Kuna Maswahaba Waliokimbia Vitani Au Hao Ni Wale Wanafiki Walioahidiwa Adhabu?
SWALI:
Assalamu aleikum warahmatullahi taala wabarakaatuhu,niliwahi kusikia ktk darsa mbalimbali kuwa kuna maswahaba wengi ambao walikuwa si waislamu wa kweli kwa maana ya kuwa walikuwa wanafiqi, na hata ikafikia hatua ya baadhi yao kukimbia vitani jambo ambalo Mwenyezi Mungu Ameliweka wazi ktk Suratil-Ahzab, swali langu ni kutaka kujua hao maswahaba waliokimbia vitani ni akina nani, na ni katika vita gani walivyokimbia, naomba nisaidieni niwafahamu hao maswahaba waliokuwa wanafiqi kwani si wote walikuwa ni waislamu wa uhakika
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu Maswahaba waliokimbia katika Vita. Awali ya yote tufahamu kuwa Swahaba ni yule mtu aliyekutana na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), akamuamini, akatekeleza ya Uislamu na akafa katika Imani. Wanafiki ni watu walioanza kuwa wafuasi wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipohamia Madiynah kwa maslahi
Pia tufahamu kuwa kukimbia vitani ni katika madhambi makubwa
Labda hapa tutoe mifano kuhusu hayo. Katika vita vya Uhud, inafahamika kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitoka kwa ajili ya vita hivyo na Maswahaba elfu moja. Lakini kabla ya vita 'Abdullaah bin Ubayy bin Saluul, mkubwa wa wanafiki alitoa hoja kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa alikuwa anataka wapigane na maadui wakiwa Madiynah na kuwa rai hiyo haikuchukuliwa yeye na watu wake hawawezi kupigana. Kwa minajili hiyo, mnafiki huyo alirudi na wafuasi wake mia tatu (300) Madiynah, kumuacha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Maswahaba zake 700. Yaliyotokea katika vita hivyo yanaeleweka vizuri
Ama mfano mwengine ni katika Vita vya Ahzaab (makundi) ambapo wanafiki ndio waliomba ruhusa kuondoka katika vita hivyo ilhali mbali na shida
"Walipokujieni kutoka juu yenu na kutoka chini yenu; na macho yalipokodoka na nyoyo zikapanda kooni, nanyi mkaanza kumdhania Allaah dhana mbali mbali" (33: 10).
Mbali na mtihani huo Waislamu walisimama imara,
"Hapo Waislamu walitiwa mtihani na wakatetemeshwa kwa matetemesho makali" (33: 11).
Lakini wanafiki walisema yafuatayo:
"Na taifa moja miongoni mwao liliposema: 'Enyi wenyeji wa Yathrib (Madiynah)! Hamna mahali pa kukaa nyinyi, basi rudini makwenu'. Na kundi jingine miongoni mwao likaomba ruhusa kwa Mtume kwa kusema: 'Hakika nyumba zetu ni tupu (hazina watu)', lakini hazikuwa tupu, hawakutaka ila kukimbia tu" (33: 13).
Mfano mwengine ni katika vita vya Mu'tah ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwachagua majemadari watatu waongoze mmoja baada ya mwengine. Nao ni Zayd bin al-Haarithah, Ja'far bin Abi Twaalib na 'Abdallaah bin Rawaahah (Radhiya Allaahu 'anhum). Katika vita hivyo Waislamu walikuwa ni elfu tatu (3,000) dhidi ya Warumi laki moja (100,000). Majemadari wote watatu waliuliwa, na ujemadari ukashikwa na Khaalid bin al-Waliyd (Radhiya Allaahu 'anhu). Mbali na vita kuwa vikali siku hiyo Waislamu waliweza kusimama imara. Usiku wake Khaalid aliweka Shuura kuzungumzia suala
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


