Fataawaa: Swalaah Ya Ijumaa

 

Fataawaa

 

 Swalaah Ya Ijumaa

 

 

Share

01-Swalaah Ya Ijumaa Ni Fardhi Kwa Kila Mwanamme Haijuzu Kuiacha Kwa Sababu Ya Kazi Au Masomo n.k

 

Swalaah Ya Ijumaa Ni Fardhi Kwa Kila Mwanamume

Haijuzu Kuiacha Kwa Sababu Ya Kazi Au Masomo Na Kadhaalika

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Swalaah ya Ijumaa ni Fardhw ‘Ayn (Fardhi kwa kila mtu mwanamme) wala haijuzu kuiacha kwa sababu ya kazi au masomo  na sababu kama hizo.

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

“Na yeyote anayemcha Allaah; Atamjaalia njia ya kutoka (shidani).”

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/184)]

 

Share

02-Swalaah Ya Ijumaa Ni Fardhi Kwa Kila Mwanamme Haijuzu Kuikhalifu Hata Ukikatazwa Na Mwajiri Wako

 

Swalaah Ya Ijumaa Ni Fardhi Kwa Kila Mwanamme

Haijuzu Kuikhalifu Hata Ukikatazwa Na Mwajiri Wako

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Swalaah ya Ijumaa ni fardhi kwa kila mwanamme mwenye kukafilika katika ‘Ibaadah, mkazi, wala haikupasi kuikhalifu kwa sababu ya kazi hata kama mwajiri wako atakukataza.

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/185)]

Share

03-Swalaah Ya Ijumaa: Wanaume Kuswali Ijumaa Misikitini Wanawake Nyumbani

 

Wanaume Kuswali Ijumaa Misikitini Wanawake Nyumbani

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Ni wajibu kwa wanaume kuswali Ijumaa pamoja na ndugu zao Waislamu katika nyumba za Allaah (Misikitini). Ama wanawake wao hawana Ijumaa na ni wajibu kwao kuswali Adhuhuri.

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/196)]

 

Share

04-Swalaah Ya Ijumaa: Haifai Kuzungumza Kamwe Pindi Khutba Ya Ijumaa Inapotolewa

Haifai Kuzungumza Kamwe Pindi Khutba Ya Ijumaa Inapotolewa

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Haifai kwa mtu anayekuweko Masjid kuongea na yeyote yule pindi khutbah ya Ijumaa inatolewa.

Ama Imaam, yeye anaweza kuongea inapombidi kwa lile analoliona lina maslahi.

 

  

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/201, 202)]

Share

05-Swalaah Ya Ijumaa: Kujuzu Swalaah Ya Ijumaa Hata Kama Idadi Ya Watu Ni Chini Ya Arubaini

 

Kujuzu Swalaah Ya Ijumaa Hata Kama Idadi Ya Watu Ni Chini Ya Arubaini

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Inajuzu kusimamisha Swalaah ya Ijumaa hata kama idadi imepunguka chini ya watu arubaini kutokana na kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ  

“Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya Swalaah siku ya Ijumaa, kimbilieni kumdhukuru Allaah.” [Al-Jumu’ah: 9]

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/215)]

 

 

Share

06-Swalaah Ya Ijumaa: Vipi Kuitikia Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam)

 

Vipi Kuitikia Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam)

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Khatwiyb (wa Ijumaa) anapomswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), waitikie wanaomsikiliza (Maamuma) bila ya kupandisha sauti.

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/217)]

 

Share

07-Swalaah Ya Ijumaa: Hukmu Ya Anayepitwa Na Rakaa Ya Swalaah Ya Ijumaa

 

Hukmu Ya Anayepitwa Na Rakaa Ya Swalaah Ya Ijumaa

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Anayepitwa na Rakaa katika Swalaah ya Ijumaa, na akaipata Rakaa nyingine, basi aiswali ile Rakaa (iliyompita) na hivyo atakuwa amepata Ijumaa kwa sababu limesihi kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hilo.

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/225)]

 

Share

08-Swalaah Ya Ijumaa: Wajibu Kwa Imaam Kuwasalimia Maamuma Baada Ya Kupanda Minbari

Wajibu Kwa Imaam Kuwasalimia Maamuma Baada Ya Kupanda Minbari

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Ni Sunnah kwa Khatwiyb (wa Ijumaa) kuwasalimia maamuma anapopanda minbari kabla ya kukaa kitako (kusubiri Adhana).

 

 

 [Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/234)]

Share

09-Swalaah Ya Ijumaa: Kuzungumza Wakati Khutbah Inapotolewa Ni Haramu

Kuzungumza Wakati Khutbah Inapotolewa Ni Haramu

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Maongezi ya watu wakati Imaam anatoa khutbah siku ya Ijumaa ni haramu.

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/240)]

 

Share

10-Swalaah Ya Ijumaa: Hukmu Ya Kumuombea Rahmah Anayepiga Chafya Au Kurudisha Salaam Wakati Imaam Anakhutubia

 

 Hukmu Ya Kumuombea Rahmah Anayepiga Chafya

Au Kurudisha Salaam Wakati Imaam Anakhutubia

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Kauli iliyo sahihi ya ‘Ulamaa ni kwamba, haijuzu kumuombea rahmah anayepiga chafya wala kurudisha salaam wakati Imaam (Khatwiyb) anakhutubia.

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/242)]

Share

11-Swalaah Ya Ijumaa: Hakuna Sunnah Rawaatib Katika Swalaah Ya Ijumaa

 

Hakuna Sunnah Rawaatib Katika Swalaah Ya Ijumaa

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Hakuna Sunnah za  Rawaatib za qabliyyah (kabla ya Swalaah) katika Swalaah ya Ijumaa. Lakini anaweza kuswali Sunnah atakazo kabla ya kuingia Imaam.

 

 

  [Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/249)]

Share

12-Swalaah Ya Ijumaa: Suwrah Za Kusomwa Katika Swalaah Ya Ijumaa

 

Suwrah Za Kusomwa Katika Swalaah Ya Ijumaa

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Iliyo katika Shariy’ah kusomwa katika Swalaah ya Ijumaa ni Suwrat “Al-A’laa” na “Al-Ghaashiyah” au “Al-Jumu’ah” na “Al-Munaafiquwn”, au “Al-Jumu’ah” na “Al-Ghaashiyah”.

 

 

  [Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/279)]

 

Share

13-Swalaah Ya Ijumaa: Hukmu Ya Anayeswalisha Ahli Zake Nyumbani Swalaah Ya Ijumaa

 

Hukmu Ya Anayeswalisha Ahli Zake Nyumbani Swalaah Ya Ijumaa

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah

 

www.alhidaaya.com

 

 

Atakayeswalisha ahli zake Swalaah ya Ijumaa nyumbani, anapaswa airudie kwa kuiswali Swalaah ya Adhuhuri, wala Swalaah (hiyo) ya Ijumaa (walioiswali nyumbani) haisihi kwao.

 

 

[Al-Lajnah Ad-Daaimah (8/196)]

Share