Kurudia Adhkaar Na Du’aa Mara Tatu Au Mara Saba; Nini Hikmah Yake?

 

 

Kurudia Adhkaar Na  Du’aa Mara Tatu Au Mara Saba; Nini Hikmah Yake?

 

 Alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Assalam Alaykum Warahmatullaahi. Alhamdullahi, tunamshukuru Allah kwa kuwaezesha kututatulia maswali yetu na InshaAllah jaza yenu iko kwa Allah. Swali langu ni hili? Kuna dua nyingine ukisoma unatakiwa uregelee 3 ama 7? Je kuna umuhimu gani kuregelea ama pengine kuna hadithi?

 

Jazakallah kheir

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

 

Zimethibiti du’aa na adhkaar kadhaa zinazopaswa kutajwa mara tatu au mara saba na baadhi ya Adkhaar zinapaswa kutajwa mara mia. Na nyenginezo mara moja moja tu.

 

Adhkaar ndio mara nyingi zinakuwa zaidi ya mara moja na hizo idadi pia huwa zimetokana na Hadiyth. Kwa mfano, Adhkaar baada ya Swalaah, Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametuagiza tuseme Subhaana Allaah mara 33, AlhamduliLLaah mara 33, Allaahu Akbar mara 33 na

 

لا إلهَ إلاّ اللّهُ وَحْـدَهُ لا شَـريكَ له، لهُ المُلـكُ ولهُ الحَمـد، وهوَ على كلّ شيءٍ قدير

Laa ilaaha illaAllaahu Wahdahu laa shariyka Lah, Lahul Mulku walahul Hamdu, wa Huwa ‘alaa kulli shay-in Qadiyr.  

Hapana muabudiwa wa haki ila Allaah, na hali ya kuwa Peke Yake Hana mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Zake Himdi na Yeye juu ya kila kitu ni Qadiyr (Muweza)

 

Mara moja na katika riwaayah nyengine mara kumi au mara mia.

 

Pia tumefundishwa kufanya Istighfaar mara sabiini au mara mia kwa siku. Mfano kusema:

 

أَسْتَغْفِرُ الَّلهَ وَ أَتُوبُ إِلَيْهِ

Astaghfiru-Allaahi wa atuwbu Ilayhi (mara mia kila siku)

Namuomba Allaah maghfirah na natubu (narejea) Kwake [Hadiyth ya Al-Agharr bin Yasaar Al-Muzaniy Radhwiya Allaahu ’anhuu katika Al-Bukhaariy[   

 

 

Hayo ndio mafundisho yalivyokuja na hatukutajiwa hikma  ya hizo idadi ila tumetajiwa baadhi ya fadhila katika Adhkaar mbalimbali tunazosoma. Na kuamini na kufuata bila kutaka kujua zaidi yasiyoelezwa kwetu kutoka Qur-aan na Sunnah ndio linalompasa Muislamu kuitakidi na ni dalili ya iymaan.

 

Kwa faida zaidi utapata kwenye kitabu hiki cha Du’aa na Adhkaar:

 

Hiswnul Muslim

 

Ama Du‘aa ni vizuri kuomba mara tatu kutokana na kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

 

 ..وَكَانَ إِذَا دَعَا دَعَا ثَلَاثًا وَإِذَا سَأَلَ سَأَلَ ثَلَاثًا ثُمَّ قَالَ: ((اللَّهُمَّ عَلَيْكَ بِقُرَيْشٍ)) ثَلَاثَ مَرَّاتٍ...

...na alikuwa anapoomba anaomba mara tatu, akiuliza anauliza mara tatu kisha akaomba: ((Ee Allaah, juu Yako Maquraysh)) mara tatu ...)) [Muslimu]

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share