Skip navigation.
Home kabah

Wasiya Kumi Wa Allaah - Wasiya wa 6 - Kutokuikaribia (Kuila) Mali ya Yatima

 

 Wasia wa sita ni kutokukaribia mali ya yatima, kwa maana kutokuitumia bila ya haki. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):

 

 

 

  ((...وَلاَ تَقْرَبُواْ مَالَ الْيَتِيمِ إِلاَّ بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ حَتَّى يَبْلُغَ أَشُدَّهُ...))

 

 

((…Wala msiyakaribie mali ya yatima ila kwa njia ya wema kabisa, mpaka afikilie utu-uzima…))  [Al-An’aam: 152]

 

 

 

 

Mwenye kula mali ya yatima bila ya haki ni kama kula moto tumboni mwake na juu yake ni adhabu ya moto. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

 

((إِنَّ الَّذِينَ يَأْكُلُونَ أَمْوَالَ الْيَتَامَى ظُلْمًا إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا وَسَيَصْلَوْنَ سَعِيرًا))

 

 

((Hakika wanaokula mali ya mayatima kwa dhulma, hapana shaka yoyote wanakula matumboni mwao moto, na wataingia Motoni)) [an-Nisaa: 10]

 

 

 

 

Hali kadhalika haifai kuikaribia kwa ubadhirifu, na kuwabadlishia vyao vilivyo vizuri kwa kuwapa vyake mtu vilivyo viovu:

 

 

((وَآتُواْ الْيَتَامَى أَمْوَالَهُمْ وَلاَ تَتَبَدَّلُواْ الْخَبِيثَ بِالطَّيِّبِ وَلاَ تَأْكُلُواْ أَمْوَالَهُمْ إِلَى أَمْوَالِكُمْ إِنَّهُ كَانَ حُوبًا كَبِيرًا))

 

 

((Na wapeni mayatima mali yao. Wala msibadilishe kibaya kwa kizuri. Wala msile mali zao pamoja na mali zenu. Hakika yote hayo ni jukumu kubwa)) [An-Nisaa: 2]

 

 

 

 

Yatima wako katika jukumu letu hivyo inatupasa tuwaangalie ipasavyo na kujiepusha na kuwadhulumu kwa vyovyote.

 

 

Zilipoteremshwa Aayah hizo kuhusu mayatima, ya mwanzo katika Wasiya pamoja na Aayah ya 10 Suratun-Nisaa tuliyoinukuu juu hapo, Maswahaba waliokuwa wakilea mayatima, walikhofu hata kuchanganyika kula nao. Khofu yao iliwafanya hadi kwamba chakula cha mayatima kilipobakia waliwawekea na kuwapa tena wakile au kiharibike. Hali hii ilikuwa ngumu kwao ndipo walipomkabili Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuuliza, hapo hapo Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Akateremsha jibu:

 

 

 

 

 

((وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْيَتَامَى قُلْ إِصْلاَحٌ لَّهُمْ خَيْرٌ وَإِنْ تُخَالِطُوهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ وَاللّهُ يَعْلَمُ الْمُفْسِدَ مِنَ الْمُصْلِحِ وَلَوْ شَاء اللّهُ لأعْنَتَكُمْ إِنَّ اللّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ))

 

((Na wanakuuliza juu ya mayatima. Sema: Kuwatengenezea ndio kheri. Na mkichanganyika nao basi ni ndugu zenu; na Allaah Anamjua mharibifu na mtengenezaji. Na Allaah Angelipenda Angelikutieni katika udhia. Hakika Allaah ni Mwenye Nguvu na Mwenye hikima)) [Al-Baqarah: 2:220]

 

 

 

Itaendelea InshaAllaah…/

 

 

assalam aleikum, Na

assalam aleikum,

Na washukuru kwa jitihadi munao fanya kutuelemisha.nimegi sana ninayojuwa wakati huu nilio pata kwenu,#.

ingawa nasikitika nimeanza kusikiza quran natafsiri ile folder iliyokuwa na msahafu mzima,sijaumaliza mumetowa ,tafadhali kama inawezekana naomba murudishe.

inshallah mweyezi mungu atawabarika na kazi jema munayofanya.

hisham

Wa 'alaykumus-salaam wa

Wa 'alaykumus-salaam wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh

Tunashukuru kwa ombi lako, ila tunapenda kukuarifu kwamba kawaida kila wiki tunabadilisha vitu na kuweka vipya hapo Home Page, na hivyo vya zamani sio kama tunaondosha moja kwa moja, bali vinakuweko katika vitengo vyake. Ungeliweza kupata Qur-aan hiyo katika Category ya Qur-aan.

Hata hivyo tumetekeleza ombi lako na tumeshairudisha Home Page.

Tunakuombea usikilizaji mzuri wenye manufaa na wingi wa iymaan na taqwa.

Ndugu Zako
AL HIDAAYA