058-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Ruhusu ya Kuchukua Kitu Bila Kuomba

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب جواز الأخذ من غير مسألة وَلاَ تطلع إليه

058-Mlango Wa Ruhusu ya Kuchukua Kitu Bila Kuomba

 

Alhidaaya.com

 

 

عن سالم بن عبد الله بن عمر ، عن أبيه عبد الله بن عمر ، عن عمر رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يُعْطيني العَطَاءَ ، فَأقُولُ : أعطِهِ مَنْ هُوَ أفْقَرُ إِلَيْهِ  مِنّي . فَقَالَ : ((  خُذْهُ ، إِذَا جَاءكَ مِنْ هَذَا المَال شَيْءٌ وَأنْتَ غَيْرُ مُشْرِفٍ وَلاَ   سَائِلٍ ، فَخُذْهُ فَتَمَوَّلْهُ ، فَإنْ شِئْتَ كُلْهُ ، وَإنْ شِئْتَ تَصَدَّقْ بِهِ ، وَمَا لا ، فَلاَ تُتبعهُ نَفْسَكَ )) قَالَ سَالِمٌ : فَكَانَ عَبدُ الله لاَ يَسألُ أحَداً شَيْئاً ، وَلاَ يَرُدُّ شَيْئاً    أُعْطِيَه . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Saalim bin 'Abdillaah bin 'Umar kutoka kwa babake 'Abdillaah bin 'Umar kutoka kwa 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: "Rasuli wa Alllaah (Swallla Alllahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akinipatia vitu (zawadi), nami nilikuwa nasema, 'Mpatie aliye fukara kuliko mimi.' Akasema: 'Chukua ikiwa utapewa katika mali hii kitu chochote bila ya wewe kutamani wala kuuliza (kuomba). Ichukue na uitie katika rasilimali au ukitaka itumie na ukitaka unaweza kuitoa swadaqah. Usitamani kupata kitu kwa njia nyengine.' Amesema Saalim: 'Alikuwa 'Abdillaah (yaani babake) hamuulizi (hamuombi) yeyeote kitu chochote wala harudishi kitu alichopatiwa'." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share