02-Kukata Undugu: Madh-har Ya Kukata Undugu

 

 

MADH-HAR YA KUKATA UNDUGU

 

Kukata undugu ni katika mambo yaliyoenea katika jamii ya Waislam, na haswa haswa katika wakati huu uliotawaliwa na mada (kupenda mali) kumepungua kutembeleana na kuungana watu wengi wamepoteza haki hii na kupituka, Allaah ndiye mwenye kutegemewa.

 

Kukata undugu kunaonekana kwa njia nyingi watu wengine hawawajui ndugu zao wa karibu kwa kuwaunga kwa mali au vyeo au tabia inapita miezi na huenda miaka hajawatembelea wala kuwafanyia wema, kuzidisha mapenzi, au kupeana zawadi au kuwazuilia dhara au maudhi, huenda yeye mwenyewe akawaudhi kwa maneno au matendo au vyote.

 

Na kuna watu hawashirikiani na ndugu zao katika furaha wala kuwaliwaza wala kuwapa sadaka maskini wao bali utamkuta anawatanguliza wengine katika kuwaunga.

 

Na katika watu wanawaunga ndugu zao pindi wakiwaunga na anawakata wakimkata huu si uungaji bali ni kulipa mema kwa mfano wake na hili linatokea kwa ndugu wa karibu na wengineo kulipa mema sio kwa ndugu peke yao.

 

Na muunga undugu wa kweli ni yule aungae nduguze kwa ajili ya Allaah, wakimuunga au wasimuunge.

 

Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam):            

 

(Sio muungaji kwa kutoa lakini muungaji ni yule ambaye ukikatwa undugu wake anauunga) Al-Bukhaariy

 

Na katika ukataji undugu unawakuta baadhi ya watu ambao Allaah Amewapa elimu na kulingania wa mbali na anaghafilika na kuwalingania watu wake (nduguze) na hili halitakikani; watu wa karibu ni bora kwa kuwaamrisha  mema.

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) kumwambia Nabii wake Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam):

 

“ Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.” Ash-Shua’raa: 214

 

Na katika madh-har ya ukataji undugu unakuta baadhi ya familia kubwa anatokea mwenye elimu au mtu mwema au mlinganiaji unamuona anakubalika zaidi na kuheshimika na watu wengine wala hapati katika familia yake ila kukanushwa na kupingwa jambo ambalo linamshushia utukufu wake kumdhoofisha nguvu zake na kupunguza athari yake.

 

 Na katika madh-har ya kukata undugu kuwagawanya ndugu na kuvunja nguvu zao.

 

Share