilifu). [An-Nisaa: 65]

 

إِنَّمَا كَانَ قَوْلَ الْمُؤْمِنِينَ إِذَا دُعُوا إِلَى اللَّـهِ وَرَسُولِهِ لِيَحْكُمَ بَيْنَهُمْ أَن يَقُولُوا سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا ۚ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿٥١﴾

Hakika kauli ya Waumini wa kweli wanapoitwa kwa Allaah na Rasuli Wake ili Awahakumu baina yao; husema: “Tumesikia na Tumetii.” Na hao ndio wenye kufaulu. [An-Nuwr: 51]

 

 

Hadiyth - 1

 

عن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: لَمَّا نَزَلَتْ عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((لِلَّهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَإِنْ تُبْدُوا مَا فِي أَنْفُسِكُمْ أَوْ تُخْفُوهُ يُحَاسِبْكُمْ بِهِ اللَّهُ)) [البقرة: 284] الآية.

اشْتَدَّ ذلِكَ عَلَى أصْحَابِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، فَأتَوا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ثُمَّ بَرَكُوا عَلَى الرُّكَبِ، فَقَالُوا: أيْ رسولَ الله، كُلِّفْنَا مِنَ الأَعمَالِ مَا نُطِيقُ: الصَّلاةَ والجِهَادَ والصِّيامَ والصَّدَقَةَ، وَقَدْ أُنْزِلَتْ عَلَيْكَ هذِهِ الآيَةُ وَلا نُطيقُها. قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((أتُرِيدُونَ أنْ تَقُولُوا كَمَا قَالَ أَهْلُ الكتَابَينِ مِنْ قَبْلِكُمْ: سَمِعْنَا وَعَصَيْنَا؟ بَلْ قُولُوا: سَمِعنَا وَأَطَعْنَا غُفْرَانَكَ رَبَّنَا وَإِلَيْكَ المَصِيرُ))  قَالُوا: سمعنا وأَطعنا غفرانك ربنا وإِليك المصير  

فَلَمَّا اقْتَرَأَهَا القومُ، وَذَلَّتْ بِهَا ألْسنَتُهُمْ أنْزَلَ اللهُ تَعَالَى في إثرِهَا: ((آمَنَ الرَّسُولُ بِمَا أُنْزِلَ إِلَيْهِ مِنْ رَبِّهِ وَالْمُؤْمِنُونَ كُلٌّ آمَنَ بِاللهِ وَمَلائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ لا نُفَرِّقُ بَيْنَ أَحَدٍ مِنْ رُسُلِهِ وَقَالُوا سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا غُفْرَانَكَ رَبَّنَا وَإِلَيْكَ الْمَصِيرُ)) [البقرة: 285]

 

فَلَمَّا فَعَلُوا ذلِكَ نَسَخَهَا اللهُ تَعَالَى، فَأنزَلَ الله- عز وجل: ((لا يُكَلِّفُ اللهُ نَفْسًا إِلا وُسْعَهَا لَهَا مَا كَسَبَتْ وَعَلَيْهَا مَا اكْتَسَبَتْ رَبَّنَا لا تُؤَاخِذْنَا إِنْ نَسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا)) قَالَ: نَعَمْ

((رَبَّنَا وَلا تَحْمِلْ عَلَيْنَا إِصْرًا كَمَا حَمَلْتَهُ عَلَى الَّذِينَ مِنْ قَبْلِنَا))  قَالَ: نَعَمْ

((رَبَّنَا وَلا تُحَمِّلْنَا مَا لا طَاقَةَ لَنَا بِه))  قَالَ: نَعَمْ

((وَاعْفُ عَنَّا وَاغْفِرْ لَنَا وَارْحَمْنَا أَنْتَ مَوْلانَا فَانْصُرْنَا عَلَى الْقَوْمِ الْكَافِرِينَ)) قَالَ: نَعَمْ. رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salaam) alipoteremshiwa Aayah hii: Ni vya Allaah Pekee vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na mkidhihirisha yale yaliyomo ndani ya nafsi zenu au mkiyaficha; basi Allaah Atakuhesabuni kwayo.” Mpaka mwisho wa Aayah. [Al-Baqarah: 284]

 

Jambo hilo likawa zito kwa Maswahaba wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salaam) wakamwendea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salaam) wakapiga magoti, wakasema: Ee Rasuli wa Allaah, tumekalifishwa ‘amali tunazoziweza; Swalaah, Jihaad, Swawm na kutoa Zakaah. Na kwa hakika umeteremshiwa Aayah hii, lakini hatuiwezi! Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salaam) akawauliza: “Je, mnataka kusema kama walivyosema Ahlul-Kitaabayni (Mayahudi na Manaswara) kabla yenu? “Tumesikia na tumeasi” Bali semeni: Tumesikia na tumetii, tunakuomba maghfirah Rabb wetu Kwako ni mahali pa kuishia.”

Maswahaba walipoisoma na ndimi zao zikaandama. Allaah Aliteremsha:

 Rasuli ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Rabb wake na Waumini (pia wameamini). Wote wamemwamini Allaah, na Malaika Wake, na Vitabu Vyake, na Rasuli Wake. (Nao husema): “Hatutofautishi baina ya yeyote kati ya Rasuli Wake.” Na wakasema: “Tumesikia na tumetii, tunakuomba maghfirah Rabb wetu na Kwako ni mahali pa kuishia.” [Al-Baqarah: 285]

 

Walipofanya hivyo, Allaah Aliifuta (hukmu ya) Aayah hiyo, Akateremsha:

“Allaah Hakalifishi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya uwezo wake. Itapata (thawabu) iliyoyachuma, na ni dhidi yake (kwa maovu) iliyojichumia. “Rabb wetu Usituchukulie tukisahau au tukikosea.” Akasema: “Na’aam”.

 

“Rabb wetu, Usitubebeshe mzigo kama Ulivyoubebesha juu ya wale waliokuwa kabla yetu.” Akasema: “Na’aam”.

 

 “Rabb wetu, Usitutwike tusiyoyaweza, na Tusamehe, na Tughufurie na Turehemu, Wewe ni Mola Mlinzi wetu, basi Tunusuru dhidi ya watu makafiri.” Akasema: “Na’aam”.  [Muslim]

 

 

Share

018-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukataza Bid’ah Na Uzushi

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب النهي عن البدع ومحدثات الأمور

018 - Mlango Wa Kukataza Bid’ah Na Uzushi

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ تَعَالَى:

 

فَمَاذَا بَعْدَ الْحَقِّ إِلَّا الضَّلَالُ ۖ

Na kuna nini baada ya haki ila upotofu? [Yuwnus: 32]

 

مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ ۚ

Hatukusuru katika Kitabu kitu chochote. [Al-An’aam: 38]

 

فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ

Mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allaah na Rasuli. [An-Nisaa: 59]

 

وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ

Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. [Al-An’aam: 153]

 

 قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi, Atakupendeni Allaah na Atakughufurieni dhambi zenu. [Aal-‘Imraan: 31]

 

 

Hadiyth – 1

عن عائشة رَضِي الله عنها، قَالَتْ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ أحْدَثَ في أمْرِنَا هَذَا مَا لَيْسَ مِنْهُ فَهُوَ رَدٌّ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

وفي رواية لمسلم: ((مَنْ عَمِلَ عَمَلًا لَيْسَ عَلَيهِ أمرُنا فَهُوَ رَدٌّ))

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Mwenye kuzua katika jambo letu hili lisilokuwemo humo litakataliwa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Muslim: “Mwenyekufanya amali isiyokuwa na hukmu yetu, itakataliwa.”

 

 

Hadiyth – 2

وعن جابر رضي الله عنه قَالَ: كَانَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا خَطَبَ احْمَرَّتْ عَينَاهُ، وَعَلا صَوتُهُ، وَاشْتَدَّ غَضَبُهُ، حَتَّى كَأنَّهُ مُنْذِرُ جَيشٍ، يَقُولُ: ((صَبَّحَكُمْ وَمَسَّاكُمْ)) وَيَقُولُ: ((بُعِثتُ أنَا والسَّاعَةُ كَهَاتَينِ)) وَيَقْرِنُ بَيْنَ أُصبُعَيهِ السَّبَّابَةِ وَالوُسْطَى، وَيَقُولُ: ((أمَّا بَعْدُ، فَإنَّ خَيْرَ الحَديثِ كِتَابُ الله، وَخَيرَ الهَدْيِ هَدْيُ مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم، وَشَرَّ الأُمُورِ مُحْدَثَاتُهَا، وَكُلَّ بِدْعَة ضَلالَةٌ)) ثُمَّ يَقُولُ: ((أنَا أوْلَى بِكُلِّ مُؤمِنٍ مِنْ نَفسِهِ، مَنْ تَرَكَ مَالًا فَلأَهْلِهِ، وَمَنْ تَرَكَ دَيْنًا أَوْ ضَيَاعًا فَإلَيَّ وَعَلَيَّ)). رواه مسلم

وعن العرباض بن سَارية رضي الله عنه حدِيثه السابق في بابِ المحافظةِ عَلَى السنةِ

وفيه: ((فإنه من يعش منكم فسيرى اختلافًا كثيرًا فعليكم بسنَّتي...))

Kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kwamba: Alipokuwa akikhutubia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) macho yake yalikuwa yakibadilika rangi na kuwa mekundu, na akinyanyua sauti yake na ghadhabu ilikuwa kali kana kwamba alikuwa akitutahadharisha na jeshi la adui. Alikuwa akisema: “Maadui watawashambulieni asubuhi na usiku.” Na pia akisema: “Nimetumwa mimi kuja siku mwisho kama hivi.” Na alikuwa anavishikanisha vidole vyake (kidole cha kati na cha shahada), na akisema tena: Ama baada (ya salamu): “Hakika mazungumzo bora ni maneno ya Allaah (Qur-aan) na uongofu bora ni uongofu wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam), na mambo yaliyomaovu ni yale yenyekuzuliwa na kila bid’ah ni upotevu.” [Muslim]

Kisha alikuwa akisema: “Mimi ni mwenyekumtakia kila Muumin masilahi yake kuliko anavyojitakia nafsi yake, hivyo yoyote atayeacha mali ni kwa watu wake, na yoyote atakayeacha deni au watoto na familia basi hayo yatakuwa juu yangu.”

Na imepokewa kwa ‘Irbaadhw bin Saariyah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Hadiyth iliyotangulia katika mlango wa: Amri ya kuhifadhi Sunnah na adabu zake: Hakika atakayeishi umri mrefu miongoni mwenu ataona khitilafu nyingi.”

 

 

Share

019-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Mwenye Kuzua Sunnah Nzuri Na Mbaya

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فيمن سن سنة حسنة أَوْ سيئة

019 – Mlango Wa Mwenye Kuzua Sunnah Nzuri Na Mbaya

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ تَعَالَى:

 

وَالَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا ﴿٧٤﴾

Na wale wanaosema: “Rabb wetu! Tutunukie katika wake zetu na dhuria wetu viburudisho vya macho yetu, na Tujaalie kuwa waongozi kwa wenye taqwa. [Al-Furqaan: 74]

 

وَجَعَلْنَاهُمْ أَئِمَّةً يَهْدُونَ بِأَمْرِنَا

Na Tukawajaalia Maimaam wanaongoza kwa amri Yetu. [Al-Anbiyaa: 73]

 

 

Hadiyth - 1

عن أَبي عمرو جرير بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: كنا في صَدْرِ النَّهَارِ عِنْدَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فَجَاءهُ قَومٌ عُرَاةٌ مُجْتَابي النِّمَار أَوْ العَبَاء، مُتَقَلِّدِي السُّيُوف، عَامَّتُهُمْ من مُضر، بَلْ كُلُّهُمْ مِنْ مُضَرَ، فَتَمَعَّرَ وَجْهُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم لما رَأَى بِهِمْ مِنَ الفَاقَة، فَدَخَلَ ثُمَّ خَرَجَ، فَأَمَرَ بِلالًا فَأَذَّنَ وَأَقَامَ، فصَلَّى ثُمَّ خَطَبَ، فَقَالَ: (({يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ مِنْ نَفْسٍ وَاحِدَةٍ} إِلَى آخر الآية: {إِنَّ اللهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا}، والآية الأُخْرَى التي في آخر الحَشْرِ: {يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللهَ وَلْتَنْظُرْ نَفْسٌ مَا قَدَّمَتْ لِغَدٍ} تَصَدَّقَ رَجُلٌ مِنْ دِينَارِهِ، مِنْ دِرهمِهِ، مِنْ ثَوبِهِ، مِنْ صَاعِ بُرِّهِ، مِنْ صَاعِ تَمْرِهِ- حَتَّى قَالَ: وَلَوْ بِشقِّ تَمرَةٍ)).

فَجَاءَ رَجُلٌ مِنَ الأَنْصَارِ بِصُرَّةٍ كَادَتْ كَفُّهُ تَعجَزُ عَنهَا، بَلْ قَدْ عَجَزَتْ، ثُمَّ تَتَابَعَ النَّاسُ حَتَّى رَأيْتُ كَومَيْنِ مِنْ طَعَامٍ وَثِيَابٍ، حَتَّى رَأيْتُ وَجْهَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَتَهَلَّلُ كَأنَّهُ مُذْهَبَةٌ. فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ سَنَّ في الإسلامِ سنَّةً حَسَنَةً فَلَهُ أجْرُهَا، وَأجْرُ مَنْ عَمِلَ بِهَا مِنْ بَعْدَهُ، مِنْ غَيرِ أنْ يَنْقُصَ مِنْ أُجُورهمْ شَيءٌ، وَمَنْ سَنَّ في الإسْلامِ سُنَّةً سَيِّئَةً كَانَ عَلَيهِ وِزْرُهَا، وَوِزْرُ مَنْ عَمِلَ بِهَا مِنْ بَعْدِهِ، مِنْ غَيرِ أنْ يَنْقُصَ مِنْ أوْزَارِهمْ شَيءٌ)). رواه مسلم

Abuu ‘Amruw Jariyr bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kwamba: Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) mchana na siku moja. Wakati huo mara wakaja watu waliokuwa hawakuvaa nguo bali nguo za magunia katika miili yao, na wengine walikuwa na kama majoho, panga zao zikiwa zinagusa chini. Takriban wote walikuwa wanatoka kabila ya Mudhar, bali wote walikuwa ni kutoka kabila la Mudhar. Uso wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) ulibadilika kwa kuwaona hawa watu katika hali hii ya shida na njaa. Akaingia nyumbani kwake kisha akatoka. Alimuamuru Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu) aadhini kisha akimu, baada ya hapo aliswalisha na kuwahutubia watu baada ya Swalah, akasema: Enyi watu! Mcheni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume na wanawake wengi. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. Hakika Allaah ni Mwenye kuwachunga daima.”

 

”Kisha akasoma ile aayah nyingine ambayo ipo mwisho wa Suwratu Al-Hashr: Enyi walioamini! Mcheni Allaah, na nafsi itazame imetanguliza nini kwa ajili ya kesho, na mcheni Allaah.”

Baada ya hayo akawaomba watu watoe sadaka katika dinari zao, dirhamu, nguo, kipimo maalumu cha ngano na tende mpaka akasema: “Hata kama ni kipande cha tende.” Kusikia haya mtu mmoja wa ki Answaar alikuja na mzigo mkubwa, ambao ulimuelemea sana kuubeba. Wengine wakamfuata kwa kuleta sadaka zao mpaka nikaona milima miwili ya chakula na nguo. Hapo nikauona uso wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) unang’aa kama dhahabu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alisema baada ya hayo: “Yeyote atakayezua katika Uislamu Sunnah nzuri atapata thawabu ya kitendo hicho na ujira (thawabu) za wenye kufanya kitendo hicho baada yake bila ya wale waliokuja baada yake kupunguziwa thawabu zao. Na yeyote atakayezua katika Uislamu Sunnah mbaya, atapata madhambi ya kufanya jambo hilo na madhambi ya wenye kumfuata yeye baada yake bila ya wao kupunguziwa chochote katika madhambi yao. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن ابنِ مسعود رضي الله عنه أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((لَيْسَ مِنْ نَفْسٍ تُقْتَلُ ظُلْمًا إلا كَانَ عَلَى ابْنِ آدَمَ الأوْلِ كِفْلٌ مِنْ دَمِهَا، لأَنَّهُ كَانَ أوَّلَ مَنْ سَنَّ القَتلَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Kutoka kwa Ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Hakuna nafsi yeyote inayouliwa kwa dhulma isipokuwa yule mwanadamu wa kwanza atapata sehemu yake ya madhambi (ya mauaji) kwani yeye ndiye wa mwanzo kuanzisha mauaji.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

020-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuhimiza Mema Na Kuwaita Watu Katika Uongofu Au Upotevu

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب في الدلالة عَلَى خير والدعاء إِلَى هدى أَوْ ضلالة

20 – Mlango Wa Kuhimiza Mema Na Kuwaita Watu Katika Uongofu Au Upotevu

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ تَعَالَى:

 

وَادْعُ إِلَىٰ رَبِّكَ ۖ

Na lingania kwa Rabb wako[Al-Qaswasw: 87]

 

ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ

Lingania katika njia ya Rabb wako kwa hikmah na mawaidha mazuri. [An-Nahl: 125]

 

وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ

Na shirikianeni katika wema na taqwa… [Al-Maaidah: 2]

 

وَلْتَكُن مِّنكُمْ أُمَّةٌ يَدْعُونَ إِلَى الْخَيْرِ

Na watokeze kutoka kwenu umati wa watu unaolingania kheri… [Aal-‘Imraan: 104]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي مسعود عُقبةَ بنِ عمرو الأنصاري البدري رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ دَلَّ عَلَى خَيْرٍ فَلَهُ مِثْلُ أجْرِ فَاعِلِهِ)). رواه مسلم

Kutoka kwa Abuu Mas’uwd ‘Uqbah bin ‘Amru Al-Answaar Al-Badriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): “Yeyote mwenye kumuelekeza mtu katika jambo jema atapata ujira wa mfano wa yule mwenye kufanya (hilo jambo jema).” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((مَنْ دَعَا إِلَى هُدَىً، كَانَ لَهُ مِنَ الأَجْرِ مِثْلُ أجُورِ مَنْ تَبِعَه، لاَ يَنْقُصُ ذلِكَ مِنْ أجُورِهمْ شَيئًا، وَمَنْ دَعَا إِلَى ضَلاَلَةٍ، كَانَ عَلَيهِ مِنَ الإثْمِ مِثْلُ آثَامِ مَنْ تَبِعَهُ، لا يَنْقُصُ ذلِكَ مِنْ آثَامِهِمْ شَيئًا)). رواه مسلم

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Yeyote anayewaita wengine katika uongofu atapata thawabu mfano wa wale wenye kumfuata wala hilo haliwapunguzii thawabu zao hata kidogo. Na yeyote atakayewaita watu katika upotevu atapata madhambi mfano wa madhambi ya wale wenye kumfuata na wala hilo halitawapunguzia madhambi hata chembe.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي العباس سهل بن سعد الساعدي رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ يوم خَيبَر: ((لأُعْطِيَنَّ الرَّايَةَ غَدًا رجلًا يَفْتَحُ الله عَلَى يَدَيهِ، يُحبُّ اللهَ وَرَسولَهُ، ويُحِبُّهُ اللهُ وَرَسُولُهُ))، فَبَاتَ النَّاسُ يَدُوكُونَ لَيْلَتَهُمْ أيُّهُمْ يُعْطَاهَا. فَلَمَّا أصْبَحَ النَّاسُ غَدَوْا عَلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم كُلُّهُمْ يَرْجُو أنْ يُعْطَاهَا. فَقَالَ: ((أينَ عَلِيُّ بنُ أَبي طالب؟)) فقيلَ: يَا رسولَ الله، هُوَ يَشْتَكي عَيْنَيهِ. قَالَ: ((فَأَرْسِلُوا إِلَيْه)) فَأُتِيَ بِهِ فَبَصَقَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم في عَيْنَيْهِ، وَدَعَا لَهُ فَبَرِئَ حَتَّى كأنْ لَمْ يكُن بِهِ وَجَعٌ، فأعْطاهُ الرَّايَةَ. فقَالَ عَليٌّ رضي الله عنه: يَا رَسُول اللهِ، أقاتِلُهمْ حَتَّى يَكُونُوا مِثْلَنَا؟ فَقَالَ: ((انْفُذْ عَلَى رِسْلِكَ حَتَّى تَنْزِلَ بسَاحَتهمْ، ثُمَّ ادْعُهُمْ إِلَى الإسْلاَمِ، وَأخْبِرْهُمْ بِمَا يَجِبُ عَلَيْهِمْ مِنْ حَقِّ اللهِ تَعَالَى فِيهِ، فَوَالله لأَنْ يَهْدِيَ اللهُ بِكَ رَجُلًا وَاحِدًا خَيرٌ لَكَ مِنْ حُمْرِ النَّعَم)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Kutoka kwa Abul-‘Abbaas Sahl bin Sa’d As-Saa’idiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alisema siku  ya Khaybar: “Kesho nitampatia mtu bendera ambaye kwa mikono yake Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) atafungua (mji huu). Mtu huyo anampenda Allaah na Rasuli wake, basi Allaah na Rasuli wake wanampenda.” Watu wakakesha wakifikiria na kuzungumza juu ya nani atayepatiwa bendera hiyo. Kulipopambazuka watu wote walikwenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) kila mmoja anatarajia kuwa atapatiwa yeye jukumu hilo. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): “Yuko wapi ‘Aliy bin Abiy Twaalib?” Wakasema: “Ee Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)! Yeye anaumwa macho.” Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): “Mleteni kwangu.” Akaletwa kwake, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) akampaka mate yake katika macho na kumwombea kwa Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa). ‘Aliy akapona kabisa na ugonjwa huo (wa macho) mpaka ikaonekana kama kwamba hakuwa na tatizo lolote na hapo akapatiwa bendera. ‘Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) akasema: “Ee Mjumbe wa Allaah! Nipigane nao mpaka wawe kama sisi?” Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): “Endelea kwenda kwa kasi yako ya kawaida mpaka ufike katika bonde lao na hapo muweke kambi yenu. Kisha waite katika Uislamu na uwapashe habari kuhusu wajibu wao na majukumu yao kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ndani yake. Naapa kwa Allaah! Allaah akimuongoa mtu mmoja kupitia kwako ni bora kuliko kundi la ngamia wekundu. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه: أن فتىً مِنْ أسلم قَالَ: يَا رَسُول الله، إنِّي أُرِيدُ الغَزْوَ وَلَيْسَ معي مَا أتَجَهَّز بِهِ، قَالَ: ((ائتِ فُلاَنًا فإنَّهُ قَدْ كَانَ تَجَهَّزَ فَمَرِضَ)) فَأتَاهُ، فَقَالَ: إنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يُقْرِئُكَ السَّلامَ، وَيَقُولُ: أعْطني الَّذِي تَجَهَّزْتَ بِهِ، فَقَالَ: يَا فُلاَنَةُ، أعْطِيهِ الَّذِي تَجَهَّزْتُ بِهِ، وَلا تَحْبِسي مِنْهُ شَيئًا، فَواللهِ لا تَحْبِسِين مِنْهُ شَيئًا فَيُبَاركَ لَكِ فِيهِ. رواه مسلم

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba kijana katika kabila la Aslam alikuja na kusema: “Ee Mjumbe wa Allaah! Mimi ninataka kushiriki katika vita, lakini sina chochote cha kujitayarisha kwayo?” Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): “Nenda kwa Fulani kwani yeye amejitayarisha lakini akashikwa na maradhi.” Huyu kijana akaenda kwa huyo mtu na kumwambia: “Kwa hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) anakutolea salamu na anakwambia: Nipatie mimi vifaa ulivyovitayarisha ili kuvitumia katika vita.” Akasema yule Fulani: “Ewe mke wangu mpatie kila kitu nilichotayarisha wala usibakishe chochote. Naapa kwa Allaah, kisha ikiwa hutamnyima chochote katika vifaa nilivyotayarisha, Allaah atakubariki kwayo.” [Muslim]

 

 

Share

021-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kusaidiana Katika Wema Na Taqwa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب التعاون عَلَى البر والتقوى

021 – Mlango Wa Kusaidiana Katika Wema Na Taqwa

 

Alhidaaya.com

                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                          

قَالَ الله تَعَالَى:

 

وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ

Na shirikianeni katika wema na taqwa… (Al-Maaidah: 2)

 

وَالْعَصْرِ ﴿١﴾

Naapa kwa Al-‘Aswr (zama).

 

إِنَّ الْإِنسَانَ لَفِي خُسْرٍ ﴿٢﴾

Hakika mwana wa Aadam bila shaka yumo katika khasara.

 

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ ﴿٣﴾

Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema na wakausiana haki na wakausiana subira. [Al-‘Aswr: 1-3]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي عبد الرحمن زيد بن خالد الجهني رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ جَهَّزَ غَازِيًا في سَبيلِ اللهِ فَقَدْ غَزَا، وَمَنْ خَلَفَ غَازيًا في أهْلِهِ بِخَيرٍ فَقَدْ غَزَا)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Kutoka Kwa Abuu ‘Abdur-Rahmaan Zayd bin Khaalid Al-Juhaniy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Yeyote atakayemtayarisha kwa kumpatia vifaa Mujahid katika njia ya Allaah ni kama yeye mwenyewe amehudhuria katika kupigana (hivyo kupata thawabu sawa). Na yeyote mwenye kuwatizama watu wanaomtegemea Mujahid (wakati ambao hayupo) ni kama pia amepigana katika vita.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بعث بعثًا إِلَى بني لِحْيَان مِنْ هُذَيْلٍ، فَقَالَ: ((لِيَنْبَعِثْ مِنْ كُلِّ رَجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا وَالأجْرُ بَيْنَهُمَا)). رواه مسلم

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alituma kikosi kwa kabila la Lihyaan wa ukoo wa Hudhayl, akasema: “Atoke katika kila watu wawili mtu mmoja na ujira (thawabu) ni baina yao.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن عباس رضي الله عنهما: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم لَقِيَ رَكْبًا بالرَّوْحَاءِ، فَقَالَ: ((مَنِ القَوْمُ؟)) قالوا: المسلمون، فقالوا: من أنتَ؟ قَالَ: ((رَسُول الله))، فرفعت إِلَيْه امرأةٌ صبيًا، فَقَالَتْ: ألِهَذَا حَجٌّ؟ قَالَ: ((نَعَمْ، وَلَكِ أجْرٌ)). رواه مسلم

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alikutana na kikundi cha watu waliokuwa wamepanda vipandio katika sehemu ya Rawhaa na akawauliza: “Hawa ni watu gani?” Wakasema: “Waislamu.” Kisha wakasema: “Wewe ni nani?” Akasema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam).” Mwanamke mmoja aliyekwepo alimnyanyua mtoto mdogo na kuuliza: “Je,huyu ana hijja?” Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): “Ndio, nawe pia utapata ujira (kwa hilo).” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم أنَّه قَالَ: ((الخَازِنُ المُسْلِمُ الأمِينُ الَّذِي يُنفِذُ مَا أُمِرَ بِهِ فيُعْطيهِ كَامِلًا مُوَفَّرًا طَيِّبَةً بِهِ نَفْسُهُ فَيَدْفَعُهُ إِلَى الَّذِي أُمِرَ لَهُ بِهِ، أحَدُ المُتَصَدِّقين)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

وفي رواية: ((الَّذِي يُعْطِي مَا أُمِرَ بِهِ))

Kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash’ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema “Muweka hazina Muislamu, ni yule aliye muaminifu mwenye kumpatia mtu anayestahiki haki yake kwa ukamilifu na kuwa na nafasi nzuri. Na kule kumpatia yule aliyeamriwa kwake inakuwa ni swadaqa.

Riwaya nyengine: “Yule ambaye anatoa katika yale aliyomrishwa.”  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

022-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Nasaha

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب النصيحة

022 – Mlango Wa Nasaha

 

Alhidaaya.com

 

 

 

قَالَ تَعَالَى:

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ

Hakika Waumini ni ndugu… [Al-Hujraat: 10]

وَأَنصَحُ لَكُمْ

Na nakunasihini… [Al-A’raaf: 62]

 

وَأَنَا لَكُمْ نَاصِحٌ أَمِينٌ ﴿٦٨﴾

Nami kwenu ni mtoaji nasiha mwaminifu. [Al-A’raaf:68]

 

 

 

Hadiyth – 1

عن أَبي رُقَيَّةَ تَمِيم بن أوس الداريِّ رضي الله عنه: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((الدِّينُ النَّصِيحةُ)) قلنا: لِمَنْ؟ قَالَ: ((لِلهِ وَلِكِتَابِهِ وَلِرَسُولِهِ وَلأئِمَّةِ المُسْلِمِينَ وَعَامَّتِهِمْ)). رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abu Ruqayyah Tamiym ibn Aws Ad-Daariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba; Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Dini ni nasiha” Tukasema, kwanini? Akasema: “Kwa Allaah, na kitabu Chake, na Rasuli Wake, na kwa viongozi wa Waislamu na watu wa kawaida.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

عن جرير بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: بَايَعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم عَلَى إقَامِ الصَّلاةِ، وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ، والنُّصْحِ لِكُلِّ مُسْلِمٍ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokelewa kutoka kwa Jariyr bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alisema kwamba: Nilimbay’ Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) juu ya kusimamisha Swalaah, kutoa Zakaah, na kumnasihi kila Muislamu. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

عن جرير بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: بَايَعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم عَلَى إقَامِ الصَّلاةِ، وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ، والنُّصْحِ لِكُلِّ مُسْلِمٍ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Hatoamini mmoja wenu mpaka ampendelee nduguye kile anachopendelea nafsi yake.” [Al-Bukhariy na Muslim]

 

 

Share

023-Riyaadhw As-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuamrisha Mema Na Kukataza Maovu

Riyaadhw As-Swaalihiyn

 

باب الأمر بالمعروف والنهي عن المنكر

023 – Mlango Wa Kuamrisha Mema Na Kukataza Maovu

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ اللهُ تَعَالَى:

 

خَيْرِ وَيَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ ۚ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفلِحُونَ ﴿١٠٤﴾

Na watokeze kutoka kwenu umati wa watu unaolingania kheri na unaoamrisha mema na unaokataza munkari. Na hao ndio waliofaulu. [Aal-‘Imraan: 104]

 

 

كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ

Mmekuwa Ummah bora kabisa uliotolewa (mfano) kwa watu; mnaamrisha mema na mnakataza munkari… [Aal-‘Imraan: 110]

 

 

خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ﴿١٩٩﴾

Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili. [Al-A’raaf: 199]

 

 

وَالْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بَعْضُهُمْ أَوْلِيَاءُ بَعْضٍ ۚ يَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ

Na Waumini wanaume na Waumini wanawake ni marafiki wandani wao kwa wao, wanaamrisha mema na wanakataza munkari… [At-Tawbah: 71]

 

 

لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ لِسَانِ دَاوُودَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ ﴿٧٨﴾

Wamelaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israaiyl kwa lisani  ya Daawuwd na ‘Iysaa mwana wa Maryam. Hivyo ni kwa sababu ya kuasi kwao na walikuwa wakitaadi.

 

 

كَانُوا لَا يَتَنَاهَوْنَ عَن مُّنكَرٍ فَعَلُوهُ ۚ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ﴿٧٩﴾

Walikuwa hawakatazani munkari waliyofanya. Uovu ulioje waliyokuwa wakiyafanya. [Al- Maaidah: 78-79]

 

 

وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ ۖ فَمَن شَاءَ فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاءَ فَلْيَكْفُرْ ۚ

Na sema: “Hii ni haki kutoka kwa Rabb wenu. Basi anayetaka aamini, na anayetaka akufuru.” [Al-Kahf: 29]

 

 

فَاصْدَعْ بِمَا تُؤْمَرُ وَأَعْرِضْ عَنِ الْمُشْرِكِينَ﴿٩٤﴾

Basi tangaza wazi yale uliyoamrishwa na jitenge na washirikina. [Al-Hijr: 94]

 

 

فَلَمَّا نَسُوا مَا ذُكِّرُوا بِهِ أَنجَيْنَا الَّذِينَ يَنْهَوْنَ عَنِ السُّوءِ وَأَخَذْنَا الَّذِينَ ظَلَمُوا بِعَذَابٍ بَئِيسٍ بِمَا كَانُوا يَفْسُقُونَ ﴿١٦٥﴾

Waliposahau yale waliyokumbushwa nayo; Tuliwaokoa wale wanaokataza uovu, na Tukawachukua wale waliodhulumu kwa adhabu mbaya kabisa kwa yale waliyokuwa wakifanya ufasiki. [Al-A’raaf: 165]

 

 

 

Hadiyth – 1

عن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه قَالَ: سَمِعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((مَنْ رَأى مِنْكُمْ مُنْكَرًا فَلْيُغَيِّرْهُ بِيَدِهِ، فَإنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَبِلِسَانِهِ، فَإنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَبِقَلْبِهِ، وَذَلِكَ أضْعَفُ الإيمَانِ)). رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Sa’iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) akisema: “Yoyote katika nyinyi atakayeona munkari na aubadilishe kwa mkono wake, na akiwa hawezi basi afanye hivyo kwa ulimi wake, na akiwa hawezi basi afanye hivyo kwa moyo wake, na huo ni udhaifu wa iymaan.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

عن ابن مسعود رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَا مِنْ نَبيٍّ بَعَثَهُ اللهُ في أمَّة قَبْلِي إلا كَانَ لَهُ مِنْ أُمَّتِهِ حَوَارِيُّونَ وَأصْحَابٌ يَأخُذُونَ بِسنَّتِهِ وَيَقْتَدُونَ بِأَمْرِهِ، ثُمَّ إِنَّهَا تَخْلُفُ مِنْ بَعْدِهِمْ خُلُوفٌ يَقُولُونَ مَا لا يَفْعَلُونَ وَيَفْعَلُونَ مَا لا يُؤْمَرونَ، فَمَنْ جَاهَدَهُمْ بِيَدِهِ فَهُوَ مُؤْمِنٌ، وَمَنْ جَاهَدَهُمْ بِقَلبِهِ فَهُوَ مُؤمِنٌ، وَمَنْ جَاهَدَهُمْ بِلسَانِهِ فَهُوَ مُؤمِنٌ، وَلَيسَ وَرَاءَ ذلِكَ مِنَ الإيمَانِ حَبَّةُ خَرْدَل)). رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Hakuna Nabiy yoyote aliyetumwa kabla yangu isipokuwa alikuwa na wateule wake (Maswahaba na wanafunzi wake) katika Ummah wake. Hawa Maswahaba (wa Manabiy) walikuwa wakifuata mwendo wake (Sunnah za Nabiy wao) na kufuata maagizo yake. Baada yao wakaja wafuasi waliozua (mambo yao wenyewe) huku wakisema wasiyotenda na kutenda wasiyoamrishwa. Hivyo, yoyote atakayepigana nao kwa mkono wake ni Muumin, na anayepigana nao kwa moyo wake pia ni Muumin, na anayepigana nao kwa ulimi wake pia ni Muumin. Hapana nyuma ya haya chembe ya iymaan.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

عن أبي الوليدِ عبادة بن الصامِت رضي الله عنه قَالَ: بَايَعْنَا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم عَلَى السَّمْعِ والطَّاعَةِ في العُسْرِ واليُسْرِ، والمَنْشَطِ وَالمَكْرَهِ، وَعَلَى أثَرَةٍ عَلَيْنَا، وَعَلَى أنْ لا نُنازِعَ الأمْرَ أهْلَهُ إلا أنْ تَرَوْا كُفْرًا بَوَاحًا عِنْدَكُمْ مِنَ اللهِ تَعَالَى فِيهِ بُرْهَانٌ، وَعَلَى أنْ نَقُولَ بالحَقِّ أيْنَمَا كُنَّا لا نَخَافُ في اللهِ لَوْمَةَ لاَئِمٍ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imeokewa kutoka kwa Abul Waliyd ‘Ubadah bin As-Swaamit (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Tulimbay’ Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) juu ya kusikia na kutii wakati wa mazito na mepesi, na katika raha na shida na kuweza kuhimilia wakati unapobaguliwa (na kushinda). Na pia tusiwe ni wenye kuzozana na viongozi isipokuwa unapoona ukafiri wa wazi kabisa, hapo mtakuwa na dalili ya wazi na ruhusa kutoka kwa Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa). Na tuwe ni wenye kusema kweli popote tulipo wala tusiogope lawama ya anaye laumu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

عن النعمان بن بشير رضي الله عنهما عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَثَلُ القَائِمِ في حُدُودِ اللهِ وَالوَاقعِ فِيهَا، كَمَثَلِ قَومٍ اسْتَهَمُوا عَلَى سَفِينَةٍ فَصَارَ بَعْضُهُمْ أعْلاها وَبَعْضُهُمْ أَسْفَلَهَا، وَكَانَ الَّذِينَ في أَسْفَلِهَا إِذَا اسْتَقَوا مِنَ المَاءِ مَرُّوا عَلَى مَنْ فَوْقهُمْ، فَقَالُوا: لَوْ أنَّا خَرَقْنَا في نَصِيبِنَا خَرْقًا وَلَمْ نُؤذِ مَنْ فَوقَنَا، فَإِنْ تَرَكُوهُمْ وَمَا أرَادُوا هَلَكُوا جَميعًا، وَإنْ أخَذُوا عَلَى أيدِيهِمْ نَجَوا وَنَجَوْا جَميعًا)). رواه البخاري

Imepokewa kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Mfano wa mwenye kusimama juu ya mipaka ya Allaah (kwa kumtii) ni wale walioingia ndani (wenye kupuuza mipaka Yake), ni mfano wa watu walioshindana (kuingia) katika Safina, baadhi yao wakawa juu ya wengine wakawa katika sehemu ya chini. Ama kwa wale waliokuwa chini walipokuwa wanataka maji ya kunywa iliwabidi wapande juu, hivyo wakasema: Lau sisi tukitoboa tundu katika sehemu yetu hii ya chini hatutokuwa ni wenye kuwaudhi wa juu. Ikiwa wataacha wafanye wanayoyataka basi wataangamia wote na wakiwashika mikono yao basi wataokoka wao na wote kwa pamoja.” [Al- Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 5

عن أُمِّ المؤمنين أم سلمة هند بنت أَبي أمية حذيفة رضي الله عنها، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم أنه قَالَ: ((إنَّهُ يُسْتَعْمَلُ عَلَيْكُمْ أُمَرَاءُ فَتَعرِفُونَ وتُنْكِرُونَ، فَمَنْ كَرِهَ فَقَدْ بَرِئَ، وَمَنْ أنْكَرَ فَقَدْ سَلِمَ، وَلَكِنْ مَنْ رَضِيَ وَتَابَعَ)) قَالوا: يَا رَسُول اللهِ، ألا نُقَاتِلهم؟ قَالَ: ((لا، مَا أَقَامُوا فيكُمُ الصَّلاةَ)). رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Mama wa Waumini Ummu Salamah Hind bint Abu Umayyah Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) ya kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Hakika kutakuwa na watu watakaochaguliwa kama viongozi wenu, mtawajua na kuwachukia, yoyote atakayechukia atakuwa hana makosa, na yoyote atayechukia atakuwa hakika amesalimika, lakini (mwenye makosa) ni yule anayeridhika na akafuata.” Wakasema: Ee Rasuli wa Allaah! Je, tusipiganae nao? Akasema: “Msipigane nao, maadamu wataendelea kusimamisha Swalaah miongoni mwenu.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 6

عن أم المؤمنين أم الحكم زينب بنتِ جحش رَضِي الله عنها: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم دخل عَلَيْهَا فَزِعًا، يقول: ((لا إلهَ إلا الله، وَيلٌ للْعَرَبِ مِنْ شَرٍّ قَدِ اقْتَرَبَ، فُتِحَ اليَوْمَ مِنْ رَدْمِ يَأجُوجَ وَمَأجُوجَ مِثلَ هذِهِ))، وحلّق بأُصبُعيهِ الإبهامِ والتي تليها، فقلتُ: يَا رَسُول الله، أنَهْلِكُ وَفِينَا الصَّالِحُونَ؟ قَالَ: ((نَعَمْ، إِذَا كَثُرَ الخَبَثُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa kutoka kwa Mama wa Waumini Ummul Hakam Zaynab bint Jahsh (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) aliingia kwake akiwa amefadhaika, akasema: “Hapana anayepaswa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah. Ole wao Waarabu! kwa shari iliyokaribia. Imefunguliwa leo tundu katika ukuta unaowazuia Juwj na Ma-ajuwj mfano huo (na akachora duara kwa kutumia kidole gumba na kile kinachofuata).” Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Tutaangamizwa na miongoni mwetu kuna watu wema? Akasema: “Ndio, pindi maovu yatakapokithiri.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 7

عن أَبي سعيد الخُدري رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إيَّاكُمْ وَالجُلُوسَ في الطُّرُقَاتِ!)) فقالوا: يَا رَسُول الله، مَا لنا مِنْ مجالِسِنا بُدٌّ، نتحدث فِيهَا. فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((فَإذَا أبَيْتُمْ إلا المَجْلِسَ، فَأَعْطُوا الطَّريقَ حَقَّهُ)). قالوا: وما حَقُّ الطَّريقِ يَا رسولَ الله؟ قَالَ: ((غَضُّ البَصَرِ، وَكَفُّ الأَذَى، وَرَدُّ السَّلامِ، وَالأمْرُ بِالمَعْرُوفِ، والنَّهيُ عن المُنْكَرِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa kutoka kwa Sa’iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Nawatahadharisha nyinyi kwa kukaa kwenu njiani” Wakasema: Ee Rasuli wa Allaah! Hatuna budi isipokuwa kukaa (katika sehemu hizo) kwani tunazungumza na kujadiliana ndani yake. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) “Ikiwa ni hivyo basi ipatieni njia haki yake” Wakasema: Ni zipi haki za njia Ee Rasuli wa Allaah? Akasema: “Kuinamisha macho chini, na kuondoka uchafu (pingamizi), na kurudisha salamu, na kuamrisha mema na kukataza maovu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 8

عن ابن عباس رضي الله عنهما: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم رأى خاتَمًا مِنْ ذهبٍ في يدِ رجلٍ فنَزعه فطرحه، وَقالَ: ((يَعْمدُ أحَدُكُمْ إِلَى جَمْرَةٍ مِنْ نَارٍ فَيَجْعَلُهَا في يَدِهِ!)) فقِيلَ لِلرَّجُلِ بَعْدَمَا ذهب رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم: خُذْ خَاتَمَكَ انْتَفِعْ بِهِ. قَالَ: لا والله لا آخُذُهُ أبَدًا وَقَدْ طَرَحَهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم. رواه مسلم

Imepokewa na ibn ‘Abbas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alimuona mtu amevaa pete ya dhahabu mkononi mwake. Alimtoa katika kidole chake na kuitupa. Kisha Akasema: “Mmoja wenu anakusudia kuliweka kaa la moto katika mkono wake!” Akaambiwa yule mtu baada ya kuondoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam). Ichukue pete yako na ufaidike nayo. Akasema: Hapana! Naapa kwa Allaah, siichukui milele baada ya kutupwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam). [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 9

عن أَبي سعيد الحسن البصري: أن عائِذَ بن عمرو رضي الله عنه دخل عَلَى عُبَيْدِ اللهِ بنِ زياد، فَقَالَ: أي بُنَيَّ، إني سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول: ((إنَّ شَرَّ الرِّعَاءِ الحُطَمَةُ)) فَإِيَّاكَ أنْ تَكُونَ مِنْهُمْ، فَقَالَ لَهُ: اجلِسْ فَإِنَّمَا أنْتَ مِنْ نُخَالَةِ أصْحَابِ مُحَمَّد صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: وهل كَانَتْ لَهُم نُخَالَةٌ إِنَّمَا كَانَتِ النُّخَالَةُ بَعْدَهُمْ وَفي غَيْرِهِمْ. رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa’iyd Al-Hasan Al-Baswariy ya kwamba: ‘Aa’idh bin ‘Amru (Radhwiya Allaahu 'anhu) alimtembelea ‘Ubaydullaah bin Ziyaad na kumwambia: Ewe mtoto wangu! hakika nimesikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) akisema: “Hakika viongozi wabaya kabisa ni wale wakali (kwa raia wao). Hivyo, kuwa na tahadhari usiwe miongoni mwao.” Kaa chini kwani wewe ni miongoni mwa kumvi wa Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam). Akasema: (‘Aa’idh) na je, yeye alikuwa na kapi, hakika kumvi walikuja baada yao na watu wengine wasiokuwa wao. [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 10

عن حذيفة رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((وَالَّذِي نَفْسي بِيَدِهِ، لَتَأْمُرُنَّ بِالمَعْرُوفِ، وَلَتَنْهَوُنَّ عَنْ المُنْكَرِ أَوْ لَيُوشِكَنَّ اللهُ أنْ يَبْعَثَ عَلَيْكُمْ عِقَابًا مِنْهُ ثُمَّ تَدْعُوْنَهُ فَلا يُسْتَجَابُ لَكُمْ)). رواه الترمذي

Imepokewa kutoka kwa Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi Mwake, mtaendelea kuamrisha mema na kukataza maovu au kama si hivyo basi Allaah Atawateremshia adhabu, kisha mtamuomba yeye kisha hatawojibu (du’aa zenu).” [At-Tirmidhiy]

 

 

 

Hadiyth – 11

عن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((أفْضَلُ الجِهَادِ كَلِمَةُ عَدْلٍ عِنْدَ سُلْطَانٍ جَائرٍ)). رواه أَبُو داود والترمذي

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa’iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ya kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Jihadi iliyo bora kabisa ni kuzungumza maneno ya haki mbele ya kiongozi mjeuri.” [Abu Daawuwd na At-Tarmidhiy]

 

 

 

Hadiyth – 12

عن أَبي عبدِ الله طارِقِ بن شِهاب البَجَليِّ الأَحْمَسِيّ رضي الله عنه: أنَّ رجلًا سأل النَّبيّ صلى الله عليه وسلم وقد وضع رِجله في الغَرْزِ: أيُّ الجِهادِ أفضلُ؟ قَالَ: ((كَلِمَةُ حَقٍّ عِنْدَ سُلْطَانٍ جَائرٍ)). رواه النسائي

Imepokewa kutoka kwa Abu ‘Abdillaah Twaariq bin Shihaab Al-Bajaliy Al-Ahmasiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ya kwamba, mtu mmoja alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye alikuwa tayari ameweka mguu kwenye kipandio cha Ngozi (au kibao) cha ngamia akasema: Ni Jihadi gani iliyobora kabisa? Akasema: “Kuzungumza maneno ya haki mbele ya kiongozi mjeuri.” [An-Nasaaiy]

 

 

 

Hadiyth – 13

عن ابن مسعود رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ أوَّلَ مَا دَخَلَ النَّقْصُ عَلَى بَنِي إسْرَائِيلَ أنَّهُ كَانَ الرَّجُلُ يَلْقَى الرَّجُلَ، فَيَقُولُ: يَا هَذَا، اتَّقِ الله ودَعْ مَا تَصْنَعُ، فَإِنَّهُ لاَ يَحِلُّ لَكَ، ثُمَّ يَلْقَاهُ مِنَ الغَدِ وَهُوَ عَلَى حَالِهِ، فَلا يَمْنَعُهُ ذلِكَ أنْ يَكُونَ أكِيلَهُ وَشَرِيبَهُ وَقَعِيدَهُ، فَلَمَّا فَعَلُوا ذلِكَ ضَرَبَ اللهُ قُلُوبَ بَعْضِهِمْ بِبَعْضٍ)) ثُمَّ قَالَ: {لُعِنَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْ بَنِي إِسْرائيلَ عَلَى لِسَانِ دَاوُدَ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ ذَلِكَ بِمَا عَصَوْا وَكَانُوا يَعْتَدُونَ * كَانُوا لا يَتَنَاهَوْنَ عَنْ مُنْكَرٍ فَعَلُوهُ لَبِئْسَ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ * تَرَى كَثِيرًا مِنْهُمْ يَتَوَلَّوْنَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَبِئْسَ مَا قَدَّمَتْ لَهُمْ أَنْفُسُهُمْ} إِلَى قوله: {فاسِقُونَ} [المائدة: 78- 81].

ثُمَّ قَالَ: ((كَلا، وَاللهِ لَتَأمُرُنَّ بالمَعْرُوفِ، وَلَتَنْهَوُنَّ عَنِ المُنْكَرِ، وَلَتَأخُذُنَّ عَلَى يَدِ الظَّالِمِ، وَلَتَأطِرُنَّهُ عَلَى الحَقِّ أَطْرًا، وَلَتَقْصُرُنَّه عَلَى الحَقِّ قَصْرًا، أَوْ لَيَضْرِبَنَّ اللهُ بقُلُوبِ بَعْضِكُمْ عَلَى بَعْضٍ، ثُمَّ ليَلْعَنَنَّكُمْ كَمَا لَعَنَهُمْ)). رواه أَبُو داود والترمذي

هَذَا لفظ أَبي داود، ولفظ الترمذي، قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((لَمَّا وَقَعَتْ بَنُو إسْرَائِيلَ في المَعَاصي نَهَتْهُمْ عُلَمَاؤهُمْ فَلَمْ يَنْتَهُوا، فَجَالَسُوهُمْ في مَجَالِسِهمْ، وَوَاكَلُوهُمْ وَشَارَبُوهُمْ، فَضَربَ اللهُ قُلُوبَ بَعضِهِمْ بِبعْضٍ، وَلَعَنَهُمْ عَلَى لِسانِ دَاوُد وعِيسَى ابنِ مَرْيَمَ ذلِكَ بما عَصَوا وَكَانُوا يَعتَدُونَ)) فَجَلَسَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وكان مُتَّكِئًا، فَقَالَ: ((لا، والَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ حَتَّى تَأطِرُوهُمْ عَلَى الحَقِّ أطْرًا)).

Imepokewa kutoka kwa ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Upungufu wa kwanza uliowafikia Banuu Israiyl ulikuwa mtu kukutana na mwenzake, akimwambia: Ewe fulani! mche Allaah na uache unayofanya kwani si halali kwako (kufanya hivyo). Kisha anakutana naye siku ya pili katika hali yake ya awali (bila ya mabadiliko), hilo halimkatazi yeye kutokula naye, kunywa na kukaa naye. Walipofanya hivyo, Allaah Alibadilisha mioyo yao baadhi yao kwa wengine.” Kisha akasema: “Wamelaaniwa wale waliokufuru miongoni mwa wana wa Israaiyl kwa lisani (lugha) ya Daawuwd na ‘Iysaa mwana wa Maryam. Hivyo ni kwa sababu ya kuasi kwao na walikuwa wakitaadi.” Walikuwa hawakatazani munkari waliyofanya. Uovu ulioje waliyokuwa wakiyafanya.” “Utawaona wengi miongoni mwao wanawafanya marafiki wandani wale waliokufuru. Ubaya ulioje yale yaliyowatangulizia nafsi zao, ndipo Allaah Amewaghadhibikia na katika adhabu wao watadumu.” “Na lau wangelikuwa wanamwamini Allaah na Nabiy (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na yale yaliyoteremshwa kwake, wasingeliwafanya hao marafiki wandani, lakini wengi miongoni mwao ni mafasiki.” [Al-Maaidah: 78-81]

Kisha akasema: “Hasha! Naapa kwa Allaah ya kwamba mtaendelea kuamrisha mema na kukataza maovu na kuushika mkono wa dhalimu na kuwashawishi (kwa upole na ulaini) wafanye uadilifu, kuwafanya wawe imara juu ya haki na ukweli. Mkishindwa kufanya hivyo, basi jueni ya kwamba Allaah Atawaadhibu pamoja na wenzenu (madhalimu wa nafsi zao) na kisha Atawalaani kama Alivyowalaani wao (Mayahudi).” [Hii ni lafdhi ya Abu Daawuwd]

 

Riwaayah ya At-Tirmidhiy: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Walipoingia Banuu Israiyl katika maasi, Wanachuoni wao waliwakataza lakini hawakuacha, hivyo wakaanza kukaa nao katika baraza zao na wakawa wanakula na kunywa pamoja nao. Hapo Allaah Aliwaadhibu wote pamoja na wakalaaniwa kwa ulimi wa Dawwuud na ‘Iysaa bin Maryam na hiyo ni kwa sababu waliasi na wakawa wanapindukia mipaka.”

Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akakaa baada ya kuwa ameegemea, kisha akasema: “Laa sivyo hivyo, naapa kwa Yule ambaye kwamba nafsi yangu ipo mikononi Mwake, mpaka muwashike mkono madhalimu ili waweze kusimama juu ya haki.” [At-Tirmidhiy]

 

 

 

Hadiyth – 14

عن أَبي بكر الصديق رضي الله عنه قَالَ: يَا أيّها النَّاس، إنّكم لتَقرؤُون هذِهِ الآية: {يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنْفُسَكُمْ لا يَضُرُّكُمْ مَنْ ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ} [المائدة: 105].

وإني سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((إنَّ النَّاسَ إِذَا رَأَوُا الظَّالِمَ فَلَمْ يأخُذُوا عَلَى يَدَيْهِ أوشَكَ أنْ يَعُمَّهُمُ اللهُ بِعِقَابٍ مِنْهُ)). رواه أَبُو داود والترمذي والنسائي

Imepokewa kutoka kwa Abu Bakr As-Swidiyq (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ya kwamba alisema: Enyi watu! Hakika nyinyi mnaisoma Aayah hii: “Enyi walioamini! Jiangalieni nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotoka ikiwa mmeongoka.” Kwa hakika nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Hakika pindi watu wanapomuona dhalimu na wasimshike mikoni yake, huenda Allaah kwa ujumla akawateremshia adhabu kutoka Kwake.” [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]

 

 

Share

024-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Adhabu Kali Kwa Mwenye Kuamrisha Mema Au Kukataza Maovu Kisha Kauli Yake Ikawa Kinyume Na Matendo Yake

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب تغليظ عقوبة من أمر بمعروف أَوْ نهى عن منكر وخالف قوله فعله

024 - Mlango Wa Adhabu Kali Kwa Mwenye Kuamrisha Mema Au Kukataza Maovu Kisha Kauli Yake Ikawa Kinyume Na Matendo Yake

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

أَتَأْمُرُونَ النَّاسَ بِالْبِرِّ وَتَنسَوْنَ أَنفُسَكُمْ وَأَنتُمْ تَتْلُونَ الْكِتَابَ ۚ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿٤٤﴾ 

Je, mnaamrisha watu watende mema na mnajisahu nafsi zenu na hali ya kuwa nyinyi mnasoma Kitabu; je hamtii akilini? [Al-Baqarah: 44]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لِمَ تَقُولُونَ مَا لَا تَفْعَلُونَ﴿٢﴾

 Enyi walioamini! Kwanini mnasema yale msiyoyafanya?  

 

كَبُرَ مَقْتًا عِندَ اللَّـهِ أَن تَقُولُوا مَا لَا تَفْعَلُونَ﴿٣﴾

 Ni chukizo kubwa mno mbele ya Allaah kwamba mnasema yale msiyoyafanya. [Asw- Swaff: 2-3 ]

 

وَمَا أُرِيدُ أَنْ أُخَالِفَكُمْ إِلَىٰ مَا أَنْهَاكُمْ عَنْهُ ۚ

…Nami sitaki kukukhalifuni kufanya ninayokukatazeni… [Huwd: 88]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي زيد أسامة بن زيد بن حارثة رضي الله عنهما، قَالَ: سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((يُؤْتَى بالرَّجُلِ يَوْمَ القيَامَةِ فَيُلْقَى في النَّارِ، فَتَنْدَلِقُ أقْتَابُ بَطْنِهِ فَيدُورُ بِهَا كَمَا يَدُورُ الحِمَارُ في الرَّحَى، فَيَجْتَمِعُ إِلَيْه أهْلُ النَّارِ، فَيَقُولُونَ: يَا فُلانُ، مَا لَكَ؟ أَلَمْ تَكُ تَأمُرُ بالمعْرُوفِ وَتنهَى عَنِ المُنْكَرِ؟ فَيقُولُ: بَلَى، كُنْتُ آمُرُ بِالمَعْرُوفِ وَلا آتِيهِ، وأنْهَى عَنِ المُنْكَرِ وَآتِيهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Kutoka kwa Abuu Zayd Usaamah bin Zayd bin Haarithah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) akisema: “Ataletwa mtu siku ya Qiyaamah na atiwe motoni. Matumbo yake yatatoka nje (huku ameyashika mkononi mwake) na atakuwa anazunguka nayo kama anavyozunguka punda anayesaga katika mtambo.” Watakusanyika mbele yake watu wa motoni na waseme: “Ee Fulani, una nini? Si wewe ndiye uliokuwa ukituamrisha mema na kutukataza maovu?” Atasema Fulani: “Ndio, nilikuwa nikiamrisha mema lakini mimi mwenyewe sifanyi na nilikuwa nikikataza maovu na nikiyaendea (nikifanya ninayokataza).” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Share

025-Riyaadhw As-Swaalihiyn: Mlango Wa Amri Ya kurudisha Amana

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

025 – Mlango Wa Amri Ya kurudisha Amana

باب الأمر بأداء الأمانة

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا

Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe. [An-Nisaa: 58]

 

إِنَّا عَرَضْنَا الْأَمَانَةَ عَلَى السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَالْجِبَالِ فَأَبَيْنَ أَن يَحْمِلْنَهَا وَأَشْفَقْنَ مِنْهَا وَحَمَلَهَا الْإِنسَانُ ۖ إِنَّهُ كَانَ ظَلُومًا جَهُولًا ﴿٧٢﴾

Hakika Sisi Tulihudhurisha amana kwa mbingu na ardhi na majabali vikakataa kuibeba na vikaiogopa; lakini insani akaibeba. Hakika yeye amekuwa dhalimu mno, jahili mno. [Al-Ahzaab: 72]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((آيةُ المُنافقِ ثلاثٌ: إِذَا حَدَّثَ كَذَبَ، وَإِذَا وَعدَ أخْلَفَ، وَإِذَا اؤْتُمِنَ خَانَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

وفي رواية: ((وَإِنْ صَامَ وَصَلَّى وَزَعَمَ أنَّهُ مُسْلِمٌ))

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Alama za mtu mnafiki ni tatu: Anaposema husema uongo, na napoahidi hatakelezi, na anapoaminiwa hufanya khiyana” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine: “Japokuwa atafunga na kuswali na akajichukulia kuwa yeye ni Muislamu.”

 

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن حذيفة بن اليمان رضي الله عنه قَالَ: حدثنا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم حدِيثَينِ قَدْ رأيْتُ أحَدَهُمَا وأنا أنتظرُ الآخر: حدثنا أن الأمانة نَزلت في جَذرِ قلوبِ الرجال، ثُمَّ نزل القرآن فعلموا مِنَ القرآن، وعلِموا من السنةِ.

ثُمَّ حدّثنا عن رفع الأمانة، فَقَالَ: ((يَنَامُ الرَّجُلُ النَّوْمَةَ فَتُقْبَضُ الأَمَانَةُ مِنْ قَلْبهِ، فَيَظَلُّ أثَرُهَا مِثلَ الوَكْتِ، ثُمَّ يَنَامُ النَّومَةَ فَتُقْبَضُ الأَمَانَةُ مِنْ قَلْبهِ، فَيَظَلُّ أثَرُهَا مِثلَ أَثَرِ المَجْلِ، كَجَمْرٍ دَحْرَجْتَهُ عَلَى رِجْلِكَ فَنَفِطَ، فَتَرَاهُ مُنْتَبرًا وَلَيسَ فِيهِ شَيءٌ)) ثُمَّ أخَذَ حَصَاةً فَدَحْرَجَهُ عَلَى رِجْلِهِ ((فَيُصْبحُ النَّاسُ يَتَبَايعُونَ، فَلا يَكَادُ أحدٌ يُؤَدّي الأَمَانَةَ حَتَّى يُقَالَ: إنَّ في بَني فُلانٍ رَجُلًا أمينًا، حَتَّى يُقَالَ لِلرَّجُلِ: مَا أجْلَدَهُ! مَا أَظْرَفَهُ! مَا أعْقَلَهُ! وَمَا في قَلْبِهِ مِثْقَالُ حَبَّة مِن خَرْدَل مِنْ إيمَان وَلَقدْ أتَى عَلَيَّ زَمَانٌ وَمَا أُبَالِي أيُّكُمْ بَايَعْتُ: لَئن كَانَ مُسْلِمًا لَيَرُدَّنَّهُ عليَّ دِينهُ، وَإنْ كَانَ نَصْرانِيًّا أَوْ يَهُودِيًا لَيَرُدَّنَّهُ عَلَيَّ سَاعِيهِ، وَأَمَّا اليَوْمَ فَمَا كُنْتُ أُبَايعُ مِنْكُمْ إلا فُلانًا وَفُلانًا)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa kutoka kwake Hudhayfah bin Al-Yamaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba: Ametuhadithia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) Hadiyth mbili, nami nimeiona Hadiyth moja kati ya hizo mbili na ninangoja kuiona hiyo ya pili. Alituhadithia ya kwamba, amana iliteremshwa na kukita katika mioyo ya watu. Wakati Qur-aan iliteremshwa waliweza kuelimishwa kwa Qur-aan na Sunnah. Kisha akatuhadithia kuhusu kunyanyuliwa amanah, akasema: “Analala mtu usiku na anapoamka na anajikuta kuwa amatolewa uaminifu katika moyo wake na kubakishwa kivuli chake tu. Kisha analala tena usiku na uaminifu unaondolewa katika moyo wake na kubakia alama ndogo mfano wa lenge lenge kama anapoguswa mmoja wenu na moto katika mguu wake na hivyo kupata lenge lenge ambalo linapasuka basi ndani huwa tupu kabisa.” Kisha akachukua vijiwe na kuanza kujipiga mguu wake: “Watu watakuwa wanapambazukia katika biashara (kuuza na kununua), lakini hakuna hata mmoja atayetekeleza uaminifu (kurudisha amanah), mpaka imesemwe, hakika katika ukoo fulani kuna mtu muaminifu, mpaka pia isemwe kwa mtu (ambaye ni hodari katika mambo ya dunia). Tazama jinsi gani alivyo hodari, jinsi gani alivyo mzuri, na jinsi gani alivyo na akili, lakini kwenye moyo wake hana hata chembe ya iymaan.” Hakika nimefikiwa na wakati ambapo sikujali mtu gani ninayefanya naye biashara. Akiwa ni Musilamu basi Dini yake ni dhamana tosha kwangu, na akiwa ni Naswara, au Myahudi  basi (mzazi) au walii wake atatimiza amana hiyo (ni dhamana tosha). Lakini ama leo sifanyi biashara miongoni mwenu isipokuwa fulani na fulani.  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن حُذَيفَة وأبي هريرة رضي الله عنهما قالا: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَجمَعُ اللهُ تبَارَكَ وَتَعَالَى النَّاسَ فَيَقُومُ المُؤمِنُونَ حَتَّى تُزْلَفَ لَهُمُ الجَنَّةُ، فَيَأتُونَ آدَمَ صَلَواتُ اللهِ عَلَيهِ، فَيقُولُونَ: يَا أَبَانَا اسْتَفْتِحْ لَنَا الجَنَّةَ، فَيقُولُ: وَهَلْ أخْرَجَكُمْ مِنَ الجَنَّةِ إلا خَطيئَةُ أبيكُمْ! لَسْتُ بِصَاحِبِ ذلِكَ، اذْهَبُوا إِلَى ابْنِي إِبْراهيمَ خَلِيل اللهِ.

قَالَ: فَيَأتُونَ إبرَاهِيمَ فَيَقُولُ إبراهيم: لَسْتُ بِصَاحِبِ ذلِكَ إِنَّمَا كُنْتُ خَليلًا مِنْ وَرَاءَ وَرَاءَ، اعْمَدُوا إِلَى مُوسَى الَّذِي كَلَّمَهُ الله تَكليمًا. فَيَأتُونَ مُوسَى، فَيَقُولُ: لستُ بِصَاحِبِ ذلِكَ، اذْهَبُوا إِلَى عِيسى كلمةِ اللهِ ورُوحه، فيقول عيسى: لستُ بصَاحبِ ذلِكَ.

فَيَأتُونَ مُحَمَّدًا صلى الله عليه وسلم فَيَقُومُ فَيُؤذَنُ لَهُ، وتُرْسَلُ الأَمَانَةُ وَالرَّحِمُ فَيَقُومانِ جَنْبَتَي الصِّرَاطِ يَمِينًا وَشِمَالًا فَيَمُرُّ أوَّلُكُمْ كَالبَرْقِ)) قُلْتُ: بأبي وَأمِّي، أيُّ شَيءٍ كَمَرِّ البَرقِ؟ قَالَ: ((ألَمْ تَرَوا كَيْفَ يمُرُّ وَيَرْجِعُ في طَرْفَةِ عَيْن، ثُمَّ كَمَرّ الرِّيحِ، ثُمَّ كَمَرِّ الطَّيْرِ، وَأَشَدِّ الرِّجَال تَجْري بهمْ أعْمَالُهُمْ، وَنَبيُّكُمْ قَائِمٌ عَلَى الصِّراطِ، يَقُولُ: رَبِّ سَلِّمْ سَلِّمْ، حَتَّى تَعْجِزَ أعْمَالُ العِبَادِ، حَتَّى يَجِيء الرَّجُلُ لا يَسْتَطِيعُ السَّيْرَ إلا زَحْفًا، وَفي حَافَتي الصِّراطِ كَلاَلِيبُ معَلَّقَةٌ مَأمُورَةٌ بِأخْذِ مَنْ أُمِرَتْ بِهِ، فَمَخْدُوشٌ نَاجٍ، وَمُكَرْدَسٌ في النَّارِ)) وَالَّذِي نَفْسُ أَبي هُرَيْرَةَ بِيَدِهِ، إنَّ قَعْرَ جَهَنَّمَ لَسَبْعُونَ خَرِيفًا. رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Hudhayfah na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ya kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) Atawakusanya watu. Watasimama waumini mpaka watakuja karibu na Jannah, na hapo watamuendea Aadam (‘Alayhis Salaam) na kumwambia: “Ee Aadam baba yetu, tufungulie Jannah. Atasema: Ni kosa la baba yenu ndio lililowatoa nyinyi katika Jannah. Mimi sina uwezo wa kuwasaidia, hivyo nendeni kwa mtoto wangu Ibraahiym (‘Alayhis Salaam), ni kipenzi cha Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa). Amasema: Watakwenda kwa Ibraahiym (‘Alayhis Salaam), na watamwambia. Atasema: Mimi sina uwezo, hakika mimi nilikuwa kipenzi tu na wala sina darja hiyo ya juu. Nendeni kwa Muwsaa ambaye Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) Alizungumza naye kwa uwazi kabisa. Watakuja kwa Muwsaa (‘Alayhis Salaam), naye atasema: Mimi si mwenyewe wa jambo hilo. Hapo watakuja kwa Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salaam). Atasimama mbele ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) na atakubaliwa kuwatetea watu. Itatumwa amana na kuunganisha kizazi, nazo zitasimama pembezoni mwa Swiraatw (njia) kulia na kushoto. Wa mwanzo wenu watapita kama umeme. Nikasema: Baba yangu na mama yangu wawe fidia kwako unamaanisha nini? Akasema: “Huoni cheche za umeme zinazokwenda na kurudi katika kupepesa jicho? Kisha watapita kama upepo, kisha kama ndege, na wengine kwa kasi ya watu wanaokimbia, na tofauti hii (ya kasi) itakuwa kwa sababu ya ‘amali za kila mmoja wenu. Na Rasuli wenu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) atakuwa amesimama juu ya Swiraatw, anasema: Mola wangu! Wasalimishe, wasalimishe. Mpaka matendo ya waja yashindwe, mpaka mtu aje hawezi kupita isipokuwa kwa kutambaa na katika pande zote mbili za Swiraatw kuna koleo zimening’ing’izwa, ambazo zimeamriwa (na Allaah Subhaanahu Wa Ta'aalaa). Yule atakayekwaruzwa atakuwa ni mwenye kufaulu na wasiokuwa wao wataingia motoni. Na yule ambaye kwamba nafsi ya Abuu Hurayrah ipo mikononi Mwake, hakika urefu wa Jahannam ni masafa miaka sabini. [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي خُبيب- بضم الخاء المعجمة- عبد الله بن الزبير رضي الله عنهما، قَالَ: لَمَّا وَقفَ الزُّبَيْرُ يَوْمَ الجَمَل دَعَانِي فَقُمْتُ إِلَى جَنْبه، فَقَالَ: يَا بُنَيَّ، إنَّهُ لا يُقْتَلُ اليَومَ إلا ظَالِمٌ أَوْ مَظْلُومٌ، وَإنِّي لا أراني إلا سَأُقْتَلُ اليوم مظلومًا، وإنَّ مِنْ أكبرَ هَمِّي لَدَيْنِي، أفَتَرَى دَيْننا يُبقي من مالِنا شَيئًا؟ ثُمَّ قَالَ: يَا بُنَيَّ، بعْ مَا لَنَا وَاقْضِ دَيْنِي، وَأوْصَى بِالثُّلُثِ وَثُلُثِهِ لِبَنِيهِ، يعني لبني عبد الله بن الزبير ثُلُثُ الثُّلُث. قَالَ: فَإنْ فَضَلَ مِنْ مَالِنَا بَعْدَ قَضَاءِ الدَّينِ شَيء فَثُلُثُه لِبَنِيكَ. قَالَ هِشَام: وَكَانَ بَعْضُ وَلَدِ عَبْدِ اللهِ قَدْ وَازى بَعْضَ بَنِي الزُّبَيْرِ خُبيبٍ وَعَبَّادٍ، وَلهُ يَوْمَئذٍ تِسْعَةُ بَنينَ وَتِسْعُ بَنَات.

قَالَ عَبدُ الله: فَجَعلَ يُوصينِي بدَيْنِهِ وَيَقُولُ: يَا بُنَيَّ، إنْ عَجَزْتَ عَن شَيْءٍ مِنْهُ فَاسْتَعِنْ عَلَيهِ بِمَوْلاَيَ. قَالَ: فَوَاللهِ مَا دَرَيْتُ مَا أرَادَ حَتَّى قُلْتُ: يَا أبَتِ مَنْ مَوْلاَكَ؟ قَالَ: الله. قَالَ: فَوَاللهِ مَا وَقَعْتُ في كُرْبةٍ مِنْ دَيْنِهِ إلا قُلْتُ: يَا مَوْلَى الزُّبَيْرِ اقْضِ عَنْهُ دَيْنَهُ فَيَقْضِيَهُ. قَالَ: فَقُتِلَ الزُّبَيْرُ وَلَم يَدَعْ دِينَارًا وَلا دِرْهمًا إلا أرَضِينَ، مِنْهَا الغَابَةُ وإحْدَى عَشْرَةَ دَارًا بالمَدِينَةِ، وَدَارَيْنِ بالبَصْرَةِ، ودَارًا بالكُوفَةِ، ودَارًا بمِصْرَ.

قَالَ: وَإِنَّمَا كَانَ دَيْنُهُ الَّذِي كَانَ عَلَيهِ أنَّ الرَّجُلَ كَانَ يَأتِيهِ بالمال، فَيَسْتَودِعُهُ إيَّاهُ، فَيَقُولُ الزُّبَيْرُ: لا، وَلَكِنْ هُوَ سَلَفٌ إنِّي أخْشَى عَلَيهِ الضَّيْعَةَ. وَمَا وَليَ إمَارَةً قَطُّ وَلا جِبَايَةً، ولا خراجًا، وَلا شَيئًا إلا أنْ يَكُونَ في غَزْوٍ مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم أَوْ مَعَ أَبي بَكْرٍ وَعُمَرَ وَعُثْمَانَ رضي الله عنهم، قَالَ عَبدُ الله: فَحَسَبْتُ مَا كَانَ عَلَيهِ مِن الدَّيْنِ فَوَجَدْتُهُ ألْفيْ ألْفٍ وَمئَتَي ألْف ‍! فَلَقِيَ حَكِيمُ بنُ حِزَام عَبْدَ الله بْنَ الزُّبَيْرِ، فَقَالَ: يَا ابْنَ أخِي، كَمْ عَلَى أخي مِنَ الدَّيْنِ؟ فَكَتَمْتُهُ وَقُلْتُ: مِائَةُ ألْف. فَقَالَ حَكيمٌ: واللهِ مَا أرَى أمْوَالَكُمْ تَسَعُ هذِهِ. فَقَالَ عَبْدُ اللهِ: أرَأيْتُكَ إنْ كَانَتْ ألْفَي ألف وَمائَتَيْ ألْف؟ قَالَ: مَا أرَاكُمْ تُطيقُونَ هَذَا، فَإنْ عَجَزْتُمْ عَنْ شَيءٍ مِنْهُ فَاسْتَعِينُوا بي.

قَالَ: وَكَانَ الزُّبَيرُ قَد اشْتَرَى الغَابَةَ بِسَبْعِينَ ومائة ألف، فَبَاعَهَا عَبدُ اللهِ بِألْفِ ألْف وَسِتّمِائَةِ ألْف، ثُمَّ قَامَ فَقَالَ: مَنْ كَانَ لَهُ عَلَى الزُّبَيرِ شَيْء فَلْيُوافِنَا بِالغَابَةِ، فَأتَاهُ عَبدُ اللهِ بنُ جَعفَر، وَكَانَ لَهُ عَلَى الزُّبَيرِ أرْبَعمائةِ ألْف، فَقَالَ لعَبدِ الله: إنْ شِئْتُمْ تَرَكْتُهَا لَكمْ؟ قَالَ عَبدُ الله: لا، قَالَ: فَإنْ شِئتُمْ جَعَلْتُمُوهَا فِيمَا تُؤَخِّرُونَ إنْ إخَّرْتُمْ، فَقَالَ عَبدُ الله: لا، قَالَ: فَاقْطَعُوا لِي قطْعَةً، قَالَ عَبدُ الله: لَكَ مِنْ هاهُنَا إِلَى هَاهُنَا. فَبَاعَ عَبدُ اللهِ مِنهَا فَقَضَى عَنْهُ دَينَه وَأوْفَاهُ، وَبَقِيَ مِنْهَا أرْبَعَةُ أسْهُم وَنِصْفٌ، فَقَدِمَ عَلَى مُعَاوِيَة وَعنْدَهُ عَمْرُو بْنُ عُثْمَانَ، وَالمُنْذِرُ بْنُ الزُّبَيْرِ، وَابْنُ زَمْعَةَ، فَقَالَ لَهُ مُعَاويَةُ: كَمْ قُوِّمَتِ الغَابَةُ؟ قَالَ: كُلُّ سَهْم بمائَة ألف، قَالَ: كَمْ بَقِيَ مِنْهَا؟ قَالَ: أرْبَعَةُ أسْهُم وَنصْفٌ، فَقَالَ المُنْذِرُ بْنُ الزُّبَيرِ: قَدْ أخَذْتُ مِنْهَا سَهمًا بِمائَةِ ألف، قَالَ عَمْرُو بْنُ عُثْمَانَ: قَدْ أخَذْتُ مِنْهَا سَهْمًا بمائَةِ ألْف. وَقالَ ابْنُ زَمْعَةَ: قَدْ أخَذْتُ سَهْمًا بِمائَةِ ألْف، فَقَالَ مُعَاويَةُ: كَمْ بَقِيَ مِنْهَا؟ قَالَ: سَهْمٌ ونصْفُ سَهْم، قَالَ: قَدْ أخَذْتُهُ بخَمْسِينَ وَمائَةِ ألْف. قَالَ: وَبَاعَ عَبدُ الله بْنُ جَعفَر نَصيبهُ مِنْ مَعَاوِيَةَ بستِّمِائَةِ ألْف.

فَلَمَّا فَرَغَ ابْنُ الزُّبَيرِ مِنْ قَضَاءِ دَيْنِهِ، قَالَ بَنُو الزُّبَيرِ: اقسمْ بَينَنَا ميراثَنا، قَالَ: وَاللهِ لا أقْسِمُ بَيْنَكُمْ حَتَّى أنَادِي بالمَوْسم أرْبَعَ سنينَ: ألا مَنْ كَانَ لَهُ عَلَى الزُّبَيرِ دَيْنٌ فَلْيَأتِنَا فَلْنَقْضِهِ. فَجَعَلَ كُلّ سَنَةٍ يُنَادِي في المَوْسِمِ، فَلَمَّا مَضَى أرْبَعُ سنينَ قَسَمَ بيْنَهُمْ وَدَفَعَ الثُّلُثَ. وَكَانَ للزُّبَيْرِ أرْبَعُ نِسْوَةٍ، فَأصَابَ كُلَّ امرَأةٍ ألْفُ ألف وَمِئَتَا ألْف، فَجَميعُ مَالِه خَمْسُونَ ألف ألْف وَمِئَتَا ألْف. رواه البخاري

Imepokwa kutoka kwa Abuu Khubayb, ‘Abdullaah bin Az-Zubayr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ya kwamba: Aliposimama Az-Zubayr katika vita vya Ngamia, aliniita nami nikasimama ubavuni mwake. Alinambia: Ee mtoto wangu! Hautauliwa leo isipokuwa dhalimu au aliyedhulumiwa. Nami nina hakika ya kuwa nitauliwa leo kwa dhulma. Na hakika hamu yangu kubwa ni deni langu. Je, unafikiria kutabakia chochote katika mali baada ya kulipa deni? Kisha akasema: Ee mtoto wangu! Uza rasimali yangu na ulipe deni langu. Na nausia ya kwamba thuluthi ya thuluthi (1/9) iwe ni ya watoto wako (yaani ‘Abdullaah bin Az-Zubayr), kwa kile kitakachobakia. Baada ya hii ikiwa kutabakia chochote basi thuluthi itakuwa ni ya watoto wako. Amasema Hishaam: Na walikuwa baadhi ya watoto wa ‘Abdullaah ni rika moja na watoto wa Az-Zubayr, kama Khubayb na ‘Abbaad, na wakati huo alikuwa na vijana tisa na mabinti tisa. Akasema: Ee mtoto wangu! Ukishindwa kulipa deni langu basi takamsaada kwa Bwana wangu. Akasema: Naapa kwa Allaah! Sikufahamu alilokusudia mpaka nilipouuliza: Ewe baba yangu! Nani bwana wako? Akasema: Allaah. Akasema tena (‘Abdullaah): Naapa kwa Allaah! Sijapatwa tena na shida ya deni lake isipokuwa nilikuwa nasema, Ee Bwana wa Az-Zubayr mwondoshee deni lake, Naye Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) Alikuwa anamuondoshea. Az-Zubayr (Radhwiya Allaahu 'anhu) aliuliwa siku hiyo na hakuacha hata dinari moja wala dirhamu isipokuwa vipande viwili vya ardhi, moja katika hiyo ikiwa katika sehemu ya Ghaabah na nyumba kumi na moja Madiynah, na nyumba mbili Basrah, na nyumba moja Kufah, na nyumba moja Misri. Na kwa hakika deni lake lilitokana na watu waliokuwa wakimjia ili awahifadhie mali zao, lakini Az-Zubayr alikuwa anawaambia: Hapana! Siwezi jukumu hilo kwani huenda ikapotea lakini naweza kuichukua hiyo amana kama deni juu yangu. Yeye hakukubali nafasi ya uongozi wala wadhifa wa kukusanya kodi wala kitu chengine chochote isipokuwa ile ngawira aliyopatiwa katika vita alivyopigana wakati wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam), au Abu Bakr, au ‘Umar, au ‘Uthmaan (Radhwiya Allaahu 'anhum). Akasema (‘Abdullaah): Nikahesabu deni lake na jumla ikafika million mbili na laki mbili. Nilikutana na Hakiym bin Hizaam, naye akasema: Ee mtoto wa ndugu yangu! Ndugu yangu anadenia la kiasi gani? Nikaficha hilo kwa kusema: Laki moja. Akasema Hakiym: Kwa Allaah, sidhani ya kwamba mali yenu itafikia kiwango hicho. Nikasema: Unaonaje deni likiwa ni milioni mbili na laki mbili? Akasema: Sidhani ya kwamba mtaweza kuubeba mzigo huo, hivyo mkiwa na uzito wa aina yoyote njooni kwangu kwa msaada. Az-Zubayr alikuwa ameinunua ile ardhi ya Ghaabah kwa laki moja na elfu sabini, nami nikauza kwa milioni moja na laki sita. Kisha akasimama ‘Abdullaah na kunadi Az-Zubayr atukute katika ardhi ya Ghaabah. Akaja ‘Abdullaah bin Ja’far, ambaye alikuwa anamdai Az-Zubayr laki nne. Alimwambia ibn Zubayr: Mkipenda nitawaachia deni hilo? Nikasema: Hapana, Akasema: Ikiwa mnataka nitawapatia muda wa kunilipa. Akasema ibn Zubayr: Hapana. Akasema ibn Ja’far basi nikatie kipande cha ardhi. Akasema ‘Abdullaah: Kipande chako ni kuanzia hapa mpaka hapa. Kwa njia hii ‘Abdullaah alimlipia baba yake deni. Baada ya hapo ikabaki ardhi yenye kipimo cha siham nne na nusu. Akaja Mu’awiyyah pamoja naye ni ‘Amru bin ‘Uthmaan na Al-Mundhir bin Az-Zubayr na ibn Zam’ah. Akasema Mu’awiyyah: Hii Ghaabah ni bei gani? Akasema: Kila siham ni laki moja. Akasema: Imebakia kiasi gani? Akasema: Siham nne na nusu. Hapo akasema Mundhir bin Zubayr: Mimi nimechukua sihim moja kwa bei hiyo ya laki moja. Akasema ‘Amru bin ‘Uthmaan: Nami nachukua sihim moja kwa bei hiyo ya laki moja. Na akasema ibn Zam’ah: Nami nimechukua sihim moja kwa bei ya laki moja. Akasema Mu’awiyyah: Imebaki kiasi gani cha ardhi? Akasema (‘Abdullaah): Sihim moja na nusu. Akasema Mu’awiyyah: Nimeichukua kwa laki moja na nusu. Baadae ‘Abdullaah bin Ja’far alimuuzia Mu’awiyyah sehemu yake ya ardhi kwa laki sita. ‘Abdullaah bin Zubayr alipomaliza shughuli hii yote ya kulipa madeni ya baba yake, walimjia warithi wa Az-Zubayr  na kumwambia: Tupatie fungu letu la mirathi. Akasema: Naapa kwa Allaah! Sitagawa mirathi mpaka mwanzo ninadi katika msimu wa Hijjah kwa miaka minne mfululizo. Mtu yoyote anayemdai Az-Zubayr basi atujie tumrudishie haki yake. Akajaalia kuwa ananadi kila mwaka katika msimu wa Hijjah. Ilipomalizika miaka minne aligawanya pesa zilizobakia baina yao akalipa thuluthi. Az-Zubayr alikuwa na wake wanne, hivyo kila mmke alipata milioni moja na laki mbili, kwani jumla ya mali yake yote ilikuwa milioni khamsini na laki mbili. [Al-Bukhaariy]

 

 

Share

026-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Uharamu Wa Dhulma Na Amri Ya Karudisha Vilivyodhulumiwa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب تحريم الظلم والأمر بردِّ المظالم

26 – Mlango Wa Uharamu Wa Dhulma Na Amri Ya Karudisha Vilivyodhulumiwa

 

Alhidaaya.com

 

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

مَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ حَمِيمٍ وَلَا شَفِيعٍ يُطَاعُ﴿١٨﴾

Madhalimu hawatokuwa na rafiki wa dhati, na wala mwombezi anayetiiwa. [Ghaafir: 18]

 

وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِن نَّصِيرٍ ﴿٧١﴾

Na madhalimu hawana yeyote mwenye kunusuru. [Al-Hajj: 71]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن جابر رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((اتَّقُوا الظُّلْمَ؛ فَإنَّ الظُّلْمَ ظُلُمَاتٌ يَوْمَ القِيَامَةِ. وَاتَّقُوا الشُّحَّ؛ فَإِنَّ الشُّحَّ أهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ. حَمَلَهُمْ عَلَى أنْ سَفَكُوا دِمَاءهُمْ، وَاسْتَحَلُّوا مَحَارِمَهُمْ)). رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Ogopeni sana dhulma, kwani kudhulumu ni viza Siku ya Qiyaamah. Na ogopeni sana ubakhili kwani ubakhili uliwaangamiza waliokuwa kabla yenu, uliwafanya wamwage damu zao na wakahalalisha walioharamishiwa.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((لَتُؤَدُّنَّ الحُقُوقَ إِلَى أهْلِهَا يَومَ القِيَامَةِ، حَتَّى يُقَادَ للشَّاةِ الجَلْحَاءِ مِنَ الشَّاةِ القَرْنَاءِ)). رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Mtaendelea kutimiza haki za wenyewe Siku ya Qiyaamah mpaka kondoo asiyekuwa na pembe alipize kisasi juu ya mwenye pembe.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن عمر رضي الله عنهما، قال: كُنَّا نَتَحَدَّثُ عَنْ حَجَّةِ الوَدَاعِ، والنَّبيُّ صلى الله عليه وسلم بَيْنَ أَظْهُرِنَا، وَلا نَدْرِي مَا حَجَّةُ الوَدَاعِ حَتَّى حَمِدَ اللهَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَأثْنَى عَلَيهِ ثُمَّ ذَكَرَ المَسْيحَ الدَّجَّال فَأطْنَبَ في ذِكْرِهِ، وَقَالَ: ((مَا بَعَثَ اللهُ مِنْ نَبيٍّ إلا أنْذَرَهُ أُمَّتَهُ، أنْذَرَهُ نُوحٌ وَالنَّبِيُّونَ مِنْ بَعْدِهِ، وَإِنَّهُ إنْ يَخْرُجْ فِيكُمْ فَما خَفِيَ عَليْكُمْ مِنْ شَأنِه فَلَيْسَ يَخْفَى عَليْكُم، إنَّ رَبَّكُمْ لَيْسَ بأعْوَرَ وإنَّهُ أعْوَرُ عَيْنِ اليُمْنَى، كَأنَّ عَيْنَهُ عِنَبَةٌ طَافِيَةٌ. ألا إنَّ الله حَرَّمَ عَلَيْكُمْ دِمَاءكُمْ وَأمْوَالَكُمْ كحُرْمَةِ يَوْمِكُمْ هَذَا، في بلدكم هذا، في شَهْرِكُمْ هَذَا، ألا هَلْ بَلّغْتُ؟)) قالُوا: نَعَمْ، قَالَ: ((اللَّهُمَّ اشْهَدْ)) ثلاثًا ((وَيْلَكُمْ- أَوْ وَيْحَكُمْ، انْظُروا: لا تَرْجعُوا بَعْدِي كُفّارًا يَضْرِبُ بَعْضُكُمْ رِقَابَ بَعْضٍ)). رواه البخاري، وروى مسلم بعضه

Imepokewa kutoka kwa ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa amesema: Tulikuwa tukizungumza Hijjah ya kuaga (Hijjatul Wadaa’) baina yetu wala hatujui nini Hijjah ya kuaga mpaka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alipomuhimidi Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) na kumtukuza. Baada ya hapo akamtaja Masiyh Dajjaal na kuzungumza kwa kirefu. Kisha akasema: “Kila Rasuli aliyetumwa na Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) amewaonya Ummah wake kuhusu (Masiyh Dajjaal). Nuwh na Rusul waliokuja baada yake walionya kumhusu. Na hakika yeye atatoka miongoni mwenu, hataweza kujificha (kwani tayari mmeshamjua), ukweli wake hautafichika nanyi. Hakika Mola wenu si chogo, bali yeye ni chogo jicho lake kulia kama kwamba jicho lake ni zabibu iliyovimba. Tahadharini! Hakika Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa) Ametahadharisha kwenu damu na mali yenu kama utukufu wa siku yenu hii (siku ya Hijjah), katika mji wenu huu (yaani Makkah), katika mwezi wenu huu (Dhul Hijjah). Je, nimefikisha ujumbe? Wakasema (Maswahaba): Ndio. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam): Ee Allaah! Shuhudia – mara tatu. Ole wenu tizameni sana! Msirudi baada yangu makafiri mnakata shingo (mnauana).” [Al-Bukhaariy na Muslim amepokea baadhi yake)

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن عائشة رضي الله عنها: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((مَنْ ظَلَمَ قيدَ شِبْرٍ مِنَ الأرْضِ، طُوِّقَهُ مِنْ سبْعِ أرَضينَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Atakaye dhulumu ardhi kiasi cha shubiri atabebeshwa ardhi saba (siku ya Qiyaamah) [A-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي موسى رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ الله لَيُمْلِي لِلظَّالِمِ، فَإِذَا أخَذَهُ لَمْ يُفْلِتْهُ))، ثُمَّ قَرَأَ: {وكَذَلِكَ أَخْذُ رَبِّكَ إِذَا أَخَذَ الْقُرَى وَهِيَ ظَالِمَةٌ إِنَّ أَخْذَهُ أَلِيمٌ شَدِيدٌ} [هود: 102] مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa na Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Hakika Allaah Anampatia muda dhalimu (kwa kumcheleweshea adhabu), lakini anapomshika hatoki katika adhabu Yake. Kisha akasoma: Na hivyo ndivyo mkamato wa Rabb wako unavyokuwa Anapokamata miji na huku ikifanya dhulma. Hakika mkamato Wake unaumiza vikali. [Huwd: 102]” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 6

وعن معاذ رضي الله عنه قَالَ: بَعَثَنِي رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: ((إنَّكَ تَأتِي قَوْمًا مِنْ أهلِ الكِتَابِ فَادْعُهُمْ إِلَى شَهَادَةِ أنْ لا إلَهَ إلا الله، وَأنِّي رسولُ الله، فَإنْ هُمْ أَطَاعُوا لِذلِكَ، فَأعْلِمْهُمْ أنَّ اللهَ قَدِ افْتَرضَ عَلَيْهِمْ خَمْسَ صَلَواتٍ في كُلِّ يَوْمٍ وَلَيلَةٍ، فَإِنْ هُمْ أطَاعُوا لِذَلِكَ، فَأعْلِمْهُمْ أنَّ اللهَ قَدِ افْتَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً تُؤخَذُ مِنْ أغْنِيَائِهِمْ فَتُرَدُّ عَلَى فُقَرَائِهِمْ، فَإنْ هُمْ أطَاعُوا لِذَلِكَ، فَإِيَّاكَ وَكَرَائِمَ أمْوَالِهِمْ، وَاتَّقِ دَعْوَةَ المَظْلُومِ؛ فإِنَّهُ لَيْسَ بَيْنَها وَبَيْنَ اللهِ حِجَابٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Mu’adh (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alinituma kwa kuniambia: “Hakika utakwenda kwa (watu wa Ahlul Kitaab). Mwanzo waite katika kushuhudia na kukubali kuwa hapana Mola Apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah na kuwa mimi ni Rasuli wa Allaah. Wanapokutii kwa hilo, wafahamishe kuwa Allaah Amewafaradhishia Swalaah tano kwa kila mchana na usiku. Wanapokutii kwa hilo, wafahamishe kuwa Allaah Amewafaradhishia Swadaqah (Zakaah) inayochukuliwa kutoka kwa matajiri wao na kurudishwa kwa mafakiri miongoni mwao. Wanapokutii kwa hilo, basi tahadhari sana na mali yao ya thamani. Na ogopa sana du’aa ya mwenye kudhulimiwa hiyo haina pazia na Allaah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 7

وعن أبي حُمَيدٍ عبد الرحمن بن سعد السَّاعِدِي رضي الله عنه قَالَ: اسْتَعْمَلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم رَجُلًا مِنَ الأزْدِ يُقَالُ لَهُ: ابْنُ اللُّتْبِيَّةِ عَلَى الصَّدَقَةِ، فَلَمَّا قَدِمَ، قَالَ: هَذَا لَكُمْ، وَهَذَا أُهْدِيَ إِلَيَّ، فَقَامَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَلَى المِنْبَرِ فَحَمِدَ الله وَأثْنَى عَلَيهِ، ثُمَّ قَالَ: ((أمَّا بَعدُ، فَإِنِّي أسْتَعْمِلُ الرَّجُلَ منْكُمْ عَلَى العَمَلِ مِمَّا وَلانِي اللهُ، فَيَأتِي فَيَقُولُ: هَذَا لَكُمْ وَهَذا هَدِيَّةٌ أُهْدِيتْ إلَيَّ، أفَلا جَلَسَ في بيت أبِيهِ أَوْ أُمِّهِ حَتَّى تَأتِيَهُ هَدِيَّتُهُ إنْ كَانَ صَادِقًا، واللهِ لا يَأخُذُ أحَدٌ مِنْكُمْ شَيئًا بِغَيرِ حَقِّهِ إلا لَقِيَ الله تَعَالَى، يَحْمِلُهُ يَوْمَ القِيَامَةِ، فَلا أعْرِفَنَّ أحَدًا مِنْكُمْ لَقِيَ اللهَ يَحْمِلُ بَعيرًا لَهُ رُغَاءٌ، أَوْ بَقَرَةً لَهَا خُوَارٌ، أَوْ شَاةً تَيْعَرُ)). ثُمَّ رفع يديهِ حَتَّى رُؤِيَ عُفْرَةُ إبْطَيْهِ، فَقَالَ: ((اللَّهُمَّ هَلْ بَلَّغْتُ)) ثلاثًا مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa na Abuu Humayd, ‘Abdur-Rahmaan bin Sa’d As- Saa’iydy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuwa amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimtuma mtu kutoka katika ukoo wa Al-Azdiy aliyekuwa akiitwa inb Al-Lutbiyyah kukusanya Zakah. Aliporudi alisema: Hili ni fungo lenu na hivi nimepewa zawadi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisimama juu ya mimbar, akamuhidi Allaah na kumtukuza pamoja na kumsifu, kisha akasema: “Ama baada ya haya; hakika mimi nimempa kazi mtu miongoni mwenu juu ya kazi niliyopewa mamlaka na Allaah. Mtu huyo anakuja na anasema: Hiki ni chenu na hiki ni zawadi nimepewa. Basi angekaa mmoja wenu kwenye nyumba ya baba yake, au mama yake mpaka imfikie yeye zawadi hiyo yake ikiwa hakika yeye ni mkweli. Wa-Allaahi hatochukua mmoja wenu kitu chochote bila ya haki yake ila atakutana na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) akiwa amekibeba siku ya Qiyaamah. Hivyo, nisije nikamjua yoyote kati yenu amekutana na Allaah akiwa amebeba ngamia anayeguna, au ng’ombe anayeroroma au mbuzi (kondoo) anayelia.” Kisha akanyanyua mikono yake mpaka uonekane weupe na makwapa yake, akasema: “Ee Allaah! Je, nimefikisha.” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

 

Hadiyth – 8

عن أَبي هريرة رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ كَانَتْ عِنْدَهُ مَظْلمَةٌ لأَخِيه، مِنْ عِرضِهِ أَوْ مِنْ شَيْءٍ، فَلْيَتَحَلَّلْهُ مِنْهُ اليَوْمَ قبْلَ أنْ لا يَكُونَ دِينَار وَلا دِرْهَمٌ؛ إنْ كَانَ لَهُ عَمَلٌ صَالِحٌ أُخِذَ مِنْهُ بِقَدْرِ مَظْلمَتِهِ، وَإنْ لَمْ يَكُنْ لَهُ حَسَنَاتٌ أُخِذَ مِنْ سَيِّئَاتِ صَاحِبِهِ فَحُمِلَ عَلَيهِ)). رواه البخاري

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwenye kitu cha dhulma cha nduguye kutokana na kumvunjia heshima au kitu kingine chochote, basi amuombe amhalalishie leo kabla haijafika siku ambayo hakutakuwa na dinar wala dirham; akiwa ana ‘amali njema itachukuliwa kwa kadiri ya alichodhulumu, na ikiwa hana ‘amali njema zitachukuliwa dhambi za aliyemdhulumu na kubebeshwa (yeye).” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((المُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ المُسْلِمُونَ مِنْ لِسَانِهِ وَيَدِهِ، وَالمُهَاجِرُ مَنْ هَجَرَ مَا نَهَى اللهُ عَنْهُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa na ‘AbduLLaah bin ‘Amru bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Muislamu ni yule ambaye Waislaam wamesalimika kwa ulimi na mkono wake, na Muhajir ni yule anayehama yale aliyoyakataza Allaah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 10

وعنه رضي الله عنه قَالَ: كَانَ عَلَى ثَقَل النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم رَجُلٌ يُقَالُ لَهُ كِرْكِرَةُ، فَمَاتَ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((هُوَ في النَّارِ)) فَذَهَبُوا يَنْظُرُونَ إِلَيْه، فَوَجَدُوا عَبَاءةً قَدْ غَلَّهَا. رواه البخاري

Kutoka kwake (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Alikuwepo mtu mmoja akiitwa Kirkirah aliyekuwa mtunzaji wa mali ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Yeye yupo motoni”. Maswahaba wakaenda kumtazama wakapata juba alilochukua kwa khiyana.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 12

وعن أَبي بكْرة نُفَيْع بن الحارث رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّ الزَّمَانَ قَدِ اسْتَدَارَ كَهَيْئَته يَوْمَ خَلَقَ اللهُ السَّمَاوَاتِ وَالأَرضَ: السَّنَةُ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا، مِنْهَا أرْبَعَةٌ حُرُمٌ: ثَلاثٌ مُتَوالِياتٌ: ذُو القَعْدَة، وذُو الحِجَّةِ، وَالمُحَرَّمُ، وَرَجَبُ مُضَرَ الَّذِي بَيْنَ جُمَادَى وَشعْبَانَ، أيُّ شَهْر هَذَا؟)) قُلْنَا: اللهُ وَرَسُولُهُ أعْلَمُ، فَسَكَتَ حَتَّى ظَننَّا أنَّهُ سَيُسَمِّيهِ بِغَيْرِ اسْمِهِ، قَالَ: ((ألَيْسَ ذَا الحِجَّةِ؟)) قُلْنَا: بَلَى. قَالَ: ((فَأيُّ بَلَد هَذَا؟)) قُلْنَا: اللهُ ورَسُولُهُ أعْلَمُ، فَسَكَتَ حَتَّى ظَنَنَّا أنَّهُ سَيُسَمِّيهِ بِغَيرِ اسْمِهِ. قَالَ: ((ألَيْسَ البَلْدَةَ؟)) قُلْنَا: بَلَى. قَالَ: ((فَأيُّ يَوْم هَذَا؟)) قُلْنَا: اللهُ ورَسُولُهُ أعْلَمُ، فَسَكَتَ حَتَّى ظَنَنَّا أنَّهُ سَيُسَمِّيهِ بغَيرِ اسْمِهِ. قَالَ: ((ألَيسَ يَوْمَ النَّحْرِ؟)) قُلْنَا: بَلَى. قَالَ: ((فَإنَّ دِمَاءكُمْ وَأمْوَالَكُمْ وَأَعْرَاضَكُمْ عليكم حَرَامٌ، كَحُرْمَةِ يَوْمِكُمْ هَذَا في بَلَدِكُمْ هَذَا في شَهْرِكُمْ هَذَا، وَسَتَلْقُونَ رَبَّكُمْ فَيَسْألُكُمْ عَنْ أعْمَالِكُمْ، ألا فَلا تَرْجعوا بعدي كُفّارًا يَضْرِبُ بَعْضُكُمْ رِقَابَ بَعْض، ألا لَيُبَلِّغ الشَّاهِدُ الغَائِبَ، فَلَعَلَّ بَعْضَ مَنْ يَبْلُغُهُ أنْ يَكُونَ أوْعَى لَهُ مِنْ بَعْض مَنْ سَمِعَهُ))، ثُمَّ قَالَ: ((ألا هَلْ بَلَّغْتُ، ألا هَلْ بَلَّغْتُ؟)) قُلْنَا: نَعَمْ. قَالَ: ((اللَّهُمَّ اشْهَدْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokelewa kutoka kwa Abu Bakr Nufay’ kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa saalam) amesema: “Hakika zama (mwaka) unapita kama ilivyo siku ya Allaah Alivyoumba mbingu na ardhi: Mwaka una miezi kumi na mbili, miongoni mwayo ni miezi minne iliyo hurum (miezi ambayo vita ni haram hata wakati wa ujahiliyyah). Miezi mitatu ni ya kufuatana: Dhul Qa’dah, Dhul Hijjah na Muharram na Rajab Mundhwar, mwezi ambao upo baina ya Jumaadah na Sha’baan. Kisha akauliza: “Je, huu ni mwezi gani?” Wakasema (Maswahaba): Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akanyamaza mpaka tukadhania atauita kwa jina lingine. Akasema: “Je, huu si mwezi wa Dhul Hijjah?” Tukasema: Ndio. Akauliza: “Je, huu ni mji gani?” Tukasema: Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akanyamaza mpaka tukadhania atauita kwa jina lingine lisilikuwa jina lake. Akasema: “Je, huu si mji wa (Makkah)?” Tukasema: Ndio. Akasema: “Je, hii ni siku gani?” Tukasema: Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akanyamaza mpaka tukadhania kuwa ataiita kwa jina lingine. Akasema: “Je, hii si ni siku ya kuchinja?” Tukasema: Ndio. Akasema: “Hakika damu zenu, mali zenu, na heshima zenu ni haramu kwenu kama uharamu (wa kufanya dhambi) siku yenu hii, katika mji wenu huu, katika mwezi wenu huu. Na bila shaka mtakutana na Mola wenu na kuwauliza juu ya ‘amali zenu. Fahamuni! Msirudi baada yangu katika ukafiri mkiuana ninyi kwa ninyi. Jueni! Aliyehudhuria amfikishie asiyekuwepo, huenda baadhi ya watakao fikishiwa wakawa wanafahamu nzuri zaidi kuliko waliosikia.” Kisha akauliza: “Je, nimefikisha?” Tukasema: Ndio. Akasema: “Ee Allaah shuhudia (hilo).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي أمامة إياس بن ثعلبة الحارثي رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَن اقْتَطَعَ حَقَّ امْرئ مُسْلِم بيَمينه، فَقدْ أوْجَبَ اللهُ لَهُ النَّارَ، وَحَرَّمَ عَلَيهِ الجَنَّةَ)) فَقَالَ رَجُلٌ: وإنْ كَانَ شَيْئًا يَسيرًا يَا رَسُول الله؟ فَقَالَ: ((وإنْ كَانَ قَضيبًا مِنْ أرَاك)). رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Abuu Umaamah Iyaas bin Tha’labah Al-Haarithiy (Radhiya Allaah ‘anhhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwenye kuchukua haki ya mtu Muislamu kwa kuapa yamini (ya uongo) imewajibika kwa Allaah kumuingiza motoni na kumharamishia Jannah.” Mtu mmoja akasema: “Hata kikiwa kitu kidogo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: “Hata kikiwa ni kigaa cha mti Arak.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 12

وعن عَدِيّ بن عَميْرَةَ رضي الله عنه قَالَ: سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((مَنِ اسْتَعْمَلْنَاهُ مِنْكُمْ عَلَى عَمَل، فَكَتَمَنَا مِخْيَطًا فَمَا فَوْقَهُ، كَانَ غُلُولًا يَأتِي به يَومَ القِيَامَةِ)) فَقَامَ إليه رَجُلٌ أسْوَدُ مِنَ الأنْصَارِ، كَأنِّي أنْظُرُ إِلَيْهِ، فَقَالَ: يَا رَسُول الله، اقْبَلْ عَنِّي عَمَلَكَ، قَالَ: ((وَمَا لَكَ؟)) قَالَ: سَمِعْتكَ تَقُولُ كَذَا وكَذَا، قَالَ: ((وَأَنَا أقُولُه الآنَ: مَنِ اسْتَعْمَلْنَاهُ عَلَى عَمَلٍ فَلْيَجِئْ بقَليله وَكَثيره، فَمَا أُوتِيَ مِنْهُ أخَذَ، وَمَا نُهِيَ عَنْهُ انْتَهَى)). رواه مسلم

Imepokewa na ‘Adiy bin ‘Umayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba nimemsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Yoyote tutakaye muajiri miongoni mwenu kwa kazi yoyote ile akawa ni mwenye kuficha sindano na zaidi yake, huo utakuwa ni wizi atakao kuja nao Siku ya Qiyaamah.” Akasema mtu mweusi mingoni mwa Answaar kana kwamba ninamtazama. Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Niruhusu nijiuzulu kazi yako (uliyonipa). Akamuuliza: “Kwanini?” Akajibu: Nimekusikia ukisema kadhaa na kadhaa. Akasema: “Yoyote atakayempa jukumu la kazi fulani basi alete kichache na kingi (alete chochote atakachopata). Atakachopewa atachukua, na atakachozuiliwa akiache.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 13

وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه قَالَ: لَمَّا كَانَ يَوْمُ خَيبَر أقْبَلَ نَفَرٌ مِنْ أصْحَابِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، فقَالُوا: فُلاَنٌ شَهِيدٌ، وفُلانٌ شَهِيدٌ، حَتَّى مَرُّوا عَلَى رَجُلٍ، فقالوا: فُلانٌ شَهِيدٌ. فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((كَلا، إنِّي رَأيْتُهُ في النَّار في بُرْدَةٍ غَلَّهَا- أَوْ عَبَاءة-)). رواه مسلم

Imepokewa na ‘Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Siku ya Vita vya Khaybar walikaribia kikundi cha Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuja kutazama waliokufa mashahidi. Wakasema: Fulani ni shahidi na fulani pia ni shahidi.” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa salaam) akasema: “Sivyo hivyo. Hakika mimi nimemuona motoni kwa juba au gauni aliloliiba.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 14

وعن أَبي قتادة الحارث بن ربعي رضي الله عنه عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: أَنَّهُ قَامَ فيهم، فَذَكَرَ لَهُمْ أنَّ الجِهَادَ في سبيلِ الله، وَالإِيمَانَ بالله أَفْضَلُ الأعْمَالِ، فَقَامَ رَجُلٌ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ الله، أرَأيْتَ إنْ قُتِلْتُ في سبيلِ الله، تُكَفَّرُ عَنّي خَطَايَايَ؟ فَقَالَ لَهُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((نَعَمْ، إنْ قُتِلْتَ في سبيلِ اللهِ، وَأنْتَ صَابرٌ مُحْتَسِبٌ، مُقْبِلٌ غَيرُ مُدْبر)) ثُمَّ قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((كَيْفَ قُلْتَ؟)) قَالَ: أرَأيْتَ إنْ قُتِلْتُ في سبيلِ الله، أتُكَفَّرُ عَنّي خَطَايَايَ؟ فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((نَعمْ، وَأنْتَ صَابرٌ مُحْتَسِبٌ، مُقْبِلٌ غَيرُ مُدْبِرٍ، إلا الدَّيْنَ؛ فإنَّ جِبريلَ قَالَ لي ذلِكَ)). رواه مسلم

Imepokewa na Abuu Qataadah bin Al-Haarith bin Rab’iyy (Radhwiya Allaahu ‘anahu) kwamba Rasuli wa Allaahu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alisimama mbele yao, akawatajia kuwa jihaad katika njia ya Allaah na kumuamini Allaah ndio ‘amali bora. Hapo alisimama mtu akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Waonaje nikiuliwa katika njia ya Allaah nitasamehewa madhambi yangu? Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Ndio, ukiuliwa katika njia ya Allaah nawe ukawa katika hali ya kusubiri na huku unatarajia malipo (kutoka kwa Allaah), ukiwa unasonga mbele katika vita wala sio kurudi nyuma (na kukimbia).” Kisha akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Umesema nini?” Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Waonaje nikiuliwa katika njia ya Allaah nitasamehewa makossa yangu? Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Ndio, ukiuliwa katika njia ya Allaah nawe ukawa katika hali ya kusubiri na huku watarajia malipo (kutoka kwa Allaah), ukiwa unasonga mbele katika vita wala sio kurudi nyuma (na kukimbia) ila deni kwani Jibriyl ameniambia hilo.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 15

وعن أبي هُريرةَ رضي الله عنه: أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((أتدرونَ مَنِ المُفْلِسُ؟)) قالوا: المفْلسُ فِينَا مَنْ لا دِرهَمَ لَهُ ولا مَتَاع، فَقَالَ: ((إنَّ المُفْلسَ مِنْ أُمَّتي مَنْ يأتي يَومَ القيامَةِ بصلاةٍ وصيامٍ وزَكاةٍ، ويأتي قَدْ شَتَمَ هَذَا، وقَذَفَ هَذَا، وَأَكَلَ مالَ هَذَا، وسَفَكَ دَمَ هَذَا، وَضَرَبَ هَذَا، فيُعْطَى هَذَا مِنْ حَسَنَاتِهِ، وهَذَا مِنْ حَسناتهِ، فإنْ فَنِيَتْ حَسَناتُه قَبْل أنْ يُقضى مَا عَلَيهِ، أُخِذَ منْ خَطَاياهُم فَطُرِحَتْ عَلَيهِ، ثُمَّ طُرِحَ في النَّارِ)). رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu Alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Je, mnamjua Muflis?” Wakasema: Muflis kwetu sisi ni yule asiyekuwa na dirham wala mali. Akasema: “Hakika Muflis katika Ummah wangu ni yule atakayekuja Siku ya Qiyaamah akiwa ana Swalaah, Swawm na Zakaah. Na anakuja amemtusi huyu, amemsingizia huyu uzinifu, amekula mali ya huyu, amemwaga damu ya huyu na kumpiga huyu. Kila aliyedhulumiwa atapewa sehemu ya mema yake, na yule atapewa sehemu ya mema yake. Pindi mema yake yatakapomalizika kabla ya hukmu kuisha, zitachukuliwa sehemu ya dhambi zao (kulingana na alivyo dhulumu) na apewe yeye, kisha atupwe motoni.” [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 16

وعن أم سلمة رضي الله عنها: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّمَا أنَا بَشَرٌ، وَإنَّكُمْ تَخْتَصِمُونَ إلَيَّ، وَلَعَلَّ بَعْضَكُمْ أنْ يَكُونَ أَلْحَنَ بِحُجّتِهِ مِنْ بَعْضٍ، فأَقْضِيَ لَهُ بِنَحْوِ مَا أسْمعُ، فَمَنْ قَضَيتُ لَهُ بِحَقِّ أخِيهِ فَإِنَّما أقطَعُ لَهُ قِطعةً مِنَ النَّارِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa kutoka kwa ummu Salamah (Radhwiya Llaahu ‘anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika mimi ni mwana Aadam, nanyi mnaniletea mashtaka yenu. Na huenda baadhi yenu mkawa mahodari kutoa hoja kuliko baadhi ya wengine wenu. Nami nikampatia haki (isiyokuwa yake) kwa niliyoyasikia. Yoyote atakaye mpatia haki ya nduguye, hakika nitakuwa nimemkatia kipande cha moto. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 17

وعن ابن عمر رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((لَنْ يَزَالَ المُؤْمِنُ في فُسْحَةٍ مِنْ دِينهِ مَا لَمْ يُصِبْ دَمًا حَرَامًا)). رواه البخاري

Imepokewa na ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Muumin atabakia katika duara la matumaini na Iymaan madamu hatamwaga damu iliyoharamishwa.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 18

وعن خولة بنتِ عامر الأنصارية وهي امرأة حمزة رضي الله عنه وعنها، قَالَتْ: سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((إنَّ رِجَالًا يَتَخَوَّضُونَ في مَالِ الله بغَيرِ حَقٍّ، فَلَهُمُ النَّارُ يَومَ القِيَامَةِ)). رواه البخاري

Imepokewa kutoka kwa Khawlah bint ‘Aamir Al-Answaariyyah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa), naye ni mke wa Hamzah bin ‘Abdul-Mutw-Twalib (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Akisema: “Hakika watu wanaotumia mali ya Allaah (mali ya Ummah) pasi na haki, hao wana Moto Siku ya Qiyaamah.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Share

027-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Kuadhimisha Mambo Matukufu Ya Waislamu, Kubainisha Haki, Kuwasikitia Na Kuwahurumia

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب تعظيم حرمات المسلمين وبيان حقوقهم والشفقة عليهم ورحمتهم

27 – Mlango Kuadhimisha Mambo Matukufu Ya Waislamu, Kubainisha Haki, Kuwasikitia Na Kuwahurumia

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّـهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ﴿٣٠﴾

Na yeyote anayeadhimisha vitukufu vya Allaah basi hivyo ni kheri kwake mbele ya Rabb wake. [Al-Hajj: 30]

 

وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّـهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ ﴿٣٢﴾

Na yeyote anayeadhimisha Ishara za Allaah, basi hayo ni katika taqwa ya nyoyo. [Al-Hajj: 32]

 

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ﴿٨٨﴾

 Na inamisha bawa lako kwa Waumini (kuwahurumia). [Al-Hijr: 88]

 

مَن قَتَلَ نَفْسًا بِغَيْرِ نَفْسٍ أَوْ فَسَادٍ فِي الْأَرْضِ فَكَأَنَّمَا قَتَلَ النَّاسَ جَمِيعًا وَمَنْ أَحْيَاهَا فَكَأَنَّمَا أَحْيَا النَّاسَ جَمِيعًا ﴿٣٢﴾

Atakayeiua nafsi bila ya nafsi (kuua), au kufanya ufisadi katika ardhi; basi ni kama ameua watu wote. [Al-Maaidah: 32]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي موسى رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((المُؤْمِنُ للْمُؤْمِنِ كَالبُنْيَانِ يَشُدُّ بَعْضُهُ بَعْضًا)) وشبَّكَ بَيْنَ أصَابِعِهِ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Muumini kwa Muumini ni mfano wa jengo, sehemu moja inatilia nguvu sehemu nyingine.” Na akaviunganisha vidole vyake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ مَرَّ في شَيْءٍ مِنْ مَسَاجِدِنا، أَوْ أَسْوَاقِنَا، وَمَعَهُ نَبْلٌ فَلْيُمْسِكْ، أَوْ لِيَقْبِضْ عَلَى نِصَالِهَا بكَفّه؛ أنْ يُصِيبَ أحَدًا مِنَ المُسْلِمِينَ مِنْهَا بِشَيْء)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Kutoka kwake Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Anayepita Misikitini au masokoni mwetu na ilhali ana mshale, basi auzuwie au akishike chemba chake kwa mkono wake, asije akamdunga nao yeyote katika Waislamu.” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 3

وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَثَلُ المُؤْمِنينَ في تَوَادِّهِمْ وتَرَاحُمهمْ وَتَعَاطُفِهمْ، مَثَلُ الجَسَدِ إِذَا اشْتَكَى مِنْهُ عُضْوٌ تَدَاعَى لَهُ سَائِرُ الجَسَدِ بِالسَّهَرِ والحُمَّى)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa na An-Nu’maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Mfano wa Waumini katika kupendana kwao, kuhurumiana kwao na kusaidiana kwao, ni mfano wa mwili, kiungo kimoja kikiumwa basi mwili mzima hukesha kwa homa.” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَبَّلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم الحَسَنَ بْنَ عَليٍّ رضي الله عنهما، وَعِنْدَهُ الأَقْرَعُ بْنُ حَابِس، فَقَالَ الأقْرَعُ: إن لِي عَشرَةً مِنَ الوَلَدِ مَا قَبَّلْتُ مِنْهُمْ أحَدًا. فَنَظَرَ إِلَيْهِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: ((مَنْ لا يَرْحَمْ لا يُرْحَمْ!)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuna wakati mmoja Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alimbusu mjukuu wake Al-Hasan bin ‘Ally (Radhwiya Allaahu 'anhu) mbele ya Al-Aqra akasema: “Hakika mimi nina watoto kumi sijambusu yeyote miongoni mwao.” Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) alimtazama, akasema: “Yeyote asiye na huruma (kwa wenziwe) basi hahurumiwi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن عائشة رضي الله عنها، قَالَتْ: قَدِمَ نَاسٌ مِنَ الأعْرَابِ عَلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فقالوا: أتُقَبِّلُونَ صِبْيَانَكُمْ؟ فَقَالَ: ((نَعَمْ)) قالوا: لَكِنَّا والله مَا نُقَبِّلُ! فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((أَوَ أَمْلِك إنْ كَانَ اللهُ نَزَعَ مِنْ قُلُوبِكُم الرَّحْمَةَ))!. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

في هذا الحديث: الشفقة على الأولاد، وتقبيلهم ورحمتهم.

Imepokewa na ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) aliyesema: Mabedui walikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam), wakasema: “Je, mnawabusu watoto wenu?” Akasema: “Ndio.” Wakasema: “Lakini sisi Wa-Allaahi hatuwabusu.” Hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) akasema: “Je, naweza kuwamiliki ikiwa Allaah Ameondosha nyoyoni mwenu rehma (huruma).” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 6

وعن جرير بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ لا يَرْحَم النَّاسَ لا يَرْحَمْهُ الله)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa na Jariyr bin ‘Abdillaahi (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Asiye wahurumia watu, Allaah Hamrehemu.” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا صَلَّى أحَدُكُمْ للنَّاسِ فَلْيُخَفِّفْ، فَإن فيهِم الضَّعِيفَ وَالسَّقِيمَ وَالكَبيرَ، وَإِذَا صَلَّى أحَدُكُمْ لِنَفْسِهِ فَلْيُطَوِّل مَا شَاءَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Anaposwalisha watu mmoja wenu basi akhafifishe, kwani wapo miongoni mwao wanyonge, wagonjwa na wazee. Na anaposwali mmoja wenu peke yake, arefushe anavyotaka.” Na katika riwayah yengine: “Wenye haja.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن عائشة رضي الله عنها، قَالَتْ: إنْ كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم لَيَدَعُ العَمَلَ، وَهُوَ يُحبُّ أنْ يَعْمَلَ بِهِ؛ خَشْيَةَ أنْ يَعمَلَ بِهِ النَّاسُ فَيُفْرَضَ علَيْهِمْ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Kutoka kwake ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) mara nyengine alikuwa akiacha 'amali naye anapenda kuitekeleza kwa kuogopea wasije wakaifanya hivyo kufaradhishwa kwao. [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 9

وَعَنْهَا رضي الله عنها قَالَتْ: نَهَاهُمُ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم عنِ الوِصَال رَحمَةً لَهُمْ، فَقَالُوا: إنَّكَ تُوَاصِلُ؟ قَالَ: ((إنّي لَسْتُ كَهَيْئَتِكُمْ، إنِّي أبيتُ يُطْعمُني رَبِّي وَيَسقِيني)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Amesema ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) aliwakataza Wiswaal kwa kuwahurumia wao. Wakasema: “Hakika wewe unaunganisha?” Akasema: “Hakika mimi si kama mmoja wenu. Hakika mimi ninalishwa na kunyweshwa na Mola wangu usiku.” [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أَبي قَتادةَ الحارثِ بن رِبعِي رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنِّي لأَقُومُ إِلَى الصَّلاة، وَأُرِيدُ أنْ أُطَوِّلَ فِيهَا، فَأسْمَع بُكَاءَ الصَّبيِّ فَأَتَجَوَّزَ في صَلاتي كَرَاهية أنْ أشُقَّ عَلَى أُمِّهِ)). رواه البخاري.

Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Haarith Ar-Ri’biy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Kwa hakika mimi husimama katika Swalah na nikataka kuirefusha, basi huwa nikisikia kilio cha mtoto, hapo naifupisha Swalah yangu kwa kuchelea nisije nikampa uzito mama yake.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 11

وعن جندب بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ صَلَّى صَلاةَ الصُّبْحِ فَهُوَ في ذِمَّةِ الله فَلا يَطْلُبَنَّكُمُ الله مِنْ ذِمَّته بشَيءٍ، فَإنَّهُ مَنْ يَطْلُبْهُ منْ ذمَّته بشَيءٍ يُدْركْهُ، ثُمَّ يَكُبُّهُ عَلَى وَجْهِهِ في نَارِ جَهَنَّمَ)). رواه مسلم.

Kutoka kwa Jundub bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Mwenye kuswali Swalaah ya Al-Fajr yuko katika dhima ya Allaah (amani na ahadi Yake). Hivyo, usijiweke katika hali ambayo utakuja laumiwa na Allaah kwa kuvunja ahadi Yake. Hakika mwenye kufanyiwa hesabu kwa kufanya khiyana ulinzi wa Allaah, Allaah Atampatiliza, na kisha kumuingiza kwa uso wake moto wa Jahannam.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 12

وعن ابن عمر رضي الله عنهما أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((المُسْلِمُ أَخُو المُسْلِم، لا يَظْلِمهُ، وَلا يُسْلمُهُ. مَنْ كَانَ في حَاجَة أخيه، كَانَ اللهُ في حَاجَته، وَمَنْ فَرَّجَ عَنْ مُسْلِم كُرْبَةً، فَرَّجَ اللهُ عَنْهُ بها كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ يَومِ القِيَامَةِ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِمًا سَتَرَهُ اللهُ يَومَ القِيامَةِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Muislamu ni ndugu yake Muislamu, hamdhulumu wala hamsalimishi (kwa adui). Mwenye kumtekelezea haja nduguye, Allaah Atamtekelezea haja yake. Mwenye kumondolea Muislamu dhiki, Allaah humondolea dhiki miongoni mwa dhiki Siku ya Qiyaamah. Na mwenye kumsitiri Muislamu, Allaah Atamsitiri Siku ya Qiyaamah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 13

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((المُسْلِمُ أخُو المُسْلِمُ، لا يَخُونُهُ، وَلا يَكْذِبُهُ، وَلا يَخْذُلُهُ، كُلُّ المُسْلِمِ عَلَى المُسْلِم حَرَامٌ عِرْضُهُ وَمَالهُ وَدَمُهُ، التَّقْوى هاهُنَا، بحَسْب امْرئٍ مِنَ الشَّرِّ أنْ يَحْقِرَ أخَاهُ المُسْلِم)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن)).

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Muislamu mwengine, hamfanyii khiyana wala hamdanganyi wala haachi kumnusuru. Kila Muislamu mwenziwe ni haramu cheo (heshima) chake, mali yake na damu yake. Taqwah ipo hapa, inatosha kwa mtu kuwa katika shari kumchukia nduguye Muislamu.” [At-Tirmidhiy]

 

 

Hadiyth – 14

وعنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((لا تَحَاسَدُوا، وَلا تَنَاجَشُوا، وَلا تَبَاغَضُوا، وَلا تَدَابَرُوا، وَلا يَبعْ بَعْضُكُمْ عَلَى بَيْع بَعْض، وَكُونُوا عِبَادَ الله إخْوَانًا، المُسْلِمُ أخُو المُسْلم: لا يَظْلِمُهُ، وَلا يَحْقِرُهُ، وَلا يَخْذُلُهُ، التَّقْوَى هاهُنَا- ويشير إِلَى صدره ثلاث مرات-- بحَسْب امْرئٍ مِنَ الشَّرِّ أنْ يَحقِرَ أخَاهُ المُسْلِمَ، كُلُّ المُسْلم عَلَى المُسْلم حَرَامٌ، دَمُهُ ومَالُهُ وعرْضُهُ)). رواه مسلم.

Kutoka kwake Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Msihusudiane, wala msiongezeane bei (katika biashara), wala msitukanane, wala msipeane nyongo (msikatane), wala baadhi yenu wasiuze juu ya wageni; na kuweni nyote ni waja wa Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa), ndugu moja. Muislamu ni ndugu ya Muislamu; hamdhulumu wala hamdharau, wala haachi kumnusuru. Uchaji Allaah uko hapa – akaashiria mara tatu kifuani mwake – yatosha mtu kutenda sharia atakapomdharau nduguye Muislamu. Kila Muislamu juu ya Muislamu mwenziwe ni haramu: damu yake, mali yake na heshima yake.” [Muslim]

 

 

Hadiyth – 15

وعن أنس رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((لا يُؤمِنُ أحَدُكُمْ حَتَّى يُحِبَّ لأخِيهِ مَا يُحِبُّ لنَفْسِهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Haamini mmoja wenu mpaka ampende nduguye kwa analolipendelea nafsi yake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 16

وعنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((انْصُرْ أخَاكَ ظَالمًا أَوْ مَظْلُومًا)) فَقَالَ رجل: يَا رَسُول اللهِ، أنْصُرُهُ إِذَا كَانَ مَظْلُومًا، أرَأيْتَ إنْ كَانَ ظَالِمًا كَيْفَ أنْصُرُهُ؟ قَالَ: ((تحْجُزُهُ- أَوْ تمْنَعُهُ- مِنَ الظُلْمِ فَإِنَّ ذلِكَ نَصرُهُ)). رواه البخاري.

Kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Mnusuru nduguyo akiwa amedhulumu au amedhulumia.” Mtu mmoja akauliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Nitamnusuru akiwa amedhulumiwa, nieleze nitamnusuru vipi akiwa amedhulumu?” Akasema: “Mzuilie asidhulumu, kufanya hivyo ndiko kumnusuru.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 17

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((حَقُّ المُسْلِم عَلَى المُسْلِم خَمْسٌ: رَدُّ السَّلامِ، وَعِيَادَةُ المَريض، وَاتِّبَاعُ الجَنَائِزِ، وَإجَابَةُ الدَّعْوَة، وتَشْميتُ العَاطِسِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) amesema: “Haki ya Muislamu kwa Muislamu mwenziwe ni tano: Kurudisha salamu, kumzuru mgonjwa, kumfuata jeneza, kuitikia mwaliko na kumwombea du’aa aliyepiga chafya (aliyechumua).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah ya Muslim: “Haki za Muislamu ni sita: Unapokutana naye umsalimie, anapokualika umwitikie, akitaka nasaha mnasihi, anapochemua na akamuhimidi Allaah muombee du’aa, akiwa mgonjwa mzuru na anapokufa fuata (jeneza lake).”

 

 

Hadiyth – 18

وعن أَبي عُمَارة البراءِ بن عازب رضي الله عنهما، قَالَ: أمرنا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بسبع، ونهانا عن سبع: أمَرَنَا بعيَادَة المَرِيض، وَاتِّبَاعِ الجَنَازَةِ، وتَشْمِيتِ العَاطسِ، وَإبْرار المُقْسِم، ونَصْرِ المَظْلُوم، وَإجَابَةِ الدَّاعِي، وَإِفْشَاءِ السَّلامِ، ونَهَانَا عَنْ خَواتِيمٍ أَوْ تَخَتُّمٍ بالذَّهَبِ، وَعَنْ شُرْبٍ بالفِضَّةِ، وَعَن الميَاثِرِ الحُمْرِ، وَعَن القَسِّيِّ، وَعَنْ لُبْسِ الحَريرِ والإسْتبْرَقِ وَالدِّيبَاجِ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية: وَإنْشَادِ الضَّالَّةِ في السَّبْعِ الأُوَل.

Kutoka kwa Abuu ‘Umaarah Al-Baraa’ bin ’Aazib (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam) ametuamuru kutekeleza mambo saba: Ametuamuru kuwazuru wagonjwa, kufuata jeneza, kumuombea aliyepiga chafya, kuamini kiapo, kumnusuru aliyedhulumiwa, kuitikia mwaliko na kutoa na kueneza salamu. Na ametukataza kuvaa pete ya dhahabu, kunywa kwenye chombo cha fedha, kupanda shogi la hariri nyekundu, Al-Qasiyy, kuvaa hariri, Istabraq na dibaji.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine: “Na kusaidia kupata kilichopotea mambo saba yaliyotajwa mwanzo.”

 

 

Share

028-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kusitiri Aibu Za Waislamu Na Katazo La Kuzieneza Pasi Na Dharura

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب ستر عورات المسلمين والنهي عن إشاعتها لغير ضرورة

028-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kusitiri Aibu Za Waislamu Na Katazo La Kuzieneza Pasi Na Dharura

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى :

إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿١٩﴾

Hakika wale wanaopenda uenee uchafu wa kashfa kwa wale walioamini; watapata adhabu iumizayo duniani na Aakhirah. Na Allaah Anajua nanyi hamjui. [An-Nuur: 19]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال‏: ((لاَ يَسْتُرُ عَبْدٌ عَبْداً في الدُّنْيَا إلاَّ سَتَرَهُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَةِ)) ‏‏  ‏رواه مسلم‏.‏‏

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah  (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mja hatamstiri mja mwenziwe duniani ila Allaah Atamstiri yeye Siku ya Qiyaamah." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أبي هريرة رضي الله عنه قال‏:‏ سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول‏:‏ ‏ ((‏كُلُّ أُمَّتِي مُعَافى :إلاَّ المُجَاهِرِينَ ، وَإنّ مِنَ المُجَاهَرَةِ أنْ يَعْمَلَ الرَّجُلُ باللَّيلِ عَمَلاً ، ثُمَّ يُصْبحُ وَقَدْ سَتَرَهُ اللهُ عَلَيهِ ، فَيقُولُ يَا فُلانُ ، عَمِلت البَارِحَةَ كَذَا وَكَذَا ، وَقَدْ بَاتَ يَسْتُرُهُ رَبُّهُ ، وَيُصبحُ يَكْشِفُ ستْرَ اللهِ عَنْه‏)).‏ ‏متفق عليه‏ ‏.

Na kutoka  kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alisema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Ummah wangu wote umesalimika ila wanaodhihirisha (maovu) ni mtu kutenda amali (ya maasiya) usiku kisha apambazukiwa ilhali amesitiriwa na Allaah, asema: 'Ee fulani, usiku wa jana nilifanya kadha na kadha.' Na hakika alikuwa amepitiwa na usiku mzima akiwa amesitiriwa na Rabb wake, na anapambazukiwa akiifunua sitara aliyositiriwa na Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ‏((إِذَا زَنَتِ الأَمَةُ فَتَبيَّنَ زِنَاهَا فَلْيَجْلِدْهَا الحَدَّ ، وَلا يُثَرِّبْ عَلَيْهَا ، ثُمَّ إنْ زَنَتِ الثَّانِيَةَ فَلْيَجْلِدْهَا الحَدَّ ، وَلا يُثَرِّبْ عَلَيْهَا ، ثُمَّ إنْ زَنَتِ الثَّالِثَةَ فَلْيَبِعْهَا وَلَوْ بِحَبْل مِنْ شَعَر‏)).‏ ‏‏متفق عليه‏ ‏.‏ 

Na kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Pindi atakapozini kijakazi na ikabainika zinaa yake, basi apigwe mijeledi ya adhabu (iliyowekwa na Shariy’ah) wala asikaripiwe. Kisha akizini mara ya pili apigwe tena mijeledi ya adhabu wala asikaripiwe. Kisha akizini tena mara ya tatu, amuuze kwa japokuwa kwa kamba iliyotengenezwa kwa nywele." [Al Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: أُتِيَ النَّبيّ  صلى الله عليه وسلم برجل قَدْ شَرِبَ خَمْراً ، قَالَ ‏:‏‏((اضْربُوهُ)) قَالَ أَبُو هريرة : فَمِنَّا الضَّارِبُ بِيَدِهِ ، والضَّارِبُ بِنَعْلِهِ ، وَالضَّارِبُ بِثَوبِهِ . فَلَمَّا انْصَرَفَ ، قَالَ بَعضُ القَومِ : أخْزَاكَ الله ، قَالَ  (( لا تَقُولُوا هكَذا ، لاَ تُعِينُوا عَلَيهِ الشَّيْطَانَ‏)).‏ ‏‏رواه البخاري‏‏‏.

Na kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaah 'anhu) amesema: Aliletwa mtu mlevi kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akasema: "Mpigeni." Akasema Abuu Hurayrah: Wapo miongoni mwetu waliompiga kwa mkono wake, wengine kwa viatu vyao na wengine kwa nguo zao. Alipoondoka (huyu mtu) walisema baadhi ya watu: "Allaah akupe hizaya (akudhililishe). "Akasema "Msiseme hivyo, msimsaidie shetani dhidi yake." [Al Bukhaariy]

 

 

 

Share

029-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwakidhia Waislamu Haja Zao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب قضاء حوائج المسلمين

029-Mlango Wa Kuwakidhia Waislamu Haja Zao

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ارْكَعُوا وَاسْجُدُوا وَاعْبُدُوا رَبَّكُمْ وَافْعَلُوا الْخَيْرَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ۩﴿٧٧﴾

Enyi walioamini! Rukuuni, na sujuduni na mwabuduni Rabb wenu, na fanyeni ya khayr ili mpata kufaulu. [Al-Hajj: 77]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال‏:‏ ‏ ((‏المُسْلِمُ أخُو المُسْلِمِ ، لاَ يَظْلِمُهُ  وَلاَ يُسْلِمُهُ . مَنْ كَانَ في حَاجَة أخِيه ، كَانَ اللهُ في حَاجَتِهِ، وَمَنْ فَرَّجَ عَنْ مُسْلِمٍ كُرْبَةً، فَرَّجَ اللهُ عَنْهُ بِهَا كُرْبَةً مِنْ كرَبِ يَومِ القِيَامَةِ ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِماً سَتَرَهُ اللهُ يَومَ القِيَامَةِ )).‏ ‏متفق عليه‏ ‏.

Na imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Muislamu ni ndugu yake Muislamu, hamdhulumu wala hamsalimishi (kwa adui).  Mwenye kumtekelezea haja nduguye Allaah Atamtekelezea haja yake. Na mwenye kumwondolea Muislamu dhiki, Allaah Atamwondolea dhiki miongoni mwa dhiki za Siku ya Qiyaamah. Na mwenye kumsitiri Muislamu, Allaah Atamsitiri Siku ya Qiyaamah." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

 

وعن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال‏:‏ (( مَنْ نَفَّسَ عَنْ مُؤْمِنٍ كُرْبَةً مِنْ كُرَبِ الدُّنيَا ، نَفَّسَ الله عَنْهُ كُربَةً مِنْ كُرَبِ يَوْمِ القِيَامَةِ ، وَمَنْ يَسَّر عَلَى مُعْسِرٍ يَسَّرَ الله عَلَيهِ في الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ ، وَمَنْ سَتَرَ مُسْلِماً سَتَرَهُ الله في الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ ، والله في عَونِ العَبْدِ مَا كَانَ العَبْدُ في عَونِ أخِيهِ ، وَمَنْ سَلَكَ طَريقاً يَلْتَمِسُ فِيهِ عِلْماً سَهَّلَ اللهُ لَهُ طَريقاً إِلَى الجَنَّةِ . وَمَا اجْتَمَعَ قَوْمٌ في بَيت مِنْ بُيُوتِ اللهِ تَعَالَى ، يَتْلُونَ كِتَابَ اللهِ ، وَيَتَدَارَسُونَهُ بَيْنَهُمْ إلاَّ نَزَلَتْ عَلَيْهِمُ السَّكِينَةُ ، وَغَشِيتْهُمُ الرَّحْمَةُ ، وَحَفَّتْهُمُ المَلاَئِكَةُ ، وَذَكَرَهُمُ الله فِيمَنْ عِندَهُ . وَمَنْ بَطَّأ بِهِ عَمَلُهُ لَمْ يُسْرِع بِهِ نَسَبُهُ)) رواه مسلم

      

Imepokewa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwenye kumfariji Muumini dhiki miongoni mwa dhiki za duniani, Allaah Atamfariji (na kumuondolea) dhiki miongoni mwa dhiki za Siku ya Qiyaamah. Na mwenye kumsahilishia mwenye uzito, Allaah Atamsahilishia duniani na Aakhirah. Na mwenye kumsitiri Muislamu, Allaah Atamsitiri duniani na Aakhirah. Na Allaah Anamsaidia mja huyu yu katika kumsaidia nduguye. Na mwenye kufuata njia akitafuta elimu katika njia hiyo, Allaah Atamsahilishia njia ya kwenda Jannah. Na  watu hawatakusanyika katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah (Ta’aalaa) wakisoma kitabu cha Allaah na wakifundishana isipokuwa huteremka utulivu, wakafunikwa na Malaika na Allaah Akawataja kwa walio Kwake. Na anayechelewesha na amali yake hatopelekwa mbele kwa nasaba yake.”  [Muslim na Ahmad].

 

 

Share

030-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Uombezi (shifaa)

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الشفاعة

030-Mlango Wa Uombezi (shifaa)

 

Alhidaaya.com

 

:قَالَ الله تَعَالَى

 

مَّن يَشْفَعْ شَفَاعَةً حَسَنَةً يَكُن لَّهُ نَصِيبٌ مِّنْهَا ۖ وَمَن يَشْفَعْ شَفَاعَةً سَيِّئَةً يَكُن لَّهُ كِفْلٌ مِّنْهَا ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقِيتًا ﴿٨٥﴾

Atakayeombea uombezi mzuri atapata fungu lake katika hayo. Na atakayeombea uombezi mbaya atapata sehemu yake katika hayo. Na Allaah daima ni Mwenye kudhibiti na Mwangalizi wa kila kitu. [An-Nisaa: 85]  

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه، قَالَ: كَانَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم إِذَا أتاهُ طَالِبُ حَاجَةٍ أقبَلَ عَلَى جُلَسَائِهِ ، فَقَالَ : (( اشْفَعُوا تُؤْجَرُوا ، وَيَقْضِي الله عَلَى لِسَانِ نَبِيِّهِ مَاأحبَّ)) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : (( مَا شَاءَ )) .

 

Na imepokewa kutoka kwake Abuu Muwsaa Al Ash'aariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa anajiliwa na mwenye haja, huwaelekea walioketi naye akiwaambia: " Ombeni mtalipwa, na Allaah Hukidhi (haja) kwa ulimi wa Rasuli Wake Anavyopenda." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na katika riwaayah nyingine: " Anavyotaka".

 

 

Hadiyth – 2

 

وعن ابن عباس رضي الله عنهما في قِصَّةِ برِيرَةَ وَزَوْجِهَا ، قَالَ : قَالَ لَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( لَوْ رَاجَعْتِهِ ؟ )) قَالَتْ : يَا رَسُولَ اللهِ تَأمُرُنِي ؟ قَالَ : (( إنَّمَا    أَشْفَع )) قَالَتْ : لاَ حَاجَةَ لِي فِيهِ . رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) Kuhusianana kisa cha Bariyrah na mumewe, Akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Waonaje lau ungerudi kwake?" Akasema (Bariyrah): " Ee Rasuli wa Allaah! Unaniamuru?" Akamjibu: "Hakika mimi naombea." Akasema (Bariyrah): "Sina haja naye." [Al-Bukhaariy]

 

 

Share

031-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kusuluhisha Baini Ya Watu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الإصلاح بَيْنَ الناس

031-Mlango Wa Kusuluhisha Baini Ya Watu

 

Alhidaaya.com

 

:قَالَ الله تَعَالَى

 

وَإِنِ امْرَأَةٌ خَافَتْ مِن بَعْلِهَا نُشُوزًا أَوْ إِعْرَاضًا فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا أَن يُصْلِحَا بَيْنَهُمَا صُلْحًا ۚ وَالصُّلْحُ خَيْرٌ ۗ وَأُحْضِرَتِ الْأَنفُسُ الشُّحَّ ۚ وَإِن تُحْسِنُوا وَتَتَّقُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا ﴿١٢٨﴾

Na ikiwa mke atakhofia kutoka kwa mumewe uonevu wa ndoa au kutengwa, basi si vibaya juu yake wakisikilizana baina yao kwa suluhu Na suluhu ni bora. Na nafsi zimewekewa uchoyo. Na mkifanya ihsaan na mkawa na taqwa, basi hakika Allaah kwa yale myatendayo ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika[An-Nisaa 128]

 

 

لَّ خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿١١٤﴾

Hakuna khayr katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha swadaqah, au mema, au kusuluhisha baina ya watu. Na atakayefanya hivyo kutaka radhi za Allaah, basi Tutampa ujira adhimu. [An-Nisaa: 114]

 

 

يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْأَنفَالِ ۖ قُلِ الْأَنفَالُ لِلَّـهِ وَالرَّسُولِ ۖ فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَصْلِحُوا ذَاتَ بَيْنِكُمْ ۖ وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَرَسُولَهُ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ﴿١﴾

Wanakuuliza (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu ngawira; sema: Ngawira ni ya Allaah na Rasuli. Basi mcheni Allaah na tengenezeni yaliyo baina yenu. Na mtiini Allaah na Rasuli Wake mkiwa ni Waumini. [Al-Anfaal:1]

 

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠﴾

Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa. [Al-Hujuraat:10]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( كُلُّ سُلاَمَى مِنَ النَّاسِ عَلَيهِ صَدَقَةٌ ، كُلَّ يَوْمٍ تَطْلُعُ فِيهِ الشَّمْسُ : تَعْدِلُ بَيْنَ الاثْنَينِ صَدَقَةٌ ، وَتُعينُ الرَّجُلَ في دَابَّتِهِ فَتَحْمِلُهُ عَلَيْهَا، أَوْ تَرْفَعُ لَهُ عَلَيْهَا مَتَاعَهُ صَدَقَةٌ ، وَالكَلِمَةُ الطَّيِّبَةُ صَدَقةٌ ، وَبِكُلِّ خَطْوَةٍ تَمشِيهَا إِلَى الصَّلاةِ صَدَقَةٌ ، وَتُميطُ الأَذى عَنِ الطَّريقِ صَدَقَةٌ )). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila kiungo cha mwanadamu kinafanya sadaka kila siku linapochomoza jua: Kusuluhisha kwa uadilifu baina ya watu wawili ni sadaka, kumsaidia mtu juu ya mnyama wake ukampandisha au ukamnyanyulia mzigo wake ni sadaka, kusema neno jema/zuri ni sadaka, kila hatua unayopiga kwenda kwenye Swalaah ni sadaka na kuondoa taka (uchafu) njiani ni sadaka. [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 2

وعن أمِّ كُلْثُوم بنت عُقْبَة بن أَبي مُعَيط رضي الله عنها ، قَالَتْ : سمِعتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يَقُولُ : (( لَيْسَ الكَذَّابُ الَّذِي يُصْلِحُ بَيْنَ النَّاسِ فَيَنْمِي خَيراً ، أَوْ يقُولُ خَيْراً )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ. وفي رواية مسلم زيادة ، قَالَتْ : "وَلَمْ أسْمَعْهُ يُرْخِّصُ في شَيْءٍ مِمَّا يَقُولُهُ النَّاسُ إلاَّ في ثَلاثٍ ، تَعْنِي : الحَرْبَ ، وَالإِصْلاَحَ بَيْنَ النَّاسِ ، وَحَدِيثَ الرَّجُلِ امْرَأَتَهُ ، وَحَدِيثَ المَرْأةِ زَوْجَهَا".

Na imepokewa kutoka kwa Umm Kulthuum bint 'Uqbah bin Abuu Mu'aytw (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Si muongo yule anayesuluhisha baina ya watu akawa anasambaza habari za kheri, au anasema kheri." [Al-Bukhaariy na Muslim].

Na katika riwaayah ya Muslim ipo ziada inayosema: "Akasema: ' Wala sijamsikia akiruhusu chochote katika uwongo kwa wanayosema watu ila katika mambo matatu, yaani katika vita, kusuluhisha baina ya watu na mazungumzo ya mwaname kwa mkewe na mke kuzungumza na mumewe."

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قَالَتْ : سَمِعَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم صَوْتَ خُصُومٍ بِالبَابِ عَاليةً أصْوَاتُهُمَا ، وَإِذَا أحَدُهُمَا يَسْتَوْضِعُ الآخَر وَيَسْتَرْفِقُهُ في شَيءٍ ، وَهُوَ يَقُولُ : والله لا أفْعَلُ، فَخَرجَ عَلَيْهِمَا رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : (( أيْنَ المُتَأَلِّي عَلَى اللهِ لاَ يَفْعَلُ المَعْرُوفَ ؟ )) ، فَقَالَ : أَنَا يَارسولَ اللهِ ، فَلَهُ أيُّ ذلِكَ أحَبَّ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa na ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisikia sauti ya watu wakiteta mlangoni wakiwa wamenyanyua sauti zao. Mmoja wapo alikuwa akimwomba mwenziwe ampunguzie deni na adai kwa upole, na yule mwingine akisema:"Wa -Allaahi sikubali?" Akawatokea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: "NI yupi aliyeapa kwa Allaah kuwa hatafanya wema?" Akasema: "Ni mimi, Ee Rasuli wa Allaah, nimempa khiyari afanye analopenda. [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي العباس سهل بن سَعد الساعِدِيّ رضي الله عنه : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بَلَغَهُ أنَّ َني عَمرو بن عَوْفٍ كَانَ بَيْنَهُمْ شَرٌّ ، فَخَرَجَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يُصْلِحُ بَينَهُمْ في أُنَاس مَعَهُ ، فَحُبِسَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَحَانَتِ الصَّلاة ، فَجَاءَ بِلالٌ إِلَى أَبي بكر رضي الله عنهما ، فَقَالَ: يَا أَبا بَكْر ، إنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَدْ حُبِسَ وَحَانَتِ الصَّلاةُ فَهَلْ لَكَ أنْ تَؤُمَّ النَّاس ؟ قَالَ : نَعَمْ ، إنْ شِئْتَ ، فَأقَامَ بِلالٌ الصَّلاةَ ، وتَقَدَّمَ أَبُو بَكْرٍ فَكَبَّرَ وَكَبَّرَ النَّاسُ ، وَجَاءَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَمشي في الصُّفُوفِ حَتَّى قَامَ في الصَّفِّ ، فَأَخَذَ النَّاسُ في التَّصْفيقِ ، وَكَانَ أَبُو بكرٍ رضي الله عنه لا يَلْتَفِتُ في الصَّلاةِ ، فَلَمَّا أكْثَرَ النَّاسُ في التَّصْفيقِ الْتَفَتَ ، فإِذَا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، فَأَشَارَإِِلَيْه رسولُ الله صلى الله عليه وسلم فَرَفَعَ أَبُو بَكْر رضي الله عنه يَدَهُ فَحَمِدَ اللهَ ، وَرَجَعَ القَهْقَرَى وَرَاءهُ حَتَّى قَامَ في الصَّفِّ ، فَتَقَدَّمَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، فَصَلَّى للنَّاسِ ، فَلَمَّا فَرَغَ أقْبَلَ عَلَى النَّاسِ ، فَقَالَ : (( أيُّهَا النَّاسُ ، مَا لَكُمْ حِينَ نَابَكُمْ شَيْءٌ في الصَّلاةِ أخَذْتُمْ في التَّصفيق ؟! إِنَّمَا التَّصفيق للنِّساء . مَنْ نَابَهُ شَيْءٌ في صَلاتِهِ فَلْيَقُلْ : سُبْحَانَ الله ، فَإِنَّهُ لاَ يَسْمَعُهُ أحدٌ حِينَ يقُولُ : سُبْحَانَ الله ، إلاَّ الْتَفَتَ . يَا أَبا بَكْر : مَا مَنَعَكَ أنْ تُصَلِّي بالنَّاسِ حِينَ أشَرْتُ إلَيْكَ ؟ )) ، فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ : مَا كَانَ يَنْبَغي لابْنِ أَبي قُحَافَةَ أنْ يُصَلِّي بالنَّاسِ بَيْنَ يَدَيْ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Abil 'Abbaas Sahl bin Sa'ad As-Saa'idiyy (Radhwiya Allaahu 'Anhu) kuwa ilimfikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa kuna mzozano baina ya vikundi vya Bani 'Amru bin 'Awf. Akatoka Rasuli wa Allaah kwenda kuwasuluhisha pamoja na kundi la maswahaba wake. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akawa ni mwenye kuzuiliwa (baada ya hiyo sulhu kwa kualikwa karamu) na wakati wa swalaah ukafika akiwa katika hali hiyo. Bilaal alikuja kwa Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) akamwambia: " Ee Abuu Bakr, hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amezuiliwa na wakati wa swalaah umefika, utaswalisha watu?" Akasema: "Ndio ukitaka." Kwa hiyo, Bilaal akakimu swalaah, naye Abuu Bakr akajongea na kufunga swalaah, nao watu wakamfuata (kwa kupiga takbiyr ya kufungia swalaah) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuja akiwa anapita katika safu mpaka akasimama katika safu. Watu wakaanza kupiga makofi, Naye Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikuwa hana tabia ya kugeuka katika Swalaah yake. watu walipokithirisha kupiga makofi (Abuu Bakr) aligeuka na kumuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwashiria aendelee, Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) alinyanyua mikono na kumuhimidi Allaah, kisha akarudi kinyumenyume nyuma yake mpaka akasimama kwenye safu. Hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alijongea mbele na kuwaswalisha watu. Alipomaliza kuswalisha aliwaelekea watu, akasema: "Enyi watu! Mna nini nyinyi linapotendeka jambo mnaanza kupiga makofi? Hakika kupiga makofi ni kwa wanawake. Linapotendeka jambo katika Swalaah (nawe unataka kumkumbusha Imaam) basi aseme mmoja wenu: Subhaana Allaah( Ametakasika Allaah, yaani hana mapungufu yoyote yale). Hiyo ni kuwa hatasikia yeyote pindi unaposema: Subhaana Allaah ila atatizama. Ee Abuu bakr! Ni lipi liliokukataza kuwaswalisha watu nilipokuashiria?" Akasema Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Haifalii kwa mtoto wa Abuu Quwhaafah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwaswalisha watu mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

Share

032-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila Za Waislamu Wanyonge, Mafakiri Wasiojulikana

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل ضعفة المسلمين والفقراء والخاملين

032-Mlango Wa Fadhila Za Waislamu Wanyonge,Mafakiri Wasiojulikana

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاصْبِرْ نَفْسَكَ مَعَ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ وَلَا تَعْدُ عَيْنَاكَ عَنْهُمْ تُرِيدُ زِينَةَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَلَا تُطِعْ مَنْ أَغْفَلْنَا قَلْبَهُ عَن ذِكْرِنَا وَاتَّبَعَ هَوَاهُ وَكَانَ أَمْرُهُ فُرُطًا ﴿٢٨﴾

Na isubirishe nafsi yako pamoja na wale wanaomuomba Rabb wao asubuhi kabla jua kucha na jioni, wanataka Wajihi Wake. Na wala macho yako yasiwavuke kwa kutaka pambo la uhai wa dunia. Na wala usimtii Tuliyemghafilisha moyo wake na Ukumbusho Wetu akafuata hawaa zake, na jambo lake limekuwa la kuzidi kuvuka mipaka. [Al-Kahf: 28]

 

 

Hadiyth – 1

وعن حارثة بن وهْبٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، يقولُ :(( ألاَ أُخْبِرُكُمْ بِأهْلِ الجَنَّةِ ؟ كُلُّ ضَعِيف مُتَضَعَّف، لَوْ أقْسَمَ عَلَى اللهِ لأَبَرَّهُ ، أَلاَ أُخْبِرُكُمْ بِأهْلِ النَّارِ ؟ كُلُّ عُتُلٍّ جَوّاظٍ مُسْتَكْبِرٍ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .  

Imepokewa kutoka kwake Haarithah bin Wahb (Radhwiya Allaahu 'anhu) aliyesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: " Je, niwajulishe nyinyi watu wa peponi? Kila mnyonge na mwenye kunyongeshwa, lau atakula yamini kwa Allaah basi atakubaliwa. Je, niwapashe habari ya watu wa motoni? Kila msusuwavu, mgumu na mwenye kiburi katika kutembea kwake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي عباس سهل بن سعد الساعِدِيِّ رضي الله عنه، قَالَ : مَرَّ رَجُلٌ عَلَى النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ لرَجُلٍ عِنْدَهُ جَالِسٌ : (( مَا رَأيُكَ في هَذَا ؟ )) ، فَقَالَ : رَجُلٌ مِنْ أشْرَافِ النَّاسِ ، هَذَا واللهِ حَرِيٌّ إنْ خَطَبَ أنْ يُنْكَحَ ، وَإنْ شَفَعَ أنْ يُشَفَّعَ . فَسَكَتَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم، ثُمَّ مَرَّ رَجُلٌ آخَرُ ، فَقَالَ لَهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: (( مَا رَأيُكَ في هَذَا ؟ )) فَقَالَ : يَا رَسُولَ الله ، هَذَا رَجُلٌ مِنْ فُقَراءِ المُسْلِمِينَ ، هَذَا حَرِيٌّ إنْ خَطَبَ أنْ لا يُنْكَحَ ، وَإنْ شَفَعَ أنْ لا يُشَفَّعَ ، وَإنْ قَالَ أنْ لاَ يُسْمَعَ لِقَولِهِ . فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( هَذَا خَيْرٌ مِنْ مِلءِ الأرْضِ مِثْلَ هَذَا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abil 'Abbaas Sahl bin Sa'ad As-Saa'idiyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mtu mmoja alipita mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye akamuuliza mtu aliyekuwa ameketi pamoja naye: "Ni Yepi maoni yako kuhusu mtu huyu?" Akasema: "Mtu huyu ni miongoni mwa watu watukufu. Wa-Allaahi, huyu anastahiki akienda kuposa aozeshwe na akiombea akubaliwe ombi lake. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akanyamaza, halafu akapita mtu mwingine, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza tena: "Ni Yepi maoni yako kuhusu mtu huyu?" Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Huyu mtu ni miongoni mwa mafakiri wa Waislamu, naye anafaa akienda kuposa asiozeshwe na akiombea asikubaliwe ombi lake na akizungumza asisikilizwe." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Huyu (fakiri) ni bora kuliko kuijaza ardhi na watu mfano wake (mtu wa kwanza). [Al-Bukhaariy na Muslim]

   

Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( احْتَجَّتِ الجَنَّةُ والنَّارُ ، فقالتِ النَّارُ : فِيَّ الجَبَّارُونَ وَالمُتَكَبِّرُونَ . وَقَالتِ الجَنَّةُ : فِيَّ ضُعَفَاءُ النَّاسِ وَمَسَاكِينُهُمْ ، فَقَضَى اللهُ بَيْنَهُمَا : إنَّكِ الجَنَّةُ رَحْمَتِي أرْحَمُ بِكِ مَنْ أشَاءُ ، وَإنَّكِ النَّارُ عَذَابِي أُعَذِّبُ بِكِ مَنْ أشَاءُ ، وَلِكلَيْكُمَا عَلَيَّ مِلْؤُهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pepo na Moto zilizozana. Moto ukasema: 'kwangu ni majabari na wenye kiburi'. Na ikasema Pepo: 'Kwangu ni wanyonge na maskini wao'. Allaah Akahukumu baina yao: "Hakika wewe pepo ni rehma Yangu, kwako Ninamrehemu Nimtakaye. Na hakika wewe Moto ni adhabu Yangu, kwako Ninamuadhibu nimtakaye, na nyote Nitawajaza." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إنَّهُ لَيَأتِي الرَّجُلُ السَّمِينُ العَظِيمُ يَوْمَ القِيَامَةِ لاَ يَزِنُ عِنْدَ اللهِ جَناحَ بَعُوضَةٍ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika atakuja mtu mkubwa na mnene siku ya Qiyaamah, hatakuwa na uzito mbele ya Allaah siku hiyo (japo uzito wa) ubawa wa mbu." [Al-Bukhaariy na Muslim]

   

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ امْرَأَةً سَوْدَاءَ كَانَتْ تَقُمُّ المَسْجِدَ ، أَوْ شَابّاً ، فَفَقَدَهَا ، أَوْ فَقَدَهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم، فَسَأَلَ عَنْهَا ، أو عنه ، فقالوا : مَاتَ . قَالَ : (( أَفَلا كُنْتُمْ آذَنْتُمُونِي )) فَكَأنَّهُمْ صَغَّرُوا أمْرَهَا ، أَوْ أمْرهُ ، فَقَالَ : (( دُلُّونِي عَلَى قَبْرِهِ )) فَدَلُّوهُ فَصَلَّى عَلَيْهَا ، ثُمَّ قَالَ : (( إنَّ هذِهِ القُبُورَ مَمْلُوءةٌ ظُلْمَةً عَلَى أهْلِهَا ، وَإنَّ اللهَ تعالى . يُنَوِّرُهَا لَهُمْ بِصَلاتِي عَلَيْهِمْ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Kutoka kwake Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa kulikuwa na mwanamke mweusi au kijana aliyekuwa akisafisha Msikiti. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamkosa, akamuulizia. Wakasema: "Amefariki." Akasema: "Kwanini hamukunieleza?" Hiyo ni kama kwamba jambo lake waliliona dogo. Akasema: "Nionyesheni kaburi yake." Wakamuonyesha, naye (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaswali hapo kaburini. Kisha akasema: "Hakika haya makaburi yamejaa kiza kwa watu wake na kuwa Allaah Aliyetukuka Anayatia mwangaza kwa mimi kuwaswalia." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( رُبَّ أشْعَثَ أغبرَ مَدْفُوعٍ بالأبْوابِ لَوْ أقْسَمَ عَلَى اللهِ لأَبَرَّهُ )) رواه مسلم .

Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Huenda mwenye nywele timtim, aliyejaa vumbi anayefukuzwa milangoni, lau atamuapia Allaah (amfanyie jambo lolote lile) Angemfanyia." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أسامة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( قُمْتُ عَلَى بَابِ الجَنَّةِ ، فَإِذَا عَامَّةُ مَنْ دَخَلَهَا المَسَاكِينُ ، وَأصْحَابُ الجَدِّ مَحْبُوسُونَ ، غَيْرَ أنَّ أصْحَابَ النَّارِ قَدْ أُمِرَ بِهِمْ إِلَى النَّارِ . وَقُمْتُ عَلَى بَابِ النَّارِ فَإِذَا عَامَّةُ مَنْ دَخَلَهَا النِّسَاءُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Usaamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "NIlisimama katika mlango wa Peponi, wengi waliokuwa wakiingia ni maskini, matajiri wamefungwa, ila watu wa Motoni wameamriwa motoni. Na nikasimama kwenye mlango wa Motoni; wengi waliokuwa wakiingia humo ni wanawake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَمْ يَتَكَلَّمْ في المَهْدِ إلاَّ ثَلاثَةٌ : عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ ، وَصَاحِبُ جُرَيْجٍ ، وَكَانَ جُرَيْجٌ رَجُلاً عَابِداً ، فَاتَّخَذَ صَوْمَعَةً فَكَانَ فِيهَا ، فَأَتَتْهُ أُمُّهُ وَهُوَ يُصَلِّي ، فَقَالَتْ : يَا جُرَيْجُ ، فَقَالَ : يَا رَبِّ أُمِّي وَصَلاتِي فَأَقْبَلَ عَلَى صَلاتِهِ فَانْصَرَفَتْ . فَلَمَّا كَانَ مِنَ الغَدِ أتَتْهُ وَهُوَ يُصَلِّي ، فَقَالَتْ : يَا جُرَيْجُ ، فَقَالَ : أيْ رَبِّ أمِّي وَصَلاتِي ، فَأقْبَلَ عَلَى صَلاتِهِ ، فَلَمَّا كَانَ مِنْ الغَدِ أتَتْهُ وَهُوَ يُصَلِّي ، فَقَالَتْ : يَا جُرَيْجُ ، فَقَالَ : أيْ رَبِّ أمِّي وَصَلاتِي ، فَأقْبَلَ عَلَى صَلاَتِهِ ، فَقَالَتْ : اللَّهُمَّ لاَ تُمِتْهُ حَتَّى يَنْظُرَ إِلَى وُجُوهِ المُومِسَاتِ . فَتَذَاكَرَ بَنُو إسْرائِيل جُرَيْجاً وَعِبَادَتَهُ ، وَكَانَتِ امْرَأةٌ بَغِيٌّ يُتَمَثَّلُ بحُسْنِهَا ، فَقَالَتْ : إنْ شِئْتُمْ لأَفْتِنَنَّهُ ، فَتَعَرَّضَتْ لَهُ ، فَلَمْ يَلْتَفِتْ إِلَيْهَا ، فَأتَتْ رَاعِياً كَانَ يَأوِي إِلَى صَوْمَعَتِهِ ، فَأَمْكَنَتْهُ مِنْ نَفْسِهَا فَوقَعَ عَلَيْهَا ، فَحَمَلَتْ ، فَلَمَّا وَلَدَتْ ، قَالَتْ : هُوَ مِنْ جُريج ، فَأتَوْهُ فَاسْتَنْزَلُوهُ وَهَدَمُوا صَوْمَعَتَهُ ، وَجَعَلُوا يَضْرِبُونَهُ ، فَقَالَ : مَا    شَأنُكُمْ ؟ قَالُوا : زَنَيْتَ بهذِهِ البَغِيِّ فَوَلَدَتْ مِنْكَ . قَالَ : أيْنَ الصَّبيُّ ؟ فَجَاؤُوا بِهِ فَقَالَ : دَعُوني حَتَّى أصَلِّي ، فَصَلَّى فَلَمَّا انْصَرفَ أتَى الصَّبيَّ فَطَعنَ في بَطْنِهِ ،  وَقالَ : يَا غُلامُ مَنْ أبُوكَ ؟ قَالَ : فُلانٌ الرَّاعِي ، فَأَقْبَلُوا عَلَى جُرَيْجٍ يُقَبِّلُونَهُ وَيَتَمَسَّحُونَ بِهِ ، وَقَالُوا : نَبْنِي لَكَ صَوْمَعَتَكَ مِنْ ذَهَب . قَالَ : لاَ ، أعِيدُوهَا مِنْ طِينٍ كَمَا كَانَتْ ، فَفَعلُوا . وبَينَا صَبِيٌّ يَرْضَعُ منْ أُمِّهِ فَمَرَّ رَجُلٌ رَاكِبٌ عَلَى دَابَّةٍ فَارِهَةٍ وَشَارَةٍ حَسَنَةٍ ، فَقَالَتْ أُمُّهُ : اللَّهُمَّ اجْعَل ابْنِي مِثْلَ هَذَا ، فَتَرَكَ الثَّدْيَ وَأقْبَلَ إِلَيْهِ فَنَظَرَ إِلَيْهِ ، فَقَالَ : اللَّهُمَّ لاَ تَجْعَلْنِي مِثْلَهُ ، ثُمَّ أقْبَلَ عَلَى ثَدْيه فَجَعَلَ يَرتَضِعُ )) ، فَكَأنِّي أنْظُرُ إِلَى رَسُول الله r وَهُوَ يَحْكِي ارْتضَاعَهُ بِأصْبَعِهِ السَّبَّابَةِ في فِيه ، فَجَعَلَ يَمُصُّهَا ، قَالَ : (( وَمَرُّوا بِجَارِيَةٍ وَهُم يَضْرِبُونَهَا ، ويَقُولُونَ : زَنَيْتِ سَرَقْتِ ، وَهِيَ تَقُولُ : حَسْبِيَ اللهُ ونِعْمَ الوَكِيلُ . فَقَالَتْ أمُّهُ : اللَّهُمَّ لاَ تَجْعَل ابْنِي مِثْلَهَا ، فَتَركَ الرَّضَاعَ ونَظَرَ إِلَيْهَا ، فَقَالَ : اللَّهُمَّ اجْعَلْنِي مثْلَهَا ، فَهُنَالِكَ تَرَاجَعَا الحَديثَ، فَقَالَتْ : مَرَّ رَجُلٌ حَسَنُ الهَيْئَةِ ، فَقُلْتُ : اللَّهُمَّ اجْعَلْ ابْنِي مِثْلَهُ ، فَقُلْتَ : اللَّهُمَّ لاَ تَجْعَلْنِي مِثْلَهُ ، وَمَرُّوا بهذِهِ الأمَةِ وَهُمْ يَضْرِبُونَهَا وَيَقُولُونَ : زَنَيْتِ سَرَقْتِ ، فقلتُ : اللَّهُمَّ لاَ تَجْعَلِ ابْنِي مِثْلَهَا ، فَقُلْتَ : اللَّهُمَّ اجْعَلْنِي    مِثْلَهَا ؟! قَالَ : إنَّ ذلك الرَّجُل كَانَ جَبَّاراً ، فَقُلْتُ : اللَّهُمَّ لا تَجْعَلْنِي مِثْلَهُ ، وَإنَّ هذِهِ يَقُولُونَ : زَنَيْتِ ، وَلَمْ تَزْنِ وَسَرقْتِ ، وَلَمْ تَسْرِقْ ، فَقُلْتُ : اللَّهُمَّ اجْعَلْنِي مِثْلَهَا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hawakuzungumza ulezini (uchangani) ila watatu: 'Iysa bin Maryam, Saahibu wa Jurayj. Jurayj alikuwa mtu mwenye kuabudu, naye akajenga kihekalumchake, akakaa humo, Alipokuja mamake akiwa anaswali Akamwuita: "Ee Jurayj." Akasema: "Ee Mola wangu! Mamangu na Swalaah yangu." Hivyo, akaendelea kuswali, basi akaondoka. Kesho yake alikuja akiwa anaswali. Akamuita: "Ee Jurayj." Akasema: "Ee Mola wangu! Mamangu na Swalaah yangu." Akaendelea kuswali, Akaondoka. Kesho yake akaja akiwa anaswali. Akamuita: "Ee Jurayj." Akasema: "Ee Mola wangu! Mamangu na Swalaah yangu." Akasema (mama): Ee Allaah, usimfishe mpaka aone nyuso za kahaba." Banu Israaiyli wakazungumza habari ya Jurayj na Ibada zake, Kulikuwa na mwanamke kahaba aliyepigiwa mfano kwa uzuri wake, akasema: "Mkitaka nitamfitini. Akamjia, hakumtazama. Akaja kwa mchungaji aliyekuwa akilala kwenye kihekalu chake, akammakinisha katika nafsi yake, akajamiiana naye. Akabeba mimba, Alipozaa, alisema: "Huyu ni mtoto wa Jurayj." Watu wakaja kwake, wakamteremsha na kuvunja kihekalu chake huku wanampiga. Akawauliza: "Mna nini nyinyi?" Wakasema: "Umezini na huyu malaya, naye kakuzalia mtoto." Akasema: "Mtoto yuko wapi?" Wakamleta akawaambia:"Niacheni ni swali." Akaswali,alipomaliza Swalaah yake akaja kwa mtoto na kumchua kwenye tumbo lake, akamuuliza:"Ee kijana! Nani baba yako?" Akasema: "Fulani mchungaji." Watu wakamkabili Jurayj kumbusu na kumwuomba msamaha. Wakasema: "Tunakujengea kihekalu chako kwa dhahabu." Akasema: "Hapana, irudisheni kama ilivyokuwa ya udongo." (Wa tatu); Mtoto akiwa ananyonya kwa mamake, akapita mtu mwenye kupanda mnyama, umbile na hali yake nzuri, na vazi lake zuri. Mamake akasema: "Ee Allaah , mjaalie mwnangu mfano wa huyu.: Mtoto akaacha kunyonya, akamtazama yule mtu, akasema: "Ee Allaah, usinijaalie kama huyu." Kisha akaelekea kwenye nyonyo na akaendelea kunyonya. Ni kana kwamba mimi namtazama Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiingiza kunyonya kwake (mtoto huyo) kwa kidole chake cha shahada mdomoni mwake. Akasema mara wakapita kwa kijakazi huku wanampiga,
wakisema: "Umezini, umeiba," naye anasema: "Allaah Ananitosha Naye ni Mbora wa kutegemewa." Mamake akasema: "Ee Allaah, usimjaalie mwanangu mfano wake." Akaacha kunyonya, akatazama, kisha akasema: "Ee Allaah , nijaalie mfano wake." Hapo mazungumzo yakajiri; Mama akasema: "Alipita mtu mwenye umbo zuri, nikasema: Ee Allaah, mjaalie mwanangu kama huyu, ukasema: 'Allaah usinifanye hivyo.' Akapita huyu kijakazi, nao wanampiga huku wakisema: Umezini, umeiba. Nikasema: 'Ee Allaah, usimjaalie mwanangu kama huyu.' Ukasema: 'Ee Allaah, nijaalie kama yeye.' Akasema mtoto: "Hakika yule mtu alikuwa jabari, hivyo nikasema: 'Ee Allaah usinijaalie kama yeye.' Na hakika huyu (kijakazi), wanamwambia: Umezidi, hajazini, Umeiba, hajaiba Nikasema: 'Ee Allaah, nijaalie kama yeye." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]
 
 
 
 

 

Share

033-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwafanyia Upole Mayatima, Mabinti, Wanyonge wote, Maskini, Waliofilisika Pamoja na Kuwafanyia Hisani, Kuwahurumia, Kuwanyenyekea na kuwainamishia Bawa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب ملاطفة اليتيم والبنات وسائر الضعفة والمساكين

والمنكسرين والإحسان إليهم والشفقة عليهم

والتواضع معهم وخفض الجناح لهم

033- Mlango Wa Kuwafanyia Upole Mayatima, Mabinti, Wanyonge wote, Maskini, Waliofilisika Pamoja na Kuwafanyia Hisani, Kuwahurumia, Kuwanyenyekea na kuwainamishia Bawa

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

لَا تَمُدَّنَّ عَيْنَيْكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعْنَا بِهِ أَزْوَاجًا مِّنْهُمْ وَلَا تَحْزَنْ عَلَيْهِمْ وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ﴿٨٨﴾

Usikodoe kabisa macho yako katika Tuliyowasterehesha makundi fulani miongoni mwao, na wala usihuzunike juu yao. Na inamisha bawa lako kwa Waumini (kuwahurumia). [Al-Hijr: 88]

 

وَاصْبِرْ نَفْسَكَ مَعَ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ وَلَا تَعْدُ عَيْنَاكَ عَنْهُمْ تُرِيدُ زِينَةَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَلَا تُطِعْ مَنْ أَغْفَلْنَا قَلْبَهُ عَن ذِكْرِنَا وَاتَّبَعَ هَوَاهُ وَكَانَ أَمْرُهُ فُرُطًا ﴿٢٨﴾

Na isubirishe nafsi yako pamoja na wale wanaomuomba Rabb wao asubuhi kabla jua kucha na jioni, wanataka Wajihi Wake. Na wala macho yako yasiwavuke kwa kutaka pambo la uhai wa dunia. Na wala usimtii Tuliyemghafilisha moyo wake na Ukumbusho Wetu akafuata hawaa zake, na jambo lake limekuwa la kuzidi kuvuka mipaka. [Al-Kahf: 28]

 

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ ﴿٩﴾ وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ ﴿١٠﴾ 

Kwa hivyo basi yatima usimuonee. Na mwombaji usimkaripie. [Adhw-Dhwuhaa: 9-10]

أَرَأَيْتَ الَّذِي يُكَذِّبُ بِالدِّينِ ﴿١﴾ فَذَٰلِكَ الَّذِي يَدُعُّ الْيَتِيمَ ﴿٢﴾ وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ﴿٣﴾

Je, umemuona yule anayekadhibisha malipo? Basi huyo ndiye anayemsukuma yatima. Na wala hahamasishi kulisha maskini. [Al-Maa'uwn: 1-3]

 

 

Hadiyth – 1

وعن سعد بن أَبي وَقَّاص رضي الله عنه، قَالَ : كُنَّا مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم سِتَّةَ نَفَرٍ ، فَقَالَ المُشْرِكُونَ للنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم: اطْرُدْ هؤلاء لا يَجْتَرِئُونَ عَلَيْنَا ، وَكُنْتُ أنَا وَابْنُ مَسْعُودٍ . وَرَجُلٌ مِنْ هُذَيْلٍ وَبِلالٌ وَرَجُلاَنِ لَسْتُ أُسَمِّيهِمَا ، فَوَقَعَ في نفس رَسُول الله صلى الله عليه وسلم مَا شَاءَ اللهُ أنْ يَقَعَ فَحَدَّثَ نَفسَهُ ، فَأنْزَلَ اللهُ تعالى : ( وَلا تَطْرُدِ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ) [ الأنعام : 52 ] رواه مسلم .

Amesema Sa'ad bin Abu Waqqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) Tulikuwa watu sita pamija na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na washirikina wakamwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Wafukuze hawa (watu sita) ili wasiwe na ujasiri wa kutukabili sisi." Watu sita hao walikuwa ni mimi, Ibn Mas'uud, mtu katika ukoo wa Hudhayl, Bilaal na watu wawili ambao sikuyajua majina yao. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akahisi alivyopenda Allaah ahisi, hivyo kuanza kuihadithia nafsi yake kuhusu hilo. Hapo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akateremsha: (Na wala usiwafukuze wale wanaomwomba Rabb wao asubuhi na jioni wanataka Wajihi Wake). [Al-An'aam:52]  Muslim

 

 

 Hadiyth – 2

وعن أَبي هُبَيرَة عائِذ بن عمرو المزنِي وَهُوَ مِنْ أهْل بيعة الرضوان رضي الله عنه: أنَّ أبا سُفْيَانَ أتَى عَلَى سَلْمَانَ وَصُهَيْبٍ وَبلاَلٍ في نَفَرٍ ، فقالوا : مَا أخَذَتْ سُيُوفُ اللهِ مِنْ عَدُوِّ الله مَأْخَذَهَا ، فَقَالَ أَبُو بَكْرٍرضي الله عنه: أتَقُولُون هَذَا لِشَيْخِ قُرَيْشٍ وَسَيدِهِمْ ؟ فَأتَى النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، فَأخْبَرهُ ، فَقَالَ : (( يَا أَبَا بَكْرٍ ، لَعلَّكَ أغْضَبتَهُمْ ؟ لَئِنْ كُنْتَ أغْضَبْتَهُمْ لَقَدْ أغْضَبتَ رَبَّكَ )) فَأَتَاهُمْ فَقَالَ : يَا إخْوَتَاهُ ، أغْضَبْتُكُمْ ؟ قالوا : لاَ ، يَغْفِرُ اللهُ لَكَ يَا أُخَيَّ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah 'Aa'idh bin 'Amr Al Muzaniy. katika maswahaba wa Bay'ah ya Ridhwaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Abu Sufyaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) alipita kwenye kikundi cha watu akiwemo Salman, Suhayb na Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu) wakasema: "Panga za Allaah hazijatekeleza haki yake kwa adui wa Allaah." Abu Bakr akasema: "Mnasema haya kwa mzee na bwana wa Maquraysh?" Wakaja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakampa habari. Akasema: "Ee Abu Bakr! Nimekuudhini? ikiwa umewaudhi umemkasirisha Mola wako." Akaenda kwao akawaambia: "Ndugu zangu, je nimewaudhi?" Wakasema: "Hapana, Ee ndugu yetu Allaah Akughufirie." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن سهل بن سعد رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أَنَا وَكَافلُ اليَتِيمِ في الجَنَّةِ هَكَذا )) وَأَشارَ بالسَّبَّابَةِ وَالوُسْطَى ، وَفَرَّجَ بَيْنَهُمَا . رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwa Sa'ad bin Sahl (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mimi na mwenye kumsimamia yatima tuko Peponi kama hivi." Akaashiria kwa kidole cha shahada na cha kati na kupambanua baina yake."  [Al-Bukhaariy]

 

 

 Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( كَافلُ اليَتيِم لَهُ أَوْ لِغَيْرِهِ أَنَا وَهُوَ كَهَاتَيْنِ في الجَنَّةِ )) وَأَشَارَ الرَّ‌اوِي وَهُوَ مَالِكُ بْنُ أنَس بالسَّبَّابَةِ وَالوُسْطَى . رواه مسلم .

Na imepokewa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mimi na mwenye kumsimamia yatima wake au mwengineo, mimi na yeye tutakuwa hivi Peponi." Maalik bin Anas ambaye ndie mpokezi akaashiria kwa kidole cha shahada na cha kati. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَيْسَ المِسْكينُ الَّذِي تَرُدُّهُ التَّمْرَةُ وَالتَّمْرَتَانِ ، وَلا اللُّقْمَةُ وَاللُّقْمَتَانِ إِنَّمَا المِسكِينُ الَّذِي يَتَعَفَّفُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية في الصحيحين : (( لَيْسَ المِسكِينُ الَّذِي يَطُوفُ عَلَى النَّاسِ تَرُدُّهُ اللُّقْمَةُ واللُّقْمَتانِ ، وَالتَّمْرَةُ والتَّمْرَتَانِ ، وَلَكِنَّ المِسْكِينَ الَّذِي لاَ يَجِدُ غنىً يُغْنِيه ، وَلاَ يُفْطَنُ بِهِ فَيُتَصَدَّقَ عَلَيهِ ، وَلاَ يَقُومُ فَيَسْأَلُ النَّاسَ )) .

Na imepokewa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si maskini mwenye kurudisha kwa ajili ya tende moja au mbili. hakika maskini ni yule anayeacha kuomba pamoja na ufakiri wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah iliyo katika Sahihi Mbili: "Sio maskini mwenye kuwazungukia watu akapewa tonge moja au mbili na tende moja au mbili lakini maskini ni yule asiyepata cha kumtosheleza wala hajulikani ili akapewa sadaka wala haombi."

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ: عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( السَّاعِي عَلَى الأَرْمَلَةِ وَالمِسْكِينِ ، كَالمُجَاهِدِ في سَبيلِ اللهِ )) وَأحسَبُهُ قَالَ : (( وَكالقَائِمِ الَّذِي لاَ يَفْتُرُ ، وَكَالصَّائِمِ الَّذِي لاَ يُفْطِرُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ . 

Na imepokewa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumsimamia mjane na maskini (kwa matumizi) ni kama Mujaahid katika Njia ya Allaah." Na nadhani alisema: "Na ni kama anayeswali usiku pasi na kupumzika na mafungaji asiyekula." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ: عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( شَرُّ الطَّعَامِ طَعَامُ الوَلِيمَةِ ، يُمْنَعُهَا مَنْ يَأتِيهَا ، وَيُدْعَى إِلَيْهَا مَنْ يَأْبَاهَا ، وَمَنْ لَمْ يُجِبِ الدَّعْوَةَ فَقَدْ عَصَى اللهَ وَرَسُولَهُ )) رواه مسلم .

وفي رواية في الصحيحين ، عن أَبي هريرة من قوله : (( بئْسَ الطَّعَامُ طَعَامُ الوَلِيمَةِ يُدْعَى إِلَيْهَا الأغْنِيَاءُ ويُتْرَكُ الفُقَراءُ )) .

Na imepokewa na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Chakula kibaya kabisa ni chakula cha walima, kinanyimwa anayekiendea na hualikwa anayekikataa. Na asiyejibu mwaliko basi amemuasi Allaah na Rasuli wake." [Muslim]

Katika riwaayah iliyo katika Sahihi Mbili: Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwa kauli yake chakula kibaya ni cha walima. wanaalikwa kwayo matajiri na kuachwa mafakiri."

 

 

Hadiyth – 8

وعن أنس رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَنْ عَالَ جَارِيَتَيْن حَتَّى تَبْلُغَا جَاءَ يَوْمَ القِيَامَةِ أنَا وَهُوَ كَهَاتَيْنِ )) وضَمَّ أصَابِعَهُ . رواه مسلم .

Na imepokewa na Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakaye wasimamia mabinti wawili mpaka akabaleghe, atakuja siku ya Qiyaamah mimi na yeye ni kama hivi." Akavishikanisha vidole vyake viwili. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

وعن عائشة رضي الله عنها ، قَالَتْ : دَخَلَتْ عَلَيَّ امْرَأةٌ وَمَعَهَا ابنتان لَهَا ، تَسْأَلُ فَلَمْ تَجِدْ عِنْدِي شَيئاً غَيْرَ تَمْرَةٍ وَاحدَةٍ ، فَأعْطَيْتُهَا إيَّاهَا فَقَسَمَتْهَا بَيْنَ ابْنَتَيْها ولَمْ تَأكُلْ مِنْهَا ، ثُمَّ قَامَتْ فَخَرجَتْ ، فَدَخَلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم عَلَينَا ، فَأخْبَرْتُهُ فَقَالَ : (( مَنِ ابْتُليَ مِنْ هذِهِ البَنَاتِ بِشَيءٍ فَأحْسَنَ إلَيْهِنَّ ، كُنَّ لَهُ سِتراً مِنَ النَّارِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Aa'ishah (Radhwiya Allaahu 'anha) amesema: "Aliingia kwangu mwanamke akiwa na binti zake wawili kuomba. sikuwa na chochote ila tende moja, ambayo nilimpatia, naye akaigawa mara mbili ili kuwapatia binti zake, naye hakula chochote. Kisha akasimama, akatoka. hapo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliingia, nami nikampasha habari kuhusu tukio hilo, akasema: "Mwenye kutahaniwa na mabinti hawa kwa chochote, naye akawafanyia ihsani, watakuwa ni kinga kwake na Moto." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

وعن عائشة رضي الله عنها ، قَالَتْ : جَاءتني مِسْكينةٌ تَحْمِلُ ابْنَتَيْنِ لَهَا ،  فَأطْعَمْتُها ثَلاثَ تَمرَات ، فَأعْطَتْ كُلَّ وَاحِدَة مِنْهُمَا تَمْرَةً وَرَفَعتْ إِلَى فِيها تَمْرَةً لِتَأكُلها ، فَاسْتَطعَمَتهَا ابْنَتَاهَا ، فَشَقَّتِ التَّمْرَةَ الَّتي كَانَتْ تُريدُ أنْ تَأكُلَهَا   بَيْنَهُما ، فَأعجَبَنِي شَأنُهَا ، فَذَكَرْتُ الَّذِي صَنَعَتْ لرسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : (( إنَّ الله قَدْ أوْجَبَ لَهَا بها الجَنَّةَ ، أَوْ أعتَقَهَا بِهَا مِنَ النَّارِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kwa 'Aa'ishah (Radhwiya Allaahu 'anha) amesema: "Maskini alikuja kwangu na mabinti wawili. Nikampa tende tatu, naye akampatia kila mmoja wao tende, akanyanyua moja mdomoni mwake ili aile. Mabinti zake wakaitaka, akagawa baina yao tende aliotaka kuila. Bikapendezwa na aliochofanya, nikamtajia jambo hilo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "hakika Allaah Amewajibisha kuingia kwake Peponi kwa kitendo hicho au kumwacha nacho na Moto." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي شُرَيحٍ خُوَيْلِدِ بن عمرو الخزاعِيِّ رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: (( اللَّهُمَّ إنِّي أُحَرِّجُ حَقَّ الضَّعِيفَينِ : اليَتِيم وَالمَرْأةِ )) حديث حسن رواه النسائي بإسناد جيد .

Imepokewa kutoka kwa Abu Shurayh Khuwaylid bin 'Ammr Al-Khuzaa'iyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee Allaah! Hakika nimemtangaza kuwa mwenye dhambi yeyote anayepoteza haki ya wanyonge wawili: Yatima na mwanamke." [Hadiyth hasan iliyonukuliwa na An-Nasaa'iy kwa isnad nzuri].

 

 

Hadiyth – 12

وعن مصعب بن سعد بن أَبي وقَّاص رضي الله عنهما ، قَالَ : رَأى سعد أنَّ لَهُ فَضْلاً عَلَى مَنْ دُونَهُ ، فَقَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: (( هَلْ تُنْصرُونَ وتُرْزَقُونَ إلاَّ بِضُعَفَائِكُمْ )) رواه البخاري هكذا مُرسلاً ، فإن مصعب بن سعد تابعيٌّ ، ورواه الحافظ أَبُو بكر البرقاني في صحيحه متصلاً عن مصعب ، عن أبيه رضي الله عنه.

Amesema Musw'ab bin Sa'ad bin waqqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Sa'ad aliona yeye ni mwenye fadhila kuliko wengine. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Hamnusuriwi na kuruzikiwa ila kwa wanyonge wenu." [Al-Bukhaariy ameipokea hivi Mursal, kwani Musw'ab bin sa'ad ni Taabi'iyy, na ameipokea Haafidh Abuu Bakr Al-Barqaaniy katika sahihi yake toka kwa Musw'ab kwa baba yake Radhwiya Allaahu 'anhu]

 

 

Hadiyth – 13

وعن أَبي الدَّرداءِ عُويمر رضي الله عنه، قَالَ : سمعتُ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم، يقول :  (( ابْغُوني الضُّعَفَاء ، فَإنَّمَا تُنْصَرُونَ وتُرْزَقُونَ ، بِضُعَفَائِكُمْ )) رواه أَبُو داود بإسناد جيد .

Kutoka kwake Abu Dardaa' 'Uwaymir Amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Nisaidieni (kwa kuwasaidia) wanyonge, hakika mnanusuriwa na kuruzukiwa kwa sababu ya wanyonge wenu." [Abuu Daawuud kwa Isnaad nzuri]

 

 

 

 

Share

034-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Wasia Kwa Wanawake

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الوصية بالنساء

034-Mlango Wa Wasia Kwa Wanawake

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ﴿١٩﴾

Na kaeni nao kwa wema. [An-Nisaa: 19]

 

وَلَن تَسْتَطِيعُوا أَن تَعْدِلُوا بَيْنَ النِّسَاءِ وَلَوْ حَرَصْتُمْ ۖ فَلَا تَمِيلُوا كُلَّ الْمَيْلِ فَتَذَرُوهَا كَالْمُعَلَّقَةِ ۚ وَإِن تُصْلِحُوا وَتَتَّقُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١٢٩﴾

Na wala hamtoweza kuadilisha baina ya wake japokuwa mkipania. Basi msimili muelemeo wote (kwa mke mmoja) mkamuacha (mwengine) kama kining’inio. Na mkisuluhisha na mkawa na taqwa, basi hakika Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa: 129]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( اسْتَوْصُوا بالنِّساءِ خَيْراً ؛ فَإِنَّ المَرْأَةَ خُلِقَتْ مِنْ ضِلعٍ ، وَإنَّ أعْوَجَ مَا في الضِّلَعِ أعْلاهُ ، فَإنْ ذَهَبتَ تُقيمُهُ كَسَرْتَهُ ، وَإنْ تَرَكْتَهُ ، لَمْ يَزَلْ أعْوجَ ، فَاسْتَوصُوا بالنِّساءِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية في الصحيحين : (( المَرأةُ كالضِّلَعِ إنْ أقَمْتَهَا كَسَرْتَهَا ، وَإن اسْتَمتَعْتَ بِهَا ، اسْتَمتَعْتَ وفِيهَا عوَجٌ )) .

وفي رواية لمسلم : (( إنَّ المَرأةَ خُلِقَت مِنْ ضِلَع ، لَنْ تَسْتَقِيمَ لَكَ عَلَى   طَريقة ، فإن اسْتَمْتَعْتَ بِهَا اسْتَمْتَعْتَ بِهَا وَفيهَا عوَجٌ ، وإنْ ذَهَبْتَ تُقِيمُهَا كَسَرْتَها ، وَكَسْرُهَا طَلاَقُهَا )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nawausieni kuwafanyia wema wanawake, kwani mwanamke ameumbwa kutokana na ubavu, na sehemu laini na yenye matatizo katika ubavu ni sehemu ya juu. Ukijaribu kuinyoosha, utaivunja; na ukiiacha, itabaki kombo. Nawausieni kuwatendea wema wanawake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah iliyo katika Sahihi Mbili: ((Mwanamke ni kama mbavu, ukuiunyoosha utauvunja. Na ukitaka kupata faida kwayo, itabidi upate faida na ujongo wake)).

Katika riwaayah ya Muslim: ((Hakika mwanamke ameumbwa kutokana na ubavu. Hakuna njia ya kuunyoosha. Ukitaka kupata faida kwayo, itabidi upate faida na ujongo wake. Na ukitaka kuunyoosha, utauvunja na kuuvunja kwako ni kumpatia talaka)).

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن زَمْعَةَ رضي الله عنه: أنَّهُ سَمِعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم يَخْطُبُ ، وَذَكَرَ النَّاقَةَ وَالَّذِي عَقَرَهَا ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إِذ انْبَعَثَ أشْقَاهَا انْبَعَثَ لَهَا رَجُلٌ عَزيزٌ ، عَارِمٌ مَنيعٌ في رَهْطِهِ )) ، ثُمَّ ذَكَرَ النِّسَاءَ ، فَوعَظَ فِيهنَّ ، فَقَالَ : (( يَعْمِدُ أحَدُكُمْ فَيَجْلِدُ امْرَأتَهُ جَلْدَ العَبْدِ فَلَعَلَّهُ يُضَاجِعُهَا مِنْ آخِرِ يَومِهِ )) ثُمَّ وَعَظَهُمْ في ضَحِكِهمْ مِنَ الضَّرْطَةِ ، وَقالَ : (( لِمَ يَضْحَكُ أَحَدُكُمْ مِمَّا يَفْعَلُ ؟! )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaahi bin Zam'ah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akihhutubu, akamtaja ngamia, na yule aliyemchinja. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Pale alipochomoka haraka muovu wao mkuu. [Ash-Shams: 12]. Alimrukia muovu wao mwenye nguvu, mfisadi, mwenye kinga ya watu wake (akamchinja)." Kisha akataja wanawake, akawa waadhi kuhusu wao, akasema: "Mmoja wenu anampiga mkewe kipigo cha mtumwa, na huenda mwisho wa siku akamwingilia." Kisha akawadhia juu ya kucheka kwao kwa sababu ya kutokwa na upepo, akasema: "kwa nini mmoja wenu anacheka analolifanya?" [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لاَ يَفْرَكْ مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَةً إنْ كَرِهَ مِنْهَا خُلُقاً رَضِيَ مِنْهَا آخَرَ )) ، أَوْ قَالَ : (( غَيْرَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini mwanamume asimchukie Muumini mwanamke. Akichukizwa na tabia yake moja, ataridhika naye kwa tabia nyengine."  [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن عمرو بن الأحوصِ الجُشَمي رضي الله عنه: أنَّهُ سَمِعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم في حَجَّةِ الوَدَاعِ يَقُولُ بَعْدَ أنْ حَمِدَ الله تَعَالَى ، وَأثْنَى عَلَيهِ وَذَكَّرَ وَوَعظَ ، ثُمَّ قَالَ : (( ألا وَاسْتَوصُوا بالنِّساءِ خَيْراً ، فَإِنَّمَا هُنَّ عَوَانٍ عِنْدَكُمْ لَيْسَ تَمْلِكُونَ مِنْهُنَّ شَيْئاً غَيْرَ ذلِكَ إلاَّ أنْ يَأتِينَ بِفَاحِشَةٍ مُبَيِّنَةٍ ، فَإنْ فَعَلْنَ فَاهْجُرُوهُنَّ في المَضَاجِع ، وَاضْرِبُوهُنَّ ضَرباً غَيْرَ مُبَرِّحٍ ، فإنْ أطَعْنَكُمْ فَلا تَبْغُوا عَلَيهنَّ سَبيلاً ؛ ألاَ إنَّ لَكُمْ عَلَى نِسَائِكُمْ حَقّاً ، وَلِنِسَائِكُمْ عَلَيْكُمْ حَقّاً ؛ فَحَقُّكُمْ عَلَيهِنَّ أنْ لا يُوطِئْنَ فُرُشَكُمْ مَنْ تَكْرَهُونَ ، وَلا يَأْذَنَّ في بُيُوتِكُمْ لِمَنْ تَكْرَهُونَ ؛ ألاَ وَحَقُّهُنَّ عَلَيْكُمْ أنْ تُحْسِنُوا إِلَيْهِنَّ في كِسْوَتِهنَّ وَطَعَامِهنَّ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Na 'Ammr bin Al-Ahwasw Al- Jushamiyy' (Radhwiya Allaahu 'anhu) amemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema katiak Hajjatil Wadaa' baada ya kumhimidi na kumsifu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), akakumbusha na kuwaidhinkisha akasema: "Jueni! nawausieni kuwatendea wema wanawake, kwani wao ni wasaidizi wenu, hamna mnachomiliki kwao isipokuwa hicho kustarehe nao isipokuwa wanapotenda uovu wa wazi. Wakifanya hivyo wahameni katika malazi, na wapigeni pigo lisiloumiza. Wakiwatii msiwatafutie njia (ya kuwaudhi). Jueni! Hakika nyinyi mna haki juu ya wake zenu, na wake zenu wana haki juu yenu. Haki yenu juu yao ni kutomruhusu mnayemchukia kulala katika vitanda vyenu, wala wasiwaruhusu kuingia majumbani mwenu mnayemchukia. Fahamuni! Na haki zao juu yenu ni kuwafanyia hisani katika mavazi na chakula chao." [At- Tirmidhiy, na akasema: Hadiyth Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 5

وعن معاوية بن حيدة رضي الله عنه، قَالَ : قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، مَا حق زَوجَةِ أَحَدِنَا عَلَيهِ ؟ قَالَ : (( أنْ تُطْعِمَهَا إِذَا طعِمْتَ ، وَتَكْسُوهَا إِذَا اكْتَسَيْتَ ، وَلاَ تَضْرِبِ الوَجْهَ ، وَلا تُقَبِّحْ ، وَلا تَهْجُرْ إلاَّ في البَيْتِ )) حديثٌ حسنٌ رواه أَبُو داود.

imepokewa kutoka kwake Mu'aawiyyah bin Haydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni ipi haki ya mke wa mmoja wetu kwa mumewe?" Akajibu: "Ni kumlisha anapokula, kumvisha anapovaa wala usimpige uso wala usimkaripie wala usimhame ila nyumbani tu." [ Hadiyth Hasan iliyonukuliwa na Abu Daawuud]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أكْمَلُ المُؤمِنِينَ إيمَاناً أحْسَنُهُمْ خُلُقاً ، وخِيَارُكُمْ خياركم لِنِسَائِهِمْ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) . 

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini mkamilifu wa Iymaani ni mzuri wa tabia, na wabora wenu ni wabora wenu kwa wake zao." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hahiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 7

وعن إياس بن عبد الله بن أَبي ذباب رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لاَ تَضْرِبُوا إمَاء الله )) فجاء عُمَرُ رضي الله عنه إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ :ذَئِرْنَ النِّسَاءُ عَلَى أزْوَاجِهِنَّ ، فَرَخَّصَ في ضَرْبِهِنَّ ، فَأطَافَ بآلِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم نِسَاءٌ كَثيرٌ يَشْكُونَ أزْواجَهُنَّ ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَقَدْ أطَافَ بِآلِ بَيتِ مُحَمَّدٍ نِسَاءٌ كثيرٌ يَشْكُونَ أزْوَاجَهُنَّ لَيْسَ أولَئكَ بخيَارِكُمْ )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .

Na imepokewa kutoka kwake Iyaas bin 'Abdillaah bin Abu Dhubaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiwapige wajakazi (wanawake) wa Allaah." Akaja 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Wanawake wamekuwa majasiri juu ya waume zao." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaruhusu wawachape wake zao. Wanawake wakawazungukia wakeze Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakishtaki kupigwa na waume zao. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Hakika wanawake wengi wamezunguka katika nyumba za Muhammad (wakeze) wakiwashtakia waume zao, waume hao si bora miongoni mwenu." [Abu Daawuud kwa Isnaad Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 8

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( الدُّنْيَا مَتَاعٌ ، وَخَيرُ مَتَاعِهَا المَرْأَةُ الصَّالِحَةُ )) رواه مسلم .

'Abdillaah bin 'Ammr bin Al- 'Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: " Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Dunia ni starehe, na bora ya starehe ni mke mwema." [Muslim]

 

 

 

 

 

Share

035-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Haki Ya Mume Juu Ya Mke

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب حق الزوج عَلَى المرأة

035-Mlango Wa Haki Ya Mume Juu Ya Mke

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّـهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَبِمَا أَنفَقُوا مِنْ أَمْوَالِهِمْ ۚ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ﴿٣٤﴾

Wanaume ni wasimamizi juu ya wanawake kwa kuwa Allaah Amefadhilisha baadhi yao kuliko wengine na pia kwa ambayo wanatoa katika mali zao. Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi. [An-Nisaa: 34]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إِذَا دَعَا الرَّجُلُ امرَأتَهُ إِلَى فرَاشِهِ فَلَمْ تَأتِهِ ، فَبَاتَ غَضْبَانَ عَلَيْهَا ، لَعَنَتْهَا المَلائِكَةُ حَتَّى تُصْبحَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية لهما : (( إِذَا بَاتَت المَرأةُ هَاجِرَةً فِرَاشَ زَوْجِهَا لَعَنَتْهَا المَلاَئِكَةُ حَتَّى تُصْبحَ )) .

وفي رواية قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( والَّذِي نَفْسِي بيَدِهِ مَا مِنْ رَجُلٍ يَدْعُو امْرَأتَهُ إِلَى فِرَاشهِ فَتَأبَى عَلَيهِ إلاَّ كَانَ الَّذِي في السَّمَاء سَاخطاً عَلَيْهَا حَتَّى يَرْضَى عَنها )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mume anapomuita mkewe kitandani mwake wala asije, akalala akiwa amemkasirikia mkewe, Malaaikah watamlaani mke huyo mpaka apambazukiwe." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na katika riwaayah yao wawili: "Mke anapolala kwa kuhama kitanda cha mumewe, Malaaikah humlani mpaka kupambazuke."

Katika riwaayah: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hakuna mwanamume yoyote anamuita mkewe kitandani, akamkatalia isipokuwa Aliye mbinguni Humkasirikia mpaka mume Amridhie."

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه أيضاً : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لاَ يَحِلُّ لامْرَأةٍ أنْ تَصُومَ وزَوْجُهَا شَاهدٌ إلاَّ بإذْنِهِ ، وَلاَ تَأذَنَ في بَيْتِهِ إلاَّ بِإذنِهِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ وهذا لفظ البخاري .

Imepokewa kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa mke kufunga na mumewe yuko (mjini) ila kwa idhini yake. Wala siruhusa (kwa mke) kumruhusu mtu kuingia nyumbani (kwao) ila kwa idhini ya mumewe." [Al-Bukhaariy na Muslim] Na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن عمر رضي الله عنهما، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( كلكم رَاعٍ ، وَكُلُّكُمْ مَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ : وَالأمِيرُ رَاعٍ ، والرَّجُلُ رَاعٍ عَلَى أهْلِ بَيتِهِ ، وَالمَرْأةُ رَاعِيةٌ عَلَى بَيْتِ زَوْجها وَوَلَدهِ ، فَكُلُّكُمْ رَاعٍ ، وَكُلُّكُمْ مَسْؤُولٌ عَنْ  رَعِيَّتِهِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ 

Imepokewa kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila mmoja wenu ni mchunga, na kila mmoja wenu ataulizwa alio wachunga. Amiri ni mchunga, na mume ni mchunga wa watu wa nyumbani kwake, na mke ni mchunga katika nyumba ya mumewe na watoto wake; nyote ni wachunga mtaulizwa mlivyovichunga." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي علي طَلْق بن علي رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا دَعَا الرَّجُلُ زَوْجَتهُ لحَاجَتِهِ فَلْتَأتِهِ وَإنْ كَانَتْ عَلَى التَّنُور)) . رواه الترمذي والنسائي ، وَقالَ الترمذي : (( حديث حسن صحيح )) .

Na imepokewa kutoka kwake Abuu 'Aliy Twalqbin 'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pindi mume anapomuita mkewe kwa haja zake (jimai) aje kwake mara moja hata akiwa kwenye tanuri." [At-Tirmidhiy na An-Nasaa'iy, na akasema At-Tirmidhiy kuwa ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَوْ كُنْتُ آمِراً أحَداً أنْ يَسْجُدَ لأحَدٍ لأمَرْتُ المَرأةَ أنْ تَسْجُدَ لزَوجِهَا )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau ningemuamuru mke kumsujudia mumewe." [At-Tirmidhiy na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أم سَلَمَة رضي الله عنها ، قَالَتْ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: (( أيُّمَا امْرَأةٍ مَاتَتْ ، وَزَوْجُهَا عَنْهَا رَاضٍ دَخَلَتِ الجَنَّةَ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Umm Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwanamke aliyekufa na mumewe yu radhi naye, ataingia Peponi." [At-Tirmidhiy na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 7

وعن معاذ بن جبل رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لاَ تُؤْذِي امْرَأةٌ زَوْجَهَا في الدُّنْيَا إلاَّ قَالَتْ زَوْجَتُهُ مِنَ الحُورِ العِينِ لاَ تُؤذِيهِ قَاتَلكِ اللهُ ‍! فَإِنَّمَا هُوَ عِنْدَكِ دَخِيلٌ يُوشِكُ أنْ يُفَارِقَكِ إِلَيْنَا )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa Mu'aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu 'anhu) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwanamke hamuudhi mumewe duniani ila anasema mkewe katika Huuril 'Iyn watamwambia, 'Usimuudhi, Allaah Akulaani! Hakika yeye ni mgeni aliye kwako na karibuni atakuacha na kuungana nasi." [At-Tirmidhiy na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أسامة بن زيد رضي الله عنهما ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَا تَرَكْتُ بَعْدِي فِتْنَةً هِيَ أضَرُّ عَلَى الرِّجَالِ مِنَ النِّساء )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Usaamah bin Zayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Sijaacha baada yangu fitna iliyo na madhara makubwa kwa wanaume kuliko ile ya wanawake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

036-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa kuilisha Familia

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب النفقة عَلَى العيال

036-Mlango Wa kuilisha Familia

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَعَلَى الْمَوْلُودِ لَهُ رِزْقُهُنَّ وَكِسْوَتُهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ﴿٢٣٣﴾

Na ni juu ya mzazi wa kiume kuwapatia chakula chao na nguo kwa mujibu wa ada. [Al-Baqarah: 233]

لِيُنفِقْ ذُو سَعَةٍ مِّن سَعَتِهِ ۖ وَمَن قُدِرَ عَلَيْهِ رِزْقُهُ فَلْيُنفِقْ مِمَّا آتَاهُ اللَّـهُ ۚ لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا مَا آتَاهَا ﴿٧﴾

Ili mwenye wasaa agharimu kwa wasaa wake, na aliyebaniwa riziki yake, basi agharimie katika kile Alichompa Allaah. Allaah Haikalifishi nafsi yeyote ile isipokuwa kwa kile Alichoipa. [Atw-Twalaaq: 7]

وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ﴿٣٩﴾

Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa [Sabaa: 39]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( دِينَارٌ أنْفَقْتَهُ في سَبيلِ اللهِ ، وَدِينار أنْفَقْتَهُ في رَقَبَةٍ ، وَدِينارٌ تَصَدَّقْتَ بِهِ عَلَى مِسْكِينٍ ، وَدِينَارٌ أنْفَقْتَهُ عَلَى أهْلِكَ ، أعْظَمُهَا أجْراً الَّذِي أنْفَقْتَهُ عَلَى أهْلِكَ )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Dinari unayotumia katika Njia ya Allaah (jihaad), na Dinari unayotumia kumwacha huru mtumwa, na Dinari unayoitoa sadaka kwa maskini, na Dinari unayotumia kwa familia yako, yenye ujira mkubwa zaidi ni ile unayotumia kwa familia yako." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي عبد الله ، ويُقالُ لَهُ : أَبو عبد الرحمان ثَوبَان بن بُجْدُد مَوْلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أفْضَلُ دِينَارٍ يُنْفقُهُ الرَّجُلُ : دِينَارٌ يُنْفِقُهُ عَلَى عِيَالِهِ ، وَدينَارٌ يُنْفقُهُ عَلَى دَابَّتِهِ في سَبيلِ الله ، وَدِينارٌ يُنْفقُهُ عَلَى أصْحَابهِ في سَبيلِ اللهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu 'Abdillaahi-pia anajulikana kama Abu 'Abdur-Rahman - Thawbaan bin Bujdud, mtumishi wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Dinari iliyo bora zaidi inayotumiwa na mtu ni ile anayotumia kwa familia yake, na Dinari anayoitumia kwa mnyama katika Njia ya Allaah, na kisha Dinari anayoitumia kwa sahibu zake katika Njia ya Allaah." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أمِّ سَلمَة رَضي الله عنها ، قَالَتْ : قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، هَلْ لِي أجرٌ فِي بَنِي أَبي سَلَمَة أنْ أُنْفِقَ عَلَيْهِمْ ، وَلَسْتُ بِتَارِكتهمْ هكَذَا وَهكَذَا إنَّمَا هُمْ   بَنِيّ ؟ فَقَالَ : (( نَعَمْ ، لَكِ أجْرُ مَا أنْفَقْتِ عَلَيْهِمْ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Amesema Umm Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je, nitakuwa na ujira nitakapotumia kwa ajili ya watoto wa Abi Salamah, ilhali mimi siwezi kuwaacha wakitangatanga huku na kule ambapo wao ni watoto wangu." Akasema: "Ndio, utapata ujira kwa unachotumia kwao." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن سعد بن أَبي وقاص رضي الله عنه في حديثه الطويل الَّذِي قدمناه في أول الكتاب في باب النِّيَةِ : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ لَهُ : (( وإنَّكَ لَنْ تُنْفِقَ نَفَقَةً تَبْتَغِي بِهَا وَجْهَ اللهِ إلاَّ أُجِرْتَ بِهَا حَتَّى مَا تَجْعَلُ في فيِّ امرأتِك )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ . 

Na imepokewa kutoka kwa Sa'ad bin Abu Waqqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) katika hadiyth ndefu tuliyo itanguliza mwanzo wa kitabu hiki katika mlango wa Nia kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Na hakika wewe hutatumia pesa kutaka radhi za Allaah isipokuwa utapata ujira kwayo mpaka utakacho jaalia katika mdomo wa mkeo (kumlisha) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي مسعود البدري رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا أنْفَقَ الرَّجُلُ عَلَى أَهْلِهِ نَفَقَةً يَحْتَسِبُهَا فَهِيَ لَهُ صَدَقَةٌ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ . 

Na imepokewa kutoka kwa Abu Mas'uud Al-Badriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu akiipa familia yake matumizi akiyatarajia thawabu basi hiyo ni sadaqa yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( كَفَى بِالمَرْءِ إثْمَاً أنْ يُضَيِّعَ مَنْ يَقُوتُ )) حديث صحيح رواه أَبُو داود وغيره .

ورواه مسلم في صحيحه بمعناه ، قَالَ : (( كَفَى بِالمَرْءِ إثْمَاً أنْ يحْبِسَ عَمَّنْ يَمْلِكُ قُوتَهُ )) .

Na imepokewa kutoka kwa 'Abdillaahi bin 'Amr bin al-'Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Inatosha mtu kuwa na dhambi kwa kumtupa anyemlisha." Hadiyth Swahiyh [ Abu Daawuud na wengineo]

Muslim ameinukuu katika Sahihi yake kwa maana yake: "Yatosha kwa mtu kuwa na dhambi kwa kumzuilia rizki anayemtegemea."

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَا مِنْ يَوْمٍ يُصْبِحُ العِبَادُ فِيهِ إلاَّ مَلَكانِ يَنْزلاَنِ ، فَيقُولُ أحَدُهُمَا : اللَّهُمَّ أعْطِ مُنْفقاً خَلَفاً ، وَيَقُولُ الآخَرُ : اللَّهُمَّ أعْطِ مُمْسِكاً تلَفاً ))  مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna siku yoyote waja wanapambazuka ndani yake, ila Malaika wawili wanateremka, mmoja wao anasema: 'Ee Allaah, mpe badali mwenye kutoa.' Na mwengine anasema: 'Ee Allaah, mpe hasara mwenye kuzuia' " [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( اليَدُ العُلْيَا خَيْرٌ مِنَ اليَدِ السُّفْلَى ، وَابْدَأ بِمَنْ تَعُولُ ، وَخَيْرُ الصَّدَقَةِ مَا كَانَ عَنْ ظَهْرِ غِنىً ، وَمَنْ يَسْتَعْفِفْ يُعِفَّهُ اللهُ ، وَمَنْ يَسْتَغْنِ يُغْنِهِ اللهُ )) رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwake Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini. Anza kwa unayemlisha. Sadaka bora inakuwa kwa mwenye kujitosha. Anayejizuia Allaah Humtosheleza, na mwenye kukinai, Allaah Humkinaisha." [Al-Bukhaariy]

 

 

Share

037-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kutoa Ukipendacho Katika Vizuri

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الإنفاق مِمَّا يحبُّ ومن الجيِّد

037-Mlango Wa Kutoa Ukipendacho Katika Vizuri

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ﴿٩٢﴾

Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda. [Al-'Imraan: 92]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ وَمِمَّا أَخْرَجْنَا لَكُم مِّنَ الْأَرْضِ ۖ وَلَا تَيَمَّمُوا الْخَبِيثَ مِنْهُ تُنفِقُونَ ﴿٢٦٧﴾

Enyi walioamini! Toeni katika vizuri mlivyochuma na katika ambavyo Tumekutoleeni kutoka katika ardhi. Na wala msikusudie vibaya kutoka humo mkavitoa. [Al-Baqarah: 267]

 

 

Hadiyth – 1

عن أنس رضي الله عنه، قَالَ : كَانَ أَبُو طَلْحَةَ رضي الله عنه أكْثَرَ الأنْصَار بالمَدِينَةِ مَالاً مِنْ نَخْل ، وَكَانَ أَحَبُّ أمْوالِهِ إِلَيْه بَيْرَحَاء ، وَكَانتْ مُسْتَقْبلَةَ المَسْجِدِ وَكَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم  يَدْخُلُهَا وَيَشْرَبُ مِنْ مَاءٍ فِيهَا طَيِّب . قَالَ أنَسٌ : فَلَمَّا نَزَلَتْ هذِهِ الآيةُ: ( لَنْ تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّى تُنْفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ) قام أَبُو طَلْحَةَ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : يَا رَسُول الله ، إنَّ الله تَعَالَى أنْزَلَ عَلَيْكَ : ( لَنْ تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّى تُنْفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ) وَإنَّ أَحَبَّ مَالِي إِلَيَّ بَيْرَحَاءُ ، وَإنَّهَا صَدَقَةٌ للهِ تَعَالَى ، أرْجُو بِرَّهَا ، وَذُخْرَهَا عِنْدَ الله تَعَالَى ، فَضَعْهَا يَا رَسُول الله حَيْثُ أرَاكَ الله ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( بَخ! ذلِكَ مَالٌ رَابحٌ ، ذلِكَ مَالٌ رَابحٌ ، وقَدْ سَمِعْتُ مَا قُلْتَ ، وَإنِّي أرَى أنْ تَجْعَلَهَا في الأقْرَبينَ )) ، فَقَالَ أَبُو طَلْحَةَ : أفْعَلُ يَا رَسُول الله ، فَقَسَّمَهَا أَبُو طَلْحَةَ في أقَارِبِهِ ، وبَنِي عَمِّهِ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Amesema Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): 'Abu Twalhah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikuwa na mali na mitende mingi kuliko Answari wote. Mali iliyompendeza zaidi ni shamba lilioko Bayrahaa', limeelekeana na Msikiti wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiingia humo na kunywa maji yake matamu. Amesema Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): Ilipoteremka aya hii: "Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda." Abu Twalhah Radhwiya Allaahu 'anhu) alimwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amekuteremshia: "Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda." Hakika mali niipendayo sana ni shamba la Bayrahaa', nimelitoa sadaka kwa ajili ya Allaah nataraji kheri na ujira kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Ee Rasulu wa Allaah, liweke atakapokuonyesha Allaah." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Bakh! Hiyo ni mali yenye faida, hiyo ni mali yenye faida. Nimesikia uliyosema. Mimi naona uwape jamaa zako wa karibu." Abu Twalhah akasema: "Nitafanya, Ee Rasuli wa Allaah!" Abu Twalhah akaligawa kwa jamaa zake na binamu zake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

 

Share

038-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Wajibu Wa Kuamrisha Mkewe, Wanawe Waliobaleghe na Wote Waliochini Yake Kumtii Allaah Aliyetukuka, na Kuwakataza Kukhalifu, na Kufanya Waliyokatazwa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب وجوب أمره أهله وأولاده المميزين

وسائر من في رعيته بطاعة الله تعالى ونهيهم عن المخالفة وتأديبهم

ومنعهم من ارتكاب مَنْهِيٍّ عَنْهُ

038-Mlango Wa Wajibu Wa Kuamrisha Mkewe, Wanawe Waliobaleghe na Wote Waliochini Yake Kumtii Allaah Aliyetukuka, na Kuwakataza Kukhalifu, na Kufanya Waliyokatazwa

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَأْمُرْ أَهْلَكَ بِالصَّلَاةِ وَاصْطَبِرْ عَلَيْهَا ﴿١٣٢﴾

Na amrisha ahli zako Swalaah, na dumisha kusubiri kwayo. Hatukuombi riziki. Sisi Ndio Tunaokuruzuku. Na khatima njema ni kwa wenye taqwa. [Twaahaa: 132]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا ﴿٦﴾

Enyi walioamini! Jikingeni nafsi zenu na ahli zenu na moto. [At-Tahriym: 6]

 

 

Hadiyth – 1

عن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : أخذ الحسن بن علي رضي الله عنهما تَمْرَةً مِنْ تَمْر الصَّدَقَةِ فَجَعَلَهَا في فِيهِ ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( كَخْ كَخْ إرْمِ بِهَا ، أمَا عَلِمْتَ أنَّا لا نَأكُلُ الصَّدَقَةَ !؟ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : (( أنَّا لا تَحِلُّ لَنَا الصَّدَقَةُ )) .

Amesema Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Al-Hasan bin 'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) Alichukua tende ya sadaqah akaitia mdomoni mwake akitaka kuila. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akamwambia: "Kikh! Kikh! Itupe, kwani hujui kuwa sisi hatuli sadaqah? [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

Katika riwaayah nyingine: "Sadaqah si halali kwetu sisi."

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي حفص عمر بن أَبي سلمة عبد الله بن عبد الأسدِ ربيبِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : كُنْتُ غلاَماً في حجر رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَكَانَتْ يَدي تَطِيشُ في الصَّحْفَةِ ، فَقَالَ لي رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( يَا غُلامُ ، سَمِّ الله تَعَالَى ، وَكُلْ بيَمِينكَ ، وَكُلْ مِمَّا يَلِيكَ )) فَمَا زَالَتْ تِلْكَ طِعْمَتي بَعْدُ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Abu afswi 'Umar bin Abu Salamah 'Abdillaah bin 'Abdil Asad (Radhwiya Allaahu 'anhu) mwanakambo wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilikuwa mvulana katika nyumba ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), mkono wangu ulikuwa unazunguka kwenye sinia. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akaniambia: "Ee kijana! Mtaje Allaah Aliyetukuka, na kula kwa kulia kwako, na kula cha mbele yako." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم،    يقول : (( كُلُّكُمْ رَاعٍ ، وَكُلُّكُمْ مسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتهِ : الإمَامُ رَاعٍ وَمَسْؤولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، والرَّجُلُ رَاعٍ في أهْلِهِ وَمَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَالمَرْأةُ رَاعِيَةٌ في بيْتِ زَوْجِهَا وَمَسْؤُولَةٌ عَنْ رَعِيَّتِهَا ، وَالخَادِمُ رَاعٍ في مَالِ سَيِّدِهِ وَمَسؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، فَكُلُّكُمْ رَاعٍ وَمَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila mmoja wenu ni mchunga, na kila mmoja wenu ataulizwa aliowachunga. Kiongozi ni mchunga ataulizwa aliowachunga, na mume ni mchunga kwa watu wa nyumbani kwake, na mke naye ni mchunga katika nyumba ya mumewe na watoto wake; hivyo kila mmoja wenu ni mchunga na nyote mtaulizwa kwa mlivyovichunga." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 4

وعن عمرو بن شعيب ، عن أبيه ، عن جدهِ رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مُرُوا أوْلادَكُمْ بِالصَّلاةِ وَهُمْ أبْنَاءُ سَبْعِ سِنينَ ، وَاضْرِبُوهُمْ عَلَيْهَا ، وَهُمْ أبْنَاءُ عَشْرٍ ، وَفَرِّقُوا بَيْنَهُمْ في المضَاجِعِ )) حديث حسن رواه أَبُو داود بإسناد حسن .

Na imepokewa kutoka kwa 'Amr bin Shu'ayb (Radhwiya Allaahu 'anhu) kutoka kwa babake kutoka kwa babu yake kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Waamrisheni watoto wenu kuswali wakiwa na miaka saba, na wapigeni (kuacha kuswali) wakiwa na miaka kumi na muwatenganishe katika malazi." [Hadiyth Hasan iliyonukuliwa na Abu Daawuud kwa Isnadi iliyo Hasan]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي ثُرَيَّةَ سَبْرَةَ بن معبدٍ الجُهَنِيِّ رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( عَلِّمُوا الصَّبِيَّ الصَّلاةَ لِسَبْعِ سِنِينَ ، وَاضْرِبُوهُ عَلَيْهَا ابْنَ عَشْرِ سِنِينَ )) حديث حسن رواه أَبُو داود والترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

ولفظ أَبي داود : (( مُرُوا الصَّبِيَّ بِالصَّلاةِ إِذَا بَلَغَ سَبْعَ سِنِينَ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Thurayyah Sabrah bin Ma'bad Al-Juhaniyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wafundisheni watoto Swalaah wakiwa na miaka saba, na wachapeni (wakiacha na kupuuza) wakiwa na miaka kumi." [Hadiyth Hasan iliyonukuliwa na Abu Daawuud na At-Tirmidhiy, naye akasema ni Hadiyth Hasan]

Na lafdhi Abu Daawuud: "Waamrisheni watoto Swalaah wakifika miaka saba."

 

 

 

Share

039-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Haki Ya Jirani na Kumtendea Wema

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب حق الجار والوصية بِهِ

039-Mlango Wa Haki Ya Jirani na Kumtendea Wema

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَالْجَارِ الْجُنُبِ وَالصَّاحِبِ بِالْجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۗ  ﴿٣٦﴾

Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni ihsaan wazazi wawili na jamaa wa karibu, na mayatima, na masikini na jirani mwenye ujamaa na jirani asiye na ujamaa na rafiki wa karibu, na msafiri aliyeishiwa masurufu, na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia. [An-Nisaa: 36]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر وعائشة رضي الله عنهما ، قالا : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَا زَالَ جِبْريلُ يُوصِيني بِالجَارِ حَتَّى ظَنَنْتُ أنَّهُ سَيُورِّثُهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Kutoka kwa ibn 'Umar na 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuwacha Jibriyl kuniusia kuhusu jirani mpaka nikadhania kuwa atamrithisha (mali)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي ذر رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( يَا أَبَا ذَرٍّ ، إِذَا طَبَخْتَ مَرَقَةً ، فَأكثِرْ مَاءهَا ، وَتَعَاهَدْ جيرَانَكَ )) رواه مسلم .

وفي رواية لَهُ عن أَبي ذررضي الله عنه، قَالَ : إنّ خليلي صلى الله عليه وسلم أوْصَاني : (( إِذَا طَبَخْتَ مَرَقَاً فَأكْثِرْ مَاءها ، ثُمَّ انْظُرْ أهْلَ بَيْتٍ مِنْ جِيرَانِكَ ، فَأصِبْهُمْ مِنْهَا بِمعرُوفٍ )) .

Na imepokewa na Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee Abu Dharr! Unapopika supu, ongeza maji, kisha utizame kama jirani yako (anahitajia)." [Al-Bukhaariy na Muslim] 

Na katika riwaayah ya Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Hakika rafiki yangu, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameniusia: "Unapotengeneza supu ongeza maji, kisha tizama kama baadhi ya jirani zako (wanahitajia), kisha wapelekee sehemu yake kwa wema."

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( واللهِ لاَ يُؤْمِنُ ، وَاللهِ لاَ يُؤْمِنُ ، وَاللهِ لاَ يُؤْمِنُ ! )) قِيلَ : مَنْ يَا رَسُول الله ؟ قَالَ : (( الَّذِي لاَ يَأمَنُ جَارُهُ بَوَائِقَهُ ! )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية لمسلم : (( لا يَدْخُلُ الجَنَّةَ مَنْ لاَ يَأمَنُ جَارُهُ بَوَائِقَهُ )) .

Imepokewa kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wa-Allaahi haamini! Wa-Allaahi haamini!Akaulizwa: "Nani Ee Rasuli wa Allaah?" Akasema: "Ambaye jirani yake hasalimiki na shari zake." [Al-Bukhaariy na Muslim] 

Na katika riwaayah ya Muslim: "Hataingia Peponi ambaye jirani yake hasalimiki na shari zake."

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( يَا نِسَاء المُسْلِمَاتِ ، لاَ تَحْقِرَنَّ جَارةٌ لِجَارَتِهَا وَلَوْ فِرْسِنَ شَاة )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwake Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Enyi wanawake wa Kiislamu! Jirani asimdharau jirani yake hata kama amepika kwato za mbuzi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لاَ يَمْنَعْ جَارٌ جَارَهُ أنْ يَغْرِزَ خَشَبَةً في جِدَارِهِ )) ، ثُمَّ يقُولُ أَبُو هريرة : مَا لِي أرَاكُمْ عَنْهَا مُعْرِضينَ ! وَاللهِ لأرْمِيَنَّ بِهَا بَيْنَ أكْتَافِكُمْ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ 

Na imepokewa kutoka kwake Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Jirani asimkataze jirani kukita mbao katika ukuta wake." Abuu Hurayrah alikuwa akisema: "Mbona nawaona mumeipa mgongo Sunnah hii! Wa-Allaahi nitawaambia (hata mkichukia)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بالله وَاليَومِ   الآخرِ ، فَلاَ يُؤْذِ جَارَهُ ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ باللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيُكْرِمْ ضَيْفَهُ ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ باللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيَقُلْ خَيْراً أَوْ لِيَسْكُتْ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwake Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho asimuudhi jirani yake. Na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho amkirimu mgeni wake. Na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho aseme maneno ya kheri (mazuri) au anyamaze." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud na At-Tirmidhiy]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي شُرَيْح الخُزَاعيِّ رضي الله عنه: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَنْ كَانَ يُؤمِنُ بِاللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيُحْسِنْ إِلَى جَارِهِ ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ باللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيُكْرِمْ ضَيْفَهُ ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيَقُلْ خَيْراً أَوْ لِيَسْكُتْ )) رواه مسلم بهذا اللفظ ، وروى البخاري بعضه . 

Imepokewa kutoka kwa Abu Shuraykh Al-Khuzaa'iyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuwa anamuamini Allaah na Siku ya Mwisho, amfanyie hisani jirani yake. Na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho amkirimu mgeni wake. Na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho asema maneno ya kheri (mazuri) au anyamaze." [Muslim kwa lafdhi hii, na Al-Bukhaariy baadhi yake]

 

 

Hadiyth – 8

وعن عائشة رضي الله عنها ، قَالَت : قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، إنَّ لِي جارَيْنِ ، فإلى أيِّهِمَا أُهْدِي ؟ قَالَ : (( إِلَى أقْرَبِهِمَا مِنكِ بَاباً )) رواه البخاري .

Kutoka kwa 'Aa'ishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) Amesema: Nilisema: "Ee Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hakika mimi nina majirani wawili, ni yupi kati yao nimpelekee zawadi?" Akasema: "Ambaye mlango wake uko karibu zaidi nawe." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 9

وعن عبدِ الله بن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( خَيْرُ الأَصْحَابِ عِنْدَ الله تَعَالَى خَيْرُهُمْ لِصَاحِبِهِ ، وَخَيرُ الجِيرَانِ عِنْدَ الله تَعَالَى خَيْرُهُمْ لِجَارِهِ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaahi bin 'Amr bin Al-'Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mbora kabisa wa sahibu mbele ya Allaah Aliyetukuka ni aliye bora kwa sahibu yake. Na mbora mno wa jirani mbele ya Allaah Aliyetukuka ni aliye bora kwa jirani yake." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

     

Share

040-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwafanyia Wema Wazazi na Kuunga Kizazi (Ujamaa)

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب بر الوالدين وصلة الأرحام

040-Mlango Wa Kuwafanyia Wema Wazazi na Kuunga Kizazi (Ujamaa)

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَالْجَارِ الْجُنُبِ وَالصَّاحِبِ بِالْجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۗ  ﴿٣٦﴾

Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni ihsaan wazazi wawili na jamaa wa karibu, na mayatima, na masikini na jirani mwenye ujamaa na jirani asiye na ujamaa na rafiki wa karibu, na msafiri aliyeishiwa masurufu, na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia. [An-Nisaa: 36]

وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ  ﴿١﴾ 

Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. [An-Nisaa:1]

وَالَّذِينَ يَصِلُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ ﴿٢١﴾

Na ambao wanaunga yale Aliyoamrisha Allaah kuungwa. [Ar-Ra'd: 21]

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ  ﴿٨﴾

Na Tumemuusia insani kuwafanyia wema wazazi wake wawili. [Al-'Ankabuwt: 8]

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۚ إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣﴾ وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

Na Rabb wako Amehukumu kwamba: Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee na (Ameamrisha) kuwafanyia ihsaan wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee naye yuko pamoja nawe, au wote wawili basi usiwaambie, Uff! Na wala usiwakemee; na waambie maneno ya heshima.Na wainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme: Rabb wangu! Warehemu kama walivyonilea udogoni. [Al-Israa: 23-24]

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حَمَلَتْهُ أُمُّهُ وَهْنًا عَلَىٰ وَهْنٍ وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ أَنِ اشْكُرْ لِي وَلِوَالِدَيْكَ ﴿١٤﴾

Na Tumemuusia insani kwa wazazi wake wawili. Mama yake ameibeba mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na kumwachisha ziwa katika miaka mwili; ya kwamba, unishukuru Mimi, na wazazi wako; [Luqmaan: 14]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي عبد الرحمان عبد الله بن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : سألت النبي صلى الله عليه وسلم: أيُّ العَمَلِ أحَبُّ إِلَى اللهِ تَعَالَى ؟ قَالَ : (( الصَّلاةُ عَلَى وَقْتِهَا )) ، قُلْتُ : ثُمَّ أي ؟ قَالَ : (( بِرُّ الوَالِدَيْنِ )) ، قُلْتُ : ثُمَّ أيٌّ ؟ قَالَ : (( الجِهَادُ في سبيلِ الله )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu 'Abdur-Rahman 'Abdillaah bin bin Mas'uud (Radhwiya Allaahu 'anhu) alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni amali gani inayompendeza zaidi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)? Akajibu: "Swalaah kwa wakati wake." Nikasema: "Kisha ipi?" Akasema: "Wema kwa wazazi wawili." Nikasema: "Kisha ipi?" Akasema: "Jihaad katika Njia ya Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لا يَجْزِي وَلَدٌ وَالِداً إلاَّ أنْ يَجِدَهُ مَمْلُوكاً ، فَيَشْتَرِيهُ فَيُعْتِقَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtoto hawezi kumlipa mzazi isipokuwa kama atamkuta amemilikiwa (mtumwa), akamnunua kisha akamuacha huru."  [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ باللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيُكْرِمْ ضَيْفَهُ ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ باللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيَصِلْ  رَحِمَهُ ، وَمَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللهِ وَاليَومِ الآخِرِ ، فَلْيَقُلْ خَيْراً أَوْ لِيَصْمُتْ ))  مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho amkirimu mgeni wake. Na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho aunge kizazi. Na mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho aseme maneno ya kheri (mazuri) au anyamaze." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ اللهَ تَعَالَى خَلَقَ الخَلْقَ حَتَّى إِذَا فَرَغَ مِنْهُمْ قَامَتِ الرَّحِمُ ، فَقَالَتْ : هَذَا مُقَامُ العَائِذِ بِكَ مِنَ القَطِيعةِ ، قَالَ : نَعَمْ ، أمَا تَرْضَيْنَ أنْ أصِلَ مَنْ وَصَلَكِ ، وَأقْطَعَ مَنْ قَطَعَكِ ؟ قَالَتْ : بَلَى ، قَالَ : فَذَلِكَ لَكِ ، ثُمَّ قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( اقْرَؤُوا إنْ شِئْتمْ : ( فَهَلْ عَسَيْتُمْ إِنْ تَوَلَّيْتُمْ أَنْ تُفْسِدُوا فِي الأَرْضِ وَتُقَطِّعُوا أَرْحَامَكُمْ أُولَئِكَ الَّذِينَ لَعَنَهُمُ اللهُ فَأَصَمَّهُمْ وَأَعْمَى أَبْصَارَهُمْ  ) [ محمد : 22 - 23 ] مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية للبخاري : فَقَالَ الله تَعَالَى : (( مَنْ وَصَلَكِ ، وَصَلْتُهُ ، وَمَنْ  قَطَعَكِ ، قَطَعْتُهُ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) baada ya kuumba viumbe vyote, mpaka Alipomaliza (kukamilisha), yalisimama matumbo (kizazi) na kusema: "Hii ni nafasi ya mtu anayetaka ulinzi  na kinga kutoka  Kwako kwa mwemye kukata (kizazi, na kihitaji ulinzi)." Akasema: "Ndio je huridhiki Kwangu kumuunga anayekuunga, na kumkata mwenye kukukata?" Kikasema: "Ndio (naridhika)." Akaambiwa: "Hilo ni lako." Kisha akasema  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Someni mkitaka: "Basi huenda nyinyi mkigeuka ndio mfanye ufisadi katika ardhi na kukata jamaa zenu wa uhusiano wa damu? Hao ndio ambao Allaah Amewalaani; Akawafanya viziwi na Akawapofua macho yao." [Muhammad: 22-23] [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: Akasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa): "Anayekuunga, Nitamuunga na anayekukata Nitamkata."

 

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ: جاء رجل إِلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: يَا رَسُول الله ، مَنْ أحَقُّ النَّاسِ بِحُسْنِ صَحَابَتِي ؟ قَالَ : (( أُمُّكَ )) قَالَ : ثُمَّ مَنْ ؟ قَالَ : (( أُمُّكَ )) ، قَالَ : ثُمَّ مَنْ ؟ قَالَ : (( أُمُّكَ )) ، قَالَ : ثُمَّ مَنْ ؟ قَالَ : (( أبُوكَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : يَا رَسُول الله ، مَنْ أَحَقُّ بحُسْنِ الصُّحْبَةِ ؟ قَالَ : (( أُمُّكَ ، ثُمَّ  أُمُّكَ ، ثُمَّ أُمُّكَ ، ثُمَّ أَبَاكَ ، ثُمَّ أدْنَاكَ أدْنَاكَ )) .

Na kutoka kwake Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Alikuja mtu kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: "Ee Rasli wa Allaah! Nani mwenye haki zaidi miongoni mwa watu wa kuwa naye na ushirikiano mzuri (na mwema)?" na Akasema: "Mama yako." Akauliza tena: "Kisha nani?" Akasema: "Mama yako." Akauliza: "Kisha nani?" Akasema: "Mama yako." Akauliza tena: "Kisha nani?" Akasema: "Baba yako." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah nyengine: "Ee Rasuli wa Allaah! Nani mwenye haki zaidi ya kusuhubiana naye kwa mema?" Akasema: "Mamako, kisha mamako, kisha mamako, kisha babako, kisha wale alio chini yao."

 

 

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( رغِم أنفُ ، ثُمَّ رَغِمَ أنْفُ ، ثُمَّ رَغِمَ أنْفُ مَنْ أدْرَكَ أبَويهِ عِنْدَ الكِبَرِ ، أَحَدهُما أَوْ كِليهمَا فَلَمْ يَدْخُلِ الجَنَّةَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Raghima anf, kisha raghima anf, kisha raghima anf (kudhalilishwa), mtu aliyewakuta wazazi wake katika uzee; mmoja wao au wote wawili na asiingie Peponi." [Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رجلاً قَالَ : يَا رَسُول الله ، إنّ لِي قَرابةً أصِلُهُمْ وَيَقْطَعُوني ، وَأُحْسِنُ إلَيْهِمْ وَيُسِيئُونَ إلَيَّ ، وَأحْلَمُ عَنْهُمْ وَيَجْهَلُونَ عَلَيَّ ، فَقَالَ :(( لَئِنْ كُنْتَ كَمَا قُلْتَ ، فَكأنَّمَا تُسِفُّهُمْ الْمَلَّ ، وَلاَ يَزَالُ مَعَكَ مِنَ اللهِ ظَهِيرٌ عَلَيْهِمْ مَا دُمْتَ عَلَى ذلِكَ )) رواه مسلم .

Na kutoka kwake Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu): "Kuna mtu alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nina jamaa zangu, ninaowaunga, nao wananikata. Nawafanyia wema wananifanyia mabaya; nawasamehe wananitukana." Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): " Ikiwa uko kama unavyosema, itakuwa ni kama unawalisha jivu la moto; na muda huachi kuwa hivyo ila Allaah atakusaidia dhidi yao." [Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 8

وعن أنسٍ رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( من أحَبَّ أنْ يُبْسَطَ لَهُ في رِزْقِهِ ، ويُنْسأَ لَهُ في أثَرِهِ ، فَلْيَصِلْ رَحِمَهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa na Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayependa akunjuliwe riziki yake, na arefushiwe maisha yake basi aunge kizazi chake." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuud]  

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن أنسٍ رضي الله عنه، قَالَ : كَانَ أَبُو طَلْحَةَ أكْثَرَ الأنْصَارِ بالمَدينَةِ مَالاً مِنْ نَخل ، وَكَانَ أحَبُّ أمْوَاله إِلَيْهِ بَيْرَحاء ، وَكَانَتْ مسْتَقْبَلَةَ المَسْجِدِ ، وَكَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَدْخُلُهَا ، وَيَشْرَبُ مِنْ مَاءٍ فِيهَا طَيِّب ، فَلَمَّا نَزَلَتْ هذِهِ الآيةُ : ( لَنْ تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّى تُنْفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ) [ آل عمران : 92 ] قَامَ أَبُو طَلْحَةَ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : يَا رَسُول الله ، إنَّ الله تبارك وتَعَالَى ، يقول : ( لَنْ تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّى تُنْفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ) وَإنَّ أَحَبَّ مَالِي إِلَيَّ بَيْرَحَاءُ ، وَإنَّهَا صَدَقَةٌ للهِ تَعَالَى ، أرْجُو بِرَّهَا وَذُخْرَهَا عِنْدَ الله تَعَالَى ، فَضَعْهَا يَا رَسُول الله ، حَيْثُ أرَاكَ الله . فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( بَخ ! ذلِكَ مَالٌ رَابحٌ ، ذلِكَ مَالٌ رَابحٌ ! وقَدْ سَمِعْتُ مَا قُلْتَ ، وَإنِّي أرَى أنْ تَجْعَلَهَا في الأقْرَبينَ )) ، فَقَالَ أَبُو طَلْحَةَ : أفْعَلُ يَا رَسُول الله ، فَقَسَّمَهَا أَبُو طَلْحَةَ في أقَارِبِهِ وبَنِي عَمِّهِ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Toka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: 'Abu Twalhah alikuwa na mitende mingi kuliko Answariwote. Mali iliyompendeza zaidi ni shamba lililokuwa Bayrahaa', lililokuwa limeelekeana na Msikiti wa Nabiy. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiingia humo na kunywa maji yake tamu. Amesema Anas: Ilipoteremka ayah hii (Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda) [Aal-'Imraan: 92] Abu Twalhah alimwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Allaah ( Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amekuteremshia: '(Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda)'. Kwa hakika mali niipendayo sana ni shamba la Bayrahaa', nimelitoa sadaka kwa ajili ya Allaah nikitaraji kheri na ujira kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Ee Rasuli wa Allaah, nakuomba uliweke Atakavyokuonyesha Allaah. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Bakhin, Hiyo ni mali yenye faida, hiyo ni mali yenye faida. Bila shaka nimesikia uliyosema. Mimi naona uwape jamaa zako wa karibu." Abu Twalhah akasema: "Nitafanya, Ee Rasuli wa Allaah! Abu Twalhah akaligawa kwa jamaa zake na binamu zake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 10

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : أقبلَ رَجُلٌ إِلَى نَبيِّ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : أُبَايِعُكَ عَلَى الهِجْرَةِ وَالجِهَادِ أَبْتَغي الأجْرَ مِنَ الله تَعَالَى . قَالَ : (( فَهَلْ لَكَ مِنْ وَالِدَيْكَ أحَدٌ حَيٌّ ؟ )) قَالَ : نَعَمْ ، بَلْ كِلاهُمَا . قَالَ : (( فَتَبْتَغي الأجْرَ مِنَ الله تَعَالَى ؟ )) قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : (( فارْجِعْ إِلَى وَالِدَيْكَ ، فَأحْسِنْ صُحْبَتَهُمَا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ ، وهذا لَفْظُ مسلِم .

وفي رواية لَهُمَا : جَاءَ رَجُلٌ فَاسْتَأذَنَهُ في الجِهَادِ ، فقَالَ : (( أحَيٌّ وَالِداكَ ؟ ))
قَالَ : نَعَمْ ، قَالَ : (( فَفيهِمَا فَجَاهِدْ )) .

Na amesema 'Abdillaahi bin 'Amr bin al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa):  Mtu mmoja alimkabili Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Nitakubai juu ya Hijra na Jihaad nikitafuta ujira kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)." Akasema: "Je, katika wazazi wako yuko aliye hai?" Akajibu: "Ndio, bali wote wawili." Akamuuliza: "je, unataka ujira kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)?" Akasema: "Ndio." Akamwambia: "Rudi kwa wazazi wako na usuhubiane nao kwa wema (wafanyie wema)." [Al-Bukhaariy na Muslim], na hii ni lafdhi ya Muslim. pia imenukuliwa na Abu Daawuud na An-Nasaa'iy.

Riwaayah ya wao wawili: Alikuja mtu akataka ruhusa ya Jihaad. Akaulizwa: "Je wazazi wako wako hai?" Akasema: "Ndio." Akaambiwa: "Kwao wao, pigana Jihaad."

 

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَيْسَ الوَاصِلُ بِالمُكَافِىء ، وَلكِنَّ الوَاصِلَ الَّذِي إِذَا قَطَعَتْ رَحِمُهُ وَصَلَهَا )) رواه البخاري .

Na kutoka kwake Ibn 'Amr bin al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa):  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayeunga si yule anayetoa anapopewa, lakini anayeunga jamaa ni ambaye jamaa zake wanapomkata, yeye huwaunga." [Al-Bukhaariy, Abu Daawuud na At-Tirmidhiy]

 

 

 

 

Hadiyth – 12

وعن عائشة ، قَالَتْ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( الرَّحِمُ مُعَلَّقَةٌ بِالعَرْشِ تَقُولُ : مَنْ وَصَلَنِي ، وَصَلَهُ اللهُ ، وَمَنْ قَطَعَنِي ، قَطَعَهُ اللهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aa'ishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kizazi kimetundikwa katika 'Arshi, kinasema: "Anayeniunga, Allaah atamuunga, na anayenikata, Allaah Atamkata." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 13

وعن أم المؤمنين ميمونة بنتِ الحارث رضي الله عنها : أنَّهَا أعْتَقَتْ وَليدَةً وَلَمْ تَستَأذِنِ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، فَلَمَّا كَانَ يَوْمُهَا الَّذِي يَدُورُ عَلَيْهَا فِيهِ ، قَالَتْ : أشَعَرْتَ يَا رَسُول الله ، أنِّي أعتَقْتُ وَليدَتِي ؟ قَالَ : (( أَوَ فَعَلْتِ ؟ )) قَالَتْ : نَعَمْ . قَالَ : (( أما إنَّكِ لَوْ أعْطَيْتِهَا أخْوَالَكِ كَانَ أعْظَمَ لأجْرِكِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Mama wa Waumini Maymuunah bint Al-Haarith (Radhwiya Allaahu 'Anhaa) kuwa alimwacha huru kijakazi bila kumuomba idhini Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alipomtembelea (Maymuunah) siku yake, alimuuliza: "Je umejua, Ee Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa nimemwacha huru kijakazi wangu?" Akamuuliza: "Je, umefanya hivyo?" Akajibu: "Ndio." Akasema: "Lau ungewapatia (kijakazi huyo) wajomba zako ungepata ujira mkubwa zaidi."  [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuud]

 

 

 

 

Hadiyth – 14

وعن أسماءَ بنتِ أَبي بكر الصديق رضي الله عنهما ، قَالَتْ : قَدِمَتْ عَلَيَّ أُمِّي وَهِيَ مُشركةٌ في عَهْدِ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فاسْتَفْتَيْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قُلْتُ : قَدِمَتْ عَلَيَّ أُمِّي وَهِيَ رَاغِبَةٌ ، أفَأصِلُ أُمِّي ؟ قَالَ : (( نَعَمْ ، صِلِي أُمَّكِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Na amesema Asmaa' bint Abu Bakr Asw-Swiddiyq (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa): Alikuja kwangu mamangu, akiwa ni mushrik katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitaka usaidizi kutoka kwangu. Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mamangu amekuja kwangu akitaka usaidizi, je nimuunge mamngu (kwa kumfanyia wema) mamako."  [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuud]

 

 

 

 

Hadiyth – 15

وعن زينب الثقفيةِ امرأةِ عبدِ الله بن مسعود رضي الله عَنْهُ وعنها ، قَالَتْ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( تَصَدَّقْنَ يَا مَعْشَرَ النِّسَاءِ وَلَوْ مِنْ حُلِيِّكُنَّ ))، قَالَتْ : فَرَجَعْتُ إِلَى عبد الله بنِ مسعود ، فقلتُ لَهُ : إنَّكَ رَجُلٌ خَفِيفُ ذَاتِ اليَدِ ، وَإنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَدْ أمَرَنَا بِالصَّدَقَةِ فَأْتِهِ ، فَاسألهُ ، فإنْ كَانَ ذلِكَ يْجُزِىءُ عَنِّي وَإلاَّ صَرَفْتُهَا إِلَى غَيْرِكُمْ . فَقَالَ عبدُ اللهِ : بَلِ ائْتِيهِ أنتِ ، فانْطَلَقتُ ، فَإذا امْرأةٌ مِنَ الأنْصارِ بِبَابِ رسولِ الله  صلى الله عليه وسلم حَاجَتي حَاجَتُها ، وَكَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَدْ أُلْقِيَتْ عَلَيهِ المَهَابَةُ ، فَخَرجَ عَلَيْنَا بِلاَلٌ ، فَقُلْنَا لَهُ : ائْتِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، فَأخْبرْهُ أنَّ امْرَأتَيْنِ بالبَابِ تَسألانِكَ : أُتُجْزِىءُ الصَّدَقَةُ عَنْهُمَا عَلَى أزْواجِهمَا وَعَلَى أيْتَامٍ في    حُجُورِهِما ؟ ، وَلاَ تُخْبِرْهُ مَنْ نَحْنُ ، فَدَخلَ بِلاَلٌ عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، فسأله ، فَقَالَ لَهُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ هُمَا ؟ )) قَالَ : امْرَأةٌ مِنَ الأنْصَارِ وَزَيْنَبُ . فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( أيُّ الزَّيَانِبِ هِيَ ؟ )) ، قَالَ : امْرَأةُ عبدِ الله ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَهُمَا أجْرَانِ : أجْرُ القَرَابَةِ وَأجْرُ الصَّدَقَةِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kwa Zaynab Ath-Thaqafiyyah (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) mke wa 'Abdillaahi bin Mas'uud kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Enyi kongamano la wanawake, toeni sadaqah japokuwa ni mapambo ya vito." Akasema: Nilirudi kwa 'Abdillaahi bin Mas'uud nikamwambia: "Hakika wewe ni mtu mwenye mali kidogo na  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuamuru tutoe sadaqah, nenda ukamuulize ikiwa inanitosheleza kukupa wewe, ikiwa si hinyo nimpatie mwengine." Akasema 'Abdillaahi: "Bali nenda mwenyewe." Nikatoka kuelekea (kwa Rasuli), hapo nikakutana na mwanamke miongoni mwa Answaar mlangoni mwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), haja yake ni kama yangu. Na tulikuwa tunamstahi sana Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Hivyo, pindi alipotutokea Bilaal (Radhwiyah Allaahu 'anhu) tulimwambia: "Nenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) umpashe habari kuwa wapo wanawake wawili mlangoni wanakuuliza: "Je, inatosha kwa wao wanawake kuwapatia waume zao swadaqah (zakaah) na pia mayatima majumbani mwao wala usimwambie sisi ni nani." Bilaal akaingia kumuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: "Wao ni nani?" Akajibu: "Mwanamke wa Ki-Answaar na Zaynab." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni Zaynab gani huyo?" Akajibu: "Ni mkewe 'Abdillaahi." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Watapata thawabu mara mbili: Ujira wa ujamaa na ujira wa swadaqah." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 16

وعن أَبي سفيان صخر بنِ حرب رضي الله عَنْهُ في حديثِهِ الطويل في قِصَّةِ هِرَقْلَ : أنَّ هرقْلَ قَالَ لأبي سُفْيَانَ : فَمَاذَا يَأمُرُكُمْ بِهِ ؟ يَعْنِي النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : قُلْتُ : يقول : (( اعْبُدُوا اللهَ وَحْدَهُ ، وَلاَ تُشْرِكُوا بِهِ شَيئاً ، واتْرُكُوا مَا يَقُولُ آبَاؤُكُمْ ، وَيَأمُرُنَا بِالصَّلاةِ ، وَالصّدْقِ ، والعَفَافِ ، والصِّلَةِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Sufyaan Swakhr bin Harb (Radhwiyah Allaahu 'anhu) katika hadiyth yake ndefu kuhusiana na kisa cha Hiraql. Hiraqal alimuuliza Abu Sufyaan: "Je, anawaamuru nini, Yani: Nabiy?" Akasema: Nikamwambia kuwa anasema: Muabuduni Allaah Peke Yake wala usimshirikishe Yeye na chochote, na acheni wanayosema baba zenu, anatuamuru kuswali, kusema ukweli, kuwa safi (kutozini) na kuunga uzazi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 17

وعن أَبي ذرّ رضي الله عَنْهُ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّكُمْ سَتَفْتَحُونَ أرْضاً يُذْكَرُ فِيهَا القِيرَاطُ )) . وفي رواية : (( سَتَفْتَحونَ مِصْرَ وَهِيَ أرْضٌ يُسَمَّى فِيهَا القِيراطُ ، فَاسْتَوْصُوا بأهْلِهَا خَيْراً ؛ فَإنَّ لَهُمْ ذِمَّةً وَرَحِماً )) وفي رواية : (( فإذا افتتحتموها ، فأحسنوا إلى أهلها ؛ فإن لهم ذمة ورحماً )) ، أَوْ قَالَ : (( ذِمَّةً وصِهْراً )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika nyinyi mtaifungua ardhi inayoitwa Qiyraatw." Na katika riwaayah nyengine: Mtaifungua Misri na hiyo ni ardhi inayoitwa Qiyraatw, wafanyieni wema watu wake; kwani wana uhusiano nanyi, katika haki ya ulinzi na kizazi", Katika riwaayah : Mapoifungua, wafanyieni wema watu wake; kwani tuna uhusiano naowa ulinzi na kizazi" au amesema: "haki na ukwe." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 18

وعن أَبي هريرة رضي الله عَنْهُ، قَالَ : لما نزلت هذِهِ الآية : ( وَأَنْذِرْ عَشِيرَتَكَ الأَقْرَبِينَ ) [ الشعراء : 214] دَعَا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قُرَيْشاً ، فَاجْتَمَعُوا فَعَمَّ وَخَصَّ ، وَقالَ : (( يَا بَنِي عَبْدِ شَمْسٍ ، يا بَنِي كَعْبِ بْنِ لُؤيٍّ ، أنقِذُوا أنْفُسَكُمْ مِنَ النَّارِ ، يَا بَنِي مُرَّةَ بن كَعْبٍ ، أنْقِذُوا أنْفُسَكُمْ مِنَ النَّارِ ، يَا بَنِي عَبْدِ مَنَاف ، أنْقِذُوا أنْفُسَكُمْ مِنَ النَّارِ ، يَا بَنِي هاشم ، أنقذوا أنفسكم من النار ، يَا بني عبد المطلب ، انقذوا أنفسكم من النار ، يَا فَاطِمَةُ ، أنْقِذي نَفْسَكِ مِنَ النَّارِ . فَإنِّي لا أمْلِكُ لَكُمْ مِنَ اللهِ شَيئاً ، غَيْرَ أنَّ لَكُمْ رَحِماً سَأبُلُّهَا بِبِلالِهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa na Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Ilipoteremka aayah hii: "Na onya (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) jamaa zako wa karibu." [Ash-Shu'araa: 214]. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaita Maquraysh katika makundi yao na watu binafsi, akasema: "Enyi Bani 'Abdi Shams, enyi Bani Ka'b bin Lu'ayy, ziokoeni nafsi zenu na Moto. Enyi Bani Murrah bin Ka'b, ziokoeni nafsi zenu na Moto; enyi Bani 'Abdi Manaaf, ziokoeni nafsi zenu na Moto, enyi Bani Haashim, ziokoeni nafsi zenu na Moto; enyi Bani 'Abdil Mutwtwalib, ziokoeni nafsi zenu na Moto; Ee Faatwimah, okoa nafsi yako na Moto, kwani siwezi kuwafanyia lolote mbele ya Allaah. Hata hivyo, baina yetu kuna unasaba, nami nitaulinda. (na kuuhifadhi)." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 19

وعن أَبي عبد الله عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : سمعت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم جِهَاراً غَيْرَ سِرٍّ ، يَقُولُ : (( إنَّ آل بَني فُلاَن لَيْسُوا بِأولِيَائِي ، إِنَّمَاوَلِيِّيَ اللهُ وَصَالِحُ المُؤْمِنينَ ، وَلَكِنْ لَهُمْ رَحِمٌ أبُلُّهَا بِبلاَلِهَا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ ، واللفظ للبخاري .

Kutoka kwa Abu Abdillaahi 'Amr bin Al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema waziwazi bila kuficha: "Hakika jamaa wa Bani fulani si rafiki zangu. Hakika rafiki yangu ni Allaah na walio wema katika Waumini, lakini wana ujamaa, nitauunga." [Al-Bukhaariy na Muslim, na lafdhi ni ya Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 20

وعن أَبي أيوب خالد بن زيد الأنصاري رضي الله عَنْهُ: أنَّ رجلاً قَالَ : يَا رَسُول الله ، أخْبِرْني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجَنَّةَ ، وَيُبَاعِدُني مِنَ النَّارِ . فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: (( تَعْبُدُ الله ، وَلاَ تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً ، وَتُقِيمُ الصَّلاةَ ، وتُؤتِي الزَّكَاةَ ، وتَصِلُ الرَّحمَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Ayyuub Khaalid bin Zayd Al-Answaariy (Radhwiyah Allaahu 'anhumma) kuwa mtu mmoja alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Nipe habari ya amali itakayo niingiza Peponi na kuniepusha na Moto?" Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Muabuduni Allaah wala usimshirikishe kwa chochote, usimamishe Swalaah, utoe Zakaah na uunge kizazi (ujamaa)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 21

وعن سلمان بن عامر رضي الله عَنْهُ ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا أفْطَرَ أحَدُكُمْ ، فَلْيُفْطرْ عَلَى تَمْرٍ ؛ فَإنَّهُ بَرَكةٌ ، فَإنْ لَمْ يَجِدْ تَمْراً ، فالمَاءُ ؛ فَإنَّهُ  طَهُورٌ )) ، وَقالَ : (( الصَّدَقَةُ عَلَى المِسكينِ صَدَقةٌ ، وعَلَى ذِي الرَّحِمِ ثِنْتَانِ : صَدَقَةٌ وَصِلَةٌ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa Salmaan bin 'Aamir (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapofuturu mmoja wenu afuturu kwa tende, kwani ina baraka. Asiopata tende, basi afungue kwa maji; kwani yanatwahirisha." Na akasema: "Sadaqah kwa maskini ni sadaqah na kumpa jamaa ina ujira mara mbili: ni sadaqah na kuunga ujamaa." [At-Tirmidhiy, na akasema Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 22

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَتْ تَحْتِي امْرَأةٌ ، وَكُنْتُ أحِبُّهَا ، وَكَانَ عُمَرُ يَكْرَهُهَا ، فَقَالَ لي : طَلِّقْهَا ، فَأبَيْتُ ، فَأتَى عُمَرُ رضي الله عَنْهُ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، فَذَكَرَ ذلِكَ لَهُ ، فَقَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: (( طَلِّقْهَا )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Amesema Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa): Nilimuoa mke niliyekuwa nampenda; lakini 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) alikuwa anamchukia. Akaniambia: "Mpatie talaka", Nikakataa. 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) alikwenda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumtajia jambo hilo. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Mtaliki." [Abu Daawuud na At-Tirmidhiy, naye akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

 

Hadiyth – 23

وعن أَبي الدرداءِ رضي الله عَنْهُ: أن رجلاً أتاه ، قَالَ : إنّ لي امرأةً وإنّ أُمِّي تَأمُرُنِي بِطَلاقِهَا ؟ فَقَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( الوَالِدُ أوْسَطُ أبْوَابِ الجَنَّةِ ، فَإنْ شِئْتَ ، فَأضِعْ ذلِكَ البَابَ ، أَو احْفَظْهُ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa (Radhwiyah Allaah 'anhu) kuwa mtu mmoja alikuja kwake, akamuuliza: "Hakika mimi nina mke, ambaye mamangu anataka nimuache?" Akamwambia: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mzazi ndiye mlango bora miongoni mwa milango ya Peponi, ukitaka upoteze huo mlango au uhifadhi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

 

Hadiyth – 24

وعن البراءِ بن عازب رضي اللهُ عنهما ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( الخَالةُ بِمَنْزِلَةِ الأُمِّ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Na imepokewa kutoka kwa Al-Baraa' bin 'Aazib (Radhiwyah Allaahu 'anhummaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Halati (mama mdogo) yu katika daraja ya mama."  [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

 

 

 

 

 

Share

041-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Uharamu wa Kuwaasi Wazazi na Kukata Kizazi

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب تحريم العقوق وقطيعة الرحم

041-Mlango Wa Uharamu wa Kuwaasi Wazazi na Kukata Kizazi

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

فَهَلْ عَسَيْتُمْ إِن تَوَلَّيْتُمْ أَن تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ وَتُقَطِّعُوا أَرْحَامَكُمْ﴿٢٢﴾ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ لَعَنَهُمُ اللَّـهُ فَأَصَمَّهُمْ وَأَعْمَىٰ أَبْصَارَهُمْ﴿٢٣﴾

Basi huenda nyinyi mkigeuka ndio mfanye ufisadi katika ardhi na kukata jamaa zenu wa uhusiano wa damu? Hao ndio ambao Allaah Amewalaani; Akawafanya viziwi na Akawapofua macho yao. [Muhammad: 22-23]

 

وَالَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهْدَ اللَّـهِ مِن بَعْدِ مِيثَاقِهِ وَيَقْطَعُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ ۙ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ اللَّعْنَةُ وَلَهُمْ سُوءُ الدَّارِ ﴿٢٥﴾

Na wale wanaovunja ahadi ya Allaah baada ya kufungamana kwake na wanakata yale Aliyoyaamrisha Allaah kuwa yaungwe na wanafanya ufisadi katika ardhi, hao watapata laana na watapata makazi mabaya (motoni). [Ar-Ra'd: 25]

 

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۚ إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣﴾ وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

Na Rabb wako Amehukumu kwamba: Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee na (Ameamrisha) kuwafanyia ihsaan wazazi wawili. Kama mmoja wao akifikia uzee naye yuko pamoja nawe, au wote wawili basi usiwaambie, Uff! Na wala usiwakemee; na waambie maneno ya heshima. Na wainamishie bawa la unyenyekevu kwa huruma, na useme: Rabb wangu! Warehemu kama walivyonilea udogoni. [Al-Israa: 23-24]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي بكرة نُفَيع بن الحارث رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( ألا أُنَبِّئُكُمْ بأكْبَرِ الكَبَائِرِ ؟ )) – ثلاثاً – قُلْنَا : بَلَى ، يَا رَسُول الله ، قَالَ : (( الإشْرَاكُ بالله ، وَعُقُوقُ الوَالِدَيْنِ )) ، وكان مُتَّكِئاً فَجَلَسَ ، فَقَالَ : (( ألاَ وَقَوْلُ الزُّورِ وَشَهَادَةُ الزُّورِ )) فَمَا زَالَ يُكَرِّرُهَا حَتَّى قُلْنَا : لَيْتَهُ سَكَتَ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa kwa Bakrah Nufay' bin Al-Haarith Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Je, hamtaki niwaambieni dhambi kubwa katika madhambi makubwa?"- mara tatu. Tukasema: "Ndio (tuambie), Ee Rasuli wa Allaah." Akawaambia: "Ni kumshirikisha Allaah na kuwaasi wazazi." Na alikuwa ameegemea, akakaa na kusema: "Eleweni pia kusema urongo na kutoa ushahidi wa urongo." Aliendelea kukariri hilo mpaka tukasema: "Laiti angenyamaza." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( الكَبَائِرُ : الإشْرَاكُ بالله ، وَعُقُوقُ الوَالِدَيْنِ ، وَقَتْلُ النَّفْس ، وَاليَمِينُ الغَمُوسُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaahi bin 'Amru bin Al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Madhambi makubwa ni kumshirikisha Allaah, kuwaasi wazazi, kuua nafsi na kiapo (yamini) cha urongo wa kusudi." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: (( مِنَ الكَبَائِر شَتْمُ الرَّجُل وَالِدَيهِ ! ))، قالوا : يَا رَسُول الله ، وَهَلْ يَشْتُمُ الرَّجُلُ وَالِدَيْهِ ؟! قَالَ : (( نَعَمْ ، يَسُبُّ أَبَا الرَّجُلِ ، فَيَسُبُّ أبَاه ، وَيَسُبُّ أُمَّهُ ، فَيَسُبُّ أُمَّهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : (( إنَّ مِنْ أكْبَرِ الكَبَائِرِ أنْ يَلْعَنَ الرَّجُلُ وَالِدَيْهِ ! )) ، قِيلَ : يَا رَسُول الله ، كَيْفَ يَلْعَنُ الرَّجُلُ وَالِدَيهِ ؟! قَالَ: (( يَسُبُّ أَبَا الرَّجُلِ ، فَيَسُبُّ أباهُ ، وَيَسُبُّ أُمَّهُ ، فَيَسُبُّ أُمَّهُ )) .

Kutoka kwa 'Abdillaahi bin 'Amru bin Al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Miongoni mwa madhambi makubwa ni mtu kuwatusi wazazi wake ." Wakauliza (yaani Maswahaba): "Ee Rasuli wa Allaah! Na je, mtu, anaweza kuwatusi wazazi wake?" Akasema: "Ndio, atamtusi baba ya mtu, naye amtusi babake, na atamtusi mama ya mtu, naye amtusi mamake." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

Katika riwaayah nyingine: "Hakika miongoni mwa madhambi makubwa ni mtu kuwalaani wazazi ake." Pakasemwa: "Ee Rasuli wa Allaah! Vipi mtu atawalaani wazazi wake?" Akasema: "Atamtusi baba ya mtu, naye amtusi babake, na atamtusi mama ya mtu, naye amtusi mamake."

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي محمد جبيرِ بن مطعم رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لاَ يَدْخُلُ الجَنَّةَ قَاطِعٌ )) قَالَ سفيان في روايته : يَعْنِي : قَاطِع رَحِم . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muhammad Jubayr bin Mutw'im (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hataingia Peponi mwenye kukata." Amesema Sufyaan katika riwaayah yake: "Yaani mwenye kukata kizazi." [Al- Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي عيسى المغيرة بن شعبة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إنَّ اللهَ تَعَالَى حَرَّمَ عَلَيْكُمْ : عُقُوقَ الأمَّهَاتِ ، وَمَنْعاً وهاتِ ، وَوَأْد البَنَاتِ ، وكَرِهَ لَكُمْ : قِيلَ وَقالَ ، وَكَثْرَةَ السُّؤَالِ ، وَإضَاعَةَ المَالِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu 'Iysa Mughyrah bin Shu'bah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameharamisha kuwaasi mama zenu; na kuzuia na lete (kuzuia kilicho wajibu kutoa na kutaka kisicho chake); na kuzika wasichana wakiwa hai; na Amechukia kwenu kusema ovyo; kuomba sana; na kufuja mali." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

042-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwafanyia Wema Marafiki wa Baba na Mama, Jamaa, Mkw na Wote Wanaopendekezwa Kuwafanyia Ukarimu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل بر أصدقاء الأب والأم والأقارب والزوجة وسائر من يندب إكرامه

042-Mlango Wa Kuwafanyia Wema Marafiki wa Baba na Mama, Jamaa, Mkw na Wote Wanaopendekezwa Kuwafanyia Ukarimu

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Hadiyth – 1

عن ابن عمر رضي الله عنهما : أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إنّ أبَرَّ البرِّ أنْ يَصِلَ الرَّجُلُ وُدَّ أبيهِ )) .رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika wema mkubwa kabisa ni mtu kuwaunga vipenzi wa baba yake." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن دينار ، عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رَجُلاً مِنَ الأعْرَابِ لَقِيَهُ بطَريق مَكَّةَ ، فَسَلَّمَ عَلَيهِ عبدُ الله بْنُ عُمَرَ ، وَحَمَلَهُ عَلَى حِمَارٍ كَانَ يَرْكَبُهُ ، وَأعْطَاهُ عِمَامَةً كَانَتْ عَلَى رَأسِهِ ، قَالَ ابنُ دِينَار : فَقُلْنَا لَهُ : أصْلَحَكَ الله ، إنَّهُمُ الأعرَابُ وَهُمْ يَرْضَوْنَ باليَسير ، فَقَالَ عبد الله بن عمر : إن أَبَا هَذَا كَانَ وُدّاً لِعُمَرَ بنِ الخطاب رضي الله عنه، وإنِّي سَمِعتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( إنَّ أبرَّ البِرِّ صِلَةُ الرَّجُلِ أهْلَ وُدِّ أبِيهِ )) .

وفي رواية عن ابن دينار ، عن ابن عمر : أنَّهُ كَانَ إِذَا خَرَجَ إِلَى مَكّةَ كَانَ لَهُ حِمَارٌ يَتَرَوَّحُ عَلَيهِ إِذَا مَلَّ رُكُوبَ الرَّاحِلةِ ، وَعِمَامَةٌ يَشُدُّ بِهَا رَأسَهُ ، فَبيْنَا هُوَ يَوماً عَلَى ذلِكَ الحِمَارِ إِذْ مَرَّ بِهِ أعْرابيٌّ ، فَقَالَ : ألَسْتَ فُلاَنَ بْنَ فُلاَن ؟ قَالَ : بَلَى . فَأعْطَاهُ الحِمَارَ ، فَقَالَ : ارْكَبْ هَذَا ، وَأعْطَاهُ العِمَامَةَ وَقالَ : اشْدُدْ بِهَا رَأسَكَ ، فَقَالَ لَهُ بعضُ أصْحَابِهِ : غَفَرَ الله لَكَ أعْطَيْتَ هَذَا الأعْرَابيَّ حِمَاراً كُنْتَ تَرَوَّحُ     عَلَيهِ ، وعِمَامةً كُنْتَ تَشُدُّ بِهَا رَأسَكَ ؟ فَقَالَ : إنِّي سَمِعتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يَقُولُ : (( إنَّ مِنْ أبَرِّ البِرِّ أنْ يَصِلَ الرَّجُلُ أهْلَ وُدِّ أبيهِ بَعْدَ أنْ يُولِّيَ )) وَإنَّ أبَاهُ كَانَ صَديقاً لعُمَرَرضي الله عنه.

رَوَى هذِهِ الرواياتِ كُلَّهَا مسلم .

Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaahi bin Diynaar  (Radhwiyah Allaahu 'anhu) Kuwa 'Abdillaahi bin 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) alikutana na Bedui katika njia ya Makkah. 'Abdillaahi bin 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) akamsalimia akampandisha kwenya punda wake aliye mpaka, akampatia kilemba kilicho kichwani mwake. Ibn Diynaar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) akasema: Tukamwambia: "Allaah Akutengeneza, Wao ni Mabedui wanaridhika na mepesi." Akasema 'Abdillaahi bin 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu): "Babake huyu alikuwa rafiki mkubwa wa 'Umar bin Al-Khatw'aab (Radhwiyah Allaahu 'anhu), nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika wema mkubwa ni kwa mtu kuunga vipenzi vya baba yake."

Katika riwaayah ya Ibn Diynaar, Ibn 'Umar (Radhiwyah Allaahu 'anhu) alikuwa anapotoka kwenda Makkah alipochoka kupanda ngamia anapumzika, kilemba anakazia kichwa chake. Alipokuwa hivyo siku moja juu ya punda, akapita bedui, akamuuliza: "Je, wewe ndiye mtoto wa fulani?" Akajibu: "Ndio." Akamtunikia punda, na kumwambia: "Mpande huyu." Na pia akampatia kilemba, kamwambia: "Kifunge kichwani mwako." Baadhi ya maswahibu zake wakamwambia: "Allaah Akughufirie, umempatia huyu bedui punda uliyekuwa ukimtumia kwa safari zako na kilemba ulichokuwa ukifunikia kichwa chako." Akasema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika wema mkubwa kabisa ni mtu kuunga vipenzi wa baba yake baada ya kufa kwake", na babake alikuwa ni rafiki wa 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu). [Zimepokewa hizi riwaayah zote na Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي أُسَيد - بضم الهمزة وفتح السين - مالك بن ربيعة الساعدي رضي الله عنه، قَالَ : بَيْنَا نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إذ جَاءهُ رَجُلٌ مِنْ بَنِي سَلَمَةَ ، فَقَالَ : يَا رسولَ اللهِ ، هَلْ بَقِيَ مِنْ برِّ أَبَوَيَّ شَيء أبرُّهُما بِهِ بَعْدَ مَوتِهمَا ؟ فَقَالَ :   (( نَعَمْ ، الصَّلاةُ عَلَيْهِمَا ، والاسْتغْفَارُ لَهُمَا ، وَإنْفَاذُ عَهْدِهِمَا مِنْ بَعْدِهِما ، وَصِلَةُ الرَّحِمِ الَّتي لا تُوصَلُ إلاَّ بِهِمَا ، وَإكرامُ صَدِيقهمَا )) رواه أَبُو داود .

Amesema Abu Usayd Maalik bin Rabi'ah As-Saa'idiy (Radhwiyah Allaahu 'anhu): "Tulipokuwa tumekaa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaja mtu kutoka katika ukoo wa Salimah akasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, kumebakia wema wa kuwatendea wazazi wangu baada ya kufa kwao?" Akasema: "Ndio, kuwaombea du'aa, kuwatakia maghfira, kutekeleza ahadi zao baada ya kufa kwao, kuunga kizazi ambacho hakiungiki ila kwa sababu yao na kuwakirimu marafiki zao." [Abu Daawuud]

 

 

Hadiyth – 4

وعن عائشة رضي الله عنها ، قَالَتْ : مَا غِرْتُ عَلَى أحَدٍ مِنْ نِسَاءِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم مَا غِرْتُ عَلَى خَدِيجَة رضي الله عنها ، وَمَا رَأيْتُهَا قَطُّ ، وَلَكِنْ كَانَ يُكْثِرُ ذِكْرَهَا ، وَرُبَّمَا ذَبَحَ الشَّاةَ ، ثُمَّ يقَطِّعُهَا أعْضَاء ، ثُمَّ يَبْعثُهَا في صَدَائِقِ خَديجَةَ ، فَرُبَّمَا قُلْتُ لَهُ : كَأنْ لَمْ يَكُنْ في الدُّنْيَا إلاَّ خَديجَةَ ‍! فَيَقُولُ : (( إنَّهَا كَانَتْ وَكَانَتْ وَكَانَ لي مِنْهَا وَلَدٌ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : وإنْ كَانَ لَيَذْبَحُ الشَّاءَ ، فَيُهْدِي في خَلاَئِلِهَا مِنْهَا مَا يَسَعُهُنَّ .

وفي رواية:كَانَ إِذَا ذبح الشاة، يقولُ : (( أَرْسِلُوا بِهَا إِلَى أصْدِقَاءِ خَديجَةَ )) .

وفي رواية : قَالَت : اسْتَأذَنتْ هَالَةُ بِنْتُ خُوَيْلِد أُخْتُ خَدِيجَةَ عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، فَعرَفَ اسْتِئذَانَ خَديجَةَ ، فَارتَاحَ لِذَلِكَ ، فَقَالَ : (( اللَّهُمَّ هَالةُ بِنْتُ   خُوَيْلِدٍ )) .

Amesema 'Aa'ishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa): "Sijamuonea wivu yeyote miongoni mwa wake wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kama nilivyomuonea wivu Khadijah ilhali sijawahi kumuona kabisa Khadijah (Radhwiyah Allahu 'anhaa), lakini Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akimtaja sana. Mara nyengine alikuwa akichinja mbuzi, akimkata vipande kisha akiwapelekea marafiki za Khadijah. Mara nyengine nilimwambia: "Kama kwamba hakuna duniani ila Khadijah." Akasema: "Alikuwa kadha wa kadha, amenizalia watoto." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah nyengine: "Alikuwa anachinja mbuzi na kuwazawadia rafikize Khadijah kinachowatosha.

Katika riwaayah nyengine: "Alikuwa anapochinja mbuzi husema: "Wapelekeeni rafiki za Khadijah."

Katika riwaayah nyengine: "Haalah bint Khuwaylid, dadake Khadijah, alibisha hodi kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Akamtambua hodi ya Khadijah (kwa  ile sauti), akafurahi kuja kwake, akasema: "Ee Allaah! Huyu ni Haalah bint Khuwaylid."

 

 

Hadiyth – 5

وعن أنس بن مالك رضي الله عنه، قَالَ : خرجت مَعَ جرير بن عبد الله البَجَليّ رضي الله عنه في سَفَرٍ ، فَكَانَ يَخْدُمُني ، فَقُلْتُ لَهُ : لاَ تَفْعَل ، فَقَالَ : إِنِّي قَدْ رَأيْتُ الأنْصَارَ تَصْنَعُ برسول الله صلى الله عليه وسلم شيئاً آلَيْتُ عَلَى نَفسِي أنْ لا أصْحَبَ أحَداً مِنْهُمْ إلاَّ خَدَمْتُهُ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Amesema Anas bin Maalik (Radhwiyah Allaahu 'anhu): "Nilisafiri na Jariyr bin 'Abdillaahi Al-Bajaliyy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) safarini, alikuwa ananitumikia, nikamwambia: "Usifanye hivyo." Akasema: "Mimi nimewaona Answari wakimfanyia hilo Rasuli Wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hivyo nikala kiapo kuwa kila nitakapofuatana na mmoja nitamhudumia." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

043-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwakirimu Watu wa Nyumba ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Kubainisha Fadhila Zao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب إكرام أهل بيت رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وبيان فضلهم

043-Mlango Wa Kuwakirimu Watu wa Nyumba ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Kubainisha Fadhila Zao

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ﴿٣٣﴾

Hakika Allaah Anataka Akuondosheeni maovu enyi ahli wa nyumba (ya Nabiy) na Akutakaseni mtakaso barabara. [Al-Ahzaab: 33]

 

 

وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّـهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ ﴿٣٢﴾

Na yeyote anayeadhimisha Ishara za Allaah, basi hayo ni katika taqwa ya nyoyo. [Al-Hajj: 22]

 

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن يزيد بن حَيَّانَ ، قَالَ : انْطَلَقْتُ أنَا وحُصَيْنُ بْنُ سَبْرَة ، وَعَمْرُو ابن مُسْلِم إِلَى زَيْد بْنِ أرقَمَ رضي الله عنه، فَلَمَّا جَلسْنَا إِلَيْهِ قَالَ لَهُ حُصَيْن : لَقَدْ لقِيتَ يَا زَيْدُ خَيْراً كَثِيراً ، رَأيْتَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، وسمعتَ حديثَهُ ، وغَزوْتَ مَعَهُ ، وَصَلَّيْتَ خَلْفَهُ : لَقَدْ لَقِيتَ يَا زَيْدُ خَيْراً كَثيراً ، حَدِّثْنَا يَا زَيْدُ مَا سَمِعْتَ مِنْ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : يَا ابْنَ أخِي ، وَاللهِ لقد كَبِرَتْ سِنِّي ، وَقَدُمَ عَهدِي ، وَنَسيتُ بَعْضَ الَّذِي كُنْتُ أعِي مِنْ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، فما حَدَّثْتُكُمْ ، فَاقْبَلُوا ، ومَا لا فَلاَ تُكَلِّفُونيهِ . ثُمَّ قَالَ : قام رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَوماً  فينا خَطِيباً بمَاء يُدْعَى خُمَّاً بَيْنَ مَكَّةَ وَالمَدِينَةِ ، فَحَمِدَ الله ، وَأثْنَى عَلَيهِ ، وَوعظَ وَذَكَّرَ ، ثُمَّ قَالَ : (( أمَّا بَعدُ ، ألاَ أَيُّهَا النَّاسُ ، فَإنَّمَا أنَا بَشَرٌ يُوشِكَ أنْ يَأتِي رسولُ ربِّي فَأُجِيبَ ، وَأنَا تارك فيكم ثَقَلَيْنِ : أوَّلُهُمَا كِتَابُ اللهِ ، فِيهِ الهُدَى وَالنُّورُ ، فَخُذُوا بِكتابِ الله ، وَاسْتَمْسِكُوا بِهِ )) ، فَحَثَّ عَلَى كِتَابِ الله ، وَرَغَّبَ فِيهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( وَأهْلُ بَيْتِي أُذكِّرُكُمُ الله في أهلِ بَيْتي ، أذكرُكُمُ الله في أهل بيتي )) فَقَالَ لَهُ حُصَيْنٌ : وَمَنْ أهْلُ بَيتهِ يَا زَيْدُ ، أَلَيْسَ نِسَاؤُهُ مِنْ أهْلِ  بَيْتِهِ ؟ قَالَ : نِسَاؤُهُ مِنْ أهْلِ بَيتهِ ، وَلكِنْ أهْلُ بَيتِهِ مَنْ حُرِمَ الصَّدَقَةَ بَعدَهُ ، قَالَ : وَمَنْ هُمْ ؟ قَالَ : هُمْ آلُ عَلِيٍّ وَآلُ عقيل وَآلُ جَعفَرَ وآلُ عَبَّاسٍ . قَالَ : كُلُّ هؤلاء حُرِمَ الصَّدَقَةَ ؟ قَالَ : نَعَمْ . رواه مسلم .

وفي رواية : (( ألاَ وَإنّي تَارِكٌ فِيكُمْ ثَقَليْنِ : أحَدُهُما كِتَابُ الله وَهُوَ حَبْلُ  الله ، مَنِ اتَّبَعَهُ كَانَ عَلَى الهُدَى ، وَمَنْ تَرَكَهُ كَانَ عَلَى ضَلالَة )) .

Amesema Yaziyd bin Hayyaan: Mimi, Huswayn bin Sabrah na 'Amru bin Muslim tulimtembelea Zayd bin Muslim (Radhwiyah Allaahu 'anhu). Tulipokaa naye, Huswayn akamwambia: "Hakika ee Zayd, umepata kheri nyingi, umemuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), ukasikia mazungumzo yake, ukapigana pamoja naye, na ukaswali nyuma yake. Hakika umepata kheri nyingi,ee Zayd! Tuhadithie Zayd uliyosikia kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Akamwambia: "Ee mpwa wangu! Wa- Allaahi, Nimezeeka, zama zangu zimepita na nimesahau baadhi ya niliyohifadhi kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Nitakacho wahadithia kipokeeni, na ambacho sikuwahadithia musinilazimishe kukizungumza." Kisha akasema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisimama siku moja mahali panapoitwa Khum baina ya Makkah na Madiynah; kutuhutubia, Akamuhimidi Allaah, akamsifu, akaedhea; kisha akasema: "Ama baada ya haya: Fahamuni enyi watu! Hakika mimi ni mwanadamu, anakaribia kunijia Mjumbe wa Mola wangu nami niitikie wito huo, nami nimewaachia vizito viwili: cha kwanza ni Kitabu cha Allaah, ambacho kina uongofu na nuru ndani yake, kichukueni Kitabu cha Allaah ns mshikamane nacho barabara." Akasisitiza mno juu ya kushikamana na Kitabu cha Allaah, kisha akasema: "Na watu wangu wa nyumbani, mkumbukeni Allaah kwa watu wa nyumbani kwangu." Huswayn akamwambia: "Ee Yaziyd, ni nani hao watu wa nyumbani kwake? Wake zake si ni watu wa nyumba yake?" Akasema: "Wake zake ni katika watu wa nyumbani kwake, lakini watu wa nyumba yake haswa ni wale waliokatazwa kula sadaqah baada yake." Akaulizwa: "Na ni kina nani hao?" Akasema: "Hao ni familia ya 'Aliy, familia ya 'Aqiyl, familia ya Ja'far na familia ya 'Abbaas." Akasema: "Wote hao wamekatazwa na kuharamishwa sadaqah?" Akasema: "Ndio." [Muslim] 

Katika riwaayah: "Fahamuni kuwa nimewaachieni vizito na vitukufu viwili: Ya kwanza Kitabu cha Allaah, nayo ni kamba ya Allaah. Mwenye kukifuata atakuwa juu ya  uongofu na mwenye kukiacha atakuwa juu ya upotevu."

 

 

Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن أَبي بكر الصديق رضي الله عنه - مَوقُوفاً عَلَيهِ - أنَّهُ قَالَ : ارْقَبُوا مُحَمداً صلى الله عليه وسلم في أهْلِ بَيْتِهِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa Abu Bakr Asw-Swiddiq (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Mheshimmuni na mkirimuni Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika familia yake." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Share

044-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwaheshimu Wanazuoni, Wakubwa na Watu Watukufu na Kuwatanguliza Juu ya Wengine, Kutukuza Vikao Vyao na Kudhihirisha Utukufu Wao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب توقير العلماء والكبار وأهل الفضل وتقديمهم عَلَى غيرهم ورفع مجالسهم وإظهار مرتبتهم

044-Mlango Wa Kuwaheshimu Wanazuoni, Wakubwa na Watu Watukufu na Kuwatanguliza Juu ya Wengine, Kutukuza Vikao Vyao na Kudhihirisha Utukufu Wao

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ ۗ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٩﴾

Sema: Je, wanalingana sawa wale wanaouja na wale wasiojua? Hakika wanakumbuka wenye akili tu.[Az-Zumar: 9]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي مسعودٍ عقبةَ بن عمرو البدري الأنصاري رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( يَؤُمُّ القَوْمَ أقْرَؤُهُمْ لِكِتَابِ الله ، فَإنْ كَانُوا في القِراءةِ سَوَاءً ، فأَعْلَمُهُمْ بِالسُّنَّةِ ، فَإنْ كَانُوا في السُّنَّةِ سَوَاءً ، فَأَقْدَمُهُمْ هِجْرَةً ، فَإنْ كَانُوا في الهِجْرَةِ سَوَاءً ، فَأقْدَمُهُمْ سِنّاً ، وَلاَ يُؤمّنَّ الرَّجُلُ الرَّجُلَ في سُلْطَانِهِ ، وَلاَ يَقْعُدْ في بَيْتِهِ عَلَى تَكْرِمَتِهِ إلاَّ بِإذْنهِ )) رواه مسلم .

وفي رواية لَهُ : (( فَأقْدَمُهُمْ سِلْماً )) بَدَلَ (( سِنّاً )) : أيْ إسْلاماً . وفي رواية :  (( يَؤُمُّ القَومَ أقْرَؤُهُمْ لِكِتَابِ اللهِ ، وَأقْدَمُهُمْ قِراءةً ، فَإنْ كَانَتْ قِرَاءتُهُمْ سَوَاءً فَيَؤُمُّهُمْ أقْدَمُهُمْ هِجْرَةً ، فَإنْ كَانُوا في الهِجْرَةِ سَواء ، فَليَؤُمُّهُمْ أكْبَرُهُمْ سِنّاً )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Mas'uud 'Uqbah bin 'Amru Al-Badriy Al-Answaarriyy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Aswalishe msomi wao wa Kitabu cha Allaah. Ikiwa wako sawa katika kisomo, basi mjuzi zaidi katika Sunnah. Ikiwa wako sawa katika Sunnah, wa mwanzo wao kuhama. Wakiwa sawa katika kuhama, basi mkubwa wao wa umri, Wala mtu hamswalishi mwingine katika mamlaka yake ila kwa idhini yake, wala asikae katika utukufu wake ila kwa ruhusa yake." [Muslim]

Katika riwaayah yake: "Wa mwanzo kusilimu" badala ya "umri mkubwa." 

Katika riwaayah nyengine: "Aswalisha watu msomi wao kwa Kitabu cha Allaah , na wa mwanzo wao kusoma,. Ikiwa kisomo chao ni sawa, basi aswalishe wa mwanzo wao kuhama. Ikiwa wapo sawa katika kuhama, basi mkubwa wao."

  

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي مسعودٍ عقبةَ بن عمرو البدري الأنصاري رضي الله عنه، قَالَ : كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَمْسَحُ مَنَاكِبَنَا في الصَّلاةِ ، ويَقُولُ : (( اسْتَوُوا وَلاَ تَخْتَلِفُوا ، فَتَخْتَلِفَ قُلُوبُكُمْ ، لِيَلِني مِنْكُمْ أُولُوا الأحْلاَمِ وَالنُّهَى ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Mas'uud 'Uqbah bin 'Amru Al-Badriy Al-Answaarriyy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akifuta mabega yetu katika swalaah na kusema: "Nyookeni wala msikhitilafiane zikatofautiana nyoyo zenu. Wanikaribie wenye utambuzi na akili miongoni mwenu, kisha wanaowafuatia wao, kisha wanaowafuatia wao." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لِيَلِني مِنْكُمْ أُولُوا الأحْلام وَالنُّهَى ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ )) ثَلاثاً (( وَإيَّاكُمْ وَهَيْشَاتِ الأسْوَاق )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaahi bin Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wanikaribie wenye akili na utambuzi miongoni mwenu, kisha wanaowafuatia wao (mara tatu) na nawatahadharisheni sana na vurumai na tangamano la watu wa masokoni." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي يَحيَى ، وقيل : أَبي محمد سهلِ بن أَبي حَثْمة - بفتح الحاءِ المهملة وإسكان الثاءِ المثلثةِ - الأنصاري رضي الله عنه، قَالَ : انطَلَقَ عَبدُ اللهِ بنُ سهْلٍ وَمُحَيِّصَة بن مَسْعُود إِلَى خَيْبَرَ وَهِيَ يَومَئذٍ صُلْحٌ ، فَتَفَرَّقَا ، فَأتَى مُحَيِّصَةُ إِلَى عبدِ اللهِ ابنِ سهل وَهُوَ يَتشَحَّطُ في دَمِهِ قَتِيلاً ، فَدَفَنَهُ ، ثُمَّ قَدِمَ المَدِينَةَ فَانْطَلَقَ عَبدُ الرحمان ابنُ سهل وَمُحَيِّصَةُ وحوَيِّصَةُ ابْنَا مَسْعُودٍ إِلَى النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، فَذَهَبَ عَبدُ الرحمان يَتَكَلَّمُ ، فَقَالَ : (( كَبِّرْ كَبِّرْ )) وَهُوَ أحْدَثُ القَوم ، فَسَكَتَ ، فَتَكَلَّمَا ، فَقَالَ : (( أتَحْلِفُونَ وتَسْتَحِقُّونَ قَاتِلَكُمْ ؟ … )) وذكر تمام الحديث . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Amesema Abu Yahyaa au Abu Muhammad Sahl bin Abi Hathmah: 'Abdillaahi bin Sahl, Muhayyiswah bin Mas'uud waliekea Khaybar wakati wa sulhu. Wakaachana. Muhayyiswah akamjia 'Abdillaahi bin Sahl akiwa ameolewa damu ameuwawa, Akamzika akarudi Madiynah. Wakaenda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), 'Abdur-Rahman bin Sahl, Muhayyiswah na Huwayyiswah watoto wa Mas'uud. 'Abdur-Rahman akazungumza. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: Azungumze mkubwa wenu" Nae alikuwa mdogo wao, akanyamaza. Wakazungumza wawili wao. Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je, mtaapa ili mstahiki fidia kwa muuaji wenu?" Akataja ukamilifu wa Hadiyth. [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

 

 

Hadiyth – 5

وعن جابر رضي الله عنه: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَجْمَعُ بَيْنَ الرَّجُلَيْنِ مِنْ قَتْلَى أُحُد يَعْنِي في القَبْرِ ، ثُمَّ يَقُولُ : (( أيُّهُما أكْثَرُ أخذاً للقُرآنِ ؟ )) فَإذَا أُشيرَ لَهُ إِلَى أحَدِهِمَا قَدَّمَهُ في اللَّحْدِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akijumuisha watu wawili katika waliouliwa Uhud, yaani katika kaburi; kisha hutuuliza: "Ni yupi kati yao amehifadhi Qur-aan?" Anapoashiriwa mmoja wao anamtanguliza katika mwana ndani." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 6

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( أرَانِي فِي المَنَامِ أتَسَوَّكُ بِسِوَاكٍ ، فَجَاءنِي رَجُلانِ ، أحَدُهُما أكبر مِنَ الآخرِ ، فَنَاوَلْتُ السِّوَاكَ الأصْغَرَ ، فَقِيلَ لِي : كَبِّرْ ، فَدَفَعْتهُ إِلَى الأكْبَرِ مِنْهُمَا )) رواه مسلم مسنداً والبخاري تعليقاً .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilijiona usingizini nikipiga msuwaki. Wakanijia watu wawili, mmoja wao ni mkubwa kuliko mwenziwe. Nikataka kumpa msuwaki yule mdogo, hapo nikaambiwa: "Mtangulize mkubwa". Nikampatia huyo mkubwa." [Muslim na Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي موسى رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ مِنْ إجْلالِ اللهِ تَعَالَى : إكْرَامَ ذِي الشَّيْبَةِ المُسْلِمِ ، وَحَامِلِ القُرآنِ غَيْرِ الغَالِي فِيهِ ، وَالجَافِي عَنْهُ ، وَإكْرَامَ ذِي السُّلْطَانِ المُقْسِط )) حديث حسن رواه أَبُو داود .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muusa kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika katika Kumtukuza Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala) ni kumkirimu mzee Muislamu, na kuiacha mbali bila kuitumia, na kumkirimu kiongozi muadilifu".  Hadiyth Hassan. [Abu Daawuud]

 

 

 

Hadiyth – 8

وعن عمرو بن شعيب ، عن أبيه ، عن جده  رضي الله عنهم، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَيْسَ مِنَّا مَنْ لَمْ يَرْحَمْ صَغِيرنَا ، وَيَعْرِفْ شَرَفَ كَبيرِنَا )) حديث صحيح رواه أَبُو داود والترمذي ، وَقالَ الترمذي : (( حديث حسن صحيح )) .

وفي رواية أبي داود : (( حَقَّ كَبيرِنَا )) .

Na imepokewa kutoka kwa 'Amru bin Shu'ayb kutoka kwa babake kutoka kwa babu yake (Radhwiyah Allaahu 'anhuma) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si katika sisi asiye warehemu wadogo wetu na kutambua heshima (utukufu) wa wakubwa wetu." Hadiyth Swahiyh iliyonukuliwa na Abu-Daawuud na At-Tirmidhiy, ambaye amesema: Hadiyth Hassan Swahiyh.

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن ميمون بن أَبي شَبيب رحمه الله : أنَّ عائشة رَضي الله عنها مَرَّ بِهَا سَائِلٌ ، فَأعْطَتْهُ كِسْرَةً ، وَمَرَّ بِهَا رَجُلٌ عَلَيهِ ثِيَابٌ وَهَيْئَةٌ ، فَأقْعَدَتهُ ، فَأكَلَ ، فقِيلَ لَهَا في ذلِكَ ؟ فقَالتْ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أنْزِلُوا النَّاسَ مَنَازِلَهُمْ )) رواه أبو داود . لكن قال : ميمون لم يدرك عائشة . وقد ذكره مسلم في أول صحيحه تعليقاً فقال : وذكر عن عائشة رضي الله عنها قالت : أمرنا رسول الله صلى الله عليه وسلم أن ننـزل الناس منازلهم ، وَذَكَرَهُ الحَاكِمُ أَبُو عبد الله في كتابه (( مَعرِفَة عُلُومِ الحَديث )) وَقالَ : (( هُوَ حديث صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwake 'Maymuuna bin Abu Shabiyb (Rahimmahu Allaah) kuwa 'Aa'ishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) alipitiwa na mwombaji, naye akampatia kisra (mkate). Baadaye, akapita mtu aliyevaa vizuri, akamuomba, naye ('Aa'ishah) akamkalisha chini na akampatia chakula ili ale. Akaulizwa kuhusu hilo, naye akasema: "Rasuli wa Allaah amesema: Wawekeni watu katika vyeo vyao." [Abu Daawuud,aliyesema Maymuun hakukutana na 'Aa'ishah] Na imetajwa na Muslim mwanzo wa Sahihi yake, akasema: Na imetajwa kuwa 'Aa'ishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuamuru kuweka watu katika vyeo vyao. Na Allaah ametuamuru kuwaweka watu kwa vyeo vyao." Ameitaja hiyo Al-Haakim Abu 'Abdillaahi katika kitabu chake (Ma'rifatu 'Uluumil Hadiyth) Akasema ni Hadiyth Swahiyh.

 

 

 

Hadiyth – 10

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَدِمَ عُيَيْنَةُ بنُ حِصْن ، فَنَزَلَ عَلَى ابْنِ أخِيهِ الحُرِّ بنِ قَيسٍ ، وَكَانَ مِنَ النَّفَرِ الَّذِينَ يُدْنِيهِمْ عُمرُ رضي الله عنه، وَكَانَ القُرَّاءُ أصْحَاب مَجْلِس عُمَرَ وَمُشاوَرَتِهِ ، كُهُولاً كاَنُوا أَوْ شُبَّاناً ، فَقَالَ عُيَيْنَةُ لابْنِ أخيهِ : يَا ابْنَ أخِي ، لَكَ وَجْهٌ عِنْدَ هَذَا الأمِيرِ ، فَاسْتَأذِنْ لِي عَلَيهِ ، فاسْتَأذَن له ، فَإذِنَ لَهُ عُمَرُ رضي الله عنه، فَلَمَّا دَخَلَ قَالَ : هِي يَا ابنَ الخَطَّابِ ، فَواللهِ مَا تُعْطِينَا الْجَزْلَ ، وَلا تَحْكُمُ فِينَا بالعَدْلِ ، فَغَضِبَ عُمَرُ رضي الله عنه حَتَّى هَمَّ أنْ يُوقِعَ بِهِ ، فَقَالَ لَهُ الحُرُّ : يَا أميرَ المُؤْمِنينَ ، إنَّ الله تَعَالَى قَالَ لِنَبيِّهِ صلى الله عليه وسلم: ( خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ) وَإنَّ هَذَا مِنَ الجَاهِلِينَ . واللهِ مَا جَاوَزَهاَ عُمَرُ حِينَ تَلاَهَا عليه ، وكَانَ وَقَّافاً عِنْدَ كِتَابِ اللهِ تَعَالَى . رواه البخاري .

Amesema Ibn 'Abbaas (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) Alikuja 'Uyaynah bin Hiswnakashukia kwa mtoto wa nduguye, Al-Hurr bin Qays, mtu wa karibu kwa 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwa ubora wake. Kamati ya shuura ya majlis ya 'Umar walikuwa wasomi, wazee na vijana. 'Uyaynah akamwambia mtoto wa nduguye: "Eemtoto wa ndugu yangu! Wewe una hadhi kwa huyu Amiri, niombee ruhusa nimuone." Akamuombea idhini, na 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) akamruhusu Alipoingia alisema: "Hiy (kutishia), ee Ibn Al-Khatwtwaab: Wa-Allaahi hutupi zawadi wala hutuhukumu kwa uadilifu." Akakasirika 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) akakaribia kumwadhibu, Al'Hurr akamwambia: "Ee Amiri wa Waumini! "Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aala) Alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili." [Al-A'raaf: 199] na huyu ni miongoni mwa wajinga." Wa-Allaahi, aliposikia maneno hayo alitulia tuli, kwani yeye ni mtu mwenye kufuata kabisa Kitabu cha Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aala). [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي سعيد سَمُرة بنِ جُندب رضي الله عنه، قَالَ : لقد كنت عَلَى عَهْدِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم غُلاماً ، فَكُنْتُ أحْفَظُ عَنْهُ ، فَمَا يَمْنَعُنِي مِنَ القَوْلِ إلاَّ أنَّ هاهُنَا رِجَالاً هُمْ أسَنُّ مِنِّي . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

AmesemaAbu Sa'iyd Samurah bin Jundub (Radhwiyah Allaahu 'anhu): Hakika nilikuwa kijana katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na nilikuwa ni mwenye kuhifadhi kutoka kwake. Hakunikataza mimi kuzungumza ila kulikuwepo na watu wakubwa (kiumri) kuniliko." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 12

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَا أكْرَمَ شَابٌّ شَيْخاً لِسِنِّهِ إلاَّ قَيَّضَ الله لَهُ مَنْ يُكْرِمُهُ عِنْدَ سِنِّه )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث غريب )) .

Na imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hatomkirimu kijana mzee kwa ajili ya umri wake isipokuwa Allaah Atamtolea atakaye mkirimu katika uzee wake." [At-Tirmidhiy, na akasema Hadiyth Ghariyb (ngeni)].

 

 

 

 

 

 

Share

045-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwazuru Watu wa Kheri, Kukaa Nao, Kuhusubiana Nao na Kuwapenda

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب زيارة أهل الخير ومجالستهم وصحبتهم ومحبتهم وطلب زيارتهم والدعاء منهم وزيارة المواضع الفاضلة

045-Mlango Wa Kuwazuru Watu wa Kheri, Kukaa Nao, Kuhusubiana Nao na Kuwapenda

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِفَتَاهُ لَا أَبْرَحُ حَتَّىٰ أَبْلُغَ مَجْمَعَ الْبَحْرَيْنِ أَوْ أَمْضِيَ حُقُبًا ﴿٦٠﴾ إِلَى قوله تَعَالَى : قَالَ لَهُ مُوسَىٰ هَلْ أَتَّبِعُكَ عَلَىٰ أَن تُعَلِّمَنِ مِمَّا عُلِّمْتَ رُشْدًا ﴿٦٦﴾

Na pindi Muwsaa alipomwambia kijana wake: Sitoacha kuendelea mpaka nifikie zinapokutana bahari mbili, na nitaendelea muda mrefu. Hadi Kauli Yake T'aalaa: ...Basi walipofika zinapoungana bahari mbili, walimsahau samaki wao; naye akachukua njia yake baharini akiponyoka chini kwa chini. [Al-Kahf: 60-66]

 

وَاصْبِرْ نَفْسَكَ مَعَ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ  ﴿٢٨﴾

Na isubirishe nafsi yako pamoja na wale wanaomuomba Rabb wao asubuhi kabla jua kucha na jioni, wanataka Wajihi Wake. [Al-Kahf: 28]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ أَبُو بكر لِعُمَرَ رضي الله عنهما بَعْدَ وَفَاةِ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم: انْطَلِقْ بِنَا إِلَى أُمِّ أيْمَنَ رضي الله عنها نَزُورُهَا كَمَا كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَزُورُهَا ، فَلَمَّا انْتَهَيَا إِلَيْهَا ، بَكَتْ ، فَقَالاَ لَهَا : مَا يُبْكِيكِ ؟ أمَا تَعْلَمِينَ أنَّ مَا عِنْدَ اللهِ خَيْرٌ لرَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَتْ : مَا أبْكِي أَنْ لاَ أَكُونَ أَعْلَم أنَّ مَا عِنْدَ الله تَعَالَى خَيْرٌ لرسول الله صلى الله عليه وسلم، ولَكِنْ أبكي أنَّ الوَحْيَ قدِ انْقَطَعَ مِنَ السَّماءِ ، فَهَيَّجَتْهُمَا عَلَى البُكَاءِ ، فَجَعَلا يَبْكِيَانِ مَعَهَا . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Abu Bakr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) alimwambia 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) baada ya kuanga dunia kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Twende tukamzuru Ummu Ayman (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) kama alivyokuwa akimzuru Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." Walipofika kwake akalia. Wakamwambia: "Nini kinachokuliza? "Kwani hujui Allaah Aliyomwandalia Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni bora?" Akasema: "Mimi nami silii kwa kuwa sijui yalio kwa Allaah ni bora kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), bali nalia kwa sababu wahyi umekatika toka mbinguni." Wakawa wanalia pamoja naye." [Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم: (( أنَّ رَجُلاً زَارَ أَخَاً لَهُ في قَريَة أُخْرَى ، فَأرْصَدَ الله تَعَالَى عَلَى مَدْرَجَتِهِ مَلَكاً ، فَلَمَّا أتَى عَلَيهِ ، قَالَ : أيْنَ تُريدُ ؟ قَالَ : أُريدُ أخاً لي في هذِهِ القَريَةِ . قَالَ : هَلْ لَكَ عَلَيهِ مِنْ نِعْمَة تَرُبُّهَا عَلَيهِ ؟   قَالَ : لا ، غَيْرَ أنِّي أحْبَبْتُهُ في الله تَعَالَى ، قَالَ : فإنِّي رَسُول الله إلَيْكَ بَأنَّ الله قَدْ أَحَبَّكَ كَمَا أحْبَبْتَهُ فِيهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: " Mtu mmoja alimzuru nduguye katika kijiji kingine. Allaah akamwakilishia Malaika njiani. Alipomfikia alisema: "Unaelekea wapi?" Akasema: "Namtaka ndugu yangu katika kijiji hiki." Akasema: "Una neema yeyote unaipata kwake?" Akasema: "La, isipokuwa mimi nampenda kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa)." Akasema: "Mimi ni mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwako; kuwa Allaah anakupenda kama ulivyompenda ndugu yako kwa ajili Yake." [Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ عَادَ مَرِيضاً أَوْ زَارَ أخاً لَهُ في الله ، نَادَاهُ مُنَادٍ : بِأنْ طِبْتَ ، وَطَابَ مَمْشَاكَ ، وَتَبَوَّأتَ مِنَ الجَنَّةِ مَنْزِلاً )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) ، وفي بعض النسخ : (( غريب )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote mwenye kumtembelea mgonjwa au akamzuru ndugu yake kwa ajili ya Allaah, anaita mwenye kuita: Uwe na furaha, na kwenda kwako kubarikiwe na utunukiwe cheo Peponi." [At-Tirmidhy], ambaye amesema hii ni Hadiyth Hassan, na katika baadhi ya nuskha ni Hadiyth Ghariib (Ngeni)

 

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِنَّمَا مَثلُ الجَلِيسِ الصَّالِحِ وَجَلِيسِ السُّوءِ ، كَحَامِلِ المِسْكِ ، وَنَافِخِ الْكِيرِ ، فَحَامِلُ الْمِسْكِ : إمَّا أنْ يُحْذِيَكَ ، وَإمَّا أنْ تَبْتَاعَ مِنْهُ ، وَإمَّا أنْ تَجِدَ مِنْهُ ريحاً طَيِّبَةً ، وَنَافِخُ الكِيرِ : إمَّا أنْ يُحْرِقَ ثِيَابَكَ ، وَإمَّا أنْ تَجِدَ مِنْهُ رِيحاً مُنْتِنَةً )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mfano wa kikao kizuri na kikao kiovu ni kama mfano wa mchukuaji (mwuzaji) manukato na mfuaji vyuma. Ama mbebaji manukato ima atakupatia (hidaya) au utanunua kutoka kwake au utapata harufu nzuri. Na kwa mfuaji chuma, ima atakuunguzia nguo yako au utapata harufu mbaya kutoka kwake." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( تُنْكَحُ المَرْأَةُ لأَرْبَعٍ : لِمَالِهَا ، وَلِحَسَبِهَا ، وَلِجَمَالِهَا ، وَلِدِينِهَا ، فَاظْفَرْ بِذاتِ الدِّينِ تَربَتْ يَدَاك )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwanamke huolewa kwa sababu nne: Mali yake, nasaba yake, uzuri wake na Dini yake. Tafuta yule mwenye Dini, isije ikafukarika mikono yako (yaani ili upate kubarikiwa)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Hadiyth – 6

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم لِجبريل : (( مَا يَمْنَعُكَ أنْ تَزُورنَا أكثَر مِمَّا تَزُورَنَا ؟ )) فَنَزَلَتْ : ( وَمَا نَتَنَزَّلُ إِلاَّ بِأَمْرِ رَبِّكَ لَهُ مَا بَيْنَ أَيْدِينَا وَمَا خَلْفَنَا وَمَا بَيْنَ ذَلِكَ ) [ مريم : 64 ] رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Jibriyl: "Ni kitu gani kinachokuzuilia kutuzuru kwa wingi zaidi kuliko unavyoturuzuku sasa." Hapo ikateremka ayah inayosema: (Na (sisi Malaika) hatuteremki ila kwa amri ya Rabb wako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم). Ni Yake Yeye yaliyoko mbele yetu, na yaliyoko nyuma yetu, na yaliyoko baina ya hayo). [Maryam: 64] [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لا تُصَاحِبْ إلاَّ مُؤْمِناً ، وَلاَ يَأْكُلْ طَعَامَكَ إلاَّ تَقِيٌّ )) . رواه أَبُو داود والترمذي بإسناد لا بأس بِهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiwe pamoja isipokuwa na Muumini na wala asile chakula chako isipokuwa mcha Mungu." [Abu Daawuud na At-Tirmidhy, kwa Isnaad ambayo si mbaya]

 

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( الرَّجُلُ عَلَى دِينِ خَلِيلِهِ ، فَليَنْظُرْ أَحَدُكُمْ مَنْ يُخَالِلُ )) رواه أَبُو داود والترمذي بإسناد صحيح ، وَقالَ الترمذي : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu  'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu anakuwa katika Dini ya rafiki yake, basi atizame mmoja wenu anayefanya urafiki naye." [Abu Daawuud na At-Tirmidhy na amesema kuwa hii ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه: أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( المَرْءُ مَعَ مَنْ أَحَبَّ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : قيل للنبي صلى الله عليه وسلم: الرَّجُلُ يُحبُّ القَومَ وَلَمَّا يَلْحَقْ بِهِمْ ؟ قَالَ : (( المَرْءُ مَعَ مَنْ أَحَبَّ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu anakuwa pamoja na wale anaowapenda." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na katika riwaayah nyengine amesema: aliambiwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mtu anawapenda watu lakini hatangamani nao?" Akasema: "Mtu anakuwa pamoja na wale aanowapenda."

 

 

 

Hadiyth – 10

وعن أنس رضي الله عنه: أنَّ أعرابياً قَالَ لرسول الله صلى الله عليه وسلم: مَتَى السَّاعَةُ ؟ قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَا أعْدَدْتَ لَهَا ؟ )) قَالَ : حُبَّ الله ورسولهِ ، قَالَ : (( أنْتَ مَعَ مَنْ أحْبَبْتَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ ، وهذا لفظ مسلم .

وفي رواية لهما : مَا أعْدَدْتُ لَهَا مِنْ كَثيرِ صَوْمٍ ، وَلاَ صَلاَةٍ ، وَلاَ صَدَقَةٍ ، وَلَكِنِّي أُحِبُّ الله وَرَسُولَهُ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ya kwamba Mbedui mmoja alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Lini Qiyaamah?" Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Je, umejiandalia nini?" Akasema: "Mapenzi ya Allaah na Rasuli Wake." Akasema: "Wewe uko pamoja na unaowapenda." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud na At-Tirmidhiy]. Na hii ni lafdhi ya Muslim.

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy na Muslim: "Sijajiandaa kwa kwa hicho Qiyaamah kwa funga nyingi wala Swalaah na Swadaqah nyingi lakini mimi nampenda Allaah na Rasuli Wake."

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن ابن مسعود  رضي الله عنه، قَالَ : جاء رجلٌ إلى رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: يَا رَسُول الله ، كَيْفَ تَقُولُ في رَجُلٍ أَحَبَّ قَوْماً وَلَمْ يَلْحَقْ بِهِمْ ؟ فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( المَرْءُ مَعَ مَنْ أحَبَّ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: "Alikuja mtu kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: "Ee Rasuli wa Allaah unasemaje kuhusu mtu ambaye anawapenda watu lakini hajatangamana nao? Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mtu anakuwa pamoja na wale anaowapenda." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 12

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( النَّاسُ مَعَادِنٌ كَمَعَادِنِ الذَّهَبِ وَالفِضَّةِ ، خِيَارُهُمْ في الجَاهِلِيَّةِ خِيَارُهُمْ في الإسْلاَمِ إِذَا فَقهُوا ، وَالأرْوَاحُ جُنُودٌ مُجَنَّدَةٌ ، فَمَا تَعَارَفَ مِنْهَا ائْتَلَفَ ، ومَا تَنَاكَرَ مِنْهَا اخْتَلَفَ )) رواه مسلم .

وروى البخاري قوله: (( الأَرْوَاحُ … )) إلخ مِنْ رواية عائشة رضي الله عنها .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watu ni kama madini ya dhahabu na fedha, mbora wao katika ujahiliya (zama za ujinga) anakuwa mbora katika Uislamu anapokuwa na ufahamu (wa Dini). Na roho zao zinakuwa kama kundi la jeshi, miongoni mwao ni wale wenye sifa zilizosawa, hivyo kuchanganyika na kuwa pamoja na wale wenye sifa tofauti wanatengana na wenziwao." [Muslim] .

Al-Bukhaariy amepokea kauli: "Roho" mpaka mwisho kuwa hii ni riwaayah ya 'Aaishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa).

 

 

 

Hadiyth – 13

وعن أُسَيْر بن عمرو ، ويقال : ابن جابر وَهُوَ - بضم الهمزة وفتح السين المهملة - قَالَ : كَانَ عُمَرُ بْنُ الخَطَّابِ رضي الله عنه إِذَا أتَى عَلَيهِ أمْدَادُ أهْلِ اليَمَنِ سَألَهُمْ : أفِيكُمْ أُوَيْسُ بْنُ عَامِرٍ ؟ حَتَّى أتَى عَلَى أُوَيْسٍ رضي الله عنه ، فَقَالَ لَهُ : أنْتَ أُوَيْسُ ابْنُ عَامِر ؟ قَالَ : نَعَمْ ، قَالَ : مِنْ مُرَادٍ ثُمَّ مِنْ قَرَنٍ ؟ قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : فَكَانَ بِكَ بَرَصٌ ، فَبَرَأْتَ مِنْهُ إلاَّ مَوْضِعَ دِرْهَمٍ ؟ قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : لَكَ وَالِدةٌ ؟ قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( يَأتِي عَلَيْكُمْ أُويْسُ بْنُ عَامِرٍ مَعَ أمْدَادِ أهْلِ اليَمَنِ مِنْ مُرَادٍ ، ثُمَّ مِنْ قَرَنٍ كَانَ بِهِ بَرَصٌ ، فَبَرَأَ مِنْهُ إلاَّ موْضِعَ دِرْهَمٍ ، لَهُ وَالدةٌ هُوَ بِهَا بَرٌّ لَوْ أقْسَمَ عَلَى الله لأَبَرَّهُ ، فإنِ اسْتَطَعْتَ أنْ يَسْتَغْفِرَ لَكَ فَافْعَل )) فَاسْتَغْفِرْ لي فَاسْتَغْفَرَ لَهُ ، فَقَالَ لَهُ عُمَرُ : أيْنَ تُريدُ ؟ قَالَ : الكُوفَةَ ، قَالَ : ألاَ أكْتُبُ لَكَ إِلَى عَامِلِهَا ؟ قَالَ : أكُونُ في غَبْرَاءِ النَّاسِ أَحَبُّ إِلَيَّ ، فَلَمَّا كَانَ مِنَ العَامِ المُقْبِلِ حَجَّ رَجُلٌ مِنْ أشْرَافِهِمْ ، فَوافَقَ عُمَرَ ، فَسَألَهُ عَنْ أُوَيْسٍ ، فَقَالَ : تَرَكْتُهُ رَثَّ البَيْتِ قَليلَ المَتَاع ، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقولُ : (( يَأتِي عَلَيْكُمْ أُوَيْسُ بْنُ عَامِرٍ مَعَ أمْدَادٍ مِنْ أهْلِ اليَمَنِ مِنْ مُرَادٍ ، ثُمَّ مِنْ قَرَنٍ ، كَانَ بِهِ بَرَصٌ فَبَرَأَ مِنْهُ إلاَّ مَوضِعَ دِرْهَمٍ ، لَهُ وَالِدَةٌ هُوَ بِهَا بَرٌّ لَوْ أقْسَمَ عَلَى اللهِ لأَبَرَّهُ ، فَإنِ اسْتَطْعتَ أنْ يَسْتَغْفِرَ لَكَ ، فَافْعَلْ )) فَأتَى أُوَيْساً ، فَقَالَ : اسْتَغْفِرْ لِي . قَالَ : أنْتَ أحْدَثُ عَهْداً بسَفَرٍ صَالِحٍ ، فَاسْتَغْفِرْ لي . قَالَ : لَقِيتَ عُمَرَ ؟ قَالَ : نَعَمْ ، فاسْتَغْفَرَ لَهُ ، فَفَطِنَ لَهُ النَّاسُ ، فَانْطَلَقَ عَلَى وَجْهِهِ . رواه مسلم .

وفي رواية لمسلم أيضاً عن أُسَيْر بن جابر رضي الله عنه: أنَّ أهْلَ الكُوفَةِ وَفَدُوا عَلَى عُمَرَ رضي الله عنه، وَفِيهمْ رَجُلٌ مِمَّنْ كَانَ يَسْخَرُ بِأُوَيْسٍ ، فَقَالَ عُمَرُ : هَلْ هاهُنَا أَحَدٌ مِنَ القَرَنِيِّينَ ؟ فَجَاءَ ذلِكَ الرَّجُلُ ، فَقَالَ عمرُ : إنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَدْ قَالَ : (( إنَّ رَجُلاً يَأتِيكُمْ مِنَ اليَمَنِ يُقَالُ لَهُ : أُوَيْسٌ ، لاَ يَدَعُ باليَمَنِ غَيْرَ أُمٍّ لَهُ ، قَدْ كَانَ بِهِ بَيَاضٌ فَدَعَا الله تَعَالَى ، فَأذْهَبَهُ إلاَّ مَوضِعَ الدِّينَارِ أَو الدِّرْهَمِ ، فَمَنْ لَقِيَهُ مِنْكُمْ ، فَلْيَسْتَغْفِرْ لَكُمْ )) . 

وفي رواية لَهُ : عن عمر رضي الله عنه، قَالَ : إنِّي سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول :(( إنَّ خَيْرَ التَّابِعِينَ رَجُلٌ يُقَالُ لَهُ : أُوَيْسٌ ، وَلَهُ وَالِدَةٌ وَكَانَ بِهِ بَيَاضٌ ، فَمُرُوهُ ، فَلْيَسْتَغْفِرْ لَكُمْ )) .

Imepokewa kutoka kwa Usayr bin 'Amru (Radhwiyah Allaahu 'anhu), Imesemwa ni Ibn Jaabir (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "'Umar bin Al-Khataab (Radhwiyah Allaahu 'anhu) anapojiwa na kundi kutoka Yemen huwauliza: "Ndani yenu yupo Uways bin 'Aamir?" Mpaka siku hiyo akamkuta Uways, akamwambia: "Wewe ni Uways bin 'Aamir?" Akasema: "Ndio." Akasema: "Kutoka kabila la Muraad, kutoka ukoo wa Qaran?" akasema: "Ndio." Akasema: "Ulikuwa na mbalanga ukapona isipokuwa sehemu kiasi cha dirhamu?" Akasema: "Ndio'" Akasema: "Una mama?" Akasema: "Ndio." Akasema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akisema: "Atakujieni Uways pamoja na kundi la watu wa Yemen kabila la Muraad, kisha kwa Qaran. Alikuwa na mbalanga akapona isipokuwa sehemu ndogo mfano wa dirhamu. Ana mama anayemtendea wema, lau ataapa kwa Allaah atamtimizia. Ukiweza kumpata ili akuombee maghfira fanya." Hivyo niombee msamaha kwa Allaah, naye akamuombea. 'Umar akamwambia: "Unakwenda wapi?" Akasema; "Kufah." Akasema: "Je, nikuandikie kwa gavana wake? Akasema; "Kuwa katika watu maskini ni bora kwangu. Ulipofika mwaka uliofuata walihiji watu watukufu kutoka Kufah nao walikutana na 'Umar, akawauliza kuhusu Uways. Akasema: "Nimemuacha katika nyumba mbaya, samani chache." Akasema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akisema: "Atakujieni Uways pamoja na kundi la watu wa Yemen kabila la Muraad, kisha kwa Qaran. Alikuwa na mbalanga akapona isipokuwa sehemu ndogo mfano wa dirhamu. Ana mama anayemtendea wema, lau ataapa kwa Allaah atamtimizia. Ukiweza kumpata ili akuombee maghfira fanya." Akamjia Uways akamwambia: "Niombee msamaha kwa Allaah." Akasema: 'Wewe umerudi punde safarini niombee msamaha."Akamuuliza: "Je, umekutana na 'Umar?" Akasema: "Ndio." Akamuombea maghfira, watu wakamgundua." [Muslim]

Na riwaayah ya Muslim toka kwa Usayr bin Jaabir (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa watu wa Kufah walipeleka wawakilishi wao kwa 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu), Miongoni mwao alikuwepo mtu aliyekuwa akimdhihaki Uways. Akasema 'Umar: "Hapa yupo yeyote kutoka ukoo wa Qaran?" Yule mtu akaja mbele. Akasema 'Umar: "Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika atakujieni mtu kutoka Yemen anaitwa Uways. Amemuacha mamake peke yake, ana weupe (mbalanga) akamuomba Allaah (Subhaanahu Wa Ta'aalaa). Allaah akauondoa isipokuwa sehemu ndogo mfano wa dinari au dirhamu. Atakayekutana naye miongoni mwenu amtake amuombee maghfira kwa Allaah." 

Katika riwaayah yake kutoka kwa 'Umar amesema: "Hakika nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mbora wa Tabi'in ni mtu anayeitwa Uways. Ana mama yake na weupe katika mwili wake. Nendeni kwake na mumuombe awaombee maghfira."

 

 

 

Hadiyth – 14

وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه، قَالَ : اسْتَأذَنْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم في العُمْرَةِ ، فَأذِنَ لِي ، وَقالَ : (( لاَ تَنْسَنا يَا أُخَيَّ مِنْ دُعَائِكَ )) فَقَالَ كَلِمَةً مَا يَسُرُّنِي أنَّ لِي بِهَا الدُّنْيَا

وفي رواية : وَقالَ : (( أشْرِكْنَا يَا أُخَيَّ في دُعَائِكَ )) .

حديث صحيح رواه أَبُو داود والترمذي، وَقالَ: (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khattaab (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye alisema: "Nilimuomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)ruhusa ya kwenda kufanya Umrah, naye alinipatia idhini. Na akasema: "Ee ndugu yangu! Usitusahau katika dua'a zako." Akasema (Radhwiyah Allaahu 'anhu):"Hili ni neno ambalo sitataka kubadilishana hata na dunia yote."

Na katika riwaayah nyingine, alisema: "Ee ndugu yangu! Tushirikishe katika dua yako."

Hadiyth Swahiyh iliyonukuliwa na Abu Daawuud na At-Tirmidhiy, ambaye amesema kuwa hii ni Hadiyth Swahiyh.

 

 

 

Hadiyth – 15

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يزور قُبَاءَ رَاكِباً وَمَاشِياً ، فَيُصَلِّي فِيهِ رَكْعَتَيْنِ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يَأتي مَسْجِد قُبَاءَ كُلَّ سَبْتٍ رَاكباً ، وَمَاشِياً وَكَانَ ابْنُ عُمَرَ يَفْعَلُهُ .

Imepokewa kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) ambaye amesema: "Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akizuru Qubaa (Msikiti wa sehemu hiyo) akiwa amepanda (mnyama) na kwa miguu. Na alikuwa akiswali katika Msikiti huo rakaa mbili." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad].

Katika riwaayah nyingine: "Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiuzuru Msikiti wa Qubaa kila siku ya Jumamosi kwa kupanda mnyama na kwa miguu (wakatika mwengine). Na Ibn 'Umar alikuwa akifanya hivyo."

 

 

 

 

 

Share

046-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila za Kupenda kwa Ajili ya Allaah na Kuhimiza hilo

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل الحب في الله والحث عَلَيهِ وإعلام الرجل من يحبه ، أنه يحبه ، وماذا يقول لَهُ إِذَا أعلمه

046-Mlango Wa Fadhila za Kupenda kwa Ajili ya Allaah na Kuhimiza hilo

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

مُّحَمَّدٌ رَّسُولُ اللَّـهِ ۚ وَالَّذِينَ مَعَهُ أَشِدَّاءُ عَلَى الْكُفَّارِ رُحَمَاءُ بَيْنَهُمْ ۖ ﴿٢٩﴾

Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ni Rasuli wa Allaah. Na wale walio pamoja naye ni wakali zaidi dhidi ya makafiri; wanahurumiana baina yao. [Al-Fat-h: 29] Hadi mwisho wa Surah.

 

وَالَّذِينَ تَبَوَّءُوا الدَّارَ وَالْإِيمَانَ مِن قَبْلِهِمْ يُحِبُّونَ مَنْ هَاجَرَ إِلَيْهِمْ ﴿٩﴾

Na wale waliokuwa na masikani (Madiynah) na wakawa na iymaan kabla yao, wanawapenda wale waliohajiri kwao. [Al-Hashr: 9]

 

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أنسٍ رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( ثَلاثٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ وَجَدَ بِهِنَّ حَلاوَةَ الإيمانِ : أنْ يَكُونَ اللهُ وَرَسُولُهُ أحَبَّ إِلَيْهِ مِمَّا سَوَاهُمَا ، وَأنْ يُحِبّ المَرْءَ لاَ يُحِبُّهُ إلاَّ للهِ ، وَأَنْ يَكْرَهَ أنْ يَعُودَ في الكُفْرِ بَعْدَ أنْ أنْقَذَهُ الله مِنْهُ ، كَمَا يَكْرَهُ أنْ يُقْذَفَ في النَّارِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Sifa tatu yeyote mwenye kuwa nazo atapata ladha (utamu) wa Imani: Kuwa Allaah na Rasuli Wake ndiyo awapendao zaidi kuliko wasiokuwa wao; (la pili) kumpenda mtu kwa ajili ya Allaah Peke Yake, (la tatu) kuchukia kurudi katika ukafiri kama anavyochukia kutupwa motoni. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( سَبْعَةٌ يُظِلُّهُمُ اللهُ في ظِلِّهِ يَوْمَ لاَ ظِلَّ إلاَّ ظِلُّهُ : إمَامٌ عَادِلٌ ، وَشَابٌّ نَشَأ في عِبَادَةِ الله (عزّ وجلّ)، وَرَجُلٌ قَلْبُهُ مُعَلَّقٌ بِالمَسَاجِدِ ، وَرَجُلاَنِ تَحَابّا في اللهِ اجْتَمَعَا عَلَيهِ وتَفَرَّقَا عَلَيهِ ، وَرَجُلٌ دَعَتْهُ امْرَأةٌ ذَاتُ حُسْنٍ وَجَمَالٍ ، فَقَالَ : إنِّي أخَافُ الله ، وَرَجُلٌ تَصَدَّقَ بِصَدَقَةٍ ، فَأخْفَاهَا حَتَّى لاَ تَعْلَمَ شِمَالُهُ مَا تُنْفِقُ يَمِينُهُ ، وَرَجُلٌ ذَكَرَ الله خَالِياً فَفَاضَتْ عَيْنَاهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watu saba atawafunika chini ya kivuli Chake siku hakuna kivuli isipokuwa kivuli Chake: Imamu (kiongozi) muadilifu, kijana aliyeinukia katika kumuabudu Allaah ('Azza wa Jall), na mtu moyo wake umetundikwa Msikitini, na watu wawili wamependana kwa ajili ya Allaah, wakajumuika juu yake, na kufarikiana kwa ajili Yake, na mtu ameitwa na mwanamke mzuri mwenye kuvutia, akasema: 'Mimi namwogoa Allaah,' na mtu aliyetoa sadaka akaificha hadi kushoto kwake kusijue ulichotoa kulia kwake, na mtu amemtaja Allaah faraghani macho yake yakabubujika machozi." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنّ الله تَعَالَى يقول يَوْمَ القِيَامَةِ : أيْنَ المُتَحَابُّونَ بِجَلالِي ؟ اليَوْمَ أُظِلُّهُمْ فِي ظِلِّي يَوْمَ لاَ ظِلَّ إلاَّ ظِلِّي )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa atasema Siku ya Qiyaamah: "Wawapi waliopendana kwa Utukufu Wangu?, Leo nitawafunika katika kivuli Changu siku hakuna kivuli isipokuwa kivuli Changu." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( والَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ ، لا تَدْخُلُوا الجَنَّةَ حَتَّى تُؤْمِنُوا ، وَلا تُؤْمِنُوا حَتَّى تَحَابُّوا ، أوَلاَ أدُلُّكُمْ عَلَى شَيْءٍ إِذَا فَعَلْتُمُوهُ تَحَابَبْتُمْ ؟ أفْشُوا السَّلامَ بينكم )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mkononi Mwake! Hamtaingia Peponi hadi Muamini, wala hamtaamini mpaka mpendane. Je niwaonyeshe kitu mkikifanya mtapendana? Enezeni salamu baina yenu." [Muslim].

 

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: (( أنَّ رَجُلاً زَارَ أخاً لَهُ في قَرْيَةٍ أخْرَى ، فَأرصَدَ اللهُ لَهُ عَلَى مَدْرَجَتِهِ مَلَكاً … )) وذكر الحديث إِلَى قوله : (( إنَّ الله قَدْ أحبَّكَ كَمَا أحْبَبْتَهُ فِيهِ )) رواه مسلم ، وقد سبق بالباب قبله .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu mmoja alimzuru nduguye katika Kijiji chengine. Allaah alimwakilisha Malaika njiani...." Akataja hadiyth hadi kauli yake: "Hakika Allaah amekupenda kama ulivyompenda ndugu yako kwa ajili Yake." [Muslim]. Imetanguliwa kutajwa katika mlango uliofuata.

 

 

 

Hadiyth – 6

وعن البرَاءِ بن عازب رضي الله عنهما ، عن النَّبيّ  صلى الله عليه وسلم أنَّهُ قَالَ في الأنصار : (( لاَ يُحِبُّهُمْ إلاَّ مُؤمِنٌ ، وَلاَ يُبْغِضُهُمْ إلاَّ مُنَافِقٌ ، مَنْ أحَبَّهُمْ أَحَبَّهُ الله ، وَمَنْ أبْغَضَهُمْ أبْغَضَهُ الله )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Al-Baraa'i bin 'Aazib (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ya kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema yafuatayo kuhusu Ansari: "Hawapendi wao isipokuwa Muumini na hawachukii isipokuwa mnafiki. Kwa hiyo Allaah Atampenda anayewapenda na Atamchukia anayewachukia." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 7

وعن معاذ رضي الله عنه، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( قَالَ الله (عزّ وجلّ) : المُتَحَابُّونَ في جَلالِي ، لَهُمْ مَنَابِرُ مِنْ نُورٍ يَغْبِطُهُمُ النَّبِيُّونَ وَالشُّهَدَاءُ )) . رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Na imepokewa kutoka kwake Mu'aadh (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Amesema Allaah ('Azza wa Jall): Wanaopendana kwa ajili ya Utukufu Wangu, watakaa katika minbari za nuru huku Manabii na mashahidi wakitamani hadhi na kheri hiyo." [At-Tirmidhiy, ambaye amesema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي إدريس الخولاني رحمه الله ، قَالَ :دخَلْتُ مَسْجِدَ دِمَشْقَ ، فَإذَا فَتَىً بَرَّاق الثَّنَايَا وَإِذَا النَّاسُ مَعَهُ ، فَإِذَا اخْتَلَفُوا في شَيْءٍ ، أَسْنَدُوهُ إِلَيْه ، وَصَدَرُوا عَنْ رَأيِهِ ، فَسَأَلْتُ عَنْهُ ، فَقيلَ : هَذَا مُعَاذُ بْنُ جَبَل رضي الله عنه. فَلَمَّا كَانَ مِنَ الغَدِ ، هَجَّرْتُ ، فَوَجَدْتُهُ قَدْ سَبَقَنِي بالتَّهْجِيرِ ، ووَجَدْتُهُ يُصَلِّي ، فانْتَظَرتُهُ حَتَّى قَضَى صَلاتَهُ ، ثُمَّ جِئْتُهُ مِنْ قِبَلِ وَجْهِهِ ، فَسَلَّمْتُ عَلَيهِ ، ثُمَّ قُلْتُ : وَاللهِ إنّي لأَحِبُّكَ لِله ، فَقَالَ : آلله ؟ فَقُلْتُ : اللهِ ، فَقَالَ : آللهِ ؟ فَقُلْتُ : اللهِ ، فَأخَذَنِي بِحَبْوَةِ رِدَائِي ، فجبذني إِلَيْهِ ، فَقَالَ : أبْشِرْ ! فإنِّي سَمِعْتُ رَسُولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( قَالَ الله تَعَالَى : وَجَبَتْ مَحَبَّتي لِلْمُتَحابين فيَّ ، وَالمُتَجَالِسينَ فيَّ ، وَالمُتَزَاوِرِينَ فيَّ ، وَالمُتَبَاذِلِينَفِيَّ )) حديث صحيح رواه مالك في الموطأ بإسناده الصحيح .

Imepokewa kutoka kwa Abu Idris Al-Khawlaani (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Niliingia Msikiti wa Damascus, nikamuona kijana ana meno meupe masafi (mwenye kutabasamu sana), watu wako pamoja naye. Watu wanapotofautiana katika jambo walikuwa wakitaka na kuichukua rai yake. Nikauliza kuhusu yeye na nikaambiwa: 'Huyu ni Mu'aadh bin Jabal (Radhwiyah Allaahu 'anhu). Siku ya pili nilifika mapema Msikitini lakini nikapata kuwa ameshafika kabla yangu. Nilimpata yeye anaswali hivyo nilingojea mpaka akamaliza Swalah yake. Hapo nilikwenda mbele yake na kumsalimia, kisha nikamwambia: 'Naapa kwa Allaah kuwa mimi nakupenda kwa ajili ya Allaah.' Akasema: 'je, ni kwa ajili ya Allaah?' Nikasema: 'Ndio, kwa ajili ya Allaah.' Akasema: 'Je, ni kwa ajili ya Allaah?' Nikasema: 'Ndio kwa ajili ya Allaah.' Hapo akanishika kwa mkunjo wa shuka yangu na kunileta karibu naye, akasema: 'Hakika nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: Amesema Allaah Ta'aalaa! Ni wajibu kuwapenda wale wanaopendana kwa ajili Yangu, na wenye kukaa pamoja kwa ajili Yangu na wenye kutembeleana kwa ajili Yangu na wenye kusaidiana kwa ajili Yangu." [Hadiyth Swahiyh iliyonukuliwa na Imam Malik katika al-Muwatta' kwa Isnaad iliyo Swahiyh]

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي كَرِيمَةَ المقداد بن معد يكرب رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا أَحَبَّ الرَّجُلُ أخَاهُ ، فَليُخْبِرْهُ أَنَّهُ يُحِبُّهُ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وَقالَ :(( حديث صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Kariimah al-Miqdaad bin Ma'diyakrib (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ndugu mmoja anapompenda mwenziwe, ampashe habari ya kuwa anampenda." [Abu Daawuud na At-Tirmidhiy, ambaye amesema kuwa ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Hadiyth – 10

وعن معاذ رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم أخذ بيدهِ ، وَقالَ : (( يَا مُعَاذُ ، وَاللهِ ، إنِّي لأُحِبُّكَ ، ثُمَّ أُوصِيكَ يَا مُعَاذُ لاَ تَدَعَنَّ في دُبُرِ كُلِّ صَلاَةٍ تَقُولُ : اللَّهُمَّ أعِنِّي عَلَى ذِكْرِكَ ، وَشُكْرِكَ ، وَحُسْنِ عِبَادَتِكَ )) حديث صحيح ، رواه أَبُو داود والنسائي بإسناد صحيح .

Imepokewa kutoka kwa Mu'aadh (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimshika mkono wake na kumwambia: "Ee Mu'aadh! Naapa kwa Allaah kuwa nakupenda, kisha nakuusia ee Mu'aadh; Usiache kusema kila baada ya Swalah ya faradhi maneno yafuatayo: 'Ee Mola Wangu! Nisaidie katika kukutaja na kukushukuru na kukuabudu katika njia bora kabisa." [Hadiyth Swahiyh iliyonukuliwa na Abu Daawuud na An-Nasai kwa isnaad swahiyh]

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن أنس رضي الله عنه: أنَّ رَجُلاً كَانَ عِنْدَ النَّبيِّ ، صلى الله عليه وسلم، فَمَرَّ رَجُلٌ بِهِ ، فَقَالَ : يَا رَسُول الله ، أنِّي لأُحِبُّ هَذَا ، فَقَالَ لَهُ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: (( أأعْلَمْتَهُ ؟ )) قَالَ : لا . قَالَ : (( أعْلِمْهُ )) فَلَحِقَهُ ، فَقَالَ : إنِّي أُحِبُّكَ في الله ، فَقَالَ : أَحَبَّكَ الَّذِي أحْبَبْتَنِي لَهُ . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .

Na imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ya kwamba: "Kwa hakika kulikuwa na mtu pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akapita mbele yao mtu mwingine. Akasema: 'Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nampenda huyu mtu.' Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: 'Je, umemjulisha hili?' Akasema: 'La! Akamwambia: 'Basi kamjulishe hilo.' Aliondoka huyu mtu na kukutana naye na hapo akamwambia: 'Hakika mimi nakupenda kwa ajili ya Allaah.' Akasema: 'Akupende Allaah ambaye kwa ajili Yake umenipenda mimi'." [Abu Daawuud kwa isnaad iliyo swahiyh]

 

 

 

 

 

Share

047-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Alama za Upendo wa Allaah kwa Waja Wake na Kuhimizwa Kujipamba Nayo na Kuitafuta

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب علامات حب الله تَعَالَى للعبد والحث عَلَى التخلق بِهَا والسعي في تحصيلها

047-Mlango Wa Alama za Upendo wa Allaah kwa Waja Wake na Kuhimizwa Kujipamba Nayo na Kuitafuta

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣١﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi, Atakupendeni Allaah na Atakughufurieni dhambi zenu. Na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Aal-'Imraan: 31]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَن يَرْتَدَّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ يَأْتِي اللَّـهُ بِقَوْمٍ يُحِبُّهُمْ وَيُحِبُّونَهُ أَذِلَّةٍ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ يُجَاهِدُونَ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَلَا يَخَافُونَ لَوْمَةَ لَائِمٍ ۚ ذَٰلِكَ فَضْلُ اللَّـهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَاللَّـهُ وَاسِعٌ عَلِيمٌ ﴿٥٤﴾

Enyi walioamini! Yeyote atakayeritadi miongoni mwenu kutoka Dini yake, basi Allaah Ataleta watu (badala yao) Atakaowapenda nao watampenda; wanyenyekevu kwa Waumini, washupavu juu ya makafiri; wanafanya jihaad katika njia ya Allaah na wala hawakhofu lawama za mwenye kulaumu. Hiyo ni fadhila ya Allaah Humpa Amtakaye. Na Allaah ni Mwenye wasaa, Mjuzi wa yote. [Al-Maaidah: 54]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ الله تَعَالَى قَالَ : مَنْ عَادَى ليَ وَلِيّاً ، فَقَدْ آذَنْتُهُ بِالحَرْبِ ، وَمَا تَقَرَّبَ إِلَيَّ عَبْدِي بِشَيءٍ أَحَبَّ إِلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُ عَلَيهِ ، وَمَا يَزالُ عَبْدِي يَتَقَرَّبُ إِلَيَّ بِالنَّوَافِلِ حَتَّى أُحِبَّهُ ، فَإِذَا أحْبَبْتُهُ ، كُنْتُ سَمْعَهُ الَّذِي يَسْمَعُ بِهِ ، وَبَصَرَهُ الَّذِي يُبْصِرُ بِهِ ، ويَدَهُ الَّتي يَبْطِشُ بِهَا ، وَرجْلَهُ الَّتِي يَمْشِي بِهَا وَإنْ سَألَنِي أعْطَيْتُهُ ، وَلَئِن اسْتَعَاذَنِي لأعِيذَنَّهُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa amesema: "Mwenye kumfanyia uadui rafiki yangu basi Nimemtangazia vita. Hajikurubishi Kwangu mja Wangu kwa kitu ninachokipenda zaidi kuliko nilichomfaradhishia, Na mja haachi kujikurubishi kwangu kwa Sunnah mpaka Nimpende. Ninapompenda, Ninakuwa sikio lake analosikilizia, na jicho lake analoonea, na mkono wake anaoshikia, na mguu wake anayotembelea, Akiniomba Nitampa, na akijilinda kwangu Nitamlinda." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا أَحَبَّ اللهُ تَعَالَى العَبْدَ ، نَادَى جِبْريلَ : إنَّ الله تَعَالَى يُحِبُّ فُلاناً ، فَأَحْبِبْهُ ، فَيُحِبُّهُ جِبريلُ ، فَيُنَادِي في أَهْلِ السَّمَاءِ : إنَّ اللهَ يُحِبُّ فُلاناً ، فَأحِبُّوهُ ، فَيُحِبُّهُ أهْلُ السَّمَاءِ ، ثُمَّ يُوضَعُ لَهُ القَبُولُ في الأرْضِ )) متفق عليه . وفي رواية لمسلم : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ الله تعالى إذا أحب عبداً دعا جبريلَ ، فقال : إنّي أُحِبُّ فلاناً فأحببهُ ، فيحبُّهُ جبريلُ ، ثمَّ ينادي في السماءِ ، فيقول : إنَّ اللهَ يحبُّ فلاناً فأحبوهُ ، فيحبُّهُ أهلُ السماءِ ، ثمَّ يوضعُ لهُ القبولُ في الأرضِ ، وَإِذَا أبْغَضَ عَبْداً دَعَا جِبْريلَ ، فَيَقُولُ : إنّي أُبْغِضُ فُلاناً فَأبْغِضْهُ . فَيُبغِضُهُ جِبريلُ ثُمَّ يُنَادِي في أَهْلِ السَّماءِ : إنَّ الله يُبْغِضُ فُلاناً فَأبْغِضُوهُ ، ثُمَّ تُوضَعُ لَهُ البَغْضَاءُ في الأَرْضِ )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah Ta'aalaa anapompenda mja anamuita Jibriyl na kumwambia: "Hakika Allaah Ta'aalaa anampenda Fulani, hivyo nawe mpende." Hivyo Jibriyl anampenda mtu huyo na baada ya hapo anatangaza kwa watu wa mbinguni kwamba: 'Hakika Allaah anampenda fulani, kwa hivyo nanyi nyote mpendeni.' Hapo watu wa mbinguni wanampenda mtu huyo. Kisha anawekewa kukubaliwa na watu wa ardhini. [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na katika riwaayah ya Muslim: Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika Allaah Ta'aalaa anapompenda mja, anamuita Jibriyl, na kumwambia: "Hakika Mimi nampenda fulani, nawe mpende." Hivyo Jibriyl anampenda mtu huyo na baada ya hapo anatangaza mbinguni kwa kusema: 'Hakika Allaah anampenda fulani, kwa hivyo nanyi nyote mpendeni.' Hapo watu wa mbinguni nao pia wanampenda mtu huyo. Kisha anawekewa kabuli (kukubaliwa) na watu wa ardhini. Na Allaah anapomchukia mtu yeyote anamuita Jibriyl na kumwambia: "Hakika Mimi namchukia fulani, nawe mchukie." Hivyo Jibriyl ('Alayhi salaam) anamchukia mtu huyo na baada ya hapo anatangaza kwa watu wa mbinguni kwamba: "Hakika Allaah anamchukia fulani, kwa hivyo nanyi nyote mchukieni." Hapo watu wa mbinguni nao pia wanamchukia mtu huyo. Kisha anawekewa chuki na watu wa ardhini." 

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بعث رجلاً عَلَى سَريَّة فَكَانَ يَقْرَأُ لأَصْحَابِهِ في صَلاَتِهِمْ فَيَخْتِمُ بـ ( قُل هُوَ الله أَحَدٌ ) ، فَلَمَّا رَجَعُوا ذَكَرُوا ذلِكَ لرسول الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : (( سَلُوهُ لأَيِّ شَيْءٍ يَصْنَعُ ذلِكَ )) ؟ فَسَألُوهُ فَقَالَ : لأَنَّهَا صِفَةُ الرَّحْمانِ فَأَنَا أُحِبُّ أنْ أقْرَأ بِهَا . فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أخْبِرُوهُ أنَّ اللهَ تَعَالَى يُحِبُّهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah alimchagua mtu kuongoza kikosi cha Sarriyah kuwaongoza wenzake katika vita. Akawa katika Swalaah zake zote alizokuwa akiswalisha wenzake akimalizia na (قُل هُوَ الله أَحَدٌ). Waliporudi (Madinah), Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alielezwa hilo, naye akawaambia: "Muulizeni ni kwa sababu gani anafanya hivyo?" Wakamuuliza, naye akasema: "Kwa sababu humo ndani zipo sifa za Ar-Rahmaan (Mwingi wa Rehma), nami napenda kuzisoma." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Mpeni habari ya kwamba Allaah Ta'aalaa anampenda." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

048-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Onyo kwa Wenye Kuwaudhi Watu Wema, Wanyonge na Masikini

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب التحذير من إيذاء الصالحين والضعفة والمساكين

048-Mlango Wa Onyo kwa Wenye Kuwaudhi Watu Wema, Wanyonge na Masikini

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾

Na wale wanaowaudhi Waumini wa kiume na Waumini wa kike bila ya kuwa wamechuma kosa, basi kwa yakini wamejibebea usingiziaji mkuu wa dhulma na dhambi bayana. [Al-Ahzaab: 58]

 

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ ﴿٩﴾وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ ﴿١٠﴾

Kwa hivyo basi yatima usimuonee.Na mwombaji usimkaripie. [Adhw-Dhwuhaa: 9-10]

 

وأما الأحاديث ، فكثيرة مِنْهَا :

حديث أَبي هريرة رضي الله عنه في الباب قبل هَذَا : (( مَنْ عَادَى لِي وَليّاً فَقَدْ آذَنْتُهُ بِالحَرْبِ )) .

ومنها حديث سعد بن أَبي وقاص رضي الله عنه السابق في باب ملاطفة اليتيم ، وقوله صلى الله عليه وسلم: (( يَا أَبَا بَكْرٍ ، لَئِنْ كُنْتَ أغْضَبْتَهُمْ لَقَدْ أغْضَبْتَ رَبَّكَ )) .

Ama Hadiyth ni nyingi, miongoni mwa hizo ni zifuatazo: Toka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu): "Yeyote atakayefanya uadui na rafiki yangu basi Nimetangaza vita naye."  

Na Hadiyth ya sa'ad bin Abi Waqqaas (Radhwiyah Allaahu 'anhu): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ee Abu Bakr! Ikiwa umewakasirisha, hakika utakuwa umemkasirisha Rabb wako." 

 

 

Hadiyth – 1

وعن جندب بن عبد الله رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ صَلَّى صَلاةَ الصُّبْحِ ، فَهُوَ في ذِمَّةِ الله ، فَلاَ يَطْلُبَنَّكُمُ الله مِنْ ذِمَّتِهِ بِشَيْءٍ ، فَإنَّهُ مَنْ يَطْلُبُهُ مِنْ ذِمَّتِهِ بِشَيْءٍ يُدْرِكْهُ ، ثُمَّ يَكُبُّهُ عَلَى وَجْهِهِ في نَارِ جَهَنَّمَ )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Jundub bin 'Abdillaah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuswali Swalaah ya Asubuhi yupo katika dhima (himaya) ya Allaah. Hivyo jihadharini Allaah Kuwadai katika dhimma yake chochote, Kwani Anayemtaka dhimmayake atamdiriki, kisha Kumtupa katika Moto wa Jahanam." [Muslim]

Na katika Riwaayah: "Atakayeswali Swalaah ta asubuhi katika Jamaa." 

 

 

 

 

Share

049-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwahukumu Watu kwa Dhahiri ya Mambo na Kumwachia Allaah Siri Zao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب إجراء أحكام الناس عَلَى الظاهر وسرائرهم إِلَى الله تَعَالَى

049-Mlango Wa Kuwahukumu Watu kwa Dhahiri ya Mambo na Kumwachia Allaah Siri Zao

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

فَإِن تَابُوا وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ فَخَلُّوا سَبِيلَهُمْ ۚ ﴿٥﴾

Lakini wakitubu, na wakasimamisha Swalaah na wakatoa Zakaah, basi iacheni njia yao (huru). [At-Tawbah: 5]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أُمِرْتُ أنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى يَشْهَدُوا أنْ لاَ إلهَ إلاَّ الله ، وَأنَّ مُحَمَّداً رَسُول الله ، وَيُقيمُوا الصَّلاةَ ، وَيُؤتُوا الزَّكَاةَ ، فَإِذَا فَعَلُوا ذلِكَ عَصَمُوا مِنِّي دِمَاءهُمْ وَأمْوَالَهُمْ إلاَّ بحَقِّ الإسْلاَمِ ، وَحِسَابُهُمْ عَلَى الله تَعَالَى )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nimeamrishwa kupigana na watu mpaka wakubali kuwa hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah, kusimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah.Wakifanya hivyo zitahifadhika damu zao na mali yao isipokuwa kwa haki ya Uislamu, na hesabu yao iko kwa Allaah Ta'aalaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي عبدِ الله طارِق بن أشَيْم رضي الله عنه، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَنْ قالَ لاَ إلهَ إلاَّ الله ، وَكَفَرَ بما يُعْبَدُ مِنْ دُونِ اللهِ ، حَرُمَ مَالُهُ وَدَمُهُ ، وَحِسَابُهُ عَلَى الله تَعَالَى )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu 'Abdillaah Twaariq bin Ushaym amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kusema Laa ilaaha illa-Allaah, na akakufuru vyote vinavyoabudiwa kinyume na Allaah, atahifadhiwa mali na damu yake, na hesabu yake itakuwa kwa Allaah Ta'aalaa." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي معبد المقداد بن الأسْود رضي الله عنه ، قَالَ : قُلْتُ لرسول الله صلى الله عليه وسلم: أرَأيْتَ إنْ لَقِيتُ رَجُلاً مِنَ الكُفَّارِ ، فَاقْتتَلْنَا ، فَضَرَبَ إحْدَى يَدَيَّ بِالسَّيْفِ ،   فَقَطَعَها ، ثُمَّ لاذَ مِنِّي بِشَجَرَةٍ ، فَقَالَ : أسْلَمْتُ لِلهِ ، أأقْتُلُهُ يَا رَسُول الله بَعْدَ أنْ قَالَهَا ؟ فَقَالَ : (( لا تَقْتُلهُ )) فَقُلْتُ : يَا رَسُول الله ، قَطَعَ إحْدَى يَدَيَّ ، ثُمَّ قَالَ ذلِكَ بَعْدَ مَا قَطَعَهَا ؟! فَقَالَ : (( لا تَقتُلْهُ ، فإنْ قَتَلْتَهُ فَإنَّهُ بِمَنْزِلَتِكَ قَبْلَ أنْ تَقْتُلَهُ ، وَإنَّكَ بِمَنْزِلَتِهِ قَبْلَ أنْ يَقُولَ كَلِمَتَهُ التي قَالَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Ma'bad Al-Miqdaad bin Al-Aswad (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ya kwamba, nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Waonaje nikikutana na mtu miongoni mwa makafiri. Tukapigana, naye akanikata mkono wangu kwa upanga, kisha akajificha kutoka kwangu nyuma ya mti, akasema: 'Nimesilimu kwa ajili ya Allaah.' Je, naweza kumuua Ee Rasuli wa Allaah baada ya kusema maneno hayo? Akasema: 'Usimuue.'Nikasema: 'Ee Rasuli wa Allaah! Ameukata mkono wangu mmoja, kisha akasema maneno hayo baada ya kuukata?' Akasema: 'Usimuue, kwani utakapofanya hivyo atakuwa katika nafasi yako kabla ya kumuua. Na hakika wewe utakuwa katika nafasi yake kabla ya yeye kutamka kauli yake hiyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أُسَامة بن زيدٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : بعثنا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إِلَى الْحُرَقَةِ مِنْ جُهَيْنَةَ فَصَبَّحْنَا القَوْمَ عَلَى مِيَاهِهِمْ ، وَلَحقْتُ أنَا وَرَجُلٌ مِنَ الأَنْصَارِ رَجُلاً مِنْهُمْ ، فَلَمَّا غَشَيْنَاهُ ، قَالَ : لاَ إلهَ إلاَّ الله ، فَكفَّ عَنْهُ الأَنْصَاري ، وطَعَنْتُهُ برُمْحِي حَتَّى قَتَلْتُهُ ، فَلَمَّا قَدِمْنَا المَدِينَةَ ، بَلَغَ ذلِكَ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ لِي : (( يَا أُسَامَة ، أقَتَلْتَهُ بَعْدَ مَا قَالَ لا إلهَ إلاَّ اللهُ ؟! )) قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، إِنَّمَا كَانَ متعوِّذاً ، فَقَالَ : (( أقَتَلْتَهُ بَعْدَ مَا قَالَ لا إلهَ إلاَّ اللهُ ؟! )) فما زَالَ يُكَرِّرُهَا عَلَيَّ حَتَّى تَمنْيَّتُ أنِّي لَمْ أكُنْ أسْلَمْتُ قَبْلَ ذلِكَ اليَوْمِ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أقالَ : لا إلهَ إلاَّ اللهُ وقَتَلْتَهُ ؟! )) قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، إِنَّمَا قَالَهَا خَوْفاً مِن السِّلاحِ ، قَالَ : (( أَفَلاَ شَقَقْتَ عَنْ قَلْبِهِ حَتَّى تَعْلَمَ أَقَالَهَا أمْ لا ؟! )) فمَا زَالَ يُكَرِّرُهَا حَتَّى تَمَنَّيْتُ أنِّي أسْلَمْتُ يَوْمَئذٍ .

Na imepokewa kutoka kwa Usamah bin Zayd (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) amesema, alitutuma Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwenda al-Huraqah, tuliwaamkia asubuhi, tukawashambulia tukawashinda. Mimi na mtu mmoja miongoni mwao, tulipompata akasema: 'Laa ilaaha illa Allaah,' Ansari akamwacha, mimi nikamchoma kwa mkuki wangu nikammuua . Tuliporudi taarifa zikamfikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naya akaniambia, "Ee Usamah! Umemuua baada ya kuwa amesema, "Laa ilaaha illa Allaah."  Nikasema: "Alikuwa akijisalimisha tu." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliendelea kulirudia hilo mpaka nikatamani heri nisingekuwa Muislamu kabla ya siku ile." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah nyingine: Alisema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Amesema Laa ilaaha illa Allaah, nawe ukamuua?" Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika amesema hilo akihofia silaha." Akasema: "Je, uliupasua moyo wake mpaka ukajua kuwa amesema hilo kweli au la." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliendelea kulirudia hilo mpaka nikatamani nisingekuwa nimesilimu wakati ule.

 

 

Hadiyth – 5

وعن جندب بن عبد الله رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بَعَثَ بَعْثاً مِنَ المُسْلِمينَ إِلَى قَومٍ مِنَ المُشرِكينَ ، وَأنَّهُمْ التَقَوْا ، فَكَانَ رَجُلٌ مِنَ المُشْركينَ إِذَا شَاءَ أنْ يَقْصِدَ إِلَى رَجُل مِنَ المُسْلِمينَ قَصَدَ لَهُ فَقَتَلَهُ ، وَأنَّ رَجُلاً مِنَ المُسْلِمِينَ قَصَدَ غَفْلَتَهُ . وَكُنَّا نتحَدَّثُ أنَّهُ أُسَامَةُ بْنُ زَيْدٍ ، فَلَمَّا رَفَعَ عَلَيهِ السَّيفَ ، قَالَ : لا إلهَ إلاَّ اللهُ ، فَقَتَلهُ ، فَجَاءَ البَشيرُ إِلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فَسَألَهُ وَأخبَرَهُ ، حَتَّى أخْبَرَهُ خَبَرَ الرَّجُلِ كَيْفَ صَنَعَ ، فَدَعَاهُ فَسَألَهُ ، فَقَالَ : (( لِمَ قَتَلْتَهُ ؟ )) فَقَالَ : يَا رَسُول اللهِ ، أوْجَعَ في المُسلِمِينَ ، وَقَتَلَ فُلاناً وفلاناً ، وسمى لَهُ نَفراً ، وَإنِّي حَمَلْتُ عَلَيهِ ، فَلَمَّا رَأى  السَّيفَ ، قَالَ : لا إلهَ إلاَّ اللهُ . قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم:  (( أقَتَلْتَهُ ؟ )) قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : (( فَكَيفَ تَصْنَعُ بلاَ إلهَ إلاَّ اللهُ ، إِذَا جَاءتْ يَوْمَ القِيَامَةِ ؟ )) قَالَ : يَا رَسُول الله ، اسْتَغْفِرْ لِي . قَالَ : (( وكَيفَ تَصْنَعُ بِلا إلهَ إلاَّ الله إِذَا جَاءتْ يَوْمَ القِيَامَةِ ؟ )) فَجَعَلَ لاَ يَزِيدُ عَلَى أنْ يَقُولَ : (( كَيفَ تَصْنَعُ بِلا إلهَ إلاَّ الله إِذَا جَاءتْ يَوْمَ القِيَامَةِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jundub bin 'Abdillaah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alituma Waisilamu kwa watu wa washirikina. Nao wakakautana, ikawa mtu katika washirikina akimkusudia mtu katika Waislamu anamkusudia na anamuua, Nakuwa mtu miongoni mwa Waislamu anakusudia kutaka kumuua, Tulikuwa tunahadithia kuwa huyo Usamah bin Zayd. Aliponyanyua upanga wake, yule mtu alisema: 'Laa ilaaha illa Allaah,' naye akamuua. Akaja mwenye kuleta bishara kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akamuuliza akampa habari hadi akampa ya mtu yule alichofanya, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuita Usaamah akamuuliza, akasema: "Kwa nini umemuua?" Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah!, Ameumiza Waislamu, amemuua fulani na fulani akataja watu, Hivyo, nilimwendea na alipouona upanga ndipo alipotamka, 'Laa ilaaha illa Allaah'." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je, umemuua?" Akasema: "Ndio." Akasema: "Siku ya Qiyaamah utasema kitu gani kwa kutamka kwake Laa ilaaha illa Allaah?" Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Niombee maghfirah." Akasema: "Siku ya Qiyaamah utasema kitu gani kwa kutamka kwake Laa ilaaha illa Allaah?" Na akawa hazidishi kauli yake: ""Siku ya Qiyaamah utasema kitu gani kwa kutamka kwake Laa ilaaha illa Allaah?" [Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن عبد الله بن عتبة بن مسعود ، قَالَ : سَمِعْتُ عمر بن الخطاب رضي الله عنه، يقولُ : إنَّ نَاساً كَانُوا يُؤْخَذُونَ بِالوَحْيِ في عَهْدِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، وَإنَّ الوَحْيَ قَدِ انْقَطَعَ ، وإِنَّمَا نَأخُذُكُمُ الآن بما ظَهَرَ لَنَا مِنْ أعمَالِكُمْ ، فَمَنْ أظْهَرَ لَنَا خَيْراً أمَّنَّاهُ وَقَرَّبْنَاهُ ، وَلَيْسَ لَنَا مِنْ سَرِيرَتِهِ شَيْء ، اللهُ يُحَاسِبُهُ فِي سَرِيرَتِهِ ، وَمَنْ أظْهَرَ لَنَا سُوءاً لَمْ نَأمَنْهُ وَلَمْ نُصَدِّقْهُ وَإنْ قَالَ : إنَّ سَرِيرَتَهُ حَسَنَةٌ . رواه البخاري .

Toka kwa 'Abdillaah bin Mas'uwd amesema: "Nimemsikia 'Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiyah Allaahu 'anhu) anasema: "Watu walikuwa wakihukumiwa kwa Wahyi wakati wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), Wahyi umekatika, sasa tunawahukumu kwa amali zenu zilizotudhihirikia, Hivyo mwenye kutudhihirishia kheri tutamuamini na kumkaribisha, na si juu yetu kuchunguza chochote katika siri zake, Allaah atamhesabu katika siri zake, Na anayotudhihirishia uovu hatutomuamini wala hatumsadiki japo atasema: Hakika niya yangu ni nzuri." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Share

050-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Hofu (Ya Allaah)

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب الخوف

050-Mlango Wa Hofu (Ya Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ ﴿٤٠﴾

Na Mimi Pekee niogopeni. [Al-Baqarah: 40]

 

إِنَّ بَطْشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ ﴿١٢﴾

Hakika mkamato wa kuadhibu wa Rabb wako bila shaka ni mkali. [Al-Buruj: 12]

 

وَكَذَٰلِكَ أَخْذُ رَبِّكَ إِذَا أَخَذَ الْقُرَىٰ وَهِيَ ظَالِمَةٌ ۚ إِنَّ أَخْذَهُ أَلِيمٌ شَدِيدٌ﴿١٠٢﴾

Na hivyo ndivyo mkamato wa Rabb wako unavyokuwa Anapokamata miji na huku ikifanya dhulma. Hakika mkamato Wake unaumiza vikali.

 

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّمَنْ خَافَ عَذَابَ الْآخِرَةِ ۚ ذَٰلِكَ يَوْمٌ مَّجْمُوعٌ لَّهُ النَّاسُ وَذَٰلِكَ يَوْمٌ مَّشْهُودٌ﴿١٠٣﴾

Hakika katika hayo mna Aayah (funzo, zingatio, dalili) kwa anayekhofu adhabu ya Aakhirah. Hiyo ni Siku ya kujumuishwa watu, na hiyo ni Siku ya kushuhudiwa.

 

وَمَا نُؤَخِّرُهُ إِلَّا لِأَجَلٍ مَّعْدُودٍ﴿١٠٤﴾

Na hatuiakhirishi isipokuwa kwa muda maalumu unaohesabiwa.  

 

يَوْمَ يَأْتِ لَا تَكَلَّمُ نَفْسٌ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ فَمِنْهُمْ شَقِيٌّ وَسَعِيدٌ﴿١٠٥﴾

Siku itakapofika; haitosema nafsi yeyote isipokuwa kwa idhini Yake (Allaah). Basi miongoni mwao ni wenye mashaka wanaostahiki adhabu, na wenye furaha na neema.

 

فَأَمَّا الَّذِينَ شَقُوا فَفِي النَّارِ لَهُمْ فِيهَا زَفِيرٌ وَشَهِيقٌ﴿١٠٦﴾

Basi ama wale walio mashakani, basi watakuwa motoni, lao humo ni upumuaji pumzi kwa mngurumo na uvutaji pumzi kwa mkoromo. [Huwd: 102-106]

 

وَيُحَذِّرُكُمُ اللَّـهُ نَفْسَهُ ۗ  ﴿٢٨﴾ 

Na Allaah Anakutahadharisheni na Nafsi yake. [Aal-'Imraan: 28]

 

 

يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ ﴿٣٤﴾ وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ ﴿٣٥﴾ وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ ﴿٣٦﴾ لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ ﴿٣٧﴾ 

Siku mtu atakapomkimbia ndugu yake. Na mama yake na baba yake. Na mkewe na wanawe.

Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na hali ya kumtosheleza. ['Abasa: 34-37]

 

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمْ ۚ إِنَّ زَلْزَلَةَ السَّاعَةِ شَيْءٌ عَظِيمٌ ﴿١﴾

Enyi watu! Mcheni Rabb wenu. Hakika zilizala la Saa (Qiyaamah) ni jambo kuu.

 

يَوْمَ تَرَوْنَهَا تَذْهَلُ كُلُّ مُرْضِعَةٍ عَمَّا أَرْضَعَتْ وَتَضَعُ كُلُّ ذَاتِ حَمْلٍ حَمْلَهَا وَتَرَى النَّاسَ سُكَارَىٰ وَمَا هُم بِسُكَارَىٰ وَلَـٰكِنَّ عَذَابَ اللَّـهِ شَدِيدٌ ﴿٢﴾

Siku mtakapoiona kila mnyonyeshaji atamsahau anayemnyonyesha, na kila mwenye mimba ataizaa mimba yake, na utawaona watu wamelewa, kumbe hawakulewa lakini ni adhabu ya Allaah kali. [Al-Hajj: 1-2]

 

وَلِمَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ جَنَّتَانِ ﴿٤٦﴾

Na kwa mwenye kukhofu kisimamo mbele ya Rabb wake atapata bustani mbili. [Ar-Rahmaan: 46]

 

وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ﴿٢٥﴾

Na watakabiliana baadhi yao kwa wengineo wakiulizana.

 

قَالُوا إِنَّا كُنَّا قَبْلُ فِي أَهْلِنَا مُشْفِقِينَ ﴿٢٦﴾

Watasema: Hakika sisi tulikuwa kabla kwenye ahli zetu wenye kuogopa

 

فَمَنَّ اللَّـهُ عَلَيْنَا وَوَقَانَا عَذَابَ السَّمُومِ ﴿٢٧﴾

Basi Allaah Akatufadhilisha, na Akatuokoa na adhabu ya moto unaobabua.

 

إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ﴿٢٨﴾

Hakika sisi tulikuwa kabla Tunamuomba Yeye Pekee, hakika yeye Ndiye Mwingi huruma na fadhila, Mwenye kurehemu. [Atw-Twuwr: 25-28]

 

 

 

Hadiyth – 1

عن ابن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : حدثنا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَهُوَ الصادق المصدوق : (( إنَّ أحَدَكُمْ يُجْمَعُ خَلْقُهُ في بَطْنِ أُمِّهِ أربَعِينَ يَوماً نُطْفَةً ، ثُمَّ يَكُونُ عَلَقَةً مِثْلَ ذلِكَ ، ثُمَّ يَكُونُ مُضْغَةً مِثْلَ ذلِكَ ، ثُمَّ يُرْسَلُ المَلَكُ ، فَيَنْفُخُ فِيهِ    الرُّوحَ ، وَيُؤْمَرُ بِأرْبَعِ كَلِمَاتٍ : بِكَتْبِ رِزْقِهِ وَأجَلِهِ وَعَمَلِهِ وَشَقِيٌّ أَوْ سَعِيدٌ . فَوَالَّذِي لا إلهَ غَيْرُهُ إنَّ أحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أهْلِ الجَنَّةِ حَتَّى مَا يَكُونُ بَيْنَهُ وبيْنَهَا إلاَّ ذِرَاعٌ فَيَسْبِقُ عَلَيهِ الكِتَابُ ، فَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أهْلِ النَّارِ فَيدْخُلُهَا ، وَإنَّ أَحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أهْلِ النَّارِ حَتَّى مَا يَكُونُ بَيْنَهُ وَبَيْنَهَا إلاَّ ذراعٌ ، فَيَسْبِقُ عَلَيهِ الكِتَابُ فَيعْمَلُ بِعَمَلِ أهْلِ الجَنَّةِ فَيَدْخُلُهَا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa na Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa: "Ametuhadithia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na yeye ni mkweli mswadikishwa: Hakika mmoja wenu hukusanywa umbo lake katika tumbo la mamake siku arobaini; kisha kuwa pande la damu muda kama huo; kisha pande la nyama muda kama huo. Kisha hutumwa Malaika anapuliza roho ndani yake, na anaamrishwa maneno manne: Kuandika riziki yake, ajali yake, amali yake, mwema au muovu. Wa-Allaahi hakuna Rabb asiyekuwa Yeye, hakika mmoja wenu hufanya amali ya watu wa Peponi, mpaka haiwi baina yake na Pepo ila dhiraa, Basi kitabu kimtangulie akafanya amali ya watu wa Motoni. Na mmoja wenu hufanya amali ya watu wa Motoni mpaka haiwi baina yake na Moto ila dhiraa, kitabu kikamtangulia na hivyo akafanya amali za watu wa Pepono na kisha akaingia humo." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

عن ابن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( يُؤتَى بِجَهَنَّمَ يَومَئذٍ لَهَا سَبْعُونَ ألفَ زِمَامٍ ، مَعَ كُلِّ زِمَامٍ سَبعُونَ ألْفَ مَلَكٍ يَجُرُّونَهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa na Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Siku ya Qiyaamah Jahanam italetwa ikiwa na hatamu elfu sabiini pamoja na kila hatamu kutakuwa na Malaika elfu sabiini  wanaoikokota." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ أهْوَنَ أهْلِ النَّارِ عَذَاباً يَوْمَ القِيَامَةِ لَرَجُلٌ يوضعُ في أخْمَصِ قَدَمَيْهِ جَمْرَتَانِ يَغْلِي مِنْهُمَا دِمَاغُهُ . مَا يَرَى أنَّ أَحَداً أشَدُّ مِنْهُ عَذَاباً ، وَأنَّهُ لأَهْوَنُهُمْ عَذَاباً )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa an-Nu'maan bin Bashiir (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) ambaye amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika watu wa Motoni watakaokuwa na adhabu duni kabisa Siku ya Qiyaamah ni mtu atakaye wekewa makaa mawili ya Moto chini ya miguu yake yatakayo lifanya bongo lake lichemke. Mtu huyo atajihisi kuwa yeye anapata adhabu kali zaidi kuliko wote, kumbe ndio amepewa adhabu ya chini kabisa." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن سمرة بن جندب رضي الله عنه: أنَّ نبيَّ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( مِنْهُمْ مَنْ تَأخُذُهُ النَّارُ إِلَى كَعْبَيهِ ، وَمنْهُمْ مَنْ تَأخُذُهُ إِلَى رُكْبَتَيهِ ، وَمنْهُمْ مَنْ تَأخُذُهُ إِلَى حُجزَتِهِ ، وَمِنْهُمْ مَنْ تَأخُذُهُ إِلَى تَرْقُوَتِهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Samurah bin Jundub (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Miongoni mwa watu wa Motoni ni wale ambao moto kwa ukali wake utawafika kwenye tindi za miguu, na wengine kwenye magoti, na wengine mpaka kiunoni, na madhambi yao." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يَقُومُ النَّاس لِرَبِّ العَالَمينَ حَتَّى يَغِيبَ أحَدُهُمْ في رَشْحِهِ إِلَى أنْصَافِ أُذُنَيهِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watasimama watu mbele ya Rabb wa walimwengu, (kwa amri Yake na kupatiwa malipo) hadi baadhi yao wapotee katika jasho lao hadi katika ya masikio yao." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ : خطبنا رَسُول الله صلى الله عليه وسلمخطبة مَا سَمِعْتُ مِثلها قطّ ، فَقَالَ : (( لَوْ تَعْلَمُونَ مَا أعْلَمُ ، لَضحِكْتُمْ قَلِيلاً وَلَبَكَيتُمْ كَثِيراً )) فَغَطَّى أصْحَابُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَجُوهَهُمْ ، وَلَهُمْ خَنَينٌ . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية : بَلَغَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم عَنْ أَصْحَابِهِ شَيْءٌ فَخَطَبَ ، فَقَالَ : (( عُرِضَتْ عَلَيَّ الجَنَّةُ وَالنَّارُ ، فَلَمْ أرَ كَاليَومِ في الخَيرِ وَالشَّرِّ ، وَلَوْ تَعْلَمونَ مَا أعلَمُ لَضَحِكْتُمْ قَلِيلاً وَلَبَكَيْتُمْ كَثِيراً )) فَمَا أتَى عَلَى أصْحَابِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يَوْمٌ أَشَدُّ مِنْهُ ، غَطَّوْا رُؤُسَهُمْ وَلَهُمْ خَنِينٌ .

Na imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Alituhutubia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hotuba sijasikia mfano wake katu, akasema: 'Lau mngejua ninayoyajua, mngecheka kidogo na kulia sana.' Swahaaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakafunika nyuso zao na kulia kwa mayowe." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah: "Habari zilimfikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) toka kwa Swahaaba zake, basi akahutubia, akasema: 'Nime onyeshwa Pepo na Moto sijaona kama leo katika mazuri na shari. Lau mngejua ninayoyajua basi mngecheka kidogo na kulia sana.' Hii ilikuwa siku nzito zaidi kwa Swahaaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Walifunika nyuso zao wakaanza kulia kwa nguvu.

 

 

Hadiyth – 7

وعن المقداد رضي الله عنه، قَالَ : سمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( تُدْنَى الشَّمْسُ يَوْمَ القِيَامَةِ مِنَ الخَلْقِ حَتَّى تَكُونَ مِنْهُمْ كَمِقْدَارِ مِيلٍ )) قَالَ سُلَيْم بنُ عامِر الراوي عن المقداد : فَوَاللهِ مَا أدْرِي مَا يعني بالمِيلِ ، أمَسَافَةَ الأرضِ أَمِ المِيلَ الَّذِي تُكْتَحَلُ بِهِ العَيْنُ ؟ قَالَ : (( فَيكُونُ النَّاسُ عَلَى قَدْرِ أعْمَالِهِمْ في العَرَقِ ، فَمِنْهُمْ مَنْ يَكُونُ إِلَى كَعْبَيْهِ ، ومنهم من يكون إِلَى ركبتيه ، ومنهم مَنْ يَكُونُ إِلَى حِقْوَيْهِ ، وَمِنْهُمْ مَنْ يُلْجِمُهُ العَرَقُ إلْجَاماً )) . قَالَ : وَأَشَارَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بيدهِ إِلَى فِيهِ . رواه مسلم.

Toka kwa Al-Miqdaad (Radhwiyah Allahu 'anhu) Nilimsikia Rasuli wa Allaahu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Siku ya Qiyaamah jua litasongezwa kwa viumbe, litakuwa kiasi cha maili." Sulaym bin 'Aamir mpokezi kutoka kwa Al-Maqdaad alisema: "Naapa kwa Allaah! Sikujua alichokusudia kwa Maili - je, ni masafa ya ardhi au ni kijiti kinachopaka jicho wanja?, Watu watatokwa jasho kadiri ya matendo yao, kuna ambao jasho itawafika katika tindi mbili za miguu, na wengine magotini, na wengine kiunoni na wengine kufunikwa kabisa kwa mkono kwenye mdomo wake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( يَعْرَقُ النَّاسُ يَومَ القِيَامَةِ حَتَّى يَذْهَبَ عَرَقُهُمْ في الأرضِ سَبْعِينَ ذِراعاً ، وَيُلْجِمُهُمْ حَتَّى يَبْلُغَ آذَانَهُمْ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaah 'anhu) amesema kuwa: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Watu watatoa jasho Siku ya Qiyaamah mpaka jasho yao ifike ardhini dhiraa sabini, naiwafunike, hadi ifike masikioni mwao." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : كُنَّا مَعَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إذْ سمع وجبة، فَقَالَ : (( هَلْ تَدْرُونَ مَا هَذَا ؟ )) قُلْنَا : الله وَرَسُولُهُ أعْلَمُ . قَالَ : (( هذَا حَجَرٌ رُمِيَ بِهِ في النَّارِ مُنْذُ سَبْعينَ خَريفاً ، فَهُوَ يَهْوِي في النَّارِ الآنَ حَتَّى انْتَهَى إِلَى قَعْرِها فَسَمِعْتُمْ وَجْبَتَهَا )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye alisilimu: "Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na mara tukasikia sauti ya kitu kilichoanguka chini. Hapo akasema: "Je, mnajua hicho ni kitu gani?" Tukasema: "Allaah na Rasuli Wake wajua zaidi." Akasema: "Hilo ni jiwe liliorushwa Motoni miaka sabini iliyopita; lilikuwa likizunguka kwa kipindi mpaka leo ndilo limefika chini na ndio mmesikia kugusa chini." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

وعن عدي بن حاتم رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَا مِنْكُمْ مِنْ أَحَدٍ إلاَّ سَيُكَلِّمُهُ رَبُّهُ لَيْسَ بَيْنَهُ وبَيْنَهُ تَرْجُمَانٌ ، فَيَنْظُرُ أيْمَنَ مِنْهُ فَلاَ يَرَى إلاَّ مَا قَدَّمَ ، وَيَنْظُرُ أشْأَمَ مِنْهُ فَلاَ يَرَى إلاَّ مَا قَدَّمَ ، وَيَنْظُرُ بَيْنَ يَدَيْهِ فَلاَ يَرَى إلاَّ النَّارَ تِلْقَاءَ وَجْهِهِ ، فَاتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa 'Adiy bin Haatim (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna yeyote miongoni mwenu isipokuwa Allaah Atazungumza naye Siku ya Qiyaamah, kutakuwa hakuna mkalimani kati yake na Allaah. Kisha ataangalia kuliani mwake na wala hatoona kitu alichokitanguliza, kisha ataagalia mbele yake ataona Moto unampokea, kwa hiyo awezaye kutoa kipande cha tende moja kama sadaqa, na afanye hivyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي ذر رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنِّي أَرَى مَا لا تَرَوْنَ ، أطَّتِ السَّمَاءُ وَحُقَّ لَهَا أنْ تَئِطَّ ، مَا فِيهَا مَوضِعُ أرْبَع أصَابعَ إلاَّ وَمَلَكٌ وَاضِعٌ جَبْهَتَهُ سَاجِداً للهِ تَعَالَى . والله لَوْ تَعْلَمُونَ مَا أعْلَمُ ، لَضَحِكْتُمْ قَلِيلاً وَلَبَكَيْتُمْ كَثِيراً ، وَمَا تَلَذَّذْتُمْ بالنِّساءِ عَلَى الفُرُشِ ، وَلَخَرَجْتُمْ إِلَى الصُّعُدَاتِ تَجْأرُونَ إِلَى اللهِ تَعَالَى )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mimi naona msiyoyaona, na ninasikia msiyosikia. Mbingu zinalia na ina haki kufanya hivyo (kulia). Hakuna nafasi yeyote hata ya vidole vinne isipokuwa yupo Malaaika ametandaza mbawa yake akimsujudia Allaah Ta'aalaa. Naapa kwa Allaah! Lau mngekuwa mnajua ninayoyajua basi mngecheka kidogo na kulia sana; hamngekuwa ni wenye kustarehe na wake zenu katika vitanda. Mngefanya haraka kutoka barabarani na njiani ili kutaka ulinzi wa Allaah." [At-Tirmidhiy, ambaye amesema hii ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 12

وعن أَبي برزة نَضْلَة بن عبيد الأسلمي رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لا تَزُولُ قَدَمَا عَبْدٍ يَومَ القِيَامَةِ حَتَّى يُسْأَلَ عَنْ عُمُرِهِ فِيمَ أفنَاهُ ؟ وَعَنْ عِلمِهِ فِيمَ فَعَلَ فِيهِ ؟ وَعَنْ مَالِهِ مِنْ أيْنَ اكْتَسَبَهُ ؟ وَفيمَ أنْفَقَهُ ؟ وَعَنْ جِسمِهِ فِيمَ أبلاهُ ؟ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Barzah Nadhlah bin 'Ubayd al-Aslamiy (Radhwiyah Allaah 'anhu) kuwa: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haitaondoka miguu ya mja Siku ya Qiyaamah mpaka aulizwe kuhusu Umri wake ameumaliza vipi; na kuhusu elimu yake ametumia vipi; na kuhusu mali yake ameichuma vipi na ameitumia vipi; na kuhusu mwili wake ameuzeesha vipi? [At-Tirmidhiy, ambaye amesema ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Hadiyth – 13

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قرأ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ( يَوْمَئِذٍ تُحَدِّثُ أَخْبَارَهَا ) [ الزلزلة : 4 ] ثُمَّ قَالَ : (( أتَدْرونَ مَا أخْبَارهَا )) ؟ قالوا : الله وَرَسُولُهُ أعْلَمُ . قَالَ : (( فإنَّ أخْبَارَهَا أنْ تَشْهَدَ عَلَى كُلّ عَبْدٍ أَوْ أمَةٍ بما عَمِلَ عَلَى ظَهْرِهَا تَقُولُ : عَملْتَ كَذَا وكَذَا في يَومِ كَذَا وكَذَا فَهذِهِ أخْبَارُهَا )) رواه الترمذي ،  وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Alisoma Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Kauli ya Allaah: (Siku hiyo itahadithia khabari zake) [Al-Zalzalah: 4]. Kisha akasema: "Je, mnajua khabari yake?" Wakasema: "Allaah na Rasuli Wake Wajua zaidi." Akasema: Hakika khabari yake ni kumshuhudia kila mja mwanamume au mwanamke kwa aliyoyafanya juu ya mgongo wake. Itasema: 'Ulifanya kadha na kadha siku kadha na kadha, hii ndiyo hiyo khabari yake.' [At-Tirmidhiy, ambaye amesema kuwa hii ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 14

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( كَيْفَ أنْعَمُ ! وَصَاحِبُ القَرْنِ قَدِ التَقَمَ القَرْنَ ، وَاسْتَمَعَ الإذْنَ مَتَى يُؤمَرُ بالنَّفْخِ فَيَنْفُخُ )) فَكَأنَّ ذلِكَ ثَقُلَ عَلَى أصْحَابِ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم فَقَالَ لَهُمْ : (( قُولُوا : حَسْبُنَا الله وَنِعْمَ الوَكِيلُ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسنٌ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iid Al-Khudriy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Vipi nitakuwa na furaha na mwenye baragumu (Malaika Israfil) ametia mdomoni mwake hilo baragumu huku akisubiri idhini ni lini atapatiwa ili apulize." Kama kwamba hilo lilikuwa zito kwa Masahaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hivyo akawaambia semeni: "Hasbuna Allaahu wa Ni'mal Wakiil yaani Allaah anatutosha, naye ni mbora wa kutegemewa." [At-Tirmidhiy, ambaye amesema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 15

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَنْ خَافَ أدْلَجَ ، وَمَنْ أدْلَجَ بَلَغَ المَنْزِلَ . ألا إنَّ سِلْعَةَ اللهِ غَالِيَةٌ ، ألاَ إنَّ سِلْعَةَ الله الجَنَّةُ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumuogopa adui hutoks wakati wa mwanzo wa usiku; na mwenye kutoka mapema (usiku), hufika sehemu ya usalama (kutokana na adui). Jueni ya kwamba bidhaa za Allaah zina thamani kubwa. Jueni ya kwamba bidhaa za Allaah ni Pepo Yake." [At-Tirmidhiy, ambaye amesema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 16

وعن عائشة رضي الله عنها ، قَالَتْ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( يُحْشَرُ النَّاسُ يَوْمَ القِيَامَةِ حُفَاةً عُرَاةً غُرْلاً )) قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، الرِّجَالُ وَالنِّساءُ جَمِيعاً يَنْظُرُ بَعضُهُمْ إِلَى بَعْض ؟! قَالَ : (( يَا عائِشَةُ ، الأمرُ أشَدُّ مِنْ أنْ يُهِمَّهُمْ ذلِكَ )) .

وفي رواية : (( الأَمْرُ أهمُّ مِنْ أنْ يَنْظُرَ بَعضُهُمْ إِلَى بَعض )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) ambaye amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Watu watafufuliwa Siku ya Qiyaamah wakiwa hawana viatu, uchi na wenye magovi." Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Wanaume na wanawake wote wakiwa pamoja, si wataangaliana wao kwa wao?" Akasema: "Ee 'Aaishah! Jambo hilo litakuwa zito (lenye kutisha) zaidi ya wao kutaka kuangaliana." Na katika riwaayah nyengine: "Jambo hilo litakuwa muhimu zaidi kuliko kuangaliana wao kwa wao (hawatakuwa na nafasi hiyo)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

 
Share

051-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwa na Matumaini

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الرجاء

051-Mlango Wa Kuwa na Matumaini

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا ۚ إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ﴿٥٣﴾

Sema: Enyi waja Wangu ambao wamepindukia mipaka juu ya nafsi zao: Msikate tamaa na rahmah ya Allaah; hakika Allaah Anaghufuria dhambi zote; hakika Yeye Ndiye Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu. [Az-Zumar: 53]

 

وَهَلْ نُجَازِي إِلَّا الْكَفُورَ ﴿١٧﴾

Na Hatuadhibu isipokuwa anayekufuru. [Sabaa: 17]

 

إِنَّا قَدْ أُوحِيَ إِلَيْنَا أَنَّ الْعَذَابَ عَلَىٰ مَن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﴿٤٨﴾

Hakika tumefunuliwa Wahy ya kwamba adhabu itakuwa kwa yule atakayekadhibisha na akakengeuka. [Twaahaa: 48]

 

وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ  ﴿١٥٦﴾

Na rahmah Yangu imeenea kila kitu. [At-A'raaf: 106]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن عبادة بن الصامتِ رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم  : (( مَنْ شَهِدَ أنَّ لا إلهَ إلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيكَ لَهُ ، وَأنَّ مُحَمداً عَبْدهُ ورَسُولُهُ ، وَأنَّ عِيسى عَبْدُ اللهِ وَرَسُولُهُ وَكَلِمَتُهُ ألْقَاهَا إِلَى مَرْيَمَ ورُوحٌ مِنْهُ ، وَأنَّ الجَنَّةَ حَقٌّ ، وَالنَّارَ  حَقٌّ ، أدْخَلَهُ اللهُ الجَنَّةَ عَلَى مَا كَانَ مِنَ العَمَلِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية لمسلم : (( مَنْ شَهِدَ أنْ لا إلَهَ إلاَّ اللهُ وَأنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللهِ ، حَرَّمَ اللهُ عَلَيهِ النَّارَ )) .

Imepokewa kutoka kwake 'Ubaadah bin Saamit (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kushuhudia kuwa hapana apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah Peke Yake hana mshirika, kuwa Muhammad ni mja na Rasuli Wake, na kuwa 'Iysa ni mja wa Allaah na Rasuli Wake, na ni Neno Lake Alilotia kwa Maryam na roho toka kwake, na kuwa Pepo ni kweli, na Moto ni kweli, Allaah atamwingiza Peponi kwa amali alizokuwa akifanya." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah ya Muslim: "Mwenye kushuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Allaah, na kuwa Muhammad ni Rasuli wa Allaah, Allaah atamharamishia Moto."

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي ذررضي الله عنه، قَالَ : قَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم : (( يقول الله (عزّ وجلّ) : مَنْ جَاء بالحَسَنَةِ فَلَهُ عَشْرُ أمْثَالِهَا أَوْ أزْيَد ، وَمَنْ جَاءَ بالسَيِّئَةِ فَجَزاءُ سَيِّئَةٍ سَيِّئَةٌ مِثْلُهَا أَوْ أغْفِرُ . وَمَنْ تَقَرَّبَ مِنِّي شِبْراً تَقَرَّبْتُ مِنْهُ ذِرَاعاً ، وَمَنْ تَقَرَّبَ مِنِّي ذِرَاعاً تَقَرَّبْتُ مِنْهُ بَاعاً ، وَمَنْ أتَانِي يَمْشِي أتَيْتُهُ هَرْوَلَةً ، وَمَنْ لَقِيني بِقُرَابِ الأرْض خَطِيئةً لا يُشْرِكُ بِي شَيئاً ، لَقِيتُهُ بِمِثْلِهَا مَغفِرَةً )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Amesema Allaah Ta'aalaa: "Mwenye kuleta jema atapata mara kumi mfano wake au zaidi, na Mwenye kuleta ovu, malipo yake ni uovu mfano wake au Namsamehe. Na Mwenye kunikaribia kwa shubiri, Nitamkaribia kwa dhiraa. Na mwenye kunikaribia kwa kutembelea, Nitamjia kwa kukimbia, Mwenye kukutana nami kwa madhambi ujazo wa ardhi, na asinishirikishe na chochote, Nitakutana naye kwa msamaha kama huo." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 3

وعن جابر رضي الله عنه، قَالَ : جاء أعرابي إِلَى النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ: يَا رَسُول الله ، مَا الموجِبَتَانِ؟ قَالَ : (( مَنْ مَاتَ لاَ يُشْرِكُ بالله شَيئاً دَخَلَ الجَنَّةَ ، وَمَنْ مَاتَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئاً دَخَلَ النَّار )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Alikuja Bedui kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alahi wa aalihi wa sallam) na kuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Ni vitu gani viwili vinavyomfanya mtu aingie Peponi au Motoni?" Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Yeyote anayekufa hakumshirikisha Allaah na chochote ataingia Peponi na mwenye kuaga dunia huku anamshirikisha Allaah basi ataingia Motoni." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه : أن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم  ومعاذ رديفه عَلَى الرَّحْل ، قَالَ : (( يَا مُعَاذُ )) قَالَ : لَبِّيْكَ يَا رَسُول الله وَسَعْدَيْكَ ، قَالَ : (( يَا مُعَاذُ )) قَالَ : لَبَّيْكَ يَا رَسُول الله وَسَعْدَيْكَ ، قَالَ : (( يَا مُعَاذُ )) قَالَ : لَبِّيْكَ يَا رَسُول الله وسَعْدَيْكَ ،   ثَلاثاً ، قَالَ : (( مَا مِنْ عَبْدٍ يَشْهَدُ أن لا إلهَ إلاَّ الله ، وَأنَّ مُحَمَّداً عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ صِدْقاً مِنْ قَلْبِهِ إلاَّ حَرَّمَهُ الله عَلَى النَّار )) قَالَ : يَا رَسُول الله ، أفَلاَ أخْبِرُ بِهَا النَّاس فَيَسْتَبْشِروا ؟ قَالَ : (( إِذاً يَتَّكِلُوا )) فأخبر بِهَا مُعاذٌ عِنْدَ موتِه تَأثُّماً . مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Mu'aadh akiwa nyuma yake, wakiwa juu ya kipndo, aliita: "Ee Mu'aadh!" Naye akajibu: "Labbaika Ee Rasuli wa Allaah wa Sa'dayka." Aliita (tena): "Ee Mu'aadh!" Naye akajibu: "Labbaika Ee Rasuli wa Allaah wa Sa'dayka." (Aliita hivi) mara tatu, kisha akasema: "Hakuna yeyote anayekiri kwa moyo na akatamka kwa ulimi kuwa hakuna Mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allaah na Muhammad ni mja na Rasuli wa Allaah kwa ukweli wa moyo wake isipokuwa Allaah Atamharamishia moto." Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah niwaeleze watu kwa hilo wakafurahi?" Akanijibu: "Kama utawaambia watabweteka!" Na hilo Mu'aadh alilieleza wakati wa kufa kwake kwa kuhofia kupata dhambi (ya kuficha mafundisho)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه- أَوْ أَبي سعيد الخدري رضي الله عنهما - شك الراوي - ولا يَضُرُّ الشَّكُّ في عَين الصَّحَابيّ ؛ لأنَّهُمْ كُلُّهُمْ عُدُولٌ – قَالَ : لَمَّا كَانَ غَزوَةُ تَبُوكَ ، أصَابَ النَّاسَ مَجَاعَةٌ ، فقالوا : يَا رَسُول الله ، لَوْ أذِنْتَ لَنَا فَنَحرْنَا نَواضِحَنَا فَأكَلْنَا وَادَّهَنَّا ؟ فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( افْعَلُوا )) فَجاء عُمَرُ رضي الله عنه ، فَقَالَ : يَا رَسُول الله ، إنْ فَعَلْتَ قَلَّ الظَّهْرُ ، وَلَكِن ادعُهُمْ بفَضلِ أزْوَادِهِمْ ، ثُمَّ ادعُ الله لَهُمْ عَلَيْهَا بِالبَرَكَةِ ، لَعَلَّ الله أنْ يَجْعَلَ في ذلِكَ البَرَكَةَ . فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( نَعَمْ )) فَدَعَا بِنَطْع فَبَسَطَهُ ، ثُمَّ دَعَا بِفضلِ أزْوَادِهِمْ ، فَجَعَلَ الرَّجُلُ يَجيءُ بكَفّ ذُرَة وَيَجيءُ بِكَفّ تمر وَيجيءُ الآخرُ بِكِسرَة حَتَّى اجْتَمَعَ عَلَى النّطعِ مِنْ ذلِكَ شَيء يَسيرٌ ، فَدَعَا رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بِالبَرَكَةِ ، ثُمَّ قَالَ : (( خُذُوا في أوعِيَتِكُمْ )) فَأَخَذُوا في أوْعِيَتهم حَتَّى مَا تَرَكُوا في العَسْكَرِ وِعَاء إلاَّ مَلأوهُ وَأَكَلُوا حَتَّى شَبعُوا وَفَضَلَ فَضْلَةٌ فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( أشْهَدُ أنْ لا إلهَ إلاَّ اللهُ وَأنّي رَسُولُ الله ، لا يَلْقَى الله بِهِما عَبْدٌ غَيْرَ شَاكٍّ فَيُحْجَبَ عَنِ الجَنَّةِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) au Abu Sa'iid Al-Khudriy (Radhwiyah Allaahu 'anhu), mpokezi ana shaka na wala shaka haidhuru katika Swahaba yoyote, kwani wote ni waadilifu: "Ilipokuwa Vita vya Taabuk, watu walipatwa na njaa, wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Lau ungeruhusu kuchinja ngamia wetu, tule na kutumia mafuta yake." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Fanyeni hivyo." Akaja 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhu) na kusema: "Ee Rasuli wa Allaah! Ikiwa tutafanya hivyo vipando vitapungua, lakini waitishe chakula chao cha ziada, Kisha muombe Allaah awabarikie hicho. Huenda Allaah akawatilia baraka." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ndio." Akaitisha busati la ngozi akalitandika, kisha akaomba watu walete vyakula vilivyozidi. Watu wakaleta vyakula, mtu analeta kifumba cha mahindi, mwingine analeta tende, mwingine analeta kipande cha mkate, Vyakula hivyo vikakusanywa katika busati hilo. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akakiombea baraka, kisha akasema: "Chukueni katika vyombo vyenu." Wakachukua katika vyombo vyao, hadi hakukubakia chombo katika kambi isipokuwa wakajaza vyombo vyao vyote katika kambi. Hapo wakala mpaka wakashiba, kingine kikabaki. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Nashuhudia ya kwamba hapana Mola isipokuwa Allaah, na mimi ni Rasuli wa Allaah. Hatokutana mja na Allaah akiwa na kauli hizi mbili na hana shaka yoyote, kisha akazuiwa kuingia Peponi." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 6

وعن عِتْبَانَ بن مالك رضي الله عنه وَهُوَ مِمَّن شَهِدَ بَدراً ، قَالَ : كنت أُصَلِّي لِقَوْمِي بَني سَالِم ، وَكَانَ يَحُولُ بَيْنِي وبَيْنَهُمْ وَادٍ إِذَا جَاءتِ الأَمْطَار ، فَيَشُقُّ عَلَيَّ اجْتِيَازُهُ قِبَلَ مسْجِدِهم ، فَجِئتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم فقلت لَهُ : إنّي أنْكَرْتُ بَصَرِي وَإنَّ الوَادِي الَّذِي بَيْنِي وبَيْنَ قَومِي يَسيلُ إِذَا جَاءتِ الأمْطَارُ فَيَشُقُّ عَلَيَّ اجْتِيَازُهُ فَوَدِدْتُ أنَّكَ تَأتِي فَتُصَلِّي في بَيْتِي مَكَاناً أتَّخِذُهُ مُصَلّى ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( سَأفْعَلُ )) فَغَدَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم وَأَبُو بكر رضي الله عنه بَعْدَ مَا اشْتَدَّ النَّهَارُ ، وَاسْتَأذَنَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فَأذِنْتُ لَهُ ، فَلَمْ يَجْلِسْ حَتَّى قَالَ : (( أيْنَ تُحِبُّ أنْ أُصَلِّيَ مِنْ بَيْتِكَ ؟ )) فَأشَرْتُ لَهُ إِلَى المَكَانِ الَّذِي أُحبُّ أنْ يُصَلِّيَ فِيهِ ، فَقَامَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فَكَبَّرَ وَصَفَفْنَا وَرَاءَهُ فَصَلَّى رَكعَتَينِ ثُمَّ سَلَّمَ وَسَلَّمْنَا حِينَ سَلَّمَ فَحَبَسْتُهُ عَلَى خَزيرَةٍ تُصْنَعُ لَهُ ، فَسَمِعَ أهلُ الدَّارِ أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم في بَيْتِي فَثَابَ رِجالٌ مِنْهُمْ حَتَّى كَثُرَ الرِّجَالُ في البَيْتِ ، فَقَالَ رَجُلٌ : مَا فَعَلَ مَالِكٌ لا أرَاهُ ! فَقَالَ رَجُلٌ : ذلِكَ مُنَافِقٌ لا يُحِبُّ الله ورسولَهُ ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( لا تَقُلْ ذلِكَ ، ألاَ تَرَاهُ قَالَ : لا إلهَ إلاَّ الله يَبْتَغي بذَلِكَ وَجهَ الله تَعَالَى )) فَقَالَ : اللهُ ورسُولُهُ أعْلَمُ أمَّا نَحْنُ فَوَاللهِ مَا نَرَى وُدَّهُ وَلاَ حَدِيثَهُ إلاَّ إِلَى المُنَافِقينَ ! فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( فإنَّ الله قَدْ حَرَّمَ عَلَى النَّارِ مَنْ قَالَ : لا إلهَ إلاَّ الله يَبْتَغِي بذَلِكَ وَجْهَ الله )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Itbaan bin Maalik (Radhwiyah Allaahu 'anhu) miongoni mwa waliohudhuria Badr, amesema: Nilikuwa nikiswali na watu wangu Bani Saalim baina yangu na wao kuna bonde, mvua ikinyesha linafurika na huwa tabu kwangu kwenda msikitini. Nikaenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) nikasema: "Macho yangu ni dhaifu na bonde lililopo baina yangu na watu wangu linafurika ikinyesha mvua hivyo nashindwa kulivuka, Hivyo Napenda uje uswali nyumbani sehemu ninayotumia kuswalia." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Nitafanya." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaja na Abu Bakr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) baada jua kuwa juu. Rasuli wa Allaah (Swallah Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akabisha nikamkaribisha, Hakukaa hadi akasema: "Ni wapi unapopenda niswali nyumbani kwako?" Nikamuashiria sehemu nilipenda aswali. Akasimama Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akapiga takbira tukasimama nyuma yake, Akaswali rakaa mbili kisha akatoa salamu, nasi tukatoa salamu baada yake. Nikamzuia kwa sababu ya chakula anachoandaliwa. Watu wa mji wakasikia kuwa Rasuli wa Allaah yupo nyumbani kwangu wakaja watu wengi hadi wakajaa nyumbani, Akasema mtu mmoja: "Maalik amefanya nini simuoni?" Akasema mwingine: "Yule ni mnafiki hampendi Allaah na Rasuli Wake." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Usiseme hivyo, kwani humuoni amesema Laa Ilaaha Illa Allaah akitaka radhi za Allaah Ta'aalaa?", Akasema: "Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi. Ama sisi hatuwaoni marafiki zake wala mazungumzo yake isipokuwa ya wanafiki." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika amemharamishia moto mwenye kusema Laa Ilaaha Illa Allaah hatafuti kwa hilo isipokuwa radhi ya Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 7

وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه ، قَالَ : قدِم رَسُول الله صلى الله عليه وسلم بسَبْيٍ فَإِذَا امْرَأةٌ مِنَ السَّبْيِ تَسْعَى ، إِذْ وَجَدَتْ صَبياً في السَّبْيِ أخَذَتْهُ فَألْزَقَتهُ بِبَطْنِهَا فَأَرضَعَتْهُ ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أتَرَوْنَ هذِهِ المَرْأةَ طَارِحَةً وَلَدَها في النَّارِ ؟ )) قُلْنَا : لاَ وَاللهِ . فَقَالَ : (( للهُ أرْحَمُ بِعِبَادِهِ مِنْ هذِهِ بِوَلَدِهَا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khattaab (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Waliletwa mateka wa vita kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Kulikuwa na mwanamke akizunguka kutafuta mwanae. Akampata katika mateka akamchukua akamuweka tumboni mwake, akamnyonyesha. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Je, munamuona huyu mwanamke anaweza kumtia mtoto wake motoni?" Tukasema: "La! Wa-Allaahi." Akasema: "Allaah ana huruma zaidi kwa waja wake kuliko huyu kwa mtoto wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَمَّا خَلَقَ الله الخَلْقَ كَتَبَ في كِتَابٍ ، فَهُوَ عِنْدَهُ فَوقَ العَرْشِ : إنَّ رَحْمَتِي تَغْلِبُ غَضَبي )) .

وفي رواية : (( غَلَبَتْ غَضَبي )) وفي رواية : (( سَبَقَتْ غَضَبي )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pindi Allaah Alipoviumba viumbe, Aliandika katika kitabu, ambacho kipo Kwake juu ya 'Arshi Yake: Hakika rehema Yangu inashinda ghadhabu Yangu." 

Na katika riwaayah nyingine: "Imeshinda ghadhabu Yangu."

Na katika riwaayah nyengine: "Imepita ghadhabu Yangu." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhy]

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( جَعَلَ الله الرَّحْمَةَ مِئَةَ جُزْءٍ، فَأمْسَكَ عِنْدَهُ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ، وَأنْزَلَ في الأرْضِ جُزْءاً وَاحِداً، فَمِنْ ذلِكَ الجُزءِ يَتَرَاحَمُ الخَلائِقُ، حَتَّى تَرْفَعَ الدَّابّةُ حَافِرهَا عَنْ وَلَدِهَا خَشْيَةَ أنْ تُصِيبَهُ )) .

وفي رواية : (( إنّ للهِ تَعَالَى مئَةَ رَحمَةٍ ، أنْزَلَ مِنْهَا رَحْمَةً وَاحِدَةً بَيْنَ الجنِّ وَالإنس وَالبهائِمِ وَالهَوامّ ، فبها يَتَعاطَفُونَ ، وبِهَا يَتَرَاحَمُونَ ، وبِهَا تَعْطِفُ الوَحْشُ عَلَى وَلَدِهَا ، وَأخَّرَ اللهُ تَعَالَى تِسْعاً وَتِسْعينَ رَحْمَةً يرْحَمُ بِهَا عِبَادَهُ يَوْمَ القِيَامَة )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

ورواه مسلم أيضاً مِنْ رواية سَلْمَانَ الفارِسيِّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ للهِ تَعَالَى مِئَة رَحْمَةٍ فَمِنْهَا رَحْمَةٌ يَتَرَاحمُ بِهَا الخَلْقُ بَيْنَهُمْ ، وَتِسْعٌ وَتِسعُونَ لِيَومِ القِيَامَةِ )) .

وفي رواية : (( إنَّ الله تَعَالَى خَلَقَ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاواتِ وَالأَرْضَ مَئَةَ رَحْمَةٍ كُلُّ رَحْمَةٍ طِبَاقُ مَا بَيْنَ السَّماءِ إِلَى الأرْضِ ، فَجَعَلَ مِنْهَا في الأرضِ رَحْمَةً فَبِهَا تَعْطفُ الوَالِدَةُ عَلَى وَلَدِهَا ، وَالوَحْشُ وَالطَّيْرُ بَعْضُهَا عَلَى بَعْض ، فَإذا كَانَ يَوْمُ القِيَامَةِ أكملَهَا بِهذِهِ الرَّحمَةِ ))

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: Allaah Amefanya rehema kuwa sehemu mia moja, Akabakia na sehemu tisini na tisa, Akateremsha ardhini sehemu moja, katika sehemu hiyo viumbe wanahurumiana, mpaka mnyama anainua kwato zake akihofia kumdhuru mwanae."

Katika riwaayah nyengine: "Hakika Allaah Ta'aalaa ana rehma mia moja, katika hizo ameteremsha rehma moja baina ya majini na wanadamu, wanyama na wadudu. Katika hiyo rehma wanasikitiana, wanahurumiana, mnyama pori anamhurumia mwanae. Allaah Amebakisha rehema tisini na tisa Arawarahamu nazo waja Wake Siku ya Qiyaamah." [Al-Bukhaary, Muslim na At-Tirmidhy]

Amepokea Muslim Hadiyth kutoka kwa Salmaan Al-Faarisy; Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa ana rehema mia moja, miongoni mwa hizo ni rehema moja, wanahurumiana viumbe baina yao, tisini na tisa ni kwa ajili ya Siku ya Qiyaamah." 

Katika riwaayah nyingine: "Hakika Allaah Ta'aalaa ameumba siku Aliyoumba mbingu na ardhi rehema mia moja; kila moja ni baina ya mbingu na ardhi. Akajalia katika ardhi rehema Mama anamhurumia mwanae, na wanyama na ndege wanahurumiana wao kwa wao, Ikifika Siku ya Qiyaamah, Allaah ataikamilisha kwa rehema hii." 

 

 

Hadiyth – 10

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فيما يحكِي عن ربهِ تبارك وتعالى ، قَالَ: (( أذْنَبَ عَبْدٌ ذَنْباً ، فَقَالَ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي ذَنْبِي ، فَقَالَ الله تَبَاركَ وَتَعَالَى : أذنَبَ عبدي ذَنباً ، فَعَلِمَ أنَّ لَهُ رَبّاً يَغْفِرُ الذَّنْبَ ، وَيَأْخُذُ بالذَّنْبِ ، ثُمَّ عَادَ فَأذْنَبَ ،   فَقَالَ : أيْ رَبِّ اغْفِرْ لِي ذَنْبي ، فَقَالَ تبارك وتعالى : أذنَبَ عبدِي ذَنباً ، فَعَلِمَ أنَّ لَهُ رَبّاً ، يَغْفِرُ الذَّنْبَ ، وَيَأْخُذُ بالذَّنْبِ ، قَدْ غَفَرْتُ لِعَبْدِي فَلْيَفْعَلْ مَا شَاءَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anayohadithia kutoka kwa Mola wake (Tabaaraka wa Ta'aalaa) kuwa Amesema: "Mja amefanya dhambi, akasema: "Ee Mola wangu nisamehe dhambi yangu." Akasema Allaah (Tabaaraka wa Ta'aalaa): "Mja Wangu amefanya dhambi, akajua kuwa anaye Mola anayesamehe dhambi, na anayehesabu dhambi." Kisha akarudi akafanya dhambi, akasema: "Ee Mola Wangu nisamehe dhambi yangu." Akasema Allaah (Tabaaraka wa Ta'aalaa): "Mja Wangu amefanya dhambi, akajua kuwa anaye Mola anayesamehe dhambi, na anayehesabu dhambi." Kisha akarudi akafanya dhambi, akasema: "Ee Mola Wangu nisamehe dhambi yangu."Akasema Allaah (Tabaaraka wa Ta'aalaa): "Mja Wangu amefanya dhambi, akajua kuwa anaye Mola anayesamehe dhambi, na mwenye kuhesabu dhambi. Nimemsamehe mja Wangu dhambi zake, hivyo afanye anavyotaka." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( والَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ ، لَوْ لَمْ تُذْنِبُوا ، لَذَهَبَ الله بِكُمْ ، وَجَاءَ بِقَومٍ يُذْنِبُونَ ، فَيَسْتَغْفِرُونَ الله تَعَالَى ، فَيَغْفِرُ لَهُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi Mwake kwamba lau hamngekuwa mkifanya dhambi Allaah angewaondosha na Akawaleta watu ambao watafanya dhambi na kisha wataomba msamaha kwa Allaah (Ta'aalaa) Naye atawasamehe." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 12

وعن أَبي أيوب خالد بن زيد رضي الله عنه، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( لَوْلاَ أنَّكُمْ تُذْنِبُونَ ، لَخَلَقَ الله خَلْقاً يُذْنِبُونَ ، فَيَسْتَغْفِرونَ ، فَيَغْفِرُ لَهُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Ayub Khalid bin Zaiyd (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Msingekuwa mnafanya dhambi basi Allaah angewaumba viumbe wenye kufanya madhambi kisha wataomba toba na Allaah atawasamehe." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 13

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : كُنَّا قُعُوداً مَعَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، مَعَنَا أَبُو بَكْرٍ وَعُمْرُ رضي الله عنهما ، في نَفَرٍ فَقَامَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم مِنْ بَيْنِ أظْهُرِنَا ، فَأبْطَأَ عَلَيْنَا فَخَشِينَا أنْ يُقتطَعَ دُونَنَا ، فَفَزِعْنَا فَقُمْنَا فَكُنْتُ أوَّلَ مَنْ فَزِعَ فَخَرَجْتُ أبْتَغِي رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، حَتَّى أتَيْتُ حَائِطاً للأنْصَارِ ... وَذَكَرَ الحَدِيثَ بِطُولِهِ إِلَى قوله : فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( اذهَبْ فَمَن لَقِيتَ وَرَاءَ هَذَا الحَائِطِ يَشْهَدُ أنْ لا إله إلاَّ الله ، مُسْتَيقِناً بِهَا قَلبُهُ فَبَشِّرْهُ بِالجَنَّةِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah(Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa tumekaa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na pamoja nasi kulikuwa na Abu Bakr na 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) miongoni mwa Swahaaba wengine Alisimama Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) baina ya migongo yetu na akakawia sana, hivyo tukawa na hofu kubwa sana kuhusu usalama wake. Hapo tulisimama ili kumtafuta, nami ndiye niliyekuwa wa mwanzo kuwa na hamu hiyo. Niliinuka ili kumtafuta Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), mpaka nikafika kwenye ukuta wa Ansaar. Hapa aliitaja Hadiyth kwa urefu na ukamilifu wake mpaka katika kauli yake: Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Nenda nyuma ya ukuta huu umbashirie Pepo kila utakayekutana naye huku anashuhudia ya kwamba hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 14

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم تَلاَ قَولَ الله (عزّ وجلّ) في إبراهيم صلى الله عليه وسلم: ( رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيراً مِنَ النَّاسِ فَمَنْ تَبِعَنِي فَإِنَّهُ مِنِّي ) [ إبراهيم : 36 ] الآية ، وقَولَ عِيسَى صلى الله عليه وسلم: ( إِنْ تُعَذِّبْهُمْ فَإِنَّهُمْ عِبَادُكَ وَإِنْ تَغْفِرْ لَهُمْ فَإِنَّكَ أَنْتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ) [ المائدة : 118 ] فَرَفَعَ يَدَيهِ وَقالَ : (( اللَّهُمَّ أُمّتي أُمّتي )) وبَكَى ، فَقَالَ الله (عزّ وجلّ) : (( يَا جِبْريلُ ، اذْهَبْ إِلَى مُحَمَّدٍ -وَرَبُّكَ أعْلَمُ - فَسَلْهُ مَا يُبْكِيهِ ؟ )) فَأتَاهُ جبريلُ ، فَأخْبَرَهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم، بِمَا قَالَ - وَهُوَ أعْلَمُ - فَقَالَ اللهُ تَعَالَى : (( يَا جِبريلُ ، اذْهَبْ إِلَى مُحَمّدٍ ، فَقُلْ : إنَّا سَنُرْضِيكَ في أُمّتِكَ وَلاَ نَسُوءكَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaahi bin 'Amru bin al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisoma kauli ya Allaah ('Azza wa Jalla) kuhusu Ibraahiym (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Rabb wangu! Hakika hao (masanamu) wamepoteza wengi kati ya watu. Basi atakayenifuata, huyo ni katika mimi." [Ibraahiym: 36] Na kauli ya 'Iyssaa (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ukiwaadhibu, basi bila shaka hao ni waja Wako; na Ukiwaghufuria basi hakika Wewe Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote." [Al-Maaidah: 118] Nabiy alinyanyua mikono yake na kusema: "Ee Mola wangu! Ummah wangu, Ummah wangu", na akaanza kulia. Akasema Allaah ('Azza wa Jalla): "Ee Jibriyl! Nenda kwa Muhammad na Rabb wako ni mjuzi zaidi na umuulize ni kipi kinachomliza (yaani analia kwa nini)?" Jibriyl ('Alayhi sallaam) alikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye akamwambia alichokisema na Allaah anajua zaidi. Akasema Allaah Ta'aalaa: "Ee Jibriyl! Nenda kwa Muhammad na umwambie: 'Hakika tutakufanya uridhike kwa Ummah wako na hatutakufanya uhuzunike'." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 15

وعن معاذ بن جبل رضي الله عنه، قَالَ : كُنْتُ رِدْفَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم عَلَى حِمَارٍ ، فَقَالَ : (( يَا مُعَاذُ ، هَلْ تَدْرِي مَا حَقُّ الله عَلَى عِبَادِهِ ؟ وَمَا حَقُّ العِبَادِ عَلَى الله ؟ )) قُلْتُ : اللهُ وَرَسُولُهُ أعْلَمُ . قَالَ : (( فإنَّ حَقَّ اللهِ عَلَى العِبَادِ أنْ يَعْبُدُوهُ ، وَلاَ يُشْرِكُوا بِهِ شَيئاً ، وَحَقَّ العِبَادِ عَلَى اللهِ أنْ لاَ يُعَذِّبَ مَنْ لا يُشْرِكُ بِهِ شَيئاً ))  فقلتُ : يَا رَسُول الله ، أفَلا أُبَشِّرُ النَّاسَ ؟ قَالَ : (( لاَ تُبَشِّرْهُمْ فَيَتَّكِلُوا )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Mu'aadh bin Jabal (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Nilikuwa nimepanda nyuma ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya punda, akaniambia: "Ee Mu'aadh! Unajua haki ya Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi." Akasema: "Hakika haki ya Allaah juu ya waja Wake wamuabudu wala wasimshirikishe na chochote. Na haki ya waja kwa Allaah, ni kumuadhibu asiyemshirikisha na chochote." Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Je nisiwabashirie wakabweteka." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 16

وعن البراءِ بن عازب رضي الله عنهما ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( المُسْلِمُ إِذَا سُئِلَ في القَبْرِ يَشْهَدُ أنْ لاَ إلَهَ إلاَّ الله ، وَأنّ مُحَمّداً رَسُول الله ، فذلك قوله تَعَالَى: ( يُثَبِّتُ اللهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي  الآخِرَة ) [ إبراهيم : 27 ] )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

Imepokewa kutoka kwa Al-Baraa'a bin 'Aazib (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muislamu atakapoulizwa kaburini, anashuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Allaah, na kuwa Muhammad ni Rasuli Wake, hiyo ni kauli Yake Ta'aalaa: "Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika uhai wa dunia na Aakhirah." [Ibraahiym: 27] 

 

 

Hadiyth – 17

وعن أنس رضي الله عنه ، عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنّ الكَافِرَ إِذَا عَمِلَ حَسَنَةً ، أُطعِمَ بِهَا طُعْمَةً مِنَ الدُّنْيَا ، وَأَمَّا المُؤْمِنُ فَإنَّ الله تَعَالَى يَدَّخِرُ لَهُ حَسَنَاتِهِ في الآخِرَةِ ، وَيُعْقِبُهُ رِزْقاً في الدُّنْيَا عَلَى طَاعَتِهِ )) .

وفي رواية : (( إنَّ الله لاَ يَظْلِمُ مُؤْمِناً حَسنَةً يُعْطَى بِهَا في الدُّنْيَا ، وَيُجْزَى بِهَا في الآخِرَةِ . وَأَمَّا الكَافِرُ فَيُطْعَمُ بِحَسَنَاتِ مَا عَمِلَ للهِ تَعَالَى في الدُّنْيَا ، حَتَّى إِذَا أفْضَى إِلَى الآخرَةِ ، لَمْ يَكُنْ لَهُ حَسَنَةٌ يُجْزَى بِهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika kafiri akifanya jema, hulishwa chakula duniani, Ama Muumini Allaah Ta'aalaa anamuwekea amali yake njema Aakhirah, na anampa riziki hapa duniani kwa sababu ya utiifu wake." 

Na katika riwaayah nyengine: "Hakika Allaah hamdhulumu Muumini aliyefanya mambo mema anampa duniani, na kumlipa nayo nayo Aakhirah. Ama kafiri analishwa kwa mema aliyoyafanya kwa ajili ya Allaah duniani; hadi akifika Aakhirah, hawi na mema yoyote ya kulipwa huko." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 18

وعن جابر رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَثَلُ الصَّلَوَاتِ الخَمْسِ كَمَثَلِ نَهْرٍ جَارٍ غَمْرٍ عَلَى بَابِ أحَدِكُمْ يَغْتَسِلُ مِنْهُ كُلَّ يَوْم خَمْسَ    مَرَّات )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: "Mfano wa Swalaah tano ni kama mfano wa mto mkubwa unaopita mbele ya mlango wa mmoja wenu, ambaye atakuwa anajiosha kila siku mara tano." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 19

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( مَا مِنْ رَجُلٍ مُسْلِمٍ يَمُوتُ ، فَيقُومُ عَلَى جَنَازَتهِ أرْبَعونَ رَجُلاً لاَ يُشْرِكُونَ بِاللهِ شَيئاً ، إلاَّ شَفَّعَهُمُ اللهُ فِيهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakuna Muislamu yeyote ambaye anaaga dunia, wakasimama watu arobaini kumswalia (Swalaah ya Jeneza) wasiomshirikisha Allaah na chochote isipokuwa Allaah anakubali maombi yao." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 20

وعن ابن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : كُنَّا مَعَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم في قُبَّة نَحْوَاً مِنْ أربَعِينَ ، فَقَالَ : (( أتَرْضَونَ أنْ تَكُونُوا رُبُعَ أهْلِ الجَنَّةِ ؟ )) قُلْنَا : نَعَمْ . قَالَ :  (( أتَرْضَوْنَ أنْ تَكُونُوا ثُلُثَ أهلِ الجَنَّةِ ؟ )) قُلْنَا : نَعَمْ ، قَالَ : (( وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمّدٍ بيَدِهِ ، إنِّي لأَرْجُو أنْ تَكُونُوا نِصْفَ أهْلِ الجَنَّةِ وذلك أنَّ الجنَّةَ لاَ يَدْخُلُهَا إلاَّ نَفْسٌ مُسْلِمَةٌ ، ومَا أنْتُم في أهْلِ الشِّركِ إلاَّ كَالشَّعْرَةِ البَيْضَاءِ في جلدِ الثَّورِ  الأَسْوَدِ ، أَوْ كَالشَّعْرَةِ السَّودَاءِ في جلدِ الثَّورِ الأحْمَر )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Tulikuwa takriban watu arobaini katika nyumba ndogo pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Je, mtaridhia kuwa robo ya watu wa Peponi?" Tulisema: "Ndio." Akasema: "Je, mtaridhia kuwa thulithi ya watu wa Peponi?" Tulisema: "Ndio." Akasema: "Naapa kwa ambaye nafsi ya Muhammad ipo mkononi Mwake, hakika nina matarajio kuwa nyinyi mtakuwa nusu ya watu wa Peponi. Na hiyo kwa sababu ya kuwa hataingia Peponi ila nafsi ya Muislamu. Na idadi yenu kulinganishwa na watu wa shirki ni kama nywele nyeupe katika ngozi ya fahali mweusi, au nywele nyeusi katika ngozi ya fahali mwekundu." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 21

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا كَانَ يَوْمُ القِيَامَةِ دَفَعَ اللهُ إِلَى كُلِّ مُسْلِم يَهُودياً أَوْ نَصْرانِياً ، فَيَقُولُ : هَذَا فِكَاكُكَ مِنَ النَّارِ )) .

وفي رواية عَنْهُ ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( يَجِيءُ يَوْمَ القِيَامَةِ نَاسٌ مِنَ المُسْلِمينَ بِذُنُوبٍ أَمْثَال الجِبَالِ يَغْفِرُهَا الله لَهُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Itakapokuwa siku ya Qiyaamah Allaah atampa kila Muislamu Yahudi au Mnasara, Atasema: 'Hii ni fidiya yako na Moto'." 

Katika riwaayah yake nyingine: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watakuja watu Siku ya Qiyaamah miongoni mwa Waislamu na madhambi mfano wa mlima, Allaah atawasamehe (madhambi yao hayo)." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 22

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم،   يقول : (( يُدْنَى المُؤْمِنُ يَوْمَ القِيَامَة مِنْ رَبِّهِ حَتَّى يَضَعَ كَنَفَهُ عَلَيهِ ، فَيُقَرِّرُهُ بذُنُوبِهِ ، فيقولُ : أتعرِفُ ذَنْبَ كَذَا ؟ أتَعرفُ ذَنْبَ كَذَا ؟ فيقول : رَبِّ أعْرِفُ ، قَالَ : فَإنِّي قَدْ سَتَرْتُهَا عَلَيْكَ في الدُّنْيا ، وَأنَا أغْفِرُهَا لَكَ اليَومَ ، فَيُعْطَى صَحيفَةَ    حَسَنَاتِهِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  akisema: "Muumini atasogezwa karibu na Mola wake Siku ya Qiyaamah na kumfunika kwa sitara Yake. Atamuulizia dhambi zake, Atasema:, 'Unajua dhambi kadhaa? Unajua dhambi kadhaa?' Atasema: 'Mola wangu najua, Atasema: Mimi nimekusitiri duniani, Nami ninaisamehe kwako leo. Atapewa sahifa ya mema yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 23

وعن ابن مسعود رضي الله عنه: أنَّ رَجُلاً أصَابَ مِن امْرَأة قُبْلَةً ، فَأتَى النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم فَأخْبَرَهُ ، فَأنْزَلَ الله تَعَالَى : ( وَأَقِمِ الصَّلاةَ طَرَفَيِ النَّهَارِ وَزُلَفاً مِنَ اللَّيْلِ إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَات ) [ هود : 114] فَقَالَ الرجل: أَليَ هَذَا يَا رَسُول الله ؟ قَالَ : (( لجميعِ أُمَّتِي كُلِّهِمْ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaah 'anhu) kuwa : Mtu mmoja alimbusu mwanamke ajnabi, akaja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kumwelezea hilo. Allaah Ta'aalaa akateremsha: "Na simamisha Swalaah katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku; hakika mema yanaondosha maovu." [Huwd: 114]. Akasema yule mtu: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, hili ni langu?" Akasema: "Ni kwa Ummah wangu wote." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 24

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ: جاء رجل إِلَى النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : يَا رَسُول الله، أَصَبْتُ حَدّاً ، فَأَقِمْهُ عَلَيَّ ، وَحَضَرَتِ الصَّلاةُ ، فَصَلَّى مَعَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، فَلَمَّا قَضَى الصَّلاةَ ، قَالَ : يَا رَسُول الله ، إنِّي أصَبْتُ حَدّاً فَأقِمْ فيَّ كِتَابَ الله . قَالَ : (( هَلْ حَضَرْتَ مَعَنَا الصَّلاةَ )) ؟ قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : (( قَدْ غُفِرَ لَكَ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Nimefanya kosa la kusimamishiwa hadd, kwa hivyo isimamishe." Wakati wa Swalaah ulifika, naye (huyo mtu) akaswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Baada ya swalaah alisema tena: "EeRasuli wa Allaah! Nimefanya kosa la kusimamishiwa hadd kwa hivyo isimamishe kulingana na Kitabu cha Allaah." Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je, umeswali na sisi?" Akasema: "Ndio." Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika umesamehe (kosa lako hilo)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 25

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ الله لَيرْضَى عَنِ العَبْدِ أنْ يَأكُلَ الأَكْلَةَ ، فَيَحْمَدُهُ عَلَيْهَا ، أَوْ يَشْرَبَ الشَّرْبَةَ ، فَيَحْمَدُهُ عَلَيْهَا )) رواه مسلم

Na imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah anamridhia mja anayekula chakula na baadae akamuhimidi (akamshukuru Allaah) au akanywa kinywaji kisha akamuhimidi kwa ajili ya kupata kinywaji hicho." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 26

وعن أَبي موسى رضي الله عنه  ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ الله تَعَالَى يَبْسُطُ يَدَهُ باللَّيلِ ليَتُوبَ مُسِيءُ النَّهَارِ ، وَيَبْسُطُ يَدَهُ بالنَّهَارِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ اللَّيلِ ، حَتَّى تَطلُعَ الشَّمْسُ مِنْ مَغْرِبِهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muuwsaa 'Abdillahi bin Qays al-Ash'ariy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ta'aalaa hunyoosha mkono Wake usiku wapate kutubia mpaka jua lichomoza upande wa magharibi." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 27

وعن أَبي نجيح عمرو بن عَبَسَة - بفتح العين والباءِ - السُّلَمِيِّ رضي الله عنه، قَالَ : كُنْتُ وأنَا في الجاهِلِيَّةِ أظُنُّ أنَّ النَّاسَ عَلَى ضَلاَلَةٍ ، وَأَنَّهُمْ لَيْسُوا عَلَى شَيْءٍ ، وَهُمْ يَعْبُدُونَ الأَوْثَانَ ، فَسَمِعْتُ بِرَجُلٍ بِمَكَّةَ يُخْبِرُ أخْبَاراً ، فَقَعَدْتُ عَلَى رَاحِلَتِي ، فَقَدِمْتُ عَلَيهِ ، فإِذَا رسولُ الله  صلى الله عليه وسلم مُسْتَخْفِياً ، جرَءاءُ عَلَيهِ قَومُهُ ، فَتَلَطَّفَتُ حَتَّى دَخَلْتُ عَلَيهِ بِمَكَّةَ ، فَقُلْتُ لَهُ : مَا أنْتَ ؟ قَالَ : (( أنا نَبيٌّ )) قُلْتُ : وما نبيٌّ ؟ قَالَ : (( أرْسَلَنِي الله )) قُلْتُ : وبأيِّ شَيْء أرْسَلَكَ ؟ قَالَ : (( أَرْسَلَنِي بِصِلَةِ الأرْحَامِ ، وَكَسْرِ الأَوْثَانِ ، وَأنْ يُوَحَّدَ اللهُ لاَ يُشْرَكُ بِهِ شَيْء )) قُلْتُ : فَمَنْ مَعَكَ عَلَى هَذَا ؟ قَالَ : (( حُرٌّ وَعَبْدٌ )) ومعه يَوْمَئذٍ أَبُو بكرٍ وبلالٌ رضي الله عنهما ، قُلْتُ : إنّي مُتَّبِعُكَ ، قَالَ : (( إنَّكَ لَنْ تَسْتَطيعَ ذلِكَ يَومَكَ هَذَا ، ألا تَرَى حَالي وحالَ النَّاسِ ؟ وَلَكِنِ ارْجعْ إِلَى أهْلِكَ فَإِذَا سَمِعْتَ بي قَدْ ظَهرْتُ فَأتِنِي )) قَالَ : فَذَهَبْتُ إِلَى أهْلِي وقَدِمَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم  المَدِينَةَ حَتَّى قَدِمَ نَفَرٌ مِنْ أهْلِي المَدِينَةَ ، فقلتُ : مَا فَعَلَ هَذَا الرَّجُلُ الَّذِي قَدِمَ المَدِينَةَ ؟ فقالوا : النَّاس إلَيهِ سِرَاعٌ ، وَقَدْ أرادَ قَومُهُ قَتْلَهُ ، فلَمْ يَسْتَطِيعُوا ذلِكَ ، فقَدِمْتُ المدينَةَ ، فَدَخَلْتُ عَلَيهِ ، فقلتُ : يَا رَسُول الله أَتَعْرِفُني ؟ قَالَ : (( نَعَمْ ، أنْتَ الَّذِي لَقَيْتَنِي بمكّةَ )) قَالَ : فقلتُ : يَا رَسُول الله ، أخْبِرنِي عَمَّا عَلَّمَكَ الله وأَجْهَلُهُ ، أخْبِرْنِي عَنِ الصَّلاَةِ ؟ قَالَ : (( صَلِّ صَلاَةَ الصُّبْحِ ، ثُمَّ اقْصُرْ عَنِ الصَّلاَةِ حَتَّى تَرْتَفِعَ الشَّمْسُ قِيدَ رُمْحٍ ، فَإنَّهَا تَطْلُعُ حِينَ تَطلُعُ بَيْنَ قَرْنَيْ شَيطَان ، وَحينَئذٍ يَسجُدُ لَهَا الكُفَّارُ ، ثُمَّ صَلِّ فَإنَّ الصَلاَةَ مَشْهُودَةٌ مَحْضُورةٌ حَتَّى يَسْتَقِلَّ الظِّلُّ بالرُّمْحِ ، ثُمَّ اقْصُرْ عَنِ الصَّلاةِ ، فَإنَّهُ حينئذ تُسْجَرُ جَهَنَّمُ ، فإذَا أقْبَلَ الفَيْءُ فَصَلِّ ، فَإنَّ الصَّلاةَ مَشْهُودَةٌ مَحضُورَةٌ حَتَّى تُصَلِّي العصرَ ، ثُمَّ اقْصرْ عَنِ الصَّلاةِ حَتَّى تَغْرُبَ الشَّمْسُ ، فإنَّهَا تَغْرُبُ بينَ قَرْنَيْ شَيطانٍ ، وَحِينَئذٍ يَسْجُدُ لَهَا الكُفّارُ )) قَالَ : فقلتُ : يَا نَبيَّ الله ، فالوضوءُ حدثني عَنْهُ ؟ فَقَالَ : (( مَا مِنْكُمْ رَجُلٌ يُقَرِّبُ وَضُوءهُ ، فَيَتَمَضْمَضُ وَيسْتَنْشِقُ فَيَسْتَنْثِرُ ، إلاَّ خَرَّتْ خَطَايَا وَجْهِهِ مِنْ أطْرَافِ لِحْيَتِهِ مَعَ المَاءِ ، ثُمَّ يَغْسِلُ يديهِ إِلَى المِرفقَيْن ، إلاَّ خَرَّتْ خَطَايَا يَدَيْهِ مِنْ أنَامِلِهِ مَعَ الماءِ ، ثُمَّ يَمْسَحُ رَأسَهُ ، إلاَّ خرّتْ خطايا رأسِهِ من أطْرَافِ شَعْرِهِ مَعَ الماءِ ، ثُمَّ يغسل قدميه إِلَى الكعْبَيْنِ ، إلاَّ خَرَّتْ خَطَايَا رِجلَيْهِ مِنْ أنَاملِهِ مَعَ الماءِ ، فَإنْ هُوَ قَامَ فَصَلَّى ، فَحَمِدَ الله تَعَالَى ، وأثنى عَلَيهِ ومَجَّدَهُ بالَّذي هُوَ لَهُ أهْلٌ ، وَفَرَّغَ قلبه للهِ تَعَالَى ، إلاَّ انْصَرفَ مِنْ خَطِيئَتِهِ كهيئته يَومَ وَلَدتهُ أُمُّهُ )) .

فحدث عَمرُو بن عَبسَة بهذا الحديث أَبَا أُمَامَة صاحِب رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ لَهُ أَبُو أُمَامَة : يَا عَمْرُو بنُ عَبسَة ، انْظُر مَا تقولُ ‍! في مقامٍ واحدٍ يُعْطَى هَذَا الرَّجُلُ ؟ فَقَالَ عَمْرٌو : يَا أَبَا أُمَامَة ، لقد كَبرَتْ سِنّي ، وَرَقَّ عَظمِي ، وَاقْتَرَبَ  أجَلِي ، وَمَا بِي حَاجَةٌ أنْ أكْذِبَ عَلَى اللهِ تَعَالَى ، وَلا عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، لَوْ لَمْ أسمعه مِنْ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، إلاَّ مَرَّةً أَوْ مَرَّتَينِ أَوْ ثَلاثاً – حَتَّى عَدَّ سَبْعَ مَرَّات – مَا حَدَّثْتُ أبداً بِهِ ، وَلكنِّي سمعتُهُ أكثَر من ذلِكَ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Najiih 'Amru bin 'Asabah As-Sulamiy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Katika siku zangu za Ujahiliyyah nilikuwa nadhani kuwa watu wapo katika upotevu na wao hawakuwa katika kitu chochote (katika kufuata Dini ya haki). Watu wakati huo walikuwa wakiabudu masanamu. Nilisikia habari ya kwamba yupo mtu Makkah aliyekuwa akieleza kuhusu jambo jipya. Nilipanda kipandio changu na nikaelekea Makkah na nilipofika nilikutana na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye alikuwa akifanya mambo yake kwa siri kwa sababu ya mateso kutoka kwa watu wake. Nilijificha mpaka nikapata nafasi ya kukutana naye hapo Makkah, na hapo nikamuuliza: "Wewe ni nani?" Akasema: "Mimi ni Nabiy" Nikasema: "Na Nabiy ni nini?" Akasema: "Nimetumwa na Allaah." Nikasema: "Amekutuma na kitu gani?" Akasema: "Amenituma kuunganisha kizazi, na kuvunja masanamu, na kumpwekesha Allaah wala asishirikishwe na chochote." Nikamuuliza: "Na ni akina nani ambao wako nawe juu ya hili?" Akasema: "Watu walio huru pamoja na watumwa." Na wakati huo alikuwa pamoja na Abu Bakr na Bilaal. Nikasema: "Mimi nakufuata wewe." Akasema: "Hakika wewe huwezi kufanya hivyo sasa, je huoni hali yangu na watu? Lakini nenda zako kwa familia yako na pindi utakaposikia ya kuwa nimefaulu katika jukumu basi wakati huo njoo kwangu." Kwa hali hiyo nilirudi kwa familia na watu wangu na Rasuli wa Allaah alihama Madinah. Nilibaki pamoja na familia yangu na huku ninafuatilia habari na nikawa nawauliza watu kuhusu Rasuli wa Allaah mpaka baadhi ya watu wangu walipozuru Madinah. Nikawauliza (waliporudi): "Huyu mtu aliyehamia Madinah amefanya nini?" Wakasema: "Watu wanakwenda kwake kukubali ujumbe wake (kusilimu) japokuwa watu wake walikuwa wanataka kumuua lakini wakashindwa." Niliwasili Madinah na nikafika kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na kumuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, unanifahamu?" Akasema: "Ndio, wewe ni yule uliyenikuta Makkah." Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Nijulishe yale aliyokuelimisha Allaah ambayo siyajui na unipe habari ya Swalaah?" Akasema: "Swali Swalaah ya Asubuhi (Swalatul Fajr), kisha jiweke kando (usiswali) mpaka jua liwe limepanda juu ya mbingu kiasi cha mkuki, kwani linapochomoza linachomoza baina ya pembe mbili za Shetani na wakati huo ndio makafiri wanalisujudia. Baada ya hapo unaweza kuswali, kwani Swalaah inashuhudiwa na inahudhuriwa na Malaika mpaka kivuli cha mkuki kiwe sawa (kwa kupotea) na urefu wa mkuki. Baada ya hapo usiswali, kwani wakati huo Moto uantiwa kuni (za kuuwakisha). Kivuli kitakaporefuka basi Swali, kwani Swalaah inashuhudiwa na ianhudhuriwa na Malaika mpaka wakati wa Alasiri. Baada ya hapo jiepushe kuswali mpaka machweo, kwani jua linakuchwa (linazama) baina ya pembe mbili za Shetani na wakati huo makafiri wanalisujudia." Hapo nikasema: "Ee Nabiy wa Allaah! Wudhu', nihadithie kuhusu hilo." Akasema: "Hakuna mtu yeyote ambaye atachukua maji ya kutawadhia, akasukutua na kusafisha pua yake isipokuwa madhambi ya pua na modomo wake yanaoshwa na kutolewa nje. Kisha anapoosha uso wake kama alivyoamrisha Allaah isipokuwa madhambi yake ya uso yanadondoka pembezoni mwa ndevu zake pamoja na maji. Kisha anaosha mikono yake mpaka vifundoni, isipokuwa hudondoka madhambi ya mikono yake kwenye vidole pamoja na maji. Kisha anapaka kichwa chake, isipokuwa hutoka madhambi yote ya kichwa kutoka katika mwisho wa nywele pamoja na maji hayo. Kisha anaosha miguu yake mpaka vifundoni isipokuwa makosa yote ya miguu hufutwa pamoja na maji yanapotoka. Na hapo anaposimama kuswali, akamuhimidi Allaah Ta'aalaa, akamsifu na kumtukuza kwa lile ambalo Yeye ndiye Mwenyewe (anastahiki zaidi) na akaufanya moyo wake unyenyekee kikamilifu kwa ajili ya Allaah Ta'aalaa isipokuwa makosa yake yote hufutwa akawa yuko katika hali kama ile siku aliyezaliwa na mamake. Pale 'Amru bin 'Abasah alipomuhadithia Hadiyth hii Abu Umamah, Swahaaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), Abu Umamah alimwambia: "Ee 'Amru: "Ee Abu Umamah! Hakika nimekuwa mzee na mifupa yangu imekauka na ajali yangu imekaribia (kufa kwangu) na wala sina haja yeyote ya kusema uwongo juu ya Allaah Ta'aalaa wala juu ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Lau kama sikumsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mara moja au mbili au tatu na akahesabu mpaka kufika mara saba nisingekuwa ni mwenye kumhadithia yeyeote milele lakini nimesikia zaidi ya hivyo." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 28

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا أرادَ الله تَعَالَى رَحمةَ أُمَّةٍ ، قَبَضَ نَبيَّهَا قَبْلَها ، فَجعلهُ لَهَا فَرطاً وسلَفاً بَيْنَ يَديْهَا ، وإذَا أرادَ هَلَكَةَ أُمَّةٍ ، عَذَّبَهَا وَنَبِيُّهَا حَيٌّ ، فَأهلكَها وَهُوَ حيٌّ يَنظُرُ ، فَأقرّ عَينَهُ بهلاكِها حِينَ كَذَّبُوهُ وَعَصَوا أمْرَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muuwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapotaka Allaah Mtukufu rahma kwa watu, Humfisha Nabiy wao kabla yao, na kufanya ishara, na mtangulizi siku ya mwisho; na Anapotaka Kuangamiza watu, Huwaadhibu na Nabiy wao yu hai, na Huwaangamiza Nabiy wao akiwatazama, Hutuliza jicho lake kwa kuangamia kwao, kwa kumkadhibisha kwao na kuasi amri yake." [Muslim]

 

 

 

 

 

Share

052-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ubora wa Matarajio Mema

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل الرجاء

052-Mlango Wa Ubora wa Matarajio Mema

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَأُفَوِّضُ أَمْرِي إِلَى اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ بَصِيرٌ بِالْعِبَادِ﴿٤٤﴾

Na naaminisha mambo yangu kwa Allaah. Hakika Allaah ni Mwenye kuona waja Wake. [Ghaafir: 44]

 

 

فَوَقَاهُ اللَّـهُ سَيِّئَاتِ مَا مَكَرُوا ۖ ﴿٤٥﴾

Basi Allaah Akamlinda na maovu ya yale waliyoyapangia njama. [Ghaafir: 45]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم، أَنَّهُ قَالَ : (( قَالَ الله (عزّ وجلّ: أَنَا عِنْدَ ظَنِّ عَبْدِي بِي ، وَأَنا معه حَيْثُ يَذْكُرنِي ، وَاللهِ ، للهُ أفْرَحُ بِتَوبَةِ عَبْدِهِ مِنْ أحَدِكُمْ يَجِدُ ضَالَّتَهُ بالفَلاَةِ ، وَمَنْ تَقَرَّبَ إلَيَّ شِبْراً ، تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ ذِرَاعاً ، وَمَنْ تَقَرَّبَ إِلَيَّ ذِرَاعاً ، تَقَرَّبْتُ إِلَيْهِ بَاعاً ، وَإِذَا أقْبَلَ إِلَيَّ يَمْشِي أقْبَلْتُ إِلَيْهِ أُهَرْوِلُ )) متفقٌ عليه ، وهذا لفظ إحدى روايات مسلم . وتقدم شرحه في الباب قبله.

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Amesema Allaah ('Azza wa Jalla): "Hakika Mimi namchukulia mja kwa anavyonichukulia, Nami nipo pamoja naye pale anaponitaja. Naapa kwa Allaah! Allaah ana furaha zaidi kwa toba ya mja Wake kuliko mmoja wenu anayempata ngamia wake aliyepotea jangwani. Na yeyote anayekuja karibu Nami kwa shibiri, Mimi nakuja karibu yake kwa dhiraa. Yule anayekuja karibu Nami kwa dhiraa, Mimi nakuja kwake kwa kiasi cha pima moja. Na anayekuja Kwangu kwa kutembea, Mimi nakuja kwake kwa kukimbia." [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na hii ni lafdhi moja wapo ya riwaayah ya Muslim. Na imepokewa katika Swahiyh mbili: "Nami niko pamoja naye anaponikumbuka na kunitaja."

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما : أنه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم قبلَ مَوْتِه بثَلاثَةِ أيّام ، يقولُ : (( لاَ يَمُوتَنّ أحَدُكُمْ إِلاَّ وَهُوَ يُحْسِنُ الظَّنَّ بالله (عزّ وجلّ) )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Jaabir bin 'Abdillaah (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa yeye amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kabla ya mauti yake kwa siku tatu akisema: "Asife mmoja wenu isipokuwa atarajie mema na mazuri kutoka kwa Allaah ('Azza wa Jalla)." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ : سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( قَالَ الله تَعَالَى : يَا ابْنَ آدَمَ ، إنَّكَ ما دَعَوْتَنِي وَرَجَوْتَنِي غَفَرْتُ لَكَ عَلَى مَا كَانَ مِنْكَ وَلاَ أُبَالِي . يَا ابْنَ آدَمَ ، لَوْ بَلَغت ذُنُوبُك عَنَانَ السماءِ ، ثُمَّ اسْتَغْفَرْتَنِي غَفَرْتُ لَكَ وَلاَ أُبَالِي . يَا ابْنَ آدَمَ ، إِنَّكَ لَوْ أتَيْتَنِي بِقُرَابِ الأَرْضِ خَطَايا ، ثُمَّ لَقَيْتَنِي لاَ تُشْرِكُ بِي شَيْئاً ، لأَتَيْتُكَ بقُرَابِها مَغْفِرَةً )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaahu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema kwamba Allaah Ta'aalaa amesema: "Ee binadamu, hakika wewe kila unapoendelea kuniomba na kunitarajia, basi Nitakusamehe dhambi ulizonazo wala sijali. Ee binadamu, hata kama dhambi zako zikifika mpaka mawinguni, kisha ukaniomba msamaha, Nitakughufiria. Ee binadamu, hakika wewe lau wanijia na makosa yenye kujaa ardhi kisha ukanikabili Mimi na hali hunishirikishi na kitu chochote, basi Nitakupa mfano wake maghfira." [At-Tirmidhiy, na alisema ni Hadiyth Hasan.

 

 

 

 

Share

053-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kujumuisha Baina ya Hofu na Matarajio

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الجمع بين الخوف والرجاء

053-Mlango Wa Kujumuisha Baina ya Hofu na Matarajio

 

Alhidaaya.com

 

اعْلَمْ أنَّ المُخْتَارَ لِلْعَبْدِ في حَالِ صِحَّتِهِ أنْ يَكُونَ خَائفاً رَاجِياً ، وَيَكُونَ خَوْفُهُ وَرَجَاؤُهُ سَواءً ، وفي حَالِ المَرَضِ يُمحَّضُ الرَّجاءُ ، وقواعِدُ الشَّرْع مِنْ نصُوصِ الكِتَابِ والسُّنَةِ وغَيْرِ ذَلِكَ مُتظاهِرَةٌ عَلَى ذلك .

Imam An-Nawawiy anasema: "Mja wa Allaah anatakiwa ajue ya kwamba inapendeza kwake akiwa katika hali ya siha nzuri awe ni mwenye kuwa na hofu kwa Allaah Ta'aalaa na matarajio. Na hofu yake na matumaini yake yawe sawa sawa. Na anapokuwa mgonjwa anatakiwa awe na Imani thabiti pamoja na matarajio yaliyo makubwa zaidi. Katika hili kanuni za sheria ya Kiislamu zipo wazi kabisa kwa naswi (maandiko) katika Kitabu (Qur-aan) na Sunnah na nyinginezo."

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩٩﴾

Basi hawaaminishi mipango ya Allaah isipokuwa watu wenye kukhasirika. [Al-A'raaf: 99]

 

إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٧﴾

Hakika hawakati tamaa na faraja ya Allaah isipokuwa watu makafiri. [Yuwsuf: 87]

 

يَوْمَ تَبْيَضُّ وُجُوهٌ وَتَسْوَدُّ وُجُوهٌ ۚ  ﴿١٠٦﴾ 

Siku nyuso zitakuwa nyeupe na nyuso (nyingine) zitakuwa nyeusi. [Aal-'Imraan: 106]

 

إِنَّ رَبَّكَ سَرِيعُ الْعِقَابِ وَإِنَّهُ لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٦٥﴾

Hakika Rabb wako ni Mwepesi wa kuakibu, na hakika Yeye bila shaka ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-An'aam: 165]

 

إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ ﴿١٣﴾ وَإِنَّ الْفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٍ ﴿١٤﴾

Hakika Waumini watendao mema kwa wingi bila shaka watakuwa katika neema (taanasa, furaha n.k). Na hakika watendao dhambi bila shaka watakuwa katika moto uwakao vikali mno. [Al-Infitwaar: 13-14]

 

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ ﴿٦﴾ فَهُوَ فِي عِيشَةٍ رَّاضِيَةٍ ﴿٧﴾ وَأَمَّا مَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ ﴿٨﴾ فَأُمُّهُ هَاوِيَةٌ ﴿٩﴾

Basi yule itakayekuwa mizani yake nzito. Huyo atakuwa katika maisha ya kuridhisha. Na yule itakayekuwa mizani yake khafifu.Basi makazi yake ni Haawiyah. [Al-Qaari-'ah: 6-9]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَوْ يَعْلَمُ الْمُؤمِنُ مَا عِنْدَ الله مِنَ العُقُوبَةِ ، مَا طَمِعَ بِجَنَّتِهِ أَحَدٌ ، وَلَوْ يَعْلَمُ الكَافِرُ مَا عِنْدَ الله مِنَ الرَّحْمَةِ ، مَا قَنَطَ مِنْ جَنَّتِهِ أحَدٌ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau kama Muumini atajua ile adhabu kamili ya Allaah, hangetamani yeyote Pepo Yake. Na lau kafiri angejua kwa ukamilifu wake rehema aliyonayo Allaah, asingekata tamaa yeyote na Pepo Yake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي سعيد الخدرِيِّ رضي الله عنه: أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( إِذَا وُضِعَتِ الجنازةُ واحْتَمَلَهَا النَّاسُ أَوِ الرِّجَالُ عَلَى أعناقِهِمْ ، فَإنْ كَانَتْ صَالِحَةً ، قالتْ: قَدِّمُونِي قَدِّمُونِي ، وَإنْ كَانَتْ غَيْرَ صَالِحَةٍ ، قالتْ : يَا وَيْلَهَا ! أَيْنَ تَذْهَبُونَ بها ؟ يَسْمَعُ صَوْتَها كُلُّ شَيْءٍ إِلاَّ الإنْسانُ ، وَلَوْ سَمِعَهُ صَعِقَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Itakapokuwa tayari jeneza na ikabebwa na watu juu ya mabega yao, akiwa ni mtu mwema atasema: 'Nipelekeni mbele, nipelekeni mbele. Na ikiwa si mwema, atasema: 'Ole wake! Mnanipeleka wapi?' Sauti yake inasikika na kila kitu isipokuwa mwanadamu na lau angesikia (mwanadamu) basi angezimia." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( الجَنَّةُ أقْرَبُ إِلى أحَدِكُمْ مِنْ شِرَاكِ نَعْلِهِ ، وَالنَّارُ مِثْلُ ذلك )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (SWalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pepo ipo karibu sana na mmoja wenu kuliko kamba zake za viatu na Moto ni mfano wa hivyo." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Share

054-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila ya Kulia Kutokana na Kumuogopa Allaah na Shauku Kwake

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل البكاء من خشية الله تَعَالَى وشوقاً إِليه

054-Mlango Wa Fadhila ya Kulia Kutokana na Kumuogopa Allaah na Shauku Kwake

 

Alhidaaya.com 

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَيَخِرُّونَ لِلْأَذْقَانِ يَبْكُونَ وَيَزِيدُهُمْ خُشُوعًا ۩﴿١٠٩﴾

Na wanaporomoka kifudifudi huku wanalia na inawazidishia unyenyekevu. [Al-Israa: 109]

 

أَفَمِنْ هَـٰذَا الْحَدِيثِ تَعْجَبُونَ ﴿٥٩﴾ وَتَضْحَكُونَ وَلَا تَبْكُونَ ﴿٦٠﴾

Je, mnastaajabu kwa Al-Hadiyth hii (ya Qur-aan)? Na mnacheka na wala hamlii? [An-Najm: 59-60]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ لِي النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: (( اقْرَأْ عليَّ    القُرْآنَ )) قلت : يَا رسول اللهِ ، أقرأُ عَلَيْكَ ، وَعَلَيْكَ أُنْزِلَ ؟! قَالَ : (( إِنِّي أُحِبُّ أنْ أسْمَعَهُ مِنْ غَيرِي )) فَقَرَأْتُ عَلَيْهِ سورةَ النِّسَاءِ ، حَتَّى جِئْتُ إِلى هذِهِ الآية :( فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِنْ كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهيدٍ وَجِئْنَا بِكَ عَلَى هؤُلاءِ شَهيداً) [ النساء : 41 ] قَالَ : (( حَسْبُكَ الآنَ )) فَالَتَفَتُّ إِلَيْهِ فإذا عَيْنَاهُ تَذْرِفَان . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Nisomee Qur-aan." Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! nikusomee Qur-aan na juu yako imeteremshwa?" Akasema: "Mimi napenda niisikie kwa mwingine Hivyo nikamsomea Suwrah an-Nisaa' mpaka nikafika katika ayah hii: "Basi itakuwaje Tutakapoleta kutoka kila Ummah shahidi, na Tukakuleta (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa shahidi juu ya hawa?" [An-Nisaa: 41]. Akasema: "Inatosha sasa." Tahamaki macho yake yanabubujika machozi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ : خطب رسول الله صلى الله عليه وسلم خُطْبَةً مَا سَمِعْتُ مِثْلَهَا قَطُّ ، فقال : (( لَوْ تَعْلَمُونَ مَا أعْلَمُ ، لَضَحِكْتُمْ قَليلاً وَلَبَكَيْتُمْ كَثِيراً )) قَالَ : فَغَطَّى أصْحَابُ رسول الله صلى الله عليه وسلم وُجُوهَهُمْ ، وَلَهُمْ خَنِينٌ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas ambaye amesema: "Alituhutubia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hotuba ambayo sijawahi kusikia mfano wake kabisa, akasema: 'Lau nyinyi mgejua ninayoyajua basi mgecheka kidogo na kulia sana.' Hapo Swahaaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) waliokuwepo walifunika nyuso zao na kuanza kumamia (kulia) kwa kwikwi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( لا يَلِجُ النَّارَ رَجُلٌ بَكَى مِنْ خَشْيَةِ اللهِ حَتَّى يَعُودَ اللَّبَنُ في الضَّرْعِ ، وَلاَ يَجْتَمِعُ غُبَارٌ في سبيلِ اللهِ وَدُخَانُ جَهَنَّمَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديثٌ حَسنٌ صحيحٌ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hataingia Motoni mtu ambaye Amelia kwa kumuogopa Allaah mpaka maziwa yarudi katika matiti yake na pia vumbi liliopatikana kwa mtu kufanya Jihadi katika njia ya Allaah na moshi wa Jahanam haziungani pamoja." [At-Tirmidhiy, na alisema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( سَبْعَةٌ يُظِلُّهُمُ اللهُ في ظِلِّهِ يَوْمَ لا ظِلَّ إِلاَّ ظِلُّهُ : إمَامٌ عَادِلٌ ، وَشَابٌ نَشَأَ فِي عِبَادَةِ اللهِ تَعَالَى ، وَرَجُلٌ قَلْبُهُ مُعَلَّقٌ بِالمَسَاجِدِ ، وَرَجُلاَنِ تَحَابّا في الله اجْتَمَعَا عَلَيْهِ وتَفَرَّقَا عَلَيْهِ ، وَرَجُلٌ دَعَتْهُ امْرَأَةٌ ذَاتُ مَنْصِبٍ وَجَمَالٍ، فَقال: إنِّي أَخَافُ الله، وَرَجُلٌ تَصَدَّقَ بِصَدَقَةٍ فَأخْفَاهَا حَتَّى لاَ تَعْلَمَ شِمَالُه مَا تُنْفِقُ يَمِينُهُ ، وَرَجُلٌ ذَكَرَ الله خَالِياً ففاضت عَيْنَاهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kwa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Saba, Allaah atawafunika chini ya kivuli Chake Siku ambayo hakuna kivuli isipokuwa kivuli Chake: Imamu (kiongozi) muadilifu, na kijana aliyeinukia katika kumuabudu Allaah Ta'aalaa, na mtu ambaye moyo wake umetundikwa katika Msikiti, na watu wawili wanaopendana kwa ajili ya Allaah, wanakuwa pamoja na kufarikiana kwa ajili Yake, na mtu ambaye ameitwa na mwanamke mzuri na mwenye kuvutia (kuzini naye), akasema: 'Mimi namwogopa Allaah.' na mtu aliyetoa swadaqah kwa kuificha sana mpaka mkono wake wa kushoto usijue kilichotolewa na mkono wa kuume, na mtu ambaye amemkumbuka Allaah peke yake na macho yake yakabubujika na machozi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن عبد الله بن الشِّخِّير رضي الله عنه ، قَالَ : أتيتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم وَهُوَ يُصَلِّي ولِجَوْفِهِ أَزِيزٌ كَأَزِيزِ المِرْجَلِ مِنَ البُكَاءِ . حديث صحيح رواه أَبو داود والترمذي في الشمائل بإسناد صحيح .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillah bin Ash-Shikhayr (Radhwiyah Allaah 'anhu) ambaye amesema: Nilikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye alikuwa anaswali. Nilisikia sauti ya kilio kutoka katika kifua chake ambacho kilikua kama sauti ya chungu kinacho chemka." [Abu Daawuud na At-Tirmidhiy katika "Shamaa'il" na Isnaad yake ni Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أنس رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم لأُبَي بن كعب رضي الله عنه: (( إنَّ الله (عزّ وجلّ أَمَرَنِي أنْ أقْرَأَ عَلَيْكَ :( لَمْ يَكُنِ الَّذِينَ كَفَروا ... )قَالَ : وَسَمَّانِي ؟ قَالَ : (( نَعَمْ )) فَبَكَى أُبَيٌّ . متفقٌ عَلَيْهِ .وفي رواية : فَجَعَلَ أُبَيٌّ يَبْكِي .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Ubayy bin Ka'b: "Hakika Allaah ('Azza wa Jalla), ameniamuru nikusomee: "Lam Yakunil Ladhiina Kafaruu..." [Al-Bayyinah]." Ubayy akauliza: "Allaah amenitaja mimi kwa jina?" Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ndio." Ubayy akawa alilia." [Al-Bukhaariy na Muslim]. Na katika riwaayah: "Ubayy akawa analia."

 

 

Hadiyth – 7

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ أَبو بكر لِعُمَرَ ، رَضِيَ اللهُ عنهما ، بعد وفاة رسول الله صلى الله عليه وسلم: انْطَلِقْ بِنَا إِلى أُمِّ أيْمَنَ رضي الله عنها نَزورُهَا ، كَمَا كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَزُورُها ، فَلَمَّا انْتَهَيَا إِلَيْهَا بَكَتْ ، فقالا لها : مَا يُبْكِيكِ ؟ أمَا تَعْلَمِينَ أنَّ مَا عِنْدَ الله تَعَالَى خَيرٌ لرسولِ الله صلى الله عليه وسلم! قالت : مَا أبْكِي أَنْ لاَ أَكُونَ أَعْلَمُ أنَّ مَا عِنْدَ اللهِ خَيْرٌ لرسولِ الله صلى الله عليه وسلم، وَلكِنِّي أبكِي أَنَّ الْوَحْيَ قَد انْقَطَعَ مِنَ السَّمَاءِ ؛ فَهَيَّجَتْهُما عَلَى البُكَاءِ ، فَجَعَلا يَبْكِيَانِ مَعَهَا . رواه مسلم.

Kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Abu Bakr alimwambia 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) baada ya kufa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Twende kumzuru Ummu Ayman (Radhwiyah Allaahu 'anhaa), kama alivyokuwa Rasuli wa Allaah anamzuru." Tulipofika kwake akalia. Wakamwambia: "Nini kinachokuliza?, kwani hujui yalio kwa Allaah ni bora kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)?" Akasema: "Mimi najua nami silii kwa sababu hiyo bali nalia kukatika wahyi toka mbinguni." Hili liliwafanya Swahaaba wawili watukufu (Abu Bakr na 'Umar Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) walie pamoja naye." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 8

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : لَمَّا اشْتَدَّ برسول الله صلى الله عليه وسلم وَجَعُهُ ، قِيلَ له في الصَّلاَةِ ، فقال : (( مُرُوا أَبَا بَكْرٍ فَلْيُصَلِّ بِالنَّاسِ )) فقالت عائشة رضي الله عنها : إنَّ أَبَا بَكْرٍ رَجُلٌ رَقِيقٌ ، إِذَا قَرَأَ القُرْآنَ غَلَبَهُ البُكَاءُ ، فقال :  (( مُرُوهُ فَليُصَلِّ )) .

وفي رواية عن عائشة ، رضي الله عنها ، قالت : قلت : إنَّ أَبَا بَكْرٍ إِذَا قَامَ مَقَامَكَ لَمْ يُسْمِعِ النَّاسَ مِنَ البُكَاءِ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) amesema: "ugonjwa wa Rasuli wa Allaahu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ulipozidi aliulizwa nani aswalishe watu. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Muamrisheni Abu Bakr aswalishe watu." 'Aaisha (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) alisema: "Hakika Abu Bakr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) moyo wake ni mwema (laini) na hivyo anaposoma Quraan huanguka kilio (hulia)." Akasema: "Muamuruni (yeye Abu Bakr) aswalishe." 

Na katika riwaayah kutoka kwa 'Aisha (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) ambaye amesema, nikasema: "Hakika Abu Bakr anaposimama (Imamu) watu hawatamsikia kwa sababu ya kulia." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

وعن إبراهيم بن عبد الرحمان بن عوف : أنَّ عبد الرحمان بن عوف رضي الله عنه أُتِيَ بطعام وكان صائِماً ، فقال : قُتِلَ مُصْعَبُ بن عُمَيْر رضي الله عنه، وَهُوَ خَيْرٌ مِنِّي ، فَلَمْ يوجَدْ له مَا يُكَفَّنُ فيهِ إِلاَّ بُرْدَةٌ إنْ غُطِّيَ بِهَا رَأسُهُ بَدَتْ رِجْلاهُ ؛ وَإنْ غُطِّيَ بِهَا رِجْلاَهُ بَدَا رَأسُهُ ، ثُمَّ بُسِطَ لَنَا مِنَ الدُّنْيَا مَا بُسِطَ – أَو قَالَ : أُعْطِينَا مِنَ الدُّنْيَا مَا أُعْطِينَا – قَدْ خَشِينا أنْ تَكُونَ حَسَنَاتُنَا عُجِّلَتْ لَنَا ، ثُمَّ جَعَلَ يَبكِي حَتَّى تَرَكَ    الطعَام . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwake Ibraahiym bin 'Abdir-Rahmaan bin 'Awf kwamba 'Abdir-Rahmaan bin 'Awf (Radhwiyah Allaahu 'anhu) aliletewa chakula akiwa ameamefunga, akasema: "Mus'ab bin 'Umayr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) aliuliwa naye ni bora kuliko mimi na hakukupatikana kitu cha kumkafini isipokuwa kitambara kilichokuwa kifupi sana. Akifinikwa kichwa miguu kichwa hubaki wazi. Baada ya hapo tukafunguliwa dunia au alisema: 'Tukapatiwa katika dunia kile tulichopatiwa (tukapatiwa mali nyingi).' Tunaogopa isiwe malipo yetu tumepatiwa mapema (yaani katika hii dunia). Kisha akaanza kulia mpaka akaacha chakula." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أَبي أُمَامَة صُدَيِّ بن عجلان الباهلي رضي الله عنه، عن النبي صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَيْسَ شَيْءٌ أحَبَّ إِلى اللهِ تَعَالَى مِنْ قطْرَتَيْنِ وَأثَرَيْنِ : قَطَرَةُ دُمُوع مِنْ خَشْيَةِ    اللهِ ، وَقَطَرَةُ دَمٍ تُهَرَاقُ في سَبيلِ اللهِ. وَأَمَّا الأَثَرَانِ : فَأَثَرٌ في سَبيلِ اللهِ تَعَالَى، وَأَثَرٌ في فَريضةٍ مِنْ فَرائِضِ الله تَعَالَى )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديثٌ حسنٌ )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Umamah Swudayyi bin 'Ajlaan Al-Baahiliy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna kitu kinachompendeza Allaah Ta'aalaa kama matone mawili na alambili. Ama matone ni machozi yanayobubujika kwa kumuogopa Allaah na damu inayotoka katika njia ya Allaah. Na alama mbili, alama katika njia ya Allaah Ta'aalaa na alama inayopatikana katika kutekeleza faradhi miongoni mwa faradhi miongoni mwa faradhi alizoamrisha Allaah Ta'aalaa." [At-Tirmidhiy, na alisema ni Hadiyth Hasan]

 

 Hadiyth – 11

حديث العرباض بن سارية رضي الله عنه، قَالَ : وعظنا رسول الله صلى الله عليه وسلم مَوعظةً وَجلَتْ منها القُلُوبُ ، وذرِفت منها الْعُيُونُ . وقد سبق في باب النهي عن البدع.

Amehadithia al-'Irbaadh bin Saariyah kwamba: "Alituaidhia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mawaidha yaliyozifanya nyoyo zikaingia hofu na macho yakatokwa na machozi." Hii ni sehemu tu ya Hadiyth ndefu iliyotangulia kutajwa katika Mlango wa Amri ya kuhifadhi Sunnah na Adabu Zake.

 

 

 

 

Share

055-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila na Ubora wa Kuupa Nyongo Ulimwengu wa Kukinai Kwa Kichache na Ubora wa Ufakiri

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل الزهد في الدنيا والحث عَلَى التقلل منها وفضل الفقر

055-Mlango Wa Fadhila na Ubora wa Kuupa Nyongo Ulimwengu wa Kukinai Kwa Kichache na Ubora wa Ufakiri

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

إِنَّمَا مَثَلُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا كَمَاءٍ أَنزَلْنَاهُ مِنَ السَّمَاءِ فَاخْتَلَطَ بِهِ نَبَاتُ الْأَرْضِ مِمَّا يَأْكُلُ النَّاسُ وَالْأَنْعَامُ حَتَّىٰ إِذَا أَخَذَتِ الْأَرْضُ زُخْرُفَهَا وَازَّيَّنَتْ وَظَنَّ أَهْلُهَا أَنَّهُمْ قَادِرُونَ عَلَيْهَا أَتَاهَا أَمْرُنَا لَيْلًا أَوْ نَهَارًا فَجَعَلْنَاهَا حَصِيدًا كَأَن لَّمْ تَغْنَ بِالْأَمْسِ ۚ كَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ الْآيَاتِ لِقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ﴿٢٤﴾

Hakika mfano wa uhai wa dunia ni kama maji Tuliyoyateremsha kutoka mbinguni, kisha yakachanganyika nayo mimea ya ardhi katika wanayoila watu na wanyama, mpaka ardhi ilipokamilisha uzuri wake na ikapambika na wakayakinisha watu wake kwamba wanao uwezo juu yake (kuivuna); tahamaki amri Yetu ikaijia usiku au mchana, Tukaifanya kama iliyofekwa kama kwamba haikusitawi jana. Hivyo ndivyo Tunavyofasili waziwazi Aayaat (ishara, hoja) kwa watu wanaotafakari. [Yuwnus: 24]

 

 

وَاضْرِبْ لَهُم مَّثَلَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا كَمَاءٍ أَنزَلْنَاهُ مِنَ السَّمَاءِ فَاخْتَلَطَ بِهِ نَبَاتُ الْأَرْضِ فَأَصْبَحَ هَشِيمًا تَذْرُوهُ الرِّيَاحُ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ مُّقْتَدِرًا ﴿٤٥﴾ الْمَالُ وَالْبَنُونَ زِينَةُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ خَيْرٌ عِندَ رَبِّكَ ثَوَابًا وَخَيْرٌ أَمَلًا ﴿٤٦﴾

Na wapigie mfano wa uhai wa dunia kama maji Tuliyoyateremsha kutoka mbinguni, yakachanganyika kwayo mimea ya ardhi (ikasitawi), kisha yakawa makavu yaliyovurugika yanapeperushwa na upepo. Na Allaah daima ni Mwenye Uwezo wa juu kabisa kwa kila kitu. Mali na watoto ni pambo la uhai wa dunia. Na mema yanayobakia ni bora mbele ya Rabb wako, kwa thawabu na matumaini. [Al-Kahf: 45-46]

 

اعْلَمُوا أَنَّمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا لَعِبٌ وَلَهْوٌ وَزِينَةٌ وَتَفَاخُرٌ بَيْنَكُمْ وَتَكَاثُرٌ فِي الْأَمْوَالِ وَالْأَوْلَادِ ۖ كَمَثَلِ غَيْثٍ أَعْجَبَ الْكُفَّارَ نَبَاتُهُ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَاهُ مُصْفَرًّا ثُمَّ يَكُونُ حُطَامًا ۖ وَفِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ شَدِيدٌ وَمَغْفِرَةٌ مِّنَ اللَّـهِ وَرِضْوَانٌ ۚ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿٢٠﴾

Jueni kwamba uhai wa dunia ni mchezo na pumbao na mapambo, na kufakharishana baina yenu na kushindana kukithiri katika mali na watoto; ni kama mfano wa mvua inayowafurahisha wakulima mimea yake, kisha yananyweya, basi utayaona yamepiga manjano, kisha yanakuwa mabua yaliyonyauka na kupondekapondeka.  Na Aakhirah kuna adhabu kali, na maghfirah kutoka kwa Allaah na radhi. Na uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni sterehe fupi za kughuri. [Al-Hadiyd: 29]

 

 

زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ الشَّهَوَاتِ مِنَ النِّسَاءِ وَالْبَنِينَ وَالْقَنَاطِيرِ الْمُقَنطَرَةِ مِنَ الذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ وَالْخَيْلِ الْمُسَوَّمَةِ وَالْأَنْعَامِ وَالْحَرْثِ ۗ ذَٰلِكَ مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۖ وَاللَّـهُ عِندَهُ حُسْنُ الْمَآبِ ﴿١٤﴾

Watu wamepambiwa huba ya matamanio miongoni mwa wanawake, na watoto, na mirundi ya mali iliyorundikwa ya dhahabu na fedha na farasi wenye chapa ya aina bora na wanyama wa mifugo na mashamba. Hayo ni starehe za uhai wa dunia, na Allaah Kwake kuna marejeo mazuri. [Aal-'Imraan: 14]

 

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ ۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا ۖ وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِاللَّـهِ الْغَرُورُ ﴿٥﴾

Enyi watu!  Hakika ahadi ya Allaah ni haki; basi usikughururini uhai wa dunia, na wala (shaytwaan) mwenye kughuri asikughururini kuhusu Allaah. [Faatwir: 5]

 

أَلْهَاكُمُ التَّكَاثُرُ ﴿١﴾ حَتَّىٰ زُرْتُمُ الْمَقَابِرَ ﴿٢﴾ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ ﴿٣﴾ ثُمَّ كَلَّا سَوْفَ تَعْلَمُونَ ﴿٤﴾ كَلَّا لَوْ تَعْلَمُونَ عِلْمَ الْيَقِينِ ﴿٥﴾

Kumekughafilisheni kutafuta wingi. Mpaka muingie makaburini. Laa hasha! Mtakuja kujua. Kisha laa hasha! Mtakuja kujua. Laa hasha! Lau mngelijua ujuzi wa yakini. [At-Takaathur: 1-5]

 

 

وَمَا هَـٰذِهِ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا لَهْوٌ وَلَعِبٌ ۚ وَإِنَّ الدَّارَ الْآخِرَةَ لَهِيَ الْحَيَوَانُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿٦٤﴾

Na huu uhai wa dunia si chochote isipokuwa ni pumbao na mchezo; na hakika Nyumba ya Aakhirah bila shaka hiyo ndiyo yenye uhai wa kweli hasa (wa milele), lau wangelikuwa wanajua! [Al-'Ankabuwt: 64]

 

 

 

والآيات في الباب كثيرة مشهورة . وأما الأحاديث فأكثر مِنْ أن تحصر فننبِّهُ بطرف منها عَلَى مَا سواه .

Na ayah katika mlango huu ni nyingi na mashuhuri. Ama Hadiyth ni nyingi zaidi hata hazihesabiki na hapa tuataja baadhi yake.

 

 

 

 

Hadiyth – 1

عن عمرو بن عوف الأنصاري رضي الله عنه: أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم بَعَثَ أَبَا عبيدة بنَ الجَرَّاح رضي الله عنه إِلَى الْبَحْرَيْنِ يَأتِي بِجِزْيَتِهَا ، فَقَدِمَ بمَالٍ مِنَ الْبَحْرَيْنِ ، فَسَمِعَتِ الأَنْصَارُ بقُدُومِ أَبي عُبيْدَةَ ، فَوَافَوْا صَلاَةَ الفَجْرِ مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَلَمَّا صَلَّى رسولُ الله صلى الله عليه وسلم ، انْصَرفَ ، فَتَعَرَّضُوا لَهُ ، فَتَبَسَّمَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم حِيْنَ رَآهُمْ ، ثُمَّ قَالَ: (( أظُنُّكُمْ سَمعتُمْ أنَّ أَبَا عُبَيْدَةَ قَدِمَ بِشَيْءٍ مِنَ الْبَحْرَيْنِ ؟ )) فقالوا : أجل ، يَا رسول الله، فقال : (( أبْشِرُوا وَأَمِّلْوا مَا يَسُرُّكُمْ، فَوالله مَا الفَقْرَ أخْشَى عَلَيْكُمْ ، وَلكِنِّي أخْشَى أنْ تُبْسَط الدُّنْيَا عَلَيْكُمْ كَمَا بُسِطَتْ عَلَى مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ ، فَتَنَافَسُوهَا كَمَا تَنَافَسُوهَا ، فَتُهْلِكَكُمْ كَمَا أهْلَكَتْهُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Amru bin Al 'Awfy Al Answaary (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimpeleka Abu 'Ubaydah 'Amir bin al-Jarraah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) Bahrayn kukusanya Jizyah yao. Akarudi na mali kutoka Bahrayn. Ma-Ansaar walipata habari ya kurudi kwa Abu 'Ubaydah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) hivyo wakaswali Swalaah ya Alfajiri pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Alipomaliza kuswali Rasuli wa Allaah, walikuja kwake. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitabasamu alipowaona, kisha akasema: "Nadhania mumesikia ya kwamba Abu 'Ubaydah amerudi na kitu kutoka Bahrayn?" Wakasema: "Ndio, ee Rasuli wa Allaah!" Akasema: "Furahini, na tarajieni vitu vitakavyo wafurahisha. Wa-Allaahi! Siwaogopeeni ufukara, lakini naogopa kukunjuliwa dunia juu yenu, kama walivyo kunjuliwa waliokuwa kabla yenu, mkaishindania kama walivyoishindania, ikakuangamizeni nyinyi kama ilivyowangamiza wao." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : جلس رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَلَى    الْمِنْبَرِ ، وَجَلَسْنَا حَوْلَهُ ، فقال : (( إنَّ ممَّا أخَافُ عَلَيْكُمْ مِنْ بَعْدِي مَا يُفْتَحُ عَلَيْكُمْ مِنْ زَهْرَةِ الدُّنْيَا وَزِينَتِهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd al-Khudriy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Alikaa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwenye mimbar nasi tukakaa duara (tukiwa tumemzunguka), akasema: "Kwa hakika yale ninayowaogopea nyinyi baada yangu ni kufunguliwa kwenu utajiri na kuvutiwa na dunia na mapambo yake." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: (( إنَّ الدُّنْيَا حُلْوَةٌ خَضِرَةٌ وَإنَّ الله تَعَالَى مُسْتَخْلِفُكُمْ فِيهَا، فَيَنْظُرُ كَيْفَ تَعْمَلُونَ، فَاتَّقُوا الدُّنْيَا وَاتَّقُوا النِّسَاءَ )) رواه مسلم.

Impokewa kutoka kwa Abu Saiyd Al-Khudriy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika dunia ni tamu na kijani (imejaa utajiri) na Allaah Ta'aalaa atawafanya nyinyi kuwa makhalifa humo na atawaangalia kwa yale mnayofanya. Hivyo tahadharini na dunia na wanawake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه : أن النبي صلى الله عليه وسلم، قَالَ: (( اللَّهُمَّ لاَ عَيْشَ إِلاَّ عَيْشَ الآخِرَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee Allaah! Hakuna starehe isipokuwa starehe ya Aakherah." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أنس رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يَتْبَعُ الْمَيِّتَ ثَلاَثَةٌ : أهْلُهُ وَمَالُهُ وَعَمَلُهُ : فَيَرْجِعُ اثْنَانِ ، وَيَبْقَى وَاحِدٌ : يَرْجِعُ أهْلُهُ وَمَالُهُ وَيبْقَى عَمَلُهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hufuata maiti mambo matatu: Watu wake, mali yake na amali yake. Viwili hurudi na kubakia jambo moja tu: Hurudi watu wake na mali yake na kubakia amali yake." [Ahmad, Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يُؤْتَى بِأنْعَمِ أهْلِ الدُّنْيَا مِنْ أهْلِ النَّارِ يَوْمَ القِيَامَةِ ، فَيُصْبَغُ في النَّارِ صَبْغَةً، ثُمَّ يُقَالُ : يَا ابْنَ آدَمَ ، هَلْ رَأيْتَ خَيْراً قَطُّ ؟ هَلْ مَرَّ بِكَ نَعِيمٌ قَطُّ ؟ فَيَقُولُ : لاَ وَاللهِ يَا رَبِّ ، وَيُؤْتَى بِأشَدِّ النَّاسِ بُؤسَاً في الدُّنْيَا مِنْ أهْلِ الجَنَّةِ ، فَيُصْبَغُ صَبْغَةً في الجَنَّةِ ، فَيُقَالُ لَهُ : يَا ابْنَ آدَمَ ، هَلْ رَأيْتَ بُؤساً قَطُّ ؟ هَلْ مَرَّ بِكَ شِدَّةٌ قَطُّ ؟ فيَقُولُ : لاَ وَاللهِ ، مَا مَرَّ بِي بُؤْسٌ قَطُّ ، وَلاَ رَأيْتُ شِدَّةً قَطُّ )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Anas kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ataletwa mtu mwenye neema zaidi katika watu duniani Siku ya Qiyaamah na kuchovya Motoni mara moja. Kisha kutasemwa: 'Ee binadamu! Je, umeona kheri yeyote? Je, ulipata neema yeyote?' Atasema: 'La! Wa-Allaahi! Sijapata, ee Rabb wangu.' Ataletwa maskini zaidi duniani katika watu wa Peponi, Atatiwa mara moja Peponi, Kutasemwa: 'Ee binadamu! Je, ulipata shida yeyeote?, Atasema: 'Wa-Allaahi! Sijapata tabu, sikupata shida yeyeote." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن المُسْتَوْرِد بن شَدَّاد رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( مَا الدُّنْيَا في الآخِرَةِ إِلاَّ مِثْلُ مَا يَجْعَلُ أَحَدُكُمْ أُصْبُعَهُ في اليَمِّ، فَلْيَنْظُرْ بِمَ يَرْجِعُ ! )) رواه مسلم.

Imepokewa kutoka kwa Al-Mustawrid bin Shaddaad (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Dunia si chochote katika Aakherah isipokuwa ni kama mfano wa mtu anayetia kidole chake katika bahari. Naangalie kiasi gani cha maji kinachukua." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم مَرَّ بالسُّوقِ وَالنَّاسُ كَنَفَتَيْهِ ، فَمَرَّ بِجَدْيٍ أَسَكَّ مَيِّتٍ ، فَتَنَاوَلَهُ فَأَخَذَ بِأُذُنِهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( أَيُّكُم يُحِبُّ أنْ يَكُونَ هَذَا لَهُ بِدرْهَم ؟ )) فقالوا : مَا نُحِبُّ أنَّهُ لَنَا بِشَيْءٍ وَمَا نَصْنَعُ بِهِ ؟ ثُمَّ قَالَ : (( أَتُحِبُّونَ أَنَّهُ لَكُمْ ؟ )) قَالُوا : وَاللهِ لَوْ كَانَ حَيّاً كَانَ عَيْباً ، إنَّهُ أسَكُّ فَكَيْفَ وَهُوَ ميِّتٌ ! فقال : (( فوَاللهِ للدُّنْيَا أهْوَنُ عَلَى اللهِ مِنْ هَذَا عَلَيْكُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiyah Allaah 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita sokoni pamoja na Swahaaba zake alimuona mbuzi mdogo amekufa na masikio yake yamekatwa. Alikishika katika masikio na kuuliza: "Nani anayemtaka (huyu mbuzi aliyekufa) kwa dirhamu moja?" Wakasema: "Hatutaki huyo awe ni wetu kwa chochote (hata bure). Na je, tutamfanya nini? " Kisha akasema: "Je, mngependa awe wenu bure?" Wakasema: "Wa-Allaahi! Hata kama angekuwa hai angekuwa na kasoro, vipi akiwa maiti?" Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Wa-Allaahu! dunia ni duni zaidi mbele ya Allaah kuliko juu yenu." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي ذر رضي الله عنه ، قَالَ : كُنْتُ أَمْشِي مَعَ النَّبي صلى الله عليه وسلم في حَرَّةٍ   بِالمَدِينَةِ ، فَاسْتَقْبَلَنَا أُحُدٌ ، فقال : (( يَا أَبَا ذَرٍّ )) قلت : لَبَّيْكَ يَا رسولَ الله . فقال : (( مَا يَسُرُّنِي أنَّ عِنْدِي مِثْلَ أُحُدٍ هَذَا ذَهَباً تَمْضي عَلَيَّ ثَلاَثَةُ أيّامٍ وَعِنْدِي مِنْهُ  دِينَارٌ ، إِلاَّ شَيْءٌ أرْصُدُهُ لِدَيْنٍ ، إِلاَّ أنْ أقُولَ بِهِ في عِبَادِ الله هكذا وَهَكَذَا وَهكَذَا )) عن يَمِينِهِ وعن شِمَالِهِ وَمِنْ خَلْفِهِ ، ثُمَّ سَارَ ، فقال : (( إنَّ الأَكْثَرينَ هُمُ الأَقَلُّونَ يَوْمَ القِيَامَةِ إِلاَّ مَنْ قَالَ بالمَالِ هكَذَا وَهكَذَا وَهكَذَا )) عن يمينِهِ وعن شِمَالِهِ وِمنْ خَلْفِهِ (( وَقَلِيلٌ مَاهُمُ )) . ثُمَّ قَالَ لي : (( مَكَانَكَ لاَ تَبْرَحْ حَتَّى آتِيكَ )) ثُمَّ انْطَلَقَ في سَوادِ اللَّيْلِ حَتَّى تَوَارَى ، فَسَمِعْتُ صَوتاً ، قَدِ ارْتَفَع ، فَتَخَوَّفْتُ أنْ يَكُونَ أحَدٌ عَرَضَ للنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَأرَدْتُ أنْ آتِيهِ فَذَكَرتُ قَوْله : (( لا تَبْرَحْ حَتَّى آتِيَكَ )) فلم أبْرَحْ حَتَّى أتَاني ، فَقُلْتُ : لَقَدْ سَمِعْتُ صَوتاً تَخَوَّفْتُ مِنْهُ ، فَذَكَرْتُ لَهُ ، فقال :   (( وَهَلْ سَمِعْتَهُ ؟ )) قلت : نَعَمْ ، قَالَ : (( ذَاكَ جِبريلُ أتَانِي . فقال : مَنْ مَاتَ مِنْ أُمَّتِكَ لاَ يُشْرِكُ بِاللهِ شَيْئاً دَخَلَ الْجَنَّةَ )) ، قلت : وَإنْ زَنَى وَإنْ سَرَقَ ؟ قَالَ : (( وَإنْ زَنَى وَإنْ سَرَقَ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Nilikuwa natembea na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika majabali Madiynah tukatokea Uhud. Akaniita: "Ee Abu Dharr." Nikasema: "Labbayka ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Lau ningekuwa na dhahabu mfano wa Uhud hii, Ipite kwangu suku tatu nibaki nayo hata dinari moja, isipokuwa kuiweka kwa ajili ya deni. Ila Ningeigawa kwa waja wa Allaah hivi na hivi na hivi', kulia, kushoto na nyuma." Kisha akatembea akasema: "Hakika wenye vingi duniani ndio wenye kidogo zaidi Siku ya Qiyaamah, isipokuwa wanaotumia mali hivi na hivi na hivi', kulia na kushoto na nyuma, "Nao wao ni wachache." Baada ya hapo akaniambia: "Hapo hapo usiondoke hadi nikujie." Kisha alitembea katika giza nene hadi akapotea. Nilisikia sauti kubwa, nikahofia mtu kumtokea Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), isiwe amepatikana na jambo baya. Nilitaka kumuendea nikakumbuka kauli yake: "Usiondoke hadi nikujie." Sikuondoka mpaka aliporudi, nikasema: "Nilisikia sauti kubwa sana nikaihofia, nikamkumbusha." Akasema: "Uliisikia?" Nikasema: "Ndio." Akasema: "Huyu alikuwa ni Jibriyl alinijia, akaniambia: 'Atakayekufa katika Ummah wako hamshirikishi Allaah na chochote ataingia Peponi." Nikauliza: "Hata akizini na kuiba?" Akasema: "Hata kama atazini na ataiba." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه  ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَوْ كَانَ لِي مِثْلُ أُحُدٍ ذَهَباً ، لَسَرَّنِي أنْ لاَ تَمُرَّ عَلَيَّ ثَلاَثُ لَيالٍ وَعِنْدِي مِنْهُ شَيْءٌ إِلاَّ شَيْءٌ أرْصُدُهُ لِدَيْنٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau ningekuwa na dhahabu mfano wa Mlima Uhud, ingenifurahisha kutopita siku tatu nami nimebakia na chochote isipokuwa kitu nakiweka kwa ajili ya kulipa madeni." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( انْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ أسْفَلَ مِنْكُمْ وَلاَ تَنْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ فَوْقَكُمْ ؛ فَهُوَ أجْدَرُ أنْ لاَ تَزْدَرُوا نِعْمَةَ الله عَلَيْكُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ مسلم .

وفي رواية البخاري : (( إِذَا نَظَرَ أَحَدُكُمْ إِلَى مَنْ فُضِّلَ عَلَيْهِ في المَالِ وَالخَلْقِ ، فَلْيَنْظُرْ إِلَى مَنْ هُوَ أسْفَل مِنْهُ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwangalie wa chini yako, wala usiangalie wa juu yako, hilo ni hakika hutopuuza neema za Allaah juu yako." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Muslim]

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: "Anapoangalia mmoja wenu aliyefadhilishwa juu yake kwa mali na sura nzuri, basi amtizame aliye chini yake."

 

 

Hadiyth – 12

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تَعِسَ عَبْدُ الدِّينَارِ ، وَالدِّرْهَمِ ، وَالقَطِيفَةِ ، وَالخَمِيصَةِ ، إنْ أُعْطِيَ رَضِيَ ، وَإنْ لَمْ يُعْطَ لَمْ يَرْضَ )) رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ameangamia mwenye kutafuta dinari na dirhamu na nguo zenye manyoa na mavazi ya thamani. Wanapopatiwa huridhia na wasipopatiwa basi hawaridhiki." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 13

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : لَقَدْ رَأيْتُ سَبعِينَ مِنْ أهْلِ الصُّفَّةِ ، مَا منهُمْ رَجُلٌ عَلَيْهِ رِدَاءٌ : إمَّا إزارٌ ، وَإمَّا كِسَاءٌ ، قَدْ رَبَطُوا في أعنَاقِهِمْ ، فَمِنْهَا مَا يَبْلُغُ نِصْفَ السَّاقَيْن ، وَمِنْهَا مَا يَبْلُغُ الكَعْبَيْنِ ، فَيَجْمَعُهُ بِيَدِهِ كَراهِيَةَ أنْ تُرَى عَوْرَتُهُ . رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwake Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: "Hakika nimeona Swahaaba sabiini katika watu wa Swuffah hakuna hata mmoja miongoni mwao mwenye kikoi: Ima ni shuka wamezifunga katika shingo zao, katika hizo kuna zinazofika katikati ya miguu, katika hizo kuna zinazofika kongo mbili, kwa hiyo wakazikusanya kiunoni kwa kuchukia kuonekana uchi wao." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 14

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( الدُّنْيَا سِجْنُ الْمُؤْمِنِ ، وَجَنَّةُ الكَافِرِ )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: "Dunia ni jela ya Muumini na Pepo ya kafiri." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 15

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : أخذ رسول الله صلى الله عليه وسلم بِمَنْكِبَيَّ ، فقال : (( كُنْ في الدُّنْيَا كَأنَّكَ غَرِيبٌ ، أَو عَابِرُ سَبيلٍ )) .

وَكَانَ ابن عُمَرَ رضي الله عنهما ، يقول : إِذَا أمْسَيتَ فَلاَ تَنْتَظِرِ الصَّبَاحَ ، وَإِذَا أَصْبَحْتَ فَلاَ تَنْتَظِرِ المَسَاءَ ، وَخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِمَرَضِكَ ، وَمِنْ حَيَاتِكَ لِمَوْتِكَ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) akisema kwamba: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alishika mabega yangu akisema: 'Kuwa duniani kama kwamba wewe ni mgeni au mpita njia.' Na Ibn 'Umar (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) alikuwa akisema: 'Na ufikiwapo na usiku usitaraji kuwa uatafika hadi asubuhi, na ukipambazukiwa usitaraji kuwa utafika hadi jioni. Na faidika na (wakati wa) siha yako kabla ya (wakati wa) uhai wako kabla ya kufa kwako." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 16

وعن أَبي العباس سهل بن سعد الساعدي رضي الله عنه ، قَالَ : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النبي صلى الله عليه وسلم ، فقال : يَا رسولَ الله ، دُلَّنِي عَلَى عَمَلٍ إِذَا عَمِلْتُهُ أحَبَّنِي اللهُ وَأحَبَّنِي  النَّاسُ ، فقال : (( ازْهَدْ في الدُّنْيَا يُحِبّك اللهُ ، وَازْهَدْ فِيمَا عِنْدَ النَّاسِ يُحِبّك   النَّاسُ )) حديث حسن رواه ابن ماجه وغيره بأسانيد حسنة .

Imepokewa kutoka kwa Abui 'Abbaas Sahl bin Sa'd As-Sa'idiy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa: Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Ee Rasuli wa Allaah, nijulishe mimi amali ambayo nikiifanya Allaah atanipenda na watu watanipenda." Akasema: "Upe nyongo ulimwengu atakupenda Allaah, na vipe nyongo viliomo mikononi mwa watu watakupenda watu." Hadiyth Hasan [Ibn Maajah na wengineo kwa isnad nzuri]

 

 

Hadiyth – 17

وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما ، قَالَ : ذَكَرَ عُمَرُ بْنُ الخَطَّابِ رضي الله عنه ، مَا أَصَابَ النَّاسُ مِنَ الدُّنْيَا ، فَقَالَ : لَقَدْ رَأيْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَظَلُّ الْيَوْمَ يَلْتَوِي مَا يَجِدُ مِنَ الدَّقَلِ مَا يَمْلأ بِهِ بَطْنَهُ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa An-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) ambaye amesema: Alitaja 'Umar bin Al-Khattaab (Radhwiyah Allaahu 'anhu) yale yaliyowafikia watu katika hii dunia, akasema: "Hakika nilimuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akipitisha siku zake akiwa na njaa hana hata tende mbaya ya kuondoa njaa yake." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 18

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : تُوفي رسول الله صلى الله عليه وسلم، وَمَا في بَيْتِي مِنْ شَيْءٍ يَأكُلُهُ ذُو كَبِدٍ إِلاَّ شَطْرُ شَعِيرٍ في رَفٍّ لي ، فَأكَلْتُ مِنْهُ حَتَّى طَالَ  عَلَيَّ ، فَكِلْتُهُ فَفَنِيَ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) amesema: "Aliaga dunia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na hakukuwa katika nyumba chakula cha sawa (kwa watu kula) isipokuwa mtama kidogo katika stoo yangu ambao nilikuwa nikiutumia kwa muda. Baadae nilitaka kuupima lakini ukawa umemalizika." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 19

وعن عمرو بن الحارث أخي جُوَيْرِيّة بنتِ الحارِث أُمِّ المُؤْمِنِينَ ، رضي الله عنهما ، قَالَ : مَا تَرَكَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عِنْدَ مَوْتِهِ دِيناراً ، وَلاَ دِرْهَماً ، وَلاَ عَبْداً ، وَلاَ أَمَةً ، وَلاَ شَيْئاً إِلاَّ بَغْلَتَهُ الْبَيضَاءَ الَّتي كَانَ يَرْكَبُهَا ، وَسِلاَحَهُ ، وَأرْضاً جَعَلَهَا لاِبْنِ السَّبِيلِ صَدَقَةً . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa 'Amri bin Al-Haarith, kakake Juwayriyyah bint Al-Haarith, Mama wa Waumini ambaye amesema: "Hakuacha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakati wa kufariki hata dinari moja wala dirhamu wala mjakazi wala kijakazi wala kitu kingine chochote isipokuwa nyumbu wake mweupe aliyekuwa akipanda na silaha zake na ardhi aliyoiacha kama swadaqah kwa wasafiri." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 20

وعن خَبابِ بن الأَرَتِّ رضي الله عنه، قَالَ : هَاجَرْنَا مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم نَلْتَمِسُ وَجْهَ اللهِ تَعَالَى ، فَوَقَعَ أجْرُنَا عَلَى اللهِ ، فَمِنَّا مَنْ مَاتَ وَلَمْ يَأكُل منْ أجْرِهِ شَيْئاً ، مِنْهُمْ : مُصْعَبُ بن عُمَيْرٍ رضي الله عنه ، قُتِلَ يَوْمَ أُحُد ، وَتَرَكَ نَمِرَةً ، فَكُنَّا إِذَا غَطَّيْنَا بِهَا    رَأْسَهُ ، بَدَتْ رِجْلاَهُ ، وَإِذَا غَطَّيْنَا بِهَا رِجْلَيْهِ ، بَدَا رَأسُهُ ، فَأمَرَنَا رسول الله صلى الله عليه وسلم ، أنْ نُغَطِّي رَأسَهُ ، وَنَجْعَل عَلَى رِجْلَيْهِ شَيْئاً مِنَ الإذْخِرِ ، وَمِنَّا مَنْ أيْنَعَتْ لَهُ ثَمَرَتُهُ ، فَهُوَ يَهْدِبُهَا . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Khabbaab bin Al-Aratt (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa amesema: "Tulihama pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa ajili ya radhi za Allaah Ta'aalaa, ujira wetu ukatoka kwa Allaah, Miongoni mwetu kuna waliokufa kabla ya kula ujira wao, Miongoni mwao ni Mus'ab bin 'Umayr (Radhwiyah Allaah 'anhu) ameuwawa siku ya Uhud, ameacha shuka tukimfunika nayo uso wake miguu yake inakuwa wazi, na tulipomfunika miguu, uso wake umakuwa wazi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alituamuru tumfunike uso wake na kumfunika miguu yake na Idhkhir (aina ya mmea ambao ni maarufu na wenye harufu nzuri). Na miongoni mwetu kuna waliopata neema kwa wingi (hapa duniani) nao wakafurahia hilo." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 21

وعن سهلِ بن سعد الساعدي رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَوْ كَانَت الدُّنْيَا تَعْدِلُ عِنْدَ الله جَنَاحَ بَعُوضَةٍ ، مَا سَقَى كَافِراً مِنْهَا شَرْبَةَ مَاءٍ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad As-Saa'idiy (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau kama uliwengu ungekuwa na thamani sawa na bawa la mbu mbele ya Allaah, hangempatia kafiri maji ya kunywa hata kiasi cha mkono mmoja." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 22

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( أَلاَ إنَّ الدُّنْيَا مَلْعُونَةٌ ، مَلْعُونٌ مَا فِيهَا ، إِلاَّ ذِكْرَ اللهِ تَعَالَى ، وَمَا وَالاهُ ، وَعالِماً وَمُتَعَلِّماً )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسنٌ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Jueni ya kuwa hii dunia imelaaniwa, na vimelaaniwa vilivyo ndani yake ispokuwa kumtaja Allaah Ta'aalaa na vile Anavyovipenda na wanavyuoni na wanafunzi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 23

وعن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( لاَ تَتَّخِذُوا الضَّيْعَةَ فَتَرْغَبُوا في الدُّنْيَا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديثٌ حسنٌ )) .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiwe ni wenye kupapia raslimali (zisizohamishika) na hivyo kupendelea dunia." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hasan]

 

 

Hadiyth – 24

وعن عبدِ الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : مَرَّ عَلَيْنَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم وَنَحْنُ نعالِجُ خُصّاً لَنَا ، فَقَالَ : (( مَا هَذَا ؟ )) فَقُلْنَا : قَدْ وَهَى ، فَنَحَنُ نُصْلِحُهُ ، فَقَالَ : (( مَا أرَى الأَمْرَ إِلاَّ أعْجَلَ مِنْ ذَلِكَ )) . رواه أَبو داود والترمذي بإسناد البخاري ومسلم ، وقال الترمذي : (( حديثٌ حسنٌ صحيحٌ )) .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amru bin Al-'Aas kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita tukiwa tunatengeneza paa (la nyumba ya mbao), akasema: "Munafanya nini?" Tukasema: "Paa limekuwa dhaifu nasi tunalitengeneza." Akasema: " Ninaona amri hiyo (Siku ya Qiyaamah) inafika kwa haraka zaidi kuliko jambo lenu hili." [Abu Dawuud na At-Tirmidhiy kwa Isnaad ya Al-Bukhaariy na Muslim, na akasema At-Tirmidhiy kuwa hii ni Hadiyth Hassan Swahiyh]

 

 

 

Hadiyth – 25

وعن كعب بن عياض رضي الله عنه  ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( إنَّ لِكُلِّ أُمَّةٍ فِتْنَةً ، وفِتْنَةُ أُمَّتِي : المَالُ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديثٌ حسنٌ صحيحٌ )) .

Na imepokewa kutoka kwa Ka'b bin 'Iyaadh (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika kila Ummah una fitnah (mtihani) na fitnah ya Ummah wangu ni mali." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 26

وعن أَبي عمرو ، ويقالُ : أَبو عبدِ الله ، ويقالُ : أَبو ليلى عثمان بن عفان رضي الله عنه  : أنَّ النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَيْسَ لاِبْنِ آدَمَ حَقٌّ في سِوَى هذِهِ الخِصَالِ : بَيْتٌ يَسْكُنُهُ ، وَثَوْبٌ يُوارِي عَوْرَتَهُ ، وَجِلْفُ الخُبز وَالماء )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu 'Amri (Radhwiyah Allaahu 'anhu), Inasemwa ni Abu 'Abdillaah, na inasemwa Abu Laylaa 'Uthmaan bin 'Affaan kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwanadamu hana haki ya kuwa na zaidi ya vitu aina tatu: nyumba atakayoishi, na mavazi ya kusitiri uchi wake na kipande cha mkate na maji." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 27

وعن عبدِ الله بن الشِّخِّيرِ - بكسر الشينِ والخاء المعجمتين - رضي الله عنه، أنه قَالَ : أتَيْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، وَهُوَ يَقْرَأُ : ( أَلْهَاكُمُ التَّكَاثُرُ ) قَالَ : (( يَقُولُ ابْنُ آدَمَ : مَالِي ، مالي ، وَهَلْ لَكَ يَا ابْنَ آدَمَ مِنْ مَالِكَ إِلاَّ مَا أكَلْتَ فَأفْنَيْتَ ، أَو لَبِسْتَ فَأَبْلَيْتَ ، أَوْ تَصَدَّقْتَ فَأَمْضَيْتَ ؟! )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Ash-Shikhiyr (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Nilikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa anasoma: "Al-Haakumut Takaathur." Akasema: "Mwanadamu anasema: Mali yangu, mali yangu. Kwani wewe mwanadamu una mali isipokuwa kile ulichokula kikapotea au ulichovaa kikamalizika au ukatoa swadaqah na ukatanguliza mbele yako?" [Muslim]

 

 

Hadiyth – 28

وعن عبدِ الله بن مُغَفَّل رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رجل للنبي صلى الله عليه وسلم :
يَا رسولَ الله ، وَاللهِ إنِّي لأُحِبُّكَ ، فَقَالَ : (( انْظُرْ مَاذَا تَقُولُ ؟ )) قَالَ : وَاللهِ إنِّي لأُحِبُّكَ ، ثَلاَثَ مَرَّات ، فَقَالَ : (( إنْ كُنْتَ تُحِبُّنِي فَأَعِدَّ لِلْفَقْرِ تِجْفَافاً ، فإنَّ الفَقْرَ أسْرَعُ إِلَى مَنْ يُحِبُّني مِنَ السَّيْلِ إِلَى مُنْتَهَاهُ ))
رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Mughaffal (Radhwiyah Allaahu 'anhu) amesema: Mtu alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ee Rasuli wa Allaah! Wa-Allaahi mimi nakupenda." Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Angalia usemalo." Akasema: "Wa-Allaahi mimi nakupenda." Mara tatu. Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ikiwa unanipenda jitayarishe kwa ufukara, kwani ufukara ni haraka zaidi kwa menye kunipenda, kuliko mafuriko na mwisho wake." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 29

وعن كعب بن مالك رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  : (( مَا ذِئْبَانِ جَائِعَانِ أُرْسِلا في غَنَمٍ بِأفْسَدَ لَهَا مِنْ حِرْصِ المَرْءِ عَلَى المَالِ وَالشَّرَفِ لِدِينهِ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Ka'abbin Maalik (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mbwa mwitu wawili wenye njaa watakao pelekwa kwenye mkao (kundi) kwa kondoo hawatatia hasara zaidi kuliko pupa ya mtu kwa mali na utukufu kwa Dini yake." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 30

وعن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه، قَالَ : نَامَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  عَلَى حَصيرٍ ، فَقَامَ وَقَدْ أثَّرَ في جَنْبِهِ ، قُلْنَا : يَا رَسُولَ اللهِ ، لَوْ اتَّخَذْنَا لَكَ وِطَاءً . فَقَالَ : (( مَا لِي وَلِلدُّنْيَا ؟ مَا أَنَا في الدُّنْيَا إِلاَّ كَرَاكِبٍ اسْتَظَلَّ تَحْتَ شَجَرَةٍ ثُمَّ رَاحَ وَتَرَكَهَا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhwiyah Allaah 'anhu) kuwa Rasuli wa sallam (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alilala mara moja juu ya majani ya mtende na alipoamka alama za majani hayo yalikuwa yanaonekana kwenye mwili wake. Tukamwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, tukutayarishie godoro laini kwa ajili yako?" Akasema: "Sina haja na mambo ya dunia. Mfano wangu hapa duniani ni kama mpandaji anapumzika chini ya kivuli cha mti, kisha akaanza tena safari na kuuacha mti." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh] 

 

 

Hadiyth – 31

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يدْخُلُ الفُقَرَاءُ الْجَنَّةَ قَبْلَ الأَغْنِيَاءِ بِخَمْسِمئَةِ عَامٍ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mafakiri wataingia Peponi miaka mia tano kabla ya matajiri." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 32

وعن ابن عباس وعِمْرَانَ بن الحُصَيْنِ رضي الله عنهما ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ: (( اطَّلَعْتُ في الجَنَّةِ فَرَأيْتُ أكْثَرَ أهْلِهَا الفُقَرَاءَ ، وَاطَّلَعْتُ في النَّارِ فَرَأيْتُ أكْثَرَ أهْلِهَا النِّسَاءَ )) متفقٌ عَلَيْهِ من رواية ابن عباس ، ورواه البخاري أيضاً من رواية عِمْرَان بن الحُصَيْن .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas na 'Imraan Ibn Al-Huswayn (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilichungulia Peponi nikaona watu wake wengi ni mafakiri. Na nikatizama Motoni nikaona watu wake wengi ni wanawake." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]

 

 

 

Hadiyth – 33

وعن أسامة بن زيد رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( قُمْتُ عَلَى بَابِ الجَنَّةِ ، فَكَانَ عَامَّةُ مَنْ دَخَلَهَا المَسَاكِينُ ، وَأصْحَابُ الجَدِّ مَحبُوسُونَ ، غَيْرَ أنَّ أصْحَابِ النَّارِ قَدْ أُمِرَ بِهِم إِلَى النَّارِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Usaamah bin Zayd (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilisimama kwenye mlango wa Pepo, ikawa wengi wanaoingia ni masikini, na wenye utajiri wamezuiwa, isipokuwa watu wa Motoni wameamriwa kuingizwa motoni." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 34

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أصْدَقُ كَلِمَةٍ قَالَهَا شَاعِرٌ كَلِمَةُ لَبِيدٍ : ألاَ كُلُّ شَيْءٍ مَا خَلاَ اللهَ بَاطِلُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Neno la kweli alilosema mshairi ni neno la Labiyd: "Tanabahi kwamba kila kitu mbali na Allaah ni batili." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

056-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila za Kuwa na Njaa na Maisha ya Kujinyima, na Kukusuru Kichache Katika Chakula na Vinywaji na Mavazi na Kujitenga na Maisha ya Fakhari na Kuacha Matamanio

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل الجوع وخشونة العيش والاقتصار عَلَى القليل من المأكول والمشروب والملبوس وغيرها من حظوظ النفس وترك الشهوات

056-Mlango Wa Fadhila za Kuwa na Njaa na Maisha ya Kujinyima, na Kukusuru Kichache Katika Chakula na Vinywaji na Mavazi na Kujitenga na Maisha ya Fakhari na Kuacha Matamanio

 

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

فَخَلَفَ مِن بَعْدِهِمْ خَلْفٌ أَضَاعُوا الصَّلَاةَ وَاتَّبَعُوا الشَّهَوَاتِ ۖ فَسَوْفَ يَلْقَوْنَ غَيًّا ﴿٥٩﴾ إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ وَلَا يُظْلَمُونَ شَيْئًا ﴿٦٠﴾

Wakafuata baada yao waovu, walipoteza Swalaah na wakafuata matamanio; basi watakutana na adhabu motoni. Isipokuwa yule aliyetubu na akaamini na akatenda mema; basi hao wataingia Jannah na wala hawatodhulumiwa chochote. [Maryam: 59-60]

 

فَخَرَجَ عَلَىٰ قَوْمِهِ فِي زِينَتِهِ ۖ قَالَ الَّذِينَ يُرِيدُونَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا يَا لَيْتَ لَنَا مِثْلَ مَا أُوتِيَ قَارُونُ إِنَّهُ لَذُو حَظٍّ عَظِيمٍ ﴿٧٩﴾ وَقَالَ الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ وَيْلَكُمْ ثَوَابُ اللَّـهِ خَيْرٌ لِّمَنْ آمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا وَلَا يُلَقَّاهَا إِلَّا الصَّابِرُونَ ﴿٨٠﴾

Akawatokea watu wake katika pambo lake. Wale wanaotaka uhai wa dunia wakasema: Ee laiti tungelipata mfano wa yale aliyopewa Qaaruwn, hakika yeye ana bahati kuu. Na wale waliopewa elimu wakasema: Ole wenu! Thawabu za Allaah ni bora zaidi kwa yule aliyeamini na akatenda mema. Na wala hazipati isipokuwa wenye kusubiri. [Al-Qaswasw: 79-80]

 

ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ ﴿٨﴾

Kisha bila shaka mtaulizwa Siku hiyo kuhusu neema. [At-Takaathur: 8]

 

مَّن كَانَ يُرِيدُ الْعَاجِلَةَ عَجَّلْنَا لَهُ فِيهَا مَا نَشَاءُ لِمَن نُّرِيدُ ثُمَّ جَعَلْنَا لَهُ جَهَنَّمَ يَصْلَاهَا مَذْمُومًا مَّدْحُورًا ﴿١٨﴾

Yeyote anayetaka (starehe za dunia) ipitayo upesi upesi Tunamharakizia humo Tuyatakayo, na kwa Tumtakaye. Kisha Tutamjaalia Jahannam aingie na kuungua hali ya kuwa mwenye kushutumiwa na kufukuziliwa mbali. [Al-Israa: 18]

 

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا شَبعَ آلُ مُحَمّد صلى الله عليه وسلم مِنْ خُبْزِ شَعِيرٍ يَوْمَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ حَتَّى قُبِضَ . متفقٌ عَلَيْهِ .

وفي رواية : مَا شَبعَ آلُ محَمّد صلى الله عليه وسلم مُنْذُ قَدِمَ المَدِينَةَ مِنْ طَعَامِ البُرِّ ثَلاثَ لَيَالٍ تِبَاعاً حَتَّى قُبِضَ.

Kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: "Haikushiba familia ya Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mkate wa shayiri siku mbili mfululizo hadi ameaga dunia (hali ilikuwa hivyo)." [Al-Bukhaariy na Muslim].

Na katika riwaayah nyingine: "Haikushiba familia ya Muhammad (Sawalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuanzia afike Madiynah kwa chakula cha ngano kwa siku tatu mfululizo mpaka ameaga dunia."

 

 

Hadiyth – 2

وعن عروة ، عن عائشة رضي الله عنها ، أنّها كَانَتْ تقول : وَاللهِ ، يَا ابْنَ أُخْتِي ، إنْ كُنَّا نَنْظُرُ إِلَى الهِلاَلِ ، ثُمَّ الهِلالِ : ثَلاَثَةُ أهلَّةٍ في شَهْرَيْنِ ، وَمَا أُوقِدَ في أبْيَاتِ رسول الله صلى الله عليه وسلم نَارٌ . قُلْتُ : يَا خَالَةُ ، فَمَا كَانَ يُعِيشُكُمْ ؟ قالت : الأَسْوَدَانِ التَّمْرُ وَالمَاءُ ، إِلاَّ أنَّهُ قَدْ كَانَ لرسول الله صلى الله عليه وسلم جِيرَانٌ مِنَ الأَنْصَارِ ، وكَانَتْ لَهُمْ مَنَائِحُ وَكَانُوا يُرْسِلُونَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم مِنْ ألْبَانِهَا فَيَسْقِينَا . متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa 'Urwah, kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa yeye alikuwa anasema: "Naapa kwa Allaah! Ee kijana wa dadangu, tulikuwa tunaona mwezi, kisha mwezi mwingine, na kisha mwezi mwengine: Miandamo mitatu katika miezi miwili na hakukuwa kukiwashwa moto katika nyumba za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." Nikasema: "Ee halati yangu! Mlikuwa mkila nini?" Akasema: "Vitu Vyeusi viwili: Tende na maji isipokuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na majirani wa ki-Answaar ambao walikuwa wakimletea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) maziwa tuliokuwa tukinywa." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد المقبُريِّ ، عن أَبي هريرة رضي الله عنهما: أَنَّهُ مَرَّ بِقَومٍ بَيْنَ أيدِيهمْ شَاةٌ مَصْلِيَّةٌ ، فَدَعَوْهُ فَأبَى أنْ يأْكُلَ . وقال : خرج رسول الله صلى الله عليه وسلم مِنَ الدُّنْيَا وَلَمْ يَشْبَعْ مِنْ خُبْزِ الشَّعيرِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abuu sa'iyd Al-Maqburiyy kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mara moja alipita baina ya watu waliokuwa wakichoma mbuzi, walimuita lakini alikataa kula. Akasema: "Aliondoka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) duniani na wala hakushiba hata siku moja makte wa mtama." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : لَمْ يَأكُلِ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم عَلَى خِوَانٍ حَتَّى مَاتَ ، وَمَا أكَلَ خُبْزاً مُرَقَّقاً حَتَّى مَاتَ . رواه البخاري .

وفي رواية لَهُ : وَلاَ رَأى شَاةً سَمِيطاً بعَيْنِهِ قَطُّ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: "Hakula Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya meza mpaka akafariki. Na wa hakula mkate mzuri na laini mpaka akaaga dunia." [Al-Bukhaariy]

Katika riwaayah nyengine: "Wala hakumuona kabisa mbuzi mzima aliyechomwa."

 

 

Hadiyth – 5

وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما ، قَالَ : لَقَدْ رَأيْتُ نَبيَّكُمْ صلى الله عليه وسلم  ، وَمَا يَجِدُ مِنَ الدَّقَلِ مَا يَمْلأُ بِهِ بَطْنَهُ . رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa an-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba amesema: "Hakika nimemuona Nabiy wenu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye hakuweza kupata hata tende mbaya ambazo zitamshibisha." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن سهلِ بن سعد رضي الله عنه، قَالَ : مَا رَأى رسول الله صلى الله عليه وسلم  النَّقِيَّ مِنْ حِين ابْتَعَثَهُ الله تَعَالَى حَتَّى قَبضَهُ الله تَعَالَى . فقِيلَ لَهُ : هَلْ كَانَ لَكُمْ في عَهدِ رسول الله صلى الله عليه وسلم  مَنَاخِلُ ؟ قَالَ : مَا رَأى رسول الله صلى الله عليه وسلم  مُنْخُلاً مِنْ حِينَ ابْتَعَثَهُ اللهُ تَعَالَى حَتَّى قَبَضَهُ اللهُ تَعَالَى ، فَقِيلَ لَهُ : كَيْفَ كُنْتُمْ تَأكُلُونَ الشَّعِيرَ غَيْرَ مَنْخُولٍ ؟ قَالَ : كُنَّا نَطحَنُهُ وَنَنْفُخُهُ ، فيَطيرُ مَا طَارَ ، وَمَا بَقِيَ ثَرَّيْنَاهُ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Hakuona mkate wa unga safi tangu Allaah Ta'aalaa Alipomtuma mpaka Allaah Ta'aalaa alipomfisha. Akauliza: "Je, katika zama za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mlikuwa na chekeche?" Akasema: "Hakuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kichungio tangu Allaah Ta'aalaa Alipomtuma hadi Allaah Ta'aalaa alipomfisha." Akauliza: "Mlikuwa mkila vipi shayiri isiochekechwa?" Akasema: "Tulikuwa tukiitwanga na kuipulizia, hupeperuka zinazopeperuka na kilichobaki tunakanda." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : خرجَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ أَوْ لَيْلَةٍ ، فَإذَا هُوَ بأَبِي بَكْرٍ وَعُمَرَ رضي الله عنهما ، فَقَالَ : (( مَا أخْرَجَكُمَا مِنْ بُيُوتِكُما هذِهِ السَّاعَةَ ؟ )) قَالا : الجُوعُ يَا رسول الله . قَالَ : (( وَأنَا ، وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ ، لأخْرَجَنِي الَّذِي أخْرَجَكُما ، قُوما )) فقَامَا مَعَهُ ، فَأتَى رَجُلاً مِنَ الأَنْصَارِ ، فَإذَا هُوَ لَيْسَ في بيْتِهِ ، فَلَمَّا رَأَتْهُ المَرْأَةُ ، قالت : مَرْحَبَاً وَأهلاً .فقال لَهَا رسول الله صلى الله عليه وسلم:(( أيْنَ فُلانُ ؟ )) قالت : ذَهَبَ يَسْتَعْذِبُ لنَا المَاءَ . إِذْ جَاءَ الأَنْصَارِيُّ ، فَنَظَرَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم وَصَاحِبَيْهِ ، ثُمَّ قَالَ : الحَمْدُ للهِ ، مَا أَحَدٌ الْيَوْمَ أكْرَمَ أضْيَافاً مِنِّي ، فَانْطَلَقَ فَجَاءهُمْ بِعِذْقٍ فِيهِ بُسْرٌ وَتَمْرٌ وَرُطَبٌ ، فَقَالَ : كُلُوا ، وَأَخَذَ الْمُدْيَةَ ، فَقَالَ لَهُ رسول الله صلى الله عليه وسلم: (( إيْاكَ وَالْحَلُوبَ )) فَذَبَحَ لَهُمْ ، فَأكَلُوا مِنَ الشَّاةِ وَمِنْ ذَلِكَ العِذْقِ وَشَرِبُوا . فَلَمَّا أنْ شَبِعُوا وَرَوُوا قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم لأَبي بَكْر وَعُمَرَ رضي الله عنهما : (( وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ ، لَتُسْأَلُنَّ عَنْ هَذَا النَّعِيمِ يَوْمَ القِيَامَةِ ، أَخْرَجَكُمْ مِنْ بُيُوتِكُمُ الْجُوعُ ، ثُمَّ لَمْ تَرْجِعُوا حَتَّى أصَابَكُمْ هَذَا النَّعيمُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Alitoka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) siku moja au usiku, akakutana na Abuu Bakr na 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhummaa) Akasema: "Nini kilichowatoa katika majumba yenu saa hii?" Wakasema: "Njaa ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mkononi Mwake, mimi pia kimenitoa nyumbani kwangu kilichowatoa nyie, simameni" Wakasimama pamoja naye Akaja mtu wa Ki-Answaar, lakini hakuwa nyumbani kwake. Mkewe alipowaona, alisema: "Karibuni sana." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: "Fulani yuko wapi?" Akasema: "Amekwenda kututekea maji." Mara akarudi yule Answaar akamwangalia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na rafiki zake, kisha akasema: "Alhamdulillaah." Hakuna leo mwenye wegeni watukufu kuniliko." Akatoka na kurudi huku amekuja na kitagaa chenye tende mbivu na mbichi. Akasema: "Kuleni naye" akachukua kisu kuwachinjia mbuzi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Usichinje mwenye maziwa." Wakala mbuzi waliochinjiwa, wakala na tende na kunywa maji. Waliposhiba na kukata kiu, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaambia Abu Bakr na 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): "Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake, Mtaulizwa neema hii Siku ya Qiyaamah. Lililowatoeni majumbani mwenu ni njaa, lakini kabla ya kurudi (majumbani kwenu) mmepata neema hii." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن خالد بن عُمَيْر العَدَوِيِّ ، قَالَ : خَطَبَنَا عُتْبَةُ بنُ غَزْوَانَ ، وَكَانَ أمِيراً عَلَى البَصْرَةِ ، فَحَمِدَ الله وَأثْنَى عَلَيْهِ ، ثُمَّ قَالَ : أَمَّا بَعْدُ ، فَإِنَّ الدُّنْيَا قَدْ آذَنَتْ بِصُرْمٍ ، وَوَلَّتْ حَذَّاءَ ، وَلَمْ يَبْقَ مِنْهَا إِلاَّ صُبَابَةٌ كَصُبَابَةِ الإنَاءِ يَتَصَابُّهَا صَاحِبُهَا ، وَإِنَّكُمْ مُنْتَقِلُونَ مِنْهَا إِلَى دَارٍ لاَ زَوَالَ لَهَا ، فَانْتَقِلُوا بِخَيرِ مَا بِحَضْرَتِكُمْ ، فَإِنَّهُ قَدْ ذُكِرَ لَنَا أنَّ الحَجَرَ يُلْقَى مِنْ شَفِيرِ جَهَنَّمَ فَيَهْوِي فِيهَا سَبْعِينَ عَاماً ، لاَ يُدْرِكُ لَهَا قَعْراً ، وَاللهِ لَتُمْلأَنَّ أَفَعَجِبْتُمْ ؟! وَلَقدْ ذُكِرَ لَنَا أنَّ مَا بَيْنَ مِصْرَاعَيْنِ مِنْ مَصَارِيعِ الْجَنَّةِ مَسيرَةُ أرْبَعِينَ عَاماً ، وَليَأتِيَنَّ عَلَيْهَا يَوْمٌ وَهُوَ كَظِيظٌ مِنَ الزِّحَامِ ، وَلَقَدْ رَأيْتُنِي سَابعَ سَبْعَةٍ مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، مَا لَنَا طَعَامٌ إِلاَّ وَرَقُ الشَّجَرِ ، حَتَّى قَرِحَتْ أشْدَاقُنَا ، فَالتَقَطْتُ بُرْدَةً فَشَقَقْتُهَا بَيْنِي وَبَيْنَ سَعْدِ بْنِ مَالِكٍ ، فاتَّزَرْتُ بِنِصْفِهَا ، وَاتَّزَرَ سَعْدٌ بِنِصْفِهَا ، فَمَا أصْبَحَ اليَوْمَ مِنَّا أحَدٌ إِلاَّ أَصْبَحَ أمِيراً عَلَى مِصرٍ مِنَ الأَمْصَارِ ، وَإنِّي أعُوذُ بِاللهِ أنْ أكُونَ فِي نَفْسِي عَظِيماً ، وَعِنْدَ اللهِ صَغِيراً .

رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Khaalid bin 'Umayr Al-'Adawiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Alituhutubia 'Utbah bin Ghazwaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) naye alikuwa ni Amiri wa Basrah. Alimuhimidi Allaah na kumtukuza, kisha akasema: "Ama baada ya hayo! Kwa hakika dunia inatangaza kumalizika kwake na imegeuza uso wake na inakimbia kwa haraka sana. Dunia imebakia ndogo sana kama mfano wa matone yanayobaki baada ya mtu kunywa maji kutoka kwenye chombo. Wapenzi wa dunia wanakunywa matone hayo. Na hakika nyinyi mtakuwa ni wenye kuhamishwa kutoka katika nyumba yenye kudumu milele. Hivyo, yakinisha kuwa utakwenda huko na vile vitu vizuri kabisa ulivyonavyo. Tumeelezwa ya kwamba jiwe litakuwa ni lenye kurushwa kwenye mdomo wa Jahanamu ambalo litachukua miaka sabiini kufika chini. Naapa kwa Allaah kuwa sehemu hiyo itajazwa (na watu waovu). Je, mnastaajabu? Na hakika tuliambiwa ya kwamba masafa baina ya mbao mbili za mlango wa Peponi ni mwendo wa miaka arobaini. Mbali ya hiyo itafika siku ambapo halaiki ya watu itajaa kwenye mlango huo. Nakumbuka nilipokuwa mmoja wa watu saba waliokuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakati ambao hatukuwa na chochote cha kula ila majani ya miti mpaka midomo yetu ikapata majeraha ya kupasuka pasuka. Hata hivyo nilipata kitambara ambacho nilikikata vipande viwili, kimoja nikatumia mimi na nusu ya pili nikampatia Sa'ad bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu). Ama leo kila moja miongoni mwetu ni Amiri wa mji miongoni mwa miji. Na kwa hakika mimi, najilinda kwa Allaah kwa hilo, kuwa katika nafsi yangu kujiona mtukufu na mbele ya Allaah nikawa mdogo sana." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه، قَالَ : أخْرَجَتْ لَنَا عَائِشَةُ رضي الله عنها كِسَاءً وَإزاراً غَلِيظاً ، قالَتْ : قُبِضَ رسول الله صلى الله عليه وسلم في هَذَيْنِ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Asha'ariy kwamba amesema: "Alituonyesha 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kitambara na kikoi kigumu, akasema: 'Ameaga dunia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa na nguo hizi mbili pekee." [Al-Bukhaariy na Muuslim]

 

 

Hadiyth – 10

وعن سعد بن أَبي وقاص رضي الله عنه، قَالَ : إنِّي لأَوَّلُ الْعَرَبِ رَمَى بِسَهْمٍ في سَبِيلِ الله ، وَلَقَدْ كُنَّا نَغْزُو مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  مَا لَنَا طَعَامٌ إِلاَّ وَرَقُ الْحُبْلَةِ ، وَهذَا السَّمُرُ ، حَتَّى إنْ كَانَ أحَدُنَا لَيَضَعُ كَمَا تَضَعُ الشَّاةُ مَا لَهُ خَلْطٌ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Sa'ad bin Abuu Waqqaas (Radhwiya Allaah 'anhu) kwamba amesema: "Mimi nilikuwa Muarabu wa kwanza kurusha mshale katika njia ya Allaah. Tulikuwa tukipigana (katika Jihad) pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hatuna kabisa chakula isipokuwa majani ya miti ya jangwani (kama acacia). Hivyo kukifanya choo chetu kuwa kigumu kama kinyesi cha mbuzi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( اللَّهُمَّ اجْعَلْ رِزْقَ آلِ مُحَمّدٍ قُوتاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee Allaah! Ijaalie riziki ya familia ya Muhammad iwe ni yenye kutosha." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]

 

 

Hadiyth – 12

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : وَاللهِ الَّذِي لاَ إِلهَ إِلاَّ هُوَ ، إنْ كُنْتُ لأَعْتَمِدُ بِكَبِدِي عَلَى الأَرْضِ مِنَ الجُوعِ ، وَإنْ كُنْتُ لأَشُدُّ الحَجَرَ عَلَى بَطنِي مِنَ الْجُوعِ . وَلَقَدْ قَعَدْتُ يَوماً عَلَى طَرِيقِهِمُ الَّذِي يَخْرُجُونَ مِنْهُ ، فَمَرَّ بِي النبي صلى الله عليه وسلم ، فَتَبَسَّمَ حِيْنَ رَآنِي ، وَعَرَفَ مَا فِي وَجْهِي وَمَا فِي نَفْسِي ، ثُمَّ قَالَ : (( أَبَا هِرٍّ )) قُلْتُ : لَبَّيْكَ يَا رسول الله ، قَالَ : (( الْحَقْ )) وَمَضَى فَاتَّبَعْتُهُ ، فَدَخَلَ فَاسْتَأذَنَ ، فَأَذِنَ لِي فَدَخَلْتُ ، فَوَجَدَ لَبَنَاً في قَدَحٍ ، فَقَالَ : (( مِنْ أَيْنَ هَذَا اللَّبَنُ ؟ )) قَالُوا : أهْدَاهُ لَكَ فُلانٌ – أَو فُلانَةٌ – قَالَ : (( أَبَا هِرٍّ )) قلتُ : لَبَّيْكَ يَا رسول اللهِ ، قَالَ : (( الْحَقْ إِلَى أهْلِ الصُّفَّةِ فَادْعُهُمْ لِي )) قَالَ : وَأهْلُ الصُّفَّة أضْيَافُ الإِسْلاَمِ ، لاَ يَأوُونَ علَى أهْلٍ وَلاَ مَالٍ وَلاَ عَلَى أحَدٍ ، وَكَانَ إِذَا أتَتْهُ صَدَقَةٌ بَعَثَ بِهَا إلَيْهِمْ ، وَلَمْ يَتَنَاوَلْ مِنْهَا شَيْئاً ، وَإِذَا أتَتْهُ هَدِيَّةٌ أرْسَلَ إلَيْهِمْ ، وَأصَابَ مِنْهَا ، وأشْرَكَهُمْ فِيهَا . فَسَاءنِي ذَلِكَ ، فَقُلْتُ : وَمَا هَذَا اللَّبَنُ في أهْلِ الصُّفَّةِ ! كُنْتُ أحَقُّ أنْ أُصِيبَ مِنْ هَذَا اللَّبَنِ شَرْبَةً أتَقَوَّى بِهَا ، فَإذَا جَاءُوا وَأمَرَنِي فَكُنْتُ أنَا أُعْطِيهِمْ ؛ وَمَا عَسَى أنْ يَبْلُغَنِي مِنْ هَذَا اللَّبَنِ . وَلَمْ يَكُنْ مِنْ طَاعَةِ اللهِ وَطَاعَةِ رسول الله صلى الله عليه وسلم بُدٌّ ، فَأَتَيْتُهُمْ فَدَعَوْتُهُمْ ، فَأقْبَلُوا وَاسْتَأذَنُوا ، فَأَذِنَ لَهُمْ وَأخَذُوا مَجَالِسَهُمْ مِنَ الْبَيْتِ ، قَالَ : (( يَا أَبَا هِرٍّ )) قُلْتُ: لَبَّيْكَ يَا رسول الله ، قَالَ : (( خُذْ فَأعْطِهِمْ )) قَالَ : فَأخَذْتُ القَدَحَ ، فَجَعَلْتُ أُعْطِيهِ الرَّجُل فَيَشْرَبُ حَتَّى يَرْوَى ، ثُمَّ يَرُدُّ عَلَيَّ الْقَدَحَ ، فَأُعْطِيهِ الرَّجُلَ فَيَشْرَبُ حَتَّى يَرْوَى ، ثُمَّ يَرُدُّ عَلَيَّ الْقَدَحَ ، فَأُعْطِيهِ الرَّجُلَ فَيَشْرَبُ حَتَّى يَرْوَى ، ثُمَّ يَرُدُّ عَلَيَّ الْقَدَحَ حَتَّى انْتَهَيْتُ إِلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، وَقَدْ رَوِيَ الْقَوْمُ كُلُّهُمْ ، فَأخَذَ الْقَدَحَ فَوضَعَهُ عَلَى يَدِهِ ، فَنَظَرَ إليَّ فَتَبَسَّمَ ، فَقَالَ : (( أَبَا هِرٍّ )) قُلْتُ : لَبَّيْكَ يَا رسول الله ، قَالَ : (( بَقيتُ أنَا وَأنْتَ )) قُلْتُ : صَدَقْتَ يَا رسول الله ، قَالَ : (( اقْعُدْ فَاشْرَبْ )) فَقَعَدْتُ فَشَرِبْتُ ، فَقَالَ (( اشْرَبْ )) فَشَرِبْتُ ، فَمَا زَالَ يَقُولُ : (( اشْرَبْ )) حَتَّى قُلْتُ: لا ، وَالَّذِي بَعَثَكَ بِالحَقِّ لاَ أجِدُ لَهُ مَسْلكاً ! قَالَ: (( فَأرِنِي )) فَأعْطَيْتُهُ الْقَدَحَ ، فَحَمِدَ الله تَعَالَى ، وَسَمَّى وَشَرِبَ الفَضْلَةَ . رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah amesema: ""Naapa kwa ambaye hapana Mola isipokuwa Yeye, nilikuwa naegemeza tumbo langu ardhini kwa njaa, nikifunga jiwe tumboni mwangu kwa njaa. Siku moja nilikaa juu ya njia yao wanayotokea. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita akatabasamu aliponiona, akajua kilicho usoni mwangu na yaliyo nafsini mwangu. Alisema: "Abuu Hirr." Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Nifuate." Aliondoka nikamfuata. Akabisha hodi akakaribishwa, akaniruhusu kuingia. Akakuta maziwa ndani ya jagi akasema: "Kutoka wapi haya maziwa?" Wakasema: "Fulani amekuzawadia." Akasema: "Abuu Hirr." Nikasema: "Labbayka, ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Nenda kaite watu wa Swuffah." Akasema: "Watu wa Swuffah ni wageni wa Waislamu, hawana isipokuwa jamaa, mali, wala yoyote," Alikuwa akipata swadaqah anawapelekea, hakutumia chochote humo. "Na anapopata zawadi anawapelekea naye anakula humo, na kuwashirikisha humo, Likaniumiza hilo, nikauliza: "Maziwa gani haya kwa watu wa Suwffah?" Nilikuwa na haki zaidi kupata haya maziwa ili yanipe nguvu. Watakapofiks ataniamuru kuwaandalia, pengine yasinifikie maziwa haya, hakukuwa na budi isipokuwa kutii amri ya Allaah na Rasuli Wake." Nilikwenda kuwaita, wakabisha hodi, wakaruhusiwa, wakakaa sehemu yao. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Abuu Hirr." Nikasema: "Labbayka, ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Chukua haya maziwa uwape." Akasema: "Nikachukua kikombe nikaanza kumpa wa kwanza, alikunywa hadi akatosheka. Kisha akanirudishia kikombe, nikampa mwengine hunywa mpaka anatosheka. Kisha hunirudishia kikombe kikamfikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wote wamemaliza kunywa. Nabiy akachukua kikombe mkononi mwake akanitazama akatabasamu, akasema: "Abuu Hirr." Nikasema: "Labbayka, ee rasuli wa Allaah." Akasema: "Tumebaki mimi na wewe." Nikasema: "Ndio, ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Kaa unywe." Nikakaa nakunywa." Akasema: "Kunywa." Nami nikanywa. Hakuacha kusema "Kunywa." Mpaka ikafika wakati nikasema: "Laa, naapa aliyekutuma kwa haki sina nafasi yake." Akasema: "Nipe." Nikampa kikombe, akamuhimidi Allaah, akasema: "Bismillaah, akanywa maziwa yaliyobakia." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 13

وعن محمد بن سيرين ، عن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : لَقَدْ رَأيْتُنِي وَإنِّي لأَخِرُّ فِيمَا بَيْنَ مِنْبَرِ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم إِلَى حُجْرَةِ عائِشَةَ رضي الله عنها مَغْشِيّاً عَلَيَّ ، فَيَجِيءُ الجَائِي ، فَيَضَعُ رِجْلَهُ عَلَى عُنُقِي ، وَيَرَى أنِّي مَجْنُونٌ وَمَا بِي مِنْ جُنُونٍ ، مَا بِي إِلاَّ الْجُوعُ . رواه البخاري.

Imepokewa kutoka kwake Muhammad bin Siiyriyn kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nilijiona naanguka baina ya mimbari ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na chumba cha 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) na kupoteza fahamu, anapita mtu anaweka mguu wake shingoni mwangu, akidhani mimi ni mwenda wazimu. Ns mimi si mwenda wazimu isipokuwa njaa." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 14

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : تُوُفِّي رسول الله صلى الله عليه وسلم وَدِرْعُهُ مَرْهُونَةٌ عِنْدَ يَهُودِي في ثَلاثِينَ صَاعاً مِنْ شَعِير . متفق عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba amesema: "Alifariki Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na dir'a (nguo ya chuma inayotumiwa katika vita) yake ameiweka rahani kwa Myahudi kwa Swaa' (takriban kilo mbili na nusu) thelathini za shayiri." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai]

 

 

Hadiyth – 15

وعن أنسٍ رضي الله عنه، قَالَ : رَهَنَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم دِرْعَهُ بِشَعِيرٍ ، وَمَشَيْتُ إِلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم بخُبْزِ شَعِيرٍ وَإهَالَة سَنِخَةٍ ، وَلَقَدْ سَمِعْتُهُ يَقُولُ : (( مَا أصْبَحَ لآلِ مُحَمّدٍ صَاعٌ وَلاَ أمْسَى )) وَإنَّهُمْ لَتِسْعَةُ أبيَات . رواه البخاري .

Imepokewa kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: "Aliweka rehani Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) dir'a yake kwa shayiri, nikamchukulia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mkate wa shayiri na samli, Nimemsikia anasema: "Haijapambazuka Familia ya Muhammad ikiwa na pishi ya chakula wala kuchwewe." Na hizo ni nyumba tisa." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 16

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : لَقَدْ رَأَيْتُ سَبْعِينَ مِنْ أَهْلِ الصُّفَّةِ ، مَا مِنْهُمْ رَجُلٌ عَلَيْهِ ردَاءٌ ، إمَّا إزَارٌ وَإمَّا كِسَاءٌ ، قَدْ رَبَطُوا في أعْنَاقِهِم مِنْهَا مَا يَبْلُغُ نِصْفَ السَّاقَيْن ، وَمِنْهَا مَا يَبْلُغُ الكَعْبَيْنِ فَيَجْمَعُهُ بِيَدِهِ كَرَاهِيَةَ أنْ تُرَى عَوْرَتُهُ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nimeona Swahaaba sabiini miongoni mwa watu wa Swuffah, hakuna mtu miongoni mwao mwenye kikoi, shuka, wamezifunga katika shingo zao. Kuna zinazofika nusu ya miguu, nyingine kwenye fundo mbili, hivyo huzishika mkononi mwake kuchukia uchi wao kuonekana." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 17

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ فِرَاشُ رسول الله صلى الله عليه وسلم مِنْ أُدْمٍ حَشْوُهُ لِيفٌ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba amesema: "Godoro la Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) lilikuwa limetengenezwa kwa ngozi iliyotiwa magamba ya mtende." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Hadiyth – 18

وعن ابن عمر رضي الله عنهما، قَالَ : كُنَّا جُلُوساً مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم، إِذْ جَاءَ رَجُلٌ مِنَ الأنْصَارِ ، فَسَلَّمَ عَلَيْهِ ، ثُمَّ أدْبَرَ الأَنْصَاريُّ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا أخَا الأنْصَارِ ، كَيْفَ أخِي سَعْدُ بْنُ عُبَادَةَ ؟ )) فَقَالَ : صَالِحٌ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ يَعُودُهُ مِنْكُمْ ؟ )) فَقَامَ وَقُمْنَا مَعَهُ ، وَنَحْنُ بضْعَةَ عَشَرَ ، مَا عَلَيْنَا نِعَالٌ ، وَلاَ خِفَافٌ ، وَلاَ قَلاَنِسُ ، وَلاَ قُمُصٌ ، نَمْشِي في تِلك السِّبَاخِ ، حَتَّى جِئْنَاهُ ، فَاسْتَأْخَرَ قَوْمُهُ مِنْ حَوْله حَتَّى دَنَا رسول الله صلى الله عليه وسلم وَأصْحَابُهُ الَّذِينَ مَعَهُ . رواه مسلم .

imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba amesema: "Tulikuwa tumekaa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuja mtu kutoka kwa Answaar na kumsalima Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Kisha yule Answaar akawa anaondoka, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: "Ee ndugu yangu wa Ki-Answaar, ndugu yangu Sa'ad bin 'Ubaadah yu hali gani?' Akasema: "Hali yake ni nzuri." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Nani atakayemzuru miongoni mwenu?" Alisimama na tukasimama pamoja naye. Na sisi tulikuwa kumi, na hakuna miongoni mwetu aliyekuwa na viatu au soksi za ngozi, wala kofia au shati. Tulikuwa tunatembea katika hali hiyo mpaka tukafika katika nyumba ya Sa'ad. Watu wake wa nyumbani (familia yake) walitupatia nafasi mpaka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaaba zake waliokuwa pamoja naye wakapata nafasi ya kuja karibu yake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 19

وعن عِمْرَان بنِ الحُصَيْنِ رضي الله عنهما ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنّه قَالَ :   (( خَيْرُكُمْ قَرْنِي ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ )) قَالَ عِمْرَانُ : فَمَا أدْري قَالَ النبي صلى الله عليه وسلم مَرَّتَيْنِ أَو ثَلاَثاً (( ثُمَّ يَكُونُ بَعْدَهُمْ قَوْمٌ يَشْهَدُونَ وَلاَ يُسْتَشْهَدُونَ ، وَيَخُونُونَ وَلاَ يُؤْتَمَنُونَ ، وَيَنْذِرُونَ وَلاَ يُوفُونَ ، وَيَظْهَرُ فِيهمُ السَّمَنُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Imraan bin Al-Huswaiyn (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mbora wenu ni (watu wa) karne yangu, kisha wanaowafuata, kisha wanaowafuata, kisha wanaowafuata, Akasema 'Imraan: "Sijui Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameisema mara mbili au mara tatu. Kisha watakuja baada yao watu watashuhudia wala hawatakiwi kushuhudia, wanakhini wala hawaaminiwi, utadhihiri miongoni mwao umeme (walionenepa)." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 20

وعن أَبي أُمَامَة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا ابْنَ آدَمَ ، إنَّكَ أنْ تَبْذُلَ الفَضْلَ خَيرٌ لَكَ ، وَأنْ تُمسِكَهُ شَرٌ لَكَ ، ولاَ تُلاَمُ عَلَى كَفَافٍ ، وَابْدأ بِمَنْ تَعُولُ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Umamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee mwanadamu! Hakika lau utatoa fadhila (hela) za ziada itakuwa bora kwako, na kuzuilia (kutotumia) ni shari kwako. Hutalaumiwa kuwa na hela kwa kadiri ya mahitaji yako. Na anza kuitumia kwa wale wenye haki kwako." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 21

وعن عُبيْدِ الله بنِ محْصن الأَنصَارِيِّ الخطميِّ رضي الله عنه  ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  : (( مَنْ أصْبَحَ مِنْكُمْ آمِناً في سربِهِ ، مُعَافَىً في جَسَدِهِ ، عِنْدَهُ قُوتُ  يَوْمِهِ ، فَكَأنَّمَا حِيزَتْ لَهُ الدُّنْيَا بِحَذَافِيرِهَا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa 'Ubaydullaah bin Muhswan Al-Answaariy Al-Khutwamiy kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote atakaye pambazukiwa (atakaye inuka asubuhi) akiwa yu salama wa nafsi yake (au familia yake), akiwa na siha mzuri ya mwili wake, anacho chakula cha siku yake hiyo. Mwenye hayo ni kama ambaye amepatiwa dunia na vilivyomo ndani yake." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Hadiyth – 22

وعن عبد الله بن عَمْرو بنِ العاص رضي الله عنهما : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم  ، قَالَ : (( قَدْ أفْلَحَ مَنْ أسْلَمَ ، وَكَانَ رِزْقُهُ كَفَافاً ، وَقَنَّعَهُ اللهُ بِمَا آتَاهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amru bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika amefanikiwa aliyesilimu na ikiwa riziki yake ni yenye kumtosha na akakinaika kwa anachopewa na Allaah." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 23

وعن أَبي محمدٍ فضَالَة بن عبيدٍ الأنصاريِّ رضي الله عنه: أنه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم، يقول : (( طُوبَى لِمَنْ هُدِيَ لِلإسْلاَمِ ، وَكَانَ عَيْشُهُ كَفَافاً وَقَنِعَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Muhammad Fadhwalah bin 'Ubayd Al-Answaariy (Radhwiya Allaah 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Habari njema kwa anayeongoka na kusilimu na akapata rizki ya kumtosha mahitaji yake na akakinai kwa hilo." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 24

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَبيتُ اللَّيَالِيَ الْمُتَتَابِعَةَ طَاوِياً ، وَأهْلُهُ لاَ يَجِدُونَ عَشَاءً ، وَكَانَ أكْثَرُ خُبْزِهِمْ خُبزَ الشَّعيرِ . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akilala akiwa na shida ya njaa kwa masiku marefu yenye kufuatana na familia yake haina chochote cha kula usiku. Na mara nyingi mkate waliokuwa wakitumia ni mkate wa shayiri." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 25

وعن فُضَالَةَ بن عبيدٍ رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا صَلَّى بِالنَّاسِ ، يَخِرُّ رِجَالٌ مِنْ قَامَتِهِمْ في الصَّلاةِ مِنَ الخَصَاصَةِ – وَهُمْ أصْحَابُ الصُّفَّةِ – حَتَّى يَقُولَ الأعْرَابُ : هؤُلاء مَجَانِينٌ . فَإذَا صلَّى رسول الله صلى الله عليه وسلم انْصَرَفَ إلَيْهِمْ ، فَقَالَ :   (( لَوْ تَعْلَمُونَ مَا لَكُمْ عِنْدَ اللهِ تَعَالَى ، لأَحْبَبْتُمْ أنْ تَزْدَادُوا فَاقَةً وَحَاجَةً )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwake Fadhwalah bin 'Ubayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswalisha watu wakianguka chini baadhi ya watu wa Swuffah kwa sababu ya njaa kali mpaka wakawa wanasema Mabedui: "Hawa ni wenda wazimu." Alipokamilisha Swalah Rasuli wa Allaah alikuwa akiwaendea na kuwaambia: "Lau mngejua yaliyoko (katika thawabu) kwa Allaah Ta'aalaa, mngependa hali ya njaa kali ikaongezeka." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 26

وعن أَبي كريمة المقدام بن معد يكرِبَ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَا مَلأَ آدَمِيٌّ وِعَاء شَرّاً مِنْ بَطْنٍ ، بِحَسْبِ ابنِ آدَمَ أُكُلاَتٌ يُقِمْنَ صُلْبَهُ ، فإنْ كانَ لا مَحالةَ فثُلُثٌ لِطَعَامِهِ ، وَثُلُثٌ لِشَرابِهِ ، وَثُلُثٌ لِنَفَسه )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Kariymah Al-Miqdaam bin Ma'di Yakrib (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hajajaza mwanadamu chombo kiovu zaidi kuliko tumbo lake. Inamtosha mwanadamu tonge la kuufanya mgongo usimame wima. Ikiwa hapana budi ila kula hicho chakula basi thuluthi ya tumbo iwe kwa chakula na thuluthi kwa kinywaji na thuluthi kwa nafsi yake (pumzi)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].

 

 

Hadiyth – 27

وعن أَبي أُمَامَة إياسِ بن ثعلبةَ الأَنْصَارِيِّ الحارثي رضي الله عنه  ، قَالَ : ذَكَرَ أصْحَابُ رسول الله r يَوماً عِنْدَهُ الدُّنْيَا ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( ألاَ تَسْمَعُونَ ؟ ألاَ تَسْمَعُونَ ؟ إنَّ البَذَاذَةَ مِنَ الإِيمَانِ ، إنَّ البَذَاذَةَ مِنَ الإِيمَانِ )) يَعْنِي : التَّقَحُّلَ . رواهُ أَبو داود

Imepokewa kutoka kwa Abu Umaamah Iyaas bin Tha'labah Al-Answaariy Al-Haarithiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Siku moja Sahaabah wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) walimtajia kuhusu dunia mbele yake. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je,hamjasikia? Je, hamjasikia? Hakika kuupa nyongo ulimwengu ni katika Imaani. Hakika kuupa nyongo ulimwengu ni katika Imaani (kwa kuacha fakhari katika mavazi na mengineo)." [Abu Daawuud]

 

 

Hadiyth – 28

وعن أَبي عبد الله جابر بن عبد الله رضي الله عنهما ، قَالَ : بَعَثَنَا رسول الله صلى الله عليه وسلم  ، وَأمَّرَ عَلَيْنَا أَبَا عُبَيْدَةَ رضي الله عنه ، نَتَلَقَّى عِيراً لِقُرَيْشٍ ، وَزَوَّدَنَا جِرَاباً مِنْ تَمْرٍ لَمْ يَجِدْ لَنَا غَيْرَهُ ، فَكَانَ أَبو عُبيدَةَ يُعْطِينَا تَمْرَةً تَمْرَةً ، فَقيلَ : كَيْفَ كُنْتُمْ تَصْنَعُونَ بِهَا ؟ قَالَ : نَمَصُّهَا كَمَا يَمَصُّ الصَّبي ، ثُمَّ نَشْرَبُ عَلَيْهَا مِنَ الْمَاءِ ، فَتَكْفِينَا يَوْمَنَا إِلَى اللَّيْلِ ، وَكُنَّا نَضْرِبُ بِعِصيِّنَا الخَبَطَ ، ثُمَّ نَبُلُّهُ بِالماءِ فَنَأكُلُهُ . قَالَ : وَانْطَلَقْنَا عَلَى سَاحِلِ الْبَحْرِ ، فَرُفِعَ لَنَا عَلَى سَاحِلِ الْبَحْرِ كَهَيْئَةِ الكَثِيبِ الضَّخْمِ ، فَأَتَيْنَاهُ فَإذَا هِيَ دَابَّةٌ تُدْعَى الْعَنْبَرَ ، فَقَالَ أَبو عُبَيْدَةَ : مَيْتَةٌ ، ثُمَّ قَالَ : لا ، بَلْ نَحْنُ رُسُلُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم  ، وفي سبيل الله وَقَدِ اضْطُرِرْتُمْ فَكُلُوا ، فَأقَمْنَا عَلَيْهِ شَهْراً ، وَنَحْنُ ثَلاَثُمِئَةٍ حَتَّى سَمِنَّا ، وَلَقَدْ رَأيْتُنَا نَغْتَرِفُ مِن وَقْبِ عَيْنِهِ بِالقِلاَلِ الدُّهْنَ وَنَقْطَعُ مِنْهُ الفِدَرَ كالثَّوْرِ أَوْ كَقَدْرِ الثَّوْرِ ، وَلَقَدْ أَخَذَ مِنَّا أَبو عُبَيْدَةَ ثَلاثَةَ عَشَرَ رَجُلاً فَأقْعَدَهُمْ في وَقْبِ عَيْنِهِ وَأخَذَ ضِلْعاً مِنْ أضْلاَعِهِ فَأقَامَهَا ثُمَّ رَحَلَ أعْظَمَ بَعِيرٍ مَعَنَا فَمَرَّ مِنْ تَحْتهَا وَتَزَوَّدْنَا مِنْ لَحْمِهِ وَشَائِقَ ، فَلَمَّا قَدِمْنَا المَدِينَةَ أَتَيْنَا رسول الله صلى الله عليه وسلم  فَذَكَرْنَا ذَلِكَ لَهُ ، فَقَالَ : (( هُوَ رِزْقٌ أخْرَجَهُ اللهُ لَكُمْ ، فَهَلْ مَعَكُمْ مِنْ لَحْمِهِ شَيْءٌ فَتُطْعِمُونَا ؟ )) فَأرْسَلْنَا إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم  مِنْهُ فَأكَلَهُ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu 'Abdillaah Jaabir bin Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: "Alitutuma Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), amiri alikuwa Abu 'Ubaydah (Radhwiya Allaahu 'anhu), ili kuteka msafara wa Makureshi. Akatupa mfuko wa tende bila kitu kingine. Abu 'Ubaydah akawa akimpa kila mmoja watu tende moja moja tu. Akaulizwa: 'Mlikuwa mnaifanya nini?, Akasema: 'Tulikuwa tunainyonya kama anavyonyonya mtoto mchanga, kisha tukinywamaji. Ilikuwa ikitutosha mchana hadi usiku. Tulikuwa tukikata majani kwa fimbo, tukizitia kati maji na kuzila.' Akasema: 'Tulikwenda tukafika ufukweni ikanyanyuliwa kwetu katika huo ufuo wa bahari mfano wa kichuguu kikubwa. Tukakijia kumbe ni mnyama anayeitwa nyangumi.' Abu 'Ubaydah akasema: 'Huyu ni maiti.' Kisha akasema: 'Bali sisi ni wajumbe wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na tuko katika njia ya Allaah, na hii ni dharura kwa hivyo kuleni.' Tukamla mwezi mzima, nasi ni mia tatu hadi tukanenepa. Tulikuwa tukimtoa mafuta jichoni na kujaza viriba vya ngozi, tunakata nyama kama ng'ombe dume au mfano wake. Abu 'Ubaydah alikalisha watu kumi na tatu kwenye shimo la jicho lake. Akatoa mfupa wa mbavu yake na kuusimamisha na kupitisha ngamia mrefu zaidi chini yake. Wakati tunarudi tulichukua mapande makubwa na kuyachemsha kwa ajili ya chakula chetu. Tulipofika Madiynah tulikwenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na tukamtajia hayo, Akasema: "Hiyo ni riziki Allaah amekutoleeni, je mna chochote katika nyama yake mtupe" Tulimpa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) sehemu yake akaila." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 29

وعن أسماء بنتِ يزيد رضي الله عنها ، قالت : كَانَ كُمُّ قَمِيصِ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِلَى الرُّصْغِ . رواه أَبو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa Asmaa' bint Yaziyd (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba amesema: "Mikono ya shati la Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ilikuwa ikifika mpaka kwenye kiungo cha viganja." [Abu Daawuud na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Hadiyth – 30

وعن جابر رضي الله عنه ، قَالَ : إنَّا كُنَّا يَوْمَ الْخَنْدَقِ نَحْفِرُ ، فَعَرَضَتْ كُدْيَةٌ شَدِيدَةٌ ، فَجَاؤُوا إِلَى النبي صلى الله عليه وسلم ، فقالوا : هذِهِ كُدْيَةٌ عَرَضَتْ في الخَنْدَقِ . فَقَالَ :    (( أنَا نَازِلٌ )) ثُمَّ قَامَ ، وَبَطْنُهُ مَعْصُوبٌ بِحَجَرٍ ، وَلَبِثْنَا ثَلاَثَة أيّامٍ لاَ نَذُوقُ ذَوَاقاً فَأخَذَ النبي صلى الله عليه وسلم المِعْوَلَ ، فَضَرَبَ فَعَادَ كَثيباً أهْيَلَ أَو أهْيَمَ ، فقلت : يَا رسول الله ، ائْذَنْ لي إِلَى البَيْتِ ، فقلتُ لامْرَأتِي : رَأيْتُ بالنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم شَيئاً مَا في ذَلِكَ صَبْرٌ فَعِنْدَكِ شَيْءٌ ؟ فقالت : عِنْدي شَعِيرٌ وَعَنَاقٌ ، فَذَبَحْتُ العَنَاقَ وَطَحَنْتُ الشَّعِيرَ حَتَّى جَعَلْنَا اللَّحْمَ في البُرْمَةِ ، ثُمَّ جِئْتُ النبي صلى الله عليه وسلم ، وَالعَجِينُ قَدِ انْكَسَرَ ، وَالبُرْمَةُ بَيْنَ الأثَافِيِّ قَدْ كَادَتْ تَنْضِجُ ، فقلتُ : طُعَيْمٌ لي ، فَقُمْ أنْتَ يَا رسول اللهِ وَرَجُلٌ أَوْ رَجُلانِ ، قَالَ : (( كَمْ هُوَ )) ؟ فَذَكَرْتُ لَهُ ، فَقَالَ : (( كثيرٌ طَيِّبٌ قُل لَهَا لاَ تَنْزَع البُرْمَةَ ، وَلاَ الخبْزَ مِنَ التَّنُّورِحتى آتِي )) فَقَالَ : (( قُومُوا )) ، فقام المُهَاجِرُونَ وَالأنْصَارُ ، فَدَخَلْتُ عَلَيْهَا فقلتُ : وَيْحَكِ قَدْ جَاءَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم وَالمُهَاجِرُونَ وَالأنْصَارُ ومن مَعَهُمْ ! قالت : هَلْ سَألَكَ ؟ قُلْتُ : نَعَمْ ، قَالَ : (( ادْخُلُوا وَلاَ تَضَاغَطُوا )) فَجَعَلَ يَكْسرُ الخُبْزَ ، وَيَجْعَلُ عَلَيْهِ اللَّحْمَ ، وَيُخَمِّرُ البُرْمَةَ وَالتَّنُّور إِذَا أخَذَ مِنْهُ ، وَيُقَرِّبُ إِلَى أصْحَابِهِ ثُمَّ يَنْزعُ ، فَلَمْ يَزَلْ يِكْسِرُ وَيَغْرِفُ حَتَّى شَبِعُوا ، وَبَقِيَ مِنْهُ ، فَقَالَ : (( كُلِي هَذَا وَأهِدي ، فَإنَّ النَّاسَ أصَابَتْهُمْ مَجَاعَةٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

وفي رواية قَالَ جابر : لَمَّا حُفِرَ الخَنْدَقُ رَأيْتُ بالنبيِّ صلى الله عليه وسلم خَمَصاً ، فَانْكَفَأْتُ إِلَى امْرَأتِي ، فقلت : هَلْ عِنْدَكِ شَيْءٌ ؟ فَإنّي رَأيْتُ برسول الله صلى الله عليه وسلم خَمَصاً شَديداً ، فَأخْرَجَتْ إلَيَّ جِرَاباً فِيه صَاعٌ مِنْ شَعِيرٍ ، وَلَنَا بَهِيمَةٌ دَاجِنٌ فَذَبَحْتُهَا ، وَطَحَنتِ الشَّعِيرَ ، فَفَرَغَتْ إِلَى فَرَاغي ، وَقَطَعْتُهَا في بُرْمَتها ، ثُمَّ وَلَّيْتُ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فقالت : لاَ تَفْضَحْنِي برسول الله صلى الله عليه وسلم وَمَنْ مَعَهُ ، فَجئتهُ فَسَارَرْتُهُ ، فَقُلْتُ : يَا رسول الله ، ذَبَحْنَا بهيمَة لَنَا ، وَطَحَنْتُ صَاعاً مِنْ شَعِيرٍ ، فَتَعَالَ أنْتَ وَنَفَرٌ مَعَكَ ، فَصَاحَ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : (( يَا أهلَ الخَنْدَقِ : إنَّ جَابِراً قَدْ صَنَعَ سُؤْراً فَحَيَّهَلا بِكُمْ )) فَقَالَ النبي صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تُنْزِلُنَّ بُرْمَتَكُمْ وَلاَ تَخْبزنَّ عَجِينَكُمْ حَتَّى أجِيءَ )) فَجِئْتُ ، وَجَاءَ النبي صلى الله عليه وسلم يَقْدُمُ النَّاسَ ، حَتَّى جِئْتُ امْرَأتِي ، فقالَتْ : بِكَ وَبِكَ ! فقُلْتُ : قَدْ فَعَلْتُ الَّذِي قُلْتِ . فَأخْرَجَتْ عَجِيناً ، فَبسَقَ فِيهِ وَبَاركَ ، ثُمَّ عَمَدَ إِلَى بُرْمَتِنا فَبصَقَ وَبَارَكَ، ثُمَّ قَالَ: (( ادْعِي خَابزَةً فَلْتَخْبِزْ مَعَكِ ، وَاقْدَحِي مِنْ بُرْمَتِكُمْ ، وَلاَ تُنْزِلُوها )) وَهُم ألْفٌ ، فَأُقْسِمُ بِالله لأَكَلُوا حَتَّى تَرَكُوهُ وَانْحَرَفُوا ، وَإنَّ بُرْمَتَنَا لَتَغِطّ كَمَا هِيَ ، وَإنَّ عَجِينَنَا لَيُخْبَزُ كَمَا هُوَ .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Siku ya Khandaq tulikuwa tunachimba pakatokea jiwe gumu, wakaja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakasema: 'Jiwe limedhihiri katika Khandaq' akasema: "Mimi nitateremka." Kisha akasimama na tumbo lake limefungwa jiwe. Tulikaa siku tatu bila kuonja chakula. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akachukua mtaimbo akalipiga likawa kichuguu laini, au mchanga. Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Niruhusu niende nyumbani." Nilimwambia mke wangu: "Nimemuona Nabiy (Swalla Allaau 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika hali ambayo siwezi kuvumilia. Una chochote?" Akasema: "Ipo shayiri na mwana mbuzi." Nilimchinja mbuzi na kutwanga shayiri hadi tukaiweka nyama katika chungu. Baada ya hapo nilikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mchunzi ukiwa unatokota na unga wa shayiri umekandwa na tayari kutiwa katika tanuri. Nilimwambia: "Nimeandaa chakula. Njoo wewe na mtu au watu wawili." Akasema: "Huo unatosha kiasi gani?" Nikamtajia. Akasema: "Wengi ni bora, mwambie mkeo asiepue chungu, motoni wala mikate katika tanuri hadi nije." Kisha akawambia Swahaba zake: "Twendeni." Wakasimama Muhaajiruun na Answaar. Nikaingia kwa mke wangu nikamwambia: "Umebarikiwa! Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), Muhaajiruun na Answaar wote wanakuja." Akasema: "Je, alikuuliza?" Nikasema: "Ndio." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alifika hapo na kuwaambia Swahaba zake: "Ingieni wala msisongamane." Akawa anakata mikate, na juu yake anaweka nyama. Anatoa mchuzi kwenye chungu na mikate kutoka kwa tanuri, kisha akaifunika na kuwapa Swahaba zake. Kisha anarudia, hakuacha hilo mpaka wakashiba na kikabaki. Akasema: "Kula hiki chakula na ukigawe, kwani watu wamepata njaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah: Jaabir amesema: "Khandaq lilipofukuliwa, nilimuona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ana njaa. Hivyo nilikwenda kwa mke wangu na kumuuliza: "Una kitu chochote kwani nimemuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ana njaa kali?" Alitoa mkoba wenye pishi ya shayiri, nasi tuna mwana mbuzi. Nikamchinja, mke wangu akakanda shayiri na akaoka mkate. Nikaikata nyama na kuitia chunguni. Kisha nilikwenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), Akaniambia mke wangu: "Usinifedheheshe kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na walio pamoja naye." Nilikuja kwake na kumnong'oneza nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Tumechinja mnyama wetu, na tuna pishi ya shayiri, njoo wewe kikundi pamoja nawe." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akaita: "Enyi watu wa Khandaq! Hakika Jaabir ameandaa karamu kwa hivyo nyote njooni." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Msiepue chungu wala msiitoe mikate yenu mpaka nije." Nilirudi nyumbani Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaja anaongoza watu. Nilimjia mke wangu. Akasema: "Kwako wewe." Nikasema: "Nimefanya ulivyoniamuru." Mke wangu alileta mkate, na Nabiy akautia mate yake na kuubariki, kisha akaenda kwenye chungu akatema ndani yake na kukibariki. Kisha akasema: "Muite muokaji aoke pamoja nawe, na toeni mchuzi kwenye chungu, wala msikiinue chungu (motoni)." Wao ni elfu. Naapa kwa Allaah! Walikula mpaka wakakiacha wakaondoka. Chungu chetu kimejaa kama kilivyokuwa, na ngano yetu iko kama mwanzo.

 

 

 

Hadiyth – 31

وعن أنسٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ أَبو طَلْحَةَ لأُمِّ سُلَيمٍ : قَدْ سَمِعْتُ صَوْتَ رسول الله صلى الله عليه وسلم ضَعيفاً أعْرِفُ فيه الجُوعَ ، فَهَلْ عِنْدَكِ مِنْ شَيْءٍ ؟ فَقَالَتْ : نَعَمْ ، فَأخْرَجَتْ أقْرَاصاً مِنْ شَعِيرٍ ، ثُمَّ أخَذَتْ خِمَاراً لَهَا ، فَلَفَّتِ الخُبْزَ بِبَعْضِهِ ، ثُمَّ دَسَّتْهُ تَحْتَ ثَوْبِي وَرَدَّتْنِي بِبَعْضِهِ ، ثُمَّ أرْسَلَتْني إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، فَذَهَبتُ بِهِ ، فَوَجَدْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، جَالِساً في المَسْجِدِ ، وَمَعَهُ النَّاسُ، فَقُمْتُ عَلَيْهمْ، فَقَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أرْسَلَكَ أَبو طَلْحَةَ ؟ )) فقلت : نَعَمْ ، فَقَالَ : (( ألِطَعَامٍ ؟ )) فقلت : نَعَمْ ، فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( قُومُوا )) فَانْطَلَقُوا وَانْطَلَقْتُ بَيْنَ أيْدِيهِمْ حَتَّى جِئْتُ أَبَا طَلْحَةَ فَأخْبَرْتُهُ ، فَقَالَ أَبو طَلْحَةَ : يَا أُمَّ سُلَيْمٍ ، قَدْ جَاءَ رسول الله صلى الله عليه وسلم بالنَّاسِ وَلَيْسَ عِنْدَنَا مَا نُطْعِمُهُمْ ؟ فَقَالَتْ : الله وَرَسُولُهُ أعْلَمُ . فَانْطَلَقَ أَبو طَلْحَةَ حَتَّى لَقِيَ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، فَأقْبَلَ رسول الله صلى الله عليه وسلم مَعَهُ حَتَّى دَخَلاَ ، فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( هَلُمِّي مَا عِنْدَكِ يَا أُمَّ سُلَيْمٍ )) فَأتَتْ بِذلِكَ الخُبْزِ ، فَأمَرَ بِهِ رسول الله صلى الله عليه وسلم فَفُتَّ ، وَعَصَرَتْ عَلَيْهِ أمُّ سُلَيْمٍ عُكّةً فَآدَمَتْهُ، ثُمَّ قَالَ فِيهِ رسول الله صلى الله عليه وسلم مَا شَاءَ اللهُ أنْ يَقُولَ ، ثُمَّ قَالَ : (( ائْذَنْ لِعَشْرَةٍ )) فأذنَ لَهُمْ فَأكَلُوا حتى شَبِعُوا ثُمَّ خَرَجُوا ، ثُمَّ قَالَ : (( ائْذَنْ لِعَشْرَةٍ )) فأذِنَ لهم حَتَّى أكَلَ الْقَوْمُ كُلُّهُمْ وَشَبِعُوا وَالقَوْمُ سَبْعُونَ رَجُلاً أَو ثَمَانُونَ . متفقٌ عَلَيْهِ .

وفي رواية : فَمَا زَالَ يَدْخُلُ عَشرَة ، وَيخرجُ عشرةٌ حَتَّى لَمْ يَبْقَ مِنْهُمْ أحَدٌ إِلاَّ دَخَلَ ، فَأكَلَ حَتَّى شَبعَ ، ثُمَّ هَيَّأهَا فَإذَا هِيَ مِثْلُهَا حِيْنَ أكَلُوا مِنْهَا .

وفي رواية : فَأَكَلُوا عَشرَةً عَشرةً ، حَتَّى فَعَلَ ذَلِكَ بِثَمَانِينَ رَجُلاً ، ثُمَّ أكَلَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم بَعْدَ ذَلِكَ وَأهْلُ البَيْتِ ، وَتَرَكُوا سُؤْراً .

وفي رواية : ثُمَّ أفْضَلُوا مَا بَلَغُوا جيرانَهُمْ .

وفي رواية عن أنس ، قَالَ : جِئتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يوماً ، فَوَجَدْتُهُ جَالِساً مَعَ أصْحَابِه ، وَقَدْ عَصَبَ بَطْنَهُ ، بِعِصَابَةٍ ، فقلتُ لِبَعْضِ أصْحَابِهِ : لِمَ عَصَبَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم بَطْنَهُ ؟ فقالوا : مِنَ الجوعِ ، فَذَهَبْتُ إِلَى أَبي طَلْحَةَ ، وَهُوَ زَوْجُ أُمِّ سُلَيْمٍ بِنْت مِلْحَانَ ، فقلتُ : يَا أبتَاهُ ، قَدْ رَأيْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم  عَصَبَ بَطْنَهُ بِعِصَابَةٍ ، فَسَألْتُ بَعْضَ أصْحَابِهِ ، فقالوا : من الجُوعِ . فَدَخَلَ أَبو طَلْحَةَ عَلَى أُمِّي ، فَقَالَ : هَلْ مِنْ شَيءٍ ؟ قالت : نَعَمْ ، عِنْدِي كِسَرٌ مِنْ خُبْزٍ وَتَمَرَاتٌ ، فَإنْ جَاءنَا رسول الله صلى الله عليه وسلم وَحْدَهُ أشْبَعْنَاهُ ، وَإنْ جَاءَ آخَرُ مَعَهُ قَلَّ عَنْهُمْ ... وَذَكَرَ تَمَامَ الْحَدِيثِ .

Kutoka kwa Anas amesema: Abuu Twalhah alimwambia Ummu Sulaym (Radhwiya Allaahu 'anhaa): "Nimesikia sauti ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni dhaifu, najua ana njaa. Una chochote?" Akasema: "Ndio." Akatoa mikate ya shayiri, kisha akachukua khimaar yake na kufinika mkate kwa sehemu yake, na kuificha ndani ya nguo yangu, kisha akanituma kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) nikaenda nao, nikamkuta Rasuli wa Allaah amekaa Msikitini pamoja na watu. Nilisimama mbele yao, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Umetumwa na Abuu Twalhah?" Nikasema: "Ndio." Akasema: "Je, ni chakula?" Nikasema: "Ndio." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Inukeni" Wakaondoka, nikatembea mbele yao, hadi nikamfikia Abuu Twalhah (Radhwiya Allaahu 'anhu) nilimwarifu yaliyojiri Msikitini. Abuu Twalhah akasema: "Ee Umm Sulaym! Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekuja na watu nasi hatuna cha kuwalisha." Akasema: "Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi." Abuu Twalhah alitoka mpaka akakutana na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye alifuatana na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hadi wakaingia nyumbani. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Ee Umm Sulaym! Lete ulichonacho." Akaleta mikate, Rasuli wa Allaah akaamuru ikakatwa katwa. Umm Sulaym akaitia siagi kwenye chupa kutayarisha mchuzi. Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema alichomjaalia Allaah kusema, kisha akasema: "Waruhusuni watu kumi." Wakaruhusiwa wakala mpaka wakashiba, kisha wakatoka. Kisha akasema: "Waruhusuni watu kumi." Wakaruhusiwa wakala mpaka wakashiba, kisha wakatoka. Kisha akasema: "Waruhusuni watu kumi." Wakaruhusiwa wakala mpaka wakashiba, kisha wakatoka. Na idadi ya watu ilikuwa ni sabiini au themanini. [Al-Bukhaariy na Muslim].

Katika riwaayah: "Hawakuacha kuingia kumi, na kutoka kumi mpaka hakubakia wakamalizika wote yoyote isipokuwa aliingia, akala hadi akashiba. Kisha wakakikusanya kikawa mfano wa kilicholiwa walipoanza kula."

Katika riwaayah: "Wakala watu kumi kumi mpaka wakafika themanini. Kisha akala Nabiy (swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), baadae ahlul bayt, wakaacha mabaki. 

Katika riwaayah: "Kisha kilichobakia kiligawiwa majirani." 

Katika riwaayah ya Anas amesema: "Nilimjia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) siku moja, Nikamkuta amekaa na Swahaba zake, Amefunga tumbo lake kwa mkanda; Nikauliza baadhi ya Swahaba zake: "Kwa nini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amefunga tumbo lake?" Wakasema: "Kutokana na njaa." Nikaenda kwa Abuu Twalhah, mume wa Umm Sulaym bint Milhaan nikamwambia: "Ee babangu! Nimemwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amefunga tumbo lake kwa mkanda, Nikauliza baadhi ya Swahaba zake wakasema: "NI kutokana na njaa." Abuu Twalhah akaingia kwa mamangu, akasema: kumwambia: "Kuna chochote?" Akasema: "Ndio, nina vipande vya mkate na tende. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitujia peke yake tutamshibisha, Akija mwingine pamoja nae kitakuwa kidogo." Akataja Hadiyth kamili.

 

 

 

 

 

Share

057-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukinai, Utohara na Kukusuru Katika Maisha na Kutoa na Uovu Wa Kuomba Bila Ya Dharura

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب القناعة والعَفاف والاقتصاد في المعيشة والإنفاق وذم السؤال من غير ضرورة

57-Mlango Wa Kukinai, Utohara na Kukusuru Katika Maisha na Kutoa na Uovu Wa Kuomba Bila Ya Dharura

 

Alhidaaya.com

 

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَمَا مِن دَابَّةٍ فِي الْأَرْضِ إِلَّا عَلَى اللَّـهِ رِزْقُهَا ﴿٦﴾

Na hakuna kiumbe chochote kitembeacho katika ardhi isipokuwa riziki yake iko kwa Allaah;  [Huwd: 6]

 

لِلْفُقَرَاءِ الَّذِينَ أُحْصِرُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ لَا يَسْتَطِيعُونَ ضَرْبًا فِي الْأَرْضِ يَحْسَبُهُمُ الْجَاهِلُ أَغْنِيَاءَ مِنَ التَّعَفُّفِ تَعْرِفُهُم بِسِيمَاهُمْ لَا يَسْأَلُونَ النَّاسَ إِلْحَافًا ۗ  ﴿٢٧٣﴾

(Swadaqah ni) Kwa ajili ya mafakiri waliozuilika katika njia ya Allaah hawawezi kwenda huku na kule katika ardhi (kutafuta rizki); asiyewajua huwadhania kuwa ni matajiri kutokana na staha ya kujizua kwao, unawatambua kwa alama zao, hawaombi watu kwa ung’ang’anizi. [Al-Baqarah: 273]

 

وَالَّذِينَ إِذَا أَنفَقُوا لَمْ يُسْرِفُوا وَلَمْ يَقْتُرُوا وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا ﴿٦٧﴾

Na wale ambao wanapotoa huwa hawafanyi israfu na wala hawafanyi uchoyo na wanakuwa wastani baina ya hayo. [Al-Furqaan: 67]

 

وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴿٥٦﴾ مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ ﴿٥٧﴾

Na Sikuumba majini na wana Aadam isipokuwa waniabudu. Sitaki kutoka kwao riziki yoyote, na wala Sitaki wanilishe. [Adh-Dhaariyaat: 56-57]

 

 

 

Hadiyth – 1

عن أَبي هريرة رضي الله عنه  ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لَيْسَ الغِنَى عَن كَثرَةِ العَرَض ، وَلكِنَّ الغِنَى غِنَى النَّفْسِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) toka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Utajiri si wingi wa mali, lakini utajiri ni kutosheka katika nafsi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( قَدْ أفْلَحَ مَنْ أسْلَمَ ، وَرُزِقَ كَفَافاً ، وقَنَّعَهُ الله بِمَا آتَاهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika amefanikiwa aliyesilimu na ikawa riziki yake ni yenye kumtosha na akakinaika kwa anachopewa na Allaah." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن حكيم بن حزام رضي الله عنه  ، قَالَ : سألتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم فَأعْطَانِي ، ثُمَّ سَألْتُهُ فَأَعْطَانِي ، ثُمَّ سَألْتُهُ فَأعْطَانِي ، ثُمَّ قَالَ : ((  يَا حَكِيم ، إنَّ هَذَا المَالَ خَضِرٌ حُلْوٌ ، فَمَنْ أخَذَهُ بِسَخَاوَةِ نَفسٍ بُورِكَ لَهُ فِيهِ ، وَمَنْ أخَذَهُ بإشرافِ نَفسٍ لَمْ يُبَارَكْ لَهُ فِيهِ ، وَكَانَ كَالَّذِي يَأكُلُ وَلاَ يَشْبَعُ ، وَاليَدُ الْعُلْيَا خَيْرٌ مِنَ اليَدِ السُّفْلَى )) قَالَ حكيم : فقلتُ : يَا رسول الله ، وَالَّذِي بَعَثَكَ بِالحَقِّ لاَ أرْزَأُ أحَداً بَعْدَكَ شَيْئاً حَتَّى أُفَارِقَ الدُّنْيَا ، فَكَانَ أَبُو بَكْرٍ رضي الله عنه يَدْعُو حَكيماً لِيُعْطِيَه العَطَاء ، فَيَأبَى أنْ يَقْبَلَ مِنْهُ شَيْئاً ، ثُمَّ إنَّ عُمَرَ رضي الله عنه  دَعَاهُ لِيُعْطِيَه فَأَبَى أنْ يَقْبَلَهُ . فقالَ : يَا مَعْشَرَ المُسْلِمِينَ ، أُشْهِدُكُمْ عَلَى حَكيمٍ أنّي أعْرِضُ عَلَيْهِ حَقَّهُ الَّذِي قَسَمَهُ اللهُ لَهُ في هَذَا الفَيء فَيَأبَى أنْ يَأخُذَهُ . فَلَمْ يَرْزَأْ حَكيمٌ أحَداً مِنَ النَّاسِ بَعْدَ النبي صلى الله عليه وسلم حَتَّى تُوُفِّي . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Hakiym bin Hizaam (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nilimuomba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye akanipatia, kisha nikamwuomba mara nyengine, naye akanipa. Kisha nikamuomba tena naye akanipatia. Hapo akaniambia: "Ee Hakiym! Hakika hii mali ni kijani na ni tamu. Mwenye kuichukua kwa nafsi ya upaji atabarikiwa, na mwenye kuichukua kutaka nayo utukufu hatabarikiwa. Naye anakuwa mfano wa mlaji asiyeshiba. Na mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini." Akasema Hakiym (Radhwiya Allaahu 'anhu) nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Naapa kwa aliyekutuma kwa haki, sitamuomba yeyote mpaka nitakapoaga dunia." Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikuwa akimuiita Hakiym ampe, anakataa kupokea. Kisha "Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) alimuiita ampe akakataa kupokea. 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) alisema: "Enyi kongamano la Waislamu! Shuhudieni kuwa juu ya Hakiym kuwa nilimpa haki yake aliyomgawia Allaah katika ngawira amekataa kuichukua." Hivyo Hakiym hakumuomba yoyote baada ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka amekufa." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasaai]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي بردة ، عن أَبي موسى الأشعري رضي الله عنه ، قَالَ : خَرَجْنَا مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم في غَزاةٍ وَنَحْنُ سِتَّةُ نَفَرٍ بَيْنَنَا بَعِيرٌ نَعْتَقِبُهُ ، فَنقِبَت أقدَامُنَا وَنَقِبَت قَدَمِي ، وسَقَطت أظْفَاري ، فَكُنَّا نَلُفُّ عَلَى أرْجُلِنا الخِرَقَ ، فَسُمِّيَت غَزْوَةَ ذَاتِ الرِّقَاعِ لِمَا كُنَّا نَعْصِبُ عَلَى أرْجُلِنَا مِنَ الخِرَقِ ، قَالَ أَبُو بُردَة : فَحَدَّثَ أَبُو مُوسَى بِهَذَا الحَدِيثِ ، ثُمَّ كَرِه ذَلِكَ ، وقال : مَا كُنْتُ أصْنَعُ بِأنْ أذْكُرَهُ ! قَالَ : كأنَّهُ كَرِهَ أنْ يَكُونَ شَيْئاً مِنْ عَمَلِهِ أفْشَاهُ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Burdah kwa Abuu Muwsaa Al-'Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa: Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuelekea vitani, tulikuwa watu sita tukipanda ngamia mmoja kwa zamu. Nyayo zetu zilipasuka, miguu yangu ikapasuka kucha zangu za miguu zikatoka. Ili kufunika majeraha, tulifunga miguu yetu matambara, kwa hiyo vikaitwa Dhaatur Riqaai, kwa sababu ya kufunga matambara miguuni mwetu. Akasema Abuu Burdah: "Abuu Muwsaa alihadithia kisa hiki kisha akachukia hilo, akasema: Sikufanya hilo ilinikumbukwe." Akasema: "Kana kwamba amechukia kufichua matendo yake (ya Jihaad) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن عمرو بن تَغْلِبَ – بفتح التاء المثناة فوق وإسكان الغين المعجمة وكسر اللام - رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم أُتِي بِمالٍ أَوْ سَبْيٍ فَقَسَّمَهُ ، فَأعْطَى رِجَالاً ، وَتَرَكَ رِجَالاً ، فَبَلغَهُ أنَّ الَّذِينَ تَرَكَ عَتَبُوا ، فَحَمِدَ اللهَ ، ثُمَّ أثْنَى عَلَيْهِ ، ثُمَّ قَالَ :     ((  أمَّا بعْدُ ، فَواللهِ إنِّي لأُعْطِي الرَّجُلَ وَأدَعُ الرَّجُلَ ، وَالَّذِي أدَعُ أحَبُّ إلَيَّ مِنَ الَّذِي أُعْطِي ، وَلَكِنِّي إنَّمَا أُعْطِي أقْوَاماً لِمَا أرَى في قُلُوبِهِمْ مِنَ الجَزَعِ وَالهَلَعِ ، وَأكِلُ أقْوَاماً إِلَى مَا جَعَلَ اللهُ في قُلُوبِهم مِنَ الغِنَى وَالخَيْرِ ، مِنْهُمْ عَمْرُو بنُ    تَغْلِبَ )) قَالَ عَمْرُو بنُ تَغْلِبَ : فَوَاللهِ مَا أُحِبُّ أنَّ لِي بِكَلِمَةِ رسول الله صلى الله عليه وسلم حُمْرَ النَّعَم . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa 'Amruw bin Taghlib (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba aliletewa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mali au ngawira akaigawa. Aliwapa baadhi ya watu na kuwaacha wengine. Ikamfikia kwamba ambao amewaacha wamelalamika, Basi Akamhimidi Allaah, Akamsifu, kisha akasema: "Amma Ba'ad, Wa-Allaahi! Mimi nampa mtu na namuacha mwingine, ninayemnyima nampenda zaidi kuliko ninayempa. Ninawapa watu niwaonao mioyoni mwao babaiko na papara, na wengine nawaegemeza kwenye majaliwa ya Allaah mioyoni mwao, ukwasi na kheri, miongoni mwao ni 'Amruw bin Taghlib." Akasema 'Amruw bin Taghlib (Radhwiya Allaahu 'anhu) : "Naapa kwa Allaah! Sipendi mbadala wa maneno ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hata kwa ngamia wekundu, (ambao walikuwa wakithaminiwa sana na Waarabu)." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 6

وعن حكيم بن حزام رضي الله عنه : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  اليَدُ العُلْيَا خَيْرٌ مِنَ اليَدِ السُّفْلَى ، وَابْدَأْ بِمَنْ تَعُولُ ، وَخَيْرُ الصَّدَقَةِ مَا كَانَ عَنْ ظَهْرِ غِنىً ، وَمَنْ يَسْتَعْفِفْ يُعِفُّهُ الله ، وَمَنْ يَسْتَغْنِ يُغنهِ الله )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Hakiym bin Hizaam: Kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini, anza kwa wanaokutegemea. Na bora ya swadaqah ni ilio nje ya kujitosha, Mwenye kujichunga Allaah atamwezesha. Na Mwenye kujitosha Allaah atamtosha." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي عبد الرحمان معاوية بن أبي سفيان رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تُلْحِفُوا في الْمَسْأَلَةِ ، فَوَاللهِ لاَ يَسْأَلُنِي أَحَدٌ مِنْكُمْ شَيْئاً ، فَتُخْرِجَ لَهُ مَسْأَلَتُهُ مِنِّي شَيْئاً وَأنَا لَهُ كَارهٌ ، فَيُبَارَكَ لَهُ فِيمَا أعْطَيْتُهُ )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Sufyaan |Swakhr bin Harb (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msing'ang'anie katika kuuliza. Wa-Allaahi! Haniombi miongoni mwenu chochote, na nikampatia hicho alichoomba nami nachukia habarikiwi katika nilichompa." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي عبدِ الرحمان عوف بن مالِك الأَشْجَعِيِّ رضي الله عنه ، قَالَ : كُنَّا عِنْدَ رسول الله صلى الله عليه وسلم تِسْعَةً أَوْ ثَمَانِيَةً أَوْ سَبْعَةً ، فَقَالَ : ((  ألاَ تُبَايِعُونَ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم )) وَكُنَّا حَديثِي عَهْدٍ ببَيْعَةٍ ، فَقُلْنَا : قَدْ بَايَعْنَاكَ يَا رسولَ اللهِ ، ثمَّ قالَ : (( ألا تُبَايِعُونَ رسولَ اللهِ )) فَبَسَطْنا أيْدينا ، وقلنا : قدْ بايعناكَ فَعَلامَ نُبَايِعُكَ ؟ قَالَ : ((  عَلَى أنْ تَعْبُدُوا اللهَ وَلاَ تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئاً ، وَالصَّلَوَاتِ الخَمْسِ وَتُطِيعُوا الله )) وأَسَرَّ كَلِمَةً خَفِيفَةً ((  وَلاَ تَسْألُوا النَّاسَ شَيْئاً )) فَلَقَدْ رَأيْتُ بَعْضَ أُولئِكَ النَّفَرِ يَسْقُطُ سَوطُ أحَدِهِمْ فَمَا يَسأَلُ أحَداً يُنَاوِلُهُ إيّاهُ . رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwake Abuu 'Abdir-Rahmaan 'Awf bin Maalik Al-Ashja'iy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kuwa: Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah watu wa tisa au nane au saba, akasema: "Kwa nini hamum-bai' Rasuli wa Allaah? Tukanyoosha mikono yetu tukasema: Tumekubali (Bay'ah) ee Rasuli wa Allaah? Je, tukuba'i juu ya nini?" Akasema: "Juu ya kumuabudu Allaah wa msimshirikishe na chochote, na Swalaah tano, hafifu: (taratibu): "Wala msiwaombe watu chochote." Hakika nimeona baadhi ya watu hao hata akaiangukwa na kikoto (kiboko), haombi yoyote kumuokotea." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

وعن ابن عمر رضي الله عنهما: أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: (( لاَ تَزَالُ الْمَسْأَلةُ بأَحَدِكُمْ حَتَّى يَلْقَى الله تَعَالَى وَلَيْسَ في وَجْهِهِ مُزْعَةُ لَحْمٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Itabaki kuomba kwa mmoja wenu hadi atakapokutana na Allaah Ta'aalaa na hana katika uso wake kipande cha nyama." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai]

 

 

Hadiyth – 10

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ وَهُوَ عَلَى المِنْبَرِ ، وَذَكَرَ الصَّدَقَةَ وَالتَّعَفُّفَ عَنِ الْمَسْأَلَةِ : ((  اليَدُ العُلْيَا خَيْرٌ مِنَ اليَدِ السُّفْلَى ، وَاليَدُ العُلْيَا هِيَ المُنْفِقَةُ ، وَالسُّفْلَى هِيَ السَّائِلَةُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alizungumza kuhusu swadaqah na kutoomba akiwa juu ya minbar na akasema: "Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini. Mkono wa juu ni wenye kutoa na wa chini ni wenye kuomba." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ سَألَ النَّاسَ تَكَثُّراً فإنَّمَا يَسْألُ جَمْراً ؛ فَلْيَسْتَقِلَّ أَوْ لِيَسْتَكْثِرْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuomba watu ili mali yake iongezeke, hakika yeye anaomba kaa la moto. Hivyo ni juu yake ima kupunguza au kuongeza." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 12

وعن سَمُرَةَ بنِ جُنْدبٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّ المَسْأَلَةَ كَدٌّ يَكُدُّ بِهَا الرَّجُلُ وَجْهَهُ ، إِلاَّ أنْ يَسْأَلَ الرَّجُلُ سُلْطاناً أَوْ في أمْرٍ لاَ بُدَّ مِنْهُ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwake Samurah bin Jundub (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika kuomba inamjeruhi mtu uso wake isipokuwa anapomuomba mtu sultani au kwa jambo ambalo hapana budi (ila kuomba)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 13

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ أصَابَتْهُ فَاقَةٌ فَأنْزَلَهَا بالنَّاسِ لَمْ تُسَدَّ فَاقَتُهُ ، وَمَنْ أنْزَلَهَا باللهِ ، فَيُوشِكُ اللهُ لَهُ بِرِزْقٍ عَاجِلٍ أَوْ آجِلٍ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote mwenye kupatwa na shida (kama njaa na ufakiri), kisha akaipeleka kwa watu ili wamsaidie, shida yake hiyo haitaondoka (kutaka uasidizi) kwa Allaah basi ataondoshewa na Allaah kwa haraka na kupatiwa riziki kwa wakati wa karibu au baadae." [Abuu Daawud na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 14

وعن ثوبان رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ تَكَفَّلَ لِي أنْ لاَ يَسْأَلَ النَّاسَ شَيْئاً ، وَأتَكَفَّلُ لَهُ بِالْجَنَّةِ ؟ )) فقلتُ : أنَا ، فَكَانَ لاَ يَسْأَلُ أحَداً شَيْئاً . رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .

Imepokewa kutoka kwake Thawbaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote atakaye nidhaminia kwamba hatamuuliza (kuomba) mtu yeyote kwa kitu chochote basi kwake nitamdhaminia Pepo. Nikasema: 'MImi.' Baada ya hapo hakumuomba (yaani Thawbaan) mtu yoyote kitu chochote." [Abuu Daawud kwa Isnaad iliyo Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 15

وعن أَبي بِشْرٍ قَبيصَةَ بنِ المُخَارِقِ رضي الله عنه ، قَالَ : تَحَمَّلْتُ حَمَالَةً فَأتَيْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم أسْأَلُهُ فِيهَا ، فَقَالَ : ((  أقِمْ حَتَّى تَأتِيَنَا الصَّدَقَةُ فَنَأمُرَ لَكَ بِهَا )) ثُمَّ قَالَ : ((  يَا قَبيصةُ ، إنَّ المَسْأَلَةَ لاَ تَحِلُّ إِلاَّ لأَحَدِ ثلاثَةٍ : رَجُلٌ تحمَّلَ حَمَالَةً ، فَحَلَّتْ لَهُ المَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَها ، ثُمَّ يُمْسِكُ ، وَرَجُلٌ أصَابَتْهُ جَائِحَةٌ اجْتَاحَتْ   مَالَهُ ، فَحَلَّتْ لَهُ الْمَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَ قواماً مِنْ عَيش - أَوْ قَالَ : سِدَاداً مِنْ عَيْشٍ - وَرَجُلٌ أصَابَتْهُ فَاقَةٌ ، حَتَّى يَقُولَ ثَلاَثَةٌ مِنْ ذَوِي الحِجَى مِنْ قَوْمِه : لَقَدْ أصَابَتْ فُلاناً فَاقَةٌ . فَحلَّتْ لَهُ الْمَسْأَلَةُ حَتَّى يصيب قواماً من عيش ، أَوْ قَالَ : سداداً من عيشِ ، فما سِوَاهُنَّ مِنَ المسألَةِ يَا قَبِيصَةُ سُحْتٌ ، يَأكُلُهَا صَاحِبُهَا سُحْتاً )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Bishr Qabiyswah bin Al-Mukhaariq amesema: Nilibeba dhamana ya fidia ya mauaji. Nilimwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kumuulizia hilo. Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ngojea mpaka itujie swadaqah tutakuamrishia chochote." Kisha akasema: "Ee Qabiyswah! Hakika kuomba si halali ila kwa moja ya matatu: Mtu anayedaiwa, ni halali kwake kuomba hadi alipate, kisha ajizuie; Na mtu amepata maafa mali yake ikaharibika ni halali kwake kuomba mpaka apate msimamo katika maisha- au alisema:' "Kukidhi maisha." Na mtu amepata ufukara, mpaka waseme watu watatu wenye akili katika watu wake: 'fulani amepata njaa.' Ni halali kwake kuomba mpaka apate msimamo wa maisha au alisema, "Kukidhi maisha." Wasiokuwa hawa kuomba ee Qabiyswah ni haramu, anaekula anakula haramu." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 16

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لَيْسَ المسكينُ الَّذِي يَطُوفُ عَلَى النَّاسِ تَرُدُّهُ اللُّقْمَةُ وَاللُّقْمَتَانِ ، وَالتَّمْرَةُ وَالتَّمْرَتَانِ ، وَلكِنَّ المِسكينَ الَّذِي لاَ يَجِدُ غِنىً يُغْنِيهِ ، وَلاَ يُفْطَنُ لَهُ فَيُتَصَدَّقُ عَلَيْهِ ، وَلاَ يَقُومُ فَيَسْألَ النَّاسَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Masikini si yule anaeranda kwa watu anarudishwa kwa tonge moja au mbili, tende moja na tende mbili, Ila masikini ni asiyepata cha kumtosheleza wala hakuna anayemjua ili ampe swadaqah, wala hasimami kuomba watu." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

 

 

Share

058-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ruhusu ya Kuchukua Kitu Bila Kuomba

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب جواز الأخذ من غير مسألة وَلاَ تطلع إليه

058-Mlango Wa Ruhusu ya Kuchukua Kitu Bila Kuomba

 

Alhidaaya.com

 

 

عن سالم بن عبد الله بن عمر ، عن أبيه عبد الله بن عمر ، عن عمر رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يُعْطيني العَطَاءَ ، فَأقُولُ : أعطِهِ مَنْ هُوَ أفْقَرُ إِلَيْهِ  مِنّي . فَقَالَ : ((  خُذْهُ ، إِذَا جَاءكَ مِنْ هَذَا المَال شَيْءٌ وَأنْتَ غَيْرُ مُشْرِفٍ وَلاَ   سَائِلٍ ، فَخُذْهُ فَتَمَوَّلْهُ ، فَإنْ شِئْتَ كُلْهُ ، وَإنْ شِئْتَ تَصَدَّقْ بِهِ ، وَمَا لا ، فَلاَ تُتبعهُ نَفْسَكَ )) قَالَ سَالِمٌ : فَكَانَ عَبدُ الله لاَ يَسألُ أحَداً شَيْئاً ، وَلاَ يَرُدُّ شَيْئاً    أُعْطِيَه . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Saalim bin 'Abdillaah bin 'Umar kutoka kwa babake 'Abdillaah bin 'Umar kutoka kwa 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: "Rasuli wa Alllaah (Swallla Alllahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akinipatia vitu (zawadi), nami nilikuwa nasema, 'Mpatie aliye fukara kuliko mimi.' Akasema: 'Chukua ikiwa utapewa katika mali hii kitu chochote bila ya wewe kutamani wala kuuliza (kuomba). Ichukue na uitie katika rasilimali au ukitaka itumie na ukitaka unaweza kuitoa swadaqah. Usitamani kupata kitu kwa njia nyengine.' Amesema Saalim: 'Alikuwa 'Abdillaah (yaani babake) hamuulizi (hamuombi) yeyeote kitu chochote wala harudishi kitu alichopatiwa'." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

059-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuhimizwa Kula Kwa Kazi ya Mkono Wake na Kujizuilia Kuomba na Kupenda Kutoa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الحث عَلَى الأكل من عمل يده والتعفف به عن السؤال والتعرض للإعطاء

059-Mlango Wa Kuhimizwa Kula Kwa Kazi ya Mkono Wake na Kujizuilia Kuomba na Kupenda Kutoa

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ ﴿١٠﴾

Na inapomalizika Swalaah, tawanyikeni katika ardhi, na tafuteni katika fadhila za Allaah, [Al-Jumua'ah: 10]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي عبد الله الزبير بن العَوَّام رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  :   ((  لأَنْ يَأخُذَ أحَدُكُمْ أحبُلَهُ ثُمَّ يَأتِيَ الجَبَلَ ، فَيَأْتِيَ بحُزمَةٍ مِنْ حَطَب عَلَى ظَهْرِهِ فَيَبِيعَهَا ، فَيكُفّ اللهُ بِهَا وَجْهَهُ ، خَيْرٌ لَهُ مِنْ أنْ يَسْألَ النَّاسَ ، أعْطَوْهُ أَوْ مَنَعُوهُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abuu 'Abdillaah Az-Zubaiyr bin Al-Awwaam (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mmoja wenu kuchukuwa kamba na kisha akaenda mlimani, akaja na mzigo wa kuni na kuziuza, Allaah akakinga uso wake, ni bora kwake kuliko kuomba watu, ima wampe au wamnyime." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  لأَنْ يَحْتَطِبَ أحَدُكُمْ حُزْمَةً عَلَى ظَهْرِهِ ، خَيْرٌ لَهُ مِنْ أنْ يَسْألَ أحداً ، فَيُعْطِيَهُ أَوْ يَمْنَعَهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mmoja wenukubeba mzigo wa kuni mgongoni mwake ni bora kwake kuliko kuomba yoyote, ampe au amnyime." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaai na Maalik]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  كَانَ دَاوُدُ عَلَيْهِ السَّلام لا يَأكُلُ إِلاَّ مِنْ عَمَلِ يَدِهِ )) رواه البخاري.

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Alikuwa Daawuud ('Alayhis sallaam) hali isipokuwa kwa chumo la mkono wake." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  كَانَ زَكرِيّا عَلَيْهِ السَّلام نَجَّاراً )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayni wa aalihi wa sallam) amesema: "Zakariyyaa ('Alayhi salaam) alikuwa ni seremala (akiendesha maisha yake kwa kufanya kazi hiyo)." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن المقدام بنِ مَعْدِ يكرِبَ رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم  ، قَالَ : ((  مَا أكَلَ أَحَدٌ طَعَاماً قَطُّ خَيْراً مِنْ أنْ يَأكُلَ مِنْ عَمَلِ يَدِه ، وَإنَّ نَبيَّ الله دَاوُدَ عَلَيْهِ السَّلام كَانَ يَأكُلُ مِنْ عَمَلِ يَدِهِ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Al-Miqdaam bin Ma'diykarib kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hajakula mmoja wenu chakula bora zaidi kuliko kile anachokula kwa kufanya juhudi kwa kutumia mikono yake. Na hakika Nabiy wa Allaah Daawuud alikuwa akila chakula anachopata kwa miono yake." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Share

060-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ukarimu na Kutoa Katika Njia za Kheri na Kuwa na Imani Kwa Allaah Ta'aalaa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير ثقةً بالله تعالى

060-Mlango Wa Ukarimu na Kutoa Katika Njia za Kheri na Kuwa na Imani Kwa Allaah Ta'aalaa

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ  ﴿٣٩﴾

Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa,. [Sabaa: 39]

 

 

وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَلِأَنفُسِكُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ اللَّـهِ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٢﴾

Na chochote cha khayr mtoacho basi ni kwa ajili ya nafsi zenu. Na hamtoi ila kutaka Wajhi wa Allaah. Na chochote mtoacho katika khayr mtalipwa kamilifu nanyi hamtodhulumiwa.

 

 لِلْفُ ۗ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣﴾

Na chochote mtoacho katika khayr basi Allaah kwacho ni Mjuzi. [Al-Baqarah: 272-273]

 

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لا حَسَدَ إِلاَّ في اثْنَتَيْنِ : رَجُلٌ آتَاهُ اللهُ مَالاً ، فَسَلَّطَهُ عَلَى هَلَكَتِهِ في الحَقّ ، وَرَجُلٌ آتَاهُ اللهُ   حِكْمَةً ، فَهُوَ يَقْضِي بِهَا ويُعَلِّمُهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uuwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa; Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana husuda ila katika mawili: Mtu Allaah amempa mali, akamsalitisha katika kuimaliza katika haki. Na Allaah amempa mtu hekima, anahukumu nayo na anawaelimisha wengine." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  أيُّكُم مَالُ وَارِثِهِ أحبُّ إِلَيْهِ مِنْ    مَالِهِ ؟ )) قالوا : يَا رسول اللهِ ، مَا مِنَّا أحَدٌ إِلاَّ مَالُهُ أحَبُّ إِلَيْهِ . قَالَ : ((  فإنَّ مَالَهُ مَا قَدَّمَ وَمَالَ وَارِثِهِ مَا أخَّرَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uuwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ni mtu gani miongoni mwenu ambaye anaipenda zaidi mali ya warithi wake kuliko mali yake mwenyewe?" Tukasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakuna miongoni mwetu isipokuwa anaipenda mali yake zaidi." Akasema: "Hakika mali yake ni ile aliyoitanguliza na mali aliyoibakisha ni ya warithi wake." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 3

وعن عَدِيِّ بن حَاتِمٍ رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  اتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بِشِقِّ تَمْرَةٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: "Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ""Ogopeni Moto ijapo kwa kipande cha tende moja." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن جابرٍ رضي الله عنه ، قَالَ : مَا سُئِلَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  شَيْئاً قَطُّ ، فقالَ : لاَ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwahi kuombwa kitu chochote mara zote, akasema: hapana." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَا مِنْ يَوْمٍ يُصبحُ العِبَادُ فِيهِ إِلاَّ مَلَكَانِ يَنْزلانِ ، فَيَقُولُ أحَدُهُمَا : اللَّهُمَّ أعْطِ مُنْفِقاً خَلَفاً ، وَيَقُولُ الآخَرُ : اللَّهُمَّ أعْطِ مُمْسِكاً تَلَفاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna siku yoyote inayopambazuka kwa waja isipokuwa Malaika wawili huteremka, mmoja wao anasema: 'Ee Mola! Mrudishie mwenye kutoa (kila anachotoa kwa wingi)'. Na mwengine naye anasema: 'Ee Mola! Mharibie mwenye kuzuia (vitu vyake)'. [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  قَالَ الله تَعَالَى : أنفِق يَا ابْنَ آدَمَ يُنْفَقْ عَلَيْكَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa tena kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Amesema Allaah Ta'aalaa: "Ee mwanadamu toa (katika njia ya Allaah) na Allaah atakupatia." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن عبد اللهِ بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ رَجُلاً سَألَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : أيُّ الإسلامِ خَيْرٌ ؟ قَالَ : ((  تُطْعِمُ الطَّعَامَ ، وَتَقْرَأُ السَّلاَمَ عَلَى مَنْ عَرَفْتَ وَمَنْ لَمْ تَعْرِفْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba kuna mtu mmoja aliyemuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni Uislamu gani ulio bora?" Akasema: "Kulisha watu chakula na kuwatolea salamu unaowajua na usiowajua." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن عبد اللهِ بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  أرْبَعُونَ خَصْلَةً : أعْلاهَا مَنِيحةُ العَنْزِ ، مَا مِنْ عَامِلٍ يَعْمَلُ بخَصْلَةٍ مِنْهَا ؛ رَجَاءَ ثَوَابهَا وَتَصْدِيقَ مَوْعُودِهَا ، إِلاَّ أدْخَلَهُ الله تَعَالَى بِهَا الجَنَّةَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amruu bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Sampuli arobaini za wema, ya juu kabisa ni kumwazima mtu ngamia (jike) wa maziwa ili apate maziwa (kisha amrudishie mwenyewe). Hakuna mfanyaji ambaye atafanya amali yeyote katika hizi akitarajia thawabu zake na kuswadikisha ile ahadi (aliyoahidiwa) isipokuwa Allaah humuingiza kwayo Peponi." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي أُمَامَة صُدّيِّ بن عَجْلانَ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم :  ((  يَا ابْنَ آدَمَ ، إنَّكَ أن تَبْذُلَ الفَضلَ خَيْرٌ لَكَ ، وَأن تُمْسِكَه شَرٌّ لَكَ ، وَلاَ تُلاَمُ عَلَى كَفَافٍ ، وَابْدَأْ بِمَنْ تَعُولُ ، وَاليَدُ الْعُلْيَا خَيْرٌ مِنَ الْيَدِ السُّفْلَى )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Umamah Sudayyi bin 'Ajlaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee mwanadamu! Hakika lau utatafutia fadhila (hela) za zaidi itakuwa bora kwako, na kuzuilia (kutotumia) ni shari kwako. Hutalaumiwa kuwa na hela kwa kadiri ya mahitaji yako. Na anza kuitumia kwa wale wenye haki kwako." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أنسٍ رضي الله عنه  ، قَالَ : مَا سُئِلَ رسول الله صلى الله عليه وسلم عَلَى الإسْلاَمِ شَيْئاً إِلاَّ أعْطَاهُ ، وَلَقَدْ جَاءهُ رَجُلٌ ، فَأعْطَاهُ غَنَماً بَيْنَ جَبَلَيْنِ ، فَرجَعَ إِلَى قَوْمِهِ ، فَقَالَ : يَا قَوْمِ ، أسْلِمُوا فإِنَّ مُحَمَّداً يُعطِي عَطَاءَ مَن لا يَخْشَى الفَقْر ، وَإنْ كَانَ الرَّجُلُ لَيُسْلِمُ مَا يُريدُ إِلاَّ الدُّنْيَا ، فَمَا يَلْبَثُ إِلاَّ يَسِيراً حَتَّى يَكُونَ الإسْلاَمُ أحَبَّ إِلَيْهِ مِنَ الدُّنْيَا وَمَا عَلَيْهَا . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Alikuwa katika Uislamu hakuombwa chochote Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isipokuwa alimpatia. Na hakika alikuja mtu, naye akampatia mbuzi wengi sana waliojaa baina ya majabali mawili. Huyu mtu aliporudi kwa watu wake aliwaambia: "Enyi watu wangu kuweni Waislamu kwani Muhammad hutoa aina ya utoaji ambao haogopi ufakiri." Japokuwa mtu alikuwa akisilimu kwa sababu ya pato la kidunia, lakini baada ya muda mchache, Uislamu unakuwa ni mwenye kupendwa zaidi na yeye kuliko dunia na vilivyomo ndani yake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 11

وعن عمر رضي الله عنه ، قَالَ : قسم رسول الله صلى الله عليه وسلم قَسْماً ، فَقُلْتُ :يَا رسولَ الله ، لَغَيْرُ هؤلاَءِ كَانُوا أحَقَّ بِهِ مِنْهُمْ ؟ فَقَالَ : ((  إنَّهُمْ خَيرُونِي أنْ يَسألُوني بالفُحْشِ ، أَوْ يُبَخِّلُونِي ، وَلَسْتُ بِبَاخِلٍ )) رواه مسلم

Imepokewa kutoka kwa 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aligawanya mali nami nikamwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Mbali na hawa kuna watu wenye haki zaidi ya kupatiwa kuliko hawa." Akasema: "Hakika wao wamenipatia uchaguzi (kutumia uamuzi wangu). Hivyo, wanatakiwa ima waniombe waziwazi, nami nitawapatia au waninasibishe na ubakhili, na mimi si bakhili." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 12

وعن جبير بن مطعم رضي الله عنه  ، قَالَ : بَيْنَمَا هُوَ يَسِيرُ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم مَقْفَلَهُ مِنْ حُنَيْن ، فَعَلِقَهُ الأعْرَابُ يَسْألُونَهُ ، حَتَّى اضْطَرُّوهُ إِلَى سَمُرَة ، فَخَطِفَت رِدَاءهُ ، فَوَقَفَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم ، فقال : ((  أعْطُوني رِدَائي ، فَلَوْ كَانَ لِي عَدَدُ هذِهِ العِضَاهِ نَعَماً ، لَقَسَمْتُهُ بَينَكُمْ ، ثُمَّ لا تَجِدُونِي بَخِيلاً وَلاَ كَذّاباً وَلاَ جَبَاناً )) رواه البخاري

Imepokewa kutoka kwa Jubaiyr bin Mutw'im (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Baada ya vita vya Hunaiyn tulikuwa tunarudi na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), baadhi ya Mabedui walimzunguka alipokuwa chini ya mti wakitaka kupatiwa fungu lao (katika ngawira) na mmoja wao akachukua shuka yake. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasimama akasema: "Nipatieni shuka yangu; lau ningekuwa na neema nyingi sawa na idadi ya majani katika huu mchongoma ningewagawia baina yenu na hamungeniona mimi kuwa bakhili wala muongo wala mwoga?" [Al-Bukhaariy] 

 

 

Hadiyth – 13

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَا نَقَصَتْ صَدَقَةٌ مِنْ مَال ، وَمَا زَادَ اللهُ عَبْداً بِعَفْوٍ إِلاَّ عِزّاً ، وَمَا تَواضَعَ أحَدٌ لله إِلاَّ رَفَعَهُ اللهُ عزوجل )) رواه مسلم .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swadaqah haipunguzi mali; na Allaah anamuongezea utukufu mwenye kusamehe. Na hakuna anayenyenyekea kwa ajili ya Allaah Ta'aalaa isipokuwa humnyanyua daraja yake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 14

وعن أَبي كبشة عمرو بن سعد الأنماري رضي الله عنه: أنّه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  ثَلاَثَةٌ أُقْسمُ عَلَيْهِنَّ ، وَأُحَدِّثُكُمْ حَدِيثاً فَاحْفَظُوهُ : مَا نَقَصَ مَالُ عَبْدٍ مِنْ صَدَقَةٍ ، وَلاَ ظُلِمَ عَبْدٌ مَظْلَمَةً صَبَرَ عَلَيْهَا إِلاَّ زَادَهُ اللهُ عِزّاً ، وَلاَ فَتَحَ عَبْدٌ بَابَ مَسألَةٍ إِلاَّ فَتَحَ اللهُ عَلَيْهِ بَابَ فَقرٍ - أَوْ كَلِمَةً نَحْوَهَا - وَأُحَدِّثُكُمْ حَديثاً فَاحْفَظُوهُ، قَالَ : ((  إنَّمَا الدُّنْيَا لأرْبَعَةِ نَفَرٍ : عَبْدٍ رَزَقَهُ اللهُ مَالاً وَعِلماً ، فَهُوَ يَتَّقِي فِيهِ رَبَّهُ ، وَيَصِلُ فِيهِ رَحِمَهُ، وَيَعْلَمُ للهِ فِيهِ حَقَّاً ، فَهذا بأفضَلِ المَنَازِلِ . وَعَبْدٍ رَزَقهُ اللهُ عِلْماً، وَلَمْ يَرْزُقْهُ مَالاً ، فَهُوَ صَادِقُ النِّيَّةِ ، يَقُولُ : لَوْ أنَّ لِي مَالاً لَعَمِلتُ بِعَمَلِ فُلانٍ ، فَهُوَ بنيَّتِهِ ، فأجْرُهُمَا سَوَاءٌ . وَعَبْدٍ رَزَقَهُ الله مَالاً ، وَلَمَ يَرْزُقْهُ عِلْماً ، فَهُوَ يَخبطُ في مَالِهِ بغَيرِ عِلْمٍ ، لاَ يَتَّقِي فِيهِ رَبَّهُ ، وَلاَ يَصِلُ فِيهِ رَحِمَهُ ، وَلاَ يَعْلَمُ للهِ فِيهِ حَقّاً ، فَهذَا بأَخْبَثِ المَنَازِلِ . وَعَبْدٍ لَمْ يَرْزُقْهُ اللهُ مَالاً وَلاَ عِلْماً ، فَهُوَ يَقُولُ : لَوْ أنَّ لِي مَالاً لَعَمِلْتُ فِيهِ بعَمَلِ فُلاَنٍ ، فَهُوَ بنِيَّتِهِ ، فَوِزْرُهُمَا سَوَاءٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Kutoka kwa Abuu Kabshah 'Amar bin Sa'd Al-Anmaariy amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Matatu naapa juu yake na nakuwahadithieni hadiyth ihifadhini: Mali ya mja haipapungui kwa swadaqah, wala mja hakudhulumiwa chochote akasubiri ila Allaah humzidisha utukufu, na hatafungua mja mlango wa kuomba isipokuwa  Allaah humfungulia mlango wa ufukara, au neno mfano wake." na ninakuhadithieni hadiyth ihifadhini, akasema: "Hakika dunia ni kwa watu wanne: Mja Allaah amempa mali na elimu naye akamcha Mola ndani yake, akaunganisha ndani yake kizazi, na akajua ndani yake haki ya Allaah, huyu ni daraja bora, na cheo bora; na mja aliyepatiwa na Allaah elimu bila kupewa mali, naye akawa na nia ya kweli, akasema: 'Lau kama ningekuwa na mali ningefanya amali ya fulani', yeye atakuwa katika hiyo nia yake na ujira wa wote wawili ni sawa; na mja aliyepewa na Allaah mali lakini hakuruzukiwa elimu, nae anaifuja mali yake pasi na elimu. Yeye hamchi Rabb wake kwayo na wala haungi kizazi na wala hajui haki za Allaah juu yake, huyu atakuwa katika daraja ya chini kabisa; na mja ambaye hakuruzukiwa na Allaah mali wala elimu, naye akawa anasema: 'Kwa hakika lau kama ningekuwa na mali ningefanya amali ya fulani (amali ya mtu wa tatu).' Hiyo ianpokuwa ndio nia yake, wote watakuwa na madhambi sawa." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh] 

 

 

Hadiyth – 15

وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّهُمْ ذَبَحُوا شَاةً ، فَقَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم  :  ((  مَا بَقِيَ مِنْهَا ؟ )) قالت : مَا بَقِيَ مِنْهَا إِلاَّ كَتِفُها . قَالَ : ((  بَقِيَ كُلُّهَا غَيْرُ   كَتِفِهَا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa wao walichinja mbuzi, (wakaigawa) kisha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuuliza: "Imebaki nyama kiasi gani?" Alijibu: "Haikubaki isipokuwa mkono wake." Akasema: "Imebaki nyama yote ila mkono." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 16

وعن أسماء بنت أَبي بكرٍ الصديق رضي الله عنهما ، قالت : قَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  لاَ تُوكِي فَيُوكى عَلَيْكِ )) .

وفي رواية : ((  أنفقي أَوِ انْفَحِي ، أَوْ انْضَحِي ، وَلاَ تُحصي فَيُحْصِي اللهُ عَلَيْكِ ، وَلاَ تُوعي فَيُوعي اللهُ عَلَيْكِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Asmaa bint Abuu Bakr As-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) Amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Usikusanye Allaah akakukatia riziki." 

Na katika riwaayah nyingine: "Toa swadaqah kwa mali yako au anfahiy (toa) au andhahiy (kutoa) wala usizuie mali yako kwa kuhesabu (kwa kuhofia itapungua), Allaah asije akakunyima rehma zake na wala usiwanyime watu kwa ile fadhila uliyopatiwa na hivyo Allaah akakunyima." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 17

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يَقولُ : ((  مَثَل البَخيل وَالمُنْفِقِ ، كَمَثَلِ رَجُلَيْنِ عَلَيْهِمَا جُنَّتَانِ مِنْ حَديد مِنْ ثُدِيِّهِمَا إِلَى تَرَاقِيهِمَا ، فَأَمَّا المُنْفِقُ فَلاَ يُنْفِقُ إِلاَّ سَبَغَتْ - أَوْ وَفَرَتْ - عَلَى جِلْدِهِ حَتَّى تُخْفِيَ بَنَانَهُ ، وَتَعْفُو أثرَهُ ، وأمَّا البَخِيلُ ، فَلاَ يُريدُ أنْ يُنْفِقَ شَيْئاً إِلاَّ لَزِقَتْ كُلُّ حَلْقَةٍ مَكَانَهَا ، فَهُوَ يُوسِّعُهَا فَلاَ تَتَّسِعُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amamsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mfano wa bakhili na yule anayetoa, ni kama mfano wa watu wawili waliovaa juba za chuma, mikono yao imelazimika kwenda kwenye maziwa na mitulinga yao. Ama yule mkarimu (mwenye kutoa swadaqah) akawa kila anapotoa swadaqah linatanuka mpaka linafunika vidole nyake, na linafunika alama zake zote. Na ama yule bakhili hataki kutoa kitu chochote ila zile kona hushikilia mahali pake na kuzidi kumbana, naye atakuwa anaitanua na wala haitanuki." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 18

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ تَصَدَّقَ بعَدلِ تَمْرَةٍ مِنْ كَسْبٍ طَيِّبٍ ، وَلاَ يَقْبَلُ اللهُ إِلاَّ الطَّيبَ ، فَإنَّ اللهَ يَقْبَلُهَا بِيَمِينِهِ ، ثُمَّ يُرَبِّيهَا لِصَاحِبِهَا كَمَا يُرَبِّي أحَدُكُمْ فَلُوَّهُ حَتَّى تَكُونَ مِثْلَ الجَبَلِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kutoa swadaqah kama tende moja, kwenye chumo zuri, Allaah hakubali isipokuwa kizuri, hakika Allaah Ataipokea kwa Mkono Wake wa kuume, kisha Atamletea (swadaqah hiyo), kama mmoja wenu anavyolea mtoto wa farasi wake, mpaka iwe kama mlima." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 19

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  بَيْنَمَا رَجُلٌ يَمْشِي بِفَلاَةٍ مِنَ الأَرْضِ ، فَسَمِعَ صَوْتاً في سَحَابَةٍ ، اسقِ حَدِيقَةَ فُلانٍ ، فَتَنَحَّى ذَلِكَ السَّحَابُ فَأفْرَغَ مَاءهُ في حَرَّةٍ ، فإِذَا شَرْجَةٌ مِنْ تِلْكَ الشِّرَاجِ قَدِ اسْتَوْعَبَت ذَلِكَ الماءَ كُلَّهُ ، فَتَتَبَّعَ المَاءَ ، فإذَا رَجُلٌ قَائمٌ في حَدِيقَتِهِ يُحَوِّلُ الماءَ بِمسحَاتِهِ، فَقَالَ لَهُ : يَا عَبْدَ اللهِ، ما اسمُكَ ؟ قال : فُلانٌ للاسم الذي سَمِعَ في السَّحابةِ ، فقال له : يا عبدَ الله ، لِمَ تَسْألُنِي عَنِ اسْمِي ؟ فَقَالَ : إنِّي سَمِعْتُ صَوتْاً في السَّحابِ الَّذِي هَذَا مَاؤُهُ ، يقولُ : اسْقِ حَدِيقَةَ فُلاَنٍ لاسمِكَ ، فَمَا تَصْنَعُ فِيهَا ، فَقَالَ : أمَا إذ قلتَ هَذَا ، فَإنِّي أنْظُرُ إِلَى مَا يَخْرُجُ مِنْهَا ، فَأتَصَدَّقُ بِثُلُثِهِ ، وَآكُلُ أنَا وَعِيَالِي ثُلُثاً ، وَأردُّ فِيهَا ثُلُثَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu alipokuwa anatembea jangwani, alisikia sauti katika wingu (ikisema): 'Nyweshea shamba la fulani.' Wingu hilo likakaribia na kumimina maji yake kwenye ardhi ya mawe. Maji hayo yakaenea katika kijito na kumiminika katika hodhi kubwa. Akafuata maji akamuona mtu amesimama ndani ya shamba lake anagawa maji kwa jembe lake. Akamwambia: 'Ee mja wa Allaah, jina lako nani?' Akasema: 'fulani.' Akataja jina ambalo amelisikia katika wingu. Akamwambia: 'Ee mja wa Allaah! kwa nini unaniuliza jina langu?' Akasema: 'Nilisikia sauti katika wingu ambalo haya ndio maji yake ikisema: Nyweshea shamba la fulani kwa jina lako. Unafanya nini katika hili?' Akasema: 'Kwa sababu umeniuliza hili, Mimi naangalia kinachotoka humo, na kutoa swadaqah thuluthi, na thuluthi nakula pamoja na ahli wangu, na narudisha humo (shambani) thuluthi yake." [Muslim]

 

 

 

 

Share

061-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukatazwa Ubakhili na Uchoyo

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب النهي عن البخل والشح

061-Mlango Wa Kukatazwa Ubakhili na Uchoyo

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾ وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾ وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ ﴿١١﴾ 

Ama yule afanyaye ubakhili na akajiona amejitosheleza. Na akakadhibisha Al-Husnaa (anayowajibika kuyasadiki). Na Tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu. Na itamsaidia nini mali yake atakapoporomoka kuangamia (motoni). [Al-Layl: 8-11]

 

وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ﴿١٦﴾

Na yeyote anayeepushwa na ubakhili na tamaa ya uchu wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu. [At-Taghaabun: 16]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  اتَّقُوا الظُّلْمَ ؛ فَإِنَّ الظُّلْمَ ظُلُمَاتٌ يَوْمَ القِيَامَةِ . وَاتَّقُوا الشُّحَّ ؛ فَإنَّ الشُّحَّ أهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ ، حَمَلَهُمْ عَلَى أنْ سَفَكُوا دِمَاءهُمْ وَاسْتَحَلُّوا مَحَارِمَهُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ogopeni dhuluma, kwani dhuluma, ni giza kwa mwenye kuifanya Siku ya Qiyaamah. Na ogopeni (tahadharini) na ubakhili, kwani ubakhili ndio uliowaangamiza waliokuwa kabla yenu. Huu (ubakhili) uliwapelekea wao kumwaga damu na kuhalalisha vilivyo haramu." [Muslim]

 

 

 

Share

062-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendelea Wengine na Kusaidiana

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الإيثار والمواساة

062-Mlango Wa Kupendelea Wengine na Kusaidiana

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ ﴿٩﴾

Na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji. [Al-Hashr: 9]

 

وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا﴿٨﴾

Na wanalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini na mayatima na mateka. [Al-Insaan: 8]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : إنِّي مَجْهُودٌ، فَأرسَلَ إِلَى بَعْضِ نِسَائِهِ ، فَقالت : وَالَّذي بَعَثَكَ بِالحَقِّ مَا عِنْدِي إِلاَّ مَاءٌ، ثُمَّ أرْسَلَ إِلَى أُخْرَى ، فَقَالَتْ مِثلَ ذَلِكَ ، حَتَّى قُلْنَ كُلُّهُنَّ مِثلَ ذَلِكَ : لا وَالَّذِي بَعَثَكَ بالحَقِّ مَا عِنْدِي إِلاَّ مَاءٌ . فَقَالَ النبي صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ يُضيفُ هَذَا اللَّيْلَةَ ؟ )) فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ الأنْصَارِ : أنَا يَا رسولَ الله ، فَانْطَلَقَ بِهِ إِلَى رَحْلِهِ ، فَقَالَ لامْرَأَتِهِ : أكرِمِي ضَيْفَ رسول الله صلى الله عليه وسلم .

وفي روايةٍ قَالَ لامْرَأَتِهِ : هَلْ عِنْدَكِ شَيْءٌ ؟ فقَالَتْ : لاَ ، إِلاَّ قُوتَ صِبيَانِي . قَالَ: فَعَلِّليهم بِشَيْءٍ وَإذَا أرَادُوا العَشَاءَ فَنَوِّمِيهمْ ، وَإِذَا دَخَلَ ضَيْفُنَا فَأطْفِئي السِّرَاجَ ، وَأريهِ أنَّا نَأكُلُ . فَقَعَدُوا وَأكَلَ الضَّيْفُ وَبَاتَا طَاوِيَيْنِ ، فَلَمَّا أصْبَحَ غَدَا عَلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ : ((  لَقَدْ عَجبَ الله مِنْ صَنِيعِكُمَا بِضَيْفِكُمَا اللَّيْلَةَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: "Alikuja mtu kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akamwambia: "Mimi nina njaa." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatuma kwa mmoja wa wakeze, Alimjibu: "Naapa kwa aliyekutuma kwa haki sina chochote isipokuwa maji." Kisha akamtuma kwa mwingine, akasema mfano wake: "Naapa kwa aliyekutuma kwa haki sina isipokuwa maji." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akauliza: "Nani atamkirimu huyu usiku wa leo?", Akasema mtu katika Answaari: "Mimi Ee Rasuli wa Allaah." Akaenda naye nyumbani kwake, akamwambia mkewe: "Mkirimu mgeni wa Rasuli wa Allaah(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." 

Na katika riwaayah: alimwambia: "Je, una chochote?" Akasema: "La, isipokuwa chakula cha watoto." Akasema: Washughulishe na vitu, wakitaka chakula walalishe. Na anapoingia mgeni wetu zima koroboi, na muonyeshe kuwa tunakula. Wakakaa, na mgeni akala, Wao wakalala na njaa. Kulipo pambazuka alikwenda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akamwambia: "Hakika Allaah ameshangazwa kwa kitendo chenu cha usiku kwa mgeni wenu." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  : ((  طَعَامُ الاثْنَيْنِ كَافِي الثَّلاَثَةِ ، وَطَعَامُ الثَّلاَثَةِ كَافِي الأربَعَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

وفي رواية لمسلمٍ عن جابر رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم  ، قَالَ : ((  طَعَامُ الوَاحِدِ يَكْفِي الاثْنَيْنِ ، وَطَعَامُ الاثْنَيْنِ يَكْفِي الأَرْبَعَةَ ، وَطَعَامُ الأَرْبَعَة يَكْفِي الثَّمَانِية ))

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Chakula cha wawili kinatosha watatu, na chakula cha watatu kinatosha wanne." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]

Na katika riwaayah ya Muslim kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Chakula cha mmoja kinatosha wawili, na chakula cha wawili kinatosha wanne, na chaula cha wanne kinatosha wanane."

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : بَيْنَمَا نَحْنُ فِي سَفَرٍ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم إذْ جَاءَ رَجُلٌ عَلَى رَاحِلَةٍ لَهُ ، فَجَعَلَ يَصرِفُ بَصَرَهُ يَميناً وَشِمَالاً ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ كَانَ مَعَهُ فَضْلُ ظَهْرٍ فَليَعُدْ بِهِ عَلَى مَنْ لا ظَهرَ لَهُ ، وَمَنْ كَانَ لَهُ فَضْلٌ مِنْ زَادٍ ، فَلْيَعُدْ بِهِ عَلَى مَنْ لا زَادَ لَهُ )) فَذَكَرَ مِنْ أصْنَافِ المالِ مَا ذكر حَتَّى رَأيْنَا أنَّهُ لاَ حَقَّ لأحَدٍ مِنَّا في فَضْلٍ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Sa'iyd Al-Khudhriy(Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Tulipokuwa katika safari pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mara akaja mtu akiwa amepanda kipandio chake na huku anatizama kuliani na kushotoni kwake. Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 'Yeyote ambaye ana kipando cha ziada (mnyama wa kupanda) basi ampatie (kama swadaqah) asiyekuwa nao; na yoyote mwenye ziada ya chakula basi atoe swadaqah kwa asiyekuwa nacho.' Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaendelea kutaja aina tofauti ya mali mpaka tukadhania kuwa hapana haki ya mmoja wetu kuwa na ziada ya chochote." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 4

وعن سهل بن سعدٍ رضي الله عنه : أنَّ أمْرَأةً جَاءَتْ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم بِبُرْدَةٍ مَنْسُوجَةٍ ، فَقَالَتْ : نَسَجْتُها بِيَدَيَّ لأَكْسُوكَهَا ، فَأَخَذَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم مُحْتَاجاً إِلَيْهَا ، فَخَرَجَ إِلَيْنَا وَإنَّهَا إزَارُهُ ، فَقَالَ فُلانٌ : اكْسُنِيهَا مَا أحْسَنَهَا ! فَقَالَ : ((  نَعَمْ )) فَجَلَسَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم في المَجْلِسُ ، ثُمَّ رَجَعَ فَطَواهَا ، ثُمَّ أرْسَلَ بِهَا إِلَيْهِ : فَقَالَ لَهُ الْقَومُ : مَا أحْسَنْتَ ! لَبِسَهَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم مُحتَاجَاً إِلَيْهَا ، ثُمَّ سَألْتَهُ وَعَلِمْتَ أنَّهُ لا يَرُدُّ سَائِلاً ، فَقَالَ : إنّي وَاللهِ مَا سَألْتُهُ لألْبِسَهَا ، إنَّمَا سَألْتُهُ لِتَكُونَ كَفنِي . قَالَ سَهْلٌ : فَكَانَتْ كَفَنَهُ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Sahl bin Sa'd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mwanamke alimjia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na shuka iliyofumwa akasema: "Nimeifuma kwa mikono yangu ili nikuvalishe." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaichukua kwani alikuwa anaihitaji, aliivaa kama izari yake (kikoi). Mtu akasema: "Nipe mimi kwani ni kizuri sana." Akasema: "Ndio." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akakaa katika kikao, aliingia ndani, akakikunja na kumpelekea. Watu wakamwambia: "Hukufanya vizuri kwani Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikivaa kwa kuwa anakihitaji nawe ukamuomba akupati huku ukijua kuwa yeye hamrudishi mtupu mwenye kumuomba." Akasema: "Wa-Allaahi mimi sikumuomba ili nikivae, bali nimemuomba ili iwe sanda yangu." Akasema Sahl: "Hiyo ndiyo iliyokuwa sanda yake." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي موسى رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّ الأشْعَرِيِّينَ إِذَا أرْمَلُوا في الغَزْوِ ، أَوْ قَلَّ طَعَامُ عِيَالِهِمْ بالمَديِنَةِ ، جَمَعُوا مَا كَانَ عِنْدَهُمْ في ثَوْبٍ وَاحِدٍ ، ثُمَّ اقْتَسَمُوهُ بَيْنَهُمْ في إنَاءٍ وَاحدٍ بالسَّوِيَّةِ فَهُمْ مِنِّي وَأنَا مِنْهُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Al'Ash'ariyy wanapoenda vitani au chakula cha ukoo kikipungua Madiynah, wana jumuisha walivyonavyo katika nguo moja, kisha wanagawana baina yao sawasawa katika chombo kimoja. Hivyo wao ni pamoja na mimi, nami ni pamoja na wao." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share

063-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kushindana Katika Mambo Yanayohusu Aakhera na Kutaka Vitu vya Baraka

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب التنافس في أمور الآخرة والاستكثار مما يتبرك بِهِ

063-Mlango Wa Kushindana Katika Mambo Yanayohusu Aakhera na Kutaka Vitu vya Baraka

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ﴿٢٦﴾

Mwisho wake ni miski. Na katika hayo basi washindane wenye kushindana …[Al-Mutwaffifiyn: 26]

 

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن سَهْلِ بن سَعدٍ رضي الله عنه  : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم أُتِيَ بِشَرابٍ ، فَشَرِبَ مِنْهُ وَعَنْ يَمِينِهِ غُلاَمٌ ، وَعَنْ يَسَارِهِ الأشْيَاخُ ، فَقَالَ لِلغُلاَمِ : ((  أتَأذَنُ لِي أنْ أُعْطِيَ هؤُلاء ؟ )) فَقَالَ الغُلامُ : لاَ وَاللهِ يَا رسولَ الله ، لا أُوْثِرُ بِنَصِيبـي مِنْكَ أحَداً . فَتَلَّهُ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم في يَدِهِ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kutoka kwa Sahl bin Sa'd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliletewa kinywaji, naye akanywa kidogo. Kulikuwa na kijana upande wake wa kulia na wazee upande wake wa kushoto.  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia yule kijana: "Je, utanipatia idhini niwapatie hawa (yaani wazee)?' Akasema yule kijana: "Ee Rasuli wa Allaah! Naapa kwa Allaah kuwa simpatii nafasi hiyo yeyeote baada yako." Hivyo, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimpatia kinywaji kilichobaki." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  بَيْنَا أيُّوبُ عَلَيْهِ السَّلام يَغْتَسِلُ عُرْيَاناً ، فَخَرَّ عَلَيْهِ جَرَادٌ مِنْ ذَهَبٍ ، فَجَعَلَ أيُّوبُ يَحْثِي في ثَوْبِهِ ، فَنَادَاهُ رَبُّهُ عز وجل : يَا أيُّوبُ ، ألَمْ أكُنْ أغْنَيتكَ عَمَّا تَرَى ؟! قَالَ : بَلَى وَعِزَّتِكَ وَلَكِنْ لاَ غِنى بي عن بَرَكَتِكَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wakati Nabiy Ayyub ('Alayhis Salaam) alikuwa akioga uchi, mara nzige wa dhahabu akadondoka juu yake. Alijaribu kumshika kwa nguo yake, Allaah ('Azza wa Jalla) akamwita: 'Ee Ayyuwb!, Je sikuwa mwenye kukutosha wewe kama uonavyo?' Akasema: Ndio! lakini mimi sitosheki na baraka zako." [Al-Bukhaariy]  

 

 

 

 

Share

064-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango wa Ubora wa Tajiri Mwenye Kushukuru na Kuchuma Mali na Halali na Kuitumia kwa Njia Iliyoamriwa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل الغَنِيّ الشاكر وهو من أخذ المال من وجهه وصرفه في وجوهه المأمور بِهَا

064-Mlango wa Ubora wa Tajiri Mwenye Kushukuru na Kuchuma Mali na Halali na Kuitumia kwa Njia Iliyoamriwa

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

 

فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾ وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧﴾

Basi yule anayetoa (mali) na akamcha Allaah. Na akasadikisha Al-Husnaa (jazaa na laa ilaaha illa Allaah). Basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi [Al-Layl: 5-7]

 

وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾ الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾ وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠﴾ وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١﴾

Na ataepushwa nao mwenye taqwa kabisa. Ambaye anatoa mali yake kujitakasa. Na hali hakuna mmoja yeyote aliyemfanyia fadhila yoyote hata amlipe. Isipokuwa kutaka Wajihi wa Rabb wake Aliyetukuka. Na bila shaka atakuja kuridhika. [Al-Layl: 17-21]

 

إِن تُبْدُوا الصَّدَقَاتِ فَنِعِمَّا هِيَ ۖ وَإِن تُخْفُوهَا وَتُؤْتُوهَا الْفُقَرَاءَ فَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّئَاتِكُمْ ۗ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٢٧١﴾

Mkidhihirisha swadaqah basi ni vizuri hivyo, na mkizificha na kuwapa mafakiri, basi hilo ni khayr kwenu. Na Atakufutieni katika maovu yenu. Na Allaah kwa yale myatendayo, ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-Baqarah: 271]

 

 

لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٩٢﴾

Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda. Na kitu chochote mnachotoa basi hakika Allaah kwacho ni Mjuzi. [Aal-'Imraan: 92]

 

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن عبدِ الله بن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  لاَ حَسَدَ إِلاَّ في اثْنَتَيْنِ : رَجُلٌ آتَاهُ اللهُ مَالاً ، فَسَلَّطَهُ عَلَى هَلَكَتِهِ فِي الحَقِّ ، وَرَجُلٌ آتَاهُ اللهُ حِكْمَةً فَهُوَ يَقضِي بِهَا وَيُعَلِّمُهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana kuoneana wivu ila kwa mambo mawili: Mtu aliyepewa na Allaah mali na akawa akaitumia katika njia ya haki (kujikurubisha na Allaah pamoja na kutii) na mtu ambaye amepatiwa na Allaah hekima, naye anahukumu watu kwayo na kuifundisha." [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

 

 

Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لاَ حَسَدَ إِلاَّ في اثْنَتَيْنِ : رَجُلٌ آتَاهُ اللهُ القُرْآنَ ، فَهُوَ يَقُومُ بِهِ آنَاءَ اللَّيْلِ وَآنَاءَ النَّهَارِ ، وَرَجُلٌ آتَاهُ مَالاً ، فَهُوَ يُنْفِقُهُ آنَاءَ اللَّيْلِ وَآنَاءَ النَّهَارِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hapana hasad (wivu) ila kwa watu wawili: Mtu ambaye amepatiwa Quraan na Allaah, naye akawa amesimama imara nayo kwa kuisoma na kuitekeleza maamrisho yake mchana na usiku; na mwengine ni yule aliyepatiwa mali na Allaah, naye akawa anaitoa (swadaqah) mchana na usiku." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ فُقَراءَ المُهَاجِرينَ أتَوْا رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالُوا : ذَهَبَ أهْلُ الدُّثُورِ بِالدَّرَجَاتِ العُلَى ، وَالنَّعِيم المُقيم ، فَقَالَ : ((  وَمَا ذَاك ؟)) فَقَالوا : يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي ، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ ، وَيَتَصَدَّقُونَ وَلاَ نَتَصَدَّقُ ، وَيَعْتِقُونَ وَلاَ نَعْتِقُ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  أفَلا أُعَلِّمُكُمْ شَيْئاً تُدْرِكُونَ بِهِ مَنْ سَبَقَكُمْ ، وَتَسْبِقُونَ بِهِ مَنْ بَعْدَكُمْ ، وَلاَ يَكُونُ أحَدٌ أفْضَلَ مِنْكُمْ إِلاَّ مَنْ صَنَعَ مِثْلَ مَا صَنَعْتُمْ ؟ )) قالوا : بَلَى يَا رسول الله ، قَالَ : ((  تُسَبِّحُونَ وَتُكَبِّرُونَ وَتَحْمِدُونَ ، دُبُرَ كُلِّ صَلاَةٍ ثَلاثاً وَثَلاثِينَ مَرَّةً )) فَرَجَعَ فُقَرَاء المُهَاجِرِينَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم ، فقالوا : سَمِعَ إخْوَانُنَا أهلُ الأمْوالِ بِمَا فَعَلْنَا ، فَفَعَلُوا مِثلَهُ ؟ فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  ذَلِكَ فَضْلُ اللهِ يُؤْتِيهِ مَنْ يَشَاءُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وَهَذا لفظ رواية مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mafakiri wa Muhaajirina walikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: "Wenye mali nyingi wamenyakuwa daraja za juu na neema za daima." Akasema: "Na inakuwa vipi hilo?" Wakasema: "Wao wanaswali kama tunavyoswali, wanafunga kam tunavyofunga, wanatoa swadaqah nasi hatutoi, wanaacha watumwa wala hatuachi." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je niwafundishe kitu mtawafikia nacho waliowapiteni, na mtawashinda wa baada yenu, wala hakuna bora kuliko nyinyi ila atakayefanya mnavyofanya?" Wakasema: "Ndio ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Msabihini Allaah, Muhimidini Allaah na leteni takbiri baada ya kila Swalaah mara thelathini na tatu." Walirudi tena mafakiri wa Muhaajirina kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakasema: 'Ndugu zetu wenye mali wamesikia tunayofanya, wakafanya mfano wake?" Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hiyo ni fadhila ya Allaah anampa amtakaye." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya riwaayah ya Muslim]

 

 

 

Share

065-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango wa Kukumbuka Mauti na Kupunguza Matarajio

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب ذكر الموت وقصر الأمل

065-Mlango wa Kukumbuka Mauti na Kupunguza Matarajio

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۗ وَإِنَّمَا تُوَفَّوْنَ أُجُورَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۖ فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ۗ وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا إِلَّا مَتَاعُ الْغُرُورِ ﴿١٨٥﴾

Kila nafsi itaonja mauti. Na hakika mtalipwa kikamilifu ujira wenu Siku ya Qiyaamah. Basi atakayewekwa mbali na moto na akaingizwa Jannah kwa yakini amefuzu. Na uhai wa dunia si lolote ila ni starehe ya udanganyifu. [Aal-'Imraan: 185]

 

وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا ۖ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤﴾

Na nafsi yoyote haijui nini itachuma kesho, na nafsi yoyote haijui itafia katika ardhi gani [Luqmaan: 34]

 

 

فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ لَا يَسْتَأْخِرُونَ سَاعَةً ۖ وَلَا يَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٤﴾

Basi utakapofika muda wao huo, hawatataakhari wala hawatatangulia saa. [Al-A'raaf: 34]

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ﴿٩﴾

Enyi walioamini! Zisikupurukusheni mali zenu na wala watoto wenu mkaacha kumdhukuru Allaah. Na yeyote atakayefanya hivyo basi hao ndio waliokhasirika.

 

وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ﴿١٠﴾

Na toeni katika yale Tuliyokuruzukuni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti akasema: Rabb wangu! Lau Ungeliniakhirisha mpaka muda wa karibu hivi, basi ningetoa swadaqah na ningelikuwa miongoni mwa Swalihina.

 

وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا ۚ وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ﴿١١﴾

Lakini Allaah Haiakhirishi kamwe nafsi yeyote inapokuja ajali yake na Allaah ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika kwa yale myatendayo. [Al-Munaafiquwn: 9-11]

 

حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩﴾

Mpaka itakapomfikia mmoja wao mauti, atasema: Rabb wangu! Nirejeshe (duniani). 

 

لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ ۚ كَلَّا ۚ إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَائِلُهَا ۖ وَمِن وَرَائِهِم بَرْزَخٌ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ﴿١٠٠﴾

Ili nikatende mema katika yale niliyoyaacha. (Ataambiwa) Laa hasha! Hakika hilo ni neno alisemaye yeye tu.  Na nyuma yao kuna barzakh mpaka Siku watakayofufuliwa.

  

فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ فَلَا أَنسَابَ بَيْنَهُمْ يَوْمَئِذٍ وَلَا يَتَسَاءَلُونَ ﴿١٠١﴾

Basi itakapopulizwa baragumu, hakutokuwa na unasaba baina yao Siku hiyo, na wala hawatoulizana. 

 

فَمَن ثَقُلَتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٠٢﴾

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, hao ndio wenye kufaulu.

  

وَمَنْ خَفَّتْ مَوَازِينُهُ فَأُولَـٰئِكَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فِي جَهَنَّمَ خَالِدُونَ ﴿١٠٣﴾

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu, basi hao ni ambao wamekhasirika nafsi zao; katika Jahannam ni wenye kudumu. 

 

تَلْفَحُ وُجُوهَهُمُ النَّارُ وَهُمْ فِيهَا كَالِحُونَ ﴿١٠٤﴾

Moto utababua nyuso zao; nao humo watakuwa ni wenye midomo iliyosinyaa na kuvutika mbali na meno.

  

أَلَمْ تَكُنْ آيَاتِي تُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ فَكُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ ﴿١٠٥﴾

(Wataambiwa): Je, hazikuwa Aayaat Zangu zinasomwa kwenu na nyinyi mkawa mnazikadhibisha?

 

إِلَى قَوْله تَعَالَى :

 

قَالَ كَمْ لَبِثْتُمْ فِي الْأَرْضِ عَدَدَ سِنِينَ ﴿١١٢﴾

(Allaah) Atasema: Muda gani mlikaa katika ardhi kwa idadi ya miaka?

  

قَالُوا لَبِثْنَا يَوْمًا أَوْ بَعْضَ يَوْمٍ فَاسْأَلِ الْعَادِّينَ ﴿١١٣﴾

Watasema: Tumekaa siku au sehemu tu ya siku. Basi waulize wanaohesabu.

 

قَالَ إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا قَلِيلًا ۖ لَّوْ أَنَّكُمْ كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١١٤﴾

(Allaah) Atasema: Hamkukaa (huko duniani) isipokuwa kidogo tu, lau mngelikuwa mnajua.

  

أَفَحَسِبْتُمْ أَنَّمَا خَلَقْنَاكُمْ عَبَثًا وَأَنَّكُمْ إِلَيْنَا لَا تُرْجَعُونَ ﴿١١٥﴾

Je, mlidhania kwamba Sisi Tulikuumbeni bila kusudio mcheze tu na kwamba nyinyi Kwetu hamtorejeshwa? [Al-Muuminuwn: 99-115]

 

 

أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ۖ وَكَثِيرٌ مِّنْهُمْ فَاسِقُونَ ﴿١٦﴾

Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa kumdhukuru Allaah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? Na wengi miongoni mwao ni mafasiki. [Al-Hadiyd: 16]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : أخذ رسول الله صلى الله عليه وسلم بِمِنْكَبي ، فَقَالَ : ((  كُنْ في الدُّنْيَا كَأَنَّكَ غَرِيبٌ أَوْ عَابِرُ سَبِيلٍ )) . وَكَانَ ابْنُ عُمَرَ رضي الله عنهما ، يقول : إِذَا أمْسَيْتَ فَلاَ تَنْتَظِرِ الصَّبَاحَ ، وَإِذَا أصْبَحتَ فَلاَ تَنْتَظِرِ المَسَاءَ ، وَخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِمَرَضِكَ ، وَمِنْ حَيَاتِكَ  لِمَوْتِكَ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) akisema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaau 'alayhi wa aalihi wa sallam) alishika mabega yangu akasema: 'kuwa duniani kana kwamba ni mgeni au mpita njia.' Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) alikuwa akisema: 'Na ukichelewa usingoje asubuhi, na unapopambazuka usingoje jioni. Na chukua uzima wako kwa ajili ya maradhi yako. Na chukua uhai wako kabla ya mauti yako." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَا حَقُّ امْرِئٍ مُسْلِمٍ ، لَهُ شَيْءٌ يُوصِي فِيهِ ، يَبيتُ لَيْلَتَيْنِ إِلاَّ وَوَصِيَّتُهُ مَكْتُوبَةٌ عِنْدَهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، هَذَا لفظ البخاري .

وفي روايةٍ لمسلمٍ : ((  يَبِيتُ ثَلاَثَ لَيَالٍ )) قَالَ ابن عمر : مَا مَرَّتْ عَلَيَّ لَيْلَةٌ مُنْذُ سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قَالَ ذَلِكَ إِلاَّ وَعِنْدِي وَصِيَّتِي .

Na imepokewa kutoka kwa 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haifai kwa Muislamu ambaye ana kitu cha kuusia (kitu ambacho kinaweza kurithiwa na warithi wake) kulala masiku mawili ila tayari ameandika usia wake." [Al-Bukhaariy na Muslim, hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]

Na katika riwaayah ya Muslim: "Analala masiku matatu." Amesema Ibn 'Umar: "Haijapita kwangu usiku mmoja baada ya kusikia maneno haya kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isipokuwa nina usia wangu."

 

 

Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : خَطَّ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم خُطُوطاً ، فَقَالَ : ((  هَذَا الإنْسَانُ ، وَهَذَا أجَلُهُ ، فَبَيْنَمَا هُوَ كَذَلِكَ إذْ جَاءَ الخَطُّ الأَقْرَبُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Alichora Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mistari mingi akasema: Huyu ni mwanadamu na 'Msitari huu ni ajali yake. Akiwa hivyo anajiwa na msitari wa karibu" (yaani mauti)." [Al-Bukhaariy] 

 

 

Hadiyth – 4

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : خَطَّ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم خَطّاً مُرَبَّعاً ، وَخَطَّ خَطّاً في الوَسَطِ خَارِجَاً مِنْهُ ، وَخَطَّ خُطَطاً صِغَاراً إِلَى هَذَا الَّذِي في الْوَسَطِ مِنْ جَانِبهِ الَّذِي في الوَسَط ، فَقَالَ : ((  هَذَا الإنْسَانُ ، وَهذَا أجَلُهُ مُحيطاً بِهِ – أَوْ قَدْ أحَاطَ بِهِ – وَهذَا الَّذِي هُوَ خَارِجٌ أمَلُهُ ، وَهذِهِ الْخُطَطُ الصِّغَارُ الأَعْرَاضُ ، فَإنْ أخْطَأَهُ هَذَا ، نَهَشَهُ هَذَا ، وَإنْ أخْطَأَهُ هَذَا ، نَهَشَهُ هَذَا )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alichora hati ya mraba, akachora msitari katikati nje yake. Akachora mistari midogo kuelekea huu wa kati toka upande wake ambao uko katikati. Akasema: 'Huyu ni mwanadamu, na hii ni ajali yake imemzunguka, au imeshamkuta. Na huu ulio nje ni matarajio yake, hii mistari midogo ni mitihani, Unapomkosa huu basi anapatwa na huu; unapomkosa huu anakutwa na huu." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه  : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  بَادِرُوا بِالأعْمَالِ سَبْعاً ، هَلْ تَنْتَظِرُونَ إِلاَّ فَقْراً مُنْسِياً ، أَوْ غِنَىً مُطْغِياً ، أَوْ مَرَضَاً مُفْسداً ، أَوْ هَرَماً مُفَنِّداً ، أَوْ مَوْتَاً مُجْهِزاً ، أَوْ الدَّجّالَ ، فَشَرُّ غَائِبٍ يُنْتَظَرُ ، أَوْ السَّاعَةَ وَالسَّاعَةُ أدْهَى وَأمَرُّ ؟! )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Harakisheni kufanya amali, kabla ya mambo saba: Je, mnangojea ufakiri unaosahaulisha, au utajiri unaopoteza, au maradhi yenye kuharibu siha, au uzee unaoharibu akili, au mauti ya ghafla, au kuja kwa Dajjaal naye ni shari iliyojificha inayongojewa, au Qiyaamah ni tukio gumu na chungu." [At-Tirmidhiy, ambaye alisema ni Hadiyth Hasan].

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  أكْثِرُوا ذِكْرَ هَاذِمِ اللَّذَّاتِ )) يَعْنِي : المَوْتَ . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameseam: "Zidisheni kukumbuka kiondoa ladha" (yaani umauti)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].

 

 

Hadiyth – 7

وعن أُبَيِّ بن كعبٍ رضي الله عنه : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا ذَهَبَ ثُلُثُ اللَّيْلِ قَامَ ، فَقَالَ : ((  يَا أَيُّهَا النَّاسُ ، اذْكُرُوا اللهَ ، جَاءتِ الرَّاجِفَةُ ، تَتْبَعُهَا الرَّادِفَةُ ، جَاءَ المَوْتُ بِمَا فِيهِ ، جَاءَ المَوْتُ بِمَا فِيهِ )) قُلْتُ : يَا رسول الله ، إنِّي أُكْثِرُ الصَّلاَةَ عَلَيْكَ ، فَكَمْ أجْعَلُ لَكَ مِنْ صَلاَتِي ؟ فَقَالَ : ((  مَا شِئْتَ )) قُلْتُ : الرُّبُع ، قَالَ :   ((  مَا شِئْتَ ، فَإنْ زِدْتَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ )) قُلْتُ : فَالنِّصْف ؟ قَالَ : ((  مَا شِئْتَ ، فَإنْ زِدْتَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ )) قُلْتُ : فالثُّلُثَيْنِ ؟ قَالَ : ((  مَا شِئْتَ ، فَإنْ زِدْتَ فَهُوَ خَيْرٌ لَكَ )) قُلْتُ : أجعَلُ لَكَ صَلاَتِي كُلَّهَا ؟ قَالَ : ((  إذاً تُكْفى هَمَّكَ ، وَيُغْفَر لَكَ ذَنْبكَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Ubayy bin Ka'b (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akiamka thuluthi ya mwisho ya usiku na kusema: "Enyi watu! Mtajeni Allaah! Tetemeko limekuja, likifuatiwa na raa-di, mauti yamekuja na yalio ndani yake." Nikamuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Mimi nimeongeza kukuswalia. Je, nikutengee kiasi gani kwenye Swalaah yangu?" Akasema: "Unavyotaka." NIkasema: "Je, robo?" Akasema: "Unavyo penda na ukizidisha ni bora kwako." Nikasema: "Je, nusu?" Akasema: "Unavyo penda na ukizidisha ni bora kwako." Nikasema: "Je, thuluthi mbili (2/3)?" Akasema: "Unavyo penda na ukizidisha ni bora kwako." Nikasema: "Je, nijaalie swalaah yangu ni yako?" Akasema: "Basi utatoshwa hamu yako, na kufutiwa dhambi yako." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].

 

 

 

 

 

Share

066-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendeza Kuzuru Makaburi kwa Wanaume na Anachosema Mwenye Kuzuru

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب استحباب زيارة القبور للرجال وما يقوله الزائر

066-Mlango Wa Kupendeza Kuzuru Makaburi kwa Wanaume na Anachosema Mwenye Kuzuru

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Hadiyth – 1

عن بُرَيْدَة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  كُنْتُ نَهَيْتُكُمْ عن زِيَارَةِ القُبُورِ فَزُوروها )) رواه مسلم .

وفي رواية : ((  فَمَنْ أرَادَ أنْ يَزُورَ القُبُورَ فَلْيَزُرْ ؛ فإنَّهَا تُذَكِّرُنَا الآخِرَةَ )) .

Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nilikuwa nimekukatazeni kuzuru makaburi, sasa yazuruni." [Muslim]

Na katika riwaayah: "Yeyote anayetaka kuzuru makaburi basi ayazuru; kwani (huko kuzuru makaburi) kutawakumbusha Aakherah."

 

 

Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم - كلَّما كَانَ لَيْلَتُهَا مِنْ رسول الله صلى الله عليه وسلم - يَخْرُجُ مِنْ آخِرِ اللَّيْلِ إِلَى البَقِيعِ ، فَيقولُ : ((  السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ دَارَ قَوْمٍ مُؤْمِنِينَ ، وَأتَاكُمْ مَا تُوعَدُونَ ، غَداً مُؤَجَّلْونَ ، وَإنَّا إنْ شَاءَ اللهُ بِكُمْ لاَحِقُونَ ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لأهْلِ بَقِيعِ الغَرْقَدِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiyah Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kila inapokuwa zamu yake, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), alikuwa anatoka mwisho wa usiku kuelekea Baqii' na anasema: "Amani juu yenu Waumini wa nyumba hii, Yamekujieni mlioahidiwa, Mmetangulizwa wakatimaalumu. Na hakika sisi akitaka Allaah tutakutana nanyi. Ee Mola wangu wasamehe watu wa Al'Baqi'i Al-Gharqad, (yenye michongoma)." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن بريدة رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يُعَلِّمُهُمْ إِذَا خَرَجُوا إِلَى المَقَابِرِ أنْ يَقُولَ قَائِلُهُمْ : ((  السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ أهلَ الدِّيَارِ مِنَ المُؤْمِنينَ وَالمُسلمينَ ، وَإنَّا إنْ شَاءَ اللهُ بِكُمْ للاَحِقونَ ، أسْألُ اللهَ لَنَا وَلَكُمُ العَافِيَةَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwafundisha dua wakitoka kwenda makaburini asema mmoja wao: "Amani juu yenu watu wa nyumba hizi miongoni mwa Waumini na Waislamu. Na hakika sisi akitaka Allaah tutakutana nanyi, Tunamuomba Allaah sisi na nyinyi afya." [Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 4

وعن ابن عباسٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : مرَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم بِقُبورٍ بالمدِينَةِ فَأقْبَلَ عَلَيْهِمْ بِوَجْهِهِ ، فَقَالَ : ((  السَّلامُ عَلَيْكُمْ يَا أهْلَ القُبُورِ ، يَغْفِرُ اللهُ لَنَا وَلَكُمْ ، أنْتُمْ سَلَفُنَا وَنَحنُ بالأثَرِ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Na imepokewa kutoka kwa bn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita katika makaburi ya Madiynah akayakabili kwa uso wake na kusema: "Amani iwashukie enyi watu wa makaburi. Allaah atusamehe sisi na nyinyi. Nyinyi mumetutangulia nasi tunawafuatia." [At-Tirmidhiy, na kasema ni Hadiyth Hasan].

 

 

 

 

Share

067-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Karaha ya Kutamani Umauti Kwa Sababu ya Dhara Iliyomkumba na Haina Tatizo Ikiwa Anahofia Fitna Katika Dini

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

بابُ كراهة تمنّي الموت بسبب ضُرّ نزل بِهِ وَلاَ بأس بِهِ لخوف الفتنة في الدين

067-Mlango Wa Karaha ya Kutamani Umauti Kwa Sababu ya Dhara Iliyomkumba na Haina Tatizo Ikiwa Anahofia Fitna Katika Dini

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Hadiyth – 1

عن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لا يَتَمَنَّ أحَدُكُمُ المَوْتَ ، إمَّا مُحْسِناً فَلَعَلَّهُ يَزْدَادُ ، وَإمَّا مُسِيئاً فَلَعَلَّهُ يَسْتَعْتِبُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .

وفي رواية لمسلم عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم  ، قَالَ : ((  لاَ يَتَمَنَّ أَحَدُكُمُ المَوْتَ ، وَلاَ يَدْعُ بِهِ مِنْ قَبْلِ أنْ يَأتِيَهُ ؛ إنَّهُ إِذَا مَاتَ انْقَطَعَ عَمَلُهُ ، وَإنَّهُ لاَ يَزِيدُ المُؤْمِنَ عُمُرُهُ إِلاَّ خَيْراً )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitamani mmoja wenu mauti kwani kama kama ni mtu mwema huenda akazidisha amali njema. Na ama akiwa ni mtu muovu (mwenye kufanya madhambi) huenda akatubia (na kutadaraki yalioyopita)." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]

Katika riwaayah ya Muslim kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitamani mmoja wenu umauti wala asiwe ni mwenye kujiombea kabla hayajamfikia, kwani akiaga dunia amali yake yote hukatika. Na kwa hakika umri wa Muumini hauongezeki ila huleta kheri zaidi."

 

 

Hadiyth – 2

وعن أنسٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  لاَ يَتَمَنَّيَنَّ أحَدُكُمُ المَوْتَ لِضُرٍّ أصَابَهُ ، فَإنْ كَانَ لاَ بُدَّ فَاعِلاً ، فَلْيَقُلْ : اللَّهُمَّ أحْيِني مَا كَانَتِ الحَيَاةُ خَيْراً لي ، وَتَوَفَّنِي إِذَا كَانَت الوَفَاةُ خَيراً لي )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitamani mmoja wenu mauti kwa sababu ya madhara yaliyomsibu. Ikiwa hapana budi mpaka atamani basi aseme: 'Ee Mola wangu nipe uhai ikiwa una kheri na mimi na unifishe ikiwa kuaga dunia kwangu ni kheri kwangu." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن قيسِ بن أَبي حازم ، قَالَ : دَخَلْنَا عَلَى خَبَّاب بن الأرَتِّ رضي الله عنه نَعُودُهُ وَقَدِ اكْتَوَى سَبْعَ كَيَّاتٍ ، فَقَالَ : إنَّ أَصْحَابَنَا الَّذِينَ سَلَفُوا مَضَوْا ، وَلَمْ تَنْقُصْهُمُ الدُّنْيَا ، وَإنَّا أصَبْنَا مَا لاَ نَجِدُ لَهُ مَوْضِعاً إِلاَّ التُّرَابَ وَلولا أنَّ النبي صلى الله عليه وسلم نَهَانَا أنْ نَدْعُوَ بالمَوْتِ لَدَعَوْتُ بِهِ . ثُمَّ أتَيْنَاهُ مَرَّةً أُخْرَى وَهُوَ يَبْنِي حَائِطاً لَهُ ، فَقَالَ : إنَّ المُسْلِمَ لَيُؤْجَرُ فِي كُلِّ شَيْءٍ يُنْفِقُهُ إِلاَّ فِي شَيْءٍ يَجْعَلُهُ في هَذَا التُّرَابِ . متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ رواية البخاري

Imepokewa kutoka kwake Qays bin Abu Haazim amesema: Tulimtembelea Khabbaab bin Al-Aratt (Radhwiya Allaahu 'anhu) alipokuwa mgonjwa. Mishipa yake ya damu ilikuwa imefunguliwa mahali saba. Alituambia: "Hakika sahibu zetu waliotangulia wamepita, Dunia haikuwapunguza. Kwa hakika sisi tumepata ambayo hayan mahali isipokuwa udongo. Na lau sio Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutukataza kuomba mauti ningeyaomba." Kisha tulimzuru mara nyingine tukamkuta anajenga ukuta wake, akasema: "Hakika Muislaamu analipwa kwa kila kitu anachotoa isipokuwa kitu anachokijalia katika huu udongo." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy] 

 

 

 

 

Share

068-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kujichunga na Kuacha Mambo Yenye Shaka

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الورع وترك الشبهات

068-Mlango Wa Kujichunga na Kuacha Mambo Yenye Shaka

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى

وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمٌ ﴿١٥﴾

Na mnalidhania ni jambo jepesi; na hali hili mbele ya Allaah ni kubwa mno. [An-Nuwr: 15]

إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ﴿١٤﴾

Hakika Rabb wako bila shaka Yu tayari Awavizia. [Al-Fajr: 14]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن النعمان بن بشيرٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  إنَّ الحَلاَلَ بَيِّنٌ ، وَإنَّ الحَرامَ بَيِّنٌ ، وَبَيْنَهُمَا مُشْتَبَهَاتٌ لاَ يَعْلَمُهُنَّ كَثيرٌ مِنَ النَّاسِ ، فَمَنِ اتَّقَى الشُّبُهَاتِ ، اسْتَبْرَأَ لِدِينهِ وَعِرْضِهِ ، وَمَنْ وَقَعَ فِي الشُّبُهَاتِ وَقَعَ في الحَرَامِ ، كَالرَّاعِي يَرْعَى حَوْلَ الحِمَى يُوشِكُ أنْ يَرْتَعَ فِيهِ ، ألاَ وَإنَّ لكُلّ مَلِكٍ حِمَىً ، ألاَ وَإنَّ حِمَى اللهِ مَحَارِمُهُ ، ألاَ وَإنَّ فِي الجَسَدِ مُضْغَةً إِذَا صَلَحَت صَلَحَ الْجَسَدُ كُلُّهُ ، وَإِذَا فَسَدَتْ فَسَدَ الْجَسَدُ كُلُّهُ ، ألاَ وَهِيَ القَلْبُ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وروياه مِنْ طرقٍ بِألفَاظٍ متقاربةٍ .

Imepokewa kutoka kwa An-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika halali iko wazi na haramu iko wazi; na baina ya vitu hivi viwili kuna mambo yenye shaka, watu wengi hawayajui. Basi mwenye kuepuka mambo yenye shaka, hakika amehifadhi Dini yake na heshima yake. Na mwenye kuingia kwenye mambo ya shaka ameingia kwenye haramu, kama mchunga anayechunga pambizoni mwa mpaka anachelea kulisha humo, jueni, hakika kila mfalme ana mpaka, na jueni kuwa hakika mwili kuna kinofu, kikitengemaa utatengemaa mwili wote, kikiharibika utaharibika mwili wote, jueni kuwa huo ni moyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أنسٍ رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم وَجَدَ تَمْرَةً فِي الطَّرِيقِ ، فَقَالَ : ((  لَوْلاَ أنِّي أخَافُ أنْ تَكُونَ مِنَ الصَّدَقَة لأَكَلْتُهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliona tende njiani, akasema: "Lau kama mimi sikuhofia kuwa hii tende ni ya swadaqah ningeila." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن النَّواسِ بن سمعان رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  البِرُّ : حُسْنُ الخُلُقِ، وَالإِثْمُ : مَا حَاكَ فِي نَفْسِكَ ، وَكَرِهْتَ أنْ يَطَّلِعَ عَلَيْهِ النَّاسُ )) رواه مسلم.

Imepokewa kutoka kwa An-Nawwaas bin Sam'aan ya kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Kutenda wema ni tabia nzuri, na kitendo kiovu ni chenye kukukera katika nafsi yako na ukachukia watu wakuone nacho." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن وَابِصَةَ بن مَعبدٍ رضي الله عنه ، قَالَ: أتَيْتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: (( جئتَ تَسْألُ عَنِ البِرِّ ؟ )) قُلْتُ : نَعَمْ ، فَقَالَ : ((  اسْتَفْتِ قَلْبَكَ ، البرُّ : مَا اطْمَأنَّت إِلَيْهِ النَّفسُ ، وَاطْمأنَّ إِلَيْهِ القَلْبُ ، وَالإثْمُ : مَا حَاكَ في النَّفْسِ ، وَتَرَدَّدَ فِي الصَّدْرِ ، وَإنْ أفْتَاكَ النَّاسُ وَأفْتُوكَ )) حديث حسن ، رواه أحمد والدَّارمِيُّ في مُسْنَدَيْهِمَا .

Imepokewa kutoka kwake Waabiswah bin Ma'bad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba nilikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), naye akaniuliza: "Je, umekuja kuuliza juu ya kutenda wema?" Nikamwambia: "Ndio." Akasema: "Ushauri moyo wako. Kutenda wema ni kufanya lenye kutuliza nafsi, na ukatulia moyo; na kitendo kiovu ni chenye kukera kwenye nafsi na kutaradadi kifuani hata kama wamekutolea fatwa watu (kuwa chafaa)." [Hadiyth Hasan, imepokewa katika Musnadi mbili: Ahmad bin Hambal na Ad-Daarimiyy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي سِرْوَعَةَ عُقبَةَ بنِ الحارِثِ رضي الله عنه : أنَّهُ تَزَوَّجَ ابنَةً لأبي إهَابِ بن عزيزٍ ، فَأتَتْهُ امْرَأةٌ ، فَقَالَتْ : إنّي قَدْ أرضَعْتُ عُقْبَةَ وَالَّتِي قَدْ تَزَوَّجَ بِهَا . فَقَالَ لَهَا عُقْبَةُ : مَا أعْلَمُ أنَّك أرضَعْتِنِي وَلاَ أخْبَرْتِني ، فَرَكِبَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم بِالمَدِينَةِ ، فَسَأَلَهُ : فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  كَيْفَ ؟ وَقَد قِيلَ )) فَفَارَقَهَا عُقْبَةُ وَنَكَحَتْ زَوْجاً غَيْرَهُ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sirwa'ah 'Uqbah bin Al-Haarith (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alimuoa bint wa Abu Wahaab bin 'Aziyz, akaja kwake mwanamke alliyemwambia: "Hakika mimi nimemnyesha 'Uqbah na mkewe." 'Uqbah akamwambia: "Sijui kama wewe umeninyonyesha wala hujanijulisha hilo." Akafunga safari kuelekea Madiyah kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na alipofika alimuuliza (kuhusu jambo hilo). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Vipi, na tayari ushaelezwa?" 'Uqbah alimuacha mkewe huyo na kuoa mwanamke mwengine." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 6

وعن الحسن بن علي رضي الله عنهما ، قَالَ : حَفِظتُ من رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  دَعْ مَا يريبُكَ إِلَى ما لاَ  يَرِيبُكَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Al-Hasan bin 'Ali (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa alisema: "Nimehifadhi kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Acha lenye kukutia shaka kwa lisilokutia shaka." [At-Tirmidhiy, na akasema kuwa ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 7

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ لأبي بَكر الصديق رضي الله عنه غُلاَمٌ يُخْرِجُ لَهُ الخَرَاجَ ، وَكَانَ أَبُو بَكْرٍ يَأكُلُ مِنْ خَرَاجِهِ ، فَجَاءَ يَوْماً بِشَيءٍ ، فَأكَلَ مِنْهُ أَبُو بَكْرٍ ، فَقَالَ لَهُ الغُلامُ : تَدْرِي مَا هَذَا ؟ فَقَالَ أَبُو بكر : وَمَا هُوَ ؟ قَالَ : كُنْتُ تَكَهَّنْتُ لإنْسَانٍ في الجَاهِلِيَّةِ وَمَا أُحْسِنُ الكَهَانَةَ ، إِلاَّ أنّي خَدَعْتُهُ ، فَلَقِيَنِي ، فَأعْطَانِي لِذلِكَ ، هَذَا الَّذِي أكَلْتَ مِنْهُ ، فَأدْخَلَ أَبُو بَكْرٍ يَدَهُ فَقَاءَ كُلَّ شَيْءٍ فِي   بَطْنِهِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Abu Bakr As-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhu)alikuwa na kijana aliyekuwa akimtolea mapato. Abu Bakr alikuwa akila humo. Akaja siku moja na kitu na  Abu Bakr akala. Kijana Akamwambia: "Unajua nini hiki?" Akasema Abu Bakr: "Ni nini hicho?" Akasema: "Nilimfanyia uchawi mtu katika jahiliyyah (ujinga) na sikujua uchawi ila nilimhadaa. Alikutana nami na kunipa kitu hicho ambacho umekula." Abu Bakr alitia mkono wake kwenye mdomo na kutapika chote kilichokuwa ndani ya tumbo lake." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 8

وعن نافِع : أن عُمَرَ بن الخَطّاب رضي الله عنه كَانَ فَرَضَ لِلمُهَاجِرينَ الأَوَّلِينَ أرْبَعَةَ الآفٍ وَفَرَضَ لابْنِهِ ثَلاَثَة آلافٍ وَخَمْسَمئَةٍ ، فَقيلَ لَهُ : هُوَ مِنَ المُهَاجِرينَ فَلِمَ نَقَصْتَهُ ؟ فَقَالَ : إنَّمَا هَاجَرَ بِهِ أبُوهُ . يقول : لَيْسَ هُوَ كَمَنْ هَاجَرَ بِنَفْسِهِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Naafi' kwamba 'Umar bin Al-Khattaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikuwa anawapatia Muhaajiriyn wa mwanzo elfu arobaini na akawa anampatia mtoto wake elfu tatu na mia tano. Akaambiwa: "Yeye pia ni miongoni mwa Muhaajiriyn kwa nini unampunguzia kiwango chake?" Akawaambia: "Hakika yeye alihama na babake, hivyo hawi sawa na yule aliyehama pake yake." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 9

وعن عَطِيَّةَ بن عُروة السَّعْدِيِّ الصحابيِّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  لاَ يَبْلُغُ الْعَبدُ أنْ يَكُونَ منَ المُتَّقِينَ حَتَّى يَدَعَ مَا لاَ بَأسَ بِهِ ، حَذَراً مِمَّا بِهِ بَأسٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa 'Atiyyah bin 'Urwah As-Sa'adiy amabaye ni Swahaaba (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna mja atakayefika daraja ya uchamngu mpaka aache yale mambo yasiyo na tatizo lolote kama tahadhari kwa yale yenye madhara." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 
Share

069-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendekeza Kujitenga Wakati wa Uharibifu na Ufisadi au Hofu ya Fitnah Katika Dini au Kujiingiza Katika Haramu na Shaka

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب استحباب العزلة عند فساد الناس والزمان

069-Mlango Wa Kupendekeza Kujitenga Wakati wa Uharibifu na Ufisadi au Hofu ya Fitnah Katika Dini au Kujiingiza Katika Haramu na Shaka

 

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

فَفِرُّوا إِلَى اللَّـهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٥٠﴾

Basi kimbilieni kwa Allaah, hakika mimi kwenu ni mwonyaji bayana kutoka Kwake. [Adh-Dhaariyaat: 50]

 

 

Hadiyth – 1

وعن سعد بن أَبي وقاص رضي الله عنه  ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  إنَّ الله يُحِبُّ الْعَبْدَ التَّقِيَّ الغَنِيّ الْخَفِيَّ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Sa'd bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika Allaah anampenda mja mchamngu mwenye utajiri wa nafsi na asiyejionesha." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رَجُلٌ : أيُّ النَّاسِ أفْضَلُ يَا رسولَ الله ؟ قَالَ : ((  مُؤْمِنٌ مُجَاهِدٌ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ في سَبيلِ اللهِ )) قَالَ : ثُمَّ مَنْ ؟  قَالَ : ((  ثُمَّ رَجُلٌ مُعْتَزِلٌ فِي شِعْبٍ مِنَ الشِّعَابِ يَعْبُدُ رَبَّهُ )) . وفي رواية : ((  يَتَّقِي اللهَ ، وَيَدَعُ النَّاسَ مِنْ شَرِّهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mtu alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Mtu gani bora zaidi?" Akasema: "Muumini anayepigana kwa nafsi yake na mali yake katika njia ya Allaah." Akasema: "Kisha ni nani?" Akasema: "Kisha mtu aliyejitenga katika bonde miongoni mwa mabonde akimuabudu Rabb wake." Katika riwaayah: "Anamcha Allaah na kuacha watu na shari yake (kutowaudhi)." [Al-Bukhaariy na Muslim] 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  : ((  يُوشِكُ أنْ يَكُونَ خَيْرَ مَالِ المُسْلِمِ غَنَمٌ يَتَّبعُ بِهَا شَعَفَ الجِبَالِ ، وَمَواقعَ الْقَطْر يَفِرُّ بِدينِهِ مِنَ الفِتَنِ )) رواه البخاري .

Na imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wakati upo karibu ambapo mali bora ya Muislamu itakuwa ni mbuzi wengi ambao atakwenda nao juu ya jabali au sehemu ya mvua ili kuilinda Dini yake kutokana na fitna." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَا بَعَثَ اللهُ نَبِيّاً إِلاَّ رَعَى الْغَنَمَ )) فَقَالَ أصْحَابُهُ : وأنْتَ ؟ قَالَ : ((  نَعَمْ ، كُنْتُ أرْعَاهَا عَلَى قَرَارِيطَ لأَهْلِ مَكَّةَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hakutuma Nabiy, ila Nabiy huyu alichunga mbuzi." Swahaabah wakauliza: "Hata wewe?" Akasema: "Ndio nilikuwa nikichunga kwa watu wa Makkah na nikilipwa Qaraarit (kipimo maalum cha dhahabu chenye wizani wa 1/24 ya dinari)." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، أنَّه قَالَ : ((  مِنْ خَيْرِ مَعَاشِ النَّاسِ لهم رَجُلٌ مُمْسِكٌ عِنَانَ فَرَسِهِ في سَبيلِ الله، يَطيرُ عَلَى مَتْنِهِ كُلَّمَا سَمِعَ هَيْعَةً أَوْ فَزعَةً ، طَارَ عَلَيْهِ يَبْتَغِي القَتْلَ ، أَوْ المَوْتَ مَظَانَّه ، أَوْ رَجُلٌ فِي غُنَيمَةٍ في رَأسِ شَعَفَةٍ مِنْ هذِهِ الشَّعَفِ ، أَوْ بَطنِ وَادٍ مِنْ هذِهِ الأَوْدِيَةِ ، يُقِيمُ الصَّلاَةَ ، وَيُؤتِي الزَّكَاةَ ، وَيَعْبُدُ رَبَّهُ حَتَّى يأتِيَهُ اليَقِينُ ، لَيْسَ مِنَ النَّاسِ إِلاَّ فِي خَيْرٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Maisha yaliyo bora miongoni mwa watu ni mtu kushika hatamu za farasi katika njia ya Allaah. Anampanda kwenye mgongo wake na kuruka nae (kwenda haraka) pindi tu anaposikia sauti ya vita (kuwa vipo tayari) au mfano wake wa fazaa. Anakimbilia sehemu hiyo akiwa tayari kupigana au kwa yule mtu anayejitenga na mbuzi wake  wachanga juu ya mlima miongoni mwa hii milima au akawa anaishi kati ya moja ya mabonde. Na hapo anasimamisha Swalaah na kutoa Zakaah na kutekeleza 'Ibadah ya Rabb wake mpaka yatakapomfikia yeye umauti na wala haingilii maisha ya watu ila kwa kutaka kheri." [Muslim]

 

 

 

Share

070-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila za Kutangamana na Watu, Kuhudhuria Mikusanyiko yao, Kushuhudia Kheri, Kushiriki Katika Vikao Vya Dhikri Pamoja nao, Kutembelea Wagonjwa, Kuhudhuria Jeneza Zao, Kukidhi Haja za Masikini Miongoni Mwao,

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب فضل الاختلاط بالناس وحضور جُمَعِهم وجماعاتهم ،

ومشاهد الخير ، ومجالس الذكر معهم ، وعيادة مريضهم ، وحضور

جنائزهم ، ومواساة محتاجهم ، وإرشاد جاهلهم ، وغير ذلك من

مصالحهم لمن قدر عَلَى الأمر بالمعروف والنهي عن المنكر ، وقمع

نفسه عن الإيذاء وصبر عَلَى الأذى

070-Mlango Wa Fadhila za Kutangamana na Watu, Kuhudhuria Mikusanyiko yao, Kushuhudia Kheri, Kushiriki Katika Vikao Vya Dhikri Pamoja nao, Kutembelea Wagonjwa, Kuhudhuria Jeneza Zao, Kukidhi Haja za Masikini Miongoni Mwao, Kuwaongoza Wajinga Wao na Mengineyo Katika Maslahi yao na Mwenye Kuweza au Kuamrisha Mema na Kukataza Mabaya na Kutoa Katika Nafsi Yake Uchafu na Kusubiri Maudhi na Shida.

 

 

Alhidaaya.com

 

 

اعْلم أنَّ الاختلاط بالنَّاسِ عَلَى الوجهِ الَّذِي ذَكَرْتُهُ هُوَ المختارُ الَّذِي كَانَ عَلَيْهِ رسول الله صلى الله عليه وسلم وسائر الأنبياء صلواتُ اللهِ وسلامه عَلَيْهِمْ ، وكذلك الخُلفاءُ الرَّاشدون ، ومن بعدَهُم مِنَ الصَّحَابَةِ وَالتَّابِعِينَ ، ومن بَعدَهُم من عُلَماءِ المُسلمين وأَخْيَارِهم ، وَهُوَ مَذْهَبُ أكثَرِ التَّابِعينَ وَمَنْ بَعدَهُمْ ، وبه قَالَ الشافعيُّ وأحمدُ وأكثَرُ الفقهاءِ رضي اللهُ عنهم أجمعين. قَالَ اللهُ تَعَالَى: ( وَتَعَاوَنُوا عَلَى البِرِّ وَالتَّقْوَى ) [ المائدة : 20 ] والآيات في معنى مَا ذكرته كثيرة معلومة .

Jua ya kwamba kutangamana na watu kwa njia niliyoitaja ndio yenye kupendeza. Ndio njia iliyokuwa ikifuatwa na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Manabii wote na hivyo hivyo Makhalifa waongofu na waliokuja baada yao miongoni mwa Swahaabah na Taabi'iyna. Na pia hiyo ilikuwa ndio sifa ya waliokuja baada yao miongoni mwa wanavyuoni Waislaamu na wabora wao. Na hii ndiyo madhehebu ya Taabi'iyna wengi na wala waliokuja baada yao. Na kwayo ndio amesema Ash-Shaafi'iy, na Ahmad na Mafakih wengi. Amesema Allaah Ta'aalaa: "Na shirikianeni katika wema na taqwa." [Al-Maaidah: 2]. Na kuna ayah nyingi katika mlango huu.

 

 

 

 

Share

071-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Unyenyekevu na Kuinamisha Bawa Waumini

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب التواضع وخفض الجناح للمؤمنين

071-Mlango Wa Unyenyekevu na Kuinamisha Bawa Waumini

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢١٥﴾

Na inamisha ubawa wako kwa anayekufuata miongoni mwa Waumini. [Ash-Shu'araa: 215]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا مَن يَرْتَدَّ مِنكُمْ عَن دِينِهِ فَسَوْفَ يَأْتِي اللَّـهُ بِقَوْمٍ يُحِبُّهُمْ وَيُحِبُّونَهُ أَذِلَّةٍ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ أَعِزَّةٍ عَلَى الْكَافِرِينَ  ﴿٥٤﴾

Enyi walioamini! Yeyote atakayeritadi miongoni mwenu kutoka Dini yake, basi Allaah Ataleta watu (badala yao) Atakaowapenda nao watampenda; wanyenyekevu kwa Waumini, washupavu juu ya makafiri.[Al-Maaidah: 54]

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن ذَكَرٍ وَأُنثَىٰ وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا ۚ إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ۚ ﴿١٣﴾

Enyi watu! Hakika Sisi Tumekuumbeni kutokana namwanamme na mwanamke, na Tukakujaalieni  mataifa na makabila ili mtambuane. Hakika aliye na hadhi zaidi miongoni mwenu mbele ya Allaah ni mwenye taqwa zaidi kati yenu. [Al-Hujuraat: 13]

 

فَلَا تُزَكُّوا أَنفُسَكُمْ ۖ هُوَ أَعْلَمُ بِمَنِ اتَّقَىٰ ﴿٣٢﴾

Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa. [An-Najm: 32]

 

وَنَادَىٰ أَصْحَابُ الْأَعْرَافِ رِجَالًا يَعْرِفُونَهُم بِسِيمَاهُمْ قَالُوا مَا أَغْنَىٰ عَنكُمْ جَمْعُكُمْ وَمَا كُنتُمْ تَسْتَكْبِرُونَ ﴿٤٨﴾ أَهَـٰؤُلَاءِ الَّذِينَ أَقْسَمْتُمْ لَا يَنَالُهُمُ اللَّـهُ بِرَحْمَةٍ ۚ ادْخُلُوا الْجَنَّةَ لَا خَوْفٌ عَلَيْكُمْ وَلَا أَنتُمْ تَحْزَنُونَ ﴿٤٩﴾

Na watu wa Al-A’raaf watawaita watu (wa motoni) wanaowatambua kwa alama zao, watasema: Hakukufaeni kujumuika kwenu (duniani) na vile mlivyokuwa mkitakabari. Je, hawa si wale ambao mliapa kwamba Allaah hatowafikishia kwa rahmah yoyote ile? (Leo wanaambiwa) Ingieni Jannah! Hakuna khofu juu yenu na wala nyinyi hamtohuzunika. [Al-A'raaf: 48-49]

 

 

Hadiyth – 1

وعن عِيَاضِ بنِ حمارٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّ الله أوْحَى إِلَيَّ أنْ تَوَاضَعُوا حَتَّى لاَ يَفْخَرَ أحَدٌ عَلَى أحَدٍ ، وَلاَ يَبْغِي أحَدٌ عَلَى أحَدٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Iyaadh bin Himaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah amenifunulia Wahyi kuwa nyenyekeeni hadi yoyote asijifakhiri mtu juu ya mwingine, wala yoyote asimfanye uadui mwingine." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : ((  مَا نَقَصَتْ صَدَقَةٌ مِنْ مَالٍ،وَمَا زادَ اللهُ عَبْداً بعَفْوٍ إِلاَّ عِزّاً، وَمَا تَوَاضَعَ أحَدٌ للهِ إِلاَّ رَفَعَهُ اللهُ (عزّ وجلّ )) رواه مسلم.

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swadaqah haipunguzi mali; na Allaah anamuongezea utukufu mwenye kusamehe. Na hanyenyekei yoyote kwa ajili ya Allaah  ('Azza wa Jalla) isipokuwa Allaah humnyanyua." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه : أنَّهُ مَرَّ عَلَى صبيَانٍ ، فَسَلَّمَ عَلَيْهِمْ ، وقال : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يفعله . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alipita mbele ya watoto na akawasalimia. Na hapo akasema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alikuwa akifanya hivyo." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : إن كَانَتِ الأَمَةُ مِنْ إمَاءِ المَدينَةِ لَتَأْخُذُ بِيَدِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَتَنْطَلِقُ بِهِ حَيْثُ شَاءتْ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa alisema: "Kijakazi miongoni mwa vijakazi wa Madiynah alikuwa anaweza kuushika mkono wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akawa anakwenda naye popote anapotaka ili amweleze shida yake." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن الأَسْوَدِ بن يَزيدَ ، قَالَ : سُئِلَتْ عائشةُ رضي الله عنها مَا كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يَصْنَعُ فِي بَيْتِهِ ؟ قالت : كَانَ يَكُون في مِهْنَةِ أهْلِهِ – يعني : خِدمَة أهلِه – فإذا حَضَرَتِ الصَّلاَةُ ، خَرَجَ إِلَى الصَّلاَةِ . رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Al-Aswad bin Yaziyd ambaye amesema, 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) aliulizwa: "Je, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akifanya nini nyumbani?" Alisema: :Alikuwa akiwahudumikia na kuwasaidia watu wake wa nyumbani, lakini wakatika wa Swalaah unapofika alikuwa akitoka kwenda kuswali." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي رِفَاعَةَ تَميم بن أُسَيْدٍ رضي الله عنه ، قَالَ : انْتَهَيْتُ إِلَى رَسولِ الله صلى الله عليه وسلم وَهُوَ يخطب ، فقلت : يَا رسول الله ، رَجُلٌ غَريبٌ جَاءَ يَسْألُ عن دِينهِ لا يَدْرِي مَا دِينُهُ ؟ فَأقْبَلَ عَليَّ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وتَرَكَ خُطْبَتَهُ حَتَّى انْتَهَى إلَيَّ ، فَأُتِيَ بِكُرْسيٍّ ، فَقَعَدَ عَلَيْهِ ، وَجَعَلَ يُعَلِّمُنِي مِمَّا عَلَّمَهُ اللهُ ، ثُمَّ أَتَى خُطْبَتَهُ فَأتَمَّ آخِرَهَا . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Rifaa'ah Tamim bin Usayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: "Nilifika kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa anakhutubu, nami nikamuuliza: 'Ee Rasuli wa Allaah! Mtu mgeni amekuja kuuliza kuhusu Dini yake kwani yeye hajui chochote kuhusu Dini yake?' Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alinikabili na akaja kwangu. Aliletewa kiti, akakikalia. Akawa ananifundisha aliyofundishwa na Allaah. Kisha alijia hutuba yake akaitimiza." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أنس رضي الله عنه : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا أكَلَ طَعَاماً ، لَعِقَ أصَابِعَهُ الثَّلاَثَ . قَالَ : وقال : ((  إِذَا سَقَطَتْ لُقْمَةُ أَحَدِكُمْ فَلْيُمِط عنها الأَذى ، وليَأكُلْها وَلاَ يَدَعْها لِلشَّيْطان )) وأمرَ أن تُسلَتَ القَصْعَةُ ، قَالَ : ((  فإنَّكُمْ لاَ تَدْرُونَ في أيِّ طَعَامِكُمُ البَرَكَة )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akilamba vidole vyake vitatu baada ya kumaliza kula. Amesema Anas kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tonge la mmoja wenu likianguka basi aondoe uchafu ulioingia na kisha alile na wala asimwachie shetani." Na pia ameamuru kufuta kabisa sahani (aliyolia mmoja wenu) na akasema: "Hakika nyinyi hamujui ni chakula chenu kipi kina baraka." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَا بَعَثَ الله نَبِيّاً إِلاَّ رَعَى الغَنَمَ )) قَالَ أصْحَابُهُ : وَأنْتَ ؟ فَقَالَ : ((  نَعَمْ ، كُنْتُ أرْعَاهَا عَلَى قَرَارِيطَ لأَهْلِ مَكَّةَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hakutuma Nabiy, ila Nabiy huyo alichunga mbuzi." Wakasema Swahaaba zake: "Hata wewe?" Akasema: "Ndio, nilikuwa nikichunga kwa watu wa Makkah na nikilipwa Qaraarit." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لَوْ دُعِيتُ إِلَى كُراعٍ أَوْ ذِرَاعٍ لأَجَبْتُ ، ولو أُهْدِيَ إِلَيَّ ذراعٌ أَوْ كُراعٌ لَقَبِلْتُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau ningealikwa kwa chakula cha muundi au bega ningeitikia na lau ningepatiwa zawadi ya muundi au bega ningekubali (ningepokea)." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَتْ ناقةُ رسول الله صلى الله عليه وسلم العضْبَاءُ لاَ تُسْبَقُ ، أَوْ لاَ تَكَادُ تُسْبَقُ ، فَجَاءَ أعْرَابيٌّ عَلَى قَعودٍ لَهُ ، فَسَبَقَهَا ، فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَى الْمُسْلِمِينَ حَتَّى عَرَفَهُ ، فَقَالَ : ((  حَقٌّ عَلَى اللهِ أنْ لاَ يَرْتَفِعَ شَيْءٌ مِنَ الدُّنْيَا إِلاَّ وَضَعَهُ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Ngamia wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiitwa 'Adhbaa', naye hakuwa akimruhusu ngamia yeyote amshinde. Wakati mmoja alikuja bedui aliyekuwa na ngamia mchanga aliyempita ngamia wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Jambo hilo lilikuwa gumu sana kwa Waislamu mpaka Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatambua hilo. Akasema: "Ni haki kwa Allaah kukutojikweza chochote duniani ila atakishusha." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

 

Share

072-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuharamishwa Kibri na Kujiona

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب تحريم الكبر والإعجاب

072-Mlango Wa Kuharamishwa Kibri na Kujiona

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

تِلْكَ الدَّارُ الْآخِرَةُ نَجْعَلُهَا لِلَّذِينَ لَا يُرِيدُونَ عُلُوًّا فِي الْأَرْضِ وَلَا فَسَادًا ۚ وَالْعَاقِبَةُ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٨٣﴾

Hiyo ni nyumba ya Aakhirah, Tunaijaalia kwa wale wasiotaka kujitukuza katika ardhi na wala ufisadi. Na hatima njema ni kwa wenye taqwa. [Al-Qaswasw: 83]

 

وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ  ﴿٣٧﴾

Na wala usitembee katika ardhi kwa majivuno. [Al-Israa: 37]

 

وَلَا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿١٨﴾

Na wala usiwageuzie watu uso wako kwa kiburi, na wala usitembee katika ardhi kwa maringo, hakika Allaah Hampendi kila mwenye kujivuna mwenye kujifakharisha. [Luqmaan: 18]

 

إِنَّ قَارُونَ كَانَ مِن قَوْمِ مُوسَىٰ فَبَغَىٰ عَلَيْهِمْ ۖ وَآتَيْنَاهُ مِنَ الْكُنُوزِ مَا إِنَّ مَفَاتِحَهُ لَتَنُوءُ بِالْعُصْبَةِ أُولِي الْقُوَّةِ إِذْ قَالَ لَهُ قَوْمُهُ لَا تَفْرَحْ ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْفَرِحِينَ ﴿٧٦﴾

Hakika Qaaruwn alikuwa miongoni mwa kaumu ya Muwsaa, lakini aliwafanyia uonevu kwa kutakabari. Na Tulimpa katika hazina ambazo funguo zake zinalemea kundi la watu wenye nguvu (kuzibeba). Walipomwambia watu wake: Usifurahi kwa kujigamba. Hakika Allaah Hapendi wanaofurahi kwa kujigamba. [Al-Qaswasw: 76]

إِلَى قَوْله تَعَالَى:

فَخَسَفْنَا بِهِ وَبِدَارِهِ الْأَرْضَ ﴿٨١﴾

Basi Tukamdidimiza yeye na nyumba yake ardhini [Al-Qaswasw: 81]

 

 

Hadiyth – 1

وعن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لاَ يَدْخُلُ الجَنَّةَ مَنْ كَانَ في قَلْبِهِ مِثْقَالُ ذَرَّة مِنْ كِبْرٍ ! )) فَقَالَ رَجُلٌ : إنَّ الرَّجُلَ يُحِبُّ أنْ يَكُونَ ثَوْبُهُ حَسَناً ، ونَعْلُهُ حَسَنَةً ؟ قَالَ : ((  إنَّ اللهَ جَمِيلٌ يُحِبُّ الجَمَالَ ، الكِبْرُ : بَطَرُ الحَقِّ وَغَمْطُ النَّاسِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillah bin Mas'uuwd (Radhwiya Alaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaah 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hataingia Peponi yeyote ambae katika moyo wake kuna chembe ya kiburi." Akasema mtu mmoja: "Hakika mtu anapenda kuwa na nguo nzuri na viatu vizuri?" Akasema: "Hakika Allaah ni mzuri na anapenda vizuri. Kiburi ni kukataa haki kwa kujiona na kuyarudisha kwa mwenyewe na kuwaona watu wengine kuwa duni." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن سلمة بن الأكوع رضي الله عنه  : أنّ رَجُلاً أكَلَ عِنْدَ رسول الله صلى الله عليه وسلم بشمالِهِ ، فَقَالَ : ((  كُلْ بيَمِينِكَ )) قَالَ : لاَ أسْتَطِيعُ ! قَالَ : ((  لا اسْتَطَعْتَ )) مَا مَنَعَهُ إِلاَّ الكِبْرُ . قَالَ : فما رفَعها إِلَى فِيهِ . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Salamah bin Al-Akwa' (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: "Kuwa mtu mmoja alikula mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mkono wa kushoto. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: 'Kula kwa wa kulia.' Akasema: 'Siwezi.' Akasema: 'Hutaweza.' Hakuna kilichomzuia kufuata agizo la Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) isipokuwa kibri, hivyo hakuweza tena kuunyanyua mdomoni mwake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن حارثة بن وهْبٍ رضي الله عنه  ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( ألا أُخْبِرُكُمْ بأهْلِ النَّار : كلُّ عُتُلٍ جَوّاظٍ مُسْتَكْبرٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وتقدم شرحه في بابِ ضعفةِ المسلمين .

Imepokewa kutoka kwa Haarithah bin Wahb (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Je, niwaeleze nyinyi kuhusu watu wa Peponi? Kila dhaifu na mwenye kudhoofishwa. Lau ataapa kwa Allaah, Allaah atamtekelezea. Je, siwapashi habari juu ya watu wa Motoni? Ni kila mkavu, safihi na mwenye kiburi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي سعيد الخدري رضي الله عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  احْتَجّتِ الجَنَّةُ وَالنَّارُ ، فَقَالَت النَّارُ : فيَّ الْجَبَّارُونَ والمُتَكَبِّرُونَ . وقالتِ الجَنَّةُ : فيَّ ضُعفاءُ الناس ومساكينُهُم ، فقضى اللهُ بَينهُما : إنكِ الجنّةُ رَحْمَتِي أرْحَمُ بِك مَنْ أشَاءُ ، وَإنَّكِ النَّارُ عَذَابِي أُعَذِّبُ بِكِ مَنْ أشَاءُ ، وَلِكِلَيْكُمَا عَلَيَّ مِلْؤُهَا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pepo na Moto zilibishana. Moto ukasema: 'Ndani yangu watakaa majabari na wenye kiburi.' Na Pepo ikasema: 'Ndani yangu watakaa madhaifu miongoni mwa watu na masikini wao.' Allaah akaamua baina yao: 'Hakika yako wewe, Pepo ni Rehema Yangu ninamrehemu kwako nimtakaye. Na hakika yako wewe, Moto ni adhabu Yangu, ninawaadhibu kwako nimtakaye, Na ni juu Yangu kuwajaza nyote wawili." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لاَ يَنْظُرُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَةِ إِلَى مَنْ جَرَّ إزَارَهُ بَطَراً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hamwangalii siku ya Qiyaamah mwenye kuburuza kikoi chake kwa kiburi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  ثَلاَثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَة ، وَلاَ يُزَكِّيهِمْ ، وَلاَ يَنْظُرُ إلَيْهِمْ ، وَلَهُمْ عَذَابٌ ألِيمٌ : شَيْخٌ زَانٍ ، وَمَلِكٌ كَذَّابٌ ، وَعَائِلٌ مُسْتَكْبِرٌ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watu watatu Allaah hatazungumza nao Siku ya Qiyaamah wala hatawatakasa wala hatawaangalia: Mzee mzinifu, na mfalme mwongo na fakiri mwenye kiburi." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  قَالَ الله (عزّ وجلّ) : العِزُّ إزَاري ، والكبرياءُ رِدائي ، فَمَنْ يُنَازِعُنِي في وَاحِدٍ منهما فَقَد عَذَّبْتُهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Amesema Allaah ('Azza wa Jalla): Utukufu ni kikoi Changu, na kiburi ni shuka Yangu, na atakayeshindana Nami katika moja wapo ya viwili hivi Nitamuadhibu." [Muslim]

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  بَيْنَمَا رَجُلٌ يَمشِي في حُلَّةٍ تُعْجِبُهُ نَفْسُهُ ، مُرَجِّلٌ رَأسَهُ ، يَخْتَالُ فِي مَشْيَتهِ ، إِذْ خَسَفَ اللهُ بِهِ ، فَهُوَ يَتَجَلْجَلُ في الأَرضِ إِلَى يَوْمِ القِيَامَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu  akiwa anatembea katika pambo akijiona nafsini mwake. Nywele zake zimechanwa, anajivuna katika kutembe kwake. Allaah akamdidimiza ardhini, Yeye anadidimia ardhini hadi Siku ya Qiyaamah.' [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 9

وعن سَلَمةَ بنِ الأكْوَعِ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  لاَ يَزَالُ الرَّجُلُ يَذْهَبُ بِنَفْسِهِ حَتَّى يُكْتَبَ في الجبَّارِين ، فَيُصيبَهُ مَا أصَابَهُمْ )) رواه الترمذي ، وقال: (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Salamah bin Al-Akwa' (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anaendelea mtu kujitenga na watu na kuwa ni mwenye kiburi mpaka anaandikwa pamoja na wenye kiburi na hivyo kupatiwa adhabu sawa na wale wenye kiburi." [At-Tirmidhiy, na akasema hii ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Share

073-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Tabia Njema

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب حسن الخلق

073-Mlango Wa Tabia Njema

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤﴾

Na hakika wewe uko juu ya kiwango adhimu cha tabia njema. [Al-Qalam: 4]

 

وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ  ﴿١٣٤﴾ 

Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. [Aal-'Imraan: 134]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أنس رضي الله عنه ، قال : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أحْسَنَ النَّاس خُلُقاً . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mwenye tabia nzuri kuliko watu wote." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : مَا مَسِسْتُ دِيبَاجاً وَلاَ حَرِيراً ألْيَنَ مِنْ كَفِّ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَلاَ شَمَمْتُ رَائِحَةً قَطُّ أطْيَبَ مِنْ رَائِحَةِ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، وَلَقَدْ خدمتُ رسول اللهِ صلى الله عليه وسلم عَشْرَ سنين ، فما قَالَ لي قَطُّ : أُفٍّ، وَلاَ قَالَ لِشَيءٍ فَعَلْتُهُ : لِمَ فَعَلْتَه ؟ وَلاَ لشَيءٍ لَمْ أفعله : ألاَ فَعَلْتَ كَذا ؟ متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Sijashika dibaji wala hariri laini zaidi kuliko kiganja cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), wala sijasikia harufu nzuri kuliko harufu ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hakika nilimtumikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) miaka kumi, hakuniambia kabisa: 'Ah.' Na wala hakuniambia kwa kitu nilichofanya kwa nini umefanya?, Wala kwa kitu ambacho sikufanya, lau ungefanya hivi?" [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن الصعب بن جَثَّامَةَ رضي الله عنه ، قَالَ : أهديتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم حِمَاراً وَحْشِيّاً ، فَرَدَّهُ عَلَيَّ ، فَلَمَّا رأى مَا في وجهي ، قَالَ : ((  إنّا لَمْ نَرُدَّهُ عَلَيْكَ إِلاَّ لأنّا حُرُمٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Swa'b bin Jathaamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nilimpatia hadiya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ya punda, naye akanirudishia. Alipoona alama ya sikitiko katika uso wangu, alisema: "Sijarudisha zawadi yako ila ni kwa sababu ya kuwa tumeshahirimia." [AL-Bukhaariy na Muslim] 

 

 

Hadiyth – 4

وعن النَّوَاس بنِ سمعان  رضي الله عنه ، قَالَ : سألتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم عن البِرِّ وَالإثم ، فَقَالَ : ((  البِرُّ : حُسنُ الخُلقِ ، والإثمُ : مَا حاك في صدرِك ، وكَرِهْتَ أن يَطَّلِعَ عَلَيْهِ النَّاسُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa An-Nawwaas bin sam'aan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu wema na dhambi akasema: "Wema ni tabia nzuri, na dhambi ni iliokera nafsini mwako na ukachukia watu kuiona." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : لَمْ يكن رسولُ الله صلى الله عليه وسلم فَاحِشاً وَلاَ مُتَفَحِّشاً ، وكان يَقُولُ : ((  إنَّ مِنْ خِيَارِكُمْ أحْسَنَكُمْ أخْلاَقاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillah bin 'Amru bin Al-'aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: "Hakuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni mwenye kuzungumza maneno machafu wala kuyasikiliza." Na alikuwa akisema: "Hakika aliye bora miongoni mwenu ni yule mwenye tabia nzuri." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na Ahmad].

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي الدرداءِ رضي الله عنه : أن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَا مِنْ شَيْءٍ أثْقَلُ في مِيزَانِ العبدِ المُؤْمِنِ يَوْمَ القِيَامَةِ مِنْ حُسْنِ الخُلُقِ ، وَإنَّ الله يُبْغِضُ الفَاحِشَ البَذِيَّ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna kitu chochote kilicho kizito zaidi katika mizani ya Muumini Siku ya Qiyaamah kuliko tabia nzuri. Na hakika Allaah anamchukia mwenye kutoa maneno machafu na ya kishenzi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سُئِلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنْ أكثرِ مَا يُدْخِلُ النَّاسَ الْجَنَّةَ ؟ قَالَ : ((  تَقْوَى اللهِ وَحُسنُ الخُلُقِ )) ، وَسُئِلَ عَنْ أكْثَرِ مَا يُدْخِلُ النَّاسَ النَّارَ، فَقَالَ : ((  الفَمُ وَالفَرْجُ )) رواه الترمذي، وقال : (( حديث حسن صحيح )).

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Aliulizwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa mambo ambayo yatawaingiza watu wengi Peponi?" Akasema: "Uchaji wa Allaah na tabia nzuri." Na akaulizwa kuhusu mambo ambayo yatawaingiza wengi Motoni. Akasema: "Ulimi na sehemu za siri." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قال: قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((  أكْمَلُ المُؤمنينَ إيمَاناً أحسَنُهُمْ خُلُقاً، وَخِيَارُكُمْ خِيَارُكُمْ لِنِسَائِهِمْ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini mkamilifu wa Iymaani ni mzuri wao wa tabia, na wabora wenu ni wabora wenu kwa wake zao." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Hadiyth – 9

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  إنَّ المُؤْمِنَ لَيُدْرِكُ بحُسْنِ خُلُقِه دَرَجَةَ الصَّائِمِ القَائِمِ )) رواه أَبُو داود .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika Muumini anafikia kwa tabia nzuri daraja ya mfungaji mwenye kusimama usiku." [Abu Daawuud]

 

 

Hadiyth – 10

وعن أَبي أُمَامَة الباهِليِّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  أنَا زَعِيمٌ ببَيتٍ في ربَض الجَنَّةِ لِمَنْ تَرَكَ المِرَاءَ ، وَإنْ كَانَ مُحِقّاً ، وَبِبَيْتٍ في وَسَطِ الجَنَّةِ لِمَنْ تَرَكَ الكَذِبَ ، وَإنْ كَانَ مَازِحاً ، وَبِبَيْتٍ في أعلَى الجَنَّةِ لِمَنْ حَسُنَ خُلُقُهُ )) . حديث صحيح ، رواه أَبُو داود بإسناد صحيح  .

Imepokewa kutoka kwa Abu Umamah Al-Baahiliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mimi ni mdhamini wa nyumba ya chini Peponi kwa mwenye kuacha kujionesha japo ana haki. Na nyumba ya katikati ya Peponi, kwa mwenye kuacha uongo, japokuwa kwa kufanya mzaha. Na kwa nyumba iliyo sehemu ya juu kabisa Peponi kwa mwenye tabia nzuri." [Hadiyth Swahiyh, Abu Daawuud kwa Isnaad Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 11

وعن جابر رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  إنَّ مِنْ أحَبِّكُمْ إليَّ ، وَأقْرَبِكُمْ مِنِّي مَجْلِساً يَوْمَ القِيَامَةِ ، أحَاسِنَكُم أخْلاَقاً ، وَإنَّ أبْغَضَكُمْ إلَيَّ وَأبْعَدَكُمْ مِنِّي يَوْمَ القِيَامَةِ ، الثَّرْثَارُونَ وَالمُتَشَدِّقُونَ وَالمُتَفَيْهقُونَ )) قالوا : يَا رسول الله ، قَدْ عَلِمْنَا (( الثَّرْثَارُونَ وَالمُتَشَدِّقُونَ )) ، فمَا المُتَفَيْهقُونَ ؟ قَالَ : ((  المُتَكَبِّرُونَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika wapendwa wenu zaidi kwangu, na wakaribu wenu zaidi wa kukaa nami Siku Ya Qiyaamah, ni wazuri wenu zaidi wa tabia. Na wabughudhiwa wenu zaidi wenu zaidi kwangu Siku ya Qiyaamah ni wale ma-tharthar (wenye kuzungumza sana) na mutashaddiquun (wanaorefusha mazungumzo yao na wanazungumza kwa kujaza midomo yao kwa majisifu) na mutafayhiquun." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika tunawajua ma-tharthar na mutashaddiquun lakini hawa mutafayhiquun ni kina nani?"  Akasema: "Wenya kiburi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

 
 
 

 

 

Share

074-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Upole, Umakini na Utaratibu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الحلم والأناة والرفق

074-Mlango Wa Upole, Umakini na Utaratibu

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾ 

Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-'Imraan: 136]

 

خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ﴿١٩٩﴾

Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili. [Al-A;raaf: 199]

 

وَلَا تَسْتَوِي الْحَسَنَةُ وَلَا السَّيِّئَةُ ۚ ادْفَعْ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ فَإِذَا الَّذِي بَيْنَكَ وَبَيْنَهُ عَدَاوَةٌ كَأَنَّهُ وَلِيٌّ حَمِيمٌ﴿٣٤﴾

Na wala haulingani sawa wema na uovu. Lipiza (uovu) kwa ambalo ni zuri zaidi; tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui, atakuwa kama ni rafiki mwandani.

 

وَمَا يُلَقَّاهَا إِلَّا الَّذِينَ صَبَرُوا وَمَا يُلَقَّاهَا إِلَّا ذُو حَظٍّ عَظِيمٍ﴿٣٥﴾

Na hapewi hayo isipokuwa wale waliovuta subira, na hapewi hayo isipokuwa mwenye fungu adhimu. [Fusw-swilat: 34 - 35]

 

وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾

Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa: 43]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله  صلى الله عليه وسلم لأَشَجِّ عَبْدِ القَيْسِ : ((  إنَّ فيكَ خَصْلَتَيْنِ يُحِبُّهُمَا اللهُ : الْحِلْمُ وَالأنَاةُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ameseam: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Ashajj 'Abdil-Qays: "Hakika wewe una sifa mbili anazozipenda Allaah: Uvumilivu na uthabiti na kuacha haraka." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّ اللهَ رفيقٌ يُحِبُّ الرِّفْقَ فِي الأَمْرِ كُلِّه )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah ni Mpole na anapenda upole katika mambo yote." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  إنَّ اللهَ رَفِيقٌ يُحِبُّ الرِّفقَ ، وَيُعْطي عَلَى الرِّفق ، مَا لاَ يُعْطِي عَلَى العُنْفِ ، وَمَا لاَ يُعْطِي عَلَى مَا سِوَاهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah ni Mpole, hivyo anapenda upole, na anatoa kwa upole asichotoa kwa ukali na wala kwa chengine chochote mbali na upole na ulaini." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  إنَّ الرِّفْقَ لاَ يَكُونُ في شَيْءٍ إِلاَّ    زَانَهُ ، وَلاَ يُنْزَعُ مِنْ شَيْءٍ إِلاَّ شَانَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika upole unafanya kitu kiwe kizuri, na pindi upole unapoondolewa katika kitu chochote isipokuwa uzuri wake huondoka." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : بَال أعْرَابيٌّ في المسجدِ ، فَقَامَ النَّاسُ إِلَيْهِ لِيَقَعُوا فِيهِ ، فَقَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : ((  دَعُوهُ وَأرِيقُوا عَلَى بَوْلِهِ سَجْلاً مِنْ مَاءٍ ، أَوْ ذَنُوباً مِنْ مَاءٍ ، فَإنَّمَا بُعِثْتُمْ مُيَسِّرِينَ وَلَم تُبْعَثُوا مُعَسِّرِينَ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Bedui mmoja alikojoa Msikitini, watu wakamsimamia ili kumpiga, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Muacheni na mwagieni ndoo ya maji juu ya mkojo wake. Hakika nyinyi mmetumwa kurahisisha, wala hamkutumwa kufanya uzito." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أنس رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  يَسِّرُوا وَلاَ تُعَسِّرُوا ، وَبَشِّرُوا وَلاَ تُنَفِّرُوا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Rahisisheni wala msiyafanye uzito, na toeni bishara wala msifukuze." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 7

وعن جريرِ بنِ عبدِ اللهِ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : ((  مَنْ يُحْرَمِ الرِفْقَ ، يُحْرَمِ الخَيْرَ كلَّهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Jariyr bin 'Abdillah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Anayeharimishiwa (kukosa) upole amekosa kheri zote." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 8

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رَجُلاً قَالَ للنبيِّ صلى الله عليه وسلم : أوْصِني . قَالَ : ((  لاَ تَغْضَبْ )) ، فَرَدَّدَ مِرَاراً ، قَالَ : ((  لاَ تَغْضَبْ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mtu mmoja alimwambia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Niusie." Akasema: "Usighadhibike." Akakariri mara nyingi. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Usighadhibike." [Al-Bukhaariy].

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي يعلى شَدَّاد بن أوسٍ رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  إنَّ الله كَتَبَ الإحْسَانَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ فَإذَا قَتَلْتُم فَأحْسِنُوا القِتْلَة ، وَإِذَا ذَبَحْتُمْ فَأحْسِنُوا الذِّبْحَةَ ، وَليُحِدَّ أَحَدُكُمْ شَفْرَتَه ، وَلْيُرِح ذَبِيحَتَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Ya'laa Shaddaad bin Aws (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah Ameamrisha Ihsaan (wema) kwa kila kitu. Kwa hivyo, mkiuwa uweni vizuri, na mkichinja chinjeni vizuri. Kila mmoja wenu akitie makali kisu chake, na akipunguzie uchungu kichinjwa chake." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 10

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا خُيِّرَ رسول الله صلى الله عليه وسلم بَيْنَ أمْرَيْنِ قَطُّ إِلاَّ أَخَذَ أيْسَرَهُمَا ، مَا لَمْ يَكُنْ إثماً ، فَإنْ كَانَ إثماً ، كَانَ أبْعَدَ النَّاسِ مِنْهُ . وَمَا انْتَقَمَ رسول الله صلى الله عليه وسلم  لِنَفْسِهِ في شَيْءٍ قَطُّ ، إِلاَّ أن تُنْتَهَكَ حُرْمَةُ الله ، فَيَنْتَقِمَ للهِ تَعَالَى . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakupewa fursa ya kuchagua baina ya mambo mawili katu isipokuwa alichadua jepesi lao, madamu si dhambi, ikiwa ni dhambi huwa mbali nalo zaidi. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakulipiza kisasi kwa nafsi yake katika jambo lolote isipokuwa mipaka ya Allaah inapokiukwa, kwa hilo hulipiza kisasi kwa ajili ya Allaah Ta'aalaa." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

Hadiyth – 11

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  ألا أخْبِرُكُمْ بِمَنْ يَحْرُمُ عَلَى النَّار ؟ أَوْ بِمَنْ تَحْرُمُ عَلَيْهِ النَّار ؟ تَحْرُمُ عَلَى كُلِّ قَرِيبٍ ، هَيّنٍ ، لَيِّنٍ ، سَهْلٍ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Niwajulishe nyinyi ambaye moto ni haramu kwake?. ni haramu kwa kila wa karibu, mwepesi, laini, mwepesi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni hadiyth Hasan]

 

 

 

 

 

 

Share

075-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kusamehe na Kupuuza Wajinga

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب العفو والإعراض عن الجاهلين

075-Mlango Wa Kusamehe na Kupuuza Wajinga

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

خُذِ الْعَفْوَ وَأْمُرْ بِالْعُرْفِ وَأَعْرِضْ عَنِ الْجَاهِلِينَ ﴿١٩٩﴾

Shikamana na usamehevu, na amrisha mema na jiepushe na majahili. [Al-A'raaf: 199]

فَاصْفَحِ الصَّفْحَ الْجَمِيلَ﴿٨٥﴾

Basi samehe msamaha mzuri. [Al-Hijr: 85]

 

وَلْيَعْفُوا وَلْيَصْفَحُوا ۗ أَلَا تُحِبُّونَ أَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَكُمْ ۗ  ﴿٢٢﴾

Na wasamehe na waachilie mbali. Je, hampendi Allaah Akughufurieni? [An-Nuwr: 22]

وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾ 

Na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-'Imraan: 134]

وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾

Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa: 43]

 

 

Hadiyth – 1

وعن عائشة رضي الله عنها : أنها قالت للنبي صلى الله عليه وسلم : هَلْ أتَى عَلَيْكَ يَوْمٌ كَانَ أشَدَّ مِنْ يَوْمِ أُحُدٍ ؟ قَالَ : ((  لَقَدْ لَقِيتُ مِنْ قَوْمِكِ ، وَكَانَ أشَدُّ مَا لَقيتُ مِنْهُمْ يَوْمَ الْعَقَبَةِ ، إذْ عَرَضْتُ نَفْسِي عَلَى ابْنِ عَبْدِ يَالِيْلَ بْنِ عَبْدِ كُلاَلٍ ، فَلَمْ يُجِبْني إِلَى مَا أرَدْتُ ، فَانْطَلَقْتُ وَأنا مَهْمُومٌ عَلَى وَجْهِي ، فَلَمْ أسْتَفِقْ إِلاَّ وأنَا بِقَرْنِ الثَّعَالِبِ ، فَرَفَعْتُ رَأْسِي ، وَإِذَا أنَا بِسَحَابَةٍ قَدْ أظَلَّتْنِي ، فَنَظَرْتُ فَإذَا فِيهَا جِبريلُ (عليه السلام) ، فَنَادَاني ، فَقَالَ : إنَّ الله تَعَالَى قَدْ سَمِعَ قَوْلَ قَوْمِكَ لَكَ ، وَمَا رَدُّوا عَلَيْكَ، وَقَد بَعَثَ إلَيْكَ مَلَكَ الجِبَالِ لِتَأْمُرَهُ بمَا شِئْتَ فِيهِمْ . فَنَادَانِي مَلَكُ الجِبَالِ ، فَسَلَّمَ عَلَيَّ ، ثُمَّ قَالَ : يَا مُحَمَّدُ إنَّ اللهَ قَدْ سَمِع قَوْلَ قَوْمِكَ لَكَ ، وَأنا مَلَكُ الجِبال ، وَقَدْ بَعَثَنِي رَبِّي إلَيْكَ لِتَأْمُرَنِي بِأَمْرِكَ ، فَمَا شِئْتَ ، إنْ شئْتَ أطْبَقْتُ عَلَيْهِمُ الأَخْشَبَيْنِ )) . فَقَالَ النبي صلى الله عليه وسلم : ((  بَلْ أرْجُو أنْ يُخْرِجَ اللهُ مِنْ أصْلاَبِهِمْ مَنْ يَعْبُدُ اللهَ وَحْدَهُ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Je umefikwa na siku ngumu zaidi kuliko siku ngumu zaidi kuliko siku ya Uhud?" Akasema: "Hakika nimekutana na watu wako, na ilikuwa ngumu zaidi kutoka kwao kuliko siku ya 'Aqabah, siku hiyo nilijipeleka kwa Ibn 'Adbil Yaaliil bin 'Abdi Kulaal, hakunijibu nililolitaka. Niliondoka nami nikiwa mzito juu ya uso wangu. Nilifarijika nilipofika Qarn Ath-Tha'alib, niliponyanyua kichwa changu na kuona kulikuwa na kiwingu kilichokuwa kimenifunika. Nilipotazama nikamuona Jibriyl ('Alayhis Salaam), aliita akisema: "Hakika Allaah Ta'aalaa amesikia kauli ya kaumu yako kwako, na walivyokujibu, Allaah Amekutumia Malaika wa jabali aliniita akanisalimia, kisha akasema: 'Ee Muhammad! Hakika Allaah amesikia kauli ya watu wako, na mimi ni Malaika wa majabali. Na hakika amenituma Mola wangu kwako uaiamuru amri yako; Utakacho, ukitaka nitawasaga na haya majabali mawili.' Akasemas Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 'Bali napenda Allaah atoe katika migongo yao watakaomuabudu Allaah Peke Yake hawamshirikishi Yenye na chochote." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا ضَرَبَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم شَيْئاً قَطُّ بِيَدِهِ ، وَلاَ امْرَأةً وَلاَ خَادِماً ، إِلاَّ أنْ يُجَاهِدَ فِي سَبيلِ اللهِ ، وَمَا نِيلَ مِنْهُ شَيْءٌ قَطُّ فَيَنْتَقِمَ مِنْ صَاحِبِهِ ، إِلاَّ أن يُنْتَهَكَ شَيْءٌ مِنْ مَحَارِمِ اللهِ تَعَالَى ، فَيَنْتَقِمُ للهِ تَعَالَى . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakupiga kitu chochote kwa mkono wake na wala hakumpiga mwanamke wala mjakazi isipokuwa anapopigana jihadi katika njia ya Allaah. Na hakulipiza kisasi kwa lolote alilofanyiwa yeye isipokuwa inapovukwa mipaka ya Allaah Ta'aalaa, hapo ndio alikuwa akilipiza kisasi." [Muslim] 

 

 

Hadiyth – 3

وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كُنْتُ أمشي مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم وَعَلَيْهِ بُرْدٌ نَجْرَانيٌّ غَلِيظُ الحَاشِيَةِ ، فأدْرَكَهُ أعْرَابِيٌّ فَجَبذَهُ بِرِدَائِهِ جَبْذَةً شَديدةً ، فَنَظَرْتُ إِلَى صَفْحَةِ عَاتِقِ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، وَقَدْ أثَّرَتْ بِهَا حَاشِيَةُ الرِّدَاءِ مِنْ شِدَّةِ جَبْذَتِهِ ، ثُمَّ قَالَ : يَا مُحَمَّدُ ، مُر لِي مِنْ مَالِ اللهِ الَّذِي عِنْدَكَ . فَالتَفَتَ إِلَيْهِ ، فَضَحِكَ ثُمَّ أَمَرَ لَهُ بِعَطَاءٍ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilikuwa nikitembea pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa amevaa shuka la Najran lililokuwa na ugumu pembezoni mwake. Akamkuta njiani Mbedui amabaye alimshika na kumvuta kwa shuka lake hilo kwa nguvu. Nilipomwangalia Nabiy (Swalla allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika shingo yake akiwa ameathirika kwa ule ugumu wa pembezoni wa shuka lake kwa ile nguvu kubwa ya kuvutwa. Kisha alisema: 'Ee Muhammad! Toa amri nipatwe katika ile mali ya Allaah uliyokuwa nayo.' Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwangalia na kucheka, kisha akaamrisha apatiwe sehemu katika mali hiyo." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : كأني أنظر إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم يَحْكِي نَبِيّاً مِنَ الأنبياءِ ، صَلَوَاتُ اللهِ وَسَلامُه عَلَيْهِمْ ، ضَرَبَهُ قَوْمُهُ فَأدْمَوْهُ ، وَهُوَ يَمْسَحُ الدَّمَ عَنْ وَجْهِهِ ، ويقول : ((  اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِقَوْمِي ؛ فَإنَّهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Kana kwamba ninamwangalia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akimzungumzia Nabiy miongoni mwa Manabiy ambaye alipigwa na watu wake mpaka akawa anatoka damu; alipokuwa anaifuta hiyo damu usoni alikuwa anasema: "Ee Mola wangu wasamehe watu wangu kwani wao hawajui." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  لَيْسَ الشَّديدُ بِالصُّرَعَةِ ، إنَّمَا الشَّدِيدُ الَّذِي يَمْلِكُ نَفْسَهُ عِنْدَ الْغَضَبِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye nguvu ni yule amabye anamiliki nafsi yake anaposhikwa na ghadhabu." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

 

 

Share

076-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuvumilia Maudhi

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب احتمال الأذى

076-Mlango Wa Kuvumilia Maudhi

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣٤﴾ 

Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. [Aal-'Imraan: 134]

 

وَلَمَن صَبَرَ وَغَفَرَ إِنَّ ذَٰلِكَ لَمِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ﴿٤٣﴾

Na atakayevuta subira na akasamehe, hakika hilo bila shaka ni katika mambo ya kuazimiwa. [Ash-Shuwraa: 43]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ رَجُلاً ، قَالَ : يَا رسول الله ، إنّ لي قَرَابةً أصِلُهم وَيَقْطَعُونِي ، وَأُحْسِنُ إلَيْهِمْ وَيُسِيئُونَ إلَيَّ ، وَأحْلُمُ عَنهم وَيَجْهَلُونَ عَلَيَّ ! فَقَالَ : ((  لَئِنْ كُنْتَ كَمَا قُلْتَ ، فَكأنَّمَا تُسِفُّهُمُ الْمَلَّ ، وَلاَ يَزَالُ مَعَكَ مِنَ اللهِ تَعَالَى ظَهيرٌ عَلَيْهِمْ مَا دُمْتَ عَلَى ذَلِكَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mtu mmoja alisema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi nina jamaa wa karibu nawaunga, wao wananikata. Nawafanyia wema wao wananitendea uovu, nawafanyia upole wao wananifanyia ujinga." Akasema: "Ukiwa kama uanvyosema basi ni kama unawalisha jivu la moto. Msaada wa Allaah hautaacha kuwa pamoja nawe maadamu utadumu juu ya hilo." [Muslim]

 

 

 

 

Share

077-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuwa na Hasira Wakati Inapokiukwa Hukumu ya Sheria na Kuinusuru Dini ya Allaah Ta'aalaa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب الغضب إِذَا انتهكت حرمات الشّرع والانتصار لدين الله تعالى

077-Mlango Wa Kuwa na Hasira Wakati Inapokiukwa Hukumu ya Sheria na Kuinusuru Dini ya Allaah Ta'aalaa

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّـهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ ۗ  ﴿٣٠﴾

Na yeyote anayeadhimisha vitukufu vya Allaah basi hivyo ni khayr kwake mbele ya Rabb wake. [Al-Hajj: 30]

 

إِن تَنصُرُوا اللَّـهَ يَنصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ﴿٧﴾

Mkisaidia kunusuru Dini ya Allaah, (Allaah) Atakunusuruni na Ataithibitisha miguu yenu. [Muhammad: 7]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي مسعود عقبة بن عمرو البدري  رضي الله عنه ، قَالَ : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : إنِّي لأَتَأخَّرُ عَن صَلاةِ الصُّبْحِ مِنْ أَجْلِ فلانٍ مِمَّا يُطِيلُ بِنَا ! فَمَا رَأيْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم غَضِبَ في مَوْعِظَةٍ قَطُّ أشَدَّ مِمَّا غَضِبَ يَوْمَئذٍ ؛ فَقَالَ : ((  يَا أَيُّهَا النَّاسُ ، إنَّ مِنْكُمْ مُنَفِّرِينَ ، فَأيُّكُمْ أمَّ النَّاسَ فَلْيُوجِزْ ؛ فَإنَّ مِنْ وَرَائِهِ الكَبِيرَ وَالصَّغِيرَ وَذَا الحَاجَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Mas'uwd 'Uqbah bin 'Amru Al-Badriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Mimi ninachelewa Swalaah ya Asubuhi kwa ajili ya fulani anarefusha kisomo." Sijaona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameghadhibika katika mawaidha yoyote kama alivyokasirika siku hiyo. Akasema: "Enyi watu! Hakika miongoni mwenu kuna wenye kufukuza, Anaposwalisha mmoja wenu afupishe, kwani nyuma yake kuna wazee, na watoto wadogo, na wenye haja zao (shughuli zao)." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad].

 

 

Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَدِمَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم مِنْ سَفرٍ ، وَقَدْ سَتَرْتُ سَهْوَةً لِي بِقِرَامٍ فِيهِ تَمَاثيلُ، فَلَمَّا رَآهُ رسول الله صلى الله عليه وسلم هتكَهُ وَتَلَوَّنَ وَجهُهُ ، وقال : ((  يَا عائِشَةُ ، أشَدُّ النَّاسِ عَذَاباً عِنْدَ اللهِ يَوْمَ القيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهُونَ بخَلْقِ اللهِ ! )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Alikuja Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka safari wakati ambao nilikuwa nimeangika pazia nyembamba iliyokuwa na sura (picha) nje ya chumba changu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipoiona hiyo pazia aliiharibu na sura zake zikabadilika, na hapo akasema: "Ee 'Aaishah! Watu watakao pata adhabu kali kutoka kwa Allaah Siku ya Qiyaamah ni wale ambao watakaokuwa wakitengeneza sura kwa mfano wa viumbe vya Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : أن قرَيشاً أهَمَّهُمْ شَأنُ المَرأَةِ المخزومِيَّةِ الَّتي سَرَقَتْ ، فقالوا : مَنْ يُكَلِّمُ فِيهَا رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟ فقالوا : مَنْ يَجْتَرِئ عَلَيْهِ إِلاَّ أُسَامَةُ بنُ زَيْدٍ حِبُّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟ فَكَلَّمَهُ أُسَامَةُ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  أتَشْفَعُ في حَدٍّ مِنْ حُدُودِ الله تَعَالَى ؟! )) ثُمَّ قامَ فَاخْتَطَبَ ، ثُمَّ قَالَ : ((  إنَّمَا أهْلَك مَنْ قَبْلَكُمْ أَنَّهُمْ كَانُوا إِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الشَّرِيفُ تَرَكُوهُ ، وَإِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الضَّعِيفُ أقامُوا عَلَيْهِ الحَدَّ ، وَايْمُ الله ، لَوْ أَنَّ فَاطمَةَ بِنْتَ مُحمّدٍ سَرَقَتْ لَقَطَعتُ يَدَهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Makureshi walishughulishwa na kesi ya mwanamke wa Makhzuum aliyeiba, wakasema: "Hakuna anayeweza kuzungumza naye ila usamah bin Zayd kipenzi cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya jambo hilo?" wakasema: "Hakuna anayeweza kuzungumza naye ila Usamah bin Zayd kipenzi cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)?" Usamah akazungumza naye, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Unamuombea msamaha kwa Hadd (adhabu) miongoni mwa adhabu za Allaah? Kisha akasimama akahutubia akasema: "Hakika waliangamia waliokuwa kabla yenu, walikuwa anapoiba kati yao mtukufu wanamwacha, na anapoiba kati yao dhaifu wanamuadhibu. Naapa kwa Allaah! Lau Faatimah bint Muhammad angeiba basi ningekata mkono wake." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنس رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم رَأى نُخَامَةً في القبلَةِ ، فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَيْهِ حَتَّى رُؤِيَ في وَجْهِهِ ؛ فَقَامَ فَحَكَّهُ بِيَدِهِ ، فَقَالَ : ((  إن أحدَكُمْ إِذَا قَامَ فِي صَلاَتِهِ فَإنَّهُ يُنَاجِي رَبَّهُ ، وَإنَّ رَبَّهُ بَيْنَهُ وَبيْنَ القِبلْةِ ، فَلاَ يَبْزُقَنَّ أحَدُكُمْ قِبَلَ الْقِبْلَةِ ، وَلَكِنْ عَنْ يَسَارِهِ ، أَوْ تَحْتَ قَدَمِهِ )) ثُمَّ أخَذَ طَرَفَ رِدَائِهِ فَبَصَقَ فِيهِ ، ثُمَّ رَدَّ بَعْضَهُ عَلَى بَعْضٍ ، فَقَالَ : ((  أَوْ يَفْعَلُ هكذا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliona kohozi kwenye Qiblah, Jambo hilo lilimkera mpaka likaonekana katika uso wake akasimama akalikwangua kwa mkono wake, Akasema: "Hakika mmoja wenu anaposimama katika Swalaah yake anazungumza na Rabb wake, na Rabb wake yuko baina yake na Qiblah. Hivyo, asiteme mmoja wenu sehemu ya Qiblah , lakini ateme kushotoni mwake au chini ya unyao wake." Kisha akashika ncha ya shuka yake juu ya nyingine akasema: "Au anaweza kufanya hivi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

078-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Jukumu la Viongozi Kuamiliana na Watu kwa Upole, Kuwanasihi, Kuwahurumia, Kukatazwa Kuwadanganya, Kuwawekea Vikwazo Bila Kuangalia Maslahi yao, Kughafilika Nao na Kutowatimizia Haja zao

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

 

باب أمر وُلاة الأمور بالرفق برعاياهم ونصيحتهم والشفقة عليهم والنهي عن غشهم والتشديد عليهم وإهمال مصالحهم والغفلة عنهم وعن حوائجهم

078-Mlango Wa Jukumu la Viongozi Kuamiliana na Watu kwa Upole, Kuwanasihi, Kuwahurumia, Kukatazwa Kuwadanganya, Kuwawekea Vikwazo Bila Kuangalia Maslahi yao, Kughafilika Nao na Kutowatimizia Haja zao

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢١٥﴾

Na inamisha ubawa wako kwa anayekufuata miongoni mwa Waumini. [Ash-Shu'araa: 215]

 

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚ يَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ﴿٩٠﴾

Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini ili huenda mkapata kukumbuka. [An-Nahl: 90]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  كُلُّكُمْ رَاعٍ ، وَكُلُّكُمْ مَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتهِ : الإمَامُ رَاعٍ وَمَسؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَالرَّجُلُ رَاعٍ في أهلِهِ وَمَسؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَالمَرْأَةُ رَاعِيَةٌ في بَيْتِ زَوْجِهَا وَمَسْؤُولَةٌ عَنْ رَعِيَّتِهَا ، وَالخَادِمُ رَاعٍ في مال سيِّدِهِ وَمَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ ، وَكُلُّكُمْ رَاعٍ وَمَسْؤُولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swaalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila mmoja ana majukumu (na ataulizwa) kwa wale walioko chini yake. Amiri ni mchunga na mwanamume ni mchunga kwa watu wake wa nyumbani na mke ni mchunga katika nyumba ya mumewe na watoto wake. Hivyo, kila mmoja wenu ni mchunga, na ataulizwa juu ya alichokichunga." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad].

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي يعلى مَعْقِل بن يَسارٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  مَا مِنْ عَبْدٍ يَستَرْعِيهِ اللهُ رَعِيَّةً ، يَمُوتُ يَوْمَ يَمُوتُ وَهُوَ غَاشٌّ لِرَعِيَّتِهِ ، إِلاَّ حَرَّمَ اللهُ عَلَيْهِ الجَنَّة )) متفقٌ عليه .

وفي رواية : ((  فَلَمْ يَحُطْهَا بِنُصْحِهِ لَمْ يَجِدْ رَائِحَةَ الجَنَّة )) .

وفي رواية لمسلم : ((  مَا مِنْ أميرٍ يلي أمور المُسْلِمينَ ، ثُمَّ لا يَجْهَدُ لَهُمْ وَيَنْصَحُ لَهُمْ ، إِلاَّ لَمْ يَدْخُلْ مَعَهُمُ الْجَنَّةَ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Ya'laa Ma'qil bin Yasaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakuna mja yeyote Allaah anampa uchungu wa raia wake, akafa siku anayokufa ameghushi raiawake, isipokuwa Allaah anamharimishia Pepo." [Al-Bukhaariy na Muslim].

Katika riwaayah nyingine: "Hakuwatizama kwa nasaha zake hatapata harufu ya Pepo." 

Katika riwaayah ya Muslim: "Hakuna Amiri anasimamia mambo ya Waislamu, kisha hakuwafanyia juhudi na hakuwanasihi, Isipokuwa hataingia pamoja nao Peponi." 

 

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول في بيتي هَذَا : ((  اللَّهُمَّ مَنْ وَلِيَ مِنْ أمْرِ أُمَّتِي شَيْئاً فَشَقَّ عَلَيْهِمْ ، فاشْقُقْ عَلَيْهِ ، وَمَنْ وَلِيَ مِنْ أَمْرِ أُمَّتِي شَيْئاً فَرَفَقَ بِهِمْ ، فَارفُقْ بِهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema katika nyumba yangu hii: "Ee Rabb wangu! Mwenye kusimamia chochote katika Ummah wangu, akawafanyia uzito. Mfanyie uzito. Na mwenye kusimamia chochote katika Ummah wangu, akawahurumia, Nawe mhurumie." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  كَانَتْ بَنُو إسرَائِيلَ تَسُوسُهُم الأَنبِيَاء ، كُلَّمَا هَلَكَ نَبِيٌّ خَلَفَهُ نَبيٌّ ، وَإنَّهُ لاَ نَبِيَّ بَعْدِي ، وَسَيكُونُ بَعْدِي خُلفَاءُ فَيَكثرُونَ )) ، قالوا : يَا رسول الله ، فَمَا تَأْمُرُنَا ؟ قَالَ : ((  أَوْفُوا بِبَيْعَةِ الأَوَّل فَالأَوَّل ، ثُمَّ أعْطُوهُمْ حَقَّهُمْ ، وَاسْأَلُوا الله الَّذِي لَكُمْ ، فَإنَّ اللهَ سَائِلُهُمْ عَمَّا اسْتَرْعَاهُمْ )) متفقٌ عليه .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Uongozi miongoni mwa Bani Israaiyl ulikuwa ukitekelezwa na Manabiy. Kila anapofariki Nabiy, Nabiy mwengine alikuwa akichukua mahali pake. Na hakika hakuna Nabiy baada yangu na kutakuwa baada yangu Makhalifa ambao watakuwa wengi." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Unatuamuru tufanye nini?" Akasema: "Kuweni watiifu kwao mmoja baada ya mwengine, kisha wapatieni haki yao na muombeni Allaah kwa mambo yenu. Hakika Allaah atawauliza kwa kile walicho chunga." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Hadiyth – 5

وعن عائِذ بن عمرو رضي الله عنه : أَنَّهُ دَخَلَ عَلَى عُبَيْد اللهِ بن زيادٍ ، فَقَالَ    لَهُ : أيْ بُنَيَّ ، إنِّي سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  إنَّ شَرَّ الرِّعَاءِ الحُطَمَةُ )) فإيَاكَ أن تَكُونَ مِنْهُمْ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaidh bin 'Amru (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alimtembelea 'Ubaydullaah bin Ziyaad na kumwambia: "Ee mtoto wangu, hakika nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: 'Hakika viongozi wabaya kabisa ni wale wakali (kwa raia zao). Hivyo, kuwa na tahadhari usiwe miongoni mwao." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي مريم الأزدِيِّ رضي الله عنه : أنّه قَالَ لِمعاوية رضي الله عنه : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  مَنْ وَلاَّهُ اللهُ شَيْئاً مِنْ أُمُورِ المُسْلِمِينَ ، فَاحْتَجَبَ دُونَ حَاجَتِهِمْ وَخَلَّتِهِمْ وَفَقْرِهِمْ ، احْتَجَبَ اللهُ دُونَ حَاجَتِهِ وَخَلَّتِهِ وَفَقْرِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ )) فجعل معاوية رجلاً عَلَى حوائج النَّاسِ . رواه أَبُو داود والترمذي .

Imepokewa kutoka kwa Abu Maryam Al-Azdiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba alimwambia Mu'aawiyah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Yeyote ambaye Allaah atamchagua kuwaongoza Waislamu katika mambo yao na akashindwa kutatua shida zao na kuwaondoshea ufakiri wao, Allaah hatamtizama haja zake (wala hatamjibu dua yake) na kumuondoshea hali yake na ufakiri wake Siku ya Qiyaamah." Hivyo, Mu;aawiyah alimchagua mtu kuangalia haja za watu." [Abuu Daawuud na at-Tirmidhiy]

 

 

 

Share

079-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kiongozi Muadilifu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الوالي العادل

079-Mlango Wa Kiongozi Muadilifu

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ ﴿٩٠﴾

Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan. [An-Nahl: 90]

وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٩﴾

Hakika Allaah Anapenda wanaotimiza haki. [Al-Hujuraat: 9]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  سَبْعَةٌ يُظِلُّهُمُ الله في ظِلِّهِ يَوْمَ لاَ ظِلَّ إِلاَّ ظِلُّهُ : إِمَامٌ عادِلٌ ، وَشَابٌ نَشَأ في عِبادة الله تَعَالَى ، وَرَجُلٌ قَلْبُهُ مُعَلَّقٌ في المَسَاجِدِ ، وَرَجُلانِ تَحَابَّا في اللهِ اجتَمَعَا عَلَيْهِ ، وَتَفَرَّقَا عَلَيْهِ ، وَرَجُلٌ دَعَتْهُ امْرَأةٌ ذاتُ مَنْصِبٍ وجَمالٍ ، فَقَالَ : إنّي أخافُ اللهَ ، وَرَجُلٌ تَصَدَّقَ بِصَدَقَةٍ فَأخْفَاهَا حَتَّى لاَ تَعْلَمَ شِمَالُهُ مَا تُنْفِقُ يَمِينُهُ ، وَرَجُلٌ ذَكَرَ الله خَالِياً فَفَاضَتْ عَيْنَاهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "(Watu) saba Allaah atawafunika chini ya kivuli Chake siku isio na kivuli isipokuwa kivuli Chake: Imamu muadilifu, na kijana ameinukia katika kumuabudu Allaah, na mtu moyo wake umefungamana na Misikiti, na watu wawili wamependana kwa ajili ya Allaah, wamejumuika juu yake na kufarikiana juu yake, na mtu ameitwa na mwanamke mwenye hadhi na uzuri, akasema: 'Mimi namwogopa Allaah', na mtu ametoa swadaqah akaificha hadi kushoto kwake kusijue kilichotoa kulia kwake, na mtu ambaye amemtaja Allaah peke yake na macho yake yakabubujika machozi." [Al-Bukaariy na muslim].

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبدِ اللهِ بن عَمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّ المُقْسِطِينَ عِنْدَ اللهِ عَلَى مَنَابِرَ مِنْ نُورٍ : الَّذِينَ يَعْدِلُونَ في حُكْمِهِمْ وأَهْلِيْهِم وَمَا وَلُوْا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amru bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika waadilifu watakuwa juu ya mimbari za nuru mbele ya Allaah: Ambao wanafanya uadilifu katika hukumu zao na familia zao, na waliyotawalishwa." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن عوفِ بن مَالِكٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  خِيَارُ أئِمَّتِكُمُ الَّذِينَ تُحِبُّونَهُمْ وَيُحِبُّونَكُمْ ، وَتُصَلُّونَ عَلَيْهِمْ وَيُصَلُّونَ عَلَيْكُمْ . وشِرَارُ أئِمَّتِكُم الَّذِينَ تُبْغِضُونَهُمْ وَيُبْغِضُونَكُمْ ، وَتَلعَنُونَهُمْ وَيَلْعَنُونَكُمْ ! )) ، قَالَ : قُلْنَا : يَا رسول اللهِ ، أفَلاَ نُنَابِذُهُم ؟ قَالَ : ((  لاَ ، مَا أقَامُوا فِيْكُمُ الصَّلاَةَ . لاَ ، مَا أقَامُوا فِيكُمُ الصَّلاَةَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Awf bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Wabora wa viongozi wenu ni ambao mnawapenda na wao wanawapenda, na mnawaombea na wao wanawaombea. Na waovu wa viongozi wenu ni mnaowachukia na wao wanawachukia, na ambao mnawalaani na wao wanawalaani." Akasema: "Tukasema: Ee Rasuli wa Allaah! "Tujitenge nao?" Akasema: "La! Madamu wamesimamisha Swalaah kati yanu. La! Madamu wamesimamisha Swallaah kati yenu." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن عِياضِ بن حِمارٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( أهلُ الجَنَّةِ ثَلاَثَةٌ : ذُو سُلطانٍ مُقْسِطٌ مُوَفَّقٌ ، وَرَجُلٌ رَحيمٌ رَقِيقُ القَلْبِ لكُلِّ ذي قُرْبَى ومُسْلِمٍ ، وعَفِيفٌ مُتَعَفِّفٌ ذو عِيالٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Iyaadh bin Himaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Watu wa Peponi ni aina tatu: Kiongozi muadilifu mwenye kutoa swadaqah kwa uwezo wake; na mtu mwenye kuwarehemu na mwenye moyo laini kwa kila jamaa yake na kwa kila Muislamu; na mtoharifu anyejizuilia na uchafu (asiezini) mwenye familia." [Muslim].

 

 

 

Share

080-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Wajibu wa Kuwatii Viongozi kwa Mambo Yasiyo ya Maasiya na Kukatazwa Kuwatii Katika Maasiya

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب وجوب طاعة ولاة الأمر في غير معصية وتحريم طاعتهم في المعصية

080-Mlango Wa Wajibu wa Kuwatii Viongozi kwa Mambo Yasiyo ya Maasiya na Kukatazwa Kuwatii Katika Maasiya

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

أَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَأُولِي الْأَمْرِ مِنكُمْ ۖ  ﴿٥٩﴾

Mtiini Allaah na mtiini Rasuli na wenye madaraka katika nyinyi. [An-Nisaa: 59]

 

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  عَلَى المَرْءِ الْمُسْلِمِ السَّمْعُ والطَّاعَةُ فِيمَا أحَبَّ وكَرِهَ ، إِلاَّ أنْ يُؤْمَرَ بِمَعْصِيةٍ ، فَإذَا أُمِرَ بِمَعْصِيةٍ فَلاَ سَمْعَ وَلاَ طَاعَةَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kusikia na kutii ni wajibu kwa kila Muislamu katika alichokipenda na alicho kichukia, kwa muda ambao hakuamrishwa kufanya maasi. Kama ataamrishwa kufanya maasi basi hakuna kusikia wala kutii." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud, At-Tirmidhiy na An-Nasai].

 

 

Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : كُنَّا إِذَا بَايَعْنَا رسولَ الله صلى الله عليه وسلم عَلَى السَّمعِ والطَّاعَةِ ، يَقُولُ لَنَا : ((  فِيمَا اسْتَطَعْتُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba amesema: Tulipokuwa tukimbai Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya kusikia na kutii alikuwa akituambia: "Kwa mnayo weza." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  مَنْ خَلَعَ يَداً مِنْ طَاعَةٍ لَقِيَ اللهَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلاَ حُجَّةَ لَهُ ، وَمَنْ مَاتَ وَلَيْسَ في عُنُقِهِ بَيْعَةٌ ، مَاتَ مِيتَةً جَاهِلِيَّةً )) رواه مسلم .

وفي رواية لَهُ : ((  وَمَنْ مَاتَ وَهُوَ مُفَارِقٌ لِلجَمَاعَةِ ، فَإنَّهُ يَمُوتُ مِيتَةً   جَاهِلِيَّةً )) .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kuondosha mkono katika kutii atamkuta Allaah Siku ya Qiyaamah hana hoja. Na atakaye kufa na shingoni mwake hana bai'ah amekufa mauti ya kijahiliya. [Muslim]

Na katika riwaayah yake nyingine: "Na atakaye kufa naye amejitenga na jamaa (kikundi cha waislamu), hakika atakufa mauti ya ujahiliyyah."

 

 

Hadiyth – 4

وعن أنسٍ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  اسْمَعُوا وأطِيعُوا ، وَإنِ استُعْمِلَ عَلَيْكُمْ عَبْدٌ حَبَشيٌّ ، كأنَّ رأْسَهُ زَبيبةٌ )) رواه البخاري .

Imepokewa kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Sikieni na mutii, japokuwa atachaguliwa juu yenu kama kiongozi mtumwa wa Habeshi (Ethiopia) kama kwamba kichwa chake kimefanana na zabibu." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 5

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  عَلَيْكَ السَّمْعُ وَالطَّاعَةُ في عُسْرِكَ وَيُسْرِكَ ، وَمَنْشَطِكَ وَمَكْرَهِكَ ، وَأثَرَةٍ عَلَيْكَ )) رواه مسلم .

Kutoka kwa abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ni juu yako kusikia na kutii katika utajiri wako na umasikini na uwe muaminifu." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 6

وعن عبدِ اللهِ بن عمرو رضي الله عنهما ، قَالَ : كنا مَعَ رسول الله صلى الله عليه وسلم في سَفَرٍ ، فَنَزَلْنَا مَنْزِلاً ، فَمِنَّا مَنْ يُصْلِحُ خِبَاءهُ ، وَمِنّا مَنْ يَنْتَضِلُ ، وَمِنَّا مَنْ هُوَ في جَشَرِهِ ، إذْ نَادَى مُنَادِي رسولِ الله صلى الله عليه وسلم : الصَّلاةَ جَامِعَةً . فَاجْتَمَعْنَا إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : ((  إنَّهُ لَمْ يَكُنْ نَبيٌّ قَبْلِي إِلاَّ كَانَ حَقّاً عَلَيْهِ أنْ يَدُلَّ أُمَّتَهُ عَلَى خَيْرِ مَا يَعْلَمُهُ لَهُمْ ، وَيُنْذِرَهُم شَرَّ مَا يَعْلَمُهُ لَهُمْ . وَإنَّ أُمَّتَكُمْ هذِهِ جُعِلَ عَافِيَتُهَا في أوَّلِهَا ، وَسَيُصيبُ آخِرَهَا بَلاَءٌ وَأمُورٌ تُنْكِرُونَهَا ، وَتَجِيءُ فِتنَةٌ يُرَقِّقُ بَعْضُهَا بَعْضاً ، وَتَجِيءُ الفتنَةُ فَيقُولُ المُؤْمِنُ : هذه مُهلكتي ، ثُمَّ تنكشفُ ، وتجيء الفتنةُ فيقولُ المؤمنُ : هذِهِ هذِهِ . فَمَنْ أحَبَّ أنْ يُزَحْزَحَ عَنِ النَّارِ، ويُدْخَلَ الجَنَّةَ، فَلْتَأتِهِ منيَّتُهُ وَهُوَ يُؤْمِنَ باللهِ واليَوْمِ الآخِرِ ، وَلْيَأتِ إِلَى النَّاسِ الَّذِي يُحِبُّ أنْ يُؤتَى إِلَيْهِ. وَمَنْ بَايَعَ إمَاماً فَأعْطَاهُ صَفْقَةَ يَدِهِ ، وَثَمَرَةَ قَلْبِهِ ، فَلْيُطِعْهُ إن استَطَاعَ ، فإنْ جَاءَ آخَرُ يُنَازِعُهُ فَاضْرِبُوا عُنْقَ الآخَرِ )) رواه مسلم .

Kutoka kwa 'Abdillah bin 'Amru (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) safarini, tukashuka mahali. Katika sisi kuna anaetengeneza hema lake, katika sisi kuna wanaoshindana, mwengine anailisha mifugo yake. Mwitaji wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Swalaah ya jamaa," Tukakusanyika mbele ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), akasema: "Hakika hakukuwa Nabiy kabla yangu ila ilikuwa ni haki yake kuonyesha Ummah wake kheri anayoijua kwa ajili yao, Na kuwaonya shari anayoijua kwa ajili yao. Hakika Umma wenu huu afya yake iko katika wa mwanzo wake, Na wa mwisho wake utapata balaa na mambo mnayo yakataa. Na itakuja fitna moja baada ya nyingine. Itakuja fitna Muumini atasema: 'Haya ni maangamivu yangu. Kisha itatoweka, na itakuja fitina muumini atasema: 'Ni haya haya Haya." Hivyo, anayependa kuepushwa na Moto na kuingizwa Peponi, Basi akutane na kifo chake akiwa anamuamini Allaah na Siku ya Mwisho, na awaletee watu ambao anapenda waletwe kwake. Na mwenye kumbai Imamu kwa kumpatia ahadi kwa mkono wake na tunda la moyo wake, Basi amtii anavyoweza. Akija mwingine kushindana naye, Basi ipigeni shingo ya yule Mwingine." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 7

وعن أَبي هُنَيْدَةَ وَائِلِ بن حُجرٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَألَ سَلَمَةُ بن يَزيدَ الجُعفِيُّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : يَا نَبِيَّ الله ، أرأيتَ إنْ قامَت عَلَيْنَا أُمَرَاءُ يَسألُونَا حَقَّهُم ، وَيمْنَعُونَا حَقَّنَا ، فَمَا تَأْمُرُنَا ؟ فَأعْرَضَ عنه ، ثُمَّ سَألَهُ ، فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  اسْمَعْوا وَأَطِيعُوا ، فإنَّمَا عَلَيْهِمْ مَا حُمِّلُوا ، وَعَلَيْكُمْ مَا حملْتُمْ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hunaydah Waail bin Hujr (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Salamah bin Yaziyd Al-Ju'fiy alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kusema: "Ee Nabiy wa Allaah! Waonaje wakisimama juu yetu viongozi wakitaka haki zao na kukataa zetu, unatuamuru nini?" Nabiy alijiepusha na kujibu swalihilo. Kisha alimuuliza mara nyengine, hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Sikieni na mtii, hakika wao watabeba mzigo waliojitikwa nanyi mtabeba wenu." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 8

وعن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّهَا سَتَكُونُ بَعْدِي أثَرَةٌ وَأُمُورٌ تُنْكِرُونَهَا ! )) قالوا : يَا رسول الله ، كَيْفَ تَأمُرُ مَنْ أدْرَكَ مِنَّا ذَلِكَ ؟ قَالَ : ((  تُؤَدُّونَ الحَقَّ الَّذِي عَلَيْكُمْ ، وَتَسْأَلُونَ اللهَ الَّذِي لَكُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kutakuwa na ubinafsi na mambo msiyoyakubali." Wakauliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Unatuamuru nini kwa yule atakaye fikiwa na hayo?" Akajibu: "Tekelezeni wajibu wenu na mumuombe Allaah (Awapeni) ambalo ni haki yenu." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Hadiyth – 9

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  مَنْ أطَاعَنِي فَقَدْ أطَاعَ اللهَ ، وَمَنْ عَصَانِي فَقَدْ عَصَى اللهَ ، وَمَنْ يُطِعِ الأَمِيرَ فَقَدْ أطَاعَنِي ، وَمَنْ يَعصِ الأميرَ فَقَدْ عَصَانِي )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kunitii mimi basi amemtii Allaah na mwenye kuniasi mimi basi amemuasi Allaah. Na mwenye kumtii amiri (kiongozi) basi amenitii mimi na mwenye kumuasi amiri basi ameniasi mimi." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 10

وعن ابن عباسٍ رضي الله عنهما : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَنْ كَره مِنْ أمِيرِهِ شَيْئاً فَلْيَصْبِرْ ، فَإنَّهُ مَنْ خَرَجَ مِنَ السُّلطَانِ شِبْراً مَاتَ مِيتَةً جَاهِلِيَّةً )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuchukia kwa amiri wake kitu basi asubiri, kwa sababu mwenye kutoka nje ya utawala wa amiri shubiri moja amekufa kifo cha kijahiliya (kikafiri)." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]

 

 

Hadiyth – 11

وعن أَبي بكرة رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  مَنْ أهانَ السُّلطَانَ أَهَانَهُ الله )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Bakrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Alaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Yeyote mwenye kumtweza kiongozi Allaah atamtweza." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

 

 

 

Share

081-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukatazwa Kuomba Uongozi na Kuchagua

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب النهي عن سؤال الإمارة واختيار ترك الولايات إذا لَمْ يتعين عليه أَوْ تَدْعُ حاجة إِلَيْهِ

081-Mlango Wa Kukatazwa Kuomba Uongozi na Kuchagua

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

تِلْكَ الدَّارُ الْآخِرَةُ نَجْعَلُهَا لِلَّذِينَ لَا يُرِيدُونَ عُلُوًّا فِي الْأَرْضِ وَلَا فَسَادًا ۚ وَالْعَاقِبَةُ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٨٣﴾

Hiyo ni nyumba ya Aakhirah, Tunaijaalia kwa wale wasiotaka kujitukuza katika ardhi na wala ufisadi. Na hatima njema ni kwa wenye taqwa. [Al-Qaswasw: 83]

 

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي سعيدٍ عبدِ الرحمانِ بن سَمُرَة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  يَا عَبْدَ الرَّحمان بن سَمُرَةَ ، لاَ تَسْأَلِ الإمَارَةَ ؛ فَإنّكَ إن أُعْطِيتَهَا عَنْ غَيْرِ مَسْألَةٍ أُعِنْتَ عَلَيْهَا ، وَإنْ أُعْطِيتَهَا عَنْ مَسْألَةٍ وُكِلْتَ إِلَيْهَا ، وَإِذَا حَلَفْتَ عَلَى يَمِينٍ ، فَرَأيْتَ غَيْرَهَا خَيْراً مِنْهَا ، فَأتِ الَّذِي هُوَ خَيْرٌ وَكَفِّرْ عَنْ يَمِينكَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd 'Abdir-Rahmaan bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Aliniambia mimi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ee 'Abdir-Rahmaan bin Samurah! Usiombe uongozi, hakika kama utapewa bila kuuomba utasaidiwa juu yake, na ukipewa kwa kuuomba utatelekezwa nao, na ukiapa juu ya yamini na ukaona vinginevyo ni bora basi lete ambalo ni kheri na toa kafara la yamini yako." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud, At-Tirmidhiy, An-Nasai na Ahmad].

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي ذرٍّ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  يَا أَبَا ذَرٍّ ، إنِّي أرَاكَ ضَعِيفاً ، وَإنِّي أُحِبُّ لَكَ مَا أُحِبُّ لِنَفْسِي . لاَ تَأمَّرَنَّ عَلَى اثْنَيْنِ ، وَلاَ تَوَلَّيَنَّ مَالَ يَتِيمٍ )) رواه مسلم .

Toka kwa Abu Dharr amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Ee Aba Dharr! Hakika mimi nakuona udhaifu, Hakika mimi nakupendelea nipendelealo nafsi yangu. Usitake uongozi hata kuongoza watu wawili wala usisimamie mali ya yatima." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي ذرٍّ رضي الله عنه ، قَالَ : قُلْتُ : يَا رسول الله ، ألا تَسْتَعْمِلُني ؟ فَضَرَبَ بِيَدِهِ عَلَى مَنْكِبي ، ثُمَّ قَالَ : ((  يَا أَبَا ذَرٍّ ، إنَّكَ ضَعِيفٌ ، وإنّها أمانةٌ ، وَإنَّهَا يَوْمَ الْقِيَامَةِ خِزْيٌ وَنَدَامَةٌ ، إِلاَّ مَنْ أخَذَهَا بِحَقِّهَا ، وَأدَّى الَّذِي عَلَيْهِ فِيهَا )) رواه مسلم .

Toka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): Kwa nini hunipi uongozi? Akanipiga Kofi kwa mkono wake mabega yangu, kisha akasema: "Ee Abu Dharr! Hakika wewe ni dhaifu, na hiyo ni amana, nao Siku ya Qiyaamah ni hizaya na majuto, ila mwenye kuuchukua kwa haki yake, na akatekeleza yanayo pasa ndani yake." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  إنَّكُمْ سَتَحْرِصُونَ عَلَى الإمَارَةِ ، وَسَتَكونُ نَدَامَةً يَوْمَ القِيَامَةِ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika nyinyi mutakuwa munapupia uongozi na utakuwa juu yenu Siku ya Qiyaamah ni majuto." [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Share

082-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuhimizwa Viongozi, Maqdhi na Wengineo Kuchagua Washauri na Mawaziri Wazuri na Wema na Kuonywa Kuwa na Marafiki Wabaya na Kuwakubali

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب حث السلطان والقاضي وغيرهما من ولاة الأمور عَلَى اتخاذ وزير صالح وتحذيرهم من قرناء السوء والقبول منهم

082-Mlango Wa Kuhimizwa Viongozi, Maqdhi na Wengineo Kuchagua Washauri na Mawaziri Wazuri na Wema na Kuonywa Kuwa na Marafiki Wabaya na Kuwakubali

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

الْأَخِلَّاءُ يَوْمَئِذٍ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ عَدُوٌّ إِلَّا الْمُتَّقِينَ﴿٦٧﴾

Marafiki wapenzi Siku hiyo watakuwa maadui wao kwa wao isipokuwa wenye taqwa. [Az-Zukhruf: 67]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي سعيدٍ وأبي هريرة رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  مَا بَعَثَ اللهُ مِنْ نَبِيٍّ ، وَلاَ اسْتَخْلَفَ مِنْ خَليفَةٍ إِلاَّ كَانَتْ لَهُ بِطَانَتَانِ : بِطَانَةٌ تَأمُرُهُ بالمَعْرُوفِ وتَحُضُّهُ عَلَيْهِ ، وَبِطَانَةٌ تَأمُرُهُ بالشَّرِّ وَتَحُضُّهُ عَلَيْهِ ، وَالمَعْصُومُ مَنْ عَصَمَ اللهُ ))رواه البخاري .

Kutoka kwa Abu Sa'iyd na Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah hakumtuma Nabiy yeyote wala hakumchagua Khalifa isipokuwa walikuwa na washauri wawili, mmoja alikuwa akimuamrisha mema na akimhimiza kwayo na mwengine akimuamrisha shari na kumhimiza kwayo. Na mtu asiyekuwa na hatia ni yule anayehifadhiwa na Allaah kutofanya madhambi." [Al-Bukhaariy].

 

 

Hadiyth – 2

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  إِذَا أرَادَ اللهُ بِالأَمِيرِ خَيْراً ، جَعَلَ لَهُ وَزِيرَ صدقٍ ، إنْ نَسِيَ ذَكَّرَهُ ، وَإنْ ذَكَرَ أعَانَهُ ، وَإِذَا أرَادَ بِهِ غَيْرَ ذَلِكَ جَعَلَ لَهُ وَزِيرَ سُوءٍ ، إنْ نَسِيَ لَمْ يُذَكِّرْهُ ، وَإنْ ذَكَرَ لَمْ يُعِنْهُ )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ جيدٍ عَلَى شرط مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah anapoktakia kheri kiongozi, anamjalia yeye waziri mkweli (mzuri) ambaye anamkumbusha anaposahau na anapokumbuka basi humsaidia. Na anapomtakia kinyume na hilo (yaani shari), anamjaalia waziri mbaya ambaye hamkumbushi anaposahau na anapokumbuka basi hamsaidii." [Abuu-Daawuud, na Isnaad yake ni Jayd (nzuri) kwa sharti ya Muslim].

 

 

 

Share

083-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kukataza Kumpatia Uongozi na Ukadhi na Nyadhifa Nyinginezo za Uongozi kwa Mwenye Kuomba Ama Kupupia

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب النهي عن تولية الإمارة والقضاء وغيرهما من الولايات لمن سألها أَوْ حرص عليها فعرَّض بها

083-Mlango Wa Kukataza Kumpatia Uongozi na Ukadhi na Nyadhifa Nyinginezo za Uongozi kwa Mwenye Kuomba Ama Kupupia

 

Alhidaaya.com

 

 

عن أَبي موسى الأشعريِّ رضي الله عنه ، قَالَ : دَخَلْتُ عَلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم أنَا وَرَجُلانِ مِنْ بَنِي عَمِّي ، فَقَالَ أحَدُهُمَا : يَا رسول الله ، أمِّرْنَا عَلَى بَعْض مَا ولاَّكَ اللهُ (عزّ وجلّ) ، وقال الآخَرُ مِثلَ ذَلِكَ ، فَقَالَ : ((  إنَّا وَاللهِ لاَ نُوَلِّي هَذَا العَمَلَ أحَداً سَألَهُ ، أَوْ أحَداً حَرَصَ عَلَيْهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilienda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) nikiwa na watu wawili katika watoto wa ami zangu. Akasema mmoja wao: "Ee Rasuli wa Allaah! Tupe uongozi kwa baadhi ya aliyokutawalisha Allaah ('Azza wa Jalla)." Mwingine akasema mfano wake, Akasema: "Wa-Allaahi, sisi hatumpi kazi yeyote anayeomba au yeyote mwenye kuonyesha dalili ya kupupia." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasai].

 

 

 

Share