38-Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Anayetokwa Majimaji Je Inasihi Aswali Qiyaamul-Layl Kwa Wudhuu Wa ‘Ishaa?

 

 

Fataawaa Mas-ala 60 Kuhusu Hedhi Na Nifaas

 

38-Anayetokwa Majimaji Je Inasihi Aswali Qiyaamul-Layl Kwa Wudhuu Wa ‘Ishaa?

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

Je inasihi kwa mwanamke huyu (anayetokwa majimaji) kuswali Qiyaamul-Layl itapokatika nusu ya pili ya usiku kwa wudhu wa ‘Ishaa?

 

JIBU:

 

 

Hapana, itakapokatika usiku wa nusu ya pili inapasa  kuchukua wudhu  mwingine.  Na imesemwa pia halazimiki kurejea kuchukua wudhu, na  hii ndiyo rai iliyokubaliwa.

Share