Skip navigation.
Home kabah

Kungu Manga Ni Dawa Ya Nini?

  

SWALI:

 

Naomba kujua maana ya kungu manga kwa kizungu/ kiarabu, pia kuwa ni dawa ya nini hasa?

 



 

JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Shukrani zetu za dhati kwa ndugu yetu kwa swali lako. Kungumanga kwa Kiingereza inaitwa nutmeg na kwa Kiarabu ni Jawzah atw-Twayyib. Kungumanga hutumika kama dawa ya kuongeza nguvu za kiume kwa wenye upungufu kwa sababu moja au nyingine, na baadhi ya wanawake hutumia kwa kuamini inawalegeza na kuwatia ashiki kwa waume zao. Lakini vyote hivyo hatuna uthibitisho nao, ni madai ya watu na yanaweza kuwa kweli au uongo. Hatukufundishwa katika Sunnah matumizi ya hiyo kungumanga kama hivyo inavyotumiwa, na pia hakuna maelezo ya kidaktari yanayoonyesha kuwa hayo yanayodaiwa ni ya kweli.

Na Allaah Anajua zaidi