079-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kiongozi Muadilifu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الوالي العادل

079-Mlango Wa Kiongozi Muadilifu

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ ﴿٩٠﴾

Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan. [An-Nahl: 90]

وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٩﴾

Hakika Allaah Anapenda wanaotimiza haki. [Al-Hujuraat: 9]

 

 

Hadiyth – 1

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  سَبْعَةٌ يُظِلُّهُمُ الله في ظِلِّهِ يَوْمَ لاَ ظِلَّ إِلاَّ ظِلُّهُ : إِمَامٌ عادِلٌ ، وَشَابٌ نَشَأ في عِبادة الله تَعَالَى ، وَرَجُلٌ قَلْبُهُ مُعَلَّقٌ في المَسَاجِدِ ، وَرَجُلانِ تَحَابَّا في اللهِ اجتَمَعَا عَلَيْهِ ، وَتَفَرَّقَا عَلَيْهِ ، وَرَجُلٌ دَعَتْهُ امْرَأةٌ ذاتُ مَنْصِبٍ وجَمالٍ ، فَقَالَ : إنّي أخافُ اللهَ ، وَرَجُلٌ تَصَدَّقَ بِصَدَقَةٍ فَأخْفَاهَا حَتَّى لاَ تَعْلَمَ شِمَالُهُ مَا تُنْفِقُ يَمِينُهُ ، وَرَجُلٌ ذَكَرَ الله خَالِياً فَفَاضَتْ عَيْنَاهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "(Watu) saba Allaah atawafunika chini ya kivuli Chake siku isio na kivuli isipokuwa kivuli Chake: Imamu muadilifu, na kijana ameinukia katika kumuabudu Allaah, na mtu moyo wake umefungamana na Misikiti, na watu wawili wamependana kwa ajili ya Allaah, wamejumuika juu yake na kufarikiana juu yake, na mtu ameitwa na mwanamke mwenye hadhi na uzuri, akasema: 'Mimi namwogopa Allaah', na mtu ametoa swadaqah akaificha hadi kushoto kwake kusijue kilichotoa kulia kwake, na mtu ambaye amemtaja Allaah peke yake na macho yake yakabubujika machozi." [Al-Bukaariy na muslim].

 

 

Hadiyth – 2

وعن عبدِ اللهِ بن عَمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : ((  إنَّ المُقْسِطِينَ عِنْدَ اللهِ عَلَى مَنَابِرَ مِنْ نُورٍ : الَّذِينَ يَعْدِلُونَ في حُكْمِهِمْ وأَهْلِيْهِم وَمَا وَلُوْا )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amru bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika waadilifu watakuwa juu ya mimbari za nuru mbele ya Allaah: Ambao wanafanya uadilifu katika hukumu zao na familia zao, na waliyotawalishwa." [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن عوفِ بن مَالِكٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  خِيَارُ أئِمَّتِكُمُ الَّذِينَ تُحِبُّونَهُمْ وَيُحِبُّونَكُمْ ، وَتُصَلُّونَ عَلَيْهِمْ وَيُصَلُّونَ عَلَيْكُمْ . وشِرَارُ أئِمَّتِكُم الَّذِينَ تُبْغِضُونَهُمْ وَيُبْغِضُونَكُمْ ، وَتَلعَنُونَهُمْ وَيَلْعَنُونَكُمْ ! )) ، قَالَ : قُلْنَا : يَا رسول اللهِ ، أفَلاَ نُنَابِذُهُم ؟ قَالَ : ((  لاَ ، مَا أقَامُوا فِيْكُمُ الصَّلاَةَ . لاَ ، مَا أقَامُوا فِيكُمُ الصَّلاَةَ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Awf bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Wabora wa viongozi wenu ni ambao mnawapenda na wao wanawapenda, na mnawaombea na wao wanawaombea. Na waovu wa viongozi wenu ni mnaowachukia na wao wanawachukia, na ambao mnawalaani na wao wanawalaani." Akasema: "Tukasema: Ee Rasuli wa Allaah! "Tujitenge nao?" Akasema: "La! Madamu wamesimamisha Swalaah kati yanu. La! Madamu wamesimamisha Swallaah kati yenu." [Muslim].

 

 

Hadiyth – 4

وعن عِياضِ بن حِمارٍ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( أهلُ الجَنَّةِ ثَلاَثَةٌ : ذُو سُلطانٍ مُقْسِطٌ مُوَفَّقٌ ، وَرَجُلٌ رَحيمٌ رَقِيقُ القَلْبِ لكُلِّ ذي قُرْبَى ومُسْلِمٍ ، وعَفِيفٌ مُتَعَفِّفٌ ذو عِيالٍ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa 'Iyaadh bin Himaar (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Watu wa Peponi ni aina tatu: Kiongozi muadilifu mwenye kutoa swadaqah kwa uwezo wake; na mtu mwenye kuwarehemu na mwenye moyo laini kwa kila jamaa yake na kwa kila Muislamu; na mtoharifu anyejizuilia na uchafu (asiezini) mwenye familia." [Muslim].

 

 

 

Share