29-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuhimizwa Swalaah ya Tahiyyatul Masjid kwa Rak'ah Mbili na Ukaraha wa Kukaa Kabla ya Kuziswali katika Wakati Wowote Anapoingia

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الحث عَلَى صلاة تحية المسجد بركعتين

وكراهة الجلوس قبل أن يصلي ركعتين في أي وقت دخل

وسواء صلَّى ركعتين بنية التَّحِيَّةِ أَوْ صلاة فريضة أَوْ سنة راتبة أَوْ غيرها

29-Mlango Wa Kuhimizwa Swalaah ya Tahiyyatul Masjid kwa Rak'ah Mbili na Ukaraha wa Kukaa Kabla ya Kuziswali katika Wakati Wowote Anapoingia

 

Alhidaaya.com

 

Hadiyth – 1

عن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا دَخَلَ أحَدُكُمُ المَسْجِدَ ، فَلاَ يَجْلِسْ حَتَّى يُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Qaatadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoingia mmoja wenu Msikitini na aswali Rak'ah mbili kabla hajakaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hadiyth – 2

وعن جابرٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : أَتَيْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم وَهُوَ في المَسْجِدِ ، فَقَالَ : (( صَلِّ رَكْعَتَيْنِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye alikuwa Msikitini. Akaniambia: "Swali Rakaa mbili." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share