Qur-aan Neno Kwa Neno
تَرْجَمَةُ مَعاَنِي كَلِماَتِ الْقُرْآنِ الْكَرِيمِ
بِالُلغَّةِ السَّوَاحِيلِيَّةِ كََلِمَةً بِكَلِمَةٍ
Tarjuma Ya Maana Ya Maneno Ya
Qur-aan Tukufu Kwa
Kiswahili Neno Kwa Neno
Assalaamu 'Alaykum
Karibuni kujifunza 'Tarjuma ya Qur-aan Tukufu Neno Kwa Neno Kwa Lugha Ya Kiswahili'.
Ingia katika kiungo kifuatacho uweze kuishusha (download).
Tunawaomba na tutashukuru mkiweza kutuma maoni yenu au makosa yoyote mtakayoyakuta humo kupitia anuani ya webmaster@alhidaaya.com
Hati Miliki (Copy Right): Qur-aan hii sio ya kuuzwa bali inatarajiwa kugaiwa bure pindi itakapochapishwa. Hivyo ni ruhusa kutolesha nakala na kugaiwa bure popote itakapohitajika. Kwa hali yoyote ile isifanyiwe mauzo.
Tunawaomba ndugu zetu msitusahau katika du'aa zenu.
Jazaakumu Allaahu Khayra
- Dibaji
- Utangulizi Wa Mfasiri
- Umuhimu Na Faida Ya Kujifunza Qur-aan Neno Kwa Neno
- Taratibu Za Utendaji Wake Qur-aan Neno Kwa Neno
- Faharasa Ya Surah
- Faharasa Ya Juzuu
- Suratul-Faatiha
- Juzuu Ya 1- Alif Laam Miym Dhaalikal-Kitaab
- Juzuu Ya 2-Sayaquulus-Sufahaau
- Juzuu Ya 3 -Tilkar-Rusulu
- Juzuu Ya 4 - Lan Tanaalul-Birra
- Juzuu Ya 5- Walmuhswanaatu
- Juzuu Ya 6- Laa Yuhibbu Allaahu
- Juzuu ya 7 - Waidhaa Sami'uu
- Vitabu Vya Marejeo
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha

Assalam aalaykum
Assalam aalaykum warahmatullahi wabarakatuh,
Najua kwamba igekuwa vizuri kwa kuanza na kuwashkuru kwa kitendo kizuri ambaco mlianza na tuombeni Du'ah mwenyezi mungu atufikishe salama kwa kumalizia kitendo hiki. Allahuma Amiin.
lakini ingekuwa vizuri ningewajulisha kuwa nna mkubwa wangu anaitwa MUSSA, Alhamdulillah amehifadhi Qor'an nzima.
Nashkuru saana.
Ndugu muislam kutoka Rwanda(Africa)
Assalaam aleykum, Natoa
Assalaam aleykum, Natoa pongezi kwa wote waliofanikisha kazi hii, inshaallah allah awalipe malipo yaliyo bora kabisa. Nategemea mtakamilisha kwa kutafsili juzuu zote zilizobaki inshaallah, allah awape nguvu na uwezo wa kufanya hayo na mengine ya kheri inshaallah.
Wa 'alaykumus-salaam wa
Wa 'alaykumus-salaam wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh
Tunashukuru kujua kwamba unafaidika na mafunzo ya Alhidaaya. Allaah Akuzidishie elimu ya Dini Yake Tukufu pamoja na sisi sote. Aamiyn.
Tuna furaha kukuarifu kwamba kazi hii tukufu imeshamalizika, ila iko katika marekebisho ya juzuu za mwishoni.
Du'aa zenu muhimu Allaah Atuwezeshe tuikamilishe na ichapishwe ili iwe mikononi mwenu na mzidi kufaidika nayo Inshaa-Allaah.
Ndugu Zako
Assalaam Aleikum,
Assalaam Aleikum,
Congratulation for translating the juzu in a manner that our children will be able to learn easier and also know arabic words.
Assalaam alaykum.! Pongezi
Assalaam alaykum.! Pongezi kubwa kwa kazi nzuri munayoifanya ktk kupigania dini ya Allah.! Inshaallah MWENYEEZI MUNGU atawalipa! Aamyn!
Nashukuru kupata uwelewa juu
Nashukuru kupata uwelewa juu ya matendo na mazingatio hapa duniani
Ninaomba mnifahamishe namna or hatua, matendo ya kusoma wakati unapomsalia maiti.
Naomba msada: tarijama ya
Naomba msada: tarijama ya cor,an neno kwa neno. njia rayisi ya kuingia kila sura ya cor,an. ahsanti
Assalaamu 'alaykum Kuhusu
Assalaamu 'alaykum
Kuhusu ombi lako, ni kwamba hii kazi bado changa, lakini pale tutakapoimaliza tutajaribu kutimiza ombi lako Inshaa-Allaah ikiwa uko uwezekano wa kufanya hivyo ulivyoomba.
Du'aa zako muhimu Allaah Atuwezeshe na Atutakabalie.
Ndugu Zako
AL HIDAAYA
Nawashukuru wote
Nawashukuru wote walioshiriki kufanikisha kupatikana kwa mafunzo ya dini kwa njia hii.
Mungu awazidishie wote