Hadiyth ya 13 - Mja Hakuonekana Na Jema Isipokuwa Kuamrisha Watu Wasamehe Wenzie
Hadiyth ya 13
Mja Hakuonekana Na Jema Isipokuwa Kuamrisha Watu Wasamehe Wenzie
عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ الأنصاري رضي الله عنه قال: قال رسول اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ((حُوسِبَ رَجُلٌ مِمَّنْ كَانَ قَبْلَكُمْ فَلَمْ يُوجَدْ لَهُ مِنْ الْخَيْرِ شَيْءٌ إِلاَّ أَنَّهُ كَانَ يُخَالِطُ النَّاسَ وَكَانَ مُوسِرًا فَكَانَ يَأْمُرُ غِلْمَانَهُ أَنْ يَتَجَاوَزُوا عَنْ الْمُعْسِرِ قَالَ: قَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ : نَحْنُ أَحَقُّ بِذَلِكَ مِنْهُ تَجَاوَزُوا عَنْهُ)) البخاري, مسلم والنسائي
Kutoka kwa Abu Mas’uud Al Answaariyرضي الله عنه ambaye alisema: Mjumbe wa Allaah صلى الله عليه وسلم amesema: ((Mtu mmoja katika wale waliokutangulieni alitakiwa ajieleze. Hakuonekana na jema lolote isipokuwa alikuwa akiamiliana na watu, na alivyokuwa ni tajiri akiwaamrisha wafanyakazi wake wamuachie (wamsamehe) mtu aliyekuwa katika hali mbaya ya pesa (asilipe deni lake). (Akasema Mtume) Allaah عَزَّ وَجَلَّ Akasema: Sisi Tuna haki zaidi kuliko yeye kumsamehe)) [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaaiy]
- Login or register to post comments
- Email this page


