Madhara Ya An-Namiymah (Kufitinisha Baina Ya Watu Wachukiane) 3 - Vipi Kutibu An-Namiymah?
Mwenye kufitinishwa
1- Inapasa mwenye kuletewa fitna kutahadhari na mfitinishaji kwani mfitinishaji ni fasiki na fasiki anahitaji kukhofiwa hadi upatikane ushahidi
((يَا أَيُّهَا الذِينَ آمَنُوا إِنْ جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَأٍ فَتَبَيَّنُوا أَنْ تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَى مَا فَعَلْتُمْ نَادِمِينَ))
((Enyi mlio amini! Akikujieni mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyoyatenda)) [Al-Hujuraat: 6]
2- Kutokuamini asemayo, uwe na dhana nzuri na nduguyo unayepatana naye, badala ya dhana mbaya
((يَا أَيُّهَا الذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ))
((Enyi mlioamini! Jiepusheni na dhana nyingi, kwani baadhi ya dhana ni dhambi)) [Al-Hujuraat: 12]
3- Mchukie mtu anayefitinisha, na anapokuja kukufitinsha ni vizuri kumpa nasaha, kuwa asiwe anafanya hivyo hata
Mwenye kufitinisha
- Ajishughulishe na kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kila aina ya dhikr.
- Afikirie na akhofu adhabu za kufitinisha.
- Afikirie ubaya ulioje kuwafitinisha watu na kutia chuki katika nyoyo za watu, je, yeye mwenyewe atapendwa kufitinishwa na kipenzi chake?
- Asome mada zote za Ghiybah ziliomo humu AL HIDAAYA ili atambue hatari ya kutouhifadhi ulimi.
Mwisho wa mada ya An-Namiymah
Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuhifadhi na Atuepushe na maovu haya na kila aina ya movu mengine tubakie katika Ridhaa Yake. Aamiyn.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


