04-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Mjumuisho: Mlango Wa Onyo Dhidi Ya Akhlaaq (Tabia) Mbaya

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلْجَامِعِ

Kitabu Cha Mjumuisho

 

بَابُ اَلرَّهَبِ مِنْ مَسَاوِئِ اَلْأَخْلَاقِ

04-Mlango Wa Onyo Dhidi Ya Akhlaaq (Tabia) Mbaya

 

 

 

 

1277.

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِيَّاكُمْ وَالْحَسَدَ، فَإِنَّ اَلْحَسَدَ يَأْكُلُ اَلْحَسَنَاتِ، كَمَا تَأْكُلُ اَلنَّارُ اَلْحَطَبَ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ

وَلِابْنِ مَاجَهْ: مِنْ حَدِيثِ أَنَسٍ نَحْوُهُ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tahadharini na hasadi,[1] hakika hasadi hula mema kama vile moto unavyokula kuni.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd. Ibn Maajah aliripoti mfano wa Hadiyth hii kutoka katika Hadiyth za Anas]

 

 

 

1278.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَيْسَ اَلشَّدِيدُ بِالصُّرَعَةِ، إِنَّمَا اَلشَّدِيدُ اَلَّذِي يَمْلِكُ نَفْسَهُ عِنْدَ اَلْغَضَبِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si mwenye nguvu mwenye kushinda mieleka, bali mwenye nguvu ni anaemiliki nafsi yake wakati wa ghadhabu.”[2] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1279.

وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{اَلظُّلْمُ ظُلُمَاتٌ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Dhulma[3] ni giza Siku ya Qiyaama.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1280.

وَعَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ : {اِتَّقُوا اَلظُّلْمَ، فَإِنَّ اَلظُّلْمَ ظُلُمَاتٌ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ، وَاتَّقُوا اَلشُّحَّ ، فَإِنَّهُ أَهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ.

Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ogopeni dhulma, hakika kudhulumu ni giza Siku ya Qiyaamah, na ogopeni ubakhili, hakika ubakhili uliangamiza waliokuwa kabla yenu.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1281.

وَعَنْ مَحْمُودِ بْنِ لَبِيدٍ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِنَّ أَخْوَفَ مَا أَخَافُ عَلَيْكُمْ اَلشِّرْكُ اَلْأَصْغَرُ: اَلرِّيَاءُ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ بِسَنَدٍ حَسَنٍ

Kutoka kwa Mahmuwd bin Labiyd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kwa hakika jambo ninalowahofia zaidi ni shirki ndogo (nayo ni) riyaa.”[4] [Imetolewa na Ahmad kwa Isnaad hasan]

 

 

 

1282.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{آيَةُ اَلْمُنَافِقِ ثَلَاثٌ: إِذَا حَدَّثَ كَذَبَ، وَإِذَا وَعَدَ أَخْلَفَ، وَإِذَا ائْتُمِنَ خَانَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Alama za mnafiki ni tatu:[5] akizungumza anaongopa, akitoa ahadi anakhalifu na akiaminiwa anakhini.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1283.

وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{سِبَابُ اَلْمُسْلِمِ فُسُوقٌ، وَقِتَالُهُ كُفْرٌ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kumtukana Muislaam ni ufasiki na kupigana naye ni ukafiri.”[6] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1284.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِيَّاكُمْ وَالظَّنَّ، فَإِنَّ اَلظَّنَّ أَكْذَبُ اَلْحَدِيثِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tahadharini kudhania,[7] hakika dhana ni mazungumzo ya uongo.” [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1285.

وَعَنْ مَعْقِلِ بْنِ يَسَارٍ‏ رضى الله عنه قَالَ سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏يَقُولُ: {مَا مِنْ عَبْدِ يَسْتَرْعِيهِ اَللَّهُ رَعِيَّةً، يَمُوتُ يَوْمَ يَمُوتُ، وَهُوَ غَاشٌّ لِرَعِيَّتِهِ، إِلَّا حَرَّمَ اَللَّهُ عَلَيْهِ اَلْجَنَّةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ma’qil bin Yasaar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Hakuna mja yeyote Allaah Amempa kuwaongoza raia, siku ya kufa akafa ilihali ni mwenye kughushi raia zake isipokuwa Allaah Atamharamishia Jannah.”[8] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1286.

وَعَنْ عَائِشَةَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا‏ قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{اَللَّهُمَّ مَنْ وَلِيَ مِنْ أَمْرِ أُمَّتِي شَيْئًا، فَشَقَّ عَلَيْهِ، فَاشْقُقْ عَلَيْهِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ee Allaah! Atakayesimamia jambo katika mambo ya ummah wangu na akawafanyia uzito, basi Nawe Mfanyie uzito.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1287.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِذَا قَاتَلَ أَحَدُكُمْ، فَلْيَتَجَنَّبِ اَلْوَجْهَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anapopigana mmoja wenu na ajiepushe (kulenga) uso.”[9] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1288.

وَعَنْهُ أَنَّ رَجُلاً قَالَ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَوْصِنِي.‏ فَقَالَ: لَا تَغْضَبْ، فَرَدَّدَ مِرَارًا.‏ قَالَ: لَا تَغْضَبْ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa mtu mmoja alimuambia Ee Rasuli wa Allaah! Niusie: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Usighadhibike.”[10] Akarudia mara nyingi (Nabiy) akasema: “Usighadhibike.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1289.

وَعَنْ خَوْلَةَ اَلْأَنْصَارِيَّةَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا‏ قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِنَّ رِجَالاً يتخوَّضون فِي مَالِ اَللَّهِ بِغَيْرِ حَقٍّ، فَلَهُمْ اَلنَّارُ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Khawlah Al-Answaariy[11] (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika watu wanaotumia mali ya Allaah[12] bila haki wana moto Siku ya Qiyaamah.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1290.

وَعَنْ أَبِي ذَرٍّ رضى الله عنه‏ عَنْ اَلنَّبِيِّ ‏صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ‏‏ فِيمَا يَرْوِي‏ عَنْ رَبِّهِ‏ قَالَ: {يَا عِبَادِي! إِنِّي حَرَّمْتُ اَلظُّلْمَ عَلَى نَفْسِي، وَجَعَلْتُهُ بَيْنَكُمْ مُحَرَّمًا، فَلَا تَظَّالَمُوا} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Dharri (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) katika anayoyapokea kutoka kwa Rabb wake, amesema: “Enyi waja Wangu, Hakika Mimi Nimejiharamishia dhulma katika Nafsi yangu na Nimeijaalia haraam miongoni mwenu; kwa hivyo msidhulumiane.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1291.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ‏ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {أَتَدْرُونَ مَا اَلْغِيبَةُ؟  قَالُوا: اَللَّهُ وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ  قَالَ: ذِكْرُكَ أَخَاكَ بِمَا يَكْرَهُ.‏  قِيلَ: أَرَأَيْتَ إِنْ كَانَ فِي أَخِي مَا أَقُولُ؟  قَالَ: إِنْ كَانَ فِيهِ مَا تَقُولُ فَقَدْ اِغْتَبْتَهُ، وَإِنْ لَمْ يَكُنْ فَقَدْ بَهَتَّهُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mnajua nini Ghiybah (kusengenya)? Wakasema Allaah na Rasuli wake Wanajua. Akasema: ‘ni kumtaja nduguyo kwa analochukia’ ikasemwa: unaonaje iwapo kwa ndugu yangu yapo nisemayo? Akasema: “Ikiwa analo usemalo umemsengenya[13] na ikiwa hana ulisemalo umemzulia.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1292.

وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا تَحَاسَدُوا وَلَا تَنَاجَشُوا، وَلَا تَبَاغَضُوا، وَلَا تَدَابَرُوا، وَلَا يَبِعْ بَعْضُكُمْ عَلَى بَيْعِ بَعْضٍ، وَكُونُوا عِبَادَ اَللَّهِ إِخْوَانًا، اَلْمُسْلِمُ أَخُو اَلْمُسْلِمِ، لَا يَظْلِمُهُ، وَلَا يَخْذُلُهُ، وَلَا يَحْقِرُهُ، اَلتَّقْوَى هَا هُنَا، وَيُشِيرُ إِلَى صَدْرِهِ ثَلَاثَ مِرَارٍ، بِحَسْبِ اِمْرِئٍ مِنْ اَلشَّرِّ أَنْ يَحْقِرَ أَخَاهُ اَلْمُسْلِمَ، كُلُّ اَلْمُسْلِمِ عَلَى اَلْمُسْلِمِ حَرَامٌ، دَمُهُ، وَمَالُهُ، وَعِرْضُهُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msihusudiane wala msipandishiane bei, wala msichukiane, wala msikatane. Wala baadhi yenu asiuze kwa mauzo ya nduguye; nyote kuweni waja wa Allaah hali ya kuwa ni ndugu. Muislaam ni ndugu wa Muislaam; hamdhulumu wala hamdharau wa hamtelekezi. Taqwa ipo hapa.”  Akaashiria mara tatu kifuani mwake. “Yatosha mtu kutenda shari atakapomdharau nduguye Muislaam. Kila Muislaam juu ya Muislaam mwenzie ni haraam: damu yake, mali yake na heshima yake.”[14] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1293.

وَعَنْ قُطْبَةَ بْنِ مَالِكٍ‏ رضى الله عنه قَالَ: كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏يَقُولُ: {اَللَّهُمَّ جَنِّبْنِي مُنْكَرَاتِ اَلْأَخْلَاقِ، وَالْأَعْمَالِ، وَالْأَهْوَاءِ، وَالْأَدْوَاءِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ وَاللَّفْظِ لَهُ

Kutoka kwa Qutwbah bin Maalik[15] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema:

اَللَّهُمَّ جَنِّبْنِي مُنْكَرَاتِ اَلْأَخْلَاقِ، وَالْأَعْمَالِ، وَالْأَهْوَاءِ، وَالْأَدْوَاءِ

“Ee Allaah! Niepushe na akhlaaq (tabia) mbaya, na amali mbaya, na matamanio na magonjwa.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha Al-Haakim

 

 

 

1294.

وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا تُمَارِ أَخَاكَ، وَلَا تُمَازِحْهُ، وَلَا تَعِدْهُ مَوْعِدًا فَتُخْلِفَهُ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ بِسَنَدٍ فِيهِ ضَعْفٌ

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Usishindane na nduguyo, wala usimfanyie mzaha, wala usimuahidi ahadi na ukamkhalifu.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy kwa isnaad dhaifu]

 

 

 

1295.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ ‏ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{خَصْلَتَانِ لَا يَجْتَمِعَانِ فِي مُؤْمِنٍ: اَلْبُخْلُ، وَسُوءُ اَلْخُلُقِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَفِي سَنَدِهِ ضَعْفٌ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mambo mawili hayakutani kwa Muumini: ubakhili na khulqa (tabia) mbaya.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na katika isnaad yake kuna udhaifu]

 

 

 

1296.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ : {اَلْمُسْتَبَّانِ مَا قَالَا، فَعَلَى اَلْبَادِئِ، مَا لَمْ يَعْتَدِ اَلْمَظْلُومُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wawili wenye kutukanana wana dhambi (kiasi wanavyosema), aliyeanza ni mwenye dhambi nyingi zaidi madamu aliyedhulumiwa hajavuka mpaka (katika kujibu).”[16] [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1297.

وَعَنْ أَبِي صِرْمَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ ضَارَّ مُسْلِمًا ضَارَّهُ اَللَّهُ، وَمَنْ شَاقَّ مُسَلِّمًا شَقَّ اَللَّهُ عَلَيْهِ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ

Kutoka kwa Abuu Swirmah[17] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumdhuru Muislaam, Allaah Atamdhuru,[18] na mwenye kumsumbua Muislaam Allaah Atamsumbua.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na kwa isnaad Hasan]

 

 

 

1298.

وَعَنْ أَبِي اَلدَّرْدَاءِ‏ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِنَّ اَللَّهَ يُبْغِضُ اَلْفَاحِشَ اَلْبَذِيءَ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ

وَلَهُ مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ مَسْعُودٍ ‏رَفَعَهُ‏: {لَيْسَ اَلْمُؤْمِنُ بِالطَّعَّانِ، وَلَا اَللَّعَّانُ، وَلَا اَلْفَاحِشَ، وَلَا اَلْبَذِيءَ} وَحَسَّنَهُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَرَجَّحَ اَلدَّارَقُطْنِيُّ وَقْفَهُ

Kutoka kwa Abuu Ad-Dardaa[19] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika Allaah Anamchukia muovu, mwenye maneno mabaya.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha]

Pia amepokea kutoka katika Hadiyth ya Ibn Mas-‘uwd marfuw’: “Muumini si mtukanaji, wala si mlaanifu,[20] wala mchafu, wala si mwenye maneno mabaya.” [Na amesema ni Hasan na akaisahihisha Al-Haakim. Ad-Daaraqutwniy ameitilia nguvu kuwa ni Marfuw’]

 

 

 

1299.

وَعَنْ عَائِشَةَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا‏ قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا تَسُبُّوا اَلْأَمْوَاتَ، فَإِنَّهُمْ قَدْ أَفْضَوْا إِلَى مَا قَدَّمُوا} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msishutumu wafu,[21] hakika wao wameshayaendea waliyoyatanguliza.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1300.

وَعَنْ حُذَيْفَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يَدْخُلُ اَلْجَنَّةَ قَتَّاتٌ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Hudhayfah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mchonganishi hataingia Jannah.”[22] [Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

1301.

وَعَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ كَفَّ غَضَبَهُ، كَفَّ اَللَّهُ عَنْهُ عَذَابَهُ} أَخْرَجَهُ اَلطَّبَرَانِيُّ فِي " اَلْأَوْسَطِ"

وَلَهُ شَاهِدٌ: مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عُمَرَ عِنْدَ اِبْنِ أَبِي اَلدُّنْيَا

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuzuwia ghadhabu zake, Allaah Atamzuilia adhabu Yake.” [Imetolewa na Atw-twabaraaniy katika kitabu cha ‘Al-Awsatw’. Nayo ina Ushahidi wa Hadiyth ya ‘Abdullaah ibn ‘Umar kwa Ibn Abuu Ad-Dunyaa]

 

 

 

1302.

وَعَنْ أَبِي بَكْرٍ اَلصِّدِّيقِ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{لَا يَدْخُلُ اَلْجَنَّةَ خِبٌّ، وَلَا بَخِيلٌ، وَلَا سَيِّئُ اَلْمَلَكَةِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَفَرَّقَهُ حَدِيثَيْنِ، وَفِي إِسْنَادِهِ ضَعْفٌ

Kutoka kwa Abuu Bakr Asw-Swiddiyq (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haingii Jannah mwenye hadaa wala bakhili wala mbaya wa kumiliki.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na ameigawa katika Hadiyth mbili, na katika isnaad yake kuna udhaifu]

 

 

 

1303.

وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ تَسَمَّعَ حَدِيثَ قَوْمٍ، وَهُمْ لَهُ كَارِهُونَ، صُبَّ فِي أُذُنَيْهِ اَلْآنُكُ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} يَعْنِي: اَلرَّصَاصَ.‏ أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayesikiliza mazungumzo ya watu na ilihali wenyewe wanachukia siku ya Qiyaamah atamiminiwa risasi masikioni mwake.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

1304.

وَعَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{طُوبَى لِمَنْ شَغَلَهُ عَيْبَهُ عَنْ عُيُوبِ اَلنَّاسِ} أَخْرَجَهُ اَلْبَزَّارُ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Furaha ni ya ambaye aibu zake zimemshughulisha, akaachana na aibu za watu.” [Imetolewa na Al-Bazzaar kwa isnaad Hasan]

 

 

 

1305.

وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ تَعَاظَمَ فِي نَفْسِهِ، وَاخْتَالَ فِي مِشْيَتِهِ، لَقِيَ اَللَّهَ وَهُوَ عَلَيْهِ غَضْبَانُ} أَخْرَجَهُ اَلْحَاكِمُ وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kujikweza nafsini mwake, akaringa katika kutembea kwake, atakutana na Allaah ilihali Amemghadhibikia.”[23] [Imetolewa na Al-Haakim na wapokezi wake ni Madhubuti]

 

 

 

1306.

وَعَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{اَلْعَجَلَةُ مِنَ اَلشَّيْطَانِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَقَالَ: حَسَنٌ

Kutoka kwa Sahl bin Sa’d (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haraka inatokana na shaytwaan.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na amesema ni Hasan]

 

 

 

1307.

وَعَنْ عَائِشَةَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا‏ قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {اَلشُّؤْمُ: سُوءُ اَلْخُلُقِ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ وَفِي إِسْنَادِهِ ضَعْفٌ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ukorofi ni khulqa (tabia) mbaya.”[24] [Imetolewa na Ahmad na katika isnaad yake kuna udhaifu]

 

 

 

1308.

وَعَنْ أَبِي اَلدَّرْدَاءِ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{إِنَّ اَللَّعَّانِينَ لَا يَكُونُونَ شُفَعَاءَ، وَلَا شُهَدَاءَ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Abuu Ad-Dardaa (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wenye kulaani hawawi waombezi wala Mashahidi Siku ya Qiyaamah.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

1309.

وَعَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رضى الله عنه‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{مَنْ عَيَّرَ أَخَاهُ بِذَنْبٍ، لَمْ يَمُتْ حَتَّى يَعْمَلَهُ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ، وَسَنَدُهُ مُنْقَطِعٌ

Kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kumuaibisha nduguye kwa dhambi hatakufa hadi aifanye.”[25] [Imetolewa na At-Tirmidhiy na amesema ni Hasan na isnaad yake imekatika]

 

 

 

1310.

وَعَنْ بَهْزِ بْنِ حَكِيمٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ: قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{وَيْلٌ لِلَّذِي يُحَدِّثُ، فَيَكْذِبُ ; لِيَضْحَكَ بِهِ اَلْقَوْمُ، وَيْلٌ لَهُ، ثُمَّ وَيْلٌ لَهُ} أَخْرَجَهُ اَلثَّلَاثَةُ، وَإِسْنَادُهُ قَوِيٌّ

Kutoka kwa Bahz bin Hakiym kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ole wake anayezungumza akadanganya ili kuwachekesha watu.[26] Ole wake! Kisha ole wake!” [Imetolewa na Ath-Thalaathah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd) na isnaad yake ina nguvu]

 

 

 

1311.

وَعَنْ أَنَسٍ‏ رضى الله عنه عَنْ اَلنَّبِيِّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏قَالَ: {كَفَّارَةٌ مَنْ اِغْتَبْتَهُ أَنْ تَسْتَغْفِرَ لَهُ} رَوَاهُ اَلْحَارِثُ بْنُ أَبِي أُسَامَةَ بِسَنَدٍ ضَعِيفٍ

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kafara ya uliyemsengenya ni kumuombea maghfirah.”[27] [Imetolewa na Al-Haarith bin Abuu Usaamah kwa isnaad dhaifu]

 

 

 

1312.

وَعَنْ عَائِشَةَ ‏رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا‏ قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏{أَبْغَضُ اَلرِّجَالِ إِلَى اَللَّهِ اَلْأَلَدُّ اَلْخَصِمُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtu anayechukiwa kabisa na Allaah ni katili mwingi wa ugomvi.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

[1] Katika lugha ya kiarabu ‘Hasad’ (husuda na wivu) hurejea kwa mtu anayemuonea wivu mwenzake na kuhusudu alichokuwa nacho na kutamani neema ile imuondokee na ije kwake. Jambo hili limekatazwa. Ikiwa mtu anatamani apate kitu fulani lakini hataki vile vile kimuondokee mwenzake, jambo hili linaitwa ‘Hiqd’. Hisia hii inahitajika katika mambo ya kidini.

[2] Hili linathibitisha umuhimu wa kusamehe, na kutopendelea kulipa kisasi haswa unapoghadhibishwa na jambo. Watu wanatakiwa wajifunze namna ya kujizuia na ghadhabu au hasira kwani hasira hasara. Mambo yanayoweza kuzuia hasira ni: Kujikinga na Allaah dhidi ya shaytwaan kwa kusema:

أَعـوذُ بِاللهِ مِنَ الشَّيْـطانِ الرَّجيـم

 Na kuchukua wudhuu na kukaa chini kama utakuwa umesimama na kulala kama utakuwa umekaa.

 

[3] Dhulma, maana yake ni kuweka kitu sehemu isiyokuwa yake, au kuficha ukweli ili usitokeze. Katika Siku ya Hukmu (Qiyaamah) itaonekana na rangi yake itakuwa ni nyeusi. Hadiyth hii inatufundisha kuwa dhulma ni kitu kibaya na ni haraam ikiwa kwa mtu, katika heshima au utajiri wake.

[4] Riyaa ni kujionyesha. Ni pale mja anapofanya tendo lolote la ki ‘ibaadah kama la kuacha makatazo na kutekeleza maamrisho, lakini mtu anafanya hivyo ili watu wamuone kuwa ni mtiifu, hivyo anaridhisha watu badala ya kumridhisha Allaah. Au anaweza kufanya tendo la ‘ibaadah kwa malengo ya kidunia. Riyaa ina namna mbili: Ya kwanza ni kutenda jambo la ‘ibaadah, na kulionyesha kwa watu. Ya pili ni kufanya ‘ibaadah ambayo watu hawajui kisha anawajulisha watu kuwa kafanya. Aina hii ya riyaa inaitwa ‘Sum’ah’ na ile ya kwanza ndio riyaa yenyewe. Zote hazitakiwi.

 

[5] Unafiki ni aina mbili: a) Unafiki wa matendo na b) Unafiki katika Iymaan. Unafiki wa matendo umeshatajwa katika Hadiyth hii. Unafiki wa Iymaan pindi anapoficha ukafiri na kudhihirisha Uislaam. Unafiki wa Iymaan ni mbaya na hatari zaidi kuliko ukafiri wenyewe. Unafiki wa kimatendo ni moja ya madhambi makubwa ambao unaweza kusamehewa.

[6] ‘Fisq’ ni mtu kuangukia katika kumuasi Allaah. Kwa mfano, Allaah Amekataza Muislaam kutumia maneno machafu, na kuwa mtu anamuasi Allaah kwa kumuita nduguye majina mabaya, mtu huyo anakuwa ‘Faasiq’ (mwenye dhambi). Lakini ikiwa mtu huyo huyo au mwingine akaamua kupigana na mwenzake ambaye ni Muislaam, katika Hadiyth hii mtu huyo ni ‘Kufr’ (kufanya jambo la ukafiri). Ikiwa mambo haya mawili hayamhusu mtu mmoja basi neno hili litakuwa limetumika kama fumbo, yaani kufanya jambo la kikafiri.

 

[7] Dhana (kufikiria kitu kisichokuwepo). Limeelezwa kama ni mazungumzo ya uongo na Wanazuoni na ni uzushi na ni moja kati ya madhambi makubwa.

[8] Hali hii ya ‘Ghasb’, kunyanga’nya ni katika madhambi makubwa, kwani ni jambo linaloweza kumzuia kuingia Jannah. Watawala wanatakiwa wawahukumu watu kwa uadilifu. Inaonya kuwa adhabu kali zinawakabili watawala dhalimu.

[9] Hadiyth hii inaonyesha makatazo ya kupiga uso, hata kama ni adhabu ya makosa ya mtu. Hata wanyama wasipigwe usoni.

[10] Hadiyth hii ni mfano halisi wa wema ambao unataka uonyeshwe katika maisha haya ya duniani. Hili linatokana na ukweli kuwa mtu anayeepushwa na khulqa (tabia)  njema ya huruma na kuwa na khulqa ya hasira kwa upande mmoja na upande wa pili khulqa ile ya hasira huwakera watu wengine. Hali hii ni mbaya kwani inamuathiri yule mtu mwenyewe na inawaathiri waliomzunguka.

 

[11] Khawlah, binti wa Thamir Al-Answaariy akiitwa Umm Muhammad na baba yake akiitwa Qays bin Qahad. Alikuwa katika Banuu Maalik bin An-Najjaar, aliolewa na Hamza bin ‘Abdil-Mutwalib, mumewe alipouwawa katika Uhud aliolewa na An-Nu’maan bin Al-‘Ajlaan Al-Answaariy Az-Zuraqi.

 

[12] Hadiyth hii ni dalili kuwa hata watawala wanaweza kutumia mali za ‘Baytul Maal’ vibaya, hili ni katika madhambi makubwa.

[13] Hadiyth hii imetajwa na Maswahaba wengi, na imepokelewa katika njia nyingi. Kuna makubaliano ya Wanazuoni kuwa kusengenya ni haraam.

[14] Tunajifunza katika Hadiyth hii Muislaam hatakiwi kuwa na kinyongo kwa Muislaam mwenzake.

[15] Alikuwa ni Swahaba kutoka kwa Banuu Tha’laba bin Sa’d bin Dhubyaan, alikuwa pia akiitwa Adh-Dhubyaan. Alikuwa ni mkazi wa Kufa mji uliopo ‘Iraq, baadhi ya Hadiyth zake zilipokewa na mpwawe Ziyaad bin ‘Alaqa.

[16] Hadiyth hii inabainisha mambo mawili: a) Suala la kulipa ubaya uliyofanyiwa na mwingine, ni suala linarohusiwa, b) suala la dhambi litamuhusu yule aliyeanzisha hali ile, maadamu yule wa pili hajavuka mipaka kwa kufanya uadui. Pamoja na yote hayo lililo bora zaidi ni kumsamehe aliyefanya makosa.

[17] Huyu ni Maalik bin Qays au Qays bin Maalik, alikuwa ni Swahaba kutoka katika kabila la Maazin. Alishiriki vita vya Badr na vita vingine vilivyofuatia na amepokea baadhi ya Hadiyth.

 

[18] Hadiyth hii inaonyesha kumdhuru Muislaam kwa jambo lolote lile hata kama litaonekana ni dogo kiasi gani hairuhusiwi.

[19] Jina halisi la Abuu Ad-Dardaa lilikuwa ni ‘Uwaymir bin Zayd au Ibn ‘Aamir au Ibn Maalik bin ‘Abdillaah bin Qays. Alikuwa ni Answaar wa kabila la Khazraj. Alikuwa ni Swahaba aliyejinyima raha na anasa za kidunia. Alisilimu katika siku ya vita vya Badr na alishiriki vita vya Uhud. ‘Umar alimhusisha katika watu waliyoshiriki Badr. Alikuwa ni katika watu walioikusanya Qur-aan na alifanywa kuwa ni Qaadhi wa Damascus. Ana fadhila nyingi. Amesikika akisema: “Umaarufu na riyaa ya saa moja inaweza kusababisha huzuni ya muda mrefu.” Alifariki 32 Hijriyyah.

 

[20] Hadiyth hii inatuelekeza kuwa si katika khulqa (tabia) ya Muumini kuwaita nduguze majina mabaya au kuwalaani. Hata hivyo inaruhusiwa kumtukana na kumlaani yule aliyelaaniwa na Allaah na Rasuli wake. Au kutaja kwa ujumla laana ya Allaah kwa makafiri. Watu wenye kufanya mambo mabaya na machafu. Vinginevyo si halaal kumlaani mtu kwa kumtaja jina lake.

 

[21] Hapa tunajifunza kuwa hairuhusiwi kabisa kuwaita waliokufa kwa majina mabaya, kuwasema vibaya. Hili linahusu kwa Waislaam hususan na hata kwa makafiri ambao wana udugu na baadhi ya Waislaam kwani kuwatusi au kuwasema vibaya kutawasikitisha ndugu zao Waislaam.

 

[22] Hafiydh Mundhir anaona kuwa makubaliano ya Wanazuoni wa Ummah huu ni kuwa mchochezi au mchukua maneno hapa na kuyapeleka kule ili kuleta utesi baina ya watu amefanya jambo la haraam na baya sana na linahesabiwa kuwa ni katika madhambi makubwa.

[23] Maelezo tunayopata kwenye Hadiyth hii ni makemeo kuhusu kibri na ni katika madhambi makubwa. Imepokewa na At-Tirmidhiy kuwa: “Mwenye sehemu ndogo ya kibri katika nafsi yake hatoingia Jannah.”

[24] Shari anazopata mwana Aadam ni kutokana na khulqa (tabia) zake mbaya. Hadiyth hii inaonyesha kuwa khulqa nzuri au mbaya za mtu zinatokana na chaguo lake binafsi.

[25] Tunajua kuwa kutaja maovu ya mtu ni dhambi. Ni vibaya sana kutaja udhaifu wa mtu na matatizo yake mbele za watu, ili kumuumbua au kumuaibisha. Hadiyth hii inatuhimiza kuwa mtu asitaje madhambi ya fulani eti kwa sababu naye amekashifiwa.

 

[26] Kusema uongo hata ikiwa ni kwa utani tu ili watu wacheke ni katika makatazo makubwa na ni sifa mojawapo ya unafiki. Uongo ambao haumnufaishi mtu hapa duniani na hata huko Aakhirah hauna maana na ni uongo mbaya sana. Kusikiliza uongo vile vile ni jambo lisilokubalika, aidha mtu azungumze ubaya wake au aondoke kwenye kikao hicho.

 

[27] Tawbah ya kusengenya ni: ikiwa mtu atamsengenya mtu mwingine ni bora amuombe msamaha. Kama hatompata mtu mwenyewe basi amuombee du’aa kwa Allaah Amghufurie madhambi yake.

 

 

Share