Kitaab At-Tawhiyd (Word Doc) Chapisho La 2 Kimehaririwa 1438H (2017M)

 

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

Share

00-Kitaab At-Tawhiyd: Historia Fupi Ya Imaam Muhammad Bin ‘Abdil-Wahhaab

00-Historia Fupi Ya Imaam Muhammad Bin ‘Abdil-Wahhaab[1]

 

 

 Asili yake

 

Jina lake ni Abul-Husayn Muhammad bin ‘Abdil-Wahhaab bin Sulaymaan bin ‘Aliy Musharrif Al-Wuhaybiy. Kabila lake ni Bani Tamiym. Amezaliwa mwaka 1115 H (1704 M) katika mji ya ‘Uyaynah kijiji cha Yamaamah ndani ya Najd, kaskazini Magharibi ya mji wa Riyadhw, Saudi Arabia. Ametoka katika familia ya Wanachuoni kwani baba yake ‘Abdul-Wahhaab alikuwa ni Mwanachuoni maarufu wa Najd na Qaadhwiy wa mji huo.

 

 

Elimu Yake

 

Alijifunza kusoma Qur-aan alipokuwa na umri mdogo na akaihifadhi akiwa chini ya umri wa miaka kumi. Na Allaah (سبحانه وتعالى) Alimjaalia kuwa na uhodari na akili nzuri, wepesi wa kufahamu na kumaizi jambo au somo. Alipendezewa mno kusoma kazi za Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah na mwanafunzi wake Ibn Al-Qayyim (رحمهما الله).

Alifanya bidii kwenye masomo yake na kuendelea kujifunza chini ya usimamizi wa baba yake. Akajifunza elimu ya Dini chini ya Wanachuoni walioko mjini mwake wakiwemo baba yake na ‘ammi yake. Alisafiri kutoka kwenda Madiynah kusoma chini ya Wanachuoni wakubwa wa huko akiwemo; Shaykh ‘Abdullaah bin Ibraahiym bin Ash-Shamariyy, na Mwanachuoni maarufu wa India Shaykh Muhammad Hayaat Al-Sindi. Alikwenda Makkah pia na alitekeleza Hajj. Hatimaye akaelekea Baswrah (Kaskazini Iraq) kutafuta elimu zaidi akasoma chini ya Wanachuoni wa huko akawa maarufu kwa mijadala baina yake na Wanachuoni.

 

Harakaat Na Mitihani

 

Watu wa Najd walikuwa katika shirki na bid’ah (uzushi). Walikuwa wakiabudu waabudiwa wengi na kuabudu makaburi, miti, mawe, mapango, majini na mashaytwaan, waja wema waliojulikana kama ni mawalii. Uchawi na unajimu (utabiri wa nyota) ulisambaa pia. Hakuna aliyekataza ‘iIbaadah potofu hizo kwani watu walikuwa katika kuchuma manufaa na starehe za dunia zaidi na wakakhofia kuyapoteza hayo. Hivyo Shaykh akaona umuhimu mkubwa uliohitajika kuwarudisha watu katika manhaj ya Qur-aan na Sunnah. Akaanza kuwalingania watu katika Tawhiyd - kumpwekesha Allaah (سبحانه وتعالى) bila ya kumshirikisha na lolote katika ‘ibaadah. Akaazimia kujitumikisha peke yake kwa uvumilivu katika konde. Akajua hakuna lolote kitachofaulu kufanyika ila jihaad katika njia ya Allaah.

 

Shaykh alikumbana na mitihani, misukosuko, na vitisho, lakini alikuwa ameshategemea hali hiyo kumfikia na alikuwa tayari kukabaliana nayo kwani alitambua kuwa hilo ni jambo lisiloepukika kwa kila mlinganiaji kwani ndio hali waliyokutana nayo Manabii wote, na Salafus-Swaalih (waja wema waliotangulia).

 

Miongoni mwa mitihani aliyokumbana nayo ni kutokana na Wanachuoni dhaifu wasiokuwa na hoja ambao walimpinga na kumfanya akabiliane na misukosuko, vitisho na kukasirikiwa. Pia alikabiliana na misukosuko na mateso chini ya mikono ya madhalimu wa Huraymilaa. Na alipowashawishi watawala wahukumu madhalimu kwa Shariy’ah ya Kiislamu, ilisababisha baadhi ya watu kuyaweka maisha yake khatarini lakini Allaah (سبحانه وتعالى) Alimnusuru.

Aliamua kurudi kwao ‘Uyaynah, ambako kipindi hicho kulikuwa chini ya utawala wa mtoto wa Mfalme ‘Uthmaan bin Muhammad bin Mu’ammar, ambaye alimpokea Shaykh kwa ukarimu na kumuahidi kumuunga mkono na kumsaidia kuwaita watu katika Uislamu.

 

Akaendelea kufundisha na kutoa da’wah hatimaye akashawishika kidhati na kwa vitendo kuondoa dini ya waabudiwa wengi pale alipoona baadhi ya watu ni wagumu kurudi katika Uislamu. Aliweza kumshawishi gavana wa mji huo kulivunja zege lililojengewa juu ya kaburi la Zayd bin Al-Khattwaab ambaye alikuwa ni kaka wa ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنهما). Akavunjavunja mangome mengineyo, mapango, miti n.k. Akaamrisha Shariy’ah ya Kiislamu itekelezwe.

Shaykh aliendelea na harakati zake za kauli na ‘amali ambazo zilimfanya azidi kuwa maarufu. Hatimaye akawa Jaji (Qaadhwiy) wa mji wa ‘Uyaynah. Lakini hakuweza kuendelea hapo kwani Mfalme alishawishiwa na viongozi wa miji ya jirani amuue Shaykh kwa vile hawakupendezewa na da’wah yake. Ikabidi afukuzwe katika mji huo.

 

Akakaribishwa mji wa Ad-Dir’iyyah ambao ulikuwa ni jirani yake. Huko akakaribishwa ingawa kwanza alitiliwa shaka. Alifikia kwa mja mwema aliyempokea ila alimkhofia kutokukubaliwa na mtoto wa Mfalme Muhammad bin Sa’uwd.  Khabari zikamfikia kwanza mke wa Ibn Sa’uwd ambaye alikuwa mkarimu na mwenye taqwa. Akamfahamisha mumewe kwa kumwambia, “Hii ni tawfiyq kubwa umeletewa kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى); huyo ni mtu ambaye anawaita watu katika Uislamu, anawaita katika Qur-aan na Sunnah za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Tawfiyq iliyoje? Mkimbilie haraka na umuunge mkono wala usimpinge au kumkataza kwa hayo.” Muhammad bin Sa’uwd akakubali ushauri wa mkewe na akaenda kwa Shaykh na akafanya mkataba naye kwamba asiondoke nchini hapo. Ndipo Shaykh akaweka makazi yake hapo na kuendelea na da’wah. Akaendelea na harakati za da’wah hapo Dar’iyyah. Akaheshimika na kupendwa mno na akaungwa mkono na watu. Da’wah yake iliwaathiri na kuwapendeza mno watu. Ikaenea katika nchi za Kiislamu na nyinginezo. Wakimiminika watu kufika hapo Dar’iyyah kujifunza kwake

 

Kama ijulikanavyo, kila jema halikosi mitihani. Wakatokeza wapinzani na waliokuwa na chuki naye. Kulikuweko waliompinga da’wah yake ya kuondosha shirki na bid’ah na kuwaita watu katika Tawhiyd. Kuna wengine waliompinga kabisa kwa sababu ya kukhofu kufukuzwa katika nafasi au vyeo vyao vya kazi. Kwa hiyo wengine walimpinga kwa ajili ya Dini, na wengine walimpinga kisiasa. Wapinzani wake walimzushia ya kumzushia walifika hadi kudai kwamba Shaykh alikuwa ni mfuasi wa Khawaarij. Na mara nyingine wakimlaumu bure bila ya dalili na nje ya upeo wa elimu zao. Hivyo yakaweko malumbano na majibishano yaliyoendelea katika mijadala kadhaa. Shaykh aliwaandikia kuwajibu madai yao, na wao walimrudishia majibu na yeye akawa akiwathibitishia ufahamu wao mbaya wa shariy’ah na Dini kwa ujumla kwa dalili. Ndipo wingi wa maswali na majibu yakawajumuisha watu na wakazidi kuongezeka. Baadhi ya mijadala hiyo iliandikwa na kuchapishwa katika vitabu.

 

Athari Ya D’awah Yake

 

Da’wah yake ya takriban miaka 50 imedhihirika na kuleta athari kubwa kwanza kwa Waislamu wa zama hizo. Watu waliacha kuabudu makaburi, miti, mawe, majini, utabiri wa nyota na kila aina ya shirki. Imewatoa pia watu katika ujinga wa kufuata mila za mababu bila ya dalili.  Maamrisho ya mema na makatazo ya maovu yakalinganiwa katika Misikiti. Na hapo msimamo wa Qur-aan na Sunnah ukahuishwa na shirki na bid’ah zikatoweka. Amani na utulivu ukawafunika watu kila mahali. Hadi zama hizi da’wah yake imekuwa na umuhimu mkubwa katika jamii ya Kiislamu. Vijana khasa kutoka nchi za Magharibi na zaidi wale wanaosilimu wamekuwa na hamasa na shauku kubwa ya kujifunza Dini iliyo sahihi na si ile iliyochanganywa na shirki na bid’ah. Kwa hiyo, mafundisho ya msimamo wake wa Ahlus-Sunnah wal-Jama’ah umekuwa ni jambo lililopewa kipaumbele katika lengo la kutafuta elimu kwa Waislamu wanaotafuta na kupenda haki.

Kazi Zake

 

Ameandika vitabu vingi vya mafunzo mbali mbali lakini alitilia mkazo zaidi katika somo la Tawhiyd na ‘Aqiydah. Na alitumia hikmah ya kuandika vitabu vidogo vidogo vilivyokusanya nukta mbalimbali muhimu kabisa kuhusiana na misingi ya Dini. Vilikuwa ni mukhtasari wa maudhui aliyotaka kuidhihirisha. Na vitabu hivyo vimekuja kufafanuliwa kwa kushereheshwa na ‘Ulamaa kadhaa na vimekuwa vina umuhimu mno katika vyuo vya Kiislamu vinavyofuata mwenendo wa Ahlus-Sunnah wal-Jama’ah.

 

Vifuatavyo ni baadhi ya vitabu vyake maarufu.

Vinne vya mwanzo ni mashuhuri zaidi. Na vinginevyo vimekusanywa na kujumuishwa katika ‘Maj’muw’at Mu-allafaatil-Imaam Muhammad bin ‘Abdil-Wahhaab’.

1.      Kitaabut-Tawhiyd - kitabu hiki kimekuwa mashuhuri mno na kimeenea sana na somo lake limekuwa ni lenye kutoa mafunzo muhimu kuhusu kumpwekesha Allaah na kuepukana na shirki.

2.      Al-Uswuul Ath-Thalaathah – kitabu kitoacho mafunzo kuhusu asili au misingi ya Uislamu.

3.      Al-Qawaaid Al-Arba’- kinatoa mafunzo ya kanuni za ufahamu wa shirki kwa ujumla.

4.      Kashf Ash-Shubuhaat - kinakanusha hoja zinazojulikana na watetezi wa shirki na bid’ah.

5.      Mukhtaswar Al-Inswaaf was-Sharh Al-Kabiyr.

6.      Mukhtaswar Zaad Al-Ma’aad.

7.      Mukhtaswar As-Siyrah.

8.      Mukhtaswar al-Fat-h.

9.       Masaail Al-Jaahiliyyah.

10.  Adaab Al-Mashiy ilaa As-Swalaah.

11.  Nawaaqidhw Al-Islaam.

 

Wanafunzi Wake

 

Alikuwa na wanafunzi wengi mno. Miongoni mwao ni watoto na wajukuu wake ambao waliendeleza kazi yake ya da’wah na Jihaad katika njia ya Allaah, walifungua vyuo karibu na kwao wakifunza watu masomo ya Dini. Kati ya watoto wake ni Al-Husayn, ‘Aliy, ‘Abdullaah na Ibraahiym. Na kati ya wajukuu wake ni ‘Aliy bin Al-Husayn, na pia ‘Abdur-Rahmaan bin Al-Hasan aliyeandika kitabu cha ‘Fat-h Al-Majiyd Sharh Kitaab At-Tawhiyd’. Wanafunzi wake wengineo ni ‘Abdul-‘Aziyz bin Muhammad bin Sa’uwd, Hamad bin Naaswir bin Mu’ammar na ‘Abdul-‘Aziyz bin ‘Abdillaah bin Husayn.

 

Familia Yake

Alikuwa na watoto sita; Al-Husayn, ‘Abdullaah, Al-Hasan, ‘Aliy, Ibraahiym, ‘Abdul-‘Aziyz.

Shaykh anatokana na kizazi kinachojulikana kwa ‘Aal-Shaykh’ ambacho kimetoa Wanachuoni kadhaa akiwemo Shaykh Muhammad bin Ibraahiym Aal-Shaykh aliyekuwa Mufti mkuu wa awali Saudi Arabia na Shaykh ‘Abdul-‘Aziyz Aal-Shaykh  ambaye ni Mufti mkuu wa sasa.

 

Kifo Chake

 

Alifariki mwaka 1206 H (1792 M) akiwa na umri wa miaka 91. Rahmah za Allaah ziwe juu yake na Allaah Amruzuku Jannah ya Firdaws. Aamiyn.

 

 

 

 

[1]Marejeo: Imaam Muhammad bin ‘Abdil-Wahhaab Da’watuhuu wa Siyraatuhu - Shaykh Ibn Baaz.

 

Share

01-Kitaab At-Tawhiyd: Fadhila Za Tawhiyd

 

Mlango Wa 1

فَضْلُ اَلتَّوْحِيدِ

Fadhila Za Tawhiyd


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli Ya Allaah Ta’aalaa:

 وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ ﴿٥٦﴾

((Na Sikuumba majini na wana Aadam isipokuwa waniabudu)) [Adh-Dhaariyaat (51: 56)]

 

وَقَوْلُهُ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ ۖ

((Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Rasuli (alinganie) kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaghuti)) [An-Nahl (16: 36).]

 

 وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

  وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۚ  

((Na Rabb wako Amehukumu kwamba: “Msiabudu isipokuwa Yeye Pekee na (Ameamrisha) kuwafanyia ihsaan wazazi wawili)) [Al-Israa (17: 23)]

 

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

 وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ  

((Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote))  [An-Nisaa (4: 36)] 

 

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا ۖ وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُم مِّنْ إِمْلَاقٍ ۖ نَّحْنُ نَرْزُقُكُمْ وَإِيَّاهُمْ ۖ وَلَا تَقْرَبُوا الْفَوَاحِشَ مَا ظَهَرَ مِنْهَا وَمَا بَطَنَ ۖ وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿١٥١﴾

((Sema: “Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote, na muwafanyie ihsaan wazazi wawili, na wala msiwaue auladi wenu kutokana na umasikini. Sisi Tunakuruzukuni pamoja nao. Na wala msikaribie machafu yaliyo dhahiri na yaliyofichika. Na wala msiue nafsi ambayo Ameiharamisha Allaah (kuiua) isipokuwa kwa haki (ya shariy’ah). Hivyo ndivyo Alivyokuusieni kwayo mpate kutia akilini”))

 

وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ حَتَّىٰ يَبْلُغَ أَشُدَّهُ ۖ وَأَوْفُوا الْكَيْلَ وَالْمِيزَانَ بِالْقِسْطِ ۖ لَا نُكَلِّفُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا ۖ وَإِذَا قُلْتُمْ فَاعْدِلُوا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۖ وَبِعَهْدِ اللَّـهِ أَوْفُوا ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ﴿١٥٢﴾

((“Na wala msiikaribie mali ya yatima isipokuwa kwa njia ya ihsaan mpaka afikie umri wa kupevuka. Na timizeni kipimo na mizani kwa uadilifu. Hatukalifishi nafsi isipokuwa kadiri ya uwezo wake. Na mnaposema basi fanyeni uadilifu japokuwa ni jamaa wa karibu. Na timizeni ahadi ya Allaah. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kukumbuka))

 

 وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ ذَٰلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٥٣﴾

((“Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. Hivyo ndivyo Alivyokuusieni (Allaah) kwayo mpate kuwa na taqwa”)) [Al-An-‘aam (6: 151-153)]

 

قَالَ اِبْنُ مَسْعُود (رضي الله عنه): مَنْ أَرَادَ أَنْ يَنْظُرَ إِلَى وَصِيَّةِ مُحَمَّدٍ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) اَلَّتِي عَلَيْهَا خَاتَمُهُ فَلْيَقْرَأْ قَوْلَهُ تَعَالَى: ((قُلْ تَعَالَوْا أَتْلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمْ عَلَيْكُمْ ۖ أَلَّا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ )) إِلَى قَوْلِهِ ((وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ۚ...)) الآيَةَ.

Amesema Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه): “Anayetaka kuangalia wasiya wa Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ambao ulikuwa na muhuri wake, basi asome kauli za Allaah: ((Sema: “Njooni nikusomeeni yale Aliyoyaharamisha Rabb wenu kwenu. Kwamba msimshirikishe na chochote…)) hadi kauli Yake: ((Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka, basi ifuateni. Na wala msifuate njia nyinginezo zitakufarikisheni na njia Yake. … ))  mpaka mwisho wa Aayah [At-Tirmidhiy (3080) At-Twabaraaniy katika Mu’jam Al-Awsatw (1208) na amesema At-Tirmidhiy : Hii ni Hadiyth Hasan Ghariyb]

 

عَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: كُنْتُ رَدِيفَ اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) عَلَى حِمَارٍ فَقَالَ لِي: ((يَا مُعَاذُ؟ أَتَدْرِي مَا حَقُّ اَللَّهِ عَلَى الْعِبَادِ، وَمَا حَقُّ الْعِبَادِ عَلَى اَللَّهِ؟)) قُلْتُ اَللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ، قَالَ: ((حَقُّ اَللَّهِ عَلَى الْعِبَادِ أَنْ يَعْبُدُوهُ، وَلاَ يُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا، وَحَقُّ الْعِبَادِ عَلَى اَللَّهِ أَنْ لاَ يُعَذِّبَ مَنْ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا)) قُلْتُ يَا رَسُولَ اَللَّهِ أَفَلاَ أُبَشِّرُ اَلنَّاسَ؟ قَالَ: ((لاَ تُبَشِّرْهُمْ فَيَتَّكِلُوا)) أَخْرَجَاهُ فِي اَلصَّحِيحَيْنِ

Imepokelewa kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) amesema: Nilikuwa nyuma ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) juu ya punda akasema: ((Ee Mu’aadh! Unajua nini haki ya Allaah juu ya waja Wake, na nini haki ya waja juu ya Allaah?)) Nikajibu: Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi: Akasema: ((Haki ya Allaah kwa waja wake ni kwamba wamwabudu na wasimshirikishe na chochote. Na haki ya waja kwa Allaah ni kwamba Hatomwadhibu yeyote ambaye hamshirikishi na chochote)). Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Niwabashirie watu? Akasema: ((Usiwabashirie wasije kuitegemea)) [wakaacha kufanya juhudi katika ‘ibaadah])) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Hekima ya kuumbwa majini na wana Aadam.

 

 

2-Al-‘Ibaadah inamaanisha (hususani) Tawhiyd kwani ndio mada kuu ya hoja (hapo juu) na kinyume chake ni shirki ambayo humbaidisha mtu na Allaah (سبحانه وتعالى) na ndio jambo walotatizana Rusuli na washirikina.

 

 

3-Asiyetekeleza masharti ya Tawhiyd, atakuwa hajamwabudu Allaah (سبحانه وتعالى) ipasavyo kwa sababu katika Tawhiyd tu ndio huthibitika maana ya kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَلَا أَنتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ ﴿٣﴾

((“Na wala nyinyi si wenye kuabudu Yule Ninayemwabudu)) [Al-Kaafiruwn (109: 3)]

 

 

4-Hekima ya kutumwa Rusuli.

 

 

5-Ujumbe huo (wa Tawhiyd) umefikishwa kwa kila ummah.

 

 

6-Dini ya Rusuli ni moja (haitofautiani).

 

 

7-Suala lenye umuhimu mkubwa hapa ni kwamba, kumwabudu Allaah hakutambuliki pasina kukanusha twaghuti. Hapo ndipo kwenye maana ya kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَمَن يَكْفُرْ بِالطَّاغُوتِ وَيُؤْمِن بِاللَّـهِ فَقَدِ اسْتَمْسَكَ بِالْعُرْوَةِ الْوُثْقَىٰ

((Basi atakayemkanusha twaghuti na akamwamini Allaah kwa hakika atakuwa ameshikilia imara kishikilio madhubuti kisichovunjika)) [Al-Baqarah (2: 256)]

 

 

8-Neno ‘twaghuti’ humaanisha kwa ujumla kila kitu kinachoabudiwa asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى), (na kinachovuka mipaka katika ‘ibaadah).

 

 

9-Salaf walitambua umuhimu mkubwa wa Aayah tatu katika Suwrat Al-An’aam kwamba ni Muhkamaat. Aayah hizi zimejumuisha mambo kumi na la awali ni kukatazwa shirki.

 

 

10-Aayah za Muhkamaat katika Suwrat Al-Israa ambazo ni kuanzia Aayah 22 hadi 39, zina mambo kumi na nane, na Allaah (سبحانه وتعالى) Anaanza kwa kauli Yake:

 

لَّا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَقْعُدَ مَذْمُومًا مَّخْذُولًا ﴿٢٢﴾

((Usifanye pamoja na Allaah muabudiwa mwengine, ukaja kushutumiwa na mwenye kutelekezwa mbali (motoni)) [Al-Israa (17: 22)]

 

Na Anayahitimisha kwa kusema:

وَلَا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتُلْقَىٰ فِي جَهَنَّمَ مَلُومًا مَّدْحُورًا ﴿٣٩﴾

((Na wala usifanye pamoja na Allaah muabudiwa mwengine ukaja kutupwa katika Jahannam hali ya kuwa mwenye kulaumiwa na kuwa mardudi (na rahmah ya Allaah)) [Al-Israa (17: 39)]

 

 Na Allaah Ametubainishia umuhimu wake kwa kauli Yake:

 

ذَٰلِكَ مِمَّا أَوْحَىٰ إِلَيْكَ رَبُّكَ مِنَ الْحِكْمَةِ ۗ

((Hayo ni miongoni mwa hikmah ambayo Amekufunulia Wahy Rabb wako)) [Al-Israa (17: 39)]

 

 

11-Aayah ya Suwrah An-Nisaa ambayo imeitwa Aayah za haki kumi. Allaah (سبحانه وتعالى) Amezianza kwa kusema:

 

وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ

((Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote)) [An-Nisaa (4: 36)]

 

 

12-Tanbihi ya wasiya wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) wakati wa kufariki kwake.

 

 

13-Kuzijua haki za Allaah (سبحانه وتعالى) juu yetu.

 

 

14-Kuzijua haki za waja juu Yake pindi wakitekeleza haki Zake.

 

 

15-Maswahaba wengi hawakuwa wakijua jambo hili.

 

 

16-Ruhusa ya kuficha elimu inapokuwa na manufaa. Kama hapo ilikuwa ni kwa ajili wajitahidi zaidi kumwabudu Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

17-Inapendekezeka kumbashiria Muislamu khabari njema ya kumfurahisha.

 

 

18-Khofu (ya watu) kutegemea wingi wa rahmah ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

19-Kauli ya mtu anayeulizwa pindi asipojua jibu, “Allaah na Rasuli Wake Wanajua zaidi.”

 

 

20-Ruhusa ya kutoa baadhi ya elimu kwa baadhi ya watu bila wengine.

 

 

21-Unyenyekevu wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kupanda mnyama pamoja na Swahaabah.

 

 

22-Kujuzu watu wawili kupanda mnyama mmoja.

 

 

23-Fadhila za Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه).

 

 

24-Umuhimu mkubwa wa jambo hili (la Tawhiyd).

 

 

Share

02-Kitaab At-Tawhiyd: Fadhila Za Tawhiyd Na Yanayofuta Madhambi

02-Mlango Wa 2

بَابُ فَضْلِ التَّوْحِيدِ وَمَا يُكَفَّرُ مِنَ الذُّنُوبِ

Fadhila Za Tawhiyd Na Yanayofuta Madhambi


 

وَقَوْلُ اللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

 الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ الْأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُونَ ﴿٨٢﴾

((Wale walioamini na hawakuchanganya iymaan zao na dhulma; hao ndio watakaopata amani nao ndio walioongoka)) [Al-An’aam (6: 82)]

 

عَنْ عُبَادَةَ بْنِ الصَّامِتِ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) ((مَنْ شَهِدَ أَنْ لاَ إلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ وَأَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ، وَأَنَّ عِيسَى عَبْدُ اللهِ وَرَسُولُهُ وَكَلِمَتُهُ أَلْقَاهَا إِلَى مَرْيَمَ وَرُوحٌ مِنْهُ، وَالْجَنَّةَ حَقٌّ وَالنَّارَ حَقٌّ أَدْخَلَهُ اللهُ الْجَنَّةَ عَلَى مَا كَانَ مِنَ الْعَمَلِ))    

Imepokelewa kutoka kwa ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayeshuhudia kwamba: Laa ilaaha illa-Allaah (hapana Muabudiwa wa haki ila Allaah) Pekee, Hana mshirikia, na kwamba Muhammad ni mja Wake na Rasuli Wake, na kwamba ‘Iysaa ni mja wa Allaah na Rasuli Wake, na Neno Lake Alilolitia kwa Maryam na Roho [imeumbwa] kutoka Kwake, na kwamba Jannah ni haki, na moto ni haki, Allaah Atamuingiza Jannah kwa kiasi chochote cha ‘amali yake itakavyokuwa)) [Al-Bukhaariy (3435), Muslim (28), At-Tirmidhiy]

 

فِي حَدِيثِ عِتْبَانَ ((فَإِنَّ اللهَ حَرَّمَ عَلَى النَّارِ مَنْ قَالَ لاَ إلَهَ إِلاَّ اللهُ يَبْتَغِي بِذَلِكَ وَجْهَ اللهِ))

Katika Hadiyth iliyopokewa toka kwa ‘Itbaan (رضي الله عنه): ((Hakika Allaah Ameharamisha moto kwa anayesema: “laa ilaaha illa-Allaah”, akikusudia kutafuta Wajihi wa Allaah)) [Al-Bukhaariy (425), Muslim (33)] 

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرَيِّ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) عَنْ رَسُولِ الله (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ ((قَالَ مُوسَى عَلَيْهِ السَّلامُ يَا رَبِّ! عَلِّمْنِي شَيْئًا أَذْكُرُكَ وَأَدْعُوكَ بِهِ. قَالَ: قُلْ يَا مُوسَى: لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللهُ.  قَالَ يَا رَبِّ! كُلُّ عِبَادِكَ يَقُولُونَ هَذَا. قَالَ: يَا مُوسَى،  لَوْ أَنَّ السَّمَوَاتِ السَّبْعَ وَعَامِرَهُنَّ غَيْرِي وَالأَرَضِينَ السَّبْعَ فِي كِفَّةٍ،  وَ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللهُ فِي كِفَّةٍ، مَالَتْ بِهِنَّ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللهُ))  رَوَاهُ ابْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ وَصَحَّحَهُ.

Amesimulia Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه):  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Muwsaa alisema: Ee Rabb wangu! Nifundishe kitu mahsusi kwangu ambacho kwacho nitakudhukuru na kukuomba duaa. (Allaah) Akasema: Ee Muwsaa!    Sema:

لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللهُ 

Laa ilaaha illa-Allaah.  

 

Muwsaa akasema: Ee Rabb wangu! Waja Wako wote wanasema hivi. (Allaah) Akasema: Ee Muwsaa, lau kama mbingu saba na kila kilichokuwemo isipokuwa Mimi, na ardhi saba zikiwekwa katika kiganja cha mizani, na laa ilaaha illa-Allaah ikawekwa katika kiganja kingine cha mizani, basi laa ilaaha illa-Allaah itazishinda hizo.[Ibn Hibaan, na Al-Haakim ameikiri kuwa ni Swahiyh]

 

 

وَلِلتِّرْمِذِيِّ وَحَسَّنَهُ، عَنْ أَنَسٍ (رضي الله عنه) قال: سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((قَالَ اللهُ تَعَالَى يَا ابْنَ آدَمَ! لَوْ آتَيْتَنِي بِقُرَابِ الأَرْضِ خَطَايَا ثُمَّ لَقِيتَنِي لاَ تُشْرِكُ بِي شَيْئًا لأَتَيْتُكَ بِقُرَابِهَا مَغْفِرَةً))

Na kwa At-Tirmidhiy aliyoipa daraja ya Hasan, Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Allaah Ta’aalaa Amesema: Ee bin Aadam! Lau ukinijia kwa dunia iliyojaa madhambi, kisha ukakutana Nami hunishirikishi na chochote, bila shaka Nitakujia kwa wingi wa maghfirah kama hayo)) [At-Tirmidhiy (3534) Ad-Daarimiy (2791), Ahmad 172/5)]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Ukunjufu wa fadhila na rahmah za Allaah (سبحانه وتعالى).

 

2-Jazaa nyingi Anazozilipa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa ajili ya Tawhiyd.

 

3-Tawhiyd inafuta dhambi juu ya kuwa ina fadhila na thawabu. 

 

4-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-An’aam (82).

 

5-Zingatia nukta tano zilizopatikana katika Hadiyth ya ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit (رضي الله عنه).

 

6-Unapounganisha nukta hizi, Hadiyth ya ‘Itbaan (رضي الله عنه) na zinayoifuatia (ya ‘Itbaan), basi maana ya Kalimah ‘Laa ilaaha illaa Allaah’ inakuwa dhahiri kabisa na kudhihirisha makosa ya walioghurika nayo.

 

7-Kuzingatia sharti liliomo katika Hadiyth ya ‘Itbaan (رضي الله عنه).

 

8-Rusuli (عليهم السلام) walikuwa na haja ya kutanabahisha fadhila za ‘Laa ilaaha illa-Allaah’.

 

9-Tanbihi muhimu kwa viumbe wote kutamka Kalimah ‘Laa ilaaha illa-Allaah’ ingawa wengi wanaoitamka mizani zao zitakuwa khafifu.

 

10-Dalili yathibitisha kuwa kuna ardhi saba kama ambavyo ziko mbingu saba.[1]

 

11-Mbingu na ardhi zimejaa viumbe.

 

12-Kuthibitisha Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) kinyume na madai ya   Ash’ariyyah[2].

 

13-Unapoifahamu Hadiyth ya Anas (رضي الله عنه), utaifahamu pia kauli katika Hadiyth ya ‘Itbaan (رضي الله عنه). ((Hakika Allaah Ameharamisha moto kwa anayesema: “laa ilaaha illa-Allaah”, akikusudia kutafuta Wajihi wa Allaah)) yaani kwa kuepuka shirki, si kwa kuitamka kwa ulimi tu.

 

14-Kutafakari na kuzingatia sifa zinazolingana baina ya ‘Iysaa (عليه السلام) na Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

15-Kutambua kuwa ‘Iysaa (عليه السلام) alipewa sifa mahususi kuwa aliumbwa kwa ‘Kalimatu-Allaah’ (neno la Allaah).

 

16-Kujua kwamba ‘Iysaa (عليه السلام) ni Ruwhun Minhu (roho Alioumba kwa amrisho kutoka Kwake).  

 

17-Kujua fadhila za iymaan huko Jannah na motoni.

 

18-Kutambua kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ((… kwa kiasi chochote cha ‘amali yake itakavyokuwa)).

 

19-Kujua kuwa Al-Miyzaan (mizani) ina pande mbili (za kipimo cha kuliani na kushotoni).

 

20-Maana ya ‘Wajihi wa Allaah’.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

[1] Rejea Surat At-Twalaaq (65:12).

[2] Baadhi ya ‘Aqiydah ya Ash’ariyyah ni kuzigeuza Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kuzifasiri vinginevyo kinyume na vile zilivyothibitishwa katika Qur-aan na Sunnah.

Share

03-Kitaab At-Tawhiyd: Atakayethibitisha Tawhiyd (Dhidi ya Shirki) Ataingia Jannah Bila Ya Hesabu

Mlango Wa 3

بَابٌ :مَنْ حَقَّقَ اَلتَّوْحِيدَ دَخَلَ الْجَنَّةَ بِغَيْرِ حِسَابٍ

Atakayethibitisha Tawhiyd (Dhidi ya Shirki) Ataingia

Jannah Bila Ya Hesabu


 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

إِنَّ إِبْرَاهِيمَ كَانَ أُمَّةً قَانِتًا لِّلَّـهِ حَنِيفًا وَلَمْ يَكُ مِنَ الْمُشْرِكِينَ ﴿١٢٠﴾

 ((Hakika Ibraahiym alikuwa Imaam mtiifu kwa Allaah, aliyeelemea haki na wala hakuwa miongoni mwa washirikina)) [An-Nahl (16: 120)]

 

وَقَالَ:

Na Anasema:

وَالَّذِينَ هُم بِرَبِّهِمْ لَا يُشْرِكُونَ ﴿٥٩﴾

((Na wale ambao Rabb wao hawamshirikishi)) [Al-Muuminuun (23:59)]

 

وَعَنْ حُصَيْنِ بْنِ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ قَالَ: كُنْتُ عِنْدَ سَعِيدِ بْنِ جُبَيْرٍ فَقَالَ: أَيُّكُمْ رَأَى الْكَوْكَبَ اَلَّذِي اِنْقَضَّ الْبَارِحَةَ؟ فَقُلْتُ أَنَا. ثُمَّ قُلْتُ: أَمَّا إِنِّي لَمْ أَكُنْ فِي صَلاةٍ وَلَكِنِّي لُدِغْتُ. قَالَ: فَمَا صَنَعْتَ؟ قُلْتُ: اِرْتَقَيْتُ. قَالَ: فَمَا حَمَلكَ عَلَى ذَلِكَ؟ قُلْتُ: حَدِيثٌ حَدَّثَنَاهُ اَلشَّعْبِيُّ. قَالَ: وَمَا حَدَّثَكُمْ؟ قُلْتُ: حَدَّثَنَا عَنْ بُرَيْدَةَ بْنِ الْحُصَيْبِ أَنَّهُ قَالَ: لاَ رُقْيَةَ إِلاَّ مِنْ عَيْنٍ أَوْ حُمَةٍ. قَالَ: قَدْ أَحْسَنَ مَنِ اِنْتَهَى إِلَى مَا سَمِعَ. وَلَكِنْ حَدَّثَنَا اِبْنُ عَبَّاسٍ عَنْ اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) أَنَّهُ قَالَ: ((عُرِضَتْ عَلَيَّ الأُمَمُ فَرَأَيْتُ اَلنَّبِيَّ وَمَعَهُ اَلرَّهْطُ وَالنَّبِيَّ وَمَعَهُ اَلرَّجُلُ وَالرَّجُلاَنِ، وَالنَّبِيَّ وَلَيْسَ مَعَهُ أَحَدٌ، إِذْ رُفِعَ لِي سَوَادٌ عَظِيمٌ فَظَنَنْتُ أَنَّهُمْ أُمَّتِي، فَقِيلَ لِي هَذَا مُوسَى وَقَوْمُهُ، فَنَظَرْتُ فَإِذَا سَوَادٌ عَظِيمٌ، فَقِيلَ لِي هَذِهِ أُمَّتُكَ، وَمَعَهُمْ سَبْعُونَ أَلْفًا يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ بِغَيْرِ حِسَابٍ وَلاَ عَذَابٍ)) ثُمَّ نَهَضَ فَدَخَلَ مَنْزِلَهُ فَخَاضَ اَلنَّاسُ فِي أُولَئِكَ فَقَالَ بَعْضُهُمْ: فَلَعَلَّهُمْ اَلَّذِينَ صَحِبُوا رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) ، وَقَالَ بَعْضُهُمْ فَلَعَلَّهُمْ اَلَّذِينَ وُلِدُوا فِي الإِسْلامِ فَلَمْ يُشْرِكُوا بِاَللَّهِ شَيْئًا وَذَكَرُوا أَشْيَاءَ. فَخَرَجَ عَلَيْهِمْ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَأَخْبَرُوهُ فَقَالَ: ((هُمُ اَلَّذِينَ لاَ يَسْتَرْقُونَ وَلاَ يَكْتَوُونَ وَلاَ يَتَطَيَّرُونَ وَعَلَى رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ)) فَقَامَ عُكَّاشَةُ بْنُ مُحْصَنٍ فَقَالَ: اُدْعُ اَللَّهَ أَنْ يَجْعَلَنِي مِنْهُمْ. فَقَالَ: ((أَنْتَ مِنْهُمْ)) ثُمَّ قَامَ رَجُلٌ آخَرُ فَقَالَ: اُدْعُ اَللَّهَ أَنْ يَجْعَلَنِي مِنْهُمْ. فَقَالَ: ((سَبَقَكَ بِهَا عُكَّاشَةُ)) البخاري ومسلم

Huswayn bin ‘Abdir-Rahmaan amehadithia: Siku moja nilipokuwa na Sa’iyd bin Jubayr, aliuliza: “Nani miongoni mwenu aliyeona kimondo (nyota inayofukuza shaytwaan) jana usiku?” Nikajibu: “Mimi nimeiona.” Kisha nikaelezea kwamba sikuwa nikiswali wakati ule sababu nilidonelewa na nge mwenye sumu. Akasema: “Kisha ukafanya nini?” Nikajibu: “Nilifanya Ruqyah (kujitibu). Akauliza: “Kitu gani kimekupeleka ufanye hivyo?” Nikasema: “Ni Hadiyth niliyoisikia kutoka

 kwa Ash-Sha’biyy.” Akauliza: “Amekuhadithieni nini Ash-Sha’biyy?” Nikajibu: “Ameripoti kutoka kwa Buraydah bin Al-Huswayb amesema kwamba Ruqyah hairuhusiwi isipokuwa kwa ajili ya kijicho na kudonelewa (na mdudu sumu).” (Sa’iyd bin Jubayr) akasema: “Amefanya vyema kukomea kwenye aliyosikia (yaani: kufanyia kazi jambo kwa ujuzi kinyume na ujahili). Lakini Ibn ‘Abbaas ametusimulia kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ummah zote zilipitishwa mbele yangu, nikamuona Nabiy akiwa na kundi dogo la watu, na Nabiy akiwa na mtu mmoja au wawili, na Nabiy akiwa hana mtu yeyote. Kisha nikaoneshwa idadi kubwa ya watu niliodhania ni katika Ummah wangu, lakini nikaambiwa: Huyo ni Muwsaa na watu wake. Kisha nikatazama nikaona kundi kubwa ambalo nikaamibwa: Hawa ni watu wako, miongoni mwao ni watu elfu sabini watakaoingia Jannah bila hesabu wala adhabu)). Kisha akainuka kuingia nyumbani kwake (na nyuma yake) watu wakaanza kujadiliaina ni nani hao watakaoweza kuwa. Wengineo wakasema: “Labda ni Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).” Wengine wakasema: “Labda ni wale waliozaliwa katika Uislamu na hawakumshirikisha Allaah kwa chochote.” (Wakataja mengine kadhaa) Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akatoka na kuja na wakamwambia (waliyokuwa wakiyajadili). Akasema: ((Ni wale ambao wasiotafuta (kuommba) kufanyiwa Ruqyah, wala kujichoma chuma cha moto, wala hawaamini twiyaarah [itikadi ya mkosi au nuksi], bali wanamtegemea Rabb wao na kutawakali Kwake Pekee)) ‘Ukaashah bin Mihswan akasimama akasema:  “Muombe Allaah niwe mmoja wao.” Akasema:  ((Wewe ni mmoja wao)). Kisha mtu mwengine akasimama akasema: Muombe Allaah niwe mmoja wao (pia). Akasema: ((‘Ukaashah amekutangulia)) [Al-Bukhaariy (3410) Muslim (220)]

 

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Watu hutofautiana katika yakini zao juu ya Tawhiyd.

 

2-Maana halisi ya kutekeleza Tawhiyd.

 

3-Allaah (سبحانه وتعالى) kumsifia Ibraahiym (عليه السلام) kwamba:  “si miongoni mwa washirikina.”

 

4-Allaah (سبحانه وتعالى) kuwasifu waja wema (awliyaa[1]) kwa kusalimika na shirki.

 

5-Kuikwepa Ruqyah na kuchomwa chuma cha moto ni miongoni mwa sifa za Tawhiyd.

 

6-Tawakkul (kumtegemea Allaah) inajumuisha sifa hizi.

 

7-Maswahaba kutambua tawakkul, kwani walijua wasingeifikia hali hiyo pasina ‘amali njema.

 

8-Utashi wa Maswahaba kwa kutenda kila lililo la khayr.

 

9-Fadhila za ummah huu (wa Kiislamu) kwa wingi na ubora.

 

10-Idadi kubwa ya wafuasi Muwsaa   (عليه السلام).

 

11-Kudhiirishwa Ummah zote mbele ya Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

12-Kila Ummah utakusanywa peke yake pamoja na Nabiy wake.

 

13-Uchache wa waliotikia wito wa Rusuli.

 

14-Rusuli ambao hawakuwa na wafuasi watahudhuria mbele ya Allaah (سبحانه وتعالى) peke yao Siku ya Qiyaamah.

 

15-Faida ya elimu hii; kuwa mtu asidanganyike kwa wingi au kukatishwa tamaa na uchache wa idadi ya watu.

 

16-Ruhusa ya Ruqyah kwa ajili ya kijicho au kudonolewa na chenye sumu.

 

17-Ujuzi wa kina wa Salaf kama inavyoonekana katika kauli. “Amefanya vyema kukomea kwenye aliyosikia…” Tambua kwamba Hadiyth ya kwanza haikinzani na ya pili.

 

18-Kujiepusha kwa Salaf kumsifu mtu bila ya kustahiki.

 

19-Kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ((Wewe ni miongoni mwao)) ni alama ya Unabiy.

 

20-Fadhila za ‘Ukaashah (رضي الله عنه).

 

21-Kutumia al-ma’aaridhw (mafumbo, mifano - kutaja kauli isiyo dhahiri, au kielezo fulani cha kutolea tafsiri mbali mbali).

 

22-Khulqa njema za Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

 

 

 

[1] Walio karibu na Allaah (سبحانه وتعالى) na vipenzi Wake.

 

Share

04-Kitaab At-Tawhiyd: Kukhofia Shirki

Mlango Wa 4

بَابُ الْخَوْفِ مِنْ اَلشِّرْكِ

Kukhofia Shirki

 


 

وَقَوْلِ اَللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ:

Na kauli Yake ‘Azza wa Jalla:  

 إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا ﴿٤٨﴾

((Hakika Allaah Haghufuri kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae)) [An-Nisaa (4: 48, 116)]

 

وَقَالَ الْخَلِيلُ عَلَيْهِ اَلسَّلامُ :

Na amesema Khaliyl (Ibraahiym  (عليه السلام

 وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعْبُدَ الْأَصْنَامَ ﴿٣٥﴾

((na Uniepushe na wanangu kuabudu masanamu)) [Ibraahiym (14: 35)]

 

وَفِي الْحَدِيثِ: ((أَخْوَفُ مَا أَخَافُ عَلَيْكُمْ اَلشِّرْكُ الأَصْغَرُ)) فَسُئِلَ عَنْهُ فَقَالَ:  ((اَلرِّيَاءُ))

Na katika Hadiyth: ((Nnachokukhofieni zaidi juu yenu ni shirki ndogo)) Akaulizwa kuhusu hiyo shirki akasema: ((Riyaa)) [Ahmad katika Musnad yake (429, 428/5)]

 

وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَنْ مَاتَ وَهُوَ يَدْعُو مِنْ دُونِ اَللَّهِ نِدًّا دَخَلَ اَلنَّارَ)) رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ.

Na Imepokelewa kwa Ibn Mas’uwd(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Yeyote atakayekufa hali anamshirikisha Allaah ataingia Motoni)) [Al-Bukhaariy]

 

وَلِمُسْلِمٍ عَنْ جَابِرٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  قَالَ: ((مَنْ لَقِيَ اَللَّهَ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا, دَخَلَ الْجَنَّةَ. وَمَنْ لَقِيَهُ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا; دَخَلَ اَلنَّارَ))

Na kwa Muslim Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayekutana na Allaah hali hamshirikishi na chochote ataingia Jannah. Na atakayekutana Naye hali anamshirikisha na chochote ataingia motoni)) [Muslim (93)]

 

 Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kukhofia shirki.

 

2-Riyaa ni aina ya shirki.

 

3-Riyaa ni shirki ndogo.

 

4-Riyaa inakhofiwa sana na waja wema (kwani rahisi mno mtu kutumbukia ndani yake)

 

5-Ukaribu wa Jannah na moto.

 

6-Ukaribu huo wa Jannah na Moto umetajwa katika Hadiyth moja.

 

7-Mwenye kukutana na Allaah (Siku ya Qiyaamah) akiwa hakumshirikisha na chochote ataingia Jannah; na mwenye kukutana Naye, huku amemshirikisha na kitu, ataingia motoni, hata kama alikuwa ni miongoni mwa wanaomwabudu mno Allaah (سبحانه وتعالى).

 

8-Umuhimu mkubwa mno wa suala hili, kiasi kwamba Al-Khaliyll (Ibraahiym) aliomba yeye na wanawe waepushwe dhidi ya kuabudu masanamu.

 

9-Kuzingatia kwake jinsi watu wengi walivyoingia katika ibaadah ya masanamu pindi aliposema:

 

رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ

((“Rabb wangu! Hakika hao (masanamu) wamepoteza wengi sana katika watu)) [Ibraahiym (14:36)]

 

10-Tafsiri ya maana ya (kauli ya) “Laa ilaaha illaa Allaah” kama alivyoitaja Al-Bukhaariy.

 

11-Fadhila za aliyesalimika na shirki.

 

 

 

 

Share

05-Kitaab At-Tawhiyd: Wito Wa Kushuhudia Kwamba Laa Ilaaha Illa-Allaah

Mlango Wa 5

بَابُ اَلدُّعَاءِ إِلَى شَهَادَةِ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ

Wito Wa Kushuhudia Kwamba Laa Ilaaha Illa-Allaah


 

وَقَوْلِهِ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

 قُلْ هَـٰذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّـهِ ۚ عَلَىٰ بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي ۖ وَسُبْحَانَ اللَّـهِ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ ﴿١٠٨﴾

((Sema: “Hii ndio njia yangu nalingania kwa Allaah, juu ya nuru za elimu na umaizi, mimi na anayenifuata. Na Subhaana-Allaah! Utakasifu ni wa Allaah, nami si miongoni mwa washirikina.”)) [Yuwsuf (12:108)]

 

 وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  لَمَّا بَعَثَ مُعَاذًا إِلَى الْيَمَنِ: قَالَ لَهُ: ((إِنَّكَ تَأْتِي قَوْمًا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ، فَلْيَكُنْ أَوَّلَ مَا تَدْعُوهُمْ إِلَيْهِ شَهَادَةَ أَن لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ)) وَفِي رِوَايَةٍ: ((إِلَى أَنْ يُوَحِّدُوا اَللَّهَ. فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوكَ لِذَلِك فَأَعْلِمْهُمْ أَنَّ اَللَّهَ اِفْتَرَضَ عَلَيْهِمْ خَمْسَ صَلَوَاتٍ فِي كُلِّ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ. فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوكَ لِذَلِكَ فَأَعْلِمْهُمْ أَنَّ اَللَّهَ اِفْتَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً تُؤْخَذُ مِنْ أَغْنِيَائِهِمْ فَتَرُدُّ عَلَى فُقَرَائِهِمْ. فَإِنْ هُمْ أَطَاعُوكَ لِذَلِكَ فَإِيَّاكَ وَكَرَائِمَ أَمْوَالِهِمْ, وَاتَّقِ دَعْوَةَ الْمَظْلُومِ فَإِنَّهُ لَيْسَ بَيْنَهَا وَبَيْنَ اَللَّهِ حِجَابٌ)) أَخْرَجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا): Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipomtuma Mu’aadh Yemen alimwambia: ((Hakika wewe utakutana na watu miongoni mwa Ahlul-Kitaab, basi jambo la kwanza la kuwalingania liwe ni kushuhudia kwamba: Laa ilaaha illa-Allaah- hapana Muabudiwa wa haki kuabudiwa ila Allaah)) Na katika riwaayah nyingine: (([Walinganie] Kumpwekesha Allaah. Watakapokutii hilo, wajulishe kwamba Allaah Amewafaradhishia Swalaah tano usiku na mchana. Watakapokutii hilo, basi wajuilshe kwamba Allaah Amewafaradhishia Zakaah iichukuliwe kutoka kwa matajiri wao na kupewa masikini wao. Watakapotii hilo, basi tahadhari kuchukua bora za mali zao [kama malipo ya Zakaah], na tahadhari na du’aa ya aliyedhulumiwa, kwani hakuna kizuizi baina yake na Allaah)) [Al-Bukhaariy (1395) Muslim (19)]

 

وَلَهُمَا عَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ يَوْمَ خَيْبَر: ((لاُعْطِيَنَّ اَلرَّايَةَ غَدًا رَجُلاً يُحِبُّ اَللَّهَ وَرَسُولَهُ وَيُحِبُّهُ اَللَّهُ وَرَسُولُهُ, يَفْتَحُ اَللَّهُ عَلَى يَدَيْهِ)) فَبَاتَ اَلنَّاسُ يَدُوكُونَ لَيْلَتَهُمْ، أَيُّهُمْ يُعْطَاهَا، فَلَمَّا أَصْبَحُوا غَدَوْا عَلَى رَسُولِ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) كُلُّهُمْ يَرْجُو أَنْ يُعْطَاهَا فَقَالَ:((أَيْنَ عَلِيُّ بْنُ أَبِي طَالِبٍ؟)) فَقِيلَ هُوَ يَشْتَكِي عَيْنَيْهِ. فَأَرْسَلُوا إِلَيْهِ، فَأُتِيَ بِهِ فَبَصَقَ فِي عَيْنَيْهِ، وَدَعَا لَهُ فَبَرَأَ كَأَنْ لَمْ يَكُنْ بِهِ وَجَعٌ، فَأَعْطَاهُ اَلرَّايَةَ، فَقَالَ: ((اُنْفُذْ عَلَى رِسْلِكَ، حَتَّى تَنْزِلَ بِسَاحَتِهِمْ، ثُمَّ اُدْعُهُمْ إِلَى الإِسْلامِ, وَأَخْبِرْهُمْ بِمَا يَجِبُ عَلَيْهِمْ مِنْ حَقِّ اَللَّهِ تَعَالَى فِيهِ، فَوَاَللَّهِ لأَنْ يَهْدِيَ اَللَّهُ بِكَ رَجُلاً وَاحِدًا خَيْرٌ لَكَ مِنْ حُمْرِ اَلنَّعَمِ))  يَدُوكُونَ أَيْ يَخُوضُونَ

Na kutoka kwao wawili pia: Imepokelewa toka kwa Sahl bin Sa’d (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema siku ya Khaybar: ((Kesho nitamkabidhi bendera mtu anayempenda Allaah na Rasuli Wake na Allaah na Rasuli Wake wanampenda. Allaah Atampa ushindi mikononi mwake)). Watu wakakesha usiku wakishughulika kujadili nani atakayepewa bendera. Asubuhi walimwendea Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa hamu wakitegemea kupewa bendera. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akauliza: ((Yuko wapi ‘Aliy bin Abiy Twaalib?)). Wakajibu: Anauguwa macho yake mawili. Akaagizwa akafika. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akatema mate machoni mwake kisha akamwombea akapona kana kwamba hakuwa na maumivu yoyote. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akampa bendera akamwambia: ((Waendee kwa taratibu na upole mpaka ufikie katikati yao, kisha waite katika Uislamu na wajulishe wajibu wao katika haki ya Allaah. Naapa kwa Allaah! Allaah Akimuongoa mtu mmoja katika Uislamu kupitia kwako, basi ni khayr kuliko ngamia wekundu)) [Al-Bukhaariy (2942) Muslim (2406)]

 

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kulingania kwa Allaah (سبحانه وتعالى) ni miongoni mwa njia za kumfuata Rasuli wa Allaah.

 

2-Msisitizo juu ya ikhlaasw kwa kuwa watu wengi wajidai kulingania katika haki lakini ni kwa ajili ya maslahi ya nafsi zao.

 

3-Kulingania kwa ‘Baswiyraa’ (busara, utambuzi, umaizi na ujuzi wa Dini yetu) ni faradhi mojawapo.

 

4-Miongoni mwa dalili za uzuri wa Tawhiyd ni kumtakasa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kumwepusha Allaah (سبحانه وتعالى) na kila aibu na kasoro. 

 

5-Miongoni mwa maovu ya shirki ni kumtukana Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kumnasibisha na yasiyomstahiki.

 

6-La muhimu kabisa ni Muislamu kujiweka mbali na watu wa shirki hata kama hafanyi shirki wakati anapokuwa pamoja nao.

 

7-Tawhiyd (na kuilingania) ni wajibu wa kwanza kabisa kwa Muislamu.

 

8-Tawhiyd iko mbele ya kila kitu, hata Swalaah.

 

9-Maana ya “wampwekeshe Allaah” katika ‘ibaadah ni sawa na maana ya kushuhudia Laa ilaaha illaa Allaah.

 

10-Ingawa mtu anaweza kuwa katika Ahlul-Kitaab na asijue maana ya Tawhiyd au kuitekeleza. Au anaweza kuwa anajua, lakini matendo yake yakawa kinyume.

 

11-Msisitizo wa kufundisha kwa utaratibu maalumu; jambo moja baada ya jingine.

 

12-Kuanza kufundisha mambo muhimu zaidi kisha linalofuatia kwa umuhimu.

 

13-Ugawaji wa Zakaah.

 

14-Mwenye elimu amuondolee mashaka mwanafunzi.

 

15-Wakusanyaji wa Zakaah wazuiwe wasichukue mali zilizo bora kabisa za watu.    

 

16-Kuogopa du’aa ya aliyedhulumiwa.

 

17-Maelezo kuwa du’aa ya aliyedhulumiwa haina kizuizi baina yake na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

18-Miongoni mwa dalili za Tawhiyd ni kuwa, Rasuli na awliyaa wa mwanzo kabisa walipata tabu, mateso, njaa na maradhi.

 

19-Kauli yake, ((nitampa bendera …)) ni alama ya Unabiy.

 

20-Kumtemea mate ‘Aliy(رضي الله عنه)  machoni mwake akapona, pia ni alama ya Unabiy.

 

21-Fadhila za ‘Aliy (رضي الله عنه).

 

22-Fadhila za Maswahaba kuwa walikesha usiku wakiwazia (nani atakayepewa bendera) na kisha kushughulishwa kwao na bishara ya ushindi wa mji.

 

23-Ukumbusho kuhusu kuamini Al-Qadar; kwa kuwa hiyo (yaani bendera) alipewa mtu ambaye hakuitaraji au kuiomba, na wakanyimwa walioitaraji.

 

24-Adabu katika kauli yake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), ((Waendee kwa taratibu na upole…)).

 

25-Kuwalingania watu katika Uislamu kabla ya vita.

 

26-Ruhusa ya kupigana na waliolinganiwa Uislamu lakini wakakataa.

 

27-Kulingania kwa hekima kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((… na wajulishe wajibu wao katika haki ya Allaah)).

 

28-Kujua haki za Allaah (سبحانه وتعالى) katika Uislamu.

 

29-Thawabu za mtu kwa da’wah yake pindi akimwongoa mtu mwengine katika Uislamu.

 

30-Kuapa kwa jina la Allaah katika kuiunga mkono Fatwa ya Shariy’ah ya  Dini.

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

06-Kitaab At-Tawhiyd: Tafsiri Ya Tawhiyd Na Shahaadah: Laa Ilaaha Illa-Allaah

 

Mlango Wa 6

بَابُ تَفْسِيرِ التَّوْحِيدِ وَشَهَادَةِ أنْ لا إِلَهَ إِلا اللَّهُ

Tafsiri Ya Tawhiyd Na Shahaadah: Laa Ilaaha Illa-Allaah


 

وَقَوْلِ اللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ وَيَرْجُونَ رَحْمَتَهُ وَيَخَافُونَ عَذَابَهُ ۚ إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ كَانَ مَحْذُورًا ﴿٥٧﴾

((Hao wanaowaomba (wao wenyewe) wanatafuta kwa Rabb wao njia ya kujikurubisha, yupi miongoni mwao awe karibu zaidi na wanataraji rahmah Yake, na wanakhofu adhabu Yake. Hakika adhabu ya Rabb wako daima ni ya kutahadhariwa)) [Al-Israa (17: 57)]

 

وَقَوْلِهِ:  

Na kauli Yake:

وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ إِنَّنِي بَرَاءٌ مِّمَّا تَعْبُدُونَ ﴿٢٦﴾

((Na Ibraahiym alipomwambia baba yake na kaumu yake: “Hakika mimi nimejitoa katika dhima na yale mnayoyaabudu.

 

إِلَّا الَّذِي فَطَرَنِي فَإِنَّهُ سَيَهْدِينِ ﴿٢٧﴾

 ((“Isipokuwa Ambaye Ameniumba, basi hakika Yeye Ataniongoza.”))

 

وَجَعَلَهَا كَلِمَةً بَاقِيَةً فِي عَقِبِهِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ﴿٢٨﴾

((Na akalifanya neno (laa ilaaha illaa-Allaah) lenye kubakia katika kizazi chake ili wapate kurejea)) [Az-Zukhruf (43: 26-28)]

 

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا إِلَـٰهًا وَاحِدًا ۖ لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۚ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٣١﴾

((Wamewafanya wanachuoni wao mafuqahaa wa dini na Wamonaki wao kuwa ni miola badala ya Allaah, na (pia wamemfanya) Al-Masiyh mwana wa Maryam (kuwa ni muabudiwa); na hali hawakuamrishwa isipokuwa kumwabudu Ilaah (Allaah) Mmoja Pekee. Hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye. Subhaanah! Utakasifu ni Wake! kutokana na yale yote wanayomshirkisha nayo)) [At-Tawbah (9: 31)]

 

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ۖ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ ۗ وَلَوْ يَرَى الَّذِينَ ظَلَمُوا إِذْ يَرَوْنَ الْعَذَابَ أَنَّ الْقُوَّةَ لِلَّـهِ جَمِيعًا وَأَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعَذَابِ ﴿١٦٥﴾

((Na miongoni mwa watu wako wenye kuchukua asiyekuwa Allaah na kuwafanya kuwa ni wanaolingana (na Allaah) wanawapenda kama mapenzi (yapasavyo) ya kumpenda Allaah. Na wale walioamini wana mapenzi zaidi kwa Allaah. Na lau wangelitambua wale waliodhulumu watakapoona adhabu kwamba nguvu zote ni za Allaah; na kwamba hakika Allaah ni Mkali wa kuadhibu)) [Al-Baqarah (2: 165)]

 

وفِي الصَّحِيحِ عَنِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) أنَّهُ قَالَ: ((مَنْ قَالَ لاَ إِلَهَ إلاَّ اللَّهُ، وَكَفَرَ بِمَا يُعْبَدُ مِنْ دُونِ اللَّهِ؛ حَرُمَ مَالُهُ وَدَمُهُ، وَحِسَابُهُ عَلَى اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ))

Na katika Swahiyh Muslim, kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwenye kusema: laa ilaaha illa-Allaah, na akakanusha yote yanayoabudiwa pasina Allaah, basi imeharamishwa mali yake [kufanywa ghanima n.k.] na damu yake na hisabu yake itakuwa kwa Allaah ‘Azza wa Jalla)) [Muslim (23) Ahmad (472/3]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Mlango huu umetaja jambo kubwa na muhimu kabisa nalo ni maelezo ya Tawhiyd na Shahaadah na kubainishwa kwake kwa mambo ya dhahiri.

 

2-Mojawapo ni Aayah ya Suwratul-Israa, ni ukanusho wa dhahiri dhidi ya washirikina wanaoomba waja wema na pia kubainisha kwamba kufanya hivyo ni shirki kubwa.

 

3-Pia Aayah ya Suratul-Baraa (At-Tawbah) imebainisha wazi kwamba Ahlul-Kitaab waliwafanya Wanachuoni wao na watawa kuwa ni waabudiwa badala ya Allaah (سبحانه وتعالى). Pia ni dhahiri kwamba hawakuamrishwa isipokuwa kumwabudu Ilaah Mmmoja; Allaah (سبحانه وتعالى). Tafsiri ya Aayah haina utata kuhusu utiifu wao kwa Wanachuoni na waja wengine wa Allaah (سبحانه وتعالى) katika yasiyo maasi; (yaani inajuzu kuwatii katika yanayaokubalika kishariy’ah), lakini haijuzu kuwaomba (du’aa) au kuwaabudu.

 

4-Pia kauli ya Ibraahiym (عليه السلام) kwa makafiri,

إِنَّنِي بَرَاءٌ مِّمَّا تَعْبُدُونَ ﴿٢٦﴾

((“Hakika mimi nimejitoa katika dhima na yale mnayoyaabudu)).

 

إِلَّا الَّذِي فَطَرَنِي

((“Isipokuwa Ambaye Ameniumba...”)).

 

Kauli yake hiyo Ibraahiym (عليه السلام) inatutambulisha kwamba amejitoa dhima (kwa kujjiweka mbali) na shirki kwa kuwa amekataa kumuabudu yeyote asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى). Pia inathibitisha Shahada ya Laa ilaaha illa-Allaah kwani Anasema:

 

وَجَعَلَهَا كَلِمَةً بَاقِيَةً فِي عَقِبِهِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ﴿٢٨﴾

((Na akalifanya neno (laa ilaaha illaa-Allaah) lenye kubakia katika kizazi chake ili wapate kurejea)).

 

5-Kuna Aayah katika Suwratul-Baqarah kuhusu makafiri ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

وَمَا هُم بِخَارِجِينَ مِنَ النَّارِ ﴿١٦٧﴾

((wala hawatokuwa wenye kutoka motoni)) [Al-Baqarah (2: 167)]

 

Imetajwa kwamba wanawapenda wanaowashirikisha na Allaah (سبحانه وتعالى) kama wanavyompenda Allaah. Na hii inathibitisha kwamba mapenzi yao juu ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni makubwa, lakini hivyo haikuwaingiza katika Uislamu. Itakuwaje basi hali ya anayempenda muabudiwa wa uongo kuliko kumpenda Allaah? Na itakuwaje basi aliyekuwa hapendi yeyote isipokuwa muabudiwa wa uongo na wala hana mapenzi na Allaah?

 

 

6-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:

مَنْ قَالَ لاَ إِلَهَ إلاَّ اللَّهُ، وَكَفَرَ بِمَا يُعْبَدُ مِنْ دُون اللَّهِ؛ حَرُمَ مَالُهُ وَدَمُهُ، وَحِسَابُهُ عَلَى اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ

((Mwenye kusema: laa ilaaha illa-Allaah, na akakanusha yote yanayoabudiwa pasina Allaah, basi imeharamishwa mali yake [kufanywa ghanima n.k.] na damu yake na hisabu yake itakuwa kwa Allaah ‘Azza wa Jalla))

 

Hii ni kauli nzito kabisa ya kufafanua maana ya laa ilaaha illa-Allaah. Inadhihirisha kwamba kuitamka tu hailindi damu na mali ya mtu. Wala haitoshelezi kufahamu maana yake au kuikiri, au hata awe hamuombi mwengine isipokuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee; bali mali na damu ya mtamkaji haiharamishwi mpaka juu ya hayo iweko nyongeza ya kwamba, akanushe kabisa kila kinachoabudiwa asiyekuwa Allaah. Na akitilia shaka au akiwa anasitasita, basi mali na damu yake haitokuwa ni haramu (haitokuwa katika ulinzi na amani). Basi mfano gani zaidi ya huu utatolewa? Kipi kitakachofafanua nukta hii waziwazi?  (Hakika) Ina hoja nzito inayokata mzozo (wa kuhusu maana ya laa ilaaha illa-Allaah)

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

07-Kitaab At-Tawhiyd: Shirki Kuva Kikuku cha Chuma, Uzi n.k Kwa Ajili Kuondosha Au Kuzuia Balaa

Mlango Wa 7

بَابٌ مِنَ الشِّرْكِ لُبْسُ الْحَلْقَة وَالْخَيْطِ وَنَحْوِهِمَا لِرَفْعِ الْبَلَاءِ أَوْ دَفْعِهِ

Ni Shirki Kuva Kikuku cha Chuma Na Uzi Na Vitu Kama Hivyo Kwa Ajili Ya Kuondosha Au Kuzuia Balaa

 


 

وَقَوْلُ اللهِ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

قُلْ أَفَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ إِنْ أَرَادَنِيَ اللَّـهُ بِضُرٍّ هَلْ هُنَّ كَاشِفَاتُ ضُرِّهِ أَوْ أَرَادَنِي بِرَحْمَةٍ هَلْ هُنَّ مُمْسِكَاتُ رَحْمَتِهِ ۚ قُلْ حَسْبِيَ اللَّـهُ ۖ عَلَيْهِ يَتَوَكَّلُ الْمُتَوَكِّلُونَ ﴿٣٨﴾

((Sema: “Je, mnaonaje wale mnaowaomba badala ya Allaah; ikiwa Allaah Atanikusudia dhara; je, wao wataweza kuondosha dhara Yake? Au Akinikusudia rahmah; je wao wataweza kuizuia rahmah Yake?” Sema: “Ananitosheleza Allaah”, Kwake watawakali wenye kutawakali)) [Az-Zumar (39: 38)]

 

عَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْن (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) أَنَّ النَّبِيَّ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) رَأَى رَجُلاً فِي يَدِهِ حَلَقَةٌ مِنْ صُفْرٍ، فَقَالَ: ((مَا هَذِهِ؟))  قَالَ: مِنَ الْوَاهِنَةِ فَقَالَ: ((انْزَعْهَا؛ فَإِنَّهَا لاَ تَزِيدُكَ إِلاَّ وَهَنًا، فَإِنَّكَ لَوْ مِتَّ وَهِيَ عَلَيْكَ؛ مَا أَفْلَحْتَ أَبَدًا))  رَوَاهُ أَحْمَدُ بِسَنَدٍ لا بَأْسَ بِهِ.

Imepokelewa kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alimwona mtu amevaa kikuku cha chuma mkononi mwake, akamuuliza: ((Nini hiki?)) Akajibu: “Kuzuia udhaifu wa uzee.” Akasema: ((Ivue, kwani haizidishi ila udhaifu. Na pindi ukifa ukiwa nacho, hutofaulu kamwe)) [Imekusanywa na Ahmad katika Musnad (4/445) kwa isnaad nzuri]

 

وَلَهُ عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ (رضي الله عنه) مَرْفُوعًا: ((مَنْ تَعَلَّقَ تَمِيمَةً؛ فَلَا أَتَمَّ اللهُ لَهُ، وَمَنْ تَعَلَّقَ وَدَعَةً؛ فَلَا وَدَعَ اللهُ لَهُ))

Ahmad amepokea pia kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir  (رضي الله عنه) Hadiyth Marfuw’ kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayetundika talasimu[1] hatopata kuona haja yake kutimizwa na Allaah. Na atakayeitundika kombe la pwani hatopata amani na utulivu kutoka kwa Allaah [yaani Allaah Hatomkhafifishia anayoyaogopea])) [Ahmad katik Musnad (4/154)]

 

وَفِي رِوَايَةٍ: ((مَنْ تَعَلَّقَ تَمِيمَةً؛ فَقَدْ أَشْرَكَ))

Na katika riwaayah nyingine: ((Atakayetundika talasimu kwa yakini ameshirikisha)) [Ahmad katika Musnad (4/156)]

 

وَلإِبْنِ أَبِي حَاتِمٍ عَنْ حُذَيْفَةَ (رضي الله عنه) أَنَّهُ رَأَى رَجُلاً فِي يَدِهِ خَيْطٌ مِنَ الْحُمَّى، فَقَطَعَهُ وَتَلا قَوْلَهُ : وَمَا يُؤْمِنُ أَكْثَرُهُم بِاللَّـهِ إِلَّا وَهُم مُّشْرِكُونَ ﴿١٠٦﴾

Ibn Haatim ameripoti kutoka kwa Hudhayfah (رضي الله عنه) kuwa alimuona mtu amevaa talasimu (kwa ajili ya kukinga homa) akaikata kisha akasoma kauli Yake Allaah ((Na wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa wao ni wenye kufanya shirki)) [Yuwsuf (12: 106)] [Yaani wanamuamini Allaah, lakini huku wanamshirikisha]

 

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Haramisho la kuvaa vikuku vya chuma nyuzi na mfano wake.

 

 

2-Ikiwa mvaaji atafariki akiwa ameivaa hatofaulu (Aakhirah). Hii inaunga mkono kauli ya Maswahaba kuwa shirki ndogo ni mbaya kuliko madhambi makubwa.

 

 

3-Kutokujua si udhuru.

 

 

4-Kuvaa vitu kama hivyo, havitonufaisha humu duniani bali vitadhuru kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((haizidishi ila udhaifu)).

 

 

5-Kemeo kali kwa mwenye kufanya jambo kama hili.

 

 

6-Inaeleza kuwa mmojawapo anapovaa vitu hivi anakuwa ameachwa alindwe na hivyo vitu (badala ya ulinzi wa Allaah (سبحانه وتعالى) na hivyo hana ulinzi wowote.

 

 

7-Maelezo kuwa mwenye kuvaa hirizi amefanya shirki.

 

 

8-Kuvaa kamba (kitambaa au uzi) kwa ajili ya homa ni sawa na hayo ya kuwa ni shirki.

 

9-Hudhayfah   (رضي الله عنه)kusoma Aayah ya Qur-aan  ni dalili ya wazi kwamba Maswahaba walikuwa wakinukuu Aayah inayohusu shirki kubwa kwa ajili ya kukanusha shirki ndogo, kama alivyofanya Ibn ‘Abbaas   (رضي الله عنهما) kuisoma Aayah ya Al-Baqarah namba (2: 165).

 

 

10-Kuvaa hirizi kwa ajili ya kujilinda na jicho baya kunaangukia katika kundi hilohilo.

 

 

11-Du’aa (ya kumlaani) mwenye kuvaa hirizi, kuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Hatomtimizia maombi yake. Na anayejifunga na kombe (la kiumbe wa baharini), hatokuwa katika amani na utulivu yaani Allaah (سبحانه وتعالى) Hatomjali.

 

 

 

 

 

[1] Hirizi: Karatasi inayotundikwa ukutani kwa ajili ya kinga au kuvaliwa shingoni au mikononi.

Share

08-Kitaab At-Tawhiyd: Tabano Au Azima Na Talasimu

Mlango Wa 8

بَابُ مَا جَاءَ فِي الرُّقَى وَالتَّمَائِمِ

Tabano Au Azima Na Talasimu[1]

 


 

 

فِي الصَّحِيحِ عَنْ أَبِي بَشِيرٍ الأَنْصَارِيِّ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) أَنَّهُ كَانَ مَعَ رَسُولِ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي بَعْضِ أَسْفَارِهِ، فَأَرْسَلَ رَسُولاً أَنْ ((لاَ يَبْقَيَنَّ فِي رَقَبَةِ بَعِيرٍ قِلادَةٌ مِنْ وَتَرٍ أَوْ قِلادَةٌ إِلاَّ قُطِعَتْ)).

Katika Swahiyh, Imepokelewa jutoka kwa Abuu Bashiyr Al-Answaariyy (رضي الله عنه)   kwamba alikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) katika safari mojawapo. Akamtuma mjumbe kuamrisha kwamba: ((Kusiachwe kidani cha uzi au kidani chochote katika shingo za ngamia isipokuwa kikatwe)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَعَنْ ابْنِ مَسْعُودٍ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((إِنَّ الرُّقَى وَالتَّمَائِمَ وَالتِّوَلَةَ شِرْكٌ)) رَوَاهُ أَحْمَدُ وَأَبُو دَاودَ.

Na Imepokelewa toka kwa Ibn Mas’uwd(رضي الله عنه)  kwamba Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Hakika Ar-Ruqaa, At-Tamaaim na At-Tiwalah zote ni shirki)) [Ahmad, Abuu Daawuwd]

 

التَّمَائِمُ: شَيْءٌ يُعَلَّقُ عَلَى الأَوْلاَدِ يَتَّقَونَ بِهِ الْعَيْنَ لَكِنْ إِذَا كَانَ الْمُعَلَّقُ مِنَ الْقُرْآنِ؛ فَرَخَّصَ فِيهِ بَعْضُ السَّلَفِ، وَبَعْضُهُمْ لَمْ يُرَخِّصْ فِيهِ، وَيَجْعَلُهُ مِنَ الْمَنْهِيِّ عَنْهُ، مِنْهُمْ ابْنُ مَسْعُودٍ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ)

 

والرُّقَى: هِيَ الَّتِي تُسَمَّى الْعَزَائِمَ، وَخَصَّ مِنْهَا الدَّلِيلُ مَا خَلاَ مِنَ الشِّرْكِ؛ فَقَدْ رَخَّصَ فِيهِ رَسُولُ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) مِنَ الْعَيْنِ وَالْحُمَةِ

 

والتِّوَلَةُ: هِيَ شَيْءٌ يَصْنَعُونَهُ يَزْعُمُونَ أَنَّهُ يُحَبِّبُ الْمَرْأَةَ إِلَى زَوْجِهَا وَالرَّجُلَ إِلَى امْرَأَتِهِ

 

At-Tamaaim: Wanachofungwa watoto (kama kitambaa cheusi au nyuzi n.k.) shingoni (au mkononi) kukinga jicho baya. Baadhi ya Salaf Swaalih wameruhusu Ikiwa imetiwa Aayah za Qur-aan, au Majina ya Allaah na Sifa Zake, lakini wengine wamekataza. Na Ibn Mas’uwd ni miongoni mwa waliokataza.

 

Ar-Ruqaa au Al-‘Azaaim: Ni tabano au azima inayosomwa. Imeruhusiwa tu inapokuwa haina shirki. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ameiruhusu inapokuwa hali ya kudonelewa na mdudu sumu au anapopatwa mtu na jicho baya (au hasad) au homa.

 

At-Tiwalah (mvuto wa ndere): Kinachodaiwa kuwa kinasababisha mwanamke apendwe zaidi na mumeme au mume apendwe zaidi na mkewe.

 

وَعَنْ عَبْدِ اللهِ بْنِ هُكَيْمٍ مَرْفُوعًا: ((مَنْ تَعَلَّقَ شَيْئًا؛ وُكِّلَ إِلَيْهِ)) رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالتِّرْمِذِيُّ

Na Hadiyth Marfuw’ Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Hukaym: ((Atakayetundika kitu[2] basi amejiweka katika ulinzi wa hicho kitu alichokivaa)) [na kitamdhalilisha] [Ahmad na At-Tirmidhiy]

 

وَرَوَى أَحْمَدُ عَنْ رُوَيْفِعٍ قَالَ؛ قَالَ لِي رَسُولُ اللهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((يَا رُوَيْفِعُ، لَعَلَّ الْحَيَاةَ سَتَطُولُ بِكَ؛ فَأَخْبِرِ النَّاسَ أَنَّ مَنْ عَقَدَ لِحْيَتَهُ، أَوْ تَقَلَّدَ وَتَرًا، أَوِ اسْتَنْجَى بِرَجِيعِ دَابَّةٍ أَوْ عَظْمٍ؛ فَإِنَّ مُحَمَّدًا بَرِيءٌ مِنْهُ))

Na Ahmad amepokea kutoka kwa Ruwayfi’ ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ameniambia: ((Ee Ruwayfi’! Huenda ukaishi zaidi baada yangu. Kwa hiyo wajulishe watu kwamba: Yeyote atakayefunga fundo ndevu zake, au akaweka nyuzi au mshipi shingoni mwake [kuwa ni talasimu] au akastanji na mkojo wa mnyama au mfupa, basi Muhammad amejitenga naye)) [Ahmad, Abuu Daawuwd]

 

وَعَنْ سَعِيدِ بْنِ جُبَيْرٍ؛ قَالَ: مَنْ قَطَعَ تَمِيمَةً مِنْ إِنْسَانٍ؛ كَانَ كَعَدْلِ رَقَبَةٍ. رَوَاهُ وَكِيعٌ وَلَهُ عَنْ إِبْرَاهِيمَ؛ قَالَ: كَانُوا يَكْرَهُونَ التَّمَائِمَ كُلَّهَا مِنَ الْقُرْآنِ وَغَيْرِ الْقُرْآن .

Kutoka kwa Sa’iyd bin Jubayr amesema: “Atakayekata talasimu au hirizi iliyovaliwa na mtu, atapata thawabu kama kuacha huru mtumwa.” Ameirekodi Wakiy’ naye pia amepokea toka kwa Ibraahiym ambaye amesema: “Walikuwa wakichukia talasimu zote ziwe za Qur-aan na zisizokuwa za Qur-aan” (walikuwa hao ni sahibu wa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) .

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Ufafanuzi kuhusu Ar-Ruqaa na At-Tamaaim.

 

2-Ufafanuzi wa At-Tiwalah.

 

3-Vitu vitatu vyote hivyo ni shirki na hakuna kinyume chake.

 

4-Ruqyah (Aayah kutoka katika Qur-aan au Adhkaar katika Sunnah) kwa ajili ya kukinga au kuondosha jicho baya au kudonelewa na mdudu sumu si shirki.

 

5-‘Ulamaa wametofautiana kuhusu kutumia hirizi zilokuwa na Aayah za Qur-aan.

 

6-Kuwavalisha mshipi (wa aina yoyote) wanyama kwa ajili ya kukinga jicho baya inapeleka katika shirki.

 

7-Onyo la adhabu kali kwa anayevaa vitu kama hvyo au kufunga fundo au mshipi wa aina yoyote kwa itikadi kuwa ni kinga au kuondosha madhara.

 

8-Thawabu za anayeikata talasimu aliyoivaa mtu.

 

9-Kauli ya Ibraahiym An-Nakha’iyy kuwa As-Salaf walikuwa wakijiepusha na talasimu hata ikiwa Aayah za Qur-aan au chochote, haipingani na tofauti za rai zilotajwa, kwani maneno hayo yanaashiria msimamo wa ‘Abdullaah bin Mas’uwd.

 

 

 

 

 

 

[1] Aina za hirizi.

[2] Talasimu, hirizi, zindiko na kuitakidi kuwa kitamfaa au kumzuia shari.

 

 

Share

09-Kitaab At-Tawhiyd: Kutabaruku Kwa Mti Au Jiwe Na Vitu Kama Hivyo

Mlango Wa 9

بَابُ مَنْ تَبَرَّكَ بِشَجَرٍ أَوْ حَجَرٍ وَنَحْوِهِمَا

Kutabaruku Kwa Mti Au Jiwe Na Vitu Kama Hivyo

 


 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

أَفَرَأَيْتُمُ اللَّاتَ وَالْعُزَّىٰ ﴿١٩﴾

((Je, mmeona Laata na ‘Uzzaa?))

 

وَمَنَاةَ الثَّالِثَةَ الْأُخْرَىٰ ﴿٢٠﴾

((Na Manaata mwengine wa tatu?))

 

أَلَكُمُ الذَّكَرُ وَلَهُ الْأُنثَىٰ ﴿٢١﴾

((Je, nyinyi mna wana wa kiume Naye Ana wana wa kike?))

 

تِلْكَ إِذًا قِسْمَةٌ ضِيزَىٰ ﴿٢٢﴾

((Hiyo basi hapo ni mgawanyo wa dhulma kubwa!))

 

إِنْ هِيَ إِلَّا أَسْمَاءٌ سَمَّيْتُمُوهَا أَنتُمْ وَآبَاؤُكُم مَّا أَنزَلَ اللَّـهُ بِهَا مِن سُلْطَانٍ ۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا الظَّنَّ وَمَا تَهْوَى الْأَنفُسُ ۖ وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ الْهُدَىٰ ﴿٢٣﴾

((Hayo si chochote isipokuwa ni majina mmeyaita nyinyi na baba zenu, wala Allaah Hakuyateremshia dalili yoyote. Hawafuati isipokuwa dhana na yale yanayotamani nafsi (zao), na hali imekwishawajia kutoka kwa Rabb wao mwongozo)) [An-Najm (53: 19-23)]

 

عن أَبِي وَاقٍد اللَّيْثِيِّ (رضي الله عنه) قَالَ: خَرَجْنَا مَعَ النَّبِيِّ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وآله وَسَلَّمَ) إِلَى حُنَيْنٍ وَنَحْنُ حُدَثَاءُ عَهْدٍ بِكُفْرٍ، وَلِلِمُشْرِكِينَ سِدْرَةٌ، يَعْكُفُونَ عِنْدَهَا وَيُنَوِّطُونَ بِهَا أَسْلِحَتَهُمْ، يُقَالَ لَهَا ذَاتُ أَنْوَاطٍ، فَمَرَرْنَا بِسِدْرَةٍ فَقُلْنَا: يَا رَسُولَ اللهِ اجْعَلْ لَنَا ذَاتَ أَنْوَاطٍ كَمَا لَهُمْ ذَاتُ أَنْوَاط. فَقَالَ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم): ((الله أكبر! هَذَا كَمَا قَالَ قَوْمُ مُوسَى "اجْعَلْ لَنَا إِلَهًا كَمَا لَهُمْ آلِهَةٌ" وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَتَرْكَبُنَّ سُنَّةَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Waaqid Al-Laythiyy(رضي الله عنه)  amesema: “Tulitoka pamoja na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwenda [vitani] Hunayn nasi ndio kwanza tumetoka katika ukafiri, na washirikina walikuwa na mkunazi wanaufanyia ‘ibaadah na walikuwa wakitundika silaha zao [kupata Baraka]. Wakiuita ‘Dhaatu Anwaatw’. Tukapita mbele ya mkunazi tukasema: “Ee Rasuli wa Allaah, tufanyie nasi dhaata-anwaatw kama walivyokuwa nao [makafiri] dhaatu-anwaatw” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Allaahu Akbar!  Hivi ni kama walivyosema watu wa Muwsaa “Tufanyie nasi muabudiwa kama walivyokuwa nao waabudiwa” Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mikononi Mwake, mtafuata nyendo za walio kabla yenu [za ujahili na kufru])) [At-Tirmidhiy na ameikiri ni Swahiyh]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah An-Najm (53:19, 20).

 

2-Kujua kiini cha jambo walilolitaka Maswahaba (kuhusu kuweka mti kama wa dhaat anwaatw).

 

3-Maswahaba hawakutekeleza walichoomba.

 

4-Niyyah yao ilikuwa kujikuruibisha kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kuomba huko, wakidhani kuwa Atalipenda hilo.

 

5-Ikiwa (Maswahaba رضي الله عنهم) hawakujua kosa hilo, wengineo ni wepesi zaidi kutokulijua kosa hilo (na kuingia katika shirki).

 

6- (Maswahaba رضي الله عنهم) wana malipo mema na walikuwa na ahadi ya kughufuriwa jambo ambalo wengineo hawana.

 

7- Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuwapa udhuru kwa hili, bali aliwakanushia kwa kusema, ((Allaahu Akbar!  Hivi ni kama… na mtafuata nyendo za walio kabla yenu…)) Hivyo alidhihirisha uzito wake kwa mambo hayo matatu.

 

8-Lililo muhimu katika jambo hili ni fundisho lililokusudiwa kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alifananisha ombii lao na ombi la wana wa Israaiyl pindi walipomuomba Muwsaa, “Tufanyie muabudiwa.”

 

9-Kukanushwa ombi hilo ni maana ya laa ilaaha illaa Allaah, ambayo juu ya kuwa ni adhimu, iliwifachikia na hawakuhisi. 

 

10-Kuapa kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipotowa hukmu, na haapi isipokuwa kwa manufaa.

 

11-Shirki inaweza kuwa ndogo au kubwa, kwa sababu Maswahaba hawakuritadi kwa ombi lao.

 

12-Kauli yao, “ndio kwanza tumetoka katika ukafiri” inatujulisha kwamba Maswahaba wengineo hawakuwa wajinga wa hilo.

 

13-Kutamka Takbiyr inaweza kuwa ni kuashiria jambo la kustaajabu, kinyume na wanavyodhania wengine (kuwa ni makruuh). 

 

14-Kufunga njia zote zinazopeleka kwenye shirki.

 

15-Kukatazwa kuwaiga watu wa Jaahiliyyah.

 

16-Mwalimu anaweza kuwa na hasira anapofundisha wanafunzi wake (kwa ajili ya kukosoa jambo ovu).

 

17-Kanuni ya jumla katika maendeleo ya mwana Aadam na kufanana kwa mawazo, imedhihirishwa katika kauli yake, ((Hizi ni njia [Sunan])).

 

18-Ni alama ya Unabiy, kwa sababu imetokea sawa na alivyojulisha.

 

19-Kile walichokemewa Mayahudi na Wakristo katika Qur-aan kimekemewa kwetu pia.

 

20-Maswahaba رضي الله عنهم walitambua kwamba matendo ya ‘ibaadah yamejengwa kwa msingi wa wazi kabisa; (‘fanya!’, ‘acha!’) Ndipo kukawa na ukumbusho kuhusu anapoulizwa kaburini; “Ni nani Rabb wako?” Hilo liko wazi. Na kuhusu “Nani Nabiy wako?” Hilo linatokana na Wahyi wa khabari za mambo ya ghaibu. Lakini kuhusu “Ni ipi Dini yako?” basi hilo linahusu ombi lao (Mayahudi kwa Muwsaa), “Tufanyie muabudiwa…” mpaka mwisho.

 

21-Desturi za Ahlul-Kitaab zinakanushwa sawa na za washirikina.

 

22-Aliyetoka katika upotofu baada ya kwishauzoea, (akaingia Uislamu) hajasalimika kabisa na itikadi hizo. Hii ni kutokana na kauli yao, “Nasi ndio kwanza tumetoka katika ukafiri.”

 

 

 

 

Share

10-Kitaab At-Tawhiyd: Kuchinja Kwa Ajili Ya Asiyekuwa Allaah

 

Mlango Wa 10

ماَ جاءَ فِي الذَّبْحِ لِغِيْرِ اللَّه

Kuchinja Kwa Ajili Ya Asiyekuwa Allaah

 


 

وقوله تعالى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٢﴾

((Sema: “Hakika Swalaah yangu, na kuchinja kafara na ‘ibaadah zangu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah Pekee Rabb wa walimwengu.”))

 

لَا شَرِيكَ لَهُ ۖ وَبِذَٰلِكَ أُمِرْتُ وَأَنَا أَوَّلُ الْمُسْلِمِينَ ﴿١٦٣﴾

((Hana mshirika, na kwa hayo ndio nimeamrishwa, nami ni Muislamu wa kwanza)) [Al-An’aam (6: 162-163)]

 

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾

((Basi swali kwa ajili ya Rabb wako na chinja kwa ajili Yake)) [Al-Kawthar (108: 2)]

 

عَنْ عَلِيِّ بن أبي طالب (رضي الله عنه) قَالَ: حَدَّثَنِي رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) بأرْبَعِ كَلِمَاتٍ: ((لَعَنَ اللَّهُ مَنْ ذَبَحَ لِغَيْرِ اللَّهِ، وَلَعَنَ اللَّهُ مَنْ لَعَنَ وَالِدَيْهِ، وَلَعَنَ اللَّهُ مَنْ آوَى مُحْدِثًا، وَلَعَنَ اللَّهُ مَنح مَنَارَ الأَرْضِ))

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aliy bin Abiy Twaalib(رضي الله عنه)  kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alinihadithia maneno manne:  ((Allaah Amemlaani anayechinja si kwa ajili ya Allaah, na Allaah Amemlaani anayewalaani wazazi wake, na Allaah Amelaani anayemkaribisha na kumhami mkhalifu, na Allaah Amelaani anayemlaani mzazi wake, na Allaah Amelaani anayebadilisha mipaka ya ardhi  [anayomiliki] )) [Muslim]

 

وَعنْ طاَرِق بْنِ شهاب (رضي الله عنه) أنَّ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَال: ((دَخَلَ الْجَنَّةَ رَجُلٌ فِي ذُبَابِ، وَدَخَلَ النَّارَ رَجُلٌ فِي ذُبَابِ)): قَالُوا: وَكَيْفَ ذَلِكَ يَا رَسُولُ الله؟ قَالَ: ((مَرَّ رَجُلانِ علَى قَوْمٍ لَهُمْ صَنَمٌ لاَ يُجاوِزُهُ أحَدٌ حَتَّى يُقَرِّبَ لَهُ شَيْئاً، َقَالُوا ِلأَحَدِهِمَا: قَرِّبْ، قَالَ: لَيْسَ عِنْدِي شَيْءٌ أُقَرِّبَ، قَالُوا: قَرِّبْ وَلَوْ ذُباَبًا، فَقَرَّبَ ذُبَاباً، فَخَلُّوا سَبِيْلَهُ، فَدَخَلَ النَّارَ، وَقَالُوا لِلآخِر: قَرِّبْ، فَقَالَ: مَا كُنْتُ لأُقَرِّبَ لأحَدٍ شَيْئًا دُونَ الله عَزَّ وَجَلَّ. فَضَرَبُوا عُنُقَهُ، فَدَخَلَ الْجَنَّةَ))

Na kutoka kwa Twaariq bin Shihaab(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah(صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  amesema: ((Mtu mmoja ameingia Jannah kwa ajili ya nzi, na ameingia motoni mtu mwengine kwa ajili ya nzi)).  Wakasema: Vipi hivyo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Watu wawili walipitia mbele ya watu walikuwa na sanamu lao, hapiti mtu hadi mtu atolee mihanga na kafara. Wakamwambia mmoja wao: Litolee kafara! Akasema: Sina kitu cha kutolea kafara. Wakasema: Toa japo kwa nzi. Akapeleka nzi [kwa sanamu lao] Wakamwachia apite njia akaingia motoni. Wakamwambia mwengine: Litolee kafara!  Akasema:  Sikuwa natoa chochote kuwa kafara kwa ajili ya yeyote asiyekuwa Allaah ‘Azza wa Jalla.  Wakampiga shingo [wakamuua] akaingia Jannah)) [Ahmad]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah:

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي

((Sema: “Hakika Swalaah yangu, na kuchinja kafara na ‘ibaadah zangu”)).

 

2-Tafsiri ya Aayah:

فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾

((Basi swali kwa ajili ya Rabb wako na chinja kwa ajili Yake)).

 

3-Kuanza laana kwa anayechinja mnyama kwa ajili ya asiyekuwa Allaah.

 

4-Kumlaani anayewalaani wazazi wake, hii inajumuisha unapowalaani wazazi wa mtu na hivyo yeye kuwalaani wazazi wako.

 

5-Kumlaani mwenye kumpa hifadhi mkhalifu au mzushi kwa kuwa kamhami baada ya kuwa anastahiki hadd (adhabu katika Shariy’ah).

 

6-Kumlaani anayebadili mipaka ya ardhi, yaani mipaka inayotofautisha baina ya mali yako na majirani, hivyo anaibadili kwa kuzidisha au kupunguza.

 

7-Kutofautisha baina ya kumlaani mtu maalumu kwa ukhalifu maalumu na kuwalaani wakhalifu kwa ujumla. 

 

8-Kisa cha nzi na umuhimu wake.

 

9-Mtu ameingizwa motoni kwa sababu ya nzi ambaye hakumkusudia kumtoa kafara, bali alifanya hivyo kwa sababu ya kuepuka vitisho vya waabudu masanamu.

 

10-Kutambua kiwango cha kuchukia shirki katika nyoyo za Waumini, mmoja alikuwa na subira ya hali juu hadi alikuwa tayari kupoteza uhai wake lakini asimfanyie shirki Allaah (سبحانه وتعالى) hata kidogo. Hakukubaliana na maombi yao licha ya kuwa walichotaka kwake ni kitendo cha dhahiri.

 

11-Aliyeingia motoni alikuwa Muislamu, kwani angelikuwa kafiri, basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) asingelisema: “Ameingia motoni kwa sababu tu ya nzi.”

 

12-Inathibitisha Hadiyth Swahiyh:

الْجَنَّةُ أَقْرَبُ إِلَى أَحَدِكُمْ مِنْ شِرَاكِ نَعْلِهِ وَالنَّارُ مِثْلُ ذَلِكَ

((Jannah iko karibu ya mmoja wenu kuliko kamba za viatu vyake, na moto kadhalika)) [Hadiyth ya ‘Abdullaah bin Mas’uwd katika Al-Bukhaariy na Ahmad]

 

13-Kujua kuwa ‘amali za moyo ndio hitajio muhimu hata baina ya waabudu masanamu.

 

 

 

Share

11-Kitaab At-Tawhiyd: Hapachinjwi Kwa Jina La Allaah Panapochinjwa Kwa Asiyekuwa Allaah

Mlango Wa 11

بَاب لَا يُذْبَحُ لِلَّهِ بِمَكَانٍ يُذْبَحُ فِيهِ لِغَيْرِ اَللَّهِ

Hapachinjwi Kwa Jina La Allaah Mahali Panapochinjwa Kwa Ajili Ya Asiyekuwa Allaah

 


 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

لَا تَقُمْ فِيهِ أَبَدًا ۚ لَّمَسْجِدٌ أُسِّسَ عَلَى التَّقْوَىٰ مِنْ أَوَّلِ يَوْمٍ أَحَقُّ أَن تَقُومَ فِيهِ ۚ فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُوا ۚ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُطَّهِّرِينَ ﴿١٠٨﴾

((Usisimame (Msikitini) humo abadani.  Bila shaka Msikiti ulioasisiwa juu ya taqwa tokea siku ya kwanza unastahiki zaidi usimame humo. Humo mna watu wanaopenda kujitwaharisha. Na Allaah Anapenda wanaojitwaharisha)) [At-Tawbah (9: 108)]

 

عن ثابت بن الضَّحَّاك (رضي الله عنه) قال: نَذَر رجلٌ أن يَنحَرَ إبلا بِبُوانَةَ فسأل النبيَّ (صلى الله عليه وسلم) فقال: ((هَلْ كانَ فيِهَا وَثَنٌ مِن أوْثانِ الجاهِليَّة يُعْبَدُ؟)) قَالوا: لاَ، قال: ((فَهَلْ كَانَ فيِهَا عِيدٌ مِن أعْيادِهِم ؟)) قَالوا: لاَ. فقال رسول الله (صلى الله عليه وسلم): ((أوْفِ بِنَذْرِكَ فإنه لاَ وَفَاء لِنَذرٍ في مَعْصِيَةِ الله وَلا فيَمَا لا يَمْلِكُ ابْنُ آدم)) رواه أبو داود وإسناده على شرطهما  

Imepokelewa kutoka kwa Thaabit bin Adhw-Dhwahaak(رضي الله عنه)  amesema: Mtu mmoja aliweka nadhiri kuchinja ngamia katika mahali paitwapo Buwaanah. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akauliza: ((Je, hapo mahali palikuwa pana sanamu miongoni mwa sanamu ya jahiliya linaloabudiwa?)) Wakajibu: “Hapana.” Akauliza: ((Je, mahali hapo palikuwa panafanywa sherehe miongoni mwa sherehe za makafiri?)) Wakajibu: “Hapana.” Akasema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Timiza nadhiri yako, kwani hakika hakuna kutimiza nadhiri katika kumuasi Allaah, au ambazo kutekelezwa kwake kuko nje ya uwezo wa bin Aadam)) [Imesimuliwa  na Abuu Daawuwd kwa sharti ya kuthibitishwa na Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Maelezo ya kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

لَا تَقُمْ فِيهِ أَبَدًا

((Usisimame (Msikitini) humo abadani)).

 

2-Maasi kumfanyia Allaah (سبحانه وتعالى) na kumtii huleta athari duniani.

 

3-Kurejesha suala lenye utata kwa lisilo na utata kwa ajili ya kuondoa utata.

 

4-Ruhusa kumuuliza Mufti atoe maelezo inapohitajika.  

 

5-Hakuna ubaya kuhusisha sehemu maalumu katika kufanya nadhiri, madamu hakuna makatazo ya Shariy’ah kufanya hivyo hapo.

 

6-Imekatazwa kuweka nadhiri mahali ambako kulikuwa na masanamu ya kijaahiliyyah, na hata kama yameshaondoshwa zamani.

 

7-Kukatazwa nadhiri mahali ambapo washirikina hupatumia kwa sherehe zao za ushirikina hata kama hawaendelei kupatumia mahali hapo.

 

8-Hairuhusiwi kutekeleza nadhiri mahali kama hapo kwa sababu hiyo ni nadhiri ya kumuasi Allaah (سبحانه وتعالى).

 

9-Onyo dhidi ya kujifananisha na washirikina katika sherehe zao, japo bila ya kukusudia.

 

10-Hakuna nadhiri katika maasi.

 

11-Haipasi kuweka nadhiri ambayo mtu hawezi kuitekeleza.  

 

Share

12-Kitaab At-Tawhiyd: Kuweka Nadhiri Kwa Asiyekuwa Allaah Ni Shirki

Mlango Wa 12

بَابٌ مِنْ اَلشِّرْكِ اَلنَّذْرُ لِغَيْرِ اَللَّهِ

Kuweka Nadhiri Kwa Asiyekuwa Allaah Ni Shirki

 


 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا ﴿٧﴾

((Ambao) Wanatimiza nadhiri na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea kwa upana)) [Al-Insaan (76: 7)]

 

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

 

وَمَا أَنفَقْتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوْ نَذَرْتُم مِّن نَّذْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُهُ ۗ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ ﴿٢٧٠﴾

((Na chochote mtoacho (kwa ajili ya Allaah) au mkiwekacho nadhiri, basi Allaah Anakijua. Na madhalimu hawana wa kuwanusuru)) [Al-Baqarah (2: 270)]

 

وفي الصحيح عن عائشة (رضي الله عنها) أن الرسول صلى الله عليه وسلم قال: ((مَنْ نَذَرَ أَنْ يطيعَ اللهَ فَلْيطعْه وَمَنْ نَذَرَ أَن يَعْصيَ اللهَ فَلاَ يَعْصِه))

Na katika Asw-Swahiyh: Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayeweka nadhiri kumtii Allaah na amtii. Na atakayeweka nadhiri kumuasi Allaah asimuasi)) [Al-Bukhaariy]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kutimizia nadhiri ni wajibu.

 

2-Ikiwa imethibitishwa kuwa nadhiri hiyo ni miongoni mwa ‘ibaadah za kumwabudu Allaah (سبحانه وتعالى), basi kumfanyia mwengine ni shirki. 

 

3-Hairuhusiwi kutekeleza nadhiri katika maasi.

 

 

Share

13-Kitaab At-Tawhiyd: Kuomba Kinga Kwa Asiyekuwa Allaah Ni Shirki

Mlango Wa 13

بَابٌ مِنَ الشِّرْكِ الِاسْتِعَاذَةُ بِغَيْرِ اللهِ

Kuomba Kinga Kwa Asiyekuwa Allaah Ni Shirki


 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَأَنَّهُ كَانَ رِجَالٌ مِّنَ الْإِنسِ يَعُوذُونَ بِرِجَالٍ مِّنَ الْجِنِّ فَزَادُوهُمْ رَهَقًا ﴿٦﴾

((“Na kwamba walikuwa wanaume miongoni mwa wana Aadam wanajikinga na wanaume miongoni mwa majini, basi wakawazidishia madhambi, uvukaji mipaka ya kuasi na khofu”)) [Al-Jinn (72: 6)]

 

عن خَوْلَةَ بِنْتَ حَكِيمٍ (رضي الله عنها) قالت: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ:  ((مَنْ نَزَلَ مَنْزلاَ ثُمَّ قَالَ: "أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّاتِ مِنْ شَرِّ مَا خَلَقَ" لَمْ يَضُرَّهُ شَيْءٌ حَتَّى يَرْتَحِلَ مِنْ مَنْزِلِهِ ذَلِكَ)) رواه مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Khawlah bint Hakiym(رضي الله عنها)  kwamba kamsikia Nabiy (صلى الله عليه وسلم) akisema: ((Atakayefikia mahali kisha akasema: A’uwdhu bikalimati-LLaahit-taammati min sharri maa Khalaq' - Najilinda kwa maneno ya Allaah yaliyotimia na shari ya Alichokiumba-  hakuna kitakachomdhuru hadi atakapoondoka mahali pake hapo)) [Muslim]

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Melezo ya Aayah katika Suwratul-Jinn.

 

2-Kuomba ulinzi kwa asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى) ni shirki.

 

3-Hii imeungwa mkono na Hadiyth kwa vile Wanachuoni huitumia kuthibitisha kuwa maneno ya Allaah (سبحانه وتعالى) (yaani Qur’aan) hayakuumbwa kwani yangelikuwa yameumbwa, tusingelitakiwa kujikinga kwa maneno ya Allaah (سبحانه وتعالى), wakasema kuwa kujikinga kwa viumbe ni shirki.

 

4-Fadhila ya du’aa hii japokuwa ni fupi.

 

5-Licha ya ukweli kuwa jambo linaweza kuongoza kwenye manufaa ya kiduna kama kuzuia madhara au kupata manufaa, lakini hilo halithibitishi kuwa silo la shirki.

 

 

 

Share

14-Kitaab At-Tawhiyd: Kustaghithi Na Kumwomba Asiyekuwa Allaah Ni Shirki

Mlango Wa 14

بَابٌ مِنْ اَلشِّرْكِ أَنْ يَسْتَغِيثَ بِغَيْرِ اَللَّهِ أَوْ يَدْعُوَ غَيْرَهُ

Kustaghithi[1] Na Kumwomba Asiyekuwa Allaah Ni Shirki


 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

  وَلَا تَدْعُ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُكَ وَلَا يَضُرُّكَ ۖ فَإِن فَعَلْتَ فَإِنَّكَ إِذًا مِّنَ الظَّالِمِينَ ﴿١٠٦﴾

 ((“Na wala usiombe badala ya Allaah visivyokufaa wala visivyokudhuru. Na ukifanya, basi hakika utakuwa miongoni mwa madhalimu.”))

 

وَإِن يَمْسَسْكَ اللَّـهُ بِضُرٍّ فَلَا كَاشِفَ لَهُ إِلَّا هُوَ ۖ وَإِن يُرِدْكَ بِخَيْرٍ فَلَا رَادَّ لِفَضْلِهِ ۚ يُصِيبُ بِهِ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۚ وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿١٠٧﴾

((Na Allaah Akikugusisha dhara, basi hakuna wa kuiondosha isipokuwa Yeye. Na Akikutakia khayr, basi hakuna wa kurudisha fadhila Zake, Anasababisha kumfikia kwayo (fadhila Yake) Amtakaye katika waja Wake. Naye ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu))  [Yuwnus (10: 106-107)]

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake: 

 

إِنَّمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَوْثَانًا وَتَخْلُقُونَ إِفْكًا ۚ إِنَّ الَّذِينَ تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ لَا يَمْلِكُونَ لَكُمْ رِزْقًا فَابْتَغُوا عِندَ اللَّـهِ الرِّزْقَ وَاعْبُدُوهُ وَاشْكُرُوا لَهُ ۖ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿١٧﴾

((“Hakika mnaabudu badala ya Allaah masanamu, na mnazua uzushi. Hakika wale mnaowaabudu badala ya Allaah hawakumilikiini riziki; basi tafuteni riziki kwa Allaah, na mwabuduni Yeye na mshukuruni, Kwake mtarejeshwa)) [Al-‘Ankabuwt (29: 17)]

 

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

 

وَمَنْ أَضَلُّ مِمَّن يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَن لَّا يَسْتَجِيبُ لَهُ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَهُمْ عَن دُعَائِهِمْ غَافِلُونَ ﴿٥﴾

((“Na nani aliyepotoka zaidi kuliko ambaye anayeomba asiyekuwa Allaah ambaye hamuitikii mpaka Siku ya Qiyaamah; nao wala hawatambui maombi yao.”)) [Al-Ahqaaf (46: 5)]

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

 

 أَمَّن يُجِيبُ الْمُضْطَرَّ إِذَا دَعَاهُ وَيَكْشِفُ السُّوءَ وَيَجْعَلُكُمْ خُلَفَاءَ الْأَرْضِ ۗ أَإِلَـٰهٌ مَّعَ اللَّـهِ ۚ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ ﴿٦٢﴾

((Au nani Anayemuitika mwenye dhiki mno anapomwomba, na Akamuondoshea ouvu na Akakufanyeni makhalifa wa ardhi? Je, yuko muabudiwa wa haki pamoja na Allaah? Ni machache mno mnayokumbuka)) [An-Naml (27: 62)]

 

وروى الطَبَرانيُّ بإسناده: أنه كان في زمن النبي (صلى الله عليه وسلم) منافق يؤذِي المؤمنين، فقال بعضهم: قوموا بنا نَسْتغيثُ برسول الله (صلى الله عليه وسلم) من هذا المنافق. فقال النبي (صلى الله عليه وسلم): ((إنه لايُسْتَغَاثُ بي، وإِنمَاَ يُسْتغاث بالله))

Amesimulia At-Twabaraaniy kwa isnaad yake kwamba katika zama za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwepo mnafiki akiwaudhi Waumini. Wakasema baadhi yao: “Simameni mtuunge tukastaghithi kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) dhidi ya mnafiki huyu.” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Hakika haipasi kustaghithi kwangu, bali inapaswa kustaghithi kwa Allaah)) [Atw-Twabaraaniy fiy Mu’jamil-Kabiyr] 

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuunganisha baina ya “kuomba” (du’aa) na “istighaathah’ ni kama kuunganisha baina ya jambo la ujumla na makhsusi.

 

2-Tafsiri ya Aayah:

وَلَا تَدْعُ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُكَ وَلَا يَضُرُّكَ ۖ

((“Na wala usiombe badala ya Allaah visivyokufaa wala visivyokudhuru)).

 

3-Kufanya hivyo ni shirki kubwa.

 

4-Hata mtu mwema akifanya hivyo; yaani kumwomba asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى), tena kwa ajili ya kuwaridhisha wengine basi anakuwa mmojawapo katika madhalimu (washirikina).

 

5-Tafsiri inayofuatia (Yuwnus: 10:107).

 

6-Kumuomba asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى), hakunufaishi duniani na juu ya hivyo ni kufuru.

 

7-Tafsiri ya Aayah ya tatu (Al-‘Ankabuwt 29:17).

 

8-Haitakiwi kuomba riziki ispokuwa kwa Allaah (سبحانه وتعالى), kama ilivyo Jannah isiombwe isipokuwa Kwake.

 

9-Tafsiri ya Aayah ya nne (Al-Ahqaaf 46: 5).

 

10-Hakuna mpotovu zaidi kuliko yule anayemwomba asiye Allaah (سبحانه وتعالى).

 

11-Anayeombwa si mwenye kumsikia muombaji, hana khabari ya lolote kati ya maombi ya muombaji.

 

12-Maombi hayo yatakuwa ni sababu ya chuki na uadui kati ya anayeomba na anayeombwa. 

 

13-Kumuomba yeyote ni aina ya ‘ibaadah basi huwa ni kumwabudu unayemuomba. 

 

14-Anayeombwa atakanusha kitendo hicho cha ‘ibaadah kinachoelekezwa kwake na mwombaji.   

 

15-Ndio maana ikawa mwombaji huyo ni mpotovu zaidi kuliko wote.

 

16-Tafsiri ya Aayah ya tano (An-Naml 27: 62).

 

17-Jambo la ajabu ni kukiri kwa washirikina kwamba hakuna anayeweza kuondoa dhiki na shida isipokuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee. Ndio maana wakawa wanaomuomba Allaah (سبحانه وتعالى) kwa ikhlaasw kabisa wanapokuwa katika janga.

 

18-Himaya ya Rasuli (صلى الله عليه وآله وسلم) katika kuihami Tawhiyd na kuwa na umakini wa kumheshimu Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

 

 

 

[1] Kuomba msaada wa uokozi katika ambayo hayamo katika uwezo wa mwana Aadam.

Share

15-Kitaab At-Tawhiyd: Kinachoombwa Haiwezekani Kuwa Kiabudiwe

Mlango Wa 15

باب: أَيُشْرِكُونَ مَا لَا يَخْلُقُ شَيْئًا وَهُمْ يُخْلَقُونَ

Kinachoombwa Haiwezekani Kuwa Kiabudiwe


 

قَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

أَيُشْرِكُونَ مَا لَا يَخْلُقُ شَيْئًا وَهُمْ يُخْلَقُونَ ﴿١٩١﴾

((Je, wanawashirikisha (na Allaah) wale ambao hawaumbi kitu na hali wao wameumbwa?))

 

وَلَا يَسْتَطِيعُونَ لَهُمْ نَصْرًا وَلَا أَنفُسَهُمْ يَنصُرُونَ ﴿١٩٢﴾

((Na wala hawawezi kuwanusuru na wala hawawezi kujinusuru nafsi zao)) [Al-A’raaf (7: 191-192]

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake: 

وَالَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِهِ مَا يَمْلِكُونَ مِن قِطْمِيرٍ ﴿١٣﴾

((Na wale mnaowaomba badala Yake hawamiliki hata kijiwavu cha kokwa ya tende))

 

إِن تَدْعُوهُمْ لَا يَسْمَعُوا دُعَاءَكُمْ وَلَوْ سَمِعُوا مَا اسْتَجَابُوا لَكُمْ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكْفُرُونَ بِشِرْكِكُمْ ۚ وَلَا يُنَبِّئُكَ مِثْلُ خَبِيرٍ ﴿١٤﴾

((Mkiwaomba, hawasikii maombi yenu, na hata wakisikia, hawatokuitikieni. Na Siku ya Qiyaamah watakanusha ushirikina wenu, na wala hakuna atakayekujulisha vilivyo kama Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika)) [Faatwir (35: 13-14)]

 

في الصحيح عن أنس (رضي الله عنه)  قال: شُجَّ النبيُّ  (صلى الله عليه وسلم) يوم أُحُدٍ وكُسِرَتْ ربَاعِيَتُهُ، فقال: ((كيف يُفْلِحُ قومٌ شَجُّوا نبيَّهم)) فنزلت: ((لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ))

 

Katika Swahiyh imepokelewa kutoka kwa Anas(رضي الله عنه)  amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alijeruhiwa Siku ya vita vya Uhud meno yake yakavunjika. Akasema: ((Watafaulu vipi watu wanaomjeruhi Nabii wao)) Ikateremka Aayah: ((Si juu yako katika jambo hili)) [Aal-‘Imraan (2: 128)]

 

وفيه عن ابْنِ عُمَر (رضي الله عنهما) أَنه سَمعَ رسول الله  (صلى الله عليه وسلم) إِذا رَفَعَ رأسَه من الرُّكُوعِ فِي الرَّكْعَةِ الأخِيرَة مِنَ الْفَجْرِ: ((اللَّهم العَنْ فُلاَناً وَفُلانًا)) بعدما يقول: سَمِعَ اللّهُ لِمَنْ حَمِدَه رَبَّنا وَلَكَ الْحَمْد فأنزل الله: ((لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ))

وفي رواية: يَدْعو على صَفوانَ بن أُميَّة وسُهَيْلِ بن عَمرو والحارثِ بن هِشَام. فنزلت: ((لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ))

Imenukuliwa humo pia kutoka kwa Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما) amemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipoinua kichwa baada ya kurukuu katika rakaa ya mwisho kwenye Swalaah ya Alfajiri: ((Allaahumma mlaani fulani na fulani)) Allaah Akateremsha:

 

لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ أَوْ يَتُوبَ عَلَيْهِمْ أَوْ يُعَذِّبَهُمْ فَإِنَّهُمْ ظَالِمُونَ ﴿١٢٨﴾

 

Jambo hili halikuhusu wewe; ima Apokee tawbah yao au Awaadhibu, kwani wao ni madhalimu”   Aal-‘Imraan (2: 128)].

 

Na katika riwaayah: Akiwaapiza Swafwaan bin Umayyah, Suhayl bin ‘Amr na Al-Haarith bin Hishaam, ikateremka:

 

لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ أَوْ يَتُوبَ عَلَيْهِمْ أَوْ يُعَذِّبَهُمْ فَإِنَّهُمْ ظَالِمُونَ ﴿١٢٨﴾

 

Jambo hili halikuhusu wewe; ima Apokee tawbah yao au Awaadhibu, kwani wao ni madhalimu”    [Aal-‘Imraan (2: 128)].

 

وفيه عن أبي هُريرةَ (رضىِ الله عنه) قال: قام رسوِل الله  (صلى الله عليه وسلم) حين أُنزل عليه ((وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ )) فقال: ((يا مَعْشَرَ قُرَيش!)) - أو كلمة نحوها: ((اشتَرُوا أنفُسَكُم، لا أُغْنِي عَنْكُم مِنَ الله شيئاً، ويا عبَّاسُ بن عَبْدِ المُطَّلِبِ لا أُغْنِي عَنْكَ مِنَ الله شيئاً، وَيا صَفِيَّةُ عَمَّةَ رسولِ الله، لا أُغْنِى عَنْكِ مِن الله شيئاً، ويا فَاطِمَةُ بِنْتَ مُحمدٍ سَلِينِي مِنْ مَالِي مَا شِئْتِ، لا أُغْنِي عَنْكِ مِنَ الله شيئاً))

Imenukuliwa humo pia kutoka Abuu Hurayrah (رضىِ الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alisimama ilipoteremshwa

 

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ

((Na onya jamaa zako wa karibu)) [Ash-Shu’araa (26: 214)].

 

Akasema: ((Enyi hadhara ya Quraysh)) - au maneno kama hayo - ((Okoeni nafsi zenu, kwani sitowafaeni kwa chochote mbele ya Allaah!  Ee ‘Abbaas bin ‘Abdil-Muttwalib! Sitokufaa kwa chochote mbele ya Allaah!  Ee Swafiyyah shangazi yake Rasuli wa Allaah! Sitokufaa kwa chochote mbele ya Allaah! Ee Faatwimah bint Muhammad! Niombe mali utakayo, [lakini] sitokufaa kwa chochote mbele ya Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri za Aayah: (Al-Araaf 7: 191-192 na Faatwir 35: 13-14).

 

2-Kisa cha Uhud.

 

3-Qunuwt (du’aa) ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Swalaah ikiitikiwa Aamiyn na Maswahaba nyuma yake.

 

4-Wale walioombewa dhidi yao du’aa, ni miongoni mwa makafiri.

 

5-Maquraysh walifanya mambo ambayo makafiri wengi hawakuyafanya, walimpiga Nabiy wao na kumjeruhi kichwani na kuazimia kumuua, kuikatakata miili ya Waislamu waliouawa japokuwa walikuwa ni banu ‘Ammi zao.  

 

6-Juuu ya hivyo, Allaah (سبحانه وتعالى) Alimpelekea Wahyi kuhusu hilo:

 

لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ 

 

Jambo hili halikuhusu wewe; 

 

7-Baada ya Wahyi kuhusu kauli yake Allaah (سبحانه وتعالى):

أَوْ يَتُوبَ عَلَيْهِمْ أَوْ يُعَذِّبَهُمْ

((ima Apokee tawbah yao au Awaadhibu)) [Aal-‘Imraan (2:128)].

 

Akawapokelea tawbah na wakaamini.

 

8-Qunuwt inajuzu wakati wa majanga.

 

9-Kuwataja wanaoapizwa du’aa katika Swalaah kwa majina yao na ya baba zao.

 

10-Kulmlaani mtu wakati wa Qunuwt.

 

11-Kisa na hali ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) wakati alipotumiwa Wahyi wa Aayah:

 

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

((Na onya jamaa zako wa karibu)) [Ash-Shu’araa (26: 214)]

 

12-Uzito wa jambo hili kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) (alifanya bidii kutekeleza da’wah hadi) kufikia kuitwa mwendawazimu na ndivyo hali itakavyokuwa kwa Muislamu yeyote atakapofanya hivyo leo. 

 

13-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliwatangazia nduguze wote wa karibu na wa mbali: ((Sitowafaeni chochote mbele ya Allaah!)) Hata alisema: ((Ee Faatwimah bint Muhammad, sitokufaa kwa chochote mbele ya Allaah)).

 

Ikiwa yeye ni Sayyid wa Manabii na kaliweka wazi hilo, kwamba hatoweza kumfaa chochote mbora wa wanawake duniani (binti yake Faatwimah) na mtu akaamini kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hasemi ila haki, kisha tazama yanayotokeza katika nyoyo za watu leo (kupendelea jamaa zao), hapo itadhihirika kwako suala la Tawhiyd na maajabu ya Dini![1]

 

 

[1] Kuhusu Hadiyth iliyosimuliwa na Muslim ((Hakika umekuja uislamu katika ugeni na utarejea tena katika ugeni na bishara njema kwa watakaokuwa wageni [watendaji watanufaika na mti wa Jannah]).

Share

16-Kitaab At-Tawhiyd: Mpaka Itakapoondolewa Fazaiko Nyoyoni Mwao, Watasema:

Mlango Wa 16

باب: حَتَّىٰ إِذَا فُزِّعَ عَن قُلُوبِهِمْ قَالُوا مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ

Mpaka Itakapoondolewa Fazaiko Nyoyoni Mwao, Watasema: “Amesema Nini Rabb Wenu?”


 

 

قَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

حَتَّىٰ إِذَا فُزِّعَ عَن قُلُوبِهِمْ قَالُوا مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ ۖ قَالُوا الْحَقَّ ۖ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ ﴿٢٣﴾

((Mpaka itakapoondolewa fazaiko nyoyoni mwao, watasema: “Amesema nini Rabb wenu?” Watasema: “Ya haki”; Naye ni Mwenye ‘Uluwa, Ametukuka, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa)) [Sabaa (34: 23)]

 

وفي الصحيح عن أبي هريرة  (رضي الله عنه) قال: قال رسول الله  (صلى الله عليه وسلم): ((إذَا قَضَى اللهُ الأَمْرَ فِي السَّمَاءِ ضَرَبَتِ الْمَلائِكَةُ بِأجْنِحَتِهَا خَضْعَاناً  لِقَوْلِهِ كَأَنَّهُ سِلْسِلَةٌ عَلى صَفْوَانٍ يَنْفُذُهُم ذَلِكَ: ((حَتَّىٰ إِذَا فُزِّعَ عَن قُلُوبِهِمْ قَالُوا مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ ۖ قَالُوا الْحَقَّ ۖ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ)) فَيَسْمَعُهَا مُسْترَقُ السَّمْعِ .ومُسْترقُ السَّمْعِ هَكَذَا بَعْضُهُ فَوْقَ بَعْضٍ)). وَصَفَهُ سُفْيَانُ بِكِفِّهِ فَحَرَّفَهَا وبَدَّدَ بَيْنَ أصابِعِهِ: ((فَيَسْمَعُ الْكَلِمَةَ فَيُلقيها إلىَ مَنْ تَحْتَهُ، ثُمَّ يُلقِيهَا الآخَرُ إلىَ مَنْ تَحْتَهُ حتى َيُلقِيهَا عَلى لِسَانِ السَّاحِرِ أَوْ الْكَاهَنِ، فَرُبَّمِا أَدْرَكَهُ الشِّهابُ قَبْلَ أنْ يُلقِيهَا. وَرُبَّما ألْقاها قَبْلَ أَنْ يُدْرِكَهُ، فَيَكْذِبُ مَعَها مائةَ كَذْبَةٍ فَيُقالُ: أَلَيْسَ قَدْ قَال لنا يَوْمَ كَذا وَكَذا: كَذا وَكَذا فَيُصَدَّقُ بِتِلْكَ الْكَلِمَةِ الَّتِي سُمِعَتْ مِنَ السَّمَاءِ))

Na katika Swahiyh Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Allaah Anapohukumu jambo mbinguni, [na kumpa Wahyi Jibriyl],Malaika hupiga mbawa zao kwa kuinyenyekea kauli [ya wahyi wa Allaah], kwa vile Malaika husikia kama kwamba ni sauti za minyororo ya chuma inyoburutwa katika juu ya jiwe gumu. [Kauli hiyo ya Allaah] Huwakumba na kuwakhofisha hadi wazimie.  Hivyo, ((Mpaka itakapoondolewa khofu nyoyoni mwao; watasema: “Amesema nini Rabb wenu?” Watasema: “Ya haki”; Naye ni Mwenye ‘Uluwa, Ametukuka, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa)) Watasikia amri hii wasikivu wa siri [mashaytwaan].  Na wasikivu wa siri hao wako kama hivi; wanarundikana mmoja juu ya wengine)): Sufyaan alionyesha kwa kuunyanyua mkono wake na kutawanya vidole. ((Wadukizi [wezi wa maneno] husikia neno ambalo hulipeleka kwa aliyechini yake, na wa pili hulipeleka kwa aliye chini yake, hubadilishabadilisha katika kupokeana kauli hiyo mpaka wa mwisho wao ambaye hulipeleka kwa mchawi au kuhani. Mara nyingine kimondo humpiga shaytwaan kabla ya kuwahi kuipeleka [siri aliyosikia] na mara nyingine huwahi kuipeleka kabla kimondo hakijampiga. Hapo mchawi huongezea uongo wake mara mia kuhusu neno hilo. Watu [huku ulimwenguni] husema: Je [mchawi] hatukujulisha kadha na kadhaa siku kadhaa na kadhaa. Hivyo mchawi huaminiwa kwa kuwa kasema ukweli kutokana na kauli iliyosikika mbinguni)) [Al-Bukhaariy]

 

عن النَّوَّاس بن سمعان (رضي الله عنه)  قال:  قال رسول الله  (صلى الله عليه وسلم): ((إذا أرَادَ اللهُ تَعَالى أنْ يُوحِيَ بِالأمِرِ تَكلَّمَ بِالوَحْي أخذت السماوات منه رَجْفَةٌ أو قال رِعْدة شديدة، خوفاً من اللّه عز وجلّ، فإذا سَمعَ ذلك أهلُ السماوات صَعِقوا وخرُّوا لله سُجَّداً، فيكون أوَّل مَنْ يرفعُ رأسه جبريل، فيُكلِّمُهُ الله من وحيه بما أراد، ثم يَمُرُّ جبريل على الملائكة، كُلّماَ مرَّ بسماء سأله ملائكتُها: ماذا قال ربنا يا جبريل؟ فيقول جبريل : قال الحقَّ، وهو العلي الكبير، فيقولون كلّهم مِثل ما قال جبريل، فينْتهي جبريل بالوحي إلى حيثُ أمَرَهُ الله عز وجل))

Kutoka kwa An-Nawaas bin Sam’aan (رضي الله عنه)   amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Anapotaka kuleta Wahyi wa jambo, Hutamka na mbingu hutetemeka kwa nguvu)) Au kasema: ((Radi ya nguvu kwa kumkhofu Allaah ‘Azza wa Jalla. Wanapoyasikia Malaika wa mbinguni, huzimia au huporomoka na kusujudu. Wa kwanza anayeinua kichwa chake huwa ni Jibriyl. Kisha Allaah Humsemesha kumpa Wahyi Autakao. Kisha Jibriyl huwapitia Malaika. Kila anapopita mbingu moja Malaika humuuliza: Amesema nini Rabb wetu ee Jibriyl? Hujibu: [Amesema]: ((Ya haki”; Naye ni Mwenye ‘Uluwa, Ametukuka, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa)) Wote husema kama alivyosema Jibriyl. Jibriyl humalizia kuufikisha Wahyi alipoamrishwa na Allaah ‘Azza wa Jalla)) [Ibn Khuzaymah fiy At-Tawhiyd (206)]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Sabaa (34:23).

 

2-Yaliyomo humo miongoni mwa hoja kuu ya kubatilisha shirki hususani kwa wenye kutegemea waja wema kwa shafaa’ah. Aayahi hii inajulikana kuwa ndiyo inayokata mizizi ya shirki.

 

3-Tafsiri ya Aayah:

قَالُوا الْحَقَّ ۖ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ ﴿٢٣﴾

((Watasema: “Ya haki”; Naye ni Mwenye ‘Uluwa, Ametukuka, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa))

  

4- Sababu ya wao (Malaika) kuuliza swali hilo (katika Aayah)

 

5-Baada ya hapo, Jibriyl alijibu swali lao kwa kusema, “Amesema kadhaa wa kadhaa.”

 

6-Kutajwa kuwa wa kwanza atakayeinua kichwa chake ni Jibriyl.

 

7-Jibriyl huwaambia wote Malaika wote walioko mbinguni kwa sababu wamemuuliza.

 

8-Athari ya tetemeko linawaenea wakazi wote wa mbinguni.

 

9-Jinsi mbingu zinavyotetemshwa kutokana na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

10-Jibriyl ndiye anayepeleka Wahyi mahali Anapomwamuru Allaah (سبحانه وتعالى).

 

11-Kuhusu udukuzi wa shaytwaan (kusikiliza siri).

 

12-Kupandiana kwa majini mmoja juu ya mwingine.

 

13-Kufyatuliwa vimondo vya moto.

 

14-Wakati mwingine vimondo vinamwangamiza shaytwaan kabla hawajafikisha khabari, na wakati mwingine humwangamiza baada ya kuifikisha khabari katika sikio la rafiki yake; shaytwaan bin Aadam.

 

15-Wakati mwingine kuhani (au mtabiri) huenda akasema ukweli.

 

16-Pamoja na ukweli huo huongezea uongo mara mia. 

 

17-Utabiri wa watabiri huenda mara nyingine ukawa ni ukweli, lakini hayo hutegemea na yaliyosikika mbinguni. 

 

18-Watu kukubali uongo (wa mtabiri). Wanawezaje kutegemea ukweli mmoja na kutokuzingatia mara 99 ya uongo wake?

 

19-Jinsi wanavyopashana maneno na wanayahifadhi na kuyatumia dalili (ya uongo mwingine).

 

20-Uthibitisho wa Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) kinyume na madai ya Ash‘ariyyah[1] na Mu’attwilah.

 

21-Ngurumo na tetemeko la mbingu ni kwa ajili ya kumkhofu Allaah (سبحانه وتعالى).

 

22-Malaika wanaporomoka chini kumsujudia Allaah (سبحانه وتعالى) baada ya kusikia maneno Yake.

 

 

 

[1] Watu wanaojinasibisha kwa ‘Abul-Hasan Ash´ariyy ambao wanakanusha Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) Alizozithibitisha katika Qur-aan kuhusu mikono, miguu n.k. Lakini alitubia na akarudia katika msimamo wa Ahlus-Sunnah. 

 

 

Share

17-Kitaab At-Tawhiyd: Ash-Shafaa’ah – Uombezi

Mlango Wa 17

بَابُ اَلشَّفَاعَةِ

Ash-Shafaa’ah – Uombezi

 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ:

Na kauli ya Allaah ‘Azza wa Jalla:

 

وَأَنذِرْ بِهِ الَّذِينَ يَخَافُونَ أَن يُحْشَرُوا إِلَىٰ رَبِّهِمْ ۙ لَيْسَ لَهُم مِّن دُونِهِ وَلِيٌّ وَلَا شَفِيعٌ

((Na waonye kwayo (Qur-aan) wale wanaokhofu ya kwamba watakusanywa kwa Rabb wao; hawana badala Yake mlinzi wala mwombezi)) [Al-An’aam (6: 51)]

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

قُل لِّلَّـهِ الشَّفَاعَةُ جَمِيعًا ۖ لَّهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٤٤﴾

((Sema: “Uombezi wote ni wa Allaah Pekee…”)) [Az-Zumar (39: 44)]

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 مَن ذَا الَّذِي يَشْفَعُ عِندَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ ۚ

((Nani huyu ambaye anashufai mbele Yake bila ya idhini Yake))  [Al-Baqarah (2: 255)]

 

وَقَوْلِهِ:   

Na kauli Yake:

 

وَكَم مِّن مَّلَكٍ فِي السَّمَاوَاتِ لَا تُغْنِي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا إِلَّا مِن بَعْدِ أَن يَأْذَنَ اللَّـهُ لِمَن يَشَاءُ وَيَرْضَىٰ ﴿٢٦﴾

((Na Malaika wangapi mbinguni haitowafaa kitu chochote uombezi wao isipokuwa baada ya kuwa Allaah Ametolea idhini kwa Amtakaye na Akaridhia)) [An-Najm (53: 26)]

 

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ  

((Sema: “Ombeni wale mnaodai kwa dhana (ni waabudiwa) badala ya Allaah, hawamiliki hata uzito wa sisimizi mbinguni wala ardhini)) [Sabaa (34: 22)]

 

قَالَ أَبُو الْعَبَّاسِ، نَفَى اَللَّهُ عَمَّا سِوَاهُ كُلَّ مَا يَتَعَلَّقُ بِهِ الْمُشْرِكُونَ، فَنَفَى أَنْ يَكُونَ لِغَيْرِهِ مُلْكٌ أَوْ قِسْطٌ مِنْهُ أَوْ يَكُونَ عَوْنًا لِلَّهِ وَلَمْ يَبْقَ إِلاَّ اَلشَّفَاعَةُ، فَبَيَّنَ أَنَّهَا لاَ تَنْفَعُ إِلاَّ لِمَنْ أَذِنَ لَهُ اَلرَّبُّ، كَمَا قَالَ: ((وَلَا يَشْفَعُونَ إِلَّا لِمَنِ ارْتَضَىٰ ))

Abuu Al-‘Abbaas[1] amesema: “Allaah Amekanusha kila kisichokuwa Yeye ambacho washirikina wanawanyenyekea.  Akakanusha kuwa hakuna isipokuwa Yeye Allaah Mwenye milki na uwezo. Hakuna mwenye kusaidia ila Yeye. Kinachobaki ni shafaa’ah. Akabainisha kwamba hautomfaa yeyote isipokuwa ambaye amepewa idhini ya Rabb kama Anavyosema: ((na wala hawataomba shafaa’ah (yeyote) isipokuwa kwa yule ambaye (Allaah) Amemridhia)) [Al-Anbiyaa (21: 28)]

 

فَهَذِهِ اَلشَّفَاعَةُ اَلَّتِي يَظُنُّهَا الْمُشْرِكُونَ هِيَ مُنْتَفِيَةٌ يَوْمَ الْقِيَامَةِ، كَمَا نَفَاهَا الْقُرْآنُ، وَأَخْبَرَ اَلنَّبِيُّ  (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  أَنَّهُ يَأْتِي فَيَسْجُدُ لِرَبِّهِ وَيَحْمَدُهُ  لاَ يَبْدَأُ بِالشَّفَاعَةِ أَوَّلاً - ثُمَّ يُقَالُ لَهُ اِرْفَعْ رَأْسَكَ وَقُلْ يُسْمَعْ وَسَلْ تُعْطَ وَاشْفَعْ تُشَفَّعْ.  

Kwa sababu hiyo shafaa’ah wanayoiamini washirikna itakanushwa Siku ya Qiyaamah kama ilivyokanushwa na Qur-aan na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliposema kwamba: Atafika kisha atamsujudia Rabb wake atamhimidi, na hatoanza kwanza kwa shafaa’ah. Kisha itasemwa: “Inua kichwa chako! Sema utasikilizwa! Omba utapewa! Omba shafaa’ah utaruhusiwa kuombeza)) [Al-Bukhaariy na Muslim]   

 

وَقَالَ لَهُ أَبُو هُرَيْرَةَ (رضي اَللَّهُ عَنْهُ): مَنْ أَسْعَدُ اَلنَّاسِ بِشَفَاعَتِكَ؟ قَالَ: ((مَنْ قَالَ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ خَالِصًا مِنْ قَلْبِهِ))

Abuu Hurayrah (رضي اَللَّهُ عَنْهُ) alimuuliza: “Nani atakayefanikiwa zaidi na shafaa’ah yako? Akajibu: ((Atakayesema Laa ilaaha illa-Allaah, hali ya kuwa na niyyah safi moyoni mwake)) [Al-Bukhaariy]

 

فَتِلْكَ اَلشَّفَاعَةُ لأَهْلِ الإِخْلاصِ بِإِذْنِ اَللَّهِ، وَلا تَكُونُ لِمَنْ أَشْرَكَ بِاَللَّهِ

Basi hiyo ndio shafaa’ah kwa watu wenye ikhlaasw kwa idhini ya Allaah, wala haitokuwa kwa anayemshirikisha Allaah.

 

وَحَقِيقَتُهُ أَنَّ اَللَّهَ سُبْحَانَهُ هُوَ اَلَّذِي يَتَفَضَّلُ عَلَى أَهْلِ الإِخْلاصِ، فَيَغْفِرُ لَهُمْ بِوَاسِطَةِ دُعَاءِ مَنْ أَذِنَ لَهُ أَنْ يَشْفَعَ، لِيُكْرِمَهُ وَيَنَالَ الْمَقَامَ الْمَحْمُودَ

Na uhakika wake (shafaa’ah hiyo) ni kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye Ambaye Anayewafanyia ihsaan watu wa ikhlaasw [katika ‘ibaadah zao]. Atawaghufuria kwa wasita wa du’aa au shafaa’ah ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ili Amkirimu na aweze (صلى الله عليه وآله وسلم) kufikia cheo cha Al-Maqaam Al-Mahmuwd[2].   

 

فَالشَّفَاعَةُ اَلَّتِي نَفَاهَا الْقُرْآنُ مَا كَانَ فِيهَا شِرْكٌ، وَلِهَذَا أَثْبَتَ اَلشَّفَاعَةَ بِإِذْنِهِ فِي مَوَاضِعَ وَقَدْ بَيَّنَ اَلنَّبِيُّ  (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) أَنَّهَا لاَ تَكُونُ إِلاَّ لأَهْلِ الإِخْلاصِ وَالتَّوْحِيدِ.  اِنْتَهَى كَلامُهُ

Basi shafaa’ah inayokanushwa na Qur-aan ni iliyo na shirki, na ndio maana shafaa’ah imethibiti kwa idhini ya Allaah sehemu nyingi na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amebainisha kwamba shafaa’ah haitokuwa isipokuwa kwa watu wa Tawhiyd na ikhlaasw [katika Dini yao]” - Mwisho wa maneno ya Ibn Taymiyyah.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah zilizotajwa.

 

2-Maelezo ya aina ya shafaa’ah iliyokanushwa.

 

3-Maelezo ya aina ya shafaa’ah iliyothibiti.

 

4-Kutajwa shafaa’ah kuu (ya Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم) na kuhusu Al-Maqaam Al-Mahmuwd.

 

5-Atakalofanya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), na kwamba hatoanza na shafaa’ah, bali atasujudu, halafu atakapopewa idhini ndipo atakapoinuka kuombea shafaa’ah.

 

6-Nani atakayefaidika kupata hadhi hiyo ya shafaa’ah ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)?

 

7-Shafaa’ah haitokuwa kwa wanaomshirikisha Allaah (سبحانه وتعالى).

 

8-Kubainisha ukweli wa shafaa’ah.

 

 

 

 

 

 

[1] Shaykhul-Islaam Taqiyyud-Diyn Ahmad bin ‘Abdil-Haliym bin ‘Abdis-Salaam, bin Taymiyyah - Fat-hul-Majiyd, uk. 168.

[2] Mahali pa kuhimidiwa katika cheo kikuu Jannah.

 

 

Share

18-Kitaab At-Tawhiyd: Hakika Wewe Huwezi Kumhidi Umpendaye

Mlango Wa 18

باب:  إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ

Hakika Wewe Huwezi Kumhidi Umpendaye


 

 

قَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ ﴿٥٦﴾

((Hakika wewe huwezi kumhidi umpendaye; lakini Allaah Humhidi Amtakaye, Naye Anawajua zaidi wenye kuongoka)) [Al-Qaswasw (28: 56)]

 

وَفِي اَلصَّحِيحِ، عَنْ اِبْنِ الْمُسَيَّبِ، عَنْ أَبِيهِ، قَالَ: لَمَّا حَضَرَتْ أَبَا طَالِبٍ الْوَفَاةُ; جَاءَهُ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) وَعِنْدَهُ عَبْدُ اَللَّهِ بْنُ أَبِي أُمِّيَّةَ وَأَبُو جَهْلٍ فَقَالَ لَهُ: ((يَا عَمِّ قُلْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ كَلِمَةً أُحَاجُّ لَكَ بِهَا عِنْدَ اَللَّهِ)) فَقَالاَ لَهُ: أَتَرْغَبُ عَنْ مِلَّةِ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ؟ فَأَعَادَ عَلَيْهِ اَلنَّبِيُّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَأَعَادَا، فَكَانَ آخَرَ مَا قَالَ: هُوَ عَلَى مِلَّةِ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ، وَأَبَى أَنْ يَقُولَ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ فَقَالَ اَلنَّبِيُّ  (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لأَسْتَغْفِرَنَّ لَكَ مَا لَمْ أُنْهَ عَنْكَ)). فَأَنْزَلَ اَللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَن يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُوا أُولِي قُرْبَىٰ)) وَأَنْزَلَ اَللَّهُ فِي أَبِي طَالِبٍ: ((إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ))

 

Katika Swahiyh, Ibn Musayyib amehadithia kutoka kwa baba yake: Mauti yalipomkaribia Abuu Twaalib, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alimwendea akamkuta ‘Abdullaah bin Abiy Umayyah na Abuu Jahl wakiwa pamoja naye. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ee ‘ammi wangu! Sema laa ilaaha illa-Allaah, hivyo utaniwezesha kukuombea shafaa’ah kwa Allaah)) Wawili hao wakamwambia: Utaacha dini ya [baba yako] ‘Abdul-Muttwalib? Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akakariri [ombi lake] na wawili hao wakakariri nao vile vile. Ikawa neno la mwisho alosema ni kubakika katika dini ya ‘Abdul-Muttwalib. Akafariki akiwa amekataa kusema ‘laa ilaaha illa-Allaah’. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Nitaendelea kukuombea maghfirah madamu sijakatazwa kufanya hivyo)). Hapo Allaah ‘Azza wa Jalla Akateremsha Aayah: ((Haimpasi Nabiy na wale walioamini kuwaombea maghfirah washirikina japokuwa ni jamaa zao wa karibu)) [At-Tawbah (9: 113)] Kisha Akateremsha kuhusu Abuu Twaalib: ((Hakika wewe huwezi kumhidi umpendaye; lakini Allaah Humhidi Amtakaye, Naye Anawajua zaidi wenye kuongoka)) [Al-Qaswasw (28: 56)]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Qaswasw (28: 56)

إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ ۚ

((Hakika wewe huwezi kumhidi umpendaye; lakini Allaah Humhidi Amtakaye)).

 

2-Tafsiri ya Aayah:

 

مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَن يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُوا أُولِي قُرْبَىٰ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمْ أَنَّهُمْ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ ﴿١١٣﴾

((Haimpasi Nabiy na wale walioamini kuwaombea maghfirah washirikina japokuwa ni jamaa zao wa karibu baada ya kuwabainikia kwamba wao ni watu wa moto uwakao vikali mno)) [At-Tawbah (9: 113)].

 

3-Suala kubwa la tafsiri ya kauli yake (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Sema, Laa ilaaha illaa Allaah)) Inakinzana na madai ya wanodai kuwa wana ujuzi wa elimu ya Dini (kudai kwao kwamba kuitamka kwake inatosheleza kusamehewa juu ya kwamba wanawaomba na kuwaabudu mawalii wao). 

 

4-Abuu Jahl na wenzake walijua kusudio la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipomwambia Abuu Twaalib: ((Sema ‘Laa ilaaha illaa Allaah)), Basi Allaah (سبحانه وتعالى) Amdhalilishe yeyote ambaye elimu yake juu ya asili ya Uislamu ni ndogo kuliko ile ya Abuu Jahl.   

 

5-Hima utashi wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kumsilimisha ‘ammi yake.

 

6-Kukanushwa yeyote anayedai kuwa ‘Abdul-Muttwalib na baba zake walikuwa Waislamu.

 

7-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alimwombea ‘ammi yake msamaha lakini hakusamehewa, na kuwa hilo limekatazwa.

 

8-Madhara ya kuandamana na waovu.

 

9-Madhara ya kuwatukuza kibubusa viongozi na wahenga (na hali ni washirikina).

 

10-Shubuha za wapotofu katika hilo ni hoja za ujaahiliyyah (kama Abuu Jahl alivyojitokeza).

 

11-Dalili kwamba ‘amali za mmojawapo zinategemea mwisho wake, kwa sababu kama angeitamka laa ilaaha illa-Allaah, angeliokoka.

 

12-Zingatio la hoja hii ya mwisho katika nyoyo za wapotofu kujivunia dini na mila za mababu, kwa sababu kisa kinathibitisha kwamba hawakujadiliana naye isipokuwa kuhusu kuing’ang’ania dini au mila zao, japokuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliendelea kumbembeleza Abuu Twaalib atamke shahaada, kwani angelishuhudia angeliokoka, lakini wao wakashikilia tu umuhimu wa kufuata dini ya wazazi wao.

 

 

 

Share

19-Kitaab At-Tawhiyd: Sababu WanaAadam Kukufuru, Kuacha Dini Kupinduka Mipaka Kutukuza Waja Wema

Mlango Wa 19

بَابُ مَا جَاءَ أَنَّ سَبَبَ كُفْرِ بَنِي آدَمَ وَتَرْكِهِمْ دِينَهُمْ هُوَ الْغُلُوُّ فِي اَلصَّالِحِينَ

Sababu Ya Wana Aadam Kukufuru Na kuacha Dini Yao Ni Kupindukia Mipaka Katika Kuwatukuza Waja Wema


 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ:  

 Na kauli ya Allaah ‘Azza wa Jalla:

 يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَا تَغْلُوا فِي دِينِكُمْ

((Enyi Ahlal-Kitaabi! Msipindukie mipaka katika dini yenu)) [An-Nisaa (4: 171)]

 

وَفِي اَلصَّحِيحِ عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) فِي قَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى: ((وَقَالُوا لَا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلَا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلَا سُوَاعًا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا )) قَالَ: ((هَذِهِ أَسْمَاءُ رِجَالٍ صَالِحِينَ مِنْ قَوْمٍ نُوحٍ ، فَلَمَّا هَلَكُوا أَوْحَى اَلشَّيْطَانُ إِلَى قَوْمِهِمْ أَنِ انْصُبُوا إِلَى مَجَالِسِهِمْ اَلَّتِي كَانُوا يَجْلِسُونَ فِيهَا أَنْصَابًا وَسَمُّوهَا بِأَسْمَائِهِمْ، فَفَعَلُوا وَلَمْ تُعْبَدْ حَتَّى إِذَا هَلَكَ أُولَئِكَ وَنُسِيَ الْعِلْمُ عُبِدَتْ))

Na katika Swahiyh Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) amesema kuhusu kauli ya Allaah Ta’aalaa: ((Wakasema: “Msiwaache waabudiwa wenu; na wala msimwache Waddaa, na wala Su’waa’a, na wala Yaghuwtha, na Ya’uwqa, na Nasraa)) [Nuwh (71: 23)] Akasema: ((Haya ni majina ya waja wema miongoni mwa kaumu ya Nuwh. Walipofariki shaytwaan aliwashawishi watu wawaweke kama masanamu kuwaheshimu na wakawaweka katika mabaraza yao waliyokuwa wakikaa. Wakawaita majina yao hao waja wema waliofariki. Hapo mwanzoni hawakuwa wakiwaabudu, hadi watu hao walipofariki, na iliposahauliwa asili yake masanamu hayo yakaanza kuabudiwa))

 

قَالَ اِبْنُ الْقَيِّمِ:  قَالَ غَيْرُ وَاحِدٍ مِنْ اَلسَّلَفِ: لَمَّا مَاتُوا، عَكَفُوا عَلَى قُبُورِهِمْ، ثُمَّ صَوَّرُوا تَمَاثِيلَهُمْ ثُمَّ طَالَ عَلَيْهِمْ الأَمَدُ فَعَبَدُوهُمْ

Ibn Al-Qayyim  (رحمه الله)amesema: “Aghlabu ya As-Salaf wamesema: “Baada ya kufariki (waja wema) wakawawekea mipaka makaburini mwao na wakaweka masanamu yao na baada ya muda kupita wakaanza kuyaabudu.”

 

وَعَنْ عُمَرَ (رضي الله عنه): أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ تُطْرُونِي كَمَا أَطْرَتِ اَلنَّصَارَى اِبْنَ مَرْيَمَ، إِنَّمَا أَنَا عَبْدٌ، فَقُولُوا عَبْدُ اَللَّهِ وَرَسُولُهُ)) أَخْرِجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza  mwana wa Maryam, hakika mimi ni mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Rasuli Wake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]   

 

وقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)): ((إِيَّاكُمْ وَالْغُلُوَّ فَإِنَّمَا أَهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ الْغُلُوُّ))

Na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Tahadharini na upindukiaji mipaka ya Dini, kwani waliokuwa kabla yenu waliangamia kwa sababu ya uvukaji mipaka ya Dini)) [Ahmad, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ibn Khuzaymah, Al-Haakim na Adh-Dhahabiy kaiwafiki kuwa ni Swahiyh]

 

 وَلِمُسْلِمٍ عَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ  (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  قَال:  ((هَلَكَ الْمُتَنَطِّعُونَ))  قَالَهَا ثَلَاثًا

Na (Swahiyh) Muslim amepokea kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Wameangamia wapindukiaji mipaka)) amesema mara tatu. [Muslim]

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Yeyote anayeelewa mlango huu hii na miwili inayofuatia, atadhihirikiwa upekee wa Uislamu na atafahamu Qudra ya Allaah (سبحانه وتعالى) ya kuzibadlisha nyoyo.

 

2-Kujua kuwa shirki ya kwanza kabisa ilyozuka duniani ilihusu waja wema (kudhania wana sifa na uwezo kama wa Allaah).

 

3-Jambo la kwanza kubadilishwa katika dini ya Rusuli na kilichosababisha hivyo, juu ya kujulikana kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Ndiye aliyewatuma.

 

4-Kutambua sababu ya kuikubali bid’ah licha ya kuwa ni kinyume na Shariy’ah (ya Dini) na maumbile.

 

5-Sababu ya yote haya ni kuchanganya haki na batili. Mwanzo ilikuwa kuwatukuza waja wema. La pili ni baadhi ya watu wa elimu walikuwa walikifanya kwa niyyah njema, lakini vizazi vilivyokuja baadaye walikusudia vinginevyo.

 

6-Tafsiri ya Aayah katika Suwratun-Nuwh (71: 23)

 

7-Maumbile ya mwana Aadam, haki hupungua moyoni mwake, na hapo upotofu huongezeka (isipokuwa ambaye Allaah (سبحانه وتعالى) Amemteremshia rahmah Yake).

 

8-Inathibitisha kauli za Salaf kuwa bid’ah ni sababu ya kufr, nayo inapendwa mno na Ibliys kuliko maasi, kwa sababu mtu hutubia maasi, ama bid’ah hatubii (kwa kuwa anadhania ni ‘amali njema). 

 

9-Ufahamu wa shaytwaan wa natija ya mwisho kuhusu bid’ah inavyopelekea (katika upotofu) hata kama niyyah ya mtu ilikuwa ni safi. 

 

10-Kujifunza kanuni ya kijumla nayo ni kukatazwa kupindukia mipaka na kufahamu inapelekea wapi. 

 

11-Madhara ya ziara ndefu makaburini hata ikiwa ni kwa niyyah ya kufanya ‘amali njema.

 

12-Kukatazwa masanamu na hekima ya kuyavunjulia mbali.

 

13-Kujua umuhimu wa kisa hiki, na kusisitiza kupata mafunzo yake na kutokughafilika nacho kwa kuwa ni jambo linalopuuzwa.

 

14-Ni ajabu kubwa, wanalisoma hilo katika vitabu vya Tafsiyr na Hadiyth, na wanaelewa maana yake, lakini juu ya hivyo, Allaah (سبحانه وتعالى) Ameziwekea vikwazo nyoyo zao hadi wakaitakidi kuwa matendo ya kaumu Nuwh (kuwatukuza waja wema waliofariki na makaburi yao) ni aina bora ya ‘ibaadah na wakaamini Alivyovikataza Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) ni kufru inayohalalisha damu na mali ya wakanushao.

 

15-Ufafanuzi kuwa wao kwa matendo yao walikusudia shafaa’ah tu.

 

16-Waliamini kuwa wenye elimu waliochonga masanamu walikuwa na niyyah hiyo hiyo.

 

17-Ufafanuzi wa kauli yake: ((Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza mwana wa Maryam)). Allaah Amshushie rahmah na amani kwa kubalighisha ujumbe wake waziwazi.

 

18-Onyo lake kwetu kwamba kupindukia mipaka ya Dini inapeleka katika maangamizi.

 

19-Maelezo kwamba masanamu hayakuabudiwa isipokuwa baada ya elimu ya asili yake kupotea. Hii inatambulisha thamani ya elimu ya historia na madhara ya kukosekana kwake.

 

20-Sababu ya kupotea elimu ni kufariki kwa Wanachuoni.

 

 

 

 

Share

20-Kitaab At-Tawhiyd: Haramisho La Kumwabudu Allaah Kwenye Kaburi La Mja Mwema

Mlango Wa 20

بَابُ مَا جَاءَ مِنْ اَلتَّغْلِيظِ فِيمَنْ عَبَدَ اَللَّهَ عِنْدَ قَبْرِ رَجُلٍ صَالِحٍ، فَكَيْفَ إِذَا عَبَدَهُ؟

Kushadidishwa Haramisho La Kumwabudu Allaah Kwenye Kaburi La Mja Mwema, Basi Ubaya Ulioje Akimuabudu Huyo Mja Mwema?


 

 فِي اَلصَّحِيحِ عَنْ عَائِشَةَ (رضي الله عنها)  أَنَّ أُمَّ سَلَمَةَ ذَكَرَتْ لِرَسُولِ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) كَنِيسَةً رَأَتْهَا بِأَرْضِ الْحَبَشَةِ، وَمَا فِيهَا مِنْ اَلصُّوَرِ فَقَالَ: ((أُولَئِكَ إِذَا مَاتَ فِيهِمْ اَلرَّجُلُ اَلصَّالِحُ أَوْ الْعَبْدُ اَلصَّالِحُ، بَنَوْا عَلَى قَبْرِهِ مَسْجِدًا، وَصَوَّرُوا فِيهِ تِلْكَ اَلصُّوَرَ، أُولَئِكَ شِرَارُ الْخَلْقِ عِنْدَ اَللَّهِ. فَهَؤُلاءِ جَمَعُوا بَيْنَ الْفِتْنَتَيْنِ فِتْنَةَ الْقُبُورِ، وَفِتْنَةَ اَلتَّمَاثِيلِ))

Katika Swahiyh, Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها)  kwamba Ummu Salamah alimtajia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba aliona kanisa zuri Abyssinia lilojaa picha na masanamu. Akasema: ((Hao, anapokufa mtu mwema miongoni mwao, au mja mwema, hujenga Msikiti juu ya kaburi lake. Kisha wakazichora ndani yake picha hizo. Hao ni viumbe waovu mbele ya Allaah. Basi hao wamejumuisha baina ya fitnah mbili; fitnah ya makaburi na fitnah ya masanamu)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

  وَلَهُمَا عَنْهَا، قَالَتْ: لَمَّا نَزَلَ بِرَسُولِ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)) طَفِقَ يَطْرَحُ خَمِيصَةً لَهُ عَلَى وَجْهِهِ، فَإِذَا اِغْتَمَّ بِهَا كَشَفَهَا فَقَالَ وَهُوَ كَذَلِكَ: ((لَعْنَةُ اَللَّهُ عَلَى الْيَهُودِ وَالنَّصَارَى، اِتَّخَذُوا قُبُورَ أَنْبِيَائِهِمْ مَسَاجِدَ)) يُحَذِّرُ مَا صَنَعُوا، وَلَوْلاَ ذَلِكَ، أُبْرِزَ قَبْرُهُ،  غَيْرَ أَنَّهُ خَشِيَ أَنْ يُتَّخَذَ مَسْجِدًا - أَخْرِجَاهُ

Na kutoka kwao pia, amesema ‘Aaishah (رضي الله عنها): Mauti yalipomkaribia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alianza kuchomoa kipande cha kitambaa [cha shuka ya kitanda] akijiwekea usoni mwake [mara akijifunika mara akijifunua kutokana na Sakaratul-Mawti]. Akasema alipokuwa katika hali hiyo: ((Allaah Awalaani Mayahudi na Manaswara kwa kufanya makaburi ya Manabii wao kuwa mahali pa ‘ibaadah)). Akawatahadharisha watu kuhusu vitendo vyao. Ingelikuwa si kuchelea hivyo [khofu ya kufanya kaburi la Nabiy kuwa mahali pa ‘ibaadah], basi kaburi lake lingeliwekwa wazi [kama yalivyowekwa wazi makaburi ya Maswahaba wake] [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَلِمُسْلِمٍ عَنْ جُنْدُبِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ قَالَ سَمِعْتُ اَلنَّبِيَّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَبْلَ أَنْ يَمُوتَ بِخَمْسٍ وَهُوَ يَقُولُ: ((إِنِّي أَبْرَأُ إِلَى اَللَّهِ أَنْ يَكُونَ لِي مِنْكُمْ خَلِيلٌ فَإِنَّ اَللَّهَ قَدْ اِتَّخَذَنِي خَلِيلاً كَمَا اِتَّخَذَ إِبْرَاهِيمَ خَلِيلاً، وَلَوْ كُنْتُ مُتَّخِذًا مِنْ أُمَّتِي خَلِيلاً، لَاِتَّخَذْتُ أَبَا بَكْرٍ خَلِيلاً، أَلَا وَإِنَّ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ كَانُوا يَتَّخِذُونَ قُبُورَ أَنْبِيَائِهِمْ مَسَاجِدَ، أَلَّا فَلَا تَتَّخِذُوا الْقُبُورَ مَسَاجِدَ، فَإِنِّي أَنْهَاكُمْ عَنْ ذَلِك))

Na Muslim kasimulia kutoka kwa Jundub bin ‘Abdullah (رضي الله عنه)  amesema: Nilimsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema siku tano kabla ya kufariki kwake: ((Mimi sina hatia kwa Allaah kumfanya mmoja wenu kuwa khalili. Hakika Allaah Amenifanya mimi kuwa ni khalili Wake kama alivyomfanya Ibraahiym kuwa khalili. Ningekuwa wa kufanya khalili katika Ummah wangu, basi ningemfanya Abuu Bakr kuwa khalili wangu Tahadharini! Waliotangulia kabla yenu walikuwa wakifanya makaburi ya Manabii wao mahali pa ‘ibaadah. Tahadharini!  Msifanye makaburi [yoyote] kuwa ni mahali pa ‘ibaadah nakukatazeni kufanya hivyo)) [Muslim]

 

 فَقَدْ نَهَى عَنْهُ فِي آخِرِ حَيَاتِهِ، ثُمَّ إِنَّهُ لَعَنَ وَهُوَ فِي اَلسِّيَاقِ مَنْ فَعَلَهُ. وَالصَّلاةُ عِنْدَهَا مِنْ ذَلِكَ وَإِنْ لَمْ يُبْنَ مَسْجِدٌ.وَهُوَ مَعْنَى قَوْلِهِ: خُشِيَ أَنْ يُتَّخَذَ مَسْجِدًا. فَإِنَّ اَلصَّحَابَةَ لَمْ يَكُونُوا لِيَبْنُوا حَوْلَ قَبْرِهِ مَسْجِدًا. وَكُلُّ  مَوْضِعٍ يُصَلَّى فِيهِ يُسَمَّى مَسْجِدًا  كَمَا قَالَ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ):  ((جُعِلَتْ لِيَ الْأَرْضُ مَسْجِدًا وَطَهُورًا))

Amekataza hilo katika mwisho wa umri wake. Kisha (baada ya kukataza kufanya makaburi kuwa Misikiti, yaani mahali pa ‘ibaadah) akalaani yeyote atakayefanya kitendo hicho. Na kuswali makaburini ni sawa na kulifanya kaburi kuwa ni Msikiti hata kama hamna Msikiti uliojengwa hapo kaburini. Hii ndio maana ya kauli yake (صلى الله عليه وآله وسلم): ‘Khofu ya kufanya (kaburi lake) kuwa ni Msikiti’. Maswahaba hawajapato kujenga Msikiti kaburini mwake. Na kila mahali panaposwaliwa panaitwa ‘Masjid’ (Msikiti) kama alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Ardhi imefanywa kwangu kuwa ni Masjid na mahali twahaarah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 وَلأَحْمَدَ بِسَنَدٍ جَيِّدٍ عَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) مَرْفُوعًا: ((إِنَّ مِنْ شِرَارِ اَلنَّاسِ مَنْ تُدْرِكُهُمْ اَلسَّاعَةُ وَهُمْ أَحْيَاءٌ،  وَاَلَّذِينَ يَتَّخِذُونَ الْقُبُورَ مَسَاجِدَ)) وَرَوَاهُ أَبُو حَاتِمٍ فِي صَحِيحِهِ  

Ahmad kwa isnaad nzuri kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه)  amesimulia Hadiyth Marfuw’: ((Hakika watu waovu kabisa kitakaowadiriki Qiyaamah nao ni hai, na wale wanaofanya makaburi kuwa ni Misikiti [mahali pa ‘ibaadah])) [Ahmad na amesimulia Abuu Haatim katika Swahiyh yake]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Onyo la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu ujenzi wa Misikiti ya kumwabudu Allaah katika makaburi ya watu wema, hata kama anayefanya hivyo ana niyyah njema.

 

2-Haramisho la masanamu na vitu kama hivyo (mapicha) na uzito wa jambo hilo.

 

3-Funzo katika msisitizo wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) wakati wa kufikisha hili, ambapo kwanza aliwaeleza (kwa upole), kisha siku tano kabla hajafariki alisema kama hapo awali. Halafu baadaye wakati wa Sakaraatul-Mawti akarudia hilo hilo. 

 

4-Aliharamisha kwa kusisitiza kuwa hili lisifanywe kaburini kwake, kabla ya kuweko kaburi lenyewe.   

 

5-Hiyo ni miongoni mwa matendo ya Wayahudi na Wakristo kuhusu makaburi ya Manabii wao.

 

6-Aliwalaani Mayahudi na Wakristo kwa sababu hiyo.

 

7-Kusudio la kufanya hivyo ni kutuonya sisi kuhusu kaburi lake tusilifanyie ‘ibaadah.

 

8-Sababu ya kutokujengewa kaburi lake.

 

9-Maana halisi ya: (makaburi) “kuyafanya Misikiti.”

 

10-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amefananisha wanaofanya makaburi kuwa Misikiti na watakaodiriki Qiyaamah wakiwa hai. Akataja njia zinazopeleka katika shirki kabla hazijatokea, pamoja na natija zake.

 

11-Alilitaja hili siku tano kabla hajafariki. Hapa kuna kukanusha makundi mawili ambao ni miongoni mwa waovu zaidi katika watu wa bid’ah (uzushi). Bali baadhi ya Wanachuoni wameyatenga kabisa makundi hayo mawil kutoka ule mjumuiko wa makundi 72 ya Waislamu. Mawili hayo ni Ar-Raafhidhwah (Shia) na Aj-Jahmiyyah. Na ni kwa sababu ya Raafidhwah ndio ikaanza shirki ya kufanya ‘ibaadah ya makaburi nao ndio wa kwanza kuyajengea Misikiti.

 

12-Kuteseka kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Sakaartul-Mawt. 

 

13-Allaah (سبحانه وتعالى) Amemkirimu kumfanya kuwa ni khalili.  

 

14-Ubainisho kuwa ukhalili huo ulikuwa zaidi ya upendo mwingine.

 

15-Ubainisho kuwa Abuu Bakr Asw-Swiddiyq (رضي الله عنه) ni Swahaba alikuwa ni mbora wa Maswahaba.

 

16-Ishara ya ukhalifa wa (Abuu Bakr).

 

 

 

Share

21-Kitaab At-Tawhiyd: Kutukuza Mno Makaburi Ya Waja Wema Huyafanya Masanamu Yaabudiwayo

Mlango Wa 21

بَابُ مَا جَاءَ أَنَّ الْغُلُوَّ فِي قُبُورِ اَلصَّالِحِينَ يُصَيِّرُهَا أَوْثَانًا تُعْبَدُ مِنْ دُونِ اَللَّهِ

Kutukuza Mno Makaburi Ya Waja Wema Huyafanya

Kama Masanamu Yaabudiwayo Badala Ya Allaah


 

 

رَوَى مَالِكٌ فِي الْمُوَطَّأِ: أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((اَللَّهُمَّ لاَ تَجْعَلْ قَبْرِي وَثَنًا يُعْبَدُ اِشْتَدَّ غَضَبُ اَللَّهِ عَلَى قَوْمٍ اِتَّخَذُوا قُبُورَ أَنْبِيَائِهِمْ مَسَاجِدَ))  

Amepokea Imaam Maalik katika Al-Muwattwaa kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ee Allaah! Usijaalie kaburi langu kuwa sanamu la kuabudiwa. Ghadhabu za Allaah zimezidi kwa watu wanaofanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti)) [Maalik fiyl Muwattwaa]

 

وَلاِبْنِ جَرِيرٍ بِسَنَدِهِ عَنْ سُفْيَانَ، عَنْ مَنْصُورٍ، عَنْ مُجَاهِدٍ: ((أَفَرَأَيْتُمُ اللَّاتَ وَالْعُزَّىٰ)) قال: كَانَ يَلُتُّ لَهُمْ اَلسَّوِيقَ،  فَمَاتَ، فَعَكَفُوا عَلَى قَبْرِهِ

Ibn Jariyr (Atw-Twabariy) kwa isnaad yake, kutoka kwa Sufyaan, kutoka kwa Manswuwr, kutoka kwa Mujaahid kuhusu Aayah: ((Je, mmeona Laata na ‘Uzzaa?)) [An-Najm (53: 19)] Amesema: “(Laata) Alikuwa akiwahudumia mahujaji sawiyq.[1] Baada ya kufa kwake, watu wakaanza kusabilia kaburi kwa ‘ibaadah.” 

 

وَكَذَا قَالَ أَبُو الْجَوْزَاءِ عَنْ اِبْنِ عَبَّاس:  كَانَ يَلُتُّ اَلسَّوِيقَ لِلْحَاجِّ.

Na Hadiyth hiyo imesimuliwa na Abu Al-Jawzaai kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema pia: “Alikuwa akiwakaribisha sawiyq kwa mahujaji.”

 

وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) قَالَ: لَعَنَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) زَائِرَاتِ الْقُبُورِ، وَالْمُتَّخِذِينَ عَلَيْهَا الْمَسَاجِدَ وَالسُّرُجَ. رَوَاهُ أَهْلُ اَلسُّنَنِ

Imepokelewa toka kwa Ibn Abbaas(رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا)  amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amewalaani wanawake wanaozuru makaburi, na wanaojenga Misikiti kwenye makaburi na kuyawashia taa makaburi” [Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Ufafanuzi kuhusu ‘awthaan’ (masanamu).

 

2-Ufafanuzi kuhusu ‘ibaadah.

 

3-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuomba kinga kwa Allaah (سبحانه وتعالى) isipokuwa kwa alichokhofia kutokea.

 

4-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuambatanisha kwake du’aa: ((Ee Allaah! Usijaalie kaburi langu…)) pamoja na (kukhofia khatari ya) ((watu wanaofanya makaburi ya Manabii kuwa Misikiti)).

 

5-Kutajwa ghadhabu kali za Allaah (kwa anayefanya kitendo hicho).

 

6-La muhimu kabisa ni maelezo kuhusu ‘ibaadah ya Laata ilivyoanza, nalo ni sanamu kuu kabisa kabla ya Uislamu.

 

7-Asili ya Laata lilikuwa ni kaburi la mja mwema.

 

8-Laata ni jina la mtu aliyezikwa katika kaburi hilo na ndio maana sanamu hilo likaitwa hivyo.

 

9-Laana (ya Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم ) kwa wanawake wanozuru makaburi. 

 

10-Laana ya Nabiy kwa wanaoweka taa kwenye makaburi.

 

[1] Mikate kutokana na unga wa shayiri uliochanganywa na maji na samli.

 

 

 

Share

22-Kitaab At-Tawhiyd: Nabiy Alivyohami Tawhiyd Kufunga Kila Njia Ipelekayo Kwenye Shirki

Mlango Wa 22

بَابُ مَا جَاءَ فِي حِمَايَةِ النَّبِي صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ جَنَابَ اَلتَّوْحِيدِ وَسَّدِّهِ كُلَّ طَرِيقٍ يُوَصِّلُ إِلَى اَلشِّرْكِ

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Alivyohami Tawhiyd Na Kufunga Kwake

Kila Njia Ipelekayo Kwenye Shirki


 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

 لَقَدْ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِكُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِتُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُم بِالْمُؤْمِنِينَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ ﴿١٢٨﴾

((Kwa yakini amekujieni Rasuli anayetokana na nyinyi wenyewe, yanamtia mashaka (na huzuni) yanayokutaabisheni, anakujalini (muongoke) mwenye huruma kwa Waumini ni mwenye huruma mno, mwenye rahmah))

 

 فَإِن تَوَلَّوْا فَقُلْ حَسْبِيَ اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ ۖ عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ ۖ وَهُوَ رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ ﴿١٢٩﴾

((Na wakikengeuka, basi sema: “Amenitosheleza Allaah; Hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye. Kwake nimetawakali. Naye ni Rabb wa ‘Arsh adhimu)) [At-Tawbah (9: 128-129)]

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لاَ تَجْعَلُوا بُيُوتَكُمْ قُبُورًا، وَلاَ تَجْعَلُوا قَبْرِي عِيدًا، وَصَلُّوا عَلَيَّ فَإِنَّ صَلاتَكُمْ تَبْلُغُنِي حَيْثُ كُنْتُمْ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ وَرُوَاتُهُ ثِقَاتٌ

Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msifanye nyumba zenu makaburi, wala msilifanye kaburi langu kuwa ni pahala pa kurejewa rejewa na niswalieni, kwani kuniswalia kwenu kunanifikia popote mlipo)) [Abuu Daawuwd kwa isnaad Hasan ya wasimuliaji wanaotegemewa]

 

وَعَنْ عَلِيِّ بْنِ الْحُسَيْنِ: أَنَّهُ رَأَى رَجُلاً يَجِيءُ إِلَى فُرْجَةً كَانَتْ عِنْدَ قَبْرِ اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَيَدْخُلُ فِيهَا فَيَدْعُو، فَنَهَاهُ وَقَالَ أَلاَ أُحَدِّثُكُمْ حَدِيثًا سَمِعْتُهُ مِنْ أَبِي عَنْ جَدِّي عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ تَتَّخِذُوا قَبْرِي عِيدًا وَلاَ بُيُوتَكُمْ قُبُورًا،  وَصَلُّوا عَلَيَّ فَإِنَّ تَسْلِيمَكُمْ لَيَبْلُغُنِي أَيْنَ كُنْتُمْ)) رَوَاهُ فِي   الْمُخْتَارَةَ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aliy bin Al-Husayn kwamba alimwona mtu akitoka kwenye upenyo uliokuwa katika ukuta wa kaburi la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akiingia na kuomba. Akamzuia akamwambia: Nikujulishe Hadiyth nilioisikia kutoka kwa baba yangu kutoka kwa babu yangu kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msifanye kaburi langu kuwa ni pahala pa kurejewa rejewa, wala [msifanye] nyumba zenu makaburi, [kwa kutokuswali ndani yake] na niswalieni kwenu kuniswalia kunanifikia popote mlipo)) [Al-Mukhtaar – mkusanyo wa Hadiyth za Imaam Al-Maqdisiyy Al-Hanbaliyyi]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Baraa-ah (At-Tawbah 9:128-129)).

 

2-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alifanya juhudi kubwa kuweka Ummah huu mbali na khatari ya shirki kadiri iwezekanavyo.         

 

3-Kujali kwake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu mafaniko yetu, furaha, amani na huruma yake kwetu.

 

4-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amekataza kuzuru kaburi lake kwa namna fulani (isiyopasa ki shariy’ah) ingawa kuzuru kaburi lake ni miongoni mwa ‘amali njema kabisa.

 

5-Makatazo ya kukithirisha mno kuzuru kaburi lake.

 

6-Himizo lake la kuswali Nawaafil (Swalaah za Sunnah) nyumbani.

 

7-Maswahaba wamekiri na kukubaliana kwamba kuswali makaburini imekatazwa.

 

8-Maelezo kwamba kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kunamfikia hata kama mtu yuko mbali vipi. Kwa hiyo hakuna haja ya kulikuribia sana kaburi lake kumtakia rahmah na amani kama inavyodhaniwa kimakosa.

 

9-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) yuko katika maisha ya Al-Barzakh ambako huonyeshwa ‘amali za ummah wake pamoja na swalaatu was-salaamu ‘alayhi (kumtakia rahmah na amani).

 

 

 

Share

23-Kitaab At-Tawhiyd: Baadhi Ya Ummah Huu Wataabudu Masanamu

 

Mlango Wa 23

بَابُ مَا جَاءَ أَنَّ بَعْضَ هَذِهِ الْأُمَّةِ يَعْبُدُ الْأَوْثَانَ

Baadhi Ya Ummah Huu Wataabudu Masanamu

 


 

 

 

وَقَوْلُهُ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ أُوتُوا نَصِيبًا مِّنَ الْكِتَابِ يُؤْمِنُونَ بِالْجِبْتِ وَالطَّاغُوتِ  

((Je, huwaoni wale waliopewa sehemu ya Kitabu wanaamini itikadi potofu na twaghuti)) [An-Nisaa (5: 51)]

 

وَقَوْلُهُ تَعَالَى :

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

قُلْ هَلْ أُنَبِّئُكُم بِشَرٍّ مِّن ذَٰلِكَ مَثُوبَةً عِندَ اللَّـهِ ۚ مَن لَّعَنَهُ اللَّـهُ وَغَضِبَ عَلَيْهِ وَجَعَلَ مِنْهُمُ الْقِرَدَةَ وَالْخَنَازِيرَ وَعَبَدَ الطَّاغُوتَ ۚ  

((Sema: “Je, nikujulisheni la shari zaidi kuliko hayo kwa malipo (mabaya) mbele ya Allaah?” Yule ambaye Allaah Amemlaani na Akamghadhibikia na Akawafanya miongoni mwao manyani na nguruwe na wakaabudu twaghuti)) [Al-Maaidah (5: 60)]

 

وَقَوْلُهُ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

قَالَ الَّذِينَ غَلَبُوا عَلَىٰ أَمْرِهِمْ لَنَتَّخِذَنَّ عَلَيْهِم مَّسْجِدًا ﴿٢١﴾

((Wakasema wale walioshinda katika shauri lao: “Bila shaka tutajenga Msikiti juu yao)) [Al-Kahf (18: 21)]

 

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لَتَتَّبِعُنَّ سُنَنَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ حَذْوَ الْقُذَّةِ  بِالْقُذَّةِ، حَتَّى لَوْ دَخَلُوا جُحْرَ ضَبٍّ لَدَخَلْتُمُوهُ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! الْيَهُودُ وَالنَّصَارَى؟ ؟قَالَ: ((فَمَنْ؟)) - أَخْرِجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa kwa Abuu Sa'iyd (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Bila shaka mtafuata nyendo za watu waliokuwa kabla yenu, hatua kwa hatua hata wakiingia kwenye shimo la kenge nanyi mtaingia)). Wakasema: Ee Rasuli wa Allaah, je, unamaanisha Mayahudi na Manaswara?" Akasema: ((Nani basi [kama si hao]?)) [Al-Bukhaariy na Muslim]  

 

وَلِمُسْلِمٍ عَنْ ثَوْبَانَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  قَالَ: ((إِنَّ اَللَّهَ زَوَى لِيَ الأَرْضَ، فَرَأَيْتُ مَشَارِقَهَا وَمَغَارِبَهَا،  وَإِنَّ أُمَّتِي سَيَبْلُغُ مُلْكُهَا مَا زُوِيَ لِي مِنْهَا. وَأُعْطِيتُ الْكَنْزَيْنِ الأَحْمَرَ وَالأَبْيَضَ. وَإِنِّي سَأَلْتُ رَبِّي لأُمَّتِي أَنْ لاَ يُهْلِكَهَا بِسَنَةٍ بِعَامَّةٍ، وَأَنْ لا يُسَلِّطَ عَلَيْهِمْ عَدُّوا مِنْ سِوَى أَنْفُسِهِمْ، فَيَسْتَبِيحَ بَيْضَتَهُمْ، وَإِنَّ رَبِّي قَالَ: يَا مُحَمَّدُ إِنِّي إِذَا قَضَيْتُ قَضَاءً فَإِنَّهُ لاَ يُرَدُّ، وَإِنِّي أَعْطَيْتُكَ لأُمَّتِكَ أَنْ لا أُهْلِكَهُمْ بِسَنَةٍ ِعَامَّةٍ، وَأَنْ لا أُسَلِّطَ عَلَيْهِمْ عَدُّوا مِنْ سِوَى أَنْفُسِهِمْ فَيَسْتَبِيحَ بَيْضَتَهُمْ، وَلَوْ اِجْتَمَعَ عَلَيْهِمْ مَنْ بِأَقْطَارِهَا حَتَّى يَكُونَ بَعْضُهُمْ يُهْلِكُ بَعْضًا، وَيَسْبِيَ بَعْضُهُمْ بَعْضًا))

Na Muslim amerekodi kutoka kwa Thawbaan (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika Allaah Amenikusanyia ardhi [dunia] nikaona Mashariki yake na Magharibi yake. Na hakika Ummah wangu utaenea na kumiliki vyote vilivyo katika sehemu hizo nilokusanyiwa. Na nimepewa hazina mbili; nyekundu [Ufalme wa Kirumi] na nyeupe [Ufalme wa Kifursi]. Hapo nikamuomba Rabb wangu Asijaalie Ummah wangu kuangamizwa kwa baa kuu la jumla na usitekwe na adui ajnabi atakayeuharibu mjii mkuu wao na kuuangusha uongozi wao.  Rabb wangu Akajibu:  Ee Muhammad! Nikihukumu amri basi hakika hairudi. Nimekadiria kwamba Ummah wako hautahiliki mara moja kwa baa kuu la jumla na kwamba hautatekwa na adui ajnabi na kuharibu mjii mkuu wao na kuuangusha uongozi wao, ila kundi moja la Ummah wako litahilikisha makundi mengine au kuwafanya mateka)) [Muslim]

 

وَرَوَاهُ الْبَرْقَانِيُّ فِي صَحِيحِهِ وَزَادَ: ((وَإِنَّمَا أَخَافُ عَلَى أُمَّتِي الأَئِمَّةَ الْمُضِلِّينَ، وَإِذَا وَقَعَ عَلَيْهِمْ اَلسَّيْفُ لَمْ يُرْفَعْ إِلَى يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَلا تَقُومُ اَلسَّاعَةُ حَتَّى يَلْحَقَ حَيٌّ مِنْ أُمَّتِي بِالْمُشْرِكِينَ وَحَتَّى تَعْبُدَ فِئَامٌ مِنْ أُمَّتِي الأَوْثَانَ، وَإِنَّهُ سَيَكُونُ فِي أُمَّتِي كَذَّابُونَ ثَلاثُونَ كُلُّهُمْ يَزْعُمُ أَنَّهُ نَبِيٌّ، وَأَنَا خَاتَمُ اَلنَّبِيِّينَ لا نَبِيَّ بَعْدِي وَلا تَزَالُ طَائِفَةٌ مِنْ أُمَّتِي عَلَى الْحَقِّ مَنْصُورَةٌ لا يَضُرُّهُمْ مَنْ خَذَلَهُمْ وَلا مَنْ خَالَفَهُمْ حَتَّى يَأْتِيَ أَمْرُ اَللَّهِ تَبَارَكَ وَتَعَالَى))

Na Al-Barqaaniyy katika Swahiyh yake akaongezea yafuatayo: ((Bali nnachokikhofia kwa Ummah wangu ni kupotezwa na viongozi wapotofu ambao wakiangukiwa na upanga, upanga huo hautonyanyuliwa hadi Siku ya Qiyaamah. Wala Qiyaamah hakitafika mpaka baadhi ya Ummah wangu wawafuate makafiri na waanze kuabudu masanamu. Nawakhofia watakuja miongoni mwao manabii wa uongo thelathini; kila mmoja anadai kuwa yeye ni nabiy na hali mimi ni Nabiy wa mwisho hakuna baada yangu. Lakini kundi moja katika ummah wangu litabakia kuwa katika haki na ushindi, hlitodhurika kwa kuanguka kwa wengine mpaka ifike amri ya Allaah Tabaraka wa Ta’aalaa)) [Al-Barqaaniy fiy Swahiyhih]  

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah An-Nisaa (4: 5).

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Maaidah (5: 60).

 

3-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Kahf (18: 21).

 

4-Jambo muhimu kabisa kuhusu maana ya Al-jibt na Atw-Twaaghuwt katika maudhui hii. Je, ni kuitakidi kwa moyo, au kukubaliana tu na wale wanaofanya (shirki) na hali wanachukia na kujua kwamba ni upotofu?

 

5-Mayahudi kudai kwamba (Makafiri Quraysh) wanaotambua hakika ya kufru yao kwamba wako katika uongofu zaidi kuliko Waumini.

 

6-   Watu kama hao (watakaopotea na kuabudu masanamu) wanapatikana katika Ummah huu wa Kiislamu kama ilivyotajwa katika Hadiyth ya Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه). Hii ndio maudhui kuu ya mlango huu.

 

7-Utabiri wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba wengi katika Ummah wake wataabudu waabudiwa wa uongo (masanamu n.k.).

 

8-La ajabu zaidi ni kutokeza kwa wale wanaodai unabiy kama Al-Mukhtaar[1] juu ya kuwa alikiri shahaadah na kukiri kwake kwamba ni miongoni mwa Ummah wa Kiislamu, na (kukiri kwake) kwamba Nabiy (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) ni haki na Qur-aan ni haki, na kukiri kwamba Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) ni Nabiy wa mwisho. Lakini inashangaza kwamba muongo kama huyo anajidai unabiy na huku anaaminiwa juu ya kudhihirika kwake kupinga shahaadah yake. Al-Mukhtaar alitokeza katika kipindi cha mwisho wa Maswahaba na akapata wafuasi wengi.

 

9-Bishara njema kwamba haki haitopotea moja kwa moja kama zamani, bali litabaki kundi moja litakalobakia katika haki.

 

10-Alama kubwa kabisa ni kwamba wao (kundi la haki) hawatodhuriwa na waliowakhalifu wala wapinzani japokuwa wao watakuwa wachache.

 

11-Hali hiyo ndivyo itakavyokuwa hadi Qiyaamah.

 

12-Bishara ya miujiza kadhaa kutokana na kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) miongoni mwazo ni:

  • Kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Alimdhihirishia ardhi Mashariki na Magharibi na kumbainishia maana ya bishara hiyo na hakika imetokea kama alivyojulisha, si Kaskazini wala Kusini.
  • Kwamba Ametunukiwa hazina mbili (Rome na Persia). 
  • Kwamba du’aa zake mbili kwa ajili ya Ummah zimetakabaliwa.
  • Kwamba du’aa yake ya tatu haikukubaliwa.
  • Kwamba utakapoanguka upanga (vita), basi vita hivyo havitosimama, akahadithia kuhusu baadhi ya Ummah huu kuangamiza baadhi yake.
  • Utabiri wake wa manabii ya uongo katika Ummah wake.
  • Kwamba daima kutakuweko kundi la ushindi.
  • Kwamba yote hayo yalitokea kama alivyojulisha japokuwa kila moja ya hayo yalionekana mbali kuyakinika akilini.

 

13-Khofu yake kubwa kwa Ummah wake kutokana na viongozi wapotofu.

 

14-Kutahadharisha na tanbihi ya maana ya ‘ibaadah ya masanamu.

           

 

[1] Al-Mukhtaar bin Abiy ‘Ubayd Ath-Thaqafiy aliyeitawala Kuwfaa mwanzo wa Khilaafah ya Ibn Zubayr.

 

 

Share

24-Kitaab At-Tawhiyd: Kuhusu Uchawi

Mlango Wa 24

بَابُ مَا جَاءَ فِي اَلسِّحْرِ

Kuhusu Uchawi


 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

 Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

وَلَقَدْ عَلِمُوا لَمَنِ اشْتَرَاهُ مَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ۚ

((na kwa yakini walijua kwamba atakayechuma haya hatopata katika Aakhirah fungu lolote)) [Al-Baqarah (2: 102)]

 وَقَوْلِهِ:

 Na kauli Yake:

يُؤْمِنُونَ بِالْجِبْتِ وَالطَّاغُوتِ

((Wanaamini itikadi potofu na twaghuti))  [An-Nisaa (5: 51)]

 

 قَالَ عُمَرُ : الْجِبْتُ اَلسِّحْرُ، وَالطَّاغُوتُ اَلشَّيْطَانُ

‘Umar  (رضي الله عنه) amesema: Al-Jibti ni uchawi na Atw-Twaaghuwt ni shaytwaan.

 

 وَقَالَ جَابِرٌ: اَلطَّوَاغِيتُ كُهَّانٌ كَانَ يَنْزِلُ عَلَيْهِمْ اَلشَّيْطَانُ فِي كُلِّ حَيٍّ وَاحِدٌ

Na Jaabir  (رضي الله عنه)  amesema: Twaaghuwt ni kuhani (mtabiri wa mambo ya ghayb) shaytwaan huwateremkia na kila kabila lina mmoja wao.

 

 وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَال: ((اِجْتَنِبُوا اَلسَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ))  قَالُوا يَا رَسُولَ اَللَّهِ! وَمَا هُنَّ؟ قَالَ: ((اَلشِّرْكُ بِاَللَّهِ، وَالسِّحْرُ، وَقَتْلُ اَلنَّفْسِ اَلَّتِي حَرَّمَ اَللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ، وَأَكْلُ اَلرِّبَا، وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ، وَالتَّوَلِّي يَوْمَ اَلزَّحْفِ، وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْغَافِلاتِ الْمُؤْمِنَاتِ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)   kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akawaambia: ((Ni kumshirikisha Allaah, uchawi, kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa kupambana na adui na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَعنْ جُنْدَبٍ مَرْفُوعًا: ((حَدُّ اَلسَّاحِرِ ضَرْبَةٌ بِالسَّيْفِ)) رَوَاهُ التِّزْمِذِيُّ وَقَالَ: اَلصَّحِيحُ أَنَّهُ مَوْقُوفٌ

Na Imepokelewa kutoka kwa Junub (رضي الله عنه)  Hadiyth ifuatayo ikiwa ni Marfuw’: ((Adhabu ya mchawi kupigwa upanga [auliwe])) [At-Tirmidhy na amesema Swahiyh lakini ni Mawquwf]

 

وَفِي صَحِيحِ الْبُخَارِيِّ: عَنْ بَجَالَةَ بْنِ عَبَدَةَ قَالَ: كَتَبَ عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْه) أَنِ اُقْتُلُوا كُلَّ سَاحِرٍ وَسَاحِرَةٍ. قَالَ: فَقَتَلْنَا ثَلاثَ سَوَاحِرَ.

Na katika Swahiyh Al-Bukhaariy kutoka kwa Bajaalah bin ‘Abadah amesema: ‘Umar bin Al-Khattwaab(رضي الله عنه)  aliandika kwamba: “Uweni kila mchawi mwanamme na mchawi mwanamke.” Akasema [Bajaalah]: “Tukaua wachawi watatu.”

 

وَصَحَّ عَنْ حَفْصَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا) أَنَّهَا أَمَرَتْ بِقَتْلِ جَارِيَةٍ لَهَا سَحَرَتْهَا فَقُتِلَتْ. وَكَذَلِكَ صَحَّ عَنْ جُنْدَبٍ

Na Hafswah(رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا)  amesimulia kwamba aliamrisha auliwe mjakazi wake alimroga. Amethibitisha haya Jundab(رضي الله عنه) .

 

قَالَ أَحْمَدُ عَنْ ثَلاثَةٍ مِنْ أَصْحَابِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم  

(Imaam) Ahmad amethibitisha pia kuuliwa kwa wachawi kutoka kwa Maswahaba watatu wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) (‘Umar, Hafswah, Jundub).

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Baqarah (2: 102).

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah An-Nisaa (4: 51).

 

3-Maana ya Al-Jibt na Atw-Twaaghuwt na tofauti baina yake.

 

4-Atw-Twaaghuwt wanaweza kuwa ni miongoni mwa majini au bin Aadam.

 

5-Maelezo ya mambo saba yanayoangamiza yaliyoharamishwa.

 

6-Watabiri na makuhani na wachawi ni makafiri.

 

7-Makuhani na wachawi wauawe na hakuna kuombwa kutubia.

 

8-Ikiwa, makuhani, wachawi walipatikana kwa Waislamu zama za ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه) seuze basi baada ya hapo?   

 

 

Share

25-Kitaab At-Tawhiyd: Bainisho La Aina Za Uchawi

Mlango Wa 25

بَابُ بَيَانِ شَيْءٍ مِنْ أَنْوَاعِ السِّحْرِ

Bainisho La Aina Za Uchawi


 

 

قَالَ أَحْمَدُ حَدَّثَنَا مُحَمَّدُ بْنُ جَعْفَرٍ، حَدَّثَنَا عَوْفٌ عَنْ حَيَّانَ بْنِ الْعَلاءِ،  حَدَّثَنَا قَطَنُ بْنُ قَبِيصَةَ عَنْ أَبِيهِ أَنَّهُ سَمِعَ النَّبِيَّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((إِنَّ الْعِيَافَةَ وَالطَّرْقَ وَالطِّيَرَةَ مِنَ الْجِبْتِ))

Imaam Ahmad amesema: Muhammad bin Ja’far amesimulia kutoka kwa ‘Awf, kutoka kwa Hayyaan bin Al-‘Alaa, kutoka kwa Qatwanu bin Qabiyswah, kutoka kwa baba yake kwamba kamsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Hakika Al-’Iyaafah na Atw-Twarqa na Atw-Twiyaarah ni Al-Jibt [uchawi])) [Ahmad]

 

قَالَ عَوْفٌ الْعِيَافَةُ زَجْرُ الطَّيْرِ، وَالطَّرْقُ الْخَطُّ يُخَطُّ بِالأَرْضِ

Amesema Al-‘Awf:

Al-’Iyaafah :           ni kumwacha ndege aruke itabiriwe jambo.

Atw-Twarqa:         ni kuchora mistari ardhini [kutabiri jambo]. 

Atw-Twiyaarah:  Itikadi za ushirikina kutumia ndege kuruka ili kubashiria ya ghayb; mkosi, nuksi).

 

وَالْجِبْتُ قَالَ الْحَسَنُ رَنَّةُ الشَّيْطَانِ إِسْنَادُهُ جَيِّدٌ

Na Hasan Al-Baswri amesema Al-Jibt ni kusikiliza sauti ya shaytwaan [Isnaad yake ni nzuri]

 

وَلأَبِي دَاوُدَ وَالنَّسَائِيِّ وَابْنِ حِبَّانَ فِي صَحِيحِهِ لَهُمُ الْمُسْنَدُ مِنْهُ

Na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na Ibn Hibbaan katika Swahiyh yake wana isnaad nzuri ya Hadiyth hiyo.

 

 وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((مَنِ اِقْتَبَسَ شُعْبَةً مِنَ النُّجُومِ، فَقَدِ اِقْتَبَسَ شُعْبَةً مِنَ السِّحْرِ، زَادَ مَا زَادَ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَإِسْنَادُهُ صَحِيحٌ

Na Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayesomea unajimu [utabiri wa nyota] basi amefanya uchawi, kadiri anavyozidisha ndivyo kosa lake linavyozidi [madhambi])) [Abuu Daawuwd na isnaad yake Swahiyh]

 

وَلِلنَّسَائِيِّ مِنْ حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَة: ((مَنْ عَقَدَ عُقْدَةً ثُمَّ نَفَثَ فِيهَا فَقَدْ سَحَرَ، وَمَن ْسَحَرَ فَقَدْ أَشْرَكَ، وَمَنْ تَعَلَّقَ شَيْئًا وُكِلَ إِلَيْهِ))

Na An-Nasaaiy kutoka Hadiyth ya Abu Hurayrah: ((Atakayefunga fundo kisha akalipuliza amefanya uchawi. Na atakayefanya uchawi amefanya shirki, na atakayetundika kitu [talasimu, au kuvaa hirizi, zindiko] basi amejiweka katika ulinzi wa hicho kitu alichokivaa)) [na itamdhalilisha]))

 

وَعَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((أَلاَ هَلْ أُنَبِّئُكُمْ مَا الْعَضْهُ؟ هِيَ النَّمِيمَةُ، الْقَالَةُ بَيْنَ النَّاسِ))  رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Na Imepokelewa kutoka kwa Ibn Mas’uwd(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Je, nikujulisheni nini Al-’Adhw-hu? Ni An-Namiymah kwa ajili ya kueneza uovu kati ya watu)) [An-Nasaaiy]

 

Al-’Adhw-hu:  kueneza uongo, uchawi n.k.

 

An-Namiymah: kupeleka uvumi kwa ajili ya kufitinisha na kugombanisha watu.

 

وَلَهُمَا عَنِ اِبْنِ عُمَرَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((إِنَّ مِنَ الْبَيَانِ لَسِحْرًا))

Nao wawili [Al-Bukhaariy na Muslim] kutoka kwa Ibn ‘Umar  (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika katika ufasaha mwengine kuna uchawi)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Al-‘Iyaafah, At-Twarqa na At-Twiyaarah ni aina tatu za uchawi.

 

2-Al-‘Iyaafah na At-Twarqa zimeelezewa.

 

3- Unajimu pia ni namna ya uchawi.

 

4-Kufunga vifundo na kuvipulizia pia ni uchawi.

 

5-An-Namiymah nayo ni namna ya uchawi.

 

6-Wakati mwengine kuzungumza kwa ufasaha hadi ukazidi mno nao ni uchawi.

 

 

 

 

Share

26-Kitaab At-Tawhiyd: Kuhusu Makuhani Na Mfano Wao

Mlango Wa 26

بَابُ مَا جَاءَ فِي الْكُهَّانِ وَنَحْوِهِمْ

Kuhusu Makuhani Na Mfano Wao


 

 

رَوَى مُسْلِمٌ فِي صَحِيحِهِ عَنْ بَعْضِ أَزْوَاجِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) عَنِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((مَنْ أَتَى عَرَّافًا فَسَأَلَهُ عَنْ شَيْءٍ فَصَدَّقَهُ، لَمْ تُقْبَلْ لَهُ صَلاةٌ أَرْبَعِينَ يَوْمًا))

Amesimulia Muslim katika Swahiyh yake kutoka baadhi ya wake wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayemwendea mtabiri akamuuliza kitu kisha akamuamini, haitokubaliwa Swalaah yake siku arubaini)) [Muslim]

 

 وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) عَنِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  قَالَ: ((مَنْ أَتَى كَاهِنًا، فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) kutoka kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayemkaribia kuhani na kuamini anayoyasema basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)) [Abuu Daawuwd]

 

وَلِلأَرْبَعَةِ وَالْحَاكِمِ وَقَالَ:صَحِيحٌ عَلَى شَرْطِهِمَا  عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ: ((مَنْ أَتَى عَرَّافًا أَوْ كَاهِنًا فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ))

Na wasimuliaji wengine wanne wa Hadiyth na Al-Haakim wamenakilii Hadiyth ya Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  na wameikiri ni Swahiyh kwa mujibu wa masharti yao kwamba: ((Atakayemwendea mtabiri au kuhani akamwamini ayasemayo basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم )) 

 

وَلأَبِي يَعَلَى بِسَنَدٍ جَيِّدٍ عَنِ ابْنِ مَسْعُودٍ مِثْلُهُ مَوْقُوفًا

Na Abuu Ya’laa ameripoti Hadiyth kama hiyo kutoka kwa Ibn Mas’uwd kwa isnaad nzuri lakini ni Hadiyth Mawquwf.  

 

وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَينٍ مَرْفُوعًا: ((لَيْسَ مِنَّا مَنْ تَطَيَّرَ أَوْ تُطُيِّرَ لَهُ، أَوْ تَكَهَّنَ أَوْ تُكُهِّنَ لَهُ، أَوْ سَحَرَ أَوْ سُحِرَ لَهُ، وَمَنْ أَتَى كَاهِنًا فَصَدَّقَهُ بِمَا يَقُولُ، فَقَدْ كَفَرَ بِمَا أُنْزِلَ عَلَى مُحَمَّدٍ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)) رَوَاهُ الْبَزَّارُ بِإِسْنَادٍ جَيِّدٍ

Na Imepokelewa toka kwa ‘Imraan bin Huswayn Hadiyth Marfuw’: ((Si miongoni mwetu anayetafuta au anayebashiriwa Atw-Twiyaarah (mkosi, nuksi) au akafanya ukuhani au akafanyiwa ukuhani, au anayefanya uchawi au anayefanyiwa uchawi, na atakayemwendea kuhani akamwamini ayasemayo basi amekanusha aliyoteremshiwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)) [Al-Bazaar kwa isnaad nzuri]

 

وَرَوَاهُ الطَّبَرَانِيُّ فِي الْأَوْسَطِ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ مِنْ حَدِيثِ ابْنِ عَبَّاسٍ دُونَ قَوْلِهِ: ((وَمَنْ أَتَى)) .. إِلَى آخِرِهِ

Hadiyth hiyo hiyo ameinakili Atw-Twabaraaniy katika Al-Awsatw kwa isnaad nzuri kutoka kwa Ibn ‘Abbaas bila ya kauli ya mwisho: ((Na atakayemwendea…)) 

 

قَالَ الْبَغَوِيُّ :الْعَرَّافُ الَّذِي يَدَّعِي مَعْرِفَةَ الأُمُورِ بِمُقَدِّمَاتٍ يُسْتَدَلُّ بِهَا عَلَى الْمَسْرُوقِ وَمَكَانِ الضَّالَّةِ وَنَحْوِ ذَلِكَ

Al-Baghaawiy amesema: Al-‘Arraaf (mtabiri) ni ambaye anadai ujuzi wa mambo fulani kama vile yanayohusu vitu vilivyoibiwa, wapi vipo vitu hivyo, au mnyama aliyepotea na kama hayo kwa njia ya uchawi.

وَقِيلَ هُوَ الْكَاهِنُ، وَالْكَاهِنُ هُوَ الَّذِي يُخْبِرُ عَنِ الْمُغَيَّبَاتِ فِي الْمُسْتَقْبَلِ

Wengine wamesema yeye ndiye kuhani, na kuhani ni anayetoa khabari za mustaqbal (za mbele) zilizofichikana.

 

وَقِيلَ الَّذِي يُخْبِرُ عَمَّا فِي الضَّمِيرِ

Na wengine wamesema ni ambaye anayetoa yaliyo katika dhamira ya mtu (siri moyoni).

 

وَقَالَ أَبُو الْعَبَّاسِ ابْنُ تَيْمِيَّةَ الْعَرَّافُ اسْمٌ لِلْكَاهِنِ، وَالْمُنَجِّمِ وَالرَّمَّالِ وَنَحْوِهِمْ مِمَّنْ يَتَكَلَّمُ فِي مَعْرِفَةِ الأُمُورِ بِهَذِهِ الطُّرُقِ

Na Abul-‘Abbaas, Ibn Taymiyyah kasema: Al-‘Arraaf ni jina la kuhani, na Al-Munajjim (mtabiri wa nyota) na Ar-Rammaal (mpiga ramli) na kama hao wanaojidai kuyajua mambo kwa njia hizo.

 

 وَقَالَ ابْنُ عَبَّاسٍ فِي قَوْمٍ يَكْتُبُونَ: أَبَا جَادٍ. وَيَنْظُرُونَ فِي النُّجُومِ مَا أَرَى مَنْ فَعَلَ ذَلِكَ لَهُ عِنْدَ اللَّهِ مِنْ خَلاقٍ

Na Ibn ‘Abbaas akasema kuhusu watu wanaoandika ‘Abaa-Jaad’ (alfabeti kutumilia utabiri, uaguzi) na wanatazamia nyota kuamini athari zake ardhini. “Sioni kuwa wana fungu lolote mbele ya Allaah.”

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kumwamini kuhani na kuamini Qur-aan ni iymaan ambazo haziwezi kuwa pamoja katika moyo wa mtu mmoja.

 

2-Tangazo kuwa kufanya hivyo (kumwamini kuhani) ni kufuru.

 

3-Kutajwa mtu anayetabiriwa.

 

4-Kutajwa aliyefanyiwa itikadi za ushirikina.

 

5-Kutajwa aliyefanyiwa uchawi.

 

6-Kutajwa anayejifundisha Abaa-Jaad (kutumia alfabeti katika utabiri, uaguzi)  

 

7-Tofauti baina ya kuhani na mtabiri.

 

 

 

Share

27-Kitaab At-Tawhiyd: An-Nushrah: Kuagua Uchawi Kwa Uchawi

Mlango Wa 27

بَابُ مَا جَاءَ فِي النُّشْرَةِ

An-Nushrah: Kuagua Uchawi Kwa Uchawi


 

 

عَنْ جَابِر: أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) سُئِلَ عَنْ النُّشْرَةِ فَقَالَ: ((هِيَ مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ)) رَوَاهُ أَحْمَدُ بِسَنَدٍ جَيِّدٍ وَأَبُو دَاوُدَ وَقَالَ: سُئِلَ أَحْمَدُ عَنْهَا: فَقَالَ ابْنُ مَسْعُودٍ يَكْرَهُ هَذَا كُلَّهُ

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliulizwa kuhusu An-Nushrah akasema: ((Hicho ni kitendo cha shaytwaan)) [Ahmad kwa isnaad nzuri na Abuu Daawuwd]

 

Na Abuu Daawuwd akasema: Aliulizwa Imaam Ahmad kuhusu hiyo [An-Nushrah] akasema: Ibn Mas’uwd alikuwa akichukizwa na yote hayo.

 

وَفِي "الْبُخَارِيِّ: عَنْ قَتَادَةَ: قُلْتُ لابْنِ الْمُسَيِّبِ: رَجُلٌ بِهِ طِبٌّ أَوْ يُؤْخَذُ عَنِ امْرَأَتِهِ، أَيُحَلُّ عَنْهُ أَوْ يُنْشَرُ؟ قَالَ: لاَ بَأْسَ بِهِ إِنَّمَا يُرِيدُونَ بِهِ الإِصْلاحَ، فَأَمَّا مَا يَنْفَعُ فَلَمْ يُنْهَ عَنْهُ

Na katika Al-Bukhaariy amesimulia kutoka kwa Qataadah(رضي الله عنه) : “Nilimuuliza Ibn Al-Musayyib: Mtu akiwa karogwa au ambaye hawezi unyumba (kumuingilia mkewe), je, ni sawa kuaguliwa kwa uchawi au tutumie njia nyingine za matibabu?” Ibn Al-Musayyib akajibu: Hapana ubaya kwa sababu wanakusudia kutengeneza. Yanayonufaisha [na kuondosha madhara] hayakukatazwa.

 

وَرُوِيَ عَنِ الْحَسَنِ أَنَّهُ قَالَ: لا يَحِلُّ السِّحَرَ إِلاَّ سَاحِرٌ.

Na imesimuliwa kutoka kwa Hasan Al-Baswriy kwamba amesema: Mchawi pekee anaweza kuagua uchawi wa mchawi mwengine”   

قال ابْنُ الْقَيِّمِ: النُّشْرَةُ حَلُّ السِّحَرِ عَنِ الْمَسْحُورِ، وَهِيَ نَوْعَانِ:

Ibn Al-Qayyim amesema: An-Nushrah ni kuondosha uchawi wa aliyerogwa. Nazo ni aina mbili:

 

 أَحَدُهُمَا حَلٌّ بِسِحْرٍ مِثْلِهِ، وَهُوَ الَّذِي مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ وَعَلَيْهِ يُحْمَلُ قَوْلُ الْحَسَنِ، فَيَتَقَرَّبُ النَّاشِرُ وَالْمُنْتَشَرُ إِلَى الشَّيْطَانِ بِمَا يُحِبُّ فَيُبْطِلُ عَمَلَهُ عَنِ الْمَسْحُورِ

 

Ya kwanza: Kuondosha uchawi kwa kutumia uchawi mwengine; na hicho ni kitendo cha shaytwaan (nayo ni haraam). Na hayo ndio maelezo ya Hasan kwamba mchawi na aliyerogwa, wote wanamkaribia shaytwaan kwa ayapendayo. Kisha shaytwaan humuondeshea aliyerogwa athari za uchawi.

 

 وَالثَّانِي النُّشْرَةُ بِالرُّقْيَةِ وَالتَّعَوُّذَاتِ وَالأَدْوِيَةِ وَالدَّعَوَاتِ الْمُبَاحَةِ، فَهَذَا جَائِزٌ

Ya pili: Ni kutibu uchawi kwa Ruqyah (Aayah za Qur-aan na adhkaar za Sunnah), dawa na du´aa zinazokubalika; hii inajuzu.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kukatazwa An-Nushrah.

 

2-Tofauti kati ya aina ya An-Nushrah inayojuzu na iliyoharamishwa katika kuondosha matatizo hayo. 

 

 

 

Share

28-Kitaab At-Tawhiyd: Itikadi Ya Tatwayyur (Kutabiri Nuksi, Mikosi Na Kadhaalika)

Mlango Wa 28

بَابُ مَا جَاءَ فِي التَّطَيُّرِ

Itikadi Ya Tatwayyur  (Kutabiri Nuksi, Mikosi Na Kadhaalika)


 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

  أَلَا إِنَّمَا طَائِرُهُمْ عِندَ اللَّـهِ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿١٣١﴾

((Tanabahi! Hakika nuksi yao iko kwa Allaah lakini wengi wao hawajui)) [Al-A’raaf (7: 131)]

 

At-Tatwayyur:  Itikadi za ushirikina kutabiri na kuamini mkosi, nuksi, dhana mbaya n.k.  

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

قَالُوا طَائِرُكُم مَّعَكُمْ ۚ أَئِن ذُكِّرْتُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ مُّسْرِفُونَ ﴿١٩﴾

((Rusuli) Wakasema: “Nuksi yenu mnayo wenyewe. Je, kwa vile mnakumbushwa? Bali nyinyi ni watu wapindukao mipaka”)) [Yaasiyn (36: 19)]

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ عَدْوَى وَلاَ طِيَرَةَ وَلَا هَامَةَ وَلاَ صَفَرَ)) أَخْرَجَاهُ  زَادَ مُسْلِمٌ: ((وَلا نَوْءَ وَلا غُولَ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakuna ‘adwaa wala twiyarah wala hakuna haamah wala hakuna swafar))  [Al-Bukhaariy na Muslim] Na Muslim amezidisha: ((Wala hakuna naw-a wala hakuna ghuwl))

 

‘Adwaa:     Uambukizaji wa magonjwa bila idhini ya Allaah.

 

Haamah:    Ukorofi, mkosi unaotokana na bundi - ndege wa usiku.

 

Swafar:      Ukorofi, mkosi unaodaiwa unatoka katika mwezi wa Swafar.

 

An-Naw-a: Kilima – ugawanyaji wa wakati kwa mujibu wa kujitokeza nyota au

                     sayari fulani.

 

Ghuwl:     Mizimu. 

 

وَلَهُمَا عَنْ أَنَسٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لَا عَدْوَى وَلَا طِيَرَةَ وَيُعْجِبُنِي الْفَأْلُ))  قَالُوا:  وَمَا الْفَأْلُ؟ قَالَ: ((الْكَلِمَةُ الطَّيِّبَةُ))

Na wawili hao [Al-Bukhaariy na Muslim] wamesimulia kutoka kwa Anas(رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakuna ‘adwaa wala hakuna twiyarah [itikadi ya kutabiri mkosi, nuksi] na inanipendekeza Al-Fa-l)) Wakauliza: Nini Al-Fa-lu? Akajibu: ((Neno zuri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَلأَبِي دَاوُدَ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ: عَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ قَالَ: ذُكِرَتِ الطِّيَرَةُ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَقَالَ: ((أَحْسَنُهَا الْفَأْلُ، وَلاَ تَرُدُّ مُسْلِمًا. فَإِذَا رَأَى أَحَدُكُمْ مَا يَكْرَهُ فَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ لاَ يَأْتِي بِالْحَسَنَاتِ إِلاَّ أَنْتَ وَلاّ يَدْفَعُ السَّيِّئَاتِ إِلاَّ أَنْتَ، وَلاَ حَوْلَ وَلاَ قُوَّةَ إِلاَّ بِكَ))

Na kwa Abuu Daawuwd, kwa isnaad Swahiyh: Imepokelewa kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رضي الله عنه) amesema: Kuliwahi kutajwa mbele ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) Atw-Twiyarah (itikadi ya kutabiri na kuamini kitu fulani kuwa kinaleta mkosi, nuksi), akasema: ((Lililo bora katika hayo ni Al-Fa-lu. Vinginevyo hayo yote hayamuzuilii Muislamu kutafuta malengo yake. [kutokutenda aliloazimia]. Mmmoja wenu atakapoona analochukia aseme: “Allaahumma laa ya-tiy bil-hasanaati illaa Anta, walaa yad-fa’us-sayyiaat illa Anta, walaa hawla walaa quwwata illaa Bika - Ee Allaah, hakuna anayeweza kuleta mambo mema isipokuwa ni Wewe, wala hakuna anayeweza kukinga mabaya isipokuwa ni Wewe. Na Hakuna uwezo wala nguvu ila kutokana Nawe)) [Hadiyth Swahiyh ameipokea Abuu Daawuwd kwa isnaad Swahiyh]

 

Al-Fa-lu: Matumaini na itikadi kuwa jambo hutokea kwa idhini ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

وعن ابْنِ مَسْعُودٍ مَرْفُوعًا: ((الطِّيَرَةُ شِرْكٌ، الطِّيَرَةُ شِرْكٌ، وَمَا مِنَّا إِلاَّ وَلَكِنَّ اللَّهَ يُذْهِبُهُ بِالتَّوَكُّلِ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَالتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ. وَجَعَلَ آخِرَهُ مِنْ قَوْلِ ابْنِ مَسْعُودٍ

Na kutoka kwa Ibn Mas’uwd ni Hadiyth Marfuw’: ((Atw-Twiyarah ni shirki, Atw-Twiyarah ni shirki. Na hakuna yeyote miongoni mwetu asiyehisi jambo moyoni [Kuhusu Atw-Twiyarah] lakini Allaah Huiondoa kwa kutawakali Kwake)) [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth hii Hasan Swahiyh] Na imetajwa kwamba kauli ya mwisho ni ya Ibn Mas’uwd.

 

وَلأَحْمَدَ مِنْ حَدِيثِ ابْنِ عَمْرِو: ((مَنْ رَدَّتْهُ الطِّيَرَةُ عَنْ حَاجَتِهِ، فَقَدْ أَشْرَكَ)) قَالُوا: فَمَا كَفَّارَةُ ذَلِكَ؟ قَالَ: ((أَنْ يَقُولَ اللَّهُمَّ لاَ خَيْرَ إِلاَّ خَيْرُكَ، وَلاَ طَيْرَ إِلاَّ طَيْرُكَ، وَلاَ إِلَهَ غَيْرُكَ))

Na Imaam Ahmad amesimuila Hadiyth ya Ibn ‘Amr: ((Atakayerudi nyuma pasina na kuitekeleza haja yake kwa sababu ya Atw-Twiyarah [itikadi ya kutabiri mkosi, nuksi] amefanya shirki)) Wakuliza: Basi nini kafara yake? Akajibu: ((Aseme: Allaahumma laa khayra illa khayruka, wa laa Twayra illa twayruka, wa laa ilaaha ghayruka – Ee Allaah, hakuna khayr ila Uiletayo Wewe, wala hakuna ubaya ila Ulioukadiria Wewe, na hapana muabudiwa wa haki zaidi Yako)) [Ahmad]

 

وَلَهُ مِنْ حَدِيثِ الْفَضْلِ بْنِ عَبَّاسٍ: ((إِنَّمَا الطِّيَرَةُ مَا أَمْضَاكَ أَوْ رَدَّكَ))

Naye [Imaam Ahmad] pia amesimulia Hadiyth: ((Hakika mtu huhukumiwa kwa dhambi za Atw-Twiyarah inapompelekea kufanya au kujizuia na jambo [aliloazimia kulitenda])) [Ahmad]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kukumbusha maana ya Aayah:

 

أَلَا إِنَّمَا طَائِرُهُمْ عِندَ اللَّـهِ

((Tanabahi!  Hakika nuksi yao iko kwa Allaah))

            na:

طَائِرُكُم مَّعَكُمْ ۚ

((Nuksi yenu mnayo wenyewe))

 

2-Kukanusha kwamba maradhi yaweza kumsibu mtu bila ya idhini ya Allaah.

 

3-Kukanusha (At-Twiyarah) – Itikadi kuwa mtu aweza kudhuriwa na mkosi, nuksi isiyokuwa katika Qadhwaa na Qadar ya Allaah.  

 

4-Kukanusha kwa haamah (nuksi inayotokana na bundi)

 

5-Kukanusha kuwa mwezi wa Swafar ni mwezi wa nuksi.

 

6-Al-Fa-al haijakatazwa, bali ni mustahabb - inapendekezwa.

 

7-Ufafanuzi wa Al-Fa-al kwa kirefu.

 

8-Hakuna ubaya ikiwa mashaka hayo yataingia katika nyoyo ilhali mtu anachukia. Bali Allaah (سبحانه وتعالى) Atamhifadhi mtu huyo kwa sababu ya kutawakali Kwake kwa dhati kabisa.

 

9-Du’aa ya kusoma ikiwa mtu atapata hisia za namna hiyo.

 

10-Kutajwa kwamba Atw-Twiyarah ni shirki.

 

11-Ufafanuzi wa Atw-Twiyarah iliyoharamishwa.

 

 

Share

29-Kitaab At-Tawhiyd: Unajimu – Utabiri Wa nyota

Mlango Wa 29

بَابُ مَا جَاءَ فِي التَّنْجِيمِ

Unajimu – Utabiri Wa nyota

 

 

قَالَ الْبُخَارِيُّ فِي صَحِيحِهِ: قَالَ قَتَادَةُ: خَلَقَ اللَّهُ هَذِهِ النُّجُومَ لِثَلاثٍ: زِينَةً لِلسَّمَاءِ، وَرُجُومًا لِلشَّيَاطِينِ، وَعَلامَاتٍ يُهْتَدَى بِهَا، فَمَنْ تَأَوَّلَ فِيهَا غَيْرَ ذَلِكَ أَخْطَأَ وَأَضَاعَ نَصِيبَهُ وَتَكَلَّفَ مَا لاَ عِلْمَ لَهُ بِه . انْتَهَى

Al-Bukhaariy amekusanya katika Swahiyh yake: Qataadah amesema: “Allaah Ameumba hizi nyota kwa malengo matatu; (i) mapambo ya mbingu (ii) vimondo vya [kuwafukuza na kuwapiga] shaytwaan, (iii) alama za kuongoza njia (wasafiri wa majangwani na baharini). Basi atakayefasiri vingine amekosea na atakuta patupu Aakhirah (atakosa thawabu) kwani atakuwa amebeba asio na elimu nayo kwa kuchupa mipaka ya ujuzi wake.” Mwisho wa kunukuu.

 

 وَكَرِهَ قَتَادَةُ تَعَلُّمَ مَنَازِلِ الْقَمَرِ وَلَمْ يُرَخِّصِ ابْنُ عُيَيْنَةَ فِيهِ ذَكَرَهُ حَرْبٌ عَنْهُمَا وَرَخَّصَ فِي تَعَلُّمِ الْمَنَازِلِ أَحْمَدُ وَإِسْحَاقُ

Harb ameripoti kwamba kujifunza manaazil (vituo) vya mwezi imeruhusiwa na Ahmad na Is-haaq lakini imechukizwa na Qataadah na imeharamishwa na ‘Uyaynah.

 

وَعَنْ أَبِي مُوسَى قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ثَلاثَةٌ لا يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ: مُدْمِنُ الْخَمْرِ، وَقَاطِعُ الرَّحِمِ، وَمُصَدِّقٌ بِالسِّحْر)) رَوَاهُ أَحْمَدُ وَابْنُ حِبَّانَ فِي "صَحِيحِهِ

Imepokelewa kutoka kwa Abu Muwsaa amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watu watatu hawatoingia Jannah; mlevi anayedumu katika pombe, mkataji undugu na anayeamini uchawi)) [Ahmad na Ibn Hibbaan katika Swahiyh yake]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Hikmah ya kuumbwa nyota.

 

2-Kuwakanusha wanajimu (watabiri nyota).

 

3-Khitilafu za Wanachuoni juu ya kujifunza manaazil ya mwezi.

 

4-Adhabu waliyoandaliwa wenye kuamini madanganyo ya kichawi ilhali inajulikana wazi kuwa uchawi ni upotofu.

 

 

Share

30-Kitaab At-Tawhiyd: Kutafuta Mvua Kwa Manazili Ya Mwezi Na Nyota

Mlango Wa 30

بَابُ مَا جَاءَ فِي الِاسْتِسقَاءِ بِالْأَنْوَاءِ

Kutafuta Mvua Kwa Manazili Ya Mwezi Na Nyota


 

 

وَقَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى: 

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa: 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

((Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha)) [Al-Waaqi’ah (56: 82)]

 

وَعَنْ أَبِي مَالِكٍ الأَشْعَرِيِّ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((أَرْبَعٌ فِي أُمَّتِي مِنْ أَمْرِ الْجَاهِلِيَّةِ لاَ يَتْرُكُونَهُنَّ: الْفَخْرُ بِالأَحْسَابِ وَالطَّعْنُ فِي الأَنْسَابِ وَالاسْتِسْقَاءُ بِالنُّجُومِ وَالنِّيَاحَةُ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Maalik Al-Ash’ariyyi (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mambo manne katika Ummah wangu ni miongoni mwa mambo ya kijaahiliyyah na hawayaachi; kujifakharisha kwa unasaba na mafaniko yao, kutukanana kwa nasabu, kutafuta mvua kwa nyota kuomboleza)) [Muslim]

 

وَقَال: ((النَّائِحَةُ إِذَا لَمْ تَتُبْ قَبْلَ مَوْتِهَا تُقَامُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَعَلَيْهَا سِرْبَالٌ مِنْ قَطِرَانٍ وَدِرْعٌ مِنْ جَرَبٍ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Na akasema (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Mwombolezi asipotubia kabla ya kufa kwake, Siku ya Qiyaamah atavalishwa kanzu ya shaba iliyoyeyuka na joho la upele [wa ukoma])) [Muslim]

 

وَلَهُمَا عَنْ زَيْدِ بْنِ خَالِدٍ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: صَلَّى لَنَا رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) صَلاةَ الصُّبْحِ بِالْحُدَيْبِيَةِ عَلَى إِثْرِ سَمَاءٍ كَانَتْ مِنَ اللَّيْلِ،  فَلَمَّا انْصَرَفَ أَقَبْلَ عَلَى النَّاسِ فَقَالَ: ((هَلْ تَدْرُونَ مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ؟)) قَالُوا: اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمَ. قَالَ: ((قَالَ أَصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي وَكَافِرٌ، فَأَمَّا مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِفَضْلِ اللَّهِ وَرَحْمَتِهِ، فَذَلِكَ مُؤْمِنٌ بِي كَافِرٌ بِالْكَوْكَبِ، وَأَمَّا مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِنَوْءِ كَذَا وَكَذَا، فَذَلِكَ كَافِرٌ بِي مُؤْمِنٌ بِالْكَوْكَبِ))

Imepokelewa kutoka kwa Zayd bin Khaalid (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alituswalisha Swalaah ya asubuhi Hudaybiyah baada ya usiku wa mvua. Alipomaliza akawakabili watu akasema: ((Je, mnajua Rabb wenu Amesema nini?)) Wakajibu: “Allaah na Rasuli Wake ndio wajuao.” Akasema: ((Allaah Amesema: Baadhi ya waja Wangu wameamka leo wakiwa wenye kuniamini, na wengine wamekufuru. Aliyesema kuwa mvua ni kutokana na fadhila na rahmah za Allaah, basi huyo ni mwenye kuniamini wala haamini nyota. Ama aliyesema: Tumenyeshewa mvua kutokana na nyota fulani, yeye ni mwenye kunikufuru na mwenye kuamini nyota)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَلَهُمَا مِنْ حَدِيثِ ابْنِ عَبَّاسٍ مَعْنَاهُ وَفِيهِ: قَالَ بَعْضُهُمْ لَقَدْ صَدَقَ نَوْءَ كَذَا وَكَذَا فَأَنْزَلَ اللَّهُ هَذِهِ الآيَاتِ:

Nao wawili (Al-Bukhaariy na Muslim) wamerekodi Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas(رضي الله عنهما)  kama hiyo na nyongeza kwamba: “Wakasema baadhi yao kwamba imenyesha mvua kwa sababu ya nyota kadhaa wa kadhaa”, kisha Allaah Akateremsha Aayah zifuatazo:

 

فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ ﴿٧٥﴾

((Basi Naapa kwa maangukio ya nyota))

 

وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ ﴿٧٦﴾

((Na hakika hicho ni kiapo adhimu lau mngelijua))

 

إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ ﴿٧٧﴾

((Hakika hii bila shaka ni Qur-aan kariym, tukufu))

 

فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ ﴿٧٨﴾

((Katika Kitabu kilichohifadhiwa))

 

لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ ﴿٧٩﴾

((Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa)

 

تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٨٠﴾

((Ni uteremsho kutoka kwa Rabb wa walimwengu))

 

أَفَبِهَـٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ ﴿٨١﴾

Je, kwa maneno haya nyinyi ni wenye kuikanusha na kuibeza?

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

((Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha)) [Al-Waaqi’ah (56:75-82)]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Waaqi’ah (56: 75-82).

 

2-Desturi nne mbaya za kipindi cha jaahiliyyah (kabla ya Uislamu).

 

3-Kufr zilizomo katika baadhi ya desturi hizo.

 

4-Baadhi ya matendo ya kufru hayamtoi mtu katika Uislamu.

 

5-Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

((أَصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي وَكَافِرٌ))

((Baadhi ya waja Wangu wameamka leo wakiwa wenye kuniamini, na wengine wamekufuru)).

 

kwa sababu ya neema, rahmah (ya mvua) waliyoteremshiwa.

 

6-Umuhimu wa iymaan katika mazingira hayo.

 

7-Kudhihiri kufru katika hali kama hizo.

 

8-Ukumbusho kuhusu usemi wao: “Tumepata mvua kwa sababu ya nyota kadhaa”

 

9-Njia ya kuwafundisha wanafunzi kwa maswali katika kueleza jambo kama Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alivyosema: ((Je, mnajua Rabb wenu Amesema nini?)).

 

10-Adhabu waliyoandaliwa wenye kuomboleza kwa sauti msibani.

 

 

 

 

Share

31-Kitaab At-Tawhiyd: Kumpenda Allaah Na Rasuli Wake Kuliko Nafsi Yako Au Yeyote Yule

Mlango Wa 31

باب: وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ

Kumpenda Allaah Na Rasuli Wake Kuliko Nafsi Yako Au Yeyote Yule


 

 

قَوْلِ اللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

((وَمِنَ النَّاسِ مَن يَتَّخِذُ مِن دُونِ اللَّـهِ أَندَادًا يُحِبُّونَهُمْ كَحُبِّ اللَّـهِ ۖ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ ۗ ))

((Na miongoni mwa watu wako wenye kuchukua asiyekuwa Allaah na kuwafanya kuwa ni wanaolingana (na Allaah) wanawapenda kama kumpenda Allaah. Na wale walioamini wana mapenzi zaidi kwa Allaah)) [Al-Baqarah (2: 165)]  

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

قُلْ إِن كَانَ آبَاؤُكُمْ وَأَبْنَاؤُكُمْ وَإِخْوَانُكُمْ وَأَزْوَاجُكُمْ وَعَشِيرَتُكُمْ وَأَمْوَالٌ اقْتَرَفْتُمُوهَا وَتِجَارَةٌ تَخْشَوْنَ كَسَادَهَا وَمَسَاكِنُ تَرْضَوْنَهَا أَحَبَّ إِلَيْكُم مِّنَ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَجِهَادٍ فِي سَبِيلِهِ فَتَرَبَّصُوا حَتَّىٰ يَأْتِيَ اللَّـهُ بِأَمْرِهِ ۗ  

((Sema: “Ikiwa baba zenu na watoto wenu na ndugu zenu na wake (au waume) zenu na jamaa zenu na mali mliyoichuma na biashara mnayoikhofia kuharibika kwake, na majumba mnayoridhika nayo, ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Allaah na Rasuli Wake na kufanya jihaad katika njia Yake; basi ngojeeni mpaka Allaah Alete Amri Yake (ya adhabu)) [At-Tawbah (9: 24)]

 

عَنْ أَنَسٍ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى أَكُونَ أَحَبَّ إِلَيْهِ مِنْ وَلَدِهِ وَوَالِدِهِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ)) أَخْرَجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Haamini mmoja wenu mpaka anipende mimi kuliko watoto wake na baba yake na watu wote)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَلَهُمَا عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ثَلاثٌ مَنْ كُنَّ فِيهِ وَجَدَ بِهِنَّ حَلاوَةَ الإِيمَانِ: أَنْ يَكُونَ اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَحَبَّ إِلَيْهِ مِمَّا سِوَاهُمَا، وَأَنْ يُحِبَّ الْمَرْءَ لاَ يُحِبُّهُ إِلاَّ لِلَّهِ، وَأَنْ يَكْرَهَ أَنْ يَعُودَ فِي الْكُفْرِ بَعْدَ إِذْ أَنْقَذَهُ اللَّهُ مِنْهُ  كَمَا يَكْرَهُ أَن ْيُقْذَفَ فِي النَّار))

Nao Al-Bukhaariy na Muslim wamerekodi Hadiyth kutoka kwake Anas(رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mambo matatu atakayekuwa nayo, atapata utamu wa Iymaan: Allaah na Rasuli Wake wawe vipenzi zaidi kwake kuliko wengineo, ampende mtu na wala asimpende isipokuwa kwa ajili ya Allaah, na achukie kurudi katika ukafiri baada ya Allaah kumwokoa kutoka huko kama anavyochukia kuingizwa motoni)) [Al-Bukhaariy na Muslim]  

وَفِي رِوَايَة:َ ((لاَ يَجِدُ أَحَدٌ حَلاوَةَ الإِيمَانِ حَتَّى...)) إِلَى آخِرِهِ

Katika riwaayah: ((Hatopata mtu utamu wa iymaan mpaka …)) mpaka mwisho wa Hadiyth

 

وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ قَالَ: مَنْ أَحَبَّ فِي اللَّهِ وَأَبْغَضَ فِي اللَّهِ، وَوَالَى فِي اللَّهِ، وَعَادَى فِي اللَّهِ، فَإِنَّمَا تُنَالُ وِلايَةُ اللَّهِ بِذَلِكَ، وَلَنْ يَجِدَ عَبْدٌ طَعْمَ الإِيمَانِ وَإِنْ كَثُرَتْ صَلاتُهُ وَصَوْمُهُ  حَتَّى يَكُونَ كَذَلِكَ، وَقَدْ صَارَتْ عَامَّةُ مُؤَاخَاةِ النَّاسِ عَلَى أَمْرِ الدُّنْيَا، وَذَلِكَ لاَ يُجْدِي عَلَى أَهْلِهِ شَيْئًا  - رَوَاهُ ابْنُ جَرِيرٍ

Na Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema: Anayependa kwa ajili ya Allaah, na akachukia kwa ajili ya Allaah, na akafanya urafiki kwa ajili ya Allaah, akafanya uadui kwa ajili ya Allaah, kwa sifa hizo, ndipo hupatikana urafiki wa Allaah. Na wala mja hatoonja utamu wa iymaan hata kama zikikithiri Swalaah zake, na Swawm zake, ila awe katika sifa hizo. Aghlabu ya urafiki wa watu ni sababu ya maslahi ya kidunia. Lakini hilo halitowafaidisha kitu (Aakhirah). [Ibnu Jariyr]

 

وَقَالَ ابْنُ عَبَّاسٍ فِي قَوْلِهِ تَعَالَى: ((وَتَقَطَّعَتْ بِهِمُ الْأَسْبَابُ)) قَالَ: الْمَوَدَّةُ

Na akasema Ibn ‘Abbaas kuhusu kauli Yake Ta’aalaa: ((na yatawakatikia mafungamano yao)) [Al-Baqarah (2:166)]. Amesema mafungamano hapa yamaanisha upendo.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Baqarah (2: 165).

 

2- Tafsiri ya Aayah katika Suwrah At-Tawbah (9: 24).

 

3-Lazima tumpende Nabiy Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) kuliko nafsi zetu, familia zetu na mali zetu.

 

4-Kutokuwa na Iymaan (katika Hadiyth: “Haamini mmoja wenu mpaka …” hakumaanishi ni kutoka nje ya Uislamu.

 

5-Iymaan ina ladha, yaani wakati mwengine Muumini hupata ladha yake na wakati mwengine hapati ladha.

 

6-Hakuna anayeweza kupata urafiki wa Allaah (سبحانه وتعالى) na ladha ya iymaan isipokuwa tu anapokuwa na ‘amali nne moyoni: (1) Kupenda kwake kwa ajili ya Allaah; (2) Kuchukia kwake kwa ajili ya Allaah; (3) Urafiki wake kwa ajili ya Allaah; (4) Uadui wake kwa ajili ya Allaah.

 

7-Ufahamu wa Maswahaba kwamba ghalibu ya mafungamano ya watu na usuhuba ni kwa ajili ya maslahi ya kidunia.

 

8-Tafsiri ya Aayah:

وَتَقَطَّعَتْ بِهِمُ الْأَسْبَابُ

((na yatawakatikia mafungamano yao)).

 

9-Hata baadhi ya washirikina humpenda sana Allaah (سبحانه وتعالى).

 

10-Tishio la adhabu kwa mtu anayependa "mambo manane" zaidi kuliko Dini yake. “Mambo manane” ni:  (1) wazee wake (2) kizazi chake (3) ndugu zake (4) mume au mke wake (5) ukoo wake (6) mali yake (7) biashara yake (8) maskani yake. 

 

11-Yeyote anayemfanyia Allaah (سبحانه وتعالى) washirika na kumpenda huyo mshirika kama pendo lake kwa Allaah (سبحانه وتعالى), basi hivyo ni shirki kuu.

 

Share

32-Kitaab At-Tawhiyd: Kumkhofu Allaah Pekee Katika Yanayomhusu Yeye Ta’aalaa

Mlango Wa 32

باب:  إِنَّمَا ذَٰلِكُمُ الشَّيْطَانُ يُخَوِّفُ أَوْلِيَاءَهُ...

Kumkhofu Allaah Pekee Katika Yanayomhusu Yeye Ta’aalaa


قَوْلِ اللَّهِ تَعَالَى :

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

إِنَّمَا ذَٰلِكُمُ الشَّيْطَانُ يُخَوِّفُ أَوْلِيَاءَهُ   

((Hakika huyo ni shaytwaan anawakhofisha marafiki wake wandani)) [Aal-‘Imraan (3: 175)]

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

 إِنَّمَا يَعْمُرُ مَسَاجِدَ اللَّـهِ مَنْ آمَنَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ وَأَقَامَ الصَّلَاةَ وَآتَى الزَّكَاةَ وَلَمْ يَخْشَ إِلَّا اللَّـهَ ۖ فَعَسَىٰ أُولَـٰئِكَ أَن يَكُونُوا مِنَ الْمُهْتَدِينَ  ﴿١٨﴾

((Hakika wanaoamirisha Misikiti ya Allaah ni (wale) wanaomwamini Allaah na Siku ya Mwisho, na wakasimamisha Swalaah na wakatoa Zakaah na hawamkhofu (yeyote) isipokuwa Allaah. Basi asaa hao wakawa miongoni mwa walioongoka)) [At-Tawbah (9: 18)]

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّـهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّـهِ جَعَلَ فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّـهِ وَلَئِن جَاءَ نَصْرٌ مِّن رَّبِّكَ لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمْ ۚ أَوَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَعْلَمَ بِمَا فِي صُدُورِ الْعَالَمِينَ ﴿١٠﴾

((Na miongoni mwa watu wako wasemao: “Tumemwamini Allaah;” lakini wanapoudhiwa kwa ajili ya Allaah, hufanya fitnah za watu kama kwamba ni adhabu ya Allaah. Na inapowajia nusura kutoka kwa Rabb wako husema: “Hakika sisi tulikuwa pamoja nanyi.” Je, kwani Allaah Hayajui yale yaliyomo katika vifua vya walimwengu?)) [Al-‘Ankabuwt (29: 10)]

 

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) مَرْفُوعًا: ((إِنَّ مِنْ ضَعْفِ الْيَقِينِ أَنْ تُرْضِيَ النَّاسَ بِسَخَطِ اللَّهِ، وَأَنْ تَحْمَدَهُمْ عَلَى رِزْقِ اللَّهِ، وَأَنْ تَذُمَّهُمْ عَلَى مَا لَمْ يُؤْتِكَ اللَّهُ، إِنَّ رِزْقَ اللَّهِ لا يَجُرُّهُ حِرْصُ حَرِيصٍ، وَلا يَرُدُّهُ كَرَاهِيَةُ كَارِه))

Abuu Sa’iyd(رضي الله عنه)  amesimulia Hadiyth Marfuw’: ((Hakika katika udhaifu wa yakini ni kuridhisha wengine hali ya kumuudhi Allaah, na kuwasifu [na kuwashukuru] wengine kwa rizki Aliyotoa Allaah, na kuwalaumu wengine kwa asilokujaalia Allaah. Hakika rizki ya Allaah haivutwi na bidii au pupa ya wenye pupa, wala haizuiwi na chuki ya mwenye inda)) [Abuu Nu’aym, Al-Hilyah]

 

وَعَنْ عَائِشَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((مَنِ الْتَمَسَ رِضَا اللَّهِ بِسَخَطِ النَّاسِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ وَأَرْضَى عَنْهُ النَّاسَ، وَمَنِ الْتَمَسَ رِضا النَّاسِ بِسَخَطِ اللَّهِ سَخِطَ اللَّهُ عَلَيْهِ وَأَسْخَطَ عَلَيْهِ النَّاسَ)) رَوَاهُ ابْنُ حِبَّانَ فِي صَحِيحِهِ

Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayemridhisha Allaah hata ikiwa watu watakasirika, huyo atapata radhi za Allaah pamoja na radhi za watu, kwa vile Allaah Atawafanya watu wamridhiye yeye. Na atakayewaridhisha watu hali ya kumkasirisha Allaah, huyo atakasirikiwa na Allaah pamoja na watu kwa vile Allaah Atawafanya watu wamkasirikie)) [Ibn Hibbaan katika Swahiyh yake]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Aal-‘Imraan (3: 175).

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah At-Tawbah (9: 18).

 

3-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-‘Ankabuwt (29: 10).

 

4-Kuna mabadiliko ya kupanda na kushuka iymaan, huwa dhaifu na wakati mwengine huwa ni ya juu kabisa.

 

5-Dalili tatu za udhaifu wa yakini na iymaan ya mtu. 

 

6-Kumpwekesha Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee kwa kumkhofu ni wajibu (katika Uislamu).

 

7-Malipo ya mtu anayemkhofu Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee kwa ikhlaasw kabisa.

 

8-Adhabu ya asiyemkhofu Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

Share

33-Kitaab At-Tawhiyd: Kutawakali Kwa Allaah Pekee

Mlango Wa 33

باب:  وَعَلَى اللَّـهِ فَتَوَكَّلُوا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ

Kutawakali Kwa Allaah Pekee


بَابُ قَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Mlango kuhusu kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

  وَعَلَى اللَّـهِ فَتَوَكَّلُوا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ﴿٢٣﴾

((Na kwa Allaah Pekee tawakalini ikiwa nyinyi ni Waumini)) [Al-Maaidah (5: 23)]

وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

 

 إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ ﴿٢﴾

((Hakika Waumini ni wale ambao Anapokumbukwa na kutajwa Allaah, nyoyo zao zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali)) [Al-Anfaal (8: 2)]

 وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ حَسْبُكَ اللَّـهُ وَمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٦٤﴾

((Ee Nabiy! Anakutosheleza Allaah na anayekufuata miongoni wa Waumini)) [Al-Anfaal (8: 64)]

 وَقَوْلِهِ:

Na kauli Yake:

  وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ ۚ  

((Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza)) [Atw-Twalaaq (65: 3)]

 

 وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ قَالَ: حَسْبُنَا اَللَّهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ، قَالَهَا إِبْرَاهِيمُ عَلَيْهِ اَلسَّلامُ حِينَ أُلْقِيَ فِي اَلنَّارِ، وَقَالَهَا مُحَمَّدٌ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) حِينَ قَالُوا لَهُ: ((الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ ﴿١٧٣﴾ رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ وَالنَّسَائِيُّ

Na Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  amesema: ‘Hasbuna-Allaahu wa Ni’mal-Wakiyl Amesema hivyo Ibraahiym alipotupwa motoni. Na amesema hivyo Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) waliposema: ((Wale walioambiwa na watu: “Hakika watu wamejumuika dhidi yenu, basi waogopeni” Lakini iliwawazidishia iymaan wakasema: “Hasbuna-Allaah! Allaah Anatutosheleza, Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote)) [Aal-‘Imraan (2: 173)]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuwa na tawakkul kwa Allaah (سبحانه وتعالى) ni wajibu wa Dini.

 

2-Kuwa na tawakkul kwa Allaah (سبحانه وتعالى) ni sharti la iymaan.

 

3-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Anfaal (8: 2).

 

4-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Anfaal (8: 64).

 

5-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Atw-Twalaaq (65: 3).

 

6-Umuhimu wa maneno: ((Hasbuna-Allaahu wa Ni’mal-Wakiyl - Haya ni maneno yaliyosemwa na Ibraahiym (عليه السلام)   na Nabiy Muhammad   (صلى الله عليه وآله وسلم) wakati wa janga.

Share

34-Kitaab At-Tawhiyd: Kuhisi Amani Dhidi Ya Mipango Ya Allaah Ni Kinyume Na Tawhiyd

Mlango Wa 34

باب:  أَفَأَمِنُوا مَكْرَ اللَّـهِ ۚ فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ

Kuhisi Amani Dhidi Ya Mipango Ya Allaah (Ya Adhabu Zake) Ni Kinyume Na Tawhiyd


قَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli Yake Ta’aalaa:

 

 أَفَأَمِنُوا مَكْرَ اللَّـهِ ۚ فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩٩﴾

((Je, wameaminisha mipango ya Allaah? Basi hawaaminishi mipango ya Allaah isipokuwa watu wenye kukhasirika)) [Al-A’raaf (7: 99)]

وَقَوْلِهِ

Na kauli Yake:

  وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِ إِلَّا الضَّالُّونَ ﴿٥٦﴾

 

((Na nani anayekata tamaa na rahmah ya Rabb wake isipokuwa wapotofu)) [Al-Hijr (15: 56)]

 

وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) سُئِلَ عَنِ الْكَبَائِرِ؟ فَقَالَ: ((اَلشِّرْكُ بِاَللَّهِ، وَالْيَأْسُ مِنْ رَوْحِ اَللَّهِ، وَالأَمْنُ مِنْ مَكْرِ اَللَّهُ))

Na kutoka kwa Ibn ‘Abbaas(رضي الله عنهما)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliulizwa kuhusu madhambi makubwa. Akasema: ((Kumshirikisha Allaah, na kukata tamaa na faraja ya Allaah, na kuaminisha mpango wa Allaah [ya adhabu])) [Al-Bayhaqiy katika Majma’ Az-Zawaaid, Al-Bazaar, Atw-Twabaraaniy]

 

وَعَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ قَالَ: ((أَكْبَرُ الْكَبَائِرِ الإِشْرَاكُ بِاَللَّهِ، وَالأَمْنُ مِنْ مَكْرِ اَللَّهِ، وَالْقُنُوطُ مِنْ رَحْمَةِ اَللَّهِ، وَالْيَأْسُ مِنْ رَوْحِ اَللَّهِ)) رَوَاهُ عَبْدُ اَلرَّزَّاقِ

Na kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه)  amesema: ((Madhambi makubwa zaidi ni kumshirikisha Allaah, na kuaminisha mipango ya Allaah [ya adhabu Zake], na kukata tamaa Rahmah ya Allaah, na kuvunjika tamaa na faraja ya Allaah)) [‘Abdur-Razaaq]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-A’raaf (7: 99).

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Hijr (15: 56).

 

3-Ukali wa adhabu iliyoahidiwa kwa anayedhani kuwa amesalimika na adhabu za Allaah (سبحانه وتعالى).

 

4-Adhabu kali iliyoahidiwa kwa anayekata tamaa na rahmah za Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

 

Share

35-Kitaab At-Tawhiyd: Kuvumilia Maqadario Ya Allaah Ni Miongoni Mwa Iymaan

 

Mlango Wa 35

بَابٌ مِنَ الْإِيمَانِ بِاللَّهِ الصَّبْرُ عَلَى أَقْدَارِ اللَّهِ

Kuvumilia Maqadario Ya Allaah Ni Miongoni Mwa Iymaan

 


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

وَمَن يُؤْمِن بِاللَّـهِ يَهْدِ قَلْبَهُ

((Na yeyote   anayemuamini Allaah, (Allaah) Huuongoza moyo wake)) [At-Taghaabun (64: 11)]

 

قَالَ عَلْقَمَةُ: هُوَ الرَّجُلُ تُصِيبُهُ الْمُصِيبَةُ فَيَعْلَمُ أَنَّهَا مِنْ عِنْدِ اللَّهِ فَيَرْضَى وَيُسَلِّمُ

‘Alqamah amesema: “Huyo ni yule ambaye anapopatwa na msiba hutambua kwamba umetoka kwa Allaah kisha akaridhika na akasalimu amri.”

 

وَفِي صَحِيحِ مُسْلِمٍ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  قَالَ: ((اِثْنَتَانِ فِي النَّاسِ هُمَا بِهِمْ كُفْرٌ، الطَّعْنُ فِي النَّسَبِ، وَالنِّيَاحَةُ عَلَى الْمَيِّتِ))

Na katika Swahiyh Muslim kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mambo mawili hupelekea kufru miongoni mwa watu; kukashifu nasaba yake na kumlilia maiti – kuomboleza)) [Muslim]

 

وَلَهُمَا عَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ (رضي الله عنه) مَرْفُوعًا: ((لَيْسَ مِنَّا مَنْ ضَرَبَ الْخُدُودَ وَشَقَّ الْجُيُوبَ وَدَعَا بِدَعْوَى الْجَاهِلِيَّةِ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) Hadiyth Marfuw’: ((Si miongoni mwetu anayejipiga mashavu, akapasua mifuko na akaomba maombi ya kijaahiliyyah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

وَ عَنْ أَنَسٍ (رضي الله عنه)  أنَّ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) قَال: َ((إِذَا أَرَادَ اللَّهُ بِعَبْدِهِ الْخَيْرَ عَجَّلَ لَهُ الْعُقُوبَةَ فِي الدُّنْيَا، وَإِذَا أَرَادَ اللَّهُ بِعَبْدِهِ الشَّرَّ أَمْسَكَ عَنْهُ بِذَنْبِهِ حَتَّى يُوَافِيَ بِهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ))

Kutoka kwa Anas kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Anapompendelea mja Wake khayr, Humharakishia adhabu yake duniani. Na Allaah Anapomtakia mja Wake shari Humzuilia dhambi zake Amlipe Siku ya Qiyaamah [Amuadhibu huko])) [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah] 

 

 وَ قال النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ عِظَمَ الْجَزَاءِ مَعَ عِظَمِ الْبَلاءِ وَإِنَّ اللَّهَ إِذَا أَحَبَّ قَوْمًا ابْتَلاهُمْ فَمَنْ رَضِيَ فَلَهُ الرِّضَا وَمَنْ سَخِطَ فَلَهُ السَّخَطُ)) رواه الترمذي وقال حديث حسن

((Hakika jazaa kubwa ipo ni kwa balaa kubwa na hakika Allaah Akiwapenda watu Huwajaribu kwa mtihani. Basi atakayeridhika Allaah Atamridhia na atakayechukia atapata ghadhabu Zake)) [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah At-Taghaabun (64:11).

 

2-Hili (Kukubali Qadhwaa na Qadar ya Allaah سبحانه وتعالى) ni sehemu ya iymaan halisi kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

3-Mtu kukashifu nasaba yake.

 

4-Adhabu kali iliyoahidiwa kwa wanaojipiga mashavu, kuchana nguo na akalia kwa maombolezi ya kijaahiliyyah.

 

5-Dalili kuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Anamtakia khayr mja Wake.

 

6-Dalili kuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Anamtakia shari mja Wake.

 

7-Dalili ya mapenzi ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa anayemuabudu.

 

8-Ubaya wa kutokuridhika na Qadhwaa na Qadar ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

9-Fadhila na thawabu za kukubali mitihani ya Allaah (سبحانه وتعالى).

Share

36-Kitaab At-Tawhiyd: Riyaa – Kujionyesha

Mlango Wa 36

بَابٌ مَا جَاءَ فِي الرِّيَاءِ

Riyaa – Kujionyesha


 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

قُلْ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖ فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

((Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi ni mtu kama nyinyi, nafunuliwa Wahy kwamba: Hakika Muabudiwa wa haki wenu ni Ilaah Mmoja Pekee. Hivyo anayetaraji kukutana na Rabb wake, basi na atende ‘amali njema na wala asishirikishe yeyote katika ‘ibaadah za Rabb wake”)) [Al-Kahf: (18:110)]

 

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ مَرْفُوعًا: ((قَالَ تَعَالَى: أَنَا أَغْنَى الشُّرَكَاءِ عَنِ الشِّرْكِ مَنْ عَمِلَ عَمَلاً أَشْرَكَ مَعِي فِيهِ غَيْرِي تَرَكْتُهُ وَشِرْكَهُ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Na kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) Hadiyth Marfuw’: ((Allaah Ta’aalaa Amesema: Mimi ni mwenye kujitosheleza, sihitaji washirika. Kwa hiyo, yule afanyae ‘amali hali ya kumshirikisha mwengine ndani yake pamoja na Mimi nitamuachilia mbali na shirki yake)) [Muslim]

 

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ مَرْفُوعًا: ((أَلا أُخْبِرُكُمْ مَا هُوَ أَخْوَفُ عَلَيْكُمْ عِنْدِي مِنَ الْمَسِيحِ الدَّجَّالِ؟)) قَالُوا بَلَى: قَالَ: ((الشِّرْكُ الْخَفِيُّ، يَقُومُ الرَّجُلُ فَيُصَلِّي فَيُزَيِّنُ صَلاتَهَ، لِمَا يَرَى مِنْ نَظَرِ رَجُلٍ إِلَيْه)) رَوَاهُ أَحْمَدُ

Na Imepokelewa kutoka kwa Abuu Sa’iyd, Hadiyth Marfuw’: ((Je, niwajulisheni nikikhofiacho zaidi juu yenu kuliko hata Masiyh Ad-Dajjaal?)) Wakasema: Ndio. Akasema: ((Ni shirki iliyojfichikana kama vile mtu kuipamba Swalaah yake kwa kuwa anaangaliwa)) [Ahmad, Ibn Maajah]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Kahf (18: 110).

 

2- Suala kuu kuwa ‘amali njema ikiwa ameshirikishwa Allaah (سبحانه وتعالى) na mwenginewe, ni yenye kukataliwa.

 

3-Sababu ya kukatakaliwa ‘amali kama hiyo ni kujitosheleza Kwake Allaah (سبحانه وتعالى) kikamilifu bila ya kumtemgemea yeyote.

 

4-Sababu nyingine ni kuwa Yeye (Allaah سبحانه وتعالى) ni Mbora wa wote kwa hivo hastahiki kushirikishwa na mwengine katika ‘ibaadah Zake. 

 

5-Khofu aliyokuwa nayo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) juu ya Riyaa kwa Maswahaba Wake (رضي الله عنهم).

 

6-Aliieleza Riyaa kwa kupigia mfano anayeswali kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى), lakini anaipamba vyema Swalaah yake anapojua kuwa wengine wanamwangalia yeye (kinyume na anapokuwa peke yake).

 

 

 

Share

37-Kitaab At-Tawhiyd: Miongoni Mwa Shirki Kutenda ‘Amali Njema Kwa Ajili Ya Manufaa Ya Kidunia

Mlango Wa 37

بَابٌ مِنَ الشِّرْكِ إِرَادَةُ الْإِنْسَانِ بِعَمَلِهِ الدُّنْيَا

Miongoni Mwa Shirki Kutenda ‘Amali Njema Kwa Ajili Ya Manufaa Ya Kidunia


 

وَقَوْلُهُ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

مَن كَانَ يُرِيدُ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا وَزِينَتَهَا نُوَفِّ إِلَيْهِمْ أَعْمَالَهُمْ فِيهَا وَهُمْ فِيهَا لَا يُبْخَسُونَ ﴿١٥﴾

((Anayetaka uhai wa dunia na mapambo yake Tutawalipa kikamilifu ‘amali zao humo, nao hawatopunjwa humo)) 

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ لَيْسَ لَهُمْ فِي الْآخِرَةِ إِلَّا النَّارُ ۖ وَحَبِطَ مَا صَنَعُوا فِيهَا وَبَاطِلٌ مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٦﴾

((Hao ndio wale ambao hawatokuwa na chochote katika Aakhirah isipokuwa moto. Na yataporomoka yale waliyoyafanya humo (duniani), na ni yenye kubatilika yale waliyokuwa wakiyatenda)) [Huwd (10: 15-16)]

 

وفِي الصَّحِيحِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((تَعِسَ عَبْدُ الدِّينَارِ، تَعِسَ عَبْدُ الدِّرْهَمِ، تَعِسَ عَبْدُ الْخَمِيصَةِ، تَعِسَ عَبْدُ الْخَمِيلَةِ، إِنْ أُعْطِيَ رَضِي، وَإِنْ لَمْ يُعْطَ سَخِطَ، تَعِسَ وَانْتَكَسَ، وَإِذَا شِيكَ فَلا اِنْتَقَشَ، طُوبَى لِعَبْدٍ آخِذٍ بِعِنَانِ فَرَسِهِ فِي سَبِيلِ اللَّهِ، أَشْعَثَ رَأْسُهُ، مُغْبَرَّةٍ قَدَمَاهُ، إِنْ كَانَ فِي الْحِرَاسَةِ كَانَ فِي الْحِرَاسَةِ، وَإِنْ كَانَ فِي السَّاقَةِ كَانَ فِي السَّاقَةِ، إِنْ اِسْتَأْذَنَ لَمْ يُؤْذَنْ لَهُ، وَإِنْ شَفَعَ لَمْ يُشَفَّعْ))

Na katika Swahiyh, Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ameangamia mtumwa wa dinari! Ameangamia mtumwa wa dirham! Ameangamia mtumwa wa Al-Khamiyswah! Ameangamia mtumwa wa Al-Khamiylah! Anapopewa huridhika, asipopewa hukasirika. Ameangamia na amehiliki mtu huyo. Na kama akichomwa na mwiba asipate mtu wa kumchomoa. Twuwbaa ashikaye khitamu za farasi wake katika njia ya Allaah hali nywele zake timu timu na miguu yake mavumbi matupu. Akiwekwa katika [kikosi cha] ulinzi huridhika na kazi yake ya ulinzi, na akiwekwa kikosi cha nyuma jeshini huifurahia kazi yake. [Hana makuu wala tamaa. Machoni mwa watu ni mtu duni] kiasi ambacho akiomba ruhusa [kwa mtawala] haruhusiwi; na akishufia, maombezi yake hukataliwa [kwa sababu ya unyenyekevu wake] [Al-Bukhaariy]

 

Al-Khamiysah:     mali na nguo nzuri za fakhari na anasa.

Al-Khamiylah:      nguo za makhmeli.

Twuwbaa:             hongera, furaha au mti wa Jannah unaoitwa hivyo.

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Mtu kutamani mambo ya kidunia kwa kisingizio cha kutenda ya Aakhirah.

 

2-Tafsiri ya Ayaah katika Suwrah ya Huwd (11:15-16).

 

3-Muislamu kuitwa mtumwa wa dinar, dirham, khamiysah (yaani mali na nguo za fakhari na anasa).

 

3-Maelezo kuwa: Yeye anapopewa tu vitu hivyo huridhika, anaponyimwa hukasirika.

 

4-Maana ya maneno: ta'isa wa intakasa: “Ameangamia na amehiliki mtu kama huyo.”

 

5-Maana ya maneno: “akichomwa na mwiba asipate mtu wa kumchomoa.”

 

6-Kuwasifu anayepigana jihaad kwa sifa zilizoelezwa (katika Hadiyth).

 

 

 

 

Share

38-Kitaab At-Tawhiyd: Anayewatii Wanachuoni Na Watawala Katika Kuharamisha Aliyohalalisha Au ...

Mlango Wa 38

بَابٌ مَنْ أَطَاعَ الْعُلَمَاءَ وَالْأُمَرَاءَ فِي تَحْرِيمِ مَا أَحَلَّ اَللَّهُ أَوْ تَحْلِيلِ مَا حَرَّمَهُ فَقَدْ اِتَّخَذَهُمْ أَرْبَابًا

Anayewatii Wanachuoni Na Watawala Katika Kuharamisha Aliyohalalisha Au Kuhalalisha Aliyoharamisha Allaah Kawafanya Ni Waabudiwa


 

وَقَالَ اِبْنُ عَبَّاسٍ: يُوشِكُ أَنْ تَنْزِلَ عَلَيْكُمْ حِجَارَةٌ مِنَ اَلسَّمَاءِ. أَقُولُ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ) وَتَقُولُونَ قَالَ أَبُو بَكْرٍ وَعُمَرُ؟

Na Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema: “Kumekurubia kukuteremkieni mawe (ya adhabu) kutoka mbinguni! Mimi nasema: Amesema Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) nanyi mnasema: Kasema Abuu Bakr na ‘Umar?!”

 

وَقَالَ الإِمَامُ أَحْمَدُ بْنُ حَنْبَلٍ: عَجِبْتُ لِقَوْمٍ عَرَفُوا الإِسْنَادَ وَصِحَّتَهُ،  وَيَذْهَبُونَ إِلَى رَأْيِ سُفْيَانَ وَاَللَّهُ تَعَالَى يَقُولُ: ((فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ))  أَتَدْرِي مَا الْفِتْنَةُ؟ الْفِتْنَةُ اَلشِّرْكُ لَعَلَّهُ إِذَا رَدَّ بَعْضَ قَوْلِهِ أَنْ يَقَعَ فِي قَلْبِهِ شَيْءٌ مِنَ اَلزَّيْغِ فَيَهْلَكَ.  

Na Imaam Ahmad amesema: “Nastajaabishwa na watu waliojua isnaad [ya Hadiyth] na usahihi wake, lakini wanashikilia rai ya Sufyaan [Ath-Thawry] na hali Allaah Anasema: ((Basi watahadhari wale wanaokhalifu amri yake, isije kuwasibu fitnah au ikawasibu adhabu iumizayo)) [An-Nuwr (24:63)]. Je, unajua hapa ni nini fitnah? Fitnah hapa ni shirki. Huenda kwa kukataa baadhi ya mafundisho yake (صلى الله عليه وآله وسلم), jambo hilo laweza kumletea mtu shaka na upotofu moyoni mwake na ikawa hiyo ni sababu ya kuangamia kwake.”

 

وَعَنْ عَدِيٍّ بْنِ حَاتِمٍ: أَنَّهُ سَمِعَ اَلنَّبِيَّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقْرَأُ هَذِهِ الآيَةَ: ((اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِّن دُونِ اللَّـهِ ...)) فَقُلْتُ لَهُ: إِنَّا لَسْنَا نَعْبُدُهُمْ. قَالَ: ((أَلَيْسَ يُحَرِّمُونَ مَا أَحَلَّ اَللَّهُ فَتُحَرِّمُونَهُ وَيُحِلُّونَ مَا حَرَّمَ اَللَّهُ فَتُحِلُّونَهُ؟)) فَقُلْتُ بَلَى. قَالَ: ((فَتِلْكَ عِبَادَتُهُم)) رَوَاهُ أَحْمَدُ وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ

Na Imepokelewa kutoka kwa ‘Adiyy bin Haatim(رضي الله عنه)  kwamba amemsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisoma Aayah: ((Wamewafanya Wanachuoni wao mafuqahaa wa dini na Wamonaki wao kuwa ni waabudiwa badala ya Allaah…)) [At-Tawbah (9: 31)] Nikasema: Hakika sisi hatuwaabudu. Akasema: ((Je, kwani hawaharamishi Aliyoyahalalisha Allaah nanyi mkayaharamisha? Na wanahalalisha Aliyoyaharamisha Allaah nanyi mnayahalalisha?)) Nikasema: Ndio. Akasema: ((Basi hivyo ndivyo kuwaabudu)) [Ahmad na At-Tirmidhiy na ameipa daraja ya Hasan]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah An-Nuwr (24: 63).

 

2-Tafsiri ya Aayh katika Suwrah Al-Baraa-ah (At-Tawbah 9: 31).

 

3-Kudhihirisha maana ya ‘ibaadah ambayo ilikanushwa na ‘Adiyy (رضي الله عنه).

 

4-Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) ametoa mfano wa Abuu Bakr na ‘Umar; na Imaam Ahmad ametoa mfano wa Sufyaan.

 

5-Hali ilibadilika mno kiasi ambacho kuwaabudu watawa imekuwa ‘amali bora kabisa ijulikanayo kwa jina la Al-Wilaayah. Na kuwaabudu wanachuoni ndio elimu na fiqhi. Kisha, hali ikabadilika tena mpaka kiasi ambacho wakawa wanaabudiwa badala ya Allaah watu ambao si hata katika waja wema na wakaabudiwa ambao ni katika majahili kabisa.   

 

 

Share

39-Kitaab At-Tawhiyd: Kutafuta Hukmu Kinyume Na Allaah Na Rasuli Wake Ni Unafiki

 

Mlango Wa 39

باب: أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُوا بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ

Kutafuta Hukmu Kinyume Na Allaah Na Rasuli Wake Ni Unafiki

 


 

 

 

قَوْلُهُ تَعَالَى:

Kauli Yake Ta’aalaa:

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آمَنُوا بِمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنزِلَ مِن قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُوا إِلَى الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُوا أَن يَكْفُرُوا بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُضِلَّهُمْ ضَلَالًا بَعِيدًا ﴿٦٠﴾

((Je, huoni wale wanaodai kwamba wao wameamini yaliyoteremshwa kwako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) na yale yaliyoteremshwa kabla yako; wanataka wahukumiane kwa twaghuti (ubatilifu) na hali wameamrishwa wakanushe hiyo. Na shaytwaan anataka awapoteze upotofu wa mbali))

 

 

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا إِلَىٰ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ وَإِلَى الرَّسُولِ رَأَيْتَ الْمُنَافِقِينَ يَصُدُّونَ عَنكَ صُدُودًا ﴿٦١﴾

((Na wanapoambiwa: “Njooni kwenye yale Aliyoyateremsha Allaah na kwa Rasuli; utawaona wanafiki wanakugeukilia mbali kwa mkengeuko))

 

فَكَيْفَ إِذَا أَصَابَتْهُم مُّصِيبَةٌ بِمَا قَدَّمَتْ أَيْدِيهِمْ ثُمَّ جَاءُوكَ يَحْلِفُونَ بِاللَّـهِ إِنْ أَرَدْنَا إِلَّا إِحْسَانًا وَتَوْفِيقًا ﴿٦٢﴾

((Basi itakuwaje utakapowafika msiba kwa sababu ya yale iliyotanguliza mikono yao? Kisha wakakujia wakiapa “Wa-Allaahi hatukutaka ila mazuri na mapatano”)) [An-Nisaa (4: 60-63)]

 

 وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ قَالُوا إِنَّمَا نَحْنُ مُصْلِحُونَ ﴿١١﴾

((Na wanapoambiwa: “Msifanye ufisadi katika ardhi.” Husema: “Hakika sisi ni watengenezaji”)) [Al-Baqarah (2: 11)]

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

وَلَا تُفْسِدُوا فِي الْأَرْضِ بَعْدَ إِصْلَاحِهَا

((Na wala msifanye ufisadi katika ardhi baada ya kutengenea kwake)) [Al-A’raaf (7: 56)]

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ ۚ وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّـهِ حُكْمًا لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ ﴿٥٠﴾

((Je, wanataka hukumu ya (enzi ya) ujahili? Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu kwa watu wenye yakini)) [Al-Maaidah (5: 50)]

 

 وَعَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ: أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى يَكُونَ هَوَاهُ تَبَعًا لِمَا جِئْتُ بِهِ)) قَالَ النَّوَوِيُّ:حَدِيثٌ صَحِيحٌ رَوَيْنَاهُ فِي كِتَابِ ألْحُجَّة بِإِسْنَادٍ صَحِيحٍ  

Na Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hatoamini mmoja wenu mpaka yawe matamanio yake ni kufuata niliyokuja nayo)) [Amesema An-Nawawy: Hadiyth Swahiyh imenukuliwa katika Kitaab Al-Hujjah ikiwa na isnaad Swahiyh]

 

وَقَالَ الشَّعْبِيُّ: كَانَ بَيْنَ رَجُلٍ مِنَ الْمُنَافِقِينَ وَرَجُلٌ مِنَ الْيَهُودِ خُصُومَةٌ. فَقَالَ الْيَهُودِيُّ:  نَتَحَاكَمُ إِلَى مُحَمَّدٍ. عَرِفَ أَنَّهُ لا يَأْخُذُ الرِّشْوَةَ.  وَقَالَ الْمُنَافِقُ: نَتَحَاكَمُ إِلَى الْيَهُود.ِ لِعِلْمِهِ أَنَّهُمْ يَأْخُذُونَ الرِّشْوَةَ. فَاتَّفَقَا أَنْ يَأْتِيَا كَاهِنًا فِي جُهَيْنَةَ فَيَتَحَاكَمَا إِلَيْهِ فَنَزلَ: ((أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ...))

Na Ash-Sha’biyy amesema: Kulitokea ugomvi baina ya Myahudi na Mnafiki. Myahudi akasema: “Tutafute hukmu kwa Muhammad.” Kwani alijua kwamba hapokei rushwa. Na mnafiki akasema: “Tutafute hukmu kwa Mayahudi.” Akijua kwamba wao wanapokea rushwa. Wakakubaliana wote wawili waende [badala yake] kwa kuhani [mtabiri] wa Juhaynah awahukumie. Ikateremshwa Aayah: ((Je, huoni wale ambao wanadai kwamba …))

 

وَقِيلَ: نَزَلَتْ فِي رَجُلَيْنِ اِخْتَصَمَا، فَقَالَ أَحَدُهُمَا: نَتَرَافَعُ إِلَى النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) وَقَالَ الآخَرُ: إِلَى كَعْبِ بْنِ الأَشْرَفِ. ثُمَّ تَرَافَعَا إِلَى عُمَرَ فَذَكَرَ لَهُ أَحَدُهُمَا الْقِصَّةَ فَقَالَ لِلَّذِي لَمْ يَرْضَ بِرَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ) أَكَذَلِكَ؟ قَالَ نَعَمْ. فَضَرَبَهُ بِالسَّيْفِ فَقَتَلَهُ

Na imesemekana kwamba imeteremka kuhusu watu wawili waliokuwa na mgogoro. Akasema mmoja wao: “Tukapeleke mashitaka yetu kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).” Mwengine akasema: “Tupeleke kwa Ka’b bin Al-Ashraf” (Myahudi). Kisha wote wawili wakamwendea ‘Umar (رضي الله عنه) . Mmoja wao akamwelezea kadhia yao. ‘Umar akamuuliza ambaye hakuridhia kupeleka kesi yake kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Je, ni kweli alivyosema [mwenzako]?” Akajibu: “Ndio!”  Akampiga panga na akamuua.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah An-Nisaa (4: 60) pamoja na masisitizo wa kuelewa maana ya Twaaghuwt.

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Baqarah (2: 11).

 

3-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-A’raaf (7: 56).

 

4-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-Maai’dah (5: 50).

   

5-Maelezo ya Ash-Sha’biyy (رحمه الله) kuhusu sababu ya kuteremshwa Aayah (Suwrah An-Nisaa 4: 60).

 

6-Tofauti baina ya iymaan ya kweli na ya uongo.

 

7-Kisa cha ‘Umar (رضي الله عنه) na Mnafiki.

 

8-Hakuna anayepata iymaan isipokuwa mpaka hawaa zake zifuate na aliyokuja nayo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

Share

40-Kitaab At-Tawhiyd: Anayekanusha Chochote Kuhusu Majina Na Sifa Za Allaah

Mlango Wa 40

بَابٌ مَنْ جَحَدَ شَيْئًا مِنَ الْأَسْمَاءِ وَالصِّفَاتِ

Anayekanusha Chochote Kuhusu Majina Na Sifa Za Allaah


 

 

 قَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

 وَهُمْ يَكْفُرُونَ بِالرَّحْمَـٰنِ ۚ قُلْ هُوَ رَبِّي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ وَإِلَيْهِ مَتَابِ ﴿٣٠﴾

((Nao wanamkufuru Ar-Rahmaan. Sema: “Yeye Ndiye Rabb wangu, hapana Muabudiwa wa haki ila Yeye, Kwake natawakali na Kwake ni mahali pangu pa kurejea kutubu”)) [Ar-Ra’d (13: 30)]

 

وَفِي صَحِيحِ الْبُخَارِيِّ،  قَالَ عَلِيٌّ: حَدِّثُوا النَّاسَ بِمَا يَعْرِفُونَ، أَتُرِيدُونَ أَنْ يُكَذَّبَ اللَّهُ وَرَسُولُهُ؟!

Na katika Swahiyh Al-Bukhaariy amesema ‘Aliyy(رضي الله عنه) : Wasemezeni watu kwa njia itakayowawezesha kufahamu kwa urahisi. Je mnataka Akadhibishwe Allaah na Rasuli Wake?!

 

وَرَوَى عَبْدُ الرَّزَّاقِ عَنْ مَعْمَرٍ، عَنِ ابْنِ طَاوُسٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ: أَنَّهُ رَأَى رَجُلاً اِنْتَفَضَ لَمَّا سَمِعَ حَدِيثًا عَنِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فِي الصِّفَاتِ، اِسْتِنْكَارًا لِذَلِكَ فَقَالَ: مَا فَرَقُ هَؤُلاءِ؟ يَجِدُونَ رِقَّةً عِنْدَ مُحْكَمِهِ وَيَهْلِكُونَ عِنْدَ مُتَشَابِهِهِ! -  اِنْتَهَى

Abdur-Razzaaq amesimulia kutoka kwa Ma’mar, kutoka kwa Ibn Twaawuws, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba: (Ibn ‘Abbaas) alimwona mtu akisimamisha miguu yake kwa kuchukiwa aliposikia Hadiyth ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Sifa za Allaah. Hapo (Ibn ‘Abbaas) akasema: Kitu gani kinachowatia uoga watu hawa? Wanachukia Aayah zilizo muhkam (waziwazi kabisa) na wanajiangamiza kwa Aayah za mutashaabihaat (Aayah zisizokuwa bayana kwao). 

 

 وَلَمَّا سَمِعَتْ قُرَيْشٌ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَذْكُرُ الرَّحْمَنَ أَنْكَرُوا ذَلِكَ فَأَنْزَلَ اللَّهُ فِيهِمْ: ((وَهُمْ يَكْفُرُونَ بِالرَّحْمَـٰنِ ۚ ))  

Na Maquraysh walipomsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akimtaja Ar-Rahmaan walikanusha Sifa hiyo. Allaah Akawateremshia: ((Nao wanamkufuru Ar-Rahmaan …))

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Hana iymaan anayekanusha lolote katika Majina au Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى).

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Ar-Ra’d (13: 30).

 

3-Epuka kuzungumza katika namna ambayo msikilizaji hataelewa waziwazi

 

4-Kutajwa sababu zinazopelekea kumkanusha Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) hata kama bila kudhamiria.

 

5-Onyo la Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنه) kuwa yeyote anayekanusha Sifa yoyote ya Allaah (سبحانه وتعالى) ataangamia.

 

Share

41-Kitaab At-Tawhiyd: Ni Kufuru Kukanusha Neema Ya Allaah Baada Ya Kuitambua

Mlango Wa 41

باب:  يَعْرِفُونَ نِعْمَتَ اللَّـهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكْثَرُهُمُ الْكَافِرُونَ

Ni Kufuru Kukanusha Neema Ya Allaah Baada Ya Kuitambua

 


 

 

 قَوْلُ اللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

يَعْرِفُونَ نِعْمَتَ اللَّـهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكْثَرُهُمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٣﴾

((Wanazijua neema za Allaah, kisha wanazikanusha; na wengi wao ni makafiri)) [An-Nahl: (16: 83)]

 

  قَالَ مُجَاهِد مَا مَعْنَاهُ: هُوَ قَوْلُ الرَّجُلِ هَذَا مَالِي، وَرِثْتُهُ عَنْ آبَائِي

Mujaahid kasema: “Maana yake ni: Mtu kusema: Hii mali yangu nimeirithi kwa baba zangu.

 

وَقَالَ عَوْنُ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ: يَقُولُونَ لَوْلا فُلانٌ لَمْ يَكُنْ كَذَا

Na ‘Awn bin ‘Abdillaah amesema: “Wanasema lau kama si fulani, isingelikuwa hivi! (hizo neema, na hali wanajua kwamba Allaah Ndiye Anayetoa uwezo na tawfiq).”

 

وَقَالَ اِبْنُ قُتَيْبَةَ يَقُولُونَ: هَذَا بِشَفَاعَةِ آلِهَتِنَا

Na Ibn Qutaybah kasema: “Wanasema hizi (neema) ni kutokana na shafaa’ah (uombezi) wa waabudiwa wetu”

 

وَقَالَ أَبُو الْعَبَّاسِ بَعْدَ حَدِيثِ زَيْدِ بْنِ خَالِدٍ الَّذِي فِيهِ وَأَنَّ اللهَ تَعَالَى قَال: ((أَصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي وَكَافِرٌ)) الْحَدِيثِ، وَقَدْ تَقَدَّمَ: وَهَذَا كَثِيرٌ فِي الْكِتَابِ وَالسُّنَّةِ، يَذُمُّ سُبْحَانَهُ مَنْ يُضِيفُ إِنْعَامَهُ إِلَى غَيْرِهِ وَيُشْرِكُ بِهِ.

Na Abuu Al-‘Abbaas (Ibn Taymiyyah) kasema baada ya Hadiyth ya Khaalid ambayo humo Allaah Ta’aalaa Amesema: ((Baadhi ya waja Wangu wameamka leo wakiwa wenye kuniamini, na wengine wamekufuru)) [Hadiyth imetangulia][1]. Na amri hizi ni nyingi katika Qur-aan na Sunnah. Allaah Anashutumu anayeegemeza neema (na rahmah) Zake kwa wengine na wanaomshirikisha Naye.

 

قَالَ بَعْضُ السَّلَفِ: هُوَ كَقَوْلِهِمْ: كَانَتِ الرِّيحُ طَيِّبَةً، وَالْمَلاَّحُ حَاذِقًا.. وَنَحْوَ ذَلِكَ مِمَّا هُوَ جَارٍ عَلَى أَلْسِنَةٍ كَثِيرَةٍ

Na baadhi ya Salaf wamesema: Ni kauli zao: “Upepo ulikuwa mzuri.” Na “Nahodha alikuwa hodari (na hali wanajua aliyewafikisha salama ni Allaah na si uzuri wa upepo wala uhodari wa nahodha) na mfano wa maneno kama hayo yanayosemwa na watu wengi.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Maelezo kuhusu neema za Allaah (سبحانه وتعالى) kisha ukanushaji wake.

 

2-Watu wengi wayasema hayo (kukanusha neema za Allaah).

 

3-Kutaja kauli hizo ni sawa na kukanusha neema za Allaah.

 

4-Kujumuisha moyoni mambo mawili yenye kupingana; kama kuitambua neema ya Allaah (سبحانه وتعالى) kisha kuzikanusha.

 

 

[1]  Taz. Mlango Wa 30.

 

 

Share

42- Kitaab At-Tawhiyd: Msimfanyie Allaah Wanaolingana Naye

Mlango Wa 42

باب: فَلَا تَجْعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ

Msimfanyie Allaah Wanaolingana Naye


 

 

قول الله تعالى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa: 

فَلَا تَجْعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا وَأَنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿٢٢﴾

((Basi msimfanyie Allaah waliolingana naye na hali ya kuwa nyinyi mnajua)) [Al-Baqarah (2: 22)]

 

  وَقَالَ اِبْنُ عَبَّاسٍ فِي الآيَةِ:  الأَنْدَادُ هُوَ: الشِّرْكُ أَخْفَى مِنْ دَبِيبِ النَّمْلِ عَلَى صَفَاةٍ سَوْدَاءَ فِي ظُلْمَةِ اللَّيْلِ وَهُوَ أَنْ تَقُولَ: وَاللَّهِ وَحَيَاتِكَ يَا فُلانُ، وَحَيَاتِي، وَتَقُولَ: لَوْلاَ كُلَيْبَةُ هَذَا لأَتَانَا اللُّصُوصُ، وَلَوْلاَ الْبَطُّ فِي الدَّارِ لأَتَى اللُّصُوصُ، وَقَوْلُ الرَّجُلِ لِصَاحِبِهِ: مَا شَاءَ اللَّهُ وَشِئْتَ، وَقَوْل الرَّجُلِ لَوْلاَ اللَّهُ وَفُلانٌ، لاَ تَجْعَلْ فِيهَا فُلانًا هَذَا كُلُّهُ بِهِ شِرْكٌ.  رَوَاهُ اِبْنُ أَبِي حَاتِمٍ

Na Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema kuhusu Aayah hiyo: ‘Andaada’ ni shirki. Nayo imefichika zaidi kama sisimizi (mweusi) apitaye juu ya jiwe jeusi katika kiza cha usiku. Mtu huingia katika shirki kama hiyo hata kwa kusema kwa utani: “Wa-Allaahi naapa kwa uhai wako na wangu ee fulani.” Pia kusema: “Lau kama si kijibwa hiki wezi wangetuingilia.” Au: “Lau sikuweko bata nyumbani wezi wangetuingilia.” Na kauli asemayo mtu kwa sahibu yake: “Maa-Shaa-Allaah wa-shiita – Kwa kupenda Allaah na wewe.” Na kauli ya mtu: “Lau kama si Allaah na fulani.”  Usitaje hivyo kwani yote hii ni shirki! [Ibn Abiy Haatim]

 

وَعَنْ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) أَنّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَال: ((مَنْ حَلَفَ بِغَيْرِ اللَّهِ فَقَدْ كَفَرَ أَوْ أَشْرَك)) رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ وَصَحَّحَهُ الْحَاكِمُ

Na Imepokelewa kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayeapa kwa asiye  Allaah, amekufuru au amefanya shirki)) [At-Tirmidhiy na ameikiri ni Hasan, na Al-Haakim ameikiri ni Swahiyh]

 

وَقَالَ اِبْنُ مَسْعُودٍ: لأَنْ أَحْلِفَ بِاللَّهِ كَاذِبًا أَحَبُّ إِلَيَّ مِنْ أَنْ أَحْلِفَ بِغَيْرِهِ صَادِقًا.

Ibn Mas’uwd  (رضي الله عنه) amesema: “Afadhali niapie kwa Allaah jambo la uongo, kuliko kuapia asiyekuwa Allaah (au kitu kingine) hali ya kusema ukweli.”

 

  وَعَنْ حُذَيْفَةَ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ تَقُولُوا مَا شَاءَ اللَّهُ وَشَاءَ فُلانٌ وَلَكِنْ قُولُوا مَا شَاءَ اللَّهُ ثُمَّ شَاءَ فُلانٌ ))  رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ

Na Imepokelewa kutoka Kwa Hudhayfah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msiseme: “Kwa kupenda Allaah na kupenda fulani” bali semeni: “Kwa kupenda Allaah kisha kupenda fulani”)) [Abuu Daawuwd kwa isnaad Swahiyh]

 

وَجَاءَ عَنْ إِبْرَاهِيمَ النَّخَعِيِّ: أَنَّهُ يُكْرَهُ أَعُوذُ بِاللَّهِ وَبِكَ، وَيَجُوزُ أَنْ يَقُولَ بِاللَّهِ ثُمَّ بِكَ. قَالَ: وَيَقُولُ لَوْلاَ اللَّهُ ثُمَّ فُلاَنٌ، وَلا تَقُولُوا لَوْلا اللَّهُ وَفُلانٌ.

Ibraahim An-Nakha‘iyyi alikuwa akichukia mtu kusema: “Najikinga kwa Allaah na kwako.” Lakini inafaa kusema: “Najikinga kwa Allaah kisha kwako.” Inajuzu kusema: “Lau kama si Allaah kisha fulani,” lakini haijuzu kusema: “Lau kama si Allaah na fulani.”

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Maelezo ya ‘Andaad’ kama ilivyotajwa katika Aayah kwenye Suwrah Al-Baqarah (2: 22).

 

2-Maswahaba (رضي الله عنهم) walisema kuwa Aayah zenye kutaja shirki kubwa zilijumuisha pia na shirki ndogo.

 

3-Kuapa kwa asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى) ni shirki.

 

4-Kuapa kwa asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى) katika kusema ukweli ni dhambi zaidi kuliko kuapia kwa Allaah (سبحانه وتعالى) katika kusema uongo.

 

5-Tofauti baina ya herufi za ‘wa’ (na) na ‘thumma’ (kisha). 

 

 

 

 

 

 

Share

43-Kitaab At-Tawhiyd: Asiyeridhika Na Kiapo Kwa Jina La Allaah

Mlango Wa 43

بَابٌ: مَا جَاءَ فِيمَنْ لَمْ يَقْنَعْ بِالْحَلِفِ بِاللَّهِ

Asiyeridhika Na Kiapo Kwa Jina La Allaah


 

 

عَنْ اِبْنِ عُمَرَ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَال: ((لاَ تَحْلِفُوا بِآبَائِكُمْ، مَنْ حَلَفَ بِاللَّهِ فَلْيَصْدُقْ، وَمَنْ حُلِفَ لَهُ بِاللَّهِ فَلْيَرْضَ، وَمَنْ لَمْ يَرْضَ فَلَيْسَ مِنَ اللَّهِ)) رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ بِسَنَدٍ حَسَنٍ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msiape kwa mababu zenu bali apeni kwa Allaah. Na atakayeapa, basi aseme ukweli. Na atakayeapiwa aridhike nayo, na asiyeridhika nayo, huyo si miongoni mwa waja [wema] wa Allaah”)) [Ibn Maajah kwa isnaad Hasan]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuapia mababu haijuzu.

 

2-Maamrisho kwa anayeapiwa kwa Allaah (سبحانه وتعالى) kuwa aridhie.

 

3-Onyo kali kwa asiyetosheka na kiapo kinachoapiwa kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

Share

44-Kitaab At-Tawhiyd: Msemo: “Kwa Kupenda Allaah Na Kupenda Kwako”

Mlango Wa 44

بَابٌ: قَوْلُ مَا شَاءَ اللَّهُ وَشِئْتَ

Msemo: “Kwa Kupenda Allaah Na Kupenda Kwako


 

 

عَنْ قُتَيْلَةَ: أَنَّ يَهُودِيًّا أَتَى النَّبِيَّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَقَالَ: إِنَّكُمْ تُشْرِكُونَ، تَقُولُونَ مَا شَاءَ اللَّهُ وَشِئْتَ، وَتَقُولُونَ وَالْكَعْبَةِ فَأَمَرَهُمُ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) إِذَا أَرَادُوا أَنْ يَحْلِفُوا أَنْ يَقُولُوا: وَرَبِّ الْكَعْبَةِ وَأَنْ يَقُولُوا: مَا شَاءَ اللَّهُ ثُمَّ شِئْتَ.  رَوَاهُ النَّسَائِيُّ وَصَحَّحَهُ

Imepokelewa kutoka kwa Qutaylah (رضي الله عنه) kwamba: Myahudi alimwendea Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: Nyinyi mnafanya shirki pindi mnaposema: “Kwa kupenda Allaah na kupenda kwako (ee Muhammad”, na mnasema: “Naapa kwa Al-Ka’bah.” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawaamrisha Maswahaba kuwa wakitaka kuapa waseme: ((“Naapa kwa Rabb Wa Al-Ka’bah” na waseme: “Kwa kupenda Allaah na kisha kwa kupenda kwako [ee Muhammad]”)) [An-Nasaaiy na ameikiri Swahiyh]

 

وَلَهُ أَيْضًا عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ: أَنَّ رَجُلاً قَالَ لِلنَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: مَا شَاءَ اللَّهُ وَشِئْتَ، فَقَالَ: ((أَجَعَلْتَنِي لِلَّهِ نِدًّا؟ بَلْ! مَا شَاءَ اللَّهُ وَحْدَهُ))

(An-Nasaaiy) amesimulia pia kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) : Mtu mmoja alimwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Kwa kupenda Allaah na kupenda kwako”, Akamjibu: ((Je, umenilinganisha na Allaah? Bali sema: Kwa kupenda Allaah Peke Yake”))

 

وَلابْنِ مَاجَهْ: عَنِ الطُّفَيْلِ أَخِي عَائِشَةَ لأُمِّهَا، قَالَ: رَأَيْتُ كَأَنِّي أَتَيْتُ عَلَى نَفَرٍ مِنَ الْيَهُودِ،  قُلْتُ:  إِنَّكُمْ لأَنْتُمُ الْقَوْمُ، لَوْلا أَنَّكُمْ تَقُولُونَ: عُزَيْرٌ ابْنُ اللَّهِ.  قَالُوا: وَأَنْتُمْ لأَنْتُمُ الْقَوْمُ، لَوْلا أَنَّكُمْ تَقُولُونَ: مَا شَاءَ اللَّهُ وَشَاءَ مُحَمَّدٌ. ثُمَّ مَرَرْتُ بِنَفَرٍ مِنْ النَّصَارَى فَقُلْتُ: إِنَّكُمْ لأَنْتُمُ الْقَوْمُ، لَوْلا أَنَّكُمْ تَقُولُونَ: الْمَسِيحُ ابْنُ اللَّهِ. قَالُوا: وَإِنَّكُمْ لأَنْتُمُ الْقَوْمُ، لَوْلا أَنَّكُمْ تَقُولُونَ: مَا شَاءَ اللَّهُ وَشَاءَ مُحَمَّدٌ.  فَلَمَّا أَصْبَحْتُ أَخْبَرْتُ بِهَا مَنْ أَخْبَرْتُ، ثُمَّ أَتَيْتُ النَّبِيَّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَأَخْبَرْتُهُ، فَقَالَ: ((هَلْ أَخْبَرْتَ بِهَا أَحَدًا؟)) قُلْتُ: نَعَمْ . قَالَ: فَحَمِدَ اللَّهَ وَأَثْنَى عَلَيْهِ ثُمَّ قَالَ: ((أَمَّا بَعْدُ؛ فَإِنَّ طُفَيْلاً رَأَى رُؤْيَا أَخْبَرَ بِهَا مَنْ أَخْبَرَ مِنْكُمْ، وَأَنَّكُمْ قُلْتُمْ كَلِمَةً يَمْنَعُنِي كَذَا وَكَذَا أَنْ أَنْهَاكُمْ عَنْهَا فَلا تَقُولُوا: مَا شَاءَ اللَّهُ وَشَاءَ مُحَمَّدٌ، وَلَكِنْ قُولُوا مَا شَاءَ اللَّهُ وَحْدَهُ))

Na Ibn Maajah amesimulia kutoka kwa Twufayl ambaye ni kaka yake ‘Aaishah kwa mama, kwamba amesema: “Niliota katika utoto kuwa nilikutana na kundi la Mayahudi nikawaambia: Mngelikuwa nyinyi ndio waja wema wa Allaah lau si kusema kwenu kuwa ‘Uzayr ni mwana wa Allaah.” Wakasema: “Mngekuwa nyinyi (Waislamu) ndio waja wema wa Allaah lau si kusema kwenu: “Kwa kupenda Allaah na kupenda Muhammad.” Kisha nikakutana na kundi la Wakristo nikawaambia: “Mngekuwa nyinyi ndio waja wema wa Allaah lau si kusema kwenu kuwa Masiyhi ni mwana wa Allaah.” Wakasema: “Mngekuwa nyinyi Waislamu ndio waja wema wa Allaah lau si kusema kwenu: “Kwa kupenda Allaah na kupenda Muhammad.” Nilipoamka nikawahadithia ndoto yangu niliowahadithia kisha nikamwendea Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) nikamuhadithia. Akaniuliza: ((Je, umemhadithia yeyote?)) Nikasema: “Ndio.” Akapanda juu ya mimbari Akamhimidi Allaah (سبحانه وتعالى) na kumtukuza, kisha akasema: ((Amma ba’ad: Hakika Twufayl ameota ndoto na ameshawahi kuwahadithia aliowahi kuwahadithia miongoni mwenu. Na hakika mlikuwa mkisema msemo ambao sikuwazuia kwa sababu kadhaa wa kadhaa. Hivyo msiseme: “Kwa kupenda Allaah na kupenda Muhammad”, bali semeni: “Kwa kupenda Allaah Pekee Yake”)) [Ibn Maajah]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Mayahudi walikuwa wakitambua shirki ndogo.

 

2-Fahamu ya mtu kuhusu shirki ikiwa atapenda kutenda. 

 

3-Kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Je, umenilinganisha na Allaah?)) Imelaumiwa kwa kiasi kikubwa basi ubaya ulioje wa mshairi aliyesema:

 يا أكرمَ الخلْقِ مَالِىْ مَنْ اَلُوْذُ بِه سِوَاك عند حدوثِ الحادثِ العَمم    

“Ee mbora wa viumbe, sina mwengine kumuomba kinga isipokuwa wewe wakati wa dhiki na misukosuko.”[1] (Na beti zinazofuatia).

 

4-Hii si shirki kubwa kwa vile Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alivyosema:  

((Sikuwazuia kwa sababu kadhaa wa kadhaa)).

 

5-Ndoto ya kweli ni aina ya Wahyi.

 

6-Ndoto ya maana na ya kweli inaweza kuwa sababu ya kuanzisha hukumu fulani katika Shariy'ah.

 

 

 

 

 

[1] Shairi la Burdah la Al-Buswayriy ambalo beti zake zinamshirikisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kumpa cheo kama cha Allaah (سبحانه وتعالى).

Share

45-Kitaab At-Tawhiyd: Anayetukana Wakati Amemuudhi Allaah

Mlango Wa 45

بَابٌ مَنْ سَبَّ الدَّهْرَ فَقَدْ آذَى اللَّهَ

Anayetukana Wakati Amemuudhi Allaah


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَقَالُوا مَا هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا الدُّنْيَا نَمُوتُ وَنَحْيَا وَمَا يُهْلِكُنَا إِلَّا الدَّهْرُ ۚ وَمَا لَهُم بِذَٰلِكَ مِنْ عِلْمٍ ۖ إِنْ هُمْ إِلَّا يَظُنُّونَ ﴿٢٤﴾

((Na wakasema: “Huu si chochote isipokuwa ni uhai wetu wa dunia, tunakufa na tunahuika, na hakuna cha kutuangamiza isipokuwa zama tu.” Na wala hawana kwayo ujuzi wowote, ila wao wanadhania tu)) [Al-Jaathiyah (45: 24)]

 

وَفِي الصَّحِيحِ: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنِ النَّبِيِّ (صَلَى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((قَالَ اللَّهُ تَعَالَى: يُؤْذِينِي ابْنُ آدَمَ يَسُبُّ الدَّهْرَ، وَأَنَا الدَّهْرُ أُقَلِّبُ الْلَّيْلَ وَالنَّهَارَ))

Na katika Swahiyh, Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Ta’aalaa Amesema: Bin Aadam ananiudhi, kwani anatukana dahari [wakati au zama], na hali Mimi ni Ad-Dahr [Namiliki kila kitu na uwezo], Nageuza usiku na mchana)).

 

وَفِي رِوَايَةٍ: ((لا تَسُبُّوا الدَّهْرَ؛ فِإنَّ اللَّهَ هُوَ الدَّهْرُ))

Na katika riwaayah: ((Msitukane dahari kwani hakika Allaah ni Ad-Dahr)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kulaani wakati kumekatazwa.

 

2-Kutukana wakati ni kumkosoa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

3-Kutafakari kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Hakika Allaah ni Ad-Dahr)).

 

4-Jambo linaweza kuwa tusi hata kama haliko katika hisia (za mtukanaji).

 

 

Share

46-Kitaab At-Tawhiyd: Kujiita Qadhi Wa Maqadhi Na Mfano Wake

Mlango Wa 46

بَابٌ التَّسَمِّي بِقَاضِي الْقُضَاةِ وَنَحْوِهِ

Kujiita Qadhi Wa Maqadhi Na Mfano Wake


 

 

 

فِي الصَّحِيحِ: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَنِ النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((إِنَّ أَخْنَعَ اِسْمٍ عِنْدَ اللَّهِ رَجُلٌ تَسَمَّى مَلَكَ الأَمْلاكِ، لاَ مَالِكَ إِلاَّ اللَّهَ))

Katika Swahiyh Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Jina ovu na  la kuchukiza mno kwa Allaah ni mtu kujiita MalakAl-Amlaak [mfalme wa milki zote]. Hakuna Maalik isipokuwa Allaah))

 

قَالَ سُفْيَانُ مِثْلُ شَاهَانْ شَاهْ .

Sufyaan amesema: mfano: “Shaahaan Shaah” (mfalme wa wafalme kwa Wafursi).

 

وَفِي رِوَايَةٍ: ((أَغْيَظُ رَجُلٍ عَلَى اللَّهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَأَخْبَثُهُ ))

Na katika riwaayah nyingine:

((Mtu mwenye kuchukiwa mno na muovu kabisa mbele ya Allaah Siku ya Qiyaamah [ni mtu anayejiita: mfalme wa wafalme])) [Al-Bukhaariy]

Na maana ya  أخنع  ni   أوضع:  duni, aliyedhalilika kabisa.

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kukatazwa kutumia cheo cha ‘mfalme wa wafalme’ kwa yeyote.

 

2-Kukatazwa mfano wake kama mfano uliotolewa na Sufyaan (رضي الله عنه).

 

3-Ufahamu na kuelewa uzito wa kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) licha ya kuwa mtu anaweza asidhamirie maana mbaya moyoni mwake.

 

4-Utambuzi na ufahamu kwamba kutukuzwa kiuabudiwa ni kwa Allaah (سبحانه وتعالى) Pekee Mtukufu kuliko wote, Asiyefikiwa hata chembe ‘Uluwa Yake, Ametakasika na kila kitu (tofauti na ‘mfalme’ wa kidunia).

 

 

 

 

 

Share

47-Kitaab At-Tawhiyd: Kuheshimu Majina Ya Allaah Na Kubadilisha Jina Lake Mtu Kwa Ajili Hiyo

Mlango Wa 47

بَابٌ اِحْتِرَامُ أَسْمَاءِ اللَّهِ تَعَالَى وَتَغْيِيرُ الِاسْمِ لِأَجْلِ ذَلِكَ

Kuheshimu Majina Ya Allaah Ta’aalaa Na Kubadilisha Jina Lake Mtu Kwa Ajili Hiyo


 

 

 

عَنْ أَبِي شُرَيْحٍ: أَنَّهُ كَانَ يُكَنَّى: أَبَا الْحَكَمِ. فَقَالَ لَهُ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْحَكَمُ وَإِلَيْهِ الْحُكْمُ)) فَقَالَ: إِنَّ قَوْمِي إِذَا اِخْتَلَفُوا فِي شَيْءٍ أَتَوْنِي فَحَكَمْتُ بَيْنَهُمْ فَرَضِي كِلا الْفَرِيقَيْنِ فَقَالَ: ((مَا أَحْسَنَ هَذَا، فَمَا لَكَ مِنَ الْوَلَدِ؟)) قُلْتُ: شُرَيْحٌ وَمُسْلِمٌ وَعَبْدُ اللَّهِ. قَالَ: ((فَمَنْ أَكْبَرُهُمْ؟))  قُلْتُ: شُرَيْحٌ. قَالَ: ((فَأَنْتَ أَبُو شُرَيْحٍ))  رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَغَيْرُهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Shurayh(رضي الله عنه)  kwamba: alikuwa akiitwa Abuu Al-Hakam. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: ((Hakika Allaah ndiye Hakimu na Kwake kuna hukmu zote)) Akasema: Hakika watu wangu wanapokhitilafiana katika jambo, hunijia kisha nikawahukumu baina yao, hapo pande mbili zote zinaridhika. Akasema: ((Uzuri ulioje huo! Je, unao watoto?)) Nikajibu: [Ndio] Shurayh na Muslim na ‘Abdullaah. Akauliza: ((Nani mkubwa wao?)) Nikasema: Shurayh.  Akasema: ((Basi wewe ni Abuu Shurayh)) [Abuu Daawuwd na wengineo].

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuheshimu Majina na Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) japokuwa    maana yake halisi haikukusudiwa kujisifia nayo (na Abuu Shurayh)  

 

2-Mtu kubadili jina lake kwa ajili hiyo.

 

3-Kutumia jina la mtoto mkubwa kwa ajili ya kun-yah.

 

 

Share

48-Kitaab At-Tawhiyd: Anayefanya Istihzai Chochote Kuhusu Dhikru-Allaah, Qur-aan Au Rasuli

Mlango Wa 48

بَابٌ مَنْ هَزَلَ بِشَيْءٍ فِيهِ ذِكْرُ اللَّهِ أَوْ الْقُرْآنِ أَوْ الرَّسُولِ

Anayefanya Istihzai Chochote Ndani Yake Kuna

Dhikru-Allaah au Qur-aan Au Rasuli (Ni Kufru)


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَلَئِن سَأَلْتَهُمْ لَيَقُولُنَّ إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَلْعَبُ ۚ قُلْ أَبِاللَّـهِ وَآيَاتِهِ وَرَسُولِهِ كُنتُمْ تَسْتَهْزِئُونَ ﴿٦٥﴾

((Na ukiwauliza, bila shaka watasema: “Hakika tulikuwa tunaporoja na tunacheza.” Sema:  Je, mlikuwa mnamfanyia istihizai Allaah na Aayaat Zake na Rasuli Wake?”)) [At-Tawbah (9: 65)]

 

  وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ وَمُحَمَّدِ بْنِ كَعْبٍ وَزَيْدِ بْنِ أَسْلَمَ وَقَتَادَةَ: دَخَلَ حَدِيثُ بَعْضِهِمْ فِي بَعْضِ أَنَّهُ:  قَالَ رَجُلٌ فِي غَزْوَةِ تَبُوكَ:  مَا رَأَيْنَا مِثْلَ قُرَّائِنَا هَؤُلاَءِ أَرْغَبَ بُطُونًا وَلا أَكْذَبَ أَلْسُنًا وَلا أَجْبَنَ عِنْدَ اللِّقَاءِ – يَعْنِي: رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) وَأَصْحَابَهُ الْقُرَّاءَ.  فَقَالَ لَهُ عَوْفُ بْنُ مَالِكٍ :كَذَبْتَ وَلَكِنَّكَ مُنَافِقٌ لأُخْبِرَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ). فَذَهَبَ عَوْفٌ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) لِيُخْبِرَه فَوَجَدَ الْقُرْآنَ قَدْ سَبَقَهُ، فَجَاءَ ذَلِكَ الرَّجُلُ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ) وَقَدْ اِرْتَحَلَ وَرَكِبَ نَاقَتَهُ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَتَحَدَّثُ حَدِيثَ الرَّكْبِ نَقْطَعُ بِهِ عَنَاءَ الطَّرِيق.  قَالَ اِبْنُ عُمَرَ كَأَنِّي أَنْظُرُ إِلَيْهِ مُتَعَلِّقًا بِنِسْعَةِ نَاقَةِ رَسُولِ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) وَإِنَّ الْحِجَارَةَ تَنْكُبُ رِجْلَيْهِ وَهُوَ يَقُولُ: إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَلْعَبُ فَيَقُولُ لَهُ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم): ((أَبِاللَّـهِ وَآيَاتِهِ وَرَسُولِهِ كُنتُمْ تَسْتَهْزِئُونَ)) ((لَا تَعْتَذِرُوا قَدْ كَفَرْتُم بَعْدَ إِيمَانِكُمْ ۚ)) مَا يَلْتَفِتُ إِلَيْهِ وَمَا يَزِيدُهُ عَلَيْهِ

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Umar, na Muhammad bin Ka’b na Zayd bin Aslam na Qataadah, wamehadithia kwamba: Katika vita vya Tabuwk, mtu mmoja alisema: “Hatujapatapo kuona watu wana uchuu wa kula, waongo zaidi, waoga zaidi vitani kama wasomaji wetu hawa,” wakimaanisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na Maswahaba zake wasomi wa Qur-aan. ‘Awf bin Maalik akamjibu: “Wewe ni muongo na mnafiki! Na nitamjulisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) [ulivyosema].” ‘Awf akaenda kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kumjulisha akakuta Aayah za Qur-aan zimeshatangulia kuteremshwa. Na yule mnafiki akamjia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hali ameshampanda ngamia wake (yaani ameanza safari ya kurudi). Akajitolea udhuru kusema: “Ee Rasuli wa Allaah! Hakika tulikuwa tunapiga porojo na soga ili kufupisha umbali wa safari.”  Ibn ‘Umar (رضي الله عنهما)   akasema: “Kama vile namuona sasa hivi akining’inia katika mkanda wa saruji ya ngamia wa Rasuli wa Allaah na huku ngamia akikimbia na miguu yake huyo mtu ikigongwagongwa na mawe ya ardhi, naye [mnafiki akiendelea kutoa udhuru wake] akisema: “Tulikuwa tunapiga porojo na kucheza.” Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: ((Je, mlikuwa mnamfanyia istihizai Allaah na Aayaat Zake na Rasuli Wake?”)) ((Msitoe udhuru. Mmekwishakufuru baada ya kuamini kwenu)) [At-Tawbah (9:65-66)]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Ni jambo la kuogopesha kuwa yeyote anayeyafanyia mchezo mambo haya (ya kufanya istihzai, dhihaka Aayah za Allaah (سبحانه وتعالى) au Rasuli Wake صلى الله عليه وآله وسلم au Waumini) amekufuru.

 

2-Maelezo yaliyotolewa ya Aayah 9: 65, yanahusu yeyote afanyae hivyo.

 

3-Kuna tofauti baina ya An-Namiymah (kufitinisha) na nasaha ya ikhlaasw kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) na Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

4-Tofauti baina ya msamaha Anaoupenda Allaah (سبحانه وتعالى) na ukali katika kukabiliana na maadui wa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

5- Nyudhuru nyingine haziruhusiwi.

 

Share

49-Kitaab At-Tawhiyd: Kusema Mali Hii Ni Natija, Juhudi, Kazi, Elimu Yangu Kinyume Na Tawhiyd

Mlango Wa 49

باب:  وَلَئِنْ أَذَقْنَاهُ رَحْمَةً مِّنَّا مِن بَعْدِ ضَرَّاءَ مَسَّتْهُ لَيَقُولَنَّ هَـٰذَا لِي

Kusema Kuwa Mali Hii Ni Natija Juhudi Kazi Na Elimu Yangu Ni Kinyume Na Tawhiyd


 

قَوْلُ اللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَلَئِنْ أَذَقْنَاهُ رَحْمَةً مِّنَّا مِن بَعْدِ ضَرَّاءَ مَسَّتْهُ لَيَقُولَنَّ هَـٰذَا لِي وَمَا أَظُنُّ السَّاعَةَ قَائِمَةً وَلَئِن رُّجِعْتُ إِلَىٰ رَبِّي إِنَّ لِي عِندَهُ لَلْحُسْنَىٰ ۚ فَلَنُنَبِّئَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا بِمَا عَمِلُوا وَلَنُذِيقَنَّهُم مِّنْ عَذَابٍ غَلِيظٍ ﴿٥٠﴾

((Na Tunapomuonjesha rahmah kutoka Kwetu baada ya dhara iliyomgusa, bila shaka husema: “Haya nayastahiki mimi na sidhani kama Saa ya Qiyaamah itasimama. Na nitakaporejeshwa kwa Rabb wangu hakika nitapata mazuri Kwake.” Basi bila shaka Tutawabainishia wale waliokufuru yale waliyoyatenda, na bila shaka Tutawaonjesha adhabu nzito)) [Fusw-swilat (41: 50)]

 

 قَالَ مُجَاهِدٌ: هَذَا بِعَمَلِي وَأَنَا مَحْقُوقٌ بِهِ

Mujaahid amesema: (kuhusu maana ya maneno: “haadhaa liy” inamaanisha): “Hii ni natija ya kazi yangu nami ndiye ninayeistahiki.”

 

وَقَالَ اِبْنُ عَبَّاسٍ: يُرِيدُ مِنْ عِنْدِي  

Na Ibn ‘Abbaas amesema: (inamaanisha): “Kilichokuwa kwangu”

 

وَقَوْلُهُ:  

Na kauli Yake:

قَالَ إِنَّمَا أُوتِيتُهُ عَلَىٰ عِلْمٍ عِندِي ۚ  

(([Qaaruwn] Akasema: “Hakika nimepewa haya kwa sababu ya elimu yangu”)) [Al-Qaswasw (28:78)]

 

قَالَ قَتَادَةُ: عَلَى عِلْمٍ مِنِّي بِوُجُوهِ الْمَكَاسِبِ.

Qataadah amesema: (katika kuifasiri Aayah hiyo): “Mali hii nimepewa mimi kwa sababu ya uhodari na uzoefu wangu katika kuchuma.”

 

وَقَالَ آخَرُونَ: عَلَى عِلْمٍ مِنَ اللَّهِ أَنِّي لَهُ أَهْلٌ، وَهَذَا مَعْنَى قَوْلِ مُجَاهِدٍ: أُوتِيتُهُ عَلَى شَرَفٍ.

Na Wanachuoni wengineo wamesema: (ina maana kwamba): “Kutokana na elimu kutoka kwa Allaah ambayo mimi khususan nimestahiki kutoka Kwake” Na hii ndio maana ya kauli ya Mujaahid: “Nimepewa hii (mali) kwa kutokana na sharafu yangu kuu.”

 

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((إِنَّ ثَلاثَةً مِنْ بَنِي إِسْرَائِيلَ أَبْرَصَ وَأَقْرَعَ وَأَعْمَى، فَأَرَادَ اللَّهُ أَنَّ يَبْتَلِيَهُمْ، فَبَعَثَ إِلَيْهِمْ مَلَكًا. فَأَتَى الأَبْرَصَ فَقَالَ: أَيُّ شَيْءٍ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ: لَوْنٌ حَسَنٌ وَجِلْدٌ حَسَنٌ وَيَذْهَبُ عَنِّي الَّذِي قَدْ قَذَرَنِي النَّاسُ بِهِ. قَالَ: فَمَسَحَهُ فَذَهَبَ عَنْهُ قَذَرَهُ، فَأُعْطِيَ لَوْنًا حَسَنًا وَجِلْدًا حَسَنًا. قَالَ: فَأَيُّ الْمَالِ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ الإِبِلُ أَوْ الْبَقَرُ (شَكَّ إِسْحَاقُ) ، فَأُعْطِيَ نَاقَةً عُشَرَاءَ وَقَالَ بَارِكَ اللَّهُ لَكَ فِيهَا.

قَالَ: فَأَتَى الأَقْرَعَ فَقَالَ: أَيُّ شَيْءٍ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ: شَعْرٌ حَسَنٌ  وَيَذْهَبُ عَنِّي الَّذِي قَدْ قَذَرَنِي النَّاسُ بِهِ. فَمَسَحَهُ فَذَهَبَ عَنْهُ وَأُعْطِيَ شَعْرًا حَسَنًا. فَقَالَ: أَيُّ الْمَالِ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ: الْبَقَرُ أَوْ الإِبِلُ. فَأُعْطِيَ بَقَرَةً حَامِلاً،  قَالَ: بَارِكَ اللَّهُ لَكَ فِيهَا .

فَأَتَى الأَعْمَى فَقَالَ: أَيُّ شَيْءٍ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ: أَنْ يَرُدَّ اللَّهُ إِلَيَّ بَصَرِي فَأُبْصِرُ بِهِ النَّاسَ، فَمَسَحَهُ فَرَدَّ اللَّهُ إِلَيْهِ بَصَرَهُ، قَالَ: فَأَيُّ الْمَالِ أَحَبُّ إِلَيْكَ؟ قَالَ: الْغَنَمُ، فَأُعْطِيَ شَاةً وَالِدًا، فَأُنْتَجَ هَذَانِ وَوَلَّدَ هَذَا فَكَانَ لِهَذَا وَادٍ مِنَ الإِبِلِ وَلِهَذَا وَادٍ مِنَ الْبَقَرِ وَلِهَذَا وَادٍ مِنَ الْغَنَمِ.

قَالَ: ثُمَّ إِنَّهُ أَتَى الأَبْرَصَ فِي صُورَتِهِ وَهَيْئَتِهِ فَقَالَ: رَجُلٌ مِسْكِينٌ وَابْنُ سَبِيلٍ قَدْ اِنْقَطَعَتْ بِيَ الْحِبَالُ فِي سَفَرِي، فَلا بَلاغَ لِيَ الْيَوْمَ إِلاَّ بِاللَّهِ ثُمَّ بِكَ، أَسْأَلُكَ بِالَّذِي أَعْطَاكَ اللَّوْنَ الْحَسَنَ وَالْجِلْدَ الْحَسَنَ وَالْمَالَ،  بَعِيرًا أَتَبَلَّغُ بِهِ فِي سَفَرِي، فَقَالَ: الْحُقُوقُ كَثِيرَةٌ. فَقَالَ لَهُ كَأَنِّي أَعْرِفُكَ! أَلَمْ تَكُنْ أَبْرَصَ يَقْذَرُكَ النَّاسُ، فَقِيرًا فَأَعْطَاكَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ الْمَالَ؟ فَقَالَ: إِنَّمَا وَرِثْتُ هَذَا الْمَالَ كَابِرًا عَنْ كَابِرٍ. فَقَالَ: إِنْ كُنْتَ كَاذِبًا فَصَيَّرَكَ اللَّهُ إِلَى مَا كُنْتَ.

قَالَ: ثُمَّ إِنَّهُ أَتَى الأَقْرَعَ فِي صُورَتِهِ فَقَالَ لَهُ مِثْلَ مَا قَالَ لِهَذَا، وَرَدَّ عَلَيْهِ مِثْلَ مَا رَدَّ عَلَيْهِ هَذَا، فَقَالَ إِنْ كُنْتَ كَاذِبًا فَصَيَّرَكَ اللَّهُ إِلَى مَا كُنْتَ.

 قَالَ "وَأَتَى الأَعْمَى فِي صُورَتِهِ فَقَالَ: رَجُلٌ مِسْكِينٌ وَابْنُ سَبِيلٍ قَدْ اِنْقَطَعَتْ بِيَ الْحِبَالُ فِي سَفَرِي، فَلا بَلاغَ لِيَ الْيَوْمَ إِلاَّ بِاللَّهِ ثُمَّ بِكَ، أَسْأَلُكَ بالَّذِي رَدَّ عَلَيْكَ بَصَرَكَ، شَاةً أَتَبَلَّغُ بِهَا فِي سَفَرِي. فَقَالَ قَدْ كُنْتُ أَعْمَى فَرَدَّ اللَّهُ إِلَيَّ بَصَرِي، فَخُذْ مَا شِئْتَ وَدَعْ مَا شِئْتَ فَوَاللَّهِ لاَ أَجْهَدُكَ الْيَوْمَ بِشَيْءٍ أَخَذْتَهُ لِلَّهِ. فَقَالَ: أَمْسِكْ مَالَكَ فَإِنَّمَا ابْتُلِيتُمْ،   فَقَدْ رَضِيَ اللَّهُ عَنْكَ وَسَخِطَ عَلَى صَاحِبَيْكَ))

Na Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba kamsikia Rasuli wa Allaah(صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Allaah alitaka kuwajaribu watu watatu katika wana wa Israaiyl; mkoma, kipofu na kipara Akawatumia Malaika. Akamwendea mkoma akamuuliza: “Kitu gani ukipendacho mno?” Akajibu: “Rangi na ngozi nzuri [ya mwili], na uniondokee [ukoma] niliokuwa nao unaowakera watu.” Akasema: [Malaika] Akamgusa ukamuondokea ugonjwa akapewa rangi na ngozi nzuri. Akamuuliza: “Mali ipi upendayo zaidi?” Akajibu: “Ngamia au ng’ombe.” [Msimuliaji Is-haaq hana uhakika ni yupi] Basi mwenye ukoma akapewa ngamia jike mwenye mimba. [Malaika] Akasema [kumuombea]: “Allaah Akubarikie navyo.”

Kisha Malaika akaenda kwa kipara akamuuliza: “Kitu gani ukipendacho mno?” Akajibu: “Nywele nzuri na kiniondokee [kipara] kinachowakera watu.” Akamgusa, kikamuondoka [kipara] akapewa nywele nzuri. Akamuuliza: “Mali ipi upendayo zaidi?” Akajibu: “Ng’ombe au ngamia.” Akapewa ng’ombe jike mwenye mimba. Akasema [kumuombea]: “Allaah Akubarikie navyo.”

Akamwendea kipofu: Akamuuliza: “Kitu gani ukipendacho mno?” Akajibu: “Allaah Anirudishie macho yangu nipate kuwaona watu.” Akamgusa, Allaah Akamrudishia macho yake. Akamuuliza: “Mali ipi uipendayo zaidi”? Akajibu: “Mbuzi.” Akapewa mbuzi mwenye mimba. Baada ya hapo, wanyama wote watatu wakazaa na kuzaliana hadi kwamba kila mmoja alikuwa na bonde la ngamia, na mwengine bonde la ng’ombe na mwengine bonde la mbuzi.

Akasema: Kisha [Malaika] akamrudia mkoma akiwa katika hali kama yake ya mtu mwenye ukoma. Akasema: “Mimi ni masikini, nimekatikiwa na nyenzo zangu safarini, kwa hiyo sina leo wa kunitimizia isipokuwa Allaah kisha wewe. Nakuomba kwa Ambaye Amekupa rangi na ngozi nzuri, na mali, unigawie ngamia ili anifikishe katika safari yangu.” Akajibu: “Nina majukumu mengi [kwa hiyo siwezi kukupa kitu!].” [Malaika] Akasema: “Kana kwamba nakujua? Si wewe uliyekuwa na ukoma wakikereka watu, na ulikuwa masikini kisha Allaah ‘Azza wa Jalla [Aliyetukuka na Utukufu] Akakupa mali [yote hii]?” Akajibu: “[Hapana ni uongo!] Hakika nimerithi yote hayo kwa mababu zangu.” [Malaika] akasema: “Ikiwa unasema uongo, basi Allaah Akurudishe kama ulivyokuwa awali.”

Akamwendea aliyenyonyoka nywele (kipara) akiwa katika hali kama yake ya mtu mwenye kipara. Akamuuliza kama alivyomuuliza huyu [mwenye ukoma], naye akamjibu kama alivyojibu naye. Akamwambia: Ikiwa unasema uongo, basi Allaah Akurudishe kama ulivyokuwa awali. 

Akasema: Akamwendea kipofu akiwa katika hali kama yake ya mtu kipofu. Akamwambia: “Mimi ni masikini na msafiri, nimekatikiwa na nyenzo zangu safarini, kwa hiyo sina leo wa kunitimizia isipokuwa Allaah kisha wewe. Nakuomba kwa Ambaye Amekupa macho yako, unigawie mbuzi ili anifikishe katika safari yangu.” Akajibu: “Bila shaka! Nilikuwa kipofu na Allaah Akanirudishia macho yangu [na nilikuwa masikini Allaah Akanitajirisha]. Chukua utakacho, na acha utakacho, kwani wa-Allaahi sitakuzuia chochote [unachohitaji] kuchukua kwa ajili ya Allaah.” Akasema [kumuombea]: “Weka mali yako, kwani hakika mmejaribiwa, na hakika Allaah Ameridhika nawe na Amewaghadhibikia wenzako”)) [Al-Bukhaariy na Muslim ]  

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Fus-Swilat (41: 50).

 

2-Maana ya: 

لَيَقُولَنَّ هَـٰذَا لِي

((Haya nayastahiki mimi)).

 

3-Maana ya:  

أُوتِيتُهُ عَلَىٰ عِلْمٍ عِندِي ۚ

((Nimepewa haya kwa sababu ya elimu yangu)).

 

4-Mafunzo makubwa katika kisa cha kusisimua.

 

 

 

Share

50-Kitaab At-Tawhiyd: Kuharamishwa Majina Yanayoabudiwa Badala Ya Allaah

Mlango Wa 50

باب: فَلَمَّا آتَاهُمَا صَالِحًا جَعَلَا لَهُ شُرَكَاءَ فِيمَا آتَاهُمَا

Kuharamishwa Majina Yanayoabudiwa Badala Ya Allaah


 

 

قَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

فَلَمَّا آتَاهُمَا صَالِحًا جَعَلَا لَهُ شُرَكَاءَ فِيمَا آتَاهُمَا ۚ فَتَعَالَى اللَّـهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿١٩٠﴾

((Basi Anapowapa (mtoto) mwema asiyekuwa na kasoro, wanamfanyia (Allaah) washirika katika kile Alichowapa. Basi Ametukuka Allaah kwa Uluwa kutokana na yale yote wanayoshirikisha)) [Al-A’raaf (7: 190)]

 

 قَالَ اِبْنُ حَزْمٍ:  اِتَّفَقُوا عَلَى تَحْرِيمِ كُلِّ اِسْمٍ مُعَبَّدٍ لِغَيْرِ اَللَّهِ كَعَبْدِ عَمْرِوٍ وَعَبْدِ الْكَعْبَةِ وَمَا أَشْبَهَ ذَلِكَ، حَاشَا عَبْدِ الْمُطَّلِبِ.

Ibn Hazm amesema: Wamekubaliana (huenda imekusudiwa Ijmaa’ - ’Ulamaa) kuharamisha kila jina linalomaanisha kuabudiwa kinyume na Allaah; mfano ‘Abd-‘Umar (mja wa ‘Umar), ‘Abdul-Ka’bah (mja wa Ka’bah), na kama hivyo isipokuwa ‘Abdul-Muttwalib – hili limeruhusiwa.

 

وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ قَالَ: ((لِمَا تَغَشَّاهَا آدَمُ حَمَلَتْ، فَأَتَاهُمَا إِبْلِيْسُ فَقَالَ: إِنِّي صَاحِبُكُمَا اَلَّذِي أَخْرَجَكُمَا مِنَ الْجَنَّة، لَتُطِيعَانِّنِي أَوْ لأَجْعَلَنَّ لَهُ قَرْنَيْ إِيِّلٍ فَيَخْرُجُ مِنْ بَطْنِكَ فَيَشُقُّهُ وَلأَفْعَلَنَّ - يُخَوِّفُهُمَا - سَمِّيَاهُ عَبْدَ الْحَارِثِ،

 فَأَبَيَا أَنْ يُطِيْعَاهُ فَخَرَجَ مَيِّتًا. ثُمَّ حَمَلَتْ فَأَتَاهُمَا فَذَكَرَ لَهُمَا فَأَدْرَكَهُمَا حُبُّ الْوَلَدِ فَسَمَّيَاهُ عَبْدَ الْحَارِثِ فَذَلِكَ قَولُهُ: ((جَعَلَا لَهُ شُرَكَاءَ فِيمَا آتَاهُمَا))   رَوَاهُ اِبْنُ أَبِي حَاتِمٍ

Na Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas(رضي الله عنهما)  katika kuifafanua Aayah hiyo, amesema: “Aadam alipombashiri Hawaa alishika mimba. Ibliys akawaendea na kusema: “Mimi ndiye mwenzenu niliyekusababisheni kutolewa Jannah. Mtanitii au sivyo nitamfanya mtoto wenu aote pembe mbili kama swala tumboni mwa mama yake ambazo zitapasua tumbo lake wakati wa kumzaa, na hakika nitafanya hivyo!”  Akawatisha - na kusema: “Muiteni ‘Abdul-Haarith” (mja wa mkulima). Lakini walikataa kumtii, akazaliwa mtoto akiwa amekufa. Kisha Hawaa aliposhika mimba mara ya pili, Ibliys akawaendea tena akakariri kauli yake (kuwataka wafanye vile na kuwatisha). Wakakataa tena kumtii. Akazaliwa mtoto akiwa amekufa. Kisha Hawaa akashika mimba tena, Ibliys akawaendea akawakumbusha yaliyotokea awali, wakajazwa mapenzi ya mtoto na wakamwita mtoto ‘Abdul-Haarith. Na hivyo ndio maana ya kauli ya Allaah: ((wanamfanyia (Allaah) washirika katika kile Alichowapa))

 

وَلَهُ بِسَنَدٍ صَحِيْحٍ عَنْ قَتَادَة:  قَالَ: شُرَكَاءُ فِي طَاعَتِهِ وَلَمْ يَكُنْ فِي عِبَادَتِهِ

Naye (Ibn Haatim) amepokea kwa isnaad Swahiyh kutoka kwa Qataadah: Amesema: “Washirika katika kumtii Kwake, na si katika kumwabudu kinyume Naye.”

 

وَلَهُ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ عَنْ مُجَاهِدٍ فِي قَوْلِهِ ((لَئِنْ آتَيْتَنَا صَالِحًا))  قَالَ: أَشْفَقَا أَلاَّ يَكُونَ إِنْسَانًا. وَذَكَرَ مَعْنَاهُ عَنْ الْحَسَنِ وَسَعِيدٍ وَغَيْرِهِمَا.

Naye (Ibn Haatim) amesimulia kutoka kwa Mujaahid kuhusu kauli Yake Allaah: ((Ukitupa (mtoto) mwema asiyekuwa na kasoro)) [Al-A’raaf (7:189)] Amesema: (Aadam na Hawaa) waliogopa mtoto asije kuwa si bin Aadam.  Maana kama hiyo imetajwa na Hasan, Sa’iyd na wengineo.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Jina lolote lenye maana ya kumwabudu asiye Allaah (سبحانه وتعالى) limeharamishwa.

 

2-Tafsiri ya Aayah katika Suwrah Al-A’raaf (7: 189).

 

3-Shirki hii inahusiana katika kulipa jina tu japokuwa haikukusudiwa maana yake, yaani kuabudiwa huyo mtoto. 

 

4-Neema kubwa ya Allaah (سبحانه وتعالى) kumruzuku mtu mtoto mwema kamili asiye na kasoro. 

5-As-Salaf wametofautisha baina ya shirki katika kutii na shirki katika kuabudu.   

 

 

Share

51-Kitaab At-Tawhiyd: Majina Mazuri Kabisa Ni Ya Allaah Basi Muombeni Kwayo

Mlango Wa 51

باب: وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ

Majina Mazuri Kabisa Ni Ya Allaah Basi Muombeni Kwayo


 

 

قَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ  

((Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanamili katika kukadhibisha Majina Yake)) [Al-A’raaf (7: 180)]

 

ذَكَرَ اِبْنُ أَبِي حَاتِمٍ عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ: ((يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ)): يُشْرِكُونَ.

Ibn Haatim ametaja kwamba Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema kuhusu: ((Wanamili katika kukadhibisha Majina Yake)) yaani: wanafanya shirki.

وَعَنْهُ: سَمُّوا اَللاَّتَ مِنَ الإِلَهِ وَالْعُزَّى مِنَ الْعَزِيزِ.

Na kasema pia: “Wamewaita Al-Laata – kutokana na ‘Ilaah’. Na Al-Uzzah kutokana na ‘Al-‘Aziyz’.

 

وَعَنِ الأَعْمَشِ: يُدْخِلُونَ فِيهَا مَا لَيْسَ مِنْهَا

Na Al-A’mash kasema: “Wanaingiza humo (katika Majina ya Allaah, Majina) yasiyokuwemo.”

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuthibitisha Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Alivyosema (Al-A’raaf 7: 180).

 

2-Majina yote ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni mazuri.

 

3-Maamrisho ya kumuomba Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Majina Yake Mazuri.

 

4-Amri ya kuepukana na majahili na wakanushaji.   

 

5-Maelezo ya wanavyopotoa na kuharibu Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

6-Adhabu imeahidiwa kwa wapotoshaji Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

Share

52-Kitaab At-Tawhiyd: Haisemwi “Assalaamu ‘Ala-Allaah”

Mlango Wa 52

بَابٌ لَا يُقَالُ اَلسَّلَامُ عَلَى اَللَّهِ

Haisemwi “Assalaamu ‘Ala-Allaah”


 

 

فِي اَلصَّحِيحِ: عَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ:  كُنَّا إِذَا كُنَّا مَعَ اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)  فِي اَلصَّلاةِ، قُلْنَا اَلسَّلامُ عَلَى اَللَّهِ مِنْ عِبَادِهِ اَلسَّلام عَلَى فُلانٍ وَفُلان. فَقَالَ اَلنَّبِيُّ  (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لاَ تَقُولُوا اَلسَّلام عَلَى اَللَّهِ، فَإِنَّ اَللَّهَ هُوَ اَلسَّلامُ))

Katika Swahiyh (Al-Bukhaariy na Muslim) kutoka kwa Ibn Mas’uwd amesema: Kila tulipokuwa tunaswali nyuma ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) tulikuwa tukisema: “Assalaamu ‘ala-Allaahi min ‘ibaadihi (amani ziwe juu ya Allaah kutoka kwa waja Wake) Assalaamu ‘alaa fulaanin wa fulaan (Amani zimfikie fulani na fulani) Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Msiseme Assalaamun ‘ala-Allaah, kwani Allaah Mwenyewe ni As-Salaam))  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Maelezo ya As-Salaam (amani).

 

2-As-Salaam ni maamkizi.

 

3-Si vyema kutumia As-Salaam kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

4-Sababu kuwa Allaah (سبحانه وتعالى) Mwenyewe ni As-Salaam.

 

5-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliwafundisha Maswahaba (رضي الله عنهم) kuomba du’aa ipasavyo kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

Share

53-Kitaab At-Tawhiyd: Kusema: Allaahumma Nighufurie Ukitaka

Mlango Wa 53

بَابٌ قَوْلُ اَللَّهُمَّ اِغْفِرْ لِي إِنْ شِئْتَ

Kusema: Allaahumma Nighufurie Ukitaka


 

 

 

فِي اَلصَّحِيحِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ : أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ): ((لا! يَقُلْ أَحَدُكُمْ: اَللَّهُمَّ اِغْفِرْ لِي إِنْ شِئْتَ، اَللَّهُمَّ اِرْحَمْنِي إِنْ شِئْتَ، لِيَعْزِمِ الْمَسْأَلَةَ، فَإِنَّ اَللَّهَ لاَ مُكْرِهَ لَهُ))

Katika Swahiyh (Al-Bukhaariy) kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Asiseme mmoja wenu: Ee Allaah nighufurie Ukitaka. Ee Allaah Nirehemu Ukitaka, bali aazimie [kumuomba] kwani hakuna wa kumlazimisha Allaah kufanya jambo dhidi ya Idhini Yake)) [Al-Bukhaariy]

 

ولِمُسْلِمٍ : ((وَلْيُعَظِّمْ اَلرَّغْبَةَ فَإِنَّ اَللَّهَ لاَ يَتَعَاظَمُهُ شَيْءٌ أَعْطَاه))

Na katika Muslim: ((Bali akuze shauku yake kwani Allaah Halioni kubwa mno jambo Alilolitoa)) [Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Kukatazwa kufanya istithnaa (kuweka masharti) katika du’aa.

 

2-Maelezo na sababu ya ubaya wa kusema ‘Ukitaka'.

 

3-Kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba aombe kwa azma na raghba, 

 

4-Omba chochote upendacho kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

5-Sababu yake (kwani hakuna limshindalo).

 

 

 

Share

54-Kitaab At-Tawhiyd: Asiseme Mtu “Mja Wangu”, “Mjakazi Wangu”

Mlango Wa 54

بَابٌ لا يَقُولُ عَبْدِي وَأَمَتِي

Asiseme Mtu “Mja Wangu”, “Mjakazi Wangu


 

 

فِي اَلصَّحِيحِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((لاَ يَقُلْ أَحَدُكُمْ: أَطْعِمْ رَبَّكَ وَضِّئْ رَبَّكَ وَلْيَقُلْ سَيِّدِي وَمَوْلايَ وَلا يَقُلْ أَحَدُكُمْ: عَبْدِي وَأَمَتِي، وَلْيَقُلْ فَتَايَ وَفَتَاتِي َغُلامِي))

Katika Swahiyh (Al-Bukhaariy) kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Asiseme mmoja wenu: Mlishe Rabbaka [Rabb wako]. Mtawadhishe Rabbaka, bali aseme: Sayyidiy au Mawlaayi [Bwana wangu][1] Na asiseme mtu: ‘Abdiy au Amatiy [mjakazi wangu], bali aseme: Fataay, na Fataatiy [kijana wangu] na ghulaamiy [mvulana wangu])) [Al-Bukhaariy]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Kukatazwa kusema: "Mtumwa wangu" au "mjakazi wangu.”

 

2-Mtumwa asiseme: "Rabb wangu” wala asiambiwe: "Mlishe Rabb wako.”

 

3-Kumfundisha bwana aseme badala ya hayo: "kijana wangu” “ee bint”, “ee mvulana”

 

4-Kumfundisha mtumwa kusema badala ya hayo: “sayyidiy” au “bwana wangu.”

 

5-La muhimu hapa ni kufafanua Tawhiyd kwa ukamilifu, hata kama ni katika maneno, majina na istilahi.

 

 

 

 

[1] Mfano aseme mtu: Mlishe bwana wako badala ya kutaja Rabbaka n.k.

 

 

 

Share

55-Kitaab At-Tawhiyd: Anayeomba kwa Jina la Allaah Hakataliwi

Mlango Wa 55

بَابٌ لا يُرَدُّ مَنْ سَأَلَ بِاَللَّهَ

Anayeomba kwa Jina la Allaah Hakataliwi


 

 

عَنِ اِبْنِ عُمَرَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((مَنْ سَأَلَ بِاَللَّهِ فَأَعْطُوهُ، وَمَنِ اسْتَعَاذَ بِاَللَّهِ فَأَعِيذُوهُ، وَمَنْ دَعَاكُمْ فَأَجِيبُوهُ، وَمَنْ صَنَعَ إِلَيْكُمْ مَعْرُوفًا فَكَافِئُوهُ، فَإِنْ لَمْ تَجِدُوا مَا تُكَافِئُونَهُ فَادْعُوا لَهُ حَتَّى تَرَوْا أَنَّكُمْ قَدْ كَافَأْتُمُوهُ))  رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَالنَّسَائِيُّ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayeomba kwa Jina la Allaah, mpeni. Na atakayejikinga kwa Jina la Allaah, mkingeni. Na atakayekualikeni muitikieni. Na atakayekufanyieni wema mlipeni [mema na ihsani]. Msipopata cha kumlipa muombeeni hadi mhisi kuwa mmelipizia wema)) [Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy kwa isnaad Swahiyh]

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kumpa ulinzi atakayeomba ulinzi kwa Jina la Allaah (سبحانه وتعالى).

 

2-Kumpa aombaye kwa Jina la Allaah (سبحانه وتعالى).

 

3-Kuitikia mwaliko.

 

4-Kumlipa wema aliyekutendea wema.

 

5-Ikiwa mtu hana cha kulipa wema, basi amuombee du’aa badala yake.

 

6-Kauli yake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((hadi mhisi kuwa mmelipizia wema)).

 

 

Share

56-Kitaab At-Tawhiyd: Kisiombwe Chochote Kwa Wajihi Wa Allaah Isipokuwa Jannah

Mlango Wa 56

بَابٌ لا يُسْأَلُ بِوَجْهِ اَللَّهِ إِلاَّ الْجَنَّةُ

Kisiombwe Chochote Kwa Wajihi Wa Allaah Isipokuwa Jannah


 

 

عَنْ جَابِرٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((لاَ يُسْأَلُ بِوَجْهِ اَللَّهِ إِلاَّ الْجَنَّةُ))  رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kisiombwe chochote kwa Wajihi wa Allaah isipokuwa Jannah)) [Abuu Daawuwd]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Makatazo ya kuomba kitu kwa Wajihi wa Allaah (سبحانه وتعالى) isipokuwa Jannah ambayo jambo kuu kabisa. 

 

2-Kuthibitisha Sifa ya Allaah (سبحانه وتعالى) kuwa Ana Wajihi.

 

 

 

Share

57-Kitaab At-Tawhiyd: Kusema: “Lau Isingekuwa Kadhaa Wa Kadhaa”

Mlango Wa 57

بَابٌ مَا جَاءَ فِي الّلو

Kusema: “Lau Isingekuwa Kadhaa Wa Kadhaa”


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

يَقُولُونَ لَوْ كَانَ لَنَا مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ مَّا قُتِلْنَا هَاهُنَا ۗ قُل لَّوْ كُنتُمْ فِي بُيُوتِكُمْ لَبَرَزَ الَّذِينَ كُتِبَ عَلَيْهِمُ الْقَتْلُ إِلَىٰ مَضَاجِعِهِمْ ۖ وَلِيَبْتَلِيَ اللَّـهُ مَا فِي صُدُورِكُمْ وَلِيُمَحِّصَ مَا فِي قُلُوبِكُمْ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿١٥٤﴾

((Wanasema: “Lau tungelikuwa tuna amri yoyote katika jambo basi tusingeliuliwa hapa.”  Sema: “Lau mngelikuwa majumbani mwenu, bila shaka wangejitokeza wale walioandikiwa kuuwawa kwenye mahali pa kuangukia wafe.” Ili Allaah Ayajaribu yale yaliyomo katika vifua vyenu na Atakase yale yaliyomo katika nyoyo zenu. Na Allaah ni Mjuzi kwa yaliyomo vifuani)) [Aal-‘Imraan (3: 154)]

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

 

الَّذِينَ قَالُوا لِإِخْوَانِهِمْ وَقَعَدُوا لَوْ أَطَاعُونَا مَا قُتِلُوا ۗ قُلْ فَادْرَءُوا عَنْ أَنفُسِكُمُ الْمَوْتَ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿١٦٨﴾ 

((Wale waliowaambia ndugu zao nao wakakaa (wasiende vitani): “Lau wangelitutii basi wasingeliuawa.” Sema: “Basi ziondoleeni nafsi zenu mauti mkiwa ni wakweli”)) [Aal-‘Imraan (3: 168)]

 

وَفِي اَلصَّحِيحِ عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((اِحْرِصْ عَلَى مَا يَنْفَعُكَ، وَاسْتَعِنْ بِاَللَّهِ وَلا تَعْجَزَنْ، وَإِنْ أَصَابَكَ شَيْءٌ فَلا تَقُلْ: لَوْ أَنِّي فَعَلْتُ كَذَا لَكَانَ كَذَا وَكَذَا وَلَكِنْ قُلْ: قَدَّرَ اَللَّهُ وَمَا شَاءَ فَعَلَ.  فَإِنَّ (لَوْ) تَفْتَحُ عَمَلَ اَلشَّيْطَانِ))

Na katika Swahiyh [Muslim] Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Pupia [kutafuta] yanayokunufaisha na omba msaada kwa Allaah Pekee na usivunjike moyo. Na linapokufika jambo usiseme: ‘Lau kama ningelifanya kadhaa, ingelikuwa kadhaa wa kadhaa’. Bali sema: ‘Qadara-Allaahu wa Maa Shaa Fa’al’ – Amekadiria Allaah na Amefanya Alichotaka - kwani [neno la] ‘lau’ linafungua ‘amali ya shaytwaan)) [Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Tafsiri ya Aayah mbili Suwrah Aal-'Imraan (3: 154 na 3: 168).

 

2-Kukatazwa waziwazi kusema: “Lau” unapopatwa na jambo.  

 

3-Sababu kufanya hivyo kunafungua njia ya ‘amali za shaytwaan.

 

4-Mwongozo wa mawazo na matamshi mazuri.

 

5-Himizo la kufanya ‘amali njema zenye manufaa (Aakhirah) na wakati huohuo kuomba msaada kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى).

 

6-Kufanya kinyume chake (yaani kutokutafuta manufaa yenye manufaa na kutaka msaada kutoka kwa asiyekuwa Allaah (سبحانه وتعالى) kumekatazwa, na hivyo ni ajizi. 

 

 

 

Share

58-Kitaab At-Tawhiyd: Makatazo Ya Kutukana Upepo

Mlango Wa 58

بَابٌ اَلنَّهْيُ عَنْ سَبِّ اَلرِّيحِ

Makatazo Ya Kutukana Upepo


 

 

عَنْ أُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)  قَالَ ((لاَ  تَسُبُّوا اَلرِّيحَ، فَإِذَا رَأَيْتُمْ مَا تَكْرَهُونَ فَقُولُوا: اَللَّهُمَّ إِنَّا نَسْأَلُكَ مِنْ خَيْرِ هَذِهِ اَلرِّيحِ وَخَيْرِ مَا فِيهَا وَخَيْرِ مَا أُمِرَتْ بِهِ، وَنَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ هَذِهِ اَلرِّيحِ وَشَرِّ مَا فِيهَا وَشَرِّ مَا أُمِرَتْ بِه))  صَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ

Na Imepokelewa kutoka kwa Ubayy bin Ka’b (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Msitukane upepo. Mtakapoona mnalochukia semeni: “Allaahumma Nas-aluka min khayri haadhihir-riyh wa khayri maa fiyhaa, wa khayri maa umirat bihi. Wa na’uwdhu Bika min sharri haadhihir-riyh wa sharri maa fiyhaa wa sharri maa umirat bih – Ee Allaah tunakuomba khayr za upepo huu na khayr zilokuwemo ndani yake, na khayr ya vile ulioamrishwa kuvileta. Na Tunajikinga Kwako na shari za upepo huu, na shari zilokuwemo ndani yake na shari ya vile ulivyoamrishwa kuvileta”)) [At-Tirmidhiy ameikiri ni Swahiyh]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Kulaani (au kutukana) upepo kumekatazwa.

 

2-Mwongozo wa du’aa ya manufaa pindi mtu anapoona asiyoyapenda.

 

3-Upepo unakwenda kwa amri ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

4-Upepo unaweza kuamrishwa na Allaah (سبحانه وتعالى) kuleta manufaa au madhara.

 

 

Share

59-Kitaab At-Tawhiyd: Haijuzu Kumwekea Allaah Dhana Mbaya

Mlango Wa 59

باب: يَظُنُّونَ بِاللَّـهِ غَيْرَ الْحَقِّ ظَنَّ الْجَاهِلِيَّةِ...

Haijuzu Kumwekea Allaah Dhana Mbaya


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

يَظُنُّونَ بِاللَّـهِ غَيْرَ الْحَقِّ ظَنَّ الْجَاهِلِيَّةِ ۖ يَقُولُونَ هَل لَّنَا مِنَ الْأَمْرِ مِن شَيْءٍ ۗ قُلْ إِنَّ الْأَمْرَ كُلَّهُ لِلَّـهِ ۗ يُخْفُونَ فِي أَنفُسِهِم مَّا لَا يُبْدُونَ لَكَ ۖ يَقُولُونَ لَوْ كَانَ لَنَا مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ مَّا قُتِلْنَا هَاهُنَا ۗ قُل لَّوْ كُنتُمْ فِي بُيُوتِكُمْ لَبَرَزَ الَّذِينَ كُتِبَ عَلَيْهِمُ الْقَتْلُ إِلَىٰ مَضَاجِعِهِمْ ۖ وَلِيَبْتَلِيَ اللَّـهُ مَا فِي صُدُورِكُمْ وَلِيُمَحِّصَ مَا فِي قُلُوبِكُمْ ۗ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿١٥٤﴾

((Wakamdhania Allaah pasi na haki dhana ya kijahili; wanasema: “Je, tuna amri yoyote sisi katika jambo hili?”  Sema: “Hakika amri yote ni ya Allaah.” Wanaficha katika nafsi zao yale wasiyokubainishia. Wanasema: “Lau tungelikuwa tuna amri yoyote katika jambo basi tusingeliuliwa hapa.”  Sema: “Lau mngelikuwa majumbani mwenu, bila shaka wangejitokeza wale walioandikiwa kuuwawa kwenye mahali pa kuangukia wafe.” Ili Allaah Ayajaribu yale yaliyomo katika vifua vyenu na Atakase yale yaliyomo katika nyoyo zenu. Na Allaah ni Mjuzi kwa yaliyomo vifuani)) [Aal-‘Imraan (3: 154)]

 

وَقَوْلُهُ:

Na kauli Yake:

 

الظَّانِّينَ بِاللَّـهِ ظَنَّ السَّوْءِ ۚ عَلَيْهِمْ دَائِرَةُ السَّوْءِ ۖ وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ وَلَعَنَهُمْ وَأَعَدَّ لَهُمْ جَهَنَّمَ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٦﴾

((Wanaomdhania Allaah dhana ovu.  Utawafikia mgeuko mbaya; na Allaah Awaghadhibikie, na Awalaani, na Awaandalie Jahannam, na paovu palioje mahali pa kuishia)) [Al-Fat-h (48: 6)]

 

 قَالَ اِبْنُ الْقَيِّمِ فِي الآيَةِ الأُولَى: فُسِّرَ هَذَا اَلظَّنُّ بِأَنَّهُ سُبْحَانَهُ لاَ يَنْصُرُ رَسُولَهُ وَأَنَّ أَمْرَهُ سَيَضْمَحِلُّ وَفُسِّرَ بِأَنَّ مَا أَصَابَهُ لَمْ يَكُنْ بِقَدَرِ اَللَّهِ وَحِكْمَتِهِ.  فَفُسِّرَ بِإِنْكَارِ الْحِكْمَةِ وَإِنْكَارِ الْقَدَرِ وَإِنْكَارٍ أَنْ يُتِمَّ أَمْرَ رَسُولِهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) وَأَنْ يُظْهِرَهُ عَلَى اَلدِّينِ كُلِّه.

Ibn Al-Qayyim amesema kuhusu Aayah ya kwanza: “Dhana za kijahili ni kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Hatomnusuru Rasuli Wake, na kwamba ujumbe Wake utashindwa na kutoweka. Dhana za kijahili pia ina maana misiba iliyompata Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) haikumpata kutokana na Qadar na hikmah ya Allaah (سبحانه وتعالى). Kwa hiyo dhana kama hizo zinapeleka kukanusha Qadar na hikmah ya Allaah (سبحانه وتعالى) na kutotarajia kwamba Ujumbe wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ungekamilika na ungezishinda dini zengine zote.

 

 وَهَذَا هُوَ ظَنُّ اَلسَّوْءِ اَلَّذِي ظَنَّهُ الْمُنَافِقُونَ وَالْمُشْرِكُونَ فِي سُورَةِ الْفَتْحِ.  وَإِنَّمَا كَانَ هَذَا ظَنُّ اَلسُّوءِ لأَنَّهُ ظَنُّ غَيْرِ مَا يَلِيقُ بِهِ سُبْحَانَهُ وَمَا يَلِيقُ بِحِكْمَتِهِ وَحَمْدِهِ وَوَعْدِهِ اَلصَّادِقِ .

Hizo ndizo dhana mbaya za wanafiki na washirikina waliotajwa katika Suwrah Al-Fat-h kuwa ni ‘suw-udh-dhwann’ (dhana mbaya), na dhana mbaya haistahiki kwa Allaah (سبحانه وتعالى) Aliyetakasika na kila ovu na Mwenye Sifa zote za ukamilifu. Wala haistahiki katika hikmah Yake na kuhimidiwa Kwake wala ahadi Yake ya kweli.

 

فَمَنْ ظَنَّ أَنَّهُ يُدِيلُ الْبَاطِلَ عَلَى الْحَقِّ إِدَالَةً مُسْتَقِرَّةً يَضْمَحِلُّ مَعَهَا الْحَقُّ أَوْ أَنْكَرَ أَنَّ مَا جَرَى بِقَضَائِهِ وَقَدَرِهِ أَوْ أَنْكَرَ أَنْ يَكُونَ قَدَرُهُ لِحِكْمَةٍ بَالِغَةٍ يَسْتَحِقُّ عَلَيْهَا الْحَمْدَ بَلْ زَعَمَ أَنَّ ذَلِكَ لِمَشِيئَةٍ مُجَرَّدَةٍ: فَ ((ذَٰلِكَ ظَنُّ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِنَ النَّارِ))

Basi atakayedhania kwamba ubatilifu (shirki, kufru, shaytwaan na upotofu wote) utashinda na kuendelea dhidi ya haki (Uislamu, Tawhiyd n.k.), au akakanusha kwamba mambo hutokea kwa Qadhwaa na Qadar (Yaliyohukumiwa na Yaliyokadiriwa), au akakanusha kwamba Ameyakadiria kwa hikmah kubwa inayostahiki kusifiwa (na kushukuriwa), au akadai kwamba hayo hutokea kwa sudfa tu, basi ((Hiyo ndio dhana ya wale waliokufuru. Basi ole wale waliokufuru kwa moto utakaowapata)) [Swaad (38: 27)]

 

 وَأَكْثَرُ اَلنَّاسِ يَظُنُّونَ بِاَللَّهِ ظَنَّ اَلسَّوْءِ فِيمَا يَخْتَصُّ بِهِمْ وَفِيمَا يَفْعَلُهُ بِغَيْرِهِمْ وَلاَ يَسْلَمُ مِنْ ذَلِكَ إِلاَّ مَنْ عَرَفَ اَللَّهَ وَأَسْمَاءَه وَصِفَاتِهِ وَمُوجَبَ حِكْمَتِهِ وَحَمْدِهِ.

Na watu wengi wanamdhania Allaah dhana mbaya katika yanayowasibu wao wenyewe na yanayowasibu wengine. Hakuna anayesalimika na hayo isipokuwa ambaye amemtambua Allaah kwa Majina Yake Mazuri na Sifa Zake, na mujibu wa hikmah Zake na kuhimidiwa Kwake.

 

فَلْيَعْتَنِ اَللَّبِيبُ اَلنَّاصِحُ لِنَفْسِهِ بِهَذَا وَلْيَتُبْ إِلَى اَللَّهِ وَلْيَسْتَغْفِرْهُ مِنْ ظَنِّهِ بِرَبِّهِ ظَنَّ اَلسَّوْءِ.

Basi mwenye akili na busara achunguze nafsi yake katika mas-alah haya, na atubie kwa Allaah, na aombe maghfirah kutokana dhana mbaya kuhusu Rabb wake.

 

وَلَوْ فَتَّشْتَ مَنْ فَتَّشْتَّ لَرَأَيْتُ عِنْدَهُ تَعَنُّتًا عَلَى الْقَدَرِ وَمَلَامَةً لَهُ وَأَنَّهُ كَانَ يَنْبَغِي أَنْ يَكُونَ كَذَا وَكَذَا  فَمُسْتَقِلٌّ وَمُسْتَكْثِرٌ.

Lau kama ungelichunguza (mtu kama huyo) ungemwona yuko katika ushupavu na ameudhika kuhusu Qadar ya Allaah (سبحانه وتعالى) akilaumu na kuinasibisha na makosa akiwaza kuwa: “Bora ingelikuwa kadhaa wa kadhaa.” Katika mtihani huu wako walioathirika kidogo na wengine kwa kuzidi mipaka.

 

وَفَتِّشْ نَفْسَكَ هَلْ أَنْتَ سَالِمٌ؟ فَإِنْ تَنْجُ مِنْهَا تَنْجُ مِنْ ذِي عَظِيمَةٍ وَإِلاَّ فَإِنِّي لاَ إِخَالُكَ نَاجِيًا

Chunguza nafsi yako. Je, wewe umesalimika na dhana mbaya kama hizo? Ikiwa umesalimika, basi umenusurika na balaa kubwa, laa sivyo basi hakika sidhanii kama umeokoka.

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Tafsiri ya Aayah Suwrah Aal-‘Imraan (3: 154).

 

2-Tafsiri ya Aayah Suwrah Al-Fat-h (48: 6).

 

3-Tambua kuwa dhana mbaya kwa Allaah (سبحانه وتعالى) ni aina nyingi.

 

4-Anayetambua (maana halisi ya) Majina na Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) ndiye pekee aliyesalimika na dhana mbaya kuhusu Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

Share

60-Kitaab At-Tawhiyd: Wanaokanusha Al-Qadar (Kudura Ya Allaah)

Mlango Wa 60

بَابٌ مَا جَاءَ فِي مُنْكِرِي الْقَدَرِ

Wanaokanusha Al-Qadar (Kudura Ya Allaah)


 

وَقَالَ اِبْنُ عُمَرَ: وَاَلَّذِي نَفْسُ اِبْنِ عُمَرَ بِيَدِهِ ، لَوْ كَانَ لأَحَدِهِمْ مِثْلُ أُحُدٍ ذَهَبًا ثُمَّ أَنْفَقَهُ فِي سَبِيلِ اَللَّهِ، مَا قَبِلَهُ اَللَّهُ مِنْهُ حَتَّى يُؤْمِنَ بِالْقَدَرِ. ثُمَّ اِسْتَدَلَّ بِقَوْلِ اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((الإِيمَانُ: أَنْ تُؤْمِنَ بِاَللَّهِ وَمَلائِكَتِهِ وَكُتُبِهِ وَرُسُلِهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ وَتُؤْمِنَ بِالْقَدَرِ خَيْرِهِ وَشَرِّهِ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ .

Na Ibn ‘Umar amesema: “Naapa kwa Ambaye nafsi ya Ibn ‘Umar imo Mkononi Mwake! Lau mmoja wenu angekuwa na dhahabu mfano wa jabali la Uhud, kisha akaitoa katika njia ya Allaah, basi Allaah Asingeipokea mpaka iwe ameamini Qadar (Makadirio ya Allaah)” Kisha akatoa dalili kwa kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Iymaan ni kumwamini Allaah, na Malaika Wake, na Vitabu Vyake, na Mitume Wake, Na Siku ya mwisho, na kuamini Qadar khayr yake na shari yake)) [Muslim]

 

وَعَنْ عُبَادَةَ بنِ اَلصَّامِتِ: أَنَّهُ قَالَ لابْنِهِ: يَا بُنَيَّ إِنَّكَ لَنْ تَجِدَ طَعْمَ الإِيمَانِ حَتَّى تَعْلَمَ أَنَّ مَا أَصَابَكَ لَمْ يَكُنْ لِيُخْطِئَكَ، وَمَا أَخْطَأَكَ لَمْ يَكُنْ لِيُصِيبَكَ. سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  يَقُولُ: ((إِنَّ أَوَّلَ مَا خَلَقَ اَللَّهُ الْقَلَمَ، فَقَالَ لَهُ: اُكْتُبْ!  فَقَالَ: رَبِّ وَمَاذَا أَكْتُبُ؟ قَالَ: اُكْتُبْ مَقَادِيرَ كُلِّ شَيْءٍ حَتَّى تَقُومَ اَلسَّاعَةُ)) يَا بُنَيَّ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ:  ((مَنْ مَاتَ عَلَى غَيْرِ هَذَا فَلَيْسَ مِنِّي))

Na Imepokelewa kutoka kwa ‘Ubaadah bin Swaamit kwamba amemwambia mwanawe: “Ee mwanangu! Hakika hutapata ladha ya iymaan mpaka utambue kwamba kilichokusibu kisingekukosa, na kilichokukosa kisingekupata; Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kitu cha mwanzo Allaah kuumba ni kalamu. Kisha Akaiambia: Andika! [Kalamu] ikasema: “Rabb wangu, niandike nini?” Akasema: Andika makadirio ya kila kitu mpaka siku itakayosimama Saa [Qiyaamah])). Ee mwanangu! Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Atakayefariki kinyume na haya, basi si miongoni mwangu)).

 

وَفِي رِوَايَةٍ لأَحْمَدَ: ((إِنَّ أَوَّلَ مَا خَلَقَ اَللَّهُ تَعَالَى الْقَلَمَ فَقَالَ لَهُ:  اُكْتُبْ! فَجَرَى فِي تِلْكَ اَلسَّاعَةِ بِمَا هُوَ كَائِنٌ إِلَى يَوْمِ الْقِيَامَةِ))   

Na katika riwaayah ya Imaam Ahmad: ((Kitu cha mwanzo Allaah kukiumba ni kalamu. Akaiambia: Andika! Na katika saa hiyo, [yakaandikwa] yote yatakayotokea mpaka Siku ya Qiyaamah))

 

وَفِي رِوَايَةٍ لابْنِ وَهْبٍ قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم): ((فَمَنْ لَمْ يُؤْمِنْ بِالْقَدَرِ خَيْرِهِ وَشَرِّهِ أَحْرَقَهُ اَللَّهُ بِالنَّار))

Na katika riwaayah ya Ibn Wahb amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Basi asiyeamini Qadar; khayr zake na shari zake, Allaah Atamuunguza motoni))

 

وَفِي الْمُسْنَدِ  وَ اَلسُّنَنِ عَنِ ابْنِ الدَّيْلَمِيِّ: قَالَ: أَتَيْتُ أُبَيَّ بْنَ كَعْبٍ، فَقُلْتُ فِي نَفْسِي شَيْءٌ مِنَ الْقَدَرِ. فَحَدِّثْنِي بِشَيْءٍ لَعَلَّ اَللَّهَ يُذْهِبُهُ مِنْ قَلْبِي، فَقَالَ: لَوْ أَنْفَقْتَ مِثْلَ أُحُدٍ ذَهَبًا مَا قَبِلَهُ اَللَّهُ مِنْكَ حَتَّى تُؤْمِنَ بِالْقَدَرِ، وَتَعْلَمَ أَنَّ مَا أَصَابَكَ لَمْ يَكُنْ لِيُخْطِئَكَ وَمَا أَخْطَأَكَ لَمْ يَكُنْ لِيُصِيبَكَ، وَلَوْ مِتَّ عَلَى غَيْرِ هَذَا، لَكُنْتَ مِنْ أَهْلِ اَلنَّارِ. قَالَ: فَأَتَيْتُ عَبْدَ اَللَّهِ بْنَ مَسْعُودٍ وَحُذَيْفَةَ بْنَ الْيَمَانِ وَزَيْدَ بْنَ ثَابِتٍ فَكُلُّهُمْ حَدَّثَنِي بِمِثْلِ ذَلِكَ عَنْ اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) حَدِيثٌ صَحِيحٌ رَوَاهُ الْحَاكِمُ فِي "صَحِيحِهِ

Na imenukuliwa katika Musnad ya Ahmad na Sunan Abiy Daawuwd kutoka kwa Ibn Ad-Daylamiyy amesema: Nilimwendea Ubayy bin Ka’b nikasema: “Nina kitu (shaka)] katika nafsi yangu kuhusu Qadar. Nihadithie chochote huenda Allaah Ataiondosha (shaka) moyoni mwangu.” Akasema: “Lau kama utatoa dhahabu mfano wa jabali la Uhud, Allaah Hatoikubali kwako mpaka uamini Qadr, na  utambue kwamba kilichokusibu kisingekukosa na kilichokukosa kisingekupata. Na lau ukifariki kinyume chake, bila shaka utakuwa miongoni mwa watu wa motoni” Akasema: “Nikamwendea ‘Abdullaahi bin Mas’uwd, Hudhayfah bin Al-Yamaani na Zayd bin Thaabit, na wote wakanihadithia kama hivyo alivyosema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)” [Hadiyth Swahiyh ameipokea Al-Haakim katika Swahiyh yake]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Maelezo ya wajibu wa kuamini Al-Qadar.

 

2- Maelezo ya maana ya kuiamini.

 

3-Kubatilika ‘amali za asiyeiamini.

 

4-Hakuna atakayepata ladha ya iymaan isipokuwa mpaka aamini Al-Qadar.

 

5-Kutajwa kilichoumbwa kwanza na Allaah (سبحانه وتعالى).

 

6-Kalamu imeshaandika yote yatakayokuja mpaka Siku ya Mwisho.

 

7-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kumkataa yeyote asiyeamini Al-Qadar.

 

8-Tabia ya As-Salaf kuwauliza wenye ujuzi kuhusu yale wasiyo na hakika nayo ili kuondoa shaka.

 

9- Wanachuoni Waislamu walijibu majibu yaliyoondoa shaka zote kuhusu Qadar kwa kunukuu kauli za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

 

Share

61-Kitaab At-Tawhiyd: Wachoraji Picha Za Viumbe Wachongaji Masanamu Vinyago n.k.

Mlango Wa 61

بَابٌ مَا جَاءَ فِي الْمُصَوِّرِينَ

Wachoraji Picha Za Viumbe Wachongaji Masanamu Vinyago n.k.


 

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((قَالَ اللهُ تَعَالَى: وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّنْ ذَهَبَ يَخْلُقُ كَخَلْقِي؛ فَلْيَخْلُقُوا ذَرَّةً، أَوْ لِيَخْلُقُوا حَبَّةً، أَوْ لِيَخْلُقُوا شَعِيْرَةً ))  أَخْرَجَاهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Allaah Aliyetukuka Amesema: Nani dhalimu zaidi kuliko anayejaribu kuumba kama kuumba Kwangu? Basi na waumbe chembe moja au waumbe punje ya nafaka, au waumbe chembe ya shayiri)) [Al-Bukhaariy na Muslim]  

 

وَلَهُمَا عَنْ عَائِشَةَ (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) قَال: ((أَشَدُّ النَّاسِ عَذَابًا يَوْمَ القِيَامَةِ الَّذِينَ يُضَاهِئُونَ بِخَلْقِ اللَّهِ))

Nao (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللهُ عَنْهَا) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watakaokuwa na adhabu kali Siku ya Qiyaamah ni wanaomuiga Allaah katika uumbaji Wake))

 

 وَلَهُمَا عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ (رضي الله عنهما) :  سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) يَقُولُ: ((كُلُّ مُصَوِّرٍ فِي النَّارِ يُجْعَلُ لَهُ بِكُلِّ صُورَةٍ صَوَّرَهَا نَفْسٌ يُعَذَّبُ بِهَا فِي جَهَنَّمَ))

Nao (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kila mchoraji picha atakuwa motoni. Kila picha aliyoichora, itatiwa roho nayo itamuadhibu katika Jahannam))

 

وَلَهُمَا عَنْهُ مَرْفُوعًا: ((مَنْ صَوَّرَ صُورَةً فِي الدُّنْيَا كُلِّفَ أَنْ يَنْفُخَ فِيهَا الرُّوحَ وَلَيْسَ بِنَافِخٍ))

Nao (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia kutoka kwake pia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) Hadiyth Marfuw’: ((Atakayechora picha duniani atalazimishwa aitie roho (Siku ya Qiyaamah), na wala hatoweza))

 

وَلِمُسْلِمٍ عَنْ أَبِي الهَيَّاجِ قَالَ: قَالَ لِي عَلِيٌّ: أَلاَ أَبْعَثُكَ عَلَى مَا بَعَثَنِي عَلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)؟: أَلاَّ تَدَعَ صُورَةً إِلاَّ طَمَسْتَهَا وَلاَ قَبْرًا مُشْرِفًا إِلاَّ سَوَّيْتَهُ  

Na Muslim amesimulia kutoka kwa Abuu Al-Hayyaaj amesema: ‘Aliyy ameniambia: “Je, nikutume lile alilonituma Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)?  Kwamba: Usibakishe sura (picha, sanamu, kinyago) yoyote ila uiharibu, wala kaburi lilonyanyuliwa ila (ulibomoe na) ulisawazishe.”

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Karipio kali kwa wenye kuchora (na kutengeneza, kuchonga) picha, masanamu, vinyago n.k.

 

2-Imekaripiwa vikali kwa sababu watengenezaji na wachoraji picha hawamuheshimu vilivyo Allaah (سبحانه وتعالى) kama Alivyosema Yeye Mwenyewe: ((Nani dhalimu zaidi kuliko anayejaribu kuumba kama kuumba Kwangu?)).

 

3-Tanbihi ya nguvu kutofuatisha uwezo wa Allaah (سبحانه وتعالى) katika kuumba na ule wa wengine kama unavyoashiria katika kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى): ((Basi na waumbe chembe moja au waumbe punje ya nafaka, au waumbe chembe ya shayiri)).

 

4-Tangazo kuwa wachoraji, watengenezaji picha wataadhibiwa vikali zaidi (Siku ya Qiyaamah).  

 

5-Allaah (سبحانه وتعالى) Ataumba roho katika kila picha (sanamu, kinyago n.k.) nayo itamuadhibu mwenye kuzitengeneza katika moto wa Jahannam.

 

6-Wafanya picha wataambiwa wazitie roho (uhai) picha zao.

 

7-Amri ya kuziharibu picha, vinyago, masanamu n.k. popote zitakapoonekana. (Pia kusawazisha makaburi yaliyonyanyuliwa).  

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share

62-Kitaab At-Tawhiyd: Makatazo Ya Kuapa Kwa Wingi

Mlango Wa 62

بَابٌ مَا جَاءَ فِي كَثْرَةِ الْحَلِفِ

Makatazo Ya Kuapa Kwa Wingi


 

 

وَقَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Na kauli ya Allaah Ta’aalaa:

وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ

((Na hifadhini yamini zenu)) [Al-Maaidah (5: 89)]

  

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  يَقُولُ:  ((الْحَلِفُ مَنْفَقَةٌ لِلسِّلْعَةِ مَمْحَقَةٌ لِلْكَسْبِ)) أَخْرَجَاهُ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah(رضي الله عنه)  amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Kwa kuapa, [muuzaji] huenda akamshawishi  mnunuaji kununua bidhaa, lakini kunafuta Baraka za Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

وَعَنْ سَلْمَانَ: أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((ثَلاثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمْ اَللَّهُ وَلاَ يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ: أُشَيمِطٌ زَانٍ وَعَائِلٌ مُسْتَكْبِرٌ وَرَجُلٌ جَعَلَ اَللَّهَ بِضَاعَتَهُ لاَ يَشْتَرِي إِلاَّ بِيَمِينِهِ وَلاَ يَبِيعُ إِلاَّ بِيَمِينِه)) رَوَاهُ اَلطَّبَرَانِيُّ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ

Na Imepokelewa kutoka kwa Salmaan kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watu watatu ambao Allaah Hatowasemesha, wala Hatowatakasa, na watapata adhabu kali: Mzinifu mzee, maskini anayetakabari, na mtu aliyejaaliwa na bidhaa, lakini hanunui ila kwa kuapa [wa-Allaahi] na hauzi ila kwa kuapa [wa-Allaahi)) [At-Twabaraaniy kwa isnaad Swahiyh]

 

وَفِي اَلصَّحِيحِ: عَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَينٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((خَيْرُ أُمَّتِي قَرْنِي، ثُمَّ اَلَّذِينَ يَلُونَهُمْ، ثُمَّ اَلَّذِينَ يَلُونَهُمْ)) قَالَ عِمْرَانُ:  فَلا أَدْرِي أَذَكَرَ بَعْدَ قَرْنِهِ مَرَّتَيْنِ أَوْ ثَلاثًا؟ ((ثُمَّ إِنَّ بَعْدَكُمْ قَوْمًا يَشْهَدُونَ وَلاَ يُسْتَشْهَدُونَ، وَيَخُونُونَ وَلاَ يُؤْتَمَنُونَ، وَيَنْذِرُونَ وَلاَ يُوفُونَ، وَيَظْهَرُ فِيهِمْ اَلسِّمَن))   

Na katika Swahiyh (Muslim) kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Ummah bora kabisa ni karne yangu, kisha wale wanaowafuatia, kisha wanowafuatia)) ‘Imraan akasema: “Lakini sijui kama alitaja mara mbili baada ya karne yake au tatu?.” ((Kisha watakuja watu baada yenu, kushuhudia bila ya kuombwa kutoa ushahidi, na watakuwa makhaini wala hawatoaminiwa, na wataweka nadhiri lakini hawatotimiza, na itadhihirika kwao unene))[1]

 

وَفِيهِ عَنِ اِبْنِ مَسْعُود: ٍ أَنَّ اَلنَّبِيَّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) قَالَ: ((خَيْرُ اَلنَّاسِ قَرْنِي، ثُمَّ اَلَّذِينَ يَلُونَهُمْ، ثُمَّ اَلَّذِينَ يَلُونَهُمْ، ثُمَّ يَجِيءُ قَوْمٌ تَسْبِقُ شَهَادَةُ أَحَدِهِمْ يَمِينَهُ وَيَمِينُهُ شَهَادَتَهُ))

Na humo (katika Muslim) imesimuliwa kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Watu bora kabisa ni karne yangu, kisha wale wanaowafuatia, kisha wanowafuatia, kisha watakuja watu ambao ushahidi wao utatangulia viapo vyao na viapo vitatangulia ushahidi wao))[2]

 

قَالَ إِبْرَاهِيمُ كَانُوا يَضْرِبُونَنَا عَلَى اَلشَّهَادَةِ وَالْعَهْدِ وَنَحْنُ صِغَارٌ 

Ibraahiym (An-Nakha’iyy) amesema: “Tulikuwa tukichapwa (na wazee wetu) tulipokuwa wadogo juu ya jambo la kuapa na kutoa ushahidi.”

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Wasia juu ya kulinda viapo.

 

2-Tanbihi kuwa japokuwa viapo vinasaidia uuzaji wa bidhaa lakini hakuna baraka katika pato la mtu.

 

3-Tishio la adhabu kali kwa wale ambao hawanunui au kuuza isipokuwa kwa kiapo.

 

4-Onyo kuwa kutenda dhambi kwa sababu ndogondogo au pasina sababu hukuza ukubwa wa dhambi.

 

5-Karipio kwa wanaoapa pasi na kutakiwa kufanya hivyo.

 

6-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kusifu vizazi vitatu au vine vya kwanza na maelezo ya kitakachotokea baadaye.

 

7-Watatoa ushahidi pasina kutakiwa hivyo.

 

8-As-Salaf walikuwa wakiwachapa watoto wao kwa kuapa au kutoa ushahidi ovyo.

 

 

 

 

 

[1] Kutokana na kughafilishwa na mambo ya dunia.

[2] Kwa sababu hawatolipa uzito jukumu lao la kutoa ushahidi na kula viapo kwa hivyo watakuwa wepesi wa kutoa ushahidi na kula viapo bila ya kujaili.

Share

63-Kitaab At-Tawhiyd: Kulinda Ahadi Za Allaah Na Nabiy Wake

Mlango Wa 63

بَابٌ مَا جَاءَ فِي ذِمَّةِ اَللَّهِ وَذِمَّةِ نَبِيِّهِ

Kulinda Ahadi Za Allaah Na Nabiy Wake


 

 

وَقَوْلُهُ تَعَالَى:

Na kauli Yake Ta’aalaa:

 

وَأَوْفُوا بِعَهْدِ اللَّـهِ إِذَا عَاهَدتُّمْ وَلَا تَنقُضُوا الْأَيْمَانَ بَعْدَ تَوْكِيدِهَا وَقَدْ جَعَلْتُمُ اللَّـهَ عَلَيْكُمْ كَفِيلًا ۚ إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا تَفْعَلُونَ ﴿٩١﴾

((Na timizeni ahadi ya Allaah mnapoahidi, na wala msivunje viapo baada ya kuvithibitisha; na mmekwishamfanya Allaah kuwa ni Mdhamini wenu. Hakika Allaah Anajua yale mnayoyafanya)) [An-Nahl (16: 91)]  

 

عَنْ بُرَيْدَةَ قَالَ: كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) إِذَا أَمَّرَ أَمِيرًا عَلَى جَيْشٍ أَوْ سَرِيَّةٍ أَوْصَاهُ بِتَقْوَى اَللَّهِ - وَمَنْ مَعَهُ مِنَ الْمُسْلِمِينَ خَيْرًا. فَقَالَ: ((اُغْزُوَا بِسْمِ اَللَّهِ فِي سَبِيلِ اَللَّهِ ، قَاتِلُوا مَنْ كَفَرَ بِاَللَّهِ اُغْزُوَا ولاَ تَغُلُّوا وَلاَ تَغْدِرُوا وَلاَ تُمَثِّلُوا وَلاَ تَقْتُلُوا وَلِيدًا.

وَإِذَا لَقِيتَ عَدُوَّكَ مِنَ الْمُشْرِكِينَ فَادْعُهُمْ إِلَى ثَلاثِ خِصَالٍ (أَوْ خِلالٍ)، فَأَيَّتُهُنَّ مَا أَجَابُوكَ فَاقْبَلْ مِنْهُمْ، وَكُفَّ عَنْهُمْ ثُمَّ اُدْعُهُمْ إِلَى الإِسْلامِ. فَإِنْ أَجَابُوكَ: فَاقْبَلْ مِنْهُمْ ثُمَّ اُدْعُهُمْ إِلَى اَلتَّحَوُّلِ مِنْ دَارِهِمْ إِلَى دَارِ الْمُهَاجِرِينَ وَأَخْبِرْهُمْ أَنَّهُمْ إِنْ فَعَلُوا ذَلِكَ فَلَهُمْ مَا لِلْمُهَاجِرِينَ، وَعَلَيْهِمْ مَا عَلَى الْمُهَاجِرِينَ، فَإِنْ أَبَوْا أَنْ يَتَحَوَّلُوا مِنْهَا فَأَخْبِرْهُمْ أَنَّهُمْ يَكُونُونَ كَأَعْرَابِ الْمُسْلِمِينَ يَجْرِي عَلَيْهِمْ حُكْمُ اَللَّهِ تَعَالَى وَلاَ يَكُونُ لَهُمْ فِي الْغَنِيمَةِ وَالْفَيءِ شَيءٌ إِلاَّ أَنْ يُجَاهِدُوا مَعَ الْمُسْلِمِينَ، فَإِنْ هُمْ أَبَوْا، فَاسْأَلْهُمْ الْجِزْيَةَ، فَإِنْ هُمْ أَجَابُوكَ فَاقْبَلْ مِنْهُمْ، وَكُفَّ عَنْهُمْ، فَإِنْ هُمْ أَبَوْا، فَاسْتَعِنْ بِاَللَّهِ وَقَاتِلْهُم.

وَإِذَا حَاصَرْتَ أَهْلَ حِصْنٍ فَأَرَادُوكَ أَنْ تَجْعَلَ لَهُمْ ذِمَّةَ اَللَّهِ وَذِمَّةَ نَبِيِّهِ، فَلا تَجْعَلْ لَهُمْ ذِمَّةَ اَللَّهِ وَذِمَّةَ نَبِيِّهِ، وَلَكِنِ اِجْعَلْ لَهُمْ ذِمَّتَكَ وَذِمَّةَ أَصْحَابِكَ، فَإِنَّكُمْ أَنْ تَخْفِرُوا ذِمَمَكُمْ وَذِمَّةَ أَصْحَابِكُمْ أَهْوَنُ مِنْ أَنْ تَخْفِرُوا ذِمَّةَ اَللَّهِ وَذِمَّةَ نَبِيِّهِ.

 وَإِذَا حَاصَرْتَ أَهْلَ حِصْنٍ فَأَرَادُوكَ أَنْ تُنْزِلَهُمْ عَلَى حُكْمِ اَللَّهِ، فَلا تُنْزِلْهُمْ عَلَى حُكْمِ اَللَّهِ وَلَكِنْ أَنْزِلْهُمْ عَلَى حُكْمِكَ فَإِنَّكَ لاَ تَدْرِي أَتُصِيبُ فِيهِمْ حُكْمَ اَللَّهِ أَمْ لاَ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Imepokelewa kutoka kwa Buraydah (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa anapomwakilisha uongozi amiri wa jeshi au kikosi, alimuusia kumcha Allaah na kuwafanyia wema Waislamu waliokuwa naye. Alikuwa akisema: ((Anzeni kupigana vita kwa BismiLLaah, katika njia ya Allaah. Piganeni na wanaomkanusha Allaah. Piganeni vita na msichukue ngawira kwa njia isiyostahiki, na msivunje mkataba wala msikate viungo vya maiti, wala kuua watoto.

 

Mnapokutana na maadui washirikina, walinganieni mambo matatu.   Wakikubali mojawapo basi wakubalini kwa ahadi yao wala msiendelee kupigana. Kisha waiteni katika Uislamu. Wakisilimu waombeni wahamie katika miji ya Muhaajirina (ya Kiislamu). Waambieni kwamba wakifanya hivyo, basi watastahiki haki zote za Muhaajirina. Wakikataa kuhama, basi watakuwa kama Mabedui Waislamu na kwamba [hawatokuwa huru bali] watanyenyekea amri za Allaah (سبحانه وتعالى) kama Waislamu wengine, lakini hawatopata ngawira yoyote mpaka wapigane bega kwa bega na Waislamu. Wakikataa [kusilimu] basi watalazimika kulipa jizyah[1].  Wakikubali basi acheni kupigana nao. Lakini wakikataa [kulipa jizyah] basi takeni msaada kwa Allaah na piganeni nao.

 

Mkizingira ngome na waliozingirwa wakikuombeni hifadhi na ulinzi kwa Jina la Allaah na Rasuli Wake, msiwape dhamana ya Allaah na Rasuli Wake, bali wapeni dhamana kwa niaba yako na wenzako kwani itakuwa ni dhambi ndogo pale isipoheshimiwa dhamana utakayoitoa wewe na wenzako kuliko kutokuheshimu dhamana ya Jina la Allaah na Rasuli Wake. Mkizingira ngome na waliozingirwa wanawatakeni muwaachie watoke kwa mujibu wa hukmu ya Allaah, msiwaachie kwa mujibu ya hukmu ya Allaah, bali   watoeni kwa hukmu yako, kwani hujui kama utaweza au hatoweza kufuata hukmu ya Allaah juu yao)) [Muslim]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Tofauti baina hifadhi ya Allaah (سبحانه وتعالى) na ya Rasuli Wake  

  (صلى الله عليه وآله وسلم) na hifadhi ya Waislamu.

 

2-Maelekezo ya kuchagua lenye khatari ndogo.

 

3-Amri ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Anzeni kupigana vita kwa BismiLLaah, katika njia ya Allaah)).

 

4-Amri ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Piganeni na wanaomkanusha  Allaah)).

 

5-Amri ya Nabiy: ((Takeni msaada kwa Allaah na piganeni nao)).

 

6-Kuna tofauti baina ya amri ya Allaah (سبحانه وتعالى) na ya 'Ulamaa.

 

7-Hukmu ya Swahaba huenda isilingane na hukmu Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

 

 

 

 

 

 

[1] Kodi wanayotozwa wasio Waislamu ya ulinzi katika serikali ya Kiislamu.

Share

64-Kitaab At-Tawhiyd: Kuapa Kwamba Allaah Hatafanya Jambo Fulani

Mlango Wa 64

بَابٌ  :مَا جَاءَ فِي الإِقْسَامِ عَلَى اللَّهِ

Kuapa Kwamba Allaah Hatafanya Jambo Fulani


 

 

عَنْ جُنْدُبِ بنِ عَبْدِ اللَّهِ (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ ((صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)): ((قَالَ رَجُلٌ: وَاللَّهِ لاَ يَغْفِرُ اللَّهُ لِفُلانٍ. فَقَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: مَنْ ذَا الَّذِي يَتَأَلَّى عَلَيَّ أَنْ لاَ أَغْفِرَ لِفُلانٍ؟ إِنِّي قَدْ غَفَرْتُ لَهُ وَأَحْبَطْتُ عَمَلَكَ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Imepokelewa kutoka kwa Jundub bin ‘Abdillaah   (رضي الله عنه)amesema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم ) amesema: ((Mtu mmoja alisema: Wa-Allaahi Allaah Hatomghufuria fulani! Allaah (عزّ وجلّ) Akasema: Ni nani huyo anayeniamulia kuwa Sitomghufuria fulani? Mimi Nimeshamghufuria fulani na Nimebatilisha ‘amali zako)) [Muslim]  

 

وَفِي حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ : أَنَّ "القَائِلَ رَجُلٌ عَابِدٌ" قَالَ أَبُو هُرَيْرَةَ : تَكَلَّمَ بِكَلِمَةٍ، أَوْبَقَتْ دُنْيَاهُ وَآخِرَتَهُ

Na katika Hadiyth ya Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba: Mtu aliyesema hivyo ni mshika ‘ibaadah. Abuu Hurayrah akasema: “Ametamka neno moja lilomharibia duniya na Aakhirah yake”

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Onyo dhidi ya kutokuapa kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Hatafanya jambo fulani.

 

2-Moto wa Jahannam uko karibu nasi kuliko kamba za viatu.

 

3-Kadhalika Jannah.

 

4-Maelezo kuwa wakati mwingine, mwana Aadam hutamka maneno pasi na kukusudia lakini athari zake ni kubwa mno kiasi ya kumuangamiza kama ilivyo katika Hadiyth:

 

عن أَبي عبد الرحمن بِلالِ بن الحارِثِ المُزَنِيِّ رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ : ((إنَّ الرَّجُلَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ رِضْوَانِ اللهِ تَعَالَى مَا كَانَ يَظُنُّ أنْ تَبْلُغَ مَا بَلَغَتْ يَكْتُبُ اللهُ لَهُ بِهَا رِضْوَانَهُ إِلَى يَومِ يَلْقَاهُ ، وإنَّ الرَّجُلَ لَيَتَكَلَّمُ بِالكَلِمَةِ مِنْ سَخَطِ اللهِ مَا كَانَ يَظُنُّ أنْ تَبْلُغَ مَا بَلَغَتْ يَكْتُبُ الله لَهُ بِهَا سَخَطَهُ إِلَى يَوْمِ يَلْقَاهُ )). رواه مالك في المُوَطَّأ ، والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

 

Abuu 'Abdir-Rahmaan Bilaal bin Al-Haarith Al-Muzniy (رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Kwa hakika mja atazungumza neno linalomridhisha Allaah, wala asidhani kuwa litafikia lilipofikia, Allaah Amuandikie kwa neno hilo Radhi Zake hadi Siku ya Qiyaamah. Na Kwa hakika mja atazungumza neno linalomkasirisha Allaah, wala asidhani kuwa litafikia lilipofikia, Allaah Amuandikie kwa neno hilo hasira Zake hadi Siku ya Qiyaamah)) [Maalik katika Muwattwa na At-Tirmidhiy ambaye amesema Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]

 

5-Wakati mwingine, mwana Aadam husamehewa dhambi zake zote kwa jambo alichukialo sana.

 

 

 

 

 

Share

65-Kitaab At-Tawhiyd: Haiombwi Shafaa-ah Ya Allaah Juu Ya Viumbe Vyake

Mlango Wa 65

بَابٌ لَا يُسْتَشْفَعُ بِاَللَّهِ عَلَى خَلْقِهِ

Haiombwi Shafaa-ah Ya Allaah Juu Ya Viumbe Vyake


 

 

عَنْ جُبَيْرِ بْنِ مُطْعِمٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ : جَاءَ أَعْرَابِيٌّ إِلَى اَلنَّبِيِّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ)  فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! نُهِكَتِ الأَنْفُسُ وَجَاعَ الْعِيَالُ وَهَلَكَتِ الأَمْوَالُ فَاسْتَسْقِ لَنَا رَبَّكَ، فَإِنَّا نَسْتَشْفِعُ بِاَللَّهِ عَلَيْكَ، وَبِكَ عَلَى اَللَّهِ. فَقَالَ اَلنَّبِيُّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((سُبْحَانَ اَللَّهِ! سُبْحَانَ اَللَّهِ!)) فَمَا زَالَ يُسَبِّحُ حَتَّى عُرِفَ ذَلِكَ فِي وُجُوهِ أَصْحَابِهِ ثُمَّ قَالَ: ((وَيْحَكَ! أَتَدْرِي مَا اَللَّهُ؟ إِنَّ شَأْنَ اَللَّهِ أَعْظَمُ مِنْ ذَلِكَ، إِنَّهُ لاَ يُسْتَشْفَعُ بِاَللَّهِ عَلَى أَحَدٍ مِنْ خَلْقِهِ)) وَذَكَرَ الْحَدِيثَ رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ

Imepokelewa kutoka kwa Jubayr bin Mutw’-im(رضي الله عنه)  amesema: Alikuja Bedui kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Watu wanaangamia, na watoto wana njaa, mali imeangamia [mimea na wanyama], basi muombe Rabb wako Atuletee mvua, kwani tunaomba shafaa’ah ya Allaah kwako na shafaa’ah yako kwa Allaah.” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Subhaana-Allaah! Subhaana Allaah!)). Akaendelea kumtakasa Allaah mpaka athari yake ikadhihiri nyusoni mwa Maswahaba. Kisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ole wako! Unamjua nani Allaah? Hakika Utukufu wa Allaah ni adhimu zaidi kuliko hilo! Haiombwi shafaa’ah ya Allaah juu ya yeyote kati ya viumbe Wake)) [Akataja Hadiyth Abuu Daawuwd]      

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Nabiy kukaripia kunaposemwa: “Tunaomba shafaa’ah ya Allaah kwako.”

 

2-Ghadhabu ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ilidhihirika kwa Maswahaba  (رضي الله عنهم).

 

3-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) hakukemea ombi la shafaa’ah yake kwa Allaah.

 

4-Maana ya Subhana-Allaah. (Allaah (سبحانه وتعالى) Yuko juu kabisa ya viumbe Vyake na Ametakasika kabisa dhidi ya ila na hahitaji lolote].

 

5-Waislamu walimuomba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aombe mvua.

 

 

Share

66-Kitaab At-Tawhiyd: Himaaya Ya Nabiy - Himaaya Ya Tawhiyd

Mlango Wa 66

بَابٌ مَا جَاءَ فِي حِمَايَةِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ حِمَى اَلتَّوْحِيدِ

Himaaya Ya Nabiy - Himaaya Ya Tawhiyd


 

 

عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ الشِّخِّيرِ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: اِنْطَلَقْتُ فِي وَفْدِ بَنِي عَامِرٍ إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)  فَقُلْنَا: أَنْتَ سَيِّدُنَا فَقَالَ: ((اَلسَّيِّدُ اَللَّهُ تَبَارَكَ وَتَعَالَى)). قُلْنَا: وَأَفْضَلُنَا فَضْلاً، وَأَعْظَمُنَا طَولاً. فَقَالَ: ((قُولُوا بِقَوْلِكُمْ أَوْ بَعْضِ قَوْلِكُمْ وَلاَ يَسْتَجْرِيَنَّكُمْ اَلشَّيْطَانُ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ بِسَنَدٍ جَيِّدٍ

 

Imepokelewa kutoka kwa ‘Abdullaah bin Ash-Shikhkhiyr(رضي الله عنه)  amesema: Nilikwenda pamoja wajumbe wa Bani ‘Aamir kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) tukamwambia: “Wewe ni Sayyidinaa (Bwana wetu).” Akasema: ((Bwana ni Allaah Aliyetukuka na Aliyebarikika)). Tukasema: “Wewe ndiye mbora wetu na mtukufu wetu.”  Akasema (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Semeni msemayo au baadhi yake tu, msimwache shaytwaan akakuvusheni mipaka [ya kunisifu])) [Abuu Daawuwd kwa isnaad nzuri]

 

وَعَنْ أَنَسٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) أَنَّ نَاسًا قَالُوا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! يَا خَيْرَنَا وَابْنَ خَيْرِنَا وَسَيِّدَنَا وَابْنَ سَيِّدِنَا! فَقَالَ:  ((يَا أَيُّهَا اَلنَّاسُ! قُولُوا بِقَوْلِكُمْ وَلاَ يَسْتَهْوِيَنَّكُمْ اَلشَّيْطَانُ، أَنَا مُحَمَّدٌ عَبْدُ اَللَّهِ وَرَسُولُهُ، مَا أُحِبُّ أَنْ تَرْفَعُونِي فَوْقَ مَنْزِلَتِي اَلَّتِي أَنْزَلَنِي اَللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ)) . رَوَاهُ النَّسَائِيُّ بِسَنَدٍ جَيِّدٍ

Na Imepokelewa kutoka kwa Anas(رضي الله عنه)  amesema: kwamba watu walisema: “Ee Rasuli wa Allaah! Ee mbora wetu na mwana wa mbora wetu, na bwana wetu, na mwana wa bwana wetu!” Akasema: ((Enyi watu! Semeni msemayo, asikupambieni shaytwaan hawaa zenu. Mimi ni Muhammad mja wa Allaah na Rasuli Wake. Sipendi mnipandishe cheo kuliko cheo changu ambacho Ameniteremshia Allaah Ázza wa Jalla)) [An-Nasaaiy kwa isnaad nzuri]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Kuwaonya watu dhidi ya kuvuka mipaka kusifu na kutukuza.

 

2-Ajibu nini mtu anapoambiwa: "Wewe ni bwana wetu.”

 

3-Kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((msimwache shaytwaan akakuvusheni mipaka [ya kunisifu])) ingawa walisema ukweli kuhusu utukufu wake.

 

4-Kauli ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): ((Sipendi mnipandishe kuliko cheo changu)),

 

 

Share

67-Kitaab At-Tawhiyd: Hawakumthamini Allaah Ipasavyo Kumthamini

Mlango Wa 67

باب:  وَمَا قَدَرُوا اللَّـهَ حَقَّ قَدْرِهِ

Hawakumthamini Allaah Ipasavyo Kumthamini


 

  قَوْلِ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَمَا قَدَرُوا اللَّـهَ حَقَّ قَدْرِهِ وَالْأَرْضُ جَمِيعًا قَبْضَتُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَالسَّمَاوَاتُ مَطْوِيَّاتٌ بِيَمِينِهِ ۚ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَىٰ عَمَّا يُشْرِكُونَ ﴿٦٧﴾

((Na hawakumkadiria Allaah kama inavyostahiki kumkadiria; na hali ardhi yote itakamtwa Mkononi Mwake Siku ya Qiyaamah; na mbingu zitakunjwa Mkononi Mwake wa kulia. Subhaanahu wa Ta’aalaa! Utakasifu ni wa Allaah na Ametukuka kwa ‘Uluwa kutokana na yale yote wanayomshirikisha)) [Az-Zumar (39: 67)]

 

عَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: جَاءَ حَبْرٌ مِنَ الأَحْبَارِ إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَقَالَ: يَا مُحَمَّدُ! إِنَّا نَجِدُ أَنَّ اَللَّهَ يَجْعَلُ اَلسَّمَاوَاتِ عَلَى إِصْبَعٍ، وَالأَرَضِينَ عَلَى إِصْبَعٍ، وَالشَّجَرَ عَلَى إِصْبَعٍ، وَالْمَاءَ عَلَى إِصْبَعٍ، وَالثَّرَى عَلَى إِصْبَعٍ، وَسَائِرَ الْخَلْقِ عَلَى إِصْبَعٍ، فَيَقُولُ أَنَا الْمَلِكُ. فَضَحِكَ اَلنَّبِيُّ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) حَتَّى بَدَتْ نَوَاجِذُهُ، تَصْدِيقًا لِقَوْلِ الْحَبْرِ، ثُمَّ قَرَأَ: (( وَمَا قَدَرُوا اللَّـهَ حَقَّ قَدْرِهِ وَالْأَرْضُ جَمِيعًا قَبْضَتُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ))

Imepokelewa kutoka kwa Ibn Mas’uwd(رضي الله عنه)  amesema: Alikuja mwanachuoni wa Kiyahudi  kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Ee Muhammad! Tumejua kwamba Allaah Ataziweka mbingu zote katika kidole kimoja, na ardhi zote katika kidole kimoja, na miti katika kidole kimoja, na maji na vumbi katika kidole kimoja, na viumbe vyote vinginevyo katika kidole kimoja. Kisha Atasema: Mimi Ndiye Mfalme.” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akacheka mpaka meno yake ya magego yakaonekana kwa kukubali maneno ya Myahudi, kisha (Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم akasoma Aayah: ((Na hawakumkadiria Allaah kama inavyostahiki kumkadiria; na hali ardhi yote itakamtwa Mkononi Mwake Siku ya Qiyaamah)) 

 

وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ: ((وَالْجِبَالَ وَالشَّجَرَ عَلَى إِصْبَعٍ، ثُمَّ يَهُزُّهُنَّ فَيَقُولُ: أَنَا الْمَلِكُ أَنَا اَللَّهُ!))

Na katika riwaayah ya Muslim: ((Na milima na miti katika kidole kimoja, kisha Ataitingisha na Aseme: Mimi Ndiye Mfalme, Mimi Ndiye Allaah!))

 

وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ: ((وَيَجْعَلُ اَلسَّمَاوَاتِ عَلَى إِصْبَعٍ وَالْمَاءَ وَالثَّرَى عَلَى إِصْبَعٍ، وَسَائِرَ الْخَلْقِ عَلَى إِصْبَعٍ)) . أَخْرِجَاهُ

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: ((Na Ataweka mbingu katika kidole kimoja, na maji na mchanga katika kidole kimoja, na viumbe vyote vilobakia katika kidole kimoja)) 

 

وَلِمُسْلِمٍ عَنْ اِبْنِ عُمَرَ مَرْفُوعًا: ((يَطْوِي اَللَّهُ اَلسَّمَاوَاتِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ثُمَّ يَأْخُذُهُنَّ بِيَدِهِ الْيُمْنَى، ثُمَّ يَقُولُ أَنَا الْمَلِكُ أَيْنَ الْجَبَّارُونَ؟ أَيْنَ الْمُتَكَبِّرُونَ؟ ثُمَّ يَطْوِي الأَرْضِينَ اَلسَّبْعَ، ثُمَّ يَأْخُذُهُنَّ بِشِمَالِهِ، ثُمَّ يَقُولُ أَنَا الْمَلِكُ، أَيْنَ الْجَبَّارُونَ؟ أَيْنَ الْمُتَكَبِّرُونَ؟))

Na Muslim amesimulia kutoka kwa Ibn ‘Umar Hadiyth Marfuw’: ((Allaah Atakunja mbingu Siku ya Qiyaamah kisha Atazichukua katika Mkono Wake wa kuume kisha Atasema: Mimi Ndiye Mfalme, wako wapi majabari? Wako wapi [leo] wanaotakabari? Kisha Atakunja ardhi saba kisha Atazichukua katika Mkono Wake wa kushoto kisha Atasema: Mimi Ndiye Mfalme, wako wapi majabari, wako wapi [leo] wanaotakabari?))

 

وَرُوِيَ عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ قَالَ: مَا اَلسَّمَاوَاتُ اَلسَّبْعُ وَالْأَرْضُونَ اَلسَّبْعُ فِي كَفِّ اَلرَّحْمَنِ إِلَّا كَخَرْدَلَةٍ فِي يَدِ أَحَدِكُمْ  

Na imesimuliwa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  kasema: “Mbingu saba na ardhi saba si chochote ila kama kama chembe ya hardali katika mkono wa mmoja wenu.”

 

وَقَالَ اِبْنُ جَرِيرٍ: حَدَّثَنِي يُونُسُ، أَخْبَرَنَا اِبْنُ وَهْبٍ، قَالَ: قَالَ اِبْنُ زَيْدٍ: حَدَّثَنِي أَبِي، قَالَ :قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((مَا اَلسَّمَاوَاتُ اَلسَّبْعُ فِي الْكُرْسِيِّ إِلاَّ كَدَرَاهِمَ سَبْعَةٍ أُلْقِيَتْ فِي تُرْسٍ))  قَالَ: وَقَالَ أَبُو ذَرٍّ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ يَقُول:ُ ((مَا الْكُرْسِيُّ فِي الْعَرْشِ إلاَّ كَحَلْقَةٍ مِنْ حَدِيدٍ أُلْقِيَتْ بَيْنَ ظَهْرَيْ فَلاةٍ مِنَ الأَرْضِ))

Na Ibn Jariyr amesema: “Yuwnus amenihadithia: Tulijulishwa na Ibn Wahb amesema: Ibn Zayd amesema: Baba yangu amenihadithia, akasema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mbingu saba kulingana na Al-Kursiy ya Allaah, ni ndogo mno kama dirham saba zilowekwa katika ngao ya askari)) Akasema Abuu Dharr: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Al-Kursiy kulingana na ‘Arshi ni kama kikuku cha chuma kilotupwa baina ya uwanja mkubwa))

 

Al-Kursiy: Kiti cha Enzi kinachomhusu Allaah Pekee.  

 

وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ  قَالَ: ((بَيْنَ اَلسَّمَاءِ اَلدُّنْيَا وَاَلَّتِي تَلِيهَا خَمْسُمِائَةِ عَامٍ،  وَبَيْنَ كُلِّ سَمَاءٍ وَسَمَاءٍ خَمْسُمِائَةِ عَامٍ، وَبَيْنَ اَلسَّمَاءِ اَلسَّابِعَةِ وَالْكُرْسِيِّ خَمْسُمِائَةِ عَامٍ، وَبَيْنَ الْكُرْسِيِّ وَالْمَاءِ خَمْسُمِائَةِ عَامٍ، وَالْعَرْشُ فَوْقَ الْمَاءِ، وَاَللَّهُ فَوْقَ الْعَرْشِ، لاَ يَخْفَى عَلَيْهِ شَيْءٌ مِنْ أَعْمَالِكُمْ)).  أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَهْدِيٍّ عَنْ حَمَّادِ بْنِ سَلَمَةَ عَنْ عَاصِمٍ عَنْ زِرٍّ عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ. 

وَرَوَاهُ بِنَحْوِهِ الْمَسْعُودِيُّ عَنْ عَاصِمٍ عَنْ أَبِي وَائِلٍ عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ. قَالَهُ الْحَافِظُ اَلذَّهَبِيُّ رَحِمَهُ اَللَّهُ، قَالَ:وَلَهُ طُرُقٌ

Imesimuliwa kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه)  amesema: ((Masafa ya baina ya mbingu ya kwanza na dunia  ni mwendo wa miaka mia tano, na baina ya kila mbingu na nyingine miaka mia tano. Na baina ya mbingu saba na Al-Kursiyy pia ni miaka mia tano. Na   baina ya Al-Kursiyy na maji ni miaka mia tano. ‘Arshi (ya Allaah) iko juu ya maji na Allaah Yuko juu ya ‘Arshi, hakifichiki chochote katika vitendo vyenu.” [Imeripotiwa na Ibn Mahdi kutoka kwa Hammaad bin Salamah, kutoka kwa ‘Aaswim kutoka kwa Zirr, kutoka kwa ‘Abdullaah (Ibn Mas’uwd(رضي الله عنه) ]

 

Na imesimuliwa na Al-Haafhidwh Adh-Dhahabiyy amesema: “Hadiyth hiyo ina njia nyingi.”

 

وَعَنْ الْعَبَّاسِ بْنِ عَبْدِ الْمُطَّلِبِ (رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ (صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((هَلْ تَدْرُونَ كَمْ بَيْنَ اَلسَّمَاءِ وَالأَرْضِ؟)) قُلْنَا: اَللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ. قَالَ: ((بَيْنَهُمَا مَسِيرَةُ خَمْسُمِائَةِ سَنَةٍ، وَمِنْ كُلِّ سَمَاءٍ إِلَى سَمَاءٍ، مَسِيرَةُ خَمْسُمِائَةِ سَنَةٍ، وَكِثَفُ كُلِّ سَمَاءٍ مَسِيرَةُ خَمْسِمِائَةِ سَنَةٍ، وَبَيْنَ اَلسَّمَاءِ اَلسَّابِعَةِ وَالْعَرْشِ بَحْرٌ بَيْنَ أَسْفَلِهِ وَأَعْلاهُ كَمَا بَيْنَ اَلسَّمَاءِ وَالأَرْضِ، وَاَللَّهُ سُبْحَانَهُ وَتَعَالَى فَوْقَ ذَلِكَ، وَلَيْسَ يَخْفَى عَلَيْهِ شَيْءٌ مِنْ أَعْمَالِ بَنِي آدَمَ))  أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ وَغَيْرُهُ

Na Imepokelewa toka kwa Al-’Abbaas bin ‘Abdil-Muttwalib(رضي الله عنه)  amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Je, mnajua masafa mangapi yapo baina ya mbingu na ardhi?)) Tukasema: “Allaah na Rasuli Wake wanajua.”  Akasema: ((Masafa baina yake ni mwendo wa miaka mia tano, na masafa baina ya mbingu moja na ya pili yake inayofuatia ni mwendo wa miaka mia tano. Na unene wa kila mbingu ni sawa na mwendo wa miaka mia tano. Na baina ya mbingu ya saba na ‘Arshi kuna bahari; kina chake ni sawa na umbali wa baina mbingu na ardhi. Na Allaah Yuko juu ya hivyo hakifichiki chochote katika vitendo vya bin Aadam)) [Abuu Daawuwd na wengineo]

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

 

1-Tafsiri ya Aayah Suwrah Az-Zumar (39: 67).

وَالْأَرْضُ جَمِيعًا قَبْضَتُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ

((Na hali ardhi yote itakamtwa Mkononi Mwake Siku ya Qiyaamah)).

 

2-Elimu ya mambo haya yalikuwepo kwa Wayahudi wakati wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), na hawakulikanusha wala kulieleza.

 

3-Pale Rabai wa dini ya Kiyahudi alipomtajia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu mambo hayo, Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alithibitisha kauli yake na Wahyi wa Qur-aan uliteremka kuthibitsha hilo (alilolitaja).

 

4-Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kucheka katika kuthibitisha elimu kubwa aliyoyasema Rabai wa dini ya Kiyahudi. 

 

5-Kutajwa Mikono miwili ya Allaah (سبحانه وتعالى) na kwamba mbingu zitakuwa katika Mkono Wake wa kuume na ardhi katika Mkono Wake wa kushoto.   

 

6- Mkono wa pili uliitwa wa kushoto.

 

7-Pamoja na hayo kumetajwa majabari na wenye kutakabari.

 

8-Kauli kwamba mbingu saba na ardhi katika Mkono wa Allaah (سبحانه وتعالى) zitakuwa kama chembe ya hardali mikononi wa mmoja wenu.

 

9-Ukubwa wa Al-Kursiyy (Kiti cha enzi cha Allaah سبحانه وتعالى) kulingana na mbingu.

 

10-Ukubwa wa Al-‘Arsh kulingana na Al-Kursiyy.

 

11-Kwamba Al-Kursiyyi, maji, na Al-‘Arsh ni vitu tofauti.

 

12-Umbali baina ya mbingu moja na nyingine.

 

13-Umbali baina mbingu ya saba na Al-Kursiyy.

 

14-Umbali baina ya Al-Kursiyy na maji.

 

15-‘Arshi ya Allaah (سبحانه وتعالى) iko juu ya maji.

 

16-Allaah (سبحانه وتعالى) Yuko juu ya Al-‘Arsh.

 

17-Umbali baina ya mbingu na ardhi.

 

18-Unene wa kila mbingu ni masafa ya mwendo wa miaka mia tano.

 

19- Bahari juu ya mbingu ya saba ina kina cha masafa ya mwendo wa miaka mia tano. Na Allaah Anajua zaidi

 

 

AlhamduliLLaah Himdi Anastahiki Allaah (سبحانه وتعالى) Rabb wa walimwengu. Swalaah na Salaam zimshukie Nabiyyunaa Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) na Maswahaba wake wote (رضي الله عنهم).

 

 

 

Share