Skip navigation.
Home kabah

Sadaka Inafaa Kupewa Ndugu Na Jamaa?

SWALI:

 

Asalam aleikum

Kwanza shukran ndugu zangu kjwa munayo yafanya katika hii website jazaa yenu aijua Allaah Azowaj Allaah, Allaah awape afya imaan na umri muendeleze kazi.

Nina swali kuhusu sadaka, je sadaka waweza kuwapa familia na ikawa kama sadaka ama itakuwa ni wajib kuwapa familia. Shukran wa jazakumAllaah bil kheir wa Allaah izidkum.


 

JIBU

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Shukran zetu za dhati kwa swali lako kuhusu sadaka. Kutoa sadaka ni wajibu aliopatiwa Muislamu na Mola wake Mlezi. Hivyo, inatakiwa tuitoe kwa misngi ya Uislamu. Sadaka haifai tu kupewa mtu mwenye nguvu ya kufanya kazi na tajiri. Ama watu ambao ni katika familia basi unapowapa sadaka huwa unapata thawabu mara mbili; thawabu ya kutoa sadaka na ya kuunga kizazi. Hii ni kutokana na kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Sadaka yenu kwa jamaa ni sadaka na pia kuunga ukoo)) [Ahmad, Ibn Maajah, An-Nasaiy, At-Tirmidhiy] 

 

Hao jamaa unaweza kuwapatia na hasa ikiwa utawapatia ili wasaidike kimaisha basi utakuwa umefanya jambo zuri sana mbele ya Allaah Aliyetukuka. Kwa hivyo, sadaka anaweza kupatiwa yeyote miongoni mwa watu ila hao tuliowataja hapo juu.

 

Kwa muhtasari ni kuwa hakuna tatizo wala katazo na kumpatia sadaka jamaa yako wa karibu au wa mbali ni thawabu zaidi. Wale ambao hufai kuwapatia, ni jamaa wa karibu ambao wanakutegemea wewe kwa yale majukumu uliyopatiwa na Allaah Aliyetukuka. Mfano ni wazazi, mke, na watoto ambao kisheria unabidi uwatimizie mahitaji yao. Mbali na kuwa mke anaweza kumpatia Zakaah yake mumewe kama ilivyokuja Hadiyth Sahihi katika Riyaadh Swaalihiyn.

 

Na Allaah Anajua zaidi