Mwenye Kufanya Na Kuelimisha Sunnah Nzuri Katika Uislam Na Mwenye Kuelimisha Upotofu
Jibu la Shaykh 'Abdul 'Aziyz bin Baaz
Imetarjumiwa na Ummu Iyyaad
SW
Je, kwanza hii ni Hadithi (Sahihi?)
Pili,
Anajibu Shaykh 'Abdul 'Aziyz bin Baaz
JIBU:
Hadithi hii ni Sahihi nayo inatuonyesha sheria (au kuruhusu) kuhuisha Sunnah na kuiitikia (kuifundisha) na kuhadharisha Bid'ah na shari. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema
((من سن في الإسلام سنة حسنة كان له أجرها وأجر من عمل بها من بعده لا ينقص ذلك من أجورهم شيئاً ومن سن في الإسلام سنة سيئة كان عليه وزرها ووزر من عمل بها من بعده لا ينقص من أوزارهم شيئاً)) خرجه مسلم في صحيحه
((Atakayefanya kitendo chema katika Uislam atapata ujira wake na ujira wa yule atakayekitenda baada yake bila ya kupungukiwa thawabu zao. Na atakayetenda kitendo kibaya katika Uislam atabeba (mzigo wa) dhambi zake na dhambi za yule atakayetenda wala hapungukiwi kitu katika (mzigo wa) dhambi hizo)) (Muslim)
Mfano wa hadithi hii iliyotoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema:
(( من دعا إلى هدى كان له من الأجر من أجور من تبعه لا ينقص من أجورهم شيئاً ومن دعا إلى ضلالة كان عليه من الإثم مثل آثام من تبعه لا ينقص ذلك من آثامهم شيئاً)) مسلم
((Atakayefanya daawa kuonyesha uongofu atapata thawabu (ujira) wa yule atakayemfuata bila ya kupungukiwa chochote katika thawabu zao na atakayeongoza katika upotofu atapata dhambi mfano wa dhambi zayule atakayefuata bila ya kupungukiwa chochote katika dhambi zao)) Muslim
Maana ya (Atakayefanya Sunnah katika Uislam) ni kuihuisha (kuifufua) Sunnah, kuidhihirisha na kuifichua Sunnah ambayo imefichika kwa watu (au imeghafiliwa na watu) basi huidhihirisha na kuibainisha, basi hupata thawabu
Kwa hiyo, ilivyokusudiwa katika hadiyth ni kuihuiisha Sunnah na kuidhihirisha.
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kasema
(( قصوا الشوارب وأعفوا اللحى وخالفوا المشركين)) متفق على
((Kateni masharubu na wacheni ndevu, muwe tofauti na washirikina))
(Hadiyth hii imesimuliwa na Al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhumaa)
Na watu walipomuona huyo mwalimu yeye mwenyewe kaziweka ndevu zake wakamfuata, kwa hiyo anakuwa kawahuiishia wao hiyo Sunnah. Nayo ni Sunnah ya waajib haifai kuiacha kwa kufuata maamrisho ya hadiyth iliyotajwa hapo juu na maana yake, akawa kwa kufanya hivyo, kapata thawabu sawa na thawabu zao.
Au mfano katika nchi watu hawaswali Swalah ya Ijumaa kutokana na kutokujua kwao (umuhimu wake) akawafundisha na kuwaswalisha akapata mfano wa thawabu zao pia. Na hivyo hivyo watu katika nchi nyingine hawatambui Swalah ya Witr akawafundisha wakamfuata au mifano
Hivyo, atakayezifufua baina
Na sio maana kwamba aanzishe (azushe) jambo katika dini lisiloamrishwa na Allaah. Kwani uzushi ni upotofu kutokana na kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika hadithi sahihi,
(( وأياكم ومحدثات الأمور فإن كل محدثة بدعة وكل بدعة ضلالة))
((Jihadharini na mambo ya uzushi kwani kila uzushi ni Bid'ah na kila Bid'ah ni upotofu))
Vile vile anasema Mtume ((Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika hadithi Sahihi:
(( من عمل عملاً ليس عليه أمرنا فهو رد)) البخاري
((Atakayetenda kitendo kisichokuwa chetu basi kitarudishwa.)) Al Bukhari.
Na katika kauli nyingine,
( من أحدث في أمرنا هذا ما ليس منه فهو رد) متفق عليه.
((Atakayezusha katika mambo yasiyokuwa yetu basi kitarudishwa))
Al-Bukhaariy na Muslim.
Na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisema katika Khutba ya Ijumaa,
((أما بعد فإن خير الحديث كتاب الله وخير الهدى هدى محمد صلى الله عليـه وسلم وشر الأمور محدثاتها وكل بدعة ضلالة)) خرجه مسلم في صحيحه
((Amma Ba'ad hakika lililokuwa bora kabisa la kuhadithia ni Kitabu cha Allaah, na uongofu ulio bora ni uongofu wa Muhammad ((Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na jambo la shari kabisa ni uzushi wake na kila uzushi ni upotofu))
Muslim katika Sahihi yake.
Kwa hiyo aina ya ibada yoyote isiyoletwa na Allaah, haifai (kuifundisha) kuifanyia daawa, wala anayeileta na kuifanya hapati thawabu bali itakuwa kuitenda na kuileta kwa watu ni Bid'ah na huyo atakayeileta (kwa kuitangaza na kuieneza kwa watu) atakuwa ni katika yule anayeongoza katika upotofu na Allaah (Subhaana wa Ta'ala) Amemlaumu na kumhoji huyo mtu mwenye kutenda hivyo kuwa je,
((Au hao wana miungu ya kishirikina waliowatungia dini asiyoitolea idhini Mwenyezi Mungu…)) [Ash Shuura:21]
Wa Allaahu A’alam
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


