24-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Sunnah ya Ijumaa

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب سنة الجمعة

24-Mlango Wa Sunnah ya Ijumaa

 

Alhidaaya.com

 

Hadiyth – 1

وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الظُّهْرِ، وَرَكْعَتْينِ بَعْدَهَا، وَرَكْعَتَيْنِ بَعْدَ الجُمُعَةِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ المَغْرِبِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ العِشَاءِ . متفقٌ عَلَيهِ

Na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Niliswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Rak'ah mbili kabla ya Adhuhuri, na Rak'ah mbili baada yake, Rak'ah mbili baada ya Ijumaa, na Rak'ah mbili baada ya Maghrib na Rak'ah mbili baada ya Isha." [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن مُغَفَّلٍ رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كل أذانين صلاة )) قال في الثَّالِثةِ : (( لِمَنْ شَاءَ )) متفقٌ عَلَيهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Mughaffal kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah (makusudio ya adhana mbili ni baina ya adhana na iqamah), baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah, baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah." Akasema katika mara ya tatu: "Kwa mwenye kupenda." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai].

 

Hadiyth – 3

عن أَبي هريرة رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا صَلَّى أَحَدُكُم الجُمُعَةَ ، فَلْيُصَلِّ بَعْدَهَا أرْبعاً )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pindi anaposwali mmoja wenu Swalaah ya Ijumaa, aswali baada yake Rakaa nne." [Muslim]

 

Hadiyth – 4

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ لاَ يُصَلِّي بَعْدَ الجُمُعَةِ حَتَّى يَنْصَرِفَ ، فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ في بَيْتِهِ . رواه مسلم .

Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Hakika Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa haswali baada ya Swalaah ya Ijumaa mpaka aondoke, hivyo huswali Rakaa mbili nyumbani kwake." [Muslim]

 

 

Share