Tafsiyr Ya Suratul-'Aswr
Imekusanywa Na:Ummu Iyyaad
بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمنِ الرَّحيم
((وَالْعَصْرِ))
((إِنَّ الإِ نسَانَ لَفِي خُسْرٍ))
((إِلاَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا))
KWA JINA LA ALLAH MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU
((Naapa kwa
((Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara))
((Ila wale walioamini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri)) [All-'Aswr:1-3]
UMUHIMU
SURATUL ‘ASRW
1. Ni katika Surah za mwanzo kabisa ziloteremka Makkah.
2. Ni mojawapo wa Surah ndogo kabisa yenye Aayah tatu tu na nyinginezo ni Suratul-Kawthar na Suratun-Naswr, kwa hiyo jumla zote pia ni tatu.
3. Surah hii imeelezea shuruti zote ambazo Muumba wetu Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amezitoa kama ni fardhi na wajibu ili aweze mtu kuridhiwa na Muumba wake na kufaulu atakaporudia Kwake (yaani Akhera).
Shuruti zenyewe ni nne
· Kuamini
· Kutenda vitendo vyema
· Kuusiana kwa haki
· Kuusiana kusubiri
Shuruti zote ni lazima kuzitimiza ili kufaulu Akhera.
Mfano wake ni
Ni sawa na Muislamu, japo kuwa anaswali Swalah tano lakini madamu hafanyi mengine aliyoamrishwa na Mola wake hatokua amemridhisha Mola wake.
4. Ingawa ni Surah ndogo lakini yaliyomo ndani yake ni muhimu na mazito
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika
((بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ))
((الَر كِتَابٌ أُحْكِمَتْ آيَاتُهُ ثُمَّ فُصِّلَتْ مِن لَّدُنْ حَكِيمٍ خَبِيرٍ))
((Alif Laam Ra. Hiki ni Kitabu ambacho Aayah zake zimewekwa wazi, kisha zikapambanuliwa, kilichotoka kwa Mwenye Hikma na Mwenye Khabari)) [Huud 11:1]
Kwa hiyo Suratul ‘Aswr ni Surah ambayo Aayah zake zimewekwa wazi kwa hikma ya juu kisha zinajichambua au zinajielezea zaidi kwa urefu katika Surah nyingine, kama vile vile Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Suratul-'Imraan:
((هُوَ الَّذِيَ أَنزَلَ عَلَيْكَ الْكِتَابَ مِنْهُ آيَاتٌ مُّحْكَمَاتٌ هُنَّ أُمُّ الْكِتَابِ وَأُخَرُ مُتَشَابِهَاتٌ ...
((Yeye Ndiye Aliyekuteremshia Kitabu (hiki Quraan) Ndani yake zimo Aayah muhkam (nyepesi kufahamika) ambazo ndizo msingi (asili) wa kitabu na ziko nyingine mutashaabihaat ... (zilizofanana) )) [Al-Imraan:7]
Mfano vile vile
Surah Nzito kabisa ambayo ni msingi katika mafundisho ya imaan ni Suratul-Faatiha.
Surah nzito kabisa ambayo ni msingi katika mafundisho ya Tawhiyd ni Suratul-Ikhlaasw.
كان الرجلان من أصحاب رسول الله صلى الله عليه وآله وسلم إذا التقيا لم يتفرقا حتى يقرأ أحدهما على الآخر سورة والعصر
ثم يسلم أحدهما على الآخر
(Walikuwa masahaba wawili kila wanapokutana hawaachani ila baada ya kusomeana Suratul 'Al-ِِِAswr ikisha ndio wanaagana ) [At-Twabarani na Bayhaaqiy]
Ingawa Surah nyingine
Nini faida waliyokuwa wakiipata maswahaba kukumbushana Surah hii?
Jibu ni kuwa :
Kwa sababu ya kukumbushana na kutanabahishana daima kuwa bila ya kutimiza maamrisho yaliyomo ndani ya Surah hii hawatafaulu au watakuwa waliokuwa katika hasara.
Imaam Shaafi'iy (Rahimahu-Llah) kasema mambo mawili mazito kuhusu Surah hii:
" لو لم ينزل الله سوى هذه السورة لكفت الناس"
" لو تدبر الناس هذه السورة لوسعتهم" ) أي لكفتهم (.
Watu wangelizingatia Surah hii maana yake ingeliwatosha kufaulu Akhera
Tunafahamu kwa usemi huo kuwa ni hidaaya (uongofu) kamili kwa watu wote Waislamu na wasio Waislamu.
5. Lugha ya Surah hii ni nyepesi kabisa, Bedui yeyote aliweza kuifahamu bila ya tabu. Na hata kwetu pia baadhi ya maneno ni mepesi kufahamu hata
6. Ingawa Surah hii ina Aayah tatu lakini, kwa hakika ni
((وَالْعَصْرِ))
))Naapa kwa zama))
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anaapa kwa zama. (maelezo ya maana hii utayapata chini ya makala hii)
Neno
Kama Anavyoapa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Surah nyingine zinazoanzia kwa:
وَالسَّمَاء وَالطَّارِقِ - وَالْفَجْرِ - وَالشَّمْس - وَاللَّيْلِ - وَالضُّحَى - وَالتِّينِ وَالزَّيْتُونِ
((Wassammai Wat-Twaariq – Walfajr – Washamsi – Wallayl – Wadhwuhaa – Wattiyn Wazzaytuun))
Katika Surah zote hizo Alizoziapia Anatoa maelezo baada ya viapo hivyo na hali kadhalika katika Surah hii Ameelezea kiapo hicho.
((إِنَّ الإِ نسَانَ لَفِي خُسْرٍ))
((Hakika binaadamu bila ya shaka yuko katika hasara))
Binaadamu yuko kwenye hasara? Vile vile utaona kuwa haikuleta maana kamili. Yuko kwenye hasara gani? Kwa kufanya kitendo gani au kwa kutokufanya kitendo gani? Lazima kuna maelezo zaidi kutujulisha sababu ya kuwa yuko kwenye hasara.
Ukisoma Aayah ya tatu ndio utajua kuwa kumbe sio wote waliokuwa katika hasara kwani Aayah inasema “ila" au "ispokuwa “ :
((إِلاَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ))
((Ila wale walioamini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri))
Hapa sasa ndio tumepata maana kamili ya Aayah hizi tatu
TAFSIYR
((وَالْعَصْرِ ))
((Naapa kwa zama))
1-Baadhi ya Wafasiri wa Qur-aan wamesema kuwa ni wakati wa Alasiri
2-Baadhi
3-Na baadhi
Wakati au zama kawaida ni za aina tatu:
Wakati uliopita.
Wakati tuliokuwepo sasa.
Wakati utakaokuja baada yetu.
Kutokana na rai ya tatu ya Wafasiri wa Qur-aan, Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anaapa kama ni ushahidi wa viumbe vyote tokea Adam ('alayhis-salaam) mpaka mwisho wa dunia, yaani watashuhudia watu wa nyakati zote hizo tatu; waliotutangulia, tulioko bado duniani na watakaokuja baada yetu kwamba:
((إِنَّ الإِ نسَانَ لَفِي خُسْرٍ)) ((إِلاَّ ... ))
((Hakika binaadamu bila ya shaka yuko katika hasara)) ((Isipokuwa…)
Kwa hiyo wakati unaendelea tu na utakwisha tu
Wale walioondoka duniani na watakaoondoka ndio watakokuwa aidha katika hasara au wamefaulu
((إِلاَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ))
((Ila wale walioamini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri))
Anaposema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) “ila wale walioamani na wakatenda mema ……..)
Mfano vile
Kisha Surah imetupa masharti ya kufaulu akhera. Watu wengi wanafikiria kuwa kufaulu ni kuwa na mali, au elimu ya juu, au cheo kikubwa na mengi mengineyo. Lakini Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anatupa hasa maana au shuruti za kufaulu duniani na akhera.
Tukiamini maneno haya ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) basi matamanio ya dunia hayatokuwa muhimu kwetu bali tutataka kuwa na imaan, na kufanya vitendo vyema na kuusiana kwa haki na kuusiana kwa subira ili tupate kufaulu huko.
Ukiangalia mfano wa Fir'awn au Qaaruun waliomiliki vyeo na mali nyingi duniani, lakini
Kinyume chao ni mfano
Kukubali kwa kusoma Aayah za Surah hii na kuamini hizi shuruti zilokuwemo ni rahisi lakini kuzitimiza ni vigumu kutokana na fitna za dunia. Ndio maana maswahaba walikuwa hawaachi kukumbushana Surah hii ili wajiepushe na kujikinga na fitna.
Na kwetu sisi ndio tunahitaji zaidi kukumbushana kwa vile fitna za dunia zinazidi na kuzidi. Na kukumbushana huku kila mara na kuzitekeleza shuruti hizo ndio tutaweza kufaulu hatutakuwa katika hasara duniani wala Akhera.
Lakini ni lazima kuzitimiza shuruti zote nne kama Alivyoziweka Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwani kila neno katika Qur-aan lazima lichukuliwe kwa makini, yote ni haki, wala Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Hakuweka hata herufi moja katika Qur-aan ila ina maana yake. Na hakuna yeyote anayeruhusiwa kupunguza au kuongeza hata herufi moja.
Shuruti zote hizo zinaweza kuwa na daraja mbali mbali, mfano :
· Imaan, kuna watu ambao imani zao ni kamili za dhati, kuna wengine imaan zao ni kiasi tu .
· Kufanya vitendo vyema, wengine watumie wakati wote kuwa katika vitendo vyema tu, na wengine mara wafanye mara wasifanye.
· Kuusiana katika kufanya haki, wengine wafanye kazi hii kwa juhudi kubwa ya kutumia wasila mbali mbali na wengine wafanye kwa watu wachache tu.
· Subira, wengine wanaweza kuvumilia mitihani hata mikubwa, na wengine japo wanayo subira lakini katika mitihani mingine huenda wakawa dhaifu kidogo kusubiri.
Ijapokuwa yote hayo yana daraja zake, lakini kutimiza yote ni lazima ili kupata kufaulu na kutokuwa katika hasara.
Mfano kama mgonjwa aliyekwenda kwa daktari akamuandikia dawa nne kutibu maradhi yake. Yule mgonjwa akaona atumie dawa tatu na aache moja labda hiyo moja ilikuwa chungu mno! Lakini kumbe ile moja aliyoiacha kutumia ni ya kumsaidia kuondosha dhara ya dawa mojawapo ya zile tatu na kwa vile yeye hakuitumia, hakuweza kupata matibabu sawa sawa. Kwa hiyo aidha atumie zote nne au aziache abakie na maradhi yake. Na hivi ndivyo Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Alivyotupa shuruti hizi nne zote kuzitimiza ili kufaulu, yaani ikiwa moja imepunguka basi hajafaulu mtu.
Imaam Ar-Raazi (RahimahuLLah) alisema maneno mazito kuhusu Aayah hizi za Suratul ‘Aswr :
إعلم ان هذه الأيات فيها وعيد شديد لأن الله حكم بالخسارة على جميع الناس إلا من كان آتياً بأشياء أربعة أو متصفاً بصفات أربع وهي : الإيمان ، والعمل الصالح، والتواصي بالحق والتواصي بالصبر . فدل ذلك على أن النجاة معلقة بمجموع هذه الأمور
"Tambua kwamba Aayah hizi zina maonyo makali kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ametoa hukumu kuwa binaadamu wote wako katika hasara ila atakayetekeleza mambo haya manne au atakayekuwa na sifa nne nazo ni; (1) kuamini, (2) kufanya vitendo vyema (3) kuusiana na hakki na (4) kuusiana na kusubiri. Akaonyesha kuwa kufaulu kunaambatana na mambo yote hayo"
Kwa hiyo ni onyo kali kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) ni lazima shuruti zote nne zitekelezwe
1. KUAMINI
Kuamini hapa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amekusudia aina mbili.
· Kuamini dini ya mwisho ya kiislamu na Mtume wa mwisho Muhammad (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Yaani kukiri kuwa
أِشْهَدُ أَن لاَ إِلَهَ إلاَّ اللَّه وَ أشْهَدُ أنَّ مُحَمَّدٌ رَسُولُ اللَّه
“Nakiri kwa moyo na kutamka kwa ulimi kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah na Muhammad ni Mjumbe Wake”
. Hii inawahusu Waislamu wote.
Kuwa na imaan baada ya kuwa Muislamu kwa sababu haiwezi kuwa mtu mwenye imaan ya kweli akawa hamtii Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) na Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)
قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي قُلُوبِكُمْ وَإِن تُطِيعُوا اللَّهَ وَرَسُولَهُ لَا يَلِتْكُم مِّنْ أَعْمَالِكُمْ شَيْئًا إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
((Mabedui wamesema: Tumeamini. Sema: Hamjaamini, lakini semeni: Tumesilimu. Kwani Imani haijaingia katika nyoyo zenu. Na mkimtii Allah na Mtume Wake, Hatakupunguzieni chochote katika vitendo vyenu. Hakika Allah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu))
((Hakika Waumini ni wale waliomuamini Allah na Mtume Wake tena wasitie shaka kabisa, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Allah kwa
2. KUFANYA VITENDO VYEMA
((وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ))
Vitendo vyote vyema mbali ya vile vya fardhi, kama sadaqa, kufunga Swawn za Sunnah, Swalah za Sunna, kutii wazazi, kusaidia wahitaji kwa njia mbali mbali, kupatanisha watu, kufundisha watu, wema na majirani, na mengi sana mengineyo hata dogo vipi kama mfano kuokota kitu cha dhara njiani au kumwambia mwenzako tamko zuri.
Na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kila mara katika Quraan Analeta Aayah inayosema :
((إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ
(([Wale walioamini na kufanya vitendo vizuri]
3. KUUSIANA KATIKA
((وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ))
Muislamu anapoona jambo lolote baya lilokuwa sio katika sheria ya Kiislam basi ni wajibu wake kulisawazisha na kujaribu kulibadilisha.
Lakini ni muhimu
((ادْعُ إِلِى سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ وَجَادِلْهُم بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ))
(([Waite (watu) katika njia ya Mola wako kwa hikma na mauidha mema na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora)) [An-Nahl:125]
Mfano kama rafiki yako haendi mwendo mzuri wa Kiislam labda haswali au labda mavazi yake zio mazuri, anza kwa kumsifia na kuusifu urafiki wenu na kuomba kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) muendelee urafiki, na kuwa unaogopa kuwa unalotaka kumnasihi asije kukasirika, na kwamba unamwambia kwa kumtakia kheri sio shari. Yaani upake mafuta urafiki kwanza.
Hapa tujue kuwa ukweli ni mchungu, si rahisi kuwa mara moja mtu anakubali kupewa nasiha. Ni jambo gumu
Vile vile
((كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللّهِ))
((Nyinyi ndio umma bora kuliko umma zilizodhihirishiwa watu, mnaamrisha yaliyo mema na mnakataza yaliyo maovu na mnamuamini Allaah] [Al-'Imraan: 110]
Vile vile Mtume wetu (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katufundisha kuwa tunapoona jambo baya la kuchukiza katika dini basi ni wajibu kulikataza na ndiyo dalili ya Imaan
عَنْ أبيِ سَعِيدٍ الْخُذْرِيٍّ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ : سَمِعْتُ رَسُولُ اللّهِ صلي الله عليه وآله وسلم يَقُولُ :((مَنْ رَأَى مِنْكُمْ مُنْكَراً فَلْيُغَيِّرْهُ بِيَدِهِ ، فَإنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَبِلِسَانِه، فإنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَبِقَلْبِه، وَذَلِكَ أَضْعَفُ الإْيمَان ))
رَوَاهُ مُسْلِم
Kutoka kwa Abi Sa'iydil-Khudhriyyi (Radhiya Allahu 'anhu) kasema kuwa: "Nimemsikia Mjumbe wa Allaah Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema: ((Atakayeona katika nyinyi maovu basi aybadilishe kwa mkono wake, kama hakuweza basi kwa ulimi wake na kama hakuweza basi kwa moyo wake (yaani achukie lile ovu) na hiyo ni imani ndogo kabisa)) [Muslim]
4. KUUSIANA KUWA
((وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ))
Baada ya kufanya kazi hiyo ya kuamrisha mema na kukataza maovu, ukae tayari kupata mitihani, misukosuko, machungu ya aina mbali mbali. Pengine upoteze urafiki wako na rafiki yako mpenzi au kama ni kubadilisha maovu yanayotendekana na jamaa wengi katika mji au kijiji basi pengine wakukatae na wakufukuze mji.
Au pengine mwenye kufanya kazi hiyo ya daawa iwe kwamba hapo zamani hakuwa katika mwendo mzuri, kisha akapata uongofu na akapenda kuwanasihi wenzake, basi hapo atakumbushwa maovu yake ya mwanzo ili avunjike moyo na apate uchungu.
Na machungu ya aina mbali mbali mengineyo yatamfika hata
Na mifano bora tunayo kutokana na visa vya Mitume waliofanya daawa kuwaita watu katika dini ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), waliofikwa na tabu na maudhi makubwa makubwa.
Basi subira ni lazima katika daawa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala). Asije mtu akavunjikwa moyo akaacha kufanya nasaha kwa watu au kuendelea kubadilisha mabaya anayoyaona. Aendelee tu kufanya kazi ya Allaah atalipwa malipo mazuri kabisa Aakhera. Hakuna kizuri kinachopatikana kwa urahisi.
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Alijua ugumu wa jambo hili ndio maana akaunga baada ya kuusiana kwa haki na kuusiana kwa subira
وَتَوَاصَوْا بِالْحَقِّ وَتَوَاصَوْا بِالصَّبْرِ
Luqumaan alipompa nasaha mwanawe kuhusu kuamrisha mema na kukataza mabaya pia alimgusia jambo
(( يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلَاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ وَاصْبِرْ عَلَى مَا أَصَابَكَ إِنَّ ذَلِكَ مِنْ عَزْمِ الْأُمُور))
((Ewe mwanangu! Simamisha Swalah na uamrishe mema, na ukataze mabaya na usubiri ju ya yale yatakayokusibu hakika haya ni katika mambo yanayostahili kuazimiwa)) [Luqmaan: 17]
أللهم اجعلنا من الذين آمنوا وعملوا الصلحات وتواصو بالحق وتواصو بالصبر – ِأمين .
Ya Allaah, Tujaaliye tuwe katika wale waliomini na kutenda vitendo vyema na kuusiana kutenda haki na kuusiana kuwa na subira. Aamiyn.
Naomba radhi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
