Kumtafuta Mungu
Na Dk Ja’afar Sheikh Idris
[imetoka Katika Journey Through Islam] Ngano Ya Karne 20
Imefasiriwa Na Shaibu H. Kifea
Mojawapo kati ya ngano za karne yetu, ngano inayosadikiwa karibu na wapinzani wote wa Mungu na waumini wengi wa Mungu ni kuwa mantiki na sayansi viko upande wa itikadi isiyoamini Mungu.
Yakiwa ni matokeo ya ngano hii, dhana ya kumkana Mungu huchukuliwa
Lakini kwa nini ukafiri ndio uchukuliwe kuwa ni jambo la kawaida? Mimi nafikiri kwa sababu inadhaniwa kimakosa, kuwa wakati muumini wa Mungu anatoa dai la kweli, mkanushaji, kama jinale linavyobainisha, yeye anakanusha kuwa Muumini ana hoja yoyote ya kutilia nguvu dai lake.
Hivyo, pande hizi mbili, kwa kosa hilo, zinakuwa
Mfano bora wa kulinganisha upande wa muumini na ule wa mkanushaji ni ule wa wanasiasa au wachumi wawili. A na B. wanaobishana kuhusu mfumko wa bei, tatizo linalowaathiri wote wawili. A anaona kuwa sababu ya mfumko wa bei ni ongezeko kubwa na la ghafla la bei ya mafuta na kwa sababu hiyo, tatizo linaweza kutatuliwa kwa hatua kadha wa kadha.
Mwenzie B anakanusha kuwa hii ndiyo sababu. Yeye haoni uhusiano kati ya mambo hayo mawili na hajasaidiwa na A kuliona tatizo.tunaweza kukubaliana na B. lakini tusidhani kabisa kuwa amefanya kazi yake kwa kukataa utafiti wa A. kwa nini? Kwa sababu mfumko wa bei ni tatizo kubwa
Hivyo, nafasi ya muumini sio kama ile ya mshitaki kwani tatizo ambalo ufumbuzi wake anautafuta kwa kudai kuwa duniya haina muumba, haihusu mtu mmoja. Kama vile mfumko wa bei.unavyozisibu pande zote mbili, upande wa yule anayeendelea kutafuta jawabu na yule anayelikataa jawabu hilo.
TATIZO
Tatizo ni nini? Kimsingi linaulizwa swali, Je sisi tulitokea wapi? Kuna mambo mengine munasibu, lakini hebu kwanza tulitazame swali hili kuu. Yule amkanushaye Mungu hulijibu swali hili kwa njia moja kati ya tatu, zote kati yao si za kimantiki wala kisayansi. Ndio kusema lile dai lake kuwa sayansi na mantiki ziko upande wake, halina msingi.
Anaweza kusema hivi, sijui wala sijali. Ninachojuwa mimi ni kuwa nipo tu hapa na kwamba nina hiari ya kujiamulia nifanye nini na hiki ndicho ninataka kukifanya “Wala sijui….” Kukiri kutojua, kwa kweli ni ishara na ipo katika utaratibu wa sayansi. Lakini vipi kuhusu “wala sijali”? Hapa mkanusha Mungu haukatai uwezekano wa kuwepo muumba ambaye amempa mwanadamu wajibu wa kufanya katika duniya hii na, atakayemwajibisha kwa matendo yake katika maisha yajayo.
Je kweli ana maana kuwa hili si lakutilia maanani au kuwa halitaleta tofauti kwake Kama jambo hili ni kweli au la? Kwa kweli hili sijambo la kimantiki, kwani kwa kweli linaleta tofauti ama mtu anakwenda peponi au motoni kuupa mgongo ukweli hakufanyi ukweli huo ufutike. miaka mingi ya kujishughulisha na starehe za maisha haya kutachangia kuleta adhabu katika maisha ya Akhera.
Jibu la pili ambalo mkanusha Mungu anaweza kutoa ni kusema hivi; “pengine tumetoka na hamna” kwa jawabu hili, swali tunalomuuliza ni hili je una maana kusema kuwa huu ndio uwezekano pekee kama yanavyobainisha matamshi yako au unasema kwa hakika kuwa sisi tumetokana na hamna? Kama ukisema hili tu ndilo linalowezekana basi huondoshi uwezekano wa sisi kuumbwa.
Ukijaalia uwezekano huu, na ukizingatia ukubwa wa tatizo, utajaribu kuihoji akili yako, lipi kati ya haya mawili linayumkinika zaidi na lenye maana zaidi. Kama, ndiyo hivyo, unadai kuwa duniya kweli imetokana na hamna , basi sisi tunawekea nukta hizi na kukukata uzitafakari kwa makini.
KWANZA, Unajuaje?
PILI je unao ushahidi wowote?
Hadi hapa tulipofika sisi tunaona hajatoa ushahidi wowote. Bila ushahidi, basi si hatua ya kimantiki wala ya kisayansi kuamua kushikilia dhana kuwa chochote kama sisi wenyewe, ambacho si cha milele kinaweza kutokana na hamna.
Je hii siyo kanuni ya kisayansi sisemi ukweli wa [kisayansi] na je hii , siyo kanuni ya maisha ya kawaida kwamba kila tukio lina sababu yake na hivyo hakuna kitokanacho na hamna? Kama ni hivyo, kwanini basi ijidanganye nafsi yako hata kudhani kuwa upande uliopo wewe ndio wa kimantiki na kisayansi zaidi?
Baada ya kuona upuuzi wa majibu haya, mkanusha Mungu sasa atachagua njia moja tu iliyosalia kwake kama bado tu anaendelea na ubishi wake wa kumkataa Mungu. Sasa atakiri kuwa ni jambo la kimantiki zaidi kuamini kuwa kipo chanzo lakini kwa vile anaikataa dhana ya Mungu aliye nje ya upeo, atashikilia kuwa chanzo hicho lazima kiwe ndani ya Ulimengu.
KUTAFUTA CHANZO
Je chanzo hicho chaweza kuwa nini?
Wakati mwingine inachukuliwa kuwa chanzo hicho ni maada iliyomo duniyani, sanamu, mnyama au mtu. Kwa vile upumbavu wa imani hizo hivi sasa ukobayana, basi zisitucheleweshe. nimezitaja tu ili kuutilia maanani ukweli kuwa ibada ya sanamu na imani ya uchawi inatokana na historia ya itikadi ya kumkana Mungu na si historia ya dini sahihi ambayo inatetea imani juu ya muumba wa Ulimwengu.
Baada ya kuona kuwa maada au mtu ambaye hutoweka hawezi kuwa muumba, baadhi ya wakanushaji waliona kuwa maumbile ya angani ambayo, Kwa mtazamo wao, yalionekana kuwa ya milele yalistahili zaidi kupewa jukumu hilo na hivyo wakayaabudia.
Lakini sayansi imethibitisha kuwa hakuna hata umbile moja la angani ambalo ni la milele. Hivyo basi dai la waumini wa Mungu muumba kuwa maumbile hayo hayawezi kuwa Miungu linathibitika kuwa ni la kweli.
Baada ya kukata tamaa ya kumpata muumba wao katika maumbile makubwa, na baada ya kuambiwa kuwa, maumbile haya yanajengeka kwa chembe chembe ndogo sana, wakanushaji wakageukia kwingine na kuanza kutafuta chembe ya umilele ambayo vitu hutengenezeka kwayo.
Hii walidhani ingebainisha kila kitu na hivyo kuifanya dhana ya Mungu aliye nje uoni kuwa upuuzi mtupu, lakini haya matofali ya milele yamebanika kuwa ni vitu visivyokuwepo. Si mseto wala mchanganyiko bali ni vichembechembe tu vinavyojengwa. Na hata hizi nazo sio, kwani nazo pia zinajengwa na molekuli ambazo zinatengenezwa na Atomu. Atomu nazo zinatengenezwa na chembe chembe ndogondogo.
Je hizi ndizo tunazozitafuta? Lakini mbona hizi sio vitu vya kushikika ni viumbe vya ajabu ambavyo hubadili tungamo yao pale zinapokuwa mwendoni.
Isitoshe vichembechembe hivi viduchu haviwezi kuonekana. kule kuwepo kwao kwathibitishwa na mwenendo tu wa kazi zao.
MUUMBA WA MILELE
Mojawapo ya hoja kuu zilizotolewa na wakanusha Mungu wa zamani ni kuwa Mungu haonekani. haikusaidia kitu kuwaambia kuwa, wao wakiwa kama viumbe wenye akili, hawakuhitaji kuona ilikuaamini, kwamba pia wengeliweza kuamini kitu ambacho kuwepo kwake kwathibitishwa na kile wanachokiona.
Kwa mara nyingine sayansi imethibitisha hoja ya waumini wa Mungu muumba. Kwa vile utaratibu huu wa kuthibitisha ndio unatumika kama njia pekee ya kufahamia chembe ndogondogo za atomu, chembe ambazo wakanushaji wanataka zionekana kama ndio chanzo kikuu au muumba. lakini hili hawawezi kulifanya. Muumba au tuseme chanzo kikuu tunachokitafuta lazima kiwe cha milele.
Yaani kisiwe na mwanzo. Kama kitu ni cha milele kwa maana hakina mwanzo basi lazima kijitegemea na kijitosheleze kwa kila kitu. Kwa mantiki hiyo, katika kuwepo na kuendelea kuwepo kwake hakiwezi kutegemea kitu kingine chochote nje yake.
Ikiwa hivyo basi ndio kusema hakitatoweka. Hii ikiwa na maana kuwa kinachotoweka au kinachoweza kutoweshwa hakiwezi kua cha milele. Aina zote za maada, hata zile chembe chembe ndogo za atomu zote hufa.
Na kwa vile kila maada ya aina fulani lazima iathiriwe maada ya aina nyingine basi maada ya aina yoyote ile haiwezi kuwa ya milele.
Hivyo basi mkanushaji hawezi kujiliwaza kwa kuegemeza imani yake katika maendeleo ya sayansi kupata jawabu la swali la maumbile. Sayansi haiwezi kuwafanyia jambo ambalo, kimantiki, haliwezekani.
JAWABU LA KIMAUMBILE
Baadhi ya wasioamini Mungu husema, kwanini tumtafute wa milele? Ikiwa tunachokitaka sisi ni ufafanuzi wa vitu vya hakika ambavyo kwavyo Ulimwengu umefanyika. Tena hili laweza kupatikana pasina kutegemea imani juu ya muumba wa milele.
Kama nikitaka kufafanua jinsi A. ilivyotokea natafuta chanzo chake cha hakika cha kimaumbile B. na nikiulizwa kuhusu B, naitafuta C na kadhalika. mlolongo wa chanzo cha tukio si lazima uishie katika chanzo kikuu bali waweza kubakia bila ukomo.
Kuonesha jinsi hoja hii isivyokuwa na nguvu, hebu tuchukue mfano wa Dikteta ambaye amesikia kuwa uvumi wa kashfa dhidi yake umezagaa na ana waamuru askari wa upelelezi kutafuta chanzo chake. Kwa kumtii mkuu wao, polisi wa upepelezi wanaanza kuhoji watuhumiwa.
A. Anawaambia kuwa yeye alisikia uvumi huo kwa B ambaye naye anawaambia amesikia kwa C ambaye naye ameusikia kwa D na kuendelea iwapo tutajaalia kuwa mlolongo huu wa msikiaji-na mpashaji hauna mwisho, basi hautaeleza chanzo halisi na kikuu cha uvumi huo, ambao yawezekana mtu tu ameutunga na hakuusikia kwa mtu yeyote. Hivyo ni dhahiri uvumi huo unaye mtu aliyeuanzisha mlolongo haukosi kuwa na ukomo. ukweli wa kutokea kwake hauwezi kufafanuliwa na kitu ambacho, chenyewe kimetokea tu. Waweza kufafanuliwa na kile kinachosababisha vingine viwe lakini chenyewe hakisababishiki
CHANZO KIKUU
Huo ndio ukosefu wa hoja na mwelekeo usio wa kisayansi wa mkanushaji Mungu katika kujibu swali “sisi” tunatokea wapi? Hoja ya Muumini wa Mungu muumba, kwa upande mwingine inajengwa kwa kuzingatia akili na haipingani na sayansi. Yeye anasema. Kwa kuwa vitu vinavyokufa haviwezi kutokea pasipo chanzo na wala kuanzishwa na vitu vingine vinavyokufa basi lazima vimeanzishwa na kile ambacho ni cha milele na hivyo kinachojitegemea.
Na kwa vile ni cha milele na hivyo hakina ukomo, sifa zake zote hazina ukomo hazikadiriki. Je hiki cha umilele kinasababishaje athari zake yaani vitu vya duniya hii. vitu hutengenezwa na vitu vingine kwa njia mbili. Ama hufuatiana kimaumbile au hutengenezwa kwa kukusudia. sababu zote za kimaumbile huonesha athari kwa njia ya kuanza ambapo viumbe vyenye akili huwa na uwezo wa kufanya kwa njia ya pili.
Hivyo basi moto hauchemshi maji kwa kutaka wenyewe, kitendo cha kuchemka hutokea kimaumbile kwa sufuria kuwekwa kwenye moto, lakini mama mwenye nyumba huchemsha chai kwa kukusudia. Katika umbile lake yeye hamna kitu ambacho kutokana nacho chai kimaumbile huchemka.
Kwa hiyo yeye huamua ama kufanya au kutofanya hivyo. Jambo ya kimaumbele halitegemei tu kile tunachokiita. Chanzo chake. Kutokea kwake hutegemea sababu nyingi. Kwa mfano ili maji yachemke haitoshi tu uwepo moto. Maji lazima yatiwe kwenye sufuria ambayo nayo lazima isogezwe jirani na moto, lazima iwepo hewa ya oksijeni n.k kwa upande mwingine chanzo chetu chenye umilele, kinajitosheleza na hivyo, katika utendaji wake hakitegemei, sababu za nje.
Ikiwa hivyo basi hakiwezi kufanya kazi Kama vifanyavyo kazi vyanzo vya kimaumbile. Hivyo, lazima kitende kwa kukusudia. Kwa kuwa kitu kinachotenda kwa kukusudia lazima pia kitende kwa kujua na kwa hivyo lazima kiwe kiumbe hai na kiumbe kisicho hai muumba wa kweli wa chochote kilichopo duniyani lazima awe na sifa hizi na nyingine ambazo zaweza kuthibitika kwa utaratibu huohuo.
Hivi ndivyo mantiki isiyo na upendeleo inavyotuambia na kile inachotuambia kinathibitishwa na kupambanuliwa na kutimizwa na kile muumba mwenyewe anachotuambia katika wahay alioawafunulia Mitume wake.
Jawabu la mtu kwa maswali ya kwa nini tuwepo hapa? Na wapi tunakwenda baada ya hapa? Yote yanategemea jawabu la swali la msingi “wapi tunatoka?” na kwa vile wasioamini Mungu hushindwa kutoa jawabu la kufaa kwa swali hili la msingi basi majawabu yake kwa maswali mengine nayo hayatofaa kimantiki na kisaikolojia.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
