05-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendeza Kukusanyika kwa Ajili ya Kusoma

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب استحباب الاجتماع عَلَى القراءة

05-Mlango Wa Kupendeza Kukusanyika kwa Ajili ya Kusoma

 

Alhidaaya.com

 

وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  وَمَا اجْتَمَعَ قَوْمٌ فِي بَيْتٍ مِنْ بُيُوتِ اللهِ يَتلُونَ كِتَابَ اللهِ ، وَيَتَدَارَسُونَهُ بينهم ، إِلاَّ نَزَلَتْ عَلَيْهِمُ السَّكِينَةُ وَغَشِيتْهُمُ الرَّحْمَةُ ، وَحَفَّتْهُمُ المَلاَئِكَةُ ، وَذَكَرَهُمُ اللهُ فِيمَنْ عِنْدَهُ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Na hawakusanyiki watu katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah, kusoma Kitabu cha Allaah na kusomeshana baina yao, ila huteremkiwa na utulivu, wakafunikwa na rehma, na wakazungukwa na malaaikah, na Allaah akawataja kwa walioko naye." [Muslim] 

Share