30-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendeza Kuswali Rak'ah Mbili Baada Wudhuu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب استحباب ركعتين بعد الوضوء

30-Mlango Wa Kupendeza Kuswali Rak'ah Mbili Baada Wudhuu

 

Alhidaaya.com

 

عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ لِبِلاَلٍ : (( يَا بِلاَلُ ، حَدِّثْنِي بِأَرْجَى عَمَلٍ عَمِلْتَهُ فِي الإسْلاَمِ ، فَإنِّي سَمِعْتُ دَفَّ نَعْلَيْكَ بَيْنَ يَدَيَّ في الجَنَّةِ )) قَالَ : مَا عَمِلْتُ عَمَلاً أرْجَى عِنْدي مِنْ أَنِّي لَمْ أتَطَهَّرْ طُهُوراً فِي سَاعَةٍ مِنْ لَيْلٍ أَوْ نَهَارٍ إِلاَّ صَلَّيْتُ بِذَلِكَ الطُّهُورِ مَا كُتِبَ لِي أنْ أُصَلِّي . متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuuliza Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Ee Bilaal! Niambie amali uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia sauti ya viatu vyako ukiwa mbele yangu Peponi." Akasema: "Sijafanya amali yoyote ambayo kwayo natarajia hayo isipokuwa ninapojitwahirisha katika wakati wowote wa usiku au mchana ila huswali kwa tohara hiyo zile Alizoniandikia Allaah kuziswali." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]

 

Share