05-Swalaah – Kuwajibika Na Fadhila Zake: Ni 'Ibaadah Muhimu Kabisa

Swalaah – Kuwajibika Na Fadhila Zake

 

05- Swalaah Ni ‘Ibaadah Muhimu Kabisa

 

Alhidaaya.com

 

 

 Swalaah ni ‘ibaadah muhimu kabisa kuliko zote nyinginezo kwa sababu:

 

 

1-Swalaah ni nguzo pekee ya Kiislamu iliyofaridhishwa kutoka mbingu ya saba:

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضي الله عنه حديث الإسراء المشهور، وفيه أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:

  ((فَأَوْحَى اللَّهُ إِلَيَّ مَا أَوْحَى فَفَرَضَ عَلَيَّ خَمْسِينَ صَلَاةً فِي كُلِّ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ، فَنَزَلْتُ إِلَى مُوسَى صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ: مَا فَرَضَ رَبُّكَ عَلَى أُمَّتِكَ؟ قُلْتُ خَمْسِينَ صَلَاةً. قَالَ ارْجِعْ إِلَى رَبِّكَ فَاسْأَلْهُ التَّخْفِيفَ... قَالَ  فَلَمْ أَزَلْ أَرْجِعُ بَيْنَ رَبِّي تَبَارَكَ وَتَعَالَى وَبَيْنَ مُوسَى عَلَيْهِ السَّلَام حَتَّى قَالَ: يَا مُحَمَّدُ إِنَّهُنَّ خَمْسُ صَلَوَاتٍ كُلَّ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ، لِكُلِّ صَلَاةٍ عَشْرٌ، فَذَلِكَ خَمْسُونَ صَلَاةً))  روى البخاري (349) ومسلم (162)

 

Kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuhusu Hadiyth ya Al-Israa Wal Mi’raaj iliyo mashuhuri ambayo imeendelea kusema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Kisha Allaah Akanifunulia Wahy Akanifaridhisha Swalaah khamsini kwa kila siku moja na usiku wake. Nikateremka kwa Muwsaa ('Alayhis-Salaam) akauliza: “Amekufaridhisha nini Rabb wako kwa ummah wako.” Nikasema:  Swalaah khamsini. Akasema: “Rudi kwa Rabb wako na muombe takhfifu (Akupunguzie)) Akasema: ((Nikawa naendelea kurudi baina ya Rabb wangu Tabaaraka wa Ta’aalaa na baina Muwsaa mpaka (Allaah) Akasema: Yaa Muhammad! Hizo ni Swalaah khamsini kila siku moja na usiku wake, lakini kila Swalaah ni (thawabu) kumi, kwa hiyo (jumla ni thawabu (khamsini)) [Al-Bukhaariy (349), Muslim (162)]

 

 

2-Swalaah imeanzwa kutajwa katika Suwrah ya pili tu katika Mswahafu na ni miongoni mwa sifa za Waumini watakaofuzu:

 

 الم ﴿١﴾

Alif Laam Miym.

 

 

ذَٰلِكَ الْكِتَابُ لَا رَيْبَ ۛ فِيهِ ۛ هُدًى لِّلْمُتَّقِينَ ﴿٢﴾

Hiki ni Kitabu kisicho na shaka ndani yake, ni mwongozo kwa wenye taqwa.

 

 

الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِالْغَيْبِ وَيُقِيمُونَ الصَّلَاةَ وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ ﴿٣﴾

Ambao huamini ya ghayb na husimamisha Swalaah na katika vile Tulivyowaruzuku hutoa. [Al-Baqarah: 1-3]

 

 

 

3-Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Ametuamrisha Swalaah mara nyingi katika Qur-aan. Anasema (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَارْكَعُوا مَعَ الرَّاكِعِينَ ﴿٤٣﴾

Na simamisheni Swalaah na toeni Zakaah na rukuuni pamoja na wanaorukuu (katika utiifu). [Al-Baqarah: 43]

 

 

 Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَانْحَرْ ﴿٢﴾

Basi swali kwa ajili ya Rabb wako na chinja kwa ajili Yake. [Al-Kawthar: 2]

 

 

 Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

  وَاسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ وَإِنَّهَا لَكَبِيرَةٌ إِلَّا عَلَى الْخَاشِعِينَ ﴿٤٥﴾

Na tafuteni msaada kupitia subira na Swalaah; na hakika hilo ni kubwa isipokuwa kwa wanyenyekevu. [Al-Baqarah: 45]

 

 Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

 حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَىٰ وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ﴿٢٣٨﴾

Shikamaneni na Swalaah na khaswa Swalaah ya katikati (Alasiri), na simameni mbele ya Allaah katika hali ya utiifu [Al-Baqarah: 238]

 

 

 Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 وَأَقِمِ الصَّلَاةَ طَرَفَيِ النَّهَارِ وَزُلَفًا مِّنَ اللَّيْلِ ۚ إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ۚ ذَٰلِكَ ذِكْرَىٰ لِلذَّاكِرِينَ﴿١١٤﴾

Na simamisha Swalaah katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku; hakika mema yanaondosha maovu. Hivyo ni ukumbusho kwa wanaokumbuka.  [Huwd: 114]

 

 Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

 أَقِمِ الصَّلَاةَ لِدُلُوكِ الشَّمْسِ إِلَىٰ غَسَقِ اللَّيْلِ وَقُرْآنَ الْفَجْرِ ۖ إِنَّ قُرْآنَ الْفَجْرِ كَانَ مَشْهُودًا ﴿٧٨﴾

Simamisha Swalaah tokea kupinduka hadi kukuchwa jua mpaka kiza cha usiku na Qur-aan ya (Swalaah ya) Alfajiri. Hakika Qur-aan ya Alfajiri ni yenye kushuhudiwa. [Al-Israa: 78]

 

 

 Na Anasema pia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 فَإِذَا قَضَيْتُمُ الصَّلَاةَ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمْ ۚ فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ ۚ إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا ﴿١٠٣﴾

Mtakapomaliza Swalaah, mdhukuruni Allaah msimamapo, na mkaapo na mnapolala ubavuni mwenu Mtakapopata utulivu, simamisheni Swalaah (kama desturi), hakika Swalaah kwa Waumini ni fardhi iliyowekwa nyakati maalumu [An-Nisaa: 103]

 

 

4-Luqmaan alimpa wasiya  mwanawe akataja Swalaah mwanzo kabisa:

 

يَا بُنَيَّ أَقِمِ الصَّلَاةَ وَأْمُرْ بِالْمَعْرُوفِ وَانْهَ عَنِ الْمُنكَرِ وَاصْبِرْ عَلَىٰ مَا أَصَابَكَ ۖ إِنَّ ذَٰلِكَ مِنْ عَزْمِ الْأُمُورِ ﴿١٧﴾

  “Ee mwanangu! Simamisha Swalaah, na amrisha mema na kataza ya munkari, na subiri juu ya yale yatakayokusibu. Hakika hayo ni katika mambo ya kuazimiwa. [Luqmaan: 17]

 

 

 

5- Swalaah ni nguzo ya pili katika nguzo tano za Kiislamu.

 

 

6-Hakuna mwenye udhuru na Swalaah za fardhi; si mgonjwa wala msafiri, hata Muislamu akiwa vitani amewekewa aina yake ya kuswali. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَإِذَا ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَقْصُرُوا مِنَ الصَّلَاةِ إِنْ خِفْتُمْ أَن يَفْتِنَكُمُ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ إِنَّ الْكَافِرِينَ كَانُوا لَكُمْ عَدُوًّا مُّبِينًا ﴿١٠١﴾

Na mtakaposafiri katika ardhi basi si dhambi kwenu kufupisha Swalaah mkikhofu kwamba waliokufuru watakushambulieni. Hakika makafiri wamekuwa kwenu ni maadui dhahiri. 

 

 

وَإِذَا كُنتَ فِيهِمْ فَأَقَمْتَ لَهُمُ الصَّلَاةَ فَلْتَقُمْ طَائِفَةٌ مِّنْهُم مَّعَكَ وَلْيَأْخُذُوا أَسْلِحَتَهُمْ فَإِذَا سَجَدُوا فَلْيَكُونُوا مِن وَرَائِكُمْ وَلْتَأْتِ طَائِفَةٌ أُخْرَىٰ لَمْ يُصَلُّوا فَلْيُصَلُّوا مَعَكَ وَلْيَأْخُذُوا حِذْرَهُمْ وَأَسْلِحَتَهُمْ ۗ وَدَّ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْ تَغْفُلُونَ عَنْ أَسْلِحَتِكُمْ وَأَمْتِعَتِكُمْ فَيَمِيلُونَ عَلَيْكُم مَّيْلَةً وَاحِدَةً ۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن كَانَ بِكُمْ أَذًى مِّن مَّطَرٍ أَوْ كُنتُم مَّرْضَىٰ أَن تَضَعُوا أَسْلِحَتَكُمْ ۖ وَخُذُوا حِذْرَكُمْ ۗ إِنَّ اللَّـهَ أَعَدَّ لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا مُّهِينًا ﴿١٠٢﴾

Na utapokuwa upo kati yao, ukawaswalisha, basi lisimame kundi miongoni mwao pamoja nawe, na wachukue silaha zao. Watakaposujudu basi wawe nyuma yenu (kuwalinda). Na lije kundi jingine ambalo halikuswali, liswali pamoja nawe, nao washike hadhari na silaha zao. Wale waliokufuru wanatamani kama mtaghafilika na silaha zenu na vifaa vyenu wakuvamieni mvamio mmoja. Na wala si dhambi kwenu ikiwa mna maudhiko kutokana na mvua au mkiwa wagonjwa kuweka (chini) silaha zenu. Na mshike hadhari zenu. Hakika Allaah Amewaandalia makafiri adhabu ya kudhalilisha.

 

فَإِذَا قَضَيْتُمُ الصَّلَاةَ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمْ ۚ فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ ۚ إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا ﴿١٠٣﴾

Mtakapomaliza Swalaah, mdhukuruni Allaah msimamapo, na mkaapo na mnapolala ubavuni mwenu Mtakapopata utulivu, simamisheni Swalaah (kama desturi), hakika Swalaah kwa Waumini ni fardhi iliyowekwa nyakati maalumu. [An-Nisaa: 101-103].

 

 

7- Swalaah ni ‘ibaadah pekee iliyowekewa masharti kama twahara, mavazi na khasa kuelekea Qiblah.

 

 

8- Anaposwali mtu, hutumia viungo vyote vya mwili; moyo, akili na ulimi.

 

9-Hairuhusiwi kushughulika kufanya lolote jengine wakati wa kuitekeleza Swalaah wala kuzungumza hata kuleta mawazo mengine ili ipatikane khushuu.

 

 

10- Swalaah ni ‘amali bora kabisa Anayoipenda Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kuliko jihaad  pindi akitimiza mja kwa wakati wake:

 

 

عن أبي مسعود رضي الله عنه قال: سألت رسول الله صلى الله عليه و سلم، أي الأعمال أفضل ؟ قال :((الصلاة على وقتها))، قلت ثم أي ؟ قال: ((بر الوالدين))  قلت ثم أي؟ قال: ((الجهاد في سبيل الله)) متفق عليه

Kutoka kwa Abdullaah bin Mas'uud (Radhwiya Allaahu 'anhu ambaye amesema: "Nilimuuliza Rasuli wa Allaah  (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni amali gani inayopendeza kwa Allaah? Akajibu: ((Ni kuswali kwa wakti wake)). Nikamuuliza tena: Kisha ni amali gani? Akajibu: ((Ni kuwafanyia ihsani wazazi)). Nikamuuliza tena: Kisha ni amali gani? Akajibu: ((Ni kupigana Jihaad katika njia ya Allaah)) [Al-Bukhaariy Na Muslim]

 

 

 

Share