Sadaka Inafaa Kupewa Ndugu Na Jamaa?
SW
Asalam aleikum
Nina swali kuhusu sadaka, je sadaka waweza kuwapa familia na ikawa
JIBU
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukran zetu za dhati kwa swali lako kuhusu sadaka. Kutoa sadaka ni wajibu aliopatiwa Muislamu na Mola wake Mlezi. Hivyo, inatakiwa tuitoe kwa misngi ya Uislamu. Sadaka haifai tu kupewa mtu mwenye nguvu ya kufanya kazi na tajiri. Ama watu ambao ni katika familia basi unapowapa sadaka huwa unapata thawabu mara mbili; thawabu ya kutoa sadaka na ya kuunga kizazi. Hii ni kutokana na kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Sadaka yenu kwa jamaa ni sadaka na pia kuunga ukoo)) [Ahmad, Ibn Maajah, An-Nasaiy, At-Tirmidhiy]
Hao jamaa unaweza kuwapatia na hasa ikiwa utawapatia ili wasaidike kimaisha basi utakuwa umefanya jambo zuri
Kwa muhtasari ni kuwa hakuna tatizo wala katazo na kumpatia sadaka jamaa yako wa karibu au wa mbali ni thawabu zaidi. Wale ambao hufai kuwapatia, ni jamaa wa karibu ambao wanakutegemea wewe kwa yale majukumu uliyopatiwa na Allaah Aliyetukuka. Mfano ni wazazi, mke, na watoto ambao kisheria unabidi uwatimizie mahitaji
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


