03-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Mjumuisho: Mlango Wa Kuipa Mgongo Dunia

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلْجَامِعِ

Kitabu Cha Mjumuisho

 

 

بَابُ اَلزُّهْدِ وَالْوَرَعِ

03-Mlango Wa Kuipa Mgongo Dunia[1]

 

 

 

 

1266.

عَنْ اَلنُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ وَأَهْوَى اَلنُّعْمَانُ بِإِصْبَعَيْهِ إِلَى أُذُنَيْهِ: {إِنَّ اَلْحَلَالَ بَيِّنٌ، وَإِنَّ اَلْحَرَامَ بَيِّنٌ، وَبَيْنَهُمَا مُشْتَبِهَاتٌ، لَا يَعْلَمُهُنَّ كَثِيرٌ مِنْ اَلنَّاسِ، فَمَنِ اتَّقَى اَلشُّبُهَاتِ، فَقَدِ اِسْتَبْرَأَ لِدِينِهِ وَعِرْضِهِ، وَمَنْ وَقَعَ فِي اَلشُّبُهَاتِ وَقَعَ فِي اَلْحَرَامِ، كَالرَّاعِي يَرْعَى حَوْلَ اَلْحِمَى، يُوشِكُ أَنْ يَقَعَ فِيهِ، أَلَا وَإِنَّ لِكُلِّ مَلِكٍ حِمًى، أَلَا وَإِنَّ حِمَى اَللَّهِ مَحَارِمُهُ، أَلَا وَإِنَّ فِي اَلْجَسَدِ مُضْغَةً، إِذَا صَلَحَتْ، صَلَحَ اَلْجَسَدُ كُلُّهُ، وَإِذَا فَسَدَتْ فَسَدَ اَلْجَسَدُ كُلُّهُ، أَلَا وَهِيَ اَلْقَلْبُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa An-Nu’maan bin Bashiyr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa alimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: (Nu’maan akaashiria vidole vyake kwenye masikio yake): “Hakika halaal iko wazi na haraam iko wazi, baina ya mawili hayo kuna mambo yenye utata.[2] Wengi katika watu hawayajui. Basi atakayejiepusha na yenye utata amejiepusha kwa Dini yake na heshima yake. Na ataketumbukia katika yenye utata atatumbukia kwenye haraam. Kama mchunga anayechunga pembeni ya mipaka, ni haraka kulisha humo. Fahamuni! Kila mfalme ana mipaka. Fahamuni! Hakika mipaka ya Allaah ni maharamisho. Zindukeni! Hakika katika mwili kuna kinofu, kinapotengamaa mwili wote unatengamaa. Kinapoaribika mwili wote unaharibika. Fahamuni! Hicho ni moyo.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1267.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {تَعِسَ عَبْدُ اَلدِّينَارِ، وَالدِّرْهَمِ، وَالْقَطِيفَةِ، إِنْ أُعْطِيَ رَضِيَ، وَإِنْ لَمْ يُعْطَ لَمْ يَرْضَ} أَخْرَجَهُ الْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ameangamia mtumwa wa dinari na dirhamu, mahameli na khamisa; akipewa huridhika, asipopewa haridhiki.”[3] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1268.

وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: أَخَذَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم بِمَنْكِبِي، فَقَالَ: {كُنْ فِي اَلدُّنْيَا كَأَنَّكَ غَرِيبٌ، أَوْ عَابِرُ سَبِيلٍ} وَكَانَ اِبْنُ عُمَرَ يَقُولُ: إِذَا أَمْسَيْتَ فَلَا تَنْتَظِرِ اَلصَّبَاحَ، وَإِذَا أَصْبَحْتَ فَلَا تَنْتَظِرِ اَلْمَسَاءَ، وَخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِسَقَمِك، وَمِنْ حَيَاتِكَ لِمَوْتِكَ.‏ أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alishika mabega yangu akaniambia: “Kuwa katika dunia kana kwamba ni mgeni au mpita njia. Ibn ‘Umar alikuwa akisema: ‘Unapochwewa usingoje asubuhi, na unapopambazukiwa usingoje jioni, chukua siha  yako kwa ajili ya ugonjwa wako, na uhai wako kwa kifo chako.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1269.

وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَنْ تَشَبَّهَ بِقَوْمٍ، فَهُوَ مِنْهُمْ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni miongoni mwao.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ibn Hibbaan]

 

 

 

1270.

وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ قَالَ: كُنْتُ خَلْفَ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم يَوْمًا، فَقَالَ: {يَا غُلَامُ! اِحْفَظِ اَللَّهَ يَحْفَظْكَ، اِحْفَظِ اَللَّهَ تَجِدْهُ تُجَاهَكَ، وَإِذَا سَأَلْتَ فَاسْأَلْ اَللَّهَ، وَإِذَا اِسْتَعَنْتَ فَاسْتَعِنْ بِاَللَّهِ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَقَالَ: حَسَنٌ صَحِيحٌ.

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema siku moja nilikuwa nyuma ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ewe kijana! Mhifadhi Allaah [4]Atakuhifadhi. Mhifadhi Allaah utamkuta mbele yako. Unapoomba muombe Allaah. Unapotaka msaada mtake msaada Allaah.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth hii ni Swahiyh Hasan]

 

 

 

1271.

وَعَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ قَالَ: {جَاءَ رَجُلٌ إِلَى اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! دُلَّنِي عَلَى عَمَلٍ إِذَا عَمِلْتُهُ أَحَبَّنِي اَللَّهُ، وَأَحَبَّنِي اَلنَّاسُ.‏ فـقَالَ: اِزْهَدْ فِي اَلدُّنْيَا يُحِبُّكَ اَللَّهُ، وَازْهَدْ فِيمَا عِنْدَ اَلنَّاسِ يُحِبُّكَ اَلنَّاسُ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَه، وَسَنَدُهُ حَسَنٌ

Kutoka kwa Sahl bin Sa’d amesema alikuja mtu kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Nijulishe amali ambayo nikiifanya Allaah Atanipenda na watu pia watanipenda. Akasema: “Chukia dunia Allaah Atakupenda[5] na chukia vilivyo kwa watu, watu watakupenda.” [Imetolewa na Ibn Maajah na isnaad yake ni hasan]

 

 

 

1272.

وَعَنْ سَعْدِ بْنِ أَبِي وَقَّاصٍ رضى الله عنه  قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: {إِنَّ اَللَّهَ يُحِبُّ اَلْعَبْدَ اَلتَّقِيَّ، اَلْغَنِيَّ، اَلْخَفِيَّ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Sa’d bin Abiy Waqqaasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Hakika Allaah Anampenda mja mwenye Taqwa mwenye kujitosha na mwenye kujificha.”[6] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1273.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مِنْ حُسْنِ إِسْلَامِ اَلْمَرْءِ، تَرْكُهُ مَا لَا يَعْنِيهِ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَقَالَ حَسَنٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Katika uzuri wa Uislaam wa mtu ni kuacha lisilomhusu.”[7] [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akasema ni Hadiyth hii ni Hasan]

 

 

 

1274.

وَعَنْ اَلْمِقْدَامِ بْنِ مَعْدِيكَرِبَ رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {مَا مَلَأَ ابْنُ آدَمَ وِعَاءً شَرًّا مِنْ بَطْنٍ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ

Kutoka kwa Al-Miqdaam bin Ma’d Yakrib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwana Aadam hakujaza chombo chenye shari zaidi kuliko tumbo lake.”[8] [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akasema kuwa Hadiyth hii ni Hasan]

 

 

 

1275.

وَعَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {كُلُّ بَنِي آدَمَ خَطَّاءٌ، وَخَيْرُ اَلْخَطَّائِينَ اَلتَّوَّابُونَ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَسَنَدُهُ قَوِيٌّ

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila mwana Aadam ni mkosaji na bora wa wakosaji ni wanayetubia.”[9] [Imetolewa na At-Tirmidhiy na Ibn Maajah, na Isnaad yake ina nguvu]

 

 

 

1276.

وَعَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {اَلصَّمْتُ حِكْمَةٌ، وَقَلِيلٌ فَاعِلُهُ} أَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ فِي " اَلشُّعَبِ" بِسَنَدٍ ضَعِيفٍ وَصَحَّحَ أَنَّهُ مَوْقُوفٌ مِنْ قَوْلِ لُقْمَانَ اَلْحَكِيمِ

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kunyamaza ni hekima,[10] na ni wachache wafanyaji wake.” [Imetolewa na Al-Bayhaqiy katika Kitabu ‘Ash-Shu’ab’ kwa Iisnaad dhaifu. Na imeswihi kuwa ni Mawquwf ni kauli ya Luqmaan mwenye hekima]

 

[1] Neno la Kiarabu linalotumika hapa ni الْوَرَعِ yenye maana ya kujitenga na mambo yenye shaka mtu asije angukia kwenye haraam.

[2] Hadiyth hii inatufungamanisha na hukmu muhimu za Kiislaam. Mushtabihaat ni yale mambo ambayo yana utata, yapo baina ya halaal na haraam. Wanazuoni wametofautiana kuhusu makatazo yake. Kuharibika kwa kiungo kimoja mwilini kunatokana na kuharibika kwa moyo wa mtu. Kwa sababu moyo wa mtu ndiyo unaongoza matendo ya mtu. Ikiwa mfalme amepotoka kimaadili basi uwezekano wa raia zake kupotoka vile vile ni mkubwa. Vivyo hivyo, ikiwa mfalme ni mwenye Taqwa raia zake watakuwa mfano wake.

 

[3] Hili linarejea kwa mtu mwenye tamaa. Akiendelea kufurahia neema za ulimwengu huu, atakuwa na furaha naye atamridhisha Allaah. Ikiwa ni kinyume chake hatopata vitu hivi basi hatofurahi kwa alichopewa na Allaah, na hatojiridhia vile vile.

[4] Kumhifadhi Allaah ni kufahamu mafundisho ya Allaah na kukatazika na makatazo yake. Kuwa ni mtu uliyehifadhiwa na Allaah ni kuwa Allaah Atakulipa malipo mazuri siku ya Qiyaamah na utapata jazaa na kusahau tabu za duniani. Hadiyth hii inaingiza hisia za Tawhiyd katika mioyo ya waja na ya kuwa hakuna kinachoweza kukudhuru kama Allaah Hakutaka.

[5] Njia sahihi na pekee ya mtu kujikurubisha na Allaah ni kujitenga na dunia hii, na kuweka iymaan ya juu kwa Allaah na kuachana na tamaa ya yaliyokuwa kwa watu.

 

[6] Allaah Anapompenda mja wake Humtakia mema, Humuongoza katika haki. Mwenye Taqwa ni yule ambaye anatekeleza maamrisho ya Allaah na kukatazika na makatazo yake. Tajiri ni yule aiyekuwa tajiri katika moyo wake na anamshkuru Allaah kwa kila alichopewa. Khafiyy ni yule mtu asiye mnafiki na wala hajioneshi, hujishughulisha tu na ‘ibaadah ya Allaah.

 

[7] Ikiwa mtu ana hakika kuwa Allaah Anamuona kwa kile anachofanya na kusema na ni mwenye elimu ya hilo, mtu huyo atakuwa ni mwepesi kujizuia na kuzungumza vibaya au na mazungumzo yasiyo na faida yoyote.

[8] Hadiyth hii inaelezea kuwa kuelekea katika kuzidisha jambo hakufai. Suala la chakula ni muhimu lakini himizo tunalopata hapa ni jinsi gani lilivyobeba shari ya mwana Aadam.

 

[9] Hadiyth hii imethibitisha kuwa wana Aaadam wote ni wakosaji isipokuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Allaah Hachukii sana kwa yule anayefanya dhambi, bali Anamfurahia zaidi yule anayeomba maghfirah na tawbah. Imepokewa na Abuu Hurayrah katika Swahiyh Muslim ikiwa wana Aadam wote watamuasi Allaah kisha wasiombe maghfirah kwake baada ya madhambi yale, Allaah Ataungamiza ulimwengu huu na kuubadilisha na watu wengine watakaotubu na kumuomba Allaah maghfirah baada ya kuyafanya madhambi.

 

[10] Hadiyth nyingi zimepokelewa zikionesha umuhimu wa mtu kunyamaza kama hana zuri la kusema. Hadiyth mojawapo inaelezea kuwa ikiwa hakuna cha kuzungumza bora kukaa kimya.

Share