Skip navigation.
Home kabah

Msichana Kumfundisha Mvulana Masomo Inafaa?

SWALI:

 

Asalamu alaikum warahmatullahi wabarakatu

 
ndugu zangu waislamu nauliza swali mimi ni msichana namfundisha mvulana mmoja ni jamaa yetu
  kijana mvulana mkubwa kwangu kwa miaka 8 namfundisha computer nyumbani kwetu  kila siku  muda ya masaa mawili lakini huwa hatuko peke yetu imma awe mamangu na sisi ama ndugu yangu nataka kujua  nini hukumu yake washukran nijibuni tafadhali. Waalaikum salam warahmatullahi wabarakatu


 

 

JIBU:

 

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kumfundisha mvulana masomo.

 

Uislamu umeweka mipaka ya kukaa faragha baina msichana na mvulana ambao wanaweza kuoana. Haifai kabisa kwa watu hao wawili kukaa faragha hata kusomeshana Qur-aan kwani watatu wao ni Shaytwaan, naye hutembea ndani ya miili yetu kama inavyotembea damu.

 

Hata hivyo, kama ulivyoeleza ndivyo, yaani mamako au ndugu yako anakuwepo wakati unapomfundisha huyo mvulana jamaa yenu kutakuwa hakuna tatizo kisheria. Lakini tunatakiwa pia ufahamu kuwa si kuwepo tu mamako au kakako hapo unapomfundisha, bali pia unatakiwa utekeleze masharti mengine yafuatayo:

 

1.      Usilegeze sauti yako wakati wa kumfundisha.

2.      Uvae nguo za heshima kama zilivyoamrishwa na Uislaam, kama ambavyo unavaa unapotoka nyumbani kwa ajili ya  shughuli za nje.

3.      Usifanye naye mzaha wala kuzungumza mengine mbali na kumsomesha.

 

Ikiwa utafuata maagizo hayo kutakuwa hakuna tatizo la kumsomesha.

 

Na Allaah Anajua zaidi