Tahadhari Na Madhara Ya Kueneza Hadiyth Dhaifu Na Visa Vya Uongo -2
Hadiyth zifuatazo zinaonyesha madhara ya mafunzo ya uongo na upotofu:
Hadiyth ya kwanza:
عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال : ( من دعا إلى هدى كان له من الأجر من أجور من تبعه لا ينقص من أجورهم شيئاً ومن دعا إلى ضلالة كان عليه من الإثم مثل آثام من تبعه لا ينقص ذلك من آثامهم شيئاً) رواه مسلم
Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: ((Atakayelingania kwenye uongofu atapata thawabu (ujira) wa yule atakayemfuata bila ya kupungukiwa chochote katika thawabu zao. Na atakayeelekeza katika upotofu atapata dhambi mfano wa dhambi za yule atakayefuata bila ya kupungukiwa chochote katika dhambi zao)) [Muslim]
Hadiyth ya pili:
عن أبي مسعود الأنصاري رضي الله عنه يقول النبي صلى الله عليه وسلم : (( من دل على خير فله مثل أجر فاعله)) خرجهما مسلم في صحيحه .
Kutoka kwa Abu Mas’uud Al-Answaariy (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mwenye kuongoza katika kheri atapata thawabu
Hadiyth ya tatu:
((من سن في الإسلام سنة حسنة كان له أجرها وأجر من عمل بها من بعده لا ينقص ذلك من أجورهم شيئاً ومن سن في الإسلام سنة سيئة كان عليه وزرها ووزر من عمل بها من بعده لا ينقص من أوزارهم شيئاً)) خرجه مسلم في صحيحه
((Atakayefanya kitendo chema katika Uislam atapata ujira wake na ujira wa yule atakayekitenda baada yake bila ya kupungukiwa thawabu zao. Na atakayetenda kitendo kibaya katika Uislam atabeba (mzigo wa) dhambi zake na dhambi za yule atakayetenda wala hapungukiwi kitu katika (mzigo wa) dhambi hizo)) [Muslim]
Kusambaza Hadiyth bila ya kuhakisha
Ataangukia katika miongoni mwa wenye kumuongopea Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
((من كذب علي متعمدا فليتبوأ مقعده من النار)) متفق عليه
((Atakayeniongopea makusudi basi ajitayarishie makazi yake motoni)) [Al-Bukhaariy Na Muslim]
Kama tunavyoona kwamba hatari yake ni kujitayarishia makazi motoni (tunamuomba Allaah Atuepushe na hilo), juu yake tutakuwa tumewaingiza na wenzetu ambao nao wataendelea kuzisambaza hizo Hadiyth na itaendelea hivyo hivyo kuwaingiza ndugu zetu wengi katika hatari kama hii. Na hatari zaidi ni kwamba kila watu wanapozidi kuzisambaza, basi dhambi huzidi kuongezeka kwa waliotuma wote nyuma
TANBIHI:
Ukipokea jambo lolote lenye mashaka na utata kuhusiana na Dini, tafadhali tuma maswali@alhidaaya.com lifanyiwe utafiti kabla ya kuwatumia wengine na kuenezwa, na utajibiwa haraka InshaAllaah.
Itaendelea InshaAllaah..../
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha



Assalam alaykum, Mimi ni
Assalam alaykum,
Mimi ni muislam na ningependa kufahamu baadhi ya dua ambazo sizifahamu kwa hiyo naomba nipate msaada:
Qunuti
Suratil ayatul qursiyu
na baadhi ya nyinginezo