Isbaal - Hukmu Ya Nguo Inayovuka Mafundo Ya Miguu Ya Mwanaume
SWALI:
Napenda kufahamu ukweli kusuhu kuvaa nguo inayopita vifundo viwili vya miguu.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Na imepokewa tena kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Hamuangalii mwenye kuburuza nguo yake kwa kiburi” (al-Bukhaariy, Muslim na Maalik).
Na imepokewa katika riwaya nyingine kutoka kwa Abu Dharr (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hatazungumza na watu aina tatu Siku ya Qiyaama wala Hatawaangalia na wala Hatawatakasa na watakuwa na adhabu iumizayo”. Akasema: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliikariri kauli hii mara tatu”. Akasema Abu Dharr: “Watu hao wamehasirika, ni kina nani ewe Mtume wa Allaah?” Akasema: “Mwenye kuburuza nguo kwa kiburi; na mwenye kujionyesha kwa fadhila aliyomfanyia mtu mwengine; na mwenye kuuza
Na imepokewa kwa Ibn ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Hatawaangalia wale watu walioburuza nguo zao
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
