Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake: أسماء الله الحسنى وصفاته

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

000-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: Utangulizi

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

000-Utangulizi

 

 

بِسْمِ الله الرَّحْمنِ الرَّحِيم

الْحمْدُ لِلَّه وَالصَّلاةُ وَالسِّلامُ عَلى خَاتم الأنْبِيَاء وَالْمُرْسَلِين، الْمَبْعُوثُ رَحْمَةً لِلْعَالَمِين، مُحَمَّد وَعَلى آلِه وَأصْحابِه أجْمَعِين وَمَنْ تَبِعَهُمْ بِإِحْسَانٍ إِلَى يَوْمِ الدِّينِ.

 

Himdi zote Anastahiki Allaah, Swalaah na Salaam ziwe juu ya Nabiy na Rasuli wa mwisho, aliyetumwa awe rahmah kwa walimwengu, Muhammad, pamoja na ahli zake na Maswahaba zake wote, na wanaowafuata kwa ihsaan mpaka Siku ya Malipo.

 

Al-Asmaaul-Husnaa imetajwa mara nne katika Qur-aan katika kauli zifuatazo za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

قُلِ ادْعُوا اللَّـهَ أَوِ ادْعُوا الرَّحْمَـٰنَ ۖ أَيًّا مَّا تَدْعُوا فَلَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ۚ

Sema; “Muiteni Allaah au muiteni Ar-Rahmaan (Mwingi wa Rahmah). Vyovyote mtakavyomwita basi Yeye Ana Majina Mazuri kabisa. [Al-Israa 17: 110]

 

Na pia:

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ﴿٨﴾

Allaah, hapana ilaaha (muabudiwa wa haki) ila Yeye. Anayo Majina Mazuri kabisa.[Twaahaa 20: 7-8]

Na:

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٨٠﴾

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanaopotoa katika Majina Yake, watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda. [Al-A’raaf 7: 180]

 

Na pia:

 

هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ۚ يُسَبِّحُ لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٢٤﴾

Yeye Ndiye Allaah, Muumbaji, Mwanzishi viumbe bila kasoro, Muundaji sura na umbile, Ana Majina Mazuri kabisa, kinamsabbih Pekee viliyoko katika mbingu na ardhi, Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote.  [Al-Hashr (59:22-24)]

 

Kumpwekesha Allaah Katika Majina Yake Na Kuthibitisha Sifa Za Allaah (سبحانه وتعالى) Na Ndio Aqiydah Ya Ahlus-Sunnah Wal-Jamaa’ah Kuhusiana Na Majina Mazuri Kabisa Ya Allaah (سبحانه وتعالى) Na Sifa Zake:

 

Aqiydah ya Ahlus-Sunnah wal-Jamaa’ah kuhusiana na Majina Mazuri kabisa ya Allaah (سبحانه وتعالى) na Sifa Zake ni Tawqiyfiyyah;  Yanathibitishwa Aliyoyathibitisha Mwenyewe Allaah (سبحانه وتعالى) katika Qur-aan na Sunnah bila kuzifanyia Ta'twiyl (kuzipinga, kukanusha uwezekano), wala Tamthiyl (kumithilisha, kufafanisha, kulinganisha), wala Takyiyf (kuainisha maana na kuziulizia namna yake au kuuliza ni vipi Sifa hiyo ipo, kuchunguza ni kwa “namna gani” zimefungamana au kuambatana na Allaah), wala Tahriyf (kubadilisha maana, kupotosha Sifa ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kutoa maana isiyo sahihi).

 

Hivyo basi, Allaah (سبحانه وتعالى) Anaposema kuwa Ana Qudra (Uwezo), na sisi tunaamini kuwa Anao Uwezo. Anaposema Yeye ni Qawiyy (Mwenye Nguvu), na sisi tunaamini kuwa Ana nguvu. Anaposema kuwa Anaona, na sisi tunaamini kuwa Anaona. Anaposema kuwa Anasikia, na sisi tunaamini kuwa Anasikia. Lakini Sifa hizo za Uwezo Wake, au Nguvu Zake, au Kuona Kwake au Kusikia Kwake hazifanani kabisa na kiumbe chochote kile! Na Anaposema kuwa Anayo Macho, na sisi tunaamini kuwa Anayo Macho. Na Anaposema kuwa Anayo Mikono na sisi tunaamini kuwa Anayo Mikono, na Anaposema kuwa Anao Wajihi, na sisi tunaamini kuwa Anao Wajihi. Lakini Macho Yake au Masikio Yake au Wajihi Wake, hakuna kabisa mfano Wake kwa kiumbe chochote kile kama Anavyosema (سبحانه وتعالى):

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ ﴿١١﴾

Hakuna chochote kinachofanana Naye, Naye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ash-Shuwraa 42: 11]

 

Kwa hiyo Anapotujulisha kuwa Yeye ni Al-‘Aliym (Mjuzi wa yote daima), hatuwezi kusema hivyo kwa bin Aadam. Na kadhalika hatuwezi pia kufananisha Sifa Zake nyinginezo kwa kiumbe chochote kile wala kumfananisha au kumlinganisha, au kumshabihisha Yeye kwa dhati Yake au Sifa Zake na yeyote yule  Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

فَلَا تَضْرِبُوا لِلَّـهِ الْأَمْثَالَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿٧٤﴾

Basi msimpigie mifano Allaah! Hakika Allaah Anajua nanyi hamjui. [An-Nahl 16: 74]

 

Kutokuzithibitisha sifa ambazo Mwenyewe Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amejipa ni kuzigeuza na kuzipotoa; Anaonya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa): 

 

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٨٠﴾

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanaopotoa katika Majina Yake, watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda. [Al-A’raaf 7: 180]

 

Hiyo ndiyo ‘Aqiydah sahihi kabisa waliyoitakidi Salaf wa ummah na ndivyo ipasavyo kuzikubali Sifa zote za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) bila ya kukisia kwa akili zetu namna yake au mfano wake, wala kuogopa kuzithibitisha zilivyo kwa kukhofia kufananisha na viumbe. Kuzithibitisha vile vile zilivyokuja kutoka katika Kitabu Chake kama Alivyoziita Mwenyewe (‘Azza wa Jalla) na Alivyotaka Yeye, hiyo ndio salama kwetu. Tujisalimishe na Alivyojithibitishia Mwenyewe na alivyothibitisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwani akili zetu haziwezi kufikia upeo wa utambuzi na ujuzi wa Sifa Zake (‘Azza wa Jalla).

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:

 

وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ ۚ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾

Na wala usiyafuate (kusema au kushuhudia) yale usiyokuwa nayo elimu. Hakika masikio na macho na moyo; vyote hivyo vitakuwa vya kuulizwa (Siku ya Qiyaamah). [Al-Israa 17:36]

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِهِ عِلْمًا ﴿١١٠﴾

Anajua yale yaliyoko mbele yao, na yale yaliyoko nyuma yao, na wala hawawezi kuzunguka elimu Yake. [Twaahaa 20: 110]

 

 

Umuhimu wa kuyajua na kujifunza Majina Mazuri kabisa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na Sifa Zake:

 

 

1-’Ilmu kuhusu Majina ya Allaah na Sifa Zake ni kumtambua Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na kutambua Utukufu Wake.

 

Unapotaka kutaamali na mtu, hakuna shaka kuwa utataka kujua jina lake, kun-yah yake na kuulizia khabari zake upate ufahamu bayana kumhusu yeye hata uridhike unapotaamali naye. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametuumba na Ndiye Anayeturuzuku kila kitu na tunakhofia ghadhabu Zake na tunataraji rahmah Zake Atughufurie madhambi yetu Asituadhibu. Kwa hiyo, hakuna budi kutambua yanayomridhia ili Naye Aridhike na sisi, na pia kutambua yanayomghadhibisha ili tujiepushe nayo. Kama vile ambavyo huwezi kumpenda usiyemjua, hali kadhaalika huwezi kumkhofu na kumpenda Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa haki apasayo kukhofiwa na kupendwa isipokuwa kwa kumtambua Utukufu Wake, na njia mojawapo ni kutambua Majina Yake Mazuri kabisa na Sifa Zake. Usipomtambua ukampenda, Naye Hatokutambua wala kukujali.

 

Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

وَلَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ نَسُوا اللَّـهَ فَأَنسَاهُمْ أَنفُسَهُمْ ۚ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ﴿١٩﴾

Na wala msiwe kama wale waliomsahau Allaah, Naye (Allaah) Akawasahaulisha nafsi zao, hao ndio mafasiki. [Al-Hashr 59: 19]

 

Hivyo, kumtambua Allaah kunapelekea katika kumpenda, na kumkhofu, na kutawakali Kwake, na kumsafishia niyyah (ikhlaasw) katika matendo na kutaraji rahmah Yake.

 

 

2-’Ilmu Ya Majina ya Allaah na Sifa Zake ni ’Ilmu ya asasi.

 

’Ilmu kuhusu Majina ya Allaah na Sifa Zake ni’ilmu ya asasi, kwani ni aina ya tatu ya Tawhiyd. Na tawhiyd ndio jambo kuu walilokuja nalo Rusuli wote katika ulinganiaji wao. Na ni ’ilmu bora na tukufu kabisa kuitambua. Na ndio lengo kuu na kuumbwa kwa kumpwekesha Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) katika ’ibaadah. 

 

 

3-’Ilmu ya Majina ya Allaah na Sifa Zake Inazidisha Iymaan.

 

 ’Ilmu kuhusu Majina ya Allaah na Sifa Zake ni sababu ya kuzidisha iymaan kama alivyosema Imaam As-Sa’dy (Rahimahu Allaah): “Hakika kuamini Asmaa Allaah Al-Husnaa na utambuzi wake, inajumuisha aina tatu za tawhiyd; Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah, Tawhiyd Al-Uluwhiyyah (’Ibaadah) na Tawhiyd Asmaa wasw-Swifaat. Na aina hizi ndio roho ya iymaan na ndio furaha halisi na kitulizo cha dhiki za moyo, na ndio asili yake na lengo lake. Basi kila mja anapozidi kutambua maarifa ya Asmaa Allaah na Sifa Zake ndipo inapozidi iymaan yake na kuthibitika yakini yake. [At-Tawdhiwyh Wal-Bayaan Lishajaratil-Iymaan Lis-Sa’dy, uk. 41]

 

 

4-’Ilmu kuhusu Majina ya Allaah na Sifa Zake ni sababu ya kupata Jannah:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((إِنَّ لِلَّهِ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ اسْمًا مِائَةً إِلا وَاحِدًا مَنْ أَحْصَاهَا دَخَلَ الْجَنَّةَ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ’anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika Allaah Ana Majina tisini na tisa, atakayejifunza moyoni ataingia Jannah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Ahswaahaa imekusudiwa: Kuyafahamu maana Zake, kuyahifadhi, kufanyia kazi, kuomba du’aa kuyatumia kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. [Al-A’raaf 7: 180]

 

Imaam Ibn ’Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema: Ahswaahaa haimaanishi kuwa ni kuyaandika Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwenye karatasi na kuyakariri mpaka mtu aweze kuyahifadhi bali inamaanisha:

  • Kujifunza kuyatamka.
  • Kufahamu maana Zake.
  • Kumwabudu Allaah kwayo, kwa njia mbili:

 

Kwanza:  Kumuomba du’aa kwayo kwa sababu Allaah Anasema:

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. [Al-A’raaf 7: 180]

 

Kwa hivyo, uyafanye kuwa ni wasiylah (kurubisho) ya du’aa yako, hivyo utachagua Jina linalowafikiana na haja yako. Unapotaka  kuomba maghfirah useme: ”Yaa Ghafuwru nighufurie.” Na si kusema: ”Yaa Shadiyd Al-’Iqaab Ighfir-liy (Ee Mkali wa kuakibu nighufurie!)” kwani hii inakuwa kama ni istihzaa. Linalopasa (ikiwa utamwita Allaah hivyo) useme ”Ee Mkali wa kuakibu, Niepushe na ikabu Yako.”

 

 

Pili:  Katika ’ibaadah zako, vitendo viashirie  Majina Yake. Kama Ar-Rahiym (Mwenye kurehemu) kusudio lake ni rahmah, basi fanya vitendo vyema vitakavyosababisha kupata rahmah ya Allaah. 

 

 

Hiyo ndio maana ya ahswaahaa. Basi itakapotekelezwa hayo ndipo itakapostahiki kuingizwa Jannah.” [Majmuw’ Fataawa wa Rasaail Ibn ’Uthaymiyn (1/74)]

’Ulamaa wamekubaliana kwamba Majina ya Allaah si tisini na tisa pekee bali yako zaidi ya hayo kwa dalili ya Hadiyth:

 

 

عن عَبْدِ اللَّهِ بن مسعود قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَا أَصَابَ أَحَدًا قَطُّ هَمٌّ وَلا حَزَنٌ فَقَالَ: اللَّهُمَّ إِنِّي عَبْدُكَ، وَابْنُ عَبْدِكَ، وَابْنُ أَمَتِكَ، نَاصِيَتِي بِيَدِكَ، مَاضٍ فِيَّ حُكْمُكَ، عَدْلٌ فِيَّ قَضَاؤُكَ، أَسْأَلُكَ بِكُلِّ اسْمٍ هُوَ لَكَ سَمَّيْتَ بِهِ نَفْسَكَ، أَوْ عَلَّمْتَهُ أَحَدًا مِنْ خَلْقِكَ، أَوْ أَنْزَلْتَهُ فِي كِتَابِكَ، أَوْ اسْتَأْثَرْتَ بِهِ فِي عِلْمِ الْغَيْبِ عِنْدَكَ، أَنْ تَجْعَلَ الْقُرْآنَ رَبِيعَ قَلْبِي، وَنُورَ صَدْرِي، وَجَلَاءَ حُزْنِي، وَذَهَابَ هَمِّي، إِلا أَذْهَبَ اللَّهُ هَمَّهُ وَحُزْنَهُ وَأَبْدَلَهُ مَكَانَهُ فَرَجًا)) فَقِيلَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، أَلا نَتَعَلَّمُهَا؟ فَقَالَ: ((بَلَى يَنْبَغِي لِمَنْ سَمِعَهَا أَنْ يَتَعَلَّمَهَا)) صححه الألباني في السلسلة الصحيحة (199)

 

Ibn Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Yeyote atakayefikiwa na dhiki na huzuni kisha akasema:

 

Allaahumma inniy ‘abduka, ibnu-‘abdika, ibnu-amatika, naaswiyatiy Biyadika, maadhwin fiyya hukmuka, ‘adlun fiyya qadhwaauka, as-aluka bikullismin huwa Laka, sammayta bihi Nafsaka aw Anzaltahu fiy Kitaabika, aw ‘Allamtahu ahadan min Khalqika, awis-staa-tharta bihi fiy ‘ilmil-ghaybi  ‘In-daka, an Taj-’alal-Qur-aana rabiy’a qalbiy, wanuwra swadriy, wajalaa-a huzniy, wa dhahaaba hammiy.

 

Ee Allaah hakika mimi ni mtumwa Wako, mtoto wa mtumwa Wako, mtoto wa kijakazi Chako, utosi wangu uko Mikononi Mwako, yaliyopita kwangu yako katika hukumu Yako, ni usawa kwangu kunihukumu Kwako, nakuomba kwa kila Jina ambalo ni Lako Ulilojiita  Mwenyewe au Uliloliteremsha katika Kitabu Chako, au Ulilomfundisha yeyote yule kati ya viumbe Vyako, au Ulilolihifadhi Wewe mwenyewe (na kujihusisha kulijua) katika ’ilmu ya ghayb Kwako, nakuomba Ujaalie Qur-aan kuwa ni rabiy' (uhuisho, raha, furaha na ustawisho) wa moyo wangu na nuru ya kifua changu, na ufumbuzi wa  huzuni yangu, na sababu ya kuondoka wahka wangu. - Akisema hivyo hakuna isipokuwa Allaah Atamuondoshea dhiki na huzuni na Atambadilisha badala yake faraja.” Ikasemwa: Ee Rasuli wa Allaah! Je tujifunze? Akasema: ”Ndio, inampasa kwa mwenye kuisikia kujifunza.” [Ameipokea Ahmad (1/391) [452], Al-Haakim (1/509) na ameisahihisha Al-Albaaniy katika As-Silsilah Asw-Swahiyhah (199) na Al-Kalimi Atw-Twayyib (124)]

 

 

Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:

 

“Hii (du’aa katika Hadiyth hiyo) ni dalili kwamba Allaah Ana Majina zaidi ya tisini na tisa.” [Majmu’w Al-Fataawa (6/374)]

 

 

Na Imaam Ibn ’Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema alipoulizwa kuhusu idadi ya Majina ya Allaah:

 

“Majina ya Allaah hayana idadi maalumu. Na dalili ni kauli ya (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika Hadiyth Swahiyh:

 

((Ee Allaah hakika mimi ni mtumwa Wako, mtoto wa mtumwa Wako, mtoto wa kijakazi Chako, utosi wangu uko Mikononi Mwako, yaliyopita kwangu yako katika hukumu Yako, ni usawa kwangu kunihukumu Kwako, nakuomba kwa kila Jina ambalo ni Lako Ulilojiita Kwako Mwenyewe au Uliloliteremsha katika Kitabu Chako, au Ulilomfundisha yeyote yule kati ya viumbe Vyako, au Ulilolihifadhi Wewe mwenyewe (na kujihusisha kulijua) katika ’ilmu ya ghayb Kwako)).

 

 

Basi ambayo Aliyoyahifadhi Allaah katika ’ilmu ya ghayb hayawezi kujulikana, na ambayo hayajulikani hayawezi kuhesabika. Ama kauli ya (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

”Hakika Allaah Ana Majina tisini na tisa, atakayejifunza moyoni ataingia Jannah.”

 

 

Haimaanishi kuwa Hana isipokuwa Majina haya tu. Lakini inayokusudiwa ni kwamba atakayehifadhi Majina haya tisini na tisa basi ataingia Jannah. Kauli yake: Man Ahswaahaa (atakayejifunza kwa moyo) ni kamilisho la sentensi ya mwanzo na si kiendelezo kilichojitenga, ni kama vile Waarabu wanaposema: “Nina farasi mia ambao nimewaandaa kwa jihaad kwa ajili ya Allaah”; Hii haimaanishi kwamba msemaji ana farasi mia tu bali hawa mia ndio aliowaandaa kwa ajili ya jambo hili.” [Majmuw’ Fataawa Ibn ‘Uthaymiyn (1/122)]

 

 

Kazi hii ya ku-tarjam na kuelezea Majina ya Allaah na Sifa Zake tuliyoyakusanya humu hakika ni mukhtasari tu kwa sababu ’ilmu yake ni pana mno haiwezekani kuijumuisha kwa makala fupi kama hizi. Lakini tunatumai kuwa mukhtasari huu utatoa maarifa ya kumtoshelezea kiasi msomaji kutambua maana za msingi za Majina ya Allaah na Sifa Zake.

 

 

Haya ndio Ambayo Allaah Ametuwezesha kwa tawfiyq Yake, huku tukimuomba Ajaalie kazi hii iwe yenye ikhlaasw Kwake na ilete manufaa kwa jamii na Atutakabalie. Aamiyn.

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Share

001-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: ALLAAH

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

الله

001-ALLAAH

 

 

 

 

ALLAAH: Mwenye Uluwhiyyah (Anayestahiki kuabudiwa Pekee bila kumshirikisha) na Al-‘Ubuwdiyyah (Unyenyekevu, mapenzi, khofu ya adhabu za Allaah na kutaraji rahma za Allaah, utiifu na udhalili kwa Allaah Aliyetukuka, na kutovuka mipaka Yake, na kutekeleza maamrisho Yake na kujizuia na makatazo Yake, kwa kujikurubisha kwa Allaah na kutaka thawabu Zake na kujihadhari na ghadhabu na ikabu Zake).

 

 

Mwenye kustahiki kupwekeshwa katika kuabudiwa kwa Alivyojisifu kwa Sifa za Uwluwhiyyah nazo ni Sifa za ukamilifu.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Mwenye Kustahiki kurejewa kwa mapenzi, kwa unyeyenyekevu, kwa khofu, matumaini, matarajio, kuadhimishwa na kutiiwa. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ ۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيْءٍ مِّنْ عِلْمِهِ إِلَّا بِمَا شَاءَ ۚ وَسِعَ كُرْسِيُّهُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۖ وَلَا يَئُودُهُ حِفْظُهُمَا ۚ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٢٥٥﴾

Allaah, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliyehai daima, Msimamia kila kitu. Haumchukui usingizi wala kulala. Ni Vyake pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Nani huyu ambaye anashufai mbele Yake bila ya idhini Yake. Anajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Wala hawawezi kuzunguka chochote katika elimu Yake isipokuwa kwa Alitakalo. Imeenea Kursiyy Yake mbingu na ardhi. Wala hakumchoshi kuvihifadhi viwili hivyo. Naye ni Mwenye Uluwa, Ametukuka, Adhimu; Mkuu kabisa. [Al-Baqarah 2: 255]

 

Maana ya Allaah kilugha:  Allaah; Asili yake ni Al-Ilaah, na Al-Ilaah katika lugha ya Kiarabu ina maana nne:

 

Kwanza:  Al-Ma’buwd:  Mwenye kuabudiwa. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَهُوَ الَّذِي فِي السَّمَاءِ إِلَـٰهٌ وَفِي الْأَرْضِ إِلَـٰهٌ ۚ  

Na Yeye Ndiye Muabudiwa wa haki mbinguni na ardhini  [Az-Zukhruf 43: 84]

 

Pili:  Mwenye kukimbiliwa katika hali ya khofu:

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لَّعَلَّهُمْ يُنصَرُونَ ﴿٧٤﴾

Na wamejichukulia badala ya Allaah miungu (ya uongo) ili (wakitumaini) watawanusuru! [Yaasiyn 36: 74]

 

Yaani; Wanategemea wawanusuru dhidi ya maadui wao, Waarabu wakawa wanaelekea miungu yao kuomba nusra.

 

Tatu:  Al-Mahbuwb Al-Mu’adhwam – Mpendwa Mtukuzwa.

 

Waarabu wakawa wanapenda masanamu yao waliyokuwa wakiyaabudu na wakayatukuza Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ۖ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ ۗ

Na miongoni mwa watu wako wenye kuchukua asiyekuwa Allaah na kuwafanya kuwa ni wanaolingana (na Allaah) wanawapenda kama kumpenda Allaah. Na wale walioamini wana mapenzi zaidi kwa Allaah. [Al-Baqarah 2: 165]  

 

Nne:  Ambaye kwayo akili zinakanganyika

 

Yaani: zinakanganya nyoyo zinapotafakari utukufu Wake (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kisha zikashindwa kufikia ufahamu wa dhati ya Ujalali Wake na Utukufu Wake (‘Azza wa Jalla).

Jina hili ni Jina tukufu kabisa kuliko yote miongoni mwa Asmaul-Husnaa, na ni lilotukuka zaidi na lililojumuisha maana za Majina Yake yote. Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Amejipwekesha Kwalo kutokana na walimwengu wote. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Akazitia khofu nyoyo za majahili na ndimi zao zikatamka bila kipingamizi wala taradadi. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ لَيَقُولُنَّ اللَّـهُ ۚ

Na ukiwauliza: “Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi?” bila shaka watasema: “Allaah.” [Luqmaan 31: 21]

 

Jina hili ni Ambalo linalokusanya Majina Mazuri yote na Sifa tukufu za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Mja anapoomba husema “Allaahumma” hivyo atakuwa ameomba kwa kila Majina Mazuri na Sifa Zake tukufu [Madaarij As-Saalikiyn (1/32)]  Ndio maana Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anaongezea Jina hili Tukufu katika Al-Asmaaul-Husnaa yote mfano kauli Yake:

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا

Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo [Al-A’raaf 7: 180]

 

Na ndio maana pia baadhi ya ‘Ulamaa wakaona kuwa Jina hili la Allaah Ndilo Jina tukufu kabisa ambalo likiombwa kwalo du’aa hutakabaliwa.

Na husemwa Ar-Rahmaan na Ar-Rahiym, Al-Qudduws, As-Salaam, Al-‘Aziyz, Al-Hakiym kuwa ni miongoni mwa Asmaaul-Husnaa wala haisemwi “Allaah” ni miongoni mwa Majina ya Ar-Rahmaan wala miongoni mwa Majina ya Al-‘Aziyz n.k, na ndipo Anaposema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ ۖ هُوَ الرَّحْمَـٰنُ الرَّحِيمُ ﴿٢٢﴾

  Yeye ni Allaah, Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki  ila Yeye. Mjuzi wa ghayb na ya dhahiri, Yeye Ndiye Mwingi wa rahmah, Mwenye kurehemu.

 

 هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki  ila Yeye. Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha, Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi, Mwenye kuaminisha, Mwenye kutawalia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mwenye kutakabari dhidi ya dhulma nk, Yuko juu ya viumbe, Utakasifu ni wa Allaah! kutokana na ambayo wanamshirikisha.

 

 هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ۚ يُسَبِّحُ لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٢٤﴾

Yeye Ndiye Allaah, Muumbaji, Mwanzishi viumbe bila kasoro, Muundaji sura na umbile, Ana Majina Mazuri kabisa, kinamsabbih Pekee kila kilichokuweko katika mbingu na ardhi, Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Hashr 59: 22-24]

 

Jina hili ndio asili ya Majina ya Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na yanayofuatia mengine yote yamejumuika ndani Yake.  

 

Jina la Allaah linamhusu Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَاعْبُدْهُ وَاصْطَبِرْ لِعِبَادَتِهِ ۚ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا ﴿٦٥﴾

Rabb wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake; basi mwabudu Yeye tu na dumisha subira katika ‘ibaadah Yake. Je, unamjua mwenye Jina kama Lake (Allaah)? [Maryam 19: 65]

 

 

Share

002-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: ILAAH

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

إله

002-ILAAH

 

 

 

ILAAH:   Muabudiwa wa haki.

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ ﴿٢٥﴾

Na Hatukutuma kabla yako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Rasuli yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana Muabudiwa wa haki ila Mimi; basi Niabuduni.” [Al-Anbiyaa 21: 25]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَإِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الرَّحْمَـٰنُ الرَّحِيمُ ﴿١٦٣﴾

“Na Ilaah wenu (Allaah) ni Ilaah Mmoja, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mwingi wa rahmah, Mwenye kurehemu.” [Al-Baqarah: 2: 163]

 

Ilaah ni mwenye kustahiki kuabudiwa na Mwenye kuabudiwa kwa mapenzi, kwa kujidhalilisha Kwake, kwa kumkhofu, kwa kutaraji, kwa kumtukuza kwa utiifu kwa sababu Yeye Ndiye Anayeabudiwa.

 

Hivyo kila chenye kuabudiwa chini ya ‘Arshi Yake hadi ardhini ni batili; Amesema Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah: “Laa Ilaaha Illa Anta” (Hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Wewe) ndani yake kuna kuthibitisha upweke Wake, Uungu Wake, na Uungu unathibitisha wema Wake kwa waja Wake. Ilaah Ndiye Mwenye kustahiki kuabudiwa, na kwa sababu Anastahiki kuabudiwa, Yeye ni kama Alivyojisifu kwa Sifa Zake ambazo zinalazimu apendwe mapenzi yote, kilele cha mapenzi, na kunyenyekewa Kwake kilele cha kumnyenyekea, na ‘ibaadah inakusanya kilele cha mapenzi, kwa lengo la kunyenyekewa. [Daqaaiq At-Tafsyir (2/364)]

 

Na jina la Ilaah linatofautiana maana yake na Ar-Rabb katika maeneo mengi, miongoni mwazo ni: Kuwa Ar-Rabb maana yake inarejea kwenye kupwekeka katika kuumba na uendeshaji. Ama Ilaah, Ambaye Anastahiki kuabudiwa na ambaye nyoyo zinamtukuza na wananyenyekea Kwake kwa mapenzi na kumtukuza, Mwenye kustahiki kuabudiwa kwa kila aina zake na kuenea kwake.

 

Ama tofauti kati ya Allaah na Ilaah ni kuwa Ilaah ni wasifu ambao washirikina walimshirikisha kwao Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa kuabudu miongoni mwao;  jua, mwezi na sayari, na hawakufanya hivyo kwa kutumia jina la Allaah, na hawakujiita kwayo yeyote. [Al-Asmaa ya Al-Qurtubiy (uk. 368)]

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

فَلَوْلَا نَصَرَهُمُ الَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ قُرْبَانًا آلِهَةً ۖ بَلْ ضَلُّوا عَنْهُمْ ۚ وَذَٰلِكَ إِفْكُهُمْ وَمَا كَانُوا يَفْتَرُونَ ﴿٢٨﴾

Basi kwa nini wasiwanusuru wale waliowafanya badala ya Allaah kuwa ni miungu ya kikurubisho (Kwake)? Bali wamewapotea, na huo ndio uongo wao na yale waliyokuwa wakiyatunga [Al-Ahqaaf 46 :28]

 

 

 

 

 

Share

003-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AR-RABB

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الرَّبّ

 003-AR-RABB

 

 

 

Ar-RABB: Rabb: Al-Maalik (Mfalme), Ar-Razzaaq (Mwenye kuruzuku), Al-Murabbi (Mlezi), Al-Khaaliq (Muumbaji), Al-Mudabbir (Mwendeshaji na Mpangaji).

 

Ni Rabb wa walimwengu na Anaundesha ulimwengu wote. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 الْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٢﴾

Himidi zote Anastahiki Allaah Rabb wa walimwengu.  [Al-Faatihah (1: 2)]

 

Na pia Ar-Rabb inamaanisha kama alivyosema Ibn Al-Mandhdwur: “Ar-Rabb katika lugha ni Al-Maalik (Mfalme), As-Sayyid (Bwana), Al-Mudabbir (Mwendeshaji na Mpangaji), Al-Murabbi (Mlezi), Al-Qayyim (Msimamiaji), Al-Mun’im (Mwenye kuneemesha).” [Lisaan Al-‘Arab (1/399)]

 

Ar-Rabb inajumuisha pia Mwenye kuabudiwa kwa dalili ya kuwa swali mojawapo la kaburini ni “Man Rabbuka” (Nani Rabb wako)” yaani; nani Muabudiwa wako”.

 

Na Ar-Rabb katika asili ni katika ulezi: yaani Yule anayelea na kukuza kidogo kidogo hadi anakamilika, wala haisemwi kwa yeyote Ar-Rabb isipokuwa kwa Allaah Pekee na huongezwa kwa kusema: “Rabbul ‘Aalamiyn”. Au kwa asiyekuwa Allaah kwa kuongezewa kitu mbele yake kama vile kusema: Rabb Ad-Daar (bwana au mwenye nyumba), Rabb Al-Faras (bwana au mwenye farasi) au ngamia kwa anayemiliki hivyo [Angalia ‘An-Nihaayah fiy Gharyib al-Hadiyth (338) na Mufradaat Alfaadhw Qur-an (336) na Al-Asmaa (1/394)]

 

Jina hili tukufu linakusanya sifa nyingi za kimatendo, “Bali linaweza kuunganishwa na majina mengine matukufu ya kiutendaji na sifa zake tukufu. [Fiqh Al-Asmaa Al-Husnaa Dr. Abdur-Razzzaq Al-Badr (79)]  Hivyo Ar-Rabb kuingia katika: Al-Qaadir, Al-Khaaliq, Al-Baariu, Al-Muswawwir, Al-Hayyu, Al-Qayyuwm, Ar-Rahmaan na mengineyo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ ﴿٥٨﴾

Salaamun”; kauli kutoka kwa Rabb Mwenye kurehemu) [Yaasiyn (36: 58)]

 

Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ambaye ni Rabb wa viumbe wote, kila kilichoko mbinguni na ardhini ni mja Kwake na katika udhibiti Wake. Yeye ndiye Aliyelea viumbe vyote kwa neema Zake, kisha Akakipa kila kitu umbo lake linalolaiki, kisha Akakiongoza kama ilivyothibiti katika Qur-aan:

قَالَ فَمَن رَّبُّكُمَا يَا مُوسَىٰ ﴿٤٩﴾

 (Fir’awn) Akasema: “Basi nani (huyo) Rabb wenu ewe Muwsaa?”

 

قَالَ رَبُّنَا الَّذِي أَعْطَىٰ كُلَّ شَيْءٍ خَلْقَهُ ثُمَّ هَدَىٰ ﴿٥٠﴾

 (Muwsaa) Akasema: “Rabb wetu ni Yule Aliyekipa kila kitu umbo lake, kisha Akakiongoza.” [Twaahaa (20: 49-50)]

 

Akawaenezea viumbe Vyake neema kubwa kubwa ambazo lau watazikosa hawatoweza kuishi. Akawakuza, Akawapa malisho, Akawalea kwa malezi kamilifu. Basi hakuna neema isipokuwa neema Yake. Ndipo Jina hili likawa tukufu, lenye umuhimu mkubwa na azizi katika nafsi na nyoyo za Manabii, na vipenzi vya Allaah, na ndipo ikawa aghlabu ya du’aa za Qur-aan na Sunnah ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Salaf zinaanzia na “Rabbanaa” au “Rabbi” kama du’aa ya Nabiy Aadam ('Alayhis-Salaam):

 

 قَالَا رَبَّنَا ظَلَمْنَا أَنفُسَنَا وَإِن لَّمْ تَغْفِرْ لَنَا وَتَرْحَمْنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ ﴿٢٣﴾

“Rabb wetu! Tumedhulumu nafsi zetu, na basi Usipotughufuria na Ukaturehemu; bila shaka tutakuwa miongoni mwa waliokhasirika.” [Al-A’raaf (7: 23)]

 

Na du’aa ya Khaliylur-Rahmaan Nabiy Ibraahiym ('Alayhis-Salaam):

 

رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَابُ ﴿٤١﴾

“Rabb wetu! Nighufurie na wazazi wangu wawili na Waumini Siku itakayosimama hesabu.[Ibraahiym (14: 41)]

 

Na Du’aa ya Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

 

وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ ﴿٩٧﴾ وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحْضُرُونِ ﴿٩٨﴾

Na sema: “Rabb wangu! Najikinga Kwako kutokana na uchochezi (na wasiwasi) wa mashaytwaan.” “Na najikinga Kwako Rabb wasinihudhurie.” [Al-Muuminuwn (23: 97-98)]

 

 

Na du’aa za wenye ‘ilmu:

 

رَبَّنَا لَا تُزِغْ قُلُوبَنَا بَعْدَ إِذْ هَدَيْتَنَا وَهَبْ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحْمَةً ۚ إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ ﴿٨﴾

“Rabb wetu, Usizipotoe nyoyo zetu baada ya kutuongoza na Tutunukie kutoka kwako rahmah. Hakika Wewe ni Mwingi wa kutunuku na kuneemesha.” [Aal-‘Imraan (3: 8)]

 

 

Na du’aa za ‘Ibaadur-Rahmaan (waja wa Mwingi wa Rahmah):

 

  رَبَّنَا هَبْ لَنَا مِنْ أَزْوَاجِنَا وَذُرِّيَّاتِنَا قُرَّةَ أَعْيُنٍ وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا ﴿٧٤﴾

“Rabb wetu! Tutunukie katika wake zetu na dhuria wetu viburudisho vya macho yetu, na Tujaalie kuwa waongozi kwa wenye taqwa [Al-Furqaan (25: 74)]

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema kuhusu Rabb kuwa mja anakuwa karibu Naye wakati wa kusujudu na ndipo ikawa kusujudu ni sababu moja wapo ya wasiylah (kujikurubisha) kwa Ar-Rabb katika kuomba du’aa:

 

أقربُ ما يكُونُ الرَّبُّ مِنَ العبدِ في جوفِ اللَّيلِ الآخِرِ،  فإنِ استطعتَ أن تكونَ ممّن يذكُرُ اللهَ في تِلكَ الساعةِ ،  فكُن

“Wakati Rabb Anakuwa karibu kabisa na mja, ni wakati wa mwisho wa usiku, kwa hiyo ukiweza kuwa miongoni mwa wanaomdhukuru Allaah katika saa hiyo basi uwe.” [Swahiyh At-Tirmidhiy (3578)]

 

 

 

 

Share

004-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AR-RAHMAAN

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الرَّحْمن

004 - AR-RAHMAAN

 

 

 

AR-RAHMAAN: Mwingi wa rahmah:

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

الرَّحْمَـٰنُ ﴿١﴾ عَلَّمَ الْقُرْآنَ ﴿٢﴾

Ar-Rahmaan; Mwingi wa rahmah. Amefundisha Qur-aan [Ar-Rahmaan: 1-2]

 

Jina hili ni pana zaidi na lenye kuenea zaidi kuliko Ar-Rahiym (Mwenye kurehemu). Hili linakusanya maana zote za rahmah, huruma n.k. Allaah Ndiye Mwenye rahmah iliyokusanya kila kitu, iliyoenea kwa viumbe Vyake vyote duniani, bin Aadam kwa majini, Waumini kwa makafiri, wanyama, mimea, hakuna yeyote au chochote katika kuwepo kwake ila rahmah Yake imemuenea, na ndio maana Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema: 

 

الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۚ الرَّحْمَـٰنُ فَاسْأَلْ بِهِ خَبِيرًا ﴿٥٩﴾

Ambaye Ameumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake katika siku sita, kisha Istawaa juu ya ‘Arsh (Yuko juu kwa namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah), Ar-Rahmaan; Mwingi wa Rahmah, basi ulizia kuhusu Yeye, (kwani Yeye) ni Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana. [Al-Furqaan: 59]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ ﴿٥﴾

Ar-Rahmaan; Mwingi wa Rahmah juu ya ‘Arshi Istawaa (Yuko juu kwa namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah) [Twaahaa 5]

 

Istawaa katika ‘Arshi kwa jina la Ar-Rahmaan, kwa sababu ‘Arshi imezungukwa na viumbe na ina wasaa kwao, na rahmah imewazunguka waja Wake, ina wasaa kwao kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ

Na rahmah Yangu imeenea kila kitu [Al-A’raaf: 156]

 

Istawaa katika kilicho kipana zaidi katika Alivyoviumba, nayo ni ‘Arsh Yake na kwa sifa iliyo pana zaidi nayo ni rahmah Yake. Na kwa ajili hiyo rahmah Yake imeenea katika kila kitu.

 

Ar-Rahmaan ni jina Analoitwa Allaah Peke Yake. Ama athari ya jina hili ni kwa wote; kwa watu wema na waovu. Na ndio maana Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amelitaja zaidi Jina hili katika Suwrah ziloteremshwa Makkah, khasa katika Suwrat Maryam ambayo imetajwa mara  nyingi zaidi ya Suwrah nyinginezo.

 

Kipindi hicho cha Makkah ni kipindi cha mwanzo cha Uislamu. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akawadhihirishia makafiri Sifa Yake hiyo kwamba Yeye ni Mwingi wa rahmah juu ya kuwa wanamshirikisha.

 

Na katika Sunnah zimethibiti Hadiyth kadhaa kuhusu rahmah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wanayorehemeana viumbe ardhini:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ، قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((إِنَّ اللَّهَ خَلَقَ الرَّحْمَةَ يَوْمَ خَلَقَهَا مِائَةَ رَحْمَةٍ، فَأَمْسَكَ عِنْدَهُ تِسْعًا وَتِسْعِينَ رَحْمَةً، وَأَرْسَلَ فِي خَلْقِهِ كُلِّهِمْ رَحْمَةً وَاحِدَةً، فَلَوْ يَعْلَمُ الْكَافِرُ بِكُلِّ الَّذِي عِنْدَ اللَّهِ مِنَ الرَّحْمَةِ لَمْ يَيْأَسْ مِنَ الْجَنَّةِ، وَلَوْ يَعْلَمُ الْمُؤْمِنُ بِكُلِّ الَّذِي عِنْدَ اللَّهِ مِنَ الْعَذَابِ لَمْ يَأْمَنْ مِنَ النَّارِ)) البخاري في الأدب، باب جعل الله الرحمة في مائة جزء  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Hakika Allaah Ameumba rahmah. Siku Aliyoumba Alizifanya rahmah mia (100) Akazuia Kwake rahmah tisini na tisa (99) Akateremsha rahmah moja kwa viumbe Vyake vyote.  Lau kafiri angelijua kuhusu rahmah zilizokuweko kwa Allaah, basi asingekata tamaa kuingia Jannah. Na lau Muumini angejua adhabu zilizoko kwa Allaah, basi asingejiaminisha na moto)) [Al-Bukhaariy fiy Ar-Riqaab Baab Ar-Rajaa ma’al-khawf]

 

وعن أبي هريرة رضي الله عنه أنه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((جَعَلَ الله الرَّحْمَةَ مِائَةَ جُزْءٍ، فَأَمْسَكَ عِنْدَهُ تِسْعَةً وَتِسْعِينَ جُزْءًا وَأَنْزَلَ فِي الأَرْضِ جُزْءًا وَاحِدًا، فَمِنْ ذَلِكَ الْجُزْءِ يَتَرَاحَمُ الْخَلْقُ حَتَّى تَرْفَعَ الْفَرَسُ حَافِرَهَا عَنْ وَلَدِهَا خَشْيَةَ أَنْ تُصِيبَهُ)) البخاري في الأدب، باب جعل الله الرحمة في مائة جزء   

Na pia amepokea Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Allaah Amejaalia rahmah mia, Akazuia Kwake rahmah tisini na tisa, Akateremsha moja tu ardhini. Basi kutokana na hiyo ndio wanayorehemeana viumbe hadi kwamba farasi huinua makwato yake kukhofia asimkanyage mtoto wake)) [Al-Bukhaariy Baab Ja’ala Allaahu Ar-Rahmah fiy miat juz’]

 

 عَنْ عَطَاءٍ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِنَّ لِلَّهِ مِائَةَ رَحْمَةٍ أَنْزَلَ مِنْهَا رَحْمَةً وَاحِدَةً بَيْنَ الْجِنِّ وَالإِنْسِ وَالْبَهَائِمِ وَالْهَوَامِّ فَبِهَا يَتَعَاطَفُونَ وَبِهَا يَتَرَاحَمُونَ وَبِهَا تَعْطِفُ الْوَحْشُ عَلَى وَلَدِهَا وَأَخَّرَ اللَّهُ تِسْعًا وَتِسْعِينَ رَحْمَةً يَرْحَمُ بِهَا عِبَادَهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ))     

Na pia imepokelewa kutoka kwa ‘Atwaa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Ana rahmah mia, Ameiteresha moja kati ya majini na wana Aadam na wanyama na wadudu, ambao wanaoneana huruma na wanarehemeana, na hiyo hiyo mpaka mnyama mwitu anamhurumia mwanawe. Akazuia Allaah rahmah tisini na tisa Atawarehemu kwazo waja Wake Siku ya Qiyaamah)) [Muslim (6/98), Ahmad (2/434), Ibn Maajah (4293)]

 

Sifa hii ya Rahmah ni ya dhati Yake Allaah ambayo haiwezi kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Makafiri wa Makkah hawakupenda Jina hili la Ar-Rahmaan wakakataa kuliandika katika mkataba wa Hudaybiyah pale Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipomuamrisha mwandishi wa mkataba andike “BismiLLaah (Kwa Jina la Allaah) Ar-Rahmaan (Mwingi wa rahmah) Ar-Rahiym (Mwenye kurehemu).” Wakasema: “Andika: Biismika-Allaahumma.”

Hapo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akateremsha:

 

قُلِ ادْعُوا اللَّـهَ أَوِ ادْعُوا الرَّحْمَـٰنَ ۖ أَيًّا مَّا تَدْعُوا فَلَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ۚ  

Sema; “Muiteni Allaah au muiteni Ar-Rahmaan; Mwingi wa rahmah, vyovyote mtakavyomwita basi Yeye Ana Majina Mazuri kabisa.   [Al-Israa: 110]

[Tafsiyr Ibn Kathiyr]

 

Na ndio maana Suwrah za Qur-aan zinaanza na BismiLLaah inayotaja Majina Yake Mawili ya Ar-Rahmaan na Ar-Rahiym, na pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametanguliza katika ufunguzi wa Suwrat Al-Faatihah Akaanza na Ar-Rahmaan (Mwingi wa rahmah) na Ar-Rahiym (Mwenye kurehemu).

 

Vipi Uweze kupata rahmah ya Allaah?

 

1. Njia ya kwanza kuweza kupata Rahmah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni yale yote yenye uhusiano wa mtu na Rabb Wake kama vile:  

 

Kujipuesha na yote yaliyoharamishwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa sababu baadhi ya yaliyoharamishwa yanamsababisha mtu kupata laana ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) inayomaanisha ni kuwekwa mbali na rahmah Zake.   

Pia katika njia ya kupata rahmah ya Allaah, ni kumtii Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَالرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٣٢﴾

Na mtiini Allaah na Rasuli mpate kurehemewa.  [Aal-‘Imraan: 132]

 

Na pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametaja sifa za waja Wake ambao amehusisha na Jina na Sifa Yake hii ya Ar-Rahmaan Anawaita: ‘Ibaadur-Rahmaan (Waja wa Rahmaan).” Pindi atakapotekeleza mtu hayo yaliyotajwa katika Suwratul-Furqaan Aayah 63 mpaka Aayah 76 basi atastahiki kuwa ni miongoni mwa ‘Ibaadur-Rahmaan.

 

وَعِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الْأَرْضِ هَوْنًا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ الْجَاهِلُونَ قَالُوا سَلَامًا ﴿٦٣﴾

Na waja wa Ar-Rahmaan Mwingi wa Rahmah ni wale wanaotembea katika ardhi kwa unyenyekevu na upole, na majahili wanapowasemesha, wao husema: Salaam!

 

وَالَّذِينَ يَبِيتُونَ لِرَبِّهِمْ سُجَّدًا وَقِيَامًا ﴿٦٤﴾

Na wale wanaokesha (baadhi ya) usiku kwa ajili ya Rabb wao wakisujudu na kusimama…..  [Al-Furqaan: 63-76]

 

Hali kadhaalika kuzidisha ‘ibaadah kwa wingi, Swalaah za usiku (tahajjud), kuomba du’aa, kuisikiliza kwa makini na kuisoma Qur-aan, kuzingatia maana zake, kuwa na taqwa, kusimamisha Swalaah na kutoa Zakaah, kufanya jihaad katika njia ya Allaah, kuvuta subira katika mitihani na misiba, kuomba maghfirah, na kwa ujumla ni kumwamini Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَاكْتُبْ لَنَا فِي هَـٰذِهِ الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ إِنَّا هُدْنَا إِلَيْكَ ۚ قَالَ عَذَابِي أُصِيبُ بِهِ مَنْ أَشَاءُ ۖ وَرَحْمَتِي وَسِعَتْ كُلَّ شَيْءٍ ۚ فَسَأَكْتُبُهَا لِلَّذِينَ يَتَّقُونَ وَيُؤْتُونَ الزَّكَاةَ وَالَّذِينَ هُم بِآيَاتِنَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٥٦﴾

“Na Tuandikie katika dunia hii mazuri na katika Aakhirah. Hakika sisi tumerudi kutubu Kwako.” (Allaah) Akasema: “Adhabu Yangu Nitamsibu nayo Nimtakaye. Na rahmah Yangu imeenea kila kitu. Basi Nitawaandikia wale wenye taqwa na wanaotoa Zakaah na ambao wao wanaziamini Aayaat (na hoja, dalili) Zetu.” [Al-A’raaf: 156]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika Aayah zifuatazo:

 

وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿٥٦﴾

Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah, na mtiini Rasuli ili mpate kurehemewa. [An-Nuwr: 56]

 

وَإِذَا قُرِئَ الْقُرْآنُ فَاسْتَمِعُوا لَهُ وَأَنصِتُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿٢٠٤﴾

Na inaposomwa Qur-aan, basi isikilizeni kwa makini na bakieni kimya (mzingatie) ili mpate kurehemewa. [Al-A’raaf: 204]

 

وَهَـٰذَا كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ فَاتَّبِعُوهُ وَاتَّقُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٥٥﴾

Na hiki Kitabu (Qur-aan) Tumekiteremsha kilichobarikiwa, basi kifuateni na muwe na taqwa mpate kurehemewa. [Al-An’aam: 155]

 

 

قَالَ يَا قَوْمِ لِمَ تَسْتَعْجِلُونَ بِالسَّيِّئَةِ قَبْلَ الْحَسَنَةِ ۖ لَوْلَا تَسْتَغْفِرُونَ اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿٤٦﴾

(Swaalih) Akasema: “Enyi kaumu yangu! Kwa nini mnahimiza uovu kabla ya mema; kwa nini msimwombe Allaah maghfirah huenda mkarehemewa?” [An-Naml:  46]

 

وَلَنَبْلُوَنَّكُم بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفِ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ مِّنَ الْأَمْوَالِ وَالْأَنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ ۗ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ ﴿١٥٥﴾

Na bila shaka Tutakujaribuni kwa kitu katika khofu na njaa na upungufu wa mali na nafsi na mazao. Na wabashirie wenye kusubiri.

 

الَّذِينَ إِذَا أَصَابَتْهُم مُّصِيبَةٌ قَالُوا إِنَّا لِلَّـهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ﴿١٥٦﴾

Wale ambao unapowafika msiba husema: “Hakika sisi ni wa Allaah na hakika sisi Kwake ni wenye kurejea.”

 

أُولَـٰئِكَ عَلَيْهِمْ صَلَوَاتٌ مِّن رَّبِّهِمْ وَرَحْمَةٌ ۖ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُهْتَدُونَ ﴿١٥٧﴾

Hao zitakuwa juu yao barakah kutoka kwa Rabb wao na rahmah, na hao ndio wenye kuongoka. [Al-Baqarah: 155-157]

 

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ هَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ أُولَـٰئِكَ يَرْجُونَ رَحْمَتَ اللَّـهِ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢١٨﴾

Hakika wale walioamini na wale waliohajiri na wakapigana jihaad katika njia ya Allaah, hao wanataraji rahmah ya Allaah, na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Baqarah:  218]

 

Na kuomba du’aa ni ambazo zimethibiti katika Sunnah za kumwomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) rahmah Yake mifano ya du’aa mbili miongoni mwa du’aa nyingi ni:

 

اللّهُـمَّ رَحْمَتَـكَ أَرْجـو فَلا تَكِلـني إِلى نَفْـسي طَـرْفَةَ عَـيْن، وَأَصْلِـحْ لي شَأْنـي كُلَّـه لَا إِلَهَ إِلَّا أنْـت

 

Allaahumma Rahmatika arjuw falaa takilniy ilaa nafsiy twarfata ‘aynin, wa aswlih liy sha-aniy kullahu, laa ilaaha illaa Anta

 

Ee Allaah, nataraji rahmah Zako, usinitegemeze  kwenye nafsi yangu japo kwa muda wa upepesa jicho, na Unitengenezee mambo yangu yote, hapana Muabudiwa wa haki ila Wewe [Hadiyth ya Abu Bakr Nafiy’ bin Haarith Ath-Thaqafiyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) - Abu Daawuwd (4/324) [5090], Ahmad (5/42),  ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy  katika Swahiyh Abi Daawuwd (3/959) ]

 

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ مُوجِبَاتِ رَحْمَتِكَ، وَعَزَائِمَ مَغْفِرَتِكَ، وَالسَّلامَةَ مِنْ كُلِّ إِثْمٍ، وَالْغَنِيمَةَ مِنْ كُلِّ بِرّ، وَالْفَوْزَ بِالْجَنَّةِ، وَالنَّجَاةَ مِنَ النَّاَرِ.

Allaahumma inniy as-aluka muwjibaati Rahmatik wa 'azaaim maghfiratik was-salaamata min kulli ithm, wal ghaniymata minkulli birr, wal fawza bil Jannati, wan najaata minan-naari

 

Ee Allaah hakika mimi nakuomba azima za rahmah Yako, azimio la maghfirah Yako, na amani katika kila dhambi, na ghanima katika kila jema, na kufuzu katika Jannah na kuokoka na moto [Al-Haakim (1/525) na ameipa daraja ya Swahiyh na ameiwafiki  Adh-Dhahabiy]

 

 

2. Njia ya pili ya kuweza kupata Rahmah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  ni yale yote yenye uhusiano wa bin Aadam na viumbe vinginevyo.

 

Imaam As-Sa’dy (Rahimahu Allaah) amesema: “Rahmah ya mja kwa viumbe ni sababu kuu inayomfikisha mtu kupata rahmah ya Allaah ambayo taathira yake ni kupata khayraat za dunia na khayraat za Aakhirah, na kukosa kwake ni kukatwa na kuzuilika kupata rahmah ya Allaah. Na mja anahitaji kwa dharura rahmah ya Allaah, asiikose hata kidogo kadiri ya muda wa upepeso wa jicho. Na kila kilichopo chenye neema na kukimbiza balaa, ni katika rahmah ya Allaah.

 

Basi anapotaka kubakia katika rahmah ya Allaah na kuzidi kuipata na afanye yote yanayosababisha kupata rahmah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Yote yanajumuika katika kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّ رَحْمَتَ اللَّـهِ قَرِيبٌ مِّنَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٥٦﴾

Hakika rahmah ya Allaah iko karibu na wafanyao ihsaan. [Al-A’raaf: 56]

[Bahjatu Quluwb Al-Abraar, uk. 197-198]

 

Hadiyth nyingi za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) zimethibiti kuhusu kupata rahmah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kufanya ihsaan na wema. Baadhi ya Hadiyth ni kama zifuatazo:

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو يَبْلُغُ بِهِ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الرَّاحِمُونَ يَرْحَمُهُمْ الرَّحْمَنُ ارْحَمُوا مَنْ فِي الْأَرْضِ يَرْحَمْكُمْ مَنْ فِي السَّمَاءِ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr  kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba amesema: ((Ar-Rahmaan Atawarehemu wenye kurehemu. Mrehemuni aliyeko ardhini Atakurehemuni Aliyeko mbinguni)) [Sunan At-Tirmidhiy (1924) Ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Tirmidhiy, Swahiyh Abiy Daawuwd (4941), Swahiyh At-Targhiyb (2256)]

 

قال رسول الله - صلى الله عليه وسلّم: ((مَنْ لاَ يَرْحَمِ النَّاسَ لاَ يَرْحَمْهُ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ‏)) رواه البخاري (6013) ومسلم (2319)

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Asiyerehemu watu hatorehemewa na Allaah Aliyetukuka na Aliye Jalali)) [Al-Bukhaariy (6013) Muslim (2319)]

 

Kusulihisha waliokhasimikiana:

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٠﴾

Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa. [Al-Hujuraat: 10]

 

Na Sifa hii ya rahmah imehusiana na Ar-Rahm (fuko la uzazi) ambalo kwalo ndugu na jamaa hurehemeana na likawa jambo la kukata undugu ni dhambi kubwa mno inayosababisha laana za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na ghadhabu Zake kama ilivyotajwa katika Qur-aan. [Muhammad: 47: 22-23] Na pia Akasisitiza mno katika Qur-aan [Al-Baqarah: 27, Ar-Ra’d: 20-21]. Na pia Hadiyth kadhaa zimethibiti makemeo na khatari ya kukata undugu hadi kwamba inamharamisha Muislamu kuingia Jannah. Na katika Hadiyth zifuatazo zimehusisha sifa hiyo ya rahmah na undugu:

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَال: ((إِنَّ الرَّحِمَ شَجْنَةٌ مِنْ الرَّحْمَنِ، فَقَالَ اللَّهُ: مَنْ وَصَلَكِ وَصَلْتُهُ وَمَنْ قَطَعَكِ قَطَعْتُهُ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Ar-Rahm [fuko la uzazi]  linatokana na Jina la Ar-Rahmaan; Basi Allaah Amesema: Atakayekuunga Nami Nitamuunga na Atakayekukata Nami Nitamkata)) [Al-Bukhaariy 5988]

 

Na pia:

عنْ عَائِشَةَ (رضي الله عنها) قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الرَّحِمُ مُعَلَّقَةٌ بِالْعَرْشِ، تَقُولُ مَنْ وَصَلَنِي وَصَلَهُ اللَّهُ وَمَنْ قَطَعَنِي قَطَعَهُ اللَّهُ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ar-Rahm [fuko la uzazi] limetundikwa katika ‘Arshi, linasema: Anayeniunga Allaah Atamuunga, na anayenikata Allaah Atamkata)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na katika kuwarehemu wanyama:

 

Mwanamke kahaba aliyemnywesha mbwa maji alighufuriwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ غُفِرَ لِامْرَأَةٍ مُومِسَةٍ مَرَّتْ بِكَلْبٍ عَلَى رَأْسِ رَكِيٍّ يَلْهَثُ قَالَ كَادَ يَقْتُلُهُ الْعَطَشُ فَنَزَعَتْ خُفَّهَا فَأَوْثَقَتْهُ بِخِمَارِهَا فَنَزَعَتْ لَهُ مِنْ الْمَاءِ فَغُفِرَ لَهَا بِذَلِكَ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ameghufuriwa mwanamke kahaba. Alimpitia mbwa akihaha (kwa kiu) karibu na kisima. Alipoona anakaribia kufa kwa kiu, alivua kiatu chake akakifunga kwenye shungi lake akamchotea maji. Allaah Akamghufuria kwa kufanya hivyo)) [Al-Bukhaariy (3143) Muslim (2245)]

 

Mwanamke aliyemuadhibu paka aliingizwa motoni:

 

 عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ (رضي الله عنهما) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((عُذِّبَتْ امْرَأَةٌ فِي هِرَّةٍ حَبَسَتْهَا حَتَّى مَاتَتْ جُوعًا فَدَخَلَتْ فِيهَا النَّارَ, لاَ هِيَ أَطْعَمْتِهَا  وَسَقَيْتِهَا إِذْ هِيَ حَبَسْتِيهَا وَلاَهِيَ تَرَكَتْها تَأكُلُ مِنْ  خَشَاشِ الأرْضِ)) متفق

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mwanamke fulani aliadhibiwa kwa sababu ya paka aliyemfungia mpaka akafa kwa njaa, akaingia motoni [kwa sababu] alipomfungia hakumpa chakula wala hakumnywesha maji wala hakumwacha aende akale vidudu ardhini. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

005-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AR-RAHIYM

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

الرَّحِيم

 

005 - AR-RAHIYM

 

 

 

AR-RAHIYM: Mwenye kurehemu:

 

Sifa mbili za Rahmaan na Rahiym zinatokana na herufi tatu za asili na hivyo maana zake ni moja, isipokuwa tu kama ilivyobainishwa katika Sifa ya Rahmaan kwamba maana yake ni pana na inaenea zaidi kwa viumbe wote; Waumini kwa makafiri, watu wema kwa watu waovu. Ama Rahiym ni Sifa khaswa kwa ajili ya Waumini pekee kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَكَانَ بِالْمُؤْمِنِينَ رَحِيمًا ﴿٤٣﴾

Naye kwa Waumini daima ni Mwenye kurehemu. [Al-Ahzaab: 43]

 

Na Anasema kuhusu waja Wake:

نَبِّئْ عِبَادِي أَنِّي أَنَا الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿٤٩﴾

(Ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Wajulishe waja Wangu, kwamba: Hakika Mimi ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Hijr: 49]

 

 Na pia kuhusu Maswahaba waliorudi kutubia:

 

لَّقَد تَّابَ اللَّـهُ عَلَى النَّبِيِّ وَالْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ فِي سَاعَةِ الْعُسْرَةِ مِن بَعْدِ مَا كَادَ يَزِيغُ قُلُوبُ فَرِيقٍ مِّنْهُمْ ثُمَّ تَابَ عَلَيْهِمْ ۚ إِنَّهُ بِهِمْ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿١١٧﴾

Kwa yakini Allaah Amepokea tawbah ya Nabiy na Muhajirina na Answaar ambao wamemfuata (Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم) katika saa ya dhiki (vita vya Tabuwk) baada ya nyoyo za kundi miongoni mwao zilikaribia kuelemea mbali na haki (Allaah) Akapokea tawbah yao. Hakika Yeye kwao ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu. [At-Tawabah: 117]

 

Na Waumini watakapoingia Jannah:

إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ ﴿٥٥﴾

Hakika watu wa Jannah leo wamo katika kushughulika wakifurahi.

 

هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِئُونَ ﴿٥٦﴾

Wao na wake zao, wakiwa katika vivuli, juu ya makochi ya fakhari wakiegemea.

 

لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ ﴿٥٧﴾

Watapata humo kila aina ya matunda, na watapata wanavyoomba.

 

سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ ﴿٥٨﴾

“Salaamun”; kauli kutoka kwa Rabb Mwenye kurehemu. [Yaasiyn: 55-58]

 

Na pia katika hali nyingine ya Waumini wanapofishwa na kubashiriwa Jannah:

 

 إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿٣٠﴾

30. Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara; Malaika huwateremkia: (wanapofishwa kuwaambia): “Msikhofu, na wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo mlikuwa mkiahidiwa.”

 

نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَشْتَهِي أَنفُسُكُمْ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ ﴿٣١﴾

31. “Sisi ni marafiki walinzi wenu katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale mtakayoomba.

 

نُزُلًا مِّنْ غَفُورٍ رَّحِيمٍ ﴿٣٢﴾

32. “Ni takrima kutoka kwa Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.” [Fusw-Swilat: 30-32]

 

Na katika du’aa, Anas bin Maalik amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Mu’aadh bin Jabal:

 

 "أَلا أُعَلِّمُكَ دُعَاءً تَدْعُو بِهِ لَوْ كَانَ عَلَيْكَ مِثْلُ جَبَلٍ دَيْنًا لأَدَّى اللهُ عَنْكَ؟ قُلْ يَا مُعَاذُ: اللَّهُمَّ مَالِكُ الْمُلْكِ، تُؤْتِي الْمُلْكَ مَنْ تَشَاءُ، وَتَنْزِعُ الْمُلْكَ مِمَّنْ تَشَاءُ، وَتُعِزُّ مَنْ تَشَاءُ، وَتُذِلُّ مَنْ تَشَاءُ، بِيَدِكَ الْخَيْرِ إِنَّكَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، رَحْمَانُ الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ، تُعْطِيهُمَا مَنْ تَشَاءُ، وَتَمْنَعُ مِنْهُمَا مَنْ تَشَاءُ، ارْحَمْنِي رَحْمَةً تُغْنِينِي بِهَا عَنْ رَحْمَةِ مَنْ سِوَاكَ"

((Je, nikufundishe duaa ambayo ukiiomba basi ikiwa una deni mfano wa mlima wa Uhud, Allaah Atakukidhia.  Sema ya Mu’aadh: “Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, Unampa ufalme Umtakaye, na Unamuondoshea ufalme Umtakaye, na Unamtukuza Umtakaye, na Unamdhalilisha Umtakaye, khayr imo Mkononi Mwako.  Hakika Wewe juu ya kila kitu ni Muweza. Mwingi wa rahmah duniani na Aakhirah Mwenye kurehemu, Unampa rahmah mbili hizo Umtakaye na Unamnyima Umtakaye. Nirehemu rahmah itakayonitosheleza kwayo rahmah isiyotoka kwa mwengine isipokuwa Wewe.)) [Hadiyth Hasan - Swahiyh At-Targhiyb (1821)]

 

Na pia Akaihusisha sifa hiyo kwa mja Wake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

لَقَدْ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِكُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِتُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُم بِالْمُؤْمِنِينَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿١٢٨﴾

Kwa yakini amekujieni Rasuli anayetokana na nyinyi wenyewe, ni yanamtia mashaka (na huzuni) yanayokutaabisheni, anakujalini (muongoke) mwenye huruma kwa Waumini ni mwenye huruma mno, mwenye rahmah. [At-Tawbah: 128]

 

Hivyo Waumini ni wenye neema na jina hili la Ar-Rahiym na lile la Ar-Rahman kama ilivyo katika Hadiyth: ((…Atakamilisha rahmah mia moja kwa mawalii Wake siku ya Qiyaamah)) [Hadiyth Swahiyh kwa sharti la Shaykhaan; Al-Bukhaariy na Muslim - angalia ‘Zawaaid Al-Muwatwaa na Al-Musnad 1/53].

 

Na Sifa au Majina haya mawili yametajwa katika Qur-aan kwa pamoja katika Aayah kadhaa mfano:

وَإِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الرَّحْمَـٰنُ الرَّحِيمُ ﴿١٦٣﴾

163. “Na Ilaah wenu (Allaah) ni Ilaah Mmoja, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mwingi wa rahmah, Mwenye kurehemu.” [Al-Baqarah: 163]

 

حم ﴿١﴾

Haa Miym.

 

 

تَنزِيلٌ مِّنَ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ ﴿٢﴾

Ni uteremsho kutoka kwa Mwingi wa Rahmah, Mwenye kurehemu. [Fusw-Swilat: 1-2]

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ ۖ هُوَ الرَّحْمَـٰنُ الرَّحِيمُ ﴿٢٢﴾

Yeye ni Allaah, Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye. Mjuzi wa ghayb na ya dhahiri, Yeye Ndiye Mwingi wa rahmah, Mwenye kurehemu. [Al-Hashr: 22]

 

Ama Sifa ya Rahiym imetajwa pamoja na Sifa au Majina Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) mbali mbali khaswa pamoja na Al-Ghafuwr (Mwingi wa kufughuria) na Al-‘Aziyz (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika). Mifano michache:

قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّـهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّـهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣١﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Mkiwa mnampenda Allaah, basi nifuateni mimi, Atakupendeni Allaah na Atakughufurieni dhambi zenu. Na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.  [Aal-‘Imraan: 31]

 

وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ وَأَنَّ اللَّـهَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٠﴾

Na lau si fadhila ya Allaah juu yenu na rahmah Yake, na kwamba Allaah ni Mwenye huruma mno, Mwenye kurehemu. [An-Nuwr: 20]

 

وَاسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي رَحِيمٌ وَدُودٌ ﴿٩٠﴾

“Na ombeni maghfirah kwa Rabb wenu, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu ni Mwenye kurehemu, Mwenye upendo khalisi.”  [Huwd: 20]

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِّنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ ۖ وَلَا تَجَسَّسُوا وَلَا يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا ۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ ﴿١٢﴾

Enyi mlioamini! Jieupusheni sana na dhana kwani hakika baadhi ya dhana ni dhambi. Na wala msifanyiane ujasusi, na wala wasisengenyane baadhi yenu wengineo. Je, anapenda mmoja wenu kwamba ale nyama ya nduguye aliyekufa? Basi mmelichukia hilo! Na mcheni Allaah! Hakika Allaah ni Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [Al-Hujuraat: 12]

 

بِنَصْرِ اللَّـهِ ۚ يَنصُرُ مَن يَشَاءُ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿٥﴾

Kwa nusura ya Allaah. Anamnusuru Amtakaye, Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu. [Ar-Ruwm: 5]

 

إِنَّا كُنَّا مِن قَبْلُ نَدْعُوهُ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ﴿٢٨﴾

Hakika sisi tulikuwa kabla Tunamuomba Yeye Pekee, hakika yeye Ndiye Mwingi wa huruma na fadhila, Mwenye kurehemu.” [Atw-Twuwr: 28]

 

 

 

 

 

Share

006-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-HAYYU

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْحَيّ

006 - AL-HAYYU

 

 

 

AL-HAYYU: Aliye hai daima

 

Aliye hai kinyume na aliyekufa, mkamilifu katika maisha yake Aliyetukuka.  Hakuna katika uwepo aliyekuwa na maisha yake mwenyewe kwa dhati yake, isipokuwa Allaah (‘Azza wa Jalla) Peke Yake.

 

Mwenye uhai mkamilifu wa uwepo Wake, na mkamilifu kwa zama Zake.

Maisha Yake yametangulia; hakutanguliwa na kutokuwepo, wala hakumfikii kutokuwepo wala kuondoka. Kila kiumbe kitatoweka isipokuwa Yeye kama Anavyosema:

 

وَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ ۘ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۚ كُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ ۚ لَهُ الْحُكْمُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٨٨﴾

Na wala usiombe pamoja na Allaah mungu mwengine. Hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye. Kila kitu ni chenye kuhiliki isipokuwa Wajihi Wake. Hukumu ni Yake Pekee na Kwake Pekee mtarejeshwa. [Al-Qaswasw: 88]

 

Na pia:

كُلُّ مَنْ عَلَيْهَا فَانٍ ﴿٢٦﴾

Kila aliyekuwa juu yake (ardhi) ni mwenye kutoweka.

 

وَيَبْقَىٰ وَجْهُ رَبِّكَ ذُو الْجَلَالِ وَالْإِكْرَامِ ﴿٢٧﴾

Na utabakia Wajihi wa Rabb wako Mwenye Ujalali Na Ukarimu.  [Ar-Rahmaan: 26-27]

 

Imaam As-Sa’dy (Rahimahu Allaah) amesema: “Yaani, kila kilichopo juu ya ardhi kati ya bin Aadamu na majini na wanyama na viumbe vyote vinginevyo vitatoweka na vitakufa na vitaangamia na Atabakia Aliye hai Ambaye hafi.”

 

Katika ukamilifu wa maisha Yake, Hachukuliwi na usingizi, wala upungufu wala udhaifu wala usahaulifu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ  

Allaah, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliye hai daima, Msimamia kila kitu. Haumchukui usingizi wala kulala.  [Al-Baqarah: 255]

 

Amethibitisha pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Jina Lake au Sifa Yake hiyo katika Aayah kadhaa nyinginezo: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَتَوَكَّلْ عَلَى الْحَيِّ الَّذِي لَا يَمُوتُ

Na tawakali kwa Aliye hai Ambaye Hafi.  [Al-Furqaan: 58]

 

هُوَ الْحَيُّ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ فَادْعُوهُ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ ۗ الْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٦٥﴾

Yeye Ndiye Aliye hai daima hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye; basi muombeni Yeye wenye kumtakasia ‘ibaadah. AlhamduliLLaah, Himidi Anastahiki Allaah Rabb wa walimwengu.  [Ghaafir: 65]

 

Na Limetajwa Jina hili la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) pamoja na Al-Qayyuwm (Msimamia kila kitu) mara tatu katika Qur-aan:

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ

Allaah, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliye hai daima, Msimamia kila kitu [Al-Baqarah: 255]

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ﴿٢﴾

Allaah, Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliye hai daima, Msimamia kila kitu. [Aal-‘Imraan: 2]

 

وَعَنَتِ الْوُجُوهُ لِلْحَيِّ الْقَيُّومِ ۖ وَقَدْ خَابَ مَنْ حَمَلَ ظُلْمًا ﴿١١١﴾

Nyuso zitanyenyekea kwa Aliye hai daima, Msimamizi wa kila kitu. [Twaahaa: 111]

 

Na Majina haya mawili ndio ambayo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema kuwa ni Majina Matukufu kabisa ambayo mtu akiomba du’aa kutawassal kwayo, du’aa yake huitikiwa, kwa dalili zifuatazo:  

 

عَنْ الْقَاسِمِ عَنْ أَبِي أُمَامَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ: ((اسْمُ اللَّهِ الأَعْظَمُ الَّذِي إِذَا دُعِيَ بِهِ أَجَابَ فِي سُوَرٍ ثَلاَثٍ: الْبَقَرَةِ ,وَآلِ عِمْرَانَ, وَطه))

Kutoka kwa Al-Qaasim, kutoka kwa Abuu Umaamaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jina Tukufu  kabisa la Allaah  Ambalo likiombewa kwalo Anaitikia, limo katika Suwrah tatu; Al-Baqarah, Aal-‘Imraan, na Twaahaa)) [Swahiyh Ibn Maajah (3124)]

 

 عَنْ أَسْمَاءَ بِنْتِ يَزِيدَ (رضي الله عنها) أَنَّ النَّبِيَّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((اسْمُ اللَّهِ الأَعْظَمُ فِي هَاتَيْنِ الأَيَتَيْنِ: (وَإِلَهُكُمْ إِلَهٌ وَاحِدٌ لاَ إِلَهَ إلاَّ هُوَ الرَّحْمَنُ الرَّحِيمُ)  وَفَاتِحَةِ آلِ عِمْرَانَ (الم اللَّهُ لاَ إِلَهَ إلاَّ هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّوم).

Kutoka kwa Asmaa bint Yaziyd  (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jina Tukufu kabisa la Allaah limo katika Aayah zifuatazo: Na Ilaah wenu (Allaah) ni Ilaah Mmoja, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mwingi wa rahmah, Mwenye kurehemu.” (Al-Baqarah: 163)  na ufunguo (mwanzo) wa Aal-‘Imraan:  “Allaah, Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliye hai daima, Msimamia kila kitu. (Aal-‘Imraan: 2). [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy,  Ibn Maajah – Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

Na katika du’aa za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):  

 

 اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمْتُ وَبِكَ آمَنْتُ وَعَلَيْكَ تَوَكَّلْتُ وَإِلَيْكَ أَنَبْتُ وَبِكَ خَاصَمْتُ. اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِعِزَّتِكَ لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ أَنْ تُضِلَّنِي أَنْتَ الْحَيُّ الَّذِي لاَ يَمُوتُ وَالْجِنُّ وَالإِنْسُ يَمُوتُونَ

Allaahumma Laka aslamtu, wa Bika aamantu, wa ‘Alayka tawakkaltu, wa Ilayka anabtu, wa Bika khaaswamtu. Allaahumma inniy a’uwdhu bi-Izzatika laa ilaaha illa Anta an-tudhwillaniy Antal-Hayyu Alladhiy  laa Yamuwtu wal-jinnu wal-insu yamuwtuwna.

Ee Allaah, Kwako najisalimisha na Kwako naamini na Kwako natawakali na Kwako narejea kutubia na Kwako nagombana [dhidi ya adui]. Ee Allaah, hakika mimi najikinga kwa ‘Izzah Utukufu wako, Hapana Muabudiwa wa haki ila Wewe Usije kunipotoa Wewe Uliye hai daima Ambaye Hafi ilihali majini na watu wanakufa.  [Muslim, Ahmad]

 

لا إلهَ إلاّ اللّه وحدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ المُلْـكُ ولهُ الحَمْـد، يُحْيـي وَيُميـتُ وَهُوَ حَيٌّ لا يَمُـوت، بِيَـدِهِ الْخَـيْرُ وَهوَ عَلىَ كلّ شيءٍ قَدِيرٌ.

Laa ilaaha illa Allaahu Wahdahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu, Yuhyiy wa Yumiytu wa Huwa Hayyun laa yamuwtu, Biyadihil-khayru wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr

Hapana Muabudiwa wa haki ila Allaah, Yu Peke Yake, Hana mshirika, ni Wake Ufalme na Himdi ni Zake,  Anahuisha na Anafisha, Naye ni hai Asiyekufa, khayr iko mikononi Mwake, na Yeye juu ya kila kitu ni Muweza. [Hadiyth ya ‘Umar bin Al-Khattwaab kaikusanya At-Tirmidhiy (5/291) [3429], Al-Haakim (1/538), Ibn Maajah [2235] Ad-Daarimiy na ameipa daraja ya Hasan Al-Albaaniy  katika Swahiyh Ibn Maajah (2/21) na Swahiyh At-Tirmidhiy (3/152). Na vilevile katika Swahiyh Al-Jaami’ (6231)] 

 

يا حَـيُّ يا قَيّـومُ بِـرَحْمَـتِكِ أَسْتَـغـيث، أَصْلِـحْ لي شَـأْنـي كُلَّـه، وَلا تَكِلـني إِلى نَفْـسي طَـرْفَةَ عَـين

Yaa Hayyu Yaa Qayyuwm bi-Rahmatika astaghiythu, Aswlih-liy sha-ani kullahu walaa takilniy ilaa nafsiy twarfata ‘aynin

Ee Uliye hai daima, Msimamizi wa kila kitu, kwa rahmah Zako ninakuomba uniokoe, nitengenezee mambo yangu  yote, wala usiniachie  mambo yangu mwenyewe (pasina kunisaidia) hata kwa (muda mdogo kama muda wa) kupepesa jicho. [Hadiyth ya Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) - Abuu  Daawuwd (4/3180), At-Tirmidhiy (5/465), Al-Haakim, Swahiyh At-Targhiyb (1/273), Swahiyh Al-Jaami’ [5820]  

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ (رضي الله عنه) قَالَ: كَانَ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) إِذَا كَرَبَهُ أَمْرٌ قَالَ: ((يَا حَيُّ يَا قَيُّومُ بِرَحْمَتِكَ أَسْتَغِيثُ))

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapofikwa na janga husema: ((Yaa Hayyu Yaa Qayyuwm bi Rahmatika astaghiythu - Ee Uliye hai daima, Msimamia wa kila kitu, kwa rahmah Zako naomba uokozi)) [At-Tirmidhy Hadiyth Hasan]

 

من قالَ: أستَغفرُ اللَّهَ الَّذي لا إلَهَ إلَّا هوَ الحيَّ القيُّومَ، وأتوبُ إليهِ، غُفِرَ لَهُ، وإن كانَ قد فرَّ منَ الزَّحفِ

Atakayesema: “AstaghfiruLLaah Alladhiy laa ilaaha illa Huwa Al-Hayyu Al-Qayyuwm, wa atuwbu Ilayhi.

Naomba maghfirah kwa Ambaye hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Yeye Aliye hai daima, Msimamizi wa kila kitu, na natubia Kwake,

Ataghufuriwa hata akiwa amekimbia katika vita. [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na Al-Haakim Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas’uwd, Zayd bin Haarithah mkombolewa wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), Abu Bakr Asw-Swiddiyq, Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy, Anas bin Maalik, Baraa bin ‘Aazib (Radhwiya Allaahu ‘anhum) – As-Silsilah Asw-Swahiyhah (2727), Swahiyh At-Targhiyb (1623). Swahiyh Abiy Daawuwd (1517)]

 

 

Share

007-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-QAYYUWM

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

الْقَيُّوم

 

007 - AL-QAYYUWM

 

 

 

AL-QAYYUWM: Msimamia kila kitu.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Qayyuwm msimamizi wa kila kitu.

Kama ilivyotangulia kutajwa katika Jina la Al-Hayyu kwamba Jina hili limetajwa pamoja na Al-Qayyuwm katika Aayah:

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ

Allaah, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliyehai daima, Msimamia kila kitu. [Al-Baqarah: 255 na Aal-‘Imraan: 2]

 

Na:

وَعَنَتِ الْوُجُوهُ لِلْحَيِّ الْقَيُّومِ ۖ وَقَدْ خَابَ مَنْ حَمَلَ ظُلْمًا ﴿١١١﴾

Nyuso zitanyenyekea kwa Aliye Hai daima, Msimamizi wa kila kitu. [Twaahaa: 111]

 

Al-Qayyuwm ni:

1. Mwenye kusimamia mambo Mwenyewe daima. Hakumuhitajia yeyote katika njia yoyote ile kwa sababu ya ukamilifu Wake na kujitosheleza Kwake na uwezo Wake.

 

2. Mwenye kuwasimamia viumbe Vyake, ardhini na mbinguni, wote ni mafakiri Kwake Naye Ndiye tajiri katika kila kitu.

يَا أَيُّهَا النَّاسُ أَنتُمُ الْفُقَرَاءُ إِلَى اللَّـهِ ۖ وَاللَّـهُ هُوَ الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ ﴿١٥﴾

Enyi watu!  Nyinyi ni mafakiri kwa Allaah! Na Allaah Ndiye Mkwasi, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Faatwir: 15]

 

 

Hata ‘Arshi imesimama kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa), na wabebaji wake vivyo hivyo.

 

3. Mwenye kusimamia ulimwengu wote, wa juu na wa chini, na waliomo katika viumbe na vitu na katika hali zote: kwa kuwapangia riziki zao, kwa kuwahifadhi na kuwalinda, kuwaongoza katika mambo yote kwa uangalizi na kuwapa kila chenye kuwahitajia wao kubaki kwake, na ustawi wake kila wakati. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

قَالَ فَمَن رَّبُّكُمَا يَا مُوسَىٰ ﴿٤٩﴾

(Fir’awn) Akasema: “Basi ni nani Rabb wenu ee Muwsaa?”

 

قَالَ رَبُّنَا الَّذِي أَعْطَىٰ كُلَّ شَيْءٍ خَلْقَهُ ثُمَّ هَدَىٰ ﴿٥٠﴾

(Muwsaa) Akasema: “Rabb wetu ni Yule Aliyekipa kila kitu umbo lake, kisha Akakiongoza.” [Twaahaa: 49-50]

 

Na Anasema:

وَمَا مِن دَابَّةٍ فِي الْأَرْضِ إِلَّا عَلَى اللَّـهِ رِزْقُهَا وَيَعْلَمُ مُسْتَقَرَّهَا وَمُسْتَوْدَعَهَا ۚ

Na hakuna kiumbe chochote kitembeacho katika ardhi isipokuwa riziki yake iko kwa Allaah; na (Allaah) Anajua mahali pake pa kustakiri na pa kuhifadhiwa kwake. [Huwd: 6]

 

4. Yeye Ta’aalaa ni Qayyuwm: Mwenye kusimamia kila kitu, na Mwenye kubaki kuendelea kusimamia kila kitu mpaka baada ya Qiyaamah kuwaingiza waja Wake; Waumini kuingia Jannah na makafiri na waovu kuingi motoni.  Haondoki wala Habadiliki, Anadumu daima kusimaimia kila kitu, Ambaye Hajaacha kuwa na Hatoacha kuwa (kuwepo), Mwenye kusifika kwa ukamilifu na utukufu, katika hali zote: kwa dhati Yake, sifa Zake, matendo yote na utawala Wake.

 

5. Yeye Ndiye Anayeisimamia kila nafsi kwa kuichunga, kuihesabu, malipo kwa kila dogo na kubwa, Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):  

أَفَمَنْ هُوَ قَائِمٌ عَلَىٰ كُلِّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ ۗ  

Je, basi Anayeisimamia kila nafsi kwa yale iliyoyachuma [Ar-Ra’d: 33]

 

6. Usimamizi Wake umekamilika: Amesimamia mbingu na ardhi nazo zimetulia; mbingu zimesimama bila ya kuwa na nguzo, hazitingishiki, mbingu wala haijawahi kuanguka katika ardhi. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

خَلَقَ السَّمَاوَاتِ بِغَيْرِ عَمَدٍ تَرَوْنَهَا ۖ وَأَلْقَىٰ فِي الْأَرْضِ رَوَاسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمْ وَبَثَّ فِيهَا مِن كُلِّ دَابَّةٍ ۚ وَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ ﴿١٠﴾

(Allaah) Ameumba mbingu bila ya nguzo mnaziona, na Akatupa katika ardhi milima isikuyumbieni yumbieni, na Akaeneza humo kila viumbe vinavyotembea. Na Tukateremsha kutoka mbinguni maji, Tukaotesha humo kila aina ya mimea mizuri yenye manufaa. [Luqmaan: 10]

 

إِنَّ اللَّـهَ يُمْسِكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ أَن تَزُولَا ۚ وَلَئِن زَالَتَا إِنْ أَمْسَكَهُمَا مِنْ أَحَدٍ مِّن بَعْدِهِ ۚ إِنَّهُ كَانَ حَلِيمًا غَفُورًا ﴿٤١﴾

Hakika Allaah Anazuia mbingu na ardhi zisitoweke. Na zikitoweka, hakuna yeyote wa kuzishikilia baada Yake, hakika Yeye daima Mpole wa kuwavumilia waja, Mwingi wa kughufuria.  [Faatwir: 41]

 

Kisha Siku ya Qiyaamah Atabaidilisha ardhi isiyo ardhi hii na mbingu hali kadhalika.

Na miongoni mwa du'aa za Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika Swalaah za usiku:

اللّهُـمَّ لَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ  نـورُ السَّمـواتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فيـهِنَّ، وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ قَـيِّمُ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ وَمَنْ فيـهِنَّ، (وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ رَبُّ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ  وَمَنْ فيـهِنَّ) (وَلَكَ الْحَمْدُ لَكَ مُلْـكُ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ  وَمَنْ فيـهِنَّ) (وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ مَلِـكُ السَّـمواتِ وَالأَرْضِ)

Allaahumma Lakal-Hamdu Anta Nuwrus-samaawati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Anta Qayyimus-samaawaati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Anta Rabbus-samawaati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Laka Mulkus-samaawaati wal ardhwi waman fiyhinna....

Ee Allaah! Himdi ni Zako Wewe Ndiye Nuru ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, Himdi ni Zako Wewe Ndiye Msimamizi wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na Himdi ni Zako Wewe Ndiye  Rabb  wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake; na Himdi ni Zako Wewe Ndiye  Mfalme wa mbingu na ardhi... [Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) - Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (3/3), (11/116), (13/371, 423, 465), na Muslim kwa ufupi kama hivyo (1/532)]

 

7. Na usimamizi Wake (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na kupanga Kwake mambo ya viumbe Vyake, na kufanya Kwake mambo kwa ukamilifu na uadilifu na haki, Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

شَهِدَ اللَّـهُ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ وَالْمَلَائِكَةُ وَأُولُو الْعِلْمِ قَائِمًا بِالْقِسْطِ ۚ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ  

Allaah Ameshuhudia kwamba hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye; na Malaika, na wenye elimu (wameshuhudia kwamba Allaah) ni Mwenye kusimamisha (uumbaji Wake) kwa uadilifu. Hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye [Aal-‘Imraan: 18]

 

8. Na Ukamilifu wa usimamizi Wake ni kwamba Hashikwi na usingizi wala kulala:

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْحَيُّ الْقَيُّومُ ۚ لَا تَأْخُذُهُ سِنَةٌ وَلَا نَوْمٌ ۚ  

Allaah, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Aliye hai daima, Msimamia kila kitu. Haumchukui usingizi wala kulala  [Al-Baqarah: 255]

 

Na du’aa ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ambayo amesema: baada ya mtu kuomba du’aa hii:

“Kwa yakini amemuomba Allaah kwa Jina Lake Tukufu Ambalo Anapoombwa kwalo Anaitikia na Anapotakwa kwalo jambo hutoa:

 اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ بِأَنَّ لَكَ الْحَـمْدُ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْـتَ وَحْـدَكَ لا شَـريكَ لَـكَ المَنّـانُ يا بَديـعَ السَّمواتِ وَالأَرْضِ يا ذا الجَلالِ وَالإِكْـرام، يا حَـيُّ يا قَـيّومُ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ الجَـنَّةَ وَأَعـوذُ بِـكَ مِنَ الـنّار

Allaahumma inniy as-aluka bi-anna Lakal-Hamdu laa ilaaha illaa Anta Wahdaka laa shariyka Laka Al-Mannaanu yaa Badiy’as-samaawaati wal-ardhwi, yaadhal-Jalaali wal Ikiraami, yaa Hayyu yaa Qayyuwmu, inniy as-alukal-Jannata wa a’uwdhu bika minan-naari

Ee Allaah hakika mimi nakuomba, kwa vile Himdi Zako, hapana Muabudiwa wa haki ila Wewe, Uko Peke Yako,  wala Huna mshirika, Mwingi wa Kuneemesha.  Ee Mwanzishi wa mbingu na ardhi, Ee Jalali na Mwenye Ukarimu, Ee Uliye hai daima, Msimamizi wa kila kitu, hakika mimi nakuomba Jannah, na najikinga Kwako kutokana na moto.” [Hadiyth ya Anas bin Maalik (Radhiywa Allaahu ‘anhu) - Abu Daawuwd [1495], An-Nasaaiy (3/52), Ibn Maajah [3858] na taz. Swahiyh Ibn Maajah (2/329)]

 

 

 

Share

008-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: ASW-SWAMADU

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الصَّمَدُ

008 - ASW-SWAMADU

 

 

 

ASW-SWAMADU:  Aliyekamilika sifa za kila aina ya utukufu Wake, Mwenye kukusudiwa kwa haja zote.

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimsikia mtu akiomba katika du’aa yake:

 

 اللَّهُمَّ إنِّي أسْأَلُكَ بِأنِّي أشْهَدُ أنَّكَ أنْتَ اللَّهُ لا إِلَهَ إِلاَّ أنْتَ الأحَدُ الصَّمَدُ الَّذِي لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ وَلَمْ يَكُنْ لَهُ‏ ‏كُفُوًا ‏‏أحَدٌ، فقال: ((وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَقَدْ سَألَ اللَّهَ بِاسْمِهِ الأعْظَمِ الَّذِي إذَا دُعِيَ بِهِ أجَابَ وَإذَا سُئِلَ بِهِ أعْطَى))   

 

“Allaahumma inni as-aluka bianniy ash-hadu Annaka Anta-Allaahu laa ilaaha illa Anta Al-Ahadu Asw-Swamadu, Alladhiy lam Yalid walam Yuwlad walam Yakun Lahuu kufuwan ahad”.

 

Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kwa kushuhudia kwamba hakika Wewe ni Allaah, hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Wewe, Mmoja, Aliyekamilika sifa za kila aina ya utukufu Wake, Mwenye kukusudiwa kwa haja zote, Ambaye Hakuzaa na wala Hakuzaliwa, Na wala haiwi Awe na yeyote anayefanana na kulingana Naye.”

Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, kwa yakini Ameomba kwa Jina Lake Tukufu kabisa ambalo Anapoombwa kwalo [du’aa] Anaitikia na Anapotakwa kwalo [jambo] Hutoa)) [Hadiyth ya Buraydah bin Al-Haswiyb Al-Aslamiyy  kutoka kwa baba yake Radhwiya Allaahu ‘anhumaa – Swahiyh Ibn Maajah (3125) Swahiyh At-Tirmidhy  (3475), Swahiyh Abi Daawuwd (1493), Swahiyh At-Targhiyb  (1640)]

 

Asw-Swamadu; As-Sayyid (Bwana) Aliyekamilika kwa ubwana Wake na Aliyekamilika katika aina zote za ubwana na utukufu mbinguni na ardhini. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَلَهُ الْكِبْرِيَاءُ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ 

Na Adhama, Utukufu, Ujalali ni Wake Pekee mbinguni na ardhini. [Al-Jaathiyah: 37]

 

Asw-Swamadu: Ni Yeye Allaah (‘Azza wa Jalla) Mwenye sifa hii, ambayo haimstahiki yeyote asiyekuwa Yeye. Yeye Ndiye Anayekusudiwa na viumbe Wake wote; wana Aadam na majini, ulimwengu wa juu na wa chini, ni Yeye tu wa kukusudiwa.

 

Hakuzaa wala hakuzaliwa, hafi wala harithiwi, kwa sababu si anayezaliwa ili afe, wala hafi ili arithiwe. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾

Sema: “Yeye ni Allaahu Mmoja Pekee.

 

اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾

“Allaah ni Aliyekamilika sifa za utukufu Wake, Mkusudiwa haja zote. 

 

لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ﴿٣﴾

“Hakuzaa na wala Hakuzaliwa.

 

وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ ﴿٤﴾

“Na wala haiwi Awe na yeyote anayefanana na kulingana Naye.” [Al-Ikhlaasw]

 

Na katika Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ كَذَّبَنِي ابْنُ آدَمَ وَلَمْ يَكُنْ لَهُ ذَلِكَ ، وَشَتَمَنِي وَلَمْ يَكُنْ لَهُ ذَلِكَ ، فَأَمَّا تَكْذِيبُهُ إِيَّايَ، فَقَوْلُهُ لَنْ يُعِيدَنِي كَمَا بَدَأَنِي وَلَيْسَ أَوَّلُ الْخَلْقِ بِأَهْوَنَ عَلَيَّ مِنْ إِعَادَتِه،ِ وَأَمَّا شَتْمُهُ إِيَّايَ فَقَوْلُهُ اتَّخَذَ اللَّهُ وَلَدًا وَأَنَا الْأَحَدُ الصَّمَدُ لَمْ أَلِدْ وَلَمْ أُولَدْ وَلَمْ يَكُنْ لِي كُفْئًا أَحَدٌ)) البخاري والنسائ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: ((Allaah Amesema: Bin Aadam amenikadhibisha na hana haki ya kufanya hivyo, na amenitukana na hana haki ya kufanya hivyo. Ama kunikadhibisha kwake ni kusema: Hatonirejesha (tena) kama Alivyoniumba (Hatonifufua kama vile Alivyoniumba). Na kuumba hakukuwa rahisi Kwangu kuliko kumfufua. Ama kunitukana kwake ni kule kusema: Allaah Ana mtoto wakati Mimi ni Ahad (Mmoja Pekee), Asw-Swamad (Aliyekamilika sifa za utukufu Wake, Mkusudiwa haja zote), Sikuzaa wala Sikuzaliwa na hakuna chochote kinachofanana na kulingana Nami)) [Al-Bukhaariy na An-Nasaaiy]

 

Na Suwrah hiyo ya Al-Ikhlaasw ni Suwrah ambayo thawabu zake katika kuisoma ni sawasawa na thawabu za kusoma thuluthi ya Qur-aan kwa dalili zifuatazo:

 

 عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ لأَصْحَابِهِ: ((أَيَعْجِزُ أَحَدُكُمْ أَنْ يَقْرَأَ ثُلُثَ الْقُرْآنِ فِي لَيْلَةٍ؟)) فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَيْهِمْ وَقَالُوا: أَيُّنَا يُطِيقُ ذَلِكَ يَا رَسُولَ اللَّهِ؟ فَقَالَ: ((اللَّهُ الْوَاحِدُ الصَّمَدُ ثُلُثُ الْقُرْآنِ))  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amewaambia Maswahaba wake: ((Je, anaweza mmoja wenu asome thuluthi ya Qur-aan katika usiku mmoja?)) Likawa jambo gumu kwao wakasema: Tuwezeje sisi kufanya hivyo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Allaah, Al-Waahidu (Mmoja Pekee, Asw-Swamadu (Mkusudiwa wa yote) ni thuluthi ya Qur-aan)) [Al-Bukhaariy  Na Muslim]

 

 عَنْ أَبِي سَعِيدٍ أَنَّ رَجُلًا سَمِعَ رَجُلًا يَقْرَأُ قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَدٌ يُرَدِّدُهَا، فَلَمَّا أَصْبَحَ جَاءَ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَذَكَرَ ذَلِكَ لَهُ ، وَكَأَنَّ الرَّجُلَ يَتَقَالُّهَا  أي يراها قليلة  فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ : ((وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ إِنَّهَا لَتَعْدِلُ ثُلُثَ الْقُرْآن))

Pia imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyyi (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba mtu mmoja alimsikia mtu akisoma Qul-Huwa-Allaahu Ahad na akiikariri. Asubuhi yake akamwendea Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamtajia hilo na alidhania kuwa ni kisomo kidogo tu. Lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, hiyo ni sawa na thuluthi ya Qur-aan)) [Al-Bukhaariy (6643)]

 

Asw-Swamadu; Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni As-Sayyid Anayetiiwa; amri zake zinatekelezwa katika ardhi yake na mbingu yake, haipitishwi amri isipokuwa kwa idhini Yake. Yeye (‘Azza wa Jalla) ni Mwenye shani ya juu na uwezo. Yeye  ni mwenye wasaa wa sifa na ukubwa ambao haukusaza sifa ya ukamilifu ila amesifika nayo, kwa upeo wake na ukamilifu wake.

 

Asw-Swamadu ni Ambaye Hali wala Halishwi. Anasema:

 

قُلْ أَغَيْرَ اللَّـهِ أَتَّخِذُ وَلِيًّا فَاطِرِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَهُوَ يُطْعِمُ وَلَا يُطْعَمُ ۗ قُلْ إِنِّي أُمِرْتُ أَنْ أَكُونَ أَوَّلَ مَنْ أَسْلَمَ ۖ وَلَا تَكُونَنَّ مِنَ الْمُشْرِكِينَ ﴿١٤﴾

Sema: “Je, nimfanye mlinzi asiyekuwa Allaah; Muanzilishi wa mbingu na ardhi, Naye Ndiye Anayelisha na wala halishwi?” [Al-An’aam: 14]

Asw-Swamadu Ambaye Hana mwisho abadan Atabakia daima baada ya kutoweka viumbe Vyake vyote.

 

Mambo yote yanaishia Kwake, wala haikidhiwi jambo bila Yeye. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

قُلْ إِنَّ الْأَمْرَ كُلَّهُ لِلَّـهِ

Sema: “Hakika amri yote ni ya Allaah.” [Aal-‘Imraan: 154]

 

وَلِلَّـهِ غَيْبُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَإِلَيْهِ يُرْجَعُ الْأَمْرُ كُلُّهُ فَاعْبُدْهُ وَتَوَكَّلْ عَلَيْهِ ۚ وَمَا رَبُّكَ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿١٢٣﴾

Na ni ya Allaah (Pekee) ghayb ya mbingu na ardhi, na Kwake hurudishwa mambo yote; basi mwabudu Yeye na tawakali Kwake. Na Rabb wako si Mwenye kughafilika na yale myatendayo. [Huwd: 123]

 

 

 

Share

009-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-AWWALU

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الأوَّلُ

009 - AL-AWWALU

 

 

 

AL-AWWALU:  Wa Awali bila ya mwanzo.

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣﴾

Yeye Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yake, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na Aliye juu kabisa hakuna kitu juu Yake, na Aliye karibu kabisa, hakuna kitu kilicho karibu kuliko Yeye, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi.  [Al-Hadiyd: 3]

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametufasiria maana ya Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) manne hayo yaliyotajwa pamoja, alikuwa akiomba katika du’aa:  

 اللهُمَّ أَنْتَ الأَوَّلُ فَليْسَ قَبْلكَ شيء، وَأَنْتَ الآخِرُ فَليْسَ بَعْدَكَ شيء، وَأَنْتَ الظَّاهِرُ فَليْسَ فَوْقَكَ شيء، وَأَنْتَ البَاطِنُ فَليْسَ دُونَكَ شيء، اقْضِ عَنَّا الدَّيْنَ وَاغْنِنَا مِنَ الفَقْرِ

Ee Allaah, Wewe wa Awali hivyo basi hakuna kitu kabla Yako, Nawe ni wa Mwisho, basi hakuna kitu baada Yako, Nawe Uko juu kabisa hakuna kitu juu yako, Nawe uko karibu kabisa, hakuna kitu kilicho karibu kuliko Wewe, Nikidhie deni langu na nitosheleze kutokana na ufakiri. [Muslim]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye wa Awali wala hakukuwepo na kitu kabla Yake hata kabla ya kuumba chochote kile:  

 عن عِمْرَانَ رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قَال: ((كَانَ اللهُ وَلمْ يَكُنْ شَيْءٌ غيرهُ، وَكَانَ عَرْشُهُ عَلى المَاءِ، ثُمَّ خَلقَ السَّمَاوَاتِ وَالأرْض، وَكَتَبَ فِي الذِّكْرِ كُل شَيْءٍ))  

Imepokelewa kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Alikuwa Allaah na hakukuwa na kitu kabla Yake, na ‘Arsh Yake ilikuwa katika maji, kisha Akaumba mbingu na ardhi, na Akaandika kila kitu katika Adh-Dhikri (Ubao Uliohifadhiwa) [Al-Bukhaariy fiy Kitaabi Bad-i Al-Khalqi]

 

Naye (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Aliyetangulia kila kitu kwa muda usiokuwa na mwisho wake katika kuwepo Kwake, na katika Sifa Zake. Amekamilika dhati Yake, shani Yake iko juu ya kila kitu, kila kitu kina mwanzo wake na mwisho wake isipokuwa Yeye (‘Azza wa Jalla). Kila kitu kinarejea Kwake kwa kupewa na kupatikana na kuendelea, wakati wote. Hakuna Alichokiumba ila tu kitarudi Kwake ndio maana pale mtu anapopatwa na msiba khasa wa kufariki mtu hutamka kalimah ya Istirjaa’

إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ

Sisi ni wa Allaah, na Kwake tunarejea [Muslim na imetajwa katika Qur-aan]  

 

Miongoni mwa faida za maarifa ya Jina hili tukufu ni kuwa, ili mwana Aadam atambue kwamba kwa vile asili yake kuumbwa ni udongo, na kwamba yeye ana mwanzo na ana uhai kwa muda na kisha ana mwisho wake wa kurudia kwa Rabb wa walimwengu. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

كَيْفَ تَكْفُرُونَ بِاللَّـهِ وَكُنتُمْ أَمْوَاتًا فَأَحْيَاكُمْ ۖ ثُمَّ يُمِيتُكُمْ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٢٨﴾

Vipi mnamkufuru Allaah na hali mlikuwa wafu Akakuhuisheni, kisha Atakufisheni, kisha Atakuhuisheni, kisha Kwake mtarejeshwa?  [Al-Baqarah: 28]

 

Na pia:

هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٥٦﴾

Yeye Ndiye Anayehuisha na Anayefisha, na Kwake (Allaah) mtarejeshwa. [Yuwnus: 56]

 

Na kutambua pia uumbaji wa yote yaliyoko duniani yana mwanzo wake. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

إِنَّهُ يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ

Hakika Yeye Anaanzisha uumbaji, kisha Anaurejesha. [Yuwnus: 4]

 

Na Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

كَمَا بَدَأْنَا أَوَّلَ خَلْقٍ نُّعِيدُهُ ۚ وَعْدًا عَلَيْنَا ۚ إِنَّا كُنَّا فَاعِلِينَ ﴿١٠٤﴾

Kama Tulivyoanza umbo la awali Tutalirudisha tena. Ni ahadi iliyo juu Yetu. Hakika Sisi ni Wenye kufanya. [Al-Anbiyaa: 103]

 

Pia mwana Aadam anapata kuona na kukumbuka fadhila za Rabb Wake, na kutangulia Kwake katika kila neema, iwe ni ya ki-Dini au ya kidunia, na sababu na msababishi ni Yeye. Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

أَمَّن يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ وَمَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ ۗ أَإِلَـٰهٌ مَّعَ اللَّـهِ ۚ قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٦٤﴾

Au nani Anayeanzisha uumbaji, kisha Anaurejesha; na nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na kwenye ardhi? [An-Naml: 64]

 

Na pia:

اللَّـهُ الَّذِي خَلَقَكُمْ ثُمَّ رَزَقَكُمْ ثُمَّ يُمِيتُكُمْ ثُمَّ يُحْيِيكُمْ ۖ هَلْ مِن شُرَكَائِكُم مَّن يَفْعَلُ مِن ذَٰلِكُم مِّن شَيْءٍ ۚ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَىٰ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٤٠﴾

Allaah, Ambaye Amekuumbeni, kisha Akakuruzukuni, kisha Anakufisheni, kisha Atakuhuisheni.  [Ar-Ruwm: 40]

 

 

 

 

Share

010-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake: أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-AAKHIRU

 

 

أسماء الله الحسنى وصفاته
 

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake:

 

Alhidaaya.com

 

 

الآخِرُ

 

010 - AL-AAKHIRU

 

 

 

AL-AAKHIRU: Wa Mwisho, hapana kitu baada Yake.

 

 

Kama ilivyotangulia katika Jina la Allaah, Al-Awwalu, kwamba Majina manne ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) yametajwa katika Aayah:

هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣﴾

Yeye Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yake, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na Aliye juu kabisa hakuna kitu juu Yake, na Aliye karibu kabisa, hakuna kitu kilicho karibu kuliko Yeye, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi.  [Al-Hadiyd: 3]

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

وَأَنْتَ الآخِرُ فَليْسَ بَعْدَكَ شيء،  

… Nawe ni wa Mwisho, basi hakuna kitu baada Yako, [Muslim

 

Majina mawili ya Al-Awwalu na Al-Aakhiru kuenea kwake (’Azza wa Jalla) katika zama zote, na kwa viumbe vyote katika kila hali.  [Madaarij As-Saalikiyn (1/31]

 

 

Allaah Mtukuka Ndiye wa Mwisho baada ya kila kitu, Asiyekuwa na ukomo, katika uwepo, sifa; sifa za kutukuka. Yeye Ndiye Mwenye kubaki baada ya kufa kila kitu na kuondoka, vyenye kuzungumza na vilivyokuwa kimya,

 كُلُّ شَيْءٍ هَالِكٌ إِلَّا وَجْهَهُ ۚ

Kila kitu ni chenye kuhiliki isipokuwa Wajihi Wake. [Al-Qaswasw: 88]

 

 

Hakuna atakayebakia ardhini wala mbinguni kwa kuwa vyote vina mwanzo na mwisho isipokuwa Yeye (‘Azza wa Jalla):

رَفِيعُ الدَّرَجَاتِ ذُو الْعَرْشِ يُلْقِي الرُّوحَ مِنْ أَمْرِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ لِيُنذِرَ يَوْمَ التَّلَاقِ ﴿١٥﴾

(Allaah) Mwenye uluwa juu ya vyeo na daraja. Mwenye ‘Arsh, Anapelekea Ar-Ruwh (Wahy) kwa amri Yake kwa Amtakaye miongoni mwa waja Wake, ili aonye Siku ya kukutana.

 

يَوْمَ هُم بَارِزُونَ ۖ لَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِنْهُمْ شَيْءٌ ۚ لِّمَنِ الْمُلْكُ الْيَوْمَ ۖ لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ ﴿١٦﴾

Siku watakayotokeza wao, hakitofichika kitu chochote chao kwa Allaah. “Ufalme ni wa nani leo?” (Allaah Mwenyewe Atajijibu): “Ni wa Allaah Pekee Mmoja, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika. [Ghaafir: 15-16]

 

Na katika Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) iliyopokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

  يَطوي اللهُ عزَّ وجلَّ السَّماواتِ يومَ القيامةِ. ثمَّ يأخذُهنَّ بيدِه اليُمنَى. ثمَّ يقولُ: أنا الملِكُ. أين الجبَّارون؟ أين المُتكبِّرون؟ ثمَّ يَطوي الأرضين بشمالِه. ثمَّ يقولُ: أنا الملِكُ. أين الجبَّارون؟ أين المُتكبِّرون؟

Allaah ‘(Azza wa Jalla) Atakunja mbingu zote Siku ya Qiyaamah kisha Atazikamata Mkononi Mwake wa kuume Atasema: Mimi Ndiye Mfalme. Wako wapi waliojifanya majabari? Wako wapi waliotakabari? Kisha Atakunja ardhi mbili kwa Mkono Wake wa kushoto Atasema: Mimi Ndiye Mfalme, wako wapi waliojifanya majabari. Wako wapi waliotakabari?)) [Muslim 2788]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Ambaye mambo ya waja Wake wote huishia Kwake, katika mambo yote ya kidunia na ya kidini. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba du’aa wakati wa kutaka kulala:

اللّهُـمَّ أَسْـلَمْتُ نَفْـسي إِلَـيْكَ، وَفَوَّضْـتُ أَمْـري إِلَـيْكَ، وَوَجَّـهْتُ وَجْـهي إِلَـيْكَ، وَأَلْـجَـاْتُ ظَهـري إِلَـيْكَ، رَغْبَـةً وَرَهْـبَةً إِلَـيْكَ، لا مَلْجَـأَ وَلا مَنْـجـا مِنْـكَ إِلاّ إِلَـيْكَ...  

Allaahumma aslamtu nafsiy Ilayka, wa fawwadhwtu amriy Ilayka, wa wajjahtu waj-hiya Ilayka, wa alja-tu dhwahriy Ilayka, raghbatan warahbatan Ilayka. Laa malja-a walaa manjaa Minka illaa Ilayka...  

Ee Allaah nimeisalimisha nafsi yangu Kwako, na nimekuachia mambo yangu Wewe na nimeuelekeza uso wangu Kwako na nimeutegemeza mgongo wangu Kwako, kwa matajarajio na kwa kukuogopa, hapana sehemu ya kukimbilia wala ya kujiokoa ila Kwako... [Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (11/113) Muslim (4/2081)]

 

Jina hili Adhimu linathibitisha kuwa hatima ya wana Aadam wote ni kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ambaye Hana Mwisho.

Anasema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

كُلُّ نَفْسٍ ذَائِقَةُ الْمَوْتِ ۖ ثُمَّ إِلَيْنَا تُرْجَعُونَ ﴿٥٧﴾

Kila nafsi itaonja mauti, kisha Kwetu mtarejeshwa. [Al-‘Ankabuwt: 57]

 

قُلْ يَتَوَفَّاكُم مَّلَكُ الْمَوْتِ الَّذِي وُكِّلَ بِكُمْ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمْ تُرْجَعُونَ ﴿١١﴾

Sema: “Atakufisheni Malaika wa mauti ambaye amewakilishwa kwenu, kisha kwa Rabb wenu mtarejeshwa.” [As-Sajdah: 11]

 

 

Na Jina hili linamtambulisha bin Aadam kwamba yeye hana budi kuwa na mwisho, kinyume na Allaah Ambaye ni Wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na kwamba mwisho wa mwana Aadam ni kurudia kwa Muumba wake (‘Azza wa Jalla) na kusimamishwa mbele Yake kuhesabiwa matendo yake:

إِنَّهُ يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ لِيَجْزِيَ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ بِالْقِسْطِ ۚ  

Hakika Yeye Anaanzisha uumbaji, kisha Anaurejesha ili Awalipe kwa uadilifu wale walioamini na wakatenda mema.  [Yuwnus: 4]

 

 Na Anasema pia:

أَفَحَسِبْتُمْ أَنَّمَا خَلَقْنَاكُمْ عَبَثًا وَأَنَّكُمْ إِلَيْنَا لَا تُرْجَعُونَ ﴿١١٥﴾

“Je, mlidhania kwamba Sisi Tulikuumbeni bila kusudio mcheze tu na kwamba nyinyi Kwetu hamtorejeshwa?”  [Al-Muuminuwn: 115]

 

 

 

 

Share

011-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: ADHW-DHWAAHIRU

 

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الظَّاهِرُ

ADHW-DHWAAHIRU

 

 

Adhw-Dhwaahiru: Aliye juu kabisa hakuna kitu juu Yake.

 

Imetajwa katika kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣﴾

Yeye Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yake, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na Aliye juu kabisa hakuna kitu juu Yake, na Aliye karibu kabisa, hakuna kitu kilichokaribu kuliko Yeye, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi.  [Al-Hadiyd: 3]

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

  وَأَنْتَ الظَّاهِرُ فَليْسَ فَوْقَكَ شيء،  

…Nawe Uko juu kabisa hakuna kitu juu yako… [Muslim]

 

Yeye ni Dhahiri kwa vitendo Vyake na hukusudiwa kwa maana nyinginezo mfano: kuwa juu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

فَمَا اسْطَاعُوا أَن يَظْهَرُوهُ

Basi (Ya-juwj na Ma-juwj) hawakuweza kuukwea. [Al-Kahf: 97]

 

yaani kupanda juu yake. Pia ina maana ya kushinda, Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

فَأَيَّدْنَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَىٰ عَدُوِّهِمْ فَأَصْبَحُوا ظَاهِرِينَ ﴿١٤﴾

Tukawatia nguvu wale walioamini dhidi ya maadui zao, wakapambaukiwa wakiwa washindi. [Asw-Swaff: 14]

 

Pia ina maana kusaidia na kama ilivyothibiti katika Suwrat At-Tahriym Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

وَإِن تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِنَّ اللَّـهَ هُوَ مَوْلَاهُ وَجِبْرِيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ بَعْدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ﴿٤﴾

Na mkisaidiana dhidi yake, basi hakika Allaah Ndiye Mlinzi Msaidizi wake na Jibriyl na Waumini wema, na zaidi ya hayo, Malaika pia watasaidia. [At-Tahriym: 4]

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّمَا يَنْهَاكُمُ اللَّـهُ عَنِ الَّذِينَ قَاتَلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَأَخْرَجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ وَظَاهَرُوا عَلَىٰ إِخْرَاجِكُمْ أَن تَوَلَّوْهُمْ ۚ وَمَن يَتَوَلَّهُمْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿٩﴾

Hakika Allaah Anakukatazeni tu kuhusu wale waliokupigeni vita katika Dini, na wakakutoeni kutoka majumbani mwenu, na wakasaidiana juu ya kukutoeni. [Al-Mumtahinah: 9]

 

yaani: wakawasaidia, au kudhihirisha kilichojificha.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Adhw-Dhwaahir:

 

1. Kila kitu kipo chini Yake, na Yeye yupo juu ya kila kitu, hakuna kilichokuwa juu yake [Ibn Jariyr (11/670)]

 

i-       Ujuu wa dhati,

ii-     Na ujuu wa ushindi,

iii-   Ujuu wa shani na uwezo na sifa ya ukamilifu.

 

2. Yeye (‘Azza wa Jalla) ni Adhw-Dhwaahir kwa dalili mbali mbali, kwa Aayah na kwa hoja madhubuti zenye kuthibitisha kupwekeka kwake.

 

3. Yeye (‘Azza wa Jalla) ni Adhw-Dhwaahir Ndiye Ambaye humuona na kumdhihirishia kila Amtakaye katika waja Wake, katika elimu na sayansi mbali mbali, na maarifa ya kiakili na ya kunukuu na ya ghayb. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

وَإِذْ أَسَرَّ النَّبِيُّ إِلَىٰ بَعْضِ أَزْوَاجِهِ حَدِيثًا فَلَمَّا نَبَّأَتْ بِهِ وَأَظْهَرَهُ اللَّـهُ عَلَيْهِ عَرَّفَ بَعْضَهُ وَأَعْرَضَ عَن بَعْضٍ ۖ فَلَمَّا نَبَّأَهَا بِهِ قَالَتْ مَنْ أَنبَأَكَ هَـٰذَا ۖ قَالَ نَبَّأَنِيَ الْعَلِيمُ الْخَبِيرُ ﴿٣﴾

Na pale Nabiy alipompa mmoja wa wake zake jambo la siri, na huyo mke alipoipasha habari na Allaah Akamdhihirishia (Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم), akataarifu baadhi yake na akaacha nyingine [At-Tahriym: 3]

 

Na Anasema (‘Azza wa Jalla):

عَالِمُ الْغَيْبِ فَلَا يُظْهِرُ عَلَىٰ غَيْبِهِ أَحَدًا ﴿٢٦﴾

Mjuzi wa ghayb na wala Hamdhihirishii yeyote ghayb Yake.

 

إِلَّا مَنِ ارْتَضَىٰ مِن رَّسُولٍ فَإِنَّهُ يَسْلُكُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ رَصَدًا ﴿٢٧﴾

Isipokuwa yule Aliyemridhia miongoni mwa Rasuli basi hakika Yeye Anamwekea walinzi mbele yake na nyuma yake.  [Al-Jinn: 26-27]

 

4. Naye ni Adhw-Dhwaahir Ambaye Ametukuza Dini hii pamoja na wenye Dini hii juu ya kila dini, na Akajaalia ni yenye kushinda katika hoja, katika upanga, kwa watu wote, Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ ﴿٣٣﴾

Yeye Ndiye Aliyemtuma Rasuli Wake (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kwa Mwongozo na Dini ya haki ili Aishindishe juu ya dini zote, japo watakirihika washirikina. [At-Tawbah: 33]

 

5. Naye (‘Azza wa Jalla) ni Adhw-Dhwaahir Mwenye kuwasaidia waja Wake wote, katika kupata riziki zao, katika maisha yao, katika kuwepesisha mambo yao, na katika manufaa ya dunia yao, na mengine maalum kwa vipenzi Vyake wenye kumpwekesha. Hao Anawaneemesha katika mambo ya dunia yao, katika marejeo yao, kuwanusuru na adui zao, na kuwazuilia na vitimbi vyao, Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

فَأَيَّدْنَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَىٰ عَدُوِّهِمْ فَأَصْبَحُوا ظَاهِرِينَ ﴿١٤﴾

Tukawatia nguvu wale walioamini dhidi ya maadui zao, wakapambaukiwa wakiwa washindi. [Asw-Swaff: 14]

 

Kwa hakika kufanya ‘ibaadah kwa kumuomba du’aa kwa Jina Lake (‘Azza wa Jalla), Adhw-Dhwaahir hukusanya moyo wa mja kwa Rabb wake, na kumfanya Ndiye Rabb Anayekusudiwa katika haja zake zote na marejeo yake ya kila kitu.  Jambo hilo likitulia kwa mja na kujua kuwa Rabb wake Ndiye haswa Adhw-Dwaahir basi uja wake utanyooka na kurejea Kwake katika kila hali na kila wakati.

 

 

 

Share

012-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-BAATWINU

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

 

الْبَاطِنُ

AL-BAATWINU

 

 

Al-Baatwinu: Aliye karibu kabisa, hakuna kitu kilichokaribu kuliko Yeye.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿٣﴾

Yeye Ndiye wa Awali hakuna kitu kabla Yake, na wa Mwisho hakuna kitu baada Yake, na Aliye juu kabisa hakuna kitu juu Yake, na Aliye karibu kabisa, hakuna kitu kilichokaribu kuliko Yeye, Naye kwa kila kitu ni Mjuzi.  [Al-Hadiyd: 3]

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

...وَأَنْتَ البَاطِنُ فَليْسَ دُونَكَ شيء...

…Nawe uko karibu kabisa, hakuna kitu kilicho karibu kuliko Wewe...  [Muslim]

 

1. Ibn Jariyr amesema: Naye Ndiye Al-Baatwin kwa vitu vyote, hakuna kitu kilicho karibu zaidi ya kitu kinginecho kuliko ukaribu Wake kama Anavyosema:

وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ الْوَرِيدِ ﴿١٦﴾

Na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa koo. [Qaaf: 16]

 

 

2. Ni wa Ndani, Mwenye kujificha, Asiyeonekana duniani. Mwenye kuweka pazia katika macho ya viumbe, hivyo haonekani duniani. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ ۖ وَهُوَ اللَّطِيفُ الْخَبِيرُ ﴿١٠٣﴾

Macho hayamzunguki bali Yeye Anayazunguka macho yote; Naye ni Mjuzi wa yaliyofichika, Mjuzi wa yaliyodhahiri na yaliyofichikana [Al-An’aam: 103]

 

Al-Idraak: Ni kuenea kwa mwenye kudiriki katika kila njia, nayo ni maalum zaidi kuliko kule kuona tu, yeye Ta’ala anaonekana Aakhirah lakini hawezi kuelezewa kwani hakika yake hakudirikiwi na macho. [Tafsiyr Ibn Kathiyr 2/161 na Ibn As-Sa’ady 268.]   

 

 

3-Mwenye kujua mambo ya dhahiri ya ndani, kama vile ambavyo neema Zake nyingi ni za baatwinah (zilizofichika) Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

أَلَمْ تَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَسْبَغَ عَلَيْكُمْ نِعَمَهُ ظَاهِرَةً وَبَاطِنَةً ۗ وَمِنَ النَّاسِ مَن يُجَادِلُ فِي اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَلَا هُدًى وَلَا كِتَابٍ مُّنِيرٍ ﴿٢٠﴾

Je, hamuoni kwamba Allaah Amekuitishieni vile vilivyomo mbinguni na vile vilivyomo ardhini, na Akakutimizieni kitimilifu neema Zake kwa dhahiri na siri?  [Luqmaan: 20]

 

Mwenye kuangalia na kujua siri za watu, dhamira na yaliyojificha na mambo ya ndani ya siri zake. Hakifichiki chochote au lolote lile la viumbe Vyake katika ‘amali zao za dhahiri wala siri. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

قُلْ إِن تُخْفُوا مَا فِي صُدُورِكُمْ أَوْ تُبْدُوهُ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ وَيَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢٩﴾

Sema: “Mkificha yale yaliyomo katika vifua vyenu au mkiyafichua, Allaah Anayajua. Na Anajua yale yaliyomo katika mbingu na yale yaliyomo katika ardhi. [Aal-‘Imraan: 29]

Na pia:

يَعْلَمُ خَائِنَةَ الْأَعْيُنِ وَمَا تُخْفِي الصُّدُورُ ﴿١٩﴾

(Allaah) Anajua khiyana za macho na yale yanayoficha vifua.  [Ghaafir: 19]

 

Kutaabadi kwa jina hili tukufu la Al-Baatwin ni kuabudu kwa mahaba ya kweli, na mapenzi na ya kuwa Allaah kuwa Kwake karibu ya kila kitu pamoja na kuwa Kwake yu dhahiri juu ya kila kitu. [Twariyq Al-Hijratayn 44.]

 

 

Share

013-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-WAAHIDU, AL-AHAD

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْوَاحِدُ - الأحَدُ

AL-WAAHIDU – AL-AHAD

 

 

 

Al-Waahid – Al-Ahad: Mmoja Pekee Asiye Na Mfano

 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Mmoja Pekee Asiye na mfano. Ni Mmoja Pekee kwa dhati Yake Na Sifa Zake.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Mmoja Pekee katika Sifa Zake za Rubuwbiyyah (Uumbaji, Ufalme, Uola, Kuruzuku, Kuendesha mambo ya Waja Wake), na katika Uluwhiyyah (kuabudiwa Kwake) na katika Asmaa na Swifaat (Majina na Sifa).

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alikuwa ni Mmoja Pekee hapo awali hapakuwa na kitu kabla Yake na Yungali Mmoja Pekee, na Atakuwa Mmoja Pekee Milele, hakuna kitu baada Yake. 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Mmoja Pekee, Hana mshirika, Hakuzaa wala Hakuzaliwa. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ ﴿١﴾

1. Sema: “Yeye ni Allaahu Mmoja Pekee.

 

اللَّـهُ الصَّمَدُ ﴿٢﴾

2. “Allaah ni Aliyekamilika sifa za utukufu Wake, Mkusudiwa haja zote. 

 

لَمْ يَلِدْ وَلَمْ يُولَدْ ﴿٣﴾

3. “Hakuzaa na wala Hakuzaliwa.

 

وَلَمْ يَكُن لَّهُ كُفُوًا أَحَدٌ ﴿٤﴾

4. “Na wala haiwi Awe na yeyote anayefanana na kulingana Naye.” [Al-Ikhlaasw: 112]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَقُلِ الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي لَمْ يَتَّخِذْ وَلَدًا وَلَمْ يَكُن لَّهُ شَرِيكٌ فِي الْمُلْكِ وَلَمْ يَكُن لَّهُ وَلِيٌّ مِّنَ الذُّلِّ ۖ وَكَبِّرْهُ تَكْبِيرًا ﴿١١١﴾

Na sema: “AlhamduliLLaah Kuhimidiwa ni kwa Allaah Ambaye Hakujifanyia mwana na wala Hakuwa na mshirika katika ufalme, na wala hakuwa dhalili hata awe (anahitaji) mlinzi, msaidizi; basi mtukuze matukuzo makubwa kabisa (Sema Allaahu Akbar!) [Al-Israa: 111]

 

 

Ni Mmoja Pekee na Atabaki kuwa Pekee na Hatokuwa na mwengine pamoja Naye [An-Nihaayah (1/35)]

  

 

Baadhi ya ‘Ulamaa wametofautisha baina ya Al-Waahid na Al-Ahad wakasema kwamba: ‘Waahid’ inawezekana kugawika katika mbili na zaidi. Mfano husemwa: Waahid (moja), ithnaan (mbili), thalaathah (tatu). Ama ‘Ahad’ maana yake ya kiasili ni kuwa haiwezekani kugawika katika mbili au zaidi; hivyo husemwa: ‘Ahad’ (moja pekee) na hiasemwi: ‘ahad, ithnaan, thalaathah n.k.  Na wakasema pia: ‘Al-Waahid’ ni Mmoja Pekee,kwa dhati Yake. Ama ‘Ahad’ Ni Mmoja Pekee katika dhati Yake na Sifa Zake. [Tafsiyr Asmaa Allaah - Az-Zajjaaj (Uk.58)].

 

Hivyo basi, Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Waahid, Al-Ahad Ambaye hakuna wa pili Naye, wala Hana mshirika, wala mfano Wake. Naye (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ambaye waja Wake wote wanamtegemea Yeye, na wanamkusudia Yeye kwa kila jambo na wala hawatawakali kwa yeyote ispokuwa Kwake Yeye [Ishtiqaaq Asmaai Allaah (90-93)]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ambaye ni Al-Waahid hakuna chochote au yeyote mwenye mfano Wake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ ﴿١١﴾

Hakuna chochote kinachofanana Naye, Naye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ash-Shuwraa: 11]

 

 

Na Ibn Jariyr akasema kuhusu maana ya ‘Kumpwekesha Allaah’ katika kuifasiri kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَإِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الرَّحْمَـٰنُ الرَّحِيمُ ﴿١٦٣﴾

“Na Ilaah wenu (Allaah) ni Ilaah Mmoja, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mwingi wa rahmah, Mwenye kurehemu.” [Al-Baqarah: 163]

 

 

“Na Ambaye Anastahiki kutiiwa nanyi enyi watu! Na imekuwajibikieni kufanya ‘ibaadah kwa Mwenye kustahiki kuabudiwa Mmoja Pekee na Rabb Mmoja Pekee, basi msimwabudu mwengine wala msimshirikishe na yeyote, kwani mkimshirikisha na mwengine katika ‘ibaadah zenu, basi huyo mnayemshirikisha ni kiumbe kama nyinyi katika viumbe vya Ilaah wenu (Mwabudiwa wa haki). Na Ilaah wenu ni Illaah Mmoja Pekee Hana  mfano Wake wala aliye sawa Naye. [Tafsiyr Atw-Twabariy].

 

Jina la  Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ‘Al-Waahid’ limetajwa katika Qur-aan zaidi ya mara  ishirini; Baadhi ya Aayah ni:

وَقَالَ اللَّـهُ لَا تَتَّخِذُوا إِلَـٰهَيْنِ اثْنَيْنِ ۖ إِنَّمَا هُوَ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ ﴿٥١﴾

Na Allaah Anasema: “Msijichukulie waungu wawili; hakika Yeye Ndiye Muabudiwa wa haki Mmoja Pekee basi niogopeni Mimi tu.  [An-Nahl: 51]

 

فَإِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ فَلَهُ أَسْلِمُوا ۗ وَبَشِّرِ الْمُخْبِتِينَ ﴿٣٤﴾

Kwa hiyo Muabudiwa wenu wa haki ni Ilaah Mmoja Pekee, basi Kwake jisalimisheni. Na wabashirie wanyenyekevu.  [Al-Hajj: 34]

 

 

قُلْ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mtu kama nyinyi, nafunuliwa Wahy kwamba: Hakika Muabudiwa wa haki wenu ni Ilaah Mmoja Pekee. Hivyo anayetaraji kukutana na Rabb wake, basi na atende ‘amali njema na wala asishirikishe yeyote katika ‘ibaadah za Rabb wake” [Al-Kahf: 110]

 

 

لَّقَدْ كَفَرَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ ثَالِثُ ثَلَاثَةٍ ۘ وَمَا مِنْ إِلَـٰهٍ إِلَّا إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۚ وَإِن لَّمْ يَنتَهُوا عَمَّا يَقُولُونَ لَيَمَسَّنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مِنْهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٣﴾

Kwa yakini wamekufuru wale waliosema: “Hakika Allaah ni watatu wa utatu. ”Na hali hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Ilaah Mmoja Pekee. Na wasipoacha yale wanayoyasema, bila ya shaka itawagusa wale waliokufuru miongoni mwao adhabu iumizayo. [Al-Maaidah: 73]

 

 

Na pia Jina hili la ‘Al-Waahid’ Limeungana mara sita katika Qur-aan pamoja na Al-Qahhaar’ (Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika):

 

لَّوْ أَرَادَ اللَّـهُ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا لَّاصْطَفَىٰ مِمَّا يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ ۚ سُبْحَانَهُ ۖ هُوَ اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿٤﴾

Lau Angelitaka Allaah kujichukulia mwana, Angelichagua Amtakaye miongoni mwa Aliowaumba. Subhaanah! Utakasifu ni Wake. Yeye Ndiye Allaah Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika. [Az-Zumar: 4]

 

 

قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ ۚ قُلْ أَفَاتَّخَذْتُم مِّن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ لَا يَمْلِكُونَ لِأَنفُسِهِمْ نَفْعًا وَلَا ضَرًّا ۚ قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الْأَعْمَىٰ وَالْبَصِيرُ أَمْ هَلْ تَسْتَوِي الظُّلُمَاتُ وَالنُّورُ ۗ أَمْ جَعَلُوا لِلَّـهِ شُرَكَاءَ خَلَقُوا كَخَلْقِهِ فَتَشَابَهَ الْخَلْقُ عَلَيْهِمْ ۚ قُلِ اللَّـهُ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ وَهُوَ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿١٦﴾

Sema: “Ni nani Rabb wa mbingu na ardhi?” Sema: “Ni Allaah.” Sema: “Je, mnawafanya wengineo badala Yake kuwa walinzi na hali hawamiliki kwa ajili ya nafsi zao manufaa wala dhara?”  Sema: “Je,   kipofu analingana sawa na mwenye kuona, au je, viza vinalingana sawa na nuru?” Au wamemfanyia Allaah washirika wameumba kama kwamba uumbaji Wake, kisha yakafanana maumbile kwao?  Sema: “Allaah  ni Muumbaji wa kila kitu, Naye ni Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Mshindi, Asiyepingika.” [Ar-Ra’d: 16]

 

يَوْمَ هُم بَارِزُونَ ۖ لَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِنْهُمْ شَيْءٌ ۚ لِّمَنِ الْمُلْكُ الْيَوْمَ ۖ لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ ﴿١٦﴾

Siku watakayotokeza wao, hakitofichika kitu chochote chao kwa Allaah. “Ufalme ni wa nani leo?” (Allaah Mwenyewe Atajijibu): “Ni wa Allaah Pekee Mmoja, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.” [Ghaafir: 16]

 

يَا صَاحِبَيِ السِّجْنِ أَأَرْبَابٌ مُّتَفَرِّقُونَ خَيْرٌ أَمِ اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿٣٩﴾

“Enyi sahibu zangu wawili wa jela. Je, marabi wengi wanaofarakana ni bora (kuabudiwa) au Allaah Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.” [Yuwsuf: 39]

 

قُلْ إِنَّمَا أَنَا مُنذِرٌ ۖ وَمَا مِنْ إِلَـٰهٍ إِلَّا اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿٦٥﴾

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hakuna Muabudiwa wa haki yeyote isipokuwa Allaah Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika. [Swaad: 65]

 

يَوْمَ تُبَدَّلُ الْأَرْضُ غَيْرَ الْأَرْضِ وَالسَّمَاوَاتُ ۖ وَبَرَزُوا لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ ﴿٤٨﴾

Siku ardhi itakapobadilishwa kuwa ardhi nyingine na mbingu pia na (viumbe wote) watahudhuria kwa Allaah Mmoja Pekee, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.” [Ibraahiym: 48]

 

 

Kutajwa Majina mawili haya mazuri kwa pamoja,  inamaanisha kuwa ni Yeye Allaah Pekee Mwenye mamlaka na uwezo wa kufanya lolote Alitakalo, Hakuna wa kumpinga na hivyo kila kilichokuwa mbinguni na ardhini kinajisalimisha Kwake Yeye Pekee Al-Waahid. 

 

 

Ama Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ‘Al-Ahad’ Limetajwa mara moja katika Suwrat Al-Ikhlaasw [114]

 

 

Vipi kuabudu na kufanyia kazi  Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ‘Al-Waahid’ na ‘Al-Ahad’:

 

1. Mdhukuru Al-Waahid kwa kutamka neno la kumpwekesha Allaah, (Tawhiyd)  “Laa ilaaha illa Allaah” kwa wingi na ambayo ni maneno yanayotajwa katika adhaan na iqaamah za Swalaah, na ufanyie kazi maana yake. Pia kutamka du’aa au nyiradi inayosomwa katika adhkaar za kila baada ya Swalaah za fardhi, pamoja na nyakati nyinginezo ambazo zimejaa fadhila na faida zake kama alivyosema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba:

 

((خَيْرُ الدُّعَاءِ دُعَاءُ يَوْمِ عَرَفَةَ، وخَيْرُ مَا قُلْتُ أنَا وَالنَّبيُّونَ مِنْ قَبْـلِي: لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيْكَ لَهُ، لَهُ الـمُلْكُ، ولَهُ الـحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيءٍ قَدِير)) روى الترمذي

((Du’aa bora kabisa ni du’aa katika siku ya 'Arafah, na yaliyo bora kabisa niliyosema mimi na Manabii kabla yangu ni: 'Laa Ilaaha illa Allaah Wah-dahu laa shariyka Lahu, Lahul-Mulku wa-Lahul-hamdu wa Huwa 'alaa kulli shay-in Qadiyr – Hapana Muabudiwa wa haki ila Allaah, Yu Pekee, Hana mshirika, ufalme wote ni Wake, na kuhimidiwa ni Kwake, Naye ni Mweza wa kila kitu daima)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3/184), Silsilah Al-Ahaadiyth Asw-Swahiyhah (4/6)]

 

 

2. Mpwekeshe Muumba wako (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Al-Waahid, kwa kutokumshirkisha na chochote kwa sababu kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ni dhulma kubwa mno.

 

 

3. Kuwa na ikhlaasw; kumsafishia niyyah Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Al-Waahid, katika ’amali zako zote kwa kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki ila Yeye, wala kuadhimishwa isipokuwa Yeye wala kutiiwa isipokuwa Yeye wala kuridhishwa isipokuwa Yeye. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٢﴾

Sema: “Hakika Swalaah yangu, na kuchinja kafara na ‘ibaadah zangu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah Pekee Rabb wa walimwengu.”

 

لَا شَرِيكَ لَهُ ۖ وَبِذَٰلِكَ أُمِرْتُ وَأَنَا أَوَّلُ الْمُسْلِمِينَ ﴿١٦٣﴾

Hana mshirika, na kwa hayo ndio nimeamrishwa, nami ni Muislamu wa kwanza.  [Al-An’aam: 162-163]

 

 

4. Tafakari na zingatia dalili za Tawhiyd ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Al-Waahid, katika uumbaji Wake (Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah) kwa kuangaza kila aina ya uumbaji Wake unaokuzunguka mahali popote ulipo, ujue kuwa hakuna yeyote awezaye kuumba kama uumbaji wa Al-Waahid.

 

5. Tawakali kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Pekee katika mambo yako yote. Usikhofu chochote kitakachokupeleka katika shirki, bali tawakali kwa Al-Waahid Al-Ahad.

 

Kumbuka kisa cha Bilaal (Radhwiya Allaahu ’anhu) ambaye alikuwa ni mtumwa wa Ummayyah bin Khalaf pale alipoghadhibika naye alipotambua kuwa ameacha dini yao ya kuabudu masanamu akaingia Uislamu.

 

Umayyah akawa anamtesa Bilaal (Radhwiya Allaahu ’anhu) kwa kumweka katika jua kali bila ya chakula wala maji huku akimwekea jiwe kubwa kifuani mwake lilokaribia kumzuia pumzi.

Aliendelea kumtesa kwa sababu Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu) alimkatalia kumtaka kwake amkanushe Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam) ili arudi katika ukafiri akimtishia kuwa atamuua pindi akikataa kumtii.

 

Lakini juu ya mateso hayo, Bilaal (Radhwiya Allaahu ’anhu) alitamka maneno mazito ya kusisimua yenye kumbukumbu katika Siyrah ya Nabiy (Swalla Allaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam) nayo ni  ”Ahadun Ahadun” (Mmoja, Mmoja Pekee).  Baada ya masiku kupita Abu Bakr (Radhwiya Allaahu ’anhu) akamnunua na kumwacha huru, na ndipo Nabiy (Swalla Allaahu ’alayhi wa aalihi wa sallam) akampa kazi tukufu kabisa ya kuadhini ambayo inashuhudia Tawhiyd ya Allaah na Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu) akawa ni mwenye hadhi kubwa na maarufu mpaka kwa watoto wa Kiislamu kutokana na kisa chake hiki chenye mafunzo kwa kila mtu.  

 

 

 

 

Share

014-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-MALIK, AL-MAALIK, AL-MALIYK

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْمَلِك – الْماَلِك - الْمَلِيك

AL-MALIK, AL-MAALIK, AL-MALIYK

 

 

 

Al-Malik:  Mfalme na mwenye mamlaka.

 

Al-Maalik: Mwenye kumiliki.

 

Al-Maliyk: Mfalme Mwenye nguvu zote daima

 

Majina hayo matatu ni ya Allaah ('Azza wa Jalla) Ambaye Mwenye sifa ya ‘Mulk’ (Mwenye kumilki): Anamiliki, Ufalme, mamlaka, nguvu, taadhima, utukufu, enzi, na utukufu. Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Pekee Mwenye kutawala na kumiliki vilivyoko mbinguni na ardhini na vilivyoko baina yake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

لَهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢﴾

Ni Wake Pekee ufalme wa mbingu na ardhi, Anahuisha na Anafisha, Naye juu ya kila kitu ni Muweza. [Al-Hadiyd: 2]

 

Al-Malik imetajwa mara tano katika Qur-aan:

 

فَتَعَالَى اللَّـهُ الْمَلِكُ الْحَقُّ ۗ وَلَا تَعْجَلْ بِالْقُرْآنِ مِن قَبْلِ أَن يُقْضَىٰ إِلَيْكَ وَحْيُهُ ۖ وَقُل رَّبِّ زِدْنِي عِلْمًا ﴿١١٤﴾

Basi Ametukuka Allaah kwa ‘Uluwa, Mfalme wa haki. Na wala usiiharakize Qur-aan (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kabla haikumalizwa kufunuliwa Wahy kwako. Na sema: “Rabb wangu! Nizidishie elimu.” [Twaahaa: 114]

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ  

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme.[Al-Hashr: 23]

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ﴿١﴾

Sema: Najikinga na Rabb wa watu.

 

مَلِكِ النَّاسِ ﴿٢﴾

Mfalme wa watu. [An-Naas: 1-2]

 

فَتَعَالَى اللَّـهُ الْمَلِكُ الْحَقُّ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْكَرِيمِ ﴿١١٦﴾

Basi Ametukuka Allaah Mfalme wa haki. Hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye. Rabb wa ‘Arsh tukufu.  [Al-Muuminuwn: 116]

 

يُسَبِّحُ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ الْمَلِكِ الْقُدُّوسِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ ﴿١﴾

Vinamsabbih Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi, Mfalme, Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Jumu’ah: 1]

 

Al-Maalik imetajwa mara mbili katika kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ ﴿٤﴾

Mfalme wa siku ya malipo. [Al-Faatihah: 4]

 

قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ

Sema: “Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, Unampa ufalme Umtakaye, na Unamuondoshea ufalme Umtakaye [Aal-‘Imraan: 26]

 

 

Ama Al-Maliyk imetajwa mara moja katika kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ ﴿٥٤﴾

Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na mito.  

 

فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ ﴿٥٥﴾

Katika makao ya haki kwa Mfalme Mwenye Nguvu zote, Mwenye Uwezo wa juu kabisa. [Al-Qamar: 54-55]

 

 

Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Ndiye Al-Malik, Al-Maalik na Al-Maliyk: Mwenye Ufalme wote, Mwenye kumiliki yote, Mwenye kuhimidiwa kwa yote. Mambo yote yapo chini Yake na Yanarejea Kwake.  Istawaa katika ‘Arshi Yake (Yuko juu kwa namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah). Yuko juu ya viumbe Vyake vyote, hakijifichi chenye kujificha katika ardhi wala katika mbingu.

 

Allaah (‘Azza wa Jalla) Anapanga Pekee mamlaka Yake. Anatoa na kuzuia, Anakirimu, Anatukuza na Anadhalilisha, Anaumba na kuruzuku, Anaamrisha na Anakataza, Anafisha na kuhuisha, Anakadiria na Anahukumu. Anaingiza usiku kwa mchana, na Anaingiza mchana kwa usiku. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَاءُ ۖ بِيَدِكَ الْخَيْرُ ۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢٦﴾

Sema: “Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, Unampa ufalme Umtakaye, na Unamuondoshea ufalme Umtakaye, na Unamtukuza Umtakaye, na Unamdhalilisha Umtakaye, khayr imo Mkononi Mwako.  Hakika Wewe juu ya kila kitu ni Muweza.

 

 تُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَتُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ ۖ وَتُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَتُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ ۖ وَتَرْزُقُ مَن تَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿٢٧﴾

Unauingiza usiku katika mchana na Unauingiza mchana katika usiku; na Unatoa kilicho hai kutokana na kilicho mfu na Unatoa kilicho mfu kutokana na kilicho hai na Unamruzuku Umtakaye bila ya hesabu.  [Aal-‘Imraan: 26-27]

 

Anatawala Atakavyo, Anamiliki Atakayo. Ni Muweza hakuna mwenye kushindana Naye katika mamlaka Yake, wala hakuna mwenye kuweza kumpinga. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ ﴿٨٢﴾

Hakika amri Yake Anapotaka chochote hukiambia: “Kun! (Kuwa), nacho huwa.”

 

فَسُبْحَانَ الَّذِي بِيَدِهِ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيْءٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٨٣﴾

Basi Subhaanah! Utakasifu ni wa Ambaye Mkononi Mwake kuna ufalme wa kila kitu, na Kwake mtarejeshwa. [Yaasiyn: 82-83]

 

Ibn Jariyr amesema: “Ni Mfalme Ambaye hakuna ufalme juu Yake wala chochote isipokuwa kiko kwenye mamlaka Yake.” [Jaami’ Al-Bayaan (28/36]

 

Na Ibn Al-Qayyim amesema: “Mfalme wa haki. Yeye Ambaye Anaamrisha na kukataza na Anasarifu Atakavyo kwa viumbe Vyake kwa kauli na Amri Zake, na hii ndio tofauti baina ya Al-Malik na Al-Maalik.

 

Hivyo basi Al-Maalik ni Mwenye kufanya Atakavyo kwa vitendo Vyake. Na Al-Malik ni Mwenye kutenda Atakavyo kwa vitendo Vyake na amri Zake Na Rabb (Ta’aalaa) ni Mfalme wa ufalme basi Hufanya Atakavyo kwa vitendo Vyake na amri Zake.” [Badaai‘u Al-Fawaaid (4/165)]

 

 

Na Ibn Kathiyr amesema kuhusu kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ  

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme… [Al-Hashr: 23]

 

Kwa maana: Ni Mfalme wa kila kitu Anayefanya Atakavyo bila ya mwenye kumkataza au kumpinga. [Tafsiyr Ibn Kathiyr]

 

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Majina ya Allaah:

Al-Malik, Al-Maalik, Al-Maliyk

 

1.     Ikiwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Mfalme wa wafalme, na hakuna anayeweza kushindana Naye kwa lolote, wala hakuna mshirika, na Ndiye rejea yetu na matarajio yetu, hatuwezi kutoshelezwa na asiyekuwa Yeye. Hivyo hakuna haja ya kuogopa, wala kutarajia asiyekuwa Yeye, wala kumpenda asiyekuwa Yeye, wala kumtegemea asiyekuwa Yeye, kwani mwenye kumtegemea na kumuogopa Yeye Al-Malik, Al-Maalik, Al-Maliyk, basi atakuwa chini ya uangalizi Wake.  

 

 

2.     Haipasi kujiita Majina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) yanayomhusu Yeye Pekee kama haya yenye kuanzia na ‘AL’ (Al-Malik) au ‘Maalik Al-Amlaak’ (mfalme wa wafalme) kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametahadharisha:

 

((أَغْيَظُ رَجُلٍ عَلَى اللَّهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَأَخْبَثُهُ وَأَغْيَظُهُ عَلَيْهِ رَجُلٌ كَانَ يُسَمَّى مَلِكَ الأَمْلاَكِ لاَ مَلِكَ إِلاَّ اللَّهُ))

Mtu anayechukiza kabisa mbele ya Allaah Siku ya Qiyaamah ni muovu kabisa na anayechukiza mno kuliko wote. Kwake ni mtu aliyekuwa akijiita: “Maalik Al-Amlaak” (Mfalme wa wafalme). Kwani hakuna mfalme isipokuwa Allaah. [Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) katika Muslim, Kitaab Al-Iymaan]

 

 

3.     Wafalme wa duniani wana mamlaka ya watu wao duniani tu na ni mamlaka ya muda mfupi tu. Ama Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Malik, Al-Maalik; Al-Maliyk, Mfalme wa wa wafalme wote, na Mwenye ufalme wa kudumu. Ni Mfalme wa duniani na Aakhirah. Siku watakapofishwa viumbe wote Atabakia Maalikul-Mulk (Mfalme wa wafalme). Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَوْمَ هُم بَارِزُونَ ۖ لَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِنْهُمْ شَيْءٌ ۚ لِّمَنِ الْمُلْكُ الْيَوْمَ ۖ لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ ﴿١٦﴾

Siku watakayotokeza wao, hakitofichika kitu chochote chao kwa Allaah. “Ufalme ni wa nani leo?” (Allaah Mwenyewe Atajijibu): “Ni wa Allaah Pekee Mmoja, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.” [Ghaafir: 16]

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَيَوْمَ تَشَقَّقُ السَّمَاءُ بِالْغَمَامِ وَنُزِّلَ الْمَلَائِكَةُ تَنزِيلًا ﴿٢٥﴾

Na Siku itakayoraruka mbingu kwa mawingu; na Malaika watateremshwa mteremsho mkubwa wa mfuatano.

 

الْمُلْكُ يَوْمَئِذٍ الْحَقُّ لِلرَّحْمَـٰنِ ۚ وَكَانَ يَوْمًا عَلَى الْكَافِرِينَ عَسِيرًا ﴿٢٦﴾

Ufalme wa haki Siku hiyo utakuwa ni wa Ar-Rahmaan; Mwingi wa Rahmah.  Na itakuwa ni siku ngumu kwa makafiri. [Al-Furqaan: 25-26]

 

Na katika Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

((يَقْبِضُ اللَّهُ تَبَارَكَ وَتَعَالَى الأَرْضَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَيَطْوِي السَّمَاءَ بِيَمِينِهِ ثُمَّ يَقُولُ أَنَا الْمَلِكُ أَيْنَ مُلُوكُ الأَرْضِ))

((Allaah Tabaaraka wa Ta’aalaa Ataikamata ardhi Mkononi na Atazikunja mbingu kwa Mkono Wake wa kulia kisha Atasema: Mimi Ndio Mfalme! Wako wapi wafalme wa duniani?)) [Hadiyth ya Abuu Hurayrah ameikusanya Al-Bukhaariy katika Kitaab At-Tafsiyr, Kitaab At-Tawhiyd, Kitaab Ar-Raqaaiq na Muslim katika Kitaabu Swiffatil-Qiyaamah Wal-Jannati Wan-Naari]

 

 

4.     Kwa mwenye madaraka, au mamlaka au cheo chochote kile duniani, au umiliki wa chochote kile, awe mnyenyekevu kwa walio chini yake kwa kuzingatia kuwa Yuko Al-Malik na Al-Maliyk Ambaye Ana mamlaka juu yake. Hivyo basi unapohukumu, uhukumu kwa haki bila ya uonevu. Unapotoa, toa bila ya kupendelea, na wala usitakabari bali ukhofie kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

يَطوي اللهُ عزَّ وجلَّ السَّماواتِ يومَ القيامةِ. ثمَّ يأخذُهنَّ بيدِه اليُمنَى. ثمَّ يقولُ: أنا الملِكُ. أين الجبَّارون؟ أين المُتكبِّرون؟ ثمَّ يَطوي الأرضين بشمالِه. ثمَّ يقولُ: أنا الملِكُ. أين الجبَّارون؟ أين المُتكبِّرون؟

Allaah ‘(Azza wa Jalla) Atakunja mbingu zote Siku ya Qiyaamah kisha Atazikamata Mkononi Mwake wa kuume Atasema: Mimi Ndiye Mfalme. Wako wapi waliojifanya majabari? Wako wapi waliotakabari? Kisha Atakunja ardhi mbili kwa Mkono Wake wa kushoto Atasema: Mimi Ndiye Mfalme, wako wapi waliojifanya majabari. Wako wapi waliotakabari?)) [Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) katika Muslim 2788, na Ibn Maajah, na Abuu Daawuwd]

 

 

5.     Kusoma adhkaar zilizothibiti zenye kutajwa Majina haya ya Allaah au Sifa Zake mfano:

اللّهُـمَّ أَنْتَ المَلِكُ لا إِلهَ إِلاّ أَنْت، أَنْتَ رَبِّـي وَأَنـا عَبْـدُك، ظَلَمْـتُ نَفْسـي وَاعْـتَرَفْتُ بِذَنْبـي فَاغْفِرْ لي ذُنوبي جَميعاً إِنَّـه لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إلاّ أَنْت،

Allaahumma Antal-Maliku laa ilaaha illa Anta. Anta Rabbiy wa ana ‘abduka, dhwalamtu nafsiy wa’-taraftu bidhanbiy faghfir-liy dhunuwbiy jamiy’an innahu laa yaghfirudh-dhunuwba illa Anta

 

Ee Allaah, Wewe Ndiye Mfalme, hapana Muabudiwa wa haki ila Wewe, Wewe Ndiye Rabb wangu na mimi ni mja Wako. Nimedhulumu nafsi yangu, na nimekiri madhambi yangu kwa hivyo nighufurie madhambi yangu yote, hakika haghufurii madhambi, ila Wewe [Miongoni mwa du’aa za kufungulia Swalaah]

 

Pia:

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وحْـدَهُ لا شريكَ لهُ، لهُ المُلكُ ولهُ الحَمْد، يُحيـي وَيُمـيتُ وهُوَ على كُلّ شيءٍ قدير.  

Laa ilaaha illa-Allaahu Wahdahu laa shariyka Lah. Lahul-Mulku wa Lahul-Hamdu, Yuhyi wa Yumiytu wa Huwa ’alaa kulli shay-in Qadiyr

Hapana Muabudiwa wa haki ila Allaah, ni Mmoja Pekee, Hana mshirika. Ni wake Ufalme, na kuhimidiwa ni Kwake, Anahuisha, Anafisha, na Yeye ni Muweza wa kila kitu.

 

 

6.     Tafakari Aayah katika Suwratul-Faatihah unayoisoma katika kila Swalaah zako:

 

مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ ﴿٤﴾

Mfalme wa siku ya malipo.

 

Kwamba umesimama mbele ya Al-Maalik na Mfalme wa wafalme duniani na kwamba utasimamishwa mbele Yake tena Siku ya Qiyaamah kulipwa mema uliyoyatenda na kuhesabiwa maovu uliyoyatenda wala hakuna cha kufichikia siku hiyo!  

 

  يَوْمَ هُم بَارِزُونَ ۖ لَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِنْهُمْ شَيْءٌ ۚ لِّمَنِ الْمُلْكُ الْيَوْمَ ۖ لِلَّـهِ الْوَاحِدِ الْقَهَّارِ ﴿١٦﴾

Siku watakayotokeza wao, hakitofichika kitu chochote chao kwa Allaah. “Ufalme ni wa nani leo?” (Allaah Mwenyewe Atajijibu): “Ni wa Allaah Pekee Mmoja, Mwenye kudhibiti na kudhalilisha, Asiyepingika.”

 

الْيَوْمَ تُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ ۚ لَا ظُلْمَ الْيَوْمَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴿١٧﴾

Leo kila nafsi italipwa kwa yale iliyoyachuma, hakuna dhulma leo!  Hakika Allaah ni Mwepesi wa kuhesabu.

 

وَأَنذِرْهُمْ يَوْمَ الْآزِفَةِ إِذِ الْقُلُوبُ لَدَى الْحَنَاجِرِ كَاظِمِينَ ۚ مَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ حَمِيمٍ وَلَا شَفِيعٍ يُطَاعُ ﴿١٨﴾

Na waonye Siku inayokurubia sana pale nyoyo zitakapofikia kooni wamejaa huzuni na majuto. Madhalimu hawatokuwa na rafiki wa dhati, na wala mwombezi anayetiiwa. [Ghaafir: 16-18]

 

Tafakari pia Aayah katika Suwratul-Infitwaar [13-19]

 

 

7.     Tafakari neema za Jannah Anazotuahidi Allaah (‘Azza wa Jalla) huko. Kwa hiyo, tenda mema na jiepushe na maovu uipate Jannah. Pale utakapoingia Jannah ukafunguliwa milango yake na Malaika wakakupokea kwa Salaamun ‘Alaykum! Ukaanza kuona Anayoyamiliki Al-Maalik, huko: 

وَإِذَا رَأَيْتَ ثَمَّ رَأَيْتَ نَعِيمًا وَمُلْكًا كَبِيرًا ﴿٢٠﴾

Na utakapoona huko, utaona neema na milki adhimu. [Al-Insaan: 20]

 

 

 

Share

015-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-QUDDUWS

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْقُدُّوس

AL-QUDDUWS

 

 

 

Al-Qudduws: Mtakatifu Ametakasika Na Sifa Zote Hasi (Pungufu)

 

 

Qudduws linatokana na ‘Qaddasa’ ambayo ina mbili:

 

Kwanza: Kutwaharika, safi, kutakasika na kuwa mbali na najisi, aibu, na upungufu. Imekuja katika Qur-aan pale Malaika waliposema:

قَالُوا أَتَجْعَلُ فِيهَا مَن يُفْسِدُ فِيهَا وَيَسْفِكُ الدِّمَاءَ وَنَحْنُ نُسَبِّحُ بِحَمْدِكَ وَنُقَدِّسُ لَكَ ۖ

Wakasema: “Utaweka humo atakayefanya ufisadi humo na kumwaga damu, na hali sisi tunakusabbih kwa Himidi Zako na tunakutukuza kwa Utakatifu Wako?” [Al-Baqarah: 30]

Az-Zajjaaj amesema maana ya نُقَدِّسُ لَكَ ni: “Tunatwaharisha nafsi zetu Kwako.”

 

Na ndio maana Masjid Al-Aqswaa ya Palestina ikaitwa Baytul-Maqdis ‘Nyumba iliyotakasika’ au sehemu ambayo mtu anajitakasa kutokana na dhambi. Na pia Palestina ikaitwa "Ardhw Al-Muqaddas" (ardhi iliyotakasika).

 

Na katika Qur-aan ametajwa Ruwh Al-Qudus kuwa ni Jibriyl (‘Alayhis-salaam) anayeteremsha maneno ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala):

قُلْ نَزَّلَهُ رُوحُ الْقُدُسِ مِن رَّبِّكَ بِالْحَقِّ لِيُثَبِّتَ الَّذِينَ آمَنُوا وَهُدًى وَبُشْرَىٰ لِلْمُسْلِمِينَ ﴿١٠٢﴾

Sema: Ameiteremsha Ruwhul-Qudus (Jibriyl) kutoka kwa Rabb wako kwa haki ili iwathibitishe wale walioamini na ni mwongozo na bishara kwa Waislamu. [An-Nahl 16:102]

 

Maana ya pili: Iliyobarikiwa, na ndani yake limetoka neno Muqaddasah (iliyobarikiwa) [Al-Lisaan (5/3549), An-Nihaayah (5/23), Ibn Jariyr (1/457), Daqaiq At-Tafsiyr ya Ibn Taymiyyah (1/310)]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametaja ardhi iliyobarikiwa katika kauli Yake:

سُبْحَانَ الَّذِي أَسْرَىٰ بِعَبْدِهِ لَيْلًا مِّنَ الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ إِلَى الْمَسْجِدِ الْأَقْصَى الَّذِي بَارَكْنَا حَوْلَهُ  

Utakasifu ni wa Ambaye Amemsafirisha usiku mja Wake kutoka Al-Masjid Al-Haraam mpaka Al-Masjid Al-Aqswaa ambao Tumevibariki vilivyoko pembezoni mwake;  [Al-Israa: 1]

 

Jina Lake hili tukufu la Al-Qudduws limetajwa katika Qur-aan mara mbili:

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ  

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi… [Al-Hashr 59:23]

 

Na pia:

يُسَبِّحُ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ الْمَلِكِ الْقُدُّوسِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ ﴿١﴾

Vinamsabbih Allaah Pekee vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi, Mfalme, Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Jumu’ah 62:1]

 

 

Imaam Ibn Al-Qayyim amesema kuhusu maana ya Al-Qudduws: “Aliyesalimika na kila shari, upungufu na aibu kama walivyosema Wafasiri (wa Qur-aan) kwamba Yeye Ametakasika na kila aibu ambayo inapingana na Utukufu Wake.” [Kitaab Asmaa Al-Husnaa, uk.103]

 

Al-Bayhaqiy amesema: “Al-Qudduws ni Ambaye Ametakasika na kila aibu inayomtia upungufu kama kuwa na watoto na kuwa na washirika, na Sifa hii (Al-Qudduws) inamstahiki dhati Yake:  [Al-I’tiqaad ya Al-Bayhqiy (Uk. 54), An-Nihaayah ya Ibn Kathiyr (4/23), Sharh Asmaa Al-Husnaa ya Ar-Raaziy (Uk. 186)]

 

Ibn Kathiyr amesema kuhusu maana ya Al-Qudduws: “Aliyeepukika na kila upungufu, na mwenye kusifika na sifa za ukamilifu." [Tafsiyr Ibn Kathiyr (4/363)]

 

 

Al-Qudduws: Mwenye kuepushwa na kila kinachopinga ukamilifu Wake, katika dhati Yake, katika Majina na Sifa Zake, katika matendo Yake, katika Utawala Wake, Yeye (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Amejitenga na kila chenye kwenda kinyume na ukamilifu Wake.

 

Al-Qudduws: Yeye Mu’adhwam [Imethibiti kutoka kwa Mujaahid] yaani ni Mkubwa na Mwenye taadhima, na kila utakatifu, utwahara na ukubwa. [Al-Haq Al-Waadhwih (81-82) na Fat-hu Ar-Rahiym (19-20)].  

 

Al-Qudduws: Ni Al-Mubaarak, Ambaye neema Zake zimekithiri na kuenea kote, na baraka Zake ardhini na mbingu za juu, wakati wote. Jina Lake limebarikiwa, na Sifa Zake zimebarikiwa, na matendo yote yamebarikiwa, na dhati Yake tukufu imebarikiwa.

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah: Al-Qudduws:

 

Kuthibitisha iymaan ya kimatendo ya sifa hii tukufu ni kumfanya Muumini kumuadhimisha na kumtukuza Rabb wake. Na inampasa Muumini kujitakasa kutokana na uchafu wa ushirikina na dhulma na maovu yote, na alazimiane na utwahara wa kihisia na kimaana katika kila wakati na katika hilo.

 

Aitakase nafsi yake na matamanio, na mambo ya utata, na moyo wake kutokana na kughafilika, na kiwiliwili chake kutokana na kwenda kinyume na maamrisho, na matamanio yake kwa anayoyaona, na hilo ni kwa kutekeleza maamrisho Yake (Ta’aalaa) na kukatazika na makatazo Yake, na kufuata taratibu na adabu zake. Akifanya hayo moyo wake utang’aa na kumcha Allaah, na hilo litaonekana katika dhahiri yake, na atawaambukiza wengine, na hivyo familia yake itatwaharika kwa twahara yake, na watoto wake, kisha kwa kiasi cha twahara yake watatwaharika wengine.

 

Na yafuatayo ni miongoni mwa ya kujitakasa na kujipatia khayr:

 

1. Jitakase kwa Tawhiyd. Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Muabudiwa wa haki Pekee, Hana mshirika wala mke wala mwana.

Anasema:

وَقَالُوا اتَّخَذَ اللَّـهُ وَلَدًا ۗ سُبْحَانَهُ ۖ بَل لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ كُلٌّ لَّهُ قَانِتُونَ ﴿١١٦﴾

Na wakasema: “Allaah Amejichukulia mwana.” Subhaanah! Utakasifu ni Wake! Bali ni Vyake vilivyomo mbinguni na ardhini, vyote vinamtii [Al-Baqarah 2:116]

 

Hata Majini wamemtakasa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) waliposema:

وَأَنَّهُ تَعَالَىٰ جَدُّ رَبِّنَا مَا اتَّخَذَ صَاحِبَةً وَلَا وَلَدًا ﴿٣﴾

“Na kwamba hakika umetukuka kabisa Ujalali wa Rabb wetu, Hakujifanyia mke wala mwana.” [Al-Jinn 72: 3]

 

Na kutokumshirikisha na lolote kwani shirki ni dhambi kubwa mno kama alivyosema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipoulizwa:

عَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ سَأَلْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم: أَيُّ اَلذَّنْبِ أَعْظَمُ؟ قَالَ: ((أَنْ تَجْعَلَ لِلَّهِ نِدًّا, وَهُوَ خَلَقَكَ))‏  

Imepokelewa kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: “Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): Je, dhambi ipi kubwa mno?” Akasema: ((Kumfanyia Allaah mlinganishi (mshirika) na hali Yeye Amekuumba)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Soma vitabu vya Tawhiyd na jifunze aina za Tawhiyd za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ili ujue yepi yenye kumshirikisha ujiepushe nayo.  

 

2. Jitakase na kwa kusoma Qur-aan kwa wingi kwa sababu Qur-aan inasafisha maradhi ya moyo yaliyotajwa katika Qur-aan na Sunnah ambayo ni shirki, kufru, unafiki, uhasidi, chuki, uchoyo n.k. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

يَا أَيُّهَا النَّاسُ قَدْ جَاءَتْكُم مَّوْعِظَةٌ مِّن رَّبِّكُمْ وَشِفَاءٌ لِّمَا فِي الصُّدُورِ وَهُدًى وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ﴿٥٧﴾

Enyi watu! Kwa yakini yamekujieni mawaidha kutoka kwa Rabb wenu, na shifaa ya yale yaliyomo vifuani, na mwongozo na rahmah kwa Waumini [Yuwnus 10: 57]

 

Hivyo basi, takasa moyo wako uwe na ikhlaasw katika ‘amali zako, kwa sababu hakuna kitakachokufaa Siku ya Qiyaamah isipokuwa kufika kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa)  na moyo msafi.  

Anasema Aliyetukuka:

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

“Siku hayatofaa mali wa watoto.

 

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

“Isipokuwa yule atakayemfikia Allaah na moyo uliosalimika." [Ash-Shu’araa 26: 88-89]

 

Na Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم): ((إِنَّ اللَّهَ لاَ يَنْظُرُ إِلى أجْسَامِكُمْ وَلاَ إِلَى صُوَرِكُمْ وَلَكِنْ يَنْظُرُ إِلَى قُلُوبِكُمْ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwammba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika Allaah Hatazami viwiliwili vyenu wala sura zenu, lakini Anatazama nyoyo zenu)). [Muslim]

 

 

Hali kadhaalika Qur-aan nzima ina barakah. Soma kwa wingi upate kubarikiwa na Allaah (Ta'aalaa)  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٢٩﴾

Kitabu Tumekiteremsha kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) chenye Baraka, ili wapate kuzingatia kwa makini Aayaat zake, na ili wapate kukumbuka wenye akili. [Swaad 38: 29]

 

3. Jitakase kwa kujifunza ‘Aqiydah sahihi kwa sababu ‘Aqiydah sahihi itakuepusha kuingia katika makundi potofu. Na itakubakisha katika utakaso wa Dini ambao ndio mwenendo wa Manabii wote pamoja na wema waliotangulia. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Taa’alaa):

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ ﴿٥﴾

Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah wenye kumtakasia Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki. [Al-Bayyinah 98: 5].

 

4. Jitakase kwa kusimamisha Swalaah tano kwa kuwa Swalaah inamwepusha mtu na machafu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

وَأَقِمِ الصَّلَاةَ ۖ إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ۗ  

…na simamisha Swalaah, hakika Swalaah inazuia machafu na munkari. [Al-‘Ankabuwt 29: 45]

 

Na Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((أَرَأَيْتُمْ لَوْ أَنَّ نَهْرًا بِبَابِ أَحَدِكُمْ يَغْتَسِلُ مِنْهُ كُلَّ يَوْمٍ خَمْسَ مَرَّاتٍ هَلْ يَبْقَى مِنْ دَرَنِهِ شَيْءٌ؟)) قَالُوا: لَا يَبْقَى مِنْ دَرَنِهِ شَيْءٌ. قَالَ: ((فَذَلِكَ مَثَلُ الصَّلَوَاتِ الْخَمْسِ يَمْحُو اللَّهُ بِهِنَّ الْخَطَايَا)) البخاري ومسلم

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mnaonaje ingelikuwa kuna mto mbele ya nyumba ya mmoja wenu kisha akawa anaoga humo kila siku mara tano, je atabakiwa na uchafu?)) Wakasema: "Habakiwi na uchafu". Akasema: ((Hivyo ni mfano wa Swalaah ambazo Allaah hufuta madhambi kwayo)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

5. Jitakase kwa Zakaah ambayo maana yake kutakasa. Na pia kutoa swadaqah na kutoa mali kwa ajili ya Allaah upate kujitakasa kama pale Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Alipomwambia Rasuli Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا  

Chukua (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) katika mali zao Swadaqah, uwatwaharishe na uwatakase kwazo. [At-Tawbah 9: 103]

 

Na unapotoa mali yako kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni sababu mojawapo nyengine ya kupata baraka katika mali yako kwa sababu Yeye Ameahidi kukuongozea maradufu kama ilivyothibiti katika Aayah kadhaa na Ahaadiyth za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

 

6. Jitakase na dhulma ambayo Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ameiharamisha. Amesema katika Hadiyth Qudsiy:

يا عِبادي إنِّي حَرَّمْتُ الظُلْمَ على نَفْسِي وَجعَلْتُهُ بَيْنَكُمْ مُحَرَّماً فلا تَظَالَمُوا.

Enyi waja Wangu, Nimeikataza nafsi Yangu dhulma na Nimeiharamisha kwenu (hiyo dhulma), kwa hivyo msidhulumiane.” [Muslim]

 

Na Anasema Allaah Aliyetukuka:

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ ۖ وَإِن تَكُ حَسَنَةً يُضَاعِفْهَا وَيُؤْتِ مِن لَّدُنْهُ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿٤٠﴾

Hakika Allaah Hadhulumu hata uzito au chembe (au sisimizi). Na ikiwa ni ‘amali njema Huizidisha na Hutoa kutoka Kwake ujira adhimu. [An-Nisaa 4:40]

 

7. Mtukuze Al-Qudduws na muombe. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametufundisha adhkaar za kumtukuza Al-Qudduws kama ifuatavyo:

Katika kurukuu na kusujudu kwenye Swalaah:

سُبـّوحٌ قُـدّْوس، رَبُّ الملائِكَـةِ وَالـرُّوح

Subbuwhun Qudduwsun Rabbul-Malaaikati war-Ruwh

Mwingi wa kutakaswa, Mtakatifu, Rabb wa Malaika na Jibriyl [Hadiyth ya Aaishah (Radhwiya Allaahu ’anhaa) - Muslim (1/353), Abuu Daawuwd (1/230)]

 

Pia du’aa ya mwisho kabisa baada ya kutoa salaam katika Swalaah ya Witr ni:

سُـبْحانَ المَلِكِ القُدّوسِ

Subhaanal-Malikil-Qudduws

 

unaisoma mara tatu, kisha ya tatu yake unaivuta kwa sauti na huku ukisema:

 ربِّ الملائكةِ والرّوح

Rabbil-Malaaikati war-Ruwh

Utakasifu ni wa Mfalme, Mtakatifu. Ee Rabb wa Malaika na wa Jibriyl  [Hadiyth ya ‘Abdur-Rahmaan bin Abzay (Radhwiya Allaahu ‘anhu) - An-Nasaaiy (3/244), Ad-Daaraqutwniy na wengineo].

 

 

 

Share

016-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AS-SALAAM

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

السَّلام

AS-SALAAM

 

 

 

As-Salaam:  Mwenye Amani,  Mwenye  kusalimika na kasoro zote.

 

Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Ndiye Mwenye haki ya jina hili tukufu Pekee ambalo lina maana zote za ukamilifu, kwani yeye ni As-Salaam katika kila hali na katika kila mazingatio.

 

Yeye Ndiye As-Salaam; Aliyesalimika na kila ovu, shari, aibu, kasoro na upungufu. Yeye ni As-Salaam katika dhati Yake. Yeye ni As-Salaam katika Majina Yake na Sifa Zake.  As-Salaam katika matendo Yake Aliyesalimika na dhuluma.

 

As-Salaam; Yeye (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Ndiye Aliyewasalimisha waja Wake na kila adhabu kwa wale ambao hawastahiki na Amewasalimisha na kila dhuluma duniani na Aakhirah.

 

As-Salaam; Yeye (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Amewasalimisha Manabii Wake kwa amani na Akawasifia na kuwatenga na aibu na maovu. Na Akawasalimisha Mawalii Wake Aliowachagua. Amewasalimisha duniani na Aakhirah:

 

Duniani: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

قُلِ الْحَمْدُ لِلَّـهِ وَسَلَامٌ عَلَىٰ عِبَادِهِ الَّذِينَ اصْطَفَىٰ ۗ

Sema: AlhamduliLLaah, Himidi Anastahiki Allaah na Salaamun! Amani iwe juu ya waja Wake Aliowachagua.  [An-Naml 27:59]

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ ﴿٧٩﴾

Salaamun! Amani iwe juu ya Nuwh ulimwenguni. [Asw-Swafaat 37:79]

 

سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ ﴿١٠٩﴾

Salaamun! Amani iwe juu ya Ibraahiym. [Asw-Swafaat 37:109]

 

 

Na pia Akamsalimisha Muwsaa na Haaruwn na Iliyaas [Asw-Swafaat 37:120,

 

Na Akawasalimisha Rusuli Wake wote Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَسَلَامٌ عَلَى الْمُرْسَلِينَ ﴿١٨١﴾

Na Salaamun! Amani iwe juu ya Rusuli.  [Asw-Swafaat 37:181]

 

 

Aakhirah: Atawasalimisha waja Wake watakapoingia Jannah. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ ﴿٥٥﴾

Hakika watu wa Jannah leo wamo katika kushughulika wakifurahi.

 

هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِئُونَ ﴿٥٦﴾

Wao na wake zao, wakiwa katika vivuli, juu ya makochi ya fakhari wakiegemea.

 

لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ ﴿٥٧﴾

Watapata humo kila aina ya matunda, na watapata wanavyoomba.

 

سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ ﴿٥٨﴾

“Salaamun!” Kauli kutoka kwa Rabb Mwenye kurehemu. [Yaasiyn 36: 55-58]

 

Na pia:

 

تَحِيَّتُهُمْ يَوْمَ يَلْقَوْنَهُ سَلَامٌ ۚ وَأَعَدَّ لَهُمْ أَجْرًا كَرِيمًا ﴿٤٤﴾

Maamkizi yao Siku watakayokutana Naye; ni ‘Salaam’; na Amewaandalia ujira wa ukarimu. [Al-Ahzaab 33:44]

 

Ni salama na amani itokayo kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) inatosheleza kuliko salama nyingine yoyote ile, na inatosheleza kuliko maamkizi mengine yoyote yale, na inamkurubisha mtu na kila tarajio lake. “Nini dhana yako na maamkizi ya Mfalme wa wafalme, Rabb ‘Adhimu, Mpole Mwenye kurehemu, kwa waja wenye kustahiki ukarimu Wake, wale waliopata radhi Zake, basi hatowaghadhibikia kamwe.” [Tafsiyr As-Sa’adiy Suwrat Yaasiyn 36: 58].

 

As-Salaam; Yeye Ndiye chanzo cha amani na usalama, kila amani hutoka Kwake, hivyo usitake amani na usalama isipokuwa Kwake tu (Tabaaraka wa Ta’aalaa).

 

As-Salaam; Yeye (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Ndiye Mwenye kuwasalimisha Awatakaye katika waja Wake kwa muktadha wa hekima Yake, na uadilifu Wake duniani.

 

عن أَبي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:  ((مَثَلُ الْمُجَاهِدِ فِي سَبِيلِ اللَّهِ - وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَنْ يُجَاهِدُ فِي سَبِيلِهِ- كَمَثَلِ الصَّائِمِ الْقَائِمِ، وَتَوَكَّلَ اللَّهُ لِلْمُجَاهِدِ فِي سَبِيلِهِ بِأَنْ يَتَوَفَّاهُ أَنْ يُدْخِلَهُ الْجَنَّةَ، أَوْ يَرْجِعَهُ سَالِمًا مَعَ أَجْرٍ أَوْ غَنِيمَةٍ)) البخاري  كتاب الجهاد والسير  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraryah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Mfano wa Mujaahid katika njia ya Allaah – na Allaah Anamjua aliye Mujaahid katika njia Yake - ni kama aliyefunga Swawm   kwa kuendeleza. Allaah Amempa dhamana  kwamba Akimfisha, Atamuingiza  Jannah au arudi salama pamoja na ujira wa ghanima.” [Al-Bukhaariy katika Kitaab Al-Jihaad Was-Sayr]

 

Na Aakhirah Atawasalimisha waja Wake kama ilivyo katika Hadiyth ya Asw-Swiraatw:

 

فَأَكُونُ أَوَّلَ مَنْ يُجِيزُ، وَدُعَاءُ الرُّسُلِ يَوْمَئِذٍ: اللَّهُمَّ سَلِّمْ سَلِّمْ

“… na nitakuwa wa kwanza kuvuka, na du’aa ya Rasuli siku hiyo itakuwa: Allaahumma Sallim, Sallim!  (Ee Allaah tusalimishe, tusalimishe)” [Al-Bukhaariy Kitaab Ar-Riqaaq]

 

 

Jina hili tukufu limetajwa mara moja tu katika Qur-aan Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ  

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha, Amesalimika na kasoro zote. [Al-Hashr 59: 23]

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah: As-Salaam:

 

1. Kuomba du’aa kwa As-Salaam kwa unyenyekevu uombe salama duniani na Aakhirah.  

 

Ya kuomba salama duniani ni kama vile kuomba afya kutokana na maradhi, maafa na mambo yote mtu anayoyachukia.

 

Ama ya kuomba salama Aakhirah ni kuomba amani na salama katika Dini yako. Uombe salama na yakini kutokana na ukafiri, shirki, unafiki, bid’ah, maasi na kadhaalika. Na utangulize kwa Rabb wako fungamano la iymaan ya nguvu kabisa na salama katika moyo wako dhidi ya yote yanayomghadhibisha Rabb wako (Tabaaraka wa Ta’aalaa) na sifa chafu na mbaya hadi utakapokutana na Rabb wako ukiwa na moyo wa salama kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

“Siku hayatofaa mali wa watoto.

 

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

“Isipokuwa yule atakayemfikia Allaah na moyo uliosalimika. [Ash-Shu’araa 26: 88-89]

 

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasisitiza kuomba hayo ya salama na amani duniani na Aakhirah na akabainisha kuwa kupata salama katika Dini ndio khayr kubwa mno baada ya iymaan na ndio kufuzu. Hadiyth mbili miongoni mwazo ni:

 

قامَ أَبُو بَكْرٍ الصّدّيقُ عَلَى المِنْبَرِ ثُمّ بَكَى فقَالَ: قامَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم عَامَ الأوّلِ عَلَى المنْبَر ثُمّ بَكَى فقَالَ: ((سَلُوا اللهَ العَفْوَ والعَافِيَةَ ، فإِنّ أَحَداً لَمْ يُعْطَ بعد اليَقِين خَيْراً مِنَ الْعَافِيَة )) صحيح الترمذي (3558)،  وصحيح الترغيب والترهيب  (3387) صحيح الجامع (3632)

Abuu Bakr Asw-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhu) alisimama juu ya minbari kisha akalia akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisimama katika minbari hiyo mwaka wa mwanzo akalia na akasema: ((Muombeni Allaah msamaha na Al-‘Aafiyah (salama, amani hifadhi ya kila baya) kwani  hakika baada ya iymaan, hakuna kilicho bora kupewa kama Al-’Aafiyah)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3558), Swahiyh At-Targhiyb (3387), Swahiyh Al-Jaami’ (3632)]

 

Na pia:

 

عنْ سَلَمَةَ بْنِ وَرْدَانَ الْمَدَنِيِّ، قَالَ: سَمِعْتُ أَنَسَ بْنَ مَالِكٍ قَالَ: جَاءَ رَجُلٌ إِلَى رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم  فَقَالَ : يَا رَسُولَ اللهِ، أَيُّ الدُّعَاءِ أَفْضَلُ ؟ قَالَ: ((تَسْأَلُ رَبَّكَ الْعَفْوَ وَالْعَافِيَةَ فِي الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ)) ثُمَّ أَتَاهُ مِنْ الْغَدِ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، أَيُّ الدُّعَاءِ أَفْضَلُ ؟ قَالَ: ((تَسْأَلُ رَبَّكَ الْعَفْوَ وَالْعَافِيَةَ  فِي الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ)) ثُمَّ أَتَاهُ الْيَوْمَ الثَّالِثَ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللهِ، أَيُّ الدُّعَاءِ أَفْضَلُ؟ قَالَ: ((تَسْأَلُ رَبَّكَ الْعَفْوَ وَالْعَافِيَةَ فِي الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ، فَإِنَّكَ إِذَا أُعْطِيتَهُمَا فِي الدُّنْيَا ثُمَّ أُعْطِيتَهُمَا فِي الآخِرَةِ فَقَدْ أَفْلَحْتَ)) أحمد، 19/ 304 واللفظ له، الترمذي 3512  وابن ماجه  3848،  والأدب المفرد للبخاري، ص 222 .

 

Imepokelewa kutoka kwa Salamah bin Wardaan Al-Madaniyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amemsikia Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) akisema: “Alikuja mtu kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Du’aa gani ni bora kabisa? Akasema: ((Umuombe Rabb wako afya na Al-‘Aafiyah (hifadhi, amani, salama) duniani na Aakhirah)). Kisha akamjia tena siku ya pili yake akamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Du’aa gani ni bora kabisa? Akasema: ((Umuombe Rabb wako afya na Al-‘Aafiyah duniani na Aakhirah)). Kisha akamjia tena siku ya tatu akamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Du’aa gani ni bora kabisa? Akasema: ((Umuombe Rabb wako afya na Al-‘Aafiyah duniani na Aakhirah, kwani ukipewa hayo mawili duniani kisha ukapewa Aakhirah basi kwa yakini umefaulu)) [Ahmad (19/304) na tamshi lake, At-Tirmidhiy (3512), Ibn Maajah (3848), Al-Adab Al-Mufrad (222)]   

 

 

Na du’aa yenyewe alikuwa akiomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika nyiradi za asubuhi na jioni kama ifuatavyo:

 

اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في الدُّنْـيا وَالآخِـرَة، اللّهُـمَّ إِنِّـي أسْـأَلُـكَ العَـفْوَ وَالعـافِـيةَ في ديني وَدُنْـيايَ وَأهْـلي وَمالـي، اللّهُـمَّ اسْتُـرْ عـوْراتي وَآمِـنْ رَوْعاتـي، اللّهُـمَّ احْفَظْـني مِن بَـينِ يَدَيَّ وَمِن خَلْفـي وَعَن يَمـيني وَعَن شِمـالي، وَمِن فَوْقـي، وَأَعـوذُ بِعَظَمَـتِكَ أَن أُغْـتالَ مِن تَحْتـي

Allaahumma inniy as-alukal ‘aafiyah fid-dun-yaa wal Aakhirah. Allaahumma inni as-alukal ‘afwa wal ‘aafiyata fiy Diyniy wa dun-yaaya, wa ahliy, wa maaliy. Allaahumma-stur ‘awraatiy, wa-aamin raw’aatiy. Allaahumma-hfadhwniy min bayni yadayya, wamin khalfiy, wa ‘an yamiyniy, wa ‘an shimaaliy, wamin fawqiy, wa a’uwdhu bi’adhwamatika an ughtaala min tahtiy

 

Ee Allaah, hakika nakuomba msamaha na Al’-Aafiyah (hifadhi, amani, salama) duniani na Aakhirah. Ee Allaah, hakika nakuomba msamaha na Al’-Aafiyah katika Dini na dunia yangu, na ahli wangu, na mali yangu. Ee Allaah aibu zangu na nitulize khofu yangu. Ee Allaah, nihifadhi mbele yangu, na nyuma yangu, na kulia kwangu, na kushoto kwangu, na juu yangu, na najikinga kwa Uadhimu Wako kwa kutekwa chini yangu. [Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaahu ’anhu) Swahiyh Ibn Maajah (2/332), Swahiyh Abiy Daawuwd (5074)].    

 

2. Kuusalimisha ulimi wako na kiwiliwili chako katika kuwaudhi watu:

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرٍو (رضي الله عنهما) قَال: قَال رَسُولُ الله صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((الْمُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ الْمُسْلِمُونَ مِنْ لِسَانِهِ وَيَدِهِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah in ‘Amr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muislamu ni yule anayeweka amani kwa watu [ambaye Waislamu wenziwe wanasalimika] kwa ulimi na mkono wake)) [Al-Bukhaariy, Muslim]  

 

3. Kutoa salaam kwa watu. Unapoamkia mtu: “Assalaamu ‘Alaykum” (Amani iwe juu yenu) inamaanisha: “Mko katika amani na hamtopata maovu yoyote kutoka Kwangu.”

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesisitiza katika Hadiyth kadhaa miongoni mwazo ni:

 

عن عبدِ اللهِ بنِ مسعودٍ قال إنَّ السَّلامَ اسمٌ من أسماءِ اللهِ وضعَهُ اللهُ في الأرضِ ، فأفشُوهُ بينكم ، إنَّ الرَّجلَ إذا سلَّم على القومِ فردُّوا عليه كانت عليهم فضلُ درجةٍ ؛ لأنَّه ذكَّرَهم بالسَّلامِ ، وإن لم يردَّ عليه ردَّ عليه مَن هو خيرٌ منه وأطيبُ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((As-Salaam ni katika Majina ya Allaah Ameweka ardhini, basi salimianeni baina yenu. Hakika mtu anaposalimia watu wakamjibu, basi hupata daraja ya juu kabisa kuliko wao kwa sababu amewakumbusha amani. Ikiwa hatomjibu mtu, atajibiwa na ambaye ni mbora zaidi kuliko yeye na mzuri zaidi. [Swahiyh Adab Al-Mufrad  (793), Swahiyh Al-Jaami’ (3697)]

 

Mwenye sifa hiyo ya kuwatolea watu salaam atapata salama na amani ya milele katika Daarus-Salaam (Jannah), kutokana na Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambayo ilikuwa ni katika mafunzo ya mwanzo kabisa kuwapa Maswahaba Madiynah:

 

((يَا أَيُّهَا النَّاسُ، أَفْشُوا السَّلَامَ، وَأَطْعِمُوا الطَّعَامَ، وَصِلُوا الْأَرْحَامَ، وَصَلُّوا بِاللَّيْلِ وَالنَّاسُ نِيَامٌ تَدْخُلُوا الْجَنَّةَ بِسَلَامٍ)) رواه الترمذي، حديث صحيح

((Enyi watu, enezeni (amkianeni) salaam, na lisheni chakula, na Swalini watu wakiwa wamelala, mtaingia  Jannahh kwa salama)) [At-Tirmidhiy – Hadiyth Swahiyh]

 

 

4. Usiache kusoma du’aa baada ya kila Swalaah:

 

أَسْـتَغْفِرُ الله، أَسْـتَغْفِرُ الله، أَسْـتَغْفِرُ الله، اللّهُـمَّ أَنْـتَ السَّلامُ، وَمِـنْكَ السَّلام، تَبارَكْتَ يا ذا الجَـلالِ وَالإِكْـرام

Astaghfiru-Allaah, Astaghfiru-Allaah, Astaghfiru-Allaah. Allaahumma Antas-Salaam, wa Minkas-salaam, Tabaarakta yaa dhal-Jalaali wal-Ikraam

 

Namuomba Allaah maghfirah, Namuomba Allaah maghfirah,  Namuomba Allaah maghfirah. Ee Allaah Wewe Ndiye As-Salaam na Kwako ndiko kutokako salama, Umebarikika Ee Mwenye Ujalali na Ukarimu. [Hadiyth ya Thawbaan Al-Haashimiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) katika  Muslim (1/414) [591]

 

5. Kithirisha kumswalia Nabiy Muhammad  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuombea salama kama Anavyoamrisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):  

   

إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ ۚ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾

Hakika Allaah na Malaika Wake wanamswalia Nabiy. Enyi walioamini mswalieni na msalimieni kwa mamkizi ya amani na kwa tasliymaa. [Al-Ahzaab 33: 56]

 

6. Unaposibiwa na maradhi, maafa, shida omba du’aa kwa kutawassal kwa Jina hili tukufu la As-Salaam. Unaweza kusema: “Allaahumma Antas-Salaam niponyeshe kadhaa.” Au “Niondoshee dhiki zangu kadhaa.“ Au “Nijaalie salama na matatizo kadhaa.” Au “Nijaalie salama na amani kutokana na adui zangu kadhaa…”

 

 

 

 

 

Share

017-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-MUUMIN

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْمُؤمِن

AL-MUUMIN

 

 

 

 

Al-Muumin: Mwenye Kusadikisha Ahadi, Mwenye Kuaminisha, Mwenye kuweka amani na usalama.

 

Jina hili Tukufu limetajwa mara moja katika Qur-aan:

اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ  

Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha, Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi, Mwenye kuaminisha,  [Al-Hashr 59: 23]

 

Maana za Jina hili Tukufu zimetumika kama zilivyokuja katika Aayah zifuatazo:

 

Maana ya kusadikisha na kuaminisha (amani):

Allaah Anasema kuhusu kisa cha nduguze Yuwsuf kwa baba yao:

قَالُوا يَا أَبَانَا إِنَّا ذَهَبْنَا نَسْتَبِقُ وَتَرَكْنَا يُوسُفَ عِندَ مَتَاعِنَا فَأَكَلَهُ الذِّئْبُ ۖ وَمَا أَنتَ بِمُؤْمِنٍ لَّنَا وَلَوْ كُنَّا صَادِقِينَ﴿١٧﴾

Wakasema: “Ee baba yetu! Hakika sisi tulikwenda tukishindana mbio na tulimwacha Yuwsuf kwenye vitu vyetu; basi mbwa mwitu akamla. Nawe hutotuamini japo tukiwa ni wakweli.” [Yuwsuf 12: 17]

 

Maana ya amani na salama: Ni kinyume na  khofu na kuogopa [Mu’ujam Maqayiys Al-Lughah (1/133) na Tafsiyr Asmaai Allaah (Uk 31)].

Allaah Ta’ala Anasema:

الَّذِي أَطْعَمَهُم مِّن جُوعٍ وَآمَنَهُم مِّنْ خَوْفٍ ﴿٤﴾

Ambaye Anawalisha kuwaokoa na njaa, na Akawapa amani kutokana na khofu. [Qurayish 106:4]

 

Jina hili Tukufu lina maana nyingi za ukamilifu na Utukufu:

 

1. Allaah (‘Azza wa Jalla) Ambaye Amewaaminisha (Amewapa amani) watu na dhulma (Hatowadhulumu). Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَظْلِمُ النَّاسَ شَيْئًا وَلَـٰكِنَّ النَّاسَ أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ ﴿٤٤﴾

Hakika Allaah Hadhulumu watu chochote, lakini watu nafsi zao wenyewe   ni wenye kujidhulumu. [Yuwnus 10:44]

 

Na Atawaaminisha wanaostahiki kuaminishwa na dhulma Siku ya Qiyaamah. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٥٤﴾

Basi leo nafsi yoyote haitodhulumiwa kitu chochote, na wala hamtalipwa isipokuwa yale mliyokuwa mkiyatenda. [Yaasiyn 36: 54]

 

2. Yeye Allaah (‘Azza wa Jalla) Ambaye Anasadikisha ahadi Zake kwa waja Wake. Kila Anachowabashiria katika mambo ya ghayb kwa njia ya Wahy. Ahadi za mazuri na maonyo Anayowaonya, hapa duniani na  huko Aakhirah:  

a. Anawasadikisha waja Wake Waumini kwa iymaan zao kwa kile Alichowaahidi katika thawabu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

جَزَاؤُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًاۖ

Jazaa yao iko kwa Rabb wao; Jannaat za milele zipitazo chini yake mito ni wenye kudumu humo abadi.  [Al-Bayyinah 98: 8]

 

b. Anawasadikisha makafiri katika Alichowaahidi ya adhabu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَعَدَ اللَّـهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ خَالِدِينَ فِيهَا ۚ هِيَ حَسْبُهُمْ ۚ وَلَعَنَهُمُ اللَّـهُ ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّقِيمٌ﴿٦٨﴾

Allaah Amewaahidi wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na makafiri moto wa Jahannam, ni wenye kudumu humo; unawatosheleza (kuwaadhibu vilivyo)! Na Allaah Amewalaani, na watapata adhabu ya kudumu. [At-Tawbah 9: 68]

 

3. Yeye Allaah (‘Azza wa Jalla) Anawaaminisha waliomuamini ambao wanampwekesha, kwamba watakuwa katika amani na hawatopata adhabu Zake kwa kuwa wamejiepusha na dhulma ya kumshirikisha.

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ الْأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُونَ ﴿٨٢﴾

Wale walioamini na hawakuchanganya iymaan zao na dhulma; hao ndio watakaopata amani nao ndio walioongoka. [Al-An’aam 6: 82]

 

4. Wanaopewa amani zaidi na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni waja wema. Huwapa tumaini katika nyoyo zao hapa duniani na Siku ya mwisho.

 

-Duniani:

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَعَدَ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَيَسْتَخْلِفَنَّهُمْ فِي الْأَرْضِ كَمَا اسْتَخْلَفَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ وَلَيُمَكِّنَنَّ لَهُمْ دِينَهُمُ الَّذِي ارْتَضَىٰ لَهُمْ وَلَيُبَدِّلَنَّهُم مِّن بَعْدِ خَوْفِهِمْ أَمْنًا ۚ  

Allaah Amewaahidi wale walioamini miongoni mwenu na wakatenda mema kwamba bila shaka Atawafanya makhalifa katika ardhi kama Alivyowafanya makhalifa wale waliokuwa kabla yao, na bila shaka Atawamakinishia Dini yao Aliyowaridhia, na bila shaka Atawabadilishia amani badala ya khofu yao... [An-Nuwr 24: 55]

 

Na katika jihaad na katika mitihani, zitateremka sababu za kuwapa amani. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِذْ يُغَشِّيكُمُ النُّعَاسَ أَمَنَةً مِّنْهُ  

(Kumbukeni) Pale Alipokufunikeni kwa usingizi (kuwa ni) amani kutoka Kwake… [Al-Anfaal 8: 11]

 

Na Akawatia utulivu nyoyo za Waumini:

هُوَ الَّذِي أَنزَلَ السَّكِينَةَ فِي قُلُوبِ الْمُؤْمِنِينَ لِيَزْدَادُوا إِيمَانًا مَّعَ إِيمَانِهِمْ ۗ  

Yeye Ndiye Aliyeteremsha utulivu katika nyoyo za Waumini ili Awazidishie iymaan pamoja na iymaan zao.  [Al-Fat-h]

 

Na Akawapa Rusuli Wake ushindi dhidi ya maadui Zake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

ثُمَّ صَدَقْنَاهُمُ الْوَعْدَ فَأَنجَيْنَاهُمْ وَمَن نَّشَاءُ وَأَهْلَكْنَا الْمُسْرِفِينَ ﴿٩﴾

Kisha Tukawasadikishia ahadi Tukawaokoa wao na wale Tuliowataka; na Tukaangamiza wapindukiaji mipaka. [Al-Anbiyaa 21;9]

 

Na Anasema tena (Subahaanu wa Ta’aalaa):

إِذْ يُوحِي رَبُّكَ إِلَى الْمَلَائِكَةِ أَنِّي مَعَكُمْ فَثَبِّتُوا الَّذِينَ آمَنُوا ۚ  

(Kumbuka) Pale Rabb wako Alipowatia ilhamu Malaika (kuwaambia): “Hakika Mimi Niko pamoja nanyi; basi wathibitisheni wale walioamini."  [Al-Anfaal 8:12]

 

-Wakati wa mauti:

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anawaaminisha Waumini pale Malakul-Mawt anapoteremka kuwatoa roho zao. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿٣٠﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara; Malaika huwateremkia: (kuwaambia): “Msikhofu, na wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo mlikuwa mkiahidiwa.”

نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَشْتَهِي أَنفُسُكُمْ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ ﴿٣١﴾

“Sisi ni rafiki zenu walinzi katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale mtakayoomba.

نُزُلًا مِّنْ غَفُورٍ رَّحِيمٍ ﴿٣٢﴾

“Ni mapokezi ya takrima kutoka kwa Mwenye kughufuria, Mwenye kurehemu.” [Fusw-Swilat 41;30]

 

-Katika Al-Barzakh (Maisha baina ya kufariki mpaka kufufuliwa)

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anawaaminsha waja Wake Waumini wanaojitolea katika jihaad, kwa kuwahifadhi na  fitna za kaburi:

عن فَضَالَةَ بْنُ عُبَيْدٍ رضي الله عنه عَنْ رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّهُ قَالَ: ((كُلُّ مَيِّتٍ يُخْتَمُ عَلَى عَمَلِهِ، إِلاَّ الَّذِي مَاتَ مُرَابِطًا فِي سَبِيلِ اللهِ، فَإِنَّهُ يُنْمَى لَهُ عَمَلُهُ إِلَى يَوْمِ القِيَامَةِ، وَيَأْمَنُ مِنْ فِتْنَةِ القَبْرِ))

Imepokelewa kutoka kwa Fadhwaalah bin ‘Ubayd  (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((‘Amali za kila anayefariki zinamalizika isipokuwa ambaye amefariki akiwa analinda mipaka ya adui katika njia ya Allaah, kwani yeye huzidishiwa ‘amali zake mpaka siku ya Qiyaamah na huaminishwa na fitna za kaburi)) [At-Tirmidhiy na amesema ni Hadiyth Hasan Swahiyh na ameisahihisha Al-Albaaniy: Swahiyh At-Tirmidhiy  (1621), Swahiyh Al-Jaami’ (4562)]

 

-Aakhirah:

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anawaaminisha Waumini katika mfazaiko mkubwa ya Siku ya Qiyaamah. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّ الَّذِينَ سَبَقَتْ لَهُم مِّنَّا الْحُسْنَىٰ أُولَـٰئِكَ عَنْهَا مُبْعَدُونَ ﴿١٠١﴾

Hakika wale ambao umewatangulia wema Wetu, hao watabaidishwa nao (moto).

 

لَا يَسْمَعُونَ حَسِيسَهَا ۖ وَهُمْ فِي مَا اشْتَهَتْ أَنفُسُهُمْ خَالِدُونَ ﴿١٠٢﴾

Hawatosikia mvumo wake. Nao watadumu katika ambayo zimetamani  nafsi zao.

 

لَا يَحْزُنُهُمُ الْفَزَعُ الْأَكْبَرُ وَتَتَلَقَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ هَـٰذَا يَوْمُكُمُ الَّذِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿١٠٣﴾

Haitowahuzunisha mfazaiko mkubwa kabisa; na Malaika watawapokea (wakiwaambia): “Hii ni ile Siku yenu mliyokuwa mkiahidiwa.” [Al-Anbiyaa 21; 101-103]

 

Na Anawaaminisha na adhabu za Jahannam:

أَفَمَن يُلْقَىٰ فِي النَّارِ خَيْرٌ أَم مَّن يَأْتِي آمِنًا يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۚ

Hakika wale wanaozipotosha Aayaat Zetu hawawezi kujificha kwetu. Je, basi yule atakayetupwa katika moto ni bora au yule atakayekuja akiwa katika amani Siku ya Qiyaamah? [Fusw-swilat 41: 40]

 

-Jannah:

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anawasadikisha ahadi Yake na Anawaaminisha katika maisha ya furaha za milele: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي صَدَقَنَا وَعْدَهُ وَأَوْرَثَنَا الْأَرْضَ نَتَبَوَّأُ مِنَ الْجَنَّةِ حَيْثُ نَشَاءُ ۖ فَنِعْمَ أَجْرُ الْعَامِلِينَ﴿٧٤﴾

“AlhamduliLLaahi, Himidi Anastahiki Allaah Ambaye Ametuhakikishia kweli ahadi Yake, na Ameturithisha ardhi tunakaa popote katika Jannah tutakapo.” Basi uzuri ulioje ujira wa watendao.  [Az-Zumar 39: 74]

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah: Al-Muumin:

 

1. Muumini anapaswa kuzingatia na kufahamu maana ya Al-Muumin na makusudio yake. Kisha atende kwa mujibu wake. Na asiwe na shaka kuamini ahadi za Allaah (Ta'aalaa) na kuaminisha Kwake na kila khofu. Kwa hiyo, marejeo yake yote katika hali ya khofu na kupungukiwa iymaan, yawe ni kwa Rabb wake (‘Azza wa Jalla):

 

2. Muumini anapaswa kuwaaminisha Waumini wenzake kutokana na shari za kila aina. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((المؤمنُ مَنْ أَمِنَهُ الناسُ، والمسلمُ مَنْ سَلِمَ المسلمُونَ من لسانِهِ ويَدِه، والمُهاجِرُ مَنْ هجرَ السُّوءَ، والذي نَفسي بيدِهِ لا يدخلُ الجنةَ عَبْدٌ لا يَأْمَنُ جارُهُ بَوَائِقَهُ))

Muumini ni yule anayeaminisha watu. Na Muislamu ni ambaye anayewaekea amani Waislamu kwa ulimi wake na mkono wake, na   Muhaajir ni ambaye anahama maovu. Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake., haingi Jannah mja ambaye jirani yake hana amani kwa uovu wake)) [Hadiyth ya Anas bin Maalik - Swahiyh At-Targhiyb (2555)]

 

Riwaaya nyingine:

 

((Je, niwajulisheni ni nani Muumini! Ni Yule ambaye anawaaminisha watu katika mali zao na nafsi zao, na Muislamu ni Yule mwenye kuwasalimisha Waislamu kutokana na ulimi wake na mkono wake)) [Swahiyh Ibn Maajah (3934), Swahiyh An-Nasaaiy (4622)]

 

Mifano ya shari za ulimi ni: ghiybah (kusengenya), An-Namiymah (kufitinisha), kuwatusi watu, kukashifu, kukaripia n.k.

 

Mifano ya shari za mikono ni: kuwaumiza watu, kuwaibia au kuwapunjia mali zao, kushika ya haraam, n.k.

 

3. Muumini anapaswa asadikishe katika kauli zake na ‘amali zake. Awe mkweli daima katika kila hali hadi aandikiwe na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuwa ni mkweli na mwenye kusadikisha.  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

((عَلَيْكُمْ بِالصِّدْقِ فَإِنَّ الصِّدْقَ يَهْدِي إِلَى الْبِرِّ وَإِنَّ الْبِرَّ يَهْدِي إِلَى الْجَنَّةِ وَمَا يَزَالُ الرَّجُلُ يَصْدُقُ وَيَتَحَرَّى الصِّدْقَ حَتَّى يُكْتَبَ عِنْدَ اللَّهِ صِدِّيقًا))

((Ni juu yenu kuwa wakweli, kwani ukweli unapeleka kwenye wema, na wema unapeleka kwenye Jannah. Mtu huendelea kuwa mkweli  na kujitahidi katika ukweli mpaka huandikiwa mbele ya Allaah kuwa ni mkweli….)) [Muslim Kitaab Al-Birr wasw-Swillah Wal-Adaab]

 

4. Muumini atende 'amali njema na aamini yaliyoahidiwa Siku ya Qiyaamah yaliyo mazuri huko Jannah na aamini ambayo ya kutishiwa na adhabu zake na mifazaiko ya Siku hiyo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

مَن جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ خَيْرٌ مِّنْهَا وَهُم مِّن فَزَعٍ يَوْمَئِذٍ آمِنُونَ ﴿٨٩﴾ ﴾

Atakayekuja na jema, basi atapata bora zaidi kuliko hilo; nao watakuwa katika amani na mafazaiko ya Siku hiyo. [An-Naml 27: 89]

 

5. Aminika kwa watu, wanapokupa amana zao uzitunze, wanapozitaka amana zao uwakabidhi. Tunza siri za watu. Mwili wako pia ni amana, basi utunze na uhifadhi na maasi.

 

6. Muombe Al-Muumin:

 

a. Akuthibitishe katika iymaan; uwe katika hali na sifa hiyo mpaka yatakapokufikia mauti.

 

b. Unapokuwa na khofu, muelekee Al-Muumin umuombe amani.

 

c. Akujaalie uwe mkweli kwa watu, uwe mwenye kuaminisha wenzako na shari.

 

d. Akuhifadhi shari ya viungo vyako kama alivyokuwa akiomba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

أللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ سَمْعِي وَمِنْ شَرِّ بَصَرِي وَمِنْ شَرِّ لِسَانِي وَمِنْ شَرِّ قَلْبِي وَمِنْ شَرِّ مَنِيِّي   

Allaahumma inniy a’uwdhu bika min sharri sam-’iy wamin sharri baswariy, wamin sharri lisaaniy wamin sharri qalbiy, wamin sharri maniyyi

 

Ee Allaah, hakika mimi najikinga Kwako shari ya kusikia kwangu [masikio yangu], na shari ya kuona kwangu [macho yangu], na shari ya ulimi wangu, na shari ya moyo wangu, na shari ya manii yangu. [Abuu Daawuwd , At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy – Taz. Swahiyh At-Tirmidhiy (3/166) na Swahiyh An-Nasaaiy (3/1108)]

 

7. Mdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa wingi pale iymaan yako inapopungua, pale unapokosa utulivu, unapokosa raha, unapokuwa katika dhiki kwani kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kunatuliza nyoyo na unabakia kuwa katika amani. Na hii ni mojawapo ya sifa ya Muumini!  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

الَّذِينَ آمَنُوا وَتَطْمَئِنُّ قُلُوبُهُم بِذِكْرِ اللَّـهِ ۗ أَلَا بِذِكْرِ اللَّـهِ تَطْمَئِنُّ الْقُلُوبُ ﴿٢٨﴾

Wale walioamini na zikatua nyoyo zao kwa kumdhukuru Allaah. Tanabahi!  Kwa kumdhukuru Allaah nyoyo hutulia! [Ar-Ra’d 13: 28]

 

 

 

 

Share

018-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-MUHAYMIN

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْمُهَيْمِن

AL-MUHAYMIN

 

 

 

 

Al-Muhaymin: Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye kudabiri mambo.

 

Jina hili Tukufu limetajwa mara moja katika Qur-aan Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ ا

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha, Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi, Mwenye kuaminisha, Mwenye kutawalia, kuchunga na kuhifadhi [Al-Hashr 59: 23]

 

Kisha sifa hiyo Akaihusisha na Qur-aan kuwa ni Muhaymin kwa maana ni Kitabu kinachodhibiti vitabu vyote vinginevyo vya mbinguni na inachunga na inahifadhi upotofu wowote ule kama potofu zilizopachikwa katika vitabu vya mbinguni. Na hata yeyote anayedai kama wanavyodai baadhi ya watu kutunga Qur-aan au kuipotosha basi Qur-aan hii Adhimu inadhibiti na kubatilisha hizo zinazotungwa. Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ الْكِتَابِ وَمُهَيْمِنًا عَلَيْهِ ۖ   

Na Tumekuteremshia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Kitabu kwa haki kinachosadikisha Vitabu vilivyokuwa kabla yake na chenye kudhibiti, kushuhudia na kuhukumu juu yake (hivo Vitabu).  [Al-Maaidah 5: 48]

 

Hivyo basi, Allaah (‘Azza wa Jalla) Ndiye Al-Muhaymin wa kila kitu:

Allaah (‘Azza wa Jalla) Mwenye kushuhudia matendo ya waja Wake, Mwenye kuwachunga na kuyatazama mambo yao; katika kauli zao, matendo yao wala hakipotei katika matendo yao chochote. Mwenye kuangalia mambo yao ya ndani yaliyojificha na yaliyo ndani ya nyoyo zao, kila kitu kimeenea katika ujuzi wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

 

وَمَا تَكُونُ فِي شَأْنٍ وَمَا تَتْلُو مِنْهُ مِن قُرْآنٍ وَلَا تَعْمَلُونَ مِنْ عَمَلٍ إِلَّا كُنَّا عَلَيْكُمْ شُهُودًا إِذْ تُفِيضُونَ فِيهِ ۚ وَمَا يَعْزُبُ عَن رَّبِّكَ مِن مِّثْقَالِ ذَرَّةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَلَا أَصْغَرَ مِن ذَٰلِكَ وَلَا أَكْبَرَ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ﴿٦١﴾

61. Na hushughuliki katika jambo lolote, na wala husomi humo katika Qur-aan, na wala hamtendi ‘amali yoyote isipokuwa Tunakuwa Mashahidi juu yenu mnaposhughulika nayo. Na hakifichiki kwa Rabb wako hata cha uzito wa chembe (au sisimizi) katika ardhi wala mbinguni na wala kidogo kuliko hicho na wala kikubwa zaidi ya hicho isipokuwa kimo katika Kitabu kilicho bayana. [Yuwnus 10: 61]

 

Allaah (‘Azza wa Jalla)  Ndiye  Anayewachunga waja Wake, Anayewahifadhi na kuwalinda Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

لَهُ مُعَقِّبَاتٌ مِّن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ يَحْفَظُونَهُ مِنْ أَمْرِ اللَّـهِ ۗ  

Ana Malaika wanaofuatana kwa zamu mbele yake na nyuma yake wanamhifadhi kwa amri ya Allaah.  [Ar-Ra’d 13: 11]

 

Allaah (‘Azza wa Jalla) Mwenye kufanya islahi ya hali zao, mambo yao, mwenye kutawalia wao kwa uwezo Wake, Naye istawaa juu ya ‘Arshi Yake Adhimu.

 

Imaam As-Sa’dy (Rahimahu Allaah) amesema: “Al-Muhaymin ni Ambaye Anayeangalia mambo yaliyojificha kwa kuwa Kwake Yeye Mjuzi. Yeye Anajua siri zako na unayoyadhihirisha. Anajua yaliyo na maslahi nawe na ambayo yenye kukufisidi kama Alivyosema:

وَاللَّـهُ يَعْلَمُ الْمُفْسِدَ مِنَ الْمُصْلِحِ ۚ

 Na Allaah Anamjua fisadi na mtengenezaji. [Al-Baqarah 2: 220]

 

Hivyo basi Yeye Huangalia mambo yaliyojificha na ambayo vifua vinayaficha. (kama Anavyosema Allaah):

يَوْمَ تُبْلَى السَّرَائِرُ ﴿٩﴾

Siku siri zitakapopekuliwa. [Atw-Twaariq 86:9]

 

Allaah (‘Azza wa Jalla) Mwenye kusadikisha, Ambaye Anawasadikisha Manabii Wake kwa uchaguzi wa Rabb wao Adhimu, kwa kuwa wao ni wakweli, na kilichodhihiri katika miujiza juu ya mikono yao. [Jaami’ Al-Bayaan (28/36) Tafsiyr Ibn Kathiyr (8/105) Fat-hul Baariy (6/366), Tafsiyr As-Sa’dy (5/488), Al-Minhaaj (1/202) Ar-Raaziy (202) Fat-hur-Rahiym Al-Malik Al-'Alaam...  (21-22)]     

 

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah, Al-Muhaymin:

 

1-Tahadhari Allaah Anakuchunga na Anashuhudia

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدٌ﴿٦﴾

...na Allaah ni Shahidi juu ya kila kitu. [Al-Mujaadilah 58: 6]

 

Na Anasema:

وَمَا اللَّـهُ بِغَافِلٍ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٨٥﴾

...na Allaah si Mwenye kughafilika kuhusu myatendayo. [Al-Baqarah 2: 85]

 

Kuwa na khofu daima kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anashuhudia matendo yetu katika hali zote kwani Yeye ni Mwenye kushuhudia ya siri na dhahiri duniani na Aakhirah. Yampasa Muumini kuwa na hisia katika hilo, katika utawala wake binafsi, kwa familia yake, katika kuchunga 'amali zake, katika majukumu yake na kutambua kwamba atakuja kusimamishwa mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuulizwa. 

Hadiyth ifuatayo ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inathibitisha hayo:

عَبْد اللَّهِ بْنِ عُمَرَ يَقُولُ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ: ((كُلُّكُمْ رَاعٍ وَكُلُّكُمْ مَسْؤول عَنْ رَعِيَّتِهِ، الإِمَامُ رَاعٍ وَمَسْؤولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ، وَالرَّجُلُ رَاعٍ فِي أَهْلِهِ وَهُوَ مَسْؤولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ، وَالْمَرْأَةُ رَاعِيَةٌ فِي بَيْتِ زَوْجِهَا وَمَسْؤولَةٌ عَنْ رَعِيَّتِهَا، وَالْخَادِمُ رَاعٍ فِي مَالِ سَيِّدِهِ ومَسْؤولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ)) قَالَ: وَحَسِبْتُ أَنْ قَدْ قَالَ((وَالرَّجُلُ رَاعٍ فِي مَالِ أَبِيهِ وَمَسْؤولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ- وَكُلُّكُمْ رَاعٍ وَمَسْؤولٌ عَنْ رَعِيَّتِهِ)).

((Nyinyi nyote ni wachunga na kila mmoja ataulizwa alichokichunga, kiongozi wa watu ni mchunga na ataulizwa kwa alichokichunga, na mwanamme ni mchunga wa familia yake na ataulizwa kwa alichokichunga, mwanamke ni mchunga wa nyumba ya mume wake na watoto wake naye ataulizwa alichokichunga, na mtumwa ni mchunga wa mali ya bwana wake naye ataulizwa kuhusu uchungaji wake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

2. Soma na ifanyie kazi Qur-aan kwa kuwa ni Muhaymin

Qur-aan itakuja kushuhudia ima juu yako kwa kuisoma na kufanya matendo mema au dhidi yako kwa kufanya matendo mabaya.

عَنْ أَبِى مَالِكٍ الأَشْعَرِىِّ  رضي الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ  صلى الله عليه وسلم: ((الْقُرْآنُ حُجَّةٌ لَكَ أَوْ عَلَيْكَ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kutoka kwa Abuu Maalik Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Qur-aan itakuwa ni hoja kwako au dhidi yako)) [Muslim]

 

Kwa hiyo, inakupasa uhalalishe yale ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameyahalalisha na uharamishe yale ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameyaharamisha na ubakie katika mipaka ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

 

 

3. Endesha utawala wako kwa kufauta shariy’ah za Qur-aan

Qur-aan ni Muhaymin kwa hiyo mwenye utawala wa aina yoyote ule atumie shariy’ah za Qur-aan kuhukumu baina ya walio katika ulinzi wake katika kesi zao, kupatansisha magomvi yao, kwani baada ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kutaja sifa ya Qur-aan kuwa ni Muhaymin, Akaamuru kuwa Qur-aan Aliyoiteremsha, itumiliwe kwa ajili ya kuhukumu baina ya watu kama Anavyosema:

وَأَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ الْكِتَابِ وَمُهَيْمِنًا عَلَيْهِ ۖ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ ۖ  

  Na Tumekuteremshia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) Kitabu kwa haki kinachosadikisha Vitabu vilivyokuwa kabla yake na chenye kudhibiti, kushuhudia na kuhukumu juu yake (hivyo Vitabu). Basi hukumu baina yao kwa yale Aliyoyateremsha Allaah.  [Al-Maaidah 5: 48]

 

 

4. Chunga moyo wako kwa kuwa ni kiungo kinachodhibiti na kuchunga viungo vinginevyo

Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

عَن النُّعْمَانَ بْنَ بَشِيرٍ (رضي الله عنهما) قَال: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:  ((الْحَلاَلُ بَيِّنٌ وَالْحَرَامُ بَيِّنٌ، وَبَيْنَهُمَا مُتَشَابِهَاتٌ لاَ يَعْلَمُهَا كَثِيرٌ مِنَ النَّاسِ، فَمَنْ اتَّقَى الشُّبُهَاتِ اسْتَبْرَأَ  لِدِينِهِ وَعِرْضِهِ، وَمَنْ وَقَعَ فِي الشُّبُهَاتِ وَقَعَ فِي الْحَرَامِ، كَالرَّاعِي يَرْعَى حَوْلَ الْحِمَى َيُوشِكُ أَنْ يَرْتَعْ فِيهِ، أَلاَ وَإِنَّ لِكُلِّ مَلِكٍ حِمًى، أَلاَ وَإِنَّ حِمَى اللَّهِ مَحَارِمُهُ، أَلاَ وَإِنَّ فِي الْجَسَدِ مُضْغَةً إِذَا صَلَحَتْ صَلَحَ الْجَسَدُ كُلُّه, وَإِذَا فَسَدَتْ فَسَدَ الْجَسَدُ كُلُّهُ أَلاَ وَهِيَ الْقَلْبُ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Hakika halali imebainika na haramu imebainika.  Baina ya mawili hayo mna yenye kutia shaka. Wengi miongoni mwa watu hawayajui. Basi atakayejiepusha na yenye kutia shaka, atakuwa amejiepushia shaka katika Dini yake na heshima yake. Na Atakayetumbukia katika yenye kutia shaka, ataingia kwenye haramu. Kama mchunga anayechunga kando ya mipaka, ni haraka kulisha humo [mpaka mwingine wa watu]. Zindukeni!  Kila mfalme ana mipaka. Zindukeni! Kwa yakini mipaka ya Allaah ni haramu Alizoziharamisha. Zindukeni! Kwa yakini katika mwili mna kinofu [cha nyama], kinapokuwa kimesalimika, mwili wote unakuwa umesalimika. Kinapoharibika, mwili wote unaharibika. Zindukeni! Kinofu hicho ni moyo)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

5. Ridhika na Qadhwaa na Qadar: (Yaliyohukumiwa na Yaliyokadiriwa) na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)

 

Kwa vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

  يَعْلَمُ الْمُفْسِدَ مِنَ الْمُصْلِحِ ۚ

Anamjua fisadi na mtengenezaji. [Al-Baqarah 2: 220]

 

 

6. Muombe Al-Muhaymin Akuchunge, Akuhifadhi, Akuendeshee Mambo yako

Unapofikwa na shida, khofu ya uadui na kadhaalika, mambo yako yanapokuwa hayaendi vizuri, maadui na shari zimekuandama, vikwazo vimekuelekea mbele yako, muombe Al-Muhaymin; Atakusaidia, Atakunusuru, Atakulinda, Atakupa tawfiyq, Atakutengeneza mambo yako. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba:

يا حَـيُّ يا قَيّـومُ بِـرَحْمَـتِكِ أَسْتَـغـيث، أَصْلِـحْ لي شَـأْنـي كُلَّـه، وَلا تَكِلـني إِلى نَفْـسي طَـرْفَةَ عَـين

Yaa Hayyu Yaa Qayyuwm bi-Rahmatika astaghiythu, Aswlihliy sha-ani kullahu walaa takilniy ilaa nafsiy twarfata ‘aynin

Ee Uliye hai daima, Msimamizi wa kila kitu, kwa Rahmah Zako ninakuomba uniokoe, nitengenezee mambo yangu  yote, wala usiniachie  mambo yangu mwenyewe (pasina kunisaidia) hata kwa muda (mdogo kama muda) wa kupepesa jicho. [Hadiyth ya Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ’anhu) - Abuu Daawuwd (4/3180), At-Tirmidhiy (5/465), Al-Haakim. Taz. Swahiyh At-Targhiyb (1/273), Swahiyh Al-Jaami’ [5820].

 

Share

019-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-'AZIYZ

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

الْعَزِيز

AL-‘AZIYZ

 

 

 

 

Al-‘Aziyz:  Azizi, Mwenye Taadhima, Mwenye enzi, Mwenye nguvu, Asiyeshindika.

 

Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Ndiye Al-Aziyz; Azizi, Mwenye Taadhima, Mwenye enzi, Mwenye nguvu,  Asiyeshindika. Ana maana zote za utukufu na wasifu na ufalme. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَلَا يَحْزُنكَ قَوْلُهُمْ ۘ إِنَّ الْعِزَّةَ لِلَّـهِ جَمِيعًا ۚ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٦٥﴾

Na wala isikuhuzunishe kauli yao. Hakika taadhima zote ni za Allaah Pekee. Yeye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote.  [Yuwnus 10: 65]

 

وَلَهُ الْكِبْرِيَاءُ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٣٧﴾

Na Adhama, Utukufu, Ujalali ni Wake Pekee mbinguni na ardhini; Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Jaathiyah 45: 37]

 

Al-Qurtwubiy amesema: “Al-‘Aziyz maana yake ni: Aliye Madhubuti Asiyedhurika, Ambaye Hadirikiwi wala Hashindwi.” [Tafsiyr Al-Qurtwubiy (2/131)]

 

Na Ibn Jariyr amesema: “Al-‘Aziyz yaani ni mkali katika kulipiza kwa adui Zake na ndio Anasema:

وَمَا نَقَمُوا مِنْهُمْ إِلَّا أَن يُؤْمِنُوا بِاللَّـهِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿٨﴾

Na hawakuwachukia isipokuwa kwa vile wamemwamini Allaah Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Al-Buruwj 85: 8]

 

Ibnul-Qayyim katika An-Nuwniyyah amesema:

“Yeye ni Al-‘Aziyz Ambaye Ubwana Wake haufikiwi (haushindwi). Atafikiwaje Mwenye kumiliki nguvu zote?

Naye ni Al-‘Aziyz Ambaye ni Mwenye kudhibiti Asiyepingika, hakuna kitu kitakachomshinda, kwa hiyo hizi ni Sifa mbili.

Naye ni Al-‘Aziyz kwa kuwa na Nguvu nayo ni Sifa Yake. Kwa hiyo Al-‘Izz ina maana tatu.

Nazo ni ambazo zimekamilika Kwake, Ametakasika kutokana na mapungufu yote, kutoka katika kila upande, Ambaye Hana mapungufu, kasoro zozote zile.”

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-‘Aziyz Ambaye Ndiye Mwenye Nguvu na Uwezo wote. Naye ni Mkali na Mkali kwa nguvu Zake, Ambaye zimedhalilika kwa nguvu Zake vyote vilivyokuwa ni vigumu, na yakalainika kwa nguvu Zake yaliyo magumu.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-‘Aziyz Ambaye Hana mfanowe, wala Hana wa kumlinganisha kwa uadilifu na kwa ukamilifu Wake katika pande zote.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-‘Aziyz, Mwenye nguvu katika kulipiza Kwake kisasi, Anapolipiza kisasi kwa adui Zake, hakuna yeyote mwenye uwezo wa kumzuia Asifanye hilo muda Anaotaka kulifanya hilo.  

 

Al-‘Aziyz; Mwenye nguvu Ambaye humpa Nguvu, mamlaka Amtakaye, Humtukuza Amtakaye, Humdhalilisha Amtakaye katika waja wake, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

قُلِ اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ تُؤْتِي الْمُلْكَ مَن تَشَاءُ وَتَنزِعُ الْمُلْكَ مِمَّن تَشَاءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَاءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَاءُ ۖ بِيَدِكَ الْخَيْرُ ۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢٦﴾

Sema: “Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, Unampa ufalme Umtakaye, na Unamuondoshea ufalme Umtakaye, na Unamtukuza Umtakaye, na Unamdhalilisha Umtakaye, khayr imo Mkononi Mwako.  Hakika Wewe juu ya kila kitu ni Muweza. [Aal-‘Imraan 3: 26]

 

Al-‘Aziyz Ambaye Mwenye nguvu, na Ambaye  Rusuli Wake hawadhalilishwi na watu, na Waumini wanapata nguvu na ‘izzah, bali makafiri ndio wenye kudhalilika. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):  

يَقُولُونَ لَئِن رَّجَعْنَا إِلَى الْمَدِينَةِ لَيُخْرِجَنَّ الْأَعَزُّ مِنْهَا الْأَذَلَّ ۚ وَلِلَّـهِ الْعِزَّةُ وَلِرَسُولِهِ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَلَـٰكِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٨﴾

Wanasema: “Tutakaporudi Madiynah, mwenye hadhi zaidi atamfukuza humo aliye dhalili.” Na hali utukufu ni wa Allaah na wa Rasuli Wake na wa Waumini, lakini wanafiki hawajui.  [Al-Munaafiquwn 63: 8]

 

Al-‘Aziyz Mwenye  shani ya juu na uwezo,p Mwenye utukufu wa dhati Yake, Mwenye Upekee katika ukamilifu Wake, katika sifa Zake zote. Na miongoni mwa ukamilifu wa nguvu Zake na ukamilifu Wake, ni kutakasika Kwake na upungufu wowote ule wa shari, aibu, na kushirikishwa. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ ﴿١٨٠﴾

Subhaana Rabbika! Utakasifu ni wa Rabb wako, Rabb Mtukufu kutokana na yale wanayoyavumisha.  [Asw-Swaaffaat 37: 180]

 

Jina hili limetajwa zaidi ya mara tisini katika Qur-aan. Limeungana na Al-Hakiym zaidi ya mara ishirini. Na Limeungana zaidi ya mara kumi na Ar-Rahiym; katika Suwrah Ash-Shu’araa Limeungana na Ar-Rahiym mara tisa. Hivyo inadhihirisha kuwa kuna hikmah ndani yake kutajwa na kukaririwa kwake kwa wingi.  

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah, Al-‘Aziyz:

 

1. Anayetaka ‘izzah, basi ‘izzah iko kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) muombe Yeye Pekee. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

مَن كَانَ يُرِيدُ الْعِزَّةَ فَلِلَّـهِ الْعِزَّةُ جَمِيعًا ۚ إِلَيْهِ يَصْعَدُ الْكَلِمُ الطَّيِّبُ وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ ۚ وَالَّذِينَ يَمْكُرُونَ السَّيِّئَاتِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ ۖ وَمَكْرُ أُولَـٰئِكَ هُوَ يَبُورُ ﴿١٠﴾

Yeyote Anayetaka utukufu, basi utukufu wote uko kwa Allaah. Kwake Pekee linapanda neno zuri na 'amali njema Huitukuza. Na wale wanaopanga njama za maovu watapata adhabu shadidi. Na njama za hao ni zenye kuangamia. [Faatwir 35: 10]

 

2. Ukitaka kutafuta nguvu, ushindi dhidi ya maadui na wanaojifanya majabari, basi tafuta nguvu kwa Al-‘Aziyz kwani Yeye Kwake hakuna linalomshinda, Analolitaka linakuwa na Asilolitaka haliwi.

Mnyenyekee kumuomba Yeye Al-‘Aziyz unaposhindwa jambo, na unapokuwa umekandamizwa na dhulma za wenye nguvu ili Allaah Mwenye nguvu zote, Asiyeshindika Akusaidie kuwashinda maadui zako. Kumbuka visa vya Manabii; mfano kisa cha Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam) jinsi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alivyomshinda Fir’awn aliyejiita yeye ni Ilaah (Muabudiwa), lakini Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alimshinda kwa kuteremsha miujiza Yake Akamvurumisha baharini na kufilia mbali.

 

3. Upe Uislamu wako ‘izzah (hadhi, utukufu) kwani utukufu si kuwa na mali wala nguvu wala mamlaka. Wala usitafute ‘izzah kwa maadui wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ukawa miongoni mwa wale ambao Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

الَّذِينَ يَتَّخِذُونَ الْكَافِرِينَ أَوْلِيَاءَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ ۚ أَيَبْتَغُونَ عِندَهُمُ الْعِزَّةَ فَإِنَّ الْعِزَّةَ لِلَّـهِ جَمِيعًا ﴿١٣٩﴾

Wale wanaofanya makafiri kuwa ni marafiki wandani badala ya Waumini. Je, wanatafuta utukufu kutoka kwao? Basi hakika utukufu wote ni wa Allaah Pekee. [An-Nisaa 4: 139]

 

Na ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema:

"نحن قوم أعزنا الله بالإسلام فمهما ابتغينا العزة بغيره أذلنا الله"

“Sisi ni watu ambao Allaah Ametupa ‘izzah kwa Uislamu, basi tutakapotafuta ‘izzah vyovyote vile kwa wengineo, Allaah Atatudhalilisha” [Mustadrak Al-Haakim (1/236/237) na Al-Haakim amesema: Swahiyh kwa sharti ya Ash-Shaykhayn]

 

Na ndio maana Uislamu utabakia kushinda Dini zote kama Anavyoahidi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ ﴿٣٣﴾

Yeye Ndiye Aliyemtuma Rasuli Wake (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kwa Mwongozo na Dini ya haki ili Aishindishe juu ya dini zote, japo watakirihika washirikina. [At-Twabah 9: 33]

 

4. Wape ‘izzah nduguzo Waumini wala usiwachafue heshima zao. Ameonya hivyo Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):   

((بِحَسْبِ امْرِئٍ مِنْ الشَّرِّ أَنْ يَحْقِرَ أَخَاهُ الْمُسْلِمَ. كُلُّ الْمُسْلِمِ عَلَى الْمُسْلِمِ حَرَامٌ دَمُهُ وَمَالُهُ وَعِرْضُهُ)) رواه مسلم

((Yatosha kuwa shari mtu kumdharau nduguye Muislamu. Kila Muislamu juu ya Muislamu mwenziwe ni haramu damu yake, mali yake, na heshima yake)) [Muslim]

 

Na pia:

وَعَنْ أَبِي اَلدَّرْدَاءِ رضى الله عنه ‏عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: ((مَنْ رَدَّ عَنْ عِرْضِ أَخِيهِ بِالْغَيْبِ ، رَدَّ اَللَّهُ عَنْ وَجْهِهِ اَلنَّارَ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ)) أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Ad-Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayetetea kuihami heshima ya nduguye kwa siri, Allaah Atauhifadhi uso wake kutokana na moto Siku ya Qiyaamah)). [At-Tirmidhiy Hadiyth Hasan. Ameikusanya Al-Abaaniy katika Swahiyh At-Tirmidhiy (1931), na Swahiyh Al-Jaami’ (6262)]

 

5. Wenye mamlaka watafakari na kukumbuka kwamba mamlaka na hadhi hazishindi za Al-‘Aziyz, kwa hiyo wasiende kabisa kinyume na amri za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wala wasivuke mipaka katika kudhulumu watu kutokana na mamlaka yao.

 

6. Rejea Qur-aan, uisome ukitaka kufaulu duniani na Aakhirah. Tafakari na zingatia maana zake, na kama ilivyotangulia kutajwa kwamba humo kumetajwa mara nyingi Jina la Al-‘Aziyz. Na Qur-aan yenyewe imeitwa Al-‘Aziyz Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بِالذِّكْرِ لَمَّا جَاءَهُمْ ۖ وَإِنَّهُ لَكِتَابٌ عَزِيزٌ ﴿٤١﴾

Hakika wale waliokanusha Ukumbusho ulipowajia (wataangamia). Na hakika hicho ni Kitabu chenye utukufu na udhibiti.

 

لَّا يَأْتِيهِ الْبَاطِلُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَلَا مِنْ خَلْفِهِ ۖ تَنزِيلٌ مِّنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ ﴿٤٢﴾

Hakitokifikia ubatili mbele yake, na wala nyuma yake; ni uteremsho kutoka kwa Mwenye hikmah wa yote, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Fusw-swilat 41: 41-42]

 

7. Miongoni mwa sababu za kupata ‘izzah na kupandishwa daraja ni kusamehe watu na kuwa na unyenyekevu mbele yao.

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا نَقَصَتْ صَدَقَةٌ مِنْ مَالٍ، وَمَا زَادَ اللَّهُ عَبْدًا بِعَفْوٍ إلاَّ عِزًّا ، وَمَا تَوَاضَعَ أَحَدٌ لِلَّهِ إِلاَّ رَفَعَهُ اللَّهُ عَزَّ وَ جَلَّ)) مسلم                               

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Kutoa swadaqah hakupunguzi mali, Allaah Humzidishia mja ‘izzah (utukufu) kwa ajili ya kusamehe kwake.  Na   yeyote anayenyenyekea kwa ajili ya Allaah, Allaah Aliyetukuka Atampandisha Daraja [Atamtukuza])) [Muslim]

 

8.Muombe Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa Jina hili la Al-‘Aziyz. Nyenyekea Kwake na utawakali Kwake kwa kila jambo, na kila shida.

Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba:

للَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمْتُ وَبِكَ آمَنْتُ وَعَلَيْكَ تَوَكَّلْتُ وَإِلَيْكَ أَنَبْتُ وَبِكَ خَاصَمْتُ.  اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِعِزَّتِكَ لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ أَنْ تُضِلَّنِي أَنْتَ الْحَيُّ الَّذِي لاَ يَمُوتُ وَالْجِنُّ وَالإِنْسُ يَمُوتُونَ

Allaahumma Laka aslamtu, wa Bika aamantu, wa ‘Alayka tawakkaltu, wa Ilayka anabtu, wa Bika khaaswamtu. Allaahumma inniy a’uwdhu bi -’izzatika laa ilaaha illa Anta an-tudhwillaniy Antal-Hayyu Alladhiy  laa yamuwtu wal-jinnu wal-insu yamuwtuwna.

Ee Allaah, Kwako najisalimisha na Kwako naamini na Kwako natawakali na Kwako narejea kutubu na Kwako nagombana [dhidi ya adui]. Ee Allaah, hakika mimi najikinga kwa ‘Izzah (Nguvu) Yako, hapana Muabudiwa wa haki ila Wewe Usije kunipotoa Wewe Uliye Hai daima Ambaye Hafi ilhali majini na watu wanakufa[ [Muslim]

 

9. Muombe pia Allaah kwa Jina hili la ‘Aziyz pale unapopata maumivu mwilini kama ilivyothibiti katika Sunnah ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba ufanye ifuatavyo:

Weka mkono wako juu ya sehemu iliyo na maumivu kisha sema mara tatu:

 بِسْمِ اللهِ

BismiLLaah  

Kisha useme mara saba:

أَعُوذُ بِعِزَّةِ اللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَ أُحاذِرُ

A’uwdhu bi ‘Izzati-LLaahi wa-Qudratihi min sharri maa ajidu wa uhaadhiru

 

Najikinga kwa ‘Izzah ya Allaah na kwa uwezo Wake kutokana na shari ya ninachokisikia na ninachokiogopa)). [Muslim, Ibn Maajah na wengineo kwa usimulizi tofauti kidogo]

 

 

Share

020-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-JABBAAR

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْجَبَّار

AL-JABBAAR

 

 

 

Al-Jabbaar:  Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo.

 

Jina hili tukufu la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) limetajwa mara moja katika kauli Yake Ta’aalaa:    

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ  

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha, Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi, Mwenye kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo [Al-Hashr: 59:23]

 

Na sifa hii imetajwa mara tisa katika Qur-aan kuwahusisha wana Aadam mfano:

 

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّ فِيهَا قَوْمًا جَبَّارِينَ وَإِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا حَتَّىٰ يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِن يَخْرُجُوا مِنْهَا فَإِنَّا دَاخِلُونَ ﴿٢٢﴾

22. Wakasema: “Ee Muwsaa! Hakika humo kuna watu majabari; nasi hatutoingia humo mpaka watoke humo; watakapotoka humo; basi hakika sisi tutaingia.” [Al-Maaidah: 22]

 

Na katika kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَتِلْكَ عَادٌ ۖ جَحَدُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ وَعَصَوْا رُسُلَهُ وَاتَّبَعُوا أَمْرَ كُلِّ جَبَّارٍ عَنِيدٍ﴿٥٩﴾

Na hao ni kina ‘Aad. Wamezikanusha kwa ushupavu Aayaat (ishara, hoja) za Rabb wao, na wakawaasi Rusuli Wake, na wakafuata amri ya kila jabari mkaidi. [Huwd 11: 59]

 

وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ ﴿١٣٠﴾

“Na mnapokamata kushambulia mnatumia nguvu kwa uadui na ujabari. [Ash-Shu’araa 26: 130]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Jabbaar Mwenye kuyaendesha mambo yote ya ardhini na mbinguni vile Atakavyo. Huamrisha, Hukataza kwa muktadha wa hekima Zake, na uadilifu na miongoni mwa hayo ni Dini Yake ambayo Amewaridhia nao waja wake.

 

Naye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Mwenye kuunga: Mwenye kurekebisha mambo ya waja Wake, Anafanya yanayowafaa wao, Ambaye huunga ufukara wao, na Akawatosha na sababu za maisha na riziki zao.

 

Al-Jabbaar Ambaye Hashindwi; Ambaye Huunga unyonge wa wanyonge katika waja Wake. Anaunga kilichovunjika. Anamtajirisha fakiri.

 

Humwepesishia mwenye uzito, uzito wake. Huunga kiungo maalumu; nyoyo za waliovunjika kwa ajili Yake, wenye kunyenyekea kwa utukufu na ukubwa Wake.

 

Huziunga nyoyo za waliokandamizwa kutokana na ambao waliojifanya majabari, kama Alivyounga moyo wa mama yake Nabiy Muwsaa ('Alayhis Salaam) baada ya kumtupa mwanawe katika mto wa Nile, akiwa kwenye sanduku, kisha mwanawe huyo akafika katika mikono ya Fir‘awn ambaye katika kipindi hicho alikuwa akiua kila mtoto aliyezaliwa.

Moyo wa mama yake Nabiy Muwsaa ('Alayhis Salaam) ukwa umejaa khofu na wahka lakini Allaah; Al-Jabbaar Aliuthibitisha akaweza kuvumilia. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَقَالَتِ امْرَأَتُ فِرْعَوْنَ قُرَّتُ عَيْنٍ لِّي وَلَكَ ۖ لَا تَقْتُلُوهُ عَسَىٰ أَن يَنفَعَنَا أَوْ نَتَّخِذَهُ وَلَدًا وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿٩﴾

9. Na mke wa Fir’awn akasema: “Kiburudisho cha macho kwangu na kwako; usimuue, asaa akatufaa, au tumfanye mwana.” Nao hawatambui.

 

وَأَصْبَحَ فُؤَادُ أُمِّ مُوسَىٰ فَارِغًا ۖ إِن كَادَتْ لَتُبْدِي بِهِ لَوْلَا أَن رَّبَطْنَا عَلَىٰ قَلْبِهَا لِتَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١٠﴾

10. Na ukawa moyo uliojaa hisia wa mama yake Muwsaa mtupu! Alikaribia kumdhihirisha (kuwa ni mwanawe) lau kama Tusingeutia nguvu moyo wake ili awe miongoni mwa Waumini.  [Al-Qaswasw: 9-10]

 

Huunga nyoyo za wapendanao kwa kuwamwagia anuai za ukarimu Wake, na aina mbali mbali za elimu, na hali mbali mbali za iymaan na uongofu na tawfiyq.

 

Humuunga mgonjwa, aliyepatwa na mitihani, aliyedhoofu kiwiliwili na hivyo hurahisisha sababu zote za ponyo kwake.  

 

Humuunga aliyepatwa na matatizo kwa tawfiyq Yake kwa subira na utulivu, na humpa badala ya malipo makubwa, pindi atakaposimamia majukumu yake.

 

Humuunga mja wake Muumini, kwa kustawisha hali zake, na malengo yake, pindi anapoomba muombaji kwa kusema: “Allahumma-Jburniy” kwani hapa anahitaji kuungwa ambayo hakika yake ni kumstawisha na kuondosha yote yenye kuchukiza. [Tafsiyr Al-Qurtwubiy (9/301)

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Jabbaar; Ni kizuizi kisichofikiwa, hafikiwi wala hawezi kuingiwa na chukizo juu Yake, Haiwapati waja Wake dhara na yeye akadhurika na wala haiwapati manufaa wakanufaika.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Jabbaar: Anapotaka kitu huwa kama Anavyotaka, wala hazuiwi na yeyote, wala hakiendi kinyume chake na hivyo basi matendo yake huwa kama kulazimisha.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Jabbaar: Ni Mkubwa Mwenye kutakabari: Ambaye hakuna mwenye kujiona ana haki zaidi yake.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Jabbaar: Mwenye kutenza nguvu kila kitu, Ambaye kila kitu kinamkurubia, na kila kitu kinanyenyekea Kwake, Ulimwengu wa juu na wa chini, pamoja ya yaliyomo miongoni mwa waja Wake watukufu, kila kimoja kimenyenyekea katika harakati zake, na utulivu wake na yanayokuja na yanayobaki kwa mmiliki wake na mpangaji wake, hana lolote katika amri yake wala katika hukumu zake chochote bali mambo yote ni kutoka kwa Allaah.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Al-Jabbaar Ambaye moto wa Jahannam unarejea Kwake kwa upungufu wake, kwa muradi wake wa kutoshelezwa.  Na pia Atauamrisha uwaingize wanaotakabari na wanaojifanya majabari. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:  

 

يَوْمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ امْتَلَأْتِ وَتَقُولُ هَلْ مِن مَّزِيدٍ ﴿٣٠﴾

30. “Siku Tutakapoiambia Jahannam: “Je, umeshajaa?” Nayo itasema: “Je, kuna ziada yoyote?”  [Qaaf 50:30]  

 

Na katika Hadiyth ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) 

 

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، رضى الله عنه قَالَ قَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم: ((تَحَاجَّتِ الْجَنَّةُ وَالنَّارُ فَقَالَتِ النَّارُ أُوثِرْتُ بِالْمُتَكَبِّرِينَ وَالْمُتَجَبِّرِينَ‏.‏ وَقَالَتِ الْجَنَّةُ مَا لِي لاَ يَدْخُلُنِي إِلاَّ ضُعَفَاءُ النَّاسِ وَسَقَطُهُمْ‏.‏ قَالَ اللَّهُ تَبَارَكَ وَتَعَالَى لِلْجَنَّةِ:  أَنْتِ رَحْمَتِي أَرْحَمُ بِكِ مَنْ أَشَاءُ مِنْ عِبَادِي ‏.‏ وَقَالَ لِلنَّارِ إِنَّمَا أَنْتِ عَذَابٌ أُعَذِّبُ بِكِ مَنْ أَشَاءُ مِنْ عِبَادِي‏.‏ وَلِكُلِّ وَاحِدَةٍ مِنْهُمَا مِلْؤُهَا، فَأَمَّا النَّارُ فَلاَ تَمْتَلِئُ حَتَّى يَضَعَ رِجْلَهُ فَتَقُولُ قَطٍ قَطٍ قَطٍ‏.‏ فَهُنَالِكَ تَمْتَلِئُ وَيُزْوَى بَعْضُهَا إِلَى بَعْضٍ، وَلاَ يَظْلِمُ اللَّهُ ـ عَزَّ وَجَلَّ ـ مِنْ خَلْقِهِ أَحَدًا، وَأَمَّا الْجَنَّةُ فَإِنَّ اللَّهَ عَزَّ وَجَلَّ يُنْشِئُ لَهَا خَلْقًا))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Jannah na moto ulibishana; moto ukasema: “Nimefadhilishwa kupokea wenye kutakabari na majabari.” Jannah ikasema: “Nina nini! Mbona hakuna anayeingia kwangu isipokuwa watu dhaifu na dhalili?” Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Akasema kuiambia Jannah: “Wewe ni rahmah Yangu, ambayo Namrehemu kwako nimtakaye katika waja wangu.” Na Akauambia moto: “Hakika wewe ni adhabu Ninayomuadhibu kwako nitamtakaye katika waja Wangu.” Na kila mmoja miongoni mwao watajaa. Ama moto, hautojaa mpaka Allaah Aweke Mguu Wake kisha utasema: “Qatw! Qatw! Qatw!” Hapo ndio utajaa, na sehemu zake mbalimbali zitakaribiana na Allaah (‘Azza wa Jalla) Hatodhulumu yeyote katika viumbe Vyake. Ama Jannah basi Allaah (‘Azza wa Jalla) Ataumba umbile jipya kuijazia)) [Al-Bukhaariy Kitaab At-Tafsiyr]

 

Katika riwaayah nyingine:

حتى يَضَع الجبَّار فيها قَدمَه

((Hadi Al-Jabbaar Atakapoweka mguu wake humo)) [Imepokewa na Ad-Daaraqutwniy katika Swifaat 15]

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah, Al-Jabbaar:

 

1. Usijfanye jabari kwa wenzako, bali kumbuka kwamba wewe ni mja wa Al-Jabbaar Ambaye Anakutosheleza kuuvunja ujabari wako. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

كَذَٰلِكَ يَطْبَعُ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ قَلْبِ مُتَكَبِّرٍ جَبَّارٍ ﴿٣٥﴾

Hivyo ndivyo Allaah Anavyopiga chapa juu ya kila moyo wa mwenye kutakabari, jabari. [Ghaafir 40: 35]

 

2. Tafakari jinsi Al-Jabbaar Anavyokulazimishia mambo katika uhai wako; kuanzia mwili wako na jinsi viungo ndani yake kama moyo, maini, matumbo, damu inavyotembea, chakula kusagika, bongo kufanya kazi, usingizi wako na kuamka kwako na kadhaalika jinsi Anavyoviendesha bila ya uwezo wako. Kutafakari kwako haya yatakuzishia iymaan kumjua Al-Jabbaar na kuzidi kumtukuza.

 

3. Unga nyoyo za nduguzo kwa kuwasamehe makosa yao kwako, na kuwasaidia kwa uwezo wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wenye kuhitaji msaada wako, ili Al-Jabbaar Akuunge nawe pindi utakapopatwa na shida.

 

4. Muombe Al-Jabbaar  kwa du’aa za Sunnah  kama ifuatavyo:

 

Unaporukuu na kusujudu kusema:

 

سُبْـحانَ ذي الْجَبَـروت، والمَلَـكوت، وَالكِبْـرِياء، وَالْعَظَـمَه

Subhaana dhil-Jabaruwti wal-malakuwti, wal-kibriyaai, wal-‘adhwamah

Ametakasika Mwenye Ujabari (Utawala, Utukufu), na Ufalme, na Ukubwa, na Uadhama. [Hadiyth ya ‘Awf bin Maalik Al-Ashja’iyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) - [Abuu Daawuwd (1/230), Ahmad (6/24), An-Nasaaiy (2/191) na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (1/166)]

 

Na baina ya sijda mbili:

 

 اللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي، وَارْحَمْـني، وَاهْدِنـي، وَاجْبُرْنـي، وَعافِنـي وَارْزُقْنـي وَارْفَعْـني

Allaahummaghfir-liy, warhamniy, wahdiniy, wajburniy, wa ’aafiniy, warzuqniy, warfa’-niy

Ee Allaah nighufurie, na unirehemu, na uniongoze, na uniungie, na unipe afya, na uniruzuku na uniinue. [Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) - Aswhaab As-Sunan isipokuwa An-Nasaaiy; Abuu Daawuwd (850), At-Tirmdihiy (284), Ibn Maajah (898),  na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/90) na Swahiyh Ibn Maajah (1/148)]

 

 

 

Share

021-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-MUTAKABBIR

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْمُتَكَبِّر

AL-MUTAKABBIR

 

 

 

Al-Mutakabbir:  Mkubwa, Aliye na nguvu dhidi ya kila shari, uovu na dhulma.

 

 

Al-Mutakabbir imetajwa katika Qur-aan mara moja kwenye kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ الْمَلِكُ الْقُدُّوسُ السَّلَامُ الْمُؤْمِنُ الْمُهَيْمِنُ الْعَزِيزُ الْجَبَّارُ الْمُتَكَبِّرُ ۚ سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٢٣﴾

Yeye Ndiye Allaah Ambaye hakuna Muabudiwa wa haki ila Yeye, Mfalme, Mtakatifu Ametakasika na sifa zote hasi, Mwenye kusalimisha, Amesalimika na kasoro zote, Mwenye kusadikisha ahadi, Mwenye kuaminisha, Mwenye kudhibiti, kushuhudia, kuchunga na kuhifadhi, Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Jabari, Asiyeshindwa kufanya Atakalo, Mkubwa na adhama, Subhaana Allaah! Utakasifu ni wa Allaah kutokana na ambayo wanamshirikisha. [Al-Hashr: 59:23]

 

Al-Mutakabbir: Mtukufu mno, Mwenye hadhi, fakhari, shani, ukubwa, Aliye na nguvu kubwa za kuwatenza nguvu viumbe Wake waasi, Yuko juu ya viumbe.

 

Al-Mutakabbir: Mwenye kustahiki kutakabari  nayo ni utukufu, hadhi ya juu, na Al-Kibriyaa kwa maana: Ufalme, hadhi, fakhari, shani, ukubwa.

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuhusu Fir’awn:

 

قَالُوا أَجِئْتَنَا لِتَلْفِتَنَا عَمَّا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا وَتَكُونَ لَكُمَا الْكِبْرِيَاءُ فِي الْأَرْضِ وَمَا نَحْنُ لَكُمَا بِمُؤْمِنِينَ ﴿٧٨﴾

Wakasema: “Je, umetujia ili utugeuze kutokana na yale tuliyowakuta nayo baba zetu, na ili muwe na ukubwa na adhama katika ardhi? Na sisi hatutawaamini nyinyi.”  [Yuwnus 10: 78]

 

Yaani Ufalme. [Imethibiti kutoka kwa Mujaahid ‘At-Tafsiyr Asw-Swahiyh’ (3/30)]

 

Pia ina maana ni ukubwa na uadhama na uongozi. [Tafsiyr Ibn Kathiyr]

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْكَبِيرُ الْمُتَعَالِ ﴿٩﴾

Mjuzi wa ghayb na dhahiri, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa, Mwenye Uluwa Aliyejitukuza kabisa. [Ar-Ra’d 13: 9]

 

Allaah (Tabaaraka wa Ta’aalaa) Ana maana zote za utukufu nazo ni ukamilifu katika Jina Lake la Al-Mutakabbir Ambalo ni Lake Pekee. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَهُ الْكِبْرِيَاءُ فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٣٧﴾

Na Ukubwa, Uadhama, Ujalali ni Wake Pekee mbinguni na ardhini; Naye Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote. [Al-Jaathiyah 45: 37]

  

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakabbir: Ndiye Mkubwa na Ametukuka katika dhati Yake na Sifa Zake, matendo Yake, ufalme Wake, na kila kitu chini Yake ni kidogo na dhalili.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakabbir: Mwenye kujiadhimisha, Ambaye Nafsi Yake iko juu ya utukuzwaji wa chochote; hana mfanowe.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakabbir: Ufalme Wake hauondoki, mwenye kudumu milele:  

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakaabir: Naye ni Mwenye kutakabari na dhulma za waja Wake, Hamdhulumu yeyote katika waja Wake, hata kama mwenye kumkufuru.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakaabir: Yeye Ndiye Mwenye kuwashinda wanaojifanya ni majabari katika Waja wake na Anaahidi kuwaadhibu kutokana na kutakabari kwao: Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَيَوْمَ يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَذْهَبْتُمْ طَيِّبَاتِكُمْ فِي حَيَاتِكُمُ الدُّنْيَا وَاسْتَمْتَعْتُم بِهَا فَالْيَوْمَ تُجْزَوْنَ عَذَابَ الْهُونِ بِمَا كُنتُمْ تَسْتَكْبِرُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ وَبِمَا كُنتُمْ تَفْسُقُونَ ﴿٢٠﴾

Na siku watakayotandazwa wale waliokufuru kwenye moto (waambiwe): “Je, mshamaliza vizuri vyenu katika uhai wenu wa dunia na mshajistarehesha navyo? Basi leo mtalipwa adhabu ya udhalilifu kwa yale mliyokuwa mkitakabari katika ardhi bila ya haki na kwa sababu mlikuwa mnafanya ufasiki.” [Al-Ahqaaf 46: 20]

 

Na Anasema pia:

 

وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ تَرَى الَّذِينَ كَذَبُوا عَلَى اللَّـهِ وُجُوهُهُم مُّسْوَدَّةٌ ۚ أَلَيْسَ فِي جَهَنَّمَ مَثْوًى لِّلْمُتَكَبِّرِينَ﴿٦٠﴾

Na Siku ya Qiyaamah utawaona wale waliomsingizia uongo Allaah, nyuso zao zimesawajika. Je, kwani si katika Jahannam ndio makazi kwa ajili ya wanaotakabari?  [Az-Zumar 389: 60]

 

Yeye ni Al-Mutakabbir kwa kila upungufu na kila aibu, Ameepukana na kila ovu na kila kisichokuwa stahiki ya utukufu Wake.

 

Al-Mutakabbir: Ni Mtukufu Mwenye kupitisha mambo Yake kwa waja Wake, hakipiti katika ufalme Wake ila tu Anachokitaka.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakaabir kwa kila ovu hakitoki Kwake isipokuwa ni khayr tupu.

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakabbir: Yuko juu ya waja Wake, kwa kila aina ya kuwa juu: Katika dhati Yake na katika Sifa Yake.

 

Al-Kibriyaa (Ukubwa, utukufu, uadhama, ujalali) wa Allaah hauna mwisho, Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِهِ عِلْمًا ﴿١١٠﴾

Anajua yale yaliyoko mbele yao, na yale yaliyoko nyuma yao, na wala hawawezi kufikia kuelewa chochote cha ujuzi Wake. [Twaahaa 20: 110]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakabbir: Mwenye kutakabari katika Uola Wake (Ar-Rubuwbiyyah), Hana mshirika katika ufalme Wake, Mwenye kutakabari katika kuabudiwa Kwake (Uluwhiyyah); Hakubali Aabudiwe asiyekuwa Yeye. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ ﴿٣٣﴾

Basi hakika wao Siku hiyo katika adhabu ni wenye kushirikiana.

 

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ ﴿٣٤﴾

Hakika hivyo ndivyo Tuwafanyavo wakhalifu.

 

إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ يَسْتَكْبِرُونَ ﴿٣٥﴾

Hakika wao walipokuwa wakiambiwa: “Laa ilaaha illa Allaah”, Hapana Muabudiwa wa haki ila Allaah, hutakabari. [Asw-Swaaffaat 37: 33-35]

 

Na pia Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika Hadiyth Al-Qudsiy:

 

عنْ ابي هريرة رضي الله عنه أنَّه صلَّى الله عليه وسلَّم قال: ((قال الله تعالى: أنا أغْنى الشُّركاء عن الشِّرْك، فمَن عمل عملاً أشْرَك فيه معي غيري تركتُه وشِرْكه))    

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam amesema: ((Allaah Ta’aalaa Anasema: "Mimi Ni Mwenye kujitosheleza kabisa, Sihitaji msaada wala mshirika. Kwa hiyo, yule afanyaye amali kwa kunishirikisha na mtu, Nitaikanusha pamoja na mshirika wake.”  Yaani: hatopata ujira wowote kwa amali hiyo. [Muslim (2985), Ibn Maajah (4202)]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni Al-Mutakabbir: Yeye ni Mwenye kustahiki kiburi chote na utukufu wote kutoka kwa waja Wake.

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Mutakabbir:

 

1. Mtukuze Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kumkabbir (Allaahu Akbar!) Muadhimishe kwa kila taadhima na ujalali. Kumbuka kwamba Yeye Ndiye Al-Mutakabbir, Mwenye ukubwa na uadhama, na Mwenye kustahiki kutakabari. Anasema katika Hadiyth Al-Qudsiy:

 

أنا الجبَّارُ أنا المُتكبِّرُ أنا الملِكُ أنا العزيزُ أنا الكريمُ

((Mimi ni Al-Jabbaar, Mimi ni Al-Mutakabbir, (Mwenye ukubwa na utukufu) Mimi ni Al-Maalik (Mfalme), Mimi ni Al-’Aziyz (Mwenye Enzi ya nguvu Asiyeshindika), Mimi ni Al-Kariym (Mkarimu, Mtukufu)) [Swahiyh Ibn Hibbaan (7327) na Taz. As-Silsilah Asw-Swahiyhah (7/596)]  

 

2. Kutakabari kulikuwa ni maasi ya kwanza yaliyotendwa na Ibliys laana ya Allaah iwe juu yake alipokataa kutii amri ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama ilivyokuja katika Qur-aan:

وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ ﴿٣٤﴾

Na pale Tulipowaambia Malaika: “Msujudieni Aadam.” Wakasujudu isipokuwa Ibliys alikataa na akatakabari na akawa miongoni mwa makafiri. [Al-Baqarah 2: 34]

 

Kwa hiyo tahadhari Muislamu usije kupinga amri za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ukawa miongoni mwa wanaotakabari.

 

3. Tahadhari pia kutokupinga haki na kujiepusha na sifa hiyo ya kutakabari kwa sababu kutakabari ni sababu mojawapo ya kupigwa chapa katika nyoyo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

الَّذِينَ يُجَادِلُونَ فِي آيَاتِ اللَّـهِ بِغَيْرِ سُلْطَانٍ أَتَاهُمْ ۖ كَبُرَ مَقْتًا عِندَ اللَّـهِ وَعِندَ الَّذِينَ آمَنُوا ۚ كَذَٰلِكَ يَطْبَعُ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ قَلْبِ مُتَكَبِّرٍ جَبَّارٍ ﴿٣٥﴾

Wale wanaobishana kuhusu Aayaat za Allaah bila ya hoja yoyote kuwafikia, ni chukizo kubwa mno mbele ya Allaah na mbele ya wale walioamini. Hivyo ndivyo Allaah Anavyopiga chapa juu ya kila moyo wa mwenye kutakabari, jabari.  [Ghaafir 40: 35]

 

4. Ukitaka ukubwa, basi jifanye  mnyenyekevu na dhalili mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na mbele ya watu kwani hivyo ndio sababu ya kupandishwa daraja:

 

((وَمَا تَوَاضَعَ أَحَدٌ لِلَّهِ إِلاَّ رَفَعَهُ اللَّهُ عَزَّ وَ جَلَّ)) مسلم

Na yeyote hanyenyekei kwa ajili ya Allaah isipokuwa, Allaah  (‘Azza wa Jalla) Atampandisha Daraja [Atamtukuza])) [Muslim]

 

5. Jiepushe na kibri hata iwe ndogo vipi kwa sababu kuwa na kibri ni kuharamika kuingia Jannah!

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَدْخُلُ الْجَنَّةَ مَنْ كَانَ فِي قَلْبِهِ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ مِنْ كِبْر)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Hatoingia Jannah ambaye moyoni mwake mna kiburi uzito wa chembe (au sisimizi)). [Muslim]

 

6. Usidharau wenzako kwa vyovyote vile kwani wanaweza wao kuwa ni bora mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuliko wewe hata kama una sifa nzuri zaidi ya wenzako; ikiwa ni wingi wa mali, au uzuri wa sura au mwili, au ubora wa kabila au cheo kikubwa, au ‘ilmu zaidi, au umaarufu na kadhaalika. Anatahadharisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ  

Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao.  [Al-Hujuraat 49: 11]

 

7. Muombe Al-Mutakabbir Akuondoshee sifa mbaya ya kutakabari na kuwa na kiburi. Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam) Alimuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَقَالَ مُوسَىٰ إِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُم مِّن كُلِّ مُتَكَبِّرٍ لَّا يُؤْمِنُ بِيَوْمِ الْحِسَابِ ﴿٢٧﴾

Na Muwsaa akasema: “Hakika mimi najikinga kwa Rabb wangu na Rabb wenu, kutokana na kila mwenye kutakabari asiyeamini Siku ya Hesabu.” [Ghaafir 40: 27]

 

 

 

Share

022-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-KHAALIQ, AL-KHALLAAQ

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْخالِقُ-الْخَلاَّق

 

AL-KHAALIQ

AL-KHALLAAQ

 

 

 

Al-Khaaliq: Muumbaji.

 

Al-Khallaaq: Mwingi wa kuumba Atakavyo

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ  

Yeye Ndiye Allaah, Muumbaji, Mwanzishi viumbe bila kasoro, Muundaji sura na umbile. [Al-Hashr: 24]

 

Al-Khaaliq au Al-Khallaaq maana yake ni kukiunda kitu kisichokuwa na mfano wake hapo kabla. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ ثُمَّ جَعَلَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَأَنزَلَ لَكُم مِّنَ الْأَنْعَامِ ثَمَانِيَةَ أَزْوَاجٍ ۚ يَخْلُقُكُمْ فِي بُطُونِ أُمَّهَاتِكُمْ خَلْقًا مِّن بَعْدِ خَلْقٍ فِي ظُلُمَاتٍ ثَلَاثٍ ۚ  

Amekuumbeni kutokana na nafsi moja, kisha Akamfanya humo mkewe na Akakuteremshieni katika wanyama wa mifugo jozi nane. Anakuumbeni matumboni mwa mama zenu umbo baada ya umbo, katika viza vitatu.  [Az-Zumar: 6]

 

Yaani; Amekuumbeni tone, kisha kipande cha nyama, kisha mfupa kama Anavyosema pia:

وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن سُلَالَةٍ مِّن طِينٍ ﴿١٢﴾

Kwa yakini Tumemuumba insani kutokana na mchujo safi wa udongo.

 

ثُمَّ جَعَلْنَاهُ نُطْفَةً فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ ﴿١٣﴾

Kisha Tukamjaalia kuwa tone la manii katika kalio makini.

 

ثُمَّ خَلَقْنَا النُّطْفَةَ عَلَقَةً فَخَلَقْنَا الْعَلَقَةَ مُضْغَةً فَخَلَقْنَا الْمُضْغَةَ عِظَامًا فَكَسَوْنَا الْعِظَامَ لَحْمًا ثُمَّ أَنشَأْنَاهُ خَلْقًا آخَرَ ۚ فَتَبَارَكَ اللَّـهُ أَحْسَنُ الْخَالِقِينَ ﴿١٤﴾

Kisha Tukaumba tone la manii kuwa pande la damu linaloning’inia, Tukaumba pande la damu hilo linaloning’inia kuwa kinofu cha nyama, Tukaumba kinofu cha nyama hiyo kuwa mifupa, Tukavisha mifupa hiyo nyama, kisha Tukamuanzisha kiumbe kingine. Basi Tabaaraka-Allaah, Amebarikika Allaah Mbora wa wenye kuumba. [Al-Muuminuwn: 12-14]

 

 

Na maana ya pili ni kukikadiria kitu na kukinyoosha. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَوْثَانًا وَتَخْلُقُونَ إِفْكًا ۚ  

“Hakika mnaabudu badala ya Allaah masanamu, na mnaunda uzushi. [Al-‘Ankabuwt: 17]

 

 

Yaani mnakadiria na kutayarisha, nayo ni uongo, kama ilivyo kauli yake Ta’aalaa:

مَا سَمِعْنَا بِهَـٰذَا فِي الْمِلَّةِ الْآخِرَةِ إِنْ هَـٰذَا إِلَّا اخْتِلَاقٌ ﴿٧﴾

“Hatukusikia haya katika mila ya mwisho, haya si chochote isipokuwa ni jambo lilozushwa tu.  [Swaad: 7]

 

 

Tofauti kati ya Al-Khaaliq na Al-Khallaaq:

 

Al-Khaaliq ni Ambaye Anakiunda kitu ambacho hakikuwepo.

 

Al-Khallaaq ni Ambaye Anayeumba  kwa kwingi zaidi,  na uumbaji Wake wa  aina mbali mbali. Anaumba Atakavyo, Apendavyo Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ ﴿٨٦﴾

Hakika Rabb wako Ndiye Mwingi wa kuumba Atakavyo, Mjuzi wa yote. [Al-Hijr: 86]

 

  يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ ۚ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ﴿١٧﴾

Anaumba Atakacho. Na Allaah juu ya kila kitu ni Muweza. [Al-Maaidah: 17]

Na Anasema pia:

 

ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ ۖ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ خَالِقُ كُلِّ شَيْءٍ فَاعْبُدُوهُ ۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ وَكِيلٌ ﴿١٠٢﴾

Huyo kwenu Ndiye Allaah, Rabb wenu. Hapana muabudiwa wa haki ila Yeye Muumbaji wa kila kitu, basi mwabuduni Yeye Pekee. Naye juu ya kila kitu ni Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.  [Al-An’aam: 102]

 

 

Al-Khaaliq Anathibitisha Mwenyewe (‘Azza wa Jalla) Tawhiyd ya Ar-Rubuwbiyyah, kwamba Yeye Ndiye Muumbaji, basi je, wale mapagani (Wanaokanusha kuweko kwa Allaah, Al-Khaaliq) wanalo la kujibu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaposema?

أَمْ خُلِقُوا مِنْ غَيْرِ شَيْءٍ أَمْ هُمُ الْخَالِقُونَ ﴿٣٥﴾

Au wameumbwa pasipo na kitu chochote au wao ndio waumbaji?

 

أَمْ خَلَقُوا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ ۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ ﴿٣٦﴾

Au wameumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini. [Atw-Tuwr: 35-36]

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Khaaliq, Al-Khallaaq:

 

1. Tafakari uumbaji wa Allaah na jinsi uumbaji Wake ulivyokuwa hauna kasoro. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

الَّذِي خَلَقَ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا ۖ مَّا تَرَىٰ فِي خَلْقِ الرَّحْمَـٰنِ مِن تَفَاوُتٍ ۖ فَارْجِعِ الْبَصَرَ هَلْ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ﴿٣﴾

Ambaye Ameumba mbingu saba matabaka, hutoona katika uumbaji wa Ar-Rahmaan tofauti yoyote. Basi rejesha jicho je, unaona mpasuko wowote ule?

 

ثُمَّ ارْجِعِ الْبَصَرَ كَرَّتَيْنِ يَنقَلِبْ إِلَيْكَ الْبَصَرُ خَاسِئًا وَهُوَ حَسِيرٌ ﴿٤﴾

Kisha rejesha jicho tena na tena litakupindukia jicho likiwa limehizika na lenye kunyong’onyezwa.  [Al-Mulk 3-4]

 

 

2. Kuwa miongoni mwa wenye kumshukuru na kumwabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kutafakari uumbaji Wake. Hii ni aina ya ‘ibaadah iliyo nzito kwa thawabu mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na  ambayo ni dalili ya kuamini Tawhiyd ya Rubuwbiyyah, na kwamba Allaah (‘Azza wa Jalla) Hakuumba Alivyoviumba kuwa ni bure bila ya lengo! Ametaja Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) hayo katika Suwrah na Aayah kadhaa, miongoni mwazo ni Aayah za mwisho katika Suwratul-‘Imraan ambazo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliamka usiku mmoja akaswali tahajjud kisha akalia mpaka ndevu zake zikarowa, kisha akasujudu na kulia mpaka akaifanya ardhi irowe, kisha akalala kwa upande wa kulia mpaka akaja Bilaal, akamuuliza: “Ee Rasuli wa Allaah  jambo gani linakuliza na hali Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amekwishakufutia madhambi yako yaliyotangulia na yanayokuja?” Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Je, nisiwe mja anayeshukuru? Nimeteremshiwa Aayah… Ole wake, yule anayezisoma lakini hazitafakari…

 

إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠﴾ 

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na mabadiliko ya mfuatano wa usiku na mchana; bila shaka ni Aayaat kwa wenye akili.

 

الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٩١﴾ 

Ambao wanamdhukuru Allaah kwa kusimama, na kwa kukaa na kwa kulala ubavuni mwao na wanatafakari katika kuumbwa mbingu na ardhi (wakisema): “Rabb wetu, Hukuumba haya bure, Subhaanak! Utakasifu ni Wako, tukinge na adhabu ya moto

[Aal-‘Imraan: 190 – mpaka 199 – Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa - Taz. As-Silsilah Asw-Swahiyhah (1/147), Swahiyh At-Targhiyb (1468)]

 

3. Tafakari uumbaji wa Al-Khallaaq Anayeumba Atakavyo; tafakari kwanza viumbe wasioonekana kwetu kama Malaika na majini. Kisha tafakari uumbaji wa wana Aadam jinsi tunavyotofautiana umbo, rangi na wingi wetu ulimwenguni. Kisha tafakari  viumbe vingapi vipya vipya vinagundulikana? Tafakari aina za wanyama wa nchi kavu unapoishi na mbali walioko katika majangwa na misitu ya ulimwengu mzima! Mfano mzuri mwengine wa kutafakari ni pale mpiga mbizi baharini anapokutana huko na aina mbali mbali za samaki wa kila rangi na kila maumbile. Pia angalia mabilioni yaliyoumbwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa aina mbali mbali na sura za kila aina katika wanyama, wadudu, ndege, samaki, miti, na viumbe vinginevyo tusivyoviona au kuvijua, lakini Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anavijua vilivyo kwani Anasema:

أَلَا يَعْلَمُ مَنْ خَلَقَ وَهُوَ اللَّطِيفُ الْخَبِيرُ﴿١٤﴾

Kwani Hajui Yule Aliyeumba! Na hali Yeye ni Mwenye kudabiri mambo kwa ulatifu, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika. [Al-Mulk 14]

 

4. Weka Iymaan thabiti moyoni kuhusu Tawhiyd ya Allaah na kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Hafanani na kiumbe chochote na wala Yeye Hakuumbwa. Basi tahadhari na shaytwaan asikutie wasiwasi kuhusu hilo, imetahadharishwa katika Hadiyth:

 

عن أبي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((يَأْتِي الشَّيْطَانُ أَحَدَكُمْ فَيَقُولُ: مَنْ خَلَقَ كَذَا، مَنْ خَلَقَ كَذَا، حَتَّى يَقُولَ: مَنْ خَلَقَ رَبَّكَ، فَإِذَا بَلَغَهُ فَلْيَسْتَعِذْ بِاللَّهِ، وَلْيَنْتَهِ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Shaytwaan humjia mmoja wenu aseme: “Nani ameumba kadhaa, nani ameumba kadhaa, mpaka mwisho husema: Nani amemuumba Rabb wako? Basi itakapofika hivyo, ajikinge kwa Allaah na aachilie mbali [mawazo hayo])) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

5. Mshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kukuumba ukiwa umekamilika viungo na uvitolee swadaqah kwa kuswali rakaa mbili za Adhw-Dhwuhaa.

 

عن أبي ذَرٍّ رضي الله ُ عنه، عن النـَبي ِّ صلـَّى الله عليه وسلم قال: ((يـُصـْبـِحُ عـَلى كـُلِّ سـُلامى مـِنْ أحـَدِكـُمْ صـَدَقةُ: فـَكُل تـَسْبـِيحـَةِ صـَدَقةٌ، وَ كُل تـَحمِيدة صـَدَقةٌ، وكُلُ تـَهْـليْلةٌ صـَدَقـَةٌ، وكُلُّ تـَكْبِيْرةِ صـَدقةٌ، وأمرٌ بالمـَعرُوف صـَدقةٌ، ونـَهىٌ عـَنِ المـُنْكرِ صـَدقةٌ ويـُجْزئ مـِنْ ذلكَ رَكـْعتـَانِ يـَركَعُهُما مـنَ الضـُّحى)) رواه مسلم

 

Kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allahu ‘alayhi wa alihi wa sallam) amesema: ((Kila kiungo katika mwili wenu hupambaukiwa kikihitaji kutolewa swadaqah, kwa hiyo kila tasbiyh - Subhaana-Allaah ni swadaqah, na kila tahmiyd - AlhamduliLLaah ni swadaqah, na kila tahliyl - La Ilaaha Illa Allaah ni swadaqa  na kila takbiyr - Allaahu Akbar ni swadaqah, na kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza maovu ni swadaqah na itamtosheleza (mtu) kwa rakaa mbili za Dhwuhaa)) [Muslim]

 

6. Msabbih Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kila mara kwani ni haki Yake kumsabbih kwa kuwa Ndiye Aliyetuumba. Anasema:

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى ﴿١﴾

Sabbih Jina la Rabb wako Mwenye ‘Uluwa Ametukuka kabisa kuliko vyote.

 

الَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ ﴿٢﴾

Ambaye Ameumba (kila kitu) kisha Akasawazisha. [Al-A’laa: 1-2]

 

7. Usijfanye wewe muumbaji, nayo ni kuchora viumbe, au kutundika picha za viumbe, kwa sababu ukifanya hivyo utakuwa miongoni mwa watu waovu kabisa Siku ya Qiyaamah na adhabu zake ni kali mno!

 

عَنْ عَائِشَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) قَال: ((أَشَدُّ النَّاسِ عَذَابًا يَوْمَ القِيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهِئُونَ بِخَلْقِ اللَّهِ))

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Watakaokuwa na adhabu kali Siku ya Qiyaamah ni wanaomuiga Allaah katika uumbaji Wake)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما): سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((كُلُّ مُصَوِّرٍ فِي النَّارِ يُجْعَلُ لَهُ بِكُلِّ صُورَةٍ صَوَّرَهَا نَفْسٌ يُعَذَّبُ بِهَا فِي جَهَنَّمَ))

Imepokelewa  kutoka kwa Ibn ‘Abbaas  (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Kila mchoraji picha atakuwa motoni. Kila picha aliyoichora, itatiwa roho nayo itamuadhibu katika Jahannam)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

8. Tafakari kuwa tunaomba du’aa zinazotaja uumbaji katika nyiradi za kulala na asubuhi na jioni. Tunapolala tunatakiwa tuombe:

 

اللّهُـمَّ إِنَّـكَ خَلَـقْتَ نَفْسـي وَأَنْـتَ تَوَفّـاهـا لَكَ ممَـاتـها وَمَحْـياها، إِنْ أَحْيَيْـتَها فاحْفَظْـها، وَإِنْ أَمَتَّـها فَاغْفِـرْ لَـها. اللّهُـمَّ إِنَّـي أَسْـأَلُـكَ العـافِـيَة

Allaahumma Innaka Khalaqta nafsiy wa Anta Tawaffahaa. Laka mamaatuhaa wamahyaahaa. In-Ahyaytahaa fahfadhw-haa wain amattahaa faghfir lahaa. Allaahumma inniy as-alukal ‘aafiyah.

 

Ee Allaah, hakika Wewe Umeiumba nafsi yangu Nawe Utaifisha. Ni Wewe Unaumiliki umauti wake na uhai wake. Ukiipa uhai basi Ihifadhi, na Ukiifisha basi Ighufurie. Ee Allaah, hakika mimi nakuomba Al-‘Aafiyah

[Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar  (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) - Muslim (4/2083) [2712], na Ahmad kwa tamshi lake (2/79)]

 

Al-‘Aafiyah ni neno linalojumuisha  Allaah (عزّ وجلّ)  kumjaalia mja Wake salama na kumpa amani, na kumlinda na maradhi, balaa, majanga, madhara, misukosuko, na kila aina za shari za wanaadam na majini na kubakia salama katika Dini yake na Aakhirah yake.

 

 

9. Tafakari kuwa baadhi ya viumbe Alivyoviumba Allaah (’Azza wa Jalla) ni viumbe vyenye shari na hivyo tunaomba kujikinga navyo tunaposoma:

 

قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ الْفَلَقِ ﴿١﴾

Sema: “Najikinga na Rabb wa mapambazuko.

 

مِن شَرِّ مَا خَلَقَ ﴿٢﴾

Kutokana na shari ya Alivyoviumba.  [Al-Falaq: 1-2]

 

 

Na pia du’aa katika nyiradi za asubuhi na jioni:

 

أَعُوْذُ بِكَلِماتِ اللَّهِ التَّامَّتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ

A’uwdhu bikalimaatiLLaahit-ttaammati minsharri maa khalaq (mara 3 jioni na asubuhi).

 

Najikinga kwa maneno ya Allaah yaliyotimia kutokana na shari Aliyoiumba.

 

[Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) - Ahmad (2/290), An-Nasaaiy katika ‘Amal Al-Yawm wal-Laylah [590], Ibn As-Sunniy [68]. Angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/187), Swahiyh Ibn Maajah (92/266), Tuhfat Al-Akhyaar  (uk.. 45). Na Taz.  katika   Swahiyh Al-Jaami’ [6427]. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayesema mara tatu jioni hatodhuriwa na mdudu wa sumu usiku huo).

 

 

 

Share

023-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL BAARIU

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

الْبَارِءُ

AL-BAARIU

 

 

 

 

Al-Baariu:  Mwanzishi viumbe bila kasoro.

 

Mwanzishi viumbe bila kasoro.

 

Al-Baariu: Muumbaji viumbe kwa maumbile yanayonasibiana na mazingira ya maisha yao.

 

Jina hili tukufu limetajwa mara mbili katika Qur-aan:

 

هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ  

Yeye Ndiye Allaah, Muumbaji, Mwanzishi viumbe bila kasoro, Muundaji sura na umbile. [Al-Hashr: 24]

 

فَتُوبُوا إِلَىٰ بَارِئِكُمْ

basi tubuni kwa Muumbaji wenu; [Al-Baqarah: 54]  

 

 

1-Al-Baariu: Mwanzishi, Mvumbuzi, Mwenye kuendelea. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي أَنفُسِكُمْ إِلَّا فِي كِتَابٍ مِّن قَبْلِ أَن نَّبْرَأَهَا ۚ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ ﴿٢٢﴾

22. Hausibu msiba wowote katika ardhi au katika nafsi zenu isipokuwa umo katika Kitabu kabla hatujautokezesha. Hakika hayo kwa Allaah ni mepesi. [Al-Hadiyd: 22]

 

 

2-Al-Baariu: Ametenganisha baadhi ya viumbe kwa baadhi yake, yaani amevipambanua kutoka aina moja kwenda aina nyingine, na kila kiumbe alikipa sura yake, inayonasibiana na malengo ya kuumbwa kwake, yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anaumba kitu kutoka kisichokuwa chochote, na kila kimoja anakipa sifa yake ya kipekee tofauti na viumbe vingine.

 

 

3-Yeye Al-Baariu Ameumba maumbile yaliyoepukana na tofauti na kuchukiza, na kudhalilika, vimejipambanua vyote na kujikosha na hivyo, Anasema (‘Azza wa Jalla):

 

الَّذِي خَلَقَ سَبْعَ سَمَاوَاتٍ طِبَاقًا ۖ مَّا تَرَىٰ فِي خَلْقِ الرَّحْمَـٰنِ مِن تَفَاوُتٍ ۖ فَارْجِعِ الْبَصَرَ هَلْ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ﴿٣﴾

Ambaye Ameumba mbingu saba matabaka, hutaona katika uumbaji wa Ar-Rahmaan tofauti yoyote. Basi rejesha jicho je, unaona mpasuko wowote ule?  [Al-Mulk: 3]

 

 

4-Yeye Al-Baariu Amemuumba mwana Aadam kutokana na udongo, na katika lugha ya Kiarabu, Al-Bariyyu ni udongo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 مِنْهَا خَلَقْنَاكُمْ وَفِيهَا نُعِيدُكُمْ وَمِنْهَا نُخْرِجُكُمْ تَارَةً أُخْرَىٰ ﴿٥٥﴾

55. Kutokana nayo (ardhi) Tumekuumbeni, na humo Tutakurudisheni, na kutoka humo Tutakutoeni mara nyingine.  [Twaahaa: 55]

 

 

5-Yeye Al-Baariu Aliyeumba maji na udongo na moto na hewa si kutoka katika kitu, kisha baada ya hapo Akaumba maumbo mbali mbali.

 

[Marejeo ya maana zilizotangulia katika: Al-Minhaaj (1/192), Al-Asmaau cha Ar-Raaziy (216), Tafsiyr Asmaai Allaah (27) Asmaau cha Al-Bayhaqiy (40) na An-Nahjul Asmaa cha Muhammad Al-Hamuwd 117]

 

 

6-Yeye Al-Baariu: Ambaye Anamtakasa aliyedhulumiwa na alichodhulumiwa, kama vile Alivyomtakasa Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ آذَوْا مُوسَىٰ فَبَرَّأَهُ اللَّـهُ مِمَّا قَالُوا ۚ وَكَانَ عِندَ اللَّـهِ وَجِيهًا ﴿٦٩﴾

Enyi walioamini! Msiwe kama wale waliomuudhi Muwsaa, lakini Allaah Akamtoa tuhumani kutokana na yale waliyoyasema. Na alikuwa mbele ya Allaah mwenye kuheshimika. [Al-Ahzaab: 69]

 

 

7-Yeye Al-Baariu Ametakasika na  upungufu wowote ule na aibu yoyote ya dhati Yake, sifa na matendo yake, na kufananishwa na chochote, kushirikishwa, usuhuba kuwa na watoto na kila anachonasibishwa nacho na makafiri.

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Baariu:

 

1-Tafakari Uumubaji wa Al-Baariu. Na kutafakari uumbaji na utukufu wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni miongoni mwa ‘ibaadah adhimu mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa. Tafakari kwa kutazama mbinguni; jua, mwezi, nyota ndege na tafakari viumbe vinginevyo visivyoonekana; Malaika, majini n.k. Tazama ardhini, milima, miti, wana Aadam, wanyama, wadudu n.k. Tazama na tafakari vya baharini; kila aina ya samaki. Tazama kila mahali utakuta uumbaji ambao hakuna awezaye kuumba kama Yeye (‘Azza wa Jalla), hivyo usije kumshirikisha na yeyote yule. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

هَـٰذَا خَلْقُ اللَّـهِ فَأَرُونِي مَاذَا خَلَقَ الَّذِينَ مِن دُونِهِ ۚ بَلِ الظَّالِمُونَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿١١﴾

Huu ni uumbaji wa Allaah, basi nionyesheni nini walichokiumba wasiokuwa Yeye. Bali madhalimu wamo katika upotofu bayana. [Luqmaan: 11]

 

Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ ﴿١٧﴾

Je, hawamtazami ngamia namna walivyoumbwa?

 

وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ ﴿١٨﴾

Na mbingu vipi zilivyonyanyuliwa?

 

وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ ﴿١٩﴾

Na majabali vipi yamekongomewa imara kabisa.

 

وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ ﴿٢٠﴾

Na ardhi vipi ilivyotandazwa?  [Al-Ghaashiyah: 17-20]

 

 

2-Mtii Al-Baariu Ambaye Amekuumba wala usimtii yeyote mwengine katika maasia ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

لا طاعةَ لِمخلُوقٍ في معصيةِ الخالِقِ

((Hakuna kumtii kiumbe katika kumuasi Muumba)) [Swahiyh Al-Jaami’ (7520)

 

 

3-Unapomuasi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), rudi kutubia Kwake kama vile Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam) alivyowaamrisha wana wa Israaiyl:

 

 وَإِذْ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوْمِهِ يَا قَوْمِ إِنَّكُمْ ظَلَمْتُمْ أَنفُسَكُم بِاتِّخَاذِكُمُ الْعِجْلَ فَتُوبُوا إِلَىٰ بَارِئِكُمْ فَاقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ عِندَ بَارِئِكُمْ فَتَابَ عَلَيْكُمْ ۚ إِنَّهُ هُوَ التَّوَّابُ الرَّحِيمُ ﴿٥٤﴾

Na pindi Muwsaa alipowaambia kaumu yake: “Enyi kaumu yangu! Hakika nyinyi mmedhulumu nafsi zenu kwa kuabudu kwenu ndama, basi tubuni kwa Muumbaji wenu;  na ziueni nafsi zenu, hivyo ni bora kwenu mbele ya Muumbaji wenu.” Akapokea tawbah yenu; hakika Yeye Ndiye Mwingi wa kupokea tawbah, Mwenye kurehemu. [Al-Baqarah: 54]

 

 

04-Muombe du’aa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kukiri kwamba Yeye ni Muumbaji wako; Du’aa inayoitwa Sayyid Al-Istighfaar ambayo ni du’aa bora kabisa kuliko nyinginezo katika kuomba maghfirah:

 

اللّهـمَّ أَنْتَ رَبِّـي لا إلهَ إلاّ أَنْتَ، خَلَقْتَنـي وَأَنا عَبْـدُك، وَأَنا عَلـى عَهْـدِكَ وَوَعْـدِكَ ما اسْتَـطَعْـت، أَعـوذُبِكَ مِنْ شَـرِّ ما صَنَـعْت، أَبـوءُ لَـكَ بِنِعْـمَتِـكَ عَلَـيَّ وَأَبـوءُ بِذَنْـبي فَاغْفـِرْ لي فَإِنَّـهُ لا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْتَ.

Allaahumma Anta Rabbiy laa ilaaha illaa Anta Khalaqtaniy wa ana ‘abduka wa anaa ‘alaa ‘ah-dika wawa’-dika mastatwa’-tu, a’uwdhu bika min sharri maa swana’-tu, abuw-u Laka bini’-matika ‘alayya wa abuw-u bidhanbiy, faghfir-liy fainnahu laa yaghfirudh dhunuwba illaa Anta

 

Ee Allaah, Wewe ni Rabb wangu, hapana muabudiwa wa haki ila Wewe, umeniumba mimi na mimi ni mja Wako, nami niko juu ya  ahadi Yako, na agano Lako, kiasi cha uwezo wangu, najikinga Kwako kutokana na shari ya nilichokifanya, nakiri  Kwako kwa kunineemesha, na nakiri kwa madhambi yangu, basi nakuomba unighufurie kwani hakuna wa kughufuria madhambi ila Wewe.  [Al-Bukhaariy (7/150) [2306]]

 

 

Share

024-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-MUSWAWWIRU

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْمُصَوِّر

AL-MUSWAWWIRU

 

 

 

Al-Muswawwir: Muundaji Sura

 

           

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

هُوَ اللَّـهُ الْخَالِقُ الْبَارِئُ الْمُصَوِّرُ ۖ  

Yeye Ndiye Allaah, Muumbaji, Mwanzishi viumbe bila kasoro, Muundaji sura na umbile. [Al-Hashr: 24]

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Muundaji sura na umbile: Ambaye ameunda sura za viumbe Wake vile Atakavyo, na Akaunda sura za viumbe vyote vilivyomo ulimwenguni, na kuvipanga na Akatoa katika kila kimoja sura maalum na umbile la kipekee ambalo kila kiumbe anatofautika kwa viumbe vingine juu ya  kuwa viumbe vya  Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  ni vingi mno visivyowezekana kuhesabika!  Allaah (Subhaanahau wa Ta'aalaa) Ameumba kila sura na Akitaka kitu husema: Kun! (Kuwa) na kikawa katika wasifu Autakao na sura Aiachaguayo.  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa): 

 

الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ ﴿٧﴾

Ambaye Amekuumba Akakusawazisha (umbo sura, viungo) na Akakupima na kukulinganisha sawa.

 

فِي أَيِّ صُورَةٍ مَّا شَاءَ رَكَّبَكَ ﴿٨﴾

Katika sura Aliyotaka Akakutengeneza. [Al-Infitwaar: 7-8]

 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ameanzisha uumbaji wake katika sura mbali mbali na maumbo mengi yanayotofautiana, urefu, ufupi, dume na jike, kila mmoja na sura na umbile lake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَقَدْ خَلَقْنَاكُمْ ثُمَّ صَوَّرْنَاكُمْ ثُمَّ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ لَمْ يَكُن مِّنَ السَّاجِدِينَ ﴿١١﴾

Na kwa yakini Tumekuumbeni kisha Tukakutieni sura; kisha Tukawaambia Malaika: “Msujudieni Aadam.” Wakasujudu isipokuwa Ibliys hakuwa miongoni mwa waliosujudu. [Al-A’raaf: 7]

 

 

Na Anasema vile vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ وَصَوَّرَكُمْ فَأَحْسَنَ صُوَرَكُمْ ۖ وَإِلَيْهِ الْمَصِيرُ﴿٣﴾

Ameumba mbingu na ardhi kwa haki, na Akakutengenezeni sura, kisha Akafanya nzuri zaidi sura zenu, na Kwake ndio mahali pa kuishia. [At-Taghaabun: 3]

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Muswawwiru:

 

 

1-Tafakari na tambua Tawhiyd ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika uundaji Wake katika viumbe Vyake.  Tafakari uundaje Wake wa sura za  wana Aadam na rangi zao, miili yao. Tafakari pia wanyama mbali mbali wa angani, baharini, na ardhini wakiwa katika sura na shepu na rangi mbali mbali wanaopendeza na wanaotisha. Tafakari pia vitu vinginevyo Alivyoviumba vilivyo katika shepu na rangi mbalimbali kama mbingu, jua, mwezi, sayari nyenginezo, bahari, milima na kadhalika.  Tafakari pia miti,  mauwa, matunda, mboga na kadhalika vyote vikiwa katika shepu na rangi mbali mbali vyenye ladha tofauti; tamu, kali chungu. Je kuna Al-Muswawwiru kama Yeye? Ndio Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anawaambia wanamoshirkisha kwamba hivyo ndivyo viumbe na vitu Alivyoviumba Yeye, basi hebu nao waonyeshe ambavyo walivyoviumba wao:

 

 خَلَقَ السَّمَاوَاتِ بِغَيْرِ عَمَدٍ تَرَوْنَهَا ۖ وَأَلْقَىٰ فِي الْأَرْضِ رَوَاسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمْ وَبَثَّ فِيهَا مِن كُلِّ دَابَّةٍ ۚ وَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ ﴿١٠﴾

(Allaah) Ameumba mbingu bila ya nguzo mnaziona, na Akatupa katika ardhi milima isikuyumbieni yumbieni, na Akaeneza humo kila viumbe vinavyotembea. Na Tukateremsha kutoka mbinguni maji, Tukaotesha humo kila aina ya mimea mizuri yenye manufaa.

 

هَـٰذَا خَلْقُ اللَّـهِ فَأَرُونِي مَاذَا خَلَقَ الَّذِينَ مِن دُونِهِ ۚ بَلِ الظَّالِمُونَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿١١﴾

Huu ni uumbaji wa Allaah, basi nionyesheni nini walichokiumba wasiokuwa Yeye. Bali madhalimu wamo katika upotofu bayana. [Luqmaan: 11]

 

 

 

2-Mshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa neema Zake na hikma Yake kubwa kukuumba na kukuunda katika sura nzuri kabisa; kila kiungo Amekiumba mahali pake panapostahiki. Tafakari lau ingelikuwa si Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ndiye Muundaji wa sura za viumbe, basi kungelikuwa na kasoro nyingi katika uuandaji huo wa viumbe. Anasema Allaah (‘Azza wa Jalla):

 

لَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ فِي أَحْسَنِ تَقْوِيمٍ ﴿٤﴾

Kwa yakini Tumemuumba mwana Aadam katika umbile bora kabisa. [At-Tiyn: 4]

 

 

3-Muombe Al-Muswawwiru Aendelee kukuweka katika hali ya ukamilifu ya uundaji Wake kwani kama isemwavyo: “Mwana Aadam hakukamilika mpaka kufa kwake.” Basi wangapi wameumbulika sura na umbo baada ya maafa wakapoteza viungo na sura zao nzuri?

 

 

4-Tumia viungo vya mwili wako katika yale ya kumridhisha Al-Muswawwiru, ikiwa mwanamke umejaaliwa sura nzuri kabisa basi jisitiri na jiepushe na kujishaua kwa kudhirisha sura yako kwa wanaume wasio mahram wako jambo ambalo litapeleka katika maasi, wala usitumie neema hiyo ya kujaaliwa na sura nzuri katika maasi yoyote yale ya Allaah ('Azza wa Jalla) kwasababu  kila kiungo kitashuhudia maovu yatakayotendwa na viungo hivo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَيَوْمَ يُحْشَرُ أَعْدَاءُ اللَّـهِ إِلَى النَّارِ فَهُمْ يُوزَعُونَ﴿١٩﴾

 

Na Siku watakayokusanywa maadui wa Allaah kwenye moto, nao watakusanywa kupangwa safusafu.

 

حَتَّىٰ إِذَا مَا جَاءُوهَا شَهِدَ عَلَيْهِمْ سَمْعُهُمْ وَأَبْصَارُهُمْ وَجُلُودُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٢٠﴾

 

Mpaka watakapoufikia yatashuhudia dhidi yao, masikio yao, na macho yao, na ngozi zao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda.

 

 

وَقَالُوا لِجُلُودِهِمْ لِمَ شَهِدتُّمْ عَلَيْنَا ۖ قَالُوا أَنطَقَنَا اللَّـهُ الَّذِي أَنطَقَ كُلَّ شَيْءٍ وَهُوَ خَلَقَكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴿٢١﴾

 

Na wataziambia ngozi zao: “Mbona mnashuhudia dhidi yetu?” Zitasema: “Ametutamkisha Allaah Ambaye Ametamkisha kila kitu, Naye Ndiye Aliyekuumbeni mara ya kwanza na Kwake mtarejeshwa.

 

 

وَمَا كُنتُمْ تَسْتَتِرُونَ أَن يَشْهَدَ عَلَيْكُمْ سَمْعُكُمْ وَلَا أَبْصَارُكُمْ وَلَا جُلُودُكُمْ وَلَـٰكِن ظَنَنتُمْ أَنَّ اللَّـهَ لَا يَعْلَمُ كَثِيرًا مِّمَّا تَعْمَلُونَ﴿٢٢﴾

 

“Na hamkuwa mkijisitiri hata yasishuhudie masikio yenu, na wala macho yenu, na wala ngozi zenu; lakini mlidhania kwamba Allaah Hajui mengi katika yale mnayoyatenda. [Fusw-Swilat: 19-22]

 

 

Na Ansema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ وَأَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٢٤﴾

Siku zitakaposhuhudia dhidi yao ndimi zao, na mikono yao, na miguu yao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda.  [An-Nuwr: 24]

 

 

5-Ridhika na vile Alivyokuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wala usilalamike au kujiumbua kwa kubadilisha umbo lako na sura yako ukataka kujiongezea ukubwa au kupunguza udogo katika viungo vya mwili wako. Hii ni katika uchochezi wa shaytwaan ambaye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Amemlaani anayejiumbua sura na maumbile yake.  [Rejea An-Nisaa: 117-121]

 

 

6-Unapoona kilema usimcheke bali mshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuwa Amekukamilisha katika kukuunda kwako na pindi unapomuona kilema sema du’aa ya Sunnah kama alivyotufundisha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye amesema:

 

((مَنْ راْ مُبْتَل فَقال: الْحَمْـدُ للهِ الّذي عافاني مِمّا ابْتَـلاكَ بِهِ، وَفَضَّلَـني عَلى كَثيـرٍ مِمَّنْ خَلَـقَ تَفْضـيلا، لَمْ يُصِبْهُ ذالك الْبَلاء))

 

((Atakayemuona aliyepatwa na mtihani akasema:

 

الْحَمْـدُ للهِ الّذي عافاني مِمّا ابْتَـلاكَ بِهِ، وَفَضَّلَـني عَلى كَثيـرٍ مِمَّنْ خَلَـقَ تَفْضـيلا.

Himdi ni za Allaah, Ambaye Ameniepusha na kile Alichokupa mtihani na Akanifanya mimi kuwa bora kuliko wengi miongoni mwa Aliowaumba.”

 

Basi hatofikwa na mtihani huo)) [Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) ameipokea At-Tirmidhiy (5/493-4), Ibn Maajah. Angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (3/153)]

 

 

 

7-Jiepushe na kumuiga Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) katika uundaji Wake kwa kuchora picha za viumbe na kuzitia sura jambo ambalo limeharamishwa katika nususi kadhaa zikiwemo:

 

عَنْ عَائِشَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) قَال: ((أَشَدُّ النَّاسِ عَذَابًا يَوْمَ القِيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهِئُونَ بِخَلْقِ اللَّهِ))

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watakaokuwa na adhabu kali Siku ya Qiyaamah ni wanaomuiga Allaah katika uumbaji Wake)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na pia:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ ((مَنْ صَوَّرَ صُورَةً فِي الدُّنْيَا كُلِّفَ أَنْ يَنْفُخَ فِيهَا الرُّوحَ وَلَيْسَ بِنَافِخٍ))

Kutoka kwa  Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) Hadiyth Marfuw’: ((Atakayechora picha duniani atalazimishwa aitie roho (Siku ya Qiyaamah), na wala hatoweza)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na pia:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) :  سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((كُلُّ مُصَوِّرٍ فِي النَّارِ يُجْعَلُ لَهُ بِكُلِّ صُورَةٍ صَوَّرَهَا نَفْسٌ يُعَذَّبُ بِهَا فِي جَهَنَّمَ))

Kutoka kwa  Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kila mchoraji picha atakuwa motoni. Kila picha aliyoichora, itatiwa roho nayo itamuadhibu katika Jahannam)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

025-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-HAKAM

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْحَكَمْ

 

AL-HAKAM

  

 

 

 

 

Al-Hakam: Hakimu/Mwamuzi: Ni Ambaye ana hukumu baina ya viumbe Wake kwa uadilifu, hamdhulumu yeyote kati yao. Naye Ndiye Aliyeleta kitabu Chake kitukufu ili kiwe hakimu baina ya watu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

أَفَغَيْرَ اللَّـهِ أَبْتَغِي حَكَمًا وَهُوَ الَّذِي أَنزَلَ إِلَيْكُمُ الْكِتَابَ مُفَصَّلًا ۚ  

 (Sema): “Je, nitafute hakimu ghairi ya Allaah na hali Yeye Ndiye Ambaye Aliyekuteremshieni Kitabu kilichofasiliwa waziwazi?”  [Al-An’aam: 114]

 

Wala hambebeshi mwingine mzigo wa mwingine, wala hamlipi mja kwa zaidi ya dhambi zake, na hufikisha haki kwa wanaostahiki, haachi kumpa mwenye haki ila atakuwa amemfikishia haki yake. [Al-Asnaa 1/437]

 

Hukumu Zake ni za aina mbili:

 

a-Hukumu za ki-Ulimwengu:

 

Ni hukmu Anazozihukumu katika uumbaji Wake mbali mbali wa vitu na uendeshaji Wake mfano mzunguko wa dunia, mabadiliko ya usiku na mchana, kuchomoza na kukuchwa jua, mwezi kuanza upya na kumalizikia idadi ya siku zake,  kama Anavyosema:

 

وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ۚ ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ ﴿٣٨﴾

Na jua linatembea hadi matulio yake. Hiyo ni takdiri ya Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mjuzi wa yote.

 

وَالْقَمَرَ قَدَّرْنَاهُ مَنَازِلَ حَتَّىٰ عَادَ كَالْعُرْجُونِ الْقَدِيمِ ﴿٣٩﴾

Na mwezi Tumeukadiria vituo mpaka ukarudi (mwembamba) kama kwamba karara la shina la mtende lililopinda la zamani.

 

 

لَا الشَّمْسُ يَنبَغِي لَهَا أَن تُدْرِكَ الْقَمَرَ وَلَا اللَّيْلُ سَابِقُ النَّهَارِ ۚ وَكُلٌّ فِي فَلَكٍ يَسْبَحُونَ ﴿٤٠﴾

Halipasi jua kuudiriki mwezi, na wala usiku kuutangulia mchana; na vyote viko katika falaki vinaogelea. [Yaasiyn: 38-40]

 

Nayo ni hali halisi ambayo haikwepeki, nayo inahusiana na matakwa Yake Allaah ('Azza wa Jalla) ambayo hayawi ila kwa maana ya kilimwengu; Anayotaka ndio yanakuwa, na Asichotaka hakiwi.  Hukmu Yake hairejeshwi wala hapana baada ya hukumu Yake na hakuna mwenye kushinda jambo lake Anapolihukumu.

 

 

b-Hukumu ya ki-Shariy’ah

 

Shariy'ah zilizowekwa kwa ajili ya wana Aadam kuzifuata zinazohusiana na maamrisho na makatazo Yake, na Shariy'ah zinazohusiana na utendaje wa 'ibaadah.  Hizi ni hukumu za kimajukumu ya ki-Shariy’ah, ambazo ni hukumu zilizokuwa nzuri zaidi, ambayo ni mambo mema na ukamilifu wake, wala Dini yao haiongoki isipokuwa kwa kufuata hukumu hizi, ambazo Amezifanya kuwa ni Shariy’ah katika ndimi za Manabii. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

 

وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّـهِ حُكْمًا لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ ﴿٥٠﴾

Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu kwa watu wenye yakini. [Al-Maaiidah: 50]

 

Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

  ((إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْحَكَمُ وَإِلَيْهِ الْحُكْمُ))  

 Hakika Allaah ndiye Hakimu na Kwake kuna hukmu zote))   [Abuu Daawuwd na wengineo].

 

Hukmu hii ndio ambayo mtu atalipwa kwayo thawabu au adhabu, katika Siku ya hesabu.

 

Na aina mbili za hukmu hizo zinaingia kwa mja. Hukmu ya kilimwengu inapita kwake, naye anadhalilishwa kwayo atake au asitake. Na hukumu za kilimwengu haiwezikani kwenda kinyume chake.  Ama hukmu za ki-Shariy’ah mja anaweza kwenda kinyume nazo, na hukmu Zake zote hizi ni kwa hekima, na uadilifu, nayo ni hukumu ya uadilifu ambayo maneno Yake yametimia kwa ukweli katika habari, na uadilifu katika maamrisho, na makatazo.  Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) aliyetekeleza hukmu Zake kwa waja Wake na Akafanya uadilifu baina yao katika hukumu zao, na kuwaenea kwa rahmah Zake Allaah ('Azza wa Jalla) na Akawaweka katika matakwa Yake.  

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Hakam:

 

1-Jina na Sifa ya Al-Hakam imethibiti kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee kama vile ambavyo hakuna mshirika pamoja naye katika kumwabudu, basi pia hakuna wa kushiriki Naye katika Hukmu Zake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

  وَلَا يُشْرِكُ فِي حُكْمِهِ أَحَدًا ﴿٢٦﴾

na wala Hamshirikishi katika hukumu Zake yeyote. [Al-Kahf: 26]

 

2-Muumini anapaswa kuelemea na kukubali  hukmu za Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجًا مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٦٥﴾

Basi Naapa kwa Rabb wako, hawatoamini mpaka wakufanye wewe ni mwamuzi katika yale wanayozozana baina yao, kisha wasipate katika nyoyo zao karaha katika yale uliyohukumu na wajisalimishe, kwa kujisalimisha kikamilifu. [An-Nisaa: 65] 

 

Na Sababu ya kuteremshwa Aayah hiyo na kama ilivyothibiti  ifuatavyo:

 

Az-Zubayr bin Al-‘Awwaam (رضي الله عنه)  na bwana mmoja katika Answaar, pale walipokhitilafiana kuhusu mfereji wa kupitisha maji ya mvua waliokuwa wakitumia maji yake. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akatoa hukmu baina yao kwamba Az-Zubayr amwagilie maji ardhini mwake kisha ayaache yatiririke kwa Answaar. Akakasirika Answaar huyo na kumwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Umempendelea yeye kwa kuwa ni mtoto wa ‘ammat yako! Hapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akabadilika uso rangi kwa hasira akamwambia tena Az-Zubayr amwagie maji kwanza kisha yatiririke kwa jirani yake huyo kwa kuwa hukumu hiyo ilikuwa kwa manufaa ya wote wawili. Hivyo akampatia Az-Zubayr haki yake. Ikateremka Aayah hii: “Basi Naapa kwa Rabb wako, hawatoamini mpaka wakufanye wewe ni mwamuzi katika yale wanayozozana baina yao… (4: 67). [Amehadithia Az-Zubayr (رضي الله عنه) ameipokea Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

3-Unapokuwa ni hakimu wa watu unapaswa uhukmu bila ya kupendelea. Allaah (‘Azza wa Jalla) Anasema:

 

وَإِذَا حَكَمْتُم بَيْنَ النَّاسِ أَن تَحْكُمُوا بِالْعَدْلِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴿٥٨﴾

Na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika uzuri ulioje Anayokuwaidhini nayo Allaah; hakika Allaah daima ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [An-Nisaa: 58]

 

Na pindi ukidhulumiwa vuta subira na muombe Al-Hakam Akuhukumie dhulma uliyotendwa kwani Yeye Ndiye Mbora wa mahakimu. Anasema Allaah (‘Azza wa Jalla):

 

  وَاصْبِرْ حَتَّىٰ يَحْكُمَ اللَّـهُ ۚ وَهُوَ خَيْرُ الْحَاكِمِينَ﴿١٠٩﴾

na subiri mpaka Allaah Ahukumu. Naye ni Mbora wa wanaohukumu.  [Yuwnus: 109]

 

Na Anasema pia (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

أَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَحْكَمِ الْحَاكِمِينَ ﴿٨﴾

Je, kwani Allaah Si Mwadilifu zaidi wa wanaohukumu kuliko mahakimu wote?   [At-Tiyn: 8]

 

 

 

 

4-Omba du’aa ya Sunnah ifuatayo unapopatwa huzuni:

 

اللّهُـمَّ إِنِّي عَبْـدُكَ، ابْنُ عَبْـدِكَ، ابْنُ أَمَتِـكَ نَاصِيَتِي بِيَـدِكَ، مَاضٍ فِيَّ حُكْمُكَ، عَدْلٌ فِيَّ قَضَاؤكَ، أَسْأَلُـكَ بِكُلِّ اسْمٍ هُوَ لَكَ، سَمَّـيْتَ بِهِ نَفْسَكَ، أِوْ أَنْزَلْتَـهُ فِي كِتَابِكَ، أَوْ عَلَّمْـتَهُ أَحَداً مِنْ خَلْقِـكَ، أَوِ اسْتَـأْثَرْتَ بِهِ فِي عِلْمِ الغَيْـبِ عِنْـدَكَ، أَنْ تَجْـعَلَ القُرْآنَ رَبِيـعَ قَلْبِـي، وَنورَ صَـدْرِي، وجَلَاءَ حُـزْنِي، وذَهَابَ هَمِّـي 

Ee Allaah hakika mimi ni mtumwa Wako, mtoto wa mtumwa Wako, mtoto wa kijakazi Chako, utosi wangu uko Mikononi Mwako, yaliyopita kwangu yako katika hukumu Yako, ni usawa kwangu kunihukumu Kwako, nakuomba kwa kila Jina ambalo ni Lako Ulilojiita Kwako Mwenyewe au Uliloliteremsha katika Kitabu Chako, au Ulilomfundisha yoyote yule kati ya viumbe Vyako, au Ulilolihifadhi Wewe mwenyewe (na kujihusisha kulijuwa) katika ilimu ya ghaibu Kwako, nakuomba Ujaalie Qur-aan kuwa ni rabiy' (uhuisho, raha, furaha na ustawisho) wa moyo wangu na nuru ya kifua changu, na ufumbuzi wa  huzuni yangu [Hadiyth ya ‘Abdullaahi bin Mas-‘uwd (رضي الله عنه) - Ahmad (1/391) [452], Al-Haakim (1/509) na ameisahihisha Al-Albaaniy (رحمه الله) katika Al-Kalimi Atw-Twayyib [124].

 

 

 

Share

026-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-HAKIYM

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

الْحَكِيم

 

AL-HAKIYM

 

 

 

 

Al-Hakiym:  Mwenye Hikmah

 

Mwenye kutenganisha baina ya mambo.  Mwenye kuweka vitu sehemu yake na Ambaye mtu hapendi kufanyiwa vitu visivyofaa.

 

Ni Mwenye Hikmah katika maneno, matendo na hukumu Zake, hivyo Hasemi, Hafanyi wala Hatenganishi isipokuwa ni haki, uadilifu, kilicho sawa.  

 

Haondoki katika Hikmah Yake kuimbe chochote.

 

Haingii katika mpangilio Wake makosa yoyote.

 

Ni Mwenye Hikmah ya juu katika uumbaji Wake na katika maamrisho Yake.

 

Haumbi kwa mchezo, wala Hafanyi Shariy’ah bila lengo, wala Hawaachi waja Wake hivi hivi tu.

 

Haamrishi kwa yasiyokuwa na maslahi wala Hakatazi ila yaliyo na madhara.

 

Mwenye Hikmah za mwanzo na mwisho na katika ukamilifu wa Hikmah Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), ni kuja kwa Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Dini ya Kiislamu na Qur-aan. Ni dalili kuu ya ukweli wake, na Akasadikisha alichokuja nacho kwa kuwa Kwake Mwenye kuhukumu kwa ukamilifu haipatikani islahi duniani na Aakhirah ila Kwake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

لَّا يَأْتِيهِ الْبَاطِلُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَلَا مِنْ خَلْفِهِ ۖ تَنزِيلٌ مِّنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ﴿٤٢﴾

Hakitokifikia ubatili mbele yake, na wala nyuma yake; ni uteremsho kutoka kwa Mwenye hikmah wa yote, Mwenye kustahiki kuhimidiwa kwa yote. [Fusw-Swilat: 42]

 

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Hakiym:

 

 

1-Zingatia Hikmah Yake Al-Hakiym jinsi Alivyoumba dunia Akaweka kila kitu na mahitajio yote ya waja Wake. Jinsi Alivyoumba mbingu, ardhi Akaitandaza na ardhi ili viumbe viweze kuishi humo.

 

 

2-Zingatia uumbaji Wake wa mwili wa mwana Aadam na jinsi Alivyojaalia kila kiungo kiko sehemu ifaayo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 الَّذِي أَحْسَنَ كُلَّ شَيْءٍ خَلَقَهُ ۖ وَبَدَأَ خَلْقَ الْإِنسَانِ مِن طِينٍ ﴿٧﴾

Ambaye Amefanya uzuri kila kitu Alichokiumba; na Akaanzisha uumbaji wa insani kutokana na udongo.

 

ثُمَّ جَعَلَ نَسْلَهُ مِن سُلَالَةٍ مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ ﴿٨﴾

Kisha Akajaalia kizazi chake kutokana na mchujo safi wa maji dhalilifu.

 

 

ثُمَّ سَوَّاهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِ ۖ وَجَعَلَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ ۚ قَلِيلًا مَّا تَشْكُرُونَ ﴿٩﴾

Kisha Akamsawazisha, na Akapuliza humo roho yake (Aliyoiumba Allaah). Na Akakujaalieni kusikia na kuona na nyoyo, ni machache mno yale mnayoshukuru. [As-Sajdah: 7-9]

 

 

3-Omba du’aa Allaah ('Azza wa Jalla) Akujaalie uwe mwenye hikmah kwani anayepewa hikmah hakika amepewa kheri nyingi kama Anavyosema Mwenyewe Allaah ('Azza wa Jalla):

 

يُؤْتِي الْحِكْمَةَ مَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُؤْتَ الْحِكْمَةَ فَقَدْ أُوتِيَ خَيْرًا كَثِيرًا ۗ وَمَا يَذَّكَّرُ إِلَّا أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٢٦٩﴾

Humpa hikmah Amtakaye. Na anayepewa hikmah basi kwa yakini huwa amepewa khayr nyingi. Na hawakumbuki isipokuwa wenye akili. [Al-BaqaraHl 269]

 

4-Tumia hikmah katika kutaamuli na watu, kama vile katika kusuluhisha watu, katika kutakwa ushauri wa jambo zito na kadhaalika.

 

5- Unapopatwa na mitihani amini kwamba ni majaaliwa ya Allaah ('Azza wa Jalla) na ni kheri kwako badala ya shari kwa sababu Yeye Al-Hakiym Anajua kwanini Amejaalia mitihani hiyo ikusibu, bila shaka kwa hikmah Yake kama Anavyosema:

 

وَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ وَعَسَىٰ أَن تُحِبُّوا شَيْئًا وَهُوَ شَرٌّ لَّكُمْ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿٢١٦﴾

Na asaa mkachukia jambo na hali lenyewe ni khayr kwenu. Na asaa mkapenda jambo na hali lenyewe ni la shari kwenu. Na Allaah Anajua na nyinyi hamjui. [Al-Baqarah: 216]

 

 

 

Share

027-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AS-SAMIY'U

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

السَّمِيع

 

AS-SAMIY’U

 

 

 

 

As-Samiy’u: Mwenye Kusikia Yote Daima

 

 

As-Samiy’u imetajwa katika Qur-aan mara arubaini na tano; hii inajulisha umuhimu wa Jina na Sifa hii tukufu ya Allaah ('Azza wa Jalla) Na Jina hili la Allaah ('Azza wa Jalla)  limejumuika na  البصير (Al-Baswiyr: Mwenye Kuona Yote Daima) mara nyingi katika Qur-aan miongoni mwayo ni Kauli Zake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ﴿١١﴾

Hakuna chochote kinachofanana Naye, Naye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ash-Shuwraa: 11]

 

 

Na pia,

 

وَاللَّـهُ يَقْضِي بِالْحَقِّ ۖ وَالَّذِينَ يَدْعُونَ مِن دُونِهِ لَا يَقْضُونَ بِشَيْءٍ ۗ إِنَّ اللَّـهَ هُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ﴿٢٠﴾

Na Allaah Anahukumu kwa haki. Na wale wanaowaomba badala Yake hawawezi kuhukumu kwa chochote. Hakika Allaah Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ghaafir: 20]

 

 

Na pia,

 

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا وَإِذَا حَكَمْتُم بَيْنَ النَّاسِ أَن تَحْكُمُوا بِالْعَدْلِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴿٥٨﴾

Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe. Na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika uzuri ulioje Anayokuwaidhini nayo Allaah; hakika Allaah daima ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [An-Nisaa: 58]

 

 

Usikivu Wake umeenea usikivu wote, kwa lugha mbali mbali, kwa haja za nyingi za watu, yaliyo siri Kwake yako wazi na minong’ono Kwake na sauti yenye kusikika, na aliye mbali na karibu Kwake, usikivu Wake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni wa aina mbili:

 

 

Kwanza: Usikivu Wake wa sauti zote za dhahiri na za siri na kuenea kwake, sauti hazitofautiani Kwake, kadiri zitakavyoongezeka na kuwa aina mbalimbali kana kwamba sauti zote hizo ni moja kwake. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)

 

سَوَاءٌ مِّنكُم مَّنْ أَسَرَّ الْقَوْلَ وَمَن جَهَرَ بِهِ وَمَنْ هُوَ مُسْتَخْفٍ بِاللَّيْلِ وَسَارِبٌ بِالنَّهَارِ ﴿١٠﴾

Ni sawasawa kwenu anayefanya siri kauli (yake), au anayeisema kwa jahara, na anayenyemelea usiku na anayatembea huru mchana.  [Ar-Ra’d: 10]

 

 

Pili: Husikiliza maombi ya waja Wake, huwajibu na huwapa malipo kama alivyoomba Nabiy Ibraahiym ('Alayhis-Salaam)

 

الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى الْكِبَرِ إِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ ۚ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٩﴾

AlhamduliLLaah (Himdi Anastahiki Allaah), Ambaye Amenitunukia juu ya umri mkubwa wangu Ismaa’iyl na Is-haaq. Hakika Rabb wangu bila shaka ni Mwenye kusikia du’aa yangu. [Ibraahiym: 39]

 

 

Yaani: Mwenye kujibu du’aa za waja Wake, kama alivyosema mtu katika Swalaah na ikathibiti katika Hadiyth:

 

 

حَدَّثَنَا إِسْمَاعِيلُ، قَالَ حَدَّثَنِي مَالِكٌ، عَنْ سُمَىٍّ، عَنْ أَبِي صَالِحٍ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ "‏ إِذَا قَالَ الإِمَامُ سَمِعَ اللَّهُ لِمَنْ حَمِدَهُ‏.‏ فَقُولُوا اللَّهُمَّ رَبَّنَا لَكَ الْحَمْدُ، فَإِنَّهُ مَنْ وَافَقَ قَوْلُهُ قَوْلَ الْمَلاَئِكَةِ، غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ ‏"‏‏.‏

 

Amesimulia Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema:  “Pindi Imaam anaposema (katika Swalaah),

 

سَمِعَ اللَّهُ لِمَنْ حَمِدَهُ‏

Sami’a Allaahu liman Hamidah

 

Allaah Anasikia Anayemhimidi

 

Semeni:

اللَّهُمَّ رَبَّنَا لَكَ الْحَمْدُ

 

Allaahumma Rabbanaa Lakal-Hamd

 

Ee Allaah Rabb wetu, Himdi ni Zako

 

Kwani yeyote mwenye kuafikiana na Malaika katika kusema hayo, ataghufuriwa madhambi yake yote yaliyotangulia.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Na usikivu wake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kwa maana ya kumfanya anayeomba kumdiriki Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa sauti; Yaani:

 

 

i-Kumtisha; Mfano wake ni Kauli Zake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

أَمْ يَحْسَبُونَ أَنَّا لَا نَسْمَعُ سِرَّهُمْ وَنَجْوَاهُم ۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيْهِمْ يَكْتُبُونَ﴿٨٠﴾

Au wanadhania kwamba Sisi Hatusikii siri zao na minong’ono yao? Sivyo! (Tunasikia!) Na Wajumbe wetu wako kwao wanaandika. [Az-Zukhruf: 80]

 

 

Na pia,

 

لَّقَدْ سَمِعَ اللَّـهُ قَوْلَ الَّذِينَ قَالُوا إِنَّ اللَّـهَ فَقِيرٌ وَنَحْنُ أَغْنِيَاءُ ۘ سَنَكْتُبُ مَا قَالُوا وَقَتْلَهُمُ الْأَنبِيَاءَ بِغَيْرِ حَقٍّ وَنَقُولُ ذُوقُوا عَذَابَ الْحَرِيقِ ﴿١٨١﴾

Kwa yakini Allaah Ameisikia kauli ya wale (Mayahudi) waliosema: Hakika Allaah ni fakiri na sisi ni matajiri. Tutayaandika waliyoyasema na kuua kwao Manabii pasi na haki na Tutasema: Onjeni adhabu ya kuunguza. [Aal-‘Imraan: 181]

 

 

 

ii-Muradi wake ni Kumuunga mkono; Mfano Kauli Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa Nabiy Muwsaa na Haaruwn ('Alayhimas-Salaam)

 

قَالَ لَا تَخَافَا ۖ إِنَّنِي مَعَكُمَا أَسْمَعُ وَأَرَىٰ ﴿٤٦﴾

(Allaah) Akasema: Msikhofu; hakika Mimi Niko pamoja nanyi, Nasikia na Naona. [Twaahaa: 46]

 

 

Yaani: Ninakuungeni mkono na kukunusuruni.

 

 

iii-Kubainisha upana na uenevu wa wa usikivu wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa); Mfano Kauli Yake:

 

قَدْ سَمِعَ اللَّـهُ قَوْلَ الَّتِي تُجَادِلُكَ فِي زَوْجِهَا وَتَشْتَكِي إِلَى اللَّـهِ وَاللَّـهُ يَسْمَعُ تَحَاوُرَكُمَا ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ بَصِيرٌ﴿١﴾

Allaah Amekwishasikia kauli ya yule mwanamke anayejadiliana nawe (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu mumewe, na anamshitakia Allaah; na Allaah Anayasikia majibizano yenu. Hakika Allaah ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Al-Mujaadalah: 1]

 

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; As-Samiy’u:

 

 

1-Tahadhari kusema maneno maovu yoyote yale utambue kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anakusikia popote pale ulipo. Tambua kuwa hakuna siri mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) lolote usemalo analisikia na linarekodiwa na Malaika wawili wanaoandika matendo ya mja hata kauli ya Ah!. Kumbuka Kauli Yake:

 

 

أَمْ يَحْسَبُونَ أَنَّا لَا نَسْمَعُ سِرَّهُمْ وَنَجْوَاهُم ۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيْهِمْ يَكْتُبُونَ﴿٨٠﴾

Au wanadhania kwamba Sisi Hatusikii siri zao na minong’ono yao? Sivyo! (Tunasikia!) Na Wajumbe wetu wako kwao wanaandika.[Az-Zukhruf: 80]

 

 

2-Jiepushe na kusikiliza yaliyoharamishwa kama muziki, nyimbo, ghiybah (kusengenya), na yote ambayo Hayamridhishi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) usije kudhani Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Hasikii au Hajui uyatendayo bali Yeye ni As-Samiy’u kwa kila hali na hatoweza kukanusha mtu Siku ya Qiyaamah kwa sababu viungo vya mwili wako vitakuja kushuhudia yote uyatendayo; yakiwemo masikio Kauli Zake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)

 

حَتَّىٰ إِذَا مَا جَاءُوهَا شَهِدَ عَلَيْهِمْ سَمْعُهُمْ وَأَبْصَارُهُمْ وَجُلُودُهُم بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿٢٠﴾ وَقَالُوا لِجُلُودِهِمْ لِمَ شَهِدتُّمْ عَلَيْنَا ۖ قَالُوا أَنطَقَنَا اللَّـهُ الَّذِي أَنطَقَ كُلَّ شَيْءٍ وَهُوَ خَلَقَكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ﴿٢١﴾ وَمَا كُنتُمْ تَسْتَتِرُونَ أَن يَشْهَدَ عَلَيْكُمْ سَمْعُكُمْ وَلَا أَبْصَارُكُمْ وَلَا جُلُودُكُمْ وَلَـٰكِن ظَنَنتُمْ أَنَّ اللَّـهَ لَا يَعْلَمُ كَثِيرًا مِّمَّا تَعْمَلُونَ﴿٢٢﴾ وَذَٰلِكُمْ ظَنُّكُمُ الَّذِي ظَنَنتُم بِرَبِّكُمْ أَرْدَاكُمْ فَأَصْبَحْتُم مِّنَ الْخَاسِرِينَ﴿٢٣﴾

Na Siku watakayokusanywa maadui wa Allaah kwenye moto, nao watakusanywa kupangwa Mpaka watakapoufikia yatashuhudia dhidi yao, masikio yao, na macho yao, na ngozi zao kwa yale waliyokuwa wakiyatenda. Na wataziambia ngozi zao: Mbona mnashuhudia dhidi yetu? Zitasema: Ametutamkisha Allaah Ambaye Ametamkisha kila kitu, Naye Ndiye Aliyekuumbeni mara ya kwanza na Kwake mtarejeshwa. Na hamkuwa mkijisitiri hata yasishuhudie masikio yenu, na wala macho yenu, na wala ngozi zenu; lakini mlidhania kwamba Allaah Hajui mengi katika yale mnayoyatenda. Na hivyo dhana yenu mliyokuwa mkimdhania Rabb wenu, imekuangamizeni, na mmekuwa miongoni mwa waliokhasirika. [Fusw-Swilat: 20 – 23]

 

 

 

3-Unapoomba du’aa, tambua kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Hasikilizi Du’aa ya mwenye kujionyesha kwa watu bali Anasikiliza du’aa ya mwenye kuomba kwa niyyah safi ya ikhlaasw kama ilivyokuja katika Hadiyth:

 

 

حَدَّثَنَا عُمَرُ بْنُ حَفْصٍ، قَالَ‏:‏ حَدَّثَنَا أَبِي، قَالَ‏:‏ حَدَّثَنَا الأَعْمَشُ قَالَ‏:‏ حَدَّثَنِي مَالِكُ بْنُ الْحَارِثِ، عَنْ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ يَزِيدَ قَالَ‏:‏ كَانَ الرَّبِيعُ يَأْتِي عَلْقَمَةَ يَوْمَ الْجُمُعَةِ، فَإِذَا لَمْ أَكُنْ ثَمَّةَ أَرْسَلُوا إِلَيَّ، فَجَاءَ مَرَّةً وَلَسْتُ ثَمَّةَ، فَلَقِيَنِي عَلْقَمَةُ وَقَالَ لِي‏:‏ أَلَمْ تَرَ مَا جَاءَ بِهِ الرَّبِيعُ‏؟‏ قَالَ‏:‏ أَلَمْ تَرَ أَكْثَرَ مَا يَدْعُو النَّاسَ، وَمَا أَقَلَّ إِجَابَتَهُمْ‏؟‏ وَذَلِكَ أَنَّ اللَّهَ عَزَّ وَجَلَّ لاَ يَقْبَلُ إِلاَّ النَّاخِلَةَ مِنَ الدُّعَاءِ، قُلْتُ‏:‏ أَوَ لَيْسَ قَدْ قَالَ ذَلِكَ عَبْدُ اللهِ‏؟‏ قَالَ‏:‏ وَمَا قَالَ‏؟‏ قَالَ‏:‏ قَالَ عَبْدُ اللهِ‏:‏ لاَ يَسْمَعُ اللَّهُ مِنْ مُسْمِعٍ، وَلاَ مُرَاءٍ، وَلا لاعِبٍ، إِلا دَاعٍ دَعَا يَثْبُتُ مِنْ قَلْبِهِ، قَالَ‏:‏ فَذَكَرَ عَلْقَمَةَ‏؟‏ قَالَ‏:‏ نَعَمْ‏.‏

 

Abdur-Rahmaan ibn Yaziyd alisema: Ar-Rabiy’ alikuwa akienda kwa ‘Alqamah kila Ijumaa. Pindi nilipokuwa siko huko, walikuwa wakiniita. Mara moja alikuja wakati mimi sikuwepo. ‘Alqamah alikutana nami na akaniambia: Je, hukuona alicholeta Ar-Rabiy’? Akasema: Je,  hauoni jinsi watu wanavyoomba du’aa mara kwa mara na jinsi wanavyojibiwa kwa nadra (uchache)? Hivyo ni kwa sababu Allaah (‘Azza wa Jalla) Anataqabali du’aa iliyo na ikhlaasw (niyyah safi) pekee.  Nikamuuliza:  Je! Kwani hivyo sivyo ndivyo alivyosema ‘Abdullaah?    Akauliza: Amesema nini?  Nikasema: ‘Abdullaah amesema kwamba Allaah Hasikilizi (du’aa ya) mtu anayetaka watu wengine wasisikie, mtu anayejivunia au mchezaji, isipokuwa Yeye Humsikiliza tu yule ambaye anaomba du’aa kwa uthibitisho  kutoka moyoni mwake.  Akasema: Je! Alimtaja ‘Alqamah?  Akasema: Naam. [Adab Al-Mufrad Kitaab Ad-Du’aa]

 

 

 

4-Unapomuomba Allaah (‘Azza wa Jalla) du’aa muombe ukitaja Jina na Sifa Yake hii tukufu ya As-Samiy’u kuwa Yeye ni Mwenye Kusikia du’aa yako.  Na katika Qur-aan zimo du’aa kama hizo:

 

 

Nabiy Ibraahiym (‘Alayhis-Salaam) alipoomba baadaya kujenga Al-Ka’bah:

 

وَإِذْ يَرْفَعُ إِبْرَاهِيمُ الْقَوَاعِدَ مِنَ الْبَيْتِ وَإِسْمَاعِيلُ رَبَّنَا تَقَبَّلْ مِنَّا ۖ إِنَّكَ أَنتَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿١٢٧﴾

Na aliponyanyua Ibraahiym na Ismaa’iyl msingi wa Nyumba (Al-Ka’bah): Rabb wetu, Tutakabalie, hakika Wewe ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote.

[Al-Baqarah: 127]

 

 

Na Maryam (‘Alayhas-Salaam) mama wa Nabiy Iysaa ('Alayhis-Salaam) alipoomba:

 

إِذْ قَالَتِ امْرَأَتُ عِمْرَانَ رَبِّ إِنِّي نَذَرْتُ لَكَ مَا فِي بَطْنِي مُحَرَّرًا فَتَقَبَّلْ مِنِّي ۖ إِنَّكَ أَنتَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٣٥﴾

Pale aliposema mke wa ‘Imraan: Rabb wangu, hakika mimi nimeweka nadhiri Kwako kilichomo katika tumbo langu kuwa ni wakfu kukutumikia, basi nitakabalie. Hakika wewe ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote. [Aal-‘Imraan: 35]

 

 

Na Nabiy Zakariyyah (‘Alayhis-Salaam) alipoomba:

 

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُ ۖ قَالَ رَبِّ هَبْ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةً طَيِّبَةً ۖ إِنَّكَ سَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٨﴾

Hapo hapo Zakariyyaa akamwomba Rabb wake, akasema: Rabb wangu Nitunukie kutoka Kwako kizazi chema hakika Wewe ni Mwenye kusikia du’aa yangu. [Aal-‘Imraan: 38]

 

 

 

5-Jikinge na Du’aa isiyosikilizwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ambaye ni As-Samiy’u kama ilivyothibiti katika du’aa ya Sunnah:

 

 

للَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ قَلْبٍ لاَ يَخْشَعُ وَمِنْ دُعَاءٍ لاَ يُسْمَعُ وَمِنْ نَفْسٍ لاَ تَشْبَعُ وَمِنْ عِلْمٍ لاَ يَنْفَعُ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَؤُلآءِ الأَرْبَعِ

 

Allaahumma inniy a’uwdhu bika min-qalbin-laa yakh-sha’u, wamin du’aain-laa yasma’u, wamin nafsin-laa tashba’u, wamin ilmin-laa yanfa’u, a’uwdhu bika min haaulail-arba’i

 

Ee Allaah, hakika mimi najikinga moyo usionyenyekea na du’aa isiyosikizwa na nafsi isiyoshiba na elimu isiyonufaisha, najikinga Kwako dhidi ya haya manne.

 

[Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Swahiyh An-Nasaaiy, Swahiyh Al-Jaami’ (1297)]

 

 

Bali omba Allaah ('Azza wa Jalla) Akunufaisha kwa masikio yako:

 

 

للَّهُمَّ مَتِّعْنِي بِسَمْعِي وَبَصَرِي  وَاجْعَلْهُمَا الْوَارِثَ مِنِّي وَانْصُرْنِي عَلَى مَنْ يَظْلِمُنِي وَخُذْ مِنْهُ بِثَأْرِي

Allaahumma matti’-niy bisam-’iy, wa baswariy, waj-’al-humal-waaritha minniy, wanswurniy ‘alaa man yadhwlimuniy, wa khudh minhu bitha-ariy

 

Ee Allaah, ninufaishe kwa masikio yangu, na macho yangu, na vijaalie viwili hivyo viwe wiratha wangu (viimarishe mpaka kufa kwangu) na ninusuru dhidi ya anayenidhulumu, na nilipizie dhidi yake.

 

[At-Tirmidhiy Taz Swahiyh At-Tirmidhiy (3/188)]

 

 

Na jikinge na shari za masikio:

 

أللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ سَمْعِي وَمِنْ شَرِّ بَصَرِي وَمِنْ شَرِّ لِسَانِي وَمِنْ شَرِّ قَلْبِي وَمِنْ شَرِّ مَنِيِّي

 

Allaahumma inniy a’uwdhu bika min sharri sam-’iy wamin sharri baswariy, wamin sharri lisaaniy wamin sharri qalbiy, wamin sharri maniyyi

 

Ee Allaah, hakika mimi najikinga Kwako shari ya masikio yangu na shari ya macho yangu, na shari ya ulimi wangu, na shari ya moyo wangu, na shari ya manii yangu

 

 

[Abuu Daawuwd , At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy –Swahiyh At-Tirmidhiy (3/166) na Swahiyh An-Nasaaiy (3/1108)]

 

 

 

6-Omba du’aa ya kijikinga na kila shari ambayo kila siku asubuhi na jioni utamdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) kwa Jina na Sifa hii tukufu ya As-Samiy’u; nayo ni du’aa iliyothibiti katika Sunnah kuwa ni katika Adhkaar za asubuhi na jioni; imekuja katika Hadiyth ifuatayo:

 

 عَنْ أَبَانَ بْنِ عُثْمَانَ، قَالَ سَمِعْتُ عُثْمَانَ بْنَ عَفَّانَ، رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ وَهُوَ يَقُولُ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَنْ قَالَ فِي أَوَّلِ يَوْمِهِ أَوْ فِي أَوَّلِ لَيْلَتِهِ بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ثَلَاثَ مَرَّاتٍ لَمْ يَضُرَّهُ شَيْءٌ فِي ذَلِكَ الْيَوْمِ أَوْ فِي تِلْكَ اللَّيْلَةِ‏.‏

 

Amesimulia ‘Abaan bin ‘Uthmaan kwamba kamsikia ‘Uthmaan bin ‘Affaan (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akisema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayesema mwanzoni wa siku yake au usiku wake:

 

بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ

BismiLLaahiLLadhiy laa yadhwuru ma’-Smihi shay-un fil-ardhwi walaa fissamaai wa Huwas-Samiy’ul-‘Aliym

(Kwa jina la Allaah Ambaye hakidhuru kwa jina Lake kitu chochote kile kilicho ardhini, wala mbinguni, Naye ni Mwenye Kusikia yote daima Mjuzi wa yote daima)

 

Mara tatu; hakuna chochote kile kitakachomdhuru siku hiyo au usiku huo.”  [Musnad Ahmad na riwaaya nyenginezo kama hizo za Abu Daawuwd (4/323) [5089, 5088]. At-Tirmidhiy (5/465) [3388], Ibn Maajah [3869], Taz Swahiyh Ibn Maajah (2/332), Swahiyh Abi Daawuwd (5088), Swahiyh Al-Jaami’ (5745)]

 

 

 

 

Share

028-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-QARIYB

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

Alhidaaya.com

 

الْقَرِيب

 

AL-QARIYB

 

 

 

Al-Qariyb: Aliye Karibu daima (kwa ujuzi Wake)

 

 

Jina hili la Allaah ('Azza wa Jalla) la Qariyb limetokea katika Qur-aan likiwa pekee katika Kauli Yake Allaah ('Azza wa Jalla):

 

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu; Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186]

 

 

Na limetokea katika Qur-aan likiwa limeshirkiana na Majina mengineyo katika Kauli Zake Allaah ('Azza wa Jalla):

 

قُلْ إِن ضَلَلْتُ فَإِنَّمَا أَضِلُّ عَلَىٰ نَفْسِي ۖ وَإِنِ اهْتَدَيْتُ فَبِمَا يُوحِي إِلَيَّ رَبِّي ۚ إِنَّهُ سَمِيعٌ قَرِيبٌ ﴿٥٠﴾

Sema: Ikiwa nimepotoka, basi hakika nimepotoka kwa khasara ya nafsi yangu, na ikiwa nimeongoka, basi ni kwa yale Aliyonifunulia Wahy Rabb wangu; hakika Yeye ni Mwenye kusikia yote, Yu Karibu. [Sabaa: 50]

 

Na pia,

 

 

وَإِلَىٰ ثَمُودَ أَخَاهُمْ صَالِحًا ۚ قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ ۖ هُوَ أَنشَأَكُم مِّنَ الْأَرْضِ وَاسْتَعْمَرَكُمْ فِيهَا فَاسْتَغْفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٌ مُّجِيبٌ﴿٦١﴾

Na kwa Thamuwd (Tulimpeleka) ndugu yao Swaalih. Akasema: Enyi kaumu yangu! Mwabuduni Allaah, hamna mwabudiwa wa haki ghairi Yake. Yeye Ndiye Aliyekuanzisheni katika ardhi, na Akakufanyieni makazi humo; basi mwombeni maghfirah, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu Yuko Karibu, Mwenye kuitikia. [Huwd: 61]

 

 

Jina na Sifa hii ya Allaah ('Azza wa Jalla) ni dalili ya ukamilifu na ukaribu wa Allaah ('Azza wa Jalla) kwa waja Wake, na ukaribu na waja ni wa aina mbili.  

 

Kwanza: Ukaribu wa Jumla: Kwa yeyote, kwa elimu Yake, kwa uzoefu Wake, na ulinzi Wake na kushuhudia Kwake, na kuenea kuenea vitu vyote, dhahiri na batini ya hisia na isiyo na hisia Naye Yuko juu ya viumbe Wake. Anasema Allaah ('Azza wa Jalla):

 

 

هُوَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ ۚ يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا ۖ وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ۚ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿٤﴾

Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha Akawa juu (Istawaa) ya ‘Arsh Anajua yale yanayoingia ardhini, na yale yatokayo humo, na yale yanayoteremka kutoka mbinguni, na yale yanayopanda humo, Naye Yu Pamoja nanyi popote mlipo. Na Allaah ni Mwenye kuona yote myatendayo. [Al-Hadiyd: 4]

 

 

Na pia,

 

أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۖ مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ وَلَا خَمْسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمْ وَلَا أَدْنَىٰ مِن ذَٰلِكَ وَلَا أَكْثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمْ أَيْنَ مَا كَانُوا ۖ ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴿٧﴾

Je, huoni kwamba Allaah Anajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini? Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao (kwa ujuzi Wake), na wala watano isipokuwa Yeye ni wa sita wao (kwa ujuzi Wake), na wala chini kuliko ya hivyo, na wala wengi zaidi isipokuwa Yeye Yu pamoja nao (kwa ujuzi Wake) popote watakapokuwa; kisha Siku ya Qiyaamah Atawajulisha yale waliyoyatenda. Hakika Allaah kwa kila kitu ni ‘Aliym. [Al-Mujaadala: 7]

 

 

Pili: Ukaribu maalum: kwa waja Wake, kwa wenye kumuomba, kwa wapenzi Wake, ni ukaribu wenye kuhitajia mapenzi na kunusuru, na kuunga mkono harakati za watu na matulivu yao, na kuitikia du’aa ya waombaji, na kuwataqabalia na kuwalipa waja Wake. Ni ukaribu ambao ukweli wake haufahamiki sawasawa, lakini athari yake inafahamika kwa wema Wake kwa waja Wake, na machungo yake na kuhudhurisha moyo wake katika hali ile aliyepta ukaribu [Tafsiyr Ibn As-Sa’diy (5/491), Al-Haq al-Waadhwih (64) na Fathu Rahiym (44)]

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu; Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186]

 

 

Na pia

 

  فَاسْتَغْفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٌ مُّجِيبٌ﴿٦١﴾

Basi mwombeni maghfirah, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu Yuko Karibu, Mwenye kuitikia. [Huwd: 61]

 

 

 

Faida, Mafunzo Tuyapatayo Na Jinsi Ya Kufanyia Kazi Jina Hili La Allaah; Al-Qariyb:

 

 

1-Ukitaka kuwa karibu na Allaah ('Azza wa Jalla), basi jikurubishe Kwake kwa kumridhisha Yeye Allaah ('Azza wa Jalla) kwa ‘amali Anazozipenda kama kutimiza fardhi khasa kuhifadhi Swalaah na kwa kuiswali kwa wakati wake. Pia kuzidisha ‘ibaadah za Sunnah, kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) kwa wingi, na mengineyo mema na ya khayraat Aliyoyaamrisha Yeye na Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa sababu kuna ukaribu maalum, uliowekwa kwa wale Waumini ambao hufanya kazi kuufikia, na Allaah ('Azza wa Jalla) Amewawekea daraja maalumu wanaojikurubisha Naye; Anasema:

 

 

وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ ﴿١٠﴾ أُولَـٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ ﴿١١﴾ فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ﴿١٢﴾ ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ ﴿١٣﴾ وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ ﴿١٤﴾

 

Na waliotangulia mbele, watatangulia mbele. Hao ndio watakaokurubishwa. Katika Jannaat za taanisi. Kundi kubwa katika wa awali. Na wachache katika wa mwishoni [Al-Waaqi’ah: 10 – 14]

 

Ibn Kathiyr amesema kuhusu

وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ ﴿١٠﴾ أُولَـٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ ﴿١١﴾

 

Wanaotangulia duniani kutenda khayraat ni kama Alivyoamrisha Allaah ('Azza wa Jalla) katika Aayah kadhaa. [Aal-‘Imraan: (133), Al-Hadiyd: (22)]. Basi atakayetangulia kwa khayraat katika dunia hii atakuwa mwenye kutangulia Aakhirah katika kukirimiwa kwani jazaa ya thawabu inalingana na aina ya ‘amali utendazo, na kama unavyotenda basi nawe utatendewa hivyo hivyo.

 

Akasema pia, wale walio karibu na Allaah ('Azza wa Jalla) ni wale ambao hutekeleza fardhi na wanatekeleza ‘amali za Mustahabb (yanayopendekezwa) na kujiepusha na na nawaahiy (yaliyokatazwa) na yanayochukiza na hata hujiepusha na mambo yaliyohurusika (mubaah: hayana dharura kuyatenda au kuyaacha).    Baadhi ya Salaf wamesema: Wao ni watu wa kwanza kwenda Msikitini na wa kwanza kutoka kwenda jihaad kwa ajili ya Allaah.

 

 

2-Jiandalie Aakhirah yako kwa khayraat za kila aina ili uwe miongoni mwa Al-Muqarrabuwn upate neema zake pindi mauti yatakapokufikia na ili usijekuwa kinyume chake. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Yu Qariyb katika hali ya Sakaraatul-Mawt ya waja, Anabainisha hali ya aina ya watu wawili hao katika Kauli Zake:

 

فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ ﴿٨٣﴾ وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ ﴿٨٤﴾ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَـٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ ﴿٨٥﴾ فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ ﴿٨٦﴾ تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٨٧﴾ فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ ﴿٨٨﴾ فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ ﴿٨٩﴾ وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ ﴿٩٠﴾ فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ ﴿٩١﴾ وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ ﴿٩٢﴾ فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ ﴿٩٣﴾ وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ ﴿٩٤﴾ إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ ﴿٩٥﴾ فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ ﴿٩٦﴾

Basi mbona roho ifikapo kooni. Nanyi wakati huo mnatazama. Nasi Tuko karibu naye zaidi kuliko nyinyi, lakini hamuoni. Basi kwa nini ikiwa hamuwajibiki malipo? Muirudishe roho (mwilini mwake), mkiwa ni wakweli? Basi akiwa miongoni mwa waliokurubishwa. Basi mapumziko ya raha na manukato na Jannah ya neema. Na kama akiwa miongoni mwa watu wa kuliani. Basi: Salaam juu yako uliye katika watu kuliani. Na kama akiwa miongoni mwa wakadhibishaji waliopotoka. Basi mapokezi yake ni maji ya moto yachemkayo. Na kuunguzwa na moto uwakao vikali mno. Hakika hii bila shaka ni haki yenye yakini. Basi sabbih kwa Jina la Rabb wako Adhimu, Mkuu kabisa. [Al-Waaqi’ah: 83 – 96]

 

 

 

3-Kumbuka kuwa Qiyaamah kiko karibu, na Allaah ('Azza wa Jalla) Ambaye Al-Qariyb Ametahadharisha ukaribu wake, kwa hiyo usije kughafilika na Qiyaamah ukasahau kujiandaa kwa ajili yake. Anasema Allaah ('Azza wa Jalla):

 

اقْتَرَبَ لِلنَّاسِ حِسَابُهُمْ وَهُمْ فِي غَفْلَةٍ مُّعْرِضُونَ ﴿١﴾

Imewakaribia watu hesabu yao, nao wamo katika mghafala wanakengeuka (na wanapuuza) [Al-Anbiyaa: 1]

 

Na Anasema pia Allaah ('Azza wa Jalla):

 

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ ﴿١﴾

Saa imekaribia na mwezi umepasuka.  [Al-Qamar: 1]

 

 

4-Unaposibiwa na mithani ukawa katika dhiki, kumbuka kuwa Allaah ('Azza wa Jalla) ni Qariyb nawe kwa ujuzi Wake, kwa hiyo kimbilia kumwelekea Yeye kwa Istighfaar nyingi na kutubia Kwake ili Akuondoshee dhiki zako na Akujaalie faraja. Kisha mnyenyekee na kumlalamikia shida na dhiki zako na kumuomba du’aa kwani Yeye Anajua na Anasikia na Yuko Karibu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)

  فَاسْتَغْفِرُوهُ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ ۚ إِنَّ رَبِّي قَرِيبٌ مُّجِيبٌ﴿٦١﴾

Basi mwombeni maghfirah, kisha tubieni Kwake. Hakika Rabb wangu Yuko Karibu, Mwenye kuitikia. [Huwd: 61]

 

 

5-Itikia wito wa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) wa kumwelekea Yeye Pekee katika kumuomba du’aa kwani Yeye ni Qariyb Anaitikia du’aa za wenye kumuomba kama Anavosema:

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu; Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186]

 

Na pia amka usiku wa manane wakati ambao Allaah ('Azza wa Jalla) huwa Qariyb na waje Wake kwa kuteremka mbingu ya dunia kuwasikiliza wenye haja Awataqabalie, wenye kuomba maghfirah Awaghufurie, wenye shida Awaondoshee. Hakika hii ni neema kubwa miongoni mwa neema za Waumini:

 

عنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَنْزِلُ رَبُّنَا تَبَارَكَ وَتَعَالَى كُلَّ لَيْلَةٍ إِلَى السَّمَاءِ الدُّنْيَا حِينَ يَبْقَى ثُلُثُ اللَّيْلِ الْآخِرُ يَقُولُ: مَنْ يَدْعُونِي فَأَسْتَجِيبَ لَهُ، مَنْ يَسْأَلُنِي فَأُعْطِيَهُ، مَنْ يَسْتَغْفِرُنِي فَأَغْفِرَ لَهُ)) البخاري و مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu)  kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah Tabaaraka wa Ta’aalaa Huteremka (kwa namna inavyolingana na utukufu Wake) kila siku katika mbingu ya dunia inapobakia thuluthi ya mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba du’aa Nimuitike? Nani Ananiomba jambo Nimpe? Nani ananiomba maghfirah Nimghufurie?)) [Al-Bukhaariy, Muslim

 

 

 

6-Tambua kuwa Allaah ('Azza wa Jalla) Yu Qariyb kwa waja Wake kulikoni  mshipa wa koo kama Anavosema:

 

وَلَقَدْ خَلَقْنَا الْإِنسَانَ وَنَعْلَمُ مَا تُوَسْوِسُ بِهِ نَفْسُهُ ۖ وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنْ حَبْلِ الْوَرِيدِ﴿١٦﴾

Na kwa yakini Tumemuumba insani na Tunajua yale yanayowaza nafsi yake, na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa koo. [Qaaf: 16]

 

Hivyo basi, tahadhari kutenda maovu kwa siri au kwa dhahiri na hata kutamka kauli ovu, au hata neno moja kwa sababu linarekodiwa na Malaika Aliowapa kazi hiyo. Anaendelea kusema hayo katika Suwrah hiyo tukufu ya Qaaf:

 

إِذْ يَتَلَقَّى الْمُتَلَقِّيَانِ عَنِ الْيَمِينِ وَعَنِ الشِّمَالِ قَعِيدٌ﴿١٧﴾ مَّا يَلْفِظُ مِن قَوْلٍ إِلَّا لَدَيْهِ رَقِيبٌ عَتِيدٌ﴿١٨﴾

 

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni. Hatamki kauli yeyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi). [Qaaf: 17 – 18]

 

 

 

7-Timiza adabu za kuomba du’aa kwa Allaah ('Azza wa Jalla), yaani unapomuomba du’aa Allaah ('Azza wa Jalla), usiombe kwa sauti kubwa ya kusikika kwa watu amekataza hivyo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Akataja Jina na Sifa hii tukufu ya Qariyb katika Hadiyth;

 

 

عَنْ أَبِي مُوسَى الأَشْعَرِيِّ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: كُنَّا مَعَ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَكُنَّا إِذَا أَشْرَفْنَا عَلَى وَادٍ هَلَّلْنَا وَكَبَّرْنَا. ارْتَفَعَتْ أَصْوَاتُنَا فَقَالَ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ: ((يَا أَيُّهَا النَّاسُ ارْبَعُوا عَلَى أَنْفُسِكُمْ فَإِنَّكُمْ لاَ تَدْعُونَ أَصَمَّ ولاَ غَائِبًا إِنَّهُ مَعَكُمْ ، إِنَّهُ سَمِيعٌ قَرِيبٌ تَبَارَكَ اسْمُهُ وَتَعَالَى جَدُّهُ))

 

Amesimulia Abu Muwsaa Al-Ash’ariyy (رضي الله عنه): Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na tukawa kila tukipanda bonde, tunafanya tahliyl (Laa Ilaaha Illa-Allaah), na tunaleta takbiyr (Allaahu Akbar). Zikapanda sauti zetu, na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Enyi watu, zihurumieni nafsi zenu, kwani hamumwombi kiziwi wala asiyekuwepo, hakika Yeye Yupo nanyi (kwa Ujuzi Wake), hakika Yeye Ni Mwenye Kusikia yote, Yupo Karibu, Limebarikika Jina Lake na Umetukuka Ujalali Wake.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

Share

029-Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake أسماء الله الحسنى وصفاته: AL-MUJIYB

 

أسماء الله الحسنى وصفاته

Majina Ya Allaah Mazuri Na Swifa Zake

 

 

Alhidaaya.com

 

الْمُجِيب

 

AL-MUJIYB

 

 

 

 

Al-Mujiyb: Mwenye Kuitikia

 

 

Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى) Ndiye mwenye kujibu maombi ya wenye kuomba, na kupokea ‘Ibaadah za wenye kuomba, Yeye (سُبْحانَهُ وَتَعالى) Hamkatishi tamaa Muumini kwa du’aa yake wala Harudishi maombi ya Muislaam. Allaah Al-Mujiyb Anaomba aombwe na waja Wake wote katika maombi ya Dini na dunia yao katika chakula, mavazi, makazi kama wanavyoomba hidaaya, maghfirah, islahi na mengineyo.  Majibu ya Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى) yako aina mbili:

 

 

Kwanza: Majibu ya jumla kwa waombaji wote:

 

 

Anaitikia maombi ya waja Wake vyovyote walivyo, popote walipo, katika hali yoyote, kama Alivyowaahidi katika ahadi Yake ya kweli ambayo haendi kinyume nayo, Anaposema Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى):

 

وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَسْتَكْبِرُونَ عَنْ عِبَادَتِي سَيَدْخُلُونَ جَهَنَّمَ دَاخِرِينَ﴿٦٠﴾

Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari katika kuniabudu wataingika Jahanam wadhalilike. [Ghaafir: 60]

 

Hilo ni jibu la wote walioomba.

 

 

Pili: Majibu maalum:

 

Wenye kumuomba Allaah Al-Mujiyb na wenye kufuata Shariy’ah Zake, wenye ikhlaasw katika ‘ibaadah  na maombi yao Anaposema Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى):

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu; Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186]

 

Basi waniitikie Mimi

 

Yaani: Wanitii amri Zangu, na waniombe, na pindi watakaponiomba, nitawajibu.

 

 

Naye Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى) ni Mwenye kuwajibu majibu maalum kwa wenye haja; Anasema:

 

أَمَّن يُجِيبُ الْمُضْطَرَّ إِذَا دَعَاهُ وَيَكْشِفُ السُّوءَ وَيَجْعَلُكُمْ خُلَفَاءَ الْأَرْضِ ۗ أَإِلَـٰهٌ مَّعَ اللَّـهِ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ ﴿٦٢﴾

Au nani Anayemuitika mwenye dhiki mno anapomwomba, na Akamuondoshea ouvu na Akakufanyeni makhalifa wa ardhi? Je, yuko mwabudiwa pamoja na Allaah? Ni machache mno mnayokumbuka. [An-Naml: 62]

 

 

Na kwa kila aliyekata matarajio Yake katika viumbe Wake na akaelemeza moyo wake kwa Rabb wake, hupata majibu kulingana nayo. Anasema Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى):

 

يَسْأَلُهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ ﴿٢٩﴾

Wanamuomba Yeye kila aliyekuweko mbinguni na ardhini, kila siku Yeye Yumo katika kujaalia mambo.  [Ar-Rahmaan: 29]

 

Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّم) akasema katika Hadiyth:

 

 

حَدَّثَنَا هِشَامُ بْنُ عَمَّارٍ، حَدَّثَنَا الْوَزِيرُ بْنُ صَبِيحٍ، حَدَّثَنَا يُونُسُ بْنُ حَلْبَسٍ، عَنْ أُمِّ الدَّرْدَاءِ، عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ ـ صلى الله عليه وسلم ـ فِي قَوْلِهِ تَعَالَى ‏كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ‏.‏ قَالَ ‏"‏ مِنْ شَأْنِهِ أَنْ يَغْفِرَ ذَنْبًا وَيُفَرِّجَ كَرْبًا وَيَرْفَعَ قَوْمًا وَيَخْفِضَ آخَرِينَ ‏"‏ ‏.‏

 

Amesimulia Abu Dardaa kwamba Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّم) amesema kuhusu Kauli ya Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى):

 

كُلَّ يَوْمٍ هُوَ فِي شَأْنٍ ﴿٢٩﴾

Kila siku Yeye Yumo katika kujaalia mambo.  [Ar-Rahmaan: 29]

 

“Kwa shani Yake Anaghufuria madhambi, na Anafariji dhiki, na Anawanyanyua watu na kuwaakuwaangusha wengine.”   [Ibn Maajah Kitaab Al-Muqaddimah]

 

 

Humnyanyua aliyevunjika, humtajirisha tajiri, na hushiba mwenye njaa na humvisha aliye uchi na humponya mgonjwa, na humnusuru mdhulumiwa na humvunja Jabari. Wote humuomba Yeye Allaah (سُبْحانَهُ وَتَعالى) juu ya kuwa wametofautiana, Naye  Hawarudishi katika muradi wao Naye ni mwenye kuwatosheleza.

 

 

 

 

 

 

Share