004-An-Nisaa: Aayah Na Mafunzo

 

 

 

004-An-Nisaa

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Share

001-Aayah Na Mafunzo: Fadhila Za Swillatur-Rahm (Kuunga Undugu) Na Matahadharisho Ya Kukata Undugu

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Fadhila Za Swillatur-Rahm (Kuunga Undugu) Na Matahadharisho Ya Kukata Undugu

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ 

 Enyi watu! Mcheni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume na wanawake wengi. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. Hakika Allaah ni Mwenye kuwachunga daima. [An-Nisaa: 1]

 

Mafunzo:

 

Swillatur-Rahm = Kuunga Undugu Na Jamaa Wenye Uhusiano Wa Damu:

 

Fadhila kadhaa zimetajwa katika Qur-aan na Sunnah za mwenye kuunga undugu na jamaa wenye uhusiano wa damu. Miongoni mwazo ni:

 

عن أنسٍ رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( من أحَبَّ أنْ يُبْسَطَ لَهُ في رِزْقِهِ ، ويُنْسأَ لَهُ في أثَرِهِ ، فَلْيَصِلْ رَحِمَهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa na Anas (Radhwiyah Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayependa akunjuliwe riziki yake, na arefushiwe maisha yake basi aunge kizazi chake." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuud] 

 

Matahadharisho ya kukata undugu: Rejea tanbihi (2: 27) Pia miongoni mwa Hadiyth alizokataza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kukata undugu ni zifuatazo:

 

عن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إنَّ اللهَ تَعَالَى خَلَقَ الخَلْقَ حَتَّى إِذَا فَرَغَ مِنْهُمْ قَامَتِ الرَّحِمُ ، فَقَالَتْ : هَذَا مُقَامُ العَائِذِ بِكَ مِنَ القَطِيعةِ ، قَالَ : نَعَمْ ، أمَا تَرْضَيْنَ أنْ أصِلَ مَنْ وَصَلَكِ ، وَأقْطَعَ مَنْ قَطَعَكِ ؟ قَالَتْ : بَلَى ، قَالَ : فَذَلِكَ لَكِ ، ثُمَّ قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( اقْرَؤُوا إنْ شِئْتمْ : ( فَهَلْ عَسَيْتُمْ إِنْ تَوَلَّيْتُمْ أَنْ تُفْسِدُوا فِي الأَرْضِ وَتُقَطِّعُوا أَرْحَامَكُمْ أُولَئِكَ الَّذِينَ لَعَنَهُمُ اللهُ فَأَصَمَّهُمْ وَأَعْمَى أَبْصَارَهُمْ  ) [ محمد : 22 - 23 ] مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية للبخاري : فَقَالَ الله تَعَالَى : (( مَنْ وَصَلَكِ ، وَصَلْتُهُ ، وَمَنْ  قَطَعَكِ ، قَطَعْتُهُ )) .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) baada ya kuumba viumbe vyote, mpaka Alipomaliza (kukamilisha), yalisimama matumbo (kizazi) na kusema: "Hii ni nafasi ya mtu anayetaka ulinzi  na kinga kutoka  Kwako kwa mwemye kukata (kizazi, na kihitaji ulinzi)." Akasema: "Ndio je huridhiki Kwangu kumuunga anayekuunga, na kumkata mwenye kukukata?" Kikasema: "Ndio (naridhika)." Akaambiwa: "Hilo ni lako." Kisha akasema  Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Someni mkitaka: "Basi huenda nyinyi mkigeuka ndio mfanye ufisadi katika ardhi na kukata jamaa zenu wa uhusiano wa damu? Hao ndio ambao Allaah Amewalaani; Akawafanya viziwi na Akawapofua macho yao." [Muhammad: 22-23] [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: Akasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa): "Anayekuunga, Nitamuunga na anayekukata Nitamkata."

 

 

Pia:

 

عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( لَيْسَ الوَاصِلُ بِالمُكَافِىء ، وَلكِنَّ الوَاصِلَ الَّذِي إِذَا قَطَعَتْ رَحِمُهُ وَصَلَهَا )) رواه البخاري .

Na kutoka kwake Ibn 'Amr bin al-'Aasw (Radhwiyah Allaahu 'anhummaa):  Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayeunga si yule anayetoa anapopewa, lakini anayeunga jamaa ni ambaye jamaa zake wanapomkata, yeye huwaunga." [Al-Bukhaariy, Abu Daawuud na At-Tirmidhiy]

 

Pia,

 

وعن عائشة ، قَالَتْ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( الرَّحِمُ مُعَلَّقَةٌ بِالعَرْشِ تَقُولُ : مَنْ وَصَلَنِي ، وَصَلَهُ اللهُ ، وَمَنْ قَطَعَنِي ، قَطَعَهُ اللهُ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aa'ishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kizazi kimetundikwa katika 'Arshi, kinasema: "Anayeniunga, Allaah atamuunga, na anayenikata, Allaah Atamkata." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share

010-Aayah Na Mafunzo: Kula Mali Ya Yatima Ni Miongoni Mwa Mambo Saba Yanayoangamiza

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kula Mali Ya Yatima Ni Miongoni Mwa Mambo Saba Yanayoangamiza

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَىٰ ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ۖ وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا ﴿١٠﴾

10. Hakika wale wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma hapana shaka kwamba wanakula katika matumbo yao moto, na watauingia moto uliowashwa vikali mno”

 

Mafunzo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه عن النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((اجْتَنِبُوا السَّبْعَ الْمُوبِقَاتِ)) قَالُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَمَا هُنَّ؟  قَالَ: ((الشِّرْكُ بِاللَّهِ وَالسِّحْرُ وَقَتْلُ النَّفْسِ الَّتِي حَرَّمَ اللَّهُ إِلاَّ بِالْحَقِّ وَأَكْلُ الرِّبَا وَأَكْلُ مَالِ الْيَتِيمِ وَالتَّوَلِّي يَوْمَ الزَّحْفِ وَقَذْفُ الْمُحْصَنَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ الْغَافلاَتِ)) متفق عليه

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:((Jiepusheni na mambo saba yanayoangamiza!)) Wakauliza: Ni yepi hayo ee Rasuli wa Allaah? Akasema: ((Ni kumshirikisha Allaah, sihri [uchawi], kuua nafsi Aliyoiharamisha Allaah isipokuwa kwa haki, kula ribaa, kula mali ya yatima, kukimbia wakati wa kupambana na adui na kuwatuhumu uzinifu wanawake Waumini waliohifadhika walioghafilika)). [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share

017-Aayah Na Mafunzo: Kukimbilia Kuomba Tawbah Kabla Ya Mauti

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa Aayah 17-18

Kukimbilia Kuomba Tawbah Kabla Ya Mauti

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّمَا التَّوْبَةُ عَلَى اللَّـهِ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السُّوءَ بِجَهَالَةٍ ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٍ فَأُولَـٰئِكَ يَتُوبُ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿١٧﴾

Hakika tawbah inayokubaliwa na Allaah ni ya wale wanaofanya uovu kwa ujahili kisha wakatubia haraka, basi hao Allaah Anapokea tawbah yao. Na Allaah ni Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

وَلَيْسَتِ التَّوْبَةُ لِلَّذِينَ يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ حَتَّىٰ إِذَا حَضَرَ أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ إِنِّي تُبْتُ الْآنَ وَلَا الَّذِينَ يَمُوتُونَ وَهُمْ كُفَّارٌ ۚ أُولَـٰئِكَ أَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿١٨﴾ 

Lakini tawbah si kwa wale wanaofanya maovu mpaka mauti yanapohudhuria kwa mmoja wao husema: “Hakika mimi sasa nimetubu.” Na wala wale wanaokufa na hali wao ni makafiri. Hao Tumewaandalia adhabu iumizayo. [An-Nisaa: 17-18]

 

Mafunzo:

 

Umuhimu wa kuomba tawbah kabla ya kufika wakati wa kutokupokelewa: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakika Allaah Huikubali tawbah ya mja Wake kabla ya roho kufika kwenye mkoromo wa mauti.” [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na wengineo; Swahiyh At-Tirmidhiy (3537), Swahiyh Ibn Maajah (3449)].

 

Na pia. “Atakayetubu kabla ya kuchomoza jua upande wa Magharibi, Allaah Atamkubalia tawbah yake.” [Muslim].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida ziyada:

 

Tawbah: Hukmu Na Fadhila Zake

 

 

 

 

Share

019-Aayah Na Mafunzo: Maamrisho Ya Kumtendea Wema Mke Na Kuvumiliana

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Maamrisho Ya Kumtendea Wema Mke Na Kuvumiliana

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَحِلُّ لَكُمْ أَن تَرِثُوا النِّسَاءَ كَرْهًا ۖ وَلَا تَعْضُلُوهُنَّ لِتَذْهَبُوا بِبَعْضِ مَا آتَيْتُمُوهُنَّ إِلَّا أَن يَأْتِينَ بِفَاحِشَةٍ مُّبَيِّنَةٍ ۚ وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ۚ فَإِن كَرِهْتُمُوهُنَّ فَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَيَجْعَلَ اللَّـهُ فِيهِ خَيْرًا كَثِيرًا ﴿١٩﴾

Enyi walioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa kuwakirihisha. Na wala msiwazuie kwa inda ili mpokonye baadhi ya vile mlivyowapa isipokuwa wakiwa wamefanya uchafu bayana. Na kaeni nao kwa wema. Na mkiwachukia, basi asaa ikiwa mnachukia jambo na Allaah Akalijaalia kuwa lenye khayr nyingi. [An-Nisaa: 19]

 

Mafunzo:

 

Maamrisho ya kumtendea wema mke yametajwa katika Hadiyth kadhaa za  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) miongoni mwazo ni:

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، عَنِ النَّبِيِّ ـ صلى الله عليه وسلم ـ قَالَ ‏ "‏ خَيْرُكُمْ خَيْرُكُمْ لأَهْلِهِ وَأَنَا خَيْرُكُمْ لأَهْلِي ‏"‏ ‏ رواه الترمذي

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema:  ((Mbora wenu ni yule aliye mbora kwa mke wake, na mimi ni mbora kwa watu wangu wa nyumbani [ahli])) [Swahiyh Ibn Maajah (1621), Swahiyh At-Targhiyb (1925)].

 

 Na pia,

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:  ((أَكْمَلُ الْمُؤْمِنِينَ إِيمَانًا أَحْسَنُهُمْ خُلُقًا  وَخِيَارُكُمْ خِيَارُكُمْ لِنِسَائِهِمْ خُلُقًا)) الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Muumin aliyekamilika iymaan ni aliye na tabia njema kabisa, na wabora wenu ni walio bora kwa wake zao kwa tabia))  [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Swahiyh Hasan]

 

Na kutomchukia: “Muumini mwanaume asimchukue (mke ambaye) ni Muumini, akichukizwa tabia moja, bila shaka ataridhika naye kwa tabia yake nyingine.” [Muslim].

 

Pia Sababun-Nuzuwl: Walikuwa Waarabu zama za Jaahiliyyah pindi anapokufa mwanaume na akaacha mke, basi wale ndugu wa mume wake wanakuwa na haki zaidi kwa mwanamke, na   baadhi yao wakitaka wanamuoa, na wakitaka wanamuozesha, na wakitaka hawamuozeshi, na wao wanakuwa wana haki naye zaidi kuliko hata ndugu zake mwanamke na wazazi wake. Ndipo Allaah (عزّ وجلّ) Akateremsha Aayah hii. [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) ameipokea Al-Bukhaary]. 

 

 

 

 

 

Share

024-Aayah Na Mafunzo: Haramisho La Ndoa Ya Mut’ah

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Haramisho La Ndoa Ya Mut’ah

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ النِّسَاءِ إِلَّا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۖ كِتَابَ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ ۚ وَأُحِلَّ لَكُم مَّا وَرَاءَ ذَٰلِكُمْ أَن تَبْتَغُوا بِأَمْوَالِكُم مُّحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ ۚ فَمَا اسْتَمْتَعْتُم بِهِ مِنْهُنَّ فَآتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةً ۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ فِيمَا تَرَاضَيْتُم بِهِ مِن بَعْدِ الْفَرِيضَةِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿٢٤﴾

24. Na (Mmeharamishiwa pia) wanawake walio katika ndoa isipokuwa iliyowamiliki mikono yenu ya kuume. Ni shariy’ah ya Allaah kwenu. Na mmehalalishiwa wengineo wasiokuwa hao, mtafute (kuwaoa) kwa mali zenu mkijistahi pasi na kuzini. Basi mliostarehe nao, wapeni mahari yao kuwa ni waajib. Na wala si dhambi kwenu katika mliyoridhiana baada ya yaliyowajibika. Hakika Allaah daima ni Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

Mafunzo:

 

Uharamisho wa ndoa ya mut’ah: Sabrah bin Ma’bad Al-Juhniy (رضي الله عنه) amehadithia kwamba baba yake aliandamana na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Fat-hi Makkah akasema: “Enyi watu! Nilikuruhusuni ndoa ya mut’ah hapo mwanzo. Leo Allaah Ameiharamisha mpaka Siku ya Qiyaamah! Basi ikiwa kuna yeyote ambaye ana mke wa ndoa ya mut’ah amwache na wala asichukue chochote katika alichompa.” [Muslim na wengineo].

 

 

 

Share

029-Aayah Na Mafunzo: Anayejiua Ataingizwa Motoni Kwa Hali Ile Ile Kujiua

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Anayejiua Ataingizwa Motoni Kwa Hali Ile Ile  Kujiua

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى)

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَكُم بَيْنَكُم بِالْبَاطِلِ إِلَّا أَن تَكُونَ تِجَارَةً عَن تَرَاضٍ مِّنكُمْ ۚ وَلَا تَقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُمْ رَحِيمًا ﴿٢٩﴾

Enyi walioamini! Msiliane mali zenu kwa ubatilifu, isipokuwa iwe biashara kwa kuridhiana baina yenu. Wala msijiue. Hakika Allaah daima kwenu ni Mwenye kurehemu.

 

وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ عُدْوَانًا وَظُلْمًا فَسَوْفَ نُصْلِيهِ نَارًا ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرًا ﴿٣٠﴾

Na atakayefanya hivyo kwa uadui na dhulma, basi Tutamuingiza motoni. Na hilo kwa Allaah ni mepesi.  [An-Nisaa: 29 - 30]

 

 

Mafunzo:

 

Haramisho la kujiua na tahadharisho la adhabu yake kwamba afanyae hivyo, atakariri kujiua Siku ya Qiyaamah: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Yeyote atakayejitupa kutoka mlimani na kujiua, atatupwa motoni milele. Atakayekunywa sumu na kujiua, basi atatupwa motoni na huko atakuwa akiinywa hiyo sumu milele. Atakayejiua kwa kipande cha chuma, atatiwa motoni akiwa na kipande hicho cha chuma akijitwanga nacho tumboni kwake humo motoni milele.” [Muslim].

 

 

Share

031-Aayah Na Mafunzo: Maana Ya Al-Kabaair (Dhambi Kubwa) Na Mifano Yake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Maana Ya Al-Kabaair Dhambi Kubwa Na Mifano Yake

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَنُدْخِلْكُم مُّدْخَلًا كَرِيمًا ﴿٣١﴾

Mkijiepusha na madhambi makubwa mnayokatazwa Tutakufutieni madhambi yenu madogo na Tutakuingizeni katika mahali patukufu. [An-Nisaa: 31]

 

Mafunzo:

 

Al-Kabaair (dhambi kubwa): ni lile lililotajiwa ndani yake laana, au haddi (adhabu) hapa duniani, au limeahidiwa juu yake ghadhabu za Allaah au moto.

 

Na Nafiy’ bin Al-Haarith Ath-Thaqafiy Abuu Bakr (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Je, nikujulisheni Al-Kabaair?” Tukasema: “Ndio ee Rasuli wa Allaah! Akasema: “Kumshirikisha Allaah, na kuwaasi wazazi wawili.” Alikuwa ameegemea, akakaa kitako akasema: “Tanabahi! Na kusema uongo na kushuhudia uongo!” “Tanabahi! Na kusema uongo na kushuhudia uongo!” Akaendelea kusema hayo mpaka nikadhani hatonyamaza. [Al-Bukhaariy (5976)].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho kwa faida zaidi:

 

Madhambi Makubwa Na Madogo

 

 

 

 

 

Share

034-Aayah Na Mafunzo: Fadhila Za Wanawake Wema Wanaotii Waume Zao Kwa Siri

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Fadhila Za Wanawake Wema Wanaotii Waume Zao Kwa Siri

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

 الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّـهُ بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَبِمَا أَنفَقُوا مِنْ أَمْوَالِهِمْ ۚ فَالصَّالِحَاتُ قَانِتَاتٌ حَافِظَاتٌ لِّلْغَيْبِ بِمَا حَفِظَ اللَّـهُ ۚ وَاللَّاتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَاهْجُرُوهُنَّ فِي الْمَضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ ۖ فَإِنْ أَطَعْنَكُمْ فَلَا تَبْغُوا عَلَيْهِنَّ سَبِيلًا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيًّا كَبِيرًا ﴿٣٤﴾

 

Wanaume ni wasimamizi juu ya wanawake kwa kuwa Allaah Amefadhilisha baadhi yao kuliko wengine na pia kwa ambayo wanatoa katika mali zao. Basi wanawake wema ni wale watiifu wenye kujihifadhi katika hali ya kutokuweko waume zao kwa kuwa Allaah Ameamrisha wajihifadhi. Na wale ambao mnakhofu uasi wao wa ndoa, basi wanasihini na wahameni katika malazi na wapigeni (kipigo kisichodhuru). Wakikutiini, basi msitafute njia dhidi yao (ya kuwaudhi). Hakika Allaah daima ni Mwenye Uluwa, Mkubwa wa dhati, vitendo na sifa. [An-Nisaa: 34]

 

Mafunzo:

 

Kuhusu: “na wahameni katika malazi.” Imekusudiwa kutokulala nao na kutokujimai nao, kwa ujumla ni kuwagomea. Ama kuhusu: “na wapigeni.”  Imekusudiwa kipigo kidogo kisichokuwa cha kumdhuru, wala haipasi kupigwa usoni. Hadiyth imethibitisha:

 

Jaabir (رضي الله عنه) amehadithia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema katika Hijja ya kuaga: “Mcheni Allaah kuhusu wanawake kwani wao ni wasaidizi wenu. Mnayo haki juu yao kuwa wasimruhusu mtu msiyempenda kukanyaga zulia lenu (kuingia katika nyumba) Lakini wakifanya hivyo, mnaruhusiwa kuwatia adabu ndogo. Wao wana haki kwenu kwamba muwatimizie matumizi yao na nguo kwa njia ya kuridhisha.” [Muslim]

 

Fadhila za mke mwema: “Mwanamke atakaposwali Swalaah zake tano, akahifadhi sehemu zake za siri (asifanye uzinifu), akamtii mume wake, ataingia Jannah kupitia mlango wowote autakao.” [Swahiyh At-Targhiyb (1932)].

 

 

Share

036-Aayah Na Mafunzo: Haki Ya Allaah Kwa Waja Wake Na Haki Ya Waja Kwa Allaah

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Haki Ya Allaah Kwa Waja Wake Na Haki Ya Waja Kwa Allaah

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا ۖ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا وَبِذِي الْقُرْبَىٰ وَالْيَتَامَىٰ وَالْمَسَاكِينِ وَالْجَارِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَالْجَارِ الْجُنُبِ وَالصَّاحِبِ بِالْجَنبِ وَابْنِ السَّبِيلِ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ مُخْتَالًا فَخُورًا ﴿٣٦﴾

Na mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe na chochote. Na wafanyieni ihsaan wazazi wawili na jamaa wa karibu, na mayatima, na masikini na jirani mwenye ujamaa na jirani asiye na ujamaa na rafiki wa karibu, na msafiri aliyeishiwa masurufu, na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia. Hakika Allaah Hapendi mwenye majivuno mwenye kujifakharisha. [An-Nisaa: 36]

 

 

Mafunzo:

 

Allaah Anaghufuria dhambi zote isipokuwa shirki. Na Mu’aadh bin Jabal (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Nilikuwa nyuma ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) juu ya punda akasema: “Ee Mu’aadh! Unajua nini haki ya Allaah juu ya waja Wake, na nini haki ya waja juu ya Allaah?” Nikajibu: Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi: Akasema: “Haki ya Allaah kwa waja wake ni kwamba wamwabudu na wasimshirikishe na chochote. Na haki ya waja kwa Allaah ni kwamba Hatomwadhibu yeyote ambaye hamshirikishi na chochote.” Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Niwabashirie watu? Akasema: “Usiwabashirie wasije kuitegemea.” (wakaacha kufanya juhudi katika ‘ibaadah) [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

Share

038-Aayah Na Mafunzo: Kufedheheshwa Siku Ya Qiyaamah Kwa Mwenye Kufanya ‘Amali Kwa Riyaa

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kufedheheshwa Siku Ya Qiyaamah Kwa Mwenye Kufanya ‘Amali Kwa Riyaa

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ رِئَاءَ النَّاسِ وَلَا يُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَلَا بِالْيَوْمِ الْآخِرِ ۗ وَمَن يَكُنِ الشَّيْطَانُ لَهُ قَرِينًا فَسَاءَ قَرِينًا ﴿٣٨﴾

Na wale wanaotoa mali zao kwa kujionyesha kwa watu na wala hawamwamini Allaah wala Siku ya Mwisho. Na yule ambaye shaytwaan amekuwa ni rafiki yake mwandani, basi mbaya alioje rafiki mwandani (huyo). [An-Nisaa: 38]

 

Mafunzo:

 

Maonyo ya kufanya ‘amali kwa riyaa (kujionyesha): Jundub bin ‘Abdillaah bin Sufyaan (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: Mwenye kudhihirisha ‘amali yake kwa riyaa, Allaah Atamfedhehesha Siku ya Qiyaamah, na mwenye kuwafanyia watu riyaa (kwa ‘amali njema ili aonekane ni mtukufu), Allaah Atazidhihirisha siri zake (Siku ya Qiyaamah).” [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Share

041-Aayah Na Mafunzo: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Alipolia Kusikia Qiraa Cha Aayah Hii

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Alipolia Kusikia Qiraa Cha Aayah Hii

Alhidaaya.com

 

 

فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِن كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهِيدٍ وَجِئْنَا بِكَ عَلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ شَهِيدًا ﴿٤١﴾

Basi itakuwaje Tutakapoleta kutoka kila Ummah shahidi, na Tukakuleta (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa shahidi juu ya hawa? [An-Nisaa: 41]

 

Mafunzo:

 

عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه  قال: قال لي النبي صلى الله عليه وسلم ((اقرأ علي)) قلت: يا رسول الله، أقرأ عليك وعليك أُنزلَ؟ قال: ((نعم، إني أحب أن أسمعه من غيري)) فقرأت سورة النساء، حتى أتيت إلى هذه الآية: (( فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِنْ كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهِيدٍ وَجِئْنَا بِكَ عَلَى هَؤُلاءِ شَهِيدًا )) قال: ((حسبك الآن)) فإذا عيناه تَذْرِفَان.

 

Amesimulia ‘Abdullaah bin Mas‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ): Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمَ) aliniambia: “Nisomee!”. Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah! Nikusomee na hali (Qur-aan) imeteremshwa kwako? Akasema: “Naam! Lakini mimi napenda kusikia wengine wakiisoma.” Nikasoma Suwratun-Nisaa mpaka nilipofikia Aayah:

 

فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِن كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهِيدٍ وَجِئْنَا بِكَ عَلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ شَهِيدًا ﴿٤١﴾

“Basi itakuwaje Tutakapoleta kutoka kila ummah shahidi, na Tukakuleta (ee Muhammad صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمَ) kuwa shahidi juu ya hawa?”

 

Akasema: “Hasbuka! (Inatosha, simama hapo).” Nikaona machozi yamejaa machoni mwake. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

 

Share

043-Aayah Na Mafunzo: Kisa Cha ‘Aishah Kuwa Ni Sababu Ya Kuteremshwa Hukmu Ya Tayammum Na Uharamisho Wa Pombe Na Kikomo Chake

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kisa Cha Kidani Cha ‘Aishah (رضي الله عنها)

Ni Sababu Ya Kuteremshwa Hukmu Ya Tayammum

Hatua Za Uharamisho Wa Pombe Na Kikomo Chake

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْرَبُوا الصَّلَاةَ وَأَنتُمْ سُكَارَىٰ حَتَّىٰ تَعْلَمُوا مَا تَقُولُونَ وَلَا جُنُبًا إِلَّا عَابِرِي سَبِيلٍ حَتَّىٰ تَغْتَسِلُوا ۚ وَإِن كُنتُم مَّرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم مِّنَ الْغَائِطِ أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَفُوًّا غَفُورًا ﴿٤٣﴾

Enyi walioamini! Msikaribie Swalaah na hali mmelewa mpaka mjue mnayoyasema, na wala mkiwa mna janaba isipokuwa mmo safarini mpaka muoge josho. Na mkiwa wagonjwa au safarini au mmoja wenu ametoka msalani au mmewagusa wanawake kisha hamkupata maji, basi ikusudieni ardhi safi ya mchanga (mtayammam), mpake nyuso zenu na mikono yenu. Hakika Allaah daima Ni Mwingi wa Kusamehe, Mwingi wa Kughufuria. [An-Nisaa: 43]

 

Mafunzo:

 

Tayammum ni katika mambo matatu tuliyofadhilishwa nayo Ummah wetu wa Kiislamu kwa dalili:  

 

Hudhayfah bin Al-Yamaani (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Tumefadhilishwa juu ya watu matatu; Swafu zetu (katika Swalaah) zimefafanishwa kama swafu za Malaika. Na tumejaaliwa ardhi yote kuwa Masjid, na mchanga wake kwetu ni twahara inapokosekana maji.” [Muslim].

 

Sababu ya kuteremshwa hukmu ya tayammum

 

Mama wa ‘Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها)  amehadithia: “Tulikwenda katika moja ya safari tukafika Al-Baydaa au Dhaatul-Jaysh ambako kidani changu kilivunjika (na kikapotea). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akawa anakitafuta, kisha pia watu wengineo wakainuka kukitafuta. Hapakuweko na maji sehemu hiyo, basi watu wakamwendea Abuu Bakr Asw-Swiddiyq na kusema: Huoni alivyofanya ‘Aaishah? Kamfanya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) pamoja na watu wakae sehemu ambayo hakuna maji! Abuu Bakr akaja wakati Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa amelaa akiwa amelaza kichwa chake mapajani mwangu. Akaniambia: Umemzuia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na watu sehemu ambako hakuna maji na wala hawana (akiba ya) maji. Basi akanigombesha na akasema Aliyomjaalia (Allaah) kusema kuhusu mimi na akanipiga ubavuni kwa mkono wake. Hakuna kilichonizuia kusogea (kutokana na maumivu) isipokuwa kwa vile Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alilala mapajani mwangu. Hapo Allaah Akateremsha Aayah ya tayammum, basi wakatayammam. ‘Usayd bin Al-Hudhwayr akasema: Ee ahli ya Abuu Bakr! Hii si baraka ya kwanza kwenu. Kisha akaendeshwa ngamia ambaye nilikuwa nimempanda na tukakipata kidani chini yake.” [Al-Bukhaariy].

 

Hatua Za Uharamisho Wa Pombe Na Kikomo Chake:

 

Hatua ya kwanza kuhusu pombe imetahadharishwa katika Suwratul-Baqarah (2:219):

 

يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ ۖ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَإِثْمُهُمَا أَكْبَرُ مِن نَّفْعِهِمَا ۗ

Wanakuuliza kuhusu pombe na kamari. Sema: Katika viwili hivyo mna dhambi kubwa na (baadhi ya) manufaa kwa watu. Na dhambi yake viwili hivyo ni kubwa kuliko manufaa yake. [Al-Baqarah (2:219)]

 

Kisha hatua ya pili ilikuwa ni kukatazwa pombe katika nyakati za Swalaah kwa sababu Swahaba walikosea kusoma Qur-aan katika Swalaah kutokana na kulewa. Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha Aayah katika Suwrah An-Nisaa (4:43):  

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْرَبُوا الصَّلَاةَ وَأَنتُمْ سُكَارَىٰ حَتَّىٰ تَعْلَمُوا مَا تَقُولُونَ  

Enyi walioamini! Msikaribie Swalaah na hali mmelewa mpaka mjue mnayoyasema [An-Nisaa (4:43)]

 

Baada ya hapo ikafutwa hukmu hiyo na ikabakia pombe kuwa ni haraam nyakati zote kwa kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu. [Al-Maaidah (5:90)]

 

Baada ya kuteremshwa Aayah hii ya Suwrah Al-Maaidah (5:90), hapo hapo Swahaba wakaacha moja kwa moja kulewa ikawa ndio kikomo cha kunywa pombe.

 

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida nyenginezo kuhusu matahadharisho ya pombe, uharamisho wake, laana na adhabu zake.

 

04-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Al-Huduwd (Adhabu): Mlango Wa Adhabu Ya Mnywaji Pombe Na Kubainisha Kileo (Ni Nini)

 

 

 

 

Share

046-Aayah Na Mafunzo: Mayahudi Na Ahlul-Bid’ah Kupotosha Maana Ya Maneno Ya Qur-aan

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Mayahudi Na Ahlul-Bid’ah Kupotosha Maana Ya Maneno Ya Qur-aan

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مِّنَ الَّذِينَ هَادُوا يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ عَن مَّوَاضِعِهِ وَيَقُولُونَ سَمِعْنَا وَعَصَيْنَا وَاسْمَعْ غَيْرَ مُسْمَعٍ وَرَاعِنَا لَيًّا بِأَلْسِنَتِهِمْ وَطَعْنًا فِي الدِّينِ ۚ وَلَوْ أَنَّهُمْ قَالُوا سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا وَاسْمَعْ وَانظُرْنَا لَكَانَ خَيْرًا لَّهُمْ وَأَقْوَمَ وَلَـٰكِن لَّعَنَهُمُ اللَّـهُ بِكُفْرِهِمْ فَلَا يُؤْمِنُونَ إِلَّا قَلِيلًا ﴿٤٦﴾

Katika Mayahudi wako wanaobadilisha maneno kuyatoa mahali pake, na husema: “Tumesikia” na “Tumeasi”; na (wanamwambia Rasuli): “Sikia bila ya kusikilizwa.” Na (husema): “raa’inaa” kwa kuzipotoa ndimi zao na kutukana Dini. Na lau wangesema: “Tumesikia na tumetii na sikia na “undhwurnaa” ingelikuwa khayr kwao na yenye kufaa zaidi. Lakini Allaah Amewalaani kwa kufru yao; basi hawaamini isipokuwa wachache tu. [An-Nisaa: 46]

 

Mafunzo:

 

Miongoni mwa ada za Mayahudi ni kuyapotosha maneno ya Allaah (عزّ وجلّ) kuyatoa kwenye makusudio yake na pia wanayatafsiri kwa isiyokuwa tafsiri yake. Na watu wa bid’ah wamejifananisha nao katika kupindisha na kupotosha maana ya Majina ya Allaah na Sifa Zake.

 

 

Share

047-Aayah Na Mafunzo: Mukhtasari Wa Historia Ya Mayahudi Kuhusu Kuasi Kwao

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Mukhtasari Wa Historia Ya Mayahudi Kuhusu Kuasi Kwao

Alhidaaya.com

 

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ آمِنُوا بِمَا نَزَّلْنَا مُصَدِّقًا لِّمَا مَعَكُم مِّن قَبْلِ أَن نَّطْمِسَ وُجُوهًا فَنَرُدَّهَا عَلَىٰ أَدْبَارِهَا أَوْ نَلْعَنَهُمْ كَمَا لَعَنَّا أَصْحَابَ السَّبْتِ ۚ وَكَانَ أَمْرُ اللَّـهِ مَفْعُولًا ﴿٤٧﴾

47. Enyi mliopewa Kitabu! Aminini yale Tuliyoyateremsha (kwa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) yanayosadikisha yale mliyonayo, kabla hatujabadilisha nyuso Tukazirudisha kisogoni, au Tukawalaani kama Tulivyowalaani watu wa As-Sabt. Na amri ya Allaah ni ya kufanyika tu. 

 

Mafunzo:

 

 

Ifahamu historia ya Mayahudi kwa mukhtasari namna walivyokuwa jeuri kwa Manabii wao: Mayahudi walikatazwa na Allaah (سبحانه وتعالى) kuvua samaki siku ya As-Sabt (Jumamosi) lakini wao kwa ujeuri wao wakavua samaki siku hiyo na kwa kutumia hila. Pia Allaah (سبحانه وتعالى) Akawakumbusha wajukuu zao kuhusu siku hiyo ya As-Sabt (Jumamosi) ambayo babu zao Mayahudi waliasi ndani yake kiasi kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Aliwageuza kuwa nyani na nguruwe. Na mwenye kusoma visa vya Mayahudi dhidi ya Manabii wao na miongoni mwa swaalihiyna katika wao, atakuta kuwa waliwaudhi mno Manabii wao na wakawapinga na kwenda kinyume nao. Na pia wakafanyia inadi na ujeuri maamrisho ya Allaah (سبحانه وتعالى) na wakawa na ujeuri uliopindukia. Miongoni mwa mifano ya hayo ni; kisa cha ng’ombe na ndama. Pia kutaka kwao kumuona Allaah (سبحانه وتعالى) wazi wazi. Tena hayo wameyafanya baada tu ya kuvukishwa bahari kwa salama na kuokolewa kutona na adui yao Fir-‘awn aliyezamishwa baharini. Pia uasi wao kuwaua baadhi ya Manabii bila ya haki. Na mifano mingine mingi kuhusu uasi na ujeuri wa Mayahudi.

 

 

Share

048-Aayah Na Mafunzo: Allaah Hamghufurii Mja Atakayefariki Bila Ya Kutubia Katika Kumshirikisha

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Allaah Hamghufurii Mja Atakayefariki Bila Ya Kutubia Katika Kumshirikisha 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ وَمَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا ﴿٤٨﴾

Hakika Allaah Haghufurii kushirikishwa; lakini Anaghufuria yasiyokuwa hayo kwa Amtakae. Na yeyote atakayemshirikisha Allaah basi kwa yakini amezua dhambi kuu.

 

Mafunzo:

 

Shirki ni dhambi kubwa ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) Hamghufurii mja wake ikiwa hajatubia kabla ya kufariki kwake. Makemeo mazito yametajwa katika Qur-aan na Sunnah, miongoni mwayo ni Hadiyth zifuatazo:

 

عن ابن مسعود رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((مَنْ مَاتَ يُشْرِكُ بِاللَّهِ شَيْئًا دَخَلَ النَّارَ))  

Kutoka kwa Ibn Mas‘uwd pia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Atakayefariki akiwa katika hali ya kumshirikisha Allaah kwa chochote ataingia Motoni)) [Al-Bukhaariy 1238, Muslim 92]

 

Na pia,

 

 عَن عبدالله بن عمر جاءَ أعرابيٌّ إلى النَّبيِّ صلَّى اللَّهُ عليْهِ وسلَّمَ فقالَ: يا رسولَ اللَّهِ إنَّ أبي كانَ يصِلُ الرَّحمَ وَكانَ وَكانَ فأينَ هوَ؟ قالَ: ((في النَّارِ)) قالَ فَكأنَّهُ وجدَ من ذلِكَ فقالَ: يا رسولَ اللَّهِ فأينَ أبوكَ قالَ رسولُ اللَّهِ صلَّى اللَّهُ عليْهِ وسلَّمَ: ((حيثُما مررتَ بقبرِ مشرِكٍ فبشِّرْهُ بالنَّارِ)) قالَ: فأسلمَ الأعرابيُّ بعدُ وقالَ: لقد كلَّفني رسولُ اللَّهِ صلَّى اللَّهُ عليْهِ وسلَّمَ تعبًا ما مررتُ بقبرِ كافرٍ إلَّا بشَّرتُهُ بالنَّارِ

 ‘Abdullaah bin ‘Umar (رضي الله عنه) amehadithia: Bedui mmoja alikuwa kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Baba yangu alikuwa akiunga undugu na alikuwa akifanya kadhaa wa kadhaa, je, yuko wapi? Akasema: “Motoni.” Ikawa kama kwamba lilikuwa jambo zito kwake. Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Je, kwani baba yako yuko wapi? Akasema: “Utakapopita kaburi la mushrik yeyote mbashirie moto.” Bedui akasilimu baada ya hapo kisha akasema: Hakika Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): amenitwika jukumu gumu kwamba kila nikipata kaburi la kafiri nimbashirie moto.” [Swahiyh Ibn Maajah 1288].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida ziyada:

 

Tawbah: Hukmu Na Fadhila Zake

 

 

 

 

Share

057-Aayah Na Mafunzo: Jannah Kuna Mti Wenye Kivuli Cha Msafara Wa Miaka Mia Moja

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Jannah Kuna Mti Wenye Kivuli Cha Msafara Wa Miaka Mia Moja

Alhidaaya.com

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَنُدْخِلُهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ۖ لَّهُمْ فِيهَا أَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ ۖ وَنُدْخِلُهُمْ ظِلًّا ظَلِيلًا ﴿٥٧﴾

Na wale walioamini na wakatenda mema Tutawaingiza Jannaat zipitazo chini yake mito, ni wenye kudumu humo abadi. Watapata humo wake waliotakasika na Tutawaingiza katika vivuli vya kina. [An-Nisaa: 57]

 

Mafunzo:

 

Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakika Jannah kuna mti, anatembea mwenye kipando chini ya kivuli chake miaka mia moja hakimalizi.” [Al-Bukhaariy].

 

 

 

Share

058-Aayah Na Mafunzo: Amri Ya Kurudisha Amana Kwa Mwenye Haki Nayo

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Amri Ya  Kurudisha Amana Kwa Mwenye Haki Nayo

Na Sababu Ya Kuteremshwa Aayah Hii

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا وَإِذَا حَكَمْتُم بَيْنَ النَّاسِ أَن تَحْكُمُوا بِالْعَدْلِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴿٥٨﴾

Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe. Na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Ni uzuri ulioje wa Anayokuwaidhini kwayo Allaah! Hakika Allaah daima ni Mwenye Kusikia yote, Mwenye Kuona yote. [An-Nisaa: 58]

 

Mafunzo:

 

Umuhimu wa kuweka na kurudisha amana ya mtu:

 

Samurah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Rudisha amana kwa aliyekuaminisha na wala usimfanyie khiyana aliyekukhini.” [Ahmad, Swahiyh Abiy Daawuwd (3535), As-Silsilah Asw-Swahiyhah (423)].

 

Sababun-Nuzuwl, Aayah Pekee Katika Suwrah hii Kuteremswa Makkah.

 

Aayah hii ni ya pekee katika Suwrah hii ya An-Nisaa (4:58) ambayo imeteremka Makkah. Imeteremshwa Siku ya Fat-h Makkah (Ushindi). Ibn Jurayj amehadithia kwamba imeteremshwa kuhusu ‘Uthmaan bin Twalhah pale Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipochukua ufunguo wa Ka’bah kutoka kwake akaingia Ka’bah. Alipotoka nje ya Ka’bah, alitoka huku akiwa anasoma:

 

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا

Hakika Allaah Anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe.”

 

Hapo akamwita ‘Uthmaan bin Twalhah na akampa funguo. [Tafsiyr Ibn Kathiyr]. Funguo hizo zimeendelea kubakia katika ukoo huo, kizazi baada ya kizazi mpaka sasa, na mpaka Siku ya Qiyaamah ukoo huo umefadhilishwa kuwa ndio wenye amana ya kukamata funguo za Al-Ka’bah.

 

 

 

 

 

Share

059-Aayah Na Mafunzo: Amri Na Masisitizo Ya Kuwatii Watawala Na Viongozi

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

 

Amri Na Masisitizo Ya Kuwatii Watawala Na Viongozi

 

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَأُولِي الْأَمْرِ مِنكُمْ ۖ فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۚ ذَٰلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلًا ﴿٥٩﴾

Enyi walioamini! Mtiini Allaah na mtiini Rasuli na wenye madaraka katika nyinyi. Mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allaah na Rasuli mkiwa mnamwamini Allaah na Siku ya Mwisho. Hivyo ni bora na matokeo mazuri zaidi. [An-Nisaa: 59]

 

Mafunzo:

 

Amri Na Masisitizo Ya Kuwatii Watawala Na Viongozi

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ameamrisha na kusisitiza katika Hadiyth kadhaa suala la kutii watawala na viongozi; miongoni mwanzo ni: “Muislamu anapaswa kusikia na kutii kwa anayoyapenda na anayoyachukia, madhali hakuamrishwa kuasi. Na pindi akiamrishwa katika maasi, basi hakuna kusikia wala kutii.” [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

Na amesema pia: “Sikieni na tiini (watawala na viongozi wenu) hata kama ni mtumwa wa Habash ambaye kichwa chake ni kama zabibu.” [Al-Bukhaariy].

 

Amri ya kuwatii kwa wema watawala na viongozi wa mambo ya Waislamu, ni jambo ambalo limenukuliwa na Ijmaa’ juu yake, bali ndiyo ‘Aqiydah iliyokuwa sahihi ya Ahlus-Sunnah wal-Jamaa’ah. Lakini kwa masikitiko makubwa jambo hili wamelipuuza wengi katika Waislamu na wale wasiofahamu mafunzo ya Dini yao. Na matokeo ya kwenda kinyume na jambo hilo na ‘Aqiydah hiyo ni kuleta munkari mkubwa katika Ummah na ufisadi mpana. Kuna wanaofanya maandamano kupinga viongozi, kuna wanaojilipua kwa mabomu na kuua watu, kuna wanaoua watu kwa njia mbali mbali na kadhalika kumwaga damu za wanaadamu bure! Na wametumia njia hiyo maadui wa Uislamu ili kuuchafua Uislamu na kuudidimiza.

 

 

Sababun-Nuzuwl: Aayah hii imeteremka kuhusu ‘Abdullaah Ibn Hudhaafah (رضي الله عنه) pale alipotumwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwenye msafara wa Jihaad. [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) ameipokea Al-Bukhaariy na Muslim].

 

Pia Imeteremshwa pale Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipotuma jeshi chini ya uongozi wa mtu mmoja wa Answaar. Walipoondoka, aliwaghadhibikia kwa sababu fulani akawaambia: Kwani Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakukuamrisheni mnitii? Wakasema: Ndio! Akasema: Okoteni kuni. Kisha akawasha moto akasema: Nakuamrisheni muingie motoni humu. Wakakaribia watu kuuingia lakini kijana mmoja miongoni mwao akasema: Nyinyi mmekimbia moto kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hivyo msikimbilie mpaka mrudi kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kisha akikuamrisheni kuingia hapo muuingie. Waliporudi kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) wakamwelezea yaliyojiri, kisha yeye akasema: “Mngeliuingia, msingetoka kamwe humo. Hakika utiifu ni katika mema.” [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

 

Share

080-Aayah Na Mafunzo: Kumtii Rasuli Ni Kumtii Allaah Na Kumuasi Ni Kumuasi Allaah

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kumtii Rasuli Ni Kumtii Allaah Na Kumuasi Ni Kumuasi Allaah

 

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

مَّن يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللَّـهَ ۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَا أَرْسَلْنَاكَ عَلَيْهِمْ حَفِيظًا ﴿٨٠﴾

Atakayemtii Rasuli basi kwa yakini amemtii Allaah. Na atakayekengeuka basi Hatukukutuma kuwa mlinzi juu yao. [An-Nisaa: 80]

 

Mafunzo:

 

عَنْ أبي هُرَيْرة رضى الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ "‏ مَنْ أَطَاعَنِي فَقَدْ أَطَاعَ اللَّهَ، وَمَنْ عَصَانِي فَقَدْ عَصَى اللَّهَ، وَمَنْ أَطَاعَ أَمِيرِي فَقَدْ أَطَاعَنِي، وَمَنْ عَصَى أَمِيرِي فَقَدْ عَصَانِي ‏"‏‏.‏

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه)  amehadithia kuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Atakayenitii basi atakuwa amemtii Allaah, na atakayeniasi atakuwa amemuasi Allaah, na atakayemtii Amiri wangu (kiongozi niliyemteua), atakuwa amenitii mimi na atakayemuasi atakuwa ameniasi mimi.” [Al-Bukhaariy, Muslim, An-Nasaaiy, Ibn Maajah]

 

Na pia,

 

عَنْ أَبي هريرةَ رضي الله عنه: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((كُلُّ أُمَّتِي يَدخُلُونَ الجَنَّةَ إلا مَنْ أبَى)). قيلَ: وَمَنْ يَأبَى يَا رَسُول الله؟ قَالَ: ((مَنْ أَطَاعَنِي دَخَلَ الجَنَّةَ، وَمَنْ عَصَانِي فَقَدْ أبَى)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amesimulia: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: “Ummah wangu wote wataingia Jannah isipokuwa atakayekataa.” Akaulizwa: Ni yupi atakayekataa Ee Rasuli wa Allaah? Akajibu: “Atakayenitii mimi ataingia Jannah, na atakayeniasi basi amekataa.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

 

 

Share

082-Aayah Na Mafunzo: Radd Kwa Mufawwidhwah Wanaodai Kuwa Sifa Za Allaah Haifahamiki

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

 

Radd Kwa Mufawwidhwah Wanaodai Kuwa Sifa Za Allaah Haifahamiki

 

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ الْقُرْآنَ ۚ وَلَوْ كَانَ مِنْ عِندِ غَيْرِ اللَّـهِ لَوَجَدُوا فِيهِ اخْتِلَافًا كَثِيرًا ﴿٨٢﴾

Je, hawaizingatii Qur-aan? Na lau ingelikuwa imetoka kwa ghairi ya Allaah, bila shaka wangelikuta ndani yake khitilafu nyingi. [An-Nisaa: 82]

 

Mafunzo:

 

Aayah hii ni miongoni mwa dalili na radd juu ya madh-hab ya Al-Mufawwidhwah (wanaokubali sifa ya Allaah lakini wakidai maana yake haijulikani; kwa hivyo, wanamzulia Allaah kuwa kawaletea mafundisho waja Wake ambayo hayajulikani maana yake!) ambao wanasema kuwa Majina ya Allaah na Swifaat Zake hazifahamiki maana yake, na hiyo ni itikadi batili mno, bali Shaykhul-Islaam (رحمه الله)  amesema alipolizungumzia hili pote la Mufawwidhwah kuwa ni katika mapote ya bid’ah yaliyokuwa ya shari. Kisha wakainasibisha kauli hii kuwa ndiyo kauli ya Salaf! Huko ni kuwazulia wema waliotangulia (رحمهم الله). Imaam Ahmad anawaona Mufawwidhwah kuwa ni wabaya zaidi kuliko Jahmiyyah.

 

 

Share

083-Aayah Na Mafunzo: Matahadharisho Ya Kutangaza Khabari Bila Kuhakikisha

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Matahadharisho Ya Kutangaza Khabari Bila Kuhakikisha

Na Sababu Ya Kuteremshwa Aayah Hii

 

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَإِذَا جَاءَهُمْ أَمْرٌ مِّنَ الْأَمْنِ أَوِ الْخَوْفِ أَذَاعُوا بِهِ ۖ وَلَوْ رَدُّوهُ إِلَى الرَّسُولِ وَإِلَىٰ أُولِي الْأَمْرِ مِنْهُمْ لَعَلِمَهُ الَّذِينَ يَسْتَنبِطُونَهُ مِنْهُمْ ۗ وَلَوْلَا فَضْلُ اللَّـهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ لَاتَّبَعْتُمُ الشَّيْطَانَ إِلَّا قَلِيلًا ﴿٨٣﴾

Na linapowafikia jambo lolote la amani au la khofu hulitangaza. Na lau wangelirudisha kwa Rasuli na kwa wenye madaraka kati yao, wangelijua wale wanaotafiti wakabainisha ya sahihi miongoni mwao. Na lau si fadhila ya Allaah juu yenu na rahmah Yake kwa yakini mngelimfuata shaytwaan ila wachache tu. [An-Nisaa: 83]

 

Mafunzo:

 

Matahadhirisho ya kutangaza khabari bila ya uhakikisho: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Inamtosheleza mtu kuwa ni muongo kwa kusema kila anachokisikia.” [Amehadithia Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ameipokea Muslim].

 

Na pia; Al-Mughiyrah bin Shu’bah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Nimemsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: “Hakika Allaah Anachukia kwenu “qiylaa wa qaala” na kupoteza mali na kuuliza maswali mengi.” [Al-Bukhaariy na wengineo]. “Qiylaa wa qaal” kwa maana: “imesemwa na amesema” ni ibaarah inayokusudiwa uvumi, utesi, udaku, umbeya, usengenyaji n.k.

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremka kama alivyohadithia ‘Umar (رضي الله عنه) kwamba: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipojitenga mbali na wake zake, niliingia Masjid nikakuta watu wakipiga ardhi kwa changarawe wakisema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amewataliki wake zake! Na hivyo ni kabla ya kuamrishwa hijaab. ‘Umar akasema: Nitatambua hilo leo. Basi nikamwendea ‘Aaishah  (رضي الله عنها) nikamwambia: Yaa bint Abiy Bakr! Je, hivi imekufikia kumuudhi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)? Akasema: Haijakuhusu jambo kwangu, nami hainihusu jambo kwako yaa bin Al-Khattwaab, juu yako kumuwaidhi (bint yako)! Nikamwendea Hafswah bint ‘Umar nikamwambia: Yaa Hafswah! Imenifikia (khabari) kwamba umemuudhi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na nimetambua kuwa hakupendi! Na lau ningekuwa (si baba yako) angekutaliki! Hafswah akalia sana. Nikamwambia: Yuko wapi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)? Akasema: Yuko chumba cha darini. Nikaenda nikamkuta Rabaah, mtumishi wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amekaa kitako kingoni mwa dirisha akinin’giniza miguu yake juu katika ufumbi wa shina la mtende ambalo likimsaidia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kupanda (chumba cha darini) na kuteremkia. Nikamwambia: Yaa Rabaah! Niombee idhini kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Rabaah akatazama chumbani kisha akanitazama mimi wala hakusema kitu. Kisha nikasema: Yaa Rabaah! Niombee idhini kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Rabaah akatazama chumbani kisha akanitazama mimi wala hakusema kitu. Kisha nikapandisha sauti yangu nikasema: Yaa Rabaah! Niombee idhini kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), mimi nadhani kuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) anadhania kuwa nimekuja kwa ajili ya Hafswah! Wa-Allaahi kama Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ataniamrisha nimpige (nimkate) shingo yake nitampiga! Nikapandisha sauti yangu akaniashiria nipande (kuingia chumba cha darini). Nikaingia kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) nikamkuta amelalia jamvi.

 

Nikakaa kitako akaivuta shuka yake na hakuwa na nyingine (isipokuwa hiyo tu) na jamvi hilo lilimfanyia alama ubavuni mwake. Nikatazama kwa macho yangu hicho kijichumba cha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) nikakuta shayiri kiasi kiasi cha kibaba kimoja na kiasi cha matawi ya mimosa yamewekwa pembeni mwa chumba na mkoba wa ngozi uliobadilishwa rangi. Nikatokwa na machozi (kuona maisha duni anayoishi).

Akasema: “Nini kinachokuliza yaa Ibn Al-Khattwaab?” Nikasema: Ee Nabiyy wa Allaah! Na kwanini nisilie na hali jamvi limekufanyia alama ubavuni mwako na sioni kitu chumbani mwako humu (isipokuwa vitu vichache mno); (Mfalme) Qayswar na Kisraa wanaishi maisha ya kifakhari lakini wewe Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ambaye Amekuteua (Allaah) hichii ndio kijichumba chako? Akasema: “Ee Ibn Al-Khattwaab! Hivi huridhiki kuwa sisi tuna Aakhirah nao wana dunia?” Nikasema: Ndio. Kisha nilipoingia kwanza niliona usoni mwake alama za ghadhabu, basi nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Unatatizwa nini na wanawake? Ungeliwataliki basi hakika Allaah Yuko pamoja nawe, na Malaika Wake na Jibriyl, na Mikaaiyl na mimi, na Abuu Bakr, na Waumini (wote) tuko nawe. Na kichache nilichosema (siku ile) na namhimidi Allaah, nilitaraji kwamba Allaah Atasadikisha kauli yangu. Basi ikateremka Aayah hii ya At-Takhyiyr (chaguo): “Ikiwa nyinyi wawili mtatubia kwa Allaah (ni khayr kwenu) kwani kwa hakika nyoyo zenu zimeelemea (kumchukiza Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم). Na mkisaidiana dhidi yake, basi hakika Allaah Ndiye Mlinzi (na Msaidizi) wake na Jibriyl na Waumini wema, na zaidi ya hayo, Malaika pia watasaidia. Akikutalikini, asaa Rabb Wake Akambadilishia wake bora kuliko nyinyi; Waislamu…” (66: 4- 5) Na walikuwa ni ‘Aaishah bint wa Abuu Bakr na Hafswah ambao walishikilia na kusaidiana (kudai mali) kuliko wake wote wengine wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم). Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Je, umewataliki? Akasema: “Hapana.” Nikasema:  Ee Rasuli wa Allaah! Hakika niliingia Masjid nikakuta Waislamu wanacheza kwa vichangarawe (huku dhana zimewashughulisha) wakisema kuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amewataliki wake zake. Je, niende kuwajulisha kuwa hukuwataliki? Akasema: “Naam ukipenda.” Nikaendelea kuongea naye mpaka (nikatanabahi) alama za ghadhabu zimepotea usoni mwake na mpaka (huzuni yake ikageuka kuwa ni furaha na hivyo) uso wake ukarudi kuwa na bashasha kama kawaida yake, akacheka na meno yake yalikuwa ya kupendeza mno kuliko watu wote! Kisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akateremka, nami nikateremka huku nikikamata shina la mtende, naye Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akateremka (kwa wepesi kabisa) bila ya kukamata chochote mkononi mwake (kujizuilia). Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah! Ulikuwa chumbani mwako siku ishirini na tisa. Akasema: (Mara nyingine) “Mwezi huwa ni siku ishirini na tisa.” Nikasimama mlangoni mwa Masjid nikaita kwa sauti yangu ya juu kabisa: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuwataliki wake zake! Hapo ikataremka Aayah hii: “Na linapowafikia jambo lolote la amani au la khofu hulitangaza. Na lau wangelirudisha kwa Rasuli na kwa wenye madaraka kati yao, wale wanaotafiti miongoni mwao wangelielewa… (4: 83). Ikawa ni mimi niliyetafiti jambo hilo. Na Allaah Akateremsha Aayah ya At-Takhyiyr (At-Tahriym 66: 4 – 5) [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

 

 

Share

086-Aayah Na Mafunzo: Umuhimu Wa Maamkizi Ya Kiislam Na Baadhi Ya Fadhila Zake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Umuhimu Wa Maamkizi Ya Kiislam Na Baadhi Ya Fadhila Zake

Alhidaaya.com

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٍ فَحَيُّوا بِأَحْسَنَ مِنْهَا أَوْ رُدُّوهَا ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَسِيبًا ﴿٨٦﴾

Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo mazuri zaidi kuliko hayo au yarudisheni hayo hayo. Hakika Allaah daima juu ya kila kitu ni Mwenye kuhesabu. [An-Nisaa: 86]

 

 

Mafunzo

 

'Imraan bin Al-Huswayn (رضي الله عنهما) amehadithia: Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamuamkia: "Assalaamu 'Alaykum." (Nabiy) akamrudishia salaam). Kisha yule mtu akaketi. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Kumi.” (kwa maana amepata thawabu kumi). Kisha akaja mtu mwengine, akasema: "Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaah." Naye akamrudishia, kisha yule mtu akaketi, Nabiy akasema: “Ishirini.” Kisha akaja mtu mwengine akasema: "Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh.” Naye akamrudishia kisha akasema: “Thelathini.” [Abuu Daawuwd na At-Trimidhiy na akasema Hadiyth Hasan].

 

Na maamkizi ya Kiislamu ni funguo za Jannah: Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hamtoingia Jannah hadi muamini, na wala hamuwezi kuamini hadi mpendane. Je, nikujulisheni jambo ambalo mtakapolifanya mtapendana? Toleaneni Salaam baina yenu.” [Muslim].

 

Pia katika khutbah yake ya mwanzo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipohajiri Madiynah alisema: “Enyi watu! Enezeni salaam, na lisheni chakula, na swalini watu wakiwa wamelala (Qiyaam), mtaingia Jannah kwa Amani.” [At-Tirmidhiy – Hadiyth Swahiyh].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida tele:

 

Maamkizi Ya Kiislaam: Maamrisho Na Fadhila Zake

 

 

 

Share

092-Aayah Na Mafunzo: Haramisho La Kuua Bila Haki Na Adhabu Zake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Haramisho La Kuua Bila Haki Na Adhabu Zake

 

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ أَن يَقْتُلَ مُؤْمِنًا إِلَّا خَطَأً ۚ وَمَن قَتَلَ مُؤْمِنًا خَطَأً فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ وَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ إِلَّا أَن يَصَّدَّقُوا ۚ فَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ عَدُوٍّ لَّكُمْ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ ۖ وَإِن كَانَ مِن قَوْمٍ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُم مِّيثَاقٌ فَدِيَةٌ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰ أَهْلِهِ وَتَحْرِيرُ رَقَبَةٍ مُّؤْمِنَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ شَهْرَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ تَوْبَةً مِّنَ اللَّـهِ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿٩٢﴾

Na haiwi kwa Muumin amuue Muumin ila kwa kukosea tu. Na atakayemuua Muumin kwa kukosea basi aachilie huru mtumwa Muumin na atoe diya kwa kuifikisha kwa ahli zake, isipokuwa kama wenyewe watasamehe. Na akiwa ni jamaa wa maadui zenu naye ni Muumin, basi (aliyeua) aachilie huru mtumwa Muumin. Na akiwa ni miongoni mwa watu ambao kuna mkataba baina yenu na baina yao, basi wapewe diya watu wake na aachiliwe huru mtumwa Muumin. Asiyepata, afunge Swiyaam miezi miwili mfululizo kuwa ni tawbah kwa Allaah. Na Allaah daima Ni Mjuzi wa yote, Mwenye Hikmah wa yote.

 

وَمَن يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا وَغَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَلَعَنَهُ وَأَعَدَّ لَهُ عَذَابًا عَظِيمًا ﴿٩٣﴾

Na atakayemuua Muumini kwa kusudi, basi jazaa yake ni Jahannam, atadumu humo, na Allaah Atamghadhibikia, Atamlaani na Atamuandalia adhabu kuu. [An-Nisaa: 92-93]

 

 

Mafunzo:

 

Dalili nyingi katika Qur-aan na Sunnah zimeharamisha kuua mtu bila ya haki. Miongoni mwa Ahaadiyth ni:

 

‘Abdullaah bin ‘Amru (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Kutokomea dunia ni kwepesi zaidi kuliko kuua Muislamu.” [Swahiyh An-Nasaaiy (3998)].

 

“Wangeshirikiana watu wa mbinguni na ardhini kumwaga damu ya Muumini, Allaah Angewaingiza motoni.” [Amehadithia Al-Baraa bin ‘Aazib (رضي الله عنه) ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Targhiyb].

 

“Muumini hatoacha kuwa katika Dini yake madamu hajagusa damu ya haramu.” (hajamwaga damu). [Al-Bukhaariy].

 

Na pia kuhusu madhambi saba yanayoangamiza bonyeza kiungo kifuatacho:

 

108-Lu-ulu-un-Manthuwrun: Madhambi Saba Yanayoangamiza

 

 

 

 

 

Share

100-Aayah Na Mafunzo: Anayehajiri Kwa Ajili Ya Allaah Akafariki Ataandikiwa Thawabu Zake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Anayehajiri Kwa Ajili Ya Allaah Akafariki Ataandikiwa Thawabu Zake

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

وَمَن يُهَاجِرْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ يَجِدْ فِي الْأَرْضِ مُرَاغَمًا كَثِيرًا وَسَعَةً ۚ وَمَن يَخْرُجْ مِن بَيْتِهِ مُهَاجِرًا إِلَى اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ يُدْرِكْهُ الْمَوْتُ فَقَدْ وَقَعَ أَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١٠٠﴾

Na anayehajiri katika njia ya Allaah atapata katika ardhi mahali pengi pa kukimbilia kujihifadhi na rizki. Na atakayetoka nyumbani kwake akiwa ni mwenye kuhajiri kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake, kisha mauti yakamfikia, basi ujira wake umehakikika kwa Allaah. Na Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa: 100]

 

Mafunzo:

 

 

عن أَمِيرِ المُؤمِنِينَ أَبي حَفْصٍ عُمَرَ بنِ الخطَّابِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ : سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ:  إِنَّما الأَعْمَالُ بالنِّيَّاتِ وإنَّما لكُلِّ امْرِىءٍ ما نَوَى، فَمَنْ كانَتْ هِجْرَتُهُ إلى اللهِ ورَسُولِهِ فَهِجْرَتُهُ إلى اللهِ ورَسُولِهِ، ومَنْ كانَتْ هِجْرَتُهُ لِدُنْيا يُصِيبُها أو امْرأةٍ يَنْكِحُها فَهِجْرَتُهُ إلى ما هَاجَرَ إليه)).  

Kutoka kwa Amiri wa Waumuni, Abu Hafs 'Umar Ibn Al Khattwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Hakika (kusihi kwa) ‘amali kunategemea niyyah, na kila mtu atapata kwa mujibu wa kile alichokinuia. Kwa hiyo ambaye hijrah yake ni kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake, basi hijrah yake ni kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake. Na ambaye hijrah yake ni kwa ajili ya manufaa ya kidunia au kwa ajili ya kumuoa mwanamke (fulani), basi hijrah yake ni kwa lile aliloliendea.[Amehadithia ‘Umar bin Khatwwaab (رضي الله عنه)  ameipokea Al-Bukhaariy na Muslim].

 

Pia Sababun-Nuzuwl: Ilipoteremka kauli ya Allaah:

 

إِنَّ الَّذِينَ تَوَفَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ ظَالِمِي أَنفُسِهِمْ قَالُوا فِيمَ كُنتُمْ ۖ قَالُوا كُنَّا مُسْتَضْعَفِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ قَالُوا أَلَمْ تَكُنْ أَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةً فَتُهَاجِرُوا فِيهَا ۚ فَأُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ ۖ وَسَاءَتْ مَصِيرًا ﴿٩٧﴾

Hakika wale ambao Malaika wamewafisha, hali wamejidhulumu nafsi zao; (Malaika) watawaambia: “Mlikuwa katika hali gani?” Watasema: “Tulikuwa tukikandamizwa katika ardhi.” (Malaika) Watasema: “Je, kwani ardhi ya Allaah haikuwa ya wasaa mkahajiri? Basi hao makazi yao yatakuwa ni Jahannam, na uovu ulioje mahali pa kuishia. [An-Nisaa: 97]

 

Palikuweko mtu mmoja Makkah akiitwa Dhwamrah, yeye alikuwa ni mgonjwa akaiambia familia yake: “Nitoeni Makkah kwani nahisi joto kali la maradhi.” Familia yake wakamuuliza: “Tukupeleke wapi?” Akaashiria kwa mkono wake kuwa wampeleke Madiynah. Hapo ikateremka Aayah hii:

 

 

وَمَن يُهَاجِرْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ يَجِدْ فِي الْأَرْضِ مُرَاغَمًا كَثِيرًا وَسَعَةً ۚ وَمَن يَخْرُجْ مِن بَيْتِهِ مُهَاجِرًا إِلَى اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ يُدْرِكْهُ الْمَوْتُ فَقَدْ وَقَعَ أَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ ۗ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١٠٠﴾

Na anayehajiri katika njia ya Allaah atapata katika ardhi mahali pengi pa kukimbilia kujihifadhi na rizki. Na atakayetoka nyumbani kwake akiwa ni mwenye kuhajiri kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake, kisha mauti yakamfikia, basi ujira wake umehakikika kwa Allaah. Na Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa: 100]

[Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) ameipokea Ibn Jariyr].

 

 

 

Share

103-Aayah Na Mafunzo: Amri Ya Kuswali Kwa Wakati Wake Na Baadhi Ya Fadhila

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Amri Ya Kuswali Kwa Wakati Wake Na Baadhi Ya Fadhila

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَإِذَا قَضَيْتُمُ الصَّلَاةَ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمْ ۚ فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ ۚ إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا ﴿١٠٣﴾

Mtakapomaliza Swalaah, basi mdhukuruni Allaah mkiwa wima, mmeketi, au mmejinyoosha. Na mtakapopata utulivu, basi simamisheni Swalaah (kama desturi), hakika Swalaah kwa Waumini ni fardhi iliyowekewa nyakati maalumu. (4:103).

 

Mafunzo:

 

Maamrisho ya kutimiza Swalaah kwa wakati wake, na makemeo ya kuipuuza yamesisitizwa katika Qur-aan ana Sunnah na miongoni mwa Hadiyth za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ni:

 

عن عَبْدِ اللَّهِ  ابن مسعود قَالَ سَأَلْتُ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم أَىُّ الْعَمَلِ أَحَبُّ إِلَى اللَّهِ قَالَ ‏"‏ الصَّلاَةُ عَلَى وَقْتِهَا ‏"‏‏.‏ قَالَ ثُمَّ أَىُّ قَالَ ‏"‏ ثُمَّ بِرُّ الْوَالِدَيْنِ ‏"‏‏.‏ قَالَ ثُمَّ أَىُّ قَالَ ‏"‏ الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ ‏"‏‏.‏

 

‘Abdullaah bin Mas'uwd  (رضي الله عنه)  amehadithia kwamba: Nilimuuliza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Ni ‘amali gani inayopendeza kwa Allaah? Akajibu: “Ni kuswali kwa wakati wake.” Nikamuuliza tena: Kisha ni ‘amali gani? Akajibu: “Ni kuwafanyia wema wazazi.” Nikamuuliza tena: Kisha ni ‘amali gani? Akajibu: “Ni kupigana jihaad katika njia ya Allaah.” [Al-Bukhaariy Na Muslim].

 

Amesema pia: “Kitu cha kwanza atakachohesabiwa nacho mja Siku ya Qiyaamah katika ‘amali zake ni Swalaah, ikitengenea atakuwa amefuzu na amefanikiwa, na ikiharibika atakuwa ameshapita patupu na amekhasirika…” [At-Tirmidhy na amesema Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh].

 

'Abdullaah bin 'Amru bin Al-‘Aasw (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)   siku moja alitaja kuhusu Swalaah akasema: “Atakayeihifadhi atakuwa na Nuru na burhaan, na ataokoka Siku ya Qiyaamah, na asiyeihifadhi hatokuwa na Nuru wala burhaan wala hatookoka na Siku ya Qiyaamah atakuwa pamoja na Qaaruwn, Fir'awn, Haamaan na ‘Ubayy bin Khalaf)) [Musnad Ahmad ikiwa na isnaad Swahiyh na amesema Al-Albaaniy Isnaad yake Hasan (Ath-Thamar Al-Mustatwaab (uk. 53)].

 

Buraydah bin Al-Haswiyb  (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akisema: “Mafungamano baina yetu na baina yao (wasio Waislamu) ni Swalaah, atakayeiacha atakuwa amekufuru.” [Ahmad, Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Maajah].

 

Imaam ibn Baaz (رحمه الله) amesema: “Yeyote atakayeweka kengele ya saa makusudi imuamshe baada ya kutoka jua akakosa Swalaah ya Alfajiri, basi mtu huyo amepuuza kuswali kwa wakati wake na hivyo ni kufru kubwa kama walivyokubaliana ‘Ulamaa wengi kwa sababu amekusudia kuswali baada ya jua kutoka. Ni sawa na mtu ambaye anachelewesha kuswali Alfajiri akaiswali karibu na Adhuhuri. [Fataawa Ibn Baaz, Kitaab As-Swalaah 10/374].

 

Kwa faida ziyada bonyeza kiungo kifuatacho:

 

Swalaah - Kuwajibika Na Fadhila Zake

 

 

 

 

 

 

Share

110-Aayah Na Mafunzo: Ukitenda Dhambi Swali Rakaa Mbili Uombe Maghfirah

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Ukitenda Dhambi Swali Rakaa Mbili Uombe Maghfirah

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَمَن يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ يَسْتَغْفِرِ اللَّـهَ يَجِدِ اللَّـهَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١١٠﴾

Na atakayetenda ovu au akajidhulumu nafsi yake, kisha akamwomba Allaah maghfirah; basi atamkuta Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mwenye Kurehemu. [An-Nisaa (4:110)]

 

 

Mafunzo:

 

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ الرَّحْمَنِ بْنُ مَهْدِيٍّ، حَدَّثَنَا شُعْبَةُ، عَنْ عُثْمَانَ بْنِ الْمُغِيرَةِ، قَالَ سَمِعْتُ عَلِيَّ بْنَ رَبِيعَةَ، مِنْ بَنِي أَسَدٍ يُحَدِّثُ عَنْ أَسْمَاءَ، أَوْ ابْنِ أَسْمَاءَ مِنْ بَنِي فَزَارَةَ قَالَ: قَالَ عَلِيٌّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ كُنْتُ إِذَا سَمِعْتُ مِنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ شَيْئًا نَفَعَنِي اللَّهُ بِمَا شَاءَ أَنْ يَنْفَعَنِي مِنْهُ وَحَدَّثَنِي أَبُو بَكْرٍ وَصَدَقَ أَبُو بَكْرٍ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ مَا مِنْ مُسْلِمٍ يُذْنِبُ ذَنْبًا ثُمَّ يَتَوَضَّأُ فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ ثُمَّ يَسْتَغْفِرُ اللَّهَ تَعَالَى لِذَلِكَ الذَّنْبِ إِلَّا غَفَرَ لَهُ وَقَرَأَ هَاتَيْنِ الْآيَتَيْنِ ‏ : (‏وَمَنْ يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ يَسْتَغْفِرْ اللَّهَ يَجِدْ اللَّهَ غَفُورًا رَحِيمًا‏)‏ ‏(‏وَالَّذِينَ إِذَا فَعَلُوا فَاحِشَةً أَوْ ظَلَمُوا أَنْفُسَهُمْ‏)‏ الْآيَةَ

رواه أحمد وابو داود و الترمذى والنسائي - وصححه الألباني في صحيح الترميذي وصحيح الترغيب  

 

‘Aliy bin Abiy Twaalib (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Kila nilioposikia jambo kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), Allaah Huninufaisha kwa Apendayo kuninufaisha. Abuu Bakr amenihadithia, na Abuu Bakr amesadikisha, amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakuna Muislamu yeyote atakayetenda dhambi, kisha akatawadha akaswali rakaa mbili, kisha aombe maghfirah, basi hakuna isipokuwa Allaah Atamghufuria.” Kisha akasoma Aayah mbili hizi:

 

وَمَن يَعْمَلْ سُوءًا أَوْ يَظْلِمْ نَفْسَهُ ثُمَّ يَسْتَغْفِرِ اللَّـهَ يَجِدِ اللَّـهَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١١٠﴾

Na atakayetenda ovu au akajidhulumu nafsi yake, kisha akamwomba Allaah maghfirah; basi atamkuta Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mwenye Kurehemu. [An-Nisaa (4:110)]

 

Na:

 

وَالَّذِينَ إِذَا فَعَلُوا فَاحِشَةً أَوْ ظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ ذَكَرُوا اللَّـهَ فَاسْتَغْفَرُوا لِذُنُوبِهِمْ وَمَن يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلَّا اللَّـهُ وَلَمْ يُصِرُّوا عَلَىٰ مَا فَعَلُوا وَهُمْ يَعْلَمُونَ ﴿١٣٥﴾

Na ambao wanapofanya machafu au wakajidhulumu nafsi zao (kwa maasi), humdhukuru Allaah wakaomba Maghfirah kwa madhambi yao. Na nani anayeghufuria madhambi isipokuwa Allaah. Na hawaendelei katika waliyoyafanya na hali wanajua. [Aal-‘Imraan (3:135)]

 

[Imepokelewa na Ahmad katika Musnad yake, Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, na Imesahihishwa na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Tirmidhiy (406) na Swahiyh At-Targhiyb (680)]

 

Bonyeza viungo vifuatavyo upate faida ziyada:

 

Tawbah: Hukmu Na Fadhila Zake

371-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuomba Maghfirah

 

 

 

 

 

 

Share

114-Aayah Na Mafunzo: Kusuluhisha Baina Ya Watu Ina Daraja Bora Kabisa

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kusuluhisha Baina Ya Watu Ina Daraja Bora Kabisa

Alhidaaya.com

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

لَّا خَيْرَ فِي كَثِيرٍ مِّن نَّجْوَاهُمْ إِلَّا مَنْ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوْ مَعْرُوفٍ أَوْ إِصْلَاحٍ بَيْنَ النَّاسِ ۚ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ فَسَوْفَ نُؤْتِيهِ أَجْرًا عَظِيمًا ﴿١١٤﴾

Hakuna khayr katika minong’ono yao mingi isipokuwa anayeamrisha swadaqah, au mema, au kusuluhisha baina ya watu. Na atakayefanya hivyo kutaka radhi za Allaah, basi Tutampa ujira adhimu. [An-Nisaa: 114]

 

 

Mafunzo:

 

Fadhila za kusuluhisha waliokhasimikiana: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Je, nikujulisheni lililo na daraja bora kuliko Swiyaam na Swalaah (Za Sunnah)  na Swadaqah? Ni kusuluhisha baina ya watu. Na ama kuharibu uhusiano baina (ya watu) ni uharibifu.” [Ahmad na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhy katika Swahiyh Al-Jaami'].

 

Kwa faida ziyada bonyeza viungo vifuatavyo:

 

Fadhila Za Kusuluhisha Waliokhasimiana -1

Fadhila Za Kusuluhisha Waliokhasimiana -2

 

 

 

 

 

 

Share

119-Aayah Na Mafunzo: Laana Ya Allaah Kwa Anayejibadilisha Umbile

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Laana Ya Allaah Kwa Anayejibadilisha Umbile

Alhidaaya.com

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

إِن يَدْعُونَ مِن دُونِهِ إِلَّا إِنَاثًا وَإِن يَدْعُونَ إِلَّا شَيْطَانًا مَّرِيدًا ﴿١١٧﴾

Hawaombi badala Yake isipokuwa miungu ya kike na hawaombi isipokuwa shaytwaan muasi.

 

لَّعَنَهُ اللَّـهُ ۘ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿١١٨﴾

Allaah Amemlaani. Na (shaytwaan) akasema: Kwa hakika nitashika katika waja Wako sehemu maalumu.

 

 

وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا ﴿١١٩﴾

Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio ya kulaghai, na nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawatukuze), na nitawaamrisha watabadili Uumbaji wa Allaah. Na atakayemfanya shaytwaan kuwa rafiki mwandani badala ya Allaah basi kwa yakini amekhasirika khasara bayana.

 

يَعِدُهُمْ وَيُمَنِّيهِمْ ۖ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلَّا غُرُورًا ﴿١٢٠﴾

Anawaahidi na anawashawishi matamanio ya uongo. Na shaytwaan hawaahidi isipokuwa ulaghai tu.

 

أُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَلَا يَجِدُونَ عَنْهَا مَحِيصًا ﴿١٢١﴾

Hao makaazi yao ni Jahannam, na wala hawatopata makimbilio ya kutoka humo. 

[An-Nisaa: 117 - 121]

 

 

Mafunzo:

 

Laana Ya Allaah Kwa Mwenye Kujibadilisha Maumbile: 

 

عَنْ عَلْقَمَةَ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ، لَعَنَ اللَّهُ الْوَاشِمَاتِ، وَالْمُسْتَوْشِمَاتِ، وَالْمُتَنَمِّصَاتِ وَالْمُتَفَلِّجَاتِ لِلْحُسْنِ، الْمُغَيِّرَاتِ خَلْقَ اللَّهِ تَعَالَى، مَالِي لاَ أَلْعَنُ مَنْ لَعَنَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم وَهْوَ فِي كِتَابِ اللَّهِ وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ‏ ‏‏.‏

Amesimulia ‘Alqamah (رضي الله عنه): Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) amesema: Allaah Amewalaani wenye kuchanja, na wenye kuchanjwa, na wenye kunyoa nyusi, na wenye kuchonga meno kwa urembo, na wenye kubadilisha umbile la Allaah (سبحانه وتعالى). Kwa nini nisimlaani yule aliyelaaniwa na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na aliyelaaniwa katika Kitabu cha Allaah?:

 

وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ﴿٧﴾

“Na lolote analokupeni Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) basi lichukueni, na analokukatazeni, basi jiepusheni.” [Al-Hashr (59:7) Hadiyth amepokea Imaam Al-Bukhaariy Kitabu Cha Mavazi (77)]

 

Na katika riwaayah nyingine imetajwa: “Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amemlaani mwenye kuunga na mwenye kuungwa (nywele)…”

 

 

 

Na ni Sababun-Nuzuwl: Sababu ya kuteremka kauli ya Allaah:

 

وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا ﴿١١٩﴾

119. Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio ya kulaghai, na nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawatukuze), na nitawaamrisha watabadili Uumbaji wa Allaah. Na atakayemfanya shaytwaan kuwa rafiki mwandani badala ya Allaah basi kwa yakini amekhasirika khasara bayana. (4:119),

 

imeteremka katika jambo la kuwahasi beberu kuwa ni katika njia ya kumtii shaytwaan. [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) Athaar hii ameipokea Ibn Jariyr]

 

Share

125-Aayah Na Mafunzo: Nabiy Muhammad Kutamani Abuu Bakr Awe Khaliyl Wake Duniani

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  Kutamani Abuu Bakr Awe Khaliyl Wake Duniani

 

 

وَمَنْ أَحْسَنُ دِينًا مِّمَّنْ أَسْلَمَ وَجْهَهُ لِلَّـهِ وَهُوَ مُحْسِنٌ وَاتَّبَعَ مِلَّةَ إِبْرَاهِيمَ حَنِيفًا ۗ وَاتَّخَذَ اللَّـهُ إِبْرَاهِيمَ خَلِيلًا ﴿١٢٥﴾

125. Na nani aliye bora zaidi kwa Dini kuliko yule aliyejisalimisha kwa Allaah naye ni mtendaji mazuri na akafuata mila (Dini) ya Ibraahiym aliyejiengua na upotofu akaelemea Dini ya haki. Na Allaah Amemchukua Ibraahiym kuwa nikipenzi.

 

Mafunzo:

 

Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipotoa khutbah yake ya mwisho alisema: “Ammaa ba’du, enyi watu! Ingekuwa kumfanya khaliyl mtu katika dunia, basi ningelimfanya Abuu Bakr bin Abi Quhaafah kuwa khaliyl wangu, lakini Swahibu wenu ni khaliyl wa Allaah.” (yaani yeye mwenyewe Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم) [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

Share

129-Aayah Na Mafunzo: Tahadharisho La Kumuelemea Mke Mmoja Pekee

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Tahadharisho La Kumuelemea Mke Mmoja Pekee

 

وَلَن تَسْتَطِيعُوا أَن تَعْدِلُوا بَيْنَ النِّسَاءِ وَلَوْ حَرَصْتُمْ ۖ فَلَا تَمِيلُوا كُلَّ الْمَيْلِ فَتَذَرُوهَا كَالْمُعَلَّقَةِ ۚ وَإِن تُصْلِحُوا وَتَتَّقُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١٢٩﴾

129. Na wala hamtoweza kuadilisha baina ya wake japokuwa mkipania. Basi msimili muelemeo wote (kwa mke mmoja) mkamuacha (mwengine) kama kining’inio. Na mkisuluhisha na mkawa na taqwa, basi hakika Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.

 

Mafunzo:

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: Atakayekuwa na wake wawili, kisha akaelemea zaidi kwa mmoja wao, atakuja Siku ya Qiyaamah akipinda upande mmoja (akiuburuza).” [Amehadithia Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ameipokea Abuu Daawuwd].

 

Share

135-Aayah Na Mafunzo: Amrisho La Kutoa Ushahidi Bila Kupendelea Jamaa Tajiri Au Maskini

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Amrisho La Kutoa Ushahidi Bila Kupendelea Jamaa Tajiri Au Maskini  

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ شُهَدَاءَ لِلَّـهِ وَلَوْ عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَوِ الْوَالِدَيْنِ وَالْأَقْرَبِينَ ۚ إِن يَكُنْ غَنِيًّا أَوْ فَقِيرًا فَاللَّـهُ أَوْلَىٰ بِهِمَا ۖ فَلَا تَتَّبِعُوا الْهَوَىٰ أَن تَعْدِلُوا ۚ وَإِن تَلْوُوا أَوْ تُعْرِضُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا ﴿١٣٥﴾

135. Enyi walioamini! Kuweni wenye kusimamisha uadilifu mtoapo ushahidi kwa ajili ya Allaah japokuwa ni dhidi ya nafsi zenu au wazazi wawili, au jamaa wa karibu. Akiwa tajiri au maskini Allaah Anawastahikia zaidi. Basi msifuate hawaa mkaacha kufanya uadilifu. Na mkiupotoa au mkikanusha basi hakika Allaah daima kwa myatendayo ni Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika.

 

Mafunzo:

 

Amrisho la kusimamia na kutoa ushahidi bila ya kupendelea wenye uhusiano wa damu, wala tajiri wala maskini. Imaam As-Sa’diy katika Tafsiyr yake amesema: Allaah (سبحانه وتعالى) Anaamrisha waja Wake Waumini wawe: “Wenye kusimamisha uadilifu mtoapo ushahidi.” Na Al-Qawwwaam ni neno lenye kuzidisha ile sifa ya usimamizi yaani kuweni katika kila hali zenu wenye kusimamia uadilifu ambao ni uadilifu katika haki za Allaah na haki za waja Wake. Hivyo, uadilifu katika haki ya Allaah ni kutotumia neema zake katika maasi yake, bali atumie kwa utii Wake.  Na Al-Qistw (uadilifu) katika haki za bin-Aadam ni kutimiza haki zote ambazo ziko juu yako kama ambavyo unavyozitaka haki zako (upatiwe au utekelezewe). Utatoa matumizi ya wajibu, (utalipia) madeni, na utaamiliana na watu kama ambavyo unavyopenda waamiliane na wewe, kwa akhlaaq na malipo na mengine yasiyo hayo.

 

 

 

Share

140-Aayah Na Mafunzo: Kufanyia Istihzai Jambo La Dini Linamtoa Mtu Nje Ya Uislamu

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Kufanyia Istihzai Jambo La Dini Linamtoa Mtu Nje Ya Uislamu

 

 

وَقَدْ نَزَّلَ عَلَيْكُمْ فِي الْكِتَابِ أَنْ إِذَا سَمِعْتُمْ آيَاتِ اللَّـهِ يُكْفَرُ بِهَا وَيُسْتَهْزَأُ بِهَا فَلَا تَقْعُدُوا مَعَهُمْ حَتَّىٰ يَخُوضُوا فِي حَدِيثٍ غَيْرِهِ ۚ إِنَّكُمْ إِذًا مِّثْلُهُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ جَامِعُ الْمُنَافِقِينَ وَالْكَافِرِينَ فِي جَهَنَّمَ جَمِيعًا ﴿١٤٠﴾

140. Na kwa yakini Amekwishakuteremshieni katika Kitabu kwamba mnaposikia Aayaat za Allaah zinakanushwa na zinafanyiwa istihzai, basi msikae pamoja nao mpaka waingie katika mazungumzo mengineyo. Au sivyo mtakuwa kama wao. Hakika Allaah Atawakusanya wanafiki na makafiri wote pamoja katika Jahannam.

 

Mafunzo:

 

Miongoni mwa yanayomtoa mtu nje ya Uislamu ni kufanyia istihzai Maneno ya Allaah (سبحانه وتعالى)! Ni kama ilivyotajwa katika Nawaaqidhw Al-Islaam: “Mwenye kufanyia istihzai (shere, dhihaka, masikhara) kwa chochote katika Dini ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) au akafanya utani katika thawabu au katika adhabu za Allaah, basi amekufuru.” [Muhammad bin ‘Abdil-Wahhaab, Nawaaqidhw Al-Islaam]

 

Ni tahadharisho kubwa kwa Waislamu kwani wengi katika mabaraza yao wakati wanaongea hupenda kufanya istihzai wakidhania kuwa ni jambo la kawaida ilhali hatari yake ni kubwa mno! Rejea At-Tawbah (9:64-66)

 

 

Share

142-Aayah Na Mafunzo: Anayemshirikisha Allaah Kwa Riyaa Hatoipokea 'Amali Yake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Anayemshirikisha Allaah Kwa Riyaa Hatoipokea 'Amali Yake

 

إِنَّ الْمُنَافِقِينَ يُخَادِعُونَ اللَّـهَ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا قَامُوا إِلَى الصَّلَاةِ قَامُوا كُسَالَىٰ يُرَاءُونَ النَّاسَ وَلَا يَذْكُرُونَ اللَّـهَ إِلَّا قَلِيلًا ﴿١٤٢﴾

142. Hakika wanafiki (wanadhani) wanamhadaa Allaah, na hali Yeye (Allaah) Ndiye Mwenye kuwahadaa. Na wanaposimama kuswali husimama kwa uvivu, wakijionyesha kwa watu na wala hawamdhukuru Allaah isipokuwa kidogo tu.

 

Mafunzo:

 

Matahadharisho ya riyaa: Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ameahadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Allaah (تعالى) Anasema: ‘‘Mimi ni Mwenye kujitosheleza kabisa, Sihitaji msaada wala mshirika. Kwa hiyo, yule afanyaye ‘amali kwa kunishirikisha na mtu, Nitaikanusha pamoja na mshirika wake.” Yaani: hatopata ujira wowote kwa ‘amali hiyo. [Muslim (2985), Ibn Maajah (4202)].

 

Aksema pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): “Mwenye kudhihirisha ‘amali yake kwa riyaa, Allaah Atamfedhehesha Siku ya Qiyaamah, na mwenye kuwafanyia watu riyaa (kwa ‘amali njema ili aonekane ni mtukufu), Allaah Atazidhihirisha siri zake (Siku ya Qiyaamah).”  [Al-Bukhaariy, Muslim].

 

 

 

 

Share

143-Aayah Na Mafunzo: Mdhabidhabina Ni Mtu Muovu Kabisa Ni Mwenye Nyuso Mbili

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Mdhabidhabina Mtu Muovu Kabisa Ni Mwenye Nyuso Mbili  

 

 

 

 

 مُّذَبْذَبِينَ بَيْنَ ذَٰلِكَ لَا إِلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ وَلَا إِلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ ۚ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَلَن تَجِدَ لَهُ سَبِيلًا ﴿١٤٣﴾

143. Madhabidhabina baina ya hayo (iymaan na kufru), huku hawako wala huko hawako. Na ambaye Allaah Amempotoa huwezi kumpatia njia (ya kumwongoa).

 

Mafunzo:

 

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mtawakuta watu wana asili wanaonasibika nazo (wa jinsia tofauti tofauti na asili tofauti tofauti); wabora wao katika ujaahiliyyah ndio wabora wao katika Uislamu watakapokuwa na ‘ilmu ya shariy’ah za Dini. Na mtamkuta mbora wa watu katika jambo hili (la uongozi) ni mwenye kulichukia mno, na mtamkuta muovu wa watu ni mwenye nyuso mbili, ambaye anawaendea hawa kwa uso huu, na anawaendea wale kwa uso mwingine.” [Al-Bukhaariy na Muslim]. 

 

 

Share

148-Aayah Na Mafunzo: Haifai Muislamu Kubishana Kwa Sauti Hadharani

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Haifai Muislamu Kubishana Kwa Sauti Hadharani

 

 

لَّا يُحِبُّ اللَّـهُ الْجَهْرَ بِالسُّوءِ مِنَ الْقَوْلِ إِلَّا مَن ظُلِمَ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ سَمِيعًا عَلِيمًا ﴿١٤٨﴾

148. Allaah Hapendi uovu utajwe hadharani isipokuwa kwa yule aliyedhulumiwa. Na Allaah daima ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote.

 

Mafunzo:

Haitakiwi kwa Muislamu, mabishano ya sauti hadharani isipokuwa ikiwa mtu amedhulumiwa haki yake na anaidai.

 

 

Share

157-Aayah Na Mafunzo: Nabiy ‘Iysaa Amenyanyuliwa Mbinguni Na Atateremka Kabla Qiyaamah

 

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

  Nabiy ‘Iysaa Amenyanyuliwa Mbinguni Na Atateremka Kabla Qiyaamah

 

Alhidaaya.com

 

 

 Kauli Zake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 وَقَوْلِهِمْ إِنَّا قَتَلْنَا الْمَسِيحَ عِيسَى ابْنَ مَرْيَمَ رَسُولَ اللَّـهِ وَمَا قَتَلُوهُ وَمَا صَلَبُوهُ وَلَـٰكِن شُبِّهَ لَهُمْ ۚ وَإِنَّ الَّذِينَ اخْتَلَفُوا فِيهِ لَفِي شَكٍّ مِّنْهُ ۚ مَا لَهُم بِهِ مِنْ عِلْمٍ إِلَّا اتِّبَاعَ الظَّنِّ ۚ وَمَا قَتَلُوهُ يَقِينًا ﴿١٥٧﴾

Na kusema kwao (kwa kujifaharisha): Hakika sisi tumemuua Al-Masiyh ‘Iysaa mwana wa Maryam, Rasuli wa Allaah. Na hawakumuua wala hawakumsulubu lakini walishabihishiwa tu. Na hakika wale waliokhitilafiana katika hayo, kwa hakika wamo katika shaka nayo. Hawana ujuzi nalo kabisa isipokuwa kufuata dhana tu. Na kwa yakini hawakumuua. 

 

بَل رَّفَعَهُ اللَّـهُ إِلَيْهِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَزِيزًا حَكِيمًا ﴿١٥٨﴾

Bali Allaah Alimnyanyua Kwake. Na Allaah daima Ni Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye hikmah wa yote.  

 

 

وَإِن مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ إِلَّا لَيُؤْمِنَنَّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكُونُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا ﴿١٥٩﴾

Na hakuna yeyote katika Watu wa Kitabu ila atamwamini kabla ya kufa kwake. Na Siku ya Qiyaamah atakuwa shahidi juu yao.

[An-Nisaa (4:157-159)]

 

Mafunzo:

 

Hizi ni Aayah dalili zinazothibitisha kwamba Nabiy ‘Iysaa (عليه السلام) hakufishwa bali amenyanyuliwa na Allaah mbinguni.

 

Pia ni dalili bayana kwa wanaokanusha kuteremka kwa Nabiy ‘Iysaa (عليه السلام) zama za mwisho kukaribia Qiyaamah kama ni dalili mojawapo kubwa ya kutokea Qiyaamah. Nabiy ‘Iysaa ('Alayhis-Salaam) atateremka kutoka mbinguni kuja duniani kama ni miongoni mwa alama kubwa za Qiyaamah. Na pia kuna Ahaadiyth nyingi nyingine za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) zimethibiti baadhi yake ni:

 

((وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ لَيُوشِكَنَّ أَنْ يَنْزِلَ فِيكُمْ ابْنُ مَرْيَمَ حَكَمًا مُقْسِطًا)) 

((Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu iko Mikononi Mwake, hivi karibuni atateremka kwenu mwana wa Maryam ('Iysaa) akiwa ni kiongozi muadilifu)). [Al-Bukhaariy, Muslim].

 

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu iko Mikononi Mwake, hivi karibuni atateremka kwenu mwana wa Maryam ('Iysaa) akiwa ni kiongozi muadilifu na atavunja misalaba, na kuua nguruwe, na ataondosha jizyah (ushuru kutoka kwa wasio Waislamu ambao wamo katika himaya ya serikali ya Waislamu). Kisha kutakuwa na mali nyingi hadi itafikia kuwa hakuna mtu wa kupokea sadaka. Wakati huu sijda moja itakuwa ni bora kwao kuliko maisha haya na yote yaliyomo (katika dunia).” Kisha Abuu Huraryah akasema: Someni mkipenda:

 

وَإِن مِّنْ أَهْلِ الْكِتَابِ إِلَّا لَيُؤْمِنَنَّ بِهِ قَبْلَ مَوْتِهِ ۖ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكُونُ عَلَيْهِمْ شَهِيدًا ﴿١٥٩﴾

Na hakuna yeyote katika Watu wa Kitabu ila atamwamini kabla ya kufa kwake. Na Siku ya Qiyaamah atakuwa shahidi juu yao.  (4: 159)   [Al-Bukhaariy]

 

 

Na pia:

 

Na pia: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mtakuwaje atakapoteremka Al-Masiyh, mwana wa Maryam (‘Iysaa) akiwa Imaam wenu miongoni mwenu wenyewe?” [Al-Bukhaariy].

 

Na pia amesema Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Manabii ni bin-‘ammi, mama zao tofauti, lakini Dini yao moja. Mimi ndiye mwenye haki zaidi kwa ‘Iysaa mwana wa Maryam kuliko yeyote mwengine, kwani hakukuwa na Nabiy baina yake na mimi. Atateremka na mtakapomuona mtamtambua. Ni mtu aliyeumbika vizuri, (rangi ya ngozi yake) baina nyekundu na nyeupe. Atateremka akiwa amevaa nguo mbili ndefu, rangi ya njano isiyokoza. Kichwa chake kitakuwa kina michirizi ya matone ya maji, japokuwa umande haukugusa. Atavunja misalaba, ataua nguruwe, ataondosha jizyah na atawaita watu katika Uislamu. Wakati huu, Allaah Ataangamiza dini zote isipokuwa Uislamu na Allaah Atamuangamiza Masiyh-Dajjaal. Usalama utajaa ardhini, hadi kwamba simba watachanganyika na ngamia, chui na ng'ombe, fisi na kondoo, watoto watacheza na nyoka na hawatowadhuru. ‘Iysaa atabakia muda wa miaka arubaini kisha atafariki, na Waislamu watamswalia Swalaah ya janaazah.” [Abuu Daawuwd, Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’ (2182)]

 

Maelezo zaidi rejea kiungo kifuatacho:

 

055-Nabiy ‘Iysaa ('Alayhis-Salaam) Hakufa Na Atakuwa Katika Alama Za Qiyaamah

 

 

 

 

Share

164-Aayah Na Mafunzo: Swiffah Ya Al-Kalaam Maneno Imethibiti Kwa Allaah

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Swiffah Ya Al-Kalaam Maneno Imethibiti Kwa Allaah

 

 

 

 

 

وَرُسُلًا قَدْ قَصَصْنَاهُمْ عَلَيْكَ مِن قَبْلُ وَرُسُلًا لَّمْ نَقْصُصْهُمْ عَلَيْكَ ۚ وَكَلَّمَ اللَّـهُ مُوسَىٰ تَكْلِيمًا ﴿١٦٤﴾

 Na Rusuli Tuliokwishakusimulia kabla, na Rusuli (wengine) Hatukukusimulia. Na bila shaka Allaah Alimsemesha Muwsaa maneno moja kwa moja. [An-Nisaa: (5:164)]

 

Mafunzo:

 

Aqiydah Ya Ahlus-Sunnah Wal-Jamaa’ah Kuhusiana Na Majina Mazuri Kabisa Ya Allaah (سبحانه وتعالى) Na Sifa Zake:

 

Allaah (سبحانه وتعالى)  Alimsemesha Muwsaa (عليه السلام)  Maneno kwa uhakika wake na si kwa majazi kama wanavyosema watu wa bid’ah,  bali ni maneno yaliyojengeka kwa herufi na sauti. Na Sifa ya Maneno ni Sifa iliyothibiti kwa Allaah kwa uhakika wake bila kuifanyia Ta'twiyl (kuzipinga, kukanusha uwezekano), wala Tamthiyl (kumithilisha, kufafanisha, kulinganisha), wala Takyiyf (kuainisha maana na kuziulizia namna yake au kuuliza ni vipi Sifa hiyo ipo, kuchunguza ni kwa “namna gani” zimefungamana au kuambatana na Allaah), wala Tahriyf (kubadilisha maana, kupotosha Sifa ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kutoa maana isiyo sahihi).

 

Na hii ndiyo kauli ya sawa ambayo wamepita kwayo Salaf na Maimamu wa haki katika Uislamu katika Sifa Zote zilizokuja ndani ya Qur-aan na Sunnah.  

 

 

 

Share

171-Aayah Na Mafunzo: Nabiy ‘Iysaa Na Mama Yake Ni Waja Wa Allaah Si Washirika Wake

Aayah Na Mafunzo

An-Nisaa

Nabiy ‘Iysaa Na Mama Yake Ni Waja Wa Allaah Si Washirika Wake

Alhidaaya.com

 

 

 

يَا أَهْلَ الْكِتَابِ لَا تَغْلُوا فِي دِينِكُمْ وَلَا تَقُولُوا عَلَى اللَّـهِ إِلَّا الْحَقَّ ۚ إِنَّمَا الْمَسِيحُ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ رَسُولُ اللَّـهِ وَكَلِمَتُهُ أَلْقَاهَا إِلَىٰ مَرْيَمَ وَرُوحٌ مِّنْهُ ۖ فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرُسُلِهِ ۖ وَلَا تَقُولُوا ثَلَاثَةٌ ۚ انتَهُوا خَيْرًا لَّكُمْ ۚ إِنَّمَا اللَّـهُ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ ۖسُبْحَانَهُ أَن يَكُونَ لَهُ وَلَدٌ ۘ لَّهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿١٧١﴾

 

Enyi Watu wa Kitabu! Msipindukie mipaka katika dini yenu, wala msimzungumzie Allaah isipokuwa ukweli. Hakika Al-Masiyh ‘Iysaa mwana wa Maryam ni Rasuli wa Allaah na ni Neno Lake (la Kun!) Alompelekea Maryam na Ruwh (roho Aliyoumba kwa amrisho) kutoka Kwake. Basi mwaminini Allaah na Rusuli Wake; wala msiseme: ‘watatu’. Komeni, ni khayr kwenu. Hakika Allaah ni Mwabudiwa wa haki Mmoja Pekee, Utakasifu ni Wake kuwa ana mwana! Ni Vyake vyote vilivyomo mbinguni na vyote vilivyomo ardhini. Na Anatosheleza Allaah kuwa Ni Mtegemewa wa yote. [An-Nisaa (4:171)]

 

Mafunzo:

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Amewakataza Watu wa Kitabu wasimfanye ‘Iysaa na Mama yake kuwa ni washirika wa Allaah bali hao ni waja wawili katika waja wema wa Allaah na si washirika Wake kama Anavyosema Allaah (سبحانه وتعالى) Akimzungumzia ‘Iysaa (عليه السلام) katika Suwrat Maryam (19: 30-36) Na pia katika Suwratul-Maaidah (5: 17, 72-76). 

 

Pia ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mwenye kushuhudia kuwa laa ilaaha illa Allaah - hapana muabudiwa wa haki isipokuwa Allaah Pekee, Hana mshirika na kwamba Muhammad ni mja wake na Rasuli Wake, na kwamba ‘Iysaa ni mja wa Allaah na Rasuli Wake, na Neno Lake (la Kun!) Aliloliweka kwa Maryam na roho ni kutoka Kwake (Ameiumba), na Jannah ni haki, na moto ni haki, Allaah Atamuingiza Jannah kwa amali zozote alizonazo." [Al-Bukhaariy]. Na katika riwaayah nyingine: “Ataingizwa Jannah katika milango minane ataingia katika wowote aupendao.” [Muslim].

 

Na pia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amekataza kutukuzwa kupindukia kiasi amesema: “Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi na mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Rasuli Wake)) [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Share