36-Fadhila Za Laa Ilaaha Illa-Allaah: Kutamka Laa Ilaaha Illa-Allaah Wakati Wa Mafazaiko

Hadiyth Kuhusu Fadhila Za Laa Ilaaha Illa Allaah

 

www.alhidaaya.com

 

36-Kutamka Laa Ilaaha Illa-Allaah Wakati Wa Mafazaiko  

 

 

عَنْ زَيْنَبَ بِنْتِ جَحْشٍ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم دَخَلَ عَلَيْهَا فَزِعًا يَقُولُ: ((لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، وَيْلٌ لِلْعَرَبِ مِنْ شَرٍّ قَدِ اقْتَرَبَ، فُتِحَ الْيَوْمَ مِنْ رَدْمِ يَأْجُوجَ وَمَأْجُوجَ مِثْلُ هَذَا))وَحَلَّقَ بِإِصْبَعِهِ وَبِالَّتِي تَلِيهَا، فَقَالَتْ زَيْنَبُ فَقُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ أَنَهْلِكُ وَفِينَا الصَّالِحُونَ؟  قَالَ: ((نَعَمْ، إِذَا كَثُرَ الْخَبَثُ))  

 

Imepokelewa kutoka kwa Zaynba Bint Jahsh (رضي الله عنها) kwamba Nabiy alingia chumbani kwake akiwa katika hali ya kufazaika akasema:

لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ

 

((Laa ilaaha illa Allaah [hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah]

 

Ole kwa Waarabu kutokana na shari iliyokaribia. Leo limefunguka shimo katika boma la kizuzi cha Ya-ajuwj na Ma-ajuwj kama hivi!)) Akafanya kiduara kwa kufunga kidole chake cha gumba na cha shahada. Zaynab akasema: Kisha nikasema: Ee Rasuli wa Allaah, hivi tutaangamia na hali tumo watu wema?”. Akasema: ((Ndio pindi maovu yakizidi)) [Al-Bukhaariy pamoja na Al-Fat-h (6/181) [3346], Muslim (4/2208) [2880] na Riwaayah nyengine: “Aliamka usingizini akasema….

 

 

Share