Skip navigation.
Home kabah

05 Wasiya Kumi Wa Allaah Wasiya wa Kwanza Kutokumshirikisha Allaah - 2

    

Tunaendelea kuelezea kuhusu makatazo ya kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

Ni haki Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kutoka kwa waja Wake kutokumshirikisha, kwani Yeye Pekee Ndiye Muumba wetu:

 

عَنْ مُعَاذِ بْنِ جَبَلٍ رضي الله عنه قَالَ: ((كُنْتُ رِدْفَ النّبِيّ صلى الله عليه وسلم ليس بيني وبينه إِلا مؤخرة الرّحْلِ، فقال: يا معاذ بن جبل قلت: لبيك رسول اللّهِ وَسَعْدَيْكَ. ثُمّ سَارَ سَاعَةً، ثُمّ قَالَ: يَا مُعَاذُ بْنَ جَبَلٍ قُلْتُ: لَبّيْكَ رَسُولَ اللّهِ وَسَعْدَيْكَ. ثُمّ سَارَ سَاعَةً، ثُمّ قَالَ: يَا مُعَاذُ بْنَ جَبَلٍ قُلْتُ: لَبّيْكَ رَسُولَ اللّهِ وَسَعْدَيْكَ. قَالَ: هل تَدْرِي مَا حَقّ الله عَلَى الْعِبَادِ؟ قَالَ: قُلْتُ: الله وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ. قَالَ: فَإِنّ حَقّ الله عَلَى الْعِبَادِ أَنْ يَعْبُدُوهُ وَلاَ يُشْرِكُوا بِهِ شَيْئا. ثُمّ سَارَ سَاعَةً، ثُمّ قَالَ: يَا مُعَاذُ بْنَ جَبَلٍ قُلْتُ: لَبّيْكَ رَسولَ اللّهِ وَسَعْدَيْكَ. قَالَ: هَلْ تَدْرِي مَا حَقّ الْعِبَادِ عَلَى الله إِذَا فَعَلُوا ذَلِكَ؟ قَالَ: قُلْتُ: الله وَرَسُولُهُ أَعْلَمُ. قَالَ: أَنْ لاَ يُعَذّبَهُمْ))  البخاري

Kutoka kwa Mu’aadh bin Jabal (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Nilikuwa nimepanda (mnyama) nyuma ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hakukuwa na chochote baina yetu isipokuwa mwisho wa tandiko la farasi akasema: ((Ewe Mu’aadh bin Jabal)) Nikasema. Labayka wa Sa’dayka ewe Mjumbe wa Allaah. Kisha akaenda muda wa saa kisha akasema: ((Ewe Mu’aadh bin Jabal)) Nikasema. Labayka wa Sa’dayka ewe Mjumbe wa Allaah. Kisha akaenda muda wa saa kisha akasema: ((Ewe Mu’aadh bin Jabal)) Nikasema. Labayka wa Sa’dayka ewe Mjumbe wa Allaah. Akasema: ((Je unajua haki ya Allaah kutoka kwa waja?)) Nikasema: Allaah na Mjumbe Wake Wanajua zaidi: Akasema: ((Basi haki ya Allaah kwa waja Zake ni wamuabudu na wasimshirikishe Naye chochote)). Kisha Akaenda muda wa saa kisha akasema: ((Ewe Mu’aadh bin Jabal)) Nikasema. Labayka wa Sa’dayka ewe Mjumbe wa Allaah. Akasema: ((Je, unajua haki ya waja kwa Allaah ikiwa watafanya hivyo?)) Nikasema: Allaah na Mjumbe wake Wanajua zaidi. Akasema: ((Kwamba Asiwaadhibu)) [Al-Bukhaariy]

 

Haki ya Allaah kutoka kwa mja wake (mja anapaswa kumfanyia) ni kumuabudu bila ya kumshirikisha. Kufanya kinyume chake ni kumfanyia dhulma Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kama Anavyosema:

((الَّذِينَ آمَنُواْ وَلَمْ يَلْبِسُواْ إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُوْلَئِكَ لَهُمُ الأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُون))

((Wale ambao wameamini, na hawakuchanganya imani yao na dhulma, hao ndio watakaopata amani na wao ndio walioongoka)) [Al-An'aam 6:82]

Aayah hii iliwatia shaka Maswahaba wakamuuliza “Ewe Mjumbe wa Allaah    nani katika sisi asiyejidhulumu?” Akasema: ((Sivyo hivyo mlivyofahamu, hamkusikia mja mwema (Luqmaan) alivyosema:

 ((يَا بُنَيَّ لَا تُشْرِكْ بِاللَّهِ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ))

((Ewe mwanangu! Usimshirikishe Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Kwani hakika ushirikina bila ya shaka ni dhulma iliyo kubwa)) [Luqmaan 31:13]

 

Itaendelea InshaAllaah…/