Wasiya Kumi Wa Allaah - Wasiya Wa 9 - Kutekeleza Ahadi Ya Allaah
Wasia wa tisa wa Allaah ni kutimiza ahadi ya Allaah
((... وَبِعَهْدِ اللّهِ أَوْفُواْ...))
((…Na ahadi ya Allaah itekelezeni…)) [Al-An’aam: 152]
Kutimiza ahadi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), kwa maana kutimiza amri Zake Alizotuamrisha na kujiepusha na makatazo yote katika Qur-aan na Sunnah. Vile vile kutimiza ahadi zote nyinigine tunazoahidiana sisi waja. Ikiwa ni za kawaida au zile ahadi za kuapa kwa jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) mfano ahadi baina ya wanandoa, ahadi katika deni, ahadi katika kuamiliana kwa aina yoyote, kwani hayo ni majukumu yapasayo kutimizwa.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
(( وَأَوْفُواْ بِالْعَهْدِ إِنَّ الْعَهْدَ كَانَ مَسْؤُولاً ))
((Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi itasailiwa)) [Al-Israa: 34]
Ahadi baina yetu na baina ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) ni ile ahadi iliyopokelewa na viumbe vyote kabla ya kuumbwa. Tokea Aadam na vizazi vyake vyote hadi siku ya mwisho. Tukashuhudia na kuchukua ahadi kwamba tutamtii Mola wetu na hatutamshirikisha.
((وَإِذْ أَخَذَ رَبُّكَ مِن بَنِي آدَمَ مِن ظُهُورِهِمْ ذُرِّيَّتَهُمْ وَأَشْهَدَهُمْ عَلَى أَنفُسِهِمْ أَلَسْتَ بِرَبِّكُمْ قَالُواْ بَلَى شَهِدْنَا أَن تَقُولُواْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّا كُنَّا عَنْ هَذَا غَافِلِينَ))
((Na pale Mola wako Mlezi Alipowaleta katika wanaadamu kutoka migongoni mwao kizazi chao, na Akawashuhudisha juu ya nafsi zao, akawaambia: Je, Mimi si Mola Mlezi wenu? Wakasema: Ndiye! Tumeshuhudia (kuwa Wewe ndiye Mola wetu) (Allaah Akawaambia). Msije mkasema Siku ya Qiyaamah sisi tulikuwa tumeghafilika na hayo)) [Al-A'araf : 172]
Anawaonya wanaovunja ahadi Zake kwamba watakuwa miongoni mwa waliokhasirika:
((الَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهْدَ اللَّهِ مِن بَعْدِ مِيثَاقِهِ وَيَقْطَعُونَ مَا أَمَرَ اللَّهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيُفْسِدُونَ فِي الأَرْضِ أُولَـئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ))
((Wanaovunja ahadi ya Allaah baada ya kwisha ifunga, na wakayakata Aliyoamrisha Allaah kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio wenye khasara)) [Al-Baqarah: 27]
Kutimiza nadhiri pia ni katika kutimiza ahadi ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
((يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْماً كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيراً))
((Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea
Pia kutokutimiza ahadi ya aina yoyote hata
Pia kutokutimiza ahadi kwa upande mwingine ni mfano kuahidi kumpa mwenzio kitu fulani, au kumuahidi kumsaidia tatizo
((الَّذِينَ يُوفُونَ بِعَهْدِ اللّهِ وَلاَ يِنقُضُونَ الْمِيثَاقَ))
((Wale ambao wanatimiza ahadi ya Allaah wala hawavunji maagano)) [Ar-Ra’d: 20]
Kutokutimiza ahadi ni alama za unafiki
((آية المنافق ثلاث : إذا حدث كذب ، وإذا وعد أخلف ، وإذا اؤتمن خان)) رواه البخاري ومسلم.
((Alama za Mnafiki ni tatu; anapozungumza huongopa, anapotoa ahadi huenda kinyume [hatimizi], na anapoaminiwa hufanya khiyana)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Itaendelea InshaAllaah…/
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


