50-Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Hijjah Ya Mwenye Hedhi Inakubalika

 

 

Fataawaa Mas-ala 60 Kuhusu Hedhi Na Nifaas

 

50-Hijjah Ya Mwenye Hedhi Inakubalika?

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

SWALI:

 

Nini hukumu ya mwanamke ambaye amekuwa na hedhi katika siku za Hajj   je, Hijjah ile itakubaliwa?

 

 

 

JIBU:

 

Hili haliwezekani kujibiwa hadi ijulikane ni wakati gani alipatwa na hedhi  na hilo ni kwa sababu baadhi ya matendo ya hija Hajj hayamkatai zmwenye hedhi na mengine yanamkataza mwenye hedhi. Kwa mfano Twawaaf hawezi kuifanya mwenye hedhi ila isipokuwa akiwa ni mwenye tohara. Ama matendo mengine yanawezekana kwa mwenye hedhi.

 

Share