50-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kupendeza Kufunga Jumatatu na Alkhamis

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب استحباب صوم الإثنين والخميس

50-Mlango Wa Kupendeza Kufunga Jumatatu na Alkhamis

 

Alhidaaya.com

 

Hadiyth – 1

عن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم سُئِلَ عَنْ صَومِ يَوْمِ الإثْنَيْنِ ، فَقَالَ : (( ذَلِكَ يَومٌ وُلِدْتُ فِيهِ ، وَيَومٌ بُعِثْتُ ، أَوْ أُنْزِلَ عَلَيَّ فِيهِ )) رواه مسلم .

Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu funga ya Jumatatu, akasema: "Hiyo ni siku niliyozaliwa na ni siku niliyopewa Utume au niliyoteremshiwa Wahyi nadani yake." [Muslim]

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تُعْرَضُ الأَعْمَالُ يَومَ الإثْنَيْنِ وَالخَمِيسِ ، فَأُحِبُّ أنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأنَا صَائِمٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) ، ورواه مسلم بغير ذِكر الصوم .

Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwa hakika matendo ya waja huonyeshwa siku ya Jumatatu na Alkhamisi, hivyo napenda amali zangu zionyeshwe nami nikiwa nimefunga." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan], Na ameipokea Muslim bila kutaja funga.

 

Hadiyth – 3

وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَتَحَرَّى صَومَ الإثْنَيْنِ وَالخَمِيس . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .

'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) ameema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akifunga sana siku ya Jumatatu na Alkhamisi. [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

Share