034-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Wasia Kwa Wanawake

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الوصية بالنساء

034-Mlango Wa Wasia Kwa Wanawake

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَعَاشِرُوهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ ﴿١٩﴾

Na kaeni nao kwa wema. [An-Nisaa: 19]

 

وَلَن تَسْتَطِيعُوا أَن تَعْدِلُوا بَيْنَ النِّسَاءِ وَلَوْ حَرَصْتُمْ ۖ فَلَا تَمِيلُوا كُلَّ الْمَيْلِ فَتَذَرُوهَا كَالْمُعَلَّقَةِ ۚ وَإِن تُصْلِحُوا وَتَتَّقُوا فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿١٢٩﴾

Na wala hamtoweza kuadilisha baina ya wake japokuwa mkipania. Basi msimili muelemeo wote (kwa mke mmoja) mkamuacha (mwengine) kama kining’inio. Na mkisuluhisha na mkawa na taqwa, basi hakika Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [An-Nisaa: 129]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( اسْتَوْصُوا بالنِّساءِ خَيْراً ؛ فَإِنَّ المَرْأَةَ خُلِقَتْ مِنْ ضِلعٍ ، وَإنَّ أعْوَجَ مَا في الضِّلَعِ أعْلاهُ ، فَإنْ ذَهَبتَ تُقيمُهُ كَسَرْتَهُ ، وَإنْ تَرَكْتَهُ ، لَمْ يَزَلْ أعْوجَ ، فَاسْتَوصُوا بالنِّساءِ )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

وفي رواية في الصحيحين : (( المَرأةُ كالضِّلَعِ إنْ أقَمْتَهَا كَسَرْتَهَا ، وَإن اسْتَمتَعْتَ بِهَا ، اسْتَمتَعْتَ وفِيهَا عوَجٌ )) .

وفي رواية لمسلم : (( إنَّ المَرأةَ خُلِقَت مِنْ ضِلَع ، لَنْ تَسْتَقِيمَ لَكَ عَلَى   طَريقة ، فإن اسْتَمْتَعْتَ بِهَا اسْتَمْتَعْتَ بِهَا وَفيهَا عوَجٌ ، وإنْ ذَهَبْتَ تُقِيمُهَا كَسَرْتَها ، وَكَسْرُهَا طَلاَقُهَا )) .

Na imepokewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nawausieni kuwafanyia wema wanawake, kwani mwanamke ameumbwa kutokana na ubavu, na sehemu laini na yenye matatizo katika ubavu ni sehemu ya juu. Ukijaribu kuinyoosha, utaivunja; na ukiiacha, itabaki kombo. Nawausieni kuwatendea wema wanawake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

Katika riwaayah iliyo katika Sahihi Mbili: ((Mwanamke ni kama mbavu, ukuiunyoosha utauvunja. Na ukitaka kupata faida kwayo, itabidi upate faida na ujongo wake)).

Katika riwaayah ya Muslim: ((Hakika mwanamke ameumbwa kutokana na ubavu. Hakuna njia ya kuunyoosha. Ukitaka kupata faida kwayo, itabidi upate faida na ujongo wake. Na ukitaka kuunyoosha, utauvunja na kuuvunja kwako ni kumpatia talaka)).

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن زَمْعَةَ رضي الله عنه: أنَّهُ سَمِعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم يَخْطُبُ ، وَذَكَرَ النَّاقَةَ وَالَّذِي عَقَرَهَا ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( إِذ انْبَعَثَ أشْقَاهَا انْبَعَثَ لَهَا رَجُلٌ عَزيزٌ ، عَارِمٌ مَنيعٌ في رَهْطِهِ )) ، ثُمَّ ذَكَرَ النِّسَاءَ ، فَوعَظَ فِيهنَّ ، فَقَالَ : (( يَعْمِدُ أحَدُكُمْ فَيَجْلِدُ امْرَأتَهُ جَلْدَ العَبْدِ فَلَعَلَّهُ يُضَاجِعُهَا مِنْ آخِرِ يَومِهِ )) ثُمَّ وَعَظَهُمْ في ضَحِكِهمْ مِنَ الضَّرْطَةِ ، وَقالَ : (( لِمَ يَضْحَكُ أَحَدُكُمْ مِمَّا يَفْعَلُ ؟! )) مُتَّفَقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwake 'Abdillaahi bin Zam'ah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akihhutubu, akamtaja ngamia, na yule aliyemchinja. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Pale alipochomoka haraka muovu wao mkuu. [Ash-Shams: 12]. Alimrukia muovu wao mwenye nguvu, mfisadi, mwenye kinga ya watu wake (akamchinja)." Kisha akataja wanawake, akawa waadhi kuhusu wao, akasema: "Mmoja wenu anampiga mkewe kipigo cha mtumwa, na huenda mwisho wa siku akamwingilia." Kisha akawadhia juu ya kucheka kwao kwa sababu ya kutokwa na upepo, akasema: "kwa nini mmoja wenu anacheka analolifanya?" [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لاَ يَفْرَكْ مُؤْمِنٌ مُؤْمِنَةً إنْ كَرِهَ مِنْهَا خُلُقاً رَضِيَ مِنْهَا آخَرَ )) ، أَوْ قَالَ : (( غَيْرَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini mwanamume asimchukie Muumini mwanamke. Akichukizwa na tabia yake moja, ataridhika naye kwa tabia nyengine."  [Muslim]

 

 

Hadiyth – 4

وعن عمرو بن الأحوصِ الجُشَمي رضي الله عنه: أنَّهُ سَمِعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم في حَجَّةِ الوَدَاعِ يَقُولُ بَعْدَ أنْ حَمِدَ الله تَعَالَى ، وَأثْنَى عَلَيهِ وَذَكَّرَ وَوَعظَ ، ثُمَّ قَالَ : (( ألا وَاسْتَوصُوا بالنِّساءِ خَيْراً ، فَإِنَّمَا هُنَّ عَوَانٍ عِنْدَكُمْ لَيْسَ تَمْلِكُونَ مِنْهُنَّ شَيْئاً غَيْرَ ذلِكَ إلاَّ أنْ يَأتِينَ بِفَاحِشَةٍ مُبَيِّنَةٍ ، فَإنْ فَعَلْنَ فَاهْجُرُوهُنَّ في المَضَاجِع ، وَاضْرِبُوهُنَّ ضَرباً غَيْرَ مُبَرِّحٍ ، فإنْ أطَعْنَكُمْ فَلا تَبْغُوا عَلَيهنَّ سَبيلاً ؛ ألاَ إنَّ لَكُمْ عَلَى نِسَائِكُمْ حَقّاً ، وَلِنِسَائِكُمْ عَلَيْكُمْ حَقّاً ؛ فَحَقُّكُمْ عَلَيهِنَّ أنْ لا يُوطِئْنَ فُرُشَكُمْ مَنْ تَكْرَهُونَ ، وَلا يَأْذَنَّ في بُيُوتِكُمْ لِمَنْ تَكْرَهُونَ ؛ ألاَ وَحَقُّهُنَّ عَلَيْكُمْ أنْ تُحْسِنُوا إِلَيْهِنَّ في كِسْوَتِهنَّ وَطَعَامِهنَّ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) .

Na 'Ammr bin Al-Ahwasw Al- Jushamiyy' (Radhwiya Allaahu 'anhu) amemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema katiak Hajjatil Wadaa' baada ya kumhimidi na kumsifu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa), akakumbusha na kuwaidhinkisha akasema: "Jueni! nawausieni kuwatendea wema wanawake, kwani wao ni wasaidizi wenu, hamna mnachomiliki kwao isipokuwa hicho kustarehe nao isipokuwa wanapotenda uovu wa wazi. Wakifanya hivyo wahameni katika malazi, na wapigeni pigo lisiloumiza. Wakiwatii msiwatafutie njia (ya kuwaudhi). Jueni! Hakika nyinyi mna haki juu ya wake zenu, na wake zenu wana haki juu yenu. Haki yenu juu yao ni kutomruhusu mnayemchukia kulala katika vitanda vyenu, wala wasiwaruhusu kuingia majumbani mwenu mnayemchukia. Fahamuni! Na haki zao juu yenu ni kuwafanyia hisani katika mavazi na chakula chao." [At- Tirmidhiy, na akasema: Hadiyth Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 5

وعن معاوية بن حيدة رضي الله عنه، قَالَ : قُلْتُ : يَا رَسُول الله ، مَا حق زَوجَةِ أَحَدِنَا عَلَيهِ ؟ قَالَ : (( أنْ تُطْعِمَهَا إِذَا طعِمْتَ ، وَتَكْسُوهَا إِذَا اكْتَسَيْتَ ، وَلاَ تَضْرِبِ الوَجْهَ ، وَلا تُقَبِّحْ ، وَلا تَهْجُرْ إلاَّ في البَيْتِ )) حديثٌ حسنٌ رواه أَبُو داود.

imepokewa kutoka kwake Mu'aawiyyah bin Haydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni ipi haki ya mke wa mmoja wetu kwa mumewe?" Akajibu: "Ni kumlisha anapokula, kumvisha anapovaa wala usimpige uso wala usimkaripie wala usimhame ila nyumbani tu." [ Hadiyth Hasan iliyonukuliwa na Abu Daawuud]

 

 

Hadiyth – 6

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( أكْمَلُ المُؤمِنِينَ إيمَاناً أحْسَنُهُمْ خُلُقاً ، وخِيَارُكُمْ خياركم لِنِسَائِهِمْ )) رواه الترمذي ، وَقالَ : (( حديث حسن صحيح )) . 

Na imepokewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Muumini mkamilifu wa Iymaani ni mzuri wa tabia, na wabora wenu ni wabora wenu kwa wake zao." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hahiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 7

وعن إياس بن عبد الله بن أَبي ذباب رضي الله عنه، قَالَ : قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لاَ تَضْرِبُوا إمَاء الله )) فجاء عُمَرُ رضي الله عنه إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ :ذَئِرْنَ النِّسَاءُ عَلَى أزْوَاجِهِنَّ ، فَرَخَّصَ في ضَرْبِهِنَّ ، فَأطَافَ بآلِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم نِسَاءٌ كَثيرٌ يَشْكُونَ أزْواجَهُنَّ ، فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: (( لَقَدْ أطَافَ بِآلِ بَيتِ مُحَمَّدٍ نِسَاءٌ كثيرٌ يَشْكُونَ أزْوَاجَهُنَّ لَيْسَ أولَئكَ بخيَارِكُمْ )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .

Na imepokewa kutoka kwake Iyaas bin 'Abdillaah bin Abu Dhubaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msiwapige wajakazi (wanawake) wa Allaah." Akaja 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Wanawake wamekuwa majasiri juu ya waume zao." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaruhusu wawachape wake zao. Wanawake wakawazungukia wakeze Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakishtaki kupigwa na waume zao. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Hakika wanawake wengi wamezunguka katika nyumba za Muhammad (wakeze) wakiwashtakia waume zao, waume hao si bora miongoni mwenu." [Abu Daawuud kwa Isnaad Swahiyh]

 

 

Hadiyth – 8

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ : (( الدُّنْيَا مَتَاعٌ ، وَخَيرُ مَتَاعِهَا المَرْأَةُ الصَّالِحَةُ )) رواه مسلم .

'Abdillaah bin 'Ammr bin Al- 'Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: " Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Dunia ni starehe, na bora ya starehe ni mke mwema." [Muslim]

 

 

 

 

 

Share