47-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Fadhila za Funga na Nyenginezo katika Kumi la Kwanza la Mwezi wa Dhul Hijjah

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب فضل الصوم وغيره في العشر الأول من ذي الحجة

47-Mlango Wa Fadhila za Funga na Nyenginezo katika Kumi la Kwanza la Mwezi wa Dhul Hijjah

 

Alhidaaya.com

 

وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا مِنْ أيَّامٍ ، العَمَلُ الصَّالِحُ فِيهَا أحَبُّ إِلَى اللهِ مِنْ هذِهِ الأَيَّام )) يعني أيام العشر . قالوا : يَا رسولَ اللهِ ، وَلاَ الجِهَادُ في سَبيلِ اللهِ ؟ قَالَ : (( وَلاَ الجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللهِ ، إِلاَّ رَجُلٌ خَرَجَ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ ، فَلَمْ يَرْجِعْ مِنْ ذَلِكَ بِشَيءٍ )) رواه البخاري .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna siku yeyote ambayo matendo mema humpendezea zaidi Allaah kuliko ndani ya siku hizi", yaani anakusudia siku kumi (za mwanzo za mwezi wa Dhul Hijjah). Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah, wala Jihadi katika njia ya Allaah?" Akasema: "Wala Jihadi katika njia ya Allaah isipokuwa mtu ametoka pamoja na nafsi na mali yake halafu asirudi na chochote." [Al-Bukhaariy]

 

Share