32-Sharh Asmaa Allaah Al-Husnaa Wa Swifaatihi: الرَّقِيبُ

Sharh Asmaa Allaah Al-Husnaa Wa Swifaatihi

 

(Maelezo Ya Majina Mazuri Ya Allaah Na Swiffah Zake)

 

Alhidaaya.com

 

الرَّقِيبُ

 

 

 

الرَّقِيبُ

Ar-Raqiyb

Mwenye Kuchunga

 

 

 

Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Ambaye huona kilichofichikana nyoyoni. Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayeihukumu kila roho kwa ilichochokichuma. Yeye Allaah (سبحانه وتعالى) ni Pekee Anayekifadhi kila kilichoumbwa na kuviendesha kwa usimamizi bora kabisa na kwa mpango timamu na kamilifu.

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ 

Enyi watu! Mcheni Rabb wenu Ambaye Amekuumbeni kutokana na nafsi moja (Aadam) na Akaumba kutoka humo mke wake (Hawwaa) na Akaeneza kutoka hao wawili wanaume na wanawake wengi. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mnaombana (haki zenu kwa kuunga) undugu. Hakika Allaah ni Mwenye kuwachunga daima. [An-Nisaa (4):1]

 

 

 

Share