Nataka Kwenda Nchi Ya Kiislamu Kusoma Dini Wapi Niende?
SW
Assalamu Aleykum ndugu zangu in Islam. Nataka kwenda nchi ya kiislam kusoma sina elimu na sina mahram nifanyaje? Nitaka kuwa alima inshaallah is my dream [make duua 4 me pls].
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu njia za kusoma nje. Hakika inakuwa ni vigumu kusaidika japo tutakupatia nasaha za jumla huenda zikakufaidisha kwa kiasi kikubwa.
InshaAllaah tuko pamoja nawe dada yetu kwa du’aa ingawa umetuandikia namba 4 hapo badala ya maneno na hali unauliza jambo muhimu. Kuandika kwa mtindo wa namba si jambo la kistaarabu na pia kunaangusha shakhsiyah ya mtu anayefanya hivyo.
Tumesema ni vigumu kukupa ushauri kirahisi kwa sababu hukutueleza wewe unaishi sehemu gani ya hii dunia. Sehemu unayoishi ni muhimu kwani ndio tungeweza kukupatia ushauri muafaka katika
Ukiwa unaishi katika maeneo ya Afrika Mashariki unaweza kupata vyuo vya karibu vifuatavyo:
i. Chuo cha Elimu, Chukwani,
ii. Chuo cha Masomo ya Kiislamu na Sheria,
iii. Chuo cha wanawake cha Kiislamu (Ma’ahad al-Banaat),
iv. Kisha ipo taasisi katika nchi inayoitwa, Munadhwamat ad-Da’wah al-Islaamiyah. Taasisi hii kila mwaka huwa inawafanyia mitihani wanafunzi wanaotaka kwenda
v. Chuo kikuu cha
vi. Chuo cha Kiislamu Morogoro.
vii. Ni kufanya bidii kwenda katika balozi za Kiislamu na kuwaelezea unachotaka nao watakuelezea mahitaji
Tunatumai tutakuwa tumekusaidia kwa kiasi fulani.
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


