005-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah

 

 

 

 

 

Sababu Za Kuteremshwa

(Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Suwrah Al-Maaidah

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

 

Share

006-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 006: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Al-Maaidah    006-Sababu ya kuteremshwa hukmu ya tayammum:

 

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ ۚ وَإِن كُنتُمْ جُنُبًا فَاطَّهَّرُوا ۚ وَإِن كُنتُم مَّرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم مِّنَ الْغَائِطِ أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُم مِّنْهُ ۚ مَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيَجْعَلَ عَلَيْكُم مِّنْ حَرَجٍ وَلَـٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمْ وَلِيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٦﴾

Enyi walioamini!  Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah, osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka kwenye visugudi, na panguseni (kwa kupaka maji) vichwa vyenu na (osheni) miguu yenu hadi vifundoni. Na mkiwa na janaba basi jitwaharisheni. Na mkiwa wagonjwa au mko safarini au mmoja wenu ametoka msalani, au mmewagusa wanawake, kisha hamkupata maji, basi ikusudieni ardhi safi ya mchanga (mtayammam), panguseni kwayo nyuso zenu na mikono yenu. Allaah Hataki kukufanyieni magumu, lakini Anataka kukutwaharisheni na Akutimizieni Neema Yake juu yenu ili mpate kushukuru.

 

Sababun-Nuzuwl

 

Sababu Ya Kuteremshwa Hukmu Ya Tayammum (Kuikusudia Ardhi Safi Ya Mchanga Kwa Ajili Ya Wudhuu):

 

Mama wa ‘Waumini ‘Aaishah (رضي الله عنها) amehadithia: “Tulikwenda katika moja ya safari tukafika Al-Baydaa au Dhaatul-Jaysh ambako kidani changu kilivunjika (na kikapotea). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akawa anakitafuta, kisha pia watu wengineo wakainuka kukitafuta. Hapakuweko na maji sehemu hiyo, basi watu wakamwendea Abuu Bakr Asw-Swiddiyq na kusema: Huoni alivyofanya ‘Aaishah? Kamfanya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) pamoja na watu wakae sehemu ambayo hakuna maji! Abuu Bakr akaja wakati Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa amelaa akiwa amelaza kichwa chake mapajani mwangu. Akaniambia: Umemzuia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) na watu sehemu ambako hakuna maji na wala hawana (akiba ya) maji. Basi akanigombesha na akasema Aliyomjaalia (Allaah) kusema kuhusu mimi na akanipiga ubavuni kwa mkono wake. Hakuna kilichonizuia kusogea (kutokana na maumivu) isipokuwa kwa vile Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alilala mapajani mwangu. Hapo Allaah Akateremsha Aayah ya tayammum (kutia Wudhuu kwa mchanga), basi wakatayammam. ‘Usayd bin Al-Hudhwayr akasema: Ee ahli ya Abuu Bakr! Hii si baraka ya kwanza kwenu. Kisha akaendeshwa ngamia ambaye nilikuwa nimempanda na tukakipata kidani kilichokuwa (kimejificha) chini yake.” [Al-Bukhaariy]

 

 

Share

033-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 033: إِنَّمَا جَزَاءُ الَّذِينَ يُحَارِبُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَادًا

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

Al-Maaidah  033-Hakika jazaa ya wale wanaompiga vita Allaah na Rasuli Wake na wakapania kufanya ufisadi...

 

 

إِنَّمَا جَزَاءُ الَّذِينَ يُحَارِبُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ وَيَسْعَوْنَ فِي الْأَرْضِ فَسَادًا أَن يُقَتَّلُوا أَوْ يُصَلَّبُوا أَوْ تُقَطَّعَ أَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم مِّنْ خِلَافٍ أَوْ يُنفَوْا مِنَ الْأَرْضِ ۚ ذَٰلِكَ لَهُمْ خِزْيٌ فِي الدُّنْيَا ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿٣٣﴾

Hakika jazaa ya wale wanaompiga vita Allaah na Rasuli Wake na wakapania kufanya ufisadi katika ardhi, wauawe au wasulubiwe au ikatwe mikono yao na miguu yao kwa kutofautisha au watolewe katika nchi. Hiyo ndiyo hizaya yao duniani. Na Aakhirah watapata adhabu kuu. (5:33)

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremshwa  kama ifuatavyo: 

 

Amesimulia Anas (رضي الله عنه): Watu wanane toka ‘Ukal walikuja kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  wakampa Bay-‘a ya kuulinda Uislamu na kuwa Waislamu wema. Hali ya hewa (ya Madiynah) haikuwapenda wakaugua. Wakamlalamikia hilo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Rasuli akawaambia: “Basi si ingekuwa vyema mkitoka na mchungaji wa ngamia wetu mkapata kunywa maziwa yao na mikojo yao?” Wakakubali na kutoka. Wakanywa maziwa na mikojo, na afya zao zikatengemaa vizuri. Walipokuwa hivyo, walimuuwa mchungaji na kutoroka na ngamia. Habari hiyo ikamfikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Akatuma watu kwenda kuwasaka, wakawapata na wakaletwa kwake. Akaamuru wakatwe mikono yao na miguu yao, na wapofuliwe macho (kwa kuwa walimpofua mchungaji). Kisha wakatelekezwa juani mpaka wakafa.

[Amehadithia Anas bin Maalik (رضي الله عنه)   na imepokelewa na Abuu Daawuwd katika Kitaab Al-Huduwd]

 

Faida: Maana ya Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَوْ تُقَطَّعَ أَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم مِّنْ خِلَافٍ

au ikatwe mikono yao na miguu yao kwa kutofautisha.

 

Ni kukatwa mikono ya kulia kwa miguu ya kushoto au miguu ya kushoto kwa mikono ya kulia.

 

Share

041-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 041: يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ لَا يَحْزُنكَ الَّذِينَ يُسَارِعُونَ فِي الْكُفْرِ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Al-Maaidah   041- Ee Rasuli, wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia kukufuru…

 

 

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ لَا يَحْزُنكَ الَّذِينَ يُسَارِعُونَ فِي الْكُفْرِ مِنَ الَّذِينَ قَالُوا آمَنَّا بِأَفْوَاهِهِمْ وَلَمْ تُؤْمِن قُلُوبُهُمْ ۛ وَمِنَ الَّذِينَ هَادُوا ۛ سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ سَمَّاعُونَ لِقَوْمٍ آخَرِينَ لَمْ يَأْتُوكَ ۖ يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ مِن بَعْدِ مَوَاضِعِهِ ۖ يَقُولُونَ إِنْ أُوتِيتُمْ هَـٰذَا فَخُذُوهُ وَإِن لَّمْ تُؤْتَوْهُ فَاحْذَرُوا ۚ وَمَن يُرِدِ اللَّـهُ فِتْنَتَهُ فَلَن تَمْلِكَ لَهُ مِنَ اللَّـهِ شَيْئًا ۚ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ لَمْ يُرِدِ اللَّـهُ أَن يُطَهِّرَ قُلُوبَهُمْ ۚ لَهُمْ فِي الدُّنْيَا خِزْيٌ ۖ وَلَهُمْ فِي الْآخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿٤١﴾

Ee Rasuli! Wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia kukufuru, miongoni mwa wasemao kwa midomo yao: Tumeamini na hali nyoyo zao hazikuamini. Na miongoni mwa Mayahudi wako wanaosikiliza kwa makini kwa ajili ya uongo, wanaosikiliza kwa makini kwa ajili ya watu wengine wasiokufikia. Wanageuza maneno kutoka mahali pake wanasema: Mkipewa haya yachukueni, na msipopewa hayo basi jihadharini! Na yule ambaye Allaah Anataka kumtia mtihanini, hutokuwa na uwezo wowote (kusaidia) kwa ajili yake mbele ya Allaah. Hao ndio ambao Allaah Hakutaka kuzitakasa nyoyo zao. Watapata hizaya duniani na Aakhirah watapata adhabu kuu.

 

سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ أَكَّالُونَ لِلسُّحْتِ ۚ فَإِن جَاءُوكَ فَاحْكُم بَيْنَهُمْ أَوْ أَعْرِضْ عَنْهُمْ ۖ وَإِن تُعْرِضْ عَنْهُمْ فَلَن يَضُرُّوكَ شَيْئًا ۖ وَإِنْ حَكَمْتَ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِالْقِسْطِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٤٢﴾

 (Hao ni) wenye kusikiliza kwa makini uongo, walaji haramu kwa pupa. Basi wakikujia wahukumu baina yao au wapuuze. Na ukiwapuuza, hawatowe za kukudhuru chochote. Na kama ukihukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika Allaah Anapenda wafanyao uadilifu.

 

 

وَكَيْفَ يُحَكِّمُونَكَ وَعِندَهُمُ التَّوْرَاةُ فِيهَا حُكْمُ اللَّـهِ ثُمَّ يَتَوَلَّوْنَ مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ ۚ وَمَا أُولَـٰئِكَ بِالْمُؤْمِنِينَ ﴿٤٣﴾

Na vipi watakufanya wewe kuwa hakimu wao na hali wana Tawraat yenye Hukumu ya Allaah ndani yake, kisha baada ya hayo wanakengeuka? Na hao si wenye kuamini.

 

 

إِنَّا أَنزَلْنَا التَّوْرَاةَ فِيهَا هُدًى وَنُورٌ ۚ يَحْكُمُ بِهَا النَّبِيُّونَ الَّذِينَ أَسْلَمُوا لِلَّذِينَ هَادُوا وَالرَّبَّانِيُّونَ وَالْأَحْبَارُ بِمَا اسْتُحْفِظُوا مِن كِتَابِ اللَّـهِ وَكَانُوا عَلَيْهِ شُهَدَاءَ ۚ فَلَا تَخْشَوُا النَّاسَ وَاخْشَوْنِ وَلَا تَشْتَرُوا بِآيَاتِي ثَمَنًا قَلِيلًا ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ ﴿٤٤﴾

Hakika Sisi Tumeteremsha Tawraat yenye mwongozo na nuru ambayo Manabii waliojisalimisha kikamilifu (kwa Allaah), pamoja na wanachuoni waswalihina na mafuqahaa weledi, wanawahukumia kwayo Mayahudi. Kwa sababu wao wamebebeshwa jukumu la kutakwa kukilinda na kukihifadhi Kitabu cha Allaah, na wakawa mashahidi juu yake. Basi msiwaogope watu, bali Niogopeni Mimi, na wala msibadilishe Aayaat Zangu kwa thamani ndogo. Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio makafiri.

 

 

وَكَتَبْنَا عَلَيْهِمْ فِيهَا أَنَّ النَّفْسَ بِالنَّفْسِ وَالْعَيْنَ بِالْعَيْنِ وَالْأَنفَ بِالْأَنفِ وَالْأُذُنَ بِالْأُذُنِ وَالسِّنَّ بِالسِّنِّ وَالْجُرُوحَ قِصَاصٌ ۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِ فَهُوَ كَفَّارَةٌ لَّهُ ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿٤٥﴾

Na Tumewaandikia Shariy’ah humo kwamba nafsi kwa nafsi, na jicho kwa jicho, na pua kwa pua, na sikio kwa sikio, jino kwa jino, na majaraha ni kisasi. Lakini atakayesamehe kwa kutolea swadaqah basi itakuwa ni kafara kwake. Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio madhalimu.

 

 

وَقَفَّيْنَا عَلَىٰ آثَارِهِم بِعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ ۖ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ فِيهِ هُدًى وَنُورٌ وَمُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ مِنَ التَّوْرَاةِ وَهُدًى وَمَوْعِظَةً لِّلْمُتَّقِينَ ﴿٤٦﴾

Na Tukamfuatishia katika njia yao (Manabii hao), ‘Iysaa mwana wa Maryam akisadikisha yale yaliyoko kabla yake katika Tawraat. Na Tukampa Injiyl yenye mwongozo na nuru ndani yake, inasadikisha yale yaliyokuwa kabla yake katika Tawraat, na Tumeifanya mwongozo na mawaidha kwa wenye taqwa.

 

 

وَلْيَحْكُمْ أَهْلُ الْإِنجِيلِ بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فِيهِ ۚ وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ ﴿٤٧﴾

Na watu wa Injiyl wahukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah ndani yake. Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio mafasiki. (5:41-47)

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

 

Aayah hii na zinazofuatia (5:41-47) zimeteremka kama alivyohadithia Al-Baraa bin ‘Aazib (رضي الله عنه)  kwamba: Myahudi mmoja aliyejaa weusi usoni na aliyepigwa mijeledi alipita kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم). Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwita akamuuliza: “Je, hivyo ndivyo mlivyokuta (shari’yah) katika Kitabu chenu kuhusu hadd (adhabu) ya mzinifu?” Wakasema: Ndio. Akamwita mtu mmoja miongoni mwa wanachuoni wao akasema: “Nakuuliza kwa kuapia Jina la Allaah Ambaye Ameteremsha Tawraat kwa Muwsaa; je, hivyo ndivyo mnavyokuta hadd ya mzinifu katika Kitabu chenu?” Akasema: Hapana! Usingeniuliza hilo kwa kuapia Jina la Allaah, nisingelikuelezea. (Ni kweli) Tunaikuta Ar-Rajm (adhabu ya kupigwa mawe mpaka kufa) kama ilivyo shari’yah katika Tawraat lakini jarima imezoeleka kwa watu wetu wenye hadhi tu. Hivyo, tunapomkamata tajiri (aliyezini) tunamuachia (huru), lakini tukimkamata aliye duni tunamsimamishia adhabu ya hadd. Kisha tukasema: Njooni tukubaliane (adhabu) tutakayoisimamisha kwa wote, matajiri na walio duni. Hivyo tukaamua kumpaka (mzinifu) masinzi usoni na kumpiga mijeledi badala ya rajm. Hapo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Ee Allaah, hakika mimi wa kwanza kuihuisha Amri Yako wakati wao (Mayahudi) wameifisha. Basi akaamrisha, na (mkhalifu huyo) akasimamishiwa rajm. Hapo Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha:

 

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ لَا يَحْزُنكَ الَّذِينَ يُسَارِعُونَ فِي الْكُفْرِ مِنَ الَّذِينَ قَالُوا آمَنَّا بِأَفْوَاهِهِمْ وَلَمْ تُؤْمِن قُلُوبُهُمْ ۛ وَمِنَ الَّذِينَ هَادُوا ۛ سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ سَمَّاعُونَ لِقَوْمٍ آخَرِينَ لَمْ يَأْتُوكَ ۖ يُحَرِّفُونَ الْكَلِمَ مِن بَعْدِ مَوَاضِعِهِ ۖ يَقُولُونَ إِنْ أُوتِيتُمْ هَـٰذَا فَخُذُوهُ  

Ee Rasuli! Wasikuhuzunishe wale wanaokimbilia kukufuru, miongoni mwa wasemao kwa midomo yao: Tumeamini na hali nyoyo zao hazikuamini. Na miongoni mwa Mayahudi wako wanaosikiliza kwa makini kwa ajili ya uongo, wanaosikiliza kwa makini kwa ajili ya watu wengine wasiokufikia. Wanageuza maneno kutoka mahali pake wanasema: Mkipewa haya yachukueni.,

 

Ikasemwa na Mayahudi: Nendeni kwa Muhammad, akikuamrisheni kukupakeni masinzi na kupigwa mijeledi basi pokeeni, lakini akikupeni hukumu ya rajm, basi tahadharini (jiepusheni). Hapo Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha:

 

وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْكَافِرُونَ ﴿٤٤﴾

.Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio makafiri. (5:44).

 

وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ ﴿٤٥﴾

Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio madhalimu. (5:45).

 

 

وَمَن لَّمْ يَحْكُم بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ ﴿٤٧﴾

Na yeyote asiyehukumu kwa yale Aliyoyateremsha Allaah, basi hao ndio mafasiki. (5:47).

 

Aayah zote hizo (5:41-47) zimeteremshwa kuwahusu makafiri.

 

 

Share

042-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 042: سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ أَكَّالُونَ لِلسُّحْتِ ۚ فَإِن جَاءُوكَ فَاحْكُم بَيْنَهُمْ أَوْ أَعْرِضْ عَنْهُمْ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Al-Maaidah  042-(Hao ni) wenye kusikiliza kwa makini uongo, walaji haramu kwa pupa

 

سَمَّاعُونَ لِلْكَذِبِ أَكَّالُونَ لِلسُّحْتِ ۚ فَإِن جَاءُوكَ فَاحْكُم بَيْنَهُمْ أَوْ أَعْرِضْ عَنْهُمْ ۖ وَإِن تُعْرِضْ عَنْهُمْ فَلَن يَضُرُّوكَ شَيْئًا ۖ وَإِنْ حَكَمْتَ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِالْقِسْطِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٤٢﴾

(Hao ni) wenye kusikiliza kwa makini uongo, walaji haramu kwa pupa. Basi wakikujia wahukumu baina yao au wapuuze. Na ukiwapuuza, hawatowe za kukudhuru chochote. Na kama ukihukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika Allaah Anapenda wafanyao uadilifu. (5:42).

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  kwamba: Walikuweko Quraydhwah na An-Nadhwiyr (makabila ya Mayahudi Madiynah). An-Nadhwiyr walikuwa wenye hadhi zaidi kuliko Quraydhwah. Ikawa pale mtu wa Quraydhwah anapoua mtu wa An-Nadhwiyr, huuliwa, lakini inapokuwa mtu wa An-Nadhwiyr ameua mtu wa Quraydhwah huitwa akapigwa mikaanga mia ya mitende kama diya. Kisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipotumwa kuwa ni Rasuli, mtu mmoja wa An-Nadhwiyr alimuua mtu wa Quraydhwah wakasema: Mleteni kwetu tumuue! Wakajibu: Sasa baina yetu na yenu yupo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) basi mleteni (atuhukumu)! Hapo ikateremka:

 

وَإِنْ حَكَمْتَ فَاحْكُم بَيْنَهُم بِالْقِسْطِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٤٢﴾

 Na kama ukihukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika Allaah Anapenda wafanyao uadilifu. (5:42).

 

Na uadilifu ni (kisasi cha) nafsi kwa nafsi. Kisha ikateremka:

 

أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ ۚ وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّـهِ حُكْمًا لِّقَوْمٍ يُوقِنُونَ ﴿٥٠﴾

Je, wanataka hukumu za kijahiliya? Na nani mbora zaidi kuliko Allaah katika kuhukumu kwa watu wenye yakini. (5:50).

 

[Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy, Ibn Hibbaan na wengineo]

 

Ibn Kathiyr amesema: Inaweza kuwa zimejumuika sababu mbili hizi (5:41-42) kwa wakati mmoja zikateremka Aayaat hizo kuhusu hayo, na Allaah Mjuzi zaidi

 

Share

067-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 067: وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

Al-Maaidah    067-Na Allaah Atakuhifadhi na watu

 

 

يَا أَيُّهَا الرَّسُولُ بَلِّغْ مَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ ۖ وَإِن لَّمْ تَفْعَلْ فَمَا بَلَّغْتَ رِسَالَتَهُ ۚ وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْكَافِرِينَ ﴿٦٧﴾

Ee Rasuli! Balighisha yale yaliyoteremshwa kwako kutoka kwa Rabb wako. Na usipofanya, basi utakuwa hukubalighisha ujumbe Wake. Na Allaah Atakuhifadhi na watu. Hakika Allaah Haongoi watu makafiri. [Al-Maaidah (5:67)]

 

Sababun-Nuzuwl:

 

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ

Na Allaah Atakuhifadhi na watu. (5:67).

 

Imeteremka pale Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliposhuka chini ya kivuli cha mti na akalitundika panga lake juu ya huo mti kisha akasinzia. Bedui mmoja akamjia akiwa katika hali ya usingizi, akalikamata panga la Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kisha akamuamsha, akamwambia huku amelishika panga lake juu: Nani ana uwezo wa kunizuia nisikuue? Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamjibu yule bedui: “Allaah Ndiye mwenye uwezo wa kukuzuia.” Hapo ikateremka Kauli hii ya Allaah (سبحانه وتعالى):

وَاللَّـهُ يَعْصِمُكَ مِنَ النَّاسِ ۗ

Na Allaah Atakuhifadhi na watu. (5:67).

 [Amehadithia Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) ,    imepokelewa na Ibn Hibbaan]

 

 

Share

082-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 082: ذَٰلِكَ بِأَنَّ مِنْهُمْ قِسِّيسِينَ وَرُهْبَانًا وَأَنَّهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

Al-Maaidah 082-Hivyo ni kwa kuwa miongoni mwao kuna Makasisi na Wamonaki  na kwamba wao hawatakabari.

 

 

لَتَجِدَنَّ أَشَدَّ النَّاسِ عَدَاوَةً لِّلَّذِينَ آمَنُوا الْيَهُودَ وَالَّذِينَ أَشْرَكُوا ۖ وَلَتَجِدَنَّ أَقْرَبَهُم مَّوَدَّةً لِّلَّذِينَ آمَنُوا الَّذِينَ قَالُوا إِنَّا نَصَارَىٰ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّ مِنْهُمْ قِسِّيسِينَ وَرُهْبَانًا وَأَنَّهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ ﴿٨٢﴾

82. Bila shaka utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa wale walioamini, ni Mayahudi na wale washirikina. Na bila shaka utawakuta walio karibu zaidi kimapenzi kwa Waumini ni wale wanaosema: “Sisi ni Manaswara.” Hivyo ni kwa kuwa miongoni mwao kuna Makasisi na Wamonaki  na kwamba wao hawatakabari.

 

وَإِذَا سَمِعُوا مَا أُنزِلَ إِلَى الرَّسُولِ تَرَىٰ أَعْيُنَهُمْ تَفِيضُ مِنَ الدَّمْعِ مِمَّا عَرَفُوا مِنَ الْحَقِّ ۖ يَقُولُونَ رَبَّنَا آمَنَّا فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَ ﴿٨٣﴾

83. Na wanaposikia yale yaliyoteremshwa kwa Rasuli utaona macho yao yanachuruzika machozi kutokana na yale waliyoyatambua ya haki. Wanasema: “Rabb wetu tumeamini, basi Tuandike pamoja na wenye kushuhudia.”

 

وَمَا لَنَا لَا نُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَمَا جَاءَنَا مِنَ الْحَقِّ وَنَطْمَعُ أَن يُدْخِلَنَا رَبُّنَا مَعَ الْقَوْمِ الصَّالِحِينَ ﴿٨٤﴾

84. “Na kwa nini Tusimwamini Allaah na haki iliyotufikia na hali tunatumai Rabb wetu Atuingize (Jannah) pamoja na Swalihina?”

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii na zinazofuatia (5: 82-85) zimeteremshwa kumzungumzia An-Najaashiy ambaye alikuwa mfalme wa Habash pamoja na watu wake. Aliwakilisha wajumbe wamwendee Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ili wamsikilize maneno yake na watambue sifa zake. Walipokutana na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), aliwasomea Qur-aan. Wakalia kwa machozi tele na wakanyenyekea na wakaingia Uislamu. Kisha wakarudi kwa An-Najaashiy kumjulisha yaliyojiri. [Athar kutoka kwa Saiy’d bin Jubayr, As-Suddi na wengineo.  Tafsiyr Ibn Kathiyr]  

 

Pia Sababun-Nuzuwl: Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amehadithia kwamba: Waislamu walipohajiri kutoka Makkah kwenda Habash wakiwa katika uongozi wa Ja’far bin Abiy Twaalib na Ibn Mas’uwd (رضي الله عنهم), walimkuta mfalme wao An-Najaashiy akiwa mkarimu na mwenye huruma kwao. Akawauliza kama wana chochote cha Wahyi kutoka kwa Allaah (سبحانه وتعالى). Walipomsomea Aayaat za Qur-aan wakati alikuwa pamoja na makasisi na wamonaki wake, walimiminikwa na machozi kutokana na kutambua haki. Ndipo Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha:

 

ذَٰلِكَ بِأَنَّ مِنْهُمْ قِسِّيسِينَ وَرُهْبَانًا وَأَنَّهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ ﴿٨٢﴾

 

Hivyo ni kwa kuwa miongoni mwao kuna Makasisi na Wamonaki na kwamba wao hawatakabari.

 

وَإِذَا سَمِعُوا مَا أُنزِلَ إِلَى الرَّسُولِ تَرَىٰ أَعْيُنَهُمْ تَفِيضُ مِنَ الدَّمْعِ مِمَّا عَرَفُوا مِنَ الْحَقِّ ۖ يَقُولُونَ رَبَّنَا آمَنَّا فَاكْتُبْنَا مَعَ الشَّاهِدِينَ ﴿٨٣﴾

Na wanaposikia yale yaliyoteremshwa kwa Rasuli utaona macho yao yanachuruzika machozi kutokana na yale waliyoyatambua ya haki. Wanasema: Rabb wetu tumeamini, basi Tuandike pamoja na wenye kushuhudia.

 

 

وَمَا لَنَا لَا نُؤْمِنُ بِاللَّـهِ وَمَا جَاءَنَا مِنَ الْحَقِّ وَنَطْمَعُ أَن يُدْخِلَنَا رَبُّنَا مَعَ الْقَوْمِ الصَّالِحِينَ ﴿٨٤﴾

Na kwa nini Tusimwamini Allaah na haki iliyotufikia na hali tunatumai Rabb wetu Atuingize (Jannah) pamoja na watu Swalihina? (5:82-84).

 

Na katika riwaayah nyengine: “Ja’far (رضي الله عنه) aliwasomea Suwrat Maryam wakamiminikwa machozi…”

 

  

 

 

Share

089-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 089: فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

Al-Maaidah    089-Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu

 

 

 

 لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّـهُ بِاللَّغْوِ فِي أَيْمَانِكُمْ وَلَـٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا عَقَّدتُّمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّـهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٨٩﴾

Allaah Hatokuchukulieni kwa viapo vyenu vya upuuzi, lakini Atakuchukulieni kwa (kuvunja) viapo mlivyoapa kwa niyyah mlioifunga thabiti. Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu, au kuwavisha nguo, au kuacha huru mtumwa. Lakini asiyeweza kupata (katika hayo), basi afunge Swiyaam siku tatu. Hiyo ndio kafara ya viapo vyenu mnapoapa. Na hifadhini yamini zenu. Hivyo ndivyo Allaah Anavyokubainishieni Aayaat (na hukmu) Zake ili mpate kushukuru. [Al-Maaidah (5:89)]

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِ مَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ  

 

Basi kafara yake ni kulisha maskini kumi chakula cha wastani mnachowalisha ahli zenu. (5:89).

 

Imeteremka kutokana na mtu ambaye alikuwa akilisha familia yake chakula kingi cha kutosheleza, lakini akilisha wengine anawapa chakula hafifu kisichotosheleza. Hapo ikateremshwa:

 

مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ  

cha wastani mnachowalisha ahli zenu.

 

[Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) , imepokelewa na Ibn Maajah]

 

 

 

 

Share

090-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 090: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Al-Maaidah    090-Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan..

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu.

 

إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ ﴿٩١﴾

Hakika shaytwaan anataka kukutilieni baina yenu uadui na bughudha katika pombe na kamari na akuzuieni kumdhukuru Allaah na Swalaah; basi je mtakoma? [Al-Maaidah (5:90-91)]

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hizi zimeteremshwa kuwazungumzia makabila mawili katika Answaar. Walikunywa pombe mpaka wakalewa mno kisha wakagombana na kuchafuana baadhi yao kwa baadhi mpaka athari zikawa zinaonekana katika nyuso zao. Kisha pale ulevi ulipowaondokea na akili zao zikawarejea, viliingia vinyongo katika nyoyo zao, hapo zikateremka Aayah hizi zinazoharamisha pombe moja kwa moja:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu.

 

إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ ﴿٩١﴾

Hakika shaytwaan anataka kukutilieni baina yenu uadui na bughudha katika pombe na kamari na akuzuieni kumdhukuru Allaah na Swalaah; basi je mtakoma? [Al-Maaidah (5:90-91)]

 

Baada ya kuteremshwa Aayah hizo za Suwrah Al-Maaidah (5:90,91), hapo hapo Swahaba wakaacha moja kwa moja kulewa ikawa ndio kikomo cha kunywa pombe.

 

[Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) – amepokea Ibn Jariyr]

 

Hadiyth yake kama ilivyothibiti:

 

عَنْ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ، قَالَ لَمَّا نَزَلَ تَحْرِيمُ الْخَمْرِ قَالَ عُمَرُ: اللَّهُمَّ بَيِّنْ لَنَا فِي الْخَمْرِ بَيَانًا شِفَاءً ، فَنَزَلَتِ الآيَةُ الَّتِي فِي الْبَقَرَةِ: ((‏يَسْأَلُونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ)) الآيَةَ قَالَ: فَدُعِيَ عُمَرُ فَقُرِئَتْ عَلَيْهِ، قَالَ: اللَّهُمَّ بَيِّنْ لَنَا فِي الْخَمْرِ بَيَانًا شِفَاءً، فَنَزَلَتِ الآيَةُ الَّتِي فِي النِّسَاءِ: ((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لاَ تَقْرَبُوا الصَّلاَةَ وَأَنْتُمْ سُكَارَى))‏ فَكَانَ مُنَادِي رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا أُقِيمَتِ الصَّلاَةُ يُنَادِي: أَلاَ لاَ يَقْرَبَنَّ الصَّلاَةَ سَكْرَانُ، فَدُعِيَ عُمَرُ فَقُرِئَتْ عَلَيْهِ  فَقَالَ: اللَّهُمَّ بَيِّنْ لَنَا فِي الْخَمْرِ بَيَانًا شِفَاءً فَنَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: ((‏فَهَلْ أَنْتُمْ مُنْتَهُونَ))‏ قَالَ عُمَرُ: انْتَهَيْنَا.‏

Amesimulia ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه) kwamba ilipoharamishwa pombe alisema: Ee Allaah Tubainishie kuhusu pombe bainisho la kuridhisha.” Hapo ikateremshwa Aayah katika Suwratul-Baqarah: 

 

فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ وَإِثْمُهُمَا أَكْبَرُ مِن نَّفْعِهِمَا ۗ

Katika viwili hivyo mna dhambi kubwa na (baadhi ya) manufaa kwa watu. Na dhambi yake viwili hivyo ni kubwa kuliko manufaa yake. [Al-Baqarah (2:219)]

 

Akaitwa ‘Umar akasomewa. Kisha akasema: “Ee Allaah Tubainishie kuhusu pombe bainisho la kuridhisha.” Kisha ikateremshwa Aayah katika Suwratun-Nisaa:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْرَبُوا الصَّلَاةَ وَأَنتُمْ سُكَارَىٰ حَتَّىٰ تَعْلَمُوا مَا تَقُولُونَ  

Enyi walioamini! Msikaribie Swalaah na hali mmelewa mpaka mjue mnayoyasema [An-Nisaa (4:43)]

Kisha muitaji wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akitangaza  pale inapokimiwa Swalaah: “Tahadharini! Aliyelewa asikaribie Swalaah!” ‘Umar akaitwa tena na akasomewa akasema: “Ee Allaah Tubainishie kuhusu pombe bainisho la kuridhisha.” Ikateremka Aayah:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِّنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴿٩٠﴾

Enyi walioamini! Hakika pombe na kamari na masanamu na kutazamia kwa mishale ya kupigia ramli, ni najisi na chukizo kutokana na kazi ya shaytwaan. Basi jiepusheni navyo mpate kufaulu.

 

إِنَّمَا يُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَن يُوقِعَ بَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةَ وَالْبَغْضَاءَ فِي الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ وَيَصُدَّكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَعَنِ الصَّلَاةِ ۖ فَهَلْ أَنتُم مُّنتَهُونَ ﴿٩١﴾

Hakika shaytwaan anataka kukutilieni baina yenu uadui na bughudha katika pombe na kamari na akuzuieni kumdhukuru Allaah na Swalaah; basi je mtakoma? [Al-Maaidah (5:90-91)]

 

 ‘Umar akasema:  “Tumekoma.” [Sunan Abiy Daawuwd Kitaab Al-Ashribah Baab Tahriym Al-Khamr. Imaam Al-Albaaniy ameisahihisha katika Swahiyh Abiy Daawuwd (3670)]

 

Share

093-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 093: لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا إِذَا مَا اتَّقَوا

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

Al-Maaidah  093-Hakuna lawama juu ya wale walioamini na wakatenda mema

 

 

 

لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا إِذَا مَا اتَّقَوا وَّآمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ثُمَّ اتَّقَوا وَّآمَنُوا ثُمَّ اتَّقَوا وَّأَحْسَنُوا ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿٩٣﴾

Hakuna lawama juu ya wale walioamini na wakatenda mema katika vile walivyokula (kabla ya kuharimishwa) ikiwa watakuwa na taqwa na wakaamini na wakatenda mema; kisha wakawa na taqwa na wakaamini, kisha wakawa na taqwa na wakafanya ihsaan. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. (5:93). [Amehadithia Anas (رضي الله عنه), imepokelewa na  Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremshwa baada ya kuteremshwa Aayah za uharamisho  wa pombe moja kwa moja (5:90-91). Kisha baadhi ya Swahaba wakasema kuwa watu wengi wamefariki wakiwa wana pombe matumboni mwao, wakataka hukmu yake, hapo ikateremka Aayah hii:

 

لَيْسَ عَلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جُنَاحٌ فِيمَا طَعِمُوا إِذَا مَا اتَّقَوا وَّآمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ ثُمَّ اتَّقَوا وَّآمَنُوا ثُمَّ اتَّقَوا وَّأَحْسَنُوا ۗ وَاللَّـهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ ﴿٩٣﴾

Hakuna lawama juu ya wale walioamini na wakatenda mema katika vile walivyokula (kabla ya kuharimishwa) ikiwa watakuwa na taqwa na wakaamini na wakatenda mema; kisha wakawa na taqwa na wakaamini, kisha wakawa na taqwa na wakafanya ihsaan. Na Allaah Anapenda wafanyao ihsaan. (5:93). [Amehadithia Anas (رضي الله عنه), imepokelewa na  Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Share

101-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 101: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

Al-Maaidah 101-Enyi walioamini! Msiulizie mambo ambayo mkifichuliwa yatakuchukizeni

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿١٠١﴾

Enyi walioamini! Msiulizie mambo ambayo mkifichuliwa yatakuchukizeni. Na mkiyaulizia pale inapoteremshwa Qur-aan mtafichuliwa. Allaah Ameyasamehe hayo. Na Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mvumilivu. [Al-Maaidah (5:101)]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

Aayah hii imeteremshwa kwa sababu ya wingi wa maswali waliyokuwa wakiuliza watu katika hali tofauti na wakati nyakati mbali mbali; ima kwa istihzaa au mitihani iliyowasibu au kwa talbiys (kufunika haki na kuipotosha). Mfano pale ilipoteremka Aayah ya kuwajibika Hajj:

 

وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ۚ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ ﴿٩٧﴾ 

Na kwa ajili ya Allaah imewajibika watu watekeleze Hajj katika Nyumba (Al-Ka’bah) hiyyo kwa mwenye uwezo.  (3:97)

 

akashikilia mtu kuuliza kuhusu kuwajibika Hajj kama inawajibikia kila mwaka, jambo ambalo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) angejibu kuwa “Naam”, basi ingewajibikia, kisha hapo ingekuwa ni amri na jambo gumu mno kulitekeleza. [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo]  

 

 

Pia Sababun-Nuzuwl:

 

Ni  kama alivyohadithia Anas bin Maalik (رضي الله عنه)  kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alitoa khutbah ambayo sijapatapo kuisikia kama hiyo kisha akasema: “Mngelikuwa mnayajua yale ninayoyajua, basi mngelicheka kidogo na mngelia sana.” Waliposikia hivyo, Swahaba wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) walijifunika nyuso zao wakalia mpaka sauti za vilio vyao vikasikika. Kisha mtu mmoja hapo akamuuliza: Nani baba yangu? Akamjibu: “Fulani.” Hapo ikateremka Aayah hii:

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿١٠١﴾

Enyi walioamini! Msiulizie mambo ambayo mkifichuliwa yatakuchukizeni. Na mkiyaulizia pale inapoteremshwa Qur-aan mtafichuliwa. Allaah Ameyasamehe hayo. Na Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mvumilivu. [Al-Maaidah (5:101)] [Al-Bukhaariy]

 

 

Pia Sababun-Nuzuwl:

 

Anas (رضي الله عنه)  amehadithia kwamba: Siku moja walianza kumuuliza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) maswali mengi mpaka akaghadhibika. Akapanda mimbar akasema: “Hamtaniuliza lolote leo ila nitawajibu tu.” Nikatazama kuliani na kushotoni nikaona kila mtu amejifunika uso wake kwa nguo akilia. Hapo alikuweko mtu mmoja ambaye kila alipogombana na wenziwe aliitwa ‘mwana wa fulani asiyekuwa ni baba yake’. Akamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah, nani baba yangu? Akasema: “Hudhaafah.” Hapo ‘Umar akainuka akasema: Tumeridhika na Allaah kuwa ni Rabb, na Uislamu kuwa Dini, na Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa ni Rasuli. Tunajikinga kwa Allaah na fitnah! Hapo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Sijapatapo kuona kheri au shari kama siku ya leo, kwani imedhihirishwa mbele yangu Jannah (Pepo) na moto hadi kwamba nimeviona viwili hivi nyuma ya ukuta.”  Qataadah alipokuwa akihadithia Hadiyth hii alikuwa akitaja Aayah hii:

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَسْأَلُوا عَنْ أَشْيَاءَ إِن تُبْدَ لَكُمْ تَسُؤْكُمْ وَإِن تَسْأَلُوا عَنْهَا حِينَ يُنَزَّلُ الْقُرْآنُ تُبْدَ لَكُمْ عَفَا اللَّـهُ عَنْهَا ۗ وَاللَّـهُ غَفُورٌ حَلِيمٌ ﴿١٠١﴾

Enyi walioamini! Msiulizie mambo ambayo mkifichuliwa yatakuchukizeni. Na mkiyaulizia pale inapoteremshwa Qur-aan mtafichuliwa. Allaah Ameyasamehe hayo. Na Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mvumilivu. [Al-Maaidah (5:101)] [Al-Bukhaariy]

 

 

Share

108-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Maaidah Aayah 108: ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يَأْتُوا بِالشَّهَادَةِ عَلَىٰ وَجْهِهَا أَوْ يَخَافُوا أَن تُرَدَّ أَيْمَانٌ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

 

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

Al-Maaidah  108-Hivyo inaelekea zaidi ya kwamba watatoa ushahidi kama…

 

ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يَأْتُوا بِالشَّهَادَةِ عَلَىٰ وَجْهِهَا أَوْ يَخَافُوا أَن تُرَدَّ أَيْمَانٌ بَعْدَ أَيْمَانِهِمْ ۗ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاسْمَعُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴿١٠٨﴾

Hivyo inaelekea zaidi ya kwamba watatoa ushahidi kama ipasavyo au watakhofu visije vikaletwa viapo (vingine) baada ya viapo vyao. Na mcheni Allaah na sikizeni!  Na Allaah Haongoi watu mafasiki. [Al-Maaidah (5:106-108)]

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

Aayah hii imeteremshwa pamoja na Aayah mbili kabla yake (5:106-107) pale bwana mmoja katika Baniy Sahm alitoka pamoja na Tamiym  Ad-Daariy na ‘Adiyy. Kisha katika msafara wao akafariki huyu mtu ambaye ni katika Baniy Sahm, na walikuwa katika kijiji ambacho hakuna Muislamu. Pale waliporejea akina Tamiym na vitu vyake alivyoviacha baada ya kufariki, walikikosa chombo kimoja cha fedha ambacho kimezibiwa kwa dhahabu. Kisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawaapisha. Kisha baada ya hapo walikuja kukipata kile chombo Makkah. Wakasema wale waliokipata huko Makkah kwamba: Tulikinunua kwa ‘Adiy na Tamiym. Wakasimama watu wawili katika ndugu wa yule As-Sahm wakaapa na wakasema kumuambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  kuwa ushahidi wetu ni bora kuliko ushahidi wao, na kwamba hao ni waongo wanamsingizia Tamiym na ‘Adiy na kuwa hicho chombo si cha huyo ndugu yao bali ni cha jamaa yao wenyewe. Hapo zikateremka Aayaat hizi:

 

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا شَهَادَةُ بَيْنِكُمْ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ حِينَ الْوَصِيَّةِ اثْنَانِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ أَوْ آخَرَانِ مِنْ غَيْرِكُمْ إِنْ أَنتُمْ ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَأَصَابَتْكُم مُّصِيبَةُ الْمَوْتِ ۚ تَحْبِسُونَهُمَا مِن بَعْدِ الصَّلَاةِ فَيُقْسِمَانِ بِاللَّـهِ إِنِ ارْتَبْتُمْ لَا نَشْتَرِي بِهِ ثَمَنًا وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ ۙ وَلَا نَكْتُمُ شَهَادَةَ اللَّـهِ إِنَّا إِذًا لَّمِنَ الْآثِمِينَ ﴿١٠٦﴾

Enyi walioamini! Ushahidi uliofaradhishwa kati yenu ni wa watu wawili waadilifu wakati wa kuandika (au kutamka) usia anapohisi mmoja wenu dalili za kukurubia kufa, au wawili wengineo wasiokuwa nyinyi pale mnapokuwa safarini ukakufikeni msiba wa mauti. Muwazuie baada ya Swalaah, na waape kwa Allaah mkitilia shaka, (waseme): Hatutovibadilisha (viapo vyetu) kwa thamani yoyote ile japo akiwa ni jamaa yetu wa karibu. Na wala hatutoficha ushuhuda wa Allaah, kwani hakika hapo tutakuwa miongoni mwa wenye kutenda dhambi.  

 

 

فَإِنْ عُثِرَ عَلَىٰ أَنَّهُمَا اسْتَحَقَّا إِثْمًا فَآخَرَانِ يَقُومَانِ مَقَامَهُمَا مِنَ الَّذِينَ اسْتَحَقَّ عَلَيْهِمُ الْأَوْلَيَانِ فَيُقْسِمَانِ بِاللَّـهِ لَشَهَادَتُنَا أَحَقُّ مِن شَهَادَتِهِمَا وَمَا اعْتَدَيْنَا إِنَّا إِذًا لَّمِنَ الظَّالِمِينَ ﴿١٠٧﴾

Ikigundulikana kwamba hao wawili wana hatia ya kukhini, basi wawili wengine wanaostahiki kudai haki ki-shariy’ah, na walio karibu zaidi (na mrithiwa) wasimame mahala pao, kisha waape kwa Allaah: Bila shaka ushahidi wetu ni wa kweli zaidi kuliko ushahidi wa wawili wao; nasi hatukufanya taksiri, kwani bila shaka hapo sisi tutakuwa miongoni mwa madhalimu.

 

 

ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يَأْتُوا بِالشَّهَادَةِ عَلَىٰ وَجْهِهَا أَوْ يَخَافُوا أَن تُرَدَّ أَيْمَانٌ بَعْدَ أَيْمَانِهِمْ ۗ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاسْمَعُوا ۗ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴿١٠٨﴾

Hivyo inaelekea zaidi ya kwamba watatoa ushahidi kama ipasavyo au watakhofu visije vikaletwa viapo (vingine) baada ya viapo vyao. Na mcheni Allaah na sikizeni!  Na Allaah Haongoi watu mafasiki. [Al-Maaidah (5:106-108)]. [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما), ameipokea Al-Bukhaariy]

 

 

An-Naasikh Wal-Mansuwkh:

 

Kufutwa hukmu kuhusu kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى): 

أَوْ آخَرَانِ مِنْ غَيْرِكُمْ

au wawili wengineo wasiokuwa nyinyi (5:106).

 

Imefutwa baada ya kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى): 

وَأَشْهِدُوا ذَوَيْ عَدْلٍ مِّنكُمْ وَأَقِيمُوا الشَّهَادَةَ لِلَّـهِ ۚ ذَ

na mshuhudishe mashahidi wawili waadilifu miongoni mwenu.  [Atw-Twalaaq (65: 2)].

 

Share