005-Al-Maaidah: Aayah Na Mafunzo

 

 

 

 

 

 

005-Al-Maaidah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Share

003-Aayah Na Mafunzo: Mayahudi Kuithamini Aayah Leo Nimekukamilishieni Dini yenu…

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Mayahudi Kuithamini Aayah Leo Nimekukamilishieni Dini yenu…

Alhidaaya.com

 

 

حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ وَلَحْمُ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ لِغَيْرِ اللَّـهِ بِهِ وَالْمُنْخَنِقَةُ وَالْمَوْقُوذَةُ وَالْمُتَرَدِّيَةُ وَالنَّطِيحَةُ وَمَا أَكَلَ السَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى النُّصُبِ وَأَن تَسْتَقْسِمُوا بِالْأَزْلَامِ ۚ ذَٰلِكُمْ فِسْقٌ ۗ الْيَوْمَ يَئِسَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن دِينِكُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِ ۚ الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ فَمَنِ اضْطُرَّ فِي مَخْمَصَةٍ غَيْرَ مُتَجَانِفٍ لِّإِثْمٍ ۙ فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣﴾

Mmeharamishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na kilichotajiwa asiyekuwa Allaah katika kuchinjwa kwake, na (pia) mnyama aliyekufa kwa kukosa hewa au aliyepigwa akafa, au aliyeporomoka toka juu, au aliyepigwa pembe, na aliyeliwa na mnyama mwitu, isipokuwa mliyewahi kumchinja kihalali (kabla ya kufa), na waliochinjwa kwa ajili ya ‘ibaadah ya waabudiwa, na kupiga ramli kwa mishale. Hayo kwenu ni ufasiki. Leo wamekata tamaa wale waliokufuru na Dini yenu, basi msiwaogope, bali Niogopeni Mimi. Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekuridhieni Uislamu uwe Dini yenu. Basi atakayelazimika katika njaa kali bila kulalia kwenye dhambi (akala vilivyoharamishwa), basi hakika Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mwenye Kurehemu. [Al-Maaidah (5:3)]

 

Mafunzo:

 

Aayah Ambayo Ingeliteremshwa Kwa Mayahudi, Wangelisherehekea Siku Iliyoteremshwa:

 

‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه)  amehadithia kwamba Myahudi mmoja alimwambia: Ee Amiri wa Waumini, lau ingeliteremka kwetu sisi Aayah hii:

 

الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ

Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekuridhieni Uislamu uwe Dini yenu.  (5:3).

 

basi tungeliifanya kuwa ni siku ya kusherehekea. ‘Umar akasema: Wa-Allaahi, naijua siku gani imeteremka Aayah hii. Imeteremka Siku ya ‘Arafah siku ya Ijumaa. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Share

024-Aayah Na Mafunzo: Kulinganisha Jibu Kati Ya Mayahudi Na Maswahaba Kwa Nabii Wao

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Kulinganisha Jibu Kati Ya Mayahudi Na Maswahaba Kwa Nabii Wao

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

قَالُوا يَا مُوسَىٰ إِنَّا لَن نَّدْخُلَهَا أَبَدًا مَّا دَامُوا فِيهَا ۖ فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ ﴿٢٤﴾

24. Wakasema: “Ee Muwsaa!  Hakika sisi hatutoingia humo abadani madamu watabakia humo, basi nenda wewe na Rabb wako mkapigane, hakika sisi tunakaa hapa hapa.”

 

Mafunzo:

 

Kulinganisha jibu la Mayahudi kwa Nabiy wao Muwsaa (عليه السلام) na jibu la Swahaba kwa Nabiy wao (صلى الله عليه وآله وسلم) katika vita vya Badr: ‘Abdullaah bin Mas’uwd (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Nimeshuhudia kutoka kwa Al-Miqdaad bin Al-Aswad (رضي الله عنه) tukio ambalo laiti ningelikuwa mimi ndio muhusika wa tukio hilo ingependeza mno kwangu kuliko kulikosa. Miqdaad bin Al-Aswad alimwendea Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamkuta akiwaombea washirikina du’aa ya maangamizi. Miqdaad akasema kumwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Wa-Allaahi Ee Rasuli wa Allaah, hatutosema sisi kama walivyosema baniy Israaiyl kumwambia Muwsaa:

 

فَاذْهَبْ أَنتَ وَرَبُّكَ فَقَاتِلَا إِنَّا هَاهُنَا قَاعِدُونَ ﴿٢٤﴾

“basi nenda wewe na Rabb wako mkapigane, hakika sisi tunakaa hapa hapa”, lakini sisi tutapigana jihaad kuliani mwako na kushotoni mwako na mbele yako na nyuma yako.”  Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) akasema: Nikaona uso wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) umejawa na bashasha na akiwa amefurahishwa na hayo maneno. [Al-Bukhaariy].

 

 

Share

027-Aayah Na Mafunzo: Tahadharisho La Kuazimia Kuua Au Kuuana

 

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Tahadharisho La Kuazimia Kuua Au Kuuana

 

Alhidaaya.com

 

 

 

وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ ابْنَيْ آدَمَ بِالْحَقِّ إِذْ قَرَّبَا قُرْبَانًا فَتُقُبِّلَ مِنْ أَحَدِهِمَا وَلَمْ يُتَقَبَّلْ مِنَ الْآخَرِ قَالَ لَأَقْتُلَنَّكَ ۖ قَالَ إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ اللَّـهُ مِنَ الْمُتَّقِينَ ﴿٢٧﴾

Na wasomee khabari ya wana wawili wa Aadam kwa haki walipotoa dhabihu ya kafara, ikakubaliwa ya mmoja wao lakini ya mwengine haikukubaliwa. (Asiyekubaliwa) akasema: Nitakuua tu!  (Aliyekubaliwa) akasema: Hakika Allaah Anatakabalia wenye taqwa. [Al-Maaidah: 27]

 

Mafunzo:

 

Tahadharisho la kuazimia kuua au kuuana: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Waislamu wawili watakapokabiliana kwa panga zao, basi wote wawili; muuaji na aliyeuliwa wataingia motoni.” [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

 

 

Share

030-Aayah Na Mafunzo: Anayeua Kwa Dhulma Atabeba Dhambi Za Mwana Wa Kwanza Wa Aadam

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Anayeua Kwa Dhulma Atabeba Dhambi Za Mwana Wa Kwanza Wa Aadam

 

Alhidaaya.com

 

 

فَطَوَّعَتْ لَهُ نَفْسُهُ قَتْلَ أَخِيهِ فَقَتَلَهُ فَأَصْبَحَ مِنَ الْخَاسِرِينَ ﴿٣٠﴾

Basi nafsi yake ikamwezesha kwa wepesi kumuua ndugu yake, akamuua na akawa miongoni mwa waliokhasirika. [Al-Maaidah: 30]

 

Mafunzo:

 

Kutoka kwa Ibn Mas’uwd (رضي الله عنه) ya kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: “Hakuna nafsi yeyote inayouliwa kwa dhulma isipokuwa yule mwana-Aadam wa kwanza atapata sehemu yake ya madhambi (ya mauaji) kwani yeye ndiye wa mwanzo kuanzisha mauaji (alipomuua nduguye).” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

 

 

 

Share

050-Aayah Na Mafunzo: Watu Watatu Wenye Kuchukiza Zaidi Kwa Allaah

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Watu Watatu Wenye Kuchukiza Zaidi Kwa Allaah

Alhidaaya.com

 

 

 أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ ۚ وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّـهِ حُكْمًا لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ ﴿٥٠﴾

50. Je, wanataka hukumu

za kijahiliya? Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu kwa watu wenye yakini.

 

Mafunzo:

 

Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amehadithia kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Watu wenye kuchukiza zaidi kwa Allaah ni; Mweye kufanya uovu katika Al-Haram (Makkah), mwenye kutafuta katika Uislamu mwenendo wa jaahiliyyah, (enzi za ujinga kabla ya Uislamu) na mwenye kutafuta damu ya mtu ili aimwage bila ya haki.” [Al-Bukhaariy].

 

 

 

Share

067-Aayah Na Mafunzo: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Ametimiza Risalah

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Ametimiza Risalah

 

 Alhidaaya.com

 

 

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٦٧﴾

Ee Rasuli! Balighisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukubalighisha ujumbe Wake. Na Allaah Atakuhifadhi na watu. Hakika Allaah Haongoi watu makafiri. [Al-Maaidah: 67]

 

Mafunzo:

 

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ametimiza Risala: Hakika Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliifikisha na kuitangaza Dini ya Allaah (سبحانه وتعالى) na akaieneza da’wah yake mpaka ikawafikia majini na watu.  Na akawafundisha yote aliyoyaweka Allaah (سبحانه وتعالى) kuwa ni shariy’ah. Akausimamia uwajibu huu kwa nguvu zote, na Allaah (سبحانه وتعالى) Hakumfisha mpaka Alipoinyoosha kupitia yeye dini iliyopindishwa na Akayafungua kupitia yeye macho yenye upofu na kuzifungua nyoyo zilizokuwa zimefunikwa na ujinga.

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Bonyeza kiungo kifuatacho:

 

067-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 067: وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ

 

 

 

 

 

Share

090-Aayah Na Mafunzo: Hatua Za Uharamisho Wa Pombe, Laana Ya Allaah Na Adhabu Zake

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Hatua Za Uharamisho Wa Pombe, Laana Ya Allaah Na Adhabu Zake

Na Sababu Ya Kuteremshwa Aayah

 

Alhidaaya.com

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu. [Al-Maaidah: 90]

 

Mafunzo:

 

 

 

 

 Hatua Za Uharamisho Wa Pombe Na Kikomo Chake:

 

Rejea Al-Baqarah (2 :219), An-Nisaa (4 :43).

 

Hatua ya kwanza kuhusu pombe ni swali alouliza Swahaba na jibu lake katika Suwratul-Baqarah (2:219):

يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ ۖ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَإِثْمُهُمَا أَكْبَرُ مِن نَّفْعِهِمَا ۗ

Wanakuuliza kuhusu pombe na kamari. Sema: Katika viwili hivyo mna dhambi kubwa na (baadhi ya) manufaa kwa watu. Na dhambi yake viwili hivyo ni kubwa kuliko manufaa yake. [Al-Baqarah (2:219)]

 

Hatua ya pili ilikuwa ni kukatazwa pombe katika nyakati za Swalaah kwa sababu Swahaba walikosea kusoma Qur-aan katika Swalaah kutokana na kulewa. Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha Aayah katika Suwrah An-Nisaa (4:43):  

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْرَبُوا الصَّلَاةَ وَأَنتُمْ سُكَارَىٰ حَتَّىٰ تَعْلَمُوا مَا تَقُولُونَ  

Enyi walioamini! Msikaribie Swalaah na hali mmelewa mpaka mjue mnayoyasema [An-Nisaa (4:43)]

 

Hatua ya tatu ndipo ilipofutwa hukmu hizo na ikabakia pombe kuwa ni haraam nyakati zote kwa kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu.

 

إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ ﴿٩١﴾

Hakika shaytwaan anataka kukutilieni baina yenu uadui na bughudha katika pombe na kamari na akuzuieni kumdhukuru Allaah na Swalaah, basi je mtakoma? [Al-Maaidah (5:90-91)]

 

Baada ya kuteremshwa Aayah hizo za Suwrah Al-Maaidah (5:90,91), hapo hapo Swahaba wakaacha moja kwa moja kulewa ikawa ndio kikomo cha kunywa pombe.

 

 

Hadiyth Za Matahadharisho Na Uharamisho Wa Pombe, Laana Ya Allaah Na Adhabu Zake:

 

 

Watu Kumi Wamelaaniwa Wanaohusika Na Pombe:

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amelaani aina ya watu kumi wanaohusika na pombe amesema: “Mwenye kugema pombe, mwenye kutaka afanyiwe, mwenye kunywa, na mwenye kubeba, mwenye kubebewa, mwenye kunywesha, mwenye kuuza, mwenye kula thamani yake, mwenye kununua, na mwenye kununuliwa.” [At-Tirmidhiy na Ibn Maajah].

 

Bonyeza kiungo kifuatacho upate faida nyenginezo kuhusu matahadharisho ya pombe, uharamisho wake, laana na adhabu zake:

 

04-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Al-Huduwd (Adhabu): Mlango Wa Adhabu Ya Mnywaji Pombe Na Kubainisha Kileo (Ni Nini)

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Pia Aayah za Suwrah Al-Maaidah (5:90,91), zimeteremshwa kuwazungumzia makabila mawili katika Answaar. Walikunywa pombe mpaka wakalewa mno kisha wakagombana na kuchafuana baadhi yao kwa baadhi mpaka athari zikawa zinaonekana katika nyuso zao. Kisha pale ulevi ulipowaondokea na akili zao zikawarejea, viliingia vinyongo katika nyoyo zao, hapo zikateremka Aayah hizi zinazoharamisha pombe moja kwa moja:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu. [Al-Maaidah (5:90)]

 

إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ ﴿٩١﴾

Hakika shaytwaan anataka kukutilieni baina yenu uadui na bughudha katika pombe na kamari na akuzuieni kumdhukuru Allaah na Swalaah; basi je mtakoma? [Al-Maaidah (5:90-91)]

 

 

[Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) – amepokea Ibn Jariyr]

 

 

 

Share

101-Aayah Na Mafunzo: Msiyadadisi Mambo Ambayo Allaah Amenyamazia

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Msiyadadisi Mambo Ambayo Allaah Amenyamazia

Alhidaaya.com

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿١٠١﴾

Enyi walioamini! Msiulizie mambo ambayo mkifichuliwa yatakuchukizeni. Na mkiyaulizia pale inapoteremshwa Qur-aan mtafichuliwa. Allaah Ameyasamehe hayo. Na Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mvumilivu.

 

 

قَدْ سَأَلَهَا قَوْمٌ مِّن قَبْلِكُمْ ثُمَّ أَصْبَحُوا بِهَا كَافِرِينَ ﴿١٠٢﴾

Walikwishayauliza hayo watu wa kabla yenu, kisha kutokana nayo, wakawa makafiri. [Al-Maaidah: 101-102]

 

 

Mafunzo:

 

Abuu Tha’labah Al-Khushaniy (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Allaah تعالى Amefaridhisha mambo ya Dini kwa hivyo msiyapuuze. Akaweka mipaka basi msiivuke, na Amekataza baadhi ya mambo kwa hivyo msiyafanye, na yale ambayo Amenyamazia ni kwa ajili ya rahmah Zake kwenu, si kwamba Ameyasahau kwa hivyo msiyadadisi.” [Ad-Daaraqutwniy na wengineo; Hadiyth Hasan].

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Bonyeza kiungo kifuatacho:

 

101-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 101: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ

 

 

 

 

Share

105-Aayah Na Mafunzo: Usipoizuia Dhulma Allaah Hukaribia Kukudhibu

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Usipoizuia Dhulma Allaah Hukaribia Kukuadhibu

Alhidaaya.com

 

 

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ ۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ ۚ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿١٠٥﴾

105. Enyi walioamini! Jiangalieni nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotoka ikiwa mmeongoka. Kwa Allaah Pekee ni marejeo yenu nyote, kisha Atakujulisheni kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.

 

 

Mafunzo:

 

Abuu Bakr Asw-Swiddiyq (رضي الله عنه) amesema: Enyi watu! Hakika nyinyi mnaisoma Aayah hii:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا عَلَيْكُمْ أَنفُسَكُمْ ۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا اهْتَدَيْتُمْ ۚ إِلَى اللَّـهِ مَرْجِعُكُمْ جَمِيعًا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿١٠٥﴾

Enyi walioamini! Jiangalieni nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotoka ikiwa mmeongoka. Kwa Allaah Pekee ndio marejeo yenu nyote, kisha Atakujulisheni yale mliyokuwa mkiyatenda. [Al-Maaidah (5 :105)]

 

Hakika mimi nimemsikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: "Watu pindi watakapomuona mfanya dhulma na wakawa hawakumzuwia na hiyo dhulma, basi wafahamu kuwa  Allaah Hukaribia kuwaadhibu wote kwa adhabu itokayo Kwake.”  [At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Hadiyth Swahiyh]

 

 

Share