165-Asbaabun-Nuzuwl: Aal-'Imraan Aayah 165: أَوَلَمَّا أَصَابَتْكُم مُّصِيبَةٌ قَدْ أَصَبْتُم مِّثْلَيْهَا قُلْتُمْ أَنَّىٰ هَـٰذَا

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Aal-‘Imraan  165-Ulipokusibuni msiba ingawa mliwasibu (maadui) mara mbili yake

 

أَوَلَمَّا أَصَابَتْكُم مُّصِيبَةٌ قَدْ أَصَبْتُم مِّثْلَيْهَا قُلْتُمْ أَنَّىٰ هَـٰذَا ۖ قُلْ هُوَ مِنْ عِندِ أَنفُسِكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٦٥﴾

165. Ulipokusibuni msiba ingawa mliwasibu (maadui) mara mbili yake mlisema: “Umetoka wapi huu?” Sema: “Huo ni kutoka kwenu wenyewe.” Hakika Allaah juu ya kila kitu ni Muweza

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremshwa kuhusu makafiri kutokana na wao kulipiza kisasi cha yale yaliyowasibu katika vita vya Badr. Wakauawa Waislamu sabini siku ya Uhud, yakavunjwa meno ya mbele ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), na likavunjwa yai juu ya kichwa chake, na damu zikachuruzika juu ya uso wake. Na hapo ikateremka Kauli ya Allaah:

 

أَوَلَمَّا أَصَابَتْكُم مُّصِيبَةٌ قَدْ أَصَبْتُم مِّثْلَيْهَا قُلْتُمْ أَنَّىٰ هَـٰذَا ۖ قُلْ هُوَ مِنْ عِندِ أَنفُسِكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١٦٥﴾

 

Ulipokusibuni msiba ingawa nyinyi mliwasibu (maadui) mara mbili yake mlisema: Umetoka wapi huu? Sema: Huo ni kutoka kwenu wenyewe. [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) na imepokelewa na Ahmad].

 

 

 

Share