05-Matendo Mema Na Athari Yake Katika Utajiri Na Ukunjufu Wa Rizki: Mambo Yapasayo Kuchunga Katika Kutafuta Rizki

 

D. MAMBO YAPASAYO KUCHUNGA KATIKA KUTAFUTA RIZKI

 

CHUMO HALALI

 

Anasema Allaah:

 

“Enyi mlioamini kuleni katika vizuri Tulivyowaruzuku.” Al-Baqarah: 

 

Kutoka kwa Abu Hurayrah amesema, amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam):

 

“Enyi watu, enyi watu! Hakika Allaah ni Mzuri hakubali ila vilivyo vizuri, na hakika Allaah Amewaamrisha Waumini Aliyowaamrisha Mitume akasema, “Enyi Mitume kuleni katika vilivyo vizuri na mtende mema, hakika Mimi Najua mnayoyafanya.” Na akasema: “Enyi mlioamini kuleni katika vizuri nilivyowaruzuku.” Kisha akamtaja mtu anaenda safari ndefu nywele zina vumbi ananyanyua mikono yake mbinguni (kuomba), Ee Mola ee Mola, hali ya kuwa chakula chake ni haramu, kinywaji chake ni haramu, na mavazi yake ni haramu na amelelewa kwa haramu, vipi atajibiwa?”

 

Kutoka kwa Anas bin Maalik kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wasallam) amesema:

 

“Kutafuta halali ni wajibu kwa kila Muislam.”

 

Share